Upload
others
View
626
Download
58
Embed Size (px)
Citation preview
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 1
OSW 233 MOFOLOJIA YA KISWAHILI (NUKUU)
MUHADHARA WA KWANZA 1: MOFOLOJIA
Fasili ya Mofolojia
Mofolojia ni taaluma ya isimu inayoshughuliki muundo wa maneno. Ni taaluma
inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa
maneno. Mofolojia : ni utanzu mmojawapo katika tanzu za isimu Tanzu hizo za isimu ni:
1. Mofolojia
2. Fonolojia
3. Sintaksia
4. Semantiki na
5. Pragmatiki Uhusiano wa Mofolojia na matawi mengine ya isimu
Mofolojia na fonolojia
Vipashio vya kifonolojia (fonimu) ndivyo vitumikavyo kuunda vipashio vya
kimofolojia (mofimu). Mfano soda limeundwa kwa fonimu /s/, /o/, /d/, /a/
na bibi limeundwa kwa fonimu /b/, /i/, /b/, /i/
Kanuni za kifonolojia huweza kutumika kuelezea maumbo ya kimofolojia
ambayo yanaathiriana. Mfano: mofimu ya umoja katika ngeli ya kwanza
inajitokeza kama m- ikifuatiwa na konsonanti ila hujitokeza kama mw-
ikifuatiwa na irabu (m + ti = mti, mu + eupe = mweupe).
Mofolojia na sintaksia
Vipashio vya kimofolojia (mofimu/neno) huunda daraja ya sintaksia. Mfano:
sentensi walitusafirisha imeundwa na mofimu wa-li-tu-safiri-sh-a
Mabadiliko ya umbo la mofimu/neno huathiri muundo wa sentensi nzima
(mf. umoja na wingi).
(i) Mtoto mefu mweusi anakuja
(ii) Watoto warefu weusi wanakuja
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 2
Mofolojia na semantiki
Semantiki ni taaluma ya maana. Mofimu ni kipashio cha lugha chenye
maana mfano; neno kisu lina mofimu mbili ambazo ni ki- umoja na – su ya
mzizi. Ukizigawanya zaidi mofimu hizi utapata k-i-s-u; ambazo ni
sauti/herufi zisizo na maana na si mofimu. Hivyo mofimu si umbo ni maana
– ikiwa ni ya kisarufi au ya kileksika.
Mofolojia hujishughulisha na uundaji wa maneno katika lugha husika;
msingi wa neno ni maana. Hivyo mpangilio wa mofimu usioleta maana
katika lugha husika hauwezi kutambuliwa kama neno. Mfano. palingunywi
ni mfuatano wa fonimu uliozingatia taratibu za lugha ya Kiswahili lakini si
neno la Kiswahili kwa sababu halina maana katika lugha hiyo.
Mambo ya kuzingatia katika taaluma ya mofolojia
Uundaji wa maneno
Hapa tunaangalia vijenzi vya neno husika. Kwa mfano neno limeundwa na
mofimu huru pekee kama papai, mofimu huru na mofimu tegemezi kama
mpapai (m + papai) au mofimu tegemezi tupu kama mtu (m + tu).
Katika uundaji wa maneno tunaangalia vilevile njia mbalimbali za uundaji
wa maneno katika lugha ya Kiswahili kama vile kutohoa, uambatishaji,
urudufu, uhulutishaji, uambishaji, n.k.
NJIA ZA UUNDAJI WA MANENO /ISTILAHI/ MSAMIATI
Uundaji wa maneno ni mchakato unaowezesha lugha kujiongezea msamiati ili
kukidhi haja ya mawasiliano na kuendana na mabadiliko yanayotokea kila siku. Maneno ya lugha ya Kiswahili hayaundwi kiholela bali hufuata taratibu na
kanuni zinazokubalika kitaalamu.
Njia zitumikazo kuunda maneno ni kama zifuatazo:
Unyambuaji
Njia hii inatumia mzizi mmoja wa neno na kuzalisha maneno mapya kwa
kupachika viambishi nyambuaji.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 3
Mfano soma
Somo
Kisomo
Msomi
Msomaji lima
Mkulima
Kilimo
Mlimaji
Uambatishaji/mwambatano
Hii ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuambatanisha maneno mawili.
Mfano
Mwana+chama - Mwanachama
Askari+kanzu – Askarikanzu
Bwana+shamba - Bwanashamba
Urudufishaji / Uradidi
Hii ni mbinu ya kurudiarudia neno au sehemu ya neno na kuunda neno jipya
ambalo huwa na maana tofauti na maneno yanayorudiwarudiwa.
Mfano
(a) Pole : polepole
(b) Sawa : sawasawa
(c) Haraka : harakaharaka
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 4
Akronimu/ufupishaji
Ufupishaji ni njia mojawapo ya kuunda maneno mapya, ufupishaji huweza
kufanyika kwa namna mbili ambazo ni.
Kufupisha kwa kuchukua herufi za mwanzo Mfano
CWT (Chama cha Walimu Tanzania) VVU (Virusi Vya Ukimwi)
Kufupisha kwa kuchukua silabi za mwanzo za maneno yanayofupishwa
Mfano
BAKITA (Baraza la Kiswahili la Taifa)
TUKI (Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili)
TATAKI (Taasisi ya Taaluma za Kiswahili)
Uhulutishaji
Ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuchukua vijisehemu vya neno pasipo
kufuata kanuni yoyote.
Mfano:
Mnyama mfu – nyamafu
Chakula cha jioni – chajio
Hati za kukataza – hataza
Mtu asiye kwao - msikwao
Utohoaji
Ni uchukuaji wa maneno toka lugha moja na kuyatumia kwenye lugha nyingine
baada ya kuyarekebisha kimatamshi na kimaandishi ili yaendane na sarufi ya
lugha inayotohoa.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 5
Mfano
Neno Lugha asilia Kiswahili
Shirt Kiingereza Shati
Schule Kijerumani Shule
Bakura Kiarabu Bakora
Benjera Kireno Bendera
Matching guys Kiingereza Machinga
Kuchukua
Hii ni mbinu ya kuongenza maneno kwa kuyachukua toka lugha yake ya asili
na kuyatumia kama yalivyo katika lugha inayotohoa. Uchukuaji hufanyika kwa
lugha zinazoendana kisarufi kama Kiswahili na lugha za kibantu.
Mfano Kitivo — kisambaa /kipare Ikulu - kinyamwezi Kigoda - kizaramo
Kubadili mpangilio wa fonimu Mfano
Lima – mila – imla - mali
Kufananisha umbo /sauti /tabia Mfano
Kufananisha umbo
Kifaru-(mnyama faru)
Mkono wa tembo-(mkonga wa tembo)
Kidole tumbo-(umbo la kidole)
Kufananisha Tabia
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 6
Ubeberu-(beberu la mbuzi) Ukupe-(mdudu kupe)
Kufananisha Sauti Pikipiki (mlio wa pikipiki) Mtutu (mlio wa bunduki) Nyau (mlio wa paka) Kuku - kokoriko (mlio wa kuku) Njia ya udondoshaji Mfano
mkwe wake - mkwewe
mwana wake - mwanawe
ndugu yake – nduguye
Kuzingatia matumizi ya kitu Mfano
Banio - (kubana)
Chanio - (kuchana)
Fyekeo - (kufyeka)
Kutarjumi/kutafsiri
Mfano;
Fluid – (ugiligili) Acquired immunal deficiency syndrome - Upungufu wa kinga mwilini
Human immunal virus – virusi vya ukimwi Anti-rentro-virus - dawa za kufubaza makali ya ukimwi
Makundi na mahusiano ya maneno
Taaluma ya mofolojia inaangalia pia makundi ya aina za maneno kama vile
nomino, kitenzi, kivumishi, kielezi, n.k. na wakati huohuo huchunguza
uhusiano uliopo baina ya makundi hayo ya maneno. Kwa mfano kuna uhusiano
wa moja kwa moja baina ya nomino na kivumishi au baina ya kitenzi na kielezi
wakati ambapo hakuna uhusiano huo baina ya kitenzi na kivumishi au baina ya
nomino na kielezi. Aidha, hakuna uhusiano wowote wa kisarufi baina ya
vihisishi na maneno mengine yaliyomo katika tungo.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 7
Kanuni za uundaji wa maneno
Uundaji wa maneno hufuata kanuni mbalimbali za kimofolojia na za
kimofofonolojia. Miongoni mwa kanuni zinazotawala katika kuunda maneno ni
kama vile uyeyushaji, ukaakaishaji, odondoshaji, uingizaji, tangamano la irabu,
mvutano wa irabu, n.k.
Hivyo mwanaisimu yeyote anayejishughulisha na uwanja huu wa mofolojia lazima
ayajue na kuyazingatia kwa kina mambo haya.
MUHADHARA WA 2 : MOFU NA MOFIMU
MOFU
Fasili ya mofu
Mofu ni kipashio cha kimofolojia kiwakilishacho mofimu.kutokana na maana
hii twaweza kusema mofu ni kiwakilishi na mofimu ndiyo iwakilishwayo na
mofu.
Mofu ni umbo linalositiri mofimu. Hivyo mofu ni umbo tu linalodhihirika
kimatamshi kama fonimu/sauti na kimaandishi kama herufi.
Aina za mofu
Mara nyingi mofu huainishwa kwa kutumia vigezo vikuu viwili. Kigezo cha
kwanza ni kwa mujibu wa maana iwakilishwayo na mofu na kigezo cha pili ni
kwa mujibu wa muundo/mofolojia ya mofu yenyewe. Kwa kutumia kigezo cha
maana iwakilishwayo na mofu tunapata mofu huru, mofu funge na mofu tata.
Mofu huru
Ni yale maumbo yanayobeba maana zinazojitosheleza/kamili. Katika
Kiswahili mizizi ya maneno mengi huwa ni mofu huru kwa mfano nomino
(baba, kalamu, Magomeni, n.k.), vivumishi (safi, imara, bora, dhaifu, n.k.),
viwakilishi (sisi, wewe, wao, n.k.), vielezi (leo, haraka, taratibu, n.k.)
viunganishi (na, halafu, lakini).
