261
Nakala ya Mtandao (Online Document) 1 BUNGE LA TANZANIA _______________ MAJADILIANO YA BUNGE ______________________ MKUTANO WA KUMI NA TANO Kikao cha Kumi na Moja Tarehe 17 Mei, 2014 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne. S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:- NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA MAENDELEOYA JAMII, JINSIA NA WATOTO): Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. MHE. JUMA SURURU JUMA – (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA ZA JAMII: Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

  • Upload
    others

  • View
    26

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

1

BUNGE LA TANZANIA

_______________

MAJADILIANO YA BUNGE

______________________

MKUTANO WA KUMI NA TANO

Kikao cha Kumi na Moja – Tarehe 17 Mei, 2014

(Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi)

D U A

Spika (Mhe. Anne. S. Makinda) Alisoma Dua

HATI ZILIZOWASILISHWA MEZANI

Hati Zifuatazo Ziliwasilishwa Mezani na:-

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO:

Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI:

Hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya

Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA

MAENDELEOYA JAMII, JINSIA NA WATOTO):

Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii Kuhusu

Utekelezaji wa Majukumu ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya

Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

MHE. JUMA SURURU JUMA – (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA HUDUMA

ZA JAMII:

Taarifa ya Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii Kuhusu Utekelezaji

wa Majukumu ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha

Page 2: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

2

2013/2014 na Maoni ya Kamati Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya

Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

MHE.SALUM K. BARWANY - MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI WA

WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO):

Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Maendeleo

ya Jamii, Jinsia na Watoto Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara

hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

MHE. CECILIA D. PARESSO (K. n. y. MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI

WA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI:

Taarifa ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani wa Wizara ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo

kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015.

SPIKA: Ahsante sana. Naona hapa kunaanzishwa ka-precedence

Manaibu Waziri wawili hapa wamekuja wanawasilisha kwa niaba ya Waziri wao

wakamtaja na jina, hapana. Ni kwamba unawasilisha kwa niaba ya Serikali na

ni Waziri anaweza akawa Waziri mwingine katika Wizara hiyo hiyo akateuliwa

Waziri mwingine akasoma sasa atakuwa sio Mheshimiwa Kawambwa wala sio

Mheshimiwa Sophia Simba.

Kwa hiyo mnawasilisha kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii, kwa

niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi. Sio kumtaja Waziri fulani,

hapana anaweza kuteuliwa mwingine hapa Waziri akasoma kwa niaba ya

Waziri. Kwa hiyo naomba hii msiiweke mnatugeuzia maneno hapa.

HOJA ZA SERIKALI

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Mwaka 2014/2015 Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu baada ya kuzingatia Taarifa

iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya

Bunge ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, sasa lijadili na Kupitisha

Makadirio ya Matumizi ya Kawaida ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto kwa Mwaka 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu mwingi

wa rehema kwa kutujalia kuwa na afya njema na hivyo kuweza kushiriki

Mkutano huu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Page 3: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

3

Mheshimiwa Spika, tafadhali niruhusu nitumie fursa hii kuwashukuru na

kuwapongeza Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa

Rais na Mheshimiwa Mizengo Kayanza Pinda, Waziri Mkuu na Mbunge wa

Katavi, kwa uongozi wao mahiri ambao umewezesha kushamiri kwa usawa wa

jinsia na uzingatiaji wa haki za mtoto katika jamii ya Watanzania. Mwenyezi

Mungu awajalie afya njema ili waendelee kutekeleza majukumu yao kwa

ufanisi.

Mheshimiwa Spika, napenda kukupongeza wewe Spika, Naibu Spika na

Wenyeviti wa Bunge kwa uendeshaji bora wa shughuli za Bunge. Tunaendelea

kumwomba Mwenyezi Mungu awajalie afya njema ili muweze kusimamia na

kuratibu shughuli za Bunge kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia muda nilionao kuwasilisha hoja yangu

naomba hotuba yote kama ilivyo katika kitabu cha hotuba iingie kwenye

Hansard.

Mapitio ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 kwa

kipindi cha Januari, 2011 hadi Machi, 2014.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha Januari 2011 hadi Machi, 2014

Wizara yangu ilitekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2010 kupitia

maeneo makuu manne. Maeneo hayo ni pamoja na ajira na uwezeshaji wa

wananchi, elimu ya juu, uendeshaji wa makundi mbalimbali na demokrasia na

madaraka ya umma. Katika kipindi husika utekelezaji wa maeneo hayo

umekuwa na mafanikio kama inavyoelezwa kwa kirefu kwenye kitabu cha

hotuba yangu ukurasa wa 3 hadi 11. Hali halisi ya Maendeleo ya Jamii na

changamoto zilizopo.

Mheshimiwa Spika, sekta ya Maendeleo hapa nchini imeendelea kukua

na kutambulika kwa wadau mbalimbali kutokana namchango wake katika

maendeleo ya Taifa letu. Naomba kuchukua fursa hii kueleza kwa kifupi hali

halisi ya sekta hii katika maeneo ya ushiriki wa wananchi katika maendeleo ya

kiuchumi, maendeleo ya jinsia, maendeleo ya watoto na ushiriki wa Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali katika maendeleo nchini Tanzania.

Mheshimiwa Spika, wataalamu wa Maendeleo ya Jamii ni muhimu katika

kuongeza ushiriki wa wananchi katika maendeleo. Kwa sasa kuna wataalamu

wa Maendeleo ya Jamii 2,675 katika ngazi ya Halmashauri na 21 katika

Sekretarieti za mikoa.

Page 4: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

4

Kwa takwimu hizo kuna upungufu asilimia 61 ya wataalamu hao katika

ngazi ya Halmashauri na asilimia 16 katika ngazi ya Sekretarieti za mikoa. Aidha,

wananchi wameendelea kunufaika na mafunzo ya muda mrefu na muda

mfupi yanayotolewa na vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi vilivyo chini ya

Wizara yangu. Mafunzo haya yanawawezesha kujiajiri na kuajiriwa.

Mheshimiwa Spika, hali ya usawa wa kijinsia katika nyanja mbalimbali

hapa nchini imeendelea kuimarika. Ukweli huu unadhihirishwa na ushahidi wa

kitakwimu na taarifa zilizopo katika maeneo ya ushiriki wa wanawake katika

siasa na ngazi za maamuzi, uwezeshaji wa wanawake kiuchumi, elimu, mafunzo

na ajira. Kuongezeka kwa wanawake wajasiriamali wadogo na wa kati na

upatikanaji wa haki za wanawake kisheria.

Mheshimiwa Spika, watoto ni sehemu muhimu ya jamii na ndio tegemeo

la taifa lolote. Watoto wanahitaji kukua na kuwa raia wema hivyo wanatakiwa

kupewa haki na mahitaji yao ya msingi ikiwa ni pamoja na kuishi, kupewa

malezi stahiki, kulindwa, kuendelezwa kiakili kwa kutambua na kukuza vipaji

vyao kutobaguliwa na kushirikishwa. Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa

ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18

Tanzania Bara ni 21,866,258 sawa na asilimia 50.1 ya idadi ya watu wote.

Kati ya hao wasichana ni 10,943,846 na wavulana ni 10,922,412 kwa

kuzingatia umuhimu wa watoto Wizara kwa kushirikiana na wadau inaendelea

kuweka mazingira wezeshi ili watoto wote hapa nchini wapate huduma stahiki

na haki zao za msingi kwa maendeleo ya sasa na ya baadaye ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, idadi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali chini ya Sheria ya

NGO Na. 24 ya mwaka 2002 iliyorekebishwa mwaka 2005 imeendelea kukua

mwaka hadi mwaka ambapo kufikia tarehe 17 Machi, 2014 idadi ya Mashirika

hayo ilifikia 6,427 kutoka Mashirika 3,000 yaliyokadiriwa kuwepo mwaka 2001

wakati Sera ya Taifa ya NGO ilipokuwa inaandaliwa sawa na ongezeko la

asilimia 100.

Mashirika haya yanajishughulisha na kazi mbalimbali ikiwemo elimu,

mazingira na mabadiliko ya tabianchi, afya maendeleo shirikishi, haki za

binadamu, maendeleo ya jinsia, ushawishi na utetezi, kinga ya jamii, haki za

watoto, kilimo, maji na ustawi wa jamii. Kuongezeka kwa idadi na shughuli za

NGO’s katika nchi yetu ni matokeo ya mazingira wezeshi yanayoendelea

kuboreka mwaka hadi mwaka.

Mheshimiwa Spika, maelezo ya kina ya hali halisi ya sekta ya maendeleo

ya jamii, mafanikio yaliyofikiwa na changamoto zilizopo yapo kwenye ukurasa

wa 11 hadi 23 wa kitabu cha hotuba. Mapitio ya utekelezaji wa Mpango wa

mwaka 2013/2014 na malengo ya mwaka 2014/2015.

Page 5: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

5

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Wizara yangu iliendelea

kusimamia utekelezaji wa majukumu yake kulingana na malengo

yaliyopangwa. Katika Bajeti mwaka 2013/2014 Wizara ya Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto iliidhinishiwa jumla ya shilingi 25,964,170,000 kwa ajili ya

Matumizi ya Kawaida na Maendeleo. Kati ya fedha za Matumizi ya Kawaida

shilingi 5,397,496,000 zilikuwa ni kwa ajili ya Matumizi Mengineo na shilingi

8,656,200,000 kwa ajili ya malipo ya mshahara na shilingi 11,910,672,000 ni kwa

ajili ya Matumizi ya Maendeleo.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 15 Mei, 2014 Wizara ilikuwa

imetumia jumla ya shilingi 10,305,162,100 sawa na asilimia mia ya fedha za

matumizi ya kawaida zilizopokelewa na shilingi 2,923,620,590 sawa na asilimia

mia ya fedha za Maendeleo zilizotolewa.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha utekelezaji wa Mpango wa

mwaka 2013/2014 na malengo ya mwaka 2014/2015 kwa kuzingatia maeneo

yafuatayo. Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha mwaka 2013/2014 Wizara yangu

ilidahili na kutoa mafunzo kwa wanachuo 2,869 kupitia vyuo 6 vya Maendeleo

ya Jamii. Wanachuo 2,036 walidahiliwa katika ngazi ya cheti, 591 katika ngazi

ya Stashahada, 234 ngazi ya Shahada na 8 katika ngazi ya Stashahada ya

Udhamili.

Aidha, Wizara yangu ilikarabati majengo na miundombinu katika Chuo

cha Maendeleo ya Jamii Mlale, Misungwi na Mabugai. Katika mwaka

2014/2015 Wizara yangu itaendelea kukamilisha jengo la Maktaba ya Chuo cha

Tengeru na Maabara ya Kompyuta katika Chuo cha Mabugai kwa lengo la

kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Wizara yangu ililipa shilingi

84,114,523 zikiwa ni gharama za ukarabati katika Vyuo Vya Maendeleo ya

Wananchi vya Mputa na Muhukuru mkoani Ruvuma. Aidha, Wizara ilifanya

ukarabati katika Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Tarime, Chuo cha

Maendeleo ya Wananchi Mwanahala, Chuo cha Maendeleo ya Wananchi

Kilwa Masoko na Vyuo vya Msaginya, Mputa, Sofi na Singida.

Vile vile Chuo cha Masasi na Chilala na kuvipatia Vyuo vya Maendeleo

ya Wananchi 25 vifaa vya kujifunzia na kufundishia masomo ya Ufundi stadi.

Katika mwaka wa 2014/2015 Wizara yangu itaendelea kudahili na kutoa

Page 6: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

6

mafunzo kwa wananchi na pia itakarabati majengo na miundombinu ya Vyuo

vya Maendeleo ya Wananchi vya Mto wa Mbu, Msaginya na Nandembo.

Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha mafunzo ya

Maendeleo ya Wananchi kwa kutoa huduma kwa watoto kupitia Vituo vya

Kulelea Watoto ndani ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi ambapo jumla ya

watoto1033 walinufaika. Kuwepo kwa vituo hivyo katika Vyuo vya Maendeleo

ya Wananchi kumewezesha watumishi katika vyuo hivi na jamii inayovizunguka

hususan wanawake kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali kwa uhuru

zaidi.

Kwa kipindi cha mwaka 2014/2015 Wizara itaendelea kuimarisha Vituo

vya Kulelea Watoto katika vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi kwa kutoa

vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Kutengeneza viwanja vya michezo na

kuwajengea uwezo wakufunzi 30 kwa namna ya kuendesha Vituo vya Kulelea

watoto wadogo na ujuzi wa kuwafundisha elimu ya awali.

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Jinsia. Uwezeshaji wanawake kiuchumi

ni suala muhimu katika kufikia usawa wa kijinsia na kupunguza umaskini wa

kipato katika jamii. Katika mwaka 2013/2014 Wizara kupitia Mfuko wa

Maendeleo ya Wanawake iliziwezesha Halmashauri 39 kutoa mikopo yenye

dhamani ya shilingi 428,000,000.

Katika kuhakikisha unafikia malengo yaliyopangwa Wizara ilifuatilia

utendaji wa Mfuko katika mikoa 9 na kuiwezesha Kamati ya Kudumu ya Bunge

ya Maendeleo ya Jamii kufuatilia utekelezaji wa Mfuko katika Halmashauri

mbalimbali.

Halmashauri ambazo Kamati ya Bunge ilifanya ufuatiliaji huo ni Kinondoni,

Ilala, Kibaha, Korogwe na Jiji la Tanga. Mikoa ambayo Wizara ilifuatilia shughuli

za Mfuko ni Arusha, Manyara, Singida, Pwani, Tanga, Katavi, Rukwa, Morogoro

na Kagera. Matokeo ya ufuatiliaji huo yameainishwa kwenye kitabu cha

hotuba ukurasa 27.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Wizara yangu itaendelea

kutoa fedha kwa Halmashauri nyingine zitakazokuwa zimemaliza marejesho

pamoja na kufanya ufuatiliaji kwa mikoa na Halmashauri zilizobaki. Napenda

kutumia fursa hii kuzikumbusha Halmashauri zote zilizokopeshwa kuzingatia

mkataba wa marejesho. Aidha, nazikumbusha Halmashauri zote nchini

kuchangia asilimia 5 ya mapato yao kwenye Mfuko wa Maendeleo ya

Wanawake ili wanawake wengi zaidi wanufaike na huduma ya Mfuko huu.

