13
Page | 0 TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR MUONGOZO WA MAADILI YA VYAMA VYA SIASA KWA UCHAGUZI MKUU, 2015 MEI, 2015

TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 0

TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

MUONGOZO WA MAADILI YA VYAMA VYA SIASA KWA

UCHAGUZI MKUU, 2015

MEI, 2015

Page 2: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 1

MUONGOZO WA MAADILI YA VYAMA VYA SIASA KWA UCHAGUZI MKUU, 2015

Utangulizi

Kwa kuwa tunahitaji kuwa na amani, uhuru wa kampeni, na kuheshimu sheria ili kufanya

uchaguzi wa huru na wa haki. Sisi vyama vya siasa tumeamua kwa hiari yetu wenyewe

kutengeneza maadili haya ili yatuongoze katika shughuli zetu za uchaguzi na tuna

kubalina sisi kama wananchi wa Zanzibar tutahakikisha kuwa maadili haya yanajulikana

kwa wagombea, mawakala na wafuasi wetu, na kwamba tutahakikisha vifungu vyote

vinatakelezwa kikamilifu. Kwa hiyo, kwa hiari yetu tunatengeneza na kujipa wenyewe

maadili yafuatayo:-

Mamlaka 1. Maadili haya yanaanzishwa chini ya kifungu cha 130 cha Sheria ya

Uchaguzi Namba 11 ya 1984

Kuanza

kutumika

2. (1) Maadili haya yametayarishwa kwa pamoja kati ya Vyama vya

Siasa vinavyoshiriki Uchaguzi Mkuu wa 2015, Serikali ya Mapinduzi

ya Zanzibar na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na yataanza kutumika

baada ya uteuzi wa wagombea na kumalizika mwezi mmoja baada

ya uchaguzi.

(2) Maadili haya pia yatatumika katika Uchaguzi Mdogo pale

utakapojitokeza.

Madhumuni 3. Madhumuni ya Maadili haya ni kuhakikisha Uchaguzi Mkuu wa

Zanzibar wa mwaka 2015 unafanyika katika mazingira ya amani na

utulivu kwa kuzingatia uhuru na haki ya ushiriki wa makundi yote ya

kijamii yakiwemo wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu, na

vigezo vya kimataifa vya uchaguzi wa kidemokrasia.

Haki na wajibu

wa Vyama vya

siasa.

4. (1) Sisi Vyama vya Siasa, tunaoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar

wa mwaka 2015, tukiwa wawakilishi wa wananchi tunaamini na

kukubali kuwa:

a. Kulinda usalama, utulivu na amani ya Zanzibar ni jukumu la msingi

la vyama na wananchi wote.

b. Vyama vitahakikisha ushiriki huru na ulinzi kwa wanawake, vijana

na watu wenye ulemavu kama wapiga kura au wagombea.

Page 3: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 2

c. Kufuata maelekezo ya Sheria, Kanuni, Miongozo ya Tume, Maadili

na Taratibu za Uchaguzi ni muhimu katika kufanya uchaguzi ulio

huru na wa haki.

d. Vyama havitatumia makundi ya wanawake na vijana katika

kuchochea vurugu na uvunjifu wa amani wakati wa uchaguzi.

e. Kujiunga na Chama chochote cha siasa na kumchagua kiongozi

anayemtaka ni uhuru na haki ya kila mwananchi mwenyewe.

f. Kila Chama cha Siasa kinachoshiriki katika Uchaguzi Mkuu wa

Zanzibar wa mwaka 2015 kina haki ya kufanya kampeni kwa

mujibu wa sheria na taratibu zilizopo nchini.

Thamani utu

na haki za

binadamu

5. (1) Sisi Vyama vya Siasa kwa umoja wetu :

a Tunathibitisha kwa imani yetu kwamba, utu, thamani, na haki ya

maisha ya mwanadamu vinastahiki kulindwa kwa nguvu zote

kama ilivyoelezwa katika Katiba ya Zanzibar 1984, nchi na

maazimio ya kimataifa

b Tunapinga kwa nguvu zetu zote hujuma dhidi ya maisha ya

mwanadamu na mali zake kwa sababu ya itikadi yake ya kisiasa;

c Tutaheshimu haki ya kila Chama cha Siasa, wanachama na

wafuasi wake kutoa na kueleza maoni yao ya kisiasa na kutekeleza

shughuli zao na malengo ya kisiasa kwa mujibu wa Sheria; na

d Tutaheshimu utu wa mwanamke na mtu mwenye ulemavu kama

wagombea na wapiga kura katika mchakato wa uchaguzi.

