Upload
others
View
28
Download
1
Embed Size (px)
Citation preview
SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR
MWELEKEO WA HALI YA UCHUMI 2019 NA MPANGO WA
MAENDELEO 2019/20
KITABU CHA PILI
TUME YA MIPANGO - ZANZIBAR
JUNI, 2019
YALIYOMOMada Ukurasa
YALIYOMO ...................................................................................................i
Orodha ya Viambatisho.............................................................................. iv
VIFUPISHO .................................................................................................. v
1.0 UTANGULIZI .......................................................................................... 1
2.0 MWELEKEO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2019 ........................... 2
2.1 Mwelekeo wa Uchumi wa Dunia ............................................................ 22.2 Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika ........................................................... 22.3 Mwelekeo wa Ukuaji wa Uchumi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara ........................................................................................................... 32.4 Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika ya Mashariki ...................................... 33.0 MWELEKEO WA UCHUMI WA ZANZIBAR 2019 .................................. 43.1. Uchumi wa Buluu ........................................................................ 43.2. Sera ya Viwanda ya Zanzibar ................................................................. 53.3 Sekta ya Utalii ......................................................................................... 53.4. Viwanda vidogo vidogo ......................................................................... 74.0 SHABAHA NA MALENGO YA UCHUMI MWAKA KWA 2019-2021. ...... 8
5.0 MFUMKO WA BEI WA ZANZIBAR ........................................................86.0 MWELEKEO WA BAJETI, 2019/2020 ................................................... 9
6.1 Mwelekeo wa Mapato na Matumizi: ....................................................... 96.1.1 Mapato ya Ndani ................................................................................ 96.1.2 Mapato ya Nje ........................................................................................ 10
6.2. Makadirio ya Matumizi kwa Mwaka 2019/20 ......................................... 10
6.2.1 Mapendekezo ya Hatua za Kuimarisha Mapato .................................... 10
7.0 MWELEKEO WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2019/20 ... 11
8.0 MAENEO YA VIPAUMBELE KWA MWAKA 2019/20 .............................. 11
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 i
9.0 RASILIMALI KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2019/20 ........................................................ 13
10.0 MWELEKEO WA PROGRAMU NA MIRADI YA MAENDELEO KWA MAENEO MAKUU YA MATOKEO ............................................................... 15
11.0 MWELEKEO WA PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO NA SHUGHULI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA 2019/20 KIWIZARA ............ 18
11.1 Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ....................... 1811.2 Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ....................................................... 19
11.2.1 Tume ya Ukimwi Zanzibar ................................................................... 22
11.2.2 Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Madawa ya Kulevya ..... 23
11.3 Wizara ya Fedha na Mipango .............................................................. 2311.3.1 Tume ya Mipango ................................................................................. 29
11.4 Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi ....................................... 32
11.5 Wizara ya Biashara na Viwanda .............................................................. 40
11.6 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ............................................... 4311.7 Wizara ya Afya .................................................................................... 4711.8 Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati ........................................ 5411.9 Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji ................................... 5911.10 Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto ............. 6211.11 Wizara ya Katiba na Sheria ................................................................ 6511.12 Ofisi ya Rais - Utumishi wa Umma na Utawala Bora ....................... 6611.12.1 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi .................. 6811.13 Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale ..................................... 69
11.13.1 Kamisheni ya Utalii ............................................................................ 70
11.14 Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo ............................. 7011.15 Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ .......................................................................................... 7211.15.1 Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM) .............................73
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 ii
11.15.2 Kikosi cha Valantia ............................................................................ 74
11.15.3 Chuo cha Mafunzo ............................................................................ 75
11.15.4 Jeshi la Kujenga Uchumi .................................................................. 75
11.15.5 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi ...................................................... 76
11.15.6 Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar ......................... 77
12.0 PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO CHINI YA MFUKO WA MIUNDOMBINU (INFRASTRUCTURE FUND) .............................................. 77
13.0 UFUATILIAJI NA TATHMINI ................................................................ 79
14.0 WASHIRIKA WA MAENDELEO ........................................................... 80
15.0 HITIMISHO ....................................................................................... 81
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 iii
Orodha ya Viambatisho
Kiambatisho 1: Mgao wa Fedha za Programu/Miradi ya Maendeleo 2019/20 Kiwizara.
Kiambatisho 2: Mgao wa Fedha za Programu/Miradi ya Maendeleo 2019/20 kwa Maeneo Makuu Matano ya Matokeo (KRAs).
Kiambatisho 3: Programu/Miradi ya Maendeleo Chini ya Mfuko wa Miundombinu (Infrastructure Fund)
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 iv
VIFUPISHO
BF Basket Funds (Mfuko wa Wafadhili)
BoT Bank of Tanzania (Benki Kuu ya Tanzania)
CCM Chama cha Mapinduzi
DCF Development Cooperation Framework (Muongozo wa Mashirikiano na Washirika wa Maendeleo)
GBS General Budget Support (Msaada wa Kibajeti)
KRAs Key Results Areas (Maeneo Makuu ya Matokeo)
M&E Monitoring and Evaluation (Ufuatiliaji na Tathmini)
MKUZA III Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar Awamu ya Tatu
NGOs Non-Government Organizations (Jumuiya Zisizo za Kiserikali)
PBZ People’s Bank of Zanzibar (Benki ya Watu wa Zanzibar)
SDGs Sustainable Development Goals (Malengo ya Maendeleo Endelevu)
SACCOS Saving and Credit Cooperative Society (Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo)
SMIDA Small and Medium Industry Development Agency (Wakala wa Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo na vya Kati)
SMT Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
SMZ Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
TRA Tanzania Revenue Authority (Mamlaka ya Mapato Tanzania)
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 v
TZS Tanzania Shilings (Shilingi ya Tanzania)
UKIMWI Upungufu wa Kinga Mwilini
UNDP United Nations Development Programme (Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa)
VAT Value Added Tax (Kodi ya Ongezeko la Thamani)
WEO World Economic Outlook (Mtazamo wa Uchumi wa Dunia)
ZECO Zanzibar Electricity Corporation (Shirika la Umeme Zanzibar)
ZRB Zanzibar Revenue Board (Bodi ya Mapato Zanzibar)
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 vi
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 1
1.0 UTANGULIZIMikakati na Mipango mbali mbali ya kukuza Uchumi na Ustawi wa Jamii inaendelea kuandaliwa na kutekelezwa ikiwa na azma ya kuinua uchumi na kupunguza umaskini pamoja na kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi. Katika kuendeleza jitihada hizo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka 2019/20 itaendelea kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2020, MKUZA III, Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020.
Juhudi za kukuza uchumi mjumuisho unaozingatia masikini zitaendelezwa kwa kasi zaidi kwa matarajio ya kufikia ukuaji wa asilimia 7.8 mwaka 2019. Maeneo yanayotarajiwa kukuza uchumi ni pamoja na kuanza utekelezaji wa shughuli za uchumi buluu, kuendeleza sekta ya Utalii, utekelezaji wa Sera ya viwanda na kukuza viwanda vidogo vidogo. Utawala Bora utazidi kuimarishwa kwa kuweka msisitizo wa kuimarisha demokrasia, kutii Sheria na uwajibikaji ili utulivu na amani uzidi kunawiri Zanzibar na hatimae uchumi kuimarika.
Mpango wa Maendeleo kwa mwaka 2019/20 utaendelea kuimarisha maeneo ya ukuzaji wa uchumi na ustawi wa kijamii kwa ujenzi wa miundombinu ya usafiri, uimarishaji miundombinu ya utoaji wa huduma za afya, kuimarisha ajira kwa vijana na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi, kuimarisha sekta ya mafuta na gesi asilia kwa kuimarisha miundombinu yake na kuongeza taaluma katika sekta hiyo. Mkazo zaidi utawekwa katika ukamilishaji wa jengo la abiria la uwanja wa ndege wa kimataifa wa Zanzibar (Terminal III), kuanza ujenzi wa bandari ya Mpigaduri na hospitali ya rufaa Binguni, utekelezaji wa program ya ajira kwa vijana yenye lengo la kuwawezesha vijana wa rika na elimu tofauti kupata ajira katika maeneo mbali mbali- kilimo, viwanda vidogo vidogo na vya kati kupitia fedha za Serikali na Mfuko wa Khalifa (Khalifa Fund), ujenzi wa Mahkama Kuu katika eneo la Tunguu na kuziimarisha hospitali za Kivunge na Wete kuwa katika hadhi ya mkoa. Aidha, Serikali pia itaendelea na kuimarisha miundombinu ya barabara kwa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Bububu – Mahonda –
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 2
Mkokotoni na barabara ya Ole – Kengeja, kuliimarisha eneo la bandari ya Mangapwani kwa uwekaji wa miundombinu ya msingi ikiwemo barabara, maji na umeme sambamba na ukamilishaji wa upembuzi yakinifu katika eneo linalotarajiwa kujengwa bandari hiyo na kusimamia shughuli za utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia.
Kitabu hiki kinaelezea Mwelekeo wa Hali ya Uchumi kwa mwaka 2019 na Mpango wa Maendeleo kwa mwaka 2019/20.
2.0 MWELEKEO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2019
2.1 Mwelekeo wa Uchumi wa Dunia
Kwa mujibu wa Mtazamo wa Uchumi wa Dunia (WEO), kasi ya ukuaji wa uchumi inatarajiwa kukuwa kwa kasi ya asilimia 3.3 kwa mwaka 2019 kutoka wastani wa asilimia 3.7 kwa mwaka 2018.Kasi ya ukuaji wa Uchumi wa nchi Zilizoendelea inatarajiwa kupungua kufikia wastani wa asilimia 1.8 mwaka 2019 kutoka wastani wa asilimia 2.2 mwaka 2018. Hali hii ni kutokana na kuendelea kwa mvutano wa kibiashara wa Umoja wa nchi ya China na Marekani, matatizo ya uchumi nchini Argentina na Uturuki, kuyumba kwa sekta ya uzalishaji viwandani ikiwemo uzalishaji wa magari nchini Ujerumani na kutokuwa na utulivu wa sera za kifedha katika nchi zenye uchumi mkubwa.
Aidha, kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia Kiuchumi inatarajiwa kufikia wastani wa asilimia 4.5 mwaka 2019, ikilinganishwa na ukuwaji wa wastani wa asilimia 4.4 kwa mwaka 2018. Kuongezeka kwa kasi ya ukuaji wa uchumi kunatokana na kuwepo kwa mfumo na sera nzuri ya udhibiti wa kifedha, kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa za kilimo na matarajio ya kuongezeka mapato yanayotokana na uzalishaji na usafirishaji wa nishati ya mafuta.
2.2 Mwelekeo wa Uchumi wa AfrikaKasi ya ukuaji wa uchumi wa Bara la Afrika inatarajiwa kuongezeka na kufikia wastani wa asilimia 4.0 mwaka 2019 kutoka wastani wa asilimia
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 3
3.5 mwaka 2018. Hii ni kutokana na kuimarika kwa Sekta ya Fedha kwa kupunguza viwango vya riba za kibenki, kuimarika kwa Sekta ya Kilimo kwa kuongeza uzalishaji na usafirishaji, kuongezeka kwa bei ya nishati ya mafuta kwa nchi wazalishaji wa mafuta na kuongezeka kwa uwekezaji binafsi. Zaidi ya nchi 40 za Afrika zinategemewa kuongezeka kwa kasi ya ukuaji wa uchumi.
2.3 Mwelekeo wa Ukuaji wa Uchumi kwa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara
Mwelekeo wa hali ya uchumi wa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara unatarajiwa kuimarika. Kasi ya ukuaji wa uchumi inatarajiwa kufikia wastani wa asilimia 3.7 kwa mwaka 2019 kutoka wastani wa asilimia 3.1 mwaka 2018. Kupanda kwa kasi ya ukuaji wa uchumi kunatarajiwa kutokana na kuongezeka kwa misaada ya kibajeti kwa nchi hizo kutoka kwa Washirika wa Maendeleo, kuongezeka kwa shughuli za uwekezaji na kuwepo kwa sera nzuri za uhimili wa sekta za kifedha.
2.4 Mwelekeo wa Uchumi wa Afrika ya Mashariki
Kwa mwaka 2019 kasi ya ukuaji wa uchumi kwa nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki inatarajiwa kuongezeka kutokana na kuimarika kwa shughuli za viwanda, sekta ya huduma na sekta ya kilimo hususani katika nchi ya Tanzania, Rwanda na Uganda. Aidha, uchumi wa Burundi unatarajiwa kushuka kwa mwaka 2019. Kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika Mashariki inatarajiwa kufikia wastani wa asilimia 5.9 kwa mwaka 2019 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 5.7 ya mwaka 2018.
Uchumi wa nchi ya Uganda unatarajiwa kukua kwa asilimia 5.5 kwa mwaka 2019 kutoka asilimia 5.3 mwaka 2018, Kenya unatarajiwa kukua kwa asilimia 6.0 kwa mwaka 2019 kutoka asilimia 5.9 mwaka 2018. Tanzania asilimia 6.6 kwa mwaka 2019 kutoka asilimia 6.7 mwaka 2018. Rwanda unatarajiwa kukua kufikia hadi asilimia 7.8 kwa mwaka 2019 kutoka asilimia 7.2 mwaka 2018 na nchi ya Burundi uchumi unatarajiwa
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 4
kushuka na kufikia asilimia 0.4 kwa mwaka 2019 kutoka asilimia 1.4 mwaka 2018.
2.5 Mwelekeo wa Mfumko wa Bei wa Dunia
Kasi ya mfumko wa bei wa Dunia inatarajiwa kushuka hadi kufikia wastani wa asilimia 3.6 kwa mwaka 2019 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 3.8 mwaka 2018. Matarajio ya kushuka kwa mfumko wa bei duniani yanachangiwa zaidi na kuwepo kwa ushindani wa kibiashara na kuongezeka uzalishaji wa bidhaa za kilimo na viwandani. Kwa nchi Zinazoendelea na Zinazoibukia kiuchumi mfumko wa bei unatarajiwa kupanda hadi kufikia asilimia 4.9 kwa mwaka 2019 kutoka wastani wa asilimia 4.5 mwaka 2018. Hata hivyo, kasi ya mfumko wa bei kwa nchi Zilizoendelea unatarajiwa kushuka hadi kufikia wastani wa asilimia 1.5 kwa mwaka 2019 kutoka wastani wa asilimia 1.7 mwaka 2018, hii ni kutokana na kushuka kwa bei za bidhaa za kilimo na kuongezeka kwa uzalishaji viwandani.
3.0 MWELEKEO WA UCHUMI WA ZANZIBAR 2019
Uchumi wa Zanzibar unatarajiwa kuzidi kuimarika. Mwelekeo wa uchumi kwa mwaka 2019 unategemea kwenda sambamba na utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2020, MKUZA III pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajia kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi kwa kuyafanyia kazi maeneo manne ambayo ni kichocheo cha ukuaji wa uchumi wa Zanzibar.
3.1. Uchumi wa Buluu
Uchumi wa Buluu unajumuisha shughuli zote zinazoambatana na maeneo ya bahari na fukwe kama vile uvuvi, utalii, usafiri wa bahari, mafuta na gesi, ufugaji wa mazao ya bahari pamoja na shughuli za kijamii za baharini. Kuwepo kwa uchumi endelevu unaotokana na Uchumi wa Buluu tunatarajia kutekeleza mambo yafuatayo:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 5
Kuanzishwa kwa Idara inayohusiana na masuala ya Uchumi i. Buluu.Kuandaa Sera ya Uchumi wa Buluu.ii. Kuwekeza zaidi katika rasilimali watu ili tuwe na wataalamu wa iii. kutosha katika eneo hili. Kufanya tathmini ya kuzitambua rasilimali zetu za bahari.iv. Kuhakikisha kuwa shughuli za baharini zinajumuishwa katika Sera v. na Sheria pamoja na miongozo katika kupunguza umasikini.
3.2. Sera ya Viwanda ya Zanzibar
Sera ya Viwanda Zanzibar imetoa muongozo katika kuwezesha wajasiriamali katika kujiongezea vipato vyao kupitia wawekezaji wa nje na ndani, mchango wa Serikali na msaada kutoka kwa washirika wa maendeleo. Baadhi ya shabaha ambazo Serikali imejiwekea kwa kusaidia Maendeleo ya viwanda vya Zanzibar ni pamoja na:
Kutenga ardhi na kui. endeleza miundombinu ya shughuli za viwanda katika maeneo tofauti ya Zanzibar katika kuvutia wawekezaji wa ndani na wa nje.Kuongeza mashirikiano baina ya Vyuo vya Ufundi vya Serikali ii. na wadau wote katika shughuli za uzalishaji viwandani. Kwa mfano kutekeleza programu jumuishi kwa kuongeza uwezo wa washonaji wa nguo, ufundi seremala na usarifu wa mazao ya Kilimo.Kuongeza usimamizi wa vyuo kwa ajili ya kutoa taaluma kwa iii. wawekezaji wadogo wadogo na wa kati ili kuongeza vipato vya wajasiriamali.Kuongeza mashirikiano baina ya taasisi, idara ambazo iv. zinazoshughulika na biashara katika kuzuia biashara haramu na ushindani usio sawa.Kushajihisha matumizi ya rasilimali inayorejesheka.v.
3.3 Sekta ya Utalii
Sekta ya utalii inatoa mchango mkubwa katika ukuaji wa Uchumi wa Zanzibar. Ni dhahiri kuwa Sera za Serikali zimelenga katika kuunganisha
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 6
baina ya sekta ya utalii na sekta nyengine za uzalishaji ili utalii uweze kuwa na faida zaidi. Hii ni pamoja na kuunganisha sekta ya kilimo na utalii kwa kuanzisha ‘agri-tourism’. Mambo yafuatayo yataendelea kufanyiwa kazi:
Kushirikisha jamii katika maendeleo ya programu ya mahoteli.i. Wana vijiji wanaozunguka maeneo ya hoteli waweze kuuza a) bidhaa za chakula na kazi za mkono;Mahoteli kuwapatia wanajamii taaluma na mbegu bora kwa b) bidhaa zinazohitajika katika mahoteli; Wazanzibari wapatiwe mafunzo ili waweze kuajiriwa badala c) ya nafasi za ajira kuchukuliwa na wageni ; Kuwawezesha wajasiriamali ili baadhi ya bidhaa ziweze d) kuzalishwa ndani.
Sekta mjumuisho ya program ya maendeleo ya utalii ii. Kuitangaza zaidi Zanzibar; a) Kuimarisha maeneo ya vivutio vya utalii vilivyopo kama vile b) shamba na viungo, urithi wa utamaduni na biashara;Kukiwezesha Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) c) kutoa wataalamu katika fani ya utalii;Kuongeza uhusiano baina ya utalii na kilimo ikiwemo kupata d) bidhaa za chakula kutoka kwa wakulima wa ndani.
Kuwaunganisha wananchi na sekta ya utalii.iii. Kuongeza usarifu wa bidhaa za chakula na kushajihisha a) viwanda vya usambazaji wa vyakula kwa mahoteli na ndege za kimataifa;Kuitangaza Zanzibar kama ni sehemu ya kutembelea kwa b) kutoa punguzo kwa mashirika ya ndege ili kuongeza uhusiano na kuongeza idadi ya watalii nchini;Kuitumia Miongozo ya Tafsiri ya Biashara ya mwaka 2016 c) (Trade Transaction Regulations of 2016) ambayo inawataka wauzaji wa bidhaa na huduma kwa mkopo kuingia katika makubaliano baina ya pande mbili);
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 7
Kuwashajihisha wananchi kununua bidhaa zilizozalishwa d) ndani kwa kuwapa wazalishaji unafuu wa kodi.
3.4. Viwanda vidogo vidogo
Viwanda vidogo vidogo vinajumuisha takribani viwanda vya usarifu na uhifadhi wa bidhaa ya chakula na zisizo za chakula. Zanzibar inayo nafasi kubwa kuongeza uzalishaji na kuleta mafanikio zaidi katika kukuza uchumi wa Zanzibar, mambo yafuatayo yataendelea kufanyiwa kazi:-
Kuvutia wawekezaji binafsi kufanyakazi na Serikali kwa njia i. ya mashirikiano (PPP) katika sekta, zikiwemo sekta ya uvuvi wa bahari kuu, ufugaji wa samaki, kuongeza thamani zao la mwani na ushajihishaji wa kilimo cha asili.Kufanya tafiti katika maeneo ya kilimo, mifugo, uvuvi na afya na ii. hatimae kufanyiwa kazi mapendekezo yatokanayo na tafiti hizo.Kuitangaza Zanzibar kwa kutengeneza tovuti, alama ya ubora wa iii. bidhaa za Zanzibar na kuwashirikisha vyombo vya kijamii katika kuitangaza Zanzibar.
Kwa mwaka 2019, Pato Halisi la Taifa linatarajiwa kukua kwa kasi ya wastani wa asilimia 7.8. Matarajio ya ukuaji wa uchumi yatatokana na kuendelea kuyafanyia kazi maeneo manne yaliyotajwa hapo juu pamoja na:-
Kuimarisha sekta ndogo ya usafirishaji. Serikali pamoja na i. wawekezaji binafsi wanatarajiwa kuongeza meli za mizigo pamoja na abiria;Kuendelea na juhudi za kuongeza uzalishaji wa vifaranga na ufugaji ii. wa samaki;Kuanza kwa uvuvi wa bahari kuu baada kupatikana boti za uvuvi;iii. Kuimarisha vituo vya utafiti vilivyopo nchini (Vituo vya utafiti wa iv. uvuvi, kilimo, mifugo na afya);Kuongezeka kwa usafirishaji wa zao la karafuu; v. Kuongezeka kwa uhamasishaji wa uwekezaji wa ndani na nje ya vi. nchi kwa kutekelezwa miradi mipya;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 8
Kuongezeka kwa kiwango cha idadi ya watalii wanaoingia nchini vii. kutokana na kupatikana kwa masoko mapya ya utalii na kuimarika kwa vivutio vya Utalii na malazi;Kutumika ipasavyo kwa dhana ya Sekta Mjumuisho kwa sekta za viii. uzalishaji (Twin Engine Approach) Kupunguza vikwazo vya kufanya biashara Zanzibar. ix.
4.0 SHABAHA NA MALENGO YA UCHUMI KWA 2019-2021.
Shabaha na malengo ya uchumi kwa kipindi cha miaka matatu ni kama ifuatavyo:-
Kasi ya ukuaji wa Pato Halisi la Taifa kwa miaka mitatu inategemewa i. kuwa baina ya asilimia 8 -10; Kuendelea kudhibiti kasi ya mfumko wa bei kuwa wastani wa chini ii. ya asilimia 5 kwa kipindi cha miaka mitatu; Mapato ya ndani kwa kipindi cha miaka mitatu yanakadiriwa kufikia iii. wastani wa asilimia 26.4 ya Pato la Taifa mwaka 2019/21 kutoka asilimia 24.2 kwa mwaka 2018/19; Matumizi ya Serikali kwa kipindi cha miaka mitatu yanakadiriwa iv. kufikia wastani wa asilimia 39.4 ya Pato la Taifa mwaka 2019/21 kutoka wastani wa asilimia 38 mwaka 2018/19;Kuendelea kuwepo kwa amani na utulivu.v.
5.0 MFUMKO WA BEI WA ZANZIBARKasi ya mfumko wa bei kwa mwaka 2019 inatarajiwa kuendelea kubakia katika tarakimu moja kutokana na sababu zifuatazo:-
Kushuka kwa bei za bidhaa za mchele na sukari duniani, kuongezeka i) kwa uzalishaji nchini na nchi jirani;Kuimarika kwa sekta ya Uvuvi kwa kuanza kwa shughuli za uvuvi ii) wa bahari kuu;Serikali kuendelea kutoa punguzo maalumu la ushuru kwa bidhaa iii) muhimu za chakula;Kuendelea kufanya ufuatiliaji wa mwenendo wa bei za bidhaa ili iv) kudhibiti upandaji wa bei usio wa lazima;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 9
Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuendelea kudhibiti kushuka kwa v) Shilingi ya Tanzania dhidi ya sarafu nyengine;Kushajihisha na kuimarisha shughuli za uzalishaji viwandani; vi) Kushajihisha uzalishaji wa ndani wa mazao ya kilimo zikiwemo vii) mboga mboga.
6.0 MWELEKEO WA BAJETI, 2019/20
Lengo Kuu la Bajeti ya Serikali litaendelea kuwa ni kujenga jamii iliyoelimika, yenye siha kwa kuwepo uhakika wa chakula, uwezo wa kiuchumi na inayothamini na kufuata misingi ya utawala bora. Bajeti ya mwaka 2019/20 itaendelea kuimarisha na kuendeleza maeneo yaliyozingatiwa katika Bajeti iliyopita yakiwemo (i) Huduma za Elimu (ii) Huduma za Afya na Ustawi wa jamii (iii) Miundombinu ya msingi; na (iv) Utawala bora.
6.1 Mwelekeo wa Mapato na Matumizi:
Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Serikali inatatarajia kukusanya jumla ya TZS 1.419.4 bilioni zikiwemo TZS 976.5 bilioni zitokanazo na vianzio vya ndani na TZS 394.6 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo, TZS bilioni 40 mikopo ya ndani na TZS 8.3 Mfuko wa Wafadhili (BF). Aidha, mwelekeo wa Serikali ni kukadiria kutumia jumla ya TZS 1.419.4 bilioni katika mwaka wa fedha 2019/20 ikiwemo matumizi ya Kazi za Kawaida ya TZS 842.4 bilioni na matumizi ya Kazi za Maendeleo ya TZS 577 bilioni.
6.1.1 Mapato ya Ndani
Jumla ya TZS 976.5 bilioni zinatarajiwa kukusanywa kwa mwaka 2019/20 kutoka katika vianzio vya ndani kwa mchanganuo ufuatao:
ZRB: inatarajiwa kukusanya TZS 488.5 bilioni a) TRA: inatarajiwa kukusanya TZS 350.2 bilioni b) Mapato ya mawizara: TZS 116.8 bilionic) Kodi ya Mapato kwa wafanyakazi wa SMT: TZS 21 bilionid)
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 10
6.1.2 Mapato ya Nje
Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Serikali inatarajia kupokea jumla ya TZS 394.6 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo; hii inajumuisha ruzuku ya TZS 95.5 bilioni na mikopo ya TZS 299.1 bilioni.
6.2. Makadirio ya Matumizi kwa Mwaka 2019/20
Kwa mwaka 2019/20 jumla ya TZS1.419.4 bilioni zimekadiriwa kutumika kwa Kazi za Kawaida na Maendeleo sawa na ongezeko la asilimia 7.9 ya makadirio ya TZS 1.315.1 bilioni ya mwaka 2018/19. Kati ya fedha hizo Matumizi ya Kawaida ni TZS 842.4 bilioni na Matumizi ya Kazi za Maendeleo ni TZS 577.0 bilioni. Aidha, kwa mwaka wa fedha 2019/20 utegemezi wa Bajeti unatarajiwa kuongezeka na kufikia asilimia 6.2 kutoka asilimia 5.7 kwa mwaka 2018/19. Hali hii imechangiwa na kuimarika kwa Mapato ya Ndani na Kuongezeka kwa ruzuku kutoka kwa Washirika wa Maendeleo.
6.2.1 Mapendekezo ya Hatua za Kuimarisha Mapato
Katika mwaka 2019/20 hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato ni pamoja na:-
Kuifanyia marekebisho Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani i. (VAT). Kutoza kodi kwa Wageni wanaolala kwenye vyombo vya Baharini. ii. Kujumuisha Gari za Mizigo zenye uwezo wa kubeba chini ya Tani iii. moja na nusu katika utaratibu wa Ushuru wa Stempu. Kuimarisha mfumo wa Ukusanyaji wa Mapato katika Wizara na iv. Taasisi za Serikali.Kuimarisha Usimamizi na ufuatiliaji wa Mapato.v. Kugomboa madeni ya walipa Kodi.vi. Kuongeza muda na ufanisi wa utoaji na usafirishaji wa Mizigo vii. kupitia Bandarini.Kuwatangaza walipa kodi wanaokwepa kulipa kodi.viii. Kuwajengea uwezo watumiaji wa mfumo wa Forodha TANCIS.ix. Kupambana na njia zinazotumika kuepuka Kodi (Tax avoidance).x.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 11
Kushajihisha wananchi kudai risiti za kielectronic. xi. Kuifanyia mapitio Sheria na Kanuni zinazotoa Misamaha ya Kodi.xii. Kufuatilia miongozo ya Kimataifa ya Misamaha ya Kodi kwa Miradi xiii. ya Maendeleo.Kuondoa zuio (Retention) la Mapato kwa Taasisi za Serikali.xiv.
7.0 MWELEKEO WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2019/20
Kwa kipindi cha mwaka 2019/20, Mwelekeo wa Mpango wa Maendeleo utaendelea kuzingatia utekelezaji wa MKUZA III kupitia programu na miradi ya kimkakati (Flagship projects), Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020 na Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein aliyoitoa katika uzinduzi wa Baraza la Tisa la Baraza la Wawakilishi. Lengo ni kuiwezesha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufikia azma ya Dira ya Maendeleo ya Zanzibar ya 2020 pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) ili kuweza Kukuza Uchumi wa Zanzibar.
Mpango huu wa mwaka 2019/20, utaendelea kuimarisha maeneo ya kukuza uchumi na ustawi wa kijamii kwa ujenzi wa miundimbinu ya usafiri, kilimo, kuimarisha ubora wa elimu, kuimarisha huduma za afya na upatikanaji wa maji safi na salama, kuimarisha mazingira bila ya kusahau masuala ya utawala bora nchini.