(Makofi)

Page 7: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

7

Mheshimiwa Spika, kupitia Benki ya Wanawake Tanzania huduma za

kibenki zimewafikia wananchi wengi zaidi wakiwepo wanawake kwani imeweza

kufungua tawi la pili la Benki ya Wanawake Tanzania eneo la Kariakoo Mkoa wa

Dar es Salaam, Mtaa wa Agrey/Likoma.

Aidha, vituo 29 vya kutolea mikopo na mafunzo kwa wajasiriamali

vimefunguliwa katika Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza. Vituo

hivyo ni kama ifuatavyo: Dar es Salaam (Tabata Kisukuru, Mbande, Sabasaba,

Ubungo Kibangu, Chanika, Chamazi na Kunduchi Mtongani); Dodoma (Airport,

Chamwino, Ipagala, Posta, Hazina Kikuyu, Kizota, Savanna Kikuyu,

Chang‟ombe, Mnadani, Veyula, Mpwapwa, Kongwa na Mbande) na Mwanza

(Nyakato, Igogo, Nyegezi, Pansiansi, Igoma, Kisesa, Magu, Misungwi na

Kitangiri). Kwa mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea kutoa ruzuku kwa

Benki ya Wanawake Tanzania ili iweze kuwafikia wananchi wengi zaidi.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukatili wa kijinsia umeendelea kuwa ni tatizo katika

jamii zetu ambapo wananchi wengi wameendelea kuumizwa na kuteseka na

hata kuuawa kutokana na vitendo vya kikatili vinavyofanyika hapa nchini.

Mwaka 2013/2014, Wizara ilifanya tathmini ya mafunzo yaliyotolewa kwa Kamati

za Ulinzi na usalama katika Mkoa wa Manyara kuhusiana na kupiga vita ukatili

wa kijinsia. Moja ya matokeo ya tathmini hiyo imeonyesha kuwa Kamati husika

zinahitaji kujengewa uwezo zaidi ili ziweze kufanya kazi zake kikamilifu.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kufanya tathmini ya

mafunzo yaliyotolewa kwa Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya kuhusu mbinu

za kutokomeza ukatili katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Mara.

Aidha, itaendelea kuzijengea uwezo kamati za ulinzi na usalama ili

ziweze kupambana na kutokomeza ukatili katika ngazi ya Wilaya na kuendelea

kuiwezesha Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia na Kuondoa Ukatili Dhidi ya Wanawake

na Watoto ili iweze kutekeleza shughuli zake kikamilifu.

Mheshimiwa Spika, suala la uingizaji wa masuala ya kijinsia katika sera,

mipango na Bajeti limekuwa likitiliwa mkazo ili kuhakikisha kuwa mipango na

Bajeti za kila sekta, idara na taasisi mbalimbali inawanufaisha wote, yaani

wanawake, wanaume, wavulana na wasichana.

Katika kipindi cha mwaka 2013/2014, Wizara kupitia wataalam wake

ilifanya tathmini ya uingizaji wa masuala ya jinsia katika Halmashauri 6 ambazo

ni Halmashauri ya Jiji la Tanga na Arusha, Halmashauri za Wilaya ya Iringa na

Moshi pamoja na Manispaa ya Temeke na Morogoro. Lengo la tathmini ilikuwa

ni kubaini mafanikio na changamoto zinazojitokeza katika uingizaji wa masuala

ya jinsia katika sera na mipango na Bajeti mbalimbali.

Page 8: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

8

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kutoa mafunzo ya

uingizaji wa masuala ya jinsia kwa wataalamu mbalimbali ili waweze kuelewa

na kutekeleza mkakati huu ikiwa ni pamoja na kukamilisha Sera ya Taifa ya

Jinsia.

Aidha, Wizara imeanza mchakato wa kuandaa taarifa ya hali ya jinsia

nchini (Tanzania Country Gender Profile) na kuanzisha benki ya Takwimu ya

usawa wa jinsia. Taarifa hii na Benki ya Takwimu zitawezesha kufanya maamuzi,

upangaji wa mipango na upimaji utekelezaji wake ushawishi na uhamasishaji

kuhusu masuala ya jinsia ili kuwa na maendeleo endelevu.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014, Wizara kwa kushirikiana na

wadau mbalimbali iliandaa rasimu ya 7 na 8 ya nchi ya Mkataba wa Kuondoa

Aina zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake. Rasimu ya Taarifa hiyo imekamilika

na inatarajiwa kujadiliwa na wadau wakiwemo Kamati ya Bunge ya Sekta ya

Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kupata maoni zaidi kwa ajili ya kuiboresha.

Mheshimiwa Spika, tarehe 8 Machi kila mwaka, Wizara imekuwa

ikishirikiana na wadau mbalimbali katika kuratibu Siku ya Wanawake Duniani.

Katika mwaka 2013/2014, Wizara yangu iliratibu maadhimisho ya siku hiyo katika

ngazi ya mikoa ambapo Kauli mbiu ilikuwa ni “Chochea Mabadiliko Kuleta

Usawa wa Kijinsia” Kauli mbiu hii inasisitiza na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu

wa kuzingatia masuala ya jinsia katika kupanga na kutekeleza mikakati na

mipango ya maendeleo kwa kuzingatia ushiriki stahiki wa wanawake,

wanaume, wavulana na wasichana katika kujiletea maendeleo yao na taifa

kwa ujumla. Kwa mwaka 2014/2015, Wizara itaratibu maadhimisho haya Kitaifa

ili kuweza kupima mafanikio yaliyopatikana katika miaka mitano (2010 – 2015)

katika juhudi za kumwendeleza mwanamke pamoja na kubainisha

changamoto zilizojitokeza kwa kipindi hicho toka maadhimisho haya

yalipofanyika kitaifa mwaka 2010.

Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza mikataba na maazimio mbalimbali

ambayo nchi imesaini na kuridhia, mwaka 2013/2014, Wizara ilishiriki katika

mkutano wa 58 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake na mkutano wa nchi za

Maziwa Makuu kuhusu masuala ya jinsia. Lengo la mikutano hiyo ni kutafuta

mbinu za pamoja za kukabiliana na changamoto mbalimbali, kubadilishana

uzoefu na kukubaliana maeneo muhimu ya utekelezaji katika kuleta usawa wa

kijinsia na maendeleo ya wanawake katika nchi husika.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kushiriki na kutoa

mchango wake katika mikutano ya kikanda na kimataifa kuhusu utekelezaji wa

masuala ya usawa wa kijinsia na kuwaendeleza wanawake.

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Watoto: Maendeleo ya taifa lolote

duniani hutegemea sana namna ambavyo linawalinda na kuwakuza watoto

Page 9: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

9

wake. Kwa kuzingatia hilo, Wizara yangu imekuwa ikichukua hatua mbalimbali

katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili watoto hapa nchini.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014, Wizara yangu iliandaa mpango

kazi wa jamii wa kudhibiti tatizo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Lengo likiwa ni kuongeza ushiriki wa wadau katika kudhibiti na kuondoa tatizo

hilo kwa kuwaelimisha na kuhamasisha ili wabebe jukumu la kuwapatia watoto

mahitaji na haki zao za msingi. Utekelezaji wa Mpango kazi unahusisha familia,

jamii, Serikali, asasi za kiraia, vyombo vya habari na wabia wa maendeleo.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itasambaza mpango katika mikoa yote na

kuratibu utekelezaji wake.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Wizara yangu imefanya

marekebisho ya Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 kuwa Sera ya

Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2014 ili iweze kujumuisha

masuala ya utoaji huduma fungamanishi na shirikishi za Malezi, Makuzi na

Maendeleo ya Mtoto.

Aidha, Sera hiyo imezingatia masuala ya kukabiliana na changamoto

zinazotokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia pamoja na upatikanaji wa

huduma za malezi na makuzi kwa watoto walio chini ya umri wa miaka nane.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itakamilisha Sera hiyo na mkakati wake wa

utekelezaji. Aidha, Wizara itasambaza kwa wadau sera na mkakati huo kwa ajili

ya utekelezaji.

Mheshimiwa Spika, ukatili dhidi ya watoto ni moja ya changamoto

zinazoathiri malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto. Katika kupunguza matukio

ya ukatili huo, mwaka 2013/2014 Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau

mbalimbali iliandaa Mpango Kazi Shirikishi wa Kuzuia Ukatili dhidi ya Watoto wa

mwaka 2013 hadi 2016.

Aidha, Wizara yangu iliwezesha kufanyika kwa mkutano wa mwaka wa

Kikosi Kazi cha Taifa cha Kuzuia Ukatili dhidi ya Mtoto ambapo sekta zote

zinazohusiana na maendeleo ya mtoto zilitoa taarifa kuhusu mapendekezo ya

namna ya kutekeleza mpango huo. (Makofi)

Pia, Wizara iliandaa mkutano uliowakutanisha watekelezaji wa

Mpangokazi wa miaka mitatu wa kuzuia ukatili wa watoto na wadau wa

maendeleo. Tayari wadau mbalimbali wa maendeleo wajitokeza kuchangia

fedha za utekelezaji wa baadhi ya kazi zilizoainishwa katika mpango huu.

Tunawashukuru sana wadau hawa. Katika mwaka 2014/2015, Wizara

itaendelea kuratibu na kusimamia mpango huo kwa kushirikiana na kikosi kazi

hicho.

Page 10: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

10

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu pia iliandaa kitini cha elimu ya malezi

kwa familia kuhusu kukabiliana na ukatili dhidi ya watoto na kukisambaza

kupitia mafunzo kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka halmashauri za Hai,

Temeke, Magu na Kasulu. Kitini hiki mkitatumiwa na wawezeshaji jamii katika

kuwajengea uwezo wazazi na walezi ili kudhibiti ukatili dhidi ya watoto. Katika

mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kuratibu usambazaji wa kitini hicho katika

halmashauri nyingine.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara iliendelea kuratibu utoaji wa taarifa za

ukatili dhidi ya watoto kupitia namba ya simu 116 inayosimamiwa na Shirika Lisilo

la Kiserikali la C-SEMA. Hadi kufikia mwaka 2014 jumla ya simu 6,188 zilipigwa

kupitia namba hiyo na kufanyiwa kazi. Mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea

kuratibu na kusimamia mtandao huo na kuendelea kutathmini ili kuwezesha

kupeleka huduma hii katika maeneo mengine ya nchi.

Mheshimiwa Spika, Watoto wanayo haki ya msingi ya kushiriki na

kushirikishwa katika masuala yote yanayowahusu. Katika kuhakikisha ushiriki wa

watoto katika kutoa maoni yao, mwaka 2013/2014, wizara iliandaa Mkutano

Mkuu wa Baraza la Watoto ili kupitia Rasimu ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania.

Aidha, wizara yangu iliratibu utekelezaji wa shughuli za mabaraza ya

watoto katika ngazi ya Wilaya/Mikoa pamoja na Azimio la Bunjumbura kuhusu

haki na ustawi wa watoto. Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea

kushirikiana na Halmashauri kuimarisha Baraza la Watoto la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania pamoja na mabaraza ya watoto ya mikoa na wilaya ili

yaweze kutoa fursa nzuri za ushiriki wa watoto katika maeneo husika.

Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2013/2014, Wizara yangu iliratibu

maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika ambayo yaliadhimishwa katika ngazi

ya mkoa.

Katika maadhimisho hayo, kila mkoa ulipata fursa ya kuadhimisha siku hii

muhimu kulingana na mazingira na uhitaji wa mkoa husika. Kauli mbiu ya

mwaka 2013/2014 ilikuwa ni “Kuondoa Mila zenye kuleta Madhara kwa Watoto:

ni Jukumu Letu Sote”. Lengo la kaulimbiu hii ni kuhamasisha jamii kubaini baadhi

ya mila ambazo zimekuwa zikileta madhara kwa watoto na kuweka mikakati ya

kuzitokomeza.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iliratibu maadhimisho ya siku ya Familia

Duniani ambayo yalifanyika kimkoa. Kauli mbiu ya maadhimisho haya ilikuwa ni

“Imarisha na Endeleza Ushirikiano na Mshikamano wa Familia na Makundi

Mbalimbali ya Jamii”. Kauli mbiu hii inasisitiza wazazi, walezi na jamii kuwajibika

kwa pamoja katika malezi ya familia. Katika mwaka 2014/2015, Wizara

Page 11: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

11

itaendelea kuratibu maadhimisho ya siku hizo kwa lengo la kuhamasisha jamii

kuhusu haki na ustawi wa mtoto na maendeleo ya familia.

Mheshimiwa Spika, Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali: Katika kipindi

cha mwaka 2013/2014, Serikali iliendelea kusajili Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

chini ya Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002. Jumla ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali 435 yalipatiwa usajili katika ngazi ya wilaya, mkoa, taifa na kimataifa.

Hii imefanya idadi ya NGOs kuongezeka kutoka mashirika 5,992 mwezi

Julai, 2013 na kufikia Mashirika 6,427 mwezi Machi, 2014 ikiwa ni ongezeko la

asilimia 7. Aidha, katika kipindi cha mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea

na usajili wa mashirika hayo.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu pia iliratibu shughuli za NGOs kwa

kuwezesha ushiriki wa wadau katika utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali.

Hii ni pamoja na kuiwezesha Bodi ya uratibu wa NGOs kukagua shughuli za

NGOs 21 na kufanya vikao vitatu katika mikoa ya Tanga, Lindi na Mbeya. Vikao

hivyo vilifikia maamuzi mbalimbali ikiwemo utatuzi wa migogoro katika Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali.

