2
JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO WANNE WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA DARASA LA PILI KWA KISWAHILI. JAMBO LA 2 WATOTO WANNE KATI YA KUMI WA DARASA LA TATU WANAWEZA KUZIDISHA HESABU NGAZI YA DARASA LA PILI. JAMBO LA 3 MTOTO MOJA KATI YA KUMI WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA NGAZI YA DARASA LA PILI KWA KIINGEREZA. JAMBO LA 4 MAHALI MTOTO ANAISHI PANAWEZA KUATHIRI UWEZO WAKE WA KUSOMA NA HESABU. JAMBO LA 5 KWA WASTANI, WATOTO SABA KATI YA KUMI HAWAJUI MAANA YA RANGI TATU ZA BENDERA YA TAIFA. Mtoto mmoja tu kati ya watoto wanne wa Darasa la Tatu anaweza kusoma hadithi ya Darasa la Pili kwa Kiswahili. Kiingereza Kiswahili UFUNGUO Hesabu 2011 2012 Watoto wanne kati ya kumi wa Darasa la Tatu wanaweza kuzidisha hesabu ngazi ya Darasa la Pili Mtoto moja kati ya kumi wa Darasa la Tatu anaweza kusoma hadithi ya ngazi ya Darasa la Pili kwa Kiingereza. Kwa wastani, watoto saba kati ya kumi hawajui maana ya rangi tatu za Bendera ya Taifa. Mahali mtoto anaishi panaweza kuathiri uwezo wake wa kusoma na hesabu. UFUNGUO Watoto wachache sana wanajifunza kusoma katika miaka ya mwanzo ya shule ya msingi. Kitaifa, mtoto 1 tu kati ya watoto 4 wa Darasa la Tatu anaweza kusoma hadithi ya ngazi ya Darasa la Pili kwa Kiswahili. Hadi wanapofika Darasa la Tano ndipo wengi wa wanafunzi wanaweza kusoma kwa ngazi ya Darasa la Pili. Ingawa kila mtoto nchini Tanzania anayesoma darasa la 3 au zaidi anapaswa kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika wa kiwango cha darasa la 2, ukweli ni kwamba lengo hili halifikiwi. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, uwezo wa kusoma na kuandika umebaki chini na kwa kiasi kikubwa haujabadilika, ingawa uwezo wao wa hesabu umeonyesha kuboreka kidogo. Yanayofuata ni mambo matano kuhusu matokeo ya watoto kujifunza; na pia mambo matano kuhusu mazingira ya kujifunzia kutokana na Tathmini ya Kitaifa ya Watoto ya Uwezo ya 2012: Viwango vya ufaulu wa soma la Hisabati katika utafiti wa mwaka 2012 vilikuwa juu zaidi kuliko miaka iliyopita. Kwa mfano, 44% ya wanafunzi wa Darasa la Tatu walifaulu mtihani wa kuhesabu ikilinganishwa na 37% mwaka 2011. Hata hivyo, tathmini ya mwaka 2012 haikuhusisha wilaya saba; na matokeo haya yanahitaji kuthibitishwa zaidi katika miaka ijayo. Umahiri katika kusoma na kufahamu hadithi kwa Kiingereza bado uko chini. Tathmini ya Uwezo ya 2012 imethibitisha kuwa viwango vya uelewa wa Kiingereza katika kiwango cha msingi ni vya chini kwa kiasi kikubwa kuliko viwango vya uelewa kwa Kiswahili katika madarasa yote. Hadi wanapofika Darasa la Saba, nusu ya wanafunzi wote wanaomaliza shule za msingi wanakuwa hawana uelewa wa Kiingereza, ingawa Kiingereza ni lugha ya kufundishia katika shule za sekondari wanapoelekea kujiunga. Bendera ya Taifa ipo kila mahali nchini Tanzania, hasa katika mazingira ya shule. Lakini watoto wengi hawaelewi maana ya rangi za bendera. Matokeo yanaonyesha kuwa 69% ya watoto wenye umri wa miaka 7-16 hawawezi kueleza maana ya rangi kuu tatu za bendera. Tofauti zipo kati ya wale waliojiunga na shule na walio nje ya shule, au kwa wale wa maeneo ya vijijini na mijini. Takwimu za 2012 zinathibitisha tofauti za wazi kati ya mikoa, wilaya; na mijini na vijijini katika matokeo ya watoto kujifunza. Kwa ujumla, tathmini inaonyesha kuwa watoto wanaoishi katika wilaya za mijini wamefanya vizuri kuliko watoto wanaoishi katika wilaya za vijijini. DONDOO MUHIMU ZA UTAFITI WA KITAIFA WA UWEZO TANZANIA 2012 4 3 2 1 5 DARASA 6 7 >7 3.1 % 5.4 % 11.6 % 5.8 % 12.7 % 25.9 % 11.9 % 26.1 % 44.4 % 21.0 % 41.7 % 60.9 % 31.7 % 57.3 % 74.5 % 42.7 % 68.4 % 83 % 53.2 % 76.0 % 89.1 % 67.0 % 79.5 % 91.8 % 0 20 40 60 80 100 4 3 2 1 5 6 7 >7 DARASA KINONDONI 5 64.5% TEMEKE 1 66.8% ARUSHA URBAN 2 66.1% TARIME 24.5% MOROGORO URBAN 3 65.4% SONGEA URBAN 4 65.1% 122 SERENGETI 23.2% 124 KASULU 21.3% 126 BIHARAMULO 24.2% 123 BARIADI 22.9% 125 + - × ÷ NAFASI ALAMA WILAYA YA MIJINI WILAYA YA KIJIJINI UFUNGUO

JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO ...JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO WANNE WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA DARASA LA PILI KWA KISWAHILI. JAMBO LA 2 WATOTO

  • Upload
    others

  • View
    28

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO ...JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO WANNE WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA DARASA LA PILI KWA KISWAHILI. JAMBO LA 2 WATOTO

JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO WANNE WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA DARASA LA PILI KWA KISWAHILI.

JAMBO LA 2 WATOTO WANNE KATI YA KUMI WA DARASA LA TATU WANAWEZA KUZIDISHA HESABU NGAZI YA DARASA LA PILI.

JAMBO LA 3 MTOTO MOJA KATI YA KUMI WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA NGAZI YA DARASA LA PILI KWA KIINGEREZA.

JAMBO LA 4 MAHALI MTOTO ANAISHI PANAWEZA KUATHIRI UWEZO WAKE WA KUSOMA NA HESABU.

JAMBO LA 5 KWA WASTANI, WATOTO SABA KATI YA KUMI HAWAJUI MAANA YA RANGI TATU ZA BENDERA YA TAIFA.

Mtoto mmoja tu kati ya watoto wanne wa Darasa la Tatu anaweza kusoma hadithi ya Darasa la Pili kwa Kiswahili.

Kiingereza Kiswahili

UFUNGUO

Hesabu

2011

2012

Watoto wanne kati ya kumi wa Darasa la Tatu wanaweza kuzidisha hesabu ngazi ya Darasa la Pili

Mtoto moja kati ya kumi wa Darasa la Tatu anaweza kusoma hadithi ya ngazi ya Darasa la Pili kwa Kiingereza.

Kwa wastani, watoto saba kati ya kumi hawajui maana ya rangi tatu za Bendera ya Taifa.

Mahali mtoto anaishi panaweza kuathiri uwezo wake wa kusoma na hesabu.

UFUNGUO

Watoto wachache sana wanajifunza kusoma katika miaka ya mwanzo ya shule ya msingi.

Kitaifa, mtoto 1 tu kati ya watoto 4 wa Darasa la Tatu anaweza kusoma hadithi ya ngazi ya Darasa la Pili kwa Kiswahili. Hadi wanapofika Darasa la

Tano ndipo wengi wa wanafunzi wanaweza kusoma kwa ngazi ya Darasa la Pili.

Ingawa kila mtoto nchini Tanzania anayesoma darasa la 3 au zaidi anapaswa kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika wa kiwango cha darasa la 2, ukweli ni kwamba lengo hili

halifikiwi. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, uwezo wa kusoma na kuandika umebaki chini na kwa kiasi kikubwa haujabadilika, ingawa uwezo wao wa hesabu

umeonyesha kuboreka kidogo.

Yanayofuata ni mambo matano kuhusu matokeo ya watoto kujifunza; na pia mambo matano kuhusu mazingira ya kujifunzia kutokana na Tathmini ya Kitaifa ya Watoto ya

Uwezo ya 2012:

Viwango vya ufaulu wa soma la Hisabati katika utafiti wa mwaka 2012 vilikuwa juu zaidi kuliko miaka iliyopita. Kwa mfano, 44% ya

wanafunzi wa Darasa la Tatu walifaulu mtihani wa kuhesabu ikilinganishwa na 37% mwaka 2011. Hata hivyo, tathmini ya mwaka

2012 haikuhusisha wilaya saba; na matokeo haya yanahitaji kuthibitishwa zaidi katika miaka ijayo.

Umahiri katika kusoma na kufahamu hadithi kwa Kiingereza bado uko chini. Tathmini ya Uwezo ya 2012 imethibitisha kuwa viwango vya uelewa wa Kiingereza katika kiwango cha

msingi ni vya chini kwa kiasi kikubwa kuliko viwango vya uelewa kwa Kiswahili katika madarasa yote. Hadi wanapofika Darasa la Saba, nusu ya wanafunzi wote wanaomaliza shule

za msingi wanakuwa hawana uelewa wa Kiingereza, ingawa Kiingereza ni lugha ya kufundishia katika shule za sekondari wanapoelekea kujiunga.

Bendera ya Taifa ipo kila mahali nchini Tanzania, hasa katika mazingira ya shule. Lakini watoto wengi hawaelewi maana ya rangi za bendera. Matokeo yanaonyesha kuwa 69% ya

watoto wenye umri wa miaka 7-16 hawawezi kueleza maana ya rangi kuu tatu za bendera. Tofauti zipo kati ya wale waliojiunga na shule na walio nje ya shule, au kwa wale wa maeneo

ya vijijini na mijini.

Takwimu za 2012 zinathibitisha tofauti za wazi kati ya mikoa, wilaya; na mijini na vijijini katika matokeo ya watoto kujifunza. Kwa ujumla, tathmini inaonyesha kuwa watoto wanaoishi katika

wilaya za mijini wamefanya vizuri kuliko watoto wanaoishi katika wilaya za vijijini.

DONDOO MUHIMU ZA UTAFITI WA KITAIFA WA UWEZO TANZANIA 2012

4321 5

DARASA

6 7 >7

3.1%

5.4%

11.6%

5.8%

12.7%

25.9%

11.9%

26.1%

44.4%

21.0%

41.7%

60.9%

31.7%

57.3%

74.5%

42.7%

68.4%

83%

53.2%

76.0%

89.1%

67.0%

79.5%

91.8%

0

20

40

60

80

100

4321 5 6 7 >7

DARASA

KINONDONI

5 64.5%

TEMEKE

1 66.8%

ARUSHA URBAN

2 66.1%

TARIME

24.5%

MOROGORO URBAN

3 65.4%

SONGEA URBAN

4 65.1%

122

SERENGETI

23.2%124

KASULU

21.3%126

BIHARAMULO

24.2%123

BARIADI

22.9%125

+ -× ÷

NAFASI

ALAMA

WILAYA YA MIJINI

WILAYA YA KIJIJINI

UFUNGUO

Page 2: JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO ...JAMBO LA 1 MTOTO MMOJA TU KATI YA WATOTO WANNE WA DARASA LA TATU ANAWEZA KUSOMA HADITHI YA DARASA LA PILI KWA KISWAHILI. JAMBO LA 2 WATOTO

JAMBO LA 1 IDADI YA WANAFUNZI DARASANI BADO NI KUBWA MNO. KWA KILA MWALIMU WA SHULE ZA MSINGI YA SERIKALI KULIKUWA NA ZAIDI YA WANAFUNZI 47.

