145
UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA WAFUNGWA: HALI YA MAGEREZA TEULE KATIKA JIMBO LA KISUMU, KENYA NA OGUTU PETER OKOTH B.ED. ARTS (MOI UNIVERSITY) TASNIFU ILIYOWASILISHWA ILI KUTIMIZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA KISWAHILI, KATIKA KITIVO CHA SANAA NA SAYANSI JAMII, IDARA YA LUGHA, ISIMU NA FASIHI, CHUO KIKUU CHA KISII NOVEMBA, 2018

UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

  • Upload
    others

  • View
    8

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA WAFUNGWA:

HALI YA MAGEREZA TEULE KATIKA JIMBO LA KISUMU, KENYA

NA

OGUTU PETER OKOTH

B.ED. ARTS (MOI UNIVERSITY)

TASNIFU ILIYOWASILISHWA ILI KUTIMIZA BAADHI YA MAHITAJI YA

SHAHADA YA UZAMILI KATIKA KISWAHILI, KATIKA KITIVO CHA SANAA

NA SAYANSI JAMII, IDARA YA LUGHA, ISIMU NA FASIHI, CHUO KIKUU

CHA KISII

NOVEMBA, 2018

Page 2: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

ii

UNGAMO

Tasnifu hii ni kazi yangu mwenyewe na haijawahi kuhudhurishwa katika chuo kikuu

chochote kwa lengo la kufuzu shahada yoyote.

Mtahiniwa :

Ogutu Peter Okoth …. ………………………….. ……………………..

(MAS16/60013/14) (Sahihi) (Tarehe)

Tasnifu hii imewasilishwa kwa madhumuni ya kutahiniwa kwa idhini yetu kama

wasimamizi walioteuliwa na Chuo Kikuu cha Kisii.

Dkt. Opande Nilson Isaac, Ph.D.

Mhadhiri, Idara ya Lugha, Isumu na Fasihi

Chuo Kikuu cha Kisii …………………………… …………………………..

(Sahihi) (Tarehe)

Dkt. Stephen Oluoch, Ph.D.

Mhadhiri, Idara ya Lugha, Isimu na Fasihi

Chuo Kikuu cha Kisii ………………………………. …………………………..

(Sahihi) (Tarehe)

Page 3: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

iii

UNGAMO LA KITAALUMA

UNGAMO LA MTAHINIWA

i) Ninaungama kuwa, nimesoma na kuelewa sheria na masharti yanayotawala

mitihani ya masomo ya juu katika Chuo Kikuu cha Kisii pamoja na nakala

zingine zinazohusu utovu wa maadili ya kiakademia.

ii) Ninaelewa kuwa kutofahamu sheria na masharti haya si kigezo cha kukiuka

sheria hizi.

iii) Kama nina maswali au atiati, ninatambua kuwa ni jukumu langu kutafuta

majibu au usaidizi hadi nipate welewa wa kutosha.

iv) Ninaelewa kuwa sharti nifanye kazi yangu mwenyewe.

v) Pia ninaelewa kuwa kama nimepatikana na hatia ya utovu wa maadili ya

kiakademia kwa mfano, wizi wa kitaaluma, tasnifu yangu inaweza kuangushwa

kwa kupewa alama „F‟.

vi) Isitoshe, ninaelewa kuwa kusoma kwangu katika Chuo Kikuu cha Kisii

kunaweza kusimamishwa kwa muda au kusitishwa kabisa kutokana na kukiuka

maadili ya kiakademia.

Jina………………………………………………

Sahihi…………………………………….

Nambari ya usajili………………………………… Tarehe………………………………….

UNGAMO LA WATAHINI

i) Tunaungama kuwa tasnifu hii imewasilishwa katika idara ya uchunguzi wa wizi

wa kitaaluma.

ii) Tasnifu hii ina chini ya asilimia 20 ya kazi ambazo asili zao hazijatambulishwa.

iii) Hivyo basi, tunatoa kibali cha usahihishaji.

1. Jina …………………………………………

Sahihi…………………………………

Idara…………………………………........... Tarehe………………………………

2. Jina ………………………………………… Sahihi………………………………..

Page 4: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

iv

UNGAMO LA IDADI YA MANENO

Jina la Mtahiniwa…………………………………………………………………………..

Nambari ya usajili ………………………………………………………………………….

Kitivo……………………………………………..Idara……………………………………

Mada :…………………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………………………

………………………………………………………………………………………………..

Ninaungama kuwa urefu wa :

1) Tasnifu hii, pamoja na maandishi ya tiniwayo ni ………………… 2) na marejeleo ni

ni…………………… na kama inawezekana, 3) Pamoja na viambatisho ni…………......

Pia, ninaungama kuwa tasnifu iliyo kwenye mfumo wa kielektroniki ni sawa na nakala

yangu ya mwisho na tena ni sawa na ile ambayo watahini walipendekeza kwa ajili ya

shahada ya uzamili.

Sahihi………………………………………………. Tarehe………………………………

Ninaungama kuwa, tasnifu ambayo imewasilishwa na mwanafunzi mtajwa hapo juu

imeafiki urefu unaohitajika kwa misingi iliyowekwa na kitengo cha masomo ya juu pamoja

na tume inayoongoza masomo katika vyuo vikuu kwa ajili ya shahada ya uzamili.

Sahihi………….Baruapepe…………..………..Na. ya simu…….………..Tarehe………….

(Msimamizi 1)

Sahihi………….Baruapepe…………..………..Na. ya simu…….………..Tarehe………….

(Msimamizi 2)

Page 5: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

v

HAKIMILIKI

Haki zote zimehifadhiwa. Sehemu yoyote ya tasnifu hii au kazi nzima hairuhusiwi kuigwa,

kunakiliwa, kupigwa chapa, kusambazwa kielektroniki au kwa njia yoyote ile bila ridhaa ya

awali ya mwandishi au ya Chuo Kikuu cha Kisii kwa niaba ya mwandishi.

© 2018, Ogutu Peter Okoth

Page 6: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

vi

TABARUKU

Tasnifu hii naitabaruku kwa wazazi wangu mzee Eliakim Ogutu na mama Anjeline Ogutu

kwa kunilea katika misingi bora ya kidini na ya kijamii kwa jumla. Nina hakika kuwa kila

hatua ninayopiga mnajivunia kuona matunda ya kazi ngumu mliyofanya ya kunielimisha.

Page 7: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

vii

SHUKURANI

Awali ya yote, shukurani za dhati zimwendee Mwenyezi Mungu ambaye kwa hakika ndiye

nahodha mkuu wa kazi hii. Namshukuru kwa kunipa nguvu na uwezo wa kuitimiza ndoto

yangu ya kupata shahada ya uzamili.

Shukrani zangu pia ziwaendee wasimamizi wangu Dkt. Opande na Dkt. Oluoch kwa

ushauri, mawaidha na mwongozo ili kutamatisha kazi hii. Kutokana na jitihada zenu,

jinamizi hili limeniondokea.

Ninamshukuru Msarifu Mwandamizi wa Shule ya St Mary‟s Yala Bwana Jacob Amunga

kwa ushauri wake hadi kukamilisha uandilizi wa tasnifu hii.

Ninamshukuru babangu Sajini Mwandamizi mstaafu wa Magereza, Eliakim Ogutu Owiti

pamoja na ndugu yangu Koplo wa Magereza, Elias Otieno Ogutu. Jitihada zenu na

kujitolea kwenu kuwarekebisha wafungwa kwa haki katika gereza kuu la Kibos kulinitia

moyo na kunichochea kufanya utafiti huu.

Kupitia kwa Idara ya Magereza ya Kenya natoa shukurani za dhati kwa watafitiwa wote

ambao walishiriki katika utafiti huu. Isitoshe, ninamshukuru Kamanda Mkuu wa Magereza

katika eneo la Nyanza, Bwana Amos K. Misik (DCP) kwa ushauri wake kuhusiana na

utafiti huu na katika ulimwengu wa kiakademia kwa ujumla.

Shukurani nyingi sana zimwendee Mrakibu wa Magereza (SP) Martin Okoko pamoja na

Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Magereza P.W. Ngara (SACP/A) kwa ushauri wao na

kwa kunisaidia kupata kibali cha kukusanya data katika magereza ya Kenya.

Shukran jaziilan!

Page 8: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

viii

IKISIRI

Utafiti huu ulilenga kuchanganua matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa wa

magereza ya Kisumu. Utafiti huu utachangia tafiti katika taasisi na vyuo vikuu kwa sababu

uliibua muktadha wa matumizi ya lugha ambao haujatafitiwa nchini Kenya. Utafiti huu

ulikuwa na madhumuni matatu; kujadili vikoa maana katika agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Pili, kufafanua mabadiliko ya kimaana yanayojitokeza

katika agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu. Tatu, kujadili mbinu za

uundaji wa agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu. Mtafiti alijikita

katika Nadharia ya Pragmatiki Leksika ambayo huchunguza jinsi maana ya neno kiisimu

hubadilika kimatumizi. Utafiti huu uliongozwa na muundo wa usoroveya elezi. Kupitia

kwayo mtafiti alifanikiwa kupata habari alizotaka kuhusu agoti za wafungwa. Data

ilikusanywa kwa kutumia kalamu na daftari. Utafiti wenyewe ulifanywa katika magereza

ya Kibos na Kodiaga mjini Kisumu. Uteuzi wa sampuli kusudio ulitumiwa kupata

watafitiwa mia moja themanini na watano ambao walishirikishwa katika utafiti. Jumla ya

agoti mia mbili sitini na tatu zilikusanywa na kutokana na idadi hii, mtafiti aliteua agoti mia

moja themanini na nane ambazo zilichanganuliwa. Agoti hizi ndizo zilizotimiza upeo na

mipaka ya utafiti huu. Usaili na mahojiano ya kimakundi yalitumiwa kama mbinu za

kukusanya data. Data ilichambuliwa kwa misingi ya nadharia iliyoteuliwa na kwa kutumia

mkabala wa kimaelezo. Utafiti huu ulifanikiwa kufafanua vikoa vitano vya maana ambavyo

agoti za wafungwa huweza kuanishwa kwayvyo. Mtafiti alidhihirisha kuwa baadhi ya

leksimu zenye maana kiisimu hubadili maana kimatumizi katika muktadha wa jela. Ubanaji

na upanuzi wa maana ulijitokeza kama mabadiliko makuu ya kimaana katika agoti za

wafungwa. Isitoshe, utafiti huu ulifanikiwa kujadili mbinu mbalimbali za uundaji wa agoti

zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu. Utafiti huu ulifikia hitimisho kuwa

agoti za wafungwa ni hazina ya maana kutokana na jinsi wafungwa walivyoonyesha

ubunifu wa kuyapa maneno maana, kubadili maana ya maneno na kwa kubuni leksimu za

kuwasiliana miongoni mwao. Hatimaye utafiti huu ulitoa mapendekezo kwa watafiti wa

baadaye ambao wangependa kushughulikia eneo la lugha ya wafungwa.

Page 9: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

ix

ABSTRACT

This study aimed at analysing the argot terms used by the inmates in Kisumu County,

Kenya. The study will contribute to research in the universities as it comes out with a

context of language usage which has not been researched in Kenya. The study had three

objectives; to discuss the sets of semantic fields in the argot terms used by the prisoners at

the Kisumu Prisons. To explain the changes in meaning in the argot terms used by the

prisoners at the Kisumu Prisons. Lastly, to discuss the techniques used in the formation of

argot terms used by the prisoners at the Kisumu Prisons. The researcher used the Lexical

Pragmatic Theory which explains how words change meaning in context. The argot terms

collected from the respondents were noted down in a book. The study was carried out at the

Kibos and Kodiaga maximum prisons in Kisumu County. Purposive sampling was used to

identify one hundred and eighty five prisoners who acted as the respondents. A total of two

hundred and sixty three argot terms were collected. Out of these, one hundred and eighty

eight terms were selected to be analysed in the study. These were the terms which met the

scope of the study. Interviews and guided group discussions were used to collect data. The

study found five semantic fileds under which different argot terms were discussed. Lexical

narrowing and lexical broadening were found to be the major lexical pragmatic processes

which caused shifts in the meaning of the argot terms. The study managed to discuss the

various techniques used in the formation of argot terms. It was found that the formation of

words in prisons was mostly accompanied by changes in meaning in the words formed.

This study reached a conclusion that prison argot is a rich resource of meaning going by the

creativity which was shown in the assigning of meaning to terms, shifting of meaning of

terms and in the creation of words used for communication in the prisons. After reaching its

objectives, the study gave out recommendations for further research in the field of prison

lingo.

Page 10: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

x

YALIYOMO

UNGAMO……………………………………………………………………….………….ii

UNGAMO LA KITAALUMA ........................................................................................... iii

UNGAMO LA IDADI YA MANENO ............................................................................... iv

HAKIMILIKI ........................................................................................................................ v

TABARUKU ......................................................................................................................... vi

SHUKURANI ..................................................................................................................... vii

IKISIRI .............................................................................................................................. viii

ABSTRACT .......................................................................................................................... ix

YALIYOMO .......................................................................................................................... x

ORODHA YA MAJEDWALI .......................................................................................... xiv

ORODHA YA VIAMBATISHO ……………………………………………….………..xv

ORODHA YA VIFUPISHO ............................................................................................. xvi

UFAFANUZI WA ISTILAHI ......................................................................................... xvii

SURA YA KWANZA

MISINGI YA UTAFITI ....................................................................................................... 1

1.1 Usuli wa suala la utafiti ................................................................................................. 1

1.2 Suala la Utafiti ............................................................................................................... 3

1.3 Misingi ya uteuzi wa mada ........................................................................................... 4

1.4 Malengo ya utafiti ......................................................................................................... 5

1.5 Maswali ya utafiti .......................................................................................................... 6

Page 11: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xi

1.6 Umuhimu wa utafiti ...................................................................................................... 6

1.7 Upeo na mipaka ya utafiti ............................................................................................. 7

1.8 Changamoto za utafiti ................................................................................................... 8

SURA YA PILI

UHAKIKI WA MAANDISHI ............................................................................................ 10

2.1 Utangulizi .................................................................................................................... 10

2.2 Dhana ya agoti ............................................................................................................. 10

2.2.1 Agoti za wafungwa ............................................................................................... 13

2.3 Msingi wa kinadharia .................................................................................................. 15

2.3.1 Semantiki Kileksika .............................................................................................. 15

2.3.4 Michakato ya Pragmatiki Leksika ........................................................................ 16

2.3.4.1 Ubanaji wa kileksika ......................................................................................... 16

2.3.4.2 Upanuzi wa kileksika ........................................................................................ 17

2.3.4.3 Kisio la maana ................................................................................................... 20

2.4 Vikoa maana katika agoti za wafungwa ...................................................................... 21

2.4.1 Vitendo vya ngono na mapenzi ............................................................................ 22

2.4.2 Marufuku .............................................................................................................. 23

2.4.3 Michakato ya kitaasisi .......................................................................................... 24

2.5 Mabadiliko ya maana .................................................................................................. 25

2.6 Uundaji wa agoti za wafungwa ................................................................................... 28

2.6.1 Ukopaji na utohozi ............................................................................................... 29

2.6.2 Mbinu ya ukatizaji ................................................................................................ 29

2.6.3 Mbinu ya uambishaji ............................................................................................ 29

2.6.4 Mbinu ya ubadilishaji silabi ................................................................................. 30

2.6.5 Onomatopia: Tanakali za Sauti ............................................................................ 30

2.7 Pengo la utafiti ............................................................................................................ 30

2.8 Hitimisho ..................................................................................................................... 31

Page 12: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xii

SURA YA TATU

MBINU ZA UTAFITI ........................................................................................................ 32

3.1 Utangulizi .................................................................................................................... 32

3.2 Mbinu za utafiti ........................................................................................................... 32

3.3 Muundo wa utafiti ....................................................................................................... 33

3.4 Eneo la utafiti .............................................................................................................. 34

3.5 Sampuli na usampulishaji ........................................................................................... 35

3.5.1 Usampulishaji ....................................................................................................... 35

3.5.2 Sampuli lengwa .................................................................................................... 35

3.5.3 Sampuli iliyoteuliwa ............................................................................................. 36

3.6 Vifaa vya kukusanya data ........................................................................................... 37

3.7 Ukusanyaji wa data ..................................................................................................... 37

3.8 Uchanganuzi wa data .................................................................................................. 37

3.9 Majaribio ya vifaa vya utafiti ...................................................................................... 38

3.9.1 Uhalali .................................................................................................................. 39

3.9.2 Utumainifu ............................................................................................................ 39

3.10 Maadili ya utafiti ....................................................................................................... 40

3.10.1 Maadili ya utafiti yanayomhusu mtafiti ............................................................. 40

3.10.2 Maadili ya utafiti yanayohusu watafitiwa .......................................................... 40

3.10.3 Maadili ya utafiti yanayohusu mchakato wa utafiti ........................................... 41

3.11 Hitimisho ................................................................................................................... 41

SURA YA NNE

UWASILISHAJI NA UCHANGANUZI WA DATA ...................................................... 42

4.1 Utangulizi .................................................................................................................... 42

4.2 Vikoa maana katika agoti za wafungwa ...................................................................... 43

4.2.1 Kikoa cha mahusiano ya kimapenzi ..................................................................... 44

4.2.2 Kikoa cha marufuku na dawa za kulevya ............................................................. 47

4.2.3 Kikoa cha mambo na shughuli za jela .................................................................. 50

4.2.4 Kikoa cha wafungwa ............................................................................................ 55

Page 13: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xiii

4.2.5 Kikoa cha maafisa wa magereza .......................................................................... 58

4.2.6 Agoti zaidi ................................................................................................................ 61

4.3 Mabadiliko ya maana .................................................................................................. 63

4.3.1 Ubanaji wa kileksia .............................................................................................. 63

4.3.2 Upanuzi wa kileksia ............................................................................................. 69

4.3.3 Kisio la maana ...................................................................................................... 86

4.4 Uundaji wa agoti za wafungwa na ubunaji wa maana mpya ...................................... 88

4.4.1 Ukopaji wa maneno .............................................................................................. 89

4.4.2 Ubadilishaji silabi katika maneno ........................................................................ 90

4.4.3 Ubunifu wa leksimu ............................................................................................. 92

4.4.5 Kuchanganya msimbo .......................................................................................... 93

4.4.6 Ubadilishaji ........................................................................................................... 96

4.5 Hitimisho ..................................................................................................................... 97

SURA YA TANO

HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ................................................................................ 99

5.1 Utangulizi .................................................................................................................... 99

5.2 Muhtasari wa utafiti .................................................................................................... 99

5.3 Matokeo ya utafiti ..................................................................................................... 101

5.4 Mchango wa utafiti ................................................................................................... 103

5.5 Hitimisho la utafiti .................................................................................................... 104

5.6 Mapendekezo ............................................................................................................ 105

MAREJELEO ................................................................................................................... 107

VIAMBATISHO ............................................................................................................... 120

Page 14: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xiv

ORODHA YA MAJEDWALI

Jedwali 4.01: Agoti zinazohusu mahusiano ……………………….……………….……..44

Jedwali 4.02: Agoti zinazohusu marufuku na dawa za kulevya……………………….… .47

Jedwali 4.03: Agoti zinazohusu mambo na shughuli za jela…………….………...……....50

Jedwali 4.04: Agoti zinazowarejelea wafungwa………………………..………………….55

Jedwali 4.05: Agoti zinazowarejelea maafisa wa magereza…………..……….……….….58

Jedwali 4.06: Agoti zaidi kutoka kwa wahojiwa……………………...…………….…..…61

Jedwali 4.07: Agoti zilizobanika kimaana…………………….…………...………………64

Jedwali 4.08: Agoti zilizopanuka kimaana…………………………………………..….…69

Jedwali 4.09: Agoti zilizopanuka kisitiari……………………………….…………..…..…75

Jedwali 4.10: Agoti zilizopanuka maana kichuku………………………..………..……….83

Jedwali 4.11: Agoti zilizopauka kikategoria…………………………..………………..….85

Jedwali 4.12: Agoti zilizopanuka kwa kukisia maana………………………………..……86

Jedwali 4.13: Agoti zilizokopwa……………………………………………………...……89

Jedwali 4.14: Mifano ya agoti zilizobadilisha silabi….……………………………...…….91

Jedwali 4.15: Agoti zilizobuniwa……………………………………………………..……92

Jedwali 4.16: Mifano ya uchanganyaji misimbo………………………………………...…94

Jedwali 4.17: Mifano ya agoti zilizobadilishana nafasi…………………...…………….…96

Page 15: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xv

ORODHA YA VIAMBATISHO

KIAMBATISHO I: MWONGOZO WA MAHOJIANO ……………….………………..120

KIAMBATISHO II: KIBALI CHA UTAFITI (KAUNTI YA KISUMU)…...…………. 121

KIAMBATISHO III: BARUA YA IDHINI (NACOSTI)………………………….…….122

KIAMBATISHO IV: CHETI CHA IDHINI (NACOSTI)…………………………….…123

KIAMBATISHO V: KIBALI CHA UTAFITI (MAGEREZA YA KENYA)……………124

KIAMBATISHO VI: KIBALI CHA KUHOJIWA………………………………...…….125

KIAMBATISHO VII: UCHAPISHAJI…………………………………………………..126

KIAMBATISHO VIII: RIPOTI YA UHALALI WA UTAFITI…………...…………….127

Page 16: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xvi

ORODHA YA VIFUPISHO

UKIMWI - Ukosefu wa Kinga Mwilini

Taz. - Tazama

N.k. - Na kadhalika

K.v. - Kama vile

N.w. - Na wenzake

Page 17: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

xvii

UFAFANUZI WA ISTILAHI

Jagoni - Ni aina mojawapo ya lugha inayotumika katika taaluma fulani mahususi kama vile

fasihi, isimu, sheria, sayansi, uhandisi, biashara na kadhalika. Ni lugha

inayofahamika na wale tu walioko katika taaluma hiyo.

Misimu - Ni misemo isiyo rasmi ambayo huhusishwa na kikundi kidogo cha wanajamii na

ambayo aghalabu hupotea baada ya muda.

Agoti - Ni maneno au lugha itumiwayo na kundi fulani la wahalifu au watu ambao

wanaficha uovu wao usifahamike katika jamii wanamoishi.

Agoti ya wafungwa - Ni lugha au maneno ambayo ni ya kipekee miongoni mwa

wafungwa gerezani.

Kirai Nomino - Neno au fungu la maneno ambayo hukitwa kwenye Nomino au

Kiwakilishi kama neno kuu.

Kirai Kitenzi – Neno au fungu la maneno ambayo hukitwa kwenye Kitenzi kama neno

kuu.

Vikoa maana – Matapo ya maneno yenye maana yanayohusiana.

Mabadiliko ya manaa – Neno kupata maana tofauti na maana yake asilia.

Pragmatiki leksika – Nadharia ambayo inashughulikia maana za leksimu kimuktadha.

Semantiki kileksika – Semantiki inayoshughulikia maana za kileksika za maneno.

Michakato ya kileksika – Mikondo ambayo leksimu hupitia kuibua fahiwa au dhana mpya

(dhana inayowasilishwa kwenye tamko).

Page 18: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

1

SURA YA KWANZA

MISINGI YA UTAFITI

1.1 Usuli wa suala la utafiti

Utafiti huu unahusu uchanganuzi wa matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa, hali ya

magereza teule katika jimbo la Kisumu. Ito na wenzake (1996) wanafafanua agoti kama jagoni

ambayo hubadili maana ya maneno ya lugha kwa njia maalumu na ambayo ni wazi tu kwa

watumiaji wa agoti hiyo. Ni lugha itumiwayo na kundi fulani la wahalifu au watu ambao

wanaficha uovu wao usifahamike katika jamii wanamoishi. Aghalabu lugha hii hutumiwa katika

mazingira yasiyo rasmi na kikundi cha watu kama vile madereva wa magari, watumiaji wa dawa

za kulevya, majambazi, vibaka na wahuni wa mtaani. Kwa mujibu wa Looser (2001) agoti ya

wafungwa ni lugha au maneno ambayo ni ya kipekee katika magereza na katika tamaduni

zingine za kihuni. Anaeleza kuwa, agoti ya wafungwa ni maneno yanayochipuka kutokana na

kutengwa kwa wafungwa na jamii pana. Anderson na Trudgil (1990) wanafafanua kuwa mahitaji

ya kimsingi ya lugha ya kundi fulani katika jamii huwasilishwa kupitia misimu. Agoti, ambayo

awali wanafafanua kama jagoni ya wezi na wafungwa, ni aina fulani ya msimu (Nielson na

Scarpitti, 1995). Kwa mujibu wa Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili- TUKI (1990) simo ni

mitindo ya lugha ambayo huzuka katika kipindi fulani na kutumiwa na kundi fulani la watu.

Ulimwenguni kote, Uingereza ndilo eneo lenye historia ndefu ya agoti za wafungwa (Coleman,

2004). Hata hivyo, taifa la Amerika ndilo taifa lenye maandishi na tafiti changamano kuhusu

lugha ya wafungwa. Hii inatokana na idadi kubwa ya wafungwa iliyokuwepo, inayozidi kukua,

na iliyofika kilele mwaka wa 2004 kwa kuwepo kwa zaidi ya wafungwa milioni mbili (Coleman,

2004). Kwa mujibu wa Szabo (2005), hadi kufikia miaka ya themanini, watu wengi waliiona

Page 19: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

2

agoti kama lugha ya majambazi na tafiti kuhusu misimu na agoti kuonekana kama zisizo na

thamani. Hata hivyo, tangu karne ya ishirini wanaisimu wamechanganua misimu na agoti na

kuzikubali kama kitengo cha isimu. Kwa mujibu wa Mekacha (2011), imekubalika kuwa hivi

leo, ndani ya jamii-lugha moja kuna migawanyiko inayofuata sulubu maalumu na kwamba ndani

ya lugha moja kuna vilugha ambavyo pia vimegawanyika kufuata sulubu maalumu. Mekacha

(2011) anaeleza kuwa kazi za Labov (1972), Gumperz (1972) na Milroy (1980) ndizo vyanzo

vya mkabala wa utofauti ndani ya lugha katika isimu. Gal (1979) anaeleza kuwa kuwepo kwa

vilugha katika jamii ni jambo la kawaida.

Kwa mujibu wa Gohodzi (2013), tafiti nyingi kuhusu agoti za wafungwa zimefanywa ughaibuni.

Mfano wa kazi hizi ni utafiti wa Looser (2001). Katika utafiti huu, Looser (2001) anachukua

mwelekeo wa kihistoria ambamo anachanganua matumizi ya agoti za wafungwa katika taifa la

New Zealand iliyotumiwa kati ya miaka ya 1996-2000. Tofauti iliyopo kati ya utafiti huu na ule

wa Looser (2001) ni kuwa ulifanywa katika muktadha wa lugha na mazingira yaliyo tofauti.

Isitoshe, kazi ya Looser (2001) aliwashirikisha wafungwa wa jinsia zote. Utafiti huu ulichunguza

agoti za wafungwa wanaume tu.

Hapa Afrika, tafiti chache sana zimefanywa kuhusu lugha za wafungwa (Gohodzi, 2013).

Gohodzi alijaribu kujaza pengo hili kwa kuchanganua matumizi ya agoti katika gereza la

Whahwa nchini Zimbabwe. Gohodzi (2013) alitumia wafungwa ambao walikuwa

wamefunguliwa kupata data zake. Nchini Kenya, tafiti nyingi zimefanywa kuhusu matumizi ya

lugha katika miktadha mbalimbali (Mekacha, 2011). Hata hivyo, tafiti hizi zaidi zimefanywa

uraiani. Binyanya (2014) anaeleza kuwa, tafiti nyingi nchini Kenya kuhusu vilugha vya

Kiswahili zimefanywa zaidi katika miktadha ya maabadini, siasa na uchuuzi. Mugendi (2016)

alichunguza matumizi ya agoti ya Gatamanyana miongoni mwa wahudumu wa magari katika

Page 20: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

3

mji wa Embu. Nyakundi (2010) naye alichunguza matumizi ya agoti ya Egesemba inayotumiwa

miongoni mwa wazungumzaji wanaume katika jamii ya Wakisii. Tafiti hizi ni muhimu lakini

zinahusu jumuiya lugha tofauti. Utafiti huu uliwachunguza wafungwa kama jumuiya lugha.

Pengine uchache wa tafiti kuhusu matumizi ya lugha katika eneo lenye hazina kubwa ya lugha

kama jela unatokana na mtazamo finyu wa baadhi ya wanaisimu kuhusu vilugha. Kwa mfano,

Ramani (2006) anaandika makala, „Leave Sheng to Matatu Touts and Musicians‟. Kobia (2006)

naye anaandika, „Sheng is not a language but a popular slang.‟

Magereza ya nchi ya Kenya yamejengwa katika misingi ya magereza ya Uingereza (Newbold,

1978). Katika kuingia kwenye taasisi jumuishi kama jela, wafungwa hupitia maingiliano ya

kitawi (Goffman, 1962). Maingiliano ya kitawi ni „Ubwiaji wa tamaduni na itikadi za „vijidunia‟

vya taasisi fulani‟ (Berger & Luckman, 1971). Jinsi upokeaji wa lugha ni jambo la lazima katika

usimilisho asilia, vivyo hivyo ujifunzaji wa lugha ni jambo la shuruti katika usimilisho huu wa

pili. Lugha anayojifundisha mfungwa gerezani si lugha ya kawaida kwani huwa na sifa za

kipekee. Hivyo basi katika utafiti huu, kulichanganuliwa agoti ambazo huwawezesha wafungwa

wa magereza ya Kisumu kuwasiliana.

1.2 Suala la Utafiti

Mawasiliano ni muhimu katika jamii. Wafungwa wanapojihusisha na mambo ya kisiri, wanaibua

na kujifundisha mitindo ya kisiri ya mawasiliano ili kukidhi mahitaji yao. Katika kufanya hivi,

wafungwa huibua lugha ya siri au agoti ambazo zinafahamika tu na kundi lao. Isitoshe,

wafungwa hubadili maana ya maneno ili kukidhi haja ya kuficha siri katika mawasiliano. Hali hii

husababisha neno kupata maana mpya ambayo huweza kutofautiana kwa kiasi fulani na maana

Page 21: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

4

yeke asilia. Wafungwa pia hubuni maneno mapya ili kurejelea hali mbalimbali katika mazingira

ya jela.

Tafiti kuhusiana na matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa zimefanywa sana katika nchi za

kimagharibi. Matumizi ya lugha katika muktadha wa magereza ya Kenya hayajashughulikiwa na

watafiti. Tafiti nyingi kuhusu vilugha vya Kiswahili zimefanywa kuhusu msimbo wa Sheng.

Tafiti zingine zimechanganua viswahili vya manamba, wauzaji nguo, msimbo wa maafisa wa

polisi na hata lugha katika muktadha wa hoteli. Hapana lolote linalosemwa kuhusu lugha ya jela.

Utafiti huu hivyo basi ulichanganua maneno ambayo wafungwa wa magereza ya Kisumu

hutumia na kuibua muktadha mwingine wa matumizi ya lugha ambao haukuwa umetafitiwa

nchini Kenya.

1.3 Misingi ya uteuzi wa mada

Utafiti huu una mchango mkubwa kwa utafiti katika taasisi na vyuo vikuu. Kama ilivyodokezwa

na Gohodzi (2013) tafiti chache kuhusu matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa

zimefanywa barani Afrika. Binyanya (2014) alithibitisha kauli hii kwa kueleza kuwa tafiti nyingi

zilizofanywa kuhusu matumizi ya vilugha zimefanywa zaidi katika miktadha ya maabadini, siasa

na uchuuzi. Hivyo basi, utafiti huu umeweka msingi kwa wanafunzi na watafiti wanaonuia

kuchanganua matumizi ya agoti za wafungwa nchini Kenya. Utafiti huu umechukua mtazamo wa

kipragmatiki ila watafiti wengine wanaweza kutumia data ya utafiti huu na kuchanganua agoti

kihistoria au kuchukua mtazamo wa kisintaksia.

