15
International Labour Organization INTERNACIONAL INSTITUT FOR LABOUR STUDIES STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY KUFANYA AJIRA BORA KUWA KICHOCHEO CHA MAENDELEO

STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

  • Upload
    others

  • View
    1

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

International

Labour

Organization

INTERNACIONAL

INSTITUT FOR

LABOUR STUDIES

STUDIES ON

GROWTH WITH EQUITY

KUFANYA AJIRA

BORA KUWA KICHOCHEO

CHA MAENDELEO

Page 2: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

MUHTASARI WA JUMLA NA

MAPENDEKEZO YA SERA

Ukuaji wa uchumi nchini Kenya umeimarika zaidi katika miaka ya hivi karibuni…

Katika mwaka wa 2003, ukuaji wa uchumi wa Kenya uliimarika: ukuaji halisi wa Jumla ya

Pato la Taifa uliimarika kila mwaka kutoka asilimia 0.3 katika mwaka wa 2002 hadi

takriban asilimia 7 katika mwaka wa 2007 sawa na ukuaji wa mataifa mengine ya Afrika,

Kusini mwa Sahara na hata juu kidogo ikilinganishwa na kiwango cha ukuaji cha

ulimwengu cha asilimia 5.4 kwa wakati huo. Kulikuwepo na ukuaji wakati huu ingawa

kulikuwa na ukame wa mara kwa mara ulioathiri sekta ya kilimo na kusababisha kuibuka

na kufufuka kwa sekta nyingine kama vile sekta ya utalii.

Hata hivyo, mwaka 2008, awamu hii ya upanuzi ilifikia kikomo chake ghafla baada ya

uwekezaji na biasharanje kuporomoka. Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na

vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka huo, ambao uliathiri sana

sekta nyingi za kiuchumi katika miezi sita ya kwanza ya mwaka wa 2008. Hali hii ya

kuzorota kwa uchumi iliharibiwa zaidi na kudorora kwa hali ya kifedha na kiuchumi

ulimwenguni hasa kufuatia kuongezeka kwa bei za bidhaa. Hata hivyo, baada ya kipindi

cha msukosuko na hali ya kukadiria, uchumi uliimarika kwa kiasi kikubwa katika mwaka

wa 2010 ambapo shughuli za biasharanje na uwekezaji zilirejea kwa ukamilifu. Kufikia

mwishoni mwa mwaka wa 2010, uchumi uliimarika kwa kiwango kikubwa cha asilimia 7.3

sawa na uchumi unaoibuka wa mataifa mengine kwa kipindi hicho. Ukuaji halisi wa Jumla

ya Pato la Taifa katika robo ya tatu ya mwaka wa 2012 ulididimia kidogo hadi asilimia 4.7

na unatarajiwa kukua kwa asilimia 5.7 katika mwaka 2013.

…japo haujakuwa thabiti kutokana na msingi hafifu wa ukuaji na pia ruwaza

legevu ya uwekezaji…

Kwa miongo mitatu iliyopita, ukuaji wa uchumi wa Kenya haujakua kiusawasawa na kwa

miaka 30, kulikuwa tu na kipindi kimoja (ikiwa ni pamoja na kipindi cha hivi majuzi cha

ukuaji) ambapo ukuaji wa uchumi ulikuwa zaidi ya asilimia 5. Ni kweli kuwa Jumla ya

Pato la Taifa la kila mwaka limekuwa asilimia 2 au hata chini ya hii kwa takriban thuluthi

tatu ya kipindi hiki cha miaka 30 na ni la kiwango cha chini sana ikilinganishwa na asilimia

wastani ya mataifa ambayo hayajaendelea sana. Sababu mojawapo inayochangia hali hii

inatokana na kasi ya chini ya mabadiliko yanayolenga mfumo wa uchumi unaotegemea

viwanda.

Page 3: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

Ukubwa wa sekta ya viwanda- ikiwa ni pamoja na shughuli za uzalishaji na zisizotegemea

uzalishaji umesalia vivyo hivyo kwa miongo miwili sasa. Utegemeaji wa kilimo –

ambacho ni asilimia 25 ya Jumla ya Pato la Taifa -umeweka uchumi katika hali ya hatari

hasa kutokana na kuongezeka kwa bei ya pembejeo kama vile mafuta na hata hali mbaya

ya anga. Hali hii ni mbaya zaidi kutokana na kwamba majani chai na kahawa pekee

huchangia asilimia 20 ya mapato ya biasharanje.

Kasi ya mabadiliko imeathiriwa pakubwa na kushuka kwa kiwango cha akiba na kukwama

kwa uwekezaji. La mno kabisa ni kuwa, Kenya ilishuhudia udidimiaji mkubwa sana katika

kiwango cha akiba ya jumla ya nchi miongoni mwa mataifa ya ulimwengu yanaoendelea.

Huku mengi ya mataifa ibuka, yale yanayokuwa na yale ambayo hayajaendelea sana

yakiweza kuimarisha kiwango cha akiba yao na kupunguza utegemezi wa ufadhili wa

kutoka nje usiojulikana kama vile ule wa uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni na ule wa

mikopo ya kigeni. Akiba ya Jumla ya Pato la Taifa la Kenya ilididimia kutoka asilimia 18.6

katika mwaka wa 1990 hadi asilimia 8.9 katika mwaka wa 2010. Kutokana na hali hii,

uundaji wa mtaji maalum wa kijumla haukupiga hatua kama za mataifa mengine

yanayoendelea. Uundaji wa mtaji maalum wa kijumla umekwama kwa asilimia 20 ya Jumla

ya Pato la Taifa kwa mwongo uliopita.

