143
Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved. HUDUMA YA KUWAIMARISHA VIONGOZI WA KANISA AFRIKA MASHARIKI THEOLOJIA YA KI-BIBLIA na Jonathan M. Menn B.A., University of Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical Divinity School, 2007 Equipping Church Leaders-East Africa 3701 N. Gillett St., Appleton, WI 54914 (920) 731-5523 [email protected] www.eclea.net December 2009; revised February 2015. Theolojia ya Ki-Biblia ni mkondo wa maelezo ya Biblia, kuanzia uumbaji wa nchi na mwanadamu katika Mwanzo, kupitia anguko la mwanadamu na matokeo yake, na historia ya ukombozi wa Mungu kwa mwanadamu, hata utimilifu wa mbingu mpya na nchi mpya katika Ufunuo. Biblia inaeleza ksimulizi inayofungamana, huku Yesu Kristo akiwa ndiye moyo wake. Theolojia ya Ki-Biblia huangalia dhana kuu ambazo zinazopitia katika Biblia nzima, zinazolenga juu ya uhusiano wa Mungu na mwanadamu. Pia huonyesha jinsi Kristo na kanisa ndio utimilizo wa maagano, ahadi, unabii, na taasisi zilizoanzishwa katika Agano la Kale. Ramani za nyakati, na Dibaji zimeambatanishwa kama nyenzo za kusaidia.

THEOLOJIA YA KI-BIBLIA - ECLEA.netMungu. ” (). ). ()

  • Upload
    others

  • View
    132

  • Download
    36

Embed Size (px)

Citation preview

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    HUDUMA YA KUWAIMARISHA VIONGOZI WA KANISA

    AFRIKA MASHARIKI

    THEOLOJIA YA KI-BIBLIA

    na

    Jonathan M. Menn

    B.A., University of Wisconsin-Madison, 1974

    J.D., Cornell Law School, 1977

    M.Div., Trinity Evangelical Divinity School, 2007

    Equipping Church Leaders-East Africa

    3701 N. Gillett St., Appleton, WI 54914

    (920) 731-5523

    [email protected]

    www.eclea.net

    December 2009; revised February 2015.

    Theolojia ya Ki-Biblia ni mkondo wa maelezo ya Biblia, kuanzia uumbaji wa nchi na mwanadamu katika Mwanzo, kupitia

    anguko la mwanadamu na matokeo yake, na historia ya ukombozi wa Mungu kwa mwanadamu, hata utimilifu wa mbingu

    mpya na nchi mpya katika Ufunuo. Biblia inaeleza ksimulizi inayofungamana, huku Yesu Kristo akiwa ndiye moyo wake.

    Theolojia ya Ki-Biblia huangalia dhana kuu ambazo zinazopitia katika Biblia nzima, zinazolenga juu ya uhusiano wa

    Mungu na mwanadamu. Pia huonyesha jinsi Kristo na kanisa ndio utimilizo wa maagano, ahadi, unabii, na taasisi

    zilizoanzishwa katika Agano la Kale. Ramani za nyakati, na Dibaji zimeambatanishwa kama nyenzo za kusaidia.

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    1

    ORODHA YA YALIYOMO

    THEOLOJIA YA KI-BIBLIA: UTANGULIZI…………………………………………………………..........................4

    I. Tabia ya Theolojia ya Ki-Biblia...…………………………………………………………………….............................4

    A. Maelezo ya Theolojia ya Ki-Biblia……………………………………………………………..….....…………………..4

    B. Fikira za Theolojia yaKi-Biblia...………………………………………………………………...….…………………...4

    II. Mtazamo wa Mkondo wa Simulizi na Dhana za Theolojia ya Ki-Biblia….……………………................................5

    A. Msingi wa mkondo wa simulizi za Biblia..…………………………………………………………...…………………..5

    B. Dhana za Theolojia ya Ki-Biblia.…..………………………………………………………………..…………………...5

    MSINGI WA SIMULIZI YA MKONDO WA BIBLIA ………………………………………….…................................6

    I. Uumbaji (Mwanzo 1-2)………………………………………………………...................................................................6

    A. Simulizi ya mkondo wa Biblia huanzia na Mungu (Mwa 1:1) ………………………………………............................7

    B. Mungu aliumba kila kitu bila kutumia chochote.…………………..………………………………...............................7

    C. Mungu alimuumba mwanadamu ili atawale viumbe vingine vyote (Mwa 1:26-28) …………………………………..7

    II. Anguko la Mwanadamu Katika Dhambi na Matokeo Yake (Mwanzo 3-11:26)……………….…………………....8

    A. Ukuu wa Mungu, wajibu wa mwanadamu, na kuwepo kwa dhambi..…………………………….................................8

    B. Adamu na Hawa watenda dhambi na kufukuzwa kutoka bustani ya Edeni (Mwanzo 3) …………………………....14

    C. Matokeo ya Anguko—kutoka kwa Kaini hadi Mnara wa Babeli (Mwanzo 4-11:26)…………….…………………...16

    III. Tukio la Ukombozi—Mungu aita Watu Kwa Ajili Yake Mwenyewe (Mwa 11:27-Ufunuo 20)………………….19

    A. Mwanzo mpya wa Mungu—Kutoka Ibrahimu hadi Yusufu (Mwa 11:27-50:26)……………………………………..19

    B. Kuanza kwa taifa la Israeli—Kutoka Misri kwenda nchi ya ahadi (Kutoka-Kumbu-kumbu)…..................................21

    C. Israeli ndani ya hiyo nchi (Yoshua-1 Samueli 7)…………………………………………………….............................23

    D. Israeli kama ufalme ulioungana (1 Samueli 8-1 Wafalme 11; 1 Nyakati 1-2 Nyakati 9;

    Zaburi-Wimbo ulio bora)……………………………………………………………………………………….....23

    E. Israeli kama ufalme uliogawanyika (1 Wafalme 12-2 Wafalme 17; 2 Nyakati 10-31; Isaya na Mika

    [utabiri kwa Israeli na Yuda]; Yoeli [utabiri kwa Yuda]; Hosea na Amosi

    [utabiri kwa Israeli]; Obadia [utabiri kwa Edomu]; Yona [utabiri kwa Ninawi])………….…………………..24

    F. Kuwepo, kushuka, na kuanguka, kwa ufalme wa Kusini (2 Wafalme 18-25; 2 Nyak 32-36:21;

    Isaya-Danieli; Nahumu-Zefania)………………………………………………………………………….……..24

    G. Kurejeshwa kwa ufalme wa Kusini (2 Nyak 36:22-Esta; Hagai-Malaki)…………………………………….…….....26

    H. Kutimizwa kwa mpango wa Mungu wa ukombozi katika Yesu Kristo (Mathayo-Ufunuo 20)……………………….27

    I. Ufunuo wa Yesu wa Masihi wa kweli, ufalme wa Mungu, na kanisa……………………………..……………….......28

    IV. Mbingu Mpya na Nchi Mpya (Ufunuo 21-22)…………………………………………..……………………….…..30

    A. Uumbaji mpya wa Ufunuo unaendana na uumbaji wa awali wa Mwanzo…………………………………………...30

    B. Uumbaji mpya wa Ufunuo unapita uumbaji wa awali wa Mwanzo …………………………………………………..30

    DHANA MBILI ZA KI-BIBLIA KUHUSU UHUSIANO WA MUNGU NA MWANADAMU.…………………......31

    I. Hekalu na Nchi: Maskani ya Mungu na Mwanadamu…………………………………………………………….....31

    A. Bustani ya Edeni (Mwanzo 2-3; ona pia Ezek 28:13-16)………………………………….………………………......31

    B. Hema ya kukutania (Kutoka 25-31, 35-40)……………………………………………………………...……………..32

    C. Hekalu (2 Sam 7:1-17; 1 Waf 6; 8:1-11; 1 Nyak 17:1-15; 22:1-16; 28:1-29:9; 2 Nyak 3-5)……..............................34

    D. Maono ya Ezekiel ya Hekalu Jipya (Ezekieli 40-48)…………… …………………………………………………….35

    E. Mbingu Mpya na Nchi Mpya (Ufunuo 21-22)…………………………………………………………........................40

    II. Uhusiano wa Mungu na Watu Wake Kuhusu Ndoa…………………………………………………………….......43

    A. Mwa 2:23-24 (mwanamke kuumbwa rasmi kwa ajili ya mwanaume; mwanaume kuwaacha babaye na

    mamaye na kuunganishwa na mkewe na kuwa “mwili moja” naye) ni mfano unaoelezea uhusiano

    ambao Mungu anautaka kwa watu.…………………………..……………………………………………….....43

    B. Katika AK kiungo cha ndoa kati ya Mungu na watu wake kiliwekwa, lakini Israeli hakuwa mwaminifu.………....43

    C. Katika AJ muktadha wa kindoa umetanuka na kufanyika rasmi kati ya Kristo na kanisa ………………………....45

    D. Katika Ufunuo, picha ya Ki-Biblia kuhusu uhusiano wa kindoa kati ya Mungu na watu wake huja

    kutimilika katika Kristo, bibi arusi (kanisa), na Nchi Mpya……………………………………………………46

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    2

    KRISTO NA KANISA KAMA UTIMILIZO WA AK……………….……….………………………………………...47

    I. Biblia Kimsingi ni Kumhusu Yesu Kristo—Yeye Ndiye Mtu Aliye Kiungo na Dhana Iunganishayo Yote.…......47

    A. Zinapotazamwa peke yao, simulizi za AK na nabii zake hazimtaji moja kwa moja Yesu Kristo, bali huwa na

    Nguzo ya kusimamia, na hutumia lugha zinazolenga, na kumwelekea mlengwa wa kuibukia taifa la

    Israeli.………………………………………………………………………………………………………….....48

    B. Yesu na waandishi wa AJ wote walitumia AK kumhusu Yesu na kwa Injili..…………………………………….....48

    II. Agano la Ibrahimu, la Daudi, na Jipya Yalielekea Kwake na Kutimilizwa Katika Kristo na Kanisa.………….49

    A. Agano la Ibrahimu limetimizwa katika Kristo na Kanisa…………………….………………..…………….………..50

    B. Agano la Daudi limetimizwa katika Kristo na Kanisa…………………………………..…….…………………….....53

    C. Agano Jipya limetimizwa katika Kristo na Kanisa………………………………………….…………………………57

    III. Yesu Ndiye Israeli Mpya, wa Kweli, na Mwaminifu.……………………………………………………………....60

    A. Yesu ageuza historia ya Israeli…………………………………………………………………………………………60

    B. AJ lamwonyesha Yesu kama Musa mpya, aliye mkuu zaidi, awakomboaye watu siyo tu kutokana na

    vifungo vya kimwili, bali kutoka utumwa wa kiroho, dhambi na mauti (Yohana 1:29; Rumi 6:3-23)……....61

    C. AJ hutumia lugha na majina ya Israeli ya AK kwa Yesu………………………….………………………………...62

    D. Katika Yesu ahadi za AK za marejesho kwa Israeli zatimizwa…………………………………………………….....62

    IV. Kwa vile Kanisa liko “Katika Kristo,” Kanisa ndilo Israeli Mpya, wa Kweli na wa Kiroho.………………......68

    A. Israeli ya AK na kanisa: neema za kimwili na za kiroho, kuchaguliwa, na imani katika AK………………………68

    B. Uhusiano kati ya Israeli ya AK na kanisa …………………………………………………………………………….70

    C. Yesu alilikataa taifa la Israeli kama chombo cha kujengea ufalme wa Mungu, na kuwapa jukumu hilo

    wafuasi wake mwenyewe, kanisa .……………………….………………………………….…………………..71

    D. Kanisa ndio watu wapya, wa kweli, wa Mungu—Israeli wa kiroho………………………………………..………...74

    E. Kama Israeli mpya, wa kweli na wa kiroho, kanisa linakabiliwa na mitihani ile ile ya uaminifu ambayo

    Israeli ya AK ya kimwili ilikumbana nayo…………………………………………….………..………………78

    V. Kristo na Kanisa Watimiliza na Kuchukua Nafasi na Hekalu……………………………………………………..78

    A. Yesu ndiye hekalu la kweli ………………………………………………………………………………………….…78

    B. Kama mwawakilishi wa Kristo aonekanaye kwa macho hapa duniani, kanisa ni “Helaku” la Mungu duniani......83

    VI. Yesu Alitimiliza na Kubadilisha Sikukuu za Kiyahudi.……………………………………………………………86

    A. Kalenda ya Israeli ya AK……………………………………………………………………………………….………86

    B. Mifumo ya AK ya Israeli ya Sikukuu.…………………………………………………………………………..……...87

    C. Yesu alitimiza Pasaka na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu..……………………………………………………88

    D. Yesu alitimiza Sikukuu ya Malimbuko na ya Majuma..………………………………………………………………89

    E. Yesu alitimiza Sikukuu ya Mabaragumu.…………………………………………………….………………………. 90

    F. Yesu alitimiza Siku ya Utakaso……………………..…………………………………………………………………..91

    G. Yesu alitimiza Sikukuu ya Vibanda……………………………………………......…………………………………..92

    H. Yesu alitimiza Mwaka wa Yubile………………………………………………………………………………….…....94

    VII. Yesu Alitimiza na Kuchukua Nafasi ya Israeli ya Mfumo Mzima wa AK wa Utoaji Dhabihu

    na Ukuhani……………………………………………………………………………………………………….95

    A. Mifumo ya AK ya Israeli ya utoaji dhabihu…………………………………………………………………………....95

    B. Yesu alitimiza mfumo mzima wa utoaji dhabihu wa Israeli wa AK ………………………….………………………96

    C. Yesu alitimiza na kusimamisha ukuhani mzima wa AK………………………………………………..……………..96

    D. Waebrania hutofautisha mfumo mzima wa desturi za dhabihu, na ukuhani wa Israeli na Kristo………………….97

    VIII. Yesu Alitimiza na Kuibadilisha Sheria ya AK.……………………………………………………………………98

    A. Sheria ya AK ilikuwa sehemu ya Agano la Musa (la Kale)……………………………………………………............98

    B. Sheria ya AK ilikuwa ni mfano tu………………………………………………………………………………………98

    C. Sheria ya AK ilikuwa ya kitambo ………………………………………………….………..........................................99

    D. Yesu alikuja kuitimiliza sheria…………………………………………………………………………………….......100

    E. Yesu alionyesha na kuthibitisha mamlaka yake juu ya sheria yote ya AK ……………………………….................101

    F. Yesu alisshi chini ya Agano la Kale, bali alikuwa mjumbe wa Agano Jipya…………………………………..….....101

    G. Wakristo hawafungwi na Agano la Musa wala sheria yoyote ya AK, bali wako chini ya “Sheria ya Kristo”……..102

    IX. Yesu Aliitimiza na Kuibadilisha Sabato ya AK…………………………………………………………………….103

    A. Yesu alionyesha na kuthibitisha mamlaka yake juu ya Sabato…………………………………………………........103

    B. AJ linabadilisha umuhimu wa Sabato………………………………………………………………………………..104

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    3

    C. Kutimizwa kwa Sabato katika Kristo kunamaanisha kuwa Jumapili siyo tu ni “Sabato ya Ki-Kristo” ya

    mapumziko sawa sawa na Jumamosi ilivyokuwa Sabato ya Kiyahudi……………….....................................104

    X. Kristo na Kanisa ndiyo “Mtumishi wa Bwana” aliyetabiriwa…………………………………………………...105

    A. Yesu ndiye “Mtumishi wa Bwana” aliyetabiriwa .…………………………………………………………………...105

    B. Kanisa ndilo kwa ujumla ni “Mtumishi wa Bwana,” kama vile Yesu alivyokuwa kibinafsi

    “Mtumishi wa Bwana”………………………………..………………………………………………………..106

    DIBAJI 1—VIFUPISHO KWA UCHACHE VYA VITABU VYA BIBLIA ……………………………………….107

    DIBAJI 2—MIPANGILIO YA MUDA WA HISTORIA YA BIBLIA.…………………………………………......110

    DIBAJI 3—BIBLIA KATIKA MPANGILIO UNAOONGOZANA.………………………………………………..112

    DIBAJI 4—MPANGILIO WA MUDA WA WAFALME NA MANABII WA ISRAELI NA YUDA………….…114

    DIBAJI 5—NABII CHACHE ZA KIMASIHI NA KUTIMIZWA KWAKE………………………………………116

    DIBAJI 6—YESU NI MUNGU KAMILI NA MWANADAMU KAMILI.………………….....…………………...117

    DIBAJI 7—YESU NA “ISHARA YA YONA” (MATH 12:38-41; 16:1-4; LUKA 11:29-32)……………………...126

    DIBAJI 8—RAMANI ZA HIMAYA ZA ASHURU, BABELI, NA UAJEMI...…………………………………….130

    DIBAJI 9—RAMANI YA HIMAYA YA RUMI & MAJIMBO YAKE...…………………………………………..130

    DIBAJI 10—RAMANI YA KANAANI: SEHEMU 12 ZA MAKABILA..………………………………………….131

    DIBAJI 11—RAMANI YA UFALME ULIOUNGANA WA ISRAELI..…………………………………………....131

    DIBAJI 12—RAMANI YA FALME ZILIZOGAWANYIKANA ZA YUDA NA ISRAELI……………………....132

    DIBAJI 13—RAMANI YA ISRAELI NYAKATI ZA AGANO JIPYA……………………………………………..132

    NUKUU ZILIZOTOLEWA…………………………………………………………………………………………….133

    KUHUSU MWANDISHI……………………………………………………………………………………………….140

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    4

    THEOLOJIA YA KI-BIBLIA: UTANGULIZI

    I. Tabia ya Theolojia ya Ki-Biblia

    A. Maelezo ya Theolojia ya Ki-Biblia

    1. Theolojia ya Ki-Biblia (TK) ni masomo yahusuyo kuweka bayana mkondo wa simulizi za Biblia kuanzia

    mwanzoni (Mwanzo) hadi mwisho (Ufunuo). Ni “kutafuta unganiko la ndani la Biblia” (Bartholomew 2005: 84).

    2. Theolojia ya Ki-Biblia “Hufuatia hatua za ufunuo tangu neno la kwanza la Mungu kwa mwanadamu

    kupitia kupambanuliwa kwa utukufu kamili wa Kristo. Huchunguza hatua mbali mbali za historia ya

    Biblia na mahusiano kati yao. Kwa hiyo, hutoa msingi wa kuelewa jinsi vifungu vya sehemu moja ya

    Biblia vinavyohusiana na vifungu vingine vyote. Tafsiri iliyo safi ya Biblia hutegemeana na yapatikanayo

    katika [TK].” (Goldsworthy 1991: 32)

    3. Kwa vile inajihusisha kuelezea kiunganisho cha ndani cha Biblia kwa namna yake yenyewe, ni “ya

    kujieleza na ya kihistoria kiasi kwamba tafsiri ya kitheolojia na theolojia ya ki-mfumo haiwezi kuwa

    hivyo” (Bartholomew 2005: 86). Ingawaje TK ni nidhamu ya kimaelezo na kihistoria, Biblia inachagua

    katika undani wa kihistoria inaoelezea. Uchaguzi huo msingi wake ni theolojia yote kiujumla ambayo

    Biblia inaweka bayana. “Umoja wa historia ya Kibiblia huegemea katika njia ya uchaguzi ambavyo

    simulizi huelezwa katika uelekeo fulani na siyo kwa mikondo mingine iwezekanayo. Kuna mwendelezo

    kwenye mkondo wa simulizi ambao unakataa kugeukia kwenye makorongo yenye upofu. Hivyo

    tunamfuata Seti, siyo Kaini; Shemu, siyo Hamu; Ibrahimu, siyo Lutu; Israeli, siyo Edomu; Daudid, siyo

    Sauli; Yuda, siyo Samaria; Yerusalemu, siyo Babeli. Mwishowe, uchaguzi muhimu ni ule wa Yesu kama

    Masihi halisi kinyume na hali ya sasa ya kumkana Yeye. Agano Jipya huona mwendelezo halisi wa

    kihistoria wa taifa la Israeli kama watu wa Mungu wapatikanao katika Yesu Kristo. Mnyambuo huo wa

    historia ni wa kitheolojia ya ndani na siyo wa kujaribisha.” (Goldsworthy 2000: 69)

    B. Fikira za Theolojia ya Ki-Biblia

    1. Biblia inaelezea simulizi inayoshikamana, na Yesu Kristo ndiye moyo wa simulizi hiyo (Luka 24:25-

    27, 44-47; Yoh 5:39). Kila kitabu cha Biblia kinachangia kitu fulani kwenye simulizi hiyo, na ujumla wa

    simulizi nzima hutoa mpangilio ambao kila kitabu kilichomo kinaweza kutafsiriwa vizuri zaidi.

    2. Ingawaje Biblia inaelezea simulizi iliyounganika, ufunuo wa Mungu ni hatua kwa hatua—hujifunua

    kila mahali katika Biblia yote. Kanuni kadhaa muhimu huibuka kutokana na kweli hizi.

    a. Andiko halitalipinga Andiko. Vifungu viwili vinavyoonekana vinapingana, vitakuja kuonyesha

    havipingani pale vitakapochunguzwa kwa umakini zaidi. Kifungu kimoja kinaweza kurekebisha

    au kuongezea sifa ya kingine, lakini hakitakipinga.

    b. Yote mawili hatua za ukombozi na “kusudi lote la Mungu” (Mdo 20:27) lazima yaangaliwe

    ili kuelewa kiusahihi kifungu chochote kile. Mafundisho ya “ufunuo wa hatua kwa hatua”

    hutueleza kwamba hatua za ukombozi lazima zizingatiwe wakati wa kutafakari kifungu chochote

    kile. Biblia ni muunganiko unaoelezea simulizi ya kisa kilichoungan. Hata hivyo, kweli za Biblia

    hazifunuliwi zote kwa mkupuo moja, bali hufunuliwa hatua kwa hatua. Maana kamili ya kifungu

    chochote husika au fundisho la Ki-Biblia laweza lisiwe wazi hadi Biblia nzima iwe

    imezingatiwa.

    c. Agano Jipya linavyolitafsiri Agano la Kale.

    (1) Maandishi yoyote ya Ki-Biblia yanapaswa kusomwa ndani ya muundo wa maneno

    yaliyotumiwa (lugha na mfumo wa maandishi husika) na mazingira ya kihistoria

    yalipoandikwa mara ya kwanza. Agano Jipya limeandikwa kwa misingi ya Agano la

    Kale. Miktadha mingi ya Agano Jipya husimamia Agano la Kale. Uelewa wetu wa

    Agano Jipya hutajirishwa kwa kiwango kikubwa kwa kulielewa Agano la Kale. Wakati

    huo huo, hatupaswi kulisoma Agano la Kale kama kwamba Jipya halipo. Yote mawili

    yapo – kutokuendeleza na mwendelezo kati ya Agano la Kale na Agano Jipya. Agano

    Jipya hujengwa juu ya miktadha ya Agano la Kale, mara nyingi katika namna za

    kushangaza. Hilo ni kweli zaidi kuhusu jinsi Agano Jipya linavyohusisha unabii wa

    Agano la Kale.

    (2) Lazima tukumbuke kwamba sheria za Agano la Kale, sikukuu, na taratibu nyingine

    zimetimilizwa na kukamilishwa katika Kristo (Math 5:17; Rum 10:4; 2 Wakor 3:12-

    16; Wagal 3:23-4:7). Kwa namna nyingi, Israeli ya kimwili ya Agano la kale, sheria

    zake, sikukuu zake, na taratibu nyingine, zilikuwa “aina,” “vivuli,” au “mifano” ya

    uhalisi wa Agano Jipya (1 Wakor 10:1-6; Wakol 2:16-17; Waeb 8; 10:1). Kwa hiyo,

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    5

    tunapoiangalia picha nzima, hasa tunapotumia Maandiko, tunapaswa “kuyasoma

    Maandiko ya Agano la Kale kwa kupitia miwani ya Maandiko ya Agano Jipya” (Lehrer

    2006: 177). Kama ilivyosemwa, “Hili Jipya, ni lile la Kale lililotimilika; la Kale ni Jipya

    lililofunuliwa.”

    II. Mtazamo wa Mkondo wa Simulizi na Dhana za Theolojia ya Ki-Biblia

    A. Msingi wa mkondo wa simulizi za Biblia

    1. Katika mtazamo wa kawaida zaidi, Biblia ni simulizi ya uumbaji, historia, na hatima ya ulimwengu na

    mwanadamu, kama ielezwavyo kimsingi kwa mtazamo wa kitheolojia. Mungu aliumba ulimwengu wa

    kupendeza sana na wanadamu kuishi kwa furaha, na maisha yaliyotimilika katika ushirika na yeye.

    Kupitia dhambi zetu tulipoteza ushirika ule na kuleta uovu na uharibifu na mauti duniani. Hata hivyo,

    Mungu hakutuacha katika dhambi zetu na mauti. Kwa njia ya mpango mahususi uliohusisha kumwita

    Ibrahimu na taifa la Israeli, aliandaa njia kwa ajili ya kuja ndani ya mwanadamu kwaYesu Kristo ili

    kuleta msamaha wa dhambi na kurejesha ushirika na yeye. Anakuja tena, kumaliza dhambi kabisa na

    mauti pasipo kutuangamiza sisi. Atakwenda kutimiliza kurejeshwa kwetu na uhusiano wetu na yeye. Na

    pia ataifanya upya nchi, hata iwe ya utukufu zaidi ya ilivyoumbwa mara ya kwanza. Katika muundo huo,

    mkondo wa simulizi hii ungeonekana namna hii: uumbaji (Mwanzo 1-2)=>Anguko na madhara yake

    (Mwanzo 3-11:26)=>Ukombozi (Mwanzo 11:27-Ufunuo 20)=>Uumbaji mpya (Ufunuo 21-22).

    Mungu mwenyewe ndiye yote mawili -mtunzi wa simulizi na ndiye mhusika mkuu wake.

    2. Biblia ni ufunuo wa Mungu kuhusu jinsi alivyo na mpango wake (Injili) kwa mwanadamu.

    a. Kiungo cha katikati cha ufunuo huo—yeye aliye kiungo mtendaji wa uumbaji, njia ya

    ukombozi, na chanzo na utimilifu wa uumbaji mpya—ni Yesu Kristo (ona 2 Wakor 1:20; Waef

    1:9-10; Wafil 2:6-11; Waeb 1:1-3).

    b. Kwa hiyo, Agano la Kale ni maandalizi ya Injili, Injlili zile ni udhihirisho wa Injili; Matendo

    ya Mitume ni upanuzi wa Injlili; Nyaraka ni maelezo ya Injili; na Ufunuo ni utimilifu wa Injili.

    3. Biblia ni simulizi ya uhusiano na mwanadamu, tangu uumbaji hadi uumbaji mpya. Wanenaji

    mbalimbali wameielezea simulizi kwa njia nyingine zinazotofautiana kidogo:

    a. “Kwa maelezo ya Ki-Kristo, dunia kwa Mungu ni muundo, na dhana ni wokovu wa dunia na

    mwanadamu aliyeanguka; vipengele vyake ni maelezo ya Biblia, kuanzia uumbaji, uteuzi, hadi

    kuutwaa mwili, kusulubiwa, ufufuo na kupaa; na mwafaka ni hukumu ya mwisho, mbingu na

    jehanamu” (Sykes 1997: 14).

    b. “Theolojia ya Ki-Biblia ni Mungu kuuleta ufalme wake ambamo mahusiano yote yanakuwa

    yamerejeshwa kwenye ukamilifu” (Goldsworthy 1991: 76).

    c. “Watu wa Mungu, katika nafasi ya Mungu, chini ya utawala wa Mungu, wakiishi kwa njia ya

    ki-Mungu, katika uwepo mtakatifu na wa upendo wa Mungu, kama familia” (Cole 2006: n.p.).

