30
www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 1 KITABU: NGUZO MAMA MWANDISHI: PENINA MUHANDO WACHAPISHAJI: DUP MWAKA: 1982 UTANGULIZI Tamthiliya ya Nguzo Mama iliyoandikwa na Penina Muhando inayasawiri na kuyaelezea matatizo mbalimbali yanayowakabili na kuwaelemea wanawake wengi wa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Wanawake wengi wamekuwa wakinyanyasika kwa kunyanyaswa na kuteswa na waume zao. Penina Muhando anathibitisha hayo kwa kutueleza maisha waliyokuwa wakiishi wanawake wa Patata. MAUDHUI DHAMIRA KUU: UKOMBOZI WA MWANAMKE Penina Muhando ndani ya kitabu hiki cha Nguzo Mama anaelezea na kuonesha juhudi mbali mbali zifanywazo na wanawake katika kujikomboa kutoka minyororo ya utumwa wa mwanaume na manyanyaso mazito anayoyapata kutoka kwa mwanaume na jamii nzima inayomzunguka. Mwandishi, baada ya kusawiri maisha halisi ya mwanamke wa Kiafrika na manyanyaso anayoyapata kama vile kupigwa, kufanyishwa kazi kuliko uwezo wake, mfano :- kulima peke yake, kufua, kuosha vyombo, kukusanya kuni n.k., anaamua kutumia kipaji chake kuelezea jinsi gani mwanamke anaweza kujikomboa. Katika kitabu cha Nguzo Mama, mwandishi anawaonesha wanawake wa Patata wahangaikavyo katika kujikomboa. Ukombozi huo umegusa nyanja zote za maisha yaani kisiasa,

KITABU: NGUZO MAMA MWANDISHI: PENINA MUHANDO …€¦Bi Nne naye hakuwa nyuma katika kazi yake ya ualimu. Akaanzisha Umoja wa Walimu, nia ikiwa kuwasaidia kutatua matatizo yao mbalimbali

  • Upload
    others

  • View
    136

  • Download
    35

Embed Size (px)

Citation preview

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 1

KITABU: NGUZO MAMA

MWANDISHI: PENINA MUHANDO

WACHAPISHAJI: DUP

MWAKA: 1982

UTANGULIZI

Tamthiliya ya Nguzo

Mama iliyoandikwa na Penina Muhando inayasawiri na kuyaelezea matatizo

mbalimbali yanayowakabili na kuwaelemea wanawake wengi wa Tanzania na

Afrika

kwa ujumla. Wanawake wengi wamekuwa wakinyanyasika kwa kunyanyaswa na

kuteswa

na waume zao. Penina Muhando anathibitisha hayo kwa kutueleza maisha

waliyokuwa

wakiishi wanawake wa Patata.

MAUDHUI

DHAMIRA KUU: UKOMBOZI WA

MWANAMKE

Penina Muhando ndani ya kitabu hiki cha Nguzo Mama anaelezea na kuonesha

juhudi

mbali mbali zifanywazo na wanawake katika kujikomboa kutoka minyororo ya

utumwa

wa mwanaume na manyanyaso mazito anayoyapata kutoka kwa mwanaume na

jamii nzima

inayomzunguka. Mwandishi, baada ya kusawiri maisha halisi ya mwanamke wa

Kiafrika na manyanyaso anayoyapata kama vile kupigwa, kufanyishwa kazi kuliko

uwezo wake, mfano :- kulima peke yake, kufua, kuosha vyombo, kukusanya kuni

n.k., anaamua kutumia

kipaji chake kuelezea jinsi gani mwanamke anaweza kujikomboa. Katika kitabu

cha

Nguzo

Mama, mwandishi anawaonesha wanawake wa Patata wahangaikavyo katika

kujikomboa. Ukombozi huo umegusa nyanja zote za maisha yaani kisiasa,

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 2

kiuchumi

na kijamii.

Kiuchumi katika kujikomboa, wanawake wa Patata wanaamua

kuanzisha miradi mbalimbali ambayo itawawezesha kujipatia fedha kwa ajili ya

maendeleo. Miradi ikashamiri sehemu zote za Patata.

‘’……….Miradi tutatilia

mikazo, miradi ya kila aina vilabu vya pombe, maduka ya khanga, ushirika wa

kushona, kupika, hoteli na mengi……..’’(uk 52).

Bila Pili yeye akaamua kuanzisha kilabu cha pombe ili

aweze kujikomboa kwenye maisha magumu yanayomkabili.

„’Kaamua Bi

Pili, Pombe kujipikia, na kilabuni kuiuza

Pesa akipata, Pesa msema

kweli

Na nguzo mama itasimama’’ (uk 14).

Mwandishi anaonesha umuhimu wa pesa katika kujikomboa

kwa wanawake, kwani pesa ndio hasa iletayo maendeleo stahiki. Hali kadhalika Bi

Moja na wenzake nao wakajiunga na kuanzisha viwanda vyao vya kufuma

mapambo ya

nyumbani.

„‟Kutokea Bi

Moja, Na lake jipya kiwa nda kuanzisha

Mapambo ya nyumbani kufuma

Mapambo akiyauza na pesa

kujipatia

Itakuwaje nguzo mama

isisimame’’ (uk 17).

Kijamii, wanawake wa Patata wamehamasika kwa kuanzisha

vikundi vya akina mama, ambavyo vitasimama imara kutetea maslahi yao na

kusaidiana wao kwa wao katika kujikomboa. Mfano mzuri ni kikundi lcha kina Bi

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 3

Nne, yeye alikuwa kiongozi wa umoja huo akiwahamasisha wanawake wenzake ili

waweze kuinua „‟nguzo Mama‟‟

„’Bi Nne anapiga

makofi nao

Anasimama na kutoa hotuba

Nguzo mama hoyee’’ (uk 11).

Bi Nne naye hakuwa nyuma katika kazi yake ya ualimu.

Akaanzisha Umoja wa Walimu, nia ikiwa kuwasaidia kutatua matatizo yao

mbalimbali yanayowakabili katika ufundishaji, Bi Nne anawashauri walimu

wenzake

kuanzisha umoja huo ili kwanza waanze na matatizo yao yanayowakabili katika

hatua ya kujikomboa kama wanawake.

