33
SHERIA YA LESENI ZA USAFIRISHAJI (SURA YA 317) _____________ KANUNI _____________ (Zimetengenezwa chini ya kifungu cha 45) _____________ KANUNI ZA LESENI ZA USAFIRISHAJI (MAGARI YA ABIRIA), ZA MWAKA 2019 _____________ MPANGILIO WA KANUNI Kanuni Jina SEHEMU YA KWANZA MASHARTI YA AWALI 1. Jina la Kanuni. 2. Matumizi ya Kanuni. 3. Tafsiri. SEHEMU YA PILI MAOMBI NA UTOAJI WA LESENI 4. Vigezo vya kuomba leseni kwa kampuni. 5. Vigezo vya kuomba leseni kwa mtu binafsi. 6. Utaratibu wa kuomba leseni. 7. Vigezo vya kuomba leseni kwa magari ya shule. 8. Utaratibu wa kuomba leseni za magari ya shule. 9. Vigezo vya kutoa leseni. 10. Aina na muda wa leseni. 11. Leseni ya Kawaida. 12. Leseni ya Muda Mfupi. 13. Leseni Maalumu. 14. Ada za leseni na tozo nyingine. 15. Uchambuzi wa maombi na utoaji wa leseni. 16. Kukataliwa kwa ombi la leseni. 17. Yaliyomo kwenye leseni ya kampuni au mtu binafsi. 18. Kubandika leseni. 19. Mfumo wa tathmini ya ubora wa huduma. 20. Uhuishwaji wa leseni. 21. Kupotea au kuharibika kwa leseni. 22. Kibali cha Dharura. SEHEMU YA TATU

SHERIA YA LESENI ZA USAFIRISHAJI (SURA YA 317) KANUNI ......SHERIA YA LESENI ZA USAFIRISHAJI (SURA YA 317) ... MASHARTI YA AWALI 1. Jina la Kanuni . 2. Matumizi ya Kanuni. 3. Tafsiri

  • Upload
    others

  • View
    161

  • Download
    23

Embed Size (px)

Citation preview

SHERIA YA LESENI ZA USAFIRISHAJI

(SURA YA 317)

_____________

KANUNI

_____________

(Zimetengenezwa chini ya kifungu cha 45)

_____________

KANUNI ZA LESENI ZA USAFIRISHAJI (MAGARI YA ABIRIA), ZA MWAKA 2019

_____________

MPANGILIO WA KANUNI

Kanuni Jina

SEHEMU YA KWANZA

MASHARTI YA AWALI

1. Jina la Kanuni.

2. Matumizi ya Kanuni.

3. Tafsiri.

SEHEMU YA PILI

MAOMBI NA UTOAJI WA LESENI

4. Vigezo vya kuomba leseni kwa kampuni.

5. Vigezo vya kuomba leseni kwa mtu binafsi.

6. Utaratibu wa kuomba leseni.

7. Vigezo vya kuomba leseni kwa magari ya shule.

8. Utaratibu wa kuomba leseni za magari ya shule.

9. Vigezo vya kutoa leseni.

10. Aina na muda wa leseni.

11. Leseni ya Kawaida.

12. Leseni ya Muda Mfupi.

13. Leseni Maalumu.

14. Ada za leseni na tozo nyingine.

15. Uchambuzi wa maombi na utoaji wa leseni.

16. Kukataliwa kwa ombi la leseni.

17. Yaliyomo kwenye leseni ya kampuni au mtu binafsi.

18. Kubandika leseni.

19. Mfumo wa tathmini ya ubora wa huduma.

20. Uhuishwaji wa leseni.

21. Kupotea au kuharibika kwa leseni.

22. Kibali cha Dharura.

SEHEMU YA TATU

2

MASHARTI YA LESENI

23. Masharti ya msingi kwa magari ya usafirishaji wa abiria.

24. Masharti ya leseni kwa usafirishaji wa abiria wa mijini.

25. Masharti ya leseni kwa magari ya abiria kati ya mji na mji na nchini na nchi

nyingine.

26. Masharti maalumu ya leseni kwa magari yaliyosajiliwa nje ya nchi.

27. Masharti ya leseni kwa basi ya shule.

SEHEMU YA NNE

KUSITISHA AU KUFUTA LESENI

28. Mamlaka ya kusitisha leseni.

29. Utaratibu wa kusitisha leseni.

30. Kufutwa kwa leseni.

SEHEMU YA TANO

UTOAJI WA TIKETI NA USHUGHULIKIAJI WA MIZIGO YA ABIRIA

31. Utozaji wa nauli iliyoidhinishwa.

32. Uwekeshaji wa tiketi.

33. Utoaji wa tiketi.

34. Wajibu wa kuandaa orodha ya wasafiri.

35. Haki ya mtoa huduma kutoza nauli iliyoidhinishwa.

36. Jukumu la kutoa usafiri.

37. Nauli ya mwanafunzi au mtoto.

38. Utozaji gharama za usafirishaji wa mizigo ya abiria.

39. Wajibu wa abiria kutambulisha mzigo.

40. Wajibu wa mtoa huduma kuweka utambulisho kwenye mzigo wa abiria.

SEHEMU YA SITA

MATUMIZI YA RATIBA, BATLI NA JEDWALI LA NAULI

41. Utoaji na matumizi ya ratiba, batli na jedwali la nauli.

42. Wajibu wa kuzingatia njia na ratiba zilizoidhinishwa.

SEHEMU YA SABA

MAKOSA NA ADHABU

43. Makosa na adhabu.

44. Uwezo wa kufifisha makosa.

45. Ufifishaji wa makosa.

3

46. Taarifa ya makosa.

47. Utaratibu wa malipo.

48. Kutolipa faini ya kosa lililofifishwa.

49. Kutosaini taarifa ya makosa.

SEHEMU YA NANE

MASHARTI YA JUMLA

50. Wajibu wa kutoa taarifa ya gari kusitisha utoaji huduma.

51. Wajibu wa kufunga na kutunza kifaa maalumu cha kufuatilia mwenendo wa gari.

52. Mamlaka ya kuzuia baadhi ya magari ya abiria kutoa huduma katika maeneo

maalum.

53. Mzigo uliosahaulika kwenye gari la abiria.

54. Mamlaka ya kusimamisha na kukagua gari.

55. Upakaji rangi na uwekaji matangazo kwenye gari la abiria.

56. Wajibu wa kutoa taarifa.

57. Kuhamisha umiliki au kuondoa gari kwenye huduma.

58. Mapitio ya uamuzi wa Mamlaka.

59. Masharti ya mpito na yanayoendelea.

60. Kufutwa kwa Kanuni. ____________

MAJEDWALI ____________

4

SHERIA YA LESENI ZA USAFIRISHAJI

(SURA YA 317)

_________

KANUNI

_________

(Zimetungwa chini ya kifungu cha 45)

___________

KANUNI ZA LESENI ZA USAFIRISHAJI (MAGARI YA ABIRIA), ZA MWAKA 2019

SEHEMU YA KWANZA

MASHARTI YA AWALI

Jina la Kanuni 1. Kanuni hizi zitaitwa Kanuni za Leseni za Usafirishaji (Magari ya Abiria), za

Mwaka 2019. Matumizi ya

Kanuni 2. Kanuni hizi zitatumika kwa magari yote yanayotoa huduma ya usafiri wa

abiria. Tafsiri 3. Katika Kanuni hizi, isipokuwa pale muktadha utakapohitaji vinginevyo:

“abiria” inamaanisha mtu yeyote anayesafiri kwenye gari la abiria mwenye

tiketi halali na inajumuisha mtoto;

“ajali” inamaanisha tukio au mlolongo wa matukio maalumu yasiyofaa, ya

uzembe au yasiyokusudiwa yenye athari kwa abiria na watumiaji wengine wa

barabara;

Sura ya 317 “Sheria ” maana yake sharia ya leseni ya Usafirishaji;

“basi la shule” inamaanisha gari la abiria linalomilikiwa au kutumiwa na shule

au linalomilikiwa na mtu binafsi au linalotumika chini ya mkataba na shule hiyo

ambalo limekusudiwa kutoa huduma kwa wanafunzi kwenda au kutoka shule, au

kwa shughuli nyingine yeyote inayohusiana na shule kwa pamoja;

“basi la wafanyakazi” inamaanisha gari la abiria ambalo limekusudiwa kutoa

huduma kwa wafanyakazi au wanafunzi wa elimu ya juu; Sura ya 197 “chama cha ushirika” inamaanisha chama kilichosajiliwa chini ya Sheria ya

Vyama vya Ushirika;

“eneo la kibiashara la mji” inamaanisha eneo la jiji, manispaa au mji kama

lililovyotamkwa na mamlaka husika; “gari la abiria” inamaanisha gari linalobeba au lililokusudiwa kubeba abiria kwa

kukodishwa au kwa malipo, linalojumuisha gari inayotumika au iliyoundwa

kutumika kwa kazi hiyo au kazi nyingine; Sura ya 337 “jumuiya” inamaanisha taasisi iliyosajiliwa kwa mujibu wa Sheria ya Jumuiya

za Kijamii na kusajiliwa kama Mdhamini;

Sura ya 168 “kadi ya usajili wa gari” inamaanisha kadi ya usajili wa gari iliyotolewa chini

ya Sheria ya Usalama Barabarani; Sura ya 212 “kampuni” inamaanisha kampuni iliyoundwa na kusajiliwa Tanzania Bara chini

5

ya Sheria ya Makampuni; “Kifaa Maalumu cha Kufuatilia Mwenendo wa Gari” inamaanisha kifaa

kinachofungwa kwenye gari la abiria kwa ajili ya kuchukua taarifa za mwenendo

wa gari husika na kuzituma wakati huo huo kwenye mfumo maalumu wa

kufuatilia mwenendo wa gari;

“leseni” inamaanisha leseni ya usafirishaji wa abiria iliyotolewa chini ya

Kanuni hizi; “leseni maalumu” inamaanisha leseni inayotolewa na Mamlaka kwa idhini ya

Waziri kwa ajili ya kutoa huduma ya usafirishaji kwa maeneo ya mjini au maeneo

mengine kwa muda maalumu utakaopangwa; Sura ya 413 “Mamlaka” inamaanisha Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini kama

ilivyoanzishwa chini ya kifungu cha 4 cha Sheria ya Mamlaka ya LATRA; “mfanyakazi” inajumuisha dereva, kondakta na mfanyakazi mwingine yeyote

wa mtoa huduma anayefanya kazi kwenye gari la abiria au gari la shule likiwa

kazini; “Mfumo Maalumu wa Kufuatilia Mwenendo wa Gari” inamaanisha mfumo

unaoweza kufuatilia na kunukuu mwendo wa gari la abiria kutembea kwa kasi

iliyoidhinishwa na Mamlaka;

Sura ya 168 “Mkaguzi wa Magari” inamaanisha mtu aliyeteuliwa chini ya Sheria ya

Usalama Barabarani kwa ajili ya ukaguzi wa magari; Sura ya 413 “Mkurugenzi Mkuu” inamaanisha Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka aliyeteuliwa

chini ya Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini;

“mmiliki” inamaanisha mtu yeyote yule ambaye jina lake linaonekana kwenye

kadi ya usajili wa gari kama mmiliki; “mtoa huduma” inamaanisha mtu, jumuiya, taasisi au kampuni iliyosajiliwa na

na Mamlaka kwa ajili ya kutoa huduma ya usafirishaji wa abiria;

“mtoto” inamaanisha mtu mwenye umri wa miaka mitatu au chini yake;

“mfanyakazi gari la abiria inamaanisha, dereva, kondakta au mfanyakazi yeyote

anayefanya kazi kwenye basi la usafiri wa umma, basi la shule, linapokuwa

safarini;

“mwanafunzi” inamaanisha mwanafunzi wa shule ya awali, msingi au sekondari

anapokuwa katika sare ya shule au mwenye kitambulisho;

“ratiba” inamaanisha utaratibu wa maandishi unaotolewa na Mamlaka

unaoonesha muda wa kuondoka na kufika kwa gari la abiria katika vituo

mbalimbali kwa kila njia; Sura ya 317 “Sheria” inamaanisha Sheria ya Leseni za Usafirishaji;

“taarifa ya ukaguzi wa gari” inamaanisha taarifa ya gari inayothibitisha ubora

wake kwa matumizi ya barabarani inayotolewa na Mkaguzi wa Magari au taasisi

nyingine yeyote inayotambuliwa na Mamlaka;

“taasisi iliyosajiliwa” inajumuisha chama cha ushirika, wadhamini, jumuiya,

kampuni au ubia ambao umesajiliwa chini ya sheria husika; Sura ya 413 “tozo ya mwaka” inamaanisha tozo inayolipwa kwa Mamlaka kwa mujibu wa

kifungu cha 41 cha Sheria ya Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini,

6

SEHEMU YA PILI

MAOMBI NA UTOAJI WA LESENI

Vigezo vya kuomba

leseni kwa kampuni

4.–(1) Mtu yeyote anayehitaji kutoa huduma za usafirishaji wa abiria

ataomba leseni kwa Mamlaka.

(2) Mtu yeyote: (a) hatatoa huduma za usafirishaji wa abiria bila kuwa na leseni halali;

(b) baada ya kuanza kutumika kwa Kanuni hizi, hatapewa leseni ya kutoa

huduma za usafirishaji wa abiria isipokuwa kama mwombaji huyo: Sura ya 212 (i) ni kampuni; na

(ii) anamiliki angalau idadi ya chini ya magari ya abiria kama

itakavyoelekezwa na Mamlaka kulingana na wakati; na

(iii) amekidhi viwango vilivyoelekezwa kwenye kanuni ya viwango

vya ubora na usalama wa huduma.

Vigezo vya kuomba

leseni kwa mtu

binafsi

5.-(1) Mamlaka inaweza kutoa leseni kwa mtu binafsi ili kutoa huduma

kwenye njia maalumu kwa kipindi maalumu.

(2) Mamlaka, baada ya kuanza kutumika kwa Kanuni hizi, haitatoa

leseni kwa mtu binafsi isipokuwa iwapo mtu huyo: (a) ni raia wa Tanzania;

(b) anamiliki idadi ya chini ya magari ya abiria kama ambavyo itaamuriwa

na Mamlaka kulingana na wakati; na

(c) amekidhi viwango vilivyoelekezwa kwenye kanuni ya viwango vya

ubora na usalama wa huduma

Utaratibu wa kuomba

leseni

6.-(1) Mtu anayekusudia kutoa huduma ya usafirishaji wa abiria atawasilisha

maombi ya leseni kwa Mamlaka kwa kujaza fomu kwa mkono au kielektroniki

kama ilivyoainishwa kwenye Jedwali la Kwanza la Kanuni hizi. (2) Maombi chini ya kanuni ndogo ya (1), yataambatishwa na: (a) nakala ya cheti cha usajili wa kampuni; (b) nakala ya kadi ya usajili wa gari; (c) taarifa ya ukaguzi wa gari; .

(3) Bila kuathiri kanuni ndogo ya (2), mwombaji wa leseni maalumu,

atahitajika kuwasilisha: (a) andiko la biashara; (b) mpango wa kusimamia usalama; (c) mpango wa kushughulikia dharura; (d) taarifa ya fedha iliyokaguliwa ya kipindi cha karibuni; (e) utaratibu wa kushughulikia malalamiko;

(f) uthibitisho wa malipo ya ada ya maombi kama ilivyoainishwa

katika Jedwali la Pili la Kanuni hizi; na

(g) nyaraka nyingine zozote ambazo Mamlaka inaweza kuzihitaji

wakati wowote. Vigezo vya

kuomba leseni kwa

magari ya shule

7.-(1) Mamlaka inaweza kutoa leseni kwa kutuo cha kulelea watoto, shule,

mtu binafsi au kampuni kwa ajili ya kutumia basi la shule kwa kipindi mahsusi.

(2) Kwa kuzingatia kifungu kidogo cha (1), Mamlaka inaweza kutoa vigezo

kwa ajili ya utoaji wa leseni za mabasi ya shule kwa kuzingatia uwezo wa

7

mabasi kama itakavyoona inafaa.

Utaratibu wa

kuomba leseni za

magari ya shule

8.-(1) Mtu anayekusudia kutoa huduma ya magari ya shule atawasilisha

maombi ya leseni kwa Mamlaka kwa kwa njia ya kujaza fomu kwa mkono au

kielektroniki. (2) Maombi chini ya kanuni ndogo ya (1), yataambatishwa na: (a) nakala ya kadi ya usajili wa gari; (b) taarifa ya ukaguzi wa gari;

(c) nyaraka nyingine zozote ambazo Mamlaka inaweza kuzihitaji wakati

wowote.

Vigezo vya kutoa

leseni

9. Mamlaka, iwapo itaona ni muhimu, inaweza -

(a) kuweka vigezo vya kutoa leseni yoyote chini ya Kanuni hizi: (i) kwa kuzingatia njia na umbali utakaotumiwa na gari la abiria; (ii) kutegemeana na uwezo wa gari na idadi ya magari ya abiria; au (b) kurekebisha vigezo vya kutoa leseni yoyote.

Aina na muda wa

leseni

10. Mamlaka inaweza kutoa aina zifuatazo za leseni kwa mmiliki wa gari la

kubeba abiria kwa ajili ya kutoa huduma za usafirishaji kwa umma: (a) Leseni ya Kawaida; (b) Leseni ya Muda Mfupi; au (c) Leseni Maalumu. Leseni ya Kawaida 11.(1) Leseni ya kawaida:

(a) itatolewa kwa mwombaji ambaye amekusudia kutoa huduma za

usafirishaji kwa

a. wafanyakazi au wanachuo wa taasisi za elimu ya juu za umma au

binafsi; b. wanafunzi; c. watalii; d. abiria katika maeneo ya mijini; e. mabasi ya kutoka na kuingia vijijini na mjini; f. abiria kati ya mji na mji au mkoa na mkoa; g. abiria wanaoingia na kutoka kati ya nchi moja na nchi nyingine; h. shughuli maalumu au kukodiwa; na i. aina nyingine ya leseni kama itakavyoamuliwa na Mamlaka; na (2) itakuwa halali kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Leseni ya Muda

Mfupi

12. Leseni ya Muda Mfupi:

(a) itatolewa kwa ajili ya biashara ya msimu au utekelezaji wa kazi

maalumu; na (b) itakuwa halali kwa kipindi kisichozidi miezi mitatu. Leseni Maalumu 13.-(1) Leseni Maalum:

(a) itatolewa kwa mwombaji ambaye anakusudia kutoa huduma ya

usafirishaji abiria kwa maeneo maalumu ya mjini au njia nyingine

yoyote kwa masharti na muda maalumu; (b) itakuwa kwa kipindi kisichopungua miaka mitano. (2) Bila kuathiri uwezo wa jumla wa Mamlaka kutoa leseni chini ya Kanuni

8

hizi, leseni maalumu itatolewa baada ya mashauriano na Waziri.

Ada za leseni na

tozo ya mwaka

14.-(1) Mwombaji atalipa kwenye Mamlaka ada na tozo nyingine kama

ilivyooneshwa kwenye Jedwali la Pili la Kanuni hizi.

(2) Ada na tozo nyingine kwenye kanuni ndogo ya (1) zitalipwa kwenye

akaunti ya Benki ya Mamlaka kwa fedha taslimu au kwa njia ya kielektoniki na

ushahidi wa malipo utawasilishwa makao makuu ya LATRA au Ofisi za Mikoa. Uchambuzi wa

maombi na utoaji wa

leseni.

15. Mamlaka, baada ya kupokea maombi ya leseni ya usafirishaji abiria,

itayachambua na, iwapo itaridhika, itatoa leseni.

Kukataliwa ombi la

leseni 16.-(1) Mamlaka inaweza kutotoa leseni kwa mwombaji endapo atakuwa:

(a) hajatimiza mahitaji yaliyoanishwa kwenye Kanuni hizi;

(b) amewasilisha nyaraka za kughushi; au

(c) ametoa taarifa zisizokuwa sahihi kuhusiana na maombi ya leseni;

(d) ameomba njia ambayo idadi ya magari yanayotakiwa

yametosheleza; au

(e) sababu nyingine yoyote ambayo Mamlaka itaona inafaa.

(2) Endapo Mamlaka itakataa kutoa leseni, itamtaarifu mwombaji kwa

maandishi, ndani ya siku kumi na nne tangu tarehe ya maombi ya leseni

yalipopokelewa, sababu ya kukataliwa kwa maombi hayo.

(3) Bila kuathiri kanuni ndogo ya (1) (b), Mamlaka inaweza kukataa kutoaa

leseni kwa mtu yeyote aliyewasilisha nyaraaka za kughushi mpaka zipite siku

tisini tangu siku alipokataliwa;

Yaliyomo kwenye

leseni ya kampuni au

mtu binafsi

17.-(1) Mamlaka inaweza kutoa leseni kwa Kampuni au mtu binafsi.

Leseni ya mtu binafsi itajumuisha mambo yafuatayo:

(a) jina na anwani ya la mtoa huduma;

(b) muda wa leseni;

(c) Masharti ya leseni;

(d) Namba ya leseni;

(e) Namba ya usajili wa gari;

(f) Idadi ya magari yaliyochini ya hiyo leseni;

(2) Leseni ya kampuni itajumuisha mambo yafuatayo

a. Jina na anwani ya Kampuni ya mtoa huduma;

b. Muda wa leseni;

c. Masharti ya leseni;

d. namba ya leseni;

e. namba ya usajili wa gari;

f. Idadi ya magari yaliyo chini ya leseni

Kubandika leseni 18.-(1) Mtoa huduma atabandika leseni sehemu ya wazi upande wa kushoto

wa kioo cha mbele cha gari la abiria.

(2) Ikiwa ni Kampuni, mtoa huduma atatakiwa kubandika kwenye sehemu

ya wazi kwa kila gari, nakala halisi ya leseni itakayotolewa na Mamlaka.

Mfumo wa tathmini

ya ubora wa huduma 19.-(1) Mtoa huduma, baada ya kupokea leseni yake, atazingatia vigezo vya

utoaji huduma vilivyopangwa na Mamlaka.

(2) Ikiwa ni kampuni iliyosajiliwa, mtoa huduma:

(a) atawasilisha Taarifa ya Mwaka ya Utendaji kwa Mamlaka; au

9

(b) anaweza kuandaa viwango vya utoaji huduma za usafiri wa abiria na

kuviwasilisha kwa Mamlaka kwa ajili ya kuidhishwa.

Uhuishwaji wa leseni 20.-(1) Mtoa huduma anayetaka kuhuisha leseni anaweza kuomba kwa

Mamlaka ndani ya siku thelathini kabla ya tarehe ya kuisha kwa leseni husika. (2) Maombi ya kuhuisha leseni yataambatishwa na:

(a) nakala iliyothibitishwa ya hati safi ya kodi, isipokuwa kwa maombi

ya leseni ya magari ya shule; (b) nakala iliyothibitishwa ya taarifa ya ukaguzi wa gari; na

(c) nyaraka nyingine zozote ambazo Mamlaka itazihitaji wakati

wowote.

