Upload
others
View
35
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
1
1. Utangulizi
Mpango ni utaratibu ambao mtu binafsi au kikundi cha watu
hujiwekea katika kutimiza malengo waliojiwekea kwa muda
waliokubaliana, mpango huwezesha kufikia malengo kwa kupita
njia sahihi. Sababu ya kuwa na Mpango kwa ufupi ni hizi
zifuatazo:-
a) Kuuweka umoja wetu (Ushirikiano) kuwa na dira na
mwelekeo.
b) Kuwawezesha wanachama kuupima utendaji wa viongozi
waliowaweka madarakani, hivyo kuongeza uwajibikaji.
c) Kuwawezesha wanaushirikiano kujua matarajio na jinsi ya
kufikia matarajio hayo.
d) Kuongeza ushirikishwaji wa wanaushirikiano katika
kupanga maendeleo yao.
Mpango huu umeandaliwa kwa kurejea mpango wa mwaka wa
fedha 2014/2015.
2. Dira na dhima (Vision and Mission statement)
a) Dira (Vision) yetu ni kuwa kikundi imara cha kijamii na
kiuchumi nchini Tanzania
b) Dhima (Mission) yetu ni kukuza ushirikiano katika mambo
ya Kijamii na Kiuchumi kwa kuunganisha nguvu zetu kwa
faida ya wanaushirikiano wote
2
3. Madhumuni ya Ushirikiano Group DSM Madhumuni ya umoja huu ni kusaidiana katika masuala ya kijamii na
kiuchumi.
4 Uchambuzi yakinifu wa Ushirikiano Group (swoc), yaani
Uimara, udhaifu,fursa na changamoto
4.1 Uimara
a) Kikundi kina wataalam wa fani mbalimbali, yaani
Wahandisi, Wahasibu, Wanasheria, Wajasiliamali na
Wafanyabiashara, WanaTEHAMA, Waalimu, Madaktari n.k.
b) Hakuna ubaguzi, upendeleo, ukabila au udini.
c) Wanachama wana malengo yanayofanana na ni marafiki
tayari.
d) Kuna uongozi imara na wenye lengo la kusonga mbele.
e) Kikundi kina mfuko wake.
f) Kikundi kina katiba na kanuni za uendeshaji.
4.2 Udhaifu
a) Tumekuwa na tabia ya kutotekeleza tunachokubaliana.
b) Tumekuwa hatuchukulii hatua wanaoturudisha nyuma.
c) Tumekuwa hatutunzi kumbukumbu za vikao na mikutano.
d) Tumekuwa wazito kuchukua maamuzi.
e) Tumekuwa tunavunjika moyo pale tunapoona mambo
hayaendi vizuri.
3
f) Tumekuwa na mahudhurio yasiyoridhisha kwenye
mikutano yetu na pengine tunachelewa sana bila sababu za
kueleweka.
g) Hatuna ofisi ya kikundi.
4.3 Fursa
a) Kuna fursa nyingi nchini zinazosaidia vikundi kama vya
kwetu.
b) Tunaweza kupata mikopo kama kikundi.
c) Kuna teknolojia ya habari na mawasiliano.
d) Kukutana (networking) na kuwa karibu zaidi miongoni mwa
wanachama.
e) Kufanya kazi kwa ubia (joint venture) miongoni mwa
wanachama.
f) Kuweza kupata bima ya afya.
g) Kuwa na uwekezaji.
4.4 Changamoto
a) Upungufu wa ajira
b) Wanaushirikiano kuwa na majukumu mengi katika kazi zao
na wengine katika masomo, kwa hiyo kukosa muda wa
kuhudhuria vikao.
c) HIV/AIDS bado ni tishio kwenye jamii pamoja na familia
zetu.
4
5 Tabia ya Kikundi (Core Values)
Hii itatutofautisha vikundi vingine na ushirikiano Group DSM.
a) Ushirikiano (Teamwork) – Kuwa na wanachama
wanaopenda ushirikiano, kuaminiana, maelewano na
kuheshimiana.
b) Uaminifu (Integrity)- kuwa na wanachama wakweli,
waminifu, watii wa sheria kanuni na taratibu.
c) Kutopendelea (Impartiality)- kuwa na wanachama wasio
wabaguzi wa aina yoyote.
d) Uwajibikaji (Accountability)- Kuwa na wanachama
wawajibikaji na wachapa kazi.
