Upload
others
View
29
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
1
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
HOTUBA YA WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA
UFUNDI MHE. DKT. SHUKURU JUMANNE KAWAMBWA
(MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO
NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2014/2015
Dodoma Mei, 2014
2
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
1
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
UTANGULIZII.
Mheshimiwa Spika1. , kufuatia taarifa iliyowasilishwa ndani ya
Bunge lako tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Huduma za Jamii iliyochambua na kujadili makadirio ya mapato
na matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, naomba
Bunge lako Tukufu sasa likubali kupokea, kujadili na kupitisha
makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo
ya Ufundi kwa mwaka 2014/15.
Mheshimiwa Spika2. , napenda kuchukua fursa hii kumshukuru
Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kunijalia afya njema na
kuniwezesha kutimiza majukumu yangu kama Waziri wa Elimu na
Mafunzo ya Ufundi. Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza
na kuwashukuru wasaidizi wangu wakuu katika kusimamia elimu
nchini walioteuliwa hivi karibuni na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni Naibu Waziri Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama (Mbunge wa Peramiho); Katibu Mkuu - Profesa Sifuni Ernest Mchome na Naibu Katibu Mkuu Bibi Consolata Philipo Mgimba. Vile vile, napenda kuwapongeza na kuwashukuru kwa ushirikiano mzuri - Kamishna wa Elimu, Profesa Eustella Peter Bhalalusesa; Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na Wakuu wa Taasisi mbalimbali za elimu zilizo chini ya Wizara yangu kwa ushirikiano wao wa karibu katika kuandaa bajeti hii. Aidha, napenda kuwashukuru Wahadhiri, Wakufunzi, Walimu na Watumishi wengine pamoja na Wanafunzi wote kwa kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara. Napenda pia kuwashukuru Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi na Vyama vya Wanataaluma, Wanafunzi na
2
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Washirika wa Maendeleo, kwa ushirikiano wao katika kuiendeleza Sekta ya Elimu. Ninawashukuru pia wazazi, walezi na wananchi wote kwa ujumla kwa jinsi ambavyo wameendelea kushirikiana na sekta ya elimu katika kuendelea kuimarisha elimu na mafunzo nchini. Ni matumaini yangu kuwa wizara itaendelea kushirikiana na wadau wote wa elimu ili kuwezesha elimu na mafunzo yanayotolewa nchini kuendelea kuimarika na kufikia ubora ambao unahitaji kwa maendeleo ya taifa.
Mheshimiwa Spika, 3. nichukue fursa hii pia kutoa salamu za pole kwako na kwa Bunge lako Tukufu kwa vifo vya Wabunge wenzetu wapendwa, Mheshimiwa William Augustao Mgimwa, aliyekuwa Mbunge wa Kalenga na Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Saidi Ramadhani Bwanamdogo, aliyekuwa Mbunge wa Chalinze. Aidha natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge na Wananchi wote waliofiwa na ndugu na wapendwa wao kutokana na maradhi, ajali, majanga na matukio mbalimbali yaliyotokea nchini mwetu. Namwomba Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi, amina. Aidha, Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa rehema awape faraja wote walioondokewa na wapendwa wao.
Mheshimiwa Spika,4. nitumie fursa hii pia kuwapongeza Wabunge wapya ambao ni Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa, Mbunge wa Kalenga, Mheshimiwa Ridhiwan Jakaya Kikwete Mbunge wa Chalinze na Mheshimiwa Yusuf Salim Hussein, Mbunge wa Chambani kwa kuchaguliwa kwao kwa kura nyingi na hivyo kupata fursa ya kuchangia maendeleo ya Taifa kwa kuwakilisha Wananchi katika
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
3
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
MAJUKUMU YA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO II.
YA UFUNDI
Mheshimiwa Spika5. , kwa mujibu wa Hati Idhini iliyounda Wizara
ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 17 Disemba, 2010,
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ina majukumu yafuatayo:
utungaji wa Sera za Elimu zinazohusu Elimu ya Awali, Elimu (a) ya Msingi, Elimu ya Sekondari, Elimu ya Ufundi, Mafunzo ya Ufundi Stadi, Elimu ya Juu na Elimu ya Watu Wazima;
utekelezaji wa Sera za Elimu katika maeneo ambayo ni ya (b) Wizara yangu
mafunzo ya Ualimu;(c)
usajili wa Shule;(d)
ukaguzi wa Shule na Vyuo vya Ualimu;(e)
uchapaji wa machapisho ya Elimu; (f)
utoaji wa huduma za Maktaba; (g)
uratibu wa shughuli zinazotekelezwa na Kamisheni ya Taifa (h) ya UNESCO;
uratibu wa shughuli za Taasisi na Wakala zilizo chini ya (i) Wizara;
usimamizi wa utekelezaji wa programu na miradi mbalimbali (j) ya Wizara; na
uendelezaji wa rasilimali watu na uongezaji tija ya (k)
watumishi walio chini ya Wizara.
4
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA MWAKA III.
2013/14
Mheshimiwa Spika6. , naomba nianze kwa kutoa tathmini ya
utekelezaji wa Bajeti ya Wizara kwa mwaka wa fedha 2013/14
kutoka tarehe 1 Julai, 2013 hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2014.
Ukusanyaji wa Maduhuli Mwaka 2013/14
Mheshimiwa Spika, 7. Wizara yangu kwa mwaka 2013/14, ilikadiria
kukusanya Sh. 171,518,704,600.00 ambapo Sh. 6,567,107,300.00
zilipangwa kukusanywa na idara na Sh. 164,951,597,360.00
zilipangwa kukusanywa na taasisi zilizo chini ya Wizara. Makusanyo
ya maduhuli yalikuwa Sh. 129,122,797,993.42 ambazo ni sawa na
asilimia 75.3 ya makadirio. Kati ya fedha hizo Sh. 5,511,631,867.42
zilikusanywa na Idara na Sh. 123,611,166,126.00 zilikusanywa na
Taasisi. Sehemu kubwa ya maduhuli hayo ilitokana na malipo ya
ada na huduma mbalimbali za kielimu zilizotolewa na Idara na
Taasisi za Elimu na Mafunzo.
Matumizi ya Fedha za Uendeshaji kwa Mwaka 2013/14
Mheshimiwa Spika, 8. katika mwaka wa fedha 2013/14, bajeti
ya Matumizi ya Kawaida ilikuwa Sh.617,083,004,000.00, kati ya
fedha hizo, mishahara ilikuwa Sh. 232,420,196,000.00, ambapo
mishahara ya Idara ilikuwa ni Sh. 44,248,528,000.00 na mishahara
ya Taasisi ilikuwa Sh.188,171,668,000.00. Matumizi mengineyo
yalikuwa Sh. 384,662,808,000.00 ambapo Sh. 54,467,335,400.00
5
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
zilikuwa kwa ajili ya Idara, Sh. 306,000,000,000.00 kwa ajili
ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu sawa na asilimia 79.5
ya matumizi mengineyo na Sh. 24,195,472,600.00 kwa ajili ya
matumizi mengineyo ya Taasisi.
Mheshimiwa Spika, 9. hadi kufikia tarehe 31 Machi 2014, Wizara
yangu ilitumia Sh. 486,573,220,250.94 sawa na asilimia
79 ya bajeti ya matumizi ya kawaida. Kati ya fedha hizo, Sh.
193,715,333,342.64 ni mishahara ambapo Sh.36,689,963,605.64
ni mishahara ya watumishi wa Idara na Sh. 157,025,369,737.00
ni mishahara ya watumishi wa Taasisi. Matumizi mengineyo ni
Sh. 292,857,886,908.30, ambapo Sh. 19,025,074,940.30
zimetumiwa na Idara na Sh. 273,832,811,968.00 sawa na asilimia
93.5 zilitumika kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu
na Taasisi.
Matumizi ya Fedha za Maendeleo Mwaka 2013/14
Mheshimiwa Spika10. , katika mwaka wa fedha 2013/14, Wizara
ilitengewa jumla ya Sh. 72,598,051,000.00 ikiwa ni Bajeti ya
Maendeleo, ambapo fedha za ndani zilikuwa Sh. 18,830,000,000.00
na fedha za nje zilikuwa Sh. 53,768,051,000.00. Matumizi
yalikuwa Sh. 14,921,545,855.46 ambapo Sh. 6,614,027,202.57
ni fedha za ndani na Sh. 8,307,518,652.89 ni fedha za nje.
6
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara kwa Mwaka 2013/14
Mheshimiwa Spika,11. wizara yangu ni mdau mmojawapo mkubwa
wa sekta ya elimu na mafunzo ambayo imejiwekea vipaumbele
vikuu viwili katika mwaka huu wa fedha. Vipaumbele hivyo ni:
a) kuinua ubora wa elimu na kujenga stadi stahiki katika ngazi zote za elimu na mafunzo; na
b) kuongeza upatikanaji wa fursa ya elimu kwa usawa katika
ngazi zote za elimu na mafunzo.
Mheshimiwa Spika,12. katika kuchangia utekelezaji wa
vipaumbele vya sekta, Wizara yangu ilifanya kazi kwa karibu sana
na wadau wengine hususan Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa
na Serikali ya Mitaa (OWM- TAMISEMI) ambayo ndiyo yenye
wajibu wa kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (1995)
kuhusu elimu ya msingi na sekondari. Aidha, Wizara na taasisi
zenye shule na vyuo pamoja na sekta binafsi ambazo zinamiliki na
kuendesha shule na vyuo mbalimbali nchini pia zilishiriki kikamilifu
katika kutimiza azma ya Serikali ya kutoa elimu na mafunzo katika
ngazi mbalimbali.
Mheshimiwa Spika,13. nichukue fursa hii sasa kutoa taarifa ya
utekelezaji wa majukumu ya wizara yangu kulingana na Hati Idhini
yake katika kuchangia mafanikio ya sekta ya elimu na mafunzo
katika kutekeleza vipaumbele vyake. Nitaeleza utekelezaji wa
jukumu moja baada ya jingine ili Bunge lako tukufu lipate fursa ya
kuyatambua kwa upana zaidi majukumu ambayo wizara yangu
ilikusudia kuyatekeleza.
7
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Utungaji wa Sera za Elimu
Mheshimiwa Spika,14. moja ya jukumu kubwa kabisa la Wizara yangu ni kubuni na kutunga sera mbalimbali kuhusu elimu ya awali, msingi, sekondari, ufundi pamoja na elimu ya juu na ya watu wazima. Lengo la sera hizi ni kutoa mwelekeo katika kutekeleza majukumu ya uendeshaji wa elimu na mafunzo katika ngazi mbalimbali. Hadi sasa sekta ya elimu ina sera nne ambazo ni Sera ya Elimu na Mafunzo (1995), Sera ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (1996), Sera ya Taifa ya Elimu ya Juu (1999) na Sera ya Matumizi ya TEHAMA katika Elimu Msingi (2007). Katika eneo hili Wizara yangu katika mwaka wa fedha 2013/14 imefanya yafuatayo:
kukamilisha uhuishaji wa Sera ya Elimu na Mafunzo (1995), (a) Sera ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (1996), Sera ya Taifa ya Elimu ya Juu (1999) na Sera ya Matumizi ya TEHAMA katika Elimu Msingi (2007) ili kuhakikisha kwamba sera na matamko yaliyopo yanakwenda na wakati na hivyo kuisaidia sekta ya elimu na mafunzo kukua. Uhuishaji huo ulibaini mambo mbalimbali ambayo yamezingatiwa katika Rasimu ya Sera ya Elimu na Mafunzo (2014). Rasimu hii imeshawasilishwa katika vikao vya juu vya maamuzi vya serikali na kwa sasa imewasilishwa Baraza la Mawaziri kwa ajili ya maamuzi;
kukamilisha rasimu ya awali ya Muswada wa Sheria ya (b) kuanzisha Bodi ya Kitaalamu ya Walimu Tanzania na kuiwasilisha katika Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri ambapo imeshajadiliwa na sasa rasimu ya pili imekamilika kwa ajili ya kuwasilishwa kwenye kamati ya kitaalamu ya
8
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Makatibu Wakuu (IMTC).
kukamilisha rasimu ya Muswada wa Sheria ya kuanzisha (c) Mamlaka ya Ithibati na Uthibiti wa Ubora wa Elimu Msingi na Sekondari ambapo shughuli mbalimbali hususan za ubora wa elimu zitaratibiwa na kusimamiwa na chombo hicho. Rasimu hii itajadiliwa na wadau na kuwasilishwa katika mamlaka husika kwa ajili ya kukamilishwa kuwa sheria;
kukamilisha na kuwasilisha katika Ofisi ya Rais - Menejimenti (d) ya Utumishi wa Umma Muundo wa Utumishi wa Walimu katika kada mbalimbali na pia Muundo wa Uongozi katika ngazi za elimu ya msingi, sekondari na ualimu ikiwemo ukaguzi;
kukamilisha rasimu ya Mkakati ya Kukabiliana na Uhaba (e) wa Walimu wa Sayansi na Hisabati kwa kutumia njia mbalimbali ili kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi na hisabati shuleni, kwa uratibu wa karibu wa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wizara kutumia vyombo vya habari imekuwa ikitoa taarifa kuhusu mkakati huu kwa lengo la kupata maoni na kuhamasisha wadau mbalimbali kushiriki katika kuendelea kuuimarisha na kuutekeleza kadri rasilimali zinavyopatika; na
kukamilisha utaratibu wa ithibati na uthibiti wa vitabu, zana (f) na vifaa vya elimu baada ya EMAC kufutwa ambapo kwa sasa masuala haya yatashughulikiwa na Taasisi ya Elimu Tanzania.
9
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimwa Spika15. , lengo na madhumuni ya kuweka sera na
mikakati ni pamoja na kuhakikisa kwamba changamoto zinazohusu
elimu na mafunzo ambazo ni za kisera au mikakati zinatatuliwa.
Baadhi ya changamoto hizo ni pamoja na mifumo, miundo na
taratibu ambazo siyo nyumbufu vya kutosha kumwezesha kijana
wa Kitanzania kupata elimu katika ngazi mbalimbali na kupitia
njia mbalimbali (progression pathways) kulingana na uwezo wake.
Ni jukumu la wizara yangu kuhakikisha sera zinaruhusu fursa
kuwepo na kuendelea kukua na kwamba vijana wa Kitanzania
wanazitumia fursa hizo kadri zinavyoendelea kubuniwa na
kupatikana. Naziomba Wizara, taasisi, mashirika na watu binafsi
ambao wana shule na vyuo katika ngazi mbalimbali kuendelea
kuwa wabunifu na kushirikiana na wizara yangu ili kutunga sera
endelevu ambazo zitaliwezesha taifa kufikia lengo lake la kuwa na
mtanzania aliyeelimika, mwenye maarifa, ujuzi na mtazamo chanya
katika kukabiliana na changamoto za maendeleo ya taifa kama
ambavyo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 inavyoelekeza.
