Upload
muhidin-issa-michuzi
View
331
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 1/126
i
HOTUBA YA MHESHIMIWA BALOZI DKT.AUGUSTINE PHILIP MAHIGA (MB), WAZIRIWA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WAAFRIKA MASHARIKI AKIWASILISHA
MAKADIRIO YA BAJETI YA MAPATO NA
MATUMIZI YA WIZARA KWAMWAKA WA FEDHA 2016/2017
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 2/126
ii
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 3/126
iii
YALIYOMO
ORODHA YA VIFUPISHO…………………………… iv
UTANGULIZI……………………………………………
1
TATHMINI YA HALI YA DUNIA……………………. 6
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAWIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2015/2016.. 12
ILIYOKUWA WIZARA YA MAMBO YA NJE NAUSHIRIKIANO WA KIMATAIFA……………………. 12
TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA…………….… 65
Chuo cha Diplomasia……………………………
65
Kituo cha Kimataifa cha Mikutano chaArusha………………………………………………
66
Mpango wa Kujitathmini Kiutawala BoraBarani Afrika……………………………………… 68
ILIYOKUWA WIZARA YA USHIRIKIANO WAAFRIKA MASHARIKI…………………………………. 70
USIMAMIZI WA MAPATO NA MATUMIZI……….. 107
CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA KATIKAUTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA WAFEDHA 2015/2016…………………………………… 108
SHUKRANI………………………………………………. 110
MALENGO YA WIZARA KWA MWAKA WA
FEDHA 2016/2017……………………………………. 111
MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YAWIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017…
113
HITIMISHO……………………………………………….
115
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 4/126
iv
ORODHA YA VIFUPISHO
AfDB – African Development Bank
COMESA – Common Market for Easternand Southern Africa
FAO – Food and Agriculture
OrganizationIAEA – International Atomic Energy
AgencyILO – International Labour
OrganizationIMF – International Monetary FundIOM – International Organization for
MigrationPSPF – Public Sector Pension Fund
SADC – Southern African DevelopmentCommunity
UNDP – United Nations DevelopmentProgamme
UNEP – United Nations EnvironmentProgamme
UNESCO – United Nations EducationalScientific and CulturalOrganization
UNFPA – United Nations PopulationFund
UN-HABITAT – United Nations Human
Settlement ProgrammeUNHCR – United Nations High
Commission
for Refugees
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 5/126
v
UNICEF – United Nations Children’sEmergency Fund
UNIDO – United Nations Industrial
Development OrganizationUNWTO – United Nations World Tourism
OrganizationUTT – Unit Trust of TanzaniaWHO – World Health OrganizationWWF – World Wildlife Fund
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 6/126
vi
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 7/126
1
UTANGULIZI
1. Mheshimiwa Spika, kutokana na Taarifa iliyowasilishwa leo Bungeni naMwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge yaMambo ya Nje, Ulinzi na Usalama naomba kutoahoja kwamba Bunge lako Tukufu likubalikujadili na kupitisha Makadirio ya Mapato naMatumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje naUshirikiano wa Afrika Mashariki kwa Mwaka waFedha 2016/2017.
2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote
nakushukuru kwa fursa hii adhimu yakuwasilisha mbele ya Bunge lako Tukufu kwamara ya kwanza Bajeti ya Wizara ya Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Aidha,naomba nitumie nafasi hii adhimu kumpongezakwa dhati Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Raiswa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania kufuatia Uchaguzi Mkuuuliofanyika tarehe 25 Oktoba, 2015.
3. Mheshimiwa Spika, naungana nawalionitangulia kumpongeza Mheshimiwa Raiskwa uongozi wake madhubuti na makiniunaoakisi kauli mbiu yake ya ‘Hapa Kazi Tu’. Sisisote ni mashahidi wa namna uongozi wakeulivyogusa si tu wananchi wa Tanzania bali pia
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 8/126
2
ulivyopokelewa na kuwa mfano wa kuigwa katikanchi za bara la Afrika na duniani kwa ujumla.Sifa zake zinasikika kila pembe ya dunia na
kutufanya tutembee kifua mbele. Nampongezasana kwa kumteua Mheshimiwa Samia Suluhukuwa Mgombea Mwenza na baadae kuchaguliwakuwa Makamu wa Rais wa kwanza mwanamkekatika historia ya nchi yetu. Kuchaguliwa kwakekumeidhihirishia dunia hatua kubwa ambayonchi yetu imepiga katika kumpa fursa sawa
mwanamke.
4. Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hiipia kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Ali MohamedShein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Serikali
ya Mapinduzi Zanzibar kwa kipindi cha pilikatika uchaguzi ulioendeshwa kwa amani nausalama. Kadhalika, nampongeza MheshimiwaKassim Majaliwa Majaliwa (Mb), kwa kuteuliwakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muunganowa Tanzania. Wizara yangu imefaidika sana nauongozi wao na miongozo mbalimbaliwanayoitoa katika utekelezaji wa majukumu
yetu.
5. Mheshimiwa Spika, niungane nawenzangu walionitangulia kuwashukuru nakuwapongeza watoa hoja waliozungumza kabla
yangu wakiongozwa na Mheshimiwa KassimMajaliwa Majaliwa (Mb), Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 9/126
3
Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango (Mb), Waziriwa Fedha na Mipango ambao hotuba zaozimeweka msingi mzuri kwa kuainisha dira na
masuala muhimu ya kitaifa na kimataifaambayo baadhi yake yanaangukia katikamajukumu ya Wizara yangu. Kama alivyoahidiMheshimiwa Rais kujenga ‘Tanzania yaViwanda’ na kama ilivyotafsiriwa katika Mpangowa Pili wa Maendeleo ya Taifa wa mwaka2016/2017 hadi 2020/2021, Wizara yangunayo imejielekeza katika kutekeleza ‘Azma yaSerikali ya kujenga Uchumi wa Viwanda’.
6. Mheshimiwa Spika, kama unavyofahamu,Wizara hii ni mpya baada ya kuunganishwa kwazilizokuwa Wizara mbili za Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa na Wizara yaUshirikiano wa Afrika Mashariki. Kwa ajili hiyo,namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe
Joseph Magufuli kwa kuniteua kuwa Mbunge naWaziri wa kwanza wa Wizara hii. Napendakumuahidi mbele ya Bunge lako Tukufu kuwanitatumia ujuzi na uzoefu mkubwa niliouvuna
katika nyanja za diplomasia ya kikanda nakimataifa kuendelea kuipaisha diplomasia ya Tanzania.
7. Mheshimiwa Spika, kazi yanguimefanywa kuwa nyepesi zaidi kutokana naushirikiano mzuri na ushauri tunaoupata mara
kwa mara kutoka kwenye Kamati ya Kudumu ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 10/126
4
Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalamachini ya uongozi wa Mheshimiwa Balozi AdadiMohammed Rajab (Mb), na Makamu wake
Mheshimiwa Kanali Mstaafu Masoud Ali Khamis(Mb) pamoja na Wajumbe wote wa Kamati hiyo.Wamekuwa wa msaada mkubwa sana kwaWizara yangu katika utekelezaji wa majukumu.
8. Mheshimiwa Spika, ukiniona nasimamambele ya Bunge lako Tukufu kwa kujiamini nikwa sababu ninao nyuma yangu viongoziwenzangu, watendaji na wafanyakaziwanaonisaidia kutekeleza majukumu yangu kwaufanisi mkubwa. Napenda kumshukuruMheshimiwa Dkt. Susan Alphonce Kolimba,Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikianowa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Balozi AzizPonary Mlima, Katibu Mkuu, Mheshimiwa BaloziRamadhan Muombwa Mwinyi, Naibu KatibuMkuu, Wakurugenzi, Mabalozi, Maafisa naWafanyakazi walioko Makao Makuu, Balozini naOfisi ya Zanzibar kwa msaada mkubwawanaonipatia. Uzalendo wao, ari yao na imani
yao kwangu, vinanipa kila sababu ya kuaminikuwa malengo tuliyojiwekea katika Bajeti hiitutayatekeleza kwa ufanisi mkubwa.
9. Mheshimiwa Spika , mwisho lakini simwisho kwa umuhimu, namshukuru kwadhati mke wangu mpendwa Mama Elizabeth
Mahiga, Watoto na familia yangu yote kwa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 11/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 12/126
6
TATHMINI YA HALI YA DUNIA
Hali ya Uchumi, Siasa na Usalama Duniani
12. Mheshimiwa Spika, hali ya duniaimeendelea kuwa ya mchanganyiko wamatumaini na mashaka. Katika kipindi chamwaka mmoja uliopita dunia imepiga hatuakwenye masuala kadhaa ya msingi kwa ustawina mustakabali wa dunia. Katika kipindi hiki
tumeshuhudia kusainiwa kwa Mkataba wa Pariskuhusu Tabianchi mwezi Desemba, 2015 ambaoumesubiriwa kwa muda mrefu. Kusainiwa kwaMkataba huu kunatoa matumaini kwa nchi zaAfrika na zile zinazoendelea kwa kuwepo kwauhakika katika Kudhibiti na Kukabili athari nachangamoto za tabianchi. Hii ni kutokana na
ukweli kuwa nchi zetu zinaathirika zaidi naathari za tabianchi wakati ni wachangiajiwadogo sana wa tatizo hilo. Kusainiwa kwaMkataba huu kunatoa fursa kwa nchi maskinikufidiwa na kujengewa uwezo katikakukabiliana na changamoto hizo. Hili ni jamboambalo nchi yetu imekuwa mstari wa mbele
kulipigania na Rais Mstaafu Dkt. Jakaya MrishoKikwete aliongoza jitihada hizi akiwa Mwenyekitiwa Kamati ya Wakuu wa Nchi wa Umoja waAfrika kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi.
13. Mheshimiwa Spika, jambo lingine lakutia matumaini ni kusainiwa kwa Malengo ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 13/126
7
Maendeleo Endelevu ambayo yanachukuanafasi ya Malengo ya Milenia ya mwaka 2000 -2015 ambayo utekelezaji wake ulifikia tamati
mwezi Septemba, 2015. Majadiliano kati ya nchizetu yaliyofikia malengo haya yalizingatia uzoefukatika utekelezaji wa Malengo ya Milenia, haja
ya kumalizia viporo vya Malengo ya Milenia naumuhimu wa kuhakikisha kuwa malengomapya yanazingatia mahitaji ya leo na keshokwa kuhakikisha kuwa ni endelevu. Malengo yaMaendeleo Endelevu ndio mwongozo wa agenda
ya maendeleo duniani kote na ndiyo yatakayokuwa rejea ya majadiliano namakubaliano mengine duniani. Sisi tumejipangavyema kutekeleza malengo hayo na bahati nzuri
yanashabihiana kwa kiwango kikubwa na Dira yetu ya Taifa ya 2025 na Mpango wa Pili waMaendeleo 2016/2017 – 2020/2021.
14. Mheshimiwa Spika, katika kipindi chamwaka mmoja uliopita kumekuwa pia namatukio ambayo yana mwelekeo mzuri kwaustawi wa amani na usalama duniani. Kwa
kuwa yako mengi, niruhusu niyataje mawilimakubwa. Kwanza, ni hatua ya nchi zaMarekani na Cuba kuamua kurejesha urafikiwao baada ya kuwepo kwa vikwazo vyaMarekani dhidi ya Cuba kwa zaidi ya miaka 50.Hatua hii ni muhimu na tunaungana nawapenda amani kote duniani kumpongeza Rais
Barack Obama wa Marekani na Rais Raul
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 14/126
8
Castro wa Cuba. Ikumbukwe kuwa Marekani naCuba ni rafiki wa Tanzania, na Tanzaniaimekuwa mstari wa mbele kupinga vikwazo vya
Marekani dhidi ya Cuba. Ni faraja kuwauhasama huo umekwisha, kwani kuondolewakwa vikwazo vya Marekani dhidi ya Cubakutawezesha Cuba kushiriki kikamilifu katikauchumi wa Dunia, na hali kadhalika itaimarishaushirikiano mzuri wa kiuchumi tulionao kati
yetu na Cuba. Makubaliano hayo yamemaliza
mabaki ya misuguano ya vita baridi ya miongo ya nyuma na kuendeleza amani duniani.
15. Mheshimiwa Spika, tukio la pili, nikuondolewa kwa vikwazo vilivyowekwa dhidi yaIran kuhusu Mpango wa Iran wa Nyuklia tarehe16 Januari, 2016, kufuatia Shirika la Kimataifa
la Nguvu za Atomiki kuthibitisha kuwa Iranimekamilisha hatua zote ilizopewa naWanachama wa Kudumu wa Baraza la Usalamala Umoja wa Mataifa na Ujerumani. Hatua hiinayo ni muhimu sana kwa kuwa inaondoa hali
ya mashaka iliyokuwa imetanda katika eneo laMashariki ya Kati kuhusu nchi ya Iran
kutengeneza silaha za nyuklia. Mashaka hayondiyo ambayo yamekuwa yakiyumbisha sanadunia kiuchumi kwa kuathiri bei za mafuta.Iran ni nchi rafiki ambayo tunashirikiana nayokiuchumi. Hivyo, kuondolewa kwa vikwazo hivyokunatoa fursa ya kukua kwa ushirikiano wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 15/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 16/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 17/126
11
Mashariki kuwa Msuluhishi wa Mgogoro wa
Burundi. Uteuzi wa Viongozi wetu Wastaafu wa
Kitaifa ni ushahidi kuwa kauli ya Tanzania
inasikilizwa na kuheshimika kwenye majukwaa
ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika.
18. Mheshimiwa Spika, Macho na masikio
ya dunia yameelekezwa huko Asia-Pacific
kutokana na fukuto la mgogoro wa umiliki wa
eneo la Bahari ya Kusini mwa Chinaunaohusisha nchi za China, Brunei, Vietnam,
Malaysia na Ufilipino. Pamoja na kuwa
kijiografia eneo hili laweza kuonekana ni mbali
sana na nchi yetu, athari za mgogoro huo
zitagusa kila pembe ya dunia kama
hautamalizika kwa njia za amani. Eneo hilo ndiopenye kitovu kikubwa cha ukuaji wa uchumi,
uzalishaji na biashara katika kipindi hiki
ambacho uchumi wa dunia kiujumla
unasuasua. Tanzania inaamini kuwa njia ya
uhakika ya kumaliza mgogoro wa Bahari ya
Kusini mwa China ni kupitia mazungumzo
baina ya nchi na nchi na kanda. Kwa sababu
hiyo, tunaunga mkono juhudi za utatuzi wa
mgogoro huo kwa njia ya mazungumzo na
mashauriano. Tunaitaka Jumuiya ya Kimataifa
na vyombo vyake kuzingatia Azimio Na. 298 la
mwaka 1982 la Mkataba wa Umoja wa Mataifa
wa Sheria ya Bahari.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 18/126
12
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU
YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA
2015/2016
ILIYOKUWA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA
USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
19. Mheshimiwa Spika, kabla ya kuelezautekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa Mwaka wafedha 2015/2016, naomba uniruhusu niainishekwa ufupi majukumu ya iliyokuwa Wizara yaMambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifakama ifuatavyo:-
i. Kubuni na Kusimamia Utekelezaji waSera ya Nchi ya Mambo ya Nje;
ii. Kusimamia Mikataba na Makubaliano ya Kimataifa;
iii. Kuratibu Masuala ya Uhusiano baina ya Tanzania na nchi mbalimbali,Ushirikiano wa Kimataifa, Bara laAfrika na Kikanda;
iv. Kulinda na kuendeleza Maslahi ya Taifa
ya Kiuchumi na Mengineyo nje ya nchi;v. Kusimamia masuala yanayohusu Kingana Haki za Kibalozi kwaWanadiplomasia waliopo nchinikulingana na Mkataba wa Vienna wamwaka 1961;
vi. Kusimamia na kuratibu masuala ya
Itifaki na Uwakilishi;
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 19/126
13
vii. Kuanzisha na Kusimamia Huduma zaKikonseli;
viii. Kuratibu shughuli za Tume za Pamojaza Kudumu za Ushirikiano; na
ix. Kusimamia utawala na Maendeleo yaUtumishi Wizarani na kwenye Balozizetu.
20. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza
majukumu hayo kwa mwaka wa fedha
2015/2016, Wizara ilitengewa kiasi cha Shilingi170,367,129,238.00. Kati ya fedha hizo, Shilingi162,367,129,238.00 ni kwa ajili ya Matumizi yaKawaida na Shilingi 8,000,000,000.00 ni kwaajili ya bajeti ya maendeleo. Katika fedhazilizotengwa kwa Matumizi ya Kawaida, shilingi153,698,142,238.00 ni kwa ajili ya Matumizi
Mengineyo na Shilingi 8,668,987,000.00
ni kwaajili ya mishahara ya Watumishi.
21. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa
fedha 2015/2016, Wizara na Balozi zakeilitarajia kukusanya maduhuli ya kiasi chashilingi 20,036,019,000.00. Hadi kufikia tarehe
30 Aprili 2016, Wizara imefanikiwa kukusanyakiasi cha shilingi 16,296,907,020.00 ikiwa nisawa na asilimia 81.3 ya makisio ya makusanyo
yote ya maduhuli kwa mwaka wa fedha2015/2016.
22. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe
30 Aprili, 2016 Wizara ilipokea jumla ya Shilingi
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 20/126
14
126,407,697,224.00 sawa na asilimia 77.8 yabajeti iliyopitishwa na Bunge. Kati ya fedha hizoShilingi 117,783,609,614.00 ni kwa ajili ya
Matumizi Mengineyo na Shilingi8,624,087,610.00 ni kwa ajili ya mishahara yaWatumishi. Hadi hivi sasa, Wizara badohaijapokea mgao wowote wa fedha za bajeti yamaendeleo.
23. Mheshimiwa Spika, katika kipindi chamwaka wa fedha 2015/2016, Wizaraimetekeleza majukumu yake kama ifuatavyo:-
Kubuni na Kusimamia Utekelezaji wa Sera yaMambo ya Nje
24. Mheshimiwa Spika, Wizara kwakushirikiana na Balozi zake, Taasisi nyingine zaSerikali na sekta binafsi imeendelea kubuni nakusimamia utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
yenye lengo la kukuza uchumi wa nchi kupitiadiplomasia ya uchumi iliyo endelevu. Aidha,
jukumu hili limepewa uzito zaidi naMheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzaniawakati alipozindua Bunge la 11 la Jamhuri yaMuungano wa Tanzania ambapo aliziagiza Balozizetu kushiriki Mikutano inayofanyika nje kwaniaba ya Wizara, Idara na Taasisi nyingine za
Serikali. Jukumu hili kubwa limetekelezwa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 21/126
15
ipasavyo na Balozi zetu na hivyo kupunguzagharama kubwa za safari ambazo zingefanywana Watumishi wa Wizara, Idara na Taasisi za
Serikali.
25. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu nakufanikisha ziara za Viongozi Wakuu wa Kitaifahapa nchini kutoka nchi za Vietnam naMsumbiji. Wizara pia iliratibu ziara za viongozimbalimbali kutoka nchi za Saudi Arabia, Oman,
Qatar, Ujerumani, Norway, Umoja wa Falme zaKiarabu, Sweden, Finland, Ireland, Czech, Italia,na Urusi. Pamoja na mambo mengine ziara hizozililenga kuimarisha, mahusiano ya biashara nauwekezaji kati ya nchi yetu na nchi hizo. Aidha,baadhi ya nchi hizo tayari zina mikataba yaUshirikiano na Tanzania na nyingine
zimeanzisha ushirikiano kwa mara ya kwanza.
