Upload
robert-okanda
View
106
Download
0
Embed Size (px)
DESCRIPTION
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
Citation preview
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
KUSOGEZWA MBELE KWA TAREHE YA MWISHO YA KUPOKEA MAOMBI YA MIKOPO
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kuwafahamisha Waombaji wa mikopo na Umma kwa ujumla kuwa muda wa kuwasilisha maombi ya mikopo umeongezwa mbele hadi tarehe 31 Julai, 2015.
Hatua hii imechukuliwa ili kuwapa fursa wale ambao kwa sababu mbalimbali hawakuweza kufanya maombi ya mikopo katika muda uliopangwa. Itakumbukwa kuwa, awali Bodi ilianza kupokea maombi kwa njia ya mtandao tarehe 4 Mei, 2015 na mwisho wa kuwasilisha maombi ulipangwa kuwa tarehe 30 Juni, 2015.
Kupitia tangazo hili, waombaji wa mikopo kwa mwaka wa masomo 2015/2016 ambao hawajakamilisha maombi yao wanatakiwa kukamilisha na kuwasilisha maombi yao ya mikopo ndani ya muda ulioongezwa. Bodi inapenda kusisitiza kuwa hakutakuwa na muda mwingine wa nyongeza baada ya tarehe 31 Julai, 2015.IMETOLEWA NA:MKURUGENZI MTENDAJI
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
PAGE
_1289030680.pdf