Mofu Funge/tegemezi
Ni maumbo ambayo husitiri maana zisizojitosheleza. Mofu funge huhitaji
kufungamana na mofu nyengine ili kuzalisha umbo lenye maana kamili.
Kwa mfano; maumbo a, li, tu, lish, na a ni maumbo ambayo hatuwezi kujua
maana zake hadi pale maumbo hayo yatakapounganishwa na kuwa umbo
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 8
moja alitulisha. Hapa sasa tunaweza kufafanua maana zilizofichwa ndani ya
maumbo haya ambazo ni:-
Mofu Maana (mofimu)
a- Nafsi (ya tatu)
Idadi (umoja)
Neli (ya kwanza A-WA)
-li- Mtenda
Wakati (uliopita)
-tu- Nafsi (ya kwanza)
Idadi (wingi)
-l- Mzizi
-ish- Usababishi/utendeshi
-a Dhamira arifu
Mofu tata
Ni mofu ambazo hubeba maana zaidi ya moja. Mfano neno ‘atanipikia’ lina
mofu sita (a-ta-ni-pik-i-a), mofu i- (ya pili kutoka kulia) inawakilisha
mofimu/inabeba maana ya utendea ambayo ndiyo chanzo cha utata; kwani
yaweza kueleweka kama:
Kupika kwa niaba yangu
Kupika kwa ajili yangu
Kigezo cha mofolojia ya mofu tunapata mofu kapa na mofu changamano.
Mofu kapa
Ni mofu zisizodhihirika kimatamshi wala kimaandishi ila athari zake zipo na
zinaeleweka kwa wamilisi wa lugha husika. Mofu hizi huwakilishwa kwa
alama Ɵ.
Mfano;
Umoja wingi
u-funguo Ɵfunguo
Ɵjani ma-jani
Ɵsimu Ɵsimu
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 9
Mofu changamano
Mofu changamano ni mofu ambazo huundwa kwa kuweka pamoja angalau
mofu huru mbili au mofu funge na mofu huru na kuunda neno lenye kuleta
maana kamili, kwa mfano:
Mofu huru + Mofu huru
- {fundi} + {chuma} = fundichuma.
- {gari} + {moshi} = garimoshi.
Mofu funge + Mofu huru
-{mw} + {ana} + nchi = mwananchi.
{ki} + {ona} + mbali = kionambali.
MOFIMU
Mofimu ni kipashio dhahania cha lugha ambacho husitiriwa na mofu. Hivyo
tunapozungumzia mofimu tunaangalia zaidi maana ambayo ni dhahania na
siyo umbo. Kwa mantiki hii kigezo kikubwa cha kubainisha/kutambua
mofimu ni maana.
Aina za mofimu
Mofimu huru
Ni mofimu inayojitosheleza kimaana bila ya kuongezwa kiambishi cha aina
yoyote. Ina uwezo wa kusimama pekee kama neno. Mfano; Maryam, paka,
simu, papai, n.k.
Mofimu tegemezi
Ni aina ya mofimu ambazo hazijitoshelezi kimaana. Mofimu hizi hukamilika
kimaana zinapoongezwa mofimu nyengine. Haziwezi kusimama pekee kama
neno. Mfano; ki-tabu, m-tu, mu-ana-funz-i, n.k.
Matatizo ya utengaji/ubainishaji wa mofimu
Tatizo la kwanza ni kukosekana kwa umbo dhahiri la mofimu
Mfano: θ+chungwa : ma+chungwa
θ+bega : ma+bega θ+jiwe : ma+we
θ+shati : ma+shati
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 10
Katika mifano hiyo mofimu za umoja ni //θ// na za wingi ni //ma//
Tatizo la pili ni kukosekana maneno asilia yanayozalisha maneno unde.
Mfano:
Fupi – fupika –fupisha Refu - refuka –refusha
*Kau – kauka – kausha
Mifano hiyo ina maneno asilia na maneno unde. Maneno (fupi na refu) ni maneno
asilia ya maneno unde fupisha na refusha. Lakini (kau) sio neno asili la neno
(kauka na kausha) kwa sababu neno hilo (kau) halikubaliki kwa maneno ya namna
hiyo.
Tatizo la tatu ni ugumu wa kutenganisha mofimu katika maneno mwambatano.
Mfano:
Mwanajeshi
Mu-ana-jeshi
Mw-ana-jeshi
Mw-an-a-jeshi
Mw-anajeshi
Maneno mwambatano yanaundwa kwa mzizi zaidi ya mmoja hivyo huwa ni
vigumu kubaini mofimu ni zipi na mizizi ni ipi.
KANUNI ZA KUTENGANISHA MOFIMU
Kanuni ya kwanza; zingatia maumbo yenye maana sawa. Maumbo hayo
huweza kufanana au kuhitilafiana kiumbo lakini hutokea katika mazingira
yaleyale.
Mfano
a) atakupiga
b) atampiga
ata-ku-pig-a
a-ta-m-pig-a
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 11
c) alikupiga -li-ku-pig-a
d) utanipiga -ta-ni-pig-a
e) utatupiga -ta-tu-pig-a
f) mlijipiga -li-ji-pig-a
Mofimu
1. mofimu nafsi --------- (a)-3-umoja
--------- (u)-2-umoja
---------- (m)-2-wingi
---------- (tu)-1-wingi
2. mofimu njeo ------------- (ta)-ijayo
------------- (li)-iliyopita
-------------- (na)-iliyopo
3. yambwa ---------------- (ku)-wewe
--------- (m)-yeye
---------- (ni)-mimi
----------- (ji)-binafsi
Kanuni ya pili; Hapa kinachozingatiwa ni maumbo yenye maana moja
lakini yasiyo na umbo sawa la kimofolojia.
Mfano; a) mtumwa b) mvulana
c) mjakazi
d) mwenzi
e) mwanadamu
watumwa wavulana wajakazi wenzi
wanadamu
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 12
mofimu mofimu za idadi
//umoja//---------m/-k -------- mw/-i
//wingi//--------- wa/-k ---------- w/-I
Kanuni ya tatu; Kanuni hii inadai kuwa alomofu moja au zaidi zimo katika
mtawanyo mkamilishano ambapo moja ikitokea basi ya pili haitokei. Yambwa na
yambiwa haziwezi kutokea katika mazingira yale yale.
Mfano
Baba alinimpigia mimi simu
Sisi tuliwamuona nyinyi
Yeye alimwakuta wao
(m) na (mu)
(wa) na (w)
Zimo katika mtawanyo mkamilishano au mgawanyo wa kiutowano
Kanuni ya nne; Umbo moja na zaidi huweza kuwa katika mpishano huru kama
maumbo hayo yana maana moja na yametokea katika mazingira yaleyale. Mfano ngombe badala ya ng’ombe
khabari badala ya habari
lafiki badala ya Rafiki
ntoto badala ya mtoto
Kanuni ya tano; inadai kuwa maumbo yenye maana tofauti ni mofimu
na maumbo tofauti yenye maana sawa ni alomofu.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 13
MUHADHARA WA 3 : ALOMOFU
Fasili ya alomofu
Alomofu ni maumbo mbalimbali yanayowakilisha dhana moja ya kisarufi.
Alomofu ni maumbo mbalimbali ya mofimu moja.
Alomofu hufafanuliwa kama maumbo zaidi ya moja (mbalimbali) ya mofimu
moja.
Mazingira ya utokeaji wa alomofu
Alomofu hazitokei kibahati nasibu tu. Mara nyingi utokeaji wa alomofu fulani
unategemea kupatikana kwa mazingira mahususi. Mazingira hayo yanaweza
kuelezeka kifonolojia, kileksika na kisarufi.
Mazingira ya kifonolojia
Kuna baadhi ya alomofu utokeaji wake hutegemea kuwepo au kutokuwepo kwa
sauti/fonimu fulani. Kwa mfano; mofimu iwakilishayo umoja katika ngeli ya KI-
VI hujitokeza kwa umbo la ki- ikifuatiwa na konsonanti lakini mofimu hiyo hiyo
huwakilishwa na umbo la ch- ikifuatwa na irabu.
Mfano:
Ki +tabu = kitabu, ki+buyu = kibuyu, ki+sima = kisima
Ki+umba = chumba, ki+ama =chama, ki+etu = chetu, ki+ekundu = chekundu
Mazingira ya kileksika (kikamusi/kimaana)
Alomofu pia hujitokeza kutokana na mazingira ya kileksika. Tofauti na mazingira
ya kifonolojia ambayo aghalabu hutabirika mazingira ya kileksika hayatabiriki na
hutegemea zaidi neno husika.
Mfano:
Mtume ---------mitume
Waziri---------mawaziri
Kiongozi ----viongozi
Malaika --------malaika
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 14
Mganga --------waganga
Kwa kuzingatia mazingira ya kileksika ya mifano hapo juu tunaweza kusema kuwa
mofu ya umoja //m// inaweza kujitokeza kama //m//, /θ/ na /ki/ wakati mofu ya
wingi //wa// inajitokeza kama //mi//, //ma//, //vi// na // θ //.
Mazingira ya kisarufi
Wakati mwengine alomofu hutokea kwa sababu za kisarufi. Mfano mzuri
unapatikana katika mofimu za njeo. Mabadiliko ya wakati unaohusishwa na tendo
husababisha kupatikana kwa maumbo mbalimbali yawakilishayo njeo. Angalia
mifano ifuatayo:
A B
Anaandika - haandiki
Aliandika - hakuandika
Ataandika - hataandika
Ameandika - hajaandika
Kutokana na mifano hii maumbo yanayowakilisha njeo katika kifungu A ni //na//,
/li//, //ta// na //me// yanayoashiria wakati uliopo, wakati uliopita (muda mrefu) na
wakati uliopita (muda mfupi) hali yakinishi na katika kifungu B ni //i//, //ku//, //ta//
na //ja// yanayowakilisha nyakati hizohizo katika ukanushi.
