Upload
others
View
2
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
1
BUNGE LA TANZANIA
____________
MAJADILIANO YA BUNGE
______________
MKUTANO WA PILI
Kikao cha Tisa – Tarehe 5 Februari, 2016
(Bunge lilianza Saa Tatu Asubuhi)
D U A
Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua
NAIBU SPIKA: Katibu.
NDG. RAMADHAN I. ABDALLAH - KATIBU MEZANI: Hati za kuwasilisha
Mezani.
HATI ZA KUWASILISHA MEZANI
Hati zifuatazo ziliwasilishwa Mezani na:-
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO:
Taarifa ya Utendaji wa Soko la Bima Nchini kwa kipindi cha Mwaka
unaoishia tarehe 31 Disemba, 2014 (The Annual Insurance Market Performance
Report for the Year ended 31st December 2014).
WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI:
Taarifa ya Mwaka ya Chuo Kikuu cha Dodoma kwa Mwaka wa Fedha
2013/2014 (The University of Dodoma Annual Report 2013/2014).
MASWALI NA MAJIBU
NAIBU SPIKA: Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Atupele Fredy
Mwakibete Mbunge wa Busokelo sasa aulize swali lake.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
2
Na.102
Tatizo la Maji – Jimbo la Busokelo
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Busokelo hasa katika Kata za Kandete, Isange,
Lutebe Lwangwa, Mpata, Kabula, Mpombo, Lufilyo Kambasegela, Ntaba,
Lupata, Itete, na Kisegese wanakabiliwa na tatizo kubwa la maji safi na salama;
na kuna maeneo mengi ambayo mabomba uyamepita lakini maji hayatoki
kutokana na kukosekana kwa matenki ya maj:-
(a) Je, ni lini Serikali itatatua kero hiyo ya maji kwa kujenga matenki ya
maji kwenye Kata hizo?
(b) Mji wa Lwangwa ni Makao Makuu ya Halmashauri mpya ya Busokelo
na kuna ongezeko kubwa la watu ukilinganisha na miundombinu ya maji
iliyopo; je, Serikali ina mpango gani wa kujenga miundombinu mipya ya
uzalilshaji wa maji kwenye eneo hilo jipya la mipango miji?
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-
TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Fredy Atupele Mwakibete,
Mbunge wa Busokelo lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka 2014/2015,
Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo ilipokea shilingi milioni 907 ambazo
zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ya Mpanda katika Kata ya
Lupata na miradi wa maji Kasyabone na Kisegese katika Kata ya Kisegese.
Miradi hii inahusisha ujenzi wa matanki yenye ujazo wa mita za ukubwa 90 kwa
Kata ya Lupata na matanki wawili ya mita za ukubwa 45 kila moja katika Kata
ya Kisegese. Katika bajeti ya mwaka 1015/2016 Serikali imefanikiwa kupeleka
shilingi milioni 171.94 kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji katika Kijiji cha
Kanyelele Kata ya Kabula, Ilamba katika Kata ya Kambasegela na kijiji cha
Mpata katika Kata ya Mpata.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, ili kukabiliana na changamoto ya
upatikanaji wa huduma ya maji katika Mji wa Lwangwa tayari Halmashauri
imekamilisha upembuzi yakinifu wa ujenzi wa mradi wa maji kutoka chanzo cha
maji Mano Sekondari. Katika bajeti ya mwaka 2015/2016 Serikali imetenga
shilingi milioni 280 ili kuanza utekelezaji wa mradi huu.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwakibete swali la nyongeza
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
3
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante kwa kunipa
nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya
Serikali, lakini kwa mujibu wa swali nilivyouliza pamoja na majibu ambayo
yametolewa ni dhahiri kwamba kwa vijiji ama Kata ambazo amezisema mimi
mwenyewe ni shahidi kwamba kuna hela ambazo hazijafika hadi sasa hivi na
katika jibu lake la msingi amesema zimefika. Kwa mfano Kata ya Mpata,
nimepeleka mabomba zaidi ya milioni 10 lakini Serikali mpaka sasa hivi haijatoa
chochote. Mheshimiwa Waziri unaweza ukathibitishia wananchi wa Mpata
kwamba hizo fedha zimefika kule? Hilo ni swali la kwanza.
Swali la pili, kuna baadhi ya Kata ya Ntaba, kijiji cha Ilamba wananchi
pamoja na wakazi wa eneo la pale wananyang’anyana maji, wananchi na
mamba, na zaidi ya wananchi kumi na moja wameshauawa na mamba ama
kuliwa na mamba kwa sababu ya kutafuta maji, je, Serikali inatoa tamko gani
kwa ajili ya wananchi hawa na ikizingatiwa kwamba kuna mradi ambao
umeshafanyiwa upembezi yakinifu tangu mwaka 2008 hadi leo hii kwa thamani
ya shilingi milioni 100, haikufanya kitu chochote.
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa
Naibu Spika, asante.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa taarifa aliyosema kwamba fedha
hazijafika ni kwamba ngoja nita-cross check vizuri katika Ofisi yangu nijue ni nini
kilichotokea lakini kikubwa ni nini? Ni kwamba kuna changamoto ya upelekaji
wa fedha, siyo mradi huo tu isipokuwa maeneo mengi sana, fedha zimeenda
kwa kusuasua na hivi karibuni ndiyo maana Waziri wa Maji juzi juzi alikuwa
anazungumza kwamba kutokana na kusuasua kwa kupeleka fedha katika
miradi ya maji na miradi hii mingi sasa mingine ilikuwa imesimama, sasa Serikali
iliamua kwamba ile outstanding payment ambazo zilikuwa zinakaribia karibuni
bilioni 28, kwamba fedha hizi sasa zipelekwe katika maeneo mbalimbali ilimradi
wale Wakandarasi walio-demise mitambo waweze kuendelea.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuambia kwamba nitazifuatilia
kwa karibu ilimradi kwamba huu mradi lengo letu liweze kufanikiwa na
wananchi waweze kupata huduma ya maji.
Lakini sehemu ya (b) ni kwamba kuna changamoto ya wananchi
wanakamatwa na Mamba. Kwanza nitoe masikitiko yangu sana katika eneo
hilo, kwa sababu kama watu wanaliwa na mamba ina maana kwamba ni
changamoto kubwa, tunapoteza jamii ya Watanzania.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikiri kwamba nimesikia hili na
nakumbuka tulifanya discussion juzi juzi kwamba katika ziara yangu
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
4
nitakapokuwa nimeenda katika Mkoa wa Mbeya nimesema kipambele katika
Jimbo lako la Busokelo litakuwa ni sehemu mojawapo ambayo nitaenda
kutembelea ilimradi mambo haya yote kwa ujumla wake tuweze kuyatazama
vizuri tukiwa site na kuweze kupanga mipango mizuri, mwisho wa siku wananchi
wa Jimbo hili waweze kupata huduma ya maji, kila mtu aweze kujiona ana
faraja na nchi yake.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa pale nyuma, samahani naomba ujitambulishe
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, Naitwa Willy
Qambalo Mbunge wa Jimbo la Karatu.
Kwa kuwa, matatizo ya maji yaliyoko Busekelo yanafanana kabisa na
matatizo ya maji yanayoukumba Mji wa Karatu na vijiji vinavyouzunguka. Na
kwa kuwa Mji wa Karatu unakua sana kutokana na shughuli za utalii
zinazoendelea katika maeneo ya jirani. Je, ni lini Serikali itamaliza kabisa
matatizo ya maji katika Mji wa Karatu na vijiji vinavyozunguka?
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa
Naibu Spika, ndugu yangu huyu tukiri kwanza Busokelo haifanani na Karatu kwa
sababu kule Busokelo kuna mamba, na naamini Karatu hakuna mamba. Lakini
kubwa zaidi ni jinsi gani kama Serikali itajielekeza kuhakikisha Mji wa Karatu
unapata maji kwanza nikiri kwamba miongoni mwa Miji ambayo Tanzania
tunaitegemea katika suala zima la uchumi ni Mji wa Karatu, kwa sababu ni
center kubwa sana ya utalii katika nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kwamba Serikali kupitia Wizara
ya maji katika programu ya pili tunayoenda nayo ambayo imeanza hii Januari,
tumeweka kipaumbele katika Mji Mikakati yote ambayo kwanza ina vivutio vya
Kitalii, lakini ni source kubwa sana ya uchumi wa nchi yetu kuipa kipaumbele
katika suala zima la huduma ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri wazi kwamba katika suala zima la utalii
kama nilivyosema awali, Karatu ni Mji tunaoutegemea sana. Kwa hiyo suala hili
tunalilchukua kwa ujumla wake, Wizara ya Maji halikadhalika Wizara ya Nchi
Ofisi ya Rais TAMISEMI, tutahakikisha jinsi gani tutaipa kipaumbele. Ile miradi
ambayo imeanza Singida haijakamilika vizuri, au ni jinsi gani tutumie vyanzo
vingine ili mradi tupate maji katika Mji wa Karatu, wananchi wa Karatu waweze
kupata manufaa katika nchi yao.
NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge niwakumbushe tu, maswali
yanayoulizwa ya nyongeza yawe mafupi, ikiwa ni pamoja na ya muuliza swali.
Lakini pia Mawaziri mjibu kwa kifupi kwa sababu kila swali limetengewa dakika
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
5
sita tu. Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba sasa aombe swali
lijibiwe.
Na.103
Kero ya Ushuru wa Mazao na Mifugo
MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:-
Wakati wa Kampeni za Urais mwaka 2015 wananchi wa Momba
walipewa ahadi ya kutatuliwa kero ya ushuru wa mazao na mifugo kwenye
vizuizi na minada:-
(a) Je, mpaka sasa Serikali imefikia hatua gani katika kushughulikia kero
hii?
(b) Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya mwenendo mbovu wa ukusanyaji
wa ushuru huo?
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
(TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge
wa Momba lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, ushuru wa mazao hutozwa kwa mujibu wa
sheria ya fedha za Serikali za Mitaa Sura Na. 290 kwenye eneo ambalo zao hilo
huzalishwa na kuuzwa. Kwa mujibu wa sheria hii ushuru unatozwa kwa mnunuzi
wa mazao kutoka kwa mkulima asilimia tatu hadi asilimia tano ya bei ya
gharama (farm gate price). Aidha, kwa upande wa ushuru wa Mifugo, ushuru
huu hutozwa mnadani au sokoni baada ya mifugo kununuliwa.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inasisitiza na kuwataka Wakurugenzi
wote wa Halmashauri kuhakikisha kuwa wanazingatia sheria, kanuni na taratibu
zinazosimamia utaratibu wa utozaji na ulipaji wa kodi katika ushuru husikia.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Pamoja na
majibu ya Mheshimiwa Waziri, ningependa kuuliza maswali mado mawili.
Moja ya kero inayowakuta wafugaji wanapokuwa minadani, inatokea
mahali mtu amekwenda kuuza bahati mbaya akiwa pale mnadani hajauza
mfugo wake, na anapotoka pale anadaiwa ushuru wakati hajapata hiyo
fedha. Sasa nilitaka nifahamu kauli ya Serikali juu ya wale wote ambao
wanashindwa kuuza mazao ama mifugo yao katika maeneo hayo?
