Mafundisho juu ya Biblia
AGANO JIPYA
MATAYO MATENDO
Maelezo ya
Maandiko Matakatifu
kwa Waamini
Mwandishi : William MacDonald
~~~~~~
Mtengenezaji wa Maneno ya Mbele: Arthur Farstad
Everyday Publications Inc.
Port Colborne, ON L3K 6A6
Canada
Traduit de langlais
par G. I. Harlow, 2011
avec collaboration de M. et J. Wolcott
Copyright 2012
par Everyday Publications, Inc.
310 Killaly Street West
Port Colborne, ON L3K 6A6
Canada
ISBN 978-0-88873-157-9
Imprim aux Etats-Unis dAmrique
2
Fahirisi
Majina ya Vitabu vya Agano Jipya 4
Utangulizi wa Mwandishi 5
Namna gani kitabu hiki kiliandikwa 5
MLANGO KWA AGANO JIPYA 6
MLANGO KWA VITABU VYA HABARI NJEMA 8
Matayo 11
Mafundisho juu ya Ufalme wa Mbinguni 19
Mafundisho juu ya Habari Njema 26
Mafundisho juu ya Mwamini na Sheria 30
Mafundisho juu ya Kuachana na Kuoa tena 33
Mafundisho juu ya Kufunga Chakula 38
Mafundisho juu ya Sabato 65
Marko 145
Luka 211
Yoane 325
Matendo 453
Mafundisho juu ya Maombi ndani ya Kitabu cha Matendo 460
Mafundisho juu ya Kanisa Nyumbani 471
Mafundisho juu ya Mkristo na Serikali 481
Mafundisho juu ya Ubatizo wa Mwamini 491
Mafundisho juu ya Utumishi wa Kila Mwamini kanisani 493
Mafundisho juu ya Utaratibu wa Kueneza Habari Njema 512
Mafundisho juu ya haki ya Kanisa Kujitawala Yenyewe 517
Mafundisho juu ya Maongozi ya Mungu 519
Maongozi juu ya Maajabu 521
Mafundisho juu ya Habari Njema ikihubiriwa kwa pahali 527
namna namna
Mafundisho juu ya Habari za Kitabu cha Matendo 556
3
Majina ya Vitabu vya Biblia
VITABU VYA
AGANO JIPYA
Jina Ufupisho
Matayo Mt.
Marko Mk.
Luka Lk.
Yoane Yn.
Matendo Mdo.
Waroma Rom.
1 Wakorinto 1 Kor.
2 Wakorinto 2 Kor.
Wagalatia Gal.
Waefeso Efe.
Wafilipi Flp.
Wakolosayi Kol.
1 Watesalonika 1 Tes.
2 Watesalonika 2 Tes.
1 Timoteo 1 Tim.
2 Timoteo 2 Tim.
Tito Tit.
Filemono Flm.
Waebrania Ebr.
Yakobo Yak.
1 Petro 1 Pet.
2 Petro 2 Pet.
1 Yoane 1 Yn.
2 Yoane 2 Yn.
3 Yoane 3 Yn.
` Yuda Yud.
Ufunuo Ufu.
VITABU VYA
AGANO LA KALE
Jina Ufupisho
Mwanzo Mwa.
Kutoka Kut.
Walawi Law.
Jina Ufupisho
Hesabu Hes.
Kumbukumbu la Tor.
Torati
Yosua Yos.
Waamuzi Amu.
Ruta Rut.
1 Samweli 1 Sam.
2 Samweli 2 Sam.
1 Wafalme 1 Fal.
2 Wafalme 2 Fal.
1 Mambo ya Siku 1 Sik.
2 Mambo ya Siku 2 Sik.
Ezra Ezr.
Nehemia Neh.
Esiteri Est.
Yobu Yob.
Zaburi Zab.
Mezali Mez.
Mhubiri Mhu.
Wimbo wa Solomono Wim.
Isaya Isa.
Yeremia Yer.
Maombolezo Omb.
Ezekieli Eze.
Danieli Dan.
Hosea Hos.
Yoeli Yoe.
Amosi Amo.
Obadia Oba.
Yona Yon.
Mika Mik.
Nahumu Nah.
Habakuki Hab.
Zefania Zef.
Hagai Hag.
Zekaria Zek.
Malaki Mal.
4
UTANGULIZI WA MWANDISHI
Kusudi la Kitabu hiki cha Mafu ndisho juu ya Biblia kwa Waamini ni kusaidiaMkristo kujifunza Biblia na kuendelea kujuana na Maandiko Matakatifu. Lakini
hakuna kitabu cha Mafundisho kinachoweza kukomboa faida ya Biblia yenyewe. Ki-
naweza kueleza tu maana yake na kusaidia msomaji kufahamu maneno anayosoma
yeye mwe nyewe ndani ya Maandiko Matakatifu. Ninaamini kabisa ya kwamba
Mkristo ye yote anayedumu kusoma na kujifunza Neno la Mungu anaweza kugeuka
mfanya kazi asiyeona haya, akifasiri vema neno la kweli (2 Tim. 2:15).
Lakini kujua tu maneno ya Biblia hakutoshi. Ni lazima kwa msomaji kutii ma-
fundisho yake ndani ya maisha yake ya kila siku. Kwa sababu hii mwandishi wa
kitabu hiki cha Mafundisho anajaribu sana kuonyesha namna gani msomaji anaweza
kuwa mtendaji wa Neno la Mungu, si msikiaji tu.Msomaji akisoma kitabu hiki cha Mafundisho peke yake, pasipo Biblia, kitabu hiki
hakitamsaidia, lakini kitageuka mtego kwake. Kitakuwa na faida tu kama kikiongeza
hamu yake kutafuta Maandiko yeye mwenyewe na kutii maagizo ya Bwana.
Ninaomba Roho Mtakatifu, aliyeongoza kuandika kwa Biblia, afungue na kutia
nuru nia ya msomaji wakati anapojitoa kwa neno hili zuri zaidi kujua Mungu kwa
njia ya Neno lake.
Namna gani kitabu hiki kiliandikwa
Vitabu vingi vimeandikwa kueleza maana ya Biblia kwa njia mbalimbali, na kwa
makusudi mbalimbali. Vingine vinaieleza kila neno moja moja, na vingine vinaieleza
sura kwa sura.
Maelezo ya vitabu vingine hayapatani na maana ya kweli ya Neno la Mungu.
Ndani ya kitabu hiki cha MAFU NDISHO YA BIBLIA kusudi la mwa ndishi William
MacDonald ni
1. kueleza maana ya Biblia waziwazi, hata maneno yale yaliyo ngumu kufahamu.
2. kuongoza msomaji kujuana na kupendana na Bwana Yesu Kristo sana, na
kugeuka mfuata na mtumishi wake mwaminifu. Unaweza kutumika na kitabu hiki kwa njia mba limbali.
1. Unaweza kusoma nusu nusu ya mafundisho ndani ya sura mbalimbali na kuonjautamu wake bila kufuata utara tibu fulani.
2. Labda wakati unaposoma Neno la Mungu, unakuta mashairi magumuambayo yanakushinda kabisa kufahamu. Maelezo ndani ya kitabu hiki yatakusaidia sana.
3. Elimu ya dini labda unataka kujua mafundisho ya Biblia juu ya neno fulani,kama sabato, ubatizo, haki ya Mungu. Ndani ya Tafsiri kwa ukurasa 3 utaona ma-
fundisho juu ya maneno 17 ya namna hii.
4. Kitabu fulani katika Biblia Labda watu wa kanisa lako, au katika Ecole du di-manche wamechagua kujifunza barua moja ya Agano Jipya pamoja. Utapata faida
kubwa kwa roho yako na kuweza kusaidia watu wengine vilevile kama ukijifunza
kila juma mbele ya kusanyiko lenu mafundisho yanayopatikana ndani ya kitabu hiki.
5. Kitabu kizima Kwa mwisho inge pasa kila Mkristo kusoma Biblia nzima.Utakutana na mashairi magumu mara kwa mara, lakini kitabu hiki cha Mafundisho
kitakusaidia sana kuyafahamu.
5
I. Jina la Agano Jipya
Mbele ya kujiingiza kabisa ndani ya
kujifunza habari za kitabu hiki, ni vizuri
tuwaze kwanza juu ya maneno mengine
ya Kitabu hiki Kitakatifu tunachoita
Agano Jipya.
Kweli kitabu hiki ni mapatano, ndiyo
agano la Mungu na watu wake.Kinaitwa Agano Jipya kuonyesha
kwamba ni namna nyingine na Agano la
Kale, ndilo Agano la zamani.
Mungu aliongoza kuandika Maagano
mbili yote, na kwa sababu hii yana faida
kwa Wakristo wote. Lakini hatushangai
kuona kwamba mwamini wa Kristo
anageuka kupita kwa sehemu ile ya
Bi blia inayopasha zaidi juu ya Bwana na
kanisa lake, na inayofundisha namna gani
anataka wanafunzi wake kuishi.
Augustine alionyesha vizuri ya kwamba
Agano Jipya lilifichwa ndani ya
Agano la Zamani;
Agano la Zamani linafunuliwa
ndani ya Agano Jipya.
II. Kanuni ya Agano Jipya
Neno hili kanuni ni tafsiri ya kanonkwa Kiyunani. Ni kama kipimo cha ma-
neno. Kanuni ya Agano Jipya ndiyo mku-
sanyo wa vitabu vilivyoandikwa kwa
maongezi ya Mungu. Tunaweza kujua
kama inafaa kwa vitabu hivi tu kuwandani ya kanuni, au kwamba inapasa
vitabu hivi vyote 27 kuwa sehemu yake?
Kulikuwa na maneno mengine yaliyo-
andikwa na Wakristo kwa wakati ule
(hata maandiko ya mafundisho ya
uwongo). Namna gani tunaweza kujua
kwamba maandiko yale 27 yanafaa kuwa
ndani ya kanuni?
Tunasikia mara nyingi ya kwamba
kuna baraza ya kanisa karibu na 400 A.D.
waliokusanya majina ya vitabu ndani ya
kanuni. Lakini vitabu hivi vilikuwa se-hemu ya kanuni mara moja nyuma yakuandikwa. Wanafunzi wenye kuogopa
Mungu na wenye ufahamu walitambua
maandiko matakatifu mara moja, kama
Petro alivyotambua maandiko ya Paulo
(2 Pet. 3:15, 16). Lakini hawakupatana
juu ya vitabu vingine (Yuda, 2 na 3
Yoane, kwa mfano) kwa wakati.
Kwa kawaida, kama kitabu kili-
andikwa na mtume, kama Matayo, Petro,
Yoane, au Paulo, au mmoja wa wale
waliotumika pamoja na mitume, hakuna
shaka ya kwamba kilikuwa sehemu ya
kanuni.
Baraza waliotambua kanuni yetu
waliyakinisha maneno yaliyokwisha ku -kubaliwa na watu kwa miaka mingi sana.Baraza hawakukusanya orodha ya vitabuvilivyoandikwa na maongozi ya Mungu,lakini waliandika orodha ya majina yavitabu vilivyoandikwa kwa maongozi yaMungu.
III. Waandishi
Mwandishi wa Agano Jipya ni Mungu
Roho Mtakatifu. Ni yeye aliyeongoza
MLANGO KWA
AGANO JIPYA
Maandiko haya ya Agano Jipya yana faida kubwa kupitaufahamu wetu, kwa maneno ya historia, na roho. Kristo wa Unabii wa Agano la Kale anageuka Kristo wa Historia ndani yavitabu vya Habari Njema; Kristo wa Uzoevu wa Maisha ndaniya Barua za Agano Jipya; na Kristo ndani ya Utukufu ndani yaUfunuo.
6
Mlango kwa Agano Jipya 7
Matayo, Marko, Luka, Yoane, Paulo,
Yakobo, Petro, na mwandishi wa Wae-
brania tusiyejua jina lake. Lakini lili -
andikwa na watu hawa vilevile. Haifai
kusema kwamba kwa sehemu lili-
andikwa na watu, na kwa sehemu na
Mungu. Njia nzuri zaidi kueleza neno
hili ni kusema ni maandiko ya Mungu
na watu pamoja kwa saa moja. Roho
Mtakatifu alizuiza waandishi wa bi-
nadamu kuandika maneno yasiyo kweli.
Hivi maandiko yao ya kwanza yalikuwa
bila makosa wala upungufu.
Kwa kutusaidia kufahamu neno hili,
tunaweza kusawanisha Neno (Biblia
iliyoandikwa na Mungu pamoja na watu),
na Neno Hai ndiye Bwana wetu Yesu
Kristo. Yeye si mtu kwa sehemu, na
Mungu kwa sehemu. Yeye ni Mungu
mkamilifu, pamoja na mtu mkamilifu.
Kwa sababu ya uungu wake haiku we -
zekana kwaye kuanguka au kufanya
zambi hata kidogo.
IV. Tarehe
Karibu miaka elfu moja ilihitajiwa
kuandika Agano la Kale (karibu 1400
400 av. J.C.). Agano Jipya liliandikwa
ndani ya muda wa miaka 50 tu (50100
A.D.)
Namna vitabu vinavyofuatana katika
Agano Jipya ni vizuri sana kwa kanisa
kwa kila wakati. Vinaanza na habari za
maisha ya Kristo, vinaendelea na habari
za kanisa, na mafundisho kwa kanisa, na
mwishoni vinafunua habari za kuja za
kanisa, na za dunia. Lakini vitabu hivi
havikuandikwa kwa utara tibu huu. Vili-
andikwa kwa wakati vilipohitajiwa. Tu-
nafikiri vitabu vya kwanza viliandikwa
kwa makanisa yaliyosimamishwa kwa -
nza, ndizo Barua ya Yakobo, kwa Wa-
galatia, na kwa Watesalonika, na
viliandikwa karibu na mwaka 96 A.D.