6.0 Utekelezaji wa malengo ya mwaka wa fedha 2014/2015
Kwa mwaka wa fedha 2014/2015, Ushirikiano Group DSM
ilitekeleza malengo iliyojiwekea kama ifuatavyo:
6.1 Kuwa na kikundi imara chenye mshikamano na
uwajibikaji
a) Wanachama kushiriki kwenye masuala ya kijamii
yanayomhusu mwanachama kwa mujibu wa katiba na
kanuni za UG.
Kipimo ni idadi ya wanaushirikiano wanaoshiriki kwenye
maswala ya kijamii. Kazi hii ilitekelezeka kwa 60%, watu
wamekuwa wakijitokeza kwenye masuala mbalimbali ya
5
kijamii yanayomhusu mwanachama, mfano misiba,
harusi/send off.
b) Wanachama kuhudhuria vikao vya kila mwezi.
Kipimo ni idadi ya wanaushirikiano kwenye mikutano ya
kila mwezi. Kazi hii imetekelezwa, wanachama
walihudhuria kwenye vikao vya kila mwezi kwa 50%.
c) Kuwa na wanachama wasiozidi familia 30.
Kipimo ni idadi ya wanaushirikiano kuongezeka. Kazi hii
imetekelezwa kwani wanachama wameongezeka kutoka
27 mwezi Juni, 2014 hadi wanachama 31 kwa sasa.
Wanachama waliridhia kuongeza mwanachama mmoja
zaidi.
d) Kufanya vikao vya kila mwezi majumbani kwa
wanachama.
Kipimo ni vikao vya kila mwezi kufanyikia majumbani
mwetu. Kazi imetekelezwa kwa 100%, vikao vinafanyika
majumbani mwa wanachama.
e) Kufanya sherehe ya Ushirikiano day.
Kipimo ni sherehe ya Ushikiano day kufanyika. Kazi
imetekelezwa kwa 100%, ushirikiano day ilifanyika.
f) Kutunga kanuni za Maadili na kurekebisha kanuni za
TEHAMA na Jamii.
Kipimo ni kikundi kuwa na kanuni za Maadili na kanuni
za TEHAMA na Jamii zilizorekebishwa. Kazi hii
imetekelezwa kwa 67%. Kanuni za Maadili zilitungwa,
6
kanuni za Jamii zilirekebishwa, bado kurekebisha kanuni
za TEHAMA.
g) Kuandaa ofisi ya kikundi.
Kipimo ni kikundi kuwa na ofisi. Kazi hii bado
haijatekelezwa.
6.2 Kuwa na uchumi imara na uwekezaji
a) Wanachama kulipa ada za kila mwezi za
uanachama.
Kipimo ni wanaushirikiano kulipa michango yao ya kila
mwezi kwa wakati. Kazi hii imetekelezwa kwa 32%,
wanachama bado wanadaiwa.
b) Kuimarisha mfuko wa uwekezaji.
Kipimo ni kila mwanaushirikiano kuchanga shilingi
1,500,000/=.
Kazi hii imetekelezwa kwa 20% tu, mpaka sasa ni
wanachama 7 tu ndiyo wamechangia. Kati ya hao, ni
watatu tu waliomaliza.
c) Kuanzisha shule ya awali.
Kipimo ni kununua kiwanja na kuanzisha shule ya awali.
Kazi hii bado haijatekelezwa kwa sababu wanaushirikiano
wengi hawajachanga michango ya mfuko wa uwekezaji.
d) Kukopesha wanachama.
Kipimo ni uwezo wa mwanachama kukopa na kulipa
mkopo pamoja na riba. Kazi hii imetekelezwa kwa 80%,
wanachama wamekopa na kurudisha mikopo na riba.
7
Tukijipima utekelezaji wa malengo hayo, lengo la “Kuwa na kikundi
imara chenye mshikamano na uwajibikaji” ndiyo
lililotekelezwa kwa ukamilifu na kuonyesha muelekeo mzuri
wa kikundi chetu. Ndiyo kusema kuwa kikundi chetu
kimefanikiwa zaidi upande wa “Kijamii”. Lakini lengo la “kuwa
na uchumi imara na uwekezaji” halijatekelezwa kwa kiwango
kikubwa, kwani kuna majukumu tuliyotakiwa kuyafanya ili
kutimiza lengo hilo hatukuyafanya. Kumbukeni kuwa na
uchumi imara ndiyo mhimili wa kusitawi kwa kikundi chetu.
