18
1 HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE MAADHIMISHO YA KITAIFA YA SIKU YA KUPIGA VITA DAWA ZA KULEVYA DUNIANI - BAGAMOYO, MKOANI PWANI,TAREHE 26 JUNI 2015 Mheshimiwa Dkt. Seif Rashid, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii; Mheshimiwa Eng. Everist Ndikilo, Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Ndugu Keneth Kaseke, Kamishna wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya; Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya; Viongozi na Watendaji Wakuu wa Serikali; Viongozi wa Vyama vya Siasa wakiongozwa na Chama Tawala; Dkt. Bwijo Bwijo, kutoka UNDP na Wawakilishi wa Jumuiya na Taasisi za Kimataifa; Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia; Wageni waalikwa;

HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA … · 2015. 6. 30. · HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

  • Upload
    others

  • View
    8

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

  • 1

    HOTUBA YA MHE. DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS

    WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWENYE

    MAADHIMISHO YA KITAIFA YA SIKU YA KUPIGA VITA

    DAWA ZA KULEVYA DUNIANI - BAGAMOYO, MKOANI

    PWANI,TAREHE 26 JUNI 2015

    Mheshimiwa Dkt. Seif Rashid, Waziri wa Afya na Ustawi

    wa Jamii;

    Mheshimiwa Eng. Everist Ndikilo, Mkuu wa Mkoa wa

    Pwani,

    Ndugu Keneth Kaseke, Kamishna wa Tume ya Kuratibu

    Udhibiti wa Dawa za Kulevya;

    Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya;

    Viongozi na Watendaji Wakuu wa Serikali;

    Viongozi wa Vyama vya Siasa wakiongozwa na Chama

    Tawala;

    Dkt. Bwijo Bwijo, kutoka UNDP na Wawakilishi wa

    Jumuiya na Taasisi za Kimataifa;

    Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia;

    Wageni waalikwa;

  • 2

    Mabibi na Mabwana;

    Ndugu wananchi;

    Salamu na Shukrani

    Nakushukuru sana Mheshimiwa Dkt. Seif Rashid,

    Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na waandazi wa

    shughuli hii kwa kunialika na kunishirikisha katika Siku ya

    Kupiga Vita Dawa za Kulevya Duniani. Natoa pongezi

    nyingi kwa wananchi na viongozi wa Mkoa wa Pwani

    wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Eng. Evarist Ndikilo

    kwa kukubali kuwa wenyeji wa sherehe hizi. Baada ya

    kuona mabango na kusikia kauli kadhaa kutoka wasanii

    mmejidhihirishia ni jinsi gani mlivyojitayarisha kufanikisha

    hafla ya leo. Nawapongeza kwa kushirikiana vyema na

    Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya na

    kufanikisha maadhimisho haya. Mwisho nitoe pongezi

    zangu kwa TAYOA kutokana na ubunifu wao mzuri wa

    mawasiliano miongoni mwa vijana. Hongereni sana! Hakika

    mambo yamefana sana.

  • 3

    Aidha, nawashukuru kwa zawadi nzuri ya saa ambayo

    itakuwa inanikumbusha wakati wa kulala na kuamka.

    Kuadhimisha kupiga Vita Matumizi na Biashara

    Haramu ya Dawa za Kulevya

    Ndugu wananchi;

    Kama alivyoeleza Mwakilishi kutoka UNDP, Dkt.

    Bwijo Bwijo tarehe 26 Juni ya kila mwaka ni siku maalum ya

    kuadhimisha kupiga vita matumizi na biashara haramu ya

    dawa za kulevya duniani. Maadhimisho haya hutupa fursa

    ya kutafakari hatua tunazopiga katika jitihada zetu za

    kudhibiti biashara na matumizi ya dawa za kulevya katika

    jamii zetu na nchi yetu kwa jumla. Katika siku hii pia,

    pamoja na kufanya tathmini ya mafanikio na changamoto za

    mapambano hayo tunapanga mikakati ya kukabiliana na

    changamoto zilizopo kwa ufanisi zaidi.

    Tujenge Jamii, Maisha na Utu wetu bila Dawa za Kulevya.

