2
HOTUBA YA MKUU WA WILAYA YA KINONDONI BW.PAUL MAKONDA YA KUWAAGA WASHINDI WA TUZO YA ANZISHA (ANZISHA PRIZE) KUTOKA TANZANIA TAREHE 09 NOVEMBA 2015. Mkurugenzi TPSF, Ndugu Waandishi wa Habari, Wageni Waalikwa, Nimeelezwa kuwa leo tunakutana hapa kuwaaga na kuwatakia kheri vijana wa kitanzania SirJeff Dennis (21) na George Mtemahaji (22) ambao watasafiri kesho kuelekea Afrika ya kusini baada ya kushinda mchakato wa awali wa Tuzo za Anzisha. Hii ni fahari kubwa sio kwa hawa vijana tu bali na kwa Taifa kwa jumla na tunawatakia kila la kheri katika fainali za kumpata mshindi mkuu (Grand Winner) wa Tuzo ya Anzisha ambapo nimeambiwa fainali itafanyika baada ya kuhitimisha mafunzo ya wiki mbili ya ujasiriamali. Nawapongeza pia Chuo cha Uongozi Afrika (African Leadership Academy) cha Afrika kusini kwa maandalizi ya Tuzo za Anzisha kwani pamoja na kuwawezesha wajasiriamali vijana lakini pia Tuzo hii inasaidia kuunganisha vijana wa Afrika kwani inahusisha vijana toka Afrika nzima. Niseme tu kwamba nimekua na imani kubwa na vijana wetu SirJeff na George na hii ni baada ya kupata taarifa kwamba kati ya maombi zaidi ya 500 yaliyoshindanishwa katika Tuzo ya Anzisha kwa mwaka 2015 mmefanikiwa kuingia katika 12 bora, hii ni hatua ya juu sana...Nawapongeza mno katika hili na

Hotuba DC Makonda- Anzisha

Embed Size (px)

DESCRIPTION

Hotuba DC Makonda- Anzisha

Citation preview

Page 1: Hotuba DC Makonda- Anzisha

HOTUBA YA MKUU WA WILAYA YA KINONDONI BW.PAUL MAKONDA YA KUWAAGA WASHINDI WA TUZO YA ANZISHA (ANZISHA PRIZE) KUTOKA TANZANIA TAREHE 09 NOVEMBA 2015.

Mkurugenzi TPSF,

Ndugu Waandishi wa Habari,

Wageni Waalikwa,

Nimeelezwa kuwa leo tunakutana hapa kuwaaga na kuwatakia kheri vijana wa

kitanzania SirJeff Dennis (21) na George Mtemahaji (22) ambao watasafiri kesho

kuelekea Afrika ya kusini baada ya kushinda mchakato wa awali wa Tuzo za

Anzisha.

Hii ni fahari kubwa sio kwa hawa vijana tu bali na kwa Taifa kwa jumla na

tunawatakia kila la kheri katika fainali za kumpata mshindi mkuu (Grand Winner)

wa Tuzo ya Anzisha ambapo nimeambiwa fainali itafanyika baada ya kuhitimisha

mafunzo ya wiki mbili ya ujasiriamali.

Nawapongeza pia Chuo cha Uongozi Afrika (African Leadership Academy) cha

Afrika kusini kwa maandalizi ya Tuzo za Anzisha kwani pamoja na kuwawezesha

wajasiriamali vijana lakini pia Tuzo hii inasaidia kuunganisha vijana wa Afrika

kwani inahusisha vijana toka Afrika nzima.

Niseme tu kwamba nimekua na imani kubwa na vijana wetu SirJeff na George na

hii ni baada ya kupata taarifa kwamba kati ya maombi zaidi ya 500

yaliyoshindanishwa katika Tuzo ya Anzisha kwa mwaka 2015 mmefanikiwa

kuingia katika 12 bora, hii ni hatua ya juu sana...Nawapongeza mno katika hili na

inawezekana kabisa katika fainali mkashinda nafasi ya kwanza na ya pili.

Page 2: Hotuba DC Makonda- Anzisha

Tunaamini kuwa safari yenu ya ujasiriamali imeongezwa nguvu katika mashindano

haya na itapanuka zaidi ili kuleta manufaa na mabadiliko chanya hapa Tanzania na

katika bara hili la Afrika.

Tunatambua kuwa vigezo vya kushiriki tuzo hii vinahitaji wajasiriamali vijana

sana kuanzia miaka 15-22 ambao tayari wanamiliki biashara zao, kwa umri huu

vijana wengi hapa Tanzania wanakua bado wapo mashuleni na hivyo kujikuta

wakishindwa kumiliki biashara lakini vijana hawa wameonyesha kuwa

inawezekana kujiajiri na kuendesha biashara yenye mafanikio hata unapokuwa

shuleni ama chuoni na bila kuathiri masomo yako.

Napenda kutoa shukrani za dhati kabisa kwa TaasisiTaasisi ya Sekta Binafsi

Tanzania (TPSF) kutokana na jitihada zao za kuinua wajasiriamali hapa nchini,

naamini kwamba jitihada hizi za TPSF zinahitaji kuungwa mkono kwani zinasaidia

ukuaji wa uchumi hapa nchini na uchumi unapokua hata mapato ya nchi yanakua

na hivyo kuiwezesha serikali kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi wake.

Nawatakia kila la kheri SirJeff Dennis na George Mtemahanji.