65
MWONGOZO WA USIMAMIZI WA DAWA ZA KUTIBU KIFUA KIKUU NA UKOMA JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII (MOHSW) MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI KIFUA KIKUU NA UKOMA (NTLP)

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII (MOHSW...3. Utoaji wa taarifa za idadi ya wagonjwa na kiasi cha shehena katika kituo cha tiba 4. Utunzaji wa kumbukumbu na utoaji wa taarifa katika

  • Upload
    others

  • View
    6

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

  • MWONGOZO WA

    USIMAMIZI WA DAWA ZA

    KUTIBU KIFUA KIKUU NA

    UKOMA

    JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA

    WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

    (MOHSW)

    MPANGO WA TAIFA WA KUDHIBITI KIFUA

    KIKUU NA UKOMA

    (NTLP)

  • 2

    SHUKRANI

    Mwongozo huu umetayarishwa kama sehemu ya msaada wa kitaalamu wa mradi wa Supply Chain

    Management System (SCMS) kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (Tanzania) kupitia Mpango wa Taifa

    wa Kudhibiti kifua kikuu na ukoma (NTLP) kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa mfumo wa ugavi wa

    dawa za kutibu kifua kikuu na ukoma. SCMS ni mradi unaodhaminiwa na Shirika la Misaada ya

    Kimaendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID) na kutekelezwa na John Snow Inc (JSI) kwa mkataba

    namba GPO-I-00-05-00032-00.

  • 3

    YALIYOMO

    VIFUPISHO NA MAANA YA MANENO YA KITAALAMU ............................................................................................ 5

    SURA YA 1: UTANGULIZI .................................................................................................................................... 6

    A: MADHUMUNI YA MWONGOZO HUU .................................................................................................................... 7

    B: DAWA ZINAZOSIMAMIWA KUPITIA MFUMO HUU ................................................................................................ 7

    C: NANI ANAPASWA KUUTUMIA MWONGOZO HUU? .............................................................................................. 9

    D: MWONGOZO HUU UTAKUSAIDIAJE? .................................................................................................................... 9

    E: UTARATIBU WA MTIRIRIKO WA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA NA TAARIFA KATIKA MFUMO WA

    USIMAMIZI WA DAWA HIZO ................................................................................................................................... 11

    F: MUHTASARI WA MFUMO .................................................................................................................................... 12

    SURA YA 2: FOMU ZA KUMBUKUMBU NA TAARIFA ZINAZOTUMIKA KATIKA MFUMO WA UGAVI WA DAWA ZA

    KIFUA KIKUU NA UKOMA .................................................................................................................................... 13

    SURA YA 3: UWAJIBIKAJI KATIKA USIMAMIZI WA UAGIZAJI NA USAMBAZAJI WA SHEHENA ZA DAWA ZA KIFUA

    KIKUU NA UKOMA ............................................................................................................................................... 14

    A. MAJUKUMU KATIKA KITUO CHA TIBA ............................................................................................................ 14

    B. MAJUKUMU KATIKA NGAZI WILAYA .............................................................................................................. 15

    C. MAJUKUMU KATIKA NGAZI YA MKOA ........................................................................................................... 17

    D. MAJUKUMU YA BOHARI KUU YA MADAWA (MSD) ........................................................................................ 17

    E. WIZARA YA AFYA (NTLP) ................................................................................................................................ 18

    SURA YA 4: UTUNZAJI WA HESABU ZA BIDHAA ZINAZOTOLEWA ..................................................................... 19

    SURA YA 5. UAGIZAJI.......................................................................................................................................... 20

    A: KUHAKIKISHA KIASI CHA KUTOSHA CHA SHEHENA ............................................................................................. 20

    B: TATHMINI YA KIASI CHA SHEHENA ...................................................................................................................... 20

    C: NAMNA YA KUTAMBUA MWEZI WA MATIBABU ATAKAOKUWA MGONJWA .................................................... 24

    D: UTOAJI WA TAARIFA WA VITUO VYA TIBA .......................................................................................................... 25

    E: JINSI WILAYA INAVYOAGIZA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA ....................................................................... 27

    F: MAOMBI YA DHARURA ........................................................................................................................................ 27

    G: UGAWAJI WA DAWA KUTOKA MSD KWENDA WILAYANI ................................................................................... 28

    H: UGAWAJI WA DAWA KUTOKA WILAYANI KWENDA VITUONI ............................................................................. 29

    SURA YA 6: KUHIFADHI DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA ........................................................................... 31

    A: HESABU YA MKONO ............................................................................................................................................ 31

    B: UKAGUZI WA BIDHAA KWA MACHO ................................................................................................................... 32

    C: KUHARIBU MALI ISIYOFAA KWA MATUMIZI ........................................................................................................ 32

    SURA YA 7: FOMU ZINAZOTUMIKA KATIKA MFUMO WA USIMAMIZI WA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA

    NA UFAFANUZI WAKE .......................................................................................................................................... 33

  • 4

    A. UFAFANUZI A: UJAZAJI WA DOZI ZILIZOGAWIWA/TOLEWA KWA MGONJWA KATIKA KADI YA WA KIFUA

    KIKUU ...................................................................................................................................................................... 34

    B. FOMU YA TAARIFA YA KITUO YA MWEZI YA DAWA ZA KUTIBU KIFUA KIKUU NA UKOMA ............................. 38

    C. UFAFANUZI B: UJAZAJI WA FOMU YA TAARIFA YA MWEZI YA KITUO ............................................................ 39

    D. FOMU YA TAARIFA YA KITUO YA MWEZI YA DAWA ZA KUTIBU KIFUA KIKUU NA UKOMA ............................. 43

    E. UFAFANUZI C: KUHAKIKI TAARIFA KWENYE FOMU YA MWEZI YA KITUO NAKUKOKOTOA KIASI CHA DAWA

    CHA KUGAWA ......................................................................................................................................................... 46

    F. UFAFANUZI D: UJAZAJI WA TAARIFA NA MAOMBI YA ROBO MWAKA YA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA

    YA WILAYA............................................................................................................................................................... 53

    G. FOMU YA KUNAKILI KIASI CHA DAWA KILICHOTOLEWA VITUONI ................................................................. 59

    H. FOMU YA TAARIFA NA MAOMBI YA ROBO MWAKA YA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA YA WILAYA ...... 60

  • 5

    VIFUPISHO NA MAANA YA MANENO YA KITAALAMU

    UFUPISHO KIINGEREZA KISWAHILI

    AMC Average Monthly Consumption. Wastani wa matumizi kwa mwezi

    ARV Antiretroviral drugs Dawa za kupoza makali ya UKIMWI

    CHMT Council Health Management Team Timu ya Halmashauri ya Usimamizi wa Afya

    DTLC District Tb and Leprosy Coordinator Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa wilaya

    DMO District Medical Officer Mganga Mkuu wa Wilaya

    DOT Directly observed therapy

    EOP Emergency order point Uwepo wa shehena inayoashiria kuwa ni lazima

    uagizaji wa dharura ufanyike

    FDC Fixed Dose Combination Kidonge cha dawa mchanganyiko

    FEFO First to Expire, First Out Tumia kwanza zinazokaribia kwisha muda wake

    wa matumizi

    GOT Government of Tanzania Serikali ya Tanzania

    JSI John Snow Inc. John Snow Inc.

    LMIS Logistics Management Information System Mfumo wa Taarifa za uagizaji na usambazaji.

    MDR-TB Multdrug Resistant Tubeculosis Kifua kikuu sugu

    MOS Months of Stock Shehena Inayotosheleza (kwa miezi)

    MSD Medical Stores Department Bohari Kuu ya Madawa

    MOHSW Ministry Of Health and Social Welfare Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

    NTLP National Tuberculosis and Leprosy

    Program

    Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua kikuu na

    ukoma

    R&R Report and Request forms Fomu za Taarifa na Maombi

    RTLC Regional Tb and Leprosy Coordinator Mratibu wa kifua kikuu na ukoma wa mkoa

    SDP Service Delivery Point Kituo cha kutolea Huduma

    SOH Stock on hand; stock in good condition that

    can be given to patients or used with clients.

    SOH does not include any damaged or

    expired stock.

    Shehena iliyopo Mikononi – Ni bidhaa iliyo katika

    hali nzuri na inayoweza kutolewa kwa mteja.

    SOH haihusu shehena iliyoharibika au kwisha

    muda wa matumizi

    SCMS Supply Chain Management System Mfumo wa usimamizi wa Ugavi

    USG United States Government Serikali ya Marekani

  • 6

    SURA YA 1: UTANGULIZI

    Mpango wa Taifa wa Kudhibiti kifua kikuu na ukoma utafanikisha malengo yake

    kutokana na kuwepo kwa jitihada mbalimbali za kuratibu mipango inayohakikisha

    kuwa mahitaji ya dawa ya wagonjwa yanatimizwa. Juhudi hizo ni pamoja na

    kuhakikisha ya kuwa na dawa zinazohitajika na vitendanishi sahihi vya kupimia

    vinapatikana katika kiasi cha kutosha, ziwe katika hali sahihi, zihifadhiwe na

    kufikishwa mahali sahihi,kwa wakati sahihi na gharama sahihi. Ili malengo ya

    mpango huo yaweze kufanikiwa ni sharti mfumo mahususi wa ugavi na usimamizi

    utumike. Utaratibu huo wa ugavi hauna budi uhakikishe kuwa shehena za bidhaa

    zinapatikana katika vituo vyote na kwamba hapatokei matatizo ya kulundikana kwa

    shehena, upungufu, kuishiwa wala ufujaji wa bidhaa hizo.

    Mfumo mzuri wa usimamizi wa dawa za kutibu kifua kikuu na ukoma utasaidia katika

    kuhakikisha kuwa dawa zinapatikana muda wote katika vituo vya kutolea tiba na

    hivyo kuokoa maisha. Upatikanaji wa uhakika wa dawa za kifua kikuu na ukoma

    utawafanya wagonjwa kuwa na imani na mfumo wa tiba na kuwafanya waendelee

    kufika vituoni kwa ajili ya kupata matibabu na pia kusaidia kupunguza tatizo la usugu

    wa vimelea vya ugonjwa na ubora wa tiba.

    Izingatiwe kuwa mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma una fanana

    na mifumo mingine ya usimamizi wa bidhaa za afya mfano Integrated Logistics

    System (ILS) katika mambo mbalimbali mfano upokeaji wa bidhaa, utunzaji wa

    bidhaa,ukaguzi wa macho,matumizi ya kitabu cha leja ya mali. Mambo kama haya

    hayajaelezewa kwa undani katika mwongozo huu isipokuwa yametajwa tu.

    Zipo tofauti muhimu kati ya mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma

    na mifumo mingine kama vile ILS. Tofauti hizo ni kama; katika mfumo huu vituo

    haviagizi dawa kama ilivyo kwenye ILS isipokuwa vinatoa taarifa tu na jukumu la

    kuagiza ni la mfamasia wa wilaya. Katika mfumo huu pia kiasi cha dawa

    zinazohusika ni kidogo ukilinganisha na bidhaa katika mfumo wa ILS. Pia idadi ya

    wagonjwa ni ndogo ikilinganishwa na ile inayohudumiwa na mfumo wa ILS.

  • 7

    A: MADHUMUNI YA MWONGOZO HUU

    Madhumuni ya mwongozo huu ni kutoa utaratibu wa namna dawa za kifua kikuu na

    ukoma zitakavyokuwa zikipatikana katika vituo vinavyotoa huduma kwa wagonjwa

    wa kifua kikuu na ukoma na namna ambavyo wilaya zitakuwa zikiagiza dawa hizi.

    Mwongozo utaainisha hatua zinazohitajika katika kukamilisha shughuli zifuatazo:

    1. Kuhakikisha kuna kiasi cha shehena kinachotakiwa kuwepo MSD, Wilayani

    na katika vituo vya tiba ili kuepusha ukosefu wa dawa na kulundikana

    kunakoweza kusababisha dawa kuisha muda wake wa matumizi kabla ya

    kumfikia mteja.

    2. Uagizaji wa dawa kutoka MSD na kutoka wilayani

    3. Utoaji wa taarifa za idadi ya wagonjwa na kiasi cha shehena katika kituo cha

    tiba

    4. Utunzaji wa kumbukumbu na utoaji wa taarifa katika ngazi ya wilaya na ya

    kituo cha tiba

    5. Ufuatiliaji mbalimbali katika mfumo katika ngazi ya wilaya na ya vituo vya

    kutolea tiba

    Mwongozo huu unaelezea majukumu na kazi za wadau mbalimbali wanaohusika

    na utekelezaji wa mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma.

    Izingatiwe kwamba mwongozo huu siyo mbadala wa mwongozo wa matibabu

    ya kifua kikuu na ukoma

    B: DAWA ZINAZOSIMAMIWA KUPITIA MFUMO HUU

    Mwongozo huu ni kwa ajili ya usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma na wala

    hauhusishi dawa zinazosimamiwa kupitia mifumo mingine kama vile ILS.Pia mwongozo

    huu hauhusishi usimamizi wa dawa za kutibu kifua kikuu sugu (multi-drug resistant

    treatment - MDR)

  • 8

    Dawa zinazohusika ni kama zinavyoonekana kwenye jedwali hapo chini:

    Dawa Ukubwa wa

    kifungashe

    RHZE = Rifampicin 150mg + Isoniazid 75mg + Pyrazinamide 400mg +

    Ethambutol 275mg

    Blista ya vidonge 28

    RH = Rifampicin 150mg + Isoniazid 75mg Blista ya vidonge 28

    RHE = Rifampicin 150mg + Isoniazid 75mg + Ethambutol 400mg Blista ya vidonge 28

    Streptomycin 1g injection Vial

    Water for injection Boksi la vial 100

    RH Rifampicin 60mg + Isoniazid 30mg Blista ya vidonge 6

    RHZ = Rifampicin 60mg + Isoniazid 30mg + Pyrazinamide 50mg Blista ya vidonge 6

    Ethambutol 100mg Boksi la vidonge 500

    Ethambutol 100mg Boksi la vidonge 100

    Isoniazid 100mg Box la vidonge 100

    Isoniazid 300mg Blista ya vidonge 28

    Presdnisolone 5mg Boksi la vidonge 1000

    Pyrazinamide 400mg tabs Boksi la vidonge 1000

    Pyrazinamide 400mg tabs Blista ya vidonge 28

    PB (adult) Rifampicin 300 + Dapsone 100 Blista ya kutumia siku

    28

    PB (peds) Rifampicin 150 + Dapsone 50 Blista ya kutumia siku

    28

    MB (adult) Rifampicin 300 + Clofazimine 100 + Dapsone 100 Blista ya kutumia siku

    28

    MB (peds) Rifampicin 150 + Clofazimine 50 + Dapsone 50 Blista ya kutumia siku

    28

    Clofazimine 50mg Boksi la vidonge 1000

    Clofazimine 100mg Boksi la vidonge 500

    Pyridoxine tabs 50mg P/100 tabs

  • 9

    C: NANI ANAPASWA KUUTUMIA MWONGOZO HUU?

    Walengwa wa mwongozo huu ni watumishi wa mpango wa taifa wa kudhibiti kifua kikuu na ukoma,

    bohari kuu ya madawa, watumishi wa afya katika ngazi ya mikoa na wilaya (wafamasia na waratibu wa

    kifua kikuu na ukoma), RHMT,CHMT, vituo vya tiba na wadau wote wanaotoa msaada katika mradi wa

    kudhibiti kifua kikuu na ukoma

    D: MWONGOZO HUU UTAKUSAIDIAJE?

    Madhumuni makuu ya mwongozo huu ni kuelezea utaratibu madhubuti na wenye ufanisi unaopaswa

    kufuatwa kuhakikisha vituo vinavyotoa huduma ya utoaji dawa kwa wagonjwa wa kifua kikuu na ukoma

    vinapata mahitaji yake ya dawa na kutoa taarifa:

    Kwa kuhakikisha kuwepo kwa shehena ya kutosha ya dawa za kifua kikuu na ukoma

    Kwa kuhakikisha kuwepo kwa hifadhi na usafirishaji wa uhakika wa dawa

    Watoaji huduma za afya wanaelewa wajibu wao katika mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua

    kikuu na ukoma

    Kupunguza uwezekano wa dawa kuisha muda wake wa matumizi zikiwa kwenye stoo au vituo

    vya tiba, ufujaji na upotevu.

    Kuhakikisha uagizaji na usambazaji wa shehena unafanyika kwa kufuata mfumo uliosahihi.

    Lengo la mwongozo huu wa utoaji taarifa uagizaji na usambazaji kama ulivyoelezwa ni kuhakikisha

    kwamba wateja na wagonjwa wanapata dawa kila wanapohitaji. Kwa kutekeleza yaliyopo katika

    mwongozo huu basi lengo kuu la mfumo wa usimamizi na usambazaji wa dawa za kifua kikuu na

    ukoma yatafikiwa

    Lengo la mwongozo huu ni kuhakikisha kuwa kuna;

    Bidhaa Sahihi

    Katika Mahali Sahihi

    Kwa Kiasi Sahihi

    Kwa Wakati Sahihi

    Katika Ubora Sahihi

    Na kwa Gharama Sahihi

    Haya ndio mambo muhimu yanayopaswa kutekelezwa katika mfumo wa uagizaji na usambazaji ili

    kuweza kukidhi mahitaji ya wateja.

  • 10

    Hivi vikimaanisha:

    Shehena Sahihi inapatikana: Dawa za kutibu kifua kikuu na ukoma zinazotakiwa kupatikana,

    zinanunuliwa, kusambazwa na kutumiwa ipasavyo.

    Mahali Sahihi: Dawa zinafikishwa katika vituo vilikoagizwa na kwamba kuna watendaji waliofunzwa

    kuhusu matumizi yake.

    Kiasi Sahihi: Kituo cha tiba kina shehena ya kutosha ya dawa. Kiasi cha kuepusha kuishiwa kabla ya

    kupokea shehena mpya, lakini sio nyingi kiasi cha kukosa nafasi ya kuihifadhi.

    Wakati Sahihi: Wateja na wagonjwa wanatakiwa wapate mahitaji yao kila wanapokwenda kwenye

    kituo cha tiba.

    Ubora Sahihi: Shehena iko katika hali nzuri, haijaharibika, kuchafuka wala kwisha muda wa matumizi.

    Gharama Sahihi: Hii ni gharama ya utaratibu mzima, ikiwa ni pamoja na uchukuzi, uhifadhi, nguvukazi,

    n.k. hata kama shehena imetolewa na wahisani au mteja amechangia gharama. Ni lazima mpango

    mzima kudhibiti kifua kikuu na ukoma uendeshwe kwa gharama zinazoeleweka. Hii hasa ni muhimu

    kwa dawa za kifua kikuu na ukoma ni za ghali.

  • 11

    E: UTARATIBU WA MTIRIRIKO WA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA NA

    TAARIFA KATIKA MFUMO WA USIMAMIZI WA DAWA HIZO

    Mtiririko wa taarifa

    Mtiririko wa dawa

    Gari la MSD

    Taarifa ya kila mwezi ya dawa

    na idadi ya wagonjwa

    Wateja

    Vituo vya tiba

    DTLC hupokea nakala ya taarifa na

    maombi yanayopelekwa MSD kila

    robo mwaka kutoka kwa mfamasia

    DTLC hupokea taarifa za mwezi za

    vituo,kukokotoa kiasi cha kugawa,

    kuidhinisha na kisha kupeleka fomu

    hizo kwa mfamasia

    Mfamasia wa wilaya humpa

    DTLC nakala ya R&R

    Mfamasia wa Wilaya

    Kutoa dawa kwa vituo baada ya

    kupokea taarifa zilizoinishwa na

    DTLC

    Kuandaa taarifa na maombi ya

    robo mwaka na kupeleka MSD

    Medical Stores

    Department

    (MSD)

    Taarifa na Maombi

    ya robo waka

    Taarifa za kiasi cha kununua kutoka NTLP kwenda MSD

    MSD kutoa taarifa za matumizi ya dawa na

    salio kwa NTLP

    RTLC- hupokea nakala ya taarifa na maombi

    yanayopelekwa MSD kila robo

    mwaka kutoka kwa DTLC

    National Tuberculosis and leprosy Program

    (NTLP)

    Taarifa mbalimbali za Utekelezaji wa mpango

    DTLC humpa mfamasia fomu

    ya kituo baada ya kukokotoa

    na kuidhinisha kiasi cha kutoa

  • 12

    F: MUHTASARI WA MFUMO

    Mtiririko wa dawa: Kama inavyoonyeshwa kwenye mchoro hapo juu mfumo wa ugavi wa dawa za

    kifua kikuu na ukoma una ngazi tatu; Ngazi ya MSD, Ngazi ya wilaya na Ngazi ya vituo vya tiba.Kiasi

    cha juu cha shehena kwa ngazi ya MSD ni dawa za matumizi ya miezi 9 wakati kisi cha chini cha

    shehena ni miezi 6 ya matumizi. Katika ngazi ya wilaya kiasi cha juu cha shehena ni miezi 6 ya

    matumizi na kiasi cha chini ni miezi 3. Wilaya itaagiza dawa moja kwa moja kutoka MSD na mkoa

    hautahifadhi shehena kama ilivyokuwa awali. Katika ngazi ya kituo, kituo kitapata mahitaji ya dawa ya

    kutosheleza wagonjwa kilionao kwa mwiezi miwili

    Majukumu ya uagizaji wa dawa za kifua kikuu na ukoma yamehamishwa toka kwa DTLC na sasa

    yatafanywa na mfamasia wa wilaya. Wilaya itatunza shehena ya vituo vyote wilayani na mfamasia

    atakuwa akigawa dawa kwa kila kituo kila mwezi baada ya kupata taarifa ya mwezi ya kituo husika

    iliyoidhinishwa na kuhakikiwa na DTLC.

    ZINGATIA: Katika kuandaa taarifa ya mwezi kituo kitatumia kadi za matibabu za wagonjwa ili

    kujua kila mgonjwa atakuwa kwenye mwezi wa ngapi wa matibabu kisha kujaza jumla ya

    wagonjwa watakaokuwa kwenye mwezi husika wa matibabu katika fomu ya taarifa ya mwezi:

    Taarifa ya mwezi ya kituo itaonyesha pia salio la kila dawa kituoni na kiasi cha dawa

    kilichoharibika au muda wake wa matumizi kuisha.

  • 13

    SURA YA 2: fomu za kumbukumbu na taarifa zinazotumika katika mfumo wa ugavi wa dawa za kifua

    kikuu na ukoma

    Fomu za kumbukumbu na taarifa zinatakiwa kutumika na watendaji wanaosimamia shehena za dawa.

    Nakala za fomu hizi na maelekezo ya namna ya kuzijaza na kuzitumia zinapatikana Sura ya 7 ya

    mwongozo huu.

    Jina la Fomu Matumizi Mtumiaji Mkuu Mahali

    itumikapo

    Fomu ya mwezi ya

    taarifa ya dawa na

    wagonjwa ya kituo

    Kutoa taarifa ya salio la dawa,kiasi

    cha dawa zilizoharibika na idadi ya

    wagonjwa katika miezi mbailmbali ya

    matibabu katika mwezi unaofuata ule

    unaotolewa taarifa.

    DOT Nurse au

    Mtumishi

    aliyeteuliwa

    kujaza fomu.

    Vituo

    vinavyotoa tiba

    ya kifua kikuu

    na ukoma

    Fomu ya taarifa na

    maombi ya robo

    mwaka ya dawa za

    kifua kikuu na ukoma

    Kutoa taarifa ya kiasi cha dawa

    zilizopo wilayani,matumizi ya wilaya

    nzima,kiasi cha upotevu na

    marekebisho na maombi ya dawa

    kwa robo mwaka inayofuata

    Mfamasia wa

    wilaya au

    mtumishi

    aliyeteuliwa

    kujaza fomu

    Ngazi ya wilaya

    Fomu ya kunakili

    kiasi cha dawa

    kilichotolewa vituoni

    kila mwezi

    Kuweka kumbukumbu ya kiasi cha

    dawa kilichotolewa kwa kila kituo

    wilayani na jumla yake. Fomu hii

    inasidia kurahisisha uandaaji wa

    taarifa ya robo mwaka

    Mfamasia wa

    wilaya au

    mtumishi

    aliyeteuliwa

    kujaza fomu

    Ngazi ya

    wilaya)

    Kadi ya mgonjwa ya

    matibabu ya kifua

    kikuu na ukoma

    Kuweka kumbukumbu ya huduma

    anazopata mgonjwa pamoja na aina

    ya dawa anazopatiwa.

    Kadi hii inasaidia kutambua mwezi wa

    matibabu wa mgonjwa wakati wa

    kujaza taarifa ya mwezi ya kituo

    DOT Nurse Kituo

    Fomu nyingine zinazotumika kwenye mifumo mingine ya usimamizi wa bidhaa za

    afya zitatumika pia katika mfumo huu kwa kuzingatia matumizi yake. Fomu hizo ni;

    issue voucher, goods received note (grn), verification and claim form, leja ya mali

  • 14

    SURA YA 3: UWAJIBIKAJI KATIKA USIMAMIZI WA UAGIZAJI NA

    USAMBAZAJI WA SHEHENA ZA DAWA ZA KIFUA

    KIKUU NA UKOMA

    Kulingana na kazi au wajibu wako ndani ya mfumo wa usimamizi wa uagizaji na usambazaji wa dawa

    za kifua kikuu na ukoma, mwongozo huu umeandaliwa kukusaidia kutekeleza shughuli zifuatazo kwa

    ufanisi na kwa wakati.

    A. MAJUKUMU KATIKA KITUO CHA TIBA

    Wajibu wa watendaji katika vituo vya tiba katika usimamizi wa mfumo wa uagizaji na usambazaji wa

    dawa za kifua kikuu na ukoma ni kama yalivyoainishwa hapa chini;

    1. Majukumu ya mtunza stoo/bohari ya dawa na vifaa

    Kuhifadhi kwa usahihi shehena za dawa za kifua kikuu na ukoma ili kudumisha ubora na

    usalama kwa matumizi na usalama wa mali.

    Kufanya hesabu kwa mkono mali iliyopo kila mwisho wa mwezi.

    Kuhakikisha kwamba ubora wa shehena unadumishwa.

    Kutunza kumbukumbu ya dawa za kifua kikuu na ukoma zinazoingia na kutoka stoo kwa

    kujaza leja mali

    Kupokea shehena ya dawa kwa mujibu wa utaratibu uliopo.

    Kutoa dawa stoo kwa kuzingatia utaratibu wa FEFO na FIFO

    Kutoa taarifa ya dawa zilizoharibika

    2. Majukumu ya DOT Nurse

    Kutunza hesabu za kila siku za dawa walizopewa wagonjwa kwa kujaza kadi za matibabu ya

    mgonjwa

    Kujaza fomu ya Taarifa ya mwezi na kumpa mkuu wa kituo kuidhinisha.

    Kutoa dawa sahihi kwa wagonjwa

    Kufuatilia idadi ya wagonjwa wanaotumia IPT wakati wa kujaza fomu ya mwezi (taarifa hii

    inapatikana kwa CTC incharge)

  • 15

    3. Majukumu ya mkuu wa kituo

    Kuhakikisha kuwa katika kituo kuna dawa za kutosha kulingana na idadi ya wagonjwa na

    mwezi mmoja wa ziada katika hatua zote za matibabu (intensive na continuation phases)

    Kuwasiliana na mfamasia wa wilaya iwapo dawa zitapungua na zitahitajika kwa dharura.

    Kurudisha dawa zilizokaribia kuisha muda wa matumizi kwa mfamasia wa wilaya.

    Kurudisha dawa za ziada au zisisohitajika kituoni (mfano wakati kinakuwa na dawa lakini

    hakina wagonjwa) kwa mfamasia wa wilaya.

    Kuteua mtu wa kufanya kazi za ujazaji wa taarifa zihusuzo usimamizi wa dawa za kifua kikuu

    na ukoma kituoni kama mhusika hayupo (kuhakikisha zoezi hili linakuwa shirikishi)

    Kuidhinisha fomu ya taarifa ya kila mwezi ya kituo

    Kupeleka taarifa ya mwezi ya kituo wilayani katika kipindi kisichozidi tarehe 5 ya mwezi

    unaoanza

    Kusimamia matumizi sahihi ya dawa

    Kutoa taarifa za madhara ya dawa na dawa duni

    Kuratibu upokeaji dawa na vifaa tiba

    Kuratibu utoaji elimu juu ya matumizi ya dawa kwa watumishi na wagonjwa

    B. MAJUKUMU KATIKA NGAZI WILAYA

    Wajibu wa watendaji katika ngazi ya wilaya katika usimamizi wa mfumo wa uagizaji na usambazaji wa

    dawa za kifua kikuu na ukoma ni kama yalivyoainishwa hapa chini;

    1. Majukumu ya Mfamasia wa Wilaya

    Mfamasia wa wilaya ana kazi kubwa kuhakikisha hakuna ukosefu wa dawa za kifua kikuu na ukoma

    katika wilaya yake.Hivyo majukumu yake ni;

    Kuhakikisha kuwa kila mwezi vituo vinapata dawa za kifua kikuu na ukoma

    Kufanya majumuisho ya taarifa za dawa alizotoa kwa kila kituo na kuandaa taarifa na maombi

    ya dawa kwa kila robo mwaka ambayo itapelekwa MSD. .

    Kuandaa taaarifa na maombi ya robo mwaka ya dawa za kifua kikuu na ukoma kwa msaada

    wa DTLC pale inapohitajika na kuipeleka MSD.

    Kupeleka taarifa na maombi ya dawa za kifua kikuu na ukoma kwa DMO kwa ajili ya uthibitisho

    Kumpatia DTLC nakala ya taarifa na maombi ya dawa za kifua kikuu na ukoma inayoenda

    MSD

  • 16

    Kuhakikisha kuwa wilaya inatunza kiasi cha juu cha shehena kisichozidi miezi 6 na kiasi cha

    chini cha shehena kisichopungua miezi 3.

    Kuhakikisha kuwa kumbukumbu za mahesabu ya dawa zinahuishwa kila wakati (leja ya mali

    nk).

    Kufanya heasabu ya mkono/kila mwezi

    Kuratibu usimamizi shirikishi

    Kufanya usimamizi shirikishi na mafunzo kazini (On-the-Job training) kwa watoa huduma ili

    kuwajengea uwezo wa kusimamia vizuri dawa za kifua kikuu na ukoma na hivyo kupunguza

    ukosefu wa dawa vituoni

    Kufanya ufuatiliaji wa karibu kwa vituo visivyotoa taarifa na vinavyochelewesha taarifa zao.

    Kuhifadhi kwa usahihi wa shehena za dawa za kifua kikuu na ukoma ili kudumisha ubora na

    usalama kwa matumizi na usalama wa mali.

    Kukusanya taarifa ya dawa zilizoharibika na zinazokaribia kuharibika vituoni na kuandaa

    taarifa

    Kutunza taarifa za mwezi za vituo zilizoletwa wilayani

    Kuratibu usambazaji wa dawa za ziada au ambazo hazitumiki kutoka kituo kimoja kwenda

    kingine au kuzirudisha wilayani.

    Kuomba na kusambaza nyenzo za usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma

    Kuingiza dawa za kifua kikuu kwenye eLMIS

    Kupokea dawa kutoka MSD

    Kufanya maombi ya dharura ya dawa

    Kushiriki katika kuandaa mipango na bajeti za usimamizi wa dawa

    2. Majukumu Ya Mratibu Wa Kifua Kikuu Na Ukoma Wa Wilaya (Dtlc)

    Kupokea na kupitia taarifa za kila mwezi kutoka vituoni na kuangalia kama zimejazwa kikamilifu

    na kwa usahihi; kujumlisha idadi ya wagonjwa katika miezi mbalimbali ya matibabu na

    kukokotoa kiasi cha dawa cha kutoa kwa kila kituo

    Kuidhinisha kiasi cha dawa za kutoa kwa kituo

    Kumsaidia mfamasia wa wilaya katika kuhakikisha kuwa vituo vya kutolea tiba wilayani

    vinapata dawa za kifua kikuu na ukoma.

    Kufanya ufuatiliaji wa karibu kwa vituo visivyotoa taarifa na vinavyochelewesha taarifa zao.

    Kushiriki katika usimamizi shirikishi

  • 17

    Kupokea nakala ya taarifa na maombi ya robo mwaka ya dawa za kifua kikuu na ukoma na

    kuipeleka kwa mratibu wa mkoa.

    Kushiriki katika kuandaa mipango na bajeti za usimamizi wa dawa

    Kusambaza miongozo na vipeperushi vituoni

    Kuratibu utoaji elimu juu ya matumizi mazuri ya dawa

    Kusimamia matumizi mazuri ya dawa

    3. Majukumu ya Mganga Mkuu wa Wilaya (DMO)

    Kuidhinisha taarifa na maombi ya dawa za wilaya

    Kusaidia katika mikakati ya kuhakikisha dawa za kifuakikuu na ukoma zinapatikana muda

    wote katika wilaya yake

    C. MAJUKUMU KATIKA NGAZI YA MKOA

    1. Majukumu ya Mratibu wa Kifua Kikuu na Ukoma wa Mkoa (RTLC)

    Kupokea nakala za taarifa na maombi ya robo mwaka zinazopelekwa MSD kutoka kwa DTLC,

    kuzikagua na kutoa ushauri kwa kadri inavyohitajika.

    Kumshirikisha mfamasia mkoa taarifa za kila robo mwaka anazozipata kutoka wilaya

    Kushiriki katika usimamizi shirikishi

    2. Majukumu ya Mfamasia wa Mkoa

    Kupitia taarifa za robo mwaka za dawa za wilaya kwa kushirikiana na RTLC na kubaini mambo

    yanayohitaji kuangaliwa au kufuatiliwa kwa karibu

    Kuratibu usimamizi shirikishi

    D. MAJUKUMU YA BOHARI KUU YA MADAWA (MSD)

    Wajibu wa watendaji Bohari Kuu ya Madawa katika usimamizi wa mfumo wa uagizaji na usambazaji wa

    shehena za dawa za kifua kikuu na ukoma ni pamoja na:

    Kufanya manunuzi ya shehena za dawa za kifua kikuu na ukoma

    Kupokea na kuhifadhi kwa usahihi wa shehena za dawa ili kudumisha ubora, usalama kwa

    matumizi.

    Kutunza hesabu za shehena iliyopo na ile ambayo iko hatarini kwisha muda wake wa matumizi

    au kuharibika au haitumiki tena MSD.

  • 18

    Kujaza Leja ya Mali na kujaza fomu zingine zote zinazohusu ugavi.

    Kufanya hesabu kwa mkono ya mali iliyopo katika wakati uliopangwa.

    Kuhakikisha kwamba ubora wa shehena za dawa unadumishwa.

    Kupokea na kushughulikia maombi ya dawa kutoka wilayani

    Kuandaa na kusambaza shehena wilayani kila baada ya miezi mitatu kwa mujibu wa maombi

    yaliyopokewa kupitia fomu za maombi na taarifa kwa ajili ya dawa.

    Kuwasilisha NTLP taarifa za matumizi na kiasi cha shehena za dawa za kifua kikuu na ukoma

    katika bohari za MSD kila baada ya miezi 3.

    Kuwasiliana na wilaya ambazo zinashindwa kuwasilisha maombi yake kwa muda muafaka

    Mfumo huu unaitaka MSD kuwa uwezo wa kuhifadhi kiasi cha shehena kinachoweza

    kutosheleza mahitaji ya vituo vyote vya tiba ya kifua kikuu na ukoma. Kiasi cha chini cha

    shehena ni kile kinachoweza kutosheleza mahitaji ya miezi sita, na kiasi cha juu ni kile

    kinachoweza kutosheleza mahitaji ya miezi tisa.

    E. WIZARA YA AFYA (NTLP)

    Wajibu wa watendaji NTLP katika usimamizi wa mfumo wa uagizaji na usambazaji wa shehena

    za dawa kifua kikuu na ukoma ni pamoja na:

    Kutathmini taarifa zilizopokewa kutoka wilayani kupitia MSD ili kuweza kuandaa makadirio ya

    mahitaji ya kiasi cha shehena ya dawa za kifua kikuu na ukoma na kuwasilisha makadirio hayo

    kwa wadau mbalimbali kwa ajili ya kupata fedha za kununua mahitaji hayo.

    Kuratibu upatikanaji wa fedha au dawa kutoka kwa washirika mbalimbali ikiwa ni pamoja na

    serikali ya Tanzania (GOT) kwa ajili ya ununuzi wa shehena za dawa

    Kuratibu mipango ya manunuzi kwa wakati na ratiba ya usafirishaji wa shehena za dawa ili

    kuhakikisha uwepo wa dawa za kiwango cha juu wakati wote.

    Kupeleka taarifa MSD kuhusu kiasi cha dawa kinachotakiwa kununuliwa.

    Kupokea taarifa kutoka MSD kuhusu ununuzi na upokeaji wa shehena.

    Kufuatilia shughuli za uagizaji na usambazaji wa shehena na kuwasimamia watekelezaji.

    Kutoa taarifa mrejesho na taarifa za mpango kwenye vituo vya tiba na watendaji wengine

    ikiwamo MSD

    Kutoa taarifa mbalimabali zihusuzo dawa za kifua kikuu na ukoma (mfano kuchelewa kufika

    nchini kwa shehena nk.)

  • 19

    Kukusanya taarifa kutoka MSD kuhusu kiasi cha shehena ambazo zimesambazwa kwenye

    wilaya mbalimbali.Pia taarifa za shehena iliyopo. Taarifa zipatikanozo hutumika kuainisha

    mahitaji ya kitaifa, manunuzi ya dawa

    SURA YA 4: UTUNZAJI WA HESABU ZA BIDHAA

    ZINAZOTOLEWA

    Ni muhimu kwa watendaji katika vituo vya tiba wanaohusika na ugawaji wa dawa za kifua kikuu na

    ukoma kuweka kumbukumbu ya matumizi ya dawa hizi. Matumizi hayo yanapaswa kujazwa kwenye

    Rejista ya DOT ambayo imekuwa ikitumika kwa muda mrefu hivyo haijaingizwa kwenye mwongozo

    huu. Kumbukumbu pia ziingizwe katika kadi za wagonjwa kama inavyofanyika hivi sasa. Kadi hii pia

    haijaingizwa kwenye mwongozo huu kwani imekuwa ikitumika kwa muda mrefu.

    Kadi ya matibabu ya mgonjwa iliyotajwa hapo juu hutoa taarifa muhimu ambazo hutumiwa na kituo cha

    tiba kujaza idadi ya wagonjwa walio katika miezi mbalimbali ya matibabu wakati wa kujaza fomu ya

    taarifa ya mwezi ya kituo.

  • 20

    SURA YA 5. UAGIZAJI

    A: KUHAKIKISHA KIASI CHA KUTOSHA CHA SHEHENA

    Moja ya kazi kuu za msimamizi wa bidhaa ni kuhakikisha kwamba daima kuna shehena ya kutosha

    kukidhi mahitaji ya mteja. Izingatiwe ya kuwa katika mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua kikuu na

    ukoma mfamasia wa wilaya pekee ndiye anayeagiza dawa kutoka MSD. Hii ina maana ya kuwa

    mfamasia wa wilaya atatoa shehena ya kutosha kukidhi mahitaji ya vituo vya tiba kulingana na taarifa

    za kila mwezi anazoletewa na vituo .Kwa vituo vya tiba hii ina maana ya kuwa daima vinatakiwa kuwa

    na bidhaa za kutosha kuwapa dawa wagonjwa wote wanaotumia dawa.

    Moja ya maswali makuu kwa wasimamizi wa bidhaa ni “Kiasi gani cha shehena kinatosha?” MSD na

    wilaya zimekwishawekewa kiasi kinachohakikisha kuwa kuna shehena ya kutosha kukidhi mahitaji ya

    wateja wao na wakati huo huo kutokuwa na shehena kubwa kupindukia na kuwa hatarini kuharibika au

    kwisha muda wa matumizi. Katika kituo cha ugavi (MSD) shehena inapaswa kuwa kati ya kiasi cha

    chini cha kutosheleza miezi sita na kiasi cha juu cha miezi tisa. Katika wilaya shehena inapaswa kuwa

    kati ya kiasi cha chini cha kutosheleza miezi mitatu na cha juu cha miezi sita.

    Pia kwa wilaya kuna utaratibu wa uagizaji wa shehena ya Dharura (Emergency Order) ikiwa shehena

    kwenye ngazi ya wilaya itapungua chini ya shehena ya kutosheleza mwezi mmoja na nusu.

    B: TATHMINI YA KIASI CHA SHEHENA

    Utaratibu wa kuwa na viwango vya kiasi cha juu na chini cha shehena ni kuhakikisha kwamba daima

    shehena inakuwepo ndani ya kiwango maalum — cha juu na cha chini. Ili kufahamu iwapo shehena

    yako imo ndani ya viwango hivyo, itakulazimu kufanya tathmini ya shehena.

    Unapofanya mapitio ya kiasi cha shehena yako unabainisha ni kiasi gani cha kila dawa ya kifua kikuu

    au ukoma inapatikana katika wilaya yako/ghala lako na kwamba kila moja ya dawa hizo itatosheleza

    kwa muda gani. Unaweza kufanya mapitio ya kiasi cha shehena yako kwa kuhesabu shehena iliyopo,

    kama unavyofanya wakati ukifanya Hesabu kwa mkono. (. Kwa kufanya hivyo utahakikisha unajua kiasi

    halisi cha shehena iliyopo. Lakini ni muhimu zaidi kufahamu shehena hiyo itadumu muda gani na

    kama una kiasi cha kutosha kukidhi mahitaji hadi kuwasili kwa shehena mpya. Hiyo inajulikana kama

    Miezi ya kipindi cha Shehena (Months of Stock-MOS).

  • 21

    Miezi ya kipindi cha Shehena(MOS) ni idadi ya miezi ambapo shehena ya dawa itachukua hadi

    kumalizika kwa kulinganisha na kasi ya matumizi kwa sasa. Unapofanya mapitio ya kiasi cha shehena

    yako inakubidi ubainishe kwamba kituo chako kimesaliwa na miezi mingapi kabla ya bidhaa kuisha.

    Miezi mitatu ya kipindi cha shehena ina maana kwamba shehena itadumu kwa miezi mitatu, alimradi

    kasi ya matumizi iendelee kuwa kwa viwango vya sasa.

    Kwa kufanya tathmini ya shehena yako utaweza kubaini iwapo kituo chako kimepungukiwa, kimezidiwa

    au kimetoshelezwa. Iwapo utajikuta umepungukiwa na bidhaa mojawapo, na unafahamu kwamba

    shehena ambayo umeiagiza hivi karibuni bado muda wa kuwasilishwa, huenda ukalazimika kuchukua

    hatua za uagizaji wa dharura (Tazama Sehemu E kwa jinsi ya kuchukua hatua ya uagizaji wa dharura).

    Iwapo utakuwa na ziada ya bidhaa, huenda ukalazimika kugawia wilaya za jirani kinachohitaji.

    NAMNA YA KUBAINI MIEZI YA KIPINDI CHA SHEHENA

    Kwa kukokotoa miezi ya kipindi cha shehena, kituo kinaweza kubaini iwapo kina kiasi cha kutosha cha

    dawa. Ili kubaini shehena itadumu kwa muda gani, kanuni nyepesi ifuatayo inaweza kutumika:

    Tuna kiasi gani?

    (Shehena Iliyopo) =

    Shehena itadumu muda gani

    (Miezi ya kipindi cha Shehena

    iliyoko) Tumetumia kiasi gani?

    (Wastani wa Matumizi ya Mwezi)

    Kabla ya kukokotoa Miezi ya Kipindi cha Shehena Iliyopo, kuna vitu viwili ambavyo unapaswa

    kufahamu — Shehena Iliyopo na Wastani wa Matumizi kwa Mwezi

    Ili kubaini Wastani wa Matumizi kwa Mwezi (Average Monthly Consumption - AMC), jumulisha matumizi

    ya miezi mitatu iliyopita ya dawa fulani halafu gawanya kwa tatu.

    Tumia kanuni ifuatayo kubaini AMC:

    Matumizi ya mwezi huu + matumizi ya miezi 2 iliyotangulia =

    Wastani wa

    Matumizi kwa Mwezi 3

    Zingatia: Unapokokotoa kutafuta Wastani wa Matumizi ya Mwezi, daima andika namba kamili ya juu

    inayofuata. Mfano uki pata 43.6 jibu litakuwa 44 na ukipata 44.2 jibu litakuwa 44

  • 22

    Matumizi ya robo mwaka ya hivi karibuni zaidi yanaweza kupatikana kwenye nakala za Taarifa na

    Maombi ya dawa za kifua kikuu na ukoma au kwenye worksheet ya ukokotozi inayoonyesha kiasi cha

    dawa kilichogawiwa katika vituo. Kwa kila dawa ambayo unataka kutathmini kiasi cha shehena, chukua

    taarifa za matumizi za miezi mitatu kamili iliyopita. (Dawa zilizotolewa kwa kituo zinahesabiaka kuwa

    zimetumiaka zote hivyo kwenye mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma jumla ya

    dawa zilizotolewa kwa vituo kwa miezi mitatu ndiyo jumla ya matumizi kwa kipindi hcho) Iwapo

    katika kipindi chochote cha robo mwaka kulitokea kwisha kwa dawa, basi rekebisha taarifa za kwisha

    kwa mali kwa kutumia kanuni za marekebisho ya ugavi, au usitumie kabisa taarifa hizo bali utumie

    taarifa zingine kamili za robo mwaka ya karibu ambapo hapakutokea kwisha kwa mali. Iwapo utakosa

    taarifa kamili kwa miezi mitatu, basi tumia taarifa zozote zitakazopatikana mfano taarifa za kipindi kama

    hicho mwaka uliopita. Kokotoa kupata wastani wa matumizi kwa mwezi, kisha gawanya shehena

    Iliyopo (inapatikana kwa Hesabu kwa mkono) kwa wastani wa matumizi kwa mwezi (AMC) uliyokokotoa

    kupata Miezi ya Kipindi cha Shehena Iliyopo. Tumia kanuni ifuatayo kubaini shehena iliyopo ya kila

    bidhaa itadumu kwa muda gani:

    Shehena Iliyopo

    = Miezi ya Kipindi cha Shehena Iliyopo Wastani wa Matumizi kwa Mwezi

    Zingatia: Ukishakokotoa idadi ya miezi ya Kipindi cha Shehena, tumia tarakimu moja tu baada ya

    desimali!!

    Iwapo namba ambayo ingefuata baada ya namba hiyo ni 4 au pungufu, punguza kwenda namba

    kamili iliyotangulia, iwapo ni 5 au zaidi, ongeza kwenda namba kamili ya juu inayofuata. Mfano kama

    jibu ulilopata ni 3.23 miezi ya shehena itakuwa 3.2 au kama jibu ulilopata ni 4.36 miezi ya shehena

    itakuwa 4.4

    Tathmini ya Kiasi cha Shehena ifanyike lini?

    Kiasi cha shehena ya katika wilaya kinapaswa kufanyiwa tathmini wakati wowote utakapokuwa na

    wasiwasi kwamba huenda viwango vya shehena haviko ndani ya viwango vya juu na chini vya kituo

    chako. Hali hiyo inaweza kutokea iwapo palitokea upotevu wa shehena kutokana na kuharibiwa, kwisha

    muda wa matumizi au wizi, au kama patatokea ongezeko au upungufu wa ghafla wa matumizi.

    Wilaya zinapaswa kufanya tathmini ya kiasi cha shehena wakati wa kujaza sehemu ya maombi katika

    fomu za R&R ya wilaya, watendaji wakague hali ya shehena za dawa za kifua kikuu na ukoma:

  • 23

    Iwapo kiasi kinachoombwa ni namba hasi, basi ina maana kwamba shehena imejaa mno wilayani na

    kuna haja ya kufanya tathmini ya hali ya sehena. Huenda shehena zikalazimika kugawiwa wilaya

    nyingine iwapo kuna uwezekano wa kwisha kwa muda wa matumizi kabla hazijaweza kutumika.

    Iwapo maombi ya kiasi cha shehena ni makubwa mno kuliko kiasi cha kawaida basi huenda wilaya ina

    upungufu wa shehena na ishauriwe kufanya tathmini ya shehena ya mara kwa mara kuepusha haja ya

    kuchukua hatua za uagizaji wa dharura.

    Iwapo wilaya inawasilisha maombi ya mara kwa mara ya hatua za uagizaji wa dharura, zifanyike juhudi

    za kubaini sababu za uagizaji wa dharura na kuchukua hatua zingine kama itakavyohitajika.

  • 24

    C: NAMNA YA KUTAMBUA MWEZI WA MATIBABU ATAKAOKUWA MGONJWA

    Mfumo wa usimamizi wa dawa za kifua kikuu na ukoma una changamoto katika utekelezaji wake hasa

    katika katika ngazi ya kituo. Changamoto inayouutofautisha mfumo huu na mifumo mingine ni

    mabadiliko ya dawa zinazotumika na wagonjwa wa kifua kikuu kulingana na muda. Katika matibabu ya

    kifua kikuu wagonjwa hutibiwa katika hatua mbili zinazojulikana kama intensive phase na continuation

    phase na kisha humaliza matibabu. Kila hatua inatumia dawa tofauti na hivyo kama utaratibu wa

    kutumia matumizi ya miezi mitatu iliyopita kuagizia dawa ungetumika kama ilivyo katika mifumo ya ILS

    na ARVs basi hatari iliyopo ni kuwa kituo kinaweza kupelekewa dawa ambazo hazihitajiki kwani

    wagonjwa watakuwa wamebadili hatua ya matibabu na hivyo kukosa dawa stahiki na kupelekea

    kukosekana kwa dawa na pia mrundikano wa dawa usiohitajika kituoni. Katika mfumo wa usimamizi wa

    dawa za kifua kikuu na ukoma utaratibu umewekwa kukiwezesha kituo kupata dawa kulingana na idadi

    ya wagonjwa kilionao ikizingatiwa hatua ya matibabu waliyopo. Kufanikisha hili kituo kinatakiwa kutoa

    taarifa ya idadi ya wagonjwa kitakaokuwa nao katika kila mwezi unaofuata na miezi ya matibabu

    watakayokuwa. Kwa mantiki hii jambo muhimu hapa ni kujua namna gani nayeandaa taarifa ya mwezi

    ya kituo atakavyoweza kutambua mwezi wa matibabu atakaokuwa mgonjwa katika mwezi unaofuata

    ule anaotolea taarifa. Hili linawezekana kufanyika kwa kutumia kadi ya matibabu ya mgonjwa.

    i. Kwa wagonjwa wa kifua kikuu mwezi wa matibabu unabainishaji wa mwezi wa matibabu

    atakaokuwa mgonjwa unafanywa kama ifuatavyo;

    a. Bainisha idadi ya dozi zilizokwishatolewa kwa mgonjwa hadi mwisho wa mwezi unaotolewa

    taarifa

    b. Kisha bainisha mwezi wa matibabu atakao kuwa kwa kufuata utaratibu ufuatao

    Na Aina ya Mgonjwa Dozi alizokwishapewa mgonjwa

    hadi mwisho wa mwezi

    unaotolewa taarifa

    Mwezi wa

    matibabu

    atakaokuwa

    1 Mtoto & Mkubwa & Retreatment Chini ya 28 1

    2 Mtoto & Mkubwa & Retreatment 28 na zaidi lakini chini ya 56 2

    3 Mtoto & Mkubwa &Retreatment 56 na zaidi lakini chini ya 84 3

    4 Mtoto & Mkubwa &Retreatment 84 na zaidi lakini chini ya 112 4

    5 Mtoto & Mkubwa & Retreatment 112 na zaidi lakini chini ya 140 5

    6 Mtoto&Mkubwa & Retreatment 140 na zaidi lakini chini ya 168 6

    7 Mtoto & Mkubwa 168 Amemaliza

  • 25

    Na Aina ya Mgonjwa Dozi alizokwishapewa mgonjwa

    hadi mwisho wa mwezi

    unaotolewa taarifa

    Mwezi wa

    matibabu

    atakaokuwa

    8 Retreatment 168 na zaidi lakini chini ya 196 7

    9 Retreatment 196 na zaidi lakini chini ya 224 8

    10 Retreatment 224 Amemaliza

    ii. Kwa wagonjwa wa ukoma mwezi wa matibabu atakaokuwa mgonjwa unabainishwa unafanywa

    kama ifuatavyo;

    a. Bainisha idadi ya mahudhurio ya mgonjwa hadi mwisho wa mwezi unaotolewa taarifa

    b. Mwezi wa matibabu wa mgonjwa utakuwa ni tarakimu inayofuata ile inayoonyesha idadi ya

    mahudhurio ilivyobainishwa. Mfano kama idadi ya mahudhurio ni 2 inamaanisha mgonjwa huyu

    atakuwa mwezi wa 3 wa matibabu au kama idadi ya mahudhurio ni 1 inamaanisha atakuwa

    mwezi wa 2 wa matibabu, nk.

