Transcript
Page 1: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI

SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

4

Page 2: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo
Page 3: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

iii

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

UTANGULIZI

Mwongozo wa mwalimu kidato cha nne ni kitabu cha kumsaidia mwalimu kufundishia kitabu cha mwanafunzi cha kidato cha nne. Mwalimu ana hiari kufuata na kukubali mpango uliopangwa na waanndishi au kubadilisha sehemu nyingine kwa kufuatana na ujuzi wa lugha hii, yaani Kiswahili.

Mwalimu anashauriwa ajaribu awezavyo kusoma sehemu ya matayarisho kabla ya kufunza somo lolote. Kutofanya hivyo kutamfanya mwalimu kushindwa kulisomesha somo lake kwa namna na hali ipasayo. Katayarisho hayawezi kabisa kufanywa siku hiyo wala si rahisi kwa vifaa vyote kupatikana siku hiyo hiyo. Kutokana na hayo yote wanafunzi wataweza kusikiliza, kutamka, kuona, kutenda, kusoma na kuandika Kiswahili vizuri zaidi na kwa urahisi kwa sababu mwalimu amejitayarisha vyema.

Kitabu hiki kinapangwa katika mihula mitatu (3) ambapo kila mhula huwa na majuma kumi na mawili (12). Katika taratibu ya kila funzo kuna vichwa vya maneno vifuatavyo: funzo, shabaha, vifaa na taratibu. Haya yote ni kutaka kumrahisishia mwalimu kazi yake. Ni muhimu kuielewa shabaha ya kila somo kwani shabaha ndiyo uti wa mgongo wa somo lolote.

Kitabu hiki pia, kimetayarishwa kwa ajili ya kurahisisha kazi ya mwalimu ya kufundisha Kiswahili. Tunakuonyesha shabaha za jumla za kila funzo, yanayohitajika kufundishwa kila juma na kila mhula. Namna mwanafunzi na mwanalimu mnavyosaidiana ili somo lenyewe liweze kufikia lengo lake pamoja na vifaa utakavyovitumia kwa kuendeleza somo.

Page 4: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo
Page 5: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

v

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

YALIYOMO

UTANGULIZI ................................................................................................................................................ iii

YALIYOMO ......................................................................................................................................................v

MPANGILIO WA KISWAHILI KIDATO CHA NNE MKONDO WA LUGHA ........................................................................................................... 1

1. Funzo: HISTORIA YA KISWAHILI (ukurasa 5-13) ................................................................................................................................... 5

2. Funzo: FASIHI (ukurasa 14-41)................................................................................................12

3. Funzo: NGELI ZA MAJINA (42-70) ..........................................................................................30

5. Funzo: UTUNGAJI (74-77) ..........................................................................................................42

6. Funzo: AINA ZA MANENO YA KISWAHILI (78-86) ................................................................................................................45

Page 6: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo
Page 7: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

1

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

MPANGILIO WA KISWAHILI KIDATO CHA NNE MKONDO WA LUGHA

MHULA WA KWANZA

WIKI

KIP

IND

I FUNZO SHABAHA

uku

rasa VIFAA MAONI

1-6 Historia ya Kiswahili

Kuwaongoza wanafunzi kujua na kuelewa historia ya Kiswahili kutokana na asili ya neno “Kiswahili” na namna kilivyoathiriwa na lugha za kigeni.

Kuwaongoza wanafunzi kueleza asili au chimbuko la Kiswahili na uhusiano wake na lugha za kigeni na kibantu kwa kuzingatia msamiati unaotumiwa katika lugha hizo.

Kuwaongoza wanafunzi kujua na kuelewa kusambaa na kuenea kwa Kiswahili Afrika ya Mashariki na kati.

- Vitu Halisi

- Vitabu

- Ubao

- Chaki za rangi tofauti

Page 8: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

2

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

7-12 Fasihi simulizi

Fasihi andishi

Kuwaongoza wanafunzi kujua kutega na kutegua vitendawili pamoja na kuvifurahia kama tanzu moja ya fasihi simulizi.

Kuwaongoza wanafunzi kueleza na kufafanua:

- Nadharia ya fasihi simulizi - Tanzu za fasihi simulizi

Kuwaongoza wanafunzi kusoma vitabu vihusuvyo fasihi andishi

Kuwaongoza wanafunzi kueleza na kufafanua:

- Nadharia ya fasihi andishi - Tanzu za fasihi andishi

- Picha tofauti

- Michoro

MHULA WA PILI

WIKI

KIP

IND

I FUNZO SHABAHA

uku

rasa VIFAA MAONI

1-8

9-12

Ngeli za majina

Usemi wa asili na usemi wa taarifa

Kuwaongoza wanafunzi kujua matumizi ya ngeli tofauti za majina kwa njia ya kimofolojia katika sentensi.

Kuwaongoza wanafunzi kuainisha ngeli za majina kwa njia ya kimofolojia.

- Chaki za rangi

- Ubao

WIKI

KIP

IND

I FUNZO SHABAHA

uku

rasa VIFAA MAONI

Page 9: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

3

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

1-6 Utungaji Kuwawezesha wanafunzi kujua namna ya kusoma na kuunda habari kwa kutumia maneno ipasavyo katika utungo wowote.

Kuwasaidia wanafunzi kufafanua, kutunga insha za wasifu kulingana na jinsi atakavyoulizwa na mwalimu.

Kuwaongoza wanafunzi kutilia mkazo uchaguzi wa maneno bora na matokeo yake kwenye matumizi.

- Vitabu (cha mwalimu na cha mwanafunzi)

- Vitu halisi

- Ubao

Kuwawezesha wanafunzi kubadili sentensi kutoka usemi wa asili hadi usemi wataarifa.

Kuwaongoza wanafunzi kutofautisha sentensi za usemi wa asili na sentensi za usemi wa taarifa.

- Vitabu vya sarufi

MHULA WA TATU

WIKI

KIP

IND

I FUNZO SHABAHA

uku

rasa VIFAA MAONI

WIKIK

IPIN

DI FUNZO SHABAHA

uku

rasa VIFAA MAONI

Page 10: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

4

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

7-12 Aina za maneno

Kuwawezesha wanafunzi kutunga hotuba fupi fupi kwa ajili ya kukuza vipaji vya kujieleza na kujiamini.

Kuwaongoza wanafunzi kutoa na kuelewa maana za nomino kama mojawapo wa aina za maneno.

Kuwawezesha wanafunzi kutaja aina za maneno na mifano mbalimbali kwa kila aina ya maneno.

Kuwawezesha wanafunzi kujua matamshi ya aina mbalimbali za maneno ipasavyo na kuyatumia katika sentensi kwa usahihi.

- Vitabu (cha mwalimu na cha mwanafunzi)

- Vitu halisi

- Ubao

WIKI

KIP

IND

I FUNZO SHABAHA

uku

rasa VIFAA MAONI

Page 11: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

5

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

1. Funzo: HISTORIA YA KISWAHILI (ukurasa 5-13)

Shabaha:

- Kuwaongoza wanafunzi kujua na kuelewa historia ya Kiswahili kutokana na asili ya neno “Kiswahili” na namna kilivyoathiriwa na lugha za kigeni.

- Kuwaongoza wanafunzi kueleza asili au chimbuko la Kiswahili na uhusiano wake na lugha za kigeni na Kibantu kwa kuzingatia msamiati unaotumiwa katika lugha hizo.

- Kuwaongoza wanafunzi kujua na kuelewa kusambaa na kuenea kwa Kiswahili katika Afrika ya Mashariki na ya kati.

Vifaa

Vitabu vinavyozungumzia historia ya Kiswahili na maeneo yake ulimwenguni, vitu halisi, maswali na majibu.

Taratibu

Hatua ya 1:

Mwalimu atawataka wanafunzi kusoma vitabu vinavyozungumzia historia ya Kiswahili ili wapate maoni tofauti ya waandishi kuhusu kazi hiyo. Mwalimu atafanya mambo hayo baada ya kutoa maelezo kuhusu haya yafuatayo:

a) Asili ya neno Kiswahili

Nadharia mbili kuhusu neno Kiswahili :

1. Nadharia ya kwanza ni ile isemayo kuwa Kiswahili ni neno lenye viambishi Ki-

swahel kumaanisha watu wa pwani au mwambao yaani sehemu za kando ya mto au bahari. Kwa hiyo Kiswahili ni lugha ya watu wa pwani.

Page 12: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

6

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

2. Nadharia ya pili ni ile isemayo kwamba Kiswahili ni neno lenye viambishi Kisiwa-hila kumaanisha watu ambao ni wenye sifa ya ujanja, ukorofi n.k. Yaani watu wanaotumia Kiswahili kwa kunyangʹanya mali za watu (Wahuni). Kwa hiyo, kutokana na nadharia hizi mbili na uchunguzi wa historia ya lugha ya Kiswahili, tunaona kuwa Kiswahili humaanisha watu wa pwani. Watu ambao hutumia lugha yenyewe ya Kiswahili.

- Kiswahili kutokana na Kiarabu

- Kiswahili kuwa lugha chotara

- Kiswahili kutokana na Kibantu

b) Historia yenyewe ya Kiswahili

- Kiswahili katika Afrika ya Mashariki

• Kiswahili katika Afrika ya Mashariki kabla ya ukoloni

• Kiswahili katika Afrika ya Mashariki wakati wa ukoloni

• Kiswahili katika Afrika ya Mashariki wakati wa harakati za uhuru

• Kiswahili wakati wa uhuru

• Kiswahili baada ya uhuru

• Kiswahili katika DRC, Burundi, nchi nyingine za Afrika na ulimwenguni

c) Lugha za kigeni kuathiri lugha ya Kiswahili

Hatua ya 2:

Mwalimu atataka wanafunzi kuzungumzia historia ya Kiswahili kutokana na waliyoyasoma kwa maoni yao wenyewe.

Hatua ya 3:

Kuwapa wanafunzi fursa ya kuchangia katika somo na kuuliza maswali. Hapa mwalimu huwasaidia kwa kujibu maswali yao na kuwafafanulia ikiwa kuna sehemu ambayo hawaelewi.

Page 13: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

7

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Majibu:

1. Asili ya lugha ya Kiswahili ni Afrika ya Mashariki sehemu za mwambao au upwa wa Afrika ya Mashariki. Kiswahili ni lugha na watu wake ni Waswahili na utamaduni au utu wao ni Uswahili.

2. Kiswahili ni lugha ya Kibantu kwani maneno mengi ya Kiswahili yanaonyesha asilimia kubwa ya mashina ya lugha za Kibantu.

Mifano ya kulinganisha Kiswahili na Kinyarwanda.

Mashina ya jumla ya lugha za kibantu

Maana katika Kiswahili Neno hilo katika Kinyarwanda

Bimba

Cing

Kenda

Temb

Tatu

(j) aka

Gongo

Koko

Joka

Tum

Mtu

Kupi

Tima

Vimba

Chinja

Kenda

Tembea

Tatu

Mwaka

Mgongo

Kuku

Nyoka

Tuma

Mtu

Fupi

Mtima

Ikibyimba

Gukinja

Ikenda

Gutembera

Gatatu

Umwaka

Umugongo

Inkoko

Inzoka

Gutuma

Umuntu

Gufi

Umutima

Page 14: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

8

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

3. Miaka ya awali baada ya kuzaliwa Kristo, yaani B.K. Waasia walifika na kuacha mimea kama minazi, migomba na kuacha mbuzi. Baada ya hapo Waarabu waliingia tena toka Oman. Mwingiliano na mawasiliano hayo yaliwaathiri Waswahili baadhi yao kwa dini na elimu hivi Kiswahili kikatohoa maneno mengi ya Kiarabu na kuyageuza na kuyafanya ya kiswahili. Kiswahili na lugha nyingine za Kiafrika baada ya majilio ya wageni msamiati wake uliathiriwa kwa kiasi fulani na lugha hizo ngeni.

Katika Kiswahili baadhi ya maneno ya Kiarabu yaliyomezwa katika Kiswahili ni haya:

Neno lenye asili ya Kiarabu Kiswahili asilia

Daima

Hidashara

Yamini

Ila

Sabiki

Ratibu

Tisa

Nadra

Wahedi

Swalah

Khabar

Milele

Kumi na moja

Kiapo

Isipokuwa

Tangulia

Panga

Kenda

Tukizi

Moja

Sala

Habari

Toka wakati huo Wareno waliingia kwa wingi tangu Msumbiji hadi Afrika ya Mashariki. Athari yao inaonekana katika lugha ya Kiswahili, ambamo mna maneno ya Kireno yaliyomezwa na kuwa ya Kiswahili.

Page 15: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

9

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Kireno Kiswahili

Mesa

Lenso

Caraco

Seti

Espada

Carta

Vinho

Meza

Leso

Korosho

Seti

Shupaza

Karata

Mvinyo

Baada ya hapo Wajerumani walitawala na hatimaye Waingereza walitawala. Maneno ya Kiingereza yameingia sana katika lugha ya Kiswahili na athari hiyo mara nyingi hadi leo umsikilizapo mzungumzaji wa Afrika ya Mashariki pengine huingiza maneno ya Kiingereza.

Kiingereza Kiswahili

Chalk

Television

School

Pipe

Notice

Chaki

Televisheni

Skuli

Paipu

Notisi

Kiswahili kimeathirika sana kimsamiati na mawasiliano na wageni, lakini kwa njia hiyo ya kufyonza maneno hayo, Kiswahili kimejitajirisha sana. Lugha iwayo yoyote duniani yenye hofu ya kufyonza msamiati ya dhana ambazo hazina hujinyima utajiri wa kuikuza lugha hiyo.

Page 16: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

10

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

4. Ukoloni wa ujerumani ulisaidia katika kukuza Kiswahili kwani walianzisha shule za kufundisha Kiswahili na wasomi wao ambao ni Velten, Seidel na Bittner walitoa maandishi ya Kiswahili kwa ajili ya masomo na kwa watumishi kujifunza Kiswahili.

5. Wamisionari walikuza Kiswahili kwani walihusika sana na mambo ya magazeti, “Msimulizi” toka 1888, “Habari za Mwezi” (1894) yote ni magazeti ya misheni za Kiingereza.

UMCA na Wamisionara wa Kijerumani Walutheri, mnamo 1910 walianzisha gazeti la “Pwani na Bara”. Mwaka huo huo Wakatoliki walianzisha gazeti “Rafiki yangu”. Mwaka huo huo kitabu “Barazani” kilitoka na kuuzwa nakala 11,000 hii ilionyesha kuwa Kiswahili kilikuwa kimepiga hatua.

6. Toka 1844 Rev. Ludwig Krapf ambaye alikuwa Mjerumani lakini aliyetumwa na Waingereza kwa njia ya chama cha kidini “Church Missionary Society” yaani C.M.S. alianzisha kanisa huko Mombasa.

Yeye alijifunza Kiswahili na kuanza kukiandika kwa hati ya Kilatini. Dkt. Krapf alipata matatizo katika kuendeleza maneno hayo katika hati ya Kilatini hasa tukilinganisha jinsi tunavyoendeleza leo, lakini amekuwa mwanzilishi wa kuandika katika hati ya Kilatini. Matatizo hayo ya maendelezo ni kama mifano hii michache.

Krapf Leo

Niugniza Nyunyiza

Gnigniniungu Nyungunyungu

Fania Fanyia

Wias Viazi

7. Krapf anakumbukwa katika historia ya Kiswahili kwani baada ya mwaka mmoja tu alitafsiri Injili ya Luka na Yohana katika Kiswahili na aliandika muhtasari wa Sarufi na msamiati ili kazi hiyo ianze kuwasaidia Wamisionari. Dkt. Krapf aliendelea na kazi hiyo na aliandika Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza.

8. Waziri wa Makoloni na Uingereza alitoa amri ya kuanzisha baraza la Kiswahili

Page 17: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

11

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

kwa ajili ya nchi zote nne yaani Uganda, Kenya, Unguja wa Tanganyika. Tarehe mosi Januari 1930 ikaundwa kamati iliyojulikana kwa jina la “Inter-Territorial Language Committee” na shabaha lake kuu lilikuwa kusanifisha lugha ya Kiswahili na kuondoa lahaja zilizokuwepo. Kwa hiyo, Kamusi mbili zilitengenezwa, “Standard Swahili-English na English-Kiswahili”.

9. Rwanda imeamua kufundisha Kiswahili sanifu kwani iliwahi kushirikiana na Tanzania katika maswali kadhaa na baadhi ya hayo ni ufundishaji wa Kiswahili sanifu.

Page 18: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

12

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

2. Funzo: FASIHI (ukurasa 14-41)

Shabaha

Kuwaongoza wanafunzi kusoma vitabu vihusuvyo fasihi simulizi na fasihi andishi.

Kuwaongoza wanafunzi kueleza na kufafanua:

- Nadharia ya fasihi

- Tanzu za fasihi simulizi na fasihi andishi

Kuwaongoza wanafunzi kujua kutega na kutegua vitendawili pamoja na kuvifurahia kama tanzu moja ya fasihi simulizi.

Vifaa

Vitabu kuhusu fasihi kwa ujumla, michoro yenye historia fulani, kusikiliza pamoja na kutizama tamthilia ambazo huigizwa mahali tofauti kama tanzu mojawapo wa fasihi andishi na vifaa halisi.

Taratibu

Utangulizi: Ili kuwachangamsha, wanafunzi wataimba wimbo wanaoupenda. Wanapofanya zoezi hili, wanafunzi wanajichangamsha wenyewe.

Hutua ya 1:

Mwalimu ataeleza fasihi na kuonyesha mifano ya kazi za fasihi.

Habari za kweli na za kubuni katika fasihi huitwa kazi. Kazi hizo hugawanyika katika tanzu

au aina kuu tatu:

Page 19: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

13

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

1. Hadithi

- Hadithi za mapokeo: kama vile visa, ngano, hekaya.

- Tawasifu: maandishi kuhusu maisha ya mtu binafsi.

- Sira: maandishi kuhusu maisha ya mtu mwengine (Shaban Robert huiita wasifu).

- Riwaya: hadithi ndefu za kubuni, hasa katika fasihi andishi.

- Methali na vitendawili

2. Ushairi

- Mashairi na tenzi (ushairi wa mapokeo)

Mashairi ya kimapokeo huwa na mfumo wake ambao haubadiliki sana. Tunapata mambo manne muhimu katika ushairi wa namna hiyo: ubeti, mizani, vina na kituo.

UBETI: Ni fungu la mistari ambalo huwa na idadi fulani na kila fungu hutoa funzo moja.

Mfano:

Titi la mama litamu

Titi la mama litamu, hata likiwa la mbwa, Kiswahili naazimu, sifayo inayofumbwa, Kwa wasiokufahamu, niimbe ilivyo kubwa, Toka kama chemchemu, furika palipozibwa, Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.

Toka kama mzalimu, juu kwa wingi furika, Mfano wa Zamuzamu, yenye rutuba Makka, Uonyeshe na muhimu, kwa wasio kutamka, Hata wafanya hamu, mapajani kukuweka, Titi la mama litamu, jingine halishi tamu.

Page 20: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

14

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Lugha yangu ya utoto, hata leo nimekua, Tangu ulimi mzito, sasa kusema na jua, Sawa na manukato, moyoni mwangu na pua, Pori, bahari na mto, napita nikitumia, Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.

Katika mashairi ya Kiswahili kuna yaliyo na beti zenye mistari mitano, minne, mitatu na hata miwili. Mashairi ya namna hiyo hupewa majina kufuatana na idadi ya mistari iliyomo katika ubeti.

Kufuatana na idadi ya mistari iliyomo katika ubeti tunaweza kuwa na:

i) Hamziya: ni utungo ulio na mistari miwili miwili katika kila ubeti.

ii) Tathlitha: ni shairi ambalo lina beti za mistari mitatu mitatu katika kila ubeti.

iii) Tarbia: ni utungo ulio na mistari minne minne katika kila ubeti.

iv) Takhmisa: shairi lenye kuwa na beti za mistari mitano mitano.

v) Tasdisa: ni shairi lenye kuwa na beti za mistari sita sita.

vi) Ukumi: ni shairi lenye kuwa na beti zenye mistari kumi kumi.

MIZANI: Ni idadi sawa ya silabi katika mistari mingi. Mizani ndiyo ambayo huleta mapigo, yaani mdundo wa shairi na mdundo huu huleta mwendo wa kimziki. Ndiyo ambayo hufanya mashairi ya Kiswahili yaimbwe.

Mf.1:

Ti/ti/la/ma/ma/li/ta/mu/, ha/ta/li/ki/wa/la/m/bwa/, Ki/swa/hi/li/na/a/zi/mu/, si/fa/yo/i/na/yo/fu/mbwa/

Mf.2:

Mswahili

Si/ni/i/te/ji/na/, mi/mi/M/swa/hi/li/, Na/sa/ba/na/ka/na/, si/ja/li/a/si/li/, Ni/na/po/ku/ta/na/, wa/tu/ki/la/ha/li/, Twa/la/Ki/swa/hi/li/, bi/la/ku/ju/a/na/.

Page 21: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

15

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Ta/nza/ni/a/na/ni/, a/so/M/swa/hi/li/, Ha/ta/ba/ra/nda/ni/, sa/sa/Wa/swa/hi/li/, Ki/swa/hi/li/kwa/ni/, si/yo/ki/dha/li/li/, I/ki/la/pa/ha/li/, si/lu/gha/ya/pwa/ni/.

KITUO: Ni mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi. Wahakiki wengine hukiita kibwagizo. Kinaitwa kibwagizo ikiwa mstari huo unarudiwa rudiwa.

Mf: Titi la mama litamu, jingine halishi hamu.

- Ngonjera: mashairi ya kujibizana baina ya watu wawili au zaidi. Ngonjera husemwa haziimbwi. Mara nyingi ngonjera huwa na mhusika mjuaji na mdadisi (mpelelezi). Hatimaye mdadisi hukiri kwamba anaelewa jambo hilo.

Maudhui ya ngonjera huwa ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.

Utoaji hadharani wa ngonjera hutumia vitabia yaani wahusika wanaotumia mikono, macho, midomo na viungovingine vya mwili. Vitabia huleta uhai wa igizo la ngonjera. Kuhusu vina na mizani na vituo na beti, ngonjera hufuata mfumo wa shairi la kawaida.

- Zuhari: wengine huita ushairi huru, mashairi huru, mashairi ya kisasa, mashairi ya kienyeji, mtiririko, n.k.

- Nyimbo

3. Michezo ya kuigiza: wengine huita tamthilia.

- Futahi: michezo ya furaha na ushindi

- Tanzia: michezo ya kuhuzunisha nay a janga.

- Yuga: nusu furaha, nusu huzuni

- Ramsa: michezo ya kejeli na mzaha

Fasihi ni kazi ya sanaa imulikayo hisi, mawazo na malengo ya jamii kwa kutumia lugha. Fasihi ni sanaa ya matumizi ya maneno kisanaa. Hakuna maneno ya kisanaa, bali maneno haya haya ya kawaida hutumiwa kisanaa na msanii.

Page 22: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

16

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Fasihi hujishughulisha na ubinadamu na mazingira yake ya kila siku. Fasihi hueleza hisi za binadamu kwa njia ya maneno kwa yote anayoyahisi, anayoyasikia, anayoyaonja, yanayomgusa na yanayomkabili. Si hayo tu, bali mambo ya ndani ya nafsi yahusuyo imani na itikadi.

Fasihi leo hugawanyika katika nyanja au taaluma mbili kuu, yaani fasihi simulizi na fasihi andishi.

Fasihi simulizi ina tanzu nyingi sana. Hapa katika kitabu hiki tutaangalia tanzu saba ambazo ni hadithi, vitendawili na mafumbo, methali, nahau, nyimbo, majigambo

na mizio/miiko.

Mambo machache kuhusu kila tanzu na matumizi yake.

1. Hadithi: Hadithi ni mambo ya kubuni ambayo huwa yanaeleza ukweli fulani katika jamii. Kwa maelezo haya, hadithi kwa asili yake ni habari ambayo inasimuliwa. Hadithi ina mtindo wake wa kusimuliwa.

Kwa mfano:

Mwanzoni

1. Msimulizi: Paukwa! (2)

Wasikilizaji: Pakawa! (2)

Msimulizi: Hapo zamani za kalepalikuwepo ………….

2. Msimulizi: Hadithi! Hadithi! (2)

Wasikilizaji: Hadithi njoo! (2)

Hapo zamani ……….

Mwishoni

- Huu ndio mwisho wa hadithi

- Hadithi inakomea hapa

Maneno haya hutumiwa kama umuhimu ufuatao:

Page 23: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

17

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

- Kuvuta na kuwaamusha wasikikilizaji

- Kuwaweka katika muktadha

Majibu kutokana na hadithi “Kobe na Nyani”

1. Baada ya kuona kwamba shoka la Kobe linakata vizuri, Nyani alimwambia Kobe amwazime shoka hilo lakini baadaye alimwarifu Kobe kwamba lile shoka lake hatalipata tena kwamba alimwazima mjomba wake naye akamuarifu kuwa wakati huo tu mwizi aliivamia nyumba yake akaliiba. Hii ilikuwa ni njia moja ya kutaka kubaki na shoka hili.

2. Ili kupata shoka lake Kobe alimwambia mkewe amkatekate katika vipande vipande halafu nyama yake iwe kitoweo kizuri kabisa. Baada ya hapo pika chakula halafu akakiweke katika njia panda. Akamwambia kwamba ahakikishe kuwa anafanya hivyo wakati Nyani yumo shambani mwake. Alimkatakata mumewe vipande. Nyama yake akaikaanga vizuri sana. Akatengeneza wali. Chakula kilipokuwa tayari, alikifunika na kukipeleka njia panda karibu na shamba la Nyani.

3. Tabia ya Nyani haikubaliki katika jamii. Kwanza alimwomba Kobe amsaidie ili shamba lisafishwe upesi kuwahi majira lakini malipo yenyewe Nyani ayomlipa Kobe ni kinyume na kitendo alichokifanya.

4. Mafunzo kutokana na hadithi ni haya yafuatayo:

- Kikulacho kinguoni mwako.

- Ubaya hatima yake mbaya.

- Ndugu mbayahumshinda rafiki mzuri

- Wema ni dhahabu na ubaya ni aibu

- Wema hauna lawama, ubaya una kilema.

2. Vitendawili ni maneno yanayotumia lugha ya mafumbo na huitaji ufumbuzi au majibu. Vitendawili ni sanaa pevu na huwa na usanii wa daraja la juu unaohitaji uwezo wa kujibu kiufundi na kimvuto.

Page 24: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

18

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Mafumbo ni kauli zinazoeleza jambo kwa njia isiyo wazi. Mafumbo hutumia taswira (picha) ili kuwafikisha wasikilizaji katika ufumbuzi.

3. Nyimbo ni maneno yaliyopangwa yakiwa na ujumbe maalumu na kutamkwa kwa sauti ya mziki. Wimbo huwa na mdundo unaosisimua na mara nyingine kunakuwepo na mlingano wa sauti katika miisho ya maneno. Kuna nyimbo ambazo hufuatana na zana za mziki, kama marimba, zeze, ngoma, zumari, nanga na zana nyingine.

Afrika ni Afrika iimbayo. Afrika ni tajiri sana katika uimbaji. Afrika yetu watu wake huimba katika shughuli mbalimbali na mahali mbalimbali na wakati mbalimbali. Toka mtoto azaliwe husikia nyimbo mpaka dakika ya mwisho ya maisha yake Mwafrika husikia nyimbo.

Aina za nyimbo

1. Nyimbo za watoto

Mtoto mchanga anapokua akaweza kwenda, kukimbia na kusema naye huanza kuimba pamoja na wenzake. Nyingi katika nyimbo hizi huimbwa katika michezo ya watoto na baadhi yake huimbwa kwa pamoja na nyingine huimbwa kwa kujibizana.

Nyingi ya nyimbo za Waswahili huhusiana na matukio ya kihistoria.

Mfano:

A- Kibaraka! Kibaraka

B- Lapee nana labee

A- Nile mtama nisile

B- Kula nana kula

A- Nile mtele (mchele) nisile

B- Kula nana kula

A- Nile mahindi nisile

Page 25: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

19

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

B- Kula nana kula

A- Bwana amekwendapi?

B- Amekwenda msikitini

Nakusali na kusoma

A- Akija nisalimie.

2. Mbembelezi

Ni nyimbo anazoimbiwa mtoto mchanga na mama yake au mtu mwingine kwa madhumuni ya kumuong’oa na kumlaza. Nyimbo kama hizi ni nyingi na karibu kila mama hubadilisha mambo fulani na kuongezea maneno fulani, mishororo na beti zake mwenyewe.