Usajili wa Shule
Mheshimiwa Spika, 16. wizara yangu pia inajukumu la kusajili
shule. Usajili wa shule ni muhimu, kwanza kwa ajili ya kuipa shule
ithibati na hivyo idhini ya kufundisha masomo husika na pili kwa ajili
ya kutathmini maendeleo ya elimu katika ngazi mbalimbali. Kwa
mwaka wa fedha 2013/14 mambo yafuatayo yalitokea katika
kutekeleza jukumu hili:
10
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
hadi kufikia Machi 2014, Shule (a) 106 zilisajiliwa ambapo
shule za elimu ya Awali pekee ni 2, Awali na Msingi ni 53,
Sekondari za Serikali ni 17, Sekondari zisizo za serikali ni
32. Vyuo vya Ualimu visivyo vya serikali 2 pia vilisajiliwa.
Kwa sasa kuna jumla ya shule za msingi na sekondari
21,182; kati ya hizo, shule za msingi ni 16,609 (za serikali
chini ya OWM TAMISEMI ni 15,576 na zisizo za serikali ni
1,033) na shule za sekondari ni 4573 (za serikali chini ya
OWM TAMISEMI ni 3,525 na zisizo za serikali ni 1,048).
Vyuo vya ualimu ngazi ya cheti na stashahada ni 123 (vya
serikali chini ya Wizara yangu ni 34 na visivyo vya serikali
ni 89);
vibali vya ujenzi wa Shule (b) 127 vilitolewa ikiwemo kwa
Shule za Awali vibali 5, Shule za Msingi vibali 3, Awali na
Msingi vibali 74, Sekondari vibali 40, Vyuo vya Ualimu
vibali 5. Iwapo ujenzi utakamilika katika shule na vyuo hivi,
hili nalo pia litachangia katika kuongeza fursa za elimu na
mafunzo kwa vijana wetu; na
Shule za msingi (c) 5, za sekondari 5 pamoja na chuo kimoja
cha ualimu zilifungiwa kwa sababu mbalimbali ikiwemo
ukiukwaji wa vigezo vya ubora wa shule.
Mheshimiwa Spika, 17. nia ya wizara yangu ni kusajili na
siyo kuzifungia shule ama vyuo lakini wakati mwingine wizara
inalazimika kufanya hivyo ili kusaidia katika harakati za kujenga
ubora wa elimu na mafunzo nchini. Aidha, nichukue fursa hii pia
11
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuzipongeza Halmashauri ambazo zimechukua hatua mbalimbali
ikiwemo wao wenyewe kuzifunga kwa muda baadhi ya shule
kutokana na changamoto mbalimbali zinazohusu ubora. Hatua za
aina hii (internal quality assurance measures) ni kati ya njia sahihi
kabisa za kuhakikisha kila mdau anajihusisha kwa namna moja au
nyingine katika kutekeleza wajibu ambao hatima yake ni kuimarika
kwa ubora wa elimu na mafunzo nchini.
Ukaguzi wa Shule na Vyuo vya Ualimu
Mheshimiwa Spika,18. ukaguzi wa shule na vyuo vya ualimu ni
jambo muhimu sana katika kuhakikisha uimarikaji katika ubora wa
elimu na mafunzo yanayotolewa. Pamoja na changamoto za uhaba
wa rasilimali watu na fedha, wizara yangu ilifanikiwa kufanya
yafuatayo:
hadi kufikia Machi 2014, asasi (a) 8,483 zikiwemo shule za
msingi 6,091 za sekondari 2,308 na vyuo vya ualimu 84
zilikaguliwa hii ikiwa ni asilimia 79.4% ya asasi 10,684
zilizolengwa katika mwaka huu wa fedha.
wakaguzi wa shule (b) 139 walioteuliwa kati ya mwaka 2010-
2013 walipata mafunzo kabilishi na Wakaguzi wa Shule
148 walipatiwa Mafunzo ya Uongozi na Uendeshaji wa
Elimu kupitia Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu
(ADEM).
12
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Wizara ilibaini walimu (c) 217 ambao wanavigezo vya
kuwa Wakaguzi na kuwaombea uhamisho kutoka OWM-
TAMISEMI ili wateuliwe kuwa wakaguzi kwa ajili ya kujaza
nafasi za wakaguzi na hivyo kuimarisha ukaguzi hususan
katika Halmashauri mpya na zile zenye upungufu.
Mfumo wa kielektroniki wa ukusanyaji na usimamizi wa (d)
taarifa za ukaguzi (Inspectorate Management Information
System - IMIS) ulikamilika na kufanyiwa majaribio katika
shule za msingi 139 katika halmashauri saba ambazo
ni Temeke, Makete, Siha, Magu, Hai, Mtwara Vijijini na
Bagamoyo. Shule 20 zilikaguliwa katika kila Halmashauri
isipokuwa Bagamoyo ambapo shule 19 zilikaguliwa.
Uchambuzi wa taarifa zinazotokana na utekelezaji wa
mfumo huu zinaendelea. Mfumo huu utasaidia katika
kuimarisha ukaguzi nchini kwa kupata habari mbalimbali
kuhusu shule na maendeleo yake katika elimu na hivyo
kusaidia katika mipango ya maendeleo ya elimu na
mafunzo nchini.
Mheshimiwa Spika19. , Wizara inaziomba Halmashauri zote
nchini kuchangia katika kuwapatia wakaguzi ofisi na samani ili
kuwawezesha wakaguzi kufanya kazi zao kwa ufanisi.
13
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mafunzo ya Ualimu
Mheshimiwa Spika,20. moja ya nguzo za kuhakikisha elimu
bora inatokea ni maandalizi ya walimu kulingana na mitaala
inayotumika. Wizara imelitekeleza jukumu hili katika mwaka wa
fedha wa 2013/14 kama ifuatavyo.
Elimu ya Ualimu iliendelea kutolewa katika vyuo vya Wizara (a) na vya binafsi na hivyo kufanikisha upatikanaji wa Walimu
wapya 36,338 waliohitimu na kuajiriwa. Kati ya idadi hiyo,
walimu wa masomo ya sayansi na Hisabati ni 2,364, ngazi
ya cheti 17,928, ngazi ya stashahada 5,416 na ngazi ya
shahada 12,994. Aidha, OWM TAMISEMI imewaajiri na
kuwapanga katika Halmashauri mbalimbali nchini na hivyo
kuendelea kupunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la uhaba wa
walimu katika ngazi mbalimbali. Baada ya ajira ya walimu
hawa kufanyika, kwa sasa, taifa litabaki na upungufu wa
walimu 30,949 wa shule ya msingi na walimu 24,596 wa
sekondari wa sayansi na hisabati ambao wizara na wadau
wake itaendelea kuwaandaa kulingana na mikakati na kadri
rasilimali zinazohitajika zinavyoendelea kupatikana;
kuimarisha vigezo na utaratibu wa kupata walimu wa elimu ya (b) msingi na sekondari kwa kutumia kigezo cha ufaulu wa daraja
la tatu katika elimu ya sekondari kuwa ndiyo sifa ya chini ya
kujiunga na kozi ya ualimu katika ngazi yeyote ya ualimu;
kuweka utaratibu wa kuanza kutoa ruzuku na mikopo (c) kwa wanachuo wenye sifa watakaojiunga na mafunzo ya
14
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
stashahada ya ualimu wa sayansi na hisabati ili kuwavutia wale
wenye ufaulu wa juu katika elimu ya sekondari na wale wenye
sifa linganishi kujiunga na fani ya ualimu katika maeneo hayo.
Wizara, kwa kushirikiana na OWM-TAMISEMI na Ofisi ya Rais
– Menejimenti ya Utumishi wa Umma, itaweka utaratibu maalum
kuhusu ajira ya walimu watakaopatikana kupitia utaratibu huu
ili walimu hao waitumikie jamii kama inavyotarajiwa;
kurejesha utaratibu wa kujiunga na mafunzo ya ualimu kwa (d) walimu wa sekondari kwa masomo ya sayansi kwa miaka
mitatu kwa wahitimu wa kidato cha Nne (half combination).
Utaratibu huu utaanza kutekelezwa rasmi mwezi Julai 2014;
kuendelea na zoezi la kuvipatia vyuo vya ualimu (e) 34 ithibati
ya NACTE ili viweze kuingia rasmi katika mfumo wa ithibati na
uthibiti wa ubora unaotambulika kitaifa katika sekta ya elimu
ya ufundi;
kukamilisha mfumo wa kielektroniki ((f) online application) wa
kudahili wanafunzi wa kujiunga na programu ya ualimu ngazi
ya stashahada na ambao utaanza kutumika kwa majaribio
kwa programu ya Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Msingi
katika Chuo Kikuu cha Dodoma. Lengo ni kupunguza usumbufu
na muda unaotumika katika kudahili wanachuo katika ngazi
ya cheti na stashahada;
kukamilisha mradi wa kuwajenga walimu katika maeneo (g) mbalimbali ikiwemo TEHAMA kupitia ushirikiano na UNESCO.
Mradi huu utaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha
15
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
wa 2014/15 na wizara imeunda timu kabambe ambayo
itashirikiana na UNESCO katika kuhakikisha mradi huu unafikia
malengo yake ili kupata mwalimu mwenye viwango stahiki
vya weledi na hivyo kuchangia katika kuinua ubora wa elimu
nchini; na
kufuatilia upatikanaji wa fedha kupitia Benki ya Maendeleo (h) ya Afrika na Serikali ya Canada ambazo, pamoja na kusaidia
kuhuisha mtaala wa Stashahada ya Ualimu na kuimarisha
matumizi ya TEHAMA katika vyuo vya ualimu, pia vyuo
vya ualimu Shinyanga, Mpuguso, Ndala, Kitangali, Tabora,
Mpwapwa, Butimba na Dakawa vitakakarabatiwa.
Mheshimiwa Spika21. , ni dhahiri kwamba, pamoja na yote haya
Wizara yangu iliyoweza kuyafanya pamoja na wadau wake katika
elimu ya ualimu, bado mwendo ni mrefu mpaka tuweze kufikia lengo
letu la kumwandaa mwalimu mahiri na mwenye weledi wa kutosha.
Hili linahitaji wadau wote tuendelee kushirikiana kama ambavyo
kauli mbiu ya Wiki ya Elimu mwaka huu ilivyosema elimu bora
inawezekana; tekeleza wajibu wako. Wizara yangu itaendelea
kutimiza wajibu wake katika upatikanaji wa walimu bora nchini.
Taasisi na Wakala
Mheshimiwa Spika, 22. Wizara yangu ina jumla ya Taasisi na
Wakala 88 kati ya taasisi na wakala mbalimbali za elimu na
mafunzo zilizopo nchini. Kati ya hizo, 3 ni za ithibati na uthibiti wa
ubora wa elimu ya ufundi stadi, elimu ya ufundi na elimu ya juu, 2 ni
16
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
za mitaala na mitihani, 2 za mikopo na ruzuku mbalimbali, 1 ni bodi
ya huduma za maktaba, 1 ni Tume ya Taifa ya UNESCO, na kituo 1
cha hazina data kilichopo Kituo cha Maendeleo Dakawa. Tassisi na
wakala hizi zilitekeleza majukumu yake kulingana na sera za elimu
na mafunzo, miongozo inayotolewa mara kwa mara na serikali na
taratibu za taasisi hizo. Aidha, zilichangia kuleta ubora wa elimu
na kutoa fursa sawa mbalimbali katika elimu na mafunzo, taasisi
hizo zilitekeleza yafuatayo:
Tume ya Vyuo Vikuu kwa Kushirikiana na Baraza la Taifa (a)
la Elimu ya Ufundi ilikamilisha na kuzindua Mwongozo wa
Gharama ya Kumsomesha Mwanafunzi wa Elimu ya Juu
(Student Unit Cost Framework). Mwongozo huo utaanza
kutumika katika mwaka wa masomo 2014/2015 na
hivyo kuondoa utozaji ada kiholela katika elimu ya juu.
Wataalamu kutoka vyuo na vyuo vikuu vyote vinavyohusika
na suala hili wameanza kupatiwa mafunzo ya jinsi ya
kuutekeleza mwongozo huu katika maeneo yao;
Rasimu ya andiko kwa ajili ya kuanzisha Mfuko wa (b)
Maendeleo ya Elimu ya Juu imekamilika. Rasimu hiyo
itawasilishwa kwa wadau ili kupata maoni yao kabla
haijawasilishwa katika vikao vya maamuzi vya IMTC na
Baraza la Mawaziri katika mwaka ujao wa fedha;
Sheria kadhaa ikiwemo Sheria ya Mamlaka ya Elimu (c)
Tanzania (Sura Na. 412) zimerekebishwa kupitia sheria ya
Written Laws (Miscellaneous Amendments) Act, No. 3/2013
17
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
ili kuupatia Mfuko wa Elimu vyanzo vya mapato vya ziada
na endelevu kwa kuweka asilimia isiyopungua 2 ya bajeti
ya Serikali ya mwaka ya matumizi ya kawaida ukitoa deni
la Taifa;
Programu za elimu mbalimbali zilianzishwa ikiwemo (d)
programu ya kitaifa ya Stashahada ya Ualimu wa Shule
za Msingi ambayo inalenga kuimarisha taaluma ya ualimu
katika elimu ya msingi na itaanza kutekelezwa kuanzia
mwaka wa elimu 2014/15 kupitia chuo Kikuu cha Dodoma
na vyuo vingine vitakavyoteuliwa kwa ajili hiyo. Aidha,
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeanza upembuzi na
maandalizi ya programu ya Shahada ya Ualimu wa Elimu
ya Msingi. Lengo la jitihada hizi za Serikali ni kuondokana
na mfumo wa sasa ambapo mwalimu wa shule ya msingi
hakuwa na programu mahususi ya kumwendeleza katika
fani yake hadi kufikia elimu ya juu na kuendelea kuwa
mwalimu wa shule ya msingi mwenye stashahada, shahada,
uzamili au uzamivu. Hali hii ya sasa karibu itakuwa historia
kulingana na mikakati inayoendelea;
kuzinduliwa na kuanza rasmi kwa ujenzi wa Hospitali ya (e)
Kufundishia ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi
Muhimbili, Kampasi ya Mloganzila. Hospitali hii itakuwa ni
kubwa kuliko zote na yenye huduma mbalimbali na hivyo
kuwa msaada mkubwa katika kupata madaktari wenye
maarifa na weledi katika tiba na afya za binadamu.
18
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Kimsingi, mradi mzima umejikita katika kujenga mji wa
hospitali (hospital city); na
kukamilika kwa upembuzi yakinifu kwa ajili ya Chuo Kikuu (f)
cha Kilimo Mwalimu Nyerere - Butiama ambapo gharama
za awali zinaonesha mahitaji ya Sh. 347 bilioni kwa miaka
saba (2014/15 hadi 2021/22) ili chuo kikamilike na kwa
kuanzia zinahitajika Sh. 22 bilioni ili chuo kianze awamu
ya kwanza. Wizara inaendelea kuwasiliana kwa karibu na
Tume ya Mipango, Hazina pamoja na wadau na wahisani
mbalimbali ili ujenzi wa chuo hiki uanze katika mwaka wa
fedha 2014/15.
Mheshimiwa Spika, Taasisi na Wakala zilizopo chini ya wizara katika
mwaka 2013/14 zilitekeleza yafuatayo:
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima
Mheshimiwa Spika, 23. taasisi hii ina jukumu la kutoa mafunzo
ya Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi, kufanya
utafiti na kutoa ushauri elekezi katika eneo hili.
Mheshimiwa Spika, 24. katika mwaka 2013/14, Taasisi ya Elimu
ya Watu Wazima, ilitekeleza yafuatayo:
iliendelea na juhudi za kuongeza walimu, wasimamizi (a)
na viongozi wataalamu wa elimu kwa kudahili wanafunzi
881 katika ngazi ya cheti, stashahada na shahada katika
programu ya elimu ya watu wazima na mafunzo endelevu;
19
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
iliendelea na juhudi za kuongeza idadi ya wataalamu wa (b)
elimu ya watu wazima na mafunzo endelevu kwa njia ya
Ujifunzaji Huria na Masafa (UHM) kwa kudahili wanafunzi
162 wa stashahada;
iliongeza fursa ya utoaji wa elimu ya sekondari kwa njia ya (c)
Ujifunzaji Huria na Masafa kwa kuandika moduli za hatua
ya tatu (sawa na kidato cha V na VI) kwa masomo kumi na
moja yakiwemo English, French, Basic Applied Mathematics,
Advanced Mathematics, History, Geography, Kiswahili,
General Studies, Economics, Commerce na Accounting; na
ilifanya utafiti na kuandaa majarida ya kitaalamu na vitabu (d)
ili kuelimisha jamii kuhusu masuala ya Elimu ya Watu Wazima
na Mtambuka.
Taasisi ya Elimu Tanzania
Mheshimiwa Spika, 25. taasisi hii ina majukumu ya kubuni na
kuandaa mitaala na mihtasari ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari,
Ualimu na Elimu Maalumu.
Mheshimiwa Spika, 26. katika mwaka 2013/14, Taasisi ya Elimu
Tanzania, imekusanya maoni ya wadau kuhusu maboresho ya
mitaala pamoja na kuchambua mihutasari ya masomo ya elimu ya
awali na msingi ili kuinua kiwango cha ubora wa utoaji wa elimu
Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania
Mheshimiwa Spika, 27. Bodi hii ina jukumu la kuanzisha, kusimamia,
kuongoza, kuimarisha, kutunza na kuendeleza Maktaba za Umma,
kuanzia ngazi za Vijiji, Wilaya hadi Mikoa, kutoa mafunzo na
20
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuendesha mitihani ya Taaluma ya Ukutubi.
Mheshimiwa Spika28. , katika mwaka 2013/14, Bodi ya Huduma
za Maktaba Tanzania, ilitekeleza yafuatayo:
imeongeza wataalamu wa fani ya ukutubi kwa kutoa mafunzo (a)
ngazi ya cheti kwa wanachuo 457, stashahada 339 pamoja
na mafunzo ya muda mfupi kwa washiriki 98 katika Chuo
cha Ukutubi Bagamoyo – “School of Library, Archives and
Documentation Studies - SLADS”;
imesimamia uendeshaji bora wa Maktaba nchini kwa kutoa (b)
ushauri wa kitaalamu kuhusu uanzishaji na uendeshaji
wa maktaba za Shule 81, Taasisi 9, Halmashauri za Miji,
Manispaa na Wilaya 6;
ime(c) imarisha huduma za maktaba kwa kuongeza vitabu na
machapisho 58,137 na hivyo kufikia jumla ya vitabu na
machapisho 1,268,610; na
imeongeza(d) udahili na kuinua ubora wa mazingira ya
kujifunzia na kufundishia kwa kuendeleza ujenzi wa hosteli ya
wanafunzi wa kike katika Chuo cha Ukutubi cha Bagamoyo.
imeendelea na ujenzi na ukarabati wa majengo kwenye Chuo (e)
cha Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (SLADS), Bagamoyo kwa
kuweka nguzo kwa ajili ya uzio, kuweka tanki la kuhifadhia
maji safi katika hosteli, kujenga madarasa mawili na ofisi
moja ya walimu na kufanya ukarabati wa awamu ya kwanza
kwa jengo la maktaba ya mkoa wa Mara na Mtwara.
21
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu
Mheshimiwa Spika,29. wakala ina majukumu makuu manne ambayo ni kuandaa na kuendesha mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika uongozi na uendeshaji wa elimu; kutoa ushauri wa kitaalamu katika mambo yanayohusu uongozi na uendeshaji wa elimu; kufanya utafiti katika masuala yanayohusu uongozi na uendeshaji wa elimu na kuandaa na kusambaza makala na vitabu mbalimbali vya uongozi na uendeshaji wa elimu.
Mheshimiwa Spika30. , katika mwaka 2013/14, Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu, ilitekeleza yafuatayo:
ilitoa mafunzo ya Stashahada ya Uongozi wa Elimu kwa (a) wanafunzi 762 katika vituo vya Bagamoyo na Mwanza yenye lengo la kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa shule;
iliandaa moduli kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uongozi (b) na uendeshaji wa shule za msingi, mpango shirikishi wa maendeleo ya shule, kuandaa andiko la mradi, kufanya ufuatiliaji na tathmini, usimamizi wa fedha na vifaa vya shule za msingi pamoja na kutoa mafunzo kwa wajumbe wa kamati za shule za msingi;
ilitoa mafunzo kwa wakuu wa shule za serikali 2,982 na (c) 2,287 wa shule zisizo za serikali ili kuimarisha menejimenti ya shule za sekondari; na
kuimarisha usimamizi wa elimu msingi kwa kutoa mafunzo (d) kwa Waratibu wa Elimu Kata 1,765 kutoka mikoa ya Arusha, Dar es salaam, Kagera, Kilimanjaro, Mbeya, Morogoro,
Mtwara, Mwanza, Ruvuma, Singida na Tabora.
22
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Tume ya Taifa ya UNESCO
Mheshimiwa Spika31. , Tume ina majukumu ya kutekeleza
programu za UNESCO nchini kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania katika nyanja za Elimu, Sayansi Asilia,
Sayansi Jamii, Utamaduni, Mawasiliano na Habari.
Mheshimiwa Spika, 32. katika kipindi cha mwaka wa fedha
2013/14, Tume ya Taifa ya UNESCO, ilitekeleza yafuatayo:
ilipitia programu ya (a) International Hydrological Programme
na kuandaa mkutano wa kanda wa watumiaji wa Bonde la
Mto Naili tarehe 3-4 Desemba 2013;
iliandaa ripoti ya hali ya uhifadhi wa maeneo ya Tanzania (b)
yaliyoorodheshwa kwenye orodha ya urithi wa Dunia ili
kutathmini utekelezwaji wa mkataba wa UNESCO wa mwaka
1972;
iliendelea kuelimisha jamii kuhusu shughuli za UNESCO (c)
hususan masuala ya Mazingira, Elimu, Sayansi Asilia, Sayansi
Jamii, Utamaduni, Mawasiliano na Habari kwa kuchapa na
kusambaza nakala 742 za Tanzania and UNESCO Magazine
na nakala 2,500 za vipeperushi; na
imeendelea kuratibu ushiriki wa Watanzania watano (5) (d)
katika mafunzo ya muda mrefu na mfupi chini ya ufadhili
wa UNESCO katika nchi mbalimbali.
23
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Baraza la Mitihani la Tanzania
Mheshimiwa Spika33. , Baraza lina jukumu la kuendesha mitihani
ya kuhitimu Elimu ya Msingi, Sekondari, Ualimu ngazi ya Cheti na
Stashahada na mtihani wa Maarifa, na kusimamia uendeshaji wa
mitihani itolewayo na bodi za nje ya nchi.
Mheshimiwa Spika34. , katika mwaka 2013/14, Baraza la
Mitihani la Tanzania, lilitekeleza yafuatayo:
iliwatahini wanafunzi waliomaliza Elimu ya Msingi (darasa la (a) VII 868,083), Elimu ya Sekondari (kidato cha IV - 427,938 na kidato cha VI - 46,378); Mtihani wa Ualimu 26,614 na kuendesha mtihani wa Maarifa (Qualifying Test ) kwa watahiniwa 18,214); na
kwa ilianza ujenzi wa kituo cha data kwa ajili ya kuimarisha (b)
utunzaji wa kumbukumbu na taarifa za mitihani
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi
Mheshimiwa Spika, 35. Baraza lina majukumu ya kusimamia na kuratibu mitaala, ubora wa mafunzo, mitihani, tuzo, usajili na ithibati za vyuo vya elimu ya ufundi vya umma na binafsi nchini.
Mheshimiwa Spika36. , katika mwaka 2013/14, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi, lilitekeleza yafuatayo:
lilikagua, kusajili na kutoa ithibati ambapo vyuo 45 (a) vilikaguliwa na kusajiliwa na vyuo 04 vilipatiwa ithibati;
liliongeza wa(b) kufunzi wa vyuo vya elimu ya ufundi kwa kusajili
wakufunzi 29;
24
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
lilira(c) tibu udahili wa wanafunzi katika vyuo vya ufundi ambapo kwa ngazi ya cheti na stashahada wanafunzi 13, 375 na shahada wanafunzi 5,081 walidahiliwa;
lilihakiki ubora wa kiwango cha elimu inayotolewa na vyuo (d) vya ufundi kwa kuidhinisha mitaala 39 na kuratibu mafunzo kwa walimu 132 ya jinsi ya kutumia mitaala inayozingatia umahiri; na
lilihamasisha wanafunzi wa kike kujiunga na Elimu ya Ufundi (e) na Mafunzo ya Ufundi Stadi baada ya kuhitimu Elimu ya Sekondari ambapo zoezi la uhamasishaji limefanyika katika shule za sekondari 40 zilizopo katika mikoa ya Njombe, Ruvuma, Mtwara, Lindi, Geita na Kagera.
Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere
Mheshimiwa Spika, 37. Chuo kina majukumu ya kuendesha mafunzo katika fani za Sayansi za Jamii; kutoa mafunzo ya uongozi; kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu kwa sekta ya umma na binafsi.
Mheshimiwa Spika38. , katika mwaka 2013/14, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, kilitekeleza yafuatayo:
kiliongeza fursa za kujiunga na elimu ya juu kwa kudahili (a) jumla ya wanafunzi 745 kati yao wanafunzi 122 wa programu za Cheti, 220 wa programu za Stashahada na 403 wa programu za Shahada ya Kwanza; na
kiligharimia mafunzo kwa wahadhiri 18 katika ngazi ya (b) uzamili na uzamivu ili kuongeza tija na ufanisi katika utendaji
kazi na kuajiri wahadhiri wapya 14 kwa lengo la kuimarisha
ufundishaji.
25
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Chuo cha Ufundi Arusha
Mheshimiwa Spika39. , Chuo kina majukumu ya kutoa elimu
na mafunzo ya ufundi katika fani za magari, ujenzi, mitambo,
umeme, barabara, sayansi na teknolojia ya maabara, eletroniki
na mawasiliano ya anga; kwa kiwango cha cheti na stashahada.
Aidha, chuo hufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu na
kitaaluma.
Mheshimiwa Spika40. , katika mwaka 2013/14, Chuo cha Ufundi
Arusha kiliendelea kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na elimu ya ufundi kwa kudahili (a)
jumla ya wanafunzi 493 wa mwaka wa kwanza (463 wa
ngazi ya Cheti na 30 wa ngazi ya Shahada);
kuanzisha programu ya (b) Biomedical Engineering kwa lengo la
kuongeza wataalamu wa kutengeneza vifaa vya maabara
ambapo jumla ya wanafunzi hamsini (50) wanaendelea na
masomo ya pogramu hii;
kuhuisha mitaala 6 ya programu zilizopo za Ufundi Sanifu (c)
(NTA 4-6) kwa lengo la kuzalisha wataalamu wanaoendana
na mahitaji ya soko la ajira;
kuongeza udahili wa wanafunzi wa kike wenye sifa pungufu (d)
kwa kutoa kozi za awali (Pre-Entry Course) ya kujiunga na
chuo kwa kushirikiana na Mfuko wa Elimu Tanzania (TEA)
ambapo jumla ya wanafunzi 126 wa kike walijiunga na chuo
kwa utaratibu huo;
26
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuongeza idadi ya watumishi kwa kuajiri wakufunzi 27 na (e)
kugharimia mafunzo kwa wakufunzi 15;
kukamilisha ujenzi wa jengo la uhandisi la umwagiliaji kwa (f)
asilimia 95;
kuendeleza juhudi za kuinua ubora wa elimu ya ufundi kwa (g)
kushirikiana na mradi wa Technical Education and Labour
Market Support Programme - TELMS ambao ulitoa msaada wa
vifaa vya kufundishia kwa fani za uhandisi na mawasiliano ya
anga, ujenzi, barabara, mitambo na magari. Pia wanafunzi
bora 6 wa kike walizawadiwa kompyuta mpakato (Laptops),
moja kila mmoja na wanafunzi 93 walipewa ufadhili wa ada
ya Tsh. 180,000/= kila mmoja;
kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kimataifa kwa kuandaa (h)
kongamano la kimataifa la vyuo vya elimu ya ufundi
ambavyo ni wanachama wa Commonwealth Association of
Polytechnics in Africa (CAPA) tarehe 24-29 Novemba 2013
ambapo washiriki 250 kutoka mataifa 14 walihudhuria;
kukamilisha utafiti wa awali wa kutengeneza mashine ya (i)
kupukuchua, na kuchambua na kufungasha mahindi kwa
ukubwa;
kutoa huduma za ushauri wa kitaalamu kuhusu ujenzi wa vituo (j)
vya kufua umeme kwa kutumia nishati ya maji, upimaji wa
udongo kwa ajili ya ujenzi wa majengo na mabwawa; na
kusimamia na kutengeneza taa za kuongoza magari na (k)
ukarabati wa vifaa katika hospitali ya Mount Meru.
