18
1 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA UFAFANUZI WA HOJA ZA WAHESHIMIWA WABUNGE WAKICHANGIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA KWA MWAKA 2017/18 NA MWONGOZO WA KUANDAA MPANGO NA BAJETI YA SERIKALI KWA MWAKA 2017/18 DODOMA NOVEMBA, 2016

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA - mof.go.tz WA HOJA.pdf · Ninatambua pia mchango wa waziri kivuli na msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu wizara ya Fedha na Mipango,

  • Upload
    dotram

  • View
    292

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

1

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

UFAFANUZI WA HOJA ZA WAHESHIMIWA WABUNGE

WAKICHANGIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO,

MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI

MAPENDEKEZO YA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA

KWA MWAKA 2017/18 NA MWONGOZO WA KUANDAA

MPANGO NA BAJETI YA SERIKALI KWA

MWAKA 2017/18

DODOMA NOVEMBA, 2016

1

A. UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kukushukuru

wewe binafsi, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa kuendesha

majadiliano kwa ufanisi kuhusu Mapendekezo ya Mpango wa

Maendeleo wa Taifa na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti kwa

Mwaka 2017/18.

2. Mheshimiwa Spika, napenda kutambua mchango mzuri

uliotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, chini ya

Mwenyekiti wake Mhe. Hawa Abdulrahman Ghasia, Mbunge wa

Mtwara Vijijini na Makamu Mwenyekiti, Mhe. Josephat Sinkamba

Kandege, Mbunge wa Kalambo. Ninatambua pia mchango wa waziri

kivuli na msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu

wizara ya Fedha na Mipango, Mhe. Halima James Mdee, Mbunge wa

Kawe. Aidha, ninawashukuru kwa dhati Waheshimiwa Wabunge wote

waliochangia mjadala huu kwa kuzungumza (45) na kwa maandishi

(30).

3. Mheshimiwa Spika, kwa ujumla mjadala ulikuwa mzuri, baadhi

ya maoni yakitolewa kwa hisia kali. Mimi naamini kwamba kwa

kuzingatia umuhimu wa uchumi katika nchi ni jambo jema

tukachambua, tukabishana na hatimaye turidhiane juu ya

vipaumbele, mikakati na hatua stahiki za kukuz auchumi kwa namna

endelevu zitakazowezesha kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya

Maendeleo 2025.

4. Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia kuwa tumepokea michango

na hoja nyingi sana kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge, naomba

niahidi hapa kuwa nitawasilisha Bungeni taarifa ya maandishi

inayofafanua hoja zote zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge.

B. MAONI NA USHAURI ULIOSISITIZWA NA WAHESHIMIWA

WABUNGE WENGI

5. Mheshimiwa Spika, yapo maoni/ushauri mbalimbali uliotolewa

na Waheshimiwa Wabunge ambayo Serikali itazingatia katika

kuandaa Mpango wa Maendeleo na Bajeti kwa Mwaka 2017/18.

Ushauri huo ni:-

2

(i) Serikali ijielekeze kubuni vyanzo vingine vya mapato (Non-tax

revenue) vitakavyosaidia kugharamia Bajeti ya Serikali;

(ii) Serikali ipunguze kukopa zaidi kutoka vyanzo vya ndani;

(iii) Kukamilisha haraka zoezi la Sovereign Rating ili kuwezesha

kukopa kutoka vyanzo vya nje;

(iv) Ujenzi wa Reli ya Kati kutoka Dar – Tabora - Kigoma (km 1,251)

kwa Standard Gauge na matawi yake;

(v) TRA iandae mapema awamu ya pili ya ukusanyaji wa kodi ya

majengo katika halmashuri na miji midogo iliyosalia;

(vi) Kutenga fedha za kutosha za matumizi mengineyo (OC) kwa

mafungu husika ili kuweza kugharamia mpango wa Serikali

kuhamia Makao Makuu – Dodoma hususan kwa upande wa

malipo ya stahili za watumishi watakaohamishwa;

(vii) Kukamilisha mifumo ya ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa

njia za kielektroniki;

(viii) Kuhamasisha na kuongeza matumizi ya mashine za EFD na

wananchi kwa ujumla kudai risiti halali pale wanaponunua

bidhaa;

(ix) Kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato hususan bandari bubu

na biashara za magendo;

(x) Kuboresha mazingira ya kufanya biashara na uwekezaji ili

kuiwezesha sekta binafsi kutoa mchango unaostahili katika

kukuza uchumi wa nchi yetu;

(xi) Kuweka mkakati wa kujenga zahanati katika kila kijiji na kituo

cha afya kwa kila kata na kuimarisha upatikanaji wa madawa

na vifaa tiba,

(xii) Kukamilisha utaratibu wa matumizi ya shilingi milioni 50 kwa

kila kijiji/mtaa/shehia na kuongeza kiasi kinachotengwa;

(xiii) Kuendeleza maeneo ya viwanda vidogo, na EPZ/SEZ;

(xiv) Kutoa kipaumbele kwa miradi ya makaa ya mawe - Mchuchuma

na chuma Liganga;

(xv) Kuboresha elimu ya juu na kuongeza wigo wa utoaji wa mikopo

kwa wanafunzi; na

(xvi) Kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara.

