Pendekezo Kuhusu Kuzuia Unyonyaji Dhidi Ya Wasanii Katika Biashara Ya Miito(Ringback Tones)

Embed Size (px)

Citation preview

  • 7/30/2019 Pendekezo Kuhusu Kuzuia Unyonyaji Dhidi Ya Wasanii Katika Biashara Ya Miito(Ringback Tones)

    1/3

    PENDEKEZO BINAFSI LA MBUNGE KUHUSU KUZUIA UNYONYAJI

    DHIDI YA WASANII WA TANZANIA KATIKA BIASHARA YA MIITO

    (RING BACK TONES)

    Kwenda kwa: DR ABDALLAH KIGODA, Waziri wa Viwanda na Biashara

    Kuhusu: BIASHARA YA MIITO YA SIMU (RINGBACK TONES)

    Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu biashara ya mauzo ya nyimbo kama

    miito kwenye simu. Malalamiko haya yalianzia kwa wasanii wenyewe na baadaye mimi

    binafsi niliwasilisha hoja zao Bungeni mwaka 2012. Hata hivyo, hadi sasa malalamiko

    haya bado hayajapatiwa ufumbuzi na hivyo wasanii kuendelea kunyonywa. Tatizo

    kubwa katika biashara hii ni USIRI na UNYONYAJI kwa wasanii wa Tanzania. Suala la

    USIRIlipo Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia. Suala la Unyonyaji lipo

    Wizara ya Viwanda na Biashara.

    USIRI

    Biashara hii ya Ring Back Tones (RBT) hufanywa na Kampuni za simu (Network

    providers) kwa kununua maudhui kutoka wachuuzi (Content Providers) ambao nao

    huingia mikataba na Wasanii (Content Creators).

    Hakuna sheria yoyote au Kanuni hapa nchini inayoongoza biashara hii na hivyo

    Network providers na Content Providers kuwa watu pekee wenye taarifa zote za

    biashara hii. Kampuni za simu hujumuisha mapato ya biashara hii na mapato yake

  • 7/30/2019 Pendekezo Kuhusu Kuzuia Unyonyaji Dhidi Ya Wasanii Katika Biashara Ya Miito(Ringback Tones)

    2/3

    mengine (Not Ringfenced), hawatoi taarifa za manunuzi ya nyimbo (au content

    nyingine yeyote) kwa wadau na hasa wasanii. Wachuuzi (Content Providers) nao

    hawatoi taarifa za mauzo kwa wasanii na wanatumia uelewa mdogo wa wasanii

    kuwasainisha mikataba inayowanyonya. Matokeo yake ni kwamba msanii hupata kiasi

    cha asilimia mbili tu (2.5%) ya mapato ghafi ya kazi yake. Hivi sasa biashara hii

    inathamani (turnover) ya takribani shilingi 44 bilioni kwa mwaka.

    Suluhisho:

    Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano iandike kanuni (regulations) zitakazolazimisha

    makampuni ya simu kuweka wazi mapato yatokanayo na biashara ya RBT (Miito ya

    simu) kila baada ya miezi 4 (disclosure rules). Kanuni hizi zielekeze makampuni kutoa

    taarifa za mauzo kwa kila kazi (nyimbo/vichekesho etc.)

    UNYONYAJI

    Kutokana na usiri ulioelezwa hapo juu, wasanii wamekuwa wakinyonywa kimapato.

    Kwa mfano Msanii hulipwa mapato yatokanayo na ununuzi wa awali wa kazi yake

    (wimbo) katika mwezi (downloads).

    Lakini mapato yatokanayo na subscriptions ambapo mlaji hukatwa shilingi 30 kila siku

    msanii hapati chochote. Hivyo katika mapato ya sh. 1,300 kila mwezi kwa kila mteja

    kwa kila wimbo, msanii hupata mgawo wake kutoka shilingi 400 tu za downloads na

    ndio maana wasanii wote nchini hupata 2.5% ya shilingi 44 bilioni zinazokusanywa na

    Kampuni za Simu.

  • 7/30/2019 Pendekezo Kuhusu Kuzuia Unyonyaji Dhidi Ya Wasanii Katika Biashara Ya Miito(Ringback Tones)

    3/3

    Nchini Marekani biashara ya miito ya simu (RBT) imetafsiriwa kama maonyesho (Public

    Performances) na hivyo copyright Association ya Marekani imeweka kiwango cha

    chini cha mrahaba (royalty) ambacho msanii hulipwa. Marekani msanii hulipwa asilimia

    10 ya patoghafi linalozalishwa na kazi yake kama muito wa simu.

    SULUHISHO

    Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara iandike kanuni kwamba mauzo ya kazi

    za wasanii kama miito ya simu inachukuliwa kama performance na kwamba Kampuni

    za simu zitalipa sio chini ya asilimia 12 (12%) ya mapato ghafi, ambapo asimilia 10%

    itakwenda kwa msanii na asilimia 2% COSOTA kwa ajili ya usimamizi na Ulinzi wa kazi

    za Wasanii.

    HITIMISHO

    Kanuni za Uwazi (disclosure rules) katika biashara hii ya Ring Back Tones na mgawo

    wa haki wa mapato (fair and just revenue share) ndio suluhisho endelevu na litakaloleta

    tija kwa wasanii wa Tanzania na hata Serikali kukusanya mapato stahili. Kanuni

    (Regulations) zinazopendekezwa zianze kutumika kuanzia tarehe 1/7/2013

    Kabwe Z. Zitto, Mb

    Kigoma Kaskazini

    Dodoma, 13 Mei 2013.