20
1 | Page TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA UTENDAJI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA LISHE ULIOFANYIKA TAREHE 28 AGOSTI, 2018 JIJINI DODOMA. 1.0 UTANGULIZI; Katika Mkuatano wa Kitaifa wa Urutubishaji Chakula (National Summit on Food Fortification) uliofanyika tarehe 23-24 mwezi Agosti, 2017 katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere, Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan alikuwa ni Mgeni Rasmi. Katika hotuba yake aliagiza kuwepo kwa mkataba wa utendaji na Wakuu wa Mikoa yote ya Tanzania Bara ili wasimamie utekelezaji wa shughuli za lishe katika Mikoa yao ili kuondoa tatizo la utapiamlo nchini. Kwa kuwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ina jukumu la kusimamia utekelezaji katika ngazi za Mikoa na Halmashauri, iliandaa mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita ili kujenga uelewa wa pamoja juu ya viashiria vya Mkataba vitakavyokuwa vikipimwa na pia kubaini maeneo ya kuboresha. 1.1. Malengo ya kuwa na Mkataba wa Lishe: 1.1.1. Lengo Kuu, Ni kusimamia masuala ya lishe ili kupunguza athari za utapiamlo katika Mikoa na Taifa kwa ujumla.

TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

  • Upload
    others

  • View
    78

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

1 | P a g e

TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA

UTENDAJI NA USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA LISHE

ULIOFANYIKA TAREHE 28 AGOSTI, 2018 JIJINI DODOMA.

1.0 UTANGULIZI;

Katika Mkuatano wa Kitaifa wa Urutubishaji Chakula (National Summit

on Food Fortification) uliofanyika tarehe 23-24 mwezi Agosti, 2017 katika

ukumbi wa kimataifa wa Julius Nyerere, Mheshimiwa Makamu wa Rais

wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan

alikuwa ni Mgeni Rasmi. Katika hotuba yake aliagiza kuwepo kwa

mkataba wa utendaji na Wakuu wa Mikoa yote ya Tanzania Bara ili

wasimamie utekelezaji wa shughuli za lishe katika Mikoa yao ili kuondoa

tatizo la utapiamlo nchini. Kwa kuwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI ina jukumu

la kusimamia utekelezaji katika ngazi za Mikoa na Halmashauri, iliandaa

mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini

ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita ili kujenga uelewa wa

pamoja juu ya viashiria vya Mkataba vitakavyokuwa vikipimwa na pia

kubaini maeneo ya kuboresha.

1.1. Malengo ya kuwa na Mkataba wa Lishe:

1.1.1. Lengo Kuu,

Ni kusimamia masuala ya lishe ili kupunguza athari za utapiamlo katika

Mikoa na Taifa kwa ujumla.

Page 2: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

2 | P a g e

1.1.2. Malengo mahsusi;

2. Kuhakikisha kuwa Mikoa inasimamia ipasavyo utekelezaji wa afua

za lishe katika maeneo yao.

3. Kuchukua hatua madhubuti za kupunguza hali duni ya lishe katika

Mikoa husika

4. Kutenga na kutumia fedha kwa ajili ya kutekeleza afua za lishe

katika mipango ya Mikoa na Halmashauri.

5. Kusimamia na kuratibu shughuli za wadau mbalimbali

wanaotekeleza na kufadhili shughuli za lishe katika maeneo yao.