26. Mheshimiwa Spika, Wizara kwakushirikiana na wadau mbalimbali ilifanikishakufanyika makongamano na maonesho yabiashara na uwekezaji yaliyolenga kutangazafursa za biashara na uwekezaji zilizopo hapa
nchini. Makongamano hayo yalijumuishawafanyabiashara na wawekezaji wa Tanzania nanchi za Oman, Urusi, Rwanda, Ujerumani,China, India, Czech, Comoro, Misri naSingapore.
27. Mheshimiwa Spika, kutokana na
makongamano hayo, Tanzania iliweza
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 22/126
16
kutangaza fursa zake mbalimbali katikabiashara na uwekezaji na kufanikisha
yafuatayo:-
(a) Kusainiwa kwa mkataba wa makubaliano ya ushirikiano baina ya Chama chaWafanyabiashara, wenye Viwanda naWakulima Tanzania na Chama chaWafanyabiashara wa Oman wa kuanzishaKampuni ya Uwekezaji kati ya Tanzaniana Oman. Kampuni hiyo imeanzishwakwa lengo la kutafuta fursa za uwekezaji
Tanzania na Oman na imeazimia kuanzana mtaji wa Dola za Marekani milioni 25ambazo zitatumika kutoa mikopo kwawawekezaji. Mkataba huo ulisainiwamwezi Aprili 2016, Dar es Salaam wakatiwa Kongamano la Biashara na Uwekezajibaina ya Tanzania na Oman;
(b)Serikali ya Oman pia imeanzamazungumzo na kiwanda cha sukariKagera kwa nia ya kuingia makubaliano
yatakayowezesha Serikali ya Omankuwekeza katika kiwanda hicho. Hatuahii inalenga kukiwezesha kiwandakuzalisha tani laki nne za sukari ambazozitauzwa hapa nchini na hivyo kupunguzatatizo la upungufu wa sukari. Ongezekohili la uzalishaji pia litawezesha
kuzalisha hamira, spiriti na umeme.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 23/126
17
Hamira itauzwa Oman na sehemunyingine wakati umeme utaingizwa katikagridi ya taifa; na
(c) Kuanzishwa kwa Kiwanda chautengenezaji wa pikipiki katika eneo laUkanda Maalum wa Kiuchumi waBagamoyo kupitia Kampuni yaGuanghzhou Fekon Motorcycle Co. Ltd.
ya China. Aidha, Kampuni hiyo imeahidi
kufungua Chuo maalum kwa ajili yamafunzo ya ufundi wa pikipiki namakenika. Vilevile, mwekezaji huyoameahidi kutoa nafasi kwa ajili ya vijanawa Tanzania kwenda China kupata ujuziwa masuala hayo katika kiwanda mamakilichopo China. Makubaliano hayo
yalifanyika wakati wa kongamano labiashara na uwekezaji baina ya Afrika naChina lililofanyika mwezi Agosti 2015mjini Guangzhou China.
28. Mheshimiwa Spika, Wizara kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali katikautekelezaji wa Sera ya Mambo ya Njeimefanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbalikatika sekta za miundombinu, nishati, viwanda,kilimo na mifugo. Baadhi ya miradiiliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwakatika mwaka wa fedha 2015/2016 ni pamoja
na:-
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 24/126
18
(a) Mradi wa barabara ya Ndundu-Somanga yenye urefu wa kilomita 60 uliozinduliwamwezi Agosti, 2015. Barabara hiyo
imejengwa kwa ufadhili wa Mfuko waMaendeleo wa Kuwait kwa kushirikianana Mfuko wa Umoja wa Nchizinazozalisha Mafuta Duniani na Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
(b) Mradi wa ujenzi wa Barabara ya Kidahwe-
Uvinza yenye urefu wa kilomita 76.6uliozinduliwa mwezi Septemba, 2015.Barabara hiyo imejegwa kwa ushirikianowa Serikali ya Umoja wa Falme zaKiarabu kupitia Mfuko wa Maendeleo waAbu Dhabi kwa gharama ya Dola zaMarekani milioni 57 pamoja na mchango
wa fedha za ndani;
(c) Mradi wa Daraja la Kikwete kwenye mtoMalagarasi mkoani Kigoma lililozinduliwamwezi Septemba, 2015. Daraja hilolimejengwa kwa ushirikiano wa Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Serikali ya Jamhuri ya Korea kupitiaMfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo yaUchumi wa Jamhuri ya Korea;
(d)Mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ukamandana Unadhimu cha Tengeru, Arushakilichozinduliwa mwezi Agosti 2015
ambao ulitekelezwa kwa ushirikiano na
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 25/126
19
Serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu;na
(e) Mradi wa ujenzi wa bandari mpya yaBagamoyo na Eneo Huru la Kiuchumiuliozinduliwa Oktoba 2015. Mradi huoutatekelezwa kwa ushirikiano baina yaSerikali ya Tanzania, China na Oman.
29. Mheshimiwa Spika, katika hatua
nyingine Wizara imeendelea kuzungumza nakuwashawishi wadau mbalimbali wa maendeleoili kusaidia jitihada za Serikali katikakukabiliana na changamoto ya ujangili hapanchini, hususan upatikanaji wa vifaa kwa ajili
ya kufanyia doria kwenye Mbuga na Hifadhi za Taifa. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu
kwamba katika kipindi hiki, Serikali yaUjerumani imeipatia Tanzania ndege mbilindogo kwa ajili ya kupambana na ujangili.
Tunaamini kuwa ndege hizo zitaongeza ari naufanisi kwa askari wetu katika utekelezaji wamajukumu yao ya kuendesha doria katikaHifadhi za Taifa na Mapori ya Akiba yaliyopo
nchini. Vilevile, nchi nyingi za Ulaya, Marekanina Mashirika ya Kimataifa kama vile WorldWildlife Fund , Frankfurt Zoological Society zimeonyesha utayari wa kuisaidia Tanzania kwahali na mali katika kulinda hifadhi zawanyamapori.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 26/126
20
30. Mheshimiwa Spika, Kadhalika, Wizara
kwa kushirikiana na wadau wengine,imefanikisha majadiliano na Serikali ya
Ufaransa kwa ajili ya kusaidia mpango wamaboresho ya jengo la abiria (Terminal II) katikaUwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JuliusNyerere. Serikali ya Ufaransa kupitia Shirikalake la Maendeleo imekubali kuipatia Serikali ya
Tanzania kiasi cha Euro Milioni 65 kwa ajili yaukarabati na uboreshaji wa uwanja huo.
31. Mheshimiwa Spika, Wizara kwakushirikiana na Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi imeendelea kutafuta fursa za masomonje ya nchi ili kuliwezesha Taifa kuwa na hazinakubwa ya wataalam katika sekta mbalimbali.Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwanchi rafiki za Algeria, Malaysia, Indonesia,Pakistan, Iran, Malta, Misri, Sri Lanka, BruneiDarussalam, Canada, Ujerumani, Uingereza,Marekani, Uholanzi, Ubelgiji, Oman, Urusi,Australia, Japan, China, Cuba, Ufaransa,
Thailand, Uswisi na Korea pia zimeendelea
kushirikiana nasi katika kuwajengea uwezoWatanzania kupitia ufadhili wa mafunzo yamuda mrefu na mfupi katika fani mbalimbali.
32. Mheshimiwa Spika , Wizara imeratibuna kufanikisha upatikanaji wa mkopo wamasharti nafuu wa Dola za Marekani milioni 20
kutoka Serikali ya Italia, kupitia Shirika la
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 27/126
21
Maendeleo la nchi hiyo. Mkopo huo utatumikakutekeleza mradi wa Technical and LabourMarket Support Programme unaolenga
kuimarisha na kukuza elimu ya Ufundi kwakuvijengea uwezo vyuo vya ufundi ili kutoamafunzo yanayokidhi mahitaji ya soko la ajira.Vyuo vitakavyonufaika na mradi huo ni pamojana Chuo cha Ufundi Dar es Salaam, Chuo chaUfundi Arusha na Chuo Kikuu cha Sayansi na
Teknolojia Mbeya.
33. Mheshimiwa Spika , Wizara inaendeleana juhudi za kuwatafutia fursa za ajira nakuwaandalia mazingira mazuri watanzaniawanaokwenda kufanya kazi nje ya nchi.Kufuatia Mkataba wa ajira baina ya Tanzania naQatar, Watanzania wapatao 250 wamekwendaQatar kufanya kazi kuanzia mwezi Desemba,2015. Timu za pande zote mbili zinaendelea nauratibu wa kuwapata Watanzania watakaowezakunufaika na fursa hiyo. Aidha, Wizara piainaendelea kuwasaidia Watanzania kupata kazikatika makampuni mbalimbali nje ya nchi
mathalani katika Mashirika ya Ndege yanayofanya safari zake hapa nchini. Katikamwaka wa fedha 2015/2016, Watanzania 18walipata kazi katika Shirika la Ndege laEmirates na jitihada kama hizo zinaendeleakufanyika kwa mashirika mengine. Nichukuefursa hii kutoa wito kwa vijana wa Tanzania
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 28/126
22
kujitokeza na kuomba kazi katika Mashirika yaKimataifa.
34. Mheshimiwa Spika,
Wizara iliratibu na
kufanikisha makubaliano kati ya Tanzania na
Poland yaliyofanyika mwezi Oktoba 2015,
ambapo Poland ilikubali kutoa mkopo wa
masharti nafuu wa kiasi cha Dola za Marekani
milioni 110. Makubaliano hayo yatawekwa saini
baina ya Shirika la Maendeleo la Taifa kwaupande wa Tanzania na kampuni ya URSUS ya
Poland. Kati ya fedha hizo, kiasi cha Dola za
Marekani milioni 55 zitatumika kwa ajili ya
uanzishaji kiwanda cha kuunganisha matrekta
hapa nchini yanayotengenezwa na kampuni
hiyo. Chini ya makubaliano hayo kampuni hiyoitafundisha vijana wetu kuunganisha na
kutengeneza matrekta. Aidha, kiasi cha Dola za
Marekani Milioni 55 kitatumika kwa ajili ya
ujenzi wa maghala ya kuhifadhia mazao.
Nafurahi kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa
utekelezaji wa miradi hii miwili utaanza hivi
karibuni.
35. Mheshimiwa Spika , katika suala zima
la utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
inayoweka msisitizo katika Diplomasia ya
Uchumi, Tanzania itaendelea kujenga
mahusiano ya karibu na mashirika mbalimbali
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 29/126
23
ya kimataifa kama vile Benki ya Dunia;
mashirika yasiyo ya kiserikali yenye nguvu za
kiuchumi na kisiasa; na makampuni ya
kimataifa ya mafuta, nishati, mawasiliano na
miundombinu ili kupata mitaji na teknolojia
inayohitajika nchini kwetu.
Kusimamia Mikataba na Makubaliano yaKimataifa
36. Mheshimiwa Spika , katika kipindi cha
mwaka wa fedha 2015/2016 Wizara iliratibu na
kusimamia uwekwaji saini wa mikataba
ifuatayo:-
(a)Hati za Makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Serikali za Sri – Lanka, Serbia, Ghana,
Malta, Qatar, Kuwait na Morocco
kuhusu masuala ya Usafiri wa Anga
yaliyotiwa saini mwezi Oktoba, 2015;
(b) Hati ya Makubaliano kati ya Wizara na Taasisi ya Maendeleo ya Miundombinu
kuhusu kuendeleza viwanja na nyumba
zinazomilikiwa na Serikali nje ya nchi,
uliowekwa saini tarehe 08 Desemba,
2015 – Dar es Salaam;
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 30/126
24
(c) Mkataba wa Uenyeji kati ya Tanzania na
Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kuhusu
Makao Makuu ya Kamisheni ya Kiswahili
ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki
yaliyoko Zanzibar. Mkataba huo
uliwekwa saini tarehe 28 Desemba,
2015; na
(d) Mkataba wa Ushirikiano kati ya
Tanzania na Ufalme wa Saudi Arabiakatika nyanja za uchumi, biashara,
uwekezaji, michezo na vijana uliosainiwa
tarehe 24 Machi, 2016.
37. Mheshimiwa Spika , Wizara inaendelea
kufuatilia utekelezaji wa mikataba hiyo ilikusimamia maslahi ya nchi.
Kuratibu Masuala ya Uhusiano baina yaTanzania na nchi mbalimbali, Ushirikiano waKimataifa, Bara la Afrika na Kikanda
Ushirikiano wa Kimataifa
Ajenda ya Maendeleo Endelevu ya Mwaka2030
38. Mheshimiwa Spika, mwaka 2015
utakumbukwa sana na Jumuiya ya Kimataifa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 31/126
25
kutokana na makubaliano na maamuzi muhimu
ya kimataifa yaliyofikiwa. Miongoni mwa
makubaliano hayo ni kupitishwa kwa Ajenda
Mpya ya Maendeleo kwenye Mkutano Maalum
wa Umoja wa Mataifa wa Wakuu wa Nchi na
Serikali uliofanyika New York, Marekani mwezi
Septemba, 2015. Katika Mkutano huo, viongozi
hao walikubaliana kuwa na dira mpya ya
maendeleo ya dunia ijulikanayo kama Ajenda ya
Maendeleo Endelevu ya mwaka 2030 yenye jumla ya Malengo 17 na shabaha 169. Ajenda
hii mpya ya maendeleo endelevu inarithi
Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya miaka 15
yaliyomalizika mwaka 2015.
39. Mheshimiwa Spika, malengo hayo yamejikita katika kutokomeza umaskini;
kuhifadhi mazingira; kupambana na mabadiliko
ya tabianchi; na kushirikisha makundi yote
kwenye jamii katika masuala ya maendeleo.
Ninajivunia kuwa Tanzania ilitoa mchango
mkubwa sana katika ngazi mbalimbali kipindichote cha majadiliano yaliyopelekea kupatikana
kwa malengo hayo na hivyo kuhakikisha kuwa
vipaumbele vya nchi vinakuwepo kwenye Ajenda
hiyo mpya ya Maendeleo. Tanzania ilikuwa ni
miongoni mwa nchi 30 zilizounda Kikundi Kazi
kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 32/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 33/126
27
Katika Mkutano huo, Mheshimiwa Majaliwaalipata nafasi ya kufafanua hatua mbalimbali zakisiasa, kisheria na utawala ambazo Serikali ya
Tanzania inachukua katika kupambana natatizo hilo sugu la rushwa na pia kuonyeshaushirikiano wa kitaifa katika kuimarisha juhudihizo.
Usimamizi wa Amani Duniani
42. Mheshimiwa Spika, miongoni mwamasuala yanayoiletea heshima kubwa nchi yetuni suala la ulinzi na utetezi wa amani nausalama kwenye ukanda wetu na sehemumbalimbali duniani. Hadi sasa Tanzaniaimepeleka askari, wanawake kwa wanaume zaidi
ya 2,328 kwenye misheni saba tofauti zakulinda amani za Umoja wa Mataifa na badotunaendelea kufanya hivyo. Tunayafanya yotehaya kwa kuwa tunaamini amani ndiyo msingiwa maendeleo na ustawi wa binadamu. Pia,tunatimiza wajibu wetu kama sehemu ya
Jumuiya ya Kimataifa katika kuhakikisha kuwa
dunia inakuwa sehemu nzuri na salama yakuishi.
43. Mheshimiwa Spika , Taifa linajivuniasana Askari wetu wanaofanya kazi hizo zakulinda amani kwani pamoja na kushambuliwamara kadhaa, wamekuwa wakiifanya kazi hiyo
kwa umahiri, kujitoa, bidii na weledi mkubwa.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 34/126
28
Ndiyo maana haishangazi kuona Watanzaniambalimbali wakiwa wanateuliwa kushikanyadhifa za juu kwenye misheni hizo za kulinda
amani. Ninatoa pongezi za pekee kwa askariwetu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Polisina raia walioshiriki kwa vipindi mbalimbalikatika vikosi vya kulinda amani vya Umoja waMataifa na Umoja wa Afrika.
44. Mheshimiwa Spika , pamoja na kazi
nzuri inayofanywa na askari hawa wazalendo,hivi karibuni tumepokea tuhuma kwambabaadhi ya askari wetu wamehusika kudhalilishakijinsia wanawake huko Jamhuri yaKidemokrasia ya Kongo. Tanzania ilizichukuliatuhuma hizi kwa uzito mkubwa sana na iliundatimu ya uchunguzi kutoka Jeshi la Wananchi
wa Tanzania ndani ya siku tano badala ya sikukumi zinazotakiwa na Umoja wa Mataifa baada
ya Nchi husika kupokea taarifa za tuhuma. Tuhuma hizi zimeisikitisha sana Serikali naendapo zitathibitika hatua kali za kinidhamudhidi ya wale wote waliohusika zitachukuliwa. Ilikuhakikisha kuwa vitendo kama hivyo
vinaepukwa siku zijazo, Tanzania itajiunga nakusimamia kikamilifu “Kigali Principles” ambazoni mwongozo wa jumla kwa nchi zinazopelekaaskari wa kulinda amani kwenye vikosi vyaUmoja wa Mataifa.
45. Mheshimiwa Spika, maendeleo ya
kisayansi na teknolojia yamesababisha
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 35/126
29
kuongezeka kwa hali ya uhatarishi kutokana nambinu za kiuhalifu zinazotumiwa na wahalifuwenye mitandao ya kimataifa. Mathalan,
tumeshuhudia ongezeko la tishio la ugaidiAfrika Mashariki, biashara haramu ya dawa zakulevya, uvuvi haramu katika Bahari ya Hindina mzunguko wa silaha ndogondogo. Wizara
yangu kupitia Jumuiya za Kikanda na Kimataifana ushirikiano tulionao na nchi zilizondelea,tunaratibu jitihada za kitaifa za kukabiliana na
uhalifu wa kimataifa. Kwa mfano, kupitiaMkutano wa Baraza la Mawaziri wa NchiWanachama wa SADC uliofanyika Gaborone,Botswana mwezi Agosti, 2015 Nchi Wanachamazilikubaliana kuandaa Mkakati wa SADC wakukabiliana na Ugaidi, Mkakati wa SADC wakukabiliana na ujangili na Mkakati wa SADC wakukabiliana na uzagaaji wa silaha ndogondogo.
46. Mheshimiwa Spika , katika kuendeleza
jitihada za kupambana na uharamia baharini,
Wizara iliratibu ushiriki wa Serikali katika
Mkutano wa Tatu wa Majadiliano ya Bahari ya
Hindi uliofanyika mwezi Machi, 2016 nchini
Indonesia. Pamoja na mambo mengine, Mkutano
huo ulijadili changamoto zinazoukabili Ukanda
huo ikiwemo vitendo vya uharamia, uhalifu wa
kutumia silaha, usafirishaji haramu na ugaidi
wa majini ambavyo vinaathiri maendeleo ya
uchumi. Kutokana na kuwepo kwa changamoto
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 36/126
30
hizo, Mkutano ulifikia Makubaliano
yajulikanayo kama Padang Consensus
yanayozitaka Nchi Wanachama kuandaa
mikakati mbalimbali kwa kutumia sheria za
kimataifa zilizopo katika kupambana na vitendo
hivyo haramu. Tanzania imejipanga kutekeleza
makubaliano hayo kupitia Kamati ya Kitaifa ya
Usalama Majini iliyo chini ya Uenyekiti wa
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na
Nchi Kavu.
