Kijitabu hiki kimetayarishwa na watendaji wa Twaweza Tanzania.
Waandishi: Abella Bateyunga na Evarist KamwagaMchoraji: Marco TibasimaMhariri: Rakesh Rajani
©Hivos/Twaweza 2011
SLP 38342, Dar es Salaam, TanzaniaSimu: +255 22 266 4301Faksi: +255 22 266 4308Barua pepe: [email protected]: www.twaweza.org
Unaruhusiwa kunakili sehemu yeyote ya kijitabu hiki kwa sababu zisizo za kibiashara tu. Unachotakiwa kufanya ni kunakili chanzo cha sehemu uliyonakilia na kutuma nakala mbili kwa Twaweza.
Utangulizi
Ndugu msomaji:
Wengi wetu tunaamini ‘elimu ni ufunguo wa maisha’. Serikali yetu vilevile
inatambua hivyo na ndio maana imeweka juhudi kubwa ka�ka elimu.
Madarasa mengi yamejengwa, uandikishwaji wa watoto umepanda, na walimu
lukuki wameajiriwa. Zaidi ya haya Tanzania iko mstari wa mbele ka�ka
kuyafikia malengo ya maendeleo ya milenia (MDGs), ka�ka hili tumepata tuzo
za kimataifa kwa kuvuka malengo ka�ka uandikishaji watoto mashuleni
(asilimia 95).
Mafanikio haya ni makubwa na Serikali inastahili kupewa pongezi.
Lakini, hebu tujiulize, ji�hada hizi zimezaa matunda gani? Tutumie kipimo kipi
kujua kama watoto wetu wameelimika?
Lengo la elimu ni kuleta mabadiliko ya maisha. Mwalimu Julius Nyerere ka�ka
Elimu ya Kujitegemea alituhimiza kwamba “Elimu inayotolewa ni lazima ijenge
mambo matatu kwa kila mwananchi; akili ya kuuliza, uwezo wa kujifunza na
uwezo wa kujiamini”. Ka�ka haya yote mkazo upo ka�ka ‘ubora’ na si
vinginevyo, yaani kumjengea mtoto maarifa ka�ka kusoma, kufanya
mahesabu, uwezo wa kudadisi, kufikiri, kusikiliza, kuuliza maswali,
kupambanua na kuwasiliana kwa kujiamini.
Ndiyo maana matokeo ya utafi� uliofanywa hivi karibuni na Uwezo yana�sha.
Utafi� umeibua matokeo tofau� na wengi wanavyotazamia elimu ya nchi yetu.
Imegundulika kuwa watoto wengi wapo madarasani lakini hawajifunzi. Kwa
mfano, watoto 9 ka� ya 10 wa darasa la tatu hawawezi kusoma Kiingereza cha
darasa la pili, 8 ka� ya 10 hawawezi kufanya Hisaba�, na 7 ka� ya 10
wanashindwa kusoma Kiswahili ipasavyo.
i
Tafakari kwa hali kama hii, miaka kumi ijayo tutakuwa na taifa la namna gani?
Kizazi hiki kipya cha waka� huo kitafanya nini? Hali hii inafanana na nyumba
iliyopambwa lakini yenye msingi mbovu, matokeo yake ni nyufa
zitakazopelekea anguko lake.
Lakini tusikate tamaa. Kuna mengi ya kufanya. Kila mmoja ana uwezo wa
kuleta mabadiliko. Unaposoma kijitabu hiki usikae kimya, shirikisha wenzio,
jadili na chukua hatua ka�ka eneo lako. Ongea na watoto na vijana, wasaidie
na kuwafariji. Wasiliana na viongozi kujadili jinsi ya kuboresha elimu. Andika
barua kwa mamlaka au kwenye vyombo vya habari kuwasilisha maoni yako.
Pamoja Twaweza! Ni sisi!
Rakesh RajaniMkuu, Twaweza
ii
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27