Upload
others
View
0
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
MASHAIRI YA MASAIBU YA
KERBALA
Kimetolewa na:
AHLUL BAYT (A.S) ASSEMBLY OF TANZANIAS.L.P 75215
DAR ES SALAAM
Haki ya kunakili imehifadhiwa na:Ahlul Bayt (A.S.) Assembly of TanzaniaP.O. Box 75215, Dar es Salaam, Tanzania
ISBN 9987 633 03 X
Chapa ya Kwanza 1998: Nakala 5,000Chapa ya Pili 2009: Nakala 500
Kimechapwa na:Bilal Muslim Mission of Tanzania
YALIYOMO
Dibaji . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 1
NAUHA - MATAM
1. Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 22. Yaa Husain . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 93. Allahu Akbar . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .114. Yaa Abbas . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 125. Waa Husainan . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .136. Yaa Lailatal Ashri Tuul . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .147. Ya Shahida Karbala . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .158. Mzuri sana Husaina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 16
UTENZI
9. Husain Akafahamu . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 1710. Ya Husaini Bin Ali . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 1911. Ya Aliy ya Aliy ya Abal-Huseina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2312. Machozi yamiminika . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2413. Hussein Amefariki . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2614. Kwa Mwezi wa Muharram . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2715. Husseini Mwana wa Ali . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2816. Sifa za Imam Hassan na Imam Husain (a.s.) . . . . . . . . . . . . . . . . . 3717. Mtoto wake Husseini . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 3818. Ya Sayyidna Huseini . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 40
MTUKUFU MTUME (S.A.W.W.) ASEMA:
1. Ee Allah! Hawa (Ali, Fatima, Hassan na Husain) ndio Ahlul-Bait wangu, basi watoharishe kwa tohari kamili.
2. Husain anatokana na mimi na mimi ninatokana na Husain...
3. Hao (Hassan na Husain) ni maua yangu katika dunia.
4. Ewe Mwanangu (Husain)! Mwili wako ni mwili wangu na damu yako ni damu yangu;
5. (Ewe Husain), wewe u Sayyid, mwana wa Sayyid, na ndugu wa Sayyid; wewe u uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu), mwana wa uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu) na ndugu wa uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu); na baba wa uthibitisho tisa ambao wa tisa wao ni Qaim wao ambaye atakuwa al-Mahdi.
6. Hassan na Husain ni Masayidi wa Vijana wa Peponi.
7. Ewe Mola wangu! Mpende yule ampedae Husain.
8. Adhabu atakayoipewa yule mwuaji wa Husain huko Motoni itakuwa sawa na nusu (nzima) ya adhabu yote watakayoipewa wenye dhambi waulimwengu.
9. ...... Allah hujirafikisha na wale wajirafikishao na Husain na yu adui wa wale walio maadui zake.
10. Yeyote awapendaye Hassan na Husein amenipenda, na yeyote anayewachukia amenichukia.
1
DIBAJI
Ahlul Bayt (A.S.) Assembly ya Tanzania (ABATA), inayo furaha kwa kutoa Kitabu hiki cha Mashairi kwa watu wazungumzao Kiswahili. Ilikuwa mapendekezo ya Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi, Mwenyekiti wa ABATA, kwamba tuchapishe vitabu vya Majlis na Mashairi (Nauha na Utenzi) juu ya “Masaibu ya Karbala.” Kwa hiyo mwezi Aprili, 1998 tulichapisha Kitabu cha Majlis kinachoitwa, “Maombolezo ya Kifo cha Imam Husain (a.s.)” ambacho kimetokea kupendwa sana Afrika ya Mashariki. Alhamdulillah.
Sayyid Murtaza Rizvi na Sheikh Abdul-Majid Nassor, kwa ushauri wa Mwenyekiti wa ABATA, wameyakusanya Mashairi haya kutoka sehemu mbalimbali, wakayapanga na kupata kitabu kiitwacho “Mashairi ya Masaibu ya Karbala” ambacho unacho mkononi mwako hivi sasa.
Hiki ni Kitabu cha tatu ambacho kimetolewa na Ahlul-Bayt (A.S.) Assembly ya Tanzania; na tunayo furaha kubwa kutoa kitabu cha Mashairi va Karbala kwa Kiswahili ambacho ni cha kwanza katika lugha ya Kiswahili.
Allah Subhanahu wa Ta'ala atoe malipo yake kwa mtunzi, mfasiri na wale wote ambao wamesaidia katika kuchapisha kwake kwa njia yoyote.
Wa ma Tawfeeqi illa Billah
S.L.P. 75215 F.A. HameerDar-es-Salaam Katibu MkuuTanzania Ahlul-Bayt (A.S.) Assembly24 Februari, 1999 ya Tanzania
2
SALAAM SALAAM, IMAMU SAYYIDNA HUSEIN
Limetungwa na:Maallim Abdul Qahari bin Said,
(wa Mtama, Lindi - Tanzania)
UTANGULIZI
Marehemu Maallim Abdul Qahari bin Saidi mwanachuoni mashuhuri wa Madhehebu ya Sunni (Shafii) ndiye aliyeandika shairi hili.
Kwa sauti kubwa na shangwe alilisoma shairi hili katika azimisho la Siku ya Imamu Husain (a.s.) iliyofanyika huko Mtama (Lindi, Tanzania) mnamo tarehe mosi Julai mwaka 1961.
Lilirekodiwa katika “Tape Recorder” na kusikilizwa katika miji mingi mingineyo Barani Afrika.
Vile vile liliwahi kuchapishwa mara mbili na “Imamia Mission”, ya Lucknow, India.
