Transcript
Page 1: BARUA YA SIRI KWA DR MOHAMED SHEIN TOKA AHELA

1

BARUA YA SIRI KWA DR MOHAMED SHEIN KUTOKA AHELA

Na Prof (Dkt) Handley Mpoki Mafwenga

Ph.D (finance -COU), MSc (finance -Strathclyde), MBA (Mg.Eco -ESAMI/MsM), LLM (taxation- UDSM), LLB (Tudarco), PGD tax mgt (IFM), AD tax mgt (IFM)]

Ilikuwa usiku wa tarehe 05 Julai Mwaka, 2010 majira ya saa tisa alfajiri nilipotokewa

kwenye ndoto na Waasisi wa Chama cha Mapinduzi Mwal Nyerere, Mzee Abeid Karume na

Mzee Thabiti Kombo, nilipokabidhiwa barua ifuatayo;

Dr Shein; ukumbuke kuwa una kazi kubwa sana ya kukabiliana na siasa za vijembe za

huko Zanzibar. Miaka mingi sasa toka umechukua uongozi kwa Dr Omar Ali Juma

umekuwa Mpole, Mkimya, Msikivu, na mwenye Hekima kubwa; Wewe ni binadamu wa

namna gani? Hata ulimi kujikwaa kidogo kisha ukasamehewa kama binadamu wengine

walivyo? Je wewe ni mithili ya Malaika?

Sisi tulifanya makosa kidogo kuondoa kofia ya Makamu wa Kwanza na wa Pili wa Rais,

tukidhani tunaboresha Muungano. Lakini tumejikuta tafsiri ya Watanzania kuhusu

Zanzibar iko tofauti sana, Zanzibar inafananishwa na Mkoa. Tumefurahi sana kumsikia

Mheshimiwa Spika wa Bunge la Jamhuri akirekebisha mawasilisho ya maelezo kuwa

Zanzibar isijumuishwe na Mikoa ni vyema basi katika maelezo mseme “na huko Zanzibar”

baada ya kutaja Mikoa. Inaonyesha kuwa kugombea kwako uongozi na kuacha nafasi ya

Makamu wa Rais ni kielelezo kuwa Zanzibar ina uthamani wa tofauti ndani ya Utaifa wa

Tanzania.

Dr Shein, Zanzibar inaitwa kikatiba “Tanzania Zanzibar” hivyo bila Tanzania ukweli

Zanzibar haipo. Utaapishwa utakaposhinda chini ya Ibara ya 103(2) ya Katiba ya

Jamhuri ya Muungano na Jaji Mkuu wa Zanzibar kulinda na kutetea Katiba ya Jamhuri

na kiapo kingine chochote chini ya Katiba ya Zanzibar katika kutekeleza majukumu yako.

Kuna kitu kinatusumbua sana. Imekuwaje leo mnaleta kauli za “Kero za Muungano”

tunaomba kuanzia sasa mseme “Changamoto za Muungano”hili ndilo neno tulilowaachia.

Muungano ni dhana ya upendo, mshikamano, na uvumilivu, ndani ya vitu hivyo vitatu

hakuna Kero; Mwambia Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda na Waziri Kiongozi

Vuai Nahodha waepuke neno hilo”Please”.

Page 2: BARUA YA SIRI KWA DR MOHAMED SHEIN TOKA AHELA

2

Hata hizo ziitwazo kero za Muungano ni maombi yanayowasilishwa na upande Mmoja

yaani Zanzibar katika aidha kuubomoa au kuuimarisha Muungano; mengi hayajajitokeza

kurekebisha Nyongeza ya 1 ya Ibara ya 4 ya Katiba inayoelezea Mambo ya Muungano.