Vitabu vya Habari Njema vilifuata,
kwanza Matayo, au labda Marko, nyu -
ma yake Luka, kisha Yoane. Kitabu cha
mwisho ni Ufunuo, karibu na mwisho
wa miaka mia moja ya kwanza A.D.
V. Muhtasari
Vitabu vya Agano Jipya vinaweza
kujumlishwa hivi:
Vitabu vya historiaVitabu vine vya Habari Njema
Matendo
Vitabu vya BaruaBarua za Paulo
Barua nyingine
Kitabu cha mwishoUfunuo
Mkristo anayefahamu mafundisho
ya vitabu hivi vizuri ametengenezwa
kabisa kwa kila tendo jema (2 Tim.
3:17).
Tunaomba kitabu hiki kiweze ku-
saidia waamini wengi kuwa watumishi
wa faida kubwa kwa Bwana.
VI. Lugha
Agano Jipya liliandikwa kwa namna
ya Kiyunani ambayo Wayunani walitu-
mika nayo kila siku. Kiliitwa koinevilevile. Kwa njia ya majeshi ya Alesan-
duro, mfalme mkubwa, watu wa inchi
nyingi nyingine walisema lugha hii.
I. Vitabu vyetu vitukufu
vya Habari Njema
Vitabu hivi ni namna nyingine na
vitabu vyote vingine vilivyoandikwa.
Ndani yao ni habari za maisha ya watu
wengine, mezali juu ya mambo mbali -
mbali, na sehemu za hotuba nyingi za
Bwana wetu, na mazungumuzo yake na
watu.
Walimu wengine wa uwongo wali -
andika vitabu ambavyo waliita habari
njema, na kufundisha maneno yasiyo -
kuwa kweli. Lakini kwa karibu miaka
elfu mbili Wakristo wa kweli wameta -
mbua vitabu vilivyoandikwa na Matayo,
Marko, Luka, na Yoane tu, kuwa se-
hemu ya Maandiko Matakatifu.
II. Mifano Mine
Wakristo wengi wanafikiri mifano ya
vitabu vine vya Habari Njema minali -
ngana na mifano mine ya vitabu vya
Ezekieli na Ufunuo. Mifano hii ndiyo
simba, ngombe ndume (au ndama ya
ngombe), mwanamume na tai. Simba
inatufikirisha Habari Njema ya Matayo,
ndiyo Habari Njema ya Simba ya Yuda.
Ngombe ndume ni nyama ya kubeba
mizigo na kutumika kazi, na inatu-
fikirisha Marko, Habari Njema ya Mtu-
mishi. Mwanamume anatufikirisha sana
Luka, Habari Njema ya Mwana wa
Watu. Ndani ya kitabu kimoja cha ma-
fundisho tunasoma kwamba tai ni
mfano wa Yoane, mwenye mawazo ya
mbingu na roho.1
III. Wasomaji namna ine
Elezo zuri zaidi la neno hili ni ya
kwamba kwa njia ya vitabu hivi vine
vya Habari Njema, Roho Mtakatifu ali-
jaribu kusema na roho za watu namna
ine. Namna hizi ine za watu wanaishi
kwa wakati wa sasa vilevile.
Watu wote wanakubali kwamba
Matayo aliandika zaidi kwa Wayuda.
Alitaja mashairi au sehemu za mashairi
toka Agano la Kale. Hotuba zake, na
kizazi chake zinatufikirisha vivyo hivyo.
Ni kama Marko alikuwa katika mji
mkubwa wa ufalme, ndio Roma, wakati
alipoandika Habari Njema yake. Hivi
aliandika zaidi kwa Waroma, na kwa
milioni za watu wanaofanana nao
wanaopenda matendo kupita mawazo.
Hivi ndani ya Habari Njema yake tuna-
soma juu ya maajabu mengi na mifano
michache. Hakuna habari za kizazi
ndani ya Habari Njema hii, kwani
Waroma hawakuweza kuweka roho juu
ya kizazi Kiyuda cha Mtumishi.
Inaonekana wazi kwamba Luka
aliandika kwa Wayunani na kwa
Waroma, wengi waliopenda picha na
maandiko ya Wayunani.
Inabaki Yoane. Habari Njema yake
iliandikwa kwa watu wote. Ndani yake
kuna maneno ya kusaidia kila mtu.
Inatangaza njia ya wokovu kwa wa-
sioamini, na mafundisho ya ndani ndani
ya imani ya Wakristo.
IV. Mifano mine mingine
Kuna mifano mitamu mine mingine
ndani ya Agano la Kale ya maneno
yanayopatana na mifano ya vitabu vine
vya Habari Njema.
Tawi ni jina la Bwana wetu ndani
ya mashairi haya:
Daudi TAWI Mfalme (Yer.
23:5,6)
Mtumwa TAWI (Zek. 3:8)
Mtu TAWI (Zek. 6:12)
Tawi la BWANA (Yehova) (Isa. 4:2)
MLANGO KWA
VITABU VYA HABARI NJEMA
Vitabu vya Habari Njema ni Malimbuko ya maandiko yote. Origen
8
Kuna Tazama ine vile vile ndani
ya Agano la Kale zinazopatana kabisa na
vitabu vya Habari Njema:
Tazama, mfalme wako (Zek. 9:9).
Tazama, mtumishi wangu (Isa.
42:1)
Tazama, mtu (Zek. 6:12)
Tazameni Mungu wenu (Isa. 40:9).
Rangi ine za nguo ndani ya hema ya
Agano la Kale, na maana yao zinatu-
fikirisha Bwana wetu kwa njia ine:
Zambarau, ndiyo rangi ya Matayo,Habari Njema ya Mfalme, kama tuna -
vyoona ndani ya Amu. 8:26.
Nyekundu ni rangi watu waliyopatazamani kwa njia ya kuponda namna
moja ya kidudu. Inatufikirisha Marko,
Habari Njema ya mtumwa, mdudu
wala si mtu (Zab. 22:6).
Meupe inasema juu ya matendo yahaki ya watakatifu (Ufu. 19:8). Habari
Njema ya Luka inaonyesha wazi sanautu mkamilifu wa Kristo.
Samawi inatufikirisha rangi yambingu tuna yoona na macho (Kut.
24:10), mfano mzuri sana wa uungu wa
Kristo ndani ya Habari Njema ya Yoane.
V. Utaratibu na Maana
Maneno tunayosoma ndani ya Ha -
bari Njema hayakuandikwa kila mara
kufuatana na namna yalivyotokea.
Vizuri tukumbuke ya kwamba Roho
Mtakatifu alichagua kufunga na ku -
andika habari za mafundisho fulani
pamoja.
Neno hili linatusaidia kufahamu kwa
sababu gani maandiko ya Habari Njema
tatu yanafuatana ndani ya habari nyingi,
lakini habari zao ni mbalimbali kidogo
juu ya maisha na masemo ya Bwana
wetu mara nyingine. Habari Njema ya
Yoane ni namna nyingine na Matayo,
Marko na Luka, kwa sababu Yoane
hakutaka kuandika tena habari zilizo-
kwisha kuandikwa na waandishi wale
wengine. Maandiko yake ni zaidi juu ya
mafundisho ya roho.
VI. Sababu ya tofauti katika Habari Njema za Matayo,Marko na Luka
Kwa sababu gani maneno mengine
yanayoandikwa ndani ya vitabu hivi ni
sawasawa kabisa, lakini kwa maneno
mengine maandiko yao ni mbalimbali?
Neno hili halifazaishi wala kusumbusha
waamini wa kweli. Kuna watu wengi
waliotoa maelezo mbalimbali kwa neno
hili, lakini hakuna msingi ndani ya
Maandiko Matakatifu kwa maelezo yao
yasiyopatana na kweli ya Mungu mara
nyingine.
Jibu zuri zaidi ndilo masemo ya
Bwana Yesu mwenyewe ndani ya Yoane
14:26: Lakini Msaidizi, Roho Mtakatifu,
ambaye Baba atatuma kwa jina langu,
yeye atawafundisha ninyi yote, na
kuwakumbusha ninyi yote ambayo nili-
waambia ninyi.
Ni Roho Mtakatifu aliyeongoza ku -
andika kwa habari za mwanzo wa Luka
(Lk. 1:1), naye alifunua kweli nyingine,
ona 1 Kor. 2:13).
Hivi tukikuta habari zilizoandikwa na
waandishi wa vitabu vya Habari Njema si
sawasawa kila mara, vizuri tufahamu
kwamba kuna sababu kwa neno hili. Kwa
mfano ndani ya Matayo, Habari Njema
iliyokuwa zaidi kwa Wayuda, watu wa -
wili waliponyeshwa (mpofu na mwenye
pepo) kwani sheria iliagiza washuhuda
kuwa wawili au watatu. Marko na Luka
waliandika juu ya kuponyeshwa kwa mtu
yule aliyeonekana, ndiye mpofu Barati-
mayo.
Kufanana kwa mashairi mengine kuna
maana na mafundisho makubwa.
Ni kama Luka 6:20-23 ni karibu sana
sawa na hotuba ya Yesu mlimani katika
Matayo 5, lakini kwa Luka 6:17 Bwana
alikuwa ameshuka kwa pahali pa uwanda.
Sifa za heri kwa Matayo zinaonyesha
tabia njema ya wenyeji kamili wa ufalme,
lakini ndani ya Luka tunaona zaidi maisha
na mwenendo wa wanafunzi wa Kristo.
Luka 6:40 na Matayo 10:24 yana -
fanana sana, lakini ndani ya Matayo, Yesu
Vitabu vya Habari Njema 9
ndiye Mwalimu na sisi ni wanafunzi
wake. Ndani ya Luka, mwenye kufanya
wa nafunzi ni mwalimu, na yule amba ye
anamfundisha ni mwanafunzi wake.
Matayo 7:22 ni juu ya utumishi kwa
Mfalme. Luka 13:25-27 ni juu ya ushirika
pamoja na Bwana.
Luka 15:4-7 ni mashitaki makali ya
Wafarisayo, lakini Matayo 18:12,13
yanaonyesha mapendo ya Mungu kwa
watoto.
Wakati waamini tu walipokuwa pa -
moja na Yoane Mbatizaji, Yoane alisema,
Atawabatiza ninyi na Roho Mtakatifu
(Mk. 1:8; Yn. 1:33). Wakati kulipokuwa
na wasioamini, na zaidi Wafarisayo,
pamoja na waamini, alisema, Atawaba-
tiza ninyi na Roho Mtakatifu na kwa
moto (ubatizo wa hukumu) (Mt. 3:11;
Lk. 3:16).
Hivi hakuna mabishano hata kama
habari nyingine namna hii ni mbali mbali
kidogo. Ni mbalimbali na kusudi, na
yanasaidia mwamini kukaa kuwaza sana
juu ya Maneno Matakatifu ya Mungu.
10 Vitabu vya Habari Njema
HABARI NJEMA KAMA ALIVYOANDIKA
MATAYO
Utangulizi
Habari Njema kama ilivyoandikwa na Matayo, ndiyo mwingiliomzuri sana kwa Agano Jipya toka Agano la Kale.
I. Nafasi ya pekee katika Kanuni
Habari Njema ya Matayo inakuta -
nisha Agano la Kale na Agano Jipya.
Shairi la kwanza linaturudisha kwa baba
mzee wa watu wa Mungu katika Agano
la Kale, ndiye Abrahamu, na kwa
mfalme mkubwa wa kwanza wa Israeli,ndiye Daudi. Inataja mashairi mengi
ya Maandiko Matakatifu yaliyoandikwa
kwa Kiebrania, nayo ni kitabu kili-
chowekwa kwanza ndani ya Agano
Jipya. Kwa sababu ya maneno haya
Matayo ndipo pahali pazuri kuanza ku-
julisha watu wa dunia habari za Kristo.
Kwa miaka mingi Habari Njema ya
Matayo ilikuwa kwa pahali pa kwanza,
mbele ya Marko, Luka na Yoane, kwa
sababu watu waliamini iliandikwakwanza. Vilevile namna habari zili-
vyoandikwa na Matayo zinafuatana
vizuri, na hivi zinafaa kwa kusoma
kanisani. Kwa sababu hii watu wali -
penda Matayo kupita Habari Njema
nyingine, lakini watu walipenda Yoane
sana vilevile.
Si neno la lazima kuamini ya
kwamba Habari Njema ya Matayo ili -
andikwa kwanza. Lakini zaidi ya Wa -
kristo wa kwanza walikuwa Wayuda,
ndio watu wengi sana. Inge kuwa akili
njema kusaidia mahitaji ya roho ya
Wakristo hawa kwanza.
II. Mwandishi
Ilionekana wazi kwa watu wote za-
mani ya kwamba Matayo, mtoza kodi,
aliyeitwa Lawi vilevile, aliandika Habari
Njema ya kwanza.
Waandishi wengine wa zamani, ndio
Justin Martyr, Dionysius wa Korinto,
Teofilo wa Antiokia, na Athenagoras,
wa Atene walifikiri vivyo.
Labda Matayo alihubiri kwa miaka
kumi na mitano katika Palestine, kisha
alikwenda kuhubiri Habari Njema katika
inchi nyingine. Labda ndani ya mwaka
45 A.D. aliachia Wayuda waliokwisha
kuamini Yesu mwandiko wa upesi wa
Habari Njema yake (au hotuba za Yesu
tu), na kwa wakati wa nyuma ali -
timiza maandiko haya kwa watu wote.
Namna Habari Njema hii ilivyo -
andikwa inashuhudu ya kwamba ili-
andikwa na Myuda mwenye kupenda
Mungu na Agano la Kale, na aliyekuwa
mwandishi mzuri. Akiwa mwenye kutu-
mikia Waroma angejua lugha yao na
alijua lugha ya watu wake vilevile, ndiyo
Kiaramaic. Ndani ya Habari Nje ma hii tu-
nasoma habari za hesabu, mifano juu ya
mali, vivyo hivyo, mambo yaliyo kuwa
kazi ya kila siku kwa mtoza kodi.
Hata hivi walimu wengi kwa wakati
wa sasa wanafikiri, kwa sababu mbali-
mbali, ya kwamba Habari Njema ya
11
HABARI YALIYOMO
1. KIZAZI NA KUZALIWA KWA MASIYA-MFALME (Sura 1)
2. MIAKA YA KWANZA YA MASIYA-MFALME (Sura 2)
3. MATAYARISHO KWA UTUMISHI WA MASIYA
NA MWANZO WA UTUMISHI WAKE (Sura 3, 4)
4. KUSIMAMISHWA KWA UTARATIBU WA UFALME (Sura 57)
5. MAAJABU YA UWEZO NA NEEMA YA MASIYA NA
MAWAZO YA WATU JUU YAO (8:19:34)
6. MITUME YA MASIYA-MFALME WANATUMWA KWA
ISRAELI (9:3510:42)
7. KUONGEZEKA KWA UADUI NA KUKATALIKA (Sura 11, 12)
8. MFALME ANATANGAZA MWANZO WA UFALME WA NAMNA
NYINGINE, KWA WAKATI TU, KWA SABABU YA
KUKATALIWA NA ISRAELI (Sura 13)
9. NEEMA YA MASIYA HAIPUNGUKI LAKINI UADUI WA
WATU UNAONGEZEKA (14:116:12)
10. MFALME ANATAYARISHA WANAFUNZI WAKE (16:1317:27
11. MFALME ANAFUNDISHA WANAFUNZI WAKE (Sura 1820)
12. KUONYESHWA NA KUKATALIWA KWA MFALME (Sura 2123)
13. HOTUBA KWA MLIMA WA MZEITUNI (Sura 24, 25)
14. MAUMIVU NA MAUTI YA MFALME (Sura 26, 27)
15. KUSHINDA KWA MFALME (Sura 28)
12 Utangulizi
Marko iliandikwa kwanza, si Matayo.
III. Tarehe
Kama ni kweli ya kwamba Matayo
aliandika mwandiko wa upesi wa Habari
Njema yake (au hotuba za Yesu tu) kwa
lugha ya Kiaramaic kwa 45 A.D. (miaka
15 nyuma ya kurudi mbinguni kwa
Yesu) wenye elimu wanafikiri kwamba
alitimiza maandiko haya kwa watu wote
kwa lugha ya Kiyunani kwa mwaka 50
au 55 A.D., au hata nyuma kupita.
IV. Msingi na Jambo Kubwa
Matayo alikuwa kijana wakati Yesu
alipomwita. Alikuwa Myuda na aliji-
funza na kufanya kazi ya mtoza kodi,
lakini aliacha vyote kufuata Kristo. Kwa
sababu hii alibarikiwa kwa njia ya
kugeuka mmoja wa mitume kumi na
wawili. Baraka nyingine ndiyo hii:
alichaguliwa ku andika Ha bari Njema hii
ambayo wenye elimu wanafikiri ni
Habari Njema ya kwanza. Inaaminiwa
vilevile ya kwamba Matayo na Lawi ni
mtu mmoja (Marko 2:14; Luka 5:27).
Ndani ya Habari Njema yake Ma tayo
anaonyesha ya kwamba Yesu ndiye
Masiya wa Israeli, ambaye watu wali -
mngojea kwa miaka mingi sana, na ya
kwamba yeye peke yake ana haki ya
kukaa juu ya kiti cha kifalme cha Daudi.
Si kusudi la kitabu hiki kuandika
habari za maisha mazima ya Yesu. Ki-
naanza na kizazi cha Kristo na miaka
yake ya kwanza, halafu kinapita kwa
mwanzo wa utumishi wake wakati
alipokuwa na miaka karibu makumi
tatu. Matayo aliongozwa na Roho Mta -
katifu kuchagua habari zile za maisha na
utumishi wa Mwokozi amba zo zina -
mwonyesha kuwa Mpakali wa waMungu (ndiyo maana ya Masiya naKristo). Kitabu che nye we kinaendelea
Maelezo
1. KIZAZI NA KUZALIWA KWA
MASIYA-MFALME (Sura 1)
1. Kizazi cha Yesu Kristo (1:1-17)
Labda wasomaji wengine wange-
fazaika kwa sababu gani Matayo alianza
kitabu chake na kizazi, ndiyo majina tu.
Faida yao nini?
Tufahamu basi ya kwamba kizazi
hiki kinahitajiwa kabisa kwani ni msingi
wa habari zote zinazofuata. Kilihitajiwa
kuonyesha ya kwamba Yesu ni mzao wa
Daudi kwa njia ya sheria kwa kuweza
kuhakikisha ya kwamba yeye ni Ma-
siya-Mfalme wa Israeli. Hivi Matayo
alianza maandiko yake na kushuhudu
ya kwamba Yesu alikuwa mriti wa haki
wa kiti cha kifalme cha Daudi.
Kizazi hiki kinaonyesha wazazi wa
Yesu Mfalme wa Israeli kwa njia ya she-ria; kizazi ndani ya Luka kinaonyesha
wazazi wake kama Mwana wa Daudi.Kizazi cha Matayo kinaonyesha wazazi
wa Yesu Mfalme kwa njia ya Solomono;
ndani ya Luka tunaona Daudi kama
mzazi wa mwana mwingine, ndiye
Natani. Kizazi katika Matayo kina -
kwisha na Yosefu ambaye alilea na ku-fanya Yesu mwana wake; ndani ya Luka3 tunaona Yesu kama Mwana aliyeza-liwa kweli na Maria.
Miaka elfu moja mbele Mungu ali-
fanya agano na Daudi, bila masharti, ya
kwamba atampa ufalme ambao utaende-
lea milele, na wazao kutawala daima
(Zaburi 89:4, 36, 37). Agano hili lime-
timizwa sasa ndani ya Kristo. Yeye ni
mriti, kwa sheria, wa kiti cha kifalme
cha Daudi kwa njia ya Yosefu, na mzao
kabisa wa Daudi kwa njia ya Maria.
Kwa sababu yeye ni hai milele ufalme
wake utaendelea kwa milele, naye ata -
tawala kwa milele kama Mwana mku -
bwa zaidi wa Daudi.
1:1-15 Mwanzo wa shairi 1, Kitabu
cha kizazi cha Kristo, Mwana wa
Daudi, Mwana wa Abrahamu, una -
fanana na mwanzo wa Mwanzo 5:1:
Hiki ni kitabu cha vizazi vya Adamu.
Mwanzo kinatupasha juu ya Adamu ya
kwanza; Matayo kinatupasha juu ya
Adamu ya mwisho. Adamu wa kwanza
alikuwa mwanzo wa muumbo wa
kwanza, ya dunia hii; Kristo ni mwanzo
wa muumbo wa mwisho, wa roho.
Neno kubwa la Habari Njema hii ni
Yesu Kristo. Jina la Yesu linamwonye-
sha kama Yehova-Mwokozi; na Kristo
(Mpakaliwa) kama Masiya wa Israeli
ambaye walikuwa wamengoja kufika
kwake kwa muda mrefu. Mwana wa
Daudi linatufikirisha kazi zake mbili
kama Masiya na Mfalme katika Agano
la Kale. Mwana wa Abrahamu lina -
sema juu ya Bwana wetu kama Yule
atakayetimiza mwishoni ahadi zilizo-
fanywa kwa mwenye kuanza taifa la
Waebrania.
Matayo 1 13
hata habari za hukumu, mauti, maziko,
ufufuko na kurudi kwa Bwana Yesu
mbinguni, habari ambazo zilizo msingi
kwa wokovu wa watu. Ni kwa sababu
hii kitabu hiki kinaitwa Habari Njema
si kwa sababu kinafundisha namna gani
wenye zambi wanaweza kupata wo -
kovu, lakini kwa sababu kinaonyesha
kazi ya Kristo kama zabihu kwa zambi,
kwa njia yake inawezekana kwa wenye
zambi kupata wokovu.
Kusudi la kitabu hiki cha Maelezo yaAgano Jipya kwa Waamini si kutafsirikila neno, lakini kuamsha ndani ya
mwamini hamu kutafuta Maandiko yeye
mwenyewe, na zaidi ya yote hamu
kubwa kwa kurudi kwa Mfalme.
14 Matayo 1
Kuna sehemu tatu kwa kizazi che -
nyewe: toka Abrahamu kufika Yese,
toka Daudi kufika Yosia, na toka Yeko-
nia kufika Yosefu. Sehemu ya kwa nza
inafika hata maisha ya Daudi; sehemu
ya pili inapasha juu ya muda wa ufalme;
sehemu ya tatu inachunga majina ya
wazao wa mfalme kwa wakati wa muda
wa uhamisho (av. J.-C. 586 na nyuma
yake vilevile).
Ndani ya mashairi haya tunaona ma-
jina ya wanawake wane: Tamari, Ra-
haba, Ruta na Batiseba (yule mke wa
Uria). Hili ndilo neno la kusha ngaza,
kwa sababu haikuwa desturi kuingiza
majina ya wanawake ndani ya vizazi.
Zaidi ya ile wawili wa wanawake wa-
likuwa makahaba (Tamari na Rahaba),
mmoja wao alitenda uzini (Batiseba), na
wawili walikuwa watu wa Mataifa (Ra-
haba na Ruta). Labda kwa njia ya ku-
ingiza majina yao ndani ya kizazi hiki
tunaweza kuona, kama kwa maficho, ya
kwamba kuja kwa Kristo kutaleta wo -
kovu kwa wenye zambi, neema kwa
Mataifa, na ya kwamba ndani ya Kristo
tofauti ya kabila na hali ya kuwa mume
au mke haiko tena.
Tuone vilevile jina la mfalme Yeko-
nia. Ndani ya Yeremia 22:30 Mungu
alilaani mtu huyu:
BWANA anasema hivi:
Andikeni habari za mtu huyu
kwamba hana watoto,
mtu asiyesitawi siku zake zote;
maana hapana mtu katika wazao
wake atakayesitawiwa,
akikaa katika kiti cha ufalme cha
Daudi,
na kutawala tena katika Yuda.
Kama Yesu angalikuwa mwana wa
hakika wa Yosefu, angalikuwa chini yalaana hili vilevile. Lakini ilikuwa lazima
kwaye kuwa mwana wa Yosefu kwa njia
ya sheria kusudi awe mwenye kuriti
haki ya ufalme wa Daudi. Neno hili lili-
wezekana kwa njia ya ajabu ya kuzaliwa
kwake na bikira Maria. Hivi Yesu
alikuwa mriti kwa sheria wa kiti chaufalme kwa njia ya Yosefu. Alikuwa
Mwana wa hakika wa Daudi kwa njia yaMaria. Laana ya Yekonia haikuwa juu ya
Maria na watoto wake kwa sababu ha -
kuwa mzao wa Yekonia.
1:16 Kwa njia ya Kiyunani tunafa-
hamu kwamba aliyezaa inasema juu
ya Maria, si juu ya Yosefu.
Kuna maneno mengine yaliyo nguvu
kufahamu ndani ya mashairi haya:
1:17 Matayo anasema waziwazi ya
kwamba kuna sehemu tatu ndani ya
kizazi hiki, na kila sehemu ina vizazi
kumi na ine ndani yake. Lakini tunafa-
hamu kwa njia ya Agano la Kale ya
kwamba hakutaja majina yote. Kwa
mfano, katikati ya Yoramu na Uzia
(sh.8): Ahaziah, Yoasi, na Amazia wa-
litawala kama wafalme vilevile (ona
2 Fal. 814; 2 Sik. 2125).
Ni kama vizazi vya Matayo na Luka
vinapitana wakitaja majina mawili, Sa -
ltieli na Zerubali (Matayo 1:12,13; Luka
3:27). Ni nguvu kufahamu kwa sababu
gani vizazi vya Yosefu na Maria vina -
ungana hivi, lakini nyuma yake vinate -
ngana tena. Na zaidi ya ile vitabu hivi
viwili vya Habari Njema vinataja, kama
Ezra 3:2, Zerubali kuwa mwana wa
Saltieli, lakini ndani ya 1 Sik. 3:19 tuna-
soma kwamba Zerubali alikuwa mwana
wa Pedaya.
Neno lingine ambalo linatufazaisha
ni ya kwamba ndani ya Matayo kuna
vizazi 27 toka Daudi kufika Yesu, lakini
ndani ya Luka kuna v izazi 42. Hata
kama waandishi hawa wawili wana -
andika habari za vizazi vya watu mba -
limbali, ni nguvu kufahamu kwa sababu
gani hesabu ya vizazi ni mbalimbali
hivi.
Basi inapasa msomaji wa Biblia ku-
fikiri nini juu ya maneno haya? Kwanza,
msingi wetu ni ya kwamba Biblia nzima
ni Neno la Mungu. Ma andiko yake yote
yameongozwa na Yeye tu. Hivi hakuna
Matayo 1 15
makosa ndani yake hata kidogo. Mengi
ya maandiko yake yanashinda ufahamu
wetu kwani yanatoka kwa Mungu.
Hivi tunaona ya kwamba tuna -
shindwa kufahamu maneno mengine
kwa sababu tuko watu wa kujua nusu tu,
si kwa sababu maandiko mengine ya
Biblia si kweli. Ingepasa maneno haya
kutusukuma kutafuta Maandiko sana
kwa kupata majibu. Ni utukufu wa
Mungu kuficha neno, lakini utukufu wa
wafalme ni kutafuta neno (Mez. 25:2).