Aina za alomofu
Alomofu za njeo : ----- -na-, -li-, -me-, -ta-, -ku-, -ja- (anasoma, alisoma,
amesoma, atasoma, hakusoma, hajasoma).
Alomofu za nafsi : ni, tu, u, m, a, wa (ninasoma, tunasoma, unasoma,
mnasoma, anasoma, wanasoma).
Alomofu za wingi : mi-, vi, wa-, ma-, n.k. (miti, vijiko, watoto, majembe)
Alomofu za umoja : ki-, m-, u-, li-, n.k. (kibanda, mkeka, ukuta, limeoza)
Alomofu za usababishi/utendeshi : ish, esh, z, fy, vy, sh (katisha, somesha,
liza, ogofya, levya, safisha)
Alomofu za ukanushi : si, ha, (hu-) (siandiki, haandiki, h(a)uandiki)
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 15
Alomofu za urejeshi : ye, cho, po, vyo, ko, n.k. (aliyeondoka, kilichozama,
nilipokosa, ulivyokurupuka, walikokimbilia)
Alomofu za masharti : ki, nge, ngeli, ngali, ngeli, kama, endapo (akija,
angekuja, angalikuja, kama atakuja, endapo atakuja)
MUHADHARA WA 4 : KIAMBISHI
Fasili ya kiambishi
Kiambishi ni mofu iongezwayo kwenye mzizi wa neno na kuwakilisha maana ya
kisarufi.
Aina za viambishi
Aghalabu viambishi huainishwa kwa kutegemea mahali ambapo viambishi hivyo
huwekwa katika neno. Hivyo kwa ujumla tunapata aina kuu tatu za viambishi
ambazo ni; viambishi awali, viambishi ndani/kati na viambishi tamati.
Viambishi awali
Ni viambishi ambavyo huwekwa kabla ya mzizi wa neno. Mfano; neno
tunakuja……tu-na-ku ni viambishi awali vilivyowekwa kabla ya mzizi wa
neno –j- . mifano mingine ni hatulimi, wanasoma, n.k.
Viambishi ndani/kati
Hivi ni viambishi ambavyo huwekwa katikati ya mzizi wa neno. Hakuna
mfano wa neno la Kiswahili lenye kiambishi ndani kwa sababu lugha ya
Kiswahili haina muundo huo. Mifano tunaweza kuipata katika lugha
nyingine kama vile lugha ya Kibari kutoka Sudani ya kusini. Katika lugha
hii mofimu ya idadi huoneshwa kwa kutumia viambishi ndani. Mfano;
Popon ------------------------ shimo (umoja)
Popojin ---------------------- mashimo (wingi) –ji ni kiambishi ndani cha
wingi.
Bun ----------------------------- kitabu (umoja)
Bukan ------------------------ vitabu (wingi) –ka- ni kiambishi ndani cha
wingi.
Viambishi tamati
Ni aina ya viambishi ambavyo huwekwa baada ya mzizi wa neno.
Mfano
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 16
Chumbani ------------------ chumba (mzizi) + -ni (kiambishi tamati)
Somo ------------------------som (mzizi) + -o (kiambishi tamati)
Pikisha --------------------- pik (mzizi) + ish + -a (viambishi tamati)
Kutokana na maelezo na mifano ya hapo juu tunaona kuwa lugha ya
Kiswahili ina aina mbili tu za viambishi; viambishi awali na viambishi
tamati. Jambo la kuzingatia ni kwamba viambishi vya aina zote huweza
kujitokeza katika neno moja la Kiswahili. Kwa mfano hatujawapigisheni-
maumbo yaliyokolezwa wino kabla ya mzizi –pig- ni viambishi awali na
yale yaliyo baada ya mzizi ni viambishi tamati. Vilevile tunaona kuwa
viambishi ni maumbo tegemezi yanayofanya kazi ya kuleta maana
yanapounganishwa na mzizi tu. Na pia tumegusia kuwa viambishi
huwakilisha maana za kisarufi tu.
Mpangilio wa viambishi
Katika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo
juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana
fulani ya kisarufi. Hivyo basi ni lazima kuwe na utaratibu maalumu wa
kuvipanga viambishi katika mzizi wa neno ili neno litoe maana na taarifa
iliyokusudiwa. Katika sehemu hii tutaonesha mpangilio wa viambishi katika
maneno ya lugha ya Kiswahili. Tutaangalia zaidi kitenzi na nomino.
Mpangilio wa viambishi awali katika kitenzi
Kwa kawaida kitenzi huanza na kiambishi nafsi, mfano a-cheka
Kiambishi nafsi hufuatiwa na kiambishi cha wakati mfano alicheka
Kiambishi cha wakati hufuatiwa na kiambishi rejeshi mfano
aliyecheka
Kiambishi rejeshi hufuatiwa na kiambishi yambwa/yambiwa mfano
aliyemcheka.
Mpangilio wa viambishi tamati katika kitenzi
Kama ilivyoelezwa awali kuwa viambishi tamati ni vile vinavyokaa baada
ya mzizi wa neno. Aghalabu viambishi tamati huwa ni vya mnyambuliko na
hutokea kimoja tu katika neno.
Mfano;
Wanapigwa – utendwa.
Wanapigana – kutendana
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 17
Wanapigika – kutendeka
Wanapigisha – kutendesha
Wanapigiana – kutendeana, n.k.
Hata hivyo, iwapo kitenzi kitakuwa na viambishi tamati zaidi basi mzizi huo
huwa ni mzizi wa mnyambuliko na aghalabu unakuwa umeundwa kwa kiini
cha neno na mofimu ya kutendana (mf. pigan). Ikiwa mzizi una kiambishi
cha kutendana //an//, baadaye huja kiambishi cha kutendesha //sh,ish,esh//
n.k. na kisha hufuata kiambishi cha utendeka //ik, ek// au kiambishi cha
utendwa //w// (hutegemea na taarifa inayotolewa) na kumalizia na kiambishi
–a kinachokamilisha maana. Chunguza utaratibu huu katika maneno
yafuatayo:
Tuliowapiganisha
Tumepiganishika
Tumepiganishwa
Mifano iliyotolewa hapo juu ni ya vitenzi yakinifu tu. Hata hivyo, ni vyema
ieleweke kuwa utaratibu huu hufanya kazi hata katika hali ya ukanushi
isipokuwa kiambishi cha ukanushi si, ha (hu) hutokea mwanzoni kabisa
kabla ya kile cha nafsi.
Mfano.
Utapika ---------------- h(a)utapika (wakati ujao)
Tumepigana ---------- hatujapigana (wakati uliopita – muda mfupi)
Walitufurahisha --------- hawakutufurahisha (wakati uliopita)
Hata hivy, hali huwa tofauti kidogo kwa upande wa wakati uliopo kwani
kiambishi cha wakati na hudondoshwa na umbo la kitenzi humalisika kwa
irabu i badala ya a kama ilivyozoeleka. Kuna wataalamu wanaodai kuwa hii
irabu ya mwisho i ndicho kiambishi cha wakati uliopo katika ukanushi.
Mfano:
Tunasoma – hatusomi (*hatunasoma)
Ninapika – sipiki (*sinapika)
Mpangilio wa viambishi katika nomino
Aghalabu nomino huweza kuandamana na viambishi vya aina tatu tu. Viambishi
hivyo ni bya idadi (umoja na wingi), ukubwa na udogo. Mfano;
Mtoto (m ya umoja) kitoto (ki ya udogo) jitoto (ji ya ukubwa) kijitoto (ki ya
umoja na udogo na ji ya udogo).
Watoto – vitoto- mitoto – mijitoto – vijitoto
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 18
Wakati mwingine hutokea nomino ikabeba viambishi vya aina mbili kwa pamoja.
Katika hali hiyo kiambishi cha idadi hutangulia na ndipo kikaja kiambishi cha
ukubwa/udogo kama ilivyo katika mifano hapo juu.
Viambishi nominishi: ni vile ambavyo vinapoambikwa katika neno lisilokuwa
nomino hulifanya neno hilo kuwa nomino.
Mfano
Ji > mchoraji, mtangazaji, uimbaji, muuaji, upimaji, n.k.
Zi> Upekuzi, uchaguzi, ufafanuzi
i > Ushindi, uchunguzi, ubishi, msomi
O > Somo, upendo, mkopo
fu > udanganyifu, usahaulifu, uchangamfu, usumbufu
kama ilivyoelezwa katika mifano hapo juu, utokeaji wa viambishi hivi aghalabu
huambatana na utokeaji wa viambishi awali vya nomino vinavyodokeza idadi,
udogo au ukubwa wa nomino (m/wa, ki/vi, u, ma, n.k.)
viambishi elezi: ni vile ambavyo vinapoambikwa katika neno lisilokuwa kielezi
hulifanya neno hilo kuwa kielezi.
Mfano
ni > sokoni, barabarani, darasani, n.k
ki > kijeuri, kiume, kikatili
vi > vizuri, vibaya
MUHADHARA WA 5 : MZIZI
Fasili ya mzizi
Mzizi ni neno au sehemu ya neno ambayo hubeba taarifa ya msingi na
haibadilikibadiliki.
Sifa bainifu za mzizi
Mzizi hubeba taarifa ya kileksika
Mzizi haubadilikibadiliki
Mzizi ni mofu muhimu kuliko mofu zote katika neno
Mzizi hauwezi kuachwa wakati wote neno linapotumika
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 19
Aina za mzizi
Mzizi huru: ni mzizi usiopokea kiambishi cha aina yoyote. Mfano; mama,
sawa, chungwa, n.k.
Mzizi funge: ni mzizi unaoandamana na viambishi ili kukamilisha maana
mfano; kisu, mti, n.k. –su na –ti ni mfano wa mizizi ya maneno ambayo
maana zake hupatikana baada ya kufungamanishwa na viambishi.
