Upload
others
View
29
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
Page 1 of 52
HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI NDUGU
KABWE ZUBERI ZITTO (MB), WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI, KUHUSU
MAPENDEKEZO YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA
SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014
(Inatolewa chini ya Kanuni ya 105(8) ya kanuni za Bunge Toleo la
mwaka 2013)
_________________________________
1. UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, Bajeti ya serikali kimsingi ni ‘policy instrument’
inayotolewa kama mpango wa hati ya mapato na matumizi. Aidha
hati hujumuisha makadirio ya makusanyo na matumizi ambayo
Serikali imetayarisha na fedha iliyotumia au ambayo itatumika kwa
mwaka ujao. Bajeti ya Serikali huoanisha makadirio ya fedha
yanayohitajiwa na Wizara zote, idara zinazojitegemea, Wakala na
Serikali za Mitaa kwa mwaka husika wa fedha. Bajeti ya Serikali ina
sehemu tatu, yaani; makadirio ya mapato, matumizi ya kawaida ya
kila siku na matumizi ya maendeleo. Matumizi ya kawaida na ya
maendeleo ndiyo hufanya jumla ya fedha yote inayotumiwa na
Serikali kwa mwaka wa fedha unaohusika. Bajeti ya Serikali pia
inajulikana kama Taarifa ya Mwaka wa Fedha ya nchi.
Page 2 of 52
Mheshimiwa Spika, katika Bajeti Mbadala za mwaka 2011/12 na
2012/13 Kambi Rasmi ya Upinzani ilipendekeza masuala kadhaa ili
kusaidia kuongeza mapato ya Serikali kwa upande mmoja na kwa
upande wa pili kusaidia kupunguza umasikini wa kipato kwa
wananchi wa kawaida na hivyo kuboresha maisha yao. Masuala
tuliyoyapendekeza ni pamoja na:
1. Kupunguza misamaha ya kodi hadi kufikia asilimia moja ya
pato la Taifa kama wenzetu wa Uganda na Kenya. Serikali
ilikubaliana na pendekezo hili kwa maneno lakini imeshindwa
kulitekeleza licha ya kutoa ahadi za kufanya hivyo kila mwaka.
Hivi sasa misamaha ya kodi imefikia asilimia 4.3 ya Pato la Taifa.
2. Kuongeza makusanyo ya mapato ya ndani hadi kufikia asilimia
20 ya Pato la Taifa. Katika Bajeti ya Mwaka huu Serikali
inatarajia kufikia lengo hili ambalo lilitolewa na Kambi ya
Upinzani Bungeni katiika bajeti zilizopita licha ya miaka yote
kubezwa kwamba haiwezekani. Iwapo Misamaha ya kodi
ikipunguzwa, utoroshaji fedha nje ukadhibitiwa na ukwepaji
kodi katika idara ya forodha ukapunguzwa, Tanzania inaweza
kukusanya asilimia 25 ya Pato la Taifa kama mapato ya ndani.
Bajeti mbadala ya upinzani inaelekea huko.
3. Kuongeza Kima cha chini cha mshahara kwa wafanyakazi wa
umma hadi Tsh 315,000 kwa Mwezi. Inashangaza kuwa katika
mwaka wa fedha 2013/14 Serikali imeshindwa hata kutangaza
Page 3 of 52
kima cha chini licha ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kueleza katika hotuba yake katika sherehe za Mei
Mosi huko Mbeya na Waziri wa Utumishi kuahidi kuwa kima cha
chini kitatangazwana Waziri wa Fedha.
4. Kuweka kiwango cha chini cha kodi ya Mapato kwa
mwananchi (PAYE) kuwa asilimia tisa (9) na kitozwe kwa
mapato yanayozidi Tshs 150,000. Kwa mwaka wa pili mfululizo
Serikali imeendelea kuwahadaa wafanyakazi nchini kwa
kushusha kiwango hicho kwa asilimia moja tu.
5. Kuifanyia marekebisho sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka
2004 kwa kufuta sehemu ya Kodi ya Mapato inayotoa fursa
kwa kampuni za madini kutumia sheria ya Kodi ya Mapato ya
mwaka 1973 iliyofutwa (grandfathering). Pendekezo letu
lilikuwa na lengo la kutaka kuweka mfumo wa ‘straightline
method of depreciation’ ya asilimia 20 badala ya sasa ambapo
Kampuni za Madini ufanya ‘100 percent depreciation’ kwenye
mitambo yao mwaka wa kwanza na hivyo kuchelewesha
kulipa ‘Corporate Tax’. Pendekezo hili ambalo lingeipatia
Serikali mapato mengi na kwa sasa bado halijatekelezwa kwa
Kampuni za madini zenye mikataba.
6. Kuanzishwa kwa Real Estate Regulatory Authority kama
tulivyofanya kwa mwaka uliopita na kwamba kila mwenye
nyumba ya kupangisha lazima atambuliwe na kulipa kodi
inavyostahili kutokana na biashara ya kupangisha
Page 4 of 52
nyumba/vyumba. Serikalibado haijatekeleza pendekezo hili,
hakuna sera ya nyumba na hivyo Serikali kupoteza mapato
mengi sana kwenye sekta ya nyumba, kodi za nyumba kuwa
juu sana na kuumiza vijana wanaoanza maisha na kutozwa
kwa mwaka mzima.
7. Kushushwa kwa tozo ya kuendeleza stadi (skills development
levy – SDL) kutoka asilimia sita (6) ya sasa mpaka asilimia nne
(4). Katika pendekezo hilo tulishauri kuwa waajiri wote walipe
kodi hii ikiwemo Serikali na Mashirika ya Umma. Serikali
imechukua pendekezo hili kwenye mapendekezo ya Bajeti ya
mwaka 2013/14 lakini bila kuhusisha mwajiri Mkuu, Serikali. Ni
vema kodi hii ilipwe na waajiri wote nchini na ishuke kuwa
asilimia 4.
8. Kuwepo na utaratibu wa kuweka stiker maalumu kwa kazi za
sanaa zinazotolewa na mamlaka za serikali kuonyesha uhalali
wa muuzaji wa kazi hizo ili wasanii wanaozitengeneza
wanufaike na kazi zao. Pendekezo hili lilikubaliwa na Serikali na
hivi sasa TRA na COSOTA wameanza kufanya kazi hii ili
kuhakikisha wasanii wetu wanafaidi jasho lao.
9. Kuzuia kabisa kusafirisha ngozi ghafi kwenda nje ya nchi na
badala yake kuwe na mpango wa kuziongezea thamani na
kuzitumia ngozi ghafi hapa nchini ili kuleta tija katika uchumi
wa taifa kwa kutengeneza ajira na kuongeza thamani ya
mauzo nje. Serikali iliamua kupandisha ushuru. Kambi ya
Page 5 of 52
Upinzani Bungeni inaamini kuwa kuna haja kubwa ya kuzuia
kuuza mazao ghafi nje ili kukuza ajira za ndani na kuongeza
thamani ya mauzo yetu nje.
10. Kujenga Mazingira ya ukuaji wa uchumi vijijini (rural
growth) kwa kuboresha miundombinu ya umeme, barabara,
maji na Umwagiliaji. Tulipendekeza kutumia shilingi bilioni 450
kila mwaka kwa ajili ya kutekeleza azma hii. Fedha hizi
zitasimamiwa na Mamlaka ya Maendeleo Vijijini (Rural
Development Authority) ambayo nayo tulipendekeza iundwe
chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Pendekezo hili Serikali imelidharau
na madhara yake ni kuwa maendeleo ya vijijini hayana uratibu
mzuri na hivyo kusahaulika kabisa.
11. Kukarabati Reli ya Kati na matawi yake ya Tanga - Arusha
na Mpanda. Tuliitaka serikali kutenga Tsh 443 bilioni kwa
RAHCO kwa ajili ya maendeleo ya reli nchini. Serikali imetenga
fedha kidogo sana kwenye miundombinu ya Reli. Mwaka huu
tunapendekeza kodi maalumu ya kuendeleza Reli.
12. Kujenga uwezo wa viwanda vya ndani ili kuviwezesha
kuzalisha na kuuza nje bidhaa za kilimo na mifugo
zilizoongezewa thamani. Tuliitaka serikali kupiga marufuku
uuzaji nje wa korosho ghafi kama ilivyovyo kwa ngozi ghafi kwa
kuanzia. Serikali haijaweka mkakati wowote wa kuhakikisha
korosho yote nchini inabanguliwa kabla ya kuuzwa nje.
Page 6 of 52
13. Kuboresha elimu na afya hasa kwa shule na
zahanati/Vituo vya Afya vilivyo katika maeneo ya vijijini kwa
kutoa motisha kwa wafanyakazi wa sekta hizi walio kwenye
Halmashauri za Wilaya. Tulipendekeza pia kuanzishwa kwa
posho za mazingira magumu ya vijiji sawa kwa kiwango cha
mara moja na nusu ya mishahara yao. Serikali haijatekeleza
pendekezo hili.
14. Kuanzisha pensheni ya uzeeni kwa wazee wote nchini
wenye umri wa zaidi ya miaka 60. Serikali ipo kimya kuhusu
suala hili muhimu sana kwa wazee nchini.
15. Kuanzisha Chuo Kikuu cha Mtwara (Mtwara University for
Petroleum Studies) ili kufundisha wataalamu wa kutosha wa
sekta ya Mafuta na Gesi na kuliandaa Taifa kuwa na wasomi
mahiri wa maeneo hayo na hivyo kufaidika na utajiri wa
Mafuta na Gesi uliopo nchini kwetu. Serikali ipo kuhusu
pendekezo hili ambalo lingeweza hata kupunguza matatizo
haya yanayoendelea mkoani Mtwara.
16. Kupunguza mzigo wa matumizi ya magari ya Serikali kwa
kupiga mnada baadhi ya ‘mashangingi’ na kuweka mfumo
wa kukopesha magari kwa watumishi wote wa umma
wanaostahili magari kama alivyofanya Gavana wa Benki Kuu
ya Tanzania. Katika Bajeti ya serikali ya mwaka ujao wa fedha
imeahidi kuwakopesha watumishi wake magari lakini hakuna
uhakika iwapo hilo liotafanyika.
Page 7 of 52
17. Aidha tulipendekeza hatua ili kuweza kukabiliana na
ukwepaji wa kodi unaofanywa na makampuni makubwa ya
kimataifa (Multinational Corporations) na hatimaye
kuliongezea taifa mapato. Hatua hizo ni pamoja na:
(i) Kutunga sheria kwa kuimarisha zaidi sheria ya Kodi ya
Mapato ya mwaka 2004 kwamba, mikopo ya makampuni
kwenye uwekezaji, kwa sababu za kikodi, isizidi asilimia 70
ya mtaji wote uliowekezwa na hii ianze mara moja bila
kujali mikataba iliyopo. Pendekezo hili limetekelezwa
kikamilifu.
