17
Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo Mwongozo huu umeandikwa Kwa ajili ya kuwasaidia watu mbalimbali ambao wangependa kupata muhtasari juu ya masuala ya biashara na Utunzaji rahisi wa hesabu za biashara. Imeandikwa na Kheri A.Rajabu

Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

  • Upload
    others

  • View
    14

  • Download
    1

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

Mafunzo ya msingi Kwa

wajasiriamali wadogo Mwongozo huu umeandikwa Kwa ajili ya kuwasaidia watu mbalimbali ambao wangependa kupata muhtasari juu ya masuala ya biashara na Utunzaji rahisi wa hesabu za biashara.

Imeandikwa na Kheri A.Rajabu

Page 2: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

2

YALIYOMO

Utunzaji wa kumbukumbu za fedha kwa wafanyabiashara wadogo………….…………………………03

Vitabu vya hesabu za biashara………………………………..…………………………………………………………….04

Huduma kwa wateja……………………………………………………………………………………………………….……..09

Njia rahisi kupambana na matumizi/gharama za lazima(fixed costs) katika biashara yako…......11

Jinsi ya kuuendesha Mkopo……………………………………………….…………………………………………………….12

Aina za biashara ambazo mtaji wake ni mdogo lakini faida yake ni kubwa……………….………………14

Page 3: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

3

Utunzaji wa kumbukumbu za fedha kwa wafanyabiashara wadogo

• Utunzaji wa hesabu za fedha ni muhimu kwa kila mfanyabiashara bila kujali ukubwa wa

biashara au ukubwa wa mtaji,unapoweka hesabu zako vizuri utakuwa na uwezo wa

kujua mapato yako,matumizi yako na kukubwa zaidi ni kujua faida au hasara

unayotengeneza kutokana na biashara yako,changamoto kubwa wanayoipata

wafanyabiashara/wajasiliamali hasa wadogo ni jinsi ambavyo wanashindwa kutofautisha

biashara zao na wao wenyewe.Inabidi kufahamika kuwa mmiliki wa biashara na biashara

ni vitu viwili tofauti,inapaswa kuiheshimu biashara yako hata kama mtaji wako ni mdogo

sana,biashara ni biashara.

Misingi ya kuheshimu biashara yako

• Tofautisha biashara yako na wewe mwenyewe binafsi.

• Unapochukua fedha toka kwenye biashara kwa ajili ya mayumizi yako

binafsihaimaanishi kuwa umechukua hela yako,hii ni gharama kwa

biashara(expenditure) na inapunguza kiasi cha faida unayopata toka kwenye biashara

yako,kiasi cha fedha unachotoa kwenye biashara yako kwa ajili ya matumizi yako binafsi

hutambulika kama “Drawing”

• Iwapo una biashara na wewe mwenyewe unafanya kazi kwenye biashara hiyo badala ya

kuajiri mtu, inakupasa ujilipe mshahara kama vile ambavyo ungemlipa mtu kwa ajili ya

kufanya kazi hiyo.

• Ainisha gharama za uchukuzi hata kama unatumia usafiri wako binafsi kwa ajili ya

kuchukua mali au mzigo wa biashara yako

• Usichukue mali ya biashara kwa matumizi yako binafsi bila kulipia,iwapo huna fedha kwa

wakati huo na unahitaji kitu kutoka kwenye biashara yako ni vyema ukachukua kwa

kukopa na uhakikishe unalipa kwa wakati vinginevyo ufanye uchukuzi huo kama

‘drawing’ na kumbuka kuwa hii itakuongezea gharama kwenye biashara yako na

kukupunguzia faida pia,hivyo tafakari mara mbili kabla hujachukua mali ya biashara kwa

ajili ya matumizi binafsi.

• Iwapo unafanya biashara katika nyumba unayoishi, hakikisha unagawanya gharama ya

vitu Kama umeme na maji iwapo vinatumika na kwenye biashara yako pia.

• Iwapo utatumia fedha ya biashara Kwa ajili ya chakula, usafiri na mengineyo hakikisha

gharama hizo unaziingiza kwenye biashara ili kupata faida halisi.

