Upload
hoangnguyet
View
575
Download
8
Embed Size (px)
Citation preview
1
Programu kuhusu msaada wa sera kwa ajira vijijini na kazi yenye heshima kwa uhimizaji maisha sawa
endelevu vijijini kulingana na mabadiliko ya tabia nchi
Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) Tanzania
Kiongozi Cha Mwezeshaji
Jaap Van Pol na Francesca Dalla Valle
Kwa kushireikiana na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC) na Muungano wa
Vyama vya Ushirika Zanzibar (CUZA).
Kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika na Wizara ya Kazi
In collaboration with the Ministry of Agriculture, Food Security and Cooperatives and Ministry of Labour
2
Juzuu ya 1
Mtaala wa Mada za Kilimo za SDSMV
3
Yaliyomo
Mada/zoezi Ukurasa
Utangulizi wa ufundishaji
0.1. Zoezi: Kutambulishana na SDSMV
Mada za Kilimo
A.1.1. Zoezi: Kujua shamba la kujifunzia na kufanya majaribio
A.1.2. Zoezi: Sifa za shamba la Kilimo
A.1.3. Zoezi: Jaribio la Utepe
A.1.4. Zoezi: Kupanga shughuli zako za Kilimo
A.1.5. Zoezi: Hatua za maisha ya mazao
A.1.6. Zoezi: Kuandaa kalenda za mazao
A.2.1. Zoezi: Kuchagua mbegu bora
A.3.1. Zoezi: Jaribio la utoaji wa mbegu
A.4.1. Zoezi: Kuandaa mpangilio wa shamba darasa
A.4.2. Zoezi: Maandalizi ya Ardhi
A.4.3. Zoezi: Kwa nini tunahitaji vitalu
A.4.4. Zoezi: Kuandaa Kitalu
A.5.1. Zoezi: Kuacha nafasi baina ya mimea
A.6.2. Zoezi: Kuelewa mifumi ikolijoa ya shmamba
A.6.1. Zoezi: Kuotesha mazao yanayostawi kwa IPM
A.6.3. Zoezi: Desturi mbalimbali za kudhibiti visumbufu vya mimea
A.6.4. Zoezi: Kanuni za Kiasili za Kudhibiti visumbufu vy mimea
A.6.5. Zoezi: Kulinda mazao dhidi ya wadudu shambani shambani na taratibu za Udhibiti
Husishi wa Visumbufu vya Mimea (IPM)
A.6.6. Zoezi: Kupata maarifa zaidi kuhusu wadudu na visumbufu vya mimea
1
3
5
6
7
8
9
10
12
12
13
14
14
15
16
18
18
19
20
20
4
vilivyochunguzwa katika shamba darasa
A.6.7. Zoezi: Utayarishaji wa dawa kutoka mti wa mwarubaini kwa kudhibiti visumbufu
A.6.8. Zoezi: Kuepuka madhara ya dawa na Kemikali za Kilimo
A.7.1. Zoezi: Kutambulisha AESA.
A.7.2. Zoezi: Ufuatiliaji wa mara kwa mara kwa Kutumia AESA.
A.8.1. Zoezi: Palizi, Kwa nini, lini na namna ya kupalilia
A.9.1. Zoezi: Upandikizaji wa miche (mboga za majani)
A.10.1. Zoezi: Kuzitambua njia mbalimbali za umwagiliaji na unyevu kwenye udongo
A.11.1. Zoezi: Urutubishaji wa Udongo
A.11.2. Zoezi: Urutubishaji wa pili
A.11.3. Zoezi: Udhibiti wa Rutuba ya Ardhi katika Kilimo Kisichotumia Mbolea za Kemikali
A.11.4. Zoezi: Rundo la mboji ni nini na tunaweza kutumia vitu gani
A.11.5. Zoezi: Kutayarisha Mboji
A.11.6. Zoezi: Kuchagua, kugeuza na kutumia mboji
A.12.1. Zoezi: Kulinda Shamba letu
A.12.2. Zoezi: Kujenga uzio
A.13.1. Zoezi: Wakati na namna ya Kuvuna
A.14.1. Zoezi: Namna ya Kupunguza Hasara ya Mazao baada ya kuvuna
A.14.2. Zoezi: Usindikaji/Uhifadhi wa vyakula
A.14.3. Zoezi: Ghala/Stoo bora
A.14.4. Zoezi: Kuuza bidhaa/mazao yetu
Kiambatisho: Mtaala wa Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV)
21
21
22
23
25
27
27
29
30
31
31
32
32
34
35
35
36
36
37
38
39
41
5
Utangulizi wa Ufundishaji SDSMV
Ufundishaji wa SDSMV
Mwezeshaji anajaribu kutumia kwa ukamilifu kujifunza kwa (vijana) watu wazima kwa njia ya ugunduzi.
Vijana watajifunza kadiri iwezekanavyo kwa vitendo, kufanya mazoezi ya kanuni zote za kilimo kwenye
mashamba darasa yao, kugundua njia mbalimbali kwa kufanya majaribio, kuiga hali za maisha kwa njia
ya igizo kifani au mchezo wa kuigiza, majadiliano katika vikundi vidogo vidogo na michezo na mbinu za
kikundi.
Maana ya mwezeshaji
Mtu anayeongoza na kuelekeza mchakato. Mtu anayehakikisha mtiririko unaofaa wa taarifa
ndani ya kikundi ili washiriki washirikiane taarifa na kufikia uamuzi
Kiongozi/msimamizi wa mchakato wa kujifunza kwa mbinu shirikishi.
Anayesaidia katika kushirikiana taarifa kwa njia shirikishi
Kiwango chakukumbuka ni kama ifuatavyo
20% wakati wanaposikia
40% wakati wanapoona
80% wakati wanapogundua
Uzoefu unaonyesha kuwa
Unaposikia,unasahau
Unapoona, unakumbuka
Unapogundua unamiliki maishani
6
Jedwali: Tofauti kati ya kuwezesha na kufundisha
Kuwezesha Kufundisha
1. Kunahusisha majadiliano Majadiliano kidogo
2. Ushiriki kwa ukamilifu Ushiriki mdogo
3. Kunahimiza mawazo yaliyopo na mapya Hutambulisha mawazo mapya tu
4. Mawasiliano miongoni mwa washiriki Mawasiliano kutoka kwa mwalimu
5. Kujifunza kusiko rasmi Kujifunza rasmi
6. Utoaji uamuzi wa pamoja Utoaji uamuzi kiasi
7. Kushirikiana mawazo Kuelekeza
8. Kuanzia chini kwenda juu Huanzia juu kwenda chini
9. Mtaala umetayarishwa kutokana na tathmini ya mahitaji
Mtaala umetayarishwa na wizara
10. Vifaa vya kujifunza vinatokanana mshiriki Vifaa vya kujifunzia vinatokana na mwalimu
K azi na Wajibu wa Mwezeshaji wa SDSMV
Msaada mkubwa wa kiufundi
Huongoza katika mchakato wa kujifunza
Huwa kiungo cha mawasilianona watendaji wa nje na wataalamu
Husaidia kikundi kufikia malengo yao
Husaidia udhibiti wa migogoro
Husaidia kuanzishwa kwa SDSMV mpya.
Huelezamalengo na mchakato wa SDSMV
Lazima asaidie uchaguzi na uchanganuzi
Hufanya majadiliano yawe ya kusisimua
Hudadisi ili kuwasaidia washiriki kufikia mahitimisho yanayofaa
Husaidia kutanzua matukio ya kukandamiza mawazo na hisia za washiriki wengine.
Husaidia washiriki kufikia mwafaka unaofaa
Usimamizi wa muda
Huwaheshimu washiriki wote na mawazo yao
Huwasaidia washiriki kubainisha fursa na na uwezekano kwenye mazingira yao.
Somo la SDSMV (saa 3 – 4).
1. Kuanza /kufungua (± dakika 5)
2. Muhtasari wa somo lililopita (± dakika 5)
3. Programu ya leo (± dakika 5)
7
4. Uchunguzi wa mfumo wa kilimo na Ikolojia (AESA) au mada ya maisha (± saa 1 - 2)
5. Mapumziko (± dakika 5)
6. Vichangamsho au group dynamics (± dakika 10)
7. Mada mahususi (kilimo au mada ya maisha ) (± dakika 50)
8. Muhtasari (± dakika 5)
9. Tathmini (± dakika 5)
10. Kufunga (± dakika 5)
Mazoezi ya SDSMV
Mazoezimbalimbali ya SDSMV yaliyochaguliwa yamekusanywa na kuwasilishwa kwenye kiongozi hiki
kutokana na moduli za mwezeshaji wa SDSMV zilizotayarishwa na kuchapishwa na (ambazo
hazijachapishwa) FAO.
Mazoezi haya yamechaguliwa kutokana na mitaala ya SDSMV iliyotayarishwa wakati wa mafunzo ya
wawezeshaji wa SDSMV yaliyofanyika Kibaha Conference Centre, Tanzania, mwezi Juni, 2011, angalia
kiambatisho kwa ajili ya nakala za Mitaala ya SDSMV, mazoezi yamepangwa kulingana na mazoezi
yanayohusu kilimo (Juzuu ya 1) na; mazoezi ya stadi za kazi na kutengeneza ajira (Juzuu ya 2)
8
Mada ndogo: Utangulizi wa SDSMV
0.1. Zoezi: Kutambulishana na SDSMV
Muda: Karibu saa 2
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
1. Wakaribishe vijana wote na washiriki wengine waliohudhuria kwenye somo lakwanza la SDSMV
2. Jitambulishe pamoja na wawezeshaji wengine. Mwambie kila kijana ajitambulishe kwa kikundi (jina,
umri, mahali wanakotoka)
3. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vya watu watano au sita. Waambie vijana wajadili kile
wanachotarajia kujifunza na kufanya wakati wa SDSMV na waandike matarajio yao kwenye karatasi
kubwa . jadili kwa muhtasari matarajio waliyoorodhesha
4. Wasilisha mchezo wa “vidoti tisa”na waambie vikundi kama wanaweza kuunganisha vidoti vyote tisa
kwa kutumia mistari minne iliyonyooka bila ya kuondoakalamu. Vipatie vikundi dakika 10 kufanya
hivyo
5. Viulize vikundi vimefanya nini kutatua tatizo hili. Kamakikundi kimeweza kutatua tatizo, waambie
waeleze ufumbuzi. Kama hakuna aliyepata ufumbuzi, kwanza jadili kwanini hakuna aliyepata jibu na
halafu onyesha namna ya kufanya.
6. Waeleze vijana kuwa SDSMV itawasiaidia kwenda zaidi ya njia za kujifunza na kutafuta ufumbuzi
zinazotumika.
7. Tambulisha moduli mbalimbali za mtaala wa SDSMV na eleza aina tofauti za shughuli
wanazotarajiwa vijana wafanye wakati wa masomo ya SDSMV – kwa mfano, shughuli kwenye
shamba darasa, kujifunza kwa vitendo na majaribio, majadiliano na shughuli za vikundi vidogo,
mchezo wa kuigiza na igizo dhima.
9
8. Waulize vijana ni aina gani ya sheria na kanuni ambazo SDSMV wafuate kujenga mazingira yenye
mafanikio kwa vijana kufanya kazi na kujifunza pamoja. Orodhesha kwenye karatasi kubwa sheria
na kanuni zote walizotaja - kwa mfano, kuwahi, kushiriki kwaukamilifu, kuheshimu mawazo ya kila
mmoja, kumsikiliza kila mmoja, kuzungumza mmoja mmoja kwa zamu, kutopigana,
9. Ongeza kanuni na sheria zilizokosekana kwenye orodha.
10. Waulize vijana kama wako tayari kushiriki kwa ukamilifu katika masomo yote ya SDSMV, wako tayari
kufanya kazi katika vikundi vidogo, kujifunza kwa vitendo na kuheshimu orodha ya sheria na kanuni
za SDSMV zilizotayarishwa.
11. Toa muhtasari wa majadiliano.
Maelezo kwa wawezeshaji
Je, unatoka wapi?
Je, umekuwa unaishi katika eneo hili kila mara?
Je, unamfahamu kijana mwingine?
Je, una jamaana ndugu katika kikundi cha vijana wanaoshiriki?
Je, unasoma shule?
Wakati wa SDSMV unataka kujifunza nini?
Je, unapenda kujifunza zaidi kuhusu kilimo?
Je, ungetaka kujifunza zaidi kuhusu aina gani za mazao au wanyama?
Je, unataka kujifunza zaidi kuhusu afya, lishe au kuhusu uanzishaji wa biashara
ndogondogo?
Je, unapenda kujifunza kwa vitendo?
Je, umezoea kufanya kazi katika vikundi?
Je,kufanya kazi na kujifunza katika vikundi kuna maanagani?
Je,unadhani nini muhimu wakati unapotakiwa kufanya kazi katika kikundi?
Je, kuna majukumu ya aina gani unayotakiwakuyatimiza ili uweze kufanyakazi katika
kikundi kwa mafanikio na ipasavyo?
Je, ni kanuni na taratibu gani zinazotakiwa kuheshimiwa wakati wa kufanya kazi katika
kikundi?
10
Mada za Kilimo
1. Mada ndogo: Kupanga katika kilimo
Malengo:
Kuelewa namna ya kuchagua mazaobora zaidi ya kupanda.
Kuelewa namna ya kuanza kupanga shughuli za kilimo
Wakati vijana wanapopanga shamba lao, ni lazima wafikirie kuhusu mambo mbalimbali kwa wakati
mmoja. Je, wanataka kuzalisha nini, aina ya ardhi na udongo waliyonayo, aina ya mbegu na zana zilizopo
kwa ajili yao, watakuwa namuda kiasi gani (na lini ) wa kuhudumia shamba lao, ni watu wengine gani
watakaowasaidia shambani, n.k.
A. 1.1. Zoezi. Kujua shamba la kujifunza na kufanya majaribio.
Mada: Karibu saa 2
Vifaa: karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Mahali muhimu katika mafunzoya SDSMV ni eneo la uwandani la kujifunza. Kwa kuwa kanuni muhimu
ya SDSMV ni kujifunza kwa kufanya majaribio, mahali pa kujifunza ni pale ambapo washiriki watajifunza
taratibu na stadi za usimamizi wa kilimo. Washiriki watagundua wenyewe njia bora zaidi ya kulima aina
fulani ya mazao na kupambana na matatizoya mmomonyoko wa udongo au masuala mengine ya kilimo.
Katika zoezi hili, vijana watatambulishwa malengo na shughuli za aina mbalimbali watakazofanya katika
shamba darasa.
1. Anzisha mada ya shamba darasa. Waulize vijana kwanini SDSMV ina eneo la uwandani la
kujifunzia na wanafikiri watafanya nini katika eneo la uwandani la kujifunzia wakati wavipindi
vya SDSMV
2. Eleza kuwa shamba darasa litatumika kujifunza kuhusu taratibu bora na stadi za usimamizi wa
kilimo kwa kufanya mazoezi kwa vitendo. Hakikisha kuwa wanaelewa uzalishaji wa kilimo si
lengo kuu.
3. Waulize vijana kama wanaruhusiwa kufanya makosa katika shamba darasa yanayoweza kuathiri
uzalishaji. Waeleze kuwa wanaruhusiwa kufanya makosa wakati wa kujifunza kwa kuwa
kujifunza kunatokana na makosa na kuyaelewa ni njia bora ya kuwaongezea maarifa alimradi
makosa hayo hayafanywi makusudi.
4. Nenda na vijana kwenye shamba darasa. Waulize wanapenda kupanda mazao gani na kwanini.
11
5. Eleza kuwa kwanza wanahitaji kuandaa mpango kuonyesha wanaopenda kupanda nini, wapi,
lakini kwanamna gani katika shamba darasa na kuwa mpango ujumuishe majaribio madogo na
mbinu mbalimbali zakilimo
6. Waulize washiriki kwa nini wanatakiwa kuingiza majaribio katika mpango
7. Eleza kuwa kuna njia nyingi za kulima mazao kulingana na hali ya shamba na ujuzi wa mkulima,
kila mkulima anatakiwa kufuata njia bora zaidi ya kulima kulingana na hali yake. Njia bora zaidi
kutekeleza hili ni kwakujaribu njia mbalimbali za katika maeneo madogo ya ardhi
8. Eleza kuwa katika wiki zijazo wataanza kupanga shughuli mbalimbali watakazotaka kufanya
katika shamba darasa kwa kufanya mazoezi kadhaa.
A.1.2. Zoezi : Sifa za shamba la Kilimo
Muda: Karibu dakika 20
Vifaa : Shamba darasa, karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Anzisha mada ya uchunguzi wa hali ya shambani. Waulize vijana kwanini wanafikiri ni muhimu
kuchunguza hali ya shamba kabla ya kupanga mazao watakayopanda
Waambie vijana wataje sifa zote muhimu za shamba la kilimo, ambazo mkulima anatakiwa kuzijua
anapoanza kulima. Orodhesha sifa zote zilizotajwa kwenye karatasi kubwa. Iwapo unafikiri kuwa kuna
kitu walichokisahau, kitaje na kujadili na vijana
Sifa muhimu za shamba lakilimo
Aina ya udongo (umbile: mwepesi – mzito, muundo: ulioshikamana - kichanga , mbolea: nyingi
– kidogo)
Kina chaudongo (kina kirefu cha kutosha kuwezesha ukuaji wa mizizi)
Mteremko wa ardhi (hatari ya mmomonyoko, maji hutiririka, haufai kulima kwa kutumia
mashine)
Hali ya mtiririko wa maji (mabonde shambani, sehemu iliyo chini zaidi shambani)
Kuwapo kwa vyanzo vya maji (kama kuna haja ya kumwagilia)
12
Mimea (je, kunamimea mingi? je, kunamajani?)
Historia (kujua kilicholimwa katika shamba hilo siku za nyuma kunatoa habari kuhusu hali ya
shamba)
Mambo gani yanayofanyika katika mashamba jirani (nyasi, wadudunamagonjwa,mara nyingi
huingia kutoka katika mashamba jirani)
Toa muhtasari wa orodha ya “sifa muhimu kwa ajili ya shamba darasa” na waombe vijana wanakili
orodha kwenye daftari zao.
A.1.3. Kuchunguza Hali ya Udongo
Majaribio rahisi yanayoweza kufanywa pamoja na vijana yametayarishwa kwa ajili ya kutambua umbile
la udongo, muundo nahali ya aina mbalimbali ya udongo
Muda: Saa 1 dakika 30
Vifaa na matayarisho: karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
1. Anzisha mada ya kuchunguza hali ya udongo (umbile, muundo na aina za udongo na sifa zake)
2. Nenda na vijana kwenye shamba darasa halafu waulizevijanahao maana yaumbile namuundo
wa udongo. Eleza maana ya rangi ya udongo, muundo wa udongona umbile la udongo
3. Chukua sampuli za udongo kutoka kwenye shamba darasa halafu waambie vijana waeleze rangi
ya udongo na tunavyoweza kutambua umbile la sampuli ya udongo.
4. Waonyeshe vijana namna ya kutambua umbile la udongo kwa kutumia ribbon test (angalia hapo
chini)
5. Waambie vijana wakusanye viganja vya udongo na warudie ribbon test
6. Toa muhtasariwa matokeo ya uchunguzi waliofanya kuhusu udongo na jadili matokeo yahaliya
udongo uliyochunguzwa kwa ukuaji wa mazao
7. Toa muhtasari na hitimisha somo
13
Je, rangi ya udongo ina maana ganikwetu?
Rangi nyeusi – Udongo mweusi wa tabakala juu la ardhi, unaonyesha kiwango kikubwa cha mbolea,
ikiwa na maana kwamba maji yanapenye kwa urahisi sana, virutubisho vingi na udongo wenye muundo
mzuri.
Rangi nyekundu - kahawia na rangi ya chungwa – maji hutiririka na kupenye vizuri , mzunguko mzuri wa
hewana maji. Kwa kuwa na maji ya kutosha ina maana rutuba pia ni ya kutosha. Hata hivyo tindikali
(acidity) inaweza kuwa tatizo.
Rangi ya manjano na buluu isiyokoza – una matatizo la utiririshaji maji katika baadhi ya misimu
(kufurika maji ) ambapo hewa hukosekana katika udongo, hasa wakati wa mvua.
Rangi ya kijivu - huwa haupitishi maji vizuri, maji mengi na hakuna hewa ya kutosha.
Chanzo: ABSA 1997
Jaribio la utoaji wa mbegu
Vifaa
Chupa ya maji
Udongo kutoka tabaka na aina mbalimbali
Uso laini wa kitu kigumu kamavile plywood au metali au kipande cha kadibodi
Namna ya Kufunga (chanzo: FAO 2000b)
Udongo lazima uwe na unyevunyevu ili kutambua umbile lake kwa kuugusa. Ongeza maji kidogo kidogo
mpaka udongo uwe laini. Pitisha udongo kati ya kidole gumba na kidole cha shahada. Vunja
chembechembe ngumu na ondoa mawe au mizizi yoyote itakayokuwemo. Utaweza kupata sifa ya
“mguso” wa udongo: wenye chembechembe za mchanga huachana, wamfinyanzi hunata, udongo wa
kitope/mchanga tope ni laini sana. Sokota vidole kati ya vidole gumba na na kidole cha shahada
kutengeneza “utepe”. Kadiri “utepe” unavyokuwa mrefu ndivyo unavyoonyesha kuwa sampuli hiyo ina
udongo mwingi wa mfinyanzi. Udongo wenye mchanga mwingi utaachana, udongo wenye udongo
mwingi wa mfinyanzi unaweza kusokotwa kutengeneza utepe mzuri wenye urefu wa zaidi ya sentimita
5. Udongo wa kitope/mchangatope ni laini sana. Udongo tifutifu ni laini japo unanata na unahali ya
14
kichanga kidogo. Mwishowe baada ya kufanya mazoezi zaidi nitaweza kutathmini kwa usahihi aina ya
udongo kwa kutumia mbinu hii.
1. Kama udongo una chembechembe za mchanga huwa unaachana (yaani haushikamani).
Umbile la udongo ni ………………………………………… mwepesi sana (mchanga mchanga)
2. Viringa udongo wa unyevunyevu kuwa gololi au mpira mdogo halafu bonyeza mpira huo
kwakidole gumba na kuunda umbo la kikombe. Kama udongo huo hauwezi kuviringwa au kama
kikombe kinamong’onyoka , umbile la udongo ni ……………………………………. Mwepesi sana
Kama mpira hauwezi kuviringwa lakini kikombe kinabaki na sura yake, endelea hatua ya 3.
3. Viringa bonge au mpira wa udongo kati ya viganja vyako, halafu kwenye kitu kigumu ili kuunda
utepe mnene kama penseli wenye urefu wa shadi entimeta 20 – 25. Kama
hakunautepeuliotengenezwa au ulikuwa mfupi zaidi, umbile la udongo ni ………………….mwepesi
(mchanga tifutifu)
Kama utepe mrefu haukutengenezwa endeleahatua ya 4
4. Finyanga udongo kutengeneza utepe wa duara. Kama mduara huo utakuwa na nyufa umbile la
udongo ni …………………………. Wastani (mfinyanzi mwepesi)
Kama umefinyangwa mduara bila nyufa,na udongo unanata sana,umbile la udongo ni
……………………….. mzito (mfinyanzi mzito).
A.1.4. Zoezi: Kupanga shughuli za kilimo
Muda: Karibu saa 2
Vifaa: Karatasi ya chatipindu na kalamu ya kuchorea.
Mkiwa shambani, waulize vijana maswali yafuatayo na orodhesha majibuyao kwenye chatipindu:
Shamba darasa letu lina ukubwa gani?
Wakati gani unafaa zaidi kulima mazao kwa kuangalia hali ya hewa na masoko?
Ni mbinu za kilimo za aina gani zinazoweza kutumika kupanda mazao?
Je, tutapanda namna gani mazao manne yaliyochaguliwa kwa shamba darasa? (moja kwa
moja au kwanza kitalu na baadaye kupandikiza miche?)
15
Waambie vijana katika vikundi vidogo vinne, kila kikundi kipatie mojawapo ya mazao manne
yaliyochaguliwa na waambie watayarishe mpango utakaoonyesha mawazo ya hatua kwa hatua
wanachopaswa kufanya ili kuzalisha zaohilo kwenye shamba darasa.
Warejeshe washiriki pamoja na wape fursa wawasilishe mipango yao. Hitimisha somo kwa kuuliza
maswali yafuatayo:
Je,ilikuwa rahisi au vigumu kupanga mipango katika kikundi?
Hatua gani za msingi tunahitaji kuzifuata ili kupanga mipango?
Je, kupanga mipango ni wazo linalofaa? Kwa nini ndiyo na kwa nini hapana?
A.1.5. Zoezi: Hatua za maisha ya mazao
Muda: Saa 1 dakika 30
Vifaa na matayarisho: Karatasi ya chatipindu, kalamu za kuchorea na mifano ya mimea
(mazao katika hatua mbalimbali iliyokusanywa na mwezeshaji kabla ya somo)
1. Waeleze washiriki mimea,kama kilivyo kiumbe kingine chochote kinachoishi, hupitia hatua
mbalimbali
2. Waulize vijana wanafikiri zao moja linapitia hatua zipi mbalimbali za ukuaji,kwa mfano mahindi,
ambayo wangependa kupanda kwenye shamba darasa?
3. Duria hatua ya 2 kwa zao moja au mawili ambayo vijana wangependa kuyapanda kwenye
shamba darasa
4. Eleza hatua nne tofauti zinazotumika zaidi katika vitabu: hatua ya awali, hatua ya ukuaji wa
mazao, hatua ya katikati ya msimu na hatua ya mwisho wa msimu. Fafanua hatua hizo
mbalimbali na waonyeshe washiriki mifano ya hatua mbalimbali.
5. Waombe vijana wataje mahitaji ya mimea/mazaoili yaweze kukua kwa afya. Yaorodheshe
kwenye karatasi kubwa na ikibidi ongeza vitu vilivyokosekana.
6. Jadiliana na vijana kuhusu mahitaji yaliyotajwa kwa kila mmea/zao moja hadi jingine
7. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vidogo na waombe kila kikundi wachague zao moja na
kujadili katika kikundi jinsi mahitaji mbalimbali ya mazao yanavyotofautiana kutoka hatua moja
ya zao hadi nyingine.Waambie kilakikundi waandike maelezo kwenye karatasi.
16
8. Waambie kila kikundi wawasilishe matokeo ya majadiliano yao
9. Toa muhtasari wa majadiliano.
Maelezo kwa Mwezeshaji: Tumia maswali yafuatayo ya mwongozo
Je, kuna hatua ambayo zao linahitaji maji kidogo?
Je, kuna hatua ambayo zao haliwezi kustawi kwa maji kidogo?
Je, kuna hatua za mazao ambapo mazao yanahitaji kuchukuliwa hatua maalumu za
kuyalinda?
Je, mahitaji ya mbolea yanatofautiana kutoka hatua moja ya zao hadi nyingine?
Usuli:
Kwa kawaida kipindi cha ukuaji wa mazao kimegawanyika katika hatua 4 za ukuaji (tazama mchoro hapa
chini)
1. Hatua ya awali: hiki ni kipindi kuanzia wakati wakusia mbegu au kupandikiza, hadi mazao
yanapofunika karibu asilimia 10 ya ardhi
2. Hatua ya ukuaji wa mazao: hiki ni kipindi cha kuanzia mwishoni mwa hatua ya awali
nakuendelea hadi itakapofikia kufunika ardhi yote (ardhi inaweza kufunikwa 70-80%)
3. Hatua ya katikati ya msimu: kipindi hiki kinaanza mwishoni mwa hatua ya ukuaji wa mazao
nakuendelea hadi kukomaa, kinajumuisha kutoa maua na kutoa punje
4. Hatua ya mwisho wa msimu: kipindi hiki kinaanza mwishoni mwa hatua ya katikati ya msimu
na kuendelea hadi siku ya mwisho ya kuvuna; kinajumuisha kuvuna.
17
Crop
needs\stages
Initial stage Crop development Mid-season Late season
Water ++ ++ +++ +
Fertilizer ++ +++ +++ -
Protection* ++++ +++ ++ +
18
A.1.6. Zoezi: Kuandaa Kalenda za Mazao
Muda: Karibu saa 2
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Mwambie kijana ajitolee kueleza awamu mbalimbali za mzunguko wa maisha ya mimea.
Chagua mojawapo ya mazao yaliyochaguliwa kwa ajili ya SDSMV (kwa mfano nyanya)
namwambie kijana aeleze mzunguko wa maisha wa zao hili, hasa katika miezi ipi zao hili
linalimwa, kupandwa na kuvunwa
Onyesha kalenda tupu ya mazao kama hii iliyo hapa chini
Nyanya
Mwezi Shughuli za Kilimo Pembejeo/Vifaa gani
vinahitajika
Januari
Februari
Machi
Aprili
Mei
Wagawe vijana katika vikundi vinne na kiambie kila kikundi kikamilishe kalenda ya mazao kwa zao
walilopewa kushughulikia (nyanya, bamia,(ladies sugar), tango, boga)
Wahimize washiriki kujaza jedwali kwa kutumia maswali kama vile:-
“Zao hili tunalipanda lini?”
“Zaohili tunalivuna lini?”
“Shughuli gani za kilimo zinafanyika katika kila awamu/hatua?”
19
Wakusanye vikundi wote pamoja na waambie wawasilishe kazi yao ya kikundi. Hakikisha kuwa
wamejumuisha shughuli muhimu zaidi (matayarisho ya shamba, utiaji mbolea wa kwanza, kupalilia,
umwagiliaji maji, kupandikiza miche (nyanya), kupalilia mara ya pili, top dressing, IPM, kuvuna, baada ya
kuvuna) na pembejeo/vifaa (mbegu (mboji) mbole, dawa za kuulia wadudu, wa mimea, zana za kilimo
na kupalilia)
A.2. Mada Ndogo: Uchaguzi wa mazao na mbegu
Lengo:
1. Kuelewa umuhimu wa kuchagua mbegu bora
Wakati wa SDSMV vijana watapanda aina nne za mazao (nyanya, tango, bamia na boga (boga)) ambayo
hulimwana wakulimakatika kipindi hicho cha mwaka. Ni muhimu kwa kila zao kutumia mbegu bora. Ni
muhimu kuelewa pia kwa nini tunapanda mboga na sifa za mbegu bora ni zipi
A.2.1. Zoezi: Kuchagua mbegu bora
Muda: Saa moja na dakika 30
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
1. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vidogo na waulize nini wanadhani nisifa za mbegu bora na
waorodheshe sifa hizo kwenye karatasi kubwa
2. Waambie kila kikundi kiwasilishe orodha yao
20
3. Jadili orodha zilizowasilishwa na hitimisha zile sifa muhimu zaidi za mbegu bora (hutoa mazao
mengi, hufaa zaidi kwamazingira na hali ya mahali (hali ya hewa), safi hazina virusi, n.k.)
4. Jadiliana na vijana kuhusu mahali watakapopata mbegu bora.
A.3. Muda Mdogo: Kuelewa “uwezo wa kutoa” wa mbegu
Lengo: kuelewa namna mbegu zinavyoota
Vijana wanahitaji kujifunza kuwa mbegu zitakuwa tu kama kiini kina afya, wakati kinapokuwa na viini
lishe vya kutosha na wakati kunapokuwa na maji na hewa ya oksijeni ya kutosha.
A.3.1. Zoezi: Jaribio la uotaji wa mbegu
Muda: Nusu siku nakaribu wiki moja ya ufuatiliji
Vifaa: Karatasi laini (au njia nyingine mbadala kama vile majani au magomeya miti); mbegu
zamazaombalimbali ya chakula/miti (mbegu za kutosha kwa kila kikundi cha vijana )
mifuko ya plastiki na maji safi
1. Wagawe vijana katika vikundi na waambie kila kikundi wahesabu mbegu 100 kutoka aina
mbalimbali zambegu.
2. Waambie waandae matabaka mawili ya karatasi laini na kunyunyiza maji safi kwa makini hadi
ziwe na unyevu zisilowe
3. Waambie vijana waweke mbegu 100 juu ya karatasi laini katika safu 10 zenye mbegu 10 (umbali
kati ya mbegu na mbegu iwe karibu sm 2)
4. Waambie vijana wafunike mbegu na tabaka jingine la karatasi laini, nyunyuzia maji kwenye
karatasi laini na zungushia karatasi laini lenye mbegu kwenye aina nyingine ya karatasi.
5. Waambie vijana waweke karatasi hiyo kwenye mfuko wa plastiki ili kutunza unyevu wa karatasi
yenye mbegu (mbegu nyingi humea vizuri zaidi katika sehemu yenye giza, hivyo mfuko wa
plastiki mweusi ni bora zaidi kutumiwa)
6. Waambie vijana waandike jina la kikundi kwenye mfuko, herufi ya bechi ya mbegu zilizomo
ndani yake, na tarehe mbegu ziliposiwa.
