View
22
Download
0
Category
Preview:
Citation preview
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 1
MADA YA 1 UUNDAJI WA MANENO
Uundaji wa maneno ni ujenzi au uzalishaji au utengenezaji wa maneno mapya.
Uundaji wa maneno mapya husaidia kuongeza msamiati katika lugha ili kukidhi
mahitaji ya mawasiliano. Uundaji wa maneno mapya husababishwa na mabadiliko
ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na maendeleo ya kisayansi yanayotokea
katika jamii. Kwa mfano tunayo maneno mapya, kama vile ufisadi, uwekezaji,
ukeketaji, ujasiriamali na mengine mengi kutokana na mabadiliko ya kijamii.
Kutumia Uambishaji
Kubainisha Mofimu katika Maneno
Uambishaji wa maneno ni kitendo cha kupata maneno kwa kubandika Mofimu
kwenye kiini cha neno, uambishaji kutokea kabla ya kiini cha neno au mzizi wa
neno. Mfano kiini pig- unaweza kuunda maneno kama inapiga, anayepiga, mpigaji,
amepigika nk.
MOFIMU
Fasili ya mofimu ni: Mofimu ni neno au sehemu ya neno yenye maana kisarufi,
ambayo haiwezi kugawanyika zaidi bila kupoteza maana. Kwa mfano:
maneno
(a) babu, hewa
mofimu
kila neno lina Mofimu moja
AINA ZA MOFIMU
1. Mofimu huru
2. Mofimu tegemezi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 2
MOFIMU HURU
Haya ni maneno kamili ambayo huwezi kugawa zaidi bila kupoteza maana.
Mfano:Baridi, kofia, hewa, kaka, mama, sana, maji. Maneno haya hayawezi
kugawanyika zaidi na yakaendelea kuwa na maana hiyohiyo kisarufi.
MOFIMU TEGEMEZI
Ni vipande vidogovidogo vya maneno vyenye maana kisarufi. Mofimu hii maneno
yamejengwa kwa kubandika vipashio kadhaa vya kisarufi ambavyo huweza
kubadilishwa na maana ya neno ikabadilika.
Mfano: neno anapika lina mfano tegemezi ufuatazo
a -na- -pik- -a
1 2 kiini 3
Mofimu zinazobadilika kwenye kiini cha neno huitwa Viambishi.
Katika lugha ya Kiswahili viambishi hutokea kabla na baada ya kiini cha neno.
Mfano
Wanapendana = Wa-na-pendan-a kiini cha neno ni-pend-.
Mofimu zilizobadilisha baada ya kiini –an-na-a viambishi vinavyotokea kabla ya
kiini cha neno huitwa viambisha awali au tangulizi. Viambisha vinavyotokea baada
ya kiini cha neno huitwa viambishi tamati au fuatishi.
Mfano 1
Angalia mifano ifuatayo:
Neno Viambisha Awali Kiini Viambisha Tamati
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 3
Unapendelea u-na- -penda- el-e-a
Waliongozana wa-li- -ongoz- an-a
Analima a-na- -lim- -a
anayeiimbisha a-na-ye -imb- -ish-a
Test Yourself
Dhima za Mofimu
Baadhi ya dhima za uambishaji ni kama ifuatavyo:
1. Kuonyesha upatanisho wa usanifu maana ya maneno yanayozalishwa
kutofautiana katika msingi wa kusanifu tu, lakini uhusiano wa maneno hayo
hutokana na kiini au mzizi wake uleule.Mfano;Fundisha kiini chake ni fund.
Unaweza kuzalisha maneno mengine kwa kutumia mzizi/kiini kilichopo
kama vile fundishana, mafundisho, mfundishaji, fundishwa, fundishana.
2. Uambishaji huonyesha nafsi
3. Uambashaji huonyesha njeo (muda)
4. Uambishaji huonyesha urejeshi
5. Uambishaji huonyesha ukanushi
6. Uambishaji huonyesha hali mbalimbali za kitenzi
Vitenzi vikiambishwa huweza kujenga/kuunda/kuzalisha vitenzi vingine au
nomino.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 4
Mfano 2
Vitenzi Kiini Nomino Vitenzi
Cheza -
chez-
Mchezaji,
mchezo wanacheza/atamchezea
Piga -pig- Mpigaji,
Mpiganaji
watanipiga,
aliyempiga/wanaompiga
Uambishaji hutumika kuzalisha viwakilishi na vielezi.
Neno (Kiwakilishi) Kiini Kielezi
Huyu, Huyo Hu Humu, humo
Wangu, wako, wake wa
Hii, hizo, hiki hi
Viambishi awali vina dhima ya kudokeza nafsi, njia, idadi urejeshi na
ukanushi.Mfano: Hawakulima
Ha-, kiambishi cha ukanushi
Ku-, kiambishi njeo/wakati
Viambishi tamati vina dhima mbalimbali hudokeza hali ya utendekaji, ukamilishaji
au kimalizio cha neno na kauli za matendo kama vile kutendwa,
kutendewa,kutendeka nk.
Dhima:Ukanusho, kutendeana, agizo na mtendwa, ukamilisho, usababishi.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 5
Mfano 3
Neno Viambishi Tamati
Anapiga -a
Wanapigana -an
Asipigwe -w
Amempigisha -ish-
Viambishi tamati vina dhima ya kutambulishwa mapema/nomino zilizoundwa
kutokana na vitenzi.
Neno Kiini Viambishi Tamati
Piga pig- -o
Mchezo chez- -o
Mtembezi tembe- -z-i
Mfiwa -fi- -us-a
ZOEZI
Katika neno “analima”, mofimu {-a-}, {-na-}, {-lim-} zina dhima gani kwa
pamoja?
A Kileksika
B Uyakinishi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 6
C Kisarufi
D Ukanushi
___ni kazi ya mofimu {mi-} katika nomino „miji‟.
A Kuonesha njeo
B Kuonesha wingi
C Kuonesha urejeshi
D Kuonesha nafsi
Katika neno „aliyebarikiwa‟, mofimu {-ye-} ina kazi ya___
A Kuonesha hali
B Ukanushi
C Uyakinishi
D Urejeshi
Mofimu {-hu-} katika neno „hucheza‟ ina dhima ya kuonesha hali ya___
A Kuendelea
B Mazoea
C Masharti
D Utimilifu
Katika kitenzi „analima‟, mofimu {-na-} ina dhima ngapi?
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 7
A Tano
B Mbili
C Tatu
D Nne
Kutumia Mnyumbuliko
Mazingira yanayosababisha Mahitaji ya Maneno Mapya
Mnyumbulisho ni neno linalotokana na neno nyumbua. Kunyumbua kitu ni kuvuta,
kuongeza urefu wa kitu hicho.
Kunyumbua katika lugha ya Kiswahili ni kuongeza vinyumbulishi katika katika
kiini ili kupata msamiati mpya. Hivyo basi, mnyumbulisho ni njia mojawapo na
inasaidia kuunda maneno kwa njia ya kunyumbulisha.
Viambishi vinapochukuliwa katika kiini cha neno, basi neno hilo huwa
limenyumbulishwa. Kwa mfano neno lima kiini chake lim- huweza
kunyumbulishwa na kupata maneno mengine mpya, kama lim-ishwa, lim-ia, lim-
w-a.
Pia maneno ya mnyumbulisho yanaweza kuundwa kwa kuongeza viambishi
kwenye shina, kwa mfano:
Neno Kiini Shina Maneno ya Mnyumbuliko
Elekea elek eleka Elekeana, elekea, elekwa, elekesha
Shikishana shik shikisha Shikishana, shikisha, shikishaneni
Kwa ujumla tunawaza kusema kuwa maneno ya kawaida hunyumbulika. Hivyo
kiini/mzizi au shina moja huweza kuzalisha maneno mengine mengi ambayo
yanatokana na msingi mmoja wa maana.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 8
ZOEZI
Neno lipi kati ya haya halijaundwa kutokana na mabadiliko ya harakati za kisiasa?
A Utandawazi
B Ugatuzi
C Ufisadi
D Udukuzi
Ni mazingira gani yamesababisha kuundwa kwa neno „nywila‟?
A Kisiasa
B Kiuchumi
C Kiutamaduni
D Kisayansi na teknolojia
___ni neno lililoundwa kutokana na mabadiliko ya kiutamaduni.
A Ukeketaji
B Ubeberu
C Ubepari
D Ujamaa
Mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia yamesababisha kuundwa kwa neno gani
kati ya haya?
A Ubepari
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 9
B Ugatuzi
C Ufisadi
D Luninga
Neno „itifaki‟ limeundwa kutokana na mabadiliko ya___.
A Kisiasa
B Kiutamaduni
C Kiuchumi
D Kisayansi
Dhima ya Uambishaji na Mnyambulikoa wa Maneno
Dhima ya uambishaji ni kuleta upatanisho wa kisarufi, kuonesha idadi na umoja na
wingi katika ngeli za majina, kuonesha njeo na kuonesha urejeshi pamoja na hali
mbalimbali kwa uambikaji wa viambishi kabla ya mzizi wa neno. Aidha dhima ya
mnyambuliko ni kuonesha matokeo ya tendo na kuzalisha kauli mbalimbali kwa
kupachika viambishi baada ya mzizi wa neno.
ZOEZI
Ipi kati ya hizi siyo dhima ya uambishaji wa maneno?
A Kuleta upatanisho wa kisarufi
B Kuonesha umoja na wingi katika ngeli
C Kuonesha njeo
D Kubadili kategoria ya neno
Kuonesha matokeo ya tendo na kuzalisha kauli mbalimbali ni mojawapo ya dhima
ya___.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 10
A Unominishaji
B Uambishaji
C Unyambulishi
D Uyakinishi
___ni neno lililohama kategoria baada ya unyambulishaji wa kitenzi „penda‟.
A Pendeza
B Pendo
C Pendaneni
D Pendezesha
Viambishi vilivyoongezwa baada ya mzizi {fagi-} katika kitenzi fagiliwa
vinaonesha dhima gani ya mnyambuliko?
A Kuonesha urejeshi
B Kuonesha idadi
C Kuzalisha kauli
D Kuonesha njeo
___ni dhima ya uambishaji inayooneshwa na kiambishi {-o-} katika kitenzi
„waliotutafuta‟.
A Kuonesha urejeshi
B Kuonesha umoja
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 11
C Kuonesha idadi
D Kuonesha hali mbalimbali
Kuunda Maneno mbalimbali kwa kutumia Mnyambuliko
Uundaji wa maneno mbalimbali kwa kutumia mnyambuliko hufanyika kwa
kupachika viambishi baada ya mzizi wa neno na hivyo kulifanya neno husika
liweze kuonesha matokeo mbalimbali ya matendo pamoja na kuzalisha kauli
mbalimbali za matendo.
ZOEZI
Maneno ya mnyambuliko „zalika‟, „twalika‟ na „kalika‟ yameundwa kwa kutumia
kinyambulishi___.
A {-ek-}
B {-ik-}
C {-lik-}
D {-lek-}
Neno „piga‟ linaweza kunyumbuliwa na kuwa maneno yafuatayo, isipokuwa:
A Pigisha
B Anapiga
C Pigiwa
D Pigisha
___ni neno ambalo halijaundwa kwa kutumia kinyambulishi {-an-}.
A Tuhumiana
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 12
B Oana
C Saidiana
D Shindana
Neno lipi kati ya haya linatokana na kiambishi cha mnyambuliko {-ek-}?
A Elekezwa
B Somesha
C Somea
D Someka
___siyo neno la mnyumbuliko wa neno „fumba‟.
A Fumbata
B Fumbiana
C Fumbia
D Wamefumba
Kutumia Maneno ya Mnyambuliko katika Miktadha mablimbali
Maneno ya mnyambuliko hutumika katika miktadha mbalimbali ambapo miktadha
hiyo hujitokeza katika kauli mbalimbali za vitenzi. Kauli hizo ni kauli ya kutenda,
kauli ya kutendwa, kauli ya kutendewa, kauli ya kutendea, kauli ya kutendeka,
kauli ya kutendesha, kauli ya kutendana, na kauli ya kutendama.
ZOEZI
Yafuatayo ni maneno ambayo hutumika katika muktadha unaorejelewa na kauli ya
kutendewa, isipokuwa:
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 13
A Zolewa
B Limiwa
C Imbika
D Somewa
Kitenzi „yatazoleka‟ hutumiwa katika muktadha wa kauli ya ___.
A Kutendewa
B Kutendea
C Kutendeka
D Kutendwa
Ni viambishi gani kati ya hivi ni vya muktadha wa kauli ya kutendwa?
A {-ian-} na {-an-}
B {-w-}, {-liw-} na {-lew-}
C {-e-}, {-li-} na {-le-}
D {-ik-}, {-ek-}, {-lik-} na {-lek-}
Ni muktadha gani ambao tendo hufanywa kwa niaba au faida ya mtu mwingine?
A Muktadha wa kutendesha
B Muktadha wa kutendea
C Muktadha wa kutendana
D Muktadha wa kutendeka
Neno „tungama‟ hutumika katika muktadha wa___.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 14
A Kufungamanisha
B Kutendewa
C Kutendwa
D Kutendana
MADA YA 2 MATUMIZI YA LUGHA KATIKA MIKTADHA
MBALIMBALI
Matumizi ya lugha ni namna ambavyo wazungumzaji wa lugha hutumia lugha kwa
kuzingatia mila, desturi na kaida mbalimbali za jamii inayohusika.
Rejesta
Kwa ujumla tunaweza kufasili rejesta kama mtindo wa lugha kutegemeana na kazi
fulani, muktadha wa matumizi, lengo na uhusiano wa wanaowasiliana. Katika
muktadha rasmi rejesta hurejelea upande mmoja kama vile, msamiati wa kiufundi,
adabu maalum na matumizi ya lugha fasaha, mfano katika elimu, mahakamani na
kadhalika.
Kuwasiliana kwa kutumia Rejesta
Rejesta za Mitaani
Haya ni mazungumzo yanayozungumzwa magengeni nayo hueleweka na
wazungumzaji wenyewe. Ni lugha ambayo huchipuka kutokana na kikundi cha
watu ambacho ni kidogo. Mfano wa maneno yanayotumika sana mitaani ni kama
vile “Mshikaji” (rafiki) Demu” (mwanamke)n.k. Kwa ujumla lugha ya mitaani ni
lugha isiyo sanifu, ni lugha iliyojaa maneno ya mitaani ambayo yanaeleweka kwa
wazungumzaji wenyewe.
Mazungumzo ya Kwenye Shughuli Maalum (Rejesta za Mahali)
Mazungumzo ya kwenye shughuli maalumu hayafanywi kiholela, bali yanafuata
taratibu na kanuni maalum zinazojitokeza katika mazingira haya. Kutokana na
kutumiwa kwake kwa muda mrefu kwenye mazingira yale yale.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 15
Mazungumzo ya kwenye shughuli maalumu ni kama vile mazungumzo ya:
Maofisini au mahali popote pa kazi
Mahakamani
Hotelini
Hospitalini
Msikitini
Kanisani n.k
Mazungumzo ya mahotelini yana utaratibu wake ambao katika hali ya kawaida
inaweza isieleweke.
Nani wali kuku?
B: Mimi
Chai moja wapi?
B: Hapa
Katika mazungumzo haya A anapouliza “Nani wali kuku”, ana maana kuwa nani
anahitaji kula wali na nyama ya kuku”. Hapa hana maana ya kumwainisha mtu
aitwaaye “wali kuku”.
Kwa upande wa lugha ya mahakamani ni tofauti na lugha ya hotelini. Lugha ya
mahakamani inasisitiza usahihi ili kuondoa migongano miongoni mwa
wanaohusika.
Mfano:
Wakili wa Utetezi: Nakuuliza jaribio la kutaka kupindua serikali litakuwa kosa la
namna gani katika sheria za Tanzania?
Kamishna Msaidizi: (Baada ya kupewa kitabu cha sheria za Tanzania na
kukisoma) Ni kosa la uhaini.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 16
Wakili wa Utetezi: Ulichukua muda mrefu kufikia jibu hili. Washitakiwa wawili
hawahusiani na makosa haya?
Kamishna Msaidizi: Sijui.
Kimsingi hii ni hali ya kawaida kabisa katika mahojiano ya mahakamani. Mara
nyingi mahojiano katika mahakama hayaendi haraka sana. Kila mtu anayehusika –
hakimu, mwendesha mashtaka, wakili, mdaiwa, shahidi, n.k. hujieleza kwa wazi
wazi bila kujali urefu wa maelezo.
Rejesta Zinazohusu Watu
Rejesta zinazohusu watu ni yale mawasiliano yasiyo rasmi, ni yale maongezi ya
kawaida ya kila siku au mazungumzo rasmi; kwa mfano mazungumzo kati ya:
Vijana wenye rika moja,
Wazee wenyewe,
Wanawake wenyewe,
Wanaume wenyewe,
Mwalimu na mwanafunzi,
Meneja na wafanyakazi wake,
Mtu na mpenzi wake, n.k.
Mazungumzo miongoni mwa marafiki wa rika moja huzungumza lugha ambayo
wao wenyewe wanaielewa na sio rahisi kwa mtu wa rika lingine kuielewa lugha
hiyo.
Mfano:
'Basi, Master jana wikiendi ilikuwa kibaridi sana. Basi nilizamia infoo kwenye
zinga la mnuso huko saiti za upanga. Nilifika getini nikakuta baunsa kanyuti
chedro likisubiri kumtoa noma kila mzamiaji. Alikuwa mnoko kishenzi. Akatema
mkwara mbuzi, nikajibu kwa mkwaradume....akabloo mimi ndani‟.
Maana ya Maneno
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 17
Wikiendi – Mwisho wa wiki
Kibaridi –tulivu
Kuzamia infoo – Kuingia mahali bila kualikwa
Zinga la Mnuso –sherehe kubwa
Saiti –sehemu
Baunsa limenyuti chedro – Ni mlinzi wa mlangoni ametulia pembeni
Noma – Hatari
Mnoko kishenzi – kinaa sana
Mkwara mbuzi – Vitisho dhaifu (Sani, Toleo Na 49).
Mtu asomapo maelezo hayo, mara moja unaona jinsi vijana hawa wa rika moja
waishio mjini wanavyozungumza Kiswahili. Si rahisi kwa mzungumzaji wa
Kiswahili sanifu kuielewa kirahisi lugha hiyo.
ZOEZI
„Chai moja wapi?‟ hii ni rejesta inayotumika katika muktadha gani?
A Hotelini
B Dukani
C Hospitalini
D Darasani
___tofauti husababisha kuwepo kwa aina mbalimbali za rejesta.
A Watu
B Lugha
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 18
C Wahusika
D Miktadha
„Je mshtakiwa una utetezi wowote?‟ rejesta hii hutumika wapi?
A Mahakamani
B Kanisani
C Msikitini
D Shuleni
Mazungumzo kati ya mwalimu na mwanafunzi ni aina gani ya rejesta?
A Lugha ya kitarafa
B Rejesta za mitaani
C Rejesta zinazohusu watu
D Rejesta za mahali
___ni rejesta ambazo hudumu kwa muda mfupi tu na baadae hufifia.
A Lugha za kitarafa
B Rejesta za mitaani
C Rejesta za mahali
D Rejesta zinazohusu watu
Dhima za Rejesta
Katika kipengele cha utambulisho wa kijamii tunaangalia namna aina ya lugha ya
mazungumzo inavyoweza kujidhihirisha miongoni mwa watumiaji wake au
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 19
kuwatambulisha na kuwatofautisha wanajamii husika. Pia katika utambaulisho wa
kijamii tunaangalia vile ambavyo mtu hutambulika katika jamii kulingana na
namna anavyoongea kulingana na hadhi, tabaka, na jinsi ambavyo mtu huyo
anavyoweza kusababisha mshikamano au mwachano katika mazungumzo. Kwa
mfano jamii itamtambua mwanajamii kuwa ni msomi kulingana na mtindo wa
lugha ya mazungumzo anaoutumia, au ni mtu wa mtaani kulingana na lugha
anayotumia.
Rejesta, ina nafasi kubwa sana katika maendeleo ya kiuchumi kwa mtu binafsi na
taifa kwa ujumla. Hii ni kutokana na kwamba, madhumuni makuu ya mawasiliano
katika biashara ni kuwavutia wateja na kuwafanya kuamini kuwa bidhaa ama
huduma wanazouziwa ni za kiwango cha juu na ni thamani bora kwa pesa zao.
Hivyo lugha ya biashara (rejesta), kwa kawaida ni lugha ya kutangaza uzuri wa
bidhaa au huduma, huwa na sentensi au vifungu vifupi, mfano “Okoa mapesa
chungu mbovu” pia huwa na lugha ya kupumbaza na kuaminisha, mfano “Kunywa
XYZ kufumba na kufumbua afya yako itakurudia”.
Pia rejesta inasaidia sana kurahisisha mawasiliano miongoni mwa wazungumzaji
katika masuala mbalimbali ya kibiashara na hata katika huduma mbalimbali za
kijamii. Mfano hospitalini “mbili mara tatu”, hotelini “kuku wali tafadhali”, sokoni
“kata nusu” na maeneo mengine.
Baadhi ya rejesta hutumika kupunguza idadi ya maneno hivyo kufanya
mazungumzo yawe mafupi na yanayoeleweka kwa urahisi mfano rejesta za
hotelini kama vile:- Muuzaji: wapi ng‟ombe? Mteja: hapa Muuzaji: wapi chai
chapati? Mteja: hapa.
Pia katika kutolea elimu ya dini kanisani na msikitini rejesta ina nafasi kubwa
katika kujenga maadili.
Vilevile rejesta ina nafasi ya kupamba mazungumzo, wazungumzaji wengi
wanapozungumza hapa na pale hupenda kutumia maneno tofautitofauti ili kufanya
mazungumzo yawe ya kuvutia. Mfano mazungumzo miongoni mwa vijana:
Kijana 1: Niaje? Nakuona umechili
Kijana 2: mzuka jembe. Kama kawa… kama dawa!
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 20
Misimu
Kuwasiliana kwa Kutumia Misimu
Misimu ni semi za muda na mahali maalum ambazo huzuka na kutoweka
kutegemea mazingira maalum. misimu inayodumu huweza kuingia katika methali,
nahau au misemo ya lugha ya jamii hiyo.
Chanzo cha misimu
Misimu huzuka kulingana na mabadiliko ya kihistoria yanayoikumba jamii
husika katika nyakati mbalimbali.
Misimu huzuka kutokana na haja ya watu kuelezea hisia zoa juu ya matukio
mbalimbali yaliyotokea katika vipindi fulani kwa mfano, njaa, mafuriko,
vita n.k.
Aina za misimu
1. Misimu ya pekee. Hii ni misimu ambayo huelezea mahusiano ya kikundi
kimoja kutoka katika utamaduni mmoja, na hujulikana miongoni mwao
pekee.
2. Misimu ya kitarafa. Misimu hii hujulikana na watu wengi katikia eneo
kubwa, yaweza kuwa ni kata, wilaya au tarafa.
3. Misimu zagao. Ni misimu iliyoenea nchi nzima au pengine kuvuka mipaka
ya nchi, misimu hii husikika redioni, magazetini na hata kwenye vitabu.
Msimu uliokita mizizi sana huweza kusanifishwa na kuwa msamiati rasmi.
Sifa za misimu
Huzuka na kutoweka kufuatana na mabadiliko ya jamii
Ni lugha isiyo sanifu
Ina chuki
Ni lugha ya mafumbo
Ina maana nyingi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 21
Dhima ya misimu
Hutumika kupamba lugha
Hutumika kukuza lugha
Hutumika kutunza historia ya jamii fulani
Hutumika kuibua hisia mbalimbali za wazungumzaji
Hufurahisha na kuchekesha
ZOEZI
___za wazungumzaji huakisiwa na misimu.
A Matukio
B Maisha
C Lugha
D Hisia
___ni maneno yasiyo rasmi ambayo huzuka katika kipindi fulani na kupotea.
A Lahaja
B Istilahi
C Rejesta
D Misimu
Miktadha ya misimu ni___.
A Mazingira rasmi
B Mazingira yasiyokuwa rasmi
C Mazingira ya shughuli maalumu
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 22
D Mazingira rasmi
Ni aina gani ya misimu ambayo huenea nchi nzima na hata kuvuka mipaka ya
nchi?
A Rejesta
B Misimu ya kitarafa
C Misimu za gao
D Misimu ya pekee
Lipi kati ya haya si mojawapo ya maeneo finyu ambayo hutumia misimu?
A Kijiji
B Tarafa
C Mtaa
D Darasani
Lugha ya Mazungumzo na ya Maandishi
Sifa ya Lugha ya Kimazungumzo
Lugha ya mazugumzo ni maongezi ya watu wawili au zaidi bila kutumia
maandishi. Lugha ya mazungumzo ambayo ndiyo lugha kongwe zaidi ya lugha ya
maandishi ina dhima kubwa ya kufanikisha mawasiliano miongoni mwa watu au
kikundi fulani. Lugha hii ya mazungumzo ilianza punde tu binadamu alipoanza
kukabiliana na mazingira yake, hivyo kimsingi lugha ya mazungumzo ndiyo nguzo
kuu ya kufanikisha shughuli zote za kibinadamu kutokana na nafasi yake
kimatumizi.
Faida ya lugha ya mazungumzo
Mzungumzaji anaweza kukaa ana kwa ana na msikilizaji, hivyo hukuza
uhusiano.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 23
Mzungumzaji anaweza kutumia ishara za mwili katika kusisitiza maelezo
yake.
Mzungumzaji anaweza kupata nafasi ya kuuliza au kuulizwa maswali.
Mzungumzaji anaweza kuonesha hisia zake kwa kulia, kupaza sauti,
kupunguza sauti, kuonyesha furaha huzuni au hasira.
Mzungumzaji anaweza kuuliza maswali, kuona hisia za mzungumzaji kwa
kusikiliza lugha zinazotolewa na kuangalia ishara za mwili zinazotumika.
Mzungumzaji anaweza kupata nafasi ya kufuta usemi wake, kuongezea
jambo au kutoa maelezo ya ziada.
Mzungumzaji anaweza kubadilisha lugha yake kulingana na mazingira
aliyomo.
Mzungumzaji anao uhuru wa kutumia lugha ya mitaani, misimu kulingana
na muktadha.
Matatizo ya lugha ya mazungumzo
Maelezo lazima yahifadhiwe kichwani, hivyo kama mtu hana kumbukumbu,
taarifa zilizotolewa hupotea na kusahaulika.
Mtumiaji wa lugha ya mazungumzo anaweza kurudiarudia vipengele fulani
na hivyo kuichosha hadhira.
Ujumbe unaweza usieleweka kama unatolewa kwenye kelele nyingi
Lugha ya maandishi
Hii ni lugha inayowasilishwa kwa njia ya maandishi. Lugha ya maandishi
huzihusiha pande mbili, mwandishi na msomaji. Lugha ya maandishi sharti iwe
fasaha ili msomaji anaposoma maandishi hayo, apate kuelewa kila kitu, yaani
asibaki akijiuliza maswali.
Lugha ya maandishi huambatana na alama za uakifishaaji, hii husaidia maandishi
kusomeka vizuri na kueleweka kwa urahisi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 24
Ubora wa lugha ya maandishi
Lugha ya maandishi huwawezesha watu walio mbali kuwasiliana.
Lugha ya maandishi hustawisha sarufi ya lugha na misingi yake, kwa sababu
mwandishi anahakikisha kwamba anazingatia vizuri kanuni za kisarufi ili
msomaji wake aweze kumwelewa.
Ili kuhakikisha maelezo yake yanaeleweka mwandishi analazimika kuandika
kwa uwazi na kwa kuzingatia kanuni na miiko yote ya uandishi.
Udhaifu wa lugha ya maandishi
Lugha hii hutumiwa na wale tu wanaojua kusoma na kuandika.
Lugha ya maandishi haina msisimko uletwao na lafudhi na matamshi.
Msomaji hukosa vidokezo vingi ambavyo katika lugha ya mazungumzo
huchangia katika mawasiliano.
Lugha ya maandshi inamnyima mwandishi nafasi ya kupima welewa wa
msomaji kwa kuwa hamwoni.
Dhima ya lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi
Lugha ya mazungumzo na lugha ya maandshi zote zina umuhimu wa pekee katika
maisha ya kila siku kwa sababu ndizo zinzaowezesha watu kuwasiliana kwa namna
mbalimbali.
Umuhimu wa lugha ya maandshi pia hutokana na dhima yake kwa watu.
Maandishi yanaweza kuhifadhiwa na kusambazwa kwa watu wengi hata walio
mbali. Maandishi yanahifadhi kumbukumbu na kwa muda mrefu. Kwa hali hii,
watu wa vizazi vingine wanaweza kusoma na kujua mambo yaliyofanyika karne
nyingi zilizopita.
Tofauti kati ya lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi
1. Lugha ya mazungumzo huwezesha mawasiliano ya ana kwa ana lakini lugha
ya maandishi haiwezeshi mawasiliano ya ana kwa ana.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 25
2. Lugha ya mazungumzo haihitaji maandalizi wakati lugha ya maandishi
huhitaji maandalizi. Mwandishi atalazimika kupata muda wa kuandika
pamoja na kuandaa vifaa kama vile kalamu, karatasi n.k
3. Lugha ya mazungumzo hailazimiki kuzingatia kanuni za kisarufi, lakini
lugha ya maandshi hutakiwa kuzingatia kanuni za kisarufi.
Tofauti nyingine kati ya lugha ya maandishi na lugha ya mazungumzo huweza
kuonyeshwa katika jedwali lifuatalo.
Kipengele Mazungumzo Maandishi
Muktadha
1. Wahusika
huonana
2. Viungo vya mwili
hutumika
3. Maandalizi na
matumizi
hufanyika wakati
mmoja
1. Wahusika
hawaonani
2. Viungo vya
mwili havitumiki
3. Maandalizi
hufanyika kabla
ya matumizi
Mada Hazina uzito mkubwa Huelekea kuwa na uzito
mkubwa.
Mpangilio
wa mada na
mawazo
Hautabiriki. Unaelekea
kutokuwa na mtiririko.
Hutabirika. Huelekea
kuwa na mtiririko.
Mjadala wa
mada
Hauelekei kuwa na kina.
Hazichujwi kwa
uaangalifu.
Unaelekea kuwa na
kina. Huchujwa.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 26
Dhima ya matumizi ya lugha
Dhima kuu ya lugha ni kupashana habari, ujuzi na maarifa mbalimbali. Vilevile
lugha husaidia kujenga uhusiano mwema baina ya watu. Uhusiano huo unaweza
kuwa wa kijamii, kielimu, kibiashara, kihuduma, kisiasa, kiuchumi n.k. Kwa hiyo,
kujua jinsi ya kuitumia lugha kama inavyotakiwa, kunasaidia kufikisha vizuri
ujumbe unaotakiwa bila kuupotosha. Vilevile kunasaidia kuepuka migongano, hasa
ya kijamii kwa kuwa utakuwa umetumia lugha kwa mujibu wa mila na desturi za
jamii inayohusika.
Mambo ya kuzingatia katika matumizi ya lugha
1. Mada inayozungumziwa:Mada za mazungumzo zipo nyingi. Kuna mada za
kijamii, kwa mafano ndoa, unyago, mapenzi, kifo, matanga, burudani,
muziki n.k. Kuna mada za kibiashara kwa mfano bidhaa, kodi, vibali, fedha,
hasara, faida n.k. Kwa hiyo, ili mazungumzo yaweze kwenda vizuri,
wazungumzaji wanatakiwa kuzingatia mada husika.
2. Muktadha wa mazungumzo:Mazungumzo yanaweza kuathiriwa na
miktadha tofauti. Kwa mfano kuna miktadha ya kidini, kiganga, huzuni,
sherehe, kisiasa, kielimu, kibiashara n.k. Mazungumzo yanaweza kufanyika
mjini, kijijini, ugenini, shuleni, dukani, hotelini n.k
3. Malengo ya mazungumzo hayo:Malengo ya mazungumzo nayo yanaathiri
matumizi ya lugha. Kwa mfano, lengo linaweza kutoa taarifa, kuhoji,
kukejeli, kutia moyo n.k. Sasa jinsi lugha itakavyotumika katika kutoa
taarifa ni tofauti na itakavyotumika katika kutia moyo au kukejeli.
4. Uhusiano uliopo baina ya wazungumzaji:Matumizi ya lugha huweza
kuathiriwa pia na mahusiano ya wazungumzaji. Kuna mazungumzo baina ya
watoto, wanafunzi, wazee, viongozi, marafiki n.k. Upo uhusiano wa daktari
na mgonjwa, mwalimu na mwanafunzi, mnunuzi na muuzaji. Kwa hiyo
mazingira baina ya pande hizi mbili yatategemea uhusiano wao, kwa hiyo
kaida za uhusiano huu utapaswa kuzingatiwa. Kwa hiyo, kwa kuzingatia
mambo haya manne, itawafanya wazungumzaji wawe makini katika uteuzi
wa maneno, miundo, mifano na kina cha ufafanuzi wa maelezo au habari
inayozungumzwa.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 27
ZOEZI
Zifuatazo ni taratibu za uandishi ambazo huambatana na lugha ya kimaandishi,
isipokuwa:
A Matumizi ya lafudhi
B Matumizi ya vituo
C Matumizi ya herufi kubwa
D Matumizi ya aya
Mtu anapoonesha umahiri wa lugha katika mazungumzo ina maana kuwa lugha ya
kimazungumzo ina sifa ya___
A Mabadiliko
B Uhai
C Uhuru
D Maandalizi ya awali
Lugha ya mazungumzo ina sifa ya kutokuwa na gharama, hii ni kwa sababu___
A Haina maandalizi
B Ni hai
C Inahitaji kuwa na ala za sauti tu
D Inahitaji kalamu na karatasi
Sifa gani ya lugha ya kimazungumzo hudhihirika pale mzungumzaji anapoonesha
hali ya hisia zake?
A Utajiri wa wahusika
B Uhusiano na hadhira
C Sifa ya mabadiliko
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 28
D Uhai
Lugha ya mazungumzo inapowakutanisha ana kwa ana msikilizaji na mzungumzaji
inadhihirisha sifa ya___
A Uhai
B Uhusiano kati ya hadhira
C Utajiri wa wahusika
D Uhuru
Dhima ya Lugha ya Kimazungumzo na ya Kimaandishi
Lugha ya kimazungumzo na ya kimaandishi zina dhima kuu ya kupasha habari,
ujuzi, na maarifa mbalimbali, husaidia kujenga uhusiano mwema baina ya watu,
kufikisha ujumbe unaotakiwa vizuri bila kupotosha, kufundishia ujuzi, kuchochea
maendeleo, kuhifadhi historia ya jamii na kueleza mawazo au hisia za watu.
ZOEZI
Lugha ya kimazungumzo inapotumika kutofautisha jamii moja na nyingine huwa
na dhima ya ___.
A Kutolea maarifa
B Utambulisho
C Kuchochea maendeleo
D Kujenga umoja
Lugha ya kimazungumzo inapowaleta watu karibu huwa na dhima ya___.
A Kujenga umoja
B Kueneza umoja
C Kuvunja umoja
D Kutetea umoja
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 29
___ni dhima inayotofautisha lugha ya kimazungumzo na ya kimaandishi.
A Kupasha habari
B Kuhifadhi kumbukumbu
C Kufikisha ujumbe mahususi
D Kuchochea maendeleo
Lugha ya kimazungumzo na kimaandishi zina dhima moja kuu ambayo ni___
A Kuwasiliana
B Kuchochea maendeleo
C Kuunganisha watu
D Kuhifadhi taarifa
Ipi ni dhima kuu ya lugha ya kimazungumzo?
A Kupasha habari na maarifa
B Kujenga uhusiano katika jamii
C Kuchochea maendeleo
D Kuhifadhi kumbukumbu
Lugha ya Kimazungumzo na ya Kimaandishi katika Miktadha Sahihi
Matumizi ya lugha ya kimazungumzo na ya kimaandishi katika muktadha sahihi
huongozwa na mambo yafuatayo, ambayo ni mada inayozungumzwa, muktadha au
mahali mazungumzo hayo yanapofanyika, malengo ya mazungumzo hayo na
uhusiano uliopo kati ya wazungumzaji.
ZOEZI
___ ni kipengele cha muhimu ambapo uteuzi wa maneno unazingatia ni nani
anahusika katika mazungumzo.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 30
A Uhusiano baina ya wahusika
B Mazingira
C Mada
D Malengo ya mazungumzo
Miongoni mwa vitu vya kuzingatia katika lugha ya kimazungumzo ni mada. Ipi
kati ya hizi ni mada ya kijamii?
A Bidhaa
B Unyago
C Fasihi
D Uhandisi
Ni muktadha gani ambao uhusisha matumizi ya risala katika lugha ya
mazungumzo?
A Kidini
B Baa
C Dukani
D Msibani
Yafuatayo ni mambo yanayotawala lugha ya kimazungumzo na kimaandishi,
isipokuwa:
A Mada
B Istilahi
C Uhusiano baina ya wahusika
D Muktadha
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 31
Kipi kati ya hivi ni cha kuzingatia wakati wa matumizi ya lugha ya mazungumzo
katika mikatdha mbalimbali?
A Mawazo ya mwandishi
B Alama za uandishi
C Herufi
D Matamshi
Matamshi na Lafudhi ya Kiswahili
Matamshi ni namna ambavyo mtu anatamka neno au jinsi mtu anavyozungumza
lugha. Unaposema fulani ana matamshi mazuri ya Kiswahili utakuwa unamaanisha
anazungumza Kiswahili fasaha.
Neno moja linaweza kuzungumzwa/kutamkwa kwa namna tofauti na watu
mbalimbali kutokana na sababu mbali mbali, sababu hizo ni pamoja na eneo la
kijiografia anakotoka huyo mtu, kabila lake, kundi lake la kijamii mfano msanii au
mwanasiasa, na elimu aliyonayo. Hizi zote zinaweza zikawa ni sababu za kufanya
watu watofautiane katika matamshi.
Lafudhi Mbalimbali za Kiswahili
Dhana ya matamshi huhusisha
Sauti za lugha husika
Mkazo
Kiimbo
Sauti za lugha ya Kiswahili
Sauti za lugha ya Kiswahili hujumuisha irabu na konsonanti, ambazo kwa ujumla
huunda sauti 24, irabu tano na konsonanti 19 (konsonanti x na q hazipo katika
matamshi ya kiswahili). Sauti za Kiswahili hutamkwa kama zilivyoandikwa, kwa
mfano maneno “data” au “dengue” wewe unayatamkaje? Wengi huyatamka kama
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 32
yalivyo hata kama wakiwa wanazungumza kiingereza, hii ni kwa sababu maneno
ya Kiswahili hutamkwa kama yalivyoandikwa.
Kwa hiyo unapotamka maneno ya Kiswahili ni sharti uzingatie sauti asilia za lugha
ya Kiswahili. Kuna watu huwa wanaandika hivi “xaxa”, hii huwa unaitamkaje? Au
“ucjal” huwa unaitamkaje? Kwa kufuata matamshi asilia ya Kiswahili “ucjal”
itatamkwa “uchijal” sijui itakuwa ina maana gani sasa. Na pengine umekuwa
ukitumia maandishi ya namna hii hata kwenye insha zako ukidhani upo sahihi au
ni kwa mazoea tu, sasa kwa kuwa umejua matamshi sahihi ya Kiswahili ni yapi,
utajifunza kuyatumia kwa usahihi katika maandishi rasmi na yasiyo rasmi.
Mkazo
Katika lugha ya Kiswahili kuna namna ya kutamka maneno ili kuleta maana mbali
mbali, kwa mfano neno “barabara” litaleta maana husika kulingana na jinsi
lilivyotamkwa. Hivyo, mkazo ni pale silabi inapotamkwa kwa kukazwa. Maneno
ya Kiswahili huwa na silabi moja ambayo hutamkwa kwa nguvu zaidi kuliko silabi
nyingine. Unapotamka silabi iliyotiwa mkazo, sauti hupandishwa juu kiasi.
Maneno mengi ya Kiswahili, hasa yale yenye asili ya Kibantu hutia mkazo katika
silabi ya pili kutoka mwisho.
Kwa mfano:ba’bu, maya’i, rama’ni (mimi nilikuwa nikitamka ra’mani), baraba'ra
(njia).
Baadhi ya maneno yenye asili ya kigeni, huwa na mkazo katika silabi nyingine.
Kwa mfano: bara'bara (sawa sawa), Alha’misi
Kiimbo
Ni utaratibu maalum wa upandaji na ushukaji wa mawimbi ya sauti unaojitokeza
katika utamkaji wa lugha fulani.
Katika utaratibu wa utamkaji, dhana ya Kiimbo huandamana pia na dhanna
ya kidatu ( yaani , kiwango cha juu, cha chini au cha kati cha sauti katika usemaj),
Kwa hivyo ni muhimu hapa kueleza tofauti zilizopo baina ya kiimbo na kidatu.
Wakati kiimbo kina maana ya kupanda na kushuka kwa mawimbi ya sauti ya
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 33
lugha, kidatu kina maana ya kiwango cha sauti isikikayo, wakati wa utamkaji ama
kuwa juu, kuwa katikati au kuwa chini.
Aina za viimbo
Kiimbo cha maelezo: Kiimbo cha maelezo ni kile ambacho kwa kawaida
msemaji wa lugha akiwa kwenye kidatu chochote kile mawimbi sauti ya
usemaji wake yanakuwa takriban katika mstari ulionyooka. Mfano,
Mwalimu anafundisha.
Kiimbo cha maulizo: Kiimbo cha kuuliza hujitokeza kwa kutumia viwango
tofauti vya kidatu kutegemeana na aina ya swali linaloulizwa. Mfano,
mwalimu anafundisha?
Kiimbo cha amri: kiimbo cha amri hakitofautiyani sana na kiimbo cha
maulizo. Kiimbo cha amri, mzungumzaji hutumia kidatu cha juu zaidi
kuliko ilivyo katika kiimbo cha maelezo. Mfano, njoo hapa!
Lafudhi ya Kiswahili
Lafudhi ni matamshi ya msemaji wa lugha fulani ambayo yanatokana na athari za
kimazingira. Mazingira hayo yanaweza kuwa eneo atokalo mtu, mahali
alikosomea, kiwango chake cha elimu, tabaka lake la kijamii na kadhalika.
Lugha ya Kiswahili ni lugha ya pili kwa watumiaji wengi wa afrika mashariki, kwa
hiyo hii inafanya kuwatambua wazungumzaji wa Kiswahili kulingana na makabila
yao au maeneo wanakotoka. Kwa mfano, kwa hapa Tanzania tunaweza
kuwatambua watu wa mwanza kwa lafudhi yao, watu wa mtwara kwa lafudhi yao,
watu wa pemba kwa lafudhi yao au watu wa Musoma kwa lafudhi yao.
Mifano
1. Usiniretee maswara ya ubaguzi wa kikabira hapa (Wakuria)
2. Amemupiga mutoto ya watu juu amemuibia mfaranga makumi mawili
(Wakongo)
3. Ukikaa nchale, ukichimama nchale (Wamakonde)
4. Wewe unakamuaga mang‟ombe tu moja kwa moja (Wasukuma)
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 34
5. Mbona unakuwa kinganganizi, nilishakwambia sikupendi lakini wewe bado
unaningangania tu! (Wahaya)
ZOEZI
Neno lipi kati ya haya linaonesha lafudhi ya mzungumzaji wa Kiswahili kutoka
jamii ya Wapare?
A Thatha
B Thelathini
C Sasa
D N'toto
„Hifi ni fiatu fyangu‟ hii ni lafudhi ya watu wa jamii gani?
A Wanyakyusa
B Wayao
C Wamakua
D Wapare
___ ni tungo ya Kiswahili yenye lafudhi ya Kimakonde.
A N‟toto amekuja.
B Juma amemupiga mutoto.
C Riereze riondoke.
D We mitu kabila gani?
Ipi kati ya hizi ni tungo ya Kiswahili yenye lafudhi ya kihaya?
A Riambie riende.
B E bhatoto hamuyambo.
C Toa ukyafu hapa.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 35
D Wewe mbona kinganganizi.
___ni tofauti ya matamshi ya wasemaji wa lugha ambayo husababishwa na athari
ya mazingira.
A Mkazo
B Mtindo wa lugha
C Lafudhi
D Utata
Utata katika Mawasiliano
Utata ni hali ya neno au sentensi kuwa na maana zaidi ya moja. Kwa hiyo tungo
tata ni tungo ambayo inaweza kuwa na maana zaidi ya moja.
Sababu za Utata
Utata katika tungo hutokea kwa sababu zifuatazo:
1. Neno kuwa na maana zaidi ya moja, kwa mfano neno mbuzi, kata n.k.
2. Kutozingatia taratibu za uandishi, Mfano; Tulimkuta Nyammy na rafiki yake,
Mazala vs Tulimkuta Nyammy na rafiki yake Mazala. Katika sentensi hizi
alama (,) ndio huleta tofauti, sentensi ya kwanza inamaana kulikuwa na watu
wawili Nyammy na rafiki yake aitwaye Mazala na sentensi ya pili isiyo na
alama (,) inamaanisha kulikuwa na watu wawili Nyammy na mtu mwingine
ambaye ni rafiki yake Mazala
3. Kutumia maneno bila kuzingatia muktadha wa matumizi ya maneno hayo.
4. Utamkaji wa maneno. Wakati mwingine utata unaweza kujitokeza katika
matamshi tu, ili hali katika maandishi utata hauonekani. Kwa mfano;
Mimina wewe, katika maandishi linaweza kuandikwa mimi na wewe, na
hivyo kuondoa utata.
5. Mjengo wa maneno. Utata huu huzuka katika vitenzi kama pigia. Chanzo
cha utata katika kitenzi hiki ni kiambishi –i-. Kiambishi hiki kinaweza
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 36
kumaanisha: kwa ajili ya…, kwa sababu ya.., kwa kutumia chombo fulani..,
au mahali fulani.
Mfano:
Alimpigia ukorofi wake (kwa sababu ya)
Alimpigia kiatu (kifaa)
Alimpigia ndani (mahali)
Mifano ya utata katika tungo
1. Patience amemwandikia Lilian barua:Sentensi hii huweza kuwa na maana
kuwa Patience ameandika barua kwenda kwa Lilian au Patience ameandika
barua kwa niaba ya Lilian
2. Umefanikiwa kununua mbuzi?Sentensi hii huweza kumaanisha ununuzi
wa mbuzi mnyama au mbuzi kifaa cha kukunia nazi.
3. Alimkuta amelala kwenye nyumba ya wageni:Sentensi hii huweza
kumaanisha, nyumba ya mtu lakini inatumika kwa ajili ya wageni kwa
malipo au ni nyumba inayomilikiwa na watu ambao ni wageni katika eneo
lile.
4. Attu ametumwa na Aritamba:Sentensi hii inaweza kueleweka
kumaanisha, Aritamba amemtuma Attu au Attu na Aritamba wametumwa
wote kwa pamoja.
ZOEZI
Zifuatazo ni sababu za utata, isipokuwa:
A Kutumia maneno ya picha
B Umahiri wa lugha
C Neno kuwa na maana zaidi ya moja
D kutumia maneno bila kuzingatia muktadha husika
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 37
Neno „mbuzi‟ ni tata, kwa sababu___
A Ni neno la Kiswahili
B Lina maana iliyofichika
C Lina maana moja tu
D Lina maana zaidi ya moja
Mojawapo ya sababu za utata ni mjengo wa maneno. Ni aina gani ya maneno
ambayo mjengo wake huleta utata?
A Vitenzi
B Viwakilishi
C Viunganishi
D Vihisishi
Tungo ipi inaonesha sababu ya utata ya kutozingatia mukutadha wa matumizi ya
meneno?
A Mwajuma ametumwa na Rama.
B Ana uma.
C Anampigia ujeuri wake.
D Juma anabuni.
Utata unaojitokeza katika maneno husababishwa na neno kuwa na___.
A Maana zaidi ya moja
B Maana mbili tu
C Maana zaidi ya mbili
D Maana moja tu
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 38
MADA YA 3 : UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI SIMULIZI
Fasihi simulizi kama zilivyo kazi nyingine za fasihi andishi hufanyiwa uhakiki.
Uhakiki huu huzingatia vipengele vya fani na maudhui ili kubainisha usanaa wa
kazi husika pamoja na kile ilichokusudia kufikishwa kwa hadhira.
Uhakiki wa Ushairi
Mashairi kama kazi nyingine za kifasihi huhakikiwa kwa kutumia vigezo sawa na
vinavyotumika katika kazi nyingine za kifasihi. Vigezo hivyo ni kwa kuzingatia
vipengele vyake viwili yaani fani na maudhui.
Vipengele vya Fani na Maudhui katika Kuhakiki Ushairi
Vipengele vya fani
Uhakiki wa fani za ushairi ni uchambuzi wa kina na kuziweka wazi mbinu za
kisanaa alizotumia mshairi katika kutunga kazi yake. Vipengele muhimu vya
kuhakiki katika fani ya ushairi ni kama vifuatavyo:
Mtindo
Jambo la kuonyesha hapa ni kwamba iwapo shairi ni la kimapokeo ama ni la
kisasa.
Muundo
Katika kuhakiki muundo wa shairi mhakiki inatakiwa aweke wazi mambo
yafutayo:
1. Idadi ya beti
2. Idadi ya mistari na aina ya vibwagizo
3. Idadi ya vipande
4. Idadi ya mizani
5. Aina na mpangilio wa vina
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 39
Wahusika
Ikiwa shairi limehusisha wahusika ni vema pia mhakiki awabainishe
Matumizi ya lugha
Katika kipengele hiki mhakiki huchunguza:
1. Mpangilio wa maneno. Mf. Wengi wari badala ya wari wengi
2. Matumizi ya : Mazida – kurefusha neno mfano, kiwembe badala ya
wembe; Ikisari – kufupisha neno mfano siombe badala ya
usiombe; Tabdila – kubadilisha mwendelezo wa neno mfano kujitanuwa
badala ya kujitanua.
3. Matumizi ya methali, misemo na nahau
4. Matumizi ya lugha ya picha
5. Matumizi ya tamathali za semi kama vile takriri, sitiari n.k
6. Mbinu nyingine za kisanaa
Mhakiki anapochunguza vipengele vya fani, jambo muhimu la kuzingatia ni jinsi
vipengele hivyo vinavyosaidia kuwasilisha maudhui.
Vipengele vya maudhui
Ili kuhakiki na kupata maudhui ya shairi inatakiwa kulisoma shairi kwa kulielewa
zaidi. Baada ya kupata picha fulani kuhusu shairi na kutafakari maana za maneno
muhimu, itatubidi tuelewe vipengele vya maudhui, ambavyo ni dhamira, mtazamo,
msimamo, falsafa ya mwandishi, ujumbe na maadili, migogoro na muktadha.
ZOEZI
Kipi kati ya hivi siyo kipengele cha fani katika uhakiki wa ushairi wa fasihi
simulizi?
A Mtindo
B Muundo
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 40
C Ujumbe
D Wahusika
Mawazo ya kisiasa na kiutamaduni huakikiwa katika kipengele gani cha maudhui
ya ushairi?
A Ujumbe
B Falsafa
C Migogoro
D Dhamira
Mafunzo mbalimbali yanayopatikana katika shairi huakikiwa katika kipengele gani
cha maudhui?
A Ujumbe
B Migogoro
C Dhamira
D Falsafa
___ni kipengele cha maudhui ya ushairi kinachobainisha mivutano na misiguano
iliyopo ndani ya shairi.
A Dhamira
B Mtazamo
C Falsafa
D Migogoro
___ ni kipengele cha fani kinachoonesha kama shairi ni la kimapokeo au la kisasa.
A Mtindo
B Muundo
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 41
C Matumizi ya lugha
D Wahusika
Uhakiki wa Maigizo
Igizo huhakikiwa kwa namna lilivyo katika maumbo yake yote mawili yaani fani
na maudhui.
Vipengele vya Fani na Maudhui katika Kuhakiki Maigizo
Fani
Uhakiki wa fani katika maigizo unajihusisha na ufundi uliotumiwa. Ufundi huu
unajumuisha mambo kadhaa kama ifuatavyo:
Mtindo
Mtindo ni sura ya maigizo inayojitokeza kupitia mpangilio wa maneno na vitendo.
Inabidi mhakiki achunguze kama kazi ni:
1. Mchezo wa jukwaani – wenye mpangilio wa mazungumzo baina ya watu na
matendo yao.
2. Majigambo
3. Vichekesho – mpangilio wa maneno yanayowasilisha ujumbe kwa
kuchekesha.
4. Mazungumzo – maongezi ya kujibizana baina ya watu.
5. Ngonjera – mpangilio wa tungo za kishairi ambapo watu wawili au makundi
mawili hukinzana.
6. Miviga – sherehe za kitamaduni kama vile matambiko
Pamoja na haya, mtindo hutegemea lengo la maigizo ambalo laweza kuwa
kuelimisha, kukejeli, kuburudisha, kuonya, kukosoa na kadhalika.
Mandhari
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 42
Mazingira ya kutendea ni kipengele muhimu cha fani. Mhakiki hana budi kujiuliza
iwapo utendaji unadhihirisha wakati au mahali halisi. Jambo hili huweza
kutekelezwa kupitia vifaa, maleba, maneno n.k.
Wahusika
Maswali ya mhakiki kuuliza ni:
Wamejitokeza kikamilifu?
Wanaaminika?
Matumizi ya lugha
Vigezo anavyotumia mhakiki kuchunguza lugha ni:
Kama usemaji ni wa kisanaa, yaani unatumia picha, tamathali za semi,
methali, nahau n.k.
Kama lugha imetumika vile inavyotumiwa katika jamii. Mfano: kiimbo,
mkazo, miguno, vihisishi n.k.
Matumizi ya maneno ya ajabu kama yale yanayotumiwa na waganga.
Maleba na vifaa
Hivi huakisi mandhari na husaidia kuzua mukatadha. Kwa hiyo ni muhimu
kuchunguza kama vimetumiwa ipasavyo.
Matumizi ya ala
Matumizi ya ala kama ngoma, baragumu, au sauti zingine ili kuamsha hisia za
hadhira ni jambo muhimu kuchunguza.
Mbinu nyingine
Mhakiki anapaswa pia kuchunguza matumizi ya nyimbo, uchezaji ngoma,
usimulizi na mbinu nyingine katika kuibua hisia za watazamaji.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 43
Maudhui
Kwa upande wa maudhui, mhakiki wa maudhui hutakiwa kuchunguza vipengele
vyote vya kimaudhui ambavyo ni dhamira, migogoro, maadili, mtazamo na
msimamo wa fanani pamoja na ujumbe bila kusahau kipengele cha falsafa. Yote
hayo kwa pamoja ndiyo humsaidia mhakiki kubaini ukinzani wa igizo na maisha
halisi ya jamii ambayo huwa ndiyo hadhira ya igizo hilo.
ZOEZI
Ni kipengele gani cha maudhui ambacho hubainisha tofauti ambazo hujitokeza
katika maigizo?
A Dhamira
B Ujumbe
C Migogoro
D Falsafa
Matumizi ya mbinu nyingine ni kipengele cha fani katika maigizo ambacho huwa
na vipengele vifuatavyo, isipokuwa:
A Uchezaji ngoma
B Matumizi ya ala
C Usimulizi
D Matumizi ya nyimbo
___ni kipengele cha maudhui ambacho huonesha busara na hekima za mtunzi wa
maigizo.
A Dhamira
B Ujumbe
C Falsafa
D Migogoro
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 44
Nasaha atoazo mtunzi wa maigizo uhakikiwa katika kipengele gani cha maudhui?
A Dhamira
B Mafunzo
C Falsafa
D Mgogoro
___ni kipengele cha fani ambacho hubainisha vitendo na mjengo wa visa katika
maigizo.
A Mandhari
B Mtindo
C Matumizi ya lugha
D Muundo
MADA YA 4 : UHIFADHI WA KAZI ZA FASIHI SIMULIZI
Ili kitu kidumu ni lazima kihifadhiwe; fasihi simulizi kama sanaa kutokana na
umuhimu wake katika jamii nayo huhufadhiwa kwa ajili ya faida ya kizazi kijacho.
Katika mada hii utaweza kujifunza umuhimu wa fasihi simulizi katika jamii.
Utajifunza njia mbalimbali zitumikazo katika uhifadhi wa fasihi simulizi pia
utaweza kubainisha ubora na udhaifu wa kila njia.
Njia za kuhifadhi Fasihi Simulizi
Kuhifadhi Fasihi Simulizi
Umuhimu wa kazi za fasihi simulizi
Ingawa kila utanzu wa fasihi una umuhimu wake, kwa pamoja tanzu zake zote zina
umuhimu mkubwa katika jamii.
Kwaza fasihi hutumika kama chombo cha kuwaelimisha watu. Kupitia fasihi
andishi na fasihi simulizi, watu hupata maarifa ya kutambua mambo maovu na
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 45
namna ya kuyakwepa. Licha ya haya, wanajamii hujifunza njia za kujitawala,
kuzalisha mali na kuishi kwa misingi ya haki, usawa na demokrasia.
Pili, fasihi ni nyenzo ya kutoa mafunzo kuhusu mambo kama vile historia, dini,
siasa, jiografia na tiba. Kwa hiyo watu hujifahamisha juu ya maumbile na asili
yake, mazingira, utawala, uchumi, sheria n.k.
Aidha fasihi huwapa watu mazoezi na kuimarisha uwezo wao wa kuzungumza kwa
ufasaha, kuimba nyimbo kwa ufundi, kuigiza mambo kwa ustadi, kucheza ngoma
kwa umahiri, kughani mashairi kwa mvuto na kusimulia matukio kwa mtindo
ufaao.
Fasihi hufahamisha, huhifadhi na hurithisha mambo kuhusu utamaduni kutoka
kizazi kimoja hadi kingine. Mambo hayo ni pamoja na mila, desturi, falsafa, imani
na itikadi. Pia hudumisha maarifa ya kijadi kama vile tiba, sayansi ya kilimo,
uhifadhi wa mazingira na sayansi ya utabiri wa hali ya hewa.
Umuhimu mwingine wa fasihi unatokana na kutumika kwake kama chombo cha
kuburudisha na kupumbaza. Watu wanaposoma kazi mbalimbali za fasihi hupata,
msisimko wa kimwili na kiakili. Kadhalika fasihi hugusa hisia za watu na
kuwafanya wafurahi au wahuzunike.
Istoshe fasihi hudumisha na kukuza lugha. Watu hupanua msamiati wao na miundo
ya lugha kupitia kazi zake. Hivyo fasihi inakuwa kama hazina ya maneno na dafina
ya kanuni za kisarufi.
Kutokana na umuhimu huu ndio maana fasihi huhifadhiwa ili isipotee. Na uhifadhi
huu hufanyika kwa njia mabalimbali.
ZOEZI
___ni njia ambayo kazi za fasihi simulizi uhifadhiwa katika programu.
A Njia ya makazi
B Njia ya vinasasauti
C Njia ya maandishi
D Njia ya kompyuta
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 46
___ni njia ya kuhifadhi fasihi simulizi inayohitaji gharama kubwa na ujuzi wa juu.
A Njia ya makazi
B Njia ya kompyuta
C Njia ya vinasasauti
D Njia ya maandishi
Rediokaseti hutumika katika njia ipi kati ya hizi za kuhifadhia fasihi simulizi?
A Njia ya vinasasauti
B Njia ya makazi
C Njia ya maandishi
D Njia ya mkanda wa video
Mikeka na picha za kuchora uhifadhiwa katika njia gani ya kuhifadhi fasihi
simulizi?
A Njia ya maandishi
B Njia ya kompyuta
C Njia ya makazi
D Njia ya kichwa
Ipi kati ya hizi ni njia kongwe inayotumika kuhifadhi fasihi simulizi?
A Njia ya vinasasauti
B Njia ya kutumia kichwa
C Njia ya maandishi
D Njia ya kanda za video
Ubora na Udhaifu wa kila Njia ya Kuhifadhi kazi za Fasihi Simulizi
Fasihi simulizi inaweza kuhifadhiwa kwa njia zifuatazo:
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 47
Kichwani
Hii ndio njia ambayo imekuwa ikitumiwa kuhifadhi kazi za fasihi tangu kale na
inaendelea kutumika hadi leo. Kwa kutumia njia hii kazi ya msanii hukaa kwenye
ubongo wa msanii, naye huweza kuiwasilisha kazi hiyo, wakati wowote bila
gharama yoyote.
Ubora wake
Uwasilishaji wa kazi hiyo unaweza kufanyika wakati wowote bila kuhitaji
kufanyika maandalizi yoyote, hususani ya kiufundi.
Hakuna gharama yoyote wakati wa uwasilishaji wa kazi ya fashi. Msanii
hahitaji kugharimia kitu chochote ili waweze kuitoa kichwani, ni uamzi
wake tu, anaweza kuimba papo kwa papo.
Kazi ya fasihi iliyohifadhiwa kichwani ni hai. Hii ni kwa sababu msanii
anakuwa ana kwa ana na hadhira yake. Kutokana na matumizi ya mbinu
tofauti za kisanaa kama vile kucheza, kubadili sauti, miondoko na
mengineyo mengi, kazi yake inapata uhalisia zaidi mbele ya hadhira.
Udhaifu wake
Uwezekano wa kazi kupotea au kuharibika hasa katika fani ni mkubwa. Kwa
mfano msanii anapokuwa amefariki dunia kazi anayokuwa ameihifadhi
kichwani nayo hupotea. Ndio maana katika baadhi ya jamii kazi za kifasihi
zimepotea. Hii ni kwa sababu wasanii wanapoondoka duniani hondoka na
fani hizo.
Kazi inapohifadhiwa kichwani ni rahisi kubadilika. Hii inatokea pale
ambapo msanii anasahau baadhi ya maneno kutokana na umri wake au
sababu nyinginezo
Njia ya maandishi
Maandishi ni njia moja wapo inayotumika kuhifadhia kazi za fasihi. Njia hii
imeanza kutumika baada ya watu kujua kusoma na kuandika. Uhifadhi wa kazi za
fasihi kwa njia hii hupitia njia mbili kubwa. Hatua ya kwanza ni kubuni kisa au
wazo; na hatua ya pili ni kuliweka wazo hilo katika maandishi. Kazi za fasihi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 48
simulizi zinazoweza kuhifadhiwa katika maandishi ni hadithi, nyimbo, mashairi,
ngonjera, majigambo n.k
Ubora wake
Kazi iliyohifadhiwa inaweza kudumu kwa muda mrefu
Kazi iliyohifadhiwa inaweza kufikia hadhira hata ya mbali na aliko msanii.
Kazi iliyohifadhiwa katika maandshi haipotezi fani yake na maudhui yake
bali huendelea kuwa katika asili yake ya awali hadi msanii atakapoamua
kuibadilisha.
Udhaifu wake
Hii njia ni kwa ajili ya watu wachache tu wanaojua kusoma na kuandika.
Wasanii wanaoweza kutumia njia hii ni wale tu wanaojua kusoma na
kuandika.
Ni aghali sana kuhifadhi kazi za kifasihi kwa njia ya maandishi. Msanii
atalazimika kununua vifaa vinavyohitajika katika maandishi ambavyo ni
kalamu, karatasi, meza. Kwa hiyo ni aghali.
Uwasilishaji wake si hai kwani hakuna kuonana ana kwa ana kati ya hadhira
na fanani. Kwa hiyo msomaji hawezi pata vionjo vya msanii hivyo itambidi
ajibunie yeye mwenyewe.
Wahusika pia hawawezi kuonekana, endapo ni igizo mabalo limehifadhiwa
katika maandishi, hivyo ubora wa kazi ya msanii huchujuka.
Njia ya vinasasauti
Vinasasauti ni miongoni mwa vyombo vinavyotumika kuhifadhi kazi za fasihi
simulizi. Hii ni njia iliyoendelea kuliko ile ya maandishi.
Ubora wake
Kazi ya msanii huweza kuwafikia watu hata walio mbali na alipo mtunzi.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 49
Ikihifadhiwa katika vinasasauti kama vile tepurekoda au CD ubora wake
huwa haupotei wala kuharibika endapo vifaa hivyo vitatunzwa vizuri.
Sauti ya mtunzi unaiskia moja kwa moja
Unaweza kusikia vionjo vya msanii
Udhaifu wake
Njia hii ni aghali kutumia, kununua vinasasauti ni gharama.
Uwasilishaji wake si hai, ingawa unaweza sikia sauti ya msanii au wahusika
lakini hahawezi kuonekana.
Kazi yoyote ya kifasihi inapohifadhiwa katika vinasasauti, kwa mfano
nyimbo, huwa ni mali ya msanii husika, mtu yeyote haruhusiwi kuitumia
kama mali yake binafsi bila kuruhusiwa na msanii.
Njia ya kompyuta
Njia hii imeanza kutumika katika miaka ya hivi karibuni baada ya watu kuanza
kujua na mna ya kutumia kompyuta.
Ubora wake
Njia hii ni ya uhakika zaidi kwa vile shuguli za kisanaa zinazohusika
huhifadhiwa katika kompyuta na hutolewa pale zinapokuwa zinahitajika.
Udhaifu
Msanii au wasanii wanohusika hawawasiliani na hadhira papo kwa papo.
Hivyo hadhira hukosa kuuliza maswali katika vipengele vinavyotatiza.
Ili kuhifadhi kazi ya fasihi kwa kutumia njia hii ni sharti msanii awe anajua
kutumia kompyuta.
Pia ni aghali sana, kuzingatia kwamba kununua komputa ni gharama kubwa.
Njia ya kanda za video
Msanii huweza kutumia kanda ya video kuhifadhi kazi yake.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 50
Ubora wake
Kwanza wasnii na vifaa wanavyotumia huonekana
Sauti zao na milio ya ala wanazotumia husikika na pia huonekana kwa
hadhira. Hii angalau huipa uhai kazi ya msanii mbele ya hadhira.
Huweza kudumu kwa muda mrefu endapo kanda ya video iliyotumika
kuhifadhi kazi ya msanii itatunzwa vizuri.
Udhaifu wake
Uhifadhi wa njia hii ni aghali, msanii atahitajika kununua, kanda ya video,
kumlipa mpiga picha na mzalishaji pia.
Watu wanoweza kunufaika na njia hii ni wacheche mno na wengi wao ni
wale wenye uwezo wa kumiliki televisheni ambao kimsingi hupatikana
maeneo ya mijini.
Ingawaje hadhira wanaweza kumwona msanii lakini hawawezi kuwasiliana
nae ana kwa ana, hivyo kukosa kuuliza swali pindi wanapohitaji kufanya
hivyo.
ZOEZI
Njia ipi ya kuhifadhi fasihi simulizi ina udhaifu wa wahusika kusikika bila ya
kuonekana na hadhira?
A Njia ya kompyuta
B Njia ya kichwa
C Njia ya maandishi
D Njia ya vinasasauti
Fani ya kazi ya fasihi simulizi huweza kupotea endapo itahifadhiwa kwa kutumia
njia ipi?
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 51
A Njia ya kanda za video
B Njia ya maandishi
C Njia ya vinasasauti
D Njia ya kichwani
Ipi ni njia yenye udhaifu wa wahusika kutokuonekana pale kazi ya fasihi simulizi
inapowasilishwa?
A Njia ya kichwani
B Njia ya kompyuta
C Njia ya vinasasauti
D Njia ya kanda za video
Ipi kati ya njia zifuatazo haitumii gharama yoyote katika kuhifadhi fasihi simulizi?
A Njia ya kanda za video
B Njia ya kompyuta
C Njia ya vinasasauti
D Njia ya kutumia kichwa
Kubadilika kwa kazi iliyohifadhiwa ya fasihi simulizi wakati wa uwasilishaji ni
udhaifu wa___
A Njia ya kichwani
B Njia ya vinasasauti
C Njia ya kanda za video
D Njia ya maandishi
Umuhimu wa kuhifadhi kazi za Fasihi Simulizi
Faida ya Kuhifadhi Fasihi Simulizi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 52
Njia zote za uhifadhi wa kazi za fasihi simulizi zina umuhimu mkubwa katika
ukuzaji na uendelezaji wa utamaduni katika jamii. Kama ambavyo tumekwishaona,
kazi za fasihi simulizi huelimisha, huburudisha, hurithisha maarifa, maadili, pia ni
vielelezo vya utamaduni wetu wa asiili. Kwa ajili hiyo ni muhimu kuzihifadhi kazi
hizo zisiharibike wala kupotea ili ziendelee kutumika kutoka kizazi kimoja hadi
kingine.
Ni muhimu ziendelee kuwepo ili kuhifadhi utamaduni wetu na huku vikitumika
kama vivutio vya watalii.
Kazi za fasihi simulizi kwa upande mwingine ni sehemu ya ajira. Kwa mfano,
shughuli mabalimbali za kisanaa kama vile ngoma, maigizo na utunzi wa vitabu,
vinawapatia vipato baadhi ya wasanii. Hivyo ni muhimu zihifadhiwe.
Kazi za fasihi simulizi pia ni kichocheo cha umoja na maelewano miongoni mwa
jamii. Yote hayo kwa ujumla wake yanabainisha kuwepo na haja ya kuendelea
kuzikusanya, kuzifanyia kazi, kuziendeleza, na kuzihifadhi kazi za fasihi simulizi.
ZOEZI
Fasihi simulizi iliyohifadhiwa ina faida gani katika lugha?
A Pambo la lugha
B Kiwakilishi cha lugha
C Ni ghala ya lugha
D Ni kivutio cha lugha
Kando na faida ya kuburudisha, kazi za fashi simulizi kama vile ngoma na maigizo
zina faida gani kwa utamaduni wa jamii?
A Kutambulisha
B Kuelimisha
C Kurithisha
D Kufundisha
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 53
Zifutazo ni faida za kuhifadhi kazi za fasihi simulizi, isipokuwa:
A Kivutio cha utalii
B Kutoa ajira
C Kurithisha utamaduni
D Kudumaza utamaduni
Fasihi simulizi ikihifadhiwa vizuri huwa dafina ya lugha, hii ina maana ya___
A Kivutio cha lugha
B Ghala ya lugha
C Msamiati wa lugha
D Sarufi ya lugha
Kazi za fasihi simulizi zitakuwa na faida kwa vizazi vijavyo endapo____.
A Zitasambazwa
B Zitafundishwa
C Zitahifadhiwa
D Zitauzwa
MADA YA 5 : UTUNGAJI WA KAZI ZA KIFASIHI
Kazi za fasihi simulizi hazikutokea tu, zilitungwa. Mtu fulani alikaa na akatunga
kazi fulani ambayo inajulikana katika jamii. Katika mada hii utajifunza kanuni
mbalimbli zinazohusika na utunzi wa kazi za fasihi simulizi. Pia utapata fursa ya
kujifunza jinsi ya kutunga kazi mbalimbali za fasihi simulizi kama vile ngonjera,
methali , nahau, vitendawili na kazi nyingine. Utajifunza pia kanuni zinazoongoza
utunzi wa kila kazi ya fasihi simulizi.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 54
Mashairi
Kanuni za Utungaji wa Mashairi
Uandishi wa kubuni unamtaka mtunzi atumie milango yake ya fahamu
kinagaubaga. Kuna milango ya fahamu mitano ambayo ni pamoja na: kuona,
kunusa, kusikia, kuhisi, na kuonja.
Kuona: je, mhusika unayemfikiria kichwani mwako unamwonaje? Umbo
lake ni la kuvutia au kuchusha? Je, macho yake yakoje – je ni ya golori au
la? Ni makubwa au madogo? Je, ni mlemavu wa macho?
Kunusa: pua zako zinakufanya usikie harufu gani? Je, ni harufu mbaya au
nzuri? Je, ni uvundo au marashi? Je, mhusika wako ananuka kikwapa au
uturi? Je, ananuka mdomo?
Kuhisi: je, unapokaa karibu naye unajihisi nini? Je, unapata mhemko
wowote au huhisi chochote? Je, akikupapasa mwilini mwako unajisikia nini?
Akikugusa bega unajisikia nini?
Kuonja: je, ukiweka kitu hicho mdomoni unaonjaje – ni chungu au tamu?
Je, ina pilipili au masala? Je, kuna chumvi au sukari? Je, kitu hicho kina
ukakasi au uchachu?
Kusikia: je, sauti unayoisikia ikoje? Inamtoa nyoka pangoni? Inakufanya
ukose usingizi? Je, ni sauti nzuri au mbaya? Ni nyororo au nzito? Kama ni
sauti ya muziki – je, iko chini au juu (kelele)?
Uzoefu wa Mwandishi
Uzoefu ni hali ya kukaa au kujishughulisha na jambo au kitu kwa muda mrefu.
Mwandishi ana uzoefu (uzoevu) wa kukabiliana na maisha kwa kiasi gani? Je, ni
matatizo gani ambayo umekutana nayo katika maisha yako? Je, ni mafanikio gani
umekutana nayo katika maisha yako? Kwa mfano, katika ajali ya MV Spice (2011)
kuna baadhi ya watu waliokolewa na magodoro ya Tanzania? Magodoro haya yana
nailoni na je kama yasingekuwa na nailoni? Uzoevu/uzoefu wako ukoje?
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 55
Uchunguzi/utafiti
Uchunguzi unapaswa ufanywe na mwandishi ili aweze kuandika jambo au tukio
bila kuongopa. Kwa kufanya udanganyifu, mwandishi atapoteza imani yake kwa
wasomaji wa kazi zake.
Uchunguzi ili ufahamu au ujue mtu, mnyama, mdudu na kadhalika – anatembeaje,
anakulaje, analalaje, anaishije, anachekaje, analiaje, anazaaje, anahusianaje na
wenzane na mazingira yake? Haya ni maswali muhimu katika kumwezesha mtunzi
kufanya utafiti wa kina ili ajue kitu anachotaka kukiandika akiandikaje na
akiwasilishaje ili aweze kuikamata hadhira yake.
Mwandishi baada ya kuzingatia mambo haya sasa anaweza kuanza kutunga kazi
yake. Hapa sisi tutajikita zaidi katika utunzi wa mashairi. Kabala hatujaenda katika
hatua ya utunzi ni muhimu kujua dhana ya shairi kwa ujumla wake, na baada ya
hapo tutakuwa tumekwisha pata maarifa yakutosha juu ya mashairi ambayo
yatatuwezesha kutunga mashairi.
Dhana ya shairi
Shairi ni kipande cha maandishi kilichopangwa kwa utaratibu katika mistari. Sauti
za silabi hufanana zikiwa kati au mwisho mwa mstari. Maandishi hayo yakisomwa
huleta ujumbe na hisia fulani ya kimaisha.
Mpango wa maneno ya shairi, ambao huweza kuimbwa hutoa picha wazi, maana
halisi na burudani ya kimuziki. Nyimbo nyingi za makabila zimepangiliwa kishairi
ijapokuwa hazikuandikwa.
Mashairi yana umbo ambalo huonekana kwa mpangilio wa sauti na idadi ya
maneno katika mistari. Umbo hili hutofautisha shairi na tenzi. Kuna mambo
kadhaa yanayotakiwa kufahamika kuhusu shairi, nayo ni:
1. Beti – Kifungu kimoja cha shairi ambacho kina uzani sawa.
2. Vina – Ni mwisho wa mistari ambayo huwa na silabi zenye sauti
ileile mwishoni mwa sentensi.
3. Mizani – Ni idadi zilizo sawa za silabi katika kila mstari, ubeti hadi ubeti.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 56
4. Kituo – Huu ni mstari wa mwisho wa ubeti. Kuna vituo vya aina tatu:Kituo
cha bahari – ni mstari unaotoka mwanzo hadi mwisho bila kubadilika katika
kila ubeti;Kituo cha kimalizio – ni kituo ambacho mstari wa mwisho maneno
yake hubadilika ubeti hadi ubeti;Kituo nusu bahari – ni mstari wa mwisho
ambao maneno yake nusu hubadilika na nusu hubaki kama ulivyo ubeti hadi
ubeti.
Katika mashairi (ya kimapokeo), kila mstari lazima uwe umekamilika na ubeti uwe
na maana kamili.
Vipengele vya fani katika mashairi
Vipengele vya fani katika shairi ni pamoja na:
Jina / anwani
Mandhari
Wahusika
Muundo –tathnia, tathlitha, tarbia, tathamisa, sabilia n.k
Mtindo – pindu, msisitizo, beti kubadilishana vina, kurudiwa kipande kizima
cha mstari wa mwisho kikiwa ni chanzo cha ubeti unaofuatia.
Vipengele vya Maudhui kati mashairi
Vipengele vya maudhui ni pamoja na: migogoro, ujumbe, falsafa, msimamo,
mtazamo, na dhamira za mwandishi.
Matumizi ya ushairi ni pamoja na: kuomboleza, kubembeleza, kuliwaza,
kufundisha, kuburudisha, kukosoa, na kadharika.
ZOEZI
Mstari wa mwisho katika kila ubeti wa shairi huitwa___
A Mizani
B Anwani
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 57
C Vina
D Kibwagizo
___ siyo sifa ya lugha inayotumika katika utunzi wa shairi.
A Mpangilio wa maneno usio wa kawaida
B Lugha inayoeleweka kwa urahisi
C Maneno ya mkato
D Lugha inayotoa picha au taswira
Jambo gani analolizingatia mtunzi wa shairi ili kuweka usiri katika shairi?
A Vituo
B Anwani
C Maana ya shairi
D Aina na idadi ya wahusika
Jina lingine la kichwa cha shairi ni___.
A Anwani
B Kituo
C Idadi ya mizani
D Maana ya shairi
Utunzi wa shairi kwa kuzingatia alama mbalimbali hujikita katika matumizi ya___.
A Anwani
B Idadi
C Vituo
D Mpangilio wa maneno
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 58
Kuigiza Ngonjera
Katika kuigiza ngonjera muigizaji hana budi kuzingatia fani yenye kanuni
zifuatazo; mtindo wa mashairi ya kimapokeo, muundo wa mashairi ya kimapokeo
wenye mizani, vina, vipande, mishororo na beti, kuteua mandhari kutegemeana na
mada, kuwepo kwa wahusika wawili au zaidi au makundi mawili au zaidi na
matumizi ya lugha ya kishairi.
ZOEZI
Muigizaji wa ngonjera hana budi kuzingatia mambo yafuatayo katika fani ya
ngonjera, isipokuwa:
A Vina
B Mizani
C Kituo
D Maonyesho
Suluhisho la tatizo linaloongelewa katika ngonjera hupatikana___mwa ngonjera.
A Mwanzoni
B Mwishoni
C Katikati
D Katikati na mwishoni
Kila ubeti katika utunzi wa ngonjera yapaswa uwe na___la kuwasilisha.
A Mambo mawili
B Jambo moja
C Mambo manne
D Mambo matatu
Muundo unaotumika katika ngonjera ni wa mashairi ya___.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 59
A Masivina
B Kimapokeo
C Mapingiti
D Kisasa
Ni lugha gani ambayo inapaswa kutumika katika kuigiza ngonjera?
A Lugha ya tamthiliya
B Lugha ya mitaani
C Lugha ya kishairi
D Lugha ya nathari
Maigizo
Kanuni za Utungaji wa Maigizo
Maigizo ni tendo la kuiga sura, tabia, matendo na mazungumzo ya watu au viumbe
wengine yaani kuiga jinsi walivyoumbwa, wanavyotembea, wanavyovaa,
wanavyosema n.k
Kanuni na hatua za kutunga maigizo
1. Kuchagua wazo, tendo, visa au tukio la kuigizwa:Ni lazima jambo hilo
liwe na uzito, umuhimu au athari fulani katika jamii. Matukio hubainika
kutokana na utafiti. Matukio yanayoweza kuwa kiini cha kutungiwa maigizo
ni kama vile matumizi mabaya ya simu za mkononi, mitindo ya mavazi,
madhara ya uganga wa kienyeji, madhara ya UKIMWI n.k.
2. Kuchagua muktadha au mahali pa kutendeka kwa jambo:Muktadha
waweza kuwa ofisini, shuleni, kijijini, mjini, barabarani, kwenye daladala
n.k
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 60
3. Kuamua mtindo wa kuwasilisha jambo la kuigizwa:Hapa mtunzi
anaweza kutumia fumbo, vichekesho, historia, tanzia n.k. Inashauriwa
mtunzi kuchanganya mbinu ili kuongeza mvuto.
4. Kupanga hoja kuu zinazojenga maudhui ya igizo:Maudhui hujikita katika
migogoro au mivutano. Suluhisho la mivutano hupatikana pale migogoro
inapofikia kilele. Kwa mfano jamabazi sugu anapokamatwa.
5. Kuweka mpangilio wa maonyesho:Maonyesho hujumuisha vitendo na
hoja zinazokamilisha sehemu inayobeba aina moja au zaidi ya maudhui.
Sehemu kadhaa nazo hukaa zikajenga kitendo ambacho hubeba jambo
mojawapo muhimu. Katika migawanyo hii yapasa mtunzi atunge kauli na
vitendo vinavyoandamana navyo.
6. Kubuni wahusika na kuweka aina au idadi yao kulingana na
matukio:Mtunzi anashauriwa kutumia wahusika wanaohitilafiana. Kwa
mfano wazee, vijana, wanawake, wanaume, wanene, wafupi n.k. Mtunzi
akishawateua anaweza kuwatungia kauli na zamu za matendo katika sehemu
mbalimbali.
7. Ni muhimu pia kwa mtunzi kuwaumba wahusika wake na kuamua
maleba yao:Uamuzi huu yapasa ufanywe kwa kuzingatia mazingira. Kwa
mfano siku hizi sio lazima wahusika wazee kuvaa ngozi, kutumia mkongojo
na kuvuta mtemba.
8. Urefu wa maigizo ni suala la kuamliwa kutegemea tukio
9. Kutunga maelezo kuhusu mandhari:Maumbile ya wahusika na vitendo
vyao, ni muhimu kuelezwa katika mabano.
10. Kuandika maigizo na kuhariri:Ni muhimu kutumia lugha ya
kimazungumzo inayovutia, yenye kuleta taharuki na yenye utamu unaoeleza
maadili kwa mnato.
ZOEZI
___hujumuisha vitendo na hoja zinazokamilisha sehemu inayobeba maudhui
katika maigizo.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 61
A Mbinu
B Mada
C Tukio
D Maonyesho
Aina na idadi ya wahusika katika utunzi wa maigizo hutegemea___.
A Matukio
B Maonyesho
C Mada
D Mtindo
Ni kanuni gani katika utungaji wa maigizo ambayo hukazia umuhimu na uzito wa
jambo husika kwa jamii?
A Kupanga hoja kuu
B Kuamua mtindo
C Kuchagua muktadha
D Kuchagua wazo
___ siyo mtindo unaotumiwa kuwasilisha maigizo.
A Vichekesho
B Tanzia
C Fumbo
D Majibizano
Uamuzi wa mavazi ya kuigizia katika maigizo unapaswa ufanywe kwa
kuzingatia___
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 62
A Visa
B Mazingira
C Hoja
D Mada
MADA YA 6 : UANDISHI
Insha za Hoja
Insha za hoja ni insha zinazoelezea jambo fulani katika hali ya kujenga hoja
ambazo zinatetea msimamo fulani alionao mwandishi wa insha hiyo juu ya jambo
analolizungumzia. Hoja ni maelezo bayana yanayotolewa na mwandishi kutetea
msimamo wake.
Katika uandishi wa insha za aina hii, mwandishi hutakiwa kuonesha ni jambo gani
ambalo analiunga mkono na ni lipi ambalo hakubaliani nalo.
Ili hoja zote zipate kueleweka ni sharti zipangwe katika mtiririko wa mawazo ulio
sahihi kiasi kwamba mtu aisomapo anapata kuelewa ni mada gani mwandishi
anaijadili na ana msimamo gani kuhusu mada hiyo.
Muundo wa Insha za Hoja
Katika uandishi wa insha, muundo wake unakuwa na vitu vifuatavyo:
1. Kichwa cha insha; kichwa cha insha hudokeza kile ulichokijadili katika
insha yako. Kwa mfano: Madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya n.k
2. Utangulizi; Mambo yaliyopo katika utangulizi ni pamoja na kutoa fasili ya
maneno muhimu na kuelezea kwa muhtasari mambo ambayo utakwenda
kuyajadili katika insha yako.
3. Kiini cha insha;katika kiini ndipo kuna maelezo ya kina juu ya kile
unachokijadili katika insha yako, maelezo haya yanakuwa katika aya kadhaa
kulingana na idadi ya hoja ulizonazo katika mjadala wako.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 63
4. Hitimisho; hapa ndipo kuna muhtasari wa kile kilichojadiliwa katika kiini
cha insha au inaweza kuwa ni msimamo juu ya kile kilichohadiliwa katika
insha
ZOEZI
___ni sehemu katika muundo wa insha za hoja ambapo mada hujadiliwa.
A Utangulizi
B Hitimisho
C Kiini cha insha
D Kichwa cha insha
Mkazo wa jambo lililojadiliwa katika insha hutolewa katika___.
A Kichwa cha insha
B Hitimisho
C Utangulizi wa insha
D Kiini cha insha
Maelezo mafupi yanayodokeza mada inayojadiliwa katika insha za hoja hutolewa
katika sehemu ya___
A Kiini cha insha
B Hitimisho
C Utangulizi
D Kichwa cha insha
Kipi kati ya hivi ni muhimu kuandikwa kwa herufi kubwa katika muundo wa insha
za hoja?
A Utangulizi wa insha
B Kichwa cha insha
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 64
C Kiini cha insha
D Hitimisho la insha
Muhtasari na msisitizo wa kile kilichojadiliwa katika insha za hoja hutolewa katika
kipengele gani?
A Hitimisho
B Kiini cha insha
C Utangulizi
D Kichwa cha insha
Barua Rasmi
Dhima ya Barua Rasmi
ZOEZI
Ipi ni dhima ya barua rasmi inapotumika kuwaita watu kuhudhuria sherehe au
harusi?
A Kuomba kazi
B Kutoa mwaliko
C Kuagiza vitu
D Kutoa taarifa
Barua rasmi zinapoandikwa na kutunzwa kwa matumizi ya baadae huwa na dhima
ya___
A Kuweka kumbukumbu
B Kuomba kazi au huduma
C Kutoa malalamiko
D Kutoa taarifa
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 65
Barua rasmi hutumika kurahisisha mawasiliano katika shughuli za___.
A Kisiasa
B Kiutamaduni
C Kijamii
D Kiofisi
Barua rasmi huwa na dhima gani inapoandikwa na mtu ili kukiri kosa?
A Kuombea cheo
B Kutolea malalamiko
C Kuombea msamaha
D Kuombea kazi
Barua rasmi huweza pia kuitwa___.
A Barua za magazetini
B Barua za kiofisi
C Barua za simu
D Barua za maandishi
Barua rasmi ni barua zinazohusu mambo rasmi ya kiofisi. Dhima za barua rasmi ni
kutoa taarifa, kuomba kazi au huduma, kuagiza vitu na kutoa mwaliko kwa mfano
kwa kiongozi fulani wa nchi, kutoa malalamiko na kuweka kumbukumbu au
marejeo.
Muundo wa Barua Rasmi
Barua rasmi au barua ya kiofisi/kibiashara huzingatia mtindo rasmi wa barua. Kwa
kawaida huwa na sehemu zifuatazo:
1. Anwani ya mwaandishi -huwekwa juu kabisa na huwa katika upande wa
kulia wa karatasi.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 66
2. Tarehe ya barua hiyo- tarehe huandikwa chini ya anwani ya mwandishi
3. Anuwani ya mpokeaji- Anwani ya anayeandikiwa huwa katika upande wa
kushoto wa karatasi, na huwekwa msitari mmoja chini ya tarehe.
4. Salamu- Chini ya anwani ya mpokeaji, barua huanza kwa kumrejelea
mpokeaji kama bwana au bi. Ni makosa kumsalimia mpokeaji wa barua
rasmi au kumwuliza hali yake.Ndugu Bwana Meshaki, => taja jina lake
ikiwa mnajuana na unayemwandikia. Kwa Bw/Bi, => Ikiwa humjui
mpokeaji wa barua, tumia bw/bi
5. Mada- Kichwa cha barua rasmi huja pindi tu baada ya salamu.
Hutangulizwa na maneno kama vile YAH:(yahusu). Ni sharti kichwa
kiandikwe kwa herufi kubwa na kipigiwe mstari. Kichwa kinapaswa kuwa
kifupi na kinachoelezea mada ya barua kiukamilifu.
6. Utangulizi– Hukaa chini kidogo ya mada ya barua. Haya ni maelezo mafupi
yasiyozidi aya moja ambayo huelezea kusudi kuu la barua kama kidokezo.
7. Ujumbe- Ujumbe wa barua rasmi lazima uwe mfupi na unaotumia lugha
rasmi.
8. Tamati– mwandishi humalizia kwa maneno ya hitimisho kama vile: Wako
mwaminifu, [jina], Sahihi
ZOEZI
Kipengele cha wadhifa wa mwandishi katika muundo wa barua rasmi huandikwa
baada ya kipengele cha___
A Hitimisho la barua
B Jina kamili la mwandishi
C Tarehe
D Kiini cha barua
Kipengele gani cha muundo wa barua rasmi kinachotoa msisitizo na kutia mkazo
kile kilichoandikwa?
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 67
A Kichwa cha barua
B Mwisho wa barua
C Utangulizi wa barua
D Kiini cha barua
Wadhifa wa mwandikiwa barua hutajwa katika kipengele gani cha muundo wa
barua rasmi?
A Kiini cha barua
B Anwani ya mwandikiwa
C Anwani ya mwandishi
D Tarehe
Vifuatavyo ni vipengele katika muundo wa barua rasmi, isipokuwa:
A Anwani ya mwandishi
B Namba ya kumbukumbu ya barua
C Tarehe
D Maamkizi
___ni kipengele cha muundo wa barua rasmi kinachorahisisha urejeaji wa barua
katika majalada.
A Mwanzo wa barua
B Namba ya kumbukumbu ya barua
C Anwani ya mwandishi
D Tarehe
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 68
Simu
Dhima ya Simu ya Maandishi
Simu za maandishi ni aina ya barua fupi ambazo husafirishwa kwa haraka sana
kuliko barua za kawaida.
Simu hizo huandikwa kwenye fomu maalumu ambazo hutolewa na shirika la
posta. Simu za maandishi hujulikana kama telegram.
Kwa kawaida simu za maandishi hutumika kutuma ujumbe wa dharura. Kuandika
simu za maandishi ni njia ya haraka ya kufikisha ujumbe kwa sababu, baada ya
kuandika simu yako ujumbe humfikia huyo unayemtumia katika muda usiozidi
siku tatu.
Gharama za simu za maandishi hutozwa kulingana na idadi ya maneno
yaliyotumika. Kwa hiyo ujumbe unaotumwa huandikwa kwa maneno machache ili
kuepuka kutozwa gharama kubwa.
Mfano wa simu ya maandishi:
MUSA KINGAMBE SLP 5299 DSM
NJOO HARAKA DADA MGONJWA
LINGIDO
ZOEZI
Simu ya maandishi ina dhima gani inapowezesha watu walio mbali kuwasiliana
kwa urahisi?
A Kuokoa gharama
B Kurahisisha mawasiliano
C Kuokoa muda
D Kuonesha umuhimu wa ujumbe
Simu ya maandishi ina dhima zifuatazo, isipokuwa:
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 69
A Kutoa mwaliko
B Kurahisisha mawasiliano
C Kufikisha ujumbe kwa haraka
D Kuokoa muda
Gharama ya simu ya maandishi hutozwa kulingana na___.
A idadi ya maneno
B umuhimu wa ujumbe
C muda uliotumika
D ukubwa wa maneno
Kutokana na dhima ya kuokoa muda na kuepusha gharama simu maandishi huwa
na___.
A Maneno mengi
B Maneno machache
C Maneno magumu
D Maneno rahisi
Simu za maandishi hutolewa na nani?
A Benki
B Mamlaka ya mawasiliano
C Posta
D Makampuni ya simu
Kuandika Simu za Maandishi kwa Kuzingatia Muundo na Taratibu za Uandishi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 70
Muundo wa kuandika simu za maandishi una mambo yafuatayo ya kuzingatia
ambayo ni anwani ya mpelekewa taarifa, ujumbe na jina la mwandishi au mtuma
simu. Mambo mengine ya kuzingatia ni kuandika maneno yote kwa herufi kubwa
ili kurahisisha usomaji na kuandika simu ya maandishi katika karatasi maalumu
ambayo hutolewa na posta.
ZOEZI
___ ni aina ya barua fupi ambazo husafirishwa kwa haraka sana kuliko barua za
kawaida.
A Barua rasmi
B Simu ya maandishi
C Simu ya mdomoni
D Simu ya magezetini
Muundo wa simu za maandishi una sehemu ngapi muhimu?
A Sita
B Nne
C Tatu
D Tano
___katika simu ya maandishi huwa ni mfupi na unaoeleweka kwa urahisi.
A Ukurasa
B Hitimisho
C Utangulizi
D Ujumbe
Jina lingine la simu ya maandishi ni___.
A Telegramu
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 71
B Simu ya haraka
C Simu ya mkononi
D Simu ya dharura
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia katika muundo wa simu ya maandishi,
isipokuwa:
A Ujumbe
B Anawani ya mpelekewa taarifa
C Tarehe
D Jina la mwandishi
Kadi za Mialiko
Kadi za mialiko ni aina ya karatasi ngumu zinazopeleka taarifa fupi za kumwomba
mtu ahudhurie katika sherehe fulani kama vile harusi, ubatizo mahafali n.k
Muundo wa Kadi ya Mialiko
Mambo muhimu yanayotakiwa kuonyeshwa katika kadi ya mwaliko:
1. Jina la mwandishi au mwalikaji
2. Jina la mwalikwa, ni muhimu kuandika cheo chake kama vile: Profesa, Bi.,
Bw. Bw&Bi n.k
3. Lengo la mwaliko
4. Mahali pa kufanyika shughuli
5. Tarehe ya mwaliko
6. Wakati wa shughuli
7. Jina na anwani ya mtu atakayepelekewa majibu.
Mialiko huweza kuandikwa kwa namna mbili yaani kama barua au kadi. Jina la
mwalikwa katika kadi ya mwaliko hutakiwa kuanza na maneno ya heshima kama
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 72
vile Bwana….Bi…..au Ndugu…ikiwa waalikwa ni mume na mke kadi itaanza na
Bwana na Bibi.
Mfano wa Kadi ya Mwaliko
Familia ya Marandu wa Mto wa Mbu
Wanapenda kukualika/kuwaalika Profesa/Dkt/Shekhe/Padri/Bi/Bw/Bw&Bi………
kwenye harusi ya kijana wao mpendwa Ibahim Joseph itakayofanyika huko Mto wa
Mbu katika ukumbi wa simba siku ya Jumapili tarehe 9/12/2016 sasa 8.00 mchana
hadi saa 3.00 usiku
Kufika kwako ndio mafanikio ya sherehe hii.
Majibu kwa (wasiofika tu)
Joseph Marandu
Simu: 0717104507
ZOEZI
___huandikwa kwa ufupi na kwa uwazi katika kadi za mialiko.
A Tarehe ya mwaliko
B Jina la mwalikaji
C Mahali pa kufanyia shughuli
D Lengo la mwalikaji
Katika kadi ya mwaliko, majina ya vyeo kama vile „Profesa na Shekhe‟ hufuatana
na___.
A Terehe ya mwaliko
B Jina la mwalikwa
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 73
C Lengo la mwalikaji
D Jina la mwandishi
___ni kipengele katika muundo wa kadi za mialiko kinachotoa nafasi ya kutoa
majibu kwa aliyeandika.
A Jina la mwalikwa
B Lengo la mwalikaji
C Jina ya mwandishi
D Jina na anwani
___ni aina ya karatasi ngumu zinazopeleka taarifa fupi za kumwomba mtu
ahudhurie katika sherehe fulani.
A Barua za kirafiki
B Barua rasmi
C Kadi za mwaliko
D Barua za magezetini
Kipi kati ya hivi siyo kipengele katika muundo wa kadi za mialiko?
A Tarehe ya mwaliko
B Lengo la mwalikaji
C Kichwa cha habari
D Jina la mwandishi
Uandishi wa Dayalojia
Dhana ya Dayolojia
Dayalojia ni mazungumzo au majibizano baina ya watu wawili au zaidi
wanaozungumza kwa kupokezana. Kama zilivyo kazi nyingine za utunagaji,
dayalojia inaweza kuwasilishwa kwa nijia ya mazungumzo au maandishi.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 74
Katika kutunga dayalojia mtunzi hana budi kujifanya kama mhusika katika
dayalojia hiyo. Kwanza anapaswa kutafakari kwa makini mada anayokusudia
kuandikia dayalojia, kutayarisha na kupanga mawazo kimantiki na kwa mtiririko
na kufikiria wahusika na kuwapangia majukumu kulingana na matendo yao. Kwa
mfano kama mhusika ni mkulima, lugha anayopewa, vifaa anavyosemekana
kuvitumia na mandhari aliyomo ni lazima vifanane na hali ya mkulima halisi.
Mambo ya kuzingatia katika dayalojia ni pamoja na haya yafuatayo:
1. Kutoa maelezo ya ufafanuzi katika mabano ili kumfahamisha
2. Kuwa na mazungumzo ya mkato na yasiyozidiana sana kati ya wahusika.
Mhusika mmoja asitawale mazungumzo kupita wengine.
3. Kutumia vihisishi ili kufanya dayalojia iwe ya kusisimua
4. Pawepo mwingiliano wa mazungumzo ya wahusika na kudakia maneno ili
dayalojia iwe na uhalisia.
Mfano wa dayalojia
Wambura:
(Anaonekana mwenye furaha,anamwita rafiki yake,
Anna)Wow, Anna! Tumekutana tena, siamini macho
yangu! (wanakumbatiana wote wakiwa na nyuso za
furaha).
Anna:
(Anatabasamu huku ameshikilia mkono wa kulia wa
Wambura, anaonesha shauku kuu)Wambura! Bado
unanikumbuka? Nina furaha sana kwa kweli, ni muda
mrefu sana.
Wambura:
(Anachekelea)Aaaah, nahisi kama naota Neema, siamini
kama nimekutana na wee leo hii ni muda mrefu sana,
nimefurahi kwa kweli.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 75
Anna: (Anachekelea)
Wambura: Mbona wachekelea tu….
ZOEZI
Mwingiliano wa mazungumzo ya wahusika na kudakia maneno huifanya dayalojia
iwe na___.
A Uhalisia
B Mvuto
C Mashiko
D Ukinzani
Wahusika katika dayalojia wanapaswa kupangiwa majukumu kulingana na nini?
A Matendo yao
B Maelezo yao
C Mitazamo yao
D Msimamo wao
Lugha na maneno ya wahusika katika dayalojia hutegemea___.
A Shughuli walizopewa
B Mtunzi
C Sarufi
D Msimamo wa wahusika
Mtunzi wa dayalojia anapaswa kujifanya kuwa___.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 76
A Hadhira
B Muulizaji
C Mhusika
D Mhakiki
Wahusika katika dayalojia huzungumza kwa___.
A Kukejeli
B Madaha
C Kupokezana
D Kugombana
MADAYA 7 USIMULIZI
Usimulizi ni jumla ya maelezo yanayotolewa na mtu au watu wengi kuhusu tukio
fulani. Tukio hilo linaweza kutokea katika wakati mfupi uliopita au zamani kidogo.
Usimuliaji wa Matukio
Njia za Usimulizi wa Matukio
Usimulizi hufanyika kwa njia kuu mbili yaani kwa njia ya maandishi na kwa njia
ya masimulizi ya mdomo. Kila njia hutegemea kwa namna msimuliaji anavyoweza
kuwasiliana na msikilizaji. Ikiwa msimuliaji na msikilizaji hawakukaribiana, njia
ambayo itatumika ni ile ya maandishi. Kwa mfano kama utahitaji kumweleza mtu
aliyembali kuhusu tukio fulani la kusisimua utalazimika kutumia maandishi, yaani
utatumia njia ya kumwandikia barua.
Lakini kama unamsimulia mtu ambaye yupo karibu nawe, utatumia njia ya
mazungumzo ya ana kwa ana.
Taratibu za usimulizi wa matukio
Usimulizi wa matukio dhamira yake ni kumweleza mtu au watu tukio ambalo wao
hawakulishuhudia. Hivyo katika usimulizi msimuliaji hutakiwa kutoa maelezo
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 77
muhimu ambayo yatawawezesha watu hao kulielewa tukio linalosimuliwa
sawasawa na huyo anayeshuhudia.
Mambo muhimu ya kutaja katika usimulizi wa matukio ni pamoja na haya
yafuatayo:
1. Aina ya tukio – msimuliaji atatakiwa kubainisha katika maelezo yake aina
ya tukio. Kwa mfano, kama ni harusi, ubatizo, ajali ya barabarani au
mkutano.
2. Mahali pa tukio – ili msimuliaji aweze kuielewa habari inayosimuliwa, ni
lazima kumwelewesha ni mahali gani tukio hilo limetokea. Kwa mfano,
kama ni mjini inafaa kutaja hata jina la mtaa.
3. Wakati – katika usimulizi ni muhimu pia kutaja muda ambao tukio
limetendeka kama ni asubuhi, mchana au jioni bila kusahau kutaja muda
halisi yaani ilikuwa saa ngapi.
4. Wahusika wa tukio – ni muhimu kutaja tukio limehusisha watu gani, wingi
wao, jinsia yao, umri wao n.k.
5. Chanzo cha tukio – kila tukio lina chanzo chake hivyo ni muhimu kutajwa
katika usimulizi.
6. Athari za tukio – athari za tukio nazo ni sharti zibainishwe. Kama ni ajali,
je watu wangapi wameumia; wangapi wamepoteza maisha n.k.
7. Hatima ya tukio – msimuliaji katika usimulizi wake ni lazima abainishe
baada ya tukio kutokea na kushughulikiwa hatima yake ilikuwaje. Kwa
mfano, kama tukio ni ajali ya barabarani hatima yake inaweza kuwa
majeruhi kupelekwa hospitalini na dereva aliyehusika kukamatwa.
Kwa hiyo misingi hii ya usimulizi hufanya usimulizi wa tukio kuwa na sehemu
kuu tatu:
Utangulizi – sehemu hii huwa na maelezo tu ya utangulizi ambayo hulenga
kuvuta hisia na umakini wa msikilizaji au wasikilizaji. Kwa kawaida
utangulizi wa tukio huwa ni maneno machache kiasi yasiyozodi aya moja.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 78
Kiini – kiini cha usimulizi huelezea tukio halisi kuanzia chanzo chake,
wahusika, muda, mahali na athari za tukio.
Mwisho – mwisho wa usimulizi ni matokeo yanayoonyesha matokeo ya
mwisho ya tukio linalohusika, wakati mwingine matukio haya yanaweza
kuambatana na maelezo ya msimuliaji kuhusu mtazamo au maoni yake
binafsi juu ya tukio ambalo amesimulia.
Mbinu za usimulizi
Ili habari inayosimuliwa ipate kueleweka vizuri, sharti msimuliaji ajue mbinu za
kusimulia katika hali inayovuta hisia za msikilizaji wake.
Baadhi ya mbinu hizo ni uigizi, utumizi wa lugha fasaha inayozingatia lafudhi
sahihi ya Kiswahili.
Kwa upande wa uigizi msimuliaji atatakiwa kuigiza mambo muhimu
yanayohusiana na tukio ambalo anasimulia. Nayo ni kama vile milio, sauti na
matendo.
Kwa upande wa usimulizi ambao unafanyika kwa njia ya maandishi, sharti
usimulizi huo uwe na kichwa cha habari. Kichwa cha habari kinatakiwa kuandikwa
kwa maneno yasiyozidi matano, yaliyoandikwa kwa herufi kubwa.
Kwa vile usimulizi wa tukio huwa unahusu tukio lililopita, maelezo yake mengi
huwa katika wakati uliopita.
ZOEZI
Kipi kati ya hivi ni cha muhimu katika njia ya usimulizi wa kutumia maandishi?
A Kichwa cha habari
B Watazamaji
C Lafudhi
D Msikilizaji
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 79
___hutakiwa kuandikwa kwa herufi kubwa katika njia ya usimulizi wa kutumia
maandishi.
A Kiini
B Utangulizi
C Kichwa cha habari
D Hitimisho
___ni maelezo ambayo hulenga kuvuta hisia na umakini wa msikilizaji katika njia
za usimulizi wa matukio.
A Mahali pa tukio
B Kiini cha usimulizi
C Hitimisho
D Utangulizi
___ni kipengele katika usimulizi ambacho hutaja aina ya watu, wingi wao na umri
wao.
A Wakati
B Mahali pa tukio
C Wahusika wa tukio
D Aina ya tukio
___ ni jumla ya maelezo yanayotolewa na mtu au watu wengi kuhusu tukio fulani.
A Ufahamu
B Ufupisho
C Ngonjera
D Usimulizi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 80
MADA YA 8 UFAHAMU
Ufahamu ni dhana inayorejelea kujua na kulielewa jambo kwa usahihi na kuweza
kulielezea upya kwa usahihi bila kupoteza maana yake ya msingi. Ufahamu wa
mtu waweza kupimwa katika kusikiliza jambo au katika kusoma.
Ufahamu wa Kusikiliza
Ufahamu wa kusikiliza ni zaidi ya kusikiliza tu kile kilichosemwa; badala yake ni
uwezo wa mtu kuelewa maana ya maneno anayoyasikia na kuweza kuhusiana nayo
kwa namna fulani. Kwa mfano mwanafunzi anaposikiliza hadithi, ufahamu mzuri
wa kusikiliza humsaidia kuielewa hadithi hiyo, kuikumbuka, kuijadili, na hata
kuisimulia tena kwa maneno yake mwenyewe.
Kujibu Maswali ya Ufahamu kutokana na Habari uliyoisikiliza
Jibu maswali ya ufahamu kutokana na habari uliyoisikiliza
Ufahamu wa kusikiliza unahusisha michakato kadhaa katika kuelewa na kupata
maana ya kile kinachozungumzwa. Michakato hii inahusisha:
Kuelewa vizuri sarufi ya lugha ile inayozungumzwa
Kuelewa vyema maana ya maneno ya mhusiaka anayezungumza
Kuelewa sintaksia (muundo wa maneno) ya sentensi kwa namna
zinavyowasilishwa.
Katika ufahamu wa kusikiliza, msikilizaji hana budi kuzingatia mambo yafutayo:
1. Kuwa makini na kuelekeza akili yote kwa mzungumzaji ili kuweza kusikia
kila anachokisema.
2. Kutilia maanani vidokezo vya maana ili kubaini iwapo msemaji anaongeza
jambo jipya, anatofautisha, anafafanua au anahitimisha hoja.
3. Msomaji anatakiwa kuandika baadhi ya mambo anayoona kuwa ni ya
muhimu ili kumasidia kukumbuka hapo baadae.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 81
4. Kuwa makini na ishara mbambali za mwili kama vile kurusha mikono,
kutingisha kichwa, kutingisha mabega au hata kupepesa macho. Ishara hizi
huwa zinachangia kwa kiasi kikubwa kupata maana katika mazungumzo.