Page 4: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

4

• Ni vizuri kuhifadhi kiasi cha fedha toka kwenye faida Kwa ajili ya kuongeza mtaji (non-

distributable profit) hii itasaidia biashara kujifadhili yenyewe kifedha (sel-f finance)

badala ya kutumia mkopo au chanzo kingine cha fedha tofauti na biashara yako.

• Marekebisho yeyote unayoyafanya katika eneo la biashara yako lazima uyaingize

kwenye gharama za uendeshaji za biashara yako.

• Iwapo utachukua mkopo kwa ajili ya kuboresha biashara yako,hakikisha fedha hiyo

unatumia kwa madhumuni ya biashara tu na sio vinginevyo,utapotumia kwa ajili ya

matumizi mengine itakuja kuwa mzigo kwako kwenye kurejesha.

• Marekebisho yeyote unayoyafanya katika eneo la biashara yako lazima uyaingize

kwenye gharama za uendeshaji za biashara yako.

• Iwapo utachukua mkopo kwa ajili ya kuboresha biashara yako,hakikisha fedha hiyo

unatumia kwa madhumuni ya biashara tu na sio vinginevyo,utapotumia kwa ajili ya

matumizi mengine itakuja kuwa mzigo kwako kwenye kurejesha.

Vitabu vya hesabu za Biashara

• Yeyote anaweza kutunza hesabu za biashara yake hata Kama hana elimu ya uhasibu

mradi ajue kusoma na kuandika.Katika vitabu hivi sio lazima kununua vitabu maalum

vilivyochapishwa, unaweza kununua kitabu cha kawaida (counter book) ambapo

gharama yake si kubwa sana (inaingia pia kwenye gharama za biashara) na kuchora

mistari kulingana na mahitaji ya kitabu husika.

• Vitabu muhimu ni kama ifuatavyo

• Kitabu cha manunuzi

• Kitabu cha mauzo

• Kitabu cha biashara,Faida na hasara

• Kitabu cha mapato na matumizi

• Kitabu cha fedha

• Kitabu cha manunuzi

• Hiki utarekodi manunuzi yote unayofanya kwa ajili ya biashara yako, kitabu hiki

kitakusaidia kufahamu manunuzi yote uliyofanya kwa ajili ya biashara yako katika kipindi

fulani pengine siku, wiki au mwezi kutegemea ni kipindi gani unafunga hesabu zako.

Page 5: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

5

• Kitabu cha mauzo

• Hiki ni kitabu ambacho kinatumika kurekodi mauzo yako ya kila siku,pia

kitakusaidia kujua kiasi cha mauzo ulichopata katika biashara yako .

Kitabu cha Biashara, Faida na hasara

• Hiki ni kitabu muhimu na ndio hutoa taarifa iwapo umepata faida au hasara

kwenye biashara yako ndani ya kipindi fulani.Huandaliwa kwa kuchukua jumla ya

manunuzi yote,unajumuisha na gharama ya manunuzi kama vile ubebaji na

kadhalika,kisha unachukua kiasi cha mauzo yote pamoja na gharama za mauzo

unajumlisha ,ukishapata jumla ya manunuzi na mauzo kisha unatoa mauzo toa

manunuzi,kama gharama za maunuzi ni kubwa kuliko mauzo hapo itakuwa ni hasara,na

iwapo mauzo ni makubwa kuliko manunuzi hapo itakuwa ni faida,faida au hasara hii

tunayopata hapa huwa ni ile ambayo si halisi,ili kupata faida halisi,inakubidi uchukue

faida isiyo halisi kisha utoe gharama nyingine mbalimbali kama vile

umeme,maji,usafiri,na gharama nyingine ambazo hutokea katika mzunguko wa

biashara,ukishatoa hizi ndo unapata faida halisi(Net Profit) na pia unaweza pata hasara

halisi(net loss) iwapo gharama nyinginezo zimekuwa kubwa kuliko faida halisi.