    B. Dhana za Theolojia ya Ki-Bibia

    TK yaweza kukabiliwa kwa njia mbali mbali. Mtu moja aweza kuikabili TK kwa kujaribu kuelezea

    mpangilio mzima wa mtiririko wa mkondo wa simulizi ya Biblia kiutaratibu kuanzia mwanzo hadi mwisho.

    Ndani ya mtiririko wa mkondo wa simulizi hiyo, dhana na miktadha muhimu hujitokeza mara kwa mara kila

    mahali katika Biblia, ambayo husaidia kukazia na “kuimarisha upya” mkondo wa simulizi nzima ya Biblia.

    mwishowe, dhana hizi, na Biblia yenyewe, huhusishwa, na huweza kutimilizwa, katika Yesu Kristo (ona Luka

    24:25-27; Yoh 5:39, 46). Baadhi ya dhana muhimu zaidi na miktadha ni:

    1. Ahadi na Kutimizwa. Mungu ni mwaminifu kutimiza ahadi zake. Lakini mara zote ahadi zake

    hutimizwa kwa njia za kushangaza. Utimilifu wa mwisho wa ahadi za Mungu hupatikana katika Yesu

    Kristo. Kama asemavyo Paulo katika Waef 1:9-10, “Akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa

    na uradhi wake, alioukusudia katika yeye huyo. Yaani, kuleta madaraka ya wakati mkamilifu

    atavijumlisha vitu vyote katika Kristo, vitu vya mbinguni na vitu vya duniani pia, naam, katika yeye

    huyo.”

    2. Agano la Mungu. Mungu alifanya Maagano kadhaa (mapatano maalum) kipindi chote cha historia ya

    Biblia. Maagano makuu ni: Agano la Nuhu (Mwa 8:20-9:17); Agano la Ibrahimu (Mwa 12:1-3; 13:14-

    17; 15:1-21; 17:1-21; na 22:15-18); Agano la Musa (Kutoka 19-24), pia hujulikana kama Agano la

    Kale (2 Wakor 3:14; Waeb 8:6, 13); Agano la Daudi (2 Sam 7:8-17; Zab 89:1-4); na Agano Jipya

    (Yer 31:31-34; 32:40; Ezek 36:22-28; 37:15-28; Luka 22:20; 1 Wakor 11:25; 2 Wakor 3:6; Waeb

    8:6-13; 10:15-17). Kwa namna nyingi, mpango mzima wa Mungu wa ukombozi waweza kuonekana

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    6

    kama ni kutenda kazi kwa Agano la Ibrahimu. Kama simulizi ya ukombozi inavyoendelea, Maagano ya

    Ibrahimu, Musa, na Daudi, yote hupata utimilifu wake katika Agano Jipya, na Agano hilo hupata

    utimilifu wake katika Kristo na watu wake, na kanisa.

    3. Aina husika-Aina-Kinyume; Kivuli-Kitu halisi. Kadiri mpango wa Mungu ulivyoendelea na wakati,

    kwanza alimwita Ibrahimu, kisha Isaka, kisha Yakobo, ambaye kupitia yeye alianzisha taifa la Israeli,

    kuwa chombo ambacho kwacho mpango wake ulifanyika uhalisi. Hata hivyo katika mtazamo wa

    kitheolojia na wa kiroho, mifano yote ya Agano la Kale au taasisi zake—kama vile Madhabahu na Hema,

    mifumo ya utoaji dhabihu. Sikukuu, Sheria, na Nchi ya Ahadi. Ufalme, Sayuni, Yerusalemu, na Israeli

    yenyewe—viliwakilisha “vielelezo” au “vivuli” vya kuonekana au vya kidunia, ambavyo vilielekeza

    kwenye Agano Jipya, na uhalisi wa kiroho wa siku za mbeleni (Wagal 4:21-31; Wakol 2:16-17; Waeb

    8:5; 9:15-10:22; 12:18-24). Uhalisi wa kweli ambao aina na vivuli vya Agano la Kale (AK) vilielekeza,

    viko katika Kristo, kanisa, mbingu, Yerusalemu mpya, na mbingu mpya na nchi mpya.

    4. Mkondo wa Mungu wa Uhusiano: Mungu huanzisha na hutenda kwa neema yake, watu wake

    wanatakiwa kuonyesha mwitikio kwa imani.

    a. Mungu siku zote ametafuta watu kwa ajili yake. Hivyo, kauli inayojirudia mara zote katika

    Biblia nzima (ikitumia maneno tofauti) ni, “Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu

    wangu” (ona Mwa 17:8; Kut 6:7; 29:45; Wal 26:12; Yer 7:23; 11:4; 24:7; 30:22; 31:1, 33;

    32:38; Ezek 11:19-20; 14:10-11; 36:28; 37:23, 27; Hos 2:23; Zek 8:8; 13:9; 2 Wakor 6:16;

    Waeb 8:10; Ufu 21:3).

    b. Mkondo unaojirudia mara kwa mara katika Biblia nzima kwa ajili ya watu kuwa na uhusiano

    mzuri na Mungu ni kwamba, Mungu huanzisha, na watu wake huonyesha mwitikio kwa imani

    (ambayo kimsingi humaanisha “kutumaini na kutii kutoka moyoni”).

    (1) Mungu hutenda kwa neema kwa watu; hata katika kuhukumu na kuwaadhibu makosa

    huonyesha neema yake. Mungu alianza mchakato kwa kumuumba Adamu na Hawa na

    alizungumza nao katika bustani ya Edeni (Mwa 2:7, 15-25; 3:8). Baada ya Adamu na

    Hawa kuanguka dhambini, kwa neema Mungu alianzisha mpango wa ukombozi kwa

    kuahidi mwokozi (Mwa 3:15) na kutoa sadaka ya wanyama ili kuwavika mavazi (Mwa

    3:21). Kwa neema, Mungu alimchagua Nuhu na familia yake waokolewe wakati

    alipoiangamiza dunia yote kwa Gharika Kuu, na Nuhu aliitikia kwa imani (Mwa 6:5-

    22). Mungu akamchagua Ibrahimu, aliyeitikia kwa imani (Mwa 12:1-5; 15:5-6). Kwa

    neema yake, Mungu alituma manabii wake kuwaonya Israeli juu ya maafa ya dhambi

    zake na kuwaita warudi kwenye uaminifu tena. Mwishowe, kwa neema yake, Mungu

    mwenyewe akafanyika mwili katika mwanadamu aitwaye Yesu Kristokuwaokoa watu

    wake na dhambi zao na kurejeza mahusiano mazuri kati ya Mungu na wanadamu.

    (2) Kwa vile wanadamu kiasili ni wadhambi, hawawezi “kustahili” au “kufanyia kazi”

    mbinu iwawezeshayo kuwa na mahusiano mazuri na Mungu (Mdo 13:39; Wagal 2:16;

    3:11; Waef 2:1-3, 12). Njia pekee ya watu kuwa na mahusiano mazuri na Mungu ni tu

    kama wataitikia kwa imani kile Mungu, kwa neema yake, alichokifanya kwa ajili yao.

    Kwa sababu hiyo, muktadha wa imani na uaminifu kwa Mungu—“mwenye haki ataishi

    kwa imani”—hujirudia kila mahali katika Biblia (Hab 2:4; War 1:17; Wagal 3:11;

    Waeb 10:38; ona pia Yoh 6:27-29; 20:26-29; 1 Yoh 3:23). Bahati mbaya, mkondo

    umekuwa mara nyingi watu wengi hawaweki imani zao kwa Mungu, ingawaje daima

    wamekuwako “mabaki wachache waaminifu” ambao wamefanya hivyo (1 Waf 19:11-

    18; Rum 11:1-5; ona pia Luka 18:8).

    MSINGI WA SIMULIZI YA MKONDO WA BIBLIA

    I. Uumbaji (Mwanzo 1-2)

    “Uumbaji si swala tu la vyanzo, bali la kusudi na mahusiano” (Goldsworthy 1991: 92). Katika uumbaji,

    twamwona Mungu kama chanzo cha kila kitu. Zaidi ya hapo, kama kila kitu kilivyoumbwa mwanzoni, twaona

    “kila kitu kuwa chema” (Mwa 1:31)—m.y., Mungu, mwanadamu, wanyama, mimea, na maumbile mengine yote

    kutimiza makusudi ya kuumbwa kwao katika mahusiano mazuri kila kimoja kwa kingine. “Wasomi wamegundua

    kwamba Sura za mwanzo za kitabu cha Mwanzo . . . zimeandaliwa ili kujibu swali la kwa nini mambo yako jinsi

    yalivyo. Seti moja ya maswali ambayo sura za mwanzo za kitabu cha Mwanzo ni, ‘Kwa nini wanadamu wako

    jinsi hii? Kwa nini wanadamu hutafuta maarifa zaidi? Kwa nini wanadamu hutafuta utawala mkubwa zaidi juu ya

    dunia? Kwa nini daima hujaribu kuvumbua vitu vipya, kutafuta matumizi mapya ya rasilimali za “asili”? Kwa

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    7

    nini wanadamu hupaka rangi, huchonga sanamu, huchora picha, hujenga majengo, hutunga nyimbo na mashairi?

    Kwa nini wanadamu mara kwa mara na kwa namna tofauti hujihusisha na utamaduni wa kisanii, sayansi, na

    teknolojia?’ Jawabu la Mwanzo 1 ni kwamba Mungu alimfanya mwanadamu awe hivyo. Mwanadamu ni mfano

    wa Mungu. Mungu ni Muumbaji na ni Mfalme. Kama mfano wake, mwanadamu hubuni na kutawala.” (Leithart

    n.d.: n.p.)

    A. Simulizi ya mkondo wa Biblia huanzia na Mungu (Mwa 1:1).

    1. Mungu pekee ni wa milele na anaishi kwa kujitegemea. Mungu si sehemu ya ulimwengu wala si

    kinyume chake pia. Kila kitu kilichopo kumwacha Mungu (vitu; malaika; wanadamu, nk) viliumbwa na

    Mungu, na humtegemea Mungu kwa kuwepo kwao (Mdo 17:28; Wakol 1:17; Waeb 1:3). Ukweli huu

    huonyesha kwamba Mungu wa kweli, wa Ki-Biblia hafanani na “miungu” ya dini nyingine. Mungu si

    kama wazo la Mashariki (n.k., Wahindu; Wabudha) kwamba Mungu na maumbile yote ni kitu “kimoja”

    (m.y; muktadha wa muunganiko katika kimoja). Mungu pia si wa dini za kiutamaduni (zikiwamo zile za

    Mashariki ya Karibu ya kale wakati Biblia ilipoandikwa), ambazo huamini kwamba vitu vilivyokufa vina

    “roho”, na wanadamu wa kwanza walikuwa kwa sehemu moja ni wanadamu na sehemu nyingine

    miungu.

    2. Mungu peke yake anajitosheleza. Yuko Mungu moja tu, lakini ni mwenye hali isiyoelezeka kabisa,

    tofauti na kila kitu kingine. Kwa hiyo, ingawaje yuko Mungu moja tu, anaishi katika nafsi tatu (Utatu):

    Baba; Mwana; na Roho Mtakatifu. Hili ni muhimu. Kama Mungu angekuwa ni wa nafsi moja (kama

    dhana ya Allah wa Ki-Islam), na si Mungu wa Utatu, Mungu asingekuwa anajitosheleza: m.y., angekuwa

    anawajibika aviumbe viumbe vingine ili awe na uhusiano navyo. Hata hivyo, Mungu hakuhitaji aumbe

    chochote (ona Mdo 17:24-26)—tayari alishaumba ulimwengu, alishakuwa na upendo kamili wa

    kiuhusiano kati ya zile nafsi tatu za Utatu kabla hajaumba ulimwengu. Kwa hiyo, Biblia (tofauti na

    Qur’an) hutueleza kwamba “Mungu ni upendo” (1 Yoh 4:8).

    B. Mungu aliumba kila kitu bila kutumia chochote.

    1. Ulimwengu haukuwa na kitu kilichokuweko kabla ambacho kwacho Mungu aliumbia nyota au mimea

    au wanyama. Badala yake, Mungu alifanya tu kutamka au kutangaza, na ulimwengu ukatokea pasipo

    kutumia chochote (Mwa 1:1, 3, 6-7, 9, 11, 14-16, 20-21, 24, 26-27). Sehemu nyingine, kote katika AK

    na AJ, Biblia inakazia kitu hicho hicho (ona Kut 20:11; 31:17; Zab 8:3-5; 33:6; Math 19:4; Yoh 1:3;

    Mdo 14:15; Rum 11:36; 1 Wakor 8:6; Wakol 1:16; Waeb 11:3; Ufu 4:11).1

    2. Mwanadamu alikuwa ni tukio la kilele katika uumbaji wa Mungu. Ni wanadamu pekee wanasemekana

    kuwa wameumbwa “kwa mfano wa Mungu” (Mwa 1:26-27); Mungu akambariki mwanaume na

    mwanamke (Mwa 1:28); na Mungu akawaambia atakuwa na ushirika nao (Mwa 1:28-30; 2:16-17, 19;

    3:8-9). Zaidi ya hapo, wakati kila siku baada ya kuumba vitu visivyo hai, mimea, au wanyama, Mungu

    aliuita uumbaji wake kuwa “mzuri (njema)” (Mwa 1:4, 10, 12, 18, 21, 25), baada ya kuumba

    wanadamu, Mungu akaona kwamba uumbaji ule ni “mwema sana” (Mwa 1:31).

    3. Tukio la uumbaji la Mwa 2:4-25 ni sambamba au nyongeza ya tukio la kiuumbaji lililoko katika Mwa

    1:1-2:3. Tukio la Mwa 2:4-25 hurudi nyuma na kujazia undani wa yaliopo katika Mwa 1:26-27

    kuhusiana na jinsi Mungu alivyoumba wanadamu. Wote wawili mwanaume na mwanamke walikuwa

    sehemu ya mpango wa Mungu tangu mwanzo (ona Mwa 1:27), ingawaje Mungu alimuumba Adamu

    kwanza na kisha Hawa baadaye ili awe msaidizi na mwenzi wake (ona Mwa 2:18-25). Hii inaonyesha

    kwamba tabia na majukumu ya mwanaume na mwanamke kwa kiwango fulani ni nyongeza, siyo ya

    kubadilishana kabisa (ona 1 Wakor 11:3-15; Waef 5:28-32; 1 Tim 2:11-13), ingawaje ni kwa kiwango

    gani yanaweza kuwa hivyo bado yanajadiliwa.

