Upload
others
View
30
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
MAFUNZO KWA WAFANYAKAZI
WA WAKALA WA MAJENGO
• ELIMU KWA
MUELIMISHAJI;YATAMBUE HAYA
KABLA HUJAANZA MAJADILIANO
• Kuishi na UKIMWI si jambo rahisi kwa
sababu ni kitu kinachotia hofu kubwa
miongoni mwa jamii
• kwa sababu mbali mbali
MAFUNZO…
• 1. Inaweza kumpa hisia mgonjwa ndio
mwisho wa maisha yake kwa kutoweza
kuyakabili maisha endapo tu atajuwa
ana tatizo
• Inaweza kumfanya mtu awe na
wasiwasi kuhusu uwezo wake wa
kujitunza na hata kutunza familia yake
MAFUNZO…
• 2. kuanza kuogopa kifo na kumpelekea
• kutokupenda kazi, kutokuwa na
matumaini,
• kukata tama na kuamini kuwa maisha
hayana thamani tena
• na kuamua hata kujiua au kuambukiza
watu wengine kwa makusudi nife na
wengi,
MAFUNZO…
• Ila kwa kupata elimu sahihi haya yote
hayatakuwepo
• Mtu ataishi maisha ya kawaida endapo
atafika katika vituo vya tiba na kupata
tiba sahihi
• Ikiwemo kutibu magonjwa nyemelezi,
dawa za kupunguza makali ya ongezeko
la virusi na kuongeza kinga ya mwili.
Ukimwi mahali pa kazi
• Kudhibiti maambukizo ya maradhi ya ngono
• Utangazaji na usambazaji wa kondomu
• Unasihi na upimaji wa hiari wa UKIMWI
• Uzuiaji wa uambukizo wa VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto
• Watu wawe wazi, wasaidiwe na wasaidiane, sheria, kanuni na taratibu za kazi zijulikane na zifuatwe
Ukimwi mahali pa kazi
• Kila mtu afahamu haki zake za ajira na gharama za matibabu zinazotolewa na mwajiri.
• Unyanyasaji unatokana na kutofahamu ukweli kuhusu ukimwi
• Kuwaelimisha wafanyakazi wenzako kutawasidia kujifunza kuishi na watu wenye virusi vya UKIMWI kwa UTU na ni njia mojawapo ya kupunguza unyanyapaa
Mambo muhimu ya kufahamu
• 1 Ukweli kuhusu ukimwi
• VVU vinavyoshambulia kinga ya mwili na
athari zake
• Umuhimu wa kujua afya yako
• Magonjwa nyemelezi yanayohusiana na
UKIMWI
• Njia za maambukizi na imani potofu
• Matibabu ya Mgonjwa wa UKIMWI
Lishe Bora
• -Umuhimu wake
-Aina ya lishe bora
• Afya na usafi
-Mwili, mavazi na malazi
-Kuimarisha afya ni pamoja na mabadiliko
ya tabia kwa makundi maalum ya watu
Kujamiana
Ni hatua muhimu katika mapambano dhidi
ya UKIMWI
• Unatakiwa kufikiri nini unapokutana kimwili
• Uanze vipi kulinda afya yako, kwa kujipima
au kwa kujiamini
• Je kutumia kondom ni kutoaminiana
• Tabia zipi hazina usalama
• Ufanyeje ukitaka kufunga ndoa?
• Magonjwa ya zinaa na athari zake
Kujali familia
• Ni pamoja na kuongea nao kuhusu afya
yako
• Kama ni muathirika lazima uwe wazi kwao
• Uiandaaje familia wakati wa matatizo
• Nani ashirikishwe na nani wa kutoa
msaada
• Kujiunga na vikundi mbalimbali vya
wanaoishi na VVU kama vile SHIDEPHA (
SERVICE HEALTH AND DEVELOPMENT
FOR PEOPLE LIVING WITH HIV/AIDS)
DODOMA
Jamii na uchumi
• Jishughulishe katika kuongeza kipato
• Usiwe mnyonge wa mawazo na fikra duni
za kusaidiwa tu
• Jiunge katika vikundi mbalimbali vya
wajasiria amali
• Pata ushauri mbalimbali kwa ndugu
,jamaa na marafiki
Uepukaji wa mila na desturi mbaya
Mirathi na wosia
• Matayarisho kwa watu wote
• Sajili kihalali uliza na fuata taratibu
• Ndoa na rasilimali, watoto, wake
• Nini cha kuandika
• Nani ahusishwe
MAISHA KWANZA
• WEWE BINAFSI
• Familia
• Marafiki
• Wengine walioathirika na VVU
• Jamii kwa ujumla
• Dini na imani zina nafasi yake katika
kumuweka sawa mgojnwa wa UKIMWI,
kwa kiwango gani na kitu gani ni muhimu
kuzingatiwa katika maisha
Dira ya taifa
• (Tanzania bila ya UKIMWI inawezekana)
-Kuwa na jamii ambayo watoto wetu waweza kukua bila ya tishio la VVU na UKIMWI
-Kuwajali na kuwasaidia ambao wameambukizwa na kuathiriwa na VVU na UKIMWI
-kuweka mikakati ya pamoja , ikiwemo mafunzo elekezi
UKIMWI
• Kifupisho cha maneno:-
• Upungufu Wa Kinga Mwilini
• Mkusanyiko wa magonjwa yanayotokana
na kudhoofika kwa nguvu za kinga ya
mwili kujikinga na maradhi
• Kunakosababishwa na V V U
Virusi Vya UKIMWI (VVU)
• Ni vimelea vidogovidogo, vinavyodhoofisha na kufanya mwili kupoteza uwezo wake wa kupambana na maradhi
• Kawaida miili yetu hukingwa dhidi ya maradhi na chembechembe nyeupe za damu (WBC)
• VVU vikiingia mwilini hushambulia chembechembe hizo na kuzipunguza
Virusi Vya UKIMWI (VVU)…
• Vinapatikana katika damu
• Majimaji mbalimbali yanayotoka kwenye
mwili
• Na viungo vya uzazi vya wanawake na
wanaume wenye maambukizo
• Njia kuu ya kueneza virusi hivi,hasa katika
Bara la Afrika
• Ni kujamiiana kusiko salama
Virusi Vya UKIMWI (VVU)…
• Njia nyingine
-ni kutoka kwa mama mjamzitomwenye VVU kumwambukiza mtoto wakati akiwa tumboni
-au wakati wa kumnyonyesha
• Pia huambukizwa kwa kuongezewa damu yenye virusi hivyo
• Kuchangia vifaa vyenye mabaki ya damu kama sindano, mikasi, wembe n.k
Njia zifuatazo haziambukizi VVU
• Kushikana mikono na mtu mwenye VVU
• kuishi pamoja na mtu mwenye VVU
• Kushiriki kula chakula pamoja na mtu wa VVU
• Kugusana au kukumbatiana na mwenye VVU
• Kushirikiana bafu na mwenye VVU
• Kuumwa na mbu, viroboto au wadudu wengine
Dalili za UKIMWI
• Hakuna njia ya hakika ya kutambua mtu
aliyeambukizwa VVU zaidi ya vipimo vya
maabara
• Watu wanaoishi na VVU wanaweza
kuonekana wazima na wasionyeshe dalili
zozote za ugonjwa
• Hata hivyo pamoja na kutokuonyesha dalili
zozote
Virusi Vya UKIMWI (VVU)…
• Mtu huyu mwenye VVU anaweza
kuambukiza watu wengine ikiwa atakuwa
na mahusiano yasiyo salama
• UKIMWI ni hatua ya mwisho ya
maambukizi ya VVU
• Hatua hii ikifikiwa
• Mwathirika huanza kushambuliwa na
magonjwa mbali mbali yaitwayo nyemelezi
Dalili za UKIMWI
• Kupungua uzito asilimia 10 au zaidi katika
mwezi mmoja, bila sababu inayoeleweka
• Kuharisha muda mrefu (mwezi 1au zaidi)
• Homa za mara kwa mara
• Utando mweupe mdomoni
• Kikohozi cha muda mrefu
• Mkanda wa jeshi
Dalili…
• Vipele sugu, vyenye kuwasha hasa
mikononi na miguuni
• Mgonjwa akiwa na dalili zaidi ya tatu
• Uwezekano wa kuwa na UKIMWI ni
mkubwa
• Hata hivyo
• vipimo vya maabara vinahitajika
kuthibitisha ugonjwa wa UKIMWI
Jinsi ya kuzuia maambukizi ya VVU
• Ni muhimu jamii ielimishwe umuhimu wa kupima afya zao na kuchukua hatua zinazostahili;
• 1. jinsi ya kuzuia maambukizi ya vvu yanayotokana na kujamiiana
-kutokujamiiana kabisa (kugunga, abstinence)
-kuwa na mpenzi mmoja muaminifu na asiye na uambukizo (be faithful)
Njia za kuzuia……
-Kujamiiana kwa kutumia kondomu ya
kike au ya kiume kwa usahihi na wakati
wote
• 2. Jinsi ya kuzuia maambukizi kwa mtoto
mchanga
-wanawake wajawazito na waume zao
wahudhurie kliniki ili kupima na kufahamu
afya zao
Njia za kuzuia……
• Wanawake wanaobainika kuwa na VVU hupatiwa maelekezo jinsi ya kumkinga mtoto kupata maambukizi kwa njia ya dawa za ART
• Kuhimiza kujifungulia hospitali ili mtoto apatiwe dawa za kumkinga na maambukizi mara tu anapozaliwa
• Ushauri kuhusu muda wa kunyonyesha na lishe mbadala
Njia za kuzuia……
• Jamii kwa ujumla ishirikishwe kutoa
msaada wa hali na mali
• kuwawezesha wakina mama
walioambukizwa VVU kutimiza masharti
ya kuzuia maambukizi
• kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto
Njia za kuzuia……
• Jinsi ya kuzuia maambukizi ya VVU wakati
wa kutoa huduma
-watoa huduma wawe waangalifu wakati
wa kuwahudumia wagonjwa na kuzingatia
mambo yafuatayo
-kuvaa mipira ya mikononi endapo mtoa
huduma au mpokea huduma ana
michubuko , majeraha au vidonda mwilini
Njia za kuzuia……
• Kuvaa mipira kabla ya kugusa nguo au
vifaa vyenye damu, matapishi, mkojo au
kinyesi cha mgonjwa na mgonjwa aelezwe
kabla ya kufanya hivyo
• Nguo au vifaa vyenye damu au maji maji
mengine ya mgonjwa
• Viwekwe kwenye maji ya moto
yanayochemka kwa dakika 20-30 au
Njia za kuzuia……
• Vilowekwe kwenye JIC kwa dakika 20-30
kabla ya kufua/kuosha
• Mhudumu afue/asafishe vifaa hivyo akiwa
amevaa mipira ya mikononi
• Taratibu za kutuma mabaki yasiyohitajika
yafuatwe ,kuchoma au kutumbukizwa
katika choo cha shimo
Njia za kuzuia……
• Viffa vyenye ncha kali vilivyotumika wakati
wa kumhudumia mgonjwa wa UKIMWI na
• Ambavyo vinaweza vikatumika tena
vilowekwe kwenye JIC halafu vichemshwe
• Vile ambavyo havitatumika tena,
vitumbukizwe kwenye choo cha shimo
• Mhudumu aoshe mikono kwa sabuni kabla
na mara baada ya kumuhudumia mgonjwa
Njia za kuzuia……
• Ni muhimu wahudumu wapime
nakufahamu afya zao, ili kujiweka
katika mazingira mazuri ya kujikinga na
maambukizi ya VVU
Kabla ya ushauri na matibabu
Baada ya ushauri na matibabu
MUELIMISHAJI
AHSANTENI KWA KUWA
PAMOJA KATIKA MAPAMBANO
DHIDI YA UKIMWI