15
1 TANGAZO LA SERIKALI Na…………la Tarehe…………. SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI) SURA 288 SHERIA NDOGO Zimetungwa Chini ya Kifungu cha 89(1) Na 62(1) na (2) SHERIA NDOGO ZA (UDHIBITI NA USIMAMIZI WA MIFUGO ZA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA, 2018 Jina na Mwanzo wa kuanza kutumika 1 Sheria ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za (Udhibiti na Usimamizi) wa Mifugo za Halmashauri ya Manispaa ya Ilala za Mwaka 2018 na zitaanza kutumika mara baada ya kutangazwa katika Gazeti la Serikali. Matumizi 2 Sheria Ndogo hizi zitatumika eneo lote lililopo chini ya Mamlaka ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Tafsiri 3 Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale itakapoelekezwa vinginevyo:- Afisa Mwidhiniwamaana yake ni afisa mifugo wa Manispaa, afisa kilimo pamoja na afisa yeyote wa Halmashauri atakayeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi. Afyamaana yake ni hali timilifu ya kimwili na kiakili ya mnyama. Halmashaurimaana yake ni Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. “Kaya” maana yake ni familia ya watu akiwemo baba, mama, mtoto au watoto na mtu mwingine yeyote anayeishi na familia hiyo, au watu wanaokaa katika nyumba moja na kuishi kama familia au mtu yeyote anayeishi peke yake katika chumba au nyumba. “Kero au Chukizo” maana yake ni kitu chochote ambacho kipo katika hali yoyote iwe kinatumika, kimewekwa, kimejengwa au ni kichafu kiasi cha kusababisha (a) Hatari kwa viumbe na maisha ya binadamu, (b) Harufu mbaya ya kuudhi.

SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI) SURA …...ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala. Tafsiri 3 Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale itakapoelekezwa ... “Kaya” maana

  • Upload
    others

  • View
    135

  • Download
    2

Embed Size (px)

Citation preview

1

TANGAZO LA SERIKALI Na…………la Tarehe………….

SHERIA YA SERIKALI ZA MITAA (MAMLAKA ZA MIJI)

SURA 288

SHERIA NDOGO

Zimetungwa Chini ya Kifungu cha 89(1) Na 62(1) na (2)

SHERIA NDOGO ZA (UDHIBITI NA USIMAMIZI WA MIFUGO ZA

HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA, 2018

Jina na Mwanzo

wa kuanza

kutumika

1 Sheria ndogo hizi zitajulikana kama Sheria Ndogo za (Udhibiti

na Usimamizi) wa Mifugo za Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

za Mwaka 2018 na zitaanza kutumika mara baada ya kutangazwa

katika Gazeti la Serikali.

Matumizi 2 Sheria Ndogo hizi zitatumika eneo lote lililopo chini ya Mamlaka

ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.

Tafsiri 3 Katika Sheria Ndogo hizi isipokuwa pale itakapoelekezwa

vinginevyo:-

“Afisa Mwidhiniwa” maana yake ni afisa mifugo wa Manispaa,

afisa kilimo pamoja na afisa yeyote wa Halmashauri

atakayeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi.

“Afya” maana yake ni hali timilifu ya kimwili na kiakili ya

mnyama.

“Halmashauri” maana yake ni Halmashauri ya Manispaa ya

Ilala.

“Kaya” maana yake ni familia ya watu akiwemo baba, mama,

mtoto au watoto na mtu mwingine yeyote anayeishi na familia

hiyo, au watu wanaokaa katika nyumba moja na kuishi kama

familia au mtu yeyote anayeishi peke yake katika chumba au

nyumba.

“Kero au Chukizo” maana yake ni kitu chochote ambacho kipo

katika hali yoyote iwe kinatumika, kimewekwa, kimejengwa au

ni kichafu kiasi cha kusababisha

(a) Hatari kwa viumbe na maisha ya binadamu,

(b) Harufu mbaya ya kuudhi.

2

(c) Kuzaliana kwa wadudu na wanyama hatari kama vile

inzi, mende, sisimizi, panya, nyoka, nyuki, kunguni au

viumbe wengine hatari.

(d) Magonjwa kwa binadamu, kuhifadhi mbu, inzi, panya na

viumbe wenye madhara

“Kibali” maana yake ni ni hati iliyotolewa chini ya sheria ndogo

hizi.