3

C. UFAFANUZI WA HOJA MBALIMBALI

Hoja Na. 1: Uchumi una hali mbaya (Umedorora) na kuna

manung’uniko mengi ya wananchi mtaani.

Hali ya Uchumi (Januari – Juni 2016)

Ukuaji wa Pato la Taifa: 6.7% (Jan-Jun 2016) Vs 5.8% (Jan-

Jun 2015).

Sekta zilizokua zaidi: uchukuzi, uhifadhi wa mizigo (17.4%),

uchimbaji wa madini na gesi (13.7%), mawasiliano (13.0%) na

sekta ya fedha & bima (13.0%).

mfumuko wa bei: 6.5% (Jan 2016), 5.5% (Jun 2016) na 4.5%

(Sept 2016).

Akiba ya fedha za kigeni: 4 months of imports cover (USD 4.1

bn) Sept 2016

Urari wa Biashara ya Nje: current account deficit USD 601.8

(Jan – Sept 2016) Vs USD 1,207.7 (Jan – Sept 2015)

Mwenendo wa sekta ya kibenki (Januari – Septemba 2016).

Sekta imeendelea kukua na ina mitaji na ukwasi wa kutosha.

a) Mitaji ikilinganishwa na mali iliyowekezwa (Total Capital to Total

Risk Weighted Assets and Off-balance Sheet Exposures) ni

19.08% Vs kiwango cha chini kinachotakiwa 12.0%.

b) Mali inayoweza kubadilishwa kuwa fedha taslimu ikilinganishwa

na kiwango cha amana zinazoweza kuhitajika katika muda mfupi

(liquid assets to demand liabilities) 34.18% Vs kiwango cha chini

kinachohitajika 20%.

But: mikopo chechefu imeongezeka (6.7% Sept 2015, 9.1% Sept 2016)

Mabenki yaliyopata Hasara Jul – Sept 2016: CRDB & TIB

Development Bank.

Sababu: mikopo chechefu (provision for loan losses);

Twiga Bancorp imewekwa chini ya uangalizi wa BOT;

4

NB: Crane Bank Ltd ya Uganda imewekwa chini ya usimamizi wa

Benki Kuu Oct 2016; Imperial Bank Kenya, Oct 2015

Benki nyingi incl. CRDB na TIB Devt, zimekuwa na mitaji na ukwasi

wa kutosha. Matarajio ni kuwa benki hizi zitafanya vizuri katika

kipindi kilchobaki cha 2016/17.

Kwa mwaka ulioshia Sept 2016 Sekta ya Kibenki kwa ujumla

ilipata faida: pato kwa rasilimali (Return on Assets) 2.53%; pato kwa

mtaji (Return on Equity) 12.05%. Mtaji na kiwango cha mali inayoweza

kubadilishwa kuwa fedha taslimu Vs amana zinazoweza kuhitajika

katika muda mfupi (liquid assets to demand liabilities) viliendelea

kuwa juu ya viwango vinavyotakiwa.

Riba za mikpo zimepungua: 16.18% Sept 2015 – 15.83% Sept

2016

Riba za amana zilibakia wastani wa 9.0%;

Tofauti kati ya riba za mikopo na amana za mwaka mmoja ilipungua

1.77% pts (Sept 2016) kutoka 3.32 % pts (Sept 2015);

Mwenendo huu umeimarisha mazingira ya kufanya biashara na

ushindani.

Viwango vya Ubadilishaji fedha

Hatua za kuimarisha thamani ya Shilingi:

(i) kuongeza mauzo ya bidhaa nje;

(ii) kuimarisha uzalishaji wa nishati; na

(iii) kupunguza matumizi ya fedha za kigeni yasiyo na tija.