    Izingatiwe kuwa wagonjwa wa PB (watoto na wakubwa) matibabu yao ni ya miezi sita (6) tu

    ilihali matibabu ya wagonjwa wa MB (watoto na wakubwa) matibabu yao ni ya miezi 12.

    D: UTOAJI WA TAARIFA WA VITUO VYA TIBA

    Kituo kinachotoa huduma kwa wagonjwa wa kifua kikuu na ukoma kinatakiwa kutoa taarifa kila mwezi

    kwa kutumia fomu maalumu ya utoaji taarifa ya mwezi. Fomu hii ni rahisi na huchukua muda mfupi

    kuijaza.

    Kama kituo hakina wagonjwa kinatakiwa kutoa taarifa kwa kuweka sifuri kwenye visanduku

    husika katika fomu ya kutolea taarifa. Hii ni muhimu ili DTLC ajue kwamba kituo hakina

    wagonjwa.

    Hata kama kituo hakina dawa kabisa kinatakiwa kutoa taarifa kwa kuweka sifuri kwenye

    visanduku mbele ya dawa husika.

    Hata kama kituo hakina dawa na hakina wagonjwa kinatakiwa kutoa taarifa pia.

    Kama kituo hakitatoa taarifa DTLC wa wilaya hatoweza kujua hali ya kituo.

  • 26

    Taarifa zinazotakiwa kwenye fomu zinapatikana kwa namna mbili;

    1. Tumia kadi za matibabu za wagonjwa kujua idadi ya wagonjwa watakaokuwa kwenye miezi

    tofauti tofauti ya matibabu mfano mwezi 2,3,4, na kadhalika. Katika mwezi wa 1 andika idadi ya

    wagonjwa ambao hawajamaliza mwezi mmoja wa matibabu hadi mwisho wa mwezi wakati

    unaandika taarifa ya mwezi pia jumuisha wagonjwa wapya wanaotarajiwa kuanza dawa katika

    mwezi unaofuata ule unaotolea taarifa (mfano kama taarifa ni ya Januari idadi ya wagonjwa

    wapya ni wale watakaoanza matibabu Februari. Pia kama kituo kina wagonjwa wa ukoma

    kitatakiwa kuwaweka kwenye sehemu husika katika jedwali la wangonjwa kulingana na idadi

    yao na miezi yao ya matibabu katika mwezi unaofuata ule unaotolewa taarifa.

    2. Fanya hesabu kwa mkono kujua kiasi cha kila aina ya dawa kilichopo mwisho wa mwezi na

    kukionyesha kama salio kwenye sanduku husika kwenye fomu ya taarifa. Izingatiwe kwamba

    salio ni dawa zinazoweza kutumika tu kama dawa zimeharibika au muda wake wa matumizi

    kuisha idadi yake iainishwe kwenye kisanduku husika kwenye fomu ya taarifa.Kiasi kiandikwe

    katika vipimo vya ugawaji tu na siyo maboksi.

    3. Uwasilishaji wa fomu ya taarifa ya mwezi wilayani.

    DTLC atapokea fomu za taarifa za mwezi zilizojazwa kutoka vituo vyote wilayani hadi kufikia

    tarehe 5 ya kila mwezi.

    DTLC atazikagua taarifa kuangalia kama zimekamilika na kama ni sahihi na kama atahitaji

    ufafanuzi anaweza kuwasiliana na mtoa huduma katika kituo husika.

    Kisha DTLC atakokotoa kiasi cha dawa kinachohitajika kituoni katika mwezi husika

    kuidhinisha na kisha kumpa mfamasia fomu ya kituo.

    Mfamasia wa wilaya atagawa dawa kwa kituo kama ilivyoidhinishwa na DTLC.

    Mfamasia atatumia issue vocha kama nyaraka husika katika kuonyesha dawa zimetolewa

    kwa kituo lakini pia ataingiza kumbukumbu katika leja ya mali ya stoo ya wilaya.

    Vituo havifanyi ukokotozi wowote wakati vikiandaa taarifa ya

    mwezi.Kazi yao ni kuweka idadi ya wagonjwa watakaokuwa kwenye

    matibabu katika miezi mbalimbali, salio la kila dawa na kiasi cha

    dawa kilichoharibika au muda wake wa matumizi kuisha. DTLC

    atafanya mahesabu kujua kiasi cha kuwapa.

    Hii ni tofauti na mfumo wa ILS na wa ARVs ambapo vituo

    hufanya ukokotozi wa kiasi cha kuagiza

  • 27

    Izingatiwe kuwa: Ni rahisi kukokotoa kiasi cha kutoa kwa kituo kwa kuzingatia taarifa zilizoletwa na

    kituo katika fomu ya taarifa ya mwezi. Kituo kitapewa mara mbili ya dawa za kutosha wagonjwa wake

    walio katika matibabu. Kama kituo kina shehena ya dawa itatolewa kwenye kiasi kinachohitajika na

    tofauti ndiyo itakayopewa kwa kituo.

    E: JINSI WILAYA INAVYOAGIZA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA

    Maombi ya wilaya yanafanyika kila baada ya miezi mitatu (robo mwaka). Mfamasia wa wilaya ndiye

    mwenye jukumu la kuagiza dawa za kifua kikuu na ukoma kwa ajili ya wilaya yake. Kiasi chaa dawa

    atakachoagiza mfamasia wa wilaya kitatokana na kanuni ya ukokotozi inayoonekana kwenye fomu ya

    taarifa na maombi ya robo mwaka ya dawa za kifua kikuu na ukoma. Mfamasia wa wilaya atampatia

    DMO fomu ya taarifa na maombi ya robo mwaka aliyokwisha ijaza kwa uthibitisho. Baada ya

    kuthibitishwa mfamasia ataipeleka fomu hii MSD.Fomu iwe imefika MSD ifikapo tarehe 14 ya mwezi wa

    kwanza war obo mwaka iliyoanza. Fomu ya taarifa na maombi ina nakala tatu halisi moja na zingine

    mbili. Nakala halisi ndiyo inayotumwa MSD moja atapewa DTLC ambaye huituma kwa RTLC na moja

    hubaki kwenye kitabu.

    Hapo MSD, watendaji watashughulikia maombi yako ipasavyo na kubaki na nakala yako halisi kwa ajili

    ya kumbukumbu zao.

    Fomu ya kutolea taarifa na maombi ya dawa za kifua kikuu na ukoma pia imewekwa kwenye

    mfumo wa ki electronic (eLMIS). Wilaya inaweza kutumia mfumo huu kuagiza dawa za kifua

    kikuu na ukoma kutoka MSD

    F: MAOMBI YA DHARURA

    Kama katika wakati wowote kiasi cha shehena ya dawa yoyote katika stoo ya wilaya kitakuwa mwezi

    mmoja na nusu wa matumizi au chini ya hapo na hakuna shehena yoyote inayotarajiwa kufika wilayani

    katika siku mbili zinazofuata maombi ya dharura yanatakiwa kufanywa na mfamasia wa wilaya.

    Wakati wa kuandaa maombi ya dharura mfamasia,

    Ajaze visanduku vyote katika mistari husika wa dawa na aagize shehena inayotosheleza

    kufikisha kiwango cha juu (miezi 6 ya matumizi)

    Aandike neno “maombi ya dharura” (EMERGENCY ORDER) kwa herufi kubwa juu kulia katika

    ukurasa wa fomu ya taarifa na maombi.

  • 28

    Apeleke maombi hayo MSD kwa njia ya haraka ili kusaidia pasiwepo na ukosefu wa dawa

    vituoni

    G: UGAWAJI WA DAWA KUTOKA MSD KWENDA WILAYANI

    Dawa za kifua kikuu na ukoma za wilaya zitatumwa kutoka ofisi ya MSD ya kanda iliyo karibu na wilaya

    husika. Gari la MSD ndilo litakalo husika na kusafirisha shehena hiyo hadi wilayani na kutoka wilayani

    dawa zitapelekwa vituoni.

    Zifuatazo ni taratibu zinazofuatwa wakati wa kugawa dawa kutoka MSD kwenda wilayani;

    1. MSD kupokea maombi na taarifa kutoka wilayani

    Maombi kutoka wilayani yanatakiwa yawe yamefika MSD mwishoni mwa juma la pili (Tarehe 14) la

    mwezi wa kwanza wa robo mwaka inayofuata ile inayotolewa taarifa.

    2. MSD Kukagua usahihi wa maombi na taarifa kwenye fomu

    Fomu zinapowasili MSD hukaguliwa kubaini usahihi wa taarifa zilizomo na kuangalia kama kiasi

    kilichoombwa kipo .

    3. MSD kufungasha shehena

    Mfanyakazi wa MSD atachukua na kufungasha shehena tayari kwa ajili ya kupelekwa wilayani. Pamoja

    na dawa katika shehena kutakuwa na nyaraka mbalimbali zinazoambatana na shehena kama ilivyo

    katika mifumo mingine ya usimamizi wa bidhaa. Nyaraka hizo ni pamoja na Fomu namba 4 (MSD Sales

    Invoice) na Fomu namba 7 (Verification and Claims Form). MSD pia wataambatanisha Fomu namba 6:

    Goods Received Note (GRN) itakayotiwa sahihi wakati wa upokeaji wa shehena wilayani.

    Uhamishaji wa dawa kutoka wilaya moja kwenda nyingine

    Katika mazingira magumu mfano umbali mkubwa kutoka MSD, uharibifu wa miundombinu

    kama wakati wa mvua nk. Ni vigumu kupata dawa haraka kwa dharura kutoka MSD hivyo

    wilaya inaweza kuazima kutoka wilaya nyingine yenye kiasi cha kutosha cha dawa .Kiasi

    kilichoazimwa kiingizwe kama marekebisho chanya katika leja ya mali ya wilaya

    iliyoazimishwa na marekebisho hasi katika leja ya wilaya iliyoazimisha..

  • 29

    4. MSD kupeleka shehena wilayani

    Shehena ya dawa za kifua kikuu na ukoma italetwa wilayani kwa kutumia gari la MSD. Shehena

    inatakiwa kuwa imefikishwa wilayani inapofikia mwisho wa wiki ya kwanza ya mwezi wa pili wa robo

    mwaka iliyoanza. Shehena hii itakuja pamoja na dawa nyingine zinazosimamiwa kupitia mifumo

    mingine . Kama shehena haitafika kwa muda unaotarajiwa mfamasia anaweza kuwasiliana na MSD

    kujua ni lini shehena italetwa.

    5. Upokeaji wa shehena ya dawa wilayani

    Mfamasia wa wilaya au mtumishi yeyote aliyeteuliwa atapokea shehena na kuikagua kujiridhisha kama

    kiasi kilicholetwa ni sahihi.

    Izingatiwe kuwa taratibu za upokeaji wa dawa za kifua kikuu na ukoma hazina tofauti na taratibu

    za upokeaji wa dawa nyingine.

    H: UGAWAJI WA DAWA KUTOKA WILAYANI KWENDA VITUONI

    Mfamasia wa wilaya atapokea taarifa za kila mwezi kutoka kwa DTLC na atatoa dawa kwa kituo

    kulingana na kiasi kilichokokotolewa na DTLC kwenye fomu ya taarifa ya mwezi ya kituo husika. Vituo

    vingi vitapata dawa siku ya kupeleka taarifa wilayani baada ya kufanyiwa ukokotozi na DTLC na fomu

    kupelekwa kwa mfamasia. Pale inapohitajika mfamasia kwa kushirikiana DTLC atashughulikia usafiri

    wa kuzipeleka dawa katika kituo husika.

    Dawa za kifua kikuu na ukoma zitolewe kwa blisters/maboksi au makopo na kama kutokana na

    ukokotozi kituo kitahitaji dawa/vidonge pungufu ya blisters basi makadirio yafanyike kutoa blister nzima.

    Mfano kituo kinahitaji blista 10.5 basi kipewe blisters 11 vivyo hivyo kwa makopo au maboksi. Kutokana

    na uchache wa wagonjwa wa kifua kikuu na ukoma mara nyingi kituo kitahitaji kiasi kidogo cha dawa.

    Mtunza stoo au mfamasia wa wilaya atatumia issue vocha kunakili kiasi cha dawa alichotoa kwenda

    kituoni na wakati wa kutoa dawa atazingatia utaratibu wa FEFO na FIFO

    Upokekeaji wa shehena ya dawa kituoni

    Kituo cha tiba kinatakiwa kuwa kimeshapata dawa za kifua kikuu na ukoma hadi ifikapo tarehe 15 ya

    kila mwezi. Wakati wa kupokea mtumishi anayefanya kazi hiyo atafanya ukaguzi kujiridhisha kuwa

    dawa zilizoletwa ziko kwenye hali nzuri na zinafaa kwa matumizi. Kama kuna zilizoharibika zirudishwe

    wilayani. Wakati wa kupokea mtumishi anayepokea ataweka sahihi yake kwenye issue vocha

    iliyoandaliwa na mtumishi wa wilayani kuthibitisha kuwa amepokea shehena. Kisha atafanya ingizo

    kwenye leja ya mali ya kituo.

  • 30

    Ugawaji wa dawa ndani ya kituo cha tiba

    Mara nyingi katika kituo kuna sehemu moja tuu ya kugawia dawa za kifua kikuu na ukoma kwa

    wagonjwa.Mtunza stoo anashauriwa agawe kiasi cha dawa kinacho tosheleza matumizi ya juma moja

    kwenda sehemu ya utoaji wa dawa. Kila anapofanya hivyo azingatie kufanya ingizo kwenye leja ya mali

    ya kituo na pia kutumia issue vocha itakayowekwa sahihi na yule anayepokea dawa.

  • 31

    SURA YA 6: KUHIFADHI DAWA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA

    Mazingira ya kuhifadhi huathiri ubora wa dawa. Ili kuhakikisha ubora na usalama, ni lazima masharti

    stahili ya uhifadhi wake yazingatiwe kabla ya kuzisambaza: Taratibu za uhifadhi wa dawa za kifua kikuu

    na ukoma hazitofautiani na taratibu za uhifadhi wa dawa zingine. Taratibu za uhifadhi wa bidhaa za

    afya zimejadiliwa kwa kina katika miongozo ya usimamizi wa dawa katika mfumo wa ILS na ARVs.

    Mwongozo huu hautarudia kuelezea taratibu hizo.

    A: HESABU YA MKONO

    Ufanyaji wa hesabu ya mkono wa dawa za kifua kikuu na ukoma unafanana na ule wa dawa au bidhaa

    nyingine za afya ambao umeelezewa kwa kina katika mwongozo wa mifumo ya ILS na ARV. Hesabu

    kwa mkono ni kitendo cha kuhesabu kwa mkono idadi ya kila mali iliyopo kwenye kituo. Hesabu kwa

    mkono ni moja ya shughuli ambazo hufanyika kila mwezi katika zahanati, vituo vya afya na hospitali na

    wakati wowote inapohitajika.

    Hesabu kwa mkono inapaswa kujumuisha taarifa ya hesabu kutoka sehemu zote ambapo mali ipo, kwa

    mfano:

    1. Kiasi kilichopo kutoka shelfu au kabati za bohari

    2. Kiasi kilichopo eneo la kugawia dawa kituoni hapo.

    Kwa mfano: kama kuna maboksi manne (4) ya RHZE stoo na kila boksi lina vidonge 672 na

    sehemu ya kugawia dawa kuna blista 4 ambayo ni sawa na vidonge

    4 * 28= 112. Hivyo jumla ya hesabu kwa mkono iliyopo kituoni ni vidonge 672+ 112 =

    784

    Kama hesabu ilifanyika mwisho wa mwezi ndiyo itakayo tumika kuandaa taarifa ya mwezi ya kituo

    itakayopelekwa wilayani.Dawa zilizo sehemu ya kugawia zisipohesabiwa zinaweza kusababisha kituo

    kikaletewa dawa zaidi ya kinazozihitaji.

    Kiasi cha mali kilicho kwenye shelfu kinaweza kupatikana kwenye Leja ya mali. Hata hivyo, katika zoezi

    la kuhesabu kwa mkono, kiasi kilichoko kwenye shelfu kinalinganishwa na hesabu iliyoingizwa kwenye

    kitabu (Leja ya mali). Iwapo kiasi kilicho kwenye shelfu hakilingani na kile kilichoandikwa kwenye Leja,

    basi Leja ihuishwe (Updated) kwa kufanya marekebisho.

  • 32

    Mali iliyopo eneo la kugawia dawa kituoni hapo pia itahitaji kuhesabiwa. Mtu anayefanya hesabu

    asiziguse dawa kwa mkono kwa sababu si lazima kuhesabu dawa kwa kuzimwaga kwenye chombo

    cha wazi, kwa kuwa kufanya hivyo kunaweza kuziharibu. Kitakachofanyika ni kukadiria ujazo wa chupa

    kwa robo iliyo karibu. Kwa chupa ya vidonge 1,000, robo ni vidonge 250 na kwa chupa ya vidonge 500

    robo ni vidonge 125.

    Unapofanya Hesabu kwa mkono zingatia yafuatayo;

    B: UKAGUZI WA BIDHAA KWA MACHO

    Taratibu za ukaguzi wa macho zinazoelezewa kwenye miongozo ya mifumo ILS na ARV ndizo hizo

    hizo zinazotumika kwenye mfumo wa dawa za kifua kikuu na ukoma Ukaguzi wa Macho unapaswa

    kufanywa kila kunapokuwa na shughuli yoyote ihusuyo bidhaa hiyo kama vile: wakati wa kupokea,

    wakati wa kutoa au wakati wa kufanya hesabu kwa kwa mkono.

    C: KUHARIBU MALI ISIYOFAA KWA MATUMIZI

    Kila liwezekanalo linapaswa kufanywa ili kuepusha kwisha kwa muda wa matumizi au kuharibika kwa

    dawa na bidhaa zingine. Fuata utaratibu wa FEFO kupunguza tatizo hili. Hata hivyo, ikitokea kuna

    dawa zilizoharibika au muda wake wa matumizi kuisha ziharibiwe kwa kufuata taratibu na kanuni

    zilizowekwa na mamlaka za udhibiti (WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII, TFDA). Zoezi la

    kuharibu linatakiwa lifanyike mapema ili kutoa nafasi kwa dawa zinazofaa kutunzwa na kuepusha

    zisitumike kwa bahati mbaya.

    Kama kuna mali iliyokwisha muda wa matumizi au imeharibika, itenge na kuiwekea

    “karantini” mara moja ili isiweze kugawiwa au kutumika. Kwenye Leja ya mali (Leja), jaza

    kiasi kilichoisha muda wa matumizi au kuharibika kama ni marekebisho hasi (negative

    adjustments).

  • 33

    SURA YA 7: FOMU ZINAZOTUMIKA KATIKA MFUMO WA

    USIMAMIZI WA DAWA ZA KIFUA KIKUU NA

    UKOMA NA UFAFANUZI WAKE

    Sehemu hii ina ufafanuzi wa utendaji wa shughuli ambazo zimetajwa katika mwongozo huu, nazo ni:

    S/N JINA LA FOMU

    1 Leja ya Mali

    2 Hati ya Kutolea Shehena (Local Issue Voucher)

    3 Kadi ya matibabu ya mgonjwa

    4 Fomu ya Taarifa ya Mwezi ya Kituo

    5 Fomu ya kunakili kiasi cha dawa kilichotolewa vituoni

    8 Fomu ya Taarifa na Maombi ya robo Mwaka ya dawa za kifua kikuu na ukoma ya wilaya

    Ufafanuzi Kinachofafanuliwa

    A Kujaza dozi zilizogawiwa kwa wagonjwa katika kadi ya mgonjwa wa kifua kikuu

    B Kujaza taarifa ya mwezi ya kituo

    C Kuhakiki fomu ya taarifa ya kituo na kukokotoa kiasi cha kugawa

    D Kujaza Fomu ya Taarifa na Maombi ya robo Mwaka ya dawa za kifua kikuu na ukoma ya

    wilaya

  • 34

    A. UFAFANUZI A: UJAZAJI WA DOZI ZILIZOGAWIWA/TOLEWA KWA

    MGONJWA KATIKA KADI YA MATIBABU YA KIFUA

    KIKUU

    SEHEMU A

    KAZI: KUJAZA DOZI ZILIZOGAWIWA/TOLEWA KWA MGONJWA KATIKA KADI YA

    MATIBABU YA KIFUA KIKUU

    INAFANYWA NA: DOT Nurse

    SABABU: Kutunza kumbukumbu ya dozi za dawa zilizokwishatolewa kwa mgonjwa

    LINI INAFANYWA: Kila dawa zinapotolewa kwa mgonjwa

    NYENZO

    ZINAZOHITAJIKA:

    Kadi ya mgonjwa na kalamu

    SEHEMU B

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    1. Visanduku vya idadi ya dawa kwenye

    intensive phase: Jaza idadi ya vidonge

    ambavyo mgonjwa atakuwa akitumia katika

    kisanduku mahususi kulingana na aina ya

    mgonjwa.Idadi ya vidonge inaendana na

    uzito/umri wa mgonjwa kulingana na

    mwongozo wa matibabu ya kifua kikuu

    (NTLP manual); Mfano kama ni mgonjwa

    mpya mwenye makohozi yaliyoonekana na

    kifua kifua (smear positive) na atatumia

    vidonge 3 vya RHZE andika 3 katika

    kisanduku cha kwanza, chenye maelezo ya

    New case AFB+ juu na RHZE chini yake

    Kama mgonjwa ni wa retreatment ingiza

    taarifa zake kwenye kisanduku cha tatu na

    kwenye kisanduku kidogo chenye S kwa chini

    andika milligram za Streptomycin ambazo

    mgonjwa atakuwa akichomwa.

    Kwa wagonjwa watoto waliokatika umri/uzito

    wa kutumia dawa za watoto ingiza taarifa zao

    katika kisanduku cha nne (Children). Kumbuka

    kuwa hawa wanatumia RHZ na Ethambutol.

    Hivyo kumbuka kujaza idadi ya vidonge vya

    Ethambutol (E) na RHZ katika visanduku

    vidogo kama inavyoongozwa.

    2. Mwezi na Mwaka Intensive phase: Jaza

    mwezi na Mwaka ambapo matibabu

    yanatolewa katika nafasi zilizopo

    Kwa kadiri matibabu yanavyoendelea mwezi

    utakuwa ukibadilika na hivyo kila mwezi ingiza

    jina na mwezi na mwaka. Mwaka pia unaweza

    kubadilika kulingana na lini mgonjwa kaanza

    matibabu

    3. Dozi zilizotolewa/alizopewa mgonjwa

    katika intensive phase; Andika namba ya

    dozi unazompa mgonjwa kwa kuanzia na

    tarehe uliyoanza kumpa. Mfano kama

    mgonjwa alianza kupewa dozi ya kwanza 10

    namba moja inapaswa kuandikwa ndani ya

    kisanduku cha kwanza chini ya tarehe 10.

    Kisha namba ya dozi zinazofuata zitaendelea

    Kama mgonjwa ananywea dawa zake

    kituoni (FACILITY DOT) kila siku namba ya

    dozi aliyopewa itaandikwa. Mfano kwa

    mgonjwa aliyetajwa hapo kushoto dozi ya pili

    itakuwa tarehe 11, ya tatu tarehe 12 ya nne

    tarehe 13 nk.

    Kama mgonjwa anakunywa dawa zake

    nyumbani (HOME BASED DOT) iandikwe

  • 35

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    katika tarehe zinazofuata namba ya dozi aliyonywea kituoni kisha mstari

    uchorwe kuonyesha siku dawa alizopewa, na

    andika namba ya dozi atakayokunywa siku ya

    kurudi kuchukua dawa. NB.

    Mara nyingi wagonjwa wanaotumia

    dawa kupitia utaratibu wa HOME

    BASED DOT katika intensive phase

    hunywa dozi moja kituoni na kisha

    hupewa dawa za wiki moja (siku saba)

    ikijumuisha dozi watakayonywea

    kituoni siku ya kurudi kuchukua dawa.

    Mfano kwa mgonjwa aliyeanza dozi ya

    1 tarehe 10 Nov namba 1 itaandikwa

    kwenye tarehe 10 Nov kisha mstari

    utapigwa hadi tarehe 16 Nov.

    Mgonjwa anatarajiwa kurudi tarehe 17

    Nov na atanywea dozi ya 8 kituoni,

    hivyo namba 8 iandikwe kwenye

    tarehe 17. Tarehe hiyo 17 Nov

    atapewa dozi 7 za kutumia hadi tarehe

    24 Nov ambapo atarudi kituoni na

    kunywa dozi 15 hivyo mstari upigwe

    kuanzia tarehe 18 Nov hadi tarehe 23

    Nov na namba 15 iandikwe kwenye

    tarehe 24 Nov

    Katika miezi ambayo ina siku pungufu

    ya 31 weka alama ya X katika

    visanduku vya tarehe hizo ili kuepuka

    mkanganyiko unaoweza kujitokeza.

    Hivyo siku zenye X hazitahesabika

    kama siku ambazo mgonjwa

    ametumia dawa.

    Matibabu ya wagonjwa wapya wa

    kifua kikuu katika intensive phase

    huchukua dozi 56

    Matibabu ya wagonjwa wa retreatment

    wa kifua kikuu katika intensive phase

    huchukua dozi 84

    4. Visanduku vya idadi ya dawa kwenye

    continuation phase: Jaza idadi ya vidonge

    ambavyo mgonjwa atakuwa akitumia katika

    kisanduku mahususi kulingana na aina ya

    mgonjwa.Idadi ya vidonge inaendana na

    Kama mgonjwa ni wa retreatment ingiza

    taarifa zake kwenye kisanduku cha pili

    chenye maelezo Retreatment juu na RHE

    kushoto

  • 36

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    uzito/umri wa mgonjwa kulingana na

    mwongozo wa matibabu ya kifua kikuu

    (NTLP manual); Mfano kama ni mgonjwa

    mpya na atatumia vidonge 3 vya RH andika

    3 katika kisanduku cha kwanza, chenye

    maelezo ya New case juu na RH kushoto

    kwake

    Kwa wagonjwa watoto walio katika

    umri/uzito wa kutumia dawa za watoto

    ingiza taarifa zao katika kisanduku cha

    tatu chenye maelezo Children juu na RH

    kushoto.

    5. Mwezi na Mwaka katika continuation

    phase: Jaza mwezi na Mwaka ambapo

    matibabu ya continuation phase yanatolewa

    katika nafasi zilizopo

    Kwa kadiri matibabu yanavyoendelea

    mwezi utakuwa ukibadilika na hivyo kila

    mwezi ingiza jina na mwezi na mwaka.

    Mwaka pia unaweza kubadilika kulingana

    na lini mgonjwa kaanza matibabu.

    6. Dozi zilizotolewa/alizopewa mgonjwa

    katika contunuation phase; Andika namba

    ya dozi unazompa mgonjwa kwa kuanzia na

    tarehe uliyoanza kumpa.

    Kwa wagonjwa wapya na watoto dozi ya

    kwanza ya continuation phase itakuwa

    dozi namba 57 (mwendelezo wa idadi

    kutoka intensive phase). Hivyo katika

    kujaza kadi hili lizingatiwe. Kwa wagonjwa wa retreatment dozi ya

    kwanza ya continuation phase ni namba

    85 kwa kufuata mwendelezo kutoka

    intensive phase.

    Kama ilivyokuwa kwenye intensive phase

    Kama mgonjwa ananywea dawa

    zake kituoni (FACILITY DOT) kila

    siku namba ya dozi aliyopewa

    itaandikwa. Mfano kwa mgonjwa

    mpya aliyeanza kutumia dawa za

    continuation phase tarehe 10 Nov

    ambayo ni dozi ya 57, dozi ya 58

    itakuwa tarehe 11 Nov, ya 59

    tarehe 12 Nov ya 60 tarehe 13

    Nov nk.

    Kwa wagonjwa wa retreatment dozi

    ya kwanza ya continuation phase

    itaanza na 85 kisha mwendelezo

    ufafuata kila siku mf, 86,87,

    88…….. (kwa kuzingatia tarehe)

    Kama mgonjwa anakunywa dawa

    zake nyumbani (HOME BASED

    DOT) iandikwe namba ya dozi

  • 37

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    aliyonywea kituoni kisha mstari

    uchorwe kuonyesha siku dawa

    alizopewa na andika namba ya

    dozi atakayokunywa siku ya kurudi

    kuchukua dawa.

    Mara nyingi wagonjwa wanaotumia

    dawa kupitia utaratibu wa HOME

    BASED DOT katika continuation

    phase hunywa dozi moja kituoni na

    kisha hupewa dawa za wiki mbili

    (siku 14) ikijumuisha dozi

    atakayonywea kituoni siku ya

    kurudi kuchukua dawa.

    Mfano kwa mgonjwa aliyeanza dozi

    ya 57 tarehe 10 Nov namba 57

    itaandikwa kwenye tarehe 10 Nov

    kisha mstari utapigwa hadi tarehe

    23. Mgonjwa anatarajiwa kurudi

    tarehe 24 na atanywea dozi ya 71

    kituoni, hivyo namba 71 iandikwe

    kwenye tarehe 24. Tarehe hiyo 24

    Nov atapewa dozi 14 za kutumia

    hadi tarehe 8 Dec ambapo atarudi

    kituoni na kunywa dozi 85 hivyo

    mstari upigwe kuanzia tarehe 25

    Nov hadi tarehe 7 Dec na namba

    85 iandikwe kwenye tarehe 8 Dec.

    Tarehe 31 itawekewa X kwa kuwa

    Nov ina siku 30

    NB.

    Dozi ya mwisho ya continuation phase kwa

    wagonjwa wapya wa kifua kikuu ni ya 168

    Dozi ya mwisho ya wagonjwa wa retreatment

    ni ya 224.

    KAZI HII INAKUWA IMEKAMILIKA BAADA YA:

    Idadi ya vidonge ambavyo mgonjwa atakuwa akitumia itakuwa imejazwa katika kisanduku husika.

    Namba ya dozi zilizokwishatolewa kwa mgonjwa kuwa zimeandikwa kwa wagonjwa walio kwenye

    FACILITY DOT

    Namba ya dozi aliyokwisha kunywa mgonjwa na mstari unaoonyesha kiasi cha siku ambazo tayari

    mgonjwa amepewa dawa za kutumia kwa wagonjwa walio kwenye HOME BASED DOT

  • 38

    B. FOMU YA TAARIFA YA KITUO YA MWEZI YA DAWA ZA KUTIBU KIFUA KIKUU NA UKOMA TB 01

    INTENSIVE PHASE : Laboratory Results

    Indicate number of tablets per dose Month Smear Lab. No.

    Body Weight

    New Case AFB+ New Case AFB-/EP Retreatment Children Date Result

    0

    RHZE RHZE S RHZE RHZ E 1

    2

    3

    5

    RHZE: Rifampicin, Isoniazid, Pyrazinamide, Ethambutol (4FDC) S: Streptomycin RHZ: Rifampicin, Isoniazid, Pyrazinamide 7/8 For patients on health-facility DOT, write the number of dose on the date of DOT. For patients on home-based DOT, draw a horizontal line to indicate the number of days supply given to supporter, and then write number of dose on return date Month Year 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31

    CONTINUATION PHASE Indicate number of

    tablets per dose New case Retreatment Children

    RH (4 Months) RHE (5 Months, daily) RH (4 Months)

    For patients on health-facility DOT,write the number of dose on the date of DOT. For patients on home-based DOT, draw a horizontal line to indicate the number of days’ supply given to supporter, and then write number of doses on return date Month Year 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31

    Treatment outcome Date : ____/____/__________

    Cure

    Treatment Completed

    Treatment Failure

    Died

    Default

    Transfer out

    Remarks ______________________________________________________________________________________________________________

  • 39

    C. UFAFANUZI B: UJAZAJI WA FOMU YA TAARIFA YA MWEZI YA KITUO

    Fomu hii ni rahisi kujaza na kituo kinatakiwa kujaza fomu hii hata kama hakina wagonjwa au dawa za

    kifua kikuu na ukoma.

    SEHEMU A

    KAZI: Kujaza FOMU YA TAARIFA YA MWEZI YA KITUO

    INAFANYWA NA: Mtumishi wa afya anayetoa dawa za kifua kikuu (DOT Nurse)

    SABABU: Kutoa taarifa za idadi ya wagonjwa walio kwenye tiba, salio la dawa na kiasi cha

    dawa zilizoharibika au muda wake wa matumizi kuisha.

    LINI INAFANYWA: Mwishoni mwa kila mwezi

    NYENZO

    ZINAZOHITAJIKA:

    Kitabu cha taarifa ya mwezi ya dawa za kifua kikuu na ukoma, hesabu ya mkono

    ya dawa ya mwisho wa mwezi, kalamu (Bluu, nyeusi), hesabu ya kiasi cha dawa

    zilichoharibika au muda wa matumizi kuisha

    SEHEMU B

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    1. Jaza namba ya utambulisho ya kituo:

    Namba hii inatolewa na Wizara ya Afya

    na Ustawi wa Jamii..

    2. Jaza jina la Kituo: Jaza jina la kituo

    chako

    3. Aina ya Kituo: Jaza aina ya kituo. Vituo vinaweza kuwa:

    (GOV) Serikali

    (NGO) Asasi zisizokuwa za kiserikali

    (FBO) Mashirika ya Dini

    Vingine

    4. Jina la (Halmashauri) Wilaya: Jaza jina

    la wilaya ambako kituo kinawajibika.

    5. Kipindi cha Taarifa: Jaza mwezi na

    mwaka unaohusika katika taarifa hii.

    Hiyo itakuwa ni kipindi cha mwezi ambao ndio

    kwanza umekamilika. Mfano taarifa ya Januari

    itaandikwa siku ya mwisho ya Januari au

    mwanzoni mwa Februari.

    6. Tarehe ya kuwasilishwa: Andika tarehe

    ambapo taarifa imewasilisha kwa DTLC

    Hakikisha fomu inajazwa na inafika wilayani kabla

    ya siku ya 5 ya mwezi unaofuata. Mfano taarifa ya

    Januari ifike wilayani ndani ya kipindi kisichozidi

    tarehe 5 ya February.

    Kituo kipeleke wilaya nakala mbili za taarifa hii

    (halisi na nakala moja). Nakala moja ibaki kwenye

  • 40

    kitabu kituoni. Kituo kisibebe kitabu chote na

    kupeleka wilayani, ispokuwa kama kimeombwa

    kufanya hivyo.

    7. Miezi ya matibabu. Katika visanduku

    vyenye miezi ya matibabu andika idadi ya

    wagonjwa watakaokuwa kwenye mwezi

    husika wa matibabu ya kifua kikuu na

    ukoma katika mwezi unaofuata ule

    unaotolea taarifa.

    Katika kujaza jedwali hili kadi za wagojwa

    ziatatumika kutambua kila mgonjwa

    atakuwa kwenye mwezi wa ngapi wa

    matibabu katika mwezi unaofuata.

    Ni vizuri kama unayeandaa taarifa

    ukachora jedwali kama hili pembeni na

    kisha kuwa anaweka tick kwenye mwezi

    husika pale anapobaini kuwa mgonjwa

    atakuwa kwenye mwezi huo wa matibabu

    baada ya kupitia kadi yake.

    Baada ya kupitia kadi zote jumlisha idadi

    ya tick kwenye kila kisanduku kasha

    jumla yake iandike kwenye fomu

    unayoandikia taarifa

    Tumia sehemu hii pia kuonyesha idadi ya

    wagonjwa wanaotumia Isoniazid kama kinga

    tiba na miezi yao tiba hii katika visanduku

    husika.

    Katika mwezi wa 1 pia andika idadi ya

    wagonjwa wapya wanaotarajiwa kuanza dawa

    katika mwezi unaofuata (mfano kama taarifa

    ni ya Januari idadi ya wagonjwa wapya ni

    wale watakaoanza matibabu Februari kama.

    Hii ifanyike kama kituo kina taarifa za kuwepo

    kwa wagonjwa hao wapya.

    Kwa wagonjwa wapya wa kifua kikuu na

    watoto kama ulikuwa na wagonjwa kwenye

    mwezi wa 6 wa matibabu mwezi ulioisha na

    hukuwa na mgonjwa kwenye mwezi wa 5 wa

    matibabu kwenye mwezi ulioisha hii

    inamaanisha utakuwa huna mgonjwa kwenye

    mwezi wa 6 wa matibabu na hivyo unatakiwa

    uandike 0. Ikumbukwe kuwa matibabu ya

    kawaida ya kifua kikuu ni ya miezi 6.

    Wagonjwa wapya ambao hali yao ya

    makohozi haibadiliki baada ya matibabu ya

    miezi miwili huendelea na matibabu ya

    intensive phase kwa mwezi mmoja zaidi

    hivyo kama kituo kina mgonjwa wa aina hii

    wakati wa kuandika taarifa ya mwezi

    ahesabike kama atakuwa mwezi wa 2

    katika mwezi unaofuata na atakapomaliza

    marudio haya ataendelea kuhesabika

    kama mwezi wa 3 katika mwezi unaofuata.

    Pia izingatiwe kuwa

    Matibabu ya wagonjwa wa retreatment ni

    ya miezi 8

    Matibabu ya wagonjwa wa ukoma wa MB

    ni miezi 12

    Matibabu ya wagonjwa wa ukoma wa PB

    ni miezi 6

    8. Salio la dawa: Jaza jumla ya

  • 41

    vidonge/kapsuli zilizopo baada ya

    kufanya hesabu kwa mkono hadi kufikia

    mwishoni mwa mwezi

    9. KIasi kilichoharibika au kuisha muda

    wa matumizi: Jaza idadi ya

    vidonge/kapsuli ambazo

    zimeharibika(hazifai kwa matumizi) au

    ambazo muda wake wa matumizi

    umeisha

    Wasiliana na mfamasia kuhusu uwepo wa dawa

    zilizoharibika au muda wake wa matumizi kuisha

    ili mkubaliane namna zitakavyorudishwa wilayani

    10. Maelezo:

    Andika maelezo ya za uharibifu wa dawa

    kama kuna kiasi chochote kimeandikwa

    kwenye safu B mf expiry, kumwagikiwa

    mafuta nk. Sehemu hii pia inaweza

    kutumika kuitaarifu wilaya juu ya uwepo

    wa dawa ambazo muda wake wa

    matumizi utaisha ndani ya miezi mitatu

    ijayo.

    11. Maelezo muhimu:

    Andika taarifa za wagonjwa wanaohitaji

    dawa nyingine tofauti na zile

    zilizoorodheshwa kwenye fomu mfano

    predinisolone nk. Ili DTLC ajue namna

    ya kusaidia.

    12. Imeandaliwa na: Mtumishi wa kituo cha

    tiba aliyeandaa taarifa hii anaandika jina

    lake, saini na tarehe.

    Jaza fomu ya taarifa siku ya mwisho ya mwezi au

    siku ya kwanza ya mwezi unaofuata. Fomu hii

    inatakiwa ifike wilayani katika muda usiozidi

    tarehe 5 ya mwezi unaofuata.

    13. Imepitiwa na: Mganga mkuu wa kituo

    aipitie na kuipitisha taarifa kwa kuweka

    sahihi na tarehe

    14. Imeidhinishwa na: DTLC Mtumishi wa

    wilaya aliyeteuliwa kupitia, kuhakiki na

    kukokotoa kiasi cha dawa cha kugawa

    ataidhinisha baada ya kuandika kiasi cha

    dawa kinachopaswa kugawiwa kituoni

    anaandika jina lake, saini na tarehe.

  • 42

    KAZI HII INAKUWA IMEKAMILIKA BAADA YA:

    Namba ya kituo, Jina la Kituo na kipindi cha taarifa kujazwa.

    Visanduku vya idadi ya wagonjwa katika miezi ya matibabu kujazwa

    Safu za Salio la Mwisho kwa kila bidhaa

    Safu ya kaisi cha dawa kilichoharibika au muda wa matumizi kuisha kujazwa

    Fomu ya taarifa imesainiwa na mtayarishaji

    Fomu imesainiwa na mkuu wa kituo

  • 43

    D. FOMU YA TAARIFA YA KITUO YA MWEZI YA DAWA ZA KUTIBU KIFUA KIKUU NA UKOMA

    TAARIFA YA KITUO YA MWEZI YA DAWA ZA KUTIBU KIFUA KIKUU NA UKOMA

    Namba ya Kituo: Jina la Kituo: Aina ya Kituo (GOV/NGO/FBO/NYINGINE): ____________ Jina la Halmashauri Kipindi cha Taarifa-- Mwezi/Mwaka: Tarehe iliyowasilishwa: ___ Andika kwenye nafasi chini idadi ya wagonjwa unaokisia kuwa watakuwa kwenye matibabu kwa mwezi unaofuata. Andika sifuri (“0”) kwa kila mwezi ambao unadhani kuwa hakutakuwa na wagonjwa walio kwenye matibabu. Soma maelezo hapo chini. Mwezi wa wa Matibabu 1 2 3 4

    5

    6

    7 8 9 10 11 12

    Kifua Kikuu Idadi ya watu wazima

    (Wapya)

    Idadi ya watoto (Wapya)

    Idadi ya watu wazima

    (Retreatment)

    Idadi ya watu wazima (IPT)

    Idadi ya watoto (IPT)

    Ukoma Idadi ya watu wazima (MB)

    Idadi ya watu wazima (PB)

    Idadi ya watoto (MB)

    Idadi ya watoto (PB)

    Hesabu idadi ya dawa zilizopo kwenye kituo. Andika kiasi kwa kipimo, kama blister, ulizonazo kwa kila dawa kwenye visanduku chini. Usijumuishe dawa zilizo kwisha muda wa matumizi au dawa zilizoharibika. Andika sifuri (“0”) kwenye nafasi kama dawa haipo. Soma maelekezo kwenye mwongozo wa ujazaji taarifa ya mwezi ya dawa za kutibu Kifua Kikuu na ukoma

  • 44

    Na SEHEMMU HII IJAZWE NA KITUO SEHEMU HII IJAZWE NA DTLC SEHEMU HII IJAZWE NA MFAMASIA

    Jina la Bidhaa

    Kipimo cha kugawa

    Kiasi kilichosalia

    Kiasi kilichoharibika/expire

    Idadi ya wagonjwa watakaotumia dawa

    mwezi ujao

    Mahitaji ya mwezi kwa

    mgonjwa mmoja

    Mahitaji ya wagonjwa

    wote

    Mahitaji ya kituo

    Kiasi cha kutoa

    kiasi kilichopendekezwa kutolewa

    Kiasi Kikichotolewa

    Maelezo

    U A B C D E = C*D

    F=E*2 G= F-A G/U

    1 RHZE 150/75/400/275

    Blista/28 112

    2 RH 150/75 Blista/28 112

    3 RHE 150/75/400

    Blista/28 112

    4 Streptomycin 1g Kichupa(Vial)

    Chupa 28

    5 Water for injection

    Kichupa (Ampoule)

    Chupa 28

    6 MB (adult) Blista Blista 1

    7 PB (adult) Blista Blista 1

    8 RHZ 60/30/150

    Blista/6 112

    9 RHZ

    60/30/150

    Blista/3 112

    10 Ethambutol 100mg

    Boksi/500 84

    11 RH 60/30 Blista/6 112

    12 RH 60/30 Blista/3 112

    13 MB (Peds) Blista Blista 1

    14 PB (Peds) Blista Blista 1

  • 45

    Na SEHEMMU HII IJAZWE NA KITUO SEHEMU HII IJAZWE NA DTLC SEHEMU HII IJAZWE NA MFAMASIA

    Jina la Bidhaa

    Kipimo cha kugawa

    Kiasi kilichosalia

    Kiasi kilichoharibika/expire

    Idadi ya wagonjwa watakaotumia dawa mwezi ujao

    Mahitaji ya mwezi kwa mgonjwa mmoja

    Mahitaji ya wagonjwa wote

    Mahitaji ya kituo

    Kiasi cha kutoa

    kiasi kilichopendekezwa kutolewa

    Kiasi Kikichotolewa

    Maelezo

    U A B C D E = C*D

    F=E*2 G= F-A G/U

    15 Isoniazid 100mg

    Boksi/100 56

    16 Isniazid 300mg Blista/28 28

    MAELEZO MUHIMU:___________________________________________________________________________________________________________

    _________________________________________________________________________________________________________________________

    IMEANDALIWA NA:______________________________________ SAHIHI:____________________________ TAREHE:________________

    IMEPITIWA NA:_________________________________________ SAHIHI:____________________________ TAREHE: _______________

    IMEIDHINISHWA NA:_____________________________________ SAHIHI:____________________________ TAREHE:________________

  • 46

    E. UFAFANUZI C: KUHAKIKI TAARIFA KWENYE FOMU YA MWEZI YA

    KITUO NAKUKOKOTOA KIASI CHA DAWA CHA

    KUGAWA

    KAZI: Kuhakiki taarifa kwenye fomu ya mwezi ya kituo nakukokotoa kiasi cha dawa

    cha kugawa

    INAFANYWA NA: DTLC

    SABABU:

    Kudhibiti ukosefu wa dawa kituoni

    Kuhakakiki kuwa vituo vinavyotoa dawa za kifua kikuu na ukoma vinatoa

    taarifa

    Kuangalia usahihi wa taarifa zinazotolewa

    Kuhakikisha kuwa kituo kinapewa kiasi sahihi cha dawa

    LINI INAFANYWA: Ndani ya kipindi kisichozidi tarehe 10 ya mwezi unaofuata mwezi wa

    taarifa ya kituo

    NYENZO

    ZINAZOHITAJIKA:

    Taarifa ya mwezi ya dawa za kifua kikuu na ukoma ya kituo,kalamu,kikokotozi,

    na worksheet ya ukokotozi

    SEHEMU B

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    A: Kuhakiki kama vituo vyote vimetuma taarifa zao

    1. Kuthibitisha kama vituo vyote vimeleta

    taarifa.

    Hesabu idadi ya fomu za taarifa ya mwezi ya dawa za kifua kikuu na ukoma zilizoletwa wilayani. Idadi inatakiwa kulingana na idadi ya vituo vinavyopaswa kuleta taarifa.

    Kama kituo hakijaleta taarifa wasiliana na kituo

    husika au kitembelee ili upate taarifa yake. Au

    wasiliana na kituo kujua idadi ya wagonjwa

    watakaokuwa katika matibabu katika miezi

    mbalimbali, salio la kila dawa na kiasi cha

    dawa kilichoharibika au kuisha muda wake wa

    matumizi. Tumia taarifa hizo kubainisha kiasi

    gani kituo kina hitaji na kwa kuandaa maombi

    ya wilaya lakini pia fanya jitihada kuhakikisha

    kituo kinaleta taarifa yake wilayani mapema

    iwezekanavyo

  • 47

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    B: Kuhakiki ukamilifu na usahihi wa taarifa

    2. Pitia taarifa za juu ya fomu na uone kama

    zimejazwa kwa ukamilifu na usahihi

    Taarifa zinazotakiwa ni;

    Namba ya kituo

    Jina la kituo

    Aina ya kituo

    Jina la halmashauri/ wilaya

    Kipindi cha taarifa

    Tarehe ya kuwasilisha

    3. Angalia idadi ya wagonjwa iliyoandikwa

    kujiridhisha kama ni ya kweli na inaleta

    mantiki. Haijaongezeka wala kupungua

    sana.

    Pale unapokuwa na mashaka ni vizuri

    kujiridhisha kwa kuangalia taarifa za miezi

    iliyopita. Mfano kama imeonyeshwa kuwa

    hakuna mgonjwa kwenye mwezi 4 wa

    matibabu lakini wapo 13 kwenye mwezi wa 5

    wa matibabu unaweza kuangalia taarifa ya

    mwezi uliopita kama kulikuwa na wagonjwa 13

    kwenye mwezi wa 4 wa matibabu. Kama kuna

    utata wowote wasiliana na kituo husika

    4. Angalia pia kiasi cha vidonge

    vulivyoandikwa kama salio la mwisho wa

    mwezi.

    Salio la dawa linatakiwa kuendana na uhalisia

    wa wagonjwa waliokuwepo kituoni katika

    mwezi unaotolewa taarifa . Kama kuna

    ongezeko au upungufu unaotia shaka basi

    hapo kuna changamoto inayohitaji kufuatiliwa.

    5. Angalia pia kiasi cha dawa zilizoharibika au

    kuisha muda wake wa matumizi.

    Kama kituo kina dawa zilizoharibika au kuisha

    muda wake wa matumizi ratibu zoezi la

    kuzirudisha wilayani.

    6. Mambo muhimu ya kuzingatia wakati wa

    uhakiki wa taarifa

    Taarifa inaonyesha kuna

    wagonjwa lakini hakuna dawa.

    Wasiliana na kituo kwa haraka

    kuthibitisha na kama ni kweli hatua

  • 48

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    za haraka za kupeleka dawa

    zichukuliwe

    Taarifa inaonyesha kuna dawa lakini

    hakuna wagonjwa: Wasiliana na kituo

    kuthibitisha na kama ni kweli angalia

    uwezekano wa kuzirudisha wilayani ili

    ziweze kutumika na vituo vingine. Kituo

    kibakiwe na dawa inayotosheleza mahitaji

    ya mwezi mmoja ya mgonjwa mmoja

    katika kila hatua ya matibabu (Initiation na

    continuation phase). Na kama dawa hizo

    zitakaa sana chukua hatua kutambua

    muda wake wa matumizi unaisha lini na

    kama kuna hatari ya kuexpire ratibu zoezi

    la kuzihamishia kituo kingine

    zitakakotumika kabla ya kuexpire

    C: Kukokotoa kiasi cha kugawa kituoni

    7 Idadi ya wagonjwa: Jumlisha idadi ya

    wagonjwa watakao kuwa wakitumia

    dawa ya aina moja katika mwezi

    unaofuata ule uliotolewa taarifa na

    kuandika jumla yao kwenye safu C ya

    fomu taarifa ya mwezi ya kituo mbele

    ya dawa husika

    Kwa wagonjwa wapya wa kifua kikuu

    watakao kuwa kwenye miezi ya 1 na 2 ya

    matibabu watakuwa wakitumia dawa ya

    aina moja (RHZE) na watakaokuwa

    kwenye miezi ya 3 hadi 6 ya matibabu

    watakuwa wakitumia dawa aina moja (RH).

    Wagonjwa wa retreatment walio mwezi wa

    1, 2 na 3 wa matibabu wanatumia pia

    RHZE. Hivyo jumla ya wagonjwa watakao

    tumia RHZE= Jumla ya wagonjwa wapya

    wakubwa watakaokuwa mwezi wa 1 na 2

    wa matibabu kujumlisha idadi ya wagonjwa

    wa retreatment watakaokuwa mwezi wa 1,

    2 na wa 3 wa matibabu.

    Jumla ya watakaotumia RH 150/75mg =

    Jumla ya idadi ya wagonjwa wakubwa

  • 49

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    wapya kwenye miezi ya 3,4,5 na 6 ya

    matibabu

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia RHE=

    jumla ya idadi ya wagonjwa wa retreatment

    watakaokuwa kwenye miezi ya 4 hadi 8 ya

    matibabu

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia

    Streptomycin na water for injection ni jumla

    ya idadi ya wagonjwa wa retreatment

    watakaokuwa miezi ya 1 na 2 ya matibabu.

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia MB

    adult ni jumla ya wagonjwa watu wazima

    watakaokuwa kuwa kwenye matibabu ya

    MB kuanzia mwezi wa 1 hadi wa 12 wa

    matibabu.

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia PB

    adult ni jumla ya wagonjwa watu wazima

    watakaokuwa kuwa kwenye matibabu ya

    PB kuanzia mwezi wa 1 hadi wa 6 wa

    matibabu.

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia RHZ ni

    jumla ya wagonjwa watoto watakaokuwa

    kuwa kwenye matibabu mwezi wa 1 na 2

    wa matibabu.

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia

    Ethambutol(100mg) ni jumla ya wagonjwa

    watoto watakaokuwa kuwa kwenye

    matibabu mwezi wa 1 na 2 wa matibabu

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia RH

    60/30 ni jumla ya wagonjwa watoto

    watakaokuwa kuwa kwenye matibabu

  • 50

    Hatua Cha kufanya Zingatia

    mwezi wa 3 hadi wa 6

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia MB pd

    ni jumla ya wagonjwa watoto watakaokuwa

    kuwa kwenye matibabu ya MB ped kuanzia

    mwezi wa 1 hadi wa 12

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia BP pd

    ni jumla ya wagonjwa watoto watakaokuwa

    kuwa kwenye matibabu ya PB ped kuanzia

    mwezi wa 1 hadi wa 12

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia

    Isoniazid 300mg ni jumla ya wagonjwa

    wote watu wazima watakaokuwa kwenye

    miezi yote ya IPT

    Jumla ya wagonjwa watakaotumia

    Isoniazid 100mg ni jumla ya wagonjwa

    wote watoto