(ii) Kutunga sheria kuhakikisha kwamba riba kwenye mikopo
kutoka Makampuni yanayohusiana (sister companies)
haitaondolewa kwenye kutoza kodi (not tax deductible).
Pendekezo hili limetekelezwa kikamilifu.
(iii) Kuhakikisha kwamba serikali inakusanya kodi kwa
kiwango cha asilimia 30 kama ‘ongezeko la mtaji’
(‘capital gains’) kutokana na mauziano ya Kampuni
yoyote ambayo mali zake zipo Tanzania. Pendekezo hili
limetekelezwa kikamilifu. Hata hivyo Wizara ya Nishati na
Madini imeshindwa kushirikiana na TRA kupata kodi ya
tshs 329 bilioni kutoka kampuni ya Mantra Resources
baada ya kuuza mradi wa Mkuju Uranium.
Page 8 of 52
Mheshimiwa Spika, baadhi ya mapendekezo yetu yalichukuliwa na
Serikali ya CCM na kuyafanyia kazi kama nilivyoonyesha hapo juu.
Kwa yale ambayo yalitekelezwa vizuri yameleta matokeo mazuri.
Lakini kuna mapendekezo mengine serikali imeyachukua lakini
imeshindwa kuyatekeleza kama ambavyo tulishauri. Licha ya
mapendekezo yaliyotekelezwa vizuri kuleta sifa kwa serikali, Kambi
Rasmi ya Upinzani itaendelea kuwaonyesha njia serikali na CCM ya
namna bora na rahisi ya kuiondoa nchi katika giza hili la uchumi na
lindi la umasikini lililotengenezwa na Serikali hii ya CCM kwa
makusudi lakini sasa inashindwa kuwa na mkakati makini wa kuweza
kutoka.
2. DENI LA TAIFA (FUNGU 22)
Mheshimiwa Spika, Deni la Taifa limeendela kuwa changamoto
kubwa Kwa uchumi wetu. Kukua Kwa Deni la Taifa kusababisha
bajeti ya Serikali kuendelea kuwa tegemezi na hivyo kushindwa
kutatua kero za kiuchumi za wananchi. Kwa bahati mbaya
wananchi wengi hawaelewi undani wa deni la taifa na athari zake
katika maisha yao ya kawaida. Jambo la kusikitisha ni kwamba
Serikali imekuwa ikitumia mwanya wa wananchi kutokufahamu kwa
undani athari za deni la taifa kuendelea kukopa mikopo mikubwa
yenye masharti ya kibiashara (kwa maana ya riba kubwa).
Kuendelea kukopa Kwa namna hiyo kunaendelea kuwabebesha
walipa kodi wa Tanzania mzigo mkubwa wa madeni ambayo
Page 9 of 52
yanazidi kufanya hali ya maisha kwa wananchi iendelee kuwa
ngumu kwa kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kulipa madeni
badala ya kuzitumia fedha hizo kugharamia miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali, deni la taifa liliongezeka kwa asilimia 38 kutoka
Shilingi trilioni 7.6 mwaka 2008 mpaka Shilingi trilioni 10.5 mwaka
2009/2010. Mwaka 2010/2011 deni hilo liliendelea kuongezeka
kutoka shilingi trilioni 10.5 na kufikia kiasi cha shilingi trilioni 14.441
Aidha, katika mwaka wa fedha 2011/2012 deni hilo liliendelea
kuongezeka zaidi kutoka shilingi trilioni 14.441 na kufikia kiasi cha
shilingi trilioni 16.975. Kwa mujibu wa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa
Taifa mwaka 2012, deni la taifa liliongezeka kwa kasi ya ajabu
kutoka shilingi trilioni 18.8 (Desemba 2011) hadi kufikia shilingi trilioni
22.7 (Desemba, 2012).
Mheshimiwa Spika, hata hivyo kwa mujibu wa hotuba ya Bajeti ya
Waziri wa Fedha aliyoisoma Juni 13, 2013 akiwasilisha bungeni
mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Mapato na Matumizi
kwa mwaka 2013/2014, hadi kufikia mwishoni mwa mwezi machi
2013, deni la Taifa lilikuwa limeongezeka tena na kufikia shilingi
trilioni 23.7. Kati ya hizo shilingi trilioni 18.3 zinawakilisha deni la nje,
ikiwa ni sawa na asilimia 77 ya deni lote la Taifa.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa
na CHADEMA inatumia fursa hii kuwajulisha wananchi wote wa
Page 10 of 52
Tanzania kwamba hali duni ya maisha waliyo nayo na umasikini
mkubwa walio nao unasababishwa kwa kiasi kikubwa na Serikali
kukopa mno nje jambo ambalo linaongeza ugumu wa maisha.
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inapenda pia kuwajulisha
wananchi kwamba jukumu la kulipa deni la taifa kimsingi ni la
wananchi na wanalilipa kwa njia mbali mbali zikiwemo kodi
mbalimbali jambo ambalo linafanya maisha yao yaendelee kuwa
magumu.
Kwa mfano ukichukuwa jumla ya deni la taifa, ukaligawanya kwa
idadi ya wananchi wote wa Tanzania, utakuta kwamba kila mtu
(bila kujali mtoto mchanga, mzee, mlemavu, mwanafunzi, asiye na
ajira nk) anadaiwa kiasi cha shilingi 526,977 kama inavyoonyeshwa
kwenye jedwali Na 1 hapa chini;
Jedwali Na. 1 Mgawanyo wa Deni la Taifa kwa Kila Mtanzania
DENI LA TAIFA1 IDADI YA WATU TANZANIA2
Shilingi 23,673,530,000,000 44,928,923
Deni la taifa ÷ Idadi ya Watu = Deni la Taifa kwa kila mtu
Hivyo; Sh. 23,673,530,000,000 ÷ 44,928,923 = Sh. 526,977
1 Deni la Taifa kwa Mujibu wa Hotuba ya Waziri wa Fedha ya tarehe 13 Juni, 2013 ni Shilingi Trilioni 23.7
2 Kwa Mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya 2012, Idadi ya Watu Tanzania ilikuwa ni 44,928,923
Page 11 of 52
Mheshimiwa Spika, ikiwa mtanzania masikini anayeishi chini ya dola
moja au shilingi 1,500 kwa siku angeamua kulipa deni hili kwa
shilingi 500 kwa siku ili abaki na shilingi 1,000 za kutumia kwa siku hiyo,
itamlazimu kulipa shilingi 15,000 kwa mwezi kama malipo ya deni la
taifa. Hii ina maana kwamba kwa mwaka mmoja atalazimika kulipa
180,000. Kwa maana hiyo, iwapo kila mtu angechukua jukumu la
kulipa deni hili la taifa kwa kiwango hicho, ingechukua miaka mingi
kumaliza kulilipa deni hilo.
Mheshimiwa Spika, kiasi hiki cha fedha cha shilingi 15,000 ambacho
kila mtanzania atatakiwa alipe kila mwezi kwa ajili ya deni la Taifa
kingekuwa kinabaki kwa mwananchi na akakifanyia ujasiriamali
angeweza kuondokana kabisa na umasikini. Hii ni kwa sababu
kiwango hicho hakina riba na atakuwa anakipata kwa miaka mitatu
mfululizo. Lakini kwa sababu Serikali imeamua kuwafukarisha
wananchi wake kwa kukopa kupita kiasi, sasa mwananchi
analazimika kurudi nyuma kimaendeleo kwa kutoa shilingi 15,000 kila
mwezi kwa miaka mitatu mfululizo kulipa deni la taifa. Fedha hizo
hazimjengi mwananchi kiuchumi bali zinambomoa kwa kuwa
zinatoka bila faida yoyote kwake.
Page 12 of 52
Mheshimiwa Spika, serikali imekuwa ikijinasibu kuwa inakopa fedha
hizi kwa ajili ya mitradi ya maendeleo. Lakini inashangaza kuwa
fedha hizo zilizokopwa zimetumika lakini miradi hiyo ambayo
imetumia fedha hizi haijaleta hayo maendeleo ambayo serikali
imekuwa ikiyasema na kumwondolea mwananchi wa kawaida
umasikini. Fedha hizo zimeendelea kutumika zikimwongezea
mwananchi deni na umasikini. Hii inathibitishwa na uhalisia kwamba
licha uchumi kukua kwa kasi ya asilimia saba kwa mwaka kwa
miaka kumi mfululizo, umasikini umepungua kwa asilimia mbili tu na
idadi ya watu masikini wa kutupwa imeongezeka kwa kiwango cha
watu milioni mbili na nusu katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita.
Mheshimiwa Spika, hali ya hatari zaidi ni kwamba kuna madeni
mengine ambayo hayajajumuishwa kwenye Deni la Taifa na hivyo
kulifanya Deni halisi la Taifa kuwa kubwa kuliko linaloonyeshwa
kwenye taarifa mbalimbali za Serikali na ile ya CAG. Kwa mfano,
kuna madai ya PSPF ya shilingi bilioni 716.6 kati ya madai ya shilingi
trilioni 6.5 ambayo Serikali imekubali kuyalipa.
Mheshimiwa Spika, katika taarifa hiyo ya CAG ya mwaka 2012, kuna
jumla ya shilingi bilioni 619 ambazo zipo kwenye Deni la Taifa lakini
hazina vithibitisho. Katika ripoti yake Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali ameandika: “Uhakiki wa mchanganuo wa
madeni ya Taifa kama ulivyokuwa tarehe 30 Juni 2012 ulibaini
kuwepo kwa marekebisho ya Deni ya shilingi 619.8 bilioni ambao
uongozi haukuweza kutoa maelezo ya kuridhisha”.
Page 13 of 52
Udhaifu kama huu unazua hisia kwamba kitengo cha Deni la Taifa
kinatumika kuiba fedha za umma kwa kisingizio kwamba ni malipo
ya Deni la Taifa. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na
CHADEMA inaitaka Serikali kutoa maelezo yaliyonyooka mbele ya
Bunge hili kuelezea ni kwanini shilingi bilioni 619.8 zimeongezwa
kwenye deni la taifa bila maelezo wala vielelezo vyovyote?
Uhimilivu wa Deni la Taifa
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa muda
mrefu imekuwa ikiitaka Serikali ipunguze au iachane kabisa na
mikopo yenye masharti ya kibiashara ambayo inazidi kuliongeza
Deni la Taifa. Kinyume na nia hii njema ya Kambi ya Upinzani ya
kujitegemea kibajeti, Serikali hii ya CCM imeendelea kupuuza
mawazo haya mazuri kwa kisingizio kwamba Deni la Taifa ni himilivu
na kwamba nchi yetu inakidhi vigezo vya kimataifa vya
kukopesheka.