27
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi
Mheshimiwa Spika, Mamlaka ina majukumu ya kuratibu, kudhibiti,
kugharimia, kutoa na kukuza elimu na mafunzo ya ufundi stadi nchini.
Mheshimiwa Spika41. , katika mwaka 2013/14, Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, ilitekeleza yafuatayo:
iliendelea na juhudi za kuongeza fursa za kujiunga na (a) mafunzo ya ufundi stadi kwa kuanza maandalizi ya awali ya ujenzi wa vyuo 5 vya Wilaya za Kilindi, Namtumbo, Ludewa, Ukerewe na Chunya ambapo zabuni zimetangazwa na ujenzi unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi Juni mwaka 2014;
iliongeza fursa ya wanafunzi ambao hawajapata nafasi za (b) kujiunga na sekondari ya juu (A Level) kwa kuanza kutoa mafunzo ya ufundi stadi katika Vyuo 25 vya Maendeleo ya Wananchi. Aidha, ujenzi wa karakana katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vya Handeni, Ikwiriri, Mbinga, Nzega na Kisangwa umekamilika; na
ilitoa mafunzo ya umahiri wa ufundishaji mafunzo ya ufundi (c) stadi kwa walimu 100 kutoka Vyuo 25 vya Maendeleo ya Jamii vinavyotoa mafunzo ya ufundi stadi.
Mamlaka ya Elimu Tanzania
Mheshimiwa Spika, 42. Mamlaka ina majukumu ya kutafuta na kubaini vyanzo mbalimbali vya mapato kwa ajili ya kugharimia maendeleo ya sekta ya elimu nchini ikiwa ni pamoja na kuwahamasisha wadau wa elimu kuchangia kwa hiari katika miradi
ya elimu.
28
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika,43. katika mwaka 2013/14, Mamlaka ya
Elimu Tanzania, ilitekeleza yafuatayo:
iligharimia mafunzo ya “(a) Pre-entry” kwa wanafunzi wa kike
260 ili kuwawezesha kupata sifa stahiki za kujiunga na vyuo
vya elimu ya ufundi nchini; na
ilihamasisha uchangiaji wa elimu kwa njia ya matembezi ya (b)
hisani na kuandika miradi ambapo kiasi cha shilingi milioni
370 zilipatikana.
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania
Mheshimiwa Spika, 44. Tume ina majukumu makuu ya kusimamia
ubora wa Elimu ya Juu, kutoa ithibati, kuratibu uanzishwaji wa
Vyuo Vikuu, na kuidhinisha programu zinazofundishwa ili zikidhi
maendeleo ya Taifa na soko la ajira.
Mheshimiwa Spika,45. katika mwaka 2013/14, Tume ya Vyuo
Vikuu Tanzania, ilitekeleza yafuatayo:
iliratibu na kusimamia udahili wa wanafunzi 52,538 katika (a)
Vyuo Vikuu na Vyuo vikuu vishiriki nchini;
ilikagua na kufanya tathmini maendeleo ya vyuo vilivyopewa (b)
ithibati ili kuweza kujua kama vinatekeleza malengo yake
ipasavyo na iliidhinisha programu 46 za masomo;
iliratibu upatikanaji wa wanataaluma 17 kutoka Vyuo (c)
29
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Vikuu nchini waliojiunga na Masomo ya Uzamivu chini ya makubaliano ya Serikali ya Tanzania na Ujerumani ( Deutscher Akademischer Austauch Diest - DAAD); na
iliratibu na kuandaa Maonyesho ya Nane ya Elimu ya Juu (d) , Sayansi na Teknolojia ili kuelimisha umma kuhusu malengo, maendeleo na mchango wa Taasisi za Elimu ya Juu katika
maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini.
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
Mheshimiwa Spika46. , Bodi hii ina majukumu ya kutoa mikopo kwa
wanafunzi raia wa Tanzania wanaosoma katika Taasisi za Elimu ya
Juu ndani na nje ya nchi na kukusanya marejesho ya mikopo hiyo.
Mheshimiwa Spika,47. katika mwaka 2013/14, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, iliendelea kutekeleza yafuatayo:
ilitoa mikopo kwa wanafunzi 95,589 na hivyo kuongeza (a) fursa za upatikanaji wa Elimu ya Juu;
ilikusanya marejesho ya mikopo ambapo (b) sh. 12,345,411,587.66 zilikusanywa mpaka kufikia mwezi Machi, 2014 sawa na asilimia 43 ya lengo la makusanyo kwa mwaka 2013/2014 na hivyo kufikia sh.47,349,582,373.11 sawa na asilimia 55 ya madeni yaliyoiva. kuhamasisha na kutoa elimu kwa umma kwa njia ya magazeti, redio na televisheni kuhusu dhana ya uchangiaji, taratibu za utoaji mikopo pamoja na urejeshwaji wake na wajibu wa kila mdau
kuchangia Elimu ya Juu;
30
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
ilifungua ofisi(c) ya Kanda ya Ziwa- Mwanza mwezi Februari
mwaka 2014. Aidha, ofisi za Kanda za Dodoma na Zanzibar
ziliunganishwa na Mfumo wa Utoaji Mikopo wa Makao
Makuu ya Bodi. Ofisi za Kanda zinafanya ufuatiliaji wa
karibu kwa waajiri na wanufaika wa mikopo ili kuongeza
kasi ya urejeshwaji wa Mikopo hiyo. Ukusanyaji wa
madeni umeimarika pia katika ofisi zilizopo Zanzibar kwa
kuweza kuzifikia taasisi nyingi zilizopo Unguja na Pemba
ikilinganishwa na kiwango kidogo cha ukusanyaji madeni
kilichofanywa na wakusanyaji madeni (debt Collectors); na
kurahisisha huduma ya utoaji mikopo kwa kufungua ofisi ya (d)
Kanda ya Ziwa na kuimarisha ofisi za Kanda ya Zanzibar
na Dodoma kwa kuziunganisha na Mfumo wa Utoaji Mikopo
wa Makao Makuu ya Bodi ya Mikopo.
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Mheshimiwa Spika,48. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa mafunzo, kufanya utafiti na kutoa ushauri na huduma za kitaalamu katika maeneo mbalimbali ya elimu na mafunzo.
Mheshimiwa Spika,49. katika mwaka 2013/14, Chuo hiki kilitekeleza yafuatayo:
kiliongeza fursa ya upatikanaji wa elimu kwa kudahili (a) wanafunzi 1,350 katika fani za Sayansi na Uhandisi na 2,435 wa uzamili na uzamivu kwa ufadhili wa mashirika mbalimbali idara ya Chemical and Mining Engineering (CME) na Technology Transfer Centre (TDTC);
31
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kiliendelea kufanya utafiti na kuandaa teknolojia ya (b) kutengeneza juisi kutokana na ndizi;
kiliendelea kufanya utafiti kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi ( (c) Climate Change and Mitigation (CCIAM)) unaotekelezwa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Dar es salaam,, Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, Chuo cha Ufundi Arusha, , Tanzania Maritime Agency (TMA) na University of Life Science (Norway), Climate Change Impact on Ecosystem Services and Food Security in Eastern Africa (CHIESA), Impacts of Climate Change on Water Resources and Agriculture - and Adaptation Strategies in Tanzania; na
iliendelea na utafiti kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi (d) wa Integrated Water Resources Management (IWRM) wa kutoa mafunzo na kufanya utafiti kwa wanafunzi wa hapa nchini na nchi jirani.
Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam
Mheshimwa Spika50. , Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa mafunzo, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu katika maeneo ya Elimu na Ualimu
Mheshimiwa Spika,51. katika mwaka 2013/14, Chuo hiki kilitekeleza yafuatayo:
kiliongeza fursa za Elimu ya Juu kwa kudahili wanafunzi (a)
1,247 (220 wa fani ya sayansi) na 42 wa Cheti katika fani
mbalimbali za elimu;
32
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuongeza vifaa vya kufundishia na kujifunzia vikiwemo (b)
madawa (chemical) kwa ajili ya matumizi ya maabara
za kufundishia na vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji
maalumu pamoja na kununua samani na vitabu kwa ajili
ya maktaba;
kiligharamia wahadhiri 25 katika mafunzo ngazi ya (c)
shahada za uzamili na 69 shahada za uzamivu ndani na
nje ya nchi ili kuwajengea uwezo na kuongeza ufanisi; na
kiliajiri wafanyakazi 25 (walimu 22 na waendeshaji 3) ili (d)
kuleta ufanisi katika utendaji kazi.
Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa
Mheshimiwa Spika,52. Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa,
ambacho ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kina
majukumu ya kufundisha, kutafiti na kutoa ushauri na huduma za
kitaalamu katika maeneo ya Elimu na Ualimu.
Mheshimiwa Spika,53. katika mwaka 2013/14, Chuo iliongeza
fursa ya upatikanaji wa Elimu ya Juu kwa kudahili wanafunzi
wanawake 255 na wanaume 723.
Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine
Mheshimiwa Spika,54. Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kina
majukumu ya kutoa mafunzo, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa
kitaalamu katika nyanja za kilimo, mifugo, mazingira na maendeleo
kwa ujumla.
33
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika55. , katika mwaka 2013/14, Chuo kilitekeleza
yafuatayo:
kilianzisha programu ya mafunzo ya “(a) Post Harvest Engineering
Systems” ngazi ya Shahada ya Uzamivu kwa lengo la
kuongeza wigo wa wataalamu katika fani hiyo;
kilifanya utafiti msingi na tumizi (Basic and Applied Research) (b)
katika Miradi 135 kwa lengo la kutatua matatizo ya jamii
na kuongeza tija;
kiliimarisha matumizi ya TEHAMA kwa kufanikisha (c)
upatikanaji wa vifaa vya mawasiliano kupitia mradi wa
AIGRI unaofadhiliwa na USAID na hivyo kuimarisha mfumo
wa taarifa za wanafunzi – “SUA Students Information
System”-‘SUASIS’na hivyo kuimarisha ubora wa mazingira
ya kufundishia na kujifunzia; na
chini ya ufadhili wa Mradi wa STHEP kwa kilikamilisha ujenzi (d)
wa majengo manne (yenye kumbi za mihadhara 9, ofisi
40, na maabara 4) yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi
10,565 na wahadhiri 881 na kukarabati bweni la kampasi
ya Solomon Mahlangu na karakana ya Idara ya Uhandisi
Kilimo; na
kilifanya utafiti wa athari za mabadiliko ya tabianchi na (e) tahafifu katika Kanda za Nyanda za Juu Kusini, Kaskazini na Kati.
34
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara cha Moshi
Mheshimiwa Spika,56. Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara
ambacho ni sehemu ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine kina majukumu ya kutoa mafunzo, kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu katika nyanja za ushirika, maendeleo ya jamii, biashara, oganaizesheni, ujasiriamali na masuala mtambuka.
Mheshimiwa Spika,57. katika mwaka 2013/14, Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara Moshi, kilitekeleza yafuatayo:
kiliongeza fursa za elimu ya juu kwa kudahili wanafunzi (a)
4,463;
kuongeza fursa za wataalamu kwa kuanzisha programu ya (b)
mafunzo ya shahada ya uzamili ya Menejimenti ya Biashara
(MBM);
kiligharimia mafunzo kwa wanataaluma 53 katika shahada (c)
za uzamili na uzamivu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa
elimu;
kilifanya utafiti 20 kwa kushirikiana na wadau nje na ndani (d)
ya nchi kwa lengo la kukabiliana na changamoto za kijamii
na kuongeza tija; na
kilitoa Elimu ya Ushirika kwa njia ya masafa kwa wadau (e)
mbalimbali kupitia vituo 13 vilivyoko mikoani.
35
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania
Mheshimiwa Spika, 58. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa Elimu
ya Juu kwa njia ya Masafa na Ana kwa Ana; kutafiti, kutoa ushauri
wa kitaalamu na kueneza maarifa kupitia vituo vyake vilivyopo
mikoani.
Mheshimiwa Spika,59. katika mwaka 2013/14, Chuo Kikuu Huria
ilitekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za Elimu ya Juu kwa kudahili Wanafunzi 8,935 (a)
katika ngazi ya Shahada na Cheti, sawa na asilimia 99 ya
lengo la kudahili wanafunzi 9,000. Aidha, wanafunzi 2,943 sawa na asilimia 105.9 ya lengo lililowekwa walidahiliwa katika Shahada za Uzamili na Uzamivu;
kuinua ubora wa mazingira ya kujifunzia kwa kujenga (b) maabara ya Kompyuta katika kituo cha Zanzibar, Mtwara, Dodoma, Shinyanga na Kinondoni pamoja na kukamilisha ukarabati wa ofisi na ukumbi wa mitihani katika kituo cha Shinyanga;
kufanya ukarabati wa awamu ya II katika kituo cha Mkoa (c) wa Zanzibar;
kurahisisha upatikanaji wa machapisho ya Shahada za (d) uzamili na uzamivu kwa kuingiza makala na vitabu katika mtandao wa intaneti (online);
ku(e) kamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa 10 kupitia mradi wa
Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu;
36
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuongeza fursa za upatikanaji wa maarifa kwa kuweka (f)
intaneti isiyotumia waya (wireless internet) katika vituo vya
Mtwara, Lindi, Simiyu, Njombe, Singida, Tabora, Dodoma,
Kagera, Zanzibar, Pemba; na katika kituo cha Kibungo
nchini Rwanda;
kuongeza fursa ya mafunzo kwa kutoa mafunzo ya ualimu (g)
kwa wanafunzi 12 katika ngazi ya shahada ya uzamili na
wanafunzi 14 kwa ngazi ya Stashahada kutoka nchi za
SADC (Angola, Kongo-DRC, Lesotho, Malawi, Zambia na
Zimbabwe); na
kufanya utafiti katika maeneo mbalimbali yakiwemo (h)
usalama wa matumizi ya TEHAMA, uimarishaji wa taratibu
za kukusanya na kuzitupa takataka katika Jiji la Dar es
salaam, matumizi ya maji ya ziwa Viktoria, matumizi ya simu
za viganjani, mafanikio na matatizo ya kujifunza kwa njia
ya elektroniki, na uimarishaji wa ufugaji wa kuku wa kienyeji
Ilima katika mkoa wa Mbeya.
Chuo Kikuu Ardhi
Mheshimiwa Spika, 60. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa mafunzo,
kutafiti na kutoa ushauri na huduma za kitaalamu katika nyanja za
maendeleo ya ardhi, nyumba, mazingira na ujenzi.