2.0. Hatua za Utekelezaji;

2.1 Timu ya kusimamia utekelezaji wa Agizo,

OR TAMISEMI iliteua jumla ya wataalam tisa (9) waliounda timu

iliyosimamia utekelezaji wa agizo la kuandaa mkataba wa kusimamia

shughuli za lishe uliosainiwa baina Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,

TAMISEMI na Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara. Timu

hii ilitekeleza agizo hili chini ya usimamizi wa Katibu Mkuu na Naibu

Katibu Mkuu anayeshughulikia Afya, Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

Page 3: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

3 | P a g e

Jedwali 1. Timu ya usimamizi wa agizo la kuandaa mkataba

Na. Jina Cheo Idara

1 Dkt. Ntuli A.Kapologwe Mkurugenzi DHS

2 Steven J. Motambi Mkurugenzi

msaidizi

DHS

3 Ibrahim Minja Mkurugenzi

msaidizi

DRA

4 Suleiman Lukanga Mwanasheria DLS

5 Mwita J.M. Waibe Afisa Lishe DHS

6 Rose Lugendo Afisa Utawala DAHRM

7 Jeremiah H. Mwambange Afisa Lishe DHS

8 Mariam Nakuwa Afisa Lishe DHS

9 Magesa Japhari Afisa Lishe DHS

Nyenzo ya kukusanyia taarifa iliandaliwa kulingana na vigezo

vilivyoainishwa kwenye Mkataba na kusambazwa katika Mikoa yote ya

Tanzania Bara.

2.2 Viashiria na vigezo vilivyotumika kupima utekelezaji wa Mkataba;

Vigezo viliandaliwa na sehemu ya huduma za Lishe katika Idara ya Afya

Ustawi wa Jamii na Lishe Ofisi ya Rais -TAMISEMI. Jumla ya Viashiria 11

viliandaliwa na kujumuishwa katika Mkataba ili kuwawezesha

Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa kusimamia utekelezaji wa mkataba

husika. Aidha, viashiria hivyo vilivyotumika wakati wa tathmini ni kama

vifuatavyo: -

Page 4: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

4 | P a g e

1. ASILIMIA YA KIASI CHA FEDHA KILICHOTENGWA KATIKA BAJETI KWA AJILI

YA AFUA ZA LISHE KULINGANA NA IDADI YA WATOTO WALIO NA UMRI

CHINI YA MIAKA MITANO KATIKA MKOA KWA MUJIBU WA MWONGOZO WA

MWAKA HUSIKA. 2. ASILIMIA YA KIASI CHA FEDHA KILICHOTENGWA KATIKA BAJETI KWA

AJILI YA URATIBU WA HUDUMA ZA LISHE KATIKA NGAZI YA MKOA KWA

MUJIBU WA MWONGOZO.

3. ASILIMIA YA KIASI CHA FEDHA KILICHOTUMIKA KUTEKELEZA AFUA ZA

LISHE UKILINGANISHA NA KIASI CHA FEDHA KILICHOTENGWA KATIKA

BAJETI KATIKA NGAZI YA MKOA NA HALMASHAURI.

4. UWEPO WA MPANGO MKAKATI WA LISHE WA MKOA.

5. IDADI YA WATOTO WENYE UMRI WA MIEZI 6 HADI MIAKA 5 WALIOPATIWA

NYONGEZA YA MATONE YA VITAMINI A UKILINGANISHA NA IDADI YA

WATOTO WENYE UMRI HUO KATIKA MKOA.

6. IDADI YA WANAWAKE WAJAWAZITO WALIOPATIWA VIDONGE VYA MADINI

YA CHUMA NA ASIDI YA FOLIKI UKILINGANISHA NA IDADI YA WAJAWAZITO

WOTE WANAOTARAJIWA KATIKA MKOA.

7. IDADI YA AKINAMAMA WENYE WATOTO WALIO NA UMRI CHINI YA MIEZI

6 WALIOPATIWA ELIMU YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA YA MAMA PEKEE

UKILINGANISHA NA IDADI YA AKINAMAMA WOTE WENYE WATOTO WALIO

NA UMRI CHINI YA MIEZI SITA KATIKA MKOA.

8. IDADI YA AKINAMAMA WENYE WATOTO WENYE UMRI WA KUANZIA MIEZI 6

HADI MIAKA 2 WALIOPATIWA ELIMU YA ULISHAJI WA VYAKULA VYA

NYONGEZA KWA WATOTO UKILINGANISHA NA IDADI YA AKINAMAMA

WOTE WENYE WATOTO WENYE UMRI HUO KATIKA MKOA.

