52
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA MIANYA YA RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAASISI YA KUZUIA … · mdogo wa wapiga kura kuhusu sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi pamoja na matumizi ya lugha za matusi, kashfa na kejeli

Embed Size (px)

Citation preview

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA

MIANYA YA RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

i

MUHTASARI (EXECUTIVE SUMMARY)

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilifanya utafiti kwa lengo la kutoa

ushauri kwa Mamlaka zinazohusika juu ya namna bora ya kudhibiti vitendo vya rushwa katika

Chaguzi nchini. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa ni: (i) Kubaini mianya ya rushwa katika

mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014; (ii) Kutathmini uelewa wa wananchi kuhusu

haki na wajibu wao katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa; (iii) Kuainisha vitendo vya rushwa

vilivyojitokeza katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014; na (iv) Kushauri namna ya kuziba

mianya ya rushwa itakayobainika katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Utafiti huu ulifanyika katika mikoa yote ya Tanzania Bara na kuhusisha jumla ya wahojiwa

1332. Aidha katika kila Wilaya, kata mbili zilichaguliwa na katika kila kata, ilichaguliwa

mitaa/vijiji viwili. Makundi ya wadau waliohojiwa ni: wananchi, wagombea na wasimamizi wa

uchaguzi. Aidha, taarifa za msingi za utafiti huu zilikusanywa kwa njia ya mahojiano/usaili na

kwa kuangalia matukio (Observation) ambapo madodoso na orodha ya ukaguzi (checklists)

zilitumika. Taarifa za upili zilikusanywa kwa kupitia nyaraka zilizohusu uchaguzi.

Matokeo ya utafiti huu kabla, wakati na baada ya uchaguzi ni kama ifuatavyo: Kabla ya

uchaguzi, baadhi ya wasimammizi wa uchaguzi hawakutoa orodha ya majina ya wapiga kura,

hawakuonesha mipaka ya Mitaa, Vijiji na Vitongoji; baadhi ya wapiga kura kutotaka

kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura, baadhi ya wagombea kutoidhinishwa na vyama

vyao vya siasa, kukosekana kwa barua za wadhamini na nyaraka za pingamizi za wagombea

ambao hawajaridhika na uendeshaji wa zoezi la uchaguzi. Aidha sababu za mapingamizi kwa

baadhi ya wagombea kutowekwa wazi (bayana), kampeni kufanyika zaidi ya muda

unaokubaliwa kisheria, chama kimoja kuingilia kampeni ya chama kingine cha siasa, uelewa

mdogo wa wapiga kura kuhusu sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi pamoja na matumizi ya

lugha za matusi, kashfa na kejeli.

Aidha, utafiti unaonesha kuwa wakati wa zoezi la upigaji kura, baadhi ya wapiga kura

walisafirishwa toka eneo moja kwenda eneo lingine kinyume na taratibu, majina ya baadhi ya

wagombea kutooneka vituoni, kutokuwepo kwa eneo la faragha la kupigia kura, upungufu wa

vifaa zikiwemo karatasi za kupigia kura (ballot papers), kuendelea kwa kampeni hata wakati wa

kupiga kura, kutokufunguliwa kwa wakati vituo vya kupiga kura, picha za baadhi ya wagombea

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

ii

kuchanwa pamoja na kukosekana/kutokuwepo kwa mawakala kwa baadhi ya vyama vya siasa.

Vilevile, utafiti umebaini uwepo wa vitendo vya rushwa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa

ambavyo ni ugawaji wa fedha taslimu, kanga, mashati, kofia, vinywaji na vyakula, mifuko ya

saruji na jezi za michezo, kwa lengo la kuwashawishi wapiga kura. Aidha baadhi ya vituo

vilichelewa kuhesabu na kutoa matokeo hali iliyo sababisha vurugu na fujo. Vitendo vya rushwa,

ukiukwaji wa Sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi huenda ni kati ya mambo yaliyosababisha

uchaguzi kurudiwa katika baadhi ya maeneo.

Kutokana na matokeo ya utafiti huu mambo yafuatayo yanapendekezwa ili kuziba mianya ya

rushwa katika chaguzi zijazo: kutoa elimu kuhusu haki na wajibu wa mpiga kura katika

mchakato mzima wa uchaguzi; Kuimarisha vyombo vinavyohusika na usimamizi wa Sheria na

taratibu za uchaguzi; vyama vyote vya siasa vinavyoshiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa,

na Uchaguzi Mkuu vinapaswa kuzingatia maadili wanayokuwa wameyaridhia kwa pamoja kama

wadau maalumu wa kukuza demokrasia nchini; wasimamizi wa uchaguzi wanapaswa kutekeleza

wajibu wao kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi; na kujiepusha na itikadi za

kisiasa au vitendo vinavyoashiria upendeleo,rushwa au ushabiki wa kisiasa.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

iii

SHUKRANI

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inatoa shukrani zake za dhati kwa

wale wote walioshiriki katika kufanikisha Utafiti huu. Kwa kuwa si rahisi kuwataja wote

waliofanikisha utafiti huu, shukrani za pekee ziwaendee Wananchi, Wasimamizi wa Uchaguzi,

Mawakala na Waangalizi wa Uchaguzi kwa kushiriki kikamilifu katika utafiti huu.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

iv

YALIYOMO

MUHTASARI (EXECUTIVE SUMMARY) .................................................................................. i

SHUKRANI ................................................................................................................................... iii

YALIYOMO .................................................................................................................................. iv

ORODHA YA CHATI ................................................................................................................. vii

ORODHA YA VIFUPISHO .......................................................................................................... ix

SURA YA KWANZA .................................................................................................................... 1

1.0 UTANGULIZI ...................................................................................................................... 1

SURA YA PILI ............................................................................................................................... 3

2.0 MAPITIO YA MAKALA ..................................................................................................... 3

2.1 MUONGOZO WA UCHAGUZI WA NGAZI ZA VIJIJI, VITONGOJI NA MITAA... 4

2.2 Rushwa katika Siasa ......................................................................................................... 7

2.3 Athari za Rushwa katika Uchaguzi .................................................................................. 9

SURA YA TATU ......................................................................................................................... 11

3.0 MBINU ZA UTAFITI .................................................................................................... 11

3.1 Maeneo na Muda wa Utafiti ....................................................................................... 11

3.2 Ukusanyaji wa Taarifa ..................................................................................................... 11

3.2.1 Taarifa za Msingi .......................................................................................................... 11

3.3 Upatikanaji wa Sampuli wakilishi. ............................................................................. 11

3.4 Ukubwa wa Sampluli.................................................................................................. 12

3.5 Uchambuzi na Unyambulisho wa Taarifa .................................................................. 12

SURA YA NNE ............................................................................................................................ 13

4.0 MATOKEO YA UTAFITI............................................................................................. 13

4.1 Wasifu wa Wahojiwa .................................................................................................. 13

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

v

4.2 Vitendo vya Rushwa Katika Michakato ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa .............. 14

4.3 Elimu kwa wapiga kura ................................................................................................... 34

SURA YA TANO ......................................................................................................................... 37

5.0 MAPENDEKEZO NA HITIMISHO ............................................................................. 37

5.1 Mapendekezo .............................................................................................................. 37

5.2 Hitimisho .................................................................................................................... 38

6.0 MAREJEO .............................................................................................................................. 39

6. VIAMBATANISHO ................................................................................................................. 40

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

vi

ORODHA YA MAJEDWALI

Jedwali 1: Mchanganuo wa mwitikio wa wahojiwa kuhusu wasifu wao

Jedwali 2: Mwitikio wa wahojiwa kuhusu kujiandikisha na orodha ya wapiga kura

Jedwali 3: Mwitikio kuhusu kuwepo kwa barua za wadhamini na mapingamizi kwa wagombea

Jedwali 4: Taarifa kwa wadau kuhusu mapingamizi mbalimbali

Jedwali 5; Mapingamizi kwa wagombea wa nafasi mbalimbali katika mikoa iliyojaza hojaji

Jedwali 6: Mwitikio wa Wahojiwa Kuhusu Mwenendo wa Kampeni za Uchaguzi wa Serikali za

Mitaa 2014.

Jedwali 7: Mwitikio wa Wahojiwa kuhusu uwepo Rushwa na aina zake katika Uchaguzi

Jedwali 8: Majina na Namaba Wapiga Kura Kuonekana Vituoni

Jedwali 9: Mwitikio wa wahojiwa kuhusu mwenendo wa upigaji kura katika Uchaguzi wa

Serikali za Mitaa 2014.

Jedwali 10: Mwitikio wa wahojiwa kuhusu elimu ya uchaguzi na aina ya elimu waliyopata

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

vii

ORODHA YA CHATI

Chati 1: Nafasi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014

Chati 2: Majina na mipaka ya mitaa, vijiji na vitongoji siku 50 kabla ya uchaguzi

Chati 3: Wagombea kuidhinishwa na vyama vyenye usajili wa kudumu

Chati 4: Uwepo wa mapingamizi katika uteuzi wa wagombea

Chati 5: Taarifa za kuwafahamisha wapingaji kuhusu kupokelewa kwa mapingamizi

Chati 6: Taarifa za kuvifahamisha vyama vya siasa kuhusu uamuzi wa mamlaka za uteuzi

kuhusu mapingamizi yaliyopokelewa

Chati 7: Ushiriki katika mikutano ya kampeni

Chati 8: Kampeni kufanyika baada ya saa kumi na mbili jioni

Chati 9: Chama kuingilia kampeni ya chama kingine

Chati 10: Wananchi waliosafirishwa kwenda katika vijiji/ mitaa mingine kupiga kura

Chati 11: Uchaguzi kufanyika sehemu faragha

Chati 12: Karatasi zote za kupigia kura zilikuwa karatasi maalum

Chati 13 Vituo vyote vya kupigia kura vilikuwa na mawakala wa vyama vya siasa

Chati 14 Matokeo ya Wenyeviti wa vijiji kwa mikoa 14

Chati 15 Matokeo ya Wenyeviti wa Vitongoji kwa Mikoa 24

Chati 16: Kupata elimu kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa

Chati 17: Maoni ya wadau kuhusu kusuia vitendo vya rushwa na kuboresha chaguzi za

serikali za mitaa

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

viii

ORODHA YA PICHA

Picha 1: Baadhi yai wananchi wakihakiki uwepo wa majina yao kwa kutumia tochi za

simu

Picha 2: Baadhi ya wananchi wakiwa katika foleni kwa ajili ya kupiga kura

Picha 3: Wapiga kura katika kituo cha kupigia kura

Picha 4 Fomu ya kupiga kura

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

ix

ORODHA YA VIFUPISHO

ACT Alliance for Change and Transparency

CCM Chama cha Mapinduzi

CHADEMA Chama cha Demokrasia na Maendeleo

CHAUMA Chama Cha Ukombozi wa Umma

CUF Civic United Front

DP Democratic Party

NCCR-M National Convention for Construction and Reform- Mageuzi/Change

NEC National Election Commitee

NLD National League for Democracy

NRA National Reconstruction Alliance

PPT Progressive Party of Tanzania

TADEA Tanzania Democratic Alliance Party

TLP Tanzania Labour Party

TAKUKURU Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa

TAMISEMI Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

UDP United Democratic Party

UMD United for Multparty Democracy

UPDP United People’s Democratic Party

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

1

SURA YA KWANZA

1.0 UTANGULIZI

Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) ndiyo iliyopewa

dhamana kuzisimamia mamlaka za Serikali za Mitaa hapa nchini. Sera mbalimbali zimekuwa

zikitekelezwa na TAMISEMI ikiwemo ile ya Ugatuaji wa Madaraka (Decentralization by

Devolution) kwa lengo la kuboresha mfumo wa Serikali za Mitaa. Ugatuaji huo wa majukumu

ukihusisha fedha, rasimali watu na vitendea kazi, kutoka Serikali Kuu kwenda Serikali za Mitaa

na kutoka Serikali za Mitaa kwenda ngazi za chini za utawala. Katika kutekeleza dhana ya

utawala bora, suala la usimamizi wa fedha kwenye mamlaka hizo lina umuhimu wa kipekee

kwani fedha za ruzuku za maendeleo zimekuwa zikipelekwa moja kwa moja kwenye

halmashauri hizo.