SHAIRI
Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
1. Bismilah nitajayo, Ni jina la Mola wangu, Rahmani isemwavyo, Ya akhera na ulimwengu, Rahimi isimuliwavyo, Akhera ya wacha Mungu, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
2. Alhamdu ni sifa za Mola, Lillahi jina Ia Hadhiya, Namwalia Rasula, Salaam na neema pia, Waalaalihi liula, Zienee kwa wote pia, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
3
3. Baada ya kumaliza, Sasa natunga shairi, Naanza kujituliza, Nitaje kisa na maamuri, Kidogo nitatambaza, Si sababu ya kujitafakhari, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
4. Ilahi kamtuma Rasuli, Muhammadi Liamini, Awe mtetezi kamili, Aidhihirishe dini, Nae kakubali, Kuwa kiongozi wa dini, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
5. Kisa ninacho eleza, Maendeleo yaamini, Agizo alitimiza, Aliyemtuma Manani, Hakuna la kumtatiza, Mwislamu moyoni, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
6. Wakati wa maisha yake, Muhamedi Rasuli, Alimzaa mtoto mke, Fatumati Libatuli, Kamuoza binamiyake, Imamu Sayyidna Ali, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
7. Mola mjuwa falagha, Alli akamzaa Husein Mwenyezi Mungu Kawapanga, Wajukuu zake amini, Dunia ikawa na mwanga, Wakafurahi Malaika mbinguni, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
8. Siku nyingi zikapita, Mustafa akatawafu, Ndipo kuanza matata, Shamu mambo machafu, Nakuzitangaza vita, Kuazimu ushupavu, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
9. Dini ikatimiya, Kwa vitendo vya Yazidi, Amani zikapotea, Maasi yakazidi, Kidogo wafuatao njia, Ya Nabii Muhamadi, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
4
10. Ikawa nyakati hizo, Zikapunguka imani, Ikakithiri michezo, Amani ya Shaitwani, Wachache wafuatao nguzo, Nakuthibiti imani, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
11. Na hali hapo zamani, Nabii alitamka, Ya Husein minni, Waana ilaika, Ndipo kasimama Husein, Naamri akazishika, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
12. Haki ikasimama, Na batili zikaondoka, Mpaka siku ya Kiyama, Dini zitabadilika, Fahimma hata Fahhama, Uislamu utatajika, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
13. Na kifo chake kwa kamili, Ni fidia ya UisIamu, Mfano wa Ismaili, Kwa Nabii Ibrahima, Dini leo ni kamili, Imesimama salama, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
14. lmamu alipo sikia, Ilivyo badilika Shamu, Aamuruvyo bini Muawiya, Mambo mengi yaharamu, Na dini imepotea, Anadai na Uimamu, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
15. Imamu moyo ukasita, Akifikiri tarafa, Yazidu anazo zipita Bila ya amali nadhifu, Akasema hai hata, Ila nende zangu Kufa, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
16. Tarekhe ishirini na Nane, Akaondoka Madina, Kwenda kulitufu Kaaba, Shariya iliyo bayana, Yazidi Kakutubu kitaba, Kujisainisha laana, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
5
17. Barua ya kutoka Shamu, Ikafika mjini Makka, Karifiwa hakimu, Husein muuwe haraka, Husein alipofahamu, Ikambidi kuondoka, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
18. Imamu Husein hashirafu, Baada hayo kufahamu, Akasema Makka ni tukufu, Kutiya damu haramu, Hicho ni kitendo dhaifu, Kakataza Rabi Karimu, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
19. Ikawa tarehe pili, Ya mwezi wa mfunguo nane, Karbala akawasili, Kiasi cha saa nane, Majeshi ya wakatili, Yakazuia maji wasione, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
20. Mpaka tarehe saba, Mtoni kuna hatari, Maadui wameziba, Na maneno ya jeuri, Maji na heri kunywa simba, Na nguruwe na makafiri, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
21. Islamu Kataharaki, Kooni kulikauka, Kila akiwalahiki, Maji yao kuwa taka, Wao kuzidi hamaki, Huruma imewatoka, Salaam Salaam, Imamu Savyidna Husein.
22. Mama mtoto taabani, Maziwa yamekauka, Hamna tone kifuani, Mtoto anahangaika, Kayabisika midomoni, Damu zina mdondoka, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
23. Wamezuiya hayo maji, Watu elfu tano, Wengi mno walindaji, Wa mishale bila mifano, Ingawaje anawahitaji, Wala hawana mapatano, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
6
24. Ikafika siku tatu, Tangu waponyimwa maji Wameshikana hao watu, Kwa hali ya uziwiyaji, Wakaona hiyana si kitu, Wana nia ya uuwaji, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
25. Tarehe tisa ilipofika, Walitaka waanze vita, Imamu Husein aliwataka, Ruhusa ya kuswali wakapata, Amuabudu Rabuka, Bila kumfika matata, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
26. Mkuu wa jeshi la Yazidi, Ana moyo mughaladha, Omar bini Saadi, Ameajiriwa kwa fedha, Akisha timiza ahadi, Hataki kwa Mungu Karadha, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
27. Asubuhi tarehe kumi, Vita ikaumuka, Ndipo kuanza uvumi, Mishale kuipachika, Omari mtaka dami, Mshale ukamtoka, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
28. Ndiye mwamrishaji, Vita kuamrisha, Hakuna tena mkaaji, Muda wao umekwisha, Hakuna tena kuhoji hoji, Kawamalizeni maisha, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
29. Ikawa hekaheka, Hali ya vita ni kali, Islamu kateseka, Maji yamewawiya mbali, Yamradi wana mashaka, Hawanywi wala hawali, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
30. Alipofika mkatili, Mlaanifu mwingi wa balaa, Na kisu chake kikali, Yuna kwitwa Shimer, Imamu aliomba aswali, Hakupenda amalize swala, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
7
31. Alipotaka amuuwe, Alitamka Imamu, Ebu nikuchungue, Nikujue mjirimu, Amuene uso wa Nguruwe, Mara alimfahamu, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
32. Aliambiwa zamani, Uhai wa babu yake, Ataye muuwa Husein, Atabadilika sura yake, Awe mnyama wa mwituni, Nguruwe kwa jina lake, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
33. Ikaja nyingi tufani, Ikatokea kusini, Jua likazama mbinguni, Kukawa giza azimu, Ikashuka mvua mbinguni, Maji mekundu ya damu Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
34. Wakati walipo mchinja, Adui walifurahi, Mwili waliuacha, Ili upondwe na ngamia, Na mtoto wakamchinja, Bila ya kumhurumia, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
35. Wanawake wakachojoa, Shungi zao za kichwani, Kipita akiwasumbua, Wakatembezwa uriani, Kwa ukatili wa kuuwa, Ataulipiza Manani, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
36. Kile kichwa ikabidi, Kama si kichwa cha mtu, Kikapelekwa kwa Yazidi, Akakanyage kwa Fimbo, Fikara za mkaidi, Si kama fikara za utu, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
37. Yazidi aliona vema, Hajui ameangamia, Ndani ya Jahanama, Ndiko aliko ingia, Na maji yaja hima, Ndiyo anaumiya, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
8
38. Hapa ninahitimu, Shairi nimekomesha, Ingawaje nina hamu, Yakutaka kuzidisha, Rabbi unirehemu, Kwa haya yangu maisha, Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
39. Na kila msikiaji, Mwenye roho ya mahaba, Rabi mwondolee balaji, Mpokelee kila toba Yarabi utufariji, Kwa baraka ya Habiba Salaam Salaam, Imamu Sayyidna Husein.
MUIENUDDIN CHISHTI AJMERI ASEMA:
Shah ast Husain Badshah ast HusainDin ast Husain Din Panah ast Husain
Sar dad, Na dad dar daste YazidHaqqa ke Binae Iailah ast Husain.
Maana yaka:
Husain ni Mfalme (ni Bwana) Husain ni Mfalme wa Wafalme (ni Bwana wa Mabwana)
Husain ni Dini Husain ndiye mhifadhi wa Dini.kichwa alikitoa, bali hakutoa mkono kuuwake juu ya mkono
wa Yazid.Hakika Husain ndiye msingi wa La ilaha illallah.
9
YAA HUSAIN
1. Yaa Husain, yaa Husain kullu yawmin Aashura Kullu ardhin Karbalaa yaa abal Ahraar x 2
2. Yaa Salilul ambiyaa, anta Imamul atqiyaa Yaa abal ahraar x 2
3. Yaa Kahfil mustajirrin, yaa shariul mudhini biin Yaa abal ahraar x 2
4. Yaa ilma fikulli waad, yaa imama filjihadi Yaa abal ahraar x 2
5. Laa ilaha illa llah, yawmi twaffi-laa nansaa x 2 Yaa abal ahraar x 2
6. Yaa sar khata thairin, Haihata annastakini x 2 Yaa abal ahraar x 2
7. Ya kahfa wal muutamad, amta zaadi wa sanaad x 2 Yaa abal ahraar x 2
8. Salmali man salamakum, Harbali man haraba kum x 2 Yaa abal ahraar x 2
9. Aaala rabbul kainati, fajrana hatma liat x 2 Yaa abal ahraar x 2
10. Yaa min haja filhayat, yaa qudwata bil abat x 2 Yaa abal ahraar x 2
10
11. Yaa man jismuhu saliib, yaaman shaibu hu khatib x 2 Yaa abal ahraar x 2
12. Yaa madhlumu yaa dhaman, abkaitalinsi wal jani x 2 Yaa abal ahraar x 2
13. Yaa mantabkiika ssamaa, yaa sayyida shuhadaa x 2 Yaa abal ahraar x 2
14. Yaa safinatu nnjaat, antamuhyii fil mamat x 2 Yaa abal ahraar x 2
15. Yaa imamal muttaqin, farrat bil haqil mubini x 2 Yaa abal ahraar x 2
16. Nahjuka nahjurrasuul, saatwiu yahdil anam x 2 Yaa abal ahraar x 2
17. Amta baaki lantazul, Haadiu Nahju rrasuli x 2 Yaa abal ahraar x 2
11
ALLAHU AKBAR
1. Allahu Akbar Allah yaa Husain ya Hussein Allahu Akbar Allah yaa Husain ya Hussein
2. Aliyu yandubu wayakulu yaa Husain ya Husain x 2
3. Alhassani yandubu wayakulu yaa Husain ya Husain x 2
4. Rasulu yandubu wayakulu yaa Husain ya Husain x 2
5. Azzahra tandubu watakulu yaa Husain ya Husain x 2
6. Fatima tandubu watakulu yaa Husain ya Husain x 2
7. Sakina tandubu yaa Husain ya Husain x 2
8. Jibrilu yandubu wayakulu yaa Husain yaa Husain x 2
9. Al-ardhu Yandubu wayakulu yaa Husain yaa Husain x 2
10. Assamaa tandubu watakulu yaa Husain yaa Husain x 2
12
YAA ABBAS
1. Yaa Abbas yaa Abbas Ya madhulum fii Karbalaa x 2
2. Yaa Madhulumaa fii Karbalaa Yaa man mata wahuwa atshan Ya madhulum fii Karbalaa x 2
3. Bakati Sakina ladaa Karbalaa Wa Muhammadahu banatuka-sabaya Yaa madhulum fii Karbalaa x 2
4. Bakati ssamaa’u liqatilil-Husain Wa sibtwahu ladaa Karbalaa Yaa madhulum fii Karbala x 2
5. Yaa madhulum fii Karbalaa Wa nazifaahu fii Karbalaa Yaa madhulum fii Karbalaa x 2
6. Raasuhu Husain fawqaa rrimahi Sibtu Nnabiyyi muqattalaa Yaa madhulum fii Karbalaa x 2
7. Sibtu Rrasuli muqqattalaa Waa sibtwahu fii Karbalaa Yaa madhulum fii Karbalaa x 2
13
WAA HUSAINAN
1. Waa Husainan waa Husainan waa Husainaa x 2 Waa Husainan Swaha Jibriilu Hazinaa
2. Ya srakhul kawnu bukaa’an wa aninaa
3. Qad Qadha ssibtu ghariban fii tufuur Wahdahu haafat bihi tilka sufuuf Min rimahin au nibalin au siyuuf Thumma dhulman Qatwau minhul watiina
4. Waidha bii ssibtwi fii twaffi gharib Jismuhu saa haati fii harbi saliib Maahu rahtul ubati swabirinaa
5. Masaqawhul-maa’fii Yawmil-fajii’li Huwa dham aanin yunadi sama uuh Maata atshanan walam yusqal mainaa
6. Innahum Lam yarhamu hataa rradhii Wa Husseinu ssibtwi kassaddil-manii Nah’wu qawmil ghadri maa maddal yamiinaa
7. Maata alul wahyi walkhatbijaliil Ma baqaa minhum siwaa shakhu su alii Wanhisaauu thakila tuu fil-awiil Qad faqadnal ahla dhulman mal baninaa
14
YAA LAILATAL ASHRI TUUL
1. Yaa Lailatal-ashri tuul Qad zaada Fiiki nnuhuul Wadidtu min Qibali kuumi Yaa hunu waq rrahiil
2. Bikar balaa mudh-nazalnaa Alimtu inda nnuzuul Biannana sawfa nabqaa Bila hami wwakafiil
3. Wadhaaka aadhamu thatwabi Min zamani jaliil Yumsil Hussein Qatiilaa Wa Yaalahu mun katiil
4. Fayaa dumuiya siilii Alayhi kulla masiil Thumma nthanat bintu twaha Bi-Ibrati wa awiil
5. Tukhatibu-llayla laakim Khitwabuha an dhuhuul Taqulu la tubdi subhaa Wadha minal mustahiil
15
YA SHAHIDA KARBALA
1. Tunasikitika sana kwa kifo chako Husain Ewe Husain ya shahida Karbala x 2
2. Mal-uni alofika kukuua ya Husain Na Mungu atayaweka makazi yake motoni Ewe Husain ya shahida Karbala x 2
3. Mbingu zilitikisika kwa kifo chako Husain Majabali kupasuka kwa khofu na kwa huzuni Ewe Husain ya shahida Karbala x 2
4. Upanga uliushika ili kutetea dini Kuchezewa yetu dini Husain hukuridhika Ewe Husain ya shahida Karbala x 2
5. Tarehe za tuonyesha kwa kifo chako Husain Husain umeondoka umeacha pengo kubwa Ewe Husain ya shahida Karbala x 2
6. Tunamuomba Manani amiani mal-uni Amlani hayawani Yazidi na jeshi lake Ewe Husain ya shahida Karbala x 2
16
MZURI SANA HUSAINA
Mzuri sana Husaina Wallahi na kuapiaGiza ilitueneya hapo ulipouliwa
1. Ee mwema mwana amani, umekufa kishahidi Kunusuru hasa dini, ya wetu Mola wadudi
2. Umejitolea muhanga, ewe mwana wa Hashima Ili kuhifadhi mwanga, Nuru kubwa ya Karima
3. Kila lote la azizi, kwa Rabuna umetoa Bila kujali ajizi, hadi kufa kuokoa
4. Wanao wenye tohara, Nduguzo waso kifani Masahaba we imara, umetoa uwanjani
5. Kunusuru haki kweli, mfano wako kuiga Ujabali wenye dhili, kupambana bila woga
6. Kuishi na madhalimu, kamwe neema hapana Ni kudhili jahanamu, maisha hayana maana
Kiit
ikio
ALLAMAH SAYYID SAEED AKHTAR RIZVI ASEMA:
Imam Hassan na Imam Husain (a.s.) wameuhurisha Uislamu kutokana na utumwa wa Wafalme na hivyo basi, wameuhifadhi kutokana na uharibifu daima. Wafalme watakuja, na Wafalme watakwenda, lakini Uislamu utadumu milele. Kwa Uislamu, majina matakatifu ya Hassan na Husain yataangaza milele.
17
HUSAIN AKAFAHAMU
Husein akafahamu Ikawa hakuna budiMauti yake metimu Dhiki imeshawazidiNa kweli yake damu Wazee kwa auladiAdul watachezea Roho zikiteketea
Adui pasi kuchoka Kiu ilo kubwa mnoWaka mwandama mpaka Joto lisilo kifanoKarbala wakafika Vijana wazi midomoKusudi wa mwandamia Maji wanahitajia
Furati wakaushika maji wanywayo wanyamaPasi nafasi kutoka punda, farasi na kimaMto wakauzunguka Mjukuu wa HashimaNa maji wakijinywea Adui wakazuja
Kiu ikazidi sana Dhiki ilipo wazidiNa joto likawabana Akamuona waladiImamu na wakewana Asifanye ukaidiDhiki ikiwazidia Adui akawendea
Kile kijana swaghiri Kijana kikalalamaImam wetu Amiri Chembe kimeshika nyamaTamaa hakuikata Na damu mwili mzimaYa maji kumpatia Mikononi akafia
Adui wasikubali Mikononi mwa ImamuJapo lau tone mbili Yote ikajaa damuMuhali wakaratili Na roho yake ghulamuPasi Imani kuingia Ikaiaga dunia
18
Alipo akikariri Ukazidi ukaidiImamu akihubiri Na jeshi la mafisadiAlipata takiswiri Ikawa hapana budiChembe wakamrushia Roho zikiangamia
Waliondoka huruma Basi huu ndio mwanzoWakawa kama wanyama Wakazidisha mkazoPasi kujali dhuluma Pasiwe hata pumbazoRoho zikiteketea Vitoto vikiumia
IMAM HUSAIN (A.S.) ASEMA:
Imam Husain (a.s.) alipokuwa safarinikwenda Karbala alisema:
“Kama Dini ya (Mtume) Muhammad (sa.w.w.)haiwezi kuendelea ila kwa kukitoa
mhanga kichwa changu, basi upangana uje ukichukue.”
19
YA HUSAINI BIN ALI
1. Kwa jina lako Jalali nasema yenye ukweli Ya Husaini Bin Ali niwe nikihadithia
2. Mama yake ni Fatima, na babu yake Hashima Na Madina mji mwema, ndiko aliko zaliwa
3. Na Sayyidi na Husain, kaka yake ni Hasan Akiwapenda amini, kisha akiwa sifia
4. Mtume amebaini, ya kama huyu Husaini Na mwingine ni Hasani, Peponi wataingia
5. Yaani wao ni mabwana, wa peponi vijana Subhana maulana, wote amewaridhia
6. Ni mwezi wa Shabani, alozaliwa Husain Na siku yake yakini, ni jumanne sikia
7. Mwaka wa nne Hijira, Ndio kazawa mbora Na siku ya saba mara, kamwakikiya Nabia
8. Mtume kamwadhinia, sikioni la kulia Kinywa kamsugulia, kwa mate alafunua
9. Alikuwa ni mzuri, wa umbo la kunawili Sura kama ya Bashiri, kwani kamshabihia
10. Akipigania dini, kwa udhati moyoni Hajali nini na nini, ila dini ya jalia
11. Husaini akiwa Makka, aliupata waraka Kuwa aende haraka, Iraqi kum-baiya
20
12. Watu wangu simameni, Twende Iraqi mjini Aliwambia Husseini, Nao wakafuatia
13. Husseini aliambiwa, Huko acha kuendea Twakusihi kusikia, Huko hapatakufaa
14. Abdallah wa Abasi, Kasema kinga nafusi Zao japo wafuasi, Japo na watoto pia
15. Wende wewe peke yako, Sio na ahali zako Bwana kwa hisani yako, Shika ninayo kwambia
16. Bwana Husseini kasema, Kwenda huko ni lazima Litalonipata nijema, Mimi nimesafi nia
17. Nikenda wakiniuwa, Peponi nitaingia Kwani nimesafi nia, Dini kuisimamia
18. Liwalo lote na liwe, Iraqi ni paendewe Sio mimi niofie Niache kupaendea
19. Hapo Seyyidi Husseini, Katoka Makka mjini Na watu wake sabini, Wote wakamfatia
20. Wenye farasi yakini, Walikuwa thalathini Wengine arubaini, Kwa miguu ilikuwa
21. Alipokuwa njiani, Wakazidi yakini Mia moja khamsini, Ndio waliozidiya
22. Hao miya khamsini, Walirudia njiani Hawakumfata Husain, Hadi Iraqi sikiya
23. Husseini na watu wake, Ni Iraqi Wapafike Na taabu iwafike, Kwa humo Karbala
21
24. Mto ulio karibu, Nae Husseini Muhubi Alizuiwa ajabu, Na maadui kutumia
25. Maji wakazuiliwa, Wasiwe wayatumia Kambi akajipigia, Bwana Husseini sikia
26. Akawa maji anyimwa, Huku kiu Chawauma Watoto wanalalama, Kwa vile wanaumia
27. Husseini na watu wake, Ati wao wateseka Na maji yasitumike, Kunywewa na watu hawa
28. Hapo Husseini hakika, Vikali aliteseka Watoto walalamika, Baba! Baba! twaumia
29. Jeshi hilo lilikuwa, Kabisa lamzuia Husseini kukaribia, Maji yale kutumia
30. Watoto waliumia, Kwa kiu kuwazidia Kati yao alikuwa, Mtoto mdogo pia
31. Mtoto huyu ni Ali, Alizidiwa kikweli Zeinabu binti Ali, Sanasana alilia
32. Machozi yalimtoka, Mengi yakatiririka Akayafonza hakika, Mtoto kujimezeya
33. Zeinabu binti Ali, Ni shangazi lake Ali Kwa ala kulihali, Machozi maji yakawa
34. Hata ile siku ya ashura, Kwa mwezi kumi dhahira Muharamu ndio mara, Wakaanza kuuwawa
35. Kwanza wafuasi wake, Kisha wa nyumbani kwake Alibaki ye na chake, Kijitoto kikilia