Mzizi asilia: ni mzizi unaotokana na kiini cha neno. Mfano wa mzizi asilia
ni andik- katika neno andika, kat- katika neno kata, n.k.
Mzizi wa mnyambuliko: ni mzizi unaotokana na mzizi asilia pamoja na
viambishi. Kwa mfano andikish- ni mzizi wa mnyambuliko unaoweza
kuzalisha maneno kama andikisha, andikishwa, andikishana, andikishia, n.k.
na pigan- ni mzizi wa mnyambuliko unaoweza kuzalisha maneno kama vile
pigana, oigania, piganiwa, piganisha, n.k
Miundo ya mzizi
Neno zima: mf. sungura, mbuzi, kopo, bibi
Konsonanti pekee: mf. –p- katika nipe, -f- katika kifo
Irabu pekee: mf. –u- katika usiniue, o- katika wameoana
Silabi moja: mf. –ki katika kiti, to- katika toa, li-katika lia
Silabi moja au zaidi pamoja na sehemu tu ya silabi nyingine : mf. som-
katika soma, kat-katika kata, andik-katika andika, tafut-katika tafuta.
Silabi zaidi ya moja : mf. kimbi- katika kimbia, fafanu-katika ufafanuzi.
MUHADHARA WA 6 : NENO
Fasili ya neno
Neno ni kipashio cha kiisimu kinachoundwa na mofimu moja au zaidi na kutoa
maana fulani katika lugha husika. Maana hiyo yaweza kuwa ya kisarufi au ya
kileksika.
Aina za maneno
Maneno hugawanywa katika aina zake kwa vigezo viwili ambavyo ni: kigezo cha
muundo na kigezo cha kazi.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 20
Aina za maneno kimuundo
Neno sahili : ni neno linaloundwa kwa mzizi huru mmoja (mf. mama, wewe,
maji, hewa, n.k)
Neno ambatani : ni neno linaloundwa kwa mizizi miwili. Yawezekana ikawa
ni mzizi funge na mzizi huru au mizizi huru miwili (mf. mwanaanga,
mwanahewa, bwanashamba)
Neno changamano : ni neno linaloundwa kwa mzizi funge pamoja na
viambishi mbalimbali (mf. mapigo, mwendeshaji, n.k.)
Aina za maneno kikazi/kiuamilifu
Kwa kutumia kigezo cha kazi/uamilifu tunapata aina zifuatazo za maneno:-
Nomino (N)
Kiwakilishi (w)
Kivumishi (V)
Kitenzi (T)
Kielezi (E)
Kihusishi (H)
Kiunganishi (U)
Kihisishi/Kiingizi (I)
TAARIFA ZINAZOPATIKANA KATIKA NENO
Taarifa ya kifonolojia
Ni kujua fonimu zilizotumika kuunda neno hilo. Mf. neno /paka/ limeundwa
na fonimu /p/, /a/ na /k/
Taarifa ya kimofolojia
Ni kujua mofimu zinazounda neno hilo. Mf. neno /paka/ limeundwa kwa
mofimu moja huru na neno /mtu/ limeundwa na mofimu tegemezi mbili m-
na -tu
Taarifa ya kisintaksia
Ni kujua aina ya neno kulingana na uamilifu wake katika tungo. Mf;
(a) Kitu chema hakidumu (b) chema hakidumu
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 21
Neno chema katika (a) ni kivumishi na neno chema katika (b) ni
kiwakilishi. Tunajua aina ya neno kwa kuangalia kazi na nafasi yake katika
tungo.
Taarifa ya kisemantiki
Ni kujua maana ya neno. Ili mkusanyiko wa silabi ukubalike kuwa ni neno
lazima uwe na maana katika lugha husika; hivyo mkusanyiko usioleta maana
si neno. Mf; paletihoju ni mkusanyiko wa silabi usioleta maana katika lugha
ya Kiswahili na hivyo hili si neno la Kiswahili.
Neno na leksimu
Imeelezwa katika fasili ya neno kwamba neno lazima liwe na maana ya
kisarufi au ya kileksika/kikamusi. Neno lenye maana kileksika huweza
kusimama peke yake kama kidahizo katika kamusi. Hivyo basi tunaweza
kusema leksimu ni kipashio cha kidhahania ambacho ni cha msingi katika
msamiati wa lugha na hubeba dhana ya kwanza ya neno. Ni maneno yenye
maana za kileksika ambayo huwa vidahizo katika kamusi.
Mfano;
Doa ji/ma – 1. Alama au tone ambalo lina rangi tofauti na mwili wa kitu
2. Aibu, dosari, ila, kasoro.
Maneno yenye maana za kisarufi ambayo hayawezi kutumika kama kidahizo
katika kamusi yanabaki kuwa maneno tu lakini si leksimu.
NENO NA MOFIMU
Neno ni mkusanyiko wa silabi zinazotamkwa au kuandikwa na kuleta maana
fulani katika lugha. Mkusanyiko huo wa silabi unaweza kuwa ishara ya
maana ya kileksa au maana kisarufi.
Mofimu kwa upande mwingine ni kipashio cha kiisimu chenye maana ya
kileksika au kisarufi. Maneno huweza kuwa na mofimu moja au zaidi lakini
si lazima wakati wote iwe neno.
LEKSIMU NA MOFIMU
Leksimu ni kipashio kidogo cha msamiati kinachoweza kusimama peke yake
katika kamusi kama kidahizo. Mofimu inaweza kusimama peke yake hasa
ikiwa mofimu huru.
MUHADHARA WA 7: NENO (Aina za Maneno – Nomino)
Nomino: ni maneno ambayo hutaja majina ya watu, vitu, mahali, vyeo,
dhana na hata tendo.
Aina za nomino
Nomino za pekee
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 22
Nomino za kawaida
Nomino za dhahania
Nomino za jumla
Dhima ya nomino
Kiima cha sentensi: Juma analima
Yambwa : Juma amenunua kitabu
Yambiwa : Juma amemnunulia Ali kitabu
Kijalizo : Juma ndiye kiongozi wetu
MUHADHARA WA 8 : NGELI ZA NOMINO (Mkabala wa Kimofolojia)
Fasili ya ngeli
Ni uwekaji wa nomino katika makundi mbalimbali kulingana na vigezo maalumu.
Vigezo hivyo vyaweza kuwa vya kimofolojia, kisintaksia n.k. kutokana na vigezo
hivyo ndipo tunapopata migawanyo tofauti ya ngeli; kama mgawanyo wa ngeli
kimapokeo na mgawanyo wa ngeli kimamboleo/kisasa.
Mgawanyo wa ngeli za nomino kimapokeo
Huu ni uainishaji wa ngeli kwa kutumia kigezo cha mofolojia ya nomino.
Tunapotumia kigezo hiki kugawa nomino za Kiswahili katika ngeli tunazingatia
zaidi viambishi awali vya idadi – umoja na wingi ambavyo ni vya kawaida katika
nomino hizo – si viambishi vyenye kuonesha dhana ya ukubwa na udogo. Kwa
kigezo hiki tunapata makundi yafuatayo ya ngeli:-
a) Ngeli ya M(U) – WA (Mtu-watu, mtoto-watoto)
b) Ngeli ya M-Mi (mti-miti, mkono-mikono)
c) Ngeli ya JI-MA (jicho-macho, jiwe-mawe)
d) Ngeli ya KI-VI (kinu-vinu, kiwete-viwete)
e) Ngeli ya U-N (ulimi-ndimi, ufa-nyufa)
f) Ngeli ya U-MA (uamuzi-maamuzi, upishi-mapishi)
g) Ngeli ya U-Ɵ (upawa- Ɵpawa, ukucha- Ɵkucha)
h) Ngeli ya Ɵ-MA (Ɵchungwa-machungwa, Ɵjani-majani)
i) Ngeli ya Ɵ- Ɵ (Ɵnyumba- Ɵnyumba, Ɵnguo- Ɵnguo)
UBORA WA KIGEZO CHA KIMOFOLOJIA
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 23
a) Uwezekano wa kuzigawa nomino nyingi za Kiswahili ni mkubwa kwa kuwa
nyingi zimegawanyika katika maumbo hayo ya umoja na wingi.
b) Ni kigezo muhimu kwani kinajikita zaidi katika nomino na kivumishi chake
peke yake hakigusi aina nyingine ya neno tofauti na kigezo cha kisintaksia
ambacho hugusa hadi kitenzi.
c) Huwasaidia wanasarufi linganishi kuonesha uhusiano wa lugha za kikoa
kimoja.
d) Kilisaidia kuondokana na uainishaji ngeli kwa kutegemea tofauti za
kibayolojia.
e) Kinasaidia kutambua mofolojia ya nomino kama ni huru au changamano.
UDHAIFU WA KIGEZO CHA KIMOFOLOJIA
a) Kuna viambishi katika ngeli tofauti vinavyofanana. Mfano Kiambishi M-
kinajitokeza katika ngeli ya 1 na 3 na MA- inajitokeza katika ngeli ya 8 na
13.
b) Kuna nomino nyingine ambazo hazijidhihirishi katika umoja na wingi.
Mfano ngeli ya 8 na 9.
c) Nomino zenye hadhi tofauti kuwekwa kwenye ngeli moja mf. (kiwete,kinu),
(sikio,tawi).
d) Kuna matumizi ya vigezo viwili kwa pamoja, kigezo cha maumbo ya idadi
na kigezo cha sifa za nomino.
e) Idadi ya ngeli ni kubwa na hivyo humfanya msomaji kupata tabu ya
kuzikariri.
f) Wanamapokeo wamegawanyika pasipo sababu za msingi, kuna wenye ngeli
18, 16 na 9.
MUHADHARA WA 9 : MGAWANYO WA NGELI ZA NOMINO KIMAMBOLEO
Huu ni uainishaji wa ngeli kwa kutumia kigezo cha sintaksia ya nomino. Uainishaji
huu huzingatia uhusiano wa nomino na maneno mengine katika tungo kwa
kuangalia viambishi vya upatanishi wa kisarufi vinavyojitokeza mwanzoni mwa
maneno yanayoandamana na nomino katika tungo. Viambishi hivyo huathiriwa na
umbo la nomino inayozungumzwa katika tungo husika. Kwa kutumia kigezo hiki
tunapata makundi yafuatayo ya ngeli:-
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 24
a) Ngeli ya YU-A/WA: mtoto yuasoma/mtoto anasoma-watoto wanasoma
b) Ngeli ya U-I: mkoba umechanika-mikoba imechanika
c) Ngali ya LI-YA: debe linauzwa-madebe yanauzwa
d) Ngeli ya KI-VI: kiatu kimetupwa-viatu vimetupwa
e) Ngeli ya I-ZI: ndizi imeiva-ndizi zimeiva
f) Ngeli ya U: ushawishi umemponza-ufisadi umekithiri
g) Ngeli ya U-YA: ugonjwa umetukatisha tamaa-magonjwa yametukatisha
tamaa
h) Ngeli ya U-ZI: ungo umeharibika-nyungo zimeharibika
i) Ngeli ya YA: maji yanamwagika, mafuta yamekwisha
j) Ngeli ya I: chai imenywewa
k) Ngeli ya KU: kulima kunakondesha, kula kwake kutamdhuru
l) Ngeli ya PA-MU-KU: kiwanjani petu panafaa, nyumba munagiza, kule
kunatisha
UBORA WA MTAZAMO WA KISASA
Kigezo cha kisintaksia kinachotumiwa katika mtazamo wa kisasa kugawa ngeli
kwa kuzingatia upatanisho wa kisarufi kina ubora wake kama ifuatavyo:
Kimepunguza makundi mengi ya ngeli za nomino
Ni rahisi kuzikariri kwani ni chache.
Kila nomino huweza kuingia katika ngeli yake kwa kuzingatia upatanisho
wa kisarufi.
Nomino hupangwa katika ngeli zake kulingana na sifa na hadhi yake.
Husaidia kubaini umoja na wingi wa nomino zisizo na maumbo dhahiri ya
idadi.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 25
Kigezo hiki kimepunguza kujirudiarudia kwa ngeli.
Husaidia kubainisha uhusiano wa nomino na maneno mengine katika tungo.
Husaidia kuonesha urejeshi wa vitenzi na nomino zake.
UDHAIFU WA MTAZAMO WA KISASA
Bado kuna ngeli za nomino zinazojirudia mf. Ngeli ya 2,6 na 7 umoja
zinatumia u.
Ngeli ya kwanza umoja ina viambishi viwili (Yu/A)
Bado kuna nomino zenye kuleta mgogoro katika ngeli mf. Makala, Jambazi,
marashi.
Pamoja na umoja na wingi kutawala, kigezo cha sifa ya nomino hujitokeza
ili kuepuka kuchanganya majina yenye sifa na hadhi tofauti mf. Kinyonga
hukubali zaidi ngeli ya (KI-VI) lakini huwekwa katika ngeli ya kwanza kwa
sifa ya kiumbe hai.
Kigezo hiki hakijaweza kuonesha mofolojia ya nomino.
MUHADHARA WA 10: VIWAKILISHI
Fasili ya viwakilishi
Viwakilishi ni maneno yanayosimama badala ya nomino au kikundi nomino.
Muundo wa viwakilishi
Kwa ujumla viwakilishi hujitokeza katika miundo miwili. Kiwakilishi huweza
kuwa huru au kiambata. Kiwakilishi huru ni kile kinachosimama pekee kikiwa
neno kamili kama vile mimi, yeye, nani, nini, n.k. kwa upande wa kiwakilishi
kiambata ni kiwakilishi ambacho huambatanishwa mwanzoni mwa kitenzi.
Aina za viwakilishi
1. Viwaklishi vya sifa : kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza
2. Viwakilishi vya idadi: wawil wameokolewa, mmoja hajulikani alipo.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 26
3. Viwakilishi vioneshi: yule habebeki, huyu nampenda
4. Viwakilishi viulizi: ipi unaitaka? Lipi limekuudhi?
5. Viwakilishi vimilikishi: wangu ni mweusi, wao amezidi mno
6. Viwakilishi nafsi: mimi sijali, nyinyi mnacheza
Nafasi ya kiwakilishi: kiwakilishi hutokea badala ya nomino/huchukua nafasi ya
nomino pale ambapo nomino haipo.
MUHADHARA WA 11 : VIVUMISHI
Fasili ya kivumishi
Vivumishi ni maneno ambayo huandamana na nomino ili kuongeza sifa au taarifa
muhimu kwa nomino (huifanya nomino ivume).
Muundo wa vivumishi
Kwa kutumia kigezo cha kimuundo kuna aina mbili za vivumishi ambazo ni:
Vivumishi vinavyoambishwa mf; dogo, refu, chungu, zuri, n.k
Vivumishi vinaweza kuambishwa kulingana na upatanishi wa kisarufi wa
nomino inayovumishwa. Hivyo tunaweza kupata tungo kama ki+dogo,
wa+refu, m+chungu, vi+zuri, n.k
Vivumishi visivyoambishwa-aghalabu vivumishi vya aina hii hutokana na
maneno yenye asili ya lugha ya Kiarabu mf; Jamali,dhaifu,n.k
Aina za vivumishi
Vivumishi vya sifa: hivi ni aina ya vivumishi vinavyotoa sifa ya nomino.
Mfano kitambaa kizuri, mti mrefu, mwanafunzi mvivu, mtandio mweupe.
Jambo la kuzingatia hapa si lazima ile sifa iwe njema hata sifa mbaya pia ni
kivumishi.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 27
Vivumishi vya idadi: hivi ni vivumishi vinavyoonesha idadi ya vitu
mbalimbali. Mfano watoto wawili, nyumba moja.
Vivumishi vya idadi vinaweza kujitokeza katika aina tatu ndogondogo.
- Vivumihi vya aina hii hutoa taarifa kuhusu idadi ya nomino ambazo kiwango
chake kimetajwa.
- Vivumishi vya idadi vinavyoweza kuvumisha nomino kwa kutaja idadi ya
nomino hizo kiujumla jumla bila kudhihirisha idadi halisi.
- Vivumishi vya idadi ambavyo huonesha nafasi iliyochukuliwa na nomino
fulani katika orodha.
Vivumishi vya kuonesha:vivumishi vya aina hii huonesha mahali au upande
kitu kilipo. Vivumishi vya aina hii hujengwa na mzizi {h} kwa vitu
vilivyopo karibu na mzizi {le} kwa vitu vilivyo mbali. mfano kijana huyu,
kuku wale
Vivumishi vya pekee: vivumishi hivi huitwa vya pekee kwa sababu kila
kimojwapo huwa na maana maalumu. Pia kila kimojawapo huchukua
upatanisho wake wa kisarufi kulingana na ngeli ya nomino ambayo
kinaivumisha. Mizizi ya vivumishi hivi ni ote, o-ote, enye, enyewe, ingine,
ingineo. Mfano chakula chochote, wakati wowote
Vivumishi viulizi: hivi ni vivumishi ambavyo hufafanua nomino kwa
kuuliza habari zake. Mfano nguo ipi? Msichana yupi?watu wangapi?
Vivumishi vya jina kwa jina: ni vivumishi ambavyo jina huvumisha jina
lililotangulia katika mfuatano. mfano mwalimu Majaliwa, Mzee kipofu
Vivumishi vimilikishi: ni vivumishi vinavyoonesha kuwa kitu fulani kina
milikiwa na mtu au kitu kingine mfano: mali yangu, paka wako, nchi yetu
MODULI 4: VITENZI, VIELIZI NA VIUNGANISHI
VITENZI (T)
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 28
Vitenzi ni maneno yanayosimamia kitendo. Kila kitenzi huwa na shina la
kitenzi (sehemu ndogo zaidi ya kitenzi ambayo ndiyo huwakilisha tendo hilo).
Shina la kitenzi huambatanishwa na viambishi ili kutoa maana iliyokusudiwa
kama vile mtendaji, mtendewa, wakati kitendo kinafanyika na pia kauli ya
kitenzi hicho.
Aina za Vitenzi
Vitenzi Halisi
Vitenzi Visaidizi + Vitenzi Vikuu
Vitenzi Vishirikishi
Vitenzi Sambamba
Vitenzi Halisi
Hivi ni vitenzi vinavyorejelea kitendo moja kwa moja. Vitenzi halisi
vinapoambatanishwa na vitenzi vidogo katika sentensi, huitwa vitenzi vikuu.
k.m: soma, kula, sikiza
Waziri Mwasimba aliwasili jana kutoka ng'ambo.
Kawia atapikia wageni.
Funga mlango wa dirisha.
Vitenzi Visaidizi
Vitenzi visaidizi hutangulia vitenzi halisi (vitenzi vikuu) katika sentensi ili
kuleta maana inayokusudiwa kulingana na wakati au hali.
k.m: -kuwa, -ngali,
Jua lilikuwa limewaka sana.
Bi Safina angali analala
Vitenzi Vishirikishi
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 29
Vitenzi vishirikishi hutumika kuelezea hali iliyopo au mazingira. Kuna aina
mbili za vitenzi vishirikishi:
a) Vitenzi Vishirikishi Vipungufu - havichukua viambishi vyovyote.
k.m: ni, si, yu
Kaka yako ni mjanja sana.
Huyo si mtoto wangu!
Paka wake yu hapa.
b) Vitenzi Vishirikishi Vikamilifu - huchukua viambishi vya nafsi au ngeli.