MIFANO YA VITABU VYA KUTUNZA KUMBUKUMBU

KITABU CHA MAUZO YA SIKU (mfano)

TAREHE MAELEZO KIASI

1.01.2016 Sukari kilo 2@1500 xxxx

02.01.2016 xxxx

03.01.2016 xxxx

xxxx

Jumla

KITABU CHA MANUNUZI YA SIKU (mfano)

TAREHE MAELEZO KIASI

1.01.2016 Sukari kilo 2@1500 xxxx

02.01.2016 xxxx

03.01.2016 xxxx

Jumla xxxx

Page 6: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

6

KITABU CHA MAPATO NA MATUMIZI

TAREHE MAELEZO MAPATO MATUMIZI

01.01.2016 Salio la kufungulia xxxx

02.01.2016 mauzo xxxx

“ usafiri xxxx

31.01.2016 Salio la kufungia

KITABU CHA FEDHA JEDWARI MOJA (Fedha taslimu tu)

Mapato matumizi

Tarehe Maelezo Fedha Taslimu

Tarehe Maelezo Fedha taslimu

01.01.2016 Salio la kufungulia xxxxx 01.01.2016 Bili ya maji xxxx

01.01.2016 mauzo xxxxx mshahara xxxx

Mapato mengine xxxxx Jumla xxx

Salio la kufungia xxx

Jumla kuu xxxx

KITABU CHA FEDHA JEDWARI MBILI (Fedha taslimu NA Benki)

Mapato matumizi

Tarehe Maelezo Fedha Taslimu

Benki Tarehe Maelezo Fedha taslimu

Benki

01.01.2016 Salio la kufungulia

xxxxx xxxx 01.01.2016 Bili ya maji xxxx

01.01.2016 dipositi xxxx 01.01.2016 dipositi xxxx

01.01.2016 mauzo xxxxx mshahara xxxx

Mapato mengine xxxxx Jumla xxx -

Salio la kufungia xxx xxxx

Jumla kuu xxxx xxxx

Page 7: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

7

KITABU CHA BIASHARA, FAIDA NA HASARA

Mali ya kuanzia xxxxx Mauzo xxxxx

Jumlisha: manunuzi xxxxx Jumlisha: gharama za mauzo xxxxx

Gharama za manunuzi xxxxx

Faida isiyo kamili xxxx

Jumla

Faida isiyo kamili xxxxx

Gharama za uendeshaji

Umeme xxxxx

Maji xxxxx

Matengenezo xxxxx

Mshahara xxxxx

Usafiri xxxxx

Matumizi mbalimbali xxxxx

Jumla: xxxxx xxxx

Faida Halisi xxxxxx

Page 8: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

8

MIZANIA (balance sheet)

MALI MADENI

Mali za sasa Madeni ya sasa

Fedha taslimu xxxx Fedha utarajiazo kulipa xxxx

Fedha zilizo benki xxxx kodi utakiwayo kulipwa xxxx

Fedha utarajiazo xxxx mishahara isiyolipwa xxxx

Gharama zilizolipwa Madeni ya muda mrefu xxxxx

Kabla xxxx Mtaji wa wanahisa

Uwekezaji wa muda Mtaji xxxxx

Mfupi xxxx faida isiyogawanywa xxxxx

Jumla ya Mali za sasa xxxxx Jumla ya mtaji ya wanahisa xxxxx

Mali za kudumu

Ardhi (toa thamani ya uchakavu)

Jengo (toa thamani ya uchakavu)

Samani (toa thamani ya uchakavu)

Jumla ya Mali xxxxx Jumla ya mtaji na Madeni xxxxx

Page 9: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

9

HUDUMA KWA WATEJA

Mteja ni ufunguo wa aina yeyote ile ya biashara iwe ni kuuza bidhaa au huduma, mteja ndio

sababu ya biashara kuwepo. Biashara yeyote ile inaanzishwa Kwa madhumuni ya kupata Mteja

ili anunue kama ni huduma aitumie na mwisho wake uweze kulipia gharama za biashara na

muhimu zaidi kupata faida kutokana na biashara unayoifanya.