Mchango mwingine kwa utafiti katika taasisi na vyuo ni kuwa, utafiti huu umehifadhi kwa mara

ya kwanza leksimu zinazotumiwa na wafungwa katika magereza ya Kenya. Hii ni muhimu

Page 22: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

5

kwani utafiti huu utakuwa kumbukumbu kwa watafiti wa baadaye ambao watapenda kutambua

jinsi lugha ya wafungwa itakavyokuwa imebadilika katika miaka ya baadaye.

Mchango kwa taaluma ni kuwa, waandishi mbalimbali katika taaluma ya Isiimujamii na

pragmatiki hawajashughulikia matumizi ya lugha gerezani. Kwa mfano, Mekacha (2011)

anaorodhesha maeneo mbalimbali ya matumizi ya lugha : nyumbani na miongoni mwa familia,

maeneo ya makazi, miongoni mwa majirani, shughuli za mila na desturi, sehemu za kazi,

michezo na burudani, masoko na biashara, usafiri wa umma, ibada na shughuli za dini, vyombo

vya habari, uandishi na usomaji wa kazi za fasihi, utawala na siasa, sheria na mahakama, elimu

na mafunzo, mawasiliano na biashara ya kimataifa. Hakuna lolote linalosemwa kuhusu

magereza. Utafiti huu hivyo basi umechangia kuwepo kwa muktadha mwingine wa matumizi ya

lugha ambao haujatafitiwa katika Kiswahili.

Mchango kwa sera ya lugha ni kuwa, kupitia kwa data ambayo ilipatikana, ilibainika ni kwa

kiwango gani wafungwa hujihusisha na lugha rasmi za nchi ya Kenya, Kiswahili na Kiingereza.

Ilidhihirika kuwa wafungwa wanatumia Kiswahili zaidi katika mawasiliano yao. Hii ilitokana na

ukweli kuwa, maneno mengi yanayotumiwa ni ya Kiswahili au yalikuwa na uhusiano na lugha

ya Kiswahili. Ngugi (1986) anaeleza kuwa watu huzibadili lugha sanifu na kuzitumia kwa

mahitaji yao. Mekacha (2011) anaeleza kuwa nchini Tanzania, lugha ya Kiswahili ndiyo ambayo

imeenea zaidi katika maeneo rasmi na yasiyo rasmi. Utafiti huu umefaidi katika kuhakikisha

ukweli wa kauli hii hapa Kenya. Isitoshe, utafiti huu umebainisha Kiswahili kama lugha ya dola,

lugha ya jamii na lugha ya vijijamii.

1.4 Malengo ya utafiti

Utafiti huu uliongozwa malengo yafuatayo :

Page 23: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

6

i) Kujadili vikoa maana katika agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya

Kisumu.

ii) Kufafanua mabadiliko ya kimaana yanayojitokeza katika agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu.

iii) Kujadili mbinu za uundaji wa agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya

Kisumu.

1.5 Maswali ya utafiti

Utafiti huu uliongozwa na maswali yafuatayo :

i) Je, agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu zinaweza kuanishwa

katika vikoa vipi vya maana ?

ii) Je, mabadiliko yapi ya kimaana hujitokeza katika agoti zinazotumiwa na wafungwa

wa magereza ya Kisumu ?

iii) Je, mbinu zipi hutumika katika uundaji wa agoti zinazotumiwa na wafungwa wa

magereza ya Kisumu ?

1.6 Umuhimu wa utafiti

Utafiti huu utawafaidi maafisa wanaoshughulikia ulinzi na urekebishaji wa wafungwa gerezani.

Urekebishaji wa mfungwa unategemea sana ufahamu wa tabia na imani za mfungwa husika. Ni

muhimu sana kwa mwelekezi kutambua lugha ya wale anaotagusana nao (Condon na Yousef,

1975). Kwa mujibu wa Cardzo-Freeman (1995), welewa wa agoti za mfungwa ni dira ya kujua

mielekeo ya kitamaduni ya jela husika pamoja na muundo wa kijamii wa jela hiyo.

Page 24: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

7

Kwa kuwa siku hizi wafungwa huruhusiwa kusoma gerezani, utafiti huu utawafaidi pakubwa

walimu, hasa walimu wa lugha wanaofundisha gerezani. Kutegemea ukweli kuwa mawasiliano

ya maana ni muhimu kati ya mwalimu na mwanafunzi (Foster, 1986) walimu wa wanafunzi-

wafungwa sharti wawe na welewa wa lugha ya wafungwa ili kurahisisha mtagusano kati yao.

Kwa mujibu wa Mclntyre na Mack (1993), walimu wa wafungwa wasiokuwa na ufahamu wa

lugha ya wanafunzi wao wamo katika hatari ya kuchezewa shere na wafungwa au hata masomo

yao kutatizwa na wafungwa hao.

Utafiti huu utakuwa muhimu kwa wanaleksikografia ambao huunda kamusi za magereza. Hii ni

muhimu kwa sababu hapa Kenya hapana kamusi inayoeleza maana za leksimu zinazotumiwa

katika mazingira ya jela, tofauti na ilivyo katika mataifa yaliyoendelea. Kwa mfano, Knight

(2014) alitunga kamusi The Dictionary of Victorian Prison Slang ambayo inafafanua maneno

yanayotumiwa na wafungwa katika muktadha wa magereza ya taifa lake.

Utafiti huu pia unaendeleza na kuikuza lugha katika idara ya magereza. Hivyo basi, utafiti huu ni

wa faida hapa nchini na kwa mataifa mengine ya ulimwengu kwani utasaidia kueneza lugha ya

jela ya Kenya ulimwenguni. Kimsingi, utafiti huu utatumika kama daraja linalounganisha jamii

ya wafungwa wa Kenya na jamii za magereza mbalimbali. Hali hii itawasaidia watafiti wa lugha

na wasimamizi wa magereza kutambua hali za magereza ulimwenguni kote au hata kufanya tafiti

changamano kuhusu lugha za wafungwa katika mabara tofauti.

1.7 Upeo na mipaka ya utafiti

Utafiti huu ulihusu uchanganuzi wa matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa wa magereza

ya Kisumu. Kwa mujibu wa Looser (2001) watafiti wa awali wa lugha na utamuduni wa

magereza wametumia mielekeo minne. Mwelekeo wa kwanza ni mfungwa binafsi kufanya

Page 25: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

8

utafiti wake anapokuwa gerezani. Pili, mtafiti kuchunguza lugha ya gereza moja. Mfano ni kazi

ya Lyons (1984). Aghalabu watu hawa huwa wameajiriwa na jela kufanya kazi hii. Mwelekeo

wa tatu ni kufanya utafiti wa kindani na wa muda mrefu wa jela fulani. Kwa mfano kazi

changamano ya Cardzo-Freeman katika gereza la Walla Walla, Washington katika mwaka wa

1984. Mwelekeo wa nne ni ule wa kutafiti lugha ya magereza mengi ya aina moja. Mfano mzuri

ni kazi ya Becker ya mwaka 1994 ambapo alitafiti magereza manne. Kwa misingi hii, utafiti huu

ulishikirikisha mwelekeo wa nne. Hii inatokana na ukweli kuwa mtafiti alichunguza magereza

mawili ya aina moja. Gereza la Kibos na Kodiaga yote ni magereza makuu katika jimbo la

Kisumu.

Utafiti huu ulijikita katika kutambua zile agoti ambazo hutumiwa katika magereza ya Kibos na

Kodiaga. Agoti hizo ziliweza kuainishwa katika vikoa maana mbalimbali. Agoti ambazo

zilizozingatiwa ni zile ambazo hubainika katika lugha ya mazungumzo tu. Matini za kimaandishi

hazikuchunguzwa. Pia mtafiti alijikita katika agoti za Kiswahili, za Sheng pamoja na zile

zilizoundwa kwa kuchanganya Kiswahili na misimbo mingine. Tulielekezwa na kauli ya

Mekacha (2011) kuwa, lugha ya Kiswahili ndiyo inatawala katika maeneo yote. Palipotokea hali

ya uchanganyaji misimbo, sababu zakuchanganywa kwa misimbo zilifafanuliwa.

1.8 Changamoto za utafiti

Mtafiti alifanikiwa kukusanya data kwa kiasi kikubwa kama alivyotarajia. Hata hivyo, kama

ilivyo ada, hakuna jambo linalokosa changamoto katika utekelezaji wake. Mtafiti kukusanya data

kutoka kwa wafungwa asiowafahamu hakukuwa rahisi. Ilimlazimu kuwatumia wafungwa na

maafisa wa magereza kuwateua wafungwa waaminifu ambao hawangeupotosha utafiti.

Page 26: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

9

Jela huwa na sheria zake kali na mambo yote hufanywa kwa muda. Wakati mwingine mtafiti

aliwapata wahojiwa wakishughulikia kazi zao za jela na ikambidi kuwasubiri hadi wakamilishe

kazi zao. Hivyo basi, pana nyakati ambapo muda ulikuwa mfupi sana na wahojiwa wengine

kutoka kabla mahojiano hayajakamilishwa. Hali kama hii ilipotokea mtafiti aliendeleza

mahojiano siku iliyofuata.

Baadhi ya maafisa waliodumisha usalama walisonga karibu nasi sana kiasi cha kuwapa

wahojiwa wasiwasi kwamba yale ambayo wangesema yangetumiwa vibaya dhidi yao. Hata

hivyo, mtafiti aliwaomba maafisa kusimama mbali kidogo na sehemu ya mahojiano ili kuwapa

wahojiwa uhuru wa kuwasiliana.

Page 27: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

10

SURA YA PILI

UHAKIKI WA MAANDISHI

2.1 Utangulizi

Sura ya kwanza ilitoa usuli na msingi ambamo utafiti huu umefanywa. Sura hii ya pili inatoa

uhakiki wa maandishi yaliyohusiana na utafiti huu na kubainisha mianya iliyopo. Kwa mujibu

wa Boswell na Cannon (2009) uhakiki wa maandishi ni kitendo cha kusoma, kuchanganua na

kuchunguza kwa urazini maandishi mbalimbali. Sehemu ya kwanza ya sura hii ni utangulizi.

Sehemu ya pili inafafanua dhana ya agoti na kutofautisha agoti na mitindo mingine ya lugha ya

mazungumzo. Kitengo hiki pia kimeangazia suala zima la agoti za wafungwa. Sehemu ya tatu

imeangazia msingi wa kinadharia. Sehemu ya nne imeangazia suala la vikoa maana. Katika

sehemu ya tano kazi mbalimbali kuhusu mabadiliko ya kimaana zimehakikiwa. Sehemu ya sita

imeshughulikia uundaji wa agoti. Sehemu ya saba imedhihirisha pengo ambalo utafiti huu

ulinuia kujaza. Sehemu ya nane ni hitimisho la sura hii.

2.2 Dhana ya agoti

Katika kufafanua dhana ya agoti ni muhimu kwanza kufafanua istilahi ambazo huwa na uhusiano

wa karibu na agoti, yaani, misimu na jagoni. Mijelezo iliyotolewa katika sura ya kwanza huenda

isitoshe mahitaji ya utafiti huu. Kwa mujibu wa Msanjila na wenzake (2009) misimu ni aina ya

misemo katika lugha ambayo huzuka na kutoweka. Sifa kuu ya misimu ni kwamba haidumu

muda mrefu na sio lugha sanifu, na watumiaji wa misimu huwa ni kikundi cha wazungumzaji wa

lugha katika jamii ambao kimsingi huishi katika eneo moja. Ngure (2003) anaonekeana

kukubaliana na Msanjila kwa kiasi ila yeye anaweka mkazo zaidi anapodai kuwa uzukaji wa

Page 28: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

11

misimu ni wa ghafla na wakati fulani hufuatana na mambo au matukio maalumu ya wakati au

msimu huo. Kwa mujibu wa McArthur (1996), sharti tutofautishe misimu na mitindo mingine ya

lugha kama vile jagoni, agoti, maneno ya kilahaja na matusi.

Maelezo haya kuhusu misimu ni muhimu kwani yalisaidia kubainisha kuwa agoti za wafungwa

hutumiwa katika mazingira yasiyo rasmi na si kila agoti huzuka na kudumu kwa muda mfupi.

Utafiti huu ulipata kuwa, pana baadhi ya istilahi kama mruru, mende na kunguru ambazo

watafitiwa walizipata zikitumiwa gerezani, wakajifundisha na kuendelea kuzitumia. Hivyo basi

kurejelea agoti za wafungwa tu kama misimu ni kuzinyima hadhi zao.

Kwa mujibu wa Yule (2006) jagoni ni lugha inayotumiwa na kundi au wataalamu wa tasnia

fulani. Ni lugha ambayo ipo, ikimaanisha kuwa haiwezi kufa kama ilivyo katika mitindo mingine

ya lugha kama vile misimu. Ni matumizi ya istilahi katika taaluma fulani. Hujitofautisha

kimsamiati na lugha zingine. Yule (keshatajwa) anapendekeza njia tatu za kutambua jagoni;

istilahi, miundo ya kisarufi na nduni za kifonolojia. Jagoni ni utambulisho wa mtu katika jamii.

Yaani, kwamba ametoka katika tasnia au nyanja ipi? Kwa mfano taaluma ya uhandisi huwa na

jagoni zake.

Yule (1996) naye anadahili kuwa jagoni ni misamiati ya kitaaluma ambayo inahusihwa na kundi

fulani spesheli na husaidia katika mwingiliano wa wale wanaojiona kama watu wa kundi la

ndani. Kwa mujibu wa Burke na Porter (1995) jagoni ni istilahi iliyopatikana kutoka lugha ya

Kifaransa katika karne za kumi na mbili na kumi na tatu, na katika Kiingereza ikatokea baadaye

ikirejelea maneno yasiyo na maana. Kazi hizi ni muhimu kwani zilimsaidia mtafiti kutambua

kuwa jagoni hutumiwa kitaaluma. Ufungwa si taaluma. Ingawa hivyo, pana wataalamu

wanaosema kuwa agoti ni jagoni ya wezi (Nielson na Scrapitti, 1995).

Page 29: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

12

Kwa upande mwingine, agoti ni maneno ambayo hutumiwa na makundi ambayo hufanya kazi

kinyume na sheria kama vile wezi, makahaba na watumiaji wa dawa za kulevya (Looser, 2001).

Watafiti wa awali walisisitiza dhana ya usiri katika agoti kama kipengele cha kuanisha agoti

lakini watafiti wa leo kama vile Partridge (1971) wamejaribu kuondoa sifa hii. Maelezo haya ni

muhimu kwani mtafiti alikusudia kuchanganua agoti zote zilizotumiwa katika muktadha wa jela,

za siri au zisizo za siri.

Maurer (1951) ambaye ni mtafiti mkuu katika mitindo ya lugha anaeleza kuwa agoti ni maneno

au lugha ambazo ni za kipekee na zinaashira maisha yanavyokuwa katika vikundi halifu. Ni

muhimu katika kutambua mielekeo, namna ya kufikiria hadi katika kueleza muundo wa kijamii

wa kundi hilo. Nielson na Scrapitti (1995) wanaeleza kuwa agoti ni jagoni ya wezi lakini pia

inaweza kutumiwa na makundi mengine katika jamii.

Ito na wenzake (1996) wanafafanua agoti kama jagoni ambayo hubadili lugha ya kawaida kwa

njia maalumu na kwa njia ambayo ni wazi tu kwa wale ambao wana welewa. Agoti huwa

misamiati ya kipekee ambayo hutumiwa na kundi ndogo la watu katika jamii ambalo aghalabu

huwa wana umoja na usiri fulani (Harris, 2012). Agoti huhusishwa zaidi na wahalifu japo watu

wa eneo fulani au tabaka fulani pia wanaweza kuitumia katika kuwasiliana (Age, 1990). Agoti

hutumiwa na kundi fulani shikamani na hivyo basi kuunda kundi la „sisi‟ na „wao.‟ Misamiati ya

agoti pia inaweza kutumiwa kuzungumza kuhusu mambo ya kiuhalifu bila woga wa kutambulika

(Harris, 2012). Kazi hizi ni muhimu kwani zinabainisha agoti kama lugha ya makundi, ifahamike

kuwa wafungwa ni kundi la jamii ambalo aghalabu huchukuliwa kuwa pambani.

Kwa mujibu wa Bullock (1996) kuna mifumo miwili ya agoti. Moja ni ya kileksia ambapo pana

ubadilishaji wa maana na ya pili inabadili sura ya neno kwa kubadili sauti au silabi katika neno

Page 30: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

13

husika. Leslau (1998) anaelekea kukubaliana na maoni haya kwa kueleza kuwa sifa za kipekee

za agoti zipo katika uundaji wa mizizi na katika uwanja wa kisemantiki.

Kazi hizi mbili ni muhimu katika utafiti huu ambao ulinuia kuchambua mbinu za uundaji wa

agoti za wafungwa ambapo ubadilishaji silabi ni miongoni mwa mbinu zilizojitokeza na

hubainika ili kufanikisha ufumbaji wa maana.

2.2.1 Agoti za wafungwa

Mahitaji maalum ya lugha na kundi fulani hujitokeza kupitia misimu (Anderson na Trudgil,

1990). Agoti, ambayo ni lugha ya wafungwa ilielezwa awali kama lugha ya wezi, pia ni aina

fulani ya misimu (Nielson na Scrapitti, 1995). Imejadiliwa kuwa wafungwa huishi, hufikiri na

kufanya kazi ndani ya duara la agoti linalotumiwa gerezani, hivyo basi, agoti ya wafungwa

imesimikwa katika dhima inayotekeleza miongoni mwa wafungwa (Bondesson, 1989).

Agoti ya wafungwa ni lugha au maneno ya kipekee yanayotumiwa na wafungwa, na asili yake ni

neno la Kifaransa lenye maana ya „misimu‟ (Sykes, 1958). Lugha ya wafungwa ilizuka kama

njia fiche ya mawasiliano baina ya wafungwa na hunuiwa kuwatenga maafisa wa magereza

katika mawasiliano yanayohusu marufuku na matendo yao gerezani. Lugha ya wafungwa

hutofautiana kulingana na jinsia (Einat na Einat, 2000). Maelezo haya ni muhimu kwa sababu

utafiti huu ulikusudia kuchanganua matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa wa magereza ya

Kisumu. Kwa ambavyo lugha ya wafungwa hutofautiana kulingana na jinsia, utafiti huu ulijikita

katika kuchunguza agoti za wafungwa wanaume.

Usimbaji wa kitabia na maendeleo yake yamefanyiwa utafiti na kurekodiwa kwa upana (Irwin,

1985; Toch, 1992). Itikadi na thamani ya msimbo huunda msingi wa utamaduni wa wafungwa,

ikiwapa wafungwa njia isiyo rasmi ya kupata nguvu na hivyo basi kuendeleza hisia za kutengwa

Page 31: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

14

na jamii na kufidia kutokuwepo kwa usalama na uhuru wa kujiamulia (Bondesson, 1989). Kwa

sababu hii, kwa mfungwa, matumizi ya agoti na usimbaji ni mchakato wa mwingiliano na

kuzoeana na maisha ya ndani ya jela. Imejadiliwa kuwa jamii ya kawaida, ishara zake,

viwakilishi vyake ni adui asilia ya mfungwa, hivyo uwepo wa agoti gerezani ni jambo la lazima

katika magereza yote ulimwenguni (Irwin, 1980). Misimbo hutazamwa kama njia ya kuingiliana

na kuzoea na mazingira ya magereza (Fisher, 1990). Maelezo haya ni muhimu kwani yalimsaidia

mtafiti kutambua kuwa agoti za wafungwa hazijitokezi katika ombwe tupu.

Lugha kama njia kuu ya mawasiliano ni msingi mkubwa katika mchakato mzima wa

mwingiliano wa kijamii na maendeleo ya tabia zao (Dean-Brown, 1992). Hivyo basi, vitengo

tofauti vya jamii huwa na sifa tofauti za lugha wanazotumia. Kimsingi, vitengo vya jamii

vitatofautishwa na lugha tofauti wanazotumia (Hudson, 1980). Lugha ya kundi fulani huweza

kuhusisha ishara mbalimbali ambazo hazimo katika lugha ya jamii pana, kwa yakini, ishara hizo

huenda zimekopwa na kupewa maana mpya (Alatis, 1992). Mahitaji ya kipekee ya kundi fulani

ndogo huwasilishwa kwa kutumia misimbo (Anderson na Tradgill, 1990). Imejadiliwa kuwa

mfungwa huishi, hufikiria na hutenda kazi ndani ya miktadha inayoamuliwa na agoti na hivyo

basi agoti ya wafungwa itasimikwa ndani ya dhima yake kwa mfungwa (Bondesson, 1989).

Tafiti kuhusu agoti za wafungwa zimefanywa zaidi katika mataifa ya Marekani, Australia

pamoja na Asia (Looser, 2001). Tafiti chache kuhusu agoti za wafungwa zimefanywa Afrika na

hasa katika nchi ya Kenya. Agoti za wafungwa katika magereza ya ughaibuni zimehifadhiwa

vitabuni na mitandaoni lakini taifa la Kenya linakosa uhifadhi na tafiti katika eneo hili muhimu.

Hivyo basi utafiti huu ulichanganua agoti za wafungwa wa magereza ya Kisumu na hivyo

kuweka msingi kwa tafiti za baadaye katika muktadha huu wa matumizi ya lugha.

Page 32: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

15

2.3 Msingi wa kinadharia

Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Pragmatiki Leksika. Nadharia hii ilianzishwa na Blutner

mwaka wa 1990. Baadaye iliendelezwa na Wilson (2003) kwenye mihadhara yake katika Chuo

Kikuu cha Havard. Pia iliendelezwa na Wilson na Carston (2007) katika miaka ya baadaye.

Nadharia hii inajikita katika kuchanganua jinsi maana hubadilika katika muktadha, kwa hivyo

mtazamo huu ni faafau zaidi katika kuwakilisha dhana.

Mtazamo huu umejikita katika stadi za mabadiliko ya maana. Mtazamo wa Pragmatiki Leksika

unaelezea mwelekeo kwamba, faridi za kileksika za lugha zinachanganuliwa kiutaratibu na

kufasiriwa kulingana na muktadha mahususi.

Mchango wa semantiki katika ufasiri wa kijumla wa tamko umebanwa kuliko ilivyodhaniwa

mwanzoni. Pragmatiki Leksika inajaribu kuelezea fenomena za kipragmatiki ambazo

zimeunganika na semantiki hiyo chini ya umahususi wa faridi za kileksika.

Nadharia hii ina mihimili mingi ila tufafanua ile iliyokuwa na uhusiano na utafiti huu.

2.3.1 Semantiki Kileksika

Semantiki kileksika inajishughulisha na maana ya neno. Maneno huweza kuchukuliwa kuashiria

vitu katika ulimwengu au katika dhana kutegemea mtazamo mahususi wa semantiki kileksika.

Kwa mujibu wa Mmbwanga (2010) vitengo vya maana katika semantiki kileksika ni vitengo vya

kileksika ambavyo kwavyo msemaji huweza kuongezea kwa mfululizo maishani pamoja na

ujifunzaji wa maneno mapya na maana hayo.

Mhimili huu ulimsaidia mtafiti katika kuanisha agoti za wafungwa katika vikoa maana

mbalimbali. Maneno yaliyowekwa katika kikoa kimoja yalikuwa na uhusiano wa kimaana.

Page 33: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

16

Kikoa maana kama dhana ya kisemantiki ilitumika katika kuweka faridi za kileksika katika

matapo mbalimbali ya kimaana. Katika utafiti huu, vikoa maana vilivyojadililiwa vilikuwa;

kikoa cha mahusiano ya kimapenzi, kikoa cha marufuku na dawa za kulevya, kikoa cha mambo

na shughuli za jela, agoti zilizowarejelea wafungwa na hatimaye, agoti zilizowarejelea maafisa

wa magereza.

2.3.4 Michakato ya Pragmatiki Leksika

Kulingana na Blutner (2011), mambo ya kimsingi yanayoshughulikiwa katika pragmatiki leksika

akiwarejelea Wilson (2003) na Cartson (2002), yanaweza kugawika katika mambo matatu ya

kimsingi ambayo tuliyatumia katika uchanganuzi.

i) Ubanaji wa kileksika

ii) Upanuzi wa kileksika

iii) Kukisia maana

2.3.4.1 Ubanaji wa kileksika

Kwa mujibu wa Kolaiti na Wilson (2012) ubanaji wa kileksika ni mchakato ambao unahusu

matumizi ya neno au kirai katika kuonesha dhana mahususi zaidi (ambayo ina maana finyu)

kuliko maana iliyosimbwa ya kiisimu. Mtafiti alikubalina na ufafanuzi huu na kushadidia kuwa,

maana pana ya neno ndiyo iliyosimbwa kiisimu. Wakati ambapo ubanaji unafanywa, tunapata

dhana ndogo katika muktadha wa uzungumzaji. Maana inayojitokeza huwa ni kisehemu cha

maana pana ambayo imesimbwa. Anusu (2015) anatoa mfano; Niko ndani ndani ya Jubliee.

Neno ndani katika Kiswahili limesimba dhana ya NDANI. Ili kuelewa maana ya ndani, sharti

msikilizaji afanye ufasiri kutegemea muktadha. Hii ni kwa sababu, maana ya ndani ndani ni pana

kwa kiwango fulani. Horn na Ward (2004) wanafafanua kuwa ubanaji kwa kiwango kikubwa ni

Page 34: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

17

mchakato ambao unaweza kusawazishwa na hutegemea muktadha. Maana iliyosimbwa inaweza

kubanwa katika viwago tofauti kutegemea muktadha. Maana pana ni kuwa ndani, maana

mahususi ni kuwa ndani ya chama na hakuna kinachoweza kukutoa humo.

Mfano wa pili, Onyango ana kirusi. Neno kirusi limesimba dhana KIRUSI ambayo inajumuisha

aina nyingi za virusi vinavyoweza kusababisha magonjwa. Lakini katika muktadha huu, maana

ya kirusi imebanwa kumaanisha UKIMWI. Kwa mujibu wa Blutner (1998) ubanaji ni kutumia

faridi leksika kupitisha maana ambayo imebanwa zaidi kuliko ile ambayo imesimbwa

kisemantiki. Kisemantiki, kirusi kina maana ya kiini kisababishacho ugonjwa (Mdee n.w, 2011).

Katika muktadha wa mazungumzo, kirusi kina maana ya kirusi cha UKIMWI. Virusi vingine

vimetengwa katika muktadha huu (Anusu, 2015).

2.3.4.2 Upanuzi wa kileksika

Kwa mujibu wa Fromkin na Rodman (1978), upanuzi wa kileksika ni mchakato ambao kwao

maana ya neno hupanuka. Neno linamaanisha kila kitu kilichokuwa kikimaanishwa na kuzidisha

maana nyingine. Mtafiti alikubaliana na maelezo haya na kuongeza kuwa, neno linapopanuka

kimaana, neno hilo huwa limeongezewa vitajwa na kujumuisha vitajwa vingine. Kwa mfano,

neno mguu linaweza kutumiwa kutoa maana nyingi. Maana ya kileksika ya neno mguu ni kiungo

cha mwili wa binadamu, mnyama au mdudu kinachomwezesha kusimama au kwenda (TUKI,

2013). Hata hivyo, neno hili linaweza kutumiwa kumaanisha mwanamke anayetumiwa katika

mapenzi kisha baadaye anaachwa. Pia, linaweza kumaanisha sehemu ya siri ya mwanamke.

Hivyo basi neno hili linapata fahiwa nyingi zaidi ya maana yake ya kisemantiki. Ullmann (1970)

anafafanua kuwa maneno yanapewa maana moja bunifu au zaidi bila ya maana asilia kupotea. Ile

maana asilia na maana ya pili zinaishi upande upande bora tu kusiwepo na ukinzano (Anusu,

2015).

Page 35: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

18

2.3.4.2.1 Upanuzi wa kisitiari

Simiyu (2016) anaeleza kuwa upanuzi wa kisitiari ni mchakato ambao kwao maana ya neno ipo

mbali na maana wazi. Yaani, maana ya neno fulani katika muktadha wa mazungumzo ni tofauti

kabisa na maana ya neno hilo kiisimu. Yaani, katika upanuzi wa kisitiari maana ya neno huwa

mbali na maana halisi kwa kuhamisha maana ya neno hilo toka kwa kiashiria kimoja hadi

kiashiria kingine. Anusu (2015) anatoa mfano wa sentensi Onyango ni mburukenge sana.

Mburukenge ni mnyama lakini Onyango ni binadamu. Hapa, Onyango anafananishwa na

mburekenge kwa sababu ya tabia zake (Aitchison, 2003). Leksimu mburukenge limesimba

dhana MBURUKENGE. Msikilizaji anatengeza dhana za dharura kama vile, mburukenge ni

mnyama asiye na akili timamu. Ukweli ni kuwa sicho anachomaanisha msemaji. Hivyo basi

msikilizaji anachukua kuwa Onyango ni mjinga. Aitchison (2003) anafafanua kuwa kwenye

sitiari ya sampuli ya kiasili, vitu ambavyo vinalinganishwa vina uwezekano wa kutofautiana,

yaani, vinatokana na vikoa maana tofauti, na kufanana. Zinalingana katika sifa chache za

kawaida.

2.3.4.2.2 Chuku

Wilson (2003) anasema kuwa hili ndilo badiliko ambalo linaonekana kuhusisha kiwango

kukubwa zaidi cha upanuzi wa maana na hivyo kunakuwepo na utengano mkubwa kutoka kwa

dhana ambayo imesimbwa. Mtafiti alikubaliana na maelezo haya na kuongeza kuwa, hili

badiliko linahusu upigaji chuku au kutia chumvi ila haimaanishi hivyo waziwazi tu. Mfano,

Onyango hatoboki.

Leksimu toboka katika lugha ya Kiswahili ina maana ya kitu kupata tundu na kuweza kupitisha

maji au hewa. Kitu kinapotoboka huvuja bila kujizuia. Tukisema Onyango hatobiki tunatilia

chumvi dhana ya kuwa Onyango hawezi kutoa pesa.

Page 36: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

19

Kwa mujibu wa Bloomfield (1933) chuku ni badiliko linalotoka kwenye maana yenye nguvu

hadi maana ambayo ni legevu.

2.3.4.2.3 Upanuzi wa kategoria

Katika aina hii ya badiliko, jina la kitu ambacho kinajulikana zaidi katika jamii linapanuliwa na

kutumiwa katika jamii nzima ambamo kitu hicho hupatikana (Wilson, 2003). Mtafiti

alikubaliana na maelezo haya na kuongeza kuwa, hili jina linapotumiwa katika jamii nzima,

huwa linafanya maana inayopitishwa kujitenga zaidi toka kwenye maana iliyosimbwa na

leksimu hiyo.

Kwa mujibu wa Wilson na Carston (2007) majina ya kipekee na nomino za kawaida huwa

zinachangia katika badiliko hili. Glucksberg (2001) anatoa mifano ya majina Chomsky na

Shakespeare.