Kupinga na

kujiepusha na

kauli za chuki,

fujo, vitisho na

vurugu

6. (1) Sisi Vyama vya Siasa kwa pamoja;-

a. Tunakataa na kupinga matumizi ya silaha za aina yoyote

kutumiwa na viongozi, mawakala, mwanachama na wafuasi wetu

kwa malengo ya kufanya hujuma katika harakati za kisiasa;

b. Tunakaa mbinu zozote zisizo halali kutumika na vyama katika

harakati za uchaguzi.

Page 4: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 3

c. Tunakataa matumizi matumizi ya vikundi vya ulinzi vya vyama

kutumiwa kwa malengo ya kuchochea fujo na kuvuruga amani

wakati wa kampeni na uchaguzi

d. Tunaamini kuwa ni jukumu na wajibu wetu wa kuwa na jamii

yenye mahusiano mema, yasiyo ya vurugu, chuki na vitisho;

e. Tunakataa kauli na vitendo vyote vinavyopelekea kuibua hisia za

chuki, vitisho, fujo, udhalilishaji wa wanawake na watu wenye

ulemavu na kutofahamiana katika kutekeleza malengo ya kisiasa;

(2) Kwa muelekeo huo kufanya Uchaguzi wa kidemokrasia

ulioandaliwa katika mazingira ya uwazi na ukweli ni jambo muhimu

sana kwa ustawi wa Zanzibar.

Sheria,

Kanuni na

Taratibu

7. Sisi Vyama vya Siasa tunakubali kuwa:

a. Tutatekeleza shughuli zote za kisiasa kwa mujibu wa Sheria ya

Uchaguzi, Kanuni, Miongozo ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na

Taratibu zinazotawala mwenendo wa Uchaguzi Zanzibar.

b. Tunakemea vitendo vya rushwa na vyengine visivyo halali, pia

tunawasisitiza wafuasi wa vyetu na wananchi kuepuka kutoa

matangazo na matamshi yatakayochochea ubaguzi wa aina

yoyote ukiwemo rangi, kabila, jinsia, dini, ulemavu, na itikadi za

kisiasa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu;

c. Tunawataka wanachama na mawakala wetu kuheshimu haki za

wengine, ili kuhakikisha kuwa haki ya mtu kutoa mawazo yake

inaheshimiwa.

Kampeni za

utulivu, amani

na heshima

kwa wengine

8. Sisi vyama vya siasa, tuko tayari kusaidia kwa uwezo wetu wote

kufikia malengo ya Uchaguzi huru na haki na tunaahidi kufanya

yafuatayo;

a) Kukataza matumizi ya lugha za matusi, lugha sizizofaa,

vitisho na vitendo vya fujo vitavyopelekea kushawishi na

kuharibu mikutano au shughuli nyingine halali za Vyama vya

Siasa.

Page 5: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 4

b) Kupinga uchapishwaji wa vijarida, vipeperushi, mabango ya

matangazo, katuni, katika mitandao ya kijamii au aina

nyingine za machapisho yatayobeba ujumbe unaochochea

na kuwashawishi watu kuvunja amani ya nchi au kudhalilisha

wagombea kutokana na jinsia zao au ulemavu;

c) Kukataza wagombea, wanachama na wafuasi wa vyama vya

siasa kufanya vitendo vya aina yoyote vitakavyoharibu

mikutano, maandamano au mikusanyiko ya chama chengine

cha siasa.

d) Kukataza na kupinga vikali vitendo vyote vitakavyopelekea

kuharibu picha za wagombea, kuchana matangazo na

machapisho mengine yanayowahusisha wagombea wa

vyama vyengine.

e) Kukataza mawakala na wafuasi wa Vyama vya siasa

kubandika picha, machapisho au matangazo ya wagombea

katika nyumba za ibada na za watu binafsi, vyombo vya

usafiri bila ya ridhaa za wamiliki.

f) Kila chama kuondosha katika maeneo ya wazi mabango,

picha za wagombea na matangazo yahusianayo na uchaguzi

ndani ya kipindi cha siku kumi nan nne baada ya

kutanganzwa kwa matokeo ya uchaguzi.

g) Kuhamasisha kampeni za amani na utulivu ambazo

zitapelekea kila chama kujiheshimu na kuheshimiwa;

Muda wa

Kampeni

9. Tunakubaliana kuwa kampeni za nje zitaanza saa mbili asubuhi na

kumalizika saa kumi na mbili jioni na vipaza Sauti vitumike kwa

muda uliolekezwa hapo juu.

Matumizi ya

magari ya

serikali na

rasilimali za

umma katika

kampeni

10. Sisi, Vyama vya Siasa tunakubaliana kutotumia:-

a. Gari za Serikali na rasilimali za umma katika kampeni.

b. Majengo, watumishi na Taasisi za umma katika shughuli za

kampeni za uchaguzi.

