Upload
othman-michuzi
View
336
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
1/24
1
SALAMU ZA MWAKA MPYA ZA RAIS WA JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA DKT. JAKAYAMRISHO KIKWETE KWA WATANZANIA,
TAREHE 31 DESEMBA, 2014
Utangulizi
Ndugu zangu;
Watanzania Wenzangu;
Kama ilivyo ada imefikia siku ya kuuaga mwaka mmoja nakuukaribisha mwaka mwingine. Leo tunauaga mwaka 2014 na
kuukaribisha mwaka mpya wa 2015. Tunamshukuru Muumba wetu
mwingi wa rehema kwa kutujaalia uzima na kutuwezesha kuifikia siku ya
leo. Kwa ndugu na jamaa zetu ambao hawakujaliwa kuiona siku ya leo
tuzidi kuwaombea mapumziko mema. Nasi tumuombe Mwenyezi Mungu,
mwingi wa rehema atujaalie umri mrefu, afya njema na mafanikio tele kwa
kila tuliombalo katika mwaka 2015 na miaka ijayo.
Ndugu wananchi;
Hizi ni salamu zangu za mwisho za mwaka mpya kutoa nikiwa Rais
wa nchi yetu. Mwakani salamu kama hizi zitatolewa na Rais wetu mpya.
Mimi wakati huo nitakuwa raia wa kawaida kijijini kwangu Msoga
nikifuatilia kwenye TV na radio hotuba ya Rais wa Awamu ya Tano ya
uongozi wa nchi yetu akitoa salamu zake za kwanza za mwaka mpya,
itakuwa siku ya furaha na faraja kubwa kwangu.
Hali ya Usalama
Ndugu Wananchi;
Tunaumaliza mwaka 2014 kwa salama na amani. Mipaka yetu iko
salama na hakuna tishio lolote la kiusalama kutoka ndani au nje ya nchi
yetu. Uhusiano wetu na nchi jirani na nyinginezo duniani ni mzuri.
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
2/24
2
Hakuna nchi iliyo adui au tunayoitilia shaka kuwa na njama za kuhatarisha
usalama wa Tanzania. Nawapongeza wanadiplomasia wetu pamoja na
viongozi na watendaji wa vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuendelea
kuifanya nchi yetu kuwa salama.Uhalifu Unapungua
Ndugu Wananchi;
Taarifa za Polisi zinaonyesha kuwa, mwaka 2014 vitendo vya uhalifu
vimepungua ikilinganishwa na mwaka 2013. Mwaka huu, matukio ya
uhalifu yaliyoripotiwaPolisi yalikuwa64,088ikilinganishwa na matukio
66,906katika mwaka 2013. Haya ni matokeo ya kazi nzuri inayofanywa na
Jeshi la Polisi wakishirikiana na vyombo vingine vya usalama pamoja naraia wema. Naomba ushirikiano huu uendelee mwaka ujao na miaka ijayo
ili tuweze kupata mafanikio makubwa zaidi.
Ajali za Barabarani
Ndugu Wananchi;
Nimefarijika kusikia pia kuwa matukio ya ajali za barabarani nchini
nayo yanaendelea kupungua. Mwaka huu kumetokea ajali14,048
zilizosababisha vifo vya watu 3,534na wengine16,166kujeruhiwa.
Mwaka 2013 kulitokea ajali22,383zilizosababisha vifo3,746na majeruhi
19,433. Hivyo mwaka huu kulikuwa na ajali8,335,vifo212na majeruhi
3,267pungufu kuliko mwaka jana. Huu ni mwelekeo mzuri na wa kutia
moyo ingawa bado ni nyingi mno. Naomba yale tuliyoyafanya
yaliyotuwezesha kupata unafuu huu mwaka huu yaendelezwe maradufu
mwaka 2015 na miaka ijayo.
Ugaidi
Ndugu Wananchi;
Mwaka huu tumefanikiwa kutambua mtandao wa viongozi na
washirika wao wanaotuhumiwa kupanga na kufanya mashambulizi ya
kigaidi kwa kutumia mabomu na kumwagia watu tindikali Tanzania Bara
na Zanzibar. Watu112wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya ugaidi
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
3/24
3
wametiwa nguvuni. Tayari watuhumiwa87kati yao wameshafikishwa
mahakamani na waliosalia watafikishwa wakati wo wote. Uchunguzi
unaendelea ili kuwatambua wahusika wengine ambao hawajakamatwa.
Ndugu wananchi;Kwa niaba ya Watanzania wenzangu wote, natoa pongezi nyingi kwa
vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kwa kazi nzuri waliyofanya ya
kutambua mtandao wa ugaidi nchini na kuchukua hatua thabiti za
kuudhibiti. Hali kadhalika nawashukuru raia wema waliotoa taarifa
zilizowezesha haya kufanyika. Hatupaswi kubweteka wala kudhani kuwa
mambo yamekwisha. Lazima tuendelee kuchukua tahadhari muda wote
kwani hatujui adui anapanga kufanya hujuma gani, lini na wapi.Dawa za Kulevya
Ndugu Wananchi;
Tumeendelea kupata mafanikio ya kutia moyo katika vita dhidi ya
biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini. Mwaka huu
watuhumiwa935wakiwemo vigogo wa biashara hii haramu duniani
wamekamatwa. Jumla ya kesi19zimefunguliwa Mahakamani. Aidha,
kiasi chakilo 400za heroine, kilo45za cocaine nakilo81,318za bangi
zimekamatwa. Narudia kutoa pongezi nyingi kwa Kikosi Kazi Maalum
cha Kukabiliana na dawa za kulevya nchini kwa mafanikio yanayoendelea
kupatikana. Matunda ya kazi yao tunayaona. Naomba juhudi ziongezwe
maradufu mwaka ujao na miaka ijayo. Serikali itaendelea kuwaunga
mkono.
Ndugu wananchi;
Kama nilivyoahidi mwaka jana, Muswada wa Sheria ya Kuthibiti na
Kupambana na Dawa za Kulevya umeshasomwa kwa mara ya kwanza
katika Mkutano wa Novemba, 2014 wa Bunge letu tukufu. Pamoja na
kupendekeza kuongeza adhabu kwa makosa ya kujihusisha na dawa za
kulevya, Muswada huo pia unapendekeza kuanzisha chombo kipya chenye
nguvu cha kuzuia na kupambana na dawa za kulevya. Muswada huu
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
4/24
4
ukipitishwa na kuwa Sheria tutakuwa tumeongeza nguvu ya mapambano
dhidi ya biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini.
