Upload
mathias-kavishe-lekundayo
View
580
Download
0
Embed Size (px)
DESCRIPTION
Mwisho wa kuomba ni june 30
Citation preview
Livestock Training Agency- Admission Office
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
WAKALA WA VYUO VYA MAFUNZO YA MIFUGO - LITA
TANGAZO LA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA STASHAHADA NA ASTASHAHADA KATIKA WAKALA WA VYUO VYA MAFUNZO YA MIFUGO (LIVESTOCK TRAINING AGENCY) KATIKA
MWAKA WA MASOMO 2014/15
1. Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) inatangaza nafasi za mafunzo katika ngazi ya Astashahada na Stashahada kama ifuatavyo: Stashahada ya Afya na Uzalishaji wa Mifugo (Diploma in Animal Health and Production -
DAHP) Astashahada ya Afya na Uzalishaji Mifugo (Animal Health and Production Certificate -
CAHP) Astashahada ya Ufundi Sanifu wa Maabara (Certificate in Veterinary Laboratory
Technology - CVLT)
2. Katika mwaka wa fedha wa 2014/2015, Serikali kupitia Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) itatoa mafunzo kwenye Kampasi zake sita na vituo vyake viwili Tengeru, Mpwapwa, Morogoro, Buhuri, Madaba, Temeke, Vituo vya Mabuki na Kikulula. Kampasi ya Temeke haina malazi hivyo watakaojiunga itabidi wajitegemee kwa malazi. Pia katika Kampasi zetu kutakuwa na nafasi chache kwa wanafunzi watakaopenda kukaa nje ya Chuo (Private day students).
3. Wakala inakaribisha maombi kutoka kwa vijana waliomaliza kidato cha Nne wanaotaka kujiunga na mafunzo ngazi ya Astashahada. Pia vijana waliomaliza Kidato cha Sita na wale wenye Astashahada katika fani zinazohusiana na kozi wanazoomba kwa ajili ya kujiunga na mafunzo ngazi ya Stashahada.
4. Kampasi zitakazohusika na mafunzo hayo ni kama inavyooneshwa kwenye jedwali hapa chini:
Na KAMPASI / KITUO
ANUANI KOZI ZITOLEWAZO
1. TENGERU S.L.P 3101 Arusha DAHP & CAHP(Bweni na kutwa)2. MPWAPWA S.L.P 51 Mpwapwa DAHP & CAHP(Bweni na kutwa)3. MOROGORO S.L.P 603 Morogoro DAHP& CAHP (Bweni na kutwa)4. BUHURI S.L.P 1483 Tanga CAHP(Bweni na kutwa)5. MADABA S.L.P 568 Songea DAHP & CAHP(Bweni na kutwa)6. TEMEKE S.L.P 39866 DSM CVLT (Kutwa)7. MABUKI S.L.P 352 Mwanza CAHP (Bweni na kutwa)8. KIKULULA S.L.P 147 Karagwe CAHP (Bweni)
For further information contact:Tel / +255 222 863 479 e-mail: [email protected] or [email protected] Payment: LITA Revenue Account, NMB Morogoro, Acc. No. 22110003142
Temeke Veterinari,Barabara ya Mandela,S. L. P. 9152,DAR ES SALAAM
Telegram: MifugoSimu: 255 022 2861910 Fax: 255 022 2861908E-mail: [email protected]: http://www.mifugouvuvi.go.tz
Livestock Training Agency- Admission Office
5. Sifa za mwombajii) Stashahada (Diploma)
Awe amemaliza elimu ya Kidato cha Sita kufaulu masomo matatu ya Sayansi kati ya Baiolojia, Kemia, Fizikia, Hisabati, Jiografia na Kilimo. Kiwango cha chini cha ufaulu kitakachomwezesha muombaji kukubaliwa ni cha subsidiaries mbili kwenye masomo ya sayansi. AU
Awe amemaliza mafunzo ya Astashahada (Certificate) katika fani ya Animal Health and Production (AHPC), Agrovet au Certificate in Agriculture and Livestock Production (CALP) ambayo ni sawa na NTA Level 5 kwenye vyuo vilivyosajiliwa na NACTE
ii) Astashahada (Certificate)
Awe amemaliza Kidato cha Nne na kufaulu masomo matatu ya sayansi kati ya Baiolojia, Kemia, Fizikia, Hisabati, jiografia na Kilimo. Kiwango cha chini cha ufaulu kitakachomwezesha muombaji kukubaliwa ni cha alama ya D kwenye masomo ya sayansi.
6. Masharti ya Uombaji Mwombaji atume fomu za maombi ya kozi anayotaka kusomea kwa kujaza fomu
akiambatanisha nakala (photocopies) za vyeti vyake vya elimu, pamoja na cheti cha kuzaliwa.
Fomu inapatikana kwenye Kampasi zetu, vituo vyetu vyote na Tuvuti ya Wizara Website: www.mifugouvuvi.go.tz /organization /Agencies/LITA
Fomu irudishwe na Bank pay-in slip ya Tshs 20,000/= iliyolipwa LITA Revenue Account, NMB Morogoro, Acc. No. 22110003142
Fomu zote zitumwe Makao Makuu ya Wakala na siyo kwenye Kampasi za Mafunzo kwa kutumia anuani au barua pepe ya hapo chini.
Waombaji watakaoomba nafasi za kutwa itabidi wajiandae kutafuta sehemu za malazi na kuonyesha Kampasi atakayopenda kusomea.
7. Gharama za MafunzoGharama za mafunzo zimeonyeshwa kwenye fomu ya maombi ambayo inapatikana kwenye Kampasi, vituo vya Wakala na tovuti ya Wizara Website: www.mifugouvuvi.go.tz /organization /Agencies/LITA
8. Mwisho wa kupokea maombiMwisho wa kupokea fomu za kujiunga na masomo ni tarehe 30/06/2014.
9. Taarifa kwa watakaochaguliwaMajina ya watakaochaguliwa yatatangazwa kwenye magazeti ya Daily News na Habari Leo, kwenye mbao za matangazo za Wizara, Kampasi, vtuo vyake vyote na kwenye tovuti: www.mifugouvuvi.go.tz /organization /Agencies/LITA
10.Utaratibu wa kutuma fomu za maombiFomu za maombi zitumwe kwa:
MTENDAJI MKUU,WAKALA WA VYUO VYA MAFUNZO YA MIFUGO - LITA,S.L.P. 9152,
For further information contact:Tel / +255 222 863 479 e-mail: [email protected] or [email protected] Payment: LITA Revenue Account, NMB Morogoro, Acc. No. 22110003142
Livestock Training Agency- Admission Office
DAR ES SALAAM
For further information contact:Tel / +255 222 863 479 e-mail: [email protected] or [email protected] Payment: LITA Revenue Account, NMB Morogoro, Acc. No. 22110003142