7.0 Malengo ya mwaka wa fedha 2015/2016
Katika mwaka wa fedha 2015/2016 Ushirikiano Group DSM
inatarajia kutimiza malengo manne kama ifuatavyo:-
7.1 Kuwa na kikundi imara chenye uwajibikaji na
mshikamano (KAMATI YA JAMII)
a) Wanachama kushiriki kwenye masuala ya kijamii
yanayomhusu mwanachama kwa mujibu wa katiba na
kanuni za UG.
Kipimo ni idadi ya wanaushirikiano wanaoshiriki kwenye
maswala ya kijamii.
b) Wanachama kuhudhuria vikao vya kila mwezi.
Kipimo ni idadi ya wanaushirikiano kwenye mikutano ya
kila mwezi.
c) Kufanya sherehe ya Ushirikiano day.
8
Kipimo ni sherehe ya Ushikiano day kufanyika.
d) Kuandaa ofisi ya kikundi.
Kipimo ni kikundi kuwa na ofisi.
e) Kuwezesha wanachama kujiunga na Mfuko wa Bima ya
Afya (NHIF).
Kipimo ni idadi ya wanachama waliojiunga na Mfuko wa
Bima ya Afya.
7.2 Kuwa na uchumi imara na uwekezaji (KAMATI YA FEDHA
NA UCHUMI)
a) Wanachama kulipa ada za uanachama kiasi cha
shilingi 30,000/= kila mwezi.
Kipimo ni wanaushirikiano kulipa ada ya 30,000/= kila
mwezi kwa wakati.
b) Kuimarisha mfuko wa uwekezaji.
Kipimo ni kila mwanaushirikiano kuchanga shilingi
1,500,000/= ndani ya muda wa miezi kumi. Kila mwezi
shilingi 150,000/=.
c) Kununua kiwanja/eneo.
Kipimo ni kiwanja/eneo kununuliwa.
d) Kukopesha wanachama.
Kipimo ni uwezo wa mwanachama kukopa na kulipa
mkopo pamoja na riba kwa wakati.
Pamoja na kiwango cha kawaida cha mikopo, wanachama
waliowekeza kwenye “Uwekezaji Fund” watapewa
motisha ya nyongeza ya uwezo wa kukopa kwa 50% ya
kiwango walichochangia kwenye mfuko wa uwekezaji.
9
e) Kufanya semina ya ujasiriamali kwa wanachama.
Kipimo ni semina ya ujasiramali kwa wanachama kufanyika.
7.3 Kuwa na kikundi chenye mawasiliano imara na ya kisasa (KAMATI YA TEHAMA)
a) Kurekebisha kanuni za TEHAMA.
Kipimo ni kuwa na kanuni za TEHAMA zilizorekebishwa.
b) Kuhuisha tovuti ya UG kwa wakati.
Kipimo ni kuwa na tovuti iliyo hai kila wakati
C) Kuwaunganisha wanaushirikiano wote na mtandao wa mawasiliano.
Kipimo ni wanaushirikiano wote kuunganishwa kwenye mtandao wa mawasiliano.
7.4 Kuwa na wanachama wenye maadili mema (KAMATI YA MAADILI)
a) Kusimamia katiba na kanuni za UG.
Kipimo ni wanachama wote kutii katiba na kanuni za UG.
b) Kupokea na kujadili mashauri ya ukiukwaji wa maadili ndani ya UG.
Kipimo ni idadi ya mashauri yaliyojadiliwa.
c) Kupendekeza adhabu dhidi ya mwanaumoja anayekiuka katiba na kanuni za UG.
Kipimo ni idadi ya mapendekezo yaliyowasilishwa kwenye mamlaka za juu.
10
8.0 Mpango kazi wa Ushirikiano Group kwa mwaka wa fedha 2015/2016
Lengo Kazi Kipimo cha utekelezaji
Muda wa utekelezaji
J A S O N D J F M A M J
1 Kuwa na kiundi
imara chenye
mshikamano na
uwajibikaji
1.Wanachama kushiriki
kwenye masuala ya
kijamii yanayomhusu
mwanachama kwa
mujibu wa katiba.
Idadi ya
wanaushirikiano
wanoshirikia katika
masuala ya kijamii.
2. Wanachama kuhudhuria vikao vya kila mwezi
Idadi ya wanaushirikiano kwenye vikao vya kila mwezi.
