329
Nakala ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA ________________ MAJADILIANO YA BUNGE _____________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Ishirini na Moja Tarehe 29 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na :- NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. AIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. CAPT. JOHN D. KOMBA K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. JEROME D. BWANAUSI K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA MADINI: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014

Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIAparliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458121631-HS...AIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi

  • Upload
    others

  • View
    9

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    1

    BUNGE LA TANZANIA

    ________________

    MAJADILIANO YA BUNGE

    _____________________

    MKUTANO WA KUMI NA TANO

    Kikao cha Ishirini na Moja – Tarehe 29 Mei, 2014

    (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi)

    D U A

    Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua

    HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI

    Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na :-

    NAIBU WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO:

    Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari,

    Vijana, Utamaduni na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

    AIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI:

    Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na

    Madini kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

    MHE. CAPT. JOHN D. KOMBA K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA

    MAENDELEO YA JAMII:

    Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu

    Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

    kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya

    Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

    MHE. JEROME D. BWANAUSI K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA NISHATI NA

    MADINI:

    Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini Kuhusu Utekelezaji

    wa Majukumu ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    2

    na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo

    kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

    MHE. MOSES J. MACHALI (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI

    KWA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO):

    Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, kwa Wizara ya Habari,

    Vijana, Utamaduni na Michezo Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya

    Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

    MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMED (K.n.y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA

    UPINZANI KWA WIZARA YA NISHATI NA MADINI):

    Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, kwa Wizara ya Nishati na

    Madini Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka

    wa Fedha 2014/2015.

    MASWALI KWA WAZIRI MKUU

    SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, leo ni maswali kwa Waziri Mkuu bahati

    ninamwona Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, kama ilivyo kwa mujibu wa Kanuni

    zetu yeye ndiye atakayeanza kumwuliza Maswali Waziri Mkuu.

    Mheshimiwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

    MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa

    nafasi ya kumwuliza Mheshimiwa Waziri Mkuu Maswali. Mheshimiwa Waziri

    Mkuu, wakati unahitimisha hoja ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, ulitanabaHisha

    kwamba, uchaguzi wa Serikali za Mitaa utafanyika kama ilivyo kawaida mwisho

    wa mwaka huu 2014.

    Vilevile, ulilifahamisha Taifa kwamba, wakati huo huo zoezi la uandikishaji

    wapiga kura katika utaratibu mpya wa biometric utakuwa unatumika.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa uzoefu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    Mwaka 2004 na zaidi Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2009 ambao

    ulisimamiwa na Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura ya 287 na Sheria ya Serikali za

    Miji, Sura ya 288, Uchaguzi huu uligubikwa na vurugu nyingi sana.

    Pia uliishawahi kutoa kauli huko nyuma kwamba, Serikali itaangalia upya

    sheria ile ili pengine kuifanyia marekebisho ya msingi kabla ya uchaguzi wa

    mwaka huu 2014 ili matatizo yale yasijirudie tena.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    3

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, ni miezi michache imebakia kabla ya Uchaguzi

    huo. Unaliambia nini Taifa kuhusu maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

    na Vijiji mwisho wa mwaka huu? (Makofi)

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba tu kueleza kwa ufupi kwamba,

    mambo ambayo tumeishaanza kuyafanyia kazi; kwanza ni maandalizi tu ya

    kibajeti ambayo tulizungumza wakati wa kuhitimisha Bajeti ya Waziri Mkuu.

    Pili, huwa tunakuwa na utaratibu wa kushirikisha wadau wote wakati wa

    kuandaa Kanuni ambazo tunafikiria zinaweza zikasaidia katika kusimamia vizuri

    zoezi hili. Kwa hiyo, nalo tumeishaanza kuliangalia kwa maana ya kutafuta

    Kanuni za mara ya mwisho turekebishe mahali gani ili tuweze kwenda vizuri.

    Mheshimiwa Spika, tatu ni hili ambalo amelieleza. Ni kweli kwamba tulitoa

    hiyo kauli na tumeishaomba watu wa TAMISEMI waangalie kama kuna maeneo

    hasa ambayo tunafikiria pengine yangeweza kufanyiwa marekebisho kabla ya

    Uchaguzi Mkuu. Sasa kama yatabainika basi tutaleta hiyo rai mbele yetu.

    Wakati huo huo labda niseme tu kwamba, kwa sababu na ninyi ni wadau

    wakubwa kwa maana ya vyama vya Upinzani, ni rai yangu tu kwamba na ninyi

    mngeanza kulitazama vilevile kama kuna maeneo ambayo mnafikiria

    yangeweza kupendekezwa ili na yenyewe tuweze kuyachukua wakati

    tunajaribu kutazama na sisi upande wetu, tutashukuru vilevile. (Makofi)

    MHE. FREEMAN A. MBOWE: Mheshimiwa Waziri Mkuu, nakushukuru kwa

    majibu yako ya awali.

    Ni kweli sisi kama wadau muhimu yako maeneo mengi sana ambayo

    yanalalamikiwa katika Kanuni hizi ambazo mara ya mwisho zilitungwa mwaka

    2009 na ni dhahiri tutatoa mapendekezo mengi tu ya mabadiliko katika Kanuni

    hizi ili kuufanya uchaguzi huu uwe huru na amani zaidi.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, hata hivyo, tatizo hapa siyo mapendekezo yetu,

    ila ni utayari wenu wa kukubali mapendekezo ambayo wadau watayatoa, kwa

    sababu tukikumbuka katika uchaguzi wa mwaka 2009 yako mapendekezo

    kadha wa kadha ambayo yalitolewa kwa Serikali lakini ikayapuuza na matokeo

    yake uchaguzi ule ukaghubikwa na vurugu nyingi.

    Sasa badala ya kusubiri wadau wapendekeze bila utaratibu

    unaoeleweka unaonaje kama leo utalipa Taifa taarifa kwamba, unakusudia

    kuita kikao cha wadau mapema sana ili mambo haya yajadiliwe mapema

    kabla hujafika hatua ya kumaliza Kanuni wewe na TAMISEMI ambao ni

    washindani katika zoezi hili? (Makofi)

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    4

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, mnaweza vilevile mkawa na Kanuni

    nzuri sana, lakini kama watu wenyewe ambao tunahusika na zoezi dhamira zetu

    nazo si nzuri, bado hiyo haiwezi kuwa ni tiba. (Makofi)

    Kwa hiyo, nadhani rai ya msingi hapa ni kwamba, sisi wote ambao ni

    washirika wakubwa katika zoezi hili pande zote mbili; upande wa Chama cha

    Mapinduzi, upande wa vyama vya Upinzani tufike mahali tuone kwamba,

    jambo hili ni letu wote na pale ambapo hapastahili kuwa na vurugu hakuna

    sababu ya kuwa na vurugu, vinginevyo nadhani rai yako kwangu haina tatizo

    hata kidogo.

    Tutajitahidi kuona wakati mwafaka, na hata ikibidi pengine kuanza na

    mawasiliano formal hivi, brain storming ya Kanuni zenyewe kwa ujumla wake

    halafu baadaye twende katika hatua sasa ya kuona ni maeneo gani ambayo

    tunafikiri tunaweza tukayafanya.

    Tutajitahidi kupitia TAMISEMI tuone wakati ambao tungeweza tukafanya

    hilo zoezi. (Makofi)

    SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kumjibu Kiongozi wa

    Kambi ya Upinzani. Ninatamani wote walioamka asubuhi wamalizike na

    inawezekana tu kama maswali yetu yatakuwa mafupi na hoja zetu fupi na

    zingine siyo lazima ku- repeat. Kwa hiyo, ninaanza na Mheshimiwa Murtaza

    Mangungu.

    MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, mwaka 1997 Serikali ilichukua uamuzi wa

    kuvunja Jiji la Dar es Salaam na liliendeshwa na Tume baadaye yakaja

    mapendekezo ya uanzishwaji wa Manispaa za Kinondoni, Ilala na Temeke. Hivi

    sasa kuna mkanganyiko mkubwa sana kwenye utekelezaji wa maamuzi kati ya

    Halmashauri hizo na Jiji.

    Je, ni lini Serikali itachukua uamuzi wa kuondoa mkanganyiko huu na

    kuweka mfumo ambao utasaidia kutekeleza majukumu ya Manispaa hizi kama

    inavyotakiwa? (Makofi)

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ni kweli suala la mfumo au muundo wa

    Jiji na uhusiano wake na manispaa zile tatu kwa muda mrefu limekuwa ni tatizo

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    5

    ambalo linajitokeza mara kwa mara na ndiyo maana Serikali kwa nyakati

    imejaribu kuona ni muundo gani pengine ungeweza ukafaa.

    Mtakumbuka mara ya mwisho tulijaribu lakini yale mapendekezo bado

    hayakuweza kutatua lile tatizo na tukalazimika kurejea tena kwenye utaratibu

    huu wa sasa.

    Mheshimiwa Spika, sasa nafikiri ushauri wangu ingekuwa, tuombe

    Manispaa zile tatu ambazo ndiyo wadau wakubwa, pamoja na Jiji lenyewe

    pengine mngekuwa ndiyo chanzo cha kuibua fikra ambazo mnadhani

    zinaweza zikafaa kwa ajili ya muundo wa Jiji la Dar es Salaam.

    Mnaweza mkafanya hivyo, kwa kujaribu kutengeneza timu kwanza ya

    Wataalam, baadaye mkajaribu kutengeneza timu ya Madiwani lakini wa

    maeneo yote, lakini mtumie na uzoefu pengine wa maeneo mengine duniani

    kuona mifumo ya miji au majiji yalivyo na kuweza kuona ni namna gani nzuri

    tunaweza tukajaribu kuitumia hapa Dar es Salaam.

    Nadhani tukifanya hilo pengine litakuwa mwanzo mzuri kwa sababu ninyi

    ndiyo wadau wakubwa, badala ya kuanzia juu na kushuka chini. Tuanzie chini ili

    tuyalete juu tuone baadaye kama litakubalika. (Makofi)

    SPIKA: Mheshimiwa Mangungu swali la pili, fupi kabisa.

    MHE. MURTAZA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Waziri Mkuu, nakushukuru

    sana kwa majibu mazuri yenye matumaini. Ningependa tu kujua kwamba, uko

    tayari kusimamia mwongozo na usimamizi wa jambo hili kwa maana hizo

    zitakuwa ni mamlaka ambazo mpaka sasa zinasuguana kama tunavyoona Jiji

    la Dar es Salaam linazidi kuwa chafu, mifereji ya maji machafu imefurika, kila

    mamlaka inasema hili ni jukumu la mwingine.

    Sasa kwa kipindi hiki cha mpito. Je, unatoa agizo gani na utayari wako

    wa kiasi gani kuweze kuzikutanisha mamlaka hizi na kulisimamia hili jambo chini

    ya ofisi yako?

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ofisi yangu ndiyo kiongozi wa shughuli

    zote za Serikali za Mitaa, ndiyo maana ninalisema hili kwa sababu Manispaa hizi

    ziko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Jiji lenyewe liko chini ya Ofisi Waziri Mkuu.

    Rai yangu ya msingi ni hiyo tu kwamba, tulianzishe kule chini ili muweze

    kubainisha maeneo ambayo mnayatazama kwamba, kwanza ni tatizo katika

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    6

    utekelezaji, tatizo kimfumo na kimuundo, yapande juu baada ya mjadala

    mpana kwenye mabaraza yote pamoja na Jiji lenyewe kama tunavyofanya

    tunapoanzisha maeneo mapya popote pale.

    Mheshimiwa Spika, mimi natamani hili lifanyike zaidi na pengine hata

    wadau nje kabisa ya mabaraza haya ili kuweze kuwa na ushiriki mpana zaidi

    tuweze kuona namna gani tutaweza kulifanya hili jambo.

    Sisi ofisi yetu na TAMISEMI kwa ujumla bado tutakuwa ndiyo wasimamizi

    pale mtakapokuwa mmeonesha nia hiyo na namna ambavyo mngependa

    zoezi hili liendelee.

    MHE. ENG. MOHAMED HABIB JUMA MNYAA: Mheshimiwa Spika, nashukuru

    kunipa nafasi ya kumwuliza swali Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye sijamwuliza

    swali muda mrefu sana.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, tunaelewa kwamba, nchi nyingi duniani

    zinakopa na sisi Tanzania hatuna budi kukopa kwa Maendeleo yetu. Hata hivyo,

    kumekuwepo na trend katika kipindi kirefu sasa kukopa na inaonekana miradi

    yote mikubwa tunakopa kutoka Exim Bank ya China. Sababu hizo zinajulikana

    kwa sababu ya unafuu wa riba, masharti na urafiki tulionao na China.

