Upload
others
View
36
Download
2
Embed Size (px)
Citation preview
WAZALENDO SACCOS LTD
Namba ya Kuandikishwa. 2065
S.L.P 474,
MOSHI
Barua Pepe: [email protected]
MASHARTI YA CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO
WAZALENDO (WAZALENDO SAVINGS AND CREDIT COOPERATIVE
SOCIETY LTD)
Agosti, 2013
ii
Yaliyomo
Ukurasa
Yaliyomo .................................................................................................................................................... ii
Utangulizi .................................................................................................................................................. 1
SEHEMU YA KWANZA ......................................................................................................................... 1
1 TAFSIRI ............................................................................................................................................ 1
1.1 Akiba .............................................................................................................................................. 1
1.2 Amana ............................................................................................................................................ 1
1.3 Bodi ................................................................................................................................................ 1
1.4 Chama ............................................................................................................................................ 1
1.5 Huduma za kifedha ........................................................................................................................ 1
1.6 Kamati ya Usimamizi ..................................................................................................................... 1
1.7 Kanuni za Sheria ya Ushirika ........................................................................................................ 1
1.8 Masharti ......................................................................................................................................... 1
1.9 Mikopo ............................................................................................................................................ 1
1.10 Mkutano Mkuu .............................................................................................................................. 2
1.11 Mwanachama ................................................................................................................................. 2
1.12 Sera ................................................................................................................................................. 2
1.13 Sheria ya Ushirika ......................................................................................................................... 2
1.14 Watumishi ...................................................................................................................................... 2
SEHEMU YA PILI ................................................................................................................................... 2
2 JINA NA MAELEZO MUHIMU YA CHAMA ............................................................................. 2
2.2 Dira ya Chama ................................................................................................................................ 3
2.3 Maarubu/Mwelekeo ....................................................................................................................... 3
SEHEMU YA TATU ................................................................................................................................ 3
3 MADHUMUNI .................................................................................................................................. 3
iii
3.1 Madhumuni Mahususi ................................................................................................................... 3
3.2 Shughuli za Chama ........................................................................................................................ 3
SEHEMU YA NNE ................................................................................................................................... 4
4 UANACHAMA ................................................................................................................................. 4
4.1 Sifa za Mwanachama ..................................................................................................................... 4
4.2 Kujiunga Uanachama .................................................................................................................... 4
4.3 Kusimamishwa au Kuachishwa Uanachama ................................................................................ 5
4.4 Ukomo wa Uanachama .................................................................................................................. 5
4.5 Wajibu na Haki ya Mwanachama ................................................................................................. 5
4.5.1 Wajibu wa Mwanachama ........................................................................................................... 6
Ufuatazo utakuwa wajibu wa mwanachama ............................................................................................... 6
4.5.2 Haki za Mwanachama ............................................................................................................... 6
SEHEMU YA TANO ................................................................................................................................ 7
5 HISA ZA WANACHAMA ............................................................................................................... 7
SEHEMU YA SITA .................................................................................................................................. 7
6 MTAJI WA CHAMA ....................................................................................................................... 7
SEHEMU YA SABA ................................................................................................................................. 7
7 FEDHA NA MALI ZA CHAMA ..................................................................................................... 7
SEHEMU YA NANE ................................................................................................................................ 8
8 DHIMA YA MWANACHAMA ....................................................................................................... 8
SEHEMU YA TISA .................................................................................................................................. 8
9 UONGOZI NA USIMAMIZI WA CHAMA ................................................................................... 8
9.1 Vyombo vya Maamuzi .................................................................................................................... 8
9.1.1 Mkutano Mkuu wa Mwaka ........................................................................................................ 9
9.1.2 Mkutano Mkuu wa Kawaida ...................................................................................................... 9
iv
9.1.3 Mkutano Mkuu Maalum .......................................................................................................... 10
9.2 Taratibu za Kuitisha Mkutano Mkuu .......................................................................................... 10
9.3 Bodi ya Uongozi ........................................................................................................................... 11
9.3.1 Sifa za Wajumbe wa Bodi ........................................................................................................ 11
9.3.2 Majukumu ya Bodi ................................................................................................................... 12
9.3.3 Majukumu ya Mwenyekiti wa Bodi ......................................................................................... 13
9.3.4 Majukumu ya Makamu Mwenyekiti wa Bodi .......................................................................... 13
9.3.5 Mikutano ya Bodi ..................................................................................................................... 13
9.3.6 Kuacha au Kusimamishwa ujumbe wa Bodi ........................................................................... 13
9.4 Kamati ya Usimamizi ................................................................................................................... 14
9.4.1 Sifa za Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi ............................................................................. 14
9.4.2 Majukumu ya Kamati ya Usimamizi ........................................................................................ 14
9.4.3 Kamati ya Mikopo .................................................................................................................... 14
9.4.5 Majukumu ya Wajumbe wa Kamati ya Mikopo ...................................................................... 15
9.5 Wajumbe wa Uwakilishi............................................................................................................... 15
9.5.1 Majukumu ya Mwakilishi wa Bodi .......................................................................................... 15
9.5.2 Majukumu ya Mwakilishi wa Wanachama ............................................................................. 15
9.6 Menejimenti/Meneja .................................................................................................................... 16
9.6.1 Kazi za Meneja zitakuwa ni; .................................................................................................... 16
SEHEMU YA KUMI .............................................................................................................................. 16
10 TARATIBU ZA UWEKAJI WA HISA, AKIBA, AMANA NA UTOAJI MIKOPO ............. 16
SEHEMU YA KUMI NA MOJA ........................................................................................................... 16
11 MGAO WA ZIADA .................................................................................................................... 16
SEHEMU YA KUMI NA MBILI .......................................................................................................... 17
12 UHASIBU .................................................................................................................................... 17
v
SEHEMU YA KUMI NA TATU ........................................................................................................... 17
13 KUHIFADHI AKIBA NA FEDHA NYINGINE ZA CHAMA ................................................ 17
SEHEMU YA KUMI NA NNE .............................................................................................................. 17
14 MAHUSIANO NA ASASI ZINGINE ZA KIFEDHA NA MITANDAO ................................ 17
SEHEMU YA KUMI NA TANO ........................................................................................................... 18
15 KUFUTWA KWA CHAMA ...................................................................................................... 18
SEHEMU YA KUMI NA SITA ............................................................................................................. 18
16 MENGINEYO ............................................................................................................................. 18
1
Utangulizi
Mamlaka ya Kutengeneza Masharti ya Chama
Masharti haya yametengenezwa na wanachama wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo
Wazalendo (Wazalendo SACCOS Ltd) kwa mamlaka ya kisheria chini ya kifungu cha 45 cha
Sheria ya Vyama vya Ushirika ya mwaka 2003 na Kanuni namba 9 ya Kanuni za Vyama vya
Ushirika ya mwaka 2004.
SEHEMU YA KWANZA
1 TAFSIRI
1.1 Akiba
Kiasi cha fedha ambacho mwanachama atakitumia kama kigezo cha kukopa.
1.2 Amana
Kiasi cha fedha za aina ya akiba ya mlaji ambayo hakitumiki kukopeshea bali ni kama akaunti ya
akiba benki ambapo wakati wowote mwanachama ataweka na kuchukua fedha kiasi chochote.
1.3 Bodi
Chombo kilichopewa dhamana ya uongozi na Mkutano Mkuu wa wanachama kusimamia, kwa
niaba ya Wanachama shughuli zote za uendeshaji na utoaji huduma za kifedha kwa Wanachama.
1.4 Chama
Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo Wazalendo (Wazalendo Savings and Credit
Coooperative Society Ltd) ambao ni muungano wa hiari wa watumishi wa Chuo Kikuu Kishiriki
cha Ushirika na Biashara (MUCCoBS) wenye nia ya kusaidiana na kuweza kutatua matatizo ya
kijamii na kiuchumi.
1.5 Huduma za kifedha
Huduma za kifedha za Akiba, Amana, Hisa, Mikopo na majanga.
1.6 Kamati ya Usimamizi
Chombo kilichopewa dhamana na Mkutano Mkuu, ya kukagua shughuli zote za uendeshaji wa
Chama na kutoa ushauri katika Mkutano Mkuu.
1.7 Kanuni za Sheria ya Ushirika
Kanuni za Vyama vya Ushirika za mwaka 2004.
1.8 Masharti
Kanuni na misingi inayoongoza mahusiano baina ya Chama , Wanachama, na Wadau wengine
kwenye sekta ya Ushirika na sekta ya Fedha kulingana na maelekezo ya Sheria ya Vyama vya
Ushirika Namba 20 ya mwaka 2003 pamoja na Kanuni za Vyama vya Ushirika za mwaka 2004.
1.9 Mikopo
Kiwango cha fedha ambacho mwanachama anachoweza kupata kutokana na akiba alizonazo kwa
kuzingatia sera ya mikopo na Kanuni za Ushirika.
2
1.10 Mkutano Mkuu
Chombo cha juu chenye dhamana ya kufanya maamuzi yote yahusuyo shughuli za utoaji
huduma za kifedha za Chama.
1.11 Mwanachama
Mtu yeyote anayemiliki Hisa katika Chama na mwenye dhamana ya kutoa maamuzi ya namna
bora ya kuendesha Chama.
1.12 Sera
Kanuni ndogondogo zinazotumika kufanikisha utekelezaji wa miongozo kama ilivyoanishwa
kwenye Masharti.
1.13 Sheria ya Ushirika
Sheria ya Vyama vya Ushirika ya mwaka 2003.
1.14 Watumishi
Watu walioajiriwa na Chama kwa mujibu wa sera ya utumishi ya Chama.
SEHEMU YA PILI
2 JINA NA MAELEZO MUHIMU YA CHAMA
(a) Jina la Chama ni: CHAMA CHA USHIRIKA WA AKIBA NA MIKOPO
WAZALENDO [WAZALENDO SACCOS LIMITED]
(b) Anwani ya Chama ni: S. L. P. 474, Barabara ya Sokoine, Moshi, Kilimanjaro Tanzania.
(c) Mfunganamo wa Uanachama ni Utumishi katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na
Biashara Moshi (MUCCoBS)
(d) Eneo la shughuli za Chama litakuwa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara
Moshi na Vituo vyake vilivyoko Mikoani. Makao Makuu ya Chama yatakuwa Chuo
Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara, Barabara ya Sokoine, Moshi, Kilimanjaro.
(e) Mwaka wa Fedha wa Chama utaanza JANUARI na kuishia DESEMBA yaani utaanzia
01/01 na kuishia 31/12 ya kila mwaka.
(f) Tarehe ya kuandikishwa: 22 Septemba, 1971 kwa Hati namba 2065.
(h) Shughuli Kuu za Chama ni kutoa Huduma za kifedha kwa wanachama ambazo ni:
(i) Huduma za Kifedha za Akiba na Amana
(ii) Huduma za Kifedha za Mikopo
(iii)Huduma za Kifedha za Bima ya Mikopo na Majanga
3
2.2 Dira ya Chama
Wazalendo SACCOS Ltd kuwa Asasi ya kifedha inayoendeshwa kwa njia shirikishi yenye
biashara pana na mfiko kwa wanachama kwa kuzingatia falsafa, kanuni na maadili ya Ushirika.
2.3 Maarubu/Mwelekeo
i. Kutumia fursa zilizopo kupanua vyanzo vya huduma za kifedha na kuhamasisha
wanachama kuweka hisa na akiba ili ziweze kujenga mtaji wa uhakika wa kuwahudumia
wanachama.
ii. Kuwahudumia wanachama kikamilifu na kwa uwazi na kukidhi mahitaji yao kwa wakati.
iii. Kujenga uhusiano bora miongoni mwa wanachama ndani ya Asasi na wanachama wa
vyama vingine vya Ushirika wa Akiba na Mikopo.
iv. Kuwa na uongozi bora na utawala mzuri wa fedha ili kujenga imani kwa wanachama.
v. Kujenga uwezo wa chama wa kifedha ili kumudu mahitaji ya kifedha kwa wanachama bila
kuwa tegemezi.
SEHEMU YA TATU
3 MADHUMUNI
3.1 Madhumuni Mahususi
Madhumuni mahususi ya Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo Wazalendo ni;
(a) Kuinua na kuimarisha hali ya kiuchumi na kijamii ya wanachama kwa kufuata Sheria,
Kanuni, Sera, na Taratibu za Vyama vya Ushirika.
(b) Kutafuta vyanzo vya fedha ili kujenga na kuimarisha Mtaji wa Chama kwa ajili ya kutoa
mikopo kwa Wanachama kwa masharti na riba nafuu.
3.2 Shughuli za Chama
Kufikia na kufanikisha madhumuni yake, Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo Wazalendo
kitafanya yafuatayo:-
(i) Kupokea na kuzihifadhi kwa usalama Hisa, Akiba na Amana kutoka kwa Wanachama.
(ii) Kuhamasisha wanachama kujenga tabia ya kujiwekea Akiba na Amana mara kwa mara.
(iii)Kuwapa Wanachama Elimu ya Ushirika itakayowajasirisha ili kuwajengea uwezo na
kuwawezesha kujenga tabia ya kukopa kwa busara, kutumia na kutunza vizuri fedha kwa
ajili ya kuinua hali zao za maisha ya kijamii na kiuchumi.
(iv) Kuwashauri Wanachama kuaandaa mipango yao ya maendeleo katika kuwekeza mitaji
kwenye miradi ya kiuchumi na huduma za kijamii.
(v) Kutafuta vyanzo vya fedha vya nje vyenye riba nafuu kwa kulinganisha na benki na isiwe
juu ya riba inayotozwa na Chama ili kuweza kumudu mahitaji ya mikopo ya wanachama
endapo vyanzo vya ndani ( makusanyo ya Hisa na Akiba kutoka kwa wanachama)
havitoshelezi kumudu mahitaji ya mikopo ya wanachama kwa wakati.
(vi) Kuanzisha huduma za kifedha za majanga zenye kuwawezesha wanachama kukabiliana
na majanga mbalimbali ya kijamii kwa njia shirikishi.
4
(vii) Kuweka usalama wa fedha za Chama na wanachama kwa kutumia huduma za bima za
fedha zinazofaa.
(viii) Kuanzisha na kuendeleza shughuli zozote za kiuchumi na kijamii kwa manufaa ya
Wanachama na Chama kama itakavyokubaliwa na Mkutano Mkuu na
kuidhinishwa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika.
SEHEMU YA NNE
4 UANACHAMA
4.1 Sifa za Mwanachama
Mtu yeyote anaweza kuwa Mwanachama akiwa na sifa zifuatazo:
(a) Awe mtumishi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Ushirika na Biashara Moshi (MUCCoBS)
au Taasisi inayofanyakazi katika eneo la Chama.
(b) Uanachama unaweza kuwa wa mtu binafsi au Taasisi zinazofanya kazi katika eneo la
Chama.
(c) Awe ametimiza umri wa miaka kumi na nane (18). Hata hivyo, mtu mwenye umri wa
miaka 15 anaweza kuwa mwanachama isipokuwa hataruhusiwa kugombea nafasi
yoyote ya uongozi au kukopa mpaka atakapotimiza umri wa miaka kumi na nane (18).
(d) Awe na akili timamu na tabia njema.
(e) Awe tayari kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za Chama.
(f) Asiwe na shughuli binafsi za kiuchumi na kijamii zinazofanana na shughuli za Chama.
4.2 Kujiunga Uanachama
Masharti ya kujiunga na Chama ni haya yafuatavyo:-
(a) Mtu anayetaka kuwa mwanachama atajaza fomu ya maombi ya uanachama na kuiwasilisha
katika ofisi ya Chama.
(b) Ombi litajadiliwa na Bodi na kutolewa pendekezo la kukubaliwa au kukataliwa
kutegemeana na sifa zilizotajwa katika masharti haya na kwa mujibu wa Sheria ya
Ushirika, Kanuni za Ushirika. Mkutano Mkuu pia utaidhinisha wale wote
waliopendekezwa kuwa Wanachama.
(c) Mwombaji atakapokubaliwa na Bodi atatakiwa kulipa kiiingilio, Hisa na akiba. Baada ya
kupokelewa na Mkutano Mkuu atatakiwa kutia saini yake au kuweka dole gumba katika
Daftari la Wanachama, mbele ya wajumbe wawili wa Bodi na atapewa kitambulisho cha
uanachama.
(d) Mwanachama atakapojiunga na Chama atalipa Kiingilio cha shilingi elfu ishirini tu
(20,000/=), Hisa kumi (10) zenye thamani ya shilingi elfu kumi (10,000/=) kila moja.
(e) Meneja wa Chama atarudisha kiingilio na Hisa zote zilizopokelewa kutoka kwa waombaji
waliokataliwa uanachama na Mkutano Mkuu. Ada ya fomu ya maombi ya uanachama
haitarudishwa.
(f) Mwanachama aliyekamilisha kulipia Hisa zote atapewa hati ya kumiliki Hisa. Kiwango
cha chini cha umiliki wa hisa ni kama ilivyoainishwa katika sera ya Hisa, Akiba na Amana.
(g) Mwanachama atamteua mrithi wake ambaye atakuwa na haki ya kulipwa hisa na faida
zozote za Chama baada ya kufariki. Mrithi yeyote hatakuwa mwanachama moja kwa moja
isipokuwa baada ya kutuma maombi na kukubaliwa na chama kulingana na Masharti haya.
5
Mwanachama atakuwa na haki ya kubadilisha jina la mrithi. Kila uteuzi wa mrithi
utaandikwa katika daftari ya wanachama na utatiwa saini na mwanachama.
(h) Chama kitakuwa na daftari la uanachama lenye maelezo muhimu ya kila mwanachama.
4.3 Kusimamishwa au Kuachishwa Uanachama
Mwanachama anaweza kuachishwa au kusimamishwa uanachama kwa ajili ya:
(a) Kukutwa na hatia ya kosa la jinai linalohusisha kutokuwa mwaminifu au kuhukumiwa
kifungo.
(b) Kushindwa kulipa kiasi chochote cha fedha kwa Chama katika muda ulioruhusiwa pasipo
kuwa na sababu yoyote inayokubalika na wajumbe wa Bodi.
(c) Kufanya kitendo chochote ambacho Wajumbe wa Bodi na Mkutano Mkuu wataridhia
kuwa ni cha kutokuwa mwaminifu au ambacho ni kinyume na madhumuni au malengo
ya Chama.
(d) Kwa sababu nyingine yoyote iliyoainishwa katika kifungu cha 26(1) cha Kanuni za
Ushirika.
4.4 Ukomo wa Uanachama
Uanachama utakoma kutokana na sababu mojawapo kati ya hizi zifuatazo;
(a) Kifo
(b) Kichaa kilichothibitishwa na Daktari.
(c) Kuacha kuwa na Hisa kwa mujibu wa masharti haya.
(d) Kujiuzulu baada ya kutoa taarifa ya siku sitini (60) ya maandishi kwa Bodi ya Chama.
(e) Kutenda kosa lolote ambalo limetajwa katika Sheria ya Ushirika na Kanuni za Ushirika.
(f) Kufukuzwa na wanachama katika Mkutano Mkuu kwa idadi ya wanachama wasiopungua
theluthi mbili (2/3) ya waliohudhuria na kupiga kura baada ya kupewa nafasi ya kujitetea.
(g) kutoshiriki katika shughuli za Chama kwa muda wa miaka mitatu.
(h) Kuhama katika eneo la shughuli za Chama.
(i) Kuthibitika kuwa amefilisika.
Hata hivyo:
(i) Mwanachama aliyejiuzulu au kufukuzwa uanachama atalipwa haki zake zote baada ya
kuthibitika kwa haki hizo katika kipindi kisichozidi siku tisini (90) kuanzia siku ya
kukoma uanachama.
(ii) Mwanachama hatahamisha Hisa zake ila kwa chama au kwa mwanachama au kwa mtu
ambaye maombi yake ya uanachama yamekubaliwa na Bodi au kama Hisa zake
zimekuwa katika chama kwa muda usiopungua miaka mitano.
(iii)Mwanachama aliyejiuzulu/aliyefukuzwa anaweza kukubaliwa na kupokelewa tena
kujiunga na Chama baada ya kulipa madeni yote aliyokuwa anadaiwa wakati anakoma
kuwa mwanachama na kutuma maombi kwa kufuata masharti haya.
4.5 Wajibu na Haki ya Mwanachama
Mwanachama yeyote atakuwa na wajibu na haki kama ifuatavyo:
6
4.5.1 Wajibu wa Mwanachama
Ufuatazo utakuwa wajibu wa mwanachama
(a) Kubeba dhamana ikiwa janga lolote litatokea.
(b) Kulipa madeni yake kwa wakati uliopangwa.
(c) Kulipa mkopo alioudhamini endapo mdhaminiwa/mkopaji atashindwa kulipa mkopo
wake.
(d) Kuwa na angalau kiwango cha chini cha amana na hisa kwa mujibu wa Masharti na Sera.
(e) Kuweka Hisa na Akiba mara kwa mara ili kujenga uwezo wa kimtaji wa Chama.
(f) Kushiriki kikamilifu katika shughuli za Chama na kuhudhuria mikutano yote
inayohusika.
(g) Kushiriki katika kutoa uamuzi wa mambo mbalimbali katika Mikutano Mikuu.
(h) Kufuata Sheria na Kanuni za Ushirika, Masharti na Sera za Chama na maamuzi ya
Mikutano Mikuu.
(i) Kutoa michango mbalimbali katika kuendeleza madhumuni ya Chama.
(j) Mwanachama atakuwa na wajibu mwingine wowote kama ulivyoainishwa katika Kanuni
ya 18 ya Kanuni za Ushirka.
4.5.2 Haki za Mwanachama
Zifuatazo zitakuwa haki za mwanachama.
(a) Kushiriki katika shughuli zote za Chama kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa.
(b) Kuhudhuria na kutoa maoni yake katika mikutano ya Chama.
(c) Kuchaguliwa kuwa mjumbe/kiongozi na kuchagua wajumbe/viongozi wa Chama.
(d) Kupiga kura chini ya misingi ya mtu mmoja kura moja bila kujali idadi ya hisa anazo
miliki.
(e) Kuwa na haki sawa kuhusu mali ya chama na kudhibiti ipasavyo matumizi yake.
(f) Kuweka na kutoa amana, akiba na hisa zake kwa kufuata kanuni za Chama.
(g) Kupewa kitabu cha mwanachama kinachoonyesha aina zote za huduma za kifedha
zinazotolewa na Chama.
(h) Kupatiwa mkopo kwa ajili ya kuongeza tija na maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
(i) Kupewa aina yoyote ya huduma ya kifedha ya mkopo wakati wowote kwa kuzingatia
misingi na taratibu kama zilivyoanishwa kwenye sera ya mikopo ya Chama.
(j) Kuwa mdhamini wa mkopo wa mwanachama mwingine kwa kuzingatia sera ya mikopo
(k) Kukagua masharti, mizania, mihtasari ya Mikutano Mikuu na nyaraka nyingine za
Chama wakati wowote wa saa za kazi.
(l) Kuitisha Mikutano Mikuu ya wanachama kwa mujibu wa Masharti haya na kwa
kuzingatia Sheria na Kanuni za Ushirika.
(m) Kuchagua mrithi anayemtaka.
(n) Kupewa hati ya hisa baada ya kumaliza kulipia hisa zake.
7
(o) Kusikilizwa.
(p) Kujulishwa mambo yote yahusuyo mwenendo wa Chama.
(q) Kujua mapato na faida/hasara iliyopatikana kutokana na shughuli za Chama.
(r) Kushiriki katika kufanya marekebisho ya Masharti na Sera za Chama.
(s) Kujitoa uanachama kwa kufuata taratibu za kisheria.
(t) Kuanzisha uchunguzi wa mwenendo wa Chama.
(u) Kukata rufaa.
SEHEMU YA TANO
5 HISA ZA WANACHAMA
(a) Kila hisa moja itakuwa na thamani kama ilivyoainishwa kwenye Sera ya Hisa, Akiba
na Amana.
(b) Hakuna mwanachama atakayeruhusiwa kuwa na hisa zaidi ya moja ya tano (1/5) ya
hisa zote za Chama kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika.
(c) Kwa mujibu wa Kanuni ya Ushirika, mwanachama anayetaka kuchukua hisa zake zote,
atatakiwa kutoa taarifa ya maandishi ya siku sitini (60).
(d) Mwanachama hataruhusiwa kuchukua wala kupunguza hisa zake hadi atakapokoma
kuwa mwanachama.
SEHEMU YA SITA
6 MTAJI WA CHAMA
Mtaji wa chama utatokana na:-
(a) Hisa za wanachama.
(b) Tengo la Ziada halisi.
(c) Akiba ya lazima na malimbikizo mengine.
(d) Akiba inayobakizwa.
(e) Michango maalum, ruzuku, na misaada.
SEHEMU YA SABA
7 FEDHA NA MALI ZA CHAMA
Fedha na Mali za Chama zitajumuisha yafuatayo:-
(a) Hisa za Uanachama.
(b) Viingilio, ruzuku na misaada.
(c) Ada ya maombi ya uanachama.
8
(d) Riba juu ya Mikopo ya Wanachama.
(e) Ziada halisi kutokana na shughuli na miradi ya kiuchumi ya Chama.
(f) Nafuu za Kibiashara.
(g) Fedha ya Akiba ya lazima na Malimbikizo.
(h) Fedha ya huduma za Bima ya Mikopo na Majanga.
(i) Asilimia kumi ya Akiba zote kwa kila mwaka.
(j) Mikopo kutoka Mabenki na Taasisi zinazotambulika, baada ya kupata idhini ya Mkutano
Mkuu na Mrajis wa Vyama vya Ushirika. Hata hivyo, kiasi kitakachokopwa hakitazidi
nusu (1/2) ya rasilimali ya Chama.
(k) Mapato mengineyo na yasiyotarajiwa.
(l) Fedha Taslimu na Fedha Benki.
(m) Mawekezo katika Taasisi za Kibiashara.
(n) Vifaa na zana zote zinazohusiana na shughuli za chama.
(o) Majengo na mali zingine za Chama kama zilivyoanishwa kwenye mizania ya chama.
SEHEMU YA NANE
8 DHIMA YA MWANACHAMA
Dhima za chama zitakuwa kama ifuatavyo:-
(a) Dhima ya mwanachama kwa ajili ya madeni ya Chama haitazidi kiwango cha hisa
anazopaswa kulipia katika Chama.
(b) Dhima ya mwanachama aliyeacha uanachama kwa madeni ya Chama yaliyokuwepo
wakati wa kuacha uanachama itaendelea kwa muda wa miaka mitatu (3) baada ya kuacha
uanachama.
SEHEMU YA TISA
9 UONGOZI NA USIMAMIZI WA CHAMA
Mikutano Mikuu ya Wanachama
Mikutano hii itajuimuisha; Mkutano Mkuu wa Mwaka, Mkutano Mkuu wa Kawaida na Mkutano
Mkuu Maalum.
9.1 Vyombo vya Maamuzi
Chama kitakuwa na vyombo mbalimbali vya maamuzi kama ifuatavyo;
a) Mikutano Mikuu ya Wanachama
b) Bodi ya Uongozi
c) Kamati ya Usimamizi
d) Kamati ya Mikopo
e) Menejimenti
9
Mchoro ufuatao unaonesha uhusiano wa vyombo vya maamuzi katika Chama
MKUTANO MKUU
KAMATI YA USIMAMIZI
BODI
KAMATI YA MIKOPO
MENEJA
9.1.1 Mkutano Mkuu wa Mwaka
(a) Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama utafanyika kila mwaka katika kipindi kisichozidi
miezi tisa (9) baada ya kufunga hesabu za mwaka za Chama. Hata hivyo Mkutano huu
unaweza kufanyika baada ya kipindi cha miezi tisa (9) kwa idhini ya Mrajis.
(b) Shughuli zitazofanyika katika Mkutano Mkuu wa Mwaka ni pamoja na;
(i) Kupokea na Kusoma na kuthibitisha mambo ya Mkutano Mkuu uliopita na
yatokanayo.
(ii) Kujadili Taarifa ya hesabu za mwaka na taarifa ya ukaguzi.
(iii) Kupokea na kujadili makisio ya mapato na matumizi kwa mwaka.
(iv) Kupokea na kujadili Taarifa ya Bodi na Kamati ya Usimamizi
(v) Kujadili namna ya kugawana ziada kwa kuzingatia Masharti ya Chama, Sheria
na Kanuni za Ushirika.
(vi) Kuidhinisha ununuzi au uuzaji wa mali za Chama.
(vii) Kuamua kiwango cha honoraria kwa ajili ya Wajumbe wa Bodi.
(viii) Kuidhinisha kiwango cha riba na faida juu ya akiba, hisa na amana.
(ix) Kuidhinisha idadi ya hisa na thamani ya hisa moja.
(x) Kuidhinisha Mpango Mkakati na Mpango wa Biashara wa Chama na program ya
utekelezaji.
(xi) Kujadili na kuidhinisha marekebisho katika Masharti na Sera kwa mujibu wa
Sheria ya Ushirika.
(xii) Kuzungumzia mambo mengine yanayohusu maendeleo ya Chama kwa ujumla
na kutoa maelekezo ya utekelezaji kwa Wajumbe Bodi.
9.1.2 Mkutano Mkuu wa Kawaida
a) Mkutano Mkuu ya kawaida unaweza kufanyika angalau mara moja kwa mwaka
ambapo utafanyika wakati wowote katika mwaka wa fedha wa Chama.
10
b) Shughuli zitazofanyika katika Mkutano Mkuu wa Kawaida ni pamoja na;
(i) Kusoma na kuthibitisha muhtasari wa mkutano uliopita na yatokanayo.
(ii) Kupokea na kujadili taarifa za maendeleo ya utekelezaji kutoka Bodi na
Kamati ya Usimamizi.
(iii) Kuamua idadi ya wajumbe Bodi.
(iv) Kuthibitisha makisio ya mapato na matumizi ya mwaka unaofuata.
(v) Kuthibitisha kuingizwa na kufukuzwa kwa wanachama.
(vi) Kuweka ukomo wa madeni kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika.
(vii) Kuchagua, kuwasimamisha au kuwafukuza wajumbe wa Bodi.
(viii) Kuchagua wajumbe wa kuwakilisha chama katika vyama na taasisi nyingine
zinazohusika na maendeleo ya Chama.
(ix) Kuidhinisha makubaliano na mikataba.
(x) Kuzungumzia mambo yote yanayohusu maendeleo ya chama kwa jumla na
kutoa maelekezo ya utekelezaji kwa Bodi.
Hata hivyo shughuli zitakazofanyika katika Mkutano huu zinaweza zikafanyika katika Mkutano
Mkuu wa Mwaka.
9.1.3 Mkutano Mkuu Maalum
(a) Mkutano Mkuu Maalum utafanyika pale ambapo theluthi moja (1/3) ya wanachama
itaonesha nia ya kutaka kuitishwa kwa mkutano huo, kwa maandishi na kutuma nakala
kwa Mrajisi wa Vyama vya Ushirika. Hata hivyo huo ni lazima uwe na agenda moja (1)
tu.
(b) Mkutano Mkuu Maalum unaweza kuitishwa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika au mtu
aliyepewa mamlaka naye. Mkutano huo utakuwa na nguvu sawa na mikutano mingine ya
Chama iliyoitishwa kwa mujibu wa Masharti ya Chama.
(c) Bodi inaweza kuitisha Mkutano Mkuu Maalum kujadili jambo la dharura ikiwemo
kujadili Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu ili kuwapa fursa Wanachama kujadili kwa undani
na kuchambua vizuri taarifa za ukaguzi kwa mwaka husika wa fedha.
9.2 Taratibu za Kuitisha Mkutano Mkuu
(a) Matangazo ya mikutano yatabandikwa katika ofisi ya chama na kwenye mbao za
matangazo za eneo la Chama.
(b) Tangazo hilo ni lazima lioneshe wazi tarehe ya mkutano, mahali pa mkutano, saa na
jambo/mambo yatakayozungumzwa.
(c) Muda wa matangazo ya mkutano:
i. Mkutano Mkuu wa mwaka si chini ya siku 21.
ii. Mkutano Mkuu wa kawaida si chini ya siku 21.
iii. Mkutano Mkuu Maalum si chini ya siku 7.
(d) Mahudhurio katika mikutano ya Chama ni lazima kuwa zaidi ya nusu (½) ya wanachama
wote au wanachama mia moja (100).
11
(e) Kwa Mkutano Mkuu Maalum ulioitishwa na Mrajis au Afisa aliyeteuliwa na Mrajis,
utafanyika kwa idadi yoyote ya wanachama waliohudhuria na yote yatakayopitishwa
yatakuwa ni halali na yatawabana wanachama wote.
(f) Kwa Mikutano Mikuu ya mwaka na kawaida ikiwa mahudhurio hayotoshi baada ya saa
moja na nusu ya saa zilizopangwa, Mkutano utaahirishwa kwa siku saba (7), na Mkutano
utakaofuata mambo yatakayozungumzwa ni yale yale ya Mkutano ulioahirishwa. Iwapo
mahudhurio hayatoshi tena Mkutano huo utafutwa.
(g) Kwa Mkutano Mkuu Maalum ulioitishwa na wanachama, Mkutano utafutwa kabisa
iwapo mahudhurio hayatatosha baada ya kupita saa moja nusu.
(h) Mwenyekiti wa Bodi ataendesha mikutano yote isipokuwa ule Mkutano Mkuu Maalum
ulioitishwa na Mrajis ambapo Mrajis au mtu yeyote atakayemteua atakuwa Mwenyekiti.
(i) Iwapo Mwenyekiti hayupo, Makamu wake atendelesha Mkutano Mkuu wa Mwaka au
wa Kawaida. Iwapo wote hawapo kwa muda wa dakika 30, mwanachama yeyote katika
waliohudhuria tachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa muda na ataongoza Mkutano huo.
(j) Hata hivyo uitishwaji wa Mikutano Mikuu itazingatia Sheria na Kanuni za Ushirika.
9.3 Bodi ya Uongozi
Bodi ya Chama itakuwa na uwezo wa kusimamia Chama kwa mujibu wa Sheria na kanuni za
Ushirika, Masharti na Sera za Chama.
Kutakuwa na Wajumbe wa Bodi saba (7) ambao watachaguliwa na Mkutano Mkuu baada ya
kujaza fomu za maombi kwa kuzingatia taratibu zilizoanishwa kwenye Sheria na Kanuni za
Ushirika.
Hakuna mjumbe wa Bodi atakaye kuwa na haki ya kudai malipo ya mshahara au posho
isipokuwa kama ilivyoelekezwa katika masharti haya na kupata idhini ya Mkutano Mkuu.
Wajumbe wa Bodi hii watashika madaraka kwa muda wa miaka mitatu (3) na ataweza
kuchaguliwa tena kwa kipindi kipindi kimoja (1) cha miaka mitatu. Mjumbe
atakayechaguliwa kushika nafasi ya mjumbe aliyeondolewa, aliyefariki au kujihuzuru
atashika madaraka kwa kipindi kilichobaki cha mjumbe huyo.
9.3.1 Sifa za Wajumbe wa Bodi
Mjumbe wa Bodi anatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:
(i) Awe na elimu ya kutosha angalau astashahada inayotambulika na mamlaka za elimu
nchini ili kumwezesha kusimamia shughuli za chama kikamilifu.
(ii) Awe mwadilifu na mwaminifu.
(iii) Awe na uwezo wa kuongoza.
(iv) Awe amelipa hisa chamani kwa mujibu wa Masharti haya.
(v) Awe hajawahi kupoteza sifa za uongozi katika ngazi yoyote ya Chama cha Ushirika.
(vi) Awe hajawahi kuwa mjumbe wa Bodi iliyoshindwa kusimamia vizuri shughuli za
Chama na kikapata hasara.
(vii) Awe anashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Chama.
(viii) Awe hajawahi kusababisha hasara katika chama chochote cha Ushirika.
(ix) Asiwe na deni alilolipata nje ya utaratibu.
(x) Asiwe na tabia ya kulaza madeni.
12
9.3.2 Majukumu ya Bodi
Bodi hii itakuwa na wajibu wa kufanya mambo yafuatayo:
(a) Kusimamia shughuli zote za kiuchumi za Chama na kuhakikisha kuwa zinaendeshwa
ipasavyo.
(b) Kutekeleza kikamilifu maazimio na maelekezo ya mikutano mikuu.
(c) Kutunza hesabu za Chama kwa usahihi.
(d) Kutunza kwa usahihi daftari la wanachama na kumbukumbu za mihtasari ya
Mikutano Mikuu na Mikutano ya Bodi.