Mheshimiwa Spika, kwa taarifa ni kwamba baadhi ya vigezo vya
kimataifa ambavyo Serikali inasema Tanzania imekidhi na hivyo
inaweza kukopesheka vimeshapitiliza ukomo wake na kwa maana
hiyo deni la taifa sio himilivu tena (Tazama Jedwali Na. 3).
Jedwali Na. 3 Matokeo ya Upimaji wa Uhimilivu wa Deni la Taifa
Kiashiria Matokeo (Asilimia) Ukomo
Deni la Taifa kwa sasa/Pato
la Taifa
18.9 50
Page 14 of 52
Chanzo: Kitabu cha Hali ya Uchumi 2012 uk. 77
Mheshimiwa Spika, matokeo ya upimaji wa uhimilivu wa deni la
taifa uliofanywa na Serikali kwa kutumia kigezo cha asilimia ya
uwiano wa Deni la Taifa na Pato la Taifa si ya kweli kwani kwa
kutumia hesabu rahisi tu za kugawanya na kutafuta asilimia ambazo
mwanafunzi wa darasa la pili anaweza kufanya ni kwamba tayari
tumeshavuka ukomo wa kukopesheka. Hii ni kwa sababu uwiano wa
deni la taifa na pato la taifa kwa sasa ni asilimia 53 wakati ukomo
wa kukopesheka ni asilimia 50. (Tazama Jedwali Na. 3)
Jedwali Na. 3 Uchambuzi wa Ustahimilivu wa Deni la Taifa
Kiashiria Matokeo (asilimia) Ukomo
Deni la Taifa ÷ Pato la Taifa
23.7tr ÷44.7tr = 0.53 0.53x100 = 53.02%
50
Chanzo: Uchambuzi wa Kambi ya Upinzani
Utata katika Deni la Taifa (Fungu 22)
Mheshimiwa Spika, mfumo wa sasa wa kuweka pamoja malipo ya
Deni la Taifa na malipo kutoka mfuko mkuu wa Hazina hauweki
uwazi wa kutosha. Jambo lenye utata katika fungu 22 - Deni la Taifa
- ni kwamba fungu hilo linajumuisha huduma za Mfuko Mkuu wa
Hazina (Consolidated Fund Services - CFS). Kwa mujibu wa
Randama ya Wizara ya Fedha, Idara ya Mhasibu Mkuu, Fungu 22 –
Deni la Taifa - jumla ya shilingi 870,717,882,000 zimetengwa ndani ya
Page 15 of 52
Mfuko Mkuu wa Hazina (ambazo zimechanganywa pamoja na Deni
la Taifa) kwa ajili ya ajili ya malipo mbalimbali kama ilivyooneshwa
kwenye jedwali Na 4.
Jedwali Na 4. Bajeti kwa ajili ya CFS Others
S/N NDANI YA CFS OTHERS KUNA MATUMIZI YAFUATAYO FEDHA
ZILIZOTENGWA
2013/2014
1. Mishahara ya Majaji, Makamishna wa Tume ya Haki za
Binadamu na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali
6,311,772,000
2. Mafao ya Wastaafu wanaofanya kazi kwa Mkataba 3,757,060,000
3. Stahili za Majaji 1,844,840.000
4. Michango ya Mwajiri kwa Watumishi wa Serikali Kuu na
Serikali za Mitaa kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.
556,809,310,000
5. Malipo ya Pensheni kwa ajili ya wastaafu hai, Mirathi,
watumishi walio katika Mikataba Serikalini na Stahili za
Majenerali kwa kila mwezi
213,498,000,000
6. Gharama za Huduma za Benki (bank charges) 6,400,000,000
7. Ada ya Usimamizi wa Amani za Serikali 1,700,000,000
8. Riba ya Mapungufu kati ya Mapato na Matumizi (Interest on
net deficit position)
80,000,000,000
9 Gharama za usafiri na malazi na posho kwa ajili ya uhakiki
na usuluhuishi wa taarifa za madeni.
396,900,000
JUMLA 870,717,882,000
Chanzo: Randama ya Wizara ya Fedha (Fungu 22) uk. 17
Page 16 of 52
Mheshimiwa Spika, mbali ya hayo fungu 21 kasma 290700
“contingencies non-emergency” kasma ndogo 290704: Domestic
Debts - Sh 436,721,151,000 ambayo matumizi yake yanaonyeshwa
kama: gharama za upigaji kura za maoni, kuhuisha Daftari la
wapiga kura kwa ajili ya uchaguzi ujao, kulipia madeni ya
wakandarasi na watumishi, gharama za Bunge la Katiba, deni la
HESLB kwa mfuko wa PSPF, mfuko wa maendeleo ya Jimbo, Ukaguzi
wa shule za msingi na Ssekondarina mengine mengi. Kambi Rasmi ya
Upinzani inaona kuwa matumizi haya hayana mtiririko unaoeleweka.
Kambi inaamini kuwa kuna uwezekano mkubwa fungu hili likatumika
kuweka fedha ambazo badaye zitakuja kukwapuliwa na wajanja.
Hivyo basi, inamtaka Mheshimiwa Waziri wa Fedha atoe uchambuzi
wa gharama ya kila kimoja kwani kurundika mambo yote kwenye
kapu moja kunaweza kusababisha jambo moja kulipwa hata mara
kumi na kusiwepo ushahidi wake wa malipo na pia watu wakikosa
ushahidi wa kuhoji.
Mheshimiwa Spika, kitendo cha kuchanganya deni la taifa na
matumizi haya ya fedha yanayohusu Mfuko Mkuu wa Hazina
kunaweza kutoa mwanya mkubwa wa ubadhirifu na matumizi
mabaya ya fedha za umma kwa kisingizio cha Deni la Taifa. Kwa
sababu hiyo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na
CHADEMA inataka mambo makubwa mawili yafanyike kama kama
ifuatavyo:
Page 17 of 52
1. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali afanye
ukaguzi maalum (Special Audit) katika kitengo cha Deni la
Taifa (fungu 22) ili tuweze kujua mikopo hii tunayoichukua
kila wakati inatumika kufanyia nini, na miradi iliyotekelezwa
kama ni miradi ya kipaumbele kwa mujibu wa mpango
wa taifa wa maendeleo. Aidha, ukaguzi huu maalum
utatuwezesha kama taifa kujua kiwango halisi cha Deni la
Taifa ambalo tunadaiwa.
2. Serikali itenganishe haraka iwezekanavyo deni halisi la
Taifa na matumizi mengine yanayohusu Mfuko Mkuu wa
Hazina (Consolidated Fund Services – Others) ili kuziba
mianya ya ubadhirifu au matumizi mabaya ya fedha za
umma kwa kisingizio cha Deni la Taifa. Tunapendekeza
kwamba Fungu namba 22 liwe la Deni la Taifa pekee na
Fungu lingine litengenezwe kwa ajili ya CFS.
3.0 UCHAMBUZI WA BAJETI YA SERIKALI.
3.1 KODI KWENYE MAFUTA
Mheshimiwa Spika, Waziri wa Fedha ameendeleza utaratibu wa kila
mwaka wa kupandisha kodi kwenye bidhaa zile zile ikiwemo mafuta
bila kutilia maanani kuwa kufanya hivyo kunahatarisha maisha ya
wananchi kwani kutaongeza gharama ya karibu kila kitu. Hotuba ya
Page 18 of 52
bajeti iliyowasilishwa na Serikali haijalenga kabisa katika kukuza
ustawi wa wananchi badala yake imejikita katika kuongeza mzigo
mkubwa wa umasikini kwa wananchi, kuongeza mfumuko wa bei
na kuzorotesha uchumi wa Tanzania kama nitakavyoelezea hapa
chini.
Wakati Bajeti ya mwaka 2012/13 ililenga kupunguza gharama za
maisha kwa mwananchi, Bajeti ya Mwaka 2013/14 kwanza haina
malengo mahususi na pili inafuta mafanikio yote yaliyopatikana
katika sera ya Bajeti ya mwaka uliotangulia.
Mheshimiwa Spika, moja ya vyanzo vipya vya mapato kwa mujibu
wa hotuba ya bajeti ya Waziri wa Fedha ni pamoja na ongezeko la
ushuru wa mafuta kama ifuatavyo.
i. Ushuru wa Dizeli umeongezwa kutoka shilingi 215 kiwango cha
sasa kwa lita hadi shilingi 217.
ii. Ushuru wa Petroli umeongezwa kutoka shilingi 339 kiwango cha
sasa kwa lita hadi shilingi 400, ikiwa ni ongezeko la shilingi 61.
Mheshimiwa Spika, Bajeti imeongeza pia tozo kwenye mafuta (fuel
levy). Kwa mujibu wa maneno ya Waziri kwenye hotuba yake ni
kwamba ameongeza tozo kwenye petroli peke yake lakini ukweli ni
kwamba, ongezeko hilo litaiathiri pia bei ya dizeli na hii ni kwa mujibu
wa Sheria ya Ushuru wa Barabara na Mafuta Sura 220 (the Road
and Fuel Tolls Act). Neno ‘fuel’ limetafsiriwa kama ‘petroli aina ya
supa, au kawaida, na dizeli kwa matumizi ya kuendeshea gari’
Page 19 of 52
("fuel" means petrol, whether super or regular, and diesel for use in
the propulsion of a vehicle).
Mheshimiwa Spika, kwa mapendekezo hayo ya Serikali, shilingi 63
kwa lita inaongezeka kwenye gharama za mafuta. Hii itaathiri bei ya
mafuta ya dizeli na petroli, na si petroli peke yake. Hata hivyo, hilo si
ongezeko peke. Kuna ongezeko zaidi lipo kwenye mapendekezo ya
Serikali kupitia hotuba ya Waziri wa Fedha Ukurasa wa 77 la ushuru
wa Petroli (petroleum levy) wa kiwango cha shilingi 50 kwa lita.
Mheshimiwa Spika, ni vyema Bunge lako tukufu na wananchi
wakaelewa kwamba ‘petroleum’ inahusisha nishati zote za mafuta
katika hali ghafi kwa kuwa aina nyingine zote za mafuta
zinatengezwa kutokana na petroleum), ikiwa ni pamoja na gesi
katika hali kimiminika (liquid gas), grisi (grease), parafini (paraffin)
dizeli, mafuta ya taa, mafuta ya ndege.
Na kwa mujibu wa Sheria ya Uhifadhi wa Petroleum - the Petroleum
(Conservation) Act, Sura ya 392, Petroleum imetafisiriwa kama
("petroleum" includes any inflammable liquid or liquid gas made
from petroleum, coal, schist, shale, peat, or any other bituminous
substance or from any product of petroleum).
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa hotuba hiyo, majumuisho ya
maongezeko mahusui ya moja kwa moja ya ushuru katika mafuta
ya dizeli, petroli, na mafuta ya taa, na ongezeko la ujumla la
petroleum yanatoa jumla inayoonekana kwenye jedwali hapa chini.
Page 20 of 52
AINA YA
MAFUTA
ONGEZEKO
MAHUSUSI
(shilingi)
FUEL LEVY
(shilingi)
ONGEZEKO LA
JUMLA(PETROLEUM)
(shilingi)
JUMLA
(shilingi)
Dizeli 2 63 50 115
Petroli 61 63 50 174
Mafuta
ya taa
- - 50 50
Mheshimiwa Spika, ongezeko hili ni dhahiri kuwa linakwenda
kuongeza gharama za usafirishaji mali, gharama za usafirishaji
chakula, gharama za uzalishaji malighafi na bidhaa kwenye
viwanda vidogo na vikubwa, yanaenda kuongeza mfumuko wa bei,
na matokeo yake kupaisha gharama za maisha kwa jumla yake na
kudumisha umasikini nchini.
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na
CHADEMA inapinga kubadilisha sheria ya Petroli sura 392 na
kuongeza kitu kinaitwa ‘Petrolium Levy’ kwa ajili ya kuongeza shilingi
50 kwa kila lita ya mafuta na ziweze kupelekwa REA. Kiasi ambacho
kitakusanya kupitia ushuru huu ni shilingi bilioni 123.725 kwa mwaka
ujao wa fedha.
Page 21 of 52
Hatupingi wazo la kuongeza fedha kwa ajili ya REA, siku zote kambi
ya Upinzani imekuwa ikitaka REA kuwezeshwa zaidi ili kubadilisha
maisha ya wananchi vijijini kwa kuwapa nishati ya Umeme. Fedha
hizi zingeweza kupatikana kwa njia nyingine ambazo hazimuumizi
mwananchi. Serikali imekwepa jukumu la kupunguza matumizi yasio
ya lazima ili kupata fedha za miradi ya maendeleo na badala yake
inakwenda kwenye njia rahisi lakini zenye kumuumiza mwananchi.
Ikumbukwe kwamba mwaka 2012/13 Bunge lilitenga zaidi ya shilingi
bilioni 300 kwa ajili ya umeme vijijini lakini fedha zote hizo
hazikwenda REA na badala yake zikaenda kununua mafuta ya
kuendesha mitambo ya kukodi ili kuzuia mgawo wa umeme.
Hakuna dhamana yeyote kuzuia fedha hizi zitakazopatikana
kutokana na kuongeza ushuru wa mafuta kwenda kuwanufaisha
asilimia 18 tu ya Watanzania ambao wameunganishwa kwenye
mtandao wa umeme.
Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Bajeti Mheshimiwa Waziri
amependekeza kufanywa kwa marekebisho ya sheria ya ushuru wa
mafuta na kuongeza kodi ya fuel levy kutoka shilingi 200 kwa lita
hadi shilingi 263 kwa lita kiasi ambacho ni sawa na ongezeko la
asilimia 31.5. Waziri wa Fedha amesema hatua hii inalenga
kuiongezea serikali mapato ya kiasi cha shilingi bilioni 155.893 katika
mwaka ujao wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya
barabara. Kambi ya Upinzani Bungeni inapinga nyongeza hii kwani
itaongeza gharama za maisha kwa mwananchi.
Page 22 of 52
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza
kwamba Bunge likatae mapendekezo yote ya kuongeza kodi
kupitia The Road and Fuel Tolls act Sura ya 220, Sheria ya Ushuru wa
Bidhaa Sura 147 eneo la Ushuru za bidhaa za Petroli na Sheria ya
Utafutaji Mafuta, sura ya 392. Mapendekezo haya ya Serikali
yataongeza gharama za maisha kwa mwananchi masikini. Mapato
yatakayopotea kutokana na kukataa mapendekezo haya
yatafidiwa na hatua za kiutawala na kikodi tutakazopendekeza
ikiwemo kupunguza matumizi, kupunguza misamaha ya kodi na
kuzuia utoroshaji fedha.
3.4 SHERIA YA KODI YA MAPATO – sura 332 NA USHURU WA BIDHAA –
SURA 147
Mheshimiwa Spika, Serikali inapendekeza mabadiliko kwenye sheria
ya kodi ya mapato ikiwemo kupunguza kiwango cha chini cha
kulipa PAYE na kuanza kutoza kodi kwenye huduma za kusafirisha
fedha kwa kupitia simu za mkononi. Vile vile Serikali inataka
kubadilisha sheria ya ushuru wa bidhaa kwa kuwalipisha kodi
wananchi asilimia 14.5 kwenye huduma zote za simu za mkononi (all
mobile phone services) na kwamba asilimia 2.5 ziende kugharamia
elimu nchini.
Mheshimiwa Spika, ushuru wa bidhaa huu ni janga jingine kwa
wananchi, kwani mpaka sasa wananchi wamekuwa wakitozwa
Page 23 of 52
pesa nyingi na kampuni kugharamia simu za mkononi, huku kampuni
zikikwepa kodi kwa kutokutoa taarifa sahihi juu ya kiasi gani cha
faida yanapata, na wakati huo Serikali haina uwezo wa kujua ni kiasi
gani hasa cha simu zinazopigwa na faida halisi ambayo kampuni hizi
zinaipata.
Mheshimiwa Spika, Kilio cha wananchi ni kampuni za simu kulipa
kodi ya mapato na sio kuhamisha ulipaji kodi na kuwabebesha
watumiaji. Serikali badala ya kupambana na kampuni zenye nguvu
kwa kuweka utaratibu wa kudhibiti matumizi yao ya uwekezaji,
imeamua kumlalia mwananchi mnyonge kwa kuongeza ushuru na
hivyo kuongeza gharama za mawasiliano.
Mheshimiwa Spika, Serikali inapanga pia kutoza kamisheni ya
asilimia 10 kwa mawakala wa huduma za mihamala ya pesa kwa
njia ya simu (mobile money transfer/transactions) kama njia ya
kuongeza mapato. Katika hotuba ya msemaji wa Kambi Rasmi ya
Upinzani wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia tuliitaka
Serikali itoze kodi na ushuru kwenye pesa kwa njia ya simu, lakini
tulitahadharisha kwamba mzigo huo wa kodi usibebeshwe kwa
wananchi bali kampuni za simu. Kwamba kampuni zilipe kutokana
na faida zinazozipata kwa sababu kwa mujibu wa sheria (the
Banking and Financial Institutions Act, 2006). Lakini cha ajabu Serikali
hii ya CCM imendelea kuziogopa kampuni za simu na imezua
pendekezo ya kuwatoza asilimia 10 mawakala, huku ikiziacha
kampuni zikipeta.
Page 24 of 52
Mheshimiwa Spika, Tozo hili jipya kwenye usafirishaji wa fedha ni tozo
linayobagua (discriminatory) kwa misingi kwamba wanaotuma
fedha kwa njia za mabenki hawatozwi kodi kama hii. Ni dhahiri
mabenki yanapiga vita mobile money transfer na hivyo Serikali
imeshawishiwa na mabenki kuongeza gharama za utumaji fedha ili
kuua sekta hii inayokua kwa kasi na inayohudumia wananchi
masikini kabisa.
Katika Azimio la Bunge kuhusu Watanzania wanaotorosha fedha na
kuzihifadhi nje ya nchi, Bunge liliazimia kwamba Serikali ianzishe kodi
ya ‘financial transaction tax’ ili kuweza kusimamia vizuri utumaji na
upokeaji wa fedha katika njia za mabenki. Kambi ya pinzani
inapendekeza kuwa tozo hili jipya kwenye mobile money transfer
litumike iwapo tu tozo kama hili litawekwa kwenye utumaji fedha
kwa njia za benki na njia nyinginezo. Vingenevyo tozo hili ni la
kibaguzi na linapendelea watu wenye uwezo mkubwa dhidi ya
wanyonge na hivyo tunatoa wito kuwa pendekezo hili lisikubaliwe
na Bunge.
Aidha, tunaendelea kupinga ongezeko hili la ushuru kwa kuwa sekta
hii ya mawasiliano ndio inaongoza katika kuchangia fedha nyingi
kwenye pato la taifa kuliko sekta nyingine yeyote hapa nchini. Sekta
hii huchangia asilimia 36.5 ya pato la taifa. Kwa mfano kwa mwaka
2012/2013 sekta hii ilichangia shilingi bilioni 287 wakati pombe, hasa
bia, ikichangia shilingi bilioni 214 na sigara shilingi bilioni 99.
Page 25 of 52
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza
mabadiliko ya Sheria ya Mawasiliano (EPOCA) ya mwaka 2009 ili
kuipa TCRA mamlaka ya kufanya ukaguzi wa uwekezaji
unaofanywa na kampuni za simu hapa nchini kwa lengo la kuzuia
ukwepaji kodi unatokana na kudanganya gharama za uwekezaji.
Kupitia TMAA ianyokagua migodi Serikali imeweza kuokoa kodi
nyingi sana. Hivyo tunataka TCRA ifanye kazi hiyo ya kukagua
gharama za uwezekaji zinazofanywa na kampuni za simu. Kambi ya
upinzani Bungeni inatarajia kuwa sekta ndogo ya mawasiliano
itaweza kuchangia sio chini ya asilimia 10 ya mapato ya ndani.
3.4.1 PAYE
Mheshimwia Spika, Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza
kushusha PAYE kutoka asilimia 14 ya sasa mpaka asilimia 9 na
kiwango cha chini cha kutoza PAYE kiwe ni Sh 250,000 kwa mwezi. Hii
itawezesha wananchi wa kipato cha chini kubakia na fedha za
kutosha na kutumia kwenye matumizi ili kuchochea uzalishaji nchini.
Uamuzi wa Serikali wa kushusha PAYE kwa asilimia moja tu (sawa na
shilingi 1,900 kwa mwezi) ni kiini macho na haina maana yeyote na
kwa kweli ni matusi kwa wafanyakazi wa Tanzania.
3.4.2 Tax Returns
Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza kwamba kwa kuwa
utaratibu wa vitambulisho vya taifa umeanza na tayari sehemu
fulani ya wananchi wamepewa vitambulisho na kwa kuwa kwa
Page 26 of 52
kupitia mfumo wa TIN na usajili wa magari kuna watanzania wengi
sana wana rekodi za kikodi ni vema sasa sheria ya kodi ya mapato
sura 332 ifanyiwe marekebisho ili kulazimisha kila mwananchi ajaze
‘tax return’ awe au asiwe na kipato. Hii itawezesha sana kupanua
wigo wa kodi kwa kuongeza idadi ya walipa kodi hapa nchini ili
kufikia lengo la anagalua Watanzania milioni 4.5 ambao wanalipa
kodi kutoka milioni moja wa sasa.
3.4.3 Kodi ya Ongezeko la thamani (VAT)
Mheshimiwa Spika, Serikali inapendekeza mabadilko kadhaa
kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani VAT ikiwemo kuondoa ushuru
wa gharama sifuri kwenye viwanda vya nguo na kuweka unafuu wa
VAT (kutoka jedwali la kwanza kwenda jedwali la tatu). Pia Serikali
inapendekeza kufanya mabadiliko kwa kuondoa msamaha wa VAT
kwenye sekta ya Utalii.