Uwaeleze mambo ya Muungano ni haya hapa; 1) Katiba ya Tanzania na Serikali ya

Jamhuri ya Muungano 2) Mambo ya Nchi za Nje 3) Ulinzi na Usalama 4) Polisi 5)

Mamlaka juu ya mambo yanayohusika na hali ya Hatari 6) Uraia 7) Uhamiaji 8) Mikopo na

Biashara za Nchi za Nje 9) Utumishi katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano 10) Kodi ya

mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, Ushuru wa Forodha, na Ushuru wa

Bidhaa zinazotengenezwa nchini Tanzania unaosimamiwa na Idara ya Forodha 11)

Bandari, mambo yanayohusika na Usafiri wa Anga, posta na simu 12) Mambo yote

yanayohusika na sarafu na fedha kwa ajili ya malipo yote halali (pamoja na noti); mabenki,

(pamoja na mabenki ya kuweka akiba) na shughuli zote za mabenki; fedha za kigeni na

usimamizi juu ya mambo yanayohusika na fedha za kigeni 13) Leseni ya viwanda na

takwimu 14) Elimu ya Juu 15) Maliasili ya mafuta, pamoja na mafuta yasiyochujwa ya

motokaa na mafuta ain ya petrol na aina nyinginezo za mafuta au bidhaa, na gesi asilia 16)

Baraza la Taifa la Mitihani la Tanzania na mambo yote yanayohusika na kazi za Baraza

hilo 17) Usafiri na Usafirishaji wa Anga 18) Utafiti 19) Utafiti wa Hali ya Hewa 20)

Takwimu 21) Mahakama ya Rufani ya Jamhuri ya Muungano na 22) Uandikishaji wa

vyama vya siasa na mambo mengine yanayohusiana navyo

Ili mambo yaweze kutekelezeka pale Zanzibar inabidi Baraza la Wawakilishi liridhie

Sheria inayotakiwa kutekelezeka hadi Zanzibar lakini ni mambo machache yanayoridhiwa

kuna nini hapo? Aidha, kwa mfano kodi zote zilizo chini ya Jamhuri ya Muungano inafaa

ziletwe kwenye mahakama za kodi (TRAT na TRAB) lakini hakuna kesi hata moja

iliyoletwa kwenye mahakama hizo angalau basi Mahakama hizo zingekasimu usikilizaji wa

kesi pale Zanzibar.

Ubinafsi, Chuki na Siasa zilizopitwa na wakati usiwe kimya yashughulikie pindi ukiwa

Rais; Kuna hili swala la “Muafaka”. kumbuka swala zima la “Utawala wa Sheria” na

maneno ya Engels kuwa” Power which is termed as State; arose from the society, but places

itself above it and alienates itself more and more from it. What does this power mainly

consist of? It consist of special bodies of armed men which have prisons etc. at their

command; public power which is attribute of every state does not coincide with the armed

population with its acting armed organization.‟ Engles alijaribu sana kuelezea nguvu ya

Umma “Public power” akisisitiza kuwa hiyo ndiyo muhimu zaidi kwani nguvu zozote za

kijeshi hazina mafanikio bila nguvu ya Umma ndani ya Utawala wa Sheria. Tunakuasa

Nguvu ya Umma ya Watanzania ni muhimu sana na haijengwi kutoka kwenye vyama ila

vyama hujengwa kutoka kwao; epuka neno muafaka linaloanzia kwenye vyama vya siasa

huo siyo msingi wa Utawala wa Sheria.

Maana ya kwanza ya Utawala wa Sheria ilitolewa kwenye Sheria ya Athens ya 1955; ya

pili kutoka kwenye „Delaration ya Delhi Mwaka 1959; na 1961 kwenye Sheria ya Lagos

ambayo ilijaribu kuleta maana ya Kiafrika; aidha, Tume ya Wanasheria ya Geneva Mwaka

Page 3: BARUA YA SIRI KWA DR MOHAMED SHEIN TOKA AHELA

3

1961; Utawala ni kuhakikisha Wanasheria wanawajibika katika kulinda na kukuza haki

za mtu za kiraia na kisiasa, kijamii, kuchumi, kielimu na kimila katika hali ya utu, uhuru

na kiitikadi bila kuingiliwa na Dola. Palipo na Muafaka ni dalili kuwa Utawala wa Sheria

una walakini na unaingiliwa zaidi na vyama vya siasa au Dola.

