21
Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020 Ukurasa wa 1 kati ya 21 Soma kwa makini maelekezo ya kujiunga na shule kisha mzazi athibitishe kukubali nafasi hii kwa kulipa ada awamu ya kwanza kabla ya tarehe 30/06/2020. Kufuatia kufungwa shule kutokana na ugonjwa wa CORVID -19, na kwa kuwa serikali hivi karibuni itatangaza tarehe ya kufungua shule, Mzazi na mwanafunzi mnashauriwa kujiandaa na kuwa tayari ili serikali itakapotangaza tarehe ya kufungua shule zote tutakuarifu tarehe ya kuripoti shule kupitia mawasiliano ya simu. 1. UTANGULIZI MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ni Shule ya Kiislamu ya bweni inayotazama Elimu kuwa ni jambo la kwanza muhimu kwa Mwanadamu.Tunajifunza katika Qur`an kuwa Nabii Adamu (a.s) kabla hajaletwa hapa ulimwenguni alifundishwa majina ya vitu vyote na kuahidiwa kuletewa mwongozo (Rejea Qur`an, sura ya (2:31, 38).Vilevile tunajifunza kuwa mtume wa mwisho Muhammad (s.a.w) kabla hajaanza kazi yake kubwa ya kuhuisha Uislamu alipewa kwanza amri ya kusoma (Rejea Qur`an 96:1-5) Mtume (s.a.w) amesisitiza kuwa ni faradhi (lazima) kwa kila Muislamu mwanaume na kila Muislamu mwanamke kutafuta Elimu.Pia Mtume (s.a.w) amesistiza Elimu itafutwe hata ikibidi ifungwe safari ya mbali (Uchina). Kwa muhutasari tunalojifunza kutoka katika Qur`an na hadithi sahihi za Mtume (s.a.w) ni kuwa; Kwanza, Elimu ni zana ya kwanza ya msingi ambayo Muislamu hana budi kuwa nayo ili aweze kuishi maisha ya kiislamu na awe Khalifa (Kiongozi) wa Allah (s.w) hapa Duniani Pili, tunajifunza kuwa katika Uislamu hapana ubaguzi wa Elimu ya dunia na Elimu ya akhera. Kila fani ya Elimu inayomwezesha Mwanadamu kufikia lengo la kuwa Khalifa wa Allah (s.w) hapa Duniani ni faradhi au wajibu kwa Waislamu wote. 2. LENGO LA SHULE Lengo kuu la MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ni kuwalea na kuwaelimisha vijana wa Kiislamu ili kuwaandaa kuwa viongozi wa kutegemewa na jamii ya Kiislamu na Taifa kwa ujumla. Tahasusi (combination) zilizopo shuleni Kidato cha tano hadi cha sita ni zifuatazo:- PCB, PCM, CBG, EGM, HGE, HGL, HGK, KLA * , HKL na ECA. TANBIHI: A* = ARABIC Masomo yanayofundishwa mbali na masomo ya tahasusi ni yafuatayo:- i. Islamic Knowledge ii. Basic Aplied Mathematics iii. General Studies iv. Introduction to Arabic 3. NAMNA YA KUFIKA SHULENI MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ipo katika Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma.

Kufuatia kufungwa shule kutokana na ugonjwa wa CORVID -19

  • Upload
    others

  • View
    2

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 1 kati ya 21

Soma kwa makini maelekezo ya kujiunga na shule kisha mzazi athibitishe kukubali nafasi hii kwa

kulipa ada awamu ya kwanza kabla ya tarehe 30/06/2020.

Kufuatia kufungwa shule kutokana na ugonjwa wa CORVID -19, na kwa kuwa

serikali hivi karibuni itatangaza tarehe ya kufungua shule, Mzazi na mwanafunzi

mnashauriwa kujiandaa na kuwa tayari ili serikali itakapotangaza tarehe ya

kufungua shule zote tutakuarifu tarehe ya kuripoti shule kupitia mawasiliano ya

simu.

1. UTANGULIZI

MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ni Shule ya Kiislamu ya bweni inayotazama Elimu

kuwa ni jambo la kwanza muhimu kwa Mwanadamu.Tunajifunza katika Qur`an kuwa Nabii

Adamu (a.s) kabla hajaletwa hapa ulimwenguni alifundishwa majina ya vitu vyote na kuahidiwa

kuletewa mwongozo (Rejea Qur`an, sura ya (2:31, 38).Vilevile tunajifunza kuwa mtume wa

mwisho Muhammad (s.a.w) kabla hajaanza kazi yake kubwa ya kuhuisha Uislamu alipewa

kwanza amri ya kusoma (Rejea Qur`an 96:1-5)

Mtume (s.a.w) amesisitiza kuwa ni faradhi (lazima) kwa kila Muislamu mwanaume na kila

Muislamu mwanamke kutafuta Elimu.Pia Mtume (s.a.w) amesistiza Elimu itafutwe hata ikibidi

ifungwe safari ya mbali (Uchina).

Kwa muhutasari tunalojifunza kutoka katika Qur`an na hadithi sahihi za Mtume (s.a.w) ni kuwa;

Kwanza, Elimu ni zana ya kwanza ya msingi ambayo Muislamu hana budi kuwa nayo ili aweze

kuishi maisha ya kiislamu na awe Khalifa (Kiongozi) wa Allah (s.w) hapa Duniani

Pili, tunajifunza kuwa katika Uislamu hapana ubaguzi wa Elimu ya dunia na Elimu ya akhera. Kila

fani ya Elimu inayomwezesha Mwanadamu kufikia lengo la kuwa Khalifa wa Allah (s.w) hapa

Duniani ni faradhi au wajibu kwa Waislamu wote.

2. LENGO LA SHULE

Lengo kuu la MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ni kuwalea na kuwaelimisha

vijana wa Kiislamu ili kuwaandaa kuwa viongozi wa kutegemewa na jamii ya Kiislamu na

Taifa kwa ujumla.

Tahasusi (combination) zilizopo shuleni Kidato cha tano hadi cha sita ni zifuatazo:-

PCB, PCM, CBG, EGM, HGE, HGL, HGK, KLA*, HKL na ECA.