    Nini hatima ya nchi yetu ukizingatia kwamba, huko nyuma kuna mikopo

    mingi tumeshindwa kulipa ikabidi tusamehewe na ukitazama pia na siasa au

    msimamo wetu wa kutofungana na upande wowote?

    Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Ndugu yangu

    Mheshimiwa Mnyaa, ingawa swali lake kidogo nadhani hakulitafiti tafiti sana.

    Ungelifanyia utafiti ungembana Waziri Mkuu vizuri sana.

    Iko sheria ambayo inasimamia suala zima la ukopaji pamoja na madeni.

    Sheria ile ndiyo inaisaidia Serikali muda wote kuzingatia yale ambayo

    yanastahili.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    7

    Ni kweli nyuma tulikopa, pia ni kweli kwamba mikopo ile ni mikubwa lakini

    zoezi lile lililoendeshwa na vyombo vya Kimataifa lilikuwa ni zoezi la jumla katika

    kujaribu kusaidia hizi nchi maskini kuziondolea mzigo wa kuja kulipa madeni

    hayo baadaye ali mradi ukidhi vigezo fulani. Tanzania tulikidhi na ndiyo maana

    tukapata ule msamaha, ulikuwa ni wa jumla na siyo sisi tu, nchi nyingi zilipata

    hiyo nafuu.

    Kwa hiyo, basi nataka nikuhakikishie tu kwamba, mimi kama Kiongozi wa

    Shughuli za Serikali, faraja niliyo nayo ni moja tu kwamba, kwa vigezo vyote sisi

    kama nchi bado tuna sifa nzuri sana ya kuendelea kukopa kwa sababu uwezo

    huo wa kuweza kulipa haujakiuka yale masharti ya msingi kwa mujibu wa sheria

    hiyo.

    MHE. ENG. MOHAMED HABIB JUMA MNYAA: Mheshimiwa Spika, nashukuru

    kwa jibu hilo zuri la Mheshimiwa Waziri Mkuu.

    Nitakuwa na swali moja tu dogo kwamba, uzoefu tulionao Tanzania

    katika miradi ambayo imetekelezwa kwa msaada wa Ndugu zetu wa China

    huko nyuma, iwe ya viwanda, hospitali na miradi mingine ya kijamii. Mifano iko

    ya TAZARA, URAFIKI, hospitali kule Zanzibar, Kiwanda cha Sukari Zanzibar na

    kadhalika.

    Baada ya muda kumalizika na wao kuondoka, miradi hii tukaachiwa

    wenyewe utakuta miradi hii mingi imetupatia na kuleta taabu, na mingine

    imetushinda. Pamoja na sababu zetu za kiutawala katika kuendesha hiyo miradi

    lakini kuna sababu za standardization ya zile mashine au materials, iwe umeme

    au mashine nyingine.

    Tumejiandaa vipi sasa na hii miradi yote ambayo tunakopeshwa na

    inajengwa kwa msaada wa China (fedha au materials zinazotoka China) ili ziwe

    sustainable baadaye baada ya kutuachia wenyewe? Tanzania tunajiandaa

    vipi?

    SPIKA: Bahati yako, karibu niseme ni swali jipya. Mheshimiwa Waziri Mkuu!

    (Makofi/Kicheko)

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ni dhahiri swali ni pana sana, lakini

    labda tutumie mifano michache tu, maana hapa nadhani anazungumza

    mikopo ya China.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    8

    Nichukue kwa mfano ujenzi wa bomba la Gesi kutoka Mtwara kwa

    sababu ule mkopo ni mkubwa. Tulichofanya katika zoezi hili wakati huu

    tunaendelea kujenga hilo bomba, of course tutakuwa na vijana ambao

    tumewaajiri mle. Watabakia na sehemu ya uwezo wa kuweza kusaidia

    kuelewa mambo yale madogo madogo ambayo yanaweza kujitokeza katika

    usimamizi wa bomba hilo.

    Lakini kupitia Nishati na Madini, tumeagiza vilevile kwamba mradi huu ni

    mkubwa sana na bomba hili litahitaji kusimamiwa vizuri. Ni vizuri katika wale

    vijana ambao tumepata fursa ya kuwapeleka nje kwenda kujifunza mambo

    mbalimbali kuhusu gesi moja ya eneo ambalo tulipe umuhimu mkubwa ni

    namna tunavyoweza kusimamia suala zima la mkopo huu unaotuwezesha

    kuwa na gesi kutumia bomba la Mtwara.

    Hivyo itatusaidia vile vile kwenye mabomba mengine ambayo

    yatajitokeza kwa sababu bomba hili haliishii Dar es Salaam tuna ndoto za

    kwenda Kaskazini, kwenda hata mpaka Kanda ya Ziwa. Kwa hiyo ni lazima

    tuwe na wataalamu watakaotuwezesha kusimamia jambo hili vizuri. Hili tunalo

    na tumeshaliingiza katika utaratibu wa kuanza kutoa mafunzo kwa vijana.

    (Makofi)

    SPIKA: Naomba tuendelee na Mheshimiwa Assumpter Mshama.

    MHE. ASSUMPTER N. MSHAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa

    kunipatia nafasi ili nimwulize Mheshimiwa Waziri Mkuu swali moja.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, kumekuweko mgogoro mkubwa sana katika

    maeneo ya ardhi hasa maeneo ambayo yamegawiwa kwa wawekezaji.

    Katika Tanzania nzima ikiwemo na Misenyi wananchi walikuwa wanamiliki

    maeneo yao lakini NARCO ikaamua kuuza hayo maeneo kwa wawekezaji.

    Lakini wawekezaji wengine wamechukua maeneo makubwa kuliko

    mahitaji yao na matokeo yake wameacha Watanzania wengi wakihangaika

    hawana mahali pa kulishia wanyama wao na ardhi yao imechukuliwa bila

    utaratibu wowote na wakauziana watu ndani ya vitalu vile.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa kuwa wewe ndio msimamizi wa mambo

    yote ya Serikali hili suala kwa Wizara ya Ardhi limeshindikana unaonaje ukiingilia

    kati zikafutwa zile hati wananchi wakarudishiwa maeneo yao na matokeo yake

    tukapata amani katika Taifa letu.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba maelezo yako.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    9

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ni kweli analolisema Mheshimiwa

    Assumpter Mshama kwamba pale Kagera tunayo maeneo ambayo ni

    mashamba ambayo zamani yalikuwa yanamilikiwa na NARCO na baadaye

    tukayatengenezea utaratibu ambao tulifikiri ungejibu haja ya Serikali ya

    kuendeleza ufugaji wa kisasa katika maeneo hayo na kwa njia hiyo tuweze

    kuboresha mifugo yetu.

    Lakini ni kweli vilevile kwamba uamuzi ule na utekelezaji wake havikuenda

    kama tulivyokuwa tumetarajia. Kwa hiyo tulichofanya Serikalini nimeagiza

    Wizara kadhaa ambazo sekta hizo zinahusiana kwa karibu sana.

    Tupitie kwenye maeneo yote ya mashamba ya NARCO kuweza kubaini

    matatizo kwa kila shamba na tuone ni maeneo yapi kwa kweli yanaweza

    yakaondolewa katika utaratibu ule. Pengine tukawapa wakulima au wafugaji

    kama watakuwepo wafugaji wadogo maana lengo ilikuwa ni kuyatumia kwa

    ajili ya kuboresha mifugo.

    Sasa ndani yake ofcourse ipo Wizara ya Kilimo, Ardhi, watu wetu wa

    TAMISEMI, tumeweka Maliasili na Utalii vilevile kwa sababu hawa wanahusiana

    kuna maeneo mengine ambapo tutahitaji utaalamu wao kidogo.

    Kwa hiyo, hiyo timu tunafikiri itakapomaliza hilo zoezi nadhani inaweza

    ikanisaidia kuweza kushauri au kumshauri Mheshimiwa Rais vizuri zaidi juu ya

    jambo hili.

    SPIKA: Mheshimiwa Mshama kwa kifupi sana.

    MHE. ASSUMPTER N. MSHAMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

    Inawezekana labda Mheshimiwa Waziri Mkuu hawakuambii ukweli, kwa sababu

    mpaka sasa hivi kwetu zimekuwepo Kamati zaidi ya saba na moja nilikuwemo

    mle na uamuzi Waziri wa Mifugo mwaka jana alituambia kwamba wameamua

    sasa kurudisha vitalu.

    Je, lini utawaambia wananchi hasa wa Misenyi kwamba sasa ni mwisho

    na sasa tunakwenda kwenye utaratibu huu?

    WAZIRI MKUU: Ziko efforts za Wizara inayohusika. Mimi ninachokisema

    hapa nimepanua tu hili wazo, sababu tatizo hili si Kagera tu, mashamba ya

    NAFCO yako sehemu mbali mbali, ndiyo maana tukasema tusiiachie Wizara hii

    peke yake tuhusishe na Wizara nyingine ili baadaye tuweze kuwa na kauli

    pamoja kwa sababu TAMISEMI wanahusika sana.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    10

    Kama hawatakuwa sehemu ya uamuzi kesho na kesho kutwa TAMISEMI

    wanaweza wakajikuta tena kupitia Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya

    hawaelewi kinachoendelea ni nini.

    Kwa hiyo, nataka nikuhakikishie tu kwamba zile jitihada za Wizara kwenye

    maeneo ambayo tayari walikuwa wameanza hatukuziingilia sisi lakini tumetaka

    tupanue zoezi sasa tuweze kuchukua maeneo yote ya NARCO kwa upana

    wake na tuone namna tunavyoweza kuwasaidia. (Makofi)

    MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMED: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri

    Mkuu, suala langu haliko mbali sana na suala ambalo ameliuliza Mheshimiwa

    Assumpter Mshama, ila mimi nitazungumzia zaidi katika madhaifu katika

    usimamizi wa rasilimali za Taifa hasa nikizingatia uhifadhi wa mazingira.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu Tanzania ina eneo la misitu ambalo halipungui

    ekari milioni 33 na wastani wa ukataji miti ndani ya nchi yetu kwa mwaka

    haupungui ekari 403,000.

    Mheshimiwa Waziti Mkuu, na ukataji huu wa miti ndio ambao

    unasababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira. Wakataji hawa mara nyingi

    wanakuwa ni wakataji haramu au huwa hawafanyi kutokana na mipango

    ambayo imewekwa na Serikali. Naomba tu kutoka kwako Mheshimiwa Waziri

    Mkuu, kauli ya Serikali juu ya ukataji huu mkubwa wa miti nchini.

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, ukataji wa miti au misitu hapa nchini ni

    kweli ni tatizo na lipo. Lakini lazima vilevile tukubali kwamba hiyo ni changamoto

    ambayo lazima tuijibu kwa kutumia mbinu mbalimbali.

    Nitoe mfano tu wananchi wetu wengi vijijini wengi wanatumia nishati ya

    kuni na baadhi ya makabila wanapenda kukata miti hii kabla hata haijakauka

    anaikausha baada ya kukata ili aweze kujiandaa vizuri. Ni ukataji haramu kama

    unavyosema, lakini ni ukataji ambao haukwepeki katika mazingira ya sasa kwa

    sababu nishati ile kwa mwananchi yule ni ya lazima.

    Lakini uko ukataji miti ambao unatokana na matumizi ya mbao na hapo

    unaweza ukachukua mifano ya shule zote ulizojenga, zahanati zote ulizojenga,

    nyumba zote tunazojenga zote tunatumia miti. Ni ukataji ambao kwa upande

    mwingine haukwepeki.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    11

    Madawati yote wanayokalia watoto wetu yote ni mbao ambazo

    zimetokana na miti. Unaweza ukauita ukataja haramu lakini bado changamoto

    yake ni lazima itafutiwe njia mbadala ya namna ya kushughulika na jambo hili.

    Kwa hiyo kwa ufupi nataka kusema nini, nakubali kwamba changamoto

    ipo lakini nadhani kama Serikali na sisi wote kama wadau wakubwa wa tatizo

    hili ni lazima tuweke vichwa pamoja tuone namna gani tutashughulikia jambo

    hili.

    Moja tamaa niliyonayo ni kwamba pengine gesi hii ambayo Mwenyezi

    Mungu ametujalia tuone namna tutakavyoitumia kikamilifu ili sisi wote wakazi

    wa mijini kwanza maana ndio watumiaji wakubwa sana wa mkaa tuondokane

    na matumizi ya mkaa tuingie katika matumizi ya gesi tutakuwa tumepunguza

    sana ile sulubu ya sasa ya mkaa kuja mijini.