Misingi ya huduma kwa wateja

Kauli nzuri

Kauli nzuri ni kitu cha Msingi sana kwa biashara yako, mara nyingi Mteja huvutiwa kuja

kwenye biashara yako kutokana na vile ambavyo unazungumza nae.Kuna baadhi ya

wateja wengine ni wakorofi, ni muhimu kujua aina ya wateja wako, iwapo wewe ni

mfanya biashara yakupasa kuongeza vizuri na Mteja wako hata kama Mteja ni mkorofi

na kauli zake si nzuri, unapozungumza vizuri na wateja itakufanya utengeneze uwigo wa

wateja wa kudumu ambao ni muhimu sana kwa biashara yako.

Uaminifu

Uaminifu kwenye biashara hapa unabeba maana kubwa sana,kwanza kama unauza

bidhaa hakikisha ya kuwa bidhaa hizo ni bora na hazijapita muda wake wa matumizi,ni

vizuri kuuza bidhaa bora hata kama bei yake ni kubwa kuliko kuuza bidhaa hafifu hata

kama bei yake ni ndogo,kamwe usiuze bidhaa ambazo ni batili(fake) au ambazo

zimepigwa marufuku na vyombo vinavyohusika hata kama unazipata kwa bei

rahisi,Mteja akigundua unamuuzia vitu visivyofaa anaweza akahama na kuamia kufanya

manunuzi yake pengine,kibaya zaidi iwapo atawataarifu watu wengine inaweza

kukusababishia kupungua kwa wateja kwenye biashara yako kwa kiasi

kukubwa.Uaminifu pia unajumuisha kurudisha chenji kwa usahihi,kama unatumia mizani

kupimia bidhaa hakikisha kuwa kipimo chako ni sahihi,pia uza bidhaa zako kwa bei ile

ambayo ni halisi bila kuweka aina yeyote ya ulanguzi.

Ushauri kwa wateja

Kutokana na dunia ya sasa kuna aina nyingi sana za bidhaa kutoka kwa watengenezaji

mbalimbali,wakati mwingine Mteja hushindwa kuchagua anunue bidhaa ipi toka kwa

mtengenezaji yupi,hapo ndipo unapokuja umuhimu wa kuwashauri wateja wako,mara

nyingi wateja hupenda unafuu wa bei,ila ni muhimu kuwashauri wateja wanunue bidhaa

ambayo si nafuu tu,bali pia ni bora,vinginevyo ni Kheri kumshauri Mteja kununua bidhaa

ambayo ni bora zaidi hata kama bei yake ni kubwa kidogo,Mteja anapopata bidhaa bora

kutoka kwako,kutamfanya awe Mteja wa kudumu ambacho ni kitu muhimu kwa

biashara yako.

Page 10: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

10

Vifungashio

Vifungashio vya bure ni muhimu pia kama sehemu ya huduma kwa Mteja, baadhi ya

wateja huwa hawapendi wajulikane wamebeba nini wanapotoka dukani au sehemu

yeyote ya kununua, ni vizuri kuwa na vifungashio vya ukubwa mbalimbali kwa ajili ya

bidhaa tofauti, hakikisha gharama ya vifungashio kama vile mifuko ya plastiki, karatasi

n.k unazijumuisha kwenye gharama zako za biashara, ili uweze kupata faida halisi pindi

unapofanya hesabu zako za biashara.

Mauzo kwa mkopo

Hii pia ni njia nzuri za kudumisha mahusiano na huduma kwa Mteja,ila ni muhimu

ifanywe kiuangalifu sana na ni kwa wale tu wateja ambao ni wa kudumu na

unawafahamu vizuri kuzingatia uwezo na sifa za ulipaji za Mteja. Mfano wateja wengi

ambao ni waajiriwa hupenda kupata mahitaji yao na kulipa gharama zote mwisho wa

mwezi,wapokeapo mshahara, hata hivyo ni vizuri kuweka ukomo wa kukopesha ili

kuepusha kutetereka au kuyumba kwa biashara yako, pia kwa wateja kama wauzao

vyakula au vitafunwa huwa ni wazuri wa kukopa na kulipa pia,ni vizuri kutoa huduma

kwa mkopo katika biashara yako,lakini hakikisha tahadhari ya hali ya juu inachukuliwa

kwenye suala hili,pia ni muhimu kutunza kitabu maalum kwa ajili ya kuhifadhi

kumbukumbu za wateja unaowadai.

