Upload
others
View
866
Download
76
Embed Size (px)
Citation preview
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 1
UHAKIKI WA RIWAYA YA VUTA N’KUVUTE
KITABU- VUTA N’KUVUTE
MWANDISHI – SHAFI ADAM SHAFI
WACHAPISHAJI – MKUKI NA NYOTA PUBLISHERS
MWAKA – 1999
Utangulizi Riwaya hii inazungumzia matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii yetu
kwa sasa. Matatizo hayo ni kama vile matabaka, umaskini, ndoa za
kulazimishwa, wivu katika ndoa, n.k
Maudhui
Dhamira kuu: Ukombozi Katika riwaya hii, mtunzi anajadili aina nne za ukombozi ambazo ni
ukombozi wa kiutamaduni, ukombozi wa kisiasa, ukombozi wa
kiuchumi na ukombozi wa kifikra.
Ukombozi wa kiutamaduni Katika kujadili ukombozi wa kiutamaduni, mwandishi anaonesha kuwa
baadhi ya mila na desturi zetu zinamkandamiza mwanamke. Baadhi ya
mila hizo ni ile ya kumlazimisha mwanamke kuolewa na mtu
asiyemtaka. Kama walivyofanya wazazi wa Yasmin kwa kumwozesha
binti yao kwa nguvu kwa Bw. Raza. Yasmin hakumpenda Raza kwa
sababu halikuwa chaguo lake. Hivyo, msanii anaonesha kuwa ili
tujikomboe kiutamaduni lazima tuachane na mila hizo.
Pili, kuna mila ya kumweka mwanamke utawani, kama alivyofanya
Shihab baada ya kumuoa Yasmin. Shihab baada ya kumuoa Yasmin
alimweka utawani. Jambo hili linazorotesha maendeleo ya mwanamke,
kwani badala ya kushughulika na kazi za kimaendeleo hukaa ndani tu na
kusubiri kuletewa kila kitu na mwanaume. Katika kupiga vita mila hii
msanii anaonesha kuwa, Yasmin alitoroka kwa shihab kwa lengo la
kuonesha kuwa mila kama hizi zimepitwa na wakati na jamii haina budi
kuzitupilia mbali mila hizo.
Hivyo, msanii anaishauri jamii kuwa, ili tuweze kujikomboa
kiutamaduni hatuna budi kuachana na mila na desturi zilizopitwa na
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 2
wakati zinazomnyanyasa mwanamke, kwani zinarudisha nyuma
maendeleo ya jamii nzima kwa ujumla.
Ukombozi wa kisiasa Hapa msanii anazungumzia harakati za wananchi wa Unguja na Pemba
za kujikomboa kutoka katika minyororo ya kunyonywa, kukandamizwa,
kunyanyaswa na kuonewa na wakoloni wa Kiingereza pamoja na
vijibwa vyao.
Katika kujadili hayo, msanii anaonesha wazi jinsi Denge na kundi lake
wanavyojishughulisha na harakati hizo kwa kutawanya vitabu vyenye
mawazo ya kijamaa, magazeti yanayopinga ukoloni na makaratasi
mengine ya uchochezi dhidi ya wakoloni. Wao waliamini kuwa kwa
kutumia vitabu, magazeti na makaratasi hayo, wananchi wa kawaida
wangeamka na kuzijua haki zao na hatimaye kuanza kupambana na
ukoloni huo.
Katika kujadili dhamira hii ya ukombozi wa kisiasa, msanii anaonesha
kuwa lazima tuwe na watu waliojitolea muhanga katika harakati hizo.
Denge na kundi lake walijitoa muhanga katika kuhakikisha kuwa nchi
yao inakombolewa kutoka katika mikono ya wakoloni kama asemavyo
Denge (uk. 145);
“Yasmin mimi najua unanipenda na mimi nakupenda vilevile, lakini
kuna kitu kimoja napenda uelewe, kuna mapenzi na wajibu wa mtu
katika jamii. Kila mtu ana wajibu fulani katika jamii na mimi wajibu
wangu mkubwa ni kufanya kila niwezalo kwa kushirikiana na wenzangu
ambao wengine unawajua na wengine huwajui ili kuona kwamba nchi
hii inakuwa huru. Hii ni kazi ngumu ina matatizo mengi na inahitaji
kujitoa muhanga na mimi ni miongoni mwa hao waliojitolea muhanga
kufa, kupona, potelea mbali. Tupo wengi tuliojitolea namna hiyo, tena
wengi sana, maelfu.”
Denge na kundi lake walifuatwa sana na askari, lakini hawakuacha
kueneleza harakati zao za kudai uhuru.
Vilevile msanii anaonesha kuwa ili tujikomboe kisiasa, lazima tuwe na
umoja na mshikamano, kwani umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.
Denge na kundi lake walishirikiana sana katika harakati zao za
kupambana na wakoloni. Walishirikiana katika kutawanya vitabu,
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 3
magazeti na makaratasi ya uchochezi dhidi ya ukoloni. Ingawaje mpaka
mwisho wa riaya hii ukombozi wa kisiasa ulikuwa bado haujapatikana,
lakini bado harakati hizo zilikuwa zinaendelea na kuna siku ukombozi
utapatikana.
Ukombozi wa kiuchumi Katika riwaya hii, msanii annaonesha harakati za watu wa Unguja na
Pemba za kujikomboa kiuchumi kutoka katika minyororo ya kunyonywa
na wakoloni wa Kiingereza. Uchumi wa Zanzibar kabla ya uhuru
ulikuwa mikononi mwa wazungu wachache ambao walikuwa
wanamiliki njia zote za uzalishaji mali.
Harakati za akina Denge na wenzake zililenga katika kuwakomboa
Waafrika kiuchumi kwa kuchukua njia kuu za kuzalisha mali toka kwa
wazungu wachache na kuziweka mikononi mwa Waafrika walio wengi.
Ukombozi wa kifikra Ukombozi wa kifikra ni ile hali ya kujua na kutambua matatizo
yanayoikabili jamii yako na wewe mwenyewe na kutafuta mbinu za
kujinasua kutoka katika matatizo hayo.
Kitendo cha Yasmin kuona kuwa baadhi ya mila na desturi
zinamnyanyasa mwanamke na kuamua kuachana nazo, inadhihirisha
wazi kuwa Yasmin alikuwa na uwezo wa kufikiri na kuona mbali. Mila
hizo ni kama vile mwanamke kulazimishwa kuolewa na mtu asiyemtaka
na kuwekwa utawani.
Pili, kitendo cha Denge na kundi lake kugundua kuwa wananyonywa,
wanaonewa na kukandamizwa na wakoloni ulikuwa ni ukombozi wa
kifikra na ndio maana walianzisha harakati za kudai haki zao za msingi.
Dhamira ndogondogo 1. Mapenzi na ndoa
Katika kujadili dhamira hii ya mapenzi, msanii ameainisha aina mbili za
mapenzi, mapenzi ya kweli na mapenzi ya pesa. Mapenzi ya kweli
tunayaona kati ya Mwajuma na Yasmin. Hawa walipendana hasa ndio
maana Yasmin baada ya kutoroka kwa mume wake, alikimbilia kwa
Mwajuma wakaishi pamoja. Katika kuonesha hayo msanii
anamwonesha Mwajuma kama mtu mwenye roho nzuri na mkarimu.
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 4
Japokuwa alikuwa mtoto wa kimaskini lakini aliamua kumsaidia rafiki
yake Yasmin. Msanii anasema (uk. 22);
“Mwajuma ijapokuwa ni mtoto wa kimaskini alikuwa na roho nzuri ya
ajabu na roho nzuri yake ilichanganyikana na ukarimu usiokuwa na
mfano. Alikuwa yuko tayari kumkirimu mtu chochote kidogo alichokuwa
nacho. Alikuwa mwingi wa huruma na siku zote alikuwa tayari
kumsaidia yeyote aliyemweleza shida zake, pindi akiwa na uwezo wa
kumsaidia mtu huyo.”
Yasmin, baada ya kumtoroka mume wake, aliishi maisha yake yote kwa
Mwajuma mpaka alipoolewa na Shihab na baada ya kifo cha Shihab,
Yasmin aliendelea kuishi kwa Mwajuma mpaka alipokuja kuolewa na
Bukheti.
Mapenzi mengine ya kweli ni kati ya Bukheti kwa Yasmin. Bukheti
alimpenda sana Yasmin na ndiyo maana alifunga safari kutoka
Mombasa kuja Unguja kwa ajili ya kumtafuta Yasmin. Msanii
anaonesha hayo (uk. 41);
“Kwa Bukheti safari ya kutoka Mombasa mpaka Unguja ni safari ndefu
lakini safari hiyo ina urefu ulioje utakaomzuia yeye kukisaka kitu azizi
kama pendo la Yasmin.”
Bukheti licha ya kukataliwa na Yasmin hakukata tama, ndiyo maana
baada ya kifo cha mume wake Yasmin, Bukheti alifunga tena safari
kutoka Mombasa kwenda Zanzibar kubahatisha tena kwa Yasmin (uk.
230-231). Bukheti licha ya kupewa masharti; bado aliyatimiza na
hatimaye akamuoa Yasmin (uk. 274-277).
Mapenzi mengine ya kweli ni kati ya Denge na Yasmin. Hawa
walipendana hasa na wote wawili walikuwa na mapenzi ya kweli kwa
kila mmoja. Denge alimpenda sana Yasmin na Yasmin vilevile alikuwa
anampenda sana Denge katika shida na raha (uk. 115-127), (214-219).
Mapenzi mengine ya kweli ni kati ya Denge na kundi lake kama vile
Mambo, Chande, Sukutua, Mwajuma, Hussein, Pazi, Salehe, n.k. hawa
walipendana hasa na ndio maana walishirikiana katika shughuli
mbalimbali.
Kwa upande wa Mwajuma, naye alikuwa na mapenzi ya pesa.
Aliwapenda watu wenye pesa na ndiyo maana alimshauri Yasmin
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 5
amwache Denge na kuolewa na Shihab ambaye alikuwa na pesa (uk.
169-179).
Kuhusu suala la mapenzi, msanii anaonesha kuwa uzuri na ubaya siyo
unaoamua mtu kupenda au kupendwa, kwani kuna wazuri wanaopendwa
na wasiopendwa. Pia kuna wazuri wasiojua kupenda wala kupendwa,
hali kadhalika kuna wabaya wanaopendwa na wasiopendwa au wabaya
wasiojua kupenda au kupendwa vilevile (uk. 88-89).
Msanii anaendelea kusisitiza kuwa, katika suala la mapenzi ni lazima
wale watu wanaohusika wapende wote, hayo ndiyo yatakuwa mapenzi
ya kweli. Kama mmoja anapenda zaidi ya mwenzake hapo kunakuwa na
walakini katika mapenzi hayo.
Katika suala la ndoa, msanii anaonesha ndoa za kulazimishana na
madhara yake kwa jamii. Yasmin alilazimishwa na wazazi wake
kuolewa na Raza lakini ndoa yao haikudumu. Kwa ujumla Yasmin
hakumpenda kabisa Raza, kwani alikuwa sawa na baba yake wa
kumzaa.
Vilevile katika suala hili, msanii anaonesha kuwa suala la ndoa lazima
waachiwe wale wanaopendana na siyo maamuzi ya wazee ndio
yatawale, kwani hayo ni mambo ya kizamani. Msanii anasema hivi (uk.
259);
“Hivyo! Humtaki huyo mchumba wako! Huyu Bashiri ana mambo ya
kizamani kwelikweli anataka akuchagulie mke yeye…..huyu ami yako
mpuuzi hayajui mambo leo. Bashiri. Hajui kama siku hizi vijana
wanatafutana wenyewe, kijana anatafuta wake. N‟do mnamwita vile siku
hizi geli-friend sijui au sivyo Bukheti.”
Hivyo anachosisitiza msanii ni uhuru katika suala zima la kuchagua
mchumba. Msanii anaeleza kuwa, suala hili lisiingiliwe na wazee.
Vilevile msanii amezungumzia suala la wivu katika ndoa. Shihab baada
ya kumwoa Yasmin kutokana na wivu aliokuwa nao, alimweka utawani
akafungwa kama wafungwa, msanii anayasema hayo (uk. 196-197);
“Wakati Denge amefungwa gerezani kumbe Yasmin naye amefungwa
kwa mumewe. Hakufungwa kama afungwavyo mahabusu ila yeye
alikuwa ametawishwa hana tofauti na mfungwa. Alikuwa hendi harudi
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 6
yumo ndani tu kama kizuka; kwa sababu ya wivu aliokuwa nao
Shihab…..”
Msanii akijadili zaidi juu ya wivu katika ndoa vilevile ameonesha
madhara ya wivu. Wivu unapozidi katika ndoa kwanza ni rahisi ndoa
hiyo kuvunjika. Mfano, kutokana na wivu, Shihab aliwaacha wanawake
watatu na Yasmin alikuwa mke wake wan ne ambaye naye aliwekwa
utawani (uk. 197).
Pili, msanii anaonesha kuwa wivu ukizidi katika ndoa unamnyima uhuru
yule anayeonewa wivu. Katika ndoa yake na Shihab, Yasmin alikosa
uhuru kabisa, msanii anaonesha hayo (uk. 197) anasema;
„Alimpa kila starehe, ila uhuru wa kutoka na starehe zake zote ziliishia
ndani ya nyumba yake kubwa iliyokuwa na kila aina ya anasa ndani
yake, zote asizione kitu, kutwa akawa ananing‟inia madirishani
akiangalia wapiti njia na kuwahusudu jinsi walivyo huru. Alijiona kama
ndege aliyefungiwa tunduni akapewa kila kitu isipokuwa uhuru wake wa
kuruka hewani.”
Ni kutokana na wivu huo ndiyo maana Yasmin alimkimbia Shihab
akarudi tena Unguja kwa Denge ambaye hakuwa na wivu (uk. 207).
Vilevile kifo cha Shihab kinatokana na wivu huohuo. Kutokana na jinsi
alivyokuwa anampenda na wivu juu yake (uk. 211), na baada ya kuona
ajali ya ndege ile aliyoamini imemchukua mke wake naye alipofika
nyumbani kwake alikata roho kwa kihoro (215).
Hivyo, msanii anatahadharisha jamii kuwa wivu katika ndoa ni kitu
chenye madhara. Kwa hiyo, ni lazima tuwe waangalifu katika
kudumisha ndoa zetu.
2. Mivutano
Mvutano huu upo katika mgongano kati ya wazee na vijana. Huu
mgongano unadhihirisha mifumo miwili inayotofautiana kiuchumi,
kifalsafa na kimawazo kwa ujumla.
Uwezo wa mwanaume au mwanamke kutaka amchague mtu wa kuishi
naye ni jambo la kisasa ambalo miaka michache iliyopita, lilileta
matatizo makubwa huku kwetu.
Riwaya ya Vuta n‟kuvute inajadili mgongano wa namna hiyo, yaani
baina ya wazazi na watoto wa kisasa akina Yasmin na Bukheti na
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 7
wazazi wao. Mgongano anaouonesha katika riwaya hii unatokana na
utamaduni wa kisasa na vile unavyopingana na utamaduni wa wakati
uliopita. Ni mvutano wa ukale na usasa.
Kwa hiyo, tunaziona taratibu mbalimbali za kijadi zilizochakaa. Kwa
mfano, wazazi wa Yasmin kumwoza binti yao kwa mzee Raza ambaye
ni sawa na baba yake wa kumzaa kwa nguvu, ni desturi za zamani
ambazo zinaendelea kupigwa kumbo na wakati. Yasmin na Raza
hawakulingana kabisa kiumri. Raza alikuwa mzee hasa kama
anavyosema msanii (uk.10);
“Alikuwa ni mume asiyelingana naye hata kidogo, si kwa umri wala
tabia kwani wakati Yasmin ni kigoli wa miaka kumi na tano tu, mumewe
Bwana Raza alikuwa zee la miaka hamsini na mbili. Wakati bwana Raza
kasha zeeka, Yasmin alikuwa mtoto mbichi asiyeelewa kitu chochote”
Yasmin alikubaliana na matakwa ya wazazi wake ili kuwaridhisha,
lakini yeye mwenyewe hakuona fahari yoyote kuolewa na mzee
anayeweza kumzaa (uk. 1) msanii anasema;
“Yasmin hakupenda hata kidogo kuolewa na mume yule kwani yeye
mwenyewe angelipendelea sana kupata mume kijana kama yeye
mwenyewe. Alipenda kumpata mume ambaye yeyote angelimuona
angelisema: “Kweli Yasmin kapata mume.” Alikuwa anatamani
kupenda lakini hakumpata wa kumpenda. Yeye alitaka kijana wa
makamu yake ambaye angelimuonesha pendo nay eye angelimmiminia
pendo lote alilokuwa nalo moyoni mwake.”
Kutokana na Yasmin kulazimishwa na wazazi wake, hakumpenda kabisa
huyo mume wake, hata akayachukia maisha yake mwenyewe. Alitamani
kufa kuliko kuendelea kuishi na bwana yule, msanii anasema (uk. 2);
“Kutokumpenda Bwana Raza pamoja na utumishi wa kutwa dukani pale
kulimfanya Yasmin ayachukie maisha ya unyumba na mumewe.
Alitamani kufa kuliko kujitolea mwili wake kwa bwana yule….”
Ni kutokana na hali hiyo, ndiyo maana Yasmin alikosa adabu kwa
mume wake na baadaye alimtoroka mume wake huko Mombasa na
kurudi Unguja kuanza maisha mapya.
Kitendo cha Yasmin kumwacha mume wake kilileta mvutano mkubwa
sana kati yake na wazazi wake. Kwanza mjomba wake alimfukuza
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 8
(uk.18) hali kadhalika na mama yake alimfukuza na kumtenga kabisa
(uk.42-43).
Hivyo msanii anaonesha kuwa mara nyingi ndoa za kulazimishwa
hazidumu na pia zinaleta mfarakano wa kifamilia kama ilivyokuwa kwa
Yasmin ambaye alitukanwa matusi mengi sana na wazazi wake kama
vile mwanaharamu, mhuni, na matusi mengine mengi.
Katika riwaya hii msanii anawashauri wazee wasiwadharau watoto wao
wa kisasa, kwa kufikiri kuwa ati hawaelewi wafanyayo. Watoto hawa
yaani Yasmin amejitolea mhanga kuonesha kuwa katika dunia hii ya leo
desturi za kizamani hazifai tena. Mtoto asichaguliwe mchumba na wazee
wao bali mtoto mwenyewe. Mapenzi na mahaba ya kweli hayashindwi
lakini yatashinda kila kitu katika kujitekeleza na kujikamilisha. Kabila,
rangi, jadi, dini, ukoo – haya yote hayana nguvu za kutosha mbele ya
mapenzi ya dhati kama anavyosema Yasmin (uk. 98);
“……mimi Bwana Raza simtaki! Nimekubali kukosana na wazee wangu,
kuhasimiana na jamaa zangu, kubughudhiwa na wote wanaonijua! Yote
nimeyakubali kwa kumkataa bwana Raza. Jambo la uke na ume ni
jambo la hiari jamani….”
Kutokana na hilo, msanii anaitaka jamii kukubaliana na mabadiliko
yanayokuja katika jamii, kung’ang’ania mambo yaliyopitwa na wakati ni
kuleta migongano ya bure kati ya wazee na vijana wa kisasa ambao
wanautaka huo uhuru. Vijana wa sasa wanataka uhuru katika suala zima
la mapenzi. Sio wachaguliwe na wazazi wao tena. Vijana wa sasa
wanachojali ni pendo la dhati na mahaba ya kudumu, wala wao hawajali
asili zao. Haja kubwa ni tabia njema na ubinadamu usio na ubaguzi wa
mambo hayo. Msanii anasisitiza hayo (uk. 170) anasema;
“…..pendo jambo la hiari, hawawezi kunilazimisha kumpenda
nisiyemtaka.”
Anachosisitiza msanii katika dondoo hiyo ni kuwa, suala la mapenzi
waachiwe wale wanaopendana na sio mila au wazee ndio waamue.
Ndiyo maana baada ya Yasmin kumwacha Raza aliandamana na Denge,
akamwacha akaolewa na Shihab naye akamwacha akaenda tena kwa
Denge kisha akaenda kuolewa na Bukheti. Huo ndio uhuru alioutaka
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 9
Yasmin navijana wenzake wa rika kama lake, uhuru wa kutoingiliwa
katika suala la mapenzi.
3. Matabaka
Mtabaka ni dhamira nyingine inayojitokeza katika riwaya hii. Katika
kuonesha matabaka, msanii ameyagawa kwa kufuata rangi zao. Hapa
tuna Wazungu, Wahindi na Waafrika. Wazungu ni wale wakoloni wa
Kiingereza kama vile Inspekta Wright na wazungu wenzake. Wahindi
wanawakilishwa na akina Raza, Gulam na wengine, hawa walikuwa
wafanyabiashara. Waafrika wanawakilishwa na watu wa kawaida wote
kama vile Denge, Mwajuma, Mambo, Koplo Matata, Chande, Salehe,
Pazi, Huseni na wengine. Hawa walikuwa watu maskini, kula yao kwa
taabu, kulala kwao kwa taabu, n.k
Kuhusiana na aina tatu hizi za matabaka, kulikuwa na ubaguzi kati ya
matabaka haya. Ilikuwa si rahisi kwa Mzungu kuchanganyikana na
Mwafrika na vilevile ilikuwa si rahisi kwa Mhindi kuchanganyikana na
Mwafrika. Ndiyo maana baada ya Yasmin kukimbilia kwa Mwajuma,
Wahindi wenzake waliona amevunja mila na miiko ya Kihindi kama
asemavyo msanii (uk. 85);
“Kwa Wahindi Yasmin alikuwa asi, aliyevunja mila na miiko yao yote
kwa kuchanganyika na Waswahili.”
Kwa upande wa makazi, Waafrika waliishi ndani ya vibanda vidogo vya
uswahilini wakati Wazungu na Wahindi wanaishi kwenye marosheni na
majumba ya watukufu (uk. 98).
Vilevile kwa upande wa huduma zingine Waafrika walikwenda kwenye
maduka ya mchangani na darajani ambayo yaliuza bidhaa hafifu,
Wazungu na Wahindi waliingia ndani ya maduka ya Shangani na
Baghani ambayo yaliuza vitu kwa bei ghali na maduka hayo yalitoa
huduma za kila namna kwa hawa Wazungu na Wahindi (uk. 126).
Kwa upande wa starehe vilevile kulikuwa na ubaguzi kati ya Waafrika,
Wazungu na Wahindi. Wakati Wahindi wakistarehe Karimjee Club (uk.