(3) Mamlaka inaweza kutoza asilimia hamsini ya ada ya maombi ya leseni

yatakayowasilishwa siku kumi na nne baada ya tarehe ya kuisha kwa leseni na

asilimia tano kwa kila mwezi utakaofuata kwenye kiasi kinachodaiwa kwa

kipindi kisichozidi miezi kumi na mbili. Kupotea au

kuharibika kwa

leseni

21.-(1) Endapo leseni:

(a) imeharibika au imechakaa, mtoa huduma ataitaarifu Mamlaka kwa

maandishi haraka iwezekanavyo pamoja na maombi ya kupewa

leseni mbadala;

(b) imepotea, mtoa huduma ataitaarifu Mamlaka haraka iwezekanavyo

kwa maandishi pamoja na kuwasilisha taarifa ya polisi ya upotevu

na maombi ya kupewa leseni mbadala.

(2) Endapo Mamlaka itaridhika kwamba leseni imepotea, imeharibika au

imechakaa, itatakiwa, baada ya mwombaji kulipa ada iliyopangwa, kutoa nakala

ya leseni kwa mtoa huduma, Isipokuwa kwamba,

(a) ikiwa leseni imechakaa, Mamlaka itatakiwa, kabla ya kutoa nakala ya

leseni, kumtaka mtoa huduma kuwasilisha leseni ya mwanzo kwa ajili

ya uhakiki;

(b) endapo leseni iliyopotea itapatikana baada ya kutolewa kwa nakala

mpya ya leseni chini ya kanuni hii, mtoa huduma atarudisha nakala ya

leseni kwa Mamlaka. Kibali cha Dharura 22.-(1) Mamlaka inaweza kutoa Kibali cha Dharura kwa mtoa huduma kwa

kipindi kisichozidi siku saba-

(a) iwapo mtoa huduma anataka kubadili gari la abiria lililoharibika ambalo

liliruhusiwa kutoa huduma ya usafirishaji wa umma; au (b) kwa ajili ya sababu nyingine ambayo Mamlaka itaamua. (2) Kwa kuzingatia kanuni ndogo ya (1), mtoa huduma anaweza kupata

Vibali vya Dharura kutoka Ofisi yoyote ya Mamlaka na kuviweka ofisini kwake

kwa ajili ya kuvitumia inapotokea dharura.

SEHEMU YA TATU

MASHARTI YA LESENI

Masharti ya msingi

kwa magari ya

usafirishaji wa

abiria

23.-(1) Mtoa huduma wa gari la abiria atahakikisha kuwa:

(a) gari la abiria halina hitilafu;

(b) idadi ya abiria, uzito na upakiaji wa mizigo, uzito wa gari na mwendo

haizidi viwango vilivyoainishwa kwenye Sheria nyingine za nchi;

10

(c) dereva mmoja haendeshi gari mfululizo kwa muda unaozidi saa nane;

(d) taarifa sahihi zinaandaliwa na kutolewa na kumbukumbu za biashara

ya usafirishaji wa abiria zinatunzwa;

(e) gari la abiria linakuwa na kisanduku cha huduma ya kwanza

kilichowekwa mahali panapoonekana, kilicho na dawa na vifaa tiba

vilivyoainishwa;

(f) chombo cha taka kinawekwa kwenye gari la abiria na taka

zinazokusanywa zinatupwa kwenye maeneo maalum ya kutupa taka;

(g) haajiri mfanyakazi ambaye ametenda kosa lililoainishwa katika

Kanuni hizi mara tatu mfululizo katika kipindi cha uhai wa leseni;

(h) anazingatia viwango vya madaraja ya mabasi ya abiria

vilivyoainishwa kwenye Jedwali la Nne kwenye kanuni hizi;

(i) anazingatia masharti mengine yoyote ambayo yatawekwa na

Mamlaka.

(2) Mfanyakazi wa basi la abiria atahakikisha kuwa:

(a) gari la abiria halibebi mzigo hatarishi;

(b) gari la abiri halibebi abiria zaidi ya idadi iliyoandikwa kwenye leseni;

(c) burudani itakayotolewa kwenye gari la abiria wakati wa safari

itazingatia maadili na tamaduni ya Kitanzania na kwa sauti ya ndogo;

na

Sura ya 168 (d) Sheria ya Usalama Barabarani na sheria nyinginezo za nchi

zinatekelezwa. Masharti ya leseni

kwa usafirishaji wa

abiria wa mijini

24.-(1) Kwa kuzingatia masharti ya msingi kama yaliyoainishwa chini ya

sehemu hii-

(a) Mtoa Huduma wa mabasi ya usafiri wa mijini atahakikisha kuwa:

(i) dereva wa gari la abiria au gari binafsi la kukodi ana umri usiopungua

miaka ishirini na tano na usiozidi miaka sitini;

(ii) tiketi ya basi inauzwa kwa mfumo wa karatasi au kielektroniki na

inatolewa kwa abiria;

(iii) gari la abiria linapakwa rangi ya utambulisho wa njia na kwa namna

iliyoelekezwa na Mamlaka;

(iv) nauli iliyoidhinishwa na Mamlaka inaandikwa karibu na mlango wa

kuingilia abiria;

(v) haajiri mfanyakazi ambaye ametenda kosa lililoainishwa katika Kanuni

hizi mara tatu mfululizo katika kipindi cha uhai wa leseni;

(vi) anazingatia masharti mengine yoyote ambayo yatawekwa na Mamlaka.

(b) Mfanyakazi wa mtoa huduma ya usafiri wa mjini atahakikisha kuwa:

(i) anavaa sare safi na nadhifu kama Mamlaka itakavyoamua;

(ii) hakuna mtu anayefanya biashara, anayehubiri, anayefanya shughuli za

siasa au kutoa burudani ambayo inakiuka kanuni ya kanuni hizi ndani ya

gari la abiria mijini;

(iii) gari la abiria linatoa huduma kwenye njia ambayo imeainishwa kwenye

leseni; na

(iv) gari la abiria halibadilishi njia au halisitishi safari kabla ya kufika

mwisho wa kituo kama ilivyooneshwa kwenye tiketi ya abiria.

Masharti ya leseni

kwa magari ya

abiria kati ya mji na

mji na nchi na nchi

25. Kwa kuzingatia masharti ya msingi kama yaliyoainishwa chini ya kanuni

ya 23-

(a) Mtoa huduma kwa gari la abiria linalofanya safari kati ya mji na mji na

11

nyingine kati ya nchi na nchi atahakikisha kuwa:

(i) dereva ana umri usiopungua miaka thelathini na usiozidi miaka

sitini;

(ii) gari la abiria lina vigezo vya madaraja ya mabasi ya abiria

vilivyoainishwa kwenye Jedwali la Nne la Kanuni hizi;

(iii) gari la abiria limefungwa kifaa maalum kilichoidhinishwa na

Mamlaka kwa ajili ya kufuatilia mwendo wa gari;

(iv) gari la abiria lina batli iliyotolewa na Mamlaka;

(v) gari la abiria lina mikanda inayofanya kazi na safi kwa kila kiti cha

abiria;

(vi) haajiri mfanyakazi ambaye ametenda kosa lililoainishwa katika

Kanuni hizi mara tatu mfululizo katika kipindi cha uhai wa leseni;

(vii) anazingatia masharti mengine yoyote ambayo yatawekwa na

Mamlaka.

(b) Mfanyakazi wa gari la abiria linalofanya safari kati ya mji na mji na kati

ya nchi na nchi atahakikisha kuwa:

(i) anavaa sare safi na nadhifu kama Mamlaka itakavyoamua;

(ii) tiketi halali ya basi inauzwa kwa mfumo wa karatasi au

kielektroniki na inatolewa kwa abiria; na

(iii) hakuna mtu anayefanya biashara, anayehubiri, anayefanya shughuli

za siasa au kutoa burudani ambayo inakiuka kanuni hizi ndani ya

gari la abiria;

(iv) gari la abiria linazingatia batli, ratiba na chati ya nauli

iliyoidhinishwa na Mamlaka;

(v) gari la abiria lina nakala tatu ya orodha ya abiria kwa kila safari

ambapo nakala moja itabaki katika gari la abiria, nakala nyingine

itawasilishwa kituo cha polisi na nakala moja nyingine itaachwa

kwenye ofisi za mtoa huduma;

(vi) wafanyakazi wanavaa vitambulisho, vinaonekana kwa urahisi kwa

mtu yeyote na ambavyo vina:

(a) jina la mfanyakazi;

(b) jina, anwani, namba ya simu na sahihi ya mtoa huduma;

(c) cheo na sahihi ya mfanyakazi; na

(d) picha ya hivi karibuni ya paspoti ya mfanyakazi;

(vii) gari la abiria linasimama kwenye maeneo ambayo huduma za choo

na huduma nyinginezo zinapatikana;

(viii) gari la abiria linatoa huduma kwenye njia ambayo imeainishwa

kwenye leseni;

(ix) safari haikatishwi kabla ya kufika kwenye kituo cha mwisho wa

safari kama inavyoonekana kwenye tiketi ya abiria na

(x) abiria wanatangaziwa masuala ya usalama kabla ya kuanza safari na

wakati wa safari. Masharti maalumu

ya leseni kwa

magari

yaliyosajiliwa nje

ya nchi

26. Mtoa huduma na mfanyakazi wa gari linalotoa huduma kati ya nchi na

nchi lenye usajili wa nchi nyingine watahakikishwa kwamba gari hilo halitoi

huduma za usafirishaji kama gari lililosajiliwa nchini.

Masharti ya leseni

kwa basi la shule

27.-(1) Mtoa huduma wa basi la shule atahakikisha kuwa:

(a) gari la abiria halina hitilafu; Tangazo la Serikali

Na. 412 of 2014 (b) amekidhi viwango vilivyoelekezwa kwenye kanuni ya viwango vya

12

ubora na usalama wa huduma

(c) dereva wa basi la shule ana umri usiopungua miaka thelathini na tano

na usiozidi miaka sitini;

(d) basi la shule linapakwa rangi ya njano yenye namba Rgb (255,255,0)

na kuandikwa maneno “School Bus” au “Basi la Shule”;

(e) basi la shule linakuwa na kisanduku cha huduma ya kwanza

kilichowekwa mahali panapoonekana, kilicho na dawa na vifaa tiba

vilivyoainishwa;

(f) haajiri mfanyakazi ambaye ametenda kosa lililoainishwa katika

Kanuni hizi mara tatu mfululizo katika kipindi cha uhai wa leseni;

(2) Mfanyakazi wa basi la shule atahakikisha kuwa:

(a) basi la shule halibebi wanafunzi zaidi ya idadi iliyoandikwa kwenye

leseni;

(b) uwezo wa gari, upakiaji na mwendo wa gari havizidi viwango

vilivyoainishwa kwenye sheria nyingine;

(c) anavaa sare safi na nadhifu kama Shule itakavyoamua;

(d) chombo cha taka kinawekwa kwenye gari la abiria na taka

zinazokusanywa zinatupwa kwenye maeneo maalum ya kutupa taka;

na

(e) anazingatia masharti mengine yoyote ambayo yatawekwa na

Mamlaka.