Aidha, Wizara kupitia Bodi ya Uratibu wa NGOs ilikutana na wadau 175 na

kujadili mafanikio na changamoto zinazozikabili NGOs katika mikoa husika na

kutoa elimu kuhusa Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka

2001 na Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002.

Wizara pia imeanzisha utaratibu wa kukutana na NGOs zinazofanya kazi za

watoto na wanawake na mapendekezo ya kuboresha ushirikiano

yameandaliwa.

Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kujenga mazingira wezeshi na

kuboresha uratibu wa mashirika haya, Wizara itatekeleza mambo mbalimbali

katika kipindi cha mwaka 2014/2015. Kazi hizo ni pamoja na kufuatilia na

kutathmini mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na hali ya uendeshaji wa

mashirika hayo hapa nchini. Aidha, itawezesha kufanyika kwa tathmini kuhusu

ufanisi wa Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kujenga mazingira

wezeshi kwa NGOs.

Page 12: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

12

Vilevile, Serikali kupitia Wizara yangu itawezesha kufanyika kwa

mafunzo ya ndani kuhusu usajili, ufuatiliaji na tathmini ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa wilaya na mikoa kwa lengo la

kuwajengea uwezo wa kiutendaji ili kuboresha utoaji wa huduma za usajili na

uratibu katika ngazi husika.

Mheshimiwa Spika, Uratibu wa Sera na Mipango: Katika mwaka

2013/14 uratibu na mapitio ya Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008

pamoja na mkakati wake ulifanyika. Katika mwaka 2014/2015, uratibu wa

mapitio ya Sera ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2001 na tathmini ya

utekelezaji wa Sera ya Wanawake na Jinsia ya mwaka 2000 na Sera ya Taifa ya

Mashirika Yasiyo Ya Kiserikali ya mwaka 2001utafanyika.

Aidha, uratibu wa mipango na bajeti ya mwaka 2015/2016 pamoja na

uandaaji wa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini wa Wizara utaandaliwa ili

kuimarisha ukusanyaji, uhifadhi na usimamizi wa takwimu na taarifa za sekta ya

maendeleo ya jamii. Katika kuwapatia motisha wafanyakazi, Wizara yangu

kwa mwaka 2013/14, ilipandisha vyeo watumishi 126 na kuwabadilisha kada

watumishi wanne. Aidha, watumishi 86 walithibitishwa kazini. Kwa kipindi cha

mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kuwapandisha vyeo watumishi wake kwa

mujibu wa Miundo ya Utumishi wa Kada zao na Sera ya Menejimenti na Ajira

katika Utumishi wa Umma ili kuongeza tija katika utendaji kazi.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imekuwa ikikabiliana na upungufu

mkubwa wa watumishi hasa katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Vyuo vya

Maendeleo ya Wananchi. Katika kukabiliana na changamoto hii mwaka

2013/2014, Wizara yangu iliajiri jumla ya watumishi 92 kutokana na kibali cha

ajira kilichotolewa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Katika

mwaka 2014/2015, Wizara inatarajia kuendelea kuajiri watumishi wengine ili

kuendelea kupunguza pengo lililopo.

Mheshimiwa Spika, katika kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa

watumishi, mwaka 2013/2014, Wizara iliwapatia watumishi vitendea kazi

mbalimbali.

Kwa mwaka 2014/2015, Wizara yangu itajenga eneo la kuegesha

magari la Makao Makuu ya Wizara, kununua jenereta na kuendelea kuwapatia

wafanyakazi vitendea kazi mbalimbali.

SPIKA: Waheshimiwa, naomba mpunguze sauti, tuko katika kikao.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Aidha, Wizara

itawawezesha watumishi kushiriki katika mashindano ya SHIMIWI ili kuboresha

afya na kuimarisha mahusiano miongoni mwa watumishi wa Serikali.

Page 13: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

13

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iliendeleza mapambano dhidi ya

UKIMWI na Virusi Vya UKIMWI mahala pa kazi. Katika mwaka 2013/2014, Wizara

iliwapatia watumishi nasaha za namna ya kujikinga na maambukizi ya Virusi Vya

UKIMWI. Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kuhamasisha watumishi

wajitokeze kupima afya zao pamoja na kuwapatia huduma ya viini lishe na

chakula.

Mheshimiwa Spika, mawasiliano kwa umma mawasiliano: Kwa mwaka

2013/2014, Wizara yangu iliandaa vipindi vya luninga, radio na mikutano na

waandishi wa habari kwa ajili ya kuelimisha umma kuhusu masuala ya

maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake, familia, haki za watoto na uratibu wa

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. Aidha, Wizara iliandaa matangazo mbalimbali

kupitia magazeti, vipeperushi na mabango.

Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2013/2014, Wizara pia ilianzisha

mawasiliano na umma kupitia mitandao ya kijamii. Mitandao hiyo ni pamoja na

Blog ya wizara, facebook ya Wizara na twitter ya Wizara. Kwa mwaka

2014/2015, Wizara itaandaa mkakati wa mawasiliano na kuendelea kuwezesha

mawasiliano kwa umma kupitia njia mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii,

radio, luninga, magazeti, gari la sinema, majarida, vipeperushi na uhamasishaji

jamii kwa kushirikiana na Maafisa Maendeleo ya Jamii katika ngazi ya Kata,

Wilaya na Mkoa.

Mheshimiwa Spika, hitimisho: Mapitio ya utekelezaji wa Mpango wa

Wizara wa mwaka 2013/14 na Malengo ya mwaka 2014/2015 yanaonesha jinsi

Wizara yangu ilivyo na umuhimu katika kuleta usawa wa jinsia, upatikanaji wa

haki na ustawi wa watoto, ongezeko la ajira kwa vijana na ushawishi wa jamii

katika kupokea na kutekeleza miradi ya maendeleo endelevu. Ili Wizara

itekeleze vema majukumu yake inahitaji ushirikiano mkubwa wa wadau

mbalimbali na rasilimali fedha za kutosha.

Mheshimiwa Spika, napenda sasa kumshukuru sana Naibu Waziri,

Mheshimiwa Dkt. Pindi Hazara Chana, kwa ushirikiano, ushauri na usaidizi

mkubwa anaonipa katika kuongoza Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, vilevile ninapenda kutoa shukrani za dhati kwa Katibu

Mkuu Bibi Tayari Maembe, Naibu Katibu Mkuu Bibi Nuru H. Milao, Wakurugenzi,

Wakuu wa Vitengo, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake Tanzania, Bibi

Magreth Chacha, Wakuu wa Vyuo na wafanyakazi wote wa Wizara yangu wa

ngazi zote, kwa jitihada zao katika utekelezaji wa majukumu ya Wizara ambayo

Page 14: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

14

ni pamoja na kuniwezesha mimi kuwasilisha Hotuba hii mbele ya Bunge lako

Tukufu.

Kabla sijamaliza hotuba yangu sina budi kuwashukuru wadau wote

tunaofanya nao kazi na wengine ambao kwa namna moja au nyingine

tunashirikiana nao, peke yetu kama Wizara tusingefikia mafanikio niliyoyataja

ninaomba kupitia Bunge lako Tukufu kutoa shukrani zangu za dhati kwa

wafuatao:-

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Asasi ya Wanawake na Maendeleo

(WAMA), Mfuko wa fursa sawa kwa wote (EOTF), Mtandao wa Jinsia Tanzania

(TGNP), Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA), Chama cha

Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Shirikisho la Vyama Vya

Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (FAWETA), Medical Women Association

of Tanzania (MEWATA), White Ribbon, Plan International Tanzania, Serve the

Children, Mashirika mbalimbali yasiyo ya Kiserikali pamoja na wale wanaofanya

kazi kwa maslahi ya jamii kwa namna moja au nyingine.

Ninapenda pia kuyashukuru Mashirika kutoka nchi rafikia ambayo

yameendelea kutusaidia katika kufanya kazi na sisi. Mashirika hayo ni pamoja

BFID, GPE, SIDA CANADA, KOIKA na UK EDUCATION.

Aidha, ninayashukuru Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo ni UNICEF,

UNDP, UNFPA na UN WOMEN kwa misaada yao mbalimbali iliyofanikisha

utekelezaji wa majukumu mengi ya Wizara yangu.

Mheshimiwa Spika, Makadirio ya Bajeti ya Wizara ya mwaka 2014/2015 ili

Wizara yangu iweze kutekeleza majukumu na malengo yake kwa mwaka

2014/2015, sasa ninaliomba Bunge lako Tukufu liidhinishe matumizi ya shilingi

bilioni thelathini milioni mia mbili thelathini na tatu laki nne na sabini na nne elfu,

(Sh. 30,233,474,000/=).

Kati ya maombi hayo shilingi bilioni ishirini na moja, milioni mia mbili na

kumi na tano, laki tisa na thelathini elfu (Sh. 21,215,930,000/=) ni kwa ajili ya

Matumizi ya Kawaida.

Shilingi bilioni kumi na mbili, milioni mia nane kumi na nane laki nne na

thelathini na nne elfu (Sh. 12,818,434,000/=) ni kwa ajili ya mishahara.

Shilingi bilioni nane, milioni mia tatu tisini na saba laki nne na tisini na sita

elfu (Sh. 8,397,496,000/=) ni kwa ajili ya matumizi mengineyo.

Shilingi bilioni tisa, milioni kumi na saba, laki tano na arobaini na nne elfu

(Sh. 9,017,544,000/=) ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo, ambapo

shilingi bilioni saba (Sh. 7,000,000,000/=) ni fedha za ndani na shilingi bilioni mbili,

Page 15: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

15

milioni kumi na saba, laki tano na arobaini na nne elfu (Sh. 2,017,544,000/=) ni

fedha za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja. (Makofi)

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naafiki.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

HOTUBA YA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

KAMA ILIVYOWASILISHWA MEZANI

HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA

MATUMIZI

YA FEDHA KWA MWAKA 2014/2015

A: UTANGULIZI

1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba bunge lako tukufu

baada ya kuzingatia taarifa iliyowasilishwa leo hapa Bungeni na Mwenyekiti wa

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii, sasa lijadili na kupitisha

Makadirio ya Matumizi ya Kawaida na ya Maendeleo ya Wizara ya Maendeleo

ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa mwaka 2014/5015.

2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninamshukuru Mwenyezi Mungu

mwingi wa rehema kwa kutujalia kuwa na afya njema na hivyo kuweza kushiriki

mkutano huu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

3. Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kuwapongeza

Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania; Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal, Makamu wa Rais na

Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, Waziri Mkuu na Mbunge wa

Mpanda Mashariki kwa uongozi wao mahiri ambao umewezesha kushamiri kwa

usawa wa jinsia na uzingatiaji wa haki za mtoto katika jamii ya watanzania.

Mwenyezi Mungu awajalie afya njema ili waendelee kutekeleza majukumu yao

kwa ufanisi.

4. Mheshimiwa Spika, napenda kukupongeza wewe Spika, Naibu

Spika na Wenyeviti wa Bunge, kwa uendeshaji bora wa shughuli za Bunge.

Page 16: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

16

Tunaendelea kumuomba Mwenyezi Mungu awajalie afya njema ili muweze

kusimamia na kuratibu shughuli za Bunge kwa ufanisi.

5. Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kuishukuru Kamati

ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii ikiongozwa na Mwenyekiti wake

mahiri Mheshimiwa Saidi Mohamed Mtanda (Mb.) na Makamu Mwenyekiti

Mheshimiwa Kapteni Mstaafu John Damiano Komba (Mb.) kwa kuichambua na

kuijadili bajeti ya Wizara yangu. Ushauri na maelekezo ya Kamati hiyo

yametuwezesha kuboresha na kukamilisha bajeti katika muda muafaka.

6. Mheshimiwa Spika, naomba nichukue fursa hii kuwapongeza

Mheshimiwa Samuel Sitta (Mb.) kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bunge

Maalum la Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa

Samiya Suluhu Hassan (Mb.) kuwa Makamu Mwenyekiti.

Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa (Mb.) kwa

kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Kalenga na Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya

Kikwete kuwa Mbunge wa Chalinze.

7. Mheshimiwa Spika, naomba nitangulize dua zangu kwa Mwenyezi

Mungu azipokee na kuzilaza mahali pema peponi roho za Marehemu William

Agustino Mgimwa aliyekuwa Mbunge wa Kalenga na marehemu Said

Bwanamdogo aliyekuwa Mbunge wa Chalinze. Bunge hili litawakumbuka

daima kwa michango yao.

8. Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa natumia fursa hii

kuwapa pole wale wote waliopatwa na majanga pamoja na kufiwa na ndugu,

jamaa na wapendwa wao katika matukio mbalimbali yaliyotokea nchini.

B: MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM YA

MWAKA 2010 KWA KIPINDI CHA JANUARI, 2011 HADI MACHI, 2014

9. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2013/2014, Wizara

yangu iliendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)

ya mwaka 2010. Mafanikio ya utekelezaji wa Ilani kwa kipindi cha kuanzia

Januari, 2011 hadi Machi, 2014 ni haya yafuatayo.

I. Ajira na Uwezeshaji wa Wananchi.

10. Mheshimiwa Spika, Ibara ya 78 ya Ilani ya CCM, imeelekeza

uimarishaji na upanuzi wa mafunzo ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi ili

viweze kupokea vijana wengi zaidi na kuwapatia mafunzo ya stadi na maarifa

ya kisasa katika fani za kilimo, biashara, ufundi na ujasiriamali.