Page 6: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 5

Kuheshimu

Sheria za

usalama

barabarani

11. Sisi vyama vya siasa tunakataza wanachama na wafuasi wa vyama

vyetu wanaosafiri kufuatilia mikutano ya kampeni, kujazana kupita

kiasi katika gari wakati wa kwenda na kurudi katika mikutano hiyo

na gari hizo hazitovunja Sheria za Usalama Barabarani.

Kuheshimu

mchakato wa

uchaguzi

12. (1) Sisi Vyama vya Siasa pamoja na wagombea, wanachama na

mawakala wa vyama vyetu:

a. Tutashirikiana na kuisaidia Tume ya Uchaguzi, watendaji na

maafisa wake katika kutekeleza majukumu na wajibu wao;

tutajizuia na lugha za matusi, vitisho na vitendo vinavyochochea

uvunjifu wa amani wakati wa shughuli za uchaguzi.

b. Tutahakikisha wagombea, mawakala na wanachama wetu

hawafanyi hila kwa njia yoyote ile katika zoezi la kupiga na

kuhesabu kura. Aidha tutawazuia kueneza uzushi kuhusiana na

matokeo ya uchaguzi.

c. Tutawaelekeza wagombea, mawakala na wanachama wetu

kutosababisha hasara ya aina yoyote katika maeneo ya uchaguzi

kwa kuondoa, kuharibu, kuchana machapisho na nyaraka mbali

mbali zinazotolewa na Tume ya uchaguzi ya Zanzibar.

Wajibu wa

Tume

13. Katika kutekeleza majukumu yake Tume ya Uchaguzi pamoja na

watendaji wake itahakikisha inatekeleza majukumu yake kwa:-

a. Kufuata Katiba, Sheria, Kanuni na Taratibu zinazoongoza

mchakato wa Uchaguzi wa Zanzibar.

b. Kutopendelea chama chochote cha siasa au Mgombea.

c. Kushirikiana na wagombea wa vyama vyote katika

kuhakikisha maelekezo ya Sheria juu ya mchakato wa

uchaguzi yanafuatwa.

d. Kutoa taarifa, ufafanuzi, na maelezo juu ya jambo ililolifanya,

inalolifanya na inalotarajia kulifanya katika hatua za

uchaguzi.

Page 7: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 6

e. Kuweka wazi milango yake kwa chama au mgombea kwa ajili

ya ufafanuzi, maelekezo, au taarifa inayohusiana na utendaji

wa Tume ya Uchaguzi.

Utoaji wa

Taarifa za

Uchaguzi

14. Tume ya uchaguzi inaahidi kutoa habari na taarifa za mwenendo wa

Uchaguzi kwa njia ya uhuru, uwazi na ukweli hatua kwa hatua hadi

kukamilika hatua zote za uchaguzi.

Wajibu wa

Serikali

15. Serikali itahakikisha kuwa:-

a. Inatoa huduma na nafasi sawa kwa vyama vyote vya siasa

bila ya upendeleo wa aina yoyote;

b. Inachukua hatua za kisheria kwa kiongozi yeyote wa Serikali

atakayebainika kuvuruga au kuhujumu shughuli au kampeni

ya chama cha siasa;

c. Kupitia vyombo vya usalama inasimamia usalama wa nchi na

kutoa ulinzi unaostahiki katika mikutano na kampeni na

mikusanyiko yote iliyo rasmi ya vyama vya siasa;

d. Majengo, watumishi na vyombo (Gari) vya Serikali havitumiwi

katika shughuli za vyama vya siasa kufanikisha kampeni za

vyama vyao;

e. Watendaji wa Serikali wanatoa ushirikiano kwa vyama vya

siasa katika kutekeleza majukumu yao hasa kampeni.

f. Watumishi wa Serikali hawatumii muda wa kazi kufanya

kampeni katika Ofisi zao.

Kuheshimu

Wagombea

wengine

16. Sisi Vyama vya Siasa tutahakikisha kuwa:-

a. Wagombea, mawakala, au wafuasi wetu hawatowi lugha ya

udhalilishaji kwa viongozi wengine wa Vyama ambao

wanagombea nafasi moja au vyenginevyo.

b. Wagombea, mawakala au wafuasi wetu hawatoi lugha za

kuwadhalilisha wagombea wengine kutokana na jinsia zao,

maumbile yao, rangi zao au sehemu wanazotoka.

Page 8: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 7

Ushirikiano na

vyombo vya

ulinzi na

usalama

17. Sisi Vyama vya Siasa tutashirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama

katika usimamizi wa sheria na kudumisha amani wakati wa kampeni,

upigaji kura na utangazaji wa matokeo.