Mfano; Onyango ni Shakespeare wa Afrika. Shakespeare ni jina la kipekee. Kwa kuwa alikuwa

mwandishi shupavu na alitambulika ulimwenguni kote kwa uandishi wake, jina lake linatumika

na watu wanaopenda uandishi wake kurejelea watu wenye ufundi katika uandishi. Dhana

ambayo inawasilishwa katika muktadha huu inajitenga na dhana ambayo imesimbwa

inayoashiria Shakespeare aliyewahi kuishi. Jeffers na Lehiste (1979) wanafafanua kuwa upanuzi

wa maana huwa unatokana na kujumuisha hali mahususi hadi katika jamii ambayo ile hali

mahusisi inashiriki. Hii ni kwa sababu, majina ya pekee yanajitokeza kurejelea jamii ya kijumla

ya ile fenomena.

2.3.4.2.4 Ubunaji wa maana mpya na uundaji wa leksimu

Ubunaji wa maana ni mchakato wa kuzua maana mpya na maneno mapya kutoka kwa yale

maneno ambayo tayari yapo katika lugha fulani. Hivyo basi ubunaji wa maana mpya unaweza

Page 37: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

20

kutokea kupitia mkondo wa uundaji wa kileksimu. Hii inaashiria kuwa tunapounda leksimu

mpya, leksimu hiyo huweza kupata maana mpya.

Kwa mfano; Onyango asilete ubeberu wake hapa. Neno hili ubeberu liliwahi kuundwa kutokana

na neno beberu lenye maana wazi ya mbuzi dume. Maana inayowasilishwa ni kuwa Onyango

asiwanyanyase wengine.

Kupitia kipengele hiki mtafiti aliweza kujadili uundaji wa agoti katika magereza ambayo

aghalabu huambatana na ubadilishaji wa maana. Kitengo hiki kimejadiliwa kwa kina katika

kitengo cha uundaji wa agoti (2.6).

2.3.4.3 Kisio la maana

Ni badiliko la maana ambalo kwalo leksimu iliyo na maana thabiti kiasi hupanuliwa ukingoni na

kujumuisha mawanda ya makundi ambayo kwa hakika yanapatikana nje ya maana yake kamili

ya kiisimu. Mifano mizuri kwa mujibu wa Wilson (2003) ni kama matumizi ya kilegevu ya

takwimu za kukadiria, misamiati ya kijiografia na misamiti ambayo inaelezwa kwa njia ya

kukanusha. Kimsingi, dhana ambazo zinapanuliwa ukingoni ndizo zinazowasilishwa na

wasemaji katika usemi huku dhana thabiti ya leksimu ikiwa ndiyo ambayo imesimbwa

kisemantiki na neno hilo.

Marisya (2017) anafafanua kuwa ni hali ambapo ufasiri wa neno ambalo lina maana finyu

hupanuka ili kuhusiana na maana ya kitu ambacho kinahusiana nacho ambacho kina maana

tofauti na maana halisi ya neno hilo kiisimu. Kwa mfano, neno karatasi hutumiwa kurejelea

ugonjwa wa ukimwi katika jamii ya Wanyore. Hii ni kwa sababu mtu ambaye anaugua ugonjwa

huu huwa amekonda na ni mwepesi kama karatasi (Anusu, 2015).

Page 38: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

21

Katika badiliko hili, dhana ambayo inawasilishwa na neno fulani hujitenga zaidi kutoka kwa ile

dhana ambayo imesimbwa kama ambavyo ipo katika upanuzi wa kisitiari. Mfano; Chakula

kimeletwa mapema, leo saa saba imefika mapema.

Saa saba ni wakati thabiti ila hapa msemaji anachukulia kuwa wakati wowote ni saa saba mradi

tu chakula kiwe kiko tayari. Hivyo basi maana hii imejitenga sana na maana halisi ya saaa saba.

Saa saba inatumika kwa njia legevu.

Kwa muhtasari, michakato hii ya kipragmatiki leksika ilimwezesha mtafiti kuchanganua

mabadiliko ya kimaana katika agoti za wafungwa pamoja na kujadili uundaji wa agoti za

wafungwa.

2.4 Vikoa maana katika agoti za wafungwa

Kwa mujibu wa Kempson (1977) semantiki ni taaluma ambayo hujishughulisha na kufafanua

maana za maneno, maana za sentensi, pamoja na maana za matini za usemaji. Kama chombo cha

mawasiliano, lugha huhitaji tafsiri ya maana zilizobebwa pamoja na maumbo ya kisarufi ili

kutimiliza wajibu wake mkuu. Maana ni za aina mbili; kwanza maana inayorejelea muktadha wa

uzungumzi huchunguzwa katika pragmatiki. Hii hueleza alichokusudia msemaji katika

mawasiliano. Pili, ni maana kileksia ambayo husawiri maana ya kila neno katika lugha. Maana

hii huwakilishwa na vidahizo katika kamusi za lugha na ndiyo maana ya msingi na

isoyobadilika. Katika utafiti huu agoti zilifafanuliwa kwa kutegemea maana zao katika muktadha

wa jela.

Maneno yanapohusiana kwa njia mbalimbali huleta ukoa maana. Kwa mujibu wa Habwe na

Karanja (2004) ukoa maana ni mahusiano ya kimuundo ambapo kuna ufinyu au upana wa maana

Page 39: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

22

za maneno. Katika utafiti huu, ukoa maana ulitumika kurejelea tapo la maneno yenye maana

yanayohusiana.

Mugambi (2007) anaainisha leksimu mbalimbali za Sheng katika vikoa maana. Aliibuka na

vikoa maana vya mapenzi, biashara, elimu, michezo na utawala. Kwa mfano, katika kikoa cha

elimu anaainisha na kufafanua maana ya leksimu bayo, kemu, ziki, pizo na swa. Maneno haya

yanahusiana kwani yanarejelea aina mbalimbali za masomo katika shule za upili. Katika kikoa

cha michezo anafafanua aina mbalimbali za michezo kama zinavyorejelewa katika Sheng, futa,

bake, kagutha na voli. Kazi hii ni muhimu kwetu kwani, japo ilishughulikia ukoa maana katika

msimbo wa Sheng, ulitupa mwelekeo wa kuziweka agoti za wafungwa katika vikoa maana

mbalimbali.

Maana zinazowasilishwa na agoti za wafungwa hutegemea muktadha na mazingira. Ellis (2005)

“Prison-House and Language: Modern American Prison Argot” anatoa vikoa mbali mbali

ambavyo kwavyo agoti za wafungwa huweza kupata maana;

2.4.1 Vitendo vya ngono na mapenzi

Ushoga katika magereza ya Marekani umeandikwa na kuhifadhiwa sana katika karne ya ishirini

(Hensley na wenzake, 2003) na maneno mengi na maana yanatokana na mapenzi na ngono.

Maneno yanaweza kuanishwa katika vitengo vya wenye nguvu na wale wanyenyekevu,

kuhusiana na dhima zinazotekelezwa na wafungwa tofauti tofauti. Kwa mfano pana neno punk

lenye maana ya mfungwa anayekuwa kama mwanamke (Cardzo-Freeman nw., 1984). Neno hili

punk linatumiwa hadi leo kule Marekani. Flipflop ni wale walio na uwezo wa kuwa kama

wanawake na pia kuwa kama wanaume (Bently nw., 1992). Neno fish anaeleza kuwa lina maana

ya wafungwa wageni (Encinas, 2001) lakini katika magereza ya leo ya Waafrika-Wazungu zaidi

Page 40: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

23

huwa neno hili lina viashiria vya ushoga (Hensley nw., 2002). Kwa kutumia mwelekeo huu

mtafiti alitafuta istilahi ambazo zilihuhisiana kimaana na mahusiano ya kimapenzi.

2.4.2 Marufuku

Pana maneno mengi yanayoashiria marufuku, haswa yanayotumiwa katika shughuli zilizo

kinyume na matakwa ya magereza. Kuna vitengo viwili vya marufuku: vitu visiyo na madhara

yoyote, dawa za kulevya na silaha. Mfano bora zaidi ya marufuku isiyo na madhara ni donuts

ambayo inarejelea mafuta inayotumiwa kupika (Cardzo nw., 1984). Mifano mingine ni tat

inayorejelea hali ya kuchora miili ya mfungwa. Kategoria hiyo ina maana mbalimbali kama vile

tat gun, tat man na tat motor (Benltely, 1992). Agoti zinazorejelea uchoraji wa mwili

zimejadiliwa zaidi na Encinas (2001). Maneno yanayorejelea dawa za kulevya huwa ni ya siri

sana na hivyo huchukua mfumo wa misimu hivi kwamba yakitambuliwa na askari, hubadilishwa.

Kwa mfano bing kurejelea dawa nyingi zisizorejelewa kwa jina moja (Cardozo- Freeman, 1984)

au binky kumaanisha sindano. Ubunifu wa mfungwa huenea zaidi katika silaha na virejelewa

vyao kwa mfano Shivs na shanks ni maneno yanayotumiwa kurejelea visu vilivyotengezwa

gerezani (Encinas, 2001). Neno lingine ni zip gun, neno linalotumiwa kurejelea bunduki rejareja

zinazoundwa na wafungwa na kutumiwa ndani ya jela, na ili kuficha maana, zaidi huitwa „Z‟

(Bentley, 1992).

Kazi hizi ni muhimu katika kuainisha agoti. Katika utafiti huu hata hivyo tofauti na (Bentley,

1992) mtafiti alijikita katika lugha ya mazungumzo tu, pasi na kutafiti maneno yaliyoandikwa

mwilini au kwenye kuta za jela.

Page 41: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

24

2.4.3 Michakato ya kitaasisi

Japo agoti kwenye kikoa hiki ndizo za kipekee toka gereza moja hadi lingine, ndizo

zinazobadilika zaidi kulingana na namna ambavyo mabadiliko ya masuala ya kisheria

yanavyoleta maneno mageni na tofauti. Maneno mahususi ya megereza ni kama oregon boots

yenye maana ya miguu ya chuma, ambayo ilipata jina hilo kutokana na gereza la kwanza

lilimotumika (Oregon). Sheria na masharti ya gereza fulani huweza pia kusababisha uundaji wa

neno fulani kurejelea hatua za kinidhamu. Kwa mfano pana maneno majors na minors kurejelea

viwango vya kosa alilofanya mfungwa. Aidha, pana maneno kama parakeet kurejelea askari

ambaye huwaiga kimzaha wakubwa wake (Jackson, 1967). Maneno mengine ni kama brown

shirt inayorejelea mavazi ya askari na tabia zao za kiukandamizi (Bentley, 1992).

Thamani ya tafiti hizi zilizofanywa kuhusiana na agoti ya wafungwa haiwezi kupuuziliwa mbali.

Hata hivyo, maneno haya yanahusiana na magereza ya ughaibuni. Afrika, na hasa nchini Kenya,

maneno macheche yanayojulikana kutumiwa gerezani yanatokana na filamu zilizoigizwa na

baadhi ya vitabu vilivyoandikwa na wafungwa waliofunguliwa. Katika miktadha hii, maneno

yanayotumiwa gerezani huwa kama maneno matano au kama zaidi maneno kumi. Na mengi yao

huwa si sahihi (Coleman, 2004). Hata hivyo kuna wengine ambao pia wamejaribu kuainisha

agoti za wafungwa kwa mfano Halliday (1978) na Clemmer (1940). Clemmer alipata maneno

1063 katika magereza yote ya Marekani na akayaweka katika vikoa vya; ngono na mapenzi,

sehemu za mwili, maelezo kuhusu wengine, pombe na dawa za kulevya, maneno yanayohusu

jela na matusi (vagabondage). Kupitia kwa maelezo haya utafiti huu ulichanganua agoti za

wafungwa na kuziweka katika vikoa maana mbalimbali.

Page 42: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

25

2.5 Mabadiliko ya maana

Dhana ya mabadiliko ya maana yalizungumziwa mwanzo na Edward Sapir aliyeeleza kuwa kila

neno na kila elementi ya kiisimu hubadilika polepole (Sapir katika Ullman, 1977). Keith na

Shuttleworth (2000) wanaeleza kuwa, „Mabadiliko ni sehemu muhimu katika maisha; bila

mabadiliko, maisha yanakoma. Lugha pia lazima ibadilike ili iwe hai.‟ Mabadiliko ya maana

hujitokeza wakati neno linapotumiwa kuwasilisha maana ambayo haikuwa nayo awali (Lourens

nw, 1992).

Bloomfield (1930) anajadili aina mbalimbali za mabadiliko ya maana. Anataja upanuzi wa

kimaana, upanuzi wa kisitiari na chuku miongoni mwa mabadiliko mengine. Anadai kuwa kila

badiliko la kimaana litaathiri maneno mengine katika kikoa maana. Kutokana na kazi hiyo ya

Bloomfiled utafiti huu ulipata mwelekeo wa kujadili mabadiliko ya kimaana yanayojitokeza

katika agoti za wafungwa wa magereza ya Kisumu. Utafiti huu ulijikita katika aina mbalimbali

za mabadiliko ya kimaana ambapo upanuzi wa kileksika unajidhihirisha kwa njia anuwai.

Katika tasnifu yake ambayo haijachapishwa, Wambugu (2010) anaangazia mabadiliko ya

kimaana katika leksimu za Kikuyu kwa kutumia mtazamo wa kipragmatiki leksika. Anaendelea

na kufafanua maana za ziada ambazo leksimu hizi zimepokea. Anahusisha kazi yake na kazi ya

Muyuku (2009).

Ullmann (1957, 1962) anaibuka na uchanganuzi ambao unaenda juu zaidi ya ufafanuzi wa

leksimu mojamoja. Anaiga kazi ya Trier (1931) ambaye alisema kuwa badiliko la kimaana

litaathiri maneno mengine katika kikoa husika.

Blank (1998) ni mtafiti mwingine ambaye aliandika kuhusu mabadiliko ya kimaana kwa

kuangazia hali mbalimbali ambazo husababisha mabadiliko ya kimaana. Blank anasema kuwa

Page 43: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

26

mabadiliko ya kimaana yanaweza kusababishwa na masuala ya kiisimu katika lugha husika.

Maneno yanaweza kutumika katika miktadha mbalimbali ili kuibua maana tofauti ambayo

msemaji ananuia kuwasilisha. Pia anafafanua hali za kisaikolojia ambazo huweza kuathiri namna

ambavyo watu huteua na kutumia maneno katika lugha kutegemea chukulizi zao kuhusu maneno

hayo. Msemaji anapoona kuwa neno fulani ni kinyume na maadili ya kijamii atatumia tasfida

katika kuwasilisha ujumbe wake.

Habwe (1999) alichunguza diskosi ya hotuba za kisiasa kwa kujikita katika Nadharia ya

Ushirikiano miongoni mwa nadharia nyingine. Alizamia katika kufafanua jinsi ambavyo

implikecha huundwa katika kufasiri ujumbe ambao umo kwenye matamko ya wanasiasa. Utafiti

huu ulimfaa mtafiti katika kuelewa implikecha za mazungumzo zinavyoundwa katika lugha ya

Kiswahili. Aidha, utafiti huu ulimfaa mtafiti katika kuelewa jinsi masuala ya kipragmatiki

huelezwa katika diskosi za Kiswahili. Utafiti huu ni tofauti na wa Habwe (keshtajwa) kwa

sababu ulishughulikia mabadiliko ya kimaana kwa kujikita katika Nadharia ya Pragmatiki

Leksika.

Carston (2002) alifafanua kwa kina mihimili mikuu ya Nadharia ya Pragmatiki Leksika.

Alifafanua namna msikilizaji anavyojenga dhana za dharura na pia kufafanua michakato ya

Pragmatiki Leksika kama vile upanuzi wa kileksika na ubanaji wa kileksika. Isitoshe,

amefafanua kwa undani upanuzi wa kisitiari kwa kuonyesha jinsi dhana zilivyosimbwa na sitiari

huweza kusimbuliwa na msikilizaji. Kazi hii ilitufaa katika kuelewa michakato ya Nadharia ya

Pragmatiki Leksika na kuitimia katika kujadili mabadiliko ya kimaana katika agoti za wafungwa.

Muyuku (2009) alitafiti jinsi uchanganyaji lugha hujitokeza katika matangazo ya benki ya

Commercial banks pamoja na Mobile Telecommunications kwa kujikita katika Nadharia ya

Page 44: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

27

Pragmatiki Leksika. Alifafanua jinsi dhana zinavyosimbwa na kusimbuliwa ili kuwavutia na

kuwashawishi wateja. Ilibainika katika kazi hii kwamba Kiswahili ni kati ya lugha ambazo

zilitumiwa kwa wingi. Utafiti huu ulimfaa mtafiti kwa kumpa mwelekeo wa jinsi maneno ya

Kiswahili husimbwa na kusimbuliwa. Tofauti ni kuwa utafiti huu ulijikita katika agoti za

wafungwa na ilichunguza mabadiliko ya kimaana na wala si uchanganyaji lugha.

Njimu (2010) naye aliangazia matumizi ya leksimu kwenye magazeti ya michezo katika taifa la

Kenya kwa kujikita katika Nadharia ya Pragmatiki Leksika. Lengo lake lilikuwa ni kuonyesha

umuhimu wa muktadha katika kuzua zile dhana za dharura. Alijikita katika magazeti matatu; The

Nation, The Standard, na The Star. Mtafiti alinufaika na utafiti huu kwani ulimwezesha kuelewa

jinsi maana hubadilika katika muktadha.

Ochoki (2010) alitumia data toka kwenye mtandao na kutumia Nadharia ya Pragmatiki Leksika

kuchunguza jinsi maana zinavyosimbwa katika nyimbo za Hip hop za nchi ya Kenya. Alitumia

michakato ya upanuzi na ubanaji wa maana katika kufafanua usimbaji huu wa maana. Mtafiti

alifaidika na utafiti huu kwani ulimwezesha kuelewa jinsi dhana zinavyosimbwa na kusimbuliwa

katika Kiswahili.

Ochichi (2013) alijikita katika kuchunguza umaanisho na usimbaji wa maana kumazungumzo

katika lugha ya Kiswahili na Ekegusii. Kufanikisha kazi yake, alitumia Nadharia ya Pragmatiki

Leksika na kategoria za kimuktadha. Isitoshe, alichunguza uwazi na umaanisho wa kauli za

Ekegusii na Kiswahili. Utafiti huu ulimsaidia mtafiti katika kufahamu namna usimbaji hujitokeza

katika Kiswahili. Tofauti ni kuwa mtafiti alijikita katika agoti za wafungwa.

Page 45: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

28

Kazi hizi ni muhimu kwani zinazungumzia mabadiliko ya kimaana. Ingawa hivyo, zinaangazia

mabadiliko ya kimaana katika jumuiya lugha iliyo tofauti na ya utafiti huu. Katika kazi hii,

mtafiti aliangazia mabadiliko ya kimaana katika katika agoti ambazo hutumiwa na wafungwa.

2.6 Uundaji wa agoti za wafungwa

Kama ilivyojadiliwa awali, uundaji wa maneno mapya pamoja na ubunaji wa maana mpya ni

kitengo cha upanuzi wa maana ambacho pia hushughulikiwa na Nadharia ya Pragmatiki Leksika

(Wilson, 2003). Hii hutoa data zaidi kwa nadharia hii na kutoa welewa wa mikakati ya kiakili na

hali za kimaumbile ambazo huhusika. Leksia huashiria umbo lenye maana msingi kama vile

vitenzi au nomino (Buliba, Njogu na Mwihaki, 2006). Utafiti huu ulichunguza namna agoti za

wafungwa huundwa.

Katika miaka ya sabini, Ohly (1977) alitoa baadhi ya ruwaza za kuanzisha misamiati mipya

katika Kiswahili. Kwanza, alifafanua ukopaji wa maneno kisha akaangazia uundaji wa maana

mpya ambao unaweza kuwa; uundaji wa maneno mpya kikamilifu, maneno yaliyokuwepo

kuidhinishiwa maana mpya au kupewa mawanda ya kisemantiki ya kipekee au kwa kutumia

makundi ya kisintaksia yenye kijalizo. Mtafiti alikubaliana na ufafanuzi huu kwani hadi nyakati

hizi pana leksimu ambazo zinaundwa au zinapata maana mpya au zinabadilishwa miundo

kimofolojia au kifonolojia na kwa njia hiyo kupata maana mpya.

Uundaji wa agoti miongoni mwa wafungwa ulikisiwa kuwa ni karibu sawa na uundaji wa

maneno katika jamii na hasa katika aina nyingine za misimbo. Kwa mujibu wa Jefwa (2010)

uundaji wa maneno ni uambatanishaji wa mofimu moja au zaidi kufikia kiwango cha mofimu

hiyo au hizo kuleta maana kileksika katika lugha yoyote ile. Kwa mujibu wa mtaalamu huyu,

mbinu za kimofolojia zitumikazo katika uundaji wa maneno katika lugha za ulimwengu ni

Page 46: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

29

pamoja na: Unominishaji, ukopaji na utohozi, uhulutishaji, ukatizaji, akronimu, uambatanishaji

na uambishaji.

2.6.1 Ukopaji na utohozi

Ukopaji ni hali inayojumuisha uhamishaji wa kipashio fulani kutoka lugha moja na kukiingiza

katika lugha nyingine. Kwa hivyo, kuna lugha changizi na lugha pokezi (Jefwa, 2010). Hock na

Joseph (1996) wanasema kuwa ukopaji ni uhamishaji wa leksimu mahususi au seti ya leksimu au

faridi fulani kutoka lugha moja au lahaja moja hadi nyingine. Kuna aina mbili za ukopaji:

ukopaji sisisi na ukopaji tohozi. Ukopaji sisisi ni pale ambapo leksimu fulani inahamishwa

kutoka katika lugha changizi hadi lugha lengwa bila ya kufanyiwa marekebisho yoyote. Maneno

yanaweza kukopwa toka lugha ya Kiswahili au lugha ya Kiingereza. Kwa mfano neno wode

limekopwa toka neno la Kiingereza water.

2.6.2 Mbinu ya ukatizaji

Ukatizaji ni mbinu ya kuunda maneno kwa kuyafupisha. Katika mbinu hii vile vile, maneno

huundwa kwa kudondosha silabi moja au zaidi (Jefwa, 2010). Kwa mujibu wa TUKI (1990)

ukatizaji ni hatua ya kufupisha neno kwa kuondoa sehemu ya mwanzoni au mwishoni. Mbinu hii

ya uundaji wa maneno hutumika na lugha nyingi ulimwenguni. Lugha ya Kiingereza kwa mfano

imeunda maneno yafuatayo kutumia mbinu hii; bike inatokana na bicycle. Prof inatokana na

Professor.

2.6.3 Mbinu ya uambishaji

Kwa mujibu wa Jefwa (2010), uambishaji huwa utaratibu wa kuongezea viambishi katika mzizi

wa leksimu ili kuunda leksimu mpya. Mbinu hii hujumuisha viambishi awali na viambishi

tamati. Viambishi hivi huambishwa kwenye mzizi wa neno ili kuunda maneno mapya.

Page 47: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

30

Matthews (1997) naye anaeleza ya kwamba uambishaji ni utaratibu wa kuongezea herufi, sauti

au makundi yao katika mzizi wa neno na kwamba nyongeza hiyo hubadilisha maana na uamilifu

wa neno hilo. Sheng kwa mfano huitumia mbinu hii ili kujiundia leksimu mpya. Hata hivyo

leksimu za Sheng zilizoundwa kwa mbinu hii huwa za mkopo. Kwa mfano msupa yenye maana

ya msichana imeundwa kwa uambishaji mofu (M+SUPA).

2.6.4 Mbinu ya ubadilishaji silabi

Ogechi (2005) anasema kwamba neno husika hukopwa kisha matamshi ya neno hilo

hurekebishwa kabla ya silabi za neno hilo kurekebishwa. Ubadilishaji silabi huu huwa utaratibu

wa kimakusudi ambao hutumiwa na Sheng kuundia leksimu zake. Kwa mfano bread kuwa dibre

na story kuwa risto.

2.6.5 Onomatopia: Tanakali za Sauti

Onomatopia pia hujulikana kama tanakali za sauti. Onomatopia ni ujenzi wa neno kwa kuiga

sauti au mlio wa kitu (TUKI, 2009). Mwangi na Mukhwana (2011) nao wanadai kwamba

onomatopea ni mbinu ya uundaji leksimu ambapo leksimu huundwa kutokana na sifa, uamilifu,

umbo, sauti au milio. Kuna madai mengine yanayosema kwamba onomatopia ni uundaji wa

maneno kutokana na sauti asilia. Kwa mfano neno kacha la Sheng linamaanisha pingu. Bling

bling nalo lina maana ya pambo ghali. Utafiti huu ulitaka kutambua ni mbinu zipi ambazo

hutumiwa katika kuunda agoti za wafungwa wa magereza ya Kisumu.

2.7 Pengo la utafiti

Kwa ujumla, lugha ya wafungwa ni moja kati ya maeneo ambayo yamefanyiwa utafiti katika

mataifa ya kimagharibi. Katika mataifa ya Afrika, tafiti kuhusu lugha za wafungwa ni chache

Page 48: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

31

mno. Ilivyojitokeza, hakukuwa na ufafanuzi wowote wa kina uliowahi kutolewa kuhusu lugha

kama inavyotumika katika magereza ya mataifa ya Afrika Mashariki.

Hivyo, utafiti huu ulikusudia kuliziba pengo hili kwa kujadili vikoa maana katika agoti

zinazotumiwa miongoni mwa wafungwa wa magereza ya Kisumu, kujadili mabadiliko ya

kimaana katika agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu na hatimaye

kubainisha mbinu zinazotumiwa katika uundaji wa agoti za wafungwa wa magereza ya Kisumu.

2.8 Hitimisho

Katika sura hii mtafiti ameonyesha dhana muhimu katika utafiti huu na namna zilivyotumiwa na

watafiti wa awali. Amehakiki namna watafiti wa awali walivyoainisha vikoa maana vya agoti za

wafungwa wa mataifa yao, maana ya agoti hizo pamoja na michakato mbalimbali ya mabadiliko

ya kimaana. Pia, ameeleza mbinu mbalimbali za uundaji wa maneno kwa ujumla. Utafiti huu

ulichunguza namna hali hizi zinavyosadifu muktadha wa taifa la Kenya. Sura inayofuata

inajadili njia na mbinu za utafiti zilizotumiwa katika utafiti huu.

Page 49: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

32

SURA YA TATU

MBINU ZA UTAFITI

3.1 Utangulizi

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa kuchanganua matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa

katika magereza teule ya jimbo la Kisumu, nchini Kenya. Kwa mujibu wa Mugenda na Mugenda

(2005), mbinu ya utafiti ni utaratibu makini wa kiuchunguzi unaotumia mbinu za kisayansi

zilizokubaliwa ili kutatua matatizo na kuibua ujuzi mpya. Sura hii imegawika katika sehemu

kumi na moja. Sehemu ya kwanza inatoa utangulizi wa sura, sehemu ya pili inafafanua mbinu za

utafiti. Sehemu ya tatu inaangazia eneo la utafiti na sehemu ya nne inaeleza kuhusu eneo la

utafiti. Katika sehemu ya tano, mtafiti anaangazia sampuli na usampulishaji. Sehemu ya sita

imeelezea vifaa vya utafiti. Sehemu ya saba imeshughulikia ukusanyaji wa data. Sehemu ya nane

imeelezea uchanganuzi wa data. Sehemu ya tisa mtafiti amefafanua jinsi vifaa vya utafiti

vilijaribiwa. Sehemu ya kumi inaeleza kuhusu maadili ya utafiti. Mwisho wa sura ni hitimisho.

3.2 Mbinu za utafiti

Kothari (2008) anaeleza kuwa mbinu za utafiti ni mwongozo uliopangwa kufuatwa katika

ukusanyaji na uchambuzi wa data ili kujibu maswali ya utafiti husika. Mtafiti alitumia

mahojiano katika utafiti huu. Kombo na Tromp (2006) wanaeleza kuwa mahojiano ni majibizano

ya ana kwa ana (au ya simu, barua, kidijiti/barua pepe) kati ya watu wawili au zaidi kwa lengo la

kukusanya taarifa au maoni kuhusu suala fulani la kiutafiti lililoainishwa. Utafiti huu ulitumia

mahojiano ya ana kwa ana. Kothari (2008) anasema kuwa, katika mahojiano ya ana kwa ana,

Page 50: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

33

mtafiti huwauliza watafitiwa maswali na wakati mwingine watafitiwa nao huuliza maswali na

mtafiti huyajibu.

Mbinu hii iliteuliwa ili kupata uthabiti wa majibu ya watafitiwa pamoja na kupata uthabiti wa

mbinu za kukusanyia data. Pia, ilikuwa ni rahisi kwa mtafiti kuthibiti sampuli kwa usahihi zaidi.

Hii ilitokea kwa sababu mtafiti alikutana na wahojiwa ana kwa ana na kuwauliza maswali kisha

akarekodi majibu yao. Tatu, ni rahisi kwa mtafiti kukusanya taarifa nyingi kwa kina zaidi kwa

sababu watafitiwa wanaweza kuuliza maswali. Mtafiti pia huwa huru kuuliza maswali ya ziada

ambayo si rahisi kufanyika unapotumia mbinu nyingine kama hojaji au utazamaji nyanjani.

Mahojiano ya kimakundi pia yalitumiwa kupata data ya utafiti huu. Mahojiano ya kimakundi ni

njia ya kupata data inayohusisha maswali na majibu yanayofanywa kwa mazungumzo kati ya

mtafiti na kundi la watafitiwa (Kothari, 2008). Mbinu hii ilimsaidia mtafiti kupata taarifa za

msingi zilizohusiana na mada ya utafiti. Katika makundi hayo ilibainika kuwa wahojiwa

waliweza kuwarekebisha wenzao walipotoa maelezo ambayo hayakufaa. Kila awamu ya

mahojiano ya kimakundi ilihusisha watafitiwa kumi.

3.3 Muundo wa utafiti

Utafiti huu ulitumia muundo wa usoroveya elezi. Kwa mujibu wa Kombo na Tromp (2006)

muundo huu hutumiwa kupata data kuhusu mielekeo, maoni, mazoea na pia mambo muhimu

yanayohusu elimu na masuala ya jamii. Good (1972) ameeleza kuwa kwa kutumia muundo huu

wa usoroveya elezi, mtafiti anaweza kupata data ya kutathmini njia mbalimbali zinazotumiwa ili

kufikia uamuzi mwafaka. Kwa kutumia muundo huu, mtafiti alifanikiwa kupata habari kuhusu

agoti za wafungwa ikiwepo maana mbalimbali za agoti na maoni yao kuhusu lugha waliyotumia

katika muktadha wa jela.

Page 51: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

34

Utafiti huu ulichukua mwelekeo wa utafiti nyanjani. Katika utafiti nyanjani, mtafiti huhusishwa,

hushirikishwa pamoja na kutangamana na watafitiwa. Lengo la kufanya hivi ni kudhihirisha hali

ilivyo na kutoa uamuzi kutegemea data iliyoshuhudiwa. Mkondo wa utafiti elezi ulichukuliwa

kwa kuwa utafiti elezi hunuia kueleza sababu, maoni, mitazamo na misukumo ya mambo

mbalimbali. Mugenda na Mugenda (2005) wanaeleza kuwa utafiti elezi ni uchunguzi wa vitu

katika hali zao asilia, na kujaribu kufasiri maana ambayo wanajamii huipa vitu hivyo.

3.4 Eneo la utafiti

Utafiti huu ulifanywa katika magereza makuu ya Kibos na Kodiaga. Gereza la Kibos lipo katika

jimbo la Kisumu takriban kilomita sita kutoka jiji la Kisumu (Owino, Omar na Akong‟a, 2015).

