Upload
others
View
19
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
i
VIONGOZI WAKUU WA WIZARA YA NISHATI
Mhe. Dkt. Medard M. C. Kalemani (Mb.)
Waziri wa Nishati
Mhe. Subira K. Mgalu (Mb.)
Naibu Waziri wa Nishati
Dkt. Hamisi H. Mwinyimvua
Katibu Mkuu
Wizara ya Nishati
ii
1
HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI MHE.
DKT. MEDARD MATOGOLO CHANANJA
KALEMANI (MB.), AKIWASILISHA
BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA
MATUMIZI YA WIZARA YA NISHATI
KWA MWAKA 2019/20
2
1
A. UTANGULIZI
1. Mheshimiwa Spika, kufuatia
Taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Nishati na Madini, naomba kutoa hoja
kwamba Bunge lako Tukufu likubali kupokea
na kujadili Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti
kwa Mwaka 2018/19 na kupitisha Makadirio
ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati
na Taasisi zake kwa Mwaka 2019/20.
2. Mheshimiwa Spika, napenda
nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu,
mwingi wa rehema kwa kuendelea kuwajalia
afya njema Viongozi wetu Wakuu wa
Kitaifa, Waheshimiwa Mawaziri wenzangu,
Waheshimiwa Wabunge na Viongozi wengine
mbalimbali. Kipekee nimshukuru Mwenyezi
Mungu kwa kunijalia afya njema na
kuniwezesha kuendelea kusimamia Sekta
ya Nishati na leo kusimama mbele ya Bunge
lako Tukufu kuwasilisha Hotuba ya Bajeti ya
Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2019/20.
3. Mheshimiwa Spika, naomba
pia niungane na Mawaziri wenzangu,
Waheshimiwa Wabunge na Watanzania kwa
2
ujumla kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John
Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa maelekezo yake
thabiti yanayonisaidia kuisimamia vema
Sekta ya Nishati. Ni dhahiri kuwa Rais wetu
amekuwa chachu katika kutekeleza mipango
mikubwa na yenye tija katika Sekta ya
Nishati hapa nchini. Mipango hiyo ni pamoja
na kuanza kutekeleza Mradi Mkubwa wa
kielelezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia
maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (MW
2,115). Napenda kuwaahidi Watanzania
kuwa Wizara yangu kwa kushirikiana na
Bunge lako Tukufu na wadau mbalimbali
tutasimamia vema Mradi huu ili ukamilike
kwa wakati.
4. Mheshimiwa Spika, nitumie fursa
hii kuwashukuru Mhe. Samia Suluhu Hassan,
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania; na Mhe. Kassim Majaliwa
Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania kwa miongozo
mbalimbali wanayonipatia katika kusimamia
Sekta ya Nishati. Nikiri kuwa maelekezo na
miongozo ya viongozi wetu hawa ni msingi
wa mafanikio ya utekelezaji wa majukumu
ya Sekta ya Nishati. Aidha, napenda
3
kumpongeza pia Mhe. Dkt. Ali Mohamed
Shein, Rais wa Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi kwa kuendelea kusimamia kwa
ufanisi utekelezaji wa shughuli za maendeleo
katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
5. Mheshimiwa Spika, nichukue
nafasi hii pia kuwapongeza Mawaziri
walioteuliwa hivi karibuni na Mhe. Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Nampongeza Mhe. Prof. Palamagamba John
Aidan Kabudi (Mb.), aliyeteuliwa kuwa Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika
Mashariki; Mhe. Angellah Jasmin Kairuki
(Mb.), aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Waziri Mkuu (Uwekezaji); Mhe. Balozi Dkt.
Augustine Philip Mahiga (Mb.), aliyeteuliwa
kuwa Waziri wa Katiba na Sheria; Mhe. Doto
Mashaka Biteko (Mb.), aliyeteuliwa kuwa
Waziri wa Madini; Mhe. Japhet Ngailonga
Hasunga (Mb.), aliyeteuliwa kuwa Waziri wa
Kilimo; na Mhe. Joseph George Kakunda
(Mb.), aliyeteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda
na Biashara.
6. Mheshimiwa Spika, niwapongeze
pia Naibu Mawaziri Mhe. Dkt. Mary
Machuche Mwanjelwa (Mb.), aliyeteuliwa
4
kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti
ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora;
Mhe. Constantine John Kanyasu (Mb.),
aliyeteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Maliasili
na Utalii; Mhe. Innocent Lugha Bashungwa
(Mb.), aliyeteuliwa kuwa Naibu Waziri wa
Kilimo; na Mhe. Mwita Mwikwabe Waitara
(Mb.), aliyeteuliwa kuwa Naibu Waziri, Ofisi
ya Rais - TAMISEMI. Nawatakia wateule wote
kila la kheri katika kutekeleza majukumu
yao ya Kitaifa.
7. Mheshimiwa Spika, napenda
nikupongeze wewe binafsi, Naibu Spika,
Wenyeviti wa Bunge, Wenyeviti wote wa
Kamati Mbalimbali za Kudumu za Bunge
pamoja na watendaji wote wa Ofisi ya Bunge
lako Tukufu kwa utendaji kazi wenu mahiri.
Kwa namna ya pekee natoa shukrani zangu
za dhati kwa Mwenyekiti wa Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Mhe.
Dunstan Luka Kitandula (Mb.), Makamu
Mwenyekiti Mhe. Mariam Ditopile Mzuzuri
(Mb.), na Wajumbe wote wa Kamati hiyo kwa
ushauri na maelekezo wanayotupatia. Nikiri
kuwa Kamati hii imefanya kazi kubwa ya
kuishauri Wizara katika masuala mbalimbali
na kuchambua kwa kina mapendekezo
5
ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka
2019/20. Wizara itaendelea kushirikiana na
Kamati hii katika kusimamia kwa ufanisi
ustawi wa Sekta ya Nishati.
8. Mheshimiwa Spika, baada ya
utangulizi huo, naomba sasa kuwasilisha
Taarifa ya Mapato, Matumizi na Utekelezaji
wa Shughuli za Wizara ya Nishati kwa Mwaka
2018/19 pamoja na Makadirio ya Mapato na
Matumizi kwa Mwaka 2019/20.
B. TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI
YA WIZARA KWA MWAKA 2018/19 NA
MWAKA 2019/20
Bajeti na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka
2018/19
9. Mheshimiwa Spika, Bajeti
iliyopitishwa kwa ajili ya Wizara ya Nishati
pamoja na Taasisi zake kwa Mwaka 2018/19
ni jumla ya Shilingi Trilioni 1.692 kwa
ajili ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya
Maendeleo. Kati ya fedha hizo, Bajeti ya
Miradi ya Maendeleo ilikuwa Shilingi Trilioni
1.665 sawa na asilimia 98.4 ya bajeti yote
ya Wizara na Bajeti ya Matumizi ya Kawaida
ni Shilingi bilioni 27.15 sawa na asilimia
1.6 ya bajeti yote ya Wizara.
6
10. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia
tarehe 15 Mei, 2019 Wizara ilikuwa imepokea
jumla ya Shilingi Trilioni 1.227. Fedha
hizi zinajumuisha Shilingi bilioni 688.65
ambazo ni malipo ya awali (advance payment)
kwa Mkandarasi wa ujenzi wa Mradi wa
kuzalisha umeme wa Rufiji na Shilingi bilioni
169.71 ambazo ni fedha za nje zilizopelekwa
moja kwa moja (D-Funds) katika miradi ya
REA, TANESCO na Sustainable Energy for
All (SE4All). Kiasi hicho kilichopokelewa na
Wizara ni sawa na asilimia 87 ya fedha
zilizotarajiwa kupokelewa katika kipindi
husika ambazo ni Shilingi trilioni 1.410.
Ukusanyaji wa Maduhuli ya Serikali
11. Mheshimiwa Spika, Wizara ya
Nishati katika mwaka 2018/19 ilipangiwa
kukusanya jumla ya Shilingi bilioni 394.45.
Kati ya makusanyo hayo, jumla ya Shilingi
bilioni 394.44 zilitarajiwa kukusanywa
kupitia shughuli za mafuta na gesi asilia na
Shilingi milioni 10.0 kupitia shughuli za
utawala. Hadi kufikia tarehe 15 Mei 2019,
Wizara kupitia shughuli za TPDC za utafiti wa
mafuta na mauzo ya gesi asilia imekusanya
Shilingi bilioni 484.33. Makusanyo hayo ni
sawa na asilimia 123 ya lengo la makusanyo ya
7
Shilingi bilioni 394.45 kwa mwaka 2018/19.
Sababu ya kuvuka lengo ni kuongezeka
kwa matumizi ya gesi asilia yanayotokana
na kuunganishwa kwa kituo cha kuzalisha
umeme cha Kinyerezi II na Kiwanda cha
Saruji cha Dangote. Matumizi ya gesi asilia
yameendelea kuongezeka na kufikia jumla ya
futi za ujazo bilioni 59.2 mwaka 2018 kutoka
futi za ujazo bilioni 32.2 mwaka 2015, sawa
na ongezeko la asilimia 84.
12. Mheshimiwa Spika, makisio
ya makusanyo ya maduhuli kwa mwaka
2019/20 ni Shilingi bilioni 602.05, sawa na
ongezeko la asilimia 52.6 ikilinganishwa na
Shilingi bilioni 394.45 lililokuwa lengo la
mwaka 2018/19. Ongezeko hilo la makisio
ya makusanyo limetokana na kuongezeka
kwa matumizi ya rasilimali ya gesi asilia.
C. UTEKELEZAJI WA BAJETI KWA MWAKA
2018/19
13. Mheshimiwa Spika, Maeneo ya
Kipaumbele ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka
2018/19 yalikuwa ni pamoja na: kuongeza
uzalishaji wa umeme kwa kutekeleza miradi
mikubwa ikiwemo Mradi wa kuzalisha
umeme katika Mto Rufiji MW 2,115; miradi
8
ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi
asilia ya Kinyerezi I - Extension MW 185 na
Kinyerezi II MW 240; kuimarisha mifumo
ya kusafirisha umeme nchini; kuendelea
na utekelezaji wa Awamu ya Tatu ya Mradi
Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini
(REA III); kuendelea na utekelezaji wa Mradi
wa Ujenzi wa Bomba la kusafirisha Mafuta
Ghafi kutoka Hoima (Uganda) hadi Tanga
(Tanzania); kuimarisha shughuli za utafutaji
wa mafuta na gesi asilia; na kuendeleza
miradi ya nishati jadidifu (jotoardhi, upepo
na umeme-jua).
14. Mheshimiwa Spika, Wizara pia
ilizingatia maeneo mengine ambayo ni pamoja
na: kuendelea kuwajengea uwezo watumishi
wa Wizara na Taasisi zake katika kusimamia
Sekta ya Nishati; kuboresha mazingira ya
ofisi kwa watumishi wa Wizara na Taasisi
zake ili kutoa huduma bora zaidi; na
kuendelea kuelimisha umma na kuboresha
mawasiliano na wadau mbalimbali kuhusu
masuala ya nishati.
15. Mheshimiwa Spika, napenda
kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa kutokana
na utekelezaji wa maeneo hayo ya kipaumbele,
Wizara imepata mafanikio makubwa 22 ikiwa
9
ni pamoja na nchi kutokuwa na mgawo wa
umeme katika kipindi chote cha utekelezaji
wa Mpango na Bajeti kwa mwaka 2018/19.
Aidha, pamoja na kutokuwa na mgawo wa
umeme, Taifa letu limeanza kuwa na ziada
ya umeme wa wastani wa MW 300 kwa siku
kwa mwaka 2018/19 tofauti na hapo awali
tulipokuwa na upungufu wa zaidi ya MW
100 kwa mwaka 2015. Mafanikio makubwa
21 ni kama ifuatavyo:
(i) Kuanza kwa utekelezaji wa mradi
mkubwa wa kuzalisha Umeme katika
Mto Rufiji wa MW 2,115 utakaokamilika
mwaka 2022. Ujenzi wa bwawa hili
kutaifanya Tanzania kuwa na umeme
wa uhakika, unaotabirika na gharama
nafuu. Aidha, Ujenzi wa bwawa la
mradi huu utaifanya Tanzania
kushika nafasi ya kwanza Afrika
Mashariki kwa kuwa na bwawa
kubwa, ya nne kwa Afrika na kuwa
kati ya nchi 70 Duniani zenye
mabwawa makubwa ya kuzalisha
umeme;
(ii) Kukamilika kwa ujenzi wa njia ya
kusafirisha umeme msongo wa kV
220 kutoka Makambako, Madaba hadi
10
Songea, pamoja na ujenzi wa vituo vya
kupoza umeme vya Madaba na Songea
na upanuzi wa kituo cha Makambako.
Kukamilika kwa njia hii ya kusafirisha
umeme kumefanya mikoa ya Njombe
na Ruvuma kuunganishwa katika
Gridi ya Taifa na hivyo kusitishwa
kwa matumizi ya mitambo ya mafuta
ambayo ilikuwa ikigharimu TANESCO
na kuokoa wastani wa Shilingi bilioni
9.8 kwa mwaka zilizokuwa zikitumika
kununua mafuta katika Vituo vya
Madaba, Ludewa, Songea, Mbinga na
Namtumbo;
(iii) Kuongezeka kwa kasi ya kusambaza
umeme vijijini ambapo hadi kufikia
tarehe 15 Mei, 2019 Serikali imepeleka
umeme katika vijiji 7,127 vya Tanzania
Bara ikilinganishwa na vijiji 2,018
vilivyokuwa vimeunganishwa umeme
Mwaka 2015. Hii ni sawa na ongezeko
la vijiji 5,109 katika kipindi cha miaka
mitatu iliyopita, ambalo ni ongezeko la
asilimia 253 ya vijiji vilivyokuwa na
umeme kufikia mwaka 2015. Aidha,
ifikapo mwezi Juni, 2020 vijiji zaidi ya
10,278 kati ya 12,268 vya Tanzania
11
Bara vitaunganishwa umeme sawa na
asilimia 84 ya vijiji vyote. Hivi sasa
Wilaya na Halmashauri 15 za nchi
yetu zimefikishiwa umeme katika vijiji
vyake vyote na kazi inayoendelea ni
kuunganisha umeme katika vitongoji
vyake. Wilaya pamoja na Halmashauri
hizo ni Mafia, Iringa Vijijini (Isimani),
Pangani, Rufiji, Bahi, Siha, Moshi, Hai,
Mwanga, Rombo, Madaba, Buhigwe,
Makambako, Korogwe Mjini na
Mafinga. Pamoja na kukamilisha wilaya
na Halmashauri hizo, kwa sasa kazi
za kuunganisha umeme zinaendelea
katika wilaya nyingine nchini;
(iv) Serikali kupitia TANESCO kuanza
kuunganisha umeme kwa Shilingi
27,000 katika maeneo yote ya vijijini
kulingana na Mpango wa Kupeleka
Umeme Vijijini;
(v) Kuunganisha Gridi ya Taifa katika
maeneo mbalimbali yakiwemo Tunduru
na Liwale na hivyo kuokoa jumla
ya Shilingi bilioni 7.33 zilizokuwa
zikitumika kununua mafuta ya
kuendesha mitambo ya umeme katika
maeneo hayo;
12
(vi) Kukamilika kwa ujenzi wa mradi wa
Kinyerezi II na kuongeza jumla ya MW
248.22 katika Gridi ya Taifa. Kituo
cha Kinyerezi II ni cha kwanza hapa
nchini kutumia teknolojia ya kisasa ya
combined cycle;
(vii) Kuendelea kutumia vifaa vya ndani
katika ujenzi wa miundombinu ya
kuunganisha umeme vikiwemo nguzo,
mashineumba (transfoma), nyaya na
mita za LUKU na hivyo kulipunguzia
gharama kubwa Shirika la Umeme
Nchini (TANESCO) na kuokoa wastani
wa Shilingi bilioni 162.57 kwa
mwaka. Mpango huu umetengeneza
ajira kwa watanzania wapatao 3,520 na
kuharakisha utekelezaji wa miradi ya
umeme. Kutokana na mafanikio hayo,
kwa sasa kuna zaidi ya viwanda vitatu
(3) vya kuzalisha transfoma badala ya
kimoja kilichokuwepo mwaka 2015,
viwanda tisa (9) vya nguzo badala ya
vitatu (3) vilivyokuwepo awali, viwanda
vitano (5) vya nyaya badala ya kimoja
cha East African Cables kilichokuwepo
na kujengwa viwanda vitatu (3) vya Mita
za LUKU tofauti na hapo awali ambapo
hapakuwa na kiwanda hata kimoja;
13
(viii) Kuanza kutekeleza mradi wa kujenga
njia ya kusafirisha umeme kV 132
ili kuunganisha mikoa ya Kigoma na
Katavi katika Gridi ya Taifa kutoka
Tabora – Urambo - Kaliua, Nguruka
hadi Kidahwe (Kigoma) kilomita 391
na kutoka Tabora – Ipole, Inyonga hadi
Nsimbo (Katavi) kilomita 381;
(ix) Shirika la Umeme (TANESCO) kutohitaji
ruzuku ya Serikali katika shughuli zake
za uendeshaji kutokana na TANESCO
kujiendesha lenyewe na kuokoa wastani
wa Shilingi bilioni 143 zilizokuwa
zikitumika kama ruzuku kutoka
Serikalini kila mwaka;
(x) Kuimarika kwa mapato ya TANESCO
kwa kiwango cha ongezeko la asilimia
1.5 mwaka 2017/18 hadi asilimia 7.6
mwaka 2018/19. Hivyo ni matarajio
kuwa TANESCO itaweza kuanza kutoa
gawio Serikalini katika kipindi cha
Mwaka 2019/20;
(xi) Kuunganishiwa umeme kwa wateja
wapya 969,431 katika kipindi cha
kuanzia Julai, 2015 hadi tarehe 15
Mei, 2019 na kufikia jumla ya wateja
14
2,442,648 ikilinganishwa na wateja
1,473,217 waliokuwepo kuanzia nchi
yetu ilipopata Uhuru hadi mwezi Juni,
2015 sawa na ongezeko la asilimia 66
kwa miaka mitatu;
(xii) Kuongeza mtandao wa kusambaza
gesi asilia viwandani na majumbani
kwa takriban kilomita 9.64 kwa
mwaka 2018/19 kutoka kilomita 6.31
kwa mwaka 2017/18. Mtandao huo
utawezesha kuunganisha wateja wa gesi
asilia majumbani zaidi ya 500 katika
Jiji la Dar es Salaam. Kwa upande
wa viwandani, viwanda vya: Dangote
(awamu ya pili); Knauf; Cocacola;
Lodhia; na kiwanda cha vifungashio
kinachomilikiwa na Goodwill Ceramics
Tanzania Limited vimeunganishwa.
Aidha, matumizi ya gesi katika magari
yameongezeka kutoka magari 80 mwaka
2017/18 na kufikia magari zaidi ya 200
mwaka 2018/19 ikiwa ni ongezeko la
zaidi ya asilimia 150;
(xiii) Kukamilika kwa ukarabati wa vituo
vya kupoza umeme vya Kigamboni na
Kurasini na hivyo kuimarisha hali ya
15
upatikanaji umeme katika Jiji la Dar es
Salaam ikiwemo maeneo ya Kigamboni;
(xiv) Kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu
ya kupeleka umeme katika Mji wa
Serikali eneo la Mtumba, Jijini Dodoma
kwa kuunganisha umeme Wizara zote
katika muda mfupi;
(xv) Kuanzisha utaratibu mpya wa
mawasiliano baina ya wateja na TANESCO kupitia mitandao ya kijamii ikiwemo kuanzisha makundi
ya whatsapp kwa kila wilaya
yanayopatikana masaa 24 kila siku
ili kuimarisha huduma kwa wateja na
hivyo kuongeza ufanisi na mapato ya
Shirika;
(xvi) Kuongezeka kwa ufanisi wa makusanyo
ya mapato ya Serikali ambapo hadi
kufikia tarehe 15 Mei, 2019 Wizara
kupitia TPDC ilikuwa imekusanya
Shilingi bilioni 484.33 sawa na
asilimia 123 ya lengo la makusanyo
ya Shilingi bilioni 394.45 kwa mwaka
2018/19;
(xvii) Kuendelea kutekeleza kazi za awali
za Mradi wa Bomba la Kusafirisha
16
Mafuta Ghafi kutoka Hoima (Uganda)
hadi Chongoleani (Tanga) zikiwemo
Geotechnical na majadiliano ya Host
Government Agreement – HGA. Kazi
hizo zitakamilika mwezi Juni, 2019 na
kazi nyingine za maandalizi ya ujenzi
zinaendelea;
(xviii) Kuongeza uzalishaji wa gesi asilia
kufikia Futi za Ujazo milioni 190 kwa
siku kwa mwaka 2018/19 kutoka Futi
za Ujazo milioni 175 kwa siku mwaka
2017/18. Ongezeko hilo ambalo ni
sawa na asilimia 8.6 limewezesha
upatikanaji wa gesi zaidi kwa matumizi
ya viwandani, majumbani na katika
kuzalisha umeme;
(xix) Kupungua kwa muda wa kushusha
mafuta katika Bandari zetu za Dar es
Salaam, Tanga na Mtwara kutoka kati
ya siku 30 na 60 hadi kati ya siku 3
na 8 kutokana na Serikali kuendelea
kuimarisha Mfumo wa Uagizaji wa
Mafuta kwa Pamoja na hivyo kupunguza
gharama zilizokuwa zinatokana na
gharama za meli kuchelewa kushusha
mafuta bandarini (Demurrage Charges);
17
(xx) Kupatikana kwa mafuta ya kutosha na
ya uhakika katika kipindi chote cha
mwaka 2018/19 ambapo hadi sasa
kuna ziada ya lita milioni 125.22 za
dizeli, lita milioni 94.67 za petroli, lita
milioni 18.95 za mafuta ya taa na ndege
yanayotosheleza kwa zaidi ya siku 32;
(xxi) Kukamilika na kupitishwa kwa miundo
ya Wizara, PURA na TPDC ambayo
itawezesha Wizara na Taasisi zake
kuendelea kutekeleza majukumu kwa
ufanisi; na
(xxii) Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la
awamu ya kwanza la Wizara na kuhamia
Ofisi mpya katika Mji wa Serikali eneo
la Mtumba Jijini Dodoma.
D. TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA
SHUGHULI ZA WIZARA KWA MWAKA
2018/19 NA MPANGO WA BAJETI
KWA MWAKA 2019/20
16. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20, Wizara ya Nishati itaendelea
kutekeleza maeneo ya vipaumbele mbalimbali
yakiwemo: kuongeza uzalishaji wa umeme
nchini ili kufikia lengo la kuwa na MW 10,000
ifikapo mwaka 2025, kwa kutekeleza miradi
18
mikubwa ikiwemo: mradi wa kuzalisha
umeme katika maporomoko ya Mto Rufiji
(MW 2,115) na mradi wa kufua umeme kwa
kutumia gesi asilia wa Kinyerezi I - Extension
(MW 185), Mradi wa kuzalisha umeme
wa Rusumo MW 80, Ruhudji MW 358 na
Rumakali MW 222; Kuimarisha mifumo ya
usafirishaji wa umeme nchini kwa kutekeleza
miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na mradi
wa North - West Grid Extension kV 400 yenye
umbali wa kilomita 1,384 inayojumuisha
Iringa – Mbeya – Sumbawanga – Mpanda –
Kigoma hadi Nyakanazi; Singida – Arusha
– Namanga kV 400, kilomita 414; Rufiji -
Chalinze – Dodoma kV 400, kilomita 512;
Rusumo – Nyakanazi kV 220, kilomita 98;
Geita – Nyakanazi kV 220, kilomita 133;
Tabora – Urambo – Kaliua – Nguruka hadi
Kidahwe Mkoani Kigoma kV 132, kilomita
391; na Tabora – Ipole – Inyonga hadi Nsimbo
(Katavi) kV 132, kilomita 381.
17. Mheshimiwa Spika, maeneo mengine
ya kisekta yatakayozingatiwa na Wizara ni:
kuendelea na utekelezaji wa Awamu ya Tatu
ya Mradi Kabambe wa Kupeleka Umeme
Vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini
(REA), katika vijiji takriban 1,990 vilivyobaki
19
kati ya vijiji 12,268; kuendelea na utekelezaji
wa Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Kusafirisha
Mafuta Ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi
Tanga, Tanzania (East African Crude Oil
Pipeline - EACOP); kuimarisha shughuli za
utafiti wa mafuta na gesi asilia; kuongeza
kasi ya usambazaji wa gesi asilia; kuendeleza
miradi ya nishati jadidifu (jotoardhi, upepo
na jua); kuvutia uwekezaji katika sekta ya
nishati; na kuendelea kuimarisha utendaji
wa Taasisi za TANESCO, TGDC, REA, TPDC,
PURA na Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa
Pamoja ili kuongeza ufanisi na ushindani
katika Sekta ya Nishati.
18. Mheshimiwa Spika, pamoja na
maeneo hayo ya kisekta, Wizara itazingatia
maeneo mengine ya kuboresha utendaji
ambayo ni pamoja na: kuendelea kuwajengea
uwezo watumishi wa Wizara na Taasisi zake
katika kusimamia Sekta ya Nishati; kuendelea
kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi
wa Wizara na Taasisi zake ili kutoa huduma
bora zaidi; na kuendelea kuelimisha umma
na kuboresha mawasiliano kati ya Wizara
na wadau mbalimbali kuhusu masuala ya
nishati.
20
SEKTA NDOGO YA UMEME
HALI YA UPATIKANAJI WA UMEME NCHINI
19. Mheshimiwa Spika, hali ya umeme
nchini imeendelea kuimarika katika kipindi
chote cha mwaka 2018/19. Aidha, mahitaji
ya umeme nchini yameendelea kuongezeka
mwaka hadi mwaka kutokana na kukua
na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi
zinazohitaji nishati ya umeme wa kutosha,
wa uhakika na wa gharama nafuu katika
uzalishaji. Katika mwaka 2018/19 uwezo
wa mitambo ya kuzalisha umeme (installed
capacity) nchini umeongezeka na kufikia MW
1,601.90 kutoka MW 1,517.47 zilizofikiwa
mwaka 2017/18 sawa na ongezeko la asilimia
5.6. Kati ya jumla ya MW 1,601.90 zilizopo
nchini, MW 1,565.72 zimeunganishwa katika
mfumo wa Gridi ya Taifa na MW 36.18 zipo
nje ya mfumo wa Gridi ya Taifa.
20. Mheshimiwa Spika, matumizi ya
juu ya umeme yamefikia MW 1,116.58
ukilinganisha na MW 1,051.27 zilizofikiwa
mwaka 2017/18 sawa na ongezeko la
asilimia 6.2. Aidha, umeme uliozalishwa
nchini uliongezeka kutoka GWh 7,114
mwaka 2017 na kufikia GWh 7,374 mwaka
21
2018 sawa na ongezeko la asilimia 3.7. Hadi
kufikia mwaka 2015, nchi yetu ilikuwa na
uwezo wa kuzalisha umeme wa MW 1,204
ikilinganishwa na uwezo wa sasa wa MW
1,601.90 sawa na ongezeko la asilimia 33.
Katika kutimiza azma ya Tanzania kuwa
nchi ya uchumi wa viwanda, Serikali kupitia
Wizara ya Nishati imelenga kuzalisha umeme
wa MW 10,000 ifikapo mwaka 2025.
MIRADI YA KUZALISHA UMEME
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Mto Rufiji (Rufiji Hydro
Power Project) – MW 2,115
21. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme
wa MW 2,115 kwa kutumia maporomoko ya
maji ya Mto Rufiji. Mkataba wa ujenzi wa
mradi ulisainiwa tarehe 12 Desemba, 2018
kati ya TANESCO na Mkandarasi Kampuni
ya Arab Contractors na Elsewedy Electric
za nchini Misri. Tukio hili lilishuhudiwa na
Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Mhe. Waziri Mkuu wa Jamhuri
ya Misri. Mkandarasi huyo alikabidhiwa eneo
la mradi tarehe 14 Februari, 2019 na kuanza
utekelezaji wa kazi za awali. Katika kipindi
22
cha mwaka 2018/19, kazi zilizotekelezwa
ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa
miundombinu wezeshi ikijumuisha: njia ya
kusafirisha umeme wa MW 8 yenye msongo
wa kV 33 kutoka Msamvu, Morogoro hadi
eneo la mradi yenye urefu wa kilomita 170;
barabara za kiwango cha changarawe za
Ubena – Zomozi na Kibiti – Mloka hadi eneo
la mradi; mifumo ya maji; mawasiliano ya
simu; na nyumba za kuishi Mkandarasi.
Vilevile, kulingana na mahitaji ya umeme
wakati wa ujenzi, TANESCO imeanza ujenzi
wa njia ya pili ya umeme msongo wa kV 33
kutoka kituo cha kupoza umeme cha Gongo
la Mboto kupitia Kisarawe hadi eneo la
mradi urefu wa kilomita 245 itakayosafirisha
umeme wa MW 22.
22. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha mwaka 2019/20 Serikali itaendelea na
utekelezaji wa mradi huu muhimu ambapo
kazi zitakazofanyika ni pamoja na: kuanza
ujenzi wa bwawa (main dam and spillways);
kuanza ujenzi wa njia za kupitisha maji
(tunnels); na kukamilisha ujenzi wa njia ya pili
ya umeme msongo wa kV 33 kutoka Gongo
la Mboto. Fedha za ndani Shilingi trilioni
1.443 zimetengwa katika mwaka 2019/20
23
kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo. Utekelezaji
wa mradi umeanza mwezi Desemba, 2018
na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni,
2022. Kwa ujumla Serikali imedhamiria
kwa dhati kutekeleza Mradi huu bila
kuyumbishwa, kucheleweshwa wala
kukwamishwa na mtu yeyote kutoka
ndani au nje ya nchi asiyeitakia mema
nchi yetu.
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Rusumo – MW 80
23. Mheshimiwa Spika, mradi huu
wa nchi tatu (3) za Tanzania, Burundi
na Rwanda unahusu ujenzi wa kituo cha
kuzalisha umeme wa MW 80 kwa kutumia
maporomoko ya maji ya Mto Kagera kwa
mgawanyo sawa kwa kila nchi. Kwa upande
wa Tanzania, Mradi unagharimu Dola za
Marekani milioni 113 sawa na takriban
Shilingi bilioni 261.75 kwa ufadhili wa
Benki ya Dunia. Kazi zilizofanyika kwa
mwaka 2018/19 ni pamoja na: kukamilika
kwa ujenzi wa barabara za kuingia eneo la
Mradi; kukamilika kwa ujenzi wa kikinga maji
(coffer dam) na kukamilika kwa uchimbaji wa
eneo la kusimika mitambo (power house).
24
24. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kufanyika mwaka 2019/20 ni
pamoja na kujenga miundombinu ya kukinga
na kuingiza maji katika handaki (Dam
and Intake); ujenzi wa kituo cha kuzalisha
umeme (powerhouse); ufungaji wa mitambo
katika kituo cha kuzalisha umeme; ujenzi wa
kituo cha kupoza umeme (Switchyard); na
kukamilisha miradi ya kijamii kwa wananchi
wanaozunguka eneo la mradi (Local Area
Development Plan – LADP na Livelihood
Restoration Program - LRP). Fedha za nje
Shilingi bilioni 3 zimetengwa na Serikali
katika mwaka 2019/20 kwa ajili ya mradi
huu. Mradi huu umeanza mwaka 2017 na
unatarajiwa kukamilika mwezi Februari,
2020.
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Ruhudji – MW 358
25. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa kituo cha kufua umeme
wa MW 358 kwa kutumia maporomoko ya
maji ya Mto Ruhudji mkoani Njombe. Ujenzi
wa mradi huu utahusisha njia ya kusafirisha
umeme wa msongo wa kV 400 yenye urefu wa
kilomita 170 kutoka Ruhudji hadi kituo cha
kupoza umeme cha Kisada mkoani Iringa.
25
Katika mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika
ni pamoja na: Serikali kuanza majadiliano
ya ufadhili na Serikali ya China kwa ajili
ya kutekeleza mradi; na kumpata Mtaalam
Mshauri kwa ajili ya kuhuisha Upembuzi
Yakinifu. Ujenzi wa mradi unakadiriwa
kugharimu Dola za Marekani milioni 407.40
sawa na takriban Shilingi bilioni 943.70 na
ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme msongo
wa kV 400 unakadiriwa kugharimu Dola za
Marekani milioni 53.2 sawa na takriban
Shilingi bilioni 123.23.
26. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20 kazi zitakazofanyika ni pamoja na:
kukamilisha taratibu za ufadhili wa mradi;
kuhuisha Upembuzi Yakinifu (Updating of
feasibility study); kumpata Mtaalam Mshauri
wa kusimamia ujenzi wa mradi; na kumpata
Mkandarasi wa kujenga mradi. Jumla ya
Shilingi bilioni 12.50 zimetengwa katika
mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati
ya fedha hizo Shilingi bilioni 10.00 ni fedha
za ndani na Shilingi bilioni 2.50 ni fedha
za nje. Mradi huu unatarajiwa kuanza mwezi
Mei, 2020 na kukamilika mwezi Aprili, 2023.
26
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Rumakali – MW 222
27. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa kituo cha kuzalisha
umeme wa MW 222 kwa kutumia maji ya
Mto Rumakali mkoani Njombe na njia ya
kusafirisha umeme msongo wa kV 220 yenye
urefu wa kilomita 150 kutoka katika mitambo
hadi kituo cha kupoza umeme cha Iganjo
mkoani Mbeya. Gharama za mradi huu kwa
pamoja zinakadiriwa kuwa jumla ya Dola za
Marekani milioni 344.22 sawa na takriban
Shilingi bilioni 899.27. Katika kipindi
cha mwaka 2018/19 kazi zilizotekelezwa
ni pamoja na: kumtafuta Mtaalam Mshauri
kwa ajili ya kuhuisha Upembuzi Yakinifu wa
mradi uliofanyika mwaka 1998; na kuanza
usanifu wa miundombinu ya mradi.
28. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2019/20 kazi zitakazofanyika ni: kuhuisha Upembuzi Yakinifu (Updating of feasibility study); kumpata Mtaalam Mshauri wa kusimamia ujenzi wa mradi; kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa mradi; kufanya tathmini ya athari za mazingira na kijamii (ESIA); na kulipa fidia. Jumla ya Shilingi bilioni 3.50 zimetengwa katika mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya
27
fedha hizo Shilingi bilioni 1.0 ni fedha za ndani na Shilingi bilioni 2.50 ni fedha za nje. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwezi Januari, 2021 na kukamilika mwezi Juni, 2023.
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Kakono – MW 87
29. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa kituo cha kuzalisha
umeme wa MW 87 kwa kutumia maji ya
Mto Kagera na ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme wa msongo wa kV 220 kutoka
Kakono hadi Kyaka yenye urefu wa kilomita
38.8. Gharama za ujenzi wa mradi ni Dola
za Marekani milioni 380 zitakazotolewa na
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), Shirika
la Maendeleo la Ufaransa (AFD) na Shirika
la Maendeleo la Norway (NORAD). Kazi
zilizofanyika kwa mwaka 2018/19 ni pamoja
na: kukamilisha utafiti wa kijiolojia na
haidrolojia; kukamilisha usanifu wa awali wa
mradi; kufanya maandalizi ya zabuni kwa ajili
ya kumpata Mkandarasi wa Ujenzi; kuhuisha
tathmini ya athari za mazingira na kijamii
(updating ESIA); na kukamilisha mpango wa
kuhamisha wananchi wanaopisha ujenzi wa
mradi (Resettlement Action Plan - RAP).
28
30. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20 kazi zitakazofanyika ni: kutwaa
ardhi na kulipa fidia katika eneo la mradi;
na kutafuta Wakandarasi kwa ajili ya ujenzi
wa mradi na njia ya kusafirisha umeme ya
msongo wa kV 220. Jumla ya Shilingi bilioni
2.50 zimetengwa katika mwaka 2019/20
ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha hizo
Shilingi milioni 500 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 2 ni fedha za nje. Mradi huu
unatarajiwa kuanza mwezi Desemba, 2019
na kukamilika mwezi Desemba, 2022.
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Malagarasi – MW 45
31. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme
wa MW 45 kwa kutumia maporomoko ya maji
ya Mto Malagarasi mkoani Kigoma na ujenzi
wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa
kV 132 yenye urefu wa kilomita 53 kutoka
Malagarasi hadi Kidahwe mkoani Kigoma.
Gharama za utekelezaji wa Mradi ni Dola za
Marekani milioni 150.0 sawa na takriban
Shilingi bilioni 346.30. Katika kipindi cha
mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika ni pamoja
na kukamilisha: Upembuzi Yakinifu wa njia
ya kusafirisha umeme wa msongo wa kV
29
132; usanifu (design) wa miundombinu ya
mradi; upimaji na uthamini wa eneo la mradi
na njia ya kusafirisha umeme; na mpango
wa kuhamisha wananchi wanaopisha mradi.
32. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20 kazi zitakazofanyika ni pamoja na:
kutwaa ardhi na kulipa fidia kwa wananchi
watakaopisha mradi; kumpata Mtaalam
Mshauri na Wakandarasi kwa ajili ya ujenzi
wa mradi na njia ya umeme msongo wa kV
132. Jumla ya Shilingi bilioni 3 zimetengwa
katika mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi
hizo. Kati ya fedha hizo Shilingi milioni
600 ni fedha za ndani na Shilingi bilioni
2.40 ni fedha za nje. Ujenzi wa mradi huu
unatarajiwa kuanza mwezi Septemba, 2020
na kukamilika mwezi Septemba, 2023.
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Maji wa Kikonge – MW 300
33. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa Mtambo wa kuzalisha
umeme wa MW 300 kwa kutumia
maporomoko ya maji ya Mto Ruhuhu mkoani
Njombe na ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme wa msongo wa kV 132 yenye urefu
wa kilomita 53 kutoka Kikonge hadi kituo
30
cha kupoza umeme cha Madaba. Gharama za
utekelezaji wa mradi zinakadiriwa kuwa Dola
za Marekani Milioni 750 sawa na takriban
Shilingi trilioni 1.737. Mradi huu pia
unahusisha upatikanaji wa maji kwa ajili ya
umwagiliaji. Kazi zilizotekelezwa kwa mwaka
2018/19 ni kumpata Mtaalamu Mshauri
wa kufanya Upembuzi Yakinifu (Feasibility
Study) na Tathmini ya Kimkakati ya Mazingira
na Kijamii (Strategic Environmental & Social
Assessment – SESA). Kazi hizi zinafadhiliwa
na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).
34. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20 kazi zitakazofanyika ni: kukamilisha
Upembuzi Yakinifu pamoja na Tathmini ya
Kimkakati ya Mazingira na Kijamii (SESA);
kukamilisha majadiliano ya ufadhili wa ujenzi
wa mradi na kumpata Mtaalam Mshauri wa
kusimamia mradi. Jumla ya Shilingi bilioni
2.50 zimetengwa katika mwaka 2019/20
ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha hizo
Shilingi milioni 500 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 2 ni fedha za nje. Mradi huu
unatarajiwa kuanza mwezi Novemba, 2020
na kukamilika mwezi Oktoba, 2023.
31
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa Kutumia
Maji wa Murongo/Kikagati – MW 14
35. Mheshimiwa Spika, mradi huu wa nchi mbili za Tanzania na Uganda unahusu ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme wa MW 14 kwa kutumia maporomoko ya maji ya Mto Kagera na ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kV 33 yenye urefu wa kilomita 0.7 kutoka Kikagati (Uganda) hadi Murongo (Tanzania). Mradi utagharimu Dola za Marekani milioni 58 ambazo ni takriban Shilingi bilioni 134.35 na unatekelezwa na mwekezaji binafsi, Kampuni ya Kikagati Power Company Ltd (KPCL).
36. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika ni pamoja na: kukamilisha ujenzi wa kambi ya kudumu ya wafanyakazi na miundombinu ya barabara za kuingia eneo la mradi; usanifu wa mitambo na vifaa ya umeme; na ujenzi wa miundombinu ya kukinga na kuingiza maji (Dam and Intake) na njia za kupitisha maji (waterways). Kazi zitakazotekelezwa kwa mwaka 2019/20 ni pamoja na: kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya kuzalisha umeme; na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme ya msongo wa kV 33. Mradi huu ulianza mwezi Novemba, 2017 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2020.
32
Matengenezo ya Mtambo wa Kuzalisha
Umeme wa Hale (Rehabilitation of Hale
Hydro Power Plant) – MW 21
37. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu uboreshaji wa mifumo ya uendeshaji
na ukarabati wa mitambo ya kufua umeme
kwa kutumia maji wa Hale mkoani Tanga.
Gharama za mradi huu zinakadiriwa kuwa
SEK milioni 200 ambazo ni takriban Shilingi
bilioni 50.96 zitakazotolewa na Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
kushirikiana na Serikali ya Sweden kupitia
Shirika lake la Maendeleo la Kimataifa (Sida).
Kazi zilizofanyika katika mwaka 2018/19 ni
kukamilisha taratibu za kumpata Mkandarasi
wa ukarabati wa mitambo.
38. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kufanyika mwaka 2019/20 ni pamoja
na kuanza uchimbaji wa handaki la kuingia
katika kituo cha kuzalisha umeme (access
tunnel). Jumla ya Shilingi bilioni 7.80
zimetengwa kutekeleza kazi hizo ambapo
kati ya fedha hizo Shilingi milioni 300 ni
fedha za ndani na Shilingi bilioni 7.50 ni
fedha za nje. Kazi za ukarabati zinatarajiwa
kuanza mwezi Agosti, 2019 na kukamilika
ifikapo mwezi Desemba, 2021.
33
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa Kutumia
Gesi Asilia wa Kinyerezi II – MW 240
39. Mheshimiwa Spika, ujenzi wa
mradi huu ulianza mwezi Machi, 2016 kwa
gharama ya Dola za Marekani milioni 344,
sawa na takriban Shilingi bilioni 794.12.
Mradi huu ulihusu ujenzi wa kituo cha
kuzalisha umeme wa MW 240 kwa kutumia
gesi asilia katika eneo la Kinyerezi Jijini
Dar es Salaam. Kituo hiki chenye jumla ya
mitambo nane (8), ambapo mitambo sita (6)
ni ya kutumia gesi asilia (gas turbines) na
mitambo miwili (2) ni ya kutumia mvuke
(steam turbines) kilikamilika na kukabidhiwa
rasmi kwa TANESCO mwezi Desemba, 2018.
Kukamilika kwa kituo hiki kumeongeza
jumla ya MW 248.22 katika Gridi ya Taifa.
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Gesi Asilia wa Kinyerezi I
Extension – MW 185
40. Mheshimiwa Spika, mradi huu
ambao upo katika hatua za mwisho za
utekelezaji unahusu upanuzi wa kituo cha
Kinyerezi I – MW 150 kwa kuongeza mitambo
itakayozalisha MW 185 na kufanya kituo
hicho kuzalisha jumla ya MW 335. Mradi
34
huu unagharamiwa na Serikali ya Tanzania
kwa asilimia 100 kwa gharama ya Dola za
Marekani milioni 188 sawa na takriban
Shilingi bilioni 435.48. Katika mwaka
2018/19 kazi zilizofanyika ni pamoja na:
kukamilika kwa utengenezwaji wa mitambo
yote minne (4) na kuanza kufungwa katika
eneo la mradi; kukamilika kwa upanuzi wa
kituo cha kupoza umeme cha Kinyerezi I kV
220 na kuendelea na upanuzi (upgrade) wa
njia ya msongo wa kV 132 kutoka Kinyerezi
I hadi kituo cha kupoza umeme cha Gongo la
Mboto. Ujenzi wa mradi huu ulianza mwezi
Juni, 2016 na unatarajiwa kukamilika mwezi
Agosti, 2019.
41. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha mwaka 2019/20 kazi zitakazotekelezwa
ni kukamilisha ufungaji wa mitambo na
kuingiza jumla ya MW 185 katika Gridi ya
Taifa. Fedha za ndani Shilingi bilioni 60.00
zimetengwa katika mwaka 2019/20 kwa ajili
ya kutekeleza kazi hizo.
35
Mradi wa Kuzalisha Umeme kwa
Kutumia Gesi Asilia wa Mtwara – MW 300
42. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa mitambo ya kuzalisha
MW 300 kwa kutumia gesi asilia katika Mkoa
wa Mtwara. Gharama za mradi zinakadiriwa
kuwa Dola za Marekani milioni 360 sawa
na takriban Shilingi bilioni 833.90. Mradi
huu utatekelezwa kwa ufadhili wa Serikali
ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo
(JICA) kwa kushirikiana na Serikali. Kazi
zilizofanyika katika mwaka 2018/19 ni
pamoja na: kukamilika kwa Upembuzi
Yakinifu (Feasibility Study) wa kituo cha
kuzalisha umeme na miundombinu wezeshi
ya maji, barabara na gesi asilia.
43. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20 kazi zitakazofanyika ni pamoja na
kukamilisha uthamini na kulipa fidia kwa
wananchi wanaopisha ujenzi wa mradi;
kumpata Mtaalam Mshauri wa kusimamia
ujenzi wa mradi; na kumpata Mkandarasi wa
ujenzi wa mradi. Jumla ya Shilingi bilioni
4.20 zimetengwa katika mwaka 2019/20
kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha hizo
Shilingi bilioni 1.00 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 3.20 ni fedha za nje. Mradi
36
huu unatarajiwa kuanza mwishoni mwa
mwezi Machi, 2020 na kukamilika mwezi
Septemba, 2022.
Miradi ya Kufua Umeme Utokanao na Jua – MW 150, Upepo – MW 200 na
Makaa ya Mawe – MW 600
44. Mheshimiwa Spika, mwezi Septemba 2018, Serikali kupitia TANESCO ilitangaza miradi ya nishati jadidifu (Jua – MW 150 na Upepo – MW 200) na Makaa ya Mawe – MW 600 kwa wawekezaji binafsi. Lengo ni kupata miradi ya kuzalisha umeme wa jumla ya MW 950 kwa njia ya ushindani na kuingizwa katika Gridi ya Taifa. Hadi kufikia mwezi Februari, 2019 tathmini ya zabuni kwa kampuni zilizoshiriki ilikamilika. Taratibu zinazoendelea kwa sasa ni kampuni zilizopita hatua ya awali kuwasilisha mapendekezo ya namna bora ya kuendeleza
miradi husika baada ya kupatiwa Request for
Proposals (RFPs).
45. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha mwaka 2019/20, TANESCO itakamilisha
taratibu za kuwapata wawekezaji binafsi
wenye bei nafuu na kuanza utekelezaji wa
miradi hiyo. Utekelezaji wa miradi hii nafuu
utapunguzia Shirika gharama za uendeshaji
37
na hivyo kuwepo matarajio ya kushuka kwa
bei ya umeme. Utekelezaji huo unatarajiwa
kuanza mwezi Novemba, 2019 na kukamilika
mwezi Oktoba, 2022.
MIRADI YA KUSAFIRISHA UMEME
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400 wa Singida –
Arusha – Namanga
46. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 400 yenye urefu wa
kilomita 414 kutoka Singida hadi Namanga
kupitia Arusha. Mradi huu pia unahusisha
ujenzi wa kituo kipya cha kupoza umeme
katika eneo la Kisongo mkoani Arusha,
upanuzi wa kituo cha kupoza umeme (bay
addition) cha Singida na usambazaji wa umeme
katika vijiji 22 vinavyopitiwa na mradi. Mradi
huu unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB), Shirika la Maendeleo la Japan
(JICA) na Serikali ya Tanzania. Gharama ya
mradi ni Dola za Marekani milioni 258.82
sawa na takriban Shilingi bilioni 599.53.
Kazi zilizofanyika kwa mwaka 2018/19 ni
kulipa fidia na kuanza shughuli za ujenzi
wa mradi.
38
47. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kufanyika kwa mwaka 2019/20 ni:
kuendelea na ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme na vituo vya kupoza umeme. Jumla
ya Shilingi bilioni 4 fedha za nje zimetengwa
katika mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi
hizo. Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi
Machi, 2017 na unatarajiwa kukamilika
mwezi Machi, 2020.
48. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa
mradi huu ni sehemu ya utekelezaji wa mradi
wa Backbone awamu ya pili (Backbone Phase
II) unaohusu kuongeza uwezo (upgrade)
wa vituo vya kupoza umeme kutoka kV
220 mpaka kV 400 katika mikoa ya Iringa
na Shinyanga kwa ufadhili wa Benki ya
Uwekezaji ya Ulaya (EIB) na katika mikoa ya
Singida na Dodoma kwa ufadhili wa Benki
ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Shirika la
Maendeleo la Japan (JICA).
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 220 kutoka Makambako
hadi Songea na Kusambaza Umeme
Vijijini kwa Mikoa ya Njombe na Ruvuma
49. Mheshimiwa Spika, mradi wa ujenzi
wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa
39
kV 220, yenye urefu wa kilomita 250 kutoka
Makambako hadi Songea kupitia Madaba
pamoja na ujenzi wa vituo vya kupoza
umeme vya Madaba na Songea na upanuzi
wa kituo cha Makambako ulianza mwezi
Mei, 2016 na kukamilika mwezi Septemba,
2018. Mradi huu ulizinduliwa rasmi na Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Dkt. John Pombe Joseph Magufuli tarehe
06 Aprili, 2019. Hadi kufikia tarehe 15 Mei,
2019 jumla ya vijiji 112 kati ya 122 vilikuwa
vimeunganishwa umeme. Jumla ya wateja
wapatao 22,700 wanatarajiwa kuunganishwa
umeme kupitia mradi huu katika wilaya
za Makambako, Njombe na Ludewa katika
Mkoa wa Njombe; na Songea Vijijini, Songea
Mjini, Namtumbo na Mbinga katika Mkoa
wa Ruvuma. Gharama ya mradi huu ilikuwa
ni Shilingi bilioni 216 chini ya ufadhili wa
Serikali za Tanzania na Sweden.
50. Mheshimiwa Spika, kazi
zilizopangwa kufanyika mwaka 2019/20
ni: kuendelea kuunganisha wateja ikiwemo
Vijiji vya Lutikila, Ifinga na Mbangamawe
mkoani Ruvuma vilivyoongezeka pamoja
na kukamilisha kazi ya kufunga Reactor na
Distribution Panels katika vituo vya kupoza
40
umeme vya Makambako, Madaba na Songea.
Jumla ya Shilingi bilioni 2.50 zimetengwa
katika mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi
hizo. Kati ya fedha hizo Shilingi bilioni 2 ni
fedha za ndani na Shilingi milioni 500 ni
fedha za nje.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 220 Bulyanhulu – Geita
51. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi ni kujenga njia ya kusafirisha umeme msongo wa kV 220 yenye urefu wa kilomita 55 kutoka Bulyanhulu hadi Geita. Mradi huu unahusisha ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Geita kV 220, upanuzi wa kituo cha kupoza umeme cha Bulyanhulu, usambazaji wa umeme katika vijiji 10 vilivyopo ndani ya eneo la mradi na kubadilisha mita za umeme za kawaida (conventional meters) 1,500 mkoani Geita. Gharama za mradi huu ni Dola za Marekani milioni 23 sawa na takriban Shilingi bilioni 53.28. Kazi zilizofanyika kwa mwaka 2018/19 ni kupatikana kwa Mkandarasi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme; kuanza ujenzi wa kituo cha kupoza umeme; kupatikana kwa
Mkandarasi wa usambazaji umeme vijijini;
na kulipa fidia kwa wananchi wanaopisha
mradi.
41
52. Mheshimiwa Spika, kazi
zitakazofanyika mwaka 2019/20 ni
kukamilisha: ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme; ujenzi wa kituo cha kupoza umeme
mkoani Geita; upanuzi wa kituo cha kupoza
umeme cha Bulyanhulu; ujenzi wa njia za
kusambaza umeme za msongo wa kV 33 na
kV 0.4 katika vijiji 10; na kuunganisha wateja
wapya 1,500. Jumla ya Shilingi bilioni
4.10 zimetengwa katika mwaka 2019/20
ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha hizo
Shilingi bilioni 1.50 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 2.60 ni fedha za nje. Ujenzi
wa mradi huu ulianza mwezi Januari, 2019
na unatarajiwa kukamilika mwezi Mei, 2020.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa
Msongo wa kV 220 Geita – Nyakanazi
53. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 220 yenye urefu
wa kilomita 133, kituo cha kupoza umeme
Nyakanazi na kusambaza umeme katika
vijiji 32 vinavyopitiwa na mradi. Gharama za
utekelezaji wa mradi huu ni EURO milioni
45 sawa na takriban Shilingi bilioni 117.79.
Kazi zilizofanyika kwa mwaka 2018/19 ni:
kukamilisha upatikanaji wa Mkandarasi;
42
kukamilisha uhakiki wa mali za wananchi
watakaopisha mradi na kuanza kulipa fidia.
54. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kufanyika mwaka 2019/20 ni
kuanza: ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
kutoka Geita hadi Nyakanazi; ujenzi wa
kituo cha kupoza umeme cha Nyakanazi;
upanuzi wa kituo cha kupoza umeme cha
Geita kitakachojengwa kupitia Mradi wa
Bulyanhulu – Geita; na usambazaji wa
umeme katika vijiji 32. Fedha za nje Shilingi
bilioni 1 zimetengwa katika mwaka 2019/20
kwa ajili ya kazi hizo. Ujenzi wa mradi huu
utaanza mwezi Agosti, 2019 na kukamilika
mwezi Julai, 2021.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 220 Rusumo – Nyakanazi
55. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
msongo wa kV 220 yenye urefu wa kilomita
98.2 kutoka kituo cha kuzalisha umeme
cha Rusumo hadi Nyakanazi. Gharama za
mradi ni Dola za Marekani milioni 35 sawa
na takriban Shilingi bilioni 81.07. Mradi
huu unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB) na Serikali ya Tanzania. Katika
43
mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika ni pamoja
na: kumpata Mkandarasi ambaye ni ubia
kati ya Kampuni ya Sterling & Wilson Pvt
ya India na Electromontaji S.A ya Romania;
kulipa fidia kwa wananchi wanaopisha
mradi, ambapo takriban Shilingi bilioni
2.5 kutoka vyanzo vya ndani vya TANESCO
zitatumika kulipa fidia hiyo; na Mkandarasi
kuanza kazi za awali za ujenzi wa mradi. Kazi
zilizopangwa kufanyika mwaka 2019/20 ni:
kujenga njia ya kusafirisha umeme. Fedha za
nje Shilingi bilioni 2.32 zimetengwa katika
mwaka 2019/20 kwa ajili ya shughuli za
mradi huu. Mradi huu unatarajiwa kuanza
Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2020.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400, Iringa - Mbeya –
Tunduma - Sumbawanga – Mpanda -
Kigoma – Nyakanazi (North West Grid)
56. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 400 kutoka Iringa -
Mbeya – Tunduma - Sumbawanga – Mpanda
- Kigoma – Nyakanazi yenye urefu wa kilomita
1,384. Mradi huu utatekelezwa kwa awamu
tatu kama ifuatavyo:
44
Awamu ya Kwanza: Ujenzi wa Njia ya
Kusafirisha Umeme Msongo wa kV 400
kutoka Iringa – Mbeya – Tunduma hadi
Sumbawanga
57. Mheshimiwa Spika, awamu hii
inahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
msongo wa kV 400 kutoka Iringa kupitia
Mbeya, Tunduma hadi Sumbawanga yenye
urefu wa kilomita 624. Mradi huu utahusisha
ujenzi wa vituo vya kupoza umeme vya Iringa,
Mbeya, Tunduma na Sumbawanga. Mradi
utagharimu jumla ya Dola za Marekani
milioni 465, sawa na takriban Shilingi
trilioni 1.08 na utafadhiliwa na Benki ya
Dunia (WB), Shirika la Maendeleo la Ufaransa
(AFD) na Serikali ya Tanzania. Hadi sasa
Benki ya Dunia imetoa Dola za Marekani
milioni 365, sawa na takriban Shilingi
bilioni 845.49. Kazi zilizofanyika kwa mwaka
2018/19 ni pamoja na kukamilisha taarifa
ya awali ya Upembuzi Yakinifu kati ya Mbeya
na Sumbawanga; kuanza uthamini wa mali
kwa wananchi watakaopisha mradi pamoja
na kuanza taratibu za kumpata Mkandarasi
wa mradi.
45
58. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kufanyika mwaka 2019/20 ni:
kukamilisha uthamini na kulipa fidia kwa
wananchi watakaopisha eneo la mradi;
kumpata Mtaalam Mshauri wa kusimamia
ujenzi wa mradi; na kumpata Mkandarasi
wa mradi. Jumla ya Shilingi bilioni 6.35
zimetengwa katika mwaka 2019/20 ili
kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha hizo
Shilingi bilioni 5 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 1.35 ni fedha za nje.
Shughuli za ujenzi zinatarajiwa kuanza
mwezi Desemba, 2019 na kukamilika
mwezi Novemba, 2022. Mradi huu ni kati ya
miradi ya kikanda itakayounganisha njia za
umeme kati ya nchi yetu na nchi jirani za
SADC kupitia Zambia. Serikali itaendelea
kutoa kipaumbele katika utekelezaji wa
miradi ya namna hii ili pamoja na faida
nyingine, kuwezesha nchi yetu kuuza
umeme katika nchi nyingine.
Awamu ya Pili: Ujenzi wa Njia ya
Kusafirisha Umeme Msongo wa kV 400
kutoka Nyakanazi hadi Kigoma
59. Mheshimiwa Spika, awamu hii
itahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
msongo wa kV 400 kutoka Nyakanazi hadi
46
Kigoma yenye urefu wa kilomita 280, ujenzi
wa kituo cha kupoza umeme Kidahwe Mkoani
Kigoma, upanuzi wa kituo cha kupoza
umeme (bay addition) cha Nyakanazi na
usambazaji umeme katika vijiji 38. Gharama
za mradi ni Dola za Marekani milioni 187
sawa na takriban Shilingi bilioni 433.17
zitakazotolewa na Benki ya Maendeleo ya
Afrika (AfDB) pamoja na Shirika la Maendeleo
la Korea (EDCF). Kazi zilizofanyika kwa mwaka
2018/19 ni: kumpata Mtaalam Mshauri wa
kusimamia ujenzi wa mradi; uthamini wa
mali zitakazoathiriwa na ujenzi wa mradi;
na kupata eneo la kujenga kituo cha kupoza
umeme Kidahwe mkoani Kigoma.
60. Mheshimiwa Spika, kazi
zilizopangwa kufanyika mwaka 2019/20
ni: kuhakiki na kulipa fidia kwa wananchi
watakaopisha mradi na kumpata Mkandarasi
wa ujenzi wa mradi. Jumla ya Shilingi
bilioni 4.50 zimetengwa katika mwaka
2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya
fedha hizo Shilingi bilioni 3.50 ni fedha za
ndani na Shilingi bilioni 1.0 ni fedha za nje.
Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kuanza
mwezi Desemba, 2019 na kukamilika mwezi
Desemba, 2021.
47
Awamu ya Tatu: Ujenzi wa Njia ya
Kusafirisha Umeme Msongo wa kV 400
kutoka Sumbawanga – Mpanda – Kigoma
61. Mheshimiwa Spika, awamu hii
inahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
msongo wa kV 400 kutoka Sumbawanga
hadi Kigoma kupitia Mpanda yenye urefu wa
kilomita 480. Mradi huu utagharimu Dola
za Marekani milioni 165 sawa na takriban
Shilingi bilioni 382.21. Benki ya Dunia
imeonesha nia ya kufadhili ujenzi wa njia ya
kusafirisha umeme na Shirika la Maendeleo
la Korea (EDCF) limeonesha nia ya kufadhili
kituo cha kupoza umeme cha Mpanda.
Kazi iliyofanyika kwa mwaka 2018/19 ni
kuendelea na majadiliano na Washirika wa
Maendeleo kuhusu upatikanaji wa fedha
kufadhili mradi huu.
62. Mheshimiwa Spika, kazi
zilizopangwa kufanyika kwa mwaka 2019/20
ni: kufanya tathmini ya mali za wananchi
zitakazoathiriwa na mradi; kuendelea na
majadiliano na Washirika wa Maendeleo
kuhusu ufadhili wa mradi; na kuandaa
nyaraka za zabuni za kumpata Mtaalam
Mshauri wa kusimamia mradi. Jumla
ya Shilingi milioni 500 fedha za ndani
48
zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo.
Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kuanza
mwezi Julai, 2021 na kukamilika mwezi
Juni, 2024.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400 Rufiji – Chalinze –
Dodoma
63. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 400 yenye urefu wa
kilomita 512 kutoka kituo cha kuzalisha
umeme Rufiji hadi Dodoma kupitia Chalinze
Mkoa wa Pwani. Mradi huu pia unahusisha
upanuzi wa vituo vya kupoza umeme (bay
addition) katika Mji wa Chalinze na Jiji la
Dodoma pamoja na kusambaza umeme
katika vijiji 37 vitakavyopitiwa na mradi.
Gharama za mradi zinakadiriwa kuwa Dola
za Marekani milioni 276.36 sawa na
takriban Shilingi bilioni 640.08. Katika
kipindi cha mwaka 2018/19 kazi iliyofanyika
ni kumpata Mtaalam Mshauri kwa ajili ya
kufanya Upembuzi Yakinifu wa mradi kutoka
Rufiji hadi Chalinze.
64. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kwa mwaka 2019/20 ni: kukamilisha
49
Upembuzi Yakinifu; kufanya uthamini wa
mali za wananchi watakaopisha mradi na
kulipa fidia; kumpata Mtaalam Mshauri wa
kusimamia mradi; na kumpata Mkandarasi
wa kujenga njia ya kusafirisha umeme.
Jumla ya Shilingi bilioni 11 zimetengwa
katika mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi
hizo. Kati ya fedha hizo Shilingi bilioni 8 ni
fedha za ndani na Shilingi bilioni 3 ni fedha
za nje. Mradi huu unatarajiwa kuanza mwezi
Machi, 2020 na kukamilika mwezi Desemba,
2021.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400 kutoka Kinyerezi
hadi Chalinze
65. Mheshimiwa Spika, mradi huu
utahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 400 yenye urefu wa
kilomita 115 kutoka Kinyerezi mkoani Dar es
Salaam hadi Chalinze mkoani Pwani pamoja
na ujenzi wa kituo cha kupoza umeme
Kinyerezi. Gharama za mradi zinakadiriwa
kuwa Dola za Marekani milioni 120 ambazo
ni takriban Shilingi bilioni 282. Katika
kipindi cha mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika
ni pamoja na: kukamilisha taratibu za kulipa
fidia kwa wananchi watakaopisha mradi;
50
na kuanza taratibu za kumpata Mtaalam
Mshauri kwa ajili ya kufanya Upembuzi
Yakinifu wa njia ya kusafirisha umeme.
66. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa mwaka 2019/20 ni: kukamilisha
Upembuzi Yakinifu; kulipa fidia kwa
wananchi watakaopisha mradi; na kumpata
Mkandarasi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme na kituo cha kupoza umeme. Jumla
ya Shilingi bilioni 15 zimetengwa katika
mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati
ya fedha hizo Shilingi bilioni 12 ni fedha
za ndani ambazo zitatumika kulipa fidia na
Shilingi bilioni 3 ni fedha za nje. Mradi
huu unatarajiwa kuanza mwezi Julai, 2020
na kukamilika mwezi Desemba, 2021.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme wa
North – East Grid (Chalinze – Segera kV
400, Segera – Tanga kV 220,
Kibaha – Bagamoyo kV 220)
67. Mheshimiwa Spika, mradi huu
utahusisha ujenzi wa: njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 400 yenye urefu
wa kilomita 104 kutoka Chalinze kwenda
Segera; njia ya umeme msongo ya kV 220
yenye urefu wa kilomita 64 kutoka Segera
51
kwenda Tanga na kilomita 40 kutoka Kibaha
kwenda Bagamoyo; na kujenga vituo vya
kupoza umeme (bay addition) vya Chalinze,
Segera, Bagamoyo na Tanga. Gharama za
mradi zinakadiriwa kuwa Shilingi bilioni
468. Katika kipindi cha mwaka 2018/19 kazi
zilizofanyika ni pamoja na: kumpata Mtaalam
Mshauri kwa ajili ya kufanya Upembuzi
Yakinifu wa mradi; na kuainisha mipaka
ya mkuza wa njia ya kusafirisha umeme na
kutathmini mali za wananchi watakaopisha
mradi katika eneo kati ya Segera na Tanga.
68. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa mwaka 2019/20 ni: kufanya
Upembuzi Yakinifu; na kuwapata Wakanda-
rasi wa ujenzi wa njia za kusafirisha umeme
na vituo vya kupoza umeme. Jumla ya
Shilingi bilioni 3 zimetengwa katika mwaka
2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha
hizo Shilingi bilioni 2 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 1.0 ni fedha za nje. Ujenzi
wa mradi huu unatarajiwa kuanzia mwezi
Julai, 2020 na kukamilika Juni, 2022.
52
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400 Mwanza – Masaka
69. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kuunganisha nchi ya Tanzania na
Uganda kwa kujenga njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 400 kutoka Mwanza,
Tanzania hadi Masaka, Uganda kupitia
mikoa ya Geita na Kagera. Gharama za mradi
huu zinakadiriwa kuwa Dola za Marekani
milioni 75 sawa na takriban Shilingi bilioni
173.73. Kazi iliyofanyika katika mwaka
2018/19 ni majadiliano na Benki ya Dunia
ili kupata fedha za kudurusu taarifa ya awali
ya Upembuzi Yakinifu. Kazi zitakazofanyika
kwa mwaka 2019/20 ni kudurusu Upembuzi
Yakinifu wa mradi na kutafuta ufadhili wa
ujenzi wa mradi. Jumla ya Shilingi bilioni
3 zimetengwa katika mwaka 2019/20 ili
kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha hizo
Shilingi milioni 500 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 2.50 ni fedha za nje. Mradi
huu unatarajiwa kuanza mwezi Machi,
2021 na kukamilika mwezi Septemba, 2023.
Utekelezaji wa mradi huo pamoja na
manufaa mengine, utaiwezesha nchi yetu
kuuza umeme kwa nchi jirani.
53
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400 kutoka Mtwara hadi
Somanga Fungu
70. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
msongo wa kV 400 yenye urefu wa kilomita
253 kutoka Mtwara hadi Somanga Fungu na
ujenzi wa kituo cha kupoza umeme katika
Mkoa wa Mtwara pamoja na kusambaza
umeme katika vijiji 29 vinavyopitiwa na mradi.
Gharama za mradi ni Dola za Marekani
milioni 230 sawa na takriban Shilingi bilioni
532.77. Fedha hizi zitatolewa na Serikali
ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo
(JICA), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB)
na Serikali ya Tanzania. Katika kipindi cha
mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika ni pamoja
na kukamilisha Upembuzi Yakinifu.
71. Mheshimiwa Spika, kazi
zilizopangwa kwa mwaka 2019/20 ni:
kufanya tathmini ya athari za mazingira
na kijamii; kufanya uthamini na kulipa
fidia kwa wananchi watakaopisha mradi;
kumpata Mtaalam Mshauri kwa ajili ya
usimamizi wa utekelezaji wa mradi; na
kumpata Mkandarasi wa ujenzi wa mradi.
Jumla ya Shilingi bilioni 10 zimetengwa
54
katika mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi
hizo. Kati ya fedha hizo Shilingi bilioni 3 ni
fedha za ndani na Shilingi bilioni 7 ni fedha
za nje. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza
mwezi Machi, 2020 na kukamilika mwezi
Aprili, 2022.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 400 kutoka Somanga
Fungu hadi Kinyerezi
72. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kujenga njia ya kusafirisha umeme wa
msongo wa kV 400 kutoka Somanga Fungu
mkoani Lindi hadi Kinyerezi Mkoani Dar es
Salaam yenye urefu wa kilomita 198. Gharama
za Mradi ni Dola za Marekani milioni 150
sawa na takriban Shilingi bilioni 347.46.
Kazi zilizofanyika kwa mwaka 2018/19
ni kukamilika kwa Upembuzi Yakinifu
na kuendelea kulipa fidia kwa wananchi
wanaopisha mradi. Hadi kufikia mwezi Mei,
2019 wananchi 3,085 kati ya 3,901 sawa na
asilimia 79 walikuwa wameshalipwa fidia ya
Shilingi bilioni 56 kati ya Shilingi bilioni
69.14.
73. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kwa mwaka 2019/20 ni: kukamilisha
55
malipo ya fidia kwa wananchi wanaopisha
mradi; kumpata Mtaalam Mshauri; na
kumpata Mkandarasi. Jumla ya Shilingi
bilioni 8.65 zimetengwa katika mwaka
2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya
fedha hizo Shilingi bilioni 5.80 ni fedha za
ndani na Shilingi bilioni 2.85 ni fedha za
nje. Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kuanza
mwezi Desemba, 2020 na kukamilika mwezi
Februari, 2022.
Mradi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 132 kutoka Tabora hadi
Kidahwe Mkoani Kigoma na kutoka
Tabora hadi Nsimbo Mkoani Katavi
74. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme msongo wa kV 132 yenye urefu wa
kilomita 391 kutoka Tabora hadi Kidahwe
mkoani Kigoma kupitia Urambo, Kaliua na
Nguruka na vituo vyake vya kupoza umeme
pamoja na ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme wa msongo wa kV 132 yenye urefu
wa kilomita 381 kutoka Tabora hadi Nsimbo
mkoani Katavi kupitia Ipole na Inyonga.
Gharama za mradi huu zinakadiriwa kuwa
Dola za Marekani milioni 92 sawa na
takriban Shilingi bilioni 213.11. Mradi huu
56
unatekelezwa na TANESCO kwa kutumia
wataalam wa Shirika na utafanikisha azma
ya Serikali ya kuiunganisha mikoa ya
Katavi na Kigoma katika Gridi ya Taifa. Kazi
zilizofanyika mwaka 2018/19 ni pamoja na:
kukamilisha Upembuzi Yakinifu wa awali
(Pre-feasibility Study); kuainisha mipaka ya
mkuza wa njia ya usafirishaji umeme; na
upatikanaji wa eneo la kujenga vituo cha
kupoza umeme.
75. Mheshimiwa Spika, kazi
zilizopangwa kwa mwaka 2019/20 ni:
kufanya tathmini ya athari za mazingira na
jamii; kufanya uthamini wa mali za wananchi
watakaopisha mradi; kulipa fidia; na kuanza
ujenzi wa mradi. Jumla ya Shilingi bilioni
1.50 fedha za ndani zimetengwa katika
mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi hizo.
Aidha, TANESCO imetenga Shilingi bilioni
4.80 kutoka katika mapato yake kwa ajili
ya utekelezaji wa mradi huo ambao ulianza
mwezi Januari, 2019 na unatarajiwa
kukamilika mwezi Agosti, 2020.
57
Ujenzi wa Njia ya Kusafirisha Umeme
Msongo wa kV 220 na Kituo cha Kupoza
Umeme katika Mkoa wa Simiyu
76. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme
msongo wa kV 220 yenye urefu wa kilomita
160 kutoka kituo cha kupoza umeme cha
Ibadakuli Mkoani Shinyanga hadi kituo cha
kupoza umeme cha Imalilo Mkoani Simiyu.
Gharama ya mradi inakadiriwa kuwa Shilingi
bilioni 75. Kazi zilizopangwa kwa mwaka
2019/20 ni: kufanya Upembuzi Yakinifu;
kufanya tathmini ya athari za mazingira na
kijamii; kuainisha mipaka ya mkuza wa njia
ya usafirishaji umeme; na kufanya uthamini
wa mali za wananchi watakaopisha mradi.
Jumla ya Shilingi milioni 100 fedha za
ndani zimetengwa katika mwaka 2019/20
ili kutekeleza kazi hizo. Aidha, TANESCO
imetenga Shilingi milioni 300 kutoka katika
mapato yake kwa ajili ya kutekeleza mradi
huo. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza
mwezi Julai, 2020 na kukamilika mwezi
Desemba, 2021.
58
MIRADI YA KUBORESHA NJIA ZA
USAMBAZAJI UMEME
Mradi wa Kuboresha Mfumo wa
Usambazaji Umeme katika Jiji
la Dodoma
77. Mheshimiwa Spika, mradi huu
utahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha
umeme ya msongo wa kV 220 kutoka Zuzu
kwenda Msalato na kutoka Zuzu kwenda
Kikombo pamoja na ujenzi wa vituo viwili (2)
vya kupoza umeme katika maeneo ya Msalato
na Kikombo mkoani Dodoma. Gharama ya
mradi ni Dola za Marekani milioni 167.7
sawa na takriban Shilingi bilioni 388.46.
Kazi zilizofanyika mwaka 2018/19 ni pamoja
na kukamilisha Upembuzi Yakinifu wa njia
ya kusafirisha umeme msongo wa kV 220;
njia ya kusambaza umeme msongo wa kV
33; vituo vya kupoza umeme vya Haneti na
Narco; na kuendelea na taratibu za kupata
ufadhili wa mradi kutoka Serikali ya Japan
kupitia Shirika lake la Maendeleo la Kimataifa
(JICA).
78. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kwa mwaka 2019/20 ni kukamilisha
taratibu za ufadhili wa mradi na kuanza
59
utekelezaji. Katika mwaka 2019/20 jumla
ya Shilingi bilioni 5.4 zimetengwa kwa
ajili ya kutekeleza kazi hizo. Kati ya fedha
hizo Shilingi milioni 400 ni fedha za ndani
na Shilingi bilioni 5 ni fedha za nje. Mradi
huu unatarajiwa kuanza mwezi Juni, 2020
na kukamilika mwaka 2022.
79. Mheshimiwa Spika, pamoja na
juhudi hizo za ujenzi wa njia za usafirishaji
umeme katika Jiji la Dodoma, Serikali pia
imedhamiria kuufanya Mji Mpya wa Serikali
kuwa Mji wa kisasa na wa Kimataifa. Katika
hatua hiyo, Serikali kupitia TANESCO
inadhamiria kusambaza umeme katika Mji
huo kwa kutumia nyaya za chini ya ardhi
(underground cables). Gharama za Mradi huo
zinakadiriwa kuwa jumla ya Shilingi bilioni
16.9.
Mradi wa Usambazaji Umeme kwa
Maeneo ya Mijini
(Urban Electrification Program)
80. Mheshimiwa Spika, lengo la mradi
huu ni kuwezesha TANESCO kuongeza kasi
ya kuunganisha wateja maeneo ya mijini
kwa kupanua miundombinu ya kusambaza
umeme ili kuhamasisha ujenzi wa viwanda.
Kazi zilizofanyika kwa mwaka 2018/19 ni
60
kuendelea na ujenzi wa njia za usambazaji
umeme katika maeneo mbalimbali ambapo
jumla ya kilomita 592 za msongo wa kV
33, kilomita 1,550 za msongo wa kV 0.4
zimejengwa na kufunga mashineumba 683
na kuunganisha jumla ya wateja 112,308.
Utekelezaji wa kazi hizo umegharimu jumla
ya Shilingi bilioni 82.2 kupitia mapato ya
ndani ya TANESCO. Serikali imeendelea
kujadiliana na washirika wa maendeleo
wakiwemo Benki ya Dunia na Benki ya
Maendeleo ya Afrika kwa ajili ya utekelezaji
endelevu wa mradi.
81. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kutekelezwa kwa mwaka 2019/20
ni: kuendelea kutanua wigo wa usambazaji
wa umeme mijini na maeneo ya pembezoni
mwa miji yanayohitaji umeme katika mikoa
yote ya Tanzania Bara. Jumla ya Shilingi
bilioni 4.0 zimetengwa katika mwaka
2019/20 ili kutekeleza kazi hizo. Kati ya
fedha hizo, Shilingi bilioni 1.0 ni fedha za
ndani na Shilingi bilioni 3.0 ni fedha za
nje. Aidha, TANESCO kupitia mapato yake
ya ndani, imetenga Shilingi bilioni 188.70
kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huu katika
maeneo ya mijini mikoa yote.
61
MIRADI YA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI
Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme
Vijijini Awamu ya Tatu (REA – III)
82. Mheshimiwa Spika, Mradi wa
Kusambaza Umeme Vijijini wa Awamu ya
Tatu kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (Rural
Energy Agency - REA) unaendelea. Mradi
huu unalenga kufikisha umeme katika vijiji
ambavyo hadi kufikia mwezi Desemba, 2015
vilikuwa havijafikiwa na miundombinu ya
umeme. Katika kipindi cha kuanzia mwezi
Januari, 2016 hadi kufikia mwezi Mei, 2019
jumla ya vijiji vipya vilivyoongezeka kwa
kuunganishwa umeme kupitia mradi huu
ni 5,109 zaidi ya vijiji 2,018 vilivyokuwa
na umeme hadi mwezi Desemba, 2015
na hivyo kufikisha jumla ya vijiji 7,127
vilivyounganishiwa umeme. Mzunguko wa
Kwanza wa mradi huu utakapokamilika
mwezi Juni, 2020 jumla ya vijiji 10,278
vitakuwa vimeunganishiwa umeme kati ya
vijiji 12,268 sawa na asilimia 84 ya vijiji vyote
Tanzania Bara. Vijiji 1,990 vitakavyobaki
sawa na asilimia 16 ya vijiji vyote vitaanza
kupelekewa umeme kuanzia Julai 2020 na
kukamilika ifikapo Juni, 2021 na kuifanya
Tanzania kufikisha miundombinu ya umeme
62
vijijini katika vijiji vyote Tanzania Bara.
Aidha, hadi sasa jumla ya Taasisi za Elimu
3,165; Maeneo ya Biashara 3,451; Pampu za
Maji 210; Taasisi za Afya 1,211 na Nyumba
za Ibada 984 zimefikishiwa umeme.
83. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa
Miradi iliyopo chini ya Mpango wa REA III ni
kama ifuatavyo:
(i) Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini
Awamu ya Tatu (Grid Extension) –
Mzunguko wa Kwanza
84. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unatekelezwa katika vijiji 3,559 vya mikoa
yote ya Tanzania Bara na kuhusisha ujenzi
wa njia za kusambaza umeme na ufungaji
wa mashineumba. Hadi kufikia tarehe
15 Mei 2019, kazi zilizofanyika ni pamoja
na: kuendelea kujenga miundombinu ya
kusambaza umeme katika maeneo mbalimbali
yamradinahivyokuunganishawatejawaawali
zaidi ya 56,920. Kazi zilizopangwa kufanyika
katika mwaka 2019/20 ni: kuendelea
kujenga miundombinu ya usafirishaji na
usambazaji wa umeme; na kuunganisha
wateja. Utekelezaji wa usambazaji wa
umeme vijijini umeongezeka kwa kasi
63
ambapo hadi kufikia tarehe 31 Desemba,
2016 upatikanaji wa umeme vijijini
ulifikia asilimia 49.5 ikilinganishwa na
upatikanaji wa umeme vijijini wa asilimia
21 mwaka 2015. Hata hivyo, kwa sasa
upatikanaji wa umeme umeongezeka
zaidi ya kipindi hicho kufikia vijiji 7,127
mwezi Mei, 2019. Ongezeko hili linaifanya
Tanzania kuwa nchi ya kwanza kwa nchi
za Afrika Mashariki katika kusambaza
umeme vijijini. Inatarajiwa kuwa ifikapo
mwezi Juni, 2020 vijiji 10,278 ambavyo ni
sawa na asilimia 84 ya vijiji vyote nchini
vitakuwa vimefikishiwa umeme.
(ii) Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini
Awamu ya Tatu (Grid Extension) – Mzunguko wa Pili
85. Mheshimiwa Spika, Mradi wa
Kusambaza Umeme Vijijini wa Awamu ya Tatu
Mzunguko wa Pili utahusisha kusambaza
umeme katika vijiji vilivyobakia 1,190 sawa
na asilimia 16 ya vijiji vyote 12,268 vya
Tanzania Bara. Mradi huu utahusisha ujenzi
wa kilomita 35,581 za njia za umeme msongo
wa kV 33; ujenzi wa kilomita 21,777 za umeme
msongo wa kV 0.4; kufunga mashineumba
7,386; na kuunganisha wateja wa awali zaidi
64
ya 582,937. Kazi zitakazofanyika katika
mwaka 2019/20 ni kutangaza zabuni za
kuwapata wakandarasi na kuanza kazi.
(iii) Mradi wa Usambazaji Umeme katika
Vijiji vilivyopo Pembezoni mwa Miji
(Peri-Urban Rural Electrification
Program)
86. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusisha kusambaza umeme katika jumla
ya maeneo 250 yakiwemo ya kibiashara, mitaa
na vitongoji/vijiji. Jumla ya wateja wa awali
zaidi ya 37,843 wataunganishwa umeme
katika wilaya za Mikoa ya Pwani na Dar es
Salaam ikiwemo Kigamboni ili kujazilizia
vitongoji vilivyoachwa na kuboresha
huduma za umeme katika maeneo hayo.
Katika mwaka 2018/19, kazi zilizofanyika
ni pamoja na kuwapata wakandarasi kwa
ajili ya kazi ya ujenzi wa miundombinu ya
kusambaza umeme ambapo zitafanyika kwa
muda wa miezi 9 kuanzia mwezi Mei 2019.
Kazi zitakazofanyika kwa mwaka 2019/20 ni
pamoja na Wakandarasi kuanza kazi za ujenzi
wa miundombinu ya kusambaza umeme na
kuunganisha wateja.
65
(iv) Mradi wa Usambazaji Umeme katika
maeneo ambayo yamefikiwa na
Miundombinu ya Umeme Mzunguko
wa Pili (Densification Round Two)
87. Mheshimiwa Spika, baada ya
Mradi wa Ujazilizi Mzunguko wa Kwanza
katika mikoa nane (8) ambayo ni Arusha,
Iringa, Mara, Mbeya, Njombe, Pwani, Tanga
na Songwe kukamilika, Serikali inaendelea
na utekelezaji wa mradi huo katika awamu
ya pili. Mradi wa ujazilizi mzunguko wa pili
unahusisha kuongeza wigo wa kuunganisha
umeme katika vitongoji vilivyobaki
(alimaarufu kurukwa) na kufanya wananchi
wengi kufikiwa na umeme. Kazi zilizopangwa
kufanyika kwa mwaka 2019/20 ni
kukamilisha taratibu za zabuni na kuwapata
wakandarasi kwa ajili ya ujenzi wa mradi
huo.
88. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia
tarehe 15 Mei, 2019, Wakala wa Nishati
Vijijini ulikuwa umepokea jumla ya Shilingi
bilioni 393.31 kati ya Shilingi bilioni 412.08
zilizopangwa kutumika kwa mwaka 2018/19
sawa na asilimia 95.4 ya bajeti. Aidha, katika
mwaka 2019/20 fedha zilizotengwa kwa ajili
ya kutekeleza miradi ya kusambaza umeme
66
vijijini ni Shilingi bilioni 423.10, kati ya hizo
Shilingi bilioni 363.10 ni fedha za ndani na Shilingi bilioni 60 ni fedha za nje.
SEKTA NDOGO YA NISHATI JADIDIFU
89. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
EWURA imekamilisha mapitio ya utaratibu
wa uendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme
(Review of Small Power Projects Framework) ili
kuvutia wawekezaji na kutatua changamoto
zilizojitokeza kwa wadau wakati wa
utekelezaji. Katika kukamilisha mapitio hayo,
EWURA imerekebisha Kanuni za Uendelezaji
wa Miradi Midogo ya Umeme za Mwaka 2018
(The Electricity (Development of Small Power
Projects) Rules, 2018) yaliyohusisha kikokotoo
cha bei ya umeme kwa miradi hiyo inayouza
umeme kwa TANESCO na ile ya gridi ndogo
(mini/micro grids) zinazouza moja kwa moja
kwa wateja. Kanuni hizo za Mwaka 2019
(The Electricity (Development of Small Power
Projects) Rules, 2019) zimetangazwa kupitia
Gazeti la Serikali GN No. 380 ya tarehe 10
Mei, 2019. Kanuni hizi zitasaidia kudhibiti
bei za umeme kutoka kwa wazalishaji
wadogo ambapo kwa sasa wanajipangia bei
wenyewe na bei hurekebishwa kunapokuwa
na malalamiko kutoka kwa wateja asilimia
15 au zaidi.
67
90. Mheshimiwa Spika, ili kuleta
usawa katika bei ya umeme kwa maeneo
ambayo yanapata huduma za umeme
kupitia mfumo wa Solar Mini Grid hususan
maeneo ya Visiwani na ambayo hayajafikiwa
na Gridi ya Taifa, maeneo hayo yataendelea
kuunganishiwa umeme kwa gharama sawa
na zinazotozwa na REA na TANESCO.
Nishati inayotokana na Nguvu ya Jua,
Upepo na Maporomoko Madogo ya Maji
91. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2018/19 Serikali iliendelea kuhamasisha
matumizi ya nishati itokanayo na nguvu
ya jua katika nyumba (Solar Home System)
na taasisi za huduma za jamii. Kupitia
mfumo huu, matumizi ya nishati ya jua
yaliongezeka kwa jumla ya MW 10 na hivyo
kufanya matumizi ya nishati hiyo hadi sasa
kufikia MW 26. Vilevile, Serikali iliendelea
na jitihada za kuhamasisha na kuvutia
uwekezaji wa sekta binafsi katika nishati jua
kwa kutumia mfumo wa gridi ndogo. Aidha,
kwa mwaka 2019/20 mchango wa miradi
midogo ya kuzalisha umeme kwa kutumia
maporomoko madogo ya maji na upepo
unatarajiwa kuongezeka kwa jumla ya MW
7.7 kutokana na kukamilika kwa miradi ya
68
Lugarawa MW 1.7 Wilayani Ludewa; Maguta
MW 1.2 Wilayani Kilolo; Luponde MW 1.0
Wilayani Njombe; Suma MW 1.4 Wilayani
Rungwe; na Mradi wa Upepo wa Mwenga MW
2.4 Wilayani Mufindi.
Matumizi Bora ya Nishati
(Energy Efficiency)
92. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha mwaka 2018/19 kazi zilizofanyika ni
pamoja na: Serikali kuridhia utekelezaji wa
Mpango Kazi wa Kitaifa wa Matumizi Bora
ya Nishati (Energy Efficiency Action Plan);
na kukamilika kwa rasimu ya Mkakati
wa Kitaifa wa Matumizi Bora ya Nishati
(Energy Efficiency Strategy). Aidha, Taasisi
ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Shirika
la Viwango Tanzania (TBS), Shirika la Utafiti
na Maendeleo ya Viwanda (TIRDO) na Chuo
cha Ufundi Arusha (ATC) zilibainishwa kama
taasisi zitakazoshiriki katika utekelezaji wa
Mpango Kazi wa Matumizi Bora ya Nishati
na kuanza kujengewa uwezo wa jinsi ya
kutekeleza Mpango kazi huu.
93. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
pangwa kutekelezwa katika Mpango Kazi
wa Matumizi Bora ya Nishati kwa mwaka
69
2019/20 ni pamoja na: kuboresha Mpango
Kazi huo kwa kuoanisha na Mkakati wa
Kitaifa wa Matumizi Bora ya Nishati; kuandaa
muundo thabiti wa kitaasisi utakaokuwa na
jukumu la kusimamia utekelezaji wa Mpango
Kazi huu; na kutoa elimu ya matumizi bora ya
nishati kwa wananchi na Taasisi za Serikali.
Programu ya Nishati Endelevu kwa Wote
(Sustainable Energy for All – SE4ALL)
94. Mheshimiwa Spika, katika
programu ya upatikanaji wa nishati endelevu
kwa wote inayolenga kuongeza mchango wa
nishati jadidifu na kukuza matumizi bora ya
nishati hapa nchini, kwa mwaka 2018/19
Serikali ilikamilisha maandalizi ya miongozo
ya utekelezaji wa programu hii ikiwemo:
mkakati wa upatikanaji wa rasilimali kwa ajili
ya kufikia malengo ya programu; Mkakati wa
Mawasiliano; Mpango wa ushirikishwaji wa
mamlaka zote na wananchi (Regionalization);
na kuzijengea uwezo Wizara na Taasisi
mbalimbali katika kusimamia utekelezaji wa
miradi ya nishati. Aidha, kupitia programu
hii, Mpango wa Kijinsia wa Utekelezaji wa
Jitihada za Upatikanaji wa Nishati kwa
Wote (Gender Action Plan for Implementation
of Sustainable Energy for All Initiatives)
70
uliandaliwa na mfumo wa ukusanyaji na
utunzaji wa takwimu za nishati jadidifu hapa
nchini ulianza kuandaliwa.
95. Mheshimiwa Spika, katika kipindi
cha mwaka 2019/20 kazi zilizopangwa
ni pamoja na: kuanza kwa utekelezaji
wa Tanzania Energy Gender Action Plan;
kukamilisha uandaaji wa mfumo wa
ukusanyaji na utunzaji wa takwimu za
nishati jadidifu; na kuendelea kuwajengea
uwezo watumishi wa Serikali na Sekta Binafsi
katika kusimamia utekelezaji wa miradi ya
nishati jadidifu nchini. Jumla ya Shilingi
bilioni 3 ambapo kati ya fedha hizo Shilingi
milioni 500 fedha za ndani na Shilingi
bilioni 2.50 fedha za nje zimetengwa katika
mwaka 2019/20 ili kutekeleza kazi hizo.
Uendelezaji wa Rasilimali ya Jotoardhi
(Geothermal)
96. Mheshimiwa Spika, katika kutimiza
azma ya nchi kuwa na usalama wa nishati
(energy security) kwa kuzalisha umeme
kwa kutumia vyanzo mbalimbali ambavyo
ni nafuu, endelevu na rafiki kwa mazingira
ikiwemo jotoardhi, Serikali kupitia Wizara ya
Nishati imelenga kuzalisha umeme MW 200
71
utokanao na Jotoardhi ifikapo mwaka 2025.
Pamoja na uzalishaji wa umeme, rasilimali
ya jotoardhi ina manufaa mengine mengi
kupitia mchango wake katika maendeleo ya
sekta nyingine za uchumi kama vile kukausha
mazao, ufugaji wa samaki, mabwawa ya maji
moto kwa ajili ya kuogelea, uchakataji wa
bidhaa za viwandani na hivyo kuboresha pato
na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
97. Mheshimiwa Spika, Serikali
inatekeleza miradi mitano (5) ya kipaumbele
katika maeneo ya Ngozi na Kiejo-Mbaka
mkoani Mbeya, Songwe mkoani Songwe,
Luhoi mkoani Pwani na Natron mkoani
Arusha. Utekelezaji wa miradi hii upo katika
hatua ya uhakiki wa rasilimali ya Jotoardhi
kwa kuchoronga visima vya utafiti isipokuwa
mradi wa Natron ambao upo katika hatua
ya utafiti wa kina. Kwa kawaida, utekelezaji
wa miradi ya jotoardhi hupitia hatua
mbalimbali muhimu ikiwa ni pamoja na (i)
utafiti (exploration), (ii) uhakiki (test drilling),
(iii) uendelezaji (development), (iv) uvunaji
(exploitation) na (v) utumiaji (utilization).
98. Mheshimiwa Spika, hatua hizo
hutekelezwa kwa mpangilio maalumu bila
kuruka hatua yoyote na unachukua muda
72
wa kati ya miaka 6 hadi 8 ili kukamilisha
hatua hizi. Pamoja na kwamba hatua za awali
za uendelezaji wa jotoardhi huchukua muda
mrefu na ni wa gharama kubwa, umeme
utokanao na jotoardhi ni wa uhakika na bei
nafuu kwa kuwa uzalishaji wake hautegemei
mafuta wala hali ya hewa. Miradi mitatu (3)
ambayo itatekelezwa katika mwaka 2019/20
ni Ngozi, Songwe na Kiejo-Mbaka.
(i) Mradi wa Ngozi (Mbeya)
99. Mheshimiwa Spika, Mradi huu
unahusu uzalishaji wa umeme unaotokana
na Jotoardhi katika eneo la Ngozi, mkoani
Mbeya kwa kuanza na uzalishaji wa MW 30.
Kwa sasa mradi upo katika hatua ya uhakiki
wa rasilimali ya Jotoardhi kwa kuchoronga
visima vitatu (3) vya utafiti (exploratory wells).
Shughuli za maandalizi ya uchorongaji wa
visima hivyo vya utafiti zilizofanyika katika
mwaka 2018/19 ni pamoja na: kuajiri
Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kuandaa
mpango na kusimamia uchorongaji; taratibu
za ununuzi wa mtambo wa uchorongaji wa
visima vya utafiti; na maandalizi ya upimaji
na uthamini wa ardhi hitajika kwa ajili ya
uchorongaji. Katika mwaka 2019/20 Serikali
itaendelea na taratibu za ununuzi wa mtambo
73
wa kuchoronga visima vya utafiti. Aidha,
Serikali imetenga fedha Shilingi bilioni 8
kwa ajili ya kuchoronga visima vitatu (3) vya
utafiti katika eneo la Ngozi. Kati ya fedha hizi
Shilingi milioni 500 ni fedha za ndani na
Shilingi bilioni 7.50 ni fedha za nje. Ujenzi
wa mtambo wa kuzalisha umeme unatarajiwa
kuanza mwaka 2021 na kukamilika mwaka
2023.
(ii) Mradi wa Songwe (Mkoani Songwe)
na Mradi wa Kiejo-Mbaka (Mbeya)
100. Mheshimiwa Spika, Miradi hii
inahusu uzalishaji wa umeme na matumizi
mengineyo (direct uses) katika maeneo
ya Songwe, mkoani Songwe na Kiejo-
Mbaka, mkoani Mbeya ambapo imefikia
hatua za uchorongaji wa visima vya utafiti.
Katika kipindi cha mwaka 2018/19 kazi
zilizokamilika katika mradi wa Songwe ni
Upembuzi Yakinifu wa Awali (Pre-feasibility
Study) wa matumizi mengineyo ya Jotoardhi
ambayo ni pamoja na kukaushia mazao ya
kilimo na mifugo, mabwawa ya kuogelea na
shughuli za utalii.
101. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
fanyika hadi sasa katika mradi wa
74
KiejoMbaka ni pamoja na kuwasilisha
maombi ya ufadhili wa mradi kwa Mfuko wa
Maendeleo ya Jotoardhi Afrika (GRMF) kwa
ajili ya uchorongaji wa visima vya utafiti. Kazi
zilizopangwa kufanyika katika kipindi cha
mwaka 2019/20 ni: kufanya maandalizi ya
uchorongaji wa visima vya utafiti; na kuanza
ujenzi wa miradi ya matumizi mengineyo
ya jotoardhi katika maeneo hayo. Shilingi
bilioni 1.31 fedha za ndani ya Kampuni
(TGDC) zimetengwa katika mwaka 2019/20
kugharamia utekelezaji wa kazi hizo.
Utekelezaji wa miradi ya matumizi mengineyo
unaendelea na unatarajiwa kukamilika
mwaka 2021.
102. Mheshimiwa Spika, sambamba
na utekelezaji wa miradi ya jotoardhi,
Serikali inaendelea na juhudi za kuandaa
mazingira wezeshi ya uendelezaji na
utumiaji wa jotoardhi. Kwa sasa leseni za
utafiti za jotoardhi zinasimamiwa na Sheria
ya Madini ya Mwaka 2010. Hata hivyo,
Serikali inaendelea kutathmini changamoto
za utekelezaji wa miradi ya jotoardhi kwa
kutumia sheria husika na kuchukua hatua
stahiki. Aidha, Serikali imeendelea kutoa
fedha za uendelezaji wa miradi ya jotoardhi
75
kupitia bajeti ya kila mwaka na kujenga
uwezo wa wataalam wa ndani. Katika kipindi
cha mwaka 2015 hadi mwezi Mei, 2019
zaidi ya wataalamu 15 walipata mafunzo
mbalimbali ya muda mrefu katika nyanja za
utafiti na uhakiki wa jotoardhi ikilinganishwa
na wataalamu 7 waliokuwepo wakati TGDC
inaanzishwa.
SEKTA NDOGO YA MAFUTA NA
GESI ASILIA
Shughuli za Utafutaji, Uzalishaji na
Usambazaji wa Mafuta na
Gesi Asilia Nchini
103. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia
mwezi Mei, 2019 jumla ya Futi za Ujazo
Trilioni 57.54 za gesi asilia zimegunduliwa
hapa nchini. Katika kipindi cha mwaka
2018/19, shughuli za utafutaji, uendelezaji
na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia
zimeendelea kutekelezwa na Shirika la
Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa
kushirikiana na Kampuni za Kimataifa
za Mafuta (IOCs). Uchukuaji wa data za
mitetemo (seismic data acquisition) za 2D
zenye kilomita 442 za mstari katika Kitalu
cha Ruvu umekamilika. Uchakataji na tafsiri
76
ya data hizo ili kubaini ukubwa wa mashapo
na eneo zuri la kuchoronga visima vya
utafutaji na uendelezaji bado unaendelea.
Aidha, maandalizi ya awali ikiwemo ujenzi
wa barabara na kupatikana kwa vibali kwa
ajili ya kuchoronga visima vya Hammerkop-1
na Kito-1 katika Kitalu cha Rukwa Kusini na
Kilosa-Kilombero sawia yamekamilika.
104. Mheshimiwa Spika, uzalishaji wa
gesi asilia nchini katika vitalu vya Mnazi
Bay na Songo Songo umeongezeka hadi
kufikia Futi za Ujazo Milioni 190 kwa siku
kwa mwaka 2018/19, ikilinganishwa na
wastani wa Futi za Ujazo Milioni 175 kwa
siku kwa mwaka 2017/18 sawa na ongezeko
la asilimia 8.6. Ongezeko hili la uzalishaji
wa gesi asilia limetokana na ongezeko
la mahitaji katika matumizi viwandani,
majumbani na kuzalisha umeme. Gesi asilia
inachangia zaidi ya asilimia 60 ya umeme
unaozalishwa nchini. Mahitaji ya gesi asilia
katika kuzalisha umeme yameendelea
kuongezeka ambapo yalifikia Futi za Ujazo
bilioni 50.53 kwa mwaka 2018 kutoka Futi
za Ujazo bilioni 42.79 mwaka 2017, sawa na
ongezeko la asilimia 18.
77
UTAFUTAJI WA MAFUTA NA GESI ASILIA
KATIKA VITALU VYA KIMKAKATI
UNAOTEKELEZWA NA SHIRIKA LA
MAENDELEO YA PETROLI TANZANIA (TPDC)
105. Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa
miradi ya kimkakati ya utafutaji wa mafuta
na gesi asilia kupitia TPDC unaendelea kwa
kutoa kipaumbele katika Vitalu vya Eyasi –
Wembere,4/1B,MnaziBayKaskazininaSongo
Songo Magharibi. Aidha, Serikali inaendelea
kukamilisha maandalizi ya Mkataba Kifani
wa Ushirikiano katika Utekelezaji (Model
Joint Operating Agreement) utakaosainiwa
baina ya TPDC na Wabia katika kuendeleza
vitalu vya kimkakati.
(i) Kitalu cha Eyasi – Wembere
106. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
TPDC imeendelea kutekeleza mradi wa
utafutaji wa mafuta na gesi asilia katika Kitalu
cha Eyasi – Wembere kilichopo katika Bonde la
Ufa la Afrika Mashariki. Kwa mwaka 2018/19,
kazi zilizotekelezwa ni pamoja na: kumpata
Mshauri Mwekelezi wa kufanya Tathmini ya
Athari za Mazingira kwa ajili ya ukusanyaji
wa data za mitetemo za 2D; kuandaa mkataba
wa awali (MoU) kati ya Serikali za Tanzania
78
na Uganda kwa ajili ya utafiti wa awali;
kukamilisha Hadidu za Rejea kwa lengo la
kumpata Mbia wa Kimkakati; kukusanya
taarifa za awali (reconnaissance survey); na
kukamilisha maandalizi ya uchorongaji wa
visima vifupi vya utafiti wa tabaka za miamba
(Stratigraphic Boreholes) ambapo Mkandarasi
wa kutekeleza kazi hiyo amepatikana.
107. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka
2019/20, kazi zitakazotekelezwa ni pamoja
na: kufanya Tathmini ya Athari za Mazingira
kwa ajili ya ukusanyaji wa data za mitetemo
za 2D; kuainisha na kufanya tathmini ya
eneo litakaloathiriwa na mradi; kuchoronga
visima vifupi vitatu (3) vya utafiti wa tabaka
za miamba; kufanya utafiti wa kimaabara
wa sampuli zitakazokusanywa kutoka katika
visima vya stratigraphic; na kukusanya,
kuchakata na kutafsiri data za mitetemo za
2D zenye urefu wa kilomita 150. Jumla ya
Shilingi bilioni 1.00 zimetengwa kwa ajili ya
utekelezaji wa kazi hizo.
(ii) Uchorongaji wa Kisima katika
Kitalu cha Mnazi Bay Kaskazini
108. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
TPDC imeendelea na mpango wa kuchoronga
79
kisima cha utafutaji mafuta na gesi asilia
katika Kitalu cha Mnazi Bay Kaskazini
kufuatia matokeo chanya ya tafsiri ya data
za awali za mitetemo (3D) zenye kilomita za
mraba 132. Tafsiri ya data hizo imeonesha
uwezekano wa kuwepo kwa gesi asilia katika
Kitalu hiki. Kwa mwaka 2018/19, Serikali
imetekeleza kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja
na: kukamilisha uchakataji na tafsiri ya data
za mitetemo kiasi cha kilomita za mraba 132;
kuandaa Mpango wa Uchorongaji wa Kisima
(Drilling Programme); na kukamilisha taratibu
za kumpata Mbia wa Kimkakati.
109. Mheshimiwa Spika, kazi zitakazo-
tekelezwa kwa mwaka 2019/20 ni pamoja na:
kumpata Mtaalamu Mshauri wa uchorongaji
(drilling management consultant); kupitia na
kutafsiri taarifa za kijiolojia; na kuchoronga
kisima cha utafutaji mwezi Mei, 2020. Fedha
za ndani Shilingi milioni 800 zimetengwa
kwa ajili ya utekelezaji wa kazi hizo.
80
(iii) Uchukuaji wa data za mitetemo
katika Vitalu Na. 4/1B na Mnazi
Bay Kaskazini
110. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ukusanyaji na uchakataji wa data
za mitetemo katika Kitalu Na. 4/1B na Mnazi
Bay Kaskazini ili kubaini uwepo wa mashapo
yenye viashiria vya mafuta au gesi asilia.