Wastani wa Shs. 2,172.38: USD 1 (Jan 2016), Shs. 2,180.54 (Jul

2016); Shs. 2,188.1: USD 1 (Sept 2016)

5

MWENENDO WA BAJETI YA SERIKALI

Bajeti2016/17

29,539,603,197,085

Matumizi ya Kawaida 17,719,100,237,510

CFS 8,010,400,471,000

MDAs 2,470,708,175,510

RSs 37,786,227,000

LGAs 332,039,536,000

LGAs own source 266,165,828,000

PE 6,602,000,000,000

Matumizi ya Maendeleo 11,820,502,959,575

Local 8,702,697,468,575

MDAs 7,993,548,468,575

RSs 55,000,000,000

LGAs 254,900,000,000

LGAs own source 399,249,000,000

Foreign 3,117,805,491,000

MDAs 2,518,396,820,000

RSs 10,940,832,000

LGAs 588,467,839,000

FedhazilizotolewaRoboya

kwanza Asilimia

5,464,422,947,958 18%

4,549,103,630,355 26%

2,293,670,167,443 29%

367,680,092,860 15%

16,416,804,465 43%

103,755,507,898 31%

64,400,691,531 24%

1,703,180,366,157 26%

915,319,317,603 8%

869,344,044,756 10%

798,787,466,850 10%

2,500,000,000 5%

11,000,000,000 4%

57,056,577,906 14%

45,975,272,847 1%

33,265,592,750 1%

690,672,965 6%

45,284,599,882 8%

Ulipaji wa Madeni ya Ndani

6. Mheshmiwa Spika, Katika kipindi cha Julai hadi Oktoba 2016

Serikali imelipa madeni mbalimbali yaliyohakikiwa na Mkaguzi wa

Ndani Mkuu wa Serikali yenye jumla ya shilingi bilioni 187.521.

Madeni haya yanajumuisha madeni ya wakandarasi wa barabara,

maji, umeme pamoja na wazabuni mbalimbali. Aidha, madeni ya

watumishi wa umma yanaendelea kulipwa kupitia mafungu yao.

Ulipaji wa Deni la Nje

7. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi kuanzia Novemba 2015 hadi

kufikia Oktoba, 2016 Serikali imetumia jumla ya shilingi bilioni

1,196.9 kwa ajili ya kulipia madeni ya nje. Kati ya kiasi hicho, malipo

ya mtaji ni shilingi bilioni 709.7 na malipo ya riba ni shilingi bilioni

487.2. Malipo ya deni la Taifa yamekuwa yakiongezeka mwaka hadi

mwaka kutokana na mikopo mipya, kumalizika kwa kipindi cha kabla

ya kuanza kulipa mtaji (Grace Period) kwa mikopo ya muda mrefu

pamoja na kushuka kwa thamani ya shilingi dhidi ya Dola ya

6

Kimarekani.

8. Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kulipa kwa wakati

mikopo yote ya nje inayoiva kwa mujibu wa mikataba. Kwa kuwa

kutofanya hivyo kutahatarisha mahusiano yaliyopo kati yetu na nchi

wahisani, taasisi za fedha za kimataifa na mabenki ya nje. Aidha, nchi

isipolipa kwa wakati inaweza kushitakiwa kwenye mahakama za

kimataifa na kuisababishia nchi hasara na kupelekea kutopata

mikopo tena kutoka nje. Kadhalika, kutokulipa kwa wakati

kutasababisha Serikali kulipa gharama za ziada (penalty) kulingana

na makubaliano na hivyo kuongeza mzigo kwa taifa.

9. Mheshmiwa Spika, Serikali imejiwekea mikakati mbalimbali ili

kuhakikisha kwamba Deni la Taifa linadhibitiwa na linaendelea kuwa

himilivu na linalipwa kwa wakati.

Ruzuku ya Pembejeo za Kilimo

10. Mheshmiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2016/17 jumla ya

shilingi bilioni 25.0 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa pembejeo

ambapo hadi kufikia mwezi Oktoba 2016 jumla ya shilingi bilioni 10.0

zimetolewa.

Ununuzi wa Chakula cha Hifadhi ya Taifa

11. Mheshmiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2016/17 jumla ya

shilingi bilioni 15.0 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa chakula cha

hifadhi ya Taifa ambapo hadi kufikia mwezi Oktoba 2016 jumla ya

shilingi bilioni 9.0 zimetolewa.

Utoaji wa Fedha za Mfuko wa Jimbo

12. Mheshmiwa Spika, Katika mwaka wa fedha 2016/17 Serikali

imetenga shilingi bilioni 10.4 kwa ajili ya Mfuko wa Kuchochea

Maendeleo Jimboni. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 9.0 ni kwa ajili

ya Tanzania Bara na shilingi bilioni 1.4 ni kwa Serikali ya Mapinduzi

ya Zanzibar. Serikali inatarajia kutoa fedha hizo mwezi Novemba

2016.

13. Mheshmiwa Spika, katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016,

kasi ya ukuaji wa Pato la Taifa imeongezeka na kufikia asilimia 6.7

ikilinganishwa na asilimia 5.8 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2015.

7

14. Mheshimiwa Spika, manung’uniko mtaani yapo na kwa kiasi

kikubwa yametokana na jitihada na hatua zilizochukuliwa na Serikali

kurudisha nchi kwenye utaratibu wa nidhamu ya kazi katika

Utumishi wa Umma, kurejesha nidhamu ya matumizi/kuondoa

matumizi ya Serikali yasiyo ya lazima, kupambana na wizi/ubadhirifu

wa fedha na mali za umma, kuhimiza ulipaji kodi na ukusanyaji wa

mapato yasiyo ya kodi n.k. Hata hivyo, Serikali inaamini kuwa hatua

hizi ni kwa maslahi mapana ya Taifa na maumivu ni ya kipindi cha

mpito cha kuweka mambo sawa/kurejesha mifumo kwenye utaratibu

unaokubalika na endelevu. “There is no game without pain”.

15. Mheshimiwa Spika, upo utaratibu wa Serikali, Taasisi binafsi

na Mashirika ya Kimataifa kufanya tathmini ya uchumi wa nchi na

kutoa maoni yao juu ya kile walichokiona. Shirika la Fedha la

Kiamtaifa – IMF ambalo lilikuwa hapa wiki moja iliyopita,

limekamilisha tathmini ya mwenendo wa uchumi wa nchi yetu

ambapo kiujumla wameridhika na hali ya uchumi wa Tanzania.

Hoja Na. 2: Misingi ya Mpango (premises) iliyowekwa inatujengea

kushindwa.

16. Mheshimiwa Spika, neno ‘Misingi’ katika Mapendekezo ya

Mpango lililenga kumaanisha “assumptions”. Hakika Serikali inajua

kwamba hali halisi ya mazingia wezeshi kwa uwekezaji nchini na

nafasi ya Tanzania kama ilivyotathminiwa na Benki ya Dunia katika

Doing Business report. Serikali inajua utabiri wa hali ya hewa na

maoteo ya upungufu wa chakula n.k. We are not naïve. Assumptions

si lazima ziwe halisi bali ziliwekwa hapa kurahisisha uwekaji wa

malengo kwa mwaka 2017/18. Utaratibu huu ni wa kawaida kabisa

kwa wachumi. Mathalani tunapotaka kuchambua biashara baina ya

mataifa tunaweka assumption kwamba dunia ina nchi 2 tu zinafanya

biashara ili kurahisisha uchambuzi japo kila mtu anafahamu dunia

ina nchi nyingi zinafanya biashara baina yao.

Hoja na 3: Fedha kutopelekwa kwenye Halmashauri kwa wakati

17. Mheshmiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2016/17 Mamlaka

za Serikali za Mitaa ziliidhinishiwa bajeti ya shilingi bilioni 5,434.7.

Kati ya kiasi hicho shilingi bilioni 3,593.9 ni kwa ajili ya mishahara,

8

shilingi bilioni 598.2 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo (OC)

ikijumuisha shilingi bilioni 266.2 za mapato yatokanayo na vyanzo vya

ndani vya Halmashauri na shilingi bilioni 332.0 ni ruzuku kutoka

Serikali Kuu. Aidha, shilingi bilioni 1,242.6 ni kwa ajili ya miradi ya

maendeleo ambapo shilingi bilioni 588.5 ni fedha za nje na shilingi

bilioni 654.1 ni fedha za ndani ikijumuisha shilingi bilioni 399.2

zinazotokana na mapato ya ndani ya Halmashauri na shilingi bilioni

254.9 ni ruzuku kutoka Serikali Kuu.

18. Mheshmiwa Spika, katika kipindi cha Julai hadi Oktoba 2016,

fedha zilizotolewa zinajumuisha mishahara shilingi bilioni 1,181.0

sawa na asilimia 33, matumizi mengineyo shilingi bilioni 192.8 sawa

na asilimia 32.2 na fedha za maendeleo shilingi bilioni 177.3 sawa na

asilimia 14.3. Aidha, mbali na fedha za ruzuku kutoka Serikali Kuu

na makusanyo ya ndani ya Halmashauri kiasi cha shilingi bilioni 271

zilitumika kutekeleza miradi ya maji vijijini (shilingi bilioni 51.1),

umeme vijijini (shilingi bilioni 132.4), Mfuko wa barabara (shilingi

bilioni 78.1) na utoaji wa pembejeo kwa wakulima (shilingi bilioni

10.0) katika Halmashauri mbalimbali nchini.

Hoja Na. 4: Mradi wa Mchuchuma na Liganga uko kwenye

Mpango wa maendeleo kila mwaka lakini utekelezaji wake

haujaanza

19. Mheshimiwa Spika, Sio kweli kuwa utekelezaji wa Mradi wa

Makaa ya Mawe, Mchuchuma na Chuma Liganga haujaanza.

Utekelezaji wa mradi huu utakaogharimu Dola za Marekani bilioni 3

umeanza na kufikia hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na:

Kukamilika kwa upembuzi yakinifu wa mradi ikiwa ni pamoja na

kutambua kiasi cha mashapo ya makaa ya mawe na chuma,

usanifu wa migodi na kiwanda cha chuma na kituo cha kuzalisha

umeme;

kupatikana kwa leseni za uchimbaji na matumizi ya madini,

leseni ya matumizi ya maji na leseni ya uzingativu wa mazingira;

Kukamilika pia kwa mkakati wa ushirikishi wa wananchi

wanaouzunguka mradi na njia ya kusafirishia umeme;

Kukamilika kwa ujenzi barabara kwa kiwango cha changarawe ili

kuruhusu usafirishaji wa mitambo kwenda kwenye eneo la mradi;

9

kuendelea na usanifu wa ujenzi wa reli ya liganga hadi Mtwara na

uwezekano wa kuiunganisha na reli ya TAZARA na kuendelea na

usanifu katika bandari ya Mtwara; na

kukamilika kwa tathmini ya fidia kwa wananchi watakaopisha

eneo la mradi imekamilika.

Hoja Na. 5: Utaratibu wa Taasisi za Umma kuweka fedha zao

katika Mabenki ya kibiashara urejeshwe ili kuwezesha mabenki

kukopesha fedha hizo kwa wafanyabishara na pia kuziwezesha

Taasisi hizo kunufaika na riba zitokanazo na amana.

20. Mheshimiwa Spika, uamuzi wa Serikali kuzitaka taasisi za

umma kufungua akaunti ya mapato Benki Kuu utaendelea kubaki

kama ulivyo. Utaratibu uliokuwa umejengeka ulizinufaisha benki

chache na haukuwa na maslahi mapana kwa Taifa. Benki hizo

zimekuwa zikipata faida kwa kutumia migongo ya maskini na hivyo

sasa basi! Benki zifanye kazi kwa kurejesha ushindani.

Mfano:

Taasisi moja ilikuwa na amana za muda maalum (fixed deposit) za

shilingi bilioni 440 ambazo ziliwekwa katika baadhi ya benki. Kiasi hiki

kilizaa faida ya shilingi bilioni 17 ambayo inamaanisha riba ya wastani

wa asilimia 4 kwa mwaka. Ijapokuwa ukweli ni kwamba, amana za

chini ya shilingi milioni 100 zinakuwa na riba ya kati ya asilimia 8 na

10 na kiasi cha amana kinapokuwa kikubwa zaidi riba inaongezeka

hadi kufikia asilimia 15. Kama riba ingekuwa asilimia 13, taasisi hiyo

ingepata faida ya bilioni 57.2 kabla ya kodi. Hivyo, kwa taasisi hiyo

moja tu, watanzania wamekuwa wakiibiwa shilingi bilioni 40 kila

mwaka.

Si hivyo tu, fedha hizo (bilioni 440) zilizokuwa katika benki za biashara

zilitumika kuikopesha Serikali kupitia hati fungani kwa riba ya asilimia

15, hivyo wananchi hulipa benki hizi riba ya hadi shilingi bilioni 66

kwa fedha ambazo ni za kwao wenyewe. Maana yake ni kuwa,

wananchi waliendelea kulipa riba kwa fedha zao wenyewe sawa na

hasara ya shilingi bilioni 106 kwa mwaka. Hatuwezi kuendelea na

utaratibu huu.

Benki na baadhi ya watanzania waliozoea kupiga dili sasa basi! Benki

ambazo zimekuwa zikipata faida kwa kutumia migongo ya maskini

10

sasa basi! Benki zifanye kazi kurejesha ushindani. Mheshimiwa Rais

alisema hadharani na ukweli utabaki hivyo, kwamba hizo fedha

hazitarudi.

Hoja Na. 6: Serikali ielekeze benki kushusha riba kutoka

asilimia 18 hdi 13 kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa

ili kuongeza mzunguko wa fedha katika uchumi. (Riba za

mikopo bado ziko juu, Serikali ielekeze benki kushusha riba

hizo)

21. Mheshimiwa Spika, Ni kweli riba za mikopo ni kubwa hasa zile

zinazotozwa na Taasisi ndogondogo za fedha (microfinance). Katika

Sekta ya Huduma Ndogo Ndogo za Fedha (Microfinance) kuna benki,

taasisi na asasi za fedha zilizo rasmi na zisizo rasmi ambazo zinatoa

huduma za kifedha kwa wateja wadogo wadogo. Pia kuna taasisi na

asasi za kifedha ambazo zinatoa huduma za mikopo kwa kutumia

mitaji binafsi bila kukusanya na kupokea amana za wateja.

22. Mheshimiwa Spika, Taasisi na asasi hizo zimeongezeka kwa

kiasi kikubwa na zimekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya

ujasiriamali na ukuaji wa uchumi wa wananchi na mikopo ya taasisi

hizo kwa kiasi kikubwa inategemewa na watanzania walio wengi.

23. Mheshimiwa Spika, Taasisi na asasi hizo zinapata leseni kutoka

katika mamlaka tofauti ikiwemo BRELA, Wizara ya Mambo ya Ndani

ya Nchi, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na

Watoto, RITA, na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Utaratibu huo umesababisha usimamizi na ufuatiliaji wa taasisi hizo

kuwa mgumu. Kutokana na hali hii zimejitokeza changamoto nyingi

na mapungufu kadhaa katika sekta ya “Microfinance”, ikiwa ni

pamoja na kutozwa riba kubwa na kuwa na mikataba yenye

mapungufu mengi. Hii inatokana na wakopeshaji kwenye sekta hii

kutokuwa na usimamizi imara na elimu ndogo ya maswala ya fedha

kwa wateja walio wengi (financial illiteracy).

24. Mheshimiwa Spika, Serikali inakiri kuwepo na malalamiko kwa

wananchi wengi nchini kuhusiana na uendeshaji wa biashara

inayofanywa na asasi hizo kama vile viwango vya juu vya riba na ada

pamoja na utaratibu mbaya wa ukusanyaji wa marejesho (loan

repayment). Hali hii inatokana na ukweli kwamba hakuna mamlaka

rasmi na halali ya kisheria yenye wajibu wa kutoa leseni, kuratibu,

11

kusimamia na kuhakikisha ulinzi wa wateja (consumer protection)

katika taasisi hizi za fedha.

25. Mheshimiwa Spika, Katika kutatua mapungufu na changamoto

hizi na kwa kuzingatia maendeleo yaliyojitokeza katika huduma za

fedha kwa wateja wadogo wadogo, Serikali imekamilisha na

kuidhinisha Sera ya Taifa ya ‘Microfinance’ na hatua za ukamilishaji

wa sheria ya Microfinance zinaendelea.

26. Mheshimiwa Spika, Sheria hiyo itaunda mfumo mahususi wa

kusimamia na kuratibu shughuli za taasisi na asasi za fedha zilizo na

zisizo rasmi ambazo zinatoa huduma za kifedha kwa wateja wadogo

wadogo ambazo haziko chini ya Sheria ya Mabenki na Taasisi za

Fedha ya mwaka 2006.

27. Mheshimiwa Spika, Kwa upande mwingine, benki na taasisi za

fedha zinazosimamiwa kisheria na Benki Kuu ya Tanzania,

zimeendelea kuwa na viwango bora vya riba katika kipindi cha mwaka

ulioishia mwezi Septemba 2016.

28. Mheshimiwa Spika, kuhusu kuweka riba elekezi, uzoefu wa

nchi nyingi unaonesha kwamba viwango vya riba huamuliwa na

nguvu ya soko. Ni dhamira ya Serikali kuona riba za benki

zinazotozwa katika mikopo zinapungu. Hivyo, Serikali itaendelea

kuweka mazingira mazuri yatakayosaidia kuleta ushindani

utakaopelekea viwango vya riba hizo kuwa nafuu zaidi. Aidha,

ikumbukwe kwamba kuna madhara ya kuweka viwango elekezi vya

riba ikiwa ni pamoja na uwezekano wa benki kupunguza mikopo kwa

sekta binafsi ikiwa kiwango hicho elekezi kitakuwa chini zaidi ya riba

ya dhamana na hati fungani za serikali; kuongezeka kwa mikopo

chechefu na kupungua kwa ushindani katika sekta ya benki na

ufanisi katika utekelezaji wa sera ya fedha.

Hoja Na. 7: TRA wanatumia vitisho, mabavu na mifumo

kandamizi katika kukusanya kodi

29. Mheshimiwa spika, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

inaendelea na jitihada za kuhakikisha kila anayestahili kulipa kodi

analipa kodi stahiki na kwa wakati. TRA inatekeleza majukumu yake

12

kwa weledi na ufanisi kulingana na taratibu zilizoainishwa katika

sheria na kanuni za kodi.

30. Mheshimiwa spika, mlipakodi anakadiriwa kodi ya kulipa na

kupewa muda wa kuilipa kodi hiyo. Endapo kodi hiyo itakukuwa

haijalipwa katika muda ulioonyeshwa kwenye taarifa ya madai (Notice

of Assesment), TRA huchukua jukumu la kumkumbusha mhusika

(reminder notice) na kumtahadharisha hatua zitakazochukuliwa

endapo kodi hiyo itaendelea kutolipwa mpaka tarehe iliyooneshwa

kwenye reminder notice. Hatua zinazochukuliwa kwa mlipa kodi

aliyekaidi ni kama vile: kukamatwa mali zake na kuuzwa kwa njia ya

mnada; na kuiagiza benki ya mlipa kodi kuhamisha fedha kutoka

kwenye akaunti yake kwenda TRA ili kulipia deni hilo. Hatua hizi zipo

kwa mujibu wa sheria na si vitisho, mabavu wala mifumo kandamizi

kwa wafanyabiashara. Ni vizuri walipakodi wakazingatia sheria na

kulipa kodi kwa hiari ili kuepuka usumbufu.

Hoja Na. 8: Serikali inasema kuwa imeokoa shilingi bilioni 19

kwa kuondoa watumishi hewa kwenye mfumo wa maliopo.

Taarifa ya gharama za watumishi ya Benki Kuu ya Juni 2015

ilionyesha malipo ya mishahara yaliongezeka kutoka bilioni

456 hadi shilingi bilioni 534 Juni 2016 ambalo ni ongezeko la

bilioni 78. Ongezeko hili limetoka wapi wakati Serikali

imesimamisha ajira mpya na kuondoa watumishi hewa?

31. Mheshimiwa spika, Zoezi la kufuta watumishi hewa kufuatia

agizo la Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

lilianza Mwezi Machi, 2016. Hata hivyo, pamoja na kufutwa kwa

watumishi hewa malipo ya mishahara katika kipindi cha Juni 2015

hadi Juni 2016 yameongezeko kutokana na sababu mbalimbali

ikiwemo:

Nyongeza ya mishahara iliyoanza kutumika Julai, 2015 ambapo

jumla ya Shilingi bilioni 59 ziliongezeka kwa mwezi;

Watumishi 25,517 waliajiriwa katika kipindi hicho wenye

mshahara wa Shilingi bilioni 16.4 kwa mwezi;

Uwianishaji wa mishahara ya watumishi wa Vyuo Vikuu ambapo

jumla ya Shilingi bilioni 2.9 ziliongezeka;

Ongezeko la posho zinazoambatana na mishahara shilingi bilioni

6.1 kwa mwezi kwa vyombo vya ulinzi na usalama;

13

Upandishwaji vyeo kwa watumishi mbalimbali; na

Uwianishaji wa maeneo ya kimishahara ambapo kuanzia mwezi

Februari, 2016 mishahara ya shilingi bilioni 33 iliyokuwa

inalipwa kupitia kwenye kasma ya matumizi mengineyo ilianza

kulipwa kupitia kwenye kasma ya mishahara.

32. Mheshimiwa spika, Hivyo, endapo watumishi hewa

wasingeondolewa matumizi ya Serikali katika eneo la mishahara

yangekewa makubwa zaidi ya kiasi hicho kilicholipwa mwezi Juni,

2016.

Hoja Na. 9: Riba kubwa zinazotozwa na mabenki ni kandamizi

na zinaumiza wanyonge

33. Mheshimiwa spika, Katika mwaka ulioshia mwezi Septemba

2016, riba za mikopo za mabenki zimekuwa zikipungua wakati zile za

amana kuimarika kwa viwango tofauti. Riba za mikopo zilipungua

hadi kufikia wastani wa asilimia 15.83 mwezi Septemba 2016 kutoka

asilimia 16.18 mwezi Septemba 2015. Wakati huo huo, riba za amana

zilibakia katika kiwango cha wastani wa asilimia 9.0. Aidha, riba za

mikopo ya mwaka mmoja ilipungua kutoka wastani wa asilimia 14.27

hadi asilimia 13.23, wakati riba za amana za mwaka mmoja

ziliongezeka kutoka asilimia 10.95 hadi asilimia 11.46. Hali hii ilifanya

tofauti kati ya riba za mikopo na amana za mwaka mmoja ipungue

hadi kufikia wastani wa asilimia 1.77 mwezi Septemba 2016 kutoka

asilimia 3.32 mwezi Septemba 2015. Mwenendo huu wa viwango vya

riba unaonesha kuendelea kuimarika kwa mazingira ya kufanya

biashara na ushindani nchini hivyo kuvutia zaidi uwekezaji wa sekta

binafsi. Aidha, hii inaashiria kuimarika kwa ushindani wa Mabenki ili

kuvutia wateja.

14

MAJIBU YA HOJA ZA WAHESHIMIWA WABUNGE WAKATI WA KUJADILI MAPENDEKEZO YA MPANGO WA

MAENDELEO WA TAIFA KWA MWAKA 2017/18 NA MWONGOZO WA KUANDAA MPANGO NA BAJETI YA

SERIKALI KWA MWAKA 2017/18

NA. MTOA HOJA HOJA UFAFANUZI WA HOJA

KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI

1. TRA inavuka lengo

kutokana na kukusanya

maduhuli na

kuyahesabu kama

sehemu ya mapato ya

kodi.

Maelezo yaliyotolewa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni

siyo sahihi.

Maelezo sahihi ni kuwa mapato ya kodi yanayokusanywa na

TRA hutolewa taarifa peke yake. Mapato yasiyo ya kodi

(maduhuli) kwa Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali

yanayokusanywa na Taasisi husika na kutolewa taarifa na

Msajili wa Hazina. Mapato yanayokusanywa na Wizara

hutolewa taarifa na Wizara husika.