Mtafiti aliyachagua magereza haya kutokana na misukumo kadha. Kwanza, mtafiti aliishi katika

mazingira ya magereza haya kwa takriban miaka ishirini kwa jumla. Hivyo basi alikuwa katika

nafasi nzuri ya kuelewana na hata kuwasiliana na maafisa wa magereza hali iliyomrahisishia

ukusanyaji wa data. Pili, ni ukaribu. Ukaribu huu ulirahisisha utafiti wenyewe kwani ulimpa

muda mzuri wa kukusanya data. Eneo la Kibos lina magereza mawili lakini mtafiti alifanya

utafiti wake katika gereza kuu la Kibos. Kama ilivyotarajiwa, wengi wa wafungwa katika gereza

hili walikuwa wameishi gerezani kwa muda mrefu na hivyo kuwa wenye hazina kubwa ya

misamiati ya wafungwa gerezani.

Eneo la Kodiaga lina magereza matatu. Magereza mengine mawili hayakuteuliwa kuwa gereza

moja ni la wanawake. Mtafiti alikusudia kuchunguza agoti zilizotumiwa na wafungwa wanaume

tu. Gereza jingine ni gereza dogo. Wafungwa wa gereza hili hufungwa kwa miaka michache

hivyo basi walitarajiwa kutokuwa na umilisi wa lugha ya jela. Gereza kuu la Kodiaga liliteuliwa

Page 52: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

35

kwa sababu huhifadhi wafungwa wanaohudumia miaka miaka mingi. Hawa walitarajiwa kuwa

na ujuzi mkubwa wa lugha ya jela.

3.5 Sampuli na usampulishaji

3.5.1 Usampulishaji

Sampuli iliyotumika katika utafiti huu ilitokana na makundi mawili ya kimsingi. Sampuli ya

watafitiwa na samupuli ya agoti zilizokusanywa kutoka kwa watafitiwa. Kwa mujibu wa Kothari

(2004), sampuli ni kundi dogo la kutafiti ambalo huchaguliwa kutoka katika kundi kubwa

ambalo kutoka kwalo mtafiti hupata data na kutoa mahitimisho yake. Sigh (2007) naye anaeleza

kuwa uteuzi wa sampuli ni mchakato wa kuteua kundi dogo kutoka kundi kubwa la watafitiwa ili

kulifanyia kundi lengwa makisio. Mugenda na Mugenda (2005) wanasema kuwa

kinachomwongoza mtafiti katika uteuzi wa sampuli yake ni sababu fulani maalumu aliyonayo.

Kwa mfano, anaweza kuteua kundi au sehemu fulani kwa sababu ni rahisi kwenda huko,

anapajua vizuri au mdhamini wake anapapendelea. Anateua wahojiwa kulingana na madhumuni

yake. Wahojiwa wanateuliwa kwa sababu wana taarifa au wana sifa anazohitaji mtafiti.

Katika utafiti huu mtafiti alitumia uteuzi wa sampuli kusudio kuteuwa watafiti na agoti za

kushirikishwa katika utafiti huu. Kwa mujibu wa Gall n.w. (1996) lengo la uteuzi wa sampuli

kusudio ni kuteua watafitiwa au vitu vya kutafiti ambavyo vina habari za kutosha katika

muktadha wa utafiti elezi.

3.5.2 Sampuli lengwa

Kwa mujibu wa Walliman (2011), sampuli au kundi lengwa ni jumla ya vitu vyote

vinavyohusika katika kufanyiwa utafiti, yaani taasisi, watu, vitu au matukio. Kimsingi, kundi

lengwa ni jumla ya walengwa wote wa utafiti ambapo sampuli inaweza kuchaguliwa. Sampuli

Page 53: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

36

lengwa ya kwanza katika utafiti huu ni wafungwa wa magereza ya Kisumu. Kwa mujibu wa

ripoti ya Tume ya Kutetea Haki za Binadamu nchini Kenya (KHRC, 2002), gereza la Kibos lina

wafungwa 647 ilhali gereza la Kodiaga lina wafungwa 1,206. Ni kutokana na sampuli hii lengwa

ambapo mtafiti aliteua sampuli ya kutafiti. Hili ndilo kundi ambalo yamkini ingeweza kutumia

agoti ambazo utafiti huu ulikuwa ukichunguza.

Sampuli ya pili ni jumla ya agoti ambazo mtafiti alikusanya kutoka kwa watafitiwa. Mtafiti

alikusanya jumla ya agoti 263. Kutokana na agoti hizi mtafiti aliteua agoti za kushirikishwa

katika utafiti.

3.5.3 Sampuli iliyoteuliwa

Gay na Diehl (1992) wanasema kuwa sampuli inayoteuliwa kutoka kwenye kundi lengwa

hutegemea aina ya utafiti. Katika utafiti elezi wanapendekeza kuwa sampuli iwe 10% ya kundi

lengwa. Kwa mwelekeo huu mtafiti aliteua wafungwa 185 kimakusudi ili kushiriki katika utafiti

huu. Yaliyozingatiwa ni: Sharti mtafitiwa angekuwa na miaka 18 au zaidi, sharti mtafitiwa

angekuwa amehudumia kufungo katika gereza hilo kwa zaidi ya miaka mitatu. Kigezo cha miaka

mitatu kilihakikisha kuwa mtafiti aliwahoji watatifitiwa wenye umilisi wa agoti za wafungwa.

Kati ya agoti 263 mtafiti aliteua agoti 188 zilizoshirikishwa katika utafiti huu. Agoti hizo 188

ziliteuliwa kimakusudi kwa sababu zilikuwa na sifa alizotaka mtafiti. Agoti hizo zilikuwa ni

leksimu za Kiswahili, Sheng au leksimu zilizoundwa kwa kuachanganya Kiswahili na lugha

nyingine. Agoti zingine 75 hazikushirikishwa katika utafiti kwa sababu zilikuwa aidha za

Kiingereza au lugha za kienyeji. Mtafiti alijikita katika virai nomino na virai vitenzi tu.

Page 54: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

37

3.6 Vifaa vya kukusanya data

Vifaa alivyotumia mtafiti ni kalamu na daftari. Kila mara watafitiwa walipojibu swali mtafiti

alilinakili kwenye daftari. Japo kinasa-sauti kingefaa zaidi katika kunasa na kurekodi sauti na

hali zote za muktadha wa mahojiano baina ya mtafiti na watafitiwa, ilibainika kuwa sheria

hazikuruhusu vyombo kama hivyo kutumiwa gerezani. Hata hivyo, mtafiti aliweza kuvitumia

vifaa alivyokuwa navyo vizuri kwa kunakili kila hoja na ufafanuzi uliotolewa na watafitiwa.

3.7 Ukusanyaji wa data

Kabla ya kuanza utafiti rasmi, mtafiti alikuwa katika harakati za kukusanya agoti zilizokuwa

zikutumiwa na wafungwa kwani aliishi katika mazingira hayo ya jela. Alizikusanya data hizo za

awali alipowasikia wafungwa wakiwasiliana katika maeneo yao ya kazi. Hata hivyo, katika

ukusanyaji rasmi wa data, mtafiti alitumia jumla ya miezi miwili katika kukusanya data yake.

Kila alipokusanya data mtafiti alishirikiana na maafisa wa magereza kuwateua wahojiwa ambao

wangeshiriki katika usaili. Mwongozo ule ule wa usaili ndio uliotumiwa katika mahojiano ya

kimakundi. Kati ya sampuli ya watafitiwa 185, mtafiti atulitumia mahojiano ya ana kwa ana

kukusanya data kutoka kwa watafitiwa 105. Mahojiano ya kimakundi yalitumiwa kukusanya

data toka kwa watafitiwa 80. Mahojiano haya ya kimakundi katika kila gereza yaliwashirikisha

watafitiwa 10 katika kila awamu.

3.8 Uchanganuzi wa data

Kwa mujibu wa Kothari (2008), uchanganuzi wa data ni kitendo cha kufupisha na kupangilia

vizuri data ambayo imekusanywa kwa njia ambayo inasaidia kujibu maswali ya utafiti husika.

Hii ni hatua muhimu katika kupata majibu ya maswali ya utafiti (Bogdan na Biklen, 1992).

Page 55: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

38

Utafiti huu ulitumia mkabala wa kimaelezo katika kuchanganua data. Enon (1998) anasema

kwamba mkabala huu ni mbinu ya kuchanganua data ambapo mtafiti huieleza data yake

kimaelezo. Kress (2008) kwa upande wake anafafanua mkabala huu kwa kusema kuwa unaeleza

vipi na ni kwa nini matukio yametokea. Mtafiti alitumia mkabala huu kwa sababu majibu

yalihitaji maelezo ya kina kuhusu agoti za wafungwa pamoja na maana yazo. Kimsingi, data

iliwasilishwa kwa kutumia majedwali kisha maelezo yakatolewa baadaye.

Aidha, data ilichanganuliwa kwa misingi ya Nadharia ya Pragmatiki Leksika. Kipengele cha

semantiki leksika kilitumiwa kutambua vikoa maana katika agoti za wafungwa na kuanisha agoti

hizo katika kila kikoa cha maana. Kipengele cha michakato ya kipragamtiki leksika kilitumiwa

kufafanua mabadiliko ya kimaana katika agoti za wafungwa. Hatimaye, kipengele cha ubunaji

mpya wa maana na uundaji wa leksimu kama aina ya upanuzi wa maana kilitumiwa kujadili

mbinu za uundaji wa agoti katika muktadha wa magereza. Data ilichanganuliwa kwa

kuiambatanisha na mifano mahususi ili kuithibitisha mada ya utafiti.

3.9 Majaribio ya vifaa vya utafiti

Wiersman (1985) anaeleza kuwa majaribio ya utafiti hubainisha udhaifu wa vifaa vya utafiti na

kurekebisha makosa yaliyomo kabla ya kuvitumia katika utafiti wenyewe. Majaribio hayo pia

hudhihirisha uhalali na utumainifu wa vifaa hivyo. Mtafiti aliifanyia mwongozo wa mahojiano

majaribio i1i kuhakiki uhalali na utumainifu wake. Mtafiti aliwatumia raia wanne aliowafahamu

ambao waliwahi kuhudumia vifungo vya jela. Kabla ya majaribio, mwongozo wa mahojiano

ulikuwa na sehemu iliyowauliza watafitiwa majukumu ya agoti. Baada ya majaribio, sehemu hii

iliondolewa kwa sababu haikusaidia katika kupata agoti kutoka kwa watafitiwa.

Page 56: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

39

3.9.1 Uhalali

Kulingana na Orodho (2005), uhalali ni kiwango ambacho vifaa vya utafiti vinatumika

vinavyofaa.Vifaa hivi sharti vichunguzwe uhalali wao kabla ya kutumiwa katika utafiti kamili.

Swala kuu la kuzingatia ni uhalali wa vifaa hivyo katika mada husika. Majaribio yalifanyiwa

vifaa vya utafti kukadiria uhalali ili kuhakikisha maswali yalilenga mada. Uhalali pia ulitathmini

kiwango cha lugha katika hojaji. Jedwali sailifu lilitumiwa kuchunguza ufaafu wa maswali

yaliyokuwa katika hojaji. Wasimamizi wa mtafiti pia walichunguza uhalali wa maswali

yaliyokuwa katika hojaji. Baadaye mwongozo sahihi wa mahojiano ulitayarishwa ili kutumika

katika ukusanyaji wa data nyanjani.

3.9.2 Utumainifu

Utumainifu wa vifaa ni kiasi ambacho vifaa vya utafiti vinaweza kuleta matokeo yaleyale

vinapotumiwa mara kadha (Orodho, 2005). Kulingana na Mugenda na Mugenda (2003)

utumainifu ni kiwango ambacho vifaa vya utafiti vinazalisha matokeo yanayotegemewa kila

wakati vinapotumiwa. Mbinu ya majaribio ya kurudiwa hutumiwa kwa kundi husika kukiwa na

mpito wa wakati baina ya jaribio la kwanza na la pili. Kipimo cha Pearson kinaruhusu kiwango

kati ya 0.5 na 1, (Ingule na Gatumu, 1996). Katika kuhakikisha utumainifu, majaribio yalifanywa

kwa kurudiwa kwa wafungwa wanne waliokwisha funguliwa. Matokeo ya majaribio katika

kipimo cha uwiano yalionyesha kuwa mwongozo wa mahojiano ungeweza kutegemewa katika

kufanya utafiti.

Page 57: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

40

3.10 Maadili ya utafiti

Ukusanyaji wa data kupitia mbinu yoyote ile huhitaji kuzingatia maadili kwa upande wa

watafitiwa, mtafiti na katika mchakato wa utafiti (Mulokozi, 2003). Utafiti huu ulizingatia

maadili kama yafuatavyo;

3.10.1 Maadili ya utafiti yanayomhusu mtafiti

Mtafiti aliandika barua ya kujitambulisha na kuomba kibali cha kukusanya data kutoka kwa

Halmashauri ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi. Halmashauri hii ilimpa barua na

cheti cha idhini ya kukusanya data gerezani (Taz. Kiambatisho III na IV). Kabla ya utafiti,

mtafiti aliwasiliana na kujitambulisha kwa mkuu wa jimbo la Kisumu. Mkuu wa jimbo alimpa

mtafiti idhini ya kukusanya data kata jimbo la Kisumu (Taz. Kiambatisho II). Hatimaye mtafiti

aliandika barua kwa mkuu wa magereza nchini ili kukusanya data kutoka kwa wafungwa. Idara

ya magereza nchini ilimpa mtafiti idhini ya kuingia katika magereza ya Kisumu na Kibos

kukusanya data.

Kabla ya kukusanya data mtafiti aliwatembelea wakuu wa magereza ya Kodiaga na Kibos na

kuwafafanulia sababu za kufanya utafiti pamoja na kuwaeleza kuhusu vifaa ambavyo angetumia

kukusanya data.

3.10.2 Maadili ya utafiti yanayohusu watafitiwa

Mtafiti alijitambulisha kwa watafitiwa kwa kuwaonyesha kitambulisho chake cha kitaifa na kwa

kuwaonyesha barua kutoka Halmashauri ya Sayansi, Teknolojia na Uvumbuzi iliyompa kibali

cha kufanya utafiti katika magereza ya Kisumu.

Kila siku kabla ya kuwahoji watafitiwa, mtafiti aliwaeleza watafitiwa sababu za kukusanya agoti

na kuwahakikishia kuwa utafiti ule ulikuwa wa kiakademia tu na wala majina yao

Page 58: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

41

hayangechapishwa popote. Mtafiti hakuwalazimisha watafitiwa kushiriki katika utafiti (Taz.

Kiambatisho VI).

3.10.3 Maadili ya utafiti yanayohusu mchakato wa utafiti

Utafiti huu ulizingatia maadili ya utafiti kwa kunukuu kazi za kitaaluma zilizohusiana na mada

ya utafiti. Vilevile, utafiti huu uliweka wazi matokeo ya utafiti na kupendekeza sehemu ambazo

zingeweza kufanyiwa utafiti wa baadaye kuhusiana na mada ya utafiti.

3.11 Hitimisho

Kwenye sura hii ya tatu mtafiti ameelezea njia na mbinu mbalimbali za utafiti alizotumia katika

kukusanya data pamoja na vifaa vilivyotumiwa wakati wa kukusanya na kuchambua data. Mbinu

hizi ndizo zilizomwongoza mtafiti katika kukusanya na kuchanganua data. Katika sura

inayofuata, yaani sura ya nne, data iliyokusanywa kwa kutumia mbinu zilizojadiliwa katika sura

hii itachanganuliwa.

Page 59: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

42

SURA YA NNE

UWASILISHAJI NA UCHANGANUZI WA DATA

4.1 Utangulizi

Lengo la sura hii ni kuwasilisha na kuchambua data iiliyokusanywa kuhusu agoti za wafungwa

katika magereza teule ya jimbo la Kisumu. Kwa mujibu wa Kombo na Tromp (2006) uchambuzi

wa data ni kuchunguza kwa undani data iliyopangwa na kuitolea mahitimisho. Wanasema kuwa

uwasilishaji wa data ni namna ya kupangilia data ili ieleweke vizuri. Data yote ambayo

ilikusanywa kwa njia ya mahojiano ya kimakundi na usaili imewasilishwa na kuchambuliwa kwa

kina katika sura hii.

Mtafiti alitumia data ya msingi. Vartanian (2011) anaeleza kuwa data ya msingi ni ile ambayo

mtafiti ameikusanya kwa kutumia mbinu kama hojaji, vikundi lengwa, uchunzaji au mbinu

nyinginezo. Hii ni data ambayo hutoka moja kwa moja kwa mtafiwa. Mtafiti aliwasilisha

matokeo yake kulingana na madhumuni mahususi ya utafiti huu pamoja na maswali

yaliyoambatana na madhumuni hayo. Mgawanyo huu ulimpa nafasi ya kuchanganua data kwa

urahisi. Baada ya kuwasilisha matokeo, mtafiti aliyajadili moja kwa moja. Sura hii ina sehemu

tano. Sehemu ya kwanza ni utangulizi wa utafiti. Sehemu ya pili inaangazia vikoa maana katika

agoti za wafungwa. Sehemu ya tatu inawasilisha na kuchambua data kuhusiana na mabadiliko ya

kimaana katika agoti za wafungwa. Katika sehemu ya nne mtafiti alishughulikia uundaji wa agoti

za wafungwa. Sehemu ya tano ya utafiti huu ni hitimisho la sura.

Page 60: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

43

4.2 Vikoa maana katika agoti za wafungwa

Semantiki kileksika inajishughulisha na maana ya maneno. Maneno huweza kuchukuliwa

kuashiria vitu katika ulimwengu au katika dhana kutegemea mtazamo mahususi wa semantiki

kileksika. Kwa mujibu wa Mmbwanga (2010) vitengo vya maana katika semantiki kileksika ni

vitengo vya kileksika ambavyo kwavyo msemaji huweza kuongezea kwa mfululizo maishani

pamoja na ujifunzaji wa maneno mapya na maana hayo.

Semantiki kileksika kama kipengele cha Nadharia ya Pragmatiki Leksika ilimsaidia mtafiti

katika kuanisha agoti za wafungwa katika vikoa maana mbalimbali. Maneno yaliyowekwa

katika kikoa kimoja yalikuwa na uhusiano wa kimaana. Dhana ya kikoa maana ya semantiki

ilitumiwa kuweka maneno katika matapo mbalimbali lakini maana ya maneno yalifafanuliwa

kimuktadha.

Uchanganuzi wa data ulidhihirisha vikoa maana mbalimbali vya agoti za wafungwa wa

magereza ya Kisumu. Pallock (2006) anaeleza kuwa misimbo hutumiwa katika tamaduni za

wafungwa ulimwenguni kote na zinaweza kuainishwa katika vikoa mbalimbali tokea vyakula

hadi kwa maafisa wa magereza. Katika utafiti huu agoti za wafungwa zimepangwa katika vikoa

vya: mahusiano ya kimapenzi, marufuku na dawa za kulevya, mambo na shughuli za jela, agoti

zinazorejelea wafungwa, maafisa wa megereza na hatimaye tulichanganua agoti zaidi tulizopewa

na wahojiwa.

Katika utafiti huu ukoa wa maana ulitumika kurejelea mahusiano yanayotokana na seti yoyote ile

ya msamiati na hivyo basi kuwa katika kundi maalum la kimantiki.

Page 61: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

44

4.2.1 Kikoa cha mahusiano ya kimapenzi

Baadhi ya wahojiwa walikiri kuwa palikuwepo na mahusiano ya kimapenzi katika magereza.

Mhojiwa mmoja alieleza kuwa, „Mahusiano hapa jela ni kitu cha kawaida kama vile kuna

marelationships pale nje‟. Yaani, mahusiano hapa gerezani ni jambo la kawaida jinsi yalivyo

mahusiano miongoni mwa raia. Mhojiwa mwingine alishadidia kwa kueleza kuwa „Hiyo ni

kawaida ya life. Hapa ndani mafeelings zetu hazijafungwa. Kwa hivyo mahusiano yapo‟. Yaani

„Hiyo ni kawaida ya maisha. Hapa gerezani hisia zetu hazijafungwa kwa hivyo mahusiano yapo.‟

Hata hivyo mhojiwa huyo alisisitiza kuwa mahusiano hayo ni ya viwango. Kulikuwa na urafiki

wa kawaida na uadui wa kawaida. Wafungwa wengine walihusiana kimapenzi japo ni kinyume

cha sheria za magereza.

Mhojiwa mwingine alisema kuwa, fikra kuhusu usenge unaoendelea gerezani wakati mwingine

hutiliwa chumvi kwa kuwa si kila mfungwa huwa na mahusiano ya kimapenzi. Kuhusiana na

maneno yanayotumiwa kurejelea mahusiano kwenye jela, wahojiwa walifafanua maneno

yafuatayo:

Jedwali 4.01: Agoti zinazohusu mahusiano

Agoti Maana

Mtoto/kijana/mwana/maua Mfungwa anayetekeleza majukumu ya

„mke‟ katika mahusiano ya kimapenzi

gerezani

Mende/ongosh

Mfungwa anayetekeleza majukumu ya

„mwanamume‟ katika mahusiano ya

kimapenzi gerezani

Page 62: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

45

Gundu Kisirani anachokuwa nacho mfungwa baada

ya tendo la ngono

Kutiana Tendo la ngono. Kufirana.

Kukula biskuti Kupiga punyeto

Marufuku

Mfungwa ambaye amekuwa na mahusiano

mengi ya kimapenzi

Malaya Mfungwa anayetoa siri kwa maafisa wa

magereza

Kuchange quarter Watoto au maua wawili wanaposhiriki

katika ngono

Kunyemelea

Mfungwa kumshurutisha mfungwa

mwenzake kushiriki ngono. Ubakaji.

Jedwali 4.01 linaonyesha agoti zinazohusu mahusiano ya kimapenzi gerezani. Kwa sababu

maneno haya yanarejelea masuala ya kimapenzi mtafiti aliongozwa na kipengele cha Semantiki

Kileksika katika kuziweka katika kikoa kimoja cha maana. Maana kuu katika tapo hili ni

mahusiano ya kimapenzi. Chini ya dhana ya mahusiano ya kimapenzi mna leksimu ambazo

zinarejelea hali mbalimbali za mahusiano katika jela.

Neno mende au ongosh linarejelea basha. Mtoto/kijana/mwana/maua ni lekzimu zinazotumiwa

kurejelea yule mfungwa anayetekeleza majukumu ya mwanamke katika mahusiano ya kimapenzi

gerezani. Gundu ni kisirani anachokuwa nacho mfungwa baada ya tendo la ngono. Kuchange

quarter ni hali ambapo wafungwa wawili wanaume ambao hutekeleza majukumu ya kike katika

mahusiano ya kimapenzi wanaposhiriki ngono. Kukula biskuti nako ni kupiga punyeto.

Page 63: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

46

Marufuku ni kama malaya katika Kiswahili sanifu. Agoti hizi zinahusiana kwa sababu zote

zinahusu mahusiano ya kimapenzi.

Leksimu hizi zilidhihirisha moja kati ya mambo mengi machungu katika jela, wafungwa

kunyimwa mahusiano ya kawaida ya kimapenzi. Data ilidhihirisha kuwa kunyimwa huku kwa

mahusiano ya kawaida ya kimapenzi huwaelekeza baadhi ya wafungwa kushiriki katika mapenzi

wenyewe kwa wenyewe ili kuziba pengo hilo. Leksimu nyingi zilipatikana kushadidia

mahusiano haya. Kutiana ni neno ambalo hutumiwa kurejelea hali ya kufirana.

Data ilidhihirisha kuwa kama ilivyo uraiani, mna umalaya gerezani. Mfungwa ambaye ana

mahusiano mengi ya kimapenzi anarejelewa kama marufuku. Mtafiti alipata kuwa hali hii

hutokea mfungwa huyo anapokuwa ni mnyonge sana au hana pesa na inambidi ajihusishe

kimapenzi ili apate baadhi ya mahitaji kama vile dawa za kulevya.

Istilahi hizi zinaelekea kufanana na tafiti zilizofanywa na wanaisimu mbalimbali katika mataifa

tofauti. Hensley n.w. (2003) walipata istilahi anuwai katika kikoa cha mapenzi na mahusiano.

Katika utafiti huu mfungwa mwanamume ambaye katika ushoga hutekeleza majukumu ya

mwanamume huitwa mende. Henseley n.w. (2003) walibaini kuwa huyu huitwa punk. Gohodzi

(2013) naye alipata kuwa mfungwa huyu huitwa Nqondo kule Zimbabwe. Kama katika utafiti

wa Gohodzi msenge hurejelewa kama mwana.

Hata hivyo, tofauti na tafiti za awali, utafiti huu ulipata maneno machache katika kikoa hiki cha

mahusiano na mapenzi. Pengine hali hii ilitokana na ukweli kuwa maafisa waliowalinda wale

wafungwa walisimama karibu sana wakati wa mahojiano na baadhi yao walitega masikio

kusikiza yale tuliyokuwa tukiyazungumzia. Hali hii pia huenda ilitokana na kutoshabikiwa kwa

tendo hili.

Page 64: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

47

Uchache wa istilahi kwenye kikoa hiki unaingiliana na kazi ya Einat & Einat (2000) ambao

walipata kuwa maneno yanayohusiana na ngono ndiyo yaliyokuwa machache mno. Isitoshe,

kutumiwa kwa neno malaya kurejelea msaliti miongoni mwa wafungwa unaingiliana na kazi ya

Einat & Einat (2003) ambao walipata kuwa maneno ambayo awali yalitumika kurejelea ngono

katika muktadha wa jela siku hizi hutumiwa kukashifu baadhi ya matendo mabaya gerezani

kama usaliti wa kutoa siri kwa askari.

4.2.2 Kikoa cha marufuku na dawa za kulevya

Watafitiwa waliombwa kufafanua istilahi zilizohusiana na marufuku pamoja na dawa za kulevya.

Jedwali 4.02: Agoti zinazohusu marufuku na dawa za kulevya

Agoti Maana

Mzigo Marufuku

Charaza Wembe

Redio Simu

Gari/ndechu/waya/mongorio Simu

Ruara Dawa za kupiga chafya

Ndovu Dawa ya kulevya ambayo hutiwa ndani ya

mdomo wa chini

Unga Kokeni

Shetani mwekundu Dawa za wendawazimu ambazo wafungwa

hutumia ili kulewa

Bichi Pombe ambayo imetengezwa na chachu

Tei/wode Pombe

Page 65: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

48

Stimu Kileo chochote

Waya/makuti Kifaa kinachotengezwa na mfungwa na

ambacho hutumiwa kuwasha sigara.

Gwara/ngwara/rwanga Chuma kinachonolewa na kutumiwa kukata

mfungwa mwingine wanapokosana

Boza/widi/godee/bata Bangi

Tinga Kifaa cha kuwasha sigara

Kochipo Bangi iliyochanganywa na kiraiko

Gife/kuku/nogwez Sigara

Buti/mtaro Shimo katikati ya makalio ambamo

marufuku hufichwa

Kinena Sehemu ya mbele ya tupu ya mwanamume

ambamo marufuku hufichwa

Kapiece/kapienga Kijisehemu cha chochote, hasa sigara au

bangi

Tigris Jiko lililotengezwa kistadi na wafungwa

ambalo hutumiwa kupikia ndani ya seli

kinyume na sheria

Jedwali 4.02 linaonyesha maneno katika kikoa cha marufuku. Maana ya jumla ya kikoa hiki ni

marufuku, yaani, vitu ambavyo usimamizi wa jela hauruhusu viwe katika mazingira ya jela.

Chini ya maana hii kuu kuliainishwa mitandao ya leksimu mbalimbali ambazo zilipigwa

Page 66: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

49

marufuku na usimamizi wa magereza. Agoti katika kikoa hiki ni zile zinazorejelea dawa za

kulevya na silaha mbalimbali ambazo wafungwa hutumia katika muktadha wa jela.

Data ilishadidia kauli ya Bondesson (1989) kuwa dawa za kulevya ni uti wa mgongo wa

utamaduni wa jela. Wafungwa hutumia dawa za kulevya ili kupunguza uchungu na utamaushi

wao gerezani. Ilidhihirika kuwa ulimwengu wa jela ni wa dawa za kulevya kutokana na istilahi

nyingi za dawa za kulevya zilizofafanuliwa katika jedwali 4.02.

Data ilidhihirisha kuwa marufuku katika jela yanaweza kuwekwa katika vikoa zaidi vya maana.

Kwa mfano, majina ya dawa za kulevya boza, widi, godee, bata au kochipo ni maneno ambayo

hurejelea bangi. Tei ni pombe na ruara ni dawa za kupiga chafya. Bichi ni pombe ambayo

imetengezwa na chachu. Sigara hurejelewa kama kuku, fegi au gife. Pia pana kikoa cha silaha ;

Waya ni kifaa maalumu kinachotengezwa na mfungwa na ambacho hutumiwa kuwasha sigara.

Kifaa hiki pia huweza kurejelewa kama makuti. Gwara au ngwara ni chuma kinachonolewa na

kutumiwa kumkata mfungwa mwingine wanapokosana. Wembe hurejelewa kama charaza.

Agoti hizi zilizorejelea silaha zilidhihirisha kuwa jamii ya jela imesheheni vita au

mashambuliano ya mara kwa mara miongoni mwa wafungwa.

Uchanganuzi wa data pia ulibaini kuwa maneno yanayohusu dawa za kulevya zaidi yalikopwa

kutoka katika msimbo wa Sheng. Kwa mfano maneno steam, tei na ruara hutumika pia na

vijana katika mawasiliano yao. Hata hivyo, maneno yaliyohusu silaha yalipatikana kuwa

yalibuniwa au yalibadilishwa kwa mfano, neno charaza hutumiwa kurejelea wembe.

Umuhimu wa dawa za kulevya unajitokeza kutokana na istalahi zilizoteuliwa kutumiwa. Kwa

mfano, bangi inarejelewa kwa maneno matano, boza, godee, widi, bata na kochipo. Huenda

uraibu huu unashabikiwa sana kifungoni.

Page 67: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

50

4.2.3 Kikoa cha mambo na shughuli za jela

Katika kikoa hiki wahojiwa walitupa istilahi zifuatazo pamoja na maelezo yaliyoandamanishwa.

Jedwali 4.03: Agoti zinazohusu mambo na shughuli za jela

Agoti (Nomino/Virai Nomino) Maana

Rotiko Korti

Mchwaa Mpesa

Baraza Mkutano wa wafungwa ambao mwenyekiti

wake huwa mfungwa msimamizi wa nyumba

Bukta Suruali ya kulalia

Kunguru Vazi la mfungwa linalovaliwa gerezani

Ugali/maharagwe/ mchele ya pan Chakula spesheli. Hukaangwa vizuri kwa

mafuta ya kutosha

Dondo Maharagwe

Sembe /mbese Ugali

Kibaba Kipimo kinachofanana na kifuniko cha chupa

ya soda ambacho hutumiwa kumpimia

mfungwa mafuta ya kutia kwenye chakula

Breki Viatu vinavyotengezwa kwa gurudumu la gari

na hutumiwa kufunga mlango kwa ndani ili

askari asiweze kuingia kwenye seli

Chepechepe/Chebechebe/mawetete

Chakula spesheli kilichoandaliwa vizuri

Page 68: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

51

Kisuguu Mnara wa ulinzi

Baruti Pilipili inayotiwa kwenye chakula

Mtoto ya laini Mtoto wa askari

Nchi ingine Uraiani

Jela ya kazi Jela ndogo

Jela ya kupumzika Jela kubwa kama gereza la Kamiti, Kibos au

Kodiaga

Randa Kiboko

Neti/ngome/chimano/shamba ya mawe/ nchi

ya saba/Zimbabwe/

Jela

Shamba ng‟aa Shamba linalolimwa gerezani. Neno hili

hutumika tu katika gereza la Kibos

Njugu mawe Mahindi ambayo hayajaoza

Biskuti Mahindi ambayo yameoza

Mpesa Karatasi

Kiswahili Ujanja/uongo

Taukuz Ukuta

Mruru Mkebe ambamo mfungwa huwekewa chakula

Pengle/kipengele Kifuniko cha mruru

Bakuli Kijisahani cha kutia mboga

Dishi Chakula

Frayola Chakula kilichokaangwa

Kijiko Kifaa cha kupima chakula

Page 69: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

52

Skanja Kifaa cha kushikilia chochote kilicho moto

Chedes/chapenda Pesa

Sheria za nyumba Zile sheria wanazozitunga wafungwa

kuwaongoza katika seli zao

Lota Mikebe wanayotumia wafungwa waislamu

kubeba maji wanapokwenda msalani

Ikulu Maeneo mazuri (kona nzuri) kwenye seli

ambamo wafungwa wenye ushawishi au wenye

nguvu hulala.

Dhochi Lugha isiyoeleweka

Bangili/chegere Pingu

Banda Sehemu katikati ya wadi mbili ambamo

wafungwa huota jua

Agoti (Vitenzi/Virai vitenzi) Maana

Kumaliziwa Ile hali ya korti ya mwisho kuhakikisha kifungo

hata baada ya kukata rufaa

Kukwachua Kupata pesa kotoka kwa raia kwa njia za

kilaghai / kutapeli

Kukaa na ndoo Kuketi tu bila kuwa na shughuli yoyote.

Kupitisha wakati

Kuonwa Kutembelewa na watu kutoka uraiani

Tero Wafungwa kufanyiwa upekuzi

Kibitiko Kupigwa kinyama

Page 70: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

53

Kukata Kiswahili/kuongeza Kiswahili Kumsingizia mfungwa ili achapwe.

Kudanganya kwa kutumia ujanja

Kuunganisha propaganda Kumsingizia mfungwa ili achapwe

Kuweka mawe Kuomba msamaha au kufinyilia kitu kibaya

kisijulikane

Kukaba Kuchutama ukisubiri maelekezi

Kuingia block Askari kufanya upekuzi kwenye seli

Tuone ukae

Toa pesa au hongo ndipo uishi vizuri gerezani

kama mfungwa

Kutoboa Kumaliza kifungo

Kutoboa namba Kujifanya kuwa mgonjwa ndipo usifanye kazi

(jela ndogo)

Kuenda Kenya

Kuenda uraiani, kufunguliwa jela, kumaliza

kifungo

Kugenya Kufa

Kuuza mtu Kumtilia mtu ujanja ili apigwe na askari

Kunyeshewa na randa Kupigwa au kuchapwa na askari

Kusaidiwa hosii Kupewa ruhusa ya kuenda hospitalini

Kukula copper Kupigwa risasi

Kuingiza boot/buti Kuficha kitu kwenye njia ya choo

Kukaa kisuguu/kutower Mfungwa kuwachungulia askari ili wenzake

wanaofanya kitu kinyume na sheria za jela

wasipatikane

Page 71: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

54

Semantiki kileksika inajuhusisha na maana ya maneno. Dhana kuu katika kikoa hiki ni shughuli

na mambo mbalimbali ambayo hupatikana katika jela. Leksimu katika kikoa hiki zinahusiana

kwani zinaonyesha jinsi mambo mbalimbali yanavyorejelewa katika jela.

Kikoa hiki kilitenganishwa katika viwango viwili. Kitengo cha kwanza ni Virai Nomino ambapo

mtafiti amefafanua namna vitu mbali mbali hurejelewa na wafungwa. Kikoa hiki kinaweza

kuainishwa katika vikoa zaidi. Palidhihirika maneno yaliyorejelea vyakula; dondo, ugali ya pan,

sembe, mbese, baruti, dishi, frayola. Maneno yaliyorejelea jela au sehemu za jela; kisuguu, jela

ya kazi, jela ya kupumzika, neti, ngome, chimano, shamba ya mawe, ikulu, banda n.k.

Katika kitengo cha pili mtafiti alifafanua virai vitenzi katika lugha ya wafungwa. Hapa alielezea

namna vitendo mbalimbali hurejelewa na wafungwa gerezani. Kwa mfano kukaa kisuguu ni

mfungwa kukaa chonjo akiwachungulia askari ili wenzake wanaofanya kitu kinyume na sheria

ya jela wasipatikane. Kunyeshewa randa humaanisha kupigwa au kuchapwa na askari.

Kusaidiwa hosii nako ni kusaidiwa ruhusa ya kuenda hospitali. Kukula copper ni kupigwa risasi.

Kutoboa ni kumaliza kifungo.

Katika utafiti huu, kikoa hiki ndicho kilichotokea kuwa na agoti nyingi. Hii ni tofauti na maelezo

ya Mulvey (2010) kuwa maeneo yenye istilahi nyingi katika lugha ya wafungwa ni kitengo cha

mahusiano na dawa za kulevya. Hata hivyo mtafiti alikubaliana na Looser (2001) kwamba kama

mfungwa anaponigiliana na mazingira yake mapya anakumbana na mazingira mapya pamoja na

michakato mipya. Lugha yake sharti iunde maneno mapya na kuyapa maana. Anaeleza kuwa

„mwingiliano wa kitawi huhitaji maneno ya kipekee‟. Maneno mengi ya kipekee yanayotumiwa

katika muktadha wa jela yalibainika.

Page 72: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

55

4.2.4 Kikoa cha wafungwa

Wahojiwa waliulizwa kueleza na kufafanua maneno ambayo wao hutumia kuwarejelea

wafungwa wenzao. Istilahi zifuatazo zilipatikana:

Jedwali 4.04: Agoti zinazowarejelea wafungwa

Agoti Maana

Maisha Wafungwa wanaohudumia vifungo vya maisha

Roho geng/roho Wafungwa wanaofanya kazi kwenye maghala

ya jela

Wasanii/wadhii/wanaboma Wafungwa

Warogoti Wafungwa ambao hukusanya mabakuli

Mfungwa staff Mfungwa ambaye ana hadhi katika jela. Si

lazima awe ana cheo. Hadhi hii inaweza

kutokana na mfungwa huyo kuwa na fedha

nyingi

Mwewe Mfungwa mlafi, asiyeshiba. Hana uwezo wa

kununua chakula. Aghalabu umasikini huo

hutokana mfungwa husika kutotembelewa

Nyoka/kanyoz Mfungwa anayependa kutoa siri kwa askari.

Msudi Mfungwa anayependa kutoa siri kwa askari.

Anayepeleka kiswahili kwa wakubwa

Trekta Mfungwa mgeni. Ndiye hufanya kazi sana

Mashujaa Wafungwa ambao wameishi sana gerezani

Page 73: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

56

Mijikumi/wazee wa nyumba Wafungwa ambao hawana cheo lakini wanapata

heshima kutokana na miaka yao. Hasa wa miaka

themanini au zaidi.

Mzee wa mtaa Ana hadhi sawa na ya mijikumi

Mzee wa boma Ni wafungwa ambao wamekaa sana kwenye jela

Kurutu

Mfungwa mpumbavu. Hajui mambo mengi

kwenye jela

Mabuluu / Nguo ya matress

Wafungwa wanaoaminiwa zaidi kwenye jela. Ni

cheo cha juu zaidi wanachopewa wafungwa

wasimamizi

Majani Wafungwa ambao huvaa beji la kijani kibichi.

Kiherehere Mfungwa anayeteuliwa na askari kufanya kazi

fulani ya kiusimamizi. Aghalabu husababisha

wafungwa wengine kuchapwa

Kairo Ni kundi la wafungwa wanaosafisha vyoo

gerezani

Kisuguu Mfungwa anayeketi kuwachunga wafungwa

wengine wasivuke mipaka/ukuta wa jela. Pia

humrejelea mfungwa anayechungulia ili askari

asiwapate wenzake wanaokikuka sheria

Mahuru/sugu Mfungwa mwenye kichwa kigumu ambaye

amezoea kufanya mambo kiyume na sheria za

magereza

Page 74: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

57

Mahuru ya jela

Mfungwa ambaye hata baada ya kufunguliwa

hufungwa tena na tena

Wazuri/malaika Wafungwa wazuri wasioasi

Simu Mfungwa anayewaita wafungwa

wanapotembelewa na wageni kutoka uraiani

Geng‟ Kundi la wafungwa wanaofanya kazi pamoja

Maana kuu katika agoti zilizo kwenye Jedwali 4.04 ni majina ya wafungwa. Chini ya dhana hii

kuu mtafiti alianisha agoti mbalimbali ambazo wafungwa huwarejelea wafungwa wenzao katika

mazingira ya jela. Wafungwa wenyewe hujirejelea kama wasanii, wadhii au wanaboma.

Wafungwa wenye kichwa kigumu hurejelewa kama mahuru. Mahuru ya jela ni wale wafungwa

ambao hata baada ya kufunguliwa hukamatwa na kufungwa tena. Kisuguu ni yule mfungwa

ambaye huketi akiwachunga wafungwa wengine wasivuke mipaka ya jela au wasipatikane na

askari wanapofanya jambo lililo kinyume na sheria za jela. Malaika ni wale wafungwa wazuri

ambao wanachukuliwa kuwa hawafanyi makosa mle gerezani.

Data ilidhihirisha umuhimu wa uaminifu gerezani (Irwin, 1985). Kwa mfano, mfungwa ambaye

anapeleka udaku kwa maafisa hurejelewa kama msudi au nyoka. Inaashiria kuwa, watu kama hao

hawajakubalika miongoni mwa wafungwa wengine. Kikoa hiki pia kilidhihirisha usinonimu wa

hali ya juu ambapo maneno tofauti yanamaanisha kitu kimoja. Kwa mfano, wafungwa

hurejelewa kama wadhii, wasanii au wanaboma.

Wafungwa huwa na majukumu au kazi wanazofanya kwenye jela. Simu ni wafungwa ambao

hufanya kazi ya kuwaita wafungwa wenzao wanapotembelewa na wageni. Kairo ni wafungwa

Page 75: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

58

ambao hufanya kazi ya kusafisha vyoo. Roho ni wafungwa ambao hufanya kazi kwenye maghala

ya jela kwa kubeba na kupanga magunia ya nafaka.

Katika jela, wafungwa huwa na hadhi tofauti kwani wafungwa wenye hadhi ya juu hurejelewa

kwa njia mahususi. Kwa mfano mashujaa ni wafungwa ambao wameishi sana gerezani. Mijikumi

huwa ni wafungwa ambao hawana cheo lakini wanapata heshima kutokana na miaka yao

maishani, hasa wale wa miaka themanini na zaidi. Mzee wa mtaa naye ana hadhi sawa na ya

mijikumi. Mfungwa staff ni yule mfungwa ambaye anafanya shughuli zake kama askari. Chakula

chake ni kizuri na pia mavazi yake ni safi, hapigi foleni ili kupokea chakula.

Ilibainika wazi kuwa pana wafungwa wenye hadhi ya chini na wana njia ya kipekee ambayo

wanarejelewa kwayo. Kwa mfano, trekta ni mfungwa mgeni na ndiye hufanya kazi sana. Kurutu

naye ni mfungwa mpumbavu ambaye hafahamu mambo mengi kwenye jela. Inaweza kufikiwa

hitimisho kuwa wafungwa wana njia zao za kujitambulisha. Wanaweza kujitambulisha kama mtu

binafsi au kama makundi ya wafungwa.

4.2.5 Kikoa cha maafisa wa magereza

Wahojiwa waliulizwa kutaja na kufafanua baadhi ya istilahi ambazo wao hutumia kuwarejelea

maafisa wa magereza. Kama katika agoti zinazorejelea wafungwa, maafisa wa magereza pia

hurejelewa kwa misimbo anuwai. Wahojiwa walifafanua maneno yafuatayo kama ambayo wao

hutumia kuwarejelea maafisa wa magereza.

Jedwali 4.05: Agoti zinazowarejelea maafisa wa magereza

Agoti Maana

Afande/gavaa/sirikali/kraoni/pai Askari wa jela

Page 76: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

59

CPL / uzi mbili Koplo wa magereza

Uzi tatu Sajini wa magereza

Mawe mbili/stone mbee Spekta wa magereza

Mawe tatu/stone tatu Spekta mkuu wa magereza

Mastone Askari walio na vyeo vya juu (zaidi ya

sajini mkuu)

Simba Sajini kambi wa gereza/sajini

mwandamizi

Simba/bigi Askari mkuu msimamizi wa jela

Kurutu Askari ambao wameajiriwa majuzi

Kurutu Askari ambaye amempata mfungwa

kwenye jela fulani. Si lazima awe

ameajiriwa karibuni

Simba kabarasi Askari wanaoogopwa sana na wafungwa,

kutokana na ukali wao

Baba yao Askari wa cheo cha juu zaidi

Malilio Askari anayepokea malalamishi ya askari

na wafungwa.

Afande mwewe Askari mlafi ambaye hula chakula cha

wafungwa

Kwekwe Askari wanaowafanyia askari wenzao

upekuzi ili wasiingize marufuku gerezani

Mzazi Askari mzuri

Page 77: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

60

Dhana kuu katika kikoa hiki ni maafisa wa magereza. Chini ya dhana hii kuu mtafiti alifafanua

agoti mbalimbali. Agoti hizi zilihusiana kimaana kwa sababu zote zilitumiwa kuwarejelea

maafisa wa magereza.

Mifano katika jedwali 4.05 inabainisha wazi kuwa maafisa hurejelewa kwa vyeo vyao kule

kwenye jela. Kulingana na mifano yetu, CPL/uzi mbili ni koplo wa magereza. Uzi tatu

humrejelea sajenti wa magereza. Mawe mbili hutumiwa kumrejelea spekta wa magereza. Mawe

tatu ambayo ni cheo kinachofuata kile cha spekta hutumiwa kumrejelea spekta mkuu wa

magereza.

Wafungwa pia hutumia majukumu ya askari kuwarejelea askari wao. Kwa mfano, askari ambaye

hushughulikia matatizo ya wafungwa yaani welfare officer hurejelewa kama malilio. Kwekwe

nao ni kundi la askari ambao huwafanyia askari wenzao upekuzi ili wasiingize marufuku

gerezani. Wanatafuta marufuku na kuyaondoa kama „kwekwe‟ inavyoondolewa shambani.

Askari hawa wanaogopwa sana na akari wenzao.

Kuna maneno ambayo hudhihirisha uhusiano mbaya uliopo baina ya askari na wafungwa au

mtazamo hasi wa wafungwa kwa askari. Afande mwewe huwa ni askari mlafi ambaye lazima

atue kwenye mali au chakula cha mfungwa. Askari kama hawa hawaheshimiwi na wafungwa.

Bondesson (1989) anaeleza kuwa kutokana na uhusiano mbaya kati ya askari na mfungwa,

wafungwa huunda istalahi ambazo huelekea kuwakejeli maafisa wa magereza. Hata hivyo kuna

wale wa hadhi ya juu kwa mfano baba yao ni askari mwenye cheo cha juu na huheshimiwa na

wafngwa. Simba kabarasi naye ni askari wanaoogopwa sana na wafungwa kutokana na ukali

wao. Maafisa wanaorejelewa hivi huwa wana hadhi kubwa katika jamii ya jela tofauti na wale

wanaorejelewa kama mwewe.

Page 78: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

61

4.2.6 Agoti zaidi

Wahojiwa waliulizwa kufafanua agoti zaidi wanazozifahamu, istilahi zifuatazo zilitolewa.

Jedwali 4.06: Agoti zaidi kutoka kwa wahojiwa

Jina Maana

Matii Godoro

Kuchukua rada Kuchungulia

Mgondii Mfungwa mwizi

Mariam Lori la kuwasafirishia wafungwa

Chapenda Kutoa hongo ili kosa lako lisitolewe

nje/pesa

Kuangusha probox Askari au mfungwa kupatikana na marufuku

akiingiza ndani ya jela

Zimbabwe

Jela. Limepata jina hili kutokana na

kwamba bei ya bidhaa ni juu sana gerezani

Awuori Basi la kuwasafirisha wafungwa

Uchanganuzi wa data ulibaini kuwa istilahi kwenye jedwali 4.06 zingeweza kuwekwa katika

vikoa vile tulivyojadili awali. Kwa mfano, matii yenye maana ya godoro, Zimbabwe kumaanisha

jela, Awuori inayorejelea basi la kuwasafirishia wafungwa tungeziweka katika kikoa cha vifaa na

michakato ya jela. Istilahi mgondii ingewekwa katika kikoa kinachohusiana na maneno

yanayorejelea wafungwa.

Page 79: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

62

Istilahi matii na mgondii ni maneno ambayo wafungwa hutumia gerezani lakini uchambuzi wetu

ulibaini kuwa ni maneno ambayo yamekopwa kutoka msimbo wa Sheng. Ni wazi kuwa katika

mazungumzo ya wafungwa, pana nyakati ambapo wanatumia maneno ambayo hutumiwa na

vijana katika mazungumzo yao. Neno mariam nalo limetolewa katika sajili ya dini. Maria ni

mamake Yesu, „mama wa ulimwengu wote‟. Wafungwa hulirejelea gari lao kama mariam kwa

sababu huwabeba wafungwa wengi mno. Husemwa kuwa gari hilo halijai. Wafungwa

hulazimishwa kujazana humo ndani wanaposafirishwa. Basi la jela lina jina la Awuori. Jina hili

lilitokana na jina la Makamu wa Rais katika serikali ya Kibaki baada ya Hayati Wamalwa. Yeye

ndiye alileta kwa mara ya kwanza matumizi ya mabasi kama mtindo wa usafirishaji wa

wafungwa tofauti na lori (Mariam) ambalo lilitumiwa awali.

Kwa muhtasari, uchanganuzi wa vikoa maana katika agoti za wafungwa ulidhihirisha mahusiano

ya kimaana ya maneno katika kila kikoa. Palikuwepo na dhana au maana kuu na chini ya maana

hiyo agoti mbalimbali ziliweza kuainishwa. Uchambuzi wa vikoa maana ulidhihirisha lugha ya

wafungwa kama kioo cha ulimwengu wa jela. Kikoa maana cha mahusiano ya kimapenzi

kilionyesha uchungu wanaopitia wafungwa kwa kutengwa na wapenzi wao wa jinsia ya kike.

Leksimu nyingi zilipatikana zililizodhihirisha kuwepo kwa ubasha gerezani. Kikoa maana cha

marufuku na dawa za kulevya kilidhihirisha jinsi baadhi wafungwa wanavyoshabikia dawa za

kulevya. Leksimu nyingi zililizojadiliwa katika kikoa hiki zilionyesha kuwepo kwa kiwango

fulani cha matumizi ya dawa za kulevya gerezani na thamani ya juu ya bangi ikilinganishwa na

sigara. Leksimu zilizotumiwa kurejelea silaha mbalimbali zilidhihirisha ulimwengu wa jela kama

ulimwengu uliojaa vita na mashambiliano ya mara kwa mara miongoni mwa wafungwa. Kikoa

maana cha wafungwa kilidhihirisha umuhimu wa uaminifu mingoni mwa wafungwa. Wafungwa

ambao si waaminifu kwa wafungwa wenzao walipewa majina ya kuwadunisha. Leksimu katika

Page 80: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

63

kikoa hiki pia zilidhihirisha ngazi za kiutawala miongoni mwa wafungwa. Hatimaye, kikoa

maana cha maafisa wa magereza kilionyesha mahusiano kati ya wafungwa na askari.

Kulijadiliwa baadhi ya leksimu zilizoonyesha mahusiano mabaya yaliokuwepo kati ya wafungwa

na askari. Agoti zingine pia zilionyesha kuwa kulikuweko na askari ambao waliheshimiwa sana

na wafungwa.

4.3 Mabadiliko ya maana

Lengo la pili la utafiti huu lililikuwa kufafanua mabadiliko ya kimaana yanayojitokeza katika

agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu. Uchanganuzi wa data ulizingatia

Nadharia ya Pragmatiki Leksika iliyoasisiwa na Blutner katika miaka ya 1990. Blutner (2011)

akimrejelea Wilson (2003), anafafanua masuala ya kimsingi ambayo yanashughulikiwa katika

Nadharia ya Pragmatiki Leksika kama; kubanika kwa neno, kupanuka kwa neno na kukisia neno.

Utafiti huu ulitumia michakato hii ya kiprakmatiki leksika katika kufafanua mabadiliko ya

kimaana yaliyojitokeza katika agoti zilizotumiwa na wafungwa. Michakato hii ya kipragmatiki

leksika hutekeleza majukumu maalumu kwani kila mojawapo humwezesha msikilizaji kufasiri

semi kwa njia tofauti na ule ufasiri wa kisemantiki. Utafiti huu uljikita katika aina mbalimbali za

mabadiliko ya kimaana ambapo upanuzi wa kileksika hujidhihirisha kwa njia anuwai.

4.3.1 Ubanaji wa kileksia

Mchakato wa kwanza wa kipragmatiki leksika ni ubanaji wa kileksika. Kwa mujibu wa Wilson

(2003) hii ni hali ambapo neno linatumiwa kuonyesha fahiwa mahususi zaidi kuliko ile

iliyosimbwa. Husababisha kutokea kwa maana finyu zaidi ya ile ya kileksia. Uchanganuzi wa

matini ulibaini leksimu zifuatazo ambazo zilipitia mchakato huu wa ubanaji wa kimaana.

Page 81: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

64

Jedwali 4.07: Agoti zilizobanika kimaana

Agoti Maana ya kisemantiki Maana mahusisi gerezani

Afande Jina la heshima ambalo askari

humwita mkubwa wake

Askari wa jela

Pai Polisi Askari wa jela

Kutia Fanya kitu kiwemo ndani ya

kingine

Kushiriki ngono

Marufuku Jambo lilokatazwa kufanyika Vitu vilivyokatazwa visiingizwe

gerezani

Kunyemelea Endea kitu kimya na polepole Kunajisi

Mzigo Kitu kizito kilichobebwa Marufuku

Unga Chochote kilichosagwa na

kuwa kama vumbivumbi

Kokeni

Kunguru Kitambaa chenye michoro ya

vyumba vyenye umbo la

mraba

Vazi la mfungwa

Baraza Mkusanyiko wa watu kwa

ajili ya mazungumzo

Mkutano unaoongozwa na mkuu

wa nyumba gerezani

Serikali Chombo chenye mamlaka ya

kuendesha utawala wa nchi

Askri au usimamizi wa jela

Kraoni Askari Askari wa jela

Tuone Tambua kitu kwa macho Kuona mfungwa ili utoe hongo

Page 82: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

65

Kumaliziwa Kufikiwa na hatua ya mwisho Kuhakikishiwa kifungo na korti

Kuonwa Kutambuliwa kwa macho Kutembelewa gerezani

Kutoboa Kufanya kuwa tundu Kumaliza kifungo

Wadhii Watu Wafungwa

Warogoti Watu wanaookota Wanaokusanya bakuli

Jedwali 4.07 linaonyesha leksimu ambazo zimepitia mchakato wa ubaniji wa maana. Neno

afande limesimba dhana AFANDE ambayo imejumuisha aina mbalimbali za askari katika taifa

la Kenya. Kwenye diskosi hii, tunachukulia kuwa, anayesikiliza anaposikia neno afande, tayari

ana maarifa mapana kuhusiana na afande. Hivyo, inambidi msikilizaji kutafuta njia rahisi ya

kumfanya kuelewa dhana inayowasilishwa na neno afande. Kupitia maarifa yake kuhusu neno

afande, anafanya ubanaji na kufikia maana mahususi inayowasilishwa. Msikilizaji ana maarifa

kuwa afande anaweza kuwa polisi wa utawala, askari wa kulinda misitu au hata mwanajeshi.

Blutner (1998) anafafanua kuwa ubanaji una maana ya kutumia faridi leksika katika kupitisha

ufasiri uliobanwa zaidi ya ule uliosimbwa kisemantiki. Kisemantiki, afande ni jina la heshima la

kumrejelea askari yeyote aliye mkuu (TUKI, 2013). Mtafiti alichukulia kwamba, maana hii

ndiyo iliyosimbwa kisemantiki. Maana hii pana inajumuisha aina mbambali za askari. Katika

muktadha wa jela, neno afande linabanwa kumrejela askari wa jela tu.

Neno pai limekopwa toka msimbo wa Sheng na hurejelea polisi. Kisemantiki, polisi ni askari

mwenye dhamana ya kuona kuwa sheria na usalama wa nchi hauvunjwi (TUKI, 2013). Inambidi

msikilizaji kufanya ubanaji wa maana pana ya neno pai ili afikie ile dhana inayowasilishwa. Pai

kama ilivyo katika afande inaweza kutumiwa kumrejelea askari yeyote. Lakini katika muktadha

wa jela mfungwa akitumia neno pai atakuwa amelibana kurejelea askari wa jela tu na si kitengo

Page 83: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

66

kingine cha askari. Mchakato huu ni sawa kwa ubanaji unaotokea katika leksimu kraoni kama

ilivyofafanuliwa kwenye jedwali.

Neno kutia kisemantiki ni kufanya kitu kiwemo ndani ya kingine (TUKI, 2013). Katika

muktadha wa jela, neno hili linabanwa kimaana ili kumaanisha ubasha au usenge. Kisemantiki,

kutia kunaweza kuwa kwingi; kutia nguo kwenye begi, kutia kalamu kwenye mfuko, kutia gari

kwenye mtaro n.k. lakini katika diskosi hii, kutia si kwingine bali ni kutia tupu katika njia ya

choo. Yaani, dhana ya kutia katika jela ni mahususi zaidi.

Leksimu marufuku kisemantiki inarejelea jambo ambalo limekatazwa kufanyika (TUKI, 2013).

Ni jambo au kitu chochote ambacho hakiruhusiwi kufanyika. Katika muktadha wa jela, inambidi

msikilizaji kufanya ubanaji wa maana pana ya neno marufuku ili kufikia dhana ambayo

inawasilishwa. Katika muktadha wa jela, marufuku haya ni yale mambo ambayo yamekatazwa tu

katika muktadha wa jela kama vile sigara au pombe. Marufuku katika muktadha wa jela ni ya

kipekee na hayajumuishi marufuku katika miktadha ya uraiani. Hivyo, maana ya marufuku

inabanwa ili kusawiri maana mahususi katika muktadha wa jela.

Maana ya kunyemelea katika kamusi ni kuendea kitu polepole na kimyakimya (TUKI, 2013).

Matumizi ya neno hili yanamhitaji msikilizaji katika muktadha wa jela afanye ubanaji wa maana

hii pana ya kunyemelea ili kufikia ukamilifu wa dhana inayopitishwa. Kunyemelea kwaweza

kuwa kwingi katika welewa wa kawaida wa neno hili. Kunyemelea ili kuona, kunyemelea kuua,

kunyemelea kushika, kunyemelea kuchunguza. Msikilizaji anaunda dhana za dharura kuhusu

njia na aina mbalimbali za kunyemelea. Anavuta maarifa yake kuhusu njia mbalimbali za

kunyemelea. Katika muktadha wa jela anafikia dhana mahususi zaidi ya kunajisi. Maana hii ni

finyu ikilinganishwa na maana pana ya kunyemelea.

Page 84: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

67

Maana ya kawaida ya neno mzigo ni kitu kizito kilichobebwa (TUKI, 2013). Maana hii ni pana

kwani inajumlisha mizigo tofauti tofauti ambayo inaweza kuwepo. Mizigo katika kichwa, mizigo

katika gari, mizigo ya dhambi, mizigo ya shida katika maisha n.k. Katika muktadha wa jela,

maana ya mzigo inabanwa kurejelea marufuku. Yaani, mizigo ni yale mambo ambayo usimamizi

wa jela umekataa kuwa hayaruhusuwi kuingizwa gerezani kama vile pombe au sigara. Maana hii

inaelekea kuwa finyu zaidi ya ile maana ya kisemantiki ambayo inajumlisha mizigo yoyote ile.

Kisemantiki neno unga lina maana ya kitu kilichosagwa na kuwa vumbivumbi (Mdee, Njogu na

Shafi, 2011). Maana hii ni pana katika muktadha wa kawaida. Neno unga linajumlisha vitu vingi

vya ungaunga, unga wa mahindi, unga wa wimbi n.k. Katika diskosi hii, maana ya unga

inabanwa na kuwa kokeni, dawa ya kulevya ambayo ni ungaunga. Mfungwa anaposikia neno

unga, anaibana kupata maana yake katika muktadha wa jela na moja kwa moja anafahamu kuwa

ni kokeni wala si aina nyingine ya unga.

Neno baraza kawaida hurejelea kundi la watu kwa majukumu maalumu, mkusanyiko wa watu

wengi kwa ajili ya kuwa na mjadala fulani au mazungumzo ya kawaida, mahali ambapo kesi

husikilizwa au kitala (Mdee n.w., 2011). Maana hii ni pana sana. Katika muktadha wa jela

baraza hurejelea mkutano wa wafungwa unaoongozwa na mkuu wa nyumba ili kuzungumzia

masuala mbalimbali yanayowahusu wafungwa kwenye seli zao. Maana hii imebanwa

ikilinganishwa na maana pana ya leksimu hii katika miktadha iliyo nje ya magereza ya Kisumu.

Maana ya kisemantiki ya neno serikali ni chombo chenye mamlaka ya kuendesha utawala wa

nchi (TUKI, 2013). Maana hii ni pana kwani inarejelea chombo cha utawala wa taifa zima

ambalo aghalabu huongozwa na rais. Katika diskosi hii, maana ya neno serikali inabanwa

kumaanisha askari wa jela au usimamizi wa jela. Jela ni chombo cha serikali kinachotumiwa

Page 85: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

68

katika kurekebisha tabia. Hivyo basi katika muktadha wa jela, askari au usimamizi wa jela

unaporejelewa kama serikali, maana hii itakuwa imebanwa katika kurejelea kitu kilicho finyu

zaidi ya hali yake ya kawaida.

Kisemantiki kuona ni kutazama kitu kwa kutumia macho, lola. Pia ni kupata fahamu ya kitu

kupitia hisi za mwili (Mdee n.w., 2011). Maana hii ni pana kwani ni kutumia macho kutazama

chochote kile. Katika muktadha wa jela, maana ya neno hili inabanwa na kusalia kumaanisha

kumwona mfungwa na kutoa hongo. Inatoka katika kutazama chochote kile hadi katika

kumwona mfungwa fulani na kutoa hongo pengine ili kitendo kiovu alichofanya mfungwa

kisiwafikie askari.

Kisemantiki, kumaliziwa huwa na maana ya kufikiwa kwa hatua ya mwisho. Yaani kuishiwa.

Maana hii ni pana zaidi kwani kunaweza kuwa kuishiwa na mali, kuishiwa na matumaini, au

kuishiwa na nguvu. Katika diskosi hii, mfungwa anapomwambia mwenzake amemaliziwa huwa

ana maana ya kuwa ameishiwa na hatua zote za kufanya ili aweze kutoka jela kwa njia za

kisheria. Ni korti ya rufaa kufikia uamuzi kuwa mfungwa atabaki kuwa gerezani. Maana hii

inajitokeza kuwa finyu zaidi ya maana ile pana.

Kuonwa ni kutambuliwa kwa macho (TUKI, 2013). Maana hii ni pana kwani inajumuisha

utazamaji wowote ule na mtazamaji yeyote yule. Hii ndiyo maana ya kisemantiki ambayo

hupatikana katika kamusi ya Kiswahili. Katika muktadha wa jela hata hivyo maana hii inajibana

katika kuonwa na mgeni kutoka uraiani. Mfungwa anapotembelewa na mgeni hurejelewa kuwa

ameonwa. Hivyo basi maana ya neno kuonwa inabanwa na kuwa mfungwa kuonwa na mgeni

katika chumba cha mazungumzo. Maana hii ni finyu kwani inafungia uonaji mwingine nje ya

maana hii mahususi.