Page 17: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

17

11. Mheshimiwa Spika, Mafunzo ya kuwapatia wananchi ujuzi na stadi

mbalimbali ili waweze kujiajiri na kuongeza uzalishaji mali na kipato ni muhimu

hasa katika kipindi hiki cha ukosefu mkubwa wa ajira. Wizara kupitia Vyuo 55

vya Maendeleo ya Wananchi, iliwapatia mafunzo wananchi 146,383

wakiwemo wanawake 70,841 na wanaume 75,542 kupitia kozi fupi, kozi ndefu

na mafunzo nje ya vyuo kwa kipindi cha Januari, 2011 hadi Machi, 2014

(Jedwali Na. 1). Mafunzo yanayotolewa ni pamoja na: uashi, useremala, ufundi

magari, ufundi chuma na uchomeleaji, kompyuta, ushonaji, umeme wa

majumbani, kilimo, ususi na upishi. Aidha, Wizara imeendelea kutoa mafunzo ya

ufundi stadi yanayoratibiwa na Mamlaka ya Ufundi Stadi (VETA) kupitia vyuo 25

vya Maendeleo ya Wananchi ambapo kumekuwa na ongezeko la wanafunzi

wanaopata mafunzo haya kutoka 1,125 mwaka 2013 hadi kufikia 2,722 mwaka

2014 (Jedwali Na. 2). Kuyaendeleza Makundi Mbalimbali Watoto.

12. Mheshimiwa Spika, Ilani ya CCM ya mwaka 2010 Ibara ya 204 (a),

(h) na (j) inaiagiza Serikali kukamilisha Sera ya Malezi na Makuzi ya Mtoto na

kupitisha Sera Fungamanishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto

ili watoto wote nchini waweze kunufaika kutokana na utekelezaji wake. Aidha,

Ibara hiyo inaitaka Serikali kutekeleza mikataba ya haki za mtoto iliyoridhiwa na

Bunge.

13. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza azma hiyo, Wizara yangu

imeendelea kufanya mapitio ya Sera ya Mtoto na kutekeleza mikataba ya

kimataifa kuhusu haki na maendeleo ya mtoto iliyoridhiwa na Bunge lako

tukufu. Wizara imefanya marekebisho ya Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya

mwaka 2008 na imeandaa rasimu ya Sera ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya

Mtoto (2014) ili iweze kubeba masuala ya utoaji huduma fungamanishi na

shirikishi kwa mtoto. Masuala mengine yaliyoingizwa katika sera hiyo ni pamoja

na kuboresha upatikanaji wa huduma muhimu kwa watoto walio chini ya umri

wa miaka nane.

Aidha, katika kuwezesha utekelezaji wa mikataba ya kimataifa inayohusu

haki na maendeleo ya mtoto, Wizara yangu inaandaa taarifa ya utekelezaji wa

mikataba hiyo ili kuiwasilisha katika vikao vya tatu, nne na tano vya Mkataba

wa Kimataifa kuhusu Haki za Mtoto (Convention on the Rights of the Child)

katika mwaka 2014. Aidha, Wizara yangu imeendelea kuratibu utekelezaji wa

Mpango wa Miaka Mitatu (2013 – 2016). Wanawake.

14. Mheshimiwa Spika, Ilani ya CCM ya mwaka 2010 Ibara ya 205 (e)

na (f) inaitaka Serikali kuimarisha mifuko iliyopo ya mikopo na Benki ya

Wanawake Tanzania ili wanawake wengi waweze kufaidika kiuchumi.

15. Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza azma hii ya Ilani, Wizara

kupitia Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake ilizipatia halmashauri 62 mikopo

yenye jumla ya shilingi milioni 612 kwa ajili ya kuwakopesha wanawake katika

Page 18: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

18

maeneo yao ili kuwaendeleza kiuchumi. Halmshauri zilizopatiwa mikopo kupitia

Mfuko huu katika kipindi cha kuanzia mwaka 2010/2011 hadi 2013/2014 ni kama

inavyoonekana kwenye kiambatisho (Jedwali Na. 3).

16. Mheshimiwa Spika, Serikali pia iliendelea kuiwezesha Benki ya

Wanawake Tanzania ili kuwafikia wananchi wengi zaidi hususan wanawake.

Katika kipindi cha Januari 2011 hadi Machi, 2014 Benki ilitoa mikopo yenye

thamani ya shilingi 24,392,382,000 kwa wananchi 11,754 Kati ya hao wanawake

ni asilimia 88 (Jedwali Na. 4 (i) na 4 (ii)). III. Elimu ya Juu.

17. Mheshimiwa Spika, Ilani ya CCM ya mwaka 2010 Ibara ya 85 (e)

imeelekeza Serikali kuongeza udahili kwa wanafunzi katika vyuo vya elimu ya

juu. Wizara kupitia Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru iliendelea kudahili

wanafunzi katika ngazi ya shahada ya kwanza katika fani za Upangaji na

Usimamizi Shirikishi wa Miradi, Maendeleo ya Jamii, Maendeleo ya Jinsia na

Stashahada ya Uzamili ya Maendeleo ya Jamii. Jumla ya wanachuo 546

wakiwemo wanawake 324 na wanaume 222 walidahiliwa kati ya Septemba,

2011 hadi Septemba, 2013 (Jedwali Na. 5 (i)).

18. Mheshimiwa Spika, pamoja na kutoa mafunzo ya elimu ya juu,

Wizara iliendelea kutoa mafunzo ya taaluma ya maendeleo ya jamii kupitia

vyuo vinane vinavyotoa mafunzo katika ngazi ya Astashahada na Stashahada.

Vyuo hivyo ni Buhare, Missungwi, Rungemba, Uyole, Ruaha, Mlale, Mabughai na

Monduli. Jumla ya wanachuo 11,368 wakiwemo wanawake 7,463 na wanaume

3,905 walidahiliwa katika vyuo hivi kwa kipindi cha Septemba, 2011 hadi

Septemba, 2013 (Jedwali Na. 5 (ii)).

Kati ya idadi hiyo, ngazi ya Stashahada ni 2,445 na Astashahada ni

wanachuo 8,923. Wahitimu katika fani hizi huajiriwa katika ngazi ya halmashauri

na huwezesha jamii kutekeleza majukumu yao ya maendeleo kwa kutumia

mbinu shirikishi na kuzingatia usawa wa kijinsia na haki za mtoto hivyo kuifanya

jamii kuwa na maendeleo endelevu. IV. Demokrasia na Madaraka ya Umma.

19. Mheshimiwa Spika, Ibara ya 188 (a) ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya

mwaka 2010, inaitaka Serikali kuhakikisha Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

yanajishughulisha na majukumu yaliyoandikishwa kutekeleza na kwamba

hayapati nafasi ya kujiendesha kinyume na malengo yao. Kwa kuzingatia agizo

hili la Ilani, Wizara yangu imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuimarisha

usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

Moja ya hatua hizo ni pamoja na kutoa elimu kwa wadau 11,674 kati ya

Januari, 2011 na Machi, 2014 kuhusu Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali na Sheria ya NGOs Na.24 ya mwaka 2002 iliyorekebishwa mwaka 2005.

Page 19: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

19

20. Mheshimiwa Spika, elimu hiyo ilitolewa kupitia Ofisi ya Msajili wa

NGOs na mikutano ya wadau iliyofanyika katika mikoa ya Morogoro, Mtwara,

Njombe, Mwanza, Ruvuma, Lindi, Mbeya na Tanga. Jumla ya Wadau 560

walipata elimu hii ikiwa ni pamoja na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa mikoa na

wilaya 24, wawakilishi kutoka katika Mashirika Yasiyo ya Kiserikali 536 na

wananchi mbalimbali. Lengo la kufanya hivyo ni kuziwezesha NGOs kufahamu

wajibu wao na kujiendesha kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

Aidha, kwa upande wa Maafisa Maendeleo ya Jamii wa ngazi ya wilaya

na mikoa elimu hiyo imelenga kuwajengea uwezo wa kufuatilia shughuli za

NGOs katika maeneo yao na kutoa taarifa kwa Wizara pindi wanapobaini

mashirika hayo kujiendesha kinyume na masharti ya usajili wao.

21. Mheshimiwa Spika, hatua nyingine ambazo Wizara yangu

imechukua katika kutekeleza agizo hili la Ilani ni pamoja na kuwateua Maafisa

Maendeleo ya Jamii kuwa wasajili wasaidizi na waratibu wa mashirika haya

katika ngazi za wilaya na mkoa ili kufuatilia shughuli za mashirika hayo katika

ngazi husika. Aidha, Wizara imekuwa ikifuatilia na kutathmini utendaji na

uendeshaji wa NGOs nchini ambapo kwa kipindi cha Januari, 2011 na Machi,

2014, NGOs 55 zilitembelewa na kukaguliwa katika maeneo yao ya utekelezaji.

Aidha, taarifa za mwaka za fedha na kazi zilizowasilishwa kutoka kwa

mashirika 1,000 zilifanyiwa uchambuzi. Kutokana na ufuatiliaji na tathmini ya

shughuli za NGOs, shirika moja lilibainika kujiendesha kinyume cha taratibu na

kufutiwa usajili wake.

Aidha, ilibainika kuwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali mengi yameendelea

kutoa mchango mkubwa katika huduma za kijamii na masuala ya kisera.

22. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyofikiwa katika

utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2010, Wizara yangu ilikabiliwa na

changamoto mbalimbali ambazo ni pamoja na:-

(i) Uhaba wa wakufunzi wa kada mbalimbali katika Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi;

(ii) Upungufu wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia katika Vyuo tisa

vya Maendeleo ya Jamii na Vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi;

(iii) Mahitaji ya mikopo ya Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake ni

mengi ikilinganishwa na fedha zinazotolewa. Aidha, mikopo inayotolewa kwa

vikundi ni midogo isiyokidhi mahitaji halisi ya biashara na mafunzo ya ujasiriamali

yanayotolewa kwa wakopaji kutotosheleza kuwajengea uwezo unaohitajika;

Page 20: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

20

(iv) Kutokuwepo kwa uwazi na uwajibikaji kwa baadhi ya Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali.

C: HALI HALISI YA SEKTA YA MAENDELEO YA JAMII NA CHANGAMOTO

ZILIZOPO

23. Mheshimiwa Spika, Sekta ya maendeleo ya jamii hapa nchini

imeendelea kukua na kutambulika na wadau mbalimbali kutokana na

mchango wake katika maendeleo ya taifa letu. Naomba kuchukua fursa hii

kueleza kwa kifupi hali halisi ya sekta hii katika maeneo ya ushiriki wa wananchi

katika maendeleo ya kiuchumi, maendeleo ya jinsia, maendeleo ya watoto na

ushiriki wa mashirika yasiyo ya kiserikali katika maendeleo nchini Tanzania.

Hali ya Ushiriki wa Wananchi katika Maendeleo.

24. Mheshimiwa Spika, maendeleo ya jamii kama dhana ni hatua mbalimbali

zinazowawezesha watu kutambua uwezo walio nao wa kubaini matatizo yao

na kutumia fursa na rasilimali zilizopo ili kuondokana na ujinga, maradhi, njaa na

umaskini kwa ujumla na hivyo kujiletea maisha bora.

Msisitizo wa dhana hii ni ushiriki wa watu katika kuamua, kupanga na

kutekeleza mambo yote yanayohusiana na maisha yao na nchi yao.

Wataalamu wa Maendeleo ya Jamii ni mhimili muhimu kwa jamii katika

kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo kwani ndiyo wenye jukumu la

kushauri, kushawishi, kuelimisha, kuhamasisha na kuraghabisha wananchi

kujiletea maendeleo kwa kutumia mbinu shirikishi katika programu mbalimbali

wanazoibua na kubuni. Hivyo, wataalamu hao ni muhimu katika kuiwezesha

jamii kuleta mabadiliko chanya kwa kushiriki katika masuala mbalimbali ya

maendeleo.

25. Mheshimiwa Spika, Wataalamu wa maendeleo ya jamii hufanya kazi

katika ngazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wizara, wakala na mamlaka za

Serikali, Sekretariat za mikoa, halmashauri za miji, wilaya, manispaa na majiji, miji,

kata na vijiji. Wataalamu hao pia hufanya kazi na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

na taasisi mbalimbali za sekta binafsi.

Mfano, katika ngazi za halmashauri takwimu zinaonesha kuwa kuna

wataalamu wa maendeleo ya jamii 2,675 ambapo 1,381 hufanya kazi katika

makao makuu ya halmashauri na 1,294 hufanya kazi katika Kata.

Aidha, katika ngazi ya Sekretariat za mikoa kuna jumla ya wataalamu 21.

Wataalamu hawa hutoa mchango mkubwa sana wa kuwaandaa wananchi

kupokea na kutekeleza programu mbalimbali za huduma kama za afya, elimu,

maji, nishati na miradi mingine ya kiuchumi na kijamii.

Page 21: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

21

26. Mheshimiwa Spika, Sera ya Maendeleo ya Jamii ya mwaka 1996

inasisitiza kuwepo kwa mtaalamu mmoja kwa kila Kata hivyo mahitaji halisi ya

wataalamu hao kwa ngazi husika ni 3,339.

Kwa takwimu hizo upungufu wa wataalamu kwenye kata ni 2,045 sawa

na asilimia 61 ya mahitaji (Jedwali 6).

Aidha, katika ngazi ya Sekretariati za mkoa upungufu wa wataalamu

hao ni asilimia 16. Hali hii inaathiri kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa shughuli za

Sekta ya Maendeleo ya Jamii. Katika kukabiliana na changamoto hii, Wizara

yangu imeendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI kuhakikisha

halmashauri zote zinaajiri wataalamu wa maendeleo ya jamii katika ngazi ya

Kata.

27. Mheshimiwa Spika, Wizara inaendelea kutoa mafunzo na kuzalisha

wataalamu wa Maendeleo ya Jamii kupitia vyuo tisa vya maendeleo ya jamii

nchini. Katika kipindi cha mwaka 2011/2012 hadi mwaka 2013/2014 jumla ya

wanachuo 11,914 walidahiliwa katika vyuo hivyo. Idadi hii kubwa ni matokeo ya

utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kuboresha mazingira ya kujifunzia na

kufundishia ikiwemo ujenzi na ukarabati wa majengo na miundombinu ya vyuo

hivyo.