Zawadi ndogondogo

Iwapo mtaji wako unaruhusu unaweza kutoa Zawadi ndogondogo Kama vile pipi au

biskuti Kwa wateja ambao wananunua zaidi Kwa siku na hii hufaa zaidi kwa watoto

ambao mara nyingi ndo hutumwa dukani hasa kwenye maduka ya rejareja.

Punguzo la bei

Wakati mwingine unaweza kuuza bidhaa fulani kwenye biashara yako kwa be3i ya

punguzo ili kuwavutia wateja, muhimu ni kuhakikisha bei hiyo ya punguzo utayouza

haitokusababishia kupata hasara, mara nyingi bei ni kigezo kukubwa katika manunuzi,

bei ikiongezeka kidogo mauzo yatashuka na ikipungua kidogo mauzo yataongezeka,

hivyo siku zote sio busara kwa mfanyabiashara kung’ang’ania kuuza vitu kwa bei ya juu

kwani kwa kufanya hivyo utakuwa unajifukuzia mwenyewe wateja katika biashara yako.

Page 11: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

11

NJIA RAHISI ZA KUPAMBANA NA MATUMIZI/GHARAMA ZA LAZIMA (FIXED COSTS)

KATIKA BIASHARA YAKO

Matumizi au gharama za lazima ni zile gharama ambazo haziepukiki katika biashara yako, vitu

hivi huwa haviepukiki na ni muhimu sana katika biashara yako,baadhi ya gharama hizo ni kama

vile; kodi ya pango(iwapo umepanga sehemu ya kufanyia biashara),kodi ya

mapato,mishahara(kama umeajiri mtu kwenye biashara yako),umeme,marejesho ya mkopo N.K

Gharama hizi huwa ni lazima zitokee kila baada ya muda Fulani katika biashara yako, gharama

hizi huwa ni mzigo sana kwa mfanyabiashara hasa kama hujafanya maandalizi ya

awali.Unachoweza kufanya ili gharama hizo zisiwe mzigo kwako ni kutenga kiasi fulani cha

fedha pembeni toka kwenye mauzo ya kila siku.Unachoweza kufanya ni kutengeneza mfumo

wa kutoa asilimia fulani ya fedha kutoka kwenye mauzo ya kila siku na kutunza pembeni.

Mfano: Mauzo ya siku ni Tsh 85,000 ambayo ni sawa na 100%

Mgawanyo:

Kodi 10% 85,000x10/100= 8,500

Mshahara 5% 85,000x 5/100 = 4,250

Marejesho ya mkopo 8% 85,000x8/100 = 6,800

Umeme 2% 85,000x 2/100 = 1700

Jumla 25% 21,850

Kwa kufanya Mgawanyo kama huo hapo juu kutegemea na mauzo yako kwa siku utakuwa na

uwezo wa kutenga fedha kwa ajili ya kulipia gharama za lazima za biashara yako bila

kukwamakwama kwa kuwa fedha utakuwa tayari umeshaiandaa hivyo ifikiapo wakati wa kulipa

ni kuchukua na kulipa tu, hii itasaidia sana kukupunguzia mzigo wa gharama kipindi mzunguko

wa biashara si mzuri na fedha fulani ni lazima ilipwe.

Page 12: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

12

JINSI YA KUENDESHA MKOPO

Mara nyingi mahitaji ya kibiashara huweza kupelekea kuhitaji mkopo ili uweze kutimiza

malengo yako.Mkopo si mzigo kwa biashara yako kama vile ambavyo wengi hudhani,cha Msingi

ni kujua tu jinsi gani unaweza kuuendesha(manage)mkopo wako.Zipo njia kadhaa ambazo ni

rahisi sana kufanya mkopo uwe na tija kwako na si mzigo. Njia hizi ni kama ifuatavyo.