    Ndugu wananchi;

  • 4

    Kila mwaka maadhimisho haya yanapofanyika

    huwepo kauli mbiu ambayo hutoa ujumbe unaosisitiza

    jambo lililokusudiwa wakati huo. Kauli mbiu ya mwaka huu

    ya, “Tujenge jamii, maisha na utu wetu bila dawa za

    kulevya” inatukumbusha sote kukaa mbali na matumizi na

    biashara ya dawa za kulevya. Dawa za kulevya ni hatari

    kwa maisha ya mwanadamu, utu wake na ustawi wa jamii

    yake. Kauli mbiu hii inatutaka tujenge jamii, maisha na utu

    wetu bila kujihusisha kwa namna yoyote ile na dawa za

    kulevya. Dawa za kulevya hazina manufaa yo yote bali

    hasara tele. Mapambano haya dhidi ya biashara na

    matumizi ya dawa za kulevya yanamhusu kila mmoja wetu

    wadogo kwa wakubwa, viongozi na wananchi wa kawaida,

    matajiri na maskini, Serikali Kuu na Serikali za Mitaa kwani

    athari zake humgusa kila mmoja wetu.

    Madhara ya dawa za Kulevya

    Ndugu Wananchi;

  • 5

    Ni jambo lililo dhahiri kuwa dawa za kulevya zina

    madhara makubwa sana. Matumizi na biashara ya dawa za

    kulevya inaathiri ustawi wa binadamu. Hudhoofisha afya za

    watumiaji, na huchochea kuenea kwa maambukizi ya virusi

    vya UKIMWI, homa ya ini na mara nyingi husababisha vifo.

    Hali kadhalika, huchochea rushwa miongoni mwa

    watumishi wa umma hasa wale wanaotegemewa kuongoza

    mapambano dhidi yake. Kwa mujibu wa tamko la

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la

    Kudhibiti Uhalifu na Dawa za Kulevya alilolitoa tarehe 5

    Juni, 2013 kwenye Mkutano wa mwaka wa Vyombo vya

    Udhibiti wa Dawa za Kulevya uliofanyika Moscow, watu

    wapatao 200,000 hupoteza maisha kila mwaka duniani

    kutokana na matumizi ya dawa za kulevya. Biashara ya

    dawa za kulevya imeleta changamoto kubwa kwa jumuiya

    ya kimataifa. Kwa baadhi ya nchi, biashara hii imekuwa ni

    janga kubwa ambalo limesababisha kuharibika kwa mifumo

    ya kiutawala na kisheria, uvunjifu wa amani na usalama,

  • 6

    kudorora kwa maendeleo ya kijamii na ya kiuchumi.

    Biashara hii huchochea kuwepo kwa magenge ya kihalifu

    yanayojihusisha na mauaji, wizi na ujambazi. Hali

    kadhalika, mapato yake yanafahamika kugharamia shughuli

    za ugaidi, usafirishaji haramu wa binadamu, biashara ya

    fedha haramu, biashara haramu ya silaha na uporaji wa

    nyara za taifa - vitendo ambavyo ni tishio kwa usalama wa

    dunia. Hivi basi kupiga vita biashara na matumizi ya dawa

    za kulevya ni vita vya haki na ni wajibu kwa kila mtu

    kushiriki. Lazima tushinde vita hii.

    Juhudi za Mapambano Kimataifa

    Ndugu wananchi;

    Mataifa mengi duniani yametambua madhara ya

    matumizi na biashara haramu ya dawa za kulevya. Pia watu

    wengi wanauona umuhimu wa kufanya juhudi za pamoja

    ndani ya nchi, kikanda na kimataifa kukabiliana na uhalifu

    huu. Matokeo yake ni kuanzishwa kwa Shirika la Umoja wa

  • 7

    Mataifa la Kudhibiti Uhalifu na Dawa za Kulevya. Pia, ni

    kufanyika kwa operesheni za pamoja za kupambana na

    biashara ya dawa za kulevya zinazofanywa na mataifa

    mbalimbali kikanda na kimataifa. Jambo lingine ni pamoja

    na kuwepo kwa mikutano ya pamoja kimataifa na kikanda

    kwa ajili kupanga mikakati ya pamoja.

    Naungana na viongozi wenzangu wa nchi mbalimbali

    duniani na mashirika wa kimataifa katika mapambano haya.