3. Kufanya sherehe ya Ushirikiano day
Sherehe ya Ushirikiano day kufanyika
4. Kuandaa ofisi ya
kikundi.
Kikundi kuwa na ofisi.
5.Kuwezesha
wanachama
kujiunga na
Mfuko wa Bima
ya Afya (NHIF).
Idadi ya wanachama waliojiunga na Mfuko wa Bima ya Afya.
2 Kuwa na uchumi
imara na
uwekezaji.
1. Wanachama kulipa ada za kila mwezi za uanachama shilingi 30,000/=.
Ada za kila mwezi shilingi 30,000/= kulipwa kwa wakati.
2. Kuimarisha mfuko wa uwekezaji
Kila mwanachama kuchanga shilingi 1,500,000/=. Kila mwezi shilingi 150,000/= kwa miezi kumi.
3. Kununua kiwanja/eneo.
Kiwanja/eneo kununuliwa.
11
4. Kukopesha wanachama
Wanachama kukopa na kulipa mikopo pamoja na riba kwa wakati.
5.Kufanya semina ya ujasiriamali kwa wanachama.
Semina ya ujasiriamali kwa wanachama kufanyika.
3 Kuwa na kikundi
chenye
mawasiliano
imara na ya
kisasa.
1. Kurekebisha kanuni za TEHAMA.
Kuwa na kanuni za TEHAMA
zilizorekebishwa.
2. Kuhuisha tovuti ya UG kwa wakati.
Kuwa na tovuti iliyo hai kila wakati.
3. Kuwaunganisha wanaushirikiano wote na mtandao wa mawasiliano.
wanaushirikiano wote kuunganishwa kwenye mtandao
wa mawasiliano.
4. Kuwa na wanachama wenye maadili mema.
1. Kusimamia katiba na kanuni za UG
wanachama wote kutii katiba na kanuni za UG.
2. Kupokea na kujadili mashauri ya ukiukwaji wa maadili ndani ya UG.
Idadi ya mashauri yaliyojadiliwa.
3. Kupendekeza adhabu dhidi ya mwanaumoja anayekiuka katiba na kanuni za UG.
Idadi ya mapendekezo yaliyowasilishwa kwenye mamlaka za juu.
8 Hitimisho
Mwisho wa mwaka wa fedha, kikundi kitatathimini
utekelezaji wa mpango wake ili kuangalia mafanikio na
mapungufu yaliyojitokeza kwenye utekelezaji wake. Ni
12
matumaini yangu kwamba baada ya kupitisha mpango huu,
wanachama watashiriki kikamilifu kwenye utekelezaji wake ili
hatimaye kikundi chetu kiweze kufikia malengo tuliyojiwekea.
Kiambatanisho
Makadirio ya mapato na matumizi ya UG kwa mwaka wa fedha
2015/2016
13
1 MAPATO
Kiasi(Tsh)
A) Mfuko wa Ushirikiano (ushirikiano fund)
i) Fedha iliyopo (balance)
17,506,561.00
ii) Ada
10,979,000.00
iii) Malimbikizo ya ada
1,140,000.00
iv) Marejesho ya mikopo ya 2014/2015
5,132,500.00
Jumla ndogo
34,758,061.00
B) Mfuko wa uwekezaji (Uwekezaji Fund)
i) Fedha iliyopo
6,300,000.00
ii) Michango ya uwekezaji
40,200,000.00
iii) Faini
650,000.00
iv) Malimbikizo ya faini
478,000.00
iv) Riba
1,400,000.00
Jumla ndogo
49,028,000.00
Jumla kuu (A +B)
83,786,061.00
2 MATUMIZI A) Mfuko wa Ushirikiano (Ushirikiano Fund)
i) Matukio ya furaha
1,000,000.00
ii) Matukio ya huzuni
3,000,000.00
iii) Ada (mtandao)
350,000.00
iv) Mikopo
20,000,000.00
v) Vikao
600,000.00
vi) Steshenari /dharura/nauli
600,000.00
vii) Ushirikiano day
3,000,000.00
viii) Ada ya usajili
50,000.00
ix) Gharama pango la ofisi
3,600,000.00
x) Gharama za benki (bank charges)
100,000.00
xi) Semina
400,000.00
Jumla ndogo
32,700,000.00
B) Mfuko wa uwekezaji (Uwekezaji Fund)
i) Kiwanja/eneo
48,000,000.00
ii) Kupigika (Kusaidiana)
360,000.00
Jumla ndogo
48,360,000.00