7. Hakikisha kuwa unahifadhi mahali penye giza.
21
Kutegemea na zao, mchakato wa uotaji unaweza kuonekana baada ya siku 1, 2 au zaidi. Andika idadi ya
mbegu zilizokwisha ota kwa kipindi hiki cha kwanza cha kuchunguza.
Mara baada ya kuangalia na kuandika idadi (na kuondoa mbegu zilizoota ) zungushia tena karatasi laini
na rudisha kwenye mfuko wa plastiki kwa ajili ya uchunguzi mwingine wa kila siku
Wakati vijana wanapochunguza na kufuatilia mbegu waulize maswali yafuatayo:
Imechukua muda gani kwa mbegukumea?
Mbegu ngapi zimemea? Je, idadi ilikuwa ndogo au kubwa?
Kwa nini ni muhimu kujua uwezo wa mbegu kumea?
A.4. Mada Ndogo: Kuandaa shamba darasa
Baada ya kuandaa mpango wa kuhusu kile watakacholima vijana kwenye shamba darasa lao itakubidi
kuanza kuandaa shamba kwa ajili ya kilimo chenyewe
A.4.1. Zoezi: Kuanda mpangilio wa shamba darasa.
Vijana hawana budi kwanza kuamua kuhusu mpangilio wa shamba darasa ili kuelewa mahali pa kupanda
na aina ya mazao
Mada: Karibu saa 1
Vifaa : Chatipindu na kalamu za kuchorea
1. Nenda na vijana katika shamba darasa na waambie wakumbuke sifa zote za shamba darasa
ambazo ni muhimu kwa kuandaa mpangilio wa shamba (mteremko, tofauti za rutuba ya udongo,
njia ya kuingilia shamba, chanzocha maji n.k)
2. Waambie wanafunzi wabainishe maeneo mbalimbali ya shamba, mahali pa kitalu na njia
zitakazojumuishwa kwenye mpangiliohuo
Zingatia kwamba kila zao litapandwa kwenye eneo moja litakalolimwa kulingana na kanuni
za IPM na wenyeji wanavyolima, ili mwishoni kuweza kuchunguza athari ya IPM.
22
3. Waambie vijana kwenye vikundi vyao vidogo waandae mipangilio ya shamba darasa zikiwemo
sehemu zote, kitalu na njia. Waambie wazingatie mahali pa kupitishia maji na umwagiliaji
shamba na mwelekeo wa matuta ya vitalu na safu/mistari
4. Waambie vikundi wawasilishe mipangilio yao na kuamua kuhusu mpangilio wa mwisho
watakaotumia.
A.4.2. Zoezi: Maandalizi ya Ardhi
Kabla ya kupanda mbegu, ardhi haina budi kuandaliwa kwanza
Muda: Karibu saa 1
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Bungua bongo na vijana kuhusu kinachotakiwa kufanywa shambani kabla ya kuanza upandaji wa mbegu
(kusafisha ardhi, kuondoa mabaki yote ya mimea, kusawazisha ardhi inapohitajiwa, kutumia mboji,
kutifua na kuandaa vitalu vya mbegu).
Jadili shughuli zote zilizotajwa, kwa nini lazima zifanywe na zifanywe namna gani. Panga shughuli
mbalimbali kwa mfuatano unaofaa.
Tayarisha mpango na vijana kuhusu lini kifanyike nini. Njia bora zaidi ya kueleza namna ya kufanya
shughuli mbalimbali ni kwa kufanya kwa vitendo shughuli hizo na vijana. Kazi kubwa (kusafisha shamba
na kulima na kutifua) lazima ifanywe na watu wazima.
Mada Ndogo: Kuandaa kitalu na kupandikiza.
Malengo:
Kuelewa umuhimu wa vitalu
Kujua namna ya kuandaa kitalu
Kujua namna ya kupandikiza miche
23
Mazao mengi ambayo tunataka kuyapanda shambani, yanahitaji kupandwa kwenye vitalu kwanza, na
kisha kuhamishiwa shambani baada ya wiki chache. Ni muhimu kwa washiriki kuelewa jinsi ya kuandaa
kitalu, kupanda mbegu, kutunza miche na jinsi ya kuhamisha miche kwenda shamba darasa kwa wakati
mwafaka. Hapa kuna baadhi ya mazoezi ya mfano ambayo unaweza kuhitaji kuyatumia.
A.4.3. Zoezi: Kwanini tunahitaji vitalu?
Muda: Karibu saa moja na dakika 30
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Waulize vijana maswali yafuatayo na andika majibu yao kwenye chatipindu
Kwa nini wakulima mara nyingi hupanda mazao ya mbogamboga kwenye vitalu kwanza na
baadaye kwenye shamba?
Kutokana na majibu yako, unatakiwa kuandaa vipina wapi kitalu chako?
Kisha wapeleke vijana mahali ambako umeamua kuandaa kitalu
Waulize vijana maswali yafuatayo:
Je, mbegu zilizosiwa kwenye kitalu zinahitaji kukingwa kutokana na vitu gani mbalimbali?
Je, tutawezaje kutoa kinga inayotakiwa?
Je, tunahitaji kutunza miche namna gani?
Je, tutaandaa vipi vitalu ili visaidiae kukinga na kutunza vizuri miche?
A.4.4. Zoezi: Kuandaa kitalu
Muda: Karibu saa 2
Vifaa: Hakuna.
Sasa vijana wataandaa kitalu kwa vitendo. Wapitishe katika hatua zifuatazo kwa kuzingatia kuwa kila
mmoja anashiriki kwenye kazi hiyo. Kulingana na idadi ya vitalu mnavyoandaa, unawezakuwagawa
washiriki katika vikundi vidogovidogo zaidi.
24
Sehemu ya 1.10
1. Tafuta udongo kwenye……., vunja mabonge ya udongo naondoa mabaki ya mizizi na mashina ya
majani
2. Tifua udongo na pandisha udongo toka pande zote ili kitalu kiwe kimeinuka na kuachaaaaa njia
pande zote ili kuruhusu kupalilia bila kukanyaga juu yake. (upana wa mita ± 1)
3. Ongeza mbolea ya samadi/mboji na mchanga wa mtoni, changa vizuri. Mchanga unaweza
kusaidia kulainisha udongo ili kuwe na mtiririko mzuri wa maji na kung’oa mizizi ya miche kwa
urahisi.
4. Sawazisha kitalu na ikibidi weka mipaka. Pasua mipaka kwa kutumia kijiti.
5. Sia mbegu (zilizowekwa dawa ya kukinga ikibidi) kwenye mistari kwa kina kilichopendekezwa.
Acha nafasi ya kutosha kwa ajili ya ukuaji wa miche.
6. Funika mistari hiyo kwa udongo kidogo usiozidi mara 2-3 ya unene wa mbegu
7. Kama kuna tatizo la mchwa na konokono, tawanya majivu kwenye kitalu chote.
8. Tandaza majani, nyasi, mabua ya mpunga, mbolea ya samadi/mboji nakiasi fulani cha tabia za
msituni kuzuia mbegu za udongo usisombwe na mvua kubwa nakuzuia magugu na kutunza
unyegu wa udongo wakati wote
9. Ikibidi, jengea vivuli, kama paa dogo
Sehemu ya 1.02. Mpangilio wa vitalu kupanga mbegu kujenga kivuli
25
MAMBO MUHIMU – Kabla ya kuandaa kitalu
Chagua mahali pazuri: Mahali panapofaa patakuwa sehemu ya karibu na shamba darasa (ili
kitalu kitembelewe mara kwa mara nakutunzwa vizuri) yenye ardhi nzuri na yenye
rutuba,karibu nachanzo cha maji kinachoaminika na ambapo maji hayatuami au kukusanyika.
Epuka kuweka kitalu mahali ambapo mimea iliyopoya jamii moja na ile unayosia ina tatizo la
wadudu waharibifu na magonjwa
Safisha eneo: Ondoa visiki, mizizi na mawe katika eneo hilo. Majani na mabakimengine ya vitu
visivyokuwa vya miti, yanaweza kutengenishwa na kufanywa mbolea ya mboji.
Mpangilio wa vitalu: Ulalo, kamainawezekana vielekee (jua) mashariki kwenda magharibi,
upana wa mita moja na nafasi kati ya kitalu na kitalu iwe nusu mita.
A.5. Mada ndogo: Kupanda: Kuelewa umuhimu wa kuacha nafasi baina ya mimea
Malengo:
Kuelewa umuhimu wa kuacha nafasi baina ya mimea
Kuelewa umuhimu wa uzazi wa mpango
Ili kuotesha mazao yaliyostawi vizuri, kila mmea unahitaji kuwa nanafasi ya kutosha. Kuipa mimea nafasi
ya kutosha ni sawa na kuupa kila mmea viini lishe na maji ya kutosha kutoka kwenye udongo
uliyozunguka. Inakuwa rahisi vilevile kuondoa magugu na kupunguza mimea wakati utakapowadia.
Wakati huo huo mkulima huwa anapenda kupanda mimea mingi kadiri iwezekanavyo. Ni muhimu
kuelewa namna ya kupata “mavuno” mengi wakati huo huo kuhakikisha kuwa mazao yamestawi vizuri.
Kuacha nafasibaina ya mimeani muhimu sana katika kuamua ni mazao gani ya kupanda na wakati gani
wa kupanda mazao hayo.
A.5.1. Zoezi: Kuacha nafasi baina ya mimea.
Muda: Karibu saa 1 na dakika 30
Vifaa: Karatasi ya chatipindu na kalamu za kuchorea, tepu ya kupimia
Andaa ziara ya kwendakwenye shambalenye mazao yaliyo komaa ili kila mtu aweze kuona nafasi baina
ya mimea mbalimbali shambani hapo.
26
Wakati unapowasili shambani, waambie vijana waangalie nafasi kati ya mimeana wajaribu kufikiria jinsi
ilivyopandwa (kwenye msatari, kwenye kitalu,bila mpangilio maalumu). Vijana mbalimbali wapime
nafasi baina ya mimea ya mazao ya aina mbalimbali (nafasi baina ya mstari na baina ya kila mmea).
Waambie waandike mambo waliyoona kwenye jedwali , wapange kulingana na mazao ya aina
mbalimbali shambani.
Waulize vijana maswali yafuatayo:-
Je, wingi wa mazao una maana gani?
Kwa nini ni muhimu kufuata nafasi fulani baina ya mimea au mbegu wakati wa kupanda
mazao?
Kuna faida au hasara gani kupanda mbegu kwenye mstari au bila mpangilio maalumu?
Unafikiri kutatokea nini kwenye mimea kama itapandwa karibu karibu?
Waeleze kwamba kupata “wingi” mzuri wa mimea, ni muhimu kupanda mbegu nyingi wakati wa msimu
wa kupanda ili kuepuka baadhi ya mimea kutoota au mingine inaweza kufa ikiwa michanga kutokana na
wadudu waharibifu au maginjwa.
A.6. Mada Ngogo: Kupanda Mazao Yenye Afya
Kupitia Kanuni za Udhibiti Husishi wa Wadudu Waharibifu (IPM) – Utangulizi.
Malengo:
Kuelewa Kanuni Kuu za Udhibiti Husishi wa Wadudu Waharibifu wa Mimea
Kuelewa maana ya mfumo wa kiikolojia
Kuelewa umuhimu wa usafi na afya, mazingira shambani kama njia ya kukinga wqadudu
waharibifu na maginjwa ya mimea
Kupanda mazao yanayostawi ni ufunguo wa kilimo bora. Mazao yaliyostawi ni imara zaidi na
yanawezakujilinda vizuri zaidi dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa. Njia mbalimbali ambazo
tunatumia katika mashamba yetu zinaleta athari kwa ustawi wa mazao na zinaweza kutumika pia
kudhibiti matatizo yoyote ya wadudu waharibifu.
Kulima mazao yenye afya na yanayostawi ni kanuni ya kwanza ya Udhibiti Husishi wa Visumbufu vya
Mimea (IPM). IPM inahusu wadudu waharibifu lakini ni zaidi ya udhibiti wa wadudu waharibifu. IPM si
27
kuhusu kuwaangamiza wadudu wote waharibifu. Baadhi ya wadudu waharibifu huhitajika kwa ajili ya
kuwaondoa maadui shambani. IPM inahusu kuwapunguza wale wadudu waharibifu ambao husababisha
uharibifu wa mazao na kuleta hasara.
Mara nyingi IPM inaweza kulenga matumizi madogo ya dawa za kuulia wadudu waharibifu kadiri
iwezekanavyo. Lakini msingi wa maamuzi ya udhibiti mzuri wa mazao ni kuelewa kwa ukamilifu mfumo
wa ikolojia ya mazao, pamoja na yale ya wadudu waharibifu, maadui wao wa asili na mazingira ya
mahali. Ufuatiliaji wa mazao ni hatua ya kwanza katika kuelewa mfumo wa ikolojia.
Ifuatayo ni baadhi ya mifumo ya shughuli unayoweza kutumia kuanza kuwafundisha vijana Mada
Maalumu ya Kilimo: Udhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mimea.
A.6.1. Zoezi: Kupanda mazao yanayostawi kwa kutumia IPM
Muda: Saa 1 na dakika 30
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Hatua:
1. Taja kanuni nne za Vdhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mimea:
Kupanda mazao yanayostawi
Kuelewa na kuhifadhi wadudu wanaolinda
Kutembelea shamba mara kwa mara
Kuwa mtaalamu katika kusimamia mazao yako
2. Waulize vijana wanafikiri kila moja ya kanuni hizo ina maana gani.
3. Wagawe vijana katika vikundi na waambie kila kikundi waandike taratibu mbalimbali za
usimamizi wa mazao ambazo wanafikiri zinaleta athari katika ustawi wa mazao
4. Mwambie mwakilishi mmoja kutoka katika kila kikundi awasilishe matokeo yao darasani.
28
A.6.2. Zoezi: Kuelewa mifumo ya ikolojia ya shamba
Ili kukinga mazao dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa, vijana kwanza wanahitaji kuelewa “mfumo
wa ikolojia” wa shamba darasa. Mfumo waikolojia ni mimea, wanyama na viumbe wadogo wote katika
eneo fulani na namna wanavyoishi na kushirikiana na kutegemeana. Vijana watachunguza mfumo wa
ikolojia wa shamba na nafasi ya wadudu wa asili katika kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa ya
mimea.
Mada: Saa 1 dakika 30
Vifaa na matayarisho: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea, mifuko ya plastiki, alkoholi na gundi.
Hatua:
1. Anzisha mada ya kukinga mazao dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa
2. Waambie vijana wataje kanuni nne za IPM na kujadili kanuni hizo nne kuhusiana na kulinda
mazao dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa ya mimea.
3. Waulize vijana wanafikiri “mfumo wa ikolojia” una maana gani.
4. Nenda na vijana kwenye shamba darasa na wagawe katika vikundi vidogo vidogo na waambie
vikundi wakusanye aina mbalimbali za viumbe shambani (mfumo wa ikolojia) kadiri
iwezekanavyo, ikiwemo mimea, mimea yenye magonjwa, wadudu, buibui, panya, nyoka n.k.
5. Waambie wanakikundi waende mahali penye kivuli. Miminia alkoholi kwenye mfuko waplastiki
na uutikise ili wadudu na buibui wafe.
6. Jadili na tengenisha pamoja na vijana viumbe waliyokusanywa kulingana na kazi zao kwenye
mfumo wa ikolojia. Waambie vijana wawapange katika matabaka mbalimbali; mimea chini, wala
mimea katika tabaka la 2, maadui wa asili katika tabaka la 3, na waozeshaji katika tabaka la 4.
Wagundishe kwenye karatasi. Kama hawana uhakika na kazi, wawekee kiumbe hicho lebo
“hawana uhakika”
7. Waulize vijana kama mimea yote waliyoipata ni “magugu”. Kwanini ndiyo au kwanini hapana?
Halafu waulize pia kama wadudu wote ni “wadudu waharibifu”. Kwa nini ndiyo au kwanini ni
hapana?
8. Jadiliana na vijana namna maadui wa asili (walinzi) wanavyomsaidia mkulima katika kudhibiti
wadudu waharibifu na magonjwa ya mimea shambani.
29
9. Toa muhtasari wa majadiliano na mambo mliyoyaona shambani.
Maelezo kwa Mwezeshaji: Maswali ya Kuongoza.
Je, wadudu wote ni wadudu waharibifu?
Je, wadudu wote waharibifu waliyopo shambani husababisha matatizo?
Je, tunahitaji maadui wa asili wangapi kudhibiti wadudu waharibifu?
Je, mdudu mharibifu ni tatizo wakati wote wa hatua za ukuaji wake au wakati wa hatua moja
au mbili tu?
Je, nini hatua za ukuaji wa mmoja wa wadudu aliyechaguliwa?
A.6.3. Zoezi: Desturi mbalimbali za kudhibiti visumbufu vya mimea
Muda: Karibu saa 1
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Eleza kuwa kwa kutumia desturi mbalimbali za kilimo, mkulima anaweza kupunguza hatari ya
mashambulizi ya wadudu waharibifu kwenye mazao yake. Waulize vijana kama wanaelewa baadhi ya
desturi hizo. Ziorodheshe kwenye karatasi kubwa.
Panga desturi hizo kwa makundi kulingana na zile za kiutamaduni, za kiutendaji na za kibiolojia na jaribu
kukamilisha orodha pamoja na vijana
Desturi za Kiutamaduni: Muda wa kulima/kupanda, kulima kwa kwa mzunguko wa mazao/kubadilisha
mazao (crop rotation), kuchanganya mazao, kutumia mitego na kutandaza majani.
Desturi za kiutendaji: Utumiaji jua/utashishaji, kupalilia, uondoaji wadudu waharibifu na/au mimea
inayoambukiza
Desturi za Kibiolojia: Wadudu wenye manufaa (adui wa asili) dawa za kuulia wadudu za viumbe (bio
pesticides) na /au dawa za kunyunyizia mimea, mitego (pheromone traps).
Jadiliana na vijana desturi zote zilizotajwa.
30
A.6.4. Zoezi : Desturi za kijadi za kudhibiti wadudu waaribifu wa mazao
Matumizi ya dawa za kuulia wadudu waharibifu (vinatilifu) na kemikali yamezoeleka sana katika kipindi
kilichopita cha miaka 30-40 kwenye nchi nyingi za tropiki na hasa kwakilimo cha biashara. Bado kuna
maarifa mengi kuhusu namna ya kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa kwa kutumia dawa za
mimeana mbinu za kijadi. Mara nyingi mbinu hizi wanazo wazee katika jamii
Muda: Karibu saa 1
Vifaa: Mwenyeji mwenye maarifa ya kilimo.
Mwalike( mzee) mtu kutoka kwenye jamii ambaye anafahamika kuwa ana maarifa mengi kuhusu
matumizi ya dawa za mimea na mbinu za kijadi katika kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa katika
kilimo.
Waambie vijana watunge baadhi ya maswali katika vikundividogo vidogo na kumwuliza mwenyeji
mwenye maarifa ya kilimo.
Kama ikiwezekana kwa kushirikiana na mwenyeji huyo mwenye maarifa ya kilimo, kusanya baadhi ya
mimea inayotumika na tayarisha dawa.
A.6.5. Zoezi: Kulinda mazao dhidi ya wadudu na magonjwa katika shamba darasa (IPM)
Muda: Karibu saa 2
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea.
1. Waambie vijana wakae kwenye vikundi vyao vidogo vidogo na kugawa mazao yanayokuwa
katika shamba darasa miongoni mwa vikundi vidogo, kwa mfano kila kikundi mazao mawili na
kila zao lishughulikiwe na angalao vikundi viwili. Kila kikundi kichore safu mbili kwenye karatasi
kubwa.
2. Kiambie kila kikundi kihorodheshe wadudu waharibifu na magonjwa ya mazao waliopangiwa
kwa msingi wa walichochunguza katika shamba darasa wakati wa uchunguzi wa mfumo wa
Ikolojia ya Kilimo (AESA) pamoja na kutokana na uzoefu katika safu ya kwanza
3. Kiambie kila kikundi kihorodheshe kwenye safu ya pili desturi za kulinda na kudhibiti wadudu
waharibifu na magonjwa waliyotajiwa.
4. Kiambie kila kikundi kiwasilishe matokeo ya majadiliano yao ya kulinganisha mawasiliano
yanayohusu wadudu waharibifu na magonjwa na desturi za kulinda za mazao hayo.
31
5. Jadili na kukubaliana kuhusu njia bora zaidi za kulinda wadudu waharibifu na magonjwa
yaliyobainishwa kwa mazao mbalimbali yanayolimwa kwenye shamba darasa.
6. Kama bado kuna maswali yasiyohitaji kukatiwa shauri kuhusu baadhi ya wadudu waharibifu na
magonjwa na namna ya kulinda, mwalike kwenye somo la SDSMV mkulima mwenyeji mwenye
uzoefu na jadili maswali haya pamoja naye
A.6.6. Zoezi: Kupata maarifa zaidi kuhusu wadudu waharibifu na magonjwa katika shamba darasa
Kama matatizo au maswali yanayohusiana na kudhibiti baadhi ya magonjwa na wadudu katika shamba
darasa hayawezi kutanzuliwa na vijana na mwezeshaji wa SDSMV, Shamba Darasa na Stadi za Maisha
kwa Vijana , italazimika kuanzisha shughuli za ziada kupata taarifa inayotakiwa kutanzulia matatizo
yaliyobainishwa.
Njia ya a) Kumwalika mkulima mwenyeji mwenye uzoefu au mtaalamu (afisa kilimo wa ugani) kwenye
somo la SDSMV na kuwapa fursa vijana kujadiliana naye matatizo hayo
Njia ya b) Kama ufumbuzi unawezekana unafahamika, fanya jaribio dogo , kupima ufumbuzi
mbalimbali. Kwa mfano, mimea michache au u2 moja imetiwa dawa ya aina moja na mimea michache au
m2 moja imetiwa dawa nyingine .
Njia ya c) Anzisha bustani ya wadudu
Kwa maelezo zaidi kuhusu matumizi
Kwa maelezo zaidi kuhusu matumizi na matayarisho ya bustani ya wadudu, tafadhali angalia
kiambatisho cha 2
A.6.7.Zoezi : Kutayarisha dawa ya Mwarubaini kwa ajili ya kudhibiti wadudu waharibifu
Mwarubaini ni dawa ya kuulia wadudu ya kiasili au ya mimea. Mwarubaini una uwezo mkubwa wa
kudhibiti wadudu wa aina mbalimbali waharibifu. Ina kiwango kidogo sana cha sumu kwa binadamu na
haiharibu mazingira. Miti ya mwarubaini inapatikana katika nchinyingi za tropiki hasa katika maeneo ya
ukame. Sehemu nyingi za mmea huo zinaweza kutumika kwa utayarishaji wa dawa ya kudhibiti wadudu
waharibifu lakini sehemu zinazotumika mara kwa mara ni mbegu na majani ya mti
Njia raisi zaidi ya kueleza matayarisho ya dawa ya mwarubaini ni kwa kufanya kwa vitendo na watoto
Muda: Karibu matayarisho ya saa 1, siku inayofuata, umaliziaji wa nusu saa.
32
Vifaa: Mbegu za mwarubaini, majani ya mwarubaini, kinu, kitambaa chepesina safi, ndoo,
kipulizia dawa cha kubeba mgongoni
1. Kusanya mbegu za mwarubaini zilizoiva, hasa zile zilizoanguka kutoka mtini, menya maganda na
zianike kivulini (ukaushaji kwa hewa). Kama ni lazima, hifadhi mbegu hizo kwenye magunia kwa
matumizi ya baadaye.
Inakadiriwa kwamba kilo 12 za mbegu za mwarubaini zisizomenywa zinatosha kutia dawa hekta
1 au eka 2.5 ya mazao yaliyoshambuliwa na wadudu waharibifu. Ili kupata uzito unaofaa wa
dawa, gramu 50 za mbegu zisizomenywa hazina budi kulowekwa kwenye lita 1 ya maji. Mkulima
anahitaji gramu 750 za mbegu za mwarubaini kama anataka kunyunyizia kwa klutumia kipuliza
dawa cha kubeba mgongoni cha ujazo wa lita 15.
2. Weka kinuni kiasi kinachotakiwa cha mbegu za mwarubaini zisizomenywa na twanga mbegu kwa
ukamilifu mpaka ziwe rojo.
3. Changanya rojo na maji na acha kwa usiku kucha
4. Itakapofika mchana, chuja maji ya mbegu kwa kitambaa safi na chepesi. Chujua/zimua
mchanganyiko huo kwa uwiano wa 1:2 halafu nyunyizia mazao yaliyoshambuliwa na wadudu
kwa kutumia kipulizia dawa cha kubeba mgongoni.
5. Changanya mabaki ya chembechembe ngumu za mbegu iliyochujwa na udongo wa kitalu ili
kudhibiti wadudu wa kwenye udongo wa kitalu.
Namna ya kutayarisha dawa ya majani ya mwarubaini.
1. Kusanya majani ya mwarubaini kabla mti haujaalika maua
2. Twanga kiasi cha kilo moja ya majani , changanya na maji kiasi cha gramu 100 (kiasi cha kiganja
kilichojaa) cha pilipili hoho mbichi kwenye kinu. Pilipili hoho zinaongeza ufanisi wa dawa ya
majani ya mwarubaini.
3. Loweka rojo la majani ya mwarubaini kwenye lita 5 za maji usiku kucha.
4. Chuja mchanganyiko kwa kitambaa safi na chepesi naongeza lita 1 ya sabuni ya maji. Sabuni ya
maji itakuwa haina kiambata.
5. Chujua/zimua mchanganyiko huo kwa uwiano wa 1:2 kwa kunyunyizia moja kwa moja kwenye
mazao ili kudhibiti wadudu.
33
A.6.8. Zoezi: Punguza matumizi ya kemikali za kilimo
Wakulima wengi hutumia kemikali za kilimo katika urutubishaji na /au udhibiti wa wadudu waharibifu na
magonjwa. Kemikali nyingi ni hatari sana na wakulima hawana budi kuzisambaza na kuzitumia kwa
makini.
Muda: Kiasi cha saa 2
Vifaa: Karatasi kubwana kalamu za kuchorea
1. Waambie vijana wataje aina mbalimbali za kemikali zinazotumiwa na wakulimakatika katika ……
na waziorodheshe kwenye karatasi kubwa
2. Jadiliana na vijana hatari mbalimbali zilizopo katika kutumia kemikali hizi na namna mkulima
anavyoweza kupunguza hatari. Orodhesha kwenye karatasi kubwa namna bora za kushughulikia
kemikali hizo.
3. Waambie vijana wataje mifano ya ajali zilizotokea katika jamii zao na kiambie kikundi kimoja
kifanye mchezo wa kugiza kuhusu mfano wa ajali
4. Jadili makosa yaliyofanywa katika kushughulikia kemikali kwenye mchezo wa kuigiza. Kaimbie
kikundi kingine kiigize tena mchezo lakini safari hii huonyesha namna bora za kushughulikia
5. Hitimisha kuhusu namna bora za kushughulikia kemikali za kilimo
Zingatia: Namna bora za kushughulikia kemikali za kilimo ni
Chagua dawa za wadudu zilizo salama zaidi na tumia kiasi kidogo sana
Tunza dawa za wadudu, kemikali za kulima na vifaa vya kupulizia dawa mahali salama na
palipotengwa
Andika majina/lebo kwenye dawa za wadudu na kemikali za kilimo (kwa kutumia Kiswahili)
Weka njia salama za kushughulikia chupa na makopo ya dawa za wadudu na kemikali
Kusanya taarifa za afya na usalama kwa mfano matumizi salama ya kemikali za kilimo na
eneza taarifa hizo kwa jamii
34
A.7. Mada ndogo: Uchunguzi wa mfumo wa kilimo na ikolojia (AESA ) – Zana ya ufuatiliaji na kufanya
maamuzi katika kilimo
Malengo: Kuelewa namna ya kuchanganua mara kwa mara jinsi mashamba yao yanavyoendelea
Wakati wakupanga shughuli zaoza shamba, vijana hawana budi kujifunza kuchanganua hali ya
mashamba yao kwanza kabla ya kufanya uamuzi kuhusu namna ya kusimamia mazao yao. AESA ni zana
inayofaa kwa ajili ya kufanya shughuli hii, pamoja na kubadilishana maarifa. AESA inahusisha uchunguzi
na uchanganuzi wa mara kwa mara wa mazao wakati wa hatua mbalimbali za ukuaji. Pia inahimiza
“kujifunza kwa kugundua”. Vipengele vya msingi vya uchanganuzi ni:-
Hakikisha mimea ina afya katika hatua mbalimbali za ukuaji wao
Wadudu na wanyama wanaokula wenzao
Hali ya udongo na maji
Hali ya hewa
A.7.1. Zoezi: Kutambulisha AESA
MUDA: Karibu saa 2
VIFAA: Karatasi kubwa ya chatipindu, kalamu za kuchorea, tepu na shamba lenye mazao.
1. Eleza kwamba ni muhimu kuchunguza mazao mara kwa mara ili kuyatunza
2. Nenda na vijana kwenye shamba lenye zao maalumu, wagawe vujana katika vikundi vya vijana
6-7 na kila kikundi kiandae orodha ya mambo muhimu wanayotaka kuyaona kuhusu mazao.
Wasaidie vijana kubaini mambo yafuatayo
Idadi ya mimea iliyopo
Idadi ya wadudu wanaoruka (wadudu waharibifu na wanyama wa asili wanaokula
mazao), kwenye mimea na eneo la jirani
Wadudu, wanyama wanaokula wenzao waliyopo kwenye eneo la udongo na kwenye
mimea
Mabaka, madoa na kuchujuka rangi kunakoonyesha kuwapo kwa magonjwa
Madhara yanayosababishwa na wadudu na aina mbalimbali za magonjwa
35
Aina za nyasi,ukubwa na wingi ikilinganishwa na mazao
Hali ya udongo
Hali ya hewa siku hiyo (kwa mfano joto, mawingu kidogo, mvua, unyevunyevu/mavunde
mavunde)
3. Chagua mmea wa mfano na waambie vijana wachunguze mambo yafuatayo
Idadi ya majani
Urefu wa mimea
Sehemu za uzazi za mmea uliyochaguliwa
Sifa nyingine zozote zitakazokusaidia kutoa uamuzi kuhusu mmea huo wiki
zitakazofuata.
4. Waonyeshe vijana muundo watakao wasilishia data zao. Mfano umeonyeshwa hapa chini
5. Kwa kushirikiana kwa vikundi vyao, waambie vijana wajaribu kufanya AESA ya sehemu ya
shamba
6. Waambie vijana wawasilishe kazi yao, na jadili tofauti zozote zilizojitokeza
7. Hitimisha somo kwa kuwauliza vijana, “ Je, AESA inawasaidiaje kufanya uamuzi?”
36
Mfano wa Muundo wa Uwasilishaji wa Data - AESA
AESA No.
Jina la kikundi
Tarehe
HALI YA HEWA
Taarifa ya
jumla
Aina ya mimea
Je, umetumia
mbolea(ya
kemikali)
Tarehe ya
kupanda
Muda wa
kuchunguza
(tarehe, saa
n.k.)
(
Wanyama
walioonekan
a
Wadudu
37
Uchunguzi
kuhusu mmea
Upana wa jani
Urefu wa
mmea
Idadi ya majani
Idadi ya vifuko
vinavyoonekan
a
Magonjwa
yaliyoonekana
Taarifa kuhusu udongo na maji
Wanyama
wanaokula
mazao wa
asili
Uchunguzi wa jumla wa hali ya mmea na
shamba
MAPENDEKEZO
38
A.7.2. Zoezi: Ufuatiliaji wa Mara kwa Mara kwa kutumia AESA.
AESA ilielezwa kwenye moduli iliyotangulia, lakini ni muhimu kukumbuka kuwa AESA inatakiwa kufanya
mara kwa mara ili vijana waelewe kwa ukamilifu na kudhibiti ukuaji wa mazao yao. Alimradi mazao yako
kwenye shamba darasa, washiriki wafanye AESA mara moja kila wiki.
Muda: Wastani saa 2
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea, tepu na kijiti
1. Endesha majadiliano ya “kukumbuka” na vijana kuhusu AESA
2. Nenda na vijana kwenye shamba darasa na wagawe katika vikundi vidogo vidogo
3. Panga eneo kwenye shamba darasa kwa kila kikundi kuchunguza ukubwa wa eneo lililochaguliwa au
idadi ya mimea (kulingana na zao)
4. Viambie vikundi waandae orodha ya mambo muhimu waliyoona kuhusu ukuaji wa mazao
5. Waambie kila kikundi wajadili habari walizoandika na kupendekeza taratibu za udhibiti ili kutatua
matatizo yoyote yatakayojitokeza. Kwa mfano, kama magugu mengi yameonekana, inawezekana
kupendekeza palizi kama pendekezo la usimamizi
6. Toa muhtasari wa matokeo kwenye karatasi ambayo inaweza kutumika kama karatasi ya ufuatiliaji
na kutunzia kumbukumbu: Michoro iwe rahisi na inayoonyesha hali/matokeo ya shamba.