1. Malengo ya Mkopo

Hakikisha unazingatia lengo la kuchukua mkopo baada ya kupata mkopo, ni vizuri kujua ni nini

hasa unataka kufanya kwa mkopo unaochukua, ukachukua mkopo bila malengo itakufanya

ujipe mzigo mkubwa na mkopo huo kutokuwa na manufaa yeyote kwako. Hivyo zingatia

kuchukua mkopo Kwa ajili ya malengo ya kibiashara au ya kimaendeleo uliojiwekea na hakikisha

unatumia katika malengo hayohayo.

2. Fanya Mgawanyo mzuri wa fedha ya mkopo

Unapochukua mkopo Kwa ajili ya biashara yako fanya Mgawanyo mzuri wa fedha hiyo ili mkopo

uwe na tija kwako. Kwanza kabisa hakikisha unatenga Marejesho mawili au matatu kutoka

kwenye fedha hiyohiyo ya mkopo ili kuwa na hakika wa kulipa hata biashara ikiyumba,pili ingiza

hela iliyobaki katika mahitaji ya biashara ila hakikisha unabakisha kidogo kwa ajili ya dharura

kwani hali ya biashara huwa inabadilika badilika kutokana na sababu mbalimbali za

kiuchumi,iwapo utatumia hela yote ya mkopo kwa bidhaa fulani halafu bidhaa ile isiuzike

utajikuta umejipa mzigo na atakosa njia ya dharura kurekebisha hali hiyo iwapo fedha yote ya

mkopo umeshaiingiza kwenye biashara.

3. Marejesho ya Mkopo

Pigia hesabu Marejesho yako ya mkopo Ili uweze kurejesha Kwa wakati na kuondoa usumbufu

wa kushindwa kulipa kiasi cha Marejesho ya mkopo kwa wakati. Njia nzuri ni kutenga asilimia

fulani ya mapato yako ya kila siku kutoka kwenye biashara yako kwa ajili ya kulipia mkopo wako

na ikifika siku ya kurejesha usiwe na wasiwasi wa kukosa rejesho lako.

Page 13: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

13

4. Kiasi cha mkopo kisizidi uhitaji

Jambo jingine la Msingi la kuzingatia ni kiasi cha mkopo utachochukua kilingane na mahitaji

yako halisi, Usichukue fedha zaidi ya mahitaji yako, hii itakufanya kujiingiza katika matumizi

yasiyo ya lazima na pia kujipa mzigo wa kulipa deni la mkopo wako. Watu wengi hudhani,cha

kuwa fedha nyingi ndio Msingi wa Maendeleo ya biashara,hufikia hatua mtu kuwa tayari hata

kutoa hongo ili aidhinishiwe mkopo maradufu ya ule anaoweza kupata.Kufanikiwa ni kuweka

mipango thabiti na inayotekelezeka ndo Msingi wa Maendeleo ya biashara yako, Unapochukua

kiasi kidogo cha mkopo na ukakitumia vizuri huleta tija zaidi kwa Maendeleo ya biashara kuliko

kuchukua kiasi kukubwa na kushindwa kukisimamia vizuri.

5. Gharama na masharti ya mkopo

Jambo kubwa na la Msingi la kuzingatia ni kuhakikisha unafanya chaguo sahihi la mkopo

unaotaka kuchukua, ni muhimu sana kuangalia gharama na masharti ya mkopo iwapo unaweza

kumudu au la,zingatia sana unafuu wa riba na gharama nyingine kabla hujafanya maamuzi ya

kuchukua mkopo kutoka kwenye taasisi tofauti za mikopo,pia angalia manufaa mengine

unayoweza kunufaika nayo kwa kuchukua mkopo kutoka katika taasisi fulani, Ni muhimu

kuangalia vitu kama Mafunzo, Ushauri na faida nyingine ambazo taasisi ya mkopo inaweza

kutoa,pia epuka taasisi za kitapeli za mikopo ambazo nyingi zimeanzishwa kiujanjaujanja ili

kuwatapeli wananchi,ikitokea bahati mbaya ukachukua mkopo toka taasisi kama hizo unaweza

kujikuta unaingia kwenye matatizo ya uchumi ikiwemo kufilisiwa mali zako pasipo kufuata

utaratibu halali unaokubalika.

Page 14: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

14

AINA ZA BIASHARA AMBAZO MTAJI WAKE NI MDOGO LAKINI FAIDA YAKE NI KUBWA

Genge la chakula,mbogamboga na matunda

Biashara hii huweza kufanywa kwa kuanzia na mtaji mdogo sana na soko lake ni kubwa hasa

maeneo ya makazi ya watu, kwa kuwa hugusa mahitaji ya kila siku ya watu,na ikiwa biashara

ipo maeneo ya makazi ya watu,mfanya biashara atakuwa na uhakika wa kuuza bidhaa zake ila ni

muhimu kuzingatia usafi na mpangilio mzuri wa biashara yake ili kuvutia zaidi wateja.

Vitafunwa na vyakula vikavu

Unaweza pia kufanya biashara ya vitafunwa na vyakula vikavu katika maeneo yetu ya makazi

huwa na uhitaji mkubwa wa vitafunwa hasa nyakati za asubuhi na kidogo jioni, watu wengi

hawapendelei kutumia vitafunwa vya aina moja kila siku (mfano mkate) hivyo vitafunwa mfano

maandazi, kachori, sambusa, vitumbua, mihogo na viazi vya kukaanga, bagia, chapati n.k

vinaweza kuwa na soko kubwa mtaani na kukupatia faida nyingi mno.

Upikaji wa chakula

Wakati mwingine biashara hii ya chakula huonekana ya kawaida Kwa kuwa imezoeleka bila

watu wengi kufahamu kuwa Ina faida kubwa Sana, inaweza kufanywa na mtu mmoja au

mkajiunga kiasi cha watu wanne hivi na mkawa na sehemu maalum ya kuuzia(kama vile mama

lishe) lakini pia kiubunifu zaidi biashara hii inaweza kufanywa kwa kutafuta oda mbalimbali

mfano kupelekea maeneo ya maofisini au maeneo ya kazi,viwandani n.k hasa nyakati za

mchana,pia kuongeza thamani na ubora wa chakula hicho unaweza kukifunga kwa kutumia

vifungashio maalum(lunch box).Pia mnaweza kutafuta oda za kusambaza chakula kwenye

sherehe mbalimbali,mikutano na kadhalika.

Ung’arishaji na ukarabati wa viatu,pochi na mabegi na bidhaa nyingine za ngozi

Hii pia ni biashara nyingine nzuri sana isiyohitaji mtaji mkubwa,ukushakuwa na sehemu ya

kufanyia biashara, gharama ya kununua vifaa vya kuanzia inaweza isizidi hata hamsini

elfu(50,000)hukugharimu sana kununua rangi za viatu,nyuzi za kushonea,sindano za

kushonea,sindano za kushonea na vifaa vingine vidogodogo.Biashara hii inapokwenda vizuri

Page 15: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

15

unaweza kuongeza vitu kama vocha,biashara ya magazeti na vitu vidogovidogo kama

sigara,pipi,karanga,kwa kuwa muda mwingi unakuwa hapo na baadhi ya wateja kama kazi

inachukua muda mrefu kusubiri huweza kuhitaji bidhaa ndogondogo kama hizo ili kusogeza

muda,mafanikio ya biashara hii yanaweza yakaonekana zaidi iwapo itafanyika sehemu zenye

mikusanyiko ya watu kama vituo vya mabasi,sokoni katikati ya mitaa yenye ofisi nyingi.