    Nakemea vikali matumizi na biashara ya dawa za kulevya

    na kuwaonya wananchi wajiepushe kabisa kujihusisha nazo.

    Ni imani yangu kuwa, Watanzania wenzangu mtafanya kila

    liwezekanalo kujiepusha na kuwaepusha watu wengine

    hasa vijana na watoto kujihusisha na balaa hili. Watanzania

    wenzangu tuongozwe na kauli mbiu ya TANU wakati wa

    kudai uhuru na kujenga nchi inasema, “Umoja ni nguvu

    utengano ni udhaifu”. Na kwa sasa kauli ya CCM isemayo,

    ”Umoja ni Ushindi”. Hakika umoja wetu ndio

    utakaotuhakikishia ushindi katika mapambano haya.

  • 8

    Vyombo vyetu Viko Macho

    Ndugu wananchi;

    Naomba niwahakikishie kuwa Serikali itaendelea

    kutimiza wajibu wake katika mapambano dhidi ya biashara

    na matumizi ya dawa ya kulevya bila kuchoka na bila

    kigugumizi au ajizi yoyote. Lengo letu ni kudhibiti hali ili

    kuzuia isizidi kuwa mbaya zaidi ya ilivyo sasa na kubadili

    mwelekeo ili hatimaye tulikomeshe kabisa tatizo hili hapa

    nchini. Kwa ajili hiyo, tumekuwa tunafanya mambo makuu

    matatu.

    Kwanza, kuimarisha vyombo vya dola vinavyoongoza

    mapambano dhidi ya uhalifu huo. Tunayo Tume ya

    Kudhibiti Dawa za Kulevya ambayo imefanya kazi kubwa

    ya kuelimisha jamii kujiepusha na matumizi na biashara ya

    dawa za kulevya. Tumeendelea kuijengea uwezo Tume

    hiyo pamoja na Jeshi la Polisi ambalo ndilo linalokamata

    wafanya biashara na watumiaji na kuwafikisha katika

  • 9

    vyombo vya Sheria. Pamoja na hayo nikaamua kuunda

    Kikosi Kazi kilichojumuisha Polisi, Idara ya Usalama wa

    Taifa na Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya. Kikosi Kazi

    hicho kimefanya kazi kubwa na nzuri. Kimeongeza nguvu

    na uwezo wa kupambana na uhalifu huu na wahalifu

    wanaojihusisha na biashara hii haramu na wanaotumia

    dawa za kulevya. Wafanya biashara wengi wadogo, wa kati

    na wakubwa wamekamtwa na kufikishwa kwenye vyombo

    vya sheria. Ukamataji wa Dawa za Kulevya nao

    umeongezeka sana na hivyo kunusuru taifa na hata dunia

    na madhara ambayo dawa hizo zingefanya. Tumezisikia

    takwimu zilizotolewa na Ndugu Keneth Kaseke, Kamishna

    wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya.

    Hiki ni kiwango kikubwa cha mafanikio hivyo vyombo

    vinastahili pongezi nyingi kutoka kwetu sote. Takwimu hizi

    zinatuonesha kuwa tatizo ni kubwa hivyo lazima tuwe

    katika hali ya tahadhari wakati wote (saa 24 kwa siku zote

    saba za wiki).

  • 10

    Pili, ili kuongeza nguvu, mbinu na maarifa ya

    kupambana na uhalifu huu wa hatari na kutisha, tumetunga

    Sheria (mpya) ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za

    Kulevya ya Mwaka 2015. Sheria hii imejengeka juu ya hali

    ilivyo sasa katika mapambano haya. Mafanikio na

    changamoto zilizopo imezingatiwa hivyo ni Sheria

    inayoimarisha mafanikio tuliyoyapata na kuyapatia

    ufumbuzi matatizo yaliyopo. Sheria inaunda chombo

    maalum cha kupambana na Dawa za Kulevya. Chombo hiki

    kitakuwa na nguvu kubwa zaidi ya kuratibu udhibiti wa

    dawa za kulevya nchini. Kimepewa mamlaka ya

    kupeleleza, kupekua na kukamata wafanya biashara na

    watumiaji wa dawa za kulevya. Nina imani kubwa kwamba

    chombo hiki kitasaidia sana kupunguza tatizo hili nchini.