Page 86: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

69

Wadhii ni leksimu ambayo imekopwa kutoka msimbo wa Sheng. Neno hili hutumiwa kurejelea

watu. Maana hii ni pana kwani inarejelea mtu yeyote yule. Katika muktadha wa utafiti huu,

wadhii hutumiwa tu kurejelea wafungwa. Maana ya neno wadhii inabanwa na kusalia tu

kumaanisha watu ambao ni wafungwa na wala si kundi jingine lolote la watu. Maana hii ni finyu

zaidi ya maana halisi ya neno hili.

4.3.2 Upanuzi wa kileksia

Mchakato wa pili wa kileksika katika Nadharia ya Pragmatiki Leksika ni upanuzi wa kimaana.

Kwa mujibu wa Fromkin na Rodman (1993) upanuzi wa kileksika ni mchakato ambao kwao

maana ya neno hupanuka. Neno linamaanisha kila kitu kilichokuwa kikimaanishwa na kuzidisha

maana nyingine. Mtafiti aliongezea maelezo haya na kusema kuwa neno linapopanuka kimaana

huwa limeongezewa vitajwa na kujumuisha vitajwa vingine. Ullmann (1970) anafafanua kuwa

maneno yanapewa maana moja bunifu au zaidi bila ya maana asilia kupotea. Ile maana asilia na

maana ya pili zinaishi upande-upande bora tu kusiwepo na mkinzano. Uchambuzi wa data

ulibaini leksimu zifuatazo ambazo zilipitia upanuzi wa kimaana katika muktadha wa jela.

Jedwali 4.08: Agoti zilizopanuka kimaana

Agoti Maana ya kisemantiki Maana ya ziada

Mtoto Kiumbe anayezaliwa hasa na mtu au

mnyama

Anayetekeleza majukumu ya

mwanamke katika mahusiano ya

kimapenzi

Charaza Piga kwa mfululizo Wembe

Gari Chombo cha kusafiri kiendacho kwa

magurudumu

Bangi

Page 87: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

70

Kuku Ndege anayefugwa na anafanana sana na

kware mkubwa

Sigara

Buti Sehemu maalumu ya kuweka mizigo

ambayo aghalabu iko upande wa nyuma

ya gari

Njia ya choo mwilini

Randa Kifaa cha seremala chenye kusawazisha

mbao

Kiboko

Njugu mawe Mmea wa jamii ya fiwi unaozaa punje

ngumu mviringo

Mahindi ambayo hayajaoza.

Mahindi magumu

Kiswahili Lugha ya kibantu yenye asili ya

mwambao wa pwani ya Afrika mashariki.

Ujanja au ukora

Kisuguu Asili yake ni kichuguu yenye maana ya

mwinuko wa ardhi

Mfungwa anayechungulia askari.

Pia ni mnara wa ulinzi

Bangili Pambo la mviringo lililotengenezwa kwa

madini

Pingu

Majani Sehemu ya mmea yenye rangi ya kijani

ambayo huota kwenye matawi

Wafungwa ambao huvaa beji la

kijani kibichi. Ni wafungwa

wasimamizi.

Kairo Mji mkuu wa Misri Wafungwa wanaosafisha vyoo

vya jela

Kurutu Askari mwanafunzi ambaye bado

hajahitimu

Askari mgeni katika jela. Pia

huwa na maana ya mfungwa

Page 88: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

71

Jedwali hili linaonyesha upanuzi wa maana unavyojitokeza katika agoti za wafungwa wa

magereza ya Kisumu. Kama tulivyoeleza awali, kupanuka kwa neno ni mchakato wa kufasiri

ujumbe ambapo maana ya neno inapanuka zaidi ya inavyotumika katika hali ya kawaida. Maana

ya kileksika ya neno mtoto ni kiumbe anayezaliwa hasa na mtu au mnyama (TUKI, 2013).

Katika muktadha wa jela maana ya neno hili inapanuliwa kurejelea mfungwa basha

anayetekeleza majukumu ya mwanamke katika mahusiano ya kimapenzi. Hivyo basi, neno mtoto

limeongeza vitajwa vingine katika maelezo ya maana yake. Ullman (1970) anasema kuwa,

maneno huweza kupewa maana moja ya ziada bila kupoteza ile maana yake asilia.

Kitenzi charaza katika muktadha wa kawaida hurejelea kupiga kwa mfululizo. Katika muktadha

wa jela kitenzi hiki kinatumiwa kurejelea nomino, wembe. Maana ya neno hili imepanuka na

kuongeza maana ya ziada kimuktadha. Hali hii inajitokeza kwa sababu wakati mwingine wembe

mjinga.

Redio Chombo kinachopokea mawimbi ya sauti

k.v. ya mtangazaji, kupitia hewani na

kumwezesha mtu mwingine kusikia

kinachotangazwa

Simu

Ndovu Mnyama mkubwa wa nchi kavu mwenye

masikio makubwa na mapana, mkonga na

pembe mbili mdomoni

Dawa ya kulevya ambayo hutiwa

ndani ya mdomo wa chini

Kwekwe Mmea unaoota mahali usipotakiwa Askari wanaowafanyia askari

wenzao upekuzi ili wasiingize

marufuku gerezani

Page 89: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

72

hutumika kama silaha. Ili kuficha maana yake ya kawaida, kitenzi charaza kinatumiwa ili askari

asiweze kufahamu mawasiliano baina ya wafungwa wanapozungumzia silaha.

Leksimu gari katika Kiswahili hurejelea chombo cha kusafiri kiendacho kwa magurudumu

(TUKI, 2013). Katika jela, maana ya neno hili inapanuliwa na kutumiwa kurejelea bangi.

Hapana uhusiano wa kisemantiki kati ya neno gari na bangi. Hata hivyo, kwa sababu gari

huchukuliwa kuwa chombo cha thamani kama ilivyo bangi katika jela maana ya neno hili

inapanuliwa kurejelea bangi ili kusimba dhana inayorejelewa.

Neno kuku katika muktadha wa kawaida hurejelea ndege anayefugwa na anafanana sana na

kware mkubwa (TUKI, 2013). Maana ya neno hili inapanuliwa kusimba dhana ya sigara. Kuku

hutumiwa kurejelea sigara kwa sababu ni marufuku isiyokuwa na thamani sana ikilinganishwa

na bangi ambayo hurejelewa kama bata. Kuku ni nyepesi kwa mizani na bei yake sokoni ni ya

chini ikilinganishwa na bata. Sigara pia bei yake iko chini ikilinganishwa na bangi katika „soko

la jela‟.

Upanuzi wa maana pia unadhihirika katika leksimu buti. Maana ya kileksika ya neno hili ni

sehemu maalumu ya kuweka mizigo ambayo aghalabu iko upande wa nyuma wa gari (Mdee

n.w., 2015). Katika muktadha wa jela maana ya neno hili inatanuliwa kurejelea njia ya choo

kwenye mwili wa mfungwa. Sehemu hii hurejelewa kama buti kwa sababu baadhi ya wafungwa

huficha marufuku kama vile bangi, sigara au hata pesa kwenye makalio yao. Kama ambavyo buti

ya gari hubeba mizigo ndivyo buti katika muktadha wa jela hutumiwa kubeba na kuficha

marufuku.

Katika mazungumzo ya kawaida, leksimu randa ni kifaa cha seremala ambacho hutumiwa

kusawazishia mbao (TUKI, 2013). Katika diskosi ya jela, maana ya randa inapanuliwa kurejelea

Page 90: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

73

viboko. Upanuzi huu unatokea kwa sababu jinsi randa inavyosawazisha mbao ndivyo viboko

vinavyotumiwa kuwasawazisha wafungwa ambao wamekataa kufuata sheria na masharti ya

magereza. Hivyo basi, maana ya kwanza ya randa pamoja na maana hii ya pili hutumiwa katika

jela.

Maana ya kikamusi ya neno Kiswahili ni lugha ya kibantu yenye asili ya mwambao wa pwani ya

Afrika Mashariki TUKI (2013). Katika muktadha wa jela, neno hili linapitia mchakato wa

upanuzi wa kimaana na kutumiwa kurejelea ujanja. Mfungwa au askari ambaye ni mjanja au ana

ukora mwingi hurejelewa kama mswahili. Uswahili ni ujuaji. Hivyo basi, maana ya neno hili

ambalo hutumiwa kurejelea lugha ya Waswahili inatumiwa kurejelea ujanja, ukora au uongo

katika muktadha wa jela.

Leksimu kisuguu imekopwa toka neno la Kiswahili kichuguu. Baada ya neno hili kukopwa

linafanyiwa mabadiliko ya kimuundo na kisha kutumiwa katika muktadha wa jela. Maana

kileksia ya neno kichuguu ni mwinuko wa ardhi. Neno hili katika muktadha wa jela linapata

fahiwa mbili za ziada. Kwanza, kibanda kwenye jela ambamo askari huketi kuchunga wafungwa.

Pili, mfungwa anayeketi kuchungulia askari anapokuja ili wafungwa wenzake wasipatikane.

Bangili ni neno ambalo hutumiwa kawaida kurejelea pambo la mviringo lililotengenezwa kwa

madini na huvaliwa na wanawake mikononi (TUKI, 2013). Katika muktadha wa jela neno hili

hupata upanuzi wa maana na kutumiwa kurejelea pingu ambazo hutumiwa kuwafunga wafungwa

mikono.

Leksimu Kairo hutumiwa kawaida kurejelea mji mkuu wa Misri. Katika muktadha wa jela, neno

hili hutumiwa kurejelea wale wafungwa ambao jukumu lao gerezani ni kuosha na kusafisha

vyoo. Wafungwa hawa hurejelewa kama kairo au geng ya kairo. Hapana uhusiano wa

Page 91: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

74

kisemantiki kati ya mji wa Misri na wafungwa wanaosafisha vyoo. Hii inatuelekeza katika

kufikia uamuzi kuwa neno hili limepata upanuzi wa maana na kupata fahiwa bunifu ya ziada

ambayo neno hili halikuwa nalo (katika muktadha wa kawaida).

Katika mazungumzo ya kawaida, kurutu ni askari mwanafunzi ambaye bado hajahitimu (TUKI,

2013). Katika muktadha wa jela, neno hili linapanuliwa na kutumiwa kurejelea askari yeyote

ambaye ni mgeni katika gereza husika. Neno hili pia wakati mwingine hutumiwa kimatusi

kumdhihaki mfungwa anayetenda jambo la kijinga. Hivyo basi, maana ya neno kurutu

imepanuliwa na kujumuisha maana ambazo awali haikuwa nayo.

Maana ya kileksia ya neno redio ni chombo kinachopokea mawimbi ya sauti k.v. ya mtangazaji,

kupitia hewani na kumwezesha mtu mwingine kusikia kinachotangazwa (TUKI, 2013). Hii

ndiyo maana ya kawaida inayojulikana na mtu yeyote yule. Katika muktadha wa jela, maana ya

neno hili inapanuliwa na kutumiwa pia kumaanisha simu. Upanuzi huu wa maana unajitokeza

kwa dhima ya kusababisha ufumbaji. Wafungwa hutaka kuzungumza mambo kuhusu simu bila

maafisa wa magereza kufahamu. Hivyo basi wanatanua maana ya kawaida ya redio na kuitumia

kurejelea simu.

Ndovu kileksia ni mnyama mkubwa wa nchi kavu mwenye masikio makubwa na mapana,

mkonga na pembe mbili mdomoni. Hii ndiyo maana kawaida inayojulikana na mjuzi wa lugha

ya Kiswahili. Hata hivyo, maana ya neno hili inatanuliwa katika muktadha wa jela na kurejelea

dawa ya kulevya ambayo hutiwa ndani ya mdomo wa chini.

Hatimaye upanuzi wa kisemantiki unajitokeza katika leksimu kwekwe. Maana ya kisemantiki ya

neno hili ni mmea unaoota mahali usipotakiwa (Mdee n.w., 2011). Katika muktadha wa jela,

maana ya neno hili inatanuliwa na kutumiwa kurejelea askari wanaowafanyia askari wenzao

Page 92: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

75

upekuzi ili wasiingize marufuku gerezani. Kisemantiki, hapana uhusiano kati ya kwekwe, mmea,

na askari wa jela, binadamu. Hata hivyo, kwa sababu askari hawa hufanya kazi ya kutafuta

kwekwe ambayo huenda askari wengine wakaingiza ndani ya jela, neno hili linatumiwa

kuwarejelea maafisa hawa na hivyo leksimu hii kupata upanuzi wa maana yake.

4.3.2.1 Upanuzi wa kisitiari

Simiyu (2016) anaeleza kuwa upanuzi wa kisitiari ni mchakato ambao kwao maana ya neno ipo

mbali na maana wazi. Yaani, maana ya neno fulani katika muktadha wa mazungumzo ni tofauti

kabisa na maana ya neno hilo kiisimu. Mtafiti anaongeza na kusema kuwa katika upanuzi wa

kisitiari, maana ya neno huwa mbali na maana halisi kwa kuhamisha maana ya neno hilo toka

kwa kiashiria kimoja hadi kiashiria kingine. Uchambuzi wa data ulibaini leksimu zifuatazo

ambazo zilipitia upanuzi wa kisitiari

Jedwali 4.09: Agoti zilipanuka kisitiari

Agoti Maana ya kisemantiki Maana iliyopanuliwa

Mtoto Kiumbe anayezaliwa hasa na mtu au

mnyama

Shoga anayetekeleza majukumu

ya mwanamke katika mahusiano

ya kimapenzi

Mwana Kiumbe aliyezaliwa na binadamu au

mnyama

Shoga anayetekeleza majukumu

ya mwanamke katika mahusiano

ya kimapenzi

Maua Sehemu ya mmea inayochanua Shoga anayetekeleza majukumu

ya mwanamke katika mahusiano

ya kimapenzi

Page 93: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

76

Mende Mdudu Shoga anayetekeleza majukumu

ya mume katika mahusiano ya

kimapenzi

Kijana Mtu ambaye si mzee wala si mtoto Shoga anayetekeleza majukumu

ya mwanamke katika mahusiano

ya kimapenzi

Malaya Mwanamke au mwanamume mwenye

tabia ya uzinzi

Mfungwa anayetoa siri za

wafunwa kwa askari

Kuku Ndege anayefugwa na anafanana sana na

kware mkubwa

Sigara

Bata Ndege wa porini au anayefugwa,

mkubwa kuliko kuku

Bangi

Baruti Unga wa kijivujivu unaolipuka Pilipili

Neti Kitambaa kinachoning‟inizwa kitandani

kukinga mbu

Jela

Roho Kitu kisichoonekana ambacho hufikiriwa

kuwa ni sehemu ya mwili ya kiumbe

ambayo hukiwezesha kuwa hai

Wafungwa wanaofanya kazi

ghalani

Nguo ya mattres Vazi la godoro Wafungwa wa cheo cha juu

zaidi.

Malaika Kiumbe asiyeonekana na ambaye

hudaiwa kuwa mtumishi wa Mungu

Wafungwa wazuri

Simba Mnyama mkubwa wa porini wa jamii ya Askari mkuu zaidi katika jela

Page 94: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

77

paka mwenye manyoya ya rangi ya

majani makavu na ambaye hula nyama

Mtaro Mfereji mpana wa kupitisha bomba la

maji

Njia ya choo kwenye mwili wa

mfungwa

Mzazi Mama au baba mtu Askari wazuri

Mwewe Ndege mkubwa anayefanana na tai

ambaye hukamata vifaranga wa kuku

Mfungwa au askari mlafi

Nyoka Mnyama mrefu na mwembamba mwenye

magamba asiye na miguu, anayetambaa

na hutaga mayai

Mfungwa ambaye hutoa siri kwa

askari

Dhana iliyosimbwa na neno mtoto ni MTOTO. Msikilizaji anaposikia neno hili anaunda dhana

za dharura kama vile mtoto ni kitu kinachopachikwa kwenye kitu kingine, kiumbe anayezaliwa

hasa na mtu au mnyama au mtoto ni kidoa cheupe kinachomea ndani ya mboni ya jicho (TUKI,

2013). Katika muktadha wa jela, dhana hizi ni wazi na haziwezi kuwa ndizo zinazowasilishwa na

neno mtoto. Katika jela neno mtoto linatumiwa kurejelea mfungwa shoga ambaye hutekeleza

majukumu ya kike katika mahusiano ya kimapenzi. Dhana hii imejitenga kutoka kwa maana

wazi ya neno hili mtoto. Kwa mujibu wa Bloomfield (1933), upanuzi wa kisitiari hutumiwa ili

kuficha ujumbe unaowasilishwa. Kwa kuwa mtoto wa binadamu huwa dhaifu na huhitaji malezi

vivyo hivyo mfungwa shoga (anayekuwa kama kike) huhitaji malezi na ulinzi kutoka kwa

mpenzi wake wa kiume. Hivyo basi, sifa hii ya mtoto inahawilishwa hadi kwa mrejelewa

(mfungwa shoga anayetekeleza majukumu ya kike kimapenzi).

Page 95: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

78

Maelezo kuhusu leksimu mwana ni sawa na yale ya mtoto. Maana ya kawaida ya mwana ni

kiumbe aliyezaliwa na binadamu au mnyama (TUKI, 2013). Maana hii ni tofauti kabisa na

maana ya leksimu hii katika muktadha wa jela. Katika jela mwana ni mfungwa shoga

anayetekeleza majukumu ya mwanamke katika mahusiano ya kimapenzi gerezani. Haya ni

mambo mawili tofauti. Hata hivyo, mwana ana sifa ambayo inamfanya kuhusishwa na mfungwa

shoga. Mwana huhitaji malezi kama alivyo mfungwa huyu shoga anayetekeleza majukumu ya

kike. Mtafiti anakubaliana na maelezo ya Aitchison (2003) kuwa kwenye sampuli ya kiasili, vitu

ambavyo vinafananishwa vinaweza kutofautiana, kwa mfano; kwa kutokana na vikoa vya

kisemantiki tofauti. Pia vinaweza kufanana hivi kwamba vinashiriki katika baadhi ya sifa za

kawaida.

Kisemantiki, maua ni sehemu ya mmea inayochanua (TUKI, 2001). Ni sehemu ambayo

hupendeza macho. Katika muktadha wa jela, maana hii inapanuliwa kurejelea mfungwa shoga

anayetekeleza majukumu ya kike kimapenzi. Hizi ni maana mbili tofauti kabisa. Upande mmoja

maua ni sehemu ya mmea, upande mwingine (katika muktadha) maua ni binadamu. Mfungwa

shoga anayetekeleza majukumu ya kike anarejelewa hivi kwa kuwa ana sifa fulani inayomfanya

kuwa mauamaua. Kwanza, kama maua, wengi wa wafungwa kama hawa huwa wana miili

myororo au laini kama ya wanawake na hivyo kutamanika na wafungwa wenzao. Pia, wana sifa

ya kimaua hivi kwamba wanaweza kunyauka. Mahusiano ya kimapenzi gerezani aghalabu

hayadumu kwa muda mrefu. Inategemea nani ana pesa zaidi au nani mwenye nguvu zaidi.

Leksimu malaya kwa maana ya kawaida ni mwanamke au mwanamume ambaye ana tabia ya

uzinzi (TUKI, 2013). Maana hii ni tofauti kabisa na maana ya neno hili katika muktadha wa jela.

Gerezani, malaya ni mfungwa ambaye ana tabia ya kutoboa siri za wafungwa wenzake kwa

maafisa wa magereza. Tabia ya malaya kawaida huonekana kama usaliti. Sifa hii ya usaliti wa

Page 96: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

79

malaya ndio inayoelekeza upanuzi wa neno hili katika muktadha wa jela hadi kurejelea mfungwa

msaliti anayetoa siri kwa askari.

Kisemantiki, kuku ni ndege anayefugwa na anafanana sana na kware mkubwa (TUKI, 2013).

Katika muktadha wa jela kuku inapanuliwa kurejelea sigara. Upanuzi huu wa kisitiari unafanywa

ili kusimba dhana inayowasilishwa kwa kuwa sigara ni marufuku katika jela. Hivyo basi

wafungwa wanatumia leksimu kuku kusimba dhana ya SIGARA. Bei ya kuku sokoni huwa chini

ikilinganishwa na bei ya bata, vivyo hivyo sigara ni marufuku yenye thamani ya chini katika jela

ikilinganishwa na bangi inayorejelewa kama bata. Inambidi msikilizaji katika muktadha wa jela

kuhawilisha sifa hii ya thamani ya chini ya kuku hadi katika thamani ya chini ya sigara kama

kitu marufuku katika jela.

Kisemantiki, baruti hurejelea unga wa kijivujivu unaolipuka (TUKI, 2013). Katika muktadha wa

jela baruti hutumiwa kurejelea pilipili. Kileksia, baruti na pilipili ni maneno mawili yenye

maana tofauti kabisa. Hata hivyo, katika muktadha wa jela, neno baruti linatumiwa kufumba

neno pilipili kwani pilipili ni marufuku gerezani. Neno baruti linapanuliwa kimaana kurejelea

pilipili kwani baruti ina sifa sawa na pilipili. Pilipili huwasha na kulipuka kwenye mdomo jinsi

baruti hulipua vifaa mbambali kama vile mawe.

Neno neti limetoholewa toka kwenye lugha ya Kiingereza net. Katika mazungumzo ya kawaida,

neti ni kitambaa cha wavuwavu kinachoning‟inizwa kitandani kukinga mbu (Mdee n.w., 2011).

Jela pia lina maana ya kipekee kisemantiki, pahali wanapowekwa wahalifu wa sheria kuadhibiwa

ili wajirekebishe (TUKI, 2013). Leksimu hizi pamoja na maana zao ni tofauti kabisa kisemantiki.

Hata hivyo, neno neti lina sifa ya kuwa humfungia binadamu ili asiumwe na mbu. Hiyo sifa ya

neti ndiyo inafanya leksimu hii kupanuliwa na kumaanisha jela ambayo hutumiwa na serikali

Page 97: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

80

kuwafungia wafungwa ili kuelekezwa na kurekebishwa. Ingawa hivyo, utafiti huu ulipata kuwa

maelezo ya kisemantiki kuhusu jela hayaingiliani na maana ya jela kama ilivyo sasa katika taifa

la Kenya. TUKI (2013) inasisitiza swala la kuadhibiwa kwa wafungwa ili kujirekebisha.

Magereza ya Kenya ya sasa hayaelekezwi katika kuadhibu bali katika kufundisha na kuelekeza

ili kuwepo kwa mabadiliko ya kitabia na wala si kama inavyofafanuliwa na TUKI (2013).

Leksimu roho ina maana ya kitu kisichoonekana ambacho hufikiriwa kuwa ni sehemu ya mwili

wa kiumbe ambayo hukiwezesha kuwa hai (TUKI, 2013). Hapana uhusiano wa moja kwa moja

katika ya neno hili roho na wafungwa. Roho inadaiwa kuwa sehemu ya mwili lakini wafungwa

ni wanadamu. Hata hivyo, pana dhehebu la ‘ROHO’ ambalo wafuasi wake huvalia mavazi

meupe pamoja na kofia. Wafungwa wanaofanya kazi katika maghala ya jela pia hujifunga kwa

vitambaa vyeupe mwilini na kuvaa kofia nyeupe ili kukinga uchafu unaotakana na magunia ya

mahindi na unga wanaobeba. Sifa hii ndiyo inayofanya leksimu roho kupanuliwa hadi kuashiria

wafungwa hawa wanaofanya kazi kwenye maghala ya jela.

Nguo kawaida hurejelea vazi analovaa mtu. Katika muktadha wa jela, nguo ya matress

hutumiwa kurejelea wale wafungwa wenye vyeo vya juu zaidi gerezani. Nguo ni vazi lakini

kirejelewa katika muktadha wa jela ni wanadamu. Hapana uhusiano wa moja kwa moja kati ya

nguo na mtu. Hata hivyo, baadhi ya magodoro hufunikwa kwa kiguo cha rangi ya buluu.

Wafungwa hawa wasimamizi pia huvalia mavazi ya rangi ya buluu. Kwa namna hii, nguo ya

matress inapanuliwa kurejelea wafungwa wasimamizi ambao huvalia nguo za rangi ya samawati.

Leksimu malaika kisemantiki humaanisha kiumbe asiyeonekana na ambaye hudaiwa kuwa

mtumishi wa Mungu (TUKI, 2013). Kiumbe huyu kawaida huchukuliwa kuwa mzuri na asiye na

doa. Hapana uhusiano wa kisemantiki ulio wa moja kwa moja kati ya malaika, ambaye ni

Page 98: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

81

kiumbe wa kiroho asiyeoonekana, na mfungwa ambaye yumo gerezani. Hata hivyo, malaika

huwa wana sifa kuwa ni wazuri tena ni walinzi wa binadamu. Sifa hii ndiyo inayowafanya

wafungwa kupanua maana ya neno hili na kulitumia kuwarejelea wafungwa ambao ni wazuri

pale gerezani. Wazuri hapa ikiwa na maana ya kuwa hawakiuki sheria na kanuni za magereza na

pia hawana ujanja wa jela (Kiswahili ya jela).

Kisemantiki, simba ni mnyama mkubwa wa porini wa jamii ya paka mwenye manyoya ya rangi

ya majani (TUKI, 2013). Simba huchukuliwa katika mazungumzo ya kawaida kuwa ndiye

mfalme wa wanyama porini. Hapana uhusiano wa moja kwa moja kati ya simba, mnyama na

askari mkuu gerezani, yaani binadamu. Hata hivyo, kwa sababu simba huwa na sifa ya kuwa

ndiye mfalme wa wanyama wa porini, maana ya neno hili hupanuliwa katika muktadha wa jela

ili kurejelea askari mkuu wa gereza ambaye ndiye mtawala mkuu katika muktadha wa jela

husika (Officer in Charge).

Katika mazungumzo ya kawaida, mzazi ni leksimu ambayo hutumiwa kurejelea baba au mama

mtu (TUKI, 2013). Katika jela, wazazi wa wafungwa hawaruhusiwi kuishi na watoto wao mle

isipokuwa ikiwa wao nao ni wafungwa. Mzazi katika muktadha wa jela ni askari mzuri. Hapana

uhusiano wa kibayolojia na hivyo basi wa kisemantiki baina ya huyu mzazi katika jela na mzazi

halisi wa mfungwa kwani ni makundi mawili tofauti ya watu. Neno mzazi hupita upanuzi wa

kimaana na kurejelea askari mzuri kwa sababu huyu askari mzuri huwa na sifa za kiuzazi. Ni

askari anayewaelewa wafungwa, anawashauri, anawatia moyo, anawasaidia wanapokuwa na

mahitaji. Yaani, ni kama mzazi anavyowalea watoto wake nyumbani.

Kisemantiki, mwewe hurejelea ndege mkubwa anayefanana na tai ambaye huwakamata vifaranga

wa kuku (TUKI, 2013). Hakuna uhusiano wa kisemantiki kati ya mwewe na askari au mfungwa.

Page 99: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

82

Mwewe ni ndege, na mfungwa au askari ni binadamau. Hata hivyo, mwewe ana sifa ya kunyakua

au kuiba vifaranga wa kuku. Gerezani pia mna wafungwa-mwewe wasioshiba ambao hata baada

ya kula hulazimika kurudi kwenye vyombo vya kupikia na kuvichokora ili kupata kitu cha

kuongeza matumboni. Pia pana afande-mwewe ambao wafungwa huwachukulia kuwa walafi.

Askari hawa hupapia na kuchukua vyakula vya wafungwa, hasa nyama. Tabia hii ya kuchukua

nyama kutoka kwenye bakuli ya mfungwa inahusishwa na tabia ya mwewe ya kuiba vifaranga

wa kuku. Hivyo basi, neno mwewe linapanuliwa kumaanisha askari mlafi au mfungwa mlafi.

Katika Kiswahili cha kawaida, nyoka ni mnyama mrefu na mwembamba mwenye magamba na

asiye na miguu, anayetambaa na hutaga mayai (TUKI, 2013). Nyoka huwa na sumu na

akimwuma binadamu bila kutibiwa, binadamu huyo huishia kufariki. Hapana uhusiano wa

kisemantiki kati ya nyoka na mfungwa. Nyoka ni mnyama lakini mfungwa ni binadamu. Ingawa

hivyo, nyoka huwa na sifa ya kuwa ana sumu kali ya kufisha. Baadhi ya wafungwa wenye kutoa

siri kwa maafisa wa magereza huweza kusababisha wafungwa wenzao kuadhibiwa au hata

kupata uhamisho. Sifa hii ya nyoka huifanya leksimu hii kupanuka kimaana katika muktadha wa

jela na kutumiwa kuwarejelea hawa wafungwa wasaliti.

4.3.2.2 Chuku

Wilson (2003) anasema kuwa hili ndilo badiliko ambalo linaonekana kuhusisha kiwango

kikubwa zaidi cha upanuzi wa maana na hivyo kunakuwepo na utengano mkubwa kutoka kwa

dhana ambayo imesimbwa. Mtafiti alikubaliana na maelezo haya na kuongeza kuwa hili

badiliko linahusu upigaji chuku au kutia chumvi.

Page 100: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

83

4.10: Agoti zilizopanuka maana kichuku

Agoti Maana ya kawaida Maana kimuktadha

Kutoboa Fanya kuwa na tundu Kumaliza kifungo

Tero Mashambulizi ya kigaidi Wafungwa kufanyiwa upekuzi

Kunyeshewa randa Kuangukiwa na randa Kuchapwa

Kuuza mtu Kubadilisha mfungwa kwa

fedha

Kumfanya mfungwa

mwenzako achapwe

Kukula copper Kukula risasi Kupigwa risasi

Nchi ingine Taifa tofauti Uraiani

Nchi ya saba Taifa la saba Jela

Leksimu toboa katika lugha ya Kiswahili ina maana kufanya kitu kuwa tundu (TUKI, 2013). Ni

wazi kuwa kitu kikitoboka huwa kinawacha nafasi na kile kilicho ndani kupita. Hii ni maana ya

kawaida ya neno hili. Katika muktadha wa jela, maana ya neno hili ni mfungwa kumaliza

kifungo chake. Hali ya kutoboka kunalinganishwa na mfungwa kufunguliwa jela na kuwa huru.

Mskilizaji anapata ufasiri kuwa jinsi maji yanavyopita katika tundu la kifaa kama chupa, ndivyo

mfungwa anavyotoka katika kifungo. Ufasiri huu unaonekana kuwa masafa ya mbali zaidi na

maana ya kitu kuwa na tundu. Hivyo basi, maana neno hili imepanuliwa kwa kutiwa chumvi.

Tero ni neno ambalo limekopwa toka lugha ya Kiingereza terrorize yenye maana ya

kushambulia kigaidi. Inachukuliwa kuwa msikilizaji ana vitomeo vya maarifa ya ufahamu wa

namna mashambulizi ya kigaidi hufanywa. Kwa mfano, mashambulizi yanapofanywa huwa pana

mateso, kupigwa au hata umwagaji damu. Katika muktadha wa jela tero hutumiwa kurejelea

Page 101: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

84

upekuzi wa dharura ambao hufanywa na maafisa wa magereza kwenye seli ya wafungwa.

Kutokana na maelezo ya wahojiwa kuwa mara nyingi upekuzi unapofanywa wafungwa huvuliwa

uchi upekuzi huu ambao ni mchakato wa kawaida wa jela unapanuliwa kwa namna ya

kuongezwa chumvi na kurejelewa kama mashambulizi ya kigaidi.

Katika maelezo ya kawaida, kunyeshewa randa ni kuangukiwa na kile chombo ambacho

hutumiwa kusawazisha mbao. Katika muktadha wa jela, kuchapwa kunarejelewa kama

kunyeshewa randa. Kunyeshewa randa ni kauli ambayo imetiliwa chumvi kudhihirisha uchungu

wa kichapo anachopata mfungwa mkononi mwa askari anapoadhibiwa. Wingi wa viboko

unahusishwa na mvua ya randa kunyesha.