Ujangili wa Wanyamapori
Ndugu Wananchi;Katika mwaka tunaomaliza leo mapambano dhidi yaujangili na
biashara haramu ya bidhaa zinazotokana na wanyama pori
yameimarishwa. Kwa ujumla kasi ya ujangili imeendelea kupungua.
Katika mwaka 2014 ndovu114waliuawa ikilinganishwa na ndovu219
waliouawa mwaka 2013 au ndovu473mwaka 2012. Aidha, majangili
1,354wamekamatwa na pembe za ndovu542na silaha mbalimbali184
nazo zilikamatwa. Naamini uamuzi wa kuifanya Idara ya Wanyamaporikatika Wizara ya Maliasili na Utalii kuwa Wakala yaaniTanzania Wildlife
Agency(TAWA) kutaongeza nguvu ya kuhifadhi wanyama pori na
mapambano dhidi ya ujangili.
Natoa pongezi nyingi kwa askari wa wanyamapori, Jeshi la Polisi na
vyombo vingine vya Serikali na raia wema kwa kazi nzuri wanayoendelea
kufanya na mafanikio yanayoendelea kupatikana. Juhudi za kupambana
na ujangili na biashara haramu ya bidhaa zinazotokana na wanyama pori
zitaendelezwa kwa nguvu zaidi mwaka ujao 2015 na miaka inayofuatia.
Napenda kutumia fursa hii kuwashukuru kwa dhati marafiki zetu wa
maendeleo wanaotuunga mkono kwa hali na mali katika mapambano
haya. Naomba waendelee kutusaidia.
Hali ya Uchumi Jumla
Ndugu wananchi;
Mwaka 2014 ulikuwa mzuri kwa uchumi wa taifa. Uzalishaji katika
sekta nyingi ulikuwa ni mzuri. Ndiyo maana tunategemea kuwa tutafikia
au hata kuvuka lengo tulilojiwekea la pato la taifa kukua kwaasilimia 7.4
mwaka huu. Mwaka 2013 pato la taifa lilikua kwaasilimia 7.3. Mfumuko
wa bei uliendelea kushuka na kufikiaasilimia 5.8Novemba, 2014
ukilinganisha na Januari 2014 ulipokuwaasilimia 6.0. Hali nzuri ya
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
5/24
5
upatikanaji wa chakula nchini imesaidia sana kufanya mfumuko wa bei
kuendelea kushuka. Ni matumaini yangu kuwa mfumuko wa bei
utaendelea kushuka na kufikiaasilimia 5ifikapo Juni, 2015.
Mauzo NjeNdugu Wananchi;
Mauzo nje yameendelea kuongezeka. Katika kipindi kilichoishia
Oktoba 31, 2014, Tanzania iliuza nje bidhaa na huduma zenye thamani ya
dola za Marekanimilioni 8,503.9ukilinganisha na mauzo ya dolamilioni
8,332.5katika kipindi kama hicho mwaka 2013. Mapato yetu yangekuwa
makubwa zaidi kama bei za kahawa, chai, korosho na pamba
zisingeanguka au bei ya dhahabu nayo isingepada.
Akiba ya Fedha za Kigeni
Ndugu Wananchi;
Akiba yetu ya fedha za kigeni ilikuwa Dola za Marekanimilioni
4,251.8 kwa kipindi kilichoishia Novemba 30, 2014. Kiasi hicho
kinatuwezesha kuagiza bidhaa toka nje kwa miezi4.1.Hii ni chini ya lengo
letu la kuwa na akiba ya fedha za kigeni ya kuagiza bidhaa kwa miezi
minne na nusu. Hata hivyo,sina wasiwasi kabisa kwamba tofauti hii
ndogo tutaweza kuiziba mwaka 2015.
Mapato ya Serikali
Ndugu Wananchi;
Makusanyo ya mapato ya Serikali kwa mwezi, kati ya Julai hadi
Novemba, 2014 yaliongezeka kutoka shilingibilioni 3,555.5kipindi kama
hicho mwaka 2013 hadi shilingibilioni3,924.1mwaka huu. Hata hivyo,
makusanyo hayo yalikuwaasilimia 90ya lengo tulilojiwekea la kukusanya
shilingibilioni 4,459.7. Kwa mujibu wa Mamlaka ya Mapato, zipo sababu
mbalimbali zilizosababisha lengo lisifikiwe katika nusu ya kwanza ya
mwaka wa fedha wa 2014/2015. Hatua zipasazo zinaendelea kuchukuliwa
kurekebisha mambo hayo ili katika nusu ya pili ya mwaka huu wa fedha
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
6/24
6
makusanyo yafikie lengo na ikiwezekana yazidi ili kufidia pengo la nusu ya
kwanza.
Takwimu Mpya za Pato la Taifa
Ndugu wananchi,Ni utaratibu wa kawaida wa nchi zote duniani kuwa na mwaka
unaotumika kuwa kizio (base year) cha kukokotoa takwimu za Pato la
Taifa. Ni utaratibu wa kawaida pia kwa kila baada ya muda fulani mwaka
wa kizio hubadilishwa. Lengo ni kuboresha takwimu husika. Katika
marekebisho hayo pia huingizwa thamani ya bidhaa na huduma mpya
katika pato la taifa na kuziondoa zilizotoweka ili kutoa picha halisi ya
ukuaji wa shughuli za kiuchumi.Katika miaka ya hivi karibuni nchi za Ghana (mwaka 2010), Nigeria
(mwaka 2013) na Kenya (mwaka 2014) wamefanya marekebisho ya
takwimu zao za pato la taifa. Na sisi Tanzania tumefanya hivyo mwaka huu
(2014). Hii ni mara ya tano kwa nchi yetu kurekebisha takwimu za pato la
taifa. Mara nne zilizopita ilikuwa mwaka 1966, 1976, 1992 na 2001.
Ndugu wananchi;
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imekamilisha marekebisho ya takwimu za
pato la taifa na kukokotoa takwimu mpya kwa kutumia mwaka 2007 kama
mwaka wa kizio. Kutokana na marekebisho yaliyofanyika, pato la taifa
kwa mwaka 2013 nishilingi trilioni70kwa kutumia bei za mwaka 2007.
Ukitumia bei za mwaka 2001, pato la taifa kwa mwaka 2013 nishilingi
trilioni 53.17.Kuongezeka kwa pato la taifa kumeongeza pia pato la
wastani la kila Mtanzania kutokashilingi 1,186,200(sawa naUS$ 742) kwa
bei za mwaka 2001 hadishilingi 1,560,050(sawa naUS$ 977) kwa bei za
mwaka 2007.