    Lakini ukifanya hivyo peke yake bado haisaidii ndiyo juhudi za Serikali ni

    kujaribu kutumia kila aina ya mbinu. Kuna matumizi ya majiko banifu katika

    jitihada za kujaribu kupunguza matumizi ya ukataji wa miti vijijini.

    Lakini nadhani tunakokwenda kama nchi zingine zilivyofanya nyingi ni

    lazima vilevile gesi hii tuitafutie utaratibu wa kuweza kuifikisha mpaka kwenye

    maeneo yale ambayo sasa yanakuwa kimiji ili na yenyewe kutusaidia kuzidi

    kupunguza jambo hili.

    Lakini mwisho kwa ujumla ni elimu, tunahitaji elimu kubwa kwa

    Watanzania kwa sababu wengine wanakata wakati mwingine hana sababu

    anaona tu limti linamkera tu. Wakati mwingine watu wanakata kwa sababu

    wanataka mifugo ipite sehemu ambako akiona anaona ng‟ombe badala ya

    kuona miti anachohitaji huyu mtu ni elimu tu.

    Kwa hiyo kwa ujumla nadhani tutahitaji interventions au njia mbalimbali

    kuweza kujaribu kutatua hili tatizo ambalo kimsingi ni kubwa sana.

    MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante pamoja

    na majibu ambayo Mheshimiwa Waziri Mkuu amenipa ambayo kwa kweli ni

    mazuri.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    12

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, hata hivyo ni asilimia nne (4) tu ya ekta hizo

    ambazo nimezitaja ndani ya nchi yetu ambazo zimewekewa mipango mizuri ya

    matumizi. Asilimia 96 bado Serikali haijaweka msimamo mzuri wa matumizi ya

    eneo hili na hii ndiyo inayosababisha hata hivi vita ambavyo sasa hivi tunaviona

    vya wafugaji kuingia katika maeneo ambayo yametengwa na mambo

    mengine.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, lakini kwa upande wa Wizara ya Maliasili

    wanasema kwamba asilimia 57 ya mapato ambayo yanatokana na mazao ya

    misitu hayakusanywi. Sasa kweli wananchi wana shida wana matatizo yao

    mambo ya kuni, madawati lakini je katika eneo hili ambalo la usimamizi wa

    upatikanaji wa fedha na matumizi mazuri haya maeneo Serikali inasemaje?

    SPIKA:Haya sekta hii halafu unaingia kwenye particular haya Mheshimiwa

    Waziri Mkuu.

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Rajab fundi sana wa kuunganisha mambo.

    Mheshimiwa Spika, analosema Mheshimiwa Rajab ni kweli bado kuna

    udhaifu katika eneo hili na utaona hata katika Bajeti yetu moja ya eneo ambalo

    hatukufanya vizuri sana ni hilo la maduhuli na Wizara ya Maliasili na Utalii wana

    eneo kubwa ambalo tunadhani lingeweza kuwa la msaada sana katika

    kuongeza Bajeti yetu.

    Serikalini tulikaa kujaribu kuona tunafanya nini na hili tatizo la maduhuli

    kutokukusanywa kwa mujibu wa Bajeti iliyowekwa. Imefika mahali watu

    wanafikiria kwamba pengine tungekuwa na chombo maalum au timu maalum

    ambayo kazi yake iwe ni kufuatilia tu maduhuli kwa kila Wizara na kwa kila

    taasisi ambayo imepewa jukumu la kukusanya hizo fedha. Kwa hiyo katika

    Bajeti ya mwaka huu tutajaribu sana kuona namna ya kuja na utaratibu

    wa jambo hili kusimamiwa hatutakuwa ni chombo kwa maana ni chombo cha

    kisheria kama TRA ilivyo.

    Lakini tumedhani kwamba ndani ya Wizara hizi sisi wenyewe tutatafuta

    timu ambayo tutataka tuipe jukumu la ufuatiliaji wa makusanyo wa maduhuli

    na hili unalolisema linaweza kuwa ni namna moja pengine ya kuweza kupata

    kile ambacho kwa sasa hivi tunakikosa.

    MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa

    fursa nimwulize swali moja dogo la nyongeza.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    13

    Mheshimiwa Waziri Mkuu hivi karibuni kumelipuka ugonjwa wa homa

    SPIKA: Hebu vipi la nyongeza kwa nani?

    MHE. MOSES J. MACHALI: Hapana swali moja.

    SPIKA: Aaa!!! Okay okay.

    MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Waziri Mkuu, hivi karibuni

    kumejitokeza ugonjwa ambao unaonekana kutishia watu wengi hapa nchini

    ugonjwa wa homa ya dengue.

    Taarifa ambazo zinatajwa na watu ambazo nimezisikia ni kwamba

    kulikuwa kuna utafiti ambao unafanywa hapa nchini na wataalamu wetu wa

    Wizara ya Afya wakitafuta mbu ambao watakuja kuangamiza mbu wa Malaria.

    Sasa katika majaribio hayo, wale mbu ndio wamepelekwa matokeo yake

    yanaleta janga hili.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, nilikuwa naomba kauli ya Serikali kuhusiana na

    taarifa hizi ni sahihi kiasi gani ili kuweza kuondoa hofu iliyoko miongoni mwa

    Watanzania?

    SPIKA: Au umesikia yule Mchungaji. (Makofi/Kicheko)

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Machali hakunitendea

    haki. Swali angemwuliza Waziri wa Afya angefanya vizuri zaidi kuliko mimi. Lakini

    ni kweli sasa hivi tuna tatizo la homa ya dengue.

    Lakini wakati huo huo ugonjwa wa malaria nao upo. Sasa kama gonjwa

    hili limetokana na hizo tafiti au hapana siwezi kulisema kwa sasa maana sijui.

    Lakini ninachojua ni kwamba homa hiyo inasababishwa na mbu aina ya aedes

    maana tuna aina tatu za mbu. Chanzo chake ni mbu anaitwa aedes.

    Sasa huyu mbu yupo muda wote wala sio kwamba ameibuka leo,

    hapana. Ni kwamba tu hapa katikati pengine jitihada zilikuwa nzuri tukaweza

    kudhibiti akakosa kupanua uwezo wake wa kueneza ugonjwa na utaona

    imejitokeza sambamba na mafuriko makubwa yaliyojitokeza.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    14

    Kwa hiyo inawezekana pengine katika kuzaliana walikuja wakapata

    upenyo hivi na ndiyo maana tatizo hili likajitokeza. Lakini labda niseme tu

    kwamba pengine nitakuwa sikukutendea haki mimi nadhani labda

    nitamwomba Waziri wa Afya kwa sababu ni jambo kubwa pengine angekuja

    na kauli ya Serikali ili aweze kulieleza vizuri zaidi kwa manufaa ya Watanzania

    wote.

    SPIKA: Ahsante sana kwa kuokoa muda, sasa nimwite Mheshimiwa

    Magdalena Sakaya. Tulikuwa na muda wa kuwasilisha.

    MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba nikuulize swali moja.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi sana za

    walipa kodi kwa ajili ya kutengeneza miundombinu ya barabara hapa nchini.

    Hata hivyo Mheshimiwa Waziri Mkuu barabara hizi kwa sehemu kubwa,

    kiasi kikubwa zilikuwa zinaharibiwa pamoja na kuwepo na sheria lakini

    wanyabiashara wasiokuwa na uzalendo wamekuwa wakizidisha mizigo kwenye

    magari yao na hivyo kuonekana barabara zote zimeharibika na tumeshuhudia

    migomo mikubwa kwenye barabara zote.

    Mheshimiwa Waziri Mkuu, wafanyabiashara wengi wamefanikiwa hata

    kuishinikiza Serikali pale sheria inaposimamiwa wamegoma na hivyo Serikali

    kuruhusu uharibifu wa barabara kuendelea. Naomba kauli ya Serikali, nini kauli

    ya Serikali kuhusiana na barabara kuharibiwa na huku wanaona na huku

    Watanzania wanaendelea kuteseka? Ahsante sana. (Makofi)

    SPIKA: Mheshimiwa Waziri Mkuu sjui kama umelielewa hili swali?

    WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, zaidi ya asilimia 80 ya usafirishaji wa

    mizigo na abiria hapa unategemea barabara. Kwa hiyo, ndio uhalisia wake

    kwa sasa. Ni hali ambayo inaikumba nchi yetu kwa sababu bado reli

    haijaweza kutoa jibu kwa tatizo hili, tutakapokuwa tumeimarisha reli chini ya

    Dkt. Harrison Mwakyembe inawezekana kabisa tatizo hili tukaanza kulipunguza.

    Lakini pili, barabara zetu hizi za lami zinatengenezwa kwa mfumo wa kitu

    kinaitwa surface dressing. Life span yake uwezo wake wa kuishi ni kati ya miaka

    10 mpaka 15. Hatutumii concrete asphalt hapana, tumejaribu kwenye

    barabara tu ya TANZAM ndio tuliweza kutumia kigezo hicho kwa historia yake.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    15

    Kwa hiyo barabara zote hizi ni za aina hiyo. Sasa unapokuwa na

    barabara hizi kwa mfumo huo ambao una mizigo mikubwa hiyo ni tosha kabisa

    kuwezesha barabara hizi kutohimili kwa muda mrefu.

    Tatu, magari yetu hapa nchini uzito tulioruhusu ni tani 56, nchi nyingi

    hawakufika huko ni tani thelathini na thelathini na kitu hivi. Kwa uhalisia wa

    kutokuwa na miundombinu ya reli, miundombinu ambayo ingeweza ikasaidia

    kupunguza huu mzigo Serikali ilijikuta ikaweka utaratibu huo kwa maana ya

    kusaidia tu kuweza kubeba mizigo hiyo kwa urahisi na kwa kutumia magari haya

    ambayo tungefikiri yangekuwa ni machache badala ya kuwa na magari mengi

    na hivyo kuzidi kuongeza tatizo la msongamano. Lakini kwa kufanya hivyo

    bado hatujasaidia sana.

    Lakini, nne niseme hili unalolisema kwa bahati mbaya sana jambo hili

    halikueleweka vizuri, tatizo hakuna anayesema mtu azidishe mzigo zaidi ya tani

    56, hakuna. Si mimi, si Waziri Magufuli si mtu mwingine yoyote na wenye malori

    na mabasi wanajua hilo tatizo hapa lipo wapi? Ni kwamba katika kupima uzito

    wa magari tunatumia axleload weight ya gari.

    Gari inaweza kuwa na excel hizi mbili, tatu, nne, kinachotokea gari hili

    katika kubeba huo mzigo unashuka milima unapanda kuna sehemu nyingine

    kuna matuta unaruka unashuka.

    Kwa hiyo, inawezekana kabisa mzigo ambao umeupima una tani 56

    ukasogea kwenye excel ya mbele na kugandamiza ile excel ya mbele. Au

    wakati unapanda mlima mzigo uka-slide back, nyuma na kugandamiza ile

    excel ya nyuma unapokwenda kupima wanapima hiyo excel weight

    kinachotokea inawezekana katika kutereza kwa ule mzigo ukajikuta ule uzito

    umeongezeka kwenye excel hiyo kwa kiwango kile ambacho wanasema

    hakizidi asilimia 5 au nyuma kwa kiwango hicho.

    Sasa sheria nyingi duniani unapokuwa na hiyo allowance wanairuhusu

    kwa nini, kwa sababu hujazidisha tani 56 inaruhusiwa na unachofanya pale

    unapopima wakakuta kuna hilo tatizo nchi nyingi wanakuambia hebu park gari

    jaribu kuona kama unaweza ukapanga hii mizigo tena vizuri halafu uendelee.

    Lakini magari mengine ni mzigo ambao ni transit good huwezi

    ukaufungua. Ndio maana wanakwambia inapotokea situation hiyo park gari

    lakini ukubali kulipa faini kidogo kwa sababu itakubidi tukuruhusu uendelee

    ingawa excel ya mbele ina uzito zaidi kuliko inavyotakiwa.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    16

    Mheshimiwa Spika, sasa ubishi ulikuwa katika hiyo allowed percentage

    ndiyo ilileta ule ubishi ndiyo maana mimi nikaingilia kati nikasema jambo hili

    linachohitaji ni ueleweshwaji na Kanuni hii kuiweka vizuri ili iweze kueleweka kwa

    sababu ilionekana kutokueleweka vizuri, tukaomba ushauri wa Mwanasheria

    Mkuu wa Serikali, akasema ni kweli Kanuni hiyo inahitaji kuandikwa vizuri.