    4. Wote wawili mwanaume na mwanamke wana mfano wa Mungu. Maana ya msingi ya “mtu”

    (Kiebrania, adam) ni neno la kiujumla “mwanadamu, watu,” ambalo hujumlisha wote wanaume na

    wanawake. Hilo linawekwa bayana katika Mwa 1:26, panaposema, “Na tumfanye mtu kwa mfano wetu .

    . . wakatawale.” Mwa 1:27 likieleza wazi kwamba wote wawili mwanaume na mwanamke wanahusika

    kiusawa, kwani panasema, “Mungu akaumba mtu [Adamu] kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu

    alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.” Zaidi, katika Mwa 1:28 Mungu akawabariki

    “hao” (mwanamume na mwanamke) kiusawa na Mungu alisema “nao”. Katika Mwa 1:29, wakati

    Mungu anasema “Nimewapa kila mche utoao mbegu,” hiyo “wa” ni uwingi, siyo umoja.

    1 Kama zile siku sita za uumbaji zitajwazo katika Mwanzo 1 ni za kweli au za kitaswira ni swala la kujadika. Ona David G. Hagopian,

    ed., David G. Hagopian, ed., The Genesis Debate: Three Views on the Days of Creation (Mission Viejo, CA: Crux, 2001).

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    8

    C. Mungu alimuumba mwanadamu ili atawale viumbe vingine vyote (Mwa 1:26-28).

    1. Adamu na Hawa wakiishi mbele za Mungu katika bustani ya Eden hutupatia mkondo wa ufalme wa

    Mungu. “Mkondo wa ufalme wa Mungu ni huu: Mungu huanzisha uumbaji ulio kamili ambao

    anaupenda na ambao yeye hutawala. Heshima kuu kabisa inatolewa kwa mwanadamu kama sehemu

    pekee ya uumbaji uliofanywa kwa mfano wa Mungu. Ufalme unamaanisha kwamba kila kitu kilichomo

    katika uumbaji kishirikiane vizuri, hiyo maana yake, kama Mungu alivyokusudia kiwe, kwa kingine

    chochote na kwa Mungu mwenyewe.” (Goldsworthy 1991: 99)

    2. Adamu na Hawa waliagizwa “Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha dunia” (Mwa 1:26-

    28). Kwa vile wanadamu wameumbwa kiajabu “kwa mfano wa Mungu,” kwa kuenea duniani wakitii

    maagizo ya Mungu, watu wangekuwa wanaukuza utukufu wa Mungu, kwa kueneza sura yake, juu ya

    dunia yote. Hali hiyo ya “dhana ya wajibu wa kutawala” huendelea kuonyesha kwamba walitakiwa

    kupanua mipaka ya kijiografia ya Edeni hadi ienee dunia nzima. Kwa kupanua Edeni hadi kuenea dunia

    nzima, Adamu na Hawa na vizazi vyao wangekuwa wanaigeuza dunia kuwa kioo cha mbinguni: m.y;

    kuifanya dunia nzima kuwa paradiso imfaayo Mungu na mwanadamu, iliyojaa watu watakatifu.

    3. Ni kwa kutegemea Neno la Mungu peke yake kwamwezesha mwanadamu kutimiliza ile dhana ya

    wajibu wa kutawala sawa-sawa. “Pale Adamu alipowapa majina wanyama, alianza mchakato wa

    uchunguzi, kupanga makundi, na maelezo toshelevu, ambayo ndiyo moyo wa uchunguzi wa maarifa ya

    kisayansi. Lakini hangeweza kamwe kufanikisha uhusiano wake mwenyewe kwa Mungu au hata kwa

    ulimwengu kwa kutegemea uchunguzi peke yake. Badala yake, lilikuwa ni Neno la Mungu lililokuja kwa

    Adamu kumwambia jinsi ya kuhusiana na Mungu na kwa ulimwengu. Ni Neno la Mungu linalomjulisha

    mwanadamu kwamba awe mwanasayansi na mwenye kuutunza kiupendo ulimwengu, badala ya kufanya

    uchawi na kuwa mtu mharibifu asukumwaye na kutaka madaraka katika dunia.” (Goldsworthy 1991: 99)

    II. Anguko la Mwanadamu Katika Dhambi na Matokeo Yake (Mwanzo 3-11:26)

    A. Ukuu wa Mungu, wajibu wa mwanadamu, na kuwepo kwa dhambi

    1. Mungu ni mkuu juu ya kila kitu, naye yuko kazini kukamilisha mpango wake (ona 1 Nyak 29:11-12;

    Ayub 12:13-25; Isa 40:21-26; Mdo 4:27-28; Rum 9:14-24; Ufu 17:14-17). “Hakuna kitu chochote

    ‘cha asilia’ kuhusu dunia katika Theolojia ya Ki-Biblia. Hii haimaanishi kupendekeza kuwa Mungu

    huitawala dunia kimaficho, bali anajihusisha kikamilifu na utendaji na matukio ya dunia.” (Walton 2009:

    8) Kwa hiyo, Biblia humwona Mungu kama mtendaji na anayejihusisha na vipengele vyote vya maisha

    ya duniani. Kwa mfano, Huumba milima, huumba upepo, na hufanya asubuhi kuwa usiku (Amosi 4:13);

    Hufanya upepo uvume na kufanya maji yatiririke (Zab 147:18); Hutawala jua, mwezina nyota, na

    aichafua bahari (Yer 31:35); Hutawala ukuaji wa mimea (Isa 41:19-20); Hutawala wanyama (Ayub 39).

    Mungu pia ni mkuu na hutawala pia maswala ya wanadamu. Kwa mfano, Husimamia uhai na mausi,

    kukiwamo pia matatizo ya kiuzazi, magonjwa, na mauti, vikiwamo vifo vya “wasio na hatia” (Mwa

    20:17-18; Kut 4:11; 2 Sam 12:15; Neh 9:6; Ayub 12:9-10; Isa 44:24; Ezek 24:15-18); Huwainua

    watu juu na kuwashusha wengine chini (1 Sam 2:7); Hutawala mataifa (2 Nyak 20:6; Zab33:10-11; Isa

    40:23-25); Huamsha roho za watu, huingiza mawazo ndani yao, na kugeuza mioyo yao (Ezra 6:22; Neh

    2:12; 7:5; Zab 105:25; Hag 1:14).

    Wakati huo huo, Mungu huheshimu unyofu wao kama wanadamu; hawatawali wato kama vile ni

    vikaragosi au kuwapangilia mambo kama vile roboti zinavyoongozwa kwa programu. Watu wana uwezo

    wa kufikiri mawazo yao wenyewe na kufanya maamuzi yao. Kwa hiyo, Biblia kwa kurudia–rudia imetoa

    maelezo ya pande tofauti za matukio: Mungu ni mkuu na ameanzisha matukio yote (hilo, kwa upande

    moja, ni maelezo kamili kwa matukio yote); hata hivyo, hilo linaendana na, na kinamna yoyote

    haliondoshi, wajibu wa watu kwa maamuzi wanayoyafanya na mambo wanayoyafanya (hilo, kwa upande

    mwingine, ni maelezo kamili kwa matukio yote). Kinamna fulani, Mungu hufanya kazi ndani ya, na

    kupitia viumbe vyake (wote, wanadamu na roho) kukamilisha mpango wake. Terrence Fretheim anaeleza

    hivi: “Uhusiano wa Mungu na dunia ni wa uwanda mkamilifu: Mungu yupo na hutenda popote ilipo

    dunia. Mungu haiumbi duniana kisha kuiacha, bali Mungu huiumba dunia na kisha huingia ndani yake,

    huishi ndani yake, kama Mungu. . . . Mungu yuko katika kila tukio na mtendaji katika kila tukio. Kuanzia

    ulimwengu wa juu hadi ulimwengu wa chini, hakuna kukwepa uwepo wa Mungu. Mungu hawezi

    akaamshwa kutoka duniani au kutokana na maisha ya kiumbe. Wakati huo huo, uwepo wa Mungu

    haumaanishi ama mwingilio wa kiungu wa kiutawala wala mapenzi ya kiungu yasiyozuilika. . . . Dunia

    hudumisha unyofu wake kama kiumbe hata wakati imejawa na uwepo wa Muumba . . . . Mungu—aliye

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    9

    tofauti na dunia—hutenda kimahusiano kutokea ndani ya dunia, na si juu ya dunia kana kwamba kutokea

    nje. . . . Hiyo maana yake, wote wawili, Mungu na viumbe wana uhusiano muhimu katika mradi wa

    kiumbaji, na maeneo ya kiutendaji yanaingiliana kwa maana ya kazi na matokeo. . . . Bali, zaidi kabisa,

    Mungu huwapa wanadamu nguvu na wajibu katika namna ambayo humwajibisha Mungu kwa aina fulani

    cha uhusiano nao. Uwajibikaji huu huhitaji usimamizi na udhibiti wa ki-ungu katika kuwepo kwa

    mamlaka ndani ya uumbaji. Kwa mfano, Mungu hatafanya hatua za kutungisha kuumbika wanyama au

    kuzalika kwa mbegu za matunda kwa njia isiyohusisha kuunganika.. La kukutisha zaidi wanadamu

    wamepewa uhuru wa kuangamizana wenyewe, ingawaje hili linasimama kinyume na mapenzi ya Mungu

    kwao. Huku kujidhatiti kutoa mamlaka ya wajibu kwa kiumbe husababisha kuendelea kutegemea

    uongozi wa ki-ungu kwa viumbe ambavyo kwa kupitia hivyo, Mungu atatenda kazi kwa uhai wa dunia.”

    (Fretheim 2005: 23-24, 26, 27)

    Maoni mengine mawili ya kufanyika kuhusu kutegemeana huku kwa mahusiano ya Uungu-

    uanadamu: (1) “Haya ni mahusiano ya wasiolingana; Ni uhusiano usiowiana. Mungu ni Mungu, na sisi

    hatuko vile.” (Ibid.: 16) na (2) Ni ukweli unaokinzana unaoelezea tafsiri au uelewa kamilifu. Hata hivyo,

    kuwepo kwa Mungu mwenye enzi yote, mwenye maarifa yote, aliyeko kote, aliye na mpango kwa dunia,

    aliye mkuu, na anautimiliza mpango wake, na amewapa viumbe walio na uwezo wa kufanya maamuzi

    halisi na kutenda mambo kihalisia ambayo wanawajibika nayo, uhusiano kati ya Mungu na viumbe Wake

    kama ulivyoelezwa hapo juu usingeweza kuwa vinginevyo.

    2. Ukuu wa Mungu juu ya kila tukio unahusisha ukuu juu ya dhambi na uovu, lakini si kwa namna

    ambayo inamfanya Yeye kuwa mdhambi au mwovu. Ingawaje watu wengi wanajaribu kumwekea kinga

    Mungu mbali na kila dhambi (huyahusisha maovu yote ama na Shetani au kwa dhambi binafsi), Biblia

    inaonyesha picha iliyo na vidokezo na utata zaidi. D. A. Carson anaonyesha kwamba waandishi wa

    Biblia “hawamwonei aibu kumhusisha Yahwe mwenyewe kwa njia ya siri (usiri ambao humlinda

    kutohusishwa na uovu) chanzo ‘kikuu’ cha maovu mengi. . . . Mungu hasimami nyuma ya tendo ovu

    kwa namna thabiti kama asimamiavyo matendo mema. Waandishi wa [Ki-Biblia] huelewa Mungu uwa

    mtakatifu, asiye na upendeleo, mwenye haki, mema, mvumilivu (Mwa. 18.25; Law. 11.44; Isa. 6.3;

    61.8; Zefania. 3.5; Zab. 5.4; 11.5; 145.17; Ayub 34.10-15; nk.). Kila kitu Mungu alichokifanya kilikuwa

    ‘chema sana ’ (Mwa 1.31). Umbali fulani huwekwa kati ya Mungu na watu pale wanapofanya dhambi.”

    (Carson 1994: 28) Ingawaje Mungu, kwa njia fulani, husimama nyuma ya dhambi na uovu, wakati huo

    huo vilevile “husimama kinyume nayo, kiasi kwamba neno hufanyika kondoo wa Mungu aichukuaye

    dhambi ya dunia, na ghadhabu ya Mungu hudhihirika juu yake ([Yohana] 1.29; 3.36)” (Ibid.: 160-61).

    “Kwa kifupi, ingawaje tunaweza kupungukiwa makundi ya maelezo kamili ya matatizo, hata hivyo ni

    lazima tusisitize kwamba nguvu ya Uungu inasimama nyuma ya mema na mabaya mtindo moja.” (Ibid.:

    36-37) Hilo linamaanisha kwamba, kwa mtazamo huo huo,kimsingi Mungu ndiye anayewajibika kwa

    maovu kwa maana kwamba Yeye ndiye mkuu juu ya kila kitu, atangazaye “mwisho tangu mwanzo” (Isa

    46:10), na ameanzisha mpango mpango kamili wa uumbaji wote , ukiwamo uovu, ambao anautimimiliza

    (Mith 16:4; Isa 46:8-11). Hata hivyo Mungu, hahusiki na uovu kwa namna ambayo anakuwa chanzo

    cha uovu wa uharibifu ule (ona Mwa 4:1-7; Isa 10:5-16; Hab 1:1-11; Mdo 2:22-24). Uhusikaji wa

    Mungu “wa pande mbili ” nyuma ya mema na maovu humaanisha kuwa “Mungu husimama nyuma ya

    uovu kwa jinsi ambayo uovu ule hautatokea nje ya mipaka ya ukuu wake, na kuwa uovu ule usihusishwe

    kimaadili kwake: uwe daima unawajibishwa kwa vitendea kazi vingine, vyanzo vingine. Kwa upande

    mwingine,Mungu husimamia mema kwa namna ambayo siyo tu hutendeka ndani ya mipaka ya ukuu

    wake, bali daima huhusishwa kwake na daima hutendwa na vitendea kazi vingine.” (Carson 1990: 213)

    Mfano wa hili huonekana katika Yakobo 1. Yak 1:2, 12 palizungumzia kuhusu watu

    waliokabiliwa na “majaribu” mbali mbali.” Yak 1:13-14 ndipo pakasema, “Mtu ajaribiwapo, asiseme

    Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu

    mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.” Neno

    “jaribu” na “shawishi” ni vitambulishi, m.y, jina na kitenzi cha neno lilelile la mzizi moja katika

    Kiyunani la neno (peirasmos [jaribu] na peirazō [shawishi]). Muktadha huonyesha utofauti wake :

    Mungu hutuweka sisi katika mazingira ya kutupima kutujaribu—ikiwa ni pamoja na mazingira ambayo

    anajua tunaweza, kusema ukweli, kutenda dhambi—hata hivyo hatushawishi tutende dhambi. Mungu

    huruhusu na kuanzisha dhambi, si kwa sababu za uovu au udhambi wa dhambi yenyewe, bali sababu ya

    miisho na makusudi yaliyo “ya hekima, matakatifu, na yaliyo bora zaidi” (Edwards 1984, Freedom, §IX:

    76; ona pia Piper 2000: 107-31). Kwa mazingira haya, Randy Alcorn anasema kwamba Mungu

    “alikusudia kuanzia mwanzo kuruhusu uovu, kisha kugeuza uovu juu ya kichwa chake, kuchukua

    malaika na watu waovu waliokusudiwa kwa ajili ya uovu na kuutumia kwa ajili ya uzuri. . . .

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    10

    Inawezekana kujipanga kwa ajili ya jambo ujualo kuwa linakuja pasipo kulilazimisha litokee. Mungu

    hakumlazimisha Adamu na Hawa kutenda uovu, bali aliwaumba wakiwa na uamuzi, na aliruhusu uwepo

    wa Shetani katika ile bustani, akijua kabisa watachagua uovu na akijua atakachokifanya katika mpango

    wake wa okombozi kitaleta matokeo mazuri zaidi.” (Alcorn 2009: 226-27) Hakika, watu wanaweza kuwa

    na msukumo moja kwa watakalolifanya (k.m., kutenda uovu), bali Mungu anaweza kuwa na msukumo

    mwingine kwa kuanzisha tukio lilelile (k.m., ili kuletesha uzuri). Mungu anao uwezo wa kufanya kazi

    ndani na kupitia viumbe vyake, pasipo kuvilazimisha kutenda nje ya mapenzi yao au shauku zao (hata

    wakati kusudio lake au nia yake ni tofauti na wa kwao) na pasipo Yeye mwenyewe kutenda dhambi

    (hata wakati viumbe vyake vinatenda, kusema ukweli, dhambi) (ona Mith 16:2). Kuuzwa kwa Yusufu

    kwenda Misri (Mwa 45:4-8; 50:20; Zab 105:17), kuvamiwa kwa Israeli na Ashuru (2 Waf 19:20-31;

    Isa 10:5-16), kuangamizwa kwa Yuda na Babeli (Ezek 11:5-12; Hab 1:5-11), kusalitiwa kwa Yesu na

    Yuda (Math 26:20-24; Yoh 6:64), hila ya Kayafa, kuhani wakuu, na Mafarisayo kumuua Yesu (Yoh

    11:47-53), na kusulubiwa kwa Yesu na Herodi, Pilato, Wamataifa, na watu wa Israeli (Isa 53:3-10; Mdo

    2:22-23; 4:27-28), ni mifano ya hili.

    Hii ni siri ambayo sisi hatuwezi kuieleweka kikamilifu, kwa sababu uhusiano wa Mungu

    muumba—asiye na mwisho, mwenye kujua yote, mwenye uweza wote—na viumbe vyenye mwisho si wa

    kawaida (m.y., hakuna tena kama hivyo) na si sawa na uhusiano ulivyo kati ya kiumbe na kiumbe

    mwingine. (Talbot 2005: audio message)2 Zaidi ya hayo, Mungu anajua kiundani kabisa hatima ya

    yote—kuchanganya na mwisho, na madhara ya moja kwa moja na yasiyo ya moja kwa moja ya muda

    mfupi, na ya muda mrefu ya kila neno, tendo, na matukio mengine. Kila kitu ni sehemu ya mpango

    mzima wa Mungu. Kwa hiyo Yeye kipekee kabisa ana sifa kujua lini kuanzisha na kuruhusu uovu na

    mateso na lini kutofanya hivyo. Matokeo yake, Yeye peke yake ndiye anayefaa kuruhusu uovu na mateso

    ambayo mtu aliye mwema (asiye na ufahamu mpana wa Mungu) atajaribu kuuzuia.

    Huenda siri kuu kuliko zote ihusuyo uovu na mateso, hata hivyo, ni kuwa Mungu alichagua kuja

    duniani na kibinafsi kukumbana na uovu na mateso ndani ya mwanadamu Yesu Kristo. Ingawaje Yesu

    mwenyewe alikuwa mwema na hakutenda dhambi, aliamua kuichukua dhambi na hatia, na kulipa

    gharama ya kudumu kwa ajili ya dhambi na hatia,yaw engine. “Katika upendo wake kwetu, Mungu

    alijihukumu mwenyewe mauti kwa niaba yetu. Kitu kimoja tusichopaswa kamwe kusema kuhusu

    Mungu—ni kusema haelewi jinsi ilivyo kuhusu kukataliwa vibaya, mateso mazito, na kufa kwa aibu. . . .

    Watu wengine hawaamini Mungu angeliumba dunia ambamo ndani yake watu wangeliteseka kiasi hiki.

    Je haishangazi zaidi kwamba Mungu angeliumba dunia ambayo hakuna mtu yeyote aliyeteseka zaidi

    kuliko yeye mwenyewe?” (Alcorn 2009: 214-15)3

    3. Ifuatayo ni mifano mingine ya Ki-Biblia inayoonyesha jinsi wote wawili, Mungu na visababisho

    vingine vinavyohusika katika uwanja moja, yakiwamo matukio yanayohusiana na dhambi na uovu:

    TUKIO LILILOFANYWA NA

    MUNGU

    LILILOFANYWA NA

    VITENDEA KAZI VINGINE

    Uumbaji wa wanyama

    Sara kupata mimba & kuzaliwa kwa Isaka

    Kufanikiwa kwa Yusufu akiwa mtumwa

    Mwa 1:25

    Mwa 21:1

    Mwa 39:3, 23

    Mwa 1:24

    Mwa 21:2, 5

    Mwa 39:3, 23

    2 Kifalsafa, neno linaloelezea uhusiano wa Mungu-mwanadamu ni “kuchukuliana”: Mungu kiuhakika ni mwenye enzi yote,

    bali uenzi wake hautendi kazi kwa jinsi ambayo majukumu ya kianadamu yanapotezwa au kuondoshwa (m.y., wanadamu

    hawageuzwi kuwa maroboti, au vinyago); vivyo hivyo, wanadamu ni viumbe vyenye kuwajibika kimaadili wawezao

    kufanya maamuzi na matendo halisi, yakiwamo kuasi kinyume na mapenzi ya Mungu yaliyofunuliwa, nao wanawajibishwa

    kisahihi kutokana na maamuzi na matendo hayo, lakini haya hayafanyiki kumfanya Mungu ni wa udharura kivile. Kwa

    maneno mengine, Mungu anao uwezo wa kujua kabla kwa uhakika kabisa; wanadamu, wao hutenda kile wakitakacho na

    wakichaguacho (m.y., Mungu hawalazimishi kufanya kinyume na matamanio yao na kutaka kwao), ila hawana uwezo kamili

    wa kutenda kinyume na mpango wa Mungu uliopangwa kabla . (Ona Carson 1994: 163-67, 201-22; Carson 1990: 199-227;

    Feinberg 2001: 625-796; Alcorn 2009: 258-69) 3 Kusulubiwa kwa Kristo pia huonyesha kiukamilifu kwamba mfungamano lazima uwe kweli ikiwa Mungu ni yote mawili

    mwenye enzi yote na ni mwema na watu wanao wajibu ki- haki kwa matendo yao. D. A. Carson anaelezea: “Ikiwa

    kisababisho kilikuwa mia kwa mia cha wala njama, na Mungu alikuja tu dakika za mwisho kujitwalia utukufu kutoka

    magego ya kushindwa kulikokuwa kunatarajiwa, basi msalaba haukuwa mpango Wake, makusudi yake, sababu hasa kwa

    nini Alimtuma Mwanaye duniani —na hayo hayafikiriki. Ikiwa kwa upande mwingine Mungu alikuwa akipangilia sana

    mambo kiasi kwamba maajenti wote wa kianadamu walikuwa vikaragosi, basi ni ujinga kuzungumzia mkakati, au hata

    dhambi—ambao kwamba hakuna dhambi za Kristo kuziondoa kwa kifo chake, basi kwa nini alipaswa afe? Mungu ki-enzi

    alikuwa kazini katika kifo cha Yesu; wanadamu walikuwa waovu katika kumuua Yesu, hata walipokamilisha mapenzi ya

    Baba; na Mungu mwenyewe akawa mwema kikamilifu.” (Carson 1990: 212)

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    11

    Kurudishiwa fedha kwa ndugu zake Yusufu

    Safari ya Israeli kutoka Misri

    Ugumu wa moyo wa Farao

    Israeli kuingia nchi ya ahadi

    Ndama wa dhahabu & Israeli kuabudu sanamu

    Utakaso wa Israeli & kuwa wakfu

    Kumshinda Sihoni

    Kumshinda Bashani

    Ushindi wa Yoshua

    Uwezo wa watu kupata utajiri

    Gideoni kuwashinda Wamidiani

    Samsoni kumuoa mwanamke wa Kifilisti

    Samsoni kuua Wafilisti 1000

    Benjamini kushindwa naIsraeli

    Watoto wa Eli kutomsikiliza

    Sauli awashinda Waamaleki

    Abigaili amwombea Nabali

    Ushauri wa Hushai wakubalika

    Daudi kuwashinda adui zake

    Daudi afanya dhambi kwa kuwahesabu watu

    Kifo cha Yoabu

    Kugawanyika kwa Israeli na Yuda

    Ahabu kwenda vitani & kumshinda Aramu

    Ahabu kwenda vitani auawa

    Kurudi kwa Rabshakehi kwao na kifo chake

    Kifo cha Sauli

    Kuvamiwa kwa Yuda na Wafilisti &Waarabu

    Kushindwa kwa Yuda & kifo chaAmazia

    Maandalizi ya hekalu kwa ibada mpya

    Kushindwa kwa Yuda & kifo cha Yosia

    Mungu kunena kupitia manabii wake

    Kuangamizwa kwa Yuda na Babeli

    Kutangazwa Wayahudi waweza kurudi

    Yerusalemu na kujenga upya hekalu

    Ezra apata kibali

    Nehemia apata kibali

    Mipango ya adui za Wayahudi kuharibika

    Kujengwa upya kuta za Yerusalemu

    Majaribu ya Ayubu

    Kuumbwa kwa watu

    Kushindwa kwa adui za Daudi

    Kukua kwa mimea

    Kujenga nyumba au tukio lolote

    Kulinda mji

    Mipango ya watu, maneno, na matendo

    Maamuzi ya wanadamu

    Kuvamiwa kwa Yuda na Waashuri

    Kuangamizwa kwa Israeli

    Kuangamizwa kwa Babeli

    Kuangamizwa kwa Misri

    Kufanikiwa kwa Tiro

    Baruki & Yeremia wamkwepa mfalme

    Gogi avamia Israeli

    Kutupwa kwa Yona baharini

    Kujengwa upya hekalu Yerusalemu

    Kuandikwa & ushuhuda wa Biblia

    Watu kuja kwa Kristo kwa wokovu

    Matendo ya haki ya waamini

    Wokovu kwa watu wa Korintho

    Mwa 42:27-28

    Kut 3:7-8

    Kut 4:21;7:3; 9:12; 10:1, 20,

    27

    Kut 23:23, 29-30; Kumb 7:1-2

    Kut 32:1-8; Mdo 7:39-41

    Law 20:8

    Kumb 2:30-31, 33, 36

    Kumb 3:2-3

    Kumb 3:21-22

    Kumb 8:18

    Waamuzi 7:7, 9, 14-15

    Waamuzi 14:4

    Waamuzi 15:18

    Waamuzi 20:28

    1 Sam 2:25

    1 Sam 15:2

    1 Sam 25:32

    2 Sam 17:14

    2 Sam 22:18-20, 40-42, 48-49

    2 Sam 24:1

    1 Waf 2:32-33

    1 Waf 12:22-24

    1 Waf 20:13, 28

    1 Waf 22:19-23

    2 Waf 19:6-7

    1 Nyak 10:14

    2 Nyak 21:12-16a

    2 Nyak 25:14-16

    2 Nyak 29:36

    2 Nyak 35:20-21

    2 Nyak 15-16

    2 Nyak 36:15-17; Yer 21:8-10

    2 Nyak 36:22; Ezra 1:1; 6:14

    Ezra 7:6, 9-10, 27-28

    Neh 2:8

    Neh 4:15

    Neh 6:16

    Ayubu 1:12, 21-22; 2:6

    Ayubu 10:8; 31:15;

    Zab 18:17-19, 43a, 47-48

    Zab 104:14a-b

    Zab 1271a

    Zab 127:1c

    Mith 16:1b, 9b

    Mith 16:33b

    Isa 7:17-20; 8:5-8

    Isa 9:8-21

    Isa 13:1-5

    Isa 19:1, 2a, 4a

    Isa 45:1-7

    Yer 36:26

    Ezek 38:1-6, 16

    Yona 2:3

    Hag 1:14

    Yoh 5:37-39; 2 Tim 3:16

    Yoh 6:37, 44, 65; Mdo 13:38

    Yoh 3:21; Waef 2:10; Wafil

    2:13

    Mwa 42:25

    Kut 3:10

    Kut 7:14, 22-23; 8:15; 9:34

    Kut 23:24, 31; Kumb 7:2

    Mdo7:42

    Law 20:7-8

    Kumb 2:32-36

    Kumb 3:1, 3-6

    Kumb 3:28

    Kumb 8:18

    Waamuzi 7:16-22

    Waamuzi 14:1-3

    Waamuzi 15:14-16

    Waamuzi 20:29-48

    1 Sam 2:22-25

    1 sam 15:3-6

    1 Sam 25:14-31

    2 Sam 17:5-14

    2 Sam 22:38-39, 43

    2 Sam 24:10, 17; 1 Nyak 21:1-4

    1 Waf 2:31, 34

    1 Waf 12:16-20

    1 Waf 20:14-21, 29-30

    1 Kgs 22:29-37

    2 Waf 19:7

    1 Nyak 10:4

    2 Nyak 21:16b-17

    2 Nyak 25:17-28

    2 Nyak 29:5-35

    2Waf 23:29; 2 Nyak 35:22-24

    2 Nyak 15-16

    2 Nyak 36:17-19; Yer 21:8-10

    2 Nyak 36:22-23; Ezra 1:1; 6:14

    Ezra 7:6, 9-10, 27-28

    Neh 2:7-9

    Neh 4:11-14

    Neh 3:1-32; 4:6, 21-22; 6:3, 15

    Ayubu 1:13-19; 2:7

    Mwa4:1; 5:3; Ayu 14:1; Zab 51:5

    Zab 18:37

    Zab 104:14c

    Zab 127:1b

    Zab 127:1d

    Mith 16:1a, 9a

    Mith 16:33a

    Isa 7:17-20; 8:5-8

    Isa 9:8-21

    Isa 13:1-5

    Isa 19:2b-3, 4b

    Isa 45:1-7

    Yer 36:19

    Ezek 38:7-16

    Yona 1:15

    Hag 1:14

    Yoh 5:46-47

    Yoh 6:37, 44, 65; Mdo 13:38

    Yoh 3:21; Waef 2:10; Wafil 2:12

    Mdo 18:9-10a

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    12

    Kuokoka kwa Sauli & manahodha katika meli

    Kuhubiri Injili

    Kuteswa kwa Wakristo

    “Miiba ya” Paulo katika mwili

    Kuhifadhiwa kwa watakatifu

    Watu wafuatao “watu waovu”

    Watu wapendako kwenda & na yale

    wayafanyayo

    Matendo ya “kahaba,” “wafalme kumi,” na

    “mnyama” wa Ufunuo

    Mdo 18:10b

    Mdo 27:21-44

    1 Wakor 2:4

    1 Wakor 4:7-11; Rev 6:9-11

    2 Wakor 12:7-9

    1 Wathes 5:23-24

    2 Wathes 2:11

    Yak 4:13-15

    Ufu 17:17

    Mdo 27:21-44

    1 Wakor 2:4

    1 Wakor 4:7-11; Ufu 6:9-11

    2 Wakor 12:7

    1 Wathes 5:12-22

    2 Wathes 2:9-10, 12

    Yak 4:13-15

    Ufu 17:1-16

    4. Mtu mwingine anaweza kutazama swala la Mungu kuruhusu dhambi na uovu kutokea kwa mantiki ya

    uhusiano wa jua na giza na baridi. “Kuna tofauti kubwa kwa Mungu kuhusiana na hivyo, kwa ruhusa,

    yake katika tukio au tendo, ambalo, kwa jinsi lilivyo na sura yake, ni dhambi, (ingawaje tukio hilo bila

    shaka litafuatana na ruhusa yake,) na kwa yeye kuhusika katika hilo kwa kulizalisha na kuongoza tendo

    la dhambi; au katika ya yeye kuamuru kitu fulani kiwepo, kwa kutokukizuia, katika mazingira fulani, na

    kwa yeye kuwa mtendaji au mmiliki astahiliye, kwa kutumika kiuzuri au kiuwezeshwaji. . . . Kama

    kulivyo na utofauti mkubwa kati ya jua kuwa chanzo cha ile nuru na ujoto wa anga, na uangavu wa

    dhahabu na almasi, kwa uwepo wake na athari njema za kuwepo kwake; na kwa kuhusiana na hiho hilo

    kunakuja giza na baridi kali, usiku, kwa mwenendo wake, itokeapo linazama kwenye miisho ya dunia.

    Mwenendo wa jua ni sababisho la aina ya matukio yanayofuatia baadaye; lakini silo sababu halisi,

    uwezeshwaji, au mzalishaji wa hayo; ingawaje lazima yatokee kutokana na mwenendo wake, katika

    mazingira hayo: hakuna tena tendo lolote la Ki-Uungu kuwa ndiyo sababu ya uovu wa mapenzi ya

    kianadamu. Kama jua lingekuwa ndiyo chemchemi ya mambo hayo, kama lilivyo chemchem ya nuru na

    joto: na kisha kitu chaweza kujadiliwa kutokana na tabia ya ubaridi na giza, kwa kulinganisha na sifa za

    jua; na pia inaweza kabisa kukubalika kwamba, jua lenyewe ni giza na baridi, na ya kuwa miali yake ni

    myeusi na yenye ukungu. Lakini kwa kufanyika sababu si kwa vinginevyo zaidi ya kutokuwepo kwake,

    hakuna kitu kama hicho kiwezacho kuhusishwa, isipokuwa kinyume chake; yawezekana kiusahihi kabisa

    ukadai, kwamba jua ni angavu na lenye joto kali, ikiwa baridi na giza ni matokeo ya kutokuwepo kwake;

    na kadiri matokeo haya yanavyounganishwa na kuwajibishwa zaidi mara kwa mara na kutokuwepo

    kwake, ndivyo inavyotia nguvu zaidi hoja kwamba jua ni chemchemi ya nuru na joto. Kwa hiyo, kama

    ambavyo dhambi si tunda litokanalo kwa jinsi yoyote ile na utendaji mwema au uvuvio mzuri wa Aliye

    Juu sana, bali, kinyume chake, hutokana na kuzuilia matendo yake na nguvu, na katika mazingira fulani,

    hufuatia ulazima wa athari ya utendaji wake; hili si hoja kusema kuwa yeye ni wa dhambi, au utendaji

    wake ni wa uovu, au una lolote la asili ya uovu; bali kinyume chake, ni kuwa Yeye, na utendaji wake,

    pamoja ni mzuri na wa utakatifu, na kwamba yeye ni chemchemi ya utakatifu wote. Itakuwa ni hoja ya

    kustaajabisha, tena sana, kusema wanadamu hawafanyi dhambi, isipokuwa tu pale Mungu anapowaachia

    wenyewe, na kulazimika kutenda dhambi afanyapo hivyo, kwamba Mungu lazima awe wa asili ya

    dhambi: ndivyo itakavyokuwa hoja ya kustaajabisha, kwani siku zote ni giza jua linapokuwa limezama,

    na kamwe hakuwi giza wakati jua likiwapo, hivyo basi, giza lote latokana na jua, na kwamba mduara

    wake na miale yake lazima iwe myeusi.” (Edwards 1984, Freedom, §IX: 77)

    5. Mungu anaweza kuagiza jambo kwa mapenzi yake ya siri (au “ki-mamlaka”) ambayo mapenzi yake

    yaliyofunuliwa (au “mtazamo”) wake unakataza. “Mungu anao uwezo wa kuitazama dunia kwa vioo

    viwili. Anaweza kuiangalia kupitia kioo cha upeo mwembamba au kupitia kioo cha upeo mpana. Mungu

    atazamapo tukio lenye kuumiza au lililo ovu kupitia kioo cha upeo mwembamba, huona maafa au

    dhambi ilivyo yenyewe na huchukizwa na kuhuzunika. ‘Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye,

    asema Bwana Mungu’ (Ezek. 18:32). Lakini Mungu anapoliangalia tukio lenye kuumiza au lililo ovu

    kwa kupitia kioo chake chenye upeo mpana, huona maafa, au ile dhambi kuhusisha na kila kitu

    kilichosababisha na kitakachotokea kutokana nayo. Huona inavyounganika na mpangilio kuelekea

    umilele. Mpangilio huo, pamoja na sehemu zake zote (nzuri na mbaya) anazotaka ziwe (Zab 115:3).”

    (Piper 2000: 126) Kwa mfano, Ayubu alielewa kwamba mabaya yote yaliyompata kiuhalisia yalikuwa

    yamepangwa na kuruhusiwa na Mungu; kwa hiyo alimwelekezea kilio na kumbariki Mungu, ingawaje

    aliyesababisha moja kwa moja uovu ule alikuwa ni Shetani (Ayub 1:21-22). Mungu aliwatumia

    Waashuri kwa kuwaadhibu Waisraeli kwa dhambi yao, bali baadaye aliwaadhibu Waashuri kwa kiburi

    chao (Isa 10:5-19). Matokeo muhimu ya hili ni kuwa hugongana na wazo la falsafa ya majaliwa. Randy

    Alcorn states, “Ikiwa Mungu anaruhusu ubaguzi wa rangi, utumwa, na biashara za watoto kwa mambo ya

    ngono, basi kwa nini tupambane nayo? Sababu ni hii: Biblia hunena kwa kiwango kikubwa kuhusu uenzi

    wa umiliki wa Mungu, lakini bado mara kwa mara huhimiza watu kuchukua hatua, pia kuongelea na

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    13

    kuwasaidia masikini na wahitaji (ona, kwa mfano, Mithali 31:8-9)—hii ndiyo kona kinyume katika

    falsafa ya majaliwa.” (Alcorn 2009: 263)

    6. Uovu wote ambao Mungu anauruhusu na anauagiza hatima yake hutumika au kuleta wema mkubwa

    zaidi kwa uumbaji wenyewe. Paulo alisema, “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya

    kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake”

    (Rum 8:28). “Hakuna mantiki yoyote kufikiria, kwamba anaweza kukichukia kitu kama kilivyo, na

    kukiona tu kuwa kiovu, na bado ikawa ni mapenzi yake kitokee, akijua maafa yake yote. . . . Wanadamu

    hupenda dhambi kama dhambi, kwa hiyo ndio waanzilishi na watendaji wake: wanaipenda kama

    dhambi, na kwa makusudio mabaya na matokeo mabaya. Mungu hakusudii dhambi kama dhambi, au

    kwa kusudio la kitu chochote cha ubaya; ingawaje huwa ni furaha yake kuagiza mambo, ambayo, kwa

    kuyaruhusu, dhambi itakuja kutendeka, kwa makusudio ya uzuri au wema mkubwa zaidi, ambao kwa

    kutimia kwake yatakuwa ndio lengo. Kule kukubali kuachia mambo ili uovu uweze kutendeka, kama

    uovu: na kama ndivyo, basi hakuna sababu kwa nini asiweze kiuzuri tu kuuzuia uovu kama uovu, na

    kuuadhibu kama ulivyo.” (Edwards 1984, Freedom, §IX: 78-79; ona pia Piper 2000: 107-31; Edwards,

    Remarks, ch. 3: 525-43). Kwa mfano, Yusufu aliuzwa utumwani na ndugu zake lakini baadaye

    aliwaambia, “nanyi kweli mlinikusudia mabaya, bali Mungu aliyakusudia kuwa mema, ili itokee kuokoa

    taifa kubwa, kama ilivyo leo” (Mwa 50:20). Huenda mfano mkubwa zaidi kuliko yote ni kusulubiwa

    kwa Kristo. Yuda, Herodi, Pilato, na watu wengine wasiomcha Mungu walimsaliti, kumlaani, na

    kumsulubisha Kristo asiyekuwa na dhambi, na bado alikuwa ndiye Mungu aliyeagiza tukio hilo lifanyike

    kama njia ya kuleta masamaha ya dhambi, mabadiliko ya maisha, na upatanisho wa mwanadamu kwa

    Mungu (Mdo 2:22-23; 4:27-28). Kusema ukweli, Mungu huchukua huzuni zetu na kuzigeuza kuwa

    kuwa furaha (Zab 30:11; Yer 31:13; Yoh 16:20). Mateso yote ya dunia hii hayawezi kufananishwa na

    utukufu mkuu, usio na mwisho ambao Mungu atauleta nyakati za miisho (Rum 8:18-21; 2 Wakor 4:16-

    18; Ufu 21:1-4). “Tutakapoishi kwa amani kuu katika Nchi Mpya, ambako furaha itatawala anga la hewa

    tutakayoivuta, tutazama nyuma kuangalia dunia hii iliyopo na kuthibitisha si kwa imani, bali kwa kuona

    kwamba uovu na mateso yote yalistahili kabisa—na kwamba Kristo kutwaa mwili na ukombozi wake

    umeufanya ulimwengu kuwa bora milele” (Alcorn 2009: 195).

    7. Kwa vile Mungu ndiye wema mkuu zaidi ya wote uwezekanao kuweko, dhambi na uovu ni vya

    lazima ili hali zote za Uungu na tabia za Mungu ziweze kufunuliwa vizuri. Hatimaye, kila kitu

    alichokianzisha Mungu—zikiwamo dhambi na uovu—ni sehemu ya mpango mkuu, ulioandaliwa kabla

    ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, kudhihirisha utukufu wa Mungu, utukufu wa Kristo, na utukufu wa

    neema ya Mungu katika Kristo (ona, k.m., Zab 24:1-10; 148:1-13; Yoh 11:1-4; 13:31-32; 17:1-5, 22-

    24; Rum 5:12-21; 8:28-29; 9:19-23; 11:32-36; Waef 1:3-6; Wafil 2:6-11; 2 Tim 1:8-9; Heb 2:9-10;

    Ufu 13:8; 15:3). “Ni jambo jema na zuri kabisa kwa utukufu wa Ki-Ungu kung’ara; na kwa sababu hiyo

    hiyo, ni vyema kwamba uangavu huo wa utukufu wa Mungu uwe kamili; yaani, sehemu zote za utukufu

    wake zing’are, kwamba uzuri wote uwe kimlingano unaangaza, kwamba mhusika awe na sura halisi ya

    Mungu. Si vyema kwamba utukufu moja udhihirishwe kupita kiasi, na mwingine usiwepo kabisa; maana

    hapo, kule kung’ara hakutaleta uhalisia. Kwa sababu hiyo hiyo si sahihi moja udhihirishwe kupita kiasi,

    na mwingine kidogo sana. Ni vyema sana ule uangavu wa Mungu utoe majibu ya unyofu wake wenyewe;

    kwamba ile enzi ya kiutukufu iwajibike kwa utukufu halisi na ulio muhimu, kwa sababu hiyo hiyo ni

    vyema na bora kabisa kwa Mungu kujitukuza mwenyewe kabisa. Kwa hiyo ni lazima, kwamba ukuu wa

    Mungu usioneneka, mamlaka yake na enzi yake ya kutisha, haki yake, na utakatifu, udhihirishwe. . . .

    Kama isingelikuwa ni vyema kwamba Mungu aagize na kuruhusu na kuiadhibu dhambi, kusingekuwa na

    udhihirisho wa utakatifu wa Mungu katika kuchukia dhambi, au katika kuonyesha lile alipendalo, katika

    upaji wake, katika uchaji mbele zake. Kusingekuwa na udhihirisho wowote wa neema ya Mungu au ucha

    Mungu wa kweli, kama kusingekuwa na dhambi za kusamehewa, hakuna maafa ya kuokolewa kwayo. . .

    . Huwa tunajali kidogo mno kiasi gani hisia ya wema inavyoinuliwa kutumia hisia ya uovu, kwa yote

    mawili–kihamasa na kiasili. Na kama ilivyo lazima kuwe na uovu, kwa sababu kuonekana kwa utukufu

    wa Mungu kusingelikuwepo na kusingekamilika, kama uovu usingalikuwepo, kwa hiyo uovu ni wa

    lazima, ili kufikia kiwango cha juu kabisa cha furaha ya kiumbe, na kukamilika mawasiliano ya Mungu,

    ambayo kwayo aliuumba ulimwengu, kwa sababu furaha ya kiumbe hujumuishwa katika kumjua Mungu,

    na hisia ya upendo wake. Na ikiwa kumjua yeye kutakuwa hakujakamilika, furaha ya kiumbe lazima iwe

    haina uwiano kimlingano.” (Edwards 1986, Remarks, ch. 3: 528; ona pia Piper 1997: n.p.; Erlandson

    1991: n.p.; Edwards 1984, The End: 94-121; Piper 2003a: 17-50; Piper 2003b: 17-35)

    B. Adamu na Hawa watenda dhambi na kufukuzwa kutoka bustani ya Edeni (Mwanzo 3).

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    14

    1. Biblia inaweka bayana kwamba Shetani “alianguka” kabla ya dhambi ya Adamu na Hawa, kwa vile

    Shetani ndiye aliyewajaribu Adamun a Hawa na kuwadanganya kuhusu sababu na matokeo ya kula tunda

    la mti wa ujuzi wa mema na mabaya (fananisha Mwa 2:16-17 na Mwa 3:1-4). Kwa hiyo, Yesu alimwita

    Shetani yote mawili, “muuaji tangu mwanzo” na “mwongo na baba wa huo” (Yoh 8:44-45).

    2. “Ujuzi wa mema na mabaya” (Mwa 2:17) huwakilisha uhuru wa kimaadili na kujitawala.

    a. Ule “mti wa ujuzi wa mema na mabaya” haukuwa mti wa kiuchawi ambao ulizaa ujuzi wa

    mema na mabaya kwa kila mtu aliyeula. “Inaelekea sana kwamba Mungu aliuandaa huo mti

    kama uwigo wa mpaka, kama njia ya kuonyesha tofauti kati ya mema na mabaya. Kwa maneno

    mengine, uchaguzi wa Adamu na Hawa haukuwa kati ya kutokujua na kujua mema na mabaya,

    bali katika kubakia wema na wenyewe kuwa wabaya. Sura ya mtihani ilikuwa kwamba lolote

    watakalolichagua, watakuja kujua mema na mabaya. Walikuwa viumbe vya kimaadili ambavyo

    vingejua yaliyo sahihi na yasiyo sahihi kwa kutumia mwitikio wao binafsi kwa Mungu.”

    (Goldsworthy 1991: 98) Kama wangefaulu mtihani huo, kule kumtegemea na kumtii Mungu

    kungeliuthibitisha wema wao, na wangelilijua hilo. Kama wangelishindwa mtihani huo,

    kutomtegemea na kutokumtii Mungu kungeliwageuza kuwa watu wenye uovu kwenye kiini

    kabisa cha uanadamu wao, na wangelilijua hilo pia.

    b. Katika vifungu Fulani vya AK (2 Sam 4:17; 1 Waf 3:9) maneno “mema na mabaya”

    huzungumzia kimsingi uwezo wa kuchukua hatua kisheria. Kwa hiyo, kilichokuwa kimekatazwa

    kwa mwanadamu kilikuwa ni ule uwezo wa kuamua nini kiwe kwa ajili ya manufaa yake na nini

    kisiwe hivyo. Mungu hakutoa maamuzi ya aina hiyo kwa mwanadamu, kwa sababu ni Mungu

    pekee ndiye ajuaye yote, mwenye hekima yote, na mwenye upendo wote. Kwa hiyo, ni Mungu

    pekee anaweza kufanya uamuzi sahihi na wenye upendo kwa ajili ya manufaa ya mwanadamu

    ya kweli, wakati wote. Mwanadamu atendapo katika hali ya kujitawala mwenyewe, hujiweka

    nafsi yake mwenyewe kuwa mhimili wa kati kwa miongozo yake ya kimaadili na hujiamulia nini

    chema na nini kibaya. Hivyo hujaribu kuwa “kama Mungu” (ona Mwa 3:5, 22). Hata hivyo,

    kwa vile mwanadamu hajui yote, hana hekima yote, na hana upendo wote, juhudi zake za kuwa

    kama Mungu ni dhahiri zitashindwa. Badala yake, ataishia kutenda zaidi kama “mungu wa dunia

    hii” (2 Wakor 4:4), na matokeo yanayofanana nayo.

    3. Shetani alimwingia nyoka na kumdanganya Hawa (Yoh 8:44; 2 Wakor 11:3; Ufu 12:9). Adamu

    alikuwapo pamoja naye, hakufanya lolote kujaribu kumzuia, na, yeye pasipo kudanganywa, alikubali kwa

    hiari kabisa kumfuata mkewe katika dhambi (Mwa 3:6; 1 Tim 2:14). Kama James Boice

    anavyobainisha, “Ikiwa Adamu hakudanganywa, kama 1 Timothy 2:14 pasemavyo bayana, basi ni lazima

    awe alifanya dhambi kwa kujua kikamilifu kile alichokuwa anakifanya. Hilo maana yake, aliamua kula

    kwa kukusudia kabisa kutomtii Mungu.” (Boice 1986: 196) Hilo laweza kuwa sababu kwa nini dhambi

    ya Adamu ni kubwa zaidi, na kwa nini matokeo yaliyowajia wanadamu wote baadaye husemekana

    kutokana na dhambi ya Adamu na siyo ya Hawa (ona Rum 5:12-14, 17-21; 1 Wakor 15:21-22).

    4. Mbinu ya Shetani ni kielelezo cha majaribu yanayotukabili.

    a. Alimjia Hawa kwanza. Huo ulikuwa ni ujanja wa juhudi za kujaribu kumdanganya mtu

    ambaye hakupokea maagizo moja kwa moja kutoka kwa Mungu, na kumgonganisha mtu moja na

    mwingine

    b. Alilenga jambo pekee ambalo Mungu alikuwa amelikataza. Licha ya Mungu kutoa mahitaji

    yote kwa wingi mkuu, kwa kule kukazia kitu pekee ambacho hawakutakiwa kukifanya, Shetani

    ndipo kama matokeo yake alipandikiza wazo ambalo limepotoka au lililokengeuka kuhusu

    uhalisi katika akili zao.

    c. Alitafuta kuingiza mashaka kwenye kweli ya Neno la Mungu (3:1). Kwa kuuliza “ati Mungu

    [kweli] alisema, ‘msile matunda ya miti yote ya bustani?’” Shetani alitafuta kuingiza mashaka na

    kupandikiza kuchanganyikiwa kuhusu kile ambacho alikitaka Mungu.

    d. Alidanganya na kuligeuza Neno la Mungu (3:4). La kushangaza, ukweli mmoja ndio Shetani

    aliushambulia kuhusiana na ghadhabu ya Mungu na madhara ya dhambi. Kama ilivyokuwa kwa

    Adamu na Hawa, tunakabiliwa na uamuzi: nani tumwamini? Kwa mbinu za Shetani (na za

    kidunia), Neno la Mungu halikubaliwi tena kama kweli inayojieleza yenyewe, bali limefanywa

    kuwa ngazi ya neno la kiumbe. Yote mawili–Mungu na Neno lake huonekana kuwa na mamlaka

    ya chini zaidi ambayo lazima yapimwe na mamlaka iliyo juu zaidi. Kwa mara nyingine, ujanja

    wa nyoka: haupendekezi wanadamu wamwachie Mungu enzi yake mwenyewe, bali wao

    wenyewe tu waangalie na kutathmini madai ya Mungu kuhusu kweli. Matokeo ya mwisho

    yalikuwa sawa tu na kumweka Shetani awe Bwana, lakini hayo hufanyika pasipo mwanadamu

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    15

    kuelewa.” (Goldsworthy 1991: 104)

    e. Ailzijumuisha sifa za Mungu mwenyewe (3:5). Kimsingi, Shetani alikuwa anasema kwamba

    Mungu alikuwa hana upendo kwa kuwazuia Adamu na Hawa vitu vya kula, na alikuwa hana

    upendo kwa kuvitaka viumbe vyake kumtegemea yeye kwa maarifa ya mema na mabaya, badala

    ya kufanya maamuzi hayo wenyewe.

    f. Alichochea kiburi cha kianadamu. Shetani alimwahidi Hawa kwamba kwa kumuasi Mungu

    angelikuwa na uzima (“hakika hutakufa”), maarifa (“na macho yako yatafumbuka”), furaha

    kutokana na hali ya kuinuka (“utakuwa kama Mungu”), na ukuu wa kujitawa kimaadili (“kujua

    mema na mabaya”). Kinyume chake, hata hivyo, kwa Adamu na Hawa kufanya maamuzi kwa

    njia yao wenyewe (m.y., kujitawala kimaadili) ni sura ya kifo kwa sababu ni kutengwa mbali na

    Mungu. Kwa hiyo, kiini cha dhambi yao kilikuwa kutokuamini (m.y., kukosa imani na tumaini

    kwa Mungu, kunakodhihirishwa kwa kumtii Mungu). Hata tangu mwanzo, mpango wa Mungu

    ulikuwa kwamba watu wamwangalie yeye na kumtumaini yeye kwa ajili ya kweli kuhusu nini ni

    chema na nini kibaya, na kwa vipi tunatakiwa kuishi maisha yetu—m.y., “mwenye haki ataishi

    kwa imani” (Hab 2:4; Rum 1:17; Wagal 3:11; Waeb 10:38).

    5. Dhambi ya Adamu na Hawa iliwadhuru si wao tu, bali kila mtu katika historia yote.

    a. Badala ya kuleta furaha na utoshelevu, Adamu na Hawa walileta hukumu, aibu, hofu,

    kufarakana na Mungu, uumbaji wote, wao kwa wao, na hatimaye mauti. (Mwa 3:7-19). Adamu

    na Hawa walitaka kujitawala (m.y., uhuru; kutengwa na Mungu), na wakapata hayo. Hata hivyo,

    kujitenga huko na Mungu ni sura ya kifo na mauti. Kutokana na kile walichokifanya, Adamu na

    Hawa kwanza walijikuta na aibu kuhusiana na hali yao ya kuwa uchi (Mwa 3:7-10). Hali yao ya

    kijinsia ingeliwakumbusha kwamba wao hawakuwa kama Mungu: hawakuwa na uwezo wa

    kuumba pasipo kutumia chochote (kama Mungu), bali tu waliweza kuzaa. “Hivyo hali yao ya

    ujinsia ilikuwa iwakumbushe [au ingepaswa iwakumbushe] juu ya uhuru wao na changamoto

    zake [au ingetoa changamoto] kwa fikira zao za uhuru na hali yao ya kuwa kama Mungu”

    (Goldsworthy 1991: 105).4 Kama matokeo ya mkondo ulioanzishwa bustanini, Mungu mara zote

    huwaachia watu waamue wenyewe njia zao na kisha kubeba madhara yao wenyewe (ona Kut

    16:1-20; Hes 11:18-20, 31-34; Rum 1:24, 26, 28).

    b. Adhabu ambayo Mungu aliiagiza (Mwa 3:16-19) kwa mwanaume (kazi inafanyika ngumut)

    na mwanamke kuzaa watoto kunakuwa kwa uchungu) zote zahusiana na uwajibikazi kimaisha

    kwa wanaume na wanawake. Zaidi ya hapo, Mwa 3:16b panaonyesha mwanzo wa mgongano

    wa kindoa na/au mvutano wa madaraka ya kindoa—tangu sasa na kuendelea, uhusiano kati ya

    waume na wake utakuwa una harufu ya dhambi (ona, k.m., kufuatia kwa mawazo mbali mbali

    yahusuyo namna ya mwingiliano kati ya “kutamani” na “kutawala” katika 3:16: Busenitz 1986:

    203-12; Cassuto 1961: 165-66; Walton 2001: 227-28; Stitzinger 1981: 41-42; Foh 1974-75: 376-

    83).

    c. Dhambi ya Adamu huathiri uumbaji wote. “Uumbaji upo hapo kwa ajili ya manufaa yetu.

    Unyenyekevu ni uwakilishi wa uumbaji wote ili kwamba Mungu aushughulikie uumbaji kwa

    msingi wa anavyoshughulika na wanadamu. . . . Mwanadamu aangukapo kwa sababu ya dhambi,

    uumbaji hufanywa kuanguka pamoja naye.” (Goldsworthy 1991: 96) Zaidi ya hapo, Adamu

    hupata baadhi ya dawa zake: kama tu jinsi alivyoasi kinyume na utawala wa Mungu, sasa

    uumbaji wote, ambao anatakiwa kuutawala, utamwasi kinyume naye. “Laana ardhini kusema

    kweli ni laana kwa Adamu. Mfalme wa dunia sasa hana mtumishi anayemtii ardhini. Uhuru wa

    kula miti yote katika bustani unabadilishwa na kwa masumbufu kuifanya dunia itoe mkate

    unaolazimika kila siku. . . . Mwisho wa mwanadamu ni kuipa ardhi mbolea kwa yeye kuurudia

    mavumbi ambako alitokea.” (Ibid.: 106)

    d. Biblia huona watu wote kuwa kama moja na Adamu (“katika Adamu”), Adamu akitenda

    kama kichwa chetu au mwakilishi wetu (ona Rum 5:12-19; 1 Wakor 15:21-22; nk., Waeb 7:9-

    10). Hatimaye, kama matokeo ya dhambi ya Adamu, kizazi chote cha mwanadamu kinapokea:

    “uhalali” wa kuwa na hatia dunia nzima, kunakoongoza kwenye kuharibika kimaadili dunia

    nzima (Zab 51:5; Yer 17:9; Rum 3:9; 7:14-25), kunakoongoza kwenye dhambi ya mtu moja

    moja dunia nzima (Rum 3:10-18, 23), kunakoongoza kwenye hatia ya mtu moja moja. Jinsi

    kamili ya namna ilivyokuwa na kwa nini na vizazi vya Adamu vimehesabiwa hatia na kuwa na

    4 Baada ya Hawa “kutwaa na kula” (Mwa 3:6), Yesu kristo ilibidi aonje umasikini na mauti kabla ya maneno “twaa, kula”

    (Math 26:26) kufanyika maneno ya wokovu badala ya mauti.

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    16

    uharibifu mkubwa kutokana na dhambi ya Adamu, ni swala la mjadala. Zifuatazo ni baadhi ya

    fikira zifikiriwazo:

    (1) Biblia siku zote hutazama makundi ya watu kama mtu “moja aliyekamilika” (ona

    Yosh 7:10-26; Rum 5:12-19; 1 Wakor 15:21-22). Hii ni sawa na kumtazama Adamu

    kama mbegu au mzizi wa mti, na uzao wake kama matawi na majani: Vyote ni mti moja;

    matawi na majani hupokea yote mawili - uzima na sura kutoka kwa ile mbegu na mzizi.

    Adamu, kama kichwa cha kizazi chote, huzalisha viumbe vilivyoanguka, vyenye uasi,

    kama vile yeye alivyifanya dhambi. Hali ya Adamu kama kichwa “huhusisha fursa za

    ndani zaidi kuliko ubaba wa kikawaida. Huhusisha utukuzaji wa kuelezea nini

    kinamaanisha kuwa mwanadamu [ona Mwa 5:3; 1 Wakor 15:49]. . . . Ikiwa wahusika

    wanataka kuasi, je wasimamie wapi ili kufanya hilo? Sioni msingi wowote wa wao

    kusimamia, hakuna kitovu cha madai yao, uhuru wao binafsi hauko huru, mshabihiano

    wenye kujitegemea. Mungu ndiye aliyeuumba kama vile alivyowaumba, ndani na kupitia

    Adamu, kama sehemu ya sifa za Adamu.” (Blocher 1997: 130)

    (2) Kwa vile Adamu aliumbwa pasipo dhambi na alikuwa na kila fursa na mazingira

    yake binafsi, hakukuwa na mtu bora zaidi yake wa kuwakilisha wanadamu katika ujumla

    wao. Kama mwakilishi wetu, dhambi ya Adamu, na hivyo hata kukosa kwake,

    kuliwekezwa kwetu (ona Johnson 1974: 298-316). Hali ilivyo ni kama taifa: “itokeapo

    mkuu wa nchi akitangaza vita na taifa jingine, watoto wote wanao zaliwa wakati huo wa

    vita huwa wako vitani na taifa jingine. Katika swala la Adamu, maafa hutenda kazi kwa

    kina cha ndani zaidi, kwa sababu mshikamano wetu wa ki-Adamu (yaani, uanadamu) ni

    muhimu zaidi na, kwa vile uhusiano ni kwa Mungu ‘ambaye tunaishi na kuenenda na

    kuwa na uhalisi ndani yake’.” (Blocher 1997: 129).

    (3) Ilikuwa lazima kabisa kwa Mungu kufanya kitu fulani kwa watu wote ili wawe na

    uharibifu kama matokeo ya dhambi ya Adamu. “Ni kutoa katika yaliyojitokeza, kama

    ilivyokuwa sahihi na lazima kwa kiwango cha juu sana afanye hivyo, kutoka kwa huyo

    mwanadamu mwasi, na kanuni zake za kiasili zikiwa zimeachwa zenyewe, kwatosha

    kumfanya awe mharibifu kabisa na aliyepindana kutenda dhambi kinyume na Mungu”

    (Edwards, 1984, Original Sin: 219).

    e. Matokeo ya anguko, na utu wetu “katika Adamu,”ni kwamba kwa jinsi yetu wenyewe, pasipo

    Kristo, tunakuwa “wafu katika makosa na dhambi zetu” (Waef 2:1). Hii inamaanisha kwamba

    kuna upungufu kupita kiasi au uharibifu kuhusiana na kila mtu (pia huitwa nguvu ya dhambi

    ikaayo ndani) ambayo huathiri kila kitu ndani yetu, kuchanganya hata jinsi tunavyofikiri,

    kuwaza, kuongea, kutenda, kujisikia, na mahusiano na watu na kwa Mungu. Matokeo ya

    uharibifu huu ni kuwa, nje ya msaada wa Kristo, tunakuwa: hatuna uwezo kabisa kumjia Kristo

    na kumwamini yeye (Yoh 6:44, 65; Waef 2:8-9); hatuwezi kabisa hata kuuona ufalme wa

    Mungu (Yoh 3:3, 5); hatuwezi kabisa kujitoa kwa sheria ya Mungu na kumtii (Rum 8:6- 8);

    hatuwezi kabisa kuelewa kweli za kiroho kumhusu Mungu (1 Wakor 2:14); hatuwezi kabisa

    kumpendeza Mungu (Waeb 11:6); tunakuwa watumwa wa dhambi, dunia, mwili, na Ibilisi,

    hatuna kabisa uzima wowote ule, na tunapaswa ghadhabu ya Mungu na hukumu yake (Rum

    6:16-17; Waef 2:1-3) (ona pia Edwards, 1984, Original Sin: 143-233; Owen 1979: passim).

    6. Hata katika hukumu yake kwa Adamu na Hawa, Mungu alidhihirisha neema yake.

    a. Alitengeneza mavazi ya kuwatosha ya ngozi ya wanyama ili kuwavika Adamu na Hawa (Mwa

    3:21).

    b. Ingawaje Mungu alimfukuza Adamu na Hawa kutoka bustanini (Mwa 3:22-24),

    hakuuondolea uwakili wao juu ya hii dunia (fananisha Mwa 2:15 na 3:23). Bila shaka,

    kufukuzwa kwao kutoka bustanini kulisaidia kukamilika kwa mpango wa Mungu wa

    mwanadamu kuijaza na kuimiliki dunia (Mwa 1:28).

    c. Katika Mwa 3:15 alitoa tamko la kwanza la mpango wake wa wokovu kwa dunia: “Nami

    nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo

    utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino.” Mtu fulani kati ya uzao wa mwanamke

    (amekuwa akitajwa kama mzao wa Ibrahimu [Kristo]) atatoa pigo la kichwa na kuleta ushindi

    kwa Shetani msalabani, wakati Shetani atamponda kisigino, au kumsababisha ateseke. Tamko

    hili limetekelezeka hatua kwa hatua katika Biblia nzima yote. Bila shaka, tamko hilo,

    likijumuishwa na swala kwamba Adamu na Hawa wasile kutoka katika mti wa uzima (Mwa

    3:22), kuliwahakikishia kuwa wasingeweza kuishi milele wakiwa katika dhambi. Badala yake,

  • Copyright © 2009-2015 by Jonathan Menn. All rights reserved.

    17

    kama Mungu alivyofunua hatua kwa hatua mpango wake, wale waishio kwa imani katika Kristo

    wataweza kula kutoka kwenye mti wa uzima katika nchi mpya milele katika haki (Ufu 22:2).

    C. Matokeo ya Anguko—kutoka kwa Kaini hadi Mnara wa Babeli (Mwanzo 4-11:26)

    “Baada ya Adamu na Hawa kutenda dhambi, uzao uliowafuatia uliendelea kuitawala dunia. Tatizo

    halikuwa kama walikuwa hawatawali. Kinyume chake, Mwanzo 4 panaonyesha michango yao katika ubunifu wa

    muziki, ufuaji vyuma, ufugaji, ustadi wa ujenzi, na siasa (‘Kaini akajenga mji, mst. 17). Tatizo kuu la

    mwanadamu mwenye dhambi halijawahi kuwa kukataa kwake kuitawala dunia. Tatizo lake kuu ni kwamba

    huitawala dunia katika namna isiyomcha Mungu. Mwanadamu huyu wa asili ya ki-Adamu hutawala ili kujifanyia

    jina mwenyewe, siyo kwa kulitukuza jina la Bwana. Wanadamu wadhambi hujaribu kutawala wakati wao

    wenyewe ni watumwa wa dhambi na Shetani. Mungu aliwaumba Adamu na Hawa ili wajenge nakala ya ule Mji

    Wake hapa duniani. Wazao wao wakajenga mji uliopotoka wa Mwanadamu.” (Leithart n.d.: n.p.)

    1. Kaini na uzao wake (Mwa 4:1-24).

    a. Kwa Kaini twaona kuongezeka kwa dhambi: kukufuru5 (4:3); hasira (4:5); wivu, udanganyifu,

    na mauaji (4:7-8); uongo (4:9); kujitafutia binafsi na kujihurumia (4:13-14); kukengeuka kutoka

    kwa Mungu (4:14, 16). Kuongezeka kwa dhambi pia kunaonekana kwamba Kaini siyo tu

    hakumuua kila mtu, bali alimuua ndugu yake mwenyewe ambaye alikuwa mtu “mwenye haki”

    (Math 23:35; Waeb 11:4). Pia, hata hivyo, angalia neema ya Mungu kwa Kaini katika kumlinda

    ili asiuawe na ndugu zake wengine wa kike na wa kiume (Mwa 4:15).

    b. Uzao wa baadaye wa Kaini, Lameki (4:18-19, 23-24) apelekea uharibifu kimaadili kuwa

    kiwango cha chini kabisa: ana kiburi na majivuno; ageuza mgongo wake kwa mpango wa

    Mungu wa mke moja (Mwa 2:23-24; Math 19:3-6). Wake wengi siyo mpango sahihi wa

    Mungu. Katika Biblia kuwa na wake wengi mara zote kumeonekana kuwa siyo sahihi, na

    kuliongoza kuletesha matokeo mabaya. Kwa hiyo, haishangazi kwamba hata aliyeanzisha kuwa

    na wake zaidi ya moja, Lameki, ni mtu mkali aliyejipatia uhuru wake kamili kutoka kwa Mungu

    kwa kuua watu kwa visasi vya maswala madogo madogo na kudai haki ya Mungu ya kulipa

    kisasi (ona Kumb 32:35). Madai yake makali ya kutaka kulipa kisasi kwa wengine “mara sabini

    na saba” (Mwa 4:24) hupata mkondo mwenza katika kauli ya Kristo kuwa tunatakiwa

    kuwasamehe wengine “mara sabini na saba” (Math 18:21-22).

    2. Tangu Seti hadi Nuhu (Mwa 4:25-6:8).

    a. Moja ya sifa kuu za kitabu cha Mwanzo ni matumizi ya vichwa vinavyofanana katika

    kutambulisha simulizi na vizazi ambavyo hubadilishana katika Kitabu kizima. “Hivyo hutokea

    katika 2:4; 5:1; 6:9; 10:1; 11:10, 27; 25:12, 19; 36:1, 9; 37:2. Kitu kinachofanana kote katika

    vichwa hivi vyote ni neno la Kiebrania [Toledot—ambalo kikawaida hutafsiriwa kama “kizazi

    (vizazi); uzao; hesabu; orodha; kumbu-kumbu”]. . . . Hivyo vichwa [Toledot] hutenda kazi mbili.

    Kwanza, huwa kama vichwa vya sura katika vitabu vya kisasa. Baadhi yao hutambulisha sehemu

    kuu za simulizi, kuonyesha hatua mpya ya kukua kwa mpango. . . . [Pili, hivyo vichwa vya

    Toledot] hukazia mtazamo wa msomaji kwa mtu maalum na watoto wake aliowazaa.

    Humwezesha mwandishi wa Mwanzo kufuatilia mema ya mkondo mzima wa familia kuu pasipo

    kulazimika kufuatilia kwa kina maisha ya ndugu zao wengine.” (Alexander 1993: 258, 259)

    b. Kuanzia Mwa 4:25 mpango wa kitabu unageukia mkondo wa Seti. Kwa hiyo, hivyo Toledot

    vya Adamu, kuanzia Mwa 5:1 hukazia kwa Seti na kIsha kwa wazao fulani wa Seti. Biblia

    hufanya hilo kwa makusudi, kwa sababu watu inaowakazia ndio kitovu cha kuanikwa wazi kwa

    simulizi nzima.6

    5 Dhabihu ya Habili ilikuwa kwa imani (Waeb 11:4); Ile ya Kaini bila shaka haikuwa hivyo. Ni lazima, bila shak