28. Mheshimiwa Spika, wananchi wameendelea kunufaika na mafunzo

yanayotolewa na Vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi vilivyo chini ya Wizara

yangu. Idadi ya wananchi wanaodailiwa katika vyuo hivyo imekuwa

ikiongezeka mwaka hadi mwaka. Mfano, kati ya mwaka 2010/2011 na mwaka

2013/2014 idadi ya wananchi waliodahiliwa kwa mafunzo ya muda mrefu na

muda mfupi iliongezeka kutoka 32,133 hadi kufikia 40,692.

Aidha, baadhi ya wananchi walipata maarifa na ujuzi kupitia mafunzo nje

ya chuo (outreach courses). Mafunzo hayo yanawawezesha washiriki kujiajiri na

kuajiriwa katika taasisi mbalimbali. Napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kuwa

Vyuo hivi kwa miaka ya hivi karibuni vimeanza kupokea vijana wengi

waliohitimu mafunzo ya sekondari sambamba na wale wa elimu ya msingi. Hali

ya Maendeleo ya Jinsia

29. Mheshimiwa Spika, hali ya usawa wa kijinsia katika nyanja mbalimbali

hapa nchni imeendelea kuimarika. Ukweli huu unadhihirishwa na ushahidi wa

kitakwimu na taarifa zilizopo katika maeneo ya ushiriki wa wanawake katika

siasa na ngazi za maamuzi; uwezeshaji wa wanawake kiuchumi; elimu, mafunzo

na ajira; kuongezeka kwa wanawake wajasiriamali (wadogo na wakati) na

upatikanaji wa haki za wanawake kisheria.

Page 22: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

22

30. Mheshimiwa Spika, kwa upande wa ushiriki wa wanawake katika ngazi za

siasa na maamuzi, idadi ya mawaziri wanawake imeongezeka kutoka asilimia

15 mwaka 2005 hadi asilimia 30 mwaka 2013, wakuu wa mikoa wanawake

kutoka asilimia 10 mwaka 2005 hadi asilimia 24 mwaka 2013. Majaji wanawake

pia wameongezeka kutoka asilimia 33 hadi 61 kwa kipindi hicho na uwakilishi

wa wanawake Bungeni umeongezeka kutoka asilimia 30.3 mwaka 2005 na

kufikia asilimia 36 ya wabunge wote mwaka 2013.

31. Mheshimiwa Spika, katika uwezeshaji wanawake kiuchumi taasisi za fedha

na mifuko mbalimbali vimeendelea kutoa mikopo ya fedha na mafunzo ya

ujasiriamali kwa wanawake. Baadhi ya taasisi na mifuko hiyo ni pamoja na

Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake, Benki ya Wanawake Tanzania, Women

Convenant Bank, VICOBA na SACCOS. Mfano, Mfuko wa Maendeleo wa

Wanawake umetoa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 705 kwa kipindi

cha kati ya mwaka 2011/2012 na mwaka 2013/2014.

32. Mheshimiwa Spika, Mila na desturi kandamizi bado ni changamoto katika

kuhakikisha kuwa kunakuwepo na usawa wa kijinsia kwa kuzingatia haki na

usawa wa binadamu. Mila zinazoleta madhara kwa wanawake na hasa

watoto wa kike kama kukeketwa na kuozesha wasichana wa kike katika umri

mdogo zimeendelea na bado ni changamoto katika maeneo kadhaa ya nchi

yetu.

Wizara inachukua hatua mbalimbali kupambana na changamoto hizi

ambazo ni pamoja na kutoa elimu kwa kushirikiana na wadau hasa NGOs na

washirika wa maendeleo na kuiwezesha Kamati ya Kitaifa ya Kutokomeza Ukatili

Dhidi ya Wanawake ili iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, Hali ya Maendeleo ya Watoto. Watoto ni sehemu

muhimu ya jamii na ndiyo tegemeo ya Taifa lolote. Watoto wanahitaji kukua na

kuwa raia wema, hivyo wanatakiwa kupewa haki na mahitaji yao ya msingi

ikiwa ni pamoja na: Kuishi, kupewa malezi stahiki, kulindwa, kuendelezwa kiakili

kwa kutambua na kukuza vipaji vyao, kutobaguliwa na kushirikishwa.

34. Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi ya

Watu na Makazi ya mwaka 2012, idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Bara ni 21,866,258 sawa na asilimia 50.1 ya idadi ya watu wote. Kati yao

wasichana ni 10,943,846 na wavulana ni 10,922,412.

35. Mheshimiwa Spika, Pamoja na Serikali kuweka mazingira wezeshi ya

kuwapatia watoto haki zao kupitia sera,sheria, mipango, programu na mikakati

mbalimbali, bado maendeleo ya mtoto yanakabiliwa na changamoto

mbalimbali. Changamoto hizo ni pamoja na: ukatili dhidi ya watoto, kuwepo

Page 23: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

23

kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi, kushuka kwa maadili, ndoa na

mimba za utotoni.

36. Mheshimiwa Spika, Kumekuwepo na jitihada mbalimbali za kukabiliana

na changamoto hizo ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa Kituo cha Huduma za

Pamoja (One Stop Centre) kwa majaribio katika Hospitali ya Amana - Manispaa

ya Ilala kwa ajili ya kuhudumia watoto mbalimbali wanaofanyiwa aina

mbalimbali za ukatili na kutoa elimu kwa wazazi na walezi juu ya wajibu wao

katika malezi ya watoto.

Aidha, Wizara kwa kushirikiana na wadau imewezesha kuanzishwa kwa

mtandao wa mawasiliano wa kusaidia watoto (Child Helpline) namba 116 kwa

ajili ya jamii inayotumika kutoa taarifa za ukatili dhidi ya watoto na ukiukwaji wa

haki za watoto. Namba hii imeanza kufanya kazi katika maeneo machache

kwa majaribio na utekelezaji wa kazi zake unaonesha mafanikio mazuri hadi

sasa.

Hali ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

37. Mheshimiwa Spika, idadi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali chini ya Sheria ya

NGOs Na. 24 ya mwaka 2002 iliyorekebishwa mwaka 2005 imeendelea kukua

mwaka hadi mwaka. Kufikia tarehe 17 Machi, 2014 idadi ya mashirika hayo

ilifikia 6,427 kutoka mashirika 3,000 yaliyokadiriwa kuwepo mwaka 2001 wakati

Sera ya Taifa ya NGOs ilipokuwa inaandaliwa (Jedwali Na.7). Hili ni ongezeko la

zaidi ya asilimia 100. Kati ya mashirika yaliyosajiliwa, 254 ni ya kimataifa na 6,173

ni ya ndani ya nchi yanayofanya kazi katika ngazi za wilaya, mkoa na taifa.

38. Mheshimiwa Spika, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yameendelea

kutambulika kama wadau na wabia muhimu katika maendeleo. Mashirika haya

yanajishughulisha na kazi mbalimbali ikiwemo elimu, mazingira na mabadiliko ya

tabianchi, afya, maendeleo shirikishi, haki za binadamu, maendeleo ya jinsia,

ushawishi na utetezi, kinga ya jamii, haki za watoto, kilimo, maji na ustawi wa

jamii.

39. Mheshimiwa Spika, kuongezeka kwa idadi na shughuli za NGOs katika

nchi yetu ni matokeo ya mazingira wezeshi yanayoendelea kuboreka mwaka

hadi mwaka. Hii ni pamoja na uwepo wa Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali ya mwaka 2001, Sheria ya NGOs Na.24 ya mwaka 2002 iliyorekebishwa

mwaka 2005 na Kanuni za Maadili za Mashirika Yasiyo ya Kiserikali za mwaka

2008.

Aidha, muundo wa kitaasisi unaowezesha NGOs kujitawala kwa uhuru na

kujiratibu umeendelea kuwepo ikiwemo: Bodi ya Uratibu wa NGOs, Baraza la

Taifa la NGOs, Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Wilaya na mikoa ambao ni

Wasajili Wasaidizi na mitandao ya NGOs ya wilaya, mkoa na taifa.

Page 24: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

24

40. Mheshimiwa Spika, pamoja na kuimarika kwa hali ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali hapa nchini, bado kuna changamoto zinazohitaji kufanyiwa kazi.

Changamoto zilizopo ni pamoja na sehemu kubwa ya shughuli za Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali kutegemea wafadhili kutoka nje na kutokuwa na vyanzo vya

uhakika vya ndani ya nchi hivyo kuathiri uendelevu wa shughuli hizo pindi

wafadhili hao wanapositisha misaada. Changamoto nyingine ni kutokuwepo

kwa Kamati za Maadili ya NGOs katika baadhi ya mikoa na wilaya kunakoathiri

uwezo wa NGOs kujitawala katika kuongeza uwazi na uwajibikaji katika

matumizi ya rasilimali na uendeshaji wa mashirika hayo.

41. Mheshimiwa Spika, katika kutatua changamoto hizo wizara yangu

imechukua hatua mbalimbali. Mojawapo ya hatua hizo ni kuhimiza Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali kutumia fursa ya marekebisho ya Sheria ya NGOs

yaliyofanyika mwaka 2005 kuanzisha na kuendeleza miradi ya kuzalisha faida

kwa ajili ya kutekeleza malengo yao hata pale wafadhili wanapositisha

misaada.

Aidha, Wizara kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la NGOs inaendelea

kutafuta fedha kwa ajili ya kuliwezesha kuanzisha Kamati za Maadili ya NGOs

katika ngazi ya wilaya na mikoa ikiwa ni utekelezaji wa Kanuni za Maadili ya

NGOs. Mafanikio.

42. Mheshimiwa Spika, mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa bajeti

ya mwaka 2013/2014, ni pamoja na:-

(i) Idadi ya vituo vya kutolea mikopo kwa wajasiriamali wadogo hususan

wanawake imeongezeka toka vituo 21 mwaka 2012/13 hadi vituo 50 mwaka

2013/14, sawa na ongezeko la asilimia 58;

(ii) Matawi ya Benki ya Wanawake Tanzania yameongezeka toka tawi

moja mwaka 2009/10 hadi matawi mawili mwaka 2013/14;

(iii) Kuongezeka kwa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yaliyosajiliwa toka mashirika

3,000 mwaka 2001/02 hadi mashirika 6,427 mwaka 2013/2014;

(iv) Wanafunzi waliojiunga na mafunzo ya ufundi stadi katika Vyuo 25 vya

Maendeleo ya Wananchi wameongezeka toka wanafunzi 1,125 mwaka 2013

hadi wanafunzi 2,722 mwaka 2014;

(v) Wanafunzi waliojiunga na mafunzo ya elimu ya wananchi (Kozi ndefu)

katika Vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi wameongezeka toka wanafunzi

6,586 mwaka 2013 hadi wanafunzi 7,144 mwaka 2014;

Page 25: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

25

(vi) Kuongezeka kwa Halmashauri zilizopata mikopo kupitia Mfuko wa

Maendeleo wa Wanawake toka Halmashauri 19 mwaka 2008/09 hadi

Halmashauri 38 mwaka 2013/2014; na

(vii) Kuongezeka kwa Madawati ya Jinsia na Watoto toka madawati 9 mwaka

2008 hadi madawati 417 mwaka 2014. Changamoto.

43. Mheshimiwa Spika, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, Sekta ya

Maendeleo ya Jamii inakabiliwa na changamoto zifuatazo:-

(i) Uhaba wa wakufunzi wa kada mbalimbali katika Vyuo vya Maendeleo

ya Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi;

(ii) Ukosefu wa vyombo vya usafiri katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi,

Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na uchakavu wa vyombo vya usafiri Makao

Makuu ya Wizara;

(iii) Upungufu wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia katika Vyuo tisa vya

Maendeleo ya Jamii na Vyuo 55 vya Maendeleo ya Wananchi;

(iv) Uchakavu wa majengo na miundombinu katika Vyuo vya Maendeleo ya

Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi;

(v) Kuendelea kukua kwa madeni ya watumishi, wakandarasi na watoa

huduma mbalimbali Wizarani. Madeni yamefikia shilingi 2,558,735,065 katika

deni hilo shilingi 774,308,379.84 ni madeni ya watumishi, shilingi 773,166,431.80 ni

madeni ya wazabuni na shilingi 1,011,260,253.36 ni madeni ya wakandarasi;

(vi) Fedha kutolewa na Wizara ya Fedha bila kuzingatia Mpango Kazi na

Mtiririko wa Mahitaji ya Fedha;

(vii) Mahitaji ya mikopo ya Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake ni mengi

ikilinganishwa na fedha zinazotolewa.

Aidha, mikopo inayotolewa kwa vikundi kuwa kidogo isiyokidhi mahitaji

halisi ya biashara na mafunzo ya ujasiriamali yanayotolewa kwa wakopaji

kutotosheleza kuwajengea uwezo unaohitajika;

(viii) Kupanua huduma za Benki ya Wanawake Tanzania ili kuwafikia

wanawake wengi zaidi; na

Page 26: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

26

(ix) Kutokuwepo kwa uwazi na uwajibikaji kwa baadhi ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali.

(x) Kuongezeka kwa matukio ya ukatili wa kijinsia katika jamii.

D: MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MWAKA 2013/14 NA MALENGO

YA MWAKA 2014/2015

44. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Wizara yangu iliendelea

kusimamia utekelezaji wa majukumu yake kulingana na malengo

yaliyopangwa. Katika bajeti ya mwaka 2013/2014, Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto iliidhinishiwa jumla ya shilingi 25,964,170,000 kwa ajili ya

matumizi ya Kawaida na Maendeleo. Kati ya fedha za matumizi ya kawaida,

shilingi 5,397,496,000 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo na shilingi 8,656,002,000

kwa ajili ya malipo ya mishahara na shilingi 11,910,672,000/= ni kwa ajili ya

matumizi ya maendeleo.

45. Mheshimiwa Spika, hadi kufikia tarehe 15 Mei, 2014, Wizara ilikuwa

imetumia jumla ya shilingi 10,305,162,100 sawa na asilimia 100 ya fedha za

Matumizi ya Kawaida zilizopokelewa na shilingi 2,923,620,590 sawa na asilimia

100 ya fedha za Maendeleo zilizotolewa.

46. Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha utekelezaji wa mpango wa

mwaka 2013/14 na malengo ya mwaka 2014/15 kwa kuzingatia maeneo

yafuatayo:-

Maendeleo ya Jamii.

47. Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2013/2014 Wizara yangu ilidahili na

kutoa mafunzo kwa wanachuo 2,869 kupitia vyuo tisa vya Maendeleo ya Jamii

vya Tengeru, Buhare, Rungemba, Monduli, Missungwi, Ruaha, Uyole, Mlale na

Mabughai. Wanachuo 2,036 walidailiwa katika ngazi ya cheti, 591 katika ngazi

ya stashahada, 234 ngazi ya shahada na 8 katika ngazi ya Stashahada ya

Uzamili. Aidha, Wizara yangu ilikarabati majengo na miundombinu katika Chuo

cha Maendeleo ya Jamii Mlale, Misungwi na Mabughai.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea kukamilisha jengo la

maktaba ya Chuo cha Tengeru na maabara ya kompyuta katika chuo cha

Mabughai kwa lengo la kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

48. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2013/14 Wizara yangu ililipa shilingi

84,114,523 zikiwa ni gharama za ujenzi zilizoongezeka katika ujenzi wa bwalo,

jiko na nyumba za watumishi katika vyuo vya Maendeleo ya Wananchi vya

Mputa na Muhukuru mkoani Ruvuma.

Page 27: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

27

Aidha, Wizara ilifanya ukarabati wa mabweni na jengo la utawala katika chuo

cha Maendeleo ya Wananchi Tarime; ukarabati wa nyumba za watumishi na

uwekaji wa mfumo wa umeme katika chuo cha Maendeleo ya Wananchi

Mwanhala; ukarabati wa jengo la utawala na bweni katika chuo cha

Maendeleo ya Wananchi Kilwa Masoko; ukarabati wa mabweni na nyumba za

watumishi katika chuo cha Maendeleo ya Wananchi Msaginya, Mputa, Sofi na

Singida; ujenzi wa vyoo katika chuo cha Maendeleo ya Wananchi Masasi na

Chilala; na kuvipatia vyuo vya Maendeleo ya Wananchi 25 vifaa vya kujifunzia

na kufundishia masomo ya ufundi stadi.

49. Katika mwaka 2014/2015 Wizara yangu itaendelea kudahili na kutoa

mafunzo kwa wananchi na pia itakarabati majengo na miundombinu ya vyuo

vya Maendeleo ya Wananchi vya Mto wa Mbu, Msaginya na Nandembo.

50. Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuboresha mafunzo ya

maendeleo ya wananchi kwa kutoa huduma kwa watoto kupitia vituo vya

kulelea watoto ndani ya vyuo vya Maendeleo ya Wananchi 55 ambapo jumla

ya watoto 1,033 walinufaika. Kuwepo kwa vituo hivi katika vyuo vya Maendeleo

ya Wananchi kumewawezesha watumishi katika vyuo hivi na jamii

inayovizunguka vyuo hususan wanawake kushiriki kikamilifu katika shughuli za

uzalishaji mali kwa uhuru zaidi. Aidha, vituo hivi vimewawezesha washiriki

wanawake 97 wenye watoto wadogo kupata mafunzo wakiwa na watoto wao

vyuoni.

51. Mheshimiwa Spika, kwa kipindi cha mwaka 2014/15, Wizara itaendelea

kuimarisha vituo vya kulelea watoto katika vyuo 55 vya maendeleo ya

wananchi kwa kutoa vifaa vya kufundishia na kujifunzia na kutengeneza

viwanja vya michezo. Aidha, Wizara itawajengea uwezo wakufunzi 30 kwa ajili

ya kuwawezesha kupata elimu ya kuendesha vituo vya kulelea watoto wadogo

ikiwa ni pamoja na kuwapatia ujuzi wa kufundisha watoto hao elimu ya awali.

Mafunzo ya kuwajengea uwezo wakufunzi katika Vyuo vya Maendeleo ya

Wananchi yatakuwa yanatolewa kwa awamu kulingana na Programu ya

Maendeleo ya Sekta ya Elimu. Maendeleo ya Jinsia.

52. Mheshimiwa Spika, uwezeshaji wanawake kiuchumi ni suala muhimu

katika kufikia usawa wa kijinsia na kupunguza umaskini wa kipato katika jamii.

Katika mwaka 2013/2014, Wizara kupitia Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake

iliziwezesha Halmashauri 39 kutoa mikopo yenye thamani ya shillingi milioni 428.

Katika kuhakikisha Mfuko unafikia malengo yaliyopangwa, Wizara ilifuatilia

utendaji wa Mfuko katika mikoa tisa na kuiwezesha Kamati ya Kudumu ya

Bunge ya Maendeleo ya Jamii kufuatilia utekelezaji wa Mfuko katika

Halmashauri mbalimbali.

Page 28: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

28

Halmashauri ambazo Kamati ya Bunge ilifanya ufuatiliaji huo ni Kinondoni,

Ilala, Kibaha, Korogwe na Jiji la Tanga. Mikoa ambayo Wizara ilifuatilia shughuli

za Mfuko ni Arusha, Manyara, Singida, Pwani, Tanga, Katavi, Rukwa, Morogoro

na Kagera. Matokeo ya ufuatiliaji yanaonesha kwamba Halmashauri nyingi

hazichangii asilimia tano ya mapato yao kama inavyotakiwa. Kutokana na

matokeo hayo, Halmashauri ziliagizwa kuchangia katika Mfuko huo.

53. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea

kutoa fedha kwa Halmashauri nyingine zitakazokuwa zimemaliza marejesho

pamoja na kufanya ufuatiliaji kwa mikoa na halmashauri zilizobaki. Napenda

kutumia fursa hii kuzikumbusha halmashauri zote zilizokopeshwa kuzingatia

mkataba wa marejesho.

Aidha, nazikumbusha halmashauri zote nchini kuchangia asilimia tano ya

mapato yao kwenye Mfuko wa Maendeleo wa wanawake ili wanawake wengi

zaidi wanufaike na huduma za Mfuko huu.

54. Mheshimiwa Spika, kupitia Benki ya Wanawake Tanzania huduma za

kibenki zimewafikia wananchi wengi zaidi wakiwepo wanawake kwani imeweza

kufungua tawi la pili la Benki ya Wanawake Tanzania eneo la Kariakoo Mkoa

wa Dar es Salaam, Mtaa wa Agrey/Likoma.

Aidha, vituo 29 vya kutolea mikopo na mafunzo kwa wajasiriamali

vimefunguliwa katika Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza. Vituo

hivyo ni kama ifuatavyo: Dar es Salaam (Tabata Kisukuru, Mbande, Sabasaba,

Ubungo Kibangu, Chanika, Chamazi na Kunduchi Mtongani); Dodoma (Airport,

Chamwino, Ipagala, Posta, Hazina Kikuyu, Kizota, Savanna Kikuyu,

Chang‟ombe, Mnadani, Veyula, Mpwapwa, Kongwa na Mbande); na Mwanza

(Nyakato, Igogo, Nyegezi, Pansiansi, Igoma, Kisesa, Magu, Misungwi na

Kitangiri). Kwa mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea kutoa ruzuku kwa

Benki ya Wanawake Tanzania ili iweze kuwafikia wananchi wengi zaidi.

55. Mheshimiwa Spika, Ukatili wa kijinsia umeendelea kuwa ni tatizo katika

jamii zetu ambapo wananchi wengi wameendelea kuumizwa na kuteseka na

hata kuuawa kutokana na vitendo vya kikatili vinavyofanyika hapa nchini.

Mwaka 2013/2014, Wizara ilifanya tathmini ya mafunzo yaliyotolewa kwa

Kamati za Ulinzi na usalama katika Mkoa wa Manyara kuhusiana na kupiga vita

ukatili wa kijinsia. Moja ya matokeo ya tathmini hiyo imeonyesha kuwa Kamati

husika zinahitaji kujengewa uwezo zaidi ili ziweze kufanya kazi zake kikamilifu.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kufanya tathmini ya mafunzo

Page 29: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

29

yaliyotolewa kwa Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya kuhusu mbinu za

kutokomeza ukatili katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Mara.

Aidha, itaendelea kuzijengea uwezo kamati za ulinzi na usalama ili ziweze

kupambana na kutokomeza ukatili katika ngazi ya wilaya na kuendelea

kuiwezesha Kamati ya Kitaifa ya Kuzuia na Kuondoa Ukatili Dhidi ya Wanawake

na Watoto ili iweze kutekeleza shughuli zake kikamilifu.

56. Mheshimiwa Spika, suala la uingizaji wa masuala ya kijinsia katika sera,

mipango na bajeti limekuwa likitiliwa mkazo ili kuhakikisha kuwa mipango na

bajeti za kila sekta, idara na taasisi mbalimbali inawanufaisha wote, yaani

wanawake, wanaume, wavulana na wasichana.

Katika kipindi cha mwaka 2013/2014, Wizara kupitia wataalamu wake

ilifanya tathmini ya uingizaji wa masuala ya jinsia katika Halmashauri 6 ambazo

ni Halmashauri ya Jiji la Tanga na Arusha, Halmashauri za Wilaya ya Iringa na

Moshi pamoja na Manispaa ya Temeke na Morogoro.

Lengo la tathmini ilikuwa ni kubaini mafanikio na changamoto zinazojitokeza

katika uingizaji wa masuala ya jinsia katika sera na mipango na bajeti

mbalimbali. Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kutoa mafunzo ya

uingizaji wa masuala ya jinsia kwa wataalamu mbalimbali ili waweze kuelewa

na kutekeleza mkakati huu ikiwa ni pamoja na kukamilisha Sera ya Taifa ya

Jinsia.

Aidha, Wizara imeanza mchakato wa kuandaa taarifa ya hali ya jinsia

nchini (Tanzania Country Gender Profile) na kuanzisha benki ya Takwimu ya

usawa wa jinsia. Taarifa hii na Benki ya Takwimu zitawezesha kufanya maamuzi,

upangaji wa mipango, ushawishi na uhamasishaji kuhusu masuala ya jinsia ili

kuwa na maendeleo endelevu. Aidha, zitasaidia kupima utekelezaji wa

mipango na programu mbalimbali kuona kama zinaweza kupunguza

changamoto za kijinsia na kuleta usawa unaotarajiwa.

57. Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014, Wizara iliandaa rasimu ya 7 na 8 ya

nchi ya Mkataba wa Kuondoa Aina zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake.

Maandalizi ya taarifa hiyo yaliwashirikisha wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na

Watendaji wa Madawati ya Jinsia kutoka Wizara mbalimbali, asasi za kijamii na

Maafisa wa Maendeleo Jamii. Rasimu ya Taarifa hiyo imekamilika na inatarajiwa

kujadiliwa na wadau mbalimbali wakiwemo Kamati ya Bunge ya Sekta ya

Maendeleo ya Jamii kwa lengo la kupata maoni zaidi kwa ajili ya kuiboresha.

58. Mheshimiwa Spika, tarehe 8 Machi kila mwaka, Wizara imekuwa

ikishirikiana na wadau mbalimbali kuratibu maadhimisho ya Siku ya Wanawake

Duniani. Kwa mwaka 2013/2014, maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani

yalifanyika kimkoa ambapo lengo kuu lilikuwa ni kuwakutanisha wanawake wa

Page 30: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

30

ngazi zote ili waweze kubadilishana uzoefu wa masuala mbalimbali

yanayowakabili, kubaini fursa zilizopo katika kujiletea maendeleo na kutafuta

ufumbuzi wa changamoto mbalimbali zinazowakabili. Katika mwaka

2013/2014, Wizara yangu iliratibu maadhimisho ya siku hiyo katika ngazi ya

mikoa ambapo Kauli mbiu ilikuwa ni “Chochea Mabadiliko Kuleta Usawa wa

Kijinsia” Kauli mbiu hii inasisitiza na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa

kuzingatia masuala ya jinsia katika kupanga na kutekeleza mikakati na

mipango ya maendeleo kwa kuzingatia ushiriki stahiki wa wanawake,

wanaume, wavulana na wasichana katika kujiletea maendeleo yao na taifa

kwa ujumla. Kwa mwaka 2014/2015, Wizara itaratibu maadhimisho haya Kitaifa

ili kuweza kupima mafanikio yaliyopatikana katika miaka mitano (2010 – 2015)

katika juhudi za kumwendeleza mwanamke pamoja na kubainisha

changamoto zilizojitokeza kwa kipindi hicho toka maadhimisho haya

yalipofanyika kitaifa mwaka 2010.

59. Mheshimiwa Spika, ili kutekeleza mikataba na maazimio mbalimbali

ambayo nchi imesaini na kuridhia, mwaka 2013/2014, Wizara ilishiriki katika

mkutano wa 58 wa Kamisheni ya Hali ya Wanawake na mkutano wa nchi za

Maziwa Makuu kuhusu masuala ya jinsia. Lengo la mikutano hiyo ni kutafuta

mbinu za pamoja za kukabiliana na changamoto mbalimbali, kubadilishana

uzoefu na kukubaliana maeneo muhimu ya utekelezaji katika kuleta usawa wa

kijinsia na maendeleo ya wanawake katika nchi husika. Katika mwaka

2014/2015, Wizara itaendelea kushiriki na kutoa mchango wake katika mikutano

ya kikanda na kimataifa kuhusu utekelezaji wa masuala ya usawa wa kijinsia na

kuwaendeleza wanawake. Maendeleo ya Watoto.

60. Mheshimiwa Spika, maendeleo ya taifa lolote duniani hutegemea sana

namna ambavyo linawalinda na kuwakuza watoto wake. Kwa kuzingatia hilo,

Wizara yangu imekuwa ikichukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na

changamoto zinazowakabili watoto hapa nchini.

61. Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014, Wizara yangu iliandaa mpango

kazi wa jamii wa kudhibiti tatizo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Lengo likiwa ni kuongeza ushiriki wa wadau katika kudhibiti na kuondoa tatizo

hilo kwa kuwaelimisha na kuhamasisha ili wabebe jukumu la kuwapatia watoto

mahitaji na haki zao za msingi. Utekelezaji wa Mpango kazi unahusisha familia,

jamii, serikali, asasi za kiraia, vyombo vya habari na wabia wa maendeleo.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itasambaza mpango katika mikoa yote na

kuratibu utekelezaji wake.

62. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Wizara yangu imefanya

marekebisho ya Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 kuwa Sera ya

Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2014 ili iweze kujumuisha

masuala ya utoaji huduma fungamanishi na shirikishi za Malezi, Makuzi na

Page 31: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

31

Maendeleo ya Mtoto. Aidha, Sera hiyo imezingatia masuala ya kukabiliana na

changamoto zinazotokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia pamoja na

upatikanaji wa huduma za malezi na makuzi kwa watoto walio chini ya umri wa

miaka nane. Katika mwaka 2014/2015, Wizara itakamilisha Sera hiyo na mkakati

wake wa utekelezaji. Aidha, Wizara itasambaza kwa wadau sera na mkakati

huo kwa ajili ya utekelezaji.

63. Mheshimiwa Spika, ukatili dhidi ya watoto ni moja ya changamoto

zinazoathiri malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto. Katika kupunguza matukio

ya ukatili huo, mwaka 2013/2014 Wizara yangu kwa kushirikiana na wadau

mbalimbali iliandaa Mpango Kazi Shirikishi wa Kuzuia Ukatili dhidi ya Watoto wa

mwaka 2013 hadi 2016.

Aidha, Wizara yangu iliwezesha kufanyika kwa mkutano wa mwaka wa

Kikosi Kazi cha Taifa cha Kuzuia Ukatili dhidi ya Mtoto ambapo sekta zote

zinazohusiana na maendeleo ya mtoto zilitoa taarifa kuhusu mapendekezo ya

namna ya kutekeleza mpango huo.

Pia, Wizara iliandaa mkutano uliowakutanisha watekelezaji wa

Mpangokazi wa miaka mitatu wa kuzuia ukatili wa watoto na wadau wa

maendeleo na tayari wadau kadhaa wa maendeleo wajitokeza na kuanza

kuchangia fedha za utekelezaji wa baadhi ya kazi zilizoainishwa katika mpango

huu. Tunawashukuru sana wadau hawa. Katika mwaka 2014/2015, Wizara

itaendelea kuratibu na kusimamia mpango huo kwa kushirikiana na kikosi kazi

hicho.

64. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu pia iliandaa kitini cha elimu ya malezi

kwa familia kuhusu kukabiliana na ukatili dhidi ya watoto. Kitini hicho kitatumiwa

na wawezeshaji jamii katika kuwajengea uwezo wazazi na walezi ili kudhibiti

ukatili dhidi ya watoto. Aidha, kuanzia ngazi ngazi ya familia Wizara ilitoa

mafunzo kuhusu Kitini hicho kwa Maafisa Maendeleo ya Jamii kutoka

halmashauri za Hai, Temeke, Magu na Kasulu. Katika mwaka 2014/2015, Wizara

itaendelea kuratibu usambazaji wa kitini hicho katika halmashauri nyingine.

65. Mheshimiwa Spika, vilevile, Wizara iliendelea kuratibu utoaji wa taarifa za

ukatili dhidi ya watoto kupitia namba ya simu 116 inayosimamiwa na Shirika Lisilo

la Kiserikali la C-SEMA. Hadi kufikia Machi, 2014 jumla ya simu 6,188 zilipigwa

kupitia namba hiyo na kufanyiwa kazi. Mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea

kuratibu na kusimamia mtandao huo na kuendelea kutathmini ili kuwezesha

kupeleka huduma hii katika maeneo mengine ya nchi.

66. Mheshimiwa Spika, Watoto wanayo haki ya msingi ya kushiriki na

kushirikishwa katika masuala yote yanayowahusu. Katika kuhakikisha ushiriki wa

watoto katika kutoa maoni yao, mwaka 2013/2014, wizara iliandaa Mkutano

Page 32: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

32

Mkuu wa Baraza la Watoto ili kupitia rasimu ya kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania.

Aidha, wizara yangu iliratibu utekelezaji wa shughuli za mabaraza ya

watoto katika ngazi ya Wilaya/Mikoa pamoja na Azimio la Bunjumbura kuhusu

haki na ustawi wa watoto. Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea

kushirikiana na Halmashauri kuimarisha Baraza la Watoto la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania pamoja na mabaraza ya watoto ya mikoa na wilaya ili

yaweze kutoa fursa nzuri za ushiriki wa watoto katika maeneo husika.

67. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2013/2014, Wizara yangu iliratibu

maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika ambayo yaliadhimishwa katika ngazi

ya mkoa. Katika maadhimisho hayo, kila mkoa ulipata fursa ya kuadhimisha siku

hii muhimu kulingana na mazingira na uhitaji wa mkoa husika. Kauli mbiu ya

mwaka 2013/2014 ilikuwa ni “Kuondoa Mila zenye kuleta Madhara kwa Watoto:

ni Jukumu Letu Sote”. Lengo la kaulimbiu hiyo ni kuhamasisha jamii kubaini

baadhi ya mila ambazo zimekuwa zikileta madhara kwa watoto na kuweka

mikakati ya kuzitokomeza.

68. Mheshimiwa Spika, Vile vile, Wizara yangu iliratibu maadhimisho ya siku ya

Familia Duniani ambayo yalifanyika kimkoa. Kauli mbiu ya maadhimisho haya

ilikuwa ni “Imarisha na Endeleza Ushirikiano na Mshikamano wa Familia na

Makundi Mbalimbali ya Jamii”. Kauli mbiu hii inasisitiza wazazi, walezi na jamii

kuwajibika kwa pamoja katika malezi ya familia. Katika mwaka 2014/2015,

Wizara itaendelea kuratibu maadhimisho ya siku hizo kwa lengo la kuhamasisha

jamii kuhusu haki na ustawi wa mtoto na maendeleo ya familia.

Uratibu wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.

69. Mheshimiwa Spika, Katika kipindi cha mwaka 2013/2014, Serikali iliendelea

kusajili Mashirika Yasiyo ya Kiserikali chini ya Sheria ya NGOs Na.24 ya mwaka

2002. Jumla ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali 435 yalipatiwa usajili katika ngazi ya

wilaya, mkoa, taifa na kimataifa. Kati ya hayo, mashirika ya kimataifa ni 23 na

mashirika ya ndani ya nchi yaani ya ngazi za wilaya, mkoa na taifa ni 412. Hii

imefanya idadi ya NGOs kuongezeka kutoka mashirika 5,992 mwezi Julai, 2013

na kufikia mashirika 6,427 mwezi Machi, 2014 ikiwa ni ongezeko la asilimia 7.

Aidha, katika kipindi cha mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea na

usajili wa mashirika hayo.

70. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu pia iliratibu shughuli za NGOs kwa

kuwezesha ushiriki wa wadau katika utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Mashirika

Yasiyo ya Kiserikali. Hii ni pamoja na kuiwezesha Bodi ya uratibu wa NGOs

kukagua shughuli za NGOs 21 na kufanya vikao vitatu katika mikoa ya Tanga,

Page 33: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

33

Lindi na Mbeya. Vikao hivyo vilifikia maamuzi mbalimbali ikiwemo utatuzi wa

migogoro katika Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. Aidha, Wizara kupitia Bodi ya

Uratibu wa NGOs ilikutana na wadau 175 na kujadili mafanikio na changamoto

zinazozikabili NGOs katika mikoa husika na kutoa elimu kuhusa Sera ya Taifa ya

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2001 na Sheria ya NGOs Na. 24 ya

mwaka 2002. Wizara pia imeanzisha utaratibu wa kukutana na NGOs

zinazofanyakazi za watoto na wanawake na mapendekezo ya kuboresha

ushirikiano yameandaliwa. Kwa mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea

kuiwezesha Bodi ya Uratibu wa NGOs kufanya vikao vinne na kukutana na

wadau ili kuboresha uratibu wa NGOs nchini na pia itaendelea na utaratibu wa

kukutana na NGOs zinazofanyakazi na watoto na wanawake ili kuboresha

ushirikiano na utekelezaji wa majukumu haya.

71. Mheshimiwa Spika, katika kuendelea kujenga mazingira wezeshi na

kuboresha uratibu wa mashirika haya, Wizara yangu itatekeleza mambo

mbalimbali katika kipindi cha mwaka 2014/2015. Kazi hizo ni pamoja na

kufuatilia na kutathmini mchango wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na hali ya

uendeshaji wa mashirika hayo hapa nchini.

Aidha, itawezesha kufanyika kwa tathmini kuhusu ufanisi wa Sera ya Taifa

ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kujenga mazingira wezeshi kwa NGOs.

Vilevile, Serikali kupitia Wizara yangu itawezesha kufanyika kwa mafunzo ya

ndani kuhusu usajili, ufuatiliaji na tathmini ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa

Maafisa Maendeleo ya Jamii wa wilaya na mikoa kwa lengo la kuwajengea

uwezo wa kiutendaji ili kuboresha utoaji wa huduma za usajili na uratibu katika

ngazi husika. Uratibu wa Sera na Mipango

72. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 uratibu na mapitio ya Sera

ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 pamoja na mkakati wake ulifanyika.

Katika mwaka 2014/2015, uratibu wa mapitio ya Sera ya Mashirika Yasiyo ya

Kiserikali ya mwaka 2001 na tathmini ya utekelezaji wa Sera ya Wanawake na

Jinsia ya mwaka 2000 na Sera ya Taifa ya Mashirika Yasiyo Ya Kiserikali ya

mwaka 2001utafanyika.

Aidha, uratibu wa mipango na bajeti ya mwaka 2015/16 pamoja na

uandaaji wa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini wa Wizara utaandaliwa ili

kuimarisha ukusanyaji, uhifadhi na usimamizi wa takwimu na taarifa za sekta ya

maendeleo ya jamii. Watumishi 20 wa Wizara watajengewa uwezo wa

ukusanyaji takwimu, ufuatiliaji na tathmini. Utawala na Usimamizi wa Rasilimali

Watu

73. Mheshimiwa Spika, watumishi ni rasimali muhimu yenye kutekeleza

majukumu ya kila siku ya Wizara. Kutokana na umuhimu wake inahitaji

kusimamiwa vizuri, kujengewa uwezo wa kiutendaji na mazingira mazuri ya kazi

Page 34: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

34

ili kuongeza ufanisi na tija. Katika mwaka 2013/2014, Wizara iliwezesha watumishi

62 kupata mafunzo ya muda mrefu na mfupi, ndani na nje ya nchi ili

kuwaongezea ujuzi na utaalamu katika utekelezaji wa majukumu yao. Katika

mwaka 2014/2015, Wizara yangu itaendelea kuwawezesha watumishi 84 kupata

mafunzo mbalimbali ya muda mfupi na mrefu ndani ya nchi.

74. Mheshimiwa Spika, katika kuwapatia motisha wafanyakazi, Wizara yangu

kwa mwaka 2013/2014, ilipandisha vyeo watumishi 126 na kuwabadilisha kada

watumishi wanne. Aidha, watumishi 86 walithibitishwa kazini. Kwa kipindi cha

mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kuwapandisha vyeo watumishi wake kwa

mujibu wa Miundo ya Utumishi wa Kada zao na Sera ya Menejimenti na Ajira

katika Utumishi wa Umma ili kuongeza tija katika utendaji kazi.

75. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu imekuwa ikikabiliwa na upungufu

mkubwa wa watumishi hasa katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Vyuo vya

Maendeleo ya Wananchi. Katika kukabiliana na changamoto hii mwaka

2013/2014, Wizara yangu iliajiri jumla ya watumishi 92 kutokana na kibali cha

ajira kilichotolewa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma chenye

Kumbukumbu Namba BC.62/97/014/2011 cha tarehe 4 Juni, 2012. Kwa mwaka

2013/14 Wizara iliwasilisha maombi ya kibali cha ajira ya watumishi 603. Katika

mwaka 2014/2015, Wizara inatarajia kuendelea kuajiri watumishi wengine ili

kuendelea kupunguza pengo lililopo.

76. Mheshimiwa Spika, katika kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa

watumishi, mwaka 2013/2014, Wizara iliwapatia watumishi vitendea kazi

mbalimbali. Kwa mwaka 2014/2015, Wizara yangu itajenga eneo la kuegesha

magari la Makao Makuu ya Wizara, kununua jenereta na kuendelea kuwapatia

wafanyakazi vitendea kazi mbalimbali. Aidha, Wizara itawawezesha watumishi

kushiriki katika mashindano ya SHIMIWI ili kuboresha afya na kuimarisha

mahusiano miongoni mwa watumishi wa Serikali.

77. Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Wizara yangu iliendelea

kuwezesha sekta binafsi za ulinzi na usafi kutoa huduma hizo kwa Wizara kwa

lengo la kuboresha mazingira ya utendaji kazi na usalama wa vifaa na mali.

Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kuwezesha sekta binafsi kutoa

huduma hizo.

78. Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iliendeleza mapambano dhidi ya

UKIMWI na Virusi Vya UKIMWI mahala pa kazi. Katika mwaka 2013/2014, Wizara

iliwapatia watumishi nasaha za namna ya kujikinga na maambukizi ya Virusi Vya

UKIMWI. Katika mwaka 2014/2015, Wizara itaendelea kuhamasisha watumishi

wajitokeze kupima afya zao pamoja na kuwapatia huduma ya viini lishe na

chakula. Mawasiliano kwa umma.