Mfano:

Howa howa kibibie U wangu bibi silie Ukaniliza na mie Yaweke yako machozi

Machozi yako yaweke Nikifa unililie Watu wakufikilie Ewe mwana wa ulizi

3. Nyimbo za sherehe (kutahiri, arusi, mavuno, maulidi, n.k.)

Kuna nyimbo nyingi sana zinazoimbwa na watu wazima katika sherehe mbalimbali. Kuna nyimbo za:

- kutahiri

- arusi

Page 26: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

20

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

- mavuno

- maulidi

- kukaribisha wageni watukufu, n.k.

Nyingi katika nyimbo hizi huimbwa katika ngoma fulani au wakati wa tukio fulani.

Mfano:

1) Lele mama

Katika ngoma ya lele mama, wanawake husimama mstari mmoja juu ya ubao wakicheza mikono juu huku wakiimba:

Mama naumiya x2

Mama naumiya hooyaa

Naambiwa nishunge bata

Ziwani kulee

Kuna madege meupe

Shungwa ndee-ru-ree…

2. Shangani

Katika ngoma hii wanawake huingia uwanjani wakajipanga duara harafu huanza kuimba beti za nyimbo mbalimbali zenye mahadhi mbalimbali huku wakichezesha mikono:

Kunguru akilia x2 Alilia mirambo x2 Akilia aliaje Kwaa! Kwa! Kwaa! Alilia mirambo….

Page 27: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

21

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Mara hurukia ubeti mwingine wenye mahadhi (kiwango) tofauti kabisa.

Kidege-eee Alalia mashua Sasa amepata ujanja Kidege ametua.

4. Taarab

Ni nyimbo ambazo huimbwa kwa lengo la kutumbuiza (kufurahisha) watu. Nyimbo hizi hufuatana na mziki unaopigwa na watu wachachewakiwa na ala mbalimbali za mziki mbele ya hadhira ya wasikilizaji. Nyingi huwa zina mafumbo fulani lakini kuna nyinginezo ambazo zina maana ya wazi.

Mfano:

Kasha langu la zamani Kitasa ndani kwa ndani Alofungua n’ nani Kasha muundo wa kale Ni kazi ya watu wale Usifanye makelele Mafundi wote wa kale Na walobaki wafilie Ilobaki mvulele.

4. Methali

Methali ni lugha ya mifano ambayo huwa na makusudi ya kutoa mafundisho, maadili, kuonya, kufumba kwa kutumia maneno machache. Methali ni misemo yenye hekima fulani. Methali hudhihirisha mkusanyiko wa mafunzo waliyopata watu wa vizazi vingi vya jumuiya fulani katika maisha yao. Ni sehemu moja ya lugha inayoweza kubaini falsafa ya watu fulani kuhusu maisha kwa ujumla.

Page 28: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

22

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Mifano ya methali na matumizi yake

1. Asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu

Maana: Mamaye ni mama yake. Asiyefunzwa na mama yake hufunzwa na ulimwengu (yaani kutokana na mambo yanayompata ulimwenguni). Mzazi ndiye mwalimu wa kwanza wa kwanza wa mtoto na ndiye anayempa maelekezo na ushauri wa yepi ya kufanya na yepi hayapaswi kufanywa. Ikiwa mtu anaupuuza ushauri huu, ataishia kupatwa na matatizo makubwa ambayo yanakuwafunzo kwake.

Matumizi: Hii ni methali inayoweza kutumiwa kumwelezea mtu aliyeupuuza ushauri wa wazazi wake na kupatwa na matatizo makubwa. Aidha ni nasaha kwetu kuhusu umuhimu wa kuyazingatia mafundisho ya wazazi au wenye uzoefu wa maisha.

2. Bibi mzuri hakosi kilema

Maana: Hata mke akawa mzuri kiasi gani hatakosa ila au dosari fulani; ila hiyo inaweza kuwa ya kimaumbile au kitabia. Hakuna kitu kizuri kisichokuwa na upungufu fulani.

Matumizi: Methali hii inaweza kutumiwa kumwelezea binadamu; kuwa kila mtu ana udhaifu fulani. Inaweza kutumiwa kutukumbusha kuwa hakuna kitu kisichokuwa na upungufu.

3. Chema hakidumu

Maana: Kitu kizuri hakina maisha; hakidumu. Baada ya muda kitu hicho huishi au kikatoweka. Mtu mzuri hana maisha marefu.

Matumizi: Hutumiwa kumliwaza mtu aliyefiwa na ndugu au jamaa yake aliyekuwa mzuri. Huweza kupigia mfano kitu kizuri ambacho kimeisha au kupotea baada ya muda mfupi tu.

4. Heri nusu ya shari kuliko shari kamili

Maana: Shari ni jambo lenye matokeo mabaya au ya hasara. Ni afadhali nusu ya shari kuliko shari kamili. Afadhali kupata taabu kidogo kuliko kukumbana na taabu kubwa.

Page 29: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

23

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Matumizi: Hutumiwa kumshauri mtu kuwa ni heri kupambana na shida ndogo au jambo dogo lenye udhia au usumbufu kuliko kubwa ambalo lina matatizo na balaa kubwa.

5. Jinga ni lako mwenyewe, la mwenzio huwezi kulitumia

Maana: Jinga ni pande kubwa la mti linalochomeka. Jinga unaloweza kulitumia kuwashia moto ni ulilo nalo; huwezi kutumia la mtu mwingine. Kitu kinachoweza kukusaidia wakati wa shida ni ulicho nacho; cha mbali hakiwezi kukusaidia.

Matumizi: Hutumiwa kuwakumbusha watu umuhimu wa kuvithamani vitu walivyo navyo hata kama si vizuri. Kitu ulicho nacho mkononi ndicho kinachoweza kukufaa wakati wa shida.

6. Karamu mbili zilimshinda fisi

Maana: Karamu ni vyakula na vinywaji vilivyoandaliwa kwa ajili ya shughuli fulani. Kuna kisa kuwa siku moja fisi alialikwa kwenye karamu mbili na alipofika penye njia panda- njia moja huku na nyingine kule – akashindwa kuamua aende karamu ipi. Alipojaribu kwenda kote akaishia kupasuka katikati. Tamaa nyingi ina madhara makubwa.

Matumizi: Methali hii hutumiwa kuwaonya watu wasiwe na uroho au tamaa.

7. Kidole kimoja hakivunji chawa

Maana: Chawa ni mdudu mdogo anayekaa kwenye mwili wa binadamu, kwenye nguochafu au kitandani na anayenyonya damu. Huwezi kumwua chawa kwa kidole kimoja. Lazima ubane baina ya vidole viwili. Mtu mmoja hawezi shughuli inayohitaji watu wengi.

Matumizi: Methali hii inatumiwakuwashauri watu kushirikiana ili wafanikiwe. Huweza pia kutumiwa kupigia mfano hali ambapo mtu mwenye kiasi kidogo cha pesa anataka kufanyan jambo linalohitaji pesa nyingi au lenye gharama kubwa.

5. Nahau: Nahau ni semi fupi zinazotofautina na maana yake ya asili. Nahau hutumia picha na kutoa maana kamili katika maisha. Ni kauli zilizojengwa kwa kutumia

Page 30: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

24

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

maneno ya kawaida lakini zinatoa maana isiyo ya kawaida, yaani maana fiche.

Maana za nahau huwa kamili na ni mara chache nahau moja iwe na maana zaidi ya moja, labda tu ilazimishwe katika matumizi.

Semi hizi huambatisha kitenzi na nomino (K+N).

Mifano:

- Kupata jiko= Kuoa

- Kupata kileo= Kulewa sana

- Kupasuka moyo= Kushtuka

- Kupasua bomu= Kusema jambo la fedheha (kukasilisha)

- Kukata kiu= Kupata kinywaji

6. Majigambo

Majigambo ni utanzu wa fasihi simulizi ambayo yana uhusiano wa karibu na mashairi. Dhana ya kujisifu ndiyo ambayohuwa dhamira kuu ya majigambo.

Majigambo yanahusiana na kujitangazia sifa, kujitakasa kuwa una makosa ambayo ni kujinaki. Tena kujigamba na kujinata (yaani kujiona bora kuliko watu wengine) au kujiketua (yaani kujifanya kuwa na mambo usiyokuwa nayo).

7. Miiko/Mizio

Kwa kawaida mzio au mwiko ni jambo au kitu kinachozuiwa mtu kutumia kwa kuogopa kupata madhara. Mzio ni jambo ambalo mtu hawezi kulitenda kwa sababu ya tabia mazoea au imani.

Mzio ni hali ya kutoweza kula kwa sababu ya kuchelea kudhurika. Miiko imejengwa kupiitia misemombalimbali kama vile:

→ “Ni mwiko au mzio ku………………”

Pengine unaweza kusema ”kufanya hivi na hivi ni…………”

→ “Inakatazwa kufanya………………… “

Page 31: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

25

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Mifano:

- Kutema mate ndani ya lindi (shimo la choo) kunaletwa kuumwa kuu.

- Mwenye kuzoea kula ndani ya chungu atapata mvua kubwa siku ya harusi yake.

- Mtoto mwenye kuchezea kivuli chake cha taa atakojoa kitandani.

- Kuuza chumvi usiku ni nuksi kwa mwenye duka.

- Kumbusu mtoto usingizini kunasababisha mtoto huyo kuwa na majivuno ukubwani mwake.

- Ukionyesha mwezi mchanga kidole basi utakatika kidole.

- Mtu akila bila kupiga Bismillahi basi baraka itaondoka na mtu hataweza kushiba.

Hatua ya 2:

Wanafunzi kutoa hadithi, vitendawili, methali, nahau, nyimbo vyao wenyewe kwa kupima uwezo wao.