Mheshimiwa Spika61. , katika mwaka 2013/14, Chuo Kikuu Ardhi
kilitekeleza yafuatayo:
37
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kukamilisha ujenzi wa ofisi 6 za walimu katika jengo la (a)
“Lands Building” kwa kutumia fedha za ndani;
kuunganisha mtandao wa TEHAMA wa Chuo kwenye mkongo (b)
wa Taifa;
kufanya utafiti na kutoa ushauri katika masuala ya ardhi na (c)
maendeleo ya makazi; yakiwemo - udhibiti wa maji taka na
mabadiliko ya tabianchi, matabaka ya miamba iliyoko chini
ya ardhi ambapo machapisho 6 yametolewa, utengenezaji
wa miundombinu ya upimaji (survey reference points), na
ilitayarisha machapisho 22 ya utafiti uliokwishafanywa na
chuo katika maeneo mbalimbali; na
ilitoa ushauri katika maeneo yafuatayo: uandaaji wa taarifa (d)
ya uimarishaji wa hali za majiji na miji ya Tanzania ambapo
rasimu ya taaarifa hiyo imekamilika; tathmini na usimamizi
bora wa ardhi; na awamu ya pili ya TACINE ya utayarishaji
wa mpango wa kujenga uwezo katika maeneo ya kubuni na
kutekeleza mipango ya kugharamia uendelezaji miji.
Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili
Mheshimiwa Spika,62. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa mafunzo,
kutafiti na kutoa ushauri na huduma za kitaalamu katika maeneo
ya tiba na afya ya binadamu.
Mheshimiwa Spika63. , katika mwaka wa 2013/14, Chuo Kikuu
cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili kilitekeleza yafuatayo:
38
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuongeza fursa za Elimu ya Juu kwa kudahili wanafunzi (a)
448 wa shahada ya kwanza (udaktari wa binadamu 256,
madawa 66, uuguzi 63, udaktari wa meno na kinywa
43, afya, sayansi na mazingira 20) na wanafunzi 220
(wanawake ni 97) wa shahada za uzamili;
kuendeleza ujenzi wa hospitali na miundombinu ya barabara, (b)
maji na umeme katika eneo la Mloganzila;
kuchambua takwimu za utafiti wa TaMoVac-I na kuwasilisha (c)
chapisho (manuscript) kwenye jarida la kimataifa mwezi
Machi 2014. Aidha, kuendeleza utafiti wa TaMoVac – II
na ufuatiliaji wa washiriki waliopatiwa chanjo unatarajiwa
kukamilika mwezi Novemba 2014; na
kugharimia mafunzo kwa wanataaluma 48, (12 shahada ya (d)
uzamili, 36 shahada ya uzamivu) kupitia miradi mbalimbali
na wafadhili ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu.
Chuo Kikuu Mzumbe
Mheshimiwa Spika,64. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa mafunzo,
kutafiti na kutoa ushauri katika maeneo ya maarifa na stadi za
menejimenti.
Mheshimiwa Spika65. , katika mwaka 2013/14, Chuo Kikuu Mzumbe
kilitekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za Elimu ya Juu kwa kudahili wanafunzi(a)
4,488 katika programu za cheti 297, stashahada 383,
39
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
shahada ya kwanza 2,087, shahada ya uzamili 1,692 na
shahada ya uzamivu 29;
kukamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa tano kwa ajili ya (b)
vyumba vya ofisi, madarasa na kumbi za mihadhara;
kuongeza ufanisi na tija katika utoaji wa elimu kwa kugharimia (c)
watumishi 21 katika mafunzo ya shahada ya uzamili na 7
shahada ya uzamivu; na
kuimarisha masuala ya menejimenti, uongozi na sayansi (d)
ya jamii kwa kukamilisha utafiti katika maeneo 9 na kutoa
ushauri wa kitaalamu katika maeneo 25.
Chuo Kikuu cha Dodoma
Mheshimiwa Spika,66. Chuo hiki kina majukumu ya kutoa mafunzo,
kufanya utafiti na kutoa ushauri wa kitaalamu katika maeneo ya
Elimu ya juu.
Mheshimiwa Spika,67. katika mwaka 2013/14, Chuo Kikuu cha
Dodoma, kilitekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa ya upatikanaji wa Elimu ya Juu kwa kudahili (a)
wanafunzi 6,101 wakiwemo 5,513 shahada ya awali, 559
shahada ya uzamili na 29 shahada ya uzamivu;
kuinua ubora wa mazingira ya kutolea mafunzo kwa (b)
kukamilisha ujenzi wa maabara na madarasa kwa asilimia
40
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
80. Aidha, ilikamilisha ujenzi wa matanki mawili yenye uwezo
wa kuhifadhi lita 7,500,000 za maji kwa ufadhili wa Benki
ya Dunia kupitia mamlaka ya maji safi na maji taka Dodoma
(DUWASA);
kukamilisha utafiti na kutoa ushauri wa miradi 4 kwa (c)
ushirikiano na Taasisi mbalimbali nje na ndani ya Tanzania;
na
kuimarisha mazingira ya kutolea mafunzo kwa kuweka (d)
miundombinu ya umeme na TEHAMA katika vyuo vya Sayansi
za Asili, Hisabati na Sayansi za Ardhi.
Usimamizi na Utekelezaji wa Programu na Miradi
Mheshimiwa Spika,68. wizara yangu pia ina programu na miradi
mbalimbali ambayo iko chini yake. Katika mwaka 2013/14, wizara
ilitekeleza yafuatayo katika eneo hili:
kuwezesha utekelezaji wa mikakati ya Mpango wa Matokeo (a)
Makubwa Sasa katika Elimu Msingi (BRNedu) kwa kutoa
mafunzo kazini kwa walimu 12,476 kati ya hao, walimu
8,400 wa masomo ya Sayansi na Hisabati na 4,076 wa
masomo yanayosomwa na wanafunzi wote (Mathematics,
Biology, English na Kiswahili) na pia Wakuu wa Shule 3,152
walipatiwa mafunzo katika mwongozo wa usimamizi na
uendeshaji wa shule.
41
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kukamilisha tathmini ya stadi za Kusoma, Kuandika na (b)
Kuhesabu (KKK) pamoja na umakini katika uongozi wa
shule kwa kutumia EGRA na EGMA ambapo changamoto
mbalimbali zilibainishwa ikiwemo kubainisha njia
mbalimbali za kukabiliana na chanagamoto hizo. Wizara
inapitia maeneo mbalimbali ikiwemo mitalaa ili kuaanda
miongozo ambayo itaanza kutekelezwa mwaka 2014/15
ili kukabiliana na changamoto zilizobainishwa;
kukamilisha awamu ya kwanza ya Mradi wa Sayansi, (c)
Teknolojia na Elimu ya Juu (Science, Technology and Higher
Education Program - STHEP) kwa ufanisi. Majengo mapya
17 yenye vyumba vya Mihadhara 48, Maabara za Sayansi
93 na ofisi 302 za wafanyakazi zilijengwa. Majengo
hayo yataongeza nafasi za kufundishia na kujifunzia kwa
wanafunzi 47,622 na ofisi za Wahadhiri 1,794, katika
kuinua ubora wa mazingira ya kufundishia na kujifunzia.
Vyuo vilivyonufaika na mradi huu ni Chuo Kikuu cha Dar
es Salaam, Chuo Kikuu Ardhi, Chuo Kikuu cha Sokoine cha
Kilimo, Chuo Kikuu Huria Tanzania, Chuo Kikuu Kishiriki
cha Elimu Dar es Salaam, Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu
Mkwawa, Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Taasisi
ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia na
Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar;
42
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kukamilisha na kuzindua Mpango wa Maendeleo ya Elimu (d)
ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Technical and
Vocational Education and Training Development Programme – TVETDP) 2013/14 – 2017/18 ulizinduliwa tarehe 13 Desemba 2013. Azma ya mpango huu ni kuongeza udahili katika ngazi mbalimbali za elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi ili kujenga uwiano na nguvukazi katika ngazi mbalimbali kwa kila fani yenye kuhimili ushindani wa soko la ajira ndani na nje ya nchi;
kukamilisha majadiliano ya mradi wa (e) Literacy and Numeracy Education Support (LANES) wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 94.8 katika kuinua kiwango cha kumudu Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) kwa wanafunzi wa Darasa la I na la II. Mradi huu utatekelezwa kwa takribani asilimia 90 katika ngazi ya Halmashauri. Wizara yangu itashughulikia masuala yote ya uaandaaji na uimarishaji wa walimu katika KKK na Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto itashughulikia masuala yaliyopo katika mpango huo kuhusu ECD. Mradi huu utaanza kutekelezwa mwezi Juni, 2014 baada ya kukamilika taratibu za utekelezaji, ili kupata ufanisi;
kuanza kutekeleza mradi wa kupata takribani vitabu (f) 6,000,000 vya sayansi na hisabati kwa elimu ya sekondari ili kupata uwiano wa kitabu kimoja kwa mwanafunzi mmoja. Mkataba wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni tisa (9,000,000) tayari umesainiwa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID); na
43
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuzindua (g) Wiki ya Elimu ya Taifa ambayo itakuwa inafanyika kuanzia ngazi ya Halmashauri, Mkoa hadi Taifa kila mwaka ili kutoa fursa kwa wananchi na wadau wa elimu kujadili masuala na maendeleo ya elimu katika maeneo yao na kubaini changamoto na mbinu za kuendeleza na kuiimarisha ubora wa elimu. Kwa mwaka 2014 wiki ya elimu ilifanyika kuanzia tarehe 3 hadi 10 Mei, kauli mbiu ilikuwa ni Elimu Bora Inawezekana, Tekeleza Wajibu
Wako.
IV. CHANGAMOTO
Mheshimiwa Spika69. , katika utekelezaji wa majukumu na bajeti
ya mwaka 2013/14, Wizara yangu ilikabiliana na changamoto
katika maeneo mbalimbali inayoyasimamia kama ifuatavyo:
kuimarisha mifumo ya usimamizi, ufuatiliaji na tathmini (a) ya utekelezaji wa sera za elimu hususan katika maeneo yaliyoguswa na ugatuaji;
upatikanaji wa rasilimali fedha za kutosha na kwa wakati (b) na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu mbalimbali ya wizara kama vile kulipia madeni ya wazabuni na huduma nyingine;
upatikanaji wa rasilimali mbalimbali wakiwemo wataalamu (c) na fedha ili kuwezesha upatikanaji wa matokeo stahiki;
kupata walimu mahiri wa kufundisha stadi za KKK kwa (d)
kiwango cha kutosha kwa wanafunzi wa madarasa ya chini
(Darasa la I na II);
44
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
namna ya kuongeza idadi ya wanafunzi wa elimu ya juu (e) ili ikaribiane na kupita ile ya nchi za Afrika Mashariki na baadhi ya nchi jirani ambazo zina kiwango cha wastani wa asilimia 5 wa rika husika ikilinganishwa na wastani wa asilimia 2.7 kwa Tanzania;
upatikanaji wa wataalam wa Kitanzania katika fani za (f) gesi, mafuta, chuma, urani, makaa ya mawe na madini mengine;
upatikanaji wa rasilimali watu na rasilimali nyingine (g) ili kuwezesha ukaguzi wa shule kufanyika kwa ufanisi kulingana na miongozo ya ukaguzi kutokana na ongezeko la mikoa na Halmashauri mpya; na
kuimarisha mfumo wa ukaguzi wa shule ili kuendana (h) na mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia na masuala mbalimbali yatokanayo na mtangamano wa kikanda na kimataifa.
Mheshimiwa Spika70. , changamoto nyingine zilizojitokeza ni hizi zifuatazo:
kuinua kiwango cha ufahamu, maarifa na ujuzi wa walimu (a) ili kuwa mahiri katika kutoa elimu na mafunzo yanayokidhi mahitaji ya jamii kulingana na mazingira na maendeleo ya nchi;
upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia katika (b) elimu ya ualimu na kuinua kiwango cha mazingira ya kufundishia na kujifunzia;
matumizi sahihi ya TEHAMA kama sehemu ya nyezo muhimu (c) katika mafunzo ya ualimu;
45
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
ongezeko la gharama ya kusomesha walimu katika vyuo (d) vya ualimu vya Serikali ngazi ya cheti na stashahada; na
ongezeko la mahitaji ya walimu wa masomo ya Sayansi na (e)
Hisabati katika ngazi zote za elimu na mafunzo. Mahitaji
ya walimu yameoneshwa katika jedwali Na. 1 hapo chini.
Jedwali Namba 1: Mahitaji ya Walimu wa Sayansi na Hisabati
Somo Wanaohitajika Waliopo Upungufu %Agriculture 905 300 605 66.9
Physics 10,203 3,748 6,455 63.3
Computer Studies 1,108 433 675 60.9
Electrical Engineering
69 29 40 58.0
Basic Mathematics 13,478 5,896 7,582 56.3Chemistry 10,541 4,887 5,654 53.6
Biology 11,144 5,561 5,583 50.1
Engineering Science
47 24 23 48.9
Mechanical Engineering
80 41 39 48.8
Food and Nutrition 220 120 100 45.5
Civil Engineering 100 60 40 40.0
Additional Mathematics
512 310 202 39.5
Total 48,407 21,409 26,998 55.8Chanzo: Basic Education Statistics in Tanzania – BEST, 2013
46
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika71. , katika kusimamia Taasisi na Wakala zilizo
chini ya wizara, changamoto zilizojitokeza ni pamoja na:
miundombinu chakavu na isiyotosheleza kutolea huduma (a)
kwa wadau wake;
upatikanaji wa fedha za kutosha kutoa mkopo ili kugharimia (b)
elimu ya juu na elimu ya ufundi; na
upatikanaji wa rasilimali za kutosha na kuwezesha (c)
kufanyika utafiti endelevu kwa maendeleo ya taifa.
uwepo wa wanafunzi wachache kuliko uwezo wa vyuo (d)
vilivyopo kama ambavyo Jedwali Na. 2 linavyoonesha
katika elimu na mafunzo ya ufundi stadi hapa chini.
