Somo la 6 kwa ajili ya Agasti 8, 2020
Yesu hakutuamuru kuihubiri tu injili kwa ulimwengu, lakini pia alitupatia karama zinazotuwezesha kutimizautume huo.
Karama za roho zina ubora wa kiungu na zimetolewa naRoho Mtakatifu ili kuujenga mwili wa Kristo nakuwawezesha waaumini kuwa mashahidi bora kwaulimwengu.
“Lakini sasa viungo ni vingi, lakini mwili ni mmoja.” (1 Wakorintho 12:20)
Paulo aliwalinganisha washiriki wa Kanisa na mwili wamwanadamu. Katika mlinganisho huu, Kanisa ndilo mwili waKristo (1Kor. 12:12-27).
Kama hivi, kila mshiriki wa Kanisa ni wa pekee na ana karama zake za pekee. Kila kiungo cha mwili kina jukumu, na hakuna mshiriki wa Kanisa asiye nakarama.
Mikono, macho, na mapafu vina utofauti sana. Kila mshiriki ana tabiana kazi za pekee.
Wote wamepewa angalau karama moja ya roho. Inatupasa kufanya kazi pamoja kuzitumiakarama hizo kuushiriki upendo na ukweli waKristo kwa ulimwengu wote.
Hakuna washiriki wa kutolewa au wasio na kazi. Wale wanaohubiri kwenye mikutano wanathamani sawa na wale wanaoomba kimyakimya.
“Ni kwa maagizo ya Bwana kwamba
watumishi wake wawe na karama
tofauti. Ni kwa uteuzi wake kuwa
wanadamu wenye akili tofauti
wameletwa kanisani, ili kuwa
watendakazi pamoja Naye. Tuna mawazo
mengi sana na yaliyo tofauti ya kukutana
nayo, na karama nyingi zinahitajiwa.
Watendakazi wa Mungu wanapaswa
kufanya kazi kwa maelewano thabiti.”
E.G.W. (This Day With God, September 10)
“Lakini kazi hizo zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.”(1Wakorintho 12:11)
Biblia inaeleza kuwa kila karama iliyobora hutoka kwa Mungu. Roho Mtakatifuhuwapatia kama apendavyo Yeye(Yakobo 1:17).
Kwanini tusijichagulie karama zetu?
Kwasababu tuna ufahamu kidogo sanajuu ya jinsi ya kuutimiza utumetuliopewa.
Pale tunaposalimisha mioyo yetu kwaYesu, Mungu hutupatia karama zilizobora Zaidi, ili zitumiwe vyema kulifanyaKanisa likue.
Kwa nyongeza katika karama maalumu, Mungu pia ametupatia kazi maalumutuzifanye kwa kushirikiana na wengine.
“Kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya hudumaitendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe.” (Waefeso 4:12)
Zipo orodha za karama zilizotolewa kwa wauminiwa kwanza katika Warumi 12:6-8, 1 Wakorintho12:8-10, 28-30 na Waefeso 4:11.
Zipo karama nyingi Zaidi ukilinganisha na za haowa kwanza, kama kuhariri picha na video, kuendesha ndege, kusimamia mitandao yakijamii… Lengo lao ni kumwezesha kila
muumini kutimiza kazi yaokatika ukuaji na kulilisha Kanisa, ili tuhubiri na kuuhudumiaulimwengu.
Karama za roho siyo talanta za asili. Japokuwa, Roho Mtakatifuanaweza kutakasa talanta za asili na kuziweka katika hudumaya Kristo (zinakuwa karama za roho).
“Wanadamu wote hawapokei karama
zilizo sawa, lakini kwa kila mtumishi
wa Bwana karama fulani ya Roho
imeahidiwa. […] Ikiwa
wameunganishwa na Kristo, ikiwa
karama za roho ni zao, walio
masikini na wasiojua kabisa kati ya
wanafunzi Wake watakuwa na nguvu
itakayoongea na mioyo. Mungu
huwafanya kuwa mfereji wa
kutekeleza jukumu la juu kabisa
katika ulimwengu.”E.G.W. (The Faith I Live By, October 13)
“Hata hamkupungukiwa na karama yo yote, mkikutazamia sana kufunuliwa kwake Bwana wetu
Yesu Kristo […]” (1 Wakorintho 1:7)
Wote tumepokea karama… ni ipi uliyonayo?
Namna nzuri ya kuzipata ni “kuzifanyia kazi”. Anza kufanyakazi ya huduma katika kanisa lako mahalia. Kwa njia hiyoutajua ikiwa una karama sahihi kwa kazi hiyo au la. Hebu tujaribu kueleza baadhi ya dhana:
Karama
HudumaKazi
Karama: Ujuzimaalumu (k.m. kufundisha kwaurahisi)
Huduma: Maeneomakuu ya huduma(k.m. ShuleSabato)
Shughuli: Matukiomalumu (k.m. kuongoza darasa la Shule Sabato)
Ikiwa unaijua karama yako tayari, utapata huduma au kazisahihi kwa urahisi.
Ukijihisi vizuri katika huduma maalumu, utaweza kugunduakarama zako katika eneo hilo na kazi zilizo nzuri kwa ajili yakrama zako.
Ukiifanya kazi Fulani vizuri, utazijua karama zako na hudumasahihi kwa ajili yako unapokuwa katika kazi hiyo.
“Kwa maana kila mwenye kitu atapewa, nakuongezewa tele; lakini asiye na kitu hatakile alichonacho atanyang’anywa.” (Mathayo
25:29)
Katika kisa cha talanta, Yesu anaeleza kuwa kilammoja anapokea karama, lakini baadhi yawatu wanapokea zaidi ya wengine(Mathayo 25:14-30).
Japokuwa, huo ni mwanzo tu. Tunaweza“kushauriana” na karama zetu za awali.
Zitakuwa kadri tunavyozitumia, na tutapokeakarama mpya. Tuwe makini, kwa kuwatunaweza kuzipoteza karama zetu kamahatutazitumia.
Mwombe Mungu akuonyeshe ni karama ganiAlizokupatia na namna ya kuzitumia. Haijalishini karama kiasi gani ulizopewa, lakini ni namnagani unazitumia.
“Kwa watumishi Wake Kristo ametoa
‘wema Wake’— jambo ililowekwa ili
walitumie kwa ajili Yake. Anampatia
‘kila mtu kazi yake.’ Kila mmoja ana
nafasi yake mbinguni katika mpango
wa uzima. Kila mmoja anapaswa
kufanya kazi kwa kushirikiana na
Kristo kwa ajili ya wokovu wa roho.
Kwa hakika hakuna sehemu Zaidi
zilizoandaliwa kwa ajili yetu katika
makazi ya mbinguni Zaidi ya sehemu
maalumu zilizojengwa duniani
mahali tunapofanya kazi ya Mungu.”E.G.W. (Christ’s Object Lessons, cp. 25, p. 326)