Kilimo na Chakula
Ndugu Wananchi;
Mwaka 2014 ulikuwa mzuri sana kwa uzalishaji wa mazao ya
chakula nchini. Uzalishaji ulikuwa tanimilioni 16.02ukilinganisha na
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
7/24
7
uzalishaji wa tanimilioni 14.38mwaka wa jana 2013.Hili ni ongezeko la
tanimilioni 1.64. Kwa mujibu wa mahitaji yetu ya chakula nchini kuna
ziada yatani milioni 3.25.Katika ziada hiyo, mahindi yanachangia tani
milioni 1.55,mchele tani794,000na kiasi kinachobakia kinachangiwa namazao mengine ya chakula.
Ndugu wananchi;
Kuna jambo moja muhimu kuhusu ununuzi wa nafaka ambalo
ningependa kulifafanua. Naomba ieleweke kuwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi
ya Chakula (NFRA) sio mnunuzi wa mahindi yote, mpunga wote na mtama
wote unaozalishwa na wakulima nchini. Wakala hununua sehemu ndogo tu
ya nafaka ya ziada iliyozalishwa na hununua kwa ajili ya kuweka akiba yataifa ya chakula cha kutumika wakati wa dharura ya watu kupata tatizo la
njaa. Aidha, Wakala hununua kiasi kinacholingana na uwezo wa maghala
yake kuhifadhi. Kwa sasa uwezo wa maghala yetu ni kuhifadhitani 246,000
ingawaje tunaendelea kujenga maghala mengine mpaka tufikie uwezo wa
kuhifadhitani 400,000ifikapo 2015.Hivyo basi kwa Wakala kununuatani
292,415.41mwaka huu ina maana kwamba kiasi cha kaributani 50,000
zinahifadhiwa nje ya maghala kwa kutumia maturubai. Huu siyo utaratibu
mzuri na haifai kuendelea nao kwani kuna hatari ya nafaka hiyo kuharibika na
kuzua mgogoro mkubwa siku moja.
Ndugu wananchi;
Baada ya NFRA kununuatani 292,415.41kuna takribanitanimilioni
2.96za nafaka ya ziada ambayo iliyobaki mikononi mwa wakulima.
Mategemeo yetu ni kuwa wafanyabiashara wetu watanunua nafaka hiyo kwa
ajili ya kuuza mijini na kwingineko inakohitajika. Bahati mbaya mwaka huu
kama ilivyokuwa mwaka wa jana, wafanyabiashara wetu hawakuweza
kununua nafaka yote ya ziada ambayo Serikali haikuweza kununua kupitia
Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula. Hali hii imezua tatizo ambalo Serikali
kwa kushirikiana na wafanyabiashara nchini hatuna budi kulitafutia
majawabu. Tunalazimika kutafuta masoko mengine ndani na hata nje ya nchi
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
8/24
8
ya kuuza mahindi, mpunga na mtama wa ziada. Nimeagiza Wizara ya Kilimo,
Chakula na Ushirika na Wizara ya Viwanda na Biashara kukaa chini na
kushirikiana na wafanyabiashara kulitafutia ufumbuzi suala hili lenye maslahi
makubwa kwa wakulima na nchi yetu kwa jumla.Ndugu Wananchi;
Katika mazingira haya, ninapopata taarifa ya kuwepo watu wanaotaka
kuuza mahindi nje ya nchi lakini wanawekewa vikwazo na maafisa wa Serikali
inanishangaza na kunisikitisha. Nawataka wale wote wanaofanya hivyo
waache mara moja na badala yake wawasaidie wafanyabiashara hao
kufanikisha azma yao. Hali kadhalika, tuwashawishi watu wengine nao
wajitokeze kufanya biashara hiyo. Jambo muhimu ninalopenda kulisisitiza nikwamba pawepo na utaratibu mzuri ili biashara hiyo ifanywe kwa kutumia
njia halali na zilizo wazi. Kutumia njia za panya hakukubaliki na wala hakuna
sababu ya kufanya hivyo.
Miradi ya Kimkakati
Ndugu wananchi;
Katika mwaka 2014 utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kwa
mujibu wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/12 2015/16)
umeendelea vizuri. Tunayo matumaini makubwa kwamba katika mwaka
2015 miradi mingi itakamilika.
Tuanze na Mradi wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara na
Songosongo hadi Dar es Salaam. Mradi huu unategemewa kukamilika
Januari, 2015. Utakapokamilika utatuwezesha kutimiza lengo letu la
kuzalishaMW 2,780zaumeme ifikapo 2016. Mipango ya kupata ardhi ya
ujenzi wa mitambo ya kuchakata gesi asili kuwa ya kumiminika (LNG) ili
iweze kusafirishwa kwenda kwenye masoko, inakwenda vizuri.
Ndugu Wananchi;
Utekelezaji wa mradi mkubwa wa kimkakati wa kusambaza umeme
vijijini umeendelea vizuri na tumepata mafanikio makubwa yasiyokuwa
na mfano wake katika historia ya nchi yetu. Hadi kufikia Novemba, 2014,
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
9/24
9
jumla ya vijiji3,836vimepatiwa umeme na vingine1,500vinategemewa
kupatiwa umeme ifikapo Juni, 2015. Hivyo basi, vijiji5,336kati ya vijiji
12,423vya Tanzania Bara vitakuwa vimepatiwa umeme. Hii ni sawa na
asilimia 43ya vijiji vyote nchini vitavyokuwa vimepata umeme. Hivi sasawananchi milioni 17.3nchi nzima sawaasilimia 36 wamefikiwa na
huduma ya umeme ikilinganishwa na watumilioni 8.1sawa naasilimia
18.4waliokuwa wamefikiwa na huduma hiyo mwaka 2012. Mwaka 2015
tunatarajia watumilioni 18.2sawa naasilimia 38watafikiwa na umeme.
Kwa upande wa vijijini mwaka 2012 watumilioni 2.3sawa naasilimia 7
walikuwa na umeme. Ifikapo Juni 2015, idadi hiyo itaongezeka na kuwa
milioni 7.4sawa naasilimia 21. Haya ni mafanikio makubwa kwawananchi wengi vijijini na mijini kupata umeme katika kipindi kifupi kiasi
hiki. Ni mageuzi ya aina yake yatokayotoa mchango muhimu katika
kuinua hali za maisha ya Watanzania.
Ndugu Wananchi;
Tunaanza kuiona nuru ya matumaini kwamba siku si nyingi kutoka
sasa, makaa ya mawe ya Mchuchuma na madini ya chuma ya Liganga
yataweza kutumika kwa maendeleo ya nchi yetu na watu wa Ludewa.
Maandalizi yote muhimu yamekamilika kwa ajili ya Januari, 2015 kuanza
ujenzi wa mgodi wa makaa ya mawe kule Mchuchuma, mtambo wa kufua
umeme, ujenzi wa mgodi wa chuma kisichoyeyushwa pale Liganga na
ujenzi wa kiwanda cha kuyeyusha chuma.