TANBIHI: A* = ARABIC

Masomo yanayofundishwa mbali na masomo ya tahasusi ni yafuatayo:-

i. Islamic Knowledge ii. Basic Aplied Mathematics

iii. General Studies iv. Introduction to Arabic

3. NAMNA YA KUFIKA SHULENI

MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL ipo katika Manispaa ya Songea mkoani

Ruvuma.

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 2 kati ya 21

Kama unatoka nje ya wilaya ya Songea, shuka kituo kikuu cha mabasi Msamala. Unaweza

kuchukua pikipiki (sh2000 – (3000 usiku)) au taxi (10,000) hapohapo wakulete shuleni au

kama ni mchana hauna mizigo unaweza kutoka nje ya stendi na kuomba uelekezwe

sehemu ya kupandia daladala za kwenda Mkuzo (Nauli Tsh 400) utashukia Mkuzo centre

kisha ulizia njia ya kuja shule utaelekezwa.

4. USAFIRI

Wanafunzi watajitegemea nauli kwa usafiri wa kuja shuleni na kurudi nyumbani wakati

wa likizo ya Mwezi Juni/Novemba. Nusu muhula, huwa hawarudi nyumbani.

Uongozi wa shule unao utaratibu mzuri sana wa kuwasafirisha wanafunzi wanaotoka

mikoani hasa wanaokwenda/kutokea Dar es Salaam, Morogoro, Iringa na Njombe

ambapo hukodi basi na wanafunzi husafiri kwa pamoja na husindikizwa na walezi wao.

Pia mikoa ya Mbeya na Mtwara siku ya kurudi nyumbani husafiri pamoja kwa utaratibu

maalumu ulioratibiwa na shule.

Siku ya safari kila mzazi atamleta /atakuja kumchukua mwanae stendi kuu ya mabasi

Ubungo (DAR)/vituo vyao vya mabasi (mikoa mingine) na kukabidhiwa kwa

mzazi/mlezi wake anayetambulika shuleni. Ni muhimu kuhakikisha kuwa mzazi amelipa

nauli kabla ya siku ya safari ili mtoto aweze kusafiri na wenzake.

ZINGATIA

Kwa wale watakaopandia njiani mfano Kibaha, Mlandizi, Morogoro n.k watafanya mawasiliano

na mwalimu mlezi anayesindikiza wanafunzi ili kujua basi litapita saa ngapi katika vituo

vyao.Namba ya mawasiliano kwa ajili ya mipango ya safari ni 0654876317/0658711844.

5. ADA YA SHULE

Mzazi anaruhusiwa kulipa ada yote kwa mkupuo mmoja au miwili au mitatu ndani ya

muda na kiwango kilichoainishwa. Viwango vya ada kwa awamu ni kama ifuatavyo: 6.

a.) Mkupuo wa kwanza Shilingi laki nane (800,000/=) kabla ya tarehe 30/06/2020.

b.) Mkupuo wa pili shilingi laki nne (600,000/=) kabla ya tarehe 25/09/2020.

c.) Mkupuo wa tatu shilingi laki nne (400,000/=) kabla ya tarehe 25/12/2020.

d.) Mkupuo wa nne shilingi laki nne (200,000/=) kabla ya tarehe 25/03/2021.

Mambo ya kuzingatia:

(i) Ada ikishalipwa hairudishwi kwa sababu yoyote ile.

(ii) Ada italipwa kupitia Amana bank kwa namba ya akaunti. 0011 2007 6370 001 au CRDB

namba ya akaunti 0150366789200. Kwa jina la Mkuzo Islamic High School.

(iii) Stakabadhi ya malipo ya benki (“Pay -in-slip”) iandikwe/ziandikwe jina la mwanafunzi

anayelipiwa ada na kidato anachosoma. (Mfano: ADA YA HAWA JUMA KIDATO CHA 5- 2020

) Mtoto au mzazi awasilishe nakala halisi ya Pay-in-slip kwa Mhasibu wa Shule siku ya kuripoti

shule ili kupatiwa Stakabadhi (risiti) ya malipo ya shule . Kama mzazi/mlezi atakuwa mbali na

shule, ni vema baada ya kulipa (kwa awamu nyingine) atume nakala ya stakabadhi kwa

“whastsApp” kwa mkuu wa shule (0764-749020) kumjulisha kuwa amelipa.

(iv) Tahadhari: Hairuhusiwi kulipa ada kwa pesa taslimu shuleni au kwa njia ya simu ya mtu

yeyote au kupitia mawakala wa mitandao ya simu au kupitia akaunti namba isiyokuwa ya shule.

7. FEDHA ZA MATUMIZI

Mwanafunzi anatakiwa kufungua akaunti ya CRDB na aje na kadi yake (ATM CARD) na

kama hajafungua aje na nakala ya cheti cha kuzaliwa kwa ajili ya kufungua akaunti akiwa

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 3 kati ya 21

shule. Akaunti hii ndio atakayoitumia mzazi kutuma pesa za matumizi na atapewa

utaratibu wa namna kutoa fedha ya matumizi. Aidha akaunti hii ataitumia pia baada ya

kumaliza kidato cha sita yaani chou kikuu kwa ajili ya kupata mkopo kutoka bodi ya

mikopo.

8. MAWASILIANO

Kutokana na kuibuka matapeli wa mitandao ya simu ambao wakati mwingine wanatoa taarifa

zisizo sahihi kwa wazazi au walezi kwa lengo la kuwatapeli, uongozi wa shule unakusisitiza

mzazi kufanya mawasiliano na shule kupitia nambari zifuatazo kwa jambo lolote

1. Mkuu wa shule - 0654876317

2. Makamu mkuu wa shule - 0653392442

3. Patron (mlezi –wavulana) - 0658711844

4. Matron (mlezi –wasichana) – 0673843319

9. SARE ZA SHULE

a.) Sare ya Darasani

Wavulana

i. Suruali mbili.

ii. Nusu kanzu mbili.

iii. Kofia mbili.

iv. Soksi nyeupe.

v. Viatu vyeusi vya ngozi vya kufunga kwa kamba (visiwe na visigino virefu au muundo

wa buti).

vi. Saa ya mkononi.

vii. Sweta 1 la kijivu (lisilo na zipu vishikizo au kofia).

viii. Mkanda mweusi (wa ngozi).

Wasichana

i. Suruali (pajama)2.

ii. Shungi 2.

iii. Baibui 2.

iv. Viatu vyeusi vya ngozi vya kufungwa kwa kamba, na vifunike miguu visiwe na kisigino

kirefu.

v. Saa ya mkononi.

vi. Skafu nyeupe.

vii. Sweta 1 la kijivu (lisilo na zipu, vishikizo au kofia).

b.) Sare za nje ya Darasani.

Wavulana.

i. Suruali mbili.

ii. T-shirt (fauna) 2.

iii. Kanzu nyeupe ya mikono mirefu.

iv. Track-suit rangi ya kijivu yenye mistari mitatu pembeni kuanzia juu mpaka chini Kwa ajili

ya michezo/mazoezi (itakayovaliwa wakati wa mazoezi tu).

v. Raba kwa ajili ya mazoezi.

vi. Jacket 1 nyeusi (siyo sweta au plova) kwa ajili ya kuzuia baridi, visiwe na picha wala

maandishi yoyote wala rangi zilizopishana na lisiwe limeunganishwa na kofia.

vii. Nguo za kulalia, Bukta 2 ndefu zinazovuka magoti.

viii. Soksi nyeusi kwa ajili ya baridi.

ix. Mkanda mweusu (wa ngozi).

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 4 kati ya 21

NB: Track-suit zinazobana miguu kwa chini (baloteli) haziruhusiwi hapa shuleni.

Wasichana.

i. Baibui refu (2).

ii. Pajama 2.

iii. Kitenge jozi moja na sio kanga.

iv. Track-suit rangi nyekundu (yenye mistari mitatu pembeni kuanzia juu mpaka chini). Iwe

pana isiyobana wala siyo balotelli; kwa ajili ya michezo /mazoezi (itakayovaliwa wakati

wa mazoezi tu).

v. Raba kwa ajili ya mazoezi.

vi. Nguo za kulalia (Night dress) –Shumizi ndefu 2.

vii. Skafu nyeusi na soksi nyeusi za kuzuia baridi.

C. NGUO ZA MICHEZO

(i) Kwa wavulana wanatakiwa wawe na truck suit za kiume na wasichana wanatakiwa wawe na truck suit za kike

na ushungi maalum pamoja gauni lnalovuka chini ya magoti-aje nazo

(ii) kwa wavulana na wasichana wanatakiwa kuwa na Raba Pamoja na soksi za michezo- aje nazo

Upatikanaji wa sare.

Ili kuondoa tatizo la kutofautiana kwa rangi za vitambaa na muundo wa sare za shule; sare zote

za shule zitashonwa hapa shuleni kwa gharama zifuatazo:-

A.) Sare za wasichana

DARASANI NJE YA DARASA

Na BIDHAA IDADI KIASI Na BIDHAA IDADI KIASI

1 Gauni 2 41,000/= 1 Gauni 2 41,000/=

2 Suruali(pajama) 2 19,000/= 2 Suruali(pajama) 2 19,000/=

3 Shungi 2 39,000/= 3 Shungi 2 39,000/=

4 Sweta 1 10,000/= 4 Jaketi 1 25,000/=

JUMLA 109,000/= JUMLA 124,000/=

JUMLA KUU 233,000/=

B.) Sare za wavulana

DARASANI NJE YA DARASA

Na BIDHAA IDADI KIASI Na BIDHAA IDADI KIASI

1 Suruali 2 30,000/= 1 Suruali 2 30,000/=

2 Nusu kanzu 2 34,000/= 2 T -shirt (fulana) 2 20, 000

3 Kofia 2 4,000/= 3 Jaketi 1 25,000/=

4 Sweta 1 10,000/= 4

JUMLA 78,000/= JUMLA 75,000/=

JUMLA KUU 153,000/=

Vipimo vya sare vitafanyika hapa shuleni

Tanbihi:

i. Baada ya kupatiwa sare mwanafunzi hataruhusiwa kuvaa nguo nyingine yoyote

kwa hiyo wakati wa likizo atatakiwa kuzirejesha nyumbani nguo alizokuja nazo.

ii. Ni marufuku mwanafunzi kuvaa mapambo ya aina yoyote wakiwa shuleni au nje

ya shule

iii. Manukato ya aina yoyote hayaruhusiwi.

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 5 kati ya 21

iv. JEZI au nguo yenye nembo ya timu ya mpira au chama cha siasa au taasisi fulani

hairuhusiwi (isipokuwa nembo ya shule au nembo ya kiwanda mfano ADIDAS,

NIKE, N.K).

10. VIFAA VYA DARASANI

Mwanafunzi anaporipoti shuleni atatakiwa kuja na vifaa vifuatavyo:-

i. Madaftari /counter books QUIRE 2-3 kulingana na masomo yake.

ii. Mfuko wa kutunzia madaftari (School bag).

iii. Scientific calculator na mkebe wa vifaa vya hisabati (Mathematical set) kwa

wanafunzi wa PCM, EGM, PCB, HGE, na CBG.

iv. Koti la Maabara (Lab coat) linaweza kupatikana shuleni kwa sh 25,000/-

v. Gloves kwa wanafunzi wa PCM, PCB na CBG na Dissection kit kwa wanafunzi

wanaosoma biology tu.

vi. Graph Paper kwa wanafunzi wanaosoma BASIC APPLIED MATHEMATICS

(BAM), ADVANCED MATHEMATICS, GEOGRAPHY na ECONOMICS yaani

combinations za PCM, PCB, EGM, CBG, HGE, ECA na HGK.

11. VIFAA VYA BWENI:

i. Godoro la upana wa futi mbili na nusu (FT2½ X4 Inch).

ii. Shuka 2, 1 ya rangi ya Pink na 1 ya rangi ya kijani pia zinapatikana shuleni kwa Tsh

11,000/= zote mbili.

iii. Mto 1 na foronya 2 rangi ya pink 1 na kijani 1.

iv. Sendo za kushindia.

v. Ndala za kwendea maliwato.

vi. Kanzu nyeupe (kwa wavulana).

vii. Taulo na ndoo ndogo ya plastic.

viii. Blanketi zito.

ix. Chandarua cha pembe nne 4x6.

x. Sabuni za kufulia za unga na za kuogea pamoja na mafuta mazito ya kujipakaa (siyo

cream)

xi. Vyombo, vya chakula; Sahani, bakuli na kikombe. Kijiko siyo lazima.