…ambayo imeathiri pakubwa uundaji wa nafasi za kazi rasmi na kuzuia uboreshaji

wa hali ya maisha…

Ukuaji wa kiwango cha chini wa kiuchumi umedhihirisha kuwa uboreshaji wa soko la kazi

umekuwa wa kasi ya chini mno. Kati ya mwaka wa 1991 na 2003, kiwango cha ajira

nchini Kenya kilipunguka kwa zaidi ya asilimia 7 kutoka asilimia 67 hadi asilimia 59.7 na

hata katika kipindi cha hivi karibuni cha ukuaji imara na endelezi, ukuaji wa ajira ulienda

sambamba na idadi ya watu wanaofanya kazi. Kwa sababu hiyo, kiwango cha ajira mwaka

wa 2012 - kilichokuwa zaidi ya asilimia 60 – kilisalia katika kiwango cha chini

kikilinganishwa na hali iliyoafikiwa katika miaka ya 1990 na ambayo ni ya chini zaidi ya

wastani ya mataifa ya Afrika, Kusini mwa Sahara (asilimia ya 65.1).

Zaidi ya yote, nafasi nyingi za kazi zimekuwa katika biashara za sekta ya juakali. Katika

mwongo uliopita tu, ajira za sekta ya juakali zisizokuwa za kilimo ziliimarika kwa hadi

takribani ajira milioni 5.1 au asilimia 7.2 kwa mwaka- hiki kikiwa kiwango cha juu zaidi

kuliko kile cha ajira ya mishahara. Kwa sababu hiyo, ajira katika sekta za juakali

zilichangia asilimia 64 ya jumla ya kazi za mwaka wa 2011 – na asilimia 85 wakati ambapo

wakulima waliojiajiri na wanaofanya kazi ndogo ndogo za ukulima wakiwa

wamejumuishwa. Jambo la muhimu ni kuwa, uzalishaji viwandani ulichukua nafasi ya pili

katika kuchangia sana ukuaji wa nafasi za ajira katika sekta ya juakali. Zaidi ya yote,

kiwango kikubwa cha ajira rasmi katika kipindi hiki zilikuwa za kibarua tu: kati ya mwaka

wa 2003 na mwaka wa 2011, nafasi za kawaida za ajira zilikua kwa asilimia 7

ikilinganishwa na asilimia 87 ya ukuaji wa ajira za vibarua.

Page 4: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

Kwa sababu hiyo, kumekuwa na mabadiliko madogo na hakuna tofauti katika hali ya

maisha ikiwekwa kwenye mizani ya Jumla ya Pato la Taifa kwa kila mwananchi. Kwa

kweli, mapato ya wastani wa jumla kwa kila mwananchi nchini Kenya yamekuwa asilimia

0.32 kwa wastani kwa mwaka katika miaka 30 iliyopita huku mapato ya wastani wa jumla

kwa kila mwananchi katika nchi ambazo hazijaendelea sana yakiimarika kwa asilimia 1.5

kwa mwaka. Maendeleo ya kadiri katika hali ya maisha yameathiriwa na mwelekeo wa

kuongezeka kwa wafanyikazi katika sekta ya juakali ambao aghalabu hupata mshahara wa

chini sana kwa mwezi ukilinganishwa na kiwango cha umaskini kilichowekwa kimataifa na

kitaifa. Mshahara huo ni kama asilimia ishirini ya ule ambao wafanyikazi wa umma katika

sekta rasmi wanapata (na ulio chini ya nusu ya ule wa wafanyikazi wa sekta za kibinafsi).

…hasa miongoni mwa vijana wa taifa la Kenya...

Vijana hasa wameathiriwa na hali ya kutokuwa na njia thabiti za kuweka misingi ya

kuzalisha nafasi za kazi, huku watu wazima wakifaidi kutokana na ugavi usiokuwa wa

kiusawasawa wa nafasi za kazi zilizozalishwa. Hususan, katika mwaka wa 2012, vijana

wenye umri wa miaka 15 hadi 24 walikuwa chini ya asilimia 19 ya nafasi zote za ajira ilhali

wao ni zaidi ya asilimia 35 ya watu wenye umri wa kufanya kazi. Kwa hivyo sasa, kiwango

cha nafasi za ajira kwa vijana kikiwa asilimia 32.8, ni chini ya nusu ya nafasi ya kiwango

cha watu wazima walioajiriwa. Kiwango hiki ni mojawapo ya viwango vya chini zaidi

katika eneo hili. Vijana wengi wamevunjika moyo na sasa wameanza kuacha soko la kazi

kabisa. Katika mwaka wa 2012, kiwango cha kukaa bila kazi cha watu wenye umri wa kati

ya miaka 15 na 24 nchini Kenya kilifikia asilimia 60.5 – ambapo kilipanda kwa pointi

asilimia 5 tangu mwaka wa 2000 pekee. Tatizo hili ni sugu sana miongoni mwa vijana wa

kike ambao kiwango chao cha kukaa bila kazi ni pointi asilimia 8 zaidi ya vijana wa kiume.

Hata hivyo, kumekuwepo na maendeleo makubwa katika kiwango cha wanaojua kusoma

na kuandika na kupata masomo ya shule ya msingi kwa jinsia zote. Katika mwaka wa

2009, asilimia 13 pekee ya wakenya wenye umri wa miaka 15 na zaidi hawakujua kusoma

na kuandika. Kiwango hiki ni cha chini kwa pointi asilimia 13 kikilinganishwa na cha

mwaka wa 2000 na chini ya pointi asilimia 24 kikilinganishwa na mataifa ya Afrika, Kusini

mwa Sahara kwa ujumla. Hata hivyo, mabadiliko haya hayajabainika sana katika masomo

ya vyuo ambapo kiwango cha wanafunzi wanaojiunga ni cha chini mno kikilinganishwa

na viwango vya kimataifa. Kwa kweli, katika mwaka 2009, ni asilimia 4 tu ya wakenya

walijiunga na elimu ya vyuo vikuu – ongezeko la pointi asilimia1.3 tangu mwaka 2000.