7. Kila kikundi kidogo kiwasilishe matokeo yao. Hakikisha watu tofauti wanawasilisha matokeo kila
wakati.
8. Jadili mawasiliano ya vikundi na njia za udhibiti zilizopendekezwa, na amueni pamoja kuhusu hatua
gani zinatakiwa kuchukuliwa – na nani watazichukua.
Maelezo kwa Mwezeshaji: Maswali kwa ajili ya majadiliano katika hatua ya miche.
Je, mimea imestawi vizuri (hatua ya miche)?
Je, kwa jumla mazao yamestawi na yenye afya?
Je, kuna hali ya majani kuwa njano? Kama ni hivyo ni kitu gani kinaweza kusababisha hali hiyo?
Hali ya hewa ina athari gani katika ukuaji wa mimea?
Je, unawaona aina gani ya wadudu waharibifu na wako wangapi?
39
Je, kuna mayai mengi ya wadudu rafiki?
Je, uharibifu wa aina gani unafanywa na wadudu waharibifu katika hatua hii ya mazao?
Je, kuna njia yoyote ya kuzuia wadudu hawa wasiongezeke?
Je, hali ya wadudu waharibifu katika kashamba mengine kwenye eneo ikoje?
Je, mashamba mengine yanaweza kuathiri shamba lako?
Je, kuna aina gani ya maadui wa asili shambani?
Je,wako wangapi? Unafikiri wanaweza kuwa wametoka wapi?
Je, wanakula nini? Na walikuwa wanakila nini kabla hawajawa wadudu waharibifu?
Je kuna wadudu ambao si waharibifu wala wadudu wa asili?
Je, kuna wadudu waozeshaji ambao hula vitu vilivyokufa ndani ya udongo?
Je, idadi ya wadudu waharibifu namaadui wa asili inaongezeka au kupungua ikilinganishwa na
wiki zilizopita?
Je, unatarajia kutatokea nini wiki ijayo?
Je, kuna wadudu waharibifu maalumu wa kufuatilia kwa makini zaidi?
Je,unafikiri kuna haja ya kutumia dawa ya kuulia wadudu waharibifu? Kama hapana,je kuna njia
mbadala?
Je, mimea imepata nafuu kutokana na uharibifu wa wadudu katika hatua iliyopita?
Je, kuna ugonjwa wowote shambani? Unawezaje kudhibitiwa au kutibiwa?
Je, mimea inakuwa kama ilivyotarajiwa (majani mangapi, kimo, n.k.)
Je, kuna magugu kwa wingi? Ni wakati gani unafaa kufanya palizi?
Je, kuna mpango gani waudhibiti kwa wiki ijayo?
Je, uamuzi wa wiki iliyopita ullikuwa na ufanisi?
40
A.8.1. Zoezi: Palizi, Kwa nini, Wakati gani na namna gani
Muda: Saa mbili
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Zingatia: Shughuli hii ni lazima ifanywe kwenye shamba la karibu ambapo mazao tayari
yanakuwa na magugu yamekuwa ni tatizo
Hatua:
1. Wakiwa shambani, waambie vijana waketi katika mduara. Waulize wanafikiri mkulima atafanya
nini kukinga mazao yasipatwe na magonjwa. Orodhesha mawazo yao yote
2. Himiza majadiliano kuhusu umuhimu wa kuzingatia usafi wamazingira katika shamba kupunguza
hatari za wadudu waharibifu namagonjwa. Waambie vijana wataje shughuli nyingi ambazo
mkulima anaweza kufanya kuweka usafi wa mazingira unaofaa shambani kwao. Orodhesha
shughuli hizo (palizi, kuondoa magugu na sehemu za mimea zilizoathiriwa shambani)
3. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vidogo na kiambie kila kikundi kichunguze sehemu moja ya
shamba. Waulize vikundi kile kinachotakiwa kufanya
4. Jaribu kuhitimisha ni wakati gani mkulima anatakiwa aanze palizi na anatakiwa aondoshe nini na
abakishe nini shambani.
A.9.1. Zoezi: Kupandikiza miche (mboga za majani n.k.)
Muda: Wastani wa saa 2
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Upandikizaji huifanya mimea iwe minyonge. Kama upandikizaji haufanywi kwa makini, mimea haiwezi
kukua vizuri. Kabla ya kwenda kwenye shamba darasa, waulize vijana maswali yafuatayo na orodhesha
majibu yao kwenye chatipindu.
Je, unadhani kupandikiza miche kuna hatua gani mbalimbali?
Je, unafikiri ni mambo gani muhimu zaidi kufanya wakati unapopandikiza miche?
Kwa nini unadhani ni muhimu kupandikiza miche jioni?
Kwa nini unadhani mkulima lazima apandikize miche imara na si ile yenye afya ambayo
imeambukizwa magonjwa?
41
Kwa nini ni muhimu kupandikiza miche ikifikia umri unaofaa, yaani si michanga sana wala si
mikubwa sana?
Je, unadhani mkulima atafanya nini kuipunguzia miche unyonge baada ya
kupandikiza?(kutandaza nyasi na majani)
Sasa unaweza kwenda na vijana kwenye shamba litakalopandikizwa miche inayotoka kwenye
kitalu/vitalu. Waulize vijana maswali yafuatayo:
Je,shamba limeandaliwa tayari kwa ajili ya kupandikiza miche? Kama ndiyo, kwanini unadhani
liko tayari? Kama bado, unadhani kunahitajika kufanywa kitu gani ili kuanza kupandikiza miche?
Sasa unaweza kuwaambia vijana washiriki katikakupandikiza miche.
1. Jadili hatua mbalimbali za kupandikiza miche
2. Mwagilia maji kitalu cha mbegu na onyesha namna ya kung’oa miche kutoka kwenye kitalu
3. Waambie vijana wote wang’oe miche mingi kutoaka kwenye kitalu
4. Onyesha namna ya kusafirisha miche mapaka shambani
5. Waambie vijana wakusnaye miche yote iliyong’olewa kutoka kwenye kitalu na waipeleke
shambani
6. Jadili na waonyeshe vijana namna ya kupandikiza miche kwenye shamba darasa
7. Waambie vijana wapandikize miche yote iliyobaki
8. Waambie vijana wamwagilie miche iliyipandikizwa
Ukishamaliza, toa muhtasari wa hatua zote za kupandikiza miche.
Taarifa ya msingi.
Hatua za upandikizaji miche Vipengele muhimu
1. Kutayarisha shamba darasa Udongo uliolimwa na kutiwa mbolea vizuri, hakuna magugu
2. Kumwagilia kitalu chamnegu
3. Kung’oa miche Jioni, chagua miche imara na yenye afya kwa ajili ya
kupandikiza, bakisha udongo kwenye mizizi na uwe mwangalifu
42
usiharibi mizizi
4. Kusafirisha miche Muda mfupi,hakikisha kuwa imelowa na iwe kivulini. Miche
iliyong’olewa iondolewe kwenye udongo kwa muda mfupi tu (<
saa moja).
5. Kupandikiza miche Jioni, kuwa mwangalifu usiharibu wala kupinda mizizi
6. Kumwagilia shamba darasa Mimea isikose maji baada ya kupandikizwa - isinyauke
A.10. Mada ndogo: Umwagiliaji maji
Malengo: Kuelewa maana ua umwagiliaji maji
Kuelewa njia mbalimbali za umwagiliaji
Kama ilivyotajwa hapo awali, kudhibiti maji shambani ni muhimu sana kwa ajili ya kulima mazao
yanayostawi. Mvuainapokuwa kidogo sana, mhulima anatakiwa kutafuta njia ya kuyapatia mazao maji.
Kuna njia mbalimbali za kumwagilia mazao. Ni muhimu kwa vijana kujua njia mbalimbali za umwagiliaji
zinazotumika katika eneo hili. Pia wanahitaji kuelewa kuwa udongo unanyonya maji kwa haraka kiasi
gani (kiasi cha udongo kupitisha maji)na kwa kiasi gani unavyoweza kuhifadhi maji (kiasi cha udongo
kuhifadhi maji). Kwa kujua mambo haya mawili kutawasaidia kumwagilia mashamba yao kwa njia bora
zaidi
A.10.1. Zoezi: Kuelewa aina ya umwagiliaji na “upitishaji maji”
Muda : Wastani wa saa2
Vifaa: Kiasi cha chupa 20 za maji ( lita 15 – 05), kisu kikali. Kilo 1ya udongo wa mchanga, kilo 1 ya
udongo wa mfinyanzi na maji
43
HATUA:
Majadiliano ya Kikundi (Dakika 30)
1. Waulize vijana kama yuko anayefahamu umwagiliaji ni nini. Mara baada ya maana ya
umwagiliaji kueleweka kwa kila mmoja,waulize vijana kwanini wanafikiria ni muhimu kumwagilia
mimea wakati wa ukame.
2. Waulize vijana kama wanafahamu njia mbalimbali za umwagiliaji mazao shambani
kwaonahalafu wabainishe njia zinazotumika na wakulima kwenye eneo/kijiji chao
3. Waulize vijana wanafikiri kuna umuhimu gani katika kumwagilia mazao yao na katika kuchagua
njia inayofaa kumwagilia
4. Toa muhtasari wa matokeoya majadiliano: aina ya mazao, hatua ya mazao (kitalu au shambani),
ukubwa wa shamba, mteremko na aina ya udongo
5. Pitia pamoja na vijana aina ya udongo uliyojadiliwa kwenye moduli iliyopita. Anza kueleza
wazola sifa za udongo na namna zinavyoathiri kiwango cha “upitishaji maji” na “uwezo ya
kuhifadhi maji”
Kuonyesha na kufanya majaribio (saa 1 dakika 30)
1. Kata sehemu ya juu ya chupa (sehemu nyembemba) za chupa nnekwa kisu halafu toboa
matundu sehemu ya kitako cha chupa mbili zamaji. Jaza udongo kwenye theluthi moja ya
udongo kwenye chupa zenye matundu – chupa moja udongo wa mchanga na chupa nyingine
kiasi sawa cha udongo wa mfinyanzi. Tayarisha kiasi cha maji cha kutosha kwenye chupa
nyingine (1/4 ya chupa) na weka alama kiwango cha maji.
2. Mwambie kijana mmoja aangalie saa. Mimina maji kwa uangalifu kwenye udongo uliyomo
kwenye mojawapo ya chupa na anza kupima muda utakaochukua kwamaji kunywea kwenye
udongo hadi kwenye chupa iliyowekwa chini ya udongo (inapoanza kudoda juu ya chupa na
inapoacha kudoda)
3. Tayarisha kiasi sawa cha maji na mwambie klijana mwingine kufuatilia muda. Mimina maji kwa
uangalifu juu ya udongo na kwenye chupa ya pili halafu pima muda utakaochukua kwa maji
kunywea kwenye udongo
4. Jadili tofauti za muda uliotumika kwa maji kunywea katika aina mbalimbali za udongo (kiwango
cha upitishaji maji)
5. Linganisha kiasi cha maji kilichoweza kunywea kwenye udongo na jadili kulitokea nini kwamaji
yaliyobaki kwenye udongo(uwezo wakuhifadhi maji)
44
6. Wagawe vijana katika vikundi vya vijana watatu watatu au wanne na waambie warudie zoezi.
Waambie kila kikundi kikusanye aina mbili tofauti za udongo karibu na wanapolutania kwa ajili
ya SDSMV au kutumia kiasi sawa cha udongo kama uliotumiwa kwa zoezi. Wasaidie vijana
wakati wa zoezi hilo na hakikisha kuchukua vipimo vyote vya majaribio
Majadiliano ya Kikundi (Dakika 15)
Jadili matokeo ya majadiliano kuhusiana na umwagiliaji. Udongo wenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi
maji unaweza kumwagiliwa mara chache zaidi ingawa kwa kutumia kiasi kikubwa cha maji. Kuhusu
udongo wenye kiwango kikubwa cha upitishaji maji, maji yatatiririka haraka sana juu ya usawa wa bonde
au mtaro kwa hiyo nilazima vijengwe kwamwinuko mkali . Toa muhtasari wa mambo yaliyoonekana
katika jaribiona majadiliano.
Maswali ya kuongoza majadiliano
Tutajuaje kuwa tumemwagilia maji ya kutosgha?
Je, tunatakiwa kumwagilia kila siku au mara moja kila baada ya siku mbili au tatu?
Je, uwezo wa udongo kuhifadhi maji unaathari gani katika umwagiliaji
Tutawezaje kukagua kama mmea/zao linahitaji kumwagiliwa?
Je, ni dalili gani zinazoonyesha upungufu wa maji katika mmea/zao?
Je, tutawezaje kutumia mteremko wa shamba kusambaza maji kwa usawa?
Je,zao linahitaji kiasi gani cha maji kinacholingana kila siku?
Mkulima afanyaje ili kupunguza mtiririko wa maji kwenye mtaro (umwagiliaji wa mtaro)?
Kwa nini inatubidi kufikiria kuhusu mifereji ya kutoa maji mashambani vilevile
tunapopanga umwagiliaji?
45
A.11.1. Zoezi: Urutubishaji Ardhi.
Muda: Wastani wa saa 1
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
1. Waulize vijana kama wanafahamu mbolea ni nini na kwa nini wakulima wengi wanatumia
mbolea kwenye mazao yao.
2. Waambie vijana wataje aina mbalimbali za mbolea wanazozifahamu ambazo mkulima anaweza
kutumia na waziorodheshe (mbolea za asili: mboji, samadi,mabakiya mimea nambolea za
kemikali: urea, DAS, TSP, Potasium Kompaundi (NPK)).
3. Viambie vikundi vijadiliane kwa vikundi vidogo tofauti kati ya aina mbalimbali za mbolea,
madhumuni yake na namna zinavyotakiwa kutumika.
4. Amua na vijana ni aina gani za mbolea zitumike kwenye shamba darasa na kiasi kinachotakiwa
A.11.2. Zoezi: Utiaji mbolea wa mara ya pili
Muda: Wastani wa saa moja
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
1. Mazao mengi hayahitaji utiaji mbolea wa mara ya pili. Waulize vijana kwa nini wanafikiri kuwa
wanahitaji (mbolea za naitrojeni zinachujisha au vukiza kwa urahisi udongo wa juu na kuhitaji
kuongezwa baada ya miezi 2-3)
2. Jadili ni mazao gani katiya manne yaliyolimwa yanahitaji utiaji mbolea wa mara ya pili na
zinahitajika mbolea za aina gani na zitumiwe lini (mazao ambayo hayajafikia hatua ya uzazi,
baada ya miezi miwili,mbolea za naitrijeni, wiki chache kabla mazao hayajafikia hatua ya uzazi).
Jadili njia bora zaidi ya kutia mbolea. Waambie vijana wafanye kwa vitendo shambani.
46
A.11.3. Zoezi: Ulindaji wa Rutuba ya udongo katika kilimo cha kutumia mbolea ya asili/kimaumbile
Muda: Wastani wa dakika 20
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Katika kilimo cha kutumia mbolea ya asili/kimaumbile wakulima wanatumia njia mbalimbali za kutunza
na kuboresha rutuba ya udongo wao
Bungua bongo na wanafunzi kuhusu njia mbalimbali mkulima anazoweza kulinda rutuba ya ardhi yake
(mbolea za kemikali, samadi kutoka kwa wanyama, matumizi ya mazao jamii ya kunde katika kilimo cha
kubadili mazao ya mizizi mifupi na mirefu, kutumia mboji).
Jadiliana na wanafunzi, iwapo mbolea za kemikali/chumvichumvi haziwezi kutumika, tutatumiaje
ainanyingine za kilimo kwenye shamba darasa letu. Tumia matokeo ya majadiliano katika kupanga
shughuli za shamba darasa
Kutegemea mboji
Mboji ni mbolea ya takataka zilizoozeshwa na bakteria na viumbe hai vingine aghalabu za kikaboni kwa
kipindi fulani. Mboji ni nafuu na rahisi kwa kutengeneza. Aina mbalimbali za vitu vya kikaboni ambavyo
mara nyingi vinaonekana kuwa ni takataka katika mashamba na nyumbani kama vile maganda ya
mboga, maagugu, matunda, majani na takataka za jikoni vinaweza kutumika.
Kutumia mboji kunaongeza rutuba ya udongo kwa uongezaji watija na mavuno shambani. Mkulima
anaweza kutengeneza mboji yeye mwenyewe ili kuokoa fedha. Ni njia salama katika kilimo na hivyo
kuhifadhi ardhi kwa vizazi vijavyo
A.11.4. Zoezi: Je, kutengeneza mboji ni nini na tunaweza kutumia vitu gani?
Muda: Wastani wa dakika 40
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea.
Ili kulinda rutuba ya udongo katika kilimo cha kutumia mbolea ya asili, mkulima anawezakutumia mboji
anayoweza kuitengeneza yeye mwenyewe. Waulize vijana kama kuna mtu wanayemfahamu katika jamii
yao anayetengeneza mboji. Kama wanamfahamu, waulize vijana iwapo wanajua mtu huyo anavyofanya.
Eleza kwa muhtasari kutengeneza mboji ni nini na kwamba tunawezakutumia aina zote za vitu vya
kikaboni vinavyoonekana kuwa ni takataka mashambani na nyumbani. Bungua bongo kuhusu aina
mbalimbali za vitu vya kikaboni vilivyopo katika jamii vinavyoweza kutumika kwa kutengenezea mboji.
47
Waambie vijana wakusanye kwenye gunia kwa jumla moja takataka za kikaboni zilizoorodheshwa na
kuzileta kwenye somo lijalo kwa ajili ya kutengeneza mboji
A.11.5. Zoezi: Kutengeneza Mboji
Muda: Wastani wa dakika 60
Vifaa: Ardhi, kasha, takataka za kikaboni, samadi, panga, sepeto, magunia, ndoo ya
kumwagilia
Eleza kuwa kuna njia mbalimbali za kutengeneza mboji. Mboji inawezakutengenezwa kwenye kasha,
rundo, shimo, na kwenye rundo lililofukiwa kidogo (nusu mita), kutegemea hali ya mtiririko wa maji
machafu mahali hapo. Jadiliana mfumo wa maji machafu na vijana na chagua namna ya kutayarisha
mboji.
Kama ni mboji ya shimo, mashimo matatu ya mboji yatachimbwa ubavuni kwa mfuatano. Mashimo hayo
yatakuwa na kina cha sentimita 50, upana wa sentimita 150, na urefu kulingana na nafasi, kama
inavyoonyeshwa kwenye Mchoro wa 1. Vitu vitakavyotumiwa, vinarundikwa kwa mpango maalumu
kama ifuatavyo.
1. Tabia ya udongo wa mfinyanzi (a) inatandazwa chini ya shimo kuzuia upotevu wa maji
yatakayomwagiliwa kwenye rundo
2. Tabaka ya matawi ya mti au mabua ya nafaka ya sentimita 15 (b) chini ya vitu vya kutengenezea
mboji, husaidia kuzuia mmomonyoko
48
3. Tabaka ya vitu vya sentimita 15-30 (c ) kama vile mabaki ya mazao yaliyovunwa, nyasi, takataka
za jikoni, n.k. huwa ndilo rundo kuu
4. Juu kuna samadi ya kina cha sentimeta 10 – 20 (d) ambayo hurutubisha mboji nakuharakisha
kuoza
5. Katika hatua hii, umwagiliaji maji wa kutosha (lita 600-800 za maji kwa kila mita ya ujazo ya
mboji) hufanywa.
6. Tabaka nyembamba ya udongo (e) huziba tabaka zilizotangulia ili kuhakikisha joto linabaki ndani
7. Rundo huongezeka kwa kurudia tabaka (c ) , (d), umwagiliaji wa maji na tabaka (e)
8. Mwisho rundo “linaezekwa” tabaka la nyasi au mabua ya mimea sentimeta 20 (f)
Rundo lililokamilika linaachwa lioze kwa siku 15 – 20 ambapo litageuzwa kutoka shimo 1 hadi la 2
ambapo litakaa kwa siku nyingine zaidi 15 – 20 kabla ya kugeuzwa na kuingizwakwenye shimo la 3.
Mboji bora ya mwisho itakuwa tayari kutumiwa baadaya siku nyingine 15 – 20.
Zingatia: Chomeka mti mrefu kwenye rundo tangu mwanzoili kuhakikisha hali joto. Kama mti una joto,
inaonyesha kwamba mboji inaoza na ikiwa baridi inaonyesha kupungua kwa uozaji wa mboji.
49
A.11.6. Zoezi: Kukagua, Kugeuza na Kutumia Mboji.
Vitu vyote vilivyotumika kutengenezea mboji ni lazima vioze kwa ukamilifu kabla ya kutumiwa shambani.
Kwa hiyo vijana ni lazima wajifunze kukagua hali mara kwa mara. Watakagua kwa mti au kwa kuingiza
mkono kwenye mboji.
Kama vitu vya kutengenezea mboji vinaoza kwa ukamilifu, halijoto itakaribia 80 0C. mti wakukagulia
utakuwa na joto kali na mvuke kidogo utaonekana kwenye mti. Kama watakagua kwamkono,
watumbukizemkono kwenye mboji kwa sekunde chache sana.
Wakati halijoto inapoanza kupungua, (baada ya wiki mbili) mboji inahitaji kugeuzwa na kuchanganywa
kwenye rundo jingine au shimo, na vitu ambavyo havijaoza kwa ukamilifu viwekwe katikati kadiri
iwezekanavyo. Lazima igeuzwe mara mbili.
Baada ya siku 45 – 60 mboji itakuwa tayari na inaweza kutumiwa shambani. Matumizi yake yataanza na
ile mimea inayohitaji virutubisho vingi zaidi,mimea jamii ya kunde na hata mazao ya kwenye ardhi
iliyorutubishwa kwa mboji msimu uliyopita, haihitaji mboji. Kiasi cha matumizi kitategemea aina ya
mazao, hata hivyo kwa kawaida mboga za majani zinahitaji mboji kiasi cha kg/m2 4-6.
Mboji ni lazima ichanganywe kwenye udongo kabla ya kupanda mazao
A.12. Mada ndogo: Kulinda shamba la Kilimo
Malengo:
Kuelewa umuhimu wa kulinda shamba la kilimo
Kubainisha na kuorodhesha njia mbalimbali za kulinda mimea shambani
Kueleza mbinu mbalimbali za kulinda shamba.
Shamba darasa ni miongoni mwa sehemu muhimu za maisha ya vijana ambazo wanahitaji kulinda.
Kuhakikisha kwamba, shamba darasa linalindwa ipasavyo, ni vizuri kwa vijana kushirikiana na jamii na
kuomba msaada wao. Kama wakiridhishwa kuhusu umuhimu wa mradi, ulinzi wa shamba/bustani
utafanikiwa. Matatizo kama ya kuingiliwa na wezi na wanyama yataepukwa kwa urahisi.
Kama matatizo ya usalama yatatokea kuhusiana na shamba darasa/bustani ya SDSMV, omba kufanya
mkutano na viongozi wa jamii kujadili tatizo hilo na kuomba kusaidiakushughulikia matatizo ya usalama.
50
A.12.1. Zoezi: Kulinda Shamba Letu
Muda: Wastani wa saa 2
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Mifano ya matatizo kwenye mashamba yasiyolindwa
mbuzi huingia na kuharibu, na kula mazao
ng'ombe huingia na kula kila kitu
sungura huingia na kula saladi na kabichi changa
panya huingia na kula mbegu za alizeti
mavuno yanaweza kuibwa wakati wa usiku
mazao hufa kutokana na ukame, wadudu au wadudu waharibifu
1. Endeshs majadiliano mafupi na vijana kupitia vipengele vyote walivyokwishapitia kabla kuhusu
wanataka kuyalinda mashamba yao kutokana na nini? Ili kuwasaidia kukumbuka, unaweza
kutaka kuuliza maswali yafuatayo
Kwa nini inatubidi kulinda shamba letu?
Kutatokea nini kama hatutalinda vizuri mashamba?
Tutafanyaje kuboresha hali hii?
2. Wagawe vijana katika makundi manne. Waambie kila kikundi waandike au kuchora:
Njia mbili za kulinda shamba dhidi ya wanyama wanaokula mimea.
Njia moja ya kulinda dhidi ya ukame
Njia mbili za kushughulikia wadudu waharibifu
Njia mbili za kulinda dhidi ya wezi
3. Waambie watu wawili kutoka kila kikundi wawasilishe na kueleza hatua walizopanga kuchukua
pamoja
51
A.12.2. Zoezi: Kujenga uzio na uzio zaidi.
Muda: wastani wa saa 1
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea, karatasina penseli
1. Wapeleke vijana kwenye matembezi katika jamii na waambie wachague aina mbalimbali za uzio
na maboma wanayoona
2. Waambie wawadadisi baadhi ya wakulima ambao wanakutana nao wakati wa matembezi yao.
Baadhi ya maswali wanayoweza kuwauliza wakulima ni:-
Kwa nini mlichagua aina hiyo ya uzio?
Kuna faida na hasara gani za uzio mlionao?
Vifaa gani mmetumia kujenga uzio wenu?
Je, uliujengaje?
Ilichukuwa muda gani kujenga?
Je, umeridhika na uzio huo?
Je, ungependelea kuwa na aina mbalimbali za uzio? Kwa nini au kwa nini hapana?
3. Baada ya matembezi na usaili, tafuta mahali penye kivuli kukaa na kufanya majadiliano ya
jumla kuhusu wamejifunza nini. Wakati wa majadiliano, andaa mpango wa jinsi ya kupata vifaa
ambavyo mtahitaji kwa ajili ya kujenga uzio na waambie vijana walete vifaa vya kujenga uzio
kutoka nyumbani kwao kwa ajili ya somo linalofuata
A.13. Mada ndogo: Kuvuna
A.13.1. Zoezi: Wakati na mbinu za kuvuna
Mazao mbalimbali katika shamba darasa yanahitaji kuvunwa siku chache kabla au wakati yamekwisha
komaa kabisa, kutegemea aina ya mazao na matumizi ya mazao yaliyovunwa. Kila zao lina njia yake ya
kuvuna.
52
Muda: Wastani wa dakika 30
Vifaa: Hakuna
Waulize vijana kama wanajua namna ya kuvuna mazao mbalimbali yaliyolimwa kwenye shamba darasa.
Je, wanawajua wakulima wowote wanaotumia mbinu mbalimbali na kwa nini wanavuna tofauti?
Jadili namna ya kuvuna mazao mbalimbali kwenye shamba darasa. Waulize vijana ni wakati gani wa siku
unaofaa zaidi kuvuna mahindi na mbogamboga
Nyanya wakati mwingine zinavunwa zikiwa bado mbichi na wakati mwingine zikiiva. Jadili kwa nini na
kwa nini ni muhimu kila mara kufikiria unachopanga kufanya na mavuno kuhusu lini na namna
inavyokubidi kuvuna zao hilo.
A.14. Baada ya Kuvuna
A.14.1. Zoezi: Namna ya kupunguza hasara baada ya kuvuna.
Mkulima bado anapoteza asilimia kubwa ya mazao yake kati ya kuvuna na utumiaji au kuvuna mazao
yake. Kama mambo mengi ambayo mkulima anaweza kufanya kupunguza hasara ya baada ya kilimo,
kuanzia wakati wa kuvuna, na kufuatiwa na usafirishaji kutoka shambani, uhifadhi na ufungashaji. Vijana
watajadili mkulima anachotakiwa kufanya kupunguza hasara baada ya mavuno wakati wa shughuli
mbalimbali za baada ya kuvuna.
Lengo: Kujifunza kuhusu mkulima anapaswa kufanya nini kupunguza hasara baada ya kuvuna
Muda: Wastani wa saa 1
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Hatua:
Kubungua bongo (Dakika 20)
1. Anza mada ya namna ya kupunguza hasara baada ya kuvuna. Waeleze vijana kuwa hasara baada
ya kuvuna inaweza kugawanyika katika hasara ya kiasi (kg) na ubora. Aina mbili zote zinafanya
hasara ya kiuchumi ya mazao.
53
2. Waulize vijana kuwa mkulima atafanya nini kupunguza hasara ya baada ya kuvuna. Andika hoja
mbalimbali za hatua za uzingatiaji uliotajwa kwenye karatasi kubwa
3. Jadili hoja mbali za hatua atakazozingatia mkulima zilizotajwa na zipange kwenye shughuli
mbalimbali za shughuli za baada ya kuvuna (kuvuna, usafirishaji wa mazao, uhifadhi, usafirishaji,
ufungashaji na uuzaji)
Majadiliano ya vikundi vidogo vidogo(Dakika 40)
4. Wagawe vijana katika vikundi vidogo na kiambie kila kikundi kichague mojawapo ya mazao
yanayolimwa katika eneo
5. Kwa zao walilolichagua, kiambie kila kikundi kijadili hoja za hatua za uzingatiaji ambazo mkulima
hana budi kuchukua kwa shughuli mbalimbali za baada ya kuvuna ili kupunguza hasara ya
mazao. Waambie kikundi watoe taarifa ya matokeo ya mazungumzo yao kwenye karatasi kubwa
6. Kiambie kila kikundi kiwasilishe matokeo ya majadiliano yao
7. Jadili mawasiliano mbalimbali
8. Toa muhtasari wa hoja za hatua za uzingatiaji ambazo mkulima hana budi kuchukua wakati wa
shughuli mbalimbali za baada ya kuvuna ili kupunguza hasara ya mazao.
Maelezo kwa Mwezeshaji: Swali lakuongoza
Je, kufanyike nini kuhifadhi ubora wa mazao yaliyovunwa
Taarifa ya Awali/Usuli: Hoja za kuzingatia wakati wa kuvuna kupunguza hasara baada ya kuvuna.
Muda unaofaa wa kuvuna (mazao yasiive sana)
Zuia kuharibika kwa mazao
Kutenganisha mazao yaliyoathiriwa na yenye magonjwa.
Matumizi ya aina safi ya kuvuna.
Uvunaji wa rejareja unapunguza haja ya kuhifadhina hasara ya uhifadhi
Punguza kuharibika kwa mazao wakati wa usafirishaji
54
A.14.1. Zoezi: Utayarishaji/Uhifadhi wa mazao
Mazao mapya ya kilimo yaliyovunwa (aina ya mizizi, mbogamboga na/au matunda) mara nyingi
yanaweza kusindikwa ili kuongeza muda wa kutunza/uhifadhi wa mazao. Kutegemea aina ya mazao,
kunahitajika kusafishwa kwa maji, kukatwakatwa silesi, kuchemshwa, kukaushwa (kwa jua), kusagwa
na/au kufungashwa kabla ya kuhifadhiwa mahali salama na pa kavu. Kwa wenyeji, njia mbalimbali za
kusindika huwa zinafahamika. Vijana watajadili na kufanya kwa vitendo na mwezeshaji mwenyeji njia
mbalimbali za kusindika mazao ya kilimo
Muda: Saa 1 na dakika 30
Vifaa na matayarisho: Bainisha mwezeshaji mwenyeji anayefahamu usindikaji wa mazao ya
kilimo ya chakula, mazao mapya, visu na sufuria.
Majadiliano ya wote (Dakika 20)
1. Anza mada ya usindikaji/ na utunzaji wa chakula. Jadili na vijana madhumuni ya
usindikaji/utunzaji wa chakula
2. Waulize vijana kama wanajua mifano mbalimbali ya utunzaji wa mazao ya kilimo (chakula)
inayofanywa na watu katika eneo
Vitendo (saa 1)
3. Mtambulishe mwezeshaji mwenyeji na mwombe aonyeshe na/au kufanya kwa vitendo na
vijana baadhi ya desturi za wenyeji za utunzaji wa chakula
4. Jadili njia mbalimbali za utunzaji wa chakula na kuna mahitaji gani muhimu na maeneo
yanayohitaji uzingativu maalumu katika utunzaji wa chakula (usafi, unyevunyevu na uhifadhi
ghalani/ufungashaji)
Majadiliano ya wote: (Dakika 10)
Toa muhtasari wa somo
A.14.3. Zoezi: Ghala bora
Hasara inayotokana na uhifadhi ni tatizo kubwa. Wadudu waharibifu na magonjwa yanaweza kuharibu
sehemu ya akiba kama mazao hayakuhifadhiwa mahali safi, pakavu na palipolindwa kwa ukamilifu.
Vijana watajifunza aina mbalimbali za ghala za kuhifadhia zinazotumiwa katika eneo lao kuhifadhi aina
mbalimbali za mazao ya kilimo
55
Lengo: Kujifunza kuhusu sifa muhimu za ghala bora
Muda: Saa 1 dakika 30
Vifaa na matayarisho: Kabla ya somo bainisha idadi ya ghala zilizopo karibu na fanya
mpango vijana waweze kuruhusiwa kuzitembelea
Bungua bongo (Dakika 15)
1. Anza mada ya ghala bora
2. Waulize vijana masharti muhimu zaidi ya uhifadhi na maghala ya kuhifadhia ni yapi kwamazao
ya kilimo kwa kipindi cha miezi kadhaa. Andika masharti hayo kwenye karatasi kubwa. Ongeza
masharti yaliyoachwa kwenye orodha kama inahitajika
3. Jadili masharti ya uhifadhi
Ziara (dakika 50)
4. Nenda na vijana kwenye ghala za kuhifadhia zilizopo karibu na jadili na vijana hali/masharti ya
ghala hizo. Kama ikiwezekana zungumza na wamiliki na waulize faida na hasara za ghala zao.