Serikali za Mitaa ndiyo mamlaka za wananchi ambazo kwa mujibu wa ibara ya 145 ya Katiba ya

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 mamlaka hizo huundwa, huendeshwa na

huwajibika kwa wananchi ambao ndiyo chimbuko la mamlaka yote katika nchi. Aidha, kwa

mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 146, Katiba inazitambua

Mamlaka ya Serikali za Mitaa kama vyombo vya haki vyenye mamlaka ya kuwashirikisha

wananchi kupanga na kutekeleza shughuli za maendeleo na utoaji wa huduma muhimu. Hizi

ndizo mamlaka za kiutawala zilizo karibu zaidi na wananchi. Hivyo basi mamlaka hizo ndizo

zilizopewa dhamana kikatiba katika kuhakikisha zinasimamia utoaji huduma za kijamii kama

vile ile ya elimu, maji, afya, kilimo, ufugaji na uvuvi, barabara, maliasili na utalii n.k. Aidha,

mamlaka hizo zipo kwa lengo la kukuza demokrasia kwa kuwashirikisha wananchi kuchagua

viongozi wao. Kwa mantiki hiyo ushiriki wa wananchi katika chaguzi za vyama vingi zilizo huru

na haki (kidemorkasia) ni nguzo muhimu ya kukuza utawala bora.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini ulifanyika tarehe 14 Desemba mwaka 2014, ukiwa ni

uchaguzi wa tano kufanyika chini ya mfumo wa vyama vingi kuwachagua viongozi wa Vijiji,

Vitongoji na Mitaa. Mamlaka za Serikali za Mitaa zilirejeshwa mwaka 1984 kwa sheria ya

Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) sura ya 287 na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka ya

Miji) sura ya 288 ambapo, uchaguzi wa Serikali za Mitaa ngazi za Mitaa, Kijiji na Kitongoji

umekuwa unafanyika kila baada ya miaka minne. Uchaguzi huu ni muhimu kwani matokeo yake

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

2

yanaweza kusaidia kukuza demokrasia nchini kwa kuitambua mianya ya rushwa na kupendekeza

namna inavyoweza kuzibwa.

Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, ambapo hadi sasa kuna vyama vya siasa 18 vyenye usajili wa

kudumu. Katika mfumo wa kidemokrasia, viongozi hupatikana kupitia uchaguzi ulio huru na

haki. Hata hivyo, zimekuwepo kasoro kadhaa katika uendeshaji na usimamizi wa chaguzi hizi.

Sababu mbalimbali zimekuwa zikitajwa zikiwemo zile za kunga’ang’ania kukaa madaraka,

ubinafsi, ukabila, urafiki, ujinga, umaskini na rushwa. Aghalabu, uwepo wa tuhuma za rushwa

katika uchaguzi huondoa imani ya wapiga kura, kutoaminiwa kwa serikali na hata kusababisha

machafuko.

Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali katika kupambana na vitendo vya rushwa katika

uchaguzi kwa kutunga na kurekebisha sheria. Sheria hizo ni; Sheria ya Vyama vya Siasa namba

5 ya mwaka 1992, Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11 ya mwaka 2007,

Sheria ya Gharama za Uchaguzi namba 6 ya mwaka 2010; Sheria ya Uchaguzi, kwa kuondolewa

kwa kifungu cha takrima na kutungwa kwa Kanuni za uchaguzi za mwaka 2009 (mfano kanuni

namba 18) zinazozuia vitendo vya rushwa katika uchaguzi za Serikali za Mitaa. Kwa mujibu wa

Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa namba 4 ya mwaka 1979, uchaguzi wa Serikali za

Mitaa unasimamiwa na Halmashauri za Majiji/Manispaa/Miji/Wilaya chini ya usimamizi wa

Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Hata hivyo, pamoja na jitihada zote

hizo za Serikali katika kusimamia chaguzi mbalimbali nchini, vitendo vya rushwa vimeendelea

kuongezeka. Kwa sababu hiyo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)

ilifanya utafiti kwa lengo la kubaini mianya ya rushwa katika uchaguzi na kisha kushauri njia

bora ya kudhibiti vitendo vya rushwa.

Aidha, madhumuni mahsusi ya utafiti huo yalikuwa kama ifuatavyo:

i) Kubaini mianya ya rushwa katika mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014;

ii) Kutathmini uelewa wa wananchi kuhusu haki na wajibu wao katika uchaguzi wa Serikali

za Mitaa

iii) Kuainisha vitendo vya rushwa wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na;

iv) Kushauri namna ya kuziba mianya ya rushwa itakayobainika katika uchaguzi wa Serikali

za Mitaa.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

3

SURA YA PILI

2.0 MAPITIO YA MAKALA

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa hapa nchini husimamiwa na Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za

Mitaa namba 4 ya mwaka 1979 sura namba 292 kama ilivofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

Pamoja na kuwepo kwa sheria hiyo, uchaguzi za Serikali za Mitaa huendeshwa pia kwa

uzingatia kanuni zitokanazo na sheria za Serikali za Mitaa za mmlaka za miji sura ya 288 na

mamlaka za wilaya sura ya 287. Kanuni hizi zinatoa taratibu na masharti yanayotakiwa

kuzingatiwa wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Aidha, tarehe 5/9/2014 Waziri mwenye

dhamana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kupitia Gazeti la Serikali

namba 320,321,322 na 323, alitoa tangazo la kufanyika kwa uchaguzi huo Decemba, 2014

ambapo Waziri husika alitangaza pia kanuni nne (4) zitakazotumika kusimamia uchaguzi huo:

Kanuni hizo ni pamoja na:

i) Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kitongoji katika Mamlaka za Mijii Midogo za

Mwaka, 2014, zilizotungwa chini ya kifungu cha 201A zinazotokana na sheria ya

Serikali za Mitaa (Mamlaka za Wilaya) sura ya 287.

ii) Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kijiji, Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji na

Mwenyekiti wa Kitongoji katika Mamlaka za Miji za Mwaka, 2014 zilizotungwa chini

ya kifungu cha 87A zinazotokana na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) sura

ya 288.

iii) Kanuni za Uchaguzi za Mwenyekiti wa Mtaa na Wajumbe wa Kamati ya Mtaa katika

Mamlaka za Miji za Mwaka, 2014 zilizotungwa chini ya kifungu cha 87A zinazotokana

na Sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za Miji) sura ya 288.

iv) Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kijiji, Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji na

Mwenyekiti wa Kitongoji katika Mamlaka za Wilaya Za Mwaka 2014, zilizotungwa

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

4

chini ya kifungu cha 201A zinazotokana na sheria ya Serikali za Mitaa (Mamlaka za

Wilaya) sura ya 287.

Tarehe 16 Oktoba, 2014 ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ilitoa

mwongozo wa uchaguzi wa viongozi wa ngazi za Vijiji, Vitongoji na Mitaa ambapo mambo

kadhaa yalitolewa ufafanuzi kuhusu mchakato mzima wa uchaguzi huo, kama inavyooneshwa

hapo chini.

2.1 MUONGOZO WA UCHAGUZI WA NGAZI ZA VIJIJI, VITONGOJI NA MITAA

a) Kutangaza majina ya Vijiji, Vitongoji, Mitaa na Mipaka ya maeneo yake

Taratibu za uchaguzi zinaelekeza wazi kuwa kila Msimamizi wa Uchaguzi alitakiwa kutangaza

majina ya maeneo na mipaka ya kila Mtaa, Kitongoji au Kijiji kwa wakazi wa maeneo yake

katika muda wa siku 50 kabla ya siku ya uchaguzi ili kuwawezesha wakazi wa maeneo hayo

kuyatambua na kufahamu wanaowajibika kupiga kura.

b) Ratiba ya Shughuli za Uchaguzi

Kila Msimamizi wa Uchaguzi/ Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ahakikishe kuwa shughuli zote

za Uchaguzi zinaanza na kukamilika katika muda uliowekwa katika Kanuni, kuzingatia ratiba,

kutoa elimu kwa umma kuhusu uchaguzi na kufahamu idadi ya Vijiji, Vitongoji au Mitaa

itakayohusika kufanya uchaguzi na kufahamu idadi ya wakazi ili iweze kupeleka idadi sawa ya

karatasi zinazohitajika kwenye upigaji kura.

c) Kutoa maelezo kuhusu Uchaguzi

Wasimamizi wa uchaguzi watatoa maelekezo kuhusu Uchaguzi siku 28 kabla ya siku ya

uchaguzi yaani tarehe 16 Novemba, 2014. Maelezo hayo yataeleza masuala ambayo ni tarehe ya

uchaguzi, mahali na muda uchaguzi utafanyika, zoezi la ujiandikishaji, nafasi za

zinazogombewa, tarehe, muda na mahali pa kuchukulia fomu na kurudisha, uteuzi wa

wagombea, muda wa kuwasilisha pingamizi na mikutano ya kampeni.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

5

d) Uteuzi wa Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi

Wasimamizi wa Uchaguzi watateua wasimamizi Wasaidizi wa uchaguzi kwa kila Mtaa,

Kitongoji na Kijiji kutoka miongoni mwa maafisa Watendaji wa Vijiji na Mitaa na ni pamoja na

Afisa yoyote wa umma atayeteuliwa na msimamizi wa uchaguzi wakati wa uchaguzi kwa

kuzingatia sifa zifuatazo wasiwe na dhamana ya au uongozi wa chama chochote cha siasa, wawe

watumishi wa umma na waadilifu. Wasimamizi wasaidizi na maafisa wengine watapaswa

kuhudhuria semina za mafunzo kuhusu mwongozo wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini.

e) Uandikishaji wa Wapiga Kura

Msimamizi wa Uchaguzi atamteua Afisa wa Umma au mtu mwingine yoyote mwenye sifa na

uadilifu ambaye ataandikisha na kuandaa orodha ya wapiga kura. Uandikishaji utafanyika

kwenye maeneo husika kwa siku 21 kabla ya siku ya uchaguzi na utafanyika kwa siku saba

kuanzia tarehe 23 hadi 29 Novemba, 2014. Uandikishaji utafanyika kwenye majengo ya umma

au sehemu ambayo Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi atakuwa amekubaliana na viongozi wa

vyama vya siasa kuanzia saa 1:30 asubuhi na kufungwa saa 10 jioni kwa kuwaorodhesha wakazi

wenye sifa tu. Vyama vya siasa vitaruhusiwa kuweka wawakilishi wao wakati wa uandikishaji

kwa gharama za chama husika, ambapo baada ya siku saba za uandikishaji wapiga kura

Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi atabandika orodha ya wapiga kura ili kutoa muda kwa

wananchi kukagua orodha ya wapiga kura. Pingamizi dhidi ya mtu kuandikishwa kuwa mpiga

kura litawasilishwa kwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ambaye atalitolea uamuzi na

kurekebisha orodha hiyo kwa muda wa siku 5 yaani kuanzia tarehe 6 Decemba hadi tarehe 10

Dcemba 2014. Orodha ya mwisho ya wapiga kuraa itabandikwa siku 3 kabla ya siku ya kupiga

kura yaani kuanzia tarehe 11 hadi tarehe 13 Decemba, 2014

f) Kuchukua fomu za kugombea uongozi

Wasimamizi wa Uchaguzi wataandaa fomu za kutosha za kugombea nafasi zilizotajwa, fomu

hizo zitatolewa siku 27 kabla ya siku ya Uchaguzi na zoezi la kutoa fomu litafanyika kwa siku 7

yaani kuanzia tarehe 16 hadi tarehe 22 Novemba, 2014. Fomu hizo zitatolewa bila masharti wala

malipo yoyote, nakala moja ya fomu hizo itabandikwa kwenye ubao wa matangazo ili mgombea

yoyote mwenye pingamizi aweze kujitokeza.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

6

g) Idadi ya wajumbe watakaochaguliwa

(i) Mwenyekiti wa Kijiji/ Mtaa

(ii) Wenyeviti wa Vitongoji walio katika eneo la kijiji

(iii) Wajumbe wa viti maalumu wanawake

(iv)Wajumbe mchanganyiko wanawake na wanaume

h) Uteuzi wa Wagombea

Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi atafanya uteuzi wa wagombea wa nafasi za uongozi ngazi

zote siku zisizopungua 20 kabla ya tarehe ya uchaguzi yaani tarehe 24 Novemba, 2014 na

mwisho wa kurudisha fomu ilikuwa ni saa 10 jioni siku ya uteuzi ya uteuzi

i) Kamati ya Rufaa

Makatibu Tawala wa Mikoa watateua wajumbe wa Kamati za Rufaa siku 7 kabla ya siku ya

uteuzi yaani tarehe 17 Novemba 2014. Wajumbe wa kamati hiyo utamuhusisha Katibu Tawala

wa Wilaya au afisa mwingine wa umma atakayeteuliwa ambaye atakuwa mwenyekiti, afisa

yoyote kutoka taasisi ya umma iliyoko katika wilaya husika ambaye atakuwa mjumbe na afisa

yoyote wa umma anayefanyakazi katika ofisi ya Katibu Tawala wa Wilaya ambaye atakuwa

Katibu.

Mgombea au Mwakilishi wake ambaye hataridhika na uamuzi wa Msimamizi Msaidizi wa

Uchaguzi kuhusu uteuzi atakuwa na haki ya kukata rufaa kwenye kamati ya ?Rufaa katika muda

usiozidi siku 4 kuanzia tarehe ya uamuzi wa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi. Kamati ya

Rufaa itasikiliza na kutoa uamuzi kuhusu uteuzi wa mgombea katika muda usiozidi siku 4 tangu

siku ya kupokea rufaa yaani kuanzia tarehe 26 Novemba hadi tarehe 29 Novemba, 2014

j) Kampeni za Uchaguzi

Kampeni za uchaguzi zitafanyika siku kumi na nne za mwisho na zitamalizika siku moja kabla

ya siku ya uchaguzi, kampeni zitaanza 30 Novemba 2014 na kumalizika tarehe 13 Desemba

2014 ambapo wagombea wa nafasi za ngazi tofauti au mwakilishi wake au chama cha siasa

kinaweza kuitisha mikutano ya kampeni kwa ajili ya kujinadi kwa wananchi kwa kufuata ratiba

iliyowasilishwa na mgombea, mwakilishi wake au chama cha siasana kuratibiwa na Msimamizi

wa Uchaguzi ambapo kampeni zitaanza saa 2 asubuhi na zitamalizika saa 10 jioni ya kila siku ya

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

7

kampeni. Vyombo vya Ulinzi na Usalama kama Jeshi la Polisi vitatumika katika kuhakikisha

kunakuwepo na usalama na utulivu katika mikutano ya kampeni na wakati wa uchaguzi. Vikundi

vya jadi, ushabiki vimepigwa marufuku kuwepo maeneo ya mikutano ya kampeni au ya

uchaguzi. Aidha, vikundi vya uhamasishaji pia vimepigwa marufuku kujihusisha na kazi ya

ulinzi wa amani au chimbuko la fujo kwenye mikutano hiyo.

k) Utaratibu wa kupiga kura

Kwa kutegemea hali na mazingira ya kila eneo muda wa kuitisha mkutano wa uchaguzi

umepangwa kuwa wakati wote kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 10 jioni. Kutakuwepo na sanduku

maalumu la kupigia kura ambalo kabla ya uchaguzi litahakikiwa likiwa wazi kabla ya kufungwa

kwa lakiri na kuanza kwa zoezi la upigaji kura. Kabla ya Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi

hajampatia mpiga kura karatasi za kupigia kura, atajiridhisha kama jina la mpiga kura

liorodheshwa karika orodha ya wapiga kura na baada ya kuridhiks atamtaka mpiga kura

ajitambulishe kwa kutumia kitambulisho kinachotambuliwa. Kura zitapigwa katika majengo ya

umma au sehemu ambayo Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ataiteua baada ya kushauriana na

wagombea, wawakilishi wao au vyama vya siasa isipokuwa majengo ya vyombo vya usalama,

taasisi za dini na vyama vya siasa.

l) Utaratibu wa kuwasilisha taarifa na matokeo ya uchaguzi

Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi katika mitaa, vitongoji na vijiji watapeleka taarifa kwa

maafisa watendaji wa kata/ Vijiji kama idadi ya watu waliojiandikisha, idadi ya wakazi

waliojitokeza katika uchaguzi na majina ya wagombea walioshinda. Matokeo ya uchaguzi kwa

ngazi tofauti yatajazwa kwenye fomu maalumu ambayo itasainiwa na wagombea au wawakilishi

wao pamoja na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi na kubandikwa kwenye mbao za matangazo.

2.2 Rushwa katika Siasa

Haibishaniwi kuwa uwepo wa rushwa huweza kusababisha athari mbaya katika jamii katika

maeneo tofauti tofauti. Zipo tafiti zinazobainisha athari ya rushwa kwenye ukuwaji wa uchumi,

utulivu na biashara (Merton 1957; Leff 1964; Nye 1967; Huntington 1968; Mo 2001), Usawa

(Li, Xu, and Zou 2000, Gupta, Davood, and Alonso- Terme 2002) Uwekezaji (Mauro 1995; Wei

2000) Uaminifu kati ya mtu na mtu (Seligson 2002) na Imani ya wananchi juu ya demokrasia

(Phar na Putnam 2002).

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

8

Mbali ya ukweli kwamba chaguzi ndiyo msingi mkuu wa demokrasia, michakato ya uchaguzi

imekuwa hatarini kwa vitendo vya rushwa na udanganyifu. Kwa kuwa chaguzi nyingi zimekuwa

zikifanyika mara kwa mara, kumejitokeza jitihada za siri za kuhakikisha chaguzi hizo

zinakumbwa na vitendo vya rushwa. Kote duniani rushwa inachangia katika kuondoa uhalali wa

kisiasa na mifumo ya kitaasisi (Rock; Sung 2004). Chaguzi zilizofanyika kwenye miji mikongwe

huko Athens na Sparta miaka mingi iliyopita (Staveley, 1972: chap 5) na pia katika miaka ya

hivi karibuni kote duniani inaonesha kuwa chaguzi hizo zilikumbwa na vitendo vya ununuzi wa

kura na udanganyifu (Posada- Carbo, 1996; 2000).

Rushwa ni neno kongwe katika historia ya maisha ya mwanadamu na limekuwa likipewa maana

tofauti katika nyakati mbalimbali za historia. Ipo tafasari inayoielezea rushwa kuwa ni matumizi

mabaya ya raslimali za umma kwa ajili ya kujipatia manufaa binafsi (Shleifer and Vishney

1993). Lipset na Lenz (2002, 112) kwamba rushwa ni kujipatia manufaa kwa kutumia gharama

ya umma na kwa Rose – Ackerman’s ametafasiri kuwa rushwa ni matumizi ya mabaya ya ofisi

kuhalalisha maslahi yanayotokana na mifumo yenye urasimu. Ipo tafasiri inayoielezea rushwa

kuwa ni tabia mchepuko toka ile ya utaratibu rasmi wa utendaji wa majukumu ya umma kwa ajili

ya manufaa binafsi, marafiki wa karibu au yale ya kikundi binafsi (Nye 1967: 420).

Herdenheimer et al (1989:10) ameeleza kwamba rushwa inatokea pale ambapo afisa mwenye

dhamana ya ofisi ya umma ameshawishika kwa kupokea fedha au manufaa mengine ili aweze

kuchukua hatua kukidhi dhamira ya mtoaji wa fedha au manufaa hayo na hivyo kuathiri maslahi

ya umma. Kwa Niccolo Machiavelli (1513) hii ilimaanisha kuporomoka kwa maadili na ile hali

ya kutokujali maslahi ya raia. Kwa Montesquieu (van Blerk, 1996) ilimaanisha kupotoshwa kwa

mfumo wa siasa bora na kuingia kwenye mfumo muovu. Kwake Jean- Jacque Rousseau (van

Blerk, 1996), hali hii ilitokea bila kuepukika kutokana na mapambano ya kugombea madaraka.

Kostadinova (2003) katika utafiti wake ameeleza kwamba kuvunjwa moyo kwa wananchi

kutokana na kukithiri kwa rushwa kunachangia wapiga kura kutojitokeza wakati wa zoezi la

upigaji kura.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

9

Birch, 2009, kwa wepesi wa uelewa, rushwa katika uchaguzi upo katika sura tatu, ambazo ni

hila katika sheria (manipulation of rules), hila katika orodha ya wapiga kura (manipulation of

voters) na ile ya hila katika zoezi la upigaji kura (manipulation of voting). Hila katika sheria

hujitokeza pale ambapo sheria/ kanuni zinazotawala/ kuongoza uchaguzi zinapokiukwa kwa

makusudi (distorted) ili kutoa upendeleo kwa chama kimoja au mgombea mfano kuzuia sehemu

idadi fulani ya watu wazima kushiriki katika zoezi la uchaguzi.

Hila katika wapiga kura (manipulation of voters); aina hii ya rushwa hubadili machaguo ya

wapiga kura (voters preferences) na juhudi kubwa kufanywa ili kubadili nia/ dhamira za wapiga

kura. Aina hii hufanywa kwa njia tofauti kama vile kukengeuka katika sheria za gharama za

uchaguzi, matumizi ya raslimali za umma, upendeleo katika matumizi ya vyombo vya habari,

ununuzi wa kura na vitisho kwa wapiga kura kwa manufaa ya chama kimoja au kwa mgombea.

Hila katika zoezi la upigaji kura (manipulation of voting); aina hii ya rushwa inahusisha

ucheleweshaji au upelekaji wa vifaa pungufu kwa kwenye vituo vya kupigia kura hasa maeneo

ambayo ni ngome ya upinzani na kukosekana kwa dhana ya uwazi katika taasisi zinazosimamia

uchaguzi.

Hivyo basi, sababu yoyote itakayochangia kutokea kwa uchaguzi mbovu, haiwezi kubishaniwa

kuwa zoezi la uchaguzi linapoharibika demokrasia na utawala bora huathirika kwa kiasi kikubwa

na huchukua muda mrefu kubadili hali hiyo.

2.3 Athari za Rushwa katika Uchaguzi

Rushwa huleta changamoto kubwa katika maendeleo ya mtu mmoja mmoja na nchi kwa ujumla.

Katika siasa, rushwa hudumaza demokrasia na utawala bora katika nchi uvunjifu na upindishaji

wa sheria au taratibu zilizowekwa. Rushwa katika siasa husababisha viongozi wanaowekwa

kutokuwa na uwajibikaji na kutokuwa na uwakilishi ufaao katika kufanya maamuzi (Wikipedia,

2010).

Aidha, athari nyingine za rushwa katika uchaguzi ni kuondoa uhuru wa mpiga kura, wagombea

wenye vipaji na uwezo wa kuwakilisha hushindwa kushiriki kugombea katika uchaguzi kwa

kukosa uwezo wa fedha, huharibu dhana nzima ya uwakilishi kwa kuwa wanaochaguliwa

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

10

hawana ridhaa kamili ya mpiga kura, viongozi waliochaguliwa kwa njia ya rushwa hawawezi

kusimamia mapambano dhidi ya rushwa wakiwa madarakani na usimamizi wa shughuli za

maendeleo hukwama kutokana na vitendo vya ubadhilifu wa rasilimali za umma. Rushwa katika

Uchaguzi inazuia wananchi kuwapigia kura viongozi wanaowataka na hivyo kupata viongozi

wabovu na kudidimiza demokrasia na kuzuia uchaguzi ulio huru na wa haki (NEC, 2010).

Mwaka 2010, Sheria ya Gharama za Uchaguzi Namba 6 ya mwaka 2010 ilipitishwa kwa lengo la

kutambua kisheria mchakato wa uchaguzi ndani ya vyama na kuusimamia kisheria, kuweka

utaratibu wa kisheria wa kudhibiti, kusimamia na kuratibu mapato na matumizi ya gharama za

kampeni kwa vyama vya siasa na wagombea katika uchaguzi, kudhibiti zawadi kutoka nje ya

nchi, kuweka utaratibu na mfumo wa uwajibikaji wa mapato na matumizi ya fedha za uchaguzi

kwa upande wa Vyama vya Siasa na wagombea. Sheria hii imeweka utaratibu wa kudhibiti

matumizi ya fedha wakati wa kampeni kwa kumtaka kila mgombea na kila chama

kitakachoshiriki katika chaguzi kutoa taarifa ya matumizi na vyanzo vya fedha inayotarajia

kutumika kama gharama ya uchaguzi.

2.4 Muhtasari wa Mapitio ya Nadharia (Summary of Literature Review)

Pamoja na kwamba zipo tafiti nyingi kuhusu Serikali za Mitaa, matokeo ya tafiti hizo

zinaonyesha kwamba rushwa bado ni tatizo sugu kwenye nchi zinazoendelea. Hata hivyo, tafiti

zinaonyesha nchi zinazoendelea na hasa nchi za Afrika zilizopo Kusini mwa Jangwa la Sahara

ndizo zimeathirika zaidi kuliko nchi za Ulaya. Moja ya sababu kubwa ni tamaa ya kung’ang’ania

kukaa madarakani ili kujineemesha pamoja na kujilimbikizia mali. Hata hivyo ukubwa wa tatizo

unatofautiana kutoka nchi moja na nyingine. Kwa sababu hiyo, bado kuna haja ya kuendelea

kufanya tafiti kwenye eneo hili ili kukuza uelewa kwa lengo la kukuza Demokrasia.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

11

SURA YA TATU

3.0 MBINU ZA UTAFITI

3.1 Maeneo na Muda wa Utafiti

Utafiti huu ulifanyika katika Mikoa ya Tanzania Bara ambapo mikoa 19 ilijaza hojaji. Utafiti

ulifanyika wakati wa kutangaza majina na mipaka ya vijiji na vitongoji, uteuzi wa wagombea,

kampeni za uchaguzi, uchaguzi na baada ya uchaguzi. Utafiti ulifanyika katika kipindi cha

kuanzia Novemba 2014 hadi Desemba 2014. Aidha, katika mikoa hiyo wilaya zote zilihusishwa

ambapo katika kila wilaya, zilichaguliwa kata mbili na katika kata hizo, vilichaguliwa vijiji

viwili au mitaa miwili.

3.2 Ukusanyaji wa Taarifa

Katika utafiti huu, taarifa za msingi na za taarifa za upili zilikusanywa.

3.2.1 Taarifa za Msingi

Taarifa za msingi zilikusanywa kwa kutumia mahojiano/usaili na kwa kuangalia matukio

(Observation). Mahojiano kwa njia ya usaili (interview schedual) pamoja na checklist orodha ya

ukaguzi (checklist).

3.2.2 Taarifa za Upili

Taarifa za upili zilikusanywa kwa kuchambua Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo

inayohusiana na chaguzi. Pia, kazi za watafiti kama machapisho, makala na majarida kuhusu

chaguzi za Serikali za Mitaa.

3.3 Upatikanaji wa Sampuli Wakilishi.

Wahojiwa katika utafiti huu walipatikana kwa kutumia njia/ mbinu zifuatazo:-

Sampuli kwa mpangilio/makusudi maalum (Non Random Sampling/Purposive

Sampling)

Njia hii ilitumika kuwapata walengwa kutokana na majukumu yao katika uchaguzi.

Walengwa waliohojiwa ni wagombea katika nafasi za mwenyekiti wa kijiji/mitaa,

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

12

kitongoji, na mjumbe wa halmashauri ya Kijiji pamoja na wasimamizi na wasimamizi

wasaidizi wa uchaguzi.

Sampuli bila Mpangilio Maalum (Random Sampling)

Njia hii ilitumika kuwapata wahojiwa walio katika makundi makubwa. Wahojiwa

waliopatikana kwa njia hii ni wananchi katika wilaya, kata na vijiji/mitaa iliyotembelewa

kwenye mikoa yote ya Tanzania Bara.

3.4 Ukubwa wa Sampuli

Ujazaji wa dodoso katika utafiti huu ulifanyika katika mikoa 19 kati ya mikoa 25 ya Tanzania

Bara iliyofanyiwa utafiti. Katika mikoa hiyo iliyojaza madodoso, utafiti ulifanyika katika Wilaya

69, kata 275 na vijiji/mitaa 402 ambapo jumla ya wadau 1332 walishiriki. Wadau walioshiriki ni

wasimamizi wa uchaguzi wilaya (84), wasimamizi wa Uchaguzi wasaidizi kata (155), wagombea

wa nafasi za mwenyekiti wa Mtaa/Kijiji (162), wagombea wa nafasi za mwenyekiti wa kitongoji

(190), wagombea wa nafasi za ujumbe katika Halmashauri za Kijiji/mtaa (242) na wananchi

(499).

3.5 Uchambuzi na Unyambulisho wa Taarifa

Taarifa zilizokusanywa kwa njia ya madodoso na orodha ya ukaguzi zilisafishwa (data cleaning),

kuchambuliwa (editing), kuwekewa alama (coding), na kunyambuliwa kwa kutumia programu

maalumu ya Statistical Package for Social Science (SPSS).

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

13

SURA YA NNE

4.0 MATOKEO YA UTAFITI

Sura hii inatoa matokeo ya utafiti na uchambuzi ikihusisha wasifu wa waliojaza dodoso na

wahojiwa. Aidha, sura hii inachambua mianya ya rushwa katika mchakato mzima wa uchaguzi

wa Serikali za Mitaa ikiwa ni pamoja na mwenendo wa kampeni katika uchaguzi na upigaji kura,

elimu na uelewa kuhusu uchaguzi wa Serikali za Mitaa, mapungufu katika uchaguzi na matukio

yaliyoathiri zoezi zima la uchaguzi kwa ujumla.

4.1 Wasifu wa Wahojiwa

Wasifu wa wahojiwa katika utafiti huu, unajumuisha mgawanyiko wao kwa umri, elimu

waliyofikia na jinsia. Utafiti huu ulilenga kufanya mahojiano na wananchi ambao kwa umri wao

wanastahili kutumia haki yao ya kupiga kura, yaani kuanzia umri wa miaka 18 na kuendelea.

Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwa asilimia 71.0 ya wahojiwa walikuwa wanaume na

asilimia 29.0 walikuwa wanawake (Jedwali 1) ambapo wanaumme walikuwa wengi zaidi

kutokana na makundi ya wagombea na wasimamizi yaliyochaguliwa kwa utaratibu maalum

(Non random sampling). Aidha, wahojiwa walikuwa na umri wa miaka 18 hadi 35 walikuwa

asilimia 36.3 ambapo zaidi ya nusu (50.8%) ya wahojiwa walikuwa na umri wa miaka 36 hadi

55 na wachache (13%) walikuwa na umri wa zaidi ya miaka 55. Kiwango cha elimu cha

wahojiwa kilitofautiana ambapo, asilimia 51.2 ya wahojiwa walikuwa na elimu ya msingi,

asilimia 33.0 walikuwa na elimu ya sekondari, asilimia 15.2 ya wahojiwa walikuwa na elimu ya

juu na asilimia 0.7 walieleza kuwa walikuwa hawajasoma.

Jedwali 1: Mchanganuo wa Mwitikio wa Wahojiwa kuhusu Wasifu Wao

Jinsi Elimu Umri

Mwitikio Asilimia Mwitikio Asilimia Mwitikio Asilimia

Wanaume 71.0 Msingi 51.2 Miaka 18 hadi 35 36.3

Wanawake

29.0

Sekondari 33.0 Miaka 36 hadi 55 50.8

Elimu ya juu 15.2 Zaidi ya miaka 55 13.0

Sijasoma 0.7

Jumla 100.0 100.0 100.0

Chanzo: Utafiti 2014

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

14

Matokeo haya yanaashiria kuwa wapiga kura wengi walikuwa wananchi wenye umri wa kati

ambapo kuna uwezekano kuwa, ufahamu wao na uzoefu katika kupiga kura ni mkubwa

ikizingatiwa kuwa ni kundi ambalo limeshiriki katika chaguzi nyingine zilizopita. Hata hivyo

kundi la wahojiwa lenye elimu ya msingi ni zaidi ya asilimia 50. Hali hiyo inaweza kuathiri

uelewa wa sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi hivyo elimu ya kutosha inapaswa kutolewa

kuhusu taratibu, haki na wajibu wa mpiga kura.

Mahojiano ya ujumla yalifanyika katika mikoa ya Tanzania Bara ambapo washiriki 1332

walijaza madodoso katika mikoa 19 ya Tanzania Bara. Katika ujazaji wa hojaji asilimia 6.3

walikuwa wasimamizi wa uchaguzi wilaya, asilimia 11.6 ulihusisha wasimamizi wasaidizi wa

uchaguzi kata, asilimia 12.2 ulihusisha wagombea katika nafasi za wenyeviti wa vijiji na mitaa,

asilimia 14.3 ulihusisha wagombea wa nafasi za wenyeviti wa vitongoji, asilimia 18.2 ulihusisha

wagombea wa nafasi za wajumbe wa halmashauri za vijiji na asilimia 37.5 ulihusisha wananchi

wapiga kura kama inavyochanganuliwa katika chati 1 hapa chini:

4.2 Vitendo vya Rushwa Katika Michakato ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Sehemu hii inatoa matokeo ya mianya na vitendo vya rushwa katika hatua mbalimbali za

uchaguzi Serikali za Mitaa. Hatua hizo ni pamoja na utangazaji wa majina na mipaka ya Mitaa,

Vijiji na Vitongoji, kujiandikisha na maandalizi ya orodha ya wapiga kura; uteuzi wa

wagombea katika nafasi mbalimbali, na kampeni za wagombea

4.2.1 Utangazaji wa Majina na Mipaka ya Mitaa, Vijiji na Vitongoji

Kanuni ya 6 ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014 inaelekeza kuwa wasimamizi wa uchaguzi

wanapaswa kutoa tangazo la majina na mipaka ya Mitaa, Vijiji na Vitongoji siku 50 kabla ya

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

15

siku ya uchaguzi. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa baadhi ya mamlaka hazikutangaza majina

na mipaka ya Mitaa, Vijiji na Vitongoji.

Aidha, utafiti ulibaini kuwa baadhi ya maeneo yalikuwa na migogoro iliyohusiana na mipaka ya

mitaa. Migogoro hiyo ilisababishwa na baadhi ya wanasiasa waliosababisha kukinzana kwa

mipaka iliyotangazwa. Aidha, katika baadhi ya maeneo, baadhi ya Wabunge na Madiwani

walisababisha kukinzana huko, ili kupata wapiga kura wanaowalenga katika Uchaguzi Mkuu wa

mwaka 2015. Wanasiasa hao walitumia uelewa mdogo wa wapiga kura kuhusu mipaka ya vijiji,

vitongoji na mitaa ili kupata wapiga kura wengi. Utafiti ulibaini pia katika baadhi ya maeneo

Viongozi wa Serikali walishirikiana na wanasiasa kuchochea migogoro hiyo. Kwa ujumla,

ushirikishwaji mdogo wa wananchi katika zoezi la kutangaza majina na mipaka ya mitaa,

vitongoji na vijiji ni chanzo kikubwa cha migogoro katika baadhi ya maeneo.

4.2.2 Kujiandikisha na Orodha ya Wapiga Kura

Kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ni hatua muhimu katika uchaguzi. Hatua hiyo

inawawezesha wapiga kura kujiandikisha na hatimae kutumia haki yao ya kidemokrasia ya

kupiga kura. Mwananchi anaruhusiwa kupiga kura baada ya kuandikishwa na kuwa katika

orodha ya wapiga kura siku 21 kabla ya siku ya Uchaguzi kwa mujibu wa Kanuni ya 8 na 9 ya

Kanuni za Uchaguzi wa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa za 2014.

Utafiti ulitaka kujua iwapo wahojiwa walijiandikisha kupiga kura kwenye daftari la wapiga

kura. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa asilimia 89.3 ya wananchi waliohojiwa,

walijiandikisha katika daftari la Wapiga Kura na asilimia 10.7 hawakuwa wamejiandikisha.

Aidha, matokeo yanaonyesha kuwa asilimia 94.5 ya wahojiwa walisema orodha ya wapiga kura

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

16

ilibandikwa mahali pa matangazo ambapo asilimia 3.4 wanasema hapana na asilimia 2.1 hawajui

(Jedwali 2). Asilimia 93.8 ya waliojaza hojaji wameonyesha kuwa maandalizi ya orodha ya

wapiga kura yalifanyika Novemba 2014, ambapo inaonyesha ni kipindi cha cha wiki tatu kabla

ya uchaguzi kama inavyoelekeza Kanuni ya 9 ya Uchaguzi Serikali za Mitaa 2014.

Jedwali 2: Mwitikio wa Wahojiwa Kuhusu Kujiandikisha na Orodha ya Wapiga Kura

Kama wamejiandikisha Orodha ya wapiga kura kubandikwa mahali pa

matangazo

Mwitikio Asilimia Mwitikio Asilimia

Ndiyo

Hapana

89.3

10.7

Ndiyo

Hapana

Sijui

94.5

3.4

2.1

Jumla 100.0 100.0

Chanzo: Utafiti 2014

Katika baadhi ya maeneo utafiti ulibaini orodha ya majina ya wapiga kura, ilikuwa na majina ya

watu wasio wakazi wa maeneo husika, majina mengine yalijirudia zaidi ya mara moja na majina

mengine, ilielezwa kuwa ni ya wakazi lakini walikuwa na umri chini ya miaka 18.

Kutokujiandikisha kupiga kura kunaashiria kuwa, huenda baadhi ya wananchi hawakuwa na

elimu ya kutosha kuhusu haki na wajibu wa mpiga kura. Elimu kwa wapiga kura inapaswa

kutolewa mapema, kabla mchakato wa uchaguzi haujaanza ili kuwachagua viongozi bora. Aidha,

kutojiandikisha huenda kumesababishwa pia na wananchi kutokuwa na ari ya kujiandikisha ili

wapige kura. Hali hiyo, inaweza kusababishwa na kutokutekelezwa kwa ahadi zinazotolewa na

baadhi ya viongozi baada ya kuchaguliwa. Aidha, ubandikaji wa orodha ya wapiga kura mahali

pa matangazo ni muhimu kwa kuwa uwazi huondoa mianya ya rushwa na malalamiko.Pia

wasimamizi wa uchaguzi wanapaswa na kuweka orodha ya wapiga kura kama inavyoelekezwa

kwenye kanuni na sheria za uchaguzi.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

17

4.2.3 Uteuzi wa Wagombea

Uteuzi wa wagombea ni msingi wa kupata wagombea wenye sifa na hatimaye kupata viongozi

bora. Aidha, kila mgombea anatakiwa kuteuliwa kutoka kwenye chama cha siasa chenye sifa ya

kushiriki uchaguzi. Asilimia 12 ya wahojiwa walieleza kuwa wagombea hawakuidhinishwa na

vyama vya siasa. Hali hiyo inaweza kuwa imesababishwa na uelewa mdogo wa taratibu za

uchaguzi na kukosekana kwa uwazi katika zoezi la uteuzi wa wagombea. Aidha, Utafiti ulibaini

kuwa usiri katika zoezi la uteuzi wa wagombea umesababisha malalamiko kutoka kwa baadhi ya

waombaji. Katika baadhi ya maeneo, taratibu za uteuzi wa wagombea umevigharimu baadhi ya

vyama vya siasa kutokana na wagombea kuvihama vyama hivyo wakipinga taratibu za uteuzi. Ni

vyema vyama vya siasa kuwa na taratibu na kanuni za uteuzi zitakazowawezesha kupata

wagombea bora na hatimae kuleta maendeleo kwa wapiga kura wao na taifa kwa ujumla (Chati

3).

Utafiti ulibaini ukiukwaji wa utaratibu katika baadhi ya maeneo ambapo barua za wadhamini na

nyaraka za mapingamizi hazikuonekana. Utafiti uliangalia uwepo wa mapingamizi kwa

wagombea na iwapo taratibu zilifuatwa katika kutoa na kushughulikia mapingamizi hayo. Katika

baadhi ya maeneo, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wagombea wa vyama vya

siasa walio wekewa mapingamizi na au kuenguliwa wakilalamikia ukiukwaji wa kanuni za

kuwekewa pingamizi. Katika baadhi ya maeneo, vyama vya siasa havikuweka wagombea na

hivyo kupunguza ushindani. Aidha vyama vingi havikupata viti katika baadhi ya maeneo

(Viambatanisho 1&2). Kwa ujumla, vyama vyote vya kisiasa ni muhimu kujijenga na

kujiimarisha kuanzia katika ngazi ya Serikali za Mitaa. Hata hivyo, uteuzi makini wa wagombea

ni msingi wa kupata ushindi katika chaguz (Jedwali 3).

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

18

Utafiti ulibaini kuwa baadhi ya wasimamizi hawakuwa wanatumia sheria na kanuni za uchaguzi

kutoa maamuzi, badala yake walitumia mamlaka waliyo nayo kutoa maamuzi yaliyokuwa na

msingi upendeleo na rushwa.

Jedwali 3: Mwitikio kuhusu kuwepo kwa barua za wadhamini na mapingamizi kwa wagombea

Zilipati

kana

Hazikup

atikana

Zilithib

itishwa

Hazikuthibiti

shwa

Barua za udhamini za

wagombea wenyeviti

wa vijiji/mitaa

87.4 12.6 Nyaraka za pingamizi

wagombea wenyeviti

wa vijiji/mitaa

63.4 36.8

Barua za udhamini za

wagombea wenyeviti

wa vitongoji

71.6 28.4 Nyaraka za ingamizi

wagombea wenyeviti

wa vitongoji

76.4 23.6

Barua za udhamini za

wagombea wajumbe

wa halmashauri

76.6 23.4 Nyaraka za ingamizi

wagombea nafasi za

ujumbe

81.7 18.3

Chanzo: Utafiti 2014

Aidha, asilimia 30.3 ya wahojiwa walieleza kuwepo kwa mapingamizi, asilimia 58.6 walieleza

kuwa hakukuwepo mapingamizi na asilimia 11 walikuwa hawajui kama mapingamizi

yalikuwepo kwa wagombea walioteuliwa na vyama vya siasa, (Chati 4).

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

19

Kanuni ya 14 na 15 ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014 zinatoa maelekezo kuhusu uteuzi wa

wagombea na endapo kuna mapingamizi. Katika baaadhi ya maeneo utafiti ulibaini kuwepo kwa

wagombea ambao hawakuridhika na uamuzi uliotolewa na hivyo kutoa mapingamizi kwa

wagombea.

Katika baadhi ya maeneo, utafiti ulibaini kuwa mapingamizi hayakufuata utaratibu wa

wagombea kujaza fomu za pingamizi za kuwataka Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi kupitia

upya maamuzi yaliyokwishafanyika. Aidha, utafiti ulibaini matumizi ya nyaraka zisizo rasmi

kama barua na fomu za mapingamizi.

Ukiukwaji wa taratibu umesababisha kuwepo kwa malalamiko/mapingamizi mengi yasiyo ya

lazima kutoka kwa wagombea (Jedwali 4). Pia katika baadhi ya maeneo wasimamizi wasaidizi

walilalamikiwa kukiuka taratibu za mapingamizi ambapo waliandika barua za kuwaengua baadhi

ya wagombea kwa kutumia nafasi zao na si kwa mujibu wa kanuni na taratibu za uchaguzi.

Utafiti ulibaini kuwa ukiukwaji huo ulisababisha baadhi ya wananchi kuhisi upendeleo kwa

baadhi ya vyama na vitendo vya rushwa.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

20

Jedwali 4: Taarifa kwa Wadau kuhusu Mapingamizi

Taarifa kujulisha: Hazikupatikana

(%)

wapingaji kupokelewa kwa mapingamizi kwa wenyeviti wa Vijiji/Mitaa 14.2

wapingaji kupokelewa kwa mapingamizi kwa wenyeviti wa Vitongoji 6.8

wapingaji kupokelewa kwa mapingamizi kwa wagombea ujumbe wa

Halmashauri

1.4

Chanzo: Utafiti 2014

Katika baadhi ya maeneo utafiti ulibaini kuwa mamlaka za uteuzi hazikuvifahamisha vyama vya

siasa kuhusu maamuzi yaliyotolewa baada ya mapingamizi.Kwa mfano kuna maeneo ambayo

taarifa za pingamizi zilitolewa siku ya kupiga kura, tarehe 14 Desemba 2014, baada ya wapiga

kura kuhoji kutokuwepo kwa wagombea wao katika orodha ya wapiga kura na kuelezwa kuhusu

pingamizi. Aidha, baadhi ya maeneo, hayakuzitunza taarifa kuhusu mapingamizi ipasavyo. Hali

hii inaashiria upungufu wa uwazi, hivyo kuwa mwanya wa rushwa na chanzo cha malalamiko

katika maeneo hayo.

Kiasi cha mapingamizi kilitofautiana kati ya eneo moja na jingine hali inayoashiria tofauti ya

mwamko wa kisiasa, uelewa wa wadau wa kanuni na taratibu za uchaguzi na uzingativu wa

kanuni, sheria na taratibu za uchaguzi (Jedwali 5)

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

21

Jedwali 5; Mapingamizi kwa Wagombea wa Nafasi Mbalimbali Katika Mikoa Iliyojaza Dodoso

Chanzo: Utafiti 2014

Sababu mbalimbali zimetolewa kuhusiana na mapingamizi kwa wagombea. Sababu zilizotolewa

ni pamoja na baadhi ya wagombea kuwa na makosa ya jinai (2.9%), wagombea kutokuwa

wakazi wa maeneo wanayogombea (28.2%), utata wa umri (5.6%) na fomu zilijazwa bila

kufuata taratibu (23.8%). Sababu nyingine za mapingamizi ni wagombea kutoidhinishwa na

vyama vya siasa (10.6), kuchelewa kuwasilisha fomu (10.3), na uhasama wa kisiasa (2.6%).

Aidha, asilimia 16 ya wahojiwa walieleza kuwa mapingamizi mengine yalitokana na wagombea

MIKOA Mapingamizi katika uteuzi wa wagombea Jumla

Ndiyo Hapana Sijui Hakuna jibu

Arusha 30 54 7 4 95

Kilimanjaro 15 91 12 5 123

Ilala 3 3 0 0 6

Temeke 13 0 2 4 19

Morogoro 24 46 10 3 83

Dodoma 24 63 10 2 99

Geita 9 22 3 0 34

Njombe 16 42 7 4 69

Rukwa 16 38 12 4 70

Iringa 16 35 3 0 54

Mbeya 76 76 10 5 167

Katavi 10 22 0 0 32

Mtwara 21 36 3 5 65

Lindi 12 30 0 0 42

Ruvuma 3 7 4 3 17

Tabora 32 80 10 0 122

Tanga 7 12 2 0 21

Simiyu 45 57 3 0 105

JUMLA 404 780 105 43 1332

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

22

kutokurudisha fomu za uteuzi kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na sheria na au kughushi

nyaraka.

4.2.4 Kampeni katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014

(a) Muda wa kujinadi

Kanuni ya 18 ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014 inaelekeza kampeni kufanyika siku kwa

14 kabla ya uchaguzi. Aidha, katika kipindi hicho cha kampeni vyama vyote vinatakiwa

kufanya kampeni kwa kufuata ratiba na taratibu zilizowekwa, na kwa kufuata makubaliano na

kanuni za maadili zilizosainiwa na vyama vya siasa vilivyosajiliwa. Utafiti ulipata maoni

mbalimbali ya wahojiwa walioshiriki katika kampeni kama inavyoonekana katika chati.

Utafiti uliangalia mwenendo wa wagombea katika kampeni za uchaguzi ambapo ulifuatiliwa ili

kubaini endapo kuna kampeni zilizoendelea zaidi ya saa kumi na mbili za jioni kama kanuni ya

18 ya Uchaguziwa Serikali za Mitaa 2014 inavyoelekeza. Katika baadhi ya maeneo kampeni

zilifanyika zaidi ya saa kumi na mbili za jioni.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

23

Mgombea, mwakilishi wake au chama cha siasa kinaweza kuitisha na kuhutubia mikutano ya

kampeni kwa kufuata ratiba itakayowasilishwa na wagombea, wawakilishi wao au vyama vya

siasa na kuratibiwa na Msimamizi wa Uchaguzi. Asilimia 10 ya wahojiwa walieleza kuwa

kampeni zilifanyika zaidi ya saa 12 jioni. Kufanyika kwa kampeni zaidi ya saa 12 za jioni

inaashiria uwepo wa vitendo vya rushwa na pia kuwa chimbuko la fujo na vurugu katika baadhi

ya maeneo.

(b) Mwenendo wa Kampeni

Katika kampeni za uchaguzi Mgombea, Mwakilishi wake au chama cha siasa hakiruhusiwi

kuendesha kampeni za Uchaguzi kwa kutumia rushwa, takrima, kashfa, lugha za matusi,

ubaguzi wa kijinsia, kidini na ukabila. Kwa ujumla, utafiti ulibaini kuwa ingawa vyama vya

siasa vilijitahidi kuzingatia kanuni za uchaguzi, baadhi ya vyama vya siasa vilikiuka kanuni za

uchaguzi na hivyo kusababisha kampeni za uchaguzi kuvurugika na hata kusababisha fujo.

Mathalani, asilimia 16.3 ya wahojiwa walieleza kuwa, chama kimoja cha siasa kiliingilia

kampeni za chama kingine kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

24

Aidha, utafiti ulibaini kuwa baadhi ya wagombea walijinadi kwa kutumia lugha za kejeli, matusi

na kashfa ili kuwashawishi wapiga kura. Pia asilimia 9.7 ya wahojiwa walieleza kuwa picha za

wagombea zilichanwa, asilimia 3.7 walieleza kuwa kulikuwa na kampeni katika makanisa na

misikiti na asilimia 12.6 walieleza kuwepo kwa fujo na vurugu katika kampeni (Jedwali 6).

Jedwali 6: Mwitikio wa Wahojiwa Kuhusu Mwenendo wa Kampeni za Uchaguzi wa

Serikali za Mitaa 2014.

Ka

mp

eni k

atik

a

misik

iti na

ma

ka

nisa

Uw

ep

o w

a v

uru

gu

na

fujo

ka

tika

ka

mp

eni

Ch

am

a k

uin

gilia

ka

mp

eni y

a ch

am

a

kin

gin

e

Ma

tum

izi ya

lug

ha

za

ka

shfa

Pich

a za

wa

go

mb

ea

zilicha

nw

a

Ndiyo (%) 6.1 25.6 18.3 35.4 9.7

Hapana (%) 85.4 70.7 78.0 62.2 74.5

Sijui (%) 8.5 3.7 3.7 2.4 5.2

Jumla 100.0 100.0 100.0 100.0 100.0

Chanzo: Utafiti 2014

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

25

c) Vitendo vya Rushwa

Vitendo vya rushwa katika kampeni za uchaguzi hudumaza demokrasia na ni adui mkubwa wa

utawala bora. Ili kubaini vitendo vya rushwa wananchi walihojiwa iwapo walishuhudia vitendo

vya rushwa katika kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014 ambapo, asilimia 54.2

walieleza kuwa hakukuwa na vitendo vya rushwa na asilimia 42.9 walieleza kuwepo kwa

vitendo vya rushwa asilimia. Aidha, asilimia 32.9 ya wahojiwa walieleza kuwa kulikuwa na

vitendo vya rushwa vilivyohusiana na ugawaji wa fedha taslimu, asilimia 9.8 walieleza kuwepo

kwa ugawaji wa kanga na Tshirt na asilimia 26.8 walieleza kuwa wapiga kura walipewa

vinywaji na vyakula (Jedwali 7).

Jedwali 7: Mwitikio wa Wahojiwa kuhusu uwepo Rushwa na aina zake katika Uchaguzi

Uwepo wa rushwa Aina za rushwa

Mwitikio Asilimia Mwitikio Asilimia

Ndiyo 54.2 Kupewa fedha taslimu 32.9

Hapana 42.9 Kupewa vinywaji na vyakula 26.8

Sijui 2.9 Kanga na Tshirt 9.8

Vitendo Vingine

Jumla 100.0 *

Chanzo: Utafiti 2014

Vitendo vingine vya rushwa vilivyobainishwa katika mchakato wa kampeni za Serikali za Mitaa

ni vitendo vilivyohusisha ugawaji wa mifuko ya saruji, ugawaji wa mipira ya miguu, harambee

kanisani, kutoa pikipiki na michango katika misiba. Utafiti ulibaini pia kuwa, katika baadhi ya

maeneo vitendo vya rushwa vilijidhihirisha kwa ugawaji wa chumvi na vitu vingine vya thamani

siku ya kupiga kura. Ugawaji huu ulifanyika kwa kupelekwa majumbani kwa wapiga kura au

wakati wapiga kura wanaelekea vituoni kupiga kura. Katika matukio hayo, utafiti ulibaini kuwa

shughuli hizo ziligharamiwa na baadhi ya wagombea na katika baadhi ya maeneo, mawakala wa

wagombea walitumika.

Utafiti ulibaini kuwa katika baadhi ya maeneo Madiwani na Wabunge walishirikiana na baadhi

ya wagombea kuwahonga wapiga kura. Madiwani na wabunge hao, walishirikiana na baadhi ya

wagombea kwa matarajio kuwa watakaposhinda watawasaidia katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

26

2015. Ili kupata viongozi bora katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa viongozi wa kisiasa hasa

madiwani na wabunge wanapaswa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha maadili, kanuni na

sheria za uchaguzi zinazingatiwa. Aidha, elimu ya kutosha inapaswa kutolewa kwa wanasiasa

kuhusu wajibu wao katika kuhakikisha viongozi bora wanapatikana.

4.2.5 Upigaji wa kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014

Upigaji wa kura unapaswa kufanyika katika eneo ambalo mpiga kura alijiandikisha. Ni kinyume

cha utaratibu kupiga kura eneo ambalo mpiga kura hakuandikishwa. Matokeo ya utafiti

yanaonesha kuwa katika baadhi ya maeneo wananchi walisafirishwa kwenda kwenye maeneo

mengine kinyume na kanuni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Utafiti ulibaini kuwa katika baadhi ya maeneo, majina ya wapiga kura hayakuonekana vituoni.

Aidha, katika baadhi ya vituo kulikuwa na majina ya wapiga kura wenye umri chini ya miaka 18

na katika baadhi ya vituo orodha ya majina ya wapiga kura ilikuwa na majina yalijirudia zaidi ya

mara moja (Jedwali 8).

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

27

Chanzo: Utafiti 2014

Pia matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa kumekuwa na ukiukwaji wa kanuni na taratibu katika

baadhi ya maeneo ambapo upigaji wa kura uliofanyika baada ya muda wa kupiga kura kupita

(10.4%), kutokufunguliwa kwa vituo vya kupiga kura kwa wakati (19.4%) na kuendelea na

kampeni hata wakati wa zoezi la kupiga kura (13.3%).

Aidha, katika baadhi ya maeneo wananchi waliendelea kupiga kura usiku na hivyo kuwalazimu

kutumia simu zao zenye tochi ili kuwawezesha kusoma majina yao katika orodha ya wapiga kura

(Picha 1).

Jedwali 8: Majina na Namba za Wapiga Kura kuonekana Vituoni

Mkoa Ndiyo Hapana Sijui Hakuna

jibu

Jumla

Arusha 80 13 1 1 95

Kilimanjaro 87 20 10 6 123

Ilala 5 1 0 0 6

Temeke 12 6 0 1 19

Morogoro 57 13 2 11 83

Dodoma 79 14 1 5 99

Geita 22 5 5 2 34

Njombe 52 9 7 1 69

Rukwa 50 10 6 4 70

Iringa 39 10 5 0 54

Mbeya 124 27 10 6 167

Katavi 29 3 0 0 32

Mwanza 86 17 5 1 109

Mtwara 49 7 9 0 65

Lindi 40 1 1 0 42

Ruvuma 9 6 2 0 17

Tabora 84 25 10 3 122

Tanga 17 1 3 0 21

Simiyu 87 14 3 1 105

Jumla 1008 202 80 42 1332

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

28

Picha 1: Baadhi ya wananchi wakihakiki uwepo wa majina yao kwa kutumia tochi za simu

baada ya saa kumi na mbili jioni

Baadhi ya maeneo yaliendelea kupiga kura zaidi ya saa kumi na mbili za jioni kutokana na vituo

kuchelewa kufunguliwa, upungufu wa vifaa vya kupigia kura, maeneo ya kupigia kura kutokuwa

na nafasi na ubora unaowezesha zoezi la upigaji kura kwenda haraka, ufanisi mdogo kwa

wasimamizi wasaidizi na vurugu. Uwepo wa rasilimali za kutosha na zenye ufanisi ni muhimu ili

kuhakikisha upigaji kura unaanza na kukamilika kwa wakati ili chaguzi ziwe zenye amani na

utulivu. Aidha, mazingira mazuri ya upigaji kura yatatoa fursa kwa wananchi wengi kujitokeza

kupiga kura na hatimae kupata viongozi bora.

Picha 2: Baadhi ya wananchi wakiwa katika foleni kwa ajili kupiga kura

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

29

Aidha, 11.2% wamebainisha kuwa kuna picha za wagombea zilichanwa wakati wa upigaji kura

na baadhi ya vituo havikuwa na mawakala wa vyama vya siasa 13.5%. Matokeo yanaonesha pia

kuwepo kwa vurugu na fujo wakati wa kupiga kura (18.9%). Hali hii inaashiria ukiukwaji wa

sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi ambapo vitendo vya rushwa vinaweza kuwa chimbuko la

hali hii. (Jedwali 9)

Katika baadhi ya maeneo utafiti ulibaini kuunganishwa vituo zaidi ya kimoja vya kupigia kura

hivyo kusababisha mlundikano, kukosekana kwa faragha na usiri wa kupiga kura, kama

tunavyoona kwenye picha hapa wapiga kura wawili tofauti wote wakipiga kura sehemu moja

kama inavyoonekana katika picha 3

Jedwali 9: Mwitikio wa wahojiwa kuhusu mwenendo wa upigaji kura katika Uchaguzi wa Serikali

za Mitaa 2014. Mw

itikio

Up

iga

ji wa

ku

ra b

aa

da

ya

mu

da

wa

ku

pig

a

ku

ra k

wish

a

Vitu

o v

ya

ku

pig

ia k

ura

ha

vik

ufu

ng

uliw

a k

wa

wa

ka

ti

Ka

mp

eni k

atik

a v

ituo

vy

a k

up

igia

ku

ra

Pich

a za

wa

go

mb

ea

zilicha

nw

a w

ak

ati w

a

up

iga

ji ku

ra

Uw

ep

o w

a v

uru

gu

na

fujo

wa

ka

ti wa

up

iga

ji

ku

ra

Ndiyo (%) 10.4 19.4 13.3 11.2 18.9

Hapana (%) 81.5 68.5 74.0 74.6 74.5

Sijui 5.0 8.4 9.5 10.0 3.4

Haihusiki (%) 3.1 3.6 3.2 4.2 3.2

Jumla 100.0 100.0 100.0 100.0 100.0

Chanzo: Utafiti 2014

4.2.6 Masuala yaliyojiri wakati na baada ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Utafiti uliangalia kama uchaguzi ulifanyika mahali pa faragha na kwa kutumia karatasi maalum.

Matokeo yanaonesha kuwa katika baadhi ya maeneo upigaji kura haukufanyika katika mahali pa

faragha hali iliyowawezesha wapiga kura kujadili wakati wakiwa katika upigaji kura (picha 3)

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

30

Picha 3: Wapiga kura katika kituo cha kupigia kura

Ni muhimu sehemu ya kupigia kura kuwa sehemu ya faragha ili mpiga kura awe huru

kumchagua mgombea anayemtaka. Utafiti ulibaini kuwa baadhi ya maeneo hayakuwa na sehemu

ya faragha kwa ajili ya kupiga kura (28.60%) kama inavyoonekana katika Chati 11.

Kukosekana kwa faragha ni kuvunja Kanuni ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa 20 (10)

inayoelekeza kuwa kura zitakuwa za siri na zitapigwa katika majengo ya umma au sehemu

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

31

ambayo Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi ataiteua baada ya kushauriana na wagombea au

wawakilishi wao au vyama vya siasa isipokuwa majengo ya serikali.

Kanuni ya 21 inabainisha kuwa karatasi za kupigia kura zilipaswa kuwa maalum zikiwa pamoja

na: Jina la Mgombea; Jina la Chama; Nembo ya Chama; na Nembo ya Halmashauri husika.

Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa katika baadhi ya maeneo karatasi za kura hazikuwa maalum

(6%). Matumizi ya karatasi maalum za kupigia kura huondoa malalamiko na migogoro. Aidha,

matumizi ya karatasi zisizo maalum huashiria uwepo wa mianya ya rushwa na matokeo yake ni

kuvuruga uchaguzi au matokeo ya uchaguzi husika kutiliwa shaka.

Utafiti umebaini kuwa katika baadhi ya maeneo karatasi za kupigia hazikuwa maalum na

nyingine zilikosewa kama inavyoonekana katika Picha 4 inayoonesha makosa katika fomu ya

kupigia kura ambapo jina la mgombea wa CCM linaonekana katika sehemu ya mgombea wa

CHADEMA na jina la mgombea wa CHADEMA kuonekana katika sehemu ya mgombea wa

CCM

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

32

Picha 4. Fomu ya kupigia Kura iliyokosewa Majina ya Wagombea.

Lengo la mawakala kuwepo kituoni ni kuhakikisha kuwa zoezi la kuchambua na kuhesabu kura

linaendeshwa kwa uwazi na haki. Matokeo yanaonesha vituo vingi vilikuwa na mawakala

ingawa kuna baadhi ya vituo havikuwa na mawakala wa vyama vya siasa (13.4%) kama

inavyooneshwa katika chati 13. Utafiti umebaini pia kwamba baadhi vyama ambavyo

havikushindanishwa katika baadhi ya maeneo, havikuweka havikujihusha kuona hali na

mwenendo wa uchaguzi katika maeneo hayo (Kiambatanisho 1)

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

33

4.2.7 Kuhesabu Kura na kutangaza Matokeo

Mchakato wa kuhesabu kura na kutangaza matokeo ni muhimu ambapo taratibu na kanuni

zisipozingatiwa zinaweza kusababisha athari kubwa. Muda wa kuhesabu kura baada ya zoezi la

upigaji kura ni suala la kuzingatiwa ili kuleta ufanisi na tija. Utafiti ulibaini kuwa katika vituo

vya kupigia kura, kura zilihesabiwa kwa muda tofauti baada ya zoezi la upigaji kura kukamilika.

Utafiti ulibaini uwepo wa vurugu katika baadhi ya maeneo kutokana na ukiukwaji wa taratibu za

kuhesabu na utangazaji wa matokeo. Ukiukwaji huo ni pamoja na ucheleweshaji wa makusudi

katika kutangaza matokeo ya uchaguzi. Hali hiyo ilisababisha hisia za uchakachuaji wa matokeo

na hivyo kusababisha vurugu na fujo katika baadhi ya maeneo. Matokeo yanaonesha baadhi ya

vyama vya siasa havikufanya vyema katika uchaguzi huu (Kiambatanisho 1& 2). Kwa kuwa

Serikali za Mitaa ni msingi wa demokrasia na maendeleo, vyama vyote vyenye usajili wa

kudumu vinapaswa kujijenga kuanzia katika ngazi hiyo.

Serikali ya Mtaa ndiyo Serikali iliyo karibu zaidi na jamii. Matokeo yanaonesha kuwa baadhi ya

vyama vya siasa havikushindana na vingine kupata ushindi kidogo sana (Chati 15) . Ukiukwaji

wa kanuni na taratibu za uchaguzi na vitendo vya rushwa vinaweza kuwa sababu ya baadhi ya

vyama vya siasa kuacha kushindanisha wagombea au kupata viti vichache. Ili kujenga Serikali za

Mitaa zitakazoweza kuleta maendeleo yanayotarajiwa vyama vyote vya siasa vinapaswa

kujijenga kutoka katika ngazi za mitaa na hatimae kuwa na uwiano mzuri wa ushindi

unaojengwa na uchaguzi ulio huru na haki (Kiambatanisho 2).

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

34

4.3 Elimu kwa wapiga kura

Elimu kwa wapiga kura ndiyo msingi wa wapiga kura kufahamu sheria na kanuni za kupiga

kura; ikiwemo haki na wajibu wao katika uchaguzi. Utafiti ulitaka kufahamu iwapo wahojiwa

waliwahi kupatiwa elimu wakati wa mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2014. Matokeo

yanaonesha kuwa asilimia 66.1 ya wananchi waliohojiwa walieleza kuwa walipatiwa elimu na

asilimia 33.9 ya wahojiwa walieleza kuwa hawajawahi kupata elimu hiyo kama inavyooneshwa

katika Chati 16. Aidha, elimu ya kutosha kwa viongozi na wanasiasa ni muhimu ili waweze

kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za uchaguzi.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

35

Utafiti unaonesha kuwa elimu iliyotolewa ilihusu: kujiandisha katika daftari la wapiga kura

(65.9%); Sheria za Uchaguzi (58%); Sheria ya Gharama za Uchaguzi 27.7%); Haki ya Mpiga

Kura (64.3%) na Athari za Rushwa katika Uchaguzi 55%). Aidha, wahojiwa walieleza kuwa

walipata elimu kupitia vipindi vya radio (65%); vipindi vya televisheni (53.9%); magazeti

(50.5%); warsha na semina (43.1%); na vipeperushi na vijarida (42.1%) (Jedwali 10). .

Jedwali 9: Mwitikio wa wahojiwa kuhusu elimu ya uchaguzi na aina ya elimu waliyopata

Kama wamepatiwa elimu Aina ya elimu waliyopata Njia iliyotumika kutoa

elimu

Mwitikio Asilimia Mwitikio Asilimia Mwitikio Asilimia

Ndiyo 66.1 Kujiandikisha katika

daftari la wapiga

65.9 Radio 65.0

Hapana 31 Sheria za uchaguzi 58.0 Televisheni

(luninga)

53.9

Hakuna jibu 0.8 Gharama za uchaguzi 27.7 Magazeti 50.5

Haki ya mpiga kura 64.3 Warsha na

semina

43.1

Athari za rushwa

katika uchaguzi

55.7 Vipeperushi na

vijarida

42.1

Chanzo: Utafiti 2014

Asilimia theluthini na moja (31%) ya wahojiwa walieleza kuwa hawakupata elimu ya uchaguzi.

Kutokupata elimu ni chanzo kikubwa cha migogoro katika chaguzi hapa nchini. Aidha, uelewa

mdogo hukwamisha ushiriki mpana wa wananchi kwenye chaguzi hizo.