Hatua ya 3:

Mwalimu atasoma vitendawili tofauti na kuwataka wanafunzi kujibu. Mwalimu atamtaka mwanafunzi mmoja mmoja asome vitendawili mbalimbali ili wanafunzi wengine wamjibu.

Majibu kuhusu fasihi:

Mazoezi1

1. Riwaya ni hadithi ndefu ya kubuni, ambayo huwa inakusudia kuifikia hadhira kwa kupitia njia ya maandishi. Riwaya aghalabu huwa na maneno yanayozidi 30,000.

2. Lugha itumikayo katika riwaya ni aina ya nathari (maandishi ya moja kwa moja, maandishi ya kawaida) na hutumia mchanganyiko wa vipengele vya lugha kama vile tamathali za usemi, methali, nahau, mafumbo, kejeli, ishara, n.k.

Page 32: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

26

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

3. Wahusika huwa ni watu, wanyama, vitu au viumbe wa kufikirika. Mwandishi wa hadithi, huwajenga wahusika wake kisanaa ili waweze kuwakilisha dhana mbalimbali za uhalisi wa maisha katika jamii.

4. a) Riwaya hujengwa na fani (ni jinsi riwaya ilivyojengeka. Kitu muhimu katika fani ya riwaya ni uchoraji wa wahusika) na maudhui (ni yale yaliyomo ndani ya riwaya au dhamira zote na ujumbe tunaobaki nao baada ya kusoma).

b) Tabia za wahusika ni ubapa, uduara na ufoili.

- Ubapa huwakilisha aina moja tu ya tabiakutoka mwanzo hadi mwisho wa hadithi. Toka mwanzo hadi mwisho tabia hii inajidhihirisha katika mhusika anayeishi katika wazo na sifa za aina moja bila kubadilishwa na wakati, mazingira, uhusiano wao na wengine, n.k. Tabia hiyo haibadiliki kufuatana na hali za kawaida za maisha ya binadamu zinazobadilika kihistoria. Tabia hii inaelezwa kwa kutumia wahusika bapa-sugu na wahusika bapa vielelezo.

- Uduara ni tabia ambayo mhusika mmoja hujenga akionyesha tabia tofauti. Tabia ya uduara humfanya mhusika kubadilikabadilika kihulka, kimawazo na kisaikolojia.

Wahusika wenye tabia hiyo huonyesha kubadilika ambako kunatokana na mazingira mapya. Sifa kuu ya wahusika wenye tabia hiyo, hadithini huishi maisha kawaida yanayofanana sana na jamii kiasi ambacho msomaji huwakubali kuwa ni wahusika hai.

- Ufoili ni tabia inayojidhihirisha kati ya wahusika duara na wahusika bapa. Lakini pia ni tabia inayoonyesha hali zaidi kuliko wahusika bapa. Ili waweze kujengeka vyema, wahusika wenye tabia hii huwategemea sana wahusika duara na wahusika bapa. Kwa hiyo, wahusika wenye tabia ya ufoili wana msukumo wa nafsi ulio tofauti na wahusika wakuu ama wahusika wengine muhimu katika kazi ya sanaa.

Page 33: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

27

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

5. Riwaya huhifadhiwa katika maandishi kwa sababu ya urefu wake ili isisahauliwe.

6. Mandhari katika riwaya ni mahali ambapo riwaya ilititolewa, yaani mahali na wakati ambapo vitendo katika riwaya au hadithi vimefanyika.

Mazoezi 2

1. Tamthilia ni mchezo wa kuigiza ulioandikwa ili uigizwe jukwaani au usomwe. Lengo kuu ni lile la kutoa maudhui na ujumbe kwa njia ya maigizo.

2. Aina za tamthilia ni hizi zifuatazo:

a) Tanzia: ni tamthilia yenye huzuni ndani mwake.

b) Ramsa: ni tamthilia zenye kuchekesha kutokana na utani, mzaha, kejeli, matendo yaonyeshayo ujinga, n.k

c) Tanzia-Ramsa: tamthilia hizi zina sifa za ramsa lakini ndani ya uchekeshaji wake huwa na tanzia kama vile kuaanguka kwa jamii au maanguko ya mhusika mkuu.

3. Tofauti kati ya tanzia na ramsa. Tanzia ni tamthilia yenye huzuni ndani mwake. Huweza kuwa na matukio ya vifo na mateso. Mwisho wa tamthilia za aina hii huwa ni wa masikitiko, maanguko na hasara kwa mhusika mkuu au jamii inayoibushwa. Wasomaji au watazamaji hujinasibisha na maangamizi ya mhusika huyo au jamii hiyo.

Kwa upande wake Ramsa ni tamthilia zenye kuchekesha kutokana na utani, mzaha, kejeli, matendo yaonyeshayo ujinga, n.k. Uchekeshaji huo hulenga katika kuikosoa jamii, watawala na tabia mbaya na watu binafsi.

4. Migogoro hufanya mchezo usonge mbele, kwa kitendo cha pili kutokana na kusababishwa na cha kwanza.

Page 34: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

28

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

5. Tofauti baina ya riwaya na tamthilia.

Riwaya Tamthilia

- Ni masimulizi ya mfululizo yaliyochanganyika na mazungumzo baina ya wahusika ambayo yakiandikwa hupambanuliwa kwa usemi”…” Mratibu wa mazungumzo ni mwandishi au mtunzi mwenyewe wa hiyo riwaya.

- Riwaya ikiandikwa hugawika katika sura au milango na ibara.

- Inatumia lugha ya nathari ndani yake.

- Ni mazungumzo ya moja kwa moja kati ya wahusika wenyewe. Hayahitaji mratibu au mdokezaji wa kutaja fulani kasema au kauliza. Hata yakiandikwa hamu na alama za usemi zinatumika, bali majina ya wahusika wanaozungumza huwekwa mbele au mwanzoni mwa maneno yao.

- Michezo ya kuigiza huchanganya maneno na vitendo ili kuyaonyesha maisha kama yalivyo.

- Michezo ikiandikwa au ikionyeshwa hugawika katika vipande vinavyoitwa vitendo au sehemu, na kila kitendo huweza kugawanywa katika maonyesho.

- Katika michezo ya kuigiza, wahusika hujieleza wenyewe kwa yale wasemayo na watendayo. Tena wahusika huweza kutumia ishara.

Mazoezi 3

1. Ushairi ni mtungo wa kisanaa unaotumia lugha ya mkato na mnato katika kuibusha mawazo, hisi na matukio juu ya maisha. Lugha ya shairi ni ya mkato, nyoofu na yenye mvuto na mnato yaani tumbuizi kwa masikio. Maneno yake ni maneno yaliyoteuliwa ili kukidhi lengo la mshairi. Shairi hutumia lugha ya picha na huwa na ulinganifu wa vina. Vina hapa, maana yake ni miisho iliyo sawa, silabi za sauti ile ile zilizoko mwisho.

Page 35: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

29

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Shairi huwa na ulinganifu wa mizani. Mizani ni idadi sawa ya silabi katika kila mstari, ubeti hadi ubeti. Shairi huwa na kituo, yaani mwisho wa ubeti. Maana kamili katika shairi hupatikana wakati shairi hilo linajitoshereza. Mashairi husomwa au huimbwa.

Utenzi kwa upande wake ni sanaa ambayo huelezea tukio maalum. Tukio hilo linaweza kuwa ni la kihistoria katika jamii, la wakati ule ambao jamii inaishi au linalotabiriwa.

Kwa sababu ya uzito wa yale ambayo tenzi huelezea, kwa kawaida tenzi nyingi huanza na dua. Mwandishi humwomba Mola amwongoze katika uandishi wake.

Tukiangalia katika fani, tungo zake huwa ndefu, yaani huwa ni beti nyingi kuliko shairi. Zaweza hata kuzidi mia tatu kufuatana na uzito wa maudhui na ubingwa wa mtunzi. Katika utunzi wa kawaida utungo huhesabiwa kuwa ni utenzi wakati ambapo beti zinavuka ishirini. Utenzi una mizani fupi na mara nyingi ni mizani nane nane katika kila mstari, ingawa kuna nyingine ambazo huwa na mizani nyingi au chache ya hapo.

Mstari wa utenzi huwa na kipande kimoja tofauti na mstari wa shairi ambao umegawanywa katika mistari miwili. Ubeti wa utenzi huwa na mistari minne. Kina cha mwisho katika mstari wowote wa mwisho wa ubeti hakibadiliki.

2. Lugha ya shairi ni ya mkato, nyoofu na yenye mvuto na mnato yaani tumbuizi kwa masikio. Shairi hutumia lugha ya picha na huwa na ulinganifu wa vina, mizani na kituo.

3. Utoaji wa ngonjera hutumia sana vitabia. Yaani wahusika hutumia mikono, macho, midomo na viungo vingine vya mwili. Hivyo penye kukonyeza, mhusika hukonyeza ili kusisitiza ujumbe. Hali kadhalika penye mshangao, mhusika huweza kutumbua macho na kuachama mdomo kama ishara ya kupigwa na bumbuwazi, n.k. Uhai wa igizo la ngonjera hutokana na sifa hii ya utumiaji wa vitabia.

4. Katika jamii ya Wanyarwanda hakuna utungo wa ngojera.

5. Tungo za utenzi huwa ndefu, yaani huwa ni beti nyingi kuliko shairi. Zaweza hata kuzidi mia tatu kufuatana na uzito wa maudhui na ubingwa wa mtunzi.

Page 36: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

30

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

3. Funzo: NGELI ZA MAJINA (42-70)

Shabaha

Kuwaongoza wanafunzi kujua matumizi ya ngeli tofauti za majina kwa njia ya kimofolojia katika sentensi.

Kuwawezesha wanafunzi kuorodhesha maneno yote yanayoweza kutumika katika ngeli mbalimbali za nomino na kuyatumia katika sentensi.

Kuwaongoza wanafunzi kuainisha ngeli za majina kwa njia ya kimofolojia.

Mifano:

Umoja Wingi

Mtoto huyu analia Watoto hawa wanalia

Mti huu unaanguka Miti hii inaanguka

Kisu kile kinakata Visu vile vinakata

Jino hili linauma Meno haya yanauma

Vifaa

Kadi zenye maneno yanayoonyesha ngeli tofauti, vitu halisi, ubao, chaki na michoro mbalimbali.

Taratibu

Utangulizi: Ili kuwachangamsha wanafunzi, mwalimu atawafunza methali nyepesi.

Mifano:

1. Fimbo ya mbali haiui nyoka

2. Maneno matamu humtoa nyoka tunduni

3. Cha mlevi huliwa na mgema

Page 37: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

31

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Hatua ya 1:

Mwalimu atawaongoza wanafunzi kwa kutaka kuwakumbusha umoja na wingi wa ngeli za majina.

Mifano:

Umoja Wingi

Duka lilifunguliwa Maduka yalifunguliwa

Wavu utakatika Nyavu zitakatika

Mkuki ule unarushwa Mikuki ile inarushwa

Ngeli za majina na upatanisho wa kisarufi

Ngeli Mifano (yakinishi) Mifano (kanushi)

I. A-WA Mtu huyu anakimbia Watu hawa wanakimbiaMbwa huyu anachokaMbwa hawa wanachoka

Mtu huyu hakimbiiWatu hawa hawakimbiiMbwa huyu hachokiMbwa hawachoki

II. U-I Mti huu unaanguka Miti hii inaanguka

Mti huu hauangukiMiti hii haianguki

III. KI-VI Kiti hiki kimekaliwa Chuma hicho kinakata Viti hivi hivi vimekaliwaVyuma hivyo vinakata

Kiti hiki hakijakaliwa Chma hicho hakikatiViti hivi havijakaliwaVyuma hivyo havikati

IV. LI-YA Jumba lile linafungwa Majumba yale yanafungwa

Jumba lile halifungwi Majumba yale hayafungwi

V. U- Werevu wake umemsaidia Werevu wake haujamsaidiaVI. U-I-ZI Wavu ule utakatika

Nyumba hii itajengwaNyavu zile zitakatika Nyumba hizi zitajengwa

Wavu ule hautakatika Nyumba hii haitajengwa Nyavu zile hazitakatika Nyumba hizi hazitajengwa

Page 38: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

32

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

VII. PA-M-KU- Hapa Gisenyi pana milima Chumbani mle mna kabati Msituni kule kuna Sokwe

Hapa Gisenyi hapana milimaChumbani mle hamna kabati Msituni kule hakuna Sokwe

VIII. KU- Kuimba kwake kunanifurahisha Kuimba kwake hakunifurahishi

1. Ngeli ya kwanza: A-WA

Inaitwa A-WA kwa sababu viambishi awali vya vitenzi vinavyofuata majina huanza na herufi “A-” katika umoja na “WA-” katika wingi.

2. Ngeli ya pili: U-I

Inaitwa U-I kwa sababu viambishi awali vya vitenzi vinavyofuata majina ya ngeli hii huanza na kiambishi “U-” katika umoja na “I-” katika wingi. Herufi U na I huitwa pia viambishi ngeli.

3. Ngeli ya tatu: KI-VI

Inaitwa KI-VI kwa sababu viambishi ngeli vyake ni KI- katika umoja na VI- katika wingi. Ngeli hii ina majina mengi sana. Majina yake hasa ni ya vitu.

4. Ngeli ya nne: LI-YA

Inaitwa LI-YA kwa sababu viambishi awali vya vitenzi vinavyofuata majina ya ngeli hii huanza na viambishi ngeli LI- katika umoja na YA- katika wingi.

5. Ngeli ya tano: U-

Karibu majina yote ya ngeli hii ya U- ni majina ya dhahania au majina ya maarifa. Kiambishi ngeli katika kitenzi ni U- umoja na wingi.

Ngeli Mifano (yakinishi) Mifano (kanushi)

Page 39: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

33

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

6. Ngeli ya sita: U-, I-ZI

Majina ya ngeli hii tunaweza kuyagawanya katika makundi mawili: yale yanayochukua viambishi ngeli U-ZI katika umoja na wingi, nay ale yanayochukua viambishi ngeli I-ZI

katika umoja na wingi.

7. Ngeli ya saba: PA-M-KU

Ngeli hii ina viambishi ngeli vitatu ambavyo hutumika kuonyesha mahali. Navyo ni PA-M-KU. Mahali pengine paweza kujulikana kwa ujumla tu (KU-) au waziwazi (PA-) pia huwa ndani ya kitu (M-).

8. Ngeli ya nane: KU-

Ngeli hii imeundwa na majina ambayo yenyewe ni vitenzi. Umbo lake ni lile la vitenzi katika nia isiyotajwa. Majina ya ngeli hiihuitwa vitenzi-majina.

Hatua ya 2:

Wanafunzi kusoma sentensi kutoka vitabuni na kutaja ngeli za maneno yanayotumika katika sentensi hizo.

Wanafunzi kutumia vitenzi-jina kutunga sentensi sahihi.

Hatua ya 3:

Wanafunzi watasoma sentensi baada ya mwalimu kuziandika.

Wanafunzi kujaribu kutoa mifano yao. Mwalimu kusahihisha, kuhimiza na kusaidia.

Hatua ya 4:

Wanafunzi kufanya zoezi walilopewa na mwalimu.

Page 40: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

34

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Majibu:

Mazoezi 1

1. a) Wakulima hawa wanalima vizuri.

b) Watoto wake hawana maringo.

c) Wanawake hawa ni wanene.

d) Mbwa wao ni wakali.

e) Madaktari wao wamefika.

2. a) Mtu huyu anakwenda wapi?

b) Mbwa wake alikufa jana.

c) Dereva huyu ana wazimu.

d) Ambia watoto wale waje hapa.

e) Kijana yule anatembea vizuri.

f) Nyuki walipoingia nyumbani, walikula watu wote.

g) Mwizi Yule amekimbia.

h) Punda anakimbia.

i) Nyani huyu ni mkubwa sana.

Mazoezi 2:

1. a) Mgu, b) Mikono, c) Miswaki, d) Mpira, e) Mshumaa, f) Michuzi, g) Mkebe, h) Mfagiaji.

2. a) mmoja, b) wa, c) huo, d) ile, e) ule.

Mazoezi 3:

1. a) vibiriti, b) vioo, c) chandarua, d) vyeo, e) viwanja, f) viboko, g) kisiwa.

2. a) Vitambaa vipya vinavutia.

Page 41: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

35

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

b) Viko vyake viko mezani.

c) Hatutaki kununua vitu vyovyote.

d) Vyandarua vile vikubwa vinafaa kufunikia vitanda.

e) Vyombo vyote vimejaa viazi.

f) Visu vikali hivi vinafaa kukatia vipande vya nyama.

g) Vikombe ambavyo vinavuja vimezibwa.

h) Vitanda vyenyewe hivi ni vibaya.

i) Vyovyote vile vinafaa kwa kazi hizi.

3. a) changu, b) kile, c) chake, d) vingi, e) chote.

4. a) Chungu kilichovunjika ni chetu.

b) Chuma kile kipelekwe pale.

c) Chumba chao cha kulia ni kichafu.

d) Chakula chote kimeharibika.

e) Mtoto wake alivunja kikombe chao.

f) Kisu chao kilipotea kesho.

g) Kibuyu ambacho kimenunuliwa kimeibiwa.

h) Nipe kijiko change.

i) Wapi unapeleka kiko hicho?

Zoezi 4:

1. a) Machungwa yale hayajaoza.

b) Sisi shatutaki majembe yale.

c) Mlinunua majumba makubwa.

d) Meno yake yanauma vibaya.

Page 42: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

36

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

e) Mashamba ambayo yamelimwa yatapandwa.

f) Magunia yale yametoboka.

g) Magoti ambayo yalijeruhiwa yamepona.

h) Majina ambayoyaliandikwa yamefutwa.

i) Mashauri haya hayakukubaliwa na wakubwa.

2. a) Maziwa haya yako na uchafu.

b) Alinipiga na jiwe lile.

c) Sitaki kununua machungwa yale na mapera haya.

d) Gari hili limebeba watu wengi sana.

e) Yeye ako karibu na jingo lile.

f) Yai analotaka kununua ni kubwa.

g) Magoti ambayo yana vidonda yamefungwa vitambaa.

h) Shoka linatiwa mpini mpya.

i) Duka lenyewe limejaa bidhaa.

j) Shamba lenye miti mingi limeuzwa.

Mazoezi 5:

1. a) zilitufikia, b) imeraruka, c) nzuri, d) zimevunjika, e) zimeiva, f) hazipitiki, g) hazijasikilizwa, h) ilijengwa, i) haijavuja.

2. a) Ulimi uliokuwa na kidonda imetibiwa.

b) Karai iliyotoboka imezibwa.

c) Wavu ambao umechanika haujatengenezwa.

d) Kamba ambayo hutengenezwa ni ngumu.

Page 43: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

37

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

e) Utambi ambao amenunua ni mweupe.

f) Wakati huu si wakucheza.

g) Kwa nini hutaki kuniletea sabuni yangu?

h) Ajali ilitokea, msafiri mmoja aliharibika uso.

i) Nguo iliyoanikwa haijakauka.

j) Nyama hii haiwezi kuliwa na kibogoyo.

k) Ulimi mwekundu.

l) Nyundo yake.

m) Ndege yote.

n) Shida hii.

o) Kazi ni ngumu.

p) Ufa ule ni mpana.

3. a) Kuta hizi zina nyufa nyingi sana.

b) Nenda pale upewe upanga mmoja.

c) Nywele zake kwisha kuwa ndefu.

d) Ukucha ule umeng’olewa.

e) Ndevu zake hunyolewa kila siku.

f) Mwambie kuwa mtakuja upande huu.

g) Uji ambao tulipewa ulikuwa mtamu.

h) Taa ambazo tunawasha usiku hazioni vizuri.

i) Karatasi ambazo tumenunua ni nzuri.

j) Ua ambalo litachanua litakatwa.

Page 44: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

38

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Mazoezi 6:

1. a) matamu, b) mweusi, c) mbaya, d) cheusi, e) kingine, f) kile kina, g) hautapona, h) nyekundu, i) kizuri, j) mkubwa, k) mirefu, l) pake mmechafuka, m) vingapi, n) vikuukuu si vipya, o) kimeingia mguuni mwake, p) hakina, r) aliibiwa vifaa vyake, s) nzuri, t) yake, u) mdogo wake.

Zoezi 7:

1. - Kuchoka kulimsababisha kushindwa mtihani wa shule.

- Kufuta kunaleta vumbi darasani.

- Kula kunafanya mtu awe na nguvu za kutosha.

2. Kutokauka, kutoadhibu, kutokunywa, kutokufa, kutolima, kutopiga, kutokula, kutoacha, kutofufuka, kutosisitiza.

3. a) Kucheza kwa mpira tunakoendea uwanjani kunavutia watazamaji.

b) Kuchelewa mwanafunzi huyu anakofanya, kunarudisha maendeleo yake nyuma.

c) Kusoma anakofanya kila siku kutamletea matunda mazuri.

d) Kulima kunakofanywa katika shamba hili kutakuza mimea upesi.

e) Kukimbia anakofanya ni hatari kwake.

4. Funzo: USEMI WA ASILI NA USEMI WA TAARIFA (71-73)

Shabaha:

Kuwawezesha wanafunzi kubadili sentensi kutoka usemi wa asili hadi usemi wataarifa.

Kuwaongoza wanafunzi kutofautisha sentensi za usemi wa asili na sentensi za usemi wa taarifa.

Page 45: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

39

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Vifaa:

Vitabu (cha mwanafunzi na cha mwalimu), vitu halisi, ubao, chaki za rangi, n.k.

Taratibu

Utangulizi: Ili kuwachangamsha wanafunzi, mwanafunzi atoe hadithi fupi (dakika 3).

Hatua ya 1:

Mwalimu atatoa maana ya usemi wa asili na usemi wa taarifa.

Maana ya Usemi wa asili

Usemi wa asili ni yale maneno yanayotamkwa na mtu yakiwa katika hali yake ya kwanza.

Maana ya Usemi wa taarifa

Iwapo mtu anataka kuwaambia wengine maneno ambayo yalizungumzwa na mtu mwingine bila ya kupotosha, kupunguza au kuongeza maana ya jambo analotaka kulitolea maelezo, basi maneno hayo anayosema huitwa usemi wa taarifa.

Katika usemi wa taarifa kuna mambo muhimu ya kuzingatiwa ili usemi huo wa taarifa uwe sahihi.

1. Nafsi ya kwanza hubadilika na kuwa katika nafsi ya tatu.

Mifano:

Mimi hugeuka yeye

Sisi hugeuka wao

2. Badala ya kutumika wakati uliopo –na-, wakati uliopita –li- ndio hutumika.

Kwa mfano.

Nina kazi nyingi ofisini. (Hugeuka)

Page 46: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

40

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Alisema kwamba alikuwa na kazi nyingi ofisini.

3. Alama za kufunga na kufungua maneno (“”) hazitumiki katika usemi wa taarifa.

4. Alama za kuuliza (?) na za kushangaa (!) hazitumiki kwenye usemi wa taarifa.

5. Katika kuandika usemi wa taarifa mahali penye wakati ujao -ta- kwenye usemi wa asili hugeuka na kuwa -nge-.

6. Baadhi ya maneno hubadilisha umbo yanapotumika katika msemo wa taarifa.

Kwa mfano.

- hapa huwa hapo

- leo jioni huwa siku hiyo jioni

- wakati huu hugeuka wakati huo

- watu hawa huwa watu hao

- kwetu hugeuka kwao

- kwangu hugeuka kwake

- sasa huwa wakati huo

7. Mojawapo ya maneno yafuatayo hutumika katika usemi wa taarifa: kuwa, kama, kwamba.

Baada ya kuona haya yote mwalimu atawaongoza wanafunzi kwa kuwataka kutoa sentensi tofauti kwa kutumia vitenzi mbalimbali.

Mifano:

- “Utanikuta nyumbani nikikusubiri”. Bora alimwambia rafiki yake.

- “Mtoto usilie nitakuletea mkate”. Mama alimjulisha mtoto wake.

- “Ukifika utanijulisha”. Tajiri alimweleza mtumishi wake.

Page 47: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

41

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Hatua ya 2:

Wanafunzi kusoma na kuelewa sentensi zilizoandikwa ubaoni. Mwalimu atawataka wanafunzi kusoma sentensi zote na kuonyesha namna zinavyoundwa moja baada ya nyingine. Atawataka wanafunzi kuelewa maana na kuwasaidia wasipoelewa.

Hatua ya 3:

Wanafunzi watasoma sentensi hizo na kuonyesha vipande vyake.

Wanafunzi kujaribu kutoa mifano yao na kuibadilisha kutoka usemi wa asili hadi usemi wa taarifa au kutoka usemi wa taarifa hadi usemi wa asili.

Mwalimu kusahihisha, kuhimiza na kusaidia.

Page 48: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

42

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

5. Funzo: UTUNGAJI (74-77)

Shabaha

- Kuwasaidia wanafunzi kufafanua, kutunga insha za wasifu kulingana na jinsi atakavyoulizwa na mwalimu.

- Kuwaongoza wanafunzi kutilia mkazo uchaguzi wa maneno bora na matokeo yake kwenye matumizi.

- Kuwawezesha wanafunzi kutunga hotuba fupi fupi kwa ajili ya kukuza vipaji vya kujieleza na kujiamini.

- Kuwaongoza wanafunzi kujua na kutumia baadhi ya msamiati utumiwao katika utungaji rasmi.

Mifano: Utangulizi, Mwili na Hitimisho.

- Kuwawezesha wanafunzi kujua namna ya kusoma na kuunda habari kwa kutumia maneno ipasavyo katika utungo wowote.

Vifaa

Vitabu vya hadithi fupi na daftari.

Taratibu

Utangulizi: Mwanafunzi atoe hadithi fupi kwa kuwaburudisha na kuwachangamsha wengine.

Hatua ya 1:

Mwalimu kutoa maelezo kuhusu dhana mbalimbali za utungaji wa insha pamoja na kutaja aina za insha.

Page 49: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

43

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Insha ni mtungo wa maneno kwa mtindo wa nathari juu ya jambo fulani. Insha ni maelezo ya mawazo au habari kuhusu jambo fulani linalokusudiwa kwa mtindo wa maandishi ya nathari.

Aina za insha

Insha kwa kawaida huwa ni za aina nyingi kutokana na namna zinavyotungwa. Aina hizo ni hizi zifuatazo:

- Insha za maelezo (Insha za wasifu)

- Insha za masimulizi

- Midahalo na mijadala

- Insha za mazungumzo

- Insha yakinifu

Hatua ya 2

Mwalimu awaulize wanafunzi maswali juu msamia unaotumiwa katika utungaji.

Mifano:

a) Kwa maoni yenu, “Utangulizi” kama kipengele mojawapo ya sehemu za utungaji ni nini?

b) Mwili wa utungaji unapatikana sehemu gani?

c) Hitimisho ina kazi gani katika kazi ya utungaji?

Hatua ya 3:

Mwanafunzi inampasa asome swali kwa makini sana na ahakikishe kuwa amelielewa swali na swali lile limemwelea. Kisha atie akili yake juu ya swali na ajiulize kichwani mwake: Mada ya swali inahusu nini? Na swali linanihitaji nifanye nini?

Tafakari kuhusu mada ya swali humwezesha mwanafunzi kufahamu na kuamua wazo lipi la maana la kuandikwa na lipi lisilofaa la kuachwa.

Page 50: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

44

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Hatua ya 4:

Mwalimu atatoa maoni yake na kuwaelekeza wanafunzi kwa kuonyesha yanayohitajika katika utungaji.

Mwanafunzi asidiriki kujibu swali ovyo bila ya matayarisho. Akishafahamu maana na mahitaji ya swali, atumie muda wa kama dakika tano hivi kuandaa vidokezi vyake vya hoja na aviandike pembeni mwa karatasi, kwa mpango mzuri. Kwa kupanga vidokezi vya hoja zake kwa uangalifu kabla ya kutunga insha, mwanafunzi:

• Huepukana na uwezekano wa kurudiarudia mawazo;

• Huandika insha iliyo na mtiririko mzuri wa mawazo;

• Huweza kuhakikisha kuwa ametimiza idadi itakikanayo ya hoja.

Iwapo ameridhishwa na vidokezi vyake vya hoja, anaweza kuanza kuandika jawabu lake. Lakini kabla ya kuanza kutunga insha yake, ni muhimu sana aandike nambari ya swali aliloamua kujibu kama ilivyo kwenye karatasi ya maswali.

Hatua ya 5:

Wanafunzi kufanya zoezi kwa kujaribu kufuata mambo yanayopaswa kutiliwa maanani katika utungaji wa insha, na vigezo vinavyozingatiwa katika usahihishaji. Kama vile: kichwa cha insha, utangulizi, maudhui (mawazo makuu), hitimisho, urefu wa insha, msamiati, mtindo, sarufi, n.k.

Page 51: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

45

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

6. Funzo: AINA ZA MANENO YA KISWAHILI (78-86)

Shabaha:

Kuwaongoza wanafunzi kutoa na kuelewa maana ya nomino kama mojawapo wa aina za maneno.

Kuwawezesha wanafunzi kutaja aina za maneno na mifano mbalimbali kwa kila aina ya maneno.

Kuwawezesha wanafunzi kujua matamshi ya aina mbalimbali za maneno ipasavyo na kuyatumia katika sentensi kwa usahihi.

Mifano: mbwa, jamaa, ghali, nzuri, nyinyi, wao, hitilafiana, nuia, hatarisha, mno, haraka, bila labda, pasipo, oyee, ala, afanaaleh, n.k.

Matayarisho/Vifaa:

Vifaa halisi, picha na michoro.

Taratibu

Utangulizi: Ili kuwachangamsha wanafunzi, mwalimu atawatolea hadithi fupi yenye kujaa maneno ya vicheko pamoja na mzaa.

Hatua ya 1:

Kwa kutumia vifaa halisi, picha au michoro, mwalimu atawataka wanafunzi wataje wanavyoviona kati ya vile walivyoonyeshwa. Wanapotaja jina, mwalimu ataliandika juu ya ubao na kuwataka wanafunzi walisome jina hilo na kujaribu kugundua aina ya neno hilo wanalolisoma.

Aina za maneno zipatikanazo katika lugha ya Kiswahili ni hizi zifuatazo: nomino/majina, vivumishi, viwakilishi, vitenzi, vielezi, vihusishi/viunganishi, vihisishi/viingizi.

Page 52: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

46

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Hatua ya 2:

Mwalimu atafundisha majina yale ambayo wanafunzi hawayajui na kuyaandika ubaoni. Wanafunzi watasoma mmoja mmoja, na kwa vikundi.

Hatua ya 3:

Wanafunzi kuulizana majina na kutaja maneno maalumu yanayotumiwa katika mazungumzo ya kila siku ili kuhakikisha msamiati umejulikana kutokana na aina yake.

Hatua ya 4:

Wanafunzi kuuliza maswali kuhusu somo lenyewe na kufanya mazoezi kwa kusaidiwa na mwalimu.

Majibu

Mazoezi 1

a) Majina ya mguso (mbuzi, ng’ombe, simba)

b) Majina ya kawaida (mtu, mkulima)

c) Majiana ya dhahania (uvuvi, ufugaji, usomi)

d) Majina ya jamii (familia, jamaa)

e) Majina pekee (malaria, UKIMWI, kaswende)

Mazoezi 2

1. Kivumishi ni neno linaloongezea jina maana. Isitoshe, kivumishi ama sifa huweza pia kujiongezea maana.

2. Vivumishi vinaweza kugawika katika migawo miwili tofauti.

Kwanza, upo mgawo ambapo kuna vivumishi vichukuavyo viambishi na vipo vile ambavyo havichukui viambishi.

Page 53: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

47

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

Mazoezi 3

1. Viwakilishi huitwa pia vijina au vibadala. Navyo ni maneno ambayo husimama badala ya majina ili kujulisha kitu kinachohusika. Maneno haya yanapotumika, jina la kitu kinachosimamiwa halitajwi.

2. Sentensi tano zinazoonyesha viwakilishi viulizi (yupi, zipi, yapi, wepi, upi, kupi, ipi, lipi, papi, n.k.).

3. Kuna viwakilishi nafsi sita katika lugha ya Kiswahili ambavyo ni Mimi, Wewe, Yeye, Sisi, Nyinyi, Wao.

4. a) Lile = kiwakilishi onyeshi.

Wapi?= kiwakilishi kiulizi

b) Wangu= kiwakilishi kimilikishi

Mimi= kiwakilishi nafsi

c) Wale= kiwakilishi onyeshi

d) Ambao= kiwakilishi kibainishi

Mazoezi 4

1. Kielezi ni neno linaloongezea kitenzi maana. Pia huweza kuongezea sifa maana na pia kujiongezea maana. Matumizi haya matatu yote ni muhimu katika sarufi ya Kiswahili.

2. a) Anakunywa haraka haraka (vielezi vya namna)

b) Hamisi amecheza vibaya mchezo huu (kielezi cha namna)

c) Usimwamshe, amechoka sana (kielezi cha namna).

3. a) Vielezi vya wakati

b) Vielezi vya kiasi au idadi

Page 54: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

48

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Mazoezi 5

1. Vihusishi, viunganishi ama vihusiano ni maneno ambayo huunganisha maneno mengine mawili ama zaidi.

2. Kutunga sentensi nne ambazo huonyesha viunganishi.

3. a) Walimu hodari hutayarisha somo japo wazembe.

b) Ni vizuri kuongea Kiingereza au Kifaransa.

c) Alifanya kazi kwa bidii akapata manufaa.

d) Mwanafunzi yule hapendi chakula wala kinywaji.

e) Yeye alipata alama nzuri katika mtihani wa taifa.

f) Msichana mpole anatembea kama Malaika.

MAREJEO

- Chiraghdin, S. na Mnyampala, E.M. (1977). Historia ya Kiswhili. Nairobi. OUP.

- Cooperative TRAFIPRO (1982). Tujifunze Kiswahili. Kigali.

- Direction des Programmes de l’Enseignement Secondaire (1986). Kitabu cha

Kiswahili IV-V A.

- Salimu, K.B. na Islam, K.I. (1996). Kiswahili Sanifu Darasa la Tatu: Mwongozo

wa Mwalimu. Oxford University Press. Nairobi.

- Kihore, Y.M, Massamba, D.P.B., Msanjila, Y.P. (2008). Sarufi Maumbo ya Kiswahili

Sanifu. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Dar es Salaam.

- Massamba, D.P.B. (2002). Historia ya Kiswahili. Oxford University Press. Nairobi.

- Mazrui, A.M. na Syambo, B.K. (1992). Uchambuzi wa Fasihi. East African Educational Publishers Ltd. Nairobi.

- Mbunda Msokile (1993). Msingi ya uhakiki wa Fasihi. East African Educational Publishers Ltd. Nairobi.

Page 55: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

KISWAHILI - S4 (Teacher Guide)

49

MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA

- Mohamed, A.M. (1986). Sarufi Mpya. Press and Publicity Centre. Dar es Salaam.

- NDALU, A. (1997). Mwangaza wa Kiswahili. East African Educational Publishers. Nairobi-Kampala.

- Nkwera, F.M. (1978). Sarufi na Fasihi, Sekondari na Vyuo. DRM, TPH.

- Polycarp S. Wekesa (2000). Uandishi wa Insha. Acacia Stantex Publishers Muthithi House, Westlands. Nairobi.

- Rocha, C. (2005). Kiswahili: Past, Present and Future Horizons. Nairobi.

- Rwabushaija, M. (1999). Masomo ya Msingi wa Kiswahili. Fountain Publishers Ltd, Kampala.

- Taasisi ya Mafunzo ya Sekondari (1987). Kitabu cha Kiswahili IV B. Wizara ya Mafunzo ya Msingi na Sekondari. Kigali.

- Taasisi ya Mafunzo ya Sekondari (1987). Kitabu cha Kiswahili IV-VA. Wizara ya Mafunzo ya Msingi na Sekondari. Kigali.

- TUKI (2002). Fasihi Simulizi: Vitendawili. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Dar es Salaam

- Wamitila, K.W. (2001). Kamusi ya Methali. Nairobi: Longhorn Publishers Ltd.

COVER

Kitabu hiki kimetayarishwa kwa ajili ya mwalimu wa shule za upili kidato cha nne. Kwa kawaida kinaundwa na sura mbalimbali ambazo zinazungumzia dhamira kutokana na uwezo wa mwanafunzi ambazo humfanya mwanafunzi kusoma, kuelewa na kuandika bila wasiwasi.

Humpa mwanafunzi na mwalimu msamiati atakaoutumia katika maisha ya kila siku na namna ya kuongea kwa ufasaha na wengine. Ndani mwake kuna majibu ya mazoezi yaliyotolewa katika kitabu cha mwanafunzi ambayo yanamwezesha mwalimu kuongoza somo lake vyema.

Page 56: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI - tanprints.com S4 (Teacher... · KISWAHILI - S4 (Teacher Guide) iii MWONGOZO WA MWALIMU KIDATO CHA DARASA LA NNE MKONDO WA LUGHA UTANGULIZI Mwongozo

50

KISWAHILI: SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI

Kitabu hiki humfanya mwalimu kutawala somo lake kupitia njia ya kusoma, kuandika na kuwashirikisha wanafunzi kufanya kazi kwa makundi.

Kitabu hiki ambacho ni “Mwongozo wa mwalimu” kinaundwa na mambo yafuatayo:

- Kina mpangilio wa masomo ya Kiswahili ambayo humwongoza mwalimu namna ya kufundisha masomo yake katika mihula mitatu ambayo inaunda mwaka wa masomo.

- Kina shabaha tofauti ambazo huonyesha namna kila funzo linapaswa kufunzwa kwa ajili ya kufikia lengo fulani linalopendekezwa katika mhutasari wa somo la Kiswahili kidato cha nne (4).

- Kina metodolojia tofauti za kutumia katika ufundishaji ambazo humtia mwanafunzi motisha ya kuendesha vizuri masomo yake na ambazo humfanya kuchangia katika somo pamoja na mwalimu.

- Kina majibu ya baadhi ya maswali yaliyoulizwa katika kitabu cha mwanafunzi.


Recommended