5. Jadiliana na vijana ni ghala gani bora zaidi waliyoioana na kwa nini ni bora.
Majadiliano ya wote: (dakika 15)
6. Toa muhtasari wa sifa muhimu za ghala ya kuhifadhia mazao
7. Jadili uwezekano wa kujenga ghala na SDSMV ya kuhifadhia mazao ya shamba darasa. Kama
ikiwezekana andaa mpango wa kazi
Maelezo kwa mwezeshaji: Maswali ya Kuongoza
Ni kiasi gani cha mazao kinapotea wakati wa uvunaji, usafirishaji na uhifadhi wa mavuno?
Je, kuna sababu gani kuu za hasara hiyo?
Je, tutawezaje kupunguza hasara hii wakati wa uhifadhi wa mavuno?
Je, tunawezaje kuzuia wadudu waharibifu na magonjwa visiingie kwenye ghala ya
kuhifadhia?
56
Je, tunawezaje kudhibiti/ kukagua ubora wa mazao yaliyohifadhiwa?
Je, aina mbalimbali ya mazao ya kilimo yanaweza kuhifadhiwa ghalani kwa muda gani?
(mapya, yasiyosindikwa)
Je, mkulima atafanya nini kuongeza muda wa kuhifadhi mazao ya kilimo?
Je, ni njia zipi zinazotumiwa zaidi katika eneo kutunza mazao ya kilimo?
Taarifa ya Awali/Usuli: Sifa muhimu za ghala2. Ghala bora haina budi kutunza mazao katika hali ya
baridi na kavu. Lazima pia iweze kulinda mazao dhidi ya panya, ndege, wanyama wa shambani na wezi.
Ghala nyingi ( isipokuwa baadhi ya ghala zenye ukuta imara za zege zinaweza kuzibwa) hazizuii kuingia
kwa wadudu
Ghala lazima ijengwe mahali pakavu, mbali na matawi ya miti, vinginevyo panya wanaweza kuruka
kutoka kwenye matawi ya miti na kuingia ghalani. Ghala lazima liwe na paa linalomwaga maji ya mvua
na lenye kivuli. Ghala hainabudi kuinuliwa juu ya usawa wa ardhi ili kuzuia maji yasinywee ghalani na
kuzuia panya na wanyama wa shambani wasifikie mazao yaliyohifadhiwa. Kama zitatumiwa nguzo za
miti/mbao kuinulia jengo la ghala ni lazima vikingwe dhidi ya mashambulizi ya mchwa, mara nyingi oili
chafu ya magari hutumiwa kuipaka miti/mbao.
Kinga dhidi ya panya lazima zifungwe kwenye miguu ya ghala kuzuia panya wasipande ghalani. Kinga
dhidi ya panya zitafanya kazi tu kama ghala itainuliwa angalau mita moja kutoka ardhini na hakuna
mimea au nguzo karibu na ghala zitakazowawezesha panya na panya buku kupanda. Ghala haina budi
kujengwa angalau umbali wa mita 1 kutoka kwenye mgongo na miti. Paka na mbwa husaidia
kuwafukuza panya
2. Chanzo: T., Namanda, S., Mwanga, R.O.M., Khisa, G., Kapinga, R. (2205) Manual for Sweetpotato Integrated Production and
Pest Management Farmer Field Schools in sub-Saharan Africa. International Potato Center, Kampala, Uganda
57
A.14.4. Zoezi: Kuuza Mazao
Muda: Saa nyingi katika masaa mbalimbali
Vifaa: Vifaa vinavyotakiwa kwa ufungashaji, utangazaji na usafiri wa mazao
Hatua:
1. Kutegemea mikakati ya soko iliyotayarishwa, saidia vikundi mbalimbali matayarisho yao kwa ajili
ya uuzaji wa mazao waliyovuna
2. Warahisishie vijana kuuza mazao yao. Waambie vijana watunze kumbukumbu zao vizuri na kiasi
cha mazao walichouza, bei waliyopata, gharama walizotumia, muda waliotumia kutayarisha na
kuuza mazao yao na faida waliyopata
3. Baada ya kuuza mazao yao, waambie vikundi wawasilishe matokeo yao ya shughuli za mauzo,
wakieleza uzoefu wote waliopata, gharama na faida waliyopata
4. Jaribu kuhitimisha masomo muhimu zaidi waliyojifunza
58
Juzuu ya 2
Mtaala wa SDSMV Mada za Stadi za Maisha na
Uanzishaji Shughuli
59
Yaliyomo:
Mada/Zoezi uk
Mazoezi ya Stadi za Maisha na Uanzishaji Shughuli
J.1.1. Zoezi: Kupanga kwa ajili ya Baadaye
J.2.1. Zoezi: Utunzaji Kumbukumbu
J.3.1. Zoezi: Kutoa maamuzi
J.4.1. Zoezi: Umuhimu wa Usafi bora
J.4.2. Zoezi: Maandalizi Bora na Usafi wa Mtu
J.5.1. Zoezi: Maji ni Uhai – Ina maana gani?
J.6.1. Zoezi: Desturi za Lishe Bora
J.7.1. Zoezi: Utunzaji wa Kumbukumbu za Ushughulikiaji Mazao
J.8.1. Zoezi: Mambo yanayolingana kuhusu kupanga biashara na kupanga katika kilimo
J.9.1. Zoezi: Kuugua na kupata nafuu
J.9.2. Zoezi: Magonjwa katika Maisha
J.9.3. Zoezi: Jaribio la Kupiga Mpira wa VVU
J.9.4. Zoezi: Mchezo wa Ugonjwa wa UKIMWI
J.10.1. Zoezi: Je, Ajira kwa Watoto ni nini?
J.10.2. Zoezi: Kutengeneza Sanamu Inayoishi
J.10.3. Zoezi: Maigizo kuhusu Ajira
J.10.4. Zoezi: Mgawanyo wa Kazi wa Kila siku wa Wavulana na Wasichana
J.11.1. Zoezi: Haki za Ardhi ya Kijiji na Mali
J.12.1. Zoezi: Kutayarisha Mkakati wa Kuuza Mazao ya Shamba Darasa
J.12.2. Zoezi: Kumtembelea Mjasirianmali
2
2
3
4
4
5
7
8
8
8
10
11
11
13
14
17
18
23
26
26
60
J.12.3. Zoezi: “P” zote (Bidhaa,Mahali, Bei, Utangazaji, Watu na Mpango)
J.12.4. Zoezi: Kuuza! Igizo Babu
J.13.1. Zoezi: Kiuzwe Bei gani?
J.13.2. Zoezi: Kutabiri Faida na Hasara
J.14.1. Zoezi: Kubungua Bongo Wazola Biashara
J.14.2. Zoezi: Uchambuzi wa Kina wa Mawazo ya Biashara
J.14.3. Zoezi: Yanahitajika Kuunda Bidhaa au Huduma
J.14.4. Zoezi: Zana za Utunzaji Hesabu za Biashara
J.15.1. Zoezi: Gharama na Faida
J.16.1. Zoezi: Kuweka Mtandao wa Utando wa Buibui
Kujitayarisha kwa siku ya mahafali
Mtaala wa SDSMV
27
29
33
36
37
41
43
46
52
57
60
61
61
Shughuli za Stadi za Maisha na Uzalishaji Shughuli
J.1.1. Zoezi: Kupanga kwa ajili ya Baadaye
Muda: Wastani wa saa 1
1. Wagawe vijana katika vikundi vya watu 8 au pungufu.
2. Kiambie kila kikundi kifikirie hadithi ( au hadithi iliyosimuliwa kwa wimbo) kuhusu umuhimu wa
kupanga kwa ajili baadaye kwenye kilimona maisha. Mpango huo hauna budi kujumuisha
maelezo mengi kuhusu watu, mahali, na hali zinazohusishwa. Wahimize watuamie kusema ,
kuimba na/au kuigiza kuwasilisha hadithi yao
3. Waambie kila kikundi kiwasilishe hadithi yao. Wahimize wasikilize hadithi nyingine kwa makini.
4. Waambie vijana watoe maoni kuhusu kila hadithi. Kwa mfano, je,ni halisi, je inafanya wajihisi
namna gani? Ni mambo gani muhimu yaliyojitokeza?
5. Vijana wakimaliza kutoa mawazo yao, wahimize watafakari mawazo hayo kwa walichokiona.
Baadhi ya maswali ya msaada ni:-
Je, hadithi zimeonyesha nini kuhusu uhusiano kati ya watu katika jamii?
Je, inaonyesha nini kuhusu mitazamo ya watu?
Je zimeonyesha nini kuhusu changamoto kubwa zaidi zinazokabili jamii?
Zingatia: Kama mbadala, wewe au mmoja wa vijana anaweza kuanza na sentensi mbili au tatu za
kwanza za hadithi. Halafu mwombe mmoja apendekeze mistarimiwili au mitatu ifuatayo. Halafu
mwambie mtu mwingine apendekeze mistari miwili au mitatu ifuatayo. Endelea kwa mtindo huo mpaka
hadithi ifikie mwisho au imeeleza hoja muhimu mbalimbali
62
J.2.1. Utunzaji Kumbukumbu
Muda: Wastani wa saa 1
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
1. Jadili na vijana umuhimu wa kutunza kumbukumbu katika kuendesha biashara (kujua kama
biashara inaingiza faida,ni mambo gani yanayohitajika, kuboreshwa siku zijazo,
kulinganishambinu mbalimbali za kazi n.k.)
2. Eleza kuwa katika shamba darasa vijana watatakiwa kupanda mazao yao kama biashara na
kwamba wanalinganisha pia desturi mbalimbali (IPM dhidi ya jodi). Kwa hiyo ni muhimu kwa
vijana kutunza kumbukumbu za kila wanachofanya kwenye shamba darasa.
3. Waulize vujana ni ainagani ya kumbukumbu wanazotakiwa kutunza na waziorodheshe kwenye
karatasi ya bango kitita (tarehe ya kupanda, kiasina bei ya mbegu, mbolea za kikaboni na dawa
za kuulia wadudu (za viumbe) walizotumia tarehe za desturi zote, muda wa kazi, (saa) zana
zinazohitajika, mavuno (kg), gharama za mauzo, fedha walizopata kwa mazao, n.k.)
4. Jadili kumbukumbu zilizoorotheshwa na kiambie kila kikundi kidogo kikamilishe orodha kwa
mazo wanayoshughulikia.
5. Kiambie kila kikundi kiwasilishe orodha yao ya mwisho ya kumbukumbu itakayotunzwa na
ongeza pale inapohitajika
6. Viarifu vikundi kwamba watatakiwa kuanza kutunza kumbukumbu kwa mashamba
yanayowahusu kuanzia sasa na kuendelea mpaka wavune na kuuza mazao/mavuno yao
7. Viambie vikundi vitunze kumbukumbu katika daftari dogo moja na kuteua mtu mmoja wa
kikundi chaokushughulikia daftari hilo la kumbukumbu.
J.3.1.Zoezi: Kutoa maamuzi.
Muda: Wastani wa saa 1 dakika 30
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
HATUA:
1. Wahadithie washiriki hadithi au elezea hali ambapo mtoto analazimika kufanya maamuzi (kwa mfano, mtoto anataka kucheza na rafiki zake, lakini mama yake anamtaka amsaidie kufanya
63
usafi wa nyumba; au mtoto mwingine ana wazazi ambao wamemweleza kuwa lazima awe mhasibu, lakini anataka kuwa dereva).
2. Waulize washiriki kuhusu maamuzi yote yanayoweza kufanywa katika hali yoyote na yaandike.
3. Wagawe washiriki katika vikundi vidogo vidogo (wavulana na wasichana). Waambie waandae mchezo wa kuigiza ambapo wataigiza mambo mawili makubwa:
A. Mtoto ambaye anafuata matakwa ya wazazi wake;
B. Mtoto ambaye anafuata ndoto zake mwenyewe.
4. Waambie kila kikundi kiiigize mchezo wao mbele ya wengine.
5. Warejeshe washiriki pamoja na waulize kuwa mambo hayo yana faida au hasara gani. Pia waulize walifanyaje maamuzi yao.
6. Waonyeshe washiriki dhana na awamu za mchakato wa kutoa maamuzi (onyesha namba kwenye ukurasa unaofuata). Waulize washiriki wanafikiri kila awamu ina maana gani:
Pokea/chunguza habari
Chambua habari
Jaribio la kutumia njia mbalimbali
Chunguza na chambua matokeo
Fanya maamuzi (pasha/amua)
DURU LA KUFANYA MAAMUZI
64
J.4. Mada Ndogo: Usafi
J.4.1. Zoezi : Umuhimu wa Usafi Bora
Muda: Saa Moja
Vifaa: Hakuna
HATUA:
1. Jadiliana na vijana umuhimu wa usafi. Waulize kama wanajua baadhi ya mifano ambayo watu
kwenye jamii yao wanapata matatizo kutokana na desturi mbaya za afya. Waambie baadhi yao
waeleze matukio/hadithi zao.
2. Kiambie kila kukindi kifanye mchezo wa kuigiza wa matukio/hadithi na kipatie kila kikundi dakika
10-15 za kujiandaa
3. Kiambie kila kikundi kionyeshe mchezo wake wa kuigiza kwa dakika 10-15. Baada ya kila igizo
kwanza kiulize kikundi walitaka kuonyesha nini halafu vikundi vyote viombwe kutoa maoni yao
4. Toa muhtasari wa mafunzo waliyopata kutokana na maigizo mbalimbali
J.4.2. Zoezi: Makuzi Bora na Usafi wa Mtu
Muda: Saa 1
Vifaa: Hakuna
HATUA:
5. Waambie vijana watayarishe onyesho kuhusu tabia mbaya na nzuri ta usafi wa mtu. Wanaweza
kutumia vifaa halisi au kuigiza tabia hizo, kwa igizo bubu.
6. Waambie vijana wengine waeleze wameona nini na kwa nini desturi hiyo ilikuwa nzuri au mbaya
7. Waulize vijana kuhusu magonjwa /maradhi mahususi yanayoweza kuenezwa au kuzuiwa na
desturi hizo, sababu kwa nini magonjwa hayo yanaweza kuenezwa na yanaweza kuenezwa kwa
nini
65
8. Jadili kama desturi zinawezekana kufuatwa mara kwa mara, na kwa nini baadhi ya desturi
mbaya zinaendelea kuwapo
9. Waulize vijana watafanya nini kufuata desturi nzuri wao wenyewe na kuwahimiza wengine nao
wafanye hivyo
J.5.1. Zoezi: Maji ni Uhai – Ina maana gani?
Lengo: Kuelewa umuhimu wa maji katika maisha yetu, na kuelewa umuhimu wa maji safi na salama kwa
usafi wetu najinsi ya kusafisha maji
1. Muda: Saa 2
2. Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea, vitu kwa ajili ya kuandaa maji ya chumvina sukari
(SRO) kwa ajili ya watu waliopungukiwa na maji mwilini kwa ugonjwa
HATUA:
1. Utangulizi na kubungua bongo (dakika 5). Je, tunaweza kupata wapi maji? Maji ya juu ya ardhi,
chini ya ardhi, hewani, ndani ya miili yetu
2. Wote: Eleza hadithi (dakika 10). Fikiria kuhusu hadithi fupi ya mtu ambaye anaugua
kipindupindu au ugonjwa mwingine inayoonyesha jinsi watu wanavyoweza kuugua kama
hawatumii maji safi na salama n.k.
3. (Wote: Majadiliano kuhusu hadithi. (Dakika 20). Kwa nini mtu anaugua? Kinatokea nini ikiwa
watu wanakunywa maji yasiyo safina kula vyakula vilivyooshwa kwa maji machafu? Kitu
ganikinasababisha ugonjwa? (kama vile, kuharisha)
Kazi ya vikundi: (Dakika 30)
Waambie wasichana na wavulana wachore njia mbalimbali ambazo tunaweza kupata na
kuambukizwa vimelea vya magonjwa, (Angalia The Support List for Topics M 3.5, about
Hygiene, Sanitation and Environment) See also the abstract of 2nd support list in the
following page.
Waambie wajadili swali lifuatalo: Hatuwezi kuishi bila maji miilini mwetu.tutawezaje kuugua
sana kutokana na kupoteza maji mwilini iwapo tutapata tatizo la kutapika na/ au kuharisha,
n.k.?
Uwasilishaji wa vikundi na majadiliano (Dakika 20)
66
Watu wanaweza kuugua kutokana na minyoo ya tumbini kutokana na kwenye mazingira ya uchafu
Wakati mwingi, minyoo ya tumbo huingia kwenye kiungo kupitia mdomo, mikono
michafu, maji yasiyochemshwa, na kutokuwa makini katika maandalizi ya chakula.
Kuna watu ambao wanaweza kuwa na spishi mbili au tatu za minyoo kwenye
matumbo yao kwa wakati mmoja. Minyoo hii hula kwenye damu yetu na chakula
chetu. Inasababisha vidonda ndani ya utumbo na kuathiri afya yetu vibaya sana,
kutufanya tuwe wadhaifu. Haituruhusu kukua kwa afya na kujifunza vizuri.
Namna ya kuepuka minyoo ya tumbo
1. Nawa mikono yako kwa sabuni mara baada ya kutoka
msalani (kumbadili vipi moto) na kabla ya kugusa chakula 2. Kunywa maji yaliyochemshwa au yaliyochujwa; 3. Osha tunda kabla ya kulila 4. Funika chakula kuepuka inzi; 5. Tumia choo kilichojengwa vizuri na kisafi. Jenga vyoo (na pia
mashimo ya maji machafu na taka) angalau umbali wa mita 40 – 50 kutoka kwenye kima chabondeni
6. Kifanyie matengenezo kisima chako, kifunike na usikitumie kutupa taka na/au kuruhusu wanyama kunywa maji kwenye kisima
7. Osha viruri vyombo vyote kabla ya kujaza maji
67
Jinsi ya kuandaa maji ya chumvi na sukari (SRO) (Mchanganyiko huu unafaa sana kama unakabiliwa na
ukosefu wa maji au kupoteza maji maji mwilini kutokana na ugonjwa )
Kama huwezi kupata mchanganyiko wa maji ya chumvi na
sukari iliyokwisha andaliwa, tayarisha kama ifuatavyo :
Lita 1 ya maji safi (yaliyochemshwa na kupoozwa)
+ chumvu ½ kijiko cha chai
+ sukari vijiko 8 vya chai
Changanya vizuri na kunywa
Mchanganyiko huu utakuwa na ladha yenye chumvi nyiingi
kidogo zaidi ya machozi
J.6. Mada Ngogo: Lishe
Malengo:
Kuelewa mambo muhimu kuhusu lishe bora
Huu ni uhusiano wa “ajabu” kwa maisha unaohusianishwa na shughuli za kilimo ambazo vijana
wamejifunza katika shamba darasa na darasani. Katika modul/somo hili, vijana wataanza kuelewa kuwa
afya yao wenyewe ni muhimu zaidi kuliko afya ya mimea yao na kwamba njia moja bora zaidi kwao
kuishi wenye afya na kwa kula vyakula bora vyenye afya
J.6.1. Zoezi: Desturi za Lishe Bora
Chakula na lishe ni muhimu katika kuweka miili yetu kuwa yenye afya. Watu wengi wanaugua kwa
sababu miili yao haina uwezo wa kukabiliana na maradhi. Ukila aina sahihi ya vyakula vya kutosha, mwili
68
wako utakuwa imara na wenye afya. Kwa hiyo ni muhimu kwa vijana kuelewa aina mbalimbali za vyakula
vyenye afya vinavyoweza kupatikana.
Muda: Wastani wa saa 2
Vifaa: Chatipindu na Karatasi
1. Waeleze vijana kuwa mwili unahitaji aina mbalimbali za chakula kuufanya uwe na afya na imara.
Uliza kama kuna kijana yeyote anayejua aina tatu tofauti za chakula. Kama hakuna waeleze
kuwa chakula kimegawanyika katika makundi matatu.
Vyakula vinavyoongeza nguvu kama vile wali/mchele, ndizi, viazi vitamu na vikuu,
sukari ya miwa, mihogo, shelisheli, mafuta ya mawese, aina mbalimbali za mkate,
na vinginevyo
Vyakula vya kujenga mwili kama vile samaki, kuku, mayai, nyama, karanga,
maharage, kabichi, maziwa ni baadhi tu
Vyakula vya kulinda mwili kama vile machungwa, mananasi, tikitimaji, tufaa, papai,
matembele, kisamvu, mafuta ya mbogamboga na nyanya
Chakula kinamakundi sita ya virutubisho vinavyotufanya tuwe na afya. Vyakula vya wanga/kabohaidreti,
mafuta, protini, madini, vitamin na maji. Tunaugua kama hatuli aina ya vyakula inayofaa
2. Waeleze vijana maana ya maneno yafuatayo:
Mlo kamili: Wakati chakula na vinywaji vinatumiwa kila siku kwa uwiano sahihi. Aina
moja isitumiwe kwa wingi na aina nyingine isiwe chache kuliko nyingine.
Lishe – wakati mtu anapokula vyakula vinavyolingana na mahitaji yamwili
Vyakula vya kujenga mwili – miili yetu inahitaji protini kwa ajili ya kujenga misuli.
Protini inapatikana kwenye nyama, samaki, kuku, karanga, koroshona maharage
Vyakula vinavyoongeza nguvu – vyakula vinavyoipa nguvu miili yetu kwa kawaida ni
vyakula vya wanga, vinavyojulikana kuwa kabohaidreti.
Vyakula vya kulinda mwili – matunda na mboga huipa miili yetu vitamin na madini
muhimu kwa ajili ya kuifanya miili yetu kuwa imara. Vitamini zinasaidia miili yetu
kukabiliana na vimelea vya ugonjwana vitu vinavyotufanya kuwa wagonjwa
3. Waambie vijana wataje aina za vyakula wanavyokula kila siku. Halafu waambie wavigawe
vyakula hivyo katika makundi matatu ya chakula kwenye karatasi ya chatipindu.
4. Waulize vijana kama matokeo yanaelekea kuonyesha mlo kamili
69
5. Wagawe vijana katika makundi matatu
“Kundi la kuongeza nguvu” “Kundi la kujenga mwili” na “Kundi la kulinda mwili”. Waambie
kila kundi liorodheshe milo kamili miwili wanayamini kwamba ni milo kamili.
6. Kila kikundi kiwasilishe milo yake na kueleza kwa nini milo hiyo ni kamili
J.7.1. Zoezi: Utunzaji wa Kumbukumbu za Ushughulikiaji mazao
Muda: Wastani wa dakika 90
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
HATUA:
1. Waambie vikundi vine tofauti watayarishe mawasiliano ya maendeleo yaliyofanywa katika
kuanzishwa mazao yanayohusika ambayo wanatakiwa kujumuisha shughuli mbili tofauti.
Waambie wajitahidi kadiri iwezekanavyo kuelekeza mawasilisho yao kwenye kumbukumbu
walizotunza (tarehe ya kupanda, ukubwa wa eneo, wingi wa mimea, n.k.).
2. Kiambie kila kikundi kiwasilishe
3. Jadiliana na vijana kuona kama kila kikundi kimeandika kumbukumbu zote zinazohitajika ili
waweze kufuatilia maendeleo yaliyofanywa na kutambua tofauti kati ya ushughulikiaji wa aina
mbili
4. Jadili umuhimu wa utunzaji bora wa kumbukumbu na matatizo yaliyokabiliwa na vikundi tofauti
katika utunzaji wa kumbukumbu hizi
5. Toa muhtasari wa mahitimisho kuhusu umuhimu wa utunzaji wakumbukumbu nzuri na
kinachohitajika kuboreshwa katika utunzaji wa kwa aina mbalimbali za mazo na ushughulikiaji
70
J.8.1. Zoezi: Mambo yanayolingana kuhusu kupanga biashara na kupanga katika kilimo
Lengo: Kupitia baadhi ya hatua za mizunguko ya mazao katika kilimo na kulinganisha hatua hizi kwa
jumla na mzunguko wa maisha ya biashara
Muda: Saa 1
Vifaa na matayarisho: Chatipindu au ubao wenye michoro ya hatua tano za biashara kama
zilivyoelezwa kwa muhtasari hapachini na baadhi ya mifano ya mimea (mazao) katika hauta
mbalimbali
Namna ya Kufanya
Pitia kilichofundishwa kuhusu hatua za maisha ya mazao katika Moduli ya 2. Rudia kueleza kwamba vitu
vyote vinavyoishi kama vile mazao hua vinapitia pia hatua mbalimbali katia maisha yake
Waulize vijana wajaribu kukumbuka kwa nini ni muhimu kabla ya kuanza kulima mazao Fulani,
kujifunzakuhusu hatua mbalimbali za ukuaji na maendeleo ya mimea (katika kila hatua,mahitaji ya
mimea yanatofautiana na tunahitaji kuzingatia masharti sahihi ya ukuaji, kwa kuwa baadhi ya hatua za
mimea/mazao zinahitaji majimengi au kidogo, mwanga wa jua, kulindwa dhidi ya wadudu waharibifu na
magonjwa na /au magugu, zinahitaji urutubishaji/utiaji wa mbolea maalumu, na kadhalika)
Pitia hatua nne tofauti za ukuaji wa mimea. Waambie vijana wakueleze tena mambo ambayo
mimea/mazao yanahitaji kukua yenye afya na kustawi vizuri. Eleza tena kwa muhtasari kwamba
kupanga katika kilimo kunaanza na uchaguzi wa mazao ya kupanda. Ni vipengele gani vitakavyoshawishi
maamuzi yako kuhusu aina gani ya mazao ya kupanda.
Eleza kwamba tunaweza kumlinganisha mkulima anayesimamia hatua kulima zao fulani na mzunguko
wa biashara. Eleza kwamba,wakati wa kufikiria kuhusu biashara, tunaweza kuwa na hatua za mipango
kama za kilimo. Eleza mifano halisi ya kuonyesha hatua tano ambazo biashara hupitia. Tumia picha au
chora michoro rahisi kusaidia kufafanua maelezo yako.
Mkulima anaanza kwa kufikiria kulima nini Tunafikiria kuhusu mawazo ya biashara
Anaanza kuandaa shamba Tunapanga na kuandaa namna ya kuweka
mawazo ya biashara katika utekelezaji
(uliza ni vipengele gani vinavyoshawishi
uamuzi kuhusu nini cha kupanga au
71
biashara gani ya kuuza)
Anapanda mbegu na miche Tunazindua au kuuza biashara (inaweza
kuwa polepole/hatua kwa hatua, kuliko
kuwa uzinduzi mmoja mkubwa)
Mimea ni lazima itunzwe Biashara inaanza kukua (ukuaji wa awali)
na baadhi ya vitu vinahitajika ili kusaidia
kukua
Mazao yanavynwa (baadhi ya mbegu
zinahifadhiwa kwa ajili ya mzunguko ujao
wa mazao)
Faida hupatikana lakini biashara ni lazima
ikue na kupanuka zaidi. Baadhi ya faida
huwekezwa kwenye kukuza zaidi biashara
Waulize vijana ni mambo ganiyanayohitajika kusaidia mimea kukua, na ni mambo gani yanayohitajika
kusaidia biashara kukua. Waambie vijana wachore hatua hizi.
Onyesha picha/michoro waliyochora vijana
Maelezo kwamwezeshaji
Kutegemea kiwango cha vijana hao, unaweza kuwauliza mapendekezo zaidikama vile kinachohitajika
kuikuza biashara (mkopo, faida, wateja,mwitikio, soko, stadi nzuri za mauzo…)
Pia unaweza kueleza kwa muhtasari tofauti za kijinsia katika usimamizi wa mazao – ni shughuli gani
ambazo kwakawaida zinafanywa na wanawake/wasichana au wanaume/wavulana katika kutayarisha
shamba na kupanda, palizi, kuvuna na kadhalika. Jaribu kuacha dhana ya mitazamo yoyote isiyotaka
mabadiliko. Sisitiza kwamba, wanawake na wanaume, wasichana na wavulana, wote wanaweza
kushirikishwa katika bishara.
Marejeo: Imechukuliwa kutoka moduli ya 1.2, Zoezi la 4, ukurasa wa 49. Bauer, S. Finnegan, G &
Haspels, N. (2004) GET Ahead for Women in Enterprise Training Package and Resource Kit.
(ILO Bangkok)
72
J.9.1. Zoezi: Kuugua na kupata nafuu
Muda: Saa 2
Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea
Zingatia: Unaweza kutaka kumshirikisha katika somo hili mwunguzi au daktari mwenyeji wa mahali
1. Waulize vijana kama wanafahamu majina yoyote yamagonjwa ya binadamu yanayotokea katika
eneolao
2. Waulize ugonjwa huo ulivyo wakati mtu anapokuwa anao
3. Andika kwenye chatipindu magonjwa yote waliyotaja
Zingatia: Unawezakuongeza baadhi ya mapendekezo, kama vijana wametaja ugonjwa mmoja au
mawili tu
4. Wagawe vijana katika vikundi na waambie wajadili maswali yafuatayo
- Unapougua, unafanya nini ili kupata nafuu?
- Je, unajua tiba yoyote kwa magonjwa uliyoyataja?
- Je, unaelewa kuhusu VVU?
- Je, unawezaje kukinga magonjwa yaliyotajwa?
- Je, kliniki/zahanati/hospitali ya karibu iko wapi?
- Je, unapougua, ni nani anayekutunza?
5. Vikusanye vikundi pamoja na kujadili
Usisahau kutaja kwamba ni muhimu kujaribu kupata matibabu wakati unapokuwa mgonjwa, na
tusijaribu kusubiri mpaka tuwe mahututi ndiyo tutafute msaada
Onyesha uhusiano kati ya walichojifunza vijana kuhusu kudhibiti/kukinga maginjwa na wadudu
waharibifu kwenye shamba darasa
73
J.9.2. Zoezi: Magonjwa katika maisha
Muda: Wastani wa saa 1 dakika 30
Vifaa: Chatipinduna kalamu za kuchorea
HATUA:
1. Waambie vijana wataje magonjwa yote yaliyopo kwenye jamii zao nakuorodhesha kwenye
karatasi kubwa
2. Chagua magonjwa mawili yanayopatikana sana (kwamfano: malaria na kuharisha). Waambie
vikundi wajadili dalili, vyanzo na namna ya kupunguza uwezekano wa kuambukizwa magonjwa
hayo. Vikundiviwili vihusike na malaria navingine viwili kuharisha
3. Kiambie kila kikundi kiwasilishe na kujadili
4. Toa muhtasari wa dalili,vyanzo na njia zinazoweza kupunguza uwezekano wa kuambukiza
magonjwa yaliyochaguliwa.
Mada ndogo: Kuelewa na Kujilinda dhidi ya VVU/UKIMWI
Malengo: Kuweza kueleza maana ya VVU na UKIMWI
Kuweza kueleza namna VVU na UKIMWI vinavyoweza kuambukizwa na madhara yake.
Kuorodhesha njia mbalimbali za kujilinda dhidi ya VVU na UKIMWI
Ni muhimu kwa vijana kuelewa jinsi ya kujilinda kutokana na magonjwa, na hususani VVU/UKIMWI.
VVU/UKIMWI ni moja ya mada tete, lakini ni muhimu kwa washiriki kuelewa ukweli kuhusu ugonjwa
huu, na vilevile wapate ujuzi wanaohitaji ili kujilinda na kuepuka kuambukizwa.
Zifuatazo ni shughuli kadhaa ambazo mnaweza kuzitumia kuwasaidia washiriki kuelewa VVU/UKIMWI.
Ingawa si lazima shughuli zote zipitiwe katika moduli hii, ni bora kuziweka kwenye mlolongo wa namna
zinavyowasilishwa.
74
J.9.3. Zoezi: Jaribio la mpira wa VVU
Hii ni shughuli inayotumia nguvu ambayo inapitia kwa haraka habari zote za msingi kuhusu VVU na
UKIMWI.
Muda: Wastani wa saa 1 na dakika 30
Vifaa: Mpira, nafasi kubwa ya wazi (ikiwezekana nje), karatasi na kalamu za kuchorea.
Hatua:
1. Waambie vijana wasimame katika duara.
2. Mshiriki wa kwanza amtupie mpira mshiriki mwingine. Mtu huyo anatakiwa kudaka mpira na kumrushia mtu mwingine na kuendelea.
3. Kama mtu atashindwa kumudu mpira (hawezi kudaka au kurusha mpira vizuri kwa mtu mwingine), lazima ajibu swali kuhusiana na VVU/UKIMWI (tazama maswali ya mfano hapo chini). Kama atajibu kwa usahihi, basi mchezo utaendelea. Kama hapana, basi mtu huyo atatoka kwenye mchezo.