Kuuza mtu, kawaida ni kule kumbadilisha na pesa. Hii ni maana ambayo imetiwa chumvi kutoa

ile dhana ya mfungwa kumfanya mwenzake kuchapwa. Maana ya kileksia ya kuuza ipo mbali

sana na maana ya kimuktadha ya neno hili ambayo ni kusaliti. Uchungu huo wa mfungwa

kumsaliti mwenzake kwa maafisa wa magereza hadi kufikia mfungwa husika kuchapwa

kunawafanya wafungwa katika muktadha huu kupanua maana ya neno hili kwa kutia chumvi ili

kurejelea hali ya kusaliti.

Kukula copper kisemantiki ni hali ya mtu kutia risasi mdomoni. Katika muktadha wa jela kukula

copper ni mtu kupigwa risasi. Kukula ni tofauti kabisa na kupigwa risasi katika muktadha wa

kawaida wa matumizi ya maneno haya. Hivyo basi, huku kukula copper kumepanuliwa maana

kwa kupigiwa chuku kumaanisha kupigwa risasi.

Maana ya kawaida ya nchi ya saba ni taifa la saba. Maneno haya yanatumiwa kurejelea jela.

Huku ni kutiwa chumvi kwani jela ni sehemu ya taifa wala si taifa tofauti. Hata hivyo, kutokana

na hali kuwa maisha ya jela ni magumu, bei ya bidhaa kuwa ghali ikilinganishwa na bei

Page 102: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

85

miongoni mwa raia wa kawaida, maana ya neno jela inapanuliwa kwa kutiwa chumvi na

kurejelewa kama nchi ya saba. Maana hii iliyopanuliwa kisitiari inaonyesha tofauti kubwa

iliyopo katika maisha ya jela na maisha ya jamii ya kawaida.

4.3.2.3 Upanuzi wa kategoria

Katika aina hii ya badiliko, jina la kitu ambacho kinajulikana zaidi katika jamii linapanuliwa

kimaana na kutumiwa katika jamii nzima ambamo kitu hicho hupatikana (Wilson, 2003). Mtafiti

alikubaliana na maelezo haya na kuongeza kuwa, hili jina linapotumiwa katika jamii nzima huwa

linafanya maana inayopitishwa kujitenga zaidi toka kwenye maana iliyosimbwa na leksimu hiyo.

Kwa mujibu wa Wilson na Carston (2007) majina ya kipekee na nomino za kawaida huwa

zinachangia katika badiliko hili.

4.11: Agoti zilizopanuka kikategoria

Agoti Maana ya kawaida Maana kimuktadha

Mariam Maria ni mamake Yesu Lori la magereza

Awuori Aliyekuwa makamu wa rais Basi la magereza

Kutokana na jedwali 4.11, Maria ni jina la kipekee. Maria ni mamake Yesu katika muktadha wa

kawaida. Kwamba Wakristo wanaamini kuwa Yesu ni Mungu, Maria anachukuliwa na baadhi

madhehebu ya kikristo kama mama ambaye amebarikiwa. Kwa sababu Maria anachukuliwa

kama mama wa madhehebu ya kikristo, ambayo ni mengi, lori la magereza hurejelewa kama

Mariam kwani huweza kubeba watu wengi sana kwa safari moja. Wahojiwa walifafanua kuwa,

mariam huchukuliwa kuwa haiwezi kujaa, walivyo wengi Wakristo. Pia, mtu yeyote huweza

kubebwa na lori hili.

Page 103: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

86

Awuori ni jina la kipekee. Alikuwa ni naibu wa raisi aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani

ya taifa. Alipokuwa waziri alianzisha rasmi matumizi ya mabasi kuwasafirisha wafungwa. Kwa

sababu ndiye aliyeanzisha matumizi haya ya mabasi, baadhi ya wafungwa hutumia jina lake

kurejelea mabasi ya magereza. Ni muhimu kutaja kuwa, Awuori ni binadamu wala si gari. Hata

hivyo, katika muktadha wa jela, jina lake linapanuliwa maana na kurejelea basi la jela. Mtafiti

alikubaliana na Jeffers na Lehiste (1979) kuwa upanuzi huu wa maana huwa unatokana na

kujumuisha hali mahususi hadi katika jamii ambayo ile hali mahusisi inashiriki. Hii ndiyo sababu

majina ya kipekee kama Awuori na Maria yanajitokeza kurejelea jamii ya kijumla ya ile

fenomena.

4.3.3 Kisio la maana

Katika Nadhria ya Pragmatiki Leksika, mchakato wa tatu wa kipragmatiki ni kisio la maana. Hili

ni badiliko ambalo kwalo leksimu iliyo na maana thabiti kiasi hupanuliwa ukingoni na

kujumuisha mawanda ya makundi ambayo kwa hakika yanapatikana nje ya maana yake kamili

ya kiisimu. Mifano mizuri kwa mujibu wa Wilson (2003) ni kama matumizi ya kilegevu ya

takwimu za kukadiria, misamiati ya kijiografia na misamiti ambayo inaelezwa kwa njia ya

kukanusha. Hapa, dhana ambayo inawasilishwa inajitenga zaidi na dhana ambayo imesimbwa.

4.12: Agoti zilizopanuka kwa kukisiwa kimaana

Agoti Maana ya kawaida Maana ya kimuktadha

Nchi ya saba Taifa la saba Jela

Kwenda Kenya Kwenda katika nchi ya Kenya Kwenda kuwa raia wa

kawaida

Page 104: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

87

Katika jedwali 4.12, agoti nchi ya saba imesimba dhana ya NCHI YA SABA. Dhana hii ambayo

imesimbwa ni mbali sana na maana ya nchi ya saba katika lugha ya Kiswahili. Nchi ni leksimu

bayana ambayo ina maana ya sehemu ya ardhi katika ulimwengu iliyogawika kisiasa kwa

mipaka na kutambuliwa kwa taifa lake au ni sehemu ya ardhi isiyofunikwa na maji (TUKI,

2013). Si bayana nchi ya saba inayozungumziwa ni nchi ya saba gani? Ni nchi ya saba, nchi ya

kwanza ikiwa ipi? Ni katika muktadha wa jela ndipo nchi hii ya saba inaweza kukadiriwa kuwa

ni jela. Agoti hii inatumiwa kudhihirisha utengano au tofauti kati ya maisha ya jela na maisha ya

kawaida ya raia. Tofauti hii inaifanya jela kuonekana kama dunia tofauti. Nchi ya saba ni legevu

ila inatumiwa kurejelea jela.

Katika muktadha wa kawaida, kuenda Kenya ni kusafiri kuenda nchi ya Kenya. Maana hii ya

kipekee inapanuliwa na kuhusisha maana ambayo kwa hakika awali haikuwepo katika maneno

haya. Msikilizaji anabaki akijiuliza, mtu anaenda vipi Kenya iwapo tayari yupo katika taifa la

Kenya? Maneno haya yanatumiwa kwa njia legevu kudhihaki mazingira ya jela kuwa mabaya

na kuwa si sehemu ya taifa la Kenya. Inambidi msikilizaji kufanya ukadiriaji ili aweze kubaini

Kenya hii inayozungumziwa i wapi ikiwa tayari yupo katika taifa la Kenya. Mtafiti alikubaliana

na Carston (2002) kuwa katika upanuzi wa maana, ile maana ya kawaida inadondoshwa ili

kuweza kuzalika kwa maana iliyosimbwa.

Kwa muhtasari, mabadiliko ya kimaana katika agoti za wafungwa yalidhihirisha kuwa lugha ya

wafungwa ni hazina ya maana. Michakato yote ya kipragmatiki leksika ilijitokeza katika agoti za

wafungwa huku upanuzi na ubanaji wa kimaana ukijitokeza kwa upana zaidi. Mabadiliko ya

kimaana katika leksimu za wafungwa pia yalidhihirisha kuwa jamii ya wafungwa imeumbika

kinyume na jamii ya kawaida nje ya jela. Wafungwa wanakiuka matumizi ya kawaida ya

maneno katika Kiswahili na kuyabadilishia maneno hayo maana kwa manufaa yao. Kutokana na

Page 105: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

88

hali hii, jamii ya wafungwa inaweza kurejelewa kama jamii yenye uasi kwa maana ya anti-

society. Isitoshe, mabadiliko ya kimaana yalidhihirisha usiri uliopo katika mawasiliano miongoni

mwa wafungwa. Utafiti huu ulibaini kuwa usiri ndio sababu kuu ya mabadiliko ya kimaana

kutokea katika lugha ya wafungwa. Wafungwa hubadili maana ya maneno ili kuficha siri zao

zisifahamike na askari au hata na wafungwa wengine.

4.4 Uundaji wa agoti za wafungwa na ubunaji wa maana mpya

Lengo la tatu la utafiti huu lilikuwa kujadili mbinu za uundaji wa agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Uundaji wa maneno mapya pamoja na ubunaji wa maana

mpya ni kitengo ambacho pia hushughulikiwa na Nadharia ya Pragmatiki Leksika (Wilson,

2003). Hii husaidia katika kutoa data zaidi kwa nadharia hii na kupeana welewa wa mikakati ya

kiakili na hali za kimaumbile ambazo huhusika.

Ohly (1977) alitoa baadhi ya ruwaza za kuanzisha misamiati mipya katika Kiswahili. Kwanza

alizungumzia ukopaji wa maneno (Kutoka lugha ya Kingereza). Pili, uundaji wa maana mpya

ambayo inaweza kuwa; uundaji wa maneno mapya kikamilifu, maneno yaliyokuwepo

kuidhinishiwa maana mpya au kupewa mawanda ya kisemantiki ya kipekee au kwa kutumia

makundi ya kisintaksia yenye kijalizo. Mtafiti alikubaliana na mawazo haya kwani hadi nyakati

hizi pana leksimu ambazo zinaundwa au zinapata maana mpya au zinabadilishwa miundo

kimofolojia au kifonolojia na kwa njia hiyo kupata maana mpya.

Utafiti huu ulitumia kipengele hiki cha upanuzi wa maana katika kujadili mbinu mbalimbali za

uundaji wa agoti za wafungwa.

Page 106: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

89

4.4.1 Ukopaji wa maneno

Agoti za wafungwa zinaundwa kwa ukopaji wa meneno. Ukopaji unahusu uhamishaji wa

kipashio fulani kutoka lugha moja na kukiingiza katika lugha tofauti. Yaani, kuna lugha pokezi

na lugha changizi (Jefwa, 2010). Hock na Joseph (1996) nao wanasema kuwa ukopaji ni

uhamishaji wa leksimu mahususi kutoka lugha moja au lahaja moja hadi nyingine. Huwepo aina

mbili za ukopaji: ukopaji sisisi na ukopaji tohozi. Ukopaji sisisi ni pale ambapo leksimu fulani

inahamishwa kutoka lugha changizi hadi lugha lengwa bila ya kufanyiwa marekebisho yoyote.

Jedwali 4.13: Mifano ya agoti zilizokopwa

Leksimu mkopo Leksimu asili Maana Lugha changizi

Karao/Krauni Crown Askari Kiingereza

Buti Boot Njia ya choo Kiingereza

Mablue Blue Mfungwa

msimamizi

Kiingereza

Geng’ Gang Kundi la wafungwa Kingereza

Wode Water Maji /pombe Kiingereza

Kurutu Recruit Asiyefahamu

mambo

Kiingereza

Wadhii Watu Wafungwa Kiswahili

Waya Wire Kifaa cha kuwasha

sigara

Kiingereza

Biskuti Biscuit Mahindi yaliyooza Kiingereza

Hoteli Hotel Jikoni Kiingereza

Page 107: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

90

Neti Net Jela Kiingereza

Trekta Tractor Mfungwa mgeni Kiingereza

Ongosh Ongogo Mende Kijaluo

Redio Radio Simu Kiingereza

Katika mifano kwenye jedwali 4.13, si lazima neno lililokopwa liwe na maana ileile iliyopo

katika lugha changizi. Kwa mfano, neno neti lina maana ya jela katika muktadha wa jela. Maana

hii ni tofauti na maana ya neno hili katika lugha ya Kiswahili na pia katika lugha yenyewe

changizi. Neno hoteli pia linakopwa kutoka lugha ya Kiingereza hotel lakini linapewa maana

tofauti ili kurejelea jikoni. Hali hiyo pia ni sawa kwa neno trekta ambalo linatarajiwa

kumaanisha – chombo kinachofanana na gari na ambacho hutumiwa kukokota vitu. Linakopwa

toka neno la Kiingereza tractor lakini linapewa maana ya wafungwa wageni katika jela. Hivyo

basi, utohozi unaojitokeza katika lugha ya wafungwa ni wa viwango. Unahusu utohozi wa

kifonolojia na kimofolojia lakini si wa kisemantiki kwani maana inayotolewa baada ya kukopwa

ni tofauti.

4.4.2 Ubadilishaji silabi katika maneno

Ubadilishaji silabi ulibainika kama mbinu ya uundaji wa agoti za wafungwa. Katika ubadilishaji

silabi, neno kopwa huweza kutoholewa kwanza. Halafu, silabi za neno hilo toholewa

hupanguliwa. Upanguaji huu upya wa silabi za neno hilo husika hulipa neno hilo ujenzi au

muundo mpya wa kinyumenyume. Kama katika maelezo kuhusu utohozi, hapa pia maana ya

neno inaweza kubadilishwa.

Page 108: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

91

Jedwali 4.14: Mifano ya agoti zilizobadilishiwa silabi

Leksimu changizi Agoti Lugha changizi

Fegi Gife Sheng

Card Dika Kiingereza

Gweno Nogwez Kijaluo

Mbwa Mbwauz Kiswahili

Ukuta Taukuz Kiswahili

Nyoka Kanyoz Kiswahili

Ngwara Rwanga -

Jedwali 4.14 linaonyesha baadhi ya istilahi zilizobadilishwa na wafungwa ili kuficha maana.

Neno fegi linabadilishwa na kuwa gife. Neno hili limekopwa kutoka msimbo wa Sheng. Card

ambalo ni neno la Kiingereza linatoholewa na kuwa kadi kisha linabadilishwa na kuwa dika.

Dika ina maana ya kitambulisho cha mfungwa. Neno gweno ambalo ni la Kijaluo linabadilishwa

na kuwa nogwez na kutumika katika mawasiliano ya Kiswahili. Nogwez yenye maana ya kuku

katika Kiswahili hutumiwa kurejelea bangi. Neno ukuta linabadilishwa na kuwa taukuz. Mageuzi

haya ya ukuta ni sawa na yale yanayotokea kwa nyoka ambayo inakuwa kanyoz. Neno ngwara

ambalo linatumika tu katika lugha ya wafungwa pia linabadilishiwa silabi na kuwa rwanga.

Kulingana na mifano hii, leksimu changizi ni maneno ambayo yanafahamika na wafungwa

pamoja maafisa wa magereza. Hata hivyo, wafungwa wanapotaka kuwapotosha askari,

wanazifanyia marekebisho leksimu zilizozoeleka ili kuwatenga askari husika. Tofauti na katika

Page 109: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

92

Sheng ambapo hali hii pia hujitokeza, ubadilishaji silabi katika agoti za wafungwa aghalabu

huambatana na kubadilika kwa maana.

Ilibainika kuwa sifa hii ya lugha ya wafungwa huwafaidi zaidi wafungwa kwa sababu

inawawezesha kuficha siri zao ili maafisa wa magereza wasipate kuwaelewa moja kwa moja.

Ogechi (2005) anaeleza kwamba, neno husika hukopwa kisha matamshi ya neno hilo

kubadilishwa. Ubadilishaji silabi huu huwa ni utaratibu wa kimakusudi ambao hutumiwa na

wafungwa kuunda leksimu zao.

4.4.3 Ubunifu wa leksimu

Agoti za wafungwa zilidhihirisha ubunifu wa leksimu kama mbinu ya uundaji wa maneno. Kwa

mujibu wa Hartmann na Stork (1972) ubunifu ni mchakato wa kuunda leksimu mpya kimakusudi

kutokana na faridi za kimofolojia ambazo zipo. Katika jamii, hali fulani hujitokeza na kuwabidi

wanajamii husika kubuni msamiati wa kurejelea kifaa au hali ambayo ni geni kwao. Leksimu

hiyo huwa haihusishwi na ukopaji wala utohozi. Wafungwa wanapokumbana na vifaa vipya au

hali mpya katika mazingira ya jela, wao huzipa urejeleo. Leksimu katika lugha ya wafungwa

ambazo zinaonyesha hali hii ni:

Jedwali 4.15: Agoti zilizobuniwa

Leksimu zilizobuniwa gerezani Maana

Kibaba Kifaa cha kuwapimia wafungwa mafuta

Ngwara Silaha ya kukata wakati wa vita

Mruru Chombo kama mkebe cha kutia chakula

Mburga Jikoni

Page 110: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

93

Chimano Jela

Kisuguu Mnara wa ulinzi

Jedwali hili linadhihirisha ubunifu wa kiwango kikubwa katika lugha ya wafungwa. Maneno

mapya yanabuniwa ili kurejelea hali mbalimbali au vitu vipya ambavyo vinapatikana katika

mazingira ya jela. Sehemu ya kupikia inavumbuliwa neno jipya mburga ambalo si neno la

kawaida katika Kiswahili sanifu. Jela pia linavumbuliwa neno jipya chimano.

Istilahi hizi zaelekea kusadifu maoni ya Irwin (1980) kuwa hali ngumu za magereza humpa

mfungwa ubunifu wa kiisimu na ule wa kufanya marekebisho (tazama pia Andersson na Trudgil,

1990)

Hivyo basi, lugha ya wafungwa wa magereza ya Kisumu ni „lugha pambani‟. Kwa mujibu wa

Looser (2001) sifa moja kati ya zile mbili za lugha pambani ni kuundwa kwa maneno mapya

kutokana na yale ambayo yapo. Maneno katika lugha ya kawaida yanabadilishwa na maneno

mapya ambayo yamebuniwa katika magereza na wafungwa. Katika data iliyopatikana, maneno

mengi yalichukua nafasi ya maneno ya Kiswahili sanifu. Nafasi ya neno jikoni ilichukuliwa na

neno jipya mburga. Nafasi ya neno jela ilichukuliwa na neno jipya chimano. Yaani, pana

uumbaji upya wa maneno (Halliday, 1978). Ingawa hivyo, ubunaji huu mpya wa maneno

kulingana na utafiti huu ni wa viwango kwani si kila neno katika Kiswahili sanifu limeumbiwa

neno jipya katika lugha ya wafungwa.

4.4.5 Kuchanganya msimbo

Uchambuzi wa data ulidhihirisha kuwa uchanganyaji msimbo kama mbinu ya uundaji wa

leksimu ni bayana. Kwa mujibu wa Fasold (1984) msimbo ni utaratibu wa mawasiliano

Page 111: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

94

unaozingatia kanuni bayana za kisarufi na hasa uteuzi wa msamiati na maumbo ya sentensi.

Kuchanganya msimbo kunafafanuliwa na Richards na wenzake (1985) kama dhana ya

kuchopeka maneno au sehemu ya neno la lugha moja kwenye usemi wa lugha nyingine. Agoti

ambazo zilidhihirisha uchanganyaji msimbo ni:

Jedwali 4.16: Mifano ya uchanganyaji msimbo

Uchangayaji msimbo Maana

Ugali ya pan Ugali spesheli

Kuingiza boot Kuficha kwenye njia ya choo ili kisipatikane

na askari

Leta steam Leta pombe

Toa finger Toa pesa/hongo ili uishi vizuri

Kukula copper Kupigwa risasi

Mtu ordinary Anayeelewa hali na njia za jela

Mfungwa staff Mfungwa mwenye hadhi, hasa kutokana na

kuwa ana fedha nyingi

Kuchange quarter Wafungwa mashoga (ambao huwa kama

kike) wakishiriki ngono. Watoto wawili

wakishiriki ngono

Kutower Mfungwa mmoja kuchungulia ili askari

asiwapate wenzake wanaokiuka sheria

Page 112: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

95

Jedwali 4.16 linaonyesha kuwa agoti za wafungwa zimesheheni uchanganyaji msimbo. Data

inaonyesha kuwa lugha zinazochanganywa zaidi katika uundaji wa agoti za wafungwa ni

Kiswahili na Kiingereza. Kwa mfano, kuingiza boot yenye maana ya kuficha kitu kwenye

makalio ili kisipatikane na askari kumeundwa kwa maneno kuingiza, ambalo ni neno la

Kiswahili pamoja na boot neno la Kiingereza. Ugali ya pan nayo ina neno la Kiingereza pan.

Hiki ni chakula kizuri kilichopikwa kwa mara ya pili; ugali uliokaangwa. Leta steam

imechanganya maneno leta ambalo ni Kitenzi katika Kiswahili na steam ambalo ni Nomino ya

Kiingereza. Kukula copper yenye maana ya kupigwa risasi imeundwa kwa kukula, neno la

Kiswahili na copper, neno la Kiingereza. Ni bayana kuwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili

ndizo zinachanganywa zaidi.

Tofauti na anavyosema Rayfields (1970) kuwa katika lugha ya kisasa, uchanganyaji msimbo

hutumiwa kusisitiza, utafiti huu ulibaini kuwa uchanganyaji msimbo hutumiwa na wafungwa

zaidi katika urejeleaji. Kwa mfano, mfungwa staff hurejelea mfungwa mwenye hadhi katika jela,

hutokana na hali kuwa mfungwa husika ana fedha nyingi, ana uwezo na anaheshimiwa. Ingawa

hivyo, sifa hii pia hujitokeza wakati ambapo mfungwa anatoa kauli au agizo. Kwa mfano,

mfungwa anapomwambia mwenzake „ingiza boot‟ anamwambia afiche vitu walivyonavyo. Toa

finger huambiwa mfungwa na mwenzake ili atoe hongo ili atetewe na wenzake gerezani.

Uchanganyaji msimbo pia unatokea katika mazingira ya jela ili kuficha siri. Kauli

zinazochanganyiwa lugha ni zile zinafahamika wazi katika Kiswahili cha kawaida. Kwa sababu

mfungwa hangetaka askari afahamu kile wanachozungumzia wanaingiza neno la Kiingereza ili

kumpotosha. Kutoa hongo linafumbwa katika maneno toa finger. Yaani, utoe kitu kidogo. Kula

copper, ni kukula risasi. Risasi ndiyo inafumbwa katika neno copper.

Page 113: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

96

4.4.6 Ubadilishaji

De Klerk (1955) anafafanua kuwa ubadilishaji ni mchakato ambapo maneno yanabadilishana

kimaana. Data ilionyesha kuwa baadhi ya maneno katika lugha ya wafungwa yalibadilishana

nafasi.

Jedwali 4.17: mifano ya agoti zilizobadilishana nafasi

Agoti Asili

Redio Simu

Hoteli Jikoni

Neti Jela

Randa Kiboko

Kiswahili Ujanja

Kwekwe Askari mpekuzi

Jedwali 4.17 linadhihirisha hali ya ubadilishaji wa maneno. Redio ambayo ni chombo

kinachopokea mawimbi ya sauti k.v. ya mtangazaji kupitia hewani ili mtu mwingine asikie

kinachotangazwa, kinachukua nafasi ya neno simu ambayo ina maana tofauti. Mfungwa

hurejelea simu kama redio katika mawasiliano yao ili askari asipate kuwaelewa. Neno hoteli

linachukua nafasi ya neno jikoni katika mazungumzo ya wafungwa. Neno neti linatumiwa

kurejelea jela badala ya neno mwafaka, jela. Neno Randa ambalo lina maana tofauti na kiboko

linatumiwa kukirejelea kiboko. Kiswahili kinachukua nafasi ya neno ujanja. Ubadilishaji huu

hutokea ili kuficha siri za wafungwa zisifahamike na askari.

Page 114: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

97

Uundaji wa agoti na ubunaji wa maana mpya ulidhihirisha ubunifu uliopo katika agoti za

wafungwa. Wafungwa walitumia mbinu mbalimbali kuunda agoti zilizotumika katika muktadha

wa jela. Hii ni kwa sababu uundaji wa agoti za wafungwa aghalabu uliandamana na ubadilishaji

wa maana au neno husika kuongezewa maana mpya. Hali ngumu za jela ziliibua ubunifu wa

kiisumu mingoni mwa wafungwa.

4.5 Hitimisho

Katika sura hii mtafiti amewasilisha na kuchanganua data aliyokusanya kupitia mahojiano ya

makundi na usaili. Uwasilishaji na uchambuzi huu wa data ulifanywa kwa kuzingatia

madhumuni mahususi ya utafiti huu na uliongozwa na mkabala wa kimaelezo. Aidha, Nadharia

Pragmatiki Leksika iliyotumika katika utafiti huu ulimsaidia mtafiti kupambanua misimbo katika

lugha ya wafungwa.

Utafiti huu ulifanikiwa kubainisha kuwepo kwa agoti zinazotumiwa na wafungwa. Mtafiti

aliziainisha agoti hizo katika vikoa maana mbalimbali. Uchambuzi wa mahusiano ya maneno

kimaana katika kila kikoa ulidhihirisha ulimwengu wa jela ulivyo. Uchambuzi wa mabadiliko ya

kimaana ulionyesha jinsi mabadiliko yote ya kimaana yalivyojitokeza katika agoti za wafungwa.

Mtafiti alifikia hitimisho kuwa agoti za wafungwa ni hazina ya maana. Michakato ya

kipragmatiki leksika pia ilionyesha jamii ya jela kama jamii yenye uasi kwa namna inavyobadili

matumizi ya kawaida ya maneno na kuyatumia katika jela kwa njia tofauti. Uasi huu

ulimwelekeza mtafiti kufikia hitimisho kuwa mabadiliko ya kimaana katika agoti za wafungwa

hutokea ili kukidhi haja ya kuficha siri katika mawasiliano miongoni mwa wafungwa. Hatimaye,

mtafiti alijadili uundaji wa agoti za wafungwa ambao ulisawiri lugha ya wafungwa kama iliyo na

Page 115: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

98

kiwango cha juu cha ubunifu. Data kutoka kwa watafitiwa ilithibitisha madhumuni yote ya utafiti

huu.

Page 116: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

99

SURA YA TANO

HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.1 Utangulizi

Sura hii inahitimisha utafiti uliohusu uchanganuzi wa matumizi ya agoti miongoni mwa

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Sura hii imegawika katika sehemu sita. Sehemu ya kwanza

imetoa utangulizi wa sura. Sehemu ya pili inaeleza muhtasari wa utafiti. Sehemu ya tatu

inaangazia matokeo ya utafiti. Sehemu ya nne inafafanua mchango wa utafiti. Sehemu ya tano ni

hitimisho la utafiti. Sehemu ya sita inapendekeza maeneo yanayohitaji kufanyiwa utafiti zaidi.

5.2 Muhtasari wa utafiti

Utafiti huu uliochunguza matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa ulifanyika katika

magereza makuu ya Kibos na Kodiaga mjini Kisumu. Utafiti wenyewe ulikuwa na madhumuni

matatu. Kwanza, kujadili vikoa maana katika agoti zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya

Kisumu. Pili, kufafanua mabadiliko ya kimaana yanayojitokeza katika agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Tatu, kujadili mbinu za uundaji wa agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Mpangilio mzima wa kazi hii ulikuwa kama ufuatavyo:

Sura ya kwanza imebainisha taarifa zinazohusiana na mada ya utafiti. Sura hii imegawika katika

sehemu nane. Sehemu ya kwanza imetoa usuli wa utafiti. Sehemu ya pili imeangazia suala la

utafiti. Sehemu ya tatu imeeleza misingi ya uteuzi wa mada. Sehemu ya nne imezungumzia

lengo la utafiti. Katika kitengo cha tano mtafiti ameangazia maswali ya utafiti. Sehemu ya sita

imeelezea umuhimu wa utafiti. Kitengo cha saba kimefafanua upeo wa utafiti. Sehemu ya nane

imeangazia changamoto za utafiti.

Page 117: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

100

Sura ya pili imechambua matini zinazohusiana na matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa.

Baada ya utangulizi mtafiti amepambanua matini kwa kujikita katika vipengele vinavyobainika

katika madhumuni ya utafiti. Sura hii pia imedhihirisha mwanya uliopo ambao utafiti huu

ulinuia kuziba.

Sura ya ya tatu ya utafiti huu unahusu njia na mbinu za utafiti. Sura hii imegawika katika sehemu

kumi. Baada ya utangulizi, sehemu ya pili inafafanua kuhusu mbinu za utafiti. Sehemu ya tatu

inaangazia muundo wa utafiti. Sehemu ya nne inaeleza kuhuu eneo la utafiti. Katika kitengo cha

tano, mtafiti ameangazia sampuli na usampulishaji. Sehemu ya sita imeelezea kuhusu vifaa vya

utafiti. Kitengo cha saba kimeshughulikia ukusanyaji wa data. Sehemu ya nane imeelezea

uchanganuzi wa data. Sehemu ya tisa imeangazia majaribio ya vifaa vya utafiti. Sehemu ya kumi

imefafanua kuhusu maadili ya utafiti.

Katika sura ya nne mtafiti ameshughulikia uwasilishaji na uchambuzi wa data. Sura hii ina

vitengo vitano. Sehemu ya pili inaangazia vikoa maana katika agoti za wafungwa. Sehemu ya

tatu inachambua na kujadili data iliyohusiana na mabadiliko ya kimaana katika agoti za

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Katika sehemu ya nne, mtafiti amewasilisha na kuchambua

data kuhusu mbinu za uundaji wa agoti za wafungwa wa magereza ya Kisumu.

Katika sura ya mwisho, sura ya tano, mtafiti ametoa hitimisho na mapendekezo ya utafiti. Katika

sehemu ya pili pametolewa muhtasari wa kijumla wa utafiti. Katika sehemu ya tatu mtafiti

amefafanua matokeo ya utafiti huu. Kitengo cha nne kimeangazia mchango wa utafiti na sehemu

ya tano imetoa hitimisho la utafiti. Mwisho, sura hii imetoa mapendekezo kwa tafiti za baadaye.

Page 118: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

101

5.3 Matokeo ya utafiti

Lengo la utafiti huu lilikuwa kuchanganua matumizi ya agoti miongoni mwa wafungwa wa

magereza ya Kisumu. Matokeo ya utafiti huu yametolewa kulingana na madhumuni mahususi ya

utafiti.

Lengo la kwanza katika utafiti huu lilikuwa kujadili vikoa maana vya agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Utafiti huu ulibainisha kuwa wafungwa wana agoti zao

ambazo huwawezesha kuwasiliana katika mazingira ya jela. Agoti zilizochambuliwa zilikuwa

katika lugha ya Kiswahili. Pahala ambapo palikuwepo na uchanganyaji wa msimbo sababu za

kuchanganya msimbo zilitolewa.

Palikuwepo na agoti zilizojumuishwa katika kikoa kipana cha mambo na shughuli za jela. Utafiti

huu ulibaini kuwa kitengo hiki ndicho chenye agoti nyingi zaidi. Agoti hizi zilihakikisha madai

kuwa wafungwa wanapoingia gerezani sharti wapitie maingiliano ya kitawi na kubuni na

kujifundisha lugha ya ulimwengu huu wa pili.

Palikuwepo pia na agoti zilizojitokeza katika kikoa maana cha wafungwa. Hizi zilikuwa leksimu

mbalimbali ambazo wafungwa hutumia kuwarejelea wafungwa wenzao katika muktadha wa jela.

Ufafanuzi wa agoti hizi ulibainisha kuwa pana wafungwa wa hadhi ya juu na wale wa hadhi ya

chini.