Natoa pongezi maalum kwa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na
wabia wenzao, Kampuni ya Sichuan Hongda ya China kwa hatua
iliyofikiwa. Inakadiriwa kuwa miradi hii ikikamilika itatoa ajira33,000za
moja kwa moja na zisizokuwa za moja kwa moja.
Ndugu Wananchi;
Mradi mwingine mkubwa wa kimkakati ni ule wa kujenga Eneo
Maalumu la Kiuchumi (Special Economic Zone) la Mbegani, Bagamoyo.
Kwa mujibu wa mpango kazi wa wabia wa mradi huo yaani Mamlaka ya
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
10/24
10
Kuendeleza Maeneo huru ya Uwekezaji (EPZA), Kampuni yaChina
Merchants Holdings Internationalna Mfuko wa Uhifadhi wa Akiba ya Mali
za Serikali ya Oman (Oman State General Reserve Fund), ujenzi wa bandari
na miundombinu mingine itakayowezesha viwanda kujengwa imepangwakuanza Julai 2015.
Miundombinu ya Usafiri na Uchukuzi
Ndugu Wananchi;
Katika mwaka huu wa 2014 kazi ya kujenga barabara za lami na
kuimarisha barabara za udongo ili ziweze kupitika wakati wote ziliendelea
kote nchini. Huu nao ni mradi mkubwa wa kimkakati. Barabara za lami19
zenye urefu wakilometa1,459zimekamilika kujengwa mwaka huu katikaMikoa ya Ruvuma, Mbeya, Rukwa, Kagera, Dar es Salaam, Dodoma, Tanga,
Morogoro, Arusha, Tabora na Shinyanga. Ujenzi unaendelea kwa barabara
nyingine24katika mikoa ya Dodoma, Iringa, Mbeya, Kilimanjaro, Rukwa,
Simiyu, Katavi, Tabora, Mwanza, Dar es Salaam, Kagera na Pwani ambazo
wakati wo wote mwaka 2015 zitakamilika. Maandalizi ya kuanza ujenzi wa
barabara nyinginenaneyanaendelea vizuri sehemu mbalimbali nchini.
Kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara, tumeendelea kufanya
kazi ya ujenzi na ukarabati wa barabara za udongo kote nchini. Mwaka
huu Mfuko huo umetengewashilingi bilioni 751.7ukilinganisha na
shilingi bilioni 504.4mwaka jana. Aidha, mwaka huu tumeweka jiwe la
msingi la ujenzi wa Daraja la Mto Kilombero. Matumini yetu ni kuwa
ujenzi wa daraja hilo na Daraja la Kigamboni utakamilika mwaka 2015.
Ujenzi wa Daraja la Malagarasi ulishakamilika mwaka jana,
kinachosubiriwa ni sherehe ya uzinduzi.
Kwa upande wa jiji la Dar es Salaam, tunategemea kukamilisha
ujenzi wa Awamu ya Kwanza ya barabara za mabasi yaendayo kasi. Ni
matarajio yetu pia kwamba mabasi yataanza kusafirisha abiria katika
kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka 2015. Halikadhalika, tunategemea
katika mwaka 2015 ujenzi utaanza wa barabara zinazozunguka jiji la Dar es
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
11/24
11
Salaam (ring roads), barabara ya Mwenge - Morocco na ile ipitayo juu ya
nyingine (flyovers) eneo la TAZARA. Vile vile, daraja jipya la Salenda
litaanza kujengwa. Aidha, kivuko cha abiria300cha MV Dar es Salaam
kitaanza kusafirisha abiria kati ya Dar es Salaam Kaskazini na Ferrymapema mwakani. Hatua zote hizi zinalenga kupunguza msongamano wa
magari katika jiji la Dar es Salaam.
Usafiri wa Anga na Reli
Ndugu wananchi;
Jitihada za kuboresha huduma ya usafiri katika Reli ya Kati
zimeendelea kwa mafanikio. Mwaka huu vichwavinanevya treni
vimekarabatiwa, mabehewa mapya22ya abiria na mabehewa274ya mzigoyamenunuliwa. Mabehewa hayo yameanza kuwasili nchini kati ya
Novemba na Desemba mwaka huu. Kati ya Januari na Mei, 2015
tunatarajia kupokea vichwa vipya vya treni13. Uboreshaji huu wa huduma
za treni unakwenda sambamba na ukarabati wa reli yenyewe, ujenzi wa
madaraja na kuimarisha maeneo yaliyo korofi katika reli hiyo.
Kuhusu ujenzi wa reli iliyo pana zaidi (standard guage), yenye
uwezo wa kubeba mabehewa mengi na kuwezesha treni kwenda kwa
mwendo wa kasi zaidi, juhudi za kutafuta fedha za ujenzi au wabia wa
kushirikiana nasi kujenga zinaendelea. Wakati huo huo, tunaendelea na
juhudi za kutafuta ufumbuzi kwa matatizo ya reli ya TAZARA ili mambo
yaende vizuri. Tutashirikiana kwa karibu na wabia wenzetu wa Zambia.
Bahati nzuri Serikali ya China iko tayari kuunga mkono juhudi zetu za
kufufua reli ya TAZARA.
Usafiri wa Anga
Ndugu Wananchi;
Sekta ya usafiri wa anga imeendelea kukua katika mwaka 2014. Idadi
ya abiria wanaowasili na kutoka katika viwanja vyetu vya ndege nchini
imeongezeka kutoka abiriamilioni 2.5mwaka 2013 hadi abiriamilioni3.5
kufikia Septemba, 2014. Safari za ndege kati ya Tanzania na nchi za nje
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
12/24
12
zimeongezeka kutoka274Januari, 2013 hadi295kufikia Septemba, 2014.
Hili ni ongezeko laasilimia 8. Safari za ndege ndani ya nchi nazo
zimeongezeka kutoka safari230,458mwaka 2013 hadi safari241,922mwaka
2014. Hii ni sawa na ongezeko laasilimia 39. Maongezeko haya nikielelezo na ushahidi kuwa shughuli za utalii na biashara nchini
zimeendelea kukua.
Ndugu Wananchi;
Ujenzi wa Jengo la3 (Terminal3)la Abiriakatika Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Julius Nyerere unaendelea vizuri. Jengo hilo
litakapokamilika mwakani, litakuwa na uwezo wa kuhudumia wastani wa
abiriamilioni 8kwa mwaka. Aidha, ukarabati wa Jengo la2(Terminal2)
utafanyika ili liweze kutoa huduma iliyo bora zaidi. Sambamba na ujenzi
huo, Wakala wa Viwanja vya Ndege wameendelea kukarabati na
kuboresha viwanja vya ndege vyaKIA, Mwanza, Songwe, Bukoba,
TaboranaKigoma. Tunatarajia ukarabati wa viwanja vya ndege vya
ShinyanganaSumbawangakuanzamapema mwaka 2015.
Elimu
Ndugu wananchi;
Tumeendelea kupiga hatua za kuridhisha katika kuboresha elimu
nchini. Tumefanikiwa kupunguza tatizo la upungufu wa maabara, vitabu
na walimu wa shule za msingi na sekondari. Mwaka huu tumeajiri walimu
36,339kati ya81,562wanaohitajika. Tumebakiwa na upungufu wa walimu
45,223yaani26,946wa shule za msingi na18,277wa shule zasekondari
hususan wa masomo ya sayansi.Hivi sasa hatuna tatizo la walimu wa
masomo ya sanaa katika shule za sekondari.
Mwaka huu tumeanza mpango maalumu wa kutoa mafunzo ya
Diploma ya Ualimu kwa masomo ya sayansi na hisabati katika Chuo Kikuu
cha Dodoma ambapo jumla ya wanafunzi5,602wa masomo hayo
wamedahiliwa. Mpango huu utatuwezesha kupunguza pengo kubwa
tulilonalo la walimu wa sayansi katika muda mfupi zaidi.
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
13/24
13
Ujenzi wa Maabara
Ndugu wananchi;
Ujenzi wa maabara za Fizikia, Kemia na Baiolojia katika shule za
sekondari za Kata3,463umekwenda vizuri kiasi. Kwa idadi hiyo ya shuleinatakiwa zijengwe maabara10,389ilipofika Novemba, 2014. Taarifa
kutoka TAMISEMI zinaonyesha kuwa hadi kufikia Desemba 29, 2014,
maabara 4,207sawa naasilimia40.5zilikuwa zimekamilika, maabara5,688
sawa naasilimia 54.8zilikuwa katika hatua mbalimbali za ukamilishwaji,
na maabara494sawa naasilimia 4.zilikuwa katika hatua za awali za
ujenzi.
Ndugu Wananchi;Natoa pongezi nyingi kwa Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya,
Wenyeviti na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri za Wilaya na Miji
nchini pamoja na wananchi, kwa jitihada kubwa iliyofanyika. Kwa
kutambua jitihada hizo, nimeongezamiezi sitazaidi kwa wale ambao
hawajakamilisha ujenzi wa maabara hizo wafanye hivyo. Sikusudii
kuongeza tena muda baada ya hapo. Naomba watumie kipindi hicho
kitumike kutafuta vifaa vya maabara. Serikali itasaidia upatikanaji wa
watunza maabara (laboratory technicians) ambao tumeanza programu
kubwa ya mafunzo yao na mahitaji mengine ya maabara.
Ununuzi wa Vitabu
Ndugu Wananchi;
Tumeendelea kupunguza tatizo la uhaba wa vitabu na vifaa vya
kufundishia katika shule za msingi na sekondari. Tumekuwa tunanunua
vitabu kwa kutumia Bajeti ya Serikali na misaada kutoka kwa marafiki zetu
wa maendeleo. Kwa mfano, Serikali ya Marekani imetupatia vitabu
milioni 2.5vya masomo ya sayansi na hisabati kwa shule za sekondari.
Ongezeko hili la vitabu linashusha uwiano uliopo sasa wakitabu kimoja
kwawanafunzi wannena kufikiakitabu kimojakwawanafunzi wawili.
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
14/24
14
Lengo letu ni kila mtoto kuwa na kitabu chake kwa kila somo ifikapo
mwaka 2016.
Sera Mpya ya Elimu na Mafunzo
Ndugu wananchi;Mafanikio mengine tuliyopata mwaka huu ni kukamilika kwa Sera ya
Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014. Hii ni hatua muhimu sana katika
maendeleo ya elimu nchini hakuna badala yake. Sera mpya inalenga
kuinua ubora wa elimu na mafunzo na kuweka mifumo na taratibu
zitakazowezesha Watanzania wengi zaidi kupata fursa za elimu iliyo bora
na inayolinga na wakati tulionao. Jambo jipya sana na la kihistoria katika
Sera mpya ya Elimu ni dhamira ya Serikali ya kuondoa ada katika elimu yasekondari kuanzia mwaka 2016. Mpaka sasa hatuna ada kwenye shule za
msingi, sasa wakati umefika kufanya hivyo pia kwa elimu ya sekondari.
Kwa mujibu wa maelezo hayo ya Sera, nimekwishatoa maagizo kwa
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa, Wizara ya Fedha na Tume ya Mipango kuanza kutafakari
namna jambo hilo litakavyotekelezwa.
Afya
Ndugu Wananchi;
Katika mwaka 2014 jitihada za kuboresha huduma ya afya kwa
Watanzania ziliendelea. Tulipambana kwa mafanikio na mlipuko wa homa
ya dengue iliyowapata watu1,039na kusababisha vifo vya watu3kati yao.
Kwa upande wa maradhi ya ebola tumejiandaa vya kutosha kutambua
watu wenye maradhi hayo wanapoingia nchini kupitia viwanja vya ndege
vya kimataifa na vituo vyote vya mpakani. Aidha, tumejipanga vyema
kuwahudumia wagonjwa wa maradhi hayo iwapo watatokea.
Mwaka huu pia, Madaktari wetuwatanowamekwenda Liberia
kusaidiana na ndugu zetu wa huko katika kukabiliana na ugonjwa wa
ebola. Madaktari wetu hao wako salama na wanaendelea vizuri kutoa
huduma. Madaktari hao watakaporejea nchini watakuwa hazina kubwa ya
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
15/24
15
taifa katika kupanga mipango ya kukabiliana na ugonjwa huu hatari. Hali
kadhalika, watakuwa viongozi wa wengine katika kutibu wagonjwa wa
maradhi ya ebola iwapo watatokea nchini.
Ndugu Wananchi;Katika kipindi cha Januari hadi Desemba, 2014, tumeweza kuajiri
watumishi wa sekta ya afya8,345ambao kati yao kuna madaktari244,
madaktari bingwa75, wauguzi2,555na wataalamu wa kada nyingine za
afya5,471. Mwaka huu pia tumefanikiwa kuongeza udahili wa wanafunzi
kutoka wanafunzi7,956katika mwaka 2012/2013 hadi wanafunzi9,730.
Kwa ongezeko hilo, sasa tumefikiaasilimia 97ya lengo letu la kudahili
wanafunzi10,000ifikapo mwaka 2017.Jitihada zetu za kuongeza fursa za mafunzo kwa Madaktari,
Wauguzi na wataalamu wengine wa afya zina muelekeo mzuri. Ujenzi wa
hospitali ya kufundishia pale Mloganzila unaendelea vizuri na hospitali ya
kufundishia ya Chuo Kikuu cha Dodoma umekamilika. Ni matarajio
yangu kuwa wakati wo wote mwakani ujenzi wa kampasi mpya ya Chuo
Kikuu cha Muhimbili pale Mloganzila utaanza. Ujenzi huo ukikamilika
Chuo kikuu cha Muhimbili kitaweza kudahiliwanafunzi 12,000kutoka
wanafunzi 2,500wa sasa jambo ambalo litafanya upungufu wa Madaktari,
Wauguzi na Wataalamu wa Afya kupata jawabu la uhakika. Tumeendelea
kufanya mambo mengine ikiwemo ujenzi wa jengo la tiba za ubongo na
mishipa ambalo limekamilika pale Muhimbili, sasa tunahangaikia kupata
vifaa.
Maji
Ndugu Wananchi;
Katika mwaka huu wa 2014 tumeendelea kutekeleza miradi
mbalimbali ya kuwapatia wananchi maji safi na salama mijini na vijijini.
Kwa ajili hiyo miradi498ya maji vijijini imekamilika na miradi740ipo
katika hatua mbalimbali za ujenzi. Miradi mingine378ipo katika
maandalizi ya ujenzi kuanza. Ni matarajio yetu kwamba katika mwaka
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
16/24
16
ujao wa 2015, miradi mingine731itatekelezwa na vituo25,790vya kuchota
maji vitajengwa. Miradi hii ikikamilika tutaweza kuwafikiaasilimia 71ya
wananchi wanaopata maji safi na salama vijijini kutokaasilimia 58ya sasa.
Kwa ajili hiyo, tutakuwa tumevuka lengo tulilojiwekea la kuwapatia watumajiasilimia 65ya Watanzania waishio vijijini ifikapo 2015. Ombi langu
kwa ndugu zetu wa Hazina waiangalie sekta hii ya maji kwa ukaribu zaidi
na wawapatie fedha kwa wakati.
Ndugu Wananchi;
Utekelezaji wa mradi wa kuipatia maji miji ya Mwanga Same
Mkomazipamoja na miji na vijiji vyote vya njiani, utaanza Februari, 2015.
Fedha zimekwishapatikana na Mkandarasi wa Awamu ya Kwanzaameshapatikana. Makandarasi wa Awamu ya Pili na Tatu watapatikana
muda si mrefu kutoka sasa. Hii pia itahusu kupata Mkandarasi wa mradi
wa maji wa mji wa Orkesment.
Ndugu Wananchi;
Mwaka huu miradi ya kuipatia maji miji kadhaa nchini ilikamilika na
tatizo la upungufu wa maji litakuwa limepatiwa ufumbuzi. Ipo miji
kadhaa ambayo miradi imefikia hatua ya juu na kwamba wakati wowote
mwakani itakamilika. Jiji la Dar es Salaam lipo katika kundi hili. Kazi ya
upanuzi wa miradi ya maji ya Ruvu Juu na Ruvu Chini kwa msaada wa
Serikali ya Marekani na mkopo kutoka Serikali ya India imefikia hatua
nzuri. Inatarajiwa kukamilika katika nusu ya kwanza ya mwaka 2015.
Mwaka ujao pia visima virefu vya Kimbiji na Kipera vitachimbwa na
Bwawa la Kidunda litaanza kujengwa.
Serikali ya India pia imekubali kutupatia mkopo waDola za
Marekani milioni 268.2kwa ajili ya kugharamia mradi wa kuipatia maji
miji ya Tabora, Nzega na Igunga kutoka Ziwa Victoria. Uwezekano wa
kujumuisha miji ya Sikonge na Urambo katika mradi huo utaangaliwa.
Bunge na Mahakama
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
17/24
17
Ndugu Wananchi;
Katika mwaka 2014, mihimili ya Bunge na Mahakama iliendelea
kutekeleza vyema majukumu yao. Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania limeweza kuendesha shughuli zake kama ilivyopangwa pamojana kulazimika kugawana Ukumbi ule wa Bunge na Bunge Maalum la
Katiba. Bunge limefanya mikutanomitatu,Miswada17ya Sheria ilisomwa
kwa mara ya kwanza, Sheriatanona maazimiosabayalipitishwa. Maswali
ya msingi569na ya nyongeza1,541yaliulizwa na kujibiwa. Aidha, sakata la
Akaunti ya Tegeta Escrow nalo lilijadiliwa na kutolewa maazimio.
Tumeshaanza kuchukua hatua kuhusu maazimio hayo na bado
tunaendelea.Napenda kuitumia nafasi hii kutoa pongezi nyingi kwa Wabunge
wetu kwa kutekeleza vizuri wajibu wao wa Kutunga Sheria na kusimamia
Serikali. Nawasihi waendelee na msimamo huo mwema na chanya kwa
maslahi ya nchi yetu na watu wake.
Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa Mahakama napenda kutambua kazi kubwa na nzuri
inayofanywa ya kupunguza mrundikano wa mashauri katika Mahakama
za ngazi zote. Wahenga wamesemamcheza kwao hutunzwa. Hatuna
budi kutoa pongezi maalum kwa Jaji Mkuu, Mheshimiwa Mohamed
Chande Othman kwa uongozi wake mahiri. Chini ya uongozi wake Majaji
wa Mahakama ya Rufani, Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakimu Wakazi
na Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo wamejiwekea malengo ya
kusikiliza na kutoa hukumu kwa mashauri yasiyopungua200kwa mwaka
kila mmoja wao.
Habari njema na ya kuleta faraja ni kwamba utekelezaji unaendelea
vizuri. Mashauri870yalisikilizwa na kuamuliwa kwenye Mahakama ya
Rufani, mashauri11,334kwenye Mahakama Kuu, mashauri8,715kwenye
Mahakama ya Mahakimu Wakazi na Mashauri25,683katika Mahakama za
Wilaya. Aidha, mkakati wa kupeleka timu ya Majaji wa Mahakama Kuu
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
18/24
18
kwa wakati mmoja kwenye maeneo yenye mashauri mengi kama
ilivyofanyika Kigoma, Shinyanga na Tabora umesaidia sana kupunguza
mrundikano wa mashauri ya siku nyingi. Haijawahi kutokea mashauri
mengi kiasi hicho kusikilizwa na kumalizwa katika historia ya Mahakamanchini.
Ndugu Wananchi;
Mkakati huu mpya umeleta matumaini mapya kwamba tatizo la
kuchelewesha kwa mashauri ambalo lilidhaniwa kuwa ni tatizo sugu sasa
limeanza kupatiwa ufumbuzi. Kwa niaba ya Watanzania wenzangu wote
natoa shukrani na pongezi nyingi kwa Jaji Mkuu, Majaji wa Rufani, Jaji
Kiongozi, Majaji wa Mahakama Kuu na Mahakimu wa ngazi zote kwa kazinzuri waifanyayo.
Hali kadhalika, nampongeza Mtendaji Mkuu wa Mahakama na
watendaji wote wa Mahakama kwa kazi nzuri waifanyayo ya kuwawezesha
Majaji na Mahakimu kutimiza ipasavyo majukumu yao. Hakika utendaji
Mahakamani umebadilika na kuwa bora zaidi. Mimi naahidi kuendelea
kusaidia Mahakama kwa kuwahimiza ndugu zetu wa Hazina kutoa kwa
wakati pesa zilizotengwa katika bajeti.
Mapambano Dhidi ya Rushwa
Ndugu Wananchi;
Mapambano dhidi ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka
yameendelea bila ya ajizi. Katika mwaka huu wa 2014 TAKUKURU
wamepokea taarifa237na wamekamilisha uchunguzi wa mashauri545.
Watuhumiwa waliofikishwa Mahakamani ni428. Mashauri yaliyomalizika
ni205, kati ya hayo125watuhumiwa waliachiliwa na80walipatikana na
hatia na kuhukumiwa. Mwaka huu wa 2014 mali na fedha taslimu zenye
thamani yashilingi bilioni 38.96zimeokolewa. Katika kuimarisha Taasisi
hiyo kiutendaji, maafisa wapya394wameajiriwa.
Sherehe za Miaka 50 ya Muungano
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
19/24
19
Ndugu Wananchi;
Mwaka huu wa 2014 tuliadhimisha miaka 50 ya Muungano wa nchi
zetu mbili yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika
kwa heshima inayostahili. Maadhimisho yalifikia kilele tarehe 26 Aprili,2014 na zilifanyika sherehe nchini kote na sherehe hizo zilifana sana. Ni
ukweli usiopingika kuwa kwa Muungano wetu kuweza kudumu kwa nusu
karne ukiwa bado imara na unazidi kustawi ni mafanikio makubwa.
Matumaini kwa siku za usoni ni mazuri. Naamini Muungano wetu
utaimarika zaidi iwapo Katiba Inayopendekezwa itapitishwa kwani yale
mambo yenye kuleta matatizo hivi sasa yatakuwa yamepatiwa ufumbuzi.
Miaka 50 ya JWTZ
Ndugu Wananchi;
Wakati nchi inasherehekea miaka 50 ya Muungano, baadhi ya
vyombo na taasisi muhimu kitaifa zilifanya hivyo hivyo. Miongoni mwa
walioadhimisha nusu karne ya kuundwa kwake ni Jeshi la Ulinzi la
Wananchi wa Tanzania kama mjuavyo JWTZ ilizaliwa tarehe 1 Septemba,
1964. Jeshi letu liliadhimisha siku yao hiyo kwa kufanya zoezi kubwa la
kivita lililoanza Kibaha mkoani Pwani na kumalizikia Monduli Mkoani
Arusha.
Nilibahatika kushuhudia siku ya mwisho ya zoezi hilo.
Nilifurahishwa sana na kiwango cha utayari kivita cha Jeshi letu. Wanajeshi
wetu walionesha weledi wa hali ya juu, umahiri mkubwa, ujasiri,
ukakamavu na uvumilivu wa aina yake wakati wa kutekeleza majukumu
yao katika mazingira magumu ya uwanja wa medani za vita.
Niliwapongeza siku ile na narudia tena leo kuwapongeza. Niliyoyaona
yamenihakikishia mimi na Watanzania wote kuwa Jeshi letu la Ulinzi la
Wananchi wa Tanzania liko imara kulinda mipaka ya nchi yetu na
kuhakikisha usalama wa taifa letu na watu wake. Jeshi letu bado ni lile
tunalolijua sisi sote, lakini limezidi lile lililomngoa mvamizi Dikteta Iddi
Amin wa Uganda, tena limezidi kwa mbali.
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
20/24
20
Mchakato wa Katiba Mpya
Ndugu Wananchi;
Mwaka huu pia tumeshuhudia kukamilika kwa zoezi muhimu la
kuandika Katiba Inayopendekezwa. Kama tujuavyo sote, mchakato uliozaaKatiba Inayopendekezwa ulikuwa na changamoto nyingi ndani na nje ya
Bunge Maalum la Katiba. Pamoja na hayo, Bunge hilo lilikamilisha kazi
yake kwa salama siku mbili kabla ya tarehe 4 Oktoba, 2014 ambayo ndiyo
ilikuwa siku ya mwisho. Mimi na Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Dkt. Ali
Mohamed Shein tulikabidhiwa nakala za Katiba Inayopendekezwa tarehe 8
Oktoba, 2014. Nimeshatimiza wajibu wangu wa kuchapisha katika Gazeti
la Serikali na kutangaza siku ya kupiga kura ya maoni kuwa tarehe 30Aprili, 2015. Nimeshatoa maagizo kwa Tume ya Uchaguzi kufanya
matayarisho husika ya kuwezesha Kura ya Maoni kufanyika.
Ndugu Wananchi;
Moja ya mambo muhimu ambayo Tume ya Uchaguzi inafanya kwa
sasa ni kuandikisha wapiga kura katika Daftari la Mpiga Kura. Tume
imeamua kutumia mfumo mpya wa Biometric Voters Register.
Uandikishaji wa majaribio umefanyika katika baadhi ya Kata katika
Majimbo ya Mlele, Kawe na Kilombero. Matatizo yaliyojitokeza yatasaidia
kuboresha mfumo huo kabla ya uandikishaji wa watu wote wenye sifa
stahiki kuanza.
Ndugu Wananchi;
Napenda kutumia nafasi hii kuwafahamisha Watanzania wenzangu
wote kuwa mfumo mpya unatengeneza Daftari Jipya la Mpiga Kura
ingawaje lugha inayotumika ni uboreshaji wa Daftari la sasa. Uboreshaji
huu wa Daftari la Mpiga Kura ni tofauti na ule tuliouzoea ambapo
walikuwa wanaandikishwa wapiga kura wapya na wale waliopoteza
vitambulisho vyao. Safari hii wanaandikishwa wote wapya na wa zamani
na wote watapata vitambulisho vipya. Hivyo basi, sisi wenye vitambulisho
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
21/24
21
vya kupiga kura vya zamani tusifanye ajizi, tujitokeze kujiandikisha wakati
ukifika.
Jambo la pili ni kwamba, Daftari la Mpiga Kura linalotayarishwa siyo
kwa ajili ya Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa peke yake, daftarihilo hilo litatumika pia kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2015. Hivyo
basi, kujiandikisha ni jambo muhimu sana. Usipofanya hivyo siyo tu
utajinyima fursa ya kushiriki kuamua kuhusu Katiba Inayopendekezwa
bali pia utakosa fursa ya kuchagua Rais wako, Mbunge wako na Diwani
wako. Katu usikubali yakukose hayo.
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Ndugu Wananchi;Kama mjuavyo tarehe 14 Desemba, 2014 na 20 Desemba, 2014
ulifanyika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kuchagua viongozi wa vitongoji,
vijiji na mitaa. Uchaguzi umekwisha na viongozi wamekwishapatikana.
Sasa ni wajibu wa viongozi hao kufanya kazi waliyoiomba. Kwa
walioendesha uchaguzi ni wakati mzuri wa kufanya tathmini ili wapate
mafunzo yatokanayo na uchaguzi huo. Kwa TAMISEMI na Wakurugenzi
Watendaji wa Halmashauri, lengo liwe ni kuona namna ya kuimarisha
mazuri na kusahihisha makosa na matatizo yaliyojitokeza. Kwa walinzi wa
amani watambue matatizo ya kiusalama yaliyotokea na kuona namna ya
kutengeneza mikakati ya kuzuia matatizo ya namna hiyo yasijitokeze tena.
Hatma ya yote, shabaha yetu ni kutaka kufanya vizuri zaidi katika chaguzi
zijazo za Serikali za Mitaa na kufanya vizuri zaidi katika Uchaguzi Mkuu
wa mwaka 2015.
Jumuiya ya Afrika Mashariki
Ndugu Wananchi;
Mwaka huu Tanzania imechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Afrika Mashariki. Ni zamu yetu kwa mujibu wa mzunguko wa uongozi
wa Jumuiya yetu kati ya nchi wanachama. Ni dhamana kubwa na kwamba
wenzetu wa Afrika Mashariki wanatutegemea tuwaongoze katika
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
22/24
22
kutekeleza malengo na madhumuni ya Jumuiya kama yalivyoainishwa
katika Mkataba ulioanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki. Hali kadhalika,
tunategemewa kuongoza katika utekelezaji wa maamuzi mbalimbali ya
vikao vya Jumuiya. Hii inahusu maamuzi yaliyokwishafanywa kabla yetuambayo utekelezaji wake unaendelea na uamuzi mpya utakaofanywa
katika kipindi cha uongozi wetu.
Kwa niaba ya Watanzania wote napenda kuwashukuru ndugu zetu
wa Burundi, Kenya, Rwanda na Uganda kwa kutuamini. Napenda kuahidi
kuwa hatutawaangusha. Sisi Watanzania tutafanya kila tuwezalo
kuimarisha Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa manufaa ya Jumuiya
yenyewe, nchi zetu na wananchi wa Afrika Mashariki. Tutajitahidi kuwawabunifu kwa nia ya kuona utangamano unakua na kustawi kwa kasi na
kuzaa matunda ya maendeleo tunayoyatarajia sote. Matunda
tuliyoyatarajia tulipoamua kuanzisha Jumuiya hii na matunda tuliyoyapata
tulipoamua kwa hiari yetu kujiunga nayo kuwa wanachama.
SADC, AU NA UN
Ndugu Wananchi;
Kuhusu Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC),Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa, tunaahidi kuendelea kuwa
wanachama waaminifu na kushiriki kwa ukamilifu katika utekelezaji wa
shughuli mbalimbali za mashirika haya ya kikanda na kimataifa. Kwa
upande wa SADC tutaendelea kushiriki katika utekelezaji wa mikakati na
mipango ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii na ile ya kisiasa na
kiusalama kama ilivyoainishwa katika RISDP (Regional Indicative Strategic
Development Plan) na SIPO (SADC Strategic Indicative Plan for the Organ).
Kwa ajili hiyo Tanzania, itaendelea kutoa mchango wake katika kukuza
utangamano wa kiuchumi katika SADC na kusaidia kuimarisha uhusiano
mwema na usalama miongoni mwa nchi wanachama wa SADC. Hii ni
pamoja na kusaidia katika kutatua migogoro ya kisiasa na kusalama kati ya
nchi wanachama.
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
23/24
23
Kwa upande wa Umoja wa Afrika tutaendelea kutekeleza maamuzi
ya vikao na taasisi mbalimbali za Umoja huo. Daima tutakuwa
wanachama waaminifu wa Umoja wa Afrika na kuchangia katika
uimarishaji wake. Kuhusu Umoja wa Mataifa tutaendelea kutimiza wajibuwetu kama wanachama wa Umoja huo wa kimataifa ulio adhimu na
muhimu kwetu na dunia nzima. Tutaendelea kushiriki katika shughuli za
ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa. Hivi sasa tunao wanajeshi
wetu katika majeshi ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa katika nchi za
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Sudan na Lebanon. Tuko tayari wakati
wote kuchangia zaidi iwapo Umoja wa Mataifa watatutaka tufanye hivyo.
Hitimisho
Ndugu Wananchi;
Namaliza hotuba yangu hii ndefu kwa kuwashukuru Watanzania
wote kwa kuiunga mkono Serikali yetu na kwa mchango wenu
uliowezesha nchi yetu kupata mafanikio haya makubwa tunayojivunia
katika mwaka 2014. Tumeweza kuvuka mitihani na nyakati zenye majaribu
mengi. Umoja wetu na mshikamano wetu ndivyo vilivyotuwezesha kufika
hapa. Tunauanza mwaka 2015 kwa matumaini makubwa. Mwaka 2015
unatupa fursa kubwa ya kuendelea kuliimarisha zaidi taifa letu. Mwaka
ujao ni mwaka wa Uchaguzi Mkuu, hivyo huenda ukawa na changamoto
na majaribu magumu zaidi kuliko mwaka huu. Uelewa wetu, umoja wetu,
mshikamano wetu na moyo wetu wa uzalendo ndivyo vitakavyotuvusha
kama ilivyokuwa kwa miaka ya nyuma. Mimi nina imani kubwa kwa
uwezo na utayari wa Watanzania wenzangu kuidumisha sifa nzuri ya nchi
yetu ya umoja na mshikamano wa watu wake uliozaa amani na utulivu.
Tumeweza mwaka huu na miaka ya nyuma, tutaweza tena mwakani na
miaka ijayo. Inawezekana, Timiza Wajibu Wako! Nawatakia heri ya mwaka
mpya.
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!
8/10/2019 HOTUBA YA MWAKA 2015 - FINAL.doc
24/24
24
Asanteni kwa kunisikiliza.