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
6
Swali la pili, je, ni kiwango gani ambacho mtu anapaswa kulipa, kwa
sababu kuna watu wanatoka mashambani labda ana mahindi wanakwenda
nyumbani kwao kuyatunza. Sasa wakikutana na kizuizi, mtu ana gunia mbili,
gunia tatu anaambiwa lazima alipe ushuru hata kwenye yale mahindi ya
kutumia.
Je, ipi ni kauli ya Serikali juu ya hili jambo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA): Mheshimiwa
Naibu Spika, ni kweli katika mazoea ya kawaida watu wengine wanapeleka
mazao yao sokoni, lakini kwa bahati mbaya wakifika pale wanakosa kuyauza.
Ina maana na concept ya ushuru wa mazao, maana inataka mtu akishauza,
yule mnunuzi sasa maana yake anatakiwa alipia ule ushuru. Lakini kama
hajauza ukimwambia kwamba yule mkulima sasa aweze kutoa ushuru maana
yake unambana mkulima. Na kauli ya Mheshimiwa Rais alipokuwa katika
kampeni alizungumza wazi kwanza lengo lake ni kutoa huu usumbufu wa ushuru
mdogo mdogo ambao unamkabili mwananchi wa kawaida.
Mheshimiwa Naibu Spika, kikubwa zaidi nawahimiza Watendaji wetu hasa
katika Halmashauri, jinsi gani wabainishe kwamba katika maeneo yao kuna
watu hawa wa kawaida ambao wanaenda kuuza. Kuna mfanya biashara
mkubwa ambaye anakuja kuchukuwa mazao pale site, akishachukua lazima
alipie ushuru. Lakini yule mtu anayefanya kazi ya kuchuuza kwa ajili ya maisha
yake tu hili ni jambo ambalo ni suala zima kuwaelekeza watendaji wetu katika
Halmashauri zetu watafanya vipi kuondoa kero hii kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ni kwa kiwango gani, nadhani suala la pili
sikulipata vizuri lakini kikubwa zaidi ni nini. Ni kwamba mifugo yote inayopelekwa
pale eneo la mnada, ndiyo maana nimesema sijalipata vizuri swali la pili,
tuangalie kwamba kwa sababu sheria ndiyo inaelekeza kati asilimia tatu mpaka
asilimia tano, sasa mtu anapoenda kuuza mfano ana ng’ombe wake mmoja,
ng’ombe wake wawili, ndiyo nimesema hapa utaratibu mkubwa unaotakiwa ni
katika Halmashauri husika. Kwa sababu tunajua Halmashauri nyingine
zinategemea asilimia karibuni 70 ya mapato yake katika ushuru wa mazao.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini jinsi gani kama Baraza la Madiwani
pamoja na Watendaji wao watafanya kuangalia mazingira ya kijiografia katika
eneo husika ili kuwasaidia wananchi hali kadhalika kuongeza uchumi katika
Halmashauri zao.
MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa
kunipa nafasi, naomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri swali dogo la nyongeza.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
7
Kwa kuwa katika Halmashauri zetu, hususani Halmashauri ya Wilaya ya
Mvomero kumekuwepo na tatizo kubwa sana la ushuru huu na unaleta
matatizo makubwa na kwa kuwa kuna ahadi ya Rais kwamba hizi shughuli
ndogondogo zitaangaliwa upya, je, Serikali sasa iko tayari kuziagiaza
Halmashauri zote ziangalie upya maeneo ambayo kuna usumbufu mkubwa na
ushuru huu, ili marekebisho yafanywe haraka na wananchi wasipate bugudha
ikiwemo Wilaya ya Mvomore?
WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza
nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu yake ya ufasaha, na mimpongeze
Mheshimiwa Murad kwa ufuatiliaji wake kwa masuala yanayohusu Jimbo lake.
Mheshimiwa Naibu Spika, niseme tu kwamba kama ambavyo nilisema
wakati nachangia, tunakaa na wenzetu wa TAMISEMI pamoja na Wizara zingine
ambazo zinahusiana na sekta ambazo zinahusu mambo ya makato makato na
tulishasema tunayafanyia kazi mambo ya makato yote ambayo yanamgusa
Mkulima na wafanyabiashara wadogowadogo. Lakini kwa leo nitamke tu
kwamba kwa yale makato ambayo hayako kisheria, kwa makato ambayo
yanawagusa wakulima ambayo hayako kisheria kuanzia leo hii wale
wanaohusika waondoke na tamko hili kwamba wayaache, yale ambayo yako
kisheria tunaenda kufuata utaratibu na kuangalia kama yote yabaki ama
yabaki kiasi ili kuweza kuhakikisha kwamba tunawapa unafuu wakulima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini yale hayako kisheria na yale ambayo
hayahusiani moja kwa moja na uendelezaji wa zao husika hayo yakome moja
kwa moja kufuatana na kwamba yamekuwa yakiwapa mzigo wakulima bila
kuleta tija katika kuongeza uzalishaji wa zao husika. Na tutachambua moja
baada ya lingine na yale ambayo yanaafikiwa kwa kupitia makubaliano ya
wadau wahusika, wasikubaliane wao na kuanza kuyatumia mpaka wapate
ridhaa ya Wizara kwamba kuna mambo haya wamekubaliana na sisi tuweze
kupima umuhimu wa kuwepo makato hayo katika uendelezaji wa zao husika.
(Makofi)
NAIBU SPIKA: Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. Mheshimiwa
Masoud Abdalla Salim, Mbunge wa Mtambile sasa aulize swali lake.
Na.104
Ajira Inayatokana na Sekta ya Viwanda
MHE. MASOUD ABDALLA SALIM aliuliza:-
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
8
Ajira iliyotarajiwa kuongezeka kutokana na ukuaji wa sekta ya viwanda
haijafikiwa hasa baada ya viwanda vingi kubinafsishwa na kuachwa bila
kuendelezwa:-
Je, Serikali inasema nini kuhusu hili?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masoud
Abdalla Salim, Mbunge wa Mtambile, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nia njema kabisa Serikali ilibinafsisha
viwanda na mashirika ya umma ikiwa na matumaini kuwa sekta binafsi
ingeliweza kuendesha taasisi hizo kwa faida na kulipa kodi kwa Serikali, kuzalisha
bidhaa au huduma na kutoa ajira kwa wananchi. Pamoja na malengo hayo
Serikali ililenga kuachana na shughuli za biashara ikielekeza nguvu zake katika
shughuli zake za msingi za Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa
Masoud, makampuni mengi yaliyobinafsishwa hayakufanya vizuri, ikiacha
mfano wa makampuni machache yakiwemo Tanzania Breweries, Morogoro
Polister ambayo inaitwa Twenty First Century na Tanzania Cigarette Company.
Mheshimiwa Naibu Spika, tathimini inayoendeshwa na Wizara yangu kwa
kushirikiana na Msajili wa Hazina juu ya viwanda, mashamba na mashirika ya
Serikalil yaliyobinafsishwa kuanzia mwaka 1992 inadhihirisha ukweli tunaoujua
kuwa wengi kati ya waliyopewa taasisi hizo hawakutekeleza mikataba ya
mauziano kikamilifu. Hivyo tunawafuatilia kwa karibu wale wote waliopewa
mashirika ya umma kwa utaratibu wa ubinafsishaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu ni kuhakikisha makampuni yote haya
yanazalisha kwa tija ili tupate bidhaa, kodi ya Serikali na ajira kwa wananchi wa
Tanzania. Wale wote watakaobainika kukiuka makubaliano yaliyomo katika
mikataba ya awali, hatua stahiki zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuvitwaa
viwanda au mashirika hayo na kutafuta Wawekezaji mahiri wa kuviendeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kutimiza adhma ya kutoa ajira kwa
Watanzania, Wizara inafanya yafuatayo chini ya viwanda vidogo na vya kati
unaoshirikisha SIDO na Halmashauri za Wilaya na Mikoa tunahamasisha shughuli
za ujasiriamali ikiwa ni pamoja na kuanzisha viwanda vya kuongeza thamani
mazao na kilimo, uvuvi na ufugaji huku Mikoani.
Pia kupitia mamlaka zetu za EPZA, TIC na NDC tunakaribisha na
kuwaongoza wawekezaji wa ndani na nje kuwekeza katika shughuli za kutoa
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
9
ajira zaidi. Serikali kupitia Wizara yetu inaboresha mazingira ya uwekezaji hali
itakayowajenga imani wawekezaji na kupelekea kupanua shughuli zao zaidi za
kibiashara kupitia njia hii ajira zaidi itaongezeka.
MHE. MASOUD ABDALLA SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru
nina maswali mawili ya nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na malalamiko mengi ya muda
mrefu kwa wafanyakazi viwandani kupewa mishahara midogo lakini zaidi
maneno ya kuudhi kwa wamiliki wa viwanda jambo ambalo halikubaliki.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, Serikali haioni
sasa ni wakati muafaka wa kuunda Tume Teule ya kufuatilia malalamiko ya
wafanyakazi hawa?
Swali la pili, katika jibu la Mheshimiwa Waziri amesema kwamba wale
wote watakaobainika kukiuka makubaliano yaliyomo katika mikataba ya awali
hatua stahiki zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na kuvitwaa na kutafuta wawekezaji
mahiri wa kuviendeleza hivyo viwanda.
Kwa kuwa viwanda vya korosho vilivyobinafsishwa miaka 1970 na 1980
ambapo Serikali ilikopa kutoka Italia na Japan dola milioni 20 na viwanda hivyo
hadi leo haviendelezwi wamiliki wake wanajulikana. Sasa tatizo nini kwa Serikali
mnaelewa kila kitu tumekuwa tukisema muda mrefu.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa uliza swali.
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Je, nini mkakati wa ziada wa kuhakikisha
kwamba viwanda vya korosho vimebinafsishwa kule Mtwara na Serikali mkatoa
kwa vigogo wengine mnaowajua kwa bei chee! Je, viwanda hivyo ni lini
vitarudi kwa wananchi?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
ni kweli katika viwanda kuna malalamiko na kama mnavyojua tunao ndugu
zetu wanafanya kazi viwandani, sioni haja ya kuunda Tume, Wizara yetu
ikishirikiana na Wizara ya Ajira tumeanza kazi ya kufuatilia masuala haya na
Kamishna wa Kazi yuko ana kazi maalum ambapo tutahakikisha kwamba
wafanyakazi wetu wanatendewa haki.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaeleze wawekezaji, sisi tunatengeneza
viwanda kutengeneza ajira, kuzalisha bidhaa na kuwafanya mlipe kodi
hatutengenezi viwanda kusudi waje kuteseka watu katika nchi yao, huo ndiyo
msimamo wa Serikali na tunawahakikishia tushirikiane Waheshimiwa Wabunge,
ninyi ndiyo macho yetu mtushauri na mtuelekeze.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
10
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kutoa viwanda, viwanda vile viliuzwa
kisheria, nimeshasema mara tatu bei waliyolipa ni pamoja na masharti ya
kuzalisha bidhaa kwa tija, kutoa ajira na kulipa kodi.
Kwa hiyo, kama ulimuuzia kisheria utamnyang’anya kisheria na
niwahakikishie watu wanaotoka kwenye ukanda wa kulima korosho hakuna
tatizo viwanda vitafanya kazi. Pamoja na hivyo wako wawekezaji wako tayari
kuwekeza kwenye kutengeneza korosho, yaani korosho inatoka pale kiwandani
inaingia mikononi mwa mteja tuna-add value, na tutatoka hapa tunakwenda
kuuza Ulaya siyo tunatoka hapa tunauza India, India ipeleke Ulaya.
Tunakwenda moja kwa moja sokoni na kazi hiyo naiweza tushirikiane. (Makofi)
MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nikushukuru
sana kwa kunipa fursa na kwa sababu ni mara yangu ya kwanza nazungumza
tangu nichaguliwe tena kuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki na mimi
niwashukuru Wanameru.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Nassari tafadhali uliza swali la nyongeza.
MHE. JOSHUA S. NASSARI: Mheshimiwa Naibu Spika, unapoongelea suala
la ukuaji wa viwanda huwezi ukaacha kuongelea habari ya viwanda ambayo
vilikuwemo lakini leo hii havifanyi kazi. General Tyre Arusha kilikuwa ni kiwanda
pekee cha kuzalisha matairi Afrika Mashariki. Mwaka juzi ndani ya Bunge hili
nimejibiwa na Mama Nagu hapa kwamba in less than a year kiwanda kingerudi
kifanye kazi, mwaka jana nimejibiwa ndani ya Bunge hili na Mheshimiwa Janeth
Mbene kwamba kufikia mwezi wa 11 mwaka jana kiwanda cha General Tyre
kingerudi kufanya kazi.
Sasa na mimi niiulize Serikali ya hapa kazi tu, kwamba ni lini kiwanda cha
General Tyre kitarudi kufanya kazi kwa sababu tumechoshwa na ahadi za
muda mrefu ndani ya Bunge hili na wananchi wa Mkoa wa Arusha ambao
walikuwa wanapata ajira ndani ya viwanda vile leo wako nyumbani na matairi
tunanunua Korea, India na Japan, lini General Tyre litaanza kufanya kazi?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
General Tyre kinachoendelea General Tyre ni nini?
Mheshimiwa Naibu Spika, General Tyre imeshatwaliwa aliyekuwa mbia
mwenzetu mwenye asilimia 26 tumemlipa chake kiwanda ni chetu,
kinachoendelea ni kurekebisha mitambo yote ya umeme. Lakini mitambo
iliyokuwepo kwa ushindani wa sasa ni absolute zimepitwa na wakati. Tulikuwa
tunatengeneza tyres zenye tube, sasa hivi soko linakula tubeless kwa hiyo,
tunapaswa kuleta mitambo mingine. Lakini tunatafakari tuende vipi tutafute
mbia mwingine au tutafute mtu wa kumwajiri afanye kazi. Kwa hiyo, sasa hivi
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
11
kinachofanyika ikitoka Government Notice NDC itakwenda kupewa pesa bilioni
60 na itafanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Catherine Magige amelifuatilia suala hili tumelizungumza
sana, siyo suala la dakika moja naomba Mheshimiwa Mbunge uje au umuone
Mheshimiwa Catherine Magige akueleze shule niliyompa masaa matatu kuhusu
General Tyre. General Tyre is coming na iko kwenye score board yangu,
nitapimwa kwa General Tyre. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi/Kicheko)
Na. 105
Matatizo Yanayowakabili Wakulima wa Tumbaku Urambo
MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-
Mfumo wa sasa wa kuwahudumia wakulima wa zao la tumbaku wa
Wilaya ya Urambo na Mkoa wa Tabora kwa ujumla una mapungufu mengi
yanayowaletea wakulima usumbufu kama vile bei za pembejeo kuwa kubwa
kutokana na kuagizwa nje na riba kubwa za benki, masoko ya tumbaku
kutokuwa na uhakika na hatimaye kusababisha kushuka thamani ya tumbaku,
bei inayobadilika pamoja na uchache wa wanunuzi:-
(a) Je, ni kwa nini hasara inayotokana na matatizo hayo ibebwe na
mkulima peke yake?
(b) Je, Serikali imejipanga vipi kuondoa matatizo hayo ili mkulima wa
tumbaku anufaike na kilimo na hatimaye ajikwamue kiuchumi?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kwa niaba ya Waziri wa Kilimo,
Mifugo na Uvuvi kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge
wa Urambo, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inakubaliana na Mheshimiwa
Mbunge kuwa yapo maeneo mbalimbali yanayomkosesha mkulima mapato.
Maeneo haya ni pamoja na mfumo wa usambazaji pembejeo uliokuwa na
mianya mingi inayosababisha madeni hewa, baadhi ya viongozi wa vyama
kukopa fedha nyingi kupita uwezo wa vyama wa kuzalisha tumbaku na
kadhalika. Kwa sasa Serikali imebadili mfumo huo na kuelekeza wagavi wa
pembejeo hizo kuzifikisha moja kwa moja kwenye vyama vya msingi tofauti na
utaratibu wa awali wa kupitisha pembejeo kwenye vyama vikuu.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
12
Aidha, ili kuwa na uhakika wa soko kilimo cha tumbaku nchini
huendeshwa kwa mkataba kati ya wanunuzi na wakulima. Hivi sasa bei
hupangwa kabla ya msimu wa kilimo kuanza ili mkulima ajue bei na kiasi
anachotakiwa kuzalisha. Tatizo la soko na bei mara nyingi huwakumba wale
wakulima wanaozalisha tumbaku bila kuwa na mikataba ambapo hujikuta
tumbaku yao ikikosa soko au wakipewa bei ya chini.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua za
kukabiliana na changamoto zinazomkabili mkulima wa tumbaku. Hatua hizo ni
pamoja na kuboresha mfumo wa upangaji wa bei ya tumbaku ambapo
wakulima upendekeza bei yenye tija kwao na kuiwasilisha kwa wanunuzi kupitia
vikao vya Halmashauri ya Tumbaku yaani Tobacco Council. Bei hiyo hujadiliwa
na hatimae kufikia muafaka. Mfumo huu wa upangaji wa bei umeanza
kutumika rasmi msimu wa mwaka 2015/2016. Sanjari na maboresho ya mfumo
huu Serikali inaendelea na jitihada za kuongeza wanunuzi wa tumbaku kutoka
China ili kuongeza ushindani kumwezesha mkulima kupata bei nzuri. Aidha,
Serikali itapitia tozo za pembejeo zinazoingia nchini na kuangalia uwezekano
wa kuziondoa ili kumpunguzia mkulimba gharama ya uzalishaji.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na
majibu mazuri ya Naibu Waziri ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza
kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri amekiri kwamba mfumo uliopo una
matatizo katika kumhudumia mkulima. Lakini Serikali inashiriki kikamilifu katika
kupanga bei katika mfumo mzima. Sasa kwa kuwa Serikali inashiriki kwa kupitia
wakala wake bodi au council, je, Serikali haioni kwamba inawajibika kubeba
sehemu ya hasara anayopata mkulima?
Kwa kiasi gani mmefaulu kupata wanunuzi zaidi kutoka China ili soko liwe
la haraka na wakulima wanufaike?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika,
Tobacco Council au Halmashauri ya Tumbaku inawakutanisha wadau
mbalimbali wa sekta ya tumbaku. Serikali yenyewe haihusiki moja kwa moja
katika kupanga bei lakini imeweka tu utaratibu ambao wadau wenyewe
wanaweza kukaa kukutana kwa uhuru wao na kupanga bei. Hata hivyo, Serikali
imechukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kwamba bei ya tumbaku
inaendelea kuwa nzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba tokea mwaka 2013
Bunge hili lilipitisha Sheria mpya ya Vyama vya Ushirika, utaratibu mpya wa
Vyama vya Ushirika ni utaratibu ambao pamoja na mambo mengine
unawaruhusu wakulima wa mazao mbalimbali kuendesha shughuli zao kwa
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
13
kuwa na uhuru zaidi. Lakini vilevile mpango ule umeunda Tume ya Ushirika
ambayo inakuwa karibu na Vyama vya Ushirika ili kuwezesha kuondoa kero
zilizopo. Tunafikiri kwamba utaratibu huu utaleta ufanisi zaidi katika kilimo cha
tumbaku pamoja na mazao mengine ikiwa ni pamoja na kusaidia katika suala
la bei.
Lakini nitumie tu fursa hii kuwawelezea vilevile Waheshimiwa Wabunge
kwamba pamoja na changamoto nyingi zilizopo kwenye sekta ndogo ya
tumbaku, tunafikiri sekta ndogo ya tumbaku ni eneo ambalo limeanza
kuonesha mifano ya kufanikiwa. Hii ni kwa sababu ndiyo sekta ndogo ya pekee
ambayo mkulima anakuwa na uhakika wa kuuza zao lake tokea siku ya kwanza
anapoanza kuweka mbegu shambani kwa sababu ni kilimo cha mkataba. Kwa
hiyo, tukiondoa changamoto zilizopo tunafikiri ni eneo ambalo bado
inawezekana kupata mafanikio makubwa. Lakini vilevile tungependa kutumia
fursa hii kuwaeleza wakulima…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri naomba ufupishe jibu lako
tafadhali.
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika,
namalizia. Kuwafahamisha kwamba kufanikiwa kutumia mfumo wa mkataba
utasaidia tu kama kila mtu akiheshimu mkataba. Kwa mfano, mwaka huu tayari
wakulima wanafahamu inatakiwa wazalishe tumbaku kiasi gani, tunaomba
wale ambao hawako kwenye mkataba usizalishe tumbaku kwa sababu
ukizalisha hautaweza kupata mnunuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kipengele cha pili cha swali ni kwamba ni kiasi
gani na kwamba tumefikia wapi na kuwapata wanunuzi kutoka China.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inajitahidi kuongea na wafanyabiashara
kutoka China, tumefika hatua nzuri sana kilichobakia sasa ni wao kumaliza
taratibu za nchi mwao ili nao waweze kuingia kwenye mfumo rasmi wa
kununua tumbuku ili kuondoa ukiritimba ambao mpaka sasa hivi nchi nzima
kampuni zinazonunua tumbaku ni nne tu.
Kwa hiyo, tunafikiri kampuni zikiwa nyingi maana yake tunaondoa
monopoly na hivyo bei itakuwa nzuri nashukuru sana.
NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tuendelee na Wizara ya Mambo
ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti Maalum,
sasa aulize swali lake.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
14
Na. 106
Usalama wa Maisha na Walemavu wa Ngozi
MHE. MGENI JADI KADIKA aliuliza:-
Kwa muda mrefu walemavu wa ngozi (albino) wamekuwa wakiishi kwa
hofu katika nchi yao kutokana na kuuawa na kukatwa viungo vyao kwa imani
za kishirikina ikiwemo kwa ajili ya kushinda uchaguzi au kujipatia mali:-
Je, Serikali ina mpango wa kuwalinda na kuwahakikishia usalama wa
maisha yao watu hao wenye ulemavu wa ngozi?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mgeni Jadi Kadika, Mbunge wa Viti
Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyowahi kujibiwa katika swali la msingi
namba 99 na swali namba 60 katika mikutano tofauti ya Bunge la Kumi la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu usalama wa ndugu zetu wenye
ulemavu wa ngozi, Serikali kupitia Jeshi la Polisi na wadau wengine imekuwa
ikichukua hatua za maksudi kukomesha mauaji hayo ikiwa ni pamoja na
kuwasaka na kuwakamata watuhumiwa pamoja na kuwafikisha mahakamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya pia juhudi za kuanzisha vituo
vya kuwahudumia watu wenye ulemavu wa ngozi ambavyo vimesaidia
kuimarisha ulinzi. Pia Jeshi la Polisi kwa kutumia falsafa ya Polisi Jamii inatoa
elimu kwa umma juu ya madhara ya vitendo vya ukatili na mauaji na kujerui
yanayofanywa na baadhi ya watu kwa msukumo wa imani potofu ya ushirikina.
