Maoni KATIBA-Zitto

Embed Size (px)

Citation preview

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    1/13

    MUUNDO WA MUUNGANO NA TAWALA ZA MIKOA

    Rasimu ya Katiba imependekeza kuendelea kuwa na Muungano wa

    Tanzania kwa kufanya marekebisho makubwa ikiwemo kupunguza

    masuala ya Muungano na kuwepo kwa Serikali 3. Mjadala umekuwa

    mkali kuhusu Serikali 3 na hata kuzuia mjadala mpana zaidi wa masuala

    ya muungano. Rasimu haikushughulika kabisa na Serikali ya Tanganyika

    maana Tume inasema wao walipewa hadidu kuangalia Katiba ya

    Muungano tu. Kwa hili Tume haikutendea Haki wananchi maana kama

    wao wamependekeza kuunda Chombo kipya ilikuwa ni lazima kusema

    chombo hicho kinaundwa namna gani bila kuathiri Katiba ya Jamhuri ya

    Muungano.

    Wakati Mabaraza ya Katiba yanaendelea nchini kote ni vema mjadala

    wa aina ya utawala kwa Serikali ya Tanganyika na mikoa yake ikapewa

    fursa pia. Ninaamini kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

    inapasa kugusia masuala ya msingi ya Katiba ya Serikali ya Zanzibar na

    Katiba ya Serikali ya Tanganyika. Nina mawazo kadhaa ambayo

    ningependa yaingie kwenye mjadala wa Katiba mpya.

    Muundo wa Muungano

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    2/13

    Kwa vyovyote vile muundo unaonekana kukubaliaka na wananchi

    wengi ni ule wa Muungano wa Serikali 3, Serikali ya Jamhuri ya

    Muungano, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Tanganyika, japo rasimu

    imeiita Serikali ya Tanzania Bara. Hata hivyo wananchi wanapoambiwa

    kuwa kutakuwa na Marais 3, wanaguna. Kwa hiyo suala hapa ni namna

    gani ya kuhakikisha kuwa tunakuwa na Muundo wa Serikali 3 yenye

    dola imara na Mamlaka ya Jamhuri yenye nguvu ilhali kila mshirika wa

    Muungano anakuwa na mamlaka kamili ya kutekeleza wajibu wake kwa

    Wananchi.

    Iwapo tunataka Muungano uwe imara na usitetereke ni lazima tufanye

    maamuzi ambayo yatabadili sura nzima ya Muungano na kuweka wazi

    wajibu wa kila Mshirika katika Muungano. Ni vema pia kuweka Muundo

    wa Serikali ambao utatoa uhuru kwa washirika kutekeleza majukumu

    yao bila bugudha lakini pia utatoa fursa kwa Dola kutekeleza majukumu

    yake ya kidola kama kuhakikisha ulinzi, usalama na utulivu wa nchi,

    kuhakikisha umoja na mshikamano wa nchi na kuhakikisha maendeleo

    sawia kwa maeneo yote ya Jamhuri ya Muungano.

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    3/13

    Napendekeza Muungano wa Serikali mbili za Tanganyika na Zanzibar

    zinazoongozwa na Mawaziri Wakuu watendaji na Serikali ya Muungano

    inayoongozwa na Rais. Pia napendekeza masuala ya Tawala za Mikoa

    kuwa masuala ya Muungano na Wakuu wa Mikoa (Gavana)

    wachaguliwe na wananchi moja kwa moja na wawe na mamlaka kamili

    kwenye masuala yatakayokabidhiwa kwa Serikali za Mikoa kwa mujibu

    wa Sheria itakayotungwa na Bunge la Muungano (Seneti). Napendekeza

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania achaguliwe na wananchi

    wote kwa kupata zaidi ya nusu ya kura zote halali na sio chini ya

    asilimia 25 ya kura kutoka kila upande wa Muungano. Gavana wa Mkoa

    pia achaguliwe na wananchi wote wa Mkoa husika.

    Nafasi nyingine za kuchaguliwa moja kwa moja ziwe ni pamoja na

    Madiwani ambao watachagua Meya/Mwenyekiti wa Halmashauri,

    Wabunge wa Mabunge ya Tanganyika na Zanzibar ambapo chama

    chenye wabunge wengi au muungano wa vyama wenye wabunge wengi

    utatoa Waziri Mkuu kuongoza Serikali za washirika na Maseneta ambao

    watachaguliwa na Mikoa kama inavyopendekezwa na rasimu ya Katiba

    ya sasa.

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    4/13

    Rais wa Jamhuri ya Muungano

    Napendekeza Rais awe Mkuu wa Nchi, Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya

    Ulinzi na Usalama na Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa

    Tanzania mwenye mamlaka kamili kwenye masuala yote ya Muungano

    yaliyoainishwa na Katiba.