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza
kwamba mfumo mzima wa ‘zero rating’ uondolewe na badala yake
kwa bidhaa zenye umuhimu na zilizopo kwenye jedwali la kwanza
zipelekwe jedwali la tatu kama ‘special relief’. Pendekezo hili
linatokana na ukweli kwamba mfumo wa ‘zero rating’ hauonyeshi
mafanikio makubwa, hupoteza mapato kwa sababu ya kutumika
vibaya na kuwa na tatizo la cash flow kwa wazalishaji wengi.
Nchi jirani ya Kenya, katika muswada wake wa sheria ya VAT,
imependekeza kuondoa mfumo mzima wa ‘zero rating’.
Page 27 of 52
4.0 UWEKEZAJI NA MISAMAHA YA KODI
Mheshimiwa Spika, Kwa muda mrefu sana tumekuwa tukijadiliana
kuhusu misamaha ya kodi kama kivutio cha uwekezaji nchini. Serikali
kupitia sheria ya uwekezaji nchini hutoa nafuu lukuki kwa wawekezaji
ili kuleta mitaji yao nchini. Tanzania inatoa pia nafuu za kisekta,
mathalani kilimo kinapata nafuu ya asilimia ishirini (20%) ya mtaji kwa
kuandaa mashamba. Kampuni za uchimbaji madini zinazochimba
madini ya dhahabu, shaba, makaa ya mawe, lime, nickel n.k
yanapata nafuu ya asilimia mia moja (100%). Utalii inapata nafuu ya
asilimia kumi (10%).
Mheshimiwa Spika, pamoja na uvutiaji wa uwekezaji toka nje kupitia
motisha za kikodi; bado fursa za ajira ni ndogo, bado hakuna urari
wa biashara, bado maendeleo ni kidogo sana katika teknolojia. Na
hii ni tasfiri kwamba motisha za kodi zinazotolewa kwa wawekezaji
hazitoi matunda yanayokusudiwa, badala yake zimeendelea
kuinyima mapato serikali.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali ya
CCM ifahamu kuwa si motisha za kodi peke yake zinazoweza
kuwavutia wawekezaji, bali hali ya utulivu wa kiuchumi na kisiasa,
uwepo wa rasilimali za asili na rasilimali watu, utulivu wa soko la
ndani, uimara wa pesa ya ndani (local currency), uwazi na
kutokuwepo kwa rushwa, ni vigezo ambavyo kwa pamoja
vinawavutia wawekezaji.
Page 28 of 52
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa kitabu cha utafiti wa Mamlaka
ya Mapato Tanzania (‘Lessons From Selected Cases of Tax
Simplification Reforms and Tax Expenditure Budgeting’) cha mwezi
Machi 2012, Tanzania ni moja nchi zenye huruma katika kulipisha
kodi vyanzo vyake kiasi cha kuzorotesha uwezo wake wa kukusanya
mapato yake ya ndani na hivyo kushindwa kutekeleza miradi yake
ya maendeleo. Kwa mujibu wa taarifa za TRA (TRA Monthly Revenue
Report) misamaha ya kodi kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT) na Ushuru wa Forodha (custom) peke yake imeipotezea
Tanzania wastani wa asilimia 4.3 (4.3%) ya Pato la Taifa kati ya
mwaka 2006/2007 - 2010/2011.
Mheshimiwa Spika, asilimia 4.3 (4.3%) ya pato la Taifa ni sawa na
Shilingi za kitanzania trillion moja, bilioni mia tisa ishirini na mbili, milioni
mia nane hamsini na tisa, kaki tano na tisa elfu (1,922, 859, 509,000/-
). Wakati Serikali inapoteza fedha zote hizi kama misamaha ya kodi,
Serikali hiyo hiyo inakwenda kukopa Uchina kiwango kama hicho
cha fedha kwa ajili ya kujenga bomba la kusafirisha gesi asilia
kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, kiasi hicho cha pesa kingetosha kulipa deni la
Shilingi 33,442,156,55, madai yote ya walimu ya malimbikizo ya
mishahara, likizo, uhamisho, masomo, matibabu, kujikimu, ajira
mpya, na mengineyo na kubaki kiasi cha Shilingi 1,919,515,293,345
pesa ambazo zingeweza kutumika kulipa askari polisi wote nchini,
madaktari na watabibu, askari magereza wote.
Page 29 of 52
Mheshimiwa Spika, kiasi hicho kingeweza, kama mbadala, kutumika
kujenga shule, kununua vitabu, kujenga zahanati na kununua dawa,
kujenga viwanda na hivyo kupanua ajira. Kuboresha maisha ya
wakulima na wafugaji, kupeleka nishati ya umeme vijijini n.k.
Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza
kwamba misamaha yote ya Kodi iwekwe wazi na ikaguliwe na
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali. Ikumbukwe
kwamba misamaha ya kodi ni ruzuku ya Serikali kwa wanaofaidika
na misamaha, hivyo ni matumizi kama matumizi mengine yeyote ya
Serikali na hivyo ni lazima yakaguliwe na ukaguzi wake kuwekwa
wazi kama taarifa nyingine za CAG.
Mheshimiwa Spika, Suala la kuweka wazi misamaha ya kodi na
kufanyiwa ukaguzi lilishughulikiwa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za
Serikali, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na
Mamlaka ya Mapato Tanzania ambapo suala hili lilikubalika na
Waziri wa Fedha alipaswa kuliwekea utaratibu wa kisheria kwenye
Sheria ya Fedha mwaka huu. Jambo la kushtusha ni kwamba Serikali
imekaa kimya kabisa kuhusu jambo hili na hivyo kuonyesha kwamba
Serikali imewekwa mfukoni na wanaofadika na misamaha hii.
Hakuna namna nyingine ya kueleza zaidi ya kusema kwamba
Serikali imeshindwa nguvu na makampuni, taasisi na watu binafsi
wanaopinga mabadiliko kwenye mfumo wa misamaha ya kodi,
wanaopinga uwazi na wanaopinga ukaguzi wa misamaha yao.
Page 30 of 52
Kama si hivyo, basi ni vema Mheshimiwa waziri wa Fedha
akalibainisha suala hilo katika Sheria ya fedha na aeleze hivyo
kinaga ubaga katika majumyuisho yake.
4.1 UKWEPAJI KODI
Mheshimiwa Spika, Tanzania ni moja ya nchi za Afrika zenye tatizo
kubwa la ukwepaji wa kodi unaofanywa na kampuni kubwa za
kimataifa zilizowekeza, kampuni za ndani na watu binafsi. Watu na
kampuni wanaokwepa kodi hutoa taarifa za uongo juu ya mauzo
na faida zao, na kuonyesha kwa udanganyifu kuwa wamepata
hasara. Tafiti nyingi ikiwemo Ripoti ya Benki ya Dunia (2008)
zinaonyesha kuwa ukwepaji kodi ni tatizo kubwa Tanzania kuliko nchi
tunazopakana nazo.
Kwa mujibu wa ripoti Benki ya Dunia kampuni nyingi Tanzania hutoa
taarifa kwa kiwango cha asilimia 69 tu ya mauzo yake, ukilinganisha
na asilimia 77 nchini Uganda, na asilimia 86 huko Kenya. Kampuni
hapa nchini zinakuwa na vitabu viwili vya hesabu; kimoja
wanaandika hesabu za kweli na kingine wanaandika taarifa za
uongo kwa madhumuni ya kupunguza kodi. Lakini hiyo ni njia moja
tu.
Mheshimiwa Spika, njia nyingine inayotumika na kampuni hizo
kukwepa kodi ni kutotoa taarifa za mauzo ya nje, kufanya biashara
Page 31 of 52
nje ya nchi kimagendo (kupitia njia za panya). Kwa mujibu wa
Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (East African Business Council)
mwaka 2008 kiasi cha biashara ya thamani ya Dola za Marekani
milioni 602 ($ 602 Milioni) zilifanyika kwenye mpaka wa Kenya na
Tanzania, pale Namanga peke yake.
Mheshimiwa Spika, mfano mmoja dhahiri wa ukwepaji kodi kwenye
mauzo ya nje umeonyeshwa na utafiti uliofanywa na Benki ya Dunia
katika Bandari ya Dar es Salaam na Bandari nyingine hapa nchini
kuhusu mauzo nje ya zao la korosho ghafi. Mwaka 2011 Tanzania
iliuza kwenda nchini India korosho kiasi cha tani 80,000 kwa mujibu
wa taarifa za Mamlaka ya Mapato Tanzania na Benki Kuu ya
Tanzania. Hata hivyo, idara ya Forodha ya India inaonyesha katika
mwaka huo, nchi hiyo ilikuwa imenunua tani 120,000 za korosho
kutoka Tanzania. Hii maana yake ni kwamba jumla ya tani 40,000 ya
korosho ambazo ni sawa na theluthi moja ya korosho zote
zilizopaswa kuwa zimeuzwa nchini India na nusu ya korosho
zilizoripotiwa kuwa Tanzania imeuza nchini India hazikuripotiwa na
hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa sana kiwango cha kodi
ambacho serikali ilipaswa kukusanya. Pia, tofauti hiyo ilipunguza urari
wa mauzo nje.
Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tumeshuhudia taarifa za ukwepaji
mkubwa sana wa kodi ya forodha kufuatia wafanyabiashara wasio
waaminifu kutumia vibaya mfumo wa kutoa mizigo. Ikumbukwe
kwamba Bunge lako tukufu katika mwaka wa fedha wa 2008/09
Page 32 of 52
lilipinga mfumo wa kuruhusu wafanyabiashara wakubwa kutoa
mizigo yao bila kukaguliwa.
Bidhaa nyingi zilizoagizwa hazikulipiwa kodi kwa sababu ama
hazikuwa zimeorodheshwa kwenye nyaraka zilizowasilishwa idara ya
forodha au kulifanyika udanganyifu wa aina ya bidhaa. Kwa mujibu
wa taarifa za TRA, ukaguzi wa mizigo uliofanyika kati ya Aprili na Juni
2013 unaonyesha kwamba jumla ya shilingi bilioni nne ziliokolewa.
Mheshimiwa Spika, kuna mtandao mzito wa wafanyabiashara
wakubwa hapa nchini kwa kushirikiana na maafisa wa forodha
wanafanya njama za kukwepa kodi. Kumekuwa na vita vya
kibiashara miongoni mwa wafanyabiashara, vita ambayo
imewagawa maafisa wa forodha wasio waaminifu na kujikuta
kufanya kazi za wafanyabishara wakubwa.