SEHEMU YA NNE

KUSITISHA AU KUFUTA LESENI

Mamlaka ya

kusitisha leseni

28.-(1) Mamlaka inaweza kusitisha leseni ikiwa imeridhika kwamba mtoa

huduma:

(a) amesababisha ajali iliyopelekea vifo au majereha makubwa kwa abiria

kutokana na ukiukwaji wa masharti ya leseni;

(b) ameshindwa kufunga kifaa cha kuratibu mwenendo wa basi; (c) ameharibu kifaa maalumu cha kuratibu mwenendo wa gari; (d) ameshindwa kulipa ada na tozo za Mamlaka; (e) amekataa kutii amri halali ya Ofisa wa Mamlaka; (f) amemzuia Ofisa wa Mamlaka kufanya ukaguzi; au

(g) ametenda kosa hilohilo chini ya Kanuni hizi zaidi ya mara tatu ndani ya

mwaka mmoja.

(2) Bila kuathiri kanuni ndogo ya (1), Mamlaka inaweza kusitisha leseni

endapo ni muhimu au inafaa kwa maslahi ya usalama barabarani.

(3) Endapo ukiukwaji unahusu kushindwa kufunga au kuharibu kifaa cha

kuratibu mwenendo wa basi, usitishaji utakuwa wa siku thelathini au zaidi.

Utaratibu wa

kusitisha leseni

29.-(1) Mamlaka inaweza, kabla ya kusitisha leseni, kutoa notisi kwa mtoa

huduma ili kutoa maelezo ni kwanini leseni yake isisitishwe.

(2) Mtoa huduma atatakiwa, baada ya kupokea notisi chini ya kanuni ndogo

ya (1), kuwasilisha maelezo ya maandishi kwa Mamlaka ndani ya siku saba tangu

tarehe ya kupokea notisi akieleza ni kwanini leseni yake isisitishwe.

(3) Mamlaka inaweza kusitisha leseni na kutoa sababu za usitishwaji wa

leseni endapo:

(a) Mamlaka haikuridhishwa na maelezo yaliyotolewa kupitia kanuni ndogo

13

ya (2); au

(b) Mtoa huduma hakufanya wasilisho lolote.

(4) Bila kujali kanuni ndogo za (1), (2) na (3), Mamlaka inaweza, endapo

itaona inafaa, kusitisha leseni bila kutoa notisi kwa mtoa huduma kuwasilisha

maelezo.

(5) Endapo leseni imesitishwa chini ya kanuni ya 28, mtoa huduma ataacha

mara moja kutoa huduma za usafirishaji na kurudisha leseni kwa Mamlaka ndani

ya siku saba tangu tarehe aliyopokea notisi ya usitishwaji wa leseni.

(6) Mamlaka, iwapo leseni itakuwa hai hadi wakati wa kumalizika kwa

kipindi cha usitishwaji, itarudisha leseni hiyo kwa mtoa huduma baada ya

kumalizika kwa kipindi cha usitishwaji na kutekelezwa kwa masharti mengine

yoyote kama yatakavyoainishwa katika notisi ya usitishwaji.

Kufutwa kwa leseni 30. Mamlaka itafuta leseni iliyositishwa kwa mara ya tatu.

SEHEMU YA TANO

UTOAJI WA TIKETI NA USHUGHULIKIAJI WA MIZIGO YA ABIRIA

Utozaji wa nauli iliyoidhinishwa

31. Mtoa huduma hatatoza nauli zaidi ya ile iliyoidhinishwa na Mamlaka

kulingana na daraja la basi husika.

Uwekeshaji wa

tiketi

32. Mtoa huduma anaweza kuruhusu wekesho la tiketi kufanyika kwa mfumo

wa karatasi au kielektroniki.

Utoaji wa tiketi

33.-(1) Mtoa huduma atatoa tiketi ya basi kwa abiria baada ya kupokea

malipo ya nauli iliyoidhinishwa kwa ajili ya safari husika kama ilivyo ainishwa

kwenye Jedwali la Tano la Kanuni hizi. (2) Tiketi ya basi itolewa kwa mfumo wa kielektroniki.

(3) Bila kuathiri kanuni (2) Mtoa huduma anaweza kutoa tiketi ya karatasi

kwa ruhusa maalumu ya Mamlaka. Sifa ya tiketi ya basi ni kama ifuatavyo: (a) kama ni basi linalotoa huduma ya usafiri kati ya mji na mji: (i) jina la abiria na namba ya kiti; (ii) muda wa kuripoti na kuondoka; (iii) kituo cha kuondokea, njia ya kupitia na kituo cha mwisho wa safari; (iv) nauli ya safari; (v) anuani kamili ya mtoa huduma pamoja na namba yake ya simu; (vi) namba ya usajili wa basi la abiria;

(vii) tarehe ya kutolewa na tarehe ya kusafiri; (viii) namba ya tiketi; (ix) namba ya dharura na taarifa ya LATRA na Polisi; na

(x) namba ya LATRA ya kuuliza viwango vya nauli.

(xi) namba ya simu ya mtoa huduma; (b) kama ni gari linalotoa huduma ya usafiri mijini: (i) namba ya usajili wa gari la abiria; (ii) jina la njia ambapo gari la abiria linatoa huduma; (iii) nauli iliyoidhinishwa; (iv) jina na anuani ya mtoa huduma; (v) tarehe ya kutolewa; na (vi) namba ya simu ya mtoa huduma.

14

(3) Tiketi iliyotolewa kwa ajili ya safari kati ya mji na mji au nchi na nchi

itakuwa na nakala mbili, nakala moja itatolewa kwa abiria na nakala ya pili

itabaki kwa mtoa huduma.

(4) Mtoa huduma atatunza taarifa za tiketi zote zilizotolewa kwa kipindi

kisichopungua mwaka mmoja kuanzia tarehe zilipotolewa.

(5) Pale ambapo abiria atafuta wekesho la tiketi yake ya safari saa ishirini na

nne au zaidi kabla ya kuanza safari, mtoa huduma, atalazimika kumrudishia

abiria nauli aliyolipa mara tu baada ya kufuta wekesho la tiketi.

(6) Pale ambapo wekesho la tiketi litafutwa kwenye muda usiozidi saa

ishirini na nne na si chini ya saa kumi na mbili kabla ya muda uliopangwa kabla

ya safari kuanza: (a) atapewa nafasi ya kubadilisha tarehe ya safari; au (b) atarudishiwa asilimia themanini na tano ya nauli aliyolipa.

(7) Bila kujali kanuni ndogo ya (5) na (6), pale ambapo tiketi ilinunuliwa kwa

mfumo wa kielektroniki, mtoa huduma atakuwa na haki ya kukata kiasi cha fedha

kutoka kwenye nauli sawa na gharama iliyotumika kutoa huduma hiyo.

(8) Mtoa huduma hataongeza taarifa yoyote kwenye tiketi ambayo ni kinyume

na Kanuni hizi na masharti ya leseni.

Wajibu wa kuandaa orodha ya wasafiri

34.-(1) Kwa madhumuni ya Kanuni hizi, mtoa huduma ataandaa orodha ya

abiria wanaosafiri kama ilivyoelekezwa na Mamlaka na kwa kuzingatia Jedwali

la Sita la Kanuni hizi. (2) Mtoa huduma atajaza orodha ya abiria wanaosafiri katika nakala tatu na:

(a) kuwasilisha nakala moja katika kituo cha jirani cha polisi ambapo gari la

abiria limeanzia safari; (b) kutunza nakala moja kwenye ofisi ya mtoa huduma; na (c) kutunza nakala moja kwenye gari husika la abiria.

(3) Mtoa huduma atahakikisha kwamba nakala ya orodha ya abiria

wanaosafiri inayotunzwa ndani ya gari inahuishwa wakati wote wa safari na

kumbukumbu zake zinatunzwa kwa kipindi cha miaka mitano.

Haki ya mtoa huduma kutoza nauli

iliyoidhinishwa

35. Mtoa huduma atakuwa na haki ya kudai malipo ya nauli halali na endapo

abiria atashindwa kulipa nauli hiyo, mtoa huduma anaweza kukataa kumsafirisha

abiria huyo. Jukumu la kutoa usafiri

36.-(1) Mtoa huduma ambaye amekwishampa tiketi abiria atawajibika

kumsafirisha abiria huyo kwa mujibu wa masharti ya leseni na ratiba ya safari

iliyoidhinishwa na Mamlaka. (2) kama mtoa huduma atashindwa kutoa huduma ya usafiri kati ya mji na mji

au nchi na nchi: (a) ndani ya saa moja tangu muda wa kuanza safari mtoa huduma

atamrudishia abiria kiwango chote cha nauli kilicholipwa isipokuwa abiria

kwa hiyari yake akubali kusubiri usafiri mbadala utakaotolewa na mtoa

huduma au; (b) gari likiharibika akiwa safarini ndani ya masaa mawili mtoa huduma

atawajibika: (i) kutoa usafiri mbadala; (ii) kurudisha nauli yote kwa abiria; au (iii)kutoa chakula na malazi, ikiwa abiria kwa hiyari yake atakubali

kusubiri usafiri mbadala wakuendealea na safari.

15

Nauli ya

mwanafunzi au

mtoto

37.-(1) Mtoa huduma atamtoza nauli mwanafunzi atakayepanda gari la abiria

linalotoa huduma ya usafiri ndani ya mji kwa kiwango cha nauli

kilichoidhinishwa na Mamlaka. (2) Mtoto anayepakatwa hatalipa nauli kwa usafiri wa mji na mji na kati ya

nchi na nchi. Utozaji gharama za

usafirishaji wa

mizigo ya abiria

38.-(1) Mtoa huduma atasafirisha bure:

(a) mzigo wa abiria wenye uzito usiopungua kilo ishirini wa abiria

anayesafiri kati ya mji na mji au nchi na nchi ambao hauzidi urefu wa

sentimita 60, upana sentimita 45 na kimo sentimita 30; (b) vifaa saidizi vinavyotumiwa mtu mwenye ulemavu wa viungo kwa ajili

ya kutembea wakati anaposafiri kwenye gari linalotoa huduma kati ya

mji na mji au nchi na nchi. (2) Mtoa huduma atapima kila mizigo wa abiria na kutoza malipo kwa uzito

unaozidi kilo ishirini na kutoa risiti. Wajibu wa abiria

kutambulisha

mzigo

39.– (1) Abiria atawajibika kutoa taarifa ya:

(a) kitu chochote cha thamani ambacho kimewekwa kwenye buti la gari;

na

(b) vitu vyovyote alivyobeba endapo atatakiwa na mtoa huduma kufanya

hivyo. (2) Endapo abiria atakataa mzigo wake kukaguliwa na mtoa huduma, mtoa

huduma anaweza kukataa kusafirisha mzigo huo. (3) Mtoa huduma atakuwa na wajibu wa kutoa taarifa ya mizigo aliobeba

kwenye gari ambao anautilia shaka kwa Afisa wa Polisi. Wajibu wa mtoa

huduma kuweka

utambulisho

kwenye mzigo wa

abiria

40. Mtoa huduma, wa gari la abiria linalotoa huduma kati ya mji na mji au

kati ya nchi na nchi, anapaswa:

(a) kuweka alama ya utambulisho wa mzigo na kumpa abiria mwenye mzigo

kadi yenye kuonyesha jina la abiria na kituo cha mwisho mzigo

unakofika; (b) kuhakikisha mzigo wa abiria unawekwa mahali salama, unalindwa na

unawasilishwa kwa abiria mara baada ya kufika kituo cha mwisho; na (c) pale mzigo wa abiria unapopotea au unapoharibika, anafidia mzigo au

analipa kiasi cha fedha kinacholingana na thamani ya mzigo kwa abiria

ndani ya siku thelathini tangu tarehe ya kupata taarifa ya tukio la upotevu

na kuwasilisha uthibitisho wa kupotea kwa mzigo huo.

SEHEMU YA SITA

MATUMIZI YA RATIBA, BATLI NA JEDWALI LA NAULI

Utoaji na matumizi

ya ratiba, batli na

jedwali la nauli

41.-(1) Mamlaka itatoa ratiba na batli kwa basi linalotoa huduma ya

usafirishaji abiria kati ya miji na miji au kati ya nchi na nchi.

(2) Mtoa huduma wa basi linalotoa huduma za usafirishaji abiria kati ya miji

na miji au kati ya nchi na nchi atahakikisha kuwa:

(a) ratiba, batli na jedwali la nauli zilizotolewa chini ya kanuni ndogo ya

(1) zinatumika wakati wote wa safari na kuhifadhiwa ndani ya basi;

(b) ratiba na jedwali la nauli vinawekwa mahali pa wazi ndani ya basi la

abiria; na

16

(c) mtoa huduma anawajibika kuonyesha batli kwa Ofisa wa Polisi au

Mamlaka wakati wa ukaguzi pale inapohitajika.

(3) Endapo mtoa huduma atatumia basi jingine, ahakikishe ratiba, batli na

jedwali la nauli zinazotumiwa na basi lenye leseni ya njia husika zinawekwa

kwenye basi hilo mbadala.

Wajibu wa

kuzingatia njia na

ratiba

42.-(1) Gari la abiria litatoa huduma kwa kufuata ratiba ya njia na kwa

kuzingatia ratiba iliyoidhinishwa.

(2) Endapo mtoa huduma anataka kubadilisha njia na ratiba, ataomba kwa

Mamlaka na kulipa gharama za maombi ya kubadilisha leseni au na ratiba. (3Mamlaka inaweza kutoa leseni mpya baada ya kujiridhisha na sababu za

kubadilisha njia.

SEHEMU YA SABA

MAKOSA NA ADHABU

Makosa na adhabu

43.-(1) Mtu atakaye kiuka masharti ya leseni au kifungu chochote cha Kanuni

hizi, atakuwa ametenda kosa na endapo atatiwa hatiani atawajibika kulipa faini

isiyopungua shilingi laki mbili za kitanzania na isiyozidi shilingi laki tano au

atafungwa jela kwa muda usiopungua mwaka mmoja na usiozidi miaka miwili au

vyote kwa pamoja.

(2) Bila kuhathiri kanuni ndogo ya (1), mtoa huduma hataajiri mfanyakazi

ambaye ametenda kosa lililoainishwa katika Kanuni hizi mara tatu mfululizo

katika kipindi cha uhai wa leseni;

Uwezo wa kufifisha

makosa

44.-(1) Mamlaka inaweza, pale mtoa huduma atakapokiri kwa maandishi

kwamba ametenda kosa kwa Mamlaka au afisa wa Mamlaka, Ofisa wa Mamlaka

anaweza, wakati wowote kabla ya kuanza kusikilizwa kwa kesi mahakamani,

kufifisha kosa hilo na kuamuru mtoa huduma alipe kiasi cha fedha kisichozidi

nusu ya kiasi cha faini ambayo angetozwa endapo angetiwa hatiani kwa kosa hilo

Mahakamani.

(2) Pale ambapo kosa limefifishwa na mtenda kosa akashtakiwa Mahakamani

kwa kosa lilelile, itakuwa ni utetezi mzuri kwa mtenda kosa kuthibitisha kwa

kiwango cha kuiridhisha Mahakama kwamba kosa ambalo mtenda kosa

alishtakiwa nalo lilishafifishwa na Mamlaka.

Ufifishaji wa

makosa

45. Mamlaka inaweza kufifisha makosa kwa kuzingatia Jedwali la Saba la

Kanuni hizi. Taarifa ya makosa 46.-(1) Mamlaka, baada ya kubaini kosa linalokiuka Kanuni hizi, itamtaarifu

mtoa huduma kwa mfumo wa kielektroniki au karatasi kwa kutumia Fomu ya

Taarifa iliyoainishwa kwenye Jedwali la Nane la Kanuni hizi kuhusu: (a) kosa lililotendwa; (b) adhabu ya kosa ; (c) kiasi kinachotakiwa kufifishwa; (d) tarehe na namna ya kufanya malipo kwa Mamlaka; na (e) taarifa nyingine yoyote ambayo Mamlaka itaona inafaa.

(2) Mtenda kosa anaweza kukiri au kukataa kukiri kutenda kosa linalotakiwa

kufifishwa kwa kusaini Fomu ya Taarifa ya Makosa kama ilivyoainishwa kwenye

Jedwali la Nane la Kanuni hizi.

17

Utaratibu wa malipo 47.-(1) Endapo mtoa huduma anakiri kosa lififishwe, atalipa kiasi

kinachotakiwa kufifishwa katika muda wa siku kumi na nne kwenye akaunti ya

benki ya Mamlaka kwa kupeleka kiasi hicho cha fedha au kwa kutumia njia ya

kielektroniki na kuwasilisha uthibitisho wa malipo hayo Makao Makuu ya

Mamlaka au kwenye Ofisi za Mikoa.

(2) Baada ya kuwasilisha uthibitisho wa malipo, Mamlaka itatoa stakabadhi ya

malipo. Kutolipa faini ya

kosa lililofifishwa 48. Endapo mtoa huduma anashindwa kutekeleza amri ya kulipa kiasi cha

fedha kinachotakiwa kufifishwa chini ya Kanuni hizi katika muda ulioainishwa,

Mamlaka: (a) itatoza riba ya asilimia tano na asilimia nyingine tano ya kiasi kinachodaiwa

kila baada ya siku thelathini kwa kipindi kisichozidi mwaka mmoja; au (b) inaweza kukazia amri sawa sawa na amri ya hukumu iliyotolewa na

Mahakama kwa ajili ya malipo ya kiasi cha fedha kilichotajwa kwenye amri.

Kutosaini taarifa ya

makosa 49.-(1) Pale ambapo mtoa huduma au dereva:

(a) hajakiri kutenda kosa, atalazimika, katika kipindi cha siku kumi na nne tangu

tarehe ya kutenda kosa hilo kuwasilisha Fomu ya taarifa ya kosa kwa

Mamlaka kwa ajili ya kufikishwa Mahakamani. (b) anashindwa kufika kwenye Ofisi za Mamlaka ndani ya muda ulioainishwa

itaamuliwa kuwa amekiri kosa na atatakiwa kulipa adhabu kama

ilivyoainishwa kwenye Kanuni hizi.

SEHEMU YA NANE

MASHARTI VYA JUMLA

Wajibu wa kutoa

taarifa ya gari

kusitisha utoaji

huduma

50. Mtoa huduma atakuwa na wajibu wa kuitaarifu Mamlaka pale ambapo

gari la abiria halitatoa huduma kwa kipindi kinachozidi siku thelathini.

Wajibu wa kufunga

na kutunza kifaa

maalumu cha

kufuatilia mwenendo

wa gari

51. Mtoa huduma wa gari la abiria atahakikisha kuwa:

(a) kifaa cha kufuatilia mwenendo wa gari kinafanya kazi vyema wakati

wote, kinatunzwa na kinalindwa dhidi ya mazingira hatarishi na

uharibifu wa makusudi wakati wote wa kutoa huduma; na

(b) hitilafu yoyote ya kifaa cha kufuatilia mwenendo wa gari inatolewa

taarifa kwa Mamlaka ndani ya saa kumi na mbili baada ya hitilafu

hiyo kutokea.

Mamlaka ya kuzuia

baadhi ya magari ya

abiria kutoa huduma

katika maeneo

maalum

52. Mamlaka inaweza:

(a) kuzuia aina fulani ya magari ya abiria kutoa huduma kwenye njia

yoyote, au maeneo ya jiji kati, manispaa au mji; na

(b) kuainisha maeneo ya jiji kati, manispaa au mji kulingana na wakati.

18

Mzigo uliosahaulika

kwenye gari la abiria 53. Endapo mzigo umeachwa na abiria kwenye gari la abiria, mtoa huduma

atahakikisha kwamba mzigo huo unahifadhiwa kwa ajili ya kuchukuliwa na

mmliki wake. Mamlaka ya

kusimamisha na

kukagua gari

54. Ofisa wa Mamlaka au Polisi anaweza:

(a) kusimamisha na kukagua gari la abiria wakati wowote au sehemu

yoyote ili kujiridhisha iwapo Kanuni hizi zinatekelezwa; au

(b) kutaka kukagua gari, kuonyeshwa leseni au nyaraka ya aina yoyote

ambayo inaweza kuhitajika kuwepo ndani ya gari la abiria. Upakaji rangi na

uwekaji matangazo

kwenye gari la abiria

55. Mtoa huduma hatapaka rangi au kuweka tangazo kwenye gari la abiria

ambalo:

(a) linaingiliana na rangi za utambulisho wa njia iliyopitishwa na Mamlaka;

au (b) linazuia abiria kuona vyema mandhari ya nje wakiwa ndani.

Wajibu wa kutoa

taarifa 56. Mtoa huduma ataitaarifu Mamlaka ndani ya siku thelathini kuhusu

mabadiliko ya anwani ya ofisi na taarifa nyingine zozote au mabadiliko ya

vigezo vyovyote vilivyotolewa wakati wa maombi ya leseni. Kuhamisha umiliki

au kuondoa gari

kwenye huduma

57. Endapo mtoa huduma anahamisha umiliki wa gari la abiria atatakiwa,

ndani ya siku saba, kutoa taarifa kwa Mamlaka.

Mapitio ya uamuzi

wa Mamlaka

58. Mtoa huduma ambaye hajaridhika na uamuzi wa Mamlaka uliotolewa

kwa mujibu wa Kanuni hizi anaweza, ndani ya siku kumi na nne tangu tarehe ya

uamuzi, kuiomba Mamlaka ifanye mapitio ya uamuzi kwa mujibu wa Kanuni za

LATRA (Utaratibu wa Malalamiko na Mapitio). Masharti ya mpito na

yanayoendelea 59. Leseni zote, maelekezo au maelezo yaliyopitishwa au kutolewa kabla ya

kuanza kutumika kwa Kanuni hizi, yataendelea kuwa na nguvu ya kisheria hadi

pale leseni hizo, maelekezo au maelezo yatakapofutwa au kubatilishwa. Kufutwa kwa Kanuni

Tangazo la Serikali

Na. 421 la mwaka

2017.

60. Kanuni za Usafirishaji Abiria (Magari ya Abiria) za mwaka 2017

zimefutwa.

________

MAJEDWALI

________

19

_________

JEDWALI LA KWANZA

_________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 6 (1))

_________

MAOMBI YA LESENI YA USAFIRISHAJI WA ABIRIA

Aina ya Maombi: Mpya Kuhuisha Kubadili njia

Muda Unaoombwa: Kubadili leseni Mwaka mmoja Muda mfupi

A. TAARIFA ZA MUOMBAJI WA LESENI

1. Jina Kamili …………...…………………………………………………………...............................................................................

(Jina/Kampuni/Wabia–kwa HERUFI KUBWA)

2. Anwani ya Posta …………………………………………………………………………………………………………………...

Namba ya Simu ya Mkononi ya Ofisi ……………………… Namba ya Simu

ya Mwombaji

……………………

Baruapepe: …………………………………………………………………………………………………………………………..

3. Anwani ya Mahali:

Mtaa: …………………………………... Namba ya Kiwanja: ………………….. Namba ya Ofisi:……........

4. Je, maombi yako ya leseni yamewahi kukataliwa/kusitishwa au kufutwa? Ndio: Hapana:

Kama ndio, eleza lini na wapi maombi yako ya siku za nyuma yalikataliwa, yalisitishwa au kufutwa…………………………..

Eleza sababu za maombi yako kukataliwa, kusitishwa au kufutwa……………………… na tarehe …………................................

5. Taarifa za Ofisa Usafirishaji au Msimamizi:

(a) Jina: ……………………………….…............................................................................................................................................

(b) Sifa ya Elimu: ……………………………………………………………………………………

(c) Namba ya Simu ya Mkononi:………………………………………………………………………

6. Taarifa ya Karakana ambapo magari yanafanyiwa/yatakuwa yakifanyiwa matengenezo:

(a) Jina la Karakana: …………………………………………………………………………………...............................

(b) Anwani ya Mahali:……………………………………………………………………………………………………

(c) Jina na sifa ya elimu ya Msimamizi wa Karakana: …………………………………………………………………………

B. TAARIFA ZA GARI LINALOOMBEWA LESENI

1. Orodha ya magari (iambatishwe endapo ni taasisi iliyosajiliwa)

2. Namba ya usajili wa gari (endapo ni mtu binafsi):…………………………………………………………………………………..

3. Aina: ……………………………………………………………………………………………………………………….............

4. Uwezo wa gari (idadi ya juu ya abiria wanaoruhusiwa) ……………………………………..……………………………………

5. Madaraja ya huduma:

Kawaida Others (specify)……………………… Daraja la Kati Chini Daraja la Kati Juu Daraja la Starehe

C. TAARIFA ZA HUDUMA INAYOOMBEWA LESENI

1. Maeneo ya njia ambayo au ambapo huduma inatarajiwa kutolewa .……………………………………...........................................

2. Jinsi/Aina ya huduma (weka ( √ ) inapostahili)

Kati ya Mji na Mji Daladala Basi la Shule Nje ya nchi

Basi la wafanyakazi Kijijini-mjini-kijijini Binafsi ya kukodi Utalii

Aina nyingine (Ainisha)………………………………………………

3. Ratiba inayopendekezwa:

Safari ya kwenda: ……………….……………………………….…... Safari ya kurudi: …………………………..…………..

Jedwali la nauli inayopendekezwa kwa huduma ya Daraja la Starehe:

Tshs. ………………… kwa kila safari

D. NYARAKA ZA KUWASILISHA WAKATI WA KUOMBA LESENI

1. Maombi ya kwanza yataambatishwa na vitu vilivyoorodheshwa chini:

(a) Kadi ya Usajili wa Gari,

(b) Cheti Safi cha Mlipa kodi,

(c) Taarifa ya Ukaguzi wa Gari, na

(d) Cheti cha Kusajiliwa (endapo ni taasisi iliyosajiliwa).

2. Maombi ya kuhuisha yataambatishwa na vitu vilivyoorodheshwa chini:

(a) Taarifa ya Ukaguzi wa Gari, na

20

(b) Cheti Safi cha Mlipa kodi.

3. Mamlaka inaweza kuhitaji taarifa zaidi au nyaraka wakati wowote.

Mimi/Sisi nina/tunatamka kuwa kwa mujibu wa ufahamu/uelewa wangu/wetu na nina/tunaamini taarifa zote

zilizotolewa kwenye maombi haya ni za kweli.

Jina Kamili: ………………………………………………………....... Saini:……...……………………................

Cheo ………………………………………………………………….. Tarehe:.…………………………...............

KWA MATUMIZI YA OFISI TU

4. Uhakiki na Uidhinishaji

(a) Hayajaidhinishwa:

Toa sababu ……………………………………………………………

(b) Yameidhinishwa:

Tarehe ya Kuanza: …………………………………………………… Tarehe ya Mwisho: …………………........

Jina kamili la la Ofisa : ……………………………………………………………………………………………………………..

Cheo: …………………………………………………………….

Saini: ………………………………………………………………….

Tarehe : ……………………………………………………………….

Kiasi kilicholipwa: ………………..………………………………….. Stakabadhi Na. …………………………..

Tarehe:...……………………………………………………………..

Saini:………………………...…………….

NAMBA YA JALADA LA MTOA HUDUMA………………... NAMBA YA LESENI …………….……..

UTAMBULISHO WA NJIA .…………………………………...

Kanuni za Leseni ya Usafirishaji (Magari ya Abiria) za Mwaka, 2019

TAHADHARI:

1. Kutoa taarifa ya uongo kwa kujua kwa ajili ya kupatiwa leseni ni kosa la jinai chini ya Sheria ya

LATRA Mwaka 2019.

2. Mabadiliko yoyote ya taarifa zilizotolewa kwenye Fomu hii yanapaswa kuwasilishwa LATRA

vinginevyo utakuwa unafanya kosa la jinai chini ya Kanuni hizi.

21

________

JEDWALI LA PILI

_________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 14(1)

_________

ADA ZA LESENI ZA MAGARI YA ABIRIA

KWA HUDUMA ZA NDANI YA NCHI KWA HUDUMA ZA NJE YA NCHI

NA KWA UTALII

UWEZO WA KUBEBA

ABIRIA

ADA YA MWAKA

(TSHS)

ADA YA MIEZI

MITATU (TSHS)

ADA YA

MWAKA

(US$)

ADA YA MIEZI

MITATU (US$)

BASI LA KAWAIDA NA KATI CHINI

Watu wasiozidi 15 35,000 17,500 50 15

Watu 15 lakini wasiozidi

watu 25 70,000 35,000 80 20

Watu 25 lakini wasiozidi

watu 45 110,000 55,000 145 35

Watu 45 lakini wasiozidi

watu 65 130,000 65,000 150 40

Watu 65 na zaidi 150,000 75,000 160 45

Ada ya fomu ya maombi 10,000 10,000 10 10

Ada ya kubadilisha njia

Asilimia hamsini (50%) ya ada ya leseni

BASI LA DARAJA LA KATI JUU NA STAREHE

Linalozidi watu 25 200,000 100,000 180 60

Ada ya maombi 10,000 10,000 10 10

Tozo ya kubadilisha njia Asilimia hamsini (50%)

ya ada ya leseni

ADA NYINGINEZO

Kwa nakala ya leseni au uidhinishwaji wa leseni iliyopotea, iliyoharibika au kuchafuliwa 20,000/=

Kwa ajili ya kutoa ratiba 10,000/=

Kwa ajili ya batli 10,000/=

22

________

JEDWALI LA TATU

_________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya ……..

_________

TOZO YA UDHIBITI

1. Tozo kwa leseni ya kawaida itakuwa ni asilimia moja (1%) ya pato ghafi inayotokana na utoaji

huduma za usafirishaji abiria.

2. Tozo kwa kampuni yenye leseni

maalumu itakuwa ni

asilimia moja (1%) ya pato ghafi inayotokana na utoaji

huduma za usafirishaji abiria.

23

JEDWALI LA NNE

_________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 23(1)(h) )

_________

MADARAJA YA MAGARI

NA. VIWANGO

VILIVYOKUBALIKA

DARAJA LA

KAWAIDA

DARAJA LA KATI

CHINI

DARAJA LA KATI

JUU

DARAJA LA

STAREHE

1. Kiwango cha juu cha

urefu wa basi

14m 14m 14m 14m

2. Kiwango cha juu cha

upana wa basi

2.6m 2.6m 2.6m 2.6m

3. Kiwango cha juu cha

kimo cha basi likiwa

limejaza abiria au

likiwa halina abiria

4.6m 4.6m 4.6m 4.6m

4. Uwezo wa kubeba

abiria kwa basi lenye

urefu wa 12.5m

Kiwango cha juu cha

uwezo wa kubeba

abiria kitakuwa ni

abiria 65 ikiwa ni

pamoja na dereva

Kiwango cha juu cha

uwezo wa kubeba

abiria kitakuwa ni

abiria 60 ikiwa ni

pamoja na dereva

Kiwango cha juu cha

uwezo wa kubeba

abiria kitakuwa ni

abiria 60 ikiwa ni

pamoja na dereva

Kiwango cha juu

cha uwezo wa

kubeba abiria

kitakuwa ni abiria

51 ikiwa ni

pamoja na dereva

5. Mahitaji ya viti

Pale ambapo viti

vimepangwa kuelekea

upande mmoja na

umbali wa ulalo kwa

mbele na nyuma

haupungui 680mm viti

vya abiria havitakiwa

kurekebishwa

(a) Viti vyote vya

abiria viwe

vinaweza

kurekebishika

(b) Pale ambapo viti

vimeelekea

upande mmoja,

umbali chini wa

ulalo kati ya

sehemu ya mbele

na sehemu ya

nyuma ya kiti

lazima

usipungue 690

mm

(a) Viti vyote vya

abiria lazima

viwe katika hali

inayoweza

kurekebishika

(b) Pale ambapo viti

vimeelekea

upande mmoja,

umbalichini wa

ulalo kati ya

sehemu ya mbele

na sehemu ya

nyuma ya kiti

lazima

usipungue 690

mm

(a) Viti vyote

vya abiria

lazima viwe

katika hali

inayoweza

kurekebishika

(b) Pale ambapo

viti

vimeelekea

upande

mmoja,

umbali chini

wa ulalo kati

ya sehemu ya

mbele na

sehemu ya

nyuma ya kiti

lazima

usipungue

690 mm

6. Mpangilio wa viti kwa

ajili ya mabasi

makubwa

3x2 au 2x2 2x2 2x2 2x2

7. Mikanda ya viti Viti vyote vya abiria

ikiwa ni pamoja na kiti

cha dereva lazima viwe

na mikanda ya viti

Viti vyote vya abiria

ikiwa ni pamoja na

kiti cha dereva lazima

viwe na mikanda ya

viti

Viti vyote vya abiria

ikiwa ni pamoja na

kiti cha dereva lazima

viwe na mikanda ya

viti

Viti vyote vya

abiria ikiwa ni

pamoja na kiti cha

dereva lazima

viwe na mikanda

ya viti

24

8. Taa za ndani Idadi ya chini ya taa

tatu ndani ya basi ziwe

katika umbali sawa

sambamba na njia ya

kupita ndani ya basi

Pamoja na taa zote

zilizopo katika gari la

kawaida, kila kiti cha

abiria lazima kiwe na

taa yake

Pamoja na taa zote

zilizopo katika gari la

kawaida, kila kiti cha

abiria lazima kiwe na

taa yake

Pamoja na taa

zote zilizopo

katika gari la

kawaida, kila kiti

cha abiria lazima

kiwe na taa yake

9. Viyoyozi Hakuna kiyoyozi Hakuna kiyoyozi Muhimu Muhimu

10. Luninga Hakuna luninga Lazima kuwa na

angalao luninga mbili

(kwa mabasi

makubwa)

Lazima kuwa na

angalao luninga mbili

(kwa mabasi

makubwa)

Lazima kuwa na

angalao luninga

mbili (kwa mabasi

makubwa)

11. Redio na redio ya

muziki

Sio lazima Gari lazima iwekewe

redio na redio ya

muziki

Gari lazima iwekewe

redio na redio ya

muziki

Gari lazima

iwekewe redio na

redio ya muziki

12. Kipaza sauti Muhimu Muhimu Muhimu Muhimu

13. Mapazia ya madirisha Sio lazima Muhimu Muhimu Muhimu

14. Msalani/chumba cha

mapumziko

Hakuna huduma za

msalani

Hakuna huduma za

msalani

Hakuna huduma za

msalani

Muhimu

15. Kipasha joto Sio lazima Sio lazima Sio lazima Lazima kuwe na

kipasha joto kwa

ajili ya

kuchemshia maji

au kupasha moto

vinywaji kama

vile kahawa, chai

nk

16. Jokofu /sanduku la

baridi

Sio lazima Sio lazima Sio lazima Lazima kuwe na

jokofu na

/sanduku la baridi

17. Vinywaji baridi Sio lazima Sio lazima Sio lazima Lazima huduma

ya vinywaji baridi

itolewe

25

JEDWALI LA TANO

________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 33(1))

________

MFANO WA TIKETI YA GARI LA ABIRIA

MABASI YA MASAFA MAREFU

NEMBO YA KAMPUNI

Namba: .....................

Jina la Kampuni: ……………………………………………………………………………………………….

Anuani ya Mmiliki…………….............................................................................................................................

Namba ya Basi: ……………. Njia ya Safari: …..…………….... Tarehe ya kuandikwa tiketi ...........................

Jina la Abiria………………………………………… Kuanza safari saa…………………………………….

Namba ya kiti ……………………………………….. Kuwasili kituoni saa ………………………………....

Kituo cha kuanzia safari ni .......................................... Kuelekea ......................................................................

Tarehe ya safari………………………………………

Nauli ni Shillingi ……………………………………

Muda wa kuanza safari: …………………………….. Tarehe ya Safari: …...………………………………..

MABASI YA MIJINI

Nembo ya Kampuni/Mmiliki (kama ipo) ……………………………….………………………………………

Namba ya Usajili wa Gari ……………………….…. Jina na Anuani ya Mmiliki...…………………………

Njia…………………………………………………... Nauli iliyoidhinishwa ya Shilingi …………………..

Tarehe ya Kutolewa …………….………………….

26

JEDWALI LA SITA

________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 34(1))

________

MFANO WA ORODHA YA ABIRIA WANAOSAFIRI

NEMBO YA KAMPUNI Namba: .....................

ORODHA YA ABIRIA WANAOSAFIRI

Jina la Kampuni: ………………………………………………………………………………………………………….

Jina la Mmiliki: ………………………….............................................................................................................................

Anwani ya Mmiliki: ……………………………………………………………………………………………….……….

Namba ya Basi: …………………………. Njia ya Safari: …..……………………………………...............................

Muda wa kuanza safari: ………………… Tarehe ya Safari: …………………………………………………………..

Na. Jina Kamili la

Abiria

Uraia Namba ya

Simu ya

Mtu wa

karibu

Namba ya

Kiti

Kituo cha

kuanza

safari

Kituo

anachokwenda

Kiwango cha

Nauli

1.

2.

3.

4.

5.

6.

7.

8.

9.

10.

11.

12.

13.

14.

15.

16.

17.

18.

19.

20.

Jumla ya Abiria: …………………………………………………………………………………………………………

Jina la Dereva (1): ….…………………….. Namba ya Leseni: ………………………… Saini: .…………………....

Jina la Dereva (2): …………..……………. Namba ya Leseni: …………………………Saini: …………………….

Jina la Kondakta: ………………………………………………………………………… Simu: ……………………..

27

JEDWALI LA SABA

_________

( Limetengenezwa chini ya kanuni ya 45)

_________

MAKOSA NA ADHABU ZINAZOFIFISHWA NA LATRA

NA. AINA YA KOSA KANUNI KIASI

KILICHOFIFISHW

A NA LATRA

MAKOSA YA JUMLA KWA AINA ZOTE ZA MAGARI

1. Kutoa huduma ya kusafirisha abiria bila kuwa na leseni

halali ya LATRA.

4 250,000/=

2. Kushindwa kubandika leseni sehemu ya wazi upande wa

kushoto wa kioo cha mbele cha gari la abiria.

18(1) & (2) 100,000/=

3. Kushindwa kuzingatia vigezo vya utendaji vilivyowekwa na

Mamlaka.

19 (1) 100,000/=

4. Kushindwa kwa Taasisi iliyosajiliwa atawasilisha Taarifa

ya Mwaka ya Utendaji kwa Mamlaka; au

19 (2) (a) 100,000/=

5. Kutumia gari jingine bila kuwa na kibali cha dharura pale

gari la abiria la njia husika linapoharibika

22 (1) 100,000/=

6. Kuendesha gari la abiria likiwa na hitilafu; 23 (1) (a) 250,000/=

7. Kushindwa kuzingatia idadi ya abiria, uzito na upakiaji wa

mizigo, uzito wa gari na mwendo kama vilivyoainishwa

kwenye Sheria nyingine za nchi.

23 (1) (b)

250,000/=

8. Dereva mmoja wa gari la abiria kuendesha gari mfululizo

zaidi ya saa nane. 23 (1) (c) 250,000/=

9. Kushindwa kuweka kumbukumbu, kuandaa na kutoa taarifa

sahihi za biashara ya usafirishaji wa abiria. 23 (1) (d) 250,000/=

10. Kuendesha gari la abiria bila kuwa na kisanduku cha

huduma ya kwanza, kilichowekwa mahali panapoonekana,

kilicho na dawa na vifaa tiba vilivyoainishwa.

23 (1) (e) 250,000/=

11. Kushindwa kuweka chombo cha taka kwenye gari la abiria

na kushindwa kutupa taka kwenye maeneo maalum. 23 (1) (f) 250,000/=

12. Kushindwa kuzingatia viwango vya gari la abiria kama

vilivyoainishwa kwenye Jedwali la Nne. 23 (1) (h) 250,000/=

13. Kubeba mzigo hatarishi kwenye gari la abiria. 23 (2) (a) 250,000/=

14. Kubeba abiria zaidi ya idadi ya watu iliyobainishwa kwenye

leseni. 23 (2) (b) 100,000/=

15. Kuruhusu au kuacha watu kupanda ndani ya gari la abiria

kufanya biashara, kuhubiri au siasa na kuweka burudani,

kuonyesha picha au kupiga mziki kwenye gari la abiria

wakati wa safari ambazo haziendani na maadili na tamaduni

za Kitanzania na kwa sauti ya juu.

23 (2) (c) 100,000/=

16. Kushindwa kutekeleza Kanuni hizi, Sheria ya Usalama

Barabarani na sheria nyinginezo za nchi. 23 (2) (d) 100,000/=

MAKOSA YA USAFIRISHAJI WA ABIRIA WA MIJINI

17. Kutotoa tiketi ya safari kwa abiria. 24 (1) (a) (ii) 100,000/=

18. (

a

)

Mtoa huduma kutopaka rangi ya utambulisho wa njia

iliyopitishwa na Mamlaka au kupaka rangi au kuweka

matangazo kwenye gari la abiria ambayo yanaingiliana na

rangi au inazuia abiria kuona vyema mandhari ya nje akiwa

ndani.

24(1)(a)(iii) 100,000/=

28

19. Kutoa huduma ya kusafirisha abiria bila kuandika nauli

iliyoidhinishwa na Mamlaka karibu na mlango wa kuingilia

abiria.

24 (1) (a)

(iv) 100,000/=

20. Mfanyakazi wa gari la abiria linalotoa huduma ya usafiri wa

mjini kutovaa sare safi au nadhifu kama ilivyoidhinishwa na

Mamlaka.

24 (1) (b) (i) 100,000/=

21. Mfanyakazi wa gari la abiria kuruhusu mtu kufanya

biashara, kuhubiri, kufanya shughuli za siasa au kutoa

burudani ambayo inakiuka kanuni ya 23 (2) (c) ndani ya gari

la abiria mijini;

24 (1) (b)

(ii) 100,000/=

22. Mfanyakazi wa gari la abiria kutoa huduma ya usafirishaji

abiria kwenye njia ambayo haijaidhinishwa kwenye leseni.

24 (1) (b)

(iii) 100,000/=

23. Mfanyakazi wa gari la abiria gari kubadilisha njia au

kusitisha safari kabla ya kufika mwisho wa kituo kama

ilivyooneshwa kwenye tiketi ya abiria.

24 (1) (b)

(iv) 100,000/=

MAKOSA KWA MAGARI YATOAYO HUDUMA KATI YA MJI NA MJI NA NCHI NA NCHI

24. Kutoa huduma ya kusafirisha abiria kwa gari ambalo

halina vigezo vya madaraja ya mabasi ya abiria

vilivyoainishwa kwenye Jedwali la Nne la Kanuni hizi;

25 (a) (ii) 250,000/=

25. Kutoa huduma ya kusafirisha abiria kati ya mji na mji

au nchi na nchi kwa gari ambalo halijafungwa kifaa

maalum kilichoidhinishwa na Mamlaka kwa ajili ya

kufuatilia mwendo wa gari;

25 (a) (iii) 250,000/=

26. Kutoa huduma ya gari la abiria bila kuzingatia batli,

ratiba na chati ya nauli iliyoidhinishwa na Mamlaka; 25 (a) (iv) 100,000/=

27. Kutoa huduma ya kusafirisha abiria bila gari kuwa na

mikanda inayofanya kazi na safi kwa kila kiti cha

abiria;

25 (a) (v) 100,000/=

28. Mfanyakazi wa gari la abiria kutovaa sare safi na

nadhifu kama ilivyoamuliwa na Mamlaka. 25 (b) (i) 100,000/=

29. Mfanyakazi wa gari la abiria kutouza tiketi halali ya

basi kwa mfumo wa karatasi au kielektroniki na

kutotolewa kwa abiria.

25 (b) (ii) 100,000/=

30. Mfanyakazi wa gari la abiria kuruhusu mtu kufanya

biashara, kuhubiri, kufanya shughuli za siasa au kutoa

burudani ambayo inakiuka kanuni ya 23 (2) (c) ndani

ya gari la abiria.

25 (b) (iii) 100,000/=

31. Mfanyakazi wa gari la abiria kutozingatia batli, ratiba

na chati ya nauli iliyoidhinishwa na Mamlaka. 25 (b) (iv) 100,000/=

32. Mfanyakazi wa gari la abiria kushindwa kuwa na

nakala tatu za orodha ya abiria kwa kila safari ambapo

nakala moja itabaki katika gari la abiria, nakala

nyingine itawasilishwa kituo cha polisi na nakala

nyingine itaachwa kwenye ofisi za mtoa huduma.

25 (b) (v) 100,000/=

33. Wafanyakazi wa gari la abiria kutoa huduma ya usafiri

bila kuvaa vitambulisho vinavyonekana kwa urahisi

kwa mtu yeyote wakati wa safari.

25 (b) (vi) 100,000/=

34. Mfanyakazi wa gari la abiria kutoa huduma kwenye

njia ambayo haijaidhinishwa kwenye leseni; 25 (b) (viii) 100,000/=

35. Mfanyakazi wa basi la abiria kukatisha safari kabla ya

kufika kituo cha mwisho wa safari kama

inavyoonekana kwenye tiketi ya abiria.

25 (b) (ix) 100,000/=

36. Mtoa huduma na mfanyakazi wa gari linalotoa huduma

kati ya nchi na nchi lenye usajili wa nchi nyingine

kutoa huduma za usafirishaji abiria kama gari

lililosajiliwa nchini na linalotoa huduma za ndani.

26 250,000/=

29

MAKOSA KWA MAGARI YA SHULE

37. Mtoa huduma wa basi la shule kutoa huduma ya

usafirishaji gari likiwa na itilafu. 27 (1) (a) 250,000/=

38. Kutoa huduma ya usafiri wa basi la shule lisilokidhi

viwango vya Usalama na Ubora wa Huduma

usafirishaji magari ya abiria

27 (1) (b) 250,000/=

39. Kutoa huduma ya usafiri wa basi la shule bila kupakwa

rangi ya njano yenye namba Rgb (255,255,0) na

kuandikwa maneno “School Bus” au “Basi la Shule”.

27 (1) (d) 100,000/=

40. Mfanyakazi wa basi la shule kubeba wanafunzi zaidi

ya idadi iliyoandikwa kwenye leseni. 27 (2) (a) 100,000/=

41. Mfanyakazi wa basi la shule kuruhusu upakiaji kupita

uwezo wa gari na mwendo wa gari kinyume na

viwango vilivyoainishwa kwenye sheria nyingine;

27 (2) (b) 100,000/=

42. Kuendesha basi la shule bila kuwa na kisanduku cha

huduma ya kwanza kilichowekwa mahali

panapoonekana, kilicho na dawa na vifaa tiba

vilivyoainishwa.

27 (1) (e) 100,000/=

43. Mfanyakazi wa basi la shule atashindwa kuvaa sare

safi na nadhifu kama Shule itakavyoamua. 27 (2) (c) 100,000/=

44. Mtoa huduma na mfanyakazi wa basi la shule

atashindwa kuweka chombo cha taka kwenye gari na

taka zinazokusanywa na zinatupwa kwenye maeneo

maalum ya kutupa taka; na

27 (2) (d) 100,000/=

MAKOSA YA JUMLA KWA MABASI YA ABIRIA

45. Mtoa huduma hatatoza nauli zaidi ya ile

iliyoidhinishwa na Mamlaka kulingana na daraja la

basi husika.

31 250,000/=

46. Mtoa huduma atarudisha kiwango cha nauli iliyolipwa

pale ambapo wekesho la tiketi litafutwa kwenye muda

usiozidi saa ishirini na nne na si chini ya saa kumi na

mbili kabla ya muda uliopangwa kabla ya safari

kuanza:

33 (6) (7) 100,000/=

47. Mtoa huduma kushindwa kuandaa orodha ya abiria

wanaosafiri kama ilivyoelekezwa na Mamlaka na kwa

kuzingatia Jedwali la Sita la Kanuni hizi.

34 (1) (3) 100,000/=

48. Kama mtoa huduma atashindwa kutoa huduma ya

usafiri kwa abiria ambaye amekwisha kupewa tiketi

atawajibika kwa mujibu wa vigezo na masharti ya

tiketi na ratiba ya safari.

36 (1) (2) 100,000/=

49. Mtoa huduma atakayemtoza nauli mwanafunzi

atakayepanda gari la abiria linalotoa huduma ya usafiri

ndani ya mji kwa kiwango cha nauli kisichoidhinishwa

na Mamlaka.

37 (1) 100,000/=

50. Mtoa huduma atakayetoza malipo ya kusafirisha mzigo

wa abiria wenye uzito usiozidi kilo ishirini. 38 (1) 100,000/=

51. Mtoa huduma atakayetoza malipo kwa vifaa saidizi

vinavyotumiwa mtu mwenye ulemavu wa viungo kwa

ajili ya kutembea wakati anaposafiri kwenye gari

linalotoa huduma kati ya mji na mji au nchi na nchi.

38 (1) (b) 100,000/=

52. Kushindwa kuweka alama kwenye mzigo wa abiria

inayotambulisha jina la abiria na kituo cha mwisho wa

safari ya abiria

40 100,000=

53. Mtoa huduma atakayeshindwa kutoa taarifa kwa

Mamlaka pale ambapo gari la abiria halitoi huduma

kwa kipindi kinachozidi siku thelathini.

51 250,000/=

54. Mtoa huduma wa gari la abiria atakaeshindwa 52 (a) (b) 250,000/=

30

kuhakikisha kuwa:

(a) kifaa cha kufuatilia mwenendo wa gari kinafanya

kazi vyema wakati wote, kinatunzwa na kinalindwa

dhidi ya mazingira hatarishi na uharibifu wa makusudi

wakati wote wa kutoa huduma; na

(b) hitilafu yoyote ya kifaa cha kufuatilia mwenendo

wa gari inatolewa taarifa kwa Mamlaka ndani ya saa

kumi na mbili baada ya hitilafu hiyo kutokea.

55. Mtoa huduma atakayepaka rangi au kuweka tangazo

kwenye gari la abiria linaloingiliana na rangi za

utambulisho wa njia iliyoidhinishwa na mamlaka.

57 100,000/=

56. Mtoa huduma atakayeshindwa kuitaitaarifu Mamlaka

ndani ya siku thelathini kuhusu mabadiliko ya anwani

ya ofisi na taarifa nyingine zozote au mabadiliko ya

vigezo vyovyote vilivyotolewa wakati wa maombi ya

leseni.

58 100,000/=

31

__________

JEDWALI LA NANE _________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 46) __________

HATI YA MAKOSA NA UTEKELEZAJI WAKE KWA DEREVA

SEHEMU YA I: TAARIFA YA KOSA

Kwa: .…………………………………………………………………………………

Anwani: ……………………………………………………………………………………

1. ……………………..………………………………………………… Mwenye Leseni ya Udereva Na. …………

Daraja …………… dereva wa gari la abiria lenye Namba za Usajili Na. ……………. Unatuhumiwa kwa

kosa/makosa dhidi ya kanuni namba ……………………………………………………..

Taarifa ya kosa:

Kwamba …..………… siku ya …….……………. mwaka………………………………

kwenye eneo la ………………………………. wewe (maelezo mafupi kuhusu kosa):

……………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………… ……………………………………………………………………………………………… 2. Iwapo HUKUBALI kuwa umefanya kosa/makosa, jaza Sehemu “A” ya fomu hii ya makosa.

3. Iwapo UNAKUBALI kuwa umetenda kosa/ makosa, jaza Sehemu “B” ya fomu hii ya Makosa.

4. Kiasi cha kufifisha makosa KITALIPWA Benki kwenye akaunti ya LATRA namba ……………….

SEHEMU YA II: TAARIFA YA DEREVA

SEHEMU A: NIA YA KWENDA MAHAKAMANI

Mimi …………………………………………………..………… wa (anuani ya eneo la makazi au biashara)

…………………………………………..…..…………………….. nina nia ya kujitetea Mahakamani dhidi ya kosa

nililotuhumiwa nalo la ……………………………………………… kinyume na kanuni ya ………………….. ya

Kanuni za Leseni ya Usafirishaji (Magari ya Abiria), za mwaka 2019.

Jina: …………………………...…………………………………………………………………..

Sahihi: …………………………...…………………………………………………………………..

SEHEMU B: KUKIRI KOSA

Mimi …………………………………………………..………… wa (anuani ya eneo la makazi au biashara)

…………………………………………..…..…………………….. nakiri kosa la

……………………………………………………………… kinyume na kanuni ya ………………….. ya Kanuni za

Leseni ya Usafirishaji (Magari ya Abiria), za mwaka 2019.

Ninaomba kosa lififishwe kwa mujibu wa kanuni ya ………… ya ya Kanuni za Leseni ya Usafirishaji (Magari ya

Abiria), za mwaka 2019.

Nitalipa faini ya Tshs……………………..ndani ya siku kumi na nne (14) tangu tarehe ya kupokea taarifa ya kosa

kama kiasi cha kufifisha kosa.

Jina: ………………………………………………………………………………………………….

Sahihi: ………………………………………………………………………………………………….

Na. ya

Kitambulisho:

………………………………………………………………………………………………….

Imetolewa na: Mkoa: Imeshuhudiwa na:

32

______________

JEDWALI LA TISA

_________

(Limetengenezwa chini ya kanuni ya 46) ______________

HATI YA MAKOSA NA UTEKELEZAJI WAKE KWA MTOA HUDUMA

SEHEMU YA I: TAARIFA YA KOSA Kwa: .…………………………………………………………………………………

Anwani: ……………………………………………………………………………………

1. Unashitakiwa kwa kosa la …………………………………………………..

Taarifa ya kosa/makosa dhidi ya kanuni namba:

Kwamba …..……… siku ya ……………………… mwaka…………………

kwenye eneo la ……………………………… wewe (maelezo maupi kuhusu kosa):

(a) ……………………………………………………………………………………….

(b) ……………………………………………………………………………………….

(c) ……………………………………………………………………………………….

(d) ……………………………………………………………………………………….

2. 2

.

Iwapo HUKUBALI kuwa umefanya kosa/makosa, jaza Sehemu III “A” ya fomu hii ya makosa.

3. 3

.

Iwapo UNAKUBALI kuwa umetenda kosa/ makosa, jaza Sehemu III “B” ya fomu hii ya Makosa.

4. 4

.

Kiasi cha kufifisha makosa KITALIPWA Benki kwenye akaunti ya LATRA namba ……………….

SEHEMU YA II: TAARIFA YA DEREVA

Mimi …………………………………………………..………… Mwenye Leseni ya Udereva Na. ………… Daraja

…………… dereva wa gari la abiria lenye Namba za Usajili Na………………….ninayefanya biashara

kama…………………… ninakiri kupokea Taarifa ya Kosa Na. ………… kwa kosa na. ……………. Ninachukua

jukumu la kuwasilisha Taarifa hii ya kosa kwa mtoa huduma wa gari lililotajwa hapo.

Sahihi: ……………………………….……………… Tarehe: ………………………………..……………...

Jina la Shuhuda: ……………………………….…… Signature: ..………………………..………………….

Tarehe: ……………………………….……………… Mkoa: ……………………………….………………..

SEHEMU YA II: TAARIFA YA MTOA HUDUMA

SEHEMU A: NIA YA KWENDA MAHAKAMANI

Mimi …………………………., mtoa huduma wa gari lenye namba za usajili ……………………..……… wa (anuani

ya eneo la makazi au biashara) ……………………………….…..…………………….. ninakiri kupokea Taarifa ya

kosa na nina nia ya kujitetea Mahakamani dhidi ya kosa nililotuhumiwa nalo la

……………………………………………… kinyume na kanuni ya ………………….. ya Kanuni za Leseni ya

Usafirishaji (Magari ya Abiria), za mwaka 2019.

Jina: …………………………...…………………………………………………………………………...

Sahihi: …………………………...…………………………………………………………………………...

SEHEMU B: KUKIRI KOSA

Mimi ………………………………………, mtoa huduma wa gari la abiria lenye namba za usajili

…………………..………… wa (anuani ya eneo la makazi au biashara)

…………………………………………..…..…………………….. nakiri kupokea Taarifa ya kosa na nnakiri kutenda

kosa hilo …………………………………………… kinyume na kanuni ya ………………….. ya Kanuni za Leseni ya

Usafirishaji (Magari ya Abiria), za mwaka 2017.

Ninaomba kosa lififishwe kwa mujibu wa kanuni ya ………… ya ya Kanuni za Leseni ya Usafirishaji (Magari ya

Abiria), za mwaka 2017.

Nitalipa faini ya Tshs……………………..ndani ya siku kumi na nne (14) tangu tarehe ya kupokea taarifa ya kosa

kama kiasi cha kufifisha kosa.

Jina: ………………………………………………………………………………………………………..

Sahihi: ………………………………………………………………………………………………………..

Na. ya

Kitambulisho:

………………………………………………………………………………………………………..

Imetolewa na:

33

Dodoma, ISACK ALOYCE KAMWELWE

……………., 2019 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano