6
Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi wa tembo ulioko kusini mwa Tanzania. Tunafanya kazi na mamlaka za uhifadhi wanyamapori na jamii inayoishi maeneo ya hifadhi ili kuwahifadhi tembo na binadamu kuendelea kuishi na tembo kwa uvumilivu. Pia tunafanya tafiti husika za kisayansi za uhifadhi. Tunayo furaha kushiriki na wewe baadhi ya habari tangu Julai hadi Septemba 2015. Mpango wa anga na uhesabuji mpya wa idadi ya Tembo Ruaha-Rungwa Timu ya STEP ya marubani Charles na Anne Nagy wameanza mpango wetu wa anga. Wakifanya ufuatiliaji na uangalizi kwa ndege katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa ndege ndogo (ijulikanayo kama “Skubie”. Tangu mwezi wa tisa, kwa mwaliko wa Taasisi ya Utafiti Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) na Wizara ya Maliasili na Utalii, timu ya marubani imekuwa ikiruka kama sehemu ya uhesabuji upya wa Tembo (2015) katika Ruaha-Rungwa. Timu ya STEP inafanya kazi kwa karibu na timu ya sensa, kuruka kwa saveyi ya awali kupitia transekti kuthibitisha kuwepo/kutokuwepo kwa tembo hai na mizoga katika hifadhi. Wakiruka chini na taratibu, na kwa kuweza kuona kwa umakini mkubwa kuliko ndege za Cessna zilizotumika katika sensa kubwa. Mpango huu wa kuruka kima cha chini kwa ndege ndogo umepangwa kwa pamoja kuongeza thamani na uhakiki wa sensa kwa kuongeza ufasaha na uwiano kwa matokeo ya mwisho. Mbinu ya kuruka kilomita 10 kwa 10 inaleta ufasaha kutoa alama zinazoonekana za shughuli haramu na kutoa taarifa haraka kwa timu za askari wa wanyamapori ardhini. SOUTHERN TANZANIA ELEPHANT PROGRAM Kulinda amani ya baadaye ya Tembo wa kusini mwa Tanzania na kwingineko

Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

  • Upload
    others

  • View
    0

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015

Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi wa tembo ulioko kusini mwa

Tanzania. Tunafanya kazi na mamlaka za uhifadhi wanyamapori na jamii inayoishi maeneo ya hifadhi

ili kuwahifadhi tembo na binadamu kuendelea kuishi na tembo kwa uvumilivu. Pia tunafanya tafiti

husika za kisayansi za uhifadhi. Tunayo furaha kushiriki na wewe baadhi ya habari tangu Julai hadi

Septemba 2015.

Mpango wa anga na uhesabuji mpya wa idadi ya Tembo Ruaha-Rungwa

Timu ya STEP ya marubani Charles na Anne Nagy

wameanza mpango wetu wa anga. Wakifanya

ufuatiliaji na uangalizi kwa ndege katika hifadhi

ya Taifa ya Ruaha kwa ndege ndogo (ijulikanayo

kama “Skubie”. Tangu mwezi wa tisa, kwa

mwaliko wa Taasisi ya Utafiti Wanyamapori

Tanzania (TAWIRI) na Wizara ya Maliasili na

Utalii, timu ya marubani imekuwa ikiruka kama

sehemu ya uhesabuji upya wa Tembo (2015)

katika Ruaha-Rungwa.

Timu ya STEP inafanya kazi kwa karibu na timu ya sensa, kuruka kwa saveyi ya awali kupitia transekti

kuthibitisha kuwepo/kutokuwepo kwa tembo hai na mizoga katika hifadhi. Wakiruka chini na taratibu,

na kwa kuweza kuona kwa umakini mkubwa kuliko ndege za Cessna zilizotumika katika sensa kubwa.

Mpango huu wa kuruka kima cha chini kwa ndege ndogo umepangwa kwa pamoja kuongeza thamani

na uhakiki wa sensa kwa kuongeza ufasaha na uwiano kwa matokeo ya mwisho. Mbinu ya kuruka

kilomita 10 kwa 10 inaleta ufasaha kutoa alama zinazoonekana za shughuli haramu na kutoa taarifa

haraka kwa timu za askari wa wanyamapori ardhini.

SOUTHERN

TANZANIA

ELEPHANT

PROGRAM

Kulinda amani ya baadaye ya Tembo wa

kusini mwa Tanzania na kwingineko

Page 2: Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

Pia tunayo furaha kusaidia kazi ya utafiti ya Mkuu wa Ruaha Dr Alex Epaphras na watafiti toka mradi

wa Hali, UC Davis, South Carolina Zoo, na WCS. Kwa kuruka ukanda wa chini kubaini makundi ya nyati

na viota vya ndege wala mizoga walio hatarini kutoweka.

Kama sehemu ya sensa awamu ya pili STEP pia ilisaidia kutayarisha camera katika Ruaha-Rungwa.

Takwimu za camera zitasaidia kuchunguza mabadiliko katika tabia za Tembo kwa ajili ya

uwindaji/ujangili, na uwezekano wa kubaini kuonekana kwa tembo toka katika anga ndani ya maeneo

mbalimbali.

Tathmini ya Tembo kwa eneo Pori la Akiba Selous

Mtafiti wa Tembo wa STEP, Lameck, na wasaidizi wake Athumani na Serafino

wamerejea hivi karibuni toka Pori la akiba la Selous, ambapo walikamilisha

saveyi ya tembo kwa kuangalia kinyesi, kwato na vipimo vya fuvu umbali wa

kilomita 900 za barabarani. Timu ilipitia changamoto nyingi - ikiwemo

kuharibika kwa gari mara nyingi katika saveyi ya Matambwe, Kingupira, na

kusini mwa Selous (Kalulu). Takwimu hizi sasa zitapitiwa ili kujua mgawanyo wa

umri na jinsia wa Selous na uelekeo tangu saveyi iliyopita mwaka 2009.

Tunapenda kuwashukuru Idara ya Wanyamapori, Utawala wa Pori la Akiba la

Selous na Lake Manze Camp kwa ushirikiano wao na kusaidia katika saveyi .

Athumani, Askari wa Selous, na Lameck Serafino akitengeneza Landrova ya STEP lililopewa

jina la utani “Labda” kwa usumbufu wake

Timu ya field ya STEP ikitayarisha Camera “Fundi” Athumani akiwa anafunga Camera

Page 3: Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

Kuchunguza mgogoro baina ya binadamu na Tembo, Hifadhi ya Taifa ya Ruaha

Mwezi wa saba na wa nane, timu yetu wachapakazi, Jenipha,

Kennedy na Kepha walisafiri kwa basi, pikipiki, na kwa miguu katika

vijiji 33 vinavyopakana na hifadhi ya Taifa Ruaha kwenda kuwahoji

viongozi wa vijiji na wakulima kuhusu mgogoro baina ya binadamu

na Tembo. Takwimu walizokusanya zitasaidia kubaini eneo

linaloathiriwa zaidi na tembo kuharibu mazao na vyanzo vingine vya

migogoro na kuamua kwa kiasi gani tunaweza kusaidia kwa

baadaye zaidi mradi wa fensi ya mizinga ya nyuki ambayo zinaweza

kuzuia uvamizi na kutoa chanzo mbadala cha mapato dhidi ya

ujangili. Pia kuwa utafiti wa kwanza mkubwa wa mgogoro wa

binadamu na Tembo katika eneo hilo, saveyi hii ilikuwa ni uzoefu

mzuri kwa timu ambayo mahojiano yao na watu ilivutia mtazamo

na fikra za watu katika uhifadhi na mambo ya kijamii na uchumi

yanayowakabili maeneo ya vijijini mwa Tanzania, na kutoa mwanya wa suluhisho la kudumu dhidi ya

migogoro ya binadamu na tembo.

Habari mpya za Udzungwa: ufuatiliaji wa Tembo na kitabu kipya

Habari njema toka Udzungwa ni kuwa tumeanza ufuatiliaji wa Tembo kwa kushirikiana na Udzungwa.

