TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

Embed Size (px)

Citation preview

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    1/8

    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

    OFISI YA WAZIRI MKUU

    TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

    TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHESHIMIWA

    JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    KATIKA ZIARA YAKE MKOANI RUKWA

    TAREHE 16 MEI, 2013.

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,S.L.P 128, Sumbawanga,RUKWA.Simu. Na. 025 - 2802137/2802138Nukushi: 2802117/2802318

    Baruapepe: [email protected] MEI 16, 2013

    mailto:[email protected]:[email protected]
  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    2/8

    1.0. UTANGULIZI.

    Mheshimiwa Jaji Mkuu, Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kwa

    Niaba ya Wananchi na Viongozi wa Mkoa wa Rukwa kukukaribisha wewe

    na Viongozi ulioambatana nao hapa Mkoani Rukwa. Ni matumaini ya

    Uongozi wa Mkoa wa Rukwa na wananchi wake kuwa, ziara hii italeta Tija

    katika Utumishi wetu kwa Umma kutokana na ukweli kwamba tunajua

    tutapata ushauri, maelekezo na maagizo kwa ajili ya kuboresha utendaji

    wetu wa kazi.

    Mheshimiwa Jaji Mkuu, Baada ya Serikali kuridhia kumega sehemu ya

    Mkoa wa Rukwa na kuanzishwa Mkoa mpya wa Katavi, kuna mabadiliko

    ya eneo la jiografia la Mkoa na maeneo ya Utawala. Kwa sasa Mkoa wa

    Rukwa unaundwa na Wilaya tatu ambazo ni:- Sumbawanga, Nkasi na

    Kalambo. Mkoa una Halmashauri nne, Halmashauri za Wilaya ya

    Sumbawanga, Nkasi, Kalambo na Manispaa ya Sumbawanga.

    Kwa kuzingatia mgawanyo huo sasa Mkoa wa Rukwa una eneo la

    kilometa za mraba 27,713 wakati kilometa za mraba 22,792 ni la ardhi

    na kilometa za mraba 4,921 ni eneo la maji. Mipaka ya sasa ya Mkoa wa

    Rukwa upande wa Kusini - Magharibi Mkoa unapakana na nchi ya

    Zambia, upande wa Kaskazini - Mashariki Mkoa wa Katavi, upande wa

    Kusini - Mashariki Mkoa wa Mbeya, na upande Magharibi nchi ya

    Kidemokrasi ya Kongo (DRC). Mkoa wa Rukwa uko Kusini-Magharibi

    mwa Tanzania kwenye Latitudo 050 na 090 Kusini na Longitudo 30 - 330

    Mashariki.

    2.0. SENSA YA WATU NA MAKAZI

    Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 Mkoa wa

    Rukwa una Jumla ya Watu 1,004,539 kwa mchanganuo wa Wanaume

    487,311 na Wanawake 517,228

    Na

    .

    Jina la Wilaya ME KE JUMLA

    1 Kalambo 100,474 107,226 207,7002 Sumbawanga DC 149,062 156,784 305,846

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    3/8

    3 Nkasi DC 137,041 144,159 281,2004 Sumbawanga MC 100,734 109,059 209,793

    JUMLA 487,31

    1

    517,22

    8

    1,004,53

    9

    3.0. SHUGHULI ZA UCHUMI ZA WAKAZI WA MKOA WA RUKWA

    Shughuli kuu za kiuchumi za Wakazi wa Mkoa wa Rukwa ni kilimo,

    ufugaji na Uvuvi.

    3.1. Kilimo

    Wakazi wengi wa Mkoa wa Rukwa hujishughulisha na Kilimo takribani

    70% ya wakulima wa Mkoa wa Rukwa wanatumia kilimo cha jembe la

    kukokotwa na Ngombe

    Katika msimu wa kilimo wa 2012/2013 Mkoa umelenga kulima jumla ya

    hekta 401,837.0 za mazao ya chakula na hekta 93,103.0 za mazao ya

    biashara ambazo tunatarajia kutupatia kiasi cha tani 1,357,836.0 za

    mazao ya chakula na tani 184,731.4 za mazao ya biashara.

    3.1.1. Kilimo cha Umwagiliaji

    Kutokana na Mpango kabambe wa Umwagiliaji Taifa wa mwaka 2002,

    ilibainika kuwa Mkoa wa Rukwa una jumla ya Hekta 527,721 zenye

    uwezo wa kumwagiliwa. Kati ya eneo hilo kekta 14,310 zina uwezo wa

    juu, hekta 42,294 zina uwezo wa kati na hekta 471,117 uwezo wake ni

    wa chini. Kwa sasa eneo linalomwagiliwa ni hekta 14,382.08 sawa na

    25.41% ya eneo lenye uwezo wa juu na kati wa kumwagiliwa.

    Mkoa una jumla ya Miradi ya Umwagiliaji 10 ambayo inaendelezwa kwa

    njia ya kisasa na Miradi ya Umwagiliaji 16 ambayo haijaendelezwa

    inamwagilia kwa kutumia njia za asili (Traditional Irrigation).

    Kwa mwaka 2011/2012 Mkoa ulipangiwa jumla ya Sh. Bilioni

    1,322,000,000/=kutoka Mfuko wa Umwagiliaji wa Wilaya (DIDF).

    Mgawanyo wa fedha hizo ni kama ifuatavyo:- Halmashauri ya Wilaya

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    4/8

    Sumbawanga TShs. 1,072, 000,000/= na Wilaya ya Nkasi TShs. 250,

    000,000/= .

    Aidha, kwa mwaka 2012/2013 Mkoa umepangiwa jumla ya

    Sh.1,031,250,000/= kutoka Mfuko wa Umwagiliaji wa Wilaya (DIDF).

    Mgawanyo wa fedha hizo ni kama ifuatavyo:- Halmashauri ya Wilaya

    Sumbawanga TShs. 515,625,000/= na Wilaya ya Nkasi TShs.

    515,625,000/=. Kazi za utekelezaji wa miradi hiyo zinaendelea.

    3.2. Hali ya ufugaji

    Kulingana na sensa ya sampuli ya kilimo ya mwaka 2002/2003 Mkoa wa

    Rukwa ni moja kati ya mikoa yenye idadi ya wastani (moderate) ya

    mifugo.

    Kufuatana na Sensa hiyo, Daftari la Mkulima na Taarifa za maendeleo ya

    mifugo za kila mwaka kutoka katika Halmashauri Idadi ya mifugo

    (mwaka 2011) inakisiwa kufikia ngombe 438,555, mbuzi 152,899,

    kondoo 22,867, nguruwe 49989, punda 6,171, kuku 470,595. Takwimu

    hizi, hususan za ngombe zinatiliwa mashaka na baadhi ya wadau ambao

    wanaamini idadi ya ngombe ni kubwa zaidi. Mikakati ya mkoa ya

    kuendeleza ufugaji ni pamoja na kuhakiki takwimu za mifugo.

    3.2.1. Mfumo wa ufugaji

    Ufugaji katika Mkoa wa Rukwa huendeshwa chini ya mifumo ya aina

    mbili kubwa, ufugaji huria (extensive) na ufugaji shadidi (intensive).

    Ufugaji shadidi ni mdogo sana; chini ya 1% na hufanyika katika ranchi ya

    Kampuni za Ranchi za Taifa (KARATA) iliyoko Kalambo pamoja na

    kwenye mashamba ya mifugo yaliyobinafsishwa ya Nkundi na Malonje.

    Ranchi ya Kalambo na shamba la mifugo la Nkundi huzalisha ngombe

    wa nyama wakati shamba la Malonje ni la ngombe wa maziwa. Kwa

    kiwango kidogo pia, ufugaji wa ngombe wa maziwa upo, hasa katika

    eneo la Manispaa ya Sumbawanga. Mkoani Rukwa kuna ngombe wa

    maziwa 5,760, na mbuzi wa maziwa 496 (Taarifa za maendeleo ya

    mifugo toka Halmashauri 2012).

    3.3. Uvuvi.

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    5/8

    Kutokana na sensa ya mwaka 1999 uzalishaji wa samaki toka Ziwa

    Rukwa unakadiriwa kuwa ni tani 7,000 na Ziwa Tanganyika linakadiriwa

    kuzalisha samaki kiasi cha tani 165,000 hadi tani 200,000 kwa mwaka

    wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 80 hadi milioni 100.

    Kuna aina mbali mbali ya samaki wanaopatikana katika maziwa na mito

    iliyopo katika Mkoa wetu. Ziwa Tanganyika linatupatia samaki aina ya

    dagaa, migebuka, sangara, kuhe, kambale na samaki wa mapambo.