9. IDADI YA WATOTO WENYE UTAPIAMLO WALIOPATIWA MATIBABU

UKILINGANISHA NA IDADI YA WATOTO WOTE WALIOGUNDULIWA KUWA NA

UTAPIAMLO.

10. IDADI YA VIKAO VYA KAMATI YA LISHE VILIVYOFANYIKA UKILINGANISHA

NA IDADI YA VIKAO 4 VINAVYOTAKIWA KUFANYIKA KWA MWAKA HUSIKA

KATIKA MKOA NA HALMASHAURI.

11. IDADI YA KAGUZI ZA CHAKULA NA DAWA ZILIZOFANYIKA

KULINGANISHA NA KAGUZI ZILIZOTAKIWA KUFANYIKA KWA MWAKA

HUSIKA KATIKA MKOA NA HALMASHAURI.

Page 5: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

5 | P a g e

2.3 Kusaini mkataba wa usimamizi wa afua za lishe,

Mkataba wa utekelezaji wa masuala ya Lishe ulisainiwa baina ya Mhe. WN

OR - TAMISEMI na Wakuu wa Mikoa yote Tanzania Bara ikiwa ni

utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan tarehe 19 Desemba,

2017 na kuanza utekelezaji wa Mkataba huu mwezi Januari, 2018.

2.4. Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe,

Tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa Lishe ulifanyika ukilenga mambo

yafuatayo: -

Mikoa kuwasilisha utekelezaji wa viashiria vilivyo kwenye Mkataba

wa Makubaliano wa Masuala ya Lishe baada ya miezi sita ya

utekelezaji.

Kujenga uelewa wa pamoja wa utekelezaji wa viashiria vilivyoko

katika Mkataba wa Lishe.

Kuongeza msukumo wa usimamizi na uelewa wa masuala ya Lishe

ili kupunguza kiwango cha utapiamlo nchini.

Kufafanua madhara na hasara ya utapiamlo katika uchumi na

maendeleo ya nchi.

2.4.1 Ukusanyaji na uchakataji wa taarifa;

Taarifa za utekelezaji wa mkataba zilikusanywa kutoka Mikoa na

kuchakatwa kulingana na viashiria na vigezo vilivyowekwa ambapo kila

Mkoa ulipangwa kulingana na utekelezaji wa kila kiashiria. Baada ya hapo

Page 6: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

6 | P a g e

taarifa ilitumwa katika Mikoa kabla ya kuwasilishwa katika Mkutano wa

tathmini uliofanyika tarehe 28 Agosti, 2018 Jijini Dodoma na kuhudhuriwa

na: -

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI,

Katibu Mkuu OR – TAMISEMI,

Manaibu Katibu Wakuu Afya na Elimu- OR – TAMISEMI,

Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa yote ya Tanzania Bara,

Makatibu Tawala wa Mikoa yote ya Tanzania Bara,

Wawakilishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu,

Wawakilishi kutoka Wizara Mbalimbali ambazo ni Wizara ya Afya,

Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika,

Wizara ya Fedha na Mipango, Wizara ya Elimu, Sayansi na

Teknolojia, Wizara ya Mifungo na Uvuvi,

Wakurugenzi na wataalamu kutoka OR TAMISEMI,

Wawakilishi kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC)

Wadau wa Lishe nchini (USAID, UNICEF, DFID, WFP na PANITA)

Wawakilishi wa Waganga Wakuu wa Mikoa na Halmashauri

Wawakilishi wa Maafisa Lishe wa Mikoa na Halmashauri

2.4.2 Matokeo ya utekelezaji wa viashiria;

Hali ya utekelezaji wa afua za lishe kwa kipindi cha miezi sita tangu

kusainiwa kwa mkataba huo ni kama inavyoonekana kwenye jedwali:

Page 7: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

7 | P a g e

2.4.2.1 Kiasi cha fedha zilizotumika kutekeleza shughuli za lishe

kulinganisha na fedha iliyotengwa,

Mkoa 1 tu wa Kilimanjaro kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara ndio

umefanikiwa kutumia zaidi ya 50% ya fedha walizopanga.

COMPACT indicator % of Gov.

fund

expended

against

budgeted

Gov. budget

spent per

under-five

child (THS.)

Availability

of regional

nutrition

strategic

plan

Completion

rate of

nutrition

quarterly

steering

committee

against

Completion

rate of

nutrition

quarterly

supportive

supervision

against

# of

quarterly

food

inspection

conducted

in the

region

% of

expected

cases of

SAM

amongst

children 0-

59 months

% of

mothers/car

egivers of

children 0-

23 months

who have

received

% of

children

aged 6-59

months

supplement

ed with

Vit.A

% of

pregnant

women who

received IFA

among

attended

casesARUSHA 14% 186 - 41% 31% 0 36% 3% 92% 61%

DAR ES SALAAM 32% 135 - 33% 63% 0 3% 0% 92% 71%

DODOMA 17% 120 - 39% 39% 0 9% 52% 101% 70%

GEITA 48% 252 - 0% 75% 0 8% 50% 97% 63%

IRINGA 18% 64 - 71% 63% 0 98% 68% 96% 59%

KAGERA 25% 62 - 67% 61% 0 17% 38% 91% 72%

KATAVI 11% 192 - 25% 25% 0 13% 39% 97% 40%

KIGOMA 3% 6 - 22% 31% 0 11% 26% 98% 48%

KILIMANJARO 58% 178 - 16% 56% 4 2% 35% 97% 69%

LINDI 31% 321 - 25% 57% 4 35% 19% 96% 55%

MANYARA 38% 439 1 63% 69% 0 2% 47% 100% 61%

MARA 18% 418 - 4% 11% 0 2% 5% 91% 51%

MBEYA 11% 119 1 43% 64% 4 78% 64% 92% 70%

MOROGORO 37% 523 - 25% 45% 4 11% 53% 96% 61%

MTWARA 21% 225 - 80% 68% 4 26% 13% 100% 53%

MWANZA 12% 89 - 47% 53% 4 5% 45% 98% 58%

NJOMBE 37% 181 - 50% 61% 4 65% 60% 113% 44%

PWANI 13% 391 - 14% 36% 4 4% 32% 99% 56%

RUKWA 24% 335 1 25% 35% 0 1% 44% 98% 51%

RUVUMA 10% 445 - 9% 31% 0 31% 24% 92% 45%

SHINYANGA 13% 98 - 86% 71% 0 21% 49% 98% 68%

SIMIYU 14% 86 - 14% 64% 4 14% 57% 96% 39%

SINGIDA 25% 377 - 33% 66% 0 17% 38% 105% 54%

SONGWE 15% 18 - 50% 58% 0 61% 64% 92% 58%

TABORA 19% 240 - 47% 28% 4 4% 29% 96% 38%

TANGA 5% 33 - 2% 11% 0 12% 17% 97% 53%

Page 8: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

8 | P a g e

Chanzo cha Taarifa: Taarifa za Mkoa

COMPACT indicator % of Gov.

fund

expended

against

budgeted

ARUSHA 14%

DAR ES SALAAM 32%

DODOMA 17%

GEITA 48%

IRINGA 18%

KAGERA 25%

KATAVI 11%

KIGOMA 3%

KILIMANJARO 58%

LINDI 31%

MANYARA 38%

MARA 18%

MBEYA 11%

MOROGORO 37%

MTWARA 21%

MWANZA 12%

NJOMBE 37%

PWANI 13%

RUKWA 24%

RUVUMA 10%

SHINYANGA 13%

SIMIYU 14%

SINGIDA 25%

SONGWE 15%

TABORA 19%

TANGA 5%

Page 9: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

9 | P a g e

2.4.2.2 Mikoa kuwa na mpango mkakati wa lishe.

Ni Mikoa mitatu tu ambayo imeshaandaa mpango mkakati wa lishe

kufikia tarehe ya kikao. Mikoa mingine ipo katika hatua mbalimbali za

uandaaji wa mpango mkakati wa lishe.

Chanzo: Taarifa ya mkoa

2.4.2.3 Ufanisi wa kutoa nyongeza ya Vitamin A

Watoto walio na umri wa miezi 6-59 waliopatiwa nyongeza ya matone ya

Vitamin A ambapo wastani wa kitaifa ni asilimia 96. Mikoa 19 ilitoa

nyongeza ya matone ya vitamin A zaidi ya wastani wa kitaifa wakati

Mikoa ya Dar Es Salaam, Arusha, Mbeya, Songwe, Ruvuma, Kagera na

Mara hawakuweza kufikia wastani huo wa kitaifa.

Page 10: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

10 | P a g e

Chanzo: CHNM campaign report June, 2018

2.4.2.4 Vidonge vya kuongeza wekundu wa damu (madini ya chuma na

asidi ya foliki).

Wastani wa wajawazito waliopatiwa vidonge vya kuongeza wekundu wa

damu (FeFo) ambapo wastani wa Kitaifa ni asilimia 76. Mikoa yaTabora,

Simiyu, Katavi, Njombe, Ruvuma na Kigoma ipo chini ya wastani wa

Kitaifa katika utoaji wa Madini Chuma na asidi ya foliki kwa Wanawake

wajawazito wanaohudhuria kliniki katika vituo vya kutolea huduma za

afya.

Page 11: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

11 | P a g e

Chanzo: DHIS 2

Matokeo ya ufanisi wa utoaji wa Madini ya Chuma na Asidi ya Foliki kwa

Mikoa yote (FeFO)

Page 12: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

12 | P a g e

Chanzo: DHIS 2

2.4.2.6 Elimu ya ulishaji wa vyakula vya nyongeza kwa watoto;

Katika utoaji wa elimu hii ni Mikoa 8 tu ya Iringa, Songwe, Mbeya,

Njombe, Simiyu, Morogoro, Dodoma na Geita imefikia zaidi ya asilimia 50

ya utoaji wa elimu hii kwa wazazi na walezi. Aidha, Mikoa mingine yote

imetekeleza kwa kiwango chini ya asilimia 50.

Chanzo: Taarifa za Mikoa

Page 13: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

13 | P a g e

2.4.2.7 Matibabu ya utapiamlo mkali katika vituo vya kutolea huduma za

afya;

Katika huduma ya matibabu ya utapiamlo mkali ni Mikoa 4 ya Iringa,

Mbeya, Njombe, Songwe ndio imefikia zaidi ya asilimia 50. Aidha Mikoa

iliyobaki imetekeleza kwa kiwango chini ya asilimia 50.

Chanzo: BNA for FY 2017/2018

2.4.2.8 Utendaji wa kamati za lishe;

Mikoa 2 ya Shinyanga na Mtwara ndiyo pekee iliweza kukaa wastani wa

vikao 3 kati ya 4 vilivyotakiwa, hii ikiwa ni asilimia 75%. Mikoa mingine

haikutekeleza kiashiria hiki kama ilivyotakiwa.

