3
UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI (UKAWA) TAARIFA KWA UMMA Utangulizi Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), uliasisiwa wakati wa Bunge Maalum la Katiba. Lengo likiwa kuunganisha nguvu za Wajumbe wote wa Bunge hilo walioamini katika kuheshimu maoni ya wananchi yaliyowasilishwa kupitia Rasimu ya Katiba iliyotayarishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba. Kundi hili lilihusisha baadhi ya Wajumbe kutoka makundi yote. Baadaye, kundi hili lilipungua na kubaki na wajumbe kutoka vyama vya NLD, NCCR - Mageuzi, CUF na CHADEMA. Aidha, Wajumbe toka kundi la 201 walibaki wachache ambao walikataa kuyumbishwa. Nje ya Bunge Maalum, viongozi na wanachama wa vyama vya siasa, makundi mbalimbali yakiwemo ya kijamii, kidini, kitaaluma, kiraia na hata raia mmoja mmoja yaliendelea kushiriki katika mijadala na wengi wao wakitaka maoni ya wananchi kama yalivyoratibiwa na Tume ya Mabadiliko ya Katibana kuungwa mkono na UKAWA yaheshimiwe. Baada ya mvutano wa muda mrefu, ni wazi sasa kuwa zoezi la kuipatia nchi yetu Katiba mpya chini ya serikali ya awamu ya nne ya uongozilimekwama. Katiba mpya inayotokana na maoni ya wananchi ni nyezo ya ku kia malengo mapana zaidi ya kuwa na taifa la wananchi walioelimika na kujitambua, wenye afya bora, kujenga uchumi imara na unaoongeza ajira kwa vijana wetu, kutokomeza umasikini, kutumia raslimali na maliasili za nchi kwa manufaa ya wananchi wote na kuwa taifa lenye utu, uzalendo, uadili , umoja, uwazi na uwajibikaji. Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015 Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 ni fursa ya kipekee ya kuleta mabadiliko makubwa katika nchi yetu ya kuondoa mfumo kandamizi uliojikita ndani ya CCM. Watanzania wanahitaji mabadiliko yatakayowapatia serikali madhubuti yenye kra mpya na bunifu kwa maslahi yao. 1

Press Ukawa Lowasa

Embed Size (px)

DESCRIPTION

PRESS UKAWA LOWASSA

Citation preview

TAARIFA KWA UMMA

UMOJA WA KATIBA YA WANANCHI(UKAWA)

TAARIFA KWA UMMA

Utangulizi

Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), uliasisiwa wakati wa Bunge Maalum la Katiba. Lengo likiwa kuunganisha nguvu za Wajumbe wote wa Bunge hilo walioamini katika kuheshimu maoni ya wananchi yaliyowasilishwa kupitia Rasimu ya Katiba iliyotayarishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Waziri Mkuu Mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba. Kundi hili lilihusisha baadhi ya Wajumbe kutoka makundi yote. Baadaye, kundi hili lilipungua na kubaki na wajumbe kutoka vyama vya NLD, NCCR - Mageuzi, CUF na CHADEMA. Aidha, Wajumbe toka kundi la 201 walibaki wachache ambao walikataa kuyumbishwa.

Nje ya Bunge Maalum, viongozi na wanachama wa vyama vya siasa, makundi mbalimbali yakiwemo ya kijamii, kidini, kitaaluma, kiraia na hata raia mmoja mmoja yaliendelea kushiriki katika mijadala na wengi wao wakitaka maoni ya wananchi kama yalivyoratibiwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kuungwa mkono na UKAWA yaheshimiwe.

Baada ya mvutano wa muda mrefu, ni wazi sasa kuwa zoezi la kuipatia nchi yetu Katiba mpya chini ya serikali ya awamu ya nne ya uongozi limekwama.

Katiba mpya inayotokana na maoni ya wananchi ni nyezo ya kufikia malengo mapana zaidi ya kuwa na taifa la wananchi walioelimika na kujitambua, wenye afya bora, kujenga uchumi imara na unaoongeza ajira kwa vijana wetu, kutokomeza umasikini, kutumia raslimali na maliasili za nchi kwa manufaa ya wananchi wote na kuwa taifa lenye utu, uzalendo, uadilifi, umoja, uwazi na uwajibikaji.

Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015

Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015 ni fursa ya kipekee ya kuleta mabadiliko makubwa katika nchi yetu ya kuondoa mfumo kandamizi uliojikita ndani ya CCM. Watanzania wanahitaji mabadiliko yatakayowapatia serikali madhubuti yenye fikra mpya na bunifu kwa maslahi yao.

Watanzania wanahitaji mabadiliko yatakayojenga demokrasia ya kweli na kuachana na uonevu, udhalilishaji, fitna na majungu unaoendelezwa na CCM.

Taifa letu linakabiliwa na ombwe la uongozi ambao umesababisha nchi yetu kuyumba na kuwa na mipasuko hatari ndani ya jamii. Watanzania wanahitaji uongozi thabiti wenye dira, nidhamu na uadilifu utakaolipeleka mbele taifa letu.

Uchaguzi wa Oktoba 2015, ukitumiwa vizuri na kimkakati utaleta mabadiliko makubwa yanayotakiwa na wananchi. Uchaguzi huu ni fursa muhimu ya kujenga mshikamano wa Taifa. Kwa mantiki hii UKAWA unaamini katika kuweka mbele maslahi mapana ya wananchi kwa kujenga mshikamano ndani na nje ya vyama vyetu tunapoelekea katika Uchaguzi Mkuu na hata baada ya Uchaguzi Mkuu.

Ili tulete mabadiliko yatakayotupatia katiba bora na kufikia malengo tajwa hapo juu ni muhimu UKAWA ushinde uchaguzi wa 2015.

Watanzania wameshuhudia hadaa, uonevu, udhalilishaji, upendeleo na ukandamizaji katika mchakato wa kupata Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM. Kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu, kanuni na katiba ya chama chao.

Katika kutafakari kwa kina maslahi mapana ya Taifa letu, UKAWA tunahitaji viongozi wenye sifa, uwezo na weledi katika kulinda, kuheshimu na kusimamia rasilimali za Taifa kwa maslahi ya Watanzania wote. Aidha, viongozi wa aina hii hawawezi kuwa ndani ya CCM maana mfumo wa CCM haumpi kiongozi binafsi kutumia vipaji vyake au ubunifu wake binafsi katika kusimamia maslahi ya taifa letu.

UKAWA tunaamini kuwa kwa maslahi mapana ya taifa letu tunamuhitaji kila Mtanzania ambaye yuko tayari kujiunga nasi katika kuhakikisha kuwa taifa letu linakuwa salama na lenye amani ya kweli ambayo msingi wake ni haki.

Hivyo basi, ni rai ya UKAWA kwa kila Mtanzania ambaye yuko tayari kuuondoa mfumo huu kandamizi na dhalimu wa CCM kushirikiana na UKAWA kwa lengo la kujenga Taifa imara.

Tunachukua fursa hii kipekee kumwalika Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mheshimiwa Edward Lowassa ajiunge na UKAWA na tuko tayari kushirikiana naye katika kuhakikisha kuwa tunaiondoa CCM madarakani katika uchaguzi mkuu ujao. Tunaamini Mheshimiwa Lowassa ana uwezo wa kuhamasisha umma kuikataa CCM yenye kusimamia mifumo isiyotenda haki. Ni mchapakazi makini na mfuatiliaji wa karibu wa utendaji katika majukumu anayokabidhiwa.

Ni lengo la UKAWA kushirikiana katika Uchaguzi Mkuu na tutaweka mgombea mmoja wa udiwani katika kila kata na wadi, mgombea mmoja wa uwakilishi na ubunge katika kila jimbo, na mgombea mmoja wa Urais wa Zanzibar na mgombea mmoja wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano.

UKAWA ndilo Tumaini la Watanzania. Tusikubali kunyamaza pale ambapo sauti zetu zinanyamazishwa kwa lazima na bila sababu. Tusikubali kunyimwa fursa ambazo tuna uwezo nazo. Tuwe tayari kushiriki michakato ya kidemokrasia ya kuleta mabadiliko na kupata viongozi bora. Mungu Ibariki Tanzania. Mungu Ibariki UKAWA.

UKAWA NDILO TUMAINI LETU.

James Francis Mbatia (Mb)Mwenyekiti wa Taifa NCCR Mageuzi(kny Wenyeviti wa UKAWA Tarehe 27 Julai 2015)

1