    Natanguliza kuwaomba wananchi na vyombo vingine vyote

    vya Serikali kutoa ushirikiano wa kutosha kwa chombo hiki

    mara kitakapoanza kazi ili tuweze kulinusuru taifa letu na

    tatizo hili.

  • 11

    Huduma za Matibabu

    Ndugu wananchi;

    Kwa kuzingatia hekima na busara za usemi wa

    Wahenga, ”Kinga ni bora kuliko tiba”, mkakati wa

    kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya unasisitiza

    sana kuelimisha jamii kuhusu kuepukana na kujihusisha na

    biashara na matumizi ya dawa za kulevya. Kwa wale

    waathirika wa matumizi ya dawa za kulevya, mkakati ni wa

    Serikali kuendeleza jitihada za kuwapatia ushauri nasaha na

    matibabu. Hilo ndilo jambo letu la tatu. Kwa sasa huduma

    hizi zinapatikana katika vitengo vya magonjwa ya akili

    katika hospitali za baadhi ya mikoa na wilaya hata nchini.

    Hata hivyo, idadi ya watumiaji wanaopata nafasi ya kupata

    huduma za tiba bado ni ndogo sana. Takwimu zinaonesha

    kuwa kuna watumiaji wa heroin wanaokadiriwa kuwa kati

    ya 200,000 na 425,000 nchini. Idadi ya watumiaji wa heroin

    wanaopata matibabu kwa kutumia tiba ya methadone

  • 12

    mpaka kufikia Mei, 2015 ni 2,300 tu. Watu hawajitokezi kwa

    wingi. Tafadhalini ndugu zangu jitokezeni mpate uponyaji.

    Ninaiagiza mikoa yote hasa ile yenye matatizo

    makubwa ya matumizi ya dawa za kulevya hususani Dar es

    Salaam, Tanga, Arusha, Mwanza, Mbeya, Pwani na

    Shinyanga kuchukua hatua thabiti za kuanzisha na

    kuendeleza huduma hizi. Lazima tutambue pia, kwamba

    hakuna Mkoa ambao uko salama, tofauti ni kiwango cha

    athari. Hivyo basi kila Mkoa ujiandae ipasavyo. Tahadhari

    kabla ya hatari. Nawataka Viongozi wa Mikoa na Wilaya

    kote nchini wafuatilie utekelezaji wa jambo hili. Kamati za

    Ulinzi na Usalama za Mikoa na Wilaya ziliweke suala la

    dawa za kuleya kuwa agenda ya kudumu katika vikao vyao.

    Napenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wale wote

    waliosaidia katika kuanzisha na kuendeleza huduma ya

    methadone na huduma nyingine za matibabu nchini.

    Niruhusuni nitoe shukrani maalum kwa Rais Barack Obama

  • 13

    na Serikali ya Watu wa Marekani kwa msaada mkubwa

    wnaotupatia kwa upande wa matibabu.

    Tusiharibu Taswira ya Nchi yetu

    Ndugu wananchi;

    Narudia kuelezea masikitiko kuhusu baadhi ya

    Watanzania wenzetu wanaojihusisha na biashara ya dawa

    za kulevya nje ya nchi. Hawa ni chachu ya kuendelea kwa

    tatizo hapa nchini. Pia, wanaharibu taswira nzuri ya nchi

    yetu kimataifa na kuhatarisha maisha yao. Zipo taarifa

    kuwa kati ya Januari 2012 na Desemba 2014, kwa mfano,

    jumla ya Watanzania 111 walikamatwa kwa kujihusisha

    biashara hiyo katika nchi za Brazil na China. Hii ni fedheha

    kubwa. Pia, naomba niwakumbushe na kuwatahadharisha

    kuwa baadhi ya nchi hutoa adhabu kali ikiwemo ya kifo

    kwa watu watakaokamatwa na kutiwa hatiani. Mfano

    mmoja wapo ni wa yale yaliyotokea Indonesia kati ya

    Januari na Aprili 2015 ilipowanyonga wasafirishaji wa dawa

  • 14

    za kulevya 12 kutoka nchi mbalimbali zikiwemo za Afrika.

    Nchi hiyo ilikataa maombi ya nchi zao kutaka adhabu hiyo

    isitekelezwe dhidi ya raia wao.

    Akitetea uamuzi wa nchi yake Mwanasheria Mkuu wa

    Indonesia Muhammad Prasetyo baada ya hukumu

    kutekelezwa alisema;

    ‘Tunapigana vita dhidi ya uhalifu wa kutisha wa dawa za kulevya

    ambao unatishia mustakabali wa taifa letu. Napenda kusema

    kwamba kuua si jambo jema, si jambo la kufurahisha. Lakini

    lazima tufanye hivyo kwa ajili ya kuliokoa taifa na hatari ya dawa

    za kulevya. Hatufanyi uadui na nchi ambazo raia wake

    walihukumiwa kifo.’

    Nawaasa Watanzania wenzangu watambue ukweli

    huu na kuachana na biashara ya dawa za kulevya ndani na

    nje ya nchi yetu. Ni hatari kwao na taifa pia. Ingawa hapa

    nchini adhabu ya kifo haitolewi kwa kosa la kujihusisha na

    dawa za kulevya, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na

  • 15

    Dawa za Kulevya ya 2015 ambayo itaanza kutumika hivi

    karibuni inatoa adhabu kali hadi kifungo cha maisha.

    Tahadhari Dhidi ya Matumizi ya Shisha

    Ndugu wananchi;

    Kwa masikitiko makubwa, Serikali imepokea malalamiko

    mengi kuhusu matumizi ya shisha nchini. Matumizi haya

    yameenea kwa haraka katika maeneo mengi ya starehe na

    huwavutia vijana wengi wa kiume na wa kike. Watumiaji

    wa kilevi hiki huonyesha dalili zinazofanana na za utumiaji

    wa dawa za kulevya. Hivyo, kuna hofu kuwa kilevi hiki

    kinachanganywa na dawa za kulevya. Kama hiyo ni kweli ni

    jambo hili ni la kusikitisha sana, halikubaliki na kwamba

    hatuna budi kuhakikisha kuwa haliachwi kuendelea.

    Nichukue nafasi hii kuziagiza mamlaka husika kufanya

    uchunguzi haraka iwezekanavyo ili kupata majibu

    yatakayosaidia kutatua tatizo hili na hatimaye kuinusuru

    jamii yetu.

  • 16

    Tusiruhusu Rushwa Ijipenyeze

    Ndugu wananchi;

    Mapambano dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za

    kulevya si lelemama. Kuna changamoto kadhaa ikiwa ni

    pamoja na vishawishi vya rushwa. Vitendo vya rushwa kwa

    baadhi ya watendaji wasiokuwa waaminifu vinachangia

    sana katika kurudisha nyuma mapambano dhidi ya tatizo la

    dawa za kulevya. Natoa agizo kwa mamlaka husika

    kuhakikisha kuwa suala la rushwa linadhibitiwa kikamilifu

    katika mapambano haya kwa kuwachukulia hatua stahiki

    wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.

    Mjitokeze kwa Wingi Kujiandikisha

    Ndugu wananchi;

  • 17

    Wote mnatambua vema kuwa mwaka huu tutakuwa

    na uchaguzi wa viongozi katika ngazi mbalimbali katika

    Taifa letu. Nawaasa wananchi wenzangu muendelee

    kujitokeza kwa wingi katika kujiandikisha katika Daftari la

    Kudumu la Mpiga Kura. Wakati wa kupiga kura

    utakapofika, mtumie haki yenu ya kikatiba kuchagua

    viongozi waadilifu ambao kwa namna yoyote ile

    hawajihusishi na biashara au matumizi ya dawa za kulevya.

    Aidha, nawaasa wazazi na walezi, viongozi wa dini,

    viongozi wa asasi za kijamii, watambue kuwa hivi ni vita

    vyetu sote. Tatizo la dawa za kulevya likiachiwa bila

    kudhibitiwa kwa dhati litaleta maafa makubwa kwa kizazi

    cha sasa na kijacho. Kwa sababu hiyo, tunao wajibu wa

    kupambana kila mtu kwa nafasi yake. Tuwalee watoto wetu

    kwa misingi ya maadili mema ili kujenga Taifa lisilokuwa na

    matumizi wala biashara ya dawa za kulevya. Inawezekana

    Timiza Wajibu wako.

    Tujenge jamii, maisha na utu wetu bila dawa za kulevya

  • 18

    Asanteni kwa kunisikiliza.