Page 14: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

14 | P a g e

Chanzo: Taarifa za Miko

Ufanisi wa Kamati za Lishe

COMPACT indicator Completion

rate of

nutrition

quarterly

steering

committee

against ARUSHA 41%

DAR ES SALAAM 33%

DODOMA 39%

GEITA 0%

IRINGA 71%

KAGERA 67%

KATAVI 25%

KIGOMA 22%

KILIMANJARO 16%

LINDI 25%

MANYARA 63%

MARA 4%

MBEYA 43%

MOROGORO 25%

MTWARA 80%

MWANZA 47%

NJOMBE 50%

PWANI 14%

RUKWA 25%

RUVUMA 9%

SHINYANGA 86%

SIMIYU 14%

SINGIDA 33%

SONGWE 50%

TABORA 47%

TANGA 2%

Page 15: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

15 | P a g e

2.4.2.10 Usimamizi Shirikishi uliofanyika;

Mkoa mmoja tu wa Geita ndio umefanya usimamizi shirikishi wa shughuli

za Lishe kwa zaidi ya 75%. Mikoa mingine imefanya usimamizi kwa chini

ya asilimia 75.

Chanzo: taarifa za Mikoa

2.4.2.11 Ukaguzi wa usafi na usalama wa vyakula;

Mikoa 10 ya Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza,

Njombe, Pwani, Simiyu na Tabora imeripoti kufanya ukaguzi wa vyakula

angalau mara moja katika kipindi cha mwaka 2017/18. Mikoa 16 iliyobaki

haijafanya kabisa.

Page 16: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

16 | P a g e

2.4.3 Maazimio na Mapendekezo;

Baada ya mawasilisho yaliyoonyesha hali halisi ya utekelezaji wa afua za

Lishe washiriki wa Mkutano walipata wasaa wa kufanya majadiliano na

kuweka maazimio kadhaa ya kuhakikisha usimamizi na utekelezaji wa

shughuli za lishe unafikia kiwango cha kuridhisha na hatimaye

kupunguza tatizo la utapiamlo nchini.

Jedwali lifuatalo limeanisha maazimio yaliyofikiwa katika majadiliano ya

kutathmini utekelezaji wa Mkataba wa Lishe nchini:

Page 17: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

17 | P a g e

Na. HOJA MAELEKEZO MUHUSIKA MUDA WA

MWISHO WA

UTEKELEZAJI

1 Kutosimamiwa kwa

karibu utekelezaji wa

Afua za Lishe kwenye

Mikoa na

Halmashauri.

Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa

Mikoa waingie Mikataba ya usimamizi wa

afua za Lishe wenye viashiria 11 na Wakuu

wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa

Majiji/Manispaa/Miji/Halmashauri.

Katibu Tawala

wa Mkoa

30 Septemba,

2018

2 Kutoingizwa kwa

shughuli za lishe za

wadau kwenye

Mipango ya Mikoa na

Halmashauri. Pamoja

na kutenga fedha

kutoka vyanzo vya

ndani na kuzitoa ili

kutekeleza afua za

lishe.

Wadau wote wanaotekeleza afua za lishe

wasimamiwe na kuhakikisha shughuli zao

zinaingizwa kwenye mipango ya Mikoa na

Halmashauri wakati wa kufanya mapitio ya

mipango mwezi Disemba 2018. Aidha, kila

mwaka wa fedha mipango yote ya wadau

iwe sehemu ya MTEF’s za Mikoa na

Halmashauri na fedha zinazopangwa

zitolewe kama zilivyowekwa kwenye bajeti.

Kutenga na kutoa fedha kwa ajili ya

utekelezaji wa afua za lishe. Kamati za fedha

zisimamie na kutoa taarifa ya utekelezaji wa

afua za lishe na matumizi ya fedha

Katibu Tawala

wa Mkoa na

Wakurugenzi

Watendaji wa

MSM

31 Januari,

2019

Katika kutenga

fedha ni kila

mwaka wa

mpango na

bajeti

Page 18: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

18 | P a g e

zilizotumika katika kutekeleza afua hizo

Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa wakati

Kwa kamati za

fedha ni kila

robo ya

utekelezaji

3 Wadau wanaofanya

shughuli za Afya na

Lishe kutotambulika.

Mikoa kusimamia na kutambua (Mapping)

wadau wote wanaotekeleza afua za Afya na

Lishe kwenye Mikoa yao.