„’Kutokea Bi

Nne, wenzake wengi

Makubwa hawakujitakia,

vizuri walishauri

Tuanze na yetu matatizo,

Ndani yah ii yetu kazi

Kazi yetu ya kufunza vyema

kuichapa

Vigingi vikitokomea, vyema vijana watafunzika

Wakifunzika wote Patata

‘’Nguzo Mama itasimama’’ (uk 20).

Hapa Penina Muhando anaonesha elimu kama njia moja

wapo itakayoweza kuwakomboa wanawake pale aliposema;

„’Vigingi

vikitokomea, vyema vijana watafunzika, wakifunzika wote Patata nguzo mama

itasimama’’

Mwandishi pia anaonesha ushirikianao wa jamii nzima,

wanawake kwa wanaume kutasaidia sana katika kuleta ukombozi wa mwanamke

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 4

na

mwanamke peke yake, abadani hatoweza kusimamisha „’Nguzo Mama’’

‘’Bi Nane ‘’Tushirikishe

wanaume pia. Nguzo mama ina faida kwa wote

Tuite na watoto wote faida

kwa wote – wao taifa la kesho’’

Kwa hiyo, mwandishi licha ya kuonesha utakiwaji wa

jamii nzima katika ukombozi wa mwanamke, pia anaonesha faida za ukombozi

huo

hazitamlenga mwanamke tu bali na jamii nzima inayomzunguka mwanamke.

Pia umoja nao unachorwa na kuoneshwa kama njia

itakayowezesha wanawake waweze kujikomboa.

„’Bora tufanye

mikutano

Labda na maandamano

Maazimio tuyatangaze

Tukupambeje maua’’ (uk 7).

Mikutano kama ilivyo kawaida yake ingewezesha

kuwapasha watu wengi zaidi juu ya ukombozi wa mwanamke na manyanyaso

wapatayo.

Hivyo watu wengi wangehabalishwa katika uwanja wa siasa. Nafasi za uongozi

kwa

wanawake ni moja kati ya njia ambazo zingemwezesha mwanamke kujikomboa.

Katika tamthiliya hii, mwandishi anaonesha juhudi

mbalimbali zifanywazo na wanawake wa Patata katika kuchukua uongozi wa

Serikali.

„‟………Akina

mama watapewa vyeo, orodha tumeshapanga. Tutapata mawaziri, mameneja,

mabalozi

na kadhalika. Wengine tayari wameshapata kama mnavyofahamu’’ (uk 52).

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 5

Baadhi ya wanawake ambao walipata uongozi ni Bi Nne

ambaye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya vyeo.

„‟He! Kweli nimekumbuka looo!

Nimechelewa mkutano wa kamati ya vyeo

Na mimi ndiye mwenyekiti, si

mnajua tunavyokazana kuwaombea mabibi vyeo maana wanasahauliwa. Lazima

tufanye

huo mkutano’’ (uk 42).

Bi Tatu yeye alikuwa mwenyekiti wa kamati ya malezi

bora

„’My God !

Mmeona! Tena Shangazi mwenyewe ndiye mwenyekiti wa malezi bora’’ (uk 50).

Ukombozi wa fikra pia umeoneshwa kama tatizo linalowasumbua

wanawake wa Patata. Mfano anamuonesha Bi Nane dhidi ya madai aliyoambiwa.

Bi

Nane hasa alipokubaliana na kila kitu alichoelezwa na Bi Nne.

DHAMIRA NDOGONDOGO

1.

UONGOZI MBAYA

Uongozi mbaya ni kati ya dhamira zilizooneshwa kwenye

tamthiliya ya Nguzo Mama. Mwandishi wa tamthiliya hii, Penina Muhando

anaanza

kwa kuonesha umuhimu wa kiongozi katika jamii yoyote ile. Pia anaonesha

kiongozi kama mtu aliyeshikilia jamii anayeweza kuipeleka jamii anayeweza

kuipeleka jamii yake kwenye neema au mdomo wa samba kutegemeana na

uongozi wake

atakavyokuwa anaupeleka.

„‟……..Tena

kwetu sie kiongozi huongoza njia

Aweza kuwapeleka kwenye

neema

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 6

Au mdomoni kwa samba……..‟‟ (uk 22).

Lakini viongozi hao, wengi wao wamekuwa wakizipeleka

jamii zao kwenye mdomo wa samba, kwani viongozi hao hutumia uongozi kama

dhama

ya kuonesha wao ni watu watukufu na walio kwenye daraja la juu katika jamii.

Wakiamuawatakavyo bila kufuata miongozo iliyopo katika uongozi huo.

„‟ Bi Nane

akawaza

Kumbe kazi hii ya uongozi au

uwenyekiti

Inampa mtu uwezo wa kufanya

Mambo kinyume cha

kawaida……‟‟ (uk 24).

Penina Muhando anaonesha uongozi mbovu kama ndio

chanzo cha matatizo yanayoikabili jamii ya Wanapatata. Viongozi kama akina Bi

Nne na Mwenyekiti wa Kamati ya Mashauri, wanaoneshwa kama viongozi

wabovu

wanaosababisha kuwa na matatizo katika jamii ya Patata.

„‟ Lahaula!

Kumbe ndio maanawatu wengi wanaulilia uwenyekiti, kwani ni rahisi kazi yake,

kiholela mambo kujifanyia masikini Patata si ajabu kumbe vurugu kutapakaa’’

(uk 25).

Mwandishi anaonesha vurugu zinazoisonga Patata kuwa

zimechangiwa na uongozi mbovu. Udikteta pia unaoneshwa kuwa ni zao la

uongozi

mbovu uliopo kwenye jamii ya wana Patata. Viongozi kama mwenyekiti wa

kamati ya

mashauri wamechorwa kama madikteta, wanaotumia uongozi wao watakavyo,

wajisikiavyo kutoka mioyoni mwao au vile waambiwavyo na watu wao wa karibu

bila

kufuata misingi na miongozo waliyowekewa

na katiba ya jamii zao. Mwenyekiti wa kamati ya mashauri anatumia vitisho

kumlazimisha Bi Nane kusemaasichokijua ili mradi tu yeye ni kiongozi. Pia

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 7

mwenyekiti anaonesha udikteta wake pale alipotaka kuamua kesi aliyosikiliza

upande mmoja tu wa mashtaka, tena maelezo hayo kapewa wakati mshtakiwa

hayupo.

„‟……..Vipi

mtu atakubali kutoa ushauri kutumia vitisho!

Kufuatilia maelezo ya

mshtaki peke yake

Tena yaliyoelezwa wakati

mshtakiwa hakuwepo

Vipi mtu atamshauri

mshtakiwa

Bila kujua mawazo yake’’ (uk 24).

Pia mwandishi anaonesha udikteta uliokithiri

unavyoitawala jamii ya Patata, yaani mtu mmoja anaweza kuamua maamuzi

yanayotakiwa

kufanywa na kamati nzima. Tena ajifanyiaye mambo bila kushirikisha kamati hiyo.

Mfano ni pale mwenyekiti wa kamati ya mashauri walipokaa na kuunda kamati ya

watu wawiliili wamshitaki Bi Nane.

„‟ ….Vipi watu hawa, wawili, moja, mbili kujifanya wao

kikao.

Katiba gani inasema

mwenyekiti peke yake

Awe na kikaocha kuamua

mashauri

Au asaidiane na mtu si

mwanakamati

Mwenyekiti na mshtaki kuwa kikao?!

Sijapata kusikia, hiki ni

kikao cha hila.

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 8

Kusema sitajisumbua, kimya

akijikalia’’ (uk 24).

Mwandishi anaendelea kutuonesha maajabu ya uongozi

mbaya ya wana Patata ulivyokithiri, kwani wale viongozi walikuwa

wanategemewa

ndio haohao wanaofanya mambo ya ajabu.

„’Na ajabu

kupita yote

Vipi mwenyekiti bila kamati

Akatoa ushauri katika

mashtaka?’’ (uk 25).

Hapa msimulizi alikuwa anaendelea kutuonesha jinsi

mambo yalivyo mabaya hapo Patata.

Kwa wema na huruma

‘’Mwanangu mie sijui labda

kamuulize Bi Nne’’

(uk 54).

Chizi anamshangaa Bi Saba, kwani licha ya kuwa

kiongozi hajui hata ninimaana ya Nguzo Mama. Chizi anaendelea kusema;

‘’Lakini juzi kachaguliwa

katibu

Sijui wa kamati gani ile.

Nimesahau’’ (uk 55).

2.

DHULUMA

Penina Muhando anaitumia vyema kazi yake ya usanii

kueleza tatizo la dhuluma lilivyoigubika jamii yetu ya leo. Katika tamthiliya

yake ya Nguzo Mama anajaribu kutuonesha jinsi jamii ya Patata, kama zilivyo

jamii nyingine, ilivyooza kwa dhuluma, hasa kwa wanawake wajane pindi tu

wanapofiwa na waume zao.

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 9

Katika tamthiliya ya Nguzo Mama, mwandishi anatumia

mhusika wake Bi Saba kuonesha jinsi ganiwanawake wengi wa Kiafrika

wanavyodhulumiwa mali na ndugu za waume zao pindi tu wanapofariki. Bi Saba

baada ya tu ya kufiwa, shemeji walikuja na kugawana vitu vya Bi Saba pasipo

kumuachia hata kitu. Watoto nao walichukuliwa, wakimwacha Bi Saba masikini

akihangaika huku na kule bila mafanikio.

‘’ Haa! Shemeji mmerudi

kuchukua hata kitanda!

Hata sufuria! Nitalala wapi

na nitapika wapi jamani?’’

(uk 43).

Mwandishi anaendelea kueleza uozo wa dhuluma ndani ya

Patata ilivyoletamatatizo na huzuni kwa wanaodhulumiwa huku wakikosekana

watu

wa kuwasaidia, hakuna mtu wa kumsaidia mwenzak, dhuluma imetapakaa kila

mahali

Patata.

„’Akalia Bi Saba

tena akalia, hana wa kumsaidia

Mumewe kafa nduguze wamekuja

juu,

Pesa wamechukua senti tano

haikubaki

Vyombo na nguo zote wakagawana

Roho ikampasuka Bi Saba

kuwaona hao ndugu

Walivyogombania mali wasiyochuma

„’Kiti hiki

changu’’ Mie lile jembe’’

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 10

‘’Mie suruali hizi’’ ili

mradi ilikuwa zogo’’

(uk 43-44).

Mwandishi pia anaelezea juu ya dhuluma, kwa kitu au

mali uliyoichuma kwa jasho lako mwenyewe, ukahangaika huku na kule kutafuta

mali hiyo lakini mwisho wanakuja wachache kukudhuluma mali hiyo. Mfano Bi

Saba.

Uongozi mbaya pia umesababisha kuondoka kwa demokrasia

kwa watu wa Patata, kwani wachache wenye

madaraka ndio wanaoonekana kupewa kipaumbele kuzidi wenzao,

wanaowaongoza.

Mfano ni pale Chizi alipokuwa anamuuliza Bi Nne akimwonesha kuwa yeye ni

mtu

mkubwa na anapewa kipaumbele zaidi. Ansema;

‘’…….Lakini bibi yangu

aliniambia

Binadamu wote sawa, lakini

wengine ni sawa zaidi.

Na huyu ni mmoja wa hao’’ (uk 58).

Pia mwenyekiti wa kamati ya mashauri hafuati demokrasia inayotakiwa kwa

kumlazimisha na

kumpa masharti yaliyo kinyume kabisa na katiba,yenye kuonesha udikteta

uliokithiri usiofuata na unaoepuka kibisa demokrasia .

„’ Jambo la pili

nakueleza kuwa hakuna mtu yeyote anayeruhusiwa kufanya mkutano bila kibali

cha

ofisi hii. Na ofisi hii lazima iletwe kumbukumbu za mikutano yote iliyofanyika

hapa Patata. Sheria hii ipo na inajulikana kwa hiyo urudi ufuate mashauri

yangu’’ (uk 25).

Viongozi wa Patata wanaoneshwa pia viongozi wasiopenda kuwajibika katika

kufanya kazi za

kuliletea taifa lao maendeleo yao, wawapo tu! Kazi kuongea maneno

yasiyotekelezwa. Mfano ni Bi Tatu, yeye ni kiongozi wa malezi bora lakini

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 11

ameshindwa hata kulea watoto wa kaka yake anayehangaika mtaani (chizi). Pia

anashindwa hata kujishughulisha kufanya vijibiashara.

„’My God!

Mmeona! Tena Shangazi mwenyewe ndiye mwenyekiti wa kamati ya malezi bora

yeye

mwenyewe hafanyikazi…..‟‟(uk 50).

Licha ya kuwa kiongozi wa Patata hawapendi kuwajibika,

lakini pia wanaoneshwa kama wasiokuwa na elimu, na wasiojua nini kinaendelea

hata kwenye uongozi wao. Viongozi kama hawawezi kubadilisha kama jamii

yoyote ile kama ilivyo kwa jamii

ya Patata. Chizi anasema;

„‟…..Siku moja nikamwendea, labda niwe kweli chizi

‘’Shikamoo’’ ‘’Marhaba’’ Bi

Saba nieleze.

Nini kitu Nguzo Mama, naona hapa Patata mambo

yamevurugika, kila ninakogeuka nasikia nguzo mama, Nguzo Mama kitu gani?

Vizuri, alijibu.

Yeye alihangaika huku na kule ili ajiletee maendeleo

yake nay a watoto wake, lakini bado mumewe alipofariki nduguze wakaja na

kumdhulumu jasho halali.

„’Atawaambiaje

watu hawa,

Kuwa vyote walivyochukua

Zaidi ni jasho lake

Watoto wake wapenzi mwenyewe

aliwalea

Wakati wao baba mnatindi

akiyachapa

Na pesa kwa pombe kuangamiza

Pesa ya ndugu yao iliishia

chooni’’ (Uk 44).

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 12

3.

ELIMU

Katika tamthiliya hii ya „‟Nguzo Mama‟‟, dhamira ya

elimu inaoneshwa kama jambo la muhimu sana kwenye maendeleo ya jamii yoyote

ile. Mwandishiameonesha kuwa kila nyumba ya mafanikio au maendeleo yoyote

yale

kuna elimu. Bi Nne anakubaliana na ukweli huu pale alipokuwa anasisitiza somo

la ushonaji liingizwe kwenye mitaala ya wanafunzi mashuleni ili waweze

kujifunza kushona vitu mbalimbali kama mapambo na nguo. Kisha wauze wapate

maendeleo.

„’……….Pia somo

la ushonaji litatiliwa mkazo mashuleni. Kila shule italifundisha ili watoto

wetu wajue kushona, wavae vizuri na kupamba nyumba zao vizuri’’ (uk 18).

Bi Nane naye anaonesha na kuthibitisha ukweli juu ya

umuhimu wa elimu kwa maendeleo ya jamii ya Patata. Yeye anaonesha kuwa

kama

watu hawatopata elimu, basi hata maendeleo hawatayasimamisha yakasimama.

„‟…….Tuvitoe

vigingi vile vituzuiavyo

Kazi yetu ya kufunza vyema

kuichapa vigingi vikitokomea, vyema vijana watafunzika

Wakifunzika wote Patata.

Nguzo Mama itasimama’’ (uk 20).

Ukosefu wa elimu nao unaoneshwa kama tatizo kubwa kwa

jamii ya Patata linalosababisha kukosekana kwa maendeleo na kuwakomboa

wanawake.

Viongozi wanaoneshwa kama watu wasiokuwa na elimu, wasiojua hata

kinachoendelea

kwenye uongozi wao. Mfano ni pale Chizi alipomuuliza Bi Saba ambaye ni

kiongozi

kuhusu maana ya Nguzo Mama. Lakini Bi Saba anaonekana hajui chochote kuhusu

Nguzo Mama. Baada ya Chizi kumuuliza Bi Saba anajibu;

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 13

„’Mwanangu mie

sijui labda kamuulize Bi Nne’’.

Yaani Bi Saba anaonekana mtu asiye na elimu kabisa,

kwani hajui hata jambo alifanyalo, Chizi anaendelea kutuhabarisha kuhusu Bi

Saba,

„’Lakini sijui

kachaguliwa katibu sijui wa kamati gani ile. Nimesahau’’ (uk 55)

Elimu pia inaoneshwa ilivyopana na katika hayo mapana

yake ya kila sehemu ina umuhimu wake. Elimu ya malezi, kama zilivyo elimu

nyingine, inaonekana kuwa na umuhimu mkubwa sana katika jamii hasa

ikizingatia

kwenye kipindi hiki ambacho magonjwa ya ajabu yanayoizunguka jamii kama vile

Kisonono, Kaswende na Ukimwi. Hivyo mwandishi anasisitiza kuwepo na elimu

ya

malezi itakayowasaidia vijana na wanawake hasa wale wanaotupa watoto kwenye

mapipa na vyooni. Sharti wapate elimu ya malezi waache tabia hiyo….

‘’……….Pia wasichana kutupa

watoto kwenye mapipa, kuna semina wiki ijayo kuzungumzia swala hili, ni aibu

kubwa sana kwetu’’

(uk 52).

4.

USALITI

Usaliti kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu ni tendo la kuchonganisha watu

kwa

kuchukua maneno ya huku na kuyapeleka huku ili wapate kugombana . Kama

tafsiri

ya usaliti ilivyo, Penina Muhando amefanikiwa kuonesha dhamira hiyo kwa ustadi

mkubwa, pale alipowachora wahusika wake kama wasaliti, mfano ni pale walimu

walipomsaliti mwenzao Bi Nane kwa kutoa siri za vikao wanavyovifanya na

kumpelekea Bi Nne, ambaye anaonekana kama adui wa Bi Nane.

„‟……..Tena

Mwenyekiti mimi nilikwambia hao walimu wengine hawampendi huyu Bi Nane,

yeye tu

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 14

ndiye anayejiweka kimbelembele kama wanampenda mbona walimu hao hao

wanatoka

wanakuja kunieleza mipango yao? Sema basi tukusikie’’ (uk 22-23).

Matokeo ya usaliti huu yalimuweka pabaya Bi Nane,

kwani alisongwasongwa na kuhangaishwa na uongozi wakimtuhumu kama msaliti

na

mvuruga Amani anayetaka kusimamisha maendeleo ya Patata.

„’Lahaula!

Sawa hawajakaa makubwa

yakawakuta!

Barazani wakaitwa mashtaka

kuyajibu’’ (uk 20).

Mwandishi anaendelea kutuonesha usaliti

ulivyosababisha Bi Nane kuingia kwenyematatizo pale mwenyekiti alipokuwa

anamuhoji.

„’Kwa kifupi ni

kwamba, tumepata habari kwamba wewe umeanzisha kikundi cha kupinga juhudi

za

wenzetu hapa Patata za kusimamisha Nguzo Mama. Tena kikundi hicho cha

walimu

watupu kinabagua wasio walimu. Tena kikundi hicho kimekuwa kikifanya

mikutano

kupanga njama za kuchafua juhudi za wenzenu’’ (uk 21).