Vitenzi hivi vinaweza kusimama peke yake au vinaweza kufuatiliwa na vitenzi
vikuu.
k.m: ndiye, ndio, ndipo
Sanita ndiye mkurugenzi wa kampuni
Huku ndiko kulikoibiwa
Muundo wa Vitenzi
Kwa kuzingatia muundo wa vitenzi, tunaweza kuweka vitenzi katika aina
zifuatazo:
1. Vitenzi vya Silabi Moja
2. Vitenzi vya Kigeni
3. Vitenzi vya Kibantu
Vitenzi vya Silabi Moja
Hivi ni vitenzi vyenye silabi moja pekee. Ili kuleta maana kamili, vitenzi hivi
huambatanishwa na kiungo KU- katika kauli ya kutenda. Kama vitenzi vingine,
vitenzi vya silabi moja vinaweza kunyambuliwa.
k.m: soma, kula, sikiza
1. -cha - kucha - jua linapochomoza asubuhi k.m kumekucha
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 30
2. -fa - kufa - kuacha kupumua, kupoteza uhai k.m amekufa
3. -ja- kuja - fika mahali hapa k.m nimekuja
4. -la- kula - kutia chakula mdomoni k.m anakula
5. -nya- kunya - kutoa mabaki ya chakula toka tumboni k.m mtoto amekunya
6. -nywa- kunywa - kutia kinywaji kama vile maji au maziwa mdomoni k.m
ninakunywa uji
7. -pa- kupa - kumkabithi/kumpatia mtu kitu k.m amenipa pesa
8. -pwa- kupwa - kujaa hadi pomoni - k.m kisima kimekupwa maji
9. -twa- kutwa - jua linapozama magharibi na usiku kuingia k.m kumekutwa
10. -wa- kuwa - kutokea katika hali au mahali fulani k.m alikuwa
Vitenzi vya Kigeni
Hivi ni vitenzi vyenye asili kutoka kwa lugha nyingine badala ya Kibantu.
Baadhi ya lugha hizo ni Kiarabu, Kizungu, Kireno, Kihispania n.k. Vitenzi hivi
havifuatilii muundo wa kawaida wa vitenzi vya Kiswahili ambavyo huishia kwa
sauti -a. Badala yake, vitenzi hivi huishia kwa sauti nyingine kama vile -e, i, -o,
na u
k.m: haribu, tubu, shukuru, salimu, thamini, amini, samehe, baleghe
Vitenzi vya Kibantu
Hivi ni vitenzi vyenye asili ya Kibantu na ambavyo huishia kwa sauti -a.
Kitengo hiki hujumuisha asilimia kubwa zaidi ya vitenzi vya Kiswahili
k.m: simama, shika, tembea, beba, soma, lia
VIELEZI (E)
Vielezi ni maneno yanayotoa habari zaidi kuhusu kitendo kilivyofanyika. Pia
vielezi hutoa habari zaidi kuhusu hali, vivumishi au vielezi vingine.
Aina za Vielezi
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 31
Vielezi vya Mahali
Vielezi vya mahali hutoa habari kuhusu mahali ambapo kitendo kilifanyika.
Aghalabu vielezi hivi huundwa kwa kutumia jina la mahali au kwa kuongeza
kiungo -NI mwishoni mwa neno linaloashiria mahali.
k.m: nyumbani, kazini, shuleni
Mtoto huyo hajatulia nyumbani tangu alipotoka Mombasa.
Msipitie sokoni mkienda kanisani.
Vielezi vya Wakati
Huelezea zaidi kuhusu wakati kitendo kipofanyika
k.m: jioni, jana, asubuhi, saa saba, mwaka juzi
Mzee Kasorogani amesema kwamba ataoga mwaka ujao
Musa alilazimishwa kuchimba mtaro saa sita usiku
Kisaka na Musa watakutana kesho
Vielezi vya Idadi
Vielezi vya idadi hutulezea kitendo kilifanyika mara ngapi
a) Idadi Kamili
Vielezi vya Idadi Kamili hutaja idadi kamili ya mara ngapi kitendo kilifanyika.
k.m: mara mbili, siku mbili kwa juma, mara kumi
Gibi alimzaba kofi mara tatu na kisha akakimbia.
Daktari alimwagiza mama huyo achukue dawa mara tatu kwa siku na arudi
hospitalini siku mbili kwa mwezi
b) Idadi Isiyodhihirika
Vielezi vya Idadi Isiyodhirika huelezea kiasi ambacho kitendo kilifanyika bila
kutaja kiasi kamili
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 32
k.m: chache, nyingi, kadhaa, kidogo, wastani
Mwizi wa kuku alipigwa mara kadhaa kabla ya kuokolewa na polisi.
Yeye hunipigia simu mara kwa mara
VIelezi Vya Namna
Huelezea jinsi au namna kitendo kinavyofanyika. Kitendo kinaweza kufanyika
kwa namna mbalimbali. Hivyo basi kuna aina mbalimbali za vielezi vya namna:
a) Vielezi vya Namna Halisi
Hutufahamisha jinsi kitendo kinavyofanyika kwa kutumia maneno halisi (bila
kuambatanishwa na maneno mengine au viambishi vingine).
k.m: vizuri, ovyo, haraka
Kioo cha bibi harusi kilianguka na kuharibika vibaya
Mama alipika chakula upesi
Amepigwa kalamu kwa kufanya kazi kiholela
b) Vielezi vya Namna Hali
Hutufahamisha hali ambayo kitendo kilifanyika. Vielezi hivi hujihusisha na
tabia ya kitu/mtendaji wa kitendo
k.m: kwa furaha, kwa makini,
Bibi harusi aliingia kanisani kwa madaha
Mtoto alilia kwa maumivu mengi
c) Vielezi vya Namna Kitumizi/Ala
Hutoa habari kuhusu kifaa, ala au mbinu iliyotumiwa kufanya kitendo fulani
k.m: kwa kisu, kwa jembe, kwa meno, kwa moto, kwa maji
Mkulima aliangusha mti mkubwa kwa shoka
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 33
Mzee huyo alimpiga mke wake kwa bakora kabla ya kuchoma nguo zake
kwa makaa
d) Vielezi Vikariri
Husisitiza kitendo kinavyofanyika kwa kutaja kielezi kinachorejelewa mara
mbili mfululizo.
k.m: haraka haraka, ovyo ovyo, juu juu
Polisi walipoingia, wezi walitawanyika haraka haraka.
Wanafunzi wengi hufanya kazi yao ovyo ovyo
e) Vielezi vya Ki-Mfanano
Vielezi mfanano hutumia KI-mfanano kuelezea kitendo kinavyofanyika kwa
kulinganisha.
k.m: kitoto, kiungwana,
Babake huongea kiungwana.
Harida hutembea kijeshi
f) Vielezi Viigizi
Vielezi hivi huigiza sauti au mlio wa kitu, kitendo kitendo kilipofanyika kwa
kutumia tanakali za sauti
k.m: tuli, chubwi, tifu, chururu
Mwanafunzi alitulia tuli mwalimu alipomzaba kofi pa!
Kaswimu aliangusha simu changaraweni tifu na kujitumbukiza majini
chubwi
g) Vielezi vya Vielezi
Vielezi hivi hutumika kuelezea kielezi kingine. Hivyo basi, hutanguliwa na
kielezi badala ya kitendo
k.m: sana, kabisa, hasa, mno
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 34
Mamake Kajino alitembea polepole sana.
Chungu kilivunjika vibaya kabisa
h) Vielezi vya Vivumishi
Hutoa habari zaidi kuhusu kivumishi
k.m: sana, kabisa, hasa, mno
Yeye ni mrefu sana
Mtoto wake ana tabia nzuri mno
VIUNGANISHI (U)
Viunganishi ni maneno yanayoutumika kuunganisha, kulinganisha au kuonesha
uhusiano wa dhana mbili au zaidi.
Aina za Viunganishi
Zifuatazo ni aina mbalimbali za viunganishi kulingana na matumizi yake
Kuonesha Umilikaji
A-Unganifu Kiatu cha Mzee Sakarani
kimepasuka.
KWA (umilikaji wa
mahali)
Mbinguni kwa kuna makao mengi.
Kujumuisha
na Baba, mama na watoto huunda familia kamili.
pamoja na Mwizi aliiba runinga pamoja na redio
fauka ya, licha Fauka ya mapigo yote, Kafa alikatakatwa kwa
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 35
ya kisu.
zaidi ya, juu
ya
Unataka nini tena zaidi ya mema yote
niliyokutendea?
pia, vilevile Alimpiga mkewe na bintiye vilevile
mbali na Mbali na hayo nitakujengea nyumba ya
kifahari.
aidha Keti akitoka shuleni atapika. Aidha atampelekea
nyanya sukuma wiki.
wala
(kukanusha)
Kutofautisha
lakini, ila Ongea nayeilausimwambie mipango yetu.
bila Tasha aliondoka bila kusema lolote.
bali Sitawaacha kama mayatima bali nitawatumia
msaidizi.
kinyume na,
tofauti na
Jana kulinyesha kinyume na utabiri wa hali ya
hewa.
ingawa,
ingawaje
Nitamtembelea ingawa sijui nitamwambia
nini.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 36
japo, ijapokuwa Nakuomba upokee nilichokileta japo ni
kidogo sana.
ilhali Fungo zimepotea ilhali zilikuwa zimewekwa
vizuri.
minghairi ya Waliendelea kutenda dhambi minghairi
ya kuhubiriwa kanisani.
dhidi ya Vita dhidi ya gonjwa hilo vingali vinaendelea.
Kuonesha Sababu
ili Hanna aliumizwa ili asikumbuke aliyoyaona.
kwa, kwa
vile
Emili alinyamaza kwa vile kugombana na
rafikize.
kwa maana,
kwa kuwa
Aria alipigwa na butwaa kwa maana mpenzi
wake aligeuka kuwa mwalimu wake.
kwani Melisa alijificha kwani hakutaka kuonekana na
Spensa.
kwa
minanjili ya
Chali alitembea mwendo huo wote kwa minanjili
ya kuongea na Katosha.
maadam Wanawake katika familia hiyo hawali
maini maadam mama mkongwe alilaani maini
katika familia hiyo.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 37
madhali Madhali sote tuko hapa, tunaweza kuanzisha
mkutano mapema
Kuonesha Matokeo
basi,
hivyo basi
Umekula ng'ombe mzima, hivyo basi huna budi
kumalizia mkia.
kwa hivyo Alipatikana na makosa ya kumnajisi bintiye, kwa
hivyo akahukumiwa miaka kumi gerezani.
ndiposa Mama Kelele alipenda kuongea
sana, ndiposa wakamkata midomo.