Kikoa maana kingine kilichochambuliwa ni kikoa cha maafisa wa magereza. Ni lesksimu

mbalimbali ambazo wafungwa hutumia kuwarejelea maafisa wa magereza. Ufafanuzi wa maana

za agoti hizi ulidhihirisha kuwepo kwa maafisa wa hadhi ya juu na wale wa hadhi ya chini kwa

mtazamo wa wafungwa. Agoti hizi pia zilidhihirisha uhusiano uliopo baina ya wafungwa na

Page 119: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

102

maafisa wa magereza. Isitoshe, agoti hizi zilibainisha majukumu mbalimbali za maafisa wa

magereza kingazi.

Hivyo basi utafiti huu ulifanikiwa kuainisha agoti za wafungwa katika vikoa maana mbalimbali

kama ilivyodhamiriwa.

Lengo la pili la tafiti huu lilikuwa kufafanua mabadiliko ya kimaana yanayojitokeza katika agoti

zinazotumiwa na wafungwa wa magereza ya Kisumu. Mtafiti alipata kuwa agoti za wafungwa

zilipitia mabadiliko ya kimaana na kupata miktadha mipya kutokana na michakato mbalimbali ya

kipragmatiki leksika.

Aina zote za mabadiliko ya kimaana zilijitokeza katika agoti zinazotumiwa na wafungwa wa

magereza ya Kisumu na ziliweza kufafanuliwa kwa kujikita katika nadharia ya Pragmatiki

Leksika. Zile aina mbili kuu za mabadiliko ya kimaana, upanuzi wa maana na ubanaji wa maana

zilijitokeza. Kisio la maana lilijitokeza kwa leksimu chache sana likilinganishwa na mabadiliko

mengine ya maana. Upanuzi wa maana ulishirikisha aina zifuatazo za mabadiliko ya maana;

chuku, upanuzi wa kisitiari na upanuzi wa kategoria.

Utafiti huu ulibainisha kuwa agoti za wafungwa hazikupoteza maana zao za kileksika ila maana

hizi zilifanyiwa mageuzi kwa kujikita katika muktadha wa jela na zikapata fahiwa mpya.

Isitoshe, mtafiti alipata kuwa mabadiliko ya kimaana hujitokeza katika agoti za wafungwa ili

kukidhi haja ya wafungwa kufumba jumbe zao wanapowasiliana.

Lengo la tatu la utafiti huu lilikuwa kujadili mbinu za uundaji wa agoti zinazotumiwa na

wafungwa wa magereza ya Kisumu. Mtafiti alitumia kipengele cha ubunaji wa maana mpya na

uundaji wa leksimu kama aina ya upanuzi wa kimaana kujadili mbinu mbalimbali za uundaji wa

agoti za wafungwa.

Page 120: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

103

Utafiti huu ulibainisha kuwa agoti za wafungwa huundwa kwa ukopaji wa maneno. Maneno

yalikopwa zaidi kutoka lugha ya Kiingereza. Ukopaji katika msimbo wa wafungwa ulipatikana

kuwa ni wa viwango kwa kuwa ulihusu utohozi wa kifonolojia na kimofolojia lakini si wa

kisemantiki. Maneno yaliyokopwa yalipewa maana tofauti na maana katika lugha changizi.

Baadhi ya agoti za wafungwa ziliundwa kwa kubadili silabi katika maneno. Neno lililozoeleka

au la kukopwa hupanguliwa kinyumenyume. Upanguaji huu upya hulipa neno husika muundo

tofauti. Ubadilishaji silabi hutumika zaidi katika kuficha siri. Mifano iliyofafanuliwa ilidhihirisha

kuwa neno lililopanguliwa upya liliweza kuongezewa silabi ili kulifumba zaidi.

Uchanganuzi wa data ulidhihirisha kuwa kulikuwepo na leksimu za wafungwa ambazo

ziliundwa kiubunifu katika mazingira ya jela. Mifano iliyotolewa ilibainisha kuwepo kwa

maneno mapya ambayo wafungwa hubuni ili kurejelea mambo mbalimbali katika mazingira ya

jela. Leksimu kama hizi mtafiti alipata kuwa hazikuhusishwa na ukopaji wala utohozi.

Uchanganyaji msimbo ulibainika kama mbinu ya uundaji wa agoti za wafungwa. Hapa, neno la

lugha ya kigeni linachopekwa katika maneno ya Kiswahili. Ilibainika kuwa wafungwa

huchanganya msimbo katika maneno ili kufumba maana za maneno, ili kurejelea mambo

mbalimbali, na kutoa agizo au kauli. Isitoshe, utafiti huu ulipata kuwa maneno katika lugha ya

wafungwa hubadilishana nafasi. Maneno mawili tofauti yaliweza kubadilishana maana. Neno

fulani lenye maana tofauti lilitumiwa kurejelea kitu kingine tofauti.

5.4 Mchango wa utafiti

Utafiti huu utachochea ari ya uundaji wa kamusi za agoti za wafungwa. Utafiti huu ulibainisha

kuwepo kwa agoti za wafungwa ambazo ziliainishwa katika vikoa maana mbalimbali. Kwa

Page 121: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

104

kutumia agoti hizi na kuongezea zingine zinazotumiwa katika magereza mengine,

wanaleksikografia wataweza kutunga kamusi zenye kufafanua maana za istilahi mbalimbali

zinazotumiwa katika magereza. Kamusi zinazofafanua maneno katika muktadha wa jela

zimeweza kutungwa katika mataifa mengine, kwa mfano, Knight (2014) alitunga kamusi The

Dictionary of Victorian Prison Slang.

Utafiti huu umeibua muktadha mwingine wa matumizi ya lugha ambao haujatafitiwa katika

Kiswahili. Tafiti nyingi zilizochunguza miktadha ya matumizi ya Kiswahili zilifanywa

miongoni mwa raia. Utafiti huu hivyo basi utaibua ari ya watafiti kushughulikia lugha ya

wafungwa katika ngazi za Sintaksia, Semantiki, Pragmatiki na Isimujamii.

Nadharia ya Pragmatiki Leksika iliyotumiwa katika utafiti huu utakuwa ya manufaa katika

Kiswahili. Nadharia hii itawafaa watafiti wengine ambao watakuwa na haja ya kuitumia katika

kuchanganua na kuchunguza masuala ya kiisimu na kifasihi. Utafiti huu utakuwa kielelezo cha

kuonesha kuwa Nadharia ya Pragmatiki Leksika inafaa zaidi katika kuchanganua mabadiliko ya

kimaana katika lugha. Hii inatokana na ukweli kuwa nadharia hii ilifaulu kufafanua mabadiliko

ya kimaana katika muktadha wa jela.

Utafiti huu pia unachangia ukuzaji na uhifadhi wa agoti ambazo hutumiwa na wafungwa. Hii

itawasaidia watafiti wa baadaye kafanya urejeleaji na kufanya tafiti kuhusu mabadiliko ya

kimaana kiwakati.

5.5 Hitimisho la utafiti

Kwa kutimilika kwa malengo ya utafiti huu, ilidhihirika kuwa agoti za wafungwa ni hazina ya

maana. Leksimu mbalimbali zinazotumiwa na wafungwa ziliweza kufafanuliwa kimaana chini

Page 122: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

105

ya kila kikoa maana. Michakato ya kipragmatiki leksika pia zilibainisha jinsi wafungwa hubadili

maana ya maneno katika muktadha wa jela ili kukidhi haja zao. Mtafiti pia alionyesha jinsi

wafungwa huunda maneno katika jela na kuyapa maana tofauti au kuyaongezea maana. Mtafiti

alifikia hitimisho kuwa lugha ya wafungwa ni hazina kuu ya isimu kutokana na jinsi wafungwa

walivyoonyesha ubunifu wa kiwango cha juu wa kuyapa maneno maana, kubadili maana ya

maneno na kubuni leksimu za kutumiwa kuwasiliana miongoni mwao.

5.6 Mapendekezo

Kwa kuwa utafiti huu ni wa kwanza kufanywa katika Kiswahili kuhusiana na lugha ya

wafungwa, na kwenye msingi wa ukweli kuwa tulibanwa kwenye upeo na mipaka yetu, pana

mambo mbalimbali ya kufanyiwa utafiti katika eneo hili la lugha ya wafungwa ambayo

hayakushughulikiwa katika utafiti huu. Hivyo basi mtafiti anapendekeza yafuatayo:

Kufanywe utafiti ambao utachunguza mabadiliko ya kidaikronia ambayo yanaweza kuwepo

katika agoti za wafungwa. Kwenye utafiti huu, mtafiti alijibana katika kujadili mabadiliko ya

kimaana katika agoti za wafungwa kwa kujikita katika muktadha wa matumizi. Hakuingia ndani

na kushughulikia etimolojia ya kale ya leksimu hizi ambayo ingempa msingi mzuri sana wa

mabadiliko ya kimaana kulingana na vipindi tofauti vya wakati.

Ni bayana kuwa utafiti huu ulijikita katika matini za kimazungumzo. Kwa kuwa sajili ya jela ni

kimuli cha msingi wa utangamano wa jamii, panahitajika utafiti zaidi ambao utashughulikia

matini andishi za jela. Watafiti wanaweza kuchunguza lugha katika hadithi mbalimbali

walizoziandika wafungwa, maandishi kwenye seli na vyoo vya wafungwa pamoja na maandishi

kwenye miili ya wafungwa.

Page 123: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

106

Mwisho, utafiti huu ulichunguza matumizi ya lugha katika gereza la wafungwa wanaume. Ni

bayana kuwa wanawake na wanaume hutumia lugha kwa njia tofauti. Hivyo basi, mtafiti

anapendekeza kuwa kufanywe tafiti kuchunguza matumizi ya lugha katika gereza la wanawake

na ulinganisho wa kina ufanywe.

Page 124: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

107

MAREJELEO

Aitchison, J. (2003). Words in the Mind: An Introduction to the Mental Lexicon. (Third Edition).

U.S. A: Blackwell Publishing Limited.

Alatias, J. (1992). Language Communication and Social Meaning. Washington, D.C: Gergetown

University Press.

Allan, K. & Burridge, K. (2009). Forbidden words: Taboo and Censoring of Language.

Cambridge: Cambridge University press.

Anderson, L., & Trudgil, P. (1990). Bad Language. Oxford, UK: Blackwell.

Anusu, A. (2015). Usawazishaji Leksimu katika Kiswahili: Utafiti wa Vihiga. Tasnifu ya uzamili

ambayo haijachapichwa, Chuo Kikuu cha Nairobi.

Bentley, William K. & James M. (1992). Prison Slang: Words and Expressions Depicting Life

Behind Bars. Jefferson: McFarland and Company.

Berger, P., & Luckman, T. (1971). The Social Construction of Reality: A Treatise in the

Sociology of Knowledge. Harmondsworth: Penguin University Books.

Binyanya, M. (2014). Sajili ya Maafisa wa Polisi: Tathmini ya Matumizi ya Lugha ya Kiswahili

katika Kituo cha Polisi cha Central, Nairobi. Tasnifu ya uzamifu ambayo

haijachapishwa, Chuo Kikuu cha Nairobi.

Blank, A. (1998). Historical Semantics and Cognition, Berlin and New York: Mouton.

Bloomfield, L. (1930). Language. New York: Holt, Reinhart and Winston.

Page 125: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

108

Bloomfield, L. (1933). Language. London: Compton Printing ltd.

Blutner, R. (1998). Lexical Pragmatics. In A Journal of Semantics, Volume 15(2).

Blutner, R. (2011). Some Perspectives on Lexical Pragmatics, Pragmatics Reader: Routledge,

London.

Bogdad, R. & Biklen, S. (1992). Quantitative research for Education: An introduction to Theory

and Methods, (2nd

ed.), Boston, Allyn and Bacon.

Bondesson, U. (1989). Prisoners in the prison societies. New-Brunswick, NJ: Transaction.

Boswell, C. & Cannon, S. (2009). Introduction to nursing research: incorporating evidence-

based practice 2nd ed. UK: Jones & Bartlett Learning.

Buliba, A., Njogu, K. na Mwihaki, A. (2006). Isimujamii Kwa Wanafunzi wa Kiswahili.

Nairobi: Jomo Kenyatta Foundation.

Bullock, B. (1996). Popular Derivation and Linguistic Inquiry; les Javanis. AATF.

Burke, P. & Porter, R. (Eds.) (1995). Languages and Jargons: Contributions to a Social History

of Language. Polity Press.

Cardozo-Freeman, I. (1995). The lingo of the Pintos. Bilingual Review, 20(1)

Carston, R. (2002) Thoughts and Utterances: The Pragmatics of Explicit Communication.

Oxford: Blackwell Publishing.

Carston, R. (2004) Thoughts and Utterances: The Pragmatics of Explicit Communication,

Oxford: Blackwell Publishers Limited.

Page 126: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

109

Ciechanowska, N. (2015). Towards the functions of prison slang. Univeristy of Rzeszow.

Clemmer, D. (1940). The Prison Community. Newyork: Elsevier.

Coleman, J. (2004). A History of Cant and Slang Dictionaries. 2Vols. Oxford: Oxford UP.

Condon, J.C. & Yousef, F. (1975). An introduction to intercultural communication. New York:

Macmillan.

Dean-Brown, J. (1992). Social Meaning in Language, Curriculum and Through Language

Curriculum. In Alatias, J. (Ed) Language Communication and Social Meaning.

Washington, DC: Georgetown University Press.

Dirk, G. (2010). Theories of Lexical Semantics. Oxford University Press: New York

Einat, T., & Einat, H. (2000). Inmate argot as an expression of prison subculture: The Israeli

Case. The Prison Journal, 80(3), 309-325.

Einat, T., & Einat, H. (2003). The Evolving Nature of Prison Argot and Sexual Hierachies. The

Prison Journal, 83 (33), 289-300.

Ellis, P. (2005). The Prison-House and Language: Modern American Prison Argot, Toronto.

Encinas, G. (2001). Prison argot: A sociolinguistic and Lexicographic Study. Lanham,

Maryland; UP of America.

Enon, C. J. (1998). Education Research and Measurement, Department of Distance Education;

Makerere University; Uganda.

Fasold, R. (1984). The Sociolinguistics of Language. Oxford: Blackwell.

Page 127: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

110

Fishman. J. A. (1972). The sociology of language: An interdisciplinary social science approach

to language in society. Rowley, M.A: Newbury House.

Fisher, S. (1990). On the Move: The Psychology of Change and Transition. Chichester, UK:

Wiley.

Foster, H. (1986). Ribbin', jivin', & playin' the dozens. Amherst, NY: Foster & Associates.

Fromkin, V. & Rodman, R. (1993). An Introduction to Language (5th

ed.). New York: Harcourt

Brace College Publishers.

Gal, S. (1979). Language Shift: Social determinants of linguistic change in bilingual Asustria.

New York: Academic Press.

Gall, M. et al. (1996) Educational Research: An Introduction. New Yorl: Longman.

Gay, L. & Diehl, P. (1992) Research Methods for Busines and Management. New York:

Mcmillan.

Glucksberg, S. (2001). Understanding Figurative Language: From Metaphors to Idioms.

Oxford: Oxford University Press.

Goffman, E. (1962). Asylums: Essays on the Social Situation of Mental Patients and Other

Inmates. Chicago: Aldine Publishing Company.

Good, C. (1972). Essentials of Education: Research Methodology and Design. New York:

Meredith Corporation.

Page 128: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

111

Gohodzi, I. (2013). A critical Analysis of Prison as Discourse Communities; an Examination of

Whahwa Prison Complex. Unpublished Research Project, Midlands State

University.

Gumperz, J. (1982). Language and Social Identity. Cambridge: Cambridge University Press.

Habwe, J. (199). Discourse Analysis of Swahili Political Speeches. Chuo Kikuu cha Nairobi.

Tasnifu ya PhD. (Haijachapishwa).

Habwe, J. & Karanja P. (2004). Misingi ya Sarufi ya Kiswahili. Nairobi: Phoenix Publishers

Limited.

Halliday, M. et al. (1964). The Linguistics Science and Language Teaching.London: Longman.

Halliday, M. (1994). An Introduction to functional grammar. 2nd edition. London: OUP

Halliday, M. (1978). Language as Social Semiotic: The Social Interpretation of Language and

Meaning. London: Edward Arnold.

Holloway, I & Wheeler, S. (2002) Qualitattive Research in Nursing. 2nd edition. Oxford:

Blackwell Publishing

Holloway, I. (1997). Basic Concepts in Qualitative Research. Oxford. Blackwell Science

Hartmann, R., & Stork, F. (1972). Dictionary of Language and Linguistics. London: Applied

Sciences.

Harris, B. (2012). What Is Argot? (n.d.). Retrieved November 20, 2017, from wise

GEEK:http://www.wisegeek.com/what-is-argot.htm. Conjecture Corporation.

Page 129: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

112

Hensley, C. (Ed.). (2002). Prison sex: Practice and policy. Boulder, CO: Lynne

RiennerPublishers.sexual hiereches.

Hensley, C. et al (2003). The evolving nature of prison argot and sexual hirechies. The Prison

Journal 83.3.

Hock, H & Joseph, B. (1996) Trends in Linguistics Studies and Monographs 93: Language

History, Language Change and Language Relationship; An Introduction to

Historical and Comperative Linguistic. New York: Mouton DeGruter.

Horn, L. & Ward, G. (2004). The Handbook of Pragmatics, Oxford: Blackwell

Hudson, R.A. (1980). Sociolinguistics. Cambridge, UK: Cambridge University Press.

Ingule, F. & Gatumu, H. (1996). Esssentials of Educational Statistics. Nairobi. East African

Educational Publishers.

Irwin, J. (1980). Prisons in turmoil. Boston: Little, Brown.

Irwin, J. (1985). The jail. Berkeley: University of California Press.

Ito, J. Y. Kitagawa & A. Mester (1996). Prosodic Faithfulness and Correspondence: Evidence

from Japanese Argot. Lingua, 237-258.

Jackson, B. (1967). Prison Nicknames. Western Folklore 26.1: pg48-54.

Jeffers, J & Lehiste, I. (1979) Principles and Methods for Historical Linguistics. London: The

MIT Press-Cambridge, Massachusetts

Jefwa, G. (2010). Utangulizi wa Isimu. Nairobi: Kenya Literature Bureau.

Page 130: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

113

Keith, G., & Shuttleworth, J. (2000). Living Language. London: Hodder and Stoughton.

Kempson, R. (1977). Semantic Theory. Cambridge University Press.

Kenya Human Rights Commission (2002). Improving Prison Conditions in Kenya: Propasals

and Recommendations

Kimani, N; Njogu, K. & Buliba, A., (2006). Isumujamii kwa wanafunzi wa Kiswahili. Nairobi:

Jomo Kenyatta Foundation.

Knight, J. (2014). A Dictionary of Victorian Prison Slang. Victoria: Australia.

Kobia, J. (2006). Sheng is not a Language but a Popular Slang. Sunday Nation, Nairobi,

February 2.

Kolaiti, P. & Wilson, D. (2012). Corpus Analysis and Lexical Pragmatics: An Overview.

http:www.phon.ucl.ac.uk? home/deride

Kress, T. (2008). Critical Praxis Research; Breathing New Life into Research Methods for

Teachers, United States of America; Springer.

Kombo, D. & Tromp, D. (2006). Proposal and Thesis Writing: An Introduction, Pauline‟s

Publications Africa, Nairobi.

Kothari, C. R. (1990). Research Methodology: Methods and Technique, Willey Eastern Limited,

New Delhi.

Kothari, C. R. (2004). Research Methodology; Methods and Techniques, 2nd Edition, New

Delhi; New Age International (P) Limited Publishers.

Page 131: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

114

Kothari, C. R. (2008). Research Methodology; Methods and Technique. New Age International

(P) Limited, New Delhi.

Labov, W. (1972). Language in the inner city. Philadelphia: Pennyslavania University Press.

Lee, D. (1992). Competing Discourses: Perspective and Ideology in Language. New York:

Longman.

Leslau, W. (1988). Fifty Years of Research: Selection of articles on Semitic, Ethiopian Semitic

and Cushitic Languages. Harrasswitz: Wobaden.

Looser, D. (2001). Boobslang: A lexicographical study of the argot of New Zealand prison

inmates, in the period 1996-200. Unpublished PhD theses, University of Cantebury.

Lourens, L et al. (1992). Only Study Guide for SEMANO-Y (Revised Ed). Pretoria: UNISA.

Lyons, G. (1984). Inmates and Convicts: The Language of Inclusion and Exclusion. The SECOL

Review: Southeastern Conference on Linguistics 8 (3). Murfreesboro, Tenn.: The

Conference.

Mathews, P. (1997). The Concise Oxford Dictionary of Linguistics. Oxford-New York: Oxford

University Press.

Maurer, D. (1981). Language of the Underland. Lexington, KY: The University Press.

Mmbwanga, K. (2010). New Words and Meanings on Facebook: A LexicalPragmatics Analysis,

Unpublished M. A. Thesis: University of Nairobi.

Page 132: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

115

McArthur, T. (1996) The Oxford Companion to The English Language. GB: Oxford University

Press

McCawley, J. (1978). Where you can shove infixes. Syllables and segments, ed. by Alan Bell &

Joan Hooper, 213-21. Amsterdam: North-Holland.

Mclntyre, T. & Mack, D. (1993). The streetsmart correc tional educator. Educating Adjudicated,

Incarcer ated & At-Risk Youth, 1, 35-43.

Mdee, J. na wenzake (2011). Kamusi ya Karne ya 21, Nairobi; Longhorn Publishers Limited.

Mekacha, D. (2011). Isimujamii: Nadharia na Muktadha wa Kiswahili. Dar es Salaam: TUKI

Milroy, L. (1980). Language and Social Networks: Oxford: Basil Blackwell.

Msanjila, Y. P na wenzake (2009). Isimujamii Sekondari na Vyuo. Dar es Salaam.TUKI.

Msanjila, Y. P na wenzake (2011) Isimujamii: Sekondari na Vyuo. TUKI. Dar es Saalam.

Mugambi, A. (2007). Utohozi Maana Katika Maneno ya Sheng. Tasnifu ambayo

haijachapishwa, Chuo Kikuu cha Kenyatta.

Mugenda, O., & Mugenda, A. (2005). Research Methods: Quantitative Approaches. Nairobi:

ACTS Press.

Mugendi, N. (2016). Morphology of the Gitamanya argot of the Matatu Crew of Embu Town;

Unpulished MA Thesis: Kenyatta University.

Mukhwana, A (2008). Language Attitudes in Urban Kenya: A Case Study of Nairobi, Kisumu

and Mombasa. Phd Theses (unpublished), University of Nairobi.

Page 133: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

116

Mulokozi, M. (2003). Utafiti wa fasihi simulizi, katika makala ya semina ya Kimataifa ya

waandishi wa Kiswahili. TUKI. Dar es Salaam. Uk 18-26.

Mulvey, C. (2013). Prison Lingo: The Language of the Prison Community. Universuty of

Wnichester, Sparkford, Winchester.

Muyuku, A. (2009). Language Mixing in the Language of Advertising: A Case Study of

Commercial Banks and Mobile Telecommunications in Kenya, Unpublished M. A.

Thesis: University of Nairobi.

Mwangi, P. & Mukhwana, A. (2011) Isimujamii. Nairobi: Focus Publishers

Nyakundi, P. (2010). Motivation, Morpho-phonological Processes in Egesembesa Argot Among

Ekegusii-Speaking Males of Western Kenya; Unpublished MA Thesis: Kenyatta

University.

Newbold, G. (1989). The Maximum Security Prisons in New Zealand. Oxford University Press.

Ngugu, T. (1986). Decolonizing the mind: language of African politics, Heinemann: London.

Ngure, A. (2003). Fasihi Simulizi kwa Shule za Sekondari. Nairobi: Pheonix Publishers.

Nielson, A., & Scrapitti, T. (1995). Argot use in theraupitic community; Deviant Behavior,

16(3), 127-129.

Njimu, P. (2010). Lexical Adjustments of Sports Language in Three Kenyan Newspapers. Chuo

Kikuu cha Nairobi. Tasnifu ya M.A (Haijachapishwa).

Page 134: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

117

Ochichi, A. (2013). Uwazi na Umaanisho: Usimbaji Maana Kimazungumzo Katika Ekegusii na

Kiswahili. Chuo Kikuu cha Nairobi. Tasnifu ya M,A (Haijachapishwa)

Ochoki, B. (2010). Pragmatics Interpretation Contraints in Kenyan Hip Hpo Lyrics. Chuo Kikuu

cha Nairobi. Tasnifu ya M.A (Haijachapishwa).

Ogechi, N.O. (2005). Lexocalization in Sheng. Nordic Journal of African Studies 14 (3), 334-33.

Ohly, R. (1977) Patterns of New-Coined Abstract Terms (Nominal forms) in Modern Swahili

katika Journal of the Institute of Kiswahili Research (Vol.47/1) Dar es Salaam:

Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Orodho, J. (2005). Elements of Educational and Social Science Research Methods. Nairobi:

Masola Publishers.

Owino, B., Omar, B., & Akong‟a, J. (2015). Looking in the Mirror: Reflections in

implementation of the principles of penal systems in Kenya‟s prisons. In the

Journal of International Academic Research for Multidisciplinary VOL 1(3).

Pallock, J. (2006). Prisons today and tomorrow. Sundbry: Jones and Burtlett Publishers.

Partridge, E. (1970). Slang today and yesterday. London: Routledge, Kegan & Paul.

Rayfields, J. (1970). The Languages of a Bilingual Community.The Hague: Mouton.

Richards et al, (1985). Longman Dictionary of Applied Linguistics. U.K, Longman Group.

Ramani, K (2006). Leave Sheng to Matatu Touts and Mucisians. The Standard, September 29.

Sigh, K. (2007). Quantitative Social Reseach Methods, India; SAGE Publication.

Page 135: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

118

Simiyu, C. (2016) The Portrayal of men and women in selected Bukusu Circumcision Songs: A

Lexical Pragmatic Approach. Chuo Kikuu cha Nairobi. Tasnifu ya M.A.

(Haijachapishwa)

Sykes, M. G. (1958). The Society of Captives. Princeton, NJ: Princeton University Press.

Sykes, M.G., & Messsinger, S.L (1960). The inmate social code and its functions: Social science

research council. 15, 401-405.

Szabo, E. (2005). Hungarian Prison Slang Today; From 1996-2005. (Phd Theses), Debrecen.

Ngugi, T. (1986). Decolonising the Mind: The Politics of Language in African Literature.

London: J. Currey Ltd

Trier, J. 1931. Der deutsche Wortschatz im Sinnbezirk des Verstandes. Heidelberg: Winter.

TUKI (1990). Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha. Dar es Salaam: Education publishers and

Distribution LTD.

TUKI (2013). Kamusi ya Kiswahili Sanifu. Oxford University Press

Toch, H. (1992). Mosaic of Despair. Washington, DC: American Psychological Association.

Toch, H., & Johnson, R. (1982). The pains of imprisonment. Beverly Hills, CA: Sage.

Ullmann, S. (1957). The Principles of Semantics, Blackwell and Mott.

Ullmann, S. (1962). An Introduction to the Science of Meaning, Oxford: Blackwell.

Ullmann, S. (1970). Semantics: An Introduction to the Science of Meaning. Oxford: Basil

Page 136: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

119

Ullman, S. (1977). Change of Meaning. In H. Hungerford et al., English Linguistics. Illinois:

Scott, Foresman and Company.

Vartanian, T. P (2011). Secondary Data Analysis, New York; Oxford University Press.

Yule, G. (1996). Pragmatics. Oxford: Oxford University Press.

Yule, G. (2006). The Study of Language: An Introduction .Cambridge: Cambridge University

Press.

Walliman, N. (2011). Research Methods; The BasicLondon & New York; Routledge Taylor&

Francis Group.

Wambugu, W. (2010). Semantic Shifts in Gikuyu Lexemes: A Lexical Pragmatic Approach.

Unpublished M.A. Thesis: University of Nairobi.

Wamitila, K. (2010). Misingi ya Uchanganuzi wa Fasihi. Vide Muwa Publishers, Kenya.

Wilson, D. (2003). Relevance and Lexical Pragmatics, in Italian Journal of Linguistics, Italy.

Wilson, D. & Cartson, R. (2007). A Unitary Approach to Lexical Pragmatics: Relevance,

Inference and ad hoc Concepts.

Page 137: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

120

KIAMBATISHO I: MWONGOZO WA MAHOJIANO

Ninaitwa Ogutu Peter. Mimi ni mwanafunzi wa somo la Isimu ya Kiswahili (uzamili) katika

Chuo Kikuu cha Kisii. Ninafanya utafiti kuhusu agoti ya wafungwa. Naomba uchukue muda

wako kujadiliana nami kuhususiana na masuala haya. Toa habari za kweli bila uoga wowote.

Jina lako halitachapishwa popote katika kazi hii. Habari zote zitashughulikiwa kama siri.

Sehemu A

1) Umri wako (age)

………………

2) Kiwango cha elimu

a) Elimu ya msingi …….b) Elimu ya sekondari…….c) Elimu ya chuo cha anuwai….d) Chuo

kikuu……….e) Nyingineyo (bainisha) ……..

Sehemu B

1) Kwa ujumla, je pana maneno ambayo mnayafahamu na lakini maafisa wenu hawawezi

kuyaelewa? Je, kuna maneno ambayo nyote mwaelewa?

2) Je pana mahusiano ya kimapenzi ndani ya magereza? Kama ndiyo maneno yepi yanatumia

kurejelea mahusiano haya? Wafungwa na vitendo vya ngono vinarejelewa vipi humu gerezani?

3) Pana marufuku, bidhaa na vifaa ambavyo haviruhusiwi kuingizwa gerezani? Maneno yapi

hutumiwa kurejelea vitu hivi?

4) Je, dawa za kulevya zinarejelewa kwa kutumia majina yapi? Nipe maana ya maneno haya

Page 138: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

121

5) Kuna baadhi ya mambo na shughuli zinazofanywa hapa gerezani. Je mnazirejelea kwa majina

gani?

6) Mnatagusana na maafisa wa magereza katika maisha yenu humu? Maneno yapi mbalimbali

ambayo ninyi hutumia kuwarejelea

7) Kuna maneno mbalimbali ambayo ninyi hutumia kuwarejelea wafungwa wenzenu? Je maneno

haya ni yapi? Tafadhali nipe maana ya maneno haya?

8) Je, pana maneno fulani ambayo yanatumiwa na kundi fulani la wafungwa? Je maneno haya ni

yapi?

Sehemu C

13) Je una maoni yoyote kuhusu lugha ya mnayozungumza humu ambayo itasaidia utafiti huu ?

Tujadiliane.

14) Pana neno lolote linalotumiwa humu ambalo hatujajadiliana kulihusu? Tafadhali liandike

katika kijikaratasi ninayokupa na unipe maana.

Page 139: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

122

KIAMBATISHO II: KIBALI CHA UTAFITI (KAUNTI YA KISUMU)

Page 140: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

123

KIAMBATISHO III: BARUA YA IDHINI (NACOSTI)

Page 141: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

124

KIAMBATISHO IV: CHETI CHA IDHINI (NACOSTI)

Page 142: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

125

KIAMBATOSHO V: KIBALI CHA UTAFITI (MAGEREZA YA KENYA)

Page 143: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

126

KIAMBATISHO VI : KIBALI CHA KUHOJIWA

Page 144: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

127

KIAMBATISHO VII: UCHAPISHAJI

Page 145: UCHANGANUZI WA MATUMIZI YA AGOTI MIONGONI MWA …

128

KIAMBATISHO VIII: RIPOTI YA UHALALI WA UTAFITI