JAMBO LA 2 RASILIMALI ZA KUSAIDIA KUJIFUNZA HUTOFAUTIANA KWA KIASI KIKUBWA KWA MIKOA.

JAMBO LA 3 KITAIFA, SHULE 4 TU KATI YA SHULE 10 ZA MSINGI ZA SERIKALI HUPATA MAJI SAFI YA KUNYWA.

JAMBO LA 4 KITAIFA, CHAKULA HUTOLEWA KATIKA SHULE 3 KATI YA 10.

JAMBO LA 5 KWA WASTANI, SHULE 3 KATI YA 10 ZINA MAKTABA.

Kitaifa, chakula hutolewa katika shule 3 kati ya 10.

Kitaifa, 29% ya shule zina utaratibu wa kutoa chakula. Idadi hii inaficha tofauti kubwa za kimkoa. Kwa mfano, hakuna shule zinazotoa chakula mkoani Kigoma, wakati 79% ya

shule mkoani Kilimanjaro zina utaratibu huo.

Idadi ya Wanafunzi darasani bado ni kubwa mno. Kwa kila mwalimu wa shule za msingi ya serikali kulikuwa na zaidi ya wanafunzi 47.

Hali imebadilika kidogo ikilinganishwa na mwaka 2011, kutoka uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 48 mpaka mwalimu mmoja kwa wanafunzi 47. Kwa angalizo, Dar es Salaam

ina uwiano mdogo zaidi wa mwalimu-wanafunai kuliko mikoa yote nchini (1:34). Kutokuwepo wa walimu umepungua kidogo kutoka asilimia 19 mwaka 2011 mpaka asilimia

18 mwaka 2012. Hii ina maana kwamba karibu mwalimu 1 kati ya walimu 5 hakuwepo shuleni siku ya tathmini ya Uwezo.

Kitaifa, Shule 4 tu kati ya shule 10 za msingi za serikali hupata maji safi ya kunywa.

Hali ya shule inaweza kuwa na athari mbaya juu ya uwezo wa kujifunza. Ukosefu wa maji ya kunywa ni kiashiria kikuu katika kutathmini mazingira ya shule; na ina uwezekano mkubwa wa

kuathiri vibaya uwezo watoto wa kuchota maarifa mapya wanapokuwa shuleni.

Rasilimali za kusaidia kujifunza hutofautiana kwa kiasi kikubwa kwa mikoa.

Kama ilivyo idadi ya vifaa shuleni, kuna tofauti kubwa kimkoa kati ya idadi ya wanafunzi wanaotumia kitabu kimoja cha kiada. Mkoani Dar es Salaam, wanafunzi 14 wanatumia kitabu

kimoja ikilinganishwa na wanafunzi 41 kwa kila kitabu Mkoani Kigoma. Hata mkoa wenye kufanya vizuri kama Dar es Salaam, bado wanafunzi wengi sana hutumia vitabu vichache sana.

Kwa wastani, shule 3 kati ya 10 zina maktaba.

Shule zote zinapaswa kuwa na maktaba, lakini shule nyingi hazina; na kuna tofauti kubwa sana nchini kote. Katika Mkoa wa Kagera 67% ya shule za msingi za serikali zina

maktaba, wakati mkoani Lindi 5% tu ndiyo zinazo.

MAMBO MATANO JUU YA MAZINGIRA YA KUJIFUNZIA

DAR ES SALAAM 1 : 14

KIGOMA 1 : 41

KIGOMA KILIMANJARO

KAGERA LINDI

0% 79%

5%

67%