“Mifugo” maana yake ni mifugo yoyote na wanyama wafugwao

na binadamu.

“Mkurugenzi” maana yaje ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya

Manispaa ya Ilala au Afisa yeyote wa umma atakayeteuliwa

kutekeleza majukumu ya Mkurugenzi.

“Ufugaji wa ndani” maana yake ni ufugaji na ulishaji wa

mifugo ndani ya jengo lililoruhusiwa (zero grazing).

“Wakala” maana yake ni mtu binafsi au kikundi cha watu,

kampuni, taasisi au shirika aliyeteuliwa kusimamia utekelezaji

wa Sheria Ndogo hizi.

“Waziri” maana yake ni Waziri mwenye dhamana ya Serikali za

Mitaa.

“Zizi” maana yake ni jengo au eneo lililozungushiwa uzio

ambalo linatumika kuhifadhi mifugo iliyokamatwa ambalo

litatunzwa na kusimamiwa na Halmashauri

Wajibu wa

Halmashauri

4 Ni wajibu wa kila Halmashauri:

(a) Kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi ya ufugaji

(b) Kuelekeza idadi ya mifugo ambayo kila mfugaji

anaruhusiwa kufuga.

(c) Kujenga majosho ya mifugo kwa kushirikiana na

wananchi.

(d) Kutoa elimu ya ufugaji bora kwa jamii ili kuongeza tija.

(e) Kufanya sensa ya mifugo, kuweka alama na kutoa kadi

za mifugo

(f) Kutoa chanjo kwa kushirikiana na wafugaji ili kudhibiti

magonjwa ya mifugo.

(g) Kudhibiti uzururaji holela wa mifugo na wanyama katika

Halmashauri kwa mujibu wa Sheria.

Wajibu wa

mfugaji

Itakuwa wajibu wa kila mfugaji chini ya Sheria Ndogo hizi

kuhakikisha kwamba:-

3

(a) Anaogesha mifugo yake ili kudhibiti magonjwa ya

wanyama kama atakavyoagizwa na Halmashauri.

(b) Anapeleka mifugo yake katika vituo vya chanjo kama

itakavyoamriwa na Halmashauri na atalipia chanjo hiyo

kama atatakiwa kufanya hivyo kwa mujibu wa viwango

vitakavyoainishwa na Sheria ndogo za Ada na Ushuru za

Halmashauri.

(c) Kuhakikisha Mifugo yake inawekwa alama maalumu

(Branding, ear tags) zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria

ya Mifugo

(d) Anafuga idadi ya mifugo katika jengo lililoidhinishwa

kulingana na maelekezo ya Sheria Ndogo hizi.

(e) Anakuwa na kadi ya mifugo itakayoonesha idadi na aina

ya mifugo aliyonayo.

(f) Anaipatia mifugo yake malisho na maji ya kutosha kwa

kuzingatia kanuni bora za ufugaji.

(g) Anakuwa na kibali cha kusafirisha mifugo na mazao

yake na kuhakikisha Sheria na Kanuni za usafirishaji

mifugo zinazingatiwa.

(h) Anafuga kwa kuzingatia mipango ya matumizi bora ya

ardhi.

(i) Anahudhuria mafunzo ya ufugaji kama atakavyo hitajiwa

na Halmashauri.

(j) Anauza mifugo yake katika masoko na minada

iliyoidhinishwa tu.

Kibali cha kufuga

mifugo

6 1 Mtu yeyote atakayetaka kufuga mifugo atalazimika kupata kibali

cha kufuga kutoka kwa Halmashauri kama ilivyoainishwa katika

jedwali la kwanza la Sheria ndogo hizi.

2 Kibali kilichotajwa katika kifungu cha 6 (1) cha Sheria Ndogo

hizi hakitakuwa na gharama na hakitozidi miaka mitano

kulingana na aina ya mifugo kuanzia tarehe kilipotolewa.

3 Kaya itaruhusiwa kufuga mifugo ndani ya eneo la Halmashauri

kama ilivyoainishwa katika jedwali la pili la Sheria Ndogo hizi.