Watafiti wa STEP Paulo na Jose watatembea kilomita 22 kila mwezi kurekodi na kupima kinyesi cha

Tembo ili kuelewa mgawanyiko na demografia ya Tembo (kwa kupima kinyesi kutambua umri wa

Tembo), na kuelewa matokeo ya matishio kama ukataji miti na ujangili.

Kujifunza zaidi kuhusu utafiti wa muda mrefu wa

STEP Udzungwa soma kitabu chapisho jipya

Udzungwa: Tales of Discovery in an East African

Rainforest ambapo Trevor Jones na Katarzyna

Nowak wamechangia kuandika sura kadhaa kuhusu

Tembo na Primates wa kipekee wa Udzungwa.

Picha: Paulo anapima transekti ya kinyesi cha tembo kwa

kutumia kifaa maalum; Jose anapima diameta ya kinyesi ili

kupima Umri.

Page 4: Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

Safari ya mafunzo na mashauriano Amboseli na Samburu

Meneja wa Fildi Josephine, Mtafiti wa Tembo Lameck, na Dereva Peter walisafiri kuelekea Kenya kwa

mafunzo na mashauriano na miradi miwili ya muda mrefu ya utafiti na uhifadhi wa Tembo. Kwanza

walitembelea mradi wa muda mrefu ulimwenguni wa utafiti wa Tembo – Mradi wa Utafiti wa Tembo

Amboseli (AERP) – ambapo walitumia siku tatu katika fildi kuwatambua umri tembo wakiwa na Norah

Njiraini, mmoja kati ya wasaidizi wa muda mrefu wa utafiti katika mradi. Timu pia ilijifunza toka kwa

mwanasayansi mkazi katika AERP, Dr. Vicki Fishlock, namna mradi unavyomudu takwimu zake za

muda wa miaka arobaini, zaidi sana “ID Database” yake ya Tembo kubwa na jinsi wanavyohifadhi

takwimu za maisha ya kila tembo kuanzia kuzaliwa hadi kufa.

Timu pia ilielekea hifadhi ya Taifa ya Samburu kaskazini mwa Kenya kutembelea kambi ya utafiti ya

Save the Elephants (STE). Ikiwemo kujifunza kuhusu kazi yao ya muda mrefu ya ufuatiliaji tembo,

tulitambulishwa matumizi ya teknolojia yao ya collar kuelewa uelekeo wa Tembo katika maeneo ya

kaskazini mwa Kenya.

Amboseli na Samburu ni mifano bora ya nini yaweza kuwa matokeo ya ufuatiliaji ya muda mrefu wa

Tembo kwa maana ya kuongeza ufahamu wa wanyama hawa wazuri, na kulinda usalama wa Tembo

katika ukanda unaotishia wa Afrika mashariki. Safari ilitujaza na mawazo ya namna ya kuendeleza

utafiti wetu, uhifadhi, uenezaji na ushauri kusini mwa Tanzania. Shukrani nyingi kwa kila mmoja

Amboseli na Samburu kwa kutushirikisha maarifa yenu, na kila mmoja aliyechangia kufanya uzoefu

huu uwezekane.

Page 5: Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

Kampeni mpya ya Tembo: “OKOA Tembo wa Tanzania”

STEP inajivunia kusaidia kampeni ya “OKOA Tembo wa Tanzania”, ambayo inalenga kupaza sauti za

Watanzania dhidi ya Ujangili wa Tembo na kuhoji utekelezaji wa ndani kumaliza tatizo hili. Kampeni

inaitaka Serikali ya Tanzania kuwakamata na kuwashitaki wafanyabiashara wakubwa wa meno ya

Tembo nchini, kuweka msukumo kwa serikali ya China kufunga soko la meno ya Tembo na kuharibu

ghala ya meno ya Tembo. Wanakampeni wa OKOA wamekuwa bize mwezi wote wa Septemba,

wakihudhuria matamasha ya Amani ya FEMA sehemu mbalimbali nchini, wakiunda vikundi vya OKOA

na pia kufanya mahojiano kwa Televisheni na Radio nyingi.