WAHESHIMIWA WABUNGE

2. Mhe.

Josephat

Sinkamba

Kandege

Pamoja na lengo zuri la

kuongeza mapato ya

ndani ili ku kugharamia

sehemu kubwa ya bajeti,

Serikali ihakikishe kuwa

vyanzo vipya vya kodi

vinavyopendekezwa

Serikali inaendelea kutekeleza azma yake ya kupunguza

kodi zinazoleta kero kwa wananchi na kuharibu mpango

mkakati wa Serikali kuchochea ari ya ulipaji kodi kwa

hiari.

Aidha, Serikali imejikita katika kuimarisha mkakati wa

kuboresha usimamizi na utawala wa kodi ili

wafanyabiashara na wananchi waweze kulipa kodi

15

NA. MTOA HOJA HOJA UFAFANUZI WA HOJA

katika bajeti ya mwaka

wa Fedha 2017/18

havitakuwa kero kwa

wafanyabiashara na

wananchi wote kwa

ujumla.

zilizopo kwa hiari kwa maendeleo ya taifa lao.

3. Mhe. Ahmed

Ally Salum

Mabenki yanapata

hasara kutokana na

kupungua mzunguko wa

fedha. Serikali ichukue

hatua kwani endapo

mabenki yatafungwa

kutakuwa na athari

katika uchumi wa nchi

Katika kipindi cha Julai hadi Septemba 2016, baadhi ya

mabenki ya biashara yalipata faida ndogo na baadhi

zilipata hasara ikilinganishwa na kipindi kama hicho

mwaka uliotangulia. Hali hii imeathiri kasi ya utoaji

mikopo na hivyo kupunguza mzunguko wa fedha.

Miongoni mwa sababu zilizochangia hali hiyo ni pamoja

na Serikali kubaini watumishi hewa ambao miongoni

mwao walikopa kwenye mabenki na hivyo kusababisha

kuwepo kwa mikopo chechefu; serikali kuhamisha fedha

za mashirika ya umma kutoka katika mabenki ambazo

zilikuwa zinatumika kukopeshea; na hatua ya serikali ya

kubana matumizi yasiyo ya lazima kama vile kufanya

mikutano katika mahoteli. Aidha, fedha zilizotumika

kugaramia mikopo chechefu (provision for loan losses)

zilipelekea baadhi ya benki kupata hasara na nyingine

kupata faida kidogo.

Hata hivyo, hali hii ni ya mpito na Serikali inashauri

16

NA. MTOA HOJA HOJA UFAFANUZI WA HOJA

mabenki ya biashara kubuni mikakati ya kuongeza

amana zao ili kuongeza uwezo wa kukopesha. Aidha,

mabenki ya biashara yanatakiwa kuendelea kutumia

mfumo wa upashanaji taarifa za wakopaji (Credit

Reference System) ili kupunguza uwezekano wa

kuongezeka kwa mikopo chechefu.

17

HITIMISHO

34. Mheshimiwa Spika, napenda kuwashukuru Waheshimiwa

Wabunge wote waliochangia na kutupatia ushauri kuhusu

vipaumbele na mambo muhimu ya kuzingatia katika kazi inayofuata

ya kuandaa Mpango na Bajeti ya Mwaka 2017/18.

35. Mheshimiwa Spika, napenda niliahidi Bunge lako Tukufu

kwamba, Serikali itazingatia ushauri tuliopokea kwa kadri

inavyowezekana. Hakika haitawezekana kuzingatia kila kitu

kilichosemwa hapa. Baadhi yataendelea kuzingatiwa katika mipango

ya maendeleo itakayofuata. Ili Bunge lione wazi kwamba Serikali

inasikia na inathamini ushauri mzuri wa Waheshimiwa Wabunge,

inakusudia kuweka bayana katika kitabu cha Mpango

utakapokamilika muhtasari wa ushauri uliozingatiwa, na ule

tunaoona unafaa uzingatiwe katika mipango itakayofuata na yale

ambayo bado yanahitaji kuchambuliwa kwa kina kabla ya

kuzingatiwa kwenye mipango.

36. Mheshimiwa Spika, Serikali ya awamu ya Tano imedhamiria

kujenga Tanzania mpya ili kuwaondoa watanzania kwenye lindi la

umaskini haraka. Uamuzi huu unahitaji kuachana na mazoea,

unahitaji sacrifice na unahitaji tufanye kazi kwa bidii, nidhamu na

uadilifu. Tunataka uchumi ambao wananchi wengi wananufaika nao.

Nirudie tena, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli

inajali wafanyabiashara lakini budi sheria za nchi zizingatiwe.

37. Mhe. Spika, naomba kutoa hoja.