Kumekua na uonevu mkubwa dhidi ya wafanyabiashara wadogo
na wanaoibukia unaofanywa na wafanyabaishara wakubwa na wa
muda mrefu. Hakuna haki kabisa katika ukaguzi wa mizigo jambo
linalosababisha wafanyabiashara wadogo wengi wa Kariakoo
kuumizwa kutokana na hila za wafanyabishara wakubwa
wanaoshirikiana na maofisa wa idara ya forodha.
Mheshimiwa Spika, hii inathibitishwa na Taarifa ya ukaguzi wa
thamani ya Fedha (Value for Money Audit Tanzania Revenue
Authority’s New Customs system) iliyotayarishwa na Bert
Cunningham kutoka Canada. Taarifa hiyo inaonyesha kuwa maofisa
Page 33 of 52
wa forodha wanashirikiana na mawakala wa mizigo na wafanya
biashara (Clearing and Forwarding Agents) kuonyesha kiwango
kidogo cha mizigo inayoingizwa nchini au thamani ndogo ya mizigo
kwa lengo la kukwepa kulipa kodi stahiki.
Kutokana na ukosefu wa maadili, rushwa na uzembe wa maafisa wa
forodha, Taifa hupoteza mapato ya zaidi ya asilimia 15 ya kiwango
kinachokusanywa na Idara ya Forodha kwa mwaka. Katika mwaka
wa Fedha 2012/13 jumla ya shilingi bilioni 477 zimepotea kupitia
idara ya forodha peke yake.
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ina mashaka
makubwa sana kwamba ukwepaji kodi kwenye eneo la kodi ya
forodha ni mkubwa mno kuliko inavyoripotiwa hivi sasa. Vyombo vya
habari vinavyoandika habari hizi, vinaandika kutokana na taarifa
ambazo zimekipata kuitoka kwa chanzo chao ambacho aghalabu
huwa hakina taarifa zote na za kina. Hivyo, ni dhahiri kuwa
kinachoandikwa ni sehemu tu na ukweli wote hausemwi. Kambi ya
Upinzani Bungeni, kwa mujibu wa kanuni ya 117 italeta hoja Bungeni
kutaka kuundwa kwa kamati teule ya Bunge kuchunguza ‘Mfumo
wa Forodha na ukwepaji kodi katika idara ya Forodha ya Mamlaka
ya Mapato Tanzania’ kwa lengo la kuhakikisha ukwepaji kodi
unadhibitiwa na wahujumu wote wanachukuliwa hatua stahili za
kisheria.
Page 34 of 52
Mheshimiwa Spika, suala la ukwepaji wa kodi linahusu pia
wanasiasa wakiwamo Wabunge. Ni dhahiri wabunge wana stahili za
kisheria za kupata msamaha wanapoagiza magari yao nk. Tunatoa
wito kwa wabunge ambao ni wafanyabiashara waliosajili biashara
zao katika Kituo cha Uwekezaji yaani TIC na kupata vyeti vya
misamaha ya kodi wawe wa kwanza kuhakikisha kuwa hawatumii
misamaha hiyo vibaya.
Hatuwezi kuwa mbele kukemea misamaha ilhali sisi wenyewe
tunaitumia vibaya misamaha hiyo. Ni dhahiri kabisa kwamba
inapaswa kuwa ni aibu kwa mbunge kutumia msamaha wa kodi
aliopata kununua kitanda, magodoro na mambo kama hayo. Sisi
wabunge tutembee kwenye maneno yetu ikibidi hata kwa kukataa
misamaha hii mikubwa ya kodi tunayopewa. Natumai baada ya
CAG kuanza kukagua misamaha ya kodi kama matumizi mengine
yeyote ya Serikali tutashuhudia aibu kubwa tutakayopata kwa
kutumia vibaya misamaha ya kodi.
Mheshimiwa Spika, hivi sasa dunia ipo kwenye ajenda ya kuzuia
utoroshaji mkubwa wa fedha kupitia ‘tax havens’ ambapo licha ya
kwamba kuna fedha zinazotokana rushwa katika utoroshaji huu
lakini pia kuna fedha nyingi zinazotokana na ukwepaji wa kodi (Tax
evasion and tax avoidance). Taarifa ya Benki ya Maendeleo ya
Afrika (The joint report from the African Development Bank (AfDB)
and Global Financial Integrity (GFI)) iliyotolewa jijini Marrakech nchini
Morocco inaonyesha kuwa jumla ya dola za Marekani trilioni 1.4
Page 35 of 52
zimetoroshwa kutoka Afrika kati ya mwaka 1980 mpaka 2009 na
hivyo kulifanya bara hili kuwa ‘net creditor’ kwenye dunia. Sehemu
kubwa ya Fedha hizi ni kodi inayokwepwa na kampuni kubwa
zinazowekeza katika bara la Afrika. Sehemu nyingine ya fedha hizi
zinatokana na udanganyifu katika akaunti ya Deni la Taifa ambapo
madeni na riba za uwongo hulipwa kutoka Afrika.
Mheshimiwa Spika, wakati dunia nzima ipo kwenye kampeni kubwa
dhidi ya ukwepaji kodi unaofanywa na kampuni kubwa duniani
zinazowekeza kwenye nchi zinazoendelea, Tanzania ipo kimya
kabisa kana kwamba hakuna linalotokea. Licha ya kwamba Bunge
la Tanzania ni Bunge la Kwanza katika nchi za SADC kupitisha Azimio
kuchunguza utoroshwaji wa Fedha (Azimio la Bunge namba 9/2012),
Serikali ya Tanzania imekaa kimya kabisa kupaza sauti yake kuhusu
ukwepaji kodi mkubwa.
Tanzania inapoteza mapato ya ndani sawa na asilimia tano (5) ya
Pato la Taifa kupitia kodi za kimataifa ambayo ni sawa na shilingi
trilioni mbili kila mwaka. Uchunguzi unaonyesha kwamba katika
orodha ya walipa kodi wakubwa 10, kampuni saba zinatumia ‘tax
havens’ kukwepa kodi. Katika kampuni kubwa tatu za simu hapa
nchini kampuni mbili zimesajiliwa ‘tax havens’ za Uholanzi na
Luxembourg na hivyo kukwepa kodi mbalimbali hapa nchini.
Kampuni moja kubwa ya madini hapa nchini ina kampuni dada tisa
(9) katika offshore hali kadhalika kampuni moja kubwa ya kutafuta
mafuta na gesi hapa nchini. Katika mahojiano na gazeti la Financial
Page 36 of 52
Times la Uingereza la mwezi June, 2013 kampuni ya African Barrick
Gold imetangaza kufunga baadhi ya kampuni zaidi ya 24 iliyoyasajili
maeneo kama Cayman Islands.
Mheshimiwa Spika, bila Serikali ya Tanzania kuamua kwa dhati
kusafisha nyumba yake, hata juhudi kubwa zinazofanywa na asasi
za kiraia kama Oxfam, ActionAid, Tax Justice Network nk katika
kupambana na ukwepaji kodi na utoroshaji wa fedha hazitafua
dafu. Wakati nchi za G8 zinaweka mipango ya kutusaidia na sisi
kama nchi tuweke mipango yetu wenyewe. Kambi ya Upinzani
Bungeni inapendekeza hatua za awali zifuatazo zichukuliwe ili
kukabiliana na utoroshaji mkubwa wa fedha unaotokana na
ukwepaji wa kodi;
(i) Tanzania ijiondoe kabisa katika mfumo wa kodi
unaopendekezwa na OECD (OECD model treaty) kwani
mkataba huu wa kikodi unalinda kampuni kubwa za nje dhidi
ya nchi changa kama Tanzania.
(ii) Tanzania ijondoe katika mikataba yote ya kikodi na nchi
ambazo ni ‘tax havens’ kama Mauritius, Uingereza (City of
London and British overseas territories), Luxembourg,
Netherlands n.k.
(iii) Kampuni yoyote ya ndani na nje yenye kampuni dada
zilizosajiliwa kwenye ‘tax havens’ zitangaze bayana na kuweka
Page 37 of 52
wazi hesabu zao kwa miaka mitano iliyopita kwa ukaguzi wa
TRA na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
(iv) Bunge litunge sheria kudhibiti matumizi ya ‘tax havens’
yanayofanywa na kampuni za uwekezaji na haswa kwenye
sekta za Mawasiliano, Madini, Mafuta na Gesi na nyinginezo.
5.0 MAENDELEO YA MICHEZO
Mheshimiwa Spika, maendeleo mazuri ya michezo katika taifa
lolote, ni utambulisho mzuri wa taifa hilo katika mataifa mengine
kutokana na ushirikiano wa kimichezo na mataifa hayo. Pamoja na
mambo mengine, michezo katika nchi yetu inaweza kutumika
kutengeneza fursa za kiuchumi kwa kuitangaza nchi yetu duniani
katika sekta za utalii na uwekezaji. Ukiacha mbali suala la manufaa
ya kiuchumi yanayoweza kupatikana kupitia michezo, michezo pia
inawajengea vijana wetu afya na hivyo kuwa na taifa la watu
wakakamavu. Kwa upande mwingine, michezo pia ni ajira.
Inasikitisha kwamba katika hotuba nzima ya Waziri wa Fedha,
hapakuwa na mpango wowote wa kukuza michezo hapa nchini
bila hata kujali kwamba timu yetu ya Taifa ya Mpira wa Miguu ipo
katika nafasi nzuri sana hivi sasa kuliko wakati mwingine wowote
katika kuweza kufuzu kucheza fainali za kombe la Dunia mwakani.
Page 38 of 52
Mheshimiwa Spika, Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii katika
barua yake ya tarehe 5/4/2013 iliomba Kamati ya Bajeti kuangalia
namna ya kusaidia kupata fedha za kujenga michezo na hasa
kusaidia Taifa Stars katika juhudi zake za kuelekea kufuzu kwenye
michuano ya kombe la Dunia huko Brazil. Hata hivyo Wizara ya
Fedha haikutoa hata senti tano kwa ajili hiyo. Kamwe hatuwezi
kufanikiwa kwenye michezo bila kuwekeza na kutegemea juhudi za
dharura za kamati za kusaidia ushindi. Tukitaka tung’ae kwenye
michezo ni lazima tuwekeze sana na kuwekeza ni gharama,
gharama ambayo thamani yake ni kubwa sana kwa nchi.
Mheshimiwa Spika, licha ya michezo kuliingizia taifa mapato kupitia
asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) inayotokana na
viingilio katika michezo mbalimbali, hakuna uwekezaji wowote wa
maana uliofanyika kwenye michezo jambo ambalo ni hatari kwa
uhai na maendeleo ya michezo hapa nchini. Aidha hakuna
mipango madhubuti ya muda mrefu kuhusu maendeleo ya michezo
hapa nchini.
Kutowepo kwa mipango madhubuti na ya muda mrefu,
kumeshababisha timu zetu kufanya vibaya katika mashindano
mengi ya kimataifa na hivyo kulifanya taifa letu lionekane kuwa ni
taifa dhaifu au kichwa cha mwendawazimu kama alivyopata
kusema Rais Mstaafu was Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi.
Kambi Rasmi ya Upinzani, inatoa angalizo kwa Serikali kwamba,
kamwe hatuwezi kufanikiwa katika michezo kwa mipango ya
Page 39 of 52
kukurupuka. Aidha ni aibu kwa Serikali kukusanya kodi kutokana na
michezo, halafu vijana wetu wanakosa fedha ya nauli kwenda nchi
nyingine kwa mashindano ya michezo mpaka wafanye harambee
ya kukusanya fedha kwa wahisani. Hivyo, Kambi Rasmi ya Upinzani
Bungeni inayoongozwa na CHADEMA inapendekeza mambo
yafuatayo yafanyike ili kunusuru tasnia ya michezo hapa nchini;
1. Timu yoyote itakayowakilisha taifa katika mashindano
yoyote ya kimichezo igharamiwe na Serikali kwa asilimia
100.
2. Viwanja vyote vya Michezo hapa nchini viundiwe Wakala
wa Serikali, Wakala wa maendeleo ya michezo (Sports
Development Agency). Wakala huo uwe na majukumu ya
kujenga viwanja vipya na kusimamia viwanja hivyo kwa
niaba ya Serikali. Viwanja vyote vya michezo vilivyoporwa
na CCM kama Lake Tanganyika – Kigoma, Ali Hasan Mwinyi
- Tabora, Kirumba – Mwanza, Maji Maji – Songea nk
virejeshwe Serikalini mara moja chini ya Wakala wa Viwanja
vya Michezo. Wakala pia ujenge academies za michezo
maeneo kama vile Mbeya, Tanga, Mtwara, Mwanza,
Manyara na Dar es Salaam ili kukuza vipaji vya watoto na
vijana.
3. Mashirika yote ya Umma, hasa mashirika makubwa yawe
na timu za michezo. Ushauri uliotolewa na IMF na Benki ya
Dunia dhidi ya Mashirika ya Umma kuwa na timu ulikuwa
Page 40 of 52
ushauri usio wa maana. Wenzetu Uganda kwa mfano,
Mamlaka ya Mapato Uganda (URA) wana timu katika ligi
Kuu, ambayo ni moja ya timu mahiri katika ukanda huu wa
bara la Afrika.
4. Serikali ianzishe Mfuko Maalum wa Michezo (Sports Fund).
Pia, Serikali ianzishe Kodi ya Maendeleo ya Michezo (Sports
Development Levy). Kodi hii ipatikane kama ifuatavyo:
Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ya asilimia 18 iliyokuwa
ikikatwa kwenye viingilio katika michezo mbalimbali
iondolewe na badala yake kiasi hichohicho kiingizwe
kwenye Mfuko wa Michezo (Sports Fund) utakaoanzishwa.
5. Matumizi ya Mfuko wa michezo yawe kama ifuatavyo:
i. Asilimia 50 ya fedha zitakazokusanywa
zitumike kujenga miundombinu ya michezo
(Sports Infrastructure) kupitia kwa Wakala
wa Maendeleo ya Michezo na Academies.
ii. Asilimia 50 inayosalia itumike kuhudumia
maandalizi ya timu za Taifa.
6.0 UKUSANYAJI WA MAPATO YA ZIADA.
6.1 BANDARI YA DAR-KAMA KICHOCHEO CHA UCHUMI
Mheshimiwa Spika, Bandari ya Dar es Salaam ni mlango mkuu wa
biashara kwa asilimia 90 kwa nchi sita zisizokuwa na bandari za
Page 41 of 52
Zambia, Malawi, Rwanda, Burundi, Uganda na eneo la Mashariki ya
nchi ya DRC. Toleo la tatu la taarifa ya Benki ya Dunia (Tanzania
Economic Update) la mwezi Mei, 2013 inaonyesha kwamba Bandari
ya Dar es Salaam inapoteza fedha na muda mwingi sana kwa
watumiaji wa bandari hiyo kwa kulinganisha na Bandari yoyote
katika mwambao wa Afrika ya Mashariki.
Mheshimiwa Spika, taarifa hiyo ya Benki ya Dunia inasema kwamba
familia za kawaida zingeweza kuepuka matumizi ya takriban dola za
Marekani 147 au asilimia 8.5 kwa mwaka kama Bandari ya Dar es
salaam ingekuwa inafanyakazi kama inavyofanyakazi Bandari ya
Mombasa.
Mheshimiwa Spika, kutokana na utafiti ni kwamba kama Bandari ya
Dar es Salaam itaboreshwa na kubadili mtizamo (mind set) wa
watendaji wake katika uwajibikaji ni dhahiri kwamba bandari ina
fursa za kuongeza mapato ya Serikali yapatayo dola za Marekani
bilioni 1.8 au shilingi trilioni 2.93 kwa mwaka au ongezeko la asilimia
saba la pato la Taifa.
Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza kuimarisha ufanisi wa
Bandari kwa mwaka huu wa fedha 2013/2014 na kufikia ufanisi wa
asilimia hamsini (50%) jambo ambalo litawezesha kuongeza mapato
ya ndani ya kiasi cha shilingi trilioni 1.46
6.2 Kudhibiti misamaha ya kodi
Page 42 of 52
Mheshimiwa Spika, katika mapendekezo ya namna bora ya
kuongeza mapato ya serikali, Kambi Rasmi ya Upinzani
tunapendekeza yafanyike marekebisha katika Sheria ya Uwekezaji
na kuweka udhibiti wa thabiti katika kutoa misamaha na nafuu za
kodi, tofauti na hali ilivyo sasa ambapo asilimia 4.3 ya pato la taifa
linapotea kwa misamaha ya kodi. Kiwango hiki ni sawa na shilingi
Trilioni Moja, Bilioni Mia tisa ishirini na mbili, milioni mia nane hamsini
na tisa, Laki tano na tisa elfu (1,922, 859, 509,000/-).
Kambi Rasmi ya Upinzani inayoongozwa na CHADEMA
inapendekeza kudhibiti misamaha hiyo ili kuishusha na kufikia asilimia
moja (1%) ya pato la taifa. Jambo hilo ni muhimu lifanyike kwa
sababu kwa kufanya hivyo nchi itakuwa imeokoa shilingi Trilioni
moja, Bilioni mia tano arubaini na tano, milioni mia sita themanini na
mbili, laki nane na elfu sabini na tisa (1,545, 682, 879, 000).
6.3 Kodi ya Mauzo na Manunuzi ya Bidhaa kutoka Nje
Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani inayoongozwa na
CHADEMA inapendekeza kuanzishwa kwa kodi maalumu (Special
Railways development levy) ya manunuzi na mauzo ya bidhaa nje.
Tunapendekeza tozo ya asilimia moja (1 %) ya bei ya bidhaa
zinazoagizwa toka nje na asilimia 0.5 (0.5%) ya thamani ya bidhaa
kwa zile zinazouzwa nje. Mapato ya tozo hii maalumu yote yatumike
kujenga miundombinu ya Reli hapa nchini.
Page 43 of 52
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taarifa ya Hali ya Uchumi wa
Taifa mwaka 2012 Tanzania iliagiza bidhaa kutoka nje ya nchi zenye
thamani ya dola za Marekani milioni 10,324.9 ambazo ni sawa na
shilingi 16,519,840,000,000 (bei ya kubadilisha dola 1 ni sawa na
shilingi 1,600). Kwa maana hiyo, asilimia moja ya mapato ya
manunuzi yote ya nje ni shilingi bilioni 165.2. Mauzo ya bidhaa nje ya
nchi kwa mwaka 2012 yalikuwa dola za Mmarekani milioni 5,912.3
ambazo ni sawa na shilingi trilioni 9.456 na asilimia 0.5 ya kiasi hicho
ni shilingi bilioni 47.298.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kodi hii ya mauzo na manunuzi ya
bidhaa kutoka na kwenda nje ya nchi, iwapo tozo hiyo ingekuwepo,
serikali ingekusanya kiasi cha shilingi bilioni 212.498 mwaka 2012.
7.0 VIPAUMBELE VYA BAJETI YA MATUMIZI 2013/2014
Mheshimiwa Spika, kutokana na mapendekezo tuliyoyatoa, Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa na CHADEMA
inapendenkeza kuwa vipaumbele vya Bajeti ya mwaka ujao wa
fedha vingekuwa kama ifuatavyo:
(i) Kujenga Mazingira ya ukuaji wa uchumi vijijini (rural
growth) kwa kuboresha miundombinu ya umeme,
barabara, maji na miundombinu ya umwagiliaji.
Tunapendekeza kutumia shilingi bilioni 450 kila mwaka
katika eneo hili. Fedha hizi zitasimamiwa na Mamlaka ya
Maendeleo Vijijini (Rural Development Authority – to be
established) itakayokuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu.
Page 44 of 52
(ii) Kukarabati Reli ya Kati na matawi yake ya Tanga - Arusha
na Mpanda. Tutatenga Tsh 212.498 bilioni kwa RAHCO
kwa ajili ya Reli. Fedha za ujenzi wa Reli zitakuwa ni fedha
endelevu kutoka Railways Development Fund
itakayotokana na tozo maalumu tunayopendekeza.
(iii) Kuboresha Elimu na Afya hasa kwa Shule na
Zahanati/Vituo vya Afya vya Vijijini kwa kutoa motisha
kwa wafanyakazi wa Sekta hizi walio kwenye Halmashauri
za Wilaya. Tunapendekeza posho za Mazingira ya Vijiji
sawa na mara moja na nusu ya Mishahara yao.
(iv) Kuongeza Kima cha chini cha Mshahara kwa
Wafanyakazi wa Umma mpaka Tsh 315,000 kwa Mwezi
(v) Kuanzisha Pensheni ya uzeeni kwa Wazee wote nchini
wenye umri wa zaidi ya miaka 60.
(vi) Kupunguza mzigo wa matumizi ya magari ya Serikali kwa
kupiga mnada baadhi ya ‘mashangingi’ na kuweka
mfumo wa kukopesha Magari kwa watumishi wote wa
umma wanaostahili magari.
(vii) Kuanzisha Chuo Kikuu cha Mtwara (Mtwara University for
Petroleum Studies) ili kuzalisha wataalamu wa kutosha wa
Sekta ya Mafuta na Gesi na kuliandaa Taifa kuwa na
wasomi mahiri wa maeneo hayo na hivyo kufaidika na
Utajiri wa Mafuta na Gesi uliopo nchini kwetu.