47. Mheshimiwa Spika, Tanzania ni mhanga
wa biashara haramu ya silaha ndogondogo
kutokana na kuzungukwa na nchi zenye
machafuko hasa kwenye Ukanda wa Maziwa
Makuu. Kutokana na kuwepo kwa hali hiyo,Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
imekuwa ikichukua hatua madhubuti za
kukabiliana na changamoto hiyo ikiwemo
kutunga sheria na kanuni za kudhibiti biashara
hiyo haramu; kuweka alama silaha
zinapoingizwa nchini na kuzisajili; na kuchoma
silaha haramu. Jitihada hizi pia zinafanyika
kimataifa ikiwemo kusaini mikataba mbalimbali
kama vile Mkataba wa Kimataifa wa Kudhibiti
Biashara ya Silaha. Aidha, jitihada hizi zinapewa
nguvu zaidi na lengo la 16 la Agenda 2030 ya
Maendeleo Endelevu ambalo linazitaka nchi
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 37/126
31
kupunguza ufadhili na usambazaji haramu wa
silaha ndogondogo ifikapo mwaka 2030.
Mkataba wa Mabadiliko ya Tabianchi wa Paris
48. Mheshimiwa Spika, katika miaka yahivi karibuni tumekuwa mashuhuda wa athariza mabadiliko ya Tabianchi yanayosababishakuwepo kwa ongezeko la ukame; mvua nyingizinazoleta mafuriko; kuzama kwa baadhi ya
visiwa; vimbunga na tufani kubwa; kupotea kwabaadhi ya mimea na wanyama na kuongezekakwa kina cha bahari. Hali hii sio tu inapotezamaisha ya binadamu wengi na mali zao, bali piainaturudisha nyuma kwenye jitihada zetu zamaendeleo na kutokomeza umaskini. Ni kwamsingi huo, Tanzania kama ilivyo nchi nyingi
zinazoendelea imeunga mkono kupatikana kwaMkataba mpya unaolenga kudhibiti mabadiliko
ya tabianchi. Mkataba huo ulikubaliwa wakatiwa Mkutano wa 21 wa Nchi Wanachama waMkataba wa Mabadiliko ya Tabianchiuliofanyika Paris, Ufaransa mwishoni mwamwaka 2015. Mkataba huo tofauti na mingine
iliyopita una mamlaka ya kisheria kuzibana nchizilizoendelea na zenye viwanda vingi kupunguzagesijoto.
49. Mheshimiwa Spika, Mkataba huouliokubaliwa na nchi zote, ulitiwa saini tarehe22 Aprili, 2016 kwenye Makao Makuu ya Umoja
wa Mataifa, New York na nchi 175 zikiwemo zile
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 38/126
32
kubwa ambazo zilikuwa zikipinga Mikatabailiyopita. Tanzania ilikuwa ni miongoni mwanchi zilizotia saini Mkataba huo. Naomba
nichukue fursa hii kuzisihi nchi zote hasa zilezilizoendelea na zinazotoa gesijoto kwa wingikuheshimu makubaliano hayo ili kupunguzaathari za mabadiliko ya tabianchi na kuitunzadunia yetu kwa manufaaa ya vizazi vya sasa navijavyo. Aidha, ninawaasa Watanzania wotekulinda misitu yetu, uoto asilia na wanyamapori
wetu kwa manufaa ya Taifa letu.
50. Mheshimiwa Spika, sitawezakuhitimisha hoja hii ya Mkataba wa Paris bilakumpongeza binti wa Kitanzania, GetrudeClement, mwenye umri wa miaka 16 ambayealipata nafasi ya kulihutubia Baraza Kuu laUmoja wa Mataifa kwa niaba ya vijana dunianiwakati wa hafla ya utiaji saini Mkataba huo.Ninaona fahari kuwa nafasi hiyo alipewa mtotowa Kitanzania miongoni mwa vijana wengiduniani kutokana na uwezo mkubwa alionao.Binti huyo ameliletea heshima Taifa na napenda
kutumia nafasi hii kuwasihi watoto na vijanawengine hapa nchini kuweka jitihada kwenyemasomo na shughuli zao wanazozifanya ili sikumoja nao wapate nafasi kama hizi nakupeperusha vizuri bendera ya Taifa. Mtotohuyu awe mfano kwa kizazi kipya chaWatanzania ambao watakuwa makini katika
kulinda urithi wa mazingira yetu.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 39/126
33
Uteuzi wa Watanzania kwenye Mashirika naTaasisi za Kimataifa
51. Mheshimiwa Spika, kutokana namahusiano mazuri tuliyonayo na nchi nyingine,Watanzania wameendelea kupewa nafasimuhimu kwenye mashirika na taasisi zakimataifa. Suala linalozidi kuipa sifa nchi yetuna kuthibitisha imani iliyowekwa na Jumuiya yaKimataifa kwa nchi hii na watu wake.
52. Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifuBunge lako Tukufu kuwa mwezi Februari 2016,Mhe. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Raiswa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliteuliwa na Bw. Ban Ki-moon, Katibu Mkuuwa Umoja wa Mataifa kuwa mmoja wa wajumbewa Jopo la Ngazi za juu la kumshauri KatibuMkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala yaUwezeshaji wa Wanawake Kiuchumi. Aidha,mwezi Januari 2016, Mheshimiwa JakayaMrisho Kikwete, Rais wa Awamu ya Nne wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliteuliwakuwa Mwakilishi wa Umoja wa Afrika kwenyeutatuzi wa mgogoro wa Libya. Uteuzi wa Mhe.Kikwete unalenga kusaidia juhudi za Umoja waAfrika katika kurejesha amani na utulivu nchiniLibya kwa kutumia uzoefu wake. Pia katikamwezi huo wa Januari, Mhe. Kikwete,alichaguliwa kuwa Mwenyekiti mwenza wa Jopo
la Watu Mashuhuri la Umoja wa Mataifa lenye
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 40/126
34
jukumu la kutoa mwongozo wa agenda ya kinamama na watoto wakati huu wa mpito kutokaMalengo ya Milenia kwenda Malengo ya
Maendeleo Endelevu.
53.Mheshimiwa Spika, uteuzi haukuishia tukwa viongozi hawa wa Kitaifa, Watanzaniawengine pia wameendelea kuchaguliwa nakuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali kubwakwenye Mashirika na Taasisi za Kimataifa. Hawa
ni pamoja na Dkt. Agnes Kijazi, MkurugenziMkuu, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzaniaalichaguliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Shirikala Hali ya Hewa Duniani; Bw. Gabriel Rugalemaambaye ameteuliwa kuwa Mwakilishi Mkazi waShirika la Chakula na Kilimo Duniani nchiniSierra Leone; Profesa Kennedy Gastorn ambayeni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaamKitivo cha Sheria, alichaguliwa kuwa KatibuMkuu wa Jumuiya ya Mashauriano ya Masuala
ya Kisheria katika nchi za Asia na Afrika nafasiambayo ataanza kuitumikia mwezi Agosti 2016;na Balozi Wilfred Ngirwa alichaguliwa kuendelea
na nafasi yake ya Mwenyekiti Huru wa Baraza laShirika la Chakula na Kilimo Duniani. Pia, Bw.Donatius Kamamba, alichaguliwa kuwa Mjumbekwenye Kamati ya Urithi wa Dunia ya Shirika laUmoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,Sayansi na Utamaduni na Dk. Frannie Leautieralichaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa Benki
ya Maendeleo ya Afrika.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 41/126
35
Kuratibu Masuala ya Ushirikiano BaraniAfrika
Umoja wa Afrika
54. Mheshimiwa Spika, Wizara kwakushirikiana na Ubalozi wetu wa Addis Ababa,Ethiopia, imeendelea kuratibu ushiriki wa
Tanzania katika shughuli mbalimbali za Umojawa Afrika. Mwezi Januari 2016, Tanzania
ilishiriki kwenye Mkutano wa 26 wa Wakuu waNchi na Serikali wa Umoja wa Afrika uliofanyikaAddis Ababa, Ethiopia. Mheshimiwa SamiaSuluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania aliongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo. Kaulimbiu yamkutano huo ilikuwa ni “Mwaka wa Haki za
Binadamu Afrika, hususan Haki za Wanawake”. Wakati wa uzinduzi wa kaulimbiu hiyo, NchiWanachama zilihimizwa kuridhia na kutekelezaItifaki na sera mbalimbali zilizoundwa na Umojahuo kwa lengo la kulinda, kukuza na kutekelezahaki za wanawake Afrika. Itifaki hizo ni pamojana Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na
Watu na Sera ya Umoja wa Afrika kuhusuMasuala ya Jinsia. Mkutano huo pamoja namasuala mengine pia ulijadili ripoti ya Baraza laAmani na Usalama la Umoja wa Afrika kuhusuhali ya amani na usalama Barani Afrika.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 42/126
36
55. Mheshimiwa Spika, mwezi Novemba,2015 Tanzania iliteuliwa na Umoja wa Afrikakusimamia uzinduzi wa Jeshi la Pamoja la
Afrika la Kulinda Amani Barani Afrika. Mimimwenyewe nilisimamia uzinduzi huo. Tanzaniavilevile iliendelea kutoa mchango wake katikakutafuta suluhu ya migogoro barani Afrika.
Tanzania ikiwa Mwenyekiti wa Jumuiya yaAfrika Mashariki, ilieleza hatua mbalimbalizilizochukuliwa na Jumuiya ya Afrika Masharikikatika kutatua mgogoro wa Burundi. Mchangowa Tanzania katika Umoja wa Afrika kuhusumgogoro wa Burundi kwa kiasi kikubwa uliwezakusaidia Umoja huo kuwa na taswira mpya yanamna ya kutafuta suluhu ya kudumu ikiwemokutoa kipaumbele katika mazungumzo
yanayohusisha pande zinazohasimiana nchiniBurundi chini ya usimamizi wa Jumuiya yaAfrika Mashariki badala ya uamuzi wa awali wakupeleka majeshi ya Umoja huo nchini Burundi.
56. Mheshimiwa Spika , napendakulifahamisha Bunge lako Tukufu kwamba
Tanzania ilichaguliwa kuwa mjumbe wa Barazala Amani na Usalama la Umoja wa Afrika kwavipindi viwili mfululizo kuanzia mwaka 2012hadi mwezi Januari, 2016. Hii inatokana namchango wake mkubwa katika kusuluhishamigogoro barani Afrika. Katika uchaguzi wawajumbe wapya wa Baraza hilo uliofanyika
mwezi Januari 2016, Kenya, Rwanda na Uganda
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 43/126
37
zilichaguliwa kuwakilisha ukanda wa AfrikaMashariki.
Mkutano wa Tatu wa Ushirikiano kati yaAfrika na India
57. Mheshimiwa Spika, Wizara pia iliratibuushiriki wa Tanzania kwenye Mkutano wa Tatuwa Ushirikiano kati ya Afrika na India,uliofanyika New Delhi, India mwezi Oktoba,
2015. Katika Mkutano huo, pamoja na masualamengine, India iliahidi kuisaidia Afrika katikakuendeleza miundombinu; umwagiliaji;kuongeza thamani ya rasilimali; kuanzishaviwanda; na teknolojia ya habari namawasiliano. Aidha, Serikali ya India iliahidikutoa mkopo wenye masharti nafuu wa Dola za
Marekani bilioni 10, ruzuku ya misaada ya Dolaza Marekani milioni 600 na kuchangia Dola zaMarekani milioni 100 kwa ajili ya Mfuko waMaendeleo. Vilevile, India iliahidi kutoa nafasi50,000 za ufadhili wa masomo kwa wanafunziwa Afrika nchini India kwa miaka mitano ijayo.Ili kunufaika na fursa hizi, nchi za Afrika
zinatakiwa kuwasilisha andiko la miradimbalimbali ya vipaumbele kwa Serikali ya India.
58. Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifu
Bunge lako Tukufu kwamba kufuatia mkutano
huo, tayari Serikali imeandaa na kuwasilisha
miradi ya kipaumbele ikiwemo miradi 17 ya maji
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 44/126
38
pamoja na Mradi wa Serikali Mtandao. Aidha,
miradi mingine itakayowasilishwa ni pamoja na
mradi wa ujenzi wa atamizi kwa ajili ya viwanda
vidogo na vya kati katika kila mkoa; mradi wa
ujenzi wa reli itakayotumika kusafirisha abiria
katika Jiji la Dar es Salaam; na mradi wa kilimo
cha umwagiliaji – Zanzibar.
Mkutano wa Sita wa Wakuu wa Nchi na
Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati yaChina na Afrika
59. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu na
kushiriki Mkutano wa Sita wa Wakuu wa Nchi
na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya
China na Afrika uliofanyika mwezi Desemba
2015, Jijini Johannesburg, Afrika Kusini. Katika
mkutano huo Serikali ya China ilitangaza
mpango mpya wa miaka mitatu kuanzia 2016
hadi 2018 wa ushirikiano kati ya China na
Afrika ambao umeweka kipaumbele katika
kuendeleza sekta ya viwanda barani Afrika. Tanzania ni miongoni mwa nchi nne za mfano
zilizochaguliwa na China kwa ajili ya kujenga
viwanda vya mfano. Nchi nyingine zilizomo
kwenye mpango huo ni Afrika Kusini, Ethiopia
na Kenya.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 45/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 46/126
40
Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa MaziwaMakuu
Mikutano ya Jumuiya ya Nchi za Ukanda waMaziwa Makuu.
62. Mheshimiwa Spika, katika kipindi hikiWizara iliratibu na kushiriki katika Mkutano waMawaziri wa Sheria wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu
uliofanyika Livingstone, Zambia mwezi Agosti,2015. Mkutano huo ulipokea taarifa kutokaNchi Wanachama kuhusu hatua zilizofikiwakatika kuridhia na kutekeleza Itifaki za Jumuiya
ya nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu hususanItifaki nne zinazopewa kipaumbele katikautekelezaji wake kwa sasa. Itifaki hizo ni; Itifaki
ya Ushirikiano wa Kiulinzi; Itifaki ya Ushirikianowa Kimahakama; Itifaki ya Kuzuia UvunajiHaramu wa Maliasili na Itifaki ya KuzuiaUnyanyasaji wa Kijinsia dhidi ya Wanawake naWatoto. Mkutano huo ulibaini itifaki hizohazijatekelezwa kikamilifu na nchi zotewananchama. Hivyo, nchi wanachama
zilikubaliana kutekeleza itifaki hizo kikamilifu.
63. Mheshimiwa Spika, katika kutekelezaItifaki hizo Serikali imechukua hatuambalimbali zikiwemo kutunga Sheria yakudhibiti uhalifu wa njia ya mawasiliano; Sheria
ya kurudishiana wahalifu waliokimbilia nchinyingine; kuanzisha vitengo maalum katika
Kuratibu Masuala ya Ushirikiano wa Kikanda
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 47/126
41
viwanja vya ndege vya Kimataifa nchini ilikudhibiti usafirishaji holela wa Maliasili;kuanzisha Mpango wa Mataifa wa kuwalinda
wanawake na watoto dhidi ya unyanyasaji wakujinsia na kuanzisha kitengo maalum katikavituo vya polisi Wilaya zote nchinikushughulikia kesi za uonevu wa kijinsia.
64. Mheshimiwa Spika, Wizara pia iliratibuushiriki wa wataalamu wa Tanzania katika
Mkutano wa Jumuiya ya Nchi za Maziwa Makuuuliofanyika Luanda, Angola mwezi Januari,2016. Miongoni mwa masuala yaliyojadiliwakatika Mkutano huo ni kutathmini hali yaulinzi na usalama katika nchi za eneo laUkanda wa Maziwa Makuu hususan katikanchi za Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasia yaKongo na Sudan Kusini. Pamoja na mambomengine Jumuiya hiyo imekuwa ikifanya kazikwa karibu na Taasisi za Kikanda katikakuratibu shughuli za kutatua migogoro. Kwamfano, mgogoro wa Burundi kwa kushirikianana Jumuiya ya Afrika Mashariki, mgogoro wa
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwakushirikiana na Jumuiya ya Maendeleo yaKusini mwa Afrika pamoja na mgogoro waSudan Kusini kwa kushirikiana na Jumuiya yaUshirikiano wa Maendeleo ya Nchi za Masharikina Pembe ya Afrika.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 48/126
42
65. Mheshimiwa Spika, Jumuiya hiyo yaNchi za Ukanda wa Maziwa Makuu ambayo
Tanzania ni mwanachama inatambua uhusiano
mkubwa uliopo kati ya uvunaji haramu warasilimali na kushamiri kwa migogoro. Hivyo,nchi wanachama zimesaini Itifaki ya Ulinzi,Usalama na Maendeleo pamoja na Itifaki yaKupinga Uvunaji Haramu wa Rasilimali ambazokwa pamoja zinazitaka nchi zote 12 wanachamakutii taratibu zinazotambulika kikanda zauvunaji rasilimali ambapo Cheti ya Kikanda chakuthibitisha uvunaji huo hutolewa. Hii kwakiasi kikubwa imesaidia kudhibiti makundi yawaasi kujipatia fedha kwa njia za uvunajiharamu wa rasilimali kwa lengo la kufadhilishughuli zao.
66. Mheshimiwa Spika, jitihada hizo zapamoja zimepelekea kutengamaa kwa hali yaulinzi na usalama katika nchi za maziwamakuu. Kwa mfano, idadi ya wakimbiziwanaoingia nchini imepungua kutoka kati yawakimbizi 200 hadi 300 kwa siku kwa mwezi
Novemba, 2015 hadi kufikia wakimbizi kati ya100 hadi 120 kwa siku kwa mwezi Mei, 2016.Hadi sasa Tanzania inahifadhi jumla yawakimbizi 136,000 kutoka Burundi na wengine2,360 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia yaKongo. Bado idadi hii ni kubwa na Serikaliinaendelea kushirikiana na wadau wengine
katika jitihada za kutatua migogoro katika
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 49/126
43
ukanda wetu wa Maziwa Makuu ili hatimayewakimbizi hao waweze kurejea nchini mwao.
Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa AfrikaMkutano wa 35 wa Wakuu wa Nchi waJumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika
67. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu nakushiriki katika Mkutano wa 35 wa Wakuu wa
Nchi na Serikali wa Jumuiya ya MaendeleoKusini mwa Afrika uliofanyika mwezi Agosti2015 Gaborone, Botswana. Mkutano huoulijadili masuala ya siasa, uchumi, uwekezaji,kijamii, ulinzi na usalama katika Kanda.
68. Mheshimiwa Spika, pamoja na Mkutano
huo kuiteua Tanzania kuwa MakamuMwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi naUsalama wa Jumuiya hiyo, Nchi Wanachamaziliazimia yafuatayo:-
i. Serikali ya Lesotho pamoja na washirikawengine wa kisiasa nchini humokuandaa mapema iwezekanavyompango wa utekelezaji wa mabadiliko
ya Katiba na Sekta ya Ulinzi;
ii. Kuhakikisha kuwa kunakuwepo naongezeko la uwakilishi wa wanawake
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 50/126
44
katika nafasi mbalimbali za maamuzi ya juu Serikalini na sekta binafsi;
iii. Kutekeleza kikamilifu Sera ya Kilimo yaKanda na Itifaki zingine ili kusaidiakuongeza kasi ya uzalishaji, biasharana ushindani katika sekta ya kilimo; na
iv. Sekretariati kufuatilia kwa karibu kwakushirikiana na Nchi Wanachamakuhakikisha UKIMWI na magonjwamengine ya kuambukiza hayaendeleikuwa tishio kwenye Sekta ya Afyakatika Kanda.
69. Mheshimiwa Spika, kutokana na nchi
yetu kujijengea sifa ya umahiri na weledi katikamasuala ya siasa, ulinzi na usalama barani
Afrika na katika Kanda, katika mkutano huo,
Tanzania iliteuliwa kuwa Makamu Mwenyekiti
wa Asasi ya SADC ya Siasa, Ulinzi na Usalama
kwa kipindi cha mwaka 2015/2016. Kutokana
na uteuzi huo, Tanzania kwa mara nyingineitakuwa Mwenyekiti wa Asasi hiyo katika kipindi
cha Agosti 2016 hadi Agosti 2017 ikiwa ni mara
ya tatu kupewa wadhifa huo. Uteuzi huu
unaonyesha imani ya wanachama wa SADC
waliyonayo kwa Tanzania katika kutatua
migogoro na kusimamia amani katika kanda
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 51/126
45
hiyo na unaendelea kuijengea nchi yetu
heshima kubwa na kuiweka juu katika medani
za Kikanda na Kimataifa.
Mkutano wa dharura wa Viongozi Wakuu waNchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwaAfrika wanaosimamia Asasi ya Siasa, Ulinzina Usalama
70. Mheshimiwa Spika , Tanzania ilishirikikwenye Mkutano wa Dharura wa ViongoziWakuu wa Nchi za Jumuiya ya MaendeleoKusini mwa Afrika wanaosimamia Asasi yaSiasa, Ulinzi na Usalama uliofanyika Gaborone,Botswana tarehe 18 Januari, 2016 kwa ajili yakujadili hali ya kisiasa nchini Lesotho. Ujumbe
wa Tanzania kwenye Mkutano huo uliongozwana Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa,Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania. Pamoja na mambo mengine, Mkutanohuo uliielekeza Serikali ya Jamhuri ya Lesothokuitoa kwa umma ripoti ya Tume Huru yaUchunguzi ya SADC na kuhakikisha kuwa
inatekeleza kwa uadilifu mapendekezo yaliyomokatika taarifa hiyo ili kuboresha hali ya siasa,ulinzi na usalama nchini humo. Vilevile,Viongozi Wakuu walisisitiza umuhimu wakusimamia kwa dhati utekelezaji wa Mikataba
yote mitatu ya amani iliyosainiwa kwa ajili yakurejesha amani nchini humo. Taarifa ya
utekelezaji wa mapendekezo yaliyomo katika
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 52/126
46
ripoti hiyo itawasilishwa kwenye Mkutano wa 36wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliopangwakufanyika mwezi Agosti, 2016 Mbabane,
Swaziland.
Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa Nchi zaJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
71. Mheshimiwa Spika , Wizara iliratibu nakushiriki katika Mkutano wa Baraza la Mawaziriwa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrikaambao ulifanyika Gaborone, Botswana mweziMachi, 2016. Pamoja na masuala mengine,Mkutano huo ulijadili hatua ya utekelezaji yaMpango wa Kikanda wa Maendeleo 2015 - 2020;hatua ya utekelezaji wa Mpango wa Kikanda waMaendeleo ya Viwanda; na Mtangamano waUtatu wa Eneo Huru la Biashara la COMESA-EAC-SADC. Mkutano huo pia ulipokea taarifa yautekelezaji wa maamuzi ya vikao vya Baraza laMawaziri ambayo ilihusisha jumla ya maeneokumi. Taarifa hiyo inaonyesha kuwa utekelezajiwa maeneo hayo unaendelea vizuri.
72. Mheshimiwa Spika , Mkutano huo pia,ulipokea maombi ya Serikali ya Visiwa vyaComoro na Serikali ya Burundi ya kutakakujiunga na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwaAfrika. Hivi sasa Sekretarieti inaendelea na zoezila kutathmini maombi ya nchi hizo kulingana na
taratibu, kanuni na sheria za Jumuiya za kuwa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 53/126
47
mwanachama. Taarifa ya tathmini hiyo itatolewakwenye Mkutano wa 36 wa Wakuu wa Nchiambao umepangwa kufanyika mwezi Agosti,
2016, Mbabane, Swaziland.
Jumuiya ya Nchi za Mwambao wa Bahari yaHindi
73. Mheshimiwa Spika, Tanzania imeendeleakuwa mwanachama wa mstari wa mbele katika
kuimarisha ushirikiano wa nchi zilizo katikamwambao wa Bahari ya Hindi kupitia Jumuiya
ya Nchi hizo.
Mkutano wa Kwanza wa Mawaziri kuhusu‘Blue Economy’
74. Mheshimiwa Spika, Wizara ilishiriki
katika Mkutano wa Kwanza wa Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi za Mwambao wa Bahari yaHindi kuhusu Blue Economy uliofanyika mweziSeptemba, 2015 nchini Mauritius. Mkutano huoulijadili maeneo manne ya kipaumbele kuhusumatumizi endelevu ya rasilimali zitokanazo nabahari. Maeneo hayo ni Fisheries andAquaculture ; Renewable Ocean Energy; Seaportand Shipping; na Seabed Exploration andMinerals . Mkutano huo pia ulidhamiria kuundamifumo madhubuti yenye Sera, Sheria naMikakati ya Matumizi Endelevu ya Rasilimali zaBahari na kusimamia Dhana ya Uchumi wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 54/126
48
Bahari ili kukuza uchumi na kuleta maendeleoendelevu kwa Nchi Wanachama.
75. Mheshimiwa Spika , katika kutekelezamaazimio ya mkutano huo, Mamlaka yaKusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu kwakushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi
Tanzania inaendelea kufanya utafiti wakutambua maeneo yenye samaki wengi hususanaina ya Jodari pamoja na majaribio ya kuwekavifaa vya kuvutia samaki katika Bahari ya Hindi.Utafiti huu unaohusisha maeneo ya Mafia,Zanzibar na Bagamoyo unalenga kuwapunguziawavuvi muda wa kutafuta samaki, kupunguzagharama za mafuta na kuwaongezea kipato.Vilevile, taarifa za utafiti huo zitatolewa kwawawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili wajekuwekeza katika uvuvi wa Bahari Kuu ya
Tanzania.
Kulinda na kuendeleza Maslahi ya Taifa yaKiuchumi na Mengineyo nje ya nchi
Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa
Mataifa
76. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu na
kushiriki kwenye Mkutano wa 70 wa Baraza
Kuu la Umoja wa Mataifa uliofanyika New York,
Marekani, mwezi Septemba, 2015 ambapo
Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 55/126
49
wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania alipata nafasi ya kulihutubia Baraza
hilo na kueleza msimamo wa nchi kwenye
masuala mbalimbali duniani, yakiwemo ya
kiuchumi na maendeleo, amani na usalama,
pamoja na mahusiano yetu na nchi nyingine.
Aidha, Mheshimiwa Kikwete alifanya
mazungumzo na nchi marafiki na washirika
wetu wa maendeleo na kukubaliana masuala
mbalimbali yenye manufaa kwa nchi ikiwemoufadhili wa miradi ya maendeleo.
Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali waJumuiya ya Madola
77. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu na
kushiriki kwenye Mkutano wa Wakuu wa Nchina Serikali wa Jumuiya ya Madola uliofanyika
Malta mwezi Novemba, 2015. Tanzania ilishiriki
kikamilifu kwenye majadiliano mbalimbali
yaliyofanyika na hivyo tamko la mwisho ya
mkutano liliakisi maslahi ya nchi hususan
kwenye masuala ya amani na usalama; haki zabinadamu na utawala bora; maendeleo
endelevu; mabadiliko ya tabianchi; biashara na
usawa wa kijinsia na kumwezesha Mwanamke.
78. Mheshimiwa Spika , kwa mara yakwanza baada ya miaka 66, Jumuiya ya Madola
ilimchagua mwanamke mwenye asili ya Afrika,
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 56/126
50
Mheshimiwa Baroness Patricia Scotland mzaliwawa Dominica na mwenye uraia pacha waDominica na Uingereza kuwa Katibu Mkuu wa
sita wa Jumuiya hiyo ambapo alianza kazitarehe 1 Aprili, 2016. Vipaumbele alivyoainishaMheshimiwa Scotland ni pamoja nakushughulikia unyanyasaji dhidi ya wanawakena watoto wa kike; athari za mabadiliko ya
Tabianchi; biashara na utawala bora; nakuanzisha majadiliano na nchi wanachamakuhusu kutokufanya suala lamahusiano/mapenzi ya jinsia moja kuwa kosala jinai. Alisisitiza kuwa nchi haziwezikulazimishwa kufuata suala hili lakiniataanzisha majadiliano na lazima pawepo namakubalino ya pande zote. Wizara itaendelea
kufuatilia kwa makini ajenda zake ilikuhakikisha masuala ambayo yanapingana nasheria, mila na desturi za nchi yetu hayawisehemu ya majadilino ya Jumuiya.
Mkutano wa 10 wa Nchi Wanachama wa
Shirika la Biashara Duniani
79. Mheshimiwa Spika, Wizara pia iliratibuna kushiriki kwenye Mkutano wa 10 waMawaziri wa Nchi Wanachama wa Shirika laBiashara Duniani uliofanyika mwezi Desemba2015, Nairobi, Kenya. Katika Mkutano huo
Tanzania ilitetea maslahi yake hasa kuhusumasuala ya biashara ya kilimo na mazao yake
ikiwemo pamba kwa kushirikiana na makundi
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 57/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 58/126
52
Wachumi, Wahadhiri na Wakufunzi katikanyanja mbalimbali na pia wafanyabishara;ambao wote hawa wametawanyika sehemu
mbalimbali duniani.
81. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu nakushiriki katika Kongamano la Pili la Diasporalililofanyika Jijini Dar es Salaam mwezi Agosti,2015. Lengo la Kongamano hilo lilikuwa nikuhamasisha Diaspora kushiriki katika kukuzasekta ya biashara ndogondogo na za kati nakuboresha mahusiano kati ya Diaspora naWajasiriamali waliopo nchini. Aidha, Wizaraimeendelea kuratibu makongamano mengine yakibiashara na uwekezaji yanayofanyika nje yanchi kama yale yanayoandaliwa na Jumuiya ya
Watanzania wanaoishi nchini Marekani.
82. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibuziara ya kitabibu ya Madaktari Watanzania kwakushirikiana na madaktari wenzao wa kiafrikawaishio nchini Marekani mwezi Julai 2015.Madaktari hao walitoa huduma za matibabu na
ushauri katika hospitali za Mwananyamala (Dares Salaam) na Mnazi Mmoja (Zanzibar) kwamagonjwa ya moyo, saratani na kinywa. Aidha,walitoa msaada wa madawa na vifaa tiba vyenyethamani ya Dola za Marekani 300,000 kwenyehospitali hizo na kukabidhi mashine ya kupimasaratani ya matiti yenye thamani ya Dola za
Marekani 200,000 katika Hospitali ya Lugalo.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 59/126
53
83. Mheshimiwa Spika, naomba kutumianafasi hii kuwapongeza na kuwashukurumadaktari hao kwa moyo wao wa dhati wa
kujitolea. Aidha, ningependa kuwahamasishaDiaspora wengine kuiga mifano hiyo. Wizara
yangu iko tayari kushirikiana nao wakati wote.
84. Mheshimiwa Spika, napenda kuliarifuBunge lako Tukufu kuwa katika kuitikia wito wakuchangia maendeleo ya nchi yetu, uwekezajiwa Diaspora katika Benki ya CRDB, Mfuko waPensheni wa PSPF na Mfuko wa Mitaji wa UTTumefikia Shilingi Bilioni 26 mwaka 2015.Aidha, uwekezaji wa Diaspora katika mifukomingine ya hifadhi za jamii, sekta za afya,viwanda na utalii umeongezeka.
85. Mheshimiwa Spika, katika kuhakikishakwamba tunaweka mazingira wezeshi kwaDiaspora, Wizara yangu imekamilisha hatua zaawali za kutengeneza Sera ya Diaspora kwaushirikiano na Mfuko wa Jumuiya ya Nchi zaAfrika, Karibiani na Pasifiki. Sera hii itatoa
mwongozo kwa wadau na kuleta uelewa wapamoja kuhusu mikakati bora ya kuwatambuaDiaspora na kuwawezesha kuchangiamaendeleo ya nchi. Rasimu ya Sera hiyoitawasilishwa kwa wadau kwa ajili ya maoni naushauri. Ni matarajio ya Serikali kuwaushirikishwaji wa Diaspora kama moja ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 60/126
54
wadau wa maendeleo utawawezesha kuchangiakatika maendeleo ya nchi yetu kwa kuletateknolojia mpya; na kuongeza uwekezaji kwenye
sekta mbalimbali kama vile viwanda, masoko yamitaji, kilimo na utalii. Ushirikishwaji huo waDiaspora utaiwezesha nchi kufikia malengo yakuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025.
86. Mheshimiwa Spika, Wizara kwakushirikiana na Benki Kuu ya Tanzania na
wadau wengine inaandaa mfumo sahihi wakutambua na kurahisisha uingiaji wa fedhakutoka kwa Diaspora ili kuwa na takwimusahihi za mchango wa Diaspora kwenyekuongeza Pato la Taifa.
Kusimamia masuala yanayohusu Kinga naHaki za Kibalozi kwa Wanadiplomasia walioponchini kulingana na Mkataba wa Vienna wamwaka 1961
87. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendeleakushirikiana na mamlaka mbalimbali nchini ili
kuhakikisha kuwa, jamii ya wanadiplomasiawaliopo nchini wanapata haki zao kamailivyoainishwa katika Mkataba wa ViennaKuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia wa mwaka1961. Wizara inasimamia kikamilifu utekelezajiwa Mkataba huo kwenye vipengele muhimu vyakinga na haki za kibalozi na wategemezi wao.
Pamoja na jamii ya kibalozi kuwa na kinga na
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 61/126
55
upendeleo maalum, Wizara inahakikisha kuwa jamii hizi zinaheshimu na kufuata sheria,kanuni na taratibu za nchi yetu.
Kusimamia na Kuratibu Masuala ya Itifaki naUwakilishi
88. Mheshimiwa Spika, mara baada yakuundwa kwa Serikali ya Awamu ya Tano,nilikutana na Mabalozi na Wakuu wa Mashirika
ya Kimataifa waliopo nchini. Kwa niaba yaMheshimiwa Rais, nilitumia fursa hiyokuwapatia taarifa ya masuala mbalimbali
yanayohusu umuhimu wa ushirikiano wa Tanzania na nchi nyingine na kutoa Dira yaSerikali ya Awamu ya Tano. Wizara yanguitaendelea kuwa na vikao vya mara kwa mara nawanadiplomasia hawa kwa lengo la kuimarishazaidi ushirikiano.
89. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibuziara za Viongozi wa Kitaifa wa Awamu ya Nnenje ya nchi ambao ni Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Rais waZanzibar na Mwenyekiti wa Baraza laMapinduzi, Waziri Mkuu wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania, Makamu wa Kwanzawa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibarna Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar. Baadhi ya ziara za
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 62/126
56
Viongozi hao zilifanywa katika nchi za Uswisi,Australia, Marekani, Misri, India, Kenya,Uganda, Botswana, Vietnam, Uingereza na
Italia. Vilevile, Wizara iliratibu ziara za Viongoziwa Kitaifa wa Awamu ya Tano nje ya nchizilizofanyika katika nchi za Afrika Kusini,Botswana, Ethiopia, Rwanda, Uganda, UingerezaZambia, Comoro na Papua New Guinea.
90. Mheshimiwa Spika, ziara hizo zimekuwana mafanikio ikiwa ni pamoja na kukuza nakuimarisha mahusiano kati ya nchi yetu na nchihizo, zimetangaza fursa za uwekezaji, biashara,utalii na kuwahamasisha Diaspora kuwekezanyumbani. Pia zinaimarisha uhusiano kati yasekta binafsi za hapa nchini na taasisi
mbalimbali za nje.
91. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendeleakuratibu na kufanikisha uwasilishaji wa hati zautambulisho za Mabalozi kutoka nchimbalimbali. Katika kipindi hiki Mabaloziwaliowasilisha hati zao za utambulisho ni
pamoja na Qutar, Argentina, India, Denmark,Uswisi, Uturuki, Finland, Sweeden, Ubelgiji,Hispania, Msumbiji, Uganda, Misri, Israeli,Ufilipino, Jamhuri ya Korea, Umoja wa Ulaya,Palestina, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,
Jamhuri ya Namibia, Brazil, Jamhuri ya Czechna Jamhuri ya Sudan Kusini.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 63/126
57
Kuanzisha na Kusimamia Huduma za
Kikonseli
92. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendeleakutoa huduma za kikonseli kwa kurahisishaupatikanaji wa viza kwa maafisa na watendajiwa Serikali, Vyama vya Siasa na Taasisinyingine zinazostahili huduma hiyo. Aidha,Wizara imeendelea kuratibu matumizi yaUkumbi wa Watu Mashuhuri wa Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, kwawatu wanaostahili wakiwemo Mabalozi naWakuu wa Mashirika ya Kimataifa, viongozi waSerikali na baadhi ya Wafanyabiashara hapanchini. Vilevile, Balozi zetu nje zimeendeleakutoa Viza kwa raia wa nje wanaoitembelea
Tanzania na kushirikiana na mamlaka nyinginekutafuta ufumbuzi wa matatizo mbalimbali
yanayowakabili Watanzania waishio nje ya nchi.
93. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kulinda maslahi ya Watanzania wanaofanya kazikwenye Balozi mbalimbali na Mashirika ya
Kimataifa hapa nchini. Katika kutekeleza jukumu hilo, Wizara yangu imebaini kuwepokwa changamoto mbalimbali ikiwemo baadhi yaWatanzania wanaofanya kazi katika Balozi namashirika hayo kutokuwa na mikataba ya ajira.Hivyo, natoa rai kwa ofisi za Kibalozi naMashirika ya Kimataifa yaliyopo hapa nchini
kutoa mikataba kwa waajiriwa wao ili kukidhi
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 64/126
58
matakwa ya kisheria. Vilevile, nawaasaWatanzania wanaofanya kazi katika Balozi naMashirika ya Kimataifa wahakikishe wana
mikataba ya ajira ili kulinda maslahi yao.
94. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kutoa huduma za kikonseli kwa Watanzaniawaliopo nje ya nchi. Naomba kutumia fursa hiikuwasihi Watanzania hao kuhakikishawanajisajili katika Balozi zetu na Konseli, napale ambapo hatuna ofisi za ubalozi wajisajilikatika ofisi za ubalozi wa Uingereza kamailivyoainishwa kwenye hati za kusafiria.
95. Mheshimiwa Spika, niruhusu nitumie
fursa hii kuliarifu Bunge lako Tukufu naWatanzania kwa ujumla kwamba miaka yakaribuni pamejitokeza wimbi la Watanzaniawanaokwenda nje ya nchi kwa ahadi zakupatiwa ajira. Kwa upande wa India, Thailand,Malaysia na China, ahadi hizo za ajira zimekuwazikitolewa na watu wasio waaminifu ambaowana mtandao wa biashara ya kusafirisha
binadamu. Mtandao huo unahusisha raia wa Tanzania waliopo ndani na nje ya nchi kwakushirikiana na raia wa kigeni waliopo kwenyenchi hizo. Watu hao wanachofanya ni pamojana kuwatafuta wasichana wenye umri kati yamiaka 18 na 24, kuwatafutia vibali vya safari nakuwalipia nauli za kuwafikisha kwenye nchi
husika kwa kuwalaghai kuwa wanakwenda
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 65/126
59
kufanya kazi katika hoteli, migahawa, madukamakubwa au kazi za nyumbani. Matokeo yake,wanapofika kwenye nchi hizo wasichana hao
wanakuta kuwa ahadi walizo ahidiwa sio zakweli na badala yake wanalazimishwa kukubalikufanya kazi za ukahaba ili kurejesha fedhawalizogharimiwa kufika huko. Kwa taarifatulizonazo, mtandao huo wa biashara yaukahaba huwataka wasichana hao kurejeshakiasi cha Dola za Marekani kati ya 5,000 hadi6,000 kiasi ambacho sio rahisi kupata kwa kazihizo ikizingatiwa kwamba mapatano na malipo
ya kazi hiyo hayafanywi na wahusika balimadalali wa mtandao huo. Madalaliwaliowapeleka vijana hao kwenye nchi hizohuwanyang’anya hati zao za kusafiiria ilikuwadhibiti wasitoroke hadi kipatikane kiasicha fedha walizogharimwa. Kwa kuwa hawanafedha na namna nyingine ya kuishi wasichanahao wamelazimika kukubali kufanya biasharahiyo.