Hata kama wenye elimu wame tafuta
maneno haya sana, hawakuweza kuonye -
sha ya kwamba maneno yali yo andikwa
ndani ya Biblia si kweli. Kuna maelezo
ya akili kwa maneno haya yote yasiyo-
patana kwa mafikiri yetu, na maelezo
haya yana maana ya faida kwa roho.
B. Yesu Kristo amezaliwa na Maria
(1:18-25)
1:18 Kuzaliwa kwa Yesu Kristo
kulikuwa namna nyingine na kuzaliwa
kwa watu wote wengine ndani ya kizazi
hiki. Pale tuliona tena na tena: Fulani
akazaa fulani, lakini sasa tunasoma juu
ya kuzaliwa kwa mtoto asiyekuwa na
baba. Lilikuwa shauri kwa Maria kuwa
mke wa Yosefu, lakini hawajaoana bado.
Kwa wakati wa Agano Jipya mume na
mke walipatana kuoana, lakini hawaku-
timiza ndoa hii kwanza. Waliweza ku-
vunja mapatano haya ya kuoana kwa
njia ya kuachana tu. Hata kama mume
na mke waliopatana kuoana hawakukaa
kwa nza pamoja kufika siku ya ndoa yao,
uzini kwa muda ule ulikuwa zambi
mbaya sana uliostahili azabu ya mauti.
Ndani ya muda huu wa kupatana
kuoa, bikira Maria alipata mimba kwa
Roho Mtakatifu; ajabu sana. Malaika
alijulisha Maria habari hizi mbele:
Roho Mtakatifu atakuja juu yako, na
nguvu zake Mungu aliye juu zitakutulia
kivuli (Luka 1:35). Lakini bila shaka
watu walianza kuwa na shaka juu ya
Maria wakati mimba yake ilipoanza
kuonekana. Tangu zamani watu hawa-
jaona bikira akipata mimba. Wakati
watu walipoona mke asiyeolewa akipata
mimba, walifikiri neno moja tu, ndilo
mke huyu alikuwa amezini.
1:19 Hata Yosefu hakujua kwanza
maana ya kweli ya mimba ya Maria. Ali-
weza kuwa na uchungu rohoni kwa
sababu ilionekana kwamba Maria ha -
kuwa mwaminifu kwake; na vilevile
watu waliweza kufikiri Yosefu mwe -
nyewe alikuwa amezini naye! Lakini
Yosefu alipenda Maria na kwa sababu
alitaka haki ifanywe, alifanya shauri ku-
vunja mapatano yao ya ndoa kwa siri.
Alitaka kuepuka haya mbele ya watu.
1:20 Wakati mtu huyu mpole alipo -
fanya shauri kuchunga Maria asipate
haya mbele ya watu, malaika ya Bwana
alitokea kwake katika ndoto aki -
mwita Yosefu, mwana wa Daudi.
Bila shaka malaika alimwita na jina hili
kumkumbusha ya kwamba yeye mwe -
nye we alikuwa mzao wa mfalme Daudi,
na kutayarisha mafikiri yake kwa ku-
tokea kwa Mfalme-Masiya wa Israeli.
Haifai kwa Yosefu kuwa na shaka juu ya
kuoa Maria. Mimba yake ilikuwa ya
Roho Mtakatifu.
1:21 Halafu malaika alimwonyesha
kama Mtoto atakayezaliwa atakuwa ki-
jana au msichana, na jina lake na kazi
yake. Maria atazaa Mwana. Ataitwa
YESU (maana yake Yehova ni wo -
kovu au Yehova, Mwokozi). Ku-
patana na jina lake, ataokoa watu wake
toka zambi zao. Mtoto huyu alikuwa
Yehova mwenyewe, akifikia dunia kwa
wakati kuokoa watu toka azabu ya
zambi, toka uwezo wa zambi, na mwi -
shoni toka hata ukaribu wa zambi.
1:22 Wakati Matayo alipoandika ma-
neno haya alifahamu kwamba kuanza
saa ile Mungu atatendea watu wa dunia
namna nyingine. Unabii ambao Isaya
alitoa zamani juu ya Masiya yalitimizwa
kwa njia ya Mtoto wa Maria: Maneno
16 Matayo 1, 2
haya yote yamekuwa litimie neno
lililosemwa na Bwana kwa nabii.
Matayo ali amini kwamba alikuwa
Mungu aliyesema maneno haya kwa
njia ya Isaya miaka 700 au zaidi mbele
ya kuzaliwa kwa Kristo.
1:23 Unabii huu kwa Isaya 7:14
ulionyesha kwamba kuzaliwa kwa
Mtoto huyu kutakuwa namna nyingine
(Tazama, bikira atachukua mimba),
mtoto atakuwa kijana (naye atazaa
mwana), na jina la mtoto (nao
watamwita jina lake Emanueli). M a -
tayo alieleza kwamba maana ya Ema -
nueli ni Mungu pamoja nasi. Hatusomi
kwa mba Kristo aliitwa na jina hili
wakati alipokuwa duniani; aliitwa
Yesu tu kila mara. Lakini maana ya
jina hili Yesu (ona maelezo juu ya sh.21)lina maana ya Mungu pamoja nasi.
Labda Kristo ataitwa Emanueli wakati
atakapokuja mara ya pili.
1:24 Kwa sababu ya masemo ya
malaika Yosefu hakuachana na Maria.
Alikaa pamoja naye kufika saa ya kuza-
liwa kwa Yesu, kisha alimwoa.
1:25 Watu wengine wanafundisha ya
kwamba Maria alikuwa bikira kwa mai -
sha yake mazima, lakini shairi hili
linaonyesha kwamba mafundisho yale si
kweli hata kidogo. Kuna mashairi me -
ngine yanayoonyesha kwamba Maria
alizaa watoto kwa njia ya Yosefu, ndiyo
Matayo 12:46; 13:55,56; Marko 6:3;
Yoane 7:3,5; Matendo 1:14; 1 Wakorinto
9:5; na Wagalatia 1:19.
Wakati Yosefu alipooa Maria kuwa
mke wake, alifanya Mtoto wa Maria
kuwa mwana wake vilevile. Neno hili
liligeuza Yesu mriti, kwa njia ya sheria,
wa kiti cha ufalme wa Daudi. Akitii
masemo ya malaika aliita jina la Mtoto
mchanga Yesu.
Hivi Masiya-Mfalme alizaliwa. Yule
aliye tangu milele, mwenye uwezo wote,
aligeuka mtoto mchanga. Bwana wa
utukufu alificha utukufu wake ndani ya
mwili wa mtu, na katika yeye utimilifu
wote wa Mungu ukakaa kwa mwili
(Kol. 2:9).
2. MIAKA YA KWANZA YA
MASIYA-MFALME (Sura 2)
A. Waakili wanakuja kuabudu
Mfalme (2:1-12)
2:1,2 Ni nyepesi kufazaika juu ya
namna matukio yalivyofuatana wakati
wa kuzaliwa kwa Kristo. Ni kama shairi
1 linaonyesha kwamba Herode alijaribu
kuua Yesu wakati Yosefu na Maria
walipokuwa kwanza ndani ya nyumba
ya kulisha ngombe, lakini habari tuna-
zosoma ndani ya mashairi mengi me -
ngine yanaonyesha kwamba miaka
miwili ilikuwa imepita. Ndani ya shairi
11 Matayo anasema kwamba waakili
waliona Yesu ndani ya nyumba. Agizo
la Herode kuua watoto wasiokuwa na
miaka miwili kwanza linaonyesha
vilevile kwamba alitoa agizo hili nyuma
ya wakati fulani tu.
Herode Mkuu huyu alikuwa mzao
wa Esau, na kama wazao wote wa Esau
alikuwa adui ya Wayuda. Aligeuka na
kushika dini ya Wayuda, lakini labda
hakufanya hivi na roho ya kweli lakini
kusaidia utawala wake tu. Waakili toka
ma shariki walifika karibu na mwisho
wa utawala wake kutafuta Mfalme wa
Wayuda. Labda wanaume hawa wa-
likuwa makuhani wapagano walioabudu
viumbe. Kwa sababu ya akili yao na
uwezo wao wa kutabiri, walichaguliwa
mara nyingi kusaidia wafalme. Hatujui
pahali gani walipokaa kwa mashariki,
kama walikuwa watu wengapi, na kama
walisafiri kwa muda gani.
Nyota ile katika mashariki iliwa -
fahamisha kwamba mfalme alikuwa
ame zaliwa, nao walikuja kumwabudu.
Ina wezekana kwamba walijuana na
unabii katika Agano la Kale juu ya kuja
kwa Masiya. Labda walisikia habari za
unabii wa Balama kwamba Nyota ata-
Matayo 2 17
toka katika Yakobo (Hes. 24:17) na wa -
liunganisha habari hizi na unabii wa
majuma makumi saba yaliyoonyesha
wakati Kristo ataka po kuja mara ya
kwanza (Dan. 9:24,25). Lakini zaidi tu-
nafikiri alikuwa Mungu ambaye aliwa-
julisha habari hizi.
Wenye elimu wamejaribu kueleza
kuonekana kwa nyota hii. Lakini kuha-
mahama kwa nyota hii kulikuwa namna
nyingine na desturi za nyota. Ilitangulia
waakili na kuwaongoza toka Yerusalema
hata nyumba pahali Yesu alipokuwa
(sh.9). Halafu ilibaki palepale. Lilikuwa
ajabu tu.
2:3 Wakati mfalme Herode alipo -
sikia ha bari za kuzaliwa kwa mtoto ata -
kayekuwa mfalme wa Wayuda ali-
fazaika sana. Mtoto namna hii ange -
weza kuwa hatari kwa utawala wake juu
ya Wayuda. Watu wa Ye rusalema pia
walifazaika vilevile. Ingalipasa watu wa
mji kupokea habari hizi na furaha, lakini
waliogopa zita kasirisha watawala wao
Waroma ambao walichukia.
2:4-6 Herode alikutanisha viongozi
vya dini Wayuda kuulizana nao pahali
gani Kristo atakapozaliwa. Wakubwa
wa makuhani walikuwa kuhani mkubwa
na wana wake (na labda watu wengine
wa jamaa yake). Waandishi wa watu wa-
likuwa wafundi wa Sheria ya Musa.
Walichunga na kufundisha sheria na
walifanya kazi ya waamuzi. Makuhani
na waandishi walitaja Mika 5:2 mara
moja, ndilo shairi lililoonyesha kwamba
Betelehemu wa Yudea ndipo pahali
Mfa lme atakapozaliwa. Katika Mika 5:2
kwa Agano la Kale pahali pale panaitwa
Betelehemu-Efurata. Kulikuwa na miji
mingine katika Palestina iliyo itwa Bete -
lehemu, na jina hili linaonyesha wazi
kwamba Betelehemu huu ulikuwa ka -
tika wilaya ya Efurata ndani ya mipaka
ya makabila ya Yuda.
2:7,8 Mfalme Herode aliita wa -
akili kwa siri kuuliza saa gani nyota
ili onekana kwanza. Akiwaita kwa siri
ilifunua kusudi lake baya: Alihitaji kujua
neno hili ili aweze kufahamu kama
Mtoto gani ndiye Kristo. Akitaka ku-
ficha kusudi lake alituma waakili
kutafuta habari hizi na kumjulisha
wakati walipokwisha kuzipata.
2:9 Wakati waakili waliposhika njia,
nyota ambayo waliona kwa mashariki
mbele ilionekana tena. Neno hili lina -
onyesha kwamba nyota ile haikuwa -
ongoza kwa safari yao nzima toka
mashariki. Lakini sasa iliwaongoza na
kuwafikisha kwa nyumba pahali Mtoto
alipokuwa.
2:10 Waakili walifurahi sana wa -
kati walipoona nyota. Watu hawa wa
Mataifa walitafuta Kristo na bidii; He -
rode alifanya shauri kumwua; ma kuhani
na waandishi hawakufikiri kwanza sana
juu yake; watu wa Yeru salema wali-
fazaika. Habari hizi zote zinaonyesha
kwa ufupi namna gani Masiya ata -
pokewa duniani.
2:11 Wakati waakili walipoingia
nyu mba waliona Mtoto pamoja na
Maria, mama yake. Wakaanguka,
wakamwa budu na kumtolea zawadi za
bei kubwa za zahabu, uvumba na mane-
mane. Ona ya kwamba waliona Yesu
pamoja na mama yake. Ilikuwa desturi
kutaja mama kwanza na mtoto nyuma
yake, lakini Mtoto huyu alikuwa namna
nyingine, na ilipasa kumpa pahali pa
kwanza. Ona vilevile mashairi 13,14,
20,21. Waakili waliabudu Yesu, si Mariawala Yosefu. (Matayo hakutaja Yosefu
hapa, na nyuma kidogo jina lake ha-
likuonekana tena ndani ya maandiko ya
Habari Njema.) Ni Yesu anayestahili
kupokea sifa na kuabudu, si Maria au
Yosefu.
Hazina waakili walizoleta zina ma -
ana kubwa. Zahabu ni mfano wa uungu
na utukufu; inatufikirisha ukami lifu wa
kungaa kwake aliye Mungu. Uvumba ni
marasi au harufu tamu; unatukumbusha
18 Matayo 2
maisha yake matamu na bila zambi.
Manemane ni majani ma chungu. Ya -
nasema juu ya maumivu yake wakati
atakapobeba azabu kwa zambi za dunia.
Watu hawa wa Mataifa wakileta zawadi
wanatukumbusha maneno ya Isaya katika
60:6. Isaya alitabiri kwamba Mataifa wa -
ta fikia Masiya na zawadi, lakini alitaja
zahabu na uvumba tu: . . . wataleta zaha -
bu na uvumba; na wa tatangaza sifa ya
Bwana. Kwa nini Isaya hakutaja mane-
mane? Kwa sababu alikuwa akisema juu
ya kuja kwa pili kwa Kristo na uwezo
na utukufu. Hatateswa kwa wakati ule,
hivi Isaya hakutaja manemane. Lakini
Matayo alitaja manemane kwa sababu
aliandika juu ya kuja kwa Kristo mara
ya kwanza. Ndani ya Matayo tunasoma
juu ya mateso ya Kristo; ma shairi haya
katika Isaya yanaonyesha utukufu wake
kwa wakati wa kuja.
2:12 Waakili walitii maonyo wal i-
yopewa katika ndoto wasirudi karibu na
Herode, wakafuata njia nyingine kurudi
kwao. Hakuna mtu anayekutana na Kristo
na roho ya kweli atakayerudi bila kugeuka
namna nyingine. Kukutana naye ku-
nageuza maneno yote ya maisha yetu.
B. Yosefu, Maria, na Yesu wana-
kimbia kwa Misri (2:13-15)
2:13,14 Tangu utoto wake Bwana
wetu alikuwa katika hatari. Ni wazi ya
kwamba alizaliwa kusudi afe kwa saa
iliyochaguliwa na Mungu. Hakuna mtu
anayeishi akifanya mapenzi ya Mungu
anayeweza kufa mbele ya kumaliza kazi
yake. Malaika ya Bwana alisema na
Yosefu katika ndoto aki mbilie Misri
pamoja na Yesu na mama yake kwa
sababu Herode alikuwa tayari kutafuta
mtoto aweze kumwua. Hivi Yosefu na
jamaa yake waligeuka wakimbizi. Hatu-
jui kama walikaa miaka mingapi katika
Misri. Wakati Herode alipokufa wali-
weza kurudi tena kwao.
2:15 Hivi unabii mwingine katika
Agano la Kale ulitimizwa na kupata
maana mpya. Mungu alikuwa amesema
kwa njia ya nabii Hosea, niliita
mwana wangu toka Misri (Hos. 11:1).
Wakati unabii huu ulipotolewa kwanza,
ulikuwa juu ya kuponyeshwa kwa Israeli
toka utumwa kwa Misri. Lakini ulikuwa
na maana nyingine vilevile kupo -
nyeshwa kwa Kristo na kurudi kwake
kwa Israeli toka Misri.
Wakati Bwana atakaporudi duniani
kuta wala katika haki Misri itakuwa
moja ya inchi zitakazoshiriki ndani
ya baraka za uta wala wa Kristo kwa
miaka elfu moja (Isa. 19:21-25; Zef.
3:9,10; Zab. 68:31). Kwa sababu gani
taifa hili waliokuwa adui wa Israeli
tangu zamani wata barikiwa hivi? La -
bda ni kama ala ma ya asante ya Mungu
kwa sababu lilikuwa kimbilio kwa
Bwana Yesu?
C. Herode anaua watoto wadogo
katika Betelehemu (2:16-18)
2:16 Wakati waakili wasiporudi He -
rode alifahamu kwamba alikuwa ame -
danganywa nao na hakuweza kutimiza
shauri lake kuvumbua pahali Mfalme ki-
jana alipokuwa. Na gazabu iliyokosa
akili aliagiza watoto waume wote wa-
siokuwa bado na miaka miwili katika
Betelehemu na kando kando kuuawa.
Hatujui kama watoto wangapi walikufa.
Mwandishi mmoja alifikiri walikuwa
karibu makumi mbili na sita.
2:17,18 Kilio kilichofuata uuaji
wa watoto kilitimiza masemo ya nabii
Yeremia:
Sauti ilisikiwa katika Rama,
Kilio na maombolezo mengi,
Rakeli akililia watoto wake,
Asitake kufarijiwa,
kwa sababu hawako. (Yer. 31:15)
Ndani ya unabii huu Rakeli ni mfano
wa Israeli wenye huzuni. Rakeli ali-
zikwa katika Rama (karibu na Betele-
hemu, pahali watoto walipouawa). Wa -
kati wazazi waliofiwa watoto wali popita
Matayo 2, 3 19
kaburi lake, ni kama Rakeli alikuwa
akitoa machozi pamoja nao. Na Herode
alijipatia aibu tu.
D. Yosefu, Maria na Yesu wanakaa
katika Nazareti (2:19-23)
Nyuma ya mauti ya Herode malaika
ya Bwana alimwambia Yosefu kwamba
waliweza kurudi sasa na salama. Wakati
Yosefu alipofikia inchi ya Israeli na ku -
sikia kwamba mwana wa Herode, ndiye
Arkelao alikuwa amekomboa baba yake
kama mfalme wa Yudea, aliogopa kufika
kule. Akikwisha ku onywa na Mungu
katika ndoto walisafiri kwenda kwa
upande wa Galilaya kwa kaskazini,
wakapanga katika Naza reti.
Mara ya ine ndani ya sura hii Matayo
alitukumbusha ya kwamba maneno yali-
yotabiriwa zamani yalikuwa yaki timizwa.
Hakutaja majina ya manabii hawa, lakini
alisema kwamba wali tabiri Masiya ata -
itwa Mnazareti. Kwa wakati ule mji na
wenyeji wa Nazareti hawakuwa na he -
shima katikati ya watu wengine, na jina la
Mnazareti lilikuwa jina la kuzarau. Hivi
Natanaeli aliuliza, Kitu kizuri kinaweza
kutoka Nazareti? (Yn.1:46). Ha kuna
shairi ndani ya Agano la Kale linalotaja
jina hili wazi, lakini ndani ya Isaya 53:3
tunasoma ya kwamba amezarauliwa na
kukataliwa na watu. Shairi lingine li -
nasema kwamba ata kuwa mdudu, wala si
mtu, laumu ya watu na mwenye kuza-
rauliwa nao (Zab. 22:6). Hivi hata kama
manabii hawakutaja jina la Mnazareti, hii
ilikuwa maana ya unabii wao.
Ni neno la kushangaza ya kwamba
wakati Mungu mwenyezi alipofika du -
ni ani, alipewa jina la laumu. Ni he -
shima kwa wafuata wake kushiriki ndani
ya laumu lake (Ebr. 13:13).
3. MATAYARISHO KWA UTUMI-
SHI WA MASIYA NA MWANZO
WA UTUMISHI HUU (Sura 3,4)
A. Yoane Mbatizaji alitayarisha njia
(3:1-12)
Nyuma ya sura 2 na mbele ya sura 3
kulikuwa muda wa miaka 28 au 29.
Matayo hakuandika juu ya maneno
yaliyotokea ndani ya muda huu. Yesu
alikuwa katika Nazareti kwa wakati ule
akijitayarisha kwa kazi yake kubwa. Ha -
kufanya maajabu ndani ya miaka ile,
lakini alipendeza Mungu Baba yake
sana (Mt. 3:17). Sura 3 inatufikisha kwa
mwanzo wa kazi yake katikati ya watu.
3:1, 2 Yoane Mbatizaji alizaliwa mie -
zi sita mbele ya Yesu, mtoto wa ndugu
ya mama yake (ona Luka 1:26,36).
Alitokea katikati ya watu kama mta -
ngulizi wa Mfalme wa Israeli. Alihubiri
katika jangwa la Yudea inchi ya
kukauka iliyoenea toka Yerusalema ku-
fika Yorodani. Habari kubwa za mahu-
biri yake zilikuwa, Tubuni, kwa sa -
babu ufalme wa mbinguni umeka -
ribia! Mfalme atatokea nyuma kidogo,
lakini ata kataa kutawala watu waliofu -
ngana na zambi zao. Lazima wageuze
mwenendo wao na kukiri na kuacha
zambi zao. Mungu alikuwa akiwaita ku-
toka katika ufalme wa giza na kuingia
ufalme wa mbinguni.
UFALME
WA MBINGUNI
Ndani ya shairi 2 tunaona maneno
haya ufalme wa mbinguni mara ya
kwanza. Tutayaona mara 32 ndani ya
Habari Njema hii. Haiwezekani kwa
mtu kufahamu Habari Njema ya Matayo
vizuri bila kufahamu maana ya maneno
haya, hivi tutajaribu kueleza.
Ufalme wa Mungu ndipo pahali watu
wanapokubali utawala wa Mungu. Neno
hili mbingu linasema juu ya Mungu.
Tunaona neno hili katika Danieli 4:25,
pahali Danieli aliposema Aliye juu
anatawala katika ufalme wa watu.
Ndani ya shairi linalofuata alisema ya
kwamba mbingu zinatawala. Ufalme
wa mbinguni ni pahali po pote watu
wana ponyenyekea utawala wa Mungu.
Tunaweza kusawanisha ufalme wa
20 Matayo 3
mbi nguni na sanduku miwili. Ndani ya
sanduku kubwa watu wote wanakiri
kwamba wanajua Mungu ni Mtawala
mwenyezi. Ndani ya sanduku ndogo
iliyo ndani ya ile kubwa ni watu wale tu
waliookolewa kweli kweli na kukiri ya
kwamba wao ni wafuata wake kabisa. Tu-
naona neno hili ndani ya mfano wa mpa -
ndaji mbegu (Mt.13:3-9), mfano wa
mbegu ya haradali (Mt. 13:31,32), na wa
chachu (Mt.13:33). Watu wale tu walioza-
liwa tena kweli kwa njia ya kuamini
Bwana Yesu Kristo wanaweza kuingia
ndani ya sanduku mdogo (Mt. 18:3).
Wakati tunapoangalia mashairi yote
ndani ya Biblia juu ya ufalme pamoja tu-
naona kwamba unaendelea kwa hatua
tano katika historia.
Kwanza kulikuwa na unabii juu yaufalme ndani ya Agano la Kale. Danieli
alitabiri ya kwamba Mungu atasima -
misha ufalme usioharibiwa kamwe wala
kushindwa na taifa lingine (Dan. 2:44).
Aliona mbele vilevile ya kwamba Kristo
atakuja kutawala dunia nzima (Dan.
7:13,14; ona vilevile Yer. 23:5,6).
Kwa hatua ya pili Yoane Mbatizaji,
Yesu, na mitume kumi na wawili wali-
hubiri juu ya ufalme, wakisema juu yake
kwamba ulikuwa karibu (Mt. 3:2; 4:17;10:7). Ndani ya Matayo 12:28, Yesu
alisema . . . mimi kwa Roho ya Mungu
nikitoa pepo wachafu, ufalme wa Mu ngu
ume kwisha kuwa fikia ninyi. Katika
Luka 17:21 alisema, ufalme wa Mungu
ni ndani yenu au katikati yenu. Ufalme
ulikuwa pale kwani Mfalme mwenyewe
alikuwa pale. Tutaona nyuma kwamba
mara nyingine unaitwa ufalme wa
Mungu na mara nyingine ufalme wa
mbinguni.
Hatua ya tatu ndiyo ufalme kwa
muda wa kati. Nyuma ya kukataliwa nataifa la Israeli Mfalme alirudia mbingu.
Lakini ufalme uko hata wakati wa sasa,
ndani ya mioyo ya wote ambao wana-
heshimu Kristo kama Mfalme wao, pa -
moja na mafundisho yote aliyotoa juu ya
Mlima. Mifano ya Matayo 13 inafu -
ndisha juu ya muda huu.
Hatua ya ine ya ufalme ni kuonekana
kwake, au ufunuo wake, wakati wautawala wa Kristo duniani kwa miaka
elfu moja. Tunaona mfano wa neno hili
wakati sura ya Yesu ilipogeuzwa juu ya
mlima, naye alionekana katika utukufu
wake kwa wakati wa utawala wake kwa
wakati wa kuja (Mt.17:1-8). Yesu ali-
fikiri juu ya hatua hii katika Matayo 8:11
wakati aliposema wengi wa takuja
toka mashariki na toka ma ngaribi, na
wataketi pamoja na Abrahamu na
Isaka na Yakobo katika ufalme wa
mbinguni.
Hatua ya mwisho ni ufalme wamilele. Tunasoma juu yake ndani ya 2 Petro 1:11, . . . ufalme wa milele wa
Bwana wetu, Mwokozi Yesu Kristo.
Maneno haya ufalme wa mbinguni
ni ndani ya Habari Njema ya Matayo tu,
lakini ufalme wa Mungu ni ndani ya
Habari Njema zote ine. Maneno yana -
yosemwa juu ya ufalme wa mbi nguni
yanasemwa juu ya ufalme wa Mungu
vilevile. Kwa mfano, ndani ya Matayo
19:23 Yesu alisema itakuwa nguvu kwa
mtajiri kuingia ufalme wa mbinguni.Marko (10:23) na Luka (18:24) vilevile
waliandika kwamba Yesu alisema hivi
juu ya ufalme wa Mungu. (Ona vilevileMt. 19:24.)
Tulisema mbele ya kwamba ufalme
wa mbinguni unaonekana kwa macho,
Matayo 3 21
lakini ni kitu cha ndani, cha hakika na
roho vilevile. Ni vivyo hivyo na ufalme
wa Mungu. Tunaona neno hili ndani ya
mifano ya mpandaji mbegu (Lk. 8:4-10),
mbegu ya haradali (Lk.13:18,19), na
chachu (Lk. 13:20,21). Wale tu wana -
ozaliwa tena kweli wanaweza kuingia
ufalme wa Mungu kwa roho na kweli
(Yn. 3:3,5).
Neno moja lingine kwa kumaliza ma-
fundisho haya: ufalme na kanisa si neno
moja. Ufalme ulianza wakati Kristo
alipoanza kazi yake katikati ya watu.
Kanisa lilianza siku ya Pentekote (Ma-
tendo 2). Ufalme utaendelea kufika wakati
dunia itakapoharibiwa; kanisa litaendelea
kufika wakati Kristo atakapotoka mbi -
nguni kupeleka waamini wote kwake
mbinguni (1 Tes. 4:13-18). Kanisa litarudi
pamoja na Kristo kama bibi-arusi yake
wakati atakapokuja mara ya pili. Kwa
wakati wa sasa watu walio ndani ya mvi -
ringo mdogo ulio ndani ya ule mkubwa ni
ndani ya kanisa vilevile.
3:3 Tuendelee sasa na mafundisho
ya Matayo 3. Ona ya kwamba Isaya ali-
toa unabii miaka mia saba mbele juu
ya kazi ya Yoane kutayarisha njia kwa
Bwana:
Sauti ya mtu anayelia katika
jangwa,
Tengenezeni njia ya BWANA,
Nyosheni mapito katika jangwa
kwa Mungu wetu! (40:3).
Yoane alikuwa sauti ile. Taifa la
Israeli lilikuwa kama jangwa ya kukauka
kwa maneno ya roho, bila matunda.
Yoane aliita watu kutayarisha njia ya
BWANA kwa njia ya kutubu zambi zao na
kuziacha, na kunyolosha njia yake kwa
njia ya kuondosha toka maisha yao vitu
vyote vilivyoweza kuzuiza BWANA asi -
tawale katika mambo yote.
3:4 Yoane alivaa vazi la singa za
ngamia namna watu waliotumika porini
walilovaa, na alikuwa na mkaba wa
ngozi vilevile. Lilifanana na mavazi ya
Elia (2 Waf.1:8) na labda Wayuda wa -
amini walitambua kwamba utumishi wa
Yoane ulifanana na ule wa Elia (Mal. 4:5;
Lk 1:17; Mt. 11:14; 17:10-12). Yoane ali -
kula nzige na asali ya pori, ndicho
chakula masikini cha mtu ana yeweka roho
kabisa juu ya kazi yake tu na kusahau ma-
neno watu wengine wanayofurahia.
Bila shaka kukutana na Yoane Mba -
tizaji kulichokoza damiri za watu sana.
Alikuwa mtu asiyeweka roho juu ya vitu
watu wengine wanavyotamania. Aliishi
kwa maneno ya roho tu, na tunafikiri
neno hili lilifahamisha watu wengine
umasikini wa roho zao wenyewe, na
lilikuwa kemeo la kukata roho zao juu
ya mapendo yao kwa vitu vya dunia.
3:5, 6 Watu wengi walitoka Yerusa -
lema, Yudea yote, na inchi zote karibu
na Yorodani kumsikia. Wengine wali -
pokea mahubiri yake vizuri, wakaba-
tizwa naye katika Yorodani, na kwa njia
hii walionyesha kwamba walikuwa ta -
yari kupokea na kutii Mfalme ambaye
alikuwa karibu kufika.
3:7 Wafarisayo na Wasadukayo
wa lifika kusikia mahubiri ya Yoane
vilevile, lakini Yoane alifahamu kwa -
mba hawakufanya hivi na roho ya kweli.
Alitambua hali ya roho za Wafarisayo,
roho za hila. Walitenda kama watu wali -
oheshimu sheria sana, lakini ndani ya
roho zao walikuwa waovu, wada nganyi -
fu na wenye hila, wakifikiri wao ni
wenye haki kabisa. Wasadukayo wa-
likuwa jamii iliyoheshimiwa na watu,
wenye mashaka kwa maneno ya roho,
waliokana kweli nyingine kabisa, kama
ufufuko wa mwili, malaika, kweli ya
kwamba roho ya mtu inaishi kwa milele,
na azabu ya milele. Hivi Yoane aliita
Wafarisayo na Wasadukayo uzao wa
nyoka waliotenda kama wenye kutaka
kuepuka hasira itakayokuja, lakini
wasiotubu kweli.
3:8 Aliwaita kuhakikisha kama wa-
litubu kweli kwa njia ya kuzaa matunda
yanayofaa na toba. Mwalimu mmoja,
22 Matayo 3
ndiye J.R. Miller, aliandika kwamba
toba inayoonekana kwa njia ya huzuni
na woga na kutoa machozi machache tu
ni bure. Lazima tuachane na zambi tu-
nazokiri na kuanza kutembea katika haki
na utakatifu.
3:9 Ilipasa Wayuda kuacha kufikiri
watafika mbinguni kwa sababu wa-
likuwa wazao wa Abrahamu. Neema
ya wokovu haipitishwi kwa njia ya
kuzaa mwilini. Ingalikuwa nyepesi kwa
Mungu ku geuza mawe katika Yorodani
kuwa watoto wa Abrahamu, kupita kwa
Wafari sayo na Wasadukayo kuokolewa.
3:10 Kwa njia ya kusema kwamba
shoka limekwisha kuwekwa katika
shina la miti, Yoane alijulisha wasikiaji
wake kwamba hukumu ya Mungu ili -
kuwa karibu kuanza. Kufika kwa Kristo
kutapima watu wote. Wale wasiozaa
matunda wataharibiwa kama mti usiozaa
matunda mazuri unakatwa na kutu -
pwa katika moto.
3:11,12 Ndani ya mashairi 7-10
Yoane alisema na Wafarisayo na Wa -
sadukayo tu (ona shairi 7), lakini ni
kama sasa alisema na watu wote, ndio
wenye imani ya kweli na wale wa -
liokosa imani. Alieleza tofauti kati ya
utumishi wake na ule wa Masiya ata -
kayetokea nyuma kidogo. Yoane aliba-
tiza kwa maji hata toba, lakini maji
haya hayakuweza kusafisha roho ya
mtu; hata mtu akitubu na roho ya
kweli, ubatizo huu haukuweza kumpatia
wokovu. Yoane alifahamu kwamba utu-
mishi wake ulikuwa utumishi wa kuta-
yarisha tu watu kwa kuja kwa Bwana.
Masiya atakuwa mkubwa kupita na
mwenye uwezo mkubwa kupita Yoane.
Atastahili kupita, kazi yake itagusa watu
wengi kupita, maana atabatiza kwa
Roho Mtakatifu na kwa moto.
Ubatizo kwa Roho Mtakatifu ni
mbali na ubatizo kwa moto. Ubatizo wa
kwanza ndio ubatizo wa baraka; ule wa
pili ni ubatizo wa hukumu. Ubatizo wa
Roho Mtakatifu ulitokea kwa Pentekote;
ule wa hukumu utatokea kwa wakati wa
kuja. Ubatizo wa kwanza ni kwa wa -
amini wote wa kweli wa Bwana Yesu;
ule wa pili utapata wasioamini wote.
Ubatizo wa kwanza utakuwa alama wa
kuonekana kwa Waisraeli waliokuwa
wametubu kweli rohoni; ule wa pili
utakuwa kwa Wafarisayo, Wasadukayo,
na wote wasiotubu na roho ya kweli.
Watu wengine wanafundisha kwa -
mba ubatizo kwa Roho Mtakatifu na
ubatizo kwa moto ni neno moja. Wa -
nafikiri ubatizo kwa moto unasema juu
ya ndimi za moto zilizoonekana wakati
Roho Mtakatifu alipotolewa siku ya
Pente kote. Tukisoma shairi 12 hatufikiri
mafundisho haya ni kweli.
Mara moja nyuma ya kusema juu ya
ubatizo wa moto, Yoane alisema juu ya
hukumu. Alisema juu ya Bwana kama
mwenye kushika pepeto mkononi na
akitupa nafaka juu kwa upepo. Ngano
(ndio waamini wa kweli) inaanguka
chini mara moja kwa udongo na ku-
pelekwa katika gala. Makanda (wa-
sioamini) yanabebwa na upepo kwa
mwendo mdogo tu mbele ya kuku-
sanywa na kuteketezwa kwa moto
usiozimika. Moto ndani ya shairi 12
unasema juu ya hukumu, na shairi hili
likiwa kama sehemu ya shairi 11, tu-
nafikiri ubatizo wa moto ndio ubatizo
wa hukumu.
B. Yoane Mbatizaji anabatiza Yesu
(3:13-17)
3:13 Yesu alitembea karibu km. 96
toka Galilaya kufikia upande wa chini
wa mto Yorodani aweze kubatizwa na
Yoane. Tendo hili lilionyesha kwamba
ubatizo ulikuwa neno kubwa kwa ma -
fikiri yake na ungepasa ubatizo kuwa na
maana kubwa kwa wafuata wake kwa
wakati wa sasa.
3:14,15 Yoane alijua kwamba Yesu
hakuhitaji kutubu, kwani hakuwa na
zambi. Hakutaka kumbatiza, akisema
ingepasa Yesu kumbatiza yeye. Yesu
Matayo 3, 4 23
hakubisha neno hili lakini aliomba
Yoane tena kumbatiza kutimiza haki
yote. Alifikiri ni taratibu kwa yeye
kushiriki kwa njia hii na Waisraeli we -
nye kupenda Mungu waliokuwa wa ki-
fika kupokea ubatizo wa toba.
Lakini ubatizo huu ulikuwa na maana
kubwa kupita kwa Yesu. Ulikuwa mfano
kwake wa namna atatimiza madai nzima
ya haki ya Mungu juu ya zambi za watu.
Kuingia maji ya ubatizo kulikuwa mfano
wa hukumu ya Mungu kwa Kalvari. Ku-
toka kwake katika maji kulikuwa mfano
wa ufufuko wake. Kwa njia ya mauti,
kuzikwa na kufufuliwa atatimiza haki
yote ya Mungu na kutayarisha njia ya
haki kwa wenye zambi kuweza kuhe -
sabiwa haki.
3:16,17 Mara moja nyuma ya ku-
toka katika maji, Yesu aliona Roho ya
Mungu akishuka kama hua, akikuja
juu yake. Katika Agano la Kale vitu
viliwekwa kwa Mungu kwa kazi fulani
kwa njia ya kuvipakaa na mafuta
matakatifu ya kupakaa (Kutoka 30:25-
30). Vivyo hivyo Yesu alipakaliwa na
Roho Mtakatifu kama Masiya.
Mungu Baba, Mungu Mwana na
Roho Mtakatifu wote walishiriki ndani
ya tukio hili takatifu. Mwana mpendwa
alikuwa pale, Roho Mtakatifu kwa
mfano wa hua alikuwa pale, na sauti ya
Baba ilisikiwa toka mbinguni akibariki
Yesu, akitaja shairi la Maandiko Mataka -
tifu Wewe ni Mwana wangu (Zaburi
2:7) . . . nafsi yangu inape ndezwa naye
(Isaya 42:1). Baba alisema mara tatu toka
mbinguni kuonyesha furaha na ukubali
wa Mwana wake asiyekuwa na kifani;
hapa, na kwa Matayo 17:5 na Yoane 12:28.
C. Yesu anajaribiwa na Shetani
(4:1-11)
4:1 Labda tunashangaa wakati tu-
napoona Roho akiongoza Yesu ja -
n gwani kuja ribiwa na Shetani. Majaribu
haya yalihitajiwa kuhakikisha ya kwa -
mba alikuwa mwema, na alifaa kabisa
kwa kazi aliyofika kufanya duniani.
Adamu wa kwanza alionyesha kwamba
hakufaa kuwa na mamlaka wakati
alipokutana na adui katika shamba la
Edeni. Hapa Adamu wa pili alikutana na
adui huyu vilevile na alimshinda.
Habari hizi za majaribu ya Bwana
wetu ni siri kubwa. Tukiuliza kama
angaliweza kufanya zambi, na tunajibu
Hapana, halafu tunafazaika kwa njia
gani lingekuwa jaribu la hakika kama
asipoweza kuangushwa nalo. Kama tu -
kijibu Ndiyo, inatupasa kuuliza,
Namna gani Mungu katika mwili
anaweza kufanya zambi?
Ni sharti kabisa kwa sisi kukumbuka
kwamba Yesu Kristo ni Mungu, na ya
kwamba Mungu hawezi kufanya zambi.
Ndiyo, yeye ni mtu vilevile, lakini ha -
kuna neno ndani ya Biblia kuonyesha
kwamba aliweza kufanya zambi kama
mtu. Waandishi wa Agano Jipya wali -
andika kwamba Kristo hakuwa na zambi.
Paulo ali andika ku sema kwamba haku-
jua zambi (2 Kor. 5:21); Petro alisema
hakutenda zambi (1 Pet. 2:22); na
Yoane alisema, zambi si ndani yake
(1 Yn. 3:5).
Kama sisi watu, Yesu aliweza ku-
jaribiwa toka nje. Shetani alifika kwakena kumjaribu kufanya maneno yasiyo -
patana na mapenzi ya Mungu. Lakini
hakuwa kama sisi kwa sababu hakuweza
kujaribiwa toka ndani ya roho yake hakuwa na tamaa. Na vilevile hakuna neno
ndani ya roho yake lililoweza kukubali
ushawishi wa Shetani (Yn. 14:30).
Hata kama Yesu hakuweza kufanya
zambi, majaribu haya yalikuwa ma-
jaribu ya hakika. Lakini hata akijaribiwa
kufanya zambi, haikuwezekana kwaye
kushindwa nayo. Aliweza kufanya tu
kama alivyoona Baba kufanya (Yoane
5:19), na hakuona Baba kamwe akifanya
zambi. Yesu hakuweza kufanya neno
peke yake mwenyewe (Yn. 5:30), na
isingaliwezekana kamwe kwa Baba
kumpa ruhusa kufanya zambi.
24 Matayo 4
Kusudi la majaribu halikuwa kuona
kama atafanya zambi, lakini kuhaki -
kisha ya kwamba hata akikutana na ma-
jaribu makubwa sana aliweza kutii Neno
la Mungu tu.
4:2, 3 Nyuma ya kushinda kwa siku
makumi ine muchana na usiku bila
chakula, Yesu akaona njaa. (Hesabu hii
makumi ine inaonekana mara na mara
ndani ya Maandiko pamoja na mapimo
au majaribu.) Basi neno hili lilimpa
mjaribu (ndiye Shetani) njia kusema na
Yesu kutumika na uwezo wake wa ajabu
kugeuza mawe ya jangwa kuwa mkate.
Alisema naye, Kama ukiwa Mwana
wa Mungu Maana ya Kama si
kuonyesha shaka, lakini Kwa sababuwewe ni Mwana wa Mungu. Mjaribu
alikuwa akikumbuka masemo ya Mungu
Baba kwa Yesu saa ya ubatizo wake,
Huyu ni Mwana wangu, mpendwa
wangu, na alisema na Yesu kutumika
na uwezo huu kusaidia njaa yake.
Lakini kwa Yesu kutumika na uwezo
wake wa Mungu kumaliza njaa yake ya
mwili kungalikuwa kuasi Mungu. Ma -
semo ya Shetani hapa yanatufikirisha
masemo yake katika Mwanzo 3:6 (uli -
kuwa mzuri kwa chakula). Kwa
mawazo ya Yoane majaribu haya yana-
sawanishwa na tamaa ya mwili (1 Yn.
2:16). Na kwa sisi watu wa sasa ni ma-
jaribu kuishi kwa anasa na usitawi,
badala ya kutafuta kwanza ufalme wa
Mu ngu na haki yake.
4:4 Yesu alijibu jaribu hili kwa njia
ya kutaja Neno la Mungu. Bwana wetu
ni mfano kwetu ya kwamba si lazimakwa sisi kuishi, lakini ni lazima kwa sisikutii Mungu. Neno kubwa zaidi kwa
maisha yetu si kujipatia mkate, lakini nikutii kila neno la Mungu. Mungu Baba
hakusema na Mwana wake kugeuza
mawe kuwa mikate. Hivi Bwana haku-
fanya neno hili kwa kutaka kwake
mwenyewe na kutii Shetani. Si neno
kama njaa yake ilikuwa kali sana.
4:5,6 Jaribu la pili lilikuwa kwa
mnara wa hekalu kwa Yerusalema.
Shetani alisukuma Yesu kujitupa chini
kama ono la kushangaza kwa watu ya
kwamba yeye ndiye Mwana wa Mungu.
Alitaja ahadi ya Mungu katika Zaburi
91:11,12 kuchunga Masiya.
Kujitupa chini toka mnara wa hekalu
bila kuumia kungalikuwa ajabu kabisa.
Kwa njia hii Yesu angaliweza kuonye-
sha kwamba alikuwa Masiya, na kujipa-
tia utukufu bila mateso. Angaliweza
kufikia kiti cha ufalme bila kufa msala-
bani kwanza. Lakini kufanya hivi ha -
kukuwa mapenzi ya Mungu. Yoane ali -
ita jaribu hili kiburi cha uzima
(1 Yn. 2:16). Linafanana na mti wa ku-
tamaaniwa katika shamba la Edeni
(Mwa. 3:6). Lilifanana na jaribu la pili
la Shetani kwa Yesu kwani lilikuwa
njia kujipatia utukufu bila kutii kutaka
kwa Mungu. Ndani ya maisha yetu ya
sasa tunajaribiwa kujipatia heshima
kama watu wa maneno ya Mungu bila
kushi riki ndani ya mateso ya Kristo.
Tunajitafutia mambo makubwa, lakini
kwa wakati wa taabu na matata tu-
nakimbia. Tunajaribu Mungu wakati
tunapojitukuza wenyewe na kuona ku-
taka kwake bure.
4:7 Yesu alijibu tena kwa njia ya
kusema Tena imeandikwa, Usijaribu
BWANA, Mungu wako (ona Tor. 6:16).
Mungu alikuwa ameahidi ku chunga
Masiya kama akitii ma penzi yake ndaniya maisha yake. Kuzania Mungu ata -
fanya hivi kama asipotii ni kujaribu
Mungu. Kwa wakati wa kutimia Yesu
atafunuliwa kama Masiya, lakini ili -
mpasa kusulibishwa kwanza. Sharti ma -
zabahu ya zabihu itangulie kiti cha
kifalme. Lazima taji ya miiba ita ngulie
taji ya utukufu. Yesu aliku sudi kungojea
wakati uliochaguliwa na Mungu na ku-
timiza mapenzi yake.
4:8,9 Kwa jaribu la tatu Shetani
alipeleka Yesu hata mlima mrefu
sana, akamwonyesha falme zote za
ulimwengu. Alisema na Yesu atampa
Matayo 4 25
hizi zote kama Yesu akimwabudu.
Jaribu hili lilikuwa juu ya kuabudu, tendo
la roho, lakini kwa njia hii Shetani
alijaribu kusukuma Yesu kujikamatia uta -
wala wa dunia kama mfalme kwa njia ya
kuabudu Shetani. Zawabu kwa kufanya
hivi, falme zote za ulimwengu, inatu-
fikirisha tamaa ya macho (1 Yn. 2:16).
Ndiyo, kwa njia nyingine falme za
ulimwengu ni mali ya Shetani kwa
wakati wa sasa. Katika 2 Kor. 4:4 ana -
itwa mungu wa dunia hii, na Yoane
anatuambia kwamba dunia yote pia
inakaa katika yule mwovu (1 Yn. 5:19).
Wakati wa kuja kwa pili kwa Yesu kama
Mfalme wa wafalme (Ufu.19:16), Ufa -
lme wa dunia utageuka ufalme wa
Bwana (Ufu. 11:15). Yesu hatageuza
shauri la Mungu na hataabudu Shetani
kamwe!
Jaribu hili linatuonya sisi watu wa
sasa juu ya maneno mawili: 1) Haifai
tubadilishe uzima na ba raka zetu zote
za roho kwa utukufu wa dunia hii iliyo
kwa wakati mdogo tu; na 2) tusiabudu
na kutumikia kiumbe kwa pahali pa
Mwu mba.
4:10 Mara ya tatu Yesu alishinda
majaribu kwa njia ya kutaja shairi toka
Agano la Kale, Uabudu BWANA Mu -
ngu wako, umtumikie yeye peke
yake. Kuabudu, na utumishi ulio tunda
la kuabudu, ni kwa Mungu peke yake.
Ku abudu Shetani ni kusema yeye ni
Mungu.
4:11 Shetani aliacha Yesu wa kati
Yesu alipomaliza kushinda majaribu
yake yote. Katika Isaya 59:19 tunasoma,
Wakati adui atakapo ingia kama garika,
Roho ya BWANA atanyanyua bendera juu
yake. Ni faraja tamu sana kwa watu wa
Mungu wakati wa mateso!
Tunasoma malaika wakakuja, wa -
ka mtumikia, lakini hakuna elezo juu
ya maneno haya. Tunafikiri walimletea
vyakula ambavyo alikataa mbele, saa ya
majaribu yake.
Majaribu ya Yesu yanatufundisha
kwamba Shetani anaweza kushindana
na watu wanaotawaliwa na Roho Mta -
katifu, lakini hana uwezo kushinda wale
ambao wanashindana naye na Neno la
Mungu.
D. Yesu anaanza utumishi wake
katika Galilaya (4:12-17)
Hatusomi hapa juu ya utumishi wa
Bwana Yesu ulioendelea kwa karibu
mwaka mmoja katika Yudea (ona Yoane
14); nyuma ya wakati wa Matayo 4:11
na mbele ya 4:12. Nyuma ya kuandika
juu ya majaribu ya Shetani, Matayo
aliendelea mara moja kuandika juu ya
utumishi wa Yesu katika Galilaya.
4:12 Wakati Yesu aliposikia kwa -
mba Yoane amefungwa, alifahamu ya
kuwa neno hili lilikuwa kama alama ya
kukataliwa kwake mwenyewe. Ni kama
wakati watu walipokataa mwenye ku-
tangulia mfalme, walikuwa wakikataa
Mfa lme mwenyewe. Lakini si woga
ambao ulimsukuma kwenda kwa upande
wa kaskazini kwa Galilaya. Gali laya
ilikuwa katikati ya ufalme wa Herode
ndiye Herode aliyefunga Yoane gerezani
sasa tu. Kwa njia ya kuhama kwa
Galilaya alionyesha kwamba Habari
Njema itafikia Mataifa kwa sababu Wa -
yuda walimkataa.
4:13 Yesu alikaa katika Nazareti ku-
fika wakati watu wa mji walipojaribu
kumwua kwa sababu alihubiri Habari
Njema kwa Mataifa (ona Luka 4:16-30).
Kisha alihama kukaa kwa Kapernaumu
kando ya bahari ya Galilaya, pahali watu
wa makabila ya Zebuluni na Nafutali
walipokaa zamani.
4:14-16 Kuhama kwa Yesu kukaa
kwa Galilaya kulitimiza unabii wa Isaya
9:1,2. Watu wa Mataifa hawa, wajinga,
na wenye kuamini ma mbo ya uchawi,
waliokaa katika Galilaya, waliona nuru
kubwa ndiye Kristo, Nuru ya dunia.
4:17 Kutoka wakati ule Yesu ali -
endelea kuhubiri habari Yoane alizo -
hubiri mbele: Tubuni; kwa maana
26 Matayo 4
ufalme wa mbinguni ume karibia.
Aliita watu kujitayarisha kwa roho na
mwenendo wao kwa kuja kwa ufalme
wake. Ufalme ulikuwa karibu, maana
Mfalme mwe nyewe alikuwa palepale.
E. Yesu anaita wavuvi wane
(4:18-22)
4:18,19 Hii ni mara ya pili Yesu ali -
yoita Petro na Anderea. Ndani ya
Yoane 1:35-42 waliitwa kupata wo kovu;
sasa Yesu aliwaita kumtumikia. Mara ya
kwanza walikuwa katika Yudea; sasa
walikuwa katika Galilaya. Petro na
Anderea walikuwa wavuvi, lakini Yesu
aliwaita kuwa wavuvi wa watu. Kazi
yao ilikuwa kufuata Kristo; ilikuwa
kazi yake kuwageuza kuwa wavuvi wa
faida. Neno lililohitajiwa kwa Petro na
Anderea halikuwa kufuata Yesu kwa
mwenendo wa mwili tu, lakini kumwiga
kwa tabia ya roho. Namna walivyokuwa
rohoni mwao lilikuwa neno kubwa ku -
pita maneno waliyo sema au kufanya.
Kwa njia ya kufuata Kristo mwanafunzi
alijifunza kwenda pahali samaki wa -
lipokuwa, kutumika na cha mbo kili-
chohitajiwa, kuvumilia masu mbuko na
taabu, kuwa na saburi, na kukaa kwa
maficho.
4:20 Petro na Anderea walisikia na
kutii mwito wa Yesu mara moja. Kwa
imani waliacha mikila yao, na walijitoa
kufuata Yesu na mapendo na bidii.
4:21,22 Nyuma yake Yesu aliita
Yakobo na Yoane, nao vilevile wali -
mfuata mara moja. Hawakuacha cho -
mbo yao tu, ndiyo njia kujipatia mali
kwa mahitaji yao, lakini waliacha baba
yao vilevile. Kwa njia hii walionyesha
kwamba kufuata Bwana ni neno kubwa
kupita jamaa, na rafiki, na watu wa
dunia.
Kwa njia ya kutii mwito wa Yesu,
wavuvi hawa walikuwa na sehemu
kubwa ndani ya kazi ya kuhubiri Habari
Njema kwa watu wa dunia. Kama wa -
ngalifu ngana na mikila yao, tusinga -
lisikia habari zao kamwe. Ni neno
kubwa sana kufuata Kristo kama Bwana
wa maisha yetu.
F. Yesu aliponyesha watu wengi
(4:23-25)
Utumishi wa Bwana Yesu uli kuwa na
sehemu tatu: Alifundisha Neno la Mu -
ngu katika masunagogi; alihubiri Ha -
bari Njema ya ufalme; na aliponyesha
wagonjwa. Kusudi moja la maajabu ya
ku ponyesha watu lilikuwa kuhakiki sha
kwamba yeye ni kweli Mwana wa
Mungu (Ebr. 2:3,4). Ndani ya Ma tayo
57 tunapata mfano wa mafundisho
yake, na sura 89 zinapasha habari za
maajabu yake.
4:23 Ndani ya shairi hili Habari
Njema linatajwa mara ya kwanza katika
Agano Jipya. Ni habari njema za wo -
kovu. Ndani ya kila muda tangu ku-
umbwa kwa dunia kumekuwa Habari
Njema moja tu, njia moja tu ya wokovu.
HABARI NJEMA
Habari Njema ilianza ndani ya nee -
ma ya Mungu (Efe.2:8), maana yake
Mungu analeta uzima wa milele bila bei
kwa watu wasiostahili hata kidogo ku-
upokea.
Msingi wa Habari Njema ni kazi ya
Kristo msalabani (1 Kor. 15:1-4). Mwo-
kozi wetu alitimiza haki yote ya Mungu,
na kwa sababu hii Mungu anawezeshwa
kuhesabia haki we nye zambi wanao -
amini. Waamini wa Agano la Kale wali -
hesabiwa haki kwa njia ya Kristo hata
kama kwa wakati ule hajakufa bado.
Labda hawakujua maneno mengi juu ya
Masiya, lakini Mungu alijua naye ali-
wahesabia faida ya kazi ya Kristo hata
mbele ya kufika kwake duniani kulipa
bei ya zambi zao. Kwa sisi watu wa
sasa, kazi hii imekwisha.
Watu wanapokea Habari Njema kwa
njia ya imani tu (Efe. 2:8). Katika Agano
la Kale watu walioko lewa kwa njia ya
kuamini maneno Mungu aliyokwisha
Matayo 4, 5 27
kuwaambia. Kwa wakati wa sasa watu
wana okolewa kwa njia ya kuamini
ushu huda wa Mungu juu ya Mwana
wake kama njia ya pekee ya wokovu
(1 Yn. 5:11,12). Kifiko cha Habari
Njema ni mbingu. Pamoja na watakatifu
wa Agano la Kale sisi vilevile tuna tu-
maini la kuishi mbinguni kwa milele
(Ebr. 11:10, 14-16; 2 Kor. 5:6-10).
Kuna Habari Njema moja tu, lakini
ni mbalimbali kidogo kwa njia nyingine,
kwa muda mbali mbali. Tuwaze juu ya
Habari Njema ya ufalme na Habari Njema
ya neema ya Mungu. Habari Njema ya
ufalme inaagiza: Tubu na pokea Masiya;
halafu utaweza kuingia ufalme wake
wakati utakaposima mi shwa duniani. Ha -
bari Njema ya neema ina sema: Tubu na
pokea Kristo; halafu uta nyanyuliwa kuku-
tana naye na kukaa pamoja naye kwa
milele. Ni Habari Njema moja tu lakini
ina simamishwa kwa njia mbali mbali ku-
patana na kusudi la Mungu kwa wakati
wa muda mbalimbali.
Wakati Yesu alipohubiri Habari Nje ma
ya ufalme, alitangaza habari za kuja
kwake kama Mfalme kwa Wayuda, na
alionyesha nini ilihitajiwa kwa watu
kuweza kuingia ndani ya ufalme wake.
4:24,25 Habari za Yesu zilienea ka -
tika Suria nzima, ndiyo inchi kwa
upande wa kaskazini-mashariki wa Isra -
eli. Wagonjwa wote na wenye pepo
wachafu na wenye kupooza wali-
saidiwa na kuponyeshwa naye. Watu
wengi walifika kwake toka Galilaya,
Dekapoli (ndiyo miji kumi ya Mataifa
iliyo fu ngana pamoja kwa upande wa
kaskazini-mashariki wa Palestina), Ye -
ru salema, Yudea, na inchi kwa ma -
shariki ya Yorodani. Watu walishangaa
sana juu ya habari zilizotoka Galilaya!
4. KUSIMAMISHWA KWA UTARA TIBU WA UFALME(Sura 57)
Hotuba hii ya Bwana Yesu iliwekwa
karibu na mwanzo wa Agano Jipya na
kusudi la kuonyesha ukubwa wa ma-
fundisho haya. Ndani yake Mfalme
alionyesha tabia ya roho na ya mwe-
nendo wa wafuata wake.
Hotuba hii si mafundisho juu ya njia
ya wokovu na si kwa wasioamini. Bwa -
na Yesu aliitoa kwa wanafunzi wake
(5:1,2), na ndani yake Bwana aliwa-
fundisha utaratibu na sheria na maagizo
ambayo alitaka watu wa ufalme wake
kutawaliwa nayo. Ilikuwa kwa watu
wote wa zamani, sasa, na kwa wakati
wa kuja wanaonyenyekea Kristo kama
Mfalme wao. Wakati Kristo ali pokuwa
duniani, mafundisho haya yalikuwa
zaidi kwa wanafunzi wake. Sasa, wakati
Bwana wetu anapotawala mbinguni, ni
kwa watu wote ambao wana mtukuza
mioyoni mwao kama mfalme wao.
Mwishoni, ni mafundisho kwa mwe-
nendo wa wafuata wa Kristo kwa wakati
wa Mateso Makubwa na kwa wakati
atakapotawala duniani.
Ni kama hotuba hii ni zaidi kwa
Wayuda na inataja Baraza (5:22), ma-
zabahu (5:23,24), na Yerusalema (5:35),
lakini haifai kusema kwamba ni kwa
waamini wa Israeli tu, wa zamani na wa
wakati wa kuja. Ni kwa watu wote wa
kila wakati wa naopokea na kunye -
nyekea Yesu Kristo kama Mfalme.
A. Sifa za heri (5:1-12)
5:1,2 Hotuba hii inaanza na sifa za
heri, au baraka. Zinaonyesha maneno
ambayo ya na paswa kuonekana ndani ya
wenyeji wazuri wa ufalme wa Kristo.
Maneno haya ni mbali kabisa na yale
ambayo watu wa dunia wanasifu.
5:3 Baraka ya kwanza ni kwa wale
walio masikini wa roho. Hawakuzaliwa
hivi, lakini walichagua kuwa hivi kwa
njia ya kujitawala wenyewe. Ni wale
wanaojua uzaifu wao kwa maneno ya
roho, na wanaotegemea uwezo mkubwa
wa Mungu kusaidia mahitaji ya roho
28 Matayo 5
zao. Ufalme wa mbinguni ni wao,
lakini kujitegemea mwenyewe na kuji-
tukuza mwenyewe ni zambi ndani ya
ufalme wa mbinguni.
5:4 Wenye huzuni ni heri; watafa -
rijiwa siku nyingine. Shairi hili halisemi
juu ya huzuni watu wanazopataga duni-
ani kama ugonjwa au kufiwa kwa
ndugu. Linasema juu ya huzuni tu-
nayoshiriki na Bwana Yesu kwa sababu
ya taabu na zambi za dunia. Hivi si
huzuni kwa sababu ya zambi zetu
wenyewe tu, lakini kwa sababu ya hali
mbaya sana ya dunia hii; huzuni kwa
sababu ya wale wa naokataa Mwokozi
na hukumu inayo ngojea wale wanao -
kataa rehema yake. Wenye huzuni kwa
sababu ya maneno haya watafarijiwa
kwa wakati wa kuja wakati Mungu
atapungusa kila chozi katika macho
yao (Ufu. 21:4). Waamini wanapata
huzuni yao yote wakati walipo hai hapa
duniani; kwa wasioamini huzuni hii ni
kama kionjo cha mbele cha taabu kubwa
ambayo inawa ngojea kwa milele.
5:5 Heri ya tatu ni kwa wenye
upole; maana watariti inchi. Labda
kwa njia ya tabia yao ya zambi watu
hawa walikuwa wenye kunungunika,
watu wakali na wenye kiburi, lakini
wakati walipo pokea Kristo walikusudi
kufanana naye, na kwa njia ya kumfuata
waligeuka wapole na wanyenyekevu wa
moyo (Mt. 11:29). Wenye upole si wa -
zaifu, lakini ni wenye kukubali pahali
pao pa chini; wasiojisimamia wenyewe,
lakini walio tayari kusimamia Mungu au
kulinda watu we ngine.
Wenye upole hawariti inchi sasa;zaidi wanariti shutumu na kutwaliwa
vitu vyao. Lakini watariti inchi kweli
wakati Kristo, Mfalme, atakapotawala
kwa miaka elfu moja na salama na
usitawi.
5:6 Kuna heri vilevile kwa wenye
njaa na kiu kwa haki: njaa yao ita -
shibishwa. Watu hawa wana njaa kubwa
sana kwa haki ndani ya maisha yao
wenyewe; wanataka kuona haki na
kweli na uaminifu ndani ya watu ambao
wanakaa katikati yao, na ndani ya
kanisa. Hamu yao itashibishwa wakati
ufalme wa Kristo utakaposimamishwa,
na haki itatawala na uovu utakapoko -
mbolewa na maisha na mwenendo wa
haki.
5:7 Ndani ya ufalme wa Bwana wetu
wenye rehema watabarikiwa kwa
sababu watapata rehema. Kuwa na re-
hema ni kutenda rehema kwa njia ya ku-
tokuazibu wale wanaostahili kuazibiwa;
ni vilevile kusaidia wenye mahitaji
ambao hawawezi kujisaidia wenyewe.
Mungu alikuwa na rehema wakati asipo-
tuacha sisi kuhukumiwa kama tulivyo -
stahili kwa sababu ya zambi zetu, na
kwa njia ya kututendea mema kwa njia
ya kazi ya Kristo msalabani. Tunaiga
Mungu wakati tunapohurumia watu
wengine.
Wenye rehema watapata rehema.
Yesu hakusema hapa juu ya rehema ya
wokovu ya Mungu kwa mwenye zambi;
mtu halazimishwi kuwa na rehema yeye
mwenyewe kusudi apate rehema ile ni
zawadi. Anasema hapa juu ya rehema
tunayohitaji kila siku kutuwezesha ku -
ishi kwa Bwana, na kwa wakati wa kuja
vilevile saa kazi ya kila mtu itakapo -
onekana na kufunuliwa (1 Kor. 3:12-15).
Siku ile mtu asiyekuwa mwenye rehema
hatapokea rehema; maana yake zawabu
zake zitapunguka.
5:8 Kuna ahadi kwa wenye moyo
safi ya kwamba wataona Mungu. Mwe -
nye moyo safi ni mtu aliye mtakatifu ro-
honi na ndani ya mafikiri yake, mwenye
damiri safi. Maneno haya wataona
Mungu yanaweza kuwa na maana
mbalimbali: 1. Wenye moyo safi wa -
naona Mungu sasa kwa njia ya Neno
lake na Roho Mtakatifu. 2. Mara nyi -
ngine Bwana anajifunua kwao kwa njia
ya ajabu au ono. 3. Wataona Mungu
Matayo 5 29
wakati watakapoona Yesu saa atakapo -
kuja tena. 4. Wataona Mungu kwa wa -
ka ti wa milele.
5:9 Kuna heri kwa wenye kufanya
salama: maana wataitwa wana wa
Mungu. Mungu hasemi hapa juu ya
watu wenye tabia ya salama, au wana -
openda kukaa na salama. Anasema juu
ya watu wanaojaribu kusaidia watu
wengine kukaa na salama. Mara nyingi
sisi watu tunataka kuangalia na macho
tu saa watu wengine wanapogombana.
Mungu anataka tusaidie watu wale ku-
patana tena na kukaa na salama, hata
kama kwa njia ya kufanya hivi sisi
wenyewe tunalaumiwa na kutukanwa.
Wenye kufanya salama wanaitwa
wana wa Mungu. Hii si namna gani
mtu anageuka mwana wa Mungu anaweza kugeuka mwana wa Mungu
kwa njia ya kupokea Yesu Kristo kama
Mwokozi wake tu (Yn. 1:12). Waamini
wakijaribu kuleta salama katikati ya
watu, wa naonyesha kwamba wao niwana wa Mungu, na siku nyingine
Mungu ata onyesha wazi kwamba wao ni
watu wa jamaa yake.
5:10 Kuna heri vilevile kwa wale
wanaoteswa, si kwa mabaya ambayo
walitenda, lakini kwa sababu ya haki.
Ufalme wa mbinguni ni kwa wale
wanaotenda haki. Mwenendo wao wa
haki unashitaki na kuhukumu wazalimu
wa dunia na kuamsha uadui wao. Watu
wanachukia mwenye maisha ya haki,
kwa sababu mwenendo wake wa haki
unafunua uzalimu wao wenyewe.
5:11 Heri hii inafanana na ile ndani
ya shairi 10. Lakini ndani ya shairi 10
mateso yalikuwa kwa sababu ya haki;
hapa ndani ya shairi 11 ni kwa ajili ya
Kristo. Bwana alijua ya kwamba wafu-
ata wake watateswa kwa sababu ya
ushirika wao naye. Na kweli tangu kufa
kwa Kristo watu wa dunia wametesa,
kufunga gerezani, na kuua wafuata wa
Yesu.
5:12 Ni heshima kupata mateso kwa
ajili ya Kristo, neno ambalo ingetufu-
rahisha. Kuna zawabu kubwa kwa wale
wanaoshiriki na manabii ndani ya ma -
teso yao. Wale watumishi wa Mungu
kwa wakati wa Agano la Kale walisi-
mama imara kwa Mungu, si neno kama
walipata mateso. Wote wanaoiga uho-
dari na uaminifu wao kwa wakati wa
sasa watatukuzwa pamoja nao kwa
wakati wa kuja.
Mashairi 3-12 ya sura hii yanatu -
onyesha namna gani kuwa mfuata na
mwenyeji mzuri ndani ya ufalme wa
Kristo. Ona haki (sh.6), salama (sh.9),na furaha (sh.12). Labda Paulo aliku -mbuka mashairi haya wakati alipo -
andika, Kwa maana ufalme wa Mungu
si kula na kunywa, lakini haki, na
salama, na furaha katika Roho Mtaka -
tifu (Rom. 14:17).
B. Waamini ni chumvi na nuru
(5:13-16)
5:13 Bwana Yesu alisawanisha wa -
nafunzi na chumvi. Kwa watu wa dunia
kazi ya chumvi ni kuzuiza vyakula vi-
sioze; inaleta kiu kwa mtu, na inaongeza
utamu wa vyakula. Vivyo hivyo wafu-
ata wa Yesu wanazuiza uovu usizidi
duniani, na wanaamsha ndani ya roho
za watu wengine hamu kuishi maisha ya
haki tuliyosoma juu yake ndani ya
mashairi yaliyotangulia.
Lakini nini itatokea kama chumvi
ikiharibika? Nini itaweza kurudisha
utamu wake wa mbele? Haiwezekani
kurudisha utamu wake. Haina faida kwa
kazi yo yote tena, ila kutupwa njiani na
kukanyagwa na watu.
Mwanafunzi wa Yesu ana kazi ku -
bwa moja, ndiyo: kuwa chumvi ya
dunia kwa njia ya kutii mafundisho ya
Bwana Yesu ndani ya mashairi 3-10 ya
hotuba hii Bwana Yesu aliyotoa mli-
mani, na katika hotuba yake nzima.
Kama manen