4.4 Maoni ya Wadau kuhusu mambo ya kufanya ili kuzuia rushwa na kuboresha uchaguzi

wa Serikali za Mitaa

Vitendo vya rushwa huathiri mchakato wa uchaguzi. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwa

rushwa bado ni tatizo. Vitendo hivyo ni kama vile kuwapa wapiga kura pesa, vyakula, vinywaji,

mavazi, ahadi za uongo, na vitisho. Aidha, vitendo vingine vinavyolalamikiwa ni wizi wa kura

na udanganyifu katika kuhesabu na kutangaza matokeo ya uchaguzi. Ili kukabiliana na vitendo

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

36

vya rushwa katika uchaguzi, maoni yafuatayo yalitolewa ikiwa ni pamoja na: kuongeza bajeti ya

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (29%); kuboresha daftari la wapiga kura (0.4%); wananchi

wapewe elimu ya kutosha kuhusu taratibu za uchaguzi, haki na wajibu wa wapiga kura (17.5%);

kutoa adhabu kali kwa wanaojihusisha na vitendo vya rushwa (14.6%); polisi kusimamia

taratibu za uchaguzi kwa usawa na haki (19%) na Tume ya Uchaguzi kusimamia uchaguzi wa

Serikali za Mitaa (15.2%) (Chati 15)

Maoni mengine katika kuboresha mchakato wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni pamoja na

kuongeza maslahi ya wasimamizi wa uchaguzi, matokeo ya uchaguzi yatangazwe mapema

iwezekanavyo mara baada ya kumaliza kuhesabu kura ili kuepusha vurugu na kuondoa hisia za

udanganyifu. Aidha, uwazi na elimu ya mpiga kura ipewe kipaumbele ili kudumisha na kukuza

demokrasia nchini. Aidha,Vyama vya Siasa, Serikali na Asasi za Kiraia pamoja na Mashirika

yasiyo ya kiserikali, wote wana wajibu mkubwa wa kuhakikisha elimu ya mpiga kura inatolewa

kwa utaratibu ulio endelevu.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

37

SURA YA TANO

5.0 MAPENDEKEZO NA HITIMISHO

5.1 Mapendekezo

NA. TATIZO MAPENDEKEZO

1. Uelewa mdogo wa

wananchi kuhusu haki na

wajibu wa mpiga kura

katika uchaguzi wa

Serikali za Mitaa.

Elimu ya haki na wajibu wa mpiga kura itolewe kwa

wananchi.

Elimu ya rushwa, gharama za uchaguzi na uraia itolewe

katika ngazi zote za elimu nchini.

Serikali itenge bajeti ya kutosha kwa ajili ya kuelimisha

wananchi.

Ushirikiano wa wadau wote katika kutoa elimu ya uraia

na mpiga kura kwa wananchi uimarishwe.

Kuhakikisha Sheria, kanuni na taratibu zinazohusiana na

uchaguzi wa Serikali za Mitaa zinapatikana kwa urahisi

na lugha inayoeleweka kwa wananchi.

Serikali iongeze fedha kwa ajili ya kuelimisha wananchi.

2. Usimamizi dhaifu wa

Sheria na taratibu za

uchaguzi wa Serikali za

Mitaa.

Kuviimalisha kielimu, kifedha na vifaa Taasisi na vyombo

vinavyohusika na usimamizi wa Sheria ya Uchaguzi wa

Serikali za Mitaa.

Kufanya tathmini ya uchaguzi na kuwachukulia hatua

watakaobanika kukiuka sheria na taratibu za uchaguzi

huu.

Kuboresha usimamizi wa maadili ya uchaguzi.

Kuandaa/kuimarisha uwajibikaji wa wadau katika

kutekeleza taratibu za uchaguzi.

Serikali iongeze Maslahi ya wasimamizi wa uchaguzi.

3. Uzingativu mdogo wa

maadili. Kuimarisha na kusimamia utekelezwaji wa kanuni za

maadili(code of conducts) kwa vyama vya siasa,Taasisi na

vyombo vinavyohusika na usimamizi wa uchaguzi.

Kutoa elimu ya maadili kwa wadau wa uchaguzi.

Viongozi wa dini, kisiasa na Serikali wawe mfano katika

mapambano dhidi ya rushwa. (Uteuzi wa viongozi wa

kisiasa na Serikali uzingatie ushauri wa vyombo

vinavyohusika na maadili ambavyo ni

TAKUKURU,Usalama wa Taifa,Tume ya maadili ya

viongozi,tume ya haki za binadamu na Utawala Bora).

Kuongeza uwazi katika uteuzi wa wagombea ndani ya

vyama, wakati wa kuhesabu kura na kutoa matokeo ya

uchaguzi.

Kuwachukulia hatua wanaokiuka maadili.

.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

38

5.2 Hitimisho

Mapambano dhidi ya rushwa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa yanahitaji mikakati

madhubuti ikiwa ni pamoja na kuongeza uelewa wa wananchi juu ya haki na wajibu wa mpiga

kura. Pia ni muhimu kuimarisha usimamizi wa Sheria na taratibu za uchaguzi wa Serikali za

Mitaa na Uzingativu wa maadili kwa wanasiasa na vyombo vyote vinavyohusika na uchaguzi

wa Serikali za Mitaa. Aidha, kuweka mikakati inayowabana wanasiasa wanaojihusisha na

vitendo vya rushwa na kuwajibika kwa matendo yao ni muhimu katika mapambano haya.

Endapo mikakati hiyo itaandaliwa na kutekelezwa na wadau, tatizo la rushwa katika uchaguzi

litapungua au kwisha kabisa.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

39

6.0 MAREJEO

Agenda Participation 2000 (2010): Elimu ya Uraia na Mpiga Kura Uchaguzi 2009-2010. Issue No.

009/10. Agenda Paricipation 2000. Dar es Salaam.

Blechinger, Venera (2002): Corr)uption and Political Parties. Sectoral Perspective on Corruption. MSI

and USAID, DCHA/DG. From www.usaid.gov .

Gymah-Baadi (2004): Remarks at the Ghana Integrity Initiative (GII) Symposium on Political

Corruption in Ghana, April 27, 2004. From www.cddghana.org visited on 12/09/2014.

http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/773740-yaliyojiri-katika-uchaguzi-serikali-za-mitaa-dec-

14-2014-

Klitgaard, R (1988), Controlling Corruption. Berkeley. University of California Press.

Polisi (2010): Haki na Wajibu wa Mpiga Kura. Ulinzi Shirikishi katika Mchakato wa Uchaguzi. Dar es

Salaam.

Rose-Ackerman, S. (2001), Trust, Honesty, and Corruption: Theories and Survey Evidence from Post-

Socialist Societies, Toward a Research Agenda for a Project of the Collegium Budapest. Prepared

for the Workshop on Honesty and Trust in Post-Socialist Societies at Collegium Budapest, May

25-26, 2001. Draft of April 24, 2001. (Available for downloading at www.colbud.hu/honesty-

trust/rose/pub 01.pdf. Sept 12, 2014).

TAKURU & IDS (2002): Uchaguzi wa Vyama vingi na Rushwa katika Tanzania….

URT (1979): The Local Authorities (Elections) Act No.4, Dar Es Salaam.

URT (1982): The Urban Authorities Act, Dar Es Salaam.

URT (1985): The National Election Act No.1, Dar Es Salaam.

URT (2007): The Prevention and combating of Corruption Act No.11/2007, Dar Es Salaam.

URT (2010): The Election Expenses Act No.6, Dar Es Salaam.

Yerevan, A (2006): The concepts of Civic Education, Electoral Education and Voters Awareness.

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

40

6. VIAMBATANISHO

Kiambatanisho 1: Matokeo ya Wenyeviti wa Vijiji kwa Mikoa 14

MKOA IDA

DI Y

A V

ITI

VYAMA VILIVYOSHINDANISHWA

CC

M

CH

AD

EMA

CU

F

NC

CR

TLP

NLD

AC

T

UP

DP

UD

P

AP

PT

NR

A

CH

AU

MA

DP

TAD

EA

AD

C

UM

D

ARUSHA 399 326 73

DODOMA 570 509 27 33 1

GEITA 473 367 94 12

IRINGA 354 347 7

KAGERA 664 477 172 13 2

KATAVI 136 97 38 1

KIGOMA 304 206 47 6 38 4 1 1 1

K/NJARO 514 336 143 27 8

LINDI 520 358 15 146 1

MARA 487 333 149 2 2 1

MBEYA 843 701 140 2

MANYARA 440 344 95 1

MOROGORO 666 527 114 24 1

MTWARA 779 616 24 135 1 1 2

JUMLA 7149 5544 1138 375 71 10 2 5 2 0 0 1 0 1 0 0 0

Chanzo: Utafiti 2014

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

41

Kiambatanisho 2: Matokeo ya Wenyeviti wa Vitongoji kwa Mikoa 24

MKOA

IDA

DI

YA

VIT

I

VYAMA VILIVYOSHINDANISHWA

CC

M

CH

AD

EM

A

CU

F

NC

CR

TL

P

NL

D

AC

T

UP

DP

UD

P

AD

C

AP

PT

NR

A

NL

D

CH

AU

MA

DP

TA

DE

A

UM

D

ARUSHA 1462 1134 327 1

DODOMA 3317 2959 187 169 1 1

GEITA 2235 1682 512 41

IRINGA 1837 1765 72

KAGERA 3703 2574 1066 53 4 6

KATAVI 704 531 167 5 1

KIGOMA 1844 1286 282 36 185 47 1 3 1 3

K/NJARO 2249 1485 603 1 126 33 1

LINDI 2387 1676 83 624 3 1

MARA 2680 1827 808 17 15 7 1 3 2

MBEYA 4455 3596 835 17 1 4 2

MANYARA 2008 1599 397 6 6

MOROGORO 3415 2664 609 141 1

MTWARA 3416 2650 151 603 4 6 2

MWANZA 3437 2529 825 65 2 3 13

NJOMBE 1826 1688 133 1 4

PWANI 1995 1596 42 356 1

RUKWA 1842 1402 436 2 2

RUVUMA 3817 3442 169 206

SHINYANGA 2746 2154 552 35 1 1 3

SIMIYU 2639 1711 848 27 2 50 1

SINGIDA 2257 1830 389 36 1 1

TABORA 3565 2967 453 128 17

TANGA 4605 4422 81 102

JUMLA 64441 51169 10027 2671 354 58 2 72 0 69 6 3 3 0 2 4 1 0

Chanzo: Utafiti 2014

RUSHWA KATIKA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2014

42

Kiambatanisho 3: Matokeo ya Wenyeviti wa Mitaa kwa Mikoa 24

MKOA

IDA

DI

YA

VIT

I

VYAMA VILIVYOSHINDANISHWA

CC

M

CH

AD

EM

A

CU

F

NC

CR

TL

P

NL

D

AC

T

UP

DP

UD

P

AD

C

AP

PT

NR

A

NL

D

CH

AU

MA

DP

TA

DE

A

UM

D

ARUSHA 154 78 76

DSM 556 398 89 69

DODOMA 169 160 8 1

GEITA 60 24 36

IRINGA 222 156 65 1

KAGERA 66 35 29 2

KATAVI 42 34 8

KIGOMA 176 123 20 20 12 1

K/NJARO 60 29 31

LINDI 117 84 33

MARA 151 72 78 1

MBEYA 252 130 120 2

MANYARA 35 24 11

MOROGORO 294 256 33 5

MTWARA 180 104 25 45 5 1

MWANZA 345 202 136 7

NJOMBE 82 55 27

PWANI 73 62 10 1

RUKWA 166 65 101

RUVUMA 95 69 24 2

SHINYANGA 86 40 45 1

SIMIYU 92 48 40 2 2

SINGIDA 50 50

TABORA 148 97 20 29 1 1

TANGA 258 192 3 63

JUMLA 3929 2587 1035 260 30 1 0 12 0 3 0 0 0 0 0 0 0 1

Chanzo: Utafiti 2014