Mwandishi Penina Muhando pia ameonesha dhamira yenye

kufanana na usaliti japokuwa kitafsiri sio usaliti. Dhamira hiyo ni watu

kuukataa ukweli ambao kimsingi upo kwa kifupi twaweza kuita „‟kana‟‟ au

„‟kukana‟‟

yaani tamka kuwa si kweli au kuwa haipo hali ya kuwa yawezekana ipo. Mfano

mzuri ni jamii ya Patata, kama zilivyo jamii nyingine, watu kuwakana na

kuwakataa ndugu zao kwasababu tu ya matatizo waliyonayo. Katika Nguzo

Mama Chizi ameonekana kulalamika

baada ya baba yake kumkana na kumkataa, na alipokwenda kwa shangazi yake

naye

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 15

pia alimkana tena huku akimdhihaki kwa kumtukana na kutaka kumuitia mbwa

wamng‟ate.

„’Niende wapi?

Kaka yako alinikana na wewe unanifukuza’’ (uk 50).

Dhamira hii inatuonesha jinsi mambo yalivyobadilika

kweny jamii zetu, wazazi kama tegemeo la watoto wao wenye matatizo na hivyo

wengi wao wamekuwa wakiwaacha na kuwaua kwa madai kuwa ni mikosi/nuksi .

Bi Tatu anaoneshwa kama ndugu wa kambo wa Chizi

anayepaswa kumsaidia lakini mambo yakawa

tofauti Chizi alipokwenda kwake,

‘’Chizi umefuata nini huku

nyumbani kwangu. Hebu toka hapa tuna shughuli za wageni’’ (uk 50).

Bi Tatu anaendelea kufoka na

kumtukana waziwazi Chizi pale alipomwambia, CHIZI ‘’Shangazisina nguo’’

Bi TATU ‘’Usiniite Shangazi

. Toa balaa lako hapa, ukirudi nitakuitia mbwa akuume’’ (uk 50).

5.

UMASIKINI NA MAGONJWA

Umasikini ni hali ya kukosa mali, yaani mtu kutoweza

kukidhi haja ya mahitaji yake ya kila siku. Kuishi chini ya kiwango

kinachotakiwa. Umasikini, kama tatizo kubwa linalozisumbua nchi za dunia ya

tatu, limejadiliwa kwa kina na Penina Muhando. Patata ni moja ya jamii za watu

masikini wasioweza kujimudu kimaisha wahangaikao huku na kule kusaka riziki

bila mafanikio. Jamii ya Patata inaonekana ikisumbuliwa na shida chungu nzima.

Bi Tano shida zimemwandama, watoto wake wanapata tabu, hata hela ya

kuwanunulia

nguo hana sembuse chakula. Watoto wake siku nyingine wanashinda na njaa

wakiangalia siku inavyopita, jua likitokea mashariki kuelekea magharibi.

‘’Taabu, taabu! Taabu!

Watoto wangu hawana chakula

Hawana nguo, hawana chakula

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 16

Watoto wanashinda na njaa.

Wanalala na njaa’’ (uk 40).

Hali kadhalika Chizi naye anaonesha hali hii ya

umasikini pale anapolalamika kuumwa na njaa, na njaa yenyewe inaonekana si ya

siku moja tu bali ni muda mrefu, bkwani anaelezea kuwa njaa hiyo huwa

haijimuisha.

„’Labda tuite

njaa

Kama hii inayomuuma

Njaa kamwe haimuishi’’ (uk 31).

Mwandishi pia anaelezea umasikini ulivyotawala Patata

kiasi ambacho watu wanashindwa hata kubadili nguo, yaani wao wamekuwa na

nguo

za „‟kauka nikuvae‟‟.

„’Bi Pili :

Nimeifua mchana huu, asubuhi si nilidamkia shambani…..’’(uk 36).

Mumewe bwana Sudi anajibu,

‘’Kelele! Sasa mimi nitavaa

nini

Utaikausha kwa moto hiyo

nakwambia

Mimi nataka kurudi, nilikotoka

nimeacha pombe kafiri unATAKA WENZANGU WAIMALIZE!

Kausha hiyo nguo haraka

kabla sijakupiga’’

(uk 36).

Mwandishi Penina Muhando haishii hapo katika kuonesha

umasikini ulivyoibuka Patata, bali anazichunguza na kuzifichua sababu

zinazoleta umasikini huo. Moja kati ya sababu hizo ni uvivu na kutojituma

katika kufanya kazi. Wananchi wa Patata ni wavivu na hawajitumi. Wanawake

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 17

wapo

tu wanapiga soga huku miguu waitandaza kwenye mikeka. Mfano Bi Moja yeye

asilani yumo ndani tu anashinda utadhani mwali anayefundwa. Kutwa domo

akilipiga tena huku miguu kainyosha , na kamwe hutamwona jasho likimtoka

akifanya kazi.

‘’Mwenzenu miye nashangazwa

na maneno ya Bi Moja

Hiyo dhahabu na fedha, na

huu wake uturi

Wapi atavipata, kumbe ndani

anashinda

Miguu kainyosha na domo

kujipigia

Kamwe sijamuona, akilitoa

jasho kazi kujifanyia

Wapi niambie inapatikana

fedha na dhahabu

Bila kazi kufanyia, niende

na mie Chizi

Nyingi nikajitolee’’ (uk 47-48).

Kama ilivyo kwa wanawake wa Patata, wanaume ikiwa ni

mara mbili yao kutwa nzima kiguu na njia, wanaume hawajui hata jembe lashikwa

vipi. Wao ni pombe tu pombe na wao, kutwa nzima wanashinda vilabuni,

wakinywa

na kupiga zogo tu mara hiki mara kile. Uvivu umewajaa hawataki kabisa

kujishughulisha. Kazi zote wamewaachia wake zao hata zile za kuihudumia

familia. Hata kile kidogo kinachozalishwa na wake zao basi huwapokonya.

‘’Huyu Bi Pili rohoni

anasikitisha, Atakufa masikini hohehahe kama mie, Lakini ninashangaa kala nini

bibi huyu, Walahi sijaonamwingine hodoni kumpita lakini yule wake mume, nini

kamlisha kazi zote afanya yeye bi Pili, matunda yote ale Bwana Sudi.

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 18

Jasho lake Bi Pili laishia

kilabuni, huyu wake bwana Sudi Matindi anayatandika usiku na mchana siku moja

nitamuuliza Bwana Sudi, Dawa gani aliyompa Bi Pili na mie nikabahatika mke

kujipatia awe kama Bi Pili ambye taabu yote atakubali, watoto anizalie na pia

anilelee, chakula anilimie na pia anipikie. Nguo anifulie na pombe anipatie.

Nikipata yote haya!

Mie my God!‟‟ (uk 48-49).

Kama ilivyo shilingi yenye pande mbili, ndivyo kila

mwenye umasikini maradhi nayo hayaeshi. Jamii ya Patata inaoneshwa kama jamii

yenye kusumbuliwa na maradhi mbalimbali hasa ya mlipuko kama vile

kipindupindu.

„‟……Nimeishi

siku nyingi, Na mengi nimeyaona, ugonjwa wa kaputula na ule wa magunia

Pia kipindupindu vile vita

vya mdachi.

Na yule Nduli Amini Lkini ya

Patata.

Sijui niite vita au

ugonjwa’’ (uk 31).

ZINGATIA

Umasikini pia umeoneshwa wakati Bi Moja alipokuwa

anamdai mume wake fedha za kununulia khanga (Shabani).

„’Nimekwambia

mie hela sina sasa unataka nikaibe?’’ (uk 35).

6.

UVIVU NA UZEMBE

Uwajibikaji ni hali ya kufanya jambo pasipo hiari,

yaani unalazimika kulifanya. Tofauti na ilivyo kawaida kwa watu wa jamii ya

Patata wenyewe wamekuwa si wawajibikaji, yaani hawawajibiki ipasavyo katika

kufanya kazi. Wananchi wa Patata wanaoneshwa kama watu wavivu wasiopenda

kujituma katika kufanya kazi. Dhamira hii, Penina Muhando anaonesha kama

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 19

chanzo

kilichosababisha kufifia na kushindwa kuinua Nguzo Mama. Mfano mzuri ni pale

wanawake wa Patata waliposhindwa kuinua „‟Nguzo Mama‟‟. Mfano Bi Moja

yeye

anaacha kuinua kuvuta Kamba na kuanza kuongea na Bi Tano kuhusu khanga.

Kwa

muktadha waliokuwepo wasingepaswa kuzungumzia mambo hayo. Bi Tano

anamuelekeza

kuwa ni kwa Mwarabu na pia anamtahadharisha kuwa anapaswa kuziwahi la sivyo

zitakwisha. Mara Bi Moja anaondoka na hapo Bi Nane anashituka na kuuliza,

„‟ Sasa jamani

Bi Moja anakwenda wapi tena!!

Bi Moja akiwa mbali anajibu,

‘’Aaa jamani nitarudi lakini

khanga hizi sizikosi’’ (uk

34).

Bi Sita naye anaoneshwa kama mwanamke asiye

muwajibikaji na asiyejali umuhimu wa kazi za maendeleo, kwani naye baadaye

anaacha kuvuta kamba na kumfuata mwanaume eti kwasababu alimkonyeza ili

amfuate

licha ya umuhimu uliopo kwenye kuinua „’Nguzo

Mama’’.

Bi Sita aliiacha na kuamua kumfuata Maganga . Bi Tano

naye kuona mumewe Maganga anamuita Bi Sita anaamua kumfuata Maganga na

Bi Sita.

„‟……Mara

anatokea Maganga, Bi Sita anamfuata wanachekeana. Maganga anamfanyia

ishara

amfuate’’

Bi Tano anaona yanayofanyika

upesi anaacha kamba na kuwafuata’’ (uk 38).

Bi Tatu naye kwake Nguzo Mama si mali kitu Zaidi ya

mume na sherehe, hivyo anawasusia wewnzake kamba kutimkia kwenye Volvo

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 20

lililomfuata na kuelekea kwenye pati ambayo kwake yeye ni muhimu Zaidi

kuliko Nguzo Mama.

‘’Jamani mie naondoka

mnaiona Volvo hiyo imenifuata mie’’. Anaendelea kusisitiza ‘’Siyo utani ndugu

nyangu, Tunakwenda kwenye pati na mume wangu leo saa moja lazima nipalilie

unga

kwa baba watoto wangu ati. Nitakula nini’’ (uk 41).

Hata viongozi nao wanaonekana wababaishaji waliojaa

maneno matamu mdomoni lakini pasipo uwajibikaji kwa vitendo. Bi Nne kama

kiongozi naye anaondoka kwenye kazi muhimu, kazi ya vitendo itakayowezesha

maendeleo ya mwanamke kupatikana na kwenda kwenye vikao, kazi ya kupiga

soga

bila utekelezaji.

„’Hee! Kweli

nimekumbuka. Loo!

Nimechelewa mkutano wa

kamati ya vyeo na mimi ndiye mwenyekiti……‟‟ (uk 42).

Kwa kutowajibika huko wanawake hao wa Patata

wakasababisha kushindikana kuinua kwa „’Nguzo

Mama‟‟, nguzo ambayo ni egemeo lao la

maendeleo. Na ndiyo ufunguo ambao ungeweza kuwaondoa kwenye minyororo ya

utumwa

na ukandamizwaji wa siku nyingi. Lakini kutowajibika kukawakosesha. Penina

Muhando pia anaonesha ugumu wa maisha wa watu wa Patata unavyotokana na

kutowajibika kwao. Bi Moja anaonekana kama mwanamke asiyejishughulisha na

kazi

yoyote ile kutwa yumo ndani tu katulia, kwa hali kama hii ya kutowajibika ndiyo

hasa chanzo cha umasikini.

‘’Mwenzenu mie nashangazwa

na maneno ya Bi Moja

Hivyo dhahabu na fedha na

huo wote uturi

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 21

Wapi ataupata, kumbe ndani

anashinda

Miguu kuinyosha na domo

kujipigia.

Kamwe sijamuona akilitoa

jasho kazi kujifanyia…….‟‟

(uk 42).

7.

MAPENZI NA NDOA

Penina Muhando katika „‟Nguzo Mama‟‟ anaelezea mapenzi

yasivyokuwa ya kweli, yanayojali pesa na usaliti kati ya wanandoa. Mfano ni

Maganga (mume wa Bi Tano) na mkewe Bi Tano, Maganga anaonekana kutokuwa

na

mapenzi ya kweli kwa kumsaliti na kumchukua Bi Sita.

„’Wee Bi Sita

mshenzi, unanichukulia mume wangu hivihivi kimachomacho’’ (uk 39).

Usaliti huu wa mapenzi unaleta sononeko la moyo kwa Bi

Tano. Pia unaleta hali ngumu kwa familia ya Bi Tano, kwani watoto wanalala njaa

kwa kukosa chakula na mahitaji muhimu kwa kuwa Maganga (baba yao)

anamaliza

pesa zote kwa wanawake.

Mwandishi pia anaonesha mapenzi yanayoendeshwa na pesa

kuliko utashi wa mtu na mgtu, mFano ni pale Bi Tatu alipowaambia wenzake

alipofuatwa na mumewe.

„’Sio utani

ndugu yangu, Tunakwenda kwenye pati na mume wangu leo saa moja usiku,

lazima

nipalilie unga kwa baba watoto wangu ati, nitakula nini’’ (uk 44).

Pia anaonesha swala la mwanaume kuwa na mke zaidi ya

mmoja lisivyokubaliwa na wanawake na jinsi gani wanavyohangaika kulibadilisha

swala hili.

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 22

8.

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA JAMII

Katika tamthiliya ya Nguzo Mama mwanamke amechorwa kama

sehemu tofauti. Kwanza amechorwa kama chombo cha starehe kilichopo kwa ajili

ya

kustarehesha wanaume. Mwanamke hapa anatumia mwili wake kama bidhaa

iuzwayo

sokoni na kumpatia faida. Mfano ni Bi Sita ambaye ni changuidoa.

“Mwenzio nautafuta huo muda

siupati.

Laiti ningeupata wengi zaidi

kunasa.

Kwani mmoja,

wawili wanafaa kitu gani?” (uk 29).

Mwanamke pia amechorwa kama jasiri anayejitoa mhanga kuusema ukweli. Hapa

tunamuona Bi Nne anayeamua kumwambia ukweli mwenyekiti juu ya

kutokubaliana

kwake na maamuzi aliyoyatoa.

“Sikubali Mwenyekiti kama

nashtakiwa haki ninayo ya kutoa maelezo vile ninavyotaka.

Nitaeleza kwa maandishi

nakala wanaohusika wote nitawapa. Kesho nitakuletea ahadi ninaweka,

ukishasoma

maelezo yangu ukae ukihukumu. Lakini kabla ya hapo sipokei hukumu wala

ushauri” (uk 29).

Mwanamke pia ameoneshwa kama kiumbe duni kisicho na

thamani wala uwezo wakugfanya jambo lolote katika jamii. Katika kijiji cha

Patata wanaume waliwadharau na kuwabeza wanawake wakiwaona kama watu

wasiokuwa

wakamilifu (uk 46).

Uvumilivu nao umeoneshwa kama sifa ya mwanamke kwenye

tamthiliya hii. Mwanamke anaonekana kutokata tama katika juhudi zake za

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 23

kuingua Nguzo Mama licha ya ugumu

unaowakabili (uk 11).

Mwanamke amechorwa kama mtu anayekandamizwa na

asiyepewa haki zake za msingi. Mfano ni Bi Saba alipodhulumiwa vitu vyake na

nduguze mumewe na kuambiwa hana haki ya kurithi vitu vya marehemu mumewe

(uk

43).

Pia katika utandawazi huu, mwanamke anaonekana kupata

misukosuko hata pale aliposimamia kwenye haki yake ya msingi. Mfano Shaba

alipompiga mkewe eti kwasababu alikwenda kwenye kikao(uk 57).

Mwanamke ameonekana kama mtumwa wa mumewe. Hii

inaonekana pale Bwana Sudi alipokuwa anamtumikisha mkewe Bi Pili kufanya

shughuli zote za nyumbani na shambani yeye akiwa anakunywa pombe tu (uk 49).

Mwanamke anachorwa kama kiongozi wa familia ndiye

aikuzaye jamii, kama hapatokuwepo na mwanamke katika jamii, hakuna jamii

itakayoweza kuwepo. (uk 44-45)

UJUMBE

*Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu

*Kwa kila jambo la maendeleo jamii nzima (yaani

wanaawake, wanaume,wazee,vijana na watoto) lazima washirikiane.

*Ulevi ni adui wa maendeleo.

*Uongozi bora ni muhimu katika kufikiamalengo.

*Malezi bora ni muhimu katika familia

*Wanawake wanafanikiwa kujikomboa siku watakayoamua

kuungana na kushirikiana

*Wanawake nao wapewe nafasi za uon gozi.

MIGOGORO

1. Bi Pili na mumewe (Bwana Sudi)

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 24

Chanzo cha mgogoro wao ni pesa. Bwana Sudi anataka

kuchukua pesa za mkewe alizouzia pombe. Suluhisho ni Sudi kumpiga mkewe

baada

ya kukataa kumpatia pesa hizo.

2. Bwana Sudi, Shaba na Totolo.

Chanzo ni baada ya Shaba na Totolo kumtetea Bi Pili

mke wa Sudi asipigwe na mumewe. Suluhisho ni Shaba na Totolo kumwacha

Bwana

Sudi aendelee na matusi juu yao, kwani waligundua kuwa alikuwa amelewa.

3. Bi Tano na Wanakikundi

Chanzo ni kutonunuliwa kwa vitambaa. Suluhisho ni

kugawana vitambaa hivyo kwa kila mwanakikundi akauze kivyake.

MSIMAMO

Msanii ana msimamo wa kimapinduzi kwa kuyatolea macho

matatizo yanayowakabili wanawake katika kujikomboa na vipi wafanye ili waweze

kujikomboa.

FALSAFA

Msanii anaamini kwamba ili wanawake wajikomboe lazima wawe na msimamo,

maelewano, pamoja na

umoja na ushirikiano pasipo wivu wala kubaguana.

FANI

MUUNDO

Msanii ametumia muundo wa moja kwa moja. Tamthiliya

hii imeanza kuonesha jinsi nguzo mama ilivyolala na harakati za kina mama

kastika kunyanyua nguzo mama. Mchezo umegawanyika katika sehemu nne.

MTINDO

Msanii ametumia mtindo wa dayolojia na masimulizi.

Vilevile ametumia lugha ya kishairi ili kuleta mvuto katika mchezo wake. Pia

msanii ametumia nyimbo na mianzo ya hadithi za fasihi simulizi. (uk 3).

MATUMIZI YA LUGHA

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 25

MISEMO/ NAHAU

a)

Utakiona

cha mtema kuni (uk 42).

b)

Watoto

ni taifa kesho (uk 55).

c)

Utakufa

kibudu (uk 22).

d)

Akachanganya

ulimi {uk 57).

e)

Dume

Malaya si dume roho yako kusumbua (uk 40).

