13
Insulators and Conductors Provided by TryEngineering - www.tryengineering.org SOMO LA 73 : INSULETA NA KONDAKTA Kusudio la Somo Onyesha dhana ya upitishaji na uzuiaji wa kupitishwa kwa umeme. Zingatia: Andalio hili la somo ni kwa ajili ya matumizi ya darasani tu, chini ya usimamizi wa mwalimu mwenye ujuzi juu ya masuala ya umeme. Muhtasari wa Somo Ufanyaji kazi wa Insuleta na kondakta unawapa hamasa wanafunzi kujaribu vifaa mbalimbali vilivyoko darasani na kubaini kuwa vifaa hivyo ni kondakta ama insuleta. Wanafunzi wafanye katika makundi kujaribu makisio yao juu ya kila kifaa, kisha vikundi vilinganishe na kujadili matokeo yao. Ngazi za Umri Kidato cha 1 – 4 Malengo Kujifunza kuhusu tabia za kiumeme za vifaa mbalimbali. Kujifunza namna ambavyo insuleta na kondakta zinavyoonesha muitikio dhidi ya mkondo wa umeme. Kutatua miundo ya kialjebra inayohusisha kipeo na kipeuo cha pili. Kujifunza kufanya madhanio na kuunda hitimisho. Kujifunza kuhusu ushirikiano na kufanya kazi katika vikundi. Matokeo Yanayotarajiwa kwa Mwanafunzi Kutokana na kazi hii, wanafunzi watatakiwa kujenga uelewa katika: Tabia za kiumeme Kondakta na insuleta Sakiti na mkondo wa umeme Kuunda na kuyajaribu madhanio Ufanyaji kazi kwa kushirikiana Shughuli za Somo P a g e 1 | 13

Home - TryEngineering.org Powered by IEEE · Web viewDK Eyewitness Series: Electricity (ISBN: 0751361321) Make Cool Gadgets for Your Room by Amy Pinchuk and Teco Rodriques (ISBN:

  • Upload
    others

  • View
    0

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Kusudio la Somo
Onyesha dhana ya upitishaji na uzuiaji wa kupitishwa kwa umeme. Zingatia: Andalio hili la somo ni kwa ajili ya matumizi ya darasani tu, chini ya usimamizi wa mwalimu mwenye ujuzi juu ya masuala ya umeme.
Muhtasari wa Somo
Ufanyaji kazi wa Insuleta na kondakta unawapa hamasa wanafunzi kujaribu vifaa mbalimbali vilivyoko darasani na kubaini kuwa vifaa hivyo ni kondakta ama insuleta. Wanafunzi wafanye katika makundi kujaribu makisio yao juu ya kila kifaa, kisha vikundi vilinganishe na kujadili matokeo yao.
Ngazi za Umri
· Kujifunza namna ambavyo insuleta na kondakta zinavyoonesha muitikio dhidi ya mkondo wa umeme.
· Kutatua miundo ya kialjebra inayohusisha kipeo na kipeuo cha pili.
· Kujifunza kufanya madhanio na kuunda hitimisho.
· Kujifunza kuhusu ushirikiano na kufanya kazi katika vikundi.
Matokeo Yanayotarajiwa kwa Mwanafunzi
· Tabia za kiumeme
· Kondakta na insuleta
· Kuunda na kuyajaribu madhanio
· Ufanyaji kazi kwa kushirikiana
Shughuli za Somo
Wanafunzi wajaribu katika sakiti aina mbalimbali za vifaa kwa lengo la kubaini kama vifaa hivyo ni insuleta au kondakta. Wanafunzi wafanye madhanio juu ya kila kifaa na kujadili matokeo katika vikundi vyao na kisha na darasa zima. Pia, vikundi vya wanafunzi pia viunde sakiti zao za kujaribia vifaa hivyo kwa kutumia nyaya, betri, na balbu.
Uhusiano wa Somo na Mtaala
Tazana ukurasa wa Uhusiano wa kimtaala mwishoni mwa somo hili.
Mahitaji ya vifaa
· Muongozo wa Mwanafunzi (Umeambatanishwa)
Uhusiano wa Somo na Mtaala
Tazama ukurasa wa "Uhusiano wa Somo na Mtaala" ulioambataniswa mwishoni.
Viunganishi vya Mtandaoni
Taarifa kuhusu vipimo na makosa katika vipimo.
· ITEA Standards for Technological Literacy: Content for the Study of Technology
· NCTM Principles and Standards for School Mathematics ( http://standards.nctm.org )
Vyanzo vya Maarifa Vilivyopendekezwa(rejea)
· DK Eyewitness Series: Electricity (ISBN: 0751361321)
· Make Cool Gadgets for Your Room by Amy Pinchuk and Teco Rodriques (ISBN: 1894379128)
· My World of Science: Conductors and Insulators kilichoandikwa na Angela Royston
(Heinemann Educational Books, ISBN: 0431137269)
Kazi ya Kuandika ya Hiyari
Andika insha(au aya kwa kutegemea umri wa mwanafunzi) kuelezea zao ambalo halitofanya kazi vizuri pale vifaa tofautitofauti vitakapotumika katika utengenezaji wa sakiti. Kwa mfano, balbu ya umeme iliyotengenezwa kwa filamenti ya plastiki haitofanya kazi.
Kwa ajili ya Mwalimu: Vyanzo vya Mwalimu;
Vifaa
· Mwongozo wa mahitaji ya mwanafunzi na karatasi ya kufanyia kazi ya mwanafunzi.
· Vipande vitatu(3) vya waya(zikwanguliwe nchani)
· Betri (saizi D)
· pini za kubania karatasi
· Vifaa mbalimbali ambavyo ni kondakta au insuleta; vinavyotosha kwa kila kikundi kuchagua vitu kumi kutoka kwenye mkusanyiko wenye angalau vitu 40 (mapendekezo: kibanio cha karatasi cha metali, karatasi, ufutio, sineri ya alminiamu, peni ya metali, mpira wa kufungia, penseli, sarafu, kibanio cha nywele, ufunguo)
Hatua
1. Unda muundo wa sakiti ya umeme darasani kwa kutumia nyaya, balbu na betri. Onyesha tabia ya upitishaji wa umeme na uzuiaji wa umeme kwa kujaribu aina mbalimbali za vifaa.
2. Mpe kila mwanafunzi nakala za rejea (Zingatio: rejea hizi pia zinaweza kutolewa kama kazi ya kujisomea kwa usiku mmoja kabla ya siku ya kazi yenyewe darasani.)
3. Onyesha muundo mmoja ukiwa na insuleta na kisha ukiwa na kondakta kuonesha namna vizuiavyo na kupitisha umeme.
4. Wagawanye wanafunzi katika vikundi vya watu watatu mpaka wanne.
5. Sambaza vifaa vinavyohitajika katika kila kikundi kama vile; nyaya, balbu na betri na uwaagize wanafunzi kuunda mfumo wao wa kujaribu upitishaji wa umeme katika vitu mbalimbali.
6. Waambie wanafunzi wachague vitu vitano kati ya vitu walivyoleewa ambavyo wanaamini vitapitisha umeme(tazama orodha ya vifaa). Vikundi piaGroups will also select five materials they believe will not conduct electricity. Selected items will be listed on the Student Worksheet.
7. Vikundi vya wanafunzi vitakabidhi madhanio yao kwa vikundi vingine kwa ajili ya kuyajaribu na kuyahakiki - hivyo kila kikundi kitayajaribu makisio ya kikundi kingine.
8. Matokeo yarekodiwe katika ukurasa wa kufanyia kazi wa mwanafunzi na washirikishane kwenye kikundi.
Muda Unaohitajika
Mawazo ya Nyongeza
Wanafunzi wakusanye vifaa mbalimbali toka nyumbani kwa ajili ya kujaribiwa ili kujua vifaa hivyo ni insuleta au kondakta.
Zana za Mwalimu: Kondakta na Insuleta ni nini?
Kondakta/Upitishaji wa Umeme
Upitishaji wa Umeme ni uwezo wa kondakta kuruhusu au kupitisha joto, umeme au sauti. Kondakta ni aina ya vifaa/vitu ambavyo umeme unaweza kupita kwa urahisi, ambavyo havizuii upitaji wa umeme. Mfano wa vitu hivyo ni: kopa, Alminiamu, stili, silva, dhahabu, na electrolaiti. Ubora wa upitishwaji wa umeme haulingani kwa vifaa/vitu vyote.
Insuleta
Insuleta ni vifaa/vitu ambavyo huzuia upitaji wa umeme, hivyo umeme haupiti kwa urahisi. Mfano wa vitu hivyo ni plastiki, mbao, ufutio, nguo, hewa, kioo. Baadhi ya vitu ni vizuizi vizuri vya umeme kuliko vingine.
Changamoto
Msumari
Insuleta
Kondakta
Insuleta
Kondakta
Kijiko
Insuleta
Sarafu
Kondakta
Insuleta
Kondakta
Chaki
Insuleta
Kondakta
Sakiti Rahisi
Sakiti rahisi huundwa na vitu visivyopungua vitatu ambavyo ndivyo vinavyohitajika kukamilisha sakiti ya umeme inayofanya kazi: chanzo cha umeme (betri), njia au kipitisha umeme (waya) na kifaa cha ukinzani (taa) ambacho ni kifaa chochote kinachohitaji umeme ili kufanya kazi. Mchoro uliopo hapa chini unaonesha sakiti rahisi iliyoundwa na betri moja, nyaya mbili na balbu. Uelekeo wa mtiririko wa umeme ni kutoka ncha chanya kuelekea kwenye ncha hasi.
Sakiti mfuatano
Mchoro Elekezi wa Sakiti Rahisi
Ufuatao ni mchoro elekezi wa sakiti rahisi ukionyesha alama za kielektroniki zinazowakilisha betri, swichi na balbu.
Mchoro wa Sakiti Rahisi
Swichi
Ukurasa wa Kufanyia Kazi wa Mwanafunzi: Kazi ya Insuleta na Kondakta
Hatua
Kiundi chako kitapewa nyaya, balbu na betri. Pangilia sakito ya kujaribia upitishani wa umeme kama ionekanavyo hapa chini.
Kisha kikundi kitakapokubaliana juu ya vitu vitano ambavyo wanakikundi wanadhan vitapitisha umeme (kondakta), na vitano visivyopitisha (insuleta). Orodhesha vitu hivyo katika ukurasa wa kufanyia kazi wa mwanafunzi. Badilishaneni orodha yenu na kikundi kingine na kisha kila kikundi kitayajaribu majibu ya wenzao.
Jaribuni kila kifaa kisha mrudishe majibu ya matokeo kwa kikundi mlichojaribu madhanio yao. Jadilini matokeo hayo katika vikundi. Je, nini kiliwashangaza?
Mpangilio wa Jaribio la Kondakta
Unganisha hapa kifaa cha kujaribu ili kuona kama kinapitisha umeme.
Unaweza kuunda mfumo wa kujaribia kondakta yabisi kwa kutumia betri, nyaya tatu, na balbu kama ionekanavyo hapo juu. Kama kifaa kinachopitisha umeme kitawekwa kati ya vibanio vya karatasi viwili vya metali, balbu itawaka. Kama kisichopitosha umeme kitawekwa kati ya vibanio vya karatasi viwili vya metali, balbu haitawaka. Kwa kuunganisha kondakta yabisi katika sakiti na kisha ukaiondoa, basi hapo utakua umeunda swichi rahisi.
Ukurasa wa Kufanyia Kazi wa Mwanafunzi:
Madhanio ya Kikundi cha Kwanza cha Wanafunzi:
Vitu ambavyo Kikundi cha Kwanza cha Wanafunzi Kinadhani kuwa ni Kondakta
Vitu ambavyo Kikundi cha Kwanza cha Wanafunzi Kinadhani kuwa ni Insuleta
1.
1.
2.
2.
3.
3.
4.
4.
5.
5.
Jaribu vitu vilivyochaguliwa na kikundi cha kwanza, kisha viorodheshe katika chumba stahiki cha jedwari.
Kondakta
Insuleta
Maswali:
1. Asilimia ngapi ya madhanio ya kikundi cha kwanza yalikua sahihi?
2. Kwanini wahandisi na wajenzi wanatakiwa kuwa na uelewa mzuri juu ya kondakta na insuleta?
Kwa Walimu: Uhusiano wa Somo na Mtaala
Andalio hili la somo limepangiliwa kwa kuzingatia mtaala mpya unaojikita kwenye uwezo, wa elimu ya sekondari ngazi ya chini nchini Uganda, ambao umezalishwa na Kituo cha Kitaifa cha Maendeleo ya Mtaala "National Curriculum Development Centre" (NCDC)
Shabaha ya Mtaala mpya unaojikita kwenye uwezo ni kujenga uelewa kupitia majaribio, uchunguzi wa kisayansi, na kufikiri kimantiki.
Wanafunzi wanatakiwa:
· Kuwa na muingiliano na hali halisi ndani na nje ya darasa.
· Kutazama picha au michoro, kudadisi takwimu au kusoma maandishi kutonga kwenye vyanzo mbalimbali.
· Wao wenyewe kugundua maarifa na fikra.
Kisha wanatarajiwa kueleza haya kwa maneno yao wenyewe, si kwa kutumia maneno ya mwalimu na kisha waoneshe kuwa wameelewa vyema walichojifunza.
Andalio hili la somo pia limefungamanishwa na stadi za kawaida zinazotarajiwa kupatwa na mwanafunzi aliyefunzwa chini ya mtaala wa sekondari ngazi ya chini nchini Uganda unaojikita katika ujuzi.
Stadi hizi za kawaida ni pamoja na:
1. Kufikiri kwa umakini na kutatua changamoto
· kupanga na kufanya uchunguzi.
· Kanga na uchanganue habari.
· Kubashiri matokeo na kufanya maamuzi bada ya kufikiri kwa makini.
· Kufanya tathmini na masuluhisho tofauti.  
2. Ubunifu na uvumbuzi
· Kutumia fikira kuchunguza uwezekano.
· Kupendekeza na kuanzisha mbinu mpya kutatua tatizo.
· Kujaribu njia mbadala za ubunifu.
· Kuangalia mifumo.
· Kuongea kwa ujasiri na kueleza mambo kwa ufasaha.
· Kusoma kwa usahihi na kwa ufasaha.
· Kuandika na uwasilisha kwa usahihi.
· Kutumia media anuwai kuwasiliana maoni.
 
· Kuwasiliana vizuri na wengine.
· Kufanya kazi kwa uhuru na uvumilivu.
· Kusimamia malengo na wakati.
· Kutumia hisabati kuhalalisha na kuunga mkono maamuzi.
· Kutumia teknolojia kuunda, kusimamia na kuchakata habari.
· Kutumia teknolojia ya kushirikiana, kuwasiliana na kusafisha kazi zao.
Page 11 | 11