Fahamu zaidi kuhusu kampeni kwa kutembvelea tovuti www.okoatembowatanzania.org, na kwenye

ukurasa wa Facebook OKOA Tembo wa Tanzania ambao tayari una watu 50,000 wanaoufuatilia!

Matamasha la Jazz kwaajili ya Tembo

Mwezi wa tisa, matamasha ya muziki wa Jazz kumshirikisha Floris Kappeyne Trio na DazzJazz

yalifanyika huko Dar es salaam kuisaidia STEP. Kwa pamoja, matamasha haya yalikusanya shilingi

milioni saba na nusu kwa mpango wa anga wa STEP na mradi wa Binadamu na Tembo. Shukrani nyingi

kwa walioshiriki matamasha haya, waandaaji wetu, kwa balozi wetu Dar, Andy Perkin, na kwa

wanamuziki wenye vipaji. Shukrani za pekee kwenu Belia Klaassen kwa kuandaa matamasha haya.

Lameck akiwa anaongea na wanafunzi kuhusu Kampeni

ya OKOA – Nane Nane, Arusha

Wadau wa “OKOA Tembo Club” - Ilula, Iringa

Floris Kappeyne Trio na DazzJazz wakiburudisha katika onyesho

dogo.

Page 6: Karibu katika Jarida la STEP! Julai Septemba 2015 · 2020. 3. 6. · Karibu katika Jarida la STEP! Julai– Septemba 2015 Southern Tanzania Elephant Program (STEP) ni mradi wa uhifadhi

Habari za Tembo

Mwezi wa nane, iliripotiwa kuwa raia watatu wa China walikamatwa na mabegi 14 ya pembe za ndovu huko uwanja wa ndege wa Zurich, wakiwa wamesafirisha moja kwa moja kutokea Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Dar es Salaam. Watu watano, wafanyakazi wa uwanja wa ndege na wanajeshi wa Tanzania wameshitakiwa kwa kuhusika. Cha kushtusha, Mamlaka za Uswizi ziliwaruhusu wachina kurudi China, na bado hakuna habari za kuwarejesha Tanzania kushitakiwa.

Inaonekana hata hivyo kuwa kukamatwa kwa wingi wafanyabiashara wa meno ya Tembo kunaanza kufanyika nchini Tanzania. Asante kwa kazi ya kishujaa ya wakiwemo wengineo, the National and Transnational Serious Crimes Investigation Unit (NTSCIU). Habari za karibuni mpaka tunaandika hii, ni kuwa raia wa China, Yang Feng Glan ameshitakiwa kwa kufanya biashara ya pembe za ndovu na kufadhili uuwaji wa Tembo kwa miaka mingi. Sote tunaamini kuwa kukamatwa na kuzuiliwa kwake kutafungua mianya ya kuwakamata wanamtandao wenzake bila kujali wanaweza kuwa na nguvu kiasi gani.

Hongera kwa Taasisi ya Wanyamapori Kenya (Kenya Wildlife Service) ambao mwezi wa tisa walimalizia kuchoma hadharani akiba yao ya meno ya tembo, ikishuhudiwa na Asasi za kiraia na washuhudiaji wa kimataifa kama hatua nyingine ya utayari kwao kuharibu ghala lote hadi mwishoni mwa mwaka huu.

Kuisaidia STEP.

STEP hutegemea zaidi ukarimu kwa namna ya pekee kutoka kwa wafadhili wetu -mnatusaidia kufanya mengi kwa ajili ya tembo. Tafadhali fikiria kutusaidia kwa kutumia njia zifuatazo:

Fuatilia STEP kwenye Facebook,Twitter, na tovuti yetu na shirikisha wengine shughuli zetu

Saidia kujenga ufahamu kwa tisheti zetu za “Okoa Tembo wa Tanzania” (Tsh 30,000) na mifuniko ya magurudumu (Tsh 80,000)

Wasaidie wakulima vijijini kwa kununua Asali rafiki wa Tembo (inapatikana Butcher Shop, Dar)

Changia katika nyanja za kazi yetu kwa chaguo lako

Asante sana kwa msaada wako!

Registered not-for-profit No. 112972

SOUTHERN

TANZANIA

ELEPHANT

PROGRAM