Kukubali

matokeo ya

uchaguzi

18. Sisi Vyama vya Siasa tunaahidi kuyakubali matokeo halali

yatakayotangazwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar ambayo ndio

yenye mamlaka ya kutangaza matokeo kisheria

Ukiukwaji wa

maadili

19. Muhusika yeyote atakayekwenda kinyume na maadili haya

atakuwa ametenda kosa na atawajibika kwa adhabu zifuatazo:-

a. Onyo au Karipio

b. Kutanganzwa katika jamii

c. Kutakiwa kuomba msamaha kwa jamii

d. Kumsimamisha mgombea au chama kuendelea na kampeni kwa

kipindi kitakachoonekana kinafaa na kamati.

e. Faini kama zinavyoelekezwa kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi.

Mamlaka ya

usimamizi wa

maadili

20. Maadili haya yatasimamiwa na Kamati ya maadili ya uchaguzi

iliyopo chini ya Tume ya uchaguzi ya Zanzibar. Kamati hii itakuwa

na mamlaka ya kusimamia utekelezaji wa maadili haya katika

ngazi zote za uchaguzi wa Rais, wajumbe wa baraza la wawakilishi

na Madiwani.

Uwasilishwaji

wa malalamiko

21. Chama kitakachoona kuwa maadili haya yamekiukwa au kina

sababu za kutosha kuwa yatakiukwa, kina haki ya kuwasilisha

malalamiko kwa kamati ndani ya saa arobaini na nane

kabla/baada ya tukio la uvunjifu wa maadili kutokea.

Muda wa

kusikiliza

Malalamiko

22. (1) Kamati mara baada ya kupokea malalamiko, itazijulisha pande

zote mbili muda, siku na wakati wa kusilizwa lalamiko hilo.

(2) Kamati itasikiliza ushahidi wa pande zote mbili na kutoa

Uamuzi ndani ya masaa sabini na mbili.

Rufaa 23. (a)Chama ambacho hakitaridhika na uamuzi wa kamati kina haki

ya kukata rufaa kwa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ndani ya siku

tatu.

(b)Tume itasikiliza rufaa iliyowasilishwa ndani ya kipindi cha siku

tatu na kutoa uamuzi.

Page 9: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 8

(c)Kama Chama hakitaridhika na uamuzi wa Tume, kina ruhusiwa

kupeleka lalamiko lake mahakamani kama ilivyo katika sheria za

uchaguzi.

Kuridhia

utekelezaji

24. (1) Sisi Vyama vya Siasa, Tume ya Uchaguzi na Serikali

tunakubaliana kusimamia kikamilifu utekelezaji wa maadili haya

kwa madhumuni ya kufanikisha uchaguzi mkuu wa mwaka 2015

ambayo kwa kiasi kikubwa yatasaidia kuwa na uchaguzi huru na

haki.

(2) Kwa uthabiti wetu tutawaagiza wagombea, wanachama na

mawakala wetu na Wananchi kwa ujumla kutekeleza maadili haya

na tunajitolea kuchukuwa hatua za ziada kuakikisha elimu juu ya

maadili inatolewa nchi nzima na yanatekelezwa kwa vitendo.

Page 10: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 9

TAMKO

SISI vyama vya siasa, Tume ya Uchaguzi na Serikali kwa hiari yetu tunatia saini na

kuridhia usimamizi na utekelezaji wa maadili haya.

NAM. JINA CHAMA WADHIFA SAINI

ACT

ADC

AFP

APPT MAENDELEO

CCM

CCK

CHADEMA

CHAUSTA

CUF

CHAUMA

DEMOKRASIA

MAKINI

DP

JAHAZI ASILIA

NCCR MAGEUZI

NLD

NRA

SAU

TADEA

TLP

UDP

UMD

UPDP

Page 11: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 10

Kwa niaba Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar

Jina ……………………………………………………………..

Cheo…………………………………………………………….

Sahihi…………………………………………………………..

Tarehe……………………………..…………………………..

Kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar

Jina ……………………………………………………………..

Cheo……………………………………………………………

Sahihi…………………………………………………………..

Tarehe……………………………..…………………………..

Page 12: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 11

CHAMA CHA ALLIANCE

FOR CHANGES

CHAMA CHA ADC CHAMA CHA WAKULIMA

CHAMA CHA UMMA

CHAMA CHA APPT

MAENDELEO

CHAMA CHA MAPINDUZI

CHAMA CHA DEMOKRASIA

NA MAENDELEO

CHAMA CHA USTAWI

TANZANIA

CHAMA CHA WANANCHI

CHAMA CHA DEMOCRATIC

PARTY

CHAMA CHA JAHAZI

ASILIA

CHAMA CHA KIJAMII

DEMOKRASIA MAKINI

CHAMA CHA NCCR

MAGEUZI

CHAMA CHA NLD

CHAMA CHA SAUTI YA

UMMA

CHAMA CHA TADEA CHAMA CHA NRA

Page 13: TUME YA UCHAGUZI YA ZANZIBAR

Page | 12

CHAMA CHA UDP

CHAMA CHA UMD

CHAMA CHA TLP

CHAMA CHA UPDP