8.0 MAENEO YA VIPAUMBELE KWA MWAKA 2019/20
Kwa mwaka 2019/20, maeneo yatakayopewa kipaumbele katika utekelezaji wa Bajeti na Mpango wa Maendeleo Zanzibar yatazingatia zaidi utekelezaji wa programu na miradi mbali mbali ya maendeleo itakayosaidia katika kukuza uchumi na kuimarisha ustawi wa wananchi. Kwa kuzingatia umuhimu na faida zitakazopatikana, vipaumbele vya mwaka 2019/20 vimepangwa katika makundi mawili kama ifuatavyo:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 12
Vipaumbele vya Juu
Serikali inakusudia kutekeleza vipaumbele vya mwanzo ambapo mkazo mkubwa utawekwa katika kutekeleza miradi ifuatayo:
Ukamilishaji wa jengo la abiria la uwanja wa ndege wa kimataifa i) wa Zanzibar (Terminal III);
Kuanza ujenzi wa bandari ya Mpigaduri;ii)
Kuanza ujenzi wa hospitali ya rufaa Binguni (Awamu ya iii) Kwanza);
Kuanza ujenzi wa Mahakama Kuu Tunguu;iv)
Kukamilisha ujenzi wa barabara ya Ole – Kengeja; v)
Kuimarisha ulinzi na usalama nchini. vi)
Vipaumbele vyengine
Miradi mengine ya itakayopewa kipaumbele na Serikali kwa mwaka 2019/20 ni kama vifuatavyo:
Program ya ajira kwa vijana;i)
Mradi wa kuwasaidia wajasiriamali wadogo wadogo; ii)
Kuimarisha hospitali za Kivunge na Wete kuwa katika hadhi ya iii) Mkoa;
Mradi wa kuendeleza bandari ya Mangapwani;iv)
Mradi wa ujenzi wa barabara ya Bububu – Mahonda – v) Mkokotoni;
Mradi wa kuendelea na ujenzi wa Ofisi na makambi ya vikosi vi) vya Idara Maalum za SMZ;
Programu ya ugatuzi wa masuala ya elimu;vii)
Programu ya ujenzi wa majengo ya Ofisi za Serikali.viii)
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 13
9.0 RASILIMALI KWA AJILI YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO KWA MWAKA 2019/20
Kwa mwaka 2019/20, Mpango wa Maendeleo unalenga kutekeleza jumla ya programu 27 na miradi 48 ya maendeleo. Jumla ya TZS 577.02 bilioni zitatumika kwa ajili ya kugharamia utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo ikiwa ni upungufu wa TZS 35.93 bilioni sawa na asilimia 5.86 ikilinganishwa na Bajeti ya Maendeleo ya mwaka 2018/19 ya TZS 612.95 bilioni.
Serikali imepanga kutumia TZS 182.40 bilioni sawa na asilimia 31.61 ya Bajeti ya Maendeleo ikiwa ni ongezeko la TZS 33.65 bilioni sawa na asilimia 22.6 ya Bajeti ya Maendeleo ya mwaka 2018/19. Kati ya fedha za Serikali (TZS 182.40 bilioni), TZS 116.44 bilioni ni kwa programu na miradi ya kimkakati, yenye mikataba au dhima ‘Commitment’ na TZS 65.96 bilioni kwa miradi mengine. Aidha, jumla ya TZS 394.62 bilioni sawa na asilimia 68.39 ya bajeti ya maendeleo zimepangwa kutoka kwa Washirika wa Maendeleo ikiwa TZS 95.52 bilioni ni ruzuku na TZS 299.10 bilioni ni mikopo. Fedha hizo ni upungufu wa TZS 69.58 bilioni sawa na asilimia 14.99 ikilinganishwa na fedha zilizotengwa kwa mwaka 2018/19 zenye jumla ya TZS 464.2 bilioni.
Mgawanyo wa fedha za bajeti kiwizara na kwa Maeneo Makuu Matano ya Matokeo (KRAs) kwa programu na miradi ya maendeleo unaonekana kwenye kiambatisho namba 1 na 2. Aidha, jadweli namba 1 hapo chini linaonesha muhtasari wa mgawanyo wa fedha kwa Maeneo Makuu Matano ya Matokeo (KRAs).
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 14
Jadw
eli n
am. 1
: Muh
tasa
ri w
a Fe
dha
Zili
zopa
ngw
a kw
a U
pand
e w
a Se
rika
li na
Was
hiri
ka w
a M
aend
eleo
kw
a Pro
gram
u/M
irad
i ya M
aend
eleo
kw
a Mae
neo M
akuu
ya M
atok
eo
2019
/20.
!"#
#Jadw
eli
nam
. 1:
Muh
tasa
ri w
a Fe
dha
Zili
zopa
ngw
a kw
a U
pand
e w
a Se
rika
li na
Was
hiri
ka w
a M
aend
eleo
kw
a
Prog
ram
u/M
irad
i ya
Mae
ndel
eo k
wa
Mae
neo
Mak
uu y
a M
atok
eo 2
019/
20.
EN
EO
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 (T
ZS.
"00
0")
SMZ
%
R
UZ
UK
U
MK
OPO
JUM
LA
YA
FED
HA
ZA
WA
SHIR
IKA
WA
MA
EN
DE
LE
O
%
JUM
LA
YA
BA
JET
I %
KR
A A
: Kuw
ezes
ha U
kuaj
i wa
Uch
umi
Jum
uish
i na
Ende
levu
11
0,93
0,00
0 53
28
,122
,245
70
,527
,723
98
,649
,968
47
20
9,57
9,96
8 36
.3
KR
A B
: Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Wat
u 3,
600,
000
32
665,
703
7,00
0,00
0 7,
665,
703
68
11,2
65,7
03
2.0
KR
A
C:
Kut
oa
Hud
uma
Bor
a kw
a
Wot
e 40
,067
,700
13
56
,970
,645
21
5,03
9,27
0 27
2,00
9,91
5 87
31
2,07
7,61
5 54
.0
KR
A D
: K
uwep
o M
azin
gira
End
elev
u
na U
him
ili w
a M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i 35
0,00
0 43
45
6,60
0 0
456,
600
57
806,
600
0.1
KR
A E
: K
ushi
kam
ana
na M
isin
gi y
a
Uta
wal
a B
ora
27
,452
,300
63
9,
305,
690
6,53
7,40
9 15
,843
,099
37
43
,295
,399
7.
6
JUM
LA
KU
U
182,
400,
000
32
95,5
20,8
83
299,
104,
402
394,
625,
285
68
577,
025,
285
100
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 15
10.0 MWELEKEO WA PROGRAMU NA MIRADI YA MAENDELEO KWA MAENEO MAKUU YA MATOKEO
Maeneo makuu ya matokeo ni maeneo yaliyoainishwa katika Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Zanzibar Awamu ya Tatu (MKUZA III) ili kuweza kutekeleza malengo na shughuli zilizopangwa katika Mkakati huo kwa ufanisi zaidi. Maeneo hayo yanatoa fursa kwa kila sekta kuweza kujua ni katika eneo lipi inaweza kujikita zaidi na kusaidia katika utekelezaji wa MKUZA III. Kwa kuzingatia hilo mgawanyo wa programu na miradi ya maendeleo umejikita katika maeneo hayo kama ifuatavyo:
Kuwezesha Ukuaji wa Uchumi Jumuishi na Endelevu i.
Eneo hili linakusudia kuimarisha mazingora bora yatakayosaidia ukuaji wa uchumi endelevu ili kupambana na umasikini wa kipato. Matarajio ya muda wa kati wa eneo hili ni kuwa na mazingira rafiki kwa ukuaji wa sekta binafsi na upatikanaji wa ajira, kuwa na uwekezaji wa umma unaotosheleza ili kusaidia miundombinu ikiwemo ya mawasiliano na vichocheo vyengine vya uchumi, kuwa na sekta yenye ushindani ya utalii yenye manufaa endelevu na jumuishi kwa wanachi, kuwepo na uzalishaji wa kisasa katika sekta za kilimo na viwanda kwa kuongeza thamani, kuwepo sekta binafsi iliyoshamiri na kuimarika kwa hifadhi ya jamii.
Kwa mwaka 2019/20 eneo hili linatarajiwa kutekeleza programu 12 na miradi 15 ya maendeleo ambapo limetengewa jumla ya TZS 209.6 bilioni sawa na asilimia 36.3 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 110.9 bilioni sawa na asilimia 53 ya bajeti ya eneo hili, Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 98.7 bilioni sawa na asilimia 47 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 28.1 bilioni na mkopo ni TZS 70.5 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 16
Kukuza Uwezo wa Watuii.
Eneo hili linakusudia kuimarisha uwezo wa watu ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Eneo lina matarajio ya kuongeza ajira kwa watu wote (vijana, wanawake,watu watu wenye ulemavu) mijini na vijijini kwa kuendeleza maarifa yao na kuongeza uwezo wa wajasiriamali ili kuimarisha fursa za kuweza kujiajiri.
Katika mwaka 2019/20 eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya programu mbili na miradi miwili ambapo limetengewa jumla ya TZS 11.3 bilioni sawa na asilimia 2.0 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 3.6 bilioni sawa na asilimia 32 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 7.7 bilioni sawa na asilimia 68 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 665.7 milioni na mkopo ni TZS 7.0 bilioni.
Kutoa Huduma Bora kwa Woteiii.
Eneo hili linakusudia kuimarisha upatikanaji wa huduma bora na za kisasa kwa jamii. Matarajio ni kuwa na huduma bora za afya na usafi wa mazingira, maji safi na salama, na kupambana na maradhi yenye kuambukiza na yasiyoambukiza; kuwa na elimu bora kwa wote na jinsia zote; kuwa na makaazi bora, matumizi bora ya ardhi na upatikanaji wa nishati; kuwa na udhibiti wa unyanyasaji wa watoto na wanawake; kuwa na uwezo na utayari wa kupambana na majanga/dharura za aina zote; na kuwa na usalama wa upatikanaji wa chakula kwa jamii yote.
Kwa mwaka 2019/20, eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya programu tisa na miradi 15 ambapo limetengewa jumla ya TZS 312.1 bilioni sawa na asilimia 54.0 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 40.1 bilioni sawa na asilimia 13 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 272.0 bilioni sawa na asilimia 87 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 57.0 bilioni na mkopo ni TZS 215.0 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 17
Kuwepo Mazingira Endelevu na Uhimili wa Mabadiliko ya iv. Tabianchi
Eneo hili linakusudia kuimarisha uwezo wetu wa kukabiliana na mabadiliko ya mazingira na tabia nchi. Matarajio ya eneo hili ni kuwa na uwezo wa kutosha wa kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi; kuwa na uhifadhi wa viumbe vya baharini na nchi kavu na kupunguza upotevu wake; kuzuia uharibifu wa mazingira na kupunguza athari za kijamii zinazotokana na shughuli za kiuchumi.
Katika mwaka 2019/20, eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya miradi miwili ambapo limetengewa jumla ya TZS 806.6 bilioni sawa na asilimia 0.1 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 350 milioni sawa na asilimia 43 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 456.6 bilioni sawa na asilimia 57 ya bajeti ya eneo hili ambazo ni ruzuku.
Kushikamana na Misingi ya Utawala Borav.
Eneo la tano la mkakati huu limejumuisha masuala yote ya kisheria na uongozi. Katika eneo hili inakusudiwa kuimarisha misingi ya utawala bora, haki na sheria katika ngazi zote. Matarajio ya eneo hili ni kuwa na mifumo ya kiutawala na kitaasisi yenye kuwajibika, ilio wazi na bila rushwa; kufikia usawa na uwiano wa kijinsia, jamii jumuishi, na uwezeshaji wa wanawake, watoto wa kike, vijana, walemavu, na watu walio katika mazingira hatarishi; kuwa na upatikanaji wa haki, kuheshimu utawala wa sheria, haki za msingi za binadamu na uimarishaji wa demokrasia; kuwa na uwajibikaji wa mashirika kwa jamii; na kuwa na mazingatio zaidi ya watu katika mipango.
Kwa mwaka 2019/20, eneo hili linatarajiwa kutekeleza jumla ya programu nne na miradi 17 ambapo limetengewa jumla ya TZS 43.3 bilioni sawa na asilimia 8 ya bajeti ya maendeleo. Serikali imetenga TZS 27.4 bilioni sawa na asilimia 63 ya bajeti ya eneo hili na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 15.8 bilioni sawa na asilimia 37 ya bajeti ya eneo hili ambapo ruzuku ni TZS 9.3 milioni na mkopo ni TZS 6.5 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 18
11.0 MWELEKEO WA PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO NA SHUGHULI ZILIZOPANGWA KUTEKELEZWA KWA MWAKA 2019/20 KIWIZARA
11.1 Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ni taasisi yenye dhamana ya kusimamia kazi za Baraza la Mapinduzi (Baraza la Mawaziri), Ofisi ya Rais Ikulu na shughuli za Ushirikiano wa Kimataifa na Wazanzibari waliopo nje ya nchi (Diaspora). Aidha, ofisi hii ni kiungo muhimu cha maendeleo ya nchi katika kusimamia utekelezaji wa kazi za Baraza la Mapinduzi na kamati zake, kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza ahadi za Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pamoja na kuwapatia taarifa za shughuli za Serikali na maendeleo. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Ofisi hii imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 2.0 bilioni.
Mradi wa Uimarishaji wa Nyumba za Viongozi na Nyumba za Serikali
Mradi umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha makaazi ya viongozi wakuu wa nchi kwa kuweka mazingira na mandhari nzuri ya makaazi yao pamoja na kuimarisha usalama wa nyumba hizo. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20 umepangiwa kiasi cha TZS 2.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuendelea na ujenzi wa ofisi pamoja na ununuzi wa samani katika i. Ikulu ya Chake Chake;Kufanya ukarabati katika Ikulu ya Mnazi Mmoja;ii. Kuifanyia matengenezo nyumba ya makaazi ya Mheshimiwa Rais iii. katika Ikulu ya Kibweni;Kuendelea na ujenzi katika Ikulu ya Micheweniiv. Kujenga nyumba ya viongozo pamoja na ukuta katika nyumba ya v. makaazi ya Mheshimiwa Rais katika Ikulu ya Dodoma;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 19
Kuzuia mmong’onyoko katika nyumba ya makaazi ya Mheshimiwa vi. Rais katika Ikulu ya Chake Chake.
11.2 Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ina jukumu la kusimamia utekelezaji wa shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta zote za SMZ, uratibu wa shughuli za Muungano baina ya Zanzibar na Tanzania Bara, pamoja na kusimamia masuala ya mazingira, Ukimwi, maafa, udhibiti wa dawa za kulevya na masuala mengine mtambuka. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Ofisi imepanga kutekeleza programu moja na miradi minne ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 8.7 bilioni (TZS 740 milioni kutolewa na Serikali na TZS 7.3 bilioni Washirika wa Maendeleo).
Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF III)
TASAF III ni Mpango wa Kitaifa ulioanza mwaka 2015, na unatekelezwa kwa kipindi cha miaka (5) kwa Tanzania Bara na Zanzibar. Mpango huu una lengo la kuziwezesha kaya masikini sana kuongeza kipato, fursa na uwezo wa kugharamia mahitaji muhimu ya kibinadamu hasa chakula, afya na elimu. Aidha, unalenga kutekeleza miradi iliyoibuliwa na wananchi katika nyanja mbali mbali za elimu, afya, maji safi na ajira za muda, ili kuwawezesha waweze kujikwamua na umasikini. Kwa mwaka 2019/20, programu imepangiwa jumla ya TZS 7.3 bilioni (TZS 40 milioni kutoka Serikalini na TZS 7.3 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuratibu shughuli za TASAF III kati ya Zanzibar na Dar es Salaam, i. ikiwemo ufuatiliaji na tathmini ya shughuli za mradi kwa Unguja na Pemba;
Kufanya vikao vinne vya Kamati ya Wataalamu na viwili vya Kamati ii. ya Uongozi wa mradi.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 20
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleo
Kufanya malipo kwa walengwa wa kaya masikini (Condition Cash i. Transfer (CCT)) na kusaidia jamii katika shehia 204 (126 Unguja na 78 Pemba).
Mradi wa Kujenga Uwezo wa Kukabiliana na Maafa
Mradi huu unatekelezwa chini ya Programu ya UNDAP II na unagharamiwa na Umoja wa Mataifa (UNDP). Mradi una lengo la kujenga uwezo wa Taifa katika kujiandaa na kukabiliana na aina zote za majanga/maafa kwa wakati na ufanisi. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 180 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuandaa ramani yenye kuonesha maeneo hatarishi ya kukumbwa na i. majanga/maafa kwa Unguja na Pemba;
Kuandaa muongozo wa ufuatiliaji na tathmini kwa mipango ya ii. kujiandaa na kukabiliana na maafa utakaotumika kwa Wilaya zote za Zanzibar.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba ya Makamu wa Pili wa Rais
Mradi unagharamiwa na Serikali pekee na una lengo la kuimarisha makaazi ya Mheshimiwa Makamu wa Pili wa Rais na wafanyakazi ili kuendana na hadhi inayostahiki. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 350 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kukamilisha ujenzi wa nyumba ya Makamu wa Pili wa Rais Pagali i. - Pemba.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 21
Mradi wa Kuimarisha Usimamizi wa Mazingira, Maliasili na Mabadiiko ya Tabianchi - Zanzibar
Mradi unatekelezwa pande zote za Zanzibar (Unguja na Pemba) kwa mashirikiano baina ya Serikali na UNDP. Mradi huu umeanza mwaka 2017 na una lengo la kuzifanyia kazi changamoto zilizojitokeza za mazingira na kuongeza uhimili wa mabadiliko ya tabianchi Zanzibar, ili kufikia maendeleo endelevu. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 756.6 milioni (TZS 300 milioni kutoka Serikalini na TZS 456.6 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuweka uzio wi. a mawe kwa ajili ya kulihami eneo lilioathirika na mabadiliko ya tabianchi la Msuka Pemba;
Ujenzi wa mtaro wa kupitishia maji ya mvua ili kuzuia mmong’onyoko ii. wa fukwe ya Msuka usiendelee.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleo
Kuimarisha uwezo wa taasisi zinazohusika na mabadiliko ya i. tabianchi;
Kukuza uwezo wa upatikanaji na usimamizi wa rasilimali ii. fedha;
Kukuza uwezo wa matumizi na upatikanaji wa habari muhimu za iii. mabadiliko ya tabianchi.
Mradi wa Kukuza Uwezo wa Kitaifa wa Kuhimili Athari za Mabadiliko ya Tabianchi
Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), kwa lengo la kuhakikisha masuala ya mabadiliko ya tabianchi yanazingatiwa katika mipango, programu na miradi ya kisekta. Kwa mwaka 2019/20, mradi
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 22
umepangiwa jumla ya TZS 50 milioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli ifuatayo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliUratibu shughuli za mradi ikiwemo kuandaa vikao na wadau kujadili i. maandiko ya miradi.
11.2.1 Tume ya Ukimwi Zanzibar
Tume ya Ukimwi ina jukumu la kuratibu na kusimamia shughuli zote zinazohusika na mapambano dhidi ya UKIMWI, pamoja na kusimamia uandaaji wa sera na mikakati inayolenga kudhibiti UKIMWI katika jamii. Kwa mwaka 2019/20, Tume imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 540 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo.
Mradi wa Kuzuia Maambukizi ya UKIMWI Zanzibar
Mradi huu umeanza 2016, unagharamiwa na Washirika wa Maendeleo (GF/UNFPA) na una lengo la kukinga na kukabiliana na athari zitokanazo na maambukizi ya UKIMWI kwenye jamii ya Wazanzibari pamoja na kutoa msaada katika huduma mjumuisho ya UKIMWI na uzazi wa mpango. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 540 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuwapatia fedha Asasi za Kiraia zilizochaguliwa kwa ajili ya i. utekelezaji wa programu ya Mfuko wa Dunia;
Kutoa huduma za upimaji, rufaa kwa maeneo yaliyombali na vituo ii. ili kuyafikia makundi maalum;
Kuvitembelea vituo vya afya vinavyotoa huduma ya UKIMWI na iii. vituo vya huduma rafiki kwa vijana ili kuangalia utoaji wa huduma za UKIMWI na afya ya uzazi.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 23
11.2.2 Tume ya Kitaifa ya Kuratibu na Udhibiti wa Madawa ya Kulevya
Tume hii ina jukumu la kuratibu mapambano dhidi ya biashara, usafirishaji na matumizi ya dawa za kulevya, kutoa taaluma kwa jamii juu ya athari za dawa za kulevya, tiba pamoja na ushauri nasaha kwa waathirika wa dawa hizo. Kwa mwaka 2019/20, Tume imepanga kutekeleza mradi mmoja utakaogharimu jumla ya TZS 680 milioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Tiba na Marekebisho ya Tabia
Mradi umeanza mwaka 2018 kwa awamu ya pili (II) na una lengo la kuimarisha kituo cha matibabu na kurekebisha tabia kwa watumiaji wa dawa za kulevya. Mradi huu unatekelezwa na Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20 umepangiwa kiasi cha TZS 680 milioni kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kukamilisha ujenzi kwa ghorofa ya pili kituo cha Tiba na i. Marekebisho ya Tabia Kidimni.
11.3 Wizara ya Fedha na Mipango
Sekta ya Fedha na Mipango inajumuisha shughuli zote zinazohusiana na maendeleo ya kifedha, kiuchumi na mipango nchini ikiwemo usimamizi wa mapato na matumizi Serikalini, mwenendo na maendeleo ya mabenki na taasisi za fedha, usimamizi wa misaada, usimamizi wa mipango ya kitaifa na kimataifa, usimamizi wa uchumi mkuu pamoja na shughuli zote za taasisi nyengine zinazojihusisha na masuala ya fedha, mipango na uwekezaji nchini. Aidha, sekta hii inajukumu la kupanga na kusimamia mipango ya maendeleo ya nchi ya muda mfupi wa kati na muda mrefu. Kwa mwaka 2019/20, Wizara hii imepanga kutekeleza programu nne na miradi minne ya maendeleo kwa gharama ya TZS 81.6 bilioni. Kati ya hizo Serikali imepanga kutoa TZS 14.5 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 67.1 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 24
Programu ya Ujenzi wa Ofisi za Serikali Zanzibar
Programu hii ina jukumu la kugharamia ujenzi wa Ofisi za Serikali katika maeneo ambayo yamependekezwa na Serikali. Aidha, program hii ina lengo la kuweka mazingira bora ya kazi kwa wafanyakazi wa Serikali. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 10.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuanza ujenzi wa Mahkama Kuu – Tunguu.i.
Programu ya Kuimarisha Huduma za Miji (ZUSP)
Programu ya Kuimarisha Huduma za Miji ina lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za miji ya Zanzibar, na uhifadhi wa eneo la urithi wa Mji Mkongwe eneo ambalo ni kivutio kwa watalii na kulinda historia ya mji wa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, programu hii itatekelezwa kwa fedha wa Washirika wa Maendeleo pekee ambapo jumla ya TZS 57.4 bilioni zimepangwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuendelea na kazi ya ujenzi wa jaa la taka Kibele;i. Kujenga kituo cha kuhifadhia taka cha muda katika eneo la ii. Maruhubi;Kuendelea na kazi ya uwekaji wa taa za barabarani (Street Light) iii. katika maeneo ya barabara ya Uwanja wa Ndege- Mnazi Mmoja, Mwanakwerekwe – Kiembesamaki, Mombasa- Mazizini (ZRB), Mikunguni- Muembenjugu kwa Unguja na kwa Pemba Chanjani- Machomane, Chake Chake (PBZ) - Tibirizi, Mkoani bandarini - Kipitacho, Limbani - Ikulu ya Wete, Mtemani - Bopwe na Mtemani – Kizimbani; Kukamilisha ubunifu na usanifu wa maelezo ya kina ya mandhari iv. ya mji (Green Corridor) na utengenezaji wa bustani katika maeneo ya Mkunazini - Kariakoo, Mnazi Mmoja – Malindi, Mlandege -Maisara;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 25
Kuendelea na kazi ya ujenzi wa mitaro katika maeneo ya Shaurimoyo, v. Nyerere, Kwa Mtumwa Jeni, Magogoni, Mwanakwerekwe, Sogea, Sebleni, Amani na Ziwatuwe.
Programu ya Upatikanaji Rasilimali Fedha
Programu hii ina lengo la kuimarisha upatikanaji wa rasilimali fedha kwa kuimarisha mapato yatokanayo na kodi na mapato yasiotokana na kodi kupitia utekelezaji wa sheria, miongozo na kanuni za fedha. Programu hii inatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20 kiasi cha TZS 300 milioni zimepangwa kutumika kwa shughuli ifuatayo:-
Shughuli iliyopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kununua na kusambaza mashine za VFD kwa watumiaji.i.
Programu ya Mageuzi Katika Usimamizi wa Fedha (PFMRP)
Programu hii ina lengo la kuhakikisha mapato na matumizi yanasimamiwa na kudhibitiwa kwa ufanisi. Katika kufanikisha lengo hilo, Serikali kwa kushirikiana na Washirika wa Maendeleo inatekeleza programu hii katika taasisi za Serikali, Wizara na Serikali za mita na kuratibiw katika Wizara ya Fedha na Mipango. Kwa mwaka 2019/20, programu hii itatekelezwa kwa fedha za Washirika wa Maendeleo pekee ambapo jumla ya TZS 1.6 bilioni zimepangwa kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kutayarisha na kusimamia mikakati, sera na sheria zitakazotumika i. katika mifumo mipya ya usajili na ulipaji kodi katika Bodi ya Mapato ya Zanzibar (ZRB);Kuimarisha mfumo wa kielektroniki wa malipo ya mishahara kwa ii. watumishi wa umma katika Serikali kuu na Serikali za mitaa;Kuimarisha mfumo wa manunuzi kwa njia ya mtandao katika taasisi iii. za Serikali, Wizara na Serikali za Mitaa;Kuandaa muongozo wa mpango wa ufuatiliaji na tathmini kwa iv. miradi inayofadhiliwa na Washirika wa Maendeleo katika taasisi za Serikali, Wizara na Serikali za Mitaa;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 26
Kufanya utafiti juu ya utekelezaji wa fedha za umma katika v. mashirika;Kuwajengea uwezo wafanyakazi wa taasisi husika kwa kuwapatia vi. mafunzo ya muda mfupi katika fani za usimamizi wa fedha;Kununua vifaa vya ofisini katika taasisi za Serikali.vii.
Mradi wa Kujenga Uwezo Taasisi za Serikali
Mradi huu una lengo la kusaidia, kuratibu, ufuatiliaji na tathmini ya MKUZA III pamoja na Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDG’s) na kutoa uelewa wa utekelezaji wa malengo yaliyopangwa ili kupata matokeo yake na kuhakikisha kwamba rasilimali zilizopo zinatumika kwa ufanisi unaohitajika kwa manufaa ya watu na taifa kiujumla. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na Washirika wa Maendeleo (UNDP) ambapo kiasi cha TZS 1.6 bilioni (TZS 50 milioni kutoka Serikalini na TZS 1.6 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zitatumika kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuandaa vikao viwili vya Kamati Kiongozi na vinne vya Kamati ya i. Wataalamu;Kununua vifaa vya ofisi.ii.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuratibu utekezaji wa Muongozo wa Mashirikiano ya pamoja baina i. ya Serikali na Washirika wa Maendeleo (DCF);Kufanya uchambuzi na kufuatilia miradi ya UNDP na Washirika wa ii. Maendeleo wengine ili kutambua changamoto zilizopo;Kutoa mafunzo kwa maafisa wa Idara ya Fedha za Nje katika fani za iii. utafutaji na usimamizi wa misaada;Kufanya tathmini ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya 2020;iv. Kuandaa Dira mpya ya Zanzibar ya 2050.v.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 27
Mradi wa Kuimarisha Utawala Bora Awamu ya Tatu
Mradi wa Uimarishaji Utawala Bora Awamu ya Tatu (ISPGG III) ni mradi unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ukiwa ni mkopo kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mradi huu umeanza kutekelezwa mwaka 2016 na unatarajiwa kukamilika mwaka 2019. Lengo kuu la mradi ni ukuzaji na uimarishaji masuala ya kifedha na kiuchumi kwa kujenga ufanisi na usimamizi wa fedha na uboreshaji wa mazingira ya kibiashara. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa kutumia jumla ya TZS 4.1 bilioni ambapo Serikali itatoa TZS 100 milioni na Washirika wa Maendeleo TZS 4.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuwapatia mafunzo wafanyakazi wa kada ya sheria;i. Kuajiri mshauri elekezi kwa ajili ya kazi ya kuandaa mkakati wa ii. sera ya sekta binafsi;Kuratibu shughuli za mradi ikiwemo vikao vya Kamati Tendaji;iii. Kuandaa matangazo nane (8) ya zabuni.iv.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuajiri mshauri elekezi wa kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu i. usimamizi wa muongozo wa mfumo wa upunguzaji majanga hatarishi;Kuimarisha sekta ya uwekezaji kwa kuiendeleza Mamlaka ya ii. Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA);Kuimarisha sekta ya viwanda katika Wizara ya Biashara na iii. Viwanda;Kuimarisha na kuijengea uwezo Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na iv. Uhujumu wa Uchumi Zanzibar (ZAECA); Kuimarisha na kuijengea uwezo Mamlaka ya Ununuzi na v. Uondoshaji Mali za Serikali Zanzibar (ZPPDA) na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG);Kusambaza na uwekaji wa mfumo wa usimamizi wa malipo ya vi. Serikali unaotumia huduma ya Epicor 10 kwa Serikali za Mitaa.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 28
Mradi wa Uimarishaji wa Rasilimali za Ndani na Usimamizi wa Maliasili
Mradi wa Uimarishaji wa Rasilimali za Ndani na Usimamizi wa Maliasili ni mradi unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ukiwa ni mkopo kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioanza mwaka 2017. Lengo kuu la mradi huu ni uimarishaji wa rasilimali za ndani na usimamizi wa mali asili. Taasisi zinazonufaika na mradi kwa upande wa Zanzibar ni Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) na Mamlaka ya Mapato, Zanzibar (TRA). Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 2.6 bilioni ambapo Serikali itatoa TZS 50 milioni na Washirika wa Maendeleo TZS 2.5 bilioni kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuratibu shughuli za mradi ikiwemo vikao vya Kamati Tendaji;i. Kuandaa mikutano na ujumbe wa AfDB;ii. Kuratibu shughuli za Kamati ya Tathmini za ununuzi.iii.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuimarisha mfumo wa usimamizi wa ulipaji kodi wa Bodi ya i. Mapato ya Zanzibar (ZRB); Kuimarisha Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati ii. Zanzibar (ZURA);Kujenga uwezo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa iii. kuwapatia mafunzo na vifaa vya ofisini.
Mradi wa Kuendeleza Bandari ya Mangapwani
Mradi huu ulianzishwa kwa lengo la kuimarisha na kuendeleza miundombinu ya barabara, umeme, maji katika eneo la bandari ya Mangapwani. Mradi huu kwa sasa unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee ambapo kiasi cha TZS 4.0 bilioni zimepangwa kutumika kwa mwaka 2019/20 kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 29
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuendelea na uwekaji wa miundombinu ya msingi ikiwemo barabara, i. maji na umeme;
Ukamilishaji wa upembuzi yakinifu wa bandari ya mafuta ii. Mangapwani.
11.3.1 Tume ya Mipango
Tume ya Mipango ya Zanzibar ni chombo cha juu cha kupanga, kuratibu na kusimamia mipango ya kiuchumi na kijamii. Aidha, chombo hiki kinashughulikia uratibu na upangaji wa vipaumbele vya Taifa, kuelekeza, kutoa miongozo na kusimamia masuala ya kiuchumi na mipango ya maendeleo. Kwa mwaka 2019/20, Tume ya Mipango imepanga kutekeleza programu moja na miradi mitatu ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 3.0 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali itatoa TZS 750 milioni na Washirika wa Maendeleo TZS 2.3 bilioni.
Programu ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania (MKURABITA)
Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za Wanyonge Tanzania umetayarishwa kwa madhumuni ya kuleta mabadiliko katika utendaji wa sekta isiyo rasmi Tanzania. Dhamira kuu ya mpango huu ni kurahisisha urasimishaji wa rasilimali na biashara zilizo katika mfumo usio rasmi ili kukidhi mahitaji ya kisheria na umiliki wa mali ndani ya mfumo wa uchumi wa kisasa. Sekta zinazohusika na mpango huu ni biashara na ardhi. Programu hii imepanga kutumia kiasi cha TZS 500 milioni kutoka Serikalini na TZS 168 milioni kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKutoa mafunzo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo katika Wilaya i. ya Magharibi B na Wete;Kutayarisha na kuchapisha hati katika maeneo yaliyotambuliwa;ii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 30
Ununuzi wa vifaa vya kutendea kazi;iii. Urasimishaji wa ardhi maeneo ya Migombani, Mbweni na Kidoti na iv. kumalizia eneo la Limbani;
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka Serikali ya Muungano
Kujenga uwezo kwa wafanyabiashara wadogo wadogo juu ya i. usimamizi na uendeshaji wa biashara kwa Unguja na Pemba;Kurasimisha ardhi katika maeneo ya Wawi, Konde na Mahonda;ii. Kuendelea na shughuli za uratibu wa mradi ikiwemo vikao vya iii. Kamati Kiongozi na Kamati ya Wataalamu.
Mradi wa Kupunguza Umasikini na Ufuatiliaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs)
Mradi umeanzishwa kwa lengo la kusaidia Serikali katika jitihada zake za kupambana na umasikini Zanzibar. Mradi umejikita katika kuandaa mikakati mbali mbali itakayosaidia nchi na wanachi wake katika kuibua na kutekeleza mipango na miradi mbali mbali itakayowawezesha kujikwamua na umasikini. Mradi huu unatekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 230 milioni ili kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuandaa dira mpya ya maendeleo ya Zanzibar ya mwaka 2050;i. Kufanya uchambuzi wa bajeti kwa programu na miradi ya maendeleo ii. inayotekelezwa Unguja na Pemba;Kutoa mafunzo kwa watendaji wa taasisi za Serikali juu ya uandaaji iii. wa Mpango Mkakati na Mpango wa utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo.
Mradi wa Kuoanisha Masuala ya Idadi ya Watu katika Afya ya Uzazi, Jinsia na Kupunguza Umasikini
Mradi huu una lengo la kuratibu utekelezaji wa masuala ya idadi ya watu kwa kuoanisha masuala ya afya ya uzazi, jinsia na umasikini katika
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 31
mipango ya maendeleo. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali na Washirika wa Maendeleo (UNFPA). Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 400 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuandaa ripoti ya uhusiano wa mgawanyiko wa idadi ya watu na i. maendeleo Zanzibar;Kushiriki katika uzinduzi wa ripoti ya idadi ya watu ya mwaka ii. 2019;Kutoa mafunzo, ufuatiliaji, uchapishaji na uhamasishaji wa daftari iii. la shehia;Kuandaa vikao vya kila robo mwaka vya wadau wa masuala ya idadi iv. ya watu Zanzibar;Kutoa mafunzo juu ya mfumo wa utoaji wa taarifa na tathmini kwa v. wajumbe wa shehia;Kununua vifaa vya ofisi na kuwajengea uwezo maafisa wa kitengo vi. cha idadi ya watu juu ya ufuatiliaji wa kazi za ofisi.
Mradi wa Uratibu na Usimamizi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) na MKUZA III
Mradi umeanzishwa kwa lengo la kujenga uwezo kwa taasisi za Serikali na zisizo za Kiserikali katika kusimamia utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, uratibu wa MKUZA III na namna ya kuandika na kutoa taarifa za programu na miradi ya maendeleo. Aidha, mradi huu umepanga kuimarisha mfumo wa takwimu Zanzibar kwa kuandaa mkakati, sera na kutoa mafunzo kwa wazalishaji na watumiaji wa takwimu. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 1.7 bilioni (TZS 20 milioni kutoka Serikalini na TZS 1.7 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 32
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuratibu shughuli za mradi.i.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kumwajiri mtaalamu elekezi kusimamia utekelezaji wa Malengo ya i. Maendeleo Endelevu;Kununua vifaa vya kitakwimu kwa taasisi za Serikali kwa ii. wanaoshughulika na takwimu;Kuandaa Mkakati wa Kuendeleza Takwimu na Sera ya Takwimu iii. Zanzibar;Kufanya kongamano la takwimu la mwaka juu ya uzalishaji na iv. utumiaji wa takwimu;Kutoa mafunzo kwa maafisa watano wa Ofisi ya Mtakwimu Mkuu v. wa Serikali juu ya uzalishaji na utumiaji wa takwimu;Kuandaa semina elekezi na uelewa wa utekelezaji wa Malengo ya vi. Maendeleo Endelevu (SDGs) kwa ngazi zote za jamii ikiwemo kwa viongozi wa dini, redio jamii na asasi zisizo za Serikali; Kuandaa vikao vya bodi na kamati ya pamoja ya watendaji wa vii. mradi;Kutoa mafunzo juu ya uratibu na usimamizi wa miradi kwa waratibu viii. wa mradi.
11.4 Wizara ya Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi
Sekta ya Kilimo inajumuisha sekta ndogo za mazao, mifugo, uvuvi na misitu. Sekta hii ni muhimu katika ukuaji wa uchumi wa Zanzibar na kuimarisha hali za wananchi walio wengi katika kupambana na umasikini na kuwapatia ajira. Kwa mwaka 2019/20, Wizara hii imepanga kutekeleza programu tano na miradi mitano ya maendeleo kwa gharama ya TZS 65.2 bilioni. Kati ya hizo Serikali imepanga kutoa TZS 4.9 bilioni na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 60.3 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 33
Programu ya Miundombinu ya Soko, Kuongeza Thamani na Misaada Vijijini (MIVARF)
Programu hii ina dhamira ya kueka mazingira endelevu ya upatikanaji wa masoko kwa mazao ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuwapatia wakulima njia sahihi za kuongeza thamani ya mazao na kuanzisha mfumo wa utoaji wa huduma za kifedha vijijini. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 399.6 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kujenga uwezo kwa wazalishaji kwa kuwapatia mafunzo kupitia i. Washauri Elekezi; Kufanya mikutano kwa wazalishaji, taasisi ndogo za kifedha na ii. SACCOS kwa ajili ya tathmini ya kazi za Washauri Elekezi.
Programu ya Umwagiliaji
Programu hii imeanzishwa kwa lengo la kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji ili kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga sambamaba na kuwajengea uwezo wa kitaalamu wakulima juu ya matumizi bora ya pembejeo za kilimo. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa jumla ya TZS 33.9 bilioni (TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini na TZS 32.9 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliUlipaji wa fidia ya mazao kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu i. ya umwagiliaji katika mabonde ya Chaani, Kinyasini, Kibokwa, Makwararani na Mlemele.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 34
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuanza ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika mabonde ya i. Chaani na Kinyasini kwa Unguja na Mlemele kwa Pemba.
Programu ya Kusaidia Kilimo na Uhakika wa Chakula (GAFSIP)
Programu hii ina lengo la kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga na mbegu bora kwa kuwapatia wakulima taaluma ya utumiaji wa technolojia na mbinu za kisasa kwa wakulima. Kwa mwaka 2019/20, programu imepangiwa jumla ya TZS 7.0 bilioni (TZS 80 milioni kutoka Serikalini na TZS 6.9 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali
Kulipa fidia kwa miti/mali wakati wa ujenzi wa miundombinu ya i. umwagiliaji katika skimu saba (Kibondemzungu, Koani, Mchangani, Bandamaji, Machigini, Dobi na Ole).
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kujenga miundombinu ya umwagiliaji katika skimu saba i. (Kibondemzungu, Koani, Mchangani, Bandamaji, Machigini, Dobi na Ole); Kutoa mafunzo ya mbinu bora za uzalishaji wa mpunga kwa ii. maafisa ugani 40 (20 Unguja na 20 Pemba);Kutoa mafunzo ya kilimo shadidi kwa wakulima kupitia iii. mashamba 50 ya mfano;Kutoa mafunzo kwa wakulima juu ya mbinu mchanganyiko za iv. kudhibiti wadudu na maradhi ya mimea;Kununua mbegu za mpunga tani 12 kwa ajili ya mpango wa v. ruzuku kwa wakulima.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 35
Programu ya Kuendeleza Miundombinu ya Mifugo na Wafugaji Wadogo Wadogo
Lengo la program hii ni kuendeleza sekta ya kilimo kwa kuendeleza miundombinu mbali mbali ya kilimo kwa ajili ya utafiti na kuongeza uzalishaji wa mazao ya sekta ya kilimo. Programu hii ina miradi miwili ifuatayo:Kuendeleza Miundombinu ya Mifugo na Wafugaji Wadogo Wadogo
Lengo la mradi huu ni kuimarisha miundombinu ya uzalishaji na masoko ya mifugo na bidhaa zake ili kuongeza kiwango cha uzalishaji na tija kwa wafugaji wadogo wadogo. Aidha, mradi unakusudia kuimarisha miundombinu ya kufanyia kazi za utafiti wa mashamba ya mifugo sambamba na kuwapatia elimu wafugaji wadogo wadogo juu ya uzalishaji bora. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuunga umeme katika shamba la mifugo Pangeni;i. Kufanya ukarabati wa ghala la kuhifadhia chakula cha akiba Tibirinzi ii. - Pemba;Kufanya ukarabati wa ghala la kuhifadhia mbegu, mbolea, mavuno iii. na pembejeo nyengine za kilimo katika maeneo ya Cheju, Kilombero, Donge na Bambi kwa Unguja, na Matangatuani, Weni na Mtambile kwa Pemba;Ukarabati wa maabara ya Agronomy-Matangatuani Pemba.iv.
Kuendeleza Utafiti wa Mifugo
Lengo la mradi huu ni kuijengea uwezo Taasisi ya Utafiti wa Mifugo kuweza kufanya tafiti kwa ufanisi zaidi ili kuweza kuongeza uzalishaji bora wa mifugo na bidhaa zake. Mradi unakusudia kuimarisha miundombinu ya utafiti wa kilimo. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.2 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 36
zifuatazo:-Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20
Ujenzi wa maabara tano za utafiti wa mifugo; i. Ujenzi wa kiwanda cha kati cha chakula cha mifugo; ii. Ujenzi wa ukuta katika Taasisi ya Utafiti wa Mifugo. iii.
Programu ya Kuimarisha Uvuvi
Programu hii ina dhamira ya kuendeleza uvuvi na kuongeza uzalishaji wa samaki na mazao ya baharini kwa njia ya ufugaji pamoja na kusimamia na kuhifadhi rasilimali za baharini kwa matumizi endelevu. Programu hii ina miradi miwili ifuatayo: Uimarishaji Uvuvi wa Bahari KuuLengo la mradi huu ni kuendeleza uvuvi wa kibiashara kwa kuimarisha ujenzi wa miundombinu ya uvuvi na kuwawezesha wavuvi kuvua katika kina cha maji marefu. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 14.6 bilioni (TZS 1.4 bilioni kutoka Serikalini na TZS 13.2 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliMchango wa Serikali wa asilimia saba katika ujenzi wa jengo la i. soko la Malindi.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Ujenzi wa jengo la soko la samaki Malindi.i.
Kuimarisha Ufugaji wa Mazao ya BahariniMradi una lengo la kuendeleza vikundi vya wafugaji wa samaki na mazao mengine ya baharini Unguja na Pemba ili kuweza kuongeza uzalishaji wa aina mbali mbali za samaki utakaoleta tija kwa haraka. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 892.4 milioni (TZS 200
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 37
milioni kutoka Serikalini na TZS 692.4 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali
Kuanzisha kituo cha kupokea vifaranga vya samaki, kaa na i. majongoo bahari eneo la Chokocho - Pemba.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kutengeneza mashamba ya mfano ya kufugia samaki, kaa na i. majongoo bahari eneo la Pujini-Pemba;
Kutoa mafunzo ya mbinu bora za ufugaji wa samaki, kaa na ii. majongoo bahari kwa wafugaji wa mazao ya baharini;
Kutoa mafunzo ya utengenezaji wa mashamba ya kufugia kaa, iii. samaki na majongoo bahari kwa vikundi vya ufugaji wa mazao ya baharini.
Mradi wa Usimamizi wa Shughuli za Uvuvi wa Kanda ya Kusini Mashariki mwa Bahari ya Hindi (SWIOFISH)
Mradi huu una lengo la kuimarisha na kusimamia uvuvi maalum uliopewa kipaumbele ambao utapelekea kuongezeka kipato kwa jamii inayojishughulisha na uvuvi huo. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 2.9 bilioni (TZS 50 milioni kutoka Serikalini na TZS 2.9 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuandaa vikao vya Kamati Tendaji na Kamati Kiongozi.i.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kujenga Ofisi ya Maabara ya Taasisi ya Uvuvi Maruhubi; i. Kuanza ujenzi wa chelezo Malindi; ii. Kutoa mafunzo kwa wavuvi juu ya uvuvi wa kipaumbele Unguja iii. na Pemba;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 38
Kuwasomesha wafanyakiv. azi 10 shahada ya uzamili (masters) na watatu shahada ya uzamivu (PhD) Kufanya mapitio ya Sheria ya Uvuviv. .
Mradi wa Kudhibiti Sumu Kuvu Inayotokana na Ulaji wa Mahindi na Njugu
Mradi huu una lengo la kuongeza taaluma na kuimarisha miundombinu na teknolojia kabla na baada ya mavuno ili kupunguza athari zinazotokana na sumu kuvu kwenye mahindi na njugu. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 988.4 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuimarisha na kusimamia teknolojia zinazotumika kabla na baada i. ya mavuno; Kufanya tathmini ya athari ya sumukuvu Unguja na Pemba;ii. Kutoa mafunzo kwa watendaji na wananchi juu ya kujikinga na iii. kudhibiti athari za sumukuvu; Kujenga uwezo kwa wafanyakazi juu ya kukinga na kudhibiti athari iv. za sumukuvu; Kufanya tathmini ya athari za kimazingira na kijamii juu ya v. uendelezaji wa miundombinu ya mradi.
Mradi wa Uhifadhi wa Misitu kwa Faida za Kiuchumi
Mradi huu una lengo la kutunza na kuendeleza rasilimali za misitu na kupunguza wimbi lisilo endelevu la bidhaa zinazotokana na misitu. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 228.2 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuanzisha mashamba yanayosimamiwa na jamii katika maeneo ya i. Mbuyuni, Makangale na Micheweni kwa Pemba na Pagali, Pwani Mchangani, Upenja na Kandwi kwa Unguja;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 39
Kuanzisha kilimo kinachohimili mabadiliko ya hali ya hewa Mahonda ii. na Makunduchi kwa Unguja na Chake Chake kwa Pemba;Kuaniii. zisha kilimo mseto kwa kutumia miti ya asili;Kupanda miti katika maeneo ya misitu ya juu na pwani yaliyoathirika iv. Donge Chechele, Pangatupu na Micheweni.
Mradi wa Kilimo cha Kushajihisha Ukulima wa Mboga na Matunda
Lengo la mradi huu ni kusaidia mnyororo wa thamani wa mazao mbali mbali ikiwemo mboga na mazao ya biashara. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 2.0 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kusaidia kuongeza uzalishaji wa mazao kwa kutoa pembejeo kwa i. wakulima; Kutoa mafunzo ya kilimo endelevu kwa wakulima;ii. Kutoa pembejeo za kilimo hasa kwa vijana na wanawake;iii. Kuboresha miundombinu na kupunguza upoteaji wa mazao baada iv. ya mavuno.
Mradi wa Kilimo Kinachohimili Mabadiliko ya Hali ya Hewa
Mradi huu una lengo la kuwapatia elimu wakulima juu ya utumiaji wa technolojia ya kisasa zinazohimili mabadiliko ya tabia ya nchi. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 44.4 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Uhamasishaji wa uanzishaji wa mashamba ya maonesho ya kilimo i. cha kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi;Kutoa mafunzo kwa wakulima kuhusiana na kilimo kinachohimili ii. mabadiliko ya tabianchi;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 40
Kuandaa mafunzo maalum kwa Chuo cha Kilimo Kizimbani iii. kuhusiana na kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi;Kufanya utafiti wa jinsia ilivyohamasika kutekeleza kilimo cha iv. mabadiliko ya tabianchi.
11.5 Wizara ya Biashara na Viwanda
Wizara ya Biashara na Viwanda malengo yake makubwa ni kukuza uchumi wa viwanda ili kuchochea mageuzi ya uchumi na kuleta maendeleo. Katika bajeti ya mwaka 2019/20, Wizara hii inatarajia kutekeleza programu na miradi ya maendeleo itakayosaidia kupunguza uagizaji wa bidhaa kutoka nje, kujenga mnyororo wa thamani, kuongeza ajira na kuongeza pato la taifa. Wizara imepanga kutekeleza programu mbili na miradi mitatu ya maendeleo kwa gharama ya TZS 8.0 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 4.6 bilioni na Washirika wa Maendeleo wanatarajiwa kuchangia TZS 3.4 bilioni.
Programu ya Mazingira Bora ya Biashara
Programu hii ina lengo la kutoa huduma za kuimarisha sekta ya biashara na kutoa msaada kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa nchini. Kwa mwaka 2019/20, programu hii inatarajia kutumia fedha za Serikali pekee na imepangiwa jumla ya TZS 200 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kufanya utafiti wa bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi;i. Kuendeleza mkakati wa “branding” awamu ya pili;ii. Ununuzi wa vifaa vya tamasha la biashara;iii. Kuimarisha mabaraza ya biashara ya Mikoa kwa kutoa mafunzo iv. kuhusiana na mikakati na kanuni za biashara.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 41
Programu ya Kuendeleza Viwanda
Katika kutekeleza programu ya viwanda, wakala wa kusimamia na kuendeleza viwanda vidogo vidogo na vya kati (SMIDA) ina jukumu la kuwalea wazalishaji kwa kuwapatia mafunzo na ushauri wa kitaalamu katika bidhaa zao. Programu hii inatekelezwa na Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20 imepangiwa jumla ya TZS 2.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kujenga uwezo kwa wazalishaji wa bidhaa ili kuwa na bidhaa i. bora;Kutoa mafunzo kwa wajasiriamali wanaojishughulisha na useremala, ii. ushoni na usarifu wa asali;Kuendeleza sekta ya uzalishaji dagaa kwa kutoa mafunzo ya iii. vifungashio;Kufanya usarifu wa zao la mwani kwa lengo la kuongeza thamani;iv. Kuimarisha uzalishaji chumvi kwa kutoa mafunzo juu ya uzalishaji v. chumvi yenye viwango vinavyokubalika kitaifa;Kuandaa Sheria ya Maendeleo ya Viwanda pamoja na Sera ya vi. Maendeleo ya Viwanda Vidogo Vidogo na vya Kati (MSMEs);Kuanzisha maeneo tengefu (Industrial Park) ya viwanda katika vii. maeneo ya Chamanangwe – Pemba na Dunga na Nungwi kwa Unguja;Kujenga Ofisi ya Makao Makuu ya SMIDA Maruhubi.viii.
Mradi wa Kuimarisha Taasisi ya Viwango ZanzibarViwango ni jambo muhimu katika kuongeza ushindani wa bidhaa zinazozalishwa nchini, Taasisi ya Viwango Zanzibar (ZBS) inasimamia ubora wa viwango vya bidhaa zote zinazoingizwa nchini na zile zinazotengenezwa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 2.0 bilioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 42
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuendelea na ujenzi wa ofisi na maabara ya Taasisi ya Viwango i. Zanzibar (ZBS).
Mradi wa Mfumo mpya wa Utoaji Leseni kwa Maendeleo ya Sekta Binafsi
Mradi huu una jukumu la kuweka taratibu na udhibiti wa utoaji leseni na kuimarisha usajili kwa njia ya kielektroniki ili kuwa na takwimu halisi za wafanyabiashara waliosajiliwa. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 400 milioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kuanzisha mfumo wa leseni utakaoratibiwa na kusimamiwa i. baina ya Baraza la Kusimamia Mfumo wa Utoaji Leseni Zanzibar (BLRC) na Taasisi nyengine zinazotoa Leseni;
Kufanya Utafiti wa Matokeo ya Mfumo wa Mageuzi ya Utoaji ii. Leseni.
Mradi wa Kuwasaidia Wajasiriamali Wadogo Wadogo
Mradi wa kuwasaidia wajasiriamali wadogo wadogo unakusudia kuwaunganisha pamoja na kuwapatia mafunzo ya vitendo wajasiriamali hao ili waweze kuendeleza biashara zao sambamba na kuwawezesha kwa kuwapatia mikopo. Mradi huu unafadhiliwa na Mfuko wa Maendeleo kutoka falme za Kiarabu katika kuwaendeleza wajasiriamali wadogo wadogo. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 3.4 bilioni kutoka Washirika wa Maendeleo kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa Mwaka 2019/20Kutoa mafunzo ya vitendo na mikopo kwa wajasiriamali wadogo i. wadogo Unguja na Pemba.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 43
11.6 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Sekta ya Elimu ni miongoni mwa sekta muhimu kwa Taifa lolote katika kuleta maendeleo ya kijamii, kiuchumi, na kisiasa. Kwa kuzingatia hilo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inahakikisha watoto, vijana na wazee wanapata fursa ya elimu kwa mujibu wa mahitaji. Sekta hii inatekeleza malengo iliyojipangia kwa kufuata Sera ya Elimu ya mwaka 2006 ambayo inalenga kufanikisha utekelezaji wa Dira ya Maendeleo 2020, malengo ya Taifa ya MKUZA III, pamoja na yale ya Kimataifa ya Malengo ya Maendeleo Endelevu (Sustainable Development Goals) ya 2015-2030. Kwa mwaka 2019/20, sekta ya elimu imepanga kutekeleza programu moja na miradi minne ya maendeleo yenye jumla ya TZS 73.4 bilioni ambapo Serikali imepanga kutoa TZS 5.8 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 67.6 bilioni.
Programu ya Miundombinu ya Elimu
Programu hii imeanzishwa kwa lengo la kuimarisha miundombinu ya sekta ya elimu kiujumla ili kuwawezesha wananchi kuweza kupata elimu bora na yenye kukidhi mahitaji yao. Programu inatekelezwa kwa kutumika fedha za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo jumla ya TZS 1.5 bilioni zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Ununuzi na ufungaji wa vifaa vya samani katika ukumbi wa mahafali i. wa Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA);
Kukamilisha madarasa 50 ya sekondari yaliyoanzishwa na wananchi ii. Unguja na Pemba.
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Maandalizi
Mradi huu umeanza mwaka 2009 ukiwa na lengo la kumuandaa mtoto katika ngazi ya maandalizi kabla ya kuanza elimu ya msingi. Mradi huu unatekelezwa na Washirika wa Maendeleo (GPE na UNICEF) ambapo jumla ya TZS 1.6 bilioni zimepangwa kutumika kwa utekelezaji wa shughuli za mwaka 2019/20 kama ifuatavyo:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 44
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kujenga madarasa 10 mapya ya maandalizi kwa kutumia mafundi i. wadogo wadogo;
Kukamilisha na kufanya ukarabati wa madarasa 400 ya maandalizi ii. na vituo vya TUTU;
Kuipitia na kuifanyia marekebisho mtaala wa mafunzo ya walimu iii. wa maandalizi;
Kutoa ruzuku kwa skuli 875 za maandalizi (TUTU, maandalizi na iv. jamii);
Kuanzisha vituo 20 vya TUTU katika Wilaya ya Kaskazini A, v. Magharibi A na B, Wete na Mkoani.
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Msingi
Lengo kuu la mradi wa umarishaji elimu ya msingi ni kutoa elimu bora kwa watoto wote wa Zanzibar kwa ngazi ya msingi. Mradi huu unatekelezwa na Washirika wa Maendeleo (GPE, UNICEF, SIDA, UNESCO na Jamuhuri ya Watu wa China) ambapo jumla ya TZS 6.9 bilioni zitatumika kwa utekelezaji wa shughuli za mwaka 2019/20 kama zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuendelea kuwapatia chakula wanafunzi katika skuli 27 za msingi;i.
Kuimarisha elimu ya msingi katika lugha ya kiingereza darasa la ii. kwanza hadi la sita;
Kutoa mafunzo ya hisabati kwa walimu wa darasa la kwanza na la iii. pili;
Kutoa mafunzo ya lugha kwa walimu wa darasa la tatu na la nne;iv.
Kuandaa vitabu mbalimbali vya kujifunza kusoma darasa la tatu na v. la nne;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 45
Kuzipatia zawadi skuli 100 zinazofanya vizuri katika mitihani ya vi. taifa ya darasa la sita;
Kutoa mafunzo kwa walimu wa msingi darasa la tano na la sita ya vii. kuwasaidia watoto wenye ufahamu mdogo;
Kuendelea na mafunzo ya walimu katika matumizi ya mfumo wa viii. utoaji wa taarifa maskulini (School Information System) katika kuweka takwimu za skuli;
Kuandaa na kuchapisha Ripoti ya Mwaka ya Takwimu;ix.
Kukamilisha mtaala na miongozo ya kusomeshea madarasa ya elimu x. mbadala;
Kutoa elimu ya ushauri nasaha juu ya udhalilishaji (ndoa za mapema, xi. mimba za utotoni, mapambano dhidi ya liwati, madawa ya kulevya na UKIMWI);Kupitia na kuandaa mtaala wa wanafunzi wa maandalizi na msingi xii. (Curriculum framework);Kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia vifaa;xiii.
Kukamilisha sera na miongozo ya elimu mjumuisho;xiv.
Kutathmini utekelezaji wa Mpango Mkuu wa Elimu kwa kufanya xv. kikao cha mwaka cha tathmini (AJESR).
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu ya Lazima
Lengo kuu la mradi wa umarishaji elimu ya lazima ni kuhakikisha kwamba Wazanzibari wote wanapata haki yao ya kupatiwa elimu na kupunguza umaskini. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo (BADEA, OPEC, KOREA, WB) ambapo jumla ya TZS 55.4 bilioni (TZS 3.3 bilioni za Serikali na TZS 52.1 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka 2019/20 kwa ajili ya kutekeza shughuli zifuatazo:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 46
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kuanza ujenzi wa skuli tatu za ghorofa katika maeneo ya Gamba, i. Mfenesini na Kifundi;
Kukamilisha ujenzi wa madarasa 50 yaliyoanzishwa na wananchi ii. Unguja na Pemba;
Kufanya ukarabati mkubwa katika skuli ya Ben-bella Unguja na iii. Madungu msingi kwa Pemba.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuwapatia mafunzo walimu 639 wa sanaa “art” wanaosomesha i. masomo ya hisabati na sayansi katika ngazi ya sekondari;
Kuzisaidia skuli gharama za kujiendesha na kuzipatia zawadi skuli ii. zinazofanya vizuri katika masomo yao (School Grant);
Kujenga skuli mbili za ghorofa za kisasa pamoja na kuzipatia samani iii. katika maeneo ya Mwanakwerekwe kwa Unguja na Wingwi kwa Pemba;
Kuendelea na ujenzi wa maabara (HUBS) katika skuli za iv. Regezamwendo, Uroa, Unguja Ukuu, Bwejuu, Mkwajuni, Kijini, Mahonda, Kitope, Chuini, Kisauni, Jang’ombe, Tumbatu, Mtonikigomeni kwa Unguja na Makangale, Mtambile, Kilindi, Pujini, Limbani, Kiuyu, Kojani, Kisiwapanza na Fundo kwa Pemba;
Kuufanyia mapitio na kuuandaa mfumo wa mitihani; v.
Kuanza ujenzi wa skuli tatu za ghorofa katika maeneo ya Gamba, vi. Mfenesini na Kifundi;
Kuimarisha mazingira ya skuli kwa kukamilisha ujenzi wa vyoo 100 vii. (67 Unguja na 33 Pemba);
Kuandaa vipindi mbalimbali vya redio na TV katika kituo cha Habari viii. cha Kwarara;
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 47
Kukipatia vifaa na kuwajengea uwezo maafisa katika uendeshaji wa ix. Kituo cha Habari cha Kwarara.
Mradi wa Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali - Awamu ya Pili (ALSD II)
Lengo kuu la mradi huu ambao utekelezaji wake ulianza mwaka 2012 ni kuwapatia vijana elimu ya vitendo ambayo itawawezesha kujiajiri wenyewe. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambapo kwa mwaka 2019/20 jumla ya TZS 8.0 bilioni (TZS 1.0 bilioni za Serikali na TZS 7.0 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kwa mwaka 2019/20 kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Ununuzi wa vifaa na samani kwa ajili ya vituo vya mafunzo ya amali i. vya Daya-Pemba na Makunduchi Unguja.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuendelea na ujenzi wa vituo vya mafunzo ya amali vya Daya – i. Pemba na Makunduchi - Unguja.
11.7 Wizara ya Afya
Sekta ya Afya ina jukumu la kuhakikisha kuwa Wazanzibari wote wanapata huduma bora za afya. Sekta hii inalenga kutekeleza lengo la MKUZA III la kuimarisha mifumo ya utoaji wa huduma za afya kwa kuzingatia makundi maalum ikiwa na shabaha ya kuimarisha uwezo wa sekta ya afya na taasisi zake juu ya upatikanaji wa huduma bora za afya. Kwa mwaka 2019/20, sekta ya afya imepanga kutekeleza programu nne na imepangiwa jumla ya TZS 34.1 bilioni ambapo Serikali imepanga kutoa TZS 17.9 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 16.2 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 48
Programu ya Kumaliza Maradhi ya Malaria Zanzibar
Program hii ina lengo la kupambana na maradhi ya malaria na kuhakikisha maradhi haya yanamalizika kabisa katika visiwa vya Unguja na Pemba. Aidha, programu hii inatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo (Global Fund) ambapo jumla ya TZS 5.4 bilioni (TZS 248 milioni kutoka Serikalini na TZS 5.2 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kwa mwaka 2019/20 kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kufanya ununuzi wa vitendanishi na vifaa vya uchunguzi wa i. vimelea vya malaria kwa njia ya darubini na vinasaba vya ugonjwa wa malaria;Kufanya mafunzo yaii. ugawaji wa dawa kwa maeneo yanayotoka wagonjwa wa malaria;Uchukuaji wa hatua za haraka za udhibiti hali ya ugonjwa wa malaria iii. na miripuko itokanayo na mbu zikiwemo upigaji dawa na ununuzi wa dawa.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuimarisha udhibiti wa mbu kwa kutia dawa ya kuua viluilui vya i. mazalio ya mbu katika vidimbwi;Kufanya ununuzi wa vifaa cha “Rapid Diagnostic Test” kwa ajili ii. kipimo cha haraka cha uchunguzi wa malaria;Kuimarisha mfumo wa manunuzi kwa kuwajengea uwezo maafisa iii. manunuzi na ugavi wa Wizara ya Afya;Kuimarisha mfumo wa kuripoti kesi za malaria kutoka vituoni.iv.
Program ya Kuimarisha Miundombinu ya Afya
Program hii ina lengo la kuimarisha huduma za afya zitolewazo nchini na inajumuisha miradi sita ifuatayo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 49
Mradi wa Kuipandisha Hadhi Hospitali ya Mnazi Mmoja
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuipandisha hadhi Hospitali ya Mnazi Mmoja kuwa ya rufaa kwa kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma za afya ili kuimarisha utoaji wa huduma katika hospitali hii zikiwemo huduma za afya ya mama na mtoto na kuimarisha huduma za matibabu ya uti wa mgongo na huduma za upasuaji wa maradhi mbali mbali. Mradi huu unatekelezwa na Serikali ambapo jumla ya TZS 2.6 bilioni zitatumika kwa mwaka 2019/20 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kukifanyia ukarabati chumba cha huduma za upasuaji katika hospital i. ya Mnazi Mmoja;Kufanya manunuzi ya vifaa mbali mbali vya utoaji wa huduma za ii. afya ikiwemo vifaa vya matibabu ya mifupa, moyo (ECHO), macho, machine ya ‘Carm’, vitanda vya upasuaji,’ cPAC machine’ pamoja na ‘operating microscope’;Kuendeleza ujenzi wa kituo cha afya cha daraja la kwanza Minazini iii. - Pemba.
Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa Binguni (Awamu ya Kwanza)
Mradi huu umeanza mwaka 2017, ukiwa na lengo la kujenga hospitali kuu ya rufaa kwa Zanzibar ambayo inatarajiwa kuwa hospitali kuu ya kufundishia kwa vitendo madaktari wetu ambao watakuwa mafunzoni. Mradi huu unatekelezwa na Serikali ambapo jumla ya TZS 6.5 bilioni zitatumika kwa utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kuanza awamu ya kwanza ya ujenzi wa hospitali ya rufaa i. Binguni;Kutoa mafunzo ya wafanyakazi kwa ajili ya matayarisho ya hospitali ii. mpya ya kisasa ya rufaa na kufundishia ya Binguni;Kufanya ununuzi wa vifaa vya Maabara ya Taasisi ya Tafiti za Afya iii. (ZAHRI).
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 50
Mradi wa Ujenzi wa Hospitali ya Wagonjwa wa Akili
Mradi huu umeanza mwaka 2017 ukiwa na lengo la kuimarisha huduma za afya ya akili nchini. Aidha, hospitali hii inatarajiwa kutumika katika kufundishia utoaji wa huduma za afya ya akili na kufanya tafiti za maradhi ya akili. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Chuo Kikuu cha Houkland - Uholanzi (Houkland University) ambapo jumla ya TZS 2.7 bilioni (TZS 1.3 bilioni za Serikali na TZS 1.4 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kwa mwaka 2019/20 kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali na Washirika wa Maendeleo
Kukamilisha ujenzi wa hospitali ya wagonjwa wa akili Kidongo i. Chekundu.
Mradi wa Kuzipandisha Hadhi Hospitali za Wilaya na Hospitali za Vijiji
Mradi huu umeanza mwaka 2011, ukiwa na lengo la kuzipandisha hadhi hospitali za Makunduchi, Kivunge na Wete kuwa za Mkoa na hospitali ya Micheweni kuwa ya Wilaya kwa ajili ya kuimarisha utoaji wa huduma za afya Unguja na Pemba. Mradi huu unatekelezwa na Serikali ambapo jumla ya TZS 4.2 bilioni zitatumika kwa mwaka 2019/20 kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kukamilisha ujenzi wa jengo jipya la wodi ya wanawake na watoto i. Kivunge na ununuzi wa vifaa tiba na samani;Kufanya ukarabati wa hospitali ya Wete;ii. Ujenzi wa nyumba za wafanyakazi katika hospitali ya Abdalla Mzee iii. na Kivunge;Ujenzi wa maabara katika hospitali ya Makunduchi;iv. Kuandaa Mpango Mkuu wa hospitali za Wilaya.v.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 51
Mradi wa Ujenzi wa Bohari Kuu ya Dawa- Pemba
Mradi huu umeanza mwaka 2018/19 ukiwa na lengo la kuondoa tatizo la uhaba wa dawa unaosababishwa na kuchelewa kupelekwa dawa kutokana na hali ya usafirishaji wa dawa Pemba. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu unatekelezwa na Serikali ambapo jumla ya TZS 1.0 bilioni zitatumika kwa utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kuendelea na ujenzi wa jengo la bohari kuu ya dawa Vitongoji. i.
Mradi wa Ujenzi wa Maabara ya Kisasa ya Mamlaka ya Dawa na Vipodozi Zanzibar
Mradi huu umeanzishwa ukiwa na lengo la kuimarisha uchunguzi wa ubora na usalama wa bidhaa za dawa na vipodozi ili kuepuka kusambaa kwa dawa zisizo na ubora na bandia katika soko la Zanzibar na Afrika ya Mashariki. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu unatekelezwa na Serikali ambapo jumla ya TZS 1.0 bilioni zitatumika kwa utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kuendelea na ujenzi wa maabara ya kisasa ya uchunguzi wa dawa, i. chakula na vipodozi Mombasa Unguja.
Programu ya Kudhibiti Maradhi ya UKIMWI, Homa ya Ini, Kifua Kikuu na Ukoma
Programu hii inajumuisha miradi ya kupambana na Ukimwi, kifua kikuu na ukoma. Lengo kuu ni kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kupunguza vifo vya maradhi ya kifua kikuu na kupunguza maambukizi ya ukoma. Aidha, programu hii inatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo (Global Fund) ambapo jumla ya TZS 5.3 bilioni (TZS 248 milioni za Serikali na TZS 5.1 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kwa mwaka 2019/20 kutekeleza shughuli zifuatazo:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 52
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali Kufanya mafunzo ya ushauri nasaha na upimaji wa VVU kwa i. wafanyakazi wa afya Pemba;Kufanya ununuzi wa dawa za matibabu ya wanaoishi na VVU na ii. UKIMWI;Ununuzi wa vifaa vya uchunguzi na dawa za matibabu ya kifua iii. kikuu na ukoma;Kuimarisha ubora wa takwimu za VVU, homa ya ini, kifua kikuu iv. na ukoma;Kuanzisha huduma za matibabu ya homa ya ini-Pemba;v. Kuanzisha huduma za chanjo ya homa ya ini B kwa makundi vi. maalum;Kukarabati Ofisi ya programu kwa upande wa Pemba ili kuweza vii. kupata ofisi za kuratibu huduma za kifua kikuu, ukoma na homa ya ini.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo:
Kufanya uhamasishaji katika jamii juu ya upimaji wa VVU na i. UKIMWI;Kupima VVU mama wajawazito pamoja na watoto wachanga ii. ambao mama zao wana mambukizi ya VVU na kuwapatia dawa kwa waliogundulika;Kutoa elimu ya kinga kwa jamii ikiwemo mikutano, matangazo na iii. vipeperushi;Kufanya upimaji wa kifua kikuuu kwa wagonjwa wa UKIMWI na iv. upimaji wa UKIMWI kwa wagonjwa wa kifua kikuu;Kukinga maambukizi ya VVU kwa watu wa makundi maalum;v. Kutoa huduma za kifua kikuu sugu.vi.
Programu Shirikishi ya Huduma za Afya ya Uzazi wa Mama na Mtoto
Programu hii ilianza mwaka 2012 kwa lengo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi pamoja na vifo vya watoto walio na umri chini ya miaka mitano. Programu hii inatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 53
ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo (UNFPA, WHO, UNICEF, JHPIEGO, D-TREE, ENGENDER) ambapo jumla ya TZS 5.3 bilioni (TZS 700 milioni za Serikali na TZS 4.6 bilioni za Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kwa mwaka 2019/20 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali
Kufanya matengenezo na ukarabati wa Ofisi ya programu Pemba;i. Kufanya ununuzi wa vifaa na mashine mbili za uchunguzi za ii. “ultrasound”;Kuimarisha mnyororo baridi na kufunga mtambo wa baridi wa ‘solar iii. system’;Kuanza ujenzi wa kituo cha kukusanyia damu Makunduchi.iv.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleo:
Kufanya uhakiki wa vifo vya wazazi na watoto wachanga;i. Kuimarisha utoaji elimu ya afya ya uzazi kwa vijana ikiwemo ujenzi ii. wa sehemu za kutolea huduma hizo;Kutoa mafunzo yanayohusiana na afya ya uzazi na watoto kwa iii. watendaji wa vituo vya afya;Kufanya mafunzo kwa wasimamizi wa watoa huduma wa kujitolea iv. vijijini;Kutoa huduma za mkoba katika jamii “Outreach service”; v. Kufanya mafunzo kwa watendaji juu ya huduma za kuharibika vi. mimba na huduma za uzazi wa mpango wa muda mrefu ikiwemo vipandikizi, kufunga kizazi nk;Kutoa mafunzo kwa wasimamizi na wanajamii wa afya;vii. Kuajiri mtaalamu wa kutengeneza mpango wa kudumisha fedha viii. kwa programu ya wanaojitolea wa afya ya jamii;Kufanya utafiti na tathmini ya mradi wa afya bora;ix. Kufanya mapitio ya muongozo wa vifo vya mama na mtoto.x.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 54
11.8 Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati
Wizara hii inajumuisha sekta ya ardhi, nyumba, maji na nishati. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Wizara hii imepanga kutekeleza jumla ya programu mbili na miradi mitatu ya maendeleo itakayogharimu kiasi cha TZS 144.1 bilioni. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 7.5 bilioni na Washirika wa Maendeleo TZS 136.6 bilioni. Shughuli za programu na miradi kwa fedha za SMZ na Washirika wa Maendeleo ni kama ifuatavyo:
Programu ya Kuimarisha Miundombinu ya Maji Mijini
Programu hii ina lengo la kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo ya mijini kwa kuendelea kutanua huduma ya maji katika maeneo mapya na kuimarisha mitandao katika maeneo ambayo huduma ya maji haipatikani vizuri. Programu hii inahusisha uchimbaji wa visima, ujenzi wa matangi, ununuzi wa mabomba na mashine za kusukumia maji. Kwa mwaka 2019/20 programu imepanga kutekeleza shughuli zake kupitia miradi minne kama ifuatavyo:
Mradi wa Uimarishaji wa Miundombinu ya Maji Mjini (JICA)
Mradi huu una lengo la kuimarisha miundombinu ya usambazaji wa maji safi na salama kwa maeneo ya mjini. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Japan kupitia JICA. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 4.5 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli zifuatazo.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Malipo ya mshauri elekezi kwa ajili ya usanifu wa mradi.i.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 55
Mradi wa Uimarishaji wa Miundombinu ya Maji na Usafi wa Mazingira wa Mkoa wa Mjini Magharibi (ADF12)
Mradi huu una lengo la kuimarisha huduma za upatikanaji wa maji safi na salama na miundombinu ya maji machafu katika Manispaa ya Mji wa Zanzibar. Mradi unatekelezwa kwa mashirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo (AfDB). Jumla ya TZS 9.4 bilioni (TZS 2.2 bilioni kutoka Serikalini na TZS 7.1 bilioni kutoka AfDB) zimepangwa kutekeleza shughuli mbali mbali katika mradi huu kama ifuatavyo: Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali
Ulipaji wa fidia katika maeneo yatakayoathirika na mradi;i. Malipo ya mshauri elekezi.ii.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Washirika wa Maendeleo
Kuendelea na ujenzi wa miundombinu ya usambazaji maji; i. Kuratibu shughuli za mradi.ii.
Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji Maji Zanzibar (INDIA)
Mradi wa Uhuishaji na Uimarishaji wa Mfumo wa Usambazaji Maji Zanzibar umeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa tatizo la maji katika maeneo ya Mjini linaondoka kabisa na wananchi wanaweza kupata maji safi na salama muda wote. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya India ambapo jumla ya TZS 89.1 bilioni (TZS 700 milioni kutoka Serikalini na TZS 88.4 bilioni kutoka India). Shughuli zilizopangwa kutekelezwa kwa mwaka 2019/20 ni kama ifuatavyo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliUlipaji wa fidia katika maeneo yatakayoathirika na mradii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 56
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Malipo ya Mshauri Elekezi kwa ajili ya usanifu wa mradi.i.
Mradi wa Uimarishaji wa Mfumo wa Maji Machafu kwa Mji wa Zanzibar
Mradi wa Uimarishaji wa Mfumo wa Maji Machafu unatarajiwa kuanza katika bajeti ya 2019/20 ukiwa na lengo la kuimarisha mfumo mzima wa maji machafu katika mji wa Zanzibar. Mradi huu utatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya India. Kwa mwaka 2019/20, fedha zilizotengwa kutekeleza shughuli za mradi huu ni kutoka Serikali ya India pekee ambapo jumla ya TZS 19.2 bilioni zinatarajiwa kutumika.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Malipo ya Mshauri Elekezi kwa ajili ya usanifu wa mradi;i. Kuanza shughuli za usambazaji maji na usafi wa mazingira. ii.
Programu ya Usambazaji Maji Vijijini
Programu hii ina lengo la kuimarisha huduma za usambazaji maji safi na salama katika maeneo ya vijijini ili kuweza kuimarisha huduma za usambazaji maji katika maeneo hayo. Kazi za usambazaji maji katika maeneo mbali mbali ya vijijini zitaendelea kwa kukamilisha miradi iliyoanza na kutanua huduma hiyo kwa maeneo mbali mbali ya vijijini Unguja na Pemba. Kwa mwaka 2019/20, programu imepanga kutekeleza shughuli zake kupitia miradi miwili kama ifuatavyo:
Mradi wa Kuendeleza Visima vya Ras el Khaimah
Mradi huu una lengo la kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama Zanzibar hususan kwa maeneo ya vijijini. Kwa sasa mradi huu unatekelezwa na Serikali pekee ambapo kwa mwaka 2019/20, umepanga kuviendeleza
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 57
visima 20 katika maeneo ya Kimara-Mtofaani, Chunga-Jangamizi, Fuoni-Kipungani, Mwera-Gudini, Mwachealale, Fuoni-Birikani, Bambi kwa Mchina, Kitogani, Dunga SS Mehta, Unguja Ukuu, Uzi, Bungi-Pangoni, Bumbwini, Mangapwani, na Kivunge Mwanzo Mgumu kwa Unguja, Penjewani, Mahuduthi, Kwapopo-Mtangani, Chanjaani-Shamiani na Kidongo kwa Pemba. Jumla ya TZS 3.0 bilioni zimepangwa kutumika katika utekelezaji wa shughuli mbali mbali za mradi zikiwemo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ununuzi na ulazaji wa mabomba;i. Ujenzi wa vibanda vya kuendeshea pampu; ii. Ununuzi na uwekaji wa pampu; iii. Uvutaji wa umeme. iv.
Mradi wa Uchimbaji wa Visima na Usambazaji Maji
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha huduma za usambazaji maji safi na salama katika maeneo ya Chaani, Donge, Kisongoni, Miwani na Kiboje. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China ambapo kwa mwaka 2019/20, jumla ya TZS 5.9 bilioni (TZS 863 milioni kutoka Serikalini na TZS 5.1 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika katika utekelezaji wa shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliUlipaji wa fidia katika maeneo yatakayoathirika na mradi;i. Ujenzi wa uzio kwa eneo la tangi la Bandamaji;ii. Ununuzi wa matangi mawili;iii. Ununuzi wa mita;iv. Uunganishaji wa mabomba madogo kwenda kwa wananchi.v.
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Ujenzi wa tangi la Bandamaji;i.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 58
Ulazaji wa mabomba kutoka Donge hadi Bandamaji.ii.
Mradi wa Usambazaji Umeme Vijijni
Mradi wa usambazaji umeme vijijini una lengo la kuvipatia huduma ya umeme vijiji mbalimbali vya Unguja na Pemba. Mradi huu unaendeleza juhudi za Serikali za kuvipatia huduma ya umeme vijiji na visiwa vidogo vidogo vyote viliopo Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, Serikali imepanga kutumia jumla ya TZS 650 milioni katika utekelezaji wa shughuli za mradi huu kama ifuatavyo:-Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20
Kuendelea na ujenzi wa laini kubwa na ndogo za umeme katika i. maeneo ya vijijini.
Mradi wa Kuijengea Uwezo Sekta ya Nishati
Mradi wa Kuijengea Uwezo Sekta ya Nishati unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Sweden kupitia SIDA. Lengo la mradi huu ni kuimarisha utekelezaji katika sekta ya nishati kwa kuzijengea uwezo taasisi zinazoshughulikia masuala ya nishati ikiwemo Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) na Idara ya Nishati na Madini. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 4.9 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuendelea na uandaaji wa mfumo mkuu wa kuhifadhi takwimu za i. nishati; Kuandaa Sheria ya Nishati ya Zanzibar na Mpango Mkuu wa ii. matumizi bora ya Nishati; Kuijengea uwezo Idara ya Nishati na Madini, Shirika la Umeme iii. Zanzibar (ZECO) na Idara ya Mipango, Sera na Utafiti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati; Kukamilisha mapitio ya Sera ya Nishati ya mwaka 2009.iv.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 59
Kukamilisha ununuzi wa mita za tukuza kwa Shirika la Umeme v. Zanzibar (ZECO)
Mradi wa Kujenga Uwezo na Matengenezo ya Miundombinu ya Umeme Zanzibar
Mradi huu una lengo la kujenga uwezo katika masuala ya kiufundi na kufanya matengenezo katika miundombinu ya umeme ili kuhakikisha upatikanaji na usambazaji wa umeme endelevu. Mradi huu unatekelezwa kwa msaada wa Serikali ya Norway na kwa mwaka 2019/20 umepangiwa jumla ya TZS 7.4 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20 i. Kubadilisha transfoma (LV Investment) - Unguja na Pemba; ii. Kubadilisha “transformer” kutoka 11kv kwa kuweka za 33kv; iii. Uvutaji wa line (triming); iv. Kupeleka umeme wa jua katika kisiwa cha Njau na Kokota.
11.9 Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji
Wizara hii ina jukumu la kusimamia sekta ya ujenzi, mawasiliano na usafirishaji. Sekta hizi ni miongoni mwa sekta kuu zinazochochea maendeleo ya sekta nyengine na ukuaji wa uchumi wa taifa. Kwa mwaka 2019/20, Wizara imepanga kutumia jumla ya TZS 115.6 bilioni (TZS 88.1 bilioni kutoka Serikalini na TZS 27.5 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) kwa utekelezaji wa program mbili na miradi miwili ya maendeleo.
Programu ya Ujenzi wa Barabara
Programu hii inahusisha ujenzi wa barabara mbalimbali Unguja na Pemba kwa kiwango cha lami. Programu hii inatekelezwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Washirika wa Maendeleo. Jumla ya TSZ 49.7 billioni (TZS 22.2 bilioni kutoka Serikalini na TZS 27.5 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo) zimepangwa kutumika kwa mwaka wa fedha 2019/20 kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa barabara zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 60
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za SerikaliKuendelea na hatua za ulipaji wa fidia Pujini Dodo hadi Kengeja;i.
Kukamilisha ujenzi wa barabara ya Ole – Kengeja kutoka Ukutini – ii. Kengeja (km 9);
Kuendelea na ulipaji fidia kwa barabara ya Koani-Jumbi (km 6.5);iii.
Kufanya tathmini ya ujenzi wa barabara ya Wete – Chake Chake iv. (km 22);
Kufanya tathmini pamoja na ujenzi wa barabara ya Bububu kituoni- v. Chuini (km 3);
Kuanza shughuli za upimaji, usafishaji na utayarishaji wa kitanda vi. cha barabara ya Jozani-Charawe – Ukongoroni.
Kukamilisha kazi ya upembuzi yakinifu kwa barabara ya Chake vii. Chake - Mkoani (km 43.5), Tunguu - Makunduchi (km 48) na Fumba –Kisauni (km 12).
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha Kutoka kwa Washirika wa Maendeleo
Kuendelea na uwekaji wa kifusi tabaka la kwanza na ujenzi wa i. makalvati Chambani - Ukutini pamoja na uwekaji wa lami na alama za barabarani kwa barabara ya Ole - Kengeja;
Usafishaji na uondoaji wa udongo, utayarishaji wa kitanda cha ii. barabara pamoja na utiaji wa lami kwa barabara ya Koani- Jumbi yenye urefu wa km 6.5;
Uwekaji wa kifusi tabaka la kwanza pamoja na ujenzi wa makalvati iii. kwa barabara ya Bububu-Mahonda-Mkokotoni.
Programu ya Kuimarisha Viwanja vya Ndege
Program hii ina lengo la kuimarisha miundombinu ya usafirishaji wa abiria na mizigo pamoja na huduma zinazotolewa katika viwanja vya ndege Unguja na Pemba. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa kiasi
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 61
cha TZS 61.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:- Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa kwa Fedha za Serikali
Kukamilisha ujenzi wa jengo jipya la abiria (Terminal III) kwa i. uwekaji wa miundombinu ya maji, umeme, vipozahewa, ngazi, lift, pamoja na uwekaji wa madaraja ya kupanda na kushukia ndege;Kuendelea na malipo ya msimamizi wa ujenzi wa jengo jipya la ii. abiria Terminal III;Kufanya tathmini pamoja na ulipaji wa fidia za vipando na iii. nyumba.
Mradi wa Ujenzi wa Bandari ya Mpigaduri
Mradi huu una lengo la kujenga bandari kubwa kwa ajili ya kuhudumia meli kubwa za mizigo ili kupunguza msongamano uliopo katika bandari ya sasa inayotoa huduma kwa abiria pamoja na mizigo ambayo hupelekea usumbufu na uchelewaji wa huduma za upakiaji na upakuaji wa mizigo. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 3.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:- Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20
Kukamilisha upembuzi yakinifu; i. Kuanza kwa shughuli za ujenzi.ii.
Mradi wa Ununuzi wa Boti (Land Craft)
Mradi huu una lengo la kurahisisha usafiri wa abiria na mizigo katika visiwa vidogo vidogo vya maeneo mbalimbali ya Zanzibar. Lengo hili linakwenda sambamba na malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Zanzibar awamu ya III (MKUZA III) ambayo yamedhamiria kuimarisha usafirishaji baina ya visiwa vidogo vidogo. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TSZ 1.9 bilioni, kutoka serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 62
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ununuzi wa boti tano za kuvushia wananchi katika visiwa vidogo i. vidogo Zanzibar (Fundo-Uvinje, Makoongwe, Kisiwa Panza, Kojani na Tumbatu).
11.10 Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto
Wizara hii inasimamia Idara na Taasisi ambazo zina jukumu la kutekeleza malengo ya Wizara ambayo ni pamoja na kusimamia utekelezaji wa sheria na kanuni za kazi, kuongeza na kutanua programu za wananchi kiuchumi pamoja na kuimarisha programu za maendeleo na hifadhi ya wanawake, wazee na watoto. Katika bajeti ya mwaka 2019/20, jumla ya TZS 2.1 bilioni zimepangwa kutekeleza programu moja na miradi minne ya maendeleo. Kati ya fedha hizo, Serikali imepanga kutoa TZS 1.0 bilioni na TZS 1.1 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo.
Programu ya Kuimarisha Jinsia
Programu hii imeanzishwa kwa lengo la kuimarisha usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake wa Zanzibar kiuchumi. Programu hii inatekelezwa kupitia miradi miwili ifuatayo:-
Usawa wa Kijinsia na Kuwawezesha Wanawake
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kukuza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake kiuchumi. Mradi unatekelezwa na Washirika wa Maendeleo (Shirika la Umoja wa Mataifa (UN-WOMEN)), ambapo kwa mwaka 2019/20 jumla ya TZS 245 milioni zimepangwa kutumika kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:- Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20
Watendaji wakuu kushiriki katika mikutano ya kimataifa kuhusu i. wanawake;Kufanya ufuatiliaji wa miradi Unguja na Pemba;ii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 63
Kuweiii. zesha utekelezaji wa mpango kazi wa kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji wa wanawake na watoto;
Kuimarisha ukusanyaji na upatikanaji wa takwimu za vitendo vya iv. udhalilishaji katika Wilaya zote Unguja na Pemba.
Mradi wa Jinsia
Mradi wa Jinsia umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha uwezo wa kitaifa katika kukuza uzingatiaji wa masuala ya kijinsia katika sera na mipango sambamba na kupambana na udhalilishaji wa kijinsia. Mradi unatekelezwa na Shirika la Kimataifa la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA). Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 420 milioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuratibu mikutano ya kila robo mwaka kwa viongozi wa dini;i. Kuratibu vikao vya Kamati ya Viongozi wa juu;ii. Kufanya maadhimisho ya harakati dhidi ya udhalilishaji;iii. Kufanya kazi na viongozi wa dini katika kupambana na iv. udhalilishaji;Kufanya shughuli za utawala na uendeshaji wa mradi.v.
Mradi wa Hifadhi ya Wazee
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha hali za wazee wanaoishi katika makaazi ya wazee yaliopo Unguja na Pemba yanaimarika pamoja na kuwapatia huduma zao za msingi kikamilifu. Mradi huu unatekelezwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na kwa mwaka 2019/20 umepangiwa jumla ya TZS 400 milioni kutoka Serikalini ili kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ujenzi wa ukuta katika nyumba za wazee Welezo;i. Ukarabati wa nyumba za wazee Sebleni;ii. Kufanya ununuzi wa vifaa na samani.iii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 64
Mradi wa Uhifadhi wa Haki za Watoto
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuhakikisha, katika ngazi ya kitaifa kunajengeka uwezo wa kutoa huduma za hifadhi ya mtoto kwa ufanisi mzuri sambamba na kuondoa masuala ya udhalilishaji wa watoto visiwani. Mradi unatekelezwa na Shirika la Watoto Duniani (UNICEF), ambapo umepangiwa jumla ya TZS 375 milioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Utekelezaji wa programu ya malezi ya dharura kwa watoto i. wanaohitaji matunzo;Kujenga uwezo kwa wadau juu ya kanuni na sheria za watoto;ii. Kuanzisha mfumo wa taarifa za hifadhi ya Watoto.iii.
Mradi wa Hifadhi ya Jamii
Mradi wa Hifadhi ya Jamii umeanzishwa ukiwa na lengo la kuhakikisha utekelezaji wa Sera ya Hifadhi ya Jamii unafanikiwa ipasavyo. Mradi umeanzishwa mwaka 2014 ambapo ulikuwa unatekelezwa kwa fedha za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, kwa sasa mradi huu unadhaminiwa na Washirika wa Maendeleo ambao ni Shirika la Watoto Duniani (UNICEF), na kwa mwaka 2019/20 umepangiwa jumla ya TZS 75 milioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kufanya mikutano ya uratibu ya kila robo mwaka;i. Kuwajengea uwezo maafisa wa ustawi wa jamii;ii. Kuandaa miongozo ya utekelezaji wa shughuli za hifadhi ya jamii;iii. Kuandaa mfumo wa taarifa kwa walengwa wa hifadhi ya jamii;iv. Kukamilisha mfumo wa pencheni jamii. v.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 65
Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kulea na Kutotolea Wajasiriamali (Incubator)
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kutoa fursa za ajira kwa vijana sambamba na kuwajengea uwezo wajasiriamali ili kupunguza umasikini Zanzibar. Aidha, mradi huu unatekelezwa kwa kutumika fedha za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo kwa mwaka 2019/20 jumla ya TZS 600 milioni zimepangwa kutumika kwa shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kujenga kituo cha kulea na kutotolea wajasiriamali Pemba.i.
11.11 Wizara ya Katiba na Sheria
Wizara ya Katiba na Sheria ina jukumu la kusimamia utekelezaji wa utawala wa sheria Zanzibar, na inahusisha Idara na Taasisi mbali mbali zinazosimamia haki na sheria, zikiwemo Mahakama, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, Ofisi ya Mufti wa Zanzibar na Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana. Kwa ujumla Taasisi hizi zina lengo la kuweka misingi bora ya kusimamia masuala yote ya kisheria Zanzibar. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Wizara imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo wenye jumla ya TZS 1.9 bilioni ambapo Serikali itachangia TZS 400 milioni na Washirika wa Maendeleo (UNDP) TZS 1.5 bilioni.
Mradi wa Usimamizi wa Upatikanaji wa Haki
Mradi huu una lengo la kuijengea uwezo wa kisheria jamii ya Wazanzibari na kuhakikisha upatikanaji wa haki nchini. Mradi huu unatekelezwa kwa mashirikiano baina ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na UNDP. Kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 400 milioni kutoka Serikalini na TZS 1.5 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo, kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 66
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/20 kwa fedha za SerikaliKutayarisha Sheria ya Msaada wa Kisheria kwa lugha nyepesi;i.
Kuandaa miongozo ya kufundishia wadau wa utoaji wa huduma ii. pamoja na kutayarisha miongozo ya utekelezaji wa sheria za msaada wa kisheria;
Kuanzisha daftari la watoa msaada wa kisheria;iii.
Kuimarisha uratibu masuala ya katiba, sheria na haki za binaadamu iv. na sekta ya sheria Wizarani.
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/20 kwa fedha za Washirika wa Maendeleo
Kuratibu na kusimamia masuala ya sheria na upatikanaji wa haki i. kwa ufanisi; Kuweka misingi imara ya usimamizi wa huduma za msaada wa ii. kisheria;Kutekeleza shughuli zitakazopelekea kuwa na mfumo imara wa iii. uendeshaji kesi mahkamani;Kutoa huduma za kisheria kwa ufanisi;iv. Kuendeleza sekta ya haki za jinai katika uendeshaji wa mashtaka. v.
11.12 Ofisi ya Rais - Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Ofisi hii ina jukumu la kusimamia masuala yote yanayohusiana na utawala bora ikiwemo kuhakikisha kuwepo kwa uadilifu, uwazi pamoja na uwajibikaji katika utendaji wa shughuli za kiutumishi, pamoja na kuratibu na kuimarisha utendaji wa watumishi wa umma. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Ofisi imepanga kutekeleza programu moja na mradi mmoja wa maendeleo yenye jumla ya TZS 2.8 bilioni ambapo Serikali itatoa TZS 300 milioni na Washirika wa Maendeleo TZS 2.5 bilioni.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 67
Programu ya Mageuzi ya Sekta ya Utumishi wa Umma Zanzibar Awamu ya II (ZPSRP)
Programu hii ina azma ya kuimarisha utendaji na uwajibikaji wa Taasisi za umma ikiwemo miundo, mifumo ya utoaji huduma bora zenye ufanisi pamoja na uadilifu kwa watu wa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa jumla ya TZS 200 milioni kutoka Serikalini na jumla ya TZS 2.5 bilioni kutoka kwa Washirika wa Maendeleo (Benki ya Dunia), kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/20 kwa fedha za SerikaliKupitia sera, sheria na kanuni za utumishi wa umma; i.
Kuimarisha utekelezaji wa Mpango wa Sera ya Malipo;ii.
Kuanzisha mkataba wa utendaji kwa maafisa watendaji wakuu wa iii. Idara na kufanya ukaguzi wa wafanyakazi kuhusiana na malipo;
Kuimarisha usimamizi na kufanya tathmini ya mpango kazi wa iv. mkakati wa mageuzi ya sekta ya utumishi wa umma.
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/20 kwa fedha za Washirika wa Maendeleo
Kuanzisha miongozo ya utayarishaji na utunzaji wa kumbukumbu i. za watumishi wa umma;
Kutanua mfumo muafaka wa vitendea kazi katika kuimarisha ii. uwajibikaji na utoaji wa huduma;
Kuimarisha mapitio ya majukumu kupitia Wizara na Idara za iii. Serikali na kupeleka katika Taasisi za Umma zinazojitegemea na wakala wa Serikali;
Kuimarisha miundo itakayowezesha Wizara, Idara, Mashirika iv. pamoja na Serikali za Mitaa kufanya kazi kwa ufanisi na tija.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 68
Mradi wa Zanzibar E - government Optical Transmission Communication Network Phase - II
Mradi huu una lengo la kukuza ufanisi katika matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano nchini na utoaji huduma za Serikali kwa wananchi. Aidha, Ofisi ya Serikali Mtandao ina wajibu wa kuandaa na kusimamia miongozo ya utoaji na upatikanaji wa huduma bora za Serikali mtandao kwa wananchi wa Zanzibar. Mradi huu katika awamu ya pili umeanza kutekelezwa mwaka 2018, na kwa mwaka 2019/20, umepangiwa jumla ya TZS 100 milioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/20.Kukamilisha utengenezaji wa tovuti kuu ya Serikali “Government i. Portal”;
Kujenga uelewa juu ya matumizi ya tovuti kuu ya Serikali;ii.
Kuweka mfumo wa usajili wa taarifa za mali na madeni kwa viongozi iii. wa umma katika Tume ya Maadili - Pemba.
11.12.1 Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi
Ofisi hii ina jukumu la kuhakikisha Zanzibar inapambana na inazuia vitendo vyote vya rushwa na uhujumu Uchumi. Lengo kuu ni kupata mafanikio endelevu ya kiuchumi na kijamii Zanzibar. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Ofisi imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo kwa gharama ya TZS 800 milioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya ZAECA
Mradi huu umeanzishwa mwaka 2018 kwa lengo la kuhakikisha Ofisi za Serikali zinapata majengo mazuri, ili kuweka mazingira bora ya kazi kwa wafanyakazi pamoja na kuimarisha utendaji wa kazi zao. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 800 milioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo-:
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 69
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/20.Kuanza ujenzi wa Ofisi ya Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu i. Uchumi.
11.13 Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale
Jukumu la Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale ni kusimamia mambo makuu matatu ambayo ni habari, utalii na mambo ya kale. Kwa mwaka 2019/20, Wizara inatarajia kutekeleza programu moja na mradi mmoja wa maendeleo itakayosaidia kutoa huduma bora katika sekta ya habari na kuongeza vivutio vya utalii katika sekta ya utalii na mambo ya kale. Wizara imepanga kutekeleza programu na mradi huo wa maendeleo kwa gharama ya TZS 3.9 bilioni kutoka Serikali.
Programu Mjumuisho ya Kuendeleza Utalii
Utalii ni sekta muhimu ambayo inakua kwa kasi ambapo hutoa fursa za ajira na kuongeza pato la taifa sambamba na kuitangaza nchi yetu katika mataifa tofauti nchi za nje. Kwa mwaka 2019/20, programu hii inatarajia kutumia kiasi cha TZS 2.4 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuimarisha na kuendeleza maeneo ya kihistoria ya Fukuchani na i. Mwinyi Mkuu kwa Unguja na eneo la Mkamandume kwa Pemba.
Ujenzi wa Jengo la Ofisi na Studio za Redio Mkanjuni - PembaLengo la mradi huu ni kuimarisha upatikanaji na usambazaji wa habari kwa kufanya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya ofisi na studio Mkanjuni Pemba. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.5 bilioni kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuendelea na ujenzi wa ofisi na studio za redio Mkanjuni, Pemba.i.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 70
11.13.1 Kamisheni ya Utalii
Jukumu la msingi la Kamisheni ya Utalii ni kusimamia na kuratibu shughuli za utalii pamoja na kuwahamasisha wananchi juu ya dhana ya utalii kwa wote. Kwa mwaka 2019/20, kamisheni ya utalii inakusudia kutekeleza mradi wa kuimarisha utalii kwa wote utakaogharimu kiasi cha TZS 1.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Kuimarisha Utalii kwa Wote
Lengo la mradi huu ni kuhakikisha kila mwananchi ananufaika na matunda ya utalii na anashiriki katika kutunza na kuendeleza utalii huo sambamba na kuimarisha huduma na vivutio kwa watalii. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa kiasi cha TZS 1.5 bilioni, kutoka Serikalini kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kujenga vivutio vyengine katika eneo la Kwa Bikhole, vikiwemo i. nyumba za sanaa (art gallery) pamoja na mgahawa (food cort and aroma center);Kuendeleza miundombinu ya utoaji wa huduma ikiwemo barabara, ii. maji na umeme;Kujenga maegesho ya boti (marina).iii.
11.14 Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo katika bajeti ya mwaka 2019/20 inakusudia kutekeleza programu moja na mradi mmoja wa maendeleo itakayosaidia kuondoa changamoto zilizopo katika sekta ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo. Wizara hii imepangiwa jumla ya TZS 4.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 71
Programu ya Ajira kwa Vijana.
Programu imeanzishwa mwaka 2018, ikiwa na malengo ya kuweka mazingira mazuri na endelevu kwa vijana ili kuwawezesha kujiimarisha kiuchumi, kiutamaduni na kijamii sambamba na kuwakinga vijana wasiingie katika vikundi viovu na biashara haramu. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 2.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli zilizopangwa kutekelezwa 2019/2020Kuimarisha kilimo cha mboga, matunda, ufugaji na uvuvi;i.
Kuendeleza programu maalum ya mafunzo kazi kwa vijana ii. waliohitimu elimu ya sekondari hadi vyuo vikuu;
Kuendeleza vipaji vya michezo kwa vijana;iii.
Kuanzisha na kuendeleza viwanda vidogo vidogo vya uchongaji, iv. usarifu wa mbao na vyuma;
Kuimarisha vikundi vya ushonaji kwa kuwapatia vifaa na mafunzo;v.
Mradi wa Uimarishaji wa Viwanja vya Michezo
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kuwa na viwanja vya michezo vyenye hadhi ya Kitaifa ambavyo vitaweza kusaidia kuimarisha na kuinua kiwango cha michezo Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, mradi huu umepangiwa jumla ya TZS 2.0 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuendeleza miundombinu ya michezo ikiwemo uwekaji wa nyasi i. bandia katika uwanja wa Amani na Kitogani.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 72
11.15 Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ
Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ ni Ofisi iliyopewa mamlaka kwa utawala wa mikoa, usimamizi wa mamlaka za Serikali za mitaa ikiwemo ugatuzi, Idara maalum za SMZ na usajili wa vitambulisho kwa kutoa huduma bora kwa jamii, kudumisha amani na usalama. Kwa mwaka wa fedha 2019/20, Wizara hii imepanga kutekeleza programu moja na miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 12.6 bilioni kutoka Serikalini.
Programu ya Ugatuzi wa Masuala ya Elimu
Programu hii imeweka utaratibu wa kutekeleza ugatuzi katika masuala ya elimu hatua kwa hatua kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kupeleka madaraka katika Serikali za Mitaa. Kwa mwaka 2019/20, programu hii imepangiwa kiasi cha TZS 1.1 bilioni kutoka Serikalini kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ujenzi wa skuli za maandalizi ya Ng’ombeni Mkoani Pemba na i. Fuoni Kitongani Unguja;
Ujenzi wa madarasa 60 yaliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi.ii.
Mradi wa Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya Ulinzi
Mradi wa Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya Ulinzi una lengo la kuimarisha ulinzi kwa kufikiwa viwango vya kimataifa ili kuweka mazingira salama kwa wananchi na wageni wakiwemo watalii katika maeneo mbali mbali ya Mji wa Zanzibar. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali na kwa mwaka 2019/20 umepangiwa kiasi cha TZS 7.0 bilioni kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 73
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuendelea na kazi za uwekaji wa vifaa vya ulinzi na usalama.i.
Mradi wa Ujenzi wa Kiwanda cha Ushoni (ZQTL)
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa mavazi ya askari kwa kushona sare za maaskari pamoja na nguo za kibiashara. Ili kuwa na ufanisi mzuri kiwanda kinahitaji kupatiwa vifaa bora ambavyo vitaendana na mfumo wa viwanda vya aina hii. Mradi unatekelezwa kwa kutumia fedha za Serikali na kwa mwaka 2019/20, umepangiwa jumla ya TZS 4.5 bilioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20
Ujenzi wa ukuta wa kiwanda cha ushoni na kiwanda cha viatu;i. Ununuzi wa vifaa vya ujenzi na zana;ii. Ununuzi wa sare za maaskari.iii.
11.15.1 Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM)
Kikosi hichi ni miongoni mwa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulikia masuala yote ya ulinzi wa baharini na nchi kavu ili kudhibiti biashara haramu ya magendo kwa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, Kikosi hiki kimepanga kutekeleza miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 3.9 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Kuimarisha Huduma za Uzamiaji na Uokozi
Mradi huu umeanzishwa kwa lengo la kukabiliana na maafa ya baharini katika ukanda wa bahari ya hindi Unguja na Pemba yanayosababishwa na majanga ya kuzama kwa meli za abiria na mizigo na vyombo vyengine vya usafiri wa baharini. Mradi unatekelezwa kupitia fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20, umepangiwa jumla ya TZS 2.9 bilioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 74
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ununuzi wa “decompression chamber” (scuba hospital - chumba i. cha huduma za uzamiaji); Ununuzi wa boti ya uzamiaji na vifaa vyake. ii.
Mradi wa Ujenzi na Ukarabati wa Kambi na Nyumba za KMKM
Mradi wa Ujenzi na Ukarabati wa Kambi na Nyumba za KMKM ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20, mradi umetengewa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kuanza ujenzi wa chuo cha KMKM – Kama.i.
11.15.2 Kikosi cha Valantia
Kikosi hichi ni miongoni mwa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulika kutoa huduma ya ulinzi na wakati wa majanga. Kwa mwaka 2019/20, Kikosi kimepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 500 milioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba na Mahanga ya Maaskari
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba na Mahanga ya Maaskari wa Kikosi cha Valantia, ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha kuwa Idara Maalum za SMZ zinapata majengo mazuri ili kuimarisha utendaji wa kazi kwa wanafanyakazi wake. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee. Kwa mwaka 2019/20, mradi umetengewa kiasi cha TZS 500 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ujenzi wa ofisi katika kambi ya Kikungwi;i. Ujenzi wa nyumba za maofisa Chake - Chake Pemba.ii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 75
11.15.3 Chuo cha Mafunzo
Chuo cha Mafunzo kimeanzishwa kwa lengo la kuwapokea, kuwahifadhi, kuwalinda na kuwarekebisha wananchi wanaofanya makosa mbali mbali na kupatiwa vifungo hapa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, chuo kimepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu jumla ya TZS 1.0 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Makaazi na Mahanga
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba za Makaazi na Mahanga kwa Chuo cha Mafunzo ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee, na umepanga kujenga majengo mapya na kukarabati majengo chakavu. Kwa mwaka 2019/20, mradi umetengewa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Ujenzi wa mahanga katika kambi ya Wete na Kangagani Pemba.i.
11.15.4 Jeshi la Kujenga Uchumi
Kikosi hichi ni miongoni mwa Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulikia masuala ya ulinzi na ujenzi wa uchumi kwa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, Kikosi hiki kimepanga kutekeleza miradi miwili ya maendeleo itakayogharimu jumla ya TZS 3.5 bilioni kutoka Serikalini.
Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Sekondari na Ufundi ya JKU – Mtoni
Mradi wa Ujenzi wa Skuli ya Sekondari na Ufundi katika Kambi ya JKU Mtoni una lengo la kuwapatia vijana elimu katika fani mbali mbali. Mradi huu, unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20, mradi umepangiwa jumla ya TZS 2.5 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 76
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kujenga jengo la ghorofa tatu la chuo cha ufundi JKU Mtoni.i.
Mradi wa Ujenzi wa Nyumba na Mahanga ya Kambi za JKU
Mradi wa Ujenzi wa Majengo ya Kambi za JKU umeanzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa kuanzia umepanga kutekeleza shughuli zake katika kambi za Pemba. Kwa mwaka 2019/20, mradi umetengewa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kujenga majengo matatu kwa ajili ya vijana watakaojiunga na JKU i. katika kambi ya Msaani Pemba.
11.15.5 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi
Kikosi cha Zimamoto na Uokozi ni miongoni mwa Idara maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kinachoshughulikia shughuli zote za uzimaji moto na uokozi wa mali na ulinzi wa raia. Kwa mwaka 2019/20, Kikosi hiki kimepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu kiasi cha TZS 500 milioni. Mradi wa Ujenzi wa Mahanga na Nyumba za MaaskariMradi wa Ujenzi wa Mahanga na Nyumba za Maaskari katika Kikosi cha Zimamoto na Uokozi ulianzishwa kwa lengo la kutekeleza azma ya Serikali ya kuhakikisha watendaji wa Idara Maalum za SMZ wanafanya kazi zao katika mazingira mazuri. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali pekee na kwa mwaka 2019/20, mradi umetengewa kiasi cha TZS 500 milioni kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kukamilisha ujenzi wa kituo cha ghorofa mbili Kijichame;i. Kuanza ujenzi wa kituo cha ghorofa moja Wete.ii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 77
11.15.6 Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar
Ofisi ya Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar ina jukumu la kuimarisha mifumo ya usajili wa taarifa za vizazi, vifo, ndoa, talaka na vitambulisho hapa Zanzibar. Kwa mwaka 2019/20, Ofisi imepanga kutekeleza mradi mmoja wa maendeleo utakaogharimu kiasi cha TZS 1.0 bilioni zinazotarajiwa kutolewa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mradi wa Kuimarisha Mfumo wa UsajiliMradi huu unatarajiwa umeanzishwa kwa lengo la kuimarisha taarifa na usalama wa mfumo wa usajili. Mradi huu unatekelezwa kwa fedha za Serikali ambapo kwa mwaka 2019/20 umepangiwa kiasi cha TZS 1.0 bilioni kwa ajili ya kutekeleza shughuli zifuatazo:-
Shughuli Zilizopangwa Kutekelezwa 2019/20Kufanya i. mnunuzi wa majenereta kwa vituo vya Kianga, Mazizini na Gamba;
Kuanza ujenzi wa uzio katika vituo vya usajili katika Wilaya ya ii. Mjini, Magharibi A na B, Kusini, Kati, Wete, Micheweni, Mkoani na Chake-Chake;
Kuanza ujenzi wa vituo viwili vya usajili Kaskazini B Unguja na iii. Wete Pemba.
12.0 PROGRAMU/MIRADI YA MAENDELEO CHINI YA MFUKO WA MIUNDOMBINU (INFRASTRUCTURE FUND)
Mfuko wa Miundombinu ni mfuko maalum ulioanzishwa mwaka 2015 chini ya kifungu nambari 11 cha Sheria ya Fedha za Umma ya mwaka 2005 kwa ajili ya kusaidia uimarishaji wa miundombinu. Mfuko huu ulianza kazi zake rasmi tarehe 1 Julai 2015. Mfuko wa miundombinu unalenga kukusanya rasimali kutoka katika kodi za miundombinu na katika vyanzo vyengine kwa lengo la kusaidia maendeleo ya Zanzibar. Aidha, rasilimali za mfuko huu zinatolewa kwa lengo kuu la kuwekeza katika miundombinu ya umma ili kusaidia kunyanyua uchumi na maendeleo ya jamii.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 78
Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo unaendelea kupata fungu kutoka mfuko huo ambapo kwa mwaka 2019/20 jumla ya TZS 41.0 bilioni zimepangwa kutumika katika kugharamia utekelezaji wa programu na miradi ya maendeleo. Hii ni ongezeko la TZS 1.55 bilioni ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2018/19 ambapo jumla ya TZS 39.45 bilioni zilitengwa kugharamia miradi 12 ya maendeleo.
Kwa mwaka 2019/20 jumla ya programu tano zimepangwa kutumia fedha za mfuko wa miundombinu kupitia maeneo yake ambazo ni:-
Programu ya Upatikanaji wa Rasilimali Fedha;i)
Programu ya Kuimarisha Uvuvi (Ujenzi wa Soko la Malindi); ii)
Programu ya Kuimarisha Miundombinu ya Afya (Ujenzi wa hospital iii) ya Binguni);
Programu ya Usambazaji Maji Vijijini (Uendelezaji wa Visima vya iv) Ras el Khaimah); na
Programu ya Ujenzi wa Barabara (Ujenzi wa Barabara za Chake v) Chake – Wete na Ole – Kengeja).
Kwa upande wa miradi jumla ya miradi 11 imepangwa kupatiwa fedha hizo kutoka Mfuko wa Miundombini ni;
Ujenzi wa Nyumba ya Makamo wa Pili wa Rais; i)
Kuimarisha Taasisi ya Viwango Zanzibar; ii)
Uimarishaji wa Elimu Mbadala na Amali (II); iii)
Usambazaji Umeme Vijijini; iv)
Ununuzi wa “Land Crafts”; v)
Uwekaji wa Kamera na Vifaa vya Ulinzi; vi)
Ujenzi wa Kiwanda cha Nguo (ZQTL) (Ununuzi wa vifaa na vii) malighafi);
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 79
Ujenzi wa Viwanja vya Michezo vya Wilaya; viii)
Kuimarisha Huduma za Uzamiaji na Uokozi; ix)
Kuimarisha Utalii kwa Wote; na x)
Ujenzi wa Ofisi za ZAECA.xi)
Mchanganuo wa mgawanyo wa fedha kwa programu na miradi ya maendeleo inayopatiwa fedha kupitia Mfuko wa Miundombinu kiwizara unaonekana katika kiambatisho nambari 3.
13.0 UFUATILIAJI NA TATHMINI
Kwa mwaka 2019/20, Serikali kupitia Tume ya Mipango Zanzibar imepanga kusimamia masuala ya Ufuatiliaji na Tathmini ya Mpango wa Maendeleo kupitia maeneo yafuatayo:-
Kushirikiana na sekta katika kuandaa Mfumo wa Ufuatiliaji na i. Tathmini (M & E System) kwa miradi ya maendeleo ikiwemo kutayarisha mpango unaozingatia matokeo, unaohusisha kuwepo malengo makuu (goals), matokeo ya muda wa kati (outcome), na muda mfupi (output), shabaha (targets) na viashiria vitakavyotumika kupima matokeo hayo;
Kufanya ufuatiliaji na tathmini kwa programu na miradi mbali mbali ii. ya maendeleo;
Kuendeleza kazi na utaratibu wa kupima matokeo juu ya utekelezaji iii. wa shughuli za programu na miradi ya maendeleo.
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 80
14.0 WASHIRIKA WA MAENDELEO
Washirika watakaochangia bajeti ya maendeleo kwa mwaka 2019/20 ni pamoja na ACRA, AfDB, BADEA, BASKET FUND, CHINA, DFID, EDF-EU, EXIM BANK, FAO, GEF, GLOBAL FUND, GPE, INDIA, IFAD, IMF, OPEC, JAPAN, JICA, KHALIFA FUND, KOREA, NORWAY, OFID, PMI, SAUDI FUND, SIDA, THPS, UK, UNDP, UNFPA, UNESCO, UNICEF, URT, USDA-USAID, UN-WOMEN na WORLD BANK.
15.0 HITIMISHO Utayarishaji wa Kitabu cha Pili cha Mwelekeo wa hali ya uchumi mwaka 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 umeshirikisha wadau mbali mbali wakiwemo Wizara, Taasisi za Serikali, Washirika wa Maendeleo na Asasi za Kiraia. Hivyo, kazi zilizoainishwa ndani ya kitabu hiki zinatarajiwa kutekelezwa na wadau wote ili kuweza kupata mafanikio ya kukuza uchumi na kupunguza umaskini ikiwa ni hatua ya kufikia Dira ya Maendeleo ya 2020.
Wizara, Idara na Taasisi za Serikali zinatakiwa kutoa Taarifa za utekelezaji wa kazi zilizoainishwa katika kitabu hiki wiki ya pili ya kila robo mwaka (2019/20) na kuziwasilisha Tume ya Mipango Zanzibar bila ya kuchelewa. Aidha, taarifa za matumizi ya fedha ziwasilishwe kwa usahihi zikiwemo za Serikali na Washirika wa Maendeleo
Mashirikiano makubwa yanahitajika kwa Wizara na Taasisi za Serikali katika kufanikisha malengo yetu. Aidha, sekta binafsi na asasi za kiraia zinahitaji kuwa na mikakati maalum inayoendana na Mipango mikuu ya nchi ili kuungana na juhudi za Serikali na kuweza kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kurasa zifuatazo zina viambatisho ambavyo vinaonesha mgawanyo wa fedha za Programu na Miradi ya Maendeleo Kiwizara (Kiambatisho nam. 1), kimaeneo makuu ya matokeo (Kiambatisho nam. 2) na programu/miradi inayopatiwa fedha kutoka Mfuko wa Miundombinu (Kiambatisho nam.3).
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 81
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 82
v)
Mra
di w
a K
uend
elez
a B
anda
ri ya
Man
gapw
ani
4,20
0,00
0 4,
000,
000
4
,000
,000
4,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
20
,500
,000
4,
500,
000
10,0
02,3
00
14,
502,
300
3,18
4,70
9 63
,944
,451
81
,631
,460
F0
3 TU
ME
YA M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha
Ras
ilim
ali n
a B
iash
ara
za W
anyo
nge
Tanz
ania
(M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
5
00,0
00
UR
T 1
68,8
83
668,
883
M
iradi
i) K
uend
elez
a Ta
fiti n
a U
buni
fu
200,
000
0
-
0
ii)
Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
230
,000
!!
!!
230,
000
iii
) Mra
di w
a U
ratib
u na
Usi
mam
izi w
a M
alen
go y
a M
aend
eleo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KU
ZA II
I
20,0
00
2
0,00
0
UN
DP
1,
689,
079
1,
709,
079
iv
) Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a A
fya
ya U
zazi
, Jin
sia
na K
upun
guza
Um
asik
ini
29,0
00
0
-
UN
FPA
40
0,40
0
400,
400
JU
MLA
YA
FU
NG
U
609,
000
750,
000
0 75
0,00
0
2,25
8,36
2 0
3,00
8,36
2 L0
1 W
IZA
RA
YA
KIL
IMO
, M
ALI
ASI
LI, M
IFU
GO
NA
UVU
VI
Pr
ogra
mu
ya M
iund
ombi
nu y
a So
ko, K
uong
eza
Tham
ani n
a M
isaa
da V
ijijin
i (M
IVA
RF)
3
00,0
00
-
-
IF
AD
/AG
RA
/ A
fDB
3
99,6
16
39
9,61
6
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0
1,00
0,00
0 1
,000
,000
K
OR
EA
32,8
67,1
20
33,8
67,1
20
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
8
0,00
0
WB
6,
950,
283
7,
030,
283
Pr
ogra
mu
ya K
uend
elez
a M
iund
ombi
nu y
a K
ilim
o 85
6,00
0
-
0
i. K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i W
adog
o W
adog
o
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
1,
000,
000
ii.
Kue
ndel
eza
Uta
fiti w
a M
ifugo
1,20
0,00
0
1,2
00,0
00
1,
200,
000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i) U
imar
isha
ji U
vuvi
wa
Bah
ari K
uu
3,66
6,00
0
1,40
0,00
0 1
,400
,000
JI
CA
13
,200
,000
14,6
00,0
00
ii)
Kui
mar
isha
Ufu
gaji
wa
Maz
ao y
a B
ahar
ini
200,
000
200,
000
2
00,0
00
FAO
/ KO
RE
A
692,
423
89
2,42
3
Mira
di
i)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki m
wa
Bah
ari y
a H
indi
(S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
5
0,00
0
WO
RLD
B
AN
K
2,
894,
693
2,94
4,69
3
ii) K
udhi
biti
Sum
u K
uvu
inay
otok
ana
na U
laji
wa
Mah
indi
na
Nju
gu
AfD
B
988
,440
988,
440
iii
) Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
i
U
ND
P
228
,200
228,
200
iv
) Kili
mo
cha
Kus
hajih
isha
Uku
lima
wa
Mbo
ga n
a M
atun
da
ED
F-E
U
2,0
00,0
00
2,
000,
000
v)
Kili
mo
Kin
acho
him
ili M
abad
iliko
ya
Hal
i ya
Hew
a
U
SD
A-U
SA
ID
44,
400
44,4
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
5,65
2,00
0 2,
530,
000
2,40
0,00
0 4
,930
,000
24,5
03,3
62
35,7
61,8
13
65,1
95,1
75
R01
W
IZA
RA
YA
BIA
SHA
RA
NA
VIW
AN
DA
Prog
ram
u ya
Maz
ingi
ra B
ora
ya B
iash
ara
150,
000
200,
000
2
00,0
00
20
0,00
0
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
2,
000,
000
M
iradi
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 83
i)K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0
2,00
0,00
0 2
,000
,000
2,00
0,00
0
ii) M
fum
o m
pya
wa
Uto
aji L
esen
i kw
a M
aend
eleo
ya
Sek
ta B
inaf
si
50,0
00
400,
000
4
00,0
00
40
0,00
0
iii) M
radi
wa
Kuw
asai
dia
Waj
asiri
amal
i Wad
ogo
Wad
ogo
KH
ALI
FA
FUN
D
3,45
0,00
0
3,45
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
4,
700,
000
2,60
0,00
0 2,
000,
000
4,60
0,00
0
3,45
0,00
0 0
8,05
0,00
0 K
01
WIZ
AR
A Y
A E
LIM
U N
A M
AFU
NZO
YA
AM
ALI
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
bnu
ya E
limu
1,19
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
1,50
0,00
0
Mira
di
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u ya
Maa
ndal
izi
-
G
PE
/UN
ICE
F 1,
590,
085
1,
590,
085
ii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
-
GP
E/S
IDA
/ U
NIC
EF/
U
NE
SC
O/
CH
INA
4,
179,
622
2,70
0,00
0 6,
879,
622
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a 3,
100,
000
3,
300,
000
3,3
00,0
00
BA
DE
A/
OP
EC
/ K
OR
EA
/WB
16
,457
,475
35
,646
,871
55
,404
,346
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
Mba
dala
na
Am
ali -
A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,
000,
000
1,0
00,0
00
AfD
B
7,
000,
000
8,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
5,
890,
000
1,50
0,00
0 4,
300,
000
5,8
00,0
00
22
,227
,182
45
,346
,871
73
,374
,053
H
01
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Prog
ram
u ya
Kum
aliz
a M
arad
hi y
a M
alar
ia
Zanz
ibar
24
8,00
0
248,
000
248
,000
P
MI/G
F 5,
190,
664
5,
438,
664
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a A
fya
i)
Kui
pand
isha
had
hi H
ospi
tali
ya M
nazi
Mm
oja
4,16
0,00
0
2,65
0,00
0 2
,650
,000
2,65
0,00
0
ii) K
uzip
andi
sha
hadh
i Hos
pita
li za
Wila
ya n
a H
ospi
tal z
a V
ijijin
i 4,
040,
000
4,
250,
000
4,2
50,0
00
4,
250,
000
iii
) Uje
nzi w
a H
ospi
tal y
a R
ufaa
Bin
guni
(Aw
amu
ya
Kw
anza
) 4,
000,
000
6
,500
,000
6,50
0,00
0
iv) U
jenz
i wa
Boh
ari K
uu y
a D
awa-
Pem
ba
250,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
1,
000,
000
v)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
amla
ka y
a D
awa
na
Vip
odoz
i 25
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
0 1,
300,
000
1
,300
,000
H
opel
and
Uni
vers
ity
1,40
0,00
0
2,70
0,00
0
Prog
ram
u Sh
iriki
shi y
a H
udum
a za
Afy
a ya
U
zazi
wa
Mam
a na
Mto
to
530,
000
700,
000
7
00,0
00
UN
FPA
/ W
HO
/ U
NIC
EF
4,56
3,86
9
5,26
3,86
9
Prog
ram
u ya
Kud
hibi
ti M
arad
hi y
a U
kim
wi,
Hom
a ya
Ini,
Kifu
a K
ikuu
na
Uko
ma
248,
000
24
8,00
0 2
48,0
00
GF/
THP
S
5,08
8,26
5
5,33
6,26
5
Mira
di
i)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
kem
ia M
kuu
900,
000
-
JU
MLA
YA
FU
NG
U
15,9
26,0
00
4,00
0,00
0 7,
396,
000
17,
896,
000
16,2
42,7
98
0 34
,138
,798
N
01
WIZ
AR
A Y
A A
RD
HI,
NYU
MB
A, M
AJI
NA
NIS
HA
TI
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
v)
Mra
di w
a K
uend
elez
a B
anda
ri ya
Man
gapw
ani
4,20
0,00
0 4,
000,
000
4
,000
,000
4,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
20
,500
,000
4,
500,
000
10,0
02,3
00
14,
502,
300
3,18
4,70
9 63
,944
,451
81
,631
,460
F0
3 TU
ME
YA M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha
Ras
ilim
ali n
a B
iash
ara
za W
anyo
nge
Tanz
ania
(M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
5
00,0
00
UR
T 1
68,8
83
668,
883
M
iradi
i) K
uend
elez
a Ta
fiti n
a U
buni
fu
200,
000
0
-
0
ii)
Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
230
,000
!!
!!
230,
000
iii
) Mra
di w
a U
ratib
u na
Usi
mam
izi w
a M
alen
go y
a M
aend
eleo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KU
ZA II
I
20,0
00
2
0,00
0
UN
DP
1,
689,
079
1,
709,
079
iv
) Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a A
fya
ya U
zazi
, Jin
sia
na K
upun
guza
Um
asik
ini
29,0
00
0
-
UN
FPA
40
0,40
0
400,
400
JU
MLA
YA
FU
NG
U
609,
000
750,
000
0 75
0,00
0
2,25
8,36
2 0
3,00
8,36
2 L0
1 W
IZA
RA
YA
KIL
IMO
, M
ALI
ASI
LI, M
IFU
GO
NA
UVU
VI
Pr
ogra
mu
ya M
iund
ombi
nu y
a So
ko, K
uong
eza
Tham
ani n
a M
isaa
da V
ijijin
i (M
IVA
RF)
3
00,0
00
-
-
IF
AD
/AG
RA
/ A
fDB
3
99,6
16
39
9,61
6
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0
1,00
0,00
0 1
,000
,000
K
OR
EA
32,8
67,1
20
33,8
67,1
20
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
8
0,00
0
WB
6,
950,
283
7,
030,
283
Pr
ogra
mu
ya K
uend
elez
a M
iund
ombi
nu y
a K
ilim
o 85
6,00
0
-
0
i. K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i W
adog
o W
adog
o
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
1,
000,
000
ii.
Kue
ndel
eza
Uta
fiti w
a M
ifugo
1,20
0,00
0
1,2
00,0
00
1,
200,
000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i) U
imar
isha
ji U
vuvi
wa
Bah
ari K
uu
3,66
6,00
0
1,40
0,00
0 1
,400
,000
JI
CA
13
,200
,000
14,6
00,0
00
ii)
Kui
mar
isha
Ufu
gaji
wa
Maz
ao y
a B
ahar
ini
200,
000
200,
000
2
00,0
00
FAO
/ KO
RE
A
692,
423
89
2,42
3
Mira
di
i)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki m
wa
Bah
ari y
a H
indi
(S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
5
0,00
0
WO
RLD
B
AN
K
2,
894,
693
2,94
4,69
3
ii) K
udhi
biti
Sum
u K
uvu
inay
otok
ana
na U
laji
wa
Mah
indi
na
Nju
gu
AfD
B
988
,440
988,
440
iii
) Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
i
U
ND
P
228
,200
228,
200
iv
) Kili
mo
cha
Kus
hajih
isha
Uku
lima
wa
Mbo
ga n
a M
atun
da
ED
F-E
U
2,0
00,0
00
2,
000,
000
v)
Kili
mo
Kin
acho
him
ili M
abad
iliko
ya
Hal
i ya
Hew
a
U
SD
A-U
SA
ID
44,
400
44,4
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
5,65
2,00
0 2,
530,
000
2,40
0,00
0 4
,930
,000
24,5
03,3
62
35,7
61,8
13
65,1
95,1
75
R01
W
IZA
RA
YA
BIA
SHA
RA
NA
VIW
AN
DA
Prog
ram
u ya
Maz
ingi
ra B
ora
ya B
iash
ara
150,
000
200,
000
2
00,0
00
20
0,00
0
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
2,
000,
000
M
iradi
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 84
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a M
aji
Miji
ni
i)
Uim
aris
haji
wa
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i Mjin
i (JI
CA
) 50
,000
-
JI
CA
4,53
5,22
6 4,
535,
226
ii)
Uim
aris
haji
wa
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i Mko
a w
a M
jini M
agha
ribi (
AD
F12)
1,
064,
787
2,
248,
000
2,2
48,0
00
AfD
B
7,
122,
428
9,37
0,42
8
iii) M
radi
wa
Uhu
isha
ji na
Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Usa
mba
zaji
Maj
i Zan
ziba
r (IN
DIA
) 70
0,00
0
700,
000
700
,000
IN
DIA
88,4
21,0
00
89,1
21,0
00
iv
) Uim
aris
haji
wa
mfu
mo
wa
Maj
i Mac
hafu
kw
a M
ji w
a Za
nzib
ar (M
iji 2
5)
-
IN
DIA
19,2
06,7
03
19,2
06,7
03
Pr
ogra
mu
ya U
sam
baza
ji M
aji V
ijijin
i
i) K
uend
elez
a V
isim
a vy
a R
as e
l Kha
imah
4,
000,
000
3,
000,
000
3,0
00,0
00
3,
000,
000
ii)
Uch
imba
ji w
a V
isim
a na
Usa
mba
zaji
Maj
i 53
6,21
3
863,
000
863
,000
C
HIN
A
5,08
1,56
2
5,94
4,56
2
Mira
di
i)
Usa
mba
zaji
Um
eme
Viji
jini
1,20
0,00
0 65
0,70
0
650
,700
650,
700
ii)
Mra
di w
a K
uije
ngea
Uw
ezo
Sek
ta y
a N
isha
ti 65
,000
-
S
IDA
4,
866,
511
4,
866,
511
iii
) Uta
fiti w
a N
isha
ti M
bada
la
134,
000
-
iv
) Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
ar
NO
RW
AY
7,
382,
230
7,
382,
230
v)
Mra
di w
a M
ashi
rikia
no y
a S
ekta
za
Ard
hi b
aina
ya
Zan
ziba
r na
Finl
and
50
,000
-
JUM
LA Y
A F
UN
GU
7,
800,
000
650,
700
6,81
1,00
0 7
,461
,700
17,3
30,3
03
119,
285,
357
144,
077,
360
P01
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a B
arab
ara
i)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a Tu
nguu
-Mak
undu
chi
(30k
m) n
a C
hake
Cha
ke -
Mko
ani (
31km
) 1,
000,
000
2,80
0,00
0
2,8
00,0
00
2,
800,
000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0
9,0
00,0
00
OFI
D
9,
000,
000
18,0
00,0
00
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
(km
7.2)
na
Jum
bi-K
oani
(km
6.3
) 3,
700,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
BA
DE
A
6,
571,
000
8,57
1,00
0
iv) U
jenz
i wa
bara
bara
ya
Cha
ke-W
ete
1,00
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni (9
.4 k
m),
Pal
e K
iong
ele
- Mkw
ajun
i (4.
6 km
), M
atem
we
- Muy
uni
(7.6
km
), Fu
oni -
Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4,0
00,0
00
4,0
00,0
00
AfD
B
11
,893
,561
15
,893
,561
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
3,00
0,00
0
vii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya K
itoga
ni -
Paj
e,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, Kin
yasi
ni -
Kiw
engw
a na
Dun
ga -
Chw
aka
4
00,0
00
4
00,0
00
40
0,00
0
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Viw
anja
vya
Nde
ge
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0
61,0
30,0
00
61,
030,
000
61,0
30,0
00
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Ban
dari
ya M
piga
duri
400,
000
3,
000,
000
3,0
00,0
00
3,
000,
000
ii)
Unu
nuzi
wa
Land
Cra
ft 2,
400,
000
1,90
0,00
0
1,9
00,0
00
1,
900,
000
i)K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0
2,00
0,00
0 2
,000
,000
2,00
0,00
0
ii) M
fum
o m
pya
wa
Uto
aji L
esen
i kw
a M
aend
eleo
ya
Sek
ta B
inaf
si
50,0
00
400,
000
4
00,0
00
40
0,00
0
iii) M
radi
wa
Kuw
asai
dia
Waj
asiri
amal
i Wad
ogo
Wad
ogo
KH
ALI
FA
FUN
D
3,45
0,00
0
3,45
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
4,
700,
000
2,60
0,00
0 2,
000,
000
4,60
0,00
0
3,45
0,00
0 0
8,05
0,00
0 K
01
WIZ
AR
A Y
A E
LIM
U N
A M
AFU
NZO
YA
AM
ALI
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
bnu
ya E
limu
1,19
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
1,50
0,00
0
Mira
di
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u ya
Maa
ndal
izi
-
G
PE
/UN
ICE
F 1,
590,
085
1,
590,
085
ii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
-
GP
E/S
IDA
/ U
NIC
EF/
U
NE
SC
O/
CH
INA
4,
179,
622
2,70
0,00
0 6,
879,
622
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a 3,
100,
000
3,
300,
000
3,3
00,0
00
BA
DE
A/
OP
EC
/ K
OR
EA
/WB
16
,457
,475
35
,646
,871
55
,404
,346
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
Mba
dala
na
Am
ali -
A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,
000,
000
1,0
00,0
00
AfD
B
7,
000,
000
8,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
5,
890,
000
1,50
0,00
0 4,
300,
000
5,8
00,0
00
22
,227
,182
45
,346
,871
73
,374
,053
H
01
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Prog
ram
u ya
Kum
aliz
a M
arad
hi y
a M
alar
ia
Zanz
ibar
24
8,00
0
248,
000
248
,000
P
MI/G
F 5,
190,
664
5,
438,
664
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a A
fya
i)
Kui
pand
isha
had
hi H
ospi
tali
ya M
nazi
Mm
oja
4,16
0,00
0
2,65
0,00
0 2
,650
,000
2,65
0,00
0
ii) K
uzip
andi
sha
hadh
i Hos
pita
li za
Wila
ya n
a H
ospi
tal z
a V
ijijin
i 4,
040,
000
4,
250,
000
4,2
50,0
00
4,
250,
000
iii
) Uje
nzi w
a H
ospi
tal y
a R
ufaa
Bin
guni
(Aw
amu
ya
Kw
anza
) 4,
000,
000
6
,500
,000
6,50
0,00
0
iv) U
jenz
i wa
Boh
ari K
uu y
a D
awa-
Pem
ba
250,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
1,
000,
000
v)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
amla
ka y
a D
awa
na
Vip
odoz
i 25
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
0 1,
300,
000
1
,300
,000
H
opel
and
Uni
vers
ity
1,40
0,00
0
2,70
0,00
0
Prog
ram
u Sh
iriki
shi y
a H
udum
a za
Afy
a ya
U
zazi
wa
Mam
a na
Mto
to
530,
000
700,
000
7
00,0
00
UN
FPA
/ W
HO
/ U
NIC
EF
4,56
3,86
9
5,26
3,86
9
Prog
ram
u ya
Kud
hibi
ti M
arad
hi y
a U
kim
wi,
Hom
a ya
Ini,
Kifu
a K
ikuu
na
Uko
ma
248,
000
24
8,00
0 2
48,0
00
GF/
THP
S
5,08
8,26
5
5,33
6,26
5
Mira
di
i)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
kem
ia M
kuu
900,
000
-
JU
MLA
YA
FU
NG
U
15,9
26,0
00
4,00
0,00
0 7,
396,
000
17,
896,
000
16,2
42,7
98
0 34
,138
,798
N
01
WIZ
AR
A Y
A A
RD
HI,
NYU
MB
A, M
AJI
NA
NIS
HA
TI
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 85
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a M
aji
Miji
ni
i)
Uim
aris
haji
wa
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i Mjin
i (JI
CA
) 50
,000
-
JI
CA
4,53
5,22
6 4,
535,
226
ii)
Uim
aris
haji
wa
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i Mko
a w
a M
jini M
agha
ribi (
AD
F12)
1,
064,
787
2,
248,
000
2,2
48,0
00
AfD
B
7,
122,
428
9,37
0,42
8
iii) M
radi
wa
Uhu
isha
ji na
Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Usa
mba
zaji
Maj
i Zan
ziba
r (IN
DIA
) 70
0,00
0
700,
000
700
,000
IN
DIA
88,4
21,0
00
89,1
21,0
00
iv
) Uim
aris
haji
wa
mfu
mo
wa
Maj
i Mac
hafu
kw
a M
ji w
a Za
nzib
ar (M
iji 2
5)
-
IN
DIA
19,2
06,7
03
19,2
06,7
03
Pr
ogra
mu
ya U
sam
baza
ji M
aji V
ijijin
i
i) K
uend
elez
a V
isim
a vy
a R
as e
l Kha
imah
4,
000,
000
3,
000,
000
3,0
00,0
00
3,
000,
000
ii)
Uch
imba
ji w
a V
isim
a na
Usa
mba
zaji
Maj
i 53
6,21
3
863,
000
863
,000
C
HIN
A
5,08
1,56
2
5,94
4,56
2
Mira
di
i)
Usa
mba
zaji
Um
eme
Viji
jini
1,20
0,00
0 65
0,70
0
650
,700
650,
700
ii)
Mra
di w
a K
uije
ngea
Uw
ezo
Sek
ta y
a N
isha
ti 65
,000
-
S
IDA
4,
866,
511
4,
866,
511
iii
) Uta
fiti w
a N
isha
ti M
bada
la
134,
000
-
iv
) Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
ar
NO
RW
AY
7,
382,
230
7,
382,
230
v)
Mra
di w
a M
ashi
rikia
no y
a S
ekta
za
Ard
hi b
aina
ya
Zan
ziba
r na
Finl
and
50
,000
-
JUM
LA Y
A F
UN
GU
7,
800,
000
650,
700
6,81
1,00
0 7
,461
,700
17,3
30,3
03
119,
285,
357
144,
077,
360
P01
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a B
arab
ara
i)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a Tu
nguu
-Mak
undu
chi
(30k
m) n
a C
hake
Cha
ke -
Mko
ani (
31km
) 1,
000,
000
2,80
0,00
0
2,8
00,0
00
2,
800,
000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0
9,0
00,0
00
OFI
D
9,
000,
000
18,0
00,0
00
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
(km
7.2)
na
Jum
bi-K
oani
(km
6.3
) 3,
700,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
BA
DE
A
6,
571,
000
8,57
1,00
0
iv) U
jenz
i wa
bara
bara
ya
Cha
ke-W
ete
1,00
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni (9
.4 k
m),
Pal
e K
iong
ele
- Mkw
ajun
i (4.
6 km
), M
atem
we
- Muy
uni
(7.6
km
), Fu
oni -
Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4,0
00,0
00
4,0
00,0
00
AfD
B
11
,893
,561
15
,893
,561
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
3,00
0,00
0
vii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
ya K
itoga
ni -
Paj
e,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, Kin
yasi
ni -
Kiw
engw
a na
Dun
ga -
Chw
aka
4
00,0
00
4
00,0
00
40
0,00
0
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Viw
anja
vya
Nde
ge
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0
61,0
30,0
00
61,
030,
000
61,0
30,0
00
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Ban
dari
ya M
piga
duri
400,
000
3,
000,
000
3,0
00,0
00
3,
000,
000
ii)
Unu
nuzi
wa
Land
Cra
ft 2,
400,
000
1,90
0,00
0
1,9
00,0
00
1,
900,
000
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 86
iii
) Unu
nuzi
wa
mel
i 18
,000
,000
-
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
42
,300
,000
20
,100
,000
68
,030
,000
8
8,13
0,00
0
0
27,4
64,5
61
115,
594,
561
Q01
W
IZA
RA
YA
KA
ZI, U
WEZ
ESH
AJI
, W
AZE
E, W
AN
AW
AK
E N
A W
ATO
TO
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
a
i) U
saw
a w
a K
ijins
ia n
a K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en
245,
703
24
5,70
3
ii) M
radi
wa
Jins
ia
UN
FPA
42
0,00
0
420,
000
M
iradi
i) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a w
azee
37
0,00
0 40
0,00
0
400
,000
400,
000
ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a K
ulea
na
Kut
otol
ea
Waj
asiri
amal
i (In
cuba
tor)
600,
000
6
00,0
00
60
0,00
0
iii) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a Ja
mii
UN
ICE
F 75
,000
75,0
00
iv
) Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Wat
oto
UN
ICE
F 37
5,00
0
375,
000
!!JU
MLA
YA
FU
NG
U
370,
000
1,00
0,00
0 0
1,00
0,00
0
1,11
5,70
3 0
2,11
5,70
3 G
01
WIZ
AR
A Y
A K
ATI
BA
NA
SH
ERIA
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Sekt
a ya
She
ria
1,
000,
000
!!!!
!!!!
!!!!
!!
Mra
di
M
radi
wa
Usi
mam
izi w
a U
patik
anaj
i wa
Hak
i
400,
000
4
00,0
00
UN
DP
1
,483
,300
1,88
3,30
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
400,
000
0 40
0,00
0
1,48
3,30
0 0
1,88
3,30
0
OFI
SI Y
A R
AIS
- U
TUM
ISH
I WA
UM
MA
NA
UTA
WA
LA B
OR
A
Pr
ogra
mu
ya M
ageu
zi y
a U
tum
ishi
wa
Um
ma
- II
20
0,00
0
200
,000
W
B
2,54
8,20
2
2,74
8,20
2
Mra
di
i)
Zanz
ibar
E-g
over
nmen
t Opt
ical
Tra
nsm
issi
on
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k P
hase
II
50,0
00
100,
000
1
00,0
00
10
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
50
,000
30
0,00
0 0
300,
000
2,
548,
202
0 2,
848,
202
G07
M
AM
LAK
A Y
A K
UZU
IA R
USH
WA
NA
UH
UJU
MU
WA
UC
HU
MI
ii)
Uje
nzi w
a O
fisi y
a ZA
EC
A
80
0,00
0
800
,000
800,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
0 80
0,00
0 0
800,
000
0
0 80
0,00
0 J0
1 W
IZA
RA
YA
HA
BA
RI,
UTA
LII N
A M
AM
BO
YA
KA
LE
Pr
ogra
mu
Mju
mui
sho
ya K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
2,4
00,0
00
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Jeng
o la
Ofis
i na
Stu
dio
za R
edio
M
kanj
uni-P
emba
5
00,0
00
1,5
00,0
00
1
,500
,000
1,5
00,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,3
50,0
00
3,9
00,0
00
-
3,9
00,0
00
-
-
3
,900
,000
J0
2 K
AM
ISH
ENI Y
A U
TALI
I
Kui
mar
isha
Uta
lii k
wa
Wot
e 1
,300
,000
1
,500
,000
1,5
00,0
00
1
,500
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1
,300
,000
1
,500
,000
-
1
,500
,000
-
-
1,5
00,0
00
S01
WIZ
AR
A Y
A V
IJA
NA
, UTA
MA
DU
NI,
SAN
AA
NA
MIC
HEZ
O
Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na
3,0
00,0
00
2
,000
,000
2
,000
,000
2,0
00,0
00
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Viw
anja
vya
Mic
hezo
vya
Wila
ya
800
,000
2
,000
,000
2,0
00,0
00
2
,000
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3
,800
,000
2
,000
,000
2
,000
,000
4
,000
,000
-
-
4,0
00,0
00
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 87
D01
O
FISI
YA
RA
IS T
AW
ALA
ZA
MIK
OA
, SER
IKA
LI Z
A M
ITA
A N
A ID
AR
A M
AA
LUM
ZA
SM
Z
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u 1,
110,
000
1,11
0,00
0
1,1
10,0
00
1,
110,
000
M
IRA
DI
i)
Uw
ekaj
i wa
Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi
20,0
00,0
00
7,
000,
000
7,0
00,0
00
7,
000,
000
ii)
Uje
nzi w
a K
iwan
da c
ha U
shon
i (ZQ
TL)
2,40
0,00
0 4,
500,
000
4
,500
,000
4,50
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
23
,510
,000
5,
610,
000
7,00
0,00
0 1
2,61
0,00
0
0
0 12
,610
,000
D
12
WA
KA
LA W
A U
SAJI
LI W
A M
ATU
KIO
YA
KIJ
AM
II ZA
NZI
BA
R
i)M
radi
wa
Kui
mar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a V
izaz
i na
Vifo
50
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
5
00,0
00
1,0
00,0
00
-
1,0
00,0
00
-
-
1
,000
,000
D
04
KIK
OSI
MA
ALU
M C
HA
KU
ZUIA
MA
GEN
DO
(KM
KM
)
i) U
jenz
i wa
Wod
i ya
Waz
azi K
MK
M
1,5
00,0
00
-
-
-
ii)
Kui
mar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i 2
,200
,000
2
,900
,000
2,9
00,0
00
2
,900
,000
iii) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a K
ambi
na
Nyu
mba
za
KM
KM
1
,300
,000
1
,000
,000
1,0
00,0
00
1
,000
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
5,
000,
000
3,90
0,00
0 0
3,9
00,0
00
0
0 3,
900,
000
D06
K
IKO
SI C
HA
VA
LAN
TIA
i) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Maa
skar
i 50
0,00
0 50
0,00
0
500
,000
500,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500,
000
500,
000
0 5
00,0
00
-
-
-
500,
000
D03
C
HU
O C
HA
MA
FUN
ZO
i)
Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Hud
uma
za K
urek
ebis
ha
Wat
oto
700,
000
0
-
0
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga
1,40
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
2,
100,
000
1,00
0,00
0 0
1,0
00,0
00
0
0 1,
000,
000
D02
JE
SHI L
A K
UJE
NG
A U
CH
UM
I
i) U
jenz
i wa
Sku
li ya
Ufu
ndi -
Mto
ni
1,65
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
ii) U
jenz
i wa
Maj
engo
ya
Kam
bi z
a JK
U P
emba
50
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
1,50
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
2,
150,
000
3,50
0,00
0 0
3,5
00,0
00
0
0 3,
500,
000
D05
K
IKO
SI C
HA
ZIM
AM
OTO
NA
UO
KO
ZI
U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i 50
0,00
0 50
0,00
0
500
,000
500,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500,
000
500,
000
0 5
00,0
00
50
0,00
0 D
07
MK
OA
WA
MJI
NI M
AG
HA
RIB
I
Usi
mam
izi w
a Ta
ka N
gum
u M
anis
paa
ya M
agha
ribi
"B"
770,
000
-
0
JU
MLA
YA
FU
NG
U
770,
000
-
0
0 0
JU
MLA
KU
BW
A
148,
750,
000
65,9
60,7
00
109,
939,
300
182,
400,
000
95
,520
,883
29
9,10
4,40
2 57
7,02
5,28
5
JU
MLA
YA
FED
HA
ZA
WA
HIS
AN
I
394,
625,
285
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!"!#$%!&'
(!)(
*+,-!.(!$
(+/0
+1+2
!34
564!
!!
!!
!!
!
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
iii
) Unu
nuzi
wa
mel
i 18
,000
,000
-
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
42
,300
,000
20
,100
,000
68
,030
,000
8
8,13
0,00
0
0
27,4
64,5
61
115,
594,
561
Q01
W
IZA
RA
YA
KA
ZI, U
WEZ
ESH
AJI
, W
AZE
E, W
AN
AW
AK
E N
A W
ATO
TO
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
a
i) U
saw
a w
a K
ijins
ia n
a K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en
245,
703
24
5,70
3
ii) M
radi
wa
Jins
ia
UN
FPA
42
0,00
0
420,
000
M
iradi
i) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a w
azee
37
0,00
0 40
0,00
0
400
,000
400,
000
ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a K
ulea
na
Kut
otol
ea
Waj
asiri
amal
i (In
cuba
tor)
600,
000
6
00,0
00
60
0,00
0
iii) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a Ja
mii
UN
ICE
F 75
,000
75,0
00
iv
) Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Wat
oto
UN
ICE
F 37
5,00
0
375,
000
!!JU
MLA
YA
FU
NG
U
370,
000
1,00
0,00
0 0
1,00
0,00
0
1,11
5,70
3 0
2,11
5,70
3 G
01
WIZ
AR
A Y
A K
ATI
BA
NA
SH
ERIA
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Sekt
a ya
She
ria
1,
000,
000
!!!!
!!!!
!!!!
!!
Mra
di
M
radi
wa
Usi
mam
izi w
a U
patik
anaj
i wa
Hak
i
400,
000
4
00,0
00
UN
DP
1
,483
,300
1,88
3,30
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
400,
000
0 40
0,00
0
1,48
3,30
0 0
1,88
3,30
0
OFI
SI Y
A R
AIS
- U
TUM
ISH
I WA
UM
MA
NA
UTA
WA
LA B
OR
A
Pr
ogra
mu
ya M
ageu
zi y
a U
tum
ishi
wa
Um
ma
- II
20
0,00
0
200
,000
W
B
2,54
8,20
2
2,74
8,20
2
Mra
di
i)
Zanz
ibar
E-g
over
nmen
t Opt
ical
Tra
nsm
issi
on
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k P
hase
II
50,0
00
100,
000
1
00,0
00
10
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
50
,000
30
0,00
0 0
300,
000
2,
548,
202
0 2,
848,
202
G07
M
AM
LAK
A Y
A K
UZU
IA R
USH
WA
NA
UH
UJU
MU
WA
UC
HU
MI
ii)
Uje
nzi w
a O
fisi y
a ZA
EC
A
80
0,00
0
800
,000
800,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
0 80
0,00
0 0
800,
000
0
0 80
0,00
0 J0
1 W
IZA
RA
YA
HA
BA
RI,
UTA
LII N
A M
AM
BO
YA
KA
LE
Pr
ogra
mu
Mju
mui
sho
ya K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
2,4
00,0
00
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Jeng
o la
Ofis
i na
Stu
dio
za R
edio
M
kanj
uni-P
emba
5
00,0
00
1,5
00,0
00
1
,500
,000
1,5
00,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,3
50,0
00
3,9
00,0
00
-
3,9
00,0
00
-
-
3
,900
,000
J0
2 K
AM
ISH
ENI Y
A U
TALI
I
Kui
mar
isha
Uta
lii k
wa
Wot
e 1
,300
,000
1
,500
,000
1,5
00,0
00
1
,500
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1
,300
,000
1
,500
,000
-
1
,500
,000
-
-
1,5
00,0
00
S01
WIZ
AR
A Y
A V
IJA
NA
, UTA
MA
DU
NI,
SAN
AA
NA
MIC
HEZ
O
Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na
3,0
00,0
00
2
,000
,000
2
,000
,000
2,0
00,0
00
M
iradi
i) U
jenz
i wa
Viw
anja
vya
Mic
hezo
vya
Wila
ya
800
,000
2
,000
,000
2,0
00,0
00
2
,000
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3
,800
,000
2
,000
,000
2
,000
,000
4
,000
,000
-
-
4,0
00,0
00
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 88
Kia
mba
tisho
nam
ba 1
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I KIW
IZA
RA
201
9/20
TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2018
/201
9 SM
Z
MA
KIS
IO K
WA
MW
AK
A 2
019/
20 S
MZ
MIC
HA
NG
O Y
A W
ASH
IRIK
A W
A
MA
END
ELEO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
MA
KIS
IO
YA
KA
WA
IDA
20
19/2
0
DH
IMA
20
19/2
0
JU
MLA
YA
M
AK
ISIO
YA
SM
Z 20
19/2
0
WA
SHIR
IKA
W
A
MA
END
ELEO
R
UZU
KU
M
IKO
PO
A01
O
FISI
YA
RA
IS N
A M
WEN
YEK
ITI W
A B
AR
AZA
LA
MA
PIN
DU
ZI
M
iradi
i) U
imar
isha
ji N
yum
ba z
a V
iong
ozi n
a N
yum
ba z
a S
erik
ali
1,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
000,
000
2,00
0,00
0 0
2,0
00,0
00
0
0 2,
000,
000
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
40,
000
W
OR
LD
BA
NK
7,3
01,3
49
7,34
1,34
9
Mira
di
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180,
000
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
3
50,0
00
35
0,00
0
iii) K
uim
aris
ha U
sim
amiz
i wa
Maz
ingi
ra,
Mal
iasi
li na
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi-Z
anzi
bar
50,0
00
300,
000
3
00,0
00
UN
DP
45
6,60
0
756,
600
iv
) Kuk
uza
Uw
ezo
wa
Kita
ifa w
a K
uhim
ili A
thar
i za
Mab
adili
ko y
a Ta
bian
chi (
AD
B-A
CC
F)
33,0
00
50,0
00
5
0,00
0
AfD
B
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
973
,000
7
40,0
00
-
740
,000
636
,600
7
,301
,349
8
,677
,949
TUM
E YA
UK
IMW
I ZA
NZI
BA
R
i)
Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I Zan
ziba
r
G
F/U
NFP
A
540,
362
54
0,36
2
JUM
LA Y
A F
UN
GU
-
-
-
-
540
,362
-
5
40,3
62
C04
TU
ME
YA K
ITA
IFA
YA
KU
RA
TIB
U N
A U
DH
IBIT
I WA
DA
WA
ZA
KU
LEVY
A
iii
) Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Tiba
na
Mar
ekeb
isho
ya
Tabi
a 5
00,0
00
680
,000
680
,000
680,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500
,000
6
80,0
00
-
680
,000
-
6
80,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Ofis
i za
Serik
ali
Zanz
ibar
15
,000
,000
10,0
02,3
00
10,
002,
300
10,0
02,3
00
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha H
udum
a za
Miji
(ZU
SP)
WO
RLD
B
AN
K
57
,407
,042
57
,407
,042
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
Kat
ika
Usi
mam
izi w
a Fe
dha
(PFM
RP)
N
OR
WA
Y
1,59
8,71
9
1,59
8,71
9
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
300,
000
M
iradi
i) K
uim
aris
ha U
taw
ala
Bor
a A
wam
u ya
Tat
u 15
0,00
0 10
0,00
0
100
,000
A
fDB
4,01
3,76
7 4,
113,
767
ii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi
wa
Mal
iasi
li 10
0,00
0 50
,000
50,
000
A
fDB
2,52
3,64
2 2,
573,
642
iii
) Mra
di w
a K
ujen
ga U
wez
o Ta
asis
i za
Ser
ikal
i 50
,000
50
,000
50,
000
U
ND
P
1,58
5,99
0
1,63
5,99
0
D01
O
FISI
YA
RA
IS T
AW
ALA
ZA
MIK
OA
, SER
IKA
LI Z
A M
ITA
A N
A ID
AR
A M
AA
LUM
ZA
SM
Z
Prog
ram
u ya
Uga
tuzi
wa
Mas
uala
ya
Elim
u 1,
110,
000
1,11
0,00
0
1,1
10,0
00
1,
110,
000
M
IRA
DI
i)
Uw
ekaj
i wa
Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi
20,0
00,0
00
7,
000,
000
7,0
00,0
00
7,
000,
000
ii)
Uje
nzi w
a K
iwan
da c
ha U
shon
i (ZQ
TL)
2,40
0,00
0 4,
500,
000
4
,500
,000
4,50
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
23
,510
,000
5,
610,
000
7,00
0,00
0 1
2,61
0,00
0
0
0 12
,610
,000
D
12
WA
KA
LA W
A U
SAJI
LI W
A M
ATU
KIO
YA
KIJ
AM
II ZA
NZI
BA
R
i)M
radi
wa
Kui
mar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a V
izaz
i na
Vifo
50
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
5
00,0
00
1,0
00,0
00
-
1,0
00,0
00
-
-
1
,000
,000
D
04
KIK
OSI
MA
ALU
M C
HA
KU
ZUIA
MA
GEN
DO
(KM
KM
)
i) U
jenz
i wa
Wod
i ya
Waz
azi K
MK
M
1,5
00,0
00
-
-
-
ii)
Kui
mar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i 2
,200
,000
2
,900
,000
2,9
00,0
00
2
,900
,000
iii) U
jenz
i na
Uka
raba
ti w
a K
ambi
na
Nyu
mba
za
KM
KM
1
,300
,000
1
,000
,000
1,0
00,0
00
1
,000
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
5,
000,
000
3,90
0,00
0 0
3,9
00,0
00
0
0 3,
900,
000
D06
K
IKO
SI C
HA
VA
LAN
TIA
i) U
jenz
i wa
Nyu
mba
na
Mah
anga
ya
Maa
skar
i 50
0,00
0 50
0,00
0
500
,000
500,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500,
000
500,
000
0 5
00,0
00
-
-
-
500,
000
D03
C
HU
O C
HA
MA
FUN
ZO
i)
Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Hud
uma
za K
urek
ebis
ha
Wat
oto
700,
000
0
-
0
ii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga
1,40
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
2,
100,
000
1,00
0,00
0 0
1,0
00,0
00
0
0 1,
000,
000
D02
JE
SHI L
A K
UJE
NG
A U
CH
UM
I
i) U
jenz
i wa
Sku
li ya
Ufu
ndi -
Mto
ni
1,65
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
2,50
0,00
0
ii) U
jenz
i wa
Maj
engo
ya
Kam
bi z
a JK
U P
emba
50
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
2,
150,
000
3,50
0,00
0 0
3,5
00,0
00
0
0 3,
500,
000
D05
K
IKO
SI C
HA
ZIM
AM
OTO
NA
UO
KO
ZI
U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i 50
0,00
0 50
0,00
0
500
,000
500,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
500,
000
500,
000
0 5
00,0
00
50
0,00
0 D
07
MK
OA
WA
MJI
NI M
AG
HA
RIB
I
Usi
mam
izi w
a Ta
ka N
gum
u M
anis
paa
ya M
agha
ribi
"B"
770,
000
-
0
JU
MLA
YA
FU
NG
U
770,
000
-
0
0 0
JU
MLA
KU
BW
A
148,
750,
000
65,9
60,7
00
109,
939,
300
182,
400,
000
95
,520
,883
29
9,10
4,40
2 57
7,02
5,28
5
JU
MLA
YA
FED
HA
ZA
WA
HIS
AN
I
394,
625,
285
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!!
!"!#$%!&'
(!)(
*+,-!.(!$
(+/0
+1+2
!34
564!
!!
!!
!!
!
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 89
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
MIR
AD
I 201
9/20
20 K
IMA
ENEO
MA
KU
U Y
A M
ATO
KEO
TZS
("00
0")
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A M
WA
KA
20
18/2
019
SMZ
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MC
HA
NG
O W
A W
ASH
IRIK
A W
A M
AEN
DEL
EO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
WA
SHIR
IKA
WA
M
AEN
DEL
EO
RU
ZUK
U
MK
OPO
KR
A A
: KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI
WA
UC
HU
MI J
UM
UIS
HI N
A E
ND
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UB
WA
ZO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Soko
, Kuo
ngez
a Th
aman
i na
Mis
aada
Viji
jini
(MIV
AR
F)
300
,000
IFA
D/A
GR
A/ A
fDB
3
99,6
16
3
99,6
16
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0 1,
000,
000
KO
RE
A
3
2,86
7,12
0
33,
867,
120
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
WB
6
,950
,283
7,0
30,2
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
!!!!
i) K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i Wad
ogo
Wad
ogo
856,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
ii) K
uend
elez
a U
tafit
i wa
Mifu
go
1,
200,
000
1
,200
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i)
Uim
aris
haji
uvuv
i wa
baha
ri ku
u 3,
666,
000
1,40
0,00
0 JI
CA
1
3,20
0,00
0
1
4,60
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
200,
000
FAO
/ KO
RE
A
692
,423
892
,423
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a 15
0,00
0 20
0,00
0
200
,000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Bar
abar
a
-
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Tun
guu-
Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
kech
ake
- Mko
ani
(31k
m)
1,0
00,0
00
2,8
00,0
00
2
,800
,000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0 O
FID
9,0
00,0
00
18,
000,
000
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni
3,70
0,00
0 2,
000,
000
BA
DE
A
6
,571
,000
8
,571
,000
iv
)Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni
(9.4
km
), P
ale
Kio
ngel
e - M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni
- Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4
,000
,000
A
fDB
11,
893,
561
1
5,89
3,56
1
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, K
inya
sini
- K
iwen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a
400
,000
400
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha V
iwan
ja v
ya N
dege
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0 61
,030
,000
61,
030,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
W
B
7
,301
,349
7
,341
,349
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha R
asili
mal
i na
Bia
shar
a za
Wan
yong
e Ta
nzan
ia (M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
UR
T 1
68,8
83
6
68,8
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
MIR
AD
I
ii)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
WO
RLD
BA
NK
2,8
94,6
93
2,9
44,6
93
iv) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a B
anda
ri ya
Mpi
gadu
ri 40
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
vi
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
!
230
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
) 2,
400,
000
4,50
0,00
0
4,5
00,0
00
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 90
viii)
Kue
ndel
eza
Tafit
i na
Ubu
nifu
20
0,00
0
ix) Z
anzi
bar E
-gov
ernm
ent O
ptic
al T
rans
imis
sion
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k P
hase
II
50,0
00
100,
000
1
00,0
00
x) U
nunu
zi w
a La
nd C
raft
2,40
0,00
0 1,
900,
000
1
,900
,000
xi
) Mfu
mo
Mpy
a w
a U
toaj
i Les
eni k
wa
Mae
ndel
eo y
a S
ekta
Bin
afsi
50
,000
40
0,00
0
400
,000
xii)
Kud
hibi
ti S
umu
Kuv
u in
ayot
okan
a na
Ula
ji w
a M
ahin
di n
a N
jugu
(TA
NIP
AC
)
A
fDB
9
88,4
40
9
88,4
40
xiii)
Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
i
U
ND
P
228
,200
228
,200
xi
v) K
ilim
o ch
a K
usha
jihis
ha U
kulim
a w
a M
boga
na
Mat
unda
E
DF-
EU
2
,000
,000
2,0
00,0
00
xv) K
ilim
o K
inac
hohi
mili
Mab
adili
ko y
a H
ali y
a H
ewa
US
DA
-US
AID
4
4,40
0
4
4,40
0
xvi)
Kui
mar
isha
Uta
lii k
wa
Wot
e 1,
300,
000
1,50
0,00
0
1,5
00,0
00
xvii)
Mra
di w
a K
uend
elez
a B
anda
ri ya
Man
gapw
ani
4,20
0,00
0 4,
000,
000
4
,000
,000
xv
iii) M
radi
wa
Kuw
asai
dia
Waj
asiri
amal
i Wad
ogo
Wad
ogo
KH
ALI
FA F
UN
D
3,4
50,0
00
3
,450
,000
JU
MLA
YA
KR
A
44,
072,
000
1
10,9
30,0
00
2
8,12
2,24
5
70,
527,
723
2
09,5
79,9
68
KR
A B
: KU
KU
ZA U
WEZ
O W
A W
ATU
PR
OG
RA
MU
Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na
3,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
a
-
i) U
saw
a w
a K
ijins
ia n
a K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en
245
,703
245
,703
ii)
Mra
di w
a K
ijins
ia
UN
FPA
4
20,0
00
4
20,0
00
MIR
AD
I
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u M
bada
la n
a A
mal
i - A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,00
0,00
0 A
fDB
7,0
00,0
00
8,0
00,0
00
ii) M
radi
wa
Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Kul
ea n
a K
utot
olea
Waj
asiri
amal
i (In
cuba
tor)
600,
000
6
00,0
00
JUM
LA Y
A K
RA
4,
600,
000
3,60
0,00
0
665,
703
7,00
0,00
0 11
,265
,703
K
RA
C: K
UTO
A H
UD
UM
A B
OR
A K
WA
WO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
hud
uma
za M
iji (Z
USP
)
W
B
5
7,40
7,04
2
57,
407,
042
Pr
ogra
mu
ya K
umal
iza
Mar
adhi
ya
Mal
aria
Zan
ziba
r 24
8,00
0 24
8,00
0 P
MI/G
F 5
,190
,664
5,4
38,6
64
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Mui
ndom
binu
ya
Afy
a
i)
Kui
pand
isha
had
hi H
ospi
tali
ya M
nazi
Mm
oja
4,16
0,00
0 2,
650,
000
2
,650
,000
ii)
Kuz
ipan
dish
a H
adhi
hos
pita
li za
Wila
ya n
a H
ospi
tal z
a V
ijiji
4,04
0,00
0 4,
250,
000
4
,250
,000
iii
) Uje
nzi w
a H
ospi
tali
ya R
ufaa
Bin
guni
(Aw
amu
ya K
wan
za)
4,00
0,00
0 6,
500,
000
6
,500
,000
iv
) Uje
nzi w
a B
ohar
i Kuu
ya
Daw
a-P
emba
25
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
amla
ka y
a D
awa
na V
ipod
ozi
250,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
0 1,
300,
000
Hop
elan
d U
n 1,
400,
000
2
,700
,000
Prog
ram
u ya
Shi
rikis
hi y
a H
udum
a za
Afy
a ya
Uza
zi w
a M
ama
na M
toto
53
0,00
0 70
0,00
0 U
NFP
A/ W
HO
/GF
4,5
63,8
69
5
,263
,869
Pr
ogra
mu
ya K
udhi
biti
Mar
adhi
ya
UK
IMW
I, H
oma
ya In
i, K
ifua
Kik
uu n
a U
kom
a 24
8,00
0 24
8,00
0 G
F/TH
PS
5
,088
,265
5,3
36,2
65
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i
-
i) U
imar
isha
ji w
a M
iund
mbi
nu y
a M
aji M
jini
50,0
00
JI
CA
4,5
35,2
26
4,5
35,2
26
ii) U
imar
isha
ji w
a M
iund
ombi
nu y
a M
aji M
jini M
agha
ribi (
AD
F12)
1,
064,
787
2,24
8,00
0 A
fDB
7,1
22,4
28
9,3
70,4
28
iii) U
huis
haji
na U
imar
isha
ji w
a M
fum
o w
a U
sam
baza
ji M
aji Z
anzi
bar
700,
000
700,
000
IND
IA
8
8,42
1,00
0
89,
121,
000
iv
) Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Maj
i Mac
hafu
kw
a M
ji w
a Za
nzib
ar (M
iji 2
5)
IND
IA
1
9,20
6,70
3
19,
206,
703
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
MIR
AD
I 201
9/20
20 K
IMA
ENEO
MA
KU
U Y
A M
ATO
KEO
TZS
("00
0")
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A M
WA
KA
20
18/2
019
SMZ
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MC
HA
NG
O W
A W
ASH
IRIK
A W
A M
AEN
DEL
EO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
WA
SHIR
IKA
WA
M
AEN
DEL
EO
RU
ZUK
U
MK
OPO
KR
A A
: KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI
WA
UC
HU
MI J
UM
UIS
HI N
A E
ND
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UB
WA
ZO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Soko
, Kuo
ngez
a Th
aman
i na
Mis
aada
Viji
jini
(MIV
AR
F)
300
,000
IFA
D/A
GR
A/ A
fDB
3
99,6
16
3
99,6
16
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0 1,
000,
000
KO
RE
A
3
2,86
7,12
0
33,
867,
120
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
WB
6
,950
,283
7,0
30,2
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
!!!!
i) K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i Wad
ogo
Wad
ogo
856,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
ii) K
uend
elez
a U
tafit
i wa
Mifu
go
1,
200,
000
1
,200
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i)
Uim
aris
haji
uvuv
i wa
baha
ri ku
u 3,
666,
000
1,40
0,00
0 JI
CA
1
3,20
0,00
0
1
4,60
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
200,
000
FAO
/ KO
RE
A
692
,423
892
,423
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a 15
0,00
0 20
0,00
0
200
,000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Bar
abar
a
-
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Tun
guu-
Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
kech
ake
- Mko
ani
(31k
m)
1,0
00,0
00
2,8
00,0
00
2
,800
,000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0 O
FID
9,0
00,0
00
18,
000,
000
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni
3,70
0,00
0 2,
000,
000
BA
DE
A
6
,571
,000
8
,571
,000
iv
)Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni
(9.4
km
), P
ale
Kio
ngel
e - M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni
- Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4
,000
,000
A
fDB
11,
893,
561
1
5,89
3,56
1
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, K
inya
sini
- K
iwen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a
400
,000
400
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha V
iwan
ja v
ya N
dege
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0 61
,030
,000
61,
030,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
W
B
7
,301
,349
7
,341
,349
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha R
asili
mal
i na
Bia
shar
a za
Wan
yong
e Ta
nzan
ia (M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
UR
T 1
68,8
83
6
68,8
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
MIR
AD
I
ii)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
WO
RLD
BA
NK
2,8
94,6
93
2,9
44,6
93
iv) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a B
anda
ri ya
Mpi
gadu
ri 40
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
vi
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
!
230
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
) 2,
400,
000
4,50
0,00
0
4,5
00,0
00
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
MIR
AD
I 201
9/20
20 K
IMA
ENEO
MA
KU
U Y
A M
ATO
KEO
TZS
("00
0")
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A M
WA
KA
20
18/2
019
SMZ
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MC
HA
NG
O W
A W
ASH
IRIK
A W
A M
AEN
DEL
EO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
WA
SHIR
IKA
WA
M
AEN
DEL
EO
RU
ZUK
U
MK
OPO
KR
A A
: KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI
WA
UC
HU
MI J
UM
UIS
HI N
A E
ND
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UB
WA
ZO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Soko
, Kuo
ngez
a Th
aman
i na
Mis
aada
Viji
jini
(MIV
AR
F)
300
,000
IFA
D/A
GR
A/ A
fDB
3
99,6
16
3
99,6
16
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0 1,
000,
000
KO
RE
A
3
2,86
7,12
0
33,
867,
120
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
WB
6
,950
,283
7,0
30,2
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
!!!!
i) K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i Wad
ogo
Wad
ogo
856,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
ii) K
uend
elez
a U
tafit
i wa
Mifu
go
1,
200,
000
1
,200
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i)
Uim
aris
haji
uvuv
i wa
baha
ri ku
u 3,
666,
000
1,40
0,00
0 JI
CA
1
3,20
0,00
0
1
4,60
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
200,
000
FAO
/ KO
RE
A
692
,423
892
,423
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a 15
0,00
0 20
0,00
0
200
,000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Bar
abar
a
-
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Tun
guu-
Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
kech
ake
- Mko
ani
(31k
m)
1,0
00,0
00
2,8
00,0
00
2
,800
,000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0 O
FID
9,0
00,0
00
18,
000,
000
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni
3,70
0,00
0 2,
000,
000
BA
DE
A
6
,571
,000
8
,571
,000
iv
)Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni
(9.4
km
), P
ale
Kio
ngel
e - M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni
- Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4
,000
,000
A
fDB
11,
893,
561
1
5,89
3,56
1
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, K
inya
sini
- K
iwen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a
400
,000
400
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha V
iwan
ja v
ya N
dege
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0 61
,030
,000
61,
030,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
W
B
7
,301
,349
7
,341
,349
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha R
asili
mal
i na
Bia
shar
a za
Wan
yong
e Ta
nzan
ia (M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
UR
T 1
68,8
83
6
68,8
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
MIR
AD
I
ii)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
WO
RLD
BA
NK
2,8
94,6
93
2,9
44,6
93
iv) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a B
anda
ri ya
Mpi
gadu
ri 40
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
vi
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
!
230
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
) 2,
400,
000
4,50
0,00
0
4,5
00,0
00
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 91
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jni
-
i)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah
4,00
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
ii)
Uch
imba
ji w
a V
isim
a na
Usa
mba
zaji
Maj
i 53
6,21
3 86
3,00
0 C
HIN
A
5,0
81,5
62
5
,944
,562
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a El
imu
1,19
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
Pr
ogra
mu
ya U
gatu
zi w
a M
asua
la y
a El
imu
1,11
0,00
0 1,
110,
000
1
,110
,000
M
IRA
DI
-
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180
,000
ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Maa
bara
ya
Mke
mia
Mku
u w
a S
erik
ali
900,
000
-
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
aand
aliz
i
G
PE
/ UN
ICE
F 1,
590,
085
1
,590
,085
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
GP
E/S
IDA
/ U
NIC
EF/
US
AID
/ P
CD
/OFI
D
/MZF
/WB
4,
179,
622
2,70
0,00
0 6
,879
,622
v) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a 3,
100,
000
3,30
0,00
0 B
AD
EA
/ OP
EC
/ K
OR
EA
/WB
/ MZF
16
,457
,475
35
,646
,871
5
5,40
4,34
6
vi) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 1,
200,
000
650,
700
6
50,7
00
vii)
Mra
di w
a K
uije
ngea
Uw
ezo
Sek
ta y
a N
isha
ti Za
nzib
ar
65,0
00
S
IDA
4
,866
,511
4,8
66,5
11
viii)
Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
ar
NO
RW
AY
7
,382
,230
7,3
82,2
30
ix) U
hifa
dhi H
aki z
a W
atot
o
U
NIC
EF
375
,000
375
,000
x)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Jam
ii
U
NIC
EF
75,
000
75,
000
xi
) Uje
nzi w
a W
odi y
a W
azaz
i KM
KM
1
,500
,000
-
xii)
Mra
di w
a M
ashi
rikia
no y
a Ta
asis
i za
Ard
hi b
aina
ya
Zanz
ibar
na
Finl
and
50,0
00
-
xiii)
Kui
mar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i 2,
200,
000
2,90
0,00
0
2,9
00,0
00
xiv)
Mra
di w
a U
tafit
i wa
Nis
hati
Mba
dala
13
4,00
0
-
xv
) Uje
nzi w
a V
iwan
ja v
ya M
iche
zo v
ya W
ilaya
80
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
xv
i) U
jenz
i wa
Sku
li ya
Sek
onda
ri na
Ufu
ndi -
Mto
ni
1,65
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
xv
ii)M
radi
wa
Kui
mar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a V
izaz
i na
Vifo
50
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
xv
iii) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a W
azee
37
0,00
0 40
0,00
0
400
,000
xx
) Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I
G
F/U
NFP
A
540
,362
540
,362
JU
MLA
YA
KR
A
36,
146,
000
3
9,56
7,70
0
5
6,97
0,64
5
215
,039
,270
3
11,5
77,6
15
KR
A D
: KU
WEP
O M
AZI
NG
IRA
EN
DEL
EVU
NA
UH
IMIL
I WA
MA
BA
DIL
IKO
YA
TA
BIA
NC
HI
MIR
AD
I
!!i)
Kui
mar
isha
Usi
mam
izi w
a M
azin
gira
, M
alia
sili
na M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i-Za
nzib
ar
50,0
00
300,
000
UN
DP
4
56,6
00
7
56,6
00
iii) K
ukuz
a U
wez
o w
a K
itaifa
wa
Kuh
imili
Ath
ari z
a M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i (A
DB
-AC
CF)
33
,000
50
,000
A
fDB
5
0,00
0
JUM
LA Y
A K
RA
83
,000
35
0,00
0
456,
600
0 80
6,60
0 K
RA
E: K
USH
IKA
MA
NA
NA
MIS
ING
I YA
UTA
WA
LA B
OR
A
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a A
fisi z
a Se
rikal
i Za
nzib
ar
15,0
00,0
00
10,0
02,3
00
1
0,00
2,30
0
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Sekt
a ya
She
ria
1,00
0,00
0 !!
!!!!
!!!!
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
Pr
ogra
mu
ya M
ageu
zi K
atik
a U
sim
amiz
i wa
Fedh
a
N
OR
WA
Y
1,5
98,7
19
1
,598
,719
Pr
ogra
mu
ya M
ageu
zi y
a U
tum
ishi
wa
Um
ma
- II
20
0,00
0 W
B
2,5
48,2
02
2
,748
,202
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
MIR
AD
I 201
9/20
20 K
IMA
ENEO
MA
KU
U Y
A M
ATO
KEO
TZS
("00
0")
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A M
WA
KA
20
18/2
019
SMZ
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MC
HA
NG
O W
A W
ASH
IRIK
A W
A M
AEN
DEL
EO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
WA
SHIR
IKA
WA
M
AEN
DEL
EO
RU
ZUK
U
MK
OPO
KR
A A
: KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI
WA
UC
HU
MI J
UM
UIS
HI N
A E
ND
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UB
WA
ZO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Soko
, Kuo
ngez
a Th
aman
i na
Mis
aada
Viji
jini
(MIV
AR
F)
300
,000
IFA
D/A
GR
A/ A
fDB
3
99,6
16
3
99,6
16
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0 1,
000,
000
KO
RE
A
3
2,86
7,12
0
33,
867,
120
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
WB
6
,950
,283
7,0
30,2
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
!!!!
i) K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i Wad
ogo
Wad
ogo
856,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
ii) K
uend
elez
a U
tafit
i wa
Mifu
go
1,
200,
000
1
,200
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i)
Uim
aris
haji
uvuv
i wa
baha
ri ku
u 3,
666,
000
1,40
0,00
0 JI
CA
1
3,20
0,00
0
1
4,60
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
200,
000
FAO
/ KO
RE
A
692
,423
892
,423
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a 15
0,00
0 20
0,00
0
200
,000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Bar
abar
a
-
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Tun
guu-
Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
kech
ake
- Mko
ani
(31k
m)
1,0
00,0
00
2,8
00,0
00
2
,800
,000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0 O
FID
9,0
00,0
00
18,
000,
000
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni
3,70
0,00
0 2,
000,
000
BA
DE
A
6
,571
,000
8
,571
,000
iv
)Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni
(9.4
km
), P
ale
Kio
ngel
e - M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni
- Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4
,000
,000
A
fDB
11,
893,
561
1
5,89
3,56
1
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, K
inya
sini
- K
iwen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a
400
,000
400
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha V
iwan
ja v
ya N
dege
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0 61
,030
,000
61,
030,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
W
B
7
,301
,349
7
,341
,349
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha R
asili
mal
i na
Bia
shar
a za
Wan
yong
e Ta
nzan
ia (M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
UR
T 1
68,8
83
6
68,8
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
MIR
AD
I
ii)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
WO
RLD
BA
NK
2,8
94,6
93
2,9
44,6
93
iv) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a B
anda
ri ya
Mpi
gadu
ri 40
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
vi
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
!
230
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
) 2,
400,
000
4,50
0,00
0
4,5
00,0
00
viii)
Kue
ndel
eza
Tafit
i na
Ubu
nifu
20
0,00
0
ix) Z
anzi
bar E
-gov
ernm
ent O
ptic
al T
rans
imis
sion
Com
mun
icat
ion
Net
wor
k P
hase
II
50,0
00
100,
000
1
00,0
00
x) U
nunu
zi w
a La
nd C
raft
2,40
0,00
0 1,
900,
000
1
,900
,000
xi
) Mfu
mo
Mpy
a w
a U
toaj
i Les
eni k
wa
Mae
ndel
eo y
a S
ekta
Bin
afsi
50
,000
40
0,00
0
400
,000
xii)
Kud
hibi
ti S
umu
Kuv
u in
ayot
okan
a na
Ula
ji w
a M
ahin
di n
a N
jugu
(TA
NIP
AC
)
A
fDB
9
88,4
40
9
88,4
40
xiii)
Uhi
fadh
i wa
Mis
itu k
wa
Faid
a za
Kiu
chum
i
U
ND
P
228
,200
228
,200
xi
v) K
ilim
o ch
a K
usha
jihis
ha U
kulim
a w
a M
boga
na
Mat
unda
E
DF-
EU
2
,000
,000
2,0
00,0
00
xv) K
ilim
o K
inac
hohi
mili
Mab
adili
ko y
a H
ali y
a H
ewa
US
DA
-US
AID
4
4,40
0
4
4,40
0
xvi)
Kui
mar
isha
Uta
lii k
wa
Wot
e 1,
300,
000
1,50
0,00
0
1,5
00,0
00
xvii)
Mra
di w
a K
uend
elez
a B
anda
ri ya
Man
gapw
ani
4,20
0,00
0 4,
000,
000
4
,000
,000
xv
iii) M
radi
wa
Kuw
asai
dia
Waj
asiri
amal
i Wad
ogo
Wad
ogo
KH
ALI
FA F
UN
D
3,4
50,0
00
3
,450
,000
JU
MLA
YA
KR
A
44,
072,
000
1
10,9
30,0
00
2
8,12
2,24
5
70,
527,
723
2
09,5
79,9
68
KR
A B
: KU
KU
ZA U
WEZ
O W
A W
ATU
PR
OG
RA
MU
Pr
ogra
mu
ya A
jira
kwa
Vija
na
3,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha J
insi
a
-
i) U
saw
a w
a K
ijins
ia n
a K
uwaw
ezes
ha W
anaw
ake
UN
-Wom
en
245
,703
245
,703
ii)
Mra
di w
a K
ijins
ia
UN
FPA
4
20,0
00
4
20,0
00
MIR
AD
I
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u M
bada
la n
a A
mal
i - A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,00
0,00
0 A
fDB
7,0
00,0
00
8,0
00,0
00
ii) M
radi
wa
Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Kul
ea n
a K
utot
olea
Waj
asiri
amal
i (In
cuba
tor)
600,
000
6
00,0
00
JUM
LA Y
A K
RA
4,
600,
000
3,60
0,00
0
665,
703
7,00
0,00
0 11
,265
,703
K
RA
C: K
UTO
A H
UD
UM
A B
OR
A K
WA
WO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
hud
uma
za M
iji (Z
USP
)
W
B
5
7,40
7,04
2
57,
407,
042
Pr
ogra
mu
ya K
umal
iza
Mar
adhi
ya
Mal
aria
Zan
ziba
r 24
8,00
0 24
8,00
0 P
MI/G
F 5
,190
,664
5,4
38,6
64
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Mui
ndom
binu
ya
Afy
a
i)
Kui
pand
isha
had
hi H
ospi
tali
ya M
nazi
Mm
oja
4,16
0,00
0 2,
650,
000
2
,650
,000
ii)
Kuz
ipan
dish
a H
adhi
hos
pita
li za
Wila
ya n
a H
ospi
tal z
a V
ijiji
4,04
0,00
0 4,
250,
000
4
,250
,000
iii
) Uje
nzi w
a H
ospi
tali
ya R
ufaa
Bin
guni
(Aw
amu
ya K
wan
za)
4,00
0,00
0 6,
500,
000
6
,500
,000
iv
) Uje
nzi w
a B
ohar
i Kuu
ya
Daw
a-P
emba
25
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
amla
ka y
a D
awa
na V
ipod
ozi
250,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
vi) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Wag
onjw
a w
a A
kili
1,30
0,00
0 1,
300,
000
Hop
elan
d U
n 1,
400,
000
2
,700
,000
Prog
ram
u ya
Shi
rikis
hi y
a H
udum
a za
Afy
a ya
Uza
zi w
a M
ama
na M
toto
53
0,00
0 70
0,00
0 U
NFP
A/ W
HO
/GF
4,5
63,8
69
5
,263
,869
Pr
ogra
mu
ya K
udhi
biti
Mar
adhi
ya
UK
IMW
I, H
oma
ya In
i, K
ifua
Kik
uu n
a U
kom
a 24
8,00
0 24
8,00
0 G
F/TH
PS
5
,088
,265
5,3
36,2
65
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
binu
ya
Maj
i
-
i) U
imar
isha
ji w
a M
iund
mbi
nu y
a M
aji M
jini
50,0
00
JI
CA
4,5
35,2
26
4,5
35,2
26
ii) U
imar
isha
ji w
a M
iund
ombi
nu y
a M
aji M
jini M
agha
ribi (
AD
F12)
1,
064,
787
2,24
8,00
0 A
fDB
7,1
22,4
28
9,3
70,4
28
iii) U
huis
haji
na U
imar
isha
ji w
a M
fum
o w
a U
sam
baza
ji M
aji Z
anzi
bar
700,
000
700,
000
IND
IA
8
8,42
1,00
0
89,
121,
000
iv
) Uim
aris
haji
wa
Mfu
mo
wa
Maj
i Mac
hafu
kw
a M
ji w
a Za
nzib
ar (M
iji 2
5)
IND
IA
1
9,20
6,70
3
19,
206,
703
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 92
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
MIR
AD
I 201
9/20
20 K
IMA
ENEO
MA
KU
U Y
A M
ATO
KEO
TZS
("00
0")
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A M
WA
KA
20
18/2
019
SMZ
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MC
HA
NG
O W
A W
ASH
IRIK
A W
A M
AEN
DEL
EO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
WA
SHIR
IKA
WA
M
AEN
DEL
EO
RU
ZUK
U
MK
OPO
KR
A A
: KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI
WA
UC
HU
MI J
UM
UIS
HI N
A E
ND
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UB
WA
ZO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Soko
, Kuo
ngez
a Th
aman
i na
Mis
aada
Viji
jini
(MIV
AR
F)
300
,000
IFA
D/A
GR
A/ A
fDB
3
99,6
16
3
99,6
16
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0 1,
000,
000
KO
RE
A
3
2,86
7,12
0
33,
867,
120
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
WB
6
,950
,283
7,0
30,2
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
!!!!
i) K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i Wad
ogo
Wad
ogo
856,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
ii) K
uend
elez
a U
tafit
i wa
Mifu
go
1,
200,
000
1
,200
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i)
Uim
aris
haji
uvuv
i wa
baha
ri ku
u 3,
666,
000
1,40
0,00
0 JI
CA
1
3,20
0,00
0
1
4,60
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
200,
000
FAO
/ KO
RE
A
692
,423
892
,423
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a 15
0,00
0 20
0,00
0
200
,000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Bar
abar
a
-
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Tun
guu-
Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
kech
ake
- Mko
ani
(31k
m)
1,0
00,0
00
2,8
00,0
00
2
,800
,000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0 O
FID
9,0
00,0
00
18,
000,
000
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni
3,70
0,00
0 2,
000,
000
BA
DE
A
6
,571
,000
8
,571
,000
iv
)Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni
(9.4
km
), P
ale
Kio
ngel
e - M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni
- Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4
,000
,000
A
fDB
11,
893,
561
1
5,89
3,56
1
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, K
inya
sini
- K
iwen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a
400
,000
400
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha V
iwan
ja v
ya N
dege
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0 61
,030
,000
61,
030,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
W
B
7
,301
,349
7
,341
,349
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha R
asili
mal
i na
Bia
shar
a za
Wan
yong
e Ta
nzan
ia (M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
UR
T 1
68,8
83
6
68,8
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
MIR
AD
I
ii)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
WO
RLD
BA
NK
2,8
94,6
93
2,9
44,6
93
iv) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a B
anda
ri ya
Mpi
gadu
ri 40
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
vi
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
!
230
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
) 2,
400,
000
4,50
0,00
0
4,5
00,0
00
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jni
-
i)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah
4,00
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
ii)
Uch
imba
ji w
a V
isim
a na
Usa
mba
zaji
Maj
i 53
6,21
3 86
3,00
0 C
HIN
A
5,0
81,5
62
5
,944
,562
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha M
iund
ombi
nu y
a El
imu
1,19
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
Pr
ogra
mu
ya U
gatu
zi w
a M
asua
la y
a El
imu
1,11
0,00
0 1,
110,
000
1
,110
,000
M
IRA
DI
-
i)
Kuj
enga
Uw
ezo
wa
Kuk
abili
ana
na M
aafa
U
ND
P
180
,000
180
,000
ii)
Mra
di w
a U
jenz
i wa
Maa
bara
ya
Mke
mia
Mku
u w
a S
erik
ali
900,
000
-
iii) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
aand
aliz
i
G
PE
/ UN
ICE
F 1,
590,
085
1
,590
,085
iv) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya M
sing
i
GP
E/S
IDA
/ U
NIC
EF/
US
AID
/ P
CD
/OFI
D
/MZF
/WB
4,
179,
622
2,70
0,00
0 6
,879
,622
v) U
imar
isha
ji w
a E
limu
ya L
azim
a 3,
100,
000
3,30
0,00
0 B
AD
EA
/ OP
EC
/ K
OR
EA
/WB
/ MZF
16
,457
,475
35
,646
,871
5
5,40
4,34
6
vi) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 1,
200,
000
650,
700
6
50,7
00
vii)
Mra
di w
a K
uije
ngea
Uw
ezo
Sek
ta y
a N
isha
ti Za
nzib
ar
65,0
00
S
IDA
4
,866
,511
4,8
66,5
11
viii)
Kuj
enga
Uw
ezo
na M
aten
gene
zo y
a M
iund
ombi
nu y
a U
mem
e Za
nzib
ar
NO
RW
AY
7
,382
,230
7,3
82,2
30
ix) U
hifa
dhi H
aki z
a W
atot
o
U
NIC
EF
375
,000
375
,000
x)
Mra
di w
a H
ifadh
i ya
Jam
ii
U
NIC
EF
75,
000
75,
000
xi
) Uje
nzi w
a W
odi y
a W
azaz
i KM
KM
1
,500
,000
-
xii)
Mra
di w
a M
ashi
rikia
no y
a Ta
asis
i za
Ard
hi b
aina
ya
Zanz
ibar
na
Finl
and
50,0
00
-
xiii)
Kui
mar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i 2,
200,
000
2,90
0,00
0
2,9
00,0
00
xiv)
Mra
di w
a U
tafit
i wa
Nis
hati
Mba
dala
13
4,00
0
-
xv
) Uje
nzi w
a V
iwan
ja v
ya M
iche
zo v
ya W
ilaya
80
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
xv
i) U
jenz
i wa
Sku
li ya
Sek
onda
ri na
Ufu
ndi -
Mto
ni
1,65
0,00
0 2,
500,
000
2
,500
,000
xv
ii)M
radi
wa
Kui
mar
isha
Mfu
mo
wa
Usa
jili w
a V
izaz
i na
Vifo
50
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
xv
iii) M
radi
wa
Hifa
dhi y
a W
azee
37
0,00
0 40
0,00
0
400
,000
xx
) Kuz
uia
Maa
mbu
kizi
ya
UK
IMW
I
G
F/U
NFP
A
540
,362
540
,362
JU
MLA
YA
KR
A
36,
146,
000
3
9,56
7,70
0
5
6,97
0,64
5
215
,039
,270
3
11,5
77,6
15
KR
A D
: KU
WEP
O M
AZI
NG
IRA
EN
DEL
EVU
NA
UH
IMIL
I WA
MA
BA
DIL
IKO
YA
TA
BIA
NC
HI
MIR
AD
I
!!i)
Kui
mar
isha
Usi
mam
izi w
a M
azin
gira
, M
alia
sili
na M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i-Za
nzib
ar
50,0
00
300,
000
UN
DP
4
56,6
00
7
56,6
00
iii) K
ukuz
a U
wez
o w
a K
itaifa
wa
Kuh
imili
Ath
ari z
a M
abad
iliko
ya
Tabi
anch
i (A
DB
-AC
CF)
33
,000
50
,000
A
fDB
5
0,00
0
JUM
LA Y
A K
RA
83
,000
35
0,00
0
456,
600
0 80
6,60
0 K
RA
E: K
USH
IKA
MA
NA
NA
MIS
ING
I YA
UTA
WA
LA B
OR
A
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a A
fisi z
a Se
rikal
i Za
nzib
ar
15,0
00,0
00
10,0
02,3
00
1
0,00
2,30
0
Prog
ram
u ya
Mag
euzi
ya
Sekt
a ya
She
ria
1,00
0,00
0 !!
!!!!
!!!!
Prog
ram
u ya
Upa
tikan
aji R
asili
mal
i Fed
ha
1,00
0,00
0 30
0,00
0
300
,000
Pr
ogra
mu
ya M
ageu
zi K
atik
a U
sim
amiz
i wa
Fedh
a
N
OR
WA
Y
1,5
98,7
19
1
,598
,719
Pr
ogra
mu
ya M
ageu
zi y
a U
tum
ishi
wa
Um
ma
- II
20
0,00
0 W
B
2,5
48,2
02
2
,748
,202
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 93
Kia
mba
tisho
nam
ba 2
:
MG
AO
WA
FED
HA
PR
OG
RA
MU
MIR
AD
I 201
9/20
20 K
IMA
ENEO
MA
KU
U Y
A M
ATO
KEO
TZS
("00
0")
JIN
A L
A P
RO
GR
AM
U/M
RA
DI
MA
KIS
IO
KW
A M
WA
KA
20
18/2
019
SMZ
MA
KIS
IO
KW
A
MW
AK
A
2019
/202
0 SM
Z
MC
HA
NG
O W
A W
ASH
IRIK
A W
A M
AEN
DEL
EO
JU
MLA
YA
B
AJE
TI
WA
SHIR
IKA
WA
M
AEN
DEL
EO
RU
ZUK
U
MK
OPO
KR
A A
: KU
WEZ
ESH
A U
KU
AJI
WA
UC
HU
MI J
UM
UIS
HI N
A E
ND
ELEV
U K
WA
SEK
TA K
UB
WA
ZO
TE
PRO
GR
AM
U
!!
Prog
ram
u ya
Miu
ndom
binu
ya
Soko
, Kuo
ngez
a Th
aman
i na
Mis
aada
Viji
jini
(MIV
AR
F)
300
,000
IFA
D/A
GR
A/ A
fDB
3
99,6
16
3
99,6
16
Prog
ram
u ya
Um
wag
iliaj
i 50
0,00
0 1,
000,
000
KO
RE
A
3
2,86
7,12
0
33,
867,
120
Pr
ogra
mu
ya K
usai
dia
Kili
mo
na U
haki
ka w
a C
haku
la (G
AFS
IP)
80,0
00
80,0
00
WB
6
,950
,283
7,0
30,2
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Miu
ndom
binu
ya
Kili
mo
!!!!
i) K
uend
elez
a m
iund
ombi
nu y
a M
ifugo
na
Waf
ugaj
i Wad
ogo
Wad
ogo
856,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
ii) K
uend
elez
a U
tafit
i wa
Mifu
go
1,
200,
000
1
,200
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i)
Uim
aris
haji
uvuv
i wa
baha
ri ku
u 3,
666,
000
1,40
0,00
0 JI
CA
1
3,20
0,00
0
1
4,60
0,00
0
ii) K
uim
aris
ha u
fuga
ji w
a m
azao
ya
baha
rini
200,
000
200,
000
FAO
/ KO
RE
A
692
,423
892
,423
Pr
ogra
mu
ya M
azin
gira
Bor
a ya
Bia
shar
a 15
0,00
0 20
0,00
0
200
,000
Pr
ogra
mu
Mju
mui
shi y
a K
uend
elez
a U
talii
8
50,0
00
2,4
00,0
00
2
,400
,000
Pr
ogra
mu
ya U
jenz
i wa
Bar
abar
a
-
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Tun
guu-
Mak
undu
chi (
30km
) na
Cha
kech
ake
- Mko
ani
(31k
m)
1,0
00,0
00
2,8
00,0
00
2
,800
,000
ii)
Uje
nzi w
a B
arab
ara
Ole
-Ken
geja
1,
500,
000
9,00
0,00
0 O
FID
9,0
00,0
00
18,
000,
000
iii
) Uje
nzi w
a ba
raba
ra z
a K
izim
bani
-Kib
oje
na J
umbi
-Koa
ni
3,70
0,00
0 2,
000,
000
BA
DE
A
6
,571
,000
8
,571
,000
iv
)Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
v) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Bub
ubu-
Mah
onda
- M
koko
toni
(31
km),
Mkw
ajun
i-Kiji
ni
(9.4
km
), P
ale
Kio
ngel
e - M
kwaj
uni (
4.6
km),
Mat
emw
e - M
uyun
i (7.
6 km
), Fu
oni
- Kom
beni
(km
8.6
) na
Bub
ubu
Pol
isi -
Chu
ini (
km3)
7
,100
,000
4
,000
,000
A
fDB
11,
893,
561
1
5,89
3,56
1
vi) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Joz
ani-C
hara
we-
Uko
ngor
oni (
km 2
3)
3,1
00,0
00
3,0
00,0
00
3
,000
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Bar
abar
a ya
Kito
gani
- P
aje,
Mah
onda
- D
onge
- M
koko
toni
, K
inya
sini
- K
iwen
gwa
na D
unga
- C
hwak
a
400
,000
400
,000
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha V
iwan
ja v
ya N
dege
i)
Uje
nzi w
a Je
ngo
Jipy
a la
Abi
ria Z
anzi
bar
4,10
0,00
0 61
,030
,000
61,
030,
000
M
pang
o w
a K
unus
uru
Kay
a M
asik
ini (
TASA
F III
) 4
0,00
0
40,
000
W
B
7
,301
,349
7
,341
,349
Pr
ogra
mu
ya M
pang
o w
a K
uras
imis
ha R
asili
mal
i na
Bia
shar
a za
Wan
yong
e Ta
nzan
ia (M
KU
RA
BIT
A)
200,
000
500,
000
UR
T 1
68,8
83
6
68,8
83
Prog
ram
u ya
Kue
ndel
eza
Viw
anda
2,
500,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
MIR
AD
I
ii)
Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Shu
ghul
i za
Uvu
vi w
a K
anda
ya
Kus
ini M
asha
riki
mw
a B
ahar
i ya
Hin
di (S
WIO
FIS
H)
50,0
00
50,0
00
WO
RLD
BA
NK
2,8
94,6
93
2,9
44,6
93
iv) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
2
,000
,000
v)
Uje
nzi w
a B
anda
ri ya
Mpi
gadu
ri 40
0,00
0 3,
000,
000
3
,000
,000
vi
) Kup
ungu
za U
mas
ikin
i na
Ufu
atili
aji w
a S
DG
s 18
0,00
0 23
0,00
0
!
230
,000
vi
i) U
jenz
i wa
Kiw
anda
cha
Ush
oni (
ZQTL
) 2,
400,
000
4,50
0,00
0
4,5
00,0
00
MIR
AD
I
i)
Uim
aris
haji
Nyu
mba
za
Vio
ngoz
i na
Nyu
mba
za
Ser
ikal
i 1,
000,
000
2,00
0,00
0
2,0
00,0
00
ii) M
radi
wa
Uw
ekaj
i Kam
era
na V
ifaa
vya
Ulin
zi
20,0
00,0
00
7,00
0,00
0
7,0
00,0
00
iii) M
radi
wa
Uje
nzi w
a K
ituo
cha
Hud
uma
za K
urek
ebis
ha W
atot
o 70
0,00
0
-
iv
) Kui
mar
isha
Uta
wal
a B
ora
Aw
amu
ya T
atu
150,
000
100,
000
AfD
B
4
,013
,767
4
,113
,767
v)
Kuo
anis
ha M
asua
la y
a Id
adi y
a W
atu
katik
a A
fya
ya U
zazi
, Jin
sia
na
Kup
ungu
za U
mas
ikin
i 29
,000
UN
FPA
4
00,4
00
4
00,4
00
viii)
Uim
aris
haji
wa
Ras
ilim
ali z
a N
dani
na
Usi
mam
izi w
a M
alia
sili
100,
000
50,0
00
AfD
B
2
,523
,642
2
,573
,642
ix
) Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850,
000
350,
000
3
50,0
00
x) U
nunu
zi w
a M
eli
18,0
00,0
00
-
xii)
Uje
nzi n
a U
kara
bati
wa
Kam
bi n
a N
yum
ba z
a K
MK
M
1,30
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
xiii)
Uje
nzi w
a N
yum
ba z
a M
akaa
zi n
a M
ahan
ga z
a K
ikos
i cha
Maf
unzo
1,
400,
000
1,00
0,00
0
1,0
00,0
00
xv) M
radi
wa
Kuj
enga
Uw
ezo
Taas
isi z
a S
erik
ali
50,0
00
50,0
00
UN
DP
1
,585
,990
1,6
35,9
90
xvi)
Mra
di w
a U
ratib
u na
Usi
mam
izi w
a M
alen
go y
a M
aend
eleo
End
elev
u (S
DG
s) n
a M
KU
ZA II
I
20,
000
U
ND
P
1,6
89,0
79
1
,709
,079
xv
ii) U
jenz
i wa
Ofis
i ya
ZAE
CA
800,
000
8
00,0
00
xviii
) Usi
mam
izi w
a Ta
ka N
gum
u M
anis
paa
ya M
agha
ribi "
B"
770,
000
-
xix)
Uje
nzi w
a N
yum
ba n
a M
ahan
ga y
a K
ikos
i cha
Val
antia
50
0,00
0 50
0,00
0
500
,000
xx
) Uje
nzi w
a M
ajen
go y
a K
ambi
za
JKU
50
0,00
0 1,
000,
000
1
,000
,000
xx
i) U
jenz
i wa
Mah
anga
na
Nyu
mba
za
Maa
skar
i wa
KZU
50
0,00
0 50
0,00
0
500
,000
xx
ii) U
jenz
i wa
Kitu
o ch
a Ti
ba n
a M
arek
ebis
ho y
a Ta
bia
500,
000
680,
000
6
80,0
00
xxiii
) Mra
di w
a U
sim
amiz
i wa
Upa
tikan
aji w
a H
aki
40
0,00
0 U
ND
P
1,4
83,3
00
1
,883
,300
xx
iii) U
jenz
i wa
Jeng
o la
Ofis
i na
Stu
dio
za R
edio
Mka
njun
i - P
emba
50
0,00
0 1,
500,
000
1
,500
,000
JU
MLA
YA
KR
A
63,8
49,0
00
27,9
52,3
00
9,
305,
690
6,53
7,40
9 43
,795
,399
JU
MLA
KU
BW
A
148,
750,
000
182,
400,
000
95
,520
,883
29
9,10
4,40
2 57
7,02
5,28
5 JU
MLA
YA
FED
HA
ZA
WA
HIS
AN
I !!
!!
394,
625,
285
!
!
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 94
Kia
mba
tisho
nam
ba 3
:
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I YA
MA
END
ELEO
CH
INI Y
A M
FUK
O W
A M
IUN
DO
MB
INU
(IN
FRA
STR
UC
TUR
E FU
ND
) TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I M
AK
ISIO
KW
A
MW
AK
A 2
018/
19
SMZ
MA
KIS
IO K
WA
M
WA
KA
201
9/20
SM
Z
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
850
,000
3
50,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
patik
anaj
i Ras
ilim
ali F
edha
1,
000,
000
300,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,00
0,00
0 30
0,00
0 L0
1 W
IZA
RA
YA
KIL
IMO
, M
ALI
ASI
LI, M
IFU
GO
NA
UVU
VI
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i) U
imar
isha
ji U
vuvi
wa
Bah
ari K
uu
1,
400,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
0 1,
400,
000
R01
W
IZA
RA
YA
BIA
SHA
RA
NA
VIW
AN
DA
i) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
2,00
0,00
0 2,
000,
000
K01
W
IZA
RA
YA
ELI
MU
NA
MA
FUN
ZO Y
A A
MA
LI
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u M
bada
la n
a A
mal
i - A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
600,
000
1,00
0,00
0 H
01
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
binu
ya
Afy
a
i) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Ruf
aa B
ingu
ni (A
wam
u ya
Kw
anza
)
6,00
0,00
0
Mra
di
i)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
kem
ia M
kuu
900,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
90
0,00
0 6,
000,
000
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 95
N01
W
IZA
RA
YA
AR
DH
I, N
YUM
BA
, MA
JI N
A N
ISH
ATI
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jini
i)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah
4,00
0,00
0 3,
000,
000
M
radi
i) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 1,
000,
000
650,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
5,00
0,00
0 3,
650,
000
P01
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a B
arab
ara
i)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
ii) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Ole
- Ken
geja
5,60
0,00
0
i)
Unu
nuzi
wa
Land
Cra
ft 2,
400,
000
1,90
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3,
400,
000
8,50
0,00
0 G
07
MA
MLA
KA
YA
KU
ZUIA
RU
SHW
A N
A U
HU
JUM
U W
A U
CH
UM
I
Uje
nzi w
a O
fisi y
a ZA
EC
A
80
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
800,
000
J02
KA
MIS
HEN
I YA
UTA
LII
K
uim
aris
ha U
talii
kw
a W
ote
1,
500,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,
500,
000
S01
WIZ
AR
A Y
A V
IJA
NA
, UTA
MA
DU
NI,
SAN
AA
NA
MIC
HEZ
O
U
jenz
i wa
Viw
anja
vya
Mic
hezo
vya
Wila
ya
2,
000,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
2,
000,
000
D01
O
FISI
YA
RA
IS T
AW
ALA
ZA
MIK
OA
, SER
IKA
LI Z
A M
ITA
A N
A ID
AR
A M
AA
LUM
ZA
SM
Z
i) U
wek
aji w
a K
amer
a na
Vifa
a vy
a U
linzi
20
,000
,000
7,
000,
000
ii)
Uje
nzi w
a K
iwan
da c
ha U
shon
i (ZQ
TL)
1,00
0,00
0 3,
600,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
21,0
00,0
00
10,6
00,0
00
D04
K
IKO
SI M
AA
LUM
CH
A K
UZU
IA M
AG
END
O (K
MK
M)
i)
Uje
nzi w
a W
odi y
a W
azaz
i KM
KM
1
,500
,000
Kia
mba
tisho
nam
ba 3
:
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I YA
MA
END
ELEO
CH
INI Y
A M
FUK
O W
A M
IUN
DO
MB
INU
(IN
FRA
STR
UC
TUR
E FU
ND
) TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I M
AK
ISIO
KW
A
MW
AK
A 2
018/
19
SMZ
MA
KIS
IO K
WA
M
WA
KA
201
9/20
SM
Z
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
850
,000
3
50,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
patik
anaj
i Ras
ilim
ali F
edha
1,
000,
000
300,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,00
0,00
0 30
0,00
0 L0
1 W
IZA
RA
YA
KIL
IMO
, M
ALI
ASI
LI, M
IFU
GO
NA
UVU
VI
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i) U
imar
isha
ji U
vuvi
wa
Bah
ari K
uu
1,
400,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
0 1,
400,
000
R01
W
IZA
RA
YA
BIA
SHA
RA
NA
VIW
AN
DA
i) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
2,00
0,00
0 2,
000,
000
K01
W
IZA
RA
YA
ELI
MU
NA
MA
FUN
ZO Y
A A
MA
LI
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u M
bada
la n
a A
mal
i - A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
600,
000
1,00
0,00
0 H
01
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
binu
ya
Afy
a
i) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Ruf
aa B
ingu
ni (A
wam
u ya
Kw
anza
)
6,00
0,00
0
Mra
di
i)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
kem
ia M
kuu
900,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
90
0,00
0 6,
000,
000
Mwelekeo wa Uchumi 2019 na Mpango wa Maendeleo 2019/20 96
ii)
Kui
mar
isha
Hud
uma
za U
zam
iaji
na U
okoz
i 2
,200
,000
2
,900
,000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3,
700,
000
2,90
0,00
0
JUM
LA K
UB
WA
39
,450
,000
41
,000
,000
!!
!!
!
N01
W
IZA
RA
YA
AR
DH
I, N
YUM
BA
, MA
JI N
A N
ISH
ATI
Prog
ram
u ya
Usa
mba
zaji
Maj
i Viji
jini
i)
Kue
ndel
eza
Vis
ima
vya
Ras
el K
haim
ah
4,00
0,00
0 3,
000,
000
M
radi
i) U
sam
baza
ji U
mem
e V
ijijin
i 1,
000,
000
650,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
5,00
0,00
0 3,
650,
000
P01
WIZ
AR
A Y
A U
JEN
ZI, M
AW
ASI
LIA
NO
NA
USA
FIR
ISH
AJI
Prog
ram
u ya
Uje
nzi w
a B
arab
ara
i)
Uje
nzi w
a ba
raba
ra y
a C
hake
-Wet
e 1,
000,
000
1,00
0,00
0
ii) U
jenz
i wa
Bar
abar
a za
Ole
- Ken
geja
5,60
0,00
0
i)
Unu
nuzi
wa
Land
Cra
ft 2,
400,
000
1,90
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
3,
400,
000
8,50
0,00
0 G
07
MA
MLA
KA
YA
KU
ZUIA
RU
SHW
A N
A U
HU
JUM
U W
A U
CH
UM
I
Uje
nzi w
a O
fisi y
a ZA
EC
A
80
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
800,
000
J02
KA
MIS
HEN
I YA
UTA
LII
K
uim
aris
ha U
talii
kw
a W
ote
1,
500,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,
500,
000
S01
WIZ
AR
A Y
A V
IJA
NA
, UTA
MA
DU
NI,
SAN
AA
NA
MIC
HEZ
O
U
jenz
i wa
Viw
anja
vya
Mic
hezo
vya
Wila
ya
2,
000,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
2,
000,
000
D01
O
FISI
YA
RA
IS T
AW
ALA
ZA
MIK
OA
, SER
IKA
LI Z
A M
ITA
A N
A ID
AR
A M
AA
LUM
ZA
SM
Z
i) U
wek
aji w
a K
amer
a na
Vifa
a vy
a U
linzi
20
,000
,000
7,
000,
000
ii)
Uje
nzi w
a K
iwan
da c
ha U
shon
i (ZQ
TL)
1,00
0,00
0 3,
600,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
21,0
00,0
00
10,6
00,0
00
D04
K
IKO
SI M
AA
LUM
CH
A K
UZU
IA M
AG
END
O (K
MK
M)
i)
Uje
nzi w
a W
odi y
a W
azaz
i KM
KM
1
,500
,000
Kia
mba
tisho
nam
ba 3
:
PR
OG
RA
MU
/MIR
AD
I YA
MA
END
ELEO
CH
INI Y
A M
FUK
O W
A M
IUN
DO
MB
INU
(IN
FRA
STR
UC
TUR
E FU
ND
) TZS
"00
0"
KIF
UN
GU
JI
NA
LA
PR
OG
RA
MU
/MR
AD
I M
AK
ISIO
KW
A
MW
AK
A 2
018/
19
SMZ
MA
KIS
IO K
WA
M
WA
KA
201
9/20
SM
Z
C01
O
FISI
YA
MA
KA
MO
WA
PIL
I WA
RA
IS
i)
Uje
nzi w
a N
yum
ba y
a M
akam
u w
a P
ili w
a R
ais
850
,000
3
50,0
00
JU
MLA
YA
FU
NG
U
850
,000
3
50,0
00
F01
WIZ
AR
A Y
A F
EDH
A N
A M
IPA
NG
O
Pr
ogra
mu
ya U
patik
anaj
i Ras
ilim
ali F
edha
1,
000,
000
300,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
1,00
0,00
0 30
0,00
0 L0
1 W
IZA
RA
YA
KIL
IMO
, M
ALI
ASI
LI, M
IFU
GO
NA
UVU
VI
Pr
ogra
mu
ya K
uim
aris
ha U
vuvi
i) U
imar
isha
ji U
vuvi
wa
Bah
ari K
uu
1,
400,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
0 1,
400,
000
R01
W
IZA
RA
YA
BIA
SHA
RA
NA
VIW
AN
DA
i) K
uim
aris
ha T
aasi
si y
a V
iwan
go Z
anzi
bar
2,00
0,00
0 2,
000,
000
JU
MLA
YA
FU
NG
U
2,00
0,00
0 2,
000,
000
K01
W
IZA
RA
YA
ELI
MU
NA
MA
FUN
ZO Y
A A
MA
LI
i)
Uim
aris
haji
wa
Elim
u M
bada
la n
a A
mal
i - A
wam
u ya
Pili
1,
600,
000
1,00
0,00
0
JUM
LA Y
A F
UN
GU
1,
600,
000
1,00
0,00
0 H
01
WIZ
AR
A Y
A A
FYA
Prog
ram
u ya
Kui
mar
isha
Miu
ndom
binu
ya
Afy
a
i) U
jenz
i wa
Hos
pita
l ya
Ruf
aa B
ingu
ni (A
wam
u ya
Kw
anza
)
6,00
0,00
0
Mra
di
i)
Uje
nzi w
a M
aaba
ra y
a M
kem
ia M
kuu
900,
000
JUM
LA Y
A F
UN
GU
90
0,00
0 6,
000,
000