Kulinganisha
kama, sawa
na
Kunywa pombe ni kama kujichimbia kaburi
mwenyewe.
kulingana na Mwalimu Makunza hafanyi kazi kulingana
na maadili ya shuleni.
kuliko, zaidi
ya
Talia ni mfupi kuliko Nuru
vile Mganga Daimoni hutibu vile alivyofunzwa na
Mganga Kuzimu.
Kuonesha Kitu kimoja kama sehemu ya kingine
kati ya Vitatu kati ya vitabu hivi vimepigwa marufuku.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 38
miongoni
mwa
Miongoni mwa walioachiliwa, ni Ngiri na
Mende.
baadhi ya Baadhi ya wasichana kutoka Vikwazoni
hawaheshimu miili yao.
mojawapo Mojawapo ya maembe uliyochuma yameoza.
Kuonesha Kitu kufanyika baada ya kingine
kisha Soma mfano huu kisha usome sentensi ifuatayo.
halafu Alichukua kisu halafu akatokomea gizani.
Kuonesha Kitu kufanyika badala ya kingine
badala ya Mapepo yalimchukua Shakawa badala ya bintiye
kwa niaba ya Mama Roga alitoa hotuba kwa niaba ya mumewe.
Kuonesha Uwezekano
labda, pengine Sina pesa leo, labda uje kesho.
ama, au Ama Anita au Katosha anaweza kuja.
huenda Huenda kesho ikifika, Mungu atende miujiza.
Kuonesha Masharti
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 39
bora, muradi Sitakuuliza bora tu usichelewe.
ikiwa, iwapo Ikiwa huna jambo muhimu la kusema, nyamaza.
VIHISISHI, VIHUSISHI NA NJIA ZA KUUNDA MANENO
Vihisishi: ni sauti, neno au kikundi cha maneno kinachotamkwa na
mwanadamu kuashiria hisia tofauti kama vie furaha, huzuni, mshituko, n.k.
mfano wa vihisishi ni kama Mungu wangu!, mama wee! Mtume simama!
Kwa kawaida vihisishi ni maneno ambayo huwa hayana uhusiano wa kisarufi
na aina nyingine za maneno katika tungo. Hivyo vihisishi hujitegemea na
kujitosheleza.
Kimuundo vihisishi haviambishwi na wala havina kanuni maalumu ya
mfuatano.
Vilevile kwa vihisishi vyenye muundo wa kikundi hauwezi kubadilisha neno
moja kwa lingine hata kama yana hadhi sawa.
Kwa mfano hatuwezi kusema
*miungu yangu! (badala ya Mungu wangu!)
*baba wee! (badala ya mama wee!)
Aina za vihisishi/viingizi
Viingizi vinaweza kugawanywa kwa kutumia vigezo vya kisemantiki.
Mkabala huu unatumika kugawa viingizi kulingana na maana zinazowakilishwa
na viingizi vyenyewe.
Maana hizo ni hisia zinazobebwa na viingizi hivyo. Kutokana na hisia hizo
tunaweza kuvigawanya katika makundi ya maana zinazohusiana kwa karibu.
Kwa mtazamo huo, viingizi vinaweza kugawanywa katika makundi matatu
makuu ambayo ni:
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 40
(a) Viingizi vinavyoonesha mhemko au hisia kali:
Viingizi hivi ni vile vinavyowakilisha hisia tofauti anazokuwa nazo
mzungumzaji ambazo zinaweza kuwa nzuri au mbaya. Kundi hili la kwanza
linaweza kugawanywa katika sehemu ndogo nne kutokana na hisia
mbalimbali alizonazo mzungumzaji zinazowakilishwa na aina hii ya
viingizi ni kama ifuatavyo:
(i) Viingizi vya furaha – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya furaha
aliyonayo mzungumzaji, kwa mfano, oyaa!, oyee!, huree!, n.k.
(ii) Viingizi vya huzuni – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya masikitiko
au huzuni iliyompata mzungumzaji, kwa mfano, pole!, maskini!
Jamani!, n.k.
(iii) Viingizi vya mshangao – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya
mshangao uliompata mzungumzaji, kama vile. Eti!, salale!, ajabu!,
kumbe!, n.k.
(iv) Viingizi vya mshituko – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya
mshituko uliompata mzungumzaji, kwa mfano loo!, amaa!, aisee!,
n.k
(b) Viingizi vya maamrisho au msisitizo wa jambo au tukio:
Viingizi vya namna hii huonesha amri anayotoa mzungumzaji, kama vile
haraka!, hima!, njoo!, nenda!, n.k.
(c) Viingizi vya maadili : hivi ni vile vinavyoonesha hisia zinazohusiana na
maadili mbalimbali, yawe mema au mabaya. Aina hii ya viingizi inaweza
kugawanywa katika makundi yafuatayo:
(i) Viingizi vya mwitiko – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za
mwitiko anaokuwa nao mzungumzaji akiwa ameitwa au
anapokabiliana na jambo katika mazungumzo, kwa mfano abee!,
bee!, rabeka!, naam!, n.k.
(ii) Viingizi vya ombi – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za ombi
kwa mfano, aha!, enhe!, simile!, astaghafirullah!, hodi!, n.k.
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 41
(iii) Viingizi vya bezo – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za bezo
na dharau ya mzungumzaji, kwa mfano aka!, zii!, sasa!, n.k.
(iv) Viingizi vya kutakia heri – hivi ni vile vinavyowasilisha hisia za
mzungumzaji za kutakia heri na kupongezana, kama vile: inshaallah!,
ahsante!, hongera!, n.k.
(v) Viingizi vya kukiri jambo – hivi ni vile vinavyowasilisha hisia za
kukiri, kwa mfano; laity! Haya! Taib!, n.k.
(vi) Viingizi vya kiapo – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za kuapa
ili kuonesha mzungumzaji wa jambo fulani atalitenda au kukana
kutenda jambo, kwa mfano; wallah!
(vii) Viingizi vya salamu – hivi ni vile vinavyotumika kutoa salamu za
mzungumzaji kwa mtu mwingine wanapokutana watu wawili au
zaidi, kwa mfano; shikamoo! Marhaba! Hujambo!, n.k.
Kwa kawaida viingizi havina uhusiano wa kimuundo na maneno mengine katika
sentensi.
Huweza kuondolewa katika sentensi bila ya kuathiri muundo wa sentensi husika.
Hata hivyo, viingizi huipa sentensi dhamira/hali fulani.
VIHUSISHI
Ni maneno yanayojitokeza baada ya nomino na kufanya kazi ya kuhusisha dhana
tofauti. Umbo kuu/muhimu la kihusishi ni a-unganifu. Imeitwa a-unganifu
kutokana na namna maumbile yake ya utendaji kazi yalivyo – kwamba ni lazima
iunganishwe na mofu zinazowakilisha aina ya ngeli inayohusika mfano;
- Mtoto wa mama – wa-inahusisha mtoto na mama (ngei ya A-WA)
- Kiti cha mbao – cha – inahusisha kiti na mbao (ngeli ya KI-VI)
- Jiko la umeme – la – inahusisha jiko na umeme (ngeli ya (LI-YA)
Vilevile, kuna umbo na na kwa ambayo pia hutumika kama vihusishi ingawa yapo
pia katika kundi la viunganishi mfano;
- Ameondoka na mkoba wako
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 42
- Ameangukiwa na jiwe
- Amejikata kwa kisu
- Tutasafiri kwa ndege, n.k.
Katika kujifunza aina za maneno ni muhimu kuelewa kuwa umbo la neno halitoshi
kutambulisha aina ya neno. Unaweza ukagundua kuwa neno moja linajitokeza
katika makundi tofauti; kwa mfano neno vizuri linaweza kuwa kiwakilishi,
kivumishi au kielezi pia, neno kulala linaweza kuwa nomino au kitenzi.
Halikadhalika neno Juma linaweza kuwa nomino au kivumishi. Hivyo ambo la
msingi ni kuangalia kazi na nafasi ambayo neno hilo huchukua katika tungo.
UUNDAJI WA MANENO (NJIA ZA UUNDAJI WA MANENO)
Uundaji wa maneno ni mchakato unaowezesha lugha kujiongezea msamiati ili
kukidhi haja ya mawasiliano na kuendana na mabadiliko yanayotokea kila siku.
Maneno ya lugha ya Kiswahili hayaundwi kiholela bali hufuata taratibu na kanuni
zinazokubalika kitaalamu.
Njia zitumikazo kuunda maneno ni kama zifuatazo:
Unyambuaji
Njia hii inatumia mzizi mmoja wa neno na kuzalisha maneno mapya kwa
kupachika viambishi nyambuaji
Mfano
Soma
Somo
Kisomo
Msomi
Msomaji
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 43
Lima
Mkulima
Kilimo
Mlimaji
Uambatishaji/mwambatano
Hii ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuambatanisha maneno mawili.
Mfano
Mwana+chama - Mwanachama
Askari+kanzu - Askarikanzu
Bwana+shamba – Bwanashamba
Urudufishaji / Uradidi
Hii ni mbinu ya kurudiarudia neno au sehemu ya neno na kuunda neno jipya
ambalo huwa na maana tofauti na maneno yanayorudiwarudiwa.
Mfano
(d) Pole : polepole
(e) Sawa : sawasawa
(f) Haraka : harakaharaka
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 44
Akronimu/ufupishaji
Ufupishaji ni njia mojawapo ya kuundia maneno mapya,ufupishaji huweza
kufanyika kwa namna mbili ambazo ni.