METHALI

i)

La

mgambo likilia lina jambo (uk 45).

ii)

Aso

mwana aeleke jiwe (uk 45).

iii)

Umoja

ni nguvu utengano ni udhaifu (uk 33).

TAMATHALI ZA SEMI

TASHIBIHA

*Anatembea kama kapigwa bumbuazi (uk 9).

* Sikilizeni na sauti kama ndege nyikani (uk 30).

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 26

*Wanaswagwa kama mbuzi (uk 44).

*Amevaa kama mkulima wa bara (uk 24).

TASHIHISI

-Hasira zikampanda Bi Nane (uk 8).

SITIARI

-Mbwa mume wako

anayefuata wanawakeovyo.

MBINU NYINGINE ZA KISANAA

TAKRIRI

-Wakajaribu , wakajaribu (uk 5).

-Mwachie! Mwachie! Mwachie! (uk 8).

-Toka! Toka! Toka usirudi tena (uk 8).

-Akaenda, akaenda, akaenda (uk 40).

MDOKEZO

*Wakavuta…….wakavuta……….(uk 35).

*Siku moja ………ngojeni niwaoneshe (uk 49).

*Ee ndiyo malezi ya watoto wetu………(uk 52).

*Hebu tutazame kwanza kwanini hawasogei….(uk 58).

TANAKALI SAUTI

*Lu lu lu lu lu lu lu lu lu! (uk 2 na 18).

*Ai ai ai ai ai ai ai ai ai ai! (uk 2).

MATUMIZI YA KIINGEREZA

-My God (uk 32,

49, 50).

LUGHA ZA MATUSI

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 27

-Shika adabu yako

(uk 39).

-Malaya mkubwa wewe (uk 39).

-Mbwa wee! (uk 39).

-Mbwa mume wako anayefuata wanawake ovyo (uk 39).

WAHUSIKA

1. Bi Moja

*Mke wa Shabani

*Hakuwa na msimamo katika kusimamisha Nguzo Mama.

*Alikuwa na tama.

*Hafai kuigwa na jamii.

2. Bi Pili

*Mke wa Sudi

*Alinyanyaswa na mume wake.

*Ni mvumilivu katika matatizo.

*Ni mlezi bora wa familia.

*Anafaa kuigwa na jamii.

3. Bi Tatu

*Ni mpenda starehe.

*Hapendi kazi ambazo hazina mshahara.

*Anambembeleza mume wake kwa kuogopa kuachwa.

*Hafai kuigwa na jamii.

4. Bi Nne

*Ni mtu asiyependa maendeleo ya wenzake.

*Ana wivu, mbinafsi, mfitini na ana chuki binafsi.

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 28

*Hafai kuigwa na jamii.

5. Bi Tano

*Ni mke wa Maganga.

*Ana hasoira sana.

*Hakumpenda Bi Sita.

6. Bi Sita

*Alikuwa kahaba na alikuwa anatembea na waume za watu.

*Ni mkorofi na hakupenda ushirikiano.

*Hafai kuigwa.

7. Bi Saba

*Alifiwa na mume wake.

*Ni mlezi swa watoto.

*Ni kiumbe duni kwani shemeji zake walimnyang‟anya

mali zake zote na hata watoto baada ya mume wake kufa.

8. Bi Nane

*Alipenda ushirikiano na swenzake.

*Alikuwa na elimuya kutosha.

*Alipenda kuelimisha wenzakekatika shughuli za

maendeleo.

*Hakuwa na chuki na mtu.

*Anafaa kuigwa.

9. Chizi

*Nmpenda demokrasia.

*Alipiga vita uoga.

*Ni mfichua maovu yaliyoko katika jamii

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 29

*Anaonesha wazi matatizo yanayosababisha

wanawakekushindwa kujikomboa.

*Anafaa kuigwa na jamii.

10. Mwenyekiti

*Ni mtu mwenye uongozi mbaya

*Anapenda kusiliza majungu na fitina.

*Anawachukia wanawake wasomi.

*Hafai kuigwa na jamii.

MANDHARI

Mandhari ya tamthiliya hii ni ya kubuni. Yanasawiri

maisha ya vijijini na kiasi maisha ya mjini, kwani tunaona mwandishi ameonesha

mandhari ya vilabuni, uwanjani na nyumbani. Mandhari yaliyooneshwa yanaoana

sana nan chi za Kiafrikaa vile Tanzania, kwani unyanyasaji na ugandamizwaji wa

wanawake wa Kitanzania ni sawa kabisa na wale wa Patata.

JINA LA KITABU

Jina la kitabu Nguzo Mama linasadifu yale yaliyomo

ndani ya kitabu hiki. Kitaswira “Nguzo Mama” ni umoja wa wanawake Tanzania

(U.W.T) ambao uliundwa kwa lengo la kuwatetea, kuwalinda na kuwapa haki na

maendeleo wanawake sawa na wanaume. Tamthiliya hii inaonesha harakati za

wanawake wa Patata wakiwemo wakulima, wasomi, waalimu, makahaba na

wanaungana

kuimarisha umoja na maendeleo yao. Wanafungua miradi mbalimbali kama vile

kushona, kupika pombe, pamoja na tofauti zilizopo kati yao kama vile uzembe,

majungu, fitina na kutoelewana.

KUFAULU NA KUTOFAULU KWA

MWANDISHI

KUFAULU

Kimaudhui mwandishi Penina Muhando amefaulu kwa kiwango cha juu

katika maudhui yaliyomo ndani ya mchezo huu, kwani amefaulu kutueleza

www.mwalimuwakiswahili.co.tz 0717104507 Uk 30

matatizo

yaliyowapata wanawake wengi wa Kiafrika hususani Tanzania.

Kifani, mwandishi ametumia lugha rahisi inayoeleweka, lugha

ya kishairi inayofurahisha pia na nyimbo zinazoburudisha. Hivyo kufanya mchezo

usichoshe.

KUTOFAULU

Kimaudhui, Penina Muhando ameshindwa kutueleza hatma ya wanawake

wa Patata na jamii nzima baada ya kushindwa kuinua nguzo mama.

Kifani, matumizi ya lugha ya matusi ni udhaifu wa mwandishi,

kwani matusi ni lugha isiyotakiwa katika jamii.