96. Mheshimiwa Spika, baadhi ya vijana
hao, waliweza kuwatoroka madalali hao, nakukimbilia kwenye ofisi zetu za Ubalozi kutafutamsaada. Kwa bahati mbaya Mheshimiwa Spika,Balozi zetu hazina fungu la kuhudumiaWatanzania wanaopata shida ughaibuni namatokeo yake maafisa wa Ubalozi kwa moyo wakibinadamu wamekuwa wakitoa fedha zao
wenyewe kusaidia kununua tiketi za
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 66/126
60
kuwarejesha Watanzania waliofanikiwakuchomoka kwenye makucha ya makuadi waukahaba. Katika jitihada za kukabiliana na
tatizo hilo, Wizara imeanzisha mazungumzo naShirika la Kimataifa la Uhamaji ili wasaidiekuwarudisha nyumbani vijana hao.
97. Mheshimiwa Spika, ni wazi kwambavitendo hivyo ni vya kinyama na vinakiuka haki
ya binadamu. Ifahamike pia kwamba usafirishaji
wa binadamu ni uhalifu kwa mujibu wa makosa ya kupangwa ya Azimio la Umoja wa Mataifa NA.55/25 la mwaka 2003 la kuzuia, kukomesha nakuadhibu usafirishaji wa binadamu hasa kwawanawake na watoto chini ya Itifaki yake.
98. Mheshimiwa Spika,
Kutokana naushirikiano kutoka kwa Jumuiya za Watanzaniawaishio nchini Thailand na India, pamoja nabaadhi ya wahanga wa biashara hiyo haramu,Serikali imepata majina ya baadhi ya wahusikawa mtandao huo na tayari mawasiliano naSerikali za nchi hizo yamefanyika ili
kuwakamata wahusika wote na kuwafikishakatika mkondo wa sheria. Kwa hapa nyumbani,uchunguzi unaendelea kwa kushirikiana naBalozi za nchi ambazo wasichana wetuwanapelekwa ili kubaini watu wote waliosehemu ya mtandao huo hususan walewanaowezesha upatikanaji wa vibali vya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 67/126
61
kusafiria kwenye Balozi hizo ili kuwakamata nakuwachukulia hatua kali za kisheria. Piatumeziomba Balozi hizo ziwe makini zaidi
kudhibiti uombaji wa vibali vya kusafiria kwashughuli mbalimbali na kuwataka wahusikakuthibitisha uwezo wa kifedha zitakazowawezesha kutalii, kufanya shughuli ama kuishikatika nchi wanazokwenda ili kuudhibitimtandao wa biashara ya watu.
99. Mheshimiwa Spika, Vilevile, kupitiaBunge hili, ninatoa wito kwa Watanzania wote,tuwe makini pale tunapopata fursa za kazi nje
ya nchi. Kama nilivyosema hapo awali, nimuhimu kuzingatia na kujiridhisha na masuala
yote ya msingi yanayohusiana na ajira za nje,
ikiwa ni pamoja na; kuwepo na mkataba rasmiwa ajira unaotambuliwa na Mamlaka husikazilizopo nchini na za Nchi unayotaka kwenda,kujisajili kweye ofisi za Ubalozi wa Tanzaniauliopo katika nchi hizo na kutokubali kuwekahati yako ya kusafiria kama rehani.
100. Mheshimiwa Spika , nasikitika kuliarifuBunge lako Tukufu kuwa bado kunaWatanzania kadhaa wanatumikia vifungo nawengine kati yao wanakabiliwa na adhabu yakifo katika magereza ya nchi mbalimbali dunianibaada ya kukutwa na hatia ya makosa yakujihusisha na biashara haramu ya madawa ya
kulevya. Idadi yao ni kama ifuatavyo: Brazil (41),
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 68/126
62
China (266), Iran (68), India (9), Nepal (4), Oman(3), Thailand (14) na Umoja wa Falme za Kiarabu(3). Naomba kuchukua nafasi hii kuwasihi
Watanzania kujiepusha na biashara hiyo kwakuwa hasara zake ni kubwa kwa familia zao na
Taifa kwa ujumla.
Kuratibu shughuli za Tume za Pamoja za
Kudumu za Ushirikiano
101. Mheshimiwa Spika , Wizaraimeendelea kuratibu Mikutano ya Tume zaPamoja za Kudumu za Ushirikiano ambazokimsingi hutoa fursa kwa nchi zetu kujadilianakwa kina kuhusu masuala muhimu katikanyanja zote za mahusiano na kuweka mikakati
ya pamoja ya maendeleo.
102. Mheshimiwa Spika , mwezi Februari2016, Wizara ilifanya kikao cha Tume ya Pamoja
ya Kudumu ya Ushirikiano kati ya Tanzania naZambia kilichofanyika hapa nchini. Katika kikaohicho, pande zote mbili zilikubaliana kuimarisha
ushirikiano katika masuala ya Ulinzi naUsalama Mipakani; kuanzisha Mashauriano yaKidiplomasia; Kupunguza Msongamano wamagari katika mpaka wa Tunduma/Nakonde;na kuanzisha majadiliano ya kutotoza kodi marambili kwenye bidhaa zinazotoka na kuingiakatika nchi hizo.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 69/126
63
103. Mheshimiwa Spika , Vilevile, mweziAprili 2016, Wizara iliratibu na kushiriki kwenyeKikao kingine cha Tume ya Pamoja ya Kudumu
ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Rwandakilichofanyika Mjini Gisenyi, Rwanda. Katikakikao hicho nchi hizi zimekubalianakushirikiana katika kukamilisha mapema ujenziwa miundombinu ya ushoroba wa kati kama vileujenzi wa reli ya kati katika kiwango chakimataifa kwa kushirikiana na wadau, kukuzaushirikiano katika sekta ya anga hususan baina
ya Shirika la Ndege la Rwanda na Shirika laNdege la Tanzania, kuimarisha ushirikianokatika sekta za sayansi na teknolojia, afya,kilimo, ufugaji, utalii na elimu. Mkutano huoumezidi kuimarisha urafiki na ushirikiano kati
ya Tanzania na Rwanda kufuatia ziara yakirafiki ya Mheshimiwa Dkt. John PombeMagufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania nchini Rwanda mwezi Aprili, 2016.
104. Mheshimiwa Spika, Wizara imeratibuna kushiriki vikao vya Ujirani Mwema kati ya
Tanzania na nchi za Msumbiji, Uganda naZambia. Vikao hivyo ni muhimu katika kukuzamahusiano katika sekta mbalimbali kati ya
Tanzania na nchi husika. Aidha, Vikao hivyovinasaidia kutatua matatizo mengi ya mpakanina kurasimisha biashara baina ya nchi yetu nanchi tunazoshirikiana nazo.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 70/126
64
Kusimamia utawala na Maendeleo yaUtumishi Wizarani na kwenye Balozi zetu
105. Mheshimiwa Spika, katika kipindi hikiWizara iliajiri watumishi 42, ambapo maafisa 30kati ya hao walipelekwa katika mafunzo maalum
ya Jeshi la Kujenga Taifa yenye lengo lakuwajengea uwezo, uadilifu na uzalendo katikakazi; mtumishi mmoja alibadilishwa kada;iliwapandisha vyeo watumishi 59; nailiwathibitisha kazini watumishi 15. Aidha,napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa,katika kipindi hiki ulifanyika uteuzi wa mabalozikuiwakilisha nchi yetu katika nchi za Uholanzi,Malawi, Kuwait, Japan, Uingereza na Zimbabwe.Vilevile, Wizara imejaza nafasi za Wakurugenzi
zilizokuwa wazi.106. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kutekeleza mpango wa mafunzo wa miakamitatu 2013/2014 - 2015/2016. Katika kipindihiki jumla ya watumishi 43 walihudhuriamafunzo ndani na nje ya nchi. Kati ya hao,Watumishi 24 walihudhuria mafunzo ya muda
mrefu na watumishi 19 walihudhuria mafunzo ya muda mfupi. Wizara imeshaanza kuandaampango mwingine wa mafunzo wa miaka mitatuambao utaanza kutekelezwa kuanzia mwezi
Julai 2016 baada ya mpango wa sasa kuishamuda wake mwezi Juni 2016.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 71/126
65
107. Mheshimiwa Spika, katika kipindi hikiWizara imewarejesha nyumbani Mabaloziwatano na watumishi tisa baada ya kustaafu na
wengine kumaliza muda wao wa kufanya kaziUbalozini. Aidha, Wizara iliwapeleka vituoniNaibu Mabalozi watatu na watumishi thelathini.Zoezi la kuwarudisha Mabalozi na watumishiwanaostaafu na wanaomaliza muda wao nakupeleka mbadala wao ni endelevu na Wizaraitaendelea kulitekeleza kadri inavyopata fedha.
TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA
108. Mheshimiwa Spika , Wizara yanguinasimamia taasisi tatu ambazo ni Chuo chaDiplomasia kilichopo Kurasini Jijini Dar es
Salaam, Mpango wa Kujitathmini KiutawalaBora Barani Afrika na Kituo cha Kimataifa chaMikutano cha Arusha, ambacho piakinasimamia Kituo cha Mikutano cha Kimataifacha Julius Nyerere kilichopo Dar es Salaam.
Chuo cha Diplomasia
109. Mheshimiwa Spika , Chuo kimeendeleakutekeleza majukumu yake ya kutoa mafunzo,kufanya tafiti, kutoa ushauri wa kitaaluma nakendesha kozi fupi kwenye nyanja za diplomasiana uhusiano wa kimataifa. Katika kutekeleza
jukumu hilo, Chuo kimejizatiti katika kutimiza
na kutekeleza viwango vilivyowekwa na Baraza
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 72/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 73/126
67
na vyanzo vyake mbalimbali vya mapatoikiwemo Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha
Julius Nyerere kilichopo Dar es Salaam
ambacho kinatarajiwa kukusanya mapato yaShilingi 3,051,000,000.00.
113. Mheshimiwa Spika , Kituo kinategemeakukopa shilingi bilioni 2.4 kwa ajili ya miradi yamaendeleo ya ujenzi wa jengo la maonesho naupanuzi wa Hospitali. Miradi yoteinayotekelezwa imeombewa kibali cha Msajili waHazina.
114. Mheshimiwa Spika , Kituo kinaendeleakufanya taratibu za kuwezesha kujengwa kituomahsusi cha mikutano kitakachoitwa Kituo chaKimataifa cha Mikutano cha Mlima Kilimanjaro.
Taarifa ya upembuzi yakinifu ya mradi wa ujenziwa Kituo hicho iliandaliwa na WataalamuWashauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar esSalaam. Taarifa hiyo ilionyesha kwamba mradihuo ni muhimu na wenye manufaa kiuchumi nakijamii kwa taifa. Aidha, makadirio ya awali ya
ujenzi wa kituo hicho ni Dola za marekanimilioni 248. Kwa hivi sasa Kituo cha Mikutano ya Kimataifa Arusha kinaendelea namazungumzo na mifuko ya hifadhi ya jamiiiliyopo nchini ili iweze kushiriki katikakutekeleza mradi huo. Ni matarajio ya Wizarakuwa kuwepo kwa Kituo hicho kutakuwa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 74/126
68
suluhisho sahihi la mahitaji ya mikutano yakimataifa na maonesho hapa nchini.
Mpango wa Kujitathmini Kiutawala BoraBarani Afrika
115. Mheshimiwa Spika , Wizaraimeendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango waKujitathmini Kiutawala Bora Barani Afrika kwaupande wa Tanzania wenye lengo la kuzisaidianchi za Kiafrika kuhakikisha kuwa changamotozinageuzwa kuwa fursa za maendeleo na mambomazuri ya kuendelezwa kwa faida ya nchi
yenyewe na hata kuwa mfano wa kuigwa nanchi nyingine. Mpango huo unaratibiwa kwamujibu wa miongozo ya Wakuu wa Nchi na
Serikali wa nchi za Afrika.
116. Mheshimiwa Spika, katika kipindi chamwaka wa fedha 2015/2016, Taasisi ya Mpangowa Kujitathmini Kiutawala Bora Barani Afrikakwa upande wa Tanzania imeendelea kutekelezashughuli zifuatazo:-
i. Kusimamia utekelezaji wa Mpango kazi
wa kuondoa changamoto za utawala bora
zilizobainishwa kwenye ripoti ya Mpango
wa Kujitathmini Kiutawala Bora Barani
Afrika kwa upande wa Tanzania. Taasisi
imeendelea kupokea na kuchambua
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 75/126
69
taarifa mbalimbali za utekelezaji kutoka
Wizara, Idara na Wakala wa Serikali
zilizoguswa na Ripoti ya Mpango wa
Kujitathmini Kiutawala Bora Barani
Afrika kwa upande wa Tanzania;
ii. Kuandaa taarifa ya utekelezaji ya mwaka
kuhusu hatua zilizochukuliwa ili kutatua
changamoto zilizojitokeza kwenye ripoti
ya Mpango wa Kujitathmini KiutawalaBora Barani Afrika kwa upande wa
Tanzania. Taarifa hiyo inatarajiwa
kuwasilishwa kwenye vikao vya Wakuu
wa Nchi za Kiafrika wanaoshiriki kwenye
mchakato wa Mpango wa Kujitathmini
Kiutawala Bora Barani Afrika;
iii. Kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi
juu ya matokeo ya tathmini ya utawala
bora kwa nchi yetu kupitia vyombo
mbalimbali vya habari na majukwaa
mengineyo; na
iv. Kutafsiri ripoti ya Mpango wa
Kujitathmini Kiutawala Bora Barani
Afrika kwa upande wa Tanzania katika
lugha ya Kiswahili na kuandaa chapisho
la muhtasari.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 76/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 77/126
71
118. Mheshimiwa Spika, katika mwaka wafedha 2015/2016 Wizara hiyo iliidhinishiwaShilingi 26,666,436,300.00. Kati ya fedha hizo,
Shilingi 24,047,468,300.00 ni kwa ajili yaMatumizi Mengineyo na Shilingi2,618,968,000.00 ni kwa ajili ya mishahara yawatumishi. Kiasi kilichotengwa kwa ajili yamatumizi mengineyo kimejumuisha mchangowa Tanzania katika Jumuiya ya AfrikaMashariki wa kiasi cha Shilingi18,570,055,300.00.
119. Mheshimiwa Spika, hadi kufikiatarehe 30 Aprili 2016, Wizara ilipokea jumla yaShilingi 19,003,440,860.00, sawa na asilimia71.26 ya fedha zote zilizotengwa. Kati ya fedhahizo Shilingi 15,506,375,000 zilitumika kulipamchango wa Tanzania kwenye Jumuiya yaAfrika Mashariki, Shilingi 1,689,936,160.00zilitumika kulipa mishahara ya watumishi naShilingi 1,807,129,700.00 zilitumika kutekelezashughuli za Wizara.
Kusimamia na kuratibu utekelezaji waMkataba wa Jumuiya ya Afrika Mashariki naItifaki zake
120. Mheshimiwa Spika, kamaunavyofahamu Mtangamano wa Jumuiya yaAfrika Mashariki umepiga hatua kubwa ambapo
Nchi wanachama wa Jumuiya zimefikia
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 78/126
72
makubaliano na kuendelea kuyatekelezamakubaliano hayo kwenye nyanja zote zakiuchumu, kijamii, kiutamaduni na kwa kiasi
fulani kisiasa pia na hivyo kutufanya tusilale nakutakiwa kuwa makini katika kila hatuatunazopiga. Itakumbukwa kuwa Jumuiya yetuilianzishwa rasmi Julai 2000 baada ya NchiWanachama kukamilisha kuridhia Mkataba waUanzishaji wa Jumuiya ya Afrika Masharikiuliotiwa saini na Wakuu wa Nchi Wanachama
tarehe 30 Novemba, 1999. Aidha, hivi sasa Nchizote Wanachama zinatekeleza Mkataba huu naItifaki zake kubwa tatu (3) na zile mbalimbali zakisekta. Maeneo yaliyobaki ambayo tunaendeleana majadiliano ni Umoja wa Fedha na Shirikishola Kisiasa.
121. Mheshimiwa Spika, juhudi hizi sasazinamaanisha kuwa eneo lote la nchi sita (6) za
Jumuiya ya Afrika Mashariki kimsingilimeungana katika nyanja mbalimbali na hivyokutoa motisha ya ushindani mkubwa wa ndani
ya Jumuiya kiuchumi na kimaendeleo. Kwa
kutambua kuwa Tanzania ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia Wizara yangu ameelekeza Wimbo na Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki zitumike hapa
nchini.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 79/126
73
122. Mheshimiwa Spika, napendakuchukua nafasi hii kupitia Bunge lako Tukufukutoa wito wa kuongezwa kwa matumizi ya
Bendera ya Jumuiya ya Afrika Masharikikwenye Ofisi zote za Umma nchini zikiwemo zaSerikali Kuu, Serikali za Mitaa na Taasisi zaUmma (tukiwemo sisi Waheshimiwa Wabungekwenye Magari yetu na ofisi zetu Majimboni) nazile za sekta binafsi sambamba na Bendera ya
Taifa letu Tukufu. Aidha, natoa rai kwa Taasisiza Serikali na vyombo vya habari viwezekuutumia Wimbo wa Jumuiya ya AfrikaMashariki pale ambapo Wimbo wa Taifa letu
Tukufu unapigwa.
123. Mheshimiwa Spika, ni imani yangu
kuwa hatua hii itasaidia kuwajengeaWatanzania uelewa, kuifahamu vyema Jumuiya yetu na hatimae waweze kujiandaa, kushiriki nakupata manufaa yanayoendana na fursa zilizopokibiashara, kiuchumi, kiuzalishaji, kijamii nakiutamaduni kwa kuzingatia uwepo wa Sokokubwa la Afrika Mashariki na fursa zinginezo.
124. Mheshimiwa Spika, wito huu ni moja ya utekelezaji wa Mkakati wetu wa mawasilianowa Wizara ambao unalenga kuwapa fursaWananchi wetu ya kujiandaa, kuiendesha,kuitumia Jumuiya yao na kutimiza matakwa yaIbara ya 7(a) ya Mkataba wa Uanzishaji wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 80/126
74
Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo inasisitizakuwa “Jumuiya yetu hii imejengwa katikaWananchi na ushirikiano wa kimasoko”. Aidha,
hatua hizi zinalenga katika kuendeleza juhudiza Mheshimiwa Dkt. John Pombe JosephMagufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kuhakikisha kuwa Jumuiya hii inakuwa kweli ni Jumuiya yaWananchi wetu, kutambua uwepo wake nawanufaike nayo katika kubadilisha maisha yao.
Mkutano wa 17 wa Viongozi Wakuu wa NchiWanachama na Mikutano ya 32 na 33 yaBaraza la Mawaziri la Jumuiya ya AfrikaMashariki
125. Mheshimiwa Spika, katika kipindihiki Wizara iliratibu na kushiriki katikaMkutano wa 17 wa Wakuu wa NchiWanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharikiuliofanyika mwezi Machi 2016 Jijini Arusha,
Tanzania. Katika Mkutano huo Tanzania
iliteuliwa kwa mara ya pili mfululizo kuwaMwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Masharikihadi mwezi Novemba 2016. Aidha, Mkutanohuo uliridhia Jamhuri ya Sudan Kusinikujiunga na Jumuiya ya Afrika Masharikiambapo tarehe 15 Aprili, 2016 nchi hiyo ilisainiMkataba wa Kujiunga na Jumuiya hiyo.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 81/126
75
126. Mheshimiwa Spika, kadhalika, katikamkutano huo Wakuu wa Nchi walizindua rasmiPasi mpya ya kielektroniki ya Kusafiria ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuelekezamatumizi ya hati hii mpya kuanza rasmi tarehe1 Januari, 2017. Pasi hii inaipandisha hadhiPasi ya sasa ya Afrika Mashariki kutumikakusafiria nje ya Afrika Mashariki. NchiWanachama zimekubaliana kuziondoa hati zakusafiria zilizopo sasa katika kipindi cha miezi
24 kuanzia tarehe 1 Januari, 2017 hadi tarehe31 Desemba, 2018. Hati hizo zitakuwa naalama za jumla za kiusalama na kila NchiMwanachama imeruhusiwa kuongeza alamazake za kiusalama katika Pasi hizo. Idara zaUhamiaji katika nchi wanachama zitaendeleana jukumu la utoaji wa hati hizo kwa raia wanchi zao.
127. Mheshimiwa Spika, Mkutano wa 32wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya AfrikaMashariki ulifanyika tarehe 14 Agosti, 2015 nakufikia maamuzi mbalimbali ikiwa ni pamojana kuidhinisha ajira kwa Mwanasheria Mkuu
wa Jumuiya, Mkurugenzi Mtendaji wa Wakalawa Usalama wa Anga na Mkurugenzi waMipango katika Jumuiya.
Umoja wa Forodha
128. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea
kuratibu utekelezaji wa hatua ya kwanza ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 82/126
76
Mtangamano ambayo ni Umoja wa Forodha waAfrika Mashariki kama ifuatavyo:
Kanuni Mpya za Utambuzi wa Uasili waBidhaa
129. Mheshimiwa Spika , katikakuziwezesha Nchi Wanachama wa Jumuiya yaAfrika Mashariki kunufaika zaidi na hatua hii yaUmoja wa Forodha, mabadiliko yamefanywa
katika kanuni za utambuzi wa uasili wa bidhaa.Katika mabadiliko hayo, Nchi Wanachamazimeacha kutumia vigezo sawa kwa bidhaa zote,na sasa zitatumia vigezo tofauti kulingana nabidhaa husika. Mabadiliko haya ni fursa kubwakwa viwanda vya Tanzania ambavyo vingi badoni vidogo na vilikuwa haviwezi kufikia vigezo vya
uasili wa bidhaa. Aidha, katika kipindi hiki, nchiWanachama wa Jumuiya zilikamilishamwongozo wa kutumika katika kurahisishautekelezaji wa kanuni hizo.
Uondoaji wa Vikwazo Visivyo vya Kiforodha
130. Mheshimiwa Spika, katika kuwekamazingira wezeshi ya biashara katika Jumuiya,Wizara imeendelea kuratibu uondoaji waVikwazo Visivyo vya Kiforodha kupitia Kamati yaKitaifa na Kikanda ya uondoaji wa vikwazohivyo. Katika mwaka wa fedha 2015/2016vikwazo 16 viliripotiwa vimeondolewa, kati ya
hivyo vinne (4) viliihusu Tanzania. Vikwazo
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 83/126
77
hivyo ni tozo ya Dola za Marekani 200 kwa kilakontena la kemikali; kutopewa upendeleo waushuru wa forodha kwa chumvi na bidhaa za
plastiki kutoka Kenya; na upimaji wa malorimatupu.
131. Mheshimiwa Spika , ili kuharakishauondoaji wa vikwazo visivyo vya kiforodha,Wizara imekuwa na utaratibu wa kuitishamikutano ya pande mbili husika. Katika kipindi
hiki Wizara ilifanya mikutano na Kenya naBurundi ambayo ilichangia kuharakishauondoaji wa vikwazo visivyo vya kiforodhavikiwemo vile vilivyotajwa hapo juu. Vilevile,tumekubaliana na Kenya kufanya utafiti juu yatozo zinazotozwa na mamlaka za Serikali zamitaa za nchi zetu zinazoathiri biashara baina
yetu kwa lengo la kurazinisha tozo hizo.
Mwenendo wa Biashara ya Bidhaa kati yaTanzania na Nchi Wanachama wa Jumuiya yaAfrika Mashariki
132. Mheshimiwa Spika, nafasi ya Tanzania katika Soko la Jumuiya imeendeleakupanda kutoka asilimia 18 mwaka 2010 hadiasilimia 26 mwaka 2014 na tunategemeakufanya vizuri zaidi kutokana na juhudizinazoendelea za kudhibiti ulanguzi wa mazaona bidhaa mipakani, utekelezaji wa sheria mpya
ya uasili wa bidhaa, kuondoa vikwazo visivyo
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 84/126
78
vya kiforodha na kuimarisha uzalishajiviwandani. Kwa mujibu wa Taarifa ya Biashara
ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya mwaka
2014, biashara ndani ya Jumuiya imekua nakufikia Dola za Marekani bilioni 5.63 kwamwaka 2014 ikilinganishwa na Dola zaMarekani bilioni 3.72 kwa mwaka 2010. Aidha,biashara baina ya Tanzania na NchiWanachama imeendelea kuimarika nakuongezeka kutoka Dola za Marekani bilioni0.69 mwaka 2010 na kufikia Dola za Marekanibilioni 1.49 mwaka 2014. Kwa mwaka 2013kiwango cha biashara kiliongezeka zaidikulingana na hali ya mahitaji ya soko nakupanda kwa uzalishaji kwenye sektambalimbali. Tanzania imeendelea kuwa na urarichanya wa biashara katika Jumuiya ya AfrikaMashariki kama inavyoonekana katikaKiambatisho Na. 1.
133. Mheshimiwa Spika, wafanyabiasharawa Tanzania wamendelea kuchangamkia fursazitokanazo na Umoja wa Forodha wa Afrika
Mashariki. Wafanyabiashara hao wamefanikiwakuuza kwa wingi katika Soko la AfrikaMashariki bidhaa za viwandani kama viletransfoma, waya za umeme, vyandarua, sarujina magunia; na bidhaa za kilimo kama vilemahindi, mchele, katani, mbogamboga, asali nachakula cha mifugo. Hii inaashiria kuendelea
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 85/126
79
kuimarika kwa biashara ya bidhaa za viwandanina mazao ya kilimo.
134. Mheshimiwa Spika, bidhaazilizonunuliwa kwa wingi kutoka NchiWanachama ni pamoja na kemikali kwa ajili yaviwanda vya nguo, vipodozi na sabuni; dawa zabinadamu na mifugo; vipuri vya magari; vifunikovya chupa za vinywaji; sabuni; vifaa vyakufanyia usafi; vifungashio; mabanda maalum
ya kilimo cha mbogamboga na maua (greenhouse); na vyumba vya baridi kwa ajili yakuhifadhia bidhaa mbalimbali.
Umoja wa Fedha
135. Mheshimiwa Spika, NchiWanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharikizimeendelea kutekeleza Mpangokazi wa MiakaKumi wa Kuelekea katika Eneo la Sarafu Mojaulioanza kutekelezwa mwaka 2014 nautakaokamilika mwaka 2024. Katika kutekelezaMpangokazi huo, Nchi Wanachama
zimekamilisha majadiliano ya Muswada waSheria ya uanzishwaji wa Taasisi ya Fedha yaAfrika Mashariki na Taasisi ya Takwimu yaAfrika Mashariki. Maandalizi ya majadiliano yamuswada wa Kamisheni ya Ufuatiliaji naUsimamizi ya Afrika Mashariki yataanza katikakipindi hiki cha mwaka wa fedha.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 86/126
80
136. Mheshimiwa Spika, matarajio yaNchi Wanachama wa Jumuiya ya AfrikaMashariki ni kuifikia hatua hii muhimu ya
kuanzisha matumizi ya sarafu moja kwenyeeneo la Jumuiya ifikapo mwaka 2024. Hatua hiiitafikiwa mara baada ya Nchi Wanachamaangalau watatu (3) kufikia vigezo vya kiuchumivilivyoainishwa kwenye Itifaki ya Umoja waFedha. Aidha, hatua hiyo itatanguliwa nauanzishwaji wa Benki Kuu ya Afrika Masharikiambayo pamoja na majukumu mengine itakuwana majukumu ya kuchapisha na kusambazasarafu hiyo ya Afrika Mashariki.
Shirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki
137. Mheshimiwa Spika, Shirikisho la
Kisiasa ni hatua ya nne na ya mwisho katikamtangamano wa Afrika Mashariki ambayoinategemea sana misingi imara itokanayo nautekelezaji wa hatua za mwanzo zamtangamano. Katika kipindi cha mwaka fedha2015/2016, Nchi Wanachama ziliendelea namajadiliano ya modeli ya shirikisho ambayoitatumika katika kuandaa Rasimu ya Katiba yaShirikisho la Kisiasa la Afrika Mashariki.
138. Mheshimiwa Spika, rasimu hiyo,
inatarajiwa kutumika katika kuelimisha na
kuhamasisha wananchi wa Afrika Mashariki
kuhusu aina ya Shirikisho linalotarajiwa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 87/126
81
kuundwa ili kuleta uelewa wa pamoja na
uungwaji mkono wa hatua hiyo wakati ukifika.
Aidha, kwa kuwa Shirikisho la Kisiasa ni
mchakato, Nchi Wanachama zimeendelea na
utekelezaji wa shughuli zinazounda msingi wa
Shirikisho hilo ikiwemo masuala ya utawala
bora, uimarishaji wa demokrasia na utawala wa
sheria.
Ushirikiano na Kanda nyingine za Kiuchumi
Majadiliano ya Kuanzisha Eneo Huru laBiashara la Utatu wa Soko la Pamoja laMashariki na Kusini mwa Afrika, Jumuiya yaAfrika Mashariki na Jumuiya ya MaendeleoKusini mwa Afrika
139. Mheshimiwa Spika, juhudi za
kuziunganisha Jumuiya za COMESA, EAC na
SADC ili kuwa eneo moja huru la kibiashara
zimefika hatua nzuri. Mkutano wa Tatu wa
Wakuu wa Nchi za COMESA, EAC na SADCuliofanyika tarehe 10 Juni, 2015 Jijini Sharm El
Sheikh, Misri ulihitimishwa kwa Wakuu wa Nchi
na Serikali kutia saini Azimio la Uanzishwaji wa
Eneo Huru la Biashara; na Mkataba wa
Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 88/126
82
140. Mheshimiwa Spika, kufuatia
kusainiwa kwa mkataba huo, Viongozi Wakuu
wa Nchi Wanachama wa Jumuiya hizo
walikubaliana kukamilisha majadiliano ya
maeneo yaliyosalia katika kipindi cha miezi 6
hadi 12 baada ya uzinduzi rasmi wa eneo huru
la biashara. Maeneo hayo ni uondoshwaji wa
kodi kwenye bidhaa, utambuzi wa uasili wa
bidhaa, usuluhishi wa migogoro ya kibiashara
na kupunguziana ushuru.
Majadiliano ya Uhuru wa Wafanyabiasharakusafiri katika Eneo la Utatu
141. Mheshimiwa Spika, ili kurahisisha
na kuwezesha wafanyabiashara kusafiri katikaEneo hilo la Utatu, Nchi Wanachamazimeendelea na majadiliano ya kuandaaMkataba wa Uhuru wa Wafanyabiasharakusafiri kwenye eneo hilo. Mkataba huounatarajiwa kuidhinishwa ifikapo Desemba,2016.
Majadiliano ya Uendelezaji wa Viwanda katikaEneo la Utatu
142. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibuushiriki wa Tanzania katika kukamilishaRasimu ya Mpango wa Maeneo ya Ushirikianokatika Maendeleo ya Viwanda; na Mpangokazi
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 89/126
83
kwa ajili ya Utekelezaji wa utaratibu waUshirikiano katika eneo la Utatu. Maeneo
yaliyoboreshwa ni Sera na Mikakati kutoka
Kanda zote tatu; Uzingatiaji wa uendelezaji waviwanda unaojali utunzaji wa mazingira; naUtambuaji Kisheria na Umiliki wa Hakizinazotokana na Uvumbuzi na Ubunifu katikamaendeleo ya Viwanda. Aidha, Nchi Wanachamazimekubaliana kushirikiana katika maeneo yauratibu na uhamasishaji wa pamoja wa sera ya
maendeleo ya viwanda na uongezaji thamanibidhaa baina ya nchi Wanachama; naUendelezaji wa Viwanda Vidogo na vya Kati nakujenga uwezo wa utaalam katika kuendelezaViwanda.
Ubia wa Kiuchumi kati ya Nchi za Jumuiya yaAfrika Mashariki na Umoja wa Ulaya
143. Mheshimiwa Spika, Wizaraimeendelea kuratibu majadiliano ya Mkataba waUbia wa Kiuchumi baina ya Nchi za Jumuiya yaAfrika Mashariki na Umoja wa Ulaya. Malengo
ya ubia huu ni kuimarisha ushirikiano wakikanda, kuleta maendeleo endelevu nakuziwezesha nchi za Afrika, Karibiani naPasifiki kupata misaada ya kimaendeleo ilikukabiliana na changamoto za uzalishaji nakuweka muda wa kuondoa vikwazo vyabiashara.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 90/126
84
144. Mheshimiwa Spika , nchi za Jumuiya
ya Afrika Mashariki na Umoja wa Ulaya
zilikamilisha mapitio ya kisheria ya Mkataba wa
Ubia wa Kiuchumi baina ya nchi hizo. Hatua
inayoendelea ni Nchi za Jumuiya ya Afrika
Mashariki kutafsiri mkataba huo katika lugha
ya Kiswahili wakati Umoja wa Ulaya unatafsiri
mkataba huo katika lugha 21 zinazotumiwa na
Jumuiya ya Ulaya. Baada ya kukamilika kwa
mchakato wa kufanya tafsiri, Nchi Wanachamawa Jumuiya ya Afrika Mashariki na Umoja wa
Ulaya zitasaini Mkataba huo, pamoja na
kuuridhia ili utekelezaji wake uanze.
145. Mheshimiwa Spika, ili kuweka
mazingira wezeshi ya kukuza na kuendelezaviwanda vya nguo na ngozi ndani ya Jumuiya,
Mkutano wa 17 wa Wakuu wa Nchi Wanachama
ulielekeza Nchi Wanachama kuhakikisha
zinapunguza uingizaji wa nguo na viatu
vilivyotumika kutoka nje ya Jumuiya na
kusitisha uagizaji wake katika kipindi chamiaka mitatu kuanzia mwaka huu wa fedha.
Aidha, Wakuu wa Nchi walielekeza Nchi
wanachama kupiga marufuku utaratibu wa
kuuza ngozi na bidhaa za ngozi ghafi nje ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 91/126
85
Kujengea uwezo na upatikanaji wa masokokwa Wajasiriamali wadogo
146. Mheshimiwa Spika, Maonesho ya 16 ya Juakali/Nguvukazi yaliyofanyika tarehe 30Novemba hadi 6 Disemba 2015 katika Viwanjavya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam katikamaonesho hayo jumla ya wajasiriamali 734kutoka Nchi zote wanachama walishiriki. Kati yahao, wajasiriamali 395 walikuwa ni washiriki
kutoka Tanzania. Lengo la maonesho hayo nikujenga uwezo wa wafanyabiashara wadogokupata masoko ya bidhaa zao katika NchiWanachama. Napenda kutoa rai kwawajasiriamali wa Tanzania kushiriki katikaMaonesho ya 17 ya Juakali/Nguvukazi
yaliyopangwa kufanyika mwezi Novemba 2016
nchini Kenya.
Uendelezaji wa Miundombinu ya Kiuchumi
147. Mheshimiwa Spika, Wizaraimeendelea kuratibu utekelezaji wa programu na
miradi ya kitaifa yenye sura ya Kikandailiyoainishwa katika Mipango ya Jumuiya yaAfrika Mashariki ya Uendelezaji waMiundombinu ya Kiuchumi. Hatua zilizofikiwakatika uendelezaji wa programu na miradi hiyoni kama ifuatavyo:
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 92/126
86
Ujenzi wa Vituo vya Kutoa Huduma kwaPamoja Mipakani
148. Mheshimiwa Spika , Wizaraimeendelea kuratibu ujenzi wa vituo vya kutoahuduma kwa pamoja mipakani. Hadi sasa vituoviwili (2) kati ya saba (7) vinavyojengwa kwauratibu wa Jumuiya ya Afrika Masharikivimekamilika na kuzinduliwa. Vituo hivyo nikituo cha Holili/Taveta mpakani mwa Tanzania
na Kenya; na kituo cha Rusumo mpakani mwa Tanzania na Rwanda.
149. Mheshimiwa Spika , vilevile, Wizarailiratibu ukamilishaji wa Kanuni za Utekelezajiwa Sheria ya Jumuiya ya KusimamiaUendeshaji wa Vituo vya Kutoa Huduma kwaPamoja Mipakani. Kanuni hizo zimepitishwa naMkutano wa 33 wa Baraza la Mawaziri la
Jumuiya uliofanyika mwezi Februari, 2016. Ilikupata uelewa wa pamoja kuhusu Vituo vyaKutoa Huduma kwa Pamoja Mipakani, Wizarailiratibu na kushiriki katika mafunzo kwa
maafisa wa Serikali, sekta binafsi nawawakilishi wa jamii kwa Vituo vya Horohoro naSirari. Taarifa kuhusu vituo vingine na hatuazilizofikiwa ili kuwezesha kuanza kutoa hudumastahiki ni kama inavyoonesha katikaKiambatisho Na. 2.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 93/126
87
150. Mheshimiwa Spika, Wizaraimeendelea kuratibu ukamilishaji wa ujenzi waDaraja la Kimataifa la Rusumo ikiwa ni sehemu
ya kurahisisha usafirishaji wa bidhaa nakuimarisha vituo vya kutoa huduma za pamojamipakani katika ushoroba wa kati. Daraja hilolenye uwezo wa kupitisha magari manne kwawakati mmoja yenye uzito wa tani 56 kila mojalilizinduliwa rasmi na Mhe. Dkt. John Pombe
Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Mhe. Paul Kagame,Rais wa Jamhuri ya Rwanda tarehe 6 Aprili,2016.
Uendelezaji wa Mtandao wa Barabara
151.Mheshimiwa Spika,
hatua zilizofikiwakatika uendelezaji wa mtandao wa barabara zaKikanda katika mwaka 2015/2016 ni kamaifuatavyo:
Mradi wa Barabara ya Arusha – Holili/Taveta – Voi
152. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu uendelezaji wa mtandao wa barabara
unaoziunganisha nchi za Tanzania na Kenya
kupitia mpaka wa Holili/Taveta yenye urefu wa
kilomita 234.3. Kwa upande wa Tanzania,
awamu ya kwanza ya ujenzi wa barabara hiyo
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 94/126
88
kwa kiwango cha lami unahusisha upanuzi wa
sehemu ya kutoka Arusha hadi Tengeru yenye
urefu wa kilometa 14.1 kuwa njia nne na
barabara ya mzunguko wa kusini mwa Jiji la
Arusha yenye urefu wa kilometa 42.41. Aidha,
kwa upande wa Kenya mradi unahusisha ujenzi
wa barabara mpya ya lami yenye urefu wa
kilomita 100 kutoka Taveta hadi Mwatate.
Gharama za mradi kwa upande wa Tanzania ni
takriban Shilingi bilioni 209.61 ambapo kati yahizo Benki ya Maendeleo ya Afrika itatoa Shilingi
bilioni 190.21 na Serikali ya Tanzania itatoa
Shilingi bilioni 19.4.
153. Mheshimiwa Spika, Jiwe la Msingi la
Ujenzi wa Barabara hiyo liliwekwa mwezi Machi,2016 na Mheshimiwa Dkt. John PombeMagufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Mheshimiwa Uhuru MuigaiKenyatta, Rais wa Jamhuri ya Kenya.
Uwianishaji wa Uzito wa Magari Katika
Barabara
154. Mheshimiwa Spika, Sheria yaUdhibiti wa Uzito wa Magari ya Mwaka 2013iliyopitishwa na Bunge la Afrika Masharikiimeridhiwa na Nchi zote Wanachama. NchiWanachama zimekamilisha majadiliano ya
kuandaa Kanuni za kuwezesha utekelezaji wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 95/126
89
Sheria hizo ambazo zilipitishwa katika Mkutanowa 33 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiyauliofanyika Jijini Arusha mwezi Februari, 2016.
Mkakati wa Kuwezesha Sekta ya Uchukuzi
155. Mheshimiwa Spika, NchiWanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharikizimeidhinisha utekelezaji wa Mkakati wa
Kuwezesha Sekta ya Uchukuzi. Mkakati huounazitaka Nchi Wanachama pamoja na masualamengine kuwianisha mitaala ya mafunzo yaudereva wa magari ya biashara; usajili wavyombo vya moto; na madaraja ya leseni. NchiWanachama zimekamilisha rasimu za mitaala yamafunzo ya udereva wa magari ya biashara.
Sekta ya Mawasiliano
156. Mheshimiwa Spika, Wizarainaendelea kuratibu utekelezaji wa Mpango waKutatua Changamoto ya Gharama Kubwa zaMaunganisho ya Simu za Mkononi katika Nchi
Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharikikama ulivyoridhiwa na Wakuu wa Nchi wa
Jumuiya hiyo mwezi Februari, 2015. Katikakutekeleza mpango huo, yamefanyika mapitio yaKanuni zinazotumika katika mfumo wakuongoza sekta ya mawasiliano nchini. Wizara
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 96/126
90
ya kisekta inafanya tathmini ya changamotozilizoibuliwa na wadau kuhusu mpango huo.
Sekta ya Hali ya Hewa
157. Mheshimiwa Spika, Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Ushirikianokatika Huduma za Hali ya Hewa ilisainiwa naMawaziri wanaosimamia masuala ya Jumuiya
ya Afrika Mashariki kutoka Nchi Wanachamakatika Mkutano wa 33 wa Baraza la Mawaziri la
Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika mweziFebruari, 2016. Itifaki hiyo inatoa mwongozowa ushirikiano wa Nchi Wanachama katikakubadilishana taarifa na ujuzi katika masuala
ya hali ya hewa. Nchi Wanachamazimekubaliana kuridhia Itifaki hiyo kabla yamwezi Julai, 2016.
Sekta ya Bandari na Usafiri Majini
158. Mheshimiwa Spika, katika jitihadaza kurahisisha usafirishaji wa watu na bidhaa
katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, NchiWanachama zinaendelea na maandalizi yaMkakati wa Usafiri wa Majini wa AfrikaMashariki. Katika kutekeleza azma hiyo, Utafitiwa Awali wa Hali ya Usafiri wa Majini na Sekta
ya Bandari umekamilika. Ripoti ya Utafiti huo,pamoja na mambo mengine, imebainisha
changamoto katika utekelezaji wa miradi ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 97/126
91
kuendeleza Bandari katika mwambao wa Bahari ya Hindi, Maziwa na Uanzishaji wa BandariKavu. Changamoto hizo ni pamoja na uhaba wa
rasilimali fedha zinazohitajika katika kutekelezaMiradi iliyoainishwa katika Mipango Mikuu yakuendeleza Bandari za Nchi Wanachama nahaja ya kuwianisha Mifumo ya Kitaasisi naUdhibiti katika Sekta ya Usafiri wa Majinimiongoni mwa Nchi Wanachama ili kuwa naviwango vinavyofanana katika udhibiti wa
vyombo vya majini. Maoni ya Ripoti hiyo yatasaidia katika maandalizi ya Mkakati waAfrika Mashariki wa Usafiri wa Majini.
Sekta ya Nishati
159. Mheshimiwa Spika , wakati waMkutano wa Kilele wa Wakuu wa NchiWanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharikiuliofanyika mwezi Machi 2016, Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Jamhuri ya Uganda walifanya Kikao cha pamoja kujadilimasuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na ujenzi
wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutokaHoima, Uganda mpaka bandari ya Tangalitakalokuwa na urefu wa kilometa 1,410.
160. Mheshimiwa Spika , kufuatia Kikaohicho cha Marais wawili, wataalam wa pandezote mbili waliendelea na majadiliano
yaliyopelekea Serikali ya Uganda kutoa tamko
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 98/126
92
rasmi kwenye Mkutano wa 13 wa Ushoroba waKaskazini uliofanyika mwezi Aprili, 2016 JijiniKampala kuwa bomba hilo litajengwa kupitia
Tanzania. Mradi huo utagharimu Dola zaMarekani bilioni nne na kukamilika baada yamiaka mitatu hadi minne. Mradi huounatarajiwa kuzalisha ajira za moja kwa mojatakriban 1,500 na ajira zisizo za moja kwa moja20,000. Aidha, Benki ya Maendeleo ya Afrikaimeidhinisha msaada wa kiasi cha Dola za
Marekani 1,691,130 kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Mradi mwingine waBomba la Mafuta la Mbarara - Mwanza - Isaka -Dar es Salaam. Fedha za nyongeza Dola zaMarekani 95,600 zinahitajika ili kukamilishaupembuzi yakinifu huo. Hivyo, kila NchiMwanachama imetakiwa kuchangia kiasi chaDola za Marekani 19,120 kabla ya mwisho wamwezi Juni, 2016 ili kukamilisha upembuzi
yakinifu wa Mradi huo.
Ushirikiano Katika Sekta za Huduma zaJamii
Sekta ya Elimu, Utamaduni na Michezo
Urazinishaji wa Mitaala
161. Mheshimiwa Spika , Wizara imeendeleana uratibu wa zoezi la urazinishaji wa Mitaala
kwa ngazi zote za Elimu pamoja na mafunzo ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 99/126
93
ualimu kwa shule za awali, msingi nasekondari.
Shindano la Insha la Jumuiya
162. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibuushiriki wa Tanzania katika shindano lauandishi wa Insha la Jumuiya ya AfrikaMashariki lililoshirikisha wanafunzi wa shule za
sekondari kutoka nchi tano (5) Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Nafurahi kuliarifuBunge lako Tukufu kuwa kijana MtanzaniaSimon Mollel Sabaya kutoka Shule ya Sekondari
ya Mzumbe aliibuka mshindi wa kwanza katikashindano hilo. Huu ni ushahidi kuwa vijanawetu wanaweza na wanauelewa wa Jumuiya
yetu. Naomba nitumie fursa hii kutoa pongezikwa kijana huyu na kuwatia moyo vijanawengine waendelee kushiriki kwenyemashindano haya ili waweze kuliletea sifa Taifaletu. Natoa wito kwa walimu na wazazikuwahamasisha wanafunzi kushiriki katikashindano hilo ili kukuza uelewa wao katikamasuala ya Jumuiya. Wizara yangu kwakushirikiana na Jumuiya ya Afrika Mashariki;Wizara za Elimu, Sayansi na Teknolojia; naWizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa naMichezo itaanzisha kampeni ya kuongeza uelewawa Jumuiya katika shule na vyuo.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 100/126
94
Mdahalo wa Nne wa Wanafunzi wa VyuoVikuu
163. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibuushiriki wa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya
Tanzania katika mdahalo wa Nne (4) waWanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Nchi Wanachamawa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyikamwezi Desemba 2015, Kampala, Uganda. Lengola mdahalo huo ni kupata washindi wawili
kutoka kila Nchi Mwanachama wa Jumuiyaambao watakuwa Mabalozi wa Nchi zao katikamasuala ya Jumuiya. Kwa upande wa Tanzania,washindi wa mwaka 2015 ni RaphaelKambamwene wa Chuo Kikuu cha Dar esSalaam na Lucy Peter Funja wa Chuo Kikuu chaArdhi. Aidha, Wizara inaendelea na jukumu la
kuwapatia taarifa Mabalozi haozitakazowawezesha kutoa elimu kwa ummahususan kwa vijana wenzao.
Kamisheni ya Kiswahili ya Afrika Mashariki
164. Mheshimiwa Spika, napendakulifahamisha Bunge lako Tukufu kwambaKamisheni ya Kiswahili ya Afrika Masharikiimeshahamia rasmi katika Makao Makuu yake
yaliyopo Zanzibar. Hii ni kufuatia kusainiwakwa Mkataba wa Uenyeji baina ya Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Sekretarieti ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 101/126
95
Jumuiya ya Afrika Mashariki tarehe 28Desemba, 2015.
Mradi wa Hifadhi ya Mazingira Katika Bondela Ziwa Victoria Awamu ya Pili
165. Mheshimiwa Spika, katikakukabiliana na athari za mazingira zinazotokanana shughuli za binadamu katika Bonde la ZiwaVictoria zilizosababisha pamoja na mambomengine kupungua kwa kina cha maji nasamaki katika ziwa, Wizara imeendelea nauratibu wa utekelezaji wa shughuli za Mradi waUsimamizi wa Mazingira katika Bonde la ZiwaVictoria. Katika kipindi hiki, Benki ya Duniailiongeza muda wa miaka miwili na nusu
kuanzia mwezi Juni 2015 hadi mwezi Desemba2017 na mkopo wa Dola za Marekani milioni 10ambazo zitatumika kukamilisha miradi ambayoilikuwa haijakamilika katika Awamu ya Pili yaMradi iliyofikia ukomo wake mwezi Juni 2015na kuandaa Awamu ya Tatu. Vilevile, udhibitiwa magugumaji katika Ziwa Victoria
umeendelea ambapo magugumaji yamepunguaZiwani kutoka hekta 520 mwezi Septemba, 2009hadi hekta 104 mwezi Novemba, 2015. Mradiumeendelea na shughuli za udhibiti wa utupajitaka na uhamasishaji wa uzalishaji boraviwandani ambapo Jumla ya viwanda 118 sawana asilimia 86 vimepata mafunzo ya uzalishaji
bora viwandani.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 102/126
96
Programu ya Hifadhi ya Mazingira kwaKuboresha Sera, Mabadiliko ya Tabianchi,Utafiti na Maendeleo ya Kiuchumi
166. Mheshimiwa Spika, katikakuhakikisha kunakuwa na matumizi endelevu
ya rasilimali maji katika Bonde la Mto Mara, Wizara yangu imefanikisha utiaji saini wa Hati
ya Makubaliano ya Usimamizi wa pamoja warasilimali maji katika Bonde la Mto Mara kati ya
Tanzania na Kenya. Makubaliano hayo yatasaidia kupunguza athari za mazingirazinazosababishwa na shughuli za binadamukatika bonde hilo.
Mradi wa Idadi ya Watu, Afya na Mazingira waJumuiya
167. Mheshimiwa Spika, ili kujengauelewa wa pamoja kwa wananchi katikamasuala ya idadi ya watu, afya na mazingirakwa ajili ya kuleta maendeleo endelevu, Wizaraimeendelea kuratibu ushiriki wa Tanzania
katika maandalizi ya Mpango Mkakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Masuala yaIdadi ya Watu, Afya na Mazingira. Mpango huoutakapokamilika utatoa mwongozo wakuzingatia masuala ya idadi ya watu, afya namazingira katika utekelezaji wa miradi yamaendeleo katika Nchi Wanachama.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 103/126
97
Sekta ya Jinsia na Maendeleo ya Jamii
168. Mheshimiwa Spika, nafasi yawanawake, watoto na vijana imeendelea kupewakipaumbele katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.Kwa muktadha huo, Wizara imeendeleakuratibu programu na miradi inayolengakuyajengea uwezo makundi hayo ili kunufaikana fursa mbalimbali zinatokanazo naMtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.Aidha, progamu hizi zimetoa fursa kwa makundihayo kutoa maoni yao ya namna bora yakuendeleza mtangamano. Vilevile, Jumuiya yaAfrika Mashariki inakamilisha Sera ya Watoto ya
Jumuiya.
Ushirikiano katika Siasa, Ulinzi na Usalama
169. Mheshimiwa Spika, naombakuchukua nafasi hii kulifahamisha Bunge lako Tukufu kuwa Jumuiya ya Afrika Masharikiimepata Katibu Mkuu mpya Balozi LiberatMfumukeko kutoka Jamhuri ya Burundiatakeyeiongoza Jumuiya kwa Kipindi cha miakamitano ijayo. Aidha, naomba kumshukuru
Balozi Dkt. Richard Sezibera kutoka Jamhuri yaRwanda kwa mchango wake mkubwa katikakuiendesha Jumuiya kwa kipindi cha miakamitano iliyopita.
Ushirikiano katika Siasa
170. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
hiki tumeendelea kushuhudia kushamiri kwa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 104/126
98
demokrasia katika Nchi Wanachama wa Jumuiya. Kwa kuzingatia kwamba demokrasiani moja ya misingi mikuu ya Jumuiya ya Afrika
Mashariki, Wizara yangu imeendelea kuratibuushiriki wa Tanzania katika timu ya waangaliziwa uchaguzi mkuu kutoka Jumuiya ya AfrikaMashariki kushiriki katika uangalizi wauchaguzi mkuu katika Nchi Wanachama. Katikakipindi hiki, Nchi tatu Wanachama wa Jumuiyazilifanya uchaguzi mkuu wa Rais na Wabunge.Nchi hizo ni Jamhuri ya Burundi, Jamhuri yaMuungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda.
Jamhuri ya Burundi ilifanya Uchaguzi wakemwezi Julai, 2015 ambapo Rais PierreNkurunziza aliibuka mshindi wa Uchaguzi huo.Aidha, kwa upande wa Uchaguzi Mkuu wa
Tanzania, Wizara iliratibu ushiriki wa waangaliziwa uchaguzi kutoka Jumuiya ya AfrikaMashariki waliokuja kufanya uangalizi ambapoMheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufulialipata ushindi katika uchaguzi huo.
171. Mheshimiwa Spika, Wizara pia
iliratibu ushiriki wa Tanzania katika timu yawaangalizi wa uchaguzi wa Jumuiya kwenyeuchaguzi mkuu wa Uganda uliofanyika mweziFebruari, 2016. Katika uchaguzi huo,Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafuwa Awamu ya Pili alipewa heshima ya kuwaKiongozi wa timu hiyo kutoka Jumuiya ya Afrika
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 105/126
99
Mashariki ambapo Mheshimiwa Rais YoweriKaguta Museveni aliibuka mshindi.
172. Mheshimiwa Spika, katikakuwashirikisha zaidi wananchi wa AfrikaMashariki kuchangia maoni yao katika maamuzimbalimbali ya uendeshaji wa Jumuiya, Wizara
yangu iliwawezesha Wananchi wa Tanzaniakupitia asasi zao kushiriki katika Mkutano waKatibu Mkuu wa Jumuiya na Asasi Zisizo zaKiserikali na Sekta Binafsi uliofanyika mweziMachi, 2016 Dar es Salaam, Tanzania. Maazimio
ya Mkutano huo yalikuwa ni pamoja nakuliomba Baraza la Mawaziri la Jumuiyakuharakisha matumizi ya vituo vya utoaji wahuduma kwa pamoja mipakani, utekelezaji wahimaya moja ya forodha; na kushirikisha sektabinafsi katika ngazi zote za mchakato wauchaguzi ili kuweka mazingira mazuri yakufanya shughuli zao.
Bunge la Afrika Mashariki
173. Mheshimiwa spika, Wizara iliratibuna kushiriki katika mikutano ya Bunge la AfrikaMashariki, ambapo Bunge hilo lilijadili nakupitisha Miswada ya Sheria za Jumuiya,Maazimio na Taarifa mbalimbali. Miswadailiyopitishwa ni pamoja na Muswada wa Sheria
ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Kupunguza
na Kukabiliana na Majanga wa mwaka 2012;
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 106/126
100
Muswada wa Sheria ya Jumuiya ya AfrikaMashariki ya Miamala ya Kielektroniki wamwaka 2014; Muswada wa Sheria ya Jumuiya
ya Afrika Mashariki wa Tasnia ya Ubunifu naUtamaduni wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wamwaka 2015; na Muswada wa Sheria ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Usimamizi naUhifadhi wa Misitu wa mwaka 2015.
174. Mheshimiwa spika, aidha, Miswadailiyosomwa Bungeni kwa mara ya kwanza ni:Muswada wa Sheria ya Jumuiya ya AfrikaMashariki ya Usawa wa Jinsia na Maendeleo wamwaka 2016; Muswada wa Sheria ya Jumuiya
ya Afrika Mashariki ya Kulinda Watoa Taarifawa mwaka 2016; Muswada wa Sheria ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki wa Mafao yaKustaafu kwa baadhi ya Wakuu wa Taasisi za
Jumuiya ya Afrika Mashariki wa mwaka 2016;Muswada wa Sheria ya Jumuiya ya AfrikaMashariki wa Marekebisho ya Sheria yaUsimamizi wa Forodha ya Afrika Mashariki wamwaka 2016; na Muswada wa Sheria ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki wa KuzuiaUsafirishaji Haramu wa Binadamu wa mwaka2016.
175. Mheshimiwa spika, Vilevile, Bungelilitoa Maazimio kwa Nchi Wanachama wa
Jumuiya ya Afrika Mashariki na kusisitiza
Kuridhia Itifaki ya Umoja wa Afrika ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 107/126
101
kuanzisha Bunge la Afrika; Kuridhia Itifaki yaSheria ya Ushauri ya Umoja wa Afrikainayohusiana na Bunge la Afrika; Kumpongeza
Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri yaMuungano wa Tanzania kwa ushindi wakekatika uchaguzi Mkuu pamoja na wananchi wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwakudumisha Amani na Demokrasia wakati waUchaguzi; Azimio la Bunge la Kuzitaka NchiWanachama wa Jumuiya ya Afrika Masharikikuchukua hatua za haraka katika kudhibitiUsafirishaji haramu wa binadamu; na Azimio laBunge la kuwashukuru Wake wa Viongozi waNchi Waanzilishi wa Jumuiya ya AfrikaMashariki.
176. Mheshimiwa spika,
Kamati yaBunge la Afrika Mashariki ya Masuala yaKikanda na Utatuzi wa Migogoro ilifanya ziara yaUangalizi na tathmini ya changamoto zautekelezaji wa Itifaki ya Soko la Pamoja katikaKanda ya Kati mwezi Novemba 2015. Kamati
hiyo na Uongozi wa Wizara ilijadili hali halisi yautekelezaji wa makubaliano ya Itifaki hiyohususan katika kanda ya kati ambapo kati yamasuala yaliyoibuliwa ni kuhusu afya yaWananchi katika kutumia uhuru wa watu wa
Jumuiya kuingia na kutoka Nchi za Jumuiyaambapo walisisitiza kuhusu umuhimu wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 108/126
102
Chanjo ya Homa ya Manjano ili kuzuiauambukizaji wa ugonjwa huo.
177. Mheshimiwa Spika, Kamatimbalimbali za Bunge la Afrika Masharikizilifanya mikutano ya kukusanya maoni yawadau kuhusu utungwaji wa sheria mbalimbaliza Jumuiya ambapo Kamati ya Mawasiliano,Biashara na Uwekezaji ilikusanya maoni yaMuswada wa Sheria ya Sectional Properties Bill,
2016 , Kamati ya Kilimo, Maliasili na Mazingirailikusanya maoni kuhusu Muswada wa Sheria
ya Usimamizi na Uhifadhi wa Misitu wa AfrikaMashariki wa mwaka 2015 na Kamati yaGeneral Purpose ilikusanya maoni kuhusuMuswada wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavuwa mwaka 2015.
178. Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibuProgramu ya Wabunge wa Tanzania katikaBunge la Jumuiya ya kutoa elimu kwa ummailiyohusisha Vyombo vya Habari, Taasisi zaElimu, Asasi za Kiraia, Wabunge na Maafisa waSerikali mwezi Aprili, 2016. Lengo la programu
hiyo pamoja na mambo mengine nikuhamasisha umma juu ya fursa zitokanazo na
Jumuiya ili kunufaika nazo.
Ushirikiano katika Ulinzi
179. Mheshimiwa Spika, ili kuimarisha
uwezo wa vyombo vya ulinzi na usalama vya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 109/126
103
Nchi Wanachama katika urejeshaji amaniwakati wa machafuko, kukabiliana na ugaidi,uharamia na majanga, Wizara iliratibu ushiriki
wa Tanzania katika zoezi la kijeshi kwa vyombovya ulinzi na usalama kutoka nchi Wanachamawa Jumuiya ya Afrika Mashariki la Vituo vyaKamandi lijulikanalo kama ‘ Ushirikiano Imara
2016’ . Zoezi hilo lilifanyika mwezi Machi 2016nchini Kenya.
Ushirikiano katika Usalama
180. Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatiakuwa amani na usalama ni nguzo kuu kwamaendeleo ya kijamii na uchumi katika
Jumuiya, Wizara yangu iliratibu ushiriki wa Tanzania katika mkutano wa Wakuu waUpelelezi toka Jeshi la Polisi, Wasajili wa Magari,Wakuu wa Kupambana na Madawa ya Kulevyana Wakuu wa Vitengo vya Kupambana naBiashara Haramu ya Watu uliofanyika mweziDesemba 2015 Nairobi, Kenya. Mkutano huoulitoa fursa kwa wakuu hao kubadilishana
uzoefu na taarifa za mienendo ya uhalifu katikamaeneo yao na kupanga mpango wa pamoja waoperesheni za kupambana na uhalifu. Aidha,Nchi Wanachama zinaendelea kutekelezaMkakati wa Kikanda wa Amani na Usalama.
181. Mheshimiwa Spika , napenda
kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa Jamhuri ya
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 110/126
104
Sudan Kusini imejiunga rasmi na Jumuiya nahivyo kuifanya idadi ya Nchi Wanachamakuongezeka kutoka tano hadi sita. Nchi ya
Sudan Kusini, iliwasilisha rasmi maombi yakujiunga na Jumuiya mwezi Novemba, 2011.Nchi Wanachama zilikamilisha mchakato wauhakiki kuthibitisha iwapo nchi hiyo inakidhivigezo kulingana na matakwa ya Mkataba waUanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.Mkutano wa 17 wa Wakuu wa Nchi Wanachama
uliofanyika mwezi Machi 2016 jijini Arushauliridhia nchi hiyo kujiunga na Jumuiya.
182. Mheshimiwa Spika, Wakuu wa Nchiwanachama wa Jumuiya walimpa heshimaMheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Raiswa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania naMwenyekiti wa Mkutano wa Wakuu wa NchiWanachama wa Jumuiya kusaini Mkataba wa
Jamhuri ya Sudan Kusini kujiunga na Jumuiyakwa niaba yao. Zoezi la utiaji saini Mkatabahuo, lilifanyika Dar es Salaam tarehe 15 Aprili,2016.
183. Mheshimiwa Spika, kujiunga kwa Jamhuri ya Sudan Kusini kumeifanya Jumuiyakuwa na jumla ya watu zaidi ya milioni 160, hiini fursa ya kipekee kwa sekta binafsi hapanchini katika kuendeleza na kukuza biasharazao. Naomba kuchukua nafasi hii kuishauri
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 111/126
105
sekta binafsi hapa nchini kuchangamkia fursazitokanazo na kupanuka kwa soko la Jumuiya.
Kutoa elimu ya Mtangamano wa AfrikaMashariki ili Wananchi waweze kuelewa nakutumia fursa zitokanazo na Mtangamano.
184. Mheshimiwa Spika, Wizaraimeendelea kutekeleza Mkakati wake waMawasiliano kwa kutoa Elimu kwa Umma
kuhusu fursa zilizopo katika Jumuiya ya AfrikaMashariki na jinsi ya kunufaika nazo. Wizarailitumia maonesho mbalimbali kama vile ya Wiki
ya Utumishi wa Umma, Saba Saba, Nane Nane,Maonesho ya Biashara Zanzibar, maonesho yaSiku ya Mara, Maonesho ya Siku yaWafanyakazi Duniani na Juakali/Nguvu Kazi ya
Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoa elimu kwaUmma. Jumla ya nakala za machapisho 11,046
yenye taarifa muhimu na fursa zipatikanazokwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki
yalisambazwa na jumla ya wananchi 7,387walitembelea Mabanda ya Wizara ili kupata
taarifa na ufafanuzi wa masuala yamtangamano. Taarifa za maonesho hayozilisambazwa kupitia vyombo mbalimbali vyahabari ikiwemo Luninga, tovuti na blogu yaWizara. Vilevile, makala ya Televisheni yenyeujumbe wa fursa mbalimbali za Jumuiya yaAfrika Mashariki ilioneshwa katika Luninga za
TBC1, Star TV, Channel 10 na Clouds TV .
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 112/126
106
185. Mheshimiwa Spika, Wizara yanguiliweka mabango saba katika mipaka yaNamanga, Horohoro, Holili, Sirari, Mutukula,
Rusumo na Kabanga yenye kuelezea taratibu zakufuatwa na wafanyabiashara wakati wa kuuzana kununua bidhaa ndani ya Jumuiya ya AfrikaMashariki.
186. Mheshimiwa Spika, Wizarailiendesha mikutano ya elimu kwa umma katikaMikoa ya Mwanza, Kilimanjaro, Arusha, Tanga,Mara, Kagera, Mtwara, Lindi na katika mipaka
ya Mutukula, Rusumo, Kabanga, Holili naNamanga. Aidha, Wizara iliendesha warsha yaWaandishi wa Habari wa Zanzibar kwa lengo lakuwaelimisha juu ya fursa na masuala yaMtangamano ili waweze kufikisha taarifa sahihiza Mtangamano kwa wananchi.
Kuimarisha Utendaji na Kujenga Uwezo waWizara
187. Mheshimiwa Spika, Wizara
iliendelea kuimarisha uwezo wa kiutendaji kwakupandisha vyeo watumishi 20 baada yakukidhi Vigezo vya Kisheria kamavilivyoainishwa katika Miundo yao ya Utumishipamoja na kutengewa fedha katika Makisio yaIkama na Bajeti ya Mishahara ya Wizara kwamwaka wa fedha 2015/2016. Aidha, Wizara
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 113/126
107
iliwabadilisha kada jumla ya watumishi watatuwa kada tofauti baada ya kujiendelezakitaaluma wakiwa kazini na kupata sifa stahiki.
Vilevile, watumishi 29 wamethibitishwa kazinina watumishi 15 wa kada mbalimbaliwalithibitishwa katika vyeo vyao vipya baada yakukidhi vigezo.
188. Mheshimiwa Spika , katikakuhakikisha kuwa Wizara inawajengea uwezowa kitaaluma watumishi wake ili wawezekutekeleza majukumu yao kwa weledi naufanisi, Wizara iliandaa na kutekeleza mpangomdogo wa mafunzo kwa mwaka wa fedha2015/2016 ambao hadi kufikia mwezi Februari2016 watumishi wawili (2) walihudhuriamafunzo ya muda mrefu na watumishi tisa (9)walihudhuria mafunzo ya muda mfupi. Mpangohuu mdogo ni utekelezaji wa mpango wamafunzo wa Wizara wa miaka mitatu kuanziamwaka 2015/2016 hadi 2017/2018.
USIMAMIZI WA MAPATO NA MATUMIZI
189. Mheshimiwa Spika, Wizaraimeendelea kuimarisha usimamizi nauwajibikaji katika Mapato na Matumizi ya Fedhaza Umma kwa kuzingatia sheria na kanuni zafedha za umma. Napenda kuliarifu Bunge lako
Tukufu kwamba, Wizara imeendelea kupata Hati
Safi ya Ukaguzi wa Hesabu. Kwa mujibu wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 114/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 115/126
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 116/126
110
kwenye taasisi za kikanda na kimataifazinapotangazwa;
iv. Kuendelea kuratibu uondoaji wavikwazo visivyo vya kiforodha nchini ilikuwavutia wafanyabiashara kutokandani ya Jumuiya kununua bidhaazinazozalishwa nchini na kutumiabandari zetu kikamilifu; na
v. Wizara itaendelea kuimarisha Balozizetu na kufungua ofisi za uwakilishikwenye maeneo yenye maslahi kwataifa.
SHUKRANI
192. Mheshimiwa Spika, Wizara imefanikiwakutekeleza sehemu ya majukumu yaliyotajwahapo juu kwa ushirikiano na washirika wamaendeleo kutoka nchi na asasi mbalimbali zakitaifa, kikanda, kimataifa pamoja na sektabinafsi. Naomba nitumie fursa hii kuwashukuruwashirika wetu wote wa maendeleo ikiwa ni
pamoja na Australia, Brazil, Canada, China,Cuba, Denmark, Finland, India, Italia, Ireland,
Japan, Korea Kusini, Kuwait, Malaysia,Marekani, Malta, Norway, Oman, Poland, Qatar,Sweden, Ubelgiji, Ufaransa, Uhispania,Uholanzi, Uingereza, Ujerumani, Umoja waFalme za Kiarabu, Ureno, Urusi, Uswisi,
Uturuki, Umoja wa Ulaya, AfDB, African
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 117/126
111
Capacity Building Facility, FAO, IAEA, ILO, IMF,IOM, Investment Climate Facility forAfrica,UNDP, UNEP, UN-HABITAT, UNWTO,
UNHCR, UNICEF, UNFPA, UNESCO, UNIDO,WHO, TradeMark East Africa, The Association ofEuropean Parliamentarians with Africa, WorldBank na WWF kwa mchango wao mkubwakatika kufanikisha utekelezaji wa Diplomasia yauchumi.
MALENGO YA WIZARA KWA MWAKA WA
FEDHA 2016/2017
193. Mheshimiwa Spika, katika mwakawa fedha 2016/2017, pamoja na mambomengine, Wizara ya Mambo ya Nje naUshirikiano wa Afrika Mashariki imepangakutekeleza malengo makuu muhimu kulinganana majukumu yake kama ifuatavyo:-
i. Kuitangaza nchi yetu kama moja yanchi duniani zenye mazingira mazurikwa ajili ya uwekezaji kutokana na
historia yake ya miaka mingi ya amani,umoja, utulivu na mshikamano wakitaifa;
ii. Kuongeza uwakilishi wetu nje ya nchikwa kufungua Balozi mpya, Ofisi zaKikonseli na kuimarisha rasilimali watuna fedha;
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 118/126
112
iii. Kuendelea kusimamia, kufuatilia nakuratibu utekelezaji wa mikatabambalimbali iliyosainiwa kati ya nchi
yetu na nchi nyingine na ile yamashirika ya kikanda na kimataifa;
iv. Kukamilisha mchakato wa kuitambua jumuiya ya watanzania wanaoishiughaibuni na kuweka utaratibuutakaowawezesha kuchangia maendeleo
ya taifa;
v. Kuratibu majadiliano kuhusu maeneo ya ushirikiano katika uendelezaji wamiundombinu ya kiuchumi, kijamii nakuendeleza ushirikiano katika sekta zauzalishaji;
vi. Kuratibu utekelezaji wa Mpango Kaziwa miaka kumi wa Umoja wa Fedhakatika kuelekea kwenye eneo la SarafuMoja ya Jumuiya ya Afrika Mashariki;
vii. Kuratibu majadiliano na kusimamiautekelezaji wa makubaliano ya
ushirikiano wa kiuchumi kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jumuiya nyingine za Kikanda kuhusukuanzisha Eneo Huru la Kibiashara naKiuchumi;
viii. Kuratibu, kushiriki na kusimamia
majadiliano na utekelezaji wa
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 119/126
113
makubaliano katika maeneo ya siasa,ulinzi na usalama;
ix. Kuratibu, kushiriki na kusimamiamajadiliano na utekelezaji wa hatua zaMtangamano wa Afrika Mashariki; na
x. Kutoa Elimu kwa Umma kuhusu Jumuiya ya Afrika Mashariki na fursazinazopatikana katika Jumuiya hiyo.
MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA
WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017
194. Mheshimiwa Spika, ili kuwezakutekeleza kikamilifu majukumu, kwa mwakawa fedha 2016/2017 Wizara imepangiwa bajeti
ya kiasi cha shilingi 151,396,775,000.00 Kati yafedha hizo shilingi 143,396,775,000.00 ni kwaajili ya Matumizi ya Kawaida na shilingi8,000,000,000.00 ni kwa ajili ya bajeti yaMaendeleo.
195. Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya
Matumizi ya Kawaida ya Wizara kwa mwaka wafedha 2016/2017, shilingi 133,056,021,000.00ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo na shilingi10,340,754,000.00 ni kwa ajili ya Mishahara.Kati ya fedha za Matumizi Mengineyo shilingi720,160,000.00 ni kwa ajili ya Mpango waKujitathmini Kiutawala Bora Tanzania, shilingi
3,154,721,000.00 ni kwa ajili ya fedha za
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 120/126
114
Mishahara na Matumizi Mengineyo ya Chuo chaDiplomasia na shilingi 686,298,378.00 ni kwaajili ya Mahakama ya Afrika ya Haki za
Binadamu na Watu.
196. Mheshimiwa Spika, katika fedha za
bajeti ya maendeleo za kiasi cha shillingi8,000,000,000.00 zilizopangwa kwa mwaka wafedha 2016/2017, kiasi cha shilingi2,375,250,000.00 zitatumika kufanikisha ujenzi
wa jengo la ofisi ya Wizara ambalo ni sehemu yaKituo cha Mikutano ya Kimataifa cha JuliusNyerere; shilingi 1,316,435,000.00 zitatatumikakukamilisha ukarabati jengo la ghorofa tisa (9),makazi ya Balozi na Mkuu wa Utawala Ubaloziwa Tanzania Maputo, Msumbiji; shilingi2,172,880,000.00 zitatumika kukarabati makazi
ya Balozi na watumishi yaliyopo Stockholm,Sweden; shilingi 1,813,871,000 zitatumikakukarabati majengo mawili yanayomilikiwa naSerikali yaliyopo Khartoum, Sudan na shilingi321,564,000.00 kwa ajili ya kuboresha mfumowa mawasiliano kati ya Wizara na Balozi za
Tanzania nje.
197. Mheshimiwa Spika, katika mwakawa fedha 2016/2017, Wizara kupitia Balozizake, inatarajia kukusanya kiasi cha shilingi24,001,150,000.00 kama maduhuli ya Serikali.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 121/126
115
HITIMISHO
198. Mheshimiwa Spika, ili kuweza
kutekeleza kikamilifu majukumu yaliyotajwahapo juu, kwa mwaka wa fedha 2016/2017,naomba Bunge lako Tukufu liidhinishe jumla yaShilingi 151,396,775,000.00. Kati ya fedha hizoShilingi 143,396,775,000.00. ni kwa ajili yaMatumizi ya Kawaida na Shilingi8,000,000,000.00. ni kwa ajili ya Bajeti yaMaendeleo.
199. Mheshimiwa Spika, naombakuchukua nafasi hii kukushukuru wewe binafsi,na Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza.
200. Mheshimiwa Spika, naomba kutoahoja.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 122/126
116
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 123/126
117
Kiambatisho Na. 1
Kielelezo Na. 1: Urari wa biashara
0.00
200.00
400.00
600.00
800.00
1000.00
1200.00
US$Mil
Mwaka
Urari
wa
Biashara
Mauzo Nje
Manunuzi Nje
Chanzo: Taarifa ya Biashara ya Afrika Mashariki, 2014
Tufe Na. 1: Mgao wa Soko Baina ya Nchi Wanachama, 2014
Chanzo : Taarifa ya Biashara ya Afrika Mashariki, 2014
U S $ M i l
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 124/126
118
Kiambatisho Na.2
Hatua Iliyofikiwa Katika Ujenzi wa Vituo Vya Utoaji wa
Huduma kwa Pamoja Mipakani (One Stop Border Posts- OSBPs)
Na. Kituo Hatua ya UjenziIliyofikiwa kwa upande waTanzania
1. Holili/Taveta(Tanzania na Kenya)
Ujenzi umekamilika. Kituohiki kinafanya kazi kwamfumo wa kutoa huduma
kwa pamoja kuanzia mweziMei, 2015. Uzinduzi rasmiwa Kituo hiki ulifanyikamwezi Februari, 2016, HoliliMkoani Kilimanjaro.
2. Sirari/Isebania(Tanzania na Kenya)
Ujenzi umekamilika naMaafisa wamehamiakwenye majengo. Hatahivyo, kituo hakijaanza
kufanya kazi kwa mfumowa kutoa huduma kwapamoja kwa kuwa majengo
yake hayajaunganishwakwa mifumo ya Teknolojia
ya Habari na Mawasilianoili kuwezesha Maafisa wa
Tanzania kutoa hudumawakiwa upande wa Kenya
na Maafisa wa Kenya kutoahuduma wakiwa upande wa
Tanzania.
3. Mutukula/Mutukula(Tanzania na Uganda)
Ujenzi wa kituo hiki kwa
upande wa Tanzania
umekamilika ambapo
maafisa wamehamia
kwenye jengo. Upande wa
Uganda ujenzi upo kwenye
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 125/126
119
Kiambatisho Na.2
hatua za mwisho.
4. Namanga/Namanga(Tanzania na Kenya).
Ujenzi wa Kituo hiki kwaupande wa Tanzania
umekamilika tangu mwezi
Januari, 2015
Taasisi zinazotoa huduma
mpakani zimeshindwa
kuhamia kwenye Kituo hiki
kutokana na changamoto
ya samani, upatikanaji wamaji ya uhakika na
kutokamilika kwa Mfumo
wa TEHAMA. Jengo la
upande wa Kenya ujenzi
upo katika hatua za mwisho
kukamilika.
Matarajio ni kuwachangamoto zilizobainishwa
zitapatiwa ufumbuzi na
Kituo kuanza kutoa
huduma mwanzoni mwa
mwaka 2016/2017.
5. Kabanga/Kobero(Tanzania na Burundi).
Ujenzi kwa pande zote mbiliunaendelea.
6. Rusumo/Rusumo(Tanzania na Rwanda)
Ujenzi umekamilika. Kituohiki kilizinduliwa rasmi naRais wa Jamhuri yaMuungano wa TanzaniaMhe. Dkt John Pombe
Joseph Magufuli na Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe.Paul Kagame tarehe 6Aprili, 2016.
8/16/2019 Hotuba Ya Bajeti ya Wizara ya Mambo Ya Nje 2016
http://slidepdf.com/reader/full/hotuba-ya-bajeti-ya-wizara-ya-mambo-ya-nje-2016 126/126
Kiambatisho Na.2
Kituo hiki kilianza kutoa
huduma kwa mfumo wakutoa huduma kwa pamoja
mpakani tarehe 1 Machi,
2016 baada ya kukamilika
kwa miundombinu ya maji,
umeme na uwekaji wa
samani upande wa
Tanzania.
7. Horohoro/Lungalunga,(Tanzania na Kenya).
Ujenzi kwa upande waTanzania umekamilika na
maafisa wamehamia
kwenye jengo. Kituo
hakijaanza kufanya kazi
kwa mfumo wa kutoa
huduma kwa pamoja kwa
kuwa majengo
hayajaunganishwa na
Mfumo ya Teknolojia ya
Habari na Mawasiliano.