Kufupisha kwa kuchukua herufi za mwanzo Mfano
CWT (Chama cha Walimu Tanzania) VVU (Virusi Vya Ukimwi)
Kufupisha kwa kuchukua silabi za mwanzo za maneno yanayo fupishwa
Mfano
BAKITA (Baraza la Kiswahili la Taifa)
TUKI (Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili)
TATAKI (Taasisi ya Taaluma za Kiswahili)
Uhulutishaji
Ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuchukua vijisehemu vya neno pasipo
kufuata kanuni yoyote.
Mfano
Mnyama mfu – nyamafu
chakula cha jioni – chajio
hati za kukataza – hataza
Mtu asiye kwao - msikwao
Utohoaji
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 45
Ni uchukuaji wa maneno toka lugha moja na kuyatumia kwenye lugha nyingine
baada ya kuyarekebisha kimatamshi na kimaandishi ili yaendane na sarufi ya lugha
inayotohoa.
Mfano
Neno Lugha asilia Kiswahili
Shirt Kiingereza Shati
Schule Kijerumani Shule
Bakura Kiarabu Bakora
Benjera Kireno Bendera
Matching Kiingereza machinga
guys
Kuchukua
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 46
Hii ni mbinu ya kuongenza maneno kwa kuyachukua toka lugha yake na
kuyatumia kama yalivyo. Uchukuaji hufanyika kwa lugha zinazoendana kisarufi
kama Kiswahili na lugha za kibantu.
Mfano
Kitivo — kisambaa /kipare
Ikulu - kinyamwezi
Kigoda - kizaramo
Kubadili mpangilio wa fonimu
Mfano
Lima – mila – imla - mali
Kufananisha umbo /sauti /tabia
Mfano
Kufananisha umbo
- kifaru-(mnyama faru)
- mkono wa tembo-(mkonga wa tembo)
- kidole tumbo-(umbo la kidole)
Kufananisha Tabia
Ubeberu-(beberu la mbuzi)
Ukupe-(mdudu kupe)
Kufananisha Sauti
Pikipiki (mlio wa pikipiki)
Mtutu (mlio wa bunduki)
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 47
Nyau (mlio wa paka)
Kuku - kokoriko (mlio wa kuku)
Njia ya udondoshaji
Mfano
mkwe wake - mkwewe
mwana wake - mwanawe
ndugu yake – nduguye
Kuzingatia matumizi ya kitu
Mfano
Banio - (kubana)
Chanio - (kuchana)
Fyekeo - (kufyeka)
Kutarjumi/kutafsiri
Mfano;
Fluid – (ugiligili)
Acquired immunal deficiency syndrome (Upungufu wa kinga mwilini)
Human immunal virus – (virusi vya ukimwi)
Anti-rentro-virus - (dawa za kufubaza makali ya ukimwi)
DHANA YA MOFOFONOLOJIA NA MOFOSINTAKSIA
Maana ya Mofofonolojia
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 48
Ni taaluma inayoshughulikia uchanganuzi na uainishaji wa vipengele vya
kifonolojia vinavyoathiri maumbo ya mofimu katika mfuatano wake.
Mofofonolojia huzalisha kanuni ambazo zinaelezea mazingira ya utokeaji wa
mofu na alomofu zake.
Kanuni hizi huelezea maathiriano ya kifonolojia yanayoathiri mofolojia ya
maneno na jinsi badiliko la kimofofonolojia la neno linavyoelezeka kikanuni.
Kanuni hizi husaidia kujua jinsi maneno yanavyobadilika toka muundo ndani
wa neno hadi muundo nje wa neno.
Kanuni za kimofofonolojia hutawaliwa na sifa zifuatazo
1. Kanuni za kifonolojia hazina vighairi mfano; hakuna vighairi katika kanuni ya
kifonolojia isemayo mkazo katika Kiswahili huwekwa silabi ya pili kutoka
mwishoni mwa neno.
2. Kanuni za kimofofonolojia huwa na vighairi vingi; Kanuni hii huhusu lugha
mahususi na hutumika katika baadhi ya mofimu tu kwa mfano katika mofu ya
utendea.
mfano
piga>
pigia
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 49
panga> pangia
funga> fungia
tenga> tengea
choma> chomea
//utendea//----->i/-mz+[a,i,u]
------->e/-mz+[e,o]
AINA ZA KANUNI ZA KIMOFOFONOLOJIA
1. Kanuni ya usilimisho
Kanuni hii inahusu maathiriano ya mofimu zinazofuatana. Maathiriano hayo
huzifanya mofimu zifanane zaidi kuliko zikiwa pekee.
Mfano(1)
a) n+goma----->{ngoma}
b) n+dizi------>{ndizi}
c) n+buzi----->{mbuzi}
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 50
d) n+bingu----->{mbingu}
n------>m/-k
Huu ni usilimisho wa nazali inayofuatwa na konsonanti
a) n+refu----->{ndefu}
b) n+limi---->{ndimi}
r------>d/n-
l------->d/n-
Huo ni usilimisho wa konsonanti inayotanguliwa na nazali(N)
2. Ukaakaishaji
Haya ni maathiriano ambayo sauti isiyo ya kaakaa gumu hulazimishwa kuwa
sauti ya kaakaa gumu.
Mfano
a) ki+ama------->chama
b) ki+ombo------->chombo
c) ki+uma-------->chuma
d) ki+eo------>cheo
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 51
3. Udondoshaji
Mofimu hudondoshwa kutokana na mfuatano wa mofimu unaoleta maathiriano
Mfano
a) wanasoma –hawasomi
b) anasoma-hasomi
c) nilikunywa-sikunywa //njeo// -------> θ/-ukanushi
4. Tangamano la irabu
Ni utaratibu wa irabu moja kukubali kuandamana na irabu nyingine katika
mazingira maalumu. Kwa kawaida irabu iliyo katika mzizi huathiri utokeaji wa
irabu ya mnyambuliko. Hivyo ikiwa irabu ya mzizi ni a,i au u irabu ya
mnyambuliko huwa i na ikiwa irabu ya mzizi ni e au o basi irabu ya
mnyambuliko huwa e.
Mfano
Panga ----- pangia
Funga …. Fungia
Piga ……pigia
Choma …..chomea
Sema …… semea
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 52
5. Mvutano wa irabu
Ni hali inayojitokeza wakati irabu ya juu na irabu ya chini zinapofuatana katika
neno. Irabu hizo huvutana na kusababisha kutokea kwa irabu isiyo ya juu wala
chini. Mfano,
ma+ino = meno
wa+ingi = wengi
ma+ingine = mengine
6. Uyeyushaji
Ni kitendo cha kubadili irabu kuwa nusu –irabu au kiyeyusho. Hali hii hutokea
wakati irabu mbili zinapokutana mfano; irabu – u hubadilika na kuwa
kiyeyusho /w/ inapokaribiana na a au i (mu+alimu=mwalimu, mu+imbaji =
mwimbaji) na irabu -i- hubadilika na kuwa kiyeyusho /y/ inapokaribiana na
irabu a, o au u (vi+ama= vyama, vi+ombo = vyombo, vi+uma = vyuma)
7. Vighairi
Ni mofimu au maneno yanayokiuka kanuni za kawaida za lugha husika. Mfano;
Kiatu………… viatu
Kisu……………visu
Choo ………….vyoo
Chama ………..vyama
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 53
Nomino choo, vyoo, chama, vyama ni vighairi kwa sababu yanaingia ngeli ya
KI-VI lakini hayabebi viambishi husika mwanzoni.
D11/9/2018HANA YA MOFOSINTAKSIA
Ni taaluma inayoshughulikia uchanganuzi na uainishaji wa vipengele vya
kisintaksia vinavyoathiri maumbo ya mofimu katika mfuatano wake.
Vipengele vya kisintaksia vinavyoathiri mofolojia ni:
(a) Umoja na wingi: maneno mengi ya Kiswahili huwa na maumbo tofauti
yanapokuwa katika hali ya umoja na yanapokuwa katika hali ya wingi.
Mfano
Umoja Wingi
Kidole vidole
Ungo nyungo
Jicho macho
Kwa kuangalia mifano ya hapo juu tunaona kuwa wingi wa kitu kinachotajwa ni
kilekile, mabadiliko ya maumbo hutokea kuingana na idadi ya kitajwa. Maneno
mengi tu ya Kiswahili huwa na tabia hii lakini sio yote. Hii ina maana kwamba
baadhi ya maneno hubaki kama yalivyo (hayabadiliki) ikiwa yapo katika umoja au
katika wingi. Mfano wa maneno hayo ni sabuni, njia, nguo, nyumba, zawadi, n.k.
(b) Njeo: katika Kiswahili kuna viambishi mbalimbali vinavyotumiwa
kuwakilisha njeo. Hivyo basi, kadiri mzungumzaji anavyofikiria dhana
Mofolojia ya Kiswahili 2018
Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 54
ya wakati fulani katika mazungumzo yake ndipo umbo la neno
linapobadilika kulingana na wakati huo. Mfano;
analima,atalima,amelima,alilima (na – wakati uliopo, ta – wakati ujao,
me – wakati uliopita timilifu, li – wakati uliopita)
(c) Ukanushi : dhana ingine ya kisintaksia inayosababisha umbo la neno
kubadilika ni ukanushi. Angalia mifano ifuatayo:
A B
Uyakinishi Ukanushi
Anapika ……………. hapiki
Amepika …………… hajapika
Alipika …………….. hakupika
Atapika …………….. hatapika
Mifano hiyo inaonesha kwamba kutokana na kuwepo kwa mofimu ha ya ukanushi
katika maneno ya jozi B maumbo yanayowakilisha wakati yamebadilika. Umbo na
la wakati uliopo halionekani katika nafasi yake badala yake kuna umbo i mwishoni
mwa kitenzi, wakati uliopita (muda mfupi) unawakilishwa na ja badala ya me na
wakati uliopita unawakilishwa na ku badala ya li. Umbo linalowakilisha wakati
ujao pekee ndilo lisiloathiriwa na mabadiliko haya.
(d)