47
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Jedw
ali n
a. 2
: Oro
dha
ya V
yuo
vya
VET
A, U
wez
o w
a K
udah
ili n
a Id
adi y
a W
anaf
unzi
W
alio
sajil
iwa,
201
3
Na
Mko
aW
ilaya
Jina
La
Chu
o
Uw
ezo
wa
Kud
ahili
W
anaf
unzi
kw
a m
wak
aId
adi y
a W
anaf
unzi
W
alio
sajil
iwa
2013
/14
%K
ozi
Nde
fuK
ozi
Fupi
Jum
laM
me
W’k
eJu
mla
1
Aru
sha
Aru
mer
uA
rush
a V
tc28
040
068
015
2816
916
9725
0
2A
rush
a M
jini
Veta
Hot
el A
nd
Tour
ism T
rain
ing
Inst
itute
300
400
700
4410
514
921
3D
ar E
s Sa
laam
Ilala
Kipa
wa
- In
stitu
te
of IC
T15
016
0017
5019
721
140
823
4Te
mek
eD
ar E
s Sa
laam
RV
TSC
1200
1000
011
200
801
530
1331
12
5D
odom
aD
odom
a M
jini
Dod
oma
Regi
onal
Vo
catio
nal T
rain
ing
Cen
tre
550
1342
1892
1329
509
1838
97
6Iri
nga
Iring
a M
jini
Iring
a RV
TSC
400
1450
1850
1133
7612
0965
7Ka
gera
Buko
ba M
jini
Kage
ra V
tc20
050
070
044
113
757
883
8Ka
tavi
Mpa
nda
Mjin
iM
pand
a Vo
catio
nal
Trai
ning
Cen
tre
365
280
645
166
3319
931
9Ki
gom
aKi
gom
a M
jini
Kigo
ma
RVTS
C40
014
5018
5019
3290
228
3415
3
10Ki
liman
jaro
Mos
hi M
jini
Mos
hi R
VTS
C50
120
0025
0112
2335
515
7863
11Li
ndi
Lind
i Mjin
iLi
ndi R
VTS
C35
050
085
079
3010
913
12M
anya
raBa
bati
Mjin
iM
anya
ra R
VTS
C13
042
055
062
3910
118
13M
ara
Mus
oma
Mjin
iM
ara
Vtc
200
500
700
997
211
1208
173
14M
beya
Mbe
ya M
jini
Mbe
ya R
VTS
C40
014
5018
5013
7425
416
2888
48
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/201515
Mor
ogor
o
Kilo
saM
ikum
i Vtc
475
600
1075
420
238
658
61
16M
orog
oro
Mjin
iKi
hond
a RV
TSC
400
700
1100
273
6433
731
17M
orog
oro
Mjin
i
Mor
ogor
o Vo
catio
nal
Teac
hers
Tra
inin
g C
olle
ge80
030
0038
0085
512
9421
4957
18M
vom
ero
Dak
awa
Vtc
200
500
700
100
3713
720
19M
twar
aM
twar
a M
jini
Mtw
ara
RVTS
C40
030
070
033
429
462
890
20M
wan
zaM
wan
za
RVTS
CRV
TSC
Mw
anza
300
400
700
1402
162
1564
223
21N
jom
beM
aket
eM
aket
e D
vtc
300
400
700
129
7220
129
22Pw
ani
Kiba
ha M
jini
Pwan
i RV
TSC
160
320
480
157
8424
150
23Ru
vum
aSo
ngea
Mjin
iSo
ngea
Vtc
260
887
1147
6478
142
12
24Sh
inya
nga
Shin
yang
a M
jini
Shin
yang
a V
tc40
060
010
0091
113
510
4610
5
25Si
ngid
aSi
ngid
a M
jini
Sing
ida
Vtc
360
300
660
290
104
394
6026
Tabo
raTa
bora
Mjin
iTa
bora
RV
TSC
360
500
860
412
6147
355
27Ta
nga
Tang
a M
jini
Tang
a RV
TSC
416
416
832
1413
403
1816
218
Ju
mla
1025
731
215
4147
218
066
6587
2465
359
Cha
nzo:
Mam
laka
ya
Elim
u na
Maf
unzo
ya
Ufu
ndi,
2014
49
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Jedwali hili ni 72. 59% ya uwezo
wa vyuo vyetu vya elimu na mafunzo ya ufundi inayotumika. Katika
hili Halmashauri zetu zinabidi zifanye kazi ya ziada ili vyuo hivi
vitumike kwa ukamilifu na wananchi katika maeneo hayo wapate
faida ya vyuo hivyo kuwa jirani na maeneo yao.
V. VIPAUMBELE NA MAKADIRIO YA MAPATO NA
MATUMIZI KWA MWAKA 2014/15
Mheshimiwa Spika, 73. baada ya kutoa taarifa ya utekelezaji wa
bajeti kwa mwaka wa fedha 2013/14, naomba sasa niwasilishe
vipaumbele vya Wizara na kisha Makadirio ya Mapato na
Matumizi kwa mwaka 2014/15.
Vipaumbele
Mheshimiwa Spika, 74. vipaumbele vya sekta ya elimu vilivyoainishwa
katika Mwongozo wa Maandalizi ya Bajeti kwa mwaka 2014/15
ni
kuinua ubora wa elimu na kujenga stadi stahiki katika ngazi (a)
zote za elimu na mafunzo; na
kuongeza upatikanaji wa fursa ya elimu kwa usawa katika (b)
ngazi zote za elimu na mafunzo.
Mheshimiwa Spika,75. katika kuchangia utekelezaji wa vipaumbele
vya sekta, wizara yangu imejipanga kutekeleza yafuatayo
kulingana na Hati Idhini yake:
50
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika,76. katika Utungaji na Utekelezaji wa Sera za
Elimu, wizara yangu itatekeleza yafuatayo:
kukamilisha Sera ya Elimu na Mafunzo na kuandaa mpango (a)
mkakati ya utekelezaji wake;
kuimarisha mfumo wa kitaasisi wa kusimamia ubora wa (b)
Elimu Msingi kwa kuanzisha Mamlaka ya Ithibati na Uthibiti
wa Elimu Msingi na Sekondari ili kuhakikisha kuwa utoaji
wa elimu unazingatia sera, miongozo na mitaala ya elimu
yenye kukidhi mahitaji ya soko na jamii;
kukamilisha taratibu za uanzishwaji wa Bodi ya Kitaalamu (c)
ya Walimu Tanzania itakayosimamia masuala ya walimu
ikiwemo, usajili, uendelezaji wa walimu na maadili ya kazi
ya ualimu na kuendelea kujadiliana na wadau wengine
ikiwemo Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma
na OWM TAMISEMI kuhusu suala la namna bora ya
kumhudumia mwalimu katika mazingira ya sasa ya ugatuaji
wa huduma mbalimbali kwenda OWM TAMISEMI;
kuendelea kuimarisha mifumo na miundo ya mitaala, (d)
ithibati, uthibiti ubora, na tathmni mbalimbali za maendeleo
ya wanafunzi katika ngazi mbalimbali;
kuimarisha Taasisi ya Elimu Tanzania katika kushughulikia (e)
ithibati na uthibiti wa vitabu, zana na vifaa mbalimbali vya
elimu msingi na sekondari;
51
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kwa kushirikiana na OWM-TAMISEMI na wadau wengine, (f)
kuweka mfumo na muundo utakaosaidia wanafunzi wengi
kuendelea na masomo ya elimu ya sekondari ya juu ili kufikia
lengo la angalau wanafunzi 250,000 ifikapo 2016;
kuhuisha mitaala na kuimarisha mfumo wa utoaji wa (g)
elimu ya ufundi na mafunzo ya ufundi stadi ili kutoa elimu
kulingana na mahitaji halisi ya soko la ajira na maendeleo
ya taifa;
kuimarisha ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa sera za (h)
elimu na mafunzo katika ngazi zote kwa kuandaa na kutoa
miongozo; na
kuhuisha na kuoanisha programu za Elimu ya Juu pamoja (i)
na Ufundi ili utoaji wa elimu hiyo uzingatie mahitaji ya soko
la ajira kwa maendeleo ya taifa.
Mheshimiwa Spika,77. katika Usajili wa Shule, wizara yangu
itatekeleza yafuatayo:
kuendelea kusajili shule za msingi na sekondari kwa kutilia (a)
mkazo zaidi shule za ufundi na sayansi;
kuimarisha mfumo wa usajili wa shule; (b)
kuhuisha mwongozo wa usajili ili uendane na wakati; na (c)
kutoa elimu kwa umma kuhusu taratibu za usajili wa (d)
shule
52
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika,78. katika Ukaguzi wa Shule na Vyuo wizara
yangu itatekeleza yafuatayo:
kuimarisha taratibu za ukaguzi na kuendelea kukagua (a)
shule na vyuo vya ualimu kwa ufanisi zaidi;
kukamilisha uundwaji wa mamlaka ya ithibati na uthibiti (b)
wa elimu msingi na sekondari ambayo itatekeleza pia
jukumu la ukaguzi wa shule; na
kufungua ofisi za ukaguzi katika Wilaya mpya na (c)
Wilaya ambazo hazina ofisi hizo.
Mheshimiwa Spika,79. katika kusimamia utoaji wa Mafunzo ya
Ualimu wizara yangu itatekeleza yafuatayo:
kuimarisha ufundishaji wa walimu wa stadi za KKK;(a)
kushirikiana na wadau wengine na kutekeleza mkakati wa (b) kupunguza uhaba wa walimu wa sayansi na hisabati;
kuanza kutoa ruzuku na mikopo kwa wanafunzi wanaosomea (c) stashahada ya ualimu wa sayansi na hisabati kulinganana na vigezo vitakavyowekwa katika vyuo vilivyoteuliwa;
kuimarisha mafunzo ya ualimu na kuweka muundo endelevu (d) (Framework for Teacher Competency and Development) wa weledi na maendeleo ya mwalimu;
kuvipatia vyuo vya ualimu (e) 34 ithibati ya NACTE ili viweze kuingia rasmi katika mfumo wa ithibati na uthibi wa ubora
unaotambulika kitaifa katika sekta ya elimu ya ufundi;
53
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kufanya uchambuzi na tathmini kwa kushirikiana na OWM-(f)
TAMISEMI ili kujua idadi ya walimu na weledi kwa kila
somo. Aidha, matokeo ya uchambuzi yatatumika kuimarisha
mkakati wa kuandaa na kuendeleza walimu na hivyo
kukabiliana na upungufu wa walimu kwa kila somo; na
kuendelea kuimarisha vyuo vya ualimu ikiwemo mfumo (g)
na muundo wake ili viwe na tija na ufanisi zaidi katika
kutekeleza jukumu la kuandaa walimu mahiri na wenye
weledi.
Mheshimiwa Spika,80. katika kusimamia Taasisi na Wakala zilizo
chini ya Wizara, yafuatayo yatatekelezwa:
kujenga uwezo wa taasisi za usimamizi wa ubora wa elimu (a)
ili kuhakikisha kuwa elimu bora inatolewa katika ngazi zote
za elimu na mafunzo;
kuendelea kuinua ubora na kuimarisha vyuo vya elimu ya (b)
juu pamoja na ufundi ili viwe ‘vyuo vya maendeleo kizazi
cha tatu’ (3rd generation development institutions) kulingana
na kasi ya maendeleo iliyopo duniani na kuweza kufikia
malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 kwa
haraka; na
kuendelea kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji kwa kuweka (c)
mifumo ya kidigitali ili kuwezesha walimu na wanafunzi
kupata maandiko mbalimbali muhimu kwa maendeleo ya
elimu na Taifa kwa ujumla kupitia TEHAMA.
54
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika, 81. kwa upande wa Taasisi na Wakala, katika
mwaka 2014/15 Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imelenga
kutekeleza yafuatayo:
kudahili wanafunzi wa programu ya Elimu ya Watu Wazima (a)
na Mafunzo Endelevu (Adult and Continuing Education Studies)
ngazi ya Cheti – 100 Stashahada – 950 na Shahada – 200
pamoja na 200 wa shahada ya programu mpya ya Elimu ya
Watu Wazima na Maendeleo ya Jamii (Adult Education and
Community Development) ;
kusimamia uanzishaji, usajili na uendeshaji wa vituo (b)
vinavyotoa Elimu ya Sekondari kwa Njia ya Ujifunzaji Huria
na Masafa (UHM) nchini ;
kuandika mihtasari na moduli za masomo ya Biashara na (c)
Sayansi hatua ya 2 (sawa na kidato cha 1 na 2) ili kuongeza
fursa ya utoaji wa Elimu ya Sekondari kwa njia ya Ujifunzaji
Huria na Masafa; na
kusimamia mpango tarajali wa “Elimu Changamani badala (d)
ya Msingi” katika wilaya 13 kwa kushirikiana na Shirika la
UNICEF; na Mpango wa Elimu Mbadala kwa wasichana
waliopata mimba wakiwa shuleni katika Wilaya za
Shinyanga Vijijini na Msalala kwa kushirikiana na Shirika la
UNESCO.
55
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika, 82. katika mwaka 2014/15 Taasisi ya Elimu
Tanzania imelenga kutekeleza yafuatayo:
kufanya tathmini ya utekelezaji, kupitia na kuboresha mtaala (a)
wa Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Ualimu;
kutoa mafunzo kuhusu utekelezaji wa mitaala kwa Walimu, (b)
Wakaguzi wa Shule, Maafisa Elimu na Waratibu Elimu
Kata;
kufanya utafiti kuhusu ufundishaji na ujifunzaji wa masomo (c)
ya sayansi na hisabati; na
kuandika vitabu vya kiada kwa shule za msingi na (d)
sekondari.
Mheshimiwa Spika, 83. katika mwaka 2014/15 Bodi ya Huduma
za Maktaba Tanzania imelenga kutekeleza yafuatayo:
kutoa machapisho 50,000 ili kuinua ubora wa huduma za (a)
Maktaba katika mikoa 21 ya Tanzania Bara;
kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu uanzishaji na uendeshaji (b)
wa Maktaba za Shule, Vyuo, Taasisi na Halmashauri za Miji,
Manispaa na Wilaya nchini;
kutoa mafunzo ya Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka kwa (c)
walengwa 700 wa cheti, 500 wa stashahada na 500 wa
mafunzo ya awali kwa ajili ya wafanyakazi wa Maktaba;
na
56
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuendeleza ujenzi na kukarabati miundombinu ya Chuo cha (d)
Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (SLADS) Bagamoyo ikiwemo
maabara ya kompyuta na nyumba ya wafanyakazi.
Mheshimiwa Spika, 84. katika mwaka 2014/15 Wakala wa
Maendeleo ya Uongozi wa Elimu imelenga kutekeleza yafuatayo:
kutoa mafunzo ya Stashahada ya Uongozi wa Elimu kwa (a)
washiriki 900 wakiwemo Walimu Wakuu, Waratibu Elimu
Kata, Maafisaelimu wa Halmashauri, Walimu wa Shule za
Awali, Msingi, Sekondari, Wafanyakazi katika mashirika
yasiyo ya kiserikali (NGOs), Mameneja na Wamiliki wa
Shule zisizo za Serikali;
kutoa mafunzo ya Stashahada ya Ukaguzi wa Shule kwa (b)
Wakaguzi 240 wa Halmashauri za Tanzania Bara na
Mafunzo ya Cheti cha Uongozi na Uendeshaji wa Elimu
kwa Walimu Wakuu 720 katika wilaya 12 za majaribio ya
UNICEF;
kutoa mafunzo ya muda mfupi ya Uongozi, Uendeshaji na (c)
Usimamizi wa Elimu kwa wajumbe 9,000 wa Kamati na Bodi
za Shule, Wakuu wa Shule 4,300, Wakaguzi wa Shule 240,
Maafisaelimu 884 wa Mikoa na Halmashauri; na
kuwajengea uwezo watumishi 44 kwa kuwagharamia (d)
mafunzo ya muda mfupi na mrefu.