4. Mchezo utaendelea hadi maswali yote yawe yameulizwa au mtu mmoja amebaki.
5. Baada ya mchezo kumalizika, kaa pamoja na washiriki na pitia kila swali tena. Eleza kila taarifa ya VVU/UKIMWI kwa makini na wahimize washiriki kuuliza maswali.
6. Waambie washiriki walinganishe kuenea na kuzuia VVU na kuenea na kuzuia magonjwa ya mazao na wanyama.
7. Wahimize washiriki kuchora kwenye karatasi au kurekodi kwa njia ya wimbo au mchezo kila moja ya taarifa kuhusu VVU/UKIMWI. Kama hawawezi kuchora au kurekodi mambo yote kutokana na muda kuwa mchache, wahimize kufanya mengi iwezekanavyo.
Maswali ya Mchezo
Kweli/Uongo: Unaweza kupata VVU mara ya kwanza unapofanya ngono. (Jibu: Kweli)
UKIMWI ni kifupi cha nini? (Jibu: Upungufu wa Kinga Mwilini)
Kweli/Si Kweli: Mara ukishapata VVU, utakuwa na VVU wakati wote. (Jibu: Kweli)
Sehemu gani ya mwili inashambuliwa na VVU? (Jibu: Mfumo wa kinga)
Kweli/Si Kweli: VVU unaweza kusambaa kwa kushikana mikono. (Jibu: Uongo)
Ina maana gani kuwa mwaminifu? (Jibu: Kuwa na mwenza mmoja wa kufanya ngono)
Kweli/Si Kweli: Mtu mwenye VVU anaweza kuishi muda mrefu kama atakula vizuri na kufanya mazoezi. (Jibu: Kweli)
Muda huu unaitwaje, mara baada ya kupata maambukizi, wakati mtu anaweza kuwa na VVU lakini bado anaweza kupima na kuonekana hana ugonjwa? (Jibu: Kipindi cha Mpito)
75
Sehemu gani ya dunia imeathirika zaidi na VVU? (Jibu: Afrika)
Njia ipi ni salama kwa 100% kujilinda kutokana na VVU? (Jibu: Kutofanya ngono, na kuwa makini kutochangia sindano, nyembe na vitu vingine vyenye ncha kali).
Kweli/Uongo: Unaweza kujua kwa kumwangalia mtu ambaye ana VVU/UKIMWI. (Jibu: Uongo)
Kweli/Uongo: Mbu wanaweza kueneza VVU. (Jibu: Uongo)
Majimaji gani ya aina mbili kati ya sita ambayo yanaeneza VVU? (Jibu: Damu, manii, maji ya ukeni, usaha na maji ya uvimbe)
Majimaji gani mengine ya aina mbili yanaweza kusambaza VVU?
Kweli/Uongo: Kondomu hupunguza hatari ya kusambaza VVU. (Jibu: Kweli)
Kweli/Si Kweli: Kina mama wenye VVU wanaweza kuwaambukiza VVU watoto wao. (Jibu: Kweli)
VVU inasimama kwa ajili ya nini? (Jibu: Virusi Vya UKIMWI)
Kweli/Si Kweli: VVU na UKIMWI ni kitu kimoja. (Jibu: Si Kweli. VVU ni virusi vinavyosababisha UKIMWI).
Kweli/Si kweli: Ugonjwa wa kuambukiza kwa ngono, huongeza hatari ya mtu kupata VVU. (Jibu: Kweli)
J.9.4. Zoezi: Mchezo wa kuenea kwa UKIMWI
Muda: Wastani wa saa 1 na dakika 30
Vifaa: Eneo kubwa la wazi, karatasi ndogo, kalamu za kuchorea.
Hatua:
1. Kwa kutumia kalamu ya kuchorea au kalamu, andika herufi A, H, C au N kwenye karatasi ndogo. (Kwa mfano, kama kuna wanafunzi 12 kwenye kikundi, wanafanya karatasi 3 za “A”, 3 za ”H”, 3 za “C” na 6 za “N”.) Kunja karatasi ili kuficha herufi zisionekane.
2. Gawa karatasi moja kwa kila mshiriki na waambie WASIFUNGUE. Waelekeze wanafunzi kutembea na kushikana mikono na watu watatu tofauti. Wakumbuke wameshikana mikono na nani.
3. Waelekeze kila mmoja kurudi kwenye nafasi yake, wakae na kufungua karatasi zao.
4. Waambie wale ambao karatasi zao zimeandikwa “H” wasimame. Waambie kuwa wanafunzi hawa wana VVU.
5. Waambie kila mmoja aliyeshikana mikono na wanafunzi wenye VVU asimame waambie kila mmoja ambaye ameshikana mikono na hao waliosimama asimame. Fanya hivyo hadi wanafunzi wote wawe wamesimama.
76
6. Waambie washiriki ambao wenye “A” wakae. Wapongeze kwa kujizuia kufanya ngono na kujilinda kutokana na VVU/UKIMWI.
7. Waambie washiriki wenye karatasi zenye “C” wakae. Kama ni watu wazima, wapongeze kwa kuvaa kondomu na kujilinda. Kwa watoto, weka wazi kuwa hawawezi kupongezwa.
8. Waambie washiriki wenye “N” kuwa hawakuwa na VVU mwanzoni mwa mchezo. Hata hivyo, kama walishikana mikono na mtu ambaye ana karatasi yenye “H” , wameshaambukizwa.
9. Eleza kuwa katika shughuli hii, kushikana mikono ni ishara ya ngono. Sisitiza kuwa katika maisha halisi, kushikana mikono hakusababishi kuenea kwa VVU. Pia, kuwa makini kuhakikisha kuwa kikundi hakiwanyanyapai wanafunzi wenye karatasi zenye “H”.
10. Baada ya shughuli hii, ongoza majadiliano kwa kutumia maswali yafuatayo kama mwongozo:
VVU vimeenea vipi miongoni mwa wanakikundi?
Hii inafanana vipi na jinsi VVU vinavyoweza kusambazwa katika jamii?
Ulijisikiaje kugundua kuwa ulikuwa na VVU?
Unafikiri watu wanajisikiaje wanapojua kuwa wana VVU?
Unajisikiaje kuambiwa kuwa ulikuwa huna VVU?
Wanakikundi wangefanyaje ili kujilinda wasiweze kuambukizwa?
11. Waambie washiriki walinganishe jinsi VVU vinavyoenea na vinavyoweza kuzuiwa, ikilinganishwa na jinsi magonjwa ya mazao na mifugo yanavyoweza kuenea na yanavyoweza kuzuiwa.
12. Pitia na washiriki masuala kuhusu VVU na UKIMWI (kutoka “jaribio la kupiga mpira la VVU/UKIMWI”). Jibu maswali yote.
13. Wahimize washiriki waonyeshe kwenye karatasi au rekodi kwa njia ya wimbo na ngoma mambo muhimu kuhusu VVU na UKIMWI
J.10. Mada Ndogo: Kupunguza mazingira hatarishi ya VVU – mchezo wa mawe ya kuvukia
Malengo:
Kuwasaidia kutofautisha kati ya ajira kwa watoto na kazi ambayo si mbaya kwao
Kujenga uelewamiongoni mwa jamii kuhusu hali za watoto wanaolazimishwa kufanya kazi badala ya kwenda kusoma shule
Kabla ya kuanza mazoezi haya, tafadhali soma “maelezo kwa mwezeshaji” wa sehemu hii.
77
J.10.1. Zoezi: Je, ajirakwa watoto ni nini?
Muda: Saa 1 – 1 na dakika 30
Vifaa: Kabla ya kufanya zoezi hili, soma Maelezo kwa Mwezeshaji kuhusu ajira kwa watoto hapa chini
Hatua:
1. Anza kwa kuuliza swali rahisi: mtoto ni nani? Fuatilia na katika umri gani unafikiri mtu si motto tena?
Maelezo: Majibu yanayotofautiana yatatolewa (kwa mfano,wakati mtuanapopitia jando na
unyago,anapo balehe au kuvunja ungo huoa au kuolewa,wanpoanza kufanya kazi,wanaondoka
nyumbani,wanapokua yatima,wanapomaliza masomo) Itakua muhimu kuhusisha kwenye maana ya
kisheria ya mtotot ili kuepuka utatizi.Kwa kawaida mtoto anafafanuliwa kama mtu mwenye umri wa
chini ya miaka 18.
Ibara ya mapato ya umoja wa mataifa kuhusu haki za mtoto inaeleza kua mototo ni binadamu yeyote mwenye umri chini ya miaka 18,isipokua kama kwa mujibu wa sheria inayohusu motto,balehe au kuvunja ungo huanza na umri mdogo zaidi.Angalia katiba ya nchi inavyoeleza
2. Fuatilia swali hili kwa kuuliza kama vijana wanafahamu kazi yoyote katika kilimo inayofanywa na watoto na kuwazuia kuhudhuria masomo au kuwachosha sana kiasi cha kushindwa kutimiza wajibuinavyopasa.Wahimize washiriki wawe wazi zaid kuhusu muda na aina ya kazi(kwa mfano:palizi kila siku kwa muda mrefu,kuchunga mifugo kuanzia alfajiri mpaka jioni ,kuwinga ndege siku nzima nyakati za masomo).Andika shughuli mbalimbaliubaoni mua chatipindu.
3. Waambie washiriki wataje shughuli zinazofanywa na watoto zinazowafanya wachoke sana,wawe dhaifu au wagonjwa au zinazowasabisha wawe na majeraha(kwa mfano,wanaweza kuwa wananyunyizia dawa ya kuulia wadudu,kubeba mizigo mizito,au palizi kwa muda mrefu).Orodhesha kazi hizo peke yake kwenye chaitpindu au ubaoni pia.
4. Halafu waambie vijana waeleze shughuli ambazo mara nyingi zinafanywa na watoto ambazo zinawafaa na wanajifunza stadimuhimu. Mfano inaweza kuwa ni kuwasaidia wazazi kuvuna.au palizi kw muda mfupi mwisho wa wiki au kujifunza shughuli kuhusu shamba/uwanja wa PROKA ADESUA orodhesha shughuli hizi pia.
5. Pitia orodha zote tatu tofauti na eleza kuwa kwa kawaida tunatumia neon ajira kwa watoto(au neon linalolingana linalotumika nchini)Ueleze aina ya kazi zililozotajwa kwenye orodha mbili za kwanza.Unaweza kutumia taarifa ya hapa nchini pia kama maelezo ya mwezeshaji ya 1.
78
Maelezo: Kusema kweli neon “ajira kwa watoto”linahusu kuwatumia watoto katika kazi na shughuli
zisizokubalika na jamii na kiuadilifu.
Kwa mfano inaweza kuwa ajira kwa watoto kama mtoto:
Anafanyakazi muda wote badal a ya kua shuleni
Anahusishwa kwenye kazi nyingi kwa muda mrefu.
Anafanya kazi hadi usiku sana.
Anafanya kazi katika hali na mazingira mabaya(hakuna chakula au maji au joto kali).
Anafanya kazi kwa vitisho(kupigwa au kulazimishwa kufanya kazi).
Anafanya kazi zaidi na malipo anapewa mtu mwingine.
Kwa maelezo zaidi angalia.Facilitators Notes 1: Basic Facts about Child Labour.
6. Anza majadiliano na watotoau walezi wao.Tumia maswali yafuatayo kuchochea majadiliano:
a) Kwa jumla wakati wa umri gani wenyeji wanafikiri kama ajira kwa watoto inajadiliwa?
Je,inaweza kua wasichana au wavulana au wote?
b) Je,ajira kwa watoto iko wapi? Ni sehemu gani ya nchi yetu au wilaya gani au miongini mwa
makundi gani ya watu?.
c) Je,wafanyakazi watoto wanalipwa? Je,wanaweza pia kufanya kazi bila malipo?.
7. Toa muhtasari na jaribu kuhakikisha kuwa imeeleweka vizuri kuwa ajira kwa watoto ni nini na ipi
si ajira kwa watoto.
79
Maelezo kwwa wawezeshaji: Ajira kwa Watoto
Watoto wanafanya kazi na shughuli nyingi tofauti.Baadhi ya kazi hizo ni za kuchosha.
Baadhi ni ngumu na zinahitaji bidii na na umakini nyingine ni hatari sana na si halali kiuadilifu.
Si kazi zote zinazofanywa na watoto zitahesabiwa kwa kuwa ajira kwa watoto ambazo ni lazma
zilengwe kutokomezwa.
Ushiriki wa watoto au vijana wa umri mdogo katika kazi isiyodhuru afya yao na maendeleo na
makuzi yake au isiyoingilia masomo,kwa kawaida inahesabiwa kuwa si mbaya.Kazi hiyo
inajumuisha shughuli kama kama vile:
- Kuwasidia wazazi/walezi.
- Kuasaidia biashara ya familia:au
- kujipatia fedha za matumizi baada ya saa za masomo na wakati wa likizo za shule.
Shughuli za namna hii zinachangia makuzi,maendeleo ya motto na ustawi wa familia zao.
Shughuli hizi huwajengea watoto stadi na uzoefuna kusaidia kuwaandaa kuwa wazalishaji mali
wakati wanapokuwa watu wazima.
Neno “ajira kwa watoto” mara nyingi linafasiriwa:
i. Kazi inayowanyima watoto utoto wao.
ii. Uwezo wao.
iii. Hadhi yao; na
iv. Yenye madhara kwa ukuaji wa mwili na akili.
Ni kazi ya hatari na yenye madhara kwa watotokiakili,kimwili,kijamii au kiuadilifu;na inaingilia
masomo yao kwa:
v. Kuwanyima fursa ya kuhudhuria masomo;
vi. Kuwalazimisha kuacha shule kabla ya kumaliza;au
vii. Kuwataka wajaribu kuchanganya mahudhurio ya shule na kazi nzito za muda mrefu.
Ikiwa katika namna mbaya zaidi,ajira kwa watoto inahusishwa kufanywa
mtumwa,kutenganishwa kutoka familia zao,kufanya kazi kutoka katika mazingira ya hatari zaidi
80
na ugonjwana/au kutelekezwa wajikimu wenyewe kwenye mitaa ya miji mikubwa-mara nyingi
katika umri mdogo sana.
Iwe ndiyo ama hapana aina mahususi ya kazi inaweza kuitwa “ajira kwa watoto”inategemea,
- Umri wa mtoto,
- Aina na muda wa kazi inayofanywa;na
- mazingira yanayofanyiwa kazi.
Jibu linalotofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine,pamoja na miongoni mwa sekta za nda ni
ya nchi
8. Viulize vikundi kama wanafikiri zifuatazo zitakua hali/mazingira ya ajira kwa mtoto au hapana.
a) Mtoto wa umri wa miaka 12 anamtunza motto wa dada yake kwa muda wa saa mbili baada ya
kutoka shule (hapana)
b) Msichana mwenye umri wa miaka 9 anaham ia kwenye nyumba ya jamaa husaidia kazi za
nyumbani,na haendi tena shule(ndiyo).
c) Mtoto mwenye umri wa miaka 10 antumia siku nzima kufanya kazi shambani kila siku ya
wiki(ndiyo)
d) Mvulana mwenye umri wa miaka 13 anongozana na kaka yake kwanye safari ya kuvua kwa siku
2 -3 wakati wa likizo(hapana,alimradi safari za kuvua haziingilii mara kwa mara mahudhurio ya
shule).
e) Mtoto mwenye umri wa miaka 15 aliyeajiriwa kunyunyizia aina zote za dawa za kuulia wadudu
bila ya mavazi ya kujikinga na hana mahali pa karibu pa kunawa na kuoga(ndiyo)
J.10.2. Zoezi: Kutengeneza sanamu inayoishi.
Muda: Saa 1
Vifaa na matayarisho: Utakuwa umesoma maelezo kwa mwezeshaji kuhusu ajira kwa
watoto mwisho wa mada ndogo.
Hatua
1. .Eleza kwa muhtasari baadhi ya vipengele vizuri vya kufanya kazi za kilimo kwa mfano kua
nnje kwenye hewa safi;huchangia kwenye uhakika wa chakula;kuweza kuongeza thamani ya
81
ziada kwenye milo;huhisi mafanikio katika kulima mazao;kuwa karibu na maumbile kuliko
kuishi mjini;hupata maarifa kuhusu kilimo…
2. . Rudia maana ya ajira kwa watoto na isiyo ajira kwa watoto.
3. Tenga nafasi katikati ya chumba au tumia nafasi ya wazi nje.
4. Kila mwan afunzi lazma achague mwenzi.
5. waleze wanafunzi,wajipange kwa jozi,na kwamba mmoja wa wenzi atatakiwa aigize bvaadhi
ya kazi za kilimo(kwa mfano,kunyunyiza dawa,kuinamisha mabega,kuinua mizigo
mizito,kujikuna,kuvuna chini ya maji,kutembea masafa m arefu na wanyama),wakati
mwenzi wake lazma aigize matokeo mabaya yanayowezokana ya shughuli hai (kwa mfano
kukohoa,maumivu ya mgongo kujikata)
6. Zipatie jozi wastani wa dkika 10, kukubaliana kuhusu jambo la kuigiza.
7. Unda duara na waambiae wenzi hao,mmoja baada ya mwingine,kutengeneza sanaa zao
katikati kwa ajili ya washiriki wengine. Sema “ganda”baada ya dakika chache ,halafu waache
jozi waeleze ni shughuli gani na matokeo mabaya wliyokua wakiigiza.Jadili kama matokeo
huenda yakatokeamara baada ya shughuli au baada ya kipindi kirefu.
8. Wape vijana fursa ya kuzungumzia kuhusu dalili za afya mbaya na majeraha.Baadhi ya dalili
ya afya mbaya inaweza isihusiane na kazi ya kilimo hata hivyo itabidi pia iorodheshwe.Kwa
mfano UKIMWI na VVU ;utapia mlo,mafua ya nguruwe n.k. Mwezeshaji anaweza
kufafanua baadhi ya majeraha au taja majeraha mengine yanayohusiana.Himiza majadiliano
kuhusu uchunguzi wa familia kutoka kwenye zoezi.
9. Anzisha majadiliano kuhusu namna utakavyopunguza hatari katika kilimo.
J.10.3. Zoezi: Maigizo kuhusu ajira kwa watoto
Kwa kuigiza matukio na hali mbalimbali za ajira kwa watoto,washiriki wa SDSMV lazima waingie kwa
wahusika wawaelewe na kujaribu kufuatisha hisia hisia zao.Vijana wanaweza kutumia uzoefu wao
wenyewe moja kwa moja hali na matukio ya vijana wenyewe ambayo yanaweza kusababisha
makabiliano makali.Maigizo yaliyomo kwenye zoezi hili yanaweza kufanywa kwa vijana wa SDSMV na
mbele ya jamii pana wakiwemo walezi.
Muda: Wastani wa saa 2
Vifaa na matayarisho: Andaa baadhi ya mpangilio wa matukio yanayoweza kuigizwa na watu
wawili wawili au watatu yanayohusu motto anayetumiwa katika ajira kwa mtoto .katika kurasa
zifuatazo kama mifano mine inayotolewa kwenye maboksi.mifano hii inaweza kubadilishwa au
kutumika kilingana na hali ya mahali husika.Kinyume chake,waambie vijana wabuni mpangilio
wa matukio yao wenyewe.
82
Mambo yafuatayo hayana budi kusisitizwa
- Jaribu kuepuka kadiri iwezekanavyo kuonyoesha taswira mbaya tu ya kazi za kilimo au
uthikitisho kwamba kilimo ni kwa ajili ya vijana walioacha shule tu.
- Hakikisha kwamba ujumbe katika igizo unazingatia maadili ya mahali kuhusu wajubu na
kazi za watoto kuwasaidia wazazi.
- Majadiliano yanye kuhoji ya kutosha hayanabudi kufanywa baada ya igizo.Hii itampa
fursa mwezeshaji na wale waliohusishwa kuibua masuala mapya.Mara nyingi fanya
majadiliano au midahalo na watazamaji baada ya igizo.
Kisa cha 1: Dembe na Mjomba wake (waigizaji wawili).
Dembe “ameazimishwa na wazazi wake kuishi na kufanya kazi kwenye shamba la ndugu sehemu
nyingine ya nchi
Ndugu walimchukua na kwenda nae mbali.Aliwahi kusikia majadiliano Fulani kati ya baba yake na
‘mjomba’wake kuhusu deni la fedha lakini hakuelewa
Dembe hawafahamu vizuri ndugu hao, na anapewa kazi mara baada ya kufika. Kazi yake kuu ni
kukata majani makavu ya migomba na mashina. Anatumia tawi dogo la mti lililopasuliwa kidogo
na kisu kilichochomekwa kwenye mpasuko huo katika pembe mraba. Kutwa nzima
anachuchumia na mti huo naa kujaribu kuvuta majani makavu ya juu ya mgomba hadi ubavuni
mwa shina. Baada ya siku chache anakabiliwa na maumivu mgongo, kiuno, mabega na kujisikia
mchovu sana – kazi hii inachosha sana. Ameumwa sana na wadudu na hivyo kuwashwa. Wakati
mwingine huwa anasaidia kukata na kubeba chakula cha mifugo.
Anapokuwa shambani,hana maji ya kutosha. Anahofu kwamba maji yenyewe si safi na salama.
Anafikiria sana kuwa mbali na kwao na kukosa masomo. Mara nyingi anafikiria namna ambavyo
angependa kurudi shuleni, lakini anaogopa kuwa atakuwa nyuma kimasomo kama akiamua
kurudi shule hivi karibuni. Siku moja Dembe anaamua kumwuliza mjomba wake shambani
kuhusu matarajio yake ya baadaye…
o Mhusika wa 1 anamwigiza Dembe akifanya kazi
o Mwigizaji 1 ni mjomba wake anayekuja kukagua kazi ya Dembe. Halafu Dembe
anamwuliza mjomba wake kuhusu matarajio yake ya baadaye.
83
Kisa cha 2: Dando, Lumusi na Baba na mama yao
(waigizaji wakuu wanne)
Kaka (Danso) na dada (Lunusi) wafanyakazi katika shamba la wazazi wao kila siku baada ya kutoka
shuleni. Wote wanafurahia kazi hiyona kila mara wanabadilishana hadithi kuhusu marafiki zao wa
shuleni waliofanikiwa kufanya mashamba yao yawe na faida sana kwa kupanda mazao mbalimbali na
kuwekeza kwenye vitu mbalimbali. Danso na Linusi mara nyingi wanashangaa kwa namna familia
nyingine zinavyomudu. Danso na Linusi wana ndugu zao wanne wa kike na wakiume. Wazazi wao
wanashughuli nyingi sana za kuhakikisha wanatimizamahitaji ya nyumbani. Baba yao haoni sababu ya
Danso na Linusi kuendelea na masomo kwa kuwapo na shughuli za shamba za kutosha. Wanabishana na
kujadiliana kwa pamoja kuhusu suala hili.
Danso na Linusi wanajaribu kumshawishi baba yao kwamba lazima waendelee na masomo na kujaribu
kumwambia mama yao asaidie kumshawishi baba yao. Lakini ni vigumu kubishana na baba yao. Kuna
kazinyingi za kufanya na unahitajika msaada. Chakula ni haba na zaidi ya mahitaji ya kila siku, watoto
hao wanatambua kuwa wanahitaji fedha pia kwa ajili ya shule
Mwigizaji wa 1 ni Dando, Mwingine ni Linusi na wote wanajaribu kumshawishi baba yao (mwigizaji
mwingine). Mtu mwingine anaweza kuwa ni mama, anayeona si rahisi kubishana na baba.
Baadaye Danso anafikiria kwenda kufanya kazi kwenye shamba kubwa lililopo jirani ili apate fedha
zitakazomwezesha kutimiza mahitaji yake ya shule bila ya kuwaomba wazazi wake. Linusi anafikiri
kwamba kama Danso atafanya kazi hiyo, hatakuwa na muda tena wa kwenda shule. Linusi anajaribu
kushauriana na Danso…
84
Kisa cha 3: Pranab baba yake na Msimamizi
(waigizaji wakuu watatu)
Pranab,mvulana mwenye umri wa miaka 12 anafanya kazi pamoja na baba yake kama mfanyakazi
anayelipwa mshahara. Leo wanawasili kwenye shamba linalomilikiwa na familia pamoja na baadhi ya
wafanyakazi wa ajira kamili na ajira ya muda. Mmiliki wa shamba amefika kijijini kwao juzi usiku
akiwaambia kwamba anahitaji msaada shambani kwake. Pranab na baba yake walipakiwa kwenye gari la
mmiliki wa shamba na kuteremshwa shambani
Leo asubuhi shambani hapo dawa za kuulia wadudu zinachanganywa na zitatumika baadaye. Pranab
amepewana kazi ya palizi na kuwinga ndege. Watoto huwa hawaruhusiwi kuchanganya dawa za kuulia
wadudu kwa kuhofia kumwaga au kuifuja. Baba yake Pranab,ambaye hajui kusoma, anamsaidia
mfanyakazi wa ajira kamili kushughulikia na kuchanganya dawa za kuulia wadudu. Pranab anamwona
baba yake. Ingawa Pranab amesoma kidogo na anasikia dawahizi za kuulia wadudu zinaweza kuwa na
hatari na kuona kuwa baba yake havai glovu. Anamjua mtu aliyetokwa na upele mwingi kutokana na
kufanya kazi kwenye shamba hilo mwaka jana. Kusema kweli Pranab anakumbuka mawingu madogo
au ukungu wa mvule hewani yaliyokuwa yakipeperushwa kuelekea alikokuwa akipalilia. Anakumbuka
hisia ya “kukosa hewa”. Lakini baba yake Pranab yuko tayari kunyunyuzia/kupulizia dawa. Pranab
anakwenda kule ambako baba yake na msimamizi wa wafanyakazi wanakofanyakazi. Pranab anajaribu
kuzungumza polepole na baba yake kuhusu dawa za kuulia wadudu, lakini msimamizi wa wafanyakazi
anasikia na yuko tayari kuwafukuza kazi kama hawaendeleina kazi. ..
o Mwigizaji wa 1 ni Pranab anayepalilia na kuwinga ndege
o Mwigizaji Mwingine ni Baba yake Pranab anayechanganya dawa za kuulia wadudu
o Mwigizaji wa tatu ni msimamizi wa wafanyakazi aliyekasirishwa na uingiliaji kati wa Pranab.
85
Kisa cha 4. Miremba na bibi yake
(waigizaji wakuu 2-4)
Mama yake Miremba amefariki. Baba yake alikuwa mvuvi na alikuwa na watoto wengi. Watoto
hawaendi shule kwa hiyo bibi yao aliamua kuwapeleka wakaishi kwa “ndugu”
Miremba ana umri wa miaka 11 (mwigizaji 1). Hivi sasa anaishina familia yenye watoto watatu. Familia
hiyo ina shamba dogo. Mkuu wa kaya anafanya kazi mahali fulani katika mji wa karibuni. Anamfanya
akose raha. Mke wake ana genge dogo. Hana tatizo lakini Miremba anampa kazi nyingi sana. Kila siku
Miremba anafagia nyumba, kuosha vyombo, anatumwa, kufua, kuteka majina kupika na kuandaa
chakula. Miremba anatarajiwa pia kutunza miche na palizi, pia anakusanya makonokono na wadudu
waharibifu
Kaya ina ng’ombe wawili na Miremba anatumia muda kulisha mifugo pia, kuwapeleka malishonina
kuwatekea maji. Wakati mwingine anafanya kazi kwa saa 12 kwa siku, na haelekei kupumzika kutokana
na kazi nyingi. Wakati mwingie anapopeleka ng’ombe malishoni anazungumza na msichana (mwigizaji
mwingine) anayeishi jirani ambaye pia ni mtumishi wa nyumbani. Mara nyingi wanajadiliana bei ya
maziwa katika mji wa jirani. Msichana huyo alimwambia kuhusu utengenezaji wa kutokana………… na
maziwa.
Hivi karibuni Miremba amekuwa akisumbuliwa namaumivu ya kichwa na kusikia kizunguzungu na
maumivu ya mgongo. Alijikata kidole kwa kisu kikali kwa bahati mbaya wakati alipokuwa akipika chakula
na kidonda hicho bado hakijapona kwa ukamilifu. Kidonda kinauma sana wakati anapobeba vitu na
wakati mwingine anapolima na kupalilia.
Chakula na malazi ya Miremba ndiyo malipo yake kwa kazi zote anazofanya, na anajua kwamba kama
hatakaa au analalamika, ataishia kuzurura mtaani.
86
Miremba hajarudi kwao tangu afike na hana uhakika kuwa amekaa hapo kwa muda gani. Leo bibi yake
anakuja kumtembelea. Hajui atamwambia nini bibi yake. Je, amwambie kuhusu mkono wake? Kwa
vyovyote vile bibi yake ataona. Je, amwambie kwamba kazi ni kubwa na nyingi? Bibi yake anawasili…
(mwigizajimwingine)
o Igiza mazungumzo kati ya Miremba na msichana mwingine
o Igiza mazungumzo kati ya Miremba na bibi yake kama vile
o Unaweza pia kuongeza waigizaji wengine kama vile mwanamke anayemfanyiakazi
Miremba na mume anayemkosesha raha Miremba
Hatua:
1. Anza kwa kueleza dhana ya igizo waeleze kwamba watatarajiwa kuigiza hali inayoonyesha mtoto
aliyekata tama kutokana na kazi. Soma mpangilio wa matukio kwa vikundi vya watoto na
waeleze kwa makini matukio hayo.Wapangie nafasi za kuigizza kuhakikisha kwamba kila mmoja
anashiriki,bila kujali udogo wa nafasi hiyo,wateue waigizaji wengine kwa kila tukio
(mwajiri,walezi wafanya kazi wengine na kadhalika).
2. Eleza kua wataigiza mchezo kwa vijana wenzao na walezi watakua watazamaji/hadhira.Lazima
waseme kwa sauti inayoeleweka na polepole.Lazima watumie mbinu za msingi za
drama/maigizo,kamakama vile kutokuwapa mgongo wazamaji/hadhira.Lazima watie chumvi
miondoko yote na vitendo.
3. Vipatie vikundi nusu saa au zaidi kwa ajili ya kuandaa igizo fupi kuhusu mpangilio wa matukio
uliyowasomea.Kama wakipenda waruhusu waendeleze zaidi maigizo hayo.
4. Vikundi vikishakua tayari kuigiza waalike watu wote wakiwemo walezi(pamoja na eneo
litakalokua jukwaa).Ttayarisha orodha ya mfuatano wa igizo.Hakikisha kwamba vikundi vyote
vinaangaliana wakati wa igizo.Kwa igizo la kwanza unda mazingira yatakayowawezesha watu
wengine kujua hali hiyo inahusu ninikwa kila igizo lipatie waigizaji wake.
5. Kila kikundi cha waigizaji lazima kipewe muda wa kati ya dakika 5 hadi 10 kuigiza.Simamia muda
Baada ya maigizo:
6. Ashiria mwisho wa maagizo na waambie watoto watoke kwenye uigizaji wao.Washukuru
waigizaji wote na waambie walivyojihisi kuhusu igizo.
87
7. Waombe maoni watazamaji waombe mawazo kuhusu wanachotakiwa kufanya watoto kwenye
maigizo.Waulize namna hali hiyo inayohusisiana na maisha ya watoto waliowazungumzia.
8. Ongoza majadiliano kuhusu kilichokua kinafanyika katika maigizo.Toa muktasari wa hoja
muhimu zilizotolewa.
MAREJEO: Adapted from ILO-IPEC (2002) SCREAM Stop Child Labour Module entitled “Role-play” (Author: Nick Grisewood),
and Activity Six Charades Game pp 43-44 Gender Equality and Child Labour, A participatory tool for facilitators. Amorim, A.,
Samouiller, S. Badrinath, S. & Murray, U. (2005) ILO/IPEC Geneva
J.10.4 Zoezi mgawanyo wa kazi kila siku wa wavulana na wasichana.
Katika zoezi hili ,vijana wataanza kuelewa shughuli mbalimbali ambazo wanaume/wavulana na
wanawake/wasichana hufanya.Pia wataona jinsi mgawanyo wa kazi katika kaya nyingi
unavyowaongezea wanawake na wasichana kazi nyingi zaidi za kufanya kwa ajili ya ustawi wa
kaya.Watajifunza zaidi athari iliyopo wakati watoto wanapotakiwa kuanza kufanya kazi za
shamba au kaya na hawana nafasi tena ya kwenda shule.
Muda: Wastani wa saa 1 na dakika 30.
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea.
1. Anza kueleza kuwa inafurahisha kuangalia mambo yanayotokea katika siku kwa wavulana na
wasichana katika jamii wakati wanapofanya kazi au wanapokwenda shule.
2. Waonyeshe washiriki jinsi ya kuchora Saa ya kazi za kila siku(tazama mchoro hapo
chini)kasha wakiwa katika vikundi vidogovidogo na vikundi mchangsnyiko(wavulana na
wasichana),waambie kila kikundi wachore saa ya kazi za kila siku,moja kwa wavulana na
nyingine kwa wasichana.Lazima waeleze sifa za mvulana na msichana huyu( umri na aina ya
kaya wanayoishi:Lazima wabaki wakati mkuu wa kaya anapokua
mzee,mwanamke,mwanaume au mtoto).
3. Vigawe vikundi,eleza kuwa nusu ya vikundi wachore saa kuonyesha mtu huyo(msichana au
mvulana)anafanya ninoi anapokwenda shule katika siku ya msimu wa mvua na wengine
watafanya hivyo kwa msichana na mvulana ambaye haendi shule na atatakiwa afanye kazi
shambani au nyumbani msimu wa mvua.Bila shaka mwezeshaji atasoma mifano miwli
ifuatayo ya msichana na mvulana wakifanya kazi.
88
Kisa cha 1: Gyan.
Gyian ni mvulana mwenye umri wa miaka 10 au 12,hana uhakika.Amekua akifanya kazi kama mtumishi
wa nyumbani na mchunga ng’ombe kwa kipindi cha miaka miwili.Kila siku anaanza kazi saa 12 asubuhi
kwa kufagia nyumba,kujaza ndoo za maji kusafisha varanda na sakafu,kutayarisha chai,anasidia kupika
na kuhakikisha kwamba watumishi sita mhadi saba watu wazima wamepata maji ya kuoga na chakula
ifikapo saa 1:00 asubuhi,wanapoondoka kwenda kazini.Halafu anchunga ng’ombe.Anafanya kazi
nyingine ndogondogo mpaka saa 7.00 mchana na kwa kawaida hupata saa chache za kupumzika
mchana.Jioni,anafanya kazi ndogondogo mpaka mnamo saa 2.00 usiku ambapo kwa kawaidahumaliza.
Gyan anlipwa kiasi cha us$2.70 kwa mwezi kwa kazi zote hizi.Anawapa wazazi wake kiasi fulani cha
fedha hizi na kutumia kiasi kilichobaki kwa ajili yake.Kila siku yumo kazini kuanzia saa 12.00 asubuhi
hadi saa 2.00 usiku,siku saba kwa juma.Gyan hajasoma shule.
Kisa cha 2: Pia
Pia alianza kufanya kazi akiwa na umri wa miaka 11 na kuhama kutoka kwenye nyumba ya familia
yao.Mwajiri wake alimwahidi mama yake kwamba atamlea Pia na kumtendea vizuri.Kuishi nyumbani
kwa mwajiri ni anasa zaidi kuliko kule aliko kulia Pia ,ambako ilikuwa nyumba ndogo ya udongo.Hata
hivyo,Pia anatakiwa kufanya kaazi kwa saa 12 kila siku,na hapati muda wa kutosha wa kupumzika.
Pia anaamka saa 11.00 alfajiri na kwenda kuleta maji kisimani kabla kaya hajaamka.Halafu anatayarisha
chai kwa kila mtu.Inapofika saa 1.00 chai tayari kutokana na hali hiyo,shughuli kuu anazofanya Pia kila
siku ni kuosha vyombo,kupika/kutayarisha vyakula vingine,kusafisha nyumba,kufua na kurekebisha
nguo.Anawalisha kuku,kukamua ng’ombe maziwa na kupalilia bustani ya mboga.Kupika na kuandaa
chakula kunachukua muda mwingi na lazima kufanywe mara tatu kwa siku,kutegemea nani anafanya
kazi na kula nyumbani siku hiyo.
Pia anaosha vyombo na kwenda kuteka maji angalau mara tano kwa siku.Kkisima hakiko mbali
sana,lakini ndoo anzotumia ni nzito.Pia kwa kawaida anafanya kazi katika bustani ya mboga mchana
89
wote kabla ya wakati wa kuanza kutayarisha chakula cha jioni.Anapopalilia na kuwinga
kuchakuro/kindh na sungura.
Mshahara wake ni anapewa zawadi ndogondogo(kama vile nguo)na wakati mwingine,fedha
kidogo,lakini hapewi fedha mara kwa mara.Pia inabidi afanye kazi hata akiwa mgonjwa.Pia,hana muda
wa kwenda shule,lakini.kisirisiri anapenda kusoma.
4. Waambie wana kikundi wachore duara kubwa linalofanana na saa kwenye ardhi au kwenye
karatasi.Eleza kuwa duara linawakilisha saa inavyoonyesha saa 24 na kua vijana watawekea
alama kila shughuli kwenye duara kulingana na wakati inapofanyika.kama kuna shughuli
ambazo zinafnyika kwa wakati mmoja.kama malezi ya mtoto na kulima bustani,zitajwe kwa
pamoja katika nafasi ya mudammoja.Eleza kua itawabidi kutumia taswira kuwakulisha
shughuli mbalimbali ili saa ieleweke kwa kila mtu.
5. Wape fursa kila kikundi kuwasilisha saa zao.
6. Waombe wana vikundi walinganishe siku ya mvulana na msichana,na aina za shughuli(kazi
na mapumziko).Masuala yafuatayo yatakusaidia katika kuwezesha majadiliano
Muda umegawanyika vipi katika saa?
Muda gani umetumika katika shughuli ambazo zinaingiza fedha?
Muda gani unatumika kwa shughuli za uzalishaji wa chakula?
Muda kiasi gani unatumika kwa ajili nya kazi za nyumbani na nani anafanya
sehemu kubwa ya kazi hizi?
Je,kuna shughuli zozoze za jamii zinazofanywa?
Vipi kuhusu muda wa mapumziko?
Je,kuna muda mkiasi gani kwa ajili ya kulala? Muda huu unabadilika kiasi
gani katika misimu mbalimbali ya mwaka?
Saa za wasichana na wavulana zinaweza kulinganishwa vipi?Je,wanafanya
mambo tofauti?Wanatumia muda kiasi gani kwa kila shughuli?
Je,ukubwa wa kazi zao utaathiri mahudhurio yao katika shamba ,darasa na
stadi za maisha kwa vijana?
Tufanye nini ili kuhakikisha kuwa hata wasichana/wavulana wenye kazi
nyingi zaidi wanaweza kushiriki shuleni na kwenye SDSMV?
90
MIFANO YA SAA SHUGHULI ZA KILA SIKU
J.11. Haki za Ardhi na Mali.
Haki za ardhi na mali masuala muhimu wakati mtu anapoanza kupanda mazao.Mkulima
anahitaji ardhi,zana za kilimo,ghala za kuhifadhia na nk.Kuweza kuanza shughuli zao wenyewe za
kilimo.
Haki za Ardhi na mali huandaliwa kupitia kanuni na sheria.Hasa kwa ardhi ya kilimo vijijini,sheria
na kanuni za kimila bado zinatumika(hasa kwa ardhi ya kijiji).Sheria na kanuni hizi za ardhi
hutofautiana katika sehemu mbalimbaliza Tanzania .Kwahiyo kwa wakulima vijana kuelewa kwa
ukamilifu kuhusu sheria na kanuni za mahali zinazohusu haki za ardhi na malinna,kwa maana
hiyo,kuna kuna uwezekano gani kwao kupatiwa ardhi na kuweza kuanza shughuli zao za kilimo.
91
J.11.1.Haki za Ardhi ya kijiji na mali.
Muda: Saa 1 na dakika 30
Vifaa matayarisho:Chatipindu na kalamu za kuchorea,mwalike kiongozi wa jadi wa kijiji
au ofisa wa kijiji anayehusika na haki na mali(kutoka kwenye ofisi ya mtendaji/kiongozi
wa Jadi au ushirika).
Htua:
1. Anza na mada ya haki za Ardhi na Mali.Waambie vijana wataje ardhi yote na mali
vinavyihitajika kua dhamana ya shughuli ako mwenyewe za kilimo(ardhi,maji ya
kumwagilia,zana,,usafirishaji,ghala za kuhifadhia nk).Viorodheshe kwenye karatasi.
2. Waulize vijana wavyofikiri wataweza kufanya mpango wa kupata mali zote hizi
zinazohitajika wakati watakapoanzisha shughuli zao wenyewe za kilimo.
3. Mtambulishe kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji na mwambie aeleze sheria za
mahali hapo ni zipi kuhusiana na haki za Ardhi na mali zinazohusu vitu vilivyotajwa
hapo na vijana.
4. Washawishi vijana wamuulize maswali kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji
kuhusu namna gani,hasa vijana wenye dhamana ndogo/fedha,watakavyopata ardhi
na mali vilivyoorodheshwa kwa ajili ya kuazishwa shughuli zao wenyewe za
kilimo(kukodi,kupitia ndugu,kama kikundi nk).
5. Muulize kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji atawasaidiaje vijana wanoshiriki
katika SDSMV kupata ardhi na mali inayohitajika kwa kuanzishwa shughuli zao
wenyewe za kilimo.
6. Toa muhtasari wa mahitimisho ya majadiliano kuhusu haki za ardhi na mali.
J.12. Mada ndogo: uuza mazao
Vijana wanaoshiriki katika SDSMV watajifunza baadhi ya stadi za kazi kuuza kwa kuuza sehemu
ya mazao kutoka kwenye shamba darasa lao.Ili waweze kufanya hivyo,kwanza watatakiwa kujua
watamuuzia mazao hayo nani na wapi,watauza kwa mashwrti gani,kwa bei gani n.k.
92
J.12.1.Zoezi: Kutayarisha mkakati wa kuuza mazao ya shamba darasa.
Muda: Saa 2
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Hatua:
7. Waarifu vijana kwamba wanatarajiwa kuuza sehemu ya mazao yao kutoka katika
shamba darasa na kwamba wanatakiwa kutayarisha wakati wa kuuza
8. Waambie vijana waketi kwenye vikundi vyao vidogo na waorodheshe masuala yote
muhimu wanayoweza kuyafikiria na kufanya uamuzi ni lini watauza sehemu ya
mazao ya mavuno wanayoyamiliki katika shamba darasa
9. Waambie vikundi vidogo wawasilishe na kujadili orodha ya mwisho ya masuala
muhimu yanayohusu kuuza mazao yao (watauza lini, wapi na watamuuzia nani,
ubora unaotakiwa, ufungashaji unaotakiwa, usindikaji, bei n.k.
10. Waambie vijana warudi kwenye vikundi vyao na kushughulikia maelezo kwa kila
suala linalohusu kuuza mazao ya mavuno wanayomiliki katika shamba darasa
11. Waambie kila kikundi kiwasilishe rasimu yao ya mkakati wa kuuza mazao yao
J.12.2. Zoezi: Kumtembelea Mjasiriamali - Je, walifanyeje?
Mjasiriamali aliyefanikiwa kiasi anakaribishwa kueleza amefanya nini hadi kufanikiwa kwenye biashara
yake. Vijana wanahimizwa kuuliza baadhi ya maswali waliyotayarisha.
Zoezi hili litawasaidia vijana wa SDSMV kubaini sifa na stadi anazotakiwa kuwa nazo kuwa mjasiriamali.
Kuwaalika wajasiriamali wenyeji mara kwa mara kutasaidia kuorodhesha msaada kwa SDSMV kutoka
katika jumuiya ya wafanyabiashara wenyeji
Muda: Saa 3
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
93
Matayarisho: Mtafute mtu kama mfugaji kuku, mfugaji wa
wanyama au mkulima wa mazao atakayekuwa tayari
kushirikiana uzoefu katika kuanza na kuendesha biashara.
Zungumza na mgeni huyo mapema, hasa kama kuna vitu
maalumu unavyotaka avitaje. Mjasiriamali mwenyeji hana budi
kueleza namna alivyoanzisha biashara au shughuli yake kwa
kiwango kidogo na kuanza kuiimarisha na kufanikiwa. Mweleze
Mjasiliamali huyo kuwa madhumuni ya ziara ni kuonyesha stadi za sifa zinazohitajika kupata biashara
yenye mafanikio
Namna ya Kufanya:
1. Ukishamchagua na kuzungumza na “Mjasiriamali” anayefaa kutembelea shule, waambie vijana
ni mjasiriamali ganina anafanya nini
2. Waambie vijana wafikirie baadhi ya maswali watakayomwuliza mgeni. Waambie wanze na
maswali rahisi na baadaye maswali ya kina zaidi. Kwa mfano: Je, alipata wapi wazo? Je, ni nani
alimsaidia? Je, alihitaji fedha za ziada kuanzisha biashara? Je, wateja wake ni kina nani? Je,
kuna matatizo gani ya kuendesha biashara? Je,ilimbidi apitie mashaka gani? Je, jambo gani zuri
kabisa na baya kuhusu kuendesha biashara yako mwenyewe
3. Kama mgeni huyo ni mwanamke, wahimize vijana kuuliza maswali kuhusu wanawake
wanaoendesha biashara
4. Andika maswali muhimu kwenye chati au ukutani na jaribu kupanga mfuatano wa maswali ya
vijana
5. Mara mgeni akifika, mtambulishe na eleza tena madhumuni ya ziara yake kwavijana
6. Mpe muda wa kutosha Mjasiriamali mgeni kushirikiana uzoefu wake na vijana bila taabu
7. Ruhusu muda wa kutosha kwa maswali kutoka kwaijana na andika hoja muhimu ubaoni ili
yajadiliwe baadaye
8. Baada ya kumalizika masuala yote (au muda umekwisha) mshukuru mjasiriamali aliyetembelea
9. Baadaya mjasiriamali kuondoka, endesha majadiliano yasiyo rasmi. Waulize ni mambo gani
aliyosema mjasiriamali ambayo yamewafurahisha sana vijana. Ni mambo gani aliyosema
mjasiriamali waliyoona magumu kuyaelewa. Eleza msamiati wowote ambao waliuona mgumu
kuuelewa.
94
10. Waulize vijana wamejifunza nini kuhusu namna mtu anavyoweza kuanzisha biashara yake
mwenyewe au waambie vijana wataje mambo machache muhimu waliyojifunza kuhusu
ujasiriamali.
11. Jadili baadhi ya sifa za mgeni zilizochangia mafanikio yake kama mfanyabiashara
12. Toa muhtasari wa majadiliano na hakikisha kuwa hoja muhimu zilizopo kwenye maelezo
kwamwezeshaji (hapa chini ) zimeelezwa
Maelezo kwa Mjasiriamali
Ujasiriamali ni kitendo cha mtu kuanzisha biashara mpya. Ni uwezo wa kukuza biashara ndogo tangu
mwanzo bila kitu kwa kuanza kubainisha na kupata rasilimali za kuzalisha bidhaa ambayo wateja
wanahitaji na kununua. Ujasiriamali unamaanisha kuwa watu na mashirika wanazalisha bidhaa na
hudumakwa kupata faida ya kiuchumi. Ujasiriamali unahitaji “utamaduni wa biashara” unafafanuliwa
kuwa ni:-
“Seti ya mitazamo, maadili na imani vinavyofanyakazi ndaniya jamii mahususi au mazingira
yanayoleta tabia ya kibiashara na matarajio ya kuelekea kujiamini”15
Mjasiriamali:-
- Mtu anayeweza kubuni na kuanzisha biashara yake ndogo ndogo
- Anabainisha bidhaa (mazao au mifugo) ya kuuza na watu watakaonunua bidhaa hiyo
- Anapata vyanzo vya kupatia malighafi (chakula chamifugo,mbegu,dawa za kuulia
wadudu n.k.) kuzalisha bidhaa na kutumia njia bora za uzalishaji ili kupata faida na
kuendesha maisha mazuri
Sifa za Mjasiriamalibora:
- Ana uwezo wa kuwashawishi watu, teknolojia na mikakati inayofaa mahitaji ya soko
- Anaweza kuchukua mashaka (kufanya uamuzi mzito bila hofu ya kushindwa)
95
- ana uwezo wa kupanga kushinda hali na mazingira magumu (kwa mfano, ukame,
magonjwa na wadudu waharibifu wanapotokea, n.k)
- Ni mtu mwenye nia na nidhamu, mwenye uwezo wa kutekeleza dira na mawazo
- Ana uwezo wa kupanga mwelekeo wabaadaye (mtazamo wa siku zijazo)
kuweza kuwa mjasiriamali, mtu ni lazima atathmini uwezo wake mwenyewe, kuafuta taarifa za ushauri,
kutoa uamuzi, kupanga muda wake, kutekeleza wajibu uliokubaliwa, kuwasiliana na kufanya mapatano,
kushughulika na watu wenye mamlaka na madaraka, kutanzua matatizo na kuamua migogoro,
kutathmini utendaji wa mtu, na kumudu msongo na mhemko.
Stadi nyingi zinazotakiwa kwa ajili ya biashara tayari zinafundishwa kwenye vipengele vingine vya mtaala
wa SDSMV. Kwa mfano, mtaala unashughulika na kutanzua tatizo (kuhusu kilimo, udhibiti wa wadudu,
mifugo, kilimo cha bustani), kupanga mipango ya baadaye na kufanya uamuzi kuhusu mbinu za
msimamizi wa mazao kwamsingi wa majaribio ya kazi. Moduli nyingi zinahusikana kujistahi,
kuwaheshimu wengine, na kadhalika. Unaweza kurejea moduli hizi kwa kujikumbusha, na kuhusisha
96
J.12.3. Zoezi: “P” zote (Bidhaa,Mahali, Bei, Utangazaji, Watu na Mpango)
Zoezi hili linalokusudia kueleza kwa ukamilifu hadithi ya kuuza mazao yaliyozalishwa katika SDSMV
kinahusisha kuelewa zaidi na si kulima mazao tu. Wanaweza kujua namna ya kulima zao Fulani, lakini
wanatakiwa pia kufikiria namna ya “kuuza” bidhaa hizo. Zoezi hili linaeleza utaratibu unaofaa wa
kufikiria namna ya kupata faida – ambao watu wa biashara na masoko wanaita “P” 6 ( Bidhaa,Mahali,
Bei, Utangazaji, Watu na Mpango)
Muda : Saa 2
Vifaa na Matayarisho: Chora chati kama iliyopo hapa chini na “P” 6 za biashara na masoko.
Kama kiwango cha kusoma, kuandika na kuhesabu ni kidogo, tumia picha kuwakilisha kila
eneo
Product
Price
Place
Promotion
Plan
People
97
Inafanyaje kazi?
1. Wekeza vijana kuwa utawaambia hadithi kuhusu kufuga kuku.Anza zoezi kwa kupitia mada ya
kufuga kuku kutokea kwenye moduli za kilimo za SDSMV za kilimo.Waulize wanafunzi
wanachokumbuka.Waulize maswali kama vile:
Je,nini tofauti kati ya kuku wanaoachiwa kujitafutia chakula na wanaofugwa kwenye
mabanda?
Kwanini unawajengea mabanda kuku?
Unahitaji vifaa gani kufuga kuku?
Je,nini sifa za mvifaa vya kulishia na kunywea maji kuku?
Unahakaikishaje kua mayai mengi zaidi yanaweza kukusanywa?
Kwa nini vitulio vya kuku ni muhimu?
Je,nini nsifa za kuku bora wa mayai ya vifaranga?
Pia pitia njia za kuwakinga kuku na aina za magonjwa wanayopata .Sisitiza namana kuku
alivyomuhimu kwa lishe kwa nyama na mayai.
1. Onyesha chati ya “P6” hapo juu na eleza maana ya kila neon kwa muhtasari (angalia
maelezo ya wawezeshaji hapo chini.) Halafu soma hadiythi ifuatayo mara mbili kwa
watoto.Wakizingatia “P6”wakati wanaposikiliza.
Moja kati ya hadithi nyingi za kuku:
Durah anakwenda mjini kumtembelea dada yake.Dada yake anamwambia Durah
kuwa anafuga na kuuza kuku anapata fedha kwa njia hiyo.Durah anadhani hili ni
wazo zuri sana.Anarudi kijiji kwake na kuwaita wawili kati ya marafiki
zake.Marafiki hao waliwahi kuhudhuria SDSMV mwaka jana na wanakumbuka kusoma kuhusu
maana ya kufuga kuku.Durah anawaambia kuhusu haja ya kuku wengizaidi na anapendekeza
kuwa wafa nye pamoja biashara hii.Kila mmoja anakubali na wote wanachangia coin 20T.Siku
inayofuata Durah na rafiki yake mmoja wanakwenda mjini kununua vifaranga 25 vyenye umri
wa siku mmoja.Kwahiyo ni lazima walale usiku mmoja mjini ili wapate vifaranga siku ya
pili.Wakati walipofika mjini hakukuwa na vifaranga vilivyobaki kutokanana na mahitaji kua
makubwa kwa vifaranga vyenye umri chini wa siku moja.Kwakua walilazimika kutumia fedha
kununulia chakula na malazi,etamudu kununua vifaranga 15 tu siku ya pili.
Baada ya kurudi kijijini wanabaini mkua wanahitaji pia chakula cha kuku.Kaka take Durah
98
anaanza kujenga banda kwa ajili ya kuku,wakati,wakati Durah na rafiki yake wanakwenda
kununua chakula cha kuku kutoka kwenye duka la kijiji.Chakula hiki ni ghali na ubora wake ni
mdogo,kwa sababu duka hilo haliwezi kumudu kununua chakula kipya kila wiki siku miliyofuata
kuku watatu wamekufa kwenye kibanda kutokana na hali ya hewa ya joto na kwa sababu kaka
yake hakumaliza kujenga paa la kuwalinda.
Katika wiki chache zijazo,kikundi kinapeana zamu ya kuwahudumia kuku wao.Kutokana na
sababu mbalimbali (kupenya kwa mbwa kwenye uzio,ugonjwa unaowana baadhi ya kuku)
walibaki kuku 7 tu kati ya 15.Hatimaye kuku wamekua wakubwa na kutoshwa kuuzwa.Hata
hivyo kijijini kwao,hakuna hata mtu anayetaka kuku,kwa sababu kila mmoja anao wa
kwake.Kutokana na kukosekana kuku kwa mahitaji wanaamua kuuza kuku kwenye soko la mjini.
Sokono hapo,inaelekea kila mtu alikua akiuza kuku,wenye afya na wakubwa kuliko wa
kwao.Kusema kweli wanawake wanaanza kuona kuwa kuna aina nyingi za kuku wa kuuza sokoni
.Hatimaye walipofanikiwa kuuza kuku wao wadogo,wanabaini kwamba hawakupata faida
yoyote kutokana na mtaji wao wa kuanzia.Waliporudi nyumbani wajadili wamekosea nini.
2. Waulize vijana :
Je,Durah na marafiki zake walipata wapi wazo la kuuza bidhaa yao (Eleza kuwa kuku
ndiyo bidhaa yao).
Kina nani walikua wateja wao (watu)?
Je,walifikiria sana kuhusu bei ya kuku?
Je,walifikiria ipasavyo kuhusu watakakouza bidhaa yao? (mahali)
Je,walifikiria namana ya kuwavutia wateja (utangazaji)?
Je,walikua na mpango wa jumloa kwenye biashara yao? (walioshorokishishwa)
Je,watu hao walijitoa kiasi gani (Durah ,marafiki wake na kaka yake)?
Kwa jumla,unadhani Durah na marafiki zake wana soko kwa ajili ya kuku wao?
Je,ulidhani bidhaa ndiyo inayofaa?
3. Eleza kuwa Durah na marafiki wake walitakiwa kutayarisha mkakati kuuza kuku wao?
4. Rudia kusoma hadithi hiyo na halafu waulize vijana watoe mapendekezo yao ku boresha
mkabala wa kila hoja ya P
5. Hitimisha kwa kuwaambia vijana kua uuzaji wa kutafuta soko unahusu mahitaji ya wateja na
kutosheleza mahitaji hayo kwa faida.
Maelezo kwa mwezeshaji.
99
P6 hizi hazitabaki kuwa P kwa lugha nyingine ifuatayo ni taarifa ya chanzo/usuli kuhusu namna
P6 zinavyochangia kwa mkakati wa mauzu/utafutaju soko.
Bidhaa
Fikiria kuhusu bidhaa au huduma: je, ni bidhaa bora?
Je, inalingana na mahitaji ya wenyeji au wateja wanaotarajiwa?
Je,wateja wanataka bidhaa ya namna gani?
Bei:
Je, ni bei nafuu kwa wateja?
Je, bidhaa inauzwa kwa bei iliyopunguzwa ikilinganishwa na wengine wanaouza bidhaa ya namna hiyo?
Je, bei itapungua kama itauzwa kwa wingi,au kwa wateja wanaotarajiwa?
Je, inawezekana kupanga bei tofauti kwa wateja tofauti? Je, ni lazima ufanye hivyo?
Utangazaji
Je, watu wanajuaje kwamba bidhaa yako inauzwa?
Je, bidhaa hiyo inatangazwa kwa usahihi?
Je, kila mmoja anaweza kuiona bidhaa hiyo ikionyeshwa eneo la mauzo?
Mahali:
Je, bidhaa inauzwa wapi?
Je, sehemu ya mauzo inafikika kwa urahisi?
Je, unaweza kuwafikishia wateja bidhaa ? je, ni wazo zuri?
Je, mahali pa kuuzia panawavutia watu waliolengwa kununua?
Watu:
100
Je, mfanyabiashara anahitaji stadi gani?
Je, kuna uhusiano gani kati ya mfanyabiashara na washitiri wake?
Je, ni mwenye tabasamu na mkarimu?
Je, ni mtu maarufu katika eneo, kijiji au mji?
Je, ana jina/sifa nzuri?
Mpago:
Je, nini mpango wa jumla kwa bidhaa ikiwemo kuitangaza na kuiuza?
Marejeo : Story and notes come from pp 152-154 GET Ahead for Women in enterprise. Training Package and Resource Kit. Page
55. Also pp 26-27 Kane, K and the staff of Tototo Home Industries. Faidiki! Mombasa, Tototo Home Industries and World Education,
Inc., 1990
101
J.12.4. Zoezi: Kuuza! Igizo Bubu
Igizo bubu ni shughuli ya kuchekesha inayoweza kutumiwa kama kichangamsho katika ti ya somola
muda mrefu au mfululizo wa masomo kuhusu ujasiriamaliau kabla ya kuanza shughuli nyingine. Igizo
bubu kwa kawaida nimchezo wa kukisia ambapomtu mmoja au kikundi cha watu wanaigiza dhamira
fulani. Mtu mmoja au wawili wanaigiza igizo babu na washiriki wengine lazima wakisiewanajaribu
kuonyesha nini. Kanuni ya msingi ya igizo babu ni kwamba wanaofanya igizo hilo hawazungumzi.
Sababu ya msingi ya kucheza igizo bubu kwenye zoezi hili na
kuigiza njia mbalimbali za kutangaza na kuuza bidhaa. Zoezi
linawezakufanywa mahali popote panapolenga shughuli za
kiujasiriamali. Halina budi kusisitiza umuhimu wa kuuza stadi
Mada: Saa moja – mbili
Vifaa na matayarisho:
1. Tayarisha orodha ya bidhaa zinazouzwa mahali hapo: aina zote za mbegu;makopa ya ndizi; ndizi
vania,karanga, mahindi, mtama, viazi vitamu, kahawa, chai, kunde, uwele,mhogo, mpunga,
pamba, alizeti, maharage ya soya, nyama ya ng’ombe, au aina nyingine ya nyama; asali,
uyoga,korosho, samaki wa kukausha, maua ya mapambo, mayai, kuku mbichi na kadhalika
2. Andaa mpangilio wa matukio yanayoweza kuigizwa kwa jozi yanayohusu kuuza bidhaa
mbalimbali zinazofaa kwa hali ya mahali. Matukio hayohayana budi kuwa kati ya mteja na
muuzaji. Tukio halina budi kuwa na maelezo machache ya shughuli ya kupanga na kuonyesha
bidhaa, kuwavutia wateja na kuuza bidhaa. Andika matukiohayo au uwe tayari kuyaeleza kwa
vijana wasiojua kusoma. Aina nyingine za matukio zinatayarishwa hapa chini lakini
utawezakuandaa matukio yanayofaa zaidi wewe mwenyewe
102
- Mwigizaji A: Unaonyesha na kuuza maua ya mapambo. Unajaribu kumpata mteja aje aangalie
jinsi yanavyovutia, kuyanusa na kuyanunua. Wewe ni mcheshi mwenye furaha na tabasamu
sana. Unajaribu kumshawishi mtu aliyehuzunika anayepita kununua baadhi ya maua
- Mwigizaji B: Una huzuni kwa sababu mama yako anaumwa. Hupendi kununua maua, ingawa
muuzaji maua mwenye mvuto na furaha anakufuata wewe. Pengine maua yatamfurahisha
mama yako? Lakini huna fedha za kutosha.
- Mwigizaji A: Unauza mafagio yenye mpini mfupi uliyotengeneza mwenyewe unataka kuonyesha
namna inavyofaa kwa kufagilia sakafu na ubora wake. Unamfuata mteja. Ana wasiwasi kuhusu
ubora wa mafagio hayo
- Mwigizaji B: Mtu mmoja anajaribu kukuuzia mafagio ya mkono. Una wasiwasi kwamba
yanaweza kuvunjika. Hutaki kuumiza mgongo waako kwa kutumia fagio la mpini mfupi
- Mwigizaji A – Umetayarisha juisi ya matunda tamu na unaiuza sokoni. Unawezaje kuwavutia
wateja katika eneo lako. Lazimauonyeshe kwamba ni kinywaji cha matunda na tunda zuri.
Unataka kuonyesha namna ilivyo tamu.
- Mwigizaji B – Una kiu sana. Kuna genge lenye juisi inayouzwa. Huna uhakika kama juisi ni nzuri
au hapana. Pia huna hakika kama imeongezwa maji mengi na kwamba maji yaliyoongezwa ni
mazauri. Hatimaye unaiyona na kuipenda
- Mwigizaji A : Una samaki wabichi (tilapia) kwa kuuza (mmoja mkubwa ba wawili wadogo ) na
wanatukutika wakati wanapowatoa kwenye maji kuwaonyesha wateja. Unataka kumuuza
samaki mkubwa lakini mteja anaelekea kutaka kuwanunua samaki wadogo kwa bei nafuu
- Mwigizaji B: Unataka kuwanunua tilapia wadogo kwa bei sawa na mkubwa. Lazima upatane na
mwuzaji. Mwuzaji anataka kuuza samaki mkubwa
103
- Mwigizaji A: Umebakiwa na kuuza kuku wawili wazuri. Kuku wako wamefugwa kwa kulishwa
nafaka nzuri na vitamin, kwa hiyo wanaonekana wenye afya. Unataka kuwaarifu watu kuwa
kuku wako ni wakubwa na kwamba kuku mmoja anaweza kulisha familia ya watu 10
- Mwigizaji B: Kuna mtu anauza kuku wakubwa. Huna hakika kama anaweza kununua kuku
wakubwa. Je ni vizuri?
- Mwigizaji A: Unauza mayai. Inabidi uwe mwangalifu yasijevunjika au kwamba wateja
wasiyashike na kuyavunja. Unaamua kuyauza nyumba hadi nyumba . unagonga mlango mmoja
na uso wenye tabasamu unajibu. Anataka kujua bei yake lakini yaelekea hana uelewa wa
kununua mayai
- Mwigizaji B: Uko nyumbani unafikiria kuku wako. Unasikia mlango unagongwa na kufunguka.
Kuna mtu anayeuza mayai. Unajaribu kuyainua na kuyashika. Unataka kujua yanauzwa bei gani,
hata kama hutaki kuyanunua
Inafanyaje kazi?
1. Pasha kwa kuwaambia kila mmoja aorodheshe vitu vinavyouzwa sokoni. Rejea kwenye safari ya
sokoni.
2. Kata mpangilio wa matukio uliyokwisha tayarisha kwa mchezo bubu. Wape vijana tukio la
kuigiza pamoja na kueleza kwa makini mpangilio wa matukio kwa kila jozi. Wape vijana dakika 5
kutayarisha tukio na kuliendeleza zaidi.
3. Vijana wanapewa fursa ya kuigiza kibubu na kuigiza mpangilio wa matukio. Kila jozi ya waigizaji
itapewa dakika 3 hadi tano kuigiza mchezo bubu wao. Wengine kikundini hawana budi kukisia
nini kinachoendelea na wanauza nini. Wawezeshaji hawana budi kuwashawishi
hadhira/watazamaji watoe mawazo. Lengo ni kuwawezesha vijana wengine kukisia nini
kinachoendelea haraka iwezekanavyo na kukisia bidhaa inayouzwa
4. Unaweza kuanzisha aina ya shindano. Watangazie kwamba mshindi ni jozi ambayo igizo bubu
lake inakisiwa haraka sana, au mtu ambaye mara nyingi anakuwa wa kwanza kukisia kwa
usahihi igizo bubu na bidhaa. Unaweza pia kutoa alama kwa kila jozi kutegemea wameigiza
vizuri kiasi gani mpangilio wa matukio. Mweeshaji anaweza kuweka alama za timu gani imekisia
104
idadi kubwa ya maigizo bubu kwa usahihi, nakutoa alama za ziada kwa timu iliyoigiza vizuri zaidi.
Timu yenye idadi kubwa ya alama inashinda.