130), Wazungu wao walistarehe English Club wakinywa bia za kila
aina, lakini Waafrika walikunywa gongo.
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 10
Kwa ujumla, Wazungu na Wahindi walikuwa wanawanyonya,
wanawaonea na kuwanyanyasa Waafrika. Ni kutokana na hali hiyo,
ndiyo maana watu hawa walianzisha harakati za kutokomeza utawala
huo wa Kiingereza kwa kutawanya vitabu vyenye mawazo ya Marx na
wengine wenye msimamo kama wake huko Zanzibar.
Watu kama Denge waliamini kuwa, kwa kutumia vitabu hivyo pamoja
na magazeti yenye misimamo hiyohiyo, ndiyo itakayowaamsha
Waafrika ili waweze kupambana na ukoloni huo.
Mpaka mwisho wa kitabu, ukombozi wa Waafrika ulikuwa bado
haujapatikana na Waafrika wenyewe walikuwa bado hawajaelimishwa
vya kutosha. Vilevile watetezi wenyewe wamefungwa gerezani. Hapa
anachotaka kuonesha mtunzi ni kwamba, ukombozi si lelemama.
Unahitaji umoja na mshikamano, pamoja na kujitoa muhanga.
4. Dhana potofu na dharau
Hii ni dhamira ingine inayojitokeza katika riwaya hii. Kwa upande wa
dharau, tunaona Wazungu na Wahindi wakiwadharau Waafrika
kutokana na rangi yao nyeusi. Pamoja na umaskini wao. Msanii
anaonesha hayo (uk. 43) anasema;
“Sasa sina mwingine ila mimi na Waafrika, nd‟o ndugu zangu. Na
wanawadharau kwa sababu gani hasa? Wao si watu? Au kwa sababu
maskini? Ikiwa wao maskini na mimi nishakuwa maskini, nakula fadhila
zao, nakula fadhila za Mwajuma….”
Wakati wa ukoloni hali hii ya kumdharau Mwafrika ilikuwa imekithiri
sana katika bara hili la Afrika. Mwafrika aliwekwa katika daraja la tatu,
Mhindi la pili na Mzungu daraja la kwanza. Kwa upande wa huduma
Wazungu na Wahindi walipata huduma nzuri na Waafrika huduma duni.
Hali hii bado inaendelea hata baada ya uhuru, Wahindi na Wazungu
bado wanawadharau Waafrika.
Kutokana na dharau waliyonayo Wazungu kwa Waafrika, ilikuwa si
rahisi kwa Mwafrika kumwoa Mhindi au Mzungu. Hayo yanaoneshwa
(uk. 251). Msanii anasema;
“Hapana. Yeye mwenyeji wa Mombasa.”
“Mswahili?”
“Ndiyo”
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 11
“Sasa Yasmin Bai unafikiri Gulam atakubali posa ya Mswahili”
“Uncle mimi n‟nachotaka ni stara. Nipate mume nistirike. Akiwa
Mswahili, akiwa Mhindi, akiwa Mzungu mimi kwangu ni sawasawa.
Wote hao ni watu.”
Yasmin alikuwa Mhindi lakini hakuwa na dharau kwa Waafrika. Aliona
nao ni watu kama watu wengine, hivyo nao wanahitaji kuheshimiwa
kama watu wengine. Katika (uk. 252) msanii anaonesha zaidi jinsi
isivyo rahisi kwa mhindi na Mwafrika (Mswahili) kuonana.
Kwa upande wa dhana potofu, kuna baadhi ya wahusika wana dhana
potofu hasa Wazungu na vibaraka wao. Koplo Matata na mabwana zake
wana dhana potofu juu ya mfumo wa kikomunisti na watu wake. Yeye
anaamini kuwa, ukomunisti ni mfumo ambao unakanusha kuwepo kwa
Mungu na dini. Vilevile kila kitu katika mfumo huu ni kugawana, msanii
anasema (uk. 100);
“Makoministi ni watu wasioamini Mungu wala dini, makafiri. Ni watu
wanaoamini kugawana kila kitu, kugawana wake zao, dada zao na hata
kugawana mama zao.”
Mawazo kama haya yanayotolewa na Koplo Matata, ambaye ni kijibwa
cha wakoloni, ni mawazo potofu. Wakoloni wanaupaka matope mfumo
huu kwani wanajua utawaamsha watawaliwa na kudai uhuru wao.
Mfumo huu unadai haki kwa kila mtu, usawa wa binadamu na mambo
mengine yanayotetea maslahi ya wengi.
Wakoloni kwa vile walitetea maslahi ya wachache waliwapiga vita sana
watu waliosomea Urusi na kuanza kuwapaka matope kuwa wanaleta
vurugu nchini. Katika kuhakikisha wananchi wa kawaida hawajihusishi
na harakati za kudai uhuru wao, wakoloni waliwaita wanaharakati hao
kama Komunisti ambao hawaamini Mungu hata dini, msanii anasema
(uk. 68);
“Sikiliza sista hawa wakoloni na vijibwa vyao ni watu wapumbavu
kabisa, kwao kila mtu ni Koministi; ukidai haki yako wewe Koministi,
ukisema kweli wewe Koministi. Ukipinga kutawaliwa wewe Koministi.
Lolote utakalolifanya madhali halina maslahi kwao basi wewe ni
Koministi. Maumau wa Kenya wameitwa makoministi. Wapigania uhuru
wa Algeria wameitwa Makoministi. Kila anayedai haki kwao ni
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 12
Koministi, na sumu yao kubwa wanayoitumia ya kutaka kuwatenganisha
watu kama hao na wananchi wenzi wao ni kusema kwamba watu hao
wanaowaita Makoministi hawaamini Mungu.”
Haya ndiyo mawazo ya wakoloni na vijibwa vyao. Mawazo
yanayochochea chuki miongoni mwa wananchi wa kawaida dhidi ya
wapigania uhuru. Haya ni mawazo ambayo yamekusudiwa
kusambaratisha umoja na mshikamano miongoni mwa Waafrika. Ni
mawazo potofu, kwani yanamdumaza mtu kifikra na hivyo hawawezi
kujikomboa kutoka katika minyororo ya kugandamizwa, kunyonywa na
kuonewa na ukoloni huo.
5. Uvumilivu na ujasiri
Uvumilivuna ujasiri katika maisha ni dhamira mojawapo inayojadiliwa
katika riwaya hii. Kwanza, Yasmin alivumilia sana kuishi na Raza
mume wake wa kwanza ambaye alikuwa mzee sawa na mzee wake wa
kumzaa. Akiwa na Raza muda wote alishinda dukani, halafu kutokana
na kuwa aliozeshwa kwa nguvu na wazazi wake, hivyo hakumpenda
kabisa mume huyo. Uvumilivu wa jambo una kikomo chake, mwisho
Yasmin alishindwa na akaamua kuondoka na kumkimbia mume wake.
Vilevile Yasmin alimvumilia sana mume wake wa pili, Shihab. Shihab
baada ya kumwoa Yasmin alimuweka utawani kwa sababu ya wivu
wake. Yasmin aliyavumilia maisha hayo kama asemavyo msanii (uk.
198);
“Taratibu Yasmin aliyazoea maisha ya utawa, akawa mke wa nyumbani
aliyewekwa akakaa, akatulia na Shihab akawa anajisifu kwa rafiki zake
wote.”
Katika ndoa yake na Shihab, Yasmin muda wote alishinda ndani tu
kama mahabusu, hakuwa na ruhusa ya kwenda apendako. Yasmin
hakuwa na rafiki, shoga au jirani wa kuongea naye kama asemavyo
msanii (uk. 211);
“Nakuambia kaniweka ndani kama mwari, hata huyo mwari ana
afadhali sina shoga, sina jirani, sina jamaa, mimi na ndani na ndani na
mimi, siendi sirudi.”
Haya ndiyo maisha aliyoishi Yasmin na mume wake Shihab, maisha ya
utawa ambayo aliyavumilia. Waswahili husema mara nyingi mvumilivu
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 13
hula mbivu lakini kwa Yasmin hakuona ukweli wowote, ndiyo maana
Yasmin aliomba ruhusa ya kwenda kuwaona wazazi wake na hakurudi
tena kwa Shihab kama Yasmin anavyosema (uk. 214);
“Sitorudi Abadan, sitorudi Abadan.”
Vilevile Yasmin aliyavumilia maisha aliyoishi kwa Mwajuma baada ya
kuachana na mume wake Raza na Shihab. Yalikuwa maisha magumu
sana kwake lakini aliyavumilia. Mwajuma na Yasmin waliishi maisha ya
dhiki na unyonge (uk. 21). Maisha yao yalitegemea rusuku kutoka kwa
marafiki na wahisani wa Mwajuma (uk. 33). Lakini Yasmin aliyavumilia
maisha haya yote.
Kwa upande wa tabaka la chini, waliishi maisha magumu sana, kula
kwao kulikuwa kwa tabu, kulala kwa tabu, lakini waliyavumilia maisha
haya. Kwa upande wa ujasiri tunaona kuwa kitendo cha Yasmin
kumkimbia mume wake wa kwanza ambaye vilevile hakumpenda,
kwani alilazimishwa na wazazi wake ni kitendo cha ujasiri. Yasmin
hakuona sababu kwanini aendelee kuishi na mume ambaye si chaguo
lake bali la wazazi wake.
Vilevile kitendo cha Yasmin kumkimbia Shihab, mume wake wa pili, ni
cha ujasiri kwani mume yule alikuwa na wivu mno na matokeo yake
ukamnyima uhuru Yasmin. Katika kutafuta uhuru huo, Yasmin
alimkimbia Shihab.
Kwa upande wa Denge na kundi lake walikuwa jasiri, ndiyo maana
waliendesha propaganda za kudai uhuru nchini Zanzibar kwa kutawanya
vitabu vya kijamaa na magazeti yanayopinga ukoloni. Walifuatwa sana
na wakoloni hao pamoja na vijibwa vyao lakini hawakuacha kudai haki
zao. Walifungwa gerezani lakini walipotoka msimamo wao ulikuwa
uleule wa kutaka wakoloni waondoke nchini mwao.
Hivyo, msanii anaonesha kuwa uvumilivu na ujasiri katika maisha ni
chachu ya maendeleo katika jamii. Na watu wasipokuwa wavumilivu
hukata tama haraka. Wasipokuwa jasiri huwa waoga. Matokeo yake ni
kurudisha nyuma maendeleo ya jamii husika.
6. Umoja na mshikamano
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 14
Umoja na mshikamano ni dhamira ingine inayojadiliwa katika riwaya
hii. Msanii anaonesha kuwa, katika harakati zozote za kudai uhuru,
umoja na mshikamano ni kitu muhimu sana.
Denge na kundi lake yaani Mambo, Chande, Zanga, Salehe, Pazi,
Huseni na wengine walishirikiana sana katika harakati za kuutishia
utawala wa kikoloni nchini Zanzibar, walishirikiana kwa kugawa vitabu
vya akina Marx, magazeti pamoja na makaratasi mengine yaliyochapwa
maalumu kwa kupinga ukoloni Zanzibar.
Vilevile tunaona wafanyakazi wa Unguja walivyoonesha mshikamano
na umoja wao katika maandamano yaliyofanyika tarehe mosi Mei.
Katika maandamano hayo, wafanyakazi walikuwa wengi sana na
walibeba mabango na vitambaa vilivyoandikwa maneno ya kuhimiza
kuungana kwa wafanyakazi na kuulaani ukoloni (uk. 139).
Katika kuhakikisha kuwa Denge anatolewa gerezani, Mambo, Yasmin,
Mwajuma na Bukheti walishirikiana sana pamoja na Sukutua. Kutokana
na ushirikiano huo waliweza kumtorosha Denge kutoka Unguja na
kumpeleka Kenya ili kukwepa mkono wa serikali ya wakoloni (uk. 272-
274).
Vilevile Mwajuma na Yasmin walikuwa na umoja na mshikamano wa
hali ya juu sana katika maisha yao yote. Yasmin baada ya kwenda kuishi
kwa Mwajuma walishirikiana katika taabu na raha bila ubaguzi wowote
kati yao.
7. Usaliti
Usaliti ni dhamira nyingine inayojadiliwa na mwandishi katika riwaya
hii. Katika kujadili dhamira hii, msanii ameonesha jinsi Yasmin
alivyowasaliti wazazi wake kwa kumwacha mume wake Raza, na
matokeo yake ni kutengwa na jamaa zake. Yasmin hakumpenda kabisa
Raza kwa sababu hakuwa chaguo lake, bali alilazimishwa na wazazi
wake kuolewa naye na hatimaye akamwacha. Huu ni usaliti mzuri kwani
hapa msanii anaitahadharisha jamii kuwa si vizuri kumlazimisha mtoto
wako kuolewa na mtu asiyemtaka.
Usaliti mwingine ni ule wa Yasmin kwa Koplo Matata na wakubwa
wake (Wazungu). Koplo Matata alimweka Yasmin amchunguze Denge
pamoja na mienendo yake yote na alitakiwa kutoa taarifa zake polisi
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 15
lakini badala ya kufanya kazi hiyo kwa siri alimwambia yote Denge (uk.
145-148). Kwa hiyo taarifa zote alizozipeleka Yasmin polisi zilipikwa
na Denge makusudi. Kama hiyo baada ya Yasmi kupewa karatasi za
kwenda kupeleka kwa Denge kwa siri ili ziwe kidhibiti cha kumtia
hatiani Yasmin alimkabidhi Denge karatasi hizo kama asemavyo
(uk.154);
“Waliingia ndani na baada ya kuingia tu, Yasmin alimkabidhi Denge
yale makaratasi. “Koplo Matata kanambia niyalete kwako, lakini wewe
usijue kama nimeyaleta.”
Usaliti wa Yasmin kwa Koplo Matata ni usaliti mzuri kwani
aliwaonesha wakoloni na vijibwa vyao kuwa hakuna hata mtu mmoja
katika nchi ile anayekubaliana na matendo yao. Vilevile aliwajulisha
kuwa katika harakati hizo Denge hayupo peke yake bali kuna wengine
pia, hivyo huo ni usaliti mzuri. Ni kutokana na usaliti huo ndio maana
Koplo Matata akafukuzwa kazi (uk. 161).
Usaliti mwingine ni wa Askari jela aliyewasaidia kina Mambo na
Yasmin kumtorosha Denge jela (uk. 143). Askari yule alikiuka maadili
ya kazi yake kwa kuwasaliti wakoloni na vibaraka wao na kuanza
kushirikiana na wapigania uhuru ambao walikuwa wakisakwa kila kona
ya nchi (uk. 245);
“Unamjua Yasmin?” aliuliza yule askari. Denge alinyamaza kimya,
hakumjibu kitu, usiwe na wasiwasi mimi mwenzako, najua mnataka
nini.”
Kwa upande wa wakoloni, huu ni usaliti mbaya lakini kwa wapigania
uhuru huu ni usaliti mzuri, kwani inaonesha kuwa hata walinzi wa
utawala huo wa kikoloni nao wamechoka kutawaliwa na kunyanyaswa
na ukoloni huo, ndiyo maana wanamua kuwasaidia wapigania uhuru.
Kama alivyofanya askari huyu kwa kusaidia kumtorosha Denge
gerezani.
Kwa upande mwingine, watu kama Koplo Matata na askari wengine wa
kiafrika waliomtumikia mkoloni. Hawa ni wasaliti wa Waafrika wenzao,
kwani walisaidiana na wakoloni katika kuwakandamiza na kuwaonea
wananchi wa kawaida. Hawa walikuwa vijibwa vya wakoloni na
walitumiwa na wakoloni kwa lengo la kutimiza malengo yao, ambayo ni
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 16
kinyume kabisa na mahitaji ya wananchi wa kawaida. Akina Koplo
Matata walikuwa vibaraka wa wakoloni hao kwani walikuwa wanalipwa
kutokana na kazi zao hizo. Hivyo msanii anaitahadharisha jamii kuwa
suala la ukombozi si lelemama, lazima tuwe macho na wasaliti.
8. Nafasi ya mwanamke
Katika riwaya hii, mwanamke amechorwa katika nafasi mbalimbali.
Kwanza mwanamke amechorwa kama kiumbe duni asiye na maamuzi
yoyote katika jamii. Mfano mzuri ni pale Yasmin anapolazimishwa na
wazazi wake kuolewa na mtu asiyemtaka (uk. 1). Hili linaonesha kuwa
mwanamke ni kiumbe duni ambaye hana maamuzi yoyote katika jamii.
Vilevile Yasmin kuwekwa utawani na Shihab inaonesha uduni wa
mwanamke katika jamii. Shihab baada ya kumuoa Yasmin alimuweka
utawani, kila wakati akawa anafungwa ndani na hivyo kukosa uhuru
aliotakiwa kuupata (uk. 197).
Pili, mwanamke amechorwa kama mwanamapinduzi ambaye hataki
kung’ang’ania mila na desturi zilizopitwa na wakati. Mfano ni Yasmin
kwenda kutafuta uhuru wake baada ya kumkimbia Raza. Vilevile
tunamuona Yasmin akimwacha Shihab ambaye alimuweka utawani
baada ya kumuoa na kwenda kwa Denge na kuishi naye. Huu wote ni
uwanamapinduzi alioonesha Yasmin katika riwaya hii.
Tatu, mwanamke anaoneshwa kama mtu mpole na mwenye huruma.
Mfano mzuri ni Mwajuma ambaye alimsaidia sana Yasmin baada ya
kumuacha mume wake Raza. Mwajuma alimchukua Yasmin na akaanza
kuishi naye katika hali yake ya umaskini, wakasaidiana katika shida na
raha.
Nne, mwanamke anaoneshwa kama chombo cha starehe. Mfano ni
Mwajuma na Yasmin. Yasmin alikuwa akimstarehesha Denge na
Mwajuma kwa Mambo.
Ujumbe 1. Suala la mapenzi waachiwe wale wanaopendana na sio wazazi
kuwalazimisha watoto na uhuru huo lazima uwe na mipaka yake.
2. Mila na desturi zilizopitwa na wakati katika jamii hazina budi
kutupiliwa mbali katika jamii
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 17
3. Uvumilivu, ujasiri, umoja na mshikamano ni mbinu muhimu za
kujikomboa
4. Ubaguzi wa rangi katika jamii ni kikwazo cha ujenzi wa jamii
5. Ushauri ni kitu muhimu, lakini lazima kuwe na mipaka yake
6. Ukweli humuweka mtu huru
Migogoro a) Yasmin v/s wazazi wake
b) Yasmin v/s Raza
c) Yasmin v/s Denge
d) Denge v/s serikali
e) Yasmin v/s Mwajuma
f) Yasmin v/s Koplo Matata
Msimamo Mwandishi anaonesha msimamo wa kimapinduzi kwani ameonesha
wazi kuwa jamii yetu ina baadhi ya mila na desturi zilizopitwa na
wakati, hivyo jamii lazima izifutilie mbali.
Falsafa
Mtunzi anaelekea kuamini kuwa mapenzi ya kweli yatapatikana katika
jamii ikiwa kutakuwa na uhuru wa kuchagua yule unayemtaka, badala
ya kulazimishwa na wazazi.
Fani
Muundo Mwandishi ametumia muundo wa moja kwa moja. Anaanza masimulizi
yake kwa kuelezea ndoa ya Raza na Yasmin, Yasmin kumwacha Raza,
Yasmin kwa Mwajuma, Yasmin kuolewa na Shihab na mwisho ndoa ya
Yasmin na Bukheti.
Mtindo Mwandishi ametumia mtindo wa monolojia (masimulizi) kwa kiasi
kikubwa ingawa pia kumejitokeza dayalojia. Katika kuukamilisha
mtindo wake msanii pia ametumia barua (uk. 168), nyimbo (uk. 85-86).
Pia nafsi zote tatu zimetumika.
Matumizi ya lugha
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 18
Mwandishi ametumia lugha rahisi inayoeleweka hata kwa msomaji wa
kawaida, pamoja na misema, methali,tamathali za semi na mbinu
nyingine za kisanaa.
Misemo/Nahau a) Kumpaka mafuta kwa mgongo wa chupa (uk. 205)
b) Hujui kama mkono wa serikali ni mrefu (uk.71)
c) Wacha kutia chumvi (uk. 54)
d) Hana mbele wala nyuma (43)
e) Alipiga moyo konde (uk. 42)
f) Kuna dansa la kukata na shoka (uk.35)
g) Maji yamezidi unga (uk. 15)
Methali a) Asiyekubali kushindwa si mshindani (uk. 271)
b) Mwangaza mbili moja humponyoka (uk. 230)
c) Mzoea punda hapandi farasi (uk. 207)
d) Heri nusu shari kuliko shari kamili (uk.42)
Tamathali za semi
Tashibiha
1. Bwana Raza amekaa juu ya kiti amevimba kama kiboko (uk. 9)
2. Kijana yule aliyekuwa na macho makali kama kurunzi (uk. 13)
3. Ametoa macho kama chui (uk. 31)
4. Yeye na ndani na ndani nay eye kama mwari (uk. 33)
5. Mweupe kama mgonjwa wa safura (uk. 82)
Tashihisi 1. Chumbani mle watu wakaanza, hawaonani na mbu wakaanza
kujiandaa kwa karamu yao (uk. 194)
2. Nuru ya jua iliingia kwa hamaki chumbani mle na ilikashifu uchafu
wote wa chumba kile (uk. 49)
Tabaini 1. Mabinti waliolelewa wakaleleka, waliofunzwa wakafunzika,
waliotunzwa wakajitunza (uk. 85)
2. Hatua si hatua, mseto si mseto, ugali si ugali (193)
3. Sina shoga, sina jirani, sina jamaa, mimi na ndani na ndani na mimi,
sirudi sirudi (uk. 211)
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 19
Mbinu nyingine za kisanaa
Takriri 1. Yeye hakuona isipokuwa Yasmin, Yasmin, Yasmin gani naye? (uk.
84)
2. Haweshi, ingia toka na kila wakija Denge, Denge na umewakosea nini
hasa? (uk. 86)
3. Haya tunywe, tunywe kwa afya ya mgeni wetu (uk. 26)
Mjalizo 1. Raha ya kuwa karibu naye wakaongea, wakacheka, wakafurahi (uk.
14)
2. Kula mkate wa ufuta, mkate wa maji, mkate wa mayai (uk. 80)
Mdokezo 1. Naona siku hizi…….(uk. 15)
2. Unani…..(uk. 16)
3. Mbona unaogopa dada, unafikiri si……(uk. 25)
4. Halafu kanigaia shilingi ishirini na ……..(uk. 67)
Tanakali sauti (Onomatopea) 1. Oooooh, Yasmin alijilaza kitandani akapumua kwa machofu ya safari
aliyokwenda (uk. 44)
2. Ngo, ngo, ngo, aligonga mlango (uk. 8)
Matumizi ya Kiingereza 1. Passing showa (uk. 17)
2. Brother, you fool (uk. 31)
3. Come on (uk. 32)
Wahusika
Yasmin Huyu ndiye mhusika mkuu katika riwaya hii. Yasmin alikuwa na kijuso
kidogo, macho makubwa, pua ndogo na nyembamba, alikuwa na nywele
nyingi. Vilevile alikuwa si mrefi lakini hakuwa mfupi.
Kwa tabia Yasmin alikuwa mwanamke aliyekuwa akipenda mabadiliko
ndiyo maana aliamua kumkikimbia mume wake wa kwanza
aliyelazimishwa na wazazi wake kuolewa naye.
Vilevile Yasmin alikuwa anapenda uhuru wa kuchagua mchumba wake
yeye mwenyewe na hakupenda wivu ndiyo maana alimkimbia Shihab
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 20
kutokana na wivu wake. Yasmin alikuwa mvumilivu na mtu jasiri sana.
Aliyavumilia maisha magumu aliyoishi kwa Mwajuma, pamoja na
vituko vyote alivyokumbana navyo.
Wahusika wadogo
Mwajuma Alikuwa na uso mwembamba uliochongoka sawasawa na macho
remburembu. Alikuwa mrefu wa wastani. Mwajuma alikuwa mpole,
mkarimu na mwenye roho nzuri, na alikuwa tayari kumsaidia mtu
chochote kidogo alichokuwa nacho. Vilevile alikuwa na huruma sana
kwa Yasmin.
Kadhalika alikuwa ni msichana asiyependa kujikera nafsi yake na
aliutumia uhuru wake wa maisha kama alivyopenda. Alikuwa tayari
kufanya lolote lile ambalo alihisi litamletea furaha bila ya kujali
wengine watasema nini. Vilevile alikuwa mwanachama wa chama cha
“Cheusi dawa”, kikundi cha taarabu. Kutokana na huruma, upole na
ukarimu wake Mwajuma anafaa kuigwa na jamii.
Denge Alikuwa mrefu wa futi sita, mwembamba na mkakamavu. Umbile lake
ni la rangi ya maji ya kunde, pua yake ilikuwa ya wastani. Denge
alikuwa mwanaharakati wa kupinga utawala wa Mwingereza kisiwani
Unguja na Pemba. Katika harakati zake alisambaza vitabu vya Karl
Marx, magazeti yanayopinga ukoloni, pamoja na makaratasi ya
uchochezi dhidi ya ukoloni.
Denge ni mfano mzuri wa vijana ambao wako mstari wa mbele katika
harakati za kupambana na ukoloni hapa nchini, hivyo ni mfano mzuri wa
kuigwa.
Wahusika wengine katika riwaya hii ni Koplo Matata, Chande, Sukutua,
Raza, Salehe, Inspekta Wright, Shihab, Bukheti, n.k
Mandhari Riwaya hii imetumia mandhari halisi ya visiwa vya Unguja, maeneo ya
Tanga na Mombasa –Kenya. Lakini matukio mengi yamefanyika
Unguja. Vilevile kuna mandhari ya dukani, gerezani, baharini,
nyumbani, mtaani, baa, klabuni, n.k
Jina la kitabu
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 21
Jina la kitabu linasadifu vizuri yaliyomo ndani ya kitabu hiki. Msanii
anaonesha mivutano mbalimbali katika kitabu hiki.
Kwanza kuna mvutano kati ya Yasmin na wazazi wake. Huu unatokana
na Yasmin kumwacha mume wake Raza ambaye wazazi wake
walimlazimisha aolewe naye.
Pili, kuna mvutano kati ya Yasmin na Raza. Yasmin hakumpenda kabisa
Raza, kwani kiumri Raza alikuwa ni sawa na baba yake wa kumzaa.
Hivyo katika maisha yake ya ndoa na Raza wakawa na mivutano ya kila
siku.
Tatu, kuna mvutano kati ya wakoloni na vijibwa vyao na wananchi wa
kawaida wakiwakilishwa na Denge, Chande, Sukutua, Mambo na
wengine. Hawa wanataka uhuru wa kujiamulia mambo yao wenyewe,
wanataka uhuru wa kumiliki njia kuu za uchumi badala ya wakoloni.
Nne, kuna mvutano kati ya Yasmin na Shihab. Huu unatokana na wivu
wa kimapenzi. Shihab alikuwa na wivu sana kwa mke wake, matokeo
yake akamnyima uhuru kwa kumweka utawani hatimaye Yasmin
akamkimbia.
Mwisho, kuna mivutano ya kinafsia ambayo iliwahusu wahusika
wenyewe. Hawa walikuwa na migongano ya kimawazo katika vichwa
vyao. Mfano ni Yasmin, Bukheti, Denge, n.k
Kufaulu kwa mwandishi - Mwandishi amefaulu sana kwa kuonesha mvutano wa vijana na
wazee.
- Kifani amefaulu sana hasa katika uteuzi mzuri wa lugha na ujenzi wa
wahusika. Lugha ni rahisi na inayoeleweka kwa kila mtu.
Kutofaulu kwa mwandishi - Suluhisho la mgogoro kati ya wakoloni na wananchi halijaoneshwa,
kwani tunaona tu wapigania uhuru wanawekwa ndani na wengine
wanatoroka kwenda nje ya nchi. Je, hawa watu watatumia mbinu gani
katika kujikomboa? Msanii hajaonesha.
- Matumizi ya lugha ya Kiingereza ni udhaifu mwingine wa msanii,
kwani mtu asiyefahamu lugha hiyo hataweza kuelewa ujumbe uliomo
kwa urahisi.
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 22
- Msanii hajaonesha mipaka ya uhuru unaotakiwa kwa watoto wetu.
Kwa mfano, Yasmin ametumia uhuru wake wa kumchagua Shihab
lakini naye ndoa yao haikudumu. Au uhuru wa Yasmin wa kuolewa na
kuachika ndio uhuru unaotakiwa? Msanii hajaonesha vizuri.
UHAKIKI WA RIWA YA MFADHILI
KIDATO CHA 5 NA 6
KITABU – MFADHILI
MWANDISHI – HUSSEIN TUWA
WACHAPAJI – MACMILAN
MWAKA – 2007
UTANGULIZI
Mfadhili ni riwaya inayoongelea suala la mapenzi na ndoa, ikonesha
matatizo mbalimbali yanayotokana na mapenzi na ndoa na athari zake
kwa wanaohusika. Ni riwaya inayoongelea juu ya penzi zito baina ya
Gaddi Bullah na Dania Theobald, na jinsi penzi hilo lilivyoingiliwa na
mitihani na majaribu makubwa. Ni riwaya ambayo kwa mapana yake
inajadili kwa kiasi kikubwa suala la mapenzi na ndoa na athari zake kwa
jamii.
MAUDHUI
Dhamira
Mwandishi katika riwaya hii licha ya kujadili dhamira ya mapenzi na
ndoa, vilevile amejadili dhamira mbalimbali kama vile usaliti, umuhimu
wa uongozi bora, wizi wa mali ya umma, chuki, uzembe kazini, dharau,
uongo na ulaghai, n.k
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 23
Dhamira kuu: Fadhila
Katika kujadili suala hili mwandishi anaonesha jinsi suala la
kufadhiliana lilivyomuhimu katika jamii bila ya kujali unayemfadhili
alikutendea mema au mabaya huko nyuma. Mfano mzuri katika suala
hili ni fadhila za Gaddi kwa Dania, ambapo mwandishi anaonesha jinsi
Gaddi alivyogeuka mfadhili wa ini kwa Dania na kuokoa maisha ya
Dania licha ya kutendwa unyama usiosemeka katika mahusiano yao.
Ukweli huu unadhihirishwa na Dkt. Viran alipokuwa akimshawishi
Dania juu ya kwenda kumuona Gaddi na hatimaye akamtobolea siri
kuwa Gaddi ndiye mfadhili wa ini lake.
Dhamira ndogondogo
1. Mapenzi na ndoa
Katika kujadili dhamira hii msanii ameainisha aina kuu mbili za
mapenzi na ndoa; mapenzi ya kweli na mapenzi ya uongo, ndoa ya kweli
na ya uongo.
Tukianza na mapenzi ya kweli, haya yanaoneshwa kati ya Gaddi
Bullah na dada yake Bi. Hanuna. Hawa walipendana kwelikweli na ndio
maana mmoja akiwa na tatizo linakuwa ni tatizo la wote wawili. Mtu
akimwudhi Gaddi amemwudhi na dada yake Bi. Hanuna, na
walisaidiana katika shida zao zote.
Mapenzi mengine ya kweli ni kati ya Gaddi na Dania. Mwanzoni
walipendana hasa; mchana walikuwa wakienda kula chakula pamoja na
hata walifikia hatua ya kutembeleana. Gaddi katika kuonesha mapenzi
kwa Dania, alimsaidia kwa kila hali hata wakati war aha na shida (uk.
101-106). Hata baada ya Dania, kumsaliti Gaddi, bado alimpenda na
hata akamfadhili baada ya kusalitiwa na Jerry kwa mara ya pili (uk. 137-
139).
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 24
Pia kuna mapenzi ya kweli kati ya Gaddi na Junior, mtoto wa Dania.
Pamoja na kwamba Junior hakuwa mtoto wake, Gaddi alimpenda sana
na ndio maana baada ya Junior kuumia mkono aliyempeleka hospitalini
ni Gaddi na wala si Baba yake Jerry (uk. 118). Vilevile, Junior aliposikia
taarifa za ugonjwa wa Gaddi alilia na wakati wa kifo cha Gaddi wosia
pekee alioutoa kwa Dania ni kumtunza vizuri Junior, anasema (uk. 146);
“Gaddi akimgeukia Dania. “Junior Dania……..Junior mtunze vizuri
Junior! Umepata bahati ya kue…ndelea kuishi ili umtunze
mwan…na….o!” Gaddi aliyasema yote hayo kutokana na mapenzi
aliyokuwa nayo kwa Junior.
Mapenzi mengine ya kweli ni ya Mama Mlole (Bi. Fausta) kwa
wafanyakazi wa chini yake kama Gaddi na Dania. Pamoja na Gaddi
kuharibu kazi, mama Mlole alimtetea sana asifukuzwe kazi bali
aangaliwe upya (uk. 69-71). Vilevile alimtetea sana Dania asifutwe kazi
kipindi anaumwa. Mama Mlole ni mfano wa viongozi wenye mapenzi
ya kweli kwa wale anaowaongoza.
Vilevile kuna mapenzi ya kweli kati ya Nunu na Dania. Nunu alikuwa
bega kwa bega na Dania wakati wa maandalizi ya harusi ya Dania na
Jerry. Nunu alimsaidia sana Dania. Vilevile alimshauri sana Dania
asirudiane na Jerry kwa vile alimsaliti mara ya kwanza (uk. 113-115).
Pia alimsaidia sana kumlea mtoto wake Junior wakati Dania yuko kituo
cha kuponya walevi (uk. 115). Kama hiyo haitoshi, Nunu alikuwa bega
kwa bega na wazazi wa Dania wakati wa ugonjwa wake na hata
akamsaidia kumtafuta Gaddi na Bi. Hanuna ili awaombe msamaha kwa
yote aliyowatendea.
Kuna mapenzi ya kweli kati ya Nunu na Boaz. Hawa walipendana kwa
dhati na ndiyo maana shida ya Nunu ilikuwa shida ya Boaz pia. Ni
kutokana na mapenzi ya dhati waliyokuwa nayo ndiyo maana
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 25
walisaidiana kwa hali na mali, kwa heri na shari katika kumtafuta Gaddi
aliyekuwa anatakiwa na rafiki yake Dania. Hata wakafikia hatua ya
kuhatarisha maisha yao kwa kumteka nyara Bi. Hanuna kwa lengo la
kumsaidia Dania (uk. 36-56).
Mapenzi mengine ya kweli ni kati ya Dakta Viran na Gaddi. Hawa
walipendana hasa, na ndiyo maana Viran alimsaidia Gaddi katika
matatizo mbalimbali. Kwa mfano, kumtibu mpenzi wake Dania,
kumtibu yeye mwenyewe alipopata shinikizo la moyo, baada ya
kuachwa na Dania na mwisho Viran anakuwa mpatanishi kati ya Gaddi
na Dania na Nunu kutokana na ugomvi wa kuachwa kwa Gaddi na
mpenzi wake Dania. Vilevile tunamwona Dakta Viran anavyohangaika
kuokoa maisha ya Gaddi kutokana na ugonjwa aliokuwa anaumwa
ingawa hakufanikiwa. Haya yote aliyafanya kwa sababu alimpenda
Gaddi kwa dhati na Gaddi vilevile alimpenda Viran.
Vilevile kuna mapenzi ya dhati kati ya wazazi wa Dania kwa mtoto wao
Dania. Wazazi wake Dania walimpenda sana mtoto wao, ndiyo maana
wakati wa shida za Dania walimsaidia kwa hali na mali hadi
wakampeleka Afrika Kusini kutibiwa ugonjwa wake wa ulevi. Wakati
wa ugonjwa wake wa ini, wazazi wake walimsaidia sana mpaka hatua
ya kuweka matangazo redioni ili kumsaidia mtoto wao kwa mtu ambaye
angejitolea ini. Gharama zote walikuwa tayari kumlipa mtu yeyote
ambaye angejitokeza kufanya hivyo. Hayo ni mapenzi ya dhati ya
wazazi kwa binti yao.
Mapenzi mengine ya dhati ni kati ya Nunu na Gaddi. Nunu alimpenda
Gaddi kwa dhati, ndiyo maana alimshauri sana Dania asimwache Gaddi
na kurudiana na Jerry. Nunu alimkatalia Dania asirudiane na Jerry si
kwa sababu alimsaliti, bali awe na Gaddi aliyemsaidia wakati wa shida
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 26
(uk. 114-115). Vilevile Gaddi alimpenda Nunu kama rafiki mzuri
anasema (uk. 146);
“………Nunu”… “A…Abee! Nunu aliitikia kwa upole huku akitiririkwa
na machozi “wewe…..ni rafiki…mzuri….. “Gaddi alimwambia……”
Baada ya kifo cha Gaddi, Nunu pamoja na wengine wote walilia sana
kuonesha mapenzi yao kwa Gaddi.
Mapenzi ya uongo
Mapenzi ya uongo ni kati ya Jerry kwa Dania. Jerry inaonesha
hakumpenda kwa dhati Dania na ndiyo maana alimsaliti wakati wa
harusi yao. Jerry alipenda zaidi masomo kuliko kufunga ndoa na Dania.
Aliona maandalizi ya harusi lakini akaondoka kwenda Marekani kusoma
kwa ahadi ya kurudi siku ya harusi. Lakini siku ilipofika Jerry
hakuonekana na hivyo ndoa ikashindikana kufungwa.
Vilevile kitendo cha Jerry kumtoroka Dania akiwa hospitalini pindi
ambapo msaada wake ulitakiwa ni usaliti unaothibitisha kuwa hakuwa
na mapenzi ya dhati kwa Dania. Jerry alitakiwa kumfadhili Dania ini ili
kuokoa maisha yake, lakini siku ilipofika hakufika hospitalini na
hawakumwona tena (uk. 133-135)
Mapenzi mengine ya uongo ni kati ya rafiki yake Gaddi kwa Gaddi.
Huyu hakuwa rafiki wa kweli kwani alimshauri vibaya Gaddi (uk. 64).
Kana kwamba hiyo haikutosha, alimtorosha mke wa Gaddi na
kumuweka kinyumba (uk. 64-67). Kuhusu suala la ndoa, nazo zipo za
aina mbili ambazo ni ndoa za kweli na ndoa za uongo. Ndoa ya kweli ni
kati ya Gaddi kwa Nyambuja. Gaddi alimpenda sana mkewe na alimjali
kwa kila kitu. Lakini mke wake hakuwa na mapenzi ya dhati katika ndoa
yao. Baada ya mwaka mmoja tu wa ndoa yao, Nyambuja alianza
kumsaliti mumewe kwa kuchelewa kurudi nyumbani, kusafiri bila
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 27
taarifa kwa mume wake na mwisho akamwacha na kwenda kuolewa na
rafiki wa mumewe (uk. 60-67).
2. Usaliti
Usaliti ni dhamira ingine ambayo imejadiliwa sana katika riwaya hii
ya Mfadhili. Katika kujadili dhamira hii, msanii anaonesha jinsi watu
mbalimbali wanavyosaliti wenzao na athari za usaliti huo kwa wahusika.
Kwanza tunaoneshwa jinsi Nyambuja alivyomsaliti mume wake na
kwenda kuolewa na rafiki wa mumewe. Kwa upande mwingine rafiki
wa Gaddi alimsaliti Gaddi na kumchukua mke wa rafiki yake. Usaliti
huu ulisababisha Gaddi kupoteza umakini kazini kutokana na msongo
wa mawazo na kuishia kupewa barua ya onyo kwa kuidhinisha malipo
hewa ya matengenezo ya magari ya kampuni (uk. 62-63).
Usaliti mwingine ni ule wa Afisa usafirishaji kwa kumsaliti Gaddi
kazini. Huyu aliandaa vocha ya malipo hewa na kuipeleka kwa Gaddi
ikasainiwe. Matokeo ya usaliti huo ni Gaddi kushushwa cheo na
kuhamishwa chake cha kazi (uk. 71-72)
Usaliti mwingine ni wa Dania kwa Gaddi. Kwanza Dania alimsaliti
Gaddi kwa kutoandaa ripoti aliyotakiwa kuiandaa kwa ajili ya kusomwa
kwenye kikao cha wakuu wa vitengo. Dania hakuandaa ripoti hiyo, na
siku ya kikao hakuonekana kazini hadi muda wa kikao ulipoanza saa
mbili na nusu Asubuhi (uk. 77-79). Matokeo yake Gaddi alimlima barua
ya onyo na kumtaka ajieleze. Lakini kwa busara za Mama Mlole
alisuluhisha mgogoro huu.
Pili, Dania alimsaliti Gaddi kwa kumwacha wakiwa katika mapenzi
mazito na wakati huohuo wanajiandaa kufunga ndoa. Dania alimwacha
Gaddi na kurudiana na Jerry ambaye alimsaliti siku ya harusi yake.
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 28
Matokeo ya usaliti huo ni Gaddi kupata ugonjwa wa shinikizo la moyo,
kupigana na Jerry, na dada yake Bi. Hanuna kuwekwa ndani (polisi).
Usaliti wa Jerry kwa Dania. Kwanza alimsaliti Dania wakati wa harusi
yao. Jerry hakuhudhuria harusi hiyo, alikuwa Marekani na wakati
huohuo aliahidi kuwa angehudhuria (uk. 83-85). Ni kutokana na usaliti
huo, harusi ilishindikana na kumfanya Dania aingie kwenye matatizo
makubwa ya ulevi wa pombe kali (uk. 87). Kutokana na ulevi huo Dania
alipata ugonjwa wa ini.
Pia Jerry alimsaliti Dania akiwa mgonjwa mahututi hospitalini kwa
kuahidi kutoa ini baada ya vipimo kuonesha inawezekana, lakini
hakufanya hivyo. Kwanza, hakumsaidia kwa kumpa ini. Pili akamtoroka
akiwa kitandani hospitalini (uk. 133-134). Katika kuokoa maisha ya
Dania, pamoja na kwamba alimsaliti, Gaddi alijitokeza kuwa mfadhili
wa ini kwa Dania.
Katika riwaya hii mtunzi anaonesha kuwa wasaliti katika jamii wapo,
anaweza kuwa mkeo (Nyambuja), mpenzi wako (Dania), mfanyakazi
mwenzako (Afisa usafirishaji), mumeo (Jerry) au rafiki yako wa karibu
(rafiki wa Gaddi), hivyo tuwe macho na wasaliti, kwani wanaharibu
mapenzi ya watu na kazi zao.
3. Umuhimu wa uongozi mzuri
Mwandishi amejadili dhamira hii katika riwaya yake ya Mfadhili. Katika
kujadili dhamira hii, msanii anamtumia mhusika Mama Mlole. Mama
Mlole alikuwa kiongozi mzuri ambaye aliwajali wale aliowasimamia,
jambo ambalo linasaidia kuongeza ufanisi katika kazi yake.
Gaddi Bullah alipopata matatizo kazini yaliyotokana na athari za
kuachwa na mke wake, Mama Mlole alimtetea sana asifukuzwe kazi
baada ya kumweleza matatizo yake (uk. 70). Na ni Mama Mlole
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 29
huyohuyo aliyependekeza Gaddi ahamishiwe Dar es Salaam ili
aangaliwe zaidi badala ya kufukuzwa kazi. Mama Mlole alifanya hivyo
kutokana na utendaji mzuri wa kazi aliokuwa nao Gaddi mwanzoni
kabla ya kukumbwa na matatizo yaliyomsibu.
Vilevile ni Mama Mlole aliyemtetea Dania asifukuzwe kazi baada ya
kuachwa na Jerry. Baada ya kuvunjika kwa ndoa yake na Jerry, utendaji
wake wa kazi uliathirika sana. Alifikia hatua ya kuja ofisini akiwa
amelewa (uk. 88) na hatua aliyofikia ilikuwa aachishwe kazi. Lakini
Mama Mlole kama Afisa utumishi wa kampuni alimtetea sana na
akapendekeza apewe likizo bila malipo kwa muda wote atakaokuwa
kwenye matibabu ya ulevi wake (uk. 88)
Kiongozi mzuri daima hupendwa na watu anaowaongoza na mara nyingi
ufanisi wake kazini vilevile huwa mzuri. Hapa msanii anachotaka
kuifundisha jamii ni kuwa cheo ni dhamana lazima kukitumia kwa faida
ya watu wote na sio kunyanyasa wengine.
4. Bidii katika kazi
Bidii katika kazi ni dhamira ingine inayojitokeza katika riwaya hii
ya Mfadhili. Katika kujadili dhamira hii, mwandishi anaonesha kuwa ili
kuleta maendeleo katika jamii lazima kuwa na bidii katika kazi.
Katika kujadili hili mtunzi anamtumia Gaddi Bullah ambaye alionesha
kuwa kijana mdogo lakini mchapakazi mzuri. Alipendwa sana na
wafanyakazi wote waliokuwa chini yake na hata wakuu wake wa kazi
huko makao makuu (uk. 59).
Pili tuna Dania, mwanzoni alikuwa mmoja kati ya wafanyakazi wenye
nidhamu, bidii na ushirikiano mkubwa hapo makao makuu. Dania akiwa
anatoka kwenye familia ya kitajiri. Aliwaheshimu wafanyakazi wote na
wala hakuruhusu utajiri wa wazazi wake umpe kichwa. Kutokana na
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 30
utendaji wake mzuri wa kazi, ndiyo maana alipewa wadhifa wa
kuongoza kitengo muhimu cha kukusanya madeni cha kampuni na
kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
Katika kujadili zaidi dhamira hii, msanii anaonesha kuwa matatizo ya
mtu binafsi au hata ya kifamilia yanaweza kupunguza bidii na ufanisi wa
mtu katika kazi anayoifanya. Kama ilivyokuwa kwa Gaddi na Dania.
Gaddi alipoachwa na mke wake alichanganyikiwa na kupoteza umakini
katika kazi hata akasaini na kuidhinisha cheki hewa (uk. 63) ambayo
ilimletea matatizo makubwa kazini kwake.
Vilevile Dania baada ya kuachwa na Jerry, ufanisi wake wa kazi
ulipingua na kufanya kazi hovyo. Kwanza, utendaji wake uliathirika
vibaya sana. Alifika ofisini akiwa amelewa. Kutokana na kitendo hicho,
wazazi wake ilibidi wampeleke kwenye kituo maalumu cha kutibu watu
wenye tatizo la ulevi wa kupindukia huko Afrika Kusini (uk. 88).
Kwa ufupi msanii anaonesha kuwa bidii katika kazi ni kichocheo cha
maendeleo ya jamii. Pindi mtu anapokumbwa na matatizo, mara nyingi
ufanisi wake wa kazi hupungua na hupata matatizo. Matatizo hayo
yanaweza kuwa ya kufukuzwa kazi au kushushwa cheo kama
ilivyokuwa kwa Gaddi. Vilevile matatizo yanaweza kumfanya mtu
achanganyikiwe, aache kazi na kuuza kila kitu kama alivyofanya Gaddi
baada ya kuachwa na Dania. Kwa hiyo, mwandishi anaitahadharisha
jamii kuepukana na matatizo.
5. Chuki
Chuki ni dhamira ingine inayojadiliwa katika riwaya ya Mfadhili. Katika
kujadili dhamira hii, msanii anaonesha wahusika mbalimbali na chuki
zao binafsi zinazosababishwa na mambo mbalimbali.
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 31
Kwanza, Bi. Hanuna alikuwa na chuki na Nunu kwa sababu ya Dania.
Kitendo cha Dania kumuacha kaka yake, Gaddi wakati wako katika
mapenzi ya raha na furaha. Kitendo hiki kilimuudhi sana Bi. Hanuna.
Hata Nunu alipokwenda kwake kuomba msaada wa kumpata Gaddi
alikataa katakata. Pia shida yao alikataa hata kuisikiliza kutokana na
chuki aliyokuwa nayo, Bi. Hanuna anasema (uk. 25);
“Shida?” Aliguna kwa kebehi”. Eti shida! Mnaijua shida ninyi? Hebu
niondokee hapa sasa hivi mwana asiye haya we! Shida niulize mimi
mliyenisweka gerezani….”
Hata Nunu anapojitetea kuwa ya zamani wayaache wagange yaliyopo,
Bi. Hanuna anamkatalia Nunu (uk. 24);
Bi. Hanuna vilevile alikuwa na chuki na Dania. Hii ilikuwa baada ya
kumwacha kaka yake, Gaddi na kumweka ndani (gerezani) Bi. Hanuna.
Hapo ndipo chuki ya Bi. Hanuna ilipoanza kwa Dania kama anavyosema
(uk. 125);
“Na ni hapo ndipo chuki ya Bi. Hanuna dhidi ya Dania Theobald
ilipodhihiri moyoni mwake. Wakati akimtazama ndugu yake akisema
maneno yake na jinsi sura yake ilivyokuwa na uchungu na kukata tama,
Bi. Hanuna alijua kuwa Dania Theobald atakuwa adui yake milele!!”
Msanii anaendelea kuonesha kuwa, jinsi Bi. Hanuna alivyokuwa
anamwona mdogo wake akiteseka ndivyo alivyozidi kumchukia Dania,
msanii anasema (uk. 126):
Bi. Hanuna alimueleza. Na kadiri alivyokuwa anamweleza kisa kile
ndivyo ghadhabu dhidi ya Dania ilivyozidi kumpanda”
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 32
Ni kutokana na chuki hiyo ndiyo maana Bi. Hanuna alikwenda kwa
Dania na kumtukana matusi mengi ambayo yalisababisha vurugu kubwa.
Msanii anaonesha chuki ya Bi. Hanuna kwa Dania hivi (uk. 126-127)
Wewe ni Malaya usiye na haya baradhuli na hayawani! Hukumstahili
mdogo wangu hata kidogo! Bi. Hanuna alimwambia kwa hamasa na
muda huo Jerry alitoka ndani na kuanza kumfukuza huku akimtukana”
Kutokana na tukio hilo, Bi. Hanuna alikamatwa na polisi na kuwekwa
rumande kwa kosa la shambulizi. Bi. Hanuna akalala rumande siku ile.
Wakati mdogo wake amelala hospitalini yeye alikuwa amelala rumande
na aliumia sana na akazidisha chuki yake kwa Dania kama anavyosema
msanii (uk. 127);
“Kwa hakika chuki yake kwa Dania iliongezeka maradufu, na aliapa
kumchukia kwa uhai wake wote uliobakia.”
Ni kutokana na chuki hiyo kwa Dania ndiyo maana alikataa kuwaeleza
Nunu na Boaz, Gaddi alipo. Vilevile alikataa hata kupeleka barua kwa
Gaddi iliyotoka kwa Dania ya kuomba msamaha (uk. 24) mpaka
alipomuona kweli Dania akiwa katika hali ya kukatisha tama ya kuishi
(uk. 56).
Mhusika mwingine aliyeonesha chuki waziwazi kwa wahusika wengine
ni Dania. Dania alikuwa na chuki na Gaddi Bullah kwa kumwona kama
mtu aliyemnyang’anya cheo chake, msanii anasema (uk. 75);
“Chuki kubwa ilijengeka moyoni mwa Dania dhidi ya Gaddi Bullah.
Kwake, Gaddi alikuwa ni mtu aliyemchukulia wadhifa wake na
kumdhalilisha kama mwanamke, na alimwona ni mmoja tu kati ya
wanaume wengi ambao kwake walikuwa wanyama na wahalifu.”
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 33
Dania anamwona Gaddi kama mnyama au mhalifu kutokana na chuki.
Matokeo yake alijikuta akizidi kumchukia zaidi na zaidi. Chuki
haikuishia ofisini tu bali hata kwenye sehemu za starehe hakutaka hata
kukaa naye, mpaka alifikia hatua ya kumfukuza kwenye meza
aliyokuwa amekaa na mtoto wake Junior kwenye baa, msanii anasema
(uk. 76);
“Naomba utupishe….hapa ni mahali petu! Dania alimjibu kifedhuli”
Kutokana na chuki aliyokuwa nayo Dania kwa Gaddi, anafikia hatua ya
kumharibia kazi ili aonekane hafai (uk. 77-79). Matokeo yake Dania
akaandikiwa barua kali na Gaddi ya onyo na kumtaka ajieleze ni
kwanini asifukuzwe kazi (uk. 79).
Dania vilevile alikuwa na chuki na Jerry hasa baada ya kumwacha
wakati maandalizi yote ya harusi yao yamekamilika. Kitendo cha Jerry
kushindwa kuja kwenye harusi kama alivyoahidi kilimwudhi sana
Dania. Dania alilia sana. Hata Jerry aliporudi kutoka Marekani
alimfukuza kama mmbwa nyumbani kwake, msanii anasema (uk. 107);
“Toka! Dania alimfokea kwa ukali huku akimwonyesha sehemu ulipo
mlango wa kutokea kwa kidole chake….Nasema ondoka Jerry na sitaki
uje tena kunifuata hapa, wala popote pale niwapo! Ondoka!”
Nunu naye alikuwa na chuki na Jerry kwa sababu ya kumwacha rafiki
yake Dania. Hata Jerry alipokwenda kwake kuomba msaada wa
kumshawishi Dania alimfukuza na kumtaka asirudi tena nyumbani
kwake (uk. 109);
Wazazi wa Dania nao walikuwa na chuki na Jerry kwa sababu ya
kumsaliti mtoto wao. Jerry alipokwenda kwao kuwaomba msamaha
walikuwa wakali zaidi ya mbogo na walimfukuza nyumbani kwao (uk.
109-110).
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 34
Msanii katika kujadili dhamira hii ya chuki, anaonesha kuwa wenye
chuki kuna wakati watasameheana. Bi. Hanuna anamsamehe Dania,
Gaddi vilevile anamsamehe Dania, Bi. Hanuna anamsamehe Nunu,
halafu Dania anamsamehe Jerry ingawa msamaha huo ulileta matatizo
mengine kwa Gaddi na Bi. Hanuna. Hivyo, msanii anaonesha kuwa
umsamehe mtu aliyekufanyia makosa ili uishi kwa amani na utulivu.
6. Dharau
Dharau ni dhamira inayojitokeza katika riwaya hii ya Mfadhili. Katika
kujadili dhamira hii, msanii anamtumia Nyambuja kama mtu mwenye
dharau kwa mumewe. Nyambuja hakuwa na upendo wowote kwa mume
wake na ndio maana alikuwa anamdharau. Hata akiulizwa swali na
mumewe majibu aliyokuwa anayatoa yalikuwa yamejaa dharau tupu (uk.
60). Vilevile kitendo cha Nyambuja kusafiri safari za ghafla na
kumtaarifu mumewe kwa simu ni sehemu ya dharau. Gaddi kama mume
wake alistahili kuagwa kwa kufuata taratibu za mume na mke zilivyo,
lakini Nyambuja hakujua hilo ila dharau ilitawala (uk. 61).
Kitendo cha Nyambuja kufanya mapenzi na rafiki yake Gaddi na
kumwacha nayo ni dharau ya hali ya juu. Hata barua aliyomwandikia
Gaddi (uk. 65) ni barua iliyojaa dharau ya Nyambuja kwa Gaddi. Mara
nyingi mwanamke mwenye dharau ndani ya nyumba kwa mume wake
husababisha kuvunjika kwa ndoa na ndivyo ilivyotokea kwa Gaddi na
Nyambuja.
Mhusika mwingine anayeonesha kuwa na dharau ni Dania. Kwanza
alimdharau Gaddi siku ya kwanza tu alipomkuta ofisini kwake. Kitendo
cha Dania kumwita Gaddi kwamba wewe ni “Gaidi Bullah” (uk. 73) ni
sehemu ya dharau aliyoionesha kwa Gaddi. Vilevile kitendo cha Dania
kumfukuza Gaddi kwenye meza aliyokuwa amekaa na mtoto wake
Junior kwenye baa ni sehemu ya dharau. Dania alimfukuza Gaddi
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 35
kwenye meza kama mbwa mwizi; ambapo katika hali ya kawaida
asingefanya hivyo, au angemwomba kwa upole awapishe na sio kwa
kumkaripia kama mtoto mdogo, hii yote ni dharau.
Vilevile Dania alionesha dharau ya hali ya juu baada ya kumwacha na
kurudi kwa Jerry. Majibu aliyokuwa anamjibu Gaddi yalikuwa majibu
ya kijeuri na dharau tupu (120-123). Lakini msanii anaitahadharisha
jamii kuwa makini juu ya suala la dharau kwani unayemdharau leo
huwezi kujua baadaye anaweza kukufaa. Dania alimwacha Gaddi,
alimdharau, lakini baadaye akawa mfadhili wa ini lake baada ya
kutelekezwa na Jerry kwa mara ya pili akiwa mgonjwa mahututi
hospitalini. Hivyo, tuepuke dharau kwani hazina maana yoyote.
7. Nafasi ya mwanamke katika jamii
Katika riwaya hii, mwanamke amechorwa katika nafasi mbbalimbali.
Kwanza amechorwa kama kiumbe asiye na msimamo katika kufanya
maamuzi. Hapa tunamuona Dania akiwa na maamuzi yasiyofaa, kwa
kutokuwa na msimamo na kuamua tena kumrudia Jerry ambaye
alimuumiza mwanzoni.
Pili, mwanamke amechorwa kama mtu mwenye huruma na mshauri
mzuri. Mfano mzuri ni Nunu alivyomhurumia rafiki yake, Dania na
kumhangaikia kwa hali na mali. Vilevile tunaoneshwa jinsi alivyokuwa
mshauri mzuri wa Dania.
Tatu, mwanamke amechorwa kama mtu katili na msaliti. Hapa
tunamuona Nyambuja na Dania walivyomtenda vibaya Gaddi na
hatimaye kumsaliti na kwenda kwa wanaume wengine.
Nne, mwanamke amechorwa kama mtu jasiri. Hapa tunamuona Nunu
ambaye alifanya kazi kubwa sana ya kumpatanisha Dania na Gaddi hata
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 36
akafikia hatua ya kumteka kwa nguvu dada yke Gaddi, Bi. Hanuna, ili
aweze kuwasaidia kumpata Gaddi.
Tano, mwanamke amechorwa kama mtu mwenye upendo, moyo wa
huruma na wa kusaidia. Hapa tunamuona Bi. Hanuna alivyokuwa na
upendo kwa kaka yake Gaddi, halafu pia tunamuona Mama Mlole
alivyokuwa na upendo kwa wafanyakazi wa chini yake.
Ujumbe
1. Rafiki wa kweli ni yule anayekusaidia au kukujali wakati wa shida.
2. Si kila king’aacho ni dhahabu
3. Mtu anapotenda kosa, lazima akubali kutubu kosa
4. Ni vigumu kumpata mtu mwenye mapenzi ya kweli au
atakayekupenda kama unavyompenda wewe
5. Bidii na ufanisi katika kazi ni chanzo cha maendeleo katika jamii
6. Matatizo, majaribu, chuki na dharau ni vitu vya kutegemewa
kwenye mapenzi na ndoa.
7. Kipenda roho hula nyama mbichi
Falsafa
Msanii anaamini kuwa katika suala la mapenzi kuna kupenda na
kutopendwa, kuna kuoa na kuachwa. Hivyo, ni vigumu kupata mtu
mwenye mapenzi ya dhati.
Msimamo
Msimamo wa mwandishi ni wa kimapinduzi, kwani anaonesha wazi
kuwa katika suala la mapenzi na ndoa kuna changamoto zake. Watu
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 37
lazima tukubali kusameheana kwani hujui ni yupi atakayekusaidia
wakati wa shida.
Mtazamo
Mwandishi anaonekana kuwa na mtazamo wa kiyakinifu, kwani
ameyaweka mambo wazi kwa kuonesha kuwa mapenzi ya dhati yapo
kwa akupendaye asiyekupenda usimtegemee anaweza kukuumiza.
Migogoro
1. Mgogoro kati ya Gaddi na Nyambuja
2. Mgogoro kati ya Gaddi na Dania
3. Mgogoro kati ya Gaddi na Jerry
4. Mgogoro kati ya Nunu, Boaz na Bi. Hanuna
5. Mgogoro kati ya Dania na Jerry
6. Mgogoro kati ya Jerry na wazazi wa Dania
7. Mgogoro kati ya Nunu na Jerry
8. Mgogoro kati ya Gaddi na rafiki yake
FANI
Muundo
Msanii ametumia muundo changamano, amechanganya muundo rejea na
moja kwa moja. Sura ya kwanza ametumia muundo wa rejea na kuanzia
sura ya pili na kuendelea ametumia muundo wa moja kwa moja mpaka
mwisho wa riwaya.
Mtindo
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 38
Msanii ametumia kwa kiasi kikubwa mtindo wa masimulizi na kiasi
kidogo mtindo wa dayalojia, nafsi zote tatu zimetumika. Vilevile kuna
matumizi ya barua (uk. 65).
Matumizi ya lugha
Lugha aliyotumia ni lugha rahisi iliyojaa misemo, methali, tamathali za
semi na mbinu nyingine za kisanaa.
Misemo/Nahau
Jibu lile lilimkata maini (uk. 36)
Methali
a Ukiyastaajabu ya Musa utayaona ya Firauni (uk. 27)
b Hakuna marefu yasiyo nan cha (uk. 117)
c Ni bora nusu shari kuliko shari kamili (uk. 127)
d Mkaidi hafaidi mpaka siku ya Iddi (uk. 135)
Tamathali za semi
Tashibiha
a Paa lake lililokuwa limejengwa kwa mithili yam domo wa
lile dege aina ya Concord (uk. 11)
b Gari iliruka mbele kama jiwe na kutimua vumbi (uk. 41)
c Kamfukuza kama mbwa kutoka kwenye nyumba ya
marehemu mumewe (uk. 60)
Mbinu nyingine za kisanaa
Tanakali sauti (Onomatopea)
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 39
a Vilitilia mkazo uharaka wa binti yule kwa kutoa sauti za Ko! Ko!
Ko! (uk. 1)
b Aaakh! Ni – niache! Uuuuuwwiiiii !! Yallaaaah (uk. 37)
Takriri
a Toka hapa ! Ondoka! Na usirudi tena! (uk. 32)
b Nimesema sitaki! Sitaki! Sitaki! (uk. 35)
c Sikubali! Sikubali! Nawaambia nitawashitaki kwa hili ! (uk. 43)
Mdokezo
a Oh! Mungu wangu, sasa itakuwaje jamani….(uk. 13)
b Ah! Ni kweli Anti….lakini…..(uk. 12)
Wahusika
Gaddi Bullah
1. Huyu ndiye mhusika mkuu wa riwaya hii. Huyu alikuwa meneja
wa kampuni
2. Kijana mchangamfu na mwenye huruma
3. Mkarimu na mchapakazi
4. Alikuwa na upendo wa dhati
5. Ni msamehefu na mwenye kuzitawala hasira zake
6. Mume wa kwanza wa Nyambuja na mpenzi wa Dania
7. Gaddi anafaa kuigwa na jamii kutokana na tabia na matendo yake
mazuri
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 40
Dania
1. Huyu ni mwanamke ambaye alizaliwa katika familia ya kitajiri
2. Ni mwenye hasira anapokuwa amechukizwa na mwenye chuki
3. Hana msimamo na hudanganyika kirahisi
4. Ni mfanyakazi mwenye nidhamu, bidii na ushirikiano
5. Alikuwa mlevi wa kutupwa baada ya kuachwa na Jerry
6. Dania ni mwanamke ambaye anafaa kuigwa kwa baadhi ya mambo
na hafai kuigwa kwa baadhi ya mambo
Bi. Hanuna
1. Huyu alikuwa dada wa Gaddi Bullah, alimpenda sana mdogo wake
kiasi cha kukataa kumsaliti
2. Alikuwa na chuki na mtu yeyote aliyemuudhi mdogo wake
3. Bi. Hanuna anafaa kuigwa na jamii kutokana na mapenzi
aliyokuwa nayo kwa mdogo wake
Jerry
1. Huyu alikuwa mpenzi wa Dania na alikuwa mtaalamu wa
kompyuta
2. Jerry alikuwa mcheshi, mtanashati na mwenye mvuto mkubwa
kwa akina dada
3. Jerry alikuwa katili na msaliti mkubwa kwani alimsaliti Dania
mara mbili
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 41
4. Jerry hakuwa na mapenzi ya kweli ndio maana alikuwa muongo na
laghai wa mapenzi
5. Jerry kutokana na tabia zake hafai kuigwa na jamii
Nunu
1. Huyu alikuwa rafiki wa Dania
2. Alikuwa na mapenzi ya kweli kwa watu na aliwasaidia sana watu,
maana aliwasaidia sana wakati wa shida. Hivyo, anafaa kuigwa na
jamii
Wahusika wengine wanaojitokeza katika riwaya hii ni Boaz, Mama
Mlole, Mary, Aisha, Agnes, Junior na wengineo.
Mandhari
Mandhari ya riwaya hii ni halisi, inatalii maeneo kama vile Arusha, Dar
es Salaam na Pemba. Katika sehemu hizo zote kuna mandhari ya ofisini,
nyumbani, baa, barabarani, hospitalini, n.k
Jina la kitabu
Kwa kiasi kikubwa jina la kitabu linasadifu yale yaliyomo katika kitabu.
Mfadhili ni mtu anayemdhamini mtu katika kugharimia kitu fulani.
Hivyo katika riwaya hii msanii anaonesha ufadhili wa aina mbalimbali
kama ifuatavyo:
Kwanza tunaona ufadhili wa Mama Mlole kwa Gaddi baada ya
kukumbwa na kashfa ofisini kwake asifukuzwe kazi. Mama Mlole ndiye
aliyemtetea Gaddi hata kumhamishia Dar es Salaam kwa uangalizi zaidi.
Pili, Mama Mlole alimfadhili Dania asifukuzwe kazi kutokana na kuwa
mlevi sugu baada ya kuachwa na mpenzi wake Jerry.
UHAKIKI WA VUTA N’KUVUTE & MFADHILI 2019
MWALIMU WA KISWAHILI 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.com Uk 42
Tatu, Mama Mlole alimfadhili Gaddi na Dania kwa kuwapatanisha
kutokana na uhasama baina yao ambao ungeathiri utendaji kazi.
Gaddi vilevile alimfadhili Dania baada ya kuachwa na Jerry hata kuwa
mlevi wa kupindukia. Pili, Gaddi alimfadhili Dania kwa kumpa ini lake
moja wakati anaumwa baada ya kusalitiwa mara ya pili na Jerry. Tatu,
Gaddi alimfadhili Junior kwa kumpeleka hospitali baada ya kuumia
mkono. Isingekuwa Gaddi pengine Junior angepata matatizo makubwa
zaidi.
KUFAULU NA KUTOFAULU KWA MWANDISHI
KUFAULU
1. Kimaudhui, msanii amefaulu kuonesha matatizo mbalimbali
yaliyoko katika jamii yetu hasa katika suala la mapenzi na ndoa na
kuonesha suluhisho la matatizo hayo.
2. Kifani, amefaulu kutumia lugha rahisi na inayoeleweka na ujenzi
mzuri wa wahusika wake.
KUTOFAULU
1. Kutumia viswahili badala ya Kiswahili sanifu (uk. 15-16)
2. Matumizi ya Kiingereza, kwa mtu asiyejua Kiingereza atashindwa
kupata ujumbe.