Kwa mwaka 2018/19 kazi zilizotekelezwa ni
pamoja na: kuboresha Mpango wa Usimamizi
wa Mazingira (Environmental Management
Plan); na kukamilika kwa Hadidu za Rejea
za kumpata mbia wa kimkakati. Kwa
mwaka 2019/20 kazi zitakazotekelezwa ni
pamoja na: kumpata Mshauri Mwelekezi
wa kukusanya, kuchakata na kutathmini
taarifa za mitetemo ya 3D zenye ukubwa wa
kilomita za mraba 693.1 kwa kitalu cha 4/1B
na Mnazi Bay Kaskazini kwa maeneo ambayo
hayajafanyiwa utafiti; na kumpata Mshauri
Mwelekezi kwa ajili ya kutathmini athari za
mazingira. Jumla ya Shilingi milioni 850
zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza kazi hizo.
(iv) Kitalu cha Songo Songo Magharibi
111. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu utafutaji wa mafuta na gesi asilia
81
katika kitalu cha Songo Songo Magharibi
chenye mashapo yenye viashiria vya uwepo
wa gesi asilia. Kwa kipindi cha mwaka
2018/19, TPDC imekamilisha kazi za
awali za kukusanya data za mitetemo za
3D (seismic scouting) za kilomita za mraba
183.4. Aidha, Hadidu za Rejea za kumpata
mbia wa kimkakati zimekamilika. Vilevile,
katika kipindi hicho, TPDC imeendelea na
taratibu za kumpata Mshauri Mwelekezi wa
kufanya Tathmini ya Athari za Mazingira.
Katika mwaka 2019/20, kazi zilizopangwa
kutekelezwa ni pamoja na: kufanya tafiti za
kijiolojia na kijiofizikia; kumpata mbia wa
kimkakati wa kutekeleza mradi; na kufanya
maandalizi ya awali ya uchorongaji wa kisima
cha utafiti. Jumla ya Shilingi milioni 55
zimetengwa na TPDC kutekeleza shughuli
hizo.
MIRADI YA KUSAFIRISHA NA
KUSAMBAZA GESI ASILIA NCHINI
112. Mheshimiwa Spika, Serikali
imeendelea na ujenzi wa miundombinu ya
kusafirisha na kusambaza gesi asilia kwa
lengo la kuhakikisha gesi hiyo inatumika
kwa matumizi mbalimbali yakiwemo ya
viwandani, majumbani, katika magari na
82
kuzalisha umeme. Miradi hiyo ni kama
ifuatayo:
(i) Mradi wa Kusambaza Gesi Asilia
Viwandani
113. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2018/19, TPDC imekamilisha ujenzi wa
miundombinu ya kusambaza gesi asilia
katika Kiwanda cha Dangote (awamu ya pili),
Lodhia, Cocacola, kiwanda cha vifungashio
kinachomilikiwa na Goodwill Ceramic
Tanzania Limited na kazi ya kuunganisha
kiwanda cha Knauf imefikia asilimia 80.
Aidha, TPDC imekamilisha majadiliano ya
mauziano ya gesi asilia na Kiwanda cha
Shreeji Silcates. Katika kuendelea kutafuta
wateja zaidi wa viwandani, TPDC imeanza
majadiliano ya mauziano ya gesi asilia na
kiwanda cha MM-1 Intergrated Steel Mills
Ltd kilichopo Mikocheni – Dar es Salaam,
pamoja na LN Future Building Materials Co.
Ltd na Kings Alluminium vilivyopo Mkuranga
- Pwani.
114. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka
2019/20, kazi za mradi zitahusu ujenzi wa
miundombinu ya kuunganisha viwanda
vya Shreeji Silicates Tanzania Limited,
83
LN Future na Kings Aluminium. Vilevile,
TPDC inatarajia kujenga trunk-line kutoka
Mwenge hadi Tegeta na kuunganisha wateja
mbalimbali wakiwemo Estim Construction,
Chem & Cortex, Polypet, Interchik, Giraffe
Hotel, Jangwani Sea Breeze, Ramada Resort
Hotel, Landmark Hotel, Seascape Hotel
na White Sands Hotel. Katika kutekeleza
mpango huo, Shirika litafanya majadiliano
na kusaini mikataba ya mauziano ya gesi
asilia na wateja hao pamoja na kumtafuta
Mkandarasi (EPC contractor). Fedha za ndani
za Shirika Shilingi bilioni 11.22 zimetengwa
kwa ajili ya kutekeleza mradi huu.
(ii) Miradi ya Kusambaza Gesi Asilia
Majumbani na Ujenzi wa Vituo vya
Kujazia Gesi Asilia katika Magari
115. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
TPDC inaendelea kusambaza gesi asilia
kwa wateja wa majumbani walio karibu na
miundombinu iliyopo katika Mkoa wa Dar
es Salaam. Mradi wa kuunganisha wateja
wa majumbani ulianza kutekelezwa mwaka
2016 na ni endelevu kupitia GASCO, kampuni
tanzu ya TPDC. Katika mwaka 2018/19, kazi
zilizotekelezwa ni pamoja na: kukamilisha
ujenzi wa mtambo wa kupunguza msukumo
84
wa gesi (Pressure Reduction Station) eneo la
Ubungo Kibo; kukamilisha kazi za awali za
ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi
asilia kutoka Ubungo Maziwa kupitia Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, Savei, Mlalakuwa,
Changanyikeni, Makongo Juu kuelekea
Tegeta. Miundombinu hiyo itawezesha
kuunganisha wateja wa gesi asilia majumbani
zaidi ya 500 katika Jiji la Dar es Salaam. Ili
kuhamasisha Watanzania wengi kutumia gesi
hii na hivyo kupunguza gharama za maisha
na kukabiliana na uharibifu wa mazingira,
gharama ya bei ya gesi majumbani ina
punguzo la asilimia 40 ukilinganisha na bei
ya gesi ya mitungi (LPG).
116. Mheshimiwa Spika, maandalizi ya kusambaza gesi katika mikoa ya Lindi na Mtwara yanaendelea ambapo kwa upande wa Mkoa wa Mtwara, kazi zilizotekelezwa ni pamoja na: kukamilisha taratibu za manunuzi ya mabomba, mita za gesi na vifaa vya kupunguza mgandamizo wa gesi (pressure reduction stations); kukamilisha michoro ya usanifu wa ujenzi wa miundombinu; na kupatikana kwa vibali vya ujenzi wa mradi. Kazi zinazoendelea kwa sasa ni kutandaza mabomba makubwa (trunk-lines) katika njia mbili, ya kwanza ikielekea Shule ya Sekondari
85
Ufundi Mtwara kwa ajili ya kusambaza gesi katika taasisi mbalimbali na makazi ya watu zaidi ya nyumba 125 za awali pembezoni mwa bomba la gesi.
117. Mheshimiwa Spika, miundombinu ya kusambaza gesi asilia katika njia ya pili itaelekea Gereza la Lilungu ikiwa na matoleo kwa wateja walio pembezoni mwa miundombinu hiyo. Maandalizi ya usambazaji wa gesi majumbani kwa Mkoa wa Lindi yameanza ambapo kazi ya kutoboa bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam kwa eneo la Lindi itakamilika mwezi Januari, 2020. Ujenzi wa miundombinu ya kusambaza gesi na kazi ya kuunganisha wateja itaanza mwezi Juni, 2020 na itakuwa endelevu.
118. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20, Serikali kupitia TPDC imepanga
kuunganisha wateja wa awali zaidi ya
nyumba 1,000 katika Jiji la Dar es Salaam
na nyumba zaidi ya 300 mkoani Mtwara.
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa ni pamoja
na: kumpata Mshauri Mwelekezi kwa ajili
ya kufanya Tathmini ya Athari za Mazingira
Jijini Dar es Salaam kupitia maeneo ya
Bagamoyo Road, Kilwa Road na Mandela
86
Road (Changombe, Kurasini, Keko); kumpata
Mshauri Mwelekezi wa kufanya Tathmini ya
Athari za Mazingira mkoani Mtwara kwa kata
za Railway, Shangani, Chikongola, Tandika,
Likombe, Magomeni, Chuno na Majengo; na
kuwapata wakandarasi (EPC contractors) wa
kuunganisha gesi asilia majumbani Jijini
Dar es Salaam na mkoani Mtwara.
119. Mheshimiwa Spika, TPDC pia
itajenga kituo mama cha kupunguza
mgandamizo wa gesi asilia (Compressed
Natural Gas – CNG Mother Station) chenye
kituo cha kujazia gesi katika magari eneo la
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Aidha, vituo
vidogo vya kupunguza mgandamizo wa gesi
asilia (CNG Daughter Stations) vitajengwa
maeneo ya Hospitali ya Muhimbili, Soko la
Samaki Feri na Ubungo. Kituo cha Ubungo
kitatumika kujaza gesi katika Mabasi ya
Mwendokasi zaidi ya 300 pamoja na magari
mengine zikiwemo daladala. Serikali imetenga
Shilingi bilioni 1.10 fedha za ndani kwa ajili
ya kutekeleza mradi huo.
120. Mheshimiwa Spika, katika
kuendelea na juhudi za kuwezesha mikoa
mingine nchini kunufaika na rasilimali ya
gesi asilia, Serikali itaendelea kufanya tafiti za
87
namna bora ya kuunganishia mikoa hiyo na
miundombinu ya kusafirisha na kusambaza
rasilimali hiyo. Kwa kuanzia, usambazaji
wa gesi asilia unatarajiwa kufanyika katika
mikoa ya Pwani, Tanga, Morogoro, Dodoma,
Kilimanjaro, Mwanza na Arusha. Mpango
huu unatarajiwa kutekelezwa kati ya sasa
na mwaka 2025. Kutokana na kuongezeka
kwa mahitaji ya gesi asilia majumbani,
TPDC itaongeza kasi ya kusambaza gesi
asilia katika maeneo mbalimbali nchini.
(iii) Mradi wa Usambazaji wa Gesi Asilia
kwa kuhusisha Sekta Binafsi katika
Mikoa ya Lindi, Mtwara na Dar es
Salaam
121. Mheshimiwa Spika, Serikali
kupitia TPDC imeanza kutekeleza mradi wa
kusambaza gesi asilia katika mikoa ya Lindi,
Mtwara na Dar es Salaam. Mradi huu ni
sehemu ya utekelezaji wa Mpango Kabambe
wa Matumizi ya Gesi Asilia nchini (Natural
Gas Utilization Master Plan - NGUMP).
Mradi unahusu ujenzi wa miundombinu
ya kusambaza gesi asilia kwa kushirikisha
wawekezaji binafsi kwa baadhi ya maeneo
katika mikoa husika.
88
122. Mheshimiwa Spika, Wawekezaji wa
sekta binafsi watapatikana kwa njia ya zabuni
za ushindani wa kimataifa ili kuweka usawa
na kupata wawekezaji wenye uzoefu na uwezo
wa kiteknolojia na fedha za kugharamia mradi
kwa masharti nafuu kwa Serikali. Kupatikana
kwa wawekezaji kutaharakisha ujenzi wa
miundombinu ya kusambaza gesi asilia na
hivyo kuwafikia Watanzania wengi zaidi kwa
muda mfupi. Katika mwaka 2018/19, kazi
zilizotekelezwa ni pamoja na: kukamilisha
Upembuzi Yakinifu wa Awali (Pre-Feasibility
Study) wa mradi; na kuendelea na taratibu
za kumpata Mshauri Mwelekezi wa kufanya
Upembuzi Yakinifu wa mradi anayetarajiwa
kupatikana mwezi Juni, 2019.
123. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20, kazi zilizopangwa kutekelezwa ni
kufanya Upembuzi Yakinifu wa mradi na
kuwapata wawekezaji binafsi kwa ajili ya
utekelezaji wa mradi. Baada ya kupatikana
kwa wawekezaji, ujenzi unatarajiwa kuanza
mwezi Juni, 2020 na awamu ya kwanza
ya ujenzi inategemewa kukamilika mwezi
Desemba, 2021.
89
(iv) Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha
Mbolea Mkoani Lindi
124. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa kiwanda cha mbolea
chenye uwezo wa kuzalisha tani milioni
1.3 za urea kwa mwaka. Kiwanda hiki
kinatarajiwa kujengwa eneo la Kilwa Masoko
– Lindi na Kampuni ya Tanzania Mbolea and
Petrochemicals Company Limited (TAMPCO)
ambayo ni ubia wa TPDC, Ferrostaal
Industrial Project GmbH ya Ujerumani, Fauji
Fertilizer Company Limited ya Pakistan na
Haldor Topsoe ya Denmark. Ujenzi wa mradi
huu utafanikisha upatikanaji wa uhakika
wa mbolea aina ya urea na hivyo kuchochea
ukuaji wa Sekta ya Kilimo nchini. Manufaa
mengine ni pamoja na: mapato yatokanayo
na gawio na kodi mbalimbali; kutoa ajira za
moja kwa moja kwa Watanzania zaidi ya 400;
kuongeza fursa za utoaji huduma na ugavi wa
bidhaa kwa kampuni za Tanzania; kujenga
uwezo wa Watanzania katika uendeshaji wa
viwanda vya mbolea; na kuongeza matumizi
ya gesi asilia kwa wastani wa futi za ujazo
milioni 70 hadi 100 kwa siku.
125. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2018/19 kazi zilizotekelezwa ni: kuendelea
90
na majadiliano ya namna bora ya utekelezaji
wa mradi kati ya wawekezaji na Serikali;
kuandaliwa kwa moduli ya kiuchumi ya
mradi; na kukamilika kwa tathmini ya madai
mapya ya fidia kwa wananchi watakaopisha
mradi. Kazi zitazotekelezwa kwa mwaka
2019/20 ni kukamilisha majadiliano kati ya
Serikali na wawekezaji ambako kutawezesha
kuanza kwa ujenzi wa mradi. Ujenzi wa
mradi unatarajiwa kuanza mwaka 2021 na
kukamilika mwaka 2024. Gharama ya mradi
ni Dola za Marekani bilioni 1.9 sawa na
takriban Shilingi trilioni 4.401.
(v) Mradi wa Kusafirisha Gesi Asilia
kutoka Tanzania kwenda Uganda
126. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa bomba la kusafirisha
gesi asilia kutoka Tanzania hadi Uganda
kwa kutumia mkuza wa bomba la mafuta
ghafi la kutoka Uganda hadi Tanga. Mradi
unalenga pia kusambaza gesi asilia maeneo
yatakayopitiwa na bomba hilo. Katika mwaka
2018/19 kazi zilizotekelezwa ni pamoja
na: kusainiwa kwa Makubaliano ya Awali
(Memorandum of Understanding – MoU) kati ya
Serikali ya Tanzania na Uganda mwezi Agosti,
2018; kuundwa kwa Kamati ya Pamoja ya
91
Wataalamu (Joint Technical Committee - JTC)
kutoka nchi zote mbili; kuandaa Mpango
Kazi wa Mradi (Project Workplan); na kuanza
taratibu za kumpata Mshauri Mwelekezi
atakayefanya Upembuzi Yakinifu wa mradi.
Katika mwaka 2019/20, kazi zilizopangwa
kutekelezwa ni pamoja na kumpata Mshauri
Mwelekezi kwa ajili ya kufanya Upembuzi
Yakinifu wa mradi. Serikali imetenga Shilingi
milioni 800 kwa ajili ya kutekeleza kazi za
awali za mradi huu kwa mwaka 2019/20.
(vi) Mradi wa Ujenzi wa Bomba la
Kusafirisha Gesi Asilia kutoka
Tegeta hadi Bagamoyo
127. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unalenga ujenzi wa bomba la kusafirisha
gesi asilia kutoka Tegeta hadi Bagamoyo ili
kusambaza gesi asilia katika eneo la viwanda
la Zinga, Bagamoyo pamoja na wateja wengine
waliopo katika maeneo yanayopitiwa na mradi
yakiwemo Bagamoyo Export Processing Zone
– EPZ, majumbani na taasisi mbalimbali.
Bomba la kusafirisha gesi asilia kwenda
maeneo hayo linakadiriwa kuwa na urefu wa
kilomita 30 na uwezo wa kusafirisha futi za
ujazo milioni 250 kwa siku. Gharama za mradi
huu ni Dola za Marekani milioni 22.74
92
sawa na takriban Shilingi bilioni 52.67.
Kukamilika kwa mradi huu kutachochea
ukuaji wa viwanda katika eneo la Bagamoyo
kwa kuhakikisha upatikanaji wa uhakika wa
nishati ya bei nafuu na kuongeza matumizi ya
gesi asilia kwa wateja mbalimbali wanaopitiwa
na miundombinu hiyo.
128. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
tekelezwa hadi sasa ni pamoja na kukamilisha
utafiti wa masoko (market survey) kwa eneo
litakalopitiwa na mradi, usanifu wa mradi
(project design) na Upembuzi Yakinifu wa
mradi (feasibility study). Katika mwaka
2019/20, shughuli zilizopangwa kutekelezwa
zinajumuisha kufanya Tathmini ya Athari
za Mazingira na Kijamii zitakazotokana na
utekelezaji wa mradi na kumpata Mkandarasi
(EPC + Financing) wa kutekeleza mradi.
Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwezi
Juni, 2020 na kukamilika mwezi Juni, 2021.
Serikali imetenga Shilingi milioni 300 fedha
za ndani kwa ajili ya kutekeleza kazi za awali
za mradi huu.
93
MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA
GESI ASILIA (Liquefied Natural Gas - LNG)
129. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
TPDC imeendelea na maandalizi ya ujenzi
wa mitambo ya kuchakata na kusindika gesi
asilia iliyopo kina kirefu cha bahari katika
Vitalu Na. 1, 2 na 4. Mitambo hiyo kwa ujumla
itakuwa na uwezo wa kusindika tani milioni
10 za gesi asilia kwa mwaka (10 MTPA).
Pamoja na gesi itakayosindikwa kusafirishwa
nje, kipaumbele ni kupatikana kwa gesi ya
kutosha kwa ajili ya matumizi ya ndani ya
nchi. Ili kuhakikisha mradi unatekelezwa
kwa maslahi mapana ya Taifa, Serikali
iliekeleza Timu ya Majadiliano ya Serikali
(Government Negotiation Team - GNT) kukutana
na mwekezaji mmoja mmoja na si kwa pamoja
kama ilivyokuwa awali. Katika kutekeleza hilo,
GNT ilianza majadiliano na wawekezaji hao
mwezi Aprili, 2019 na yanatarajiwa kukamilika
ndani ya miezi saba (7).
130. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
tekelezwa kwa mwaka 2018/19 ni:
kukamilisha Tathmini ya Athari za Mazingira
na Kijamii (ESIA); kukamilisha Mpango wa
uhamishaji wananchi watakaopisha Mradi
(Resettlement Action Plan); kuanza kwa
94
majadiliano ya kimkataba (Host Government
Agreement – HGA) baina ya Serikali na
wawekezaji na kuandaliwa kwa moduli ya
kiuchumi (economic model) ya Mradi.
131. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unatarajiwa kuleta manufaa makubwa
nchini yakiwemo: kuongezeka kwa mapato
ya Serikali yatakayotokana na mauzo ya
gesi asilia; kuongezeka kwa fursa za ajira
kwa Watanzania; kupatikana kwa gesi
kwa ajili ya matumizi mbalimbali nchini;
fursa kwa wafanyabiashara wa Kitanzania
kutoa huduma na bidhaa katika mradi; na
kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi katika
mikoa ya Lindi na Mtwara. Katika mwaka
2019/20, kazi zitakazotekelezwa ni pamoja na
kukamilisha majadiliano ya mradi na kulipa
fidia kwa wananchi watakaopisha mradi.
Jumla ya fedha za ndani Shilingi bilioni 6.7
zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi.
Gharama za mradi ni Dola za Marekani
bilioni 30 sawa na takriban Shilingi trilioni
69.49. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza
mwaka 2022 na kukamilika mwaka 2028.
95
MIRADI YA KUHIFADHI NA
KUSAFIRISHA MAFUTA
(i) Mradi wa Hifadhi ya Kimkakati ya
Mafuta ya Akiba na Dharura Nchini
132. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unatekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya
Petroli, 2015. Mradi huu pia unahusu ujenzi
wa miundombinu ya kuhifadhi mafuta ya
akiba ili kuhakikisha upatikanaji wa mafuta
ya kutosha nchini wakati wote. Kwa kuanzia,
TPDC imeainisha maeneo katika Mikoa ya
Dar es Salaam, Morogoro na Tanga ambapo
miundombinu hiyo itajengwa. Kwa upande
wa Dar es Salaam, tathmini ya awali ya
ardhi imekamilika na maandalizi ya kufanya
tathmini kwa mikoa ya Tanga na Morogoro
inaendelea.
133. Mheshimiwa Spika, kazi zilizo-
tekelezwakwamwaka2018/19ni:kuandaliwa
kwa Andiko la Biashara (Business Plan)
pamoja na moduli ya kiuchumi; kuandaliwa
kwa Hadidu za Rejea za kumpata mbia wa
kimkakati; na kukamilika kwa kazi ya ukaguzi
na usanifu wa Tenki Na. 8 litakalotumika
kuhifadhia mafuta. Kazi zitakazotekelezwa
kwa mwaka 2019/20 ni kukarabati Tenki Na.
8 na kuendelea na taratibu za kutwaa ardhi
96
katika Mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na
Tanga. Shilingi milioni 400 fedha za ndani
zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa kazi
hizo. Jumla ya Dola za Marekani milioni
250 sawa na takriban Shilingi bilioni
579.10 zinahitajika kwa kuanza uagizaji wa
mafuta ya hifadhi.
(ii) Mradi wa Bomba la Kusafirisha
Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki
(EACOP) kutoka Kabaale (Uganda)
hadi Bandari ya Tanga (Tanzania)
134. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa bomba la kusafirisha
mafuta ghafi (crude oil) kutoka Kabaale nchini
Uganda hadi mkoani Tanga nchini Tanzania.
Gharama za mradi zinakadiriwa kuwa
Dola za Marekani bilioni 3.5 ambazo ni
takriban Shilingi trilioni 8.1. Katika mwaka
2018/19 kazi zilizotekelezwa ni pamoja na:
kuendelea na majadiliano ya mkataba kati
ya kampuni ya mradi na Nchi Hodhi (Host
Government Agereement – HGA); kuendelea
na maandalizi ya majadiliano ya Mkataba wa
Ubia (Shareholding Agreement – SHA) ambayo
yanategemewa kukamilika mwezi Juni 2019;
na kukamilika kwa tathmini ya fidia kwa
maeneo ya kipaumbele (camps and coating
yard) na eneo lote la mkuza.
97
135. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unatarajiwa kuleta manufaa makubwa nchini yakiwemo: kuongeza mapato ya Serikali
kutokana na gawio la uwekezaji katika mradi
kupitia TPDC na kodi mbalimbali; kuongeza
ajira kwa Watanzania; fursa kwa Watanzania
kutoa huduma na bidhaa katika mradi;
kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi katika
mikoa itakayopitiwa na Bomba; na ukuaji wa
Bandari ya Tanga. Kwa mwaka 2019/20 kazi
zilizopangwa kutekelezwa ni kukamilisha
majadiliano ya Mkataba wa Ubia (SHA) kati
ya nchi washirika na kampuni zilizowekeza
katika mradi pamoja na kulipa fidia wakazi
watakaohamishwa kupisha eneo la mkuza
litakapopita bomba hili. Serikali imetenga
Shilingi bilioni 7 kwa ajili ya utekelezaji wa
Mradi. Ujenzi wa mradi unategemewa kuanza
mwezi Septemba, 2019 na kukamilika mwaka
2021.
(iii) Mradi wa Ujenzi wa Bomba la
Kusafirisha Mafuta Safi (White
Petroleum Products) kutoka Dar
es Salaam (Tanzania) hadi Ndola
(Zambia)
136. Mheshimiwa Spika, mradi huu
unahusu ujenzi wa bomba la kusafirisha
mafuta safi (white petroleum products)
98
kutoka Dar es Salaam (Tanzania) hadi Ndola
(Zambia). Mradi utakuwa na matoleo (take–
off points) katika maeneo ya Morogoro, Iringa,
Njombe, Mbeya na Songwe. Utekelezaji wa
mradi huu utaongeza uhakika wa upatikanaji
mafuta katika mikoa inayopitiwa na bomba
hilo sambamba na kuongeza mapato na
ajira. Aidha, utekelezaji wa mradi utaepusha
uharibifu wa miundombinu ya barabara na
kupunguza msongamano wa magari jijini Dar
es Salaam. Mradi huu vilevile utapunguza
changamoto ya usambazaji mafuta kwa nchi
zinazotumia bandari zetu kuingizia mafuta
yao na pia utafungua fursa za kibiashara
katika ukanda wa nyanda za juu kusini.
Mradi huu unatekelezwa kwa ushirikiano
baina ya Tanzania na Zambia.
137. Mheshimiwa Spika, hadi sasa, kazi
zilizotekelezwa ni pamoja na: kuandaa Andiko
la Mradi; na kuandaa Hadidu za Rejea za
kumpata Mshauri Mwelekezi atakayefanya
Upembuzi Yakinifu wa mradi na Tathmini
ya Athari za Mazingira na Kijamii (ESIA).
Kazi iliyopangwa kutekelezwa kwa mwaka
2019/20 ni kufanya Upembuzi Yakinifu
(feasibility study) utakaoainisha gharama za
99
mradi na namna bora ya kutekeleza mradi.
Serikali imetenga Shilingi milioni 800 kwa
ajili ya kazi hiyo. Gharama za mradi huu
zinakadiriwa kuwa Dola za Marekani bilioni
1.5 sawa na takriban Shilingi trilioni 3.474.
UDHIBITI WA SHUGHULI ZA MKONDO WA
JUU WA MAFUTA NA GESI ASILIA
138. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2018/19, Serikali kupitia PURA imeendelea
na udhibiti wa shughuli za utafutaji,
uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na
gesi asilia nchini katika vitalu 11 kupitia
mikataba ya Uzalishaji na Ugawanaji Mapato
(Production Sharing Agreements – PSAs).
Mikataba iliyopo ilisainiwa katika miaka ya
2001 hadi 2012 kabla ya Sheria ya Petroli ya
Mwaka 2015. Aidha, Sheria za Natural Wealth
and Resources (Permanent Sovereignty)
pamoja na Natural Wealth and Resources
(Re-negotiations of unconscionable terms) za
mwaka 2017 zinahitaji mikataba mbalimbali
kupitiwa upya ili iendane na mahitaji ya sasa
yanayolenga rasilimali ya gesi kunufaisha
ipasavyo Serikali na wananchi. Kutokana na
matakwa hayo, kazi ya kudurusu mikataba
hii inaendelea kutekelezwa chini ya Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
139. Mheshimiwa Spika, katika
100
kutekeleza jukumu la kudhibiti shughuli
za mkondo wa juu wa petroli kwa mwaka
2018/19, Serikali kupitia PURA imeendelea:
kusimamia uchukuaji wa data za mitetemo za
2D zenye kilomita 442 za mstari katika Kitalu
cha Ruvu; na kusimamia maandalizi ya awali
ya uchorongaji wa Visima vya Hammerkop-1
na Kito-1 katika vitalu vya Rukwa Kusini na
Kilosa-Kilombero sawia. Vilevile, Mamlaka
imeendelea kufanya kaguzi katika maeneo
ya utafutaji na uzalishaji wa gesi asilia.
140. Mheshimiwa Spika, PURA
imeendelea na shughuli za uhakiki wa
gharama za uwekezaji, ambapo hadi kufikia
mwezi Aprili, 2019 gharama na mapato kwa
mikataba yote 11 kwa miaka ya 2016 na
2017 vimehakikiwa. Lengo ni kuhakikisha
kuwa nchi inaendelea kupata stahiki yake
kulingana na mikataba iliyopo. Vilevile,
Mamlaka hiyo imehakiki na kupitisha
Mpango Kazi na Bajeti ya mwaka 2019 kwa
kampuni zote zinazotekeleza shughuli za
utafutaji na uzalishaji wa gesi asilia.
141. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka
2019/20, Serikali kupitia PURA itadhibiti
shughuli za uchorongaji wa kisima cha Kito-
101
1 katika Kitalu cha Kilosa-Kilombero, Kisima
cha Hammerkop-1 katika Kitalu cha Rukwa
Kusini na visima viwili katika Kitalu cha
Ruvu. PURA itasimamia uchukuaji data za
mitetemo za 2D zenye jumla ya kilomita za
mstari 150 katika Kitalu cha Eyasi-Wembere
na data za 3D zenye jumla ya kilomita za
mraba 693.1 katika kitalu cha 4/1B na
Mnazi Bay Kaskazini. Serikali imetenga
Shilingi billioni 1.69 kwa ajili ya kuwezesha
Mamlaka hiyo kutekeleza shughuli zake kwa
mwaka 2019/20.
HALI YA UPATIKANAJI WA
MAFUTA NCHINI
142. Mheshimiwa Spika, hali ya
upatikanaji wa mafuta nchini imeendelea
kuimarika. Serikali kupitia Wakala wa
Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (Petroleum Bulk
Procurement Agency - PBPA) inaendelea
kuagiza na kupokea mafuta ya kutosha
wakati wote. Kampuni za mafuta zimeendelea
kuagiza mafuta kupitia Mfumo wa Uagizaji
wa Mafuta kwa Pamoja (Bulk Procurement
System - BPS) kupitia PBPA. Kati ya mwezi
Januari hadi Desemba, 2018 jumla ya lita
bilioni 5.70 za mafuta ziliagizwa kupitia
Bandari za Dar es Salaam, Tanga na
102
Mtwara sawa na ongezeko la asilimia 6.3
ikilinganishwa na lita za mafuta bilioni 5.36
zilizoagizwa mwaka 2017. Kati ya kiasi hiki,
lita bilioni 3.27 sawa na asilimia 57.4 ya
mafuta yote yaliyoingizwa yalikuwa ni kwa
ajili ya matumizi ya ndani, sawa na ongezeko
la asilimia 2.5 ikilinganishwa na lita bilioni
3.19 zilizoingizwa mwaka 2017.
143. Mheshimiwa Spika, kwa upande
mwingine, lita bilioni 2.43, sawa na asilimia
42.6 ya mafuta yote yaliyoingizwa yalikuwa
ni kwa ajili ya nchi jirani (on transit) sawa
na ongezeko la asilimia 12 ikilinganishwa
na mafuta ya transit yaliyoingizwa mwaka
2017. Kiasi cha mafuta ya dizeli yaliongezeka
kwa asilimia 1.3 tu wakati mafuta ya taa na
mafuta mazito yalipungua kwa asilimia 11
na asilimia 54.4 sawia ikilinganishwa na
mwaka 2017. Hii inatokana na kupungua
kwa matumizi ya mafuta ya dizeli na mafuta
mazito katika uzalishaji wa umeme. Pia,
matumizi ya mafuta ya taa yanaendelea
kupungua kutokana ongezeko la usambazaji
wa umeme nchini hasa vijijini.
144. Mheshimiwa Spika, kuanzia mwezi
Julai, 2018 Bandari ya Mtwara ilianza
kupokea mafuta kwa ajili ya matumizi ya ndani
103
sambamba na Bandari za Dar es Salaam na
Tanga. Kuanza kutumika tena kwa bandari
hii kupokea mafuta kumeleta unafuu wa
bei na upatikanaji wa mafuta kwa wananchi
wa mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Unafuu huu wa bei umetokana na kupungua
au kuondolewa kabisa kwa gharama za
usafirishaji kutoka Dar es Salaam kwenda
mikoa hiyo. Mathalan, kwa Mkoa wa Mtwara
takriban Shilingi 72 kwa lita zilizokuwa
zinatumika kusafirisha mafuta kutoka Dar es
Salaam hadi Mtwara zimeondolewa. Pamoja
na unafuu wa bei, kuanza kutumika kwa
bandari hii kumepunguza muda uliokuwa
ukitumika kusafirisha mafuta kutoka Dar
es Salaam hadi mikoa hiyo ya kusini na
kupunguza uharibifu wa barabara.
145. Mheshimiwa Spika, Mfumo wa
Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja umewezesha
upatikanaji wa mafuta ya kutosha
yanayotabirika na gharama nafuu. Manufaa
mengine ni pamoja na: upatikanaji wa
mafuta yanayotosheleza mahitaji ya nchi
na yenye viwango vya ubora unaotakiwa;
kupungua kwa gharama za uagizaji wa
mafuta ikiwemo Demurrage Charges ambazo
zimeshuka kutoka kati ya siku 30 na 60 hadi
104
kati ya siku 3 na 8; kupatikana kwa takwimu
sahihi za mafuta nchini na hivyo kuimarisha
ukusanyaji wa kodi na tozo mbalimbali
za Serikali; kuvutia uwekezaji katika
miundombinu ya kupokelea na kuhifadhi
mafuta katika Bandari za Tanzania na sehemu
mbalimbali za kimkakati (Strategic Areas)
nchini; na kuendelea kuvutia nchi za jirani
(Uganda, Rwanda, Burundi, DRC, Zambia na
Malawi) kupokea mafuta yao kupitia Bandari
za Tanzania na hivyo kuongeza mapato ya
nchi.
146. Mheshimiwa Spika, pamoja na
manufaa hayo Serikali inaendelea kuvutia
wawekezaji zaidi kutumia mfumo huu ambapo
Serikali ya Tanzania imeanza majadiliano
na Rwanda ili kuanza kutumia Bandari ya
Kemondo iliyopo Bukoba kupokea mafuta
kwa ajili ya matumizi ya nchi hiyo. Mafuta
hayo yatasafirishwa kwa njia ya reli kutoka
Dar es Salaam au Tanga. Aidha, Serikali ya
Tanzania imedhamiria kukamilisha ujenzi
wa miundombinu ya Bandari ya Mbamba
Bay pamoja na barabara ili kuleta wepesi
kwa nchi ya Malawi kupitisha mafuta yake
nchini kupitia Bandari ya Mtwara.
105
147. Mheshimiwa Spika, Serikali
inaendelea na tafiti za namna bora ya
kutekeleza uagizaji wa pamoja wa gesi ya
mitungi kwa ajili ya kupikia majumbani
(Liquefied Petroleum Gas LPG) nchini kwa
Mfumo wa Uagizaji wa Pamoja (BPS). Kiwango
cha uagizaji wa gesi ya LPG kimeongezeka
kufikia tani 142,940 kwa mwaka 2018
ikilinganishwa na tani 107,263 kwa mwaka
2017, sawa na ongezeko la asilimia 33.
Ongezeko hili linatokana na: kuongezeka kwa
uelewa wa watumiaji kuhusu faida za kutumia
gesi; na kuongezeka kwa miundombinu ya
kujazia, kuhifadhia, na kusambaza LPG.
148. Mheshimiwa Spika, Serikali
inatambua kuwa katika maeneo mengi ya
vijijini mafuta yanatunzwa na kuuzwa kwa
namna hatarishi. Hali hiyo imetokana na
kusuasua kwa uwekezaji wa ujenzi wa vituo
vya mafuta katika maeneo hayo. Katika
kutafuta ufumbuzi wa suala hilo, mwezi
Septemba, 2018 EWURA iliingia mkataba na
Kitengo cha Ushirikiano na Viwanda (Bureau
of Industrial Cooperation - BICO) cha Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam ili kubuni namna
bora na salama ya kusambaza mafuta vijijini
kwa kutumia vituo vinavyohamishika (mobile
106
fuel dispensing facilities). Tayari BICO
wameshaanza kutengeneza mfumo huo
kwa ajili ya majaribio ambao unatarajiwa
kukamilika mwezi Juni, 2019. Ili kuwezesha
Mfumo huo kufanya kazi, EWURA
imeshaandaa Kanuni zitakazotumika
kusimamia mfumo husika na zitapelekwa
kwa wadau ili kupata maoni kabla ya kuanza
kutumika. Lengo la Serikali ni kuhakikisha
usalama na upatikanaji wa mafuta katika
maeneo ya vijijini.
MRADI WA KUJENGA UWEZO KATIKA
SEKTA NDOGO YA MAFUTA NA GESI
ASILIA
149. Mheshimiwa Spika, Mradi wa
Usimamizi wa Rasilimali za Mafuta na Gesi
Asilia Nchini (Institutional Support Project for
Domestic Resource Mobilization and Natural
Resource Governance) una lengo la kujenga
uwezo kwa watendaji wa tasnia ya uziduaji
(extractive industry). Lengo kuu likiwa ni
kuwezesha Serikali kusimamia mapato
hususan katika sekta ndogo ya mafuta na
gesi asilia. Mradi huu unatekelezwa kwa
makubaliano kati ya Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na Mfuko wa
Maendeleo ya Afrika (African Development
107
Fund) ulio chini ya Benki ya Maendeleo ya
Afrika.
150. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2018/19 kazi zilizotekelezwa ni: kukamilisha
mikataba itakayowezesha ujenzi wa skana
ya Bandari ya Dar es Salaam pamoja na
ununuzi wa vifaa vya kuhifadhia data za
Petroli za PURA. Aidha, kupitia mradi huu
TPDC imefanikiwa kuchakata na kutafsiri
data za mitetemo za 3D na kuandaa Mpango
wa Uchorongaji kisima cha utafiti katika
Kitalu cha Mnazi Bay Kaskazini. Vilevile,
mradi umewezesha mafunzo ya muda mrefu
kwa watumishi 8 kutoka TPDC na mafunzo
ya muda mfupi kwa watumishi 50 wa Wizara,
PURA, EWURA, TRA na Timu ya Majadiliano
ya Mradi wa LNG katika masuala ya usimamizi
na uendeshaji ya miradi ya mafuta na gesi
asilia.
151. Mheshimiwa Spika, kwa mwaka
2019/20, kazi zilizopangwa kutekelezwa ni
pamoja na: ununuzi wa mifumo ya ukusanyaji
mapato, skana, mfumo wa kielektroniki wa
uondoshaji shehena bandarini na katika
mipaka, kukamilisha ununuzi na ufungaji
wa vifaa vya kuhifadhia data za petroli.
108
Jumla ya Shilingi bilioni 6.34 zimetengwa
kwa ajili ya utekelezaji wa mradi kwa mwaka
2019/20 ambapo kati ya fedha hizo Shilingi
bilioni 2.60 ni fedha za ndani na Shilingi
bilioni 3.74 ni fedha za nje.
E. UIMARISHAJI WA MAWASILIANO
KATI YA WIZARA NA JAMII
152. Mheshimiwa Spika, katika hatua
ya kuimarisha mawasiliano kati ya Wizara
na Jamii kuhusu masuala yanayotekelezwa
na Serikali chini ya Sekta ya Nishati, Wizara
imeendelea kuandaa na kutoa taarifa kwa
wadau wa ndani na nje ya nchi. Taarifa
hizo zinajumuisha: kuratibu mahojiano kati
ya Waziri wa Nishati na Jarida la Forbes
Afrika litakalochapisha mafanikio ya Sekta
ya Nishati; kuratibu mikutano ya wadau wa
umeme kuhusu Mradi wa Rufiji iliyofanyika
katika mikoa ya Morogoro, Iringa, Mbeya,
Njombe na Pwani kwa lengo la kujenga
uelewa kwa wananchi na kuwahamasisha
juu ya utunzaji wa vyanzo vinavyotiririsha
maji katika Mto Rufiji; kuratibu uandaaji
na urushaji wa makala (documentary)
iliyoeleza mafanikio ya Sekta ya Nishati ya
miaka mitatu (2015-2018) ambayo ilirushwa
na Kituo cha Televisheni ya Taifa (TBC 1)
109
tarehe 13 Septemba, 2018; na kusambaza
habari za Wizara na Taasisi zake katika
Magazeti na Mitandao ya Kijamii ikiwemo
ya facebook, Twitter, Instagram na You Tube
pamoja na kushughulikia kero za wananchi
zinazotumwa katika mitandao hiyo. Aidha,
Wizara imezindua jarida (Nishati News
Bulletin) linalotoa taarifa mbalimbali kuhusu
Sekta ya Nishati.
153. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2019/20, Wizara kwa kushirikiana na
wadau mbalimbali itaendelea kuimarisha
mawasiliano na Jamii ili kuendelea kukuza
uelewa wa masuala yanayotekelezwa na
Serikali chini ya Sekta ya Nishati. Pamoja
na mambo mengine, Wizara itaendelea kutoa
taarifa mbalimbali katika maeneo muhimu
na miradi mikubwa inayotekelezwa na Wizara
katika kipindi husika.
F. AJIRA NA MAENDELEO YA
RASILIMALIWATU
154. Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza
majukumu ya Wizara kwa ufanisi baada
ya kugawanywa kwa iliyokuwa Wizara
ya Nishati na Madini, Wizara ya Nishati
iliandaa na kutekeleza Muundo wake ambao
110
uliidhinishwa mwezi Juni, 2018. Kutokana
na kuidhinishwa kwa Muundo huo, Wizara
imeandaa Mahitaji ya Kazi (Job Listing);
Maelezo ya Kazi (Job Descripitions) na
mapendekezo ya kujaza nafasi mbalimbali za
Uongozi kulingana na Muundo huo. Nyaraka
hizo ziliwasilishwa katika Mamlaka husika
kwa hatua zaidi. Wizara pia ilisimamia
maandalizi ya Miundo ya Taasisi zilizo chini
yake (TPDC na PURA) baada ya Miundo yake
kuidhinishwa. Taratibu za kujaza nafasi
kulingana na Miundo hiyo zinaendelea
kutekelezwa. Vilevile, Miundo ya TANESCO
na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa pamoja
(PBPA) bado inaendelea kukamilishwa
ili kuziwezesha Taasisi hizo kutekeleza
majukumu yake kwa ufanisi.
155. Mheshimiwa Spika, ili kuongeza
tija na motisha kwa Watumishi, katika
mwaka 2018/19 Wizara iliwapandisha
vyeo Watumishi 41 na kubadilisha kada
(re-categorization) Watumishi watatu (3).
Katika mwaka 2019/20, Wizara inatarajia
kubadilisha kada za Watumishi wanne (4),
kujaza nafasi 13 za uongozi na kuwapandisha
vyeo Watumishi 48. Aidha, Wizara na Taasisi
zake zinatarajia kuajiri jumla ya Watumishi
111
217 ambapo kati ya idadi hiyo, Wizara itaajiri
Watumishi 53; TPDC Watumishi 116; REA
Watumishi 9 na PURA Watumishi 39.
156. Mheshimiwa Spika, kwa kutambua
umuhimu wa masuala ya mafuta na gesi asilia
nchini, Wizara imeendelea kushirikiana na
Washirika wa Maendeleo ili kutoa ufadhili wa
masomo kwa Watanzania katika Shahada ya
Kwanza, Uzamili na Uzamivu ili kuhakikisha
kuwa nchi inakuwa na Wataalamu wake wa
kutosha katika sekta hiyo. Katika mwaka
2018/19 Watanzania 18 walipata fursa
ya ufadhili wa masomo kutoka Serikali ya
Jamhuri ya Watu wa China katika tasnia
ya mafuta na gesi asilia. Aidha, Watanzania
wengine 22 wanatarajiwa kwenda masomoni
kupitia ufadhili wa Serikali ya China kwa
mwaka 2019/20. Wizara imewasilisha
Ubalozi wa China mapendekezo ya waombaji
wenye sifa kwa ajili ya kukamilisha hatua
muhimu za uchambuzi.
157. Mheshimiwa Spika, vilevile, katika
kuwajengea uwezo Watumishi wa Wizara na
Taasisi nyingine za Serikali, katika mwaka
2018/19 Wizara imewezesha na kutoa
ufadhili wa mafunzo ya muda mrefu kwa
Watumishi 10 na mafunzo ya muda mfupi
112
kwa Watumishi 47. Kwa mwaka 2019/20,
Watumishi 10 wanatarajiwa kupata fursa ya
mafunzo ya muda mrefu na Watumishi 75
mafunzo ya muda mfupi.
158. Mheshimiwa Spika, Wizara
imeendelea kutoa huduma ya lishe na mlo
kamili pamoja na fedha kwa ajili ya usafiri
wakati wa kuhudhuria matibabu kwa
watumishi wanaoishi na Virusi vya UKIMWI
ili waendelee kulitumikia Taifa. Wizara pia
iliendesha mafunzo ya namna ya kujikinga
na Virusi vya UKIMWI na Magonjwa Sugu
Yasiyoambukizwa (MSY), Ushauri Nasaha
na Lishe Bora. Sambamba na jitihada hizo,
Wizara pia inaendelea kuwahamasisha
Watumishi kufanya mazoezi ya mwili na
kupima afya hususan katika Magonjwa
Sugu Yasiyoambukiza kama vile magonjwa
ya shinikizo la damu, kisukari na saratani.
159. Mheshimiwa Spika, katika mwaka
2018/19, Wizara imekamilisha awamu ya
kwanza ya ujenzi wa jengo la Ofisi za Makao
Makuu ya Wizara katika Mji Mpya wa Serikali
eneo la Mtumba Jijini Dodoma. Utekelezaji
wa mradi huo ulianza mwezi Desemba 2018
na kukamilika mwezi Aprili 2019. Aidha,
jengo hilo la Wizara limeanza kutumiwa rasmi
113
tarehe 15 Aprili, 2019 na Viongozi Wakuu
wa Wizara, Wakuu wa Idara na baadhi ya
Wakuu wa Vitengo na Sehemu. Katika mwaka
2019/20 Wizara inatarajia kuanza ujenzi wa
jengo la pili la ofisi litakalokidhi mahitaji ya
watumishi wote ambapo Shilingi bilioni 2.4
zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza ujenzi
huo.
G. USHIRIKIANO WA KIKANDA NA
KIMATAIFA
160. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia
Wizara ya Nishati inapenda kuwashukuru
Washirika wa Maendeleo na nchi wahisani
ambao wameendelea kutoa michango yao
katika kufanikisha utekelezaji wa shughuli
mbalimbali za Wizara. Kwa niaba ya Serikali,
napenda kutambua mchango wa: Benki ya
Maendeleo ya Afrika (AfDB), Benki ya Dunia
(WB), Benki ya Ushirikiano wa Kimataifa
ya Japan (JBIC), United Bank for Africa
(UBA); Economic Development Cooperation
Fund (EDCF - Korea), Mfuko wa Uendelezaji
Jotoardhi (Geothermal Risk Mitigation
Facility - GRMF) pamoja na Taasisi na
Mashirika ya: JICA (Japan), KfW (Germany),
AFD (Ufaransa), Sida (Sweden), Umoja wa
Ulaya (EU), Shirika la Maendeleo la Umoja
114
wa Mataifa (UNDP), Shirika la Maendeleo la
Canada (CIDA) na USAID (Marekani).
161. Mheshimiwa Spika, pia natoa
shukrani kwa Serikali za Burundi, Canada,
China, Finland, Iceland, Japan, Sweden,
Ufaransa, Ujerumani, Norway, Korea ya
Kusini, Misri, Rwanda, Uganda na Zambia
kwa ushirikiano wao katika kuendeleza
Sekta ya Nishati. Vilevile, nishukuru
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC) kwa ushirikiano katika masuala ya
kikanda yanayohusu Sekta hii. Kwa kipindi
cha mwaka 2019/20 Wizara itaendelea
kushirikiana kwa karibu na Washirika
hawa wa maendeleo na wadau wengine
watakaojitokeza ili kuhakikisha kuwa
Sekta ya Nishati inaendelea kuwa
chachu ya sekta nyingine katika kuleta
maendeleo nchini.
H. SHUKRANI
162. Mheshimiwa Spika, naomba
kutumia fursa hii kumshukuru Naibu Waziri
wa Nishati, Mhe. Subira Khamis Mgalu, (Mb.)
kwa kunisaidia kwa kiasi kikubwa na kwa
dhati kabisa katika kutekeleza majukumu
115
yangu. Aidha, napenda kumshukuru Katibu
Mkuu Dkt. Hamisi Hassan Mwinyimvua kwa
uchapakazi mahiri na ushirikiano anaonipa
katika kutekeleza shughuli za kila siku za
Wizara. Vilevile, nawashukuru Makamishna,
Wakuu wa Idara na Vitengo, Wenyeviti na
Wajumbe wa Bodi, Wakuu wa Taasisi zilizo
chini ya Wizara na Watumishi wote kwa
ujumla kwa ushirikiano wao na juhudi
zao wanazofanya kwa ajili ya kufanikisha
kufikiwa kwa malengo ya Wizara.
163. Mheshimiwa Spika, kwa kipekee
napenda nichukue nafasi hii kuwashukuru
wananchi wa Jimbo la Chato kwa ushirikiano
wanaonipa katika kutekekeleza shughuli
mbalimbali za maendeleo ya jimbo. Nawaahidi
kuwa sitawaangusha na nitaendelea
kushirikiana nanyi katika kubuni mikakati
mbalimbali ya kuendeleza shughuli za jimbo.
Naishukuru sana familia yangu ikiongozwa
na mke wangu Mama Kalemani pamoja na
watoto wangu kwa kuendelea kuniombea
na kuniunga mkono katika kutekeleza
majukumu ya kitaifa.
116
I. HITIMISHO
164. Mheshimiwa Spika, Bajeti ya
Mwaka 2019/20 inalenga kutekeleza
dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kuwa
inazalisha umeme wa kutosha, wa uhakika,
unaotabirika na wenye gharama nafuu.
Vilevile, bajeti imelenga kuimarisha shughuli
za utafutaji na biashara ya mafuta na gesi
asilia pamoja na kuwezesha wananchi
kunufaika na rasilimali hizo. Lengo ni
kuiwezesha Serikali kufikia azma ya kujenga
uchumi wa viwanda na kufikia uchumi wa
kati ifikapo mwaka 2025.
165. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka
2019/20, Wizara ya Nishati inakadiria
kutumia jumla ya Shilingi trilioni 2.142
ikilinganishwa na Shilingi trilioni 1.692
iliyotengwa kwa Mwaka 2018/19, sawa na
ongezeko la asilimia 26.6. Ongezeko hili
limetokana na kuanza kutekelezwa kwa
mradi mkubwa wa Rufiji utakaozalisha MW
2,115.
166. Mheshimiwa Spika, fedha nyingi za
ndani za miradi ya maendeleo zilizotengwa
kwa mwaka 2019/20 zimeelekezwa katika
miradi mitatu (3) ya kimkakati ambazo ni
117
Shilingi trilioni 1.86, sawa na asilimia
95.1 ya Bajeti yote ya Ndani. Miradi hiyo ni:
Mradi wa Kuzalisha Umeme katika Mto Rufiji,
MW 2,115 (Shilingi trilioni 1.44); Mradi
Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini
Awamu ya Tatu (Shilingi bilioni 363.11); na
Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Kinyerezi I
Extension MW 185 (Shilingi bilioni 60).
167. Mheshimiwa Spika, naomba
kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu
sasa liidhinishe bajeti ya jumla ya Shilingi
2,142,793,309,000 kwa ajili ya matumizi
ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake.
Mchanganuo wa fedha hizo ni kama ifuatavyo:
(i) Shilingi 2,116,454,000,000 sawa
na asilimia 98.8 kwa ajili ya Miradi ya
Maendeleo. Kati ya fedha hizo za maendeleo,
Shilingi 1,956,372,000,000 ni fedha za
ndani na Shilingi 160,082,000,000 ni fedha
za nje; na
(ii) Shilingi 26,339,309,000 sawa na
asilimia 1.2 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida.
Kati ya fedha hizo Shilingi 15,025,821,000
kwa ajili ya Matumizi Mengineyo (OC) na
Shilingi 11,313,488,000 kwa ajili ya
mishahara (PE) ya watumishi wa Wizara na
118
Taasisi zilizo chini yake.
168. Mheshimiwa Spika, naomba tena
nitoe shukrani zangu za dhati kwako na kwa
Waheshimiwa Wabunge wote kwa kunisikiliza.
Hotuba hii pia inapatikana katika Tovuti ya
Wizara kwa anuani ya www.nishati.go.tz.
Vilevile, Hotuba hii ina vielelezo mbalimbali
ambavyo vimeambatishwa kwa ajili ya
ufafanuzi wa masuala muhimu yanayohusu
Sekta ya Nishati.
169. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa
hoja.
119
1A: Mfumo wa Gridi ya Taifa
Na.
Jina la Kituo
Uwezo (MW)
1 Kidatu 204.00
2 Kihansi 180.00
3 Mtera 80.00
4 New Pangani Falls 68.00
5 Hale 21.00
6 Nyumba ya Mungu 8.00
7 Uwemba 0.84
8 Mwenga 4.00
9 Yovi 0.95
10 Matembwe 0.59
11 Darakuta 0.32
12 Andoya 1.00
13 Tulila 5.00
Jumla Ndogo - Maji
573.70
1 Songas 189.00
2 Ubungo Gas PP I 102.00
3 Tegeta Gas PP 45.00
VIELELEZO KUHUSU SEKTA YA
NISHATI
1.0 UMEME NA NISHATI JADIDIFU
Kielelezo Na. 1: Uwezo wa Mitambo ya
Kufua Umeme Nchini hadi Mwezi Mei,
2019
120
4 Ubungo Gas PP II 129.00
5 Kinyerezi I 150.00
6 Kinyerezi II 248.22
7 Mtwara Gas PP 22.00
8 Somanga Gas PP 7.50
Jumla Ndogo - Gesi 892.72
1 Zuzu 7.40
2 Nyakato 63.00
3 Biharamuro 4.14
4 Ngara 2.50
5 Songea 7.67
6 Namtumbo 0.34
7 Ludewa 1.27
8 Mbinga 2.00
9 Madaba 0.48
Jumla Ndogo - Mafuta 88.80
1 TANWAT 1.50
2 TPC 9.00
Jumla Ndogo - Biomass 10.50
Jumla - Gridi 1,565.72
Chanzo: TANESCO
121
1B: Mfumo Nje ya Gridi ya Taifa
Na.
Jina la Kituo
Uwezo (MW)
1 Bukoba 2.56
2 Kasulu 2.50
3 Kibondo 2.50
4 Kigoma 8.25
5 Liwale 0.85
6 Loliondo 5.00
7 Mafia 1.89
8 Mpanda 4.16
9 Sumbawanga 5.00
10 Tunduru 3.00
11 Inyonga 0.48
Jumla – Nje ya Gridi 36.18
Jumla Kuu 1,601.90
Chanzo: TANESCO
122
Kielelezo Na. 2: Njia za Kusafirisha
Umeme na Vituo vya Kupoza Umeme
Na.
Njia za Usafirishaji Umeme
(Transmission Lines)
Urefu (km)
hadi Mei,
2019
1 Njia kuu za msongo wa 400kV 670
2 Njia kuu za msongo wa 220kV 2,940.7
3 Njia kuu za msongo wa 132kV 1,697.47
4 Njia kuu za msongo wa 66kV 543
Jumla 5,851.17
Na. Vituo Vya Kupoza Umeme
(Substations)
Idadi
1 Vituo vya msongo wa 220kV 20
2 Vituo vya msongo wa 132kV 27
3 Vituo vya msongo wa 66kV 7
4 Vituo vya msongo wa
33/11kV
67
Jumla 121
Na. Urefu wa Mkongo wa
Mawasiliano wa TANESCO
Urefu
1 Mkongo wa Mawasiliano (Op-
tic Fibre Cable) – km
3,200
Chanzo: TANESCO
123
Kielelezo Na. 3: Taasisi Zilizopatiwa Umeme Kupitia REA hadi
kufikia tarehe 15 Mei, 2019
Na Mradi Taasisi
za Elimu
Biasha-
ra
Pump
za Maji
Taasisi
za Afya
Nyumba
za Ibada
1 Miradi ya Awali 1,099 1,648 64 412 813
2 Turnkey Phase II 1,931 1,743 126 752 53
3 Turnkey Phase III 38 27 10 22 15
4 BTIP_VEI 25 15 3 7 7
5 Densification Round I 21 10 4 1 3
6 Makambako-Songea 45 8 3 11 66
7 Solar za Makonteina 6 0 0 6 27
Jumla 3,165 3,451 210 1,211 984 Chanzo: REA
Kielelezo Na. 4: Maeneo yenye Viashiria
vya Jotoardhi Nchini
Chanzo: TGDC
124
125
2.0 MAFUTA NA GESI ASILIA
Kielelezo Na. 5: Matumizi ya Gesi Asilia katika Kipindi cha
Mwaka 2016 – 2018 (BCF)
Chanzo: TPDC
126
Kielelezo Na. 6: Mwenendo wa Uagizaji Mafuta kwa Matumizi
ya Ndani kwa Mwaka 2018
Chanzo: PBPA
127
Kielelezo Na. 7: Ujenzi wa Miundombinu ya Kusambaza Gesi
Asilia Majumbani (Mikocheni – Dar es Salaam)
Chanzo: TPDC
128
Kielelezo Na. 8: Mtambo wa Kupunguza Msukumo wa Gesi
Asilia (Pressure Reduction and Metering Station – PRSM)
uliosimikwa Ubungo Kibo katika Valvu Na. 15
Chanzo: TPDC
129
Kielelezo Na. 9: Mpango wa Kusambaza Gesi Asilia Mtwara
(kwa kuanzia eneo la Bandari)
Chanzo: TPDC
Kielelezo Na. 10: Mpango wa Kusambaza
Gesi Asilia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
(UDSM)
Chanzo: TPDC
130
131
Kielelezo Na. 11: Gesi ya Kupikia (LPG) iliyoagizwa Nchini kwa
Mwaka 2010 – 2018
Chanzo: EWURA
132
Kielelezo Na. 12: Wastani wa Mauzo ya Mafuta Kimkoa katika
Vituo mbalimbali Nchini
Mikoa Wastani wa Matumizi
ya Mafuta kwa
Mwaka (Lita)
Idadi ya
Vituo vya
Mafuta
Wastani wa
Mauzo kwa
Kituo kwa
Mwaka
(Lita)
Arusha 96,950,638 98 989,292
Coast 74,434,223 94 791,853
Dar es Salaam 493,472,968 200 2,467,365
Dodoma 54,953,984 66 832,636
Geita 18,332,546 55 333,319
Iringa 43,023,787 34 1,265,405
Kagera 32,530,523 70 464,722
Katavi 4,839,897 9 537,766
Kigoma 13,708,412 44 311,555
Kilimanjaro 52,070,384 92 565,982
133
Mikoa Wastani wa Matumizi
ya Mafuta kwa
Mwaka (Lita)
Idadi ya
Vituo vya
Mafuta
Wastani wa
Mauzo kwa
Kituo kwa
Mwaka
(Lita)
Lindi 14,020,811 32 438,150
Manyara 15,105,887 48 314,706
Mara 14,038,293 55 255,242
Mbeya 80,767,764 62 1,302,706
Morogoro 61,203,623 73 838,406
Mtwara 51,121,346 36 1,420,037
Mwanza 137,426,041 88 1,561,660
Njombe 29,818,207 32 931,819
Rukwa 13,741,841 17 808,344
Ruvuma 30,352,084 39 778,259
Shinyanga 35,280,506 53 665,670
Simiyu 3,654,477 26 140,557
134
Mikoa Wastani wa Matumizi
ya Mafuta kwa
Mwaka (Lita)
Idadi ya
Vituo vya
Mafuta
Wastani wa
Mauzo kwa
Kituo kwa
Mwaka
(Lita)
Singida 16,445,910 20 822,296
Songwe 9,187,073 28 328,110
Tabora 18,125,550 30 604,185
Tanga 59,305,549 59 1,005,179
Jumla 1,473,912,325 1,460 20,775,220
Chanzo: EWURA
135
Kielelezo Na. 13: Mwenendo wa Bei za Mafuta Safi katika
Soko la Dunia kwa Mwaka 2017 na 2018
Chanzo: EWURA
136
Kielelezo Na. 14: Idadi ya Vituo vya
Mafuta Nchini hadi Mwezi Aprili, 2019
MKOA
JUMLA YA
VITUO VYA
MAFUTA HADI
TAREHE 31
DESEMBA 2018
JUMLA YA
VITUO VYA
MAFUTA HADI
TAREHE 30
APRILI 2019
Arusha 98 98
Coast 94 104
Dar es Salaam 200 220
Dodoma 66 64
Geita 55 60
Iringa 34 35
Kagera 70 65
Katavi 9 11
Kigoma 44 39
Kilimanjaro 92 92
Lindi 32 25
Manyara 48 50
Mara 55 56
Mbeya 62 64
Morogoro 73 71
Mtwara 36 36
Mwanza 88 89
Njombe 32 32
Rukwa 17 18
Ruvuma 39 37
Shinyanga 53 59
137
MKOA
JUMLA YA
VITUO VYA
MAFUTA HADI
TAREHE 31
DESEMBA 2018
JUMLA YA
VITUO VYA
MAFUTA HADI
TAREHE 30
APRILI 2019
Simiyu 26 28
Singida 20 22
Songwe 28 29
Tabora 30 31
Tanga 59 65
JUMLA YA
IDADI YA
VITUO VYA
MAFUTA
1460
1500
Chanzo: EWURA
138
Waziri wa Nishati, Dkt Medard Kalemani (wa pili kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori (wa kwanza kushoto), wakiwasha jiko linalotumia gesi asilia tayari kwa matumizi ya nyumbani katika eneo la Mikocheni Mtaa wa TPDC jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu akiwasha rasmi umeme katika Kijiji cha Palangu wilayani Songea, mkoani Ruvuma. Kulia kwake ni Mkuu wa Wilaya ya Songea,
Pololiti Mgema.