Page 45 of 52
8.0 SURA YA BAJETI MBADALA KWA MWAKA 2013/14
Mheshimiwa Spika, kambi rasmi ya upinzani bungeni katika kupanga
bajeti yake imezingatia heshima ya taifa kwa kuhakiki nchi inaweza
kutumia vema rasilimali zake na kufuta utegemezi. Naomba kunukuu
maneno ya Abraham Lincoln anayesema; “You cannot help people
permanently by doing for them, what they could and should do for
themselves”. Kwa tafsiri ya haraka haraka anamaanisha kuwa
hauwezi kuwasaidia watu kwa kuwafanyia, wakati wote, kile
ambacho wanaweza na wanapaswa kukifanya. Leo hii, kama nchi
tunategemea kuendelea kusaidiwa na mataifa wahisani kwa vitu
ambavyo tunauwezo wa kuvifanya na tunapaswa kuvifanya. Pia
tunajenga taifa tegemezi lisilo na heshima mbele ya dunia na kujipa
matumaini ya kuwa bado tunao uwezo wa kukopesheka. Ni lazima
kuongeza wigo wa kodi ili kuondokana na utamaduni wa
kupandisha kodi zile zile kila mwaka na hivyo kuonekana kana
kwamba hatuna ubunifu wowote.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia heshima ya taifa letu kambi rasmi
imependekeza bajeti mbadala ya mwaka 2013/2014 yenye jumla
ya makusanyo ya ndani ya shilingi billion 15,698.937 kwa kujikita
katika kupanua wigo wa mapato ya ndani na kuachana na mikopo
yenye masharti ya kibiashara ili kupunguza mzigo mkubwa
ulioingizwa katika deni la taifa. Asilimia 75.8 ya bajeti nzima ni
mapato ya ndani ikijumuisha mapato ya halmashauri. Hivyo ni
Page 46 of 52
asilimia 24.2 tu ya bajeti ndio itatukana na misaada ya kibajeti na
mikopo isiyo na riba za kibiashara.
Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya upinzani bungeni inapendekeza
kuondoa kabisa mikopo yenye masharti ya kibiashara na
kupendekeza vyanzo mbadala vya mapato ili kuondokana na adha
ya madeni na kukusanya mapato yetu ya ndani kugharimia
uendeshaji wa bajeti, pia kupunguza matumizi yasio ya lazima na
fedha hizo kuelekezwa katika miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Spika, kutokana na ongezeko kubwa la matumizi yasiyo
ya lazima katika bajeti ya serikali, kambi rasmi ya upinzani
imependekeza kupunguza asilimia 30 ya gharama za posho za
vikao, semina, usafiri, viburudisho, mafuta na vilainishi. Kwa mwaka
2012/2013 serikali inatumia shilingi billion 681 kwa matumizi yasiyo ya
lazima na 2013/2014 imepanga kutumia shilingi bilioni 714 (kwa
mujibu wa taarifa ya Shirika la Sikika) sawa na ongezeko la asilimia
tano kinyume na kauli ya Waziri Mkuu ya kupunguza gharama za
matumizi yasiyo ya lazima. Hivyo kambi imedhamiria kuwepo na
punguzo hilo la shilingi bilioni 214 kutoka katika eneo hili ambazo
zitaelekezwa katika miradi ya maendeleo.
JEDWALI LA VYANZO VYA MAPATO MBADALA.
Page 47 of 52
CHANZO CHA MAPATO. MAKISIO SHILINGI BILIONI
Kuongeza Ufanisi wa bandari ya
Dar Es Salaam
1,465.000
Marekebisho ya kodi za misitu 220.416
Kupunguza misamaha ya kodi 1,545.000
Kodi ya 0.5% kwenye Mauzo na
ya 1% manunuzi ya nje kwa ajili
ya kujenga Reli
212.498
Kuzuia ukwepaji kodi
unaofanywa na Kampuni za
kimataifa
718.500
Jumla 4,161.414
SURA YA BAJETI MBADALA YA MWAKA 2013/2014.
MAPATO % SHILINGI BILIONI
A Mapato ya ndani 15,315.485
i)Mapato ya Kodi (TRA) 13,855.851
ii)Mapato yasiyo ya Kodi 1,459.634
B Mapato ya Halmashauri 383.452
C Mikopo na misaada ya Kibajeti 1,163,131
D Mikopo na Misaada ya miradi
ya maendeleo ikijumuisha MCA
(T)
2,692,069
Page 48 of 52
E Mikopo ya ndani 1,156,400
Jumla ya Misaada na mikopo.
5,011.600
JUMLA YA MAPATO YOTE 20,710.537
MATUMIZI
E Matumizi ya Kawaida 13,132.121
(i) Deni la Taifa 3,319.156
(ii) Mishahara 5,706.399
(iii) Matumizi Mengineyo 4,106.566
Wizara 3,352,316
Mikoa 49,701
Halmashauri 704,549
H Matumizi ya Maendeleo 7,578.416
(i)Fedha za ndani 6,537.467
(ii)Fedha za Nje 1,040,949
JUMLA YA MATUMIZI YOTE. 20,710.537
Page 49 of 52
TOFAUTI KATI YA BAJETI YA SERIKALI NA BAJETI MBADALA YA KAMBI
RASMI YA UPINZANI.
BAJETI MBADALA YA KAMBI YA
UPINZANI 2013/2014
BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA
2013/2014
Bajeti yenye kuondoa mikopo
yenye masharti ya kibiashara ili
kulipunguzia taifa mzigo wa
madeni.
Bajeti yenye mikopo ya shilingi
1.156 trilioni yenye masharti ya
kibiashara
Bajeti yenye kujikita katika
utekelezaji wa mpango wa
maendeleo kwa kutenga zaidi
ya asilimia 41 ya mapato ya
ndani kugharimia miradi ya
maendeleo.
Bajeti inayopingana na
mpango wa maendeleo wa
taifa kwa kutenga asilimia 22.4
kinyume na matakwa ya
mpango wa serikali ambao
unahitaji asilimia 35.
Imeanzisha kodi maalum ya
michezo na wakala wa
maendeleo ya michezo
Haijali michezo na wala sio
kipaumbele chake
Kulipa pensheni kwa wazee
wote kuanzia miaka 60 na
kuendelea.
Bajeti isiyo na mfumo wa
pensheni kwa wazee.
Kushusha kiwango cha chini
cha kodi ya mapato (PAYE)
kutoka 14% mpaka 9%
Haijali wafanyakazi, kodi ya
mapato (PAYE) imeendelea
kuwa kubwa 13%
Kupunguza matumizi yasiyo ya Ina matumizi yasiyokuwa ya
Page 50 of 52
lazima kwa kuondoa 30% ya
OC kwenye wizara na idara .
lazima kiasi cha shilingi bilioni
214
Bajeti inayojitegemea kwa
makusanyo ya mapato ya
ndani ya asilimia 75.8
Bajeti tegemezi kwa asilimia
37.8 kutokana na kukopa kwa
kiwango kikubwa.
Bajeti yenye punguzo la
misamaha ya kodi na kufikia 1%
ya pato la taifa
Bajeti yenye misamaha ya kodi
kiasi cha 4.3% ya pato la taifa
(sawa na shilingi trilioni 1.922)
Bajeti itakayokabiliana na
mfumuko wa bei kwa bidhaa
muhimu
Bajeti isiyozingatia mfumuko wa
bei
Bajeti yenye maslahi bora kwa
wafanyakazi kwa kuongeza
kima chini cha mshahara
kuanzia 315,000
Bajeti iliyo na kima cha chini
cha shilingi 170,000
kisichoendana na gharama za
maisha kwa sasa.
Bajeti inayofuta ongezeko la
kodi kwenye mafuta ya dizeli na
petroli
Bajeti inayoongeza kodi kwenye
mafuta, dizeli 6.1% na petroli
8.5%
Bajeti inayoondoa ongezeko la
kodi kwenye ngano na hivyo
bidhaa za ngano kama mikate,
maandazi, chapati kutopanda
bei
Bajeti inayoongeza bei ya
ngano kwa 10% na hivyo
kutowajali wananchi wa
kipatyo cha chini wanaotumia
bidhaa hizi kwa wingi
Inafuta ongezeko la kodi Inaongeza kodi kwenye simu za
Page 51 of 52
kwenye matumizi ya simu za
mkononi
mkononi na hivyo mtumiaji
kutakiwa kulipa kodi
/tozo/ushuru wa 36.5%
9.0 HITIMISHO.
Mheshimiwa Spika, wakati waziri wa fedha alipokuwa anawasilisha
hotuba yake ya bajeti wiki iliyopita wapo wabunge ambao
walikuwa wanapiga makofi kuashiria kuwa waliridhika na hotuba ya
bajeti na walikuwa wanaiunga mkono.
Aidha, baada ya mawasilisho yake hayo wananchi wa kada
mbalimbali kuanzia wasomi, wafanyakazi, wanasiasa, wakulima na
wafanyabiashara pamoja na makundi mbalimbali ya kijamii katika
maeneo mbalimbali ya nchi yetu wamekuwa wakipaza sauti zao
kuhusiana na jinsi ambavyo bajeti ya serikali itakavyokwenda
kuongeza gharama za maisha na kuwafanya waendelee kuogelea
kwenye wimbi la umasikini katika nchi yenye rasilimali za kutosha.
Mheshimiwa Spika, ni rai yangu na ya kambi rasmi ya upinzani kuwa
sisi wabunge wote bila kujali itikadi zetu tusikilize kilio cha watanzania
wenzetu hawa na tuwe na huruma juu ya maisha yao na
tutakapokuwa tunajadili bajeti hii tuangalie maslahi ya taifa letu na
wananchi wetu kwa kuhakikisha kuwa tunatimiza wajibu wetu wa
kuisimamia serikali ili itimize wajibu wake wa kutoa huduma kwa
wananchi wake. Nawashauri waheshimiwa wabunge wenzangu
Page 52 of 52
kuwa kamwe tusikubali kuwaongezea wananchi mzigo wa gharama
za maisha kwa kukubaliana na serikali katika kupandisha kodi
kwenye bidhaa za mafuta, ngano, matumizi ya simu za mkononi,
malighafi za sabuni na kodi zozote ambazo zitawaumiza wananchi
wetu. Tuiambie serikali itumie vyanzo vingine vya mapato kwa ajili ya
kupata fedha za kujiendesha bila ya kuwaumiza wananchi wetu.
Sote tutimize wajibu wetu kwa taifa letu. Njia hizo zipo na baadhi
tunmezipendekeza kupitia hotuba yetu hii na hotuba zilizopita. Ni
jukumu la serikali kuhakikisha kuwa inayachukua mapendekezo
haya na kuyatekeleza kwa ajili ya kumwokoa mwananchi masikini.
Imeshajidhihirisha kuwa pale ambapo serikali imeyachukua
mapendekezo yetu na kuyatekeleza kwa ufanisi, kumekuwepo na
mabadiliko chanya. Serikali isione aibu kuyachukua mapendekezo
yetu na kuyatekeleza kwa sababu tunayatoa kwa moyo wa
uzalendo wa kulisaidia taifa letu na watu wake. Sisi si wabinafsi.
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo kwa niaba ya kambi ya
upinzani naomba kuwasilisha.