5. Baadaye huna budi kuongoza majadiliano kuhusu kuuza bidhaa na kuzitangaza
Maelezo kwa Mwezeshaji
Kama ilivyo kwa michezo mingi, sheria na mbinu za michezo zinatofautiana sana kutoka nchi moja hadi
nyingine na wawezeshaji hawana budi kutumia muundo wowote wa maigizo bubu waliyoizoea zaidi.
Wakati mwingine jozi zinahitaji msaada katika uigizaji wao, au vijana wote wanaweza kuhitaji vidokezo
zaidi ili kukisia kile kinachoendelea , hasa kama igizo bubu ni gumu mno au vijana wanaoigiza si stadi wa
kuigiza kuruhusu kusema na mchezo wa kuigiza kuliko igizo bubu
Marejeo: Imechukuliwa kutoka Adapted from Activity Six Charades Game pp 43-44 Gender Equality and Child Labour, A
participatory tool for facilitators. Murray, U., Amorim, A., Samouiller, S. Badrinath, S. (2005) ILO/IPEC Geneva
Mada ndogo: Kupata Faida
Kujifunza namna kukokotoa faida na hasara na kueleza umuhimu wa kutunza kumbukumbu, hakuna
hata mtu mmoja atakayepata hasara kwenye shughuli ya biashara. Lazima tujue maana ya “faida”
Faida = mapato ya mauzo kutoa gharama za kufanya mauzo hayo
J.13.1. ZOEZI: Je, Kiuzwe Bei Gani?
Muda: Saa moja
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea na andaa mifuko mitatu yenye mawe 10 kila mmoja.
Inafanyaje kazi
1. Wagawe wanafunzi wa SDSMV katika makundi matatu. Kilaki kundimfuko wenye mawe 10
madogo. Waambie kwamba kila mfuko umenunuliwa kutoka mji wa jirani kwa senti 50.
Waambie kwamba kila jiwe kusema kweli ni jiwe maalumu (jiwe la thamani) na kila moja
litauzwa peke yake. Kiambie kila kikundi kiamue watauza kila jiwe kwa bei gani. Mawe yote
kwenye mfuko lazima yawe bei moja. Wanapewa dakika 10 za kujadili na kuamua
105
2. Wakati huo huo, chora jedwali lifuatalo ubaoni
Bei Mapato ya Mauzo Gharama Faida
Kikundi la 1
Kikundi la 2
Kikundi cha 3
3. Waambie wanafunzi wa SDSMV tuchukulie kwamba kila kikundi kimeuza mawe yao yote.
Waulize je, kila jiwe wameuza bei gani? Jaza majibu kwa kila kikundi na kujua namna hesabu
zao ni sahihi. Je, hesabu zao ni sawa au tofauti? Kwa mfano kama kikundi kimoja kinauza jiwe
kwa coin 5, kikundi kingine kwa coin 10 kila jiwe nakikundi cha tatu kwa coin 7 kila jiwe, cati
iliyojazwa itakuwa kama hivi.
Chati ya Mfano
Bei Mapato ya Mauzo Gharama Faida
Kikundi la 1 5 50 50 0
Kikundi la 2 10 100 50 50
Kikundi cha 3 7 70 50 20
4. Hakikisha kama kuna jibu lolote kutoka kwenye shamba linaloonyesha kwamba wanapata
hasara. Kwa kikundi kinachotoza gharama kubwa zaidi kwa kila jiwe, waulize kama wanafikiri bei
zao ni halisi
5. Unawezakutaka kufanya zoezi hili mara nyingine kwa kutumia mfano mwingine: Unaweza
kufanya zoezi kuwa gumu zaidi, kwa mawe makubwa kuwa na bei tofauti ikilinganishwa na
mawe madogo
106
6. Kama wanafunzi wa SDSMV wanaelekea kuwa tayari, unaweza kujadili gharama zaidi kuliko
kuanzia coin 50 zilizotumika kununulia jiwe. Kwa mfano, waulize wanafunzi wa SDSMV kama
wanafikiri kuwa watalazimika kulipa mahali (genge) sokoni kuuza mawe. Je watalipia kupata
kupata nafasi sokoni? Je, watamlipa mtu kuwauzia mawe? Je, watafunga kila jiwe wanalouza?
J.13.2. Zoezi: Kutabiri Faida na Hasara.
Muda : Saa 1
Vifaa: Chatipindu na karatasi za kuchorea
Inafanyaje kazi?
1. Soma hadithi ifuatayo au tunga hadithi inayofaa zaidi yenye majina tofauti na kadhalika. Kama
wanafuzi wa SDSMV hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu, tumia michoro/picha kwenye
chati badala ya maeno
Bashir, Gamba na Pili wanaishi pamoja katika kijiji kidogo katika eneo lenye joto na ukame.
Wanataka kununua mbuzi. Walijadiliana wazo hilo pamoja na kufikiri kwamba kuna vichaka na
mbuga za kutosha jirani kumlisha mbuzi.
Walijadiliana wazo hilo pamoja na kufikiri kwamba kuna vichaka
na mbuga za kutosha jirani kumlisha mbuzi. Wanafikiri kuwa
maziwa ya mbuzi yana virutubisho vingi, na kama mambo
yatakuwa mazuri yataweza hata kumwuza. Waliamua waweke
akiba ili wanunue mbuzi atakaye gharimu coin 50
107
Wasaidie kutafuta ni lini watakuwa na fedha za kutosha kununulia mbuzi mwaka ujao
Bashir analipwa coin 20 kwa mwezi kwa kufaya kazi ya palizi. Hata hivyo kazi kama hiyo
inapatikana tu mwezi Januari, Machi na Juni. Gamba analipwa coin 20 kwa kufanya kazi ya
kibarua kwenye shamba lililopo jirani mwezi Agosti, Oktoba na Desemba.
Katika mwezi wa Mei na Septemba, Pili na lipwa coin 50 kutokana na mboga anazolima
Bashir, Gamba na Pili wanakadiria kwamba wanahitaji coin 10 kila mwezi kwa ajili ya gharama
zao
Je, lini watakuwa na fedha za kutosha kununulia Mbuzi?
2. Chora kalenda kama iliyopo hapa chini kwa Bashir, Gamba na Pili. Mwambie kijana mmoja wa
SDSMV ajaze mapato ya Bashir, mahali panapohusika, mwingine ajaze mapato ya Gamba na
mwingine ajaze ya Pili
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir
Gamba
Pili
3. Jumlisha kila safu na ingiza mapato kwenye nafasi wazi. Kalenda haina budi kuwa kama iliyopo
hapa chini
108
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
mapato
20 0 20 0 50 0 0 20 50 20 0 20 220
4. Ongeza safu nyingine kwa gharama
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
mapato
20 0 20 0 50 20 0 20 50 20 0 20 220
Gharama
109
5. Mwulize mshiriki wa SDSMV ajaze gharama kwa kila mwezi
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
mapato
20 0 20 0 50 20 0 20 50 20 0 20 220
Gharama 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 120
6. Ongeza safu ya wazi na mwambie mshiriki mwingine wa SDSMV kukokotoa kama wamepata au
wametuma fedha zaidi kila mwezi
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
Mapato
20 0 20 0 50 20 0 20 50 20 0 20 220
Gharama 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 120
Faida au
Hasara
110
7. Majibu lazima yawe kama kalenda ya hapa chini. Eleza kuwa alama “_” ina maana “hawana
fedha” kwa kiasi hicho
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
Mapato
20 0 20 0 50 20 0 20 50 20 0 20 220
Gharama 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 120
Faida au
Hasara
8. Eleza kwamba safari hii, baada ya kutafuta kama kuna fedha za kutosha kila mwezi, lazima
watafute ni kiasi gani cha fedha kimebaki kila mwezi ikiwemo fedha zinazoendelezwa kwenye
mwezi ujao (faida au hasara limbikivu kila mwezi). Futa safu yenye faida au hasara kwa kila
mwezi na weka jina tofauti kwenye safu yenye jina kiasi gani kimebaki au kuendelezwa kwenye
mwezi mwingine? Waambie wanafunzi wafikirie kuhusu suala hilo na eleza namna ya kutafuta
kiasi hiki. Kwa mfano, mwezi Januari, coin 20 zimeingia kwenye kaya, gharama zilikuwa coin 10,
kama hakuna matumizi yoyote mwezi huo, coin 10 zitakwenda mwanzoni mwa mwezi ujao.
Mwezi Februari kuanza na coin 10 zilizochukuliwa kutoka Januari, lakini baada ya kutumia coin
10 kwa gharama, hakuna kilichobaki.
111
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
Mapato
20 0 20 0 50 20 0 20 50 20 0 20 220
Matumizi 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 120
Kiasi gani
kimebaki au
kimeendelezwa
kwenye mwezi
ujao
112
9. Takwimu ni lazima ziwe kama ilivyoonyeshwa kwenye chati kamali ya hapa chini. Zingatia
faida/hasara limbikizi maana yake ni kiasi gani kinahamishiwa mwezi ujao
Mwezi J F M A M J J A S O N D Jumla
Bashir 20 20 20 60
Gamba 20 20 20 60
Pili 50 50 100
Jumla ya
Mapato
20 0 20 0 50 20 0 20 50 20 0 20 220
Matumizi 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 10 120
Faida/Hasara
limbikizi
10 0 10 0 40 50 40 50 90 100 90 100 100
10. Uliza ni lini Bashir, Gamba na Pili wanunue mbuzi (amegharimu coin 50)?
11. Kama kuna mtu atajibu Juni – mwulize kijana huyo kama Bashir, Gamba na Pili watakuwa na
fedha za kutosha kwa matumizi ya Julai. Kama kuna atakayesema Agosti, mwulize kijana huyo
kama Bashir, Gamba na Pili watakuwa wametumia fedha zao zote.
12. Kama vijana wanaeleza kwa urahisi zoezi hili, unaweza kuendeleza zaidi na kuongeza kwenye
matumizi mengine. Je mbuzi atasababisha gharama za ziada? (atakula kwenye vichaka na
mboga, lakini itakuwaje kuhusu dawa za minyoo kabla na baada ya mvua za mara kwa mara,
kupunguza kwato, je, atahitaji kupuliziwa dawa? )
13. Waambie wanafunzi wa SDSMV wafikirie ni lini na nama gani mbuzi ataanza kutoa mapato
kwao? Je, kuna mashaka yoyote? (kuuza maziwa ya mbuzi, majira ya joto). Pia jadili umuhimu
wa kuweka fedha kwa ajili ya matumizi yasiyopangwa au dharura.
Utunzaji Hesabu za Fedha
14. Kama makundi yako tayari, anzisha wazo la utunzaji wa kumbukumbu za mauzo na gharama za
mauzo. Eleza kwamba, anachofanya Bashir, Gamba na Pili kwenye kalenda ya hapo juu ni
kuandika wanachopata na kuandika matumizi yao. Eleza kwamba ni muhimu kuandika kiasi cha
113
fedha kilichotumika kwa ajili gani na fedha zilizopokewa. Kumbukumbu zinaweza kutunzwa kwa
njia rahisi ili uweze kuelewa fedha zilikokwenda na fedha zilizopokewa zimefanyiwa nini. Ili
uweze kufanya hivyo, ni lazima uelewe hesabu na uwe na mpangilio mzuri. Eleza kuwa
tulichokifanya kwa Bashir, Gamba na Pili ni utunzaji wa hesabu za fedha au kuandika
kinachofanyka katika mapato yao na matumizi.
15. Rudia kweye hadithi ua Uzuzi – alitakiwa kuwa amefanya nini kabla? Kwa mfano, alitakiwa
ameuliza kabla kuwa ingemgharimu kiasi gani kupata genge; ongeza ni kiasi gani angepata
kutokana na kuuza mbatata zake zote kwa bei ya coin moja kila moja, na kutoa jumla kutoka bei
ya kutumia genge na kuona kama kungekuwa na faida yoyote. Kama angeendelea kuuza
mbatata zake gengeni siku ya pili, angetoza gharama zaidi kwa mazao yake. Hatimaye
angejumlisha kiasi alichopata, na kutoa kiasi ambacho angemlipa mwenye genge.
16. Eleza kwamba watu wengi hawaandiki kiasi cha fedha wanazopata na wanazotoa kwenye
biashara yao. Hii ni kwa sababu hawajui namna ya kufanya. Kwa hiyo watu hawajui kiasi cha
fedha wanachopata, ni wateja gani wamekopa , yaani wamechukua bila kulipa. Eleza kwamba
utunzaji wa hesabu za fedha maana yake unaadika fedha zote zinazoingia kwenye biashara yako
na fedha zote zinazotolewa kwenye biashara yako.
17. Hitimisha kwa kuuliza nini faida ya utunzaji hesabu za fedha. Majibu yaayoweza kutolewa ni
pamoja na :-
Utajua ni kiasi gani cha fedha ulichopokea, ni kiasi gani umetumia na jinsi ulivyotumia;
Unaweza kukokotoa kujua kama unata faida au hasara;
Utaweza kufanya maamuzi mazuri kuhusu unachotaka kuuza na kununua;
Unaweza kutunza kumbukumbu za kununua na kuuza kwa mkopo,ili watu
wasikudanganye;
Unanaweza kutunza kumbkumbu za fedha zinazoingia na kutoka kwa kukundi (kama
Bashiri,Gomba na Pili) na hivyokuizuia matumizi mabaya ya fedha na kuepuka
kutoaminiwa.
Utaboresha biashara yako na faida.
114
MAREJEO: Doing a feasibility study: Training Activities for Starting or Reviewing a Small Business. Edited by Kindervatter, S.
(1992) OEF International, distributed by Women, Ink. Step Four: calculate Business Expenses pp 64 –87 & Step Five: Estimate
Sales Income pp 90-99
FAO (1994) Simple Bookkeeping and Business Management Skills. Facilitator’s Guide Ria Meijerink November 1994.
RAFR/WID/002/94
FAO (1995) The group enterprise book A practical guide for Group Promoters to assist groups in setting up and running successful
small enterprises. ftp://ftp.fao.org/sd/sda/sdar/geb_en.pdf
MAELEZO KWA MWEZESHAJI:
Baadhi ya wanafunzi wa SDSMV tayari watakuwa na uelewa wa faida,hali ya kuwa wengine
watakuwa hawaelewi dhana ya faida na hasara kabisa.
Wanafunzi wengi wa SDSMV hawatashughulikia au kuhesabu fedha katika maisha yao ya kila
siku.Kama ni hivyo,litakuwa wazo zuri kuleta fedha tofauti na kuwaonyesha vijana.Waulize kama
wanaelewa rangi tofauti za noti.Waonyeshe wanafunzi wa SDSMV alama za fedha zinazotumika
kuonyesha kiasi cha fedha.Fanhya hesabu rahisi kwa kutumia fedha za viwango tofauti,kuonyesha
namna coin mbili zinavyoweza kufanya coin nyingine.
Kama SDSMV tayari inazalisha mazao au wana wanyama watakaoweza kuuzwa,tumia kama mifano
na jaribu kukokotoa faida inayoweza kupatikana kama vitu hivyo vingeuzwa.Kama wanafuga kuku na
hata kama mayai yanayozalishwa na SDSMV hayauzwi fanya hesabu rahisi ya mauzo ya kinadharia
ya mayai darizeni moja kila siku,kwa kuzingatia gharama za kuzalisha kuku na chakula cha kila siku
cha washiriki.
J.14.1.Zoezi: kubungua Bongo Wazo la Biashara
Malengo.
Kuchochea ubanifu katika kupata mawazo ya biashara
Kuchuja mawazo ya biashara kwa msingi wa rasilimali zilizopo
Kuchagua wazo 1-3 ya biashara kwa ajili ya uchunguzi mdogo
115
Muda: Dakika 6
Vifaa: Chatipindu mbili zenye karatasi kubwa,kalamu za kuchora;gundi za
kubandikia,mpira,chatipindu yenye vigezo vya kuchagulia mawazo ya Biashara
Inafanyikaje?
Hatua
1. Fahamisha maudhi ya bunguabongo hii.kupata mawazo mengi kadiri iwezekanavyo kwa
biashara mpya.Matokeo yatakuwa
Mawazo yote kwa ajili ya biashara ya uzalishaji au huduma ambazo wanakikundi wanaweza
kufikiria.Mawazo haya yanaweza kuwa msingi muhimu wa kubainisha fursa za biashara mpya.
2. Anza kubunguabongo: Washiriki wanatupiana au kusukumiana mpira miongoni
mwao.Anayeupokea atatakiwa kutoa wazo katika muda wa sekunde 3.Kama hana wazo
haraka,mwezeshaji hana budi kuhimiza wanakikundi wenye mifano ya fikra za ubunifu.Kama
mtu hana mawazo yoyote atasema “Napitisha”.Andika mawazo kwenye chatipindu wakati zoezi
limefanyika.Zoezi linaisha wakati kuna mawzo mengi na mtirirko wa mawazo umekwisha.
3. Anza vigezo vitatu vya kuchagua mawazo ya biashara yenye uhakika (kigoda cha miguu mitatu)
Stadi alizonazo kijana
Rasilimali zilizopo(kama vile fedha,watumishi,malighafi)
Jambo maalumu kuhusu wazo la biashara linalofanya livutie na kutakiwa,kama vile
bidhaa au huduma zisizopatikana katika jamii,stadi zisizo za jadi na mpya;au mahitaji
tofauti yanayoelezwa na watu au taasisi.
4. Kwa kila kigezo jadili taarifa zote muhimu kama ifuatavuo;
Stadi shawisho kikundi kiorodheshe stadi zote ambazo tayari wanazo kwa sababu huenda
wakazitumia katika maisha yao ya kila siku. Jumuisha stadi za jadi na zisizo za jadi,kwa
mfano,Stadi zza kompyuta,huduma za matengenezo.Jadili namna ya kuanzisha biashara
kwenye (kwa mfano,huduma za chakula,Mkahawa ,duka la mboga,duka la pikipiki n.k)
8 Marejeo; Imechukuliwa kutoka zoezi la 12 Adapted from Exercise 12. “Gender and Entrepreneurship Together: GET Ahead
for Women in Enterprise: Training Package and Resource Kit”, Susanne Bauer, Gerry Finnegan and Nelien Haspels,
Bangkok, Berlin and Geneva, International Labour Office, 2004
Rasilimali: Orodhesha rasilimali zilizopo katika kijiji,jamii au mkoa wa washiriki:
Fedha:akiba,mikopo,shamba la kilimo
116
Watumishi: wanafamilia/kikundi,vijana wenye utaalam .
Malighafi: mboga na matunda ,samaki,mbao,mwanzi,udongo wa
mfinyanzi,mawe,n.k
Halafu,anza kubunguabongo kuhusu mawazo ya biashara na huduma yatakayozingatiwa kuhusu
rasilimali hizi (kwa mfano,matunda,jemu,matunda makavu,juisi ya matunda)
Mahitaji: Waambie waorodheshe mawazo yanayohitajiwa na kijiji,lakini kwa sasa hakuna.Hii
inaweza kuwa kwa sababu inawabidi wasafiri kwenda sehemu nyingine kununua bidhaa au
huduma kwa mfano: sabuni,nyama,huduma za afya,.Jumuisha aina mbalimbali za mahitaji
yanayotajwa na vukundi mbalimbali ambayo wakati mwingine yanayopuuzwa,kwa mfano: zaidi
ya mahitaji binafsiya haja ya familia,kuna taasisi za mahali au biashara ambazo zinaweza pia
kuhitaji bidhaa zako.Mifano ni hospitali,shule,baraza la kijiji,kituo cha biashara,hoteli na
mikahawa na miradi ya maendeleo.
5. Waambie washiriki watafakari kuhusu mawazo yate ya biashara na shughuli za uongezaji kipato
mbazo waliweza kufikiria katika hatua ya 2.Wapange washikiriki katika jozi au vikundi
vidogovidogo,na waambie wabainishe mawazo matatu ya biashara yenye matumaini
zaidi,kulingana na uzoefu wao na uamuzi.Unaweza kuwwambia washiriki waunde jozi au
vikundi kulingana na mawzo ya biashara waliyopanga,kama baadhi ya mawazo hayo
yamechaguliwa na washiriki wengi.Hii inaweza kusababisha majadiliano makubwa kuhusu faida
na hasr haya ya miradi ya biashara na ruhusa kuundwa kwa vikundi(mshikamano)wakati wa
mafunzo.Hatua hii ya kuhitimisha ni hatua ya matayarisho ya zoezi lifuatalo la 13.Uchambuzi wa
kina wa mawazo ya biashara
J.14.2. Zoezi: Uchambuzi wa Kina wa mawazo ya Biashara:
Malengo:
Kuboresha na kuchagua mawazo ya biashara
Kutambulisha “Soko”kama dhana
Muda: Dakika 90-120
Vifaa: Mbao,Chatipindindu: Vigezo vya Uchaguzi wa Mawazo ya Biashara na Chati ya uchambuzi
wa kina.
117
Inafanyikaje?
Hatua:
1. Kumbusha matokeo ya zoezi la 56.Washirika walibainisha mawazo yenye matumaini kwa
shughuli za uongezaji kipato ambayo lazima yaende mbele kwa ajili ya uchaguzi wa
mwisho.Ni wazo 1 hadi 3 tu ndiyo yatakayochambuliwa kwa kina.
2. Kama zana ya kusaidia katika uteuzi wa mwisho wa wazo la biashara,wakumbushe washiriki
kuhusu vigezo vya utenzi vilivyoelezwa kwenye Zoezi 56.
Stadi: Je,kuna ujuzi wa kutosha wa kufanya shughuli hii?
Rasilimali: Je,tutaweza kugharimia kutokana na rasilimali zetu?
Mahitaji: Je,watu watanunua huduma/bidhaa zetu?Je,bidhaa au huduma inahitajiwa
na wateja (wanaotarajiwa) wataweza kumudu?
3. Wagawe washiriki katika vikundi vidogovidogo.Unaweza kuwapanga washiriki kulingana na
aina ya wazo la biashara kama ilivyokuwa kwenye zoezi la 56, na waulize washiriki kama
wamepata hoja nyingine muhimu za kufukiriwa zinazohusiana na utenzi wa wazo la
biashara.Waulize washiriki kama wana vipengele vipya kama vilivyopendekezwa na
washiriki.Kama ni lazima,waongoze kwenye vigezo muhimu viwili au zaidi kwa ya uchaguzi
wa wazo la biashara,kwa mfano kuwepo kwa washindani,upataji wa mikopo;idhini ya
kisheria;vivutio vya maendeleo.Wahakikishe washiriki kuwa m awazo hayo ya biashara
yaliyopewa nafasi ya pili au ya tatu yataangaliwa upya baadae iwapo zoezi hili la uchambuzi
wa kina linaonyesha kuwa wazo lao la biashara waipendayo halina maslahi na halitelezeki.
4. Anza kueleza chati Uchambuzi wa kina kwenye karatasi ya chatippindu,na toa mifano ya kila
kigezo cha uchambuzi.Chukua mifano inayohusu mazingira na hali ya walengwa.Angalia
hapa chini kwenye “maelezo”laini iwe kwa muhtasari. Usianze kutoa mhadhara na usitoe
maelezo mengi sana katika hatua hii.Kama washiriki walibainisha vigezo vya ziada vya
uchaguzi katika hatua ya 3,viongeze kwenye uchambuzi.Hakikisha kuwa kuna viashirio vingi
kadiri iwezekanavyo,ikiwemo bidhaa,huduma,pamoja na zinazizingatia soko.Kama
inafaa,kiambie kikundi kijadili hali ambapo kuna washindani wengi na kupungua kwa mauzo
Chati ya Uchambuzi wa kina:
Tumia alama zifuatazo;
Linafaa sana au
hakika
Nzuri inafaa Ni ya kawaida Ngumu au haifai Mahitaji ya
kutosha
118
Chati ya Uchambuzi wa Kina
Jina wazo la
biashara Stadi za Ujuzi Vifaa vilivyopo
Upataji wa
Malighafi
Fedha (za
kuanzia mtaji
unaotumika)
Mahitaji ya
Kutosha
Maelezo zaidi kuhusu upangaji daraja yanaweza kutolewa kwa washiriki kama ifuatavyo;
Stadi na ujuzi: Tathmini upeo ambao unazo Stadi zinazotakiwa (kwa mikono,binafsi,jamii).Kama
wewe mwenyewe huna Stadi zote zinazotakiwa,jaribu kutafuta kama utapata mtu mwingine
mwenye stadi hizi atakayesaidia.Jiulize kama unamudu kumlipa mtu huyu na wasaidizi
wao(gharama za ziada za kumwajiri mtu zinaweza kumaanisha kupungua kwa faida).Kama stadi
zinazotolewa zinawezwa kufanywa na mjasiria mali mwambie bila ya matatizo yoyote,huyu
lazima apewe alama za juu.Kama kiwango chake cha stadi kiko chini au hana kabisa,na hana mtu
wa kumsaidia, basi itabidi apewe alama za chini
Rasilimali: Vifaa vilivyopo: Wakumbushe washiriki kua wanapotumia aina Fulani za vifaa
mtu mwingine pia anahitaji stadi Fulani.Katika hali nyingine,vifaa vinavyotakiwa havipatikani
mahali hapo,au haviwezi kukarabatiwa kwa urahisi,au wakati mwigine ni ghali mno na
havina sababu kununuliwa.
Upataji wa mlighafi: Sisistiza kuwa shughuli yoyote ya kiuchumi inahitaji kuingia kwa
nyenzo muhimu,kama vile malighafi.Malighafi hay yanaweza kugeuzwa kwa bidhaa
nyingine (uzalishaji),kutumika kutolea huduma au pengine huuzwa kwa bei ya
juu(biashara).Kama malighafi yote inayotakiwa inapatikana kwa urahisi, mwaka
mzima basi ipe alama ya juu. Lakini kama kuna matatizo au mabadiliko ya msimu
katika upatikanaji na bei, basi ipewe alama ya chini ipasavyo
Rasilimali Fedha; Kama vile mtaji wa kuanzia au mtaji unaotumika. Wakati wa kuanzisha
biashara mpya, mara nyingi kuna haja ya kupata fedha za kukuwezesha kuwekeza katika vifaa,
ardhi au gharama nyingine za kuanzia. Hizi zinaweza kupatikana kwa kuchukua mkopo au
kukodi. Fedha taslimu zitatakiwa kwa mahitaji ya kila siku ya mtaji unaotumika na kuendesha
biashara kama vile kwa kugharimia ununuzi wa malighafi, kulipa mishahara ya nyenzo nyingine.
119
Utoaji alama wa uhakika ( ) utatumika tu kama washiriki wanadhani kuwa wana fedha zote
zinazotakiwa kuanzia biashara. Utoaji alama wa chini kabisa ( ) unaonyesha kuwa hawawezi
kupata chochote iwe fedha taslimu au akiba
Mahitaji: Mahitaji yabidhaa au huduma maana yake, upeo ambao unatafutwa na wateja;
Wakati wa kufikiria vipengele vya mahitaji ni muhimu kuzingatia viwango vyote vya ushindani
katika sokola mahali, upeo ambao mahitaji yanaweza kutimizwa kwa kutumia ama stadi za jadi
au zisizo za jadi, na mahitaji yanayotajwa kutoka kwa watuhusika, taasisi na biashara nyigine.
Upeo wa mahitaji pia unahusiana na uwezo wa kununua wa wateja; wanaweza kuwa na haja ya
kuwana bidhaa au huduma lakini hakuna fedha za kulipia. Katika hali kama hiyo, mahitaji halisi
yanakuwa ya kiwango cha chini. Taarifa ya kina zaidi kuhusu mahitaji inaweza kupatikana
kwenye zoezi la 15. Eleza kwamba kwa kila kigezo, lazima uandike nyuso nyingi zenye furaha, za
wastani au za huzuni kadiri iwezekanavyo, kutegemea upeo ambao kigezo hicho kinaridhika.
Wazo la biashara linalopata nyuso nyingi zenye furaha sana, huesabiwa kuwa inayofaa na
kutekeleza vilele, vigezo vinavyopata nyuso chache zenye furaha au hakuna kabisa au hupata
nyuso za wastani na zenye huzuni, kuwakilisha matatizo katika kuendeleza wazo la bidhaa au
huduma.
Upangaji kiwango hufanywa kwa kipimo cha kila kigezo kama ifuatavyo: Kwa mfano, kuhusiana na
kigezo cha uteuzi wa “mahitaji”, nyuso mbili zenye huzuni (upande wa kulia) inaonyesha kuwa hakuna
mahitaji yoyote au bidhaa hii; na nyuso mbili zenye furaha (upande wa kushoto) huonyesha mahitaji
yako juu wakati wowote (mahitaji makubwa mwaka mzima, bila mabadiliko yoyote ya msimu) kwa
kawaida, viwango ni kati yauso mmoja wenye furaha na mmoja wenye huzuni. Waambie vikundi
wachambue mawazo matatu ya biashara. Inaweza kuwa muhimu kurudia maelezo kwa kipimo cha
uwekaji kiwango.
5. Waambie vikundi wawasilishe mawazo yao ya mradi waliyoyapendelea zaidi na
waonyeshe viwango vya kundi lao kwa “nyuso”. Wambie washiriki wengine watoe
mawazo yao. Mchakato huu wa mwitiko hauna budi kutumiwa kwa kila kundi kwa
namna hiyo, uzoefu wa washiriki unaweza kutumiwa kwa ukamilifu kusaidia vikudi
katika kutathmini upya mawazo yao ya biashara. Hakikisha kwamba ni mtu
anayewasilisha taarifa kuhusu hoja muhimu za majadiliano.
6. Pitia angalau wazo moja lililochaguliwa kwa kila kikundi kwenye majadilianoya wote.
Ongeza viwango vyote kwa kila wazo la biashara na andika jumlakwenye safu
inayohusika kwenye chatipindu yenye pande mbili.
7. Kila mtu mpe muda wa kufikiria upya na kuangaliaupya wazo laola biashara, kwa
kuzigatia maoni yote. Kama kuna wasiwasi kuhusu wazo lililochaguliwa, vikundi
vinaweza kurudi kwenye mawazo ya biashara yaliyochaguliwa kama chaguola 2 au
3, na kurudia mchakato pamojana mawazo mengine ya biashara. Wape muda wa
120
kukamilisha zoezi hili ili kila kikundi (au mtu) anachagua wazo moja la biashara
watakaloliendeleza zaidi wakati wa SDSMV
8. Waambie washiriki kuagalia tena alama za viwango vyao kwenye vikundi vidogo, na
pitia upya viwago hivyo kulinganana tathmini yao ya mwisho. Katika hatua hii, taja
vile vinavyojulikana kuwa “mashaka yanayofisha” vinavyoweza kukwaza biashara
yote ingawa vinaweza kuwa mwanzoni vimepokea kiwango cha jumla cha juu au cha
wastani
“Mifano ya mashaka yanayofisha”: Bidhaa za sanaa zamikono huuzwa kwa mtu mmoja tu wa
kati. Katika hali kama hiyo, mtu wa kati (wakala au msambazaji) “ndiye” kigezo halisi cha
mzalishaji. Hata hivyo kusema kweli, mzalishaji anategemea soko la mbali zaidi, mara nyingi
soko ambalo halifahamu kabisa (kama vile wateja wan chi za nje) na wanaunda mahitaji halisi
kwa bidhaa zake. Kutkeapo mgogoro wa uchumi, au wanapokabiliwa na mienendo mipya na
mitindo inayotokea kwenye soko hilo, wakala au msambazaji (mtu wa kati) anaweza kupoteza
biashara na matokeo yake – na hata mzalishaji wa nchini. Timu yz mafunzo inaweza pia kutaja
suala la ushindani kwa kuwa suala hili ni muhumu sana katika biashara za wanawake na
maendeleo ya jamii. Itajitokeza tena wakati wa utafiti wa soko, na washiriki watakuwa
wamekwishaanza kufikiria kuhusu washuindani wao.
9. Hitimisha zoezi la uchambuzi wa kina kwa kuwaambia washiriki wachangie mawazo
yao kwenye matokeo, yakiwamo yale yanayohusu mashaka yote yanayoweza
kutokea (hatua ya sita). Usijenge wazo kuwa vigezo hivi vinatoa jibu la mwisho kwa
maswali yote. Wanatoa tathmini halisi kuhusu matarajio ya mafanikio katika soko.
Hata hivyo kuna mengi ya kujifunza kuhusu taratibu za soko; na hivyo mawazo ya
miradi iliyochaguliwa itakuwa kama mahali muhimu pa kuingilia sehemu za baadaye
za mafunzo.
Hitimisha zoezi hili kwa kutaja hatua ziazofuata katika kozi ya mafunzo itakayoshughulikia kwa
karibu zaidi na namna soko linavyofaya kazi. Washiriki wote wanajua kuwa “soko” ni mahali
ambapo bidhaa au huduma zinauzwa. Eleza kwamba dhana ya “soko” inatumiwa katika biashara
kama dhana ya jumla inayomaanisha ‘mauzo’ kama sehemu ya biashara kuna baadhi ya “sheria
za msingi”na “taratibu” kwa aina yoyote ya shighuli katika soko, na hatimaye ni mahitaji ya soko
yaayoamua mafanikio kwa mradi. Wakumbushe washiriki kuwa mahitaji yaliyptathminiwa
wakati wa zoezi , bado yana upungufu wa “hoja nzito na takwimu”, kamavile utafiti wa soko
kwa njia ya mahojiana/usaili, maoni hutokea kwa wajasiriamali wanaoshiriki kwa ukamilifu
katika soko,au uchanganuzi wa takwimu.
121
J.14.3.Zoezi: Yanayohitajika Kuunda Bidhaa au Huduma.
Malengo:
KUbainisha na kujifunza namna ya kusimamia vipengele muhimu vy uzalishaji wa bidhaa au
huduma:malighafi,nguvu kazi,zana na vifaa.
Kuelewa hatua mbalimbali katika mchakato wa uzalishaji.
Muda : Dakika 90
Vifaa Chatipindu,kalamu za kuchorea,kikokotezi.Bidhaa au huduma yoyote inayofaa mahali
panapohusika-anagalia mfano
Mfano wa uzlishaji-utengenezaji saladi
- Seti 1 ya vyombo vya jikoni kwa ajili ya kutengenezea saladi (kikombe ch
kupimia,kijiko,sahani,bakuli,n.k).
- Malighafi kwa kutayarishia aina ya vyakula vilivyochaguliwa(kwa mfano saladi ya
tambi,saladi ya papai).
Mfano wa hudumu-utengenezwaji nywele.
- Seti moja ya vyombo vya kutengenezea nywele,bakuli la maji,kitana,taulo,mkasi,kioo.
- Malighafi yanayohitajiwa kama nyenzo:maji,shampoo.
Namna ya Kufanya.
Hatua;
1. Anza kueleza madhumuni ya zoezi hili.Kujifunza namna ya kusimamia vipengele muhimu
katika uzalishaji wa bidhaa au huduma.Hii inajumuisha kubainisha uwezekano wa
kutekeleza mradi wa biashara,gharama za kutengeneza bidhaa au kutoa
huduma,pamoja na mahitaji ya soko na bei ambayo soko litakuwa tayari kulipa kwa
bidhaa au huduma Fulani.
2. Waeleze kuwa washiriki wataangalia kwa vitendo michakato miwili mifupi ya
uzalishaji.Kwa utengenezaji bidhaa na utoaji huduma.Vijana wawili watakua kama
wajasiriamali na kuonyesha mchakato wa uzalishaji na kugeuza malighafi kwa kutumi
nguvu kazi na zana kwa bidhaa au huduma iliyokubalika.Kwa kuchunguza na
kuchanganua,washiriki watabainisha vipengele muhimu vya mchakato wa uzalishaji
mdogo.Pia wanabainisha gharama mbalimbali zinazohusika katika mchakato wa
uzalishaji,na kujifunza namna ya kukokotoa gharama kwa bidhaa au huduma
3. Anza na eleza chati zifuatazo kwa washiriki
Chati ya uzalishaji (kielelezo cha kufundishia 1)
Orodha ya Gharama za malighafi(“ “2)
Orodha ya muda wa nguvu kazi(“ “ “3)
Orodha ya bei ya zana na Vifaa(“ “ “4)
4. Waambie washiriki wafuatilie kwa makini kitendo na waandike maelezo.Washiriki
wanaweza kuwa katika vikundi watafanya hesabu za kubainisha gharama za vifaa na
122
zana,malighafi,na muda wa nguvu kazi wa biashara ya uzalishaji na vikundi vingine
vitafanya kama hivyo kwa biashara ya huduma
5. Kila mjasiriamali ataeleza biashara yao ya “uzalishaji au huduma”na kuonyesha namna
inavyoweza kutengenezwa mitindo ya nywele ya kupendeza.Wakati wa kazi za
vikundi,washiriki wanabainisha mipango ya uzalishaji.Wanapata utambuzi kwa vitendo
katika kubuni na kuboresha biashara ndogondogo ya uzalishaji au huduma na kuweka
matokeo yao kwenye chati pindu.
6. Waambie vikundi wawasilishe matokeo yao.Pitia vitu mbalimbali na gharama kwenye
orodha tatu kila aina biashara na kujadili.
Kwa malighafi:hakikisha kama vitu vyote vimetumika,na kama kuna
vilivyobaki.Gharama haina budi kujumuisha bei ya vitu vilivyotumika tu.
Kwa ajili ya nguvukazi: hakikisha kama washiriki wameandika muda uliohitajika
kwa kila hatua kwenye uzalishaji wa chakula au huduma.Jumuisha muda
uliotumika na wasaidizi kama wapo.Jumuisha muda uliotumika kwa
kuzungumza na wateja.Waambie vikundi wakisie jumla ya gharama za muda wa
nguvu
Kazi kwa mfanyabiashara mwanamke:
Kwa dhana na vifaa: Hakikisha kama washiriki wameorodhesha dhana na
vifaa vyote, na gharama zao. Eleza kwamba dhana nyingi zinaweza
kutumiwa mara yingi. Waambie vikundi wakisie bidhaa au huduma ngapi
zinaweza kutolewa kabla ya kuhitaji kuunua dhana mpya, halafu kufaya
hesabu ya gharama ya zana zilizotumika katika uonyeshaji kwa vitendo kwa
wafanyabiashara wanawake wawili.
Matokeo ya sehemu hii ya zoezi yana budi kuandikwa kwa vizuri na kila
kikundi kwenye chatipindu au karatasi nyepesi na huweza kupatikana kwa
kazi ya kikundi kwnye zoezi linalofuata kuhusu upangaji wa gharama na bei
7. Wahimize washiriki wachanganue zaidi na kubadilishana uzoefu kuhusu muda wa
nguvu kazi, gharama ya ubora, wingi/idadi, nyenzo na matokeo. Anza majadiliano ya
jumla kuhusu mchakato wa uzalishaji kwa kutumia hoja zifuatazo:-
Mtu anawezaje kurekebisha /kubadili vifaa na zana kuongeza uzalishaji /tija au
kurahisisha na kuboresha mchakato wa uzalishaji au huduma?
Kama washiriki watarejea kwenye gharama za kudumu na/au zinazobadilika katika
hatua hii, eleza tofauti kwa mujibu wa mahitaji yao na maslahi (Kielelezo cha mafunzo
cha 5 na/au 6). Onyesha kuwa mada hii itafundishwa kwa kina zaidi katika mazoezi
yanayofuata
8. Eleza kuwa kila mchakato wa uzalishaji una hatua kuu 3
Kuandaa: Hii inahususika kutayarisha vijenzi vinavyotakiwa na kupata mali ghafi
(usafiri); kupima viambato (nkaguzi na mtendaji ); kukata mboga, kutayarisha
slesi za nyama, kuosha saladi (utendaji)
123
Kutenda: Kuweka mafuta ya kupikia kwenye kikaango (utendaji), kuweka slesi
za nyama au mboga kwenye kikaango; kupika na kukaanga (utendaji na
kuchelewa)
Kuondoa: Kuondoa bidhaa iliyokamilika kutoka kwenye kikaango (usafiri);
kuweka slesi zilizokaangwa kwenye chombo (uhifadhi)
9. Waambie washiriki waangalie vipengele muhimu vya “mchakato wa uzalishaji” katika
biashara inayozalisha na kuuza bidhaa na katika shughuli ya huduma
Wasilisha michakato ya uzalishaji iliyoonyeshwa katika vielelezo vya mafunzo ya 7 na 8 na jadili kila
moja ya hatua pamoja na washiriki.Waambie waeleze hatua kuu katika mchakato wa uzalishaji wa
biashara yao wenyewe.Waambie watoe baadhi ya mifano kutoka kwenye kazi ya kikundi
kuonyesha.Mchakato wa uzalishaji.Je,kilihitajika kiasi gani cha fedha na ilichukua muda gani kukamilisha
hatua zote? Katika kuhitimisha,sisitiza kuwa kila mchakato wa uzalishaji unaweza kuboreshwa.Hakikisha
kwamba washiriki wameelewa kwa ukamilifu vipengele mbalimbali vya uzalishaji,kwa sababu vitakuwa
muhimu kwa uelewa mzuri wa masuala ya fedha baadye.
Kielelezo cha Mafunzo cha 1: CHATI YA UZALISHAJI
UZALISHAJI/HUDUMA MALI GHAFI KAZI VIFAA NA
ZANA
Saladi Saladi
Mboga au matunda
Maji ya ndimu
Chumvi
Nyama au Samaki
Pilipili
Osha & safisha
Panga
Kata
Changanya
Pasha moto
Kaanga
Poza
Meza
Bakuli
Kikaango
Vikombe
Sahani
Vijiko
Visu na uma
124
Kutengeneza nywele Shampuu
Maji
Rangi
Kitana
Osha & safisha
kitana
kata
Kitana
Brashi
Mkasi
Kioo
Kikausha nywele
Kielelezo cha Mafunzo cha 2: Orodha ya Bei ya Malighafi
Vitu
Bei (fedha za ndani)
Makisio ya Bei kwa
bidhaa/huduma moja
Maoni
125
Kielelezo cha Mafunzo cha 3: Oridha ya Muda wa Kazi
Mchakato/Hatua Muda (dakika) Maoni
126
Kielelezo cha Mafunzo cha 4: Orodha ya Zana na Vifaa
Vitu Bei (fedha za nchi) Makisio ya Gharama
kwa bidhaa/huduma
moja
Maoni
127
Kielelezo cha Mafunzo cha 5. GHARAMA ZA KUDUMU NA ZINAZOBADILIKA
GHARAMA ZA KUDUMU: GHARAMA ZINAZOBADILIKA:
Gharama zisizobadilika
kwa idadi ya bidhaa
au huduma
Gharama zinazobadilika
Kwa idadi ya bidhaa
au huduma
Mifani :
Mishahara ya Watumishi wa kudumu
Kodi ya Nyumba
Majengo
Mitambo
Mifano:
Mali ghafi
(k.m. saladi,nyama,shampuu)
Maji
Umeme
Mishahara ya watumishi
Wasiokuwa wa kudumu
Vipindi vya shughuli nyingi tu
Kielelezo cha Mafunzo cha 6: Gharama za kudumu na zinazobadilika - Mifano
GHARAMA ZA
KUDUMU
BEI YA BIDHAA
Bidha za chakula Useremala Rejareja Huduma
Mali Ghafi
Mishahara na
Ujira;
Mboga
Matunda
Mbao
Bawaba
Gharama za
bidhaa zilizouzwa
dukani
Kununua
vijenzi
128
Huduma za jamii
(= utunzaji afya;
chekechea,
shule n.k.);
Mshahara wa
Mjasiriamali ;
Kodi ya nyumba ;
Usafiri ;
Huduma za umma
(= manispaa,
Ofisi ya ujasiri wa
biashara n.k.);
Matengenezo ;
Uchakavu ;
Mengineyo
Chumvi
Mafuta, siagi
Maji ya ndimu
Nyama
Viungo
Rangi
Tina
Skrubu
Mafuta ya
Turpentine
Gundi
malighafi
spea
Mengineyo
Mishahara ya
Watumishi wa
kudumu
Mishahara kwa
bidhaa
Mishahara kwa
bidhaa
Mishahara kwa
kazi mahususi
dukani
Mishahara kwa kila
shughuli
iliyotolewa
Hii inajumuisha
wewe mwenyewe
na wafanyakazi wa
kudumu
Mishahara
inayobadilika
inaweza
kukokotolewa kwa
Mishahara
inayobadilika
inaweza
kukokotolewa kwa
Mishahara
inayobadilika
inaweza
kukokotolewa kwa
Mishahara
inayobadilika
inaweza
kukokotolewa kwa
129
bidhaa k.m.
Kwa kg ya saladi
au kwa kiwango
cha mauzo
kitu k.m
Idadi ya
vitu
vilivyotengenezwa.
saa zilizofanyiwa
kazi.
saa zilizofanyiwa
kazi au idadi ya
huduma
zilizotolewa
Kielelezo cha Mafunzo cha 7: Mchakato wa Uzalishaji: Biashara ya Uzalishaji
Mauzo
Ufungashaji
Udhibiti
waUbora &
Ukaguzi
Kununua
Bidhaa
Ugeuzaji
Kuunganisha
Kumaliza
Usafiri
Malighafi Bidhaa
zilizotengen
ezwa
130
Kielelezo cha Mafunzo cha 8: Mchakatowa Uzalishaji – Biashara ya Huduma
J.14.4.Zoezi: Zana za Utunzaji Hesabu za Fedha”
Malengo:
Kuelewa umuhimu wa utunzaji wa kumbukumbu kwa ajili ya usimamizi mzuri wa biashara.
Kujifunza kuhusu kumbukumbu za msingi xa fedha na zana za kukokotelea kwa biashsra
Muda: Dakika 60-90
Vifaa: Chatipindu,kalamu8 za kuchorea,vielezo vy a mafunzo
9. Mfano utunzaji Rahisi wa Hesabu za Fedha:Tupu
Namna ya Kufanya:
Hatua:
Mauzo
Utangazaji
Udhibiti wa
Ubora na
Ukaguzi
Kumalizia
Ugeuzaji
Matayarisho
Zana na Vifaa
Kununua
131
1. Je,utunzaji wa kumbukumbu ni nini? Anza mada kwa kuwauliza washiriki
manachofahamu kuhusu utunzaji wa kumbukumbu wa hesabu wa hesabu za fedha,na
waulize kama hivi sasa wametunza kumbukumbu au wamewahi kufanya hivyo
kabla.Wauhimize washiriki washirikiane kueleza hata mbinu za kawaida mno za
“ufuatiliaji”wa mahali faedha zinakotumika.
Utunzaji wa kumbukumbu: Kuandika/kufuatilia ili kuelewa/kijikumbusha
Kiasi gani cha fedha kinachopokewa na biashara yako
Kiasi gani cha fedha kinacholipwa na biahara yako
Je,watu mbalimbali wanaokudai kiasi gani
Je,watu mbalimbali unaowadai kiasi gani
2. Eleza maana ya muamala: Muamala ni ubadilishaji wa fedha (au thamani) kwa bidhaa au
huduma.Fedha (au thamani) huingia na kutoka katika biashara kwa miamala.
Mifano miwili ya miamala ya “fedha zinazoingia”
Mteja ananunua bidhaa (bidhaa,huduma) kutoka kwenye biashara yako-
biashara yako inapata fedha kutoka kwa mteja
Unaweka fedha zako za biashara kwenye akaunti ya akiba-benki inakulipa riba
3. Tafuta mfano zaidi kuhusu miamala na vijana inayoonyesha fedha zinaingiaje na
zinatoka wapi kwenye biashara.Halafu tafuta mifano ya fedha zinakokwenda nje ya
biashara (Kulipia bidhaa,malighafi,nguvu kazi,kodi ya nyumba,umeme na gharama
nyingine zota). Mifano miwili ya miamala ya “fedha zinatoka”
Biashara yako imeingiza bidhaa na malighafi:wangapi wanaleta bidhaa hizo na
biashara yako inawalipa kutokana na huduma yao.
Wawe mmiliki,au mwanakikundi na unafanya kazi katika biashara.Biashara hiyo
inakulipa mshahara au inapata”hisa ya faida”kwenye biashara.
4. Waulize vijana kuhusunfaida ya kutunza kumbukumbu,na namna kumbukumbu hizi
zinavyosaidia biashara yako(ama kwa kikundi au mtu).Toa muhtasari wa majadiliano
kama ifuavyo:-
Kumbukumbu zinasaidia kudhibiti fedha zako: Kumbukumbu zako zinaonyesha
kiasi gani cha fedha ambacho biashara yako inatakiwa kuwa nazo katika hatua
yoyote. Tumia kumbukumbu hizo kuhakikisha kuwa fedha hazipotei au
kutoelezwa matumizi yake
Marejeo: Imechukuliwa kutoka zoezi la 23“Gender and Entrepreneurship Together: GET Ahead for Women in Enterprise:
Training Package and Resource Kit”, Susanne Bauer, Gerry Finnegan and Nelien Haspels, Bangkok, Berlin and Geneva,
International Labour Office, 2004
132
Kumbukumbu zinakuonyesha wewe namna gani biashara yako inavyoendelea.
Kumbukumbu zako zinakusaidia kutafuta matatizo kabla mambo hayajaharibika.
Tumia kumbukumbu zako kubaini kama kuna jambo haliendi vizuri, kama bei
ziko juu sana, kama mauzo yanapungua, kamakuna upotevu mahali Fulani
(wewe mwenyewe au mtu mwingine aafuja au kutumia vibaya fedha) na
kadhalika
Kumbukumbu zinawaonyesha WATU WENGINE namna biashara yako inavyoedelea.
Unahitaji kuwa na kumbukumbu sahihi wakati unapoomba mkopo na kulipa kodi zako.
Tumia kumbukumbu zako kuonyesha kuwa kila kitu kiko kwenye utaratibu na kwamba
unadhibiti biashara yako
Kumbukumbu zinakusaidia kupanga mambo yabaadaye: Kumbukumbu zinakuonyesha
mafanikio ya biashara yako siku zilizopita na mafanikio ya sasa . Kama unajua uwezo na
udhaifu wa biashara yako, unaweza kupanga vizuri kwa maendeleo ya baadaye
Kumbukumbu zinakusaidia kukumbuka wadai na wadaiwa: Kumbukumbu zako
ziakusaidia kujua jumla ya fedha unazotakiwa kupokea kutoka kwa wateja wako pamoja
na majina yao. Pia zinakusaidia kukumbuka kiasi cha fedha unachotakiwa kuwalipa
wengine ( kwa mfano wagavi wako)
Sehemu ya 2: Mifano ya Utunzaji Kumbukumbu
5. Mifumo ya utunzaji kumbukumbu inatakiwa kuwa rahisi kadiri iwezekanavyo. Waeleze
kuwamfumo hauna budi kujumuisha taarifa unayotaka kuweka kwenye kumbukumbu
kwa ajili ya usimamizi wako wa fedha – na si zaidi ya hayo! Eleza zana za utunzaji
kumbukumbu za msingi ambazo ni muhimu (angalia hapochini )na waambie washiriki
wachague ni kumbukumbu zipi wanazotaka kuanza kuzitumia kwenye biashara yao.
Mfumo wautunzaji kumbukumbu una sehemu zifuatazo (zinawezakutumika kwa mujibu
wa mahitaji ya washiriki). Onyesha Mfano Rahisi wa utunzaji Kumbukumbu za fedha
(kielelezo cha mafunzo cha 9 ) ambao mara nyingi hutumiwa na wafanyabiashara
waawake na wasaidizi wao katika maduka ya biashara, na wape nakala washiriki wote
Zana za utunzaji Kumbukumbu
1. Daftari ya Kumbukumbu: Hii ni kitovu cha mtunzaji kumbukumbu wako. Katika
daftariya kumbukumbu, andika yafuatayo:-
Fedha zote zinazoingia kwenye biashara yako na zinazotoka
Fedha zote zinazotoka kwenye biashara yako na zimetumika kwa ajili gani
Jenga tabia ya kuingiza miamala yote kwenye Daftari ya Kumbukumbu kila siku mwanzo
wakati wa shughuli na mwisho wa kila siku
133
Kielelezo cha Mafunzo cha 9: Mfano wa Utunzaji Rahisi wa Kumbukumbu za Fedha
Mtupu/wazi
Tarehe
Utendaji/Muamala
Fedha
zinazotoka
Fedha
zinazoingia
Malinganisho
J. 15. Mada Ndogo: Uchanganuzi wa Gharama na Faida
Kutokana na kumbukumbu zilizotunzwa wakati wa kilimo cha mazao mbalimbali kwenye shamba darasa
na matokeo ya zoezi la uuzaji na utafutaji soko. Vijana watatayarisha uchanganuzi wa gharama na faida
kwa kila zao lililolimwa kwenye shamba darasa. Kutokana na uchanganuzi wa gharama na faida watajua
kama wamepata faida na kutokana na kiasi cha nguvukazi kilichotumika, wamefanikiwa kupata kiasigani
kwa saa ya nguvukazi iliyotumika.
134
J.15.1.Zoezi: Ghrama na Faida
Muda : Saa moja
Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea
Hatua
1. Waambie vikundi mbalimbali watayarishe achanganuzi wa gharama na faida kwa mazao waliyokuwa
wanyashughulikia kwenye shamba darasa,kutokana na kumbukumbu walizotunza na matokeo ya
somo la utafutaji soko na uuzaji
2. Waambie vikundi wawasilishe uchanganuzi wao wa gharama na faida
3. Linganisha faida iliyopatikana kutoka mazao mbalimbali na bainisha ni kilimo cha mazao gani
kimeleta faida kubwa
4. Bainisha pamoja na vijana ni zao gani lililotumia nguvukazi kubwa na linganisha mapato kwa saa kwa
mazao tofauti
5. Jadili ni kilimo gani kilikuwa na gharama kubwa.Kama ungekopa fedha kwa ajili ya kilimo,je unafikiri
faida ilitosha kulipia riba ya fedha ulizokopa?
J.16.1. Zoezi : Kuweka mtandao wa Utando wa Buibui
Zoezi hili linalenga uundaji wa kikundi na kueleza kwa muhtasari masuala yanayohusiana kufanya kazi
pamoja kwa vikundi madhumuni ya uzlishaji.Watoto wanatengeza utando wa buibui wa mawazo
yaliyofumwa kwa uzi.Kupatia shughuli hii unaweza pia kusisitiza faida za kushirikishwa katika kikundi
kwa madhumini ya uzalishaji
Muda : Saa 1
Vifaa na matayarisho: Utahitaji uzi mrefu wa mpira,au kamba wa mita mia kadhaa.
Namna ya kufanya:
1. Washiriki wote waunde duara na kukaa chini.Kama kundi ni kubwa ,ligawe katika vikundi
vidogovidogo viwili au vitatu
2. Waambie vijana wafikirie kwa nini watu wanaunda vikundi.Je,wanajua mifano yoyote ya watu
wanaofanya kazi pamoja kwa vikundi kwa uzalishaji?Waambie wafikirie vikundi vya watu
wanaozalisha pamoja.Kwa mfano inaeweza kuwa uzalishaji wa bidhaa za kusafirisha nje ys
nchi,kufanya kazi pamoja mashambani,kufanya kazi kwa vikundi kwenye mashamba
makubwa,kutema kuni kwa vikundi,kuzalisha chakula na kuuza kwenye genge moja
sokoni,kuuza chakula kwenye magenge.Wape muda wanafunzi wafikirie kuhusu kwa nini wati
wanaunda vikundi.
3. Mpe mpira wa kamba au uzi mmoja wa wanafunzi na uwaambie waseme faida moja ya
kushirikishwa kwenye kikundi na kwa nini.Kwa mfano unaweza kujifunza kutoka kwa wengine
135
katika kikundi.Bila ya kujali mtu ansema nini;usiamue au kuwaruhusu wengine kubisha
alichosema.
4. Akimaliza,ashike imara ncha moja ya kamba,na kurusha au kupasiana mpira na mtu mmoja au
wengi au asiyekuwa mbali sana kwenye duara.Hii itaunda mstari wa kamba/nyuzi kwenye
duara.Halafu ayepokea kamba/uzi anataja faida nyingine ya kishikishwa katika kikundi.Hii
inaweza kuwa jambo lolote analofikiri au kulihusisha au kulinganisha na alichosema kijana
aliyepita.Halafu anaikaza kamba mkononi mna kupasia na kurusha mpira mshiriki mwengine
kwenye duara,anayeeleza mpaka kila mtuawe “amepata fursa”na wote kuwa wamefumwa
kwenye utando wa kamba wa buibui.
5. Kutegemea kikundi kimesema nini,unaweza kuongeza baadhi ya mapendekezo kukamilisha
utando wa buibui,kwa mafano:
- Kikundi kinaweza kufanya mengi zaidi
- Kusaidiana
- Kujifunza wenyewe kwa wenyewe
- Kupunguza gharama za kununua nyenzo
- Udhibiti wa ubora
- Kuweza kupata mkopo kama kikundi
- Ulinzi
- Kutoshondana moja kwa moja kwa watu wengine wanaotengeneza bidhaa ya aina moja.
- Kushirikiana taarifa
- Wnaweza kutathmini kwa pamoja mashaka ya soko
- Baadhi ya wana kikundi watapata stadi wasizokuwanazo wengine hii itachangia katika
mafanikio ya jumla kikundi.
- Ushirikiano
- Asasi za serikali au wengine watakuwa tayari zaidi kusaidia kikundi kuliko mtu mmoja
mmojaa.
- Kama mteja mmoja hakupendi (kwa mfano,anahusishafamilia yako na VVU(UKIMWI)bidhaa
inaweza kuendelea kununuliwa na kikundi
7. Baadaye wakati utando utakapokuwa umefunuliwa, toa muhtasari wa shababa za watu kujiunga au
kutojiunga katika vikundi vya uzalishaji. Hitimisha kwa kueleza kuwa watu mmoja mmoja peke yao
hukabiliwa na matatizo katikakuanzisha biashara na huwa ni hatari sana. Waambie kikundi wanyoshe
mikono kama wanafikiri ni wazo zuri kuunda kikundi. Halafu wale wanaofikiri kuwa si wazo zuri, nao
wanyoshe mikono. Hii inaweza kusababisha majadiliano ya kufurahisha na toa muhtasari wa hoja
muhimu zilizotolewa
136
Maelezo kwa Mwezeshaji.
Wahimize vijana wafikirie hoja za wanawake au wasichana kuunda vikundi na kushinda matatizo
ambayo wangeyakabili peke yao. Kama kuna vyama vya ushirika vyovyote vinavyoendeshwa jirani, vitaje
na zungumza vinafanya nini wakati unajadili faida za kuunda kikundi
Matayarisho kwa ajili ya siku ya Mahafali
Muda: Masomo mengi na wakati wa mahafali
Hatua:
1. Endesha majadiliano ya vikundi na vijana kubainisha kwa mujibu wao, kuwa wamejifunza
masuala/vitu/maarifa/stadi gani wakati wa SDSMV
2. Andika maoni haya kwa ajili ya tatmini ya mwisho ya programu ya SDSMV
3. Waambie vikundi mbalimbali watayarishe uwasilishaji namabango, kuonyesha kwa vitendo na/
au maigizo yanayoonyesha vitu muhimu zaidi waliyojifunza wakati wa SDSMV
4. Fanya mazoezi ya uonyeshaji kwa vitendo/maigizo na vikundi
5. Wasilisha vijijini mabango mbalimbali, uonyeshaji kwa vitendo na/au maigizo siku ya mahafali
137
Mtaala wa SDSMV
Mtaala wa SDSMV- Mahindi, Mpunga wa maji ya mvua, Mpunga wa kuwagilia maji, (kipindi cha miezi
4 -5 ya ukuaji wa mazao)
Mwezi Shughuli katika shamba darasa Mada maalumu za kilimo Mada maalumu za maisha/Shughuli za
kuongeza ajira
1 (4x) Kuandaa shamba (mahindi)
Kuandaa kitalu (mpunga)
Kusia (mahindi, mpunga)
Kupanga katika kilimo
Uchaguzi wa mbegu
Jaribio la uotaji wa mbegu
Kuandaa shamba + kitalu
Kusia
Kupanga kwa ajili ya baadaye
Umuhimu wa utunzaji kumbukumbu
2 (4x) Umwagiliaji (mpunga)
Urutubishaji
AESA
Palizi
Kuandaa shamba (mpunga)
Upandikizaji (mpunga)
Utangulizi IPM
Ikutambulisha ASEA
Palizi
Upandikizaji
Udhibiti wa maji
Urutubishaji
Ulinzi
Kufanya uamuzi katika maisha
Usafi
Maji ya kunywa safi/salama
Lishe
Utunzaji wa kumbukumbu za shughuli
mbalimbali katika shamba darasa
(gharama, nguvukazi, n.k.)
Kilimo kama biashara
3 (4x) AESA
Umwagiliaji Urutubishaji
Kulinda wadudu waharibifu
IPM
Urutubishaji mara ya pili
Palizi ya pili
Magonjwa katika maisha (malaria,
VVU/UKIMWI, n.k..)
Ajira kwa watoto
Haki za mali
4 (4x) AESA
Palizi
Kulinda wadudu waharibifu
IPM
Kuvuna
Ushughulikiaji baada ya kuvuna
Mikakati ya kuuza
Kupata faida
Shughuli za uongezaji ajira katika kilimo
5 (4x) Kuvuna (mpunga,mahindi)
Kuhifadhi ghalani
Kuuza
Usindikaji chakula
Ufungashaji
Kuuza
Uchanganuzi wa Gharama & Faida
Kuongeza thamani katika uzalishaji wa
Kilimo
6 (4x) Kuuza Vuna kwa maisha
Kutayarisha mipango ya kuanzisha
shughuli za kiuchumi
Mahafali ya SDSMV
138
Mtaala wa SDSMV – Mihogo (zao la miezi 6)
Mwezi Shughuli katika shamba darasa Mada maalumu za kilimo Mada maalumu za maisha/Shughuli za kuongeza ajira
1 (4x) Kuandaa shamba
Kuandaa kitalu
(maharage,mboga mboga)
Kupanda (mihogo)
Kupanga katika kilimo
Uchaguzi wa mbegu
Jaribio la uotaji wa mbegu
Kuandaa shamba + kitalu
Kusia
Kupanga kwa ajili ya baadaye
Umuhimu wa utunzaji kumbukumbu
2 (4x) Umwagiliaji (mpunga)
Urutubishaji
AESA
Palizi
Upandikizaji
(maharage,mbogamboga)
Utangulizi IPM
Ikutambulisha ASEA
Palizi
Upandikizaji
Udhibiti wa maji
Urutubishaji
Ulinzi
Kufanya uamuzi katika maisha
Usafi
Maji ya kunywa safi/salama
Lishe
Utunzaji wa kumbukumbu za shughuli mbalimbali katika shamba darasa
(gharama, nguvukazi, n.k.)
Kilimo kama biashara
3 (2x) AESA
Umwagiliaji Urutubishaji
Kulinda wadudu waharibifu
IPM
Palizi ya pili
Magonjwa katika maisha (malaria, VVU/UKIMWI, n.k..)
Ajira kwa watoto
4 (2x) AESA
Kuvuna (maharage)
Palizi
Pest management
IPM
Mikakati ya Kuuza
Haki za Mali
5 (2x) AESA
Kulinda wadudu waharibifu
Kupata faida
Shughuli za uongezaji ajira katika kilimo
6 (2x) AESA
Kulinda wadudu waharibifu
Kuvuna
Ushughulikiaji baada ya
kuvuna
Shughuli za uongezaji ajira katika kilimo
7 (4x) Kuvuna
Kuhifadhi ghalani
Kuuza
Usindikaji chakula
Ufungashaji
Kuuza
Uchanganuzi wa Gharama & Faida
Kuongeza thamani katika uzalishaji wa Kilimo
8 (4x) Kuuza Vuna kwa maisha
Kutayarisha mipango ya kuanzisha shughuli za kiuchumi after JFFLS
Mahafali ya SDSMV
139
Mtaala wa SDSMV – Spinachi (zao la mwezi mmoja)
Mwezi Shughuli katika shamba darasa Mada maalumu za kilimo Mada maalumu za maisha/Shughuli za kuongeza ajira
1 (8x)
Zao la kwanza
Kuandaa shamba
Kuandaa kitalu
Kumwagilia kitalu
Kusia
Kuandaa shamba
Kupandikiza
Kutambulisha AESA
Kumwagilia shamba kuu
Palizi
Kudhibiti visumbufu
Kuvuna
Kupanga katika kilimo
Uchaguzi wa mbegu
Jaribio la uotaji wa mbegu
Kuandaa shamba na kitalu
Kusia
Kupandikiza
Kudhibiti maji
Kutambulisha IPM
Kutambulisha ASEA
Urutubishaji
Kulinda
Kupanga kwa ajili ya baadae
Umuhimu wa kutunza kumbukumbu
2 (8x)
Zao la pili
Kuandaa shamba
Kuandaa kitalu
Kumwagilia kitalu
Kusia
Kuandaa shamba
Kupandikiza
Kutambulisha AESA
Kumwagilia maji mshamba
Palizi
Kudhibiti visumbufu
Kuvuna
Kuvuna
Ushughulikiaji baada ya
kulima
Kufanya uamuzi katika maisha
Usafi
Maji safi na salama
Lishe
Magonjwa katika maisha (Malaria,VVU/UKIMWI,n.k.)
Utunzaji wa kumbukumbu za ishughulikaji,mazao ya shamba darasa
gharama,nguvukazi n.k.)
Kilimo kama biashara
Ajira kwa watoto
Haki za mali
Mikakati ya kuuza
3 (8x) Uhifadhi ghalani
Utafutaji soko/uuzaji
Usindikaji chakula
Ufungashaji
Kuuza
Kupata faida
Uongezaji ajira katika kilimo
Uchanganuzi wa Gharama na faida
Shughuli za kuongeza thamani katika uzalishaji wa kilimo
Kuvuna kwa ajili ya maisha
Kutayarisha mipango kwa ajili ya kuanzisha shughuli za kiuchumi
baada ya SDSMV
Mahafali ya SDSMV
140