Katibu Tawala na

Wakurugenzi

Watendaji wa

MSM

1 Disemba,

2018

4 Kutofanyika kwa

vikao vya kamati za

lishe katika Mikoa na

Halmashauri kwa

mujibu wa miongozo

Vikao vya kila robo vya kamati ya lishe

viwekwe kwenye Kalenda ya vikao ya

Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa na

vifanyike kwa mujibu wa ratiba hiyo.

Aidha, vikao vya kamati ya lishe vijadili

taarifa za lishe kabla hazijawasilishwa katika

ngazi inayofuata na pia mikutano

mbalimbali itumike katika kujenga uelewa

wa pamoja kuhusu masuala ya Lishe nchini

KatibuTawala wa

Mkoa na

Wakurugenzi wa

MSM

30 Septemba,

2018

Page 19: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

19 | P a g e

5 Kutokufanyika kwa

usimamizi shirikishi

katika afua za Lishe

Ngazi zote (Mikoa na Halmashauri) kufanya

usimamizi shirikishi kwa kila robo ya

mwaka kwa mujibu wa miongozo.

Katibu Tawala

wa Mkoa na

Mkurugenzi wa

MSM

Kila robo

mwaka.

6 Wadau kutowasilisha

taarifa ya utekelezaji

ya afua za lishe

kwenye Mikoa na

Halmashauri

Taarifa za utekelezaji wa afua za lishe

zinazofanywa na wadau ziwasilishwe

kwenye Mikoa na Halmashauri kila robo

kwa ajili ya tathimini na ufuatiliaji.

Makatibu Tawala

na Wakurugenzi

Watendaji wa

MSM

Kila robo

mwaka.

7 Vikao mbalimbali

kutojadili masuala ya

lishe.

Lishe iwe Ajenda ya kudumu katika vikao

vya RCC, DCC, CMT na vikao vingine

tendaji. Aidha, vikao hivyo vitumike katika

kuwawezesha viongozi wa ngazi mbalimbali

kupata uelewa wa pamoja katika utekelezaji

wa afua za Lishe.

Mkuu wa Mkoa

na Mkuu wa

Wilaya

Endelevu

Page 20: TAARIFA YA TATHIMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA …€¦ · mkataba huo wenye viashiria vya upimaji vipatavyo 11. Aidha, tathimini ya kwanza ilipangwa kufanyika baada ya miezi sita

20 | P a g e

2.5 Changamoto katika uchakataji wa taarifa za mkataba;

Taarifa zilizopokelewa kuwa na mapungufu ya kitakwimu hivyo

kukosa ubora

Ucheleweshaji wa taarifa kufikia Wizara kwa wakati kwa mujibu wa

taratibu.

Taarifa kutojadiliwa katika mamlaka husika za Mikoa na

Halmashauri.

Kutotekelezwa kwa ufanisi kwa baadhi ya viashiria ndani ya

Mkataba wa Lishe.

2.6 Maeneo ya kuboresha;

1. Mipango na bajeti kuzingatia matatizo yaliyopo katika Halmashauri

na Mkoa husika.

2. Kuendelea kuwajengea uwezo Maafisa Lishe na watoa huduma juu

ya ubora katika ukusanyaji na utoaji wa taarifa.

3. Kutumia mifumo iliyopo kupata taarifa sahihi mf. Epicor, DHIS n.k

HITIMISHO;

Kwa ujumla baada ya tathmini ya utekelezaji wa Mkataba wa kusimamia

shughuli za Lishe kulingana na viashiria pamoja na vigezo vilivyowekwa

matokeo yake si ya kuridhisha japo kuna baadhi ya Mikoa imeonyesha

mwelekeo mzuri kwenye utekelezaji. Hivyo, OR TAMISEMI itaendelea

kusimamia kwa ukaribu utekelezaji na itaendelea kufanya tathmini ndani

ya miezi sita ili kupima mafanikio yanayofikiwa.