36. Umri miezi sita, Hivyo hanavyo matata Hivyo maji angepata, Yangali msaidia
22
37. Mtoto mchanga yule, Wakampiga mishale Na mtoto pale pale, Aliiaga dunia
38. Kisha wakamzunguka, Husseini mwenye baraka Wakamuuwa hakika, Nae kaaga dunia
39. Baada ya kumuuwa, Hema moto walitia Hata wakawachukua, Banati zake Nabiya
40. Wakawafanya mateka, Kisha wakawapeleka Huko Kufa kupafika, Bila kuwahurumia
41. Ni kwa Ibni Ziyadi, Ndiko iliko wabidi Gavana wake Yazidi, Yeye ndie alikiuwa
42. Hivyo watu wa Iraqi, Walikataa haki Kumuuwa mwenye haki, Kipenzi chake Nabia
43. Kuuwawa kwa Husseini, Ni jambo lenye huzuni Katu haiwezekani, Machozi kuyazuia
44. Machozi shuti kutoka, Na watu kuhuzunika Kwa kipenzi msifika, Kinyume alofanyiwa
45. Ewe Seyyidi Husseini, Ulotoka duniani Kwa kupigania dini, Peponi wenda ingia
46. Umekufa ni shahidi, Hivyo ni kama zawadi Allahu Mola wadudi, Shahidi kakwandikia
47. Waswalatu wa Salamu, Zimfikie Hashimu Na Husseini Muadhamu, Na walio bakiya
Na: Saidi MusaZANZIBAR
23
YA ALIY YA ALIY YA ABAL-HUSEINA
1. Vikali mmeteswa Na pepo mtaingia Na waliowatesa motoni wataingia
2. Aliy Bunal Hussaini kauwawa Karbala Mishale pia vyuma vyote kuwa juuye
3. Aliomba ruhusa kwenda kupigania Akapigwa mshale na Ibn Fadhili Kichwani mwake huyo Aliy Ibunil Husaini
4. Ashahidul Abasi kauwawa vibaya Mikono ilikatwa yote miwili pia
5. Imam wetu Husein Kauwawa Karbala Mikuki na mishale vyote kuwa juuye
6. Kadhulumiwa Husaini huo mji Karbala Humo usoni mwake mawe alirushiwa
7. Vitoto vililalama midomo ilikauka Maji wahitajia adui wamezuiwia
8. Midomo ilipasuka damu pia zilitoka Akina mama pia maziwa hayakutoka
9. Imamu wetu Husaini alichinjwa kinyama Na hao maluuni Fii ardhi Karbala
10. Ya Aliy ya Aliy ya Abal-Huseina Kutilal-Husaina Fii ardhi Karbala Fii ardhi Karbala Kutilal-Hussaina
24
MACHOZI YAMIMINIKA
1. Kwa Jina la Rahmani Na Anza nudhumuhini
Na Muhammad AminiKwa Machungu na Kuliya
2. Siku hizi za Ashura Kwa kubwa mno hasara
Twazitaja kila maraMaadui walotiya
3. Kiswache cha tuumiza Hatuwezi kunyamaza
Na roho kutuunguzaMashingo kuvumiliya
4. Twadhihirisha Majonzi Na nyoyo zina simanzi
Kwa Imamu na kipenziKwa haya yalotokea
5. Twakumbuka siku hini Ya kuuwawa Huseini
Ya vilio na huzuniMjukuu wa Nabiya
6. Wallahi Tunakatika Mitilizi inashuka
Machozi ya miminikaHatuna budi kuliya
7. Huseini kudhulumiwa Kanyimwa maji kupewa
Kwa machungu kuuliwaYeye na wake dhuriya
8. Hata watoto wachanga Kwa mishale kuwadunga
Wasibali kuwanyongaNa maji kuwazuwiya
9. Wakamchinja Huseini Mjukuu wa Amini
Bila kite na imaniPasina kuzingatiya
10. Na kicha kukitundika Kwa mizozo na dhihaka
Kwa shangwe wakizungukaKwa kipenzi cha Nabiya
25
11. Tuliye kiliyo gani Kwa kiongozi wa dini
Tudhihirishe ImaniHuyu walo tuuliya
12. Walomuuwa Imamu Hao ndio madhalimu
Wakashika yake damuTarikhi inatwambiya
13. Bila shaka yupeponi Owe nao makhaini
Yeye na tumwa AminiHuseini kutuuliya
14. Kula alo muumini Kwa kifo chake Huseini
Atajawa na huzuniKipenzi cha Hashimiya
15. Na mengi tukiyaeleza Ya akili kushangaza
Maovu ya kuchukizaNa moyo kutosheya
16. Tumefika kikomoni Atupe nyingi Imani
Tushukuru MananiYa dini kusimamiya
17. Muliyoko Hadhirani Rabi atiye auni
Amina kikieniDini kuipiganiya
Umetungwa na:
Sheikh Ahmed Sheikh NabhanyP.O. Box 86876
Mombasa, Kenya
26
HUSSEIN AMEFARIKI
1. Hakika ni ujahili Kuuwa pasi kujali
Uovu na ukatiliBila ya kuzingatia
2. Asikiyae Hakika Ma machozi yatatoka
Moyo utasikitikaBila yakufikiria
3. Kwa huyu mtoto wake Muda kiu imshike
Hussein kina chakeMaji akihitajia
4. Kufika kwa makafiri Na mwana huyu saghiri
Hussein alopojiriMaji alimuombea
5. Maadui wasijibu Mmoja wao kajibu
Kwa kuwazidi ghadhabuMshale kuutumia
6. Jibu lake ni mshale Akafia pale pale
Kumfunma mwana yuleKifo cha kukusudia
7. Hapo ndipo Hussein Akaingia vitani
Kwa uchungu wamoyoniBila tena kungojea
8. Hussein akapigana Akauwa wengi sana
Kishujaa kukazanaKwa nguvu zake jalia
9. Naye mwisho kifo chake Akafa hali yu pweke
Afanyeje peke yakeShahidi akajifia
10. Hussein amefariki Na hao ni yao dhiki
Hali yukatika hakiWalomtenda ubaya
27
KWA MWEZI WA MUHARRAMNaanziliza kauliNa Swalawati Rasul
Kwa Jina Lake JalaliNa-ali zake pamoja
Mswiba ulo adhimuDhuriya zake Hashimu
Kwa mwezi wa MuharramuKarbala wakingiya
Hadithi imetuwambiyaWapendwa wake dhuriya
Rasuli ameuswiyaKinyume wakatumiya
Umati walibadiliIkawa ni kuwadhili
Mahabba yao kwa AliNa maji kuwaziwiya
Yasitoshe walofanyaDhuluma wakamuonya
Ya Mtume kuyakanyaVijana kumuuliya
Hawakujali hishimaVijana waliye wema
Ya Sayyidati FatimaWa Haidari Aliya
Sina budi nitaliaIwe kwetu mazoweya
Kukosa kuwateteaAshura ikingiliya
Hadithi walisahauWakawauwa na kiu
Mapenzi wakadharauFurati wakangaliya
Walikunwa KauthariPamoja na Answari
Maji mema ya fakhariDini waloitetea
Yalopita tayakidhiNa kwa Mungu ni fawidhi
Kwa Tumwa nipate radhiNa Aya kiisomeya
INNA LILLAHI WA INNA ILAIHI RAJEUN
Sharif Mohammed Ahmed Al-HuseiniJomvu Station, Mombasa
28
HUSSEINI MWANA WA ALI
Naanziliza kwajinaMola asiye kijana
Lake yeye SubhanaWala mke asiliye
Ndie watangu natanguMuumba nchi na mbingu
Kabula ya ulimwenguMilele Atabakiya
Asie na mshirikaAmeketi pasi shaka
Na wala hakuzalikaEnzie imetimiya
Sasa penda kuwelezaNa moyo nitaukaza
Kisa kenye kuchukizaHadi mwisho kufikiya
Ni rafiki wa RasuliHusseini mwana wa Ali
Muhammadi mur saliNa Fatuma Hashimiya
Kipenzi chake NabiyaUhai wake sikia
Kuliko viumbe piyaHusseini akimwambiya
Wewe mtu wa peponiApendae kubaini
Huna shaka asilaniNamtizame Husseini
Baada kufa RasuliNa Alii mjamali
Muda ulipotawiliAlipoaga duniya
Kukazidi wasiwasiPasiwe mwenye nafasi
Ulimwengu ukahisiMatumbo kupiganiya
Baada yote kufikaWaso haya wakatoka
Na damu zikimwaikaVita wakaandaliya
Vikaandaliwa vitaUmbea nausalata
Na mengi mno matataVigaro vikatimiya
29
Vigaro vya mahasidiChini ya yeye Yazidi
Nyoyo zenye ufisadiVitani wakaingia
Husseini yuko ndianiKuwapinga mashetani
Kutaka ihami diniNakuituza duniya
Kwa moyo uso imaniNa damu waitamani
Majeshi yakawa kaniYa Husseni na dhuriya
Wakawa wajikatakataNaimamu washamwita
Watakayo washapataMjini kwao kungiya
Habari hiyo hanayoKumbe mambo sasa siyo
Amekaza wake moyoMauti yamngojea
Yunjiani enda zakeWaume na wanawake
Akaweta watu wakeNa radhi akawiliya
Kuwajuza kwa yakiniPasipo matumaini
Hila zote kwa makiniIraqi kufikiliya
Kawambiya kimbieniEla mini niwacheni
Atakae samahaniNimuhali kukimbiya
Baada yeye kukuliKama vile mafahali
Wengi hawakuhimiliNyumbani wakarudia
Akabakiya HusseiniNa baadhi ikhiwani
Na dhuriya wa nyumbaniAkali wakasaliya
Alipofika IraqiFuraha na kujinaki
Jamii ya halaikiJeshi likamwingilia
Akawa hana namnaPamwe na wake vijana
Pande zote amebanwaWapi watakimbiliya
30
Akasema kwa lafudhiAdui kuwapa radhi
Ka fasaha na mahadhiKuwatajia Jalia
Akawaonya mifanoBarua zilizo nono
Hati zao za mkonoWalizo kumwandikia
Kayesha yote manenoYote yasiwe ni neno
Wala pasipo usonoYao wakashikilia
Wakamuonya adhabuZimewaingia ghadhabu
Na nyingi mno sulubuBila sababu ya njia
Adui pasi kuchokaKarbala wakafika
Wakamwandama M-makaKusudi wa mwandamiya
Furati wakaushikaMto wakauzunguka
Pasi nafasi kutokaNa maji wakijinyweya
Kiu ikazidi sanaImamu na wake wana
Najoto likawabanaDhiki ikawadhidiya
Ikawa hakuna budiWazee kwa auladi
Dhiki imeshawazidiRoho zikiteketea
Kiu ilo kubwa mnoVijana wazi midomo
Joto lisilo kifaniMaji wanahitajiya
Maji wanywayo wanyuaMjukuu wa Hashima
Punda farasi na kimaAdui akawendeya
Akenda kwao salamaAbdallah anawana
Karibu roho kutemaKwa kiu kumzidiya
Kile kijana swaghiriTamaa hakukasiri
Imamu wetu AmiriYa mali kumpatiya
31
Adui wasikubaliMahali wakaratili
Japo lau tone mbiliPasi imani kuingiya
Mipo akikaririAlipata takisiri
Imamu akihubiriChembe wakamrushiya
Wakamba ha ndiyo majiMnyweshe yamfereji
Katu huyaonji majiNi leo mtatubiya
Kijana kikalalamaNa damu mwili nzima
Chembe limeshika nyamaMikononi kikafiya
Mikononi mwa ImamuNa roho yake ghulamu
Yote ikajaa damuIkaiaga duniya
Katu wakamba aduiMtayaona jamii
Maji yetu situmaiKanwani hamtotiya
Ukazidi ukaidiIkawa hapana budi
Kwa jeshi la mafisadiRoho zikiteketeya
Basi huu ndiyo mwanzoPasiwe hata pumbazo
Wakazidisha mikazoVitoto vikiumiya
Kajaribu kwa upoleMaji yote yako tele
Kuwaeleza walo paleJapo tone kutumiya
Akenda huko karibuAlipotaka jaribu
Kiu ilimughilibuChembe kikamuingiya
Kikamwingia ImamuMdomoni kikadumu
Chembe chao mahasimuNa damu ikamweneya
Huku kiu imemshikaMsiba umemfika