Sahani kikombe na bakuli visiwe udongo au plastiki (Nunua Stainless steel au mfupa)

xii. Begi gumu la kufunga na kufuli (mbao, chuma, plastiki au kawaida) kwa ajili ya

kuhifadhia vitabu na vifaa vingine bwenini.

Angalizo: Taulo za kike (PEDI) ziwe za kufua. Mwanafunzi yeyote akija na taulo tofauti

na hizo, zitachukuliwa na kuteketezwa maramoja na hatarudishiwa.

Muhutasari wa Gharama zinazotakiwa kulipwa shuleni wakati wa kuwasili: -

Na Mahitaji Wavulana Wasichana Malipo 1. Ada (awamu ya kwanza) 800,000/= 800,000/= BANK

2. Sare za darasani jozi (pea) 2 78,000/= 109,000/= CASH 3. Sare za nje jozi (pea) 2 75,000/= 124,000/= CASH 4. Kitambulisho 5,000/= 5,000/= CASH 5. Shuka 2 11,000/= 11,000/= CASH 6. Vitabu 3 vya Islamic knowledge 20,000/= 20,000/= CASH

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 6 kati ya 21

Pesa ya TEHAMA ilipwe shuleni kwa mhasibu

Angalizo: Vitabu au vifaa ambavyo bei zake hazijaorodheshwa, mzazi amnunulie mtoto

aje navyo.

12 UANDIKISHWAJI

Siku ya kuripoti Shuleni, Mwanafunzi aje na vitu vifuatavyo: -

(i) Nakala Cheti cha kuzaliwa.

(ii) Nakala ya matokeo ya kidato cha nne (result sleep).

(ii) Fomu za utambulisho wa mwanafunzi na wazazi/Mlezi wa mwanafunzi zikiwa

zimejazwa na kubandikiwa picha.

(iii) Fomu ya daktari (Medical Examination form) iliyojazwa na Daktari wa Hospitali ya

Serikali ya wilaya au ya rufaa (imeambatanishwa).

(iv) Fomu ya wajibu wa mzazi/mlezi iliyojazwa na mzazi husika

(v) Nakala halisi za Pay-in-slip ya malipo ya ada.

(vi) Vitabu vya kiada (textbooks) vya kidato cha tano na sita vinapatikana (bei ziko

ukurasa wa mwisho). Mwanafunzi aje na pesa atalipia shuleni.

(vii) Kitabu cha dua (HISNUL MUSLIM). Kinaweza kupatikana shuleni kwa shilingi

2,000/=

(viii) fedha za Tehama (compyuta) sh.30,000/-

13. MAENDELEO YA DARASANI.

Shule inaweka mkazo wanafunzi kusoma kwa bidii ili kuweza kufanya vizuri katika

mitihani yao. Kwa hiyo shule imeweka utaratibu mzuri wa kuwashindanisha wanafunzi na

kuwapa zawadi pamoja na walimu wao.

14.KAZI ZA NJE YA DARASA.

Kujibidisha katika kazi ni miongoni mwa nidhamu ya Kiislamu. Hivyo, kila mwanafunzi

atawajibika kushiriki kikamilifu katika kazi za usafi wa mazingira, huduma za kijamii na kazi

nyinginezo kama atakavyoelekezwa na walimu, walezi au viongozi wa wanafunzi. Kutega

kazi, iwe ya darasani au nje ya darasa ni kukiuka maadili anayotarajiwa awe nayo

mwanfunzi wa shule hii.

8. TEHAMA 30,000/= 30,000/= CASH

9. Qur’an ya tafsiri 15,000/= 15,000/= CASH

Jumla 1,039,000/= 1,158,000/=

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 7 kati ya 21

15.MALEZI

Shule hii ni ya Kiislamu. Kwa hiyo mwenendo wa wanafunzi na walezi unatarajiwa

uzingatie mafundisho ya Qur`an tukufu na Sunnah. Malezi ya shule yanalenga

kumwezesha mwanafunzi kuishi kwa kumuiga Mtume Muhammad (s.a.w).Upo mfumo

mzuri wa malezi ambapo wanafunzi wanapangwa kifamilia na kila familia inakuwa na

kaka au dada na baba au mama mlezi ambaye ni mwalimu. Wanafunzi wanaishi kama

familia kwa kupendana na kuhurumiana.

16.USTAWI WA WANAFUNZI

(i) Huduma za afya

Shule ina wahudumu wa afya na chumba maalum chenye vifaa na dawa kwa ajili ya

kuwahudumia wanafunzi muda wote. Kwa wanafunzi wenye maradhi yanayohitaji

matibabu ya juu na vipimo zaidi, mhudumu wa afya wa shule huwasindikiza kwenda

hospitali ya Mkoa iliyopo Songea Mjini kilometa chache kutoka Mkuzo. Kwa hiyo, watoto

wenye kadi za bima ya Afya wanatakiwa waje nazo ili kurahisisha matibabu nje ya shule

kwani gharama zake hutolewa na mzazi/mlezi na sio shule. Kwa wanafunzi wasio na kadi

ya bima ya Afya (chini ya miaka 18) waje na sh.54,000 ili wafunguliwe Bima ya Afya

(NHIF).

(ii) Chakula na malazi

Chakula cha shule ni kizuri (na cha kutosha-kushiba) kwa kuwa kinapikwa vizuri na bora yaani

mlo kamili ( hasa vitamini,wanga na protini) : matunda,maharage/mboga za majani,nyama

wali,ugali, mkate (skonzi).Kwa mwanafunzi mwenye matatizo ya kutokula vyakula vilivyotajwa

hapo juu, mzazi anashauriwa kutoa taarifa mapema kwa mkuu wa shule kabla mtoto hajaripoti

shule ili kujadiliana naye namna ya kumsaidia.

(iii) Mawasiliano ya wazazi na wanafunzi wakiwa shuleni

Uongozi wa shule unao utaratibu mzuri sana wa wazazi kuwapigia simu watoto wao pale

wanapokuwa na haja hiyo. Ofisi ya malezi ina jukumu la kuratibu mawasiliano ya

wanafunzi na wazazi wao ambapo wanao utaratibu wa wanafunzi kupiga simu kwa

kutumia simu maalumu zilizonunuliwa kwa shughuli hiyo.