Kufupisha kwa Mdomo Habari uliyoisikiliza
Ili kuweza kufupisha kwa mdomo habari uliyoisikiliza yapo mambo ya kuzingatia.
Mambo hayo ni kubaini mawazo makuu yanayopaswa yajitokeze katika habari
iliyofupishwa, kupanga maelezo kwa usahihi katika usemaji, kuzingatia kichwa
cha habari ambacho kinapaswa kihusiane na ufupisho na wazo kuu na mwisho ni
kusema ufupisho kwa ufasaha na kwa lugha ambayo ni nzuri.
ZOEZI
Lipi kati ya haya ni muhimu kuzingatia katika ufupisho wa kusema kwa mdomo?
A Matumizi ya lugha fasaha
B Idadi ya maneno
C Aina ya matini
D Aina ya maswali
Nini kinapaswa kibainishwe katika kila aya ya habari unayoisikiliza ili kuifupisha
kwa mdomo?
A Idadi ya mistari
B Mawazo makuu
C Maneno ya ziada
D Ishara za mwili
Kupanga maelezo kwa usahihi katika kufupisha habari kwa mdomo kunasaidia
nini?
A Kusema kwa ufupi
B Mtiririko wa mawazo
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 82
C Kuelewa kichwa cha habari
D Kuelewa wazo kuu
Kichwa cha habari katika habari iliyofupishwa ni lazima kihusiane na ___.
A Vidokezo vya maana
B Idadi ya maneno
C Maneno ya mzungumzaji
D Wazo kuu
Ufupisho wa kusema kwa mdomo hutokana na___.
A Mtiririko wa hoja
B Mawazo makuu
C Maswali
D Habari uliyoisikiliza
Ufahamu wa Kusoma
Ufahamu wa kusoma ni ule mtu anaoupata kwa njia ya kusoma makala, kifungu
cha habari, kitabu au gazeti.
Kusoma kwa Sauti kwa kuzingatia Lafudhi ya Kiswahili
Kuna vipengele viwili vinavyounda mchakato wa ufahamu wa kusoma:
Uelewa wa msamiati na
Uelewa wa matini
Ili kuilelewa habari/matini ni lazima msomaji awe na uwezo wa kuelewa msamiati
uliotumika katika matini hiyo. Endapo maneno yaliyotumika hayataeleweka
vilevile matini yote hataeleweka.
Katika ufahamu wa kusoma, msomaji anatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 83
1. Kubaini mawazo makuu; msomaji anaposoma habari fulani au kitabu
inatakiwa ajiulize, Je, kinachoongelewa hapa ni nini? Ni jambo gani hasa
analolizungumzia mwandishi? Msomaji akiwa na maswali haya akilini
mwake basi itakuwa rahisi kwake kuielewa habari hiyo.
2. Kuzingatia alama za uakifishi; msomaji ni lazima azingatie alama za
uakifishi, kwa kufanya hivyo itamsaidia kuelewa ujumbe wa habari hiyo na
endapo hatazingatia alama za uakifishaji anaweza kupotosha maana ya
mwandishi.
3. Kubaini maana ya maneno na misemo mbalimbali; habari nyingine huwa
zina maneno ya kisanaa hivyo ni muhimu msomaji kubaini maana ya
maneno hayo katika muktadha wa habari hiyo, hii itamsaidia kuelewa vyema
maana ya mwandishi.
4. Vilevile msomaji anatakiwa kumakinikia kile anachokisoma, kila kipengele
anachokisoma inampasa akielewe vizuri.
Kwa kuzingatia haya yote msomaji atakuwa na uelewa mzuri juu ya habari
aliyoisoma na pia anaweza kufupisha habari hiyo aliyoisoma.
ZOEZI
Katika kusoma kwa sauti kwa kuzingatia lafudhi ya Kiswahili ni alama gani ya
kituo huonesha hali ya furaha?
A Alama ya kuuliza
B Alama ya mshangao
C Alama ya koma
D Alama ya nukta
Kusoma kwa sauti kwa kuzingatia lafudhi ya Kiswahili humaanisha kuzingatia___.
A Matini za Kiswahili
B Fasihi
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 84
C Usahihi wa matamshi ya Kiswahili
D Matamshi ya lugha zote
Ipi siyo mojawapo ya alama za vituo zinazopaswa kuzingatiwa na msomaji pale
anaposoma kwa sauti?
A Nukta
B Kidahizo
C Nukta pacha
D Mkato
___huonesha kupanda na kushuka kwa sauti katika kusoma kwa sauti kwa
kuzingatia lafudhi ya Kiswahili.
A Msito
B Vituo
C Kiimbo
D Matamshi
Usomaji wa sauti kwa kuzingatia lafudhi ya Kiswahili husaidia___.
A kuwa mkalimani mzuri
B Kuokoa muda
C Kujifunza maneno ya lugha
D Kufaulu mitihani
Kujibu Maswali kutokana na Habari uliyoisoma
Ili kujibu maswali yanayotokana na habari uliyoisoma inatakiwa kuzingatia
mambo yafuatayo; kubaini mawazo makuu, kuzingatia alama za uandishi, kubaini
maana ya maneno na misemo mbalimbali na kutilia maanani vidokezo vya maana.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 85
Aidha mawazo yanapaswa kuelekezwa katika jambo linalosomwa, kujiuliza
maswali kadri unavyosoma na kuandika ufupisho.
ZOEZI
Vidokezi vya maana kama vile „lakini, isipokuwa na hata hivyo‟ hutumika ___
A Kutofautisha
B Kuongeza wazo
C Kuonesha mtiririko
D Kuhitimisha
Maana ya mwandishi katika habari inaweza kupotoshwa endapo msomaji
hatazingatia___
A Idadi ya maneno
B Aya
C Alama za uandishi
D Aina ya insha
Msomaji anapaswa afanye nini kadri anavyosoma ili kujibu maswali yatokanayo
na habari husika?
A Kuhesabu maneno
B Kujiuliza maswali
C Kusoma kwa sauti
D Kukaa kimya
Yafuatayo yanapaswa yazingatiwe katika usomaji ili kujibu maswali ya habari
husika, isipokuwa:
A Aina ya ufahamu
B Mawazo makuu
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 86
C Alama za uandishi
D Vidokezi vya maana
Mbinu ipi husaidia kuelewa hitaji la swali wakati wa kujibu maswali ya habari
uliyoisoma?
A Kukosa umakini
B Kujibu kwa urefu
C Kusoma kwa makini
D Kukaa kimya
Kufupisha Habari uliyoisoma
Ili kuandika ufupisho mzuri wa habari uliyosoma yapaswa kuzingatia yafuatayo:
kuisoma habari uliyopewa zaidi ya mara moja, kubainisha mawazo makuu,
kuandika ufupisho kwa lugha fasaha na yenye mtirirko mzuri wa hoja, kuhesabu
idadi ya maneno na kuhakikisha haizidi idadi inayotakiwa na kupitia habari ya
mwanzo na kisha ufupisho ili kuona kama taarifa muhimu haijaachwa au
kusahaulika.
ZOEZI
Kutambua mawazo makuu katika habari ni sawa na ___ mawazo makuu.
A Kufafanua
B Kuandika
C Kubaini
D Kueleza
Katika ufupisho wa habari uliyoisoma ni muhimu kuonesha___.
A Maswali
B Njeo
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 87
C Kichwa cha habari
D Nafsi
___ni kitendo cha kuifanya habari ndefu kuwa fupi na kwa maneno machache pia.
A Kubainisha mawazo
B Ufahamu
C Ufupisho
D Kufupisha habari
___hufanyika ili kuhakikisha idadi ya maneno haizidi ile inayohitajika katika
ufupisho wa habari.
A Kupitia habari yote
B Kupunguza mawazo makuu
C Kuhesabu maneno
D Kurudia habari
Kipi kati ya hivi hakitakiwi kukosa kwenye habari iliyofupishwa?
A Mawazo makuu
B Vivumishi
C Vielezi
D Maneno ya ziada
Kusoma kwa Burudani
Huu ni usomaji ambao lengo lake kuu huwa ni kujiburudisha tu. Katika usomaji
wa aina hii, msomaji hujisomea zaidi magazeti, majarida na vitabu tofauti na vile
vinavyotumika darasani.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 88
Wakati mwingine sio lazima msomaji awe na vitabu vyote ambavyo anahitaji
kuvisoma au magazeti na majarida. Inapotokea hivyo, msomaji anaweza kwenda
maktaba kuazima kitabu nachokihitaji.
Ingawa lengo la msomaji huwa ni kujiburudisha tu, lakini pia hujiongezea maarifa.
Hii ni kwa sababu, magazeti, majarida na vitabu sambamba na kutumia lugha
sanifu huelezea mambo mabalimbali yanayoihusu jamii.
Msomaji kutokana na kusoma vitabu na majarida mbalimbali hujiongezea kiwango
cha welewa wa lugha na mambo mengine ya kijamaii yanayojadiliwa humo.
Ni jambo zuri kwa msomaji kujijengea tabia ya kujipima ili aweze kuelewa
kiwango cha maarifa aliyopata katika kujisomea. Kujipima huku kunaweza
kufanywa kwa kujiundia utaratibu w kuweka kumbukumbu ya vitu au makala
zilizosomwa na kufanya ufupisho wa kila makala.
Utaratibu unaopendekezwa katika kujipima na kujiwekea kumbukumbu ya usomaji
wa burudani ni kama ufuatao:
1. Tarehe...
2. Jina la kitabu/makala/gazeti....
3. Mchapishaji......
4. Mwaka/tarehe ya uchapishaji.....
5. Ufupisho wa habari(yasizidi maneno 20)
6. Fundisho/ujumbe mkuu ni.....
7. Jambo lililokuvutia sana......
8. Maoni kwa ujumla kama yapo...
ZOEZI
Kupitia usomaji wa burudani msomaji huweza kuelewa kiwango cha maarifa
aliyopata kwa kuwa na tabia ya___.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 89
A Kukariri
B Kununua vitabu
C Kuazima vitabu
D Kujipima
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia katika usomaji wa burudani, isipokuwa:
A Kuweka kumbukumbu
B Kuandaa vitabu au makala
C Kujiburudisha
D Kufanya ufupisho wa kinachosomwa
___ni mojawapo ya kipengele cha kujiwekea kumbukumbu katika usomaji wa
burudani.
A Mawazo makuu
B Utangulizi
C Fundisho kuu
D Kiini cha habari
___ni mahali maalumu ambapo msomaji anaweza kuazima kitabu kwa ajili ya
kujisomea kwa burudani.
A Ofisini
B Maabara
C Dukani
D Maktaba
Lipi kati ya haya ni jambo la kuzingatia katika usomaji wa burudani?
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 90
A Kujipima
B Kujiandaa kwa mtihani
C Kujibu maswali
D Kuweka kumbukumbu
Matumizi ya Kamusi
Kamusi ni kitabu cha marejeo chenye msamiati uliokusanywa kutoka kwa
wazungumzaji wa jamii fulani na kupangwa katika utaratibu maalumu, kisha
kufafanuliwa kwa namna ambayo wasomaji wanaweza kuelewa. Au kamusi ni
orodha ya maneno yaliyo katika karatasi au nakala tepe yaliyopangwa kialfabeti na
kutolewa maana pamoja na maelezo mengine na kuhifadhiwa katika kitabu,
santuri, simu, tarakilishi au katika mfumo wowote wa kielekroniki.
Jinsi ya Kutumia Kamusi
Maneno yanayoingizwa katika kamusi hupangwa kwa utaratibu wa alfabeti.
Maneno yanayoanza na herufia, yote huwekwa chini ya herufiA. Maneno
yanayoanza na herufi fulani nayo hupangwa katika utaratibu wa alfabeti kwa
kuzingatia herufi ya pili, ya tatu, nne au tano ya neno kama mfano hapa chini
unavyoonyesha.
Mfano:ja, jabali, jabiri, jadhibika, jadi.
Maneno yote yanaanza na herufi [j]. herufi ya pili kwa maneno yote ni [a]. herufi
ya tatu ni [b] na [d]. Kwa kuwa [b] hutangulia [d] katika mpangilio wa alfabeti
maneno yenye [b] kabla ya yale yenye [d]. Kwa kuwa maneno yenye herufi [b] ni
mawili itabidi tutazame herufi ya nne ya hya maneno ili tuchague
litakaloorodheshwa mwanzo. Neno „jabali‟ litaorodhewshwa kabla ya „jabiri‟ kwa
kuwa [a] (herufi ya nne) ya „jabali‟ hutangulia [i] ya „jabiri‟ ambayo pia ni herufi
ya nne. Kisha tunatazama maneno yenye [d] kama herufi ya tatu. Hapa tunaangalia
pia herufi ya nne ili kubaini neno litakaloandikwa mwanzo kati ya „jadhibika‟ na
„jadi‟. Kwa kuwa [h] hutangulia [i] basi „jadhibika‟ huorodheshwa mwanzo ndipo
lifuatiwe na „jadi‟.
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 91
Kwa hiyo hivi ndivyo unavyopaswa kutafuta neno kwenye kamusi. Nenda kwenye
herufi ya neno ulalotafuta alafu litafute kwa kufuata mlolongo huo huo wa herufi
ya kwanza kuorodheshwa.
Neno linaloorodheshwa kwenye kamusi ili lifafanuliwe linaitwa kidahizo.
Kidahizo huandikiwa maelezo ya kukifafanua. Maelezo haya ni matamshi ya
kidahizo, maana ya kidahizo, kategoria ya kisarufi, sentensi ya mfano wa matumizi
ya kidahizo n.k. Kidahizo pamoja na maelezo yake ndio huitwakitomeocha
kamusi.
Kutafuta maana unayoitaka
Neno linaweza kuwa na maana moja au zaidi ya moja. Maana inapokuwa moja
mtumiaji kamusi hana tatizo kwani hiyo ndiyo atakayoipata na kuichukua. Lakini
neno linapokuwa na maana zaidi ya moja, mtumiaji kamusi hutatizika asijue ni ipi
aichague. Ili kupata maana inayosadifu itafaa mtumiaji kamusi kutafuta maana
ambayo inahusiana na muktadha wa neno linalotafutwa.
Mfano:kifungonm vi-
kitu cha kufungia
kitu kinachotumiwa kufungia vazi kama vile shati, gauni, suruali n.k
adhabu ya mtu kuwekwa jela kwa muda fulani
Iwapo mtumiaji aliona neno „kifungo‟ kwa muktadha wa: “Juma alihukumiwa
kifungo cha miaka kumi baada ya kupatikana na hatia ya kubaka….” Maana ya
mukatadha huu itakuwa ni ile maana ya 3 kwa sababu ndiyo yenye kuhusiana na
muktadha ambapo neno kifungo limetumika na wala sio maana ya 1 wala ya 2.
ZOEZI
Neno lipi kati ya haya yafuatayo linatangulia kuorodheshwa katika kamusi?
A Mdukuzi
B Mdubiri
C Mdoya
KIDATO CHA PILI 2019
Maeda T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 92
D Mdumizi
Maneno katika kamusi hupangwa katika utaratibu wa___
A Namba
B Herufi
C Alfabeti
D Kategoria
___ni alfabeti ambayo haina maneno katika kamusi ya Kiswahili.
A Alfabeti T
B Alfabeti X
C Alfabeti Z
D Alfabeti Y
Neno “wanacheza” hupatikana katika kamusi kwa kuangalia ___.
A Alfabeti
B Viambishi awali
C Shina la neno
D Viambishi tamati
Neno unganifu katika kamusi linahesabiwa kama___
A Maneno matatu
B Neno moja
C Maneno manne
D Maneno mawili
Recommended