Page 35: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

35

79. Mheshimiwa Spika, mawasiliano ni nguzo muhimu katika kuwawezesha

wananchi kufahamu huduma zinazotolewa na Wizara na pia kuiwezesha

kupata mrejesho kutoka kwa wadau ili kuboresha huduma hizo. Kwa mwaka

2013/2014, Wizara yangu iliandaa vipindi vya luninga, radio na mikutano na

waandishi wa habari kwa ajili ya kuelimisha umma kuhusu masuala ya

maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake, familia, haki za watoto na uratibu wa

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali. Aidha, Wizara iliandaa matangazo mbalimbali

kupitia magazeti, vipeperushi na mabango.

80. Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2013/2014, Wizara pia ilianzisha

mawasiliano na umma kupitia mitandao ya kijamii. Mitandao hiyo ni pamoja

na:

Blog ya wizara, www.maendeleoyajamiijinsianawatoto.blogspot.com;

Facebook ya wizara, facebook.com/maendeleoyajamii; na twitter ya wizara,

Twitter.com/wmjjwtz.

Kwa mwaka 2014/2015, Wizara itaandaa mkakati wa mawasiliano na

kuendelea kuwezesha mawasiliano kwa umma kupitia njia mbalimbali ikiwemo

mitandao ya kijamii, radio, luninga, magazeti, gari la sinema, majarida,

vipeperushi na uhamasishaji jamii kwa kushirikiana na Maafisa Maendeleo ya

Jamii katika ngazi ya kata, wilaya na mkoa.

E: HITIMISHO

81. Mheshimiwa Spika, mapitio ya utekelezaji wa Mpango wa Wizara wa

mwaka 2013/2014 na Malengo ya mwaka 2014/2015 yanaonesha jinsi Wizara

yangu ilivyo na umuhimu katika kuleta usawa wa jinsia, upatikanaji wa haki na

ustawi wa watoto, ongezeko la ajira kwa vijana na ushawishi wa jamii katika

kupokea na kutekeleza miradi ya maendeleo endelevu. Ili Wizara itekeleze

vema majukumu yake inahitaji ushirikiano mkubwa wa wadau mbalimbali na

rasilimali fedha za kutosha.

F: SHUKRANI

82. Mheshimiwa Spika, napenda sasa kumshukuru sana Naibu Waziri,

Mheshimiwa Dk. Pindi Hazara Chana (Mb.), kwa ushirikiano, ushauri na usaidizi

mkubwa anaonipa katika kuongoza Wizara hii. Vilevile, napenda kutoa shukrani

za dhati kwa: Katibu Mkuu, Bibi Anna Tayari Maembe, Naibu Katibu Mkuu, Bibi

Nuru H. M. Millao; Wakurugenzi; Wakuu wa Vitengo; Mkurugenzi Mtendaji wa

Benki ya Wanawake Tanzania - Bibi Magreth Chacha; Wakuu wa Vyuo; na

Wafanyakazi wote wa Wizara yangu wa ngazi zote, kwa jitihada zao katika

utekelezaji wa majukumu ya Wizara, ambayo ni pamoja na kuniwezesha mimi

kuwasilisha hotuba hii mbele ya Bunge lako Tukufu.

Page 36: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

36

83. Mheshimiwa Spika, kabla sijamaliza hotuba yangu, sina budi kuwashukuru

wadau wote tunaofanya nao kazi na wengine ambao kwa namna moja au

nyingine tunashirikiana. Peke yetu kama Wizara tusingefikia mafanikio

niliyoyataja. Naomba kupitia Bunge lako tukufu, kutoa shukrani zangu za dhati

kwa wafuatao: Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Asasi ya Wanawake na

Maendeleo (WAMA); Mfuko wa Fursa Sawa kwa Wote (EOTF); Mtandao wa

Jinsia Tanzania (TGNP); Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA);

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA); Shirikisho la

Vyama vya Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (FAWETA); Medical Women

Association of Tanzania (MEWATA); White Ribon; Plan International; Save the

Children; Mashirika mbalimbali yasiyo ya Kiserikali pamoja na wale wanaofanya

kazi kwa maslahi ya jamii kwa namna moja au nyingine.

Napenda pia kuyashukuru Mashirika kutoka nchi rafiki ambayo yameendelea

kutusaidia na kufanya kazi na sisi. Mashirika hayo ni pamoja na: DFID; GPE;

CIDA; KOICA na UK Education.

Aidha, nayashukuru Mashirika ya Umoja wa Mataifa ambayo ni: UNICEF;

UNDP; UNFPA na UN WOMEN kwa misaada yao mbalimbali iliyofanikisha

utekelezaji wa majukumu mengi ya Wizara yangu.

G. MAKADIRIO YA BAJETI YA WIZARA MWAKA 2014/2015.

84. Mheshimiwa Spika, ili Wizara yangu iweze kutekeleza majukumu na

malengo yake kwa mwaka 2014/15, sasa naliomba Bunge lako tukufu liidhinishe

matumizi ya shilingi 30,233,474,000. Kati ya maombi haya:-

(a) Shilingi 21,215,930,000 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida;

(b) Shilingi 12,818,434,000 ni kwa ajili ya mishahara;

(c) Shilingi 8,397,496,000 ni kwa ajili ya matumizi mengineyo;

(d) Shilingi 9,017,544,000 ni kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo

ambapo shilingi 7,000,000,000 ni fedha za ndani na shilingi 2,017,544,000 ni fedha

za nje.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

MHE. MARY P. CHATANDA (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA

BUNGE YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO): Kwanza kabisa

ninaomba kuchukua nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi

ya kuweza kuwasilisha Taarifa hii hapa, na ni mara yangu ya kwanza kuweza

kusimama hapa.

Page 37: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

37

Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Maendeleo ya Jamii,

ninaomba kuwasilisha Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo

ya Jamii, Kuhusu Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jmii, Jinsia

na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 Pamoja na Maoni ya Kamati

Kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara hiyo kwa Mwaka Fedha

2014/2015.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 99(9) na Kanuni ya 117(11)

za Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Aprili, 2013, nakushukuru kwa kunipa

nafasi hii, ili niwasilishe Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya

Jamii, Kuhusu Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto, kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 Pamoja na Makadirio ya Mapato

na Matumizi ya Wizara hii kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, na kuliomba Bunge

lako Tukufu lipokee Taarifa hii na kuijadili.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza wajibu wake Kamati ilikutana na

watendaji wa Wizara walio chini ya Fungu 53 tarehe 1 Mei, 2014 na tarehe 2

Mei, 2014 Jijini Dar es salaam na kupokea taarifa kuhusu utekelezaji wa

majukumu wa Wizara, malengo yaliyopangwa kutekelezwa katika Mwaka wa

Fedha 2013/2014 pamoja na kujadili Bajeti iliyohusu Makadirio ya Mapato na

Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka wa Fedha

2014/2015. Aidha, Kamati ilipokea Taarifa ya Utekelezaji wa Maoni na Maagizo

ya Kamati kuhusu Bajeti ya Wizara hii kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014.

Mheshimiwa Spika, Mapitio ya utelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka

2013/2014. Katika Mwaka wa Fedha 2013/2014, Wizara ilipangiwa Bajeti ya

shilingi 25,964,470,000/= kati ya fedha hizo shilingi 8,656,002,000/= inajumuisha

mishahara na shilingi 5,397,496,000/= ni kwa ajili ya matumizi mengineyo. Shilingi

11,910,672,000/= kwa ajili ya Miradi mbalimbali ya Maendeleo ambapo shilingi

6,500,000,000/= ni fedha za ndani na shilingi 5,410,672,000/= ni fedha za nje.

Hadi kufikia Machi, 2014 Wizara ilikuwa imepokea shilingi 1,964,133,299/=

sawa na asilimia 36 ya Bajeti ya matumizi mengineyo. Aidha, katika fedha za

Miradi ya Maendeleo Wizara ilikuwa imepokea shilingi 2,923,620,590/= sawa na

asilimia 25 ya Bajeti ya maendeleo iliyoidhinishwa na Bunge ambapo

2,706,106,502/= ni fedha za ndani na shilingi 217,514,088/= ni fedha za nje.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kutopatikana kwa fedha hizo Kamati

inaitaka Serikali ikamilishe utoaji wa fedha hizi kwa kipindi kilichosalia ili Wizara

iweze kutekeleza majukumu iliyojipangia kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014.

Mheshimiwa Spika, Utekelezaji wa maoni na ushauri wa Kamati kwa Mwaka

wa Fedha 2013/2014. Katika Mwaka wa Fedha unaoisha Juni 30, 2014, Kamati

Page 38: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

38

ilitoa maoni na ushauri kwenye maeneo mbalimbali, hasa kwenye maeneo

yanayohusu:-

1. Kuongeza fedha za ndani kwenye miradi ya maendeleo.

2. Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

3. Kuongeza Bajeti kwa ajili ya kuimarisha Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na

Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.

4. Benki ya Wanawake Tanzania kuuza hisa zake ili kuongeza mtaji

utakaosaidia kuweza kufungua matawi na kutimiza azma ya Serikali ya

kuwawezesha wanawake wa Tanzania kiuchumi na kupanua wigo wa

huduma zake hadi vijijini.

5. Serikali kupitia Halmashauri za Wilaya zitenge Bajeti kwa ajili ya kuajiri

Maafisa Maendeleo ya Jamii na zipange Bajeti ya kutosha na kutoa

kipaumbele katika ukarabati wa majengo na miundombinu.

6. Asilimia tano (5%) ya fedha za maendeleo ya mfuko wa wanawake

ziende katika mfuko wa wanawake kupitia Halmashauri husika.

7. Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iangalie

namna nzuri ya kuhakikisha mabaraza ya watoto yanatambulika na

kupata nguvu ya kisheria.

8. Serikali itafiti na kubaini michango inayotolewa na mashirika yasiyo ya

kiserikali katika kuleta mandeleo ya jamii.

Mheshimiwa Spika, nafurahi kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa kwa kiasi

kikubwa ushauri wa Kamati umezingatiwa, hata hivyo Kamati inaitaka Serikali

kutekeleza ushauri wa Kamati kwenye maeneo ambayo bado hayajafanyiwa

kazi. Maeneo hayo ni pamoja na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaona marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya

mwaka 1971 ni mtambuka na haijapewa uzito unaostahili kwenye mpango wa

maendeleo vijijini kwani inawahusisha wanawake katika ustawi wa amani ya

Taifa letu na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 inabainisha wazi kuwa

umri unaoruhusiwa kuingia katika ndoa ni kuanzia miaka 18 kwa kijana wa

kiume na kuanzia miaka 15 kwa kijana wa kike. Hata hivyo, Sheria hii inakinzana

na Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009 ambayo inamtambua mtu yeyote aliye

chini ya umri wa miaka 18 kama mtoto. Kwa mantiki hii, Sheria ya Ndoa

ambayo imekuwepo na kutumika kwa takribani miaka 41 sasa inaruhusu watoto

Page 39: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

39

kuingia katika ndoa. Kwa kuwa Tume ya Marekebisho ya Sheria

imekwishapeleka mapendekezo ya kurekebisha Sheria ya Ndoa kwenye Wizara

ya Katiba na Sheria, Kamati inasisitiza kuwa marekebisho ya Sheria hii yafanywe

haraka ili kuweza kuwanusuru watoto.

Mheshimiwa Spika, umaskini na jamii kutotambua umuhimu wa elimu kwa

watoto wa kike vimekuwa vikichagiza baadhi ya jamii kuwaozesha watoto wa

kike katika umri mdogo ili kupata mali na kama njia ya kuwaondoa katika

familia hasa kwa kuwa hawaoni umuhimu wa kuwasomesha. Baadhi ya jamii

zenye utamaduni huu, wasichana wamekuwa wakifungishwa ndoa kabla ya

kufikisha umri wa miaka 18. Kamati inaishauri Serikali kuajiri wafanyakazi wa

kutosha katika sekta ya maendeleo ya jamii ambao watasaidia kuelimisha jamii

kuhusu umuhimu wa elimu kwa mtoto wa kike na athari za ndoa za utotoni

ambazo huchangia kiwango kikubwa vifo vya akina mama na watoto.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaamini kwamba elimu ikitolewa kwa jamii

husika kutakuwa na mwamko mkubwa wa kupinga ndoa za utotoni, watoto wa

kike wataelimishwa na hatimaye Taifa litakuwa na jamii iliyoelimika.

Aidha, Serikali iendelee kuwaelimisha wanawake juu ya sheria mbalimbali

zinazotoa fursa kwa wanawake kumiliki ardhi na mali pamoja na sheria

zinazowalinda dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.

Mheshimiwa Spika, Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa

Fedha 2014/2015; Makadirio ya ukusanyaji wa mapato. Ukusanyaji katika

Mwaka wa Fedha wa 2014/2015 Wizara inatarajia kukusanya jumla ya shilingi

1,845,300,000/= kupitia ada za wanafunzi kutoka katika vyuo vinane vya

Maendeleo ya Jamii vya Buhare, Uyole, Rungemba, Mlale, Misungwi, Ruaha,

Mabughai na Monduli.

Mheshimiwa Spika, Makadirio ya Matumizi ya kawaida na Maendeleo. Ili

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto iweze kutekeleza majukumu

yake katika mwaka wa fedha wa 2014/2015, Wizara imetengewa jumla ya

shilingi 30,233,474,000/= kati ya fedha hizo shilingi 21,215,930,000/= ni kwa ajili ya

Matumizi ya Kawaida na shilingi 9,017,544,000/= ni kwa ajili ya Miradi ya

Maendeleo. Kati ya fedha za Matumizi ya Kawaida shilingi 12,818,434,000/= ni

kwa ajili ya mishahara na shilingi 8,397,496,000 ni kwa ajili ya Matumizi

Mengineyo. Aidha, kati ya fedha za Miradi ya Maendeleo, shilingi

7,000,000,000/= ni fedha za ndani na shilingi 2,017,544,000 ni fedha za nje.

Page 40: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

40

Mheshimwa Spika, maeneo yaliyopewa kipaumbele kwa mwaka

2014/2015 ni pamoja na:-

(i) Kampeni ya utokomezaji wa ukatili dhidi ya wanawake, wasichana

na watoto.

(ii) Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi.

(iii) Uboreshaji wