105
i UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA YA LUGHA YA KISWAHILI KAMA LUGHA RASMI NCHINI KENYA KAUNTI YA NAIROBI. NA KIIO MARY MUENI TASNIFU HII IMETOLEWA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO KIKUU CHA KENYATTA NOVEMBA, 2017

UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

  • Upload
    others

  • View
    5

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

i

UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA

YA LUGHA YA KISWAHILI KAMA LUGHA RASMI NCHINI

KENYA

KAUNTI YA NAIROBI.

NA

KIIO MARY MUENI

TASNIFU HII IMETOLEWA KUTOSHELEZA BAADHI YA

MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO

KIKUU CHA KENYATTA

NOVEMBA, 2017

Page 2: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

ii

Page 3: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

iii

TABARUKU

Kazi hii ninaitabarukia baba yangu mzazi Joseph Musyimi, mama yangu Jennifer

Kiio. Nawashukuru kwa kunihimiza na kunitia moyo niendelee na shahada hii ya

uzamili. Kwa ndugu zangu Emanuel Mutiso na David Musyimi nawasihi msome

kwa bidii.

Page 4: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

iv

SHUKRANI

Mwanzo kabisa, ningependa kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye

ameniwezesha na kunipa nguvu katika kufanikisha kazi hii yangu.

Shukrani nyingi ni kwa wasimamizi wangu Prof, Ireri Mbaabu na Dkt Onyango

kwa juhudi zao katika kunisimamia, kuisahihisha na kunielekeza kila nilipohitaji

kuelekezwa , hadi kazi hii ikafikia upeo wa juu, na kunipa moyo ulioniwezesha

kuifanya kazi hii kwa subira kubwa.

Ningependa kukishukuru Chuo Kikuu cha Kenyatta kwa jumla na hasa Idara ya

Kiswahili na lugha za Kiafrika kwa ushirikiano mzuri ulioniwewzesha

kufanikisha kazi hii.

Shukrani zangu maalum ni kwa wahadhiri wangu walionifunza Kiswahili katika

Chuo Kikuu cha Kenyatta. Wote nawapa tahania kwa kunielekeza kwa njia

ambayo imeniwezesha kupiga hatua kubwa katika umilisi wa lugha ya Kiswahili

Mwisho ni kwa walionisaidia kwa njia moja au nyingine katika kufanikisha kazi

hii kukamilika Mwendwa Stephen na Samuel Mbogo. Asanteni kwa usaidizi

wenu.

Page 5: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

v

IKISIRI

Utafiti huu ulijikita katika kutathmini utayari wa Wakenya katika utekelezaji wa

sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya. Utafiti ulilenga

wakaazi wa mji wa Nairobi hasa katika ofisi za shughuli za kiutawala na vyombo

vya habari vinavyopatikana humo. Utayari wa utekelezaji wa sera ya lugha ya

Kiswahili umeathiriwa na mambo mbalimbali. Baadhi ya mambo hayo ni kama

vile: hadhi ambayo lugha hii imepewa, manufaa ya lugha hii miongoni mwa

athari nyingine. Malengo ya utafiti huu yalikuwa; kubaini iwapo kuna utayari

katika kutekeleza sera ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi. Na namna utayari

huu utakavyosaidia katika kuimarisha sera hii mpya ya lugha ya Kiswahili hasa

katika urasmi wake, kuchunguza changamoto zinazokabiliwa katika shughuli za

kiutawala na vyombo vya habari kuhusu hadhi mpya ya lugha ya Kiswahili na

mwisho kutambua ni vipi utayari wa utekelezaji katika sera hii unavyoweza

kutekelezwa ili kuweza kufanikisha lengo lake la kuwa lugha rasmi. Utafiti huu

ulitumia mitazamo miwili ya upangaji wa lugha. Tulizingatia upangaji lugha

kihadhi ambao huzingatia juhudi zinazochukuliwa ili kubadilisha matumizi na

majukumu ya lugha katika jamii na mtazamo wa upangaji lugha kifahari

unaolenga kutoa mielekeo chanya ya kisaikolojia ambayo ni muhimu ikiwa

kutakuwepo na ufanisi wa muda mrefu katika upangaji lugha. Utafiti huu

uliongozwa na Nadharia ya Utekelezaji iliyoasisiwa na Spencer (1971). Utafiti

wa kina nyanjani ulifanywa ili kubaini ni changamoto zipi ambazo zinakumba

utayari wa utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi. Mtafiti

alitumia sampuli finyu ili kupata matokeo bora zaidi. Data ilikusanywa nyanjani

kwa kutumia hojaji na mahojiano ili kubaini mambo yanayohusu utayari wa

utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili hasa baada ya lugha hii kufanywa

lugha rasmi. Uchanganuzi wa data ulifanywa kwa kutumia programu ya SPSS.

Kutokana na matokeo ya utafiti ilidhihirika kuwa hakuna usawa katika matumizi

ya lugha yaKiswahili na ile ya Kiingereza. Utafiti ulionyesha kuwa lugha ya

Kiswahili ilitumika sana katika idara ya polisi, Kiingereza kilitumika sana katika

vyombo vya habari. Hata hivyo, ni bora wabunge wapitishe miswada

inayohusiana na lugha ya Kiswahili ili iwe sheria. Utafiti huu utasaidia wadau

wanaohusika na maswala ya sera ya lugha na kuweka mikakati ya kuhakikisha

kuwa inatekelezwa. Mapendekezo yaliyofanywa na mtafiti yakizingatiwa na

kutekelezwa, hadhi ya lugha ya Kiswahili itaweza kuwa bora katika sekta

zilizofanyiwa utafiti kwa nchi nzima kwa ujumla.

Page 6: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

vi

YALIYOMO

UNGAMO ......................................................................................................... ii

TABARUKU .................................................................................................... iii

SHUKRANI ..................................................................................................... iv

IKISIRI ............................................................................................................. v

YALIYOMO .................................................................................................... vi

MAJEDWALI ................................................................................................. ix

VIELELEZO .................................................................................................... x

UFAFANUZI WA ISTILAHI NA VIFUPISHO ............................................ xi

SURA YA KWANZA ....................................................................................... 1

UTANGULIZI .................................................................................................. 1

1.1 Usuli wa Mada .......................................................................................... 1

1.2 Suala la Utafiti .......................................................................................... 7

1.3 Maswali ya Utafiti .................................................................................... 8

1.4 Malengo ya Utafiti .................................................................................... 8

1.5 Upeo na Mipaka ....................................................................................... 9

1.6 Sababu za Kuchagua Mada ....................................................................... 9

1.7 Yaliyoandikwa Kuhusu Mada ................................................................. 10

1.8 Misingi ya Nadharia ............................................................................... 17

1.9 Mbinu za Utafiti ..................................................................................... 21

1.9.1 Eneo la Utafiti .................................................................................. 22

1.9.2 Uteuzi wa Sampuli ........................................................................... 22

1.9.3 Ukusanyaji wa Data ya Utafiti.......................................................... 23

1.9.4 Uchanganuzi na Uwasilishaji wa Data .............................................. 24

1.9.5 Hitimisho ......................................................................................... 25

Page 7: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

vii

SURA YA PILI ............................................................................................... 26

HISTORIA YA UTAYARI WA WAKENYA KUHUSU URASMI WA

LUGHA YA KISWAHILI NCHINI KENYA. .............................................. 26

2.1 Kipindi cha Ukoloni ............................................................................... 26

2.1.1 Kipindi cha Kabla ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia ........................ 26

2.1.2 Wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia ........................................ 28

2.1.3 Baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia .......................................... 29

2.2 Kipindi cha Baada ya Ukoloni ................................................................ 32

2.2.1 Shughuli za Kiutawala ..................................................................... 33

i) Sekta ya Umma ..................................................................................... 33

ii) Vyombo vya Habari ............................................................................. 37

2.3 Hitimisho ................................................................................................ 38

SURA YA TATU ............................................................................................ 39

UTAYARI WA WAKENYA KATIKA SERA MPYA YA KISWAHILI .... 39

3.0 Utangulizi ............................................................................................... 39

3.1 Uchanganuzi wa kauli za utayari wa Wakenya katika sera mpya ya

Kiswahili katika............................................................................................ 39

kuimarisha lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi. ........................................ 39

3.2: Kuimarika kwa Lugha ya Kiswahili ....................................................... 51

3.3 Muhtasari ............................................................................................... 59

SURA YA NNE ............................................................................................... 60

CHANGAMOTO NA MIKAKATI YA KUIMARISHA SERA HII MPYA

YA LUGHA YA KISWAHILI ....................................................................... 60

4.0 Utangulizi ............................................................................................... 60

4.1 Changamoto zinazowakabili wafanyikazi katika sekta zilizozingatiwa

katika utafiti ................................................................................................. 61

katika sera mpya ya Kiswahili kuwa lugha rasmi. ......................................... 61

4.2 Mikakati ya kuifanya lugha ya Kiswahili kuwa bora katika sekta

zilizotafitiwa ili ............................................................................................ 67

kukabiliana na changamoto zinazozuia kiwango kinachohitajika .................. 67

4.3 Muhtasari ............................................................................................... 73

Page 8: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

viii

SURA YA TANO ............................................................................................ 74

HITIMISHO NA MAPENDEKEZO ............................................................. 74

5.0 Utangulizi ............................................................................................... 74

5.1 Muhtasari wa Utafiti ............................................................................... 74

5.2 Matokeo ya utafiti ................................................................................... 75

5.2.1 Lengo la kwanza ............................................................................ ..75

5.2.2. Lengo la pili .................................................................................... 76

5.2.3 Lengo la tatu .................................................................................... 77

5.2.4. Lengo la nne ................................................................................... 78

5.3 Matatizo ................................................................................................. 80

5.4 Mapendekezo ya Utafiti .......................................................................... 80

5.5 HITIMISHO ........................................................................................... 82

MAREJELEO ................................................................................................ 83

KIAMBATISHO CHA A: Hojaji .................................................................. 88

KIAMBATISHO CHA B: Mwongozo wa Mahojiano................................... 93

Page 9: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

ix

MAJEDWALI

Jedwali 3.1.1: Lugha ambayo wafanyikazi wanapenda kuitumia sana katika

mawasiliano ya kimaongezi ...................................................................... 40

Jedwali 3.1.2 : Sababu zinazowafanya kutumia Kiswahili ......................... 42

Jedwali 3.1.3: Sababu zinazowafanya kutumia lugha ya Kiingereza .......... 43

Jedwali 3.1.4: Matumizi ya lugha ya Kiswahili kabla ya kuidhinishwa kwa

katiba mwaka wa 2010 ............................................................................. 45

Jedwali 3.1.5: Mabadiliko ya utekelezaji wa sera hii baada ya kuidhinishwa

kwa katiba ................................................................................................ 47

Jedwali 3.1.6: Sababu za waliosema kuwa hakuna mabadiliko ya sera ya

lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi ........................................................ 50

Jedwali 3. 2. 1: Sera mpya ya Kiswahili huimarisha hadhi yake ya kirasmi51

Jedwali 3.2.2: Sababu zinazofanya Kiswahili kuimarika kama lugha rasmi

................................................................................................................. 53

Jedwali 3.2.3: Sababu zinazofanya Kiswahili kutoimarika kama lugha rasmi

................................................................................................................. 55

Jedwali 3.2.4: Pendekezo la njia moja nzuri ambayo inaweza kufanya

Kiswahili kikubalike kama lugha rasmi ................................................... 57

Jedwali ya 4.1.1: Iwapo kuna sheria ambazo zimefanya Kiswahili kutofikia

kiwango kinachohitajika ........................................................................... 61

Jedwali ya 4.1.2: Changamoto zinazokumba lugha ya Kiswahili kuhusu

hadhi mpya ya Kiswahili katika sekta zilizotafiwa .................................... 64

Jedwali 4.1.3: Sababu zinazofanya Kiswahili bado kutofikia hadhi yake ya

kuwa rasmi na nini kilichochangia kutokuwepo na ukamilifu wa utayari wa

Wakenya .................................................................................................. 66

Jedwali 4.2.1: Njia ambazo zinawekwa katika kukipa Kiswahili nafasi yake

kwa mujibu wa katiba wa Katiba 2010 ..................................................... 68

Jedwali 4.2.2: Mapendekezo ya vile Kiswahili kinaweza kutekelezwa ili

kufanikisha lengo lake la kuwa lugha rasmi .............................................. 70

Kauli 4.2.3: Pendekezo moja muhimu kwa serikali kuhusiana na matumizi

ya lugha ya Kiswahili kufikia lengo linalohitajika. .................................... 72

Page 10: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

x

VIELELEZO

Chati 3.1.1: Lugha inayotumiwa sana na wafanyikazi katika mawasiliano ya

kimaongezi ………………………………………………………….................. 40

Chati 3.1.2: Sababu za kutumia Kiswahili............................................................42

Chati 3.1.3: Sababu za kutumia lugha ya Kiingerez.............................................44

Chati 3.1.4: Matumizi ya Kiswahili kabla ya kuidhinishwa kwa katiba mwaka wa

2010 ……………………………………………………………………………..46

Chati 3.1.5: Mabadiliko ya sera hii baada ya kuidhinishwa kwa katiba mwaka wa

2010.......................................................................................................................48

Chati 3.2.1: Sera mpya ya Kiswahili huimarisha hadhi yake ya

Kiswahili………………………………………………………………………...52

Chati 3.2.2: Sababu za Kiswahili kuimarika kama lugha rasmi...........................53

Chati 3.2.3: Sababu za Kiswahili kutoimarika kama lugha rasmi........................55

Chati 3.2.4: Mapendekezo ya kukifanya Kiswahili kikubalike kama lugha rasmi

...............................................................................................................................57

Chati 4.1.1: Sheria zinazofanya Kiswahili kutofikia kiwango kinachohitajika....62

Chati 4.1.2: Changamoto zinazokumba lugha ya Kiswahili katika sekta

zilizotafitiwa..........................................................................................................64

Chati 4.2.1: Mikakati ya kukipa Kiswahili nafasi yake kwa mujibu wa Katiba..68

Chati 4.2.2: Mapendekezo ya vile Kiswahili kinaweza kufanikisha lengo la kuwa

lugha rasmi............................................................................................................71

Page 11: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

xi

UFAFANUZI WA ISTILAHI NA VIFUPISHO

Lugha rasmi- Ni lugha ambayo hutumika katika miktadha rasmi ili kuwasiliana

kwa mfano katika shughuli za kiutawala kama vile bunge.

ITLC- Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki (Inter Territorial Language

Committee)

Sera ya lugha- mpango wa serikali kuhusu matumizi ya lugha nchini.

SPSS- Statistical Package for the Social Sciences. (Mtindo Changanuzi wa

Tarakimu Sayansi).

Page 12: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

i

Page 13: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

1

SURA YA KWANZA

UTANGULIZI

1.1 Usuli wa Mada

Sera ya lugha ni maamuzi katika maandishi kuhusu jinsi lugha zinavyopaswa

kutumika katika jamii ili kutekeleza majukumu mbalimbali. Kwa majibu wa

Mbaabu (1996) ni sera ya umma. Madhumuni ya utafiti huu ni kujadili utayari wa

Wakenya katika utekelezaji waKiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya: Kaunti

ya Nairobi. Mekacha (2011) anasema kuwa sera ya lugha huwa ni kipengele

kimojawapo cha mpango-lugha. Dhana hizi huingiliana sana na wakati mwingine

si rahisi kuzitofautisha. Ni jumla ya mawazo, matamko, sheria, kanuni na taratibu

zenye kuelezea taratibu za utekelezaji wa mabadiliko ya nafasi na matumizi ya

lugha katika jamii.

Aidha, katika mawasiliano na shughuli zote za jamii, sera ya lugha huelekeza

shughuli za kiutawala, elimu na vyombo vya habari. Nchini Kenya, lugha ya

Kiswahili imekuwa ikitumika kama lugha ya taifa kwa mujibu wa serikali, na

ilifanywa lugha rasmi mnamo mwaka wa 2010 (Katiba ya Kenya , 2010).

Kaplan na Balauf wakinukuliwa na Mekacha (2011) wanaziita sera

zilizotayarishwa kwa namna ya maandishi kuwa “ sera halisi” na zile ambazo ni

jumla tu ya matamko, kauli na nyaraka kuwa sera za “kiishara” kwa vile zipo tu

kama ishara ya kukidhi matakwa ya kisiasa. Naye Bamgbose (1991) anadai kuwa

‘sera za lugha’ katika nchi nyingi za Kiafrika ni za kiishara na zimebakia kuwa

matamko au maazimio ya nia ya kufanya mabadiliko lakini ambayo

hayatekelezwi. Mfano, nchini Kenya Kiswahili kimefanywa kuwa rasmi sawia na

Page 14: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

2

Kiingereza lakini hakijapewa hadhi inayostahili katika maeneo mbalimbali: barua

rasmi na mihadhara rasmi,

Sera ya lugha ya Kiswahili nchini Kenya imekuwa ikipitia mabadiliko tangu

ukoloni. Baada ya uhuru, sera hiyo pia ilitiliwa mkazo na rais wa kwanza wa

Kenya. Kwa mujibu wa Mbaabu (1978) mnamo mwezi wa Agosti mwaka wa

1969, Rais wa Kenya Mhe. Jomo Kenyatta anaeleza kuwa Kiswahili kitakuwa

lugha rasmi ya Taifa la Kenya. Alisema kwamba Kiswahili kitatumika katika

Bunge la Kenya kwa sababu ndiyo lugha ya wananchi. Lugha hii ilianza

kutumika kama lugha rasmi katika majadiliano ya Bunge mwaka wa 1975. Jambo

hili lilipingwa na watu wengi kwa kudai kuwa Kiswahili hakina maneno ya

kutosha ya sayansi na ufundi na kuwa hakifai kuwa lugha rasmi ya Taifa la

kisasa. Hivyo, utayari wa utekelezaji wake haukufanywa kama ilivyotarajiwa

hivyo kutochukua nafasi iliyostahili. Ni dhahiri wapinzani hawa walikwepa

ukweli kuwa lugha ina uwezo wa kukua na kama ingeungwa mkono tangu wakati

huo ingetumika kihadhi sawa na lugha ya Kiingereza.

Sera ya lugha ya Kiswahili iliongozwa na mapendekezo ya Tume mbalimbali

zilizoteuliwa kuchunguza masuala yanayohusu Kiswahili. Tume ambayo

ilichangia pakubwa katika kuendeleza lugha ya Kiswahili ni tume ya Mackay ya

1981. Tume hii ilipendekeza kuanzishwa kwa chuo cha pili nchini na Kiswahili

kifundishwe chuoni kama somo la lazima. Somo hili pia lilipaswa kusomeshwa

katika shule za msingi na za upili, (Mbatiah, 2012). Haya yalitokana na

uchunguzi kuwa wanafunzi wengi hawakuweza kujieleza kwa ufasaha katika

Page 15: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

3

lugha ya taifa. Pendekezo hili liliafikiwa pale ambapo, Chuo cha pili nchini cha

Moi kilianzishwa pamoja na idara ya Kiswahili mwaka wa 1987.

Katika mwaka wa 2010, tume ya mabadiliko ya katiba ilichangia pakubwa katika

kukifanya Kiswahili kuwa lugha rasmi hasa baada ya kuidhinishwa kwa katiba

mpya. Shitemi (2011) anaeleza kuwa, tangazo la Kiswahili kuwa lugha ya

kwanza rasmi na lugha ya taifa, linahitaji kuwekwa katika vitendo vya kimitaala,

kiutendaji, kiuwezeshaji na pia katika asasi zote za kutumia lugha. Hii ni

kumaanisha kuwa bado Kiswahili hakijaweza kukita mizizi katika hadhi yake ya

kuwa lugha rasmi, hivyo, utayari miongoni mwa watu kutumia lugha hii

haudhihiriki.

Hata baada ya kuwepo kwa mabadiliko kadhaa katika sera ya lugha ya Kiswahili

bado watu wengi wanaipuuza na kuiona kama lugha ya kiwango cha chini.

Katika shule za msingi wanafunzi wasisitiziwa kutumia lugha ya Kiswahili katika

maongezi yao. Siku ya ijumaa ndiyo siku imetengwa kama siku ya kuzungumza

lugha ya Kiswahili. Lugha hii haitumiki katika hadhi sawa na lugha ya

Kiingereza. Katika baadhi ya shule kuna sheria kwamba wanafunzi hawapaswi

kuzungumza lugha ya Kiswahili hivyo wanazungumza lugha ya Kiingereza

pekee. Hali hii huwalazimu wanafunzi kuwa na mazoea ya kuongea lugha ya

Kiingereza na kuona lugha ya Kiswahili kwamba haina umuhimu wowote. Hali

hii inawanyima wanafunzi fursa ya kujifunza lugha ya Kiswahili. Hata hivyo,

kwa upande mwingine wanafunzi wengi wanaosomea katika vyuo vikuu hasa

katika somo la Kiswahili, hawapendi kuwasiliana kwa lugha hii.

Page 16: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

4

Hali hii si tofauti hasa tukiangazia katika shughuli za kiserikali na vyombo vya

habari. Katika shughuli za kiserikali hasa ofisini za umma, lugha ya Kiingereza

ndio imetumika kwa kina. Wakati unapoenda katika ofisi hizi na kujieleza katika

lugha ya Kiswahili, huenda usishughulikiwe ikilinganishwa na mtu ambaye

anatumia lugha ya Kiingereza. Ni ofisi chache mno ambazo unaweza

ukazungumza lugha ya Kiswahili na kuhudumiwa, mfano ni katika idara ya

polisi, pale ambapo lugha ya Kiswahili inatumika zaidi kuliko lugha ya

Kiingereza. Katika sikukuu ya taifa ya Madaraka, tarehe 1/06/2015 Rais wa

Jamhuri ya Kenya Uhuru Kenyatta alitoa hotuba yake kwa muda mrefu sana

katika lugha ya Kiingereza na ilibidi wananchi kumwambia azungumze lugha ya

Kiswahili. Hili ni dhihirisho kuwa ingawa kikatiba lugha ya Kiswahili ni lugha

rasmi, haizingatiwi kuwa hivyo sawa na lugha ya Kiingereza.

Katika vyombo vya habari, ni dhahiri kwamba taarifa ya habari na baadhi ya

mijadala huendelezwa katika lugha ya Kiingereza kwa wakati mwingi. Kwa

mfano ukiangalia muda unaotumika katika kusoma taarifa ya habari katika

runinga ‘Citizen Nipashe’ kwa lugha ya Kiswahili si mwingi ukilinganishwa na

taarifa ya lugha ya Kiingereza. Kisha katika magazeti, magazeti mengi yanatumia

sana lugha ya Kiingereza. Ni gazeti la “Taifa Leo” pekee ambalo ni la Kiswahili.

Hivyo, ni dhahiri kuwa bado lugha ya Kiswahili haipo katika hadhi sawa na

lugha ya Kiingereza.

Maoni ya wataalamu kama vile King’ei (2010) na Mukhwana (2008) ni kwamba

sera ya lugha nchini Kenya imekuwa na utata tangu nyakati za ukoloni (1895-

1963). Wanaeleza kwamba, kukwezwa kwa Kiingereza juu ya lugha zote nchini

Page 17: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

5

Kenya ni hali inayoendelea kutinga maendeleo ya Kiswahili na lugha nyingine

asilia hasa kupitia sera ya lugha katika sekta ya elimu, vyombo vya habari na

shughuli za Kiserikali. Wanajamii basi wamekuwa wakikionea fahari Kiingereza

kama lugha inayoweza kuwaletea ufanisi wa kikazi katika jamii. Kulingana na

Mukhwana (2008) hii ni kwa sababu kutoka nyakati za ukoloni, lugha ya

Kiingereza imenasibishwa na elimu bora ambapo elimu bora kwa wengi ni daraja

ya kupata ajira nzuri.

Maoni ya Mirianga (2014) yanabainika kuwa, Wakenya wengi hasa waliosoma

hupendelea na kuonea fahari matumizi ya lugha ya Kiingereza hasa katika

miktadha rasmi, huku wakipuuza lugha ya Kiswahili. Ili matumizi ya lugha ya

Kiswahili kutekelezwa , ni muhimu kuipa nafasi nzuri katika mfumo wa elimu na

shughuli za kiutawala. Ni muhimu pia kuondoa dhana kuwa, lugha ya Kiswahili

ni lugha ya kiwango cha chini, dhana iliyoenezwa na sera ya lugha ya wakoloni

nchini Kenya na kuangamiza matumizi ya lugha ya Kiswahili.

Kulingana na Mbatiah (2012), baada ya Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Kenya

Mzee Jomo Kenyatta kutoa agizo Kiswahili kiwe lugha ya taifa nchini na iwe

lugha ya bungeni, jambo hili lilinuia kukipa Kiswahili hadhi ya kuwa lugha ya

taifa kikatiba. Hata hivyo, hili halikutekelezwa ipasavyo. Ngigge (2014)

akimnukuu Mohochi (2011) anaeleza kuwa tume ya marekebisho ya katiba

nchini Kenya ilipendekeza Kiswahili kuwa lugha rasmi na pia kuwa lugha ya

taifa. Kuidhinishwa kwa katiba mwaka wa 2010 kulikifanya Kiswahili kuwa

lugha rasmi na pia kuwa lugha ya Taifa. Baada ya mabadiliko hayo mtafiti alitaka

kubaini, iwapo kuna utayari wa kutekeleza mabadiliko haya ipasavyo kwa

Page 18: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

6

kuangazia vyombo vya habari na shughuli za kiutawala ambavyo ni viungo

muhimu katika kuangazia sera ya lugha.

Kwa mujibu wa Mirianga (2014) kuteuliwa kwa lugha ya Kiswahili kama lugha

ya taifa na kuongezewa jukumu la kuwa lugha rasmi sambamba na Kiingereza

kutasaidia lugha hii kutumika katika nyanja tofauti tofauti nchini Kenya. Jambo

hili pia litasaidia katika ukuaji na ustawi wa lugha hii, ili kuwezesha haya

yatekelezwe, sharti kuwepo utayari miongoni mwa watu ili kutekeleza sera hii

ipasavyo.

Hivyo, kutokana na maelezo ya wataalamu hawa, ni wazi kuwa utayari wa

kuitekeleza sera hii sharti uzingatiwe kwa kuwa bado sera hii haijakita mizizi

ipasavyo ikilinganishwa na lugha ya Kiingereza ambapo lugha hizi zapaswa

kuwa katika hadhi moja. Imebainika wazi kuwa katika miktadha mingi ya shule,

shughuli za kiutawala na hata katika vyombo vya habari bado lugha ya Kiswahili

haitekelezwi ipasavyo na hivyo bado Kiingereza kinaenziwa zaidi.

Ufahamu na ukubalifu kuhusu majukumu yaliyopewa lugha ya Kiswahili kuwa

lugha rasmi, nchini Kenya kama inavyojitokeza katika Katiba ya Kenya ni swala

muhimu. Ni kutokana na majukumu haya mapya na hadhi yake mpya, ambapo

mtafiti alichunguza ili kubaini kama kuna utayari wa kutekeleza sera hii au la, na

kuchunguza ni matatizo yepi yanayokumba utayari wa Wakenya katika

utekelezaji huo na kisha changamoto zinazokumba shughuli za kiutawala na

vyombo vya habari katika kutekeleza Kiswahili kama lugha rasmi kama

ilivyoidhinishwa kikatiba.

Page 19: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

7

1.2 Suala la Utafiti

Utafiti huu ulichunguza sera ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya na

utayari wa Wakenya katika utekelezaji unavyodhihirika, iwapo inapewa hadhi

yake ya urasmi kama inavyobainika katika katiba iliyopitishwa mwaka wa 2010

au la. Mtafiti alifanya utafiti wa kina ili kubaini iwapo sera hii ya Kiswahili kuwa

lugha rasmi inafuatwa ipasavyo na iwapo watu wapo tayari kuimudu hali hii.

Alichunguza jinsi utekelezaji wake unavyoathiriwa katika shughuli za kiutawala

na vyombo vya habari. Pia alichunguza changamoto zinazokabili utayari wa watu

katika utekelezaji wa sera hii katika nyanja hizi.

Nchini Kenya lugha ya Kiswahili imekuwa ikitumika kama lugha ya Taifa kwa

miaka mingi sasa. Baada ya kuidhinishwa kwa katiba mwaka wa 2010, lugha ya

Kiswahili ilipata hadhi mpya ya kuwa lugha rasmi. Kwa kuzingatia hali ilivyo

sasa lugha ya Kiswahili ni maarufu katika miktadha isiyo kuwa rasmi miongoni

mwa wanasiasa kwani wao hutumia lugha hii kwa mikutano yao lakini lugha hii

bado haijapokelewa vyema kama lugha rasmi na hivyo utafiti huu ulinuia kubaini

utayari wa Wakenya katika matumizi ya Kiswahili kama lugha rasmi. Hii ni kwa

kuwa lugha ya Kiswahili imekuwa ikipuuzwa nchini Kenya na hadhi yake ya

kuwa lugha rasmi kama ilivyo katika katiba haizingatiwi kwa kina. Utayari huu

una umuhimu upi hasa katika urasmi wake kisha ni vipi utayari katika sera hii

mpya ya lugha ya Kiswahili unavyoweza kutekelezwa ili kuweza kufanikisha

lengo lake la kuwa lugha rasmi. Utafiti huu ulichunguza jinsi utayari wa

Wakenya hasa wakaazi wa Nairobi ulivyo katika matumizi ya Kiswahili katika

shughuli za kiutawala na vyombo vya habari.

Page 20: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

8

1.3 Maswali ya Utafiti

i) Je, kuna utayari katika kutekeleza sera ya Kiswahili kuwa lugha rasmi?

ii) Utayari huu utasaidiaje katika kuimarisha lugha ya Kiswahili hasa katika

urasmi wake?

iii) Je, ni changamoto zipi zinazokabiliwa katika shughuli za kiutawala na

vyombo vya habari

kuhusu hadhi mpya ya Kiswahili?

iv) Je, ni vipi utayari huu katika sera hii mpya ya lugha ya Kiswahili unavyoweza

kutekelezwa ili kuweza kufanikisha lengo lake na kuwa lugha rasmi?

1.4 Malengo ya Utafiti

i) Kubaini iwapo kuna utayari katika kutekeleza sera ya lugha ya Kiswahili kuwa

lugha rasmi.

ii) Kubaini namna utayari huu utakavyosaidia katika kuimarisha sera hii mpya ya

lugha ya Kiswahili hasa

katika urasmi wake.

iii) Kuchunguza changamoto zinazokabiliwa katika shughuli za kiutawala na

vyombo vya

habari kuhusu hadhi mpya ya lugha ya Kiswahili.

iv) Kutambua ni vipi utayari wa utekelezaji katika sera hii unavyoweza

kutekelezwa ili

kuweza kufanikisha lengo lake la kuwa lugha rasmi.

Page 21: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

9

1.5 Upeo na Mipaka

Sera ya lugha kimsingi huelezwa kwa kushughulikia shughuli za kiutawala, elimu

na vyombo vya habari. Sera ya lugha ya Kiswahili inapaswa kutumika katika

mawanda yaliyotajwa hapo juu lakini utafiti huu ulijikita katika shughuli za

kiutawala na vyombo vya habari ili kuonyesha kama kuna utayari katika

utekelezaji wa sera hii.

1.6 Sababu za Kuchagua Mada

Kama ilivyoelezwa hapo awali, utafiti huu ulilenga kudhihirisha utayari katika

utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya, na

iwapo kuna changamoto zinazokabiliwa katika sera hii hasa katika utekelezaji

wake, katika shughuli za kiutawala na vyombo vya habari. Kwa mujibu wa katiba

mpya ambayo ilipitishwa mwaka wa 2010, sera ya lugha ya Kiswahili ilipata

hadhi mpya na kuwa lugha rasmi. Ilipotambulika kuwa lugha rasmi, lugha hii

ilitarajiwa kutumika katika kiwango sawa na ile ya Kiingereza.

Sababu nyingine ni kuwa hakuna utafiti uliofanywa ambao ni sawa na huu.

Ingawa kuna tafiti nyingi ambazo zimefanywa kuhusu sera ya lugha kwa mfano

ni ‘Mielekeo na changamoto za maafisa wa kaunti katika utekelezaji wa katiba

kuhusu sera ya lugha Kaunti ya Nakuru (Nggige, 2014)’, ‘Mielekeo ya

wafanyakazi kuhusu Kiswahili kama lugha rasmi katika wizara za serikali nchini

Kenya’ Kaunti ya Kisii (Nyandwaro, 2015). Kuna tafiti chache ambazo

zimefanywa kuhusiana na utayari wa utekelezaji wa sera ya lugha kama lugha

rasmi. Utafiti uliofanywa unaokaribiana na huu uliangazia mielekeo na

changamoto za maafisa wa kaunti katika utekelezaji wa katiba kuhusu sera ya

lugha katika kaunti ya Nakuru, (Ngigge, 2014) kisha wa Nyandwaro (2015)

Page 22: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

10

ambaye alitafiti mielekeo ya wafanyakazi kuhusu Kiswahili kama lugha rasmi

katika wizara za serikali nchini Kenya.

Sababu nyingine ni kwamba lugha ya Kiswahili haipewi nafasi mwafaka katika

uimarishaji wake; baadhi ya watafitiwa wanakiona Kiswahili kama lugha duni na

wanaipuuza (Mirianga, 2014). Pia kutokana na swala la utayari katika utekelezaji

wake sharti kuwe na changamoto zinazoifanya sera ya lugha ya Kiswahili kuwa

lugha rasmi kuafikiwa kama ilivyo katika katiba. Utafiti huu ulisaidia kuonyesha

utayari katika utekelezaji na changamoto hizo ili kupata jinsi tunavyoweza

kuimarisha sera hii ili itumike ipasavyo.

Mwisho, utafiti huu uliweza kutoa mwanga kuhusu utayari wa utekelezaji wa

sera ya lugha ya Kiswahili. Iwapo matokeo ni chanya tutaangazia mbinu ambazo

zinaweza kuifanya sera hii iwe bora zaidi. Iwapo hakuna athari yoyote, itakuwa

bora ikiwa mikakati mingine ya kufanya sera hii ya lugha ya Kiswahili kubuniwa

ili umaarufu wake upatikane hasa katika urasmi wake miongoni mwa watumizi

wake.

1.7 Yaliyoandikwa Kuhusu Mada

Katika utafiti huu, mtafiti alieleza baadhi ya watafiti walioshughulikia sera ya

lugha na wale walioangazia utekelezaji wa sera hii ya lugha kwa kuangazia

changamoto na hali ya utekelezaji wake. Waandishi ambao wameshughulikia

swala la sera ya lugha nchini Kenya ni pamoja na Mbaabu (1996), Harries

(1968) kisha utekelezaji wa sera hii ya lugha ni Shitemi (2011). Waandishi

mbalimbali walitumiwa kuelezea chngamoto zinazokumba utekelezaji wa sera ya

Page 23: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

11

lugha, jinsi tunavyoweza kuimarisha sera mpya ya Kiswahili kuwa bora ili

kukidhi hadhi yake ya kuwa lugha rasmi na kuonyesha kiwango cha utayari wa

Wakenya katika utekelezaji wa lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi.

Kuna tafiti nyingi ambazo zimejihusisha na maswala haya lakini hakuna utafiti

ambao umejihusisha moja kwa moja na Utekelezaji wa sera ya lugha ya

Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya. Hata hivyo, utafiti huu

ulijishughulisha na wataalamu wengi iwezekanavyo ambao wamechangia kwa

njia moja au nyingine kuhusu suala la sera ya lugha au utekelezaji wa sera ya

lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi.

Kwa mujibu wa Sikma (1990), hadhi ya lugha hutegemea majukumu ambayo

lugha hiyo huyatekeleza katika jamii. Lugha inayowawezesha watu kuboresha

maisha yao hushikilia nafasi ya juu katika ngazi ya umuhimu wa lugha na ile

isiyotoa mchango wowote hudharauliwa. Lugha tofauti huwa na hadhi tofauti.

Anaendelea kwa kusema kuwa lugha ya wanajamii wengi hutazamwa kama

lugha bora. Hivyo, watu wana imani kuwa ina hadhi ya juu kijamii na kwa

kuitumia mzungumzaji hupata hadhi ya juu. Utafiti wa Sikma una uhusiano

mkubwa na utafiti huu kwa kuwa lugha ya Kiswahili ilifanywa kuwa lugha rasmi.

Mtafiti alitaka kubaini iwapo baada ya lugha ya Kiswahili kufanywa lugha rasmi

hadhi yake iliongezeka na hivyo kutekelezwa kwa kuongezewa majukumu zaidi.

Wasomi maarufu kama vile Charles Njonjo, aliyekuwa wakati mmoja mkuu wa

sheria, alitoa madai kuhusu lugha ya Kiswahili. Katika tafsiri ya Onyango

(1990), madai hayo ni ‘Kiswahili ni lugha ya mwananchi wa kawaida, si lugha ya

mtu kama mimi’. Onyango (1990) pia alishughulikia mielekeo ya wasomi

Page 24: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

12

kuhusu matumizi ya lugha ya Kiswahili. Matokeo yake yanabainika kuwa, wengi

wa wasomi hao nchini Kenya hawapendelei kutumia lugha ya Kiswahili,

wanapenda zaidi kutumia Kiingereza hasa katika miktadha rasmi. Hali hii

inafanya watu wengi kutotumia lugha hii ya Kiswahili. Akimnukuu Harries

(1968), anaendelea kwa kusema kuwa lugha ya mawasiliano kati ya watu wa

tabaka la chini na tabaka la juu ni Kiingereza. Hili linamaanisha kuwa hata baada

ya Kiswahili kutangazwa kuwa lugha ya taifa nchini Kenya, bado kinaendelea

kudunishwa na kupewa hadhi ya chini. Utafiti huu ulimsaidia mtafiti kwani

alifahamu ni kwa nini watu wengi hupuuza lugha ya Kiswahili na ni nini haswa

kinachoweza kufanywa ili utekelezaji wa lugha hii uwe katika kiwango

kinachohitajika.

Mbaabu (1996) ameshughulikia sera ya lugha katika Afrika Mashariki. Kulikuwa

na Kamati ya Kiswahili ya Afrika Mashariki – the Inter Territorial Language

(Swahili) Committee (ITLC) ambayo ilitilia mkazo sana lugha ya Kiswahili na

lugha hii iliinuliwa sana hasa katika miaka ya mwanzo mwanzo ya kamati hii.

Hata hivyo, mabadiliko kuhusu sera ya lugha yaliendelea hasa wakati wa

wakoloni pale ambapo lugha ya Kiswahili ilidunishwa na pahali pake

pakachukuliwa na Kiingereza. Baada ya vita vya pili vya dunia ufadhili

uliokuwepo na misaada iliyotolewa ilipungua; hili lilifanya umaarufu wa

Kiswahili kupungua. Wakoloni nao walihakikisha kwamba waliibua sera ambayo

iliifanya lugha ya Kiswahili kuwa na majukumu machache sana. Anaendelea kwa

kutoa mfano, Kiingereza kilikuzwa shuleni kwa kuadhibu wanafunzi

waliozungumza Kiswahili na lugha za kiasili. Akimnukuu Fasold, 1984 anaeleza

kuwa, ingawa sera ya lugha huundwa na kutekelezwa na serikali, hatua za

Page 25: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

13

kiserikali hufanikiwa zaidi iwapo zinaungwa mkono na mashirika yasiyo ya

kiserikali kama waandishi wa vitabu vya shule, waandishi binafsi na magazeti.

Kutokana na maoni ya Mbaabu, ni dhahiri kuwa mawazo haya yalisaidia katika

utafiti huu kwa kuwa serikali inaweza kuwa katika mstari wa mbele katika

utekelezaji na kuinua lugha fulani. Hivyo, kuna uwezekano kuwa iwapo serikali

itaungana na mashirika mengine yasiyo ya kiserikali utekelezaji wa sera hii mpya

utatekelezwa ipasavyo.

Mohochi (2002) amezungumzia kuhusu mchango wa vyombo vya habari katika

kuendeleza lugha ya Kiswahili kama vile radio, televisheni na magazeti.

Anaeleza kuwa kwa muda mrefu sana vyombo vya habari vya Afrika Mashariki

na vingine vya kigeni vimekuwa katika mstari wa mbele kukitumia Kiswahili.

Hata hivyo, vingi bado vinapendeleza lugha ya Kiingereza. Matangazo yake

hufanywa kwa lugha ya Kiingereza kwa wakati mwingi. Katika upande wa

magazeti nchini Kenya, magazeti mengi sana yamechapishwa kwa lugha ya

Kiingereza kwa mfano ni gazeti la ‘Daily Nation’, ‘The Standard’, ‘Peoples

Daily’ na moja tu ndilo la Kiswahili ambalo ni la “Taifa Leo”. Utafiti huu

ulimfaa mtafiti kwa kuwa aliweza kujua iwapo vyombo hivi vya habari

vinapendelea lugha ya Kiingereza hata baada ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha

rasmi. Je, mapendeleo haya yanaathiri vipi utayari katika utekelezaji wa sera ya

lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi. Hata hivyo, hakushughulikia utekelezaji

wa sera ya lugha ya Kiswahili jambo ambalo ni tofauti kati ya utafiti huu na

wake.

Page 26: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

14

Ali (2011) alifanya utafiti uliohusu Kiswahili kama Lugha rasmi. Aliangazia

changamoto zinazowakumba watu wanapowasiliana ofisini wakitumia Kiswahili

kama lugha rasmi. Alifanya utafiti wake katika ofisi mbili; moja ya kibinafsi na

nyingine ya umma katika eneo la Nairobi. Utafiti wake ulionyesha kuwa

matumizi ya lugha ya Kiswahili ni ya kiwango cha chini na waliohojiwa

walisema kuwa ni lugha iliyozungumzwa na watu wa tabaka la chini. Utafiti huu

ulitupa mwanga ya hali ya Kiswahili ilivyo katika shughuli za kiutawala. Hivyo

kubaini utayari wa Wakenya katika kutumia lugha ya Kiswahili kama lugha

rasmi.

Shitemi (2011) alieleza kuwa faida ya kutokana na uwepo wa tamko kuhusu

swala la lugha katika katiba mpya ya Kenya (2010). Hii ni kufuatia mapendekezo

ya tume ya marekebisho ya katiba, yanahitaji kudumishwa na kutekelezwa

ipasavyo. Tangazo la Kiswahili kuwa lugha ya kwanza rasmi na lugha ya taifa

linahitaji kuwekwa katika vitendo kimitaala, kiutendaji, kiuwezeshaji, na pia

katika asasi zote za kutumia lugha. Tangazo hilo linakabiliwa na changamoto za

kiutekelezaji katika usambazaji wa mbinu za utekelezaji na majukumu ya

Kiswahili katika sekta mbalimbali. Kuna uhusiano kati ya haya na utafiti huu kwa

kuwa mtafiti alitaka kubaini ni changamoto zipi ambazo zinakumba utayari

katika utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya.

Mbatiah (2012) anaeleza kuwa katika baada ya ukoloni kulikuwa na mikabala

hasi kuhusiana na Kiswahili. Hivi ni kusema kwamba walikuwa na kasumba ya

kiukoloni kiasi kwamba walikidharau Kiswahili na kupendelea Kiingereza.

Hawakuamini kuwa lugha ya Kiafrika kama Kiswahili ingeweza kutumika

Page 27: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

15

kutekeleza shughuli rasmi za kitaifa. Hali hii ni ya kutamausha sana kwa kuwa

inatajiriwa viongozi kama hawa ndio wanapaswa kuwa katika mstari wa mbele

katika kukikuza Kiswahili. Hii ni kuonyesha kuwa licha ya kuwepo kwa

mabadiliko ya sera ya lugha hii bado kuna Wakenya ambao wanaidunisha lugha

hii na kuinasibisha na wale walio katika kiwango cha chini. Utafiti huu ulilenga

kubaini iwapo hii ni mojawapo ya changamoto ambayo inakumba utekelezaji wa

sera ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi.

Kulingana na Hudon (2013) bunge lilihakikisha kuwa limeteua waziri na mkuu

wa fedha ambao wangewajibikia mambo mbalimbali kuhusiana na lugha hizi

rasmi. Mifumo hii ilihakikisha kuwa kuna haki ya wafanyikazi katika vituo

mbalimbali kutumia lugha yoyote waipendao kwa watu wanaowahudumia.

Serikali pia ilitoa nafasi sawa kwa watu wanaozungumza Kiingereza na

Kifaransa katika nchi hiyo.

Lugha hizi rasmi zilitekelezwa kwa njia zifuatazo; kwanza serikali ya Canada

ilijitolea katika kuhakikisha kuwa lugha hizi rasmi zimetekelezwa ipasavyo. Pia

ilitoa fedha katika vituo mbalimbali kuendeleza lugha hizi. Pili serikali imetoa

mwongozo jinsi utekelezaji wa lugha hizi unavyoweza kutumika katika sekta za

umma katika kuwahudumia watu. Tatu, waziri anayehusika na maswala ya lugha

aliweka mikakati ya lugha hizi ambayo inahusu masomo, maendeleo ya kijamii

na umma. Kupitia juhudi za waziri huyo, katika mwaka wa 2012 fedha zaidi

zilipangiwa kutolewa katika masomo ya lugha, viwanda vya lugha, maendeleo ya

kiuchumi, usaidizi katika jamii na kuimarisha uwililugha katika umma.

Page 28: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

16

Katika makala ya Osore na Midika (2016) nchi ya Kenya, Canada na Afrika

kusini yamejaribu kutekeleza sera ya lugha katika kufanya lugha mbalimbali

kuwa lugha rasmi. Kwa mfano nchini Canada sawa na Kenya kuna ukwasi wa

tamaduni tofauti ambapo kuna lugha nyingi ambazo hutumika. Nchini Canada

kuna lugha mbili rasmi Kifaransa na Kiingereza ambazo hutumika katika Quebec

na maeneo mengine ya Canada mtawalia. Hata hivyo, kuna lugha nyingine

ambazo pia hutumika ingawa lugha hizi si rasmi.Hali hii si tofauti sana na ile ya

humu nchini kwa kuwa lugha ya Kiiingereza na ile ya Kiswahili ni lugha rasmi

kwa mujibu wa Katiba ya mwaka wa 2010.

Nchini Canada sera ya lugha huongozwa na mifumo maalum ambayo husaidia

kuendeleza lugha hizi rasmi. Mifumo hii imechangia pakubwa katika kuhakikisha

kuwa lugha hizi zinazungumzwa. Changamoto ambayo ilidhihirika katika nchi

hii ni pale ambapo hakukuwa na mwelekeo wazi katika matumizi ya lugha ya

Kifaransa kule Quebec.

Tukiangazia sera ya lugha nchini Afrika Kusini utekelezaji wake pia

umetekelezwa na bunge kupitia njia zifuatazo; Kwanza mikoa mbalimbali

imechukua jukumu kuhusiana na lugha rasmi ambayo ina makala yanayoonyesha

lugha ambazo zinatambulikana kama lugha rasmi, pili, kuna makala kuhusu sera

ya lugha ambayo idara ya wizara ya utamaduni, sayansi na teknolojia huangazia

mambo halisi ya tafsiri na lugha ya teknolojia. Tatu, kuna asasi kumi na nne za

kitaifa kuhusiana na lugha ambazo zina majukumu ya kuangazia maendeleo ya

lugha. Kazi hii ni muhimu katika utafiti wetu kwa kuwa ilisaidia katika

Page 29: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

17

kuonyesha mambo mbalimbali tunayoweza kufanya ili kuimarisha lugha ya

Kiswahili na kuweza kutumika nchini Kenya.

Kutokana na wasomi mbalimbali kama vile Mbaabu, Shitemi, Mohochi, Osore

na Midika kuhusiana na swala hili la utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili, ni

dhahiri kuwa tafiti hizo zinahusiana kwa njia moja au nyingine na utafiti huu.

Hivyo basi, zina umuhimu katika kufanikisha utafiti huu wa utayari wa Wakenya

katika utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya.

Iwapo Kiswahili kitatumika katika kutekeleza majukumu ya kirasmi na katika

maeneo yote katika sera ya lugha, hali hii itaendelea kuipa lugha ya Kiswahili

nafasi na hadhi zaidi katika jamii na hili litarahisisha utekelezaji wa sera hii kwa

mujibu wa katiba iliyoidhinishwa katika mwaka wa 2010. Utafiti huu ulilenga

kutambua iwapo kuna utayari wa utekelezaji wa sera ya lugha ya Kiswahili

katika shughuli za kiutawala na vyombo vya habari kama lugha rasmi.

1.8 Misingi ya Nadharia

Ni muhimu kuelewa kwamba ili kutekeleza sera yoyote ya lugha sharti kuwe na

upangaji lugha. Mwanaisimu wa Kijerumani Heinz Kloss (1967, 1969) kama

anavyonukuliwa na Mesthrie (2000) anaeleza aina mbili za upangaji lugha

ambazo ni upangaji lugha wa kikongoo na upangaji wa kihadhi. Aina hizi mbili

ndizo zinazungumziwa pia na Ngugi na Chacha (2004). Upangaji wa kikongoo

ndio unahusu muundo wa lugha katika vipengele vya othografia, msamiati, hijai

na maendelezo ya sarufi. Upangaji wa kihadhi unahusishwa na uamuzi

unaozingatia majukumu ya kila lugha kulingana na maeneo : jimbo, mkoa au

Page 30: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

18

taifa. Huzingatia juhudi zinazochukuliwa ili kubadilisha matumizi na majukumu

ya lugha katika jamii, (Mesthrie, 2000).

Van Els (2005) anasema kuwa upangaji kikongoo unahusu uasili wa lugha ya

kufundisha. Shughuli hii inategemea mbinu na miktadha ya kiisimu lakini

ikizingatia mipaka yake katika upangaji kihadhi. Mafanikio na matokeo yake

huwa yanachangia sana kwa ufunzaji na ufundishaji wa lugha na huchangia

vilevile kuhusu umaarufu wa lugha katika jamii.

Mtazamo wa upangaji wa kihadhi ulifaa katika utafiti huu kwa kuwa unahusu

lugha kupewa majukumu mapya. Katika muktadha huu, lugha ya Kiswahili

imepewa hadhi mpya ya kuwa lugha rasmi nchini Kenya. Hii ni kumaanisha

kuwa lugha ya Kiswahili sawa na Kiingereza zinatambulikana kihalali katika

matumizi ya kisiasa na kitamaduni katika nchi ya Kenya.

Kutwika kwa jukumu mpya katika lugha ya Kiswahili kunahitaji mabadiliko ya

mfumo wa kiisimu kama vile kuzindua mitindo mipya na leksimu za maeneo

tofauti. Uzinduzi wa leksimu mpya katika lugha ni muhimu kwa kuwa

unaiwezesha lugha hiyo kufanikisha jukumu lake jipya. Mesthrie (2000)

anaeleza mtazamo wa upangaji lugha kifahari ni ule unaolenga kutoa mielekeo

chanya ya kisaikolojia ambayo ni muhimu ikiwa kutakuwepo na ufanisi wa muda

mrefu katika upangaji lugha. Upangaji kifahari huwa muhimu pale ambapo lugha

ambayo imeteuliwa huwa ya hadhi ya chini. Ili watu wakubali hadhi ya lugha

hiyo, kuna haja ya kuboresha na kuendeleza ufahari wa lugha hiyo na ndiyo

sababu upangaji kifahari hutangulia upangaji wa kihadhi. Naye Van Els (2005)

alitoa maoni yake akisema kuwa upangaji kifahari unahusu mambo matatu ya

Page 31: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

19

kuzingatiwa: kwanza kuna taswira ambayo inahusu ukabila au utambulisho wa

uraia na uendelezaji wa lugha kama ilivyokuwa katika jimbo la Quebec; pili

kuna taswira inayoelekea kueleza mbinu ya utekelezaji na urekebishaji wa sera ya

lugha na mwisho kuna taswira inahusiana na msukumo na shughuli za

watekelezaji wenyewe hasa hasa na jamii inayohusika.

Nadharia ya Utekelezaji ilishughulikia malengo tuliyojiwekea. Imeasisiwa na

watu mbalimbali wakiwemo Spencer (1971) na Durkheim. Spencer (1971)

anaeleza kuwa katika matumizi ya kawaida, kugawa vipande vinavyotokana na

kitu kimoja ni hatari. Kauli hii ya kweli kwa kuwa hatuwezi tenganisha lugha na

jami.. Hii ni kwa kuwa Kiswahili hakiwezi kutenganishwa na jamii yake ya

Kiafrika na badala yake kuingizwa kwa lugha za kigeni kama vile Kiingereza.

Nadharia ya utekelezaji hujumuisha weledi wa mfumo na viasilia vyake. Kila

kiasilia kina mchango unaoupa uhai mfumo ili uendelee kufanya kazi ama

kuukwamisha iwapo viasilia vitatenganishwa. Kila mfumo ni muungano wa

viasilia ambavyo huunda umbo fulani lionekalo. Kila jamii ni muundo wenye

viasilia vinavyohusiana na kufungamana kwa kipekee. Viasilia katika jamii ni

watu katika jamii na lugha wanayoitumia.

Kutokana na maelezo haya nchini Kenya lugha ya Kiswahili ingeweza kutumika

katika shughuli zote za kirasmi bila kupuuzwa lakini hakitumiwi katika shughuli

zote. Ingawa tunajua ukweli kwamba lugha hii inapaswa kutumiwa kama lugha

rasmi, hatutekelezi wajibu huu. Mbona ukweli hautumiki kwa mambo ambayo

yanafaa? Ili kuweza kuakisi matumizi ya lugha inavyohitajika ndipo tunahitaji

Page 32: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

20

kutafuta ukweli. Mjadala kuhusiana na nadharia hii ya utekelezaji unaungwa

mkono na wasomi wa leo kama Mbaabu (1996) na Mazrui (1995).

Hivyo ili mfumo fulani kuweza kuendelea kufanya kazi, kuna mambo ya

kimsingi ambayo yanaupa mfumo huo matokeo yanayofaa kama yafuatayo

i) Mawasiliano.

ii) Utambuzi wa pamoja juu ya umuhimu wa kila kipengele kinachounda

umbo fulani linalojadiliwa.

iii) Uzoefu wa ufungamano wa viasilia katika muundo au mfumo wa

jamii.

iv) Kuwepo kwa uhusiano kati ya mahitaji, uwezo na mazingira

yanayoshabihi mkabala (Ngigge, 2014)

Kupitia mitazamo na nadharia tulizozijadili hapo juu ni dhahiri kuwa nadharia hii

ilifaa katika utafiti huu. Ni muhimu hasa kwa kuzingatia shughuli za kutumia

lugha ambazo zinapaswa kutumiwa kwa minajili ya mawasiliano. Mitazamo ya

upangaji lugha ilitusaida katika utafiti huu kwa kutufahamisha jukumu jipya ya

kihadhi katika lugha ya Kswahili kisha katika ile ya utekelezaji ilifaa kwa

kushughulikia malengo yetu. Katika mapitio ya vitabu mbalimbali, kuhusiana na

matumizi mbalimbali ya lugha ya Kiswahili katika nchi za Afrika Mashariki

hususan Kenya, lugha hii imepewa majukumu ya lugha rasmi kwa mujibu wa

katiba iliyoidhinishwa 2010.

Page 33: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

21

1.9 Mbinu za Utafiti

Katika sehemu hii mtafiti alijadili njia za utafiti. Njia hizi za utafiti ziligawanywa

katika makundi manne: eneo la utafiti, uteuzi wa sampuli, ukusanyaji wa data na

uchanganuzi na uwasilishaji wa data. Kwa kuwa lugha ya Kiswahili inatumika

katika nchi nzima ya Kenya, utafiti huu ulifanywa katika kaunti ya Nairobi kwa

kuwa katika kaunti hii ndiko kuna ofisi nyingi za kiutawala na pia vyombo vingi

vya habari vinapatikana huko. Pili, kuna mtagusano wa watu wa jamii

mbalimbali zinazopatikana nchini Kenya na pia kuna wataalamu wa kila aina

wanaopatikana katika kaunti ya Nairobi. Sampuli iliyotumiwa ilikuwa kiwakilishi

mwafaka cha jumuiya katika kaunti ya Nairobi na Kenya kwa ujumla.

Waliohojiwa ni washikadau kama vile Kamati ya Nyachae ya ‘Commission on

the Implementation of the Constitution’ (Kamati ya Utekelezaji wa Katiba) katika

utekelezaji wa sera mpya ya lugha ya Kiswahili. Kamati zingine za bunge na

wizara ya utamaduni Utafiti huu ulifanywa katika Wizara ya Utamaduni, watu

waliohusika katika kamati ya Nyachae ambayo iliundwa ili kuhakikishwa

utekelezaji wa Katiba ya Kenya ya mwaka 2010 unatekelezwa ipasavyo; baadhi

ya majukumu yalikuwa ni, kufanya kazi na kamati ya Katiba kuhakikisha kuwa

Katiba inaheshimiwa; kutoa ripoti kila mara kwa kamati ya Utekelezaji wa

Katiba kuhusu maendeleo ya utekelezaji wa katiba, idara ya Polisi, vyombo vya

habari ambavyo ni ‘KBC’, ‘KTN’, ‘NTV’ na ‘Citizen’. Maeneo haya yataonyesha

vile ambavyo utayari wa Wakenya katika matumizi ya lugha ya Kiswahili kama

lugha rasmi yalivyo nchini Kenya, na kama kuna juhudi zozote katika kuimarisha

lugha hii kuwa bora zaidi.

Page 34: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

22

1.9.1 Eneo la Utafiti

Utafiti huu ulifanywa katika kaunti ya Nairobi ambao ni mji mkuu wa nchi ya

Kenya. Kaunti hii ina ofisi za kiutawala na kuna mashirika mbalimbali ya

vyombo vya habari. Utafiti huu ulimulika kaunti hii kwa kuwa huku ndiko kuna

ofisi nyingi za kiutawala na pia vyombo vya habari vimeenea huku. Jambo

lingine ni kuwa kuna wataalamu wa kila aina. Hili lilimwezesha mtafiti kuzuru

maeneo yaliyohitajika ili kupata habari msingi zilizosaidia katika utafiti huu.

1.9.2 Uteuzi wa Sampuli

Ili kuweza kupata kundi wakilishi katika jamii pana, utafiti huu ulitumia uteuzi

wa sampuli ya kimakusudi. Hatua hii ilimwezesha mtafiti kupata walengwa

binafsi ili kupata data hiyo. Mtafiti alitumia vibadala vine ambavyo ni elimu,

jinsia, umri na lugha ya mzungumzaji. Kitengo cha lugha kiligawanywa katika

vikundi viwili: Kiswahili na Kiingereza.

Mtafiti aliwahoji washiriki arobaini na wawili. Idadi hii ilizingatiwa kwa kuwa

iliwezesha mtafiti kupata data ya kina. Kila jinsia ilikuwa na watafitiwa ishirini

na mmoja. Mtafiti alichagua watafitiwa ishirini na mmoja katika kila idara

mbalimbali. Watafitiwa tano walifanyiwa mahojiano.

Page 35: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

23

Jedwali la 1.9.2.1: Mgao wa watafitiwa kutegemea vibadala vine: jinsia, elimu,

jinsia na lugha ya mzungumzaji katika sehemu zilizotafitiwa.

kiwango Idadi kiwango idadi kiwango idadi jumla

Jinsia kiume 21 Kike 21 42

Elimu stashahada 20 Shahada

ya kwanza

17 Shahada

ya

uzamili

5 42

Umri 25-35 15 35 na zaidi 27 42

Lugha ya

mzungumzaji

Kiswahili 27 Kiingereza 11 Lugha

mseto

4 42

Kutokana na jedwali la 1.9.2.1 , ni wazi kuwa uteuzi huu ulimsaidia mtafiti

kupata data isiyoegemea upande mmoja.

1.9.3 Ukusanyaji wa Data ya Utafiti

Hojaji na mahojiano ndizo njia mbili kuu zilizotumiwa katika utafiti huu. Mtafiti

alikusanya habari kuhusu taaluma ya mtafitiwa pamoja na matumizi yake ya

lugha. Hojaji ililenga maswali juu ya utayari wa Wakenya kuhusu utekelezaji wa

matumizi ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi na changamoto zinazokabiliwa

katika utayari huo. Hojaji hiyo ilikuwa na maswali funge na maswali wazi.

Katika hojaji funge mtafitiwa alihitajika kuchagua jibu kati ya majibu aliyopewa.

Hii ilimsaidia mtafiti katika kumwelekeza mtafitiwa kwenye jibu mahususi. Njia

hii ilimwezesha mtafitiwa kujaza hojaji haraka bila kuchoka

Page 36: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

24

Hojaji wazi ilimwezesha mtafitiwa kutoa maoni yake kuhusiana na kile

alichoulizwa hivyo mtafiti alipata maoni tofauti kuhusiana na jambo hilo.

Kutokana na hojaji kuwa na sehemu hizi mbili, mtafiti aliweza kupata data nzuri

ambayo aliweza kujua vyema jambo aliloliangazia.

Maswali na majibu yalitungwa kwa njia ambayo ilidhihirisha jinsi lugha ya

Kiswahili inavyoendelezwa kama lugha rasmi katika utekelezaji wake na pia

iliangazia changamoto za utaayari wa Wakenya kuhusiana na lugha ya

Kiswahili.. Maswali na majibu yalitungwa kwa kuzingatia vigezo vifuatavyo:

nia, matendo na athari kwa nyanja mbalimbali. Maswali pia yalijikita katika

vigezo vya mitazamo ya upangaji lugha, ambavyo vilimwongoza mtafitiwa

kutambua utayari wa utekelezaji wa sera hii mpya ya lugha ya Kiswahili kama

lugha rasmi.

Mahojiano yasiyo ya moja kwa moja yaliyofanyiwa watafitiwa yalilenga

kumwelekeza mtafiti kuhusu sera mpya ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi

hasa kuhusiana na jinsi sera hii inavyotekelezwa. Jambo hili lilimfaidi sana kwa

kuwa wahojiwa walitoa maelezo mengi na hivyo kupata habari muhimu.

Wengine walihojiwa moja kwa moja. Mwisho, mtafiti alisoma vitabu

vilivyohusiana na mada hii ili kuweza kuendeleza mada ipasavyo.

1.9.4 Uchanganuzi na Uwasilishaji wa Data

Baada ya data kukusanywa ilichanganuliwa kwa kutumia program ya SPSS

(Mtindo Changanuzi wa Tarakimu Sayansi) ili kuweza kupata matokeo mwafaka

na ya kuaminika. Mtindo changanuzi wa tarakimu sayansi ni program ya

kompyuta ambayo hutumiwa kuingiza data za utafiti na huchanganua data hizo za

Page 37: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

25

utafiti. Uchanganuzi huu pia ulifanywa kwa kuzingatia kipengee cha mitazamo

ya upangaji lugha. Vielelezo vya chati mraba na michoro pia vilitumika katika

uwasilishaji ili data iweze kueleweka kwa njia rahisi. Data iliyochanganuliwa,

ilikuwa imetokana na maswali ambayo watafitiwa walijibu.

1.9.5 Hitimisho

Katika sura hii ya kwanza, vipengele vya utafiti vilivyojadil;iwa ni: usuli wa

mada, suala la utafiti, maswali na malengo ya utafiti yaliyoongoza utafiti huu,

sababu za kuchagua mada, misingi na mihimili ya Nadharia ya Utekelezaji,

mbinu za utafiti kwa jumla zilizotumiwa katika utafiti huu na jinsi matokeo ya

utafiti huu yalivyokusanywa, kuchanganuliwa na kuwasilishwa.

Page 38: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

26

SURA YA PILI

HISTORIA YA UTAYARI WA WAKENYA KUHUSU URASMI

WA LUGHA YA KISWAHILI NCHINI KENYA.

2.0 Utangulizi

Utayari wa Wakenya kuhusu matumizi ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini

Kenya ni muhimu sana katika utafiti huu. Hii ni kwa kuwa kutokana na utayari

wao, lugha hii inaweza kutumika katika nyanja mbalimbali hasa katika shughuli

za kiutawala miongoni mwa wafanyakazi wa wizara za kiserikali na pia kutumika

katika vyombo vya habari. Katika kujadili historia ya utayari wa Wakenya

kuhusu Kiswahili, mtafiti aligawa historia hii katika vipindi viwili. Kipindi cha

kwanza ni kipindi cha ukoloni na kipindi cha pili ni kipindi cha baada ya ukoloni.

Lengo kuu la sura hii ni kubaini ni vipi utayari wa lugha ya Kiswahili kama lugha

rasmi umekuwa ukipokelewa kupitia vipindi tofauti kihistoria.

2.1 Kipindi cha Ukoloni

Kipindi hiki kimegawanywa katika sehemu tatu; Sehemu ya kwanza ni kipindi

kabla ya vita vikuu vya pili vya dunia, sehemu ya pili ni wakati wa vita vikuu vya

pili vya dunia na mwisho ni baada ya vita vikuu vya pili vya dunia.

2.1.1 Kipindi cha Kabla ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia

Katika kipindi hiki kulikuwa na wadau wengi waliochangia katika kuunda sera ya

lugha nchini Kenya. Miongoni mwa wadau hao walikuwa Wamishenari. Baadhi

yao walifikiria kuwa injili ingeenezwa vizuri kupitia lugha za kienyeji huku

wakisema Kiswahili kilikuwa kimefungamana sana na dini ya Kiislamu (Nabea,

2009). Kuna wale ambao waliona ni muhimu kutumia lugha ya Kiswahili kwani

ni lugha iliyokuwa imeenea sana miongoni mwa Wakenya.

Page 39: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

27

Kongamano la Umoja wa Wamishenari nchini Kenya (United Missionary

Conference) mwaka wa 1909 liliidhinisha matumizi ya lugha mama katika

madarasa matatu ya kwanza katika shule za msingi, Kiswahili katika madarasa

mawili ya kati katika shule za msingi na Kiingereza kilikuwa kitumike katika

madarasa yaliyosalia hadi chuo kikuu (Gorman, 1974).

Kwa upande wa wakoloni, wakoloni walipenda kuwafunza Waafrika Kiingereza

ili wapate wafanyakazi ambao wangewasaidia katika utawala wao. Waafrika

kufahamu Kiingereza ilikuwa hatua muhimu kwani mawasiliano kati ya Waafrika

na wakoloni yangekuwa na hitilafu. Kwa upande mwingine, walowezi walipinga

hoja ya kuwafunza Waafrika Kiingereza kwani waliona hali hiyo ingewafanya

Waafrika kuwa kama wao na wangetaka wafanye kazi za mapato ya chini.

Kutokana na maoni haya ni dhahiri kuwa lugha ya Kiswahili imekuwa na

changamoto tangu enzi za ukoloni. Utayari wa matumizi ya lugha ya Kiswahili

umepitia changamoto na hivyo hali ya wamishenari na wakoloni kuwafunza

Waafrika Kiingereza inaashiria kuwa lugha ya Kiswahili haikutambuliwa kuwa

yenye umuhimu. Ingekuwa bora iwapo wangesisitiza matumizi ya lugha

Kiswahili sawa na Kiingereza.

Kufikia mwaka wa 1924, kamati ya Phelps-Stoke ilizuru Kenya na walilalamikia

mzozo uliokuwa kati ya wamishenari, wakoloni na walowezi kuhusa sera ya

lugha (Mbaabu, 2007). Tume hiyo ilipendekeza kuwa lugha za kienyeji zitumiwe

kuwafunza wanafunzi shuleni na lugha ya Kiswahili itumike tu katika maeneo

ambayo ilikuwa lugha ya kwanza kama vile Pwani.

Page 40: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

28

Kupitia maoni haya, sera hii inaonyesha kuwa katika kipindi hiki kabla ya vita

vikuu vya pili, wakoloni, wamishenari na walowezi walikuwa na mwelekeo hasi

kuhusu lugha ya kiswahili ikilinganishwa na lugha za kienyeji na lugha ya

Kiingereza licha ya Kiswahili kuenea.

Walipendekeza kuwa lugha ya Kiingereza ifunzwe kuanzia madarasa ya juu

katika shule za upili hadi Chuo Kikuu. Tume hii iligundua kwamba ili wazazi

Waafrika wawapeleke watoto wao shuleni, shule hizo zilipaswa kufunza

Kiswahili kama kichocheo. Hii inadhihirisha kwamba Waafrika walikuwa tayari

kutumia lugha ya Kiswahili kama tu ingetumika katika shule hizo.

Hivyo, katika kipindi hiki inadhihirika kuwa utayari wa matumizi ya lugha ya

Kiswahili yalikuwa na changamoto sana.

2.1.2 Wakati wa Vita Vikuu vya Pili vya Dunia

Ni kipindi ambacho kilikuwa hatari kwa kuwa hakukuwa na usalama na hivyo

basi machache yalitekelezwa katika kipindi hiki kuhusu masuala ya lugha. Hata

hivyo, kuna baadhi ya sera za lugha zilizopendekezwa katika kipindi hiki kuhusu

lugha nchini Kenya ambazo zilikuwa ni kubalifu katika matumizi ya lugha ya

Kiswahili. Sera hizi ziliathiri utayari wa Wakenya kwa ujumla kuhusu Kiswahili.

Katika mwaka wa 1941, Kamati ya Mashauri kwa Mkoloni iliundwa ili

kuchunguza njia bora zaidi ya kuwafunza watu wote kusoma na kuandika.

Kamati hii ilipendekeza kusomeshwa kwa lugha za Kienyeji na Kiingereza

(Mbaabu, 2007). Hali hii ilikuza lugha ya Kiingereza na zile za Kienyeji na

hivyo lugha ya Kiswahili haikutiliwa mkazo.

Page 41: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

29

Mwaka wa 1942, tume ya Beecher iliundwa ili kushughulikia ufunzaji wa lugha

katika shule za Afrika. Waliandaa ripoti ambayo walipendekeza itumiwe baada

ya vita vikuu vya pili. Tume hiyo ilipendekeza kuwa kusomeshwa kwa lugha za

kienyeji kutiliwe mkazo na lugha ya Kiingereza ichukue nafasi ya Kiswahili

kama lugha ya mawasiliano nchini Kenya. Ripoti hii ilipinga matumizi ya

Kiswahili katika elimu na hivyo matumizi yake katika elimu yakakatizwa

(Mbaabu, 2007:102). Katika mwaka wa 1943, kumbukumbu ya ofisi ya mkoloni

kuhusu lugha katika shule za Waafrika ilitilia mkazo kusomeshwa kwa lugha ya

Kiingereza na lugha za Kienyeji.

Kupitia maoni haya inadhihirika kuwa matumizi ya lugha ya Kiswahili yalikuwa

katika kiwango cha chini. Utayari wa matumizi ya lugha hii haukutumika katika

hali zozote rasmi. Hivyo Kiswahili ilitumika kama lugha ya maongezi ya

kawaida. Msisitizo wa lugha ya Kiingereza kama lugha ya ufundishaji ulifanya

lugha ya Kiswahili kupuuzwa. Hivyo, Wakenya na wakoloni hawakuwa tayari na

hawakudhihirisha ukubalifu katika kutumia lugha ya Kiswahili.

2.1.3 Baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia

Baada ya vita vya pili vya dunia, kulikuwa na mabadiliko kuhusu sera ya lugha

mwaka wa 1948. Wakati wakoloni walipobaini wazi kuwa nchi ya Kenya ilikuwa

inaelekea kujinyakulia uhuru wake, wakoloni walianzisha harakati za kuwa na

kikundi cha wasomi nchini ambacho kingelinda maslahi yao baada ya uhuru.

Hatua hii kwa kiasi kikubwa iliimarisha lugha ya Kiingereza.

Page 42: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

30

Mbaabu (2007) anaeleza kwamba tume ya Beecher ilitoa ripoti ya pili ambayo

pia ilijulikana kwa jina la Ripoti ya Elimu ya Waafrika nchini Kenya mwaka 1949

ikifafanua mapendekezo ya mwaka wa 1942. Walipendekeza kuwa lugha ishirini

za kienyeji zitumike katika shule za msingi. Lugha hizo zilikuwa Kikamba,

Kikuyu, Kimeru, Kimaasai, Kitaveta, Kikisii, Kitende, Kiborana, Kipokomo,

Kijaluo, Kigiriama, Kigala, Kisagala, Kisuk, Kinandi, Kidabida, Kiteso,

Kiturkana, Kiluhya na Kisomali. Kufikia mwaka wa 1950, shirika la uchapishaji

la East Africa Literature Bureau liliagizwa lichapishe vitabu katika lugha hizo

ishirini zilizopendekezwa. Shirika hili halikuweza kuchapisha vitabu vingi vya

lugha hizo kwa sababu zilikuwa nyingi na kulikuwa na uhaba wa rasilimali.

Licha ya Kiswahili kupingwa, vitabu vya Kiswahili viliweza kuchapishwa na

kampuni hiyo. Hii inadhihirisha kuwa ingawa Kiswahili kilikumbwa na matatizo

hapa na pale bado kuna washika dau ambao walizingatia lugha hii kuenea.

Katika miaka ya 1950, wanafunzi wote nchini Kenya katika shule za msingi

walifunzwa kwa lugha zao za mama katika miaka minne ya kwanza nacho

Kiingereza kikafunzwa kama somo kwa miaka miwili kisha kikawa somo la

kufundishia kuanzia darasa la tano hadi la nane (Chimera 2000). Mwaka wa

1953- 1955, ripoti ya East Africa Royal Commission ilitaka lugha ya Kiingereza

ifunzwe kama somo na pia itumiwe kama lugha ya kufundishia kuanzia madarasa

ya chini. Ripoti hii iliendelea kusema kuwa ufunzaji wa lugha ya Kiswahili

ulikuwa ni upotezaji wa wakati na nguvu (Ngigge, 2014). Kufikia mwaka wa

1957, mabadiliko ya lugha ya kufundishia kutoka kwa lugha mama hadi lugha ya

Page 43: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

31

Kiingereza katika aina zote za shule yalikuwa na nguvu sana hivi kwamba

yalikuwa na athari ya kudumu katika sera ya lugha hata baada ya Kenya kupata

uhuru (Mbaabu, 1996). Kulikuwepo na Idara ya Ukaguzi iliyoanzishwa na

Wizara ya Elimu katika mwaka wa 1957 ili kuja na mbinu mpya ya kufundishia

lugha ya Kiingereza. Shule za Aga Khan zilikuwa zikitumia Kiingereza kama

lugha ya kusomeshea kuanzia darasa la kwanza. Ni mfumo ulioanzishwa mwaka

wa 1961 na kufikia mwaka wa 1962, shule zote za Nairobi zilikuwa zikitumia

Kiingereza kama lugha ya kusomeshea kuanzia darasa la kwanza.

Katika maoni haya, ripoti ya East Africa Royal Commission kusema kuwa

ufunzaji wa lugha ya Kiswahili ulikuwa ni kupoteza wakati na nguvu yalikuwa

potovu kwa kuwa hii ilikuwa lugha ya Waafrika hivyo ingesisitizwa miongoni

mwa Waafrika kama lugha moja kuu zikiwepo lugha zingine. Kupuuzwa kwa

lugha ya Kiswahili katika nyakati hizi zimechangia katika lugha ya Kiswahili

kutozingatiwa katika hadhi sawa na lugha ya Kiingereza katika hali ya sasa.

Nyandwaro (2015) anaeleza katika mwaka huo huo wa 1961, mitihani ya Kenya

African Preliminary Examination ya kuingilia shule za sekondari iliondolewa na

nafasi yake ikachukuliwa na Kenya Preliminary Examination. Lugha ya

Kiswahili iliondolewa kabisa na haikutahiniwa katika mtihani huo.

Lugha ya Kiingereza ilipata umaarufu sana. Waliopatikana shuleni wakiongea

lugha mama au Kiswahili ambayo ilikuwa lingua franca, waliadhibiwa (Mbaabu,

1996). Hali hii iliifanya lugha hii kustahimili kuwa lugha rasmi nchini Kenya

baada ya uhuru. Kiswahili kilitengwa na wakoloni ili kudhoofisha uwezo wake

Page 44: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

32

kama lugha ya kuwazindua Waafrika dhidi ya utawala wao (Mazrui & Mazrui

1995).

Katika kipindi hiki lugha ya Kiingereza ilienezwa katika shule hizo kama somo

na sio lugha ya kufundishia. Kulikuwa na shule chache sana za Waafrika. Katika

shule za upili za wakoloni, lugha ya Kiingereza ilitumika kama lugha ya kufunzia

na Waafrika ambao walifuzu kutoka shule hizo, walikuwa na misingi dhabiti ya

lugha hiyo. Hali hii ilileta utabaka wa kielimu kwa kuwa waliofuzu kutoka shule

za wakoloni walichukuliwa kuwa wasomi katika jamii. Hii inaonyesha kuwa

wakati huu athari ya wakoloni iliwafanya Waafrika kutozingatia lugha ya

Kiswahili na hivyo hawakuwa tayari kujifunza lugha hii. Kifuatacho ni kipindi

cha baada ya ukoloni.

2.2 Kipindi cha Baada ya Ukoloni

Katika kipindi hiki, hali ya lugha nchini Kenya inajadiliwa katika shughuli za

kiutawala hasa katika sekta ya umma na pia kibinafsi na vyombo vya habari huku

swala la utayari wa Wakenya kuhusu matumizi ya Kiswahili likizingatiwa.

Baada ya Kenya kupata uhuru mwaka wa 1963, lugha ya Kiingereza ilitangazwa

kuwa lugha rasmi. Ilikuwa itumike katika sekta zote za serikali ikiwemo elimu.

Lugha hii ilichukuliwa kama lugha ya wasomi na ilipewa hadhi ya juu kuliko

lugha ya Kiswahili katika mashirika mbalimbali. Chimerah (1998) anaeleza kuwa

nchini Kenya, makabila ambayo hayakuwa ya Kibantu yalipinga matumizi ya

Kiswahili kwa sababu waliona Kiswahili kimewabagua kimaendeleo hasa kabila

la Wajaluo. Viongozi wengi na wasomi wakati huo hawakutaka kujifunza

Kiswahili kikamilifu. Kiswahili kilitumika tu katika masuala yasiyo rasmi na

Page 45: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

33

wakati walitaka kuleta hali ya kusikizana miongoni mwa wananchi. Hali hii

ilionyesha kuwa kulikuwa na utayari wat matumizi ya lugha ya Kiswahili kwa

kiwango cha chini.

2.2.1 Shughuli za Kiutawala

i) Sekta ya Umma

Kufikia mwaka wa 1963 wakati Wakenya walipata uhuru, viongozi wengi

walikuwa wamejifunza na kuzungumza lugha ya Kiswahili vizuri. Walifanya

hivyo ili kuweza kuwasiliana na wanajamii wote. Kuna mswada uliopitishwa

bungeni kuwa lugha ya Kiswahili iweze kuwa lugha rasmi nchini Kenya katika

mwaka wa 1969, hatua hii haikupokelewa vyema kwa kuwa kuna baadhi ya watu

waliopinga na wale waliounga mkono. Walipinga lugha ya Kiswahili kwa

kusema kuwa kujifunza Kiswahili kulikuwa ni kupoteza wakati. Waliona kuwa

Kiswahili kingewatenganisha Wakenya ambao lugha yao ya kwanza haikuwa

Kiswahili na ujuzi wa lugha hii ulihitajika katika kazi duni.

Mbaabu (2007) anaeleza kuwa baadhi ya wale waliopinga ni G.G Kariuki

aliyesema kuwa Kiswahili ni lugha ya Kiarabu inayotumiwa na Waislamu katika

dini yao, naye Charles Njonjo ambaye alikuwa mwanasheria alipinga kwa

kusema kuwa ni lugha ya Kiarabu na ni lugha geni kama vile Kiingereza.

Maongezi haya yanadhihirisha kuwa baadhi ya watu hawakuwa tayari kutumia

lugha ya Kiswahili kama ilivyokuwa wakati wa ukoloni. Hakukuwepo na utayari

wa kutumia lugha ya Kiswahili na hali hii iliendelezwa na viongozi wa serikali.

Hata hivyo, kuna baadhi ya wabunge ambao waliunga mkono mswada kuwa

lugha ya Kiswahili iwe lugha rasmi, waliona kuwa ndio lugha pekee ambayo

Page 46: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

34

inawaleta pamoja Wakenya wanaotumia lugha tofauti tofauti. Walisema ni lugha

ya Kiafrika kinyume na Kiingereza ambayo ilikuwa lugha geni (Mbaabu, 1978)

Rais Jomo Kenyatta alikipenda Kiswahili na alitumia lugha hiyo katika

kuwahutubia wananchi. Kutokana na hali hii aliweza kupitisha miswada

mbalimbali bungeni ambayo ilikuza lugha ya Kiswahili. Katibu mkuu mtendaji

Robert Matano alitangaza mpango wa kuinua hadhi ya Kiswahili mwaka wa 1974

na serikali ilipanga kutekeleza mpango huo katika awamu mbili. Awamu ya

kwanza ilipaswa kutekelezwa mwaka wa 1971, ambapo ilihitajika Wakenya wote

wazungumze Kiswahili miongoni mwao na pia kwa wale ambao si Wakenya

katika shughuli rasmi na shughuli zisizo rasmi. Katika awamu ya pili walisema

kuwa lugha ya Kiswahili ndio lugha ambayo ingetekeleza shughuli zote rasmi

isipokuwa katika vyuo vikuu na korti (Mbaabu,1996). Anaendelea kwa kuelezea

kuwa, wafanyakazi wote wa serikali walipaswa kufanya mtihani wa Kiswahili na

kupita ili waweze kupandishwa cheo kazini. Wabunge walihitajika kujua

Kiswahili ili waweze kuwasiliana na wananchi. Vituo mbalimbali vya kufunza

Kiswahili vilijengwa katika kila mkoa ili Wakenya waweze kujifunza Kiswahili

kama ilivyopendekezwa na serikali.

Nyandwaro (2015) akimnukuu Mbaabu (1996) anaeleza kuwa, kuna mabadiliko

yaliyofanywa kwenye katiba ya awali kuhusu lugha. Kifungu cha 53 kilifanyiwa

mabadiliko pale ambapo lugha ya Kiswahili ilipewa hadhi mpya ya kuwa lugha

rasmi bungeni badala ya Kiingereza. Hali hii iliwakanganya wabunge kwani

walihitajika kufanya mitihani ya Kiingereza na wala sio Kiswahili. Kutokana na

Page 47: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

35

haya, mwaka wa 1975 Julai, marekebisho yalifanywa katika kifungu hicho hivyo

basi lugha ya Kiswahili na Kiingereza zikachaguliwa kuwa lugha rasmi za bunge.

Katika miaka ya 1990, viongozi walitoa hotuba zao katika lugha ya Kiswahili.

Jambo hili lilifanya Kiswahili kupata hadhi mpya pale ambapo kiliweza kutumika

katika siasa. Wanasiasa walitumia Kiswahili katika kuwasiliana na wananchi

hasa wakati wa uchaguzi. Hali hii si tofauti na sasa kwa kuwa wanasiasa

wanafanya hivi hadi sasa. Pia mijadala bungeni inafanywa kwa lugha ya

Kiswahili na Kiingereza.

Lugha ya Kiswahili kwa sasa inatumika hadi mashinani (Ryanga, 2001). Hii

inatokana na mfumo wa elimu kuwa kila mtu kutoka jamii yoyote anaweza

kutumia lugha ya Kiswahili.

Ni wazi kuwa nchini Kenya hivi leo kuna lugha mbili rasmi, Kiingereza na

Kiswahili. Hii ni kwa mujibu wa katiba ya Kenya ya sasa (2010) sura ya pili

kifungu cha 7 ibara (ii). Jambo hili linadhihirisha kuwa lugha ya Kiswahili

imepewa hadhi ya juu na serikali. Hivi sasa, Kiswahili chaweza kuwekwa katika

lugha pana za mawasiliano au lugha ya kimataifa kwa kuwa inatumika na

wazungumzaji wengi katika mataifa kumi na manne ya Afrika Mashariki na kati.

Lugha hii inatumika sambamba na Kiingereza katika shughuli za makanisa na pia

machifu na wasaidizi wa machifu hutumia Kiswahili wanapowahudumia

mashinani ambapo wengi hukifahamu Kiswahili kuliko Kiingereza.

Hutumika kutolea mafunzo katika taasisi za ualimu, taasisi za kutolea stashahada

na pia katika vyuo vyote vya umma na vingine vya kibinafsi. Chimerah (2000)

anaeleza kwamba Kiswahili hufunzwa kama lugha ya kigeni katika takriban vyuo

Page 48: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

36

mia moja kule Marekani na mataifa mengine ulimwenguni. Hatua zingine

ambazo lugha ya Kiswahili imepiga ni pamoja na toleo la kamusi ya Kiswahili –

Kiswahili.

Hutumika katika kutolea huduma za stakabadhi za serikali kwa kuwa

zimetafsiriwa kwa Kiswahili kwa mfano katika wizara ya uhamiaji na usajili wa

watu zimetafsiriwa kwa Kiswahili. Wizara ya afya ina maelezo ya Kiswahili

kama ya kuhusu magonjwa ya zinaa, Ukimwi na matibabu. Hutumika pia katika

ujazaji wa fomu za usafiri na pia kitambulisho cha kitaifa. Stakabadhi zingine ni

za vifo, ndoa pasipoti na vyeti vya kuzaliwa. Hali hii inaonyesha kuwa Kiswahili

kimekubalika miongoni mwa Wakenya kwa wakati huu ikilinganishwa na hapo

awali. Katika idara ya polisi na vikosi vyake, Kiswahili hutumika wakati wa

mawasiliano ya mdomo hasa wanapowahudumia wananchi. Hata hivyo,

wananchi wengi hukifahamu Kiswahili kutokana na hafla mbalimbali ambazo

huangazia matumizi ya Kiswahili.

Wananchi wengi wamekifahamu Kiswahili kutokana na hafla mbalimbali

ambazo huangazia matumizi ya Kiswahili katika ngazi za kitaifa na pia kimataifa.

Mfano mzuri ni ule wa Wakfu wa Jomo Kenyatta wa kutunza waandishi wa

vitabu vya Kiswahili (Ngigge, 2014). Hali hii ilichangia kuandikwa kwa vitabu

vingi na tuzo nyingi zikapatikana.

Katika makongamano yanayoandaliwa na chama cha Kiswahili, lugha ya

Kiswahili imekuwa ikitumika na hii imechangia kuimarika kwake. Kumekuwepo

na tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanywa, hasa baada ya Kiswahili kufanywa

lugha rasmi ili kutafuta njia za kuifanya ikidhi mahitaji ya lugha rasmi. Hata

Page 49: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

37

hivyo, wasomi wameweza kuonyesha mtazamo kubalifu kuhusu Kiswahili. Hatua

kama hizi bila shaka zitaendelea kuendeleza hadhi zote mbili za Kiswahili na pia

kujenga utayari wake kimatumizi miongoni mwa wakenya.

ii) Vyombo vya Habari

Vyombo vya habari vimesaidia kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili katika

viwango mbalimbali nchini Kenya. Kwa sasa Kiswahili kinatumika katika

mashirika ya utangazaji ndani na nje ya Kenya (Ngigge, 2014). Katika

televisheni tuna vipindi ambavyo hutumia Kiswahili. Taarifa za habari za

Kiswahili husomwa saa moja jioni katika kila kituo cha runinga na saa kumi

alasiri katika runinga ya KBC, Citizen, NTV, na KTN. Kuna vipindi mbalimbali

ambavyo hupeperushwa kwa lugha ya Kiswahili, vipindi kama ‘Inspekta Mwala’

na Machachari katika kituo cha Citizen. Hii ni kuonyesha kuwa lugha hii

inakubalika ingawa si kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na ile ya Kiingereza.

Katika redio kuna idhaa mbalimbali za redio ambazo hupeperusha vipindi,

matangazo na habari kwa lugha ya Kiswahili. Idhaa hizi za Kiswahili husikilizwa

na watu wengi hasa watu wa mashambani na hupeperusha vipindi

vinavyowaelimisha wananchi na pia kuwaburudisha. Idhaa hizi ni kama vile

idhaa ya Taifa, Redio Citizen, Redio Milele, Redio Maisha, Redio Jambo na Q-

fm. Katika Redio Citizen kuna kipindi ambacho watangazaji hutoa mijadala na

michango ya lugha ya Kiswahili. Kipindi hicho hutoa mafunzo mengi kwa

wasikilizaji wake hasa wanafunzi na wasomi wa Kiswahili.

Kuna gazeti la ‘Taifa Leo’ ambalo ndilo gazeti pekee linalochapishwa katika

lugha ya Kiswahili. Gazeti hili huwa limegawanywa katika sehemu mbalimbali

Page 50: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

38

kama vile taarifa za spoti, taarifa ya nchi na kimataifa, dondoo za hapa na pale,

shindano la uandishi wa insha, sehemu ya fasihi ambapo waandishi mbalimbali

huandika makala yao wakitoa michango mbalimbali kuhusiana na mambo tofauti

na kisha sehemu ya sokomoko ambapo mashairi huchapishwa.

Hata ingawa vyombo hivi vya habari vinaendeleza lugha ya Kiswahili na

kuonyesha ukubalifu miongoni mwa wananchi, bado si watu wote ambao

wanadhihirisha ukubalifu huu. Hii ni kwa kuwa kuna baadhi ya vipindi ambavyo

vinadhihirisha utabaka pale ambapo maonyesho katika vipindi hutumia lugha ya

Kiingereza hasa kule ofisini katika sehemu ya wafanyakazi ambao wanafanya

kazi za hadhi ya chini kama mayaya; waajiriwa wao huwasiliana nao kwa lugha

ya Kiswahili.

2.3 Hitimisho

Kutokana na maelezo ya sura hii, ni wazi kwamba lugha ya Kiswahili imeweza

kuwa na ukubalifu tofauti kulingana na hali tofauti tofauti. Katika kipindi cha

ukoloni, Kiswahili hakikukubalika na wakoloni na Wakenya waliona ni lugha

ambayo haingewafaa kimaendeleo. Baada ya ukoloni, lugha hii ilianza

kukubalika kutokana na sera mbalimbali zilizowekwa na serikali na sasa ni lugha

rasmi. Hii ilikuwa hatua muhimu kwa kuwa sasa watu wamekubali kutumia

lugha hii katika sehemu mbalimbali ijapokuwa bado haitumiki kila mahali.

Page 51: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

39

SURA YA TATU

UTAYARI WA WAKENYA KATIKA SERA MPYA YA

KISWAHILI

3.0 Utangulizi

Katika sura ya pili, tumejadili Historia ya utayari wa Wakenya hasa kuhusiana na

sera ya urasmi wa lugha ya Kiswahili nchini Kenya. Sura hiyo ilionyesha utayari

wa Wakenya wanavyotumia lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi na pia

matumizi yao kimaongezi. Katika sura hii ya tatu, lengo lililojadiliwa lilionyesha

utayari wa Wakenya katika kutumia Kiswahili ili kuimarisha lugha ya Kiswahili

kama lugha rasmi. Katika utafiti huu, kuna vigezo mbalimbali ambavyo

vilitumiwa ili kusaidia katika uchanganuzi wa data hili kuonyesha jinsi ambavyo

utayari wa Wakenya katika matumizi ya Kiswahili ulivyo, kwa mujibu wa

mtazamo wa upangaji wa lugha kihadhi. Upangaji lugha ni swala muhimu hasa

tukizingatia katika sera ya Kiswahili, ambapo tunahitaji Kiswahili kitumike kama

lugha rasmi.

3.1 Uchanganuzi wa kauli za utayari wa Wakenya katika sera mpya ya

Kiswahili katika

kuimarisha lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi.

Changanuzi hizi zilionyesha jinsi washiriki walivyotoa majibu yao kuhusiana na

utayari wao katika matumizi ya lugha ya kiswahili. Matokeo ni kama ifuatavyo

Page 52: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

40

Jedwali 3.1.1: Lugha ambayo wafanyikazi wanapenda kuitumia sana katika

mawasiliano ya kimaongezi

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Kiswahili 27 64.3

Kiingereza 11 26.2

Lugha mseto 4 9.5

Jumla 42 100

Chati 3.1.1: Lugha inayotumiwa sana na wafanyikazi katika mawasiliano ya

kimaongezi

Watafitiwa arobaini na wawili (42) walijibu swali hili. Watafitiwa ishirini na saba

ambao ni asilimia 64.3 walisema wanapenda kutumia lugha ya Kiswahili,

watafitiwa kumi na mmoja ambao ni asilimia 26.2 walisema wanapenda kutumia

lugha ya Kiingereza, watafitiwa wanne ambao ni asilimia 10 walisema

wanapenda kutumia lugha mseto. Katika uchanganuzi huo, ilidhihirika kuwa

64%

26%

10%

0%

Kiswahili

Kiingereza

Page 53: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

41

asilimia kubwa ya watafitiwa ambao walipenda kutumia lugha ya Kiswahili

katika maongezi yao ya kila siku walikuwa na miaka thelathini na tano (35) na

zaidi, wengi wao walitoka katika idara ya polisi. Waliopenda kutumia

Kiingereza walitoka katika sekta ya utamaduni na vyombo vya habari.

Ilidhihirika wazi kuwa Kiswahili kilitumika tu katika vitengo vichache katika

sekta ya utangazaji. Aidha, jinsia ya kike ilionekana sana kupendelea kutumia

lugha ya Kiingereza sana kuliko lugha ya Kiswahili. Hata hivyo, lugha mseto

ambayo ni mchanganyiko wa lugha ya Kiswahili na Kiingereza vilevile ilitumika.

Matumizi ya Kiswahili katika idara ya Polisi yalionekana kutumika sana,

walisema kuwa Wananchi wengi walijieleza kwa lugha hii na hivyo kwa wakati

mwingi lugha hiyo ndiyo iliyotumika. Lugha hii imeonekana kutumika kwa

wingi katika maongezi lakini bado haijakita mizizi kama lugha rasmi kama

ilivyoidhinishwa kikatiba. Sababu ni kuwa, watu wengi bado wanaichukulia

kuwa ni ya hadhi ya chini. Hii ni kuonyesha kuwa lugha hii bado haijafikia

kiwango cha urasmi. Kwa mujibu wa mtazamo wa upangaji lugha kihadhi,

huzingatia juhudi zinazochukuliwa ili kubadilisha matumizi na majukumu ya

lugha katika jamii. Hali ndiyo hii nchini Kenya ambapo lugha ya Kiswahili

inatumika lakini si kwa misingi ya kama lugha rasmi kwa wingi katika

mawasiliano.

Swali lililofuata lililenga kuelezea ni kwa nini wao hutumia lugha hiyo ya

mawasiliano. Jibu hilo limeonyeshwa katika jedwali na chati

Page 54: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

42

Jedwali 3.1.2 : Sababu zinazowafanya kutumia Kiswahili

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Ni lugha ya taifa 6 22.2

Hutumiwa na matabaka

mbalimbali kurahisisha

mawasiliano

3 11.1

Ni rahisi kueleweka 18 66.7

Jumla 27 100

Chati 3.1.2: Sababu za kutumia Kiswahili

Watafitiwa waliosema kuwa huzungumza lugha ya Kiswahili walikuwa 27. Kati

ya hao 27, asilimia 66.7 walisema kuwa lugha ya Kiswahili ni rahisi kueleweka

na kuzungumza. Watafitiwa 6, ambao ni asilimia 22.1 walisema lugha ya

Kiswahili ni lugha ya taifa. Watafitiwa 3 wakiwakilisha asilimia 11.1 walisema

kuwa wao hutumia lugha ya Kiswahili kwa kuwa hutumiwa na matabaka

mbalimbali kurahisisha mawasiliano.

22%

11%

67%

0%

Ni lugha ya Taifa

Hutumiwa na matabaka mbalimbali

Ni rahisi kueleweka

Page 55: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

43

Kutokana na maelezo haya, lugha ya Kiswahili inatumika sana kutokana na

kueleweka kwake kwa urahisi.

Jambo hili huenda limetokana na mazoea ya watu kutumia lugha hii katika

mawasiliano yao ya kila siku na pia lugha hii ina asili ya Afrika hasa Afrika

Mashariki. Kwa kuwa Kiswahili ni lugha yenye asili ya Kibantu, watu wengi

hujihusisha nayo.

Kutokana na historia fupi tuliyoitoa katika sura ya pili, kumedhihirika ukubalifu

wa sera hii miongoni mwa Wakenya pale ambapo wameweza kuitumia katika

shughuli zao. Ukubalifu huu unadhihirisha kuwa lugha hii wanaiona rahisi na

inaeleweka. Hata hivyo, lugha ya Kiingereza hutumika katika miktadha rasmi

ilhali katika kimaongezi lugha ya Kiswahili ndio inayotumika kwa wingi zaidi.

Jedwali 3.1.3: Sababu zinazowafanya kutumia lugha ya Kiingereza

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Ina hadhi ya juu 3 27.3

Ni rahisi kujieleza 7 63.6

Ni lugha rasmi 1 9.1

Jumla 11 100

Page 56: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

44

Chati 3.1.3: Sababu za kutumia lugha ya Kiingereza

Waliosema kuwa hutumia lugha ya Kiingereza, asilimia 63.6 walisema kuwa ni

lugha rahisi katika mazungumzo yao wanapojieleza. Asilimia 27.3 walisema

kwamba lugha ya Kiingereza ni lugha ya hadhi ya juu. Asilimia 9.1 walisema

wao hutumia lugha ya Kiingereza kwa kuwa ni lugha rasmi na kwa njia hiyo

kunadhihirika kuwa lugha hii bado inaonekana kuwa na umaarufu.

Maelezo haya yanaonyesha kuwa lugha hii ni rahisi katika mazungumzo ya

watumiaji wake wakati wanapojieleza katika miktadha mbalimbali. Hali hii

inadhihirisha kuwa lugha ya Kiswahili bado haijafaulu katika hadhi yake ya kuwa

lugha rasmi, na hivyo bado Wakenya hawajaweza kuitumia lugha hii kikamilifu.

Hii ni kwa kuwa lugha ya Kiingereza imetiliwa mkazo na kutumika sana katika

sekta nyingi sana hapa nchini, ikilinganishwa na lugha ya Kiswahili ambayo

27%

64%

9%

0%

Ina hadhi ya juu

Ni rahisi kujieleza

Nilugha rasmi

Page 57: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

45

hutumika kama lugha ya mawasiliano pekee. Lugha hii ilionekana kukita mizizi

katika matumizi yake hasa katika vyombo vya habari pale ambapo katika vitengo

vya utangazaji. Watu wengi waliotumia lugha ya Kiingereza walieleza kuwa

katika vitengo vyao hakukuwepo na istilahi mwafaka zilizowawezesha kutumia

Kiswahili hivyo wao walipendelea kutumia lugha ya Kiingereza. Kwa kurejelea

nadharia ya Utekelezaji mambo ya kimsingi ambayo nadharia hii huzingatia ni

mawasiliano. Ijapokuwa tunatambua kuwa lugha ya Kiswahili inaweza kutumiwa

katika miktadha rasmi, Wakenya wengi hawafuati kauli hii. Ili kuweza kuwa na

matokeo yananyofaa sharti tuzingatie mifumo inayofaa.

Swali lingine lililenga kutathmini matumizi ya lugha ya Kiswahili kabla ya

kuidhinishwa kwa katiba mpya. Majibu ya swali hili yameonyeshwa katika

jedwali lifuatalo

Jedwali 3.1.4: Matumizi ya lugha ya Kiswahili kabla ya kuidhinishwa kwa

katiba

mwaka wa 2010

Maelezo Idadi ta Watafitiwa Asilimia

Mazuri 13 31

Mazuri kiasi 21 50

Mabaya 8 19

Jumla 42 100

Page 58: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

46

Chati 3.1.4: Matumizi ya Kiswahili kabla ya kuidhinishwa kwa katiba

mwaka wa 2010

Swali hili lilijibiwa na watafitiwa wote 42. Watafitiwa ishirini na mmoja ambao

ni asilimia 50 walisema kuwa matumizi ya lugha hii yalikuwa mazuri kiasi. Hii ni

nusu ya watafitiwa waliohojiwa. Watafitiwa 13 ambao ni asilimia 31 walisema

kuwa matumizi ya sera hii ya lugha kabla ya katiba kuidhinishwa yalikuwa

mazuri, ilhali watafitiwa 8 ambao ni asilimia 19 wakasema yalikuwa mabaya.

Kutokana na waliotafitiwa, matokeo yao yanaonyesha kuwa, matumizi ya

Kiswahili kabla ya katiba ya 2010 yalikuwa mazuri kiasi. Hii ni kuonyesha kuwa

Kiswahili kilitumika kama lugha rasmi ingawa kwa kiwango kidogo sana. Hivyo,

hungeweza kujieleza kwa lugha hii katika miktadha rasmi na hivyo lugha hii

kihadhi ilikuwa lugha ya taifa pekee. Asilimia 19 ambayo ilisema kuwa matumizi

ya Kiswahili yalikuwa mabaya kabla kuidhinishwa kwa katiba 2010, inaweza

kuelezwa kwa misingi kuwa iwapo mtu angejieleza kwa lugha hii katika ofisi za

31%

50%

19%

0%

Mazuri

Mazuri kiasi

Mabaya

Page 59: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

47

umma hangepuuzwa hivyo, hali hii inaonyesha hali ya matumizi ya lugha hii

yalivyokuwa. Hata hivyo, kuna wale walioona kuwa matumizi ya lugha ya

Kiswahili yalikuwa yakitumika vizuri.

Swali lililofuatia lilinuia kutathmini mabadiliko ya utekelezaji wa sera hii baada

ya kuidhinishwa kwa katiba mwaka wa 2010. Majibu ya swali hilo

yameonyeshwa katika jedwali lifuatalo

Jedwali 3.1.5: Mabadiliko ya utekelezaji wa sera hii baada ya kuidhinishwa

kwa katiba

mwaka wa 2010

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Mazuri Sana 11 26.2

Mazuri 19 45.2

Mazuri kiasi 4 9.5

Hayajabadilika 8 19.1

Jumla 42 100

Page 60: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

48

Chati 3.1.5: Mabadiliko ya sera hii baada ya kuidhinishwa kwa katiba

mwaka wa 2010

Watafitiwa wote 42 walijibu swali hili, hii ikiwa ni asilimia 100 ya watafitiwa.

Asilimia kubwa ya waliotafitiwa walibaini kuwa mabadiliko ya utekelezaji wa

sera ya Kiswahili yalikuwa mazuri. Hii ilikuwa ni watafitiwa kumi na tisa ambao

ni asilimia 45.2 ya waliohojiwa. Watafitiwa kumi na mmoja ambao ni asilimia

26.2 walisema kuwa mabadiliko hayo yalikuwa mazuri sana, watafitiwa wanane

ambao ni asilimia 19.1 wakasema kuwa hakukuwa na mabadiliko yoyote ilhali

asilimia 9.5 wakasema kuwa mabadiliko hayo yalikuwa mazuri kiasi.

Kwa mujibu wa mtazamo wa upangaji lugha kihadhi, ili lugha kubadilisha

matumizi na majukumu yake katika jamii, sharti kuwe na juhudi fulani

zinazowekwa ili mabadiliko hayo kufikiwa. Haya ndiyo yanayojitokeza.

Kiswahili kilipata mabadiliko ya kihadhi baada ya katiba ya 2010 kuidhinishwa.

Lugha huweza kuimarika kwa watumiaji wake iwapo; majukumu yake

26%

45%

10%

19%

Mazuri sana

Mazuri

Mazuri kiasi

Hayajabadilika

Page 61: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

49

yanaongezeka kwa kuwa huwa kuna manufaa kwa watumiaji hao hasa ikiwa

lugha hiyo inapewa hadhi ya juu. Kufanywa kwa Kiswahili kuwa lugha rasmi,

kuliwafanya watafitiwa wengi kukubali kutumia lugha hii na kuitumia kwa wingi

huku wakiwa na matarajio kuwa lugha hii ingewafaa zaidi na kujipatia umaarufu.

Kutokana na majibu hayo, ni wazi kuwa kuna kundi la waliotafitiwa ambao

hawakuona mabadiliko yoyote katika sera ya Kiswahili baada ya kuidhinishwa

kwa katiba mpya ya 2010. Kikundi hiki kilitoa maoni haya kwa misingi kuwa,

Kiswahili bado hakikupata ukubalifu miongoni mwao na hivyo bado walisita

kutumia lugha hiyo, aidha baadhi yao walisema kuwa hakukuwa na mikakati

kabambe ya kutekeleza Kiswahili kuchukua mahali pake pa kuwa lugha rasmi.

Hata hivyo, kuna wale waliosema kuwa kulikuwa na mabadiliko ya sera ya

Kiswahilli na yalichangia lugha hii kukubalika na kupokelewa vyema kama

lugha rasmi. Ni wazi kuwa mabadiliko haya yalikubaliwa kwani hakuna

aliyesema kuwa alikichukia Kiswahili zaidi baada ya kuidhinishwa kwa katiba ya

mwaka wa 2010. Hii inaonyesha kuwa majukumu mapya yaliyopewa lugha ya

Kiswahili yalipokelewa vyema.

Swali lililofuatia lililenga kuonyesha sababu zilizowafanya wale waliosema kuwa

hakuna mabadiliko ya sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi

Page 62: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

50

Jedwali 3.1.6: Sababu za waliosema kuwa hakuna mabadiliko ya sera ya

lugha ya

Kiswahili kama lugha rasmi

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Ukosefu wa mikakati

mwafaka katika sekta zao

5 58.1

Uhaba wa istilahi katika

Nyanja mbalimbali

2 27.50

Ukosefu wa vifaa

muhimu vya kuinua

lugha ya Kiswahili

1 14.4

Jumla 8 100

Watafitiwa 5 ambao ni asilimia 58.1 ya waliotafitiwa walisema kuwa hakuna

mabadiliko katika sera ya Kiswahili kama lugha rasmi walieleza kuwa hakuna

mikakati yoyote katika sekta wanazofanya kazi. Hata hivyo, ilibainika wazi kuwa

katika sekta ya utangazaji baadhi ya waliohojiwa walisema kuwa hawakujua

kuwa lugha ya Kiswahili ilipata hadhi mpya ya kuwa lugha rasmi. Watafitiwa 2

ambao ni asilimia 27.50 yao walisema kuwa hakuna istilahi za kutosha ili kukidhi

mabadiliko na ukuaji wa teknolojia ilhali mtafitiwa mmoja ambaye ni asilimia

14.4 alieleza kuwa Kiswahili kina ukosefu wa vifaa muhimu kama vile vitabu na

majarida ya kutosha ili kuiinua lugha ya Kiswahili.

Swali hilo lililenga wale ambao hawakuona mabadiliko yoyote katika mabadiliko

ya sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi baada ya kuidhinishwa kwa

katiba ya 2010. Matokeo ya swali hilo yanadhihirisha kuwa hakukuwa na

mikakati yoyote ya kukifanya Kiswahili kuwa bora. Hali hii inawafanya wao

Page 63: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

51

kuona lugha hii kama haina manufaa na kwa misingi hii, lugha hii haijapokelewa

vyema kwa kuwa iwapo hakuna utekelezaji au ukiwa wa hali ya chini

hakutakuwa na mabadiliko yanayofaa.

3.2: Kuimarika kwa Lugha ya Kiswahili

Sehemu hii ya utafiti ililenga kuchunguza iwapo mabadiliko ya Kikatiba kuhusu

hadhi mpya ya lugha ya Kiswahili nchini Kenya imeimarika. Mabadiliko

yaliyolengwa ni yale yaliyofanywa mnamo mwaka wa 2010. Maswali

yaliyoulizwa yalilenga kumwelekeza mtafitiwa kutoa majibu ambayo

yangemsaidia mtafiti kufikia lengo hilo.

Swali la kwanza katika sehemu hii lililenga kutambua kuimarika au kutoimarika

kwa hadhi mpya ya lugha ya Kiswahili baada ya kuidhinishwa kwa katiba ya

2010. Majibu ya swali hilo yameonyeshwa kama ifuatavyo

Jedwali 3. 2. 1: Sera mpya ya Kiswahili huimarisha hadhi yake ya kirasmi

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Ndio 23 54.8

La 19 45.2

Jumla 42 100

Page 64: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

52

Chati 3.2.1: Sera mpya ya Kiswahili huimarisha hadhi yake ya Kiswahili

Watafitiwa ishirini na watatu ambao ni asilimia 54.8 walikubali kuwa Kiswahili

kwa hakika kilikuwa kimeimarika zaidi tangu kuidhinishwa kwa katiba mpya ya

2010 kuwa lugha rasmi. Watafitiwa kumi na tisa ambao ni asilimia 45.2 ya

walieleza kuwa Kiswahili hakikuwa kimeimarika hata baada ya kuidhinishwa

kwa katiba ya 2010 kuhusiana na hadhi yake ya kuwa lugha rasmi.

Kwa mujibu wa washiriki wanaonyesha wazi kuwa Kiswahili kimeimarika na

kuwa lugha rasmi zaidi tangu kuidhinishwa kwake. Uimarikaji huu unatokana na

matarajio makuu ambayo watafitiwa wanayo. Lugha inapoinuka kihadhi watu

wengi hutaka kufaidika kutokana nayo na pia wanaionea fahari

wanapoizungumza. Hali hii mpya ya Kiswahili iliwafanya watafitiwa kuhisi

kwamba Kiswahili kitawafaa watu wengi kwa njia mbalimbali.

Swali lilofuatia lililenga watafitiwa kuelezea sababu moja kuu ya jibu

walilolichagua katika swali la (3.2.1). Majibu yake ni kama ifuatavyo

55%

45%

0% 0%

Ndio

La

Page 65: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

53

Jedwali 3.2.2: Sababu zinazofanya Kiswahili kuimarika kama lugha rasmi

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Kutumiwa katika ofisi

mbalimbali za serikali

3 13.0

Kutumiwa katika

shughuli za kitaifa

3 13.0

Watu wengi hutumia

lugha hii

15 65.2

Kutumika katika sekta ya

utangazaji

2 8.7

Jumla 23 100

Chati 3.2.2: Sababu za Kiswahili kuimarika kama lugha rasmi

13%

13%

65%

9%

kutumiwa katika ofisi mbalimbali za serikali

kutumiwa katika shughuli za kitaifa

watu wengi kutumia lugha hii

kutumika katika sekta ya utangazaji

Page 66: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

54

Waliosema kuwa lugha ya Kiswahili imeimarika kama lugha rasmi walitoa

sababu zao huku watafitiwa 15 ambao ni asilimia 65.2 ya wakisema kuwa watu

wengi katika sekta zilizotafitiwa walitumia lugha hii ikilinganishwa na hapo

awali ambapo lugha hii haingetumika katika miktadha rasmi hasa katika ofisi

zao. Watafitiwa 3 ambao ni asilimia 13 walidai kuwa lugha hii ilitumika katika

shughuli za kitaifa mfano ni pale ambapo lugha ya Kiswahili sasa inatumika

katika sherehe za Kitaifa na halfa mbalimbali kukiwepo na makongamano

ambayo yanaendeshwa kwa lugha ya Kiswahili hivyo lugha hii imeimarika kama

lugha rasmi.

Watafitiwa 3 ambao ni asilimia 13 walieleza kuwa lugha hii imetumiwa katika

ofisi mbalimbali za Kiserikali. Hii ni kuonyesha kuwa kuna ukubalifu ingawa

matarajio ni kwamba asilimia hiyo ingekuwa bora iwapo ingekuwa ya juu zaidi.

Mtafiti mmoja ambaye ni asilimia 8.7 ya waliotafitiwa alieleza kuwa Kiswahili

kiliweza kutumika katika sekta ya utangazaji kwa kuwa idadi ya vipindi

vilivyotumia lugha ya Kiswahili vilikuwa vimeongezeka ikilinganishwa na hapo

awali.

Mtafiti pia alinuia kujua sababu za watafitiwa kusema kuwa Kiswahili

hakijaimarika kirasmi. Baadhi ya sababu zilizotolewa na watafitiwa

zimefafanuliwa katika kauli la (3.2.3)

Page 67: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

55

Jedwali 3.2.3: Sababu zinazofanya Kiswahili kutoimarika kama lugha rasmi

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Matumizi ya lugha ya

sheng

3 15.8

Ukosefu wa serikali

kuendeleza shughuli za

kukuza Kiswahili kama

lugha rasmi

8 42.1

Lugha ya Kiingereza

bado kutumika sana

katika nyanja mbalimbali

3 15.8

Stakabadhi nyingi

zinapatikana katika lugha

ya Kiingereza

5 26.3

Jumla 19 100

Chati 3.2.3: Sababu za Kiswahili kutoimarika kama lugha rasmi

16%

42% 16%

26%

Matumizi ya lugha ya Sheng

Ukosefu wa sera za kiserikali kuendeleza shughuli za kukuza kama lugha rasmi

Lugha ya Kiingereza bado kutumika sana katika nyanja mbalimbali

Stakabadhi nyingi zinapatikana katika lugha ya Kiingereza

Page 68: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

56

Waliosema kuwa Kiswahili hakikuwa kimeimarika katika hadhi yake ya kuwa

lugha rasmi, walitoa sababu zao ili kuunga madai yao. Asilimia 42.1 walisema

kuwa ukosefu wa sera za kiserikali kuendeleza Kiswahili kama lugha rasmi

ndiyo ilikuwa sababu kuu ya lugha hii kutoimarika. Asilimia 26.3 walieleza

kuwa stakabadhi nyingi rasmi zilipatikana katika lugha ya Kiingereza hivyo

jambo hili lilizuia kuimarika kwa lugha hii kuwa rasmi. Asilimia 15.8 ya

waliohojiwa walisema kuwa lugha ya Kiingereza bado ilitumika sana katika

nyanja mbalimbali, ilhali asilimia nyingine sawa na hiyo ya 15.8 ya waliohojiwa

walisema kuwa matumizi ya sheng yalizuia hali ya Kiswahili kutoimarika na

kuwa lugha rasmi. Swala la sheng limekuwa changamoto katika lugha ya

Kiswahili kwa kuwa watu wana dhana kuwa lugha ya Kiswahili ni ngumu na

hivyo wanapendelea kutumia ‘Sheng’ katika mazungumzo yao.

Watafitiwa pia walihitajika kupendekeza njia moja nzuri ambayo walifikiria

ingeweza kukifanya Kiswahili kiimarike nchini Kenya, kama lugha rasmi. Jibu

la swali hilo limeelezwa na kauli (3.2.4)

Page 69: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

57

Jedwali 3.2.4: Pendekezo la njia moja nzuri ambayo inaweza kufanya

Kiswahili

kikubalike kama lugha rasmi

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Kiswahili kupewa hadhi

sawa na Kiingereza

9 21.4

Kuwepo na magazeti zaidi

ambayo yanachapishwa

kwa lugha ya Kiswahili

3 7.1

Kiswahili kutumika katika

shughuli zote za Kiserikali

rasmi

30 71.4

Jumla 42 100

Chati 3.2.4: Mapendekezo ya kukifanya Kiswahili kikubalike kama lugha

rasmi

21%

7%

72%

0%

Kupewa hadhi sawa na Kiingereza

Kuwepo kwa magazeti zaidi ambayo yanachappishwa kwa lugha ya Kiswahili

Kiswahili kutumika katika shughuli zote za Kiserikali rasmi

Page 70: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

58

Asilimia 71.4 ya watafitwa walipendekeza Kiswahili kitumike katika shughuli

zote za Kiserikali rasmi, jambo hili litawezesha lugha hii kuafikia lengo lake la

kuwa lugha rasmi kwa kuwa itawalazimu kutumika katika maeneo mengi

Serikalini. Hata hivyo, hadhi yake mpya iliyopewa kikatiba 2010 itaweza

kuafikiwa na kukomesha hali yake ya kuchukuliwa kuwa ni lugha yenye hadhi ya

chini. Asilimia 21.4 ya watafitiwa walipendekeza kuwa Kiswahili kupewa hadhi

sawa na Kiingereza kwa sasa jinsi hali ilivyo ni kuwa bado watu katika sekta

zilizofanyiwa utafiti wanaona kuwa lugha ya Kiingereza ina hadhi ya juu kuliko

Kiswahili ingawa Kikatiba lugha hizi zina hadhi sawa. Asilimia 7.1 ya

watafitiwa walipendekeza kuwepo na ongezeko la magazeti zaidi ya lugha ya

Kiswahili, kwa sasa tuna gazeti la ‘Taifa Leo’ pekee ambalo huchapisha habari

kwa lugha ya Kiswahili.

Kutokana na mapendekezo haya, ni wazi kuwa watafitiwa wengi walihisi kuwa

ukosefu wa Serikali kutumia lugha ya Kiswahili katika shughuli zote za kiserikali

ndio hasa sababu kuu ya lugha ya Kiswahili kutoimarika na kuwa lugha rasmi.

Kwa hivyo, ni wajibu wa serikali kuhakikisha kuwa kwanza, waifanye hadhi hii

mpya ya lugha kisheria kisha wahakikishe kuwa inatumika katika shughuli za

kiserikali kwa wingi. Pia jibu la Kiswahili kutopewa hadhi sawa na lugha ya

Kiingereza lilionekana kuwa pingamizi la kutoimarika kwa Kiswahili na hali hii

inatambulikana kikatiba. Lugha ya Kiswahili ni lugha muhimu na hivyo ni

jukumu la serikali kuhakikisha kuwa kisheria, hadhi hiyo imewekwa na

kuzingatiwa ili matumizi yake yadhihirike katika nyanja zake mbalimbali.

Page 71: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

59

3.3 Muhtasari

Katika sura hii, mtafiti ameshughulikia uchanganuzi wa data kuhusu utayari wa

Wakenya kuhusiana na sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini

Kenya kulingana na walioshiriki kwenye utafiti. Kutokana na matokeo ya utafiti

imedhihirika kuwa Wakenya wapo tayari kuitumia lugha ya Kiswahili kama

lugha rasmi baada ya kuidhinishwa kwa katiba ya 2010. Pia, matokeo ya

kuimarika kwa lugha ya Kiswahili kwa kuzingatia hadhi yake ya kuwa lugha

rasmi katika katiba bado yanaonyesha kuwa kuna chngamoto zinazokumba

uimarikaji wake.

.

Page 72: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

60

SURA YA NNE

CHANGAMOTO NA MIKAKATI YA KUIMARISHA SERA

HII MPYA YA LUGHA YA KISWAHILI

4.0 Utangulizi

Katika sura ya tatu tumejadili suala la utayari wa Wakenya kuhusiana na sera

mpya ya lugha ya Kiswahili na pia uimarikaji wa Kiswahili kama lugha rasmi

baada ya mabadiliko ya katiba ya 2010 nchini. Katika sehemu hiyo, imebainika

kuwa asilimia kubwa ya watafitiwa wapo tayari kutumia lugha ya Kiswahili

katika hadhi yake ya kuwa lugha rasmi. Imedhihirika pia, lugha ya Kiswahili

haijapokelewa ipasavyo na Wakenya wote huku pia swala la kuimarika likiwa

halijatimizika inavyotakikana kwa kuwa serikali haijaweza kuendeleza sera hii

mpya kadri ya uwezo wao.

Katika sura hii, mtafiti ametumia nadharia ya Utekelezaji kuchanganua data.

Nadharia hii inafaa katika sehemu hii kwa kuwa imejaribu kutathmini jinsi sera

ya lugha inavyopaswa kutekelezwa ili kuafikia madhumuni yake na wakati huo

huo kuangazia changamoto ambazo zaweza kujitokeza katika kuwezesha sera

hiyo mpya kutumika.

Watafitiwa waliulizwa maswali yaliyolenga kumpa mtafiti majibu ambayo

yangemwezesha kufahamu changamoto na pia mbinu wanazotumia wafanyikazi

wa sekta ya Idara ya Polisi, vyombo vya habari na wizara ya utamaduni ili

kuimarisha na kukabiliana na changamoto wanazokumbana nazo katika

kuimarisha lugha ya Kiswahili. Waliweza kutoa maoni yao jinsi wanavyoona ni

Page 73: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

61

bora sera hii mpya kuendelezwa ili kuafikia malengo yake ya kuwa lugha rasmi

katika sekta zao mbalimbali.

Sura hii imegawika katika sehemu mbili: sehemu ya kwanza inazungumzia

changamoto zinazokumba wafanyikazi katika sekta zilizohusika katika utafiti

kisha sehemu ya pili inazungumzia mikakati inayowekwa au inayozingatiwa na

watu katika sekta hizi ili kuimarisha na kufanya Kiswahili kuwa na hadhi ya

urasmi na kuonyesha ukubalifu kamili miongoni mwa Wakenya nchini.

4.1 Changamoto zinazowakabili wafanyikazi katika sekta zilizozingatiwa

katika utafiti

katika sera mpya ya Kiswahili kuwa lugha rasmi.

Katika kushughulikia sehemu ya changamoto kulikuwa na maswali kadhaa

yaliyoulizwa watafitiwa kuhusiana na Kiswahili kuwa lugha rasmi. Swali la

kwanza lililenga kubaini iwapo kuna vikwazo katika kufanya Kiswahili kutofikia

malengo yake yanayohitajika. Majibu ya swali hilo yameonyeshwa kama

ifuatavyo katika kauli ya (4.1)

Jedwali ya 4.1.1: Iwapo kuna sheria ambazo zimefanya Kiswahili kutofikia

kiwango

kinachohitajika

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Ndio 16 38.1

La 26 61.9

Jumla 42 100

Page 74: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

62

Chati 4.1.1: Sheria zinazofanya Kiswahili kutofikia kiwango kinachohitajika

Watafitiwa wote (42) walijibu swali hilo. Asilimia 61.9 ya watafitiwa walisema

kuwa hakuna sheria ambazo zimewekwa ili kuzuia Kiswahili kisifikie kiwango

cha juu cha ufanisi ilhali asilimia 38.1 ya watafitiwa walidai walieleza kuwa

kuna sheria ambazo zimewekwa kukandamiza ukuaji wa lugha ya Kiswahili.

Waliosema kuwa zipo sheria ambazo zimewekwa kufanya Kiswahili

kutoimarika, baadhi yao walisema kuwa, katika ofisi nyingi sharti mtu kujieleza

kwa lugha ya Kiingereza na uandishi wa ripoti au maombi ya chochote

huandikwa kwa lugha ya Kiingereza ambayo ndiyo inayotambulikana kuwa

lugha rasmi. Wengine walisema kuwa vipindi vingi huwa katika lugha ya

Kiingereza. Ingawa tunasema idadi ya vipindi vya Kiswahili vimeongezeka

bado idadi hii haifikii idadi ya vipindi vya Kiingereza. Taarifa kwa mara nyingi

pia ilisemekana kusomwa kwa lugha ya Kiingereza na kwa mara chache

kusomwa kwa lugha ya Kiswahili; wengine walieleza kuwa mawasiliano ya

kimaongezi rasmi baina ya wakubwa kwa wadogo wao hutumia lugha ya

Kiingereza.

38%

62%

0% 0%

Ndio

La

Page 75: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

63

Kutokana na matokeo ya swali hili la kuwepo kwa sheria zinazozuia kufikia

malengo katika lugha ya Kiswahili, Asilimia 38.1 walisema kuwa kuna sheria

kuonyesha kuwa bado kuna vikwazo ambavyo vinaifanya lugha ya Kiswahili

kutofikia kiwango chake kinachohitajika. Matumizi ya kukuzwa kwa lugha ya

Kiingereza yanafanya Kiswahili kukandamizwa pale ambapo lugha ya

Kiswahili huonekana ikiwa lugha duni. Lugha zote hizi zapaswa kupewa nafasi

sawa kwa kuwa zote zina hadhi sawa kikatiba. Hivyo ni muhimu iwapo wakuu

katika sekta za utangazaji wanaweza kukipa Kiswahili nafasi sawa

ikilinganishwa na lugha ya Kiingereza hivyo basi kutakuwa na mabadiliko

katika sekta hii.

Swali lingine lililenga kuonyesha changamoto ambazo wafanyikazi wa sekta

zilizotafitiwa hukumbana nazo kuhusu hadhi ya Kiswahili kuwa lugha rasmi.

Page 76: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

64

Jedwali ya 4.1.2: Changamoto zinazokumba lugha ya Kiswahili kuhusu

hadhi mpya ya

Kiswahili katika sekta zilizotafiwa

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Sera za utangazaji

kupendelea matumizi ya

Kiingereza zaidi

9 21.4

Ukosefu wa nafasi sawa

baina ya Kiswahili na

Kiingereza

13 31

Matumizi ya lugha ya

mama

12 28.6

Serikali bado kusisitiza

matumizi ya Kiingereza

katika shughuli zake

8 19

Jumla 42 100

Chati 4.1.2: Changamoto zinazokumba lugha ya Kiswahili katika sekta

zilizotafitiwa

21%

31%

29%

19% Sera za utangazaji kupendelea matumizi ya kiingereza zaidi

Ukosefu wa nafasi sawa baina ya Kiingereza na Kiswahili

Matumizi ya lugha ya mama

Serikali bado kusisitiza matumizi ya Kiingereza katika shughuli zake

Page 77: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

65

Watafitiwa wote arobaini na wawili (42) walijibu swali hili. Watafitiwa kumi na

tatu ambao ni asilimia 31 ya watafitiwa walisema kuwa changamoto kuu

wanayokumbana nayo ni kuwa kuna ukosefu wa nafasi sawa baina ya

Kiingereza na Kiswahili. Watafitiwa kumi na wawili ambao ni asilimia 28.6 ya

watafitiwa walieleza kuwa changamoto wanayokumbana nayo ni matumizi ya

lugha ya mama katika maeneo yao ya kazi. Asilimia 21.4 ya watafitiwa ambao

walikuwa tisa walisema kuwa changamoto waliyokumbana nayo ni sera za

utangazaji kupendelea lugha ya Kiingereza kisha watafitiwa wanane

waliowakilishwa na asilimia 19 walisema kuwa changamoto waliokumbana

nayo ni jinsi serikali bado imesisitiza matumizi ya Kiingereza katika shughuli

zake.

Kutokana na majibu haya ni dhahiri kuwa idadi kubwa ya watafitiwa walidai

kuwa lugha ya Kiingereza inakuzwa zaidi kuliko lugha ya Kiswahili kama lugha

iliyo bora zaidi. Tokeo hilo linaafikiwa pale ambapo kunadhihirika kuwa

asilimia 21.4 ilisema kuwa katika sera za utangazaji lugha ya Kiingereza

hupendelewa zaidi. Kulikuwa pia na matumizi ya lugha ya mama kama

changamoto. Ni jambo la kushangaza kuwa bado watu wanatumia lugha mama

katika miktadha rasmi, wakati tuna lugha mbili ambazo zinaweza kutumika

katika miktadha hiyo. Hata hivyo, sharti kubuniwe mipango maalum ya kuweza

kufanya lugha hizo kuwa na usawa.

Swali lililofuatia lilieleza kwa nini bado Kiswahili hakijakita mizizi kama lugha

rasmi kikatiba aidha pia mtafiti alitaka kubaini ni nini kilichochangia

Page 78: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

66

kutokuwepo ukamilifu katika utayari wa wakenya katika matumizi ya lugha ya

Kiswahili.

Jedwali 4.1.3: Sababu zinazofanya Kiswahili bado kutofikia hadhi yake ya

kuwa rasmi na nini kilichochangia kutokuwepo na ukamilifu wa utayari wa

Wakenya

Mahojiano yaliyofanyika miongoni mwa watu walioko serikalini yalibaini

kuwa, kuna mswada ambao upo bungeni ambao haujapitishwa rasmi. Mswada

huo ni ‘Sera ya lugha za Kenya’. Kupitishwa kwa mswada huu hakuzui nafasi

ya lugha ya Kiingereza ya hali yoyote ile. Mswada huu hapo awali ulikuwa

umejadiliwa katika wizara ya michezo na utamaduni kisha ukapelekwa katika

wizara ya mawasiliano na teknolijia. Katika hatua za mwanzo washika dau

waliamini kuwa mswada huu ungepitishwa kwa haraka lakini mambo haya

yalikwenda kinyume na matarajio yao. Kamati ya Afrika Mashariki tayari

inatekeleza majukumu yake lakini nchi ya Kenya bado haijaweza kuwa na

baraza la kitaifa la Kiswahili. Katika kuendeleza lugha ya Kiswahili inatoa

nafasi ya uhakika wa kitaifa kupitia kusherekea kwa lugha na tamaduni

mbalimbali.

Wabunge wamekuwa wakipitisha baadhi ya miswada ambayo inawafaidi wao

na hivyo hali hii imechelewesha kupitishwa kwa mswada wa Kiswahili kuwa

lugha rasmi kuwa mswada huu ukipitishwa itakuwa sheria maalum na hivyo

itaweza kutumika ipasavyo katika ofisi zote za Kiserikali.

Ilibainika kuwa serikali haijawajibika kwa ambavyo mikakati iliyowekwa

haijatekelezwa kikamilifu hivyo hiyo ni sababu nyingine ya kuifanya Kiswahili

kutofikia hadhi yake ya kuwa lugha rasmi.

Page 79: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

67

Pia ilibainika kuwa kufungwa kwa kituo cha ‘QTV’ kulisababishwa na

kutozalisha kwa fedha. Kituo hiki ni moja ya vituo ambavyo vinaendeleza lugha

ya Kiswahili. Kituo hiki kilitumia lugha ya Kiswahili kwa kiwango kikubwa

sana na hivyo kwa kuwa hakikuzalisha fedha hali hii ilifanya kituo hiki

kufungwa. Hoja kuwa kituo hiki kilikuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili

haikuzingatiwa. Hii ni kudhihirisha kuwa biashara ndio ilikuwa ya maana sana.

Hivyo hayo ndiyo baadhi ya maoni ambayo yalitolewa na wahojiwa.

4.2 Mikakati ya kuifanya lugha ya Kiswahili kuwa bora katika sekta

zilizotafitiwa ili

kukabiliana na changamoto zinazozuia kiwango kinachohitajika

Sehemu inayofuata imeshughulikia mikakati ambayo viongozi katika sekta

zilizofanyiwa utafiti wameweka na mapendekezo yao kwa serikali kuu nchini ili

kuweza kukabiliana na changamoto zinazofanya Kiswahili kutofikia hadhi yake

ya urasmi.

Ili kupata data iliyokamilika na ambayo ilimwezesha mtafiti kufikia malengo

yake, mtafiti aliwahoji watafitiwa wachache na kuuliza maswali aliyonuia

kupata majibu ambayo yalimwezesha mtafiti kupata matokeo aliyonuia.

Swali la kwanza katika sehemu hii lililenga mtafitiwa aeleze iwapo kuna njia

ambazo anafikiri serikali inaweza kubuni ili kukabiliana na changamoto ya hadhi

yake ya kuwa lugha rasmi.

Matokeo ya swali hilo yamefafanuliwa katika kauli ifuatayo

Page 80: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

68

Jedwali 4.2.1: Njia ambazo zinawekwa katika kukipa Kiswahili nafasi yake

kwa mujibu

wa Katiba 2010

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Sekta ya utangazaji kuzingatia

matumizi ya Kiswahili

17 40.5

Kuwepo kwa hati nyingi zaidi

kwa lugha ya Kiswahili

16 38.1

Kuhimizwa kwa watu kutumia

lugha ya Kiswahili kwa wingi

9 21.4

Jumla 42 100

Chati 4.2.1: Mikakati ya kukipa Kiswahili nafasi yake kwa mujibu wa

Katiba

41%

38%

21%

0%

Sekta ya utangazaji kuzingatia matumizi ya Kiswahili

Kuwepo kwa hati nyingi zaidi kwa lugha ya Kiswahili

Kuhimizwa kwa watu kutumia lugha ya Kiswahili kwa Wingi

Page 81: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

69

Kutokana na kauli hii watafitiwa wote arobaini na wawili (42) walijibu swali hili

ambao ni asilimia 100 ya watahiniwa waliojibu swali hilo. Wote walikubali kuwa

kuna njia ambazo zinaweza kutumiwa ili kufanya Kiswahili kichukue mahali

pake kwa mujibu wa katiba ya 2010. Kati ya njia zilizopendekezwa ni; sekta ya

utangazaji kuzingatia matumizi ya Kiswahili kwa wingi zaidi ili kuinua hadhi

yake kwa kuwa bado lugha hii huchukuliwa kuzungumzwa na watu ambao

hawajasoma. Hali hii ikizingatiwa kutakuwa na mabadiliko katika hadhi ya lugha

hii. Njia hii ilipendekezwa na watafitiwa kumi na saba ambao ni asilimia 41.

Watafitiwa kumi na sita ambao ni asilimia 38.1 walipendekeza kuwa kuwepo

kwa hati nyingi za lugha ya Kiswahili mfano Magazeti na vitabu. Lugha sharti

iwe na ukwasi mwingi wa vitabu ili wazungumzaji wake wafaidike nayo. Lugha

ya Kiingereza ina vitabu vingi na matumizi yake ni mapana zaidi hivyo tunaweza

kutafsiri baadhi ya vitabu vilivyoandikwa kwa lugha ya Kiingereza hadi lugha ya

Kiswahili kuongezea ukwasi wa lugha hii. Watafitiwa tisa ambao ni asilimia 21.4

walieleza kuwa itakuwa bora iwapo watu wengi wataweza kutumia lugha ya

Kiswahili katika miktadha rasmi. Maeneo mengi yale ya kiserikali na yasiyo ya

kiserikali yaweze kutumia lugha ya Kiswahili kama moja wapo ya lugha ya

mawasiliano, kwa njia hii Kiswahili kitapata idadi nyingi ya wazungumzaji wa

lugha hii.

Kutokana na kauli hii ya (4.2.1) mapendekezo kuhusu mikakati ambayo yaweza

kutumika katika kufanya Kiswahili kuwa lugha rasimi yamebainika. Hata hivyo,

ni wazi kuwa watafitiwa kumi na saba ambao ni asilimia 41 walitaka sekta zote

za utangazaji kutumia lugha ya Kiswahili katika mawasiliano yao ya kirasmi.

Page 82: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

70

Matokeo haya yanaoana vizuri na mtazamo wa upangaji lugha kihadhi

unaoelezea kuwa ili sharti kuwe na juhudi zinazochukuliwa ili kuhakikisha kuwa

jukumu la lugha limeafikiwa katika jamii. Hivyo, ni wajibu wa viongozi katika

baadhi ya sekta za utangazaji kuhakikisha Kiswahili kinapewa hadhi kwa

kukitumia ipasavyo.

Swali linalofuatia linaeleza maoni yao kuhusiana na matumizi ya lugha ya

Kiswahili kama lugha rasmi. Matokeo ya swali hilo yameelezwa kwa mhutasari

katika jedwali lifuatalo la kauli (4.2.2)

Kauli 4.2.2: Mapendekezo ya vile Kiswahili kinaweza kutekelezwa ili

kufanikisha lengo

lake la kuwa lugha rasmi

Maelezo Idadi ya Watafitiwa Asilimia

Matumizi ya Lugha ya

Kiswahili na Kiingereza yawe

sawa

22 52.4

Kuzingatiwa kwa lugha ya

Kiswahili kimasomo katika

madarasa ya chini

4 9.5

Kiswahili kizingatiwe kama

lugha ya Taifa na rasmi ofisini

8 19.0

Kuhimiza watu kutumia

Kiswahili sanifu

8 19.0

Jumla 42 100

Page 83: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

71

Chati 4.2.2: Mapendekezo ya vile Kiswahili kinaweza kufanikisha lengo la

kuwa lugha rasmi

Kwa mujibu wa kauli (4.2.2) watafitiwa wote arobaini na wawili (42) walijibu

swali hili wakiwakilisha asilimia 100 ya watafitiwa. Watafitiwa 22 ambao ni

asilimia 52.4 walipendekeza matumizi ya Kiswahili kuwa sawa na ya lugha ya

Kiingereza ili kufikia lengo linalohitajika. Watafitiwa 8 ambao ni asilimia 19

walipendekeza kuwa lugha ya Kiswahili itumike kama lugha rasmi huku

watafitiwa wengine 8 ambao ni asilimia 19 wakapendekeza kuwa watu

wahimizwe kutumia Kiswahili sanifu. Watafitiwa 4 ambao ni asilimia 9.5

walipendekeza kuwa Kiswahili kizingatiwe kimasomo kuanzia madarasa ya

chini.Walimu waweze kufunza watoto kwa kudumisha kuwa lugha ya Kiswahili

na Kiingereza zina hadhi sawa hivyo ni muhimu kuzingatia lugha hizo.

Kutokana na mapendekezo ambayo watafitiwa walitoa ni dhahiri kuwa wengi

wanaonelea kuwa lugha ya Kiingereza inatumika kwa hadhi ya juu zaidi

ikilinganishwa na lugha ya Kiswahili hivyo viongozi katika sekta mbalimbali

52%

10%

19%

19%

Matumizi ya lugha ya Kiswahili na Kiingereza yawe sawa

Kuzingatiwa kwa lugha ya Kiswahili kimasomo katika madarasa ya chini

Kiswahili kizingatiwe kama lugha ya taifa na rasmi ofisini

Kuhimiza watu kutumia Kiswahili sanifu

Page 84: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

72

wanapaswa kuhakikisha kuwa lugha hizi zinatumika katika kiwango sawa.

Tamko la Kiswahili kusisitizwa kimasomo kama somo na lugha muhimu kama

lugha ya Kiingereza na kuwa ni lugha rasmi ni muhimu sana. Kudumisha usanifu

wa Kiswahili ni jambo muhimu kwa kuwa humwezesha mzungumzaji

kuzungumza kwa ufasaha.

Swali lililofuatia lililenga watafitiwa kutoa pendekezo moja muhimu kwa serikali

kuhusiana na matumizi ya lugha ya Kiswahili kufikia lengo linalohitajika

Kauli 4.2.3: Pendekezo moja muhimu kwa serikali kuhusiana na matumizi

ya lugha ya

Kiswahili kufikia lengo linalohitajika.

Maelezo Idadi ya watafitiwa Asilimia

Uundwaji wa sheria zinazofanya

Kiswahili kutumika ipasavyo

20 48.23

Kuhimiza watu kutumia Kiswahili

kuwahoji wanaotafuta kazi

13 32.5

Kubuniwa kwa kamati ya

kutekeleza sera ya lugha

9 19.27

Jumla 42 100

Watafitiwa wote 42 walihusika katika utafiti. Watafitiwa ishirini ambao ni

asilimia 48.23 walipendekeza kuwa serikali iunde sheria zinazofanya Kiswahili

kutumika ipasavyo. Hali hii itawezesha lugha hii kutumika kama lugha rasmi

kama inavyotakikana na kuondoa dhana kuwa Kiswahili ni lugha duni

inayozungumzwa na watu ambao si wastaarabu. Watafitwa 13 ambao ni asilimia

32.5 walipendekeza watu kuhimizwa kutumia Kiswahili kuwahoji wanaotafuta

kazi na pia kuwataka wajieleze kwa lugha ya Kiswahili. Watafitiwa 9 ambao ni

Page 85: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

73

asilimia 19.27 walipendekeza kubuniwa kwa kamati ya kutekeleza sera ya lugha

ya Kiswahili.

Kutokana na mapendekezo yaliyotolewa na watafitiwa, ni dhahiri kuwa wengi

wao wanaamini kuwa sheria ni muhimu na kuwepo kwa sheria kandamizi kama

vile kuwepo na lugha ambayo inapaswa kutumika wakati fulani kunainyima

Kiswahili kuwa na nafasi katika jamii kwa hivyo sheria hizo ziondolewe. Ni

vyema iwapo sheria ambazo zinakuzwa katika sekta zilizotafitiwa, zinaruhusu

lugha ya Kiswahili kutumiwa kwa wingi katika sekta hizo. Hali hii itaifanya

lugha ya Kiswahili kuimarika zaidi na kutumika katika miktadha mbalimbali

iliyo rasmi. Waliopendekeza kubuniwa kwa kamati kutekeleza sera ya lugha

walielewa kuwa serikali ina uwezo mkubwa wa kuwezesha lugha hii kutumika

bora zaidi. Nadharia ya Utekelezaji yaonyesha kuwa, ili utekelezaji ufaulu, ni

lazima serikali ijitolee na kutoa tamko rasmi kuhusu matumizi ya lugha.

4.3 Muhtasari

Katika sura hii, mtafiti ameshughulikia uchanganuzi na upangaji wa data kuhusu

changamoto na mikakati ya kufanya lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi

kikatiba. Kutokana na matokeo ya utafiti, ni wazi kuwa kuna changamoto nyingi

ambazo zinazikumba sekta zilizotafitiwa katika matumizi ya lugha ya Kiswahili

kama lugha rasmi kwa mujibu wa katiba ya 2010. Matokeo ya utafiti huu

yamedhihirisha kuwa mikakati inafaa kuwekwa ili kuinua hadhi mpya ya lugha

ya Kiswahili. Katika sura inayofuata mtafiti ameshughulikia hitimisho na

mapendekezo ya utafiti kwa ujumla.

Page 86: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

74

SURA YA TANO

HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

5.0 Utangulizi

Utafiti huu ulinua kubaini utayari wa Wakenya katika utekelezaji wa sera ya

lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi. Malengo ya utafiti huu yalikuwa, kubaini

iwapo kuna utayari katika kutekeleza sera ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha

rasmi, kubaini utayari huu utasaidiaje katika kuimarisha sera hii mpya ya lugha

ya Kiswahili hasa katika urasmi wake kuchunguza changamoto zinazokabiliwa

katika shughuli za kiutawala na vyombo vya habari kuhusu hadhi mpya ya lugha

ya Kiswahili. kutambua ni vipi utayari wa utekelezaji katika sera hii unavyoweza

kutekelezwa ili kuweza kufanikisha lengo la Kiswahili la kuwa lugha rasmi.

Malengo haya yaliongozwa na Nadharia ya Utekelezaji na mtazamo wa upangaji

lugha kihadhi.

Katika sura hii ya tano, matokeo ya utafiti, changamoto za utafiti, mapendekezo

na hitimisho zimejadiliwa kama ifuatavyo.

5.1 Muhtasari wa Utafiti

Utafiti huu ulichukua sura tano. Katika sura ya kwanza vipengele vilivyojadiliwa

ni pamoja na usuli wa mada, suala la utafiti, malengo na maswali ya utafiti, upeo

na mipaka, sababu za kuchagua mada, misingi ya nadharia, yaliyoandikwa

kuhusu mada na mbinu za utafiti.

Page 87: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

75

Sura ya pili, historia na utayari wa wakenya kuhusu urasmi wa lugha ya

Kiswahili nchini Kenya iliweza kujadiliwa ili kuweza kudhihirisha miktadha

mbalimbali ya Wakenya kuhusu Kiswahili hadi sasa.

Katika sura ya tatu, mtafiti ameonyesha upangaji na uchanganuzi wa data kwa

kujadili utayari wa Wakenya katika sera ya lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi

katika idara ya polisi, wizara ya utamaduni na katika vyombo vya habari.

Sura ya nne imeangazia changamoto zinazokumba utayari wa Wakenya katika

sera ya Kiswahili kama lugha rasmi na pia mikakati inayowekwa ili kukabiliana

na changamoto hizo ili kuona iwapo zitaweza kuimarisha lengo la utendakazi wa

lugha ya Kiswahili kama lugha rasmi. Sura ya tano muhtasari, matokeo ya utafiti

na mapendekezo zilijadiliwa

5.2 Matokeo ya utafiti

Katika sehemu hii tumejadili malengo manne na kurejelea matokeo ya utafiti.

Kila lengo limejadiliwa kwa mujibu wa matokeo ya utafiti

5.2.1 Lengo la kwanza

Utafiti huu ulikuwa na malengo manne. Lengo la kwanza lilikuwa kubaini iwapo

kuna utayari katika kutekeleza sera ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi.

Kutokana na data iliyokusanywa, mtafiti aliweza kubaini kuwa kulikuwa na

ukubalifu wa kuitekeleza lugha ya Kiswahili miongoni mwa Wakenya kama

lugha rasmi. Kwa kuzingatia mtazamo wa upangaji lugha kihadhi, baada ya lugha

hii kupewa jukumu mpya ilionekana kuzingatiwa huku ikidhihirika kuwa watu

wengi walijaribu kuitumia lugha hii katika miktadha rasmi. Hii imejitokeza pale

ambapo baadhi yao waliona mabadiliko ya utekelezaji wa lugha ya Kiswahili

Page 88: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

76

baada ya katiba ya 2010. Kuna wale ambao waliona utekelezaji wa Kiswahili

ulikuwa mzuri baada ya kupata katiba mpya ya 2010 ikilinganishwa na hapo

awali ambapo utekelezaji wake ulikuwa mzuri kiasi. Hakuna aliyeona kuwa hali

ya Kiswahili kuwa mbaya baada ya hadhi yake mpya ya kuwa lugha rasmi. Hii ni

kubainisha kuwa wengi wa watafitiwa wanaona kuwa lugha ya Kiswahili ina

matumaini na itaweza kuafikia malengo na majukumu yake ambayo yalipewa

lugha hii na hili litakuwa na manufaa zaidi kwa wazungumzaji wake.

5.2.2. Lengo la pili

Lengo la pili la utafiti lilikuwa kubaini utayari huu utasaidiaje katika kuimarisha

sera hii mpya ya lugha ya Kiswahili hasa katika urasmi wake. Kwa kuzingatia

mtazamo wa upangaji lugha kihadhi, lugha ya Kiswahili ilipewa hadhi ya kuwa

lugha rasmi na lugha ya taifa. Kutokana na maelezo yaliyotolewa ni kuwa hadhi

ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi imeimarika. Hii ni kwa kuwa watu

wengi wameweza kuitumia lugha hii katika miktadha rasmi na pia katika maeneo

mengine. Kutokana na matokeo ya uchanganuzi wa data tuliyopata kutoka kwa

watafitiwa, ni wazi kuwa Kiswahili kimeimarika kwa kuwa hadhi mpya ya

Kiswahili kama lugha rasmi imefanya lugha hii kupata hadhi ya juu. Baada ya

katiba ya 2010 kuidhinisha lugha hii kuwa rasmi, hali hii ilifanya Kiswahili kuwa

na hadhi mbili tofauti; hadhi ya kuwa lugha ya taifa na lugha rasmi.

Matokeo ya utafiti yameonyesha kuwa hali hii imefanya Kiswahili kuimarika

zaidi. Kutokana na majibu yaliyopatikana, ni bayana kuwa lugha hii imeanza

kutumika katika shughuli za kitaifa na katika ofisi za kiserikali hivyo hali hii

imeimarika ikilinganishwa na hapo awali. Pia imebainika kuwa lugha hii imeanza

Page 89: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

77

kutumiwa katika utangazaji pale ambapo idadi ya vipindi ambavyo vinatumia

lugha ya Kiswahili vinaendelea kuongezeka. Ijapokuwa hali hii mpya ya

Kiswahili haijaafikiwa kikamilifu kuna matumaini kuwa lugha hii itafikia lengo

lake la kuwa lugha rasmi, kwa kuwa matokeo haya yanaonyesha kuwa lugha hii

inaendelea kukubalika kutumika katika miktadha rasmi.

5.2.3 Lengo la tatu

Lengo la tatu la utafiti huu lilikuwa kuchunguza changamoto zinazokabiliwa

katika shughuli za kiutawala na vyombo vya habari kuhusu hadhi mpya ya lugha

ya Kiswahili. Kutokana na matokeo ya utafiti, ilibainika kuwa kuna changamoto

nyingi zinazokabili shughuli za kiutawala na vyombo vya habari katika

kufanikisha hadhi mpya ya lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi.

Baadhi ya changamoto ambazo zilijitokeza ni kwamba katika sekta ya utangazaji

kuna kupendelea matumizi ya Kiingereza sana katika mawasiliano, usomaji wa

habari na hata uandishi wa magazeti. Hii inaendeleza ukosefu wa nafasi sawa

baina ya Kiingereza na Kiswahili. Hiki ni kikwazo katika kuimarisha lugha ya

Kiswahili. Hivi karibuni pia runinga ya ‘QTV’ ilifungwa ambayo kiwango

kikubwa iliendeleza lugha ya Kiswahili. Sababu za kufungwa kwake ni kuwa

haikuleta faida kifedha hivyo ni dhahiri kuwa lengo la kuendeleza Kiswahili

kutumika kwa ufasaha na kama lugha rasmi halikuwa la umuhimu sana.

Changamoto nyingine iliyobainika ni kuwa watu walitumia lugha ya mama

katika maeneo yao ya kazi. Hali hii ilibainika wazi katika ofisi za kiutawala. Ni

jambo la kutamausha hasa kwa kuwa kuna lugha mbili rasmi ambazo zaweza

kutumika katika ofisi za kiutawala badala ya kutumia lugha ya mama. Pia,

Page 90: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

78

ilisemekana kuwa serikali bado inasisitiza matumizi ya Kiingereza katika

shughuli zake. Hii inadhihirika katika Bunge pale ambapo wabunge huzungumza

lugha ya Kiingereza sana kuliko lugha ya Kiswahili.

Ukosefu wa maandishi ya lugha ya Kiswahili ili kuimarisha lugha hii pia ni

changamoto nyingine. Kunahitajika vitabu, magazeti na majarida ya kutosha ili

kuendeleza kuimarisha hali ya Kiswahili nchini na pia ili watu wengi waweze

kutumia lugha hii. Changamoto nyingine ilikuwa ni kukawia kwa sera ya

Kiswahili kutumika kama lugha rasmi. Ilibainika kuwa mswada wa sera ya lugha

ya Kiswahili kama lugha rasmi bado haujapitishwa bungeni na hivyo hii ni

sababu lugha hii haijapata hadhi yake kikamilifu. Changamoto hizi ndizo

zinazoikabili lugha ya Kiswahili kutoafikia lengo lake la kutekeleza kazi yake

kama lugha rasmi kwa mujibu wa watafitiwa.

5.2.4. Lengo la nne

Lengo la nne lilitaka kutambua ni vipi utayari wa utekelezaji katika sera hii

unavyoweza kutekelezwa ili kuweza kufanikisha lengo la Kiswahili la kuwa

lugha rasmi. Mtafiti aliazimia kutambua njia ambazo zinaweza kutumika ili lengo

la Kiswahili katika kutekeleza kazi yake kama lugha rasmi kuafikiwa katika

maeneo yaliyohusika katika utafiti huu.

Kutokana na maswali yaliyoulizwa, ilibainika kuwa sekta zote za utangazaji

ziweze kutumia lugha ya Kiswahili ili kuweza kuimarisha lugha hii zaidi na

kuweza kufanikisha hadhi yake mpya ya kuwa lugha rasmi. Hata hivyo, idadi ya

vipindi vinavyotumia lugha ya Kiswahili iongezwe katika vituo vya runinga.

Pana haja ya kuwa na hati nyingi zaidi kwa lugha ya Kiswahili kama vile vitabu,

Page 91: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

79

magazeti na hata majarida. Ilibainika pia matumizi ya lugha ya Kiswahili yawe

sawa na ya Kiingereza. Wale ambao walipendelea matumizi ya Kiingereza katika

mawasiliano yao, walihimizwa kutumia lugha ya Kiswahili katika nyanja zote

rasmi. Hata hivyo lugha ya Kiswahili itumike kuwahoji wanaotafuta kazi. Kupitia

kufanyika kwa mambo haya, lugha zote mbili zitaweza kutumika kulingana na

majukumu yaliyowekewa lugha hizi kwa mujibu wa Katiba ya Kenya ya 2010.

Pendekezo lililotolewa kutokana na kuwepo kwa sheria kandamizi ni kuwa,

sheria hizo ziondolewe kuhusu matumizi ya lugha ya Kiswahili na lugha hiyo

izingatiwe kama lugha rasmi. Ili lugha hii iendelee kuenziwa ilipendekezwa

kutumiwa katika shughuli zote za umma na pia za kibinafsi. Baadhi ya majibu

yaliyopatikana yalionyesha kwamba wahojiwa walitaka wabunge kutumia lugha

ya Kiswahili katika mijadala yao na katika hotuba zao. Kwa kufanya hivi

wataonyesha umuhimu wa kutumia Kiswahili kwa kuwa wana ushawishi

mkubwa.

Kuna wale waliopendekeza kuwa lugha ya Kiswahili izingatiwe katika madarasa

ya chini kimasomo. Watafitiwa walieleza kuwa wanafunzi huhimizwa kuongea

lugha ya Kiingereza na walimu wao na kutokana na haya mtoto hukua akijua

kuwa lugha ya Kiingereza ni bora kuliko ya Kiswahili ndio maana hadi sasa

lugha hii inapuuzwa kwa kuhusishwa na hadhi ya chini. Hivi sasa Kiswahili

kimepewa hadhi mpya ya kuwa rasmi hivyo, kinastahili kuwa na hadhi ya juu

kuliko Kiingereza kwani ni lugha rasmi na pia ni lugha ya taifa nchini Kenya.

Page 92: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

80

5.3 Matatizo

Mtafiti alikumbana na matatizo katika ukusanyaji wa data. Katika ukusanyaji wa

data, kuna baadhi ya wafanyakazi ambao walikataa kujaza hojaji na pia waliojaza

walichukua muda mwingi kujaza hojaji hizo. Haikuwa kazi rahisi kuwapata

waliohojiwa kwa kuwa walikuwa na shughuli nyingi ingawa wengine walikataa

kuhojiwa. Baadhi ya waliojaza hojaji walisema kuwa Kiswahili ni lugha ngumu

hivyo ilibidi watoe maelezo yao kwa lugha ya Kiingereza. Hata hivyo baadhi ya

waliohojiwa walitumia lugha ya Kiswahili. Maelezo yaliyotolewa kwa lugha ya

Kiingereza yalimlazimu mtafiti kutafsiri kwa lugha ya Kiswahili.

5.4 Mapendekezo ya Utafiti

Kutokana na majibu yaliyotolewa, ni wazi kuwa kuna changamoto zinazokumba

utayari wa Wakenya katika sera ya Kiswahili kama lugha rasmi nchini Kenya.

Ingawa baada ya kuidhinishwa kwa katiba ya 2010 hali ya Kiswahili ilibadilika

na kuwa bora zaidi, bado Kiswahili hakijafikia lengo lake la utendakazi wake wa

kuwa lugha rasmi haujafikiwa kikamilifu. Kutokana na maelezo haya ni jukumu

la serikali kuwezesha lugha ya Kiswahili kuwa na hadhi yake kama lugha rasmi.

Hata hivyo, mtafiti anapendekeza mapendekezo yafuatayo kwa kuzingatia majibu

yaliyopatikana.

Kwa watafitiwa wajao wanaweza kuangazia changamoto zinazokabili ukosefu

wa nafasi sawa baina ya Kiswahili na Kiingereza. Baadhi ya wafanyikazi katika

vituo vya habari hupendelea kutumia lugha ya Kiingereza ambayo ina hadhi

sawa na lugha ya Kiswahili. Ukosefu wa nafasi sawa kwa lugha ya kiswahili

umesababisha lugha hii kutotumika ipasavyo. Mtafiti katika suala hili azingatie

Page 93: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

81

kuwa wazungumzaji wengi wanapendelea kutumia lugha ya Kiingereza na hivyo

ajiami katika kutafsiri data atakazokusanya kwenye hojaji.

Pendekezo lingine ni kuwa, Bunge lihakikishe kuwa linapitisha mswada wa sera

ya lugha ya Kiswahili kufanya kazi kama lugha rasmi ili mswada huu uweze

kuwa sheria. Wabunge wakifanya hivyo watawezesha lugha hii kutumika katika

maeneo mengi zaidi yakiwa yale ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali. Jambo hili

litaimarisha lugha hii zaidi.

Kuwe na matumizi sawa ya lugha ya Kiswahili na Kiingereza katika vyombo vya

habari. Idadi ya vipindi vinavyopeperushwa kwa lugha ya Kiswahili viweze

kuzingatiwa katika vituo vya runinga. Mawasiliano katika sekta hii pia

yazingatiwe na dhana kuwa lugha ya Kiswahili ni lugha duni kuondolewa kwa

wanaopendelea kutumia lugha ya Kiingereza. Hali hii ikizingatiwa lugha ya

Kiswahili itapata hadhi yake.

Kuwe na hati nyingi zaidi kwa lugha ya Kiswahili. Pale ambapo waandishi wa

Magazeti na vitabu waweze kuandika vitabu vingi zaidi kwa lugha ya Kiswahili.

Hali hii itaweza kukuza lugha ya Kiswahili kwa wasomaji wake.

Kuhimizwa kwa watu kutumia lugha ya Kiswahili kwa wingi kama moja wapo

ya lugha ya mawasiliano. Hivyo basi, lugha hii itapata wazungumzaji wengi zaidi

na kutumika katika maeneo pana zaidi.

Kuhimizwa kwa usawazishaji wa vipindi vya lugha ya kiswahili kuwa sawa na

vya Kiingereza kwa kufanya hivi walimu watakuwa na muda wa kutosha katika

kufafanua mada wanazozishughulika nazo kikamilifu. Serikali kuajiri wasomi wa

Page 94: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

82

Kiswahili ili waweze kutoa mafunzo ya ziada kwa wafanyakazi kuhusu

Kiswahili. Hili liwe jambo la lazima kwa wafanyakazi wote.

5.5 HITIMISHO

Kijumla katika uchanganuzi wa utafiti huu tumeona changamoto ambayo

inakumba sera ya lugha ya Kiswahili ni kwamba lugha hii haijafiki lengo

lakekatika utendakazi wake wa kuwa lugha rasmi. Hata hivyo, mapendekezo

kadhaa yametolewa ili kuonyesha jinsi ambavyo athari hii inavyoweza

kukabiliwa.

Page 95: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

83

MAREJELEO

Ali, J N, (2011) ‘Changamoto zinazokumba Mawasilianoya Kiofisi kwa Kutumia

Kiswahili kama Lugha Rasmi’. Mradi wa Shahada ya Kwanza.

Chuo Kikuu cha katoliki cha Afrika Mashariki (Haijachapishwa

Bamgbose, A. (1991). Language and Nation. The Language Question in Sub-

Sahara Africa. England: Eanglewood University Press.

Chimerah, R. (1998) Kiswahili Past, Present and Future Horizons. Nairobi:

Nairobi University Press

Gorman, T. P. (1974) “The Development of Language Policy in Kenya with

Particular reference to Education System”. In Whiteley,

W.H. (ed.) Language in Kenya. Nairobi: Oxford

University Press, 397-446

Harries, L, (1968 ) “ Nationalisation of Swahili in kenya” Katika Kennedy,

C.(ed). Language and planning and Language and

Education. London: George Allen and Unwin

Page 96: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

84

Hudon, M. (2013) Official Languages in Canada, Federal Policy (Background

Paper), Library of Parliament, Ottawa, Canada

King’ei, K. (2010). Misingi ya Isimujamii. Dar es Salaam: TUKI

Masinde, E. (2012). Kiswahili katika Ujenzi na Utangamano. K. Njogu, C.

Momanyi & M. Mukuthuria (Wahar.) Kiswahili na Utaifa

Nchini Kenya Kenya waweza Communications. Uk 17-25

Mazrui, A. A. and Mazrui. A.M (1995) Swahili State and Society. Nairobi: East

African

Mbaabu, I. (2007) Historia ya Usanifishaji wa Kiswahili. Dar-es- Salaam: Taasisi

ya Uchunguzi wa Kiswahili

Mbaabu, I. (1996). Language Policy in East Africa. Educational Resesarch and

Publication. (ERAP)

(1978a). Kiswahili Lugha ya Taifa. Nairobi: Kenya Literature Bureau

Mbatiah, M. (2012). Suala la Utaifa wa Kenya: Nafasi ya Kiswahili. K. njogu, C.

Momanyi & M. Mukuthuria (Wahar.) Kiswahili na Utaifa

Nchini Kenya Kenya Twaweza Communications. Uk 3-10

Mekacha, R. D. K. (2011). Isimujamii: Nadharia na Muktadha wa Kiswahili. Dar

es Salaam: TUKI.

Page 97: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

85

Mesthrie, R. S. (2000) Introducing Sociolinguistics. Edinburgh: University Press

Mirianga, R .K. (2014). Mielekeo ya Walimu wa Shule za Msingi Kuhusu Suala

La Lugha kama Linavyoelezwa Katika Katiba ya Kenya.

Tasnifu ya Uzamili Chuo Kikuu cha Nairobi, Kenya

Mohochi, E.S. (2002). Kiswahili na Vyombo vya Habari Nchini Kenya: Matatizo

katika Matumizi ya Lugha. K Njogu & C. Momanyi

(Wahar.) Kiswahili Katika Karne ya Ishirini na Moja.

Cape town: CASA. Uk 147-157

Mukhwana, A. (2008). Language Attitudes in Urban Kenya: The Case Study of

Kisumu, Nairobi and Mombasa.Tasnifu ya Uzamifu

ambayo haijachapishwa, Chuo Kikuu cha Nairobi

Nabea, W. (2009) Language Policy in Kenya: Negociation with Hegemony

katika The Journal of Pan Arican Studies. Vol.3 No 1

September 2009 uk. 121-138

Ngigge, B. N. (2014). Mielekeo na Changamoto za Maafisa wa Kaunti katika

Utekelezaji wa Katiba Kuhusu Sera ya Lugha: Mfano wa

Kaunti ya Nakuru. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha

Kenyatta, Kenya

Page 98: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

86

Ngugi, P. na Chacha, L. (2004). Sociolinguistics. Nairobi: KUIOL

Nyandwaro, L.K.( 2015) Mielekeo ya Wafanyakazi Kuhusu Kiswahili kama

Lugha Rasmi katika Wizara za Serikali Nchini Kenya.

Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha Kenyatta

Onyango, J. O. (1990). Mielekeo ya Wasomi Kuhusu Matumizi ya Kiswahili

Nchini Kenya. Tasnifu ya Uzamili, Chuo Kikuu cha

Kenyatta, Kenya

Osore, K. M na Midika, B. (2016) Operationalizing Kiswahili as a Second

Official Language Examples from Canadian

and South African Language Policy

Frameworks. (Makala) Hayajachapishwa

Ryanga, S. (2001) Reaching out for Linguistic Identity: The State of Kiswahili in

Kenya. In: Naomi Shitemi na Mwanakombo Noordin (eds.).

Kiswahili: A Tool for Development. Moi University Press.

24-35

Shitemi, L. N. (2011). Kubidhaaisha na Kuwezesha Lugha kama Sarafu ya

Kiuchumi na Kijamii: Kielezo cha Taaluma za Kiswahili

Page 99: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

87

na Tafsiri.Kenya: Moi University Press

Sikma, J. (1990). The Education of Minority Languages and Conflicting

Attitudes. In PNelde (ed.). Language Attitudes and Language

Conflict. (pp 86-92). Bonn: Duemmler

Spencer, J. (1971). Colonial Language Policies and their Legacies. In Sebeok,

Thomas (ed.). Current Trends in Linguistics, Vol, 537- 547.

The Hague: Mouton de Gruyter

Van Els, T. (2005). Status planning for learning and teaching. In E. Hinkel (Ed.)

Handbook of Research in Second Language Teaching and

Learning (Chapt 53). Mahwah, NJ: Erlbaum. (in press).

http://www.kenyaembassy.com/pdfs/Constitution of Kenya.pdf. Accessed on

Monday 7th

NOV,2016 7:28PM

Page 100: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

88

KIAMBATISHO CHA A: Hojaji

Sehemu ya A: Maelezo ya Kibinafsi.

Weka alama ya (×) mahali panapofaa.

1. Umri: (25-35) [ ] (36 na zaidi) [ ]

2. Jinsia Kiume [ ] (kike) [ ]

3. Kiwango cha elimu: Cheti [ ]

Stashahada [ ]

Shahada ya kwanza [ ]

Shahada ya Uzamili [ ]

Sehemu ya B: Maswali ya hojaji

Tafadhali jibu maswali uliyoulizwa kama ulivyooagizwa

1 a) Wewe kama mfanyikazi katika sekta hii, ni lugha gani unapenda kuitumia

sana katika mawasiliano ya maongezi

A) Kiswahili [ ] B) Kiingereza [ ] C) Lugha mama [ ] D) Lugha mseto [ ]

b) Ni sababu zipi hukufanya kutumia lugha hiyo ya mawasiliano? Toa hoja moja

muhimu

Page 101: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

89

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

………………………………………………….

2 a) Kabla ya kuidhinishwa kwa Katiba ya 2010, utekelezaji wa lugha ya

Kiswahili katika sekta hii ulikuwa vipi?

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

b) Baada ya kuidhinishwa kwa Katiba ya 2010, mabadiliko katika sera hii ya

Kiswahili yanatekelezwa vipi?

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

3a) Kwa maoni yako, sera hii mpya ya Kiswahili imesaidia katika kuimarisha

hadhi yake ya kirasmi?

Page 102: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

90

Ndio [ ] La [ ]

b) Toa maelezo ikiwa jibu lako ni ndio

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

c) Ikiwa jibu lako ni la, eleza njia moja nzuri ambayo unafikiria inaweza kufanya

Kiswahili kikubalike kama lugha rasmi

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

4. Je, kunazo sheria katika sekta hii ambazo unafikiri zimefanya Kiswahili

kutofikia kiwango kinachohitajika? Kama zipo taja mojawapo

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

Page 103: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

91

5. Ni lugha ipi ya mawasiliano ya kimaongezi ambayo watu hupendelea kuitumia

katika sekta hii. Toa sababu kuu za uteuzi huo

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

…………………………………………………

6. Ni mikakati ipi ambayo inawekwa katika sekta hii ili kukipa Kiswahili nafasi

yake kwa mujibu wa Katiba ya 2010? Taja miwili

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

7. Je, kunazo changamoto mnazokumbana nazo katika utekelezaji wa katiba

kuhusu hadhi mpya ya Kiswahili? Kama zipo, taja mbili kuu

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………

Page 104: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

92

8. Kwa maoni yako Kiswahili kinaweza kutekelezwa vipi katika sekta hii ili

kuweza kufanikisha lengo lake la kuwa lugha rasmi

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

……………………………………………………………………………………

…………………………………………………….

Page 105: UTAYARI WA WAKENYA KATIKA UTEKELEZAJI WA SERA KENYA …

93

KIAMBATISHO CHA B: Mwongozo wa Mahojiano

1. Wewe kama mmoja mwanakamati wa tume iliyoshughulikia maswala ya sera

ya lugha ya Kiswahili katika hadhi ya urasmi kikatiba, unafikiria mabadiliko

yanayotokea kuhusu sera ya lugha husaidia kuimarisha kiwango cha lugha ya

Kiswahili?

2. Je, watu wanapokea vipi mabadiliko hayo?

3. Ni mambo yepi unafikiria serikali inafaa kufanya ili kuhakikisha ndoto yake ya

kufanya Kiswahili kuwa lugha ya rasmi inaafikiwa?

4. Imebainika kuwa utekelezaji wa Katiba ni jambo ambalo huwa ngumu mno. Ni

njia zipi mtachukua kuhakikisha kuwa Kiswahili kimepata mahali pake kwa

mujibu wa katiba mpya?