Damu ikichirizikaHana pakukimbiliya
32
Kakishika kakizuwaKamshukuru Moliwa
Kwa nguvu akakitowaMuumba wa waja piya
Zikazidishwa sulubuRafikize wakaghibi
Mno na nyingi taabuMauti kuyandamiya
Rafiki wakaangukaNa damu zikimwaika
Imamu kumzungukaAkawa aogeleya
Katikati kwenye damuKatu yako hayatimu
Adui wakakalimuMauti yakungojea
Mauti yenye taabuYatakufika karibu
Usumbufu na adhabuKaa ukiliadhania
Ni leo, leo ni leoNa wote hao watu
Utaiona kwa leoWote tutawalemeya
Kakalimu muungwanaNa Molawe kalingana
Kamshukuru RabanaNa dua kujiombeya
Akatamka HusseiniKwako wewe shukrani
Kamwambia Mola mananiNyoyo zimefurahiya
Hatuna katu huzuniMauti twayatamani
Kwa ulio yasainiKuliko kuangukia
Vita vikauma sanaNa Imamu akawana
Pasipo kusemeyanaPasi nyuma kurejeya
Lakini ifae niniNa ziyada ilondani
Kwa adui elfeniHusseini akalegeya
Akalegeya kwa dhikiAsimpate rafiki
Aloikuta hilakiHuruma kumuonea
33
Ukweli ulodhihiriHaikuweko ni siri
Ikakabili ni shariShida zikawachachiya
Kutamka kwa upoleSahibuze kuwambile
Pasipo nyingi keleleAtakaye kukiribiya
Usiku huo gizaniNamimi radhi moyoni
Kawambia kimbiyaniNa dua nawaombea
Jamii wakakataaKuliko kuyakimbia
Heri kwao kujifiaMauti wakaridhiya
Adui likadhihiriNa upesi ikaswiri
Moyo umetahayariImamu kumjiliya
Mtoto wake HusseiniKaruka pasi makini
Naye alipobainiAmie kumteteya
Pasi khofu wala shakaNa maneno katamka
Adui akamshikaMsihaya kamwambiya
Kamwambiya huna hayaUtaikuta hizaya
Bure wayatenda hayaMbele ya Mola jaliya
Adui likazungukaHusseini akimtaka
Mtoto akamshikaKijana kumuusiya
Huku mepiga pambajaNa huku akiwapiga
Na adui huko wajaMpaka mwisho kufikiya
Yakamzidi machunguAkaaga Ulimwengu
Akamsabihi MunguMjukuu wa Nabiya
Ghafula akijiliwaAdui lake Moliwa
Roho yake ikatwawaImamu akamwendeya
34
Akamwendeya kwa dhatiJiadui afiriti
Akamendesha mautiDharuba kumwemezeya
Alipokufa HusseiniNa tatu yaliyo ndani
Yalitimu thelathiniMafumu yalowingiya
Kuna tena thethiniPanga za hao wahuni
Na nne mwake mwiliniMwilini zimesaliya
Mbali mengi majarahaMoyo hauna furaha
Kuyataja ni karahaKwa Imamu kujifiya
Ndio huo mwisho wakeCha Imamu tusichoke
Hiki ndicho kisa chakeMilele kujisomeya
Walipokwisha sainiSasa hii ni yakini
Adui wakabainiUshindi umewajiya
Wakendewa majohariMatekani wakaswiri
Mabanati wa AmiriHuku wakiwachezeya
Pasi haya za usoKuwatia taabani
Wakaona ni kifaniJamaa zake Nabiya
Wakazidisha jeuriNa kichwa chake Amiri
Wala pasipo na siriFumoni wakakitiya
Huku wakikichezeyaPasi imani kuwaingia
Na huku wakiimbiyaWote wamefurahiya
Njiani walikipitaZimekwisha jaa vita
Nyoyo zao mezipataShetwani amewaingia
Alipopata habariYazidi akaamuri
Kwa ambayo yamejiriIli kwehwa kumwiliya
35
Furahani vibarakaKwa Yazidi kikafika
Haraka kukipelekaMeyowe kufurahiya
Akawa kukitozeyaHuku akimbiliya
Na vijiti kukitiyaChini kukiumbiriya
Msihaya wake diniUchunguwe wa moyoni
Yazidi akatamaniUtatowa kwa duniya
Na huku akikigotaUovu na usalata
Meno akiyaambataHakuna alodhaniya
Ajabu hii ajabuKumfikiya ikabu
Kwa kijanache swahibuWala pasipo hatiya
Muili ukiwa mbaliWakawachiwa mahuli
Kijana cha MurisaliNa nyama kukitezeya
Basi haya ni mautiLakini kwao laiti
Walotenda asheratiMilele wamejutiya
Walitenda pasi hayaYa Mola kuyachezeya
Dini kutotegemeyaPasi nyuma kurejeya
Yapasa tuyalilieIslamu natulie
Mauti yake HusseiniKwa kifo chake Husseini
Hapa napenda kukomaBali mengi sikusema
Hadithie kuisomaDhiki nikiisikiya
Kisomoni waungwanaMpate jua maana
Majumbani na vijanaMambo yaliyo tukiya
Yatupasa IsilamuKumliliya Imamu
Machozi hadi ya damuKwetu imetupasiya
36
Rabi atamtukuzaKuzidi akimjaza
Peponi kum-bakizaNeema kumshushiya
Hapa naweka kalamuWala mbele siyo tamu
Nimefikiya makamuHapa nitakomeleya
YAPASA TUYALILIE MAUTI YAKE HUSSEIN
Na: Masoud Abdallali Muh’d,Mombasa - Kenya
IMAM SHAFII ASEMA:
1. Hussein! aliuliwa shidi pasi na makosa yoyote na kanzu yake ikatapakazwa wekundu.
2. Ikiwa dhambi zangu ni kuwapenda watoto wa Mtume Mohammad (s.a.w.) basi ni dhambi ambazo sitatubiya.
3. Kwa sababu ya Ahlil-Beit wa Mtume (s.a.w.) Ulimwengu mzima ulitetema na majabali na milima ilikaribia kuyeyuka.
4. Ni nani atakayemfikishia Hussein ujumbe wangu na hata kama nyoyo zatukia?
37
SIFA ZA IMAM HASSAN NA IMAM HUSAIN (A.S.)