Aidha, Jeshi la Polisi limekuwa likifanya operesheni maalum za mara kwa mara
zikiwamo za kukamata waganga wa jadi wanaopiga ramli chonganishi
ambazo ni kichocheo kikubwa cha ukatili dhidi ya walemavu wa ngozi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu kupitia Jeshi la Polisi ikishirikiana
na Kamati ya Ulinzi na Usalama za Vijiji, Kata, Wilaya na Mikoa imeanzisha vikosi
kazi hususan kwenye Mikoa na Wilaya zilizojitokeza kukithiri kwa matukio haya ili
kuratibu na kusimamia kwa karibu ulinzi wa ndugu zetu wenye ulemavu wa
ngozi. Vikosikazi hivyo hufanya kazi kwa kukusanya taarifa za kiintelejensia na
kuzifanyia kazi.
MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu
mazuri aliyonijibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
15
Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni kesi ngapi zilizolipotiwa kwa kipindi hiki cha
mwaka wa uchaguzi?
Mheshimiwa Naibu Spika, pia ni kwa nini kesi zinacheleweshwa wale
walemavu hawapi haki zao kwa haraka?
Na je, ni mikoa mingapi inayoongoza kwa mauaji ya maalbino? (Makofi)
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kadika umeuliza maswali matatu, Naibu Waziri
tafadhali jibu maswali mawili.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,
kwanza kuhusu Mikoa ambayo inaongoza ni Mkoa wa Mwanza, Mkoa wa
Shinyanga na Kigoma.
Swali lake la pili anauliza kwamba ni kesi ngapi, takwimu halisi zilizotokea
baada ya kumalizika uchaguzi naomba nimpatie baadaye lakini ninachoweza
kusema ni kwamba toka mauaji haya yameanza mwaka 2006 mpaka mwaka
jana takribani watu wanakadiriwa kwenye 40 mpaka 43 wameweza kufariki,
lakini watuhumiwa karibu 133 na kati ya hao watuhumiwa ambao
wamehukumiwa kwa adhabu ya kifo ni 19 tayari ambao wameonekana wana
hatia. Kwa hiyo, hizi takwimu za baada ya uchaguzi mpaka saa hivi, hizi
naomba nikupatie baadaye. (Makofi)
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa
kuwa matatizo yaliyoulizwa na Mheshimiwa Mgeni kwenye swali namba 106
yanafanana kabisa na matatizo yaliyoko Jimbo la Geita Vijijini. Takribani
wanawake wazee wanne kwa mwezi wanauwawa kwa kukatwa mapanga
kwa imani ya kishirikina na Jeshi la Polisi halijawahi kufanikiwa kuwakamata
wakataji mapanga hao kwa kuwa jiografia ya kutoka Geita kwenda eneo
husika ni mbali.
Je, Serikali inajipangaje kupeleka gari maalum na kuunda Kanda Maalum
kwa ajili ya kuokoa akina mama wanaokatwa mapanga kwenye Jimbo hilo?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,
Jeshi la Polisi linajitahidi sana kuweza kukabiliana na mauaji haya, lakini kama
ambavyo nimezungumza wakati nikijibu maswali wiki iliyopita kuhusiana na
changamoto ambazo zinakabili Jeshi la Polisi. Naomba nichukue fursa hii
kuweka sawa kidogo takwimu wakati nilikuwa najibu swali la Mheshimiwa
Selasini juzi, nilieleza kwamba moja katika changamoto inakabili Jeshi letu la
Polisi ni kwamba idadi ya polisi tulionao ni kidogo na kiukweli kihalisia takwimu
zinaonyesha kwamba ukiangalia takwimu za kidunia polisi mmoja anatakiwa
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
16
ahudumie kati ya watu 400 mpaka 450 takriban na siyo 300 mpaka 350. Sisi
hapa nchi yetu polisi mmoja kwa upande wa Tanzania Bara anahudumia watu
kwenye 1000 mpaka 1200. Kwa hiyo utaona ni tofauti kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa changamoto hizi na changamoto nyingine
ambazo tumekuwa tukikabiliana nazo hatua kwa hatua kama hii ya usafiri,
nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Musukuma kwamba tumekuwa na
changamoto ya usafiri kwa muda mrefu lakini tumepata magari takribani
magari 387 ambayo yameweza kugawiwa katika maeneo mbalimbali.
Tutaangalia eneo hilo kama halijafika gari tuone ni jinsi gani na uzito wa hali
yenyewe ilivyo tushauriane tuone ni nini tutakachofanya ili tuweze kukabiliana
na tatizo hilo. Lakini mengine ni changamoto ambazo tunaenda nazo kadri ya
uwezo wa bajeti unavyoruhusu.
Na. 107
Uhaba wa Magari na Mafuta katika Vituo vya Polisi
Wilaya ya Magharibi
MHE. HAFIDH ALI TAHIR aliulliza:-
Bunge la Jamhuri ya Muungano hupitisha Bajeti ya Serikali kwa kila Wizara
kwa mwaka ikiwemo Wizara ya Mambo ya Ndani:-
(a) Je, inakuwaje Wilaya yenye vituo saba vya polisi ina gari moja tu na
inapatiwa lita tano hadi saba tu za mafuta kwa siku?
(b) Je, Serikali iko tayari kuziongezea mafuta na magari Wilaya za
Magharibi A na B zenye vituo vya polisi vya Fumba, Mbweni, Mazizini,
Mwanakwerekwe, Kijitoupele, Fuoni, Airport na Mfenesini ambazo ni gari moja tu
kila Wilaya ili kukongeza ufanisi na kuendana na kasi ya hapa kazi tu hasa
ukizingatia kuwa Zanzibar inajiandaa na marudio ya Uchaguzi Mkuu?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya
Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hafidh Ali Tahir, Mbunge wa Dimani
lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kuwa
Wilaya ya Magharibi A na B hazina magari na mafuta ya kutosha kwa shughuli
za polisi. Hali hii ni changamoto kwa vituo vingi vya polisi hapa nchini, hata
hivyo, mgawo wa vitendea kazi yakiwemo magari huzingatia jiografia ya
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
17
Wilaya. Hali ya uhalifu na idadi ya watu wanaohudumiwa na kituo husika na
siyo idadi ya vituo vidogo vya Polisi vilivyopo katika Wilaya husika.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani
ya Nchi, inakusudia kuwasilisha bajeti mbele ya Bunge lako Tukufu ili kuboresha
hali ya vyombo vya usafiri, mafuta na vilainishi ili kukidhi mahitaji halisi ya Jeshi la
Polisi hapa nchini, vikiwemo Vituo vya Polisi alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge.
MHE. HAFIDH ALI TAHIR: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru
Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jawabu zake, lakini swali langu lilikuwa na msisitizo
ukizingatia kuwa Zanzibar inajiandaa na marudio ya Uchaguzi Mkuu, ndiyo
sababu swali langu kubwa lilikwenda huko. Kurudiwa kwa Uchaguzi Zanzibar
siyo jambo geni, mwaka 1961 Uchaguzi ulifutwa na ukarudiwa mwaka1963.
(Makofi)
Sasa kwa tokeo hili Mheshimiwa Waziri swali langu la kwanza, huoni
kwamba kuna haja ya kuweka umaksudi wa kupatia usafiri Wilaya nilizozitaja
wakati huu tukielekea katika uchaguzi ili yale mazombi yanayozungumzwa
yapunguke kufanya kazi?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, namwomba Waziri aniambie
kwamba kwenye Bajeti ijayo ameahidi kwamba atatupatia magari Wilaya
alizozitaja, Mheshimiwa Naibu Waziri naomba ukubali hii ni ahadi na nikungoje
kwenye bajeti? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,
naomba nimhakikishie kwamba nilizungumza vilevile kuhusiana na hili suala la
magari ambalo kwa bahati mbaya kuna baadhi ya Waheshimiwa Wabunge
wamelipotosha kwa makusudi ama hawajalielewa. Lakini naomba nichukue
fursa hii kwa kueleza tu kwa ufupi ni kwamba Jeshi la Polisi na ninyi Wabunge ni
mashahidi mara nyingi mmekuwa mkihoji, vituo vyangu havina magari, Jimbo
langu kwenye kituo fulani hakuna magari, na ndiyo kwa kuzingatia hilo Serikali
kupitia Jeshi la Polisi, likaandaa mkakati kabambe wa kupunguza hiyo hali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kulimaliza kwa wakati mmoja, siyo rahisi kwa
sababu katika nchi tuna zaidi ya vituo 4,500, kwa hiyo, kupata gari 4,500 kwa
mpigo ili kila kituo kiweze kupata gari ni jambo ambalo ni gumu. Kwa hiyo
kulikuwa kuna mpango wa kwanza wa kuweza kupata gari 777 kupitia mkopo
wa Exim Bank ya India, ambapo kati ya hizo tuliweza kupata gari 104, lakini pia
Serikali iliweza kutoa gari takribani 203 kwa hiyo kufanya jumla ya idadi ya gari
ambazo zilipatikana kuwa ni 387. Kati ya gari hizo, gari 37 zilipelekwa Zanzibar
na nimhakikishie Mheshimiwa Hafidh Ali Tahir kwamba gari hizi bado
hazijagawiwa katika Wilaya, nina hakika kwamba wakati mgao utakapokuwa
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
18
umefanyika, basi Wilaya hizo ambazo zimezungumzwa vituo vya Wilaya yake ya
Magharibi A na Magharibi B vitapata gari.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake la pili, alizungumzia kuhusiana
na hali ya usalama kwa ujumla. Mimi nataka nimhakikishie tu kwamba pamoja
niichukue fursa hii, kuwaeleza Wananchi wa Zanzibar kwamba Jeshi la Polisi
ama Serikali itahakikisha inalinda usalama wa raia kama ambavyo majukumu
yake ya msingi yanavyotaka. Kwa hiyo, wasiwe na wasiwasi wajitokeze kwa
wingi kushiriki uchaguzi utakaporudiwa na hakuna wasiwasi wowote kila mtu
ambaye atakuwa na haki ya kupiga kura, apige kura kwa usalama na amani.