    Rais wa Jamhuri ya Muungano awe na wajibu wa kikatiba wa

    kuhakikisha kuwa kuna ulinganifu wa maendeleo kwa mikoa yote ya

    Jamhuri ya Muungano.

    Rais awe na Mamlaka ya kukikaribisha chama chenye wingi wa

    wabunge kwenye mabunge ya Tanganyika na Zanzibar kuunda Serikali.

    Pale ambapo hakuna chama pekee chenye wingi wa wabunge wa

    kutosha kuunda Serikali, Rais awe na Mamlaka ya kukipa fursa ya

    kwanza chama chenye idadi kubwa ya wabunge kujaribu kuunda

    muungano wa vyama ili kuweza kuunda Serikali.

    Rais awe na wajibu wa kila mwaka kuongoza kikao cha Mkutano Mkuu

    wa magavana wa mikoa yote nchini na pia kuhutubia Baraza la Taifa

    (Seneti, Bunge la Tanganyika, Bunge la Muungano na Mkutano wa

    Magavana kwa pamoja).

    Rais atakuwa na mamlaka ya kuthibitisha kuondolewa madarakani kwa

    Waziri Mkuu kufuatia kura ya kutokuwa na imani iliyopigwa na Bunge

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    5/13

    (Baraza la Wawakilishi) la nchi Mshirika au pale Waziri Mkuu

    anapopoteza uwingi wa viti ndani ya Baraza.

    Rais atakuwa na mamlaka, kupitia Tume ya Maadili ya Umma,

    kusimamia maadili ya viongozi wa Umma.

    Bunge la Tanzania

    Kuwe na Bunge la Jamhuri ya Muungano lenye sehemu kuu 2, Bunge la

    juu (seneti) na Bunge la chini (Bunge la Tanganyika na Bunge la

    Zanzibar au twaweza kuita Mabaraza ya Wawakilishi).

    Maseneta wachaguliwe kutoka kila mkoa kwa utaratibu kwamba kila

    mkoa utatoa maseneta wawili, mwanamke na mwanaume. Kila Bunge la

    mshirika (Baraza la Wawakilishi) litachagua wananchi 5 ambao sio

    wajumbe wa Bunge hilo kuwa Maseneta. Wananchi hawa watakuwa

    wawakilishi wa makundi ya kijamii kama watu wenye ulemavu, vijana

    na watu wenye ujuzi maalumu. Kila mgombea Urais wa Jamhuri ya

    Muungano aliyepata zaidi ya asilimia 5 ya kura za Urais atakuwa

    amechaguliwa kuwa Seneta moja kwa moja.

    Bunge (Baraza la Wawakilishi) la Washirika wa Muungano

    watachaguliwa kwa mujibu wa Sheria zitakazotunngwa na na watatoka

    kwenye majimbo ambayo ni Halmashauri za Wilaya/Miji/Manispaa/Jiji.

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    6/13

    Kila nchi washirika wataweka utaratibu wa kuhakikisha usawa wa

    kijinsia kulingana na mazingira ya kijiografia ya nchi hizo isipokuwa sio

    chini ya asilimia 40 ya Wawakilishi watakuwa wanawake.

    Waziri Mkuu

    Atakuwa Mkuu wa Serikali ya nchi mshirika wa Muungano na atakuwa

    na mamlaka kamili kwa masuala yote yasiyo ya muungano.

    Waziri Mkuu atatokana na chama chenye Wabunge wengi kwenye

    Bunge la Nchi mshirika au kama hakuna chama chenye wabunge wengi

    peke yake kuweza kuunda Serikali, basi atatoka kwenye muungano wa

    vyama kwa mujibu wa makubaliano ya vyama hivyo na kuthibitishwa na

    Rais wa Jamhuri ya Muungano. Waziri Mkuu hatokuwa Mbunge na

    Mawaziri wake hawatakuwa Wabunge isipokuwa uteuzi wao

    utathibitishwa na Bunge kupitia Kamati maalumu itakayoundwa na

    Bunge.

    Waziri Mkuu pamoja na Serikali yake watawajibika kwa Bunge (Baraza

    la Wawakilishi).

    Gavana (Mkuu) wa Mkoa

    Atakuwa Mkuu wa Serikali ya Mkoa mwenye mamlaka kamili juu ya

    masuala yote yaliyoidhinishwa kwa mujibu wa Sheria itakayotungwa na

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    7/13

    Baraza la Wawakilishi (Bunge). Mkuu wa Mkoa (Gavana) atachaguliwa

    na wananchi wote wa Mkoa husika na atawajibika kwa BARAZA LA

    MKOA.