Duka la rejareja

Aina hii ya biashara hupatikana Sana kwenye maeneo tunayoishi na ni biashara iliyozoeleka

sana. Biashara hii ina gharama ndogo za uendeshaji na pia uhakika wa mauzo, pia haihitaji

taratibu nyingi za kuirasimisha kuifanya,ukipata leseni na namba ya utambulisho wa mlipa kodi

(TIN)inatosha kuifanya biashara yako iwe rasmi na pia unaweza kupata fursa za kupata mikopo

toka taasisi mbalimbali za fedha kwa ajili ya biashara yako.Ili ufanukiwe zingatia kuuza vitu

ambavyo vinahitajika zaidi na pia uwe makini kwenye udhibiti wa mzigo wako wa biashara,

bidhaa zinazohitajika kwa wingi na mzunguko wake ni mkubwa uziweke kwa wingi kuliko zile

ambazo hazihitajiki sana na mzunguko wake ni mdogo.

Ufugaji wa kuku

Ufugaji wa kuku una faida kubwa na uendeshaji wake huitaji fedha kidogo hasa kwa kuku wa

kienyeji.Ukiwa na banda zuri lenye nafasi ya kutosha unaweza kununua kuku wadogo kwa bei

rahisi kiasi cha 3,000 hadi 4,000 na kuwalisha vizuri na kuwakuza na baada ya miezi kadhaa

ukauza kwa kiasi cha 8,000 hadi 10,000,kwa harakaharaka unaweza kuona jinsi gani unaweza

kutengeneza faida kubwa kutokana na biashara hii,uzuri ni kwamba kuku hawa huwa hawaugui

mara kwa mara na wala hawahitaji mlo maalum wenye gharama kubwa kama walivyo kuku wa

kisasa,pia mabanda yao hayana mahitaji mengi maalum na kizuri zaidi ni kwamba wanataga na

kutotoa mayai hivyo mayai inaweza ikawa ni zao lingine kwa biashara lakini pia vifaranga

ukiwatunza nao pia utakuja kuwafanyia biashara hivyo baada ya mda fulani unakuwa na

uhakika wa mzunguko mzuri wa biashara. Biashara hii ya kuku unaweza kuipeleka mbali na

kuwa ya kisasa zaidi na kuweza kukupatia kipato kukubwa sana.Mfano unaweza kuwachinja

kuku hao,kuwaandaa na kuwafunga kwenye vifungashio vizuri na kutafuta soko la jumla

Page 16: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

16

kwenye maduka makubwa (supermarkets) au ukawa na sehemu yako ya kuuzia ukawaweka

kwenye jokofu na ukaweza kuwauza kwa urahisi kutokana na harakati nyingi za kimaisha watu

wengi hupenda vitu vya namna hii ambavyo vimeshaandaliwa .Faida nyingine kubwa ni

kwamba unaweza kupata kipato zaidi kwani unafunga kuku na kuuza peke yake na pia virigisi

unazifunga na kuuza peke yake hivyo kwenye kila kuku watano unapata mfuko mmoja wa

firigisi ambao unaweza ukauza hadi elfu tano,ila hadi kufukia hatua hizi zote inabidi uwe

umeendesha mradi huu kwa muda mrefu kidogo ili kujizalishia fedha za kuweza kufanya yote

hayo,japo pia iwapo unaweza kupata fursa ya kupata mkopo inaweza kukufikisha haraka

kwenye hatua hii.

Bustani ya mbogamboga

Bustani ya mbogamboga pia ni biashara nyingine ambayo inaweza kukuongezea kipato kwa njia

rahisi sana.Kama una eneo zuri sehemu unayoishi na kuna huduma ya maji hiyo ni fursa.

Unaweza kulima Bustani na kupanda vitu kama nyanya, vitunguu, karoti, mbogamboga, pilipili,

bamia, bilinganya na kadhalika, ukizitunza na zikamea vizuri unaweza kutafuta sehemu ya

kwenda kuuzia au ukawa na eneo lako la kuuzia au pia watu wanaweza wakaja kwako na

ukawauzia pia.Mradi huu ni mzuri kwani utakupatia kipato lakini pia utakupunguzia matumizi

kwa kujipatia mahitaji yako muhimu ya chakula toka kwenye Bustani yako na fedha utayokua

umeiokoa waweza kuifanyia mambo mengine ya Maendeleo.

*****MWISHO*****

Page 17: Mafunzo ya msingi Kwa wajasiriamali wadogo

17