(e) Kuhakikisha kuwa lakiri ya chama inakuwepo na inatumika ipasavyo
(f) Kuchukua uamuzi ikingojea uithibitisho wa Mkutano Mkuu, juu ya kupokelewa
wanachama wapya, kujiuzulu wanachama na kusimamishwa kwa wajumbe wa Bodi.
(g) Kubuni na kutayarisha Sera na kanuni za Uendeshaji chama zinazohusu fedha,
biashara, utawala, mikopo na bohari ili kufanikisha madhumuni ya Chama.
(h) Kuwasilisha kwenye Mkutano Mkuu wa wanachama taarifa ya hali ya uchumi na
maendeleo ya Chama pamoja na hesabu ya mapato na matumizi, mizania
iliyothibitishwa kwa mwaka uliopita na makisio ya mapato na matumizi kwa mwaka
unaofuata.
(i) Kupokea na kujadili taarifa za Kamati ya Mikopo na kamati ya Usimamizi..
(j) Kupitia na kujadili maombi ya mikopo kutoka kwa Wajumbe wa Bodi, wajumbe wa
Kamati ya Mikopo na wajumbe wa Kamati ya Usimamizi.
(k) Kuteua mwanachama atakayeshika nafasi iliyoachwa wazi katika Kamati ya Mikopo.
(l) Kumwezesha mtu aliyeidhinishwa kukagua vitabu vya Chama na kuhakikisha kuwa
hatua zinachukuliwa kutokana na taarifa ya ukaguzi.
(m) Kuhakikisha kuwa wanachama wanafuata na kuzingatia Sheria na Kanuni za
Ushirika, masharti ya Chama, Sera, mikataba na taratibu mbalimbali za Chama.
(n) Kufungua akaunti Benki na kuhakikisha kuwa fedha zote za Chama zinatunzwa
katika Benki.
(o) Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa mpango mkakati na mpango wa biashara wa
Chama.
(p) Kuhakikisha kwamba Chama kinawakilishwa katika mashitaka yoyote.
(q) Kuhakikisha kuwa mali, bidhaa, vifaa na nyaraka/Hati za Chama zinahifadhiwa vizuri
na kwa usalama.
(r) Kuamua idadi, uwezo na sifa za watu ambao wanaweza kuajiriwa kuendesha shughuli
za Chama.
(s) Kuteua wajumbe watakaotia saini kwenye hundi za Chama.
(t) Kuajiri kwa niaba ya wanachama Meneja/Katibu, Mhasibu au watumishi wengine
ambao wataendesha shughuli za kila siku za Chama.
(u) Kuingia mikataba mbalimbali kwa niaba ya Chama baada ya kupata idhini ya
Mkutano Mkuu na Mrajis.
(v) Kuhakikisha kuwa wakopaji wanalipa madeni yao kama walivyoahidi, kuwachukulia
hatua za kisheria wakopaji wasio waaminifu na kupendekeza kwa Mkutano Mkuu
ufutaji wa mikopo mibaya ambayo haiwezi kulipwa kabisa.
(w) Kupendekeza kwenye Mkutano Mkuu mabadiliko au viwango vya riba au masharti
ya ulipaji mikopo na/au mgawanyo wa mikopo.
13
(x) Kuandaa mapendekezo ya marekebisho ya Masharti ya Chama pale itakapobidi na
kuwasilisha kwenye Mkutano Mkuu.
(y) Kutekeleza majukumu mengine ya Bodi ni pamoja na;
(i) Kuandikisha mikataba yote ya kibiashara kwa Mrajis wa Vyama vya Ushirika.
(ii) Kuchunguza mara kwa mara shughuli za Chama kwa kumtaka Meneja/Katibu
atoe taarifa ya matokeo ya uendeshaji wa shughuli za Chama.
(iii)Kutayarisha/kuchapisha Hati za kumiliki hisa kwa ajili ya wanachama.
(iv) Kufanya mambo mengine yote ambayo yataoneakana ni lazima katika
kutimiza Sheria na Kanuni za Ushirika, Masharti na Sera za Chama.
9.3.3 Majukumu ya Mwenyekiti wa Bodi
Mwenyekiti wa Bodi atakuwa na kazi zifuatazo:-
(a) Kuongoza Mikutano Mikuu yote isipokuwa Mkutano Mkuu maalum ulioitishwa na
Mrajis.
(b) Kuongoza mikutano yote ya Bodi ya Chama.
(c) Kuitisha Mikutano Mikuu yote na ya Bodi kwa mujibu wa Masharti haya.
(d) Kuweka saini kumbukumbu za Mikutano Mikuu na Mikutano ya Bodi ambayo
ameiongoza.
(e) Kuweka saini kwa niaba ya chama kumbukumbu zote ikiwa ni pamoja na zinazohitaji
kuwekwa lakiri na/au muhuri wa Chama.
(f) Kuwa msemaji Mkuu wa Chama, kama haitaamriwa vinginevyo na Bodi au Mkutano
Mkuu wa wanachama.
9.3.4 Majukumu ya Makamu Mwenyekiti wa Bodi
Makamu Mwenyekiti atafanya kazi zote za Mwenyekiti wakati Mwenyekiti hayupo.
9.3.5 Mikutano ya Bodi
(a) Mikutano ya Bodi itaitishwa na mwenyekiti wa Chama kwa kushauriana na Meneja.
(b) Bodi itapaswa kufanya mikutano angalau minne (4) kwa mwaka. Mahudhurio ya zaidi
ya nusu yatahitajika ili kuendesha Mkutano. Iwapo Mwenyekiti na Makamu
Mwenyekiti hawapo, kikao kitachagua mwenyekiti wa muda miongoni mwa wajumbe
waliopo.
(c) Kila mjumbe wa Bodi atakuwa na kura moja. Iwapo kura zitalingana, Mwenyekiti
atakuwa na kura ya ziada.
(d) Mambo yote yaliyozungumzwa katika mkutano yataandikwa ndani ya kitabu cha mambo
ya mikutano ya Bodi na kuwekwa saini na Mwenyekiti na Meneja/Katibu.
9.3.6 Kuacha au Kusimamishwa ujumbe wa Bodi
(a) Mjumbe wa Bodi ataacha madaraka kwa sababu yoyote kama zilivyoainishwa katika
Kanuni za ushirika.
(b) Mjumbe wa Bodi atakayeshindwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo bila sababu
inayokubalika anaweza kusimamishwa Uongozi hadi Mkutano Mkuu utakaofuata.
14
9.4 Kamati ya Usimamizi
(a) Kutakuwepo na Kamati ya Usimamizi ya watu watatu nje ya wajumbe wa Bodi.
(b) Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi watachaguliwa na Mkutano Mkuu.
(c) Mjumbe yeyote wa Bodi au mtumishi yeyote wa Chama hatastahili kuchaguliwa kuwa
mjumbe wa kamati hii.
(d) Wajumbe wa Kamati hii watashika madaraka kwa muda wa miaka tisa (9), na theluthi
moja (1/3) ya wajumbe wataondolewa kila baada ya miaka mitatu.
(e) Wajumbe wa Kamati hii watatengeneza utaratibu wa kutekeleza kazi zao, pia watachagua
mwenyekiti na mwandishi/katibu miongoni mwao. Mwandishi/katibu atatengeneza na
kuhifadhi kumbukumbu zote pamoja na hatua zinazochukuliwa na kamati hii.
9.4.1 Sifa za Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi
Zifuatazo ni sifa za Mjumbe wa Kamati ya Usimamizi.
(a) Awe na elimu angalau stashahada ya kumuwezesha kusimamia shughuli za chama kwa
ufanisi. Angalau wajumbe wawili (2) wawe na uelewa wa utunzaji wa vitabu vya hesabu
au wa uhasibu au ukaguzi na uongozi/usimamizi wa fedha na sheria.
(b) Awe mwadilifu na mwaminifu.
(c) Awe na uwezo wa kuongoza.
(d) Awe amelipa hisa chamani kwa mujibu wa Masharti ya Chama.
(e) Awe hajawahi kupoteza sifa za uongozi katika ngazi yoyote ya chama cha Ushirika.
(f) Awe hajawahi kuwa mjumbe wa Bodi iliyoshindwa kusimamia vizuri shughuli za
Chama na kikapata hasara.
(g) Awe anashiriki kikamilifu katika shughuli zote za Chama.
(h) Awe hajawahi kusababisha hasara katika chama chochote cha Ushirika.
(i) Asiwe na deni alilolipata nje ya utaratibu.
(j) Asiwe na tabia ya kulaza madeni.
9.4.2 Majukumu ya Kamati ya Usimamizi
Yafuatayo ni majukumu ya Kamati ya Usimamizi:-
(a) Kusimamia fedha na mali zote za Chama kwa niaba ya wanachama.
(b) Kusababisha kufanyika japo mara moja katika miezi mitatu (3), uchunguzi wa
shughuli za Chama pamoja na ukaguzi wa vitabu na kutengeneza au kuamuru
utengenezaji wa taarifa itakayotolewa katika Mkutano Mkuu kwa maandishi.
(c) Kufuatilia maendeleo ya miradi mikubwa ambayo imepatiwa mkopo na Chama
mpaka wahusika wanapomaliza marejesho.
(d) Kutayarisha taarifa ya maandishi juu ya hali ya fedha na huduma zitolewazo kwa
wanachama na kuiwasilisha kwenye Mkutano Mkuu, na nakala kutumwa kwa Afisa
Ushirika wa Wilaya na Mrajis Msaidizi kila baada ya miezi mitatu (3).
(e) Kusimamia ukaguzi wa ndani na kupokea taarifa ya mkaguzi wa ndani
atakapoteuliwa.
(f) Kusikiliza malalamiko ya wanachama na kuyatafutia ufumbuzi kwa kushirikiana na
Bodi.
9.4.3 Kamati ya Mikopo
(a) Kamati itaundwa na wajumbe kati ya wajumbe wa Bodi.
15
(b) Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi hawatakuwa wajumbe wa kamati ya
mikopo.
(c) Kamati itakuwa na wajumbe watatu (3).
(d) Kamati itafanya mkutano angalau mmoja kila mwezi, lakini inaweza kufanya mkutano
wa dharura wakati wowote. Mkutano utaweza kuendeshwa endapo theluthi mbili (2/3)
ya wajumbe wa kamati watahudhuria. Taarifa ya mikopo itatolewa kwa wanachama
katika mikutano mikuu.
9.4.4 Sifa za Wajumbe wa Kamati ya Mikopo
Mbali na sifa zilizotajwa katika nafasi ya ujumbe wa Bodi, angalau mjumbe mmoja (1) wa
kamati hii awe na elimu ya fedha na shughuli za kibenki.
9.4.5 Majukumu ya Wajumbe wa Kamati ya Mikopo
Majukumu ya Kamati ya Mikopo ni haya yafuatayo:-
(a) Kusimamia/kutekeleza sera za mikopo zilizopitishwa na mkutano Mkuu.
(b) Kupanga na kutekeleza shughuli zote za mikopo.
(c) Kupokea maombi ya mikopo, kuchambua na kutolea maamuzi.
(d) Kuhakiki shughuli/hesabu za wakopaji.
(e) Kufuatilia mikopo iliyopita muda wa kurejeshwa.
(f) Kushiriki katika ukusanyaji wa mikopo iliyocheleweshwa.
(g) Kutathmini shughuli zote za mikopo.
(h) Kutoa taarifa ya shughuli za mikopo kwa bodi na Mkutano Mkuu.
9.5 Wajumbe wa Uwakilishi
Kutakuwepo na wajumbe wawili (2) wa uwakilishi. Mjumbe mmoja (1) atatokana na wajumbe
wa Bodi na mmoja nje ya wajumbe wa Bodi (toka kwa wanachama).
9.5.1 Majukumu ya Mwakilishi wa Bodi
Majukumu ya mwakilishi wa Bodi ni haya yafuatayo:-
(a) Kuwakilisha Bodi kwenye masuala yote ya nje pale ambapo uwakilishi huu hauhitaji
Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti.
(b) Kutoa taarifa kwa Bodi juu ya yale yote yaliyofanyika anapokuwa kwenye uwakilishi.
(c) Kufanya ziara za mafunzo na kutoa ushauri kwa Bodi juu ya mambo ya kuboresha
Chama kinapotoa huduma za kifedha kwa wanachama.
9.5.2 Majukumu ya Mwakilishi wa Wanachama
Majukumu ya Mwakilishi wa wanachama ni haya yafuatayo:-
(a) Kutafuta habari kutoka kwa wanachama na kuzifanyia kazi ili zilete ufanisi wa kiutendaji
katika kutoa huduma za kifedha kwa wanachama.
(b) Kuwawakilisha wanachama kwenye masuala yote yanayohusu wanachama.
(c) Kuhudhuria vikao vya Bodi kama mjumbe aliyekaribishwa ili kuwasilisha hoja za
wanachama kadri anavyozipokea na kufuatilia utekelezaji wake.
(d) Kuhudhuria vikao vya Kamati ya Mikopo ili kushiriki na kuona kama hakuna
wanachama wanaopendelewa wakati wa kutoa mikopo.
16
(e) Kutoa taarifa katika Mkutano Mkuu juu ya hoja ambazo zitakuwa zimefanyiwa kazi na
ambazo hazijafanyiwa kazi.
9.6 Menejimenti/Meneja
Chama kitaajiri Meneja atakayewajibika kwa Bodi na ambaye atasimamia shughuli zote za
uendeshaji za kila siku kwa niaba ya Bodi.
9.6.1 Kazi za Meneja zitakuwa ni;
Zifuatazo ni kazi za meneja.
(i) Kulinda Ukwasi wa Chama kulingana na Vyanzo vya fedha na misingi ya fedha iliyopo.
(ii) Kuandaa na Kutekeleza Mpango Mkakati na Mpango wa Biashara wa Chama ili
kuwezesha Chama kutoa huduma bora za kifedha kwa wanachama.
(iii) Kuandaa makisio ya mapato na matumizi ya Chama na kuyawasilisha kwa Bodi na
Mkutano Mkuu kwa ili kuidhinishwa.
(iv) Kubuni, kuandaa na kuuza bidhaa za huduma za kifedha zinazokidhi mahitaji ya kifedha
ya wanachama.
(v) Kuhamasisha wanachama kuweka Hisa, Akiba na Amana pamoja na kutafuta fedha
kutoka vyanzo vya nje ili kuweza kumudu mahitaji ya mikopo kwa wanachama.
(vi) Kusimamia shughuli zote za kiuendeshaji na kiutawala za Chama.
(vii) Kuainisha na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya watumishi wengine
anaowasimamia
(viii) Kuandaa na kuwasilisha kwenye Bodi taarifa za uendeshaji kila mwezi, zinazohusu utoaji
huduma za kifedha kwa wanachama.
(ix) Kuhakikisha kuwa taarifa za hesabu za kila mwaka za Chama zinaandaliwa, kukaguliwa
na kuwasilishwa kwenye Mkutano Mkuu, kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria na
Kanuni za Ushirika.
(x) Kutoa tathmini ya kiutendaji wa ofisi kwenye Bodi kwa kipindi cha robo mwaka.
(xi) Kufuata kanuni zote za fedha na uendeshaji wa ofisi zenye kuzingatia utawala bora.
(xii) Kufanya kazi zingine kadri atakavyoelekezwa na Bodi.
SEHEMU YA KUMI
10 TARATIBU ZA UWEKAJI WA HISA, AKIBA, AMANA NA UTOAJI MIKOPO
Taratibu za uwekaji hisa, akiba, amana na utoaji wa mikopo utazingatia Sera ya Huduma za
Kifedha za Hisa, Akiba, na Amana, na Sera ya Mikopo.
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
11 MGAO WA ZIADA
(a) Kila mwaka chama kitatenga kiasi kisichopungua asilimia ishirini (20%) kutokana na
faida halisi kwa ajili ya akiba ya lazima ili kukiendeleza Chama. Akiba ya lazima
itabakia kuwa ni mali ya Chama na haitaweza kugawanywa isipokuwa kama kinavunjwa.
(b) Chama kitatenga asilimia kumi na tano (15%) kwa ajili ya mfuko wa kukombolea hisa,
za walioacha uanachama lakini kiasi hicho kisizidi asilimia kumi na tano (15%) ya hisa
zote.
17
(c) Asilimia kumi na tano (15%) ya faida halisi itatengwa kwa ajili ya kinga ya madeni
mabaya. Lakini kiasi hicho kisizidi asilimia kumi na tano (15%) ya madeni yote.
(d) Chama kitatenga asilimia kumi (10%) ya faida kwa ajili ya fungu la vitega uchumi.
(e) Bodi inaweza mara kwa mara kupendekeza katika Mkutano Mkuu kuongeza mifuko
mingine kwa ajili ya maendeleo ya baadaye ya Chama iwapo ina faida halisi ya kutosha.
(f) Ziada itakayobaki baada ya matengo ya kisheria kufanyika, itagawanywa kama
itakavyoamuliwa na Mkutano Mkuu wa wanachama na kwa mujibu wa Sheria na Kanuni
za Ushirika.
(g) Hisa zitakazostahili kulipwa ziada ni zile zilizokamilika na ambazo zilichangwa miezi
mitatu (3) kabla ya mwaka fedha unaohusika na ziada itakayogawanywa. Mkutano Mkuu
unaweza kuidhinisha wanachama warejeshewe sehemu ya faida juu ya mikopo yao. Hii
itafanyika kwa uwiano, kwa wakopaji ambao walitumia huduma ya mikopo kwa mwaka
huo.
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
12 UHASIBU
Chama kitafuata miongozi ya uandaji wa hesabu wa kimataifa na mfumo wa uhasibu
ulioidhinishwa na Mrajis wa Vyama vya Ushirika katika kutunza vitabu vya hesabu na
kumbukumbu zingine.
SEHEMU YA KUMI NA TATU
13 KUHIFADHI AKIBA NA FEDHA NYINGINE ZA CHAMA
(a) Fedha za Chama zitahifadhiwa katika benki na kuwekeza katika taasisi za kifedha
ikiwa ni pamoja na kununua dhamana za Serikali.
(b) Mahitaji ya mikopo ya wanachama yakishatoshelezwa fedha ambayo itazidi inaweza
kuwekwa benki katika akaunti za amana za muda maalum ili zipate faida kubwa.
(c) Fedha yote ya chama isipokuwa ile inayohitajika kwa matumizi madogo madogo
itahifadhiwa benki.
(d) Bodi inaweza kuruhusu Meneja awe na taslim kiasi kitakachoamuliwa na kuingizwa
katika masharti kwa ajili hiyo.
(e) Malipo yote yatafanyika kwa njia ya hundi.
SEHEMU YA KUMI NA NNE
14 MAHUSIANO NA ASASI ZINGINE ZA KIFEDHA NA MITANDAO
(a) Chama kinaweza kuwa na mtandao wa kutoa huduma za kifedha kwa wanachama wake kwa
kushirikiana na Asasi nyingine za kifedha na kuweza kunufaika na utaratibu wa
kukopeshana kwa Vyama vya Akiba na Mikopo vyenyewe kwa vyenyewe.
(b) Chama kinaweza kuridhia kuwa sehemu ya mtandao wa Asasi za kifedha baada ya kuridhika
kuwa mtandao huo ni wa manufaa kwa wanachama.
18
(c) Mahusiano haya yataandaliwa na kuchambuliwa na Kamati ya Usimamizi ili yasiathiri
shughuli za kifedha za chama na kuleta athari kwa wanachama.
SEHEMU YA KUMI NA TANO
15 KUFUTWA KWA CHAMA
(a) Chama kinaweza kufutwa kwa amri ya Mrajis wa Vyama vya Ushirika au kwa maombi
ya wanachama wasiopungua robo tatu (3/4) ya wanachama wote.
(b) Kufutwa kwa Chama kutafuata utaratibu wa kisheria uliowekwa katika Sheria na Kanuni
za Ushirika.
SEHEMU YA KUMI NA SITA
16 MENGINEYO
(a) Hakuna Mjumbe yeyote wa Bodi au mfanyakazi wa Chama atakayeidhinisha au kutoa
maamuzi ya maombi ya fedha ikiwa anahusika na maombi hayo kwa namna yoyote.
(b) Wajumbe wa Bodi, wajumbe wa Kamati ya Usimamizi, watendaji wakuu na watumishi wa
Chama watatunza siri kuhusu kumbukumbu zote za mwanachama.
(c) Vitabu vya hesabu na kumbukumbu nyingine za Chama zinaweza kuchunguzwa wakati
wowote na wajumbe wa Bodi.
(d) Kiasi fedha kinaweza kutolewa na Mkutano Mkuu kama honoraria kwa mtu yeyote
aliyejitolea na kuteulewa Bodi kufanyakazi maalum za Chama.
(e) Mgogoro au malalamiko yoyote kuhusu masharti au huduma za Chama kati ya mwanachama
au wanachama na watu wanaodai kupitia wanachama, na wajumbe wa Bodi au Afisa yeyote,
au kati ya Chama na chama kingine cha ushirika, yatapelekwa kwa Mrajis wa Vyama vya
Ushirika.
(f) Masharti haya yanaweza kurekebishwa pale itakaonekana inafaa kwa kupitishwa katika
Mkutano Mkuu na kupata idhini ya Mrajisi.
(g) Masharti haya yatanza kutumika mara baada ya kuwekwa saini na Wajumbe wa Bodi na
Mrajis wa Vyama vya Ushirika.
1
Wajumbe wa Bodi.
Na. Jina Kamili Wadhifa Saini
1. Tito Bartholomew Haule Mwenyekiti
2. Ndenengo Exaud Mwende Makamu Mwenyekiti
3. Tumaini Hashimu Yarumba Mjumbe
4. Mwanahawa Mhina Mjumbe
5. George Ntakimanzi Mjumbe
6. Martin Mwangalimi Mjumbe
7. Martha Lyimo Mjumbe
Mrajis wa Vyama Vya Ushirika................................................................
Saini............................................................................................................
Tarehe.........................................................................................................