    Mkuu wa mkoa (gavana) atateua Kamati tendaji wa Mkoa kutokana na

    Idara zitakazoundwa na Baraza la Mkoa kutokana na Sheria ndogo

    zitakazotungwa.

    Baraza la Mkoa

    Baraza la Mkoa litaundwa na Wajumbe wote wa Baraza la

    Wawakilishi/Bunge waliomo kwenye mkoa husika, maseneta wote wa

    mkoa husika, Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya za mkoa

    husika na madiwani 2, mwanamke na mwanaume, watakaochaguliwa

    na Baraza la Madiwani la Halmashauri husika.

    Baraza la Mkoa litakuwa na mamlaka ya kujadili na kupitisha mipango

    ya maendeleo ya mkoa, kushauri na kusimamia kamati tendaji ya mkoa,

    kupitisha sheria ndogo za kuendesha mkoa (by laws), kujadili na

    kuidhinisha Bajeti ya Mkoa na kuthibitisha mikataba yote ambayo mkoa

    unaingia. Baraza la Mkoa pia litakuwa na wajibu wa kupokea na kujadili

    na kutoa maelekezo kuhusu taarifa za utendaji za Halmashauri za

    Wilaya ndani ya mkoa husika.

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    8/13

    Mambo ya Muungano

    Rasimu ya Katiba imeainisha masuala saba ya muungano. Hata hivyo

    masuala haya hayatoi nguvu ya kikatiba kwa Jamhuri ya Muungano

    kubakia moja na imara. Masuala kadhaa hayana budi kuongezwa.

    Usimamizi wa Hifadhi ya jamii (social security) ni suala linahusu uhai

    wa Taifa na wananchi wake. Pia hifadhi ya jamii ni kama Deni la Taifa

    (obligation of the State), kwa hiyo ni lazima liwe suala la Muungano. Kila

    nchi Mshirika anaweza kuwa na Shirika lake la Hifadhi ya Jamii, lakini

    usimamizi wa Sekta ni vema ufanywe na chombo cha Muungano. Vile

    vile Usimamizi wa masuala ya Bima na Mabenki kwa sababu haya ni

    masuala ya sera za fedha. Monetary policy huko tunakokwenda ni

    suala la monetary Union ya Afrika Mashariki, hivyo suala hili halina

    budi kuwa suala la Muungano na hakuna mjadala kwenye hilo.

    Usimamizi na udhibiti wa Sekta ya Nishati (Mafuta na Gesi Asilia na

    masuala ya Atomiki) yanapaswa kuwa masuala ya Muungano. Kila nchi

    mshirika anaweza kuwa na kampuni yake ya Taifa ya Mafuta na Gesi

    lakini masuala ya usimamizi wa sekta ni vema yawe chini ya chombo

    cha muungano ili kuhakikisha kuwa utajiri wa nchi unanyonywa kwa

    uendelevu na pia kutoa mamlaka kwa Bunge la Muungano

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    9/13

    kupitisha/kuidhinisha mikataba ya kuvuna rasilimali hizo za Mafuta na

    Gesi. Ni vema pia kuwa na sera moja ya masuala ya atomiki na nyuklia

    kwa Jamhuri ya Muungano.

    Rasimu ya Katiba imeondoa suala la usimamizi na udhibiti wa anga

    kwenye masuala ya Muungano. Nadhani ni vema kuhakikisha kuwa

    avition, civil and military yanakuwa ni masuala chini ya mamlaka ya

    Jamhuri ya Muungano. Kila nchi inaweza kuwa na Shirika lake la ndege

    usafiri wa anga lakini masuala ya usimamizi na udhibiti wa anga

    yabakie kuwa masuala ya Muungano.

    Hivi sasa Tanzania nzima inatumia nambari +255 kuitambulisha katika

    masuala ya mawasiliano ya simu. Rasimu ya Katiba imeondoa suala la

    mawasiliano ya simu katika orodha ya masuala ya Muungano. Nadhani

    ni makosa makubwa sana. Suala la usimamizi na udhibiti wa

    mawasiliano linapaswa kubakia kuwa suala la Muungano na Tanzania

    nzima ibakie na +255 chini ya mamlaka ya Jamhuri ya Muungano.

    Rasimu itatupelekea kuwa na code nambari nyingine kwa Tanganyika,

    nyingine kwa Zanzibar!

    Masuala ya biashara ya kimataifa na forodha ni masuala yanayoratibiwa

    na Jumuiya ya Afrika Mashariki na hivyo haikuwa sawa kuyaondoa

    kwenye masuala ya Muungano. Kwa mfano, hivi sasa Bunge la Tanzania

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    10/13

    au la Uganda au la Burundi hayana mamlaka kabisa kwenye masuala ya

    forodha maana Bunge la Afrika Mashariki ndio lenye mamlaka hayo na

    hutunga Sheri ya forodha (Customs Management Act, 2004). Afrika

    Mashariki ipo kwenye Umoja wa Forodha na kuelekea Soko la Pamoja,

    hivyo kuondoa forodha na biashara ya kimataifa kwenye masuala ya

    Muungano ni kutoona mbali.

    Kama tunataka kujenga Taifa lenye uwiano sawia kielemu ni vema

    kuoanisha sera za Elimu ya juu angalau. Napendekeza kuwa Elimu ya

    Juu iwe suala la muungano. Kila nchi washirika inaweza kuwa na vyuo

    vikuu vyake lakini ni muhimu kuwa na Chuo Kikuu cha Taifa chini ya

    Serikali ya Muungano. Mikoa inaweza kuanzisha vyuo vikuu vyake

    isipokuwa SERA ya Elimu ya Juu iwe jambo la Muungano. Usimamizi wa

    vyo vya ufundi unaweze kuwa chini ya mikoa. Serikali za nchi washirika

    wanaweza kuwa na sera ya jumla ya elimu na mafunzo ya ufundi.

    Mapato

    Rasimu ya Katiba imependekeza kuwa ushuru wa forodha na mapato

    kutoka Mashirika ya Muungano ndiwe fedha za muungano. Ninaamini

    kabisa kwamba Tume ya Katiba haikupata ushauri mzuri kuhusu suala

    hili. Kwa uzoefu wangu kama Waziri Kivuli wa Fedha, vyanzo hivyo

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    11/13

    havitoshi kuendesha DOLA. Dola inapasa kuwa na rasilimali za kutosha

    na ziada inaweza kugawa kwa washirika na mikoa katika wajibu wa

    kuhakikisha maendeleo yanawiana. Dola pia inaweza kuwa na miradi ya

    Muungano. Vile vile, hayo Mashirika ambayo Tume inasema ni yepi

    maana muungano umependekezewa masuala saba tu. Kuna haja ya

    kuangalia kwa umakini mkubwa suala hili kama kweli kuna nia ya dhati

    ya kuendelea kuwa na Muungano.

    Mapato ya Muungano

    1. Ushuru wa Forodha2. Mrahaba wa uvunaji wa Rasilimali ambapo 25% itabaki kwenye

    mkoa wenye rasilimali na 75% itatumika na Serikali ya Muungano

    kugawa kwenye mikoa kwa mujibu wa formulae

    itakayokubaliwa kwa kuzingatia idadi ya watu, kiwango cha

    umasikini na ukubwa wa kijiografia.

    3. Ushuru wa Bidhaa ambapo 60% itagawiwa kwa nchi washirikakwa ajili ya miradi maalumu.

    4. Mapato kutoka kwenye kampuni za kibiashara za Serikali yaMuungano na gawio la Benki Kuu ya Tanzania.

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    12/13

    Mapato ya Washirika

    1. Kodi ya Mapato ya watu binafsi na Makampuni2.

    Kodi ya Ongezeko la Thamani au kodi kama hiyo

    3. Tozo mbalimbali zitakazotungwa kwa mujibu wa sharia4. Mapato yasiyo ya kikodi kutoka idara na Wizara za Serikali.

    Mapato ya Mikoa

    1. 25% ya Mrahaba kutokana na uvunaji wa Rasilimali/maliasiliinayopatikana katika mkoa husika

    2. 10% ya makusanyo ya kodi ya mapato ya watu binafsi namakampuni kutoka katika mkoa husika

    3. Mgawo kutoka Serikali ya Muungano4. Mgawo kutoka Serikali ya Washirika5. Tozo mbalimbali zitakazoanzishwa kwa mujibu wa sharia ndogo

    ndogo.

    Deni la Taifa

    Napendekeza kuwa Deni la Taifa lisimamiwe kikamilifu na Jamhuri ya

    Muungano. Akaunti ya Deni la Taifa iwe chini ya hazina ya Jamhuri ya

    Muungano, Jamhuri ya muungano itakopa kwa niaba ya Washirika wa

  • 7/28/2019 Maoni KATIBA-Zitto

    13/13

    muungano baada ya mikopo hiyo kuthibitishwa na Baraza la

    wawakilishi (Bunge ) la nchi mshirika na Seneti. Jamhuri ya Muungano

    pia itadhamini mikopo ya ndani na ya nje ya Mikoa na Halmashuri za

    Wilaya.