Nawapa na taarifa Walikuwa wana sifa
Japo kuwa walikufaNjema ilotimilia
Walikuwa watukufuWalo na njema sharafu
Tena ni waaminifuAlowajazi Jalia
Walikuwa MaimamuMashujaa walotimu
Kuongoza IsilamuDini kuipigania
Walikuwa watu wemaAkiwapenda Hashima
Vijana wenye heshimaWajukuu wa Nabiya
Walikuwa wenye diniNa nyingi mno imani
Maovu hawathaminiNyoyoni ilowangia
Walikuwa na hurumaToka kwa watu wazima
Isilamu wenye himaNa vijana wote pia
Walikuwa wasifikaTena waliyoumbia
Duniani kutukukaKwa uzuri na tabia
Walikuwa makarimuKisha ni wenye ilimu
Huwezi kuwalaumuYa dini na ya dunia
Walikuwa wafalumeMashujaa wenye tume
Wajukuu wa MtumeVitani kushambulia
Sifa zao ni kathiriWala hazina akhiri
Tena zote ni nzuriWallahi zimezidia
38
MTOTO WAKE HUSSEINI
Jambo jengine ni hili Hiki si kisa cha piliNi cha kijana rijali
La majonzi ikhiwaniAmbacho ni cha huzuniMtoto wake Husseini
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
Naye kafa madhulumuMuovu huyo KhasimuBure kaimwaga damu
Kijana wa mikononiAdui aso imaniYa kijana maskini
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
Kifo chake ni dhulumaAdui aso hurumaKwa mshale kamfuma
Kijana huyu yakiniAso Imani moyoniUkamwingia mwilini
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
Mshale ulimdungaIkawa hapana kingaAkafa mwana mchanga
Mtoto wake HusseiniYa kuiyepuka zaniKiumbe cha Rahamani
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
Ovu liso wezekanaKiumbe chake rabanaWalimu-uwa kijana
Kupata chake kifaniKilo safi cha peponiBila kosa asilani
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
39
Huyo ni wake uweleAlomdunga mshaleNaye piya vile vile
Alo mughuri shetaniKipenzi chake aminiAtaingia motoni
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
Kwa kumuuwa kijanaHata akatubu sanaAdhabu yake ragana
Malaika kwa yakiniHaipati samahaniKwake haiwezekani
Kadhulumiwa Husseini Na wake mwana mchanga
IMAM HUSAIN (A.S.) ASEMA:
“Kufa kwa heshima ni bora kuliko kuishi kwa aibu”.
40
YA SAYYIDNA HUSEINI
Kukuomba sina budi Ili utimu mradi
Ya razaku ya wadudiYote nalo kusudia
Sikutaka kusimamaNi mambo kunisukuma
Mengi mno kuyasemaNi lazima kuelezea
Natokeza hadharaniYalomfika Husseini
Kwa ufupi nibainiYa Rabbi niafikia
Yale ni mambo adhimuSina shaka mwafahamu
Yalomfika ImamuNami tawahadithia
Ule mwaka wa sitiniKaondoka duniani
Wahijira sikianiMuawiya kajifiya
Yazidi alitangazaDini ataiongoza
Nchi zote kaenezaIli watu kumbaiya
Barua aliandikaKwa walioikafika
Madina kaipelekaNae akimwelezea
Kwa makini isomeniKahitaji kura zenu
Mfahamu yalo ndaniIsilamu wote pia
Nazidi kuyabainiNi kura yake Husseini
Yalio mwangu moyoniUfike kumwelezea
Husseini kastakimuHuyo ni mtu dhwalimu
Akasema yakatimuKidini hakutimiya
Kama mimi ni haramuSitaki wake msemu
Kukubali ya dhwalimuMwambiye sitoridhia
41
Kwanza yeye nakiburiKajaa kila fujuri
Ni mlevi hana siriNyote mnamtambua
Sitokuwa chini yakeTaji hilo silo lake
Hapa na pale afikeHata yeye yamwelea
Mtume alibainiNi Maimamu yakini
Kwa Hassani na HusseiniKila mtu kasikia
Alifu kumi na mbiliKwa mjukue Rasuli
Barua ziliwasiliIraq Zilitokea
Barua ZilimtakaUkhalifa kuushika
Husseini huko kufikaDini kuisimamia
Yazidi si mtu mwemaNa haya tunayosema
Sisi sote twafahamiaWewe twakushtakia
Husseini hakutwawiliIli kujua ukweli
Katuma Ibn AkiliWa mambo yalomfikiya
Alipokewa vizuriWalimfanya safiri
Wadogo hatakibariWa Husseini Msifiwa
Kisha mambo ligeukaMapanga wakayashika
Balozi walimwepukaMuslimu kumuwa
Mwezi nane kutimiaHusseini kashika njia
Mfungo tatu sikiaIraqi kaelekea
Naswaha zilimfikaIraqi usije fika
Twakuomba kutotokaWatu wakakukimbia
Husseini aliwambiyaNitakwenda nadhuria
Hayo yote nasikiaMtume kani uswiya
42
Wakiniuwa sijaliKua hayo majangili
Aliniambiya RasuliDhulima watatumia
Alipofika njianiNi hayuko duniani
Ilimaka yakiniMuslim kauwawa
Iraq waligeukaHivi waja kukushika
Unafiki wakashikaHusseini aliambiwa
Ule msiba adhimuYeye na wake kaumu
Ulomfika ImamuNakizaziche pamoja
Hapa ni pahali ganiNi Karbala jangwani
Niambiyeni jamaniHuseini aliambiwa
Ibn Saad OmariMaudhi na ujeuri
Najeshile waliswiriImamu wamfanyia
Unyama walifanyiwaNa maji kuzuiliwa
Na kiu iliwauwaHayo yote watendewa
Kauwawa AkbariNa hao watu mashari
Pia hata AsghariMungu yuwashuhudia
Asghari ni kijanaNa kiu ilimbana
Ni mdogo tena sanaKwa chembe walimuua
Husseini aliuuiizaKosa gani tulifanza
Fikirini mukiwazaKutendewa kama haya
Himambo yenye huzuniNashindwa kuyabaini
Alotendewa HusseiniUkumbuni ngatokea
Yangu haki mumetwaaNa leo mwanisumbua
Ya ukhalifa sisawaNilipi mwafikiria
43
Au hamkusikiaHapo akiwauswia
Usemi wahashimiaKuhusu wake dhuria
Mama yangu ni BatuliNa baba yangu ni Ali
Binti yake RasuliWaswii wake Nabia
Ya Husseini walimwagaWalijifanya wajinga
Damu yake bila wogaUfasiki mewashika
Kijukuu cha RasuliAchinjwa kama ghazali
Ni Husseini bin AliWallahi twakulilia
Alipewa kila dhuliAteswa na majangili
Mwanao ewe BatuliWaso dini sikiya
Walisahau ahadiNa wote ni mashahidi
Ya Mtume MuhammadiMtume akiwauswia
Alimchinja HusseiniNa Mungu si Athumani
Bila khofu na huzuniNae atamlipia
Ni kifo chenye kutishaWallahi chahuzunisha
Tena kina babaishaKila kinapo tolewa
Na Mungu si AthmaniWa kesho wenda motoni
Twalipa dunianiAdhabu yawangojea
Hapo ndipo nitafikaKwa huzuni lonishika
Kalamu chini nawekaSiwezi kuendelea
Mola atupe ImaniTuwe nae na peponi
Yakumpenda HusseiniDua zetu zipokea
Kisha Swala na SalamuNa alize Mainwnu
Zende hadi kwa HashimuHasidi angachukia
ISBN 9987 633 03 X
kimetolewa naAHLUL-BAYT (A.S.) ASSEMBLY OF TANZANIA
S.L.P. 75215DAR ES SALAAM
TANZANIA