Pia wazazi wanapokuwa na shida wanaweza kuwasiliana na uongozi wa shule kwa njia ya

simu muda wowote.

(iv) Siku ya wazazi na walezi kuwatembelea watoto (visiting day) ni Jumapili ya kila

mwisho wa mwezi tu (kwa miezi ya Februari,Machi,Aprili, Agosti,Septemba na Oktoba

tu) kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi kamili jioni).Ikitokea dharura mzazi au mlezi

kutaka kumuona mtoto katika siku tofauti anaweza kufanya hivyo kwa kupata kibali cha

mkuu wa shule au makamo wake.

Kwa miezi ya MACHI na AGOSTI, tutakuwa na kikao cha wazazi na uongozi wa shule

JUMAMOSI ya mwisho ya miezi hiyo. Hivyo, wazazi watatumia siku hizo kusalimiana na

watoto wao baada ya kikao

Tabihi: Kwa wazazi watakaoshindwa kuwatembelea watoto wao, wanaweza kusalimiana nao

kwa njia ya simu za ofisi ya malezi (matron na patron).

Endapo mzazi atapokea taarifa yoyote kutoka namba nyingine tofauti na hizo, au siyo namba ya

mkuu wa shule au makamu wake, asifanye jambo lolote la kimaamuzi bila kuwasiliana na mkuu

wa shule au makamo wake.

17.SAFARI ZA KIMASOMO NA KIMALEZI

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 8 kati ya 21

Tuna utaratibu wa safari za kimasomo na kimalezi kila mwaka/muhula. Mzazi/mlezi

atafahamishwa sehemu ya kwenda kwa muda husika na kiasi cha gharama za safari hiyo.

18.Vitu vifuatavyo haviruhisiwi mwanafunzi kuja navyo au kuvitumia

I. Marashi, Perfume, lotion, Cream na Sabuni za kuchubua ngozi

II. Mapambo ya aina yoyote kama vile pete, hereni, bangili, mikufu, vibanio vya

nywele n.k.

III. Nguo yeyote yenye maandishi au namba.

IV. Rangi za kucha, hina, piko n.k.

V. Redio, simu, CD’s, Camera, Memory Card, Flash, Laini ya simu, Pass na mashine

za kunyolea.

VI. Visu, panga au silaha ya aina yoyote

NB: Jezi wala (baloteli) au track-suit ambayo haijaelekezwa hairuhusiwi. Atakayekamatwa na

vitu hivi atachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kunyang’anywa vitu hivyo na

hatarudishiwa.

19.KANUNI NA MWENENDO BORA WA SHULE

i. Kila mwanafunzi wa shule hii anapaswa kutambua kuwa yupo hapa kwa ajili ya Uislamu.

Kwa sababu hiyo mwenendo wake, matendo na maneno yake yanatakiwa yawe ya

Kiislamu.

ii. Kila mwanafunzi ajitahidi kukuza upendo wake kwa Allah(s.w), Mtume wake (s.aw) na

kwa waumini wenzake.

iii. Pamoja na haki za muumba zilizo juu ya kila Muislamu, yamwajibikia kila mwanafunzi

achunge haki za nafsi yake na atumie vipaji vyake katika uchamungu ndani na nje ya

shule.

iv. Kila mwanafunzi atumie muda wake vizuri katika kujielimisha kwa kutafuta radhi za

Allah.

v. Kila mwanafunzi atalazimika kuhudhuria vipindi vya masomo yote, kufanya mazoezi,

majaribio na mitihani yote itakayotolewa shuleni. Mwanafunzi atakayeshindwa

kuhudhuria darasani bila sababu yoyote ya msingi atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

vi. Wakati wote wa shule au wakati wa kwenda na kurudi likizo vazi rasmi ni sare ya shule

(ya darasani).

vii. Wanafunzi wote wanatakiwa wazingatie kanuni na sheria za mavazi ya Kiislamu wakiwa

ndani na nje ya shule. Wasichana wavae nguo za kuenea mwili mzima isipokuwa uso na

vitanga vya mikono rejea (24:31). Nikabu haziruhusiwi shuleni.

viii. Ni marufuku kwa mwanafunzi mvulana au msichana kuvaa mapambo aina yoyote.

ix. Ni marufuku kwa wavulana kuvaa suruali mlegezo au modo

x. Ni marufuku kwa mwanafunzi mvulana au msichana kuvaa nguo za kubana au

zinazoonesha rangi ya ngozi ya mwili (Transparent) akiwa shuleni au nje ya shule

xi. Ni marufuku kwa mwanafunzi yeyote kufuga kucha, kujipaka rangi za kucha, rangi za

midomo, kupaka hina, kunyoa nyusi, kuvaa viatu vya kuchuchumia au vinavyotoa mlio

(sauti), kukali nywele, kutia rangi, kusuka rasta au kubadilisha nywele, kucha au ngozi

kwa namna yeyote ile.

xii. Ni marufuku mwanafunzi kuchochea, kushawishi, kuhamasisha, au kushiriki mgomo kwa

namna moja au nyingine. Ni kosa kubwa kugomea amri au maelekezo ya viongozi wa

shule kwa ujumla

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 9 kati ya 21

xiii. Wanafunzi wasionekane katika vilabu vya pombe, nyumba za kupangisha wageni (guest

house), vibanda vya video au pahala pengine pasiporuhusiwa.

xiv. Kila mwanafunzi ni mlinzi wa mali ya shule, mali binafsi na mali za wenzake. Mwanafunzi

atakayeharibu, kusababisha mali ya shule kuharibika, kuibiwa au kupotea atachukuliwa

hatua kali za kinidhamu ikiwa ni pamoja na kulipa. Hivyo mwanafunzi atakapogundua

wizi wa mali ya shule au ya mwanafunzi mwingine atoe taarifa kwa walimu au viongozi

wanaohusika mara moja

xv. Kuiba ni kosa kubwa. Mwanafunzi atakayethibitika kuiba mali ya shule, na wenzake au

nje ya shule atachukuliwa hatua kali za kinidhamu.