4

Masharti kwa

Mfugaji

7 Ni marufuku kwa mfugaji au mtu yeyote

1 Kuchunga, kulisha,au kunywesha maji mifugo katika maeneo

ambayo hayakutengwa kwa shughuli hiyo

2 Kusafirisha mifugo kwa kuiswaga barabarani

3 Kusafirisha au kuhamisha mifugo kutoka eneo moja hadi lingine

bila kibali kutoka kwa Halmashauri

4 Kuingiza mifugo katika eneo la Halmashauri bila kibali

5 Kuuza au kununua mifugo katika maeneo ambayo siyo mnada,

masoko au magulio ya mifugo yaliyoaidhinishwa na

Halmashauri.

6 Kufuga mifugo zaidi ya idadi iliyoainishwa katika Sheria

Ndogo hizi,

7 Kununua, kuuza au kufanya Biashara ya kubadilishana aina

yoyote ya mifugo katika eneo lolote la Halmashauri isipokuwa

kwenye minada au magulio yaliyotengwa kwa shughuli hiyo na

Halmashauri.

Kibali cha

kusafirisha

mifugo

8 1 Itakuwa ni wajibu kwa mtu yeyote anayetaka kusafirisha mifugo

na mazao yake kutoka au kuingia katika eneo la halmashauri

kuwa na kibali maalumu kitakachoruhusu kusafirisha mifugo

hiyo kama ilivyoainishwa katika Sheria Ndogo hizi na Sheria

zilizotungwa na Bunge

2 Kibali cha kusafirisha mifugo au mazao ya mifugo au vyote kwa

pamoja nje na ndani ya Halmashauri kitatolewa na Halmashauri

baada ya kujiridhisha kuwa mifugo hiyo ina afya nzuri,

imeogeshwa na kupatiwa chanjo kabla ya kusafirishwa.

3 Halmashauri itatoa kibali cha usafirishaji mifugo kwa kuweka

utaratibu ikiwa ni pamoja na:

(a) Mfugaji kutoa uthibitisho wa kumiliki mifugo au

mnyama huyo kutoka kwa Mtendaji wa Mtaa.

(b) Kukagua vibali vyote vya usafirishaji mifugo.

4 Afisa Mwidhiniwa atakuwa na uwezo wa kukamata na kutoza

faini na adhabu kwa mifugo yoyote inayosafirishwa kinyume na

Sheria Ndogo hizi au Sheria yeyote iliyotungwa na Bunge la

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Taratibu za

ufugaji

9 Wafugaji wote watatakiwa kuzingatia masharti ya kufuga kama

yalivyo katika Sheria Ndogo hizi au Sheria yoyote iliyotungwa

na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

5

Kudhibiti mifugo

inayozurura

hovyo

10 1 Halmashauri itakamata mifugo au mfugo wowote

Utakaoonekana unazurura hovyo katika eneo la Halmashauri na

utahifadhiwa katika zizi.

2 Mfugo wowote utakaokamatwa utalipiwa faini ya shilingi elfu

kumi (10,000/=) kwa kila siku na gharama nyingine

zitakazojitokeza kama itakavyoamriwa na Halmashauri na baada

ya kulipia hizo gharama atarudishiwa mifugo yake.

3 Endapo mifugo iliyokamatwa haitachukuliwa na mmiliki ndani

ya kipindi cha siku saba (7) tangu kukamatwa kwa mifugo hiyo,

Halmashauri itakuwa na haki ya kuuza kwa mnada mfugo au

mifugo hiyo baada ya kupata idhini ya Mahakama.

4 Halmashauri itatoa tangazo la mnada kwa njia ya vyombo vya

habari au kadri atakavyoona inafaa

5 Baada ya mauzo, Halmashauri itakata fedha za faini, gharama za

mnada na gharama za ulinzi na fedha zitakazobaki atapewa

mwenye mifugo na kama hataonekana ndani ya siku kumi na nne

fedha hizo zitaingizwa katika vyanzo vya mapato vya

Halmashauri.

6 Endapo mwenye mifugo hiyo atakuwa na sababu za msingi za

kutofika kwake katika muda uliopangwa na Halmashauri,

Halmashauri itarudisha fedha zake.

7 Endapo kutatokea kufa kwa mifugo au mfugo kutokana na

sababu yoyote ile, Halmashauri haitawajibika na ulipaji wa

gharama zozote.

Ukaguzi wa

mifugo na bidhaa

za mifugo

11 1 Afisa mwidhiniwa atakuwa na uwezo wa kukataa aina yoyote ya

mifugo au bidhaa kuingia au kuuzwa ndani ya eneo la

Halmashauri iwapo mifugo hiyo au bidhaa hizo zinaweza

kuhatarisha afya au usalama wa mifugo mingine au watumiaji

wengine.

2 Itakuwa halali kwa Afisa Mwidhiniwa wa Halmashauri

atakayeteuliwa kusimamia utekelezaji wa Sheria Ndogo hizi

kuingia katika nyumba au jengo lolote wakati wowote kwa

madhumuni ya kukagua kwa kadri atakavyoona inafaa.

3 Mtu yeyote atakaye wazuia maafisa waidhiniwa kutekeleza

wajibu wao chini ya Sheria Ndogo hizi au Sheria nyingine

yoyote iliyotungwa na Bunge atakuwa ametenda kosa.

6

Taratibu ya

biashara ya

mifugo na mazao

yake

12 1 Mfanyabiashara wa mifugo na mazao ya mifugo anatakiwa kuwa

na leseni ya mifugo, utambulisho na vibali vilivyotolewa na

Mamlaka nyingine za Serikali kabla ya kuanza biashara ya kuuza

na kununua mifugo na mazao ya mifugo na atatakiwa

kuwasilisha vibali vyake kwa Halmashauri kwa ajili ya uhakiki.

2 Mifugo yoyote itakayosafirishwa kutoka mnadani itapelekwa

machinjioni na itatakiwa kuwa na kibali (movement permit) na

inatakiwa kusafirishwa katika vyombo vya usafiri

vinavyokubalika kwa mujibu wa sheria.

3 Mifugo yote inayopelekwa mnadani itatakiwa iwe na barua ya

utambulisho kutoka kwenye mamlaka halali inakotoka mifugo

hiyo.

4 Mifugo yote itauzwa na kununuliwa katika minada na masoko

yanayotambulika kwa mujibu wa Sheria.

5

6.

Mifugo itakayokamatwa ikisafirishwa bila kibali au kuuzwa

sehemu isiyosajiliwa kihalali na mamlaka zinazohusika, mhusika

atalazimika kulipa faini ya shilingi elfu 10,000 kwa kila mfugo

au mnyama.

Minada yote ya Mifugo au Magulio ya Mifugo itafanyika kwa

kibali maalumu cha Halmashauri na kwenye maeneo

yaliyoruhusiwa.

Udhibiti wa

bucha na maduka

ya nyama

13 1 Itakuwa ni wajibu wa kila mfanyabiashara ya nyama au mmiliki

wa bucha au duka la kuuza nyama kuhakikisha kwamba:-

(a) Jengo lake la biashara ya nyama limejengwa kwa mujibu

wa Sheria na lina mwanga wa kutosha, umeme, maji safi

na salama, visu, meza, mzani wa kawaida /mzani wa

kielektroniki, na misumeno maalumu ya kukatia nyama.

(b) Kuna kabati la vioo la kuzuia inzi na wadudu wengine

wataambao na jokofu la kuhifadhia nyama.

(c) Kuna pipa la kuhifadhia taka ngumu na nyepesi

(d) Nyama iwe imekaguliwa na mkaguzi aliyeidhinishwa na

kuwekwa muhuri na inauzwa ndani ya jengo

lililothibitishwa na Sheria za mamlaka husika na sio nje

ama mahali popote pa wazi.

(e) Muuzaji anavaa sare nyeupe muda wote ambazo ni

gunboot, koti na kofia

(f) Muuzaji anapima afya yake na kuwa na cheti na

kuhakikisha anapima afya yake kila baada ya miezi

mitatu (3)

(g) Mmiliki au muuzaji wa nyama anatoa ushirikiano wa

kutosha kwa wakaguzi mara atakapotakiwa kufanya

7

hivyo wakati wowote wa ukaguzi.

2 Mmiliki atatakiwa kuwa na leseni halali, kutambuliwa na

kusajiliwa na Mamlaka nyingine za Serikali kwa mujibu wa

Sheria zilizotungwa na Bunge.

3 Kuhakikisha kuwa biashara ya nyama inafanyika katika bucha na

maduka maalumu (super market) na sio vinginevyo.

Magari ya

Kubeba Nyama

14. 1 Nyama zote zinazotoka machinjioni zitabebwa kwa gari

maalumu (meat van) ambazo zitakuwa zimekaguliwa,

zimesajiliwa na kupewa cheti maalumu cha ukaguzi na gari hizo

zitakaguliwa kila baada ya miezi mitatu (3)

2 Ni marufuku kwa mfanyabiashara yeyote kusafirisha nyama kwa

kutumia pikipiki au baiskeli

3 Itakuwa ni wajibu wa kila mmiliki wa gari la kubeba nyama

kuhakikisha kwamba gari lake:-

(a) Limesajiliwa na Halmashauri

(b) Lina sanduku la aluminium lenye mfuniko na limepakwa

rangi nyeupe, mstari mwekundu na namba.

(c) Halibebi kitu kingine kinachoweza kuleta madhara/athari

kwa afya ya mlaji.

(d) Atalipia gharama za usafirishaji kama zilivyowekwa na

Halmashauri.

Udhibiti wa

uchinjaji

machinjioni

15 1 Watu wote wanaohusika na shughuli za machinjio, watatakiwa

kupima afya kwa mganga au tabibu aliyeteuliwa na watapima

afya kila baada ya miezi 3 katika Hospitali au Vituo vya Afya

vilivyoteuliwa na Serikali kufanya kazi hiyo.

2 Watu wanaohusika na machinjio wanatakiwa kuwa wasafi, na

kuvaa mavazi maalumu kwa ajili ya kazi hiyo.

3 Hairuhusiwi kukaa au kufanya mkusanyiko wa aina yoyote

katika eneo la machinjio ya Halmashauri isipokuwa kwa kibali

maalumu kitakachotolewa na Halmashauri.

4 Machinjio mpya zitaanzishwa kwa kufuata kanuni, taratibu na

sheria zilizowekwa.

5 Uendeshaji wa machinjio utafuata sheria na taratibu zilizowekwa

na Mamlaka husika.

6 Hairuhusiwi kufanya biashara ya aina yoyote katika eneo la

machinjio.

7 Hairuhusiwi kuweka Bucha au duka la nyama ndani ya mita 200

8

kutoka eneo la Machinjio

8 Mfanyabiashara ya nyama anapaswa kuwa na leseni halali ya

biashara

9 Mifugo yote itachinjwa katika machinjio na hakuna kulaza

mifugo katika machinjio isipokuwa kwa idhini maalumu ya

mamlaka husika.

10 Kila mfanyabiashara ya nyama anapaswa kutumia leseni yake ya

biashara ya nyama yeye mwenyewe.

11 Hakuna nyama itakayoruhusiwa kutumika kwa matumizi ya

binadamu bila kufanyiwa ukaguzi wa mwisho (Post-mortem

meat Inspection)

12 Hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kuingiza Mifugo katika

Machinjio ya Manispaa kwa ajili ya kuchinjwa baada ya saa

11:00 jioni isipokuwa kwa kibali maalumu kutoka katika

mamlaka husika.

13 Mifugo yote haitachinjwa bila kufanyiwa ukaguzi wa awali

(Ante mortem inspection)

14 Hairuhusiwi kutoa lugha za kashfa, kuudhi, kudhalilisha au

matusi kwa Mtaalamu au mtu yeyote katika eneo la machinjio

15 Kila mfugaji atatakiwa kupeleka mfugo/mnyama wake

machinjioni au mahali huduma hiyo inapopatikana. Hairuhusiwi

mtu yeyote kuchinjia nyama mahali pengine popote.

Udhibiti ufugaji

mbwa na paka

16 1 Hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kufuga katika eneo la

Halmashauri bila kibali cha ufugaji toka Halmashauri.

2 Kibali cha ufugaji kitatolewa bure na kitadumu kwa mwaka

mmoja tu,

3 Kila mfugaji atawajibika kumpatia chanjo mnyama wake na

atawajibika kulipia ada ya chanjo pale atakavyoelekezwa na

Halmashauri.

4 Mfugaji atalazimika kuonesha cheti cha chanjo ya kichaa cha

mbwa wake kabla ya kupata kibali au kuhuisha kibali kilichoisha

muda wake.

5 Mfugaji atawajibika kumfungia mbwa wake wakati wote wa

mchana na atawafungulia wakati wa usiku kuanzia saa nne na

kuwafungia saa 11 alfajiri.

9

6 Mfugaji atatakiwa kuogesha mnyama wake kila baada ya siku 7

ili kudhibiti magonjwa na wadudu wasumbufu kwa gharama

zake ama kama atakavyoelekezwa na Halmashauri.

7 Mfugaji atalazimika kumfunga mbwa wake kwa mnyororo

maalumu wakati wa kumsafirisha kutoka sehemu moja kwenda

sehemu nyingine kwa mujibu wa Sheria.

Mbwa na paka

wanaozurura

17 Mnyama (mbwa na paka) atakayepatikana anazurura atakamatwa

na kuhifadhiwa katika kizuizi kwa muda usiozidi sikumbili

(masaa 48) na baada ya hapo halmashauri inamtaifisha au

kufanya maamuzi mengine ya kisheria pale itakapoona inafaa.

Makosa 18 1 Mfugaji yeyote atakuwa ametenda kosa iwapo:-

(a) Atashindwa au kukataa kuogesha au kuchanja mifugo

yake ili kuzuia magonjwa au

(b) Atalisha mifugo yake kwenye maeneo yasiyoruhusiwa au

(c) Ataruhusu mifugo yake kuzurura hovyo au

(d) Atakuwa hana utambulisho na kibali cha kufuga au

(e) Atashindwa au atazembea kutoa taarifa juu ya uwepo wa

au dalili za ugonjwa au kifo cha ghafla cha mfugo katika

banda lake au

(f) Atashindwa kutoa ushirikiano wa uwekaji wa alama

kwa mnyama wake au mifugo yake kwa mujibu wa

Sheria Ndogo hizi.

(g) Kumzuia afisa Muidhiniwa kutekeleza majukumu yake

Kufifisha kosa 19 Mkurugenzi atakuwa na uwezo wa kufifilisha kosa kwa kumtoza

faini mtu yeyote aliyetenda kosa kwa mujibu wa Sheria Ndogo

hizi, kiasi kisichopungua shilingi Laki Mbili (200,000) na

kisichozidi laki tano (500,000) iwapo mkosaji atakiri kosa kwa

hiari na kuwa tayari kujaza fomu maalumu iliyoambatanishwa

kwenye jedwali la tatu la Sheria Ndogo hizi.

Adhabu 20 Mtu yeyote atakayekwenda kinyume na masharti ya Sheria

Ndogo hizi atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia

atatozwa faini ya kiasi kisichopungua shilingi laki

mbili(200,000) au kisichozidi Milioni moja (1,000,000) au

kifungo kisichopungua miezi kumi na miwili (12) au kisichozidi

miezi ishirini na nne (24) jela au adhabu zote mbili kwa pamoja.

10

JEDWALI LA KWANZA

KIBALI CHA KUFUGA WANYAMA

(Chini ya kifungu 6 (1))

Jina:…………………………………………….

Anuani:…………………………………………

Ameruhusiwa kufugwa wanyama wafuatao katika eneo la………………………..

Na Aina ya mnyama Idadi

1 Ng’ombe

2 Mbuzi

3 Kondoo

4 Nguruwe

5 Ngamia

6 Punda

7 Paka

8 Farasi

9 Sungura

10 Mbwa

11 Kuku /Bata

12 Wanyama wengine (wataje)

Kibali hiki kitakuwa kwa muda wa miezi kumi na mbili (12) kuanzia tarehe………………..hadi

tarehe…………..

Kimetolewa na :

Jina la Afisa Mwidhiniwa:……………………………………….

Tarehe:………………………………….

Muhuri:

11

JEDWALI LA PILI

KIBALI CHA KUSAFIRISHA WANYAMA

(Chini ya kifungu cha 8(1))

Jina:…………………………………………….

Anuani:…………………………………………

Ameruhusiwa kusafirisha wanyama wafuatao kutoka ………………………kupitia njia

za…………… ………………………………………..hadi……………………..…..

Na Aina ya mnyama Idadi

1 Ng’ombe

2 Mbuzi

3 Kondoo

4 Nguruwe

5 Ngamia

6 Punda

7 Paka

8 Farasi

9 Sungura

10 Mbwa

11 Kuku /Bata

12 Wanyama wengine (wataje)

Kibali hiki kitakuwa cha muda wa siku………….. kuanzia tarehe………………..hadi

tarehe…………..

Barua toka kwa Afisa Mtendaji wa Mtaa/Afisa Mifugo Mtaa/Kata inayothibitisha uhalali wa

kumiliki mifugo /wanyama hao imeambatanishwa.

Kimetolewa na :

Jina la Afisa Mwidhiniwa:……………………………………….

Tarehe:………………………………….

Muhuli:

12

JEDWALI LA TATU

HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA

(SHERIA NDOGO ZA WANYAMA MWAKA 2018)

KIBALI CHA JUMLA CHA KUSAFIRISHA WANYAMA

Jina:…………………………………………….

Anuani:…………………………………………

Ameruhusiwa kusafirisha wanyama wafuatao

Na Aina ya mnyama Idadi

1 Ng’ombe

2 Mbuzi

3 Kondoo

4 Nguruwe

5 Punda

Kutoka …………………………kwenda………..………………..kupitia………………………..

Kwa muda wote wa masaa ya mchana kwa kipindi cha kuanzia ………………..hadi…………….

Namba ya gari…………………………….Namba ya trela………………………..

Kibali hiki kitakuwa cha muda wa siku………….. kuanzia tarehe………………..hadi

tarehe…………..

Barua toka kwa Afisa Mtendaji wa Mtaa/Afisa Mifugo Mtaa/Kata inayothibitisha uhalali wa

kumiliki mifugo /wanyama hao imeambatanishwa. Aidha, kibali cha kusafirisha mifugo

Na……………….kimeambatishwa

Kimetolewa na :

Jina la Afisa Mwidhiniwa:……………………………………….

Tarehe:………………………………….

Muhuli:

13

JEDWALI LA NNE

IDADI YA WANYAMA WANAOTAKIWA KUFUGWA

KATIKA ENEO LA HALMASHAURI

(Chini ya kifungu 6 (1))

Na Aina ya mnyama Idadi

1 Ng’ombe 4

2 Mbuzi 4

3 Kondoo 4

4 Nguruwe Kundi moja (flock)

5 Ngamia 4

6 Punda 4

7 Paka 4

8 Farasi 4

9 Sungura Kundi moja (flock)

10 Mbwa 4

11 Kuku /Bata Kundi moja (flock)

12 Wanyama wengine (wataje) Kulingana na aina ya wanyama husika

14

HATI YA KUFIFISHA KOSA

(Limetungwa kwa chini ya kifungu cha 16)

Mimi ……………………………………..nakiri kwa hiari yangu mwenyewe mbele ya

……………………………….……ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala

kwamba mnamo tarehe ……….ya Mwezi………..Mwaka…………nilitenda kosa la kukiuka

masharti ya Sheria Ndogo hizi za Udhibiti na Usimamizi wa Mifugo za Halmashauri ya

Manispaa ya Ilala za mwaka 2018.

Kwa mamlaka aliyopewa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa niko tayari kulipa kiasi cha

shilingi,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,kama faini ninayodaiwa.

NATHIBITISHA KWAMBA MAELEZO HAPO JUU NI YA KWELI NA NIMEYATOA

KWA HIARI YANGU KADRI YA UFAHAMU WANGU

Leo tarehe………………..ya Mwezi…………….Mwaka………….

Jina:………………………………….

Saini:………………………………

Mbele ya:………………………………..

Cheo:……………………………………

Saini:……………………………………

Tarehe:………………………………….

15

Nembo ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala imebandikwa kwenye Sheria Ndogo hizi kufuatia

Azimio lililopitishwa kwenye mkutano wa Halmashauri ulioitishwa na kufanyika

Tarehe………………Mwezi……………..2018 mbele ya:-

…………………………..

JUMANNE K. SHAURI

MKURUGENZI WA MANISPAA

HALMASHAURI YA MANISPAA ILALA

…………………………..

CHARLES KUYEKO

MSTAHIKI MEYA

HALMASHAURI YA MANISPAA ILALA

NAKUBALI,

…………………………..

Mhe. SULEIMAN JAFO (MB)

WAZIRI WA NCHI – OR-TAMISEMI

DODOMA

Tarehe……………………..