    Ziwa Rukwa linatupatia kambale, gege na mamba. Dagaa na migebuka

    wanaopatikana ziwa Tanganyina na gege toka ziwa Rukwa mara nyingi

    hukaushwa na kupelekwa kuuzwa kweye masoko makubwa ndani na nje

    ya nchi mfano Zambia, Kongo na Burundi.

    4.0. HALI YA ULINZI NA USALAMA.

    Mheshimiwa Jaji Mkuu, Kwa upande wa Kisiasa viko vyama tisa (9)

    vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu kwa mwaka 2010 wa Rais, Wabunge na

    Madiwani. Chama Cha Mapinduzi, ndicho chama chenye nguvu kisiasa

    katika Mkoa wa Rukwa. Kati ya Waheshimiwa Wabunge 7, wote

    wanatoka Chama Cha Mapinduzi na kati ya Wahe. Madiwani 86 wa

    kuchaguliwa, 78 wanatoka Chama Cha Mapinduzi, 6 kutoka CHADEMA, 1

    kutoka CUF na 1 kutoka UDP.

    Taarifa ya Waheshimiwa Wabunge hao saba inajumlisha matokeo ya

    kurejesha kiti cha ubunge kwa Mhe. Aeshi Khalifan Hilaly baada ya

    mchakato wa kisheria kufanyika.

    Kwa ujumla hali ya Ulinzi na Usalama katika Mkoa ni shwari japo kuwa

    kuna changamoto mbalimbali za uhalifu ambazo Mkoa umeendelea

    kudhibiti na kuzishughulikia kupitia Kamati za Ulinzi na Usalama za Mkoa

    na Wilaya.

    4.1. MATUKIO YASIYO YA KAWAIDA NDANI YA MKOA

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    6/8

    Ndani ya mwezi Februari, 2013 Mkoa umekubwa na matukio makubwa

    mawili mabaya, ambayo Serikali ya Mkoa kupitia vyombo vya Ulinzi na

    Usalama tulijitahidi kuhakikisha wale wote waliohusika wanawajibishwa

    kwa mujibu wa Sheria.

    4.1.1. Tukio la kukatwa Mkono Albino Mwanamke Miangalua

    Mnamo tarehe 14/02/2013 Albino Bibi. Maria Chambanenge miaka 39

    Mkazi wa Kata ya Miangalua Wilaya ya Sumbawanga alikatwa mkono

    kwa kile kinachosadikika ni imani za kishirikina. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

    kwa kushirikiana na Vyombo vya Ulinzi na Usalama, ilitoa msaada wa

    haraka ili kuokoa maisha ya Bibi Maria Chambanenge kwa kumuwahisha

    Hospitali ya Mkoa kwa ajili ya matibabu na aliweza kuhudumiwa.

    Kupitia vyombo vya Ulinzi na Usalama Mkono wa Bibi. Maria

    Chambanenge uliweza kupatikana na kuhifadhiwa katika chumba cha

    maiti Hospitali ya Mkoa.

    Katika tukio hilo wahusika wa uhalifu huo wanne (4) walikamatwa na

    suala hilo lipo katika vyombo vya sheria hadi sasa.

    4.1.2. Tukio la kukatwa Mkono kwa Albino Mtoto - Milepa

    Mnamo siku ya tarehe 15/02/2013 Majira ya Mchana katika Kijiji cha Msia

    huko Milepa Wilaya ya Sumbawanga Mtoto wa kiume Mwigulu

    Mwasonange miaka 12 akiwa na mtoto mwenzake wakioga mtoni ghafla

    walivamiwa, na Mtoto Mwigulu Mwasonange alikatwa mkono na watu

    wasiojulikana na kuweza kutokomea nao kusikojulikana na kuacha mtoto

    akipoteza fahamu kutokana na maumivu makali na kuvuja damu kwa

    wingi.

    Mtoto Mwigulu Mwasonange alipatiwa matibabu na hali yake kiafya

    iliweza kuimarika. Kwa sasa Mtoto Mwigulu Mwasonange alipata ufadhili

    wa kusomeshwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Under the Same Sun

    nanaendelea na Masomo yake Jijini Dar es Salaam.