Ni muhimu kutambua kwamba, kiwango cha juu cha watu wasiofanya kazi kinaweza

kukwamiza ukuaji wa kiuchumi wa baadaye kutokana na kuzorota kwa ujuzi na uzalishaji

na pia upungufu wa utendakazi, hasa kwa kuzingatia idadi kubwa ya wasomi nchini

Kenya. Hali ya kutojihusisha na soko la kazi pia inaweza kuwa na madhara makubwa ya

kijamii na inalingana na kutoridhishwa, jambo ambalo linaweza kuleta mvutano wa kijamii

– kama ilivyodhihirika kupitia machafuko ya hivi karibuni ya Kaskazini mwa Afrika na

Page 5: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

kwingineko. Kwa kweli, nchini Kenya, vijana wamepoteza matumaini ya kupata nafasi za

ajira na hasa nafasi yao katika jamii kwa jumla. Katika mwaka wa 2011, ni asilimia 15.8 tu

ya idadi ya watu wenye umri wa miaka kati ya 15 na 34 nchini Kenya walioamini kuwa hali

ya uchumi katika maeneo yao ya makaazi ilikuwa inaimarika na ni robo moja tu ndio

walikuwa na imani kwamba ulikuwa wakati mwafaka wa kutafuta kazi. Idadi hii ni

miongoni mwa idadi za chini sana katika bara la Afrika.

…licha ya juhudi kubwa za serikali za kuimarisha soko la kazi.

Katika ngazi ya kitaifa, mipango miwili ya maendeleo iliundwa mwongo mmoja uliopita –

Mkakati wa Kufufua Uchumi kwa Ajili ya Utajiri na Uzalishaji wa Nafasi za Ajira kwa

kipindi cha kati ya mwaka wa 2003 hadi 2007 na ule wa Rajua ya mwaka wa 2030 kwa kati

ya mwaka wa 2008 hadi 2030 (ambao uliupiku ule wa Mkakati wa Kufufua Uchumi kwa

Ajili ya Utajiri na Uzalishaji wa Nafasi za Ajira). Rajua ya mwaka wa 2030 ni mpango wa

muda mrefu wa maendeleo unaolenga kuboresha hali ya maisha ya watu nchini Kenya.

Inajumuisha zaidi ya miradi 120 itakayotekelezwa kwa mipango ya muda wa awamu ya

miaka mitano huku awamu ya kwanza ikikamilika mwaka wa 2012. Kuhusiana na ajira

kama ilivyoratibiwa katika Rajua ya mwaka wa 2030, jumla ya nafasi za kazi zinatarajiwa

kukua kama matokeo ya juhudi za kuimarisha ukuaji wa kiuchumi hivyo basi ndio maana

ya kutokuwepo na juhudi za kipekee au mikakati ya kuzalisha nafasi za kazi.

Rajua hii, hata hivyo, inaonyesha umuhimu wa kuwezesha vijana kupata ujuzi wa hali ya

juu na ustawi. Mipango kwa vijana imependekezwa katika sehemu mbalimbali ikiwemo

kuboresha maarifa ya utendakazi pamoja na kutambua vizuizi katika nafasi ya ajira kwa

vijana. Hii inachangia msururu wa miradi ya serikali, taasisi na mifumo ya sera ambayo

imetekelezwa hivi karibuni kukabiliana na changamoto zinazowakumba vijana, kama vile:

(i) Katika mwaka wa 2005, wizara mpya ya Maswala ya Vijana na Michezo ilibuniwa; (ii)

Katika mwaka wa 2007, serikali ilibuni Sera ya Kitaifa kuhusu Vijana - mifumo ya kisheria

ambayo ililenga kuhakikisha kuwa vijana wanajumuishwa katika maendeleo ya taifa, (iii)

Katika mwaka 2008, Wizara ya Maswala ya Vijana na Michezo ilizindua Mpango wa

Kuwatafutia Vijana Ajira(Youth Employment Marshall Plan) ikiwa na malengo ya

kukabiliana na tatizo la muda mrefu la ajira kwa vijana na (iv) Katika mwaka wa 2010,

Mradi wa Kuwezesha Vijana wa Kenya (Kenya Youth Empowerment Program)

ulibuniwa na serikali ya Kenya kwa ushirikiano na Benki ya Dunia. Mradi huu

ulishughulikia baadhi ya masuala yaliyokuwa yakizingatiwa na mpango wa kutafuta ajira

na pia ukajumuisha shughuli nyingi kama vile utoaji mafunzo na uendelezaji wa sera.

Hata hivyo, miradi ya sera na mikakati ya ukuaji ya hivi karibuni haijafanikiwa ili kuweza

kujumuisha sera za kazi kama sehemu kubwa ya kuimarisha muundo wa sera za mawanda

pana ya kiuchumi. Kwa kweli, kukua kwa Jumla ya Pato la Taifa nchini Kenya

hakujaonyesha kuimarika kwa hali ya soko la kazi hususan kwa vijana. Kwa sasa, mipango

mingi kwa vijana imekosa malengo maalum na vigezo mwafaka vya kupima utendakazi

Page 6: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

na hivyo basi si wazi kama kweli mipango hii ni bora na ni kwa kiwango gani inalenga –

au kufaulu katika kukabiliana na changamoto zinazowakumba vijana. Kwa hivyo, ili

kuweza kufaidika na kiwango kikubwa cha ukuaji wa kiuchumi unaotarajiwa, lazima kuwe

na uwiano mkubwa baina ya ukuaji, ajira na usawa. Tunapoendelea, serikali inahitajika

kuangazia mambo matatu muhimu: (i) kuimarisha ukuaji thabiti wa uchumi na faida za

uzalishaji; (ii) kutia bidii katika kuzalisha nafasi za kazi rasmi na (iii) kuhakikisha kuwa

kuna ugavi sawa wa faida zitokanazo na ukuaji hasa za kuhusiana na ajira ya vijana.

Tukiendelea mbele, kutokana na tajriba ya kimataifa, msaada utatolewa kwa

kuzingatia mifumo ya mawanda mapana ya kiuchumi inayolenga ajira...

Kenya itahitaji kiwango cha ukuaji wa kiuchumi kwa mwaka cha asilimia 5 ambacho

ndicho kinalengwa kuwa cha mwaka 2013 ili kuweza kuchukua idadi kubwa ya watu

wenye umri wa kufanya kazi; na ya karibu asilimia 10 ili kuhakikisha faida ya ajira hasa

kwa vijana. Hivyo basi, mkakati thabiti wa mawanda mapana ya kiuchumi ambao

unakabiliana na hali mbaya iliyopo sasa utakuwa muhimu sana kuwezesha Kenya kuafikia

kiwango cha ukuaji ambacho kitapelekea kuzalisha nafasi za kutosha za ajira. Ingawa

kumekuwa na maendeleo katika nyanja fulani, maendeleo zaidi yatategemea nyanja

nyinginezo.

• Kuhakikisha kwamba kuna mazingira mwafaka ya uwekezaji: Ingawa sera za mawanda

mapana ya kiuchumi za kupunguza gharama ya kukopa na kuongeza uwezekano

wa kupata mikopo ni muhimu, sera hizi pekee hazitoshi kuhakikisha kuwa

mazingira mwafaka ya uwezekaji yameafikiwa.. Sera nyinginezo na bora za

mawanda mapana ya kiuchumi zinaweza kufikiriwa. Hii itapelekea kuwepo kwa

mazingira bora ya uwekezaji ambayo yanahitaji kuimarishwa na sera faafu za sekta.

Kwa mfano;

o Kuboresha kiwango cha kuweka akiba: Serikali inaweza kufikiria mbinu mpya

na bora ili kupunguza matumizi ya kinyumbani na kuhimiza uwekaji wa

akiba nchini kwa mfano kwa kutoa ishara ya mfumko wa bei na pia ile

bondi inayohusiana na Jumla ya Pato la Taifa. Bondi za ishara ya mfumko

wa bei huenda zikawashawishi watu kuweka akiba zaidi huku bondi

inayohusiana na Jumla ya Pato la Taifa ikisaidia taifa kulipa kiwango cha

deni ambacho kinaoana na kiwango cha ukuaji wa Jumla ya Pato la Taifa.

Mataifa mengi kama vile Ajentina, Meksiko, Nijeria na Jamhuri ya Bolivia

ya Venezuela yalitoa rasimu tofauti za bondi zinazohusishwa na Jumla ya

Pato la Taifa kwa miongo mitatu iliyopita hali ambayo ilisaidia sana katika

kupunguza gharama ya kukopa na ikaimarisha uwezo wa kupata mitaji

nchini na kimataifa. Utoaji wa bondi zinazohusishwa na Pato la Jumla la

Taifa inaweza hususan kusaidia katika kuhakikisha kuwa matumizi muhimu

Page 7: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

yanayohitajika katika sekta za kijamii kama vile za afya, elimu na ile ya

usalama wa kijamii hazipati pigo pindi kunapotokea matatizo ya kiuchumi.

o Ukopeshaji kwa sekta muhimu: Wafadhili wanaweza kutumia hitaji la kuwa na

akiba ya rasilimali ili kuzifanya benki kutoa mkopo kwa sekta muhimu za

uchumi. Mbinu hii itawezesha benki kurekebisha viwango vya hifadhi zao

za fedha kulingana na sekta wanazohitaji kukopesha. Kwa mfano, Reserve

Bank of India imeanzisha mpango wa kutoa Mkopo kwa Sekta Muhimu

(Priority Sector Lending) ili kulenga sekta ambazo ziko tayari kutoa nafasi

zaidi za ajira rasmi kwa muda mfupi na ule wa kadiri. Zaidi ya yote, benki

za kibiashara zinaweza kupewa jukumu la kukidhi malengo maalum ya

kutoa mkopo kwa sekta muhimu na kunaweza kuwepo na adhabu kali

ikiwemo kupoteza akiba ya ziada na hata utoaji huduma ya mikopo ya

kulipiwa kwa mishahara ikiwa benki haitaafikia malengo muhimu ya

ukopeshaji kwa sekta muhimu.

• Mikakati ya kuboresha uzalishaji: Kenya inahitaji kuweka mikakati mwafaka ili

kusisimua utendakazi na uzalishaji kwa jumla ili kuhakikisha kuwa uchumi na

wafanyikazi wake umesalia kuwa wenye ushindani mkubwa ulimwenguni. Hii

inaweza kuafikiwa kutokana na kuondoa motisha ya ushuru kwa biashara zilizo na

mbinu bora za kutoa maarifa na zenye kuendeleza uzalishaji katika uwekezaji wao.

Serikali pia inaweza kuanzisha “Hazina ya Uzalishaji” ambayo itatoa misaada na

hata mikopo kwa mashirika ili kuwekeza katika utoaji wa mafunzo kwa wafanyi

kazi wao na kuboresha kiwango chao cha uzalishaji. Zaidi ya yote, sehemu kubwa

ya sera ya kiviwanda ambayo inalenga kupunguza kuwepo kwa idadi kubwa ya

wafanyikazi wa maarifa fulani na kuendeleza sekta ambazo zinazalisha kwa

kiwango kikubwa inaweza kuwa mkakati wa jumla wa kuendeleza uzalishaji. Sera

hizi zitahitaji kuhakikisha mfungamano na utaratibu uliowekwa kuonyesha

mfumko na sera za kiwango cha ubadilishanaji wa sarafu kwa upande mmoja na

sera za ajira na elimu kwa upande mwingine. Kwa sababu hii, ni muhimu

kutambua kuwa maendeleo katika uzalishaji wa ajira kwa kawaida hayapunguzi

mahitaji ya kazi. Kwa hakika, tajriba ya uchumi wa mataifa ya Asia Mashariki

unaonyesha kuwa nafasi ya ajira na ukuaji wa uzalishaji wa kazi haufai kuwa

mchezo wa patapotea.

• Kufanya biasharanje kuwa anuwai: Kupanua aina za bidhaa za biasharanje

kunakoandama pamoja na kutunga sera za kiviwanda kutaifanya Kenya kudhibiti

mapato ya nje, kupunguza hatari ya kuanguka kwa bei za bidhaa na kupunguza

madhara yanayotokana na kuanguka ghafla kwa uzalishaji wa bidhaa za kilimo

kutokana na hali mbaya ya hewa. Sera hii, mwanzo kabisa, itapelekea ukuaji thabiti

wa kiuchumi hali ambayo itaongeza nafasi za ajira. Zaidi ya yote, uzalishaji anuwai

na bidhaa za biasharanje utakuwa na uwezo wa kuboresha ajira hasa katika sekta

Page 8: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

zenye kuleta faida. Ili kuafikia hili, ukopeshaji kwa sekta muhimu (kama

ilivyoelezwa hapo juu) unaweza kuwa suluhu. Hata hivyo, sera ya kiviwanda

inayolenga mbele itakuwa muhimu katika kuhakikisha kuwa taasisi za elimu

zinatoa elimu, mafunzo maarifa mwafaka ili kufanikisha sekta za biasharanje zenye

uwezo.

Ingawa mfumo thabiti wa mawanda mapana ya kiuchumi na kuimarika kwa ukuaji wa

uchumi ni muhimu, bado hautoshelezi. Kwa kweli, mwelekeo wa ukuaji wa uchumi wa

sasa hautaweza kuleta mabadiliko katika sekta ya ajira. Kwa hivyo, kunahitajika juhudi za

kipekee ili kukabiliana na changamoto za suala la ajira linalokumba Kenya hasa kwa

kuzingatia mwelekeo wa kuongezeka kwa kutoajiriwa kirasmina vilevile ongezeko la

ukosefu wa ajira na hali ya kutoridhika miongoni mwa vijana.

… pili, ili kuchangia urasimishaji wa miradi ya sekta rasmi na kuboresha

mazingira ya wafanyikazi katika sekta ya jua kali...

Juhudi za kubadili ongezeko la sekta za nafasi za kazi za juakali na kuendeleza

urasimishaji wa kampuni utapelekea maendeleo katika ukuaji wa nafasi za ajira na kutia

nguvu juhudi za uzalishaji na uwekezaji. Kusisimua uzalishaji wa nafasi za ajira rasmi

kutasaidia kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na kupunguza hali ya uchumi

kuyumbayumba. Ili kuafikia hili, tunaweza kuzifikiria mbinu zifuatazo:

• Kuimarisha maendeleo ya sekta za kibinafsi na urasimishaji wa biashara za sekta ya juakali

na kazi: Mojawapo ya vikwazo vya uzalishaji wa nafasi za kazi rasmi ni kuwepo

kwa vizuizi vya kujiunga na uchumi rasmi. Hii inajumuisha mifumo ya sheria na

kanuni zinazomuumiza mfanyibiashara katika shughuli zake, sera dhalimu katika

utozaji ushuru na taratibu za kuchosha za kusajilisha biashara. Japo Kenya imepiga

hatua katika siku za hivi karibuni, bado kampuni za Kenya zinahitaji kukabiliana

na asasi za serikali kuu pamoja na za serikali za mashinani ili kupata leseni ya

biashara. Hii hulifanya zoezi hili kuwa refu (data za hivi karibuni zinaonyesha

kuwa huchukua siku 32 kuanzisha biashara hapa Kenya) na la gharama kubwa.

Ingawa hatua thabiti zimechukuliwa katika miaka ya hivi karibuni katika uwanja

huu, juhudi za ziada zinahitajika katika kupunguza vikwazo vya kufanya biashara

na vile vya ushuru (hasa kwa biashara ndogondogo) ili kuwapa moyo wajasiriamali

kurasimisha biashara zao. Kwa kuongezea, hali ya kutokuwa na haki za umiliki

thabiti ni kikwazo kingine kinachozuia urasimishaji wa biashara. Mifano kutoka

mataifa mengine katika mambo haya yaweza kuwa muhimu:

o Brazili imechangia urasimishaji kwa kuwapa mikopo wenye biashara

ndogondogo, vyama vya ushirika, miradi yenye juhudi za uzalishaji katika

sekta rasmi. Brazili pia imepunguza hatua zinazohitajika katika kurasimisha

biashara kutoka hatua 41 hadi hatua 7 na pia kupunguza mzigo wa ushuru

Page 9: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

kwa wenye biashara ndogondogo zilizoajiri mtu mmoja. Pia serikali ya

Tanzania imechukua hatua za kupunguza vizuizi vya kurasimisha biashara

kupitia njia tatu za kuboresha usajili wa biashara, kanuni za biashara (kama

vile utoaji leseni) na utengenezaji wa mapato ya serikali (kama vile utozaji

ushuru, ukusanyaji wa kodi n.k).

o Peru imechukua hatua mwafaka ya kukabiliana na hali ya ukosefu wa haki

za umiliki wa mali kwa kubuni Mfumo wa Usajili wa Praedial ambao

uliwapa familia zaidi ya milioni 1.2 hati miliki na ikasaidia zaidi ya biashara

380,000 kujiunga na uchumi rasmi.

o Mataifa kama vile Urugwai na Liberia yamepunguza sana muda wa

kuanzisha biashara kwa kuanzisha mfumo wa ‘one stop shop’ ambao

unaleta shughuli zote za vyeti, habari na fomu zinazohitajika kuanzisha

biashara mahali pamoja panapoweza kufikika wa urahisi. Shughuli kama

hizi pia zinaweza kuchangia ujasiriamali wa vijana (Tazama hapo chini).

o China imeimarisha maendeleo ya kuondoa shughuli za uzalishaji wa

mashinani zisizokuwa za kilimo ili kuweka mwingiliano thabiti baina ya

sekta ya kilimo na uchumi, huku ikizalisha nafasi ya ajira rasmi. Kwa kweli,

ukuaji mkubwa wa sekta ya shughuli zisizo za kilimo mashinani

umechangia pakubwa katika ukuaji wa uchumi wa hina huku ikiimarisha

pato la kaya za mashambani na hivyo kuchangia maendeleo ya mashinani.

• Kubuni mikakati ya usalama wa kijamii kama chombo cha kuboresha hali ya utendakazi wa

wafanyikazi wa sekta za juakali: Wafanyakazi wengi wa sekta ya juakali hapa Kenya

hukosa huduma za kimsingi za usalama wa kijamii huku wakiwa katika hali hatari

bila kinga yoyote ya afya ya kikazi pamoja na hatari za kiusalama na kukosa kinga

katika maswala ya kukosa ajira, ajali, ugonjwa au hata uzee. Huduma nzuri za

kijamii zinaweza kuimarisha hali ya afya ya mtu pamoja na ile ya wafanyikazi wa

sekta za juakali na kuimarisha uwezo wao wa kujipanga na kudai mazingira bora ya

kikazi. Baadhi ya mifano ni pamoja na mpango wa UMASIDA huko Tanzania.

Huu ni mfumo wa kijamii wa bima ambao unalenga kupunguza matatizo ya

wafanyikazi wa sekta za juakali kupata matibabu. Pia, kuna Chama cha Muungano

wa Wanawake Waliojiajiri ambacho kilibuniwa kukabiliana na matatizo ya

wanawake wa Kihindi. Wanawake hao ambao hufanya kazi zisizo rasmi

walichukua jukumu la kuhakikisha kuwa wanapata matibabu, usalama wa mapato

na kujiimarisha. Kijumla, watengenezaji wa sera wanafaa kutilia maanani kuwa

matumizi katika shughuli hizi za kijamii ni jambo la uwekezaji wa muda mrefu na

wala si chombo cha kukabiliana na majanga tu.

Page 10: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

...na tatu, kubuni mkakati wa ajira ya kitaifa kwa lengo haswa la kuzalisha nafasi

za ajira kwa vijana.

Serikali ya Kenya imepiga hatua katika kukabiliana na changamoto za ajira kupitia

mipango maalum, sera na asasi ya soko la kazi. Hata hivyo, mkakati wa pamoja wa kitaifa

wa ajira ambapo sera za ajira hujumuishwa katika mikakati ya maendeleo na mipango ya

ukuaji huenda ikaleta mchango zaidi. Kwa kweli, kuna utambuzi mpya kuhusu umuhimu

wa ajira kama jambo la msingi katika ukuaji wa uchumi na ufanisi. Kiungo muhimu cha

mkakati huu kitakuwa ni kuwahusisha vijana katika utaratibu wa kufanya maamuzi.

Mataifa mengi yameweka mikakati ya kitaifa ya ajira ikiwemo juhudi zinazolenga miaka

mingi ya utekelezi kama vile ‘Action Plan for Jobs’ iliyotekelezwa huko Ireland na

ambayo inatunga sera nzuri za ajira ambazo ni hatua ya kuimarisha sekta hii. Wenye

kubuni sera nchini Kenya wanaweza kujifunza kutokana na ubora na udhaifu wa juhudi

hizi katika kutayarisha mikakati yao ya maendeleo. Hii haitasaidia tu kuboresha

utayarishaji wa yale yaliyomo na vielelezo katika miradi ya vijana bali pia itasaidia

kutayarisha mchakato jumlishi ambao utawaona vijana kuwa muhimu katika kuleta suluhu

kinyume na kuwaona kuwa vyanzo vya matatizo. Juhudi za aina mbalimbali zinaweza

kuwa mojawapo ya mikakati hiyo kama vile:

• Kubadilisha mipango iliyopo sasa ili iweze kuafikia changamoto za ajira kwa vijana: Ingawa

juhudi za hadi sasa za kukabiliana na hali ya ukosefu wa ajira kwa vijana

zinasherehekewa, bado zimesalia kuwa za kijumla katika utekelezaji wake. Hii ina

maana kuwa, zinawalenga vijana kwa jumla lakini zinakosa kutambua vijana walio

na uhitaji zaidi na kukabiliana na changamoto maalum za vijana nchini Kenya

kama vile; (i) Ukosefu wa nafasi za kazi kwa vijana na (ii) uwezo wao wa chini wa

kupata nafasi hizo za kazi zilizo chache. Sera na miradi inayolenga changamoto

maalum – kama vile kuwa na ujuzi ufaao – zinafaa zaidi kuliko kulenga tu kiwango

fulani cha umri. Ili kuimarisha umuhimu wa mipango iliyopo sasa kwa vijana,

masuala yafuatayo yanahitaji kushughulikiwa:

o Kuanzisha ujuzi na soko la kazi, kuwezesha mabadiliko ya kutoka shule na kuingia

katika ajira inayojumuisha vipengele vya ujuzi wa mahusian: Kuna mawazo

yanayofanana miongoni mwa washikadau mbalimbali hapa Kenya kuwa

mojawapo ya sababu za kuwa na kiwango kikubwa cha vijana wasio na ajira

ni kutowiana kwa ujuzi wao na ule unaohitajika katika soko la kazi. Ripoti

hii inatilia mkazo umuhimu wa sera za elimu za utoaji mafunzo lakini

muhimu zaidi zinapochukuliwa kwa ajili ya mahitaji ya ajira. Kwa mfano,

Jamhuri ya Korea na Singapore hazikuzingatia tu suala la elimu bora

(ikiwemo ya shule za upili na vyuo) bali pia ujuzi wa kiufundi ulio bora,

mambo ambayo waliamini yalikuwa mihimili katika kuboresha utendakazi

na ushindani. Mataifa haya mawili yalianzisha malipo ya mafunzo ili

kuwashawishi wajasiriamali kushiriki katika kuwapa wafanyikazi wao

Page 11: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

mafunzo. Zaidi ya yote kuoanisha elimu na mafunzo kungeweza

kuimarishwa na sera ambazo zinawasaidia vijana kupata tajriba ya kazi ili

kuwawezesha kujumuishwa katika ajira kwa muda mrefu. Miradi ya Joven

huko Chile na Juventud y Empleo huko Jamhuri ya Dominika ililenga sio

tu kutoa ujuzi wa kitaaluma kwa vijana bali pia ujuzi wa kukabiliana na

maisha katika soko la ajira.

o Kuhakikisha usawa katika kushiriki kwenye mipango hasa kwa wanawake na vijana

wa mashinani: Ili kuhakikisha usawa katika kushiriki kwenye mipango na

kuzuia ubaguzi, Mradi wa Kuimarisha Watoto na Vijana (Programme for

the Promotion of Children and Youth) ulitekelezwa nchini Uganda kati ya

mwaka wa 2003 na 2006. Mpango huu ulitekelezwa kwa ushirikiano wa

serikali ya Uganda na Ujerumani na ulikuwa na mbinu ya kuendeleza

matakwa ya wale vijana wasiojiweza wanaoishi mashinani, ambao walikuwa

wakiteseka kutokana na aidha ukosefu wa ajira au kuwepo kwa nafasi

chache za ajira.

o Kuwasaidia wasiojiweza: Sera za zamani za ajira zinaweza kuwa zimepitwa na

wakati kwa nia ya kutaka kuwachochea vijana ambao wamekufa moyo na

ambao hawajakuwa na ajira kwa kipindi kirefu. Kwa mfano, nchini Misri

juhudi za kutaka kuwajumuisha tena vijana katika ajira na kwa ujumla katika

jamii, mradi uliofadhiliwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la

Umoja wa Mataifa (UNESCO) unatoa mafunzo ya kusoma na kuandika,

elimu ya kiufundi, mbinu za kukabiliana na maisha na vilevile mafunzo ya

tarakilishi na ujuzi wa lugha za kigeni.

• Kuboresha hali ya uchumi ili kuwezesha ajira: Kuimarisha ukuaji wa kiuchumi na

kuhakikisha uthabiti ni muhimu lakini hakutoshi katika kukabiliana na changamoto

za vijana. Huku kutahitaji juhudi zaidi ambazo zitabuniwa ili kuboresha hali ya

uchumi kuweza kuajiri na kuchochea mahitaji ya ajira kwa vijana. Kwa kweli,

katika juhudi za kuhakikisha ugavi sawa wa faida kutokana na ukuaji, mataifa

mengi yametilia mkazo shughuli za kutoa motisha kwa wajasiriamali ili kuwaajiri

vijana kama wafanyikazi wao huku wengine wakiendeleza ujasiriamali miongoni

mwa vijana. Baadhi ya juhudi hizi zimeainishwa hapa chini:

o Kulenga ruzuku na mbinu nyingine zitakazochangia kuajiriwa kwa vijana: Serikali

zinaweza kuchangia mahitaji ya vijana ya ajira kwa kutoa motisha kwa

wajasiriamali watakaowaajiri vijana kama wafanyikazi wa kupitia kwa malipo

ya ruzuku au kuondolewa ushuru. Mradi wa ajira wa The First

Employment Programme ulioanzishwa Brazili, Kolumbia, Paragwai na hivi

karibuni Meksiko na Mradi wa Mshahara wa Vijana kupitia Ruzuku

(Youth Wage Subsidy Programme) huko Uturuki ni mfano wa mipango

Page 12: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

ambayo inayalipa makampuni ruzuku ili kuyafanya yawaajiri vijana wengi.

Ili miradi hii ifanikiwe ni muhimu ihakikishwe kuwa imelengwa kwa idadi

ya watu walioathiriwa kama vile kwa kutoa msaada wa mafunzo ya gharama

ya chini kwa wenye kampuni zinazowaajiri vijana ambao wanatarajia

kukamilisha masomo ya shule ya upili au kutoa malipo ya gharama ya chini

kwa vijana ambao hawajaajiriwa kwa muda. Hili ndilo lengo la mradi wa

‘First Employment Programme’ unaolenga vijana ambao hawana tajriba ya

ajira.

o Kuhimiza ujasiriamali miongoni mwa vijana: Mbinu nyingine ambayo inaweza

kusaidia katika kuongeza kiwango cha ajira miongoni mwa vijana ni ile ya

kuhimiza ujasiriamali miongoni mwa vijana. Miradi iliyofanikiwa ya

ujasiriamali haijumuishi tu msaada wa kuanzisha pekee bali pia maarifa ya

jinsi ya kukuza na kuimarisha shughuli za biashara. Kwa mfano, Mradi wa

Nafasi za Vijana wa Kaskazini mwa Uganda unawapa vijana wenye umri wa

kati ya miaka 16 na 35 pesa taslimu za kushughulikia mipango ya mafunzo

na vyombo vya kimsingi vinavyohitajika kuanzisha biashara.

o Kuhimiza uhusiano baina ya vijana na wazee: Ni muhimu kukumbuka kuwa

vijana na wazee si vibadala katika sekta ya ajira na kwamba kumkweza au

kumuumbua mmoja wao si hasara wala faida kwa mwingine. Mara kwa

mara inawaziwa kimakosa kuwa kustaafu mapema kwa wazee kutatoa

nafasi ya ajira kwa vijana – wazo ambalo limepelekea kuwepo kwa uhusiano

mbaya baina ya makundi haya mawili. Makundi yote mawili ya vijana na

wazee ni muhimu katika uzalishaji hasa katika sekta ya ajira. Zaidi ya yote,

kutokana na mwingiliano na wafanyikazi wenye tajriba kupitia ushauri,

wafanyikazi wachanga wanaweza kudumisha maadili katika sehemu zao za

kazi na kuchangia katika kuzitupilia mbali imani potovu za vijana. Juhudi

za hivi majuzi za serikali ya Kenya za kuzindua mpango wa ukufunzi

nyanjani ni wazo zuri lakini litahitaji kufuatiliwa kwa makini ili kuhakikisha

kuwa sera za vigezo na kanuni zilizotajwa zinahusishwa na kutiliwa

maanani.

• Mkakati wa utatu wenye mshikamano unahitajika ili kuinua vijalizo vilivyotajwa: Kushiriki

katika mazungumzo ya pamoja na washikadau wafaao hasa wakati wa kuzingatia

juhudi za sera kwa vijana ni muhimu kuhakikisha kuwa hatua hizo zinakabiliana na

mahitaji ya sekta ya ajira. Ni kweli kuwa mazungumzo ya pamoja na washikadau

husika yanaweza kusaidia katika kuleta uwiano wa habari kati ya serikali, waajiri na

vijana, kukabiliana na mahitaji maalum ya wafanyikazi na waajiri na pia kuanzisha

uhusiano wa kimikakati kwa lengo la kuafikia matokeo thabiti kwa muda mrefu.

Baadhi ya mifano ambayo Kenya inaweza kujifunza siku za baadaye imeainishwa

hapa chini:

Page 13: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

o Kujenga ushirikiano na sekta za kibinafsi na mashirika ya kimataifa: Kukuza

ushirikiano na mashirika haya ni muhimu sana sio tu katika kufanikisha

kujumuishwa kwa mahitaji ya wabia katika sera za kitaifa ya ajira lakini pia

kuwaruhusu washirika wa kibinafsi kujumuishwa katika utayarishaji wa

bajeti na mipangilio ya mikakati ya ajira. Afrika Kusini, kwa mfano, iliasisi

ushuru wa kisheria mnamo Aprili mwaka wa 2000 ambao ulihitajika

kuwekezwa na waajiri kugharamia mafunzo na maendeleo kama mkakati wa

ujuzi wa serikali. Kwa upande mwingine, ushirikiano na mashirika ya

kimataifa unaweza pia kuchangia pakubwa. Mradi wa Shirika la Leba

Ulimwenguni wa Ajira kwa Vijana, (Youth Employment Programme)

huzingatia mtazamo jumlishi unaohusisha sera za mawanda mapana za

kiuchumi na malengo maalum ya kukabiliana na matakwa na ugavi pamoja

na kiwango na ubora wa ajira.

o Kuhimiza ushirikishi wa vijana katika mchakato mzima: Vijana wenyewe ni

washikadau muhimu katika mjadala, uundaji na utekelezaji wa sera na

miradi ya ajira kwa vijana. Vijana ni wafanyikazi wa siku za usoni na kwa

hivyo wana fursa nzuri na uwezekano kwa maendeleo yajayo ya taifa.

Mfano moja wa nchi iliyojizatiti kuwashirikisha vijana au makundi ya vijana

katika sera na mipango yake ya ajira kwa vijana ni Sri Lanka. Mpango

Tekelezi wa Kitaifa wa Ajira kwa Vijana wa Sri Lanka (The National Action

Plan for Youth Employment) ulihusisha vijana kote nchini katika mfumo

na uendelezaji wa mchakato wa mashauriano. Matokeo ya mashauriano

haya yalikuwa kwamba hoja muhimu ziliafikiwa, kama vile mapendekezo ya

marekebisho kumi na -tano ambayo yalitiliwa maanani katika kuchapisha

mswada wa mwisho wa Mpango Tekelezi wa Kitaifa.

o Kuboresha ufuatilizi na utathmini wa miradi: Uwezo wa waundaji sera wa

kuboresha ufaafu wa miradi iliyopo na ile mipya unategemea muundo bora

wa utathmini. Kijumla, hata hivyo, kuna machache zaidi yanayojulikana

kuhusiana na juhudi zilizopo sasa. Kwanza kabisa, ni muhimu kukusanya

na kuchunguza habari na matokeo ya kabla na baada ya mradi wowote.

Kwa kiasi kinachowezekana, habari ya kutosha inatakiwa kukusanywa:

gharama, hali ya ajira, malipo, habari za idadi ya watu, kiwango cha elimu

n.k. Pili, ni muhimu kuwafuatilia washiriki kwa muda mrefu. Kwa kuwa

katika hali nyingi, mafanikio ya miradi, hasa katika kuwapa vijana mafunzo,

hukua kwa kipindi fulani cha muda. Kufuatilia washiriki na matokeo hata

baada ya mradi kukamilika kwa mfano baada ya miaka 3-5 kunafaa kuwa

sehemu ya mkakati wa ufuatilizi na utathmini. Kwa kuhitimisha, serikali

inafaa kuanzisha, tokea mwanzo, malengo yaliyo wazi na yenye kupimika

kwa mujibu wa matokeo yanayotarajiwa katika kipindi kifupi au kirefu.

Page 14: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka

Kazi hii si nyepesi lakini inawezekana muradi malengo ya ajira yajumuishwe

katika mkakati wa sasa wa mpango wa maendeleo.

Uchaguzi uliofanyika mwanzoni mwa mwezi Machi 2013 ulitoa mwanya wa nafasi ya

kutekeleza mabadiliko yaliyopendekezwa Kenya kujumuisha ajira katika shughuli nzima

ya ukuaji na maendeleo. Hususan, awamu ya kwanza ya mpango wa muda wa miaka tano

(Medium-Term Plan) wa Rajua ya Mwaka wa 2030 ulikamilika mwaka wa 2012 na awamu

ya pili ya utaratibu huu inaanza mwaka wa 2013 hadi 2017. Awamu hii itatoa nafasi bora

zaidi katika kuingiza sera za sekta ya ajira katika mipango ya maendeleo.

Serikali mpya, hata hivyo, itahitajika kushirikiana na waajiriwa na waajiri. Kwa kweli,

mazungumzo faafu ya pamoja yanaweza kutoa mwelekeo bora zaidi wa mabadiliko na

kuleta sera zenye usawa na uthabiti za kutekelezwa. Kwa sababu hii, Shirika la Leba

ulimwenguni (ILO) kupitia ujuzi wake wa kitafiti na kitaaluma na ambao unawezesha

mazungumzo yanayohusu pande hizi tatu lina jukumu muhimu la kutekeleza pamoja na

serikali na washikadau wengine wa kijamii ili kuhakikisha kuwa kuna ukuaji na usawa.

Page 15: STUDIES ON GROWTH WITH EQUITY - International Labour … · 2020. 2. 19. · Ufifiaji huu ulisababishwa kwa kiwango fulani na vita vya baada ya uchaguzi vilivyozuka mwanzoni mwa mwaka