57
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika, 85. katika mwaka wa fedha 2014/15, Tume ya Taifa ya UNESCO imelenga kutekeleza yafuatayo:
kushirikisha na kuhakikisha wadau wanashiriki katika (a) kupanga na kutekeleza program za UNESCO katika Nyanja za Elimu, Sayansi Asilia, Sayansi ya Jamii, Utamaduni, Habari na Mawasiliano;
kushirikiana na wadau katika kutafuta fedha za kutekeleza (b) miradi saba (7) ya ushirikishwaji “Participation Projects”; na
kuchapisha na kusambaza nakala 800 za toleo la jarida la (c) “Tanzania and UNESCO Magazine”.
Mheshimiwa Spika, 86. katika mwaka 2014/15 Baraza la Mitihani la Taifa limelenga kutekeleza yafuatayo:
kuendesha mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kwa (a) watahiniwa 998,295 wanaotarajiwa kufanya mtihani huo mwaka 2014;
kuendesha mitihani ya sekondari kidato cha nne kwa (b) watahiniwa 492,129, Maarifa (Qualifying Test – QT) Watahiniwa 20,946 kwa mwaka 2014 na kidato cha sita Watahiniwa 61,335 kwa mwaka 2015; na
kuendesha mitihani ya Ualimu kwa Watahiniwa 35,297 kwa (c) mwaka 2015.
Mheshimiwa Spika87. , katika mwaka 2014/15 Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi limelenga kutekeleza yafuatayo:
kuratibu udahili wa wanafunzi 60,000 katika ngazi ya (a) cheti, stashahada, na shahada katika vyuo vilivyosajiliwa na Baraza;
58
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kukagua, kusajili na kutoa ithibati kwa vyuo vya ufundi 50 ili (b) kudhibiti ubora wa elimu;
kubaini na kusajili walimu 400 katika vyuo vya ufundi;(c)
kutoa mwongozo na kusimamia utengenezaji wa mfumo wa (d) kuhakiki ubora wa mafunzo katika vyuo vya ufundi 20 ; na
kutengeneza mitaala ya kitaifa 10 (ngazi ya cheti na (e) stashahada) na kuidhinisha mitaala 40 ya ngazi za cheti, stashahada na shahada, pamoja na kuratibu mafunzo ya walimu 150 kuhusu kufundisha kwa kutumia mitaala inayozingatia umahiri, katika vyuo vya ufundi.
Mheshimiwa Spika, 88. katika mwaka 2014/15, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kudahili wanafunzi wapya 300 wa Cheti, 400 wa Stashahada (a) na 600 wa Shahada ya Kwanza;
kuanzisha mafunzo ya Cheti na Stashahada katika (b) Rasilimali Watu (Certificate and Diploma in Human Resource Management) na Cheti katika Maendeleo ya Uchumi (Certificate in Economic Development);
kuajiri wafanyakazi waendeshaji 25 na kugharamia mafunzo (c) ya wanataaluma 18 na wafanyakazi waendeshaji 3; na
kuendeleza ujenzi wa hosteli katika kampasi ya Kivukoni.(d)
Mheshimiwa Spika, 89. katika mwaka 2014/15, Chuo cha Ufundi Arusha kimelenga kutekeleza yafuatayo:
59
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kudahili wanafunzi 550 wa mwaka wa kwanza (Cheti na (a) Stashahada 520, Shahada 30);
kuanzisha program ya stashahada ya Ualimu wa masomo (b) ya Sayansi na ya Ufundi Sanifu (NTA 4-6) katika fani ya Magari na Mitambo Mikubwa (Heavy Duty Equipment);
kuhuisha mitaala 12 ya programu za Ufundi Sanifu (NTA (c) 4-6);
kuandaa mpango mkakati wa kuanzisha kituo cha mafunzo (d) ya kutengeneza mashine ndogondogo za kuzalisha umeme na wa Kukarabati Kituo cha Kuzalisha Umeme Kikuletwa;
kuendeleza ujenzi wa jengo la Uhandisi Umwagiliaji, kununua (e) samani na kuimarisha vyanzo na miundombinu ya umwagiliaji katika shamba la Oljoro;
kuajiri wafanyakazi 22 waendeshaji na 20 wanataaluma (f) pamoja na kugharimia mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa wafanyakazi 15 wanataaluma na 10 waendeshaji; na
kufanya tafiti za Kisayansi na kutoa ushauri wa kitaalamu (g) katika nyanja za Sayansi na Teknolojia.
Mheshimiwa Spika, 90. katika mwaka 2014/15 Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi imelenga kutekeleza yafuatayo:
kuratibu uanzishwaji wa mafunzo ya asubuhi na jioni pamoja (a) na kuongeza mafunzo ya muda mfupi ili kuongeza udahili wa wanafunzi katika Vyuo vya Ufundi Stadi kutoka 145,511 hadi 175,000;
60
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo na umahiri walimu (b) 150 wa VETA na wasio wa VETA;
kutoa mafunzo mbalimbali ya ufundi stadi kwa wafanyakazi (c) wa kampuni 50 na wafanyakazi 3,000 wa sekta isiyo rasmi ili kuimarisha stadi, tija na ajira;
kuanza ujenzi wa Vyuo 4 vya VETA vya Mikoa ya Geita, (d) Simiyu, Njombe na Rukwa na vya Wilaya za Kilindi, Chunya, Ukerewe, Ludewa na Namtumbo pamoja na kukarabati Vyuo vya Wilaya za Korogwe na Karagwe;
kufanya utafiti wa soko la ajira katika maeneo ya Machimbo (e) ya Gesi, Madini ya Chuma na Makaa ya Mawe katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Iringa, Njombe na Ruvuma pamoja na kufanya mapitio na kuandaa mitaala kwa ajili ya mafunzo katika Sekta ya Gesi na Mafuta;
kujenga mitandao ya TEHAMA katika vituo vitano vya VETA (f) vya Oljoro Arusha, Dakawa Morogoro, Singida, Ulyankulu Tabora na Mpanda na kukarabati karakana saba (7) za Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi Stadi vya Mwanza, Moshi , Mtwara, Kihonda na Chuo cha Walimu wa Ufundi Stadi cha Morogoro; na
kutambua na kurasimisha ujuzi wa Ufundi Stadi uliopatikana (g) katika mfumo wa mafunzo usio rasmi.
Mheshimiwa Spika, 91. Jendwali Namba 3 linaonesha uwezo wa kudahili wanafunzi kwa vyuo vya elimu na mafunzo ya ufundi stadi
kwa mwaka 2014/15
61
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Jedw
ali n
amba
3: U
wez
o w
a V
yuo
vya
Elim
u ya
Ufu
ndi V
itaka
vyoj
engw
a 20
14/1
5
Na
Mko
aW
ilaya
Jina
la C
huo
Uw
ezo
wa
Kud
ahili
W
anaf
unzi
(Id
adi)
Koz
i N
defu
Koz
i Fu
piJu
mla
1G
eita
Gei
ta M
jini
Gei
ta R
egio
nal V
ocat
iona
l Tra
inin
g C
entr
e35
075
011
00
2M
beya
Chu
nya
Chu
nya
DVTC
200
350
550
3M
wan
zaU
kere
we
Uke
rew
e DV
TC20
035
055
0
4N
jom
beN
jom
be M
jini
Njo
mbe
Reg
iona
l Voc
atio
nal
Trai
ning
and
Ser
vice
Cen
tre
350
600
950
5N
jom
beLu
dew
aLu
dew
a D
istric
t Voc
atio
nal T
rain
ing
and
Serv
ice
Cen
tre
200
350
550
6Ru
kwa
Sum
baw
anga
Mjin
iRu
kwa
Regi
onal
Voc
atio
nal T
rain
ing
and
Serv
ice
Cen
tre
350
600
950
7Ru
vum
aN
amtu
mbo
Nam
tum
bo D
VTC
200
350
550
8Si
miy
uBa
riadi
Mjin
iSi
miy
u Re
gion
al V
ocat
iona
l Tra
inin
g an
d Se
rvic
e C
entr
e35
060
095
0
9Ta
nga
Kilin
diKi
lindi
Dist
rict V
ocat
iona
l Tra
inin
g an
d Se
rvic
e C
entr
e20
035
055
0
Ju
mla
2400
4300
6700
Cha
nzo:
Mam
laka
ya
Elim
u na
Maf
unzo
ya
Ufu
ndi S
tadi
, Mei
201
4
62
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika, 92. napenda kuwaasa wananchi katika maeneo
vyuo hivi vitakapojengwa watumie fursa zilizopo na kujipatia elimu
na mafunzo ya ufundi stadi ili kuinua kiwango chao cha elimu na
ujuzi na kuchangia maendeleo ya Taifa
Mheshimiwa Spika, 93. katika mwaka 2014/15 Mamlaka ya Elimu
Tanzania imelenga kutekeleza yafuatayo:
kuinua ubora wa mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa (a)
kuendelea kutoa ufadhili na kutekeleza miradi ya elimu iliyo
katika mikakati ya mpango wa Matokeo Makubwa Sasa;
kuimarisha uwezo wa ugharimiaji elimu kwa kuendelea na (b)
uchangishaji wa fedha ili kupata Sh. bilioni 2.3 kwa ajili ya
ujenzi wa mabweni 30 ya wasichana kwenye Halmashauri 7
za Wilaya za Geita, Lushoto, Kasulu, Lindi, Musoma, Songea
na Manyara;
kuandaa maandiko ya miradi 12 ya Elimu na kuyawasilisha (c)
kwa wadau mbalimbali wa elimu wa ndani na nje ya nchi ili
kupata fedha kwa ajili ya kugharimia miradi hiyo; na
kuongeza fursa kwa wasichana kujiunga na elimu ya (d)
ufundi kwa kuendelea kufadhili mpango wa Pre-Entry kwa
wanafunzi wa kike wanaojiunga na vyuo vya ufundi.
Mheshimiwa Spika94. , katika mwaka 2014/15 Tume ya Vyuo Vikuu
Tanzania imelenga kutekeleza yafuatayo:
63
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kukagua na kutathimini mipango ya kuanzisha/kuhuisha (a)
Vyuo Vikuu 20 ili kusimamia ubora wa elimu itolewayo na
Vyuo Vikuu nchini;
kuendelea kuratibu na kusimamia udahili na ukaguzi wa (b)
wanafunzi wapatao 60,000 wanaojiunga na Vyuo Vikuu
ili kufikia lengo la kuwa na wanafunzi wapatao 300,000
kwenye Taasisi za Elimu ya Juu nchini ifikapo mwaka 2015;
kuendelea kuboresha mfumo wa udahili (CAS) ili uweze (c)
kufanya kazi kwa ufanisi zaidi;
kuvijengea uwezo Vyuo Vikuu katika kuandaa na kuhuisha (d)
programu za masomo kwa kuzingatia mfumo wa tuzo
unaotumika (University Qualification Framework);
kutathimini programu 150 za masomo toka Vyuo Vikuu (e)
nchini;
kuratibu upatikanaji wa wanataaluma 30 toka Vyuo Vikuu (f)
Nchini watakaojiunga na Masomo ya Uzamili na Uzamivu
chini ya makubaliano ya Serikali ya Tanzania na Ujerumani
(DAAD);
kuendelea kuratibu na kuandaa Maonyesho ya Tisa ya Elimu (g)
ya Juu , Sayansi na Teknolojia ili kuelimisha umma kuhusu
malengo, maendeleo na mchango wa Taasisi za Elimu ya Juu
katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini; na
kuanza ujenzi wa ofisi za kudumu za Tume katika kiwanja (h)
cha Uporoto, Dar es Salaam.
64
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika,95. katika mwaka 2014/15, Bodi ya Mikopo
ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu imepanga kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na elimu ya sayansi za tiba (a)
kwa kutoa ruzuku kwa wanafunzi 1,900 wanaosoma fani za
udaktari wa binadamu, meno na mifugo wa Vyuo vya Elimu
ya Juu;
kuongeza fursa za wanafunzi kujiunga na Elimu ya Juu kwa (b)
kutoa mikopo kwa wanafunzi ambapo wanafunzi 95,831
watapatiwa mkopo wakiwemo waombaji wa mara ya
kwanza 27,878 na wanafunzi wanaoendela 67,953, wa
Vyuo vya Elimu ya Juu; 3,000 wa stashahada ya Elimu ya
ualimu wa masomo ya sayansi na hisabati ;
kuimarisha uwezo wa Bodi wa kukusanya mikopo iliyokomaa (c)
kwa kukusanya marejesho ya mikopo yanayofikia Shilingi
39,610,694,361; na
kuimarisha uwezo wa Bodi kwa kuzipa vitendea kazi ofisi za (d)
Kanda ili ziweze kutekeleza majukumu yao kikamilifu.
Mheshimiwa Spika,96. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu cha
Dar es Salaam kimepanga kutekeleza yafuatayo:
kitaendelea kuboresha miundombinu ya kufundishia na (a)
kuboresha mazingira ya kufanyia utafiti;
kuinua ubora wa kitengo cha udhibiti wa ubora ((b) Quality
Assurance Bureau);
65
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuongeza udahili wa wanafunzi wa uzamili na uzamivu ili (c)
kutoa mchango zaidi wa wataalam kwenye vyuo vichanga;
na
kukarabati miundombinu ya maji taka pamoja na maeneo (d)
ya makazi ya wanafunzi.
Mheshimiwa Spika,97. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu
Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili (a)
wanafunzi 1,800 (500 wa fani ya sayansi);
kuongeza ubora wa elimu kwa kununua vifaa vya maabara (b)
na vifaa vya kufundishia na kujifunzia kwa ajili ya wanafunzi
wenye mahitaji maalumu;
kuendelea kuinua ubora wa mazingira ya kufundishia na (c)
kujifunzia kwa kukarabati jengo la kitivo cha sayansi za
jamii na humanitia (humanities), jengo la utawala kwa ajili
ya ofisi za wafanyakazi waendeshaji, jengo la maabara na
madarasa katika shule ya sekondari ya mazoezi na uzio
(fence) (Phase II) kuzunguka Chuo;
kuendelea kuinua ubora wa mazingira ya kufundishia na (d)
kujifunzia kwa kuimarisha miundombinu ya TEHAMA na
kukarabati miundombinu ya umeme na barabara;
kushirikiana na vyuo na taasisi za ndani na nje ya nchi (e)
katika utafiti na mafunzo, hususan kwa shahada za uzamili
na uzamivu;
66
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuinua ubora wa elimu kwa kuajiri wafanyakazi 105 (walimu (f)
43 na waendeshaji 62);
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kupata (g)
ardhi nyingine kubwa zaidi kwa ajili ya upanuzi wa chuo;
na
kuzuia mmomonyoko wa udongo ili kunusuru majengo ya (h)
hosteli ya Mbagala.
Mheshimiwa Spika,98. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu
Kishiriki cha Elimu Mkwawa kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili (a) wanafunzi wapya 1,200 wa mwaka wa kwanza 2014/15
kutoka 978 wa 2013/14;
kuimarisha ubora wa mazingira ya kufundishia na kujifunzia (b) na kuongeza fursa za wanafunzi kujiunga na Elimu ya Juu kwa
kukamilisha ujenzi wa ukumbi wa mihadhara wenye uwezo
wa kuchukua wanafunzi 1,000 na kukarabati miundombinu
ya Chuo;
kuendelea kugharimia masomo ya wahadhiri 16 walioko (c) masomoni katika viwango vya shahada za uzamili (6) na
uzamivu (10); na
kuinua ubora wa utoaji elimu kwa kuajiri wafanyakazi wapya (d) 65 (wanataaluma 51 na waendeshaji 14).
67
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika,99. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu cha
Sokoine cha Kilimo kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kuanzisha Shahada mpya za kwanza 3 na 3 za Uzamili na (a) masomo yasiyo ya shahada 5 ili kuelekea katika kufikia lengo la kuongeza Idadi ya wanafunzi kutoka waliopo 8,281 hadi 11,000 mwaka 2017;
kufufua na kuimarisha vitengo vya uzalishaji kwa lengo la (b) kuongeza mapato ya ndani;
kukamilisha miundombinu na majengo mapya (c) yanayogharimiwa na mradi wa Science Technology and Higher Education Project - STHEP na kuanza maandalizi ya ujenzi wa maabara kubwa moja kwa ajili ya Kitivo cha Sayansi inayogharamiwa na mradi wa Enhancing Pro-Poor Innovation for Natural Resources and Agricultural Value Chains - EPINAV. Aidha kuendeleza ujenzi wa jengo moja la ghorofa moja linalogharamiwa na Mradi wa Climate Change, Impact, Adaptation and Mitigation in Tanzania - CCIAM ambalo litakuwa na vyumba vya semina, ofisi, maabara za kompyuta pamoja na vyumba vya mihadhara, kukarabati kumbi 10 za mihadhara na nyumba za wafanyakazi zilizopo Kampasi ya Solomoni Mahlangu na Kampasi kuu;
kukarabati nyumba 50 za wafanyakazi, mabweni 4 ya (d) wanafunzi Kampasi ya Solomon Mahlangu, Mabweni 2 Kampasi kuu, na kukamilisha ukarabati wa barabara za ndani zilizopo Kampasi Kuu zenye km 3.6; na
68
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kukarabati baadhi ya Miundo mbinu iliyopo Kampasi za (e) Olmotonyi, Mazumbai, Mgeta na Mbinga; na
kuendeleza ujenzi wa jengo la kufundishia kwa ufadhili wa (f) CCIAM.
Mheshimiwa Spika,100. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu
Kishiriki cha Ushirika na Biashara Moshi, kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kukamilisha mchakato wa kuwa Chuo Kikuu kamili;(a)
kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka 4,700 kwa mwaka (b) wa fedha 2013/2014 hadi kufikia wanafunzi 4,911 kwa mwaka wa fedha 2014/2015;
kuendeleza mafunzo ya wafanyakazi, hususani Wahadhiri (c) 63 katika ngazi za Uzamili na Uzamivu;
kuboresha utafiti na uchapishaji wa makala mbalimbali ili (d) kusambaza elimu inayokidhi mahitaji ya sasa ya jamii, ikiwa ni pamoja na vyama vya ushirika, maendeleo ya ushirika, utunzaji mazingira na upunguzaji wa umaskini;
kuimarisha vituo vinne vya Mikoani: Mtwara, Iringa, Mwanza (e) na Singida ili kuielimisha jamii katika masuala ya vyama vya ushirika, maendeleo ya ushirika, utunzaji mazingira, na mikakati ya upunguzaji wa umaskini;
kuboresha kiwango cha huduma za utafiti na(f) ushauri kwa
kushirikiana na vyuo vingine vya ndani na nje ya nchi; na
69
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuimarisha mipango ya uenezi wa elimu ya ushirika nje ya (g) Chuo Kikuu Kishiriki ili kuchochea ari ya maendeleo katika
jamii kwa kushirikiana na wadau wengine;
Mheshimiwa Spika,101. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu Huria
cha Tanzania kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili (a)
wanafunzi 5,500 wa Shahada ya Kwanza, 5,000 wa cheti,
4,550 wa shahada ya uzamili na 50 wa shahada ya
uzamivu;
kuimarisha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa (b)
kukamilisha ujenzi wa maabara za kompyuta katika mikoa
ya Dodoma, Lindi, Mtwara, Mara, Njombe na Tabora;
kuongeza fursa za wanafunzi kujiunga na Elimu ya Juu kwa (c)
kukarabati majengo ya chuo awamu ya II katika mikoa ya
Kagera, Mtwara, Lindi, Kilimanjaro, Ruvuma, Kinondoni na
Rukwa; na
kuinua ubora wa elimu kwa kujenga maabara ya sayansi (d)
(Science Multi-purpose Lab) na jengo la madarasa makao
makuu ya chuo, Bungo Kibaha.
Mheshimiwa Spika,102. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu Ardhi
kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili (a)
wanafunzi 4,138 katika program mbalimbali za Chuo;
70
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuinua ubora wa utoaji elimu kwa kuendelea na ujenzi wa (b)
“Lands Building”na kukarabati karakana za mafunzo;
kuhamasisha uvumbuzi kwa kugharamia miradi ya utafiti (c)
73 inayoendelea na kuandaa machapisho na kusambaza
taarifa za utafiti;
kutoa ushauri wa kitaalamu na huduma kwa jamii ikiwa ni (d)
pamoja na kutafuta na kupata miradi 32 ya ushauri wa
kitaalamu;
kugharimia mafunzo ya watumishi 52 katika ngazi ya cheti, (e)
stashahada, shahada ya kwanza, shahada ya uzamili na
uzamivu ili kuleta tija na ufanisi; na
kuboresha ustawi wa wanafunzi ikiwa ni pamoja na; (f)
kukarabati mabweni ya wanafunzi, kutayarisha michoro kwa
ajili ya ujenzi wa kituo cha wanafunzi (Students Centre) na
kutoa huduma za ushauri nasaha kwa wanafunzi.
Mheshimiwa Spika,103. katika mwaka 2014/15, Chuo kimelenga
kutekeleza yafuatayo:
kuendeleza rasilimaliwatu kwa ajili ya sekta ya afya ili (a)
kukidhi mahitaji ya maendeleo ya nchi;
kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya kufundishia ya kampasi (b)
ya Mloganzila; na
kukarabati hosteli za wanafunzi katika eneo la Chole.(c)
71
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Mheshimiwa Spika,104. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu
Mzumbe kimelenga kutekeleza yafuatayo:
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili (a) wanafunzi wapya 3,620 katika ngazi ya cheti, stashahada
na shahada ya kwanza, shahada ya uzamili 1,800 na
shahada ya uzamivu 20;
kuimarisha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa (b) kuendeleza ujenzi wa madarasa na kumbi mbili za mihadhara
pamoja na kukarabati mabweni manne (4) ya wanafunzi,
mfumo wa maji na majengo ya kilichokuwa Kitengo cha
uchapaji ili kuyabadili kuwa Kituo cha Wanafunzi (Student
Services Centre) katika Kampasi Kuu Mzumbe;
kuwajengea uwezo wa kitaaluma na kitaalamu watumishi (c) 44 kwa kugharimia mafunzo katika ngazi ya shahada ya
uzamili (22) na shahada ya Uzamivu (22);
kuchapisha vitabu 11, makala za kufundishia 4 na makala (d) nyinginezo 42; na
kukamilisha utafiti katika maeneo 16 na kutoa ushauri wa (e) kitaalamu katika maeneo 37 ya menejimenti, uongozi na
sayansi ya jamii kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika,105. katika mwaka 2014/15, Chuo Kikuu cha
Dodoma kimelenga kutekeleza yafuatayo:
72
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili (a) wanafunzi wapya 6,400 katika shahada ya awali na 600
katika shahada za uzamili na uzamivu;
kuimarisha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kwa (b) kuendeleza ujenzi wa Chuo cha Tiba, Chuo cha Sayansi za
Asilia na Hisabati, Chuo cha Sayansi za Ardhi, ukumbi wa
mihadhara katika Chuo cha Elimu, miundombinu ya maji safi
na maji taka na miundombinu ya mawasiliano (ICT);
kuendeleza utafiti katika maeneo ya mazingira, rasilimali, (c) uchumi na tabianchi; na
kuendelea na ujenzi wa nyumba za wafanyakazi na (d) barabara zinazounganisha majengo ya Chuo cha Elimu na
nyumba hizo.
Mheshimiwa Spika,106. katika Bodi ya Huduma za Maktaba
Tanzania, katika mwamaka wa fedha 2014/15 itatekeleza
yafuatayo:
kuendelea kuimarisha huduma za maktaba nchini kwa (a) kushirikiana na OWM-TAMISEMI na wadau wengine; na
kuhamasisha wananchi kupenda kusoma majarida na maandiko (b) mbalimbali ili kuongeza ufahamu wa mambo muhimu katika
maendeleo ya nchi.
Mheshimiwa Spika,107. katika Usimamizi na Utekelezaji wa
Programu na Miradi, Wizara yangu itatekeleza yafuatayo:
73
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kuendelea kuwezesha mikakati ya Mpango wa Matokeo (a) Makubwa Sasa katika Elimu (BRNedu) ikiwemo kuandaa Wiki
ya Elimu 2015 kwa kushirikiana na wadau wa elimu;
kuimarisha maendeleo na matumizi ya TEHAMA katika ngazi (b) zote za elimu na mafunzo ili kuongeza fursa za upatikanaji wa
mada za masomo zenye ubora unaolingana na mahitaji halisi
ya wanafunzi kwa maendeleo ya taifa;
kuimarisha mfumo wa upatikanaji na utoaji wa taarifa za elimu (c) (Education Sector Management Information System - ESMIS)
katika ngazi zote za elimu na mafunzo ili kuwezesha maendeleo
ya sera, kuandaa mipango na kutoa maamuzi kulingana na
matokeo na uthibitisho uliopo;
kuendelea na ujenzi wa kampasi ya Mloganzila ya Chuo Kikuu (d) cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili; na
kukamilisha maandalizi ya uanzishwaji wa Chuo Kikuu cha Kilimo (e) na Sayansi Shirikishi cha Mwalimu Julius Nyerere, Butiama.
VI. SHUKRANI NA HITIMISHO
Mheshimiwa Spika108. , ninapenda tena kutoa shukurani zangu za
dhati kwako binafsi na kwa Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza.
Kwa niaba ya Wizara yangu, ninapenda pia kuwashukuru
kwa dhati wadau wote wa sekta ya elimu, ikiwa ni pamoja na
Washirika wetu wa Maendeleo, viongozi wa ngazi mbalimbali na
wananchi wa Tanzania kwa ujumla ambao wamechangia katika
74
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
kufanikisha utekelezaji wa mipango ya Elimu na Mafunzo. Baadhi
ya Washirika wetu wa Maendeleo ni serikali za: Algeria, China,
Cuba, India, Japani, Kanada, Marekani, Misri, Norway, Pakistan,
Poland, Sweden, Ubelgiji,Ufaransa,Uholanzi, Uingereza, Ujerumani,
na Uturuki. Aidha, mashirika yaliyochangia katika kufanikisha
programu za Elimu na Mafunzo ni pamoja na: Aga Khan Education
Services, Airtel, Barclays Bank, Benki Kuu, Benki ya Dunia, Benki
ya Maendeleo ya Afrika, Benkiya Taifa ya Biashara, Book Aid
International, British Council, CAMFED, Care International, Children
International, Children’s Book Project, CIDA, COL, Commonwealth
Secretariat, CRDB, DAAD, DANIDA, DfID, EDC, FEMINA, Ford
Foundation, GIZ, ILO, International Reading Association, Irish Aid,
JICA, JOVC,KOICA, Mwananchi Communications, NMB, NORAD,
OPEC, Oxfam, Peace Corps, Plan International, Rockefeller, Shirika
la Volkswagen, Sida, Sight Savers International, TENMET, Tigo,
Umoja wa Nchi za Ulaya (European Union EU), UNAIDS, UNDP,
UNESCO, UNESCO Institute for Life Long Learning (UIL), UNFPA,
UNICEF, USAID, VODAC na wengine ambao wamechangia katika
Wiki ya Elimu 2014 ambayo ilifana sana.
VII. MAOMBI YA FEDHA KWA MWAKA 2014/15
Mheshimiwa Spika109. , baada ya taarifa hii, sasa naliomba Bunge
lako Tukufu liidhinishe makadirio ya matumizi ya Wizara ya Elimu
na Mafunzo ya Ufundi ya jumla ya Shilingi 799,020,389,000.00
kwa mwaka wa fedha 2014/15, ili kuiwezesha Wizara kutekeleza
majukumu yake. Katika maombi haya:
75
Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe. Dkt. Shukuru Jumanne Kawambwa (Mb) Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2014/2015
Shilingi 93,247,873,000.00 (a) zinaombwa kwa ajili ya Matumizi
ya Kawaida ya Idara ambapo: Shilingi 52,976,832,000.00 ni
kwa ajili ya mishahara na Shilingi 40,271,041,000.00 ni kwa
ajili ya matumizi mengineyo;
Shilingi 250,959,183,000.00(b) zinaombwa kwa ajili ya
Matumizi ya Kawaida ya Taasisi. Kati ya hizo, Shilingi
215,779,416,000.00 ni kwa ajili ya mishahara, na Shilingi
35,179,767,000.00 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo; na
Shilingi 454,813,333,000.00(c) zinaombwa kwa ajili ya Miradi
ya Maendeleo. Kati ya hizo, Shilingi 383,734,000,000.00
(Shilingi 306,000,000,000 ni kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi
wa Elimu ya Juu sawa na asilimia 79.7) ni fedha za ndani na
Shilingi 71,079,333,000.00 ni fedha kutoka kwa washirika
wa maendeleo.
Mheshimiwa Spika110. , Hotuba hii inapatikana pia katika tovuti
ya Wizara kwa anwani ya: http://www.moe.go.tz.
Mheshimiwa Spika111. , naomba kutoa hoja.