xvi. Mwanafunzi anapokuwa na shida yeyote hapa shuleni, kwanza aanze kwa viongozi

wanafunzi na ndipo aende kumuona mwalimu wa zamu au wa darasa lake, au walimu

wengine wanaohusika. Kama wanafunzi baada ya kufuata ngazi hizo shida yake

haijatatuliwa aende kwa makamu Mkuu wa shule,kisha kwa mkuu wa shule, mwanafunzi

asishitakie shida zake nje ya shule kabla hajamuona mkuu wa shule .

xvii. Kila mwanafunzi awe msafi na ashiriki vyema katika usafi wa mwili wakebinafsi; kitanda,

nguo, nywele, kucha, na usafi wa madarasa, bweni bwalo la chakula na mazingira ya

shule kwa jumla.

xviii. Kelele za aina yoyote hazirusiwi, iwe darasani, kwenye baraza za madarasa, ndani ya

bweni, au popote iwe kwa mwanfunzi mmoja au wengi (kundi).Tunalazimika kuonesha

maadili ya Kiislamu katika mazungumzo yetu yote (Rejea Qur`an 31:19)

xix. Hairusiwi mwanafunzi kutoka na kulala nje ya shule bila ya kibali malum cha maandishi

kilichoidhinishwa na mkuu wa shule.

xx. Ni kosa KUBWA Mwanfunzi kulala au kwenda katika nyumba za watumishi isipokuwa

kwa kibali maalum.

xxi. Michanganyiko ya wavulana na wasichana hairusiwi. Pale itakapokuwa lazima wanfunzi

kusoma katika chumba kimoja lazima pawe na mwalimu. Kupigana ni kosa kubwa.

Mwanafunzi atakayepigana au kumpiga mwenzake atachukuliwa hatua kali za

kinidhamu.

xxii. Mwanafunzi anapaswa kuripoti shuleni kutoka likizo katika tarehe na muda uliopangwa.

Ikitokea kuchelewa kwa dharura, mzazi apige simu kwa mkuu wa shule au makamo wa

mkuu wa shule kueleza dharura hiyo.

xxiii. Wakati wa kuwatembelea wanafunzi, mzazi /mlezi haruhusiwi kuleta vyakula au vinywaji

vya kutengeneza nyumbani. Hii ni kwa sababu shule ni jumuiya ya watu wengi na

vyakula vinavyotengenezwa nyumbani vinatofautiana kwani kila mtu ana namna yake ya

upishi ndio maana tunachukua tahadhari hiyo. Aidha Mzazi anaweza kumletea mtoto

wake bidhaa za viwandani ziwe SILDI (HAZIJAFUNGULIWA) zenye TBS na matunda tu.

Vyakula au vifaa vitakavyoletwa ni lazima vithibitishwe na mwalimu mwenye jukumu

hilo kabla ya kukabidhiwa kwa mwanafunzi husika. Ni vyema kufahamu kwamba

tahadhari hii imetolewa na wataalamu wa afya wa serikali.

xxiv. Wanafunzi hawaruhusiwi kufanya biashara ya aina yoyote wakiwa shuleni. Kwa hiyo ni

marufuku mwanafunzi kuuza vifaa vyake au kununua vifaa vya mwenzake kwa muda

wote atakapo kuwa shuleni hata ikiwa amemaliza masomo yake. Mwanafunzi

anaruhusiwa kutoa sadaka kumpa mwenzake vifa kama anayo ziada.

xxv. Zaidi ya mashine ya kufanyia hesabu (calculator) na saa za mkononi, vifaa vya electronics

kama vile simu, camera, radio cassette, compyuta, Tv, hita, n.k havirusiwi mwanafunzi

kuwa navyo katika mazingira ya shule. Mwanafunzi atakaekutwa navyo vitu hivyo hapa

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 10 kati ya 21

shuleni, atachukuliwa hatua kali za kinidhamu, pamoja na kunyang’anywa vyote na

hatarudishiwa.Kwa mzazi mwenye compyuta anaruhusiwa kuitoa sadaka kwa shule ili

zitumike kwa wanafunzi wote, mtoto wake akiwepo.

xxvi. Mwanafunzi haruhusiwi kununua au kuagiza chakula kutoka nje ya shule.

xxvii. Kila mwanafunzi ana haki ya kumhoji mtu asiyemfahamu ambae yupo katika mazingira ya

bweni au mazingira ya shule.

20. MAKOSA YATAKAYOPELEKEA MWANAFUNZI KUFUKUZWA SHULE NI:-

Makosa makubwa ni yale yenye kukiuka maadili ya Uislamu, kufanya makosa ya jinai,

kusababisha kuvuruga amani na usalama wa jumuia ya shule, kuharibu mali ya Umma kwa

makusudi. Baadhi ya makosa hayo ni haya yafuatayo:

i. Kunywa pombe na kula au kunywa vitu haramu

ii. Kwenda nyumba za starehe kama vile kumbi za madansi disko n.k

iii. Uzinzi, kulawiti, usagaji au kukaribia zinaa kwa kuwa na rafiki wa jinsia tofauti (Boy

friend/ girlfriend)

iv. Kuvuta bangi, madawa ya kulevya, n.k

v. Kutosimamisha swala

vi. Kumiliki au kutunza vitu vya electronics kama simu au line ya simu, redio kamera,

compyuta, Cd, dvd, Tv, flash, n.k

vii. Utoro: Kukaa nje ya shule kwa muda wa siku 3 mfululizo bila kibali maalum

kilichoainishwa na mkuu wa shule

viii. Kueneza fitina, kuanzisha/kuchochea mgomo/vurugu kupigana au kuchochea watu wapigane.

ix. Kutoroka /kutofanya mitihani/jaribio bila ya sababu za msingi

x. Kutohudhuria vipindi darasani kwa zaidi ya siku tatu mfululizo bila sababu maalumu

za msingi.

xi. Migomo ya aina yoyote.

21. HITIMISHO

Ni matarajio yetu kuwa umesoma na kuelewa maelekezo yote ya shule. Uongozi wa shule

utaendelea kukumbusha kanuni za shule mara kwa mara.Hatutarajii mwanafunzi kukiuka

au kuvunja kanuni hizi kwani kuzikIuka kwa makusudi kutakupelekea kuchukuliwa hatua

za kinidhamu.

Nakutakia maisha ya furaha na amani kwa muda wote utakapokuwa hapa MKUZO ISLAMIC

SECONDARY SCHOOL KWA TAALUMA NA MALEZI BORA.

Kauli mbiu yetu ni``Soma Kwa Jina La Mola Wako Aliyeumba``

Wabillah Tawfiiq

Sombi JR

MKUU WA SHULE

“Best performance is our focuss”

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 11 kati ya 21

ORODHA YA VITABU VYA KIADA VILIVYOANDIKWA NA TAASISI YA ELIMU TANZANIA

(TET) VINAVYOPATIKANA MADUKANI MPAKA SASA NA BEI ZAKE

NO. JINA LA KITABU BEI YA KITABU

1. In organic chemistry Form five and six 15,500/=

2. Organic Cheistry form five and six 17,500/=

3. Physical chemistry form five and six 17,500/=

4. General chemistry form five and six 15,500/=

5. Biology form five 17,000/=

6. Biology form six 17,000/=

7. Basic Aplied Mathematics form five and six 20,000/=

8. Kiswahili kidato cha tano na sita (sarufi na lugha) 15,000/=

9. Kiswahili kidato cha tano na sita(fasihi) 15,000/=

10. Physics for Secondary school form five 17,000/=

11. Physics for Secondary school form six 17,000/=

TANBIHI: Vitabu hivi vinapatikana shuleni mtoto aje na pesa atalipa kwa mhasibu na kupatiwa vitabu

kwa mujibu wa tahasusi (combination yake) .

bei hizi zinaweza kubadilka.

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 12 kati ya 21

Kiambatanisho D

UTHIBITISHO WA KUKUBALI NAFASI

Shukrani zote anastahiki Allah (sw) na Rehema na Amani zimuendee Mtume Muhammad (s.a.w)

na wafuasi wake wote pamoja na wale wanaopigana katika njia ya Allah (sw).

Mimi Mzazi/Mlezi wa …………………………………………………………………………..…….

Kwanza nachukua fursa hii kushukuru kwa mtoto wangu kupata nafasi ya kujiunga na shule ya

sekondari ya mkuzo Islamic secondary school.

Nachukua fursa hii kwa niaba ya mwanafunzi mtarajiwa kuthibitisha kukubali nafasi hii baada ya

kupokea taarifa za kuchaguliwa mwanangu kujiunga na shule hii.

Ninaahidi kutekeleza wajibu wangu wa kulipa ada ya shule kabla ya tarehe ya mwisho ya kuthibitisha

kukubali nafasi hii.

Jina la Mzazi/Mlezi……………………………………….sahihi………………………Tarehe………………………….

Fomu hii ijazwe na irudishwe moja kwa moja shuleni .

Wabillah Tawfiiq

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 13 kati ya 21

Kiambatanisho C

WAJIBU WA MZAZI / MLEZI

Mzazi au mlezi ana wajibu wa kutimiza mambo yafuatayo:

1. Kulipa Ada ya shule kwa wakati

2. Kufuatilia maendeleo ya kila siku ya mtoto wake. Kwa hiyo mzazi au mlezi anatakiwa ashirikiane na

walimu kwa kuhudhuria siku ya wazazi kutembelea shule.

3. Mzazi / Mlezi ana wajibu wa kumnunulia mtoto wake vifaa / vitabu vyote na vitini anavyohitaji.

4. Mzazi / Mlezi anatakiwa atoe taarifa pindi mtoto wake anapokuwa na dharura

ya kumzuia kufika shule kwa wakati uliopangwa. Dharura zinazokubalika ni ugonjwa , kifo cha mtu

wa

karibu kama baba, mama n.k. Ada isiwe kigezo cha mtoto kuchelewa shule.

5. Mzazi / Mlezi ana wajibu wa kuhakikisha mwanae ana sare kamili za shule kama ilivyoelekezwa

katika

Maelekezo ya Kujiunga (Joining Instructions)

Nimesoma kwa makini na naahidi kutimiza wajibu wangu kwa kadiri ya uwezo wangu

Insha Allah.

Jina kamili la Mzazi/Mlezi……………………………………………..Sahihi……………………… Tarehe…………………

NB: Nakala moja Mzazi / Mlezi nakala nyingine irudishwe shuleni ikiwa imesainiwa.

Wabillah Tawfiiq

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 14 kati ya 21

WAJIBU WA MZAZI / MLEZI

Mzazi au Mlezi ana wajibu wa kutimiza mambo yafuatayo:

1. Kulipa Ada ya shule kwa wakati

2. Kufuatilia maendeleo ya kila siku ya mtoto wake. Kwa hiyo mzazi au mlezi anatakiwa ashirikiane na

walimu kwa kuhudhuria siku ya wazazi kutembelea shule.

3. Mzazi / Mlezi ana wajibu wa kumnunulia mtoto wake vifaa / vitabu vyote na vitini anavyohitaji.

4. Mzazi / Mlezi anatakiwa atoe taarifa pindi mtoto wake anapokuwa na dharura

ya kumzuia kufika shule kwa wakati uliopangwa. Dharura zinazokubalika ni ugonjwa , kifo cha mtu

wa

karibu kama Baba, Mama n.k. Ada isiwe kigezo cha mtoto kuchelewa shule.

5. Mzazi / Mlezi ana wajibu wa kuhakikisha mwanae ana sare kamili za shule kama ilivyoelekezwa katika

Maelekezo ya Kujiunga (Joining Instruction

Nimesoma kwa makini na naahidi kutimiza wajibu wangu kwa kadiri ya uwezo wangu

Insha Allah.

Jina kamili la Mzazi / Mlezi……………………………………………..Sahihi………………………

Tarehe……………………………

NB: Nakala moja Mzazi / Mlezi nakala nyingine irudishwe shuleni ikiwa imesainiwa.

Wabillah Tawfiiq

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 15 kati ya 21

Kiambatanisho A

UTAMBULISHO WA MWANAFUNZI

1. Jina kamili…………………………………………………………………

Tarehe ya kuzaliwa………………………umri……………………

Mkoa……………………………Kijiji/Mtaa……………………… Nyumba na:…………

2 Jina kamili la Baba………………………………………………

Kazi yake …………………………………………………………………

Anwani S.L.P………………………………………………

Simu ya nyumbani……………………………Simu ya Kazini………………………………

Kiwango chake cha Elimu…………………………………………………………………………

Mahali anapofanyia kazi……………………………………………………………………………

3. Jina kamili la Mama mzazi………………………………………………………………….……

Kazi yake ……………………………………………………………………….…………………………

Kiwango chake cha Elimu…………………………………………………………………………

Mahali anapofanyia kazi……………………………………………………………………………

4. Je, Wazazi wako wamezaliwa waislam au wamesilimu ukubwani ?

5. Je, umewahi kuhudhuria madrasa (chuo)? [Ndiyo/Hapana (kata

isiyohusika)]

Kama ndiyo kwa ujumla chuoni ulijifunza nini? ( Eleza kwa ufupi)

……………………………………………………………………………………………………………………

6. Je, kwa sasa unaishi na wazazi wako au unaishi na mlezi?

…………………………………………………………Kama unaishi na

Picha ya hivi

karibuni

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 16 kati ya 21

mlezi wazazi wako wapi?…………………………………………………………….……………Uhusiano na

mlezi…………………….(kaka,shangazi,n.k)

7. Jina kamili la Mlezi……………………………………………………………………………………

Anwani yake ni P.O. Box……………………………………………………………………….…

Simu yake ya nyumbani………………………….…Simu ya kazini……………………

UTHIBITISHO:

Nina/tunathibitisha kwa Jina la Allah (s.w) kuwa taarifa zilizotolewa hapa ni sahihi na za

kweli.

Sahihi ya Mwanafunzi……………………………………… Tarehe…………………………………

Sahihi ya Mzazi/ Mlezi……………………………………… Tarehe…………………………….……

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 17 kati ya 21

Kiambatanisho B

UTAMBULISHO WA WAZAZI / WALEZI WA MWANAFUNZI

Ili kuwa na uhakika ya wazazi (Baba na Mama) na walezi tutakaoshirikiana nao , tunaomba

wazazi / walezi wajitambulishe kama ifuatavyo:

WAZAZI WAWILI

Jina kamili………………………………………… Jina kamili……………………….………………

Anuani ……………………………………………… Anuani ……………………………………………

Simu namba …………………………………… Simu namba ……………………………………

Sahihi…………………………………………… Sahihi……………………………………………..

1 2

WALEZI

Jina kamili……………………………………….. Jina kamili………………………………………

Anuani…………………………………………….. Anuani……………………………………………

Simu namba …………………………………… Simu namba ………………………………….

Sahihi……………………………………………… Sahihi……………………………………………

MAMA BABA

Picha ya hivi

karibuni

Picha ya hivi

karibuni

Picha ya hivi

karibuni

Picha ya hivi

karibuni

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 18 kati ya 21

MUHIMU

1. Ni Wazazi / walezi hawa tu wenye picha na sahihi zao ndio

tutakaowasiliana nao kwa ajili ya maendeleo ya mwanafunzi.

2. Yeyote atakayetumwa kwa niaba ya wazazi / walezi wa mwanafunzi

waliotambulishwa kwa shule aje na barua yenye sahihi ya mmoja wao.

3. Jambo hili la wazazi / walezi kujitambulisha kwa shule ni muhimu sana kwani baadhi

ya wanafunzi watundu wakati mwingine huleta wazazi / walezi wa bandia.

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 19 kati ya 21

MEDICAL REPORT FORM

Admission to Mkuzo Islamic secondary School is condition upon receipt of a satisfactory

medical report. Report should be sent to:

HEAD MASTER

MKUZO ISLAMIC SECONDARY SCHOOL

P.O.BOX 346

SONGEA

STUDENT’S SURNAME-----------------------------

OTHER NAMES ----------------------

SEX-------------

AGE------------

Has the examinee suffered from any of the following? If yes indicate date and Diagnosis. If NO

please write in appropriate space.

1. Tuberculosis------------

2. Pneumonia--------------

3. Pleurisy------------------

4. Asthma------------------

5. Rheumatic fever-------

6. Allergic disorder-------

7. Heart disease----------

8. Gastric or duodenal ulcer----

9. Recurrent indigestion----------

10. Jaundice-------------------------

11. Varicose Veins------------------

12. Kidney or Urinary disease-----

13. Rapture spleen-----------------

14. Diabetes------------------------

15. Epilepsy-------------------------

16. Poliomyelitis or other Neurological

disorder-----------

17. Nervous breakdown--------------

18. Psychiatric disorder---------------

19. Eye disorder-----------------------

20. Ear, Nose, or Throat disorder---

21. Skin disease------------------------

22. Anaemia-----------------------------

23. Gynacological disorder------------

24. Malaria or other Tropical disease-----

------------------------

25. Cholera-----------------------------

26. Operations-------------------------

27. Serious accident-------------------

28. Any other serious disorder------

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 20 kati ya 21

PHYSICAL EXAMINATION

1 Height-----------------------

2. weight-----------------------

3. Skin disease-----------------

4. Eye conjunctivae ----------

Sight without glasses-----

With glasses----------------

5. Please state condition of ears(if any

discharge)----------------

mouth and throat------- nose-------

Any clinical evidence of hyperacidity

or gastric-deodenal ulcer?

6. Respiratory System:

Any Abnormality ------------

7. Cardiovascular System;

Blood pressure--------------

Heart: Any murmer?----------

Arteries and Veins-----------

8. Abdomen:Hernia ------------Masses----

Kidneys---------- Hectal---------

Hydrocele-------- Masses--------

LABORATORY

1. Urine albumen---------------------

Sugar-------------------------------

(special emphasis on hookworms

and bilharzias)

Leucocytes----------------------

Bilharzia-------------------------

2.Stools------------------------------

3. Blood examination:

(a) Neutrophils--------------------------------

(b) Eosinophils-------------------------------

(c) Basophils------------------------------------

(d) Lymphocytes-----------------------------

(e) Monocytes--------------------------------

(f) X-Examination-----------------------------

(g) Blood group ---------------------------------

(h) HIV/AID’S------------------------------------

Maelekezo ya kujiunga kidato cha tano Julai 2020

Ukurasa wa 21 kati ya 21

CONCLUSION

I have examined Br/ Sr ------------------------------------- and consider that he /she is/ not physically and

mentally fit to be admitted to Mkuzo Islamic Secondary School.

Name---------------------------

Signature--------------------- Date ----------------------------

Title---------------------------

Qualification------------------

Address------------------------

Phone No.-------------------------

Official stamp

(GOVT HOSPITAL)