    Vinginevyo mizigo hii isingekuwa inasafiri inaingia Zambia, mizigo hii

    ikasafiri ikaingia Burundi kama utakuwa umeweka uzito zaidi ya kiwango

    kinachotakiwa. Ndiyo maana nikaingilia kati kwasababu niliona ugomvi ule

    haukuwa na tija sana kwa sababu malori yale ndiyo jukumu la kusafirisha mizigo

    na hali ilishakuwa mbaya.

    Kwa hiyo, hatukupishana na magufuli ingawa watu wanaweza kusema

    angalia Waziri Mkuu ameruhusu mizigo ibebe zaidi ya tani 56 hapana tulikuwa

    tunazungumza allowable percentage wheather mtu ashushe afanye nini au

    vinginevyo ni hilo tu ambalo nimeona nimalizie katika ku-clarify. (Makofi)

    SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, Kanuni hazinilamishi kumwambia mtu

    aulize swali la nyongeza. Kwa hiyo, tunakushukuru kwa majibu mengine

    yalikuwa ni ya kitaalam hasa hili la mwisho na ninawashukuru. Kanuni

    hazinilazimishi, muda umepita. Kwa hiyo, tunaendelea Katibu!

    MASWALI NA MAJIBU

    Na.148

    Mkakati wa Kupunguza Maambukizo ya Ukimwi

    MHE. MBAROUK SALIM ALI aliuliza:-

    Ukimwi bado ni tishio na taarifa zinaonyesha kuwa maambukizi bado ni

    makubwa hasa kwa baadhi ya maeneo hapa nchini.

    Je, Serikali ina mkakati gani mahsusi wa kupunguza maammbukizi katika

    maeneo yaliyoathirika zaidi?

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    17

    WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE

    alijibu:-

    Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba kujibu swali la Mhe. Mbarouk Salim

    Ali, Mbunge wa Wete, kama ifuatavyo:-

    Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Ukimwi bado ni tishio hasa Katika

    makundi maalumu kama vile wanaofanya biashara ya ngono, wanaojidunga

    sindano wanafanya ngono nzembe na wanaofanya ngono kinyume cha

    maumbile.

    Mheshimiwa Spika, Serikali ina mikakati kadhaa mahususi ya kupunguza

    maambukizi hasa katika maeneo yaliyoathirika zaidi. Baadhi ya mikakati hiyo ni

    kama ifuatavyo:-

    (i) Kupitia mkakati wa kudhibiti Ukimwi kwa kipindi cha mwaka 2008-2012 na

    kuandika mkakati mpya kwa kipindi cha mwaka 2013-2018.

    (ii) Kupitia Sera ya Taifa ya Ukimwi ya mwaka 2001 na kuboresha ili kutoa

    miongozo bora zaidi ya kupunguza maambukizi.

    (iii) Serikali imeandaa mwongozo wa kuelekeza Mikoa namna ya kuandaa

    mpango kazi wa Mkoa na kipaumbele ni kuzuia maambukizi kwa kubainisha

    viashiria au vichocheo kwa kila Mkoa, Wilaya, Kata, Kijiji na mtu mmoja mmoja.

    (iv) Serikali ina andaa mpango wa kuwa mwitikio wa Ukimwi kwa mfumo wa

    Kikanda ambapo Wakuu wa Mikoa wa Kanda watakaa pamoja na kuwa na

    mikakati ya pamoja.

    (v) Kuimarisha huduma za kinga katika Mikoa yenye maambukizi makubwa.

    (vi) Kupitia mkakati wa kinga 2009-2012 ili kuhakikisha mkakati wa Taifa

    kuhusu Kinga inawekwa kwenye mkakati huu na baadae kutumika katika

    maeneo yote hususan maeneo yenye maambukizi makubwa.

    (vii) Kuendelea kutoa elimu ya Ukimwi na kubadili tabia kupitia kwa wadau

    mbalimbali na vyombo vya habari hususani radio.

    (viii) Mifumo ya uratibu usimamizi wa huduma za ukimwi imeimarishwa katika

    ngazi za Halmashauri.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    18

    Mheshimiwa Spika, ninapenda kuipongeza Pemba kwa kuzingatia

    mikakati ya kupunguza maambukizi ambapo viwango vya maambukizi kwa

    Pemba ni vya chini Kitaifa ni kati ya 0.1% hadi 0.4%.

    MHE. MBAROUK SALIM ALI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru na pia

    nimshukuru Waziri kwa majibu yake ingawa amaenda zaidi ki mikakati ya Kisera

    kuliko ile mikakati mahususi ambayo nilitegemea niipate lakini pamoja na hayo

    ninapenda kumuuliza mawili madogo.

    Kwa sasa Serikali imejikita zaidi kupunguza maambukizi ya Mama kwa

    Mtoto na pamoja na kwamba Mheshimiwa Waziri ametaja makundi mengi

    hapa ambayo ni tishio kwa magonjwa haya sasa nimuulize. Mheshimiwa Waziri

    kwamba ana kauli gani. Serikali inasemaje kuhusiana na mkakati wa sifuri tatu

    ifikapo 2015 ambapo bado kama miezi sita. malengo hayo yatafikiwaje ikiwa

    bado Serikali imejikita zaidi katika kipengele cha kuzuia maambukizi ya Mama

    na Mtoto.

    Lakini lingine nimwulize Mheshimiwa Waziri kwamba inaonyesha

    kwamba katika baadhi ya maeneo kuna baadhi ya makabila hasa katika

    maeneo ambayo yana maambukizi makubwa, kuna tatizo sugu la tohara kwa

    wanaume, kwamba hawataki kufanyiwa tohara na watu wengi

    hawajafanyiwa tohara.

    Hili ni tatizo kubwa lakini pia kuna sumu kali inayoenezwa na makabila

    hayo hayo kuwa iwapo watu watakubali kufanyiwa tohara ni kuingizwa katika

    Uislamu.

    Je, Waziri ana kauli gani kuhusiana na suala hilo? Ahsante sana.

    NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kupata

    nafasi hii kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii ningepeda

    kuongezea jibu la nyongeza kama ifuatavyo:-

    Kuhusu suala la sifuri tatu, kwa maana ya kwamba kuna suala zima la

    unyanyapaa, kuna suala zima la maambukizi mapya na suala zima la vifo

    kutokana na ukimwi. Mkakati uliopo kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu,

    Wizara ya Afya imeandaa maelezo maalumu ambayo tumeshasambaza nchi

    nzima kupitia vituo vyote ambavyo tunatoa huduma ya Afya.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    19

    Nitumie fursa hii kuwaeleza Watanzania kazi kubwa ambayo imefanyika

    kutokana na tafiti za viashiria katika ngazi ya jamii yaani indicator survey 2008

    hali ya ukimwi nchini ilikuwa ni 5.7% lakini katika matokeo ya 2012 ambayo

    Mheshimiwa Rais alizindua tarehe 27 Machi, 2013 tafiti hizi zimeonyesha hali ya

    ukimwi kushuka na kufikia 5.1% katika nchi.

    Kwa hiyo, tunawaomba Waheshimiwa Wabunge nyaraka hizi na

    miongozo na mafundisho ambayo tumetoa nchi nzima kupitia vikao vya

    maamuzi vya Mikoa ikiwamo Kamati ya Sheria yaani RCC na ngazi ya

    Hamashauri katika Baraza yaani Full Council tufuatilie kuhusu utekelezaji

    unakwendaje ili tuweze kuangalia hali ya jamii itakuwaje mwaka 2015/2016.

    SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa nchi swali la pili.

    WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE: Ni

    kweli lile alilolisema Mheshimiwa Mbarouk kwamba utafiti umeonyesha hata

    kwa Tanzania kwamba wale ambao hawajapata tohara na wale waliopata

    tohara wanaoweza kupata maambukizi kwa haraka ni wale ambao

    hawajapata tohara.

    Utafiti umeonyesha, ndiyo maana hivi sasa kuna jitihada maalum za

    Serikali na kampeni hii imeanza kufanikiwa vizuri sana katika Mikoa ambayo

    imeoekana ina maambukizi makubwa sana ya Ukimwi.

    Labda niseme tu kwamba Mikoa ambayo inaongoza sasa hivi kwa

    kiwango cha juu ni Njombe ambayo ni 14.8%, Iringa 9.1%, Mbeya 9%, Shinyanga

    7.4%, Ruvuma 7%, Dar es salaam 6.9% Katavi 5.9% na Pwani ni 5.9% tumeanza

    kampeni ya makusudi ya kuhakikisha kwamba watu kwa hiari yao

    wanakwenda kufanya tohara bila ya gharama na zoezi hili limefanikiwa sana.

    (Makofi)

    Kwa hiyo, ninataka kutoa wito tu kwa wananchi hasa wanaume

    wajitokeze kwa umri wowote ili kuweza kufanya jambo hili kwa sababu

    limeonekana kwamba ina faida na inaweza kuwasaidia katika kupunguza

    maambukizi.

    MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa

    kunipatia fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza.

    Kwa kuwa, sasa hivi takwimu zinaonyesha kwamba maambukizi ya

    Ukimwi yanaongezeka sana katika makundi maalumu ikiwamo watumiaji wa

    madawa ya kulevya.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    20

    Je, ni lini Seerikali italeta Muswada wa Sheria wa kudhibiri Madawa ya

    Kulevya?

    SPIKA: Mheshimiwa Waziri ninaomba uende kwenye meza ndiyo

    utaratibu.

    WAZIRI WA NCHI,OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, URATIBU NA BUNGE:

    Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninapenda kujibu

    swali la Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni, swali la

    nyongeza kama ifuatavyo:-

    Ni kweli Serikali pamoja na marekebisho makubwa ya Sera na Sheria hayo

    anayoyasema Mheshimiwa Dkt. Ndugulile, Serikali tunafanya maandalizi

    pamoja na Sera ili kuhakikisha kwamba tuna dhibiti na kuimarisha mapambano

    dhidi ya madawa ya kulevya.

    SPIKA: Tunaendelea swali mnalipenda hilo badilisheni tabia. Mheshimiwa

    Suleiman Nchambi.

    Na. 149

    Ujenzi wa Vituo Afya na Zahanati Kishapu

    MHE. SULEIMAN N. SULEIMAN aliuliza:-

    Vituo vingi vya Afya pamoja na Zahanati katika Jimbo la Kishapu

    vimefikia lenta katika Ujenzi.

    Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza vituo hivyo ili wananchi wapate

    huduma?

    NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA

    MITAA (TAMISEMI) alijibu:-

    Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, ninaomba

    kujibu swali la Mheshimiwa Suleiman Nchambi Suleiman, Mbunge wa Jimbo la

    Kishapu, kama ifuatavyo:-

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    21

    Miradi ya ujenzi wa zahanati na vituo vya Afya huibuliwa na wananchi

    wenyewe kupitia mpango wa Fursa na Vikwazo katika Maendeleo (O&OD) na

    unatekelezwa kwa ubia kati ya wananchi na Halmashauri. Halmashauri

    huchangia gharama ndogo za utekelezaji wa miradi hiyo kwa kuwezesha

    upatikanaji wa vifaa pamoja na usimamizi.

    Mheshimiwa Spika, ni kweli katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu vipo

    vituo vya Afya 6 na Zahanati 26 ambazo ujenzi wake umeanza na

    haujakalimika. Ujenzi wa vituo na zahanati ulianza mwaka 2012/2013 kwa

    gharama ya shilingi milioni 77.7 hadi sasa jumla ya Zahanati 6 zipo katika hatua

    ya lenta ambazo ni Mangu, Mwaweja, Mwamashimba, Isagala, Busongo na

    Msagala na kituo kimoja cha Afya cha Bubiki na vituo vya afya vya Dulisi na

    Ng‟wanghalanga vimepanuliwa.

    Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Halmashauri iliidhinishiwa

    shilingi milioni 215.8 kutoka katika Mfuko wa Maendeleo wa Afya ya Msingi

    (MMAM) kati ya fedha hizo kiasi kilichopokelewa ni shilingi milioni 187.5 sawa na

    87% ya Bajeti Halmashauri imetumia fedha hizi katika ujenzi wa majengo ya

    wagonjwa wa nje (OPD) katika vituo vya Afya vya Dulisi na Ng‟wanghalanga.

    Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya mwaka 2014/2015 Halmashauri ya

    Wilaya ya Kishapu ilitengewa milioni 149.8 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya

    MMAM. Kipaumbele cha Halmashauri katika matumizi ya Fedha ni katika

    kukamilisha ujenzi wa OPD na kujenga nyumba moja (two in one) katika kituo

    cha afya cha Dulisi.

    Serikali itaendelea kutenga Bajeti kila mwaka ili kuhakikisha majengo

    hayo yanakamilishwa kwa kushirikisha nguvu za wananchi ili Sera ya afya ya

    kuwa na kituo cha afya kila Kata na Zahanati kila kijiji iweze kutekelezwa

    kikamilifu.

    Aidha, ninachukua fursa hii kuzikumbusha Halmashauri zote kuhakikisha

    kuwa kipaumbele kinawekwa katika kumalizia miradi ya zamani kabla ya

    kuanza miradi mipya. (Makofi)

    MHE. SULEIMAN N. SULEIMAN: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana

    kwanza ninaomba nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kupitia Wizara

    yake ya TAMISEMI kupitia Wizara yake kwa ushirikiano anaotupa wananchi wa

    Kishapu na Halmashauri yetu, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    22

    Kwa kufuata utaratibu wa Bajeti ya milioni mia mbili na mia moja na

    hamsini na kwa kuwa Halmashauri ya Kishapu inayo miradi takribani 26 ya

    Zahanati za 2013/2014 na Vituo vya Afya zaidi ya kumi kwa 2013/2014.

    Sasa swali langu ni hili. Kwa kuwa Vituo vya Afya vitakuwa na thamani ya

    zaidi ya shilingi bilioni tatu na Zahanati zitakuwa na thamani ya takribani bilioni

    tatu. Kama tutafuata utaratibu wa Bajeti ni wazi kuwa tutakamilisha baada ya

    miaka isiyopungua ishirini.

    Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kupokea maombi maalum kama

    ulivyofanya katika Hospitali yetu ya Wilaya ukatusaidia?

    Kwa kuwa Kishapu miradi ya Zahanati na Vituo vya Afya na hospitali ya Wilaya

    inakwenda kwa kasi kama nilivyoeleza kuwa watu wa Kishapu ni sharp Mbunge

    wao sharp, na wananchi wote ni sharp.

    Je, Wizara iko tayari kutuandalia Wafanyakazi ili tunapokamilisha mara

    moja wafanyakazi wawepo ili wananchi wa Kishapu wanufaike na Serikali yao

    ya Chama cha Mapinduzi (CCM) makini?

    SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri ninaomba ujibu kwa kifupi sana.

    NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA

    MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa niaba ya

    Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa pongezi zake ambazo amezitoa kwa Ofisi ya

    Waziri Mkuu.

    Lakini la pili la ushuhuda huyu Kiongozi anayezungumza hapa amefanya

    mambo makubwa katika Wilaya yake amehakikisha wamepata Ambulance

    tano pale, amehakikisha kwamba amesaidia hospitali ya Wilaya ikafikia hatua

    hiyo anayozungumzia hapa.

    Amehakikisha kwamba amechangia mifuko 4,000 katika hiyo Halmashauri

    yake kwa ajili ya kujenga hiyo Hospitali ya Wilaya. It is my judgment kama

    Member wa Parliament kusema kwamba huyu Mbunge ni Mbunge serious

    anajua anachofanya katika Halmashauri yake.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    23

    Sasa kuhusu hizi hela anazozizungumza hapa huyu Bwana anazungumza

    habari ya shilingi nbilioni sita ndizo zinazungumzwa hapa hela za mwaka huu

    tunaokwenda nao ni shilingi bilioni moja na themanini na saba ndizo

    walizotengewa kwa ajili ya Bajeti yote kwa mambo ya afya.

    Mwaka huu tunaokwenda nao tumewatengea shilingi milioni mia tisa na

    hamsini na tatu Development ni shilingi milioni mia mbili na hamsini na

    Development kwa mwaka huu tunaokwenda nao ambayo imepitishwa hapa ni

    mia moja na arobaini na saba.

    Tutakachofanya hapa tutakwenda kuangalia hiyo special request

    anayozungumza. Special request ikiombwa na ili watu wengine wajue,

    Halmshauri inaambiwa kuwa wewe special request yako uliyoomba

    umekubaliwa kiasi hiki. Tutakwenda kuangalia kwenye special request na kwa

    kipaumbele chao kwa maana ya (O&OD), tutapeleka huko kama anavyotaka

    kushauri Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

    Na. 150

    Ucheleweshaji wa Kupandishwa Daraja Wakufunzi

    wa Vyuo vya Elimu.

    MHE. MARTHA M. MLATA (K.n.y. DIANA M. CHILOLO) aliuliza:-

    Kumekuwa na malalamiko ya wakufunzi wa vyuo vya Ualimu nchini

    kuhusu kucheleweshwa kupandishwa madaraja.

    (a) Je, hadi sasa ni wakufunzi wangapi wa vyuo vya Ualimu nchini

    hawajapandishwa madaraja?

    (b) Je, Serikali gani ina mkakati gani wa kuhakikisha malalamiko hayo

    yanamalizwa?

    WAZIRI WA NCHI,OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA

    alijibu:-

    Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Diana Mkumbo

    Chilolo, Mbunge, lenye sehemu(a) na (b), kama ifuatavyo:-

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    24

    (a) Mheshimiwa Spika, Watumishi hupandishwa vyeo kwa kuzingatia sifa

    zilizoainishwa katika miundo ya maendeleo ya Utumishi, Ikama

    iliyodhihirishwa, Fedha za kulipa mishahara ya Vyeo vipya na utendaji

    mzuri wa kazi hakuna sababu ya Watumishi kukaa kwenye Cheo

    Kimoja kwa muda mrefu endapo ametimiza vigezo hivi.

    (b)

    Katika mwaka wa fedha 2013/2014 Serikali ilipanga kuwapandisha vyeo

    wakufunzi 696 na hadi kufikia mwezi Machi, 2014 wakufunzi 282 walikuwa

    wamepandishwa vyeo wakufunzi 414 hawakupandishwa cheo na kati yao

    wakufunzi 247 hawakutimiza masharti ya muundo wao wa maendeleo ya

    Utumishi na wakufunzi 167 hawakuleta taarifa zao kiutendaji kazi.

    Mheshimiwa Spika, idara ya Utumishi wa walimu (TSD) imewahimiza waajiri

    wa wakufunzi hao kuwasilisha taarifa zao ili nao waweze kupandishwa vyeo.

    (c) Mheshimiwa Spika, ili kuondokana na malalamiko ya wakufunzi wa vyuo

    vya Elimu nchini Serikali imepanga mikakati ifuatayo:-

    (i) Kusafisha taarifa za kiutumishi na mishahara ya wakufunzi wa vyuo vya

    elimu sambamba na Watumishi wengine wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya

    Ufundi ili kuhakikisha kwamba kila mwanafunzi analipwa mshahara sahihi

    kulingana na cheo chake cha sasa.

    (ii) Kurekebisha mishahara ya wakufunzi hawa kwa wakati kupitia Mfumo wa

    Taarifa za kiutumishi na mishahara (HCMIS) pale wanapopandishwa cheo ili

    kuepuka madai ya malimbikizo ya mshahara.

    (iii) Kuwataka Wakuu wa Vyuo kujaza mkikataba ya utendaji kazi

    (Performance Contract) kila mwanzo wa mwaka wa fedha (Mwezi Julai)

    kufanya tathimini ya nusu mwaka (Mid-year Performance Review) mwezi

    Desemba kwa kufanya tathimini ya ya mwisho wa mwaka (Annual Perfomance

    Review) mwezi Juni kwa wakati ili kuepuka uwezekano wa baadhi ya wakufunzi

    kukosa taarifa za utendaji kazi wakati wa zoezi la kuwapandisha vyeo.

    Mheshimiwa Spika, ninapenda kuwahimiza wakufunzi wa Vyuo vya

    Ualimu kuhakikisha kuwa wanasoma na kuelewa sifa zinazotakiwa kwa mujibu

    wa Muundo wao wa Utumishi.

    MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Namshukuru

    Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, lakini naomba nimuulize tu maswali

    mawili ya nyongeza. Kwanza, matatizo ya Walimu pamoja na Wakufunzi wote

    yanatokana na kutokuwa na chombo maalum cha kushughulikia matatizo yao

    na kwa sababu Mheshimiwa Waziri aliahidi kuitisha kikao maalum cha wadau

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    25

    kwa ajili ya kushughulikia na kuhakikisha chombo hicho kinapatikana, naomba

    alieleze Bunge hili na Watanzania wote, je, hatua hiyo imefikia wapi?

    Mshahara anaopata Mkuu wa Chuo yeyote anaoufahamu yeye

    Mheshimiwa Waziri pamoja na Wakuu wa Vyuo hao. Je, unastahili kulingana na

    wadhifa huo walionao?

    Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

    SPIKA: Haya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, hicho chombo kina hoja inakuja.

    WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA:

    Mheshimiwa Spika, ni kweli niliahidi hapa Bungeni kwamba tutawaita wadau

    kuhusu kuanzishwa kwa chombo maalum cha kushughulikia masuala ya

    Walimu, lakini nilikaa pamoja na Mwenyekiti wa Kamati yako ya Huduma za

    Jamii, Mheshimiwa Mama Sitta, tumekaa pamoja, tulishauriana, akaomba

    kwanza kabla ya kuwaita wadau, mimi na ofisi yangu twende kwanza

    tukajifunze kwa wenzetu Kenya kama walivyofanya wao na baada ya hapo

    ndio tuite kikao cha wadau. Kwa hiyo, tumeshaelewana kuhusu suala hili.

    Mheshimiwa Spika, suala kuhusu mshahara wa Wakuu wa Vyuo hivi vya

    Wlimu. Mshahara wa Mkuu wa Chuo cha Walimu unaendana na muundo wa

    utumishi wa wakufunzi wa vyuo hivyo. Kwa hiyo, mshahara ule anastahili na ni

    kulingana na muundo wao wa utumishi na pia kuna nyongeza ambayo

    anapata kama Mwalimu au kama Mkuu wa Chuo cha Ualimu.

    SPIKA: Ngoja tuendelee na swali lingine muda umekwenda. Tunakwenda

    Wizara ya Nishati na Madini, Mheshimiwa Profesa Kahigi atauliza swali hilo.

    Na. 151

    Ukosefu wa Umeme Shule za Bukombe

    MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI aliuliza:-

    Ukosefu wa umeme katika shule za Msingi na Sekondari katika Wilaya ya

    Bukombe ni kikwazo kikubwa katika ufundishaji na kujifunza mashuleni:-

    Je, ni lini mradi wa Umeme Vijijini utapeleka umeme katika shule hizo ili

    kuboresha huduma ya utoaji na upokeaji elimu ikiwa ni pamoja na elimu ya

    TEHAMA?

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    26

    NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI, (MHE. CHARLES M. KITWANGA)

    alijibu:-

    Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa

    Kulikoyela Kanalwanda Kahigi, kama ifuatavyo:-

    Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kupeleka umeme Makao

    Makuu ya Wilaya ya Bukombe (Ushirombo) pamoja na Vijiji/ maeneo ya jirani

    kupitia mradi wa Electricty “v”, ambao ni miongoni mwa miradi iliyopata ufadhili

    wa Benki ya Manedeleo ya Afrika (AFDB), Mradi huo unahusu kupeleka umeme

    kwenye Vijiji/maeneo zaidi ya 25 Wilayani Bukombe.

    Mheshimiwa Spika, umeme katika Mradi huu utaunganishwa kutokea

    kituo cha kupozea umeme katika Kijiji cha Ilogi kutoka kwenye kituo kikubwa

    cha kupozea umeme cha Bulyankulu. Kazi za Mradi zitahusisha; Ujenzi wa laini

    yenye urefu wa kilometa 190 yenye msongo wa kilovoti 33 kutoka Kijiji cha Ilogi

    hadi Ushirombo; ufungaji wa vipoza umeme 41; ujenzi wa laini za umeme wa

    msongo wa volti 400/230 zenye urefu wa kilometa 88; na kuunganisha wateja

    wa awali wapatao 5000.

    Mradi huu utagharimu kiasi cha Dola za Marekani 10,328,228. Hatua

    iliyofikiwa kwa sasa ni pamoja na vifaa vya ujenzi wa mradi kufika Ushirombo na

    Mkandarasi (Eltel Networks) anaendelea na ujenzi wa laini ya msongo wa

    kilovoti 33. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2014.

    Mheshimiwa Spika, Serikali pia itatekeleza mradi wa umemenuru katika

    maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Wilaya ya Bukombe kupitia Mradi wa SSMP

    II (Sustainable Solar Market Programme II) utakaoanza kutekelezwa mwezi Julai,

    2014. Katika Wilaya ya Bukombe, Mradi utanufaisha wakazi wa vijiji 52, vituo vya

    afya viwili (2), dispensary kumi (10), shule 13 na vituo vya Polisi vitatu (3).

    Gharama ya utekelezaji wa Mradi kwa loti ya Bukombe ni jumla ya Dola za

    Marekani 1,277,023.68 na Mradi unategemewa kukamilika mwezi Juni, 2016.

    SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Profesa Kahigi, swali la nyongeza.

    MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninayo

    maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, namshukuru Naibu Waziri kwa majibu

    ambayo yanatia matumaini, lakini tatizo kubwa la miradi hii ya umeme ni

    kwamba, ama inachelewa kuanza au inachelewa kukamilika. Mradi huu

    alioutaja wa electricity five kwamba ulikuwa ukamilike Juni mwaka huu, lakini

    taarifa nilizonazo asubuhi hii ni kwamba, bado upo katika hatua za mwanzo.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    27

    Swali langu la kwanza, Mradi huu utakamilika lini? Maana ulitakiwa ukamilike

    Juni mwaka huu.

    La pili, umesema kwamba umemenuru utapelekwa Bukombe kuanzia

    Julai mwaka huu, naomba tu majina ya Shule kumi na tatu ambazo umesema

    kwamba zitapelekewa umeme.

    Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

    SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri majibu!

    NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI(MHE. CHARLES M. KITWANGA):

    Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi kwamba mradi huu

    utakamilika Septemba mwaka huu na mkataba ndivyo ulivyo.

    Swali lake la pili, naomba mpatie majina ya shule ambazo anazihitaji kwa

    sababu siwezi kuyataja yote hapa.

    SPIKA: Ahsante naomba muangalie muda na nina swali langu moja

    Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Mheshimiwa Josephine Chagula atauliza

    swali hilo!

    Na. 152

    Mlipuko wa Malaria Mkoa wa Geita

    MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:-

    Mkoa wa Geita una tatizo kubwa sana la maambukizi ya malaria

    yanayosababishwa na mashimo makubwa yalioachwa wazi baada ya

    uchimbaji wa madini:-

    Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti uharibifu huo wa mazingira

    katika Mkoa huo na kuondoa tatizo la mlipuko wa malaria?

    NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII alijibu:-

    Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,

    naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Thabita Chagula, Mbunge wa

    Viti Maalum kama ifuatavyo:-

    Mheshimiwa Spika, Geita ilipewa hadhi ya kuwa Mkoa Julai, 2011.

    Takwimu za matokeo ya utafiti wa Taifa katika ngazi ya kaya (Tanzania HIV,

    Malaria Indicator Survey- THMIS), za mwaka 2011/2012, zilionesha kiwango cha

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    28

    maambukizi ya malaria Mkoa wa Geita kuwa ni asilimia 33. Kwa takwimu hizi, ni

    dhahiri Mkoa wa Geita una kiwango kikubwa cha maambukizi ya malaria kuliko

    Mikoa yote nchini, utafiti unaofuata utafanyika 2015/2016 kwani tafiti hizi

    hufanyika kila baada ya miaka minne.

    Mheshimiwa Spika, mashimo yaliyoachwa wazi baada ya kuchimba

    madini husababisha maji kutuama na kuwa chanzo cha mazalio ya mbu.

    Vyanzo vingine vya mbu kuzaliana ni vidimbwi, matairi chakavu ya magari,

    mashimo ya vyoo na kadhalika. Sheria ya Uchimbaji wa Madini namba 14 ya

    2010, pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya 2004 na Kanuni

    zake za Athari kwa Mazingira za 2005, zinawataka wachimbaji kuonesha

    “Mining Closure Plan,” lengo likiwa kuwabana kisheria wenye migodi kufukia

    mashimo baada ya uchimbaji wa madini kumalizika. Upande wa mazingira,

    mwekezaji anahitajika kufanya tathmini ya athari za mazingira (environmental

    impact assessment) na kuacha mazingira yakiwa salama.

    Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais

    (Mazingira) na Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, Wizara inazitaka Mamlaka ya

    Usimamizi katika mikoa yote kuhakikisha zinasimamia kikamilifu utekelezaji wa

    Sheria hizi na kanuni zake.

    Mheshimiwa Spika, kutokana na ukubwa wa tatizo la malaria katika

    Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa, ikiwemo Geita, hatua zinazochukuliwa

    kupunguza maambukizi ya malaria ni:- upulizaji wa dawa ya ukoko katika

    majumba ili kudhibiti mbu wapevu wa malaria; kuongeza matumizi ya

    vyandarua kwa kupitia kampeni ya ugawaji kwa watu wa kaya (Replacement

    Universal Mass Campaign kama utakavyofanyika mwakani 2014/2015, Geita

    watapata vyandarua vipatavyo 900,000.

    Mheshimiwa Spika, aidha, mpango wa kuangamiza mazalio ya mbu kwa

    kutumia viuatilifu vya kibaiolojia (bioarvicides) katika Mitaa ya Mji wa Geita

    utaanza mara baada ya Kiwanda cha Kuzalisha Viuatililafu iliyojengwa Kibaha

    kwa kushirikiana na Serikali ya Cuba kuanza uzalishaji.

    SPIKA: Ahsante Mheshimiwa Josephine Chagula, swali la nyongeza.

    MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa

    nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru sana kwa majibu ya Naibu

    Waziri lakini nina swali moja tu. Kwa kuwa Naibu Waziri amekiri kwamba, Mkoa

    wa Geita unaongoza kwa kuwa na wagonjwa wengi sana wa malaria na hii ni

    kutokana na mashimo mengi yayoachwa wazi kwa muda mrefu na wachimbaji

    wa madini.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    29

    Je, Serikali sasa haioni kuna haja ya kuleta Sheria ambayo itawataka

    wachimbaji hawa wa madini kufukia mashimo yao ya awali kabla ya kuanza

    tena kuchimba mashimo mengine, ili tuweze kunusuru afya na maisha ya

    wananchi wa Mkoa wa Geita? (Makofi)

    SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri majibu!

    NAIBU WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII: Mheshimiwa Spika, suala hili

    la mazingira kulingana na Mining Closure Plan ambayo kisheria inabidi wenye

    migodi watimize masharti haya. Ndio sababu inalazimu kuainisha bayana

    kabisa suala zima la tafiti ya mazingira (Enviromental Impact Assessment)

    ambayo inakuwa katika mpango mzima. Lakini kwa kushirikiana na Wizara ya

    Madini na Nishati, suala hili tutashirikiana kufuatilia ili kuona taratibu zote za

    kisheria zimefuatwa.

    SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge najua mnapenda kuuliza

    maswali, lakini muda wenyewe umekwisha. Kwa hiyo, niwatambue wageni

    waliopo humu ndani.

    Tuna wageni wa Mheshimiwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na

    Michezo ambao ni Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi, Wenyeviti wa Bodi,

    Maafisa kutoka Wizarani na Watumishi kutoka Asasi mbalimbali zilizo chini ya

    Wizara hiyo. Yupo anayeongoza timu hiyo ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara,

    Ndugu Sihaba Nkinga, asimame alipo! Halafu pia yupo na Naibu Katibu Mkuu

    Profesa Elisante Ole Gabriel. (Makofi)

    Tuna Wageni wa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo

    (Mheshimiwa Juma Nkamia), ambao ni Mkurugenzi wa Steps Entertainments

    and Steps Solar huyo Ndugu Dileshi Solanky. Kama nime-mess up the names I

    am sorry.

    Halafu kuna Ndugu Juma Mtetwa-TBC-Ulimwengu wa filamu, asimame

    alipo. Okay ahsante, yupo upande huu hapa. (Makofi)

    Yupo ndugu Francis Robert ambaye ni Mkurugenzi wa Radio Five.

    (Makofi)

    Tuna wageni wengine wa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana,

    Utamaduni na Michezo ni wanafunzi nane kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma.

    Wasimame walipo. (Makofi)

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    30

    Wageni wa Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba ambao ni wanafunzi

    20 kutoka Shule ya Sekondari Tumaini, Singida wakiongozwa na Walimu wao

    Ndugu Atupele Mbila Joel na Ndugu Khard Mtoi. Wasimame wanafunzi hawa

    kama wapo ndani! Ahsante sana karibuni naomba msome kwa bidii. (Makofi)

    Kuna Mkurugenzi Mtendaji wa Mwananchi Communication, Bwana Tido

    Mhando alipo asimame! Yeye amekosa nafasi? Okay alikosa nafasi labda,

    halafu tuna wageni 27 wa Mheshimiwa Freeman Aikaeli Mbowe, Kiongozi wa

    Kambi Rasmi ya Upinzani, Bungeni pamoja nao yupo Diwani wa CHADEMA,

    Ndugu Sinock Olenairuko, nimesema vibaya? Wameniandikia CHADEMA.

    (Makofi)

    Halafu wameniandikia pia na Ndugu Tehera Kipara, Mwenyekiti wa CCM

    Kata, hawakusema! Naomba hawa wageni wawili wasimame walipo kama

    nimembatiza Chama basi Kiongozi wao, ahsanteni sana. Kwa hiyo, inaonesha

    Kiongozi wa Kambi ya Upinzani hana ubaguzi. (Makofi)

    Nina wageni wa Mheshimiwa Rajab Mbarouk Mohammed, ambaye ni

    Waziri Kivuli, Sera, Uratibu na Bunge ambao ni Wanakwaya wa kwaya ya

    Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Chuo Kikuu. Haya msimame wanakwaya nyie,

    ahsante sana. Ahsante sana sijui Kwaya ya kitu gani hiyo. (Makofi)

    Kuna wageni watatu wa Mheshimiwa Dkt. Anthony Mbassa kutoka

    Bihalamuro Magharibi wakiongozwa na Ndugu Severine Stephano. Huyu yupo

    wapi? Wageni wako wapi? Haya Zephrine yupo pale na wageni wengine

    wasimame. (Makofi)

    Kuna wageni wa Mheshimiwa Paul Lwanji, Mbunge wa Manyoni

    Magharibi ambao ni Mwenyekiti wa Riadha Mkoa wa Singida ambaye ni Ndugu

    Elia Nollo na Mwenyekiti wa CCM mstaafu Kata ya Sanjaranda, Ndugu Hassan

    Kashinje naomba wasimame walipo, kuna wengine watakosa nafasi. (Makofi)

    Kuna Mheshimiwa Profesa Msolla wa Kilolo ambao wanaongozwa na

    ndugu Sifuni Makongwa, Mwenyekiti wa UVCCM, Kilolo. Wasimame hao

    wageni. Ahsanteni sana. (Makofi)

    Kuna wageni wa Mheshimiwa Ester Bulaya ambao ni wanafunzi wa Chuo

    Kikuu cha Dodoma na wenyewe wasimame walipo. Ahsanteni sana msome

    kwa bidii. (Makofi)

    Tuna wageni wanne wa Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, Waziri Kivuli Habari,

    Vijana, Utamaduni na Michezo wakiongozwa na Ndugu John Mwambigija,

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    31

    Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbeya Mjini. Wasimame hao wote walipo.

    Ahsanteni sana. (Makofi)

    Nina wageni waliokuja Bungeni kwa ajili ya mafunzo hawa ni wanafunzi

    42 na Walimu watatu kutoka Chuo cha Red Cross, Makole. Naomba

    wasimame wote walipo, okay ahsante sana na tunawatakia kazi njema.

    (Makofi)

    Tuna wanafunzi 31 kutoka Chuo cha Mipango, Dodoma, naomba

    msimame mlipo kama mpo. Ahsante sana msome kwa bidii. (Makofi)

    Tuna wageni watatu kutoka Aseki Business School wakiongozwa na

    Ndugu Omari Kiputiputi, Mkuu wa Chuo cha Aseki hiyo, wasimame walipo.

    Ahsanteni karibuni sana na wageni wengine ambao hamkukaribishwa

    mnakaribishwa. (Makofi)

    Matangazo ya kazi; Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za

    Jamii, Mheshimiwa Margaret Sitta, anaomba niwatangazie Wajumbe wa

    Kamati yake kwamba leo saa saba mchana kutakuwa na Kikao katika ukumbi

    wa Pius Msekwa C.

    Pia mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Mheshimiwa

    Victor Mwambalaswa anaomba niwatangazie Wajumbe wa Kamati yake

    kwamba, leo mchana watakuwa na Kikao chao ambacho kitafanyika ukumbi

    wa Hazina ndogo Na.125.

    Waheshimiwa Wabunge, tumekula sana muda, naomba tuendelee!

    MHE. JOHN J. MNYIKA: Mwongozo wa Spika.

    SPIKA: Mwongozo baadaye.

    HOJA ZA SERIKALI

    Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa

    Mwaka 2014/2015 – Wizara ya Habari,

    Vijana, Utamaduni na Michezo

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    32

    SPIKA: Sasa namwita Mtoa hoja!

    Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara

    ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa Mwaka 2014/2015 Kama

    Ilivyosomwa Bungeni

    WAZIRI WA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO: Mheshimiwa

    Spika, naomba nianze kutumia fursa hii kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa

    kunilinda na kunipa nguvu ya kutekeleza majukumu yangu na kuniwezesha

    kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha bajeti hii.

    Mheshimiwa Spika, napenda kutoa pongezi kwa Wabunge wapya

    waliochaguliwa hivi karibuni kwa ushindi wa kishindo ambao ni Mheshimiwa

    Yusuf Salim Hussein, Mbunge wa Chambani; Mheshimiwa Godfrey William

    Mgimwa, Mbunge wa Jimbo la Kalenga; na Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya

    Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Chalinze. (Makofi)

    Mheshimiwa Spika, napenda pia kuchukua fursa hii kuwapa pole familia

    za wanahabari, wasanii na wanamichezo pamoja na tasnia nzima za Habari,

    Utamaduni na Michezo kwa kuondokewa na wapendwa wetu. Mungu azilaze

    roho za marehemu mahali pema peponi. Amina.

    Mheshimiwa Spika, kufuatia taarifa iliyowasilishwa leo kwenye Bunge lako

    Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii,

    sasa naomba kutoa hoja kwamba, Bunge lako Tukufu lipokee, lijadili na

    kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Habari, Vijana,

    Utamaduni na Michezo na Asasi zake kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015.

    Mheshimiwa Spika, hotuba yangu imegawanyika katika maeneo makuu

    matano kama ifuatavyo:-

    Eneo la kwanza, ni Utangulizi; eneo la pili ni Majukumu ya Wizara; eneo la

    tatu ni Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka 2013/2014;

    eneo la nne ni Mpango na Bajeti kwa mwaka 2014/2015; na eneo la tano ni

    Hitimisho.

    Mheshimiwa Spika, majukumu ya Wizara; Wizara yangu inatekeleza

    majukumu yafuatayo:-

    (i) Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Sera za Sekta za Habari, Vijana,

    Utamaduni na Michezo;

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    33

    (ii) Kuratibu na kusimamia masuala ya maendeleo ya vijana ili kuwawezesha

    kujitambua, kujiajiri, kuajirika, kuwajibika na kujitegemea;

    (iii) Kuwa Msemaji Mkuu wa Serikali na kusimamia vyombo vya Habari nchini;

    Kuratibu na kusimamia maendeleo ya utamaduni nchini;

    (iv) Kuratibu na kusimamia maendeleo ya michezo nchini;

    (v) Kusimamia utendaji kazi wa Asasi, Miradi na programu zilizo chini ya

    Wizara; na

    (vi) Kuendeleza, kuwezesha na kuratibu masuala ya kuwajengea uwezo

    watumishi wa Wizara.

    Mheshimiwa Spika, Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa

    mwaka wa fedha 2013/2014. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014,

    Wizara ilipanga kukusanya mapato ya jumla ya shilingi milioni mia nane

    themanini na mbili, mia mbili na tatu elfu (882,203,000) kutoka vyanzo

    mbalimbali. Hadi kufikia mwezi Aprili, 2014, jumla ya shilingi milioni mia sita sitini

    na tatu, ishirini na tisa elfu, mia tano sitini na tisa (663,029,569)zilikusanywa

    ambazo ni sawa na asilimia sabini na tano (75%) ya lengo la makusanyo kwa

    mwaka. Kwa upande wa fedha za Matumizi ya kawaida, Wizara ilitengewa

    jumla ya shilingi bilioni kumi na saba, milioni mia sita ishirini na nane, arobaini na

    tano elfu (17,628,045,000).

    Mheshimiwa Spika, fedha hizo zilijumuisha Mishahara ya Wizara; shilingi

    bilioni mbili, milioni mia sita kumi na saba, mia tano tisini na nane elfu

    (2,617,598,000) na Asasi ni Shilingi bilioni sita, milioni mia sita thelathini na tisa, mia

    tano ishirini na saba elfu (6,639,527,000). Matumizi Mengineyo ya Wizara ni Shilingi

    bilioni nne, milioni mia tisa arobaini na moja, mia tisa ishirini elfu

    (4,941,920,000)na Asasi ni shilingi bilioni tatu, milioni mia nne ishirini na tisa

    (3,429,000,000).

    Mheshimiwa Spika, hadi mwezi Aprili, 2014, jumla ya shilingi bilioni kumi na

    tatu, milioni mia mbili tisini na mbili, mia tano thelathini na tisa elfu, mia nne tisini

    na nane (13,292,539,498) za Matumizi ya Kawaida zilipokelewa na kutumika.

    Kati ya fedha hizo Matumizi Mengineyo ni shilingi bilioni nne, milioni mia saba

    arobaini, mia tisa hamsini na saba elfu (4,740,957,000)na Mishahara ni shilingi

    bilioni nane, milioni mia tano hamsini na moja, mia tano themanini na mbili elfu,

    mia nne tisini na nane (8,551,582,498).

    Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Miradi ya Maendeleo, Wizara

    ilitengewa jumla ya shilingi bilioni kumi na mbili, milioni mia saba

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    34

    (12,700,000,000). Hadi kufikia mwezi Aprili, 2014 jumla ya shilingi bilioni nne, milioni

    mia tatu ishirini na saba, mia tano elfu (4,327,500,000) zilipokelewa ambazo ni

    sawa na asilimia 34 na shilingi bilioni mbili, milioni mia tatu na kumi na ishirini na

    moja elfu (2,310,021,000) zilitumika.

    Miradi iliyotekelezwa ni pamoja na Upanuzi wa Usikivu wa Shirika la

    Utangazaji Tanzania (TBC), Ujenzi wa Ofisi - BAKITA, Programu ya Urithi wa

    Ukombozi wa Bara la Afrika na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.

    Mheshimiwa Spika, Sekta ya Habari; katika mwaka 2013/2014, Wizara

    ilikabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na baadhi ya

    Vyombo vya Habari kukiuka sheria kwa kuandika na kurusha habari ambazo

    hazizingatii kanuni na maadili ya taaluma ya habari. Pia ongezeko la mifumo

    na njia za mawasiliano kama mitandao ya kijamii ambayo mingine imetumiwa

    kuathiri maudhui ya habari zinazotolewa.

    Mheshimiwa Spika, Wizara imechukua hatua mbalimbali za kukabiliana

    na changamoto hizo kwa kutoa onyo na kufungia baadhi ya vyombo vya

    habari vilivyokiuka maadili. Wizara pia imeelekeza Mamlaka ya Mawasiliano

    Tanzania (TCRA) kutekeleza kikamilifu mpango wa kusajili wamiliki wote wa

    mitandao hiyo. Aidha, Wizara inaendelea kutoa elimu na kuwaelekeza wamiliki

    na Wahariri wa vyombo vya habari kufuata sheria, kanuni na miongozo

    iliyowekwa. Wizara inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kukataa kutumia

    fursa hizi za mitandao ya kijamii kueneza chuki, uchochezi na vijiwe vya udaku.

    Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa

    Serikali, Wizara imekamilisha maandalizi ya Muswada wa Sheria ya Kusimamia

    Vyombo vya Habari na sasa uko katika hatua nzuri za mwisho. Kwa kuzingatia

    utaratibu uliopo, Muswada huu utafikishwa katika Bunge lako Tukufu lijalo la

    kutunga Sheria.

    Mheshimiwa Spika, ili kuweza kuimarisha njia za mawasiliano kati ya

    Serikali na wananchi wake, Wizara yangu inafanya maboresho ya Tovuti ya

    Wananchi ili kuweza kuimarisha mifumo na muonekano wa Tovuti hiyo.

    Maboresho hayo yakikamilika, yatawawezesha wananchi popote walipo

    kuwasiliana na Serikali kwa kutumia njia za kisasa. Aidha, itawapunguzia

    wananchi gharama za kuwasilisha kero, hoja na maoni mbalimbali katika taasisi

    za Serikali. Kazi ya kuijenga upya na kuimarisha Tovuti hiyo ili kuwa na

    muonekano mpya unaokidhi mabadiliko ya sasa ya sayansi na teknolojia

    inatarajiwa kukamilishwa mwisho wa mwaka wa fedha 2013/2014.

    Mheshimiwa Spika, Wizara, imeendelea kukusanya habari, kupiga picha

    za matukio mbalimbali ya Serikali na kuzihifadhi katika maktaba; pamoja na

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    35

    kuzisambaza kwenye vyombo mbalimbali vya habari kwa lengo la kutoa habari

    na kuelimisha jamii. Wizara kama Msemaji Mkuu wa Serikali ilifafanua masuala

    na hoja mbalimbali zinazohusu Serikali.

    Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuratibu na kusimamia Vitengo

    vya Mawasiliano Serikalini kwa lengo la kutoa habari na kuelimisha umma juu ya

    utekelezaji wa majukumu ya Serikali. Wizara imetoa mwongozo ulioainisha

    taratibu za kuendesha vitengo hivyo na kuhimiza Wizara na Asasi zote za umma

    kuajiri Maafisa Mawasiliano Serikalini.

    Mheshimiwa Spika, jumla ya mikutano 255 ya wasemaji wa Asasi za

    Serikali na Vyombo vya Habari ilifanyika kuwaelimisha wananchi kuhusu shughuli

    mbalimbali za Serikali zinazofanyika.

    Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, Wizara imeendelea kuratibu

    ushiriki wa Vyombo vya Habari katika vikao vya Bunge vilivyofanyika Dodoma

    na pia kuhakikisha inawapatia vitambulisho waandishi wa habari wa ndani na

    nje wenye sifa za taaluma ya Uandishi wa Habari.

    Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa kushirikiana na Wizara ya

    Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kupitia TCRA ilikamilisha awamu ya kwanza

    ya uhamaji wa kutoka katika mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda dijiti.

    Baada ya zoezi hili tathmini imefanyika ambayo ilionesha mwitikio mzuri wenye

    mafanikio. Hivi sasa zoezi hili limeingia katika awamu ya pili iliyoanza tarehe 31

    Machi, 2014 na inatarajiwa kukamilika kabla ya tarehe 30 Juni, 2015.

    Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2013/2014, Wizara kwa

    kushirikiana na TCRA imesajili vituo nane (8) vya redio na vituo viwili (2) vya

    televisheni na hivyo kuwezesha Tanzania kuwa na jumla ya vituo tisini na tatu

    (93) vya redio na ishirini na nane (28) vya televisheni. Pia uhamaji kutoka mfumo

    wautangazaji wa analoji kwenda mfumo wa dijiti umesaidia kupanua wigo wa

    masafa na kuongeza ubora wa matangazo.

    Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2013/2014, Kamati ya

    Maudhui ilipokea na kushughulikia malalamiko saba ya vituo vya televisheni na

    redio kutokana na kurusha vipindi ambavyo vilikiuka maadili ya utangazaji. Kituo

    binafsi cha televisheni kilicholalamikiwa kwa kurusha kipindi kilichokiuka kanuni

    na maadili ya utangazaji kilipewa onyo. Pia vituo sita vya redio vilivyolalamikiwa

    kwa kurusha vipindi vilivyokiuka kanuni za utangazaji na maadili ya uandishi wa

    habari vilipewa onyo na vingine kutozwa faini kati ya shilingi laki mbili (200,000)

    na shilingi milioni tano (5,000,000).

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    36

    Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Shirika la Utangazaji

    Tanzania (TBC) imeendelea kuimarisha upanuzi wa usikivu wa Redio na

    Televisheni ya Taifa. TBC ilirusha pia matangazo ya vikao vya Bunge moja kwa

    moja, pamoja na matangazo ya Bunge Maalum la Katiba kwa lugha za alama,

    kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum.

    Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi hizo, TBC inakabiliwa na tatizo la

    uchakavu wa vifaa vya kurushia matangazo. Uchakavu huo wakati mwingine

    umesababisha tatizo la kukatika kwa matangazo yakiwemo matangazo ya

    Bunge.

    Mheshimiwa Spika, naomba Waheshimiwa Wabunge wawe wavumilivu

    kwani Wizara imejipanga katika kuendelea kutatua changamoto hizo ili

    kuboresha huduma zitolewazo na TBC. Kupitia Bunge lako Tukufu niwaombe

    Waheshimiwa Wabunge watuunge mkono kufanikisha malengo tuliyojiwekea

    ya kuimarisha TBC.

    Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kutatua changamoto za TBC,

    mwezi Aprili, 2014, imepokea gari jipya la kisasa la matangazo kutoka Serikali ya

    Watu wa China. Gari hili litasaidia sana kuongeza nguvu katika kutatua tatizo la

    uchakavu wa vifaa. Sambamba na hatua hizo, wataalam watano (5) wa TBC

    walipelekwa nchini China kupata mafunzo maalum ya namna ya kutumia gari

    hilo pamoja na vifaa husika.

    Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha wa 2013/2014, Kampuni ya

    Magazeti ya Serikali (TSN) imeendelea na mkakati wa upanuzi wa Kiwanda cha

    Uchapaji. Katika Mkakati huo, Makubaliano na Benki ya Rasilimali Tanzania (TIB)

    yamekamilika ambapo TIB itaipatia TSN mkopo wa shilingi bilioni 2.7 kwa ajili ya

    kujenga jengo la kitega uchumi. Hatua hii itasaidia Kampuni kuongeza uzalishaji

    na kuweza kufikisha huduma kwa wananchi wengi zaidi.

    Mheshimiwa Spika, katika kupanua wigo wa mapato, TSN na Mamlaka ya

    Mawasiliano Tanzania (TCRA) wameingia mkataba wa ubia wa kuendeleza

    kiwanja kilichopo Kitalu Na. 27, Central Business Park, Dodoma, kwa ajili ya

    kujenga jengo la kupangisha. Maandalizi ya ujenzi yameanza. Ukamilishaji wa

    Mradi huu utasaidia Kampuni kujiongezea mapato zaidi.

    Mheshimiwa Spika, katika kuboresha usambazaji wa magazeti, Kampuni

    imepata pikipiki 20 toka Serikali ya Watu wa China kwa ajili ya usambazaji wa

    mijini. TSN pia imeingia makubaliano na kampuni za usafirishaji ili kusafirisha

    magazeti ndani na nje ya nchi ili kuwezesha upatikanaji wa habari za ukweli

    kwa wakati.

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    37

    Mheshimiwa Spika, Sekta ya Maendeleo ya Vijana; katika kushughulikia

    masuala ya vijana mwaka 2013/2014, changamoto mbalimbali zimejitokeza

    ambazo ni pamoja na baadhi ya Sekretarieti za Mikoa na Halmashauri za

    Wilaya kutokuajiri Maafisa Vijana.

    Uelewa mdogo wa vijana katika kubuni na kutayarisha maandiko ya

    miradi, kuanzisha na kutekeleza miradi endelevu, vijana wengi kukosa ujuzi na

    maarifa ya ujasiriamali na biashara ikiwa ni pamoja na kukosa ujuzi wa matumizi

    sahihi ya fedha za mikopo wanazopata kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana

    na vijana kushindwa kujitambua na kufanya maamuzi sahihi kuhusu maisha yao.

    Mheshimiwa Spika, Sekta ya Maendeleo ya Vijana chini ya Wizara yangu

    ina vitengo mahsusi vya kushughulikia hizi changamoto za Vijana. Vitengo hivi

    ni Uratibu na Uwezeshaji wa Vijana Kiuchumi; Ushauri Nasaha, Makuzi na

    Maongozi, pamoja na Mafunzo na Maendeleo ya Ujuzi. Hii ni kwa mujibu wa

    instrument ya Wizara.

    Mheshimiwa Spika, kwa kupitia vitengo hivi na kushirikiana na Wadau

    mbalimbali kama muundo na majukumu ya Wizara yangu yanavyoelekeza,

    Wizara yangu imeendelea kuwajengea vijana uwezo wa kiuchumi kwa kuwapa

    mafunzo na ujuzi katika maeneo ya ujasiriamali, uanzishaji wa miradi endelevu

    ya uzalishaji mali, uongozi, stadi za maisha na matumizi sahihi ya mikopo kwa

    kushirikiana na Benki ya NMB. Katika mwaka wa fedha 2013/2014, jumla ya

    Viongozi wa vikundi vya vijana 457 na Watendaji 211 kutoka Wilaya na Mikoa

    yote nchini wamenufaika na mafunzo hayo.

    Mheshimiwa Spika, ili kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana

    hasa wanaomaliza Vyuo Vikuu na Vyuo vya Kati, Wizara kwa kushirikiana na

    wadau wa maendeleo ya vijana na Wizara mbalimbali kama vile Kilimo na

    Ushirika; Ufugaji; Madini na Nishati na Viwanda imeendelea kuhamasisha vijana

    kuunda makampuni binafsi ya biashara na vikundi vya kuzalisha mali ili waweze

    kujiajiri na kuajiri wengine na kujiletea maendeleo.

    Mheshimiwa Spika, pia Wizara inaendeleza mpango wa kutafutia kazi za

    kujitolea vijana hawa ili kuwawezesha kupata uzoefu kabla ya ajira. Mpango

    umeanzia Dar es Salaam, mfano ambapo vijana 27 wanafanya kazi sehemu

    mbalimbali kwa kujitolea. Wizara pia imehamasisha vijana wa Vyuo Vikuu

    kujitolea mashuleni kufundisha kwa kusaidiana na Walimu husika.

    Mheshimiwa Spika, Wizara vile vile kwa kushirikiana na Shirika la IYF

    imeendelea kuandaa kambi za mafunzo yenye lengo la kubadilisha fikra za

    vijana nchini kwa malengo chanya ya kujituma, kupenda kazi, kushirikiana,

    kupendana, kupenda nchi na kutii sheria. Kwa mfano, mwaka 2013 vijana 800

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    38

    kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani walihudhuria kambi ya

    Kimataifa iliyofanyika mjini Dar es Salaam.

    Mheshimiwa Spika, naendelea kutoa wito na kuhimiza wadau wote wa

    maendeleo ya vijana nchini, tuendelee kushirikiana katika kuhakikisha kuwa

    vijana wetu wanapata uwezo wa kuwajibika na kuchangia katika maendeleo

    ya maisha yao na ya Taifa kwa ujumla. Wizara inaendelea kuhimiza Wakuu wa

    Mikoa kutenga maeneo kwa kazi za vijana na muitikio unaendelea kuwa mzuri.

    Mheshimiwa Spika, kuhusu Mfuko wa Maendelo ya Vijana; napenda

    kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba, mwongozo wa kusimamia Mfuko huu

    umeandaliwa na kusambazwa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa yote tangu

    mwezi Agosti, 2013. Kulingana na Mwongozo huu, kila Halmashauri inahitajika

    kuanzisha SACCOS ya Vijana ambayo itashughulikia utoaji wa mikopo hii. Hadi

    kufikia Aprili, 2014, Halmashauri 22 kati ya 151 zimeanzisha SACCOS za Vijana.

    Nawapongeza sana wale wote walioweza kufanikisha uanzishaji wa SACCOS

    hizi kwa wakati.

    Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013/2014, jumla ya Shilingi bilioni 6.1

    zilitengwa kwa ajili ya Mfuko huu. Hadi Aprili, 2014, Wizara imepokea kiasi cha

    shilingi bilioni mbili (2,000,000,000). Kati ya fedha hizo zilizokopeshwa ni shilingi

    milioni mia moja sabini na mbili, mia sita na tisa elfu (172,609,000) kwa Miradi ya

    vikundi vya vijana 25. Hata hivyo, Wizara inaendelea na uchambuzi wa maombi

    ya vikundi 1,178 yenye thamani ya shilingi bilioni nane, milioni mia nne ishirini na

    moja, mia tisa na sita elfu, mia saba hamsini (8,421,906,750) ili kuweza

    kuvikopesha vikundi vitakavyotimiza vigezo vilivyobainishwa kwenye mwongozo.

    Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2013, Mbio za Mwenge wa Uhuru

    zilizinduliwa na Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na

    Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi tarehe 5 Mei, 2013 katika Kijiji cha

    Chokocho, Mkoani Kusini Pemba na kufikia kilele Mkoani Iringa tarehe 14

    Oktoba, 2013 na Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,

    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    Mheshimiwa Spika,kupitia mbio hizo, jumla ya miradi ya maendeleo 1,229

    yenye thamani ya shilingi bilioni mia moja hamsini na nane, milioni mia tano

    themanini na saba, mia sita sitini na saba elfu, mia sita kumi na tatu na senti

    arobaini (158,587,667,613.40) ilizinduliwa au kuwekewa mawe ya msingi.

    Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2014 umefanyika tarehe 2 Mei,

    2014 Mkoani Kagera; na Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt. Mohamed

    Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

    Mheshimiwa Spika, dhamana ya kuhakikisha hili linafanyika vizuri

    wamepewa vijana. Mbio hizi zinalenga kuhamasisha maendeleo ya wananchi,

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    39

    kudumisha umoja, amani, upendo na mshikamano wa Kitaifa. Hivyo basi,

    hatuna budi sisi sote kuthamini na kuenzi Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa

    mustakabali wa Taifa letu.

    Mheshimiwa Spika, sambamba na maadhimisho ya kilele cha Mbio za

    Mwenge wa Uhuru, Wizara iliratibu maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa

    ambayo yalianza tarehe 8 hadi 14 Aprili, 2013, Mkoani Iringa. Maonyesho katika

    Wiki ya Vijana yalishirikisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Ofisi za Mikoa

    10, Idara za Serikali 16, Halmashauri za Wilaya 21, Asasi za Kiraia 14, Vikundi vya

    Vijana Wajasiriamali 53, Vyuo Vikuu vya Elimu vitatu na Taasisi za Kibenki tatu.

    Mheshimiwa Spika, aidha, katika Wiki hiyo, Vijana 300 kutoka makundi

    mbalimbali ya Vijana walishiriki katika midahalo ambapo pia walipatiwa

    mafunzo ya aina tofauti yenye lengo la kuwajengea uelewa wa masuala

    mbalimbali ya maendeleo ya vijana. Kwa mfano, umuhimu wa kuwa na Wiki ya

    Vijana kila mwaka, ujasiriamali, dhana ya uwajibikaji, umuhimu wa Mifuko ya

    Hifadhi ya Jamii na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana.

    Mheshimiwa Spika, Sekta ya Maendeleo ya Utamaduni; katika mwaka wa

    fedha wa 2013/2014, Wizara ilikabiliana na changamoto zilizotokana na athari

    za utandawazi na maendeleo yenye kasi kubwa ya sayansi na teknolojia,

    mmomonyoko wa maadili kwa watu wa rika mbalimbali, wizi wa kazi za wasanii

    kutokana na upatikanaji kirahisi wa kurudufu kazi husika. Malalamiko makubwa

    yamekuwa kwamba, hali hii imekuwa ikiwaneemesha mapromota na

    wasambazaji wa bidhaa za filamu na muziki ambao sio wasanii.

    Mheshimiwa Spika, pamoja na changamoto hizi, Wizara kupitia Sekta ya

    Maendeleo ya Utamaduni:- imeimarisha ukusanyaji na uhifadhi wa takwimu za

    tasnia ya utamaduni; imetoa mafunzo ya namna ya kuainisha namba za

    misimbo (code numbers) za sekta ya utamaduni ambazo zitatumika Kitaifa na

    Kimataifa; imefanya tafiti za maktabani za lugha za jamii 10 na utafiti wa

    uwandani katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani ili kuhifadhi sarufi, misamiati

    na istilahi za lugha ya Taifa – Kiswahili; imefanya utafiti wa kina kuhusu mila za

    jando na unyago miongoni mwa jamii za Wamakonde, Wamakua na Wayao.

    Mheshimiwa Spika, utafiti huo umewezesha kukamilisha maandalizi ya

    pendekezo la elementi ya urithi usioshikika ambao hatimaye Serikali itaomba

    urithi huo uingizwe kwenye orodha ya urithi wa utamaduni wa dunia

    unaotambuliwa na UNESCO. Elementi hiyo ni ya ngoma ya “Nankachanga”

    kutoka Kijiji cha Namahonga, Wilaya ya Tandahimba, Mkoa wa Mtwara.

    Mheshimiwa Spika, Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Habari,

    Utamaduni, Utalii na Michezo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, iliratibu zoezi la

  • Nakala ya Mtandao (Online Document)

    40

    kuwapata Watanzania wenye sifa stahiki ili kunufaika na fursa zinazotokana na

    Tanzania kuwa Makao Makuu ya Kamisheni ya Kiswahili ya Jumuiya ya Afrika

    Mashariki. Fursa za ajira katika Kamisheni zitashindaniwa na nchi zote

    wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hivyo ni muhimu kwa Tanzania

    kuwa na wagombea sadifu ili kuhimili vishindo vya kinyang‟anyiro hicho. Wizara

    hizi mbili zitaendelea kusimamia zoezi hili kuhakikisha fursa ziliz