    4.2. Mgogoro wa Uchinjaji wa Kitoweo

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    7/8

    Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Mhandisi Stella Martin Manyanya (Mb)

    aliandaa Mkutano wa pamoja baina yake na Viongozi wa Madhehebu ya

    Dini ya Waislamu na Wakristo, tarehe 23 Machi, 2013. katika Mkutano

    ambao ulihudhuriwa na Viongozi Waandamizi wa Serikali.

    Mkuu wa Mkoa aliitisha mkutano huo, akiwa na malengo ya kuwasihi

    Viongozi hao wa madhehebu ya Dini kuvumiliana, kwa kila mtu kuabudu

    kulingana na imani yake. Pamoja na kuhubiri Amani kufuatia Viongozi wa

    pande zote mbili kutoa Matamko mbalimbali. Hali iliyokuwa ikitishia

    Amani na Usalama wa Mkoa.

    5.0 MIGOGORO YA ARDHI

    Migogoro ya ardhi ipo Mkoani kwetu, katika sura tatu.

    (i) Mgogoro unaotokana na pande mbili kuuziana viwanja na

    kugombania mipaka au kukosa nyaaka muhimu za kuhalarisha

    umiliki . Ambapo sehemu kubwa migogoro hii uamuliwa na

    Baraza la Ardhi na Nyumba la Sumbawanga.

    (ii) Mgogoro wa pili ni baina ya Wakulima na Wafugaji. Mkoa

    umeuhisha TAMKO LA MTOWISA kwa kuzitaka Wilaya kuwa na

    Master plan ambazo zitaonesha matumizi bora ya ardhi. Pia

    Halmashauri zote zimeagizwa kuwa Vyama vya Wafugaji kama

    kile cha Wilayani Nkasi ambacho kinawaunganisha wafugaji na

    kuwataka kuwa na mifugo kulinana na maeneo ya malisho

    (iii) Eneo la tatu la mgogoro ni baina ya Wawekezaji wakubwa wa

    mashamba na Vijiji jirani. Ili kutatua matatizo kama haya Mkoa

    huunda Kamati ya uchunguzi ili kubaini ukweli na baadaye suala

    husika huwasilishwa OWM TAMISEMI na Wizara ya Ardhi kwa

    maamuzi.

    6.0. MSONGAMANO WA MAHABUSU

    Mheshimiwa Jaji, Tunakabiliwa na msongamano mkubwa wa

    mahabusu katika Gereza la Mahabusu la Sumbawanga mara tatu zaidi

    ya uwezo wake; hii inatokana na kwamba Wilaya ya Nkasi na Kalambo

    hazina mahabusu wala Mahakama za Wilaya hivyo kupelekea mashauri

  • 7/30/2019 TAARIFA YA MKOA WA RUKWA KWA MHE. JAJI MKUU WA TANZANIA MOHAMMED CHANDE OTHMAN

    8/8

    yote kutoka Wilaya zote za mkoa huu kutajwa katika Wilaya ya

    Sumbawanga pekee.

    Katika kukabiliana na hili Mkoa ulifanya mawasiliano kwa njia ya barua

    na kwa njia ya ana kwa ana na Wizara ya Katiba ya Sheria kuhusu

    mpango wa Mkoa kujenga Mahakama za Wilaya na Wizara ifanye

    umaliziaji wa majengo hayo. Tunashukuru ramani za majengo ya

    Mahakama za Wilaya tumeshapokea na tuliahidiwa maombi yetu

    yatawekwa katika bajeti ya mwaka 2013/2014. Ni matumaini yetu suala

    hilo litafanyika kama tulivyoahidiwa.

    7.0. HITIMISHO

    Mheshimiwa Jaji Mkuu,Tumewasilisha Taarifa ya Mkoa kwa Muhtasari

    ili uweze kupata mwanga kuhusu Mkoa wetu, kwa niaba ya Wananchi wa

    Mkoa wa Rukwa na Wananchi napenda kutumia fursa hii kukukaribisha

    tena Mkoani kwetu wewe na msafara wako ulioambatana nao, tupo

    tayari kuufanyia kazi maagizo, ushauri, maoni au maelekezo

    utakayotupatia kwa ajili ya Ustawi na Maendeleo ya Taifa letu.

    Karibu sana Mkoani Rukwa Mheshimiwa Jaji.

    Salum Mohamed Chima (Alhaj)

    Katibu Tawala wa Mkoa Rukwa