Upload
rajabmumbee
View
251
Download
0
Embed Size (px)
DESCRIPTION
repo
Citation preview
SHIRIKA LA KUHUDUMIA VIWANDA VIDOGO
OFISI YA SIDO MANYARA
(SIDO)
RIPOTI YA WIKI (FLASH REPORT)
MKOA: MANYARA
A: MASUALA YALIYOJITOKEZA
Tarehe 12-19 /08/2010
NA. SUALA LILILOJITOKEZA
HATUA ZILIZOCHUKULIWA
MAELEZO/FAIDA
1. Huduma za Ugani Mchakato wa kuendesha warsha ya uhamasishaji wa programu ya MUVI unaendelea
Uandaaji wa warsha ya kujinadi kwa wadau wa programu wa BDG umekamilika
Kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa {RSMEAC} kilifanyika siku ya ijumaa tarehe 13 Aug 2010
Wajasiriamali na Wadau wa programu ya BDG kwa awamu zote mbili walitembelea na walihamasishwa kuhudhuria kikao cha tarehe 23 Aug 2010
2. Huduma za mikopo Makusanyo kwa RRF ilikuwa 1,057,000 na kwa mfuko wa NEDF ilikuwa 4,048,500
3. Huduma za mafunzo kwa wajasiriamali
Mafunzo juu ya usimamizi wa mikopo kwa vikundi vya VICOBA vya Minjingu yamefanyika na jumla ya wanawake 35 wameshiriki mafunzo hayo
Mafunzo ya uchakataji wa Asali na utengenezaji wa Nta yalifanyika Wilayani Simanjiro jumla ya washiriki 35 walihudhulia
Elimu waliyopata itawasaidia kusimamia vizuri mikopo watakayopewa na kufanya biashara kwa faida
4. Usambazaji wa Teknolojia Vijijini.
Vikundi vya mafundi bati kata ya Gallapo vilivyopata vifaa
SIDO itaendelea kutoa ushauri kwa vikundi
kutoka TFSR vimetembelewa na kushauriwa kutengeneza bidhaa zenye ubora na ushindani katika soko
hivyo na huduma za mikopo pale itakapoona kuna tija
B. MASUALA YANAYOTARAJIWA
Tarehe 20-26/08/2010
NA. MASUALA LINALOTARAJIWA MAELEZO
1. Huduma za Ugani Taratibu za kutoa mikopo kwa vikundi vya VICOBA vya Minjingu zitaendelea baada ya kupata mafunzo
2. Huduma za mikopo Maandalizi ya vikao vya kamati za mikopo LAC na CMC yatafanyika sambamba na kukusanya malimbikizo ya mikopo
3. Huduma za mafunzo kwa wajasiriamali Kutakuwa na warsha ya BDG tarehe 23 Aug 2010 pia kutakuwa na maandalizi ya warsha ya kuhasisha mradi wa MUVI kwa mkoa wa Manyara
4. Usambazaji wa teknolojia vijijini Mafunzo juu ya kutengeneza mizinga ya kisasa ya ufugaji wa nyuki yatafanyika mjini Babati na mkufunzi aliyepata utaalamu wa kutengeneza mizinga hiyo.Jumla ya washiriki 5 watashiriki mafunzo hayo