(Makofi)
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana,
ninaomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa shida ya ulinzi iliyopo Dimani
inafanana sana na Jimbo la Ukonga, nina Kata 13, sina kituo kikubwa cha Polisi,
na ni eneo la pembezoni ikiwepo Msitu wa Kazimzumbwi, lakini hata kituo cha
Sitakishari ambacho kinahudumia Jimbo la Segerea na Ukonga hakuna gari,
sasa nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, atatujengea Kituo cha Polisi Ukonga
au apeleke gari Segerea Sitakishari ili ihudumie wakati mipango mingine
inaendelea?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwasilishe, ahsanteni.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,
nadhani ule umuhimu wa magari ambayo nimekuwa nikiuzungumza
umeongezeka uzito wake, sasa niweke tu wazi kwamba katika yale magari
ambayo tumeyapata, magari mengi ni kwa ajili ya doria, operation na matumizi
ya kawaida ya polisi. Hayo magari yanayoitwa ya washawasha sidhani hata 24
sujui kama yanafika.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Waitara nadhani utakubaliana na mimi na
Wabunge wengine kwamba, Jeshi la polisi linahitaji magari zaidi, ikiwemo katika
Kituo chako ulichozungumza, mimi naomba hili nilichukue tuone tutalifanyia kazi
vipi.
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Naibu Spika, wabheja sana.
Kwa kuwa Jimbo la Kishapu halikupata mgao wa magari mapya ya polisi katika
awamu hii na Jimbo hili lenye watu sharp na askari wanaofanya kazi zao kwa u-
sharp, lina magari mawili mabovu yenye umri wa zaidi ya miaka mitano.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, nilipata ahadi kuwa mwezi wa pili tutapata
magari mapya ya polisi, uko tayari kunihakikishia Jimbo sharp litapata magari
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
19
mapya ili Wananchi waweze kupata huduma hasa za kiusalama wanapohitaji
kuliko hivi sasa polisi wangu wa Kishapu wanavyohangaika? Wabheja.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Nchambi wakati Naibu Waziri akija, hayo
maneno wabheja siyo lugha ya Kibunge, kwa hiyo nayafuta kwenye record
karibu Mheshimiwa Naibu Waziri. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika,
nataka nimhakikishie Mheshimiwa Nchambi kwamba Serikali hii ya Awamu ya
Tano ya hapa kazi tu huwa haina desturi za kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki.
Kwa hiyo, kama ni ahadi ambayo imetolewa, basi nitaifuatilia hiyo ahadi
yenyewe halafu tuone hatua zilizofikiwa zimefikiwaje na kama imekwama
imekwama vipi, halafu tutaonana mimi na yeye tuone ni jinsi gani ya kufanya.
NAIBU SPIKA: Tuendelee Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia
Wazee na Watoto, Mheshimiwa Halima Ali Mohamed, Mbunge wa Viti Maalum,
sasa aulize swali lake.
Na. 108
Tatizo la Ugonjwa wa Moyo, Kisukari na Vidonda vya Tumbo
MHE. HALIMA ALI MOHAMMED aliuliza:-
Takwimu zinaonyesha kuwa kuna kasi kubwa ya ongezeko la wagonjwa
wa maradhi ya moyo, kisukari na vidonda vya tumbo (ulcers):-
Je, Serikali ina mkakati gani kukabiliana na tatizo hili?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima Ali
Mohammed, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania imeshuhudia kasi kubwa ya ongezeko
la magonjwa ya moyo, magonjwa ya kisukari na magonjwa ya vidonga vya
tumbo, ambayo ni magonjwa yasiyo ya kuambukiza. Hii imechangiwa na
mabadiliko ya mfumo wa maisha kama ulaji usiyo sahihi, kutokufanya mazoezi,
kutokula matunda na mboga mboga kwa wingi, uvutaji wa sigara na tumbaku
na unywaji wa pombe uliyokithiri.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
20
Mheshimiwa Naibu Spika, matokeo ya utafiti wa STEPS uliyofanyika
mwaka 2012 yalionesha kuongezeka kwa viashiria yaani indicators
vinavyosababisha magonjwa yasiyo ya kuambukiza. Aidha, utafiti pia ulionesha
karibu asilimia 9 ya Watanzania, wanaugua ugonjwa wa kisukari na wengi wao
kwa bahati mbaya hawajijui. Kwa kutambua ongezeko hili Wizara yetu
imeanzisha sehemu ya kushughulikia huduma ya magonjwa haya yaani kitengo
cha Non Communicable Diseases, Mental Health and Substance Abuse chini ya
Kurugenzi ya Tiba pale Wizarani. Miongozo na mikakati mbalimbali imekwisha
kutengezezwa ikiwa ni pamoja na mkakati wa Kitaifa wa kukabiliana na
magonjwa yasiyo ya kuambukiza yaani magonjwa ya kisukari, moyo na
mengineyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, wito wangu kwa jamii ni kubadili mtindo wa
maisha yaani life style kwa kula vyakula vinavyofaa, kupunguza unywaji wa
pombe na uvutaji wa sigara na tumbaku na kuwa na tabia ya kufanya mazoezi
ili kuepuka uwezekano wa kupata maradhi haya.
MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa ya Naibu Waziri nina maswali mawili
madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tafiti zinaonyesha kwamba
wanawake wanaathirika zaidi na maradhi ya moyo kuliko wanaume.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia wanawake hawa ambao
ndiyo walezi wa familia hasa wale waliopo kule vijijini?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Serikali ina mkakati gani wa
kudhibiti uingizwaji wa vyakula vibovu ambavyo havina kiwango katika nchi
yetu? Ahsante (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA
WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali ya
nyongeza kama ifuatavyo:-
Swali la kwanza Serikali ina mkakati gani wa kupunguza kiasi cha
magonjwa haya kwa wanawake ambao wanaathirika zaidi kuliko wanaume.
Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti ya upatikanaji wa magonjwa haya, kwa
jinsia kwa maana ya baina ya wanawake na wanaume ni ndogo sana na kwa
maana hiyo, mkakati wa kupambana na kuenea kwa magonjwa haya hauwezi
kutofautishwa kwa jinsia. Hivyo mkakati wetu utakuwa ni wa pamoja na tayari
Wizara ya Afya imeanza kutekeleza mkakati huo, kwanza kwa kutia umuhimu
wa kipekee kwenye kuimarisha Kitengo cha NCD yaani Kitengo cha Magonjwa
Yasiyo ya Kuambukiza pale Wizarani chini ya Kurugenzi ya Tiba.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
21
Mheshimiwa Naibu Spika, kitengo hiki tayari kimeishaaza mkakati wa
kuandika mkakati wa kupambana na magonjwa haya na mkakati huu
utawafikia hao akinamama wa vijijini na watu wote kwa ujumla wake kuanzia
ngazi ya huduma za afya kule vijijini, kwa maana ya ngazi ya zahanati, ngazi ya
vituo vya afya na ngazi ya hospitali za Wilaya, Mikoa na hata ngazi ya Kanda.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kweli kumekuwa na hisia kwamba
kuna vyakula visivyo na viwango vinaingia nchini mwetu kutoka nchi za mbali.
Serikali kwa kushirikiana kwa maana ya Wizara yetu Wizara ya Afya, ambayo ina
kitengo cha TFDA (Tanzania Food and Drugs Authority) ambacho kipo chini ya
Wizara yetu ya Afya, pamoja na Kitengo cha Viwango (TBS), wanaendelea
kushirikiana kwa pamoja, kukagua mizigo yote ambayo inaingia nchini kwa njia
za halali.
Lakini pia vyombo vingine vya kusimamia Sheria kama Majeshi ya Polisi na
Uhamiaji, wataendelea kuwa makini kwenye mipaka yetu yote, katika njia zilizo
halali na hata zile ambazo siyo halali kudhibiti uingizwaji wa vifaa hivi ikiwemo
vyakula na dawa ambavyo havijapitishwa kwa viwango vinavyostahili, kwa
mujibu wa Sheria za nchi yetu. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Wizara ya Maji na Umwagiliaji Mheshimiwa Risala Saidi
Kabongo Mbunge wa Viti Maalum, sasa aulize swali lake.
Na. 109
Kuongezeka na Kuboresha Vyanzo vya Maji Arusha
MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:-
Vijiji vya Ngiresi, Sokoni II na Oldadai Kata ya Sokoni II Jimbo la Arumeru
Magharibi vinakabiliwa na tatizo la ukosefu wa maji ya bomba, kwa muda
mrefu licha ya kwamba vijiji hivyo kuna vyanzo vingi vya maji na mabomba
yanayopeleka maji Arusha Mjini:-
(a) Je, Mamlaka ya Maji Jiji la Arusha inashindwa kutekeleza maombi ya
wananchi wa vijiji hivyo ya kupatiwa maji kutoka kwenye mabomba kwa
utaratibu wa kulipia?
(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza na kuboresha vyanzo vya
maji katika Jiji la Arusha na Halmashauri zake kutokana na ongezeko kubwa la
wakazi wake?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
22
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji,
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Risala Saidi Kabomgo, Mbunge wa Viti
Maalum, lenye vipengele (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika kuondoa tatizo la maji Jiji la
Arusha, imepata mkopo wa dola za Kimarekani milioni 210.96 kutoka Benki ya
Maendeo ya Afrika (AfDB) ili kutekeleza mradi wa upanuzi wa mtandao maji
safi na maji taka sambamba na kuboresha vyanzo vya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huu mkubwa utawezesha Jiji la Arusha
pamoja na viunga vyake, ikiwa ni pamoja na vijiji vyote vilivyopo umbali wa
kilometa 12 kando kando ya bomba kuu, vikiwemo vijiji vya Ngilesi, Sokoni II na
Oldadai ili kupata huduma ya majisafi na majitaka. Jumla ya gharama za ujenzi
ni dola za Marekani milioni 233.92 sawa na shilingi za Kitanzania bilioni 476.44.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkataba wa mkopo huu nafuu umesainiwa na
Mamlaka ya Maji Arusha, kwa sasa inaendelea na taratibu za kupata Mhandisi
Mshauri wa kusimamia mradi pamoja na Wakandarasi wa Ujenzi. Ujenzi wa
mradi huu unatarajiwa kuanza mwaka wa fedha 2016/2017 na kukamilika
mwaka 2019/2020. Mradi huu ukikamilika utaboresha vyanzo vya maji na
utaongeza upatikanaji wa huduma ya maji katika Jiji la Arusha na Halmashauri
zake ambazo zimekumbwa na ongezeko kubwa la wakazi.
MHE RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa, Naibu Spika nakushukuru.
Nakushukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yako.
Kwa kuwa, mradi huu ni Mkubwa na ni wa miaka mitano; je, Serikali
inavipa vipaumbele gani vijiji hivi vya Oldadai na Sokoni II na Ngilesi, kwa kuwa
wamekuwa na kero kubwa na ya muda mrefu ya kupata maji?
Eneo la pili, nitaomba Mheshimiwa Waziri, atakapopata nafasi baada ya
Bunge hili, aweze kutembelea maeneo haya na kujionea hali halisi katika
vyanzo hivi ambavyo vinatunza maji yanayosaidia katika Mkoa wa Arusha.
Ahsante. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri, la pili nadhani lilikuwa ni ombi, swali ni
moja tu lililoulizwa.
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza
kabisa ni kweli tumepata ufadhili wa mradi mkubwa ambao utekelezaji wake
utachukua miaka mitatu. Jana tulikuwa na Mkurugenzi wa Jiji la Arusha,
amekuja ofisini kwangu pamoja na Meya, pamoja na Mbunge na
tumekubaliana kwamba, tutatengeneza mpango wa muda mfupi ili hivyo vijiji
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
23
unavyovisema tuweze kuvitafutia angalau wapate maji wakati tunatekeleza
huu mradi mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa kulikuwa na Mradi wa Vijiji Kumi,
tumekubaliana kwamba Jiji la Arusha litakabidhi kwenye mamlaka yetu ya
Arusha ili kusudi waweze kuunganisha kwenye mtandao baadhi ya maeneo
ambayo Arusha hayapati maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana pia kwamba na mimi nitakuja
kuangalia utekelezaji wa mpago huu. (Makofi)
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi
hii. Suala la Arumeru Magharibi linafanana sana na tatizo ambalo lipo Mikumi,
je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa kero ya maji katika Kata ya Mikumi,
Ruaha, Uleling’ombe na maeneo ya Tindiga?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika na
Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Waziri katika majibu yake ametoa taarifa
kwamba tunaingia katika progamu ya pili kupitia sera ya mwaka 2002 ya
kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2020 asilimia 85 ya Watanzania wote
watakuwa wanapata maji katika vijiji na asilimia 95 katika miji.
Mheshimiwa Mbunge, kwa upande wa Jimbo lako la Mikumi na Kata
zake, tutahakikisha kwamba tunazipa kipaumbele kuhakikisha zinapata maji
katika hii progamu ya pili. Na ninakuomba sana baada ya Bunge hili tuwasiliane
ili tuweze kupata taarifa iliyo nzuri zaidi tuanze utekelezaji.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa
kuniona. Kwa kuwa tatizo la Arumeru Mashariki linafanana kabisa na tatizo la
maji la Lushoto.
Je, ni lini Serikali itaondoa adha hii kwa wananchi wa Lushoto?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
kwanza Wilaya ya Lushoto mlalo wake wa ardhi ni mzuri kuruhusu ujenzi wa
mabwawa. Tumeweka mpango wa kujenga mabwawa katika awamu hii ya
programu ya pili ambayo yatasaidia kwenye irrigation pamoja na kuhakikisha
kwamba tunapata maji ya kunywa kwa wananchi wa Jimbo lake.
Na. 110
Kuanza kwa Mradi wa Bomba la Maji Ziwa Victoria
MHE. RICHARD M. NDASSA aliuliza:-
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
24
Je, ni lini mradi wa ujenzi wa bomba la maji ya Ziwa Victoria kutoka Magu
- Sumve - Malya utaanza?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji
naomba kujibu swali la Mheshimiwa Richard Mganga Ndassa, Mbunge wa
Sumve kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji
ya Ulaya (EIB) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mwanza
(MWAUWASA) inatekeleza miradi ya maji safi na maji taka kwa Jiji la Mwanza
pamoja miradi ya maji safi katika miji mitatu ya Magu, Misungwi na Lamadi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mji wa Magu mradi huu unakadiriwa
kugharimu kiasi cha Euro milioni 5.3 na Mkandarasi anatarajiwa kuanza ujenzi
wa mradi ifikapo mwezi Julai, 2016. Idadi ya wananchi watakaonufaika na
mradi huu inakadiriwa kuwa wananchi 73,363 ifikapo mwaka 2040.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miji ya Sumve na Malya, Serikali
inaendelea kufanya uchunguzi wa awali ili kubaini gharama za eneo la
kupitisha mradi. Kazi ya upimaji pamoja na usanifu itakamalika mwezi Aprili, 2016
na ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwaka wa fedha 2016/2017.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Kwanza naomba nisahishe jina langu hapa inasomeka Ngassa, siyo Ngassa ni
Ndassa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na maelezo mazuri sana ya
Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba Serikali itambue kwamba suala la maji
ni suala kila Mtanzania, kila mwananchi anahitaji maji na ndiyo maana unaona
Wabunge wote wanasema kuhusu maji.
(a) Swali langu, kwa sababu Serikali katika mwaka 2000 na 2004 iliamua,
maamuzi magumu yenye tija, kuyatoa maji ya Ziwa Victoria kuyapeleka
Kahama, Shinyanga. Je, Serikali ina mpango gani mrefu wa kupeleka maji ya
Ziwa Victoria katika Mikoa tisa ili maji hayo yawanufaishe Watanzania na mikoa
hiyo ni Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu, Singida na Dodoma. Serikali ina mpango
gani kwa sababu mahitaji ya maji ni makubwa na maji ya Ziwa Victoria yapo
hayana kazi nyingine. Je, Serikali ina mpango mkakati gani wa kuhakikisha
kwamba maji yanafika katika maeneo hayo?
(b) Mheshimiwa Waziri wa Maji, wananchi wa Jimbo la Sumve katika Kata
ya Nkalalo na Mabomba wanashida kubwa ya maji, naomba nikuombe
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
25
pamoja na maelezo haya utembelee tuende ukajionee mwenyewe jinsi
wananchi wa Tanzania wa Jimbo la Sumve wanavyopata taabu ya maji katika
Jimbo langu.
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika,
nimezungumza jana kwamba tumeleta mapendekezo ya mwongozo kwa
kutengeneza mpango wa miaka 2016/2017 na nilisema katika sekta ya maji
tumetoa ahadi kwamba katika miji yote ya Mikoa inayozungukiwa na Ziwa
Victoria tutahakikisha tunachukua maji ya kutosha kuyafikisha kwenye maeneo
husika kwa kiwango ambacho tumeshasema kwenye Ilani, kwamba Miji Mikuu
ya Mikoa ipate asilimia 95 ikifika 2020 na ipate asilimia 100 ikifika 2025.
Kwa hiyo, naomba nilihakikishie Bunge hili kwamba azma hiyo ambayo
pia Mheshimiwa Rais wetu ameahidi tutakwenda kufanya, tutaomba
Waheshimiwa Wabunge muweze kutuunga mkono katika kupanua vyanzo vya
upatikanaji wa fedha hasa kuongeza Mfuko wa Maji ili tuweze kutekeleza miradi
yote hii ambayo kila Mbunge ameomba Serikali iweze kufanya, ahsante.
(Makofi)
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbarouk
MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, jina langu naitwa
Mussa Mbarouk, Mbunge wa Tanga Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ilianzisha mpango wa maji safi
na salama vijijini katika mradi uliofadhiliwa na World Bank na mradi ule
umekwama. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha katika Halmashauri ya Jiji la Tanga
ili kuondoa kero ya maji katika Kata za Mabokweni, Chongoleani, Kilale na
Marungu?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni
kweli Serikali ilianzisha mradi wa vijiji 10 kupitia progamu ya Benki ya Dunia na
mradi huo ungali unaendelea. Katika mradi huo tulikuwa na miradi 1,855 kama
nilivyotoa taarifa ya awali kwamba katika miradi hiyo miradi 1,143 imekamilika
na miradi 454 inaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tatizo la fedha ndiyo lililofanya hii
miradi isikamilike kwa wakati lakini nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba
katika eneo lako la Tanga kufuatia juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kukusanya fedha, fedha zimeanza kutoka na nikupe tu
taarifa Mheshimiwa Mbunge kwamba wiki iliyopita tumeletewa shilingi bilioni 10
kwa ajili ya kuendelea kulipa miradi hiyo mingi ambayo ilikuwa imesimama na
siyo Tanga tu, ni karibu Mikoa yote miradi ilikuwa imesimama.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
26
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nikuhakikishie kwamba Serikali inatoa
fedha kuhakikisha miradi hiyo inakamilika ili katika progamu ya pili tuanze
kuweka tena miradi mingine. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Wizara ya Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano, Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge
wa Lupa sasa aulize swali lake.
Na. 111
Kuweka Mizani katika Barabara ya Mbeya – Chunya – Makongorosi
ili Kuilinda Iweze Kudumu kwa Muda Mrefu
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:-
Barabara ya Mbeya – Chunya - Makongorosi imejengwa kwa kiwango
cha lami kwa asilimia 80. Je, ni lini Serikali itaweka mizani katika barabara hiyo
ya lami ili kuilinda iweze kudumu muda mrefu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa,
Mbunge wa Jimbo la Lupa kama ifuatavyo:-
Barabara ya Mbeya – Chunya – hadi Makongorosi yenye urefu wa
kilometa 117 ni barabara kuu inayohudumiwa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano kupitia Wakala wa Barabara Mkoa wa Mbeya. Barabara hii
imejengwa kwa kiwango cha lami, sehemu ya barabara kati ya Mbeya hadi
Chunya ambayo ni kilometa 72 na imekamilika hivi karibuni. Aidha, Serikali
inafanya maandalizi ili kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu ya Chunya
hadi Makongorosi ambayo ni kilometa 45.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara yangu inatambua kuwa katika Wilaya
ya Chunya kuna shughuli nyingi za kiuchumi kama vile uchimbaji wa madini,
kilimo na mazao ya misitu ambayo huchangia kwa kiwango kikubwa upitishaji
wa magari yenye mizigo mizito na hivyo kuna umuhimu wa kuweka mizani
kwenye barabara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali itajenga mizani katika barabara ya
Mbeya - Chunya hadi Makongorosi wakati wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa
sehemu ya Chunya - Makongorosi. Aidha, katika kipindi hiki ambacho ujenzi wa
mizani ya kudumu haujafanyika, Serikali kupitia TANROADS itaendelea kudhibiti
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
27
uzito wa magari katika barabara hiyo kwa kutumia mizani ya kuhamishika
(mobile weighbridge).
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika,
ninakushukuru. Napenda kumshukuru sana Naibu Waziri amejibu vizuri sana na
amejibu kitaalamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesema Chunya ina mazao mengi
ambayo yakibebwa ndiyo yanaharibu barabara, sasa napenda nimwambie
Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba wanaosomba tumbaku, magari
yanayobeba tumbaku au mbao au mkaa yanabeba lumbesa, yanakuwa mara
mbili, yakifika Mbeya yanagawa kwa sababu kuna mizani kule ndiyo yawe
magari mawili na Serikali hapa imesema kwamba itadhibiti hiyo kwa kuweka
mobile weighbridges.
Je, ni lini itaweka kwa sababu Chunya sasa hivi sijaiona mobile
weighbridge hata moja? Hilo ni swali la kwanza
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nashukuru Serikali imesema kwamba
ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Chunya kwenda Makongorosi karibu utaanza,
napenda nimwambie Naibu Waziri kwamba Mheshimiwa Rais akiwa
Makongorosi aliwaahidi wananchi wa Makongorosi kwamba atawapa kilomita
nne za lami pale Makongorosi na kwamba barabara hiyo ya Chunya
Makongorosi itaanza kujengwa Makongorosi kuja Chunya.
Je, hiyo barabara itanza lini kujengwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, kama tulivyosema kwenye jibu la msingi la swali la msingi kwamba
weighbridge itaanza hivi karibuni. Naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia
Mheshimiwa Mwambalaswa kama yeye alivyo-concerned na uharibifu wa
barabara hiyo na sisi ambao ndiyo wenye dhamana hiyo tuko concerned kwa
kiwango kikubwa, ninamhakikishia hiyo weighbridge inatafutwa hivi karibuni
itaanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili naomba kumjulisha Mheshimiwa
Mwambalaswa kwamba mara fedha zitakapopatikana barabara hii itaanza
kujengwa na suala la ianzie wapi whether ianzie Makongorosi au ianzie Chunya
nadhani ni muhimu tuwaachie wataalamu na ahadi ya kilomita Nne nayo
katika eneo la Makongorosi itaangaliwa kwa umakini wake. (Makofi)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
28
Na. 112
Uhakika wa Fidia kwa Wananchi Waliopisha Barabara
MHE. DUA W. NKURUA aliuliza:-
Katika ujenzi wa barabara ya Mangaka - Mtambaswala na Mangaka -
Nakapanya, wapo wananchi ambao walishafanyiwa tathmini ya fidia ya
kupisha ujenzi huo hawajalipwa na wengine wamepunjwa.
Je, Serikali italeta lini wataalamu wa kuhakiki fidia hizo ili kila mwananchi
apate haki yake?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dua William Nkurua,
Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ujenzi wa barabara ya Mangaka –
Mtambaswala na Mangaka - Nakapanya, Serikali ilitenga fedha shilingi milioni
3,023.528 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi waliokwisha fanyiwa tathmini ya
mazao yao kati ya mwaka 2009 na 2012. Aidha, baada ya uthamini
kuidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali mwaka 2013, fidia ililipwa mwaka
2014 kwa kufuata taratibu na sheria.
Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya wananchi ambao mali zao
hazikufanyiwa tathmini katika kipindi hicho hawakulipwa fidia. Tathmini ya fidia
kwa mali za wananchi hao imefanyika mwezi Oktoba 2015 na taarifa ya
uthamini imekamilika na imewasilishwa kwa Mthamini Mkuu wa Serikali kwa
hatua ya kuidhinishwa ili malipo yaweze kufanyika.
MHE. DUA W. NKURUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa majibu
mazuri ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika wale ambao walifanyiwa tathmini ya
awamu ya kwanza, wapo ambao mpaka sasa hawakulipwa, Majina yao
yalirukwa katika Kijiji cha Misawaji, lakini pia wapo ambao walifanyiwa tathmini
kwamba nyumba zao zitabomolewa nusu lakini zimebomolewa zote na hivi
ninavyokwambia wamechanganyikiwa kabisa.
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kutuma watu tumuoneshe watu ambao
wameathirika ili wapate haki yao?
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
29
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara kutoka Masasi
mpaka Mangaka imekamilika, hadi sasa magari yenye uzito mkubwa kutoka
Songea kuelekea Masasi yanatumia hiyo barabara.
Je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kuleta mizani katika Mji wa
Mangaka ili kuokoa barabara ambayo Serikali imetumia gharama kubwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, nakubaliana nae kwamba tutatuma watu waende
wakalichunguze hilo suala na hatimaye tuweze kulipatia ufumbuzi stahiki.
Ninachoomba kumhakikishia tu ni kwamba Serikali hii inafuata sheria na yeyote
mwenye haki ya kulipwa fidia atalipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili nadhani anafahamu
kwamba hizo barabara anazoziongelea bado hazijakamilika na hivi karibuni
nimepiata katika eneo lake ingawa kwa bahati sikumjulisha kwa sababu ilikuwa
ni dharura wakati natokea Jimbo la Namtumbo. Ninamhakikishia mara
barabara hizi zitakapokamilika na umuhimu utakapoonekana kwamba kuna
umuhimu mkubwa wa kuweka mizani, Serikali itafanya maamuzi stahiki. (Makofi)
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Keissy.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa
kuwa barabara ya kutoka Sumbawanga kwenda Mpanda takriban kilometa 50
zimeshatengenezwa na magari makubwa ya mahindi zaidi ya tani 60, 70
yanapita kuelekea Mpanda. Nimeshamwomba Waziri wa Ujenzi kupeleka gari
ya mizani ili kudhibiti uharibifu wa barabara kabla wakandarasi hawajakabidhi
kwa sababu barabara inaanza kuharibika kabla haijakabidhiwa. Je, ni lini
Serikali itapeleka gari ya mizani ili kudhibiti barabara hiyo isiendelee kuharibika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Keissy na
wananchi wa Sumbawanga hadi Mpanda kwamba barabara ile kwanza
tutaikamilisha kuijenga. Tutakapoona umuhimu wa kuweka mizani kutokana na
tathmini ya wataalam tutakaowapeleka kufanya shughuli hiyo tutaweka mizani
hiyo.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbunge kule nyuma ujitambulishe tafadhali.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa
nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Naitwa Alex Raphael Gashaza,
Mbunge wa Jimbo la Ngara.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
30
Kwa kuwa barabara ya Murugarama – Rulenge – Nyakahura yenye
kilometa 85 ni barabara ambayo iliahidiwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2008
kwamba itaweza kujengwa kwa kiwango cha lami na miaka miwili iliyopita
wananchi wa Jimbo la Ngara walikuwa wakielezwa kwamba tayari upembuzi
yakinifu wa barabara hii umeanza.
Naomba kumuuliza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ni lini
mkandarasi atakuwepo site kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, tumepata taarifa kutoka kwa Waziri mwenyewe wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano juu ya upatikanaji wa fedha za kulipa madeni ya
wakandarasi, kama jana mlimsikia alisema ni karibu shilingi bilioni 419
zimeshatolewa. Kwa hiyo, katika lile deni la shilingi trilioni 1.268 sasa tumeshuka
tuko kwenye shilingi bilioni 800 na zaidi. Naomba kuchukua nafasi hii
kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mara fedha zitakapopatikana
kwa mradi huo, barabara yake itashughulikiwa kama ilivyoahidiwa na
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Na. 113
Mkoa wa Shinyanga na Simiyu Kuunganishwa kwa Barabara za Lami
MHE. GIMBI D. MASABA aliuliza:-
Mkoa wa Shinyanga na Simiyu inaunganishwa kwa barabara ya vumbi,
tofauti na mikoa mingine ambayo imeunganishwa kwa barabara za lami.
(a) Je, Serikali itaunganisha lini mikoa hiyo kwa barabara ya kiwango cha
lami kwa kumalizia kilometa 102 zilizobaki katika barabara ya Lamadi -
Mwigumbi kupitia Bariadi?
(b) Je, Serikali itaona umuhimu wa kuunganisha makao makuu ya Wilaya
za Mkoa wa Simiyu kuunganishwa kwa barabara za kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gimbo Dotto Masaba,
Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama
ifuatavyo:-
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
31
Mweshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na ujenzi kwa kiwango cha
lami wa barabara ya Mwigumbi - Maswa - Bariadi - Lamadi yenye urefu wa
kilometa 171.8 kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha ikiwa na lengo
la kuunganisha Mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mara na Mwanza na kwa
barabara ya lami. Sehemu ya barabara hii kuanzia Bariadi - Lamadi yenye urefu
wa kliometa 71.8 tayari imejengwa kwa kiwango cha lami na imekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2015/2016, TANROADS
ilitia saini mkataba wa ujenzi na mkandarasi CHICO kutoka China kwa ajili ya
ujenzi kwa kiwango cha lami sehemu ya pili ya barabara hiyo kuanzia
Mwigumbi - Maswa ambazo ni kilometa 50.3 kwa gharama ya shilingi bilioni
61.462. Hadi sasa mkandarasi yuko katika eneo la mradi na anaendelea na kazi
za kujenga kambi, kuleta mitambo na wataalam kwa ajili ya kutelekeza mradi
huo. Aidha, kwa sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa
kiwango cha lami wa sehemu ya Maswa - Bariadi ambazo ni kilometa 50.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni wazi kuwa kukamilika kwa barabara hii
inayoendelea kujengwa kutawezesha Makao Makuu ya Wilaya za Busega,
Bariadi na Maswa zilizoko katika Mkoa wa Simiyu kuunganishwa kwa barabara
za lami. Wilaya nyingine zilizobaki zitaungwanishwa kwa barabara za lami kwa
awamu kutegemeana na upatikanaji wa fedha.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Masaba swali la nyongeza.
MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa
nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu ya Mheshimiwa
Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa vile nchi yetu ina uhaba
wa majengo ya shule, zahanati na vituo vya afya, je, Serikali iko tayari
kumuagiza mkandarasi ambaye sasa hivi yuko site kujenga majengo ya
kudumu ili baada ya mradi kukamilika majengo hayo yaweze kutumika kwa ajili
ya matumizi ya shule, zahanati na vituo vya afya? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara za Mkoa wa
Simiyu zinaunganishwa na barabara za vumbi na kwa sasa hazipitiki kutokana
na mvua zinazoendelea.
Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kutoka kwenye Mfuko wa Barabara ili
kuweza kutengeneza barabara hizo na ziweze kupitika kwa urahisi tofauti na
ilivyo sasa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, mkandarasi aliyeko site mkataba wake ulishasainiwa. Hata hivyo,
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
32
nawaagiza TANROADS Mkoa wa Simiyu waangalie uwezekano katika mkataba
huo kama inaweza ikafanyika variation au kama kifungu hicho kipo wahakikishe
majengo yanayojengwa na mkandarasi huyo yaweze kuangalia matumizi ya
baadaye ambayo Mheshimiwa Mbunge ameomba. Kama itashindikana,
Serikali itatafuta njia nyingine kupitia Wizara husika ya Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili, naomba
nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mfuko huo anaoungelea ndiyo
tunaoutumia kujenga na kukarabati barabara zote nchi nzima. Naomba
akubali mfumo tulio nao ndiyo huo, hatuna mfuko maalum kwa ajili ya
barabara hii peke yake.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Gekul.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa
kuniona niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika Mpango wa
Maendeleo wa mwaka mmoja ulio mbele yetu, miundombinu si kipaumbele.
Kwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa
Magufuli wakati akiomba kura aliahidi ujenzi wa barabara za lami nchini kote
ikiwemo Jimbo langu la Babati Mjini ambako aliahidi ujenzi wa kilometa 20 za
lami. Naomba nifahamu, ni lini ahadi hii itatekelezwa kwa wananchi wa Babati?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, ahadi zote ambazo zimetolewa kwanza na Chama Tawala kupitia
Ilani yake ya mwaka 2015 - 2020 Serikali hii ina wajibu wa kuzitekeleza. na
tutaitekeleza
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hiyo anayoiongelea namuomba
awasiliane na TANROADS mkoa ili kuangalia vipaumbele vya sasa vilivyopo
katika mkoa ule. Kama barabara hiyo ni moja kati ya vipaumbele vya mkoa,
namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaitekeleza katika kipindi hiki
kama ambavyo iliahidiwa katika kipindi cha kampeni.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Martha Mlata.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa
kunipa nafasi. Na mimi kama swali la msingi lilivyoongea kuhusu Mkoa wa Simiyu
kuunganishwa na mikoa mingine, ni wazi kwamba Mkoa wa Simiyu bado
haujaunganishwa na Mkoa wa Singida ambao unapitia katika Daraja la Sibiti –
Mkalama - Nduguti - Iguguno. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, je,
anafahamu kwamba Daraja la Mto Sibiti ndilo kiunganishi kikubwa katika Mkoa
wa Simiyu na Singida na mpaka sasa mkandarasi hayupo site? Ahsante.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
33
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, tunafahamu kwamba Daraja la Sibiti ni muhimu katika mawasiliano
kati ya Mkoa wa Simiyu na Singida na ndiyo maana kazi kubwa inafanywa sasa
kutokana na matatizo yaliyotokea ili kuhakikisha mawasiliano yanakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mkandarasi, kwa kuwa fedha za kulipa
madeni ya wakandarasi tumeanza kupata ambapo huyu naye ni mmoja kati
ya wakandarasi wanaotakiwa kulipwa ili waendelee na kazi. Mara fedha
zitakapopatikana, mkandarasi atarudi site ili aweze kukamilisha kazi ambayo
alisaini kuifanya.
Na. 114
Serikali Kuanzisha na Kumiliki Bureau de Change
MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha na kumiliki Bureau de Change
zake yenyewe badala ya kuacha huduma hiyo kuendelea kutolewa na watu
au taasisi binafsi?
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango,
napenda kujibu swali la Mheshimiwa Faida Mohamed Bakar, Mbuge wa Viti
Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haina mkakati wa kufungua au
kuanzisha Bureau de Change zake kwa sababu imejitoa kuhusika moja kwa
moja na biashara ya fedha kama vile benki na Bureau de Change kutokana
na mabadiliko ya mfumo katika sekta ya fedha nchini unaotekelezwa kuanzia
mwaka 1991. Sekta binafsi imeachiwa jukumu la kuanzisha na kuendesha
biashara ya fedha nchini chini ya usimamizi wa Benki Kuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imebaki na jukumu la kuweka mazingira
mazuri na salama ya uwekezaji katika sekta zote, ikiwemo sekta ya fedha ili
kuiwezesha sekta binafsi kuanzisha, kuendesha na kutoa huduma bora za
kifedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeweka sheria na taratibu za kusaidia
nguvu na juhudi za wananchi katika kuanzisha benki au taasisi za fedha katika
maeneo yao ikiwa ni pamoja na maduka ya kubadilisha fedha za kigeni.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
34
Kwa hiyo, Serikali inategemea kuwa wananchi watatumia fursa hii ya
mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyopo nchini na kuanzisha huduma za
kubadilisha fedha za kigeni katika maeneo yenye uhitaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania itaendelea
kusimamia kwa ukaribu zaidi maduka ya kubadilisha fedha za kigeni nchini ili
yaweze kutoa huduma bora na inayokidhi matakwa ya sheria na kanuni za
biashara ya fedha. Hivi karibuni Benki Kuu imetoa kanuni mpya kwa lengo la
kuimarisha usimamiaji wa maduka hayo. Maduka yote ya kubadilisha fedha za
kigeni yanatakiwa kufunga mashine za EFDs ili kuiwezesha TRA na BoT kupata
taarifa za moja kwa moja juu ya miamala inayofanywa kwenye maduka hayo.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Bakar swali la nyongeza.
MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana
kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu
mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amesema
kwamba Serikali imebaki katika kuweka mazingira mazuri, lakini naona kwamba
mazingira mazuri hayo si kweli sana kwa sababu hayaonekani maana
wananchi wanalalamika sana. Kwa sababu ukienda Bureau de Change hii ina
rate hii, ukienda Bureau de Change nyingine ina rate tofauti na zimetapakaa
sehemu zote kama sisimizi. Je, Serikali inachukua hatua gani kuhakikisha rates
hizo zinalingana? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Naibu
Waziri amekiri kuwa Serikali imejitoa katika biashara hii ya kumiliki Bureau de
Change lakini huo ulikuwa ni uamuzi wa zamani na tujue kwamba sasa hivi
dunia imebadilika, ni dunia ya sasa. Je, atakubaliana nami kwamba sasa
umefika wakati wa Serikali kumiliki huduma hii ili kuwaondolea wananchi wake
matatizo ambayo wanakabaliana nayo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza
nianze kwa kumshukuru kwa kuuliza maswali mazuri ya nyongeza ambayo
yanakidhi haja na yanaakisi kinachoendelea katika maduka yetu ya kubadilisha
fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, jibu la swali lake la kwanza kwamba rates ni
tofauti sana kutoka duka moja kwenda duka lingine, nakubaliana naye na hii
yote ni kuonesha kwamba tuko ndani ya soko huria na kila mtu anatakiwa ku-
charge anavyoona inafaa. Pia kiuchumi, sisi wachumi tunafahamu kwamba bei
ya bidhaa yoyote ile hutegemea na demand na supply. Kwa hiyo, kama
demand ya bidhaa hiyo ni kubwa bei zitakuwa tofauti kutoka kwa muuzaji
mmoja kwenda kwa muuzaji mwingine. (Makofi)
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
35
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, Serikali iweze kurudi kwenye
kuendesha biashara kama hizi na kwamba huo ulikuwa ni uamuzi wa zamani,
naamini uamuzi ule ulikuwa ni sahihi na bora. Kama nilivyosema katika jibu
langu la msingi kwamba tangu mwaka 1991 Serikali ilishajitoa kuendesha
mabenki haya. Tunaendelea kusisitiza, sisi kama Serikali tutaendelea kutunga
sera na sheria mbalimbali za kusimamia maduka haya ili yaweze kutoa huduma
zilizo bora kwa wananchi wetu.
Na.115
Fursa Zitokanazo wa Mgodi wa Stamigold - Biharamulo
MHE. OSCAR R. MUKASA aliuliza:-
Mgodi wa Stamigold, Biharamulo uko kijijini Mavota katika Wilaya ya
Biharamulo na wananchi wa Kijiji cha Mavota kwa sasa hawana fursa hata
kidogo ya kufanya uchimbaji mdogo mdogo licha ya kwamba mgodi huo upo
kijijini kwao, hali ambayo imekuwa chanzo kikubwa cha migogoro
inayosababisha uvunjifu wa amani:-
(a) Je, Serikali iko tayari kuwa na mazungumzo ya kimkakati na
wananchi wa Kijiji cha Mavota kupitia Mbuge wao kwa
manufaa ya uwekezaji na wanakijiji wa Mavota?
(b) Kama Serikali haiko tayari kufanya mazungumzo hayo, je, ni kwa
sababu zipi?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini,
napenda kujibu swali la Mheshimwa Oscar Rwegasira Mukasa, Mbunge wa
Biharamulo Magharibi, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ipo tayari kuwa na mazungumzo na
wananchi wa Kijiji cha Mavota kwa lengo la kuwawezesha wananchi hao
kutumia fursa zilizopo katika Mgodi wa Stamigold karibu na Mavota. Mgodi huo
kwa sasa unamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100 kupitia STAMICO ambapo
Stamigold kampuni tanzu ya STAMICO ndiyo inayofanya shughuli za uchimbaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mambo muhimu yatakayozingatiwa ni pamoja
na kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji hao wadogo, kuwaelimisha
namna ya kupata mitaji ya uchimbaji ikiwa ni pamoja na kutumia fursa za
kuomba ruzuku Serikalini. Kadhalika, pamoja na kuwapa elimu na
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
36
kuwahamasisha kuunda vikundi vya uchimbaji ili waweze kusaidiwa kwa
pamoja. Aidha, Mgodi wa Biharamulo utawapatia mafunzo ya utaalamu wa
kuchimba madini pamoja na kuwafundisha kanuni za usalama, afya na utunzaji
wa mazingira katika migodi yao. Lakini pia watapewa mafunzo kwa vitendo
katika mgodi wa Stamigold pale itakapohitajika kufanya hivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, mgodi huo uko tayari na ulishaanza
kuwasaidia wananchi wa Kijiji cha Mavota. Kati ya tarehe 26 na 30 Juni, 2015,
Mavota Gold Mine Group kilipewa ushauri wa namna bora ya kuendesha
shughuli za uchimbaji na utafiti wa dhahabu katika eneo walilomilikishwa leseni.
Kikundi hicho kilimilikishwa leseni ya uchimbaji mdogo yenye Namba PL
001493WLZ iliyotolewa tarehe 23 Februari, 2015. Eneo hilo lina ukubwa wa hekta
9.43.
Mheshimiwa Naibu Spika, mgodi umetoa fursa za ajira kwa vijiji vya jirani.
Vijana wenye ajira za muda mrefu kutoka vijiji vya jirani ni 15 na wafanyakazi
wenye mikataba ya muda mfupi ni 54.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, mgodi umetoa fursa za kibiashara kwa
vikundi vitatu kutoka vijiji vya Mavota pamoja na Mkukwa ambapo wanavikundi
hushirikiana kutafuta mazao ya kuuza mgodini kwa kuwasilisha mazao hayo kila
wiki. Mazao hayo ni pamoja na viazi vitamu, mihogo, mboga za majani pamoja
na matunda. Kutokana na kufanya biashara na Stamigold kati ya kipindi cha
Julai 2014 na Disemba 2015, vikundi vyote vitatu vimeweza kujipatia zaidi ya
shilingi milioni 200.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mukasa swali la nyongeza.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu
mazuri yenye kuakisi nia ya Wizara na Serikali kushirikiana nasi, nina swali moja la
nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali la msingi, imeelezwa vizuri kabisa
kwamba uvunjifu wa amani ni moja ya matokeo hasi ya kukosekana kwa fursa
hizi za wananchi wa Mavota kushiriki kwenye uchumi uliowazunguka. Kwa
sababu suala la uvunjifu wa amani si suala la kusuburi, ni la haraka, je, Serikali na
Wizara iko tayari kutoa kauli inayothibitisha uharaka wao katika kuja
kuzungumza na wananchi wa Mavota?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza
kabisa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua ambazo Serikali
imechukua kupitia Wizara yetu ni pamoja na kuhakikisha kwamba uchimbaji
salama na makini unafanyika kwenye eneo hilo.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
37
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia umuhimu huo, ofisi yetu iko
tayari kwenda kuzumgumza na wananchi kuwahakikishia amani zaidi kwenye
shughuli za uchimbaji eneo la Mavota.
NAIBU SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tumefikia mwisho wa maswali yetu
lakini nina matangazo kadhaa hapa, nitayasoma kabla hatujaendelea.
Tangazo la kwanza linahusu wageni waliopo Bungeni asubuhi hii,
tunaanza na wageni wa Waheshimiwa Wabunge.
Kundi la kwanza ni wageni watano wa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani
Bungeni, Mheshimiwa Freeman Mbowe, ambao ni viongozi wa Baraza la Vijana
la CHADEMA wakiongozwa na Ndugu Patrobas Katambi, Mwenyekiti wa
BAVICHA, karibuni sana. (Makofi)
Kundi lingine ni wageni 18 wa Mheshimiwa Engineer Stella Manyanya,
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, ambao ni wanafunzi wa
Chuo Kikuu cha Dodoma, karibuni sana. (Makofi)
Wageni wawili wa Mheshimiwa Godbless Lema ambao ni Meya wa Jiji la
Arusha, Ndugu Kalisti Lazaro na Diwani wa Kata ya Baraza, Ndugu George
Mbitika, karibuni sana. (Makofi)
Wageni wawili wa Mheshimiwa January Makamba, Waziri wa Nchi, Ofisi
ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ambao ni wapiga kura wake,
karibuni sana. (Makofi)
Wageni wawili wa Mheshimiwa Oscar Rwegasira Mukasa kutoka Jimbo la
Biharamulo Magharibi ambao ni wat