Kuna hili la mihimili mitatu ya dola; yaani Bunge, Mahakama, na Serikali. Imetokea

wabunge wanaiagiza Serikali badala ya kushauri ingawa Ibara ya 45 (2) Bunge laweza

kuweka utaratibu utakaofuatwa na Rais katika kutekeleza majukumu yake; Bunge

linaweza kupitisha Azimio la kumuonda Rais (Vote of No Confidence), madarakani endapo

itatolewa hoja ya Bunge kumshitaki Rais chini ya Sheria Na 20 ya Mwaka 1992 Ibara ya 8

na Sheria Na 12 ya Mwaka 1985 Ibara ya 4. Aidha, Bunge linaweza kupitisha hoja ya

kuunda Kamati ya Uchunguzi na ikiwa hivyo Rais atahesabika kuwa hayupo kazini ndani

ya siku saba na Bunge litampa Rais nafasi ya kujieleza na Kamati itatoa taarifa kwa Spika

ndani ya siku tisini n.k. Lakini ikumbukwe kwamba kwenye Ibara ya 63 (2) ya Katiba ya

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikisomwa pamoja na Sheria Na 15 ya Mwaka 1984

Ibara ya 12 Bunge lina wajibu kwa niaba ya Wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali

ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa Majukumu yake

kwa mujibu wa Katiba. Sasa hili la kuiagiza Serikali liko wapi ndani ya Katiba?

Hii imesababisha pia vyama vya siasa kukosa mwelekeo na nafasi ya utambuzi katika

Nchi, hasa kwa chama Tawala na ndiyo maana hivi karibuni kulitokea wabunge kutumia

Bunge kujibu hoja za maelekezo ya Halmashauri Kuu (NEC). Halmashauri Kuu ni

Chombo cha kuheshimika katika chama ndiyo maana Makamu wa Pili wa Rais Hayati

Rashid Kawawa October, 1968 alibainisha kuwa TANU na ASP ni vyama shika hatamu

lakini wabunge walipinga. Alisisitiza kuwa NEC ina uwezo wa kufukuza watu kwenye

chama; katika kikao cha NEC wabunge wawili Ndugu Oscar Kambona na Ndugu

Anangisye walifukuzwa kwa sababu ya kukiuka maadili, na misingi ya chama. Hii ni kwa

vile vifungu Na 27,30,32 na 33 vya Katiba ya Mpito vilibainisha kuwa Mwananchi yeyote

ili awe mbunge lazima awe mwanachama wa chama cha siasa; hivyo kufukuzwa kwao moja

kwa moja kunapoteza nafasi yao ya ubunge. Hii ipo pia katika Ibara ya 67(1) ukisoma

pamoja na Sheria Na 15 ya Mwaka 1984 Ibara ya 13. Katika hili tunaomba

muwakumbushe wabunge nafasi ya vyama vya siasa katika nchi. Hadhi ya chama isiwe

wakati wa mchakato wa kupata ubunge na urais bali wakati wote katika kulida heshima,

utu, na haki ya watanzania.

Kumbuka maneno ya Patrice Lumumba tarehe 30 Juni, 1960 alisema “We are going to re-

examine all former laws and make new ones which will be just and noble. We are going to

put an end to suppression of free thought and make it possible for all citizens fully to enjoy

the fundamental liberties set down in the declaration of the rights of man” Kama wabunge

wanataka kuagiza Serikali warundi kubadili Sheria zilizopo ku-enzi hata maneno ya

Lumumba. Tunajua wewe ni Muislamu lakini ebu Fungua Samwel 23(1)(b) neno linasema

“Atawalaye wanadamu kwa haki akitawala katika hicho cha Mungu, atakuwa kama nuru

ya asubuhi jua lichapo, asubuhi isiyo na mawingu” .

Page 4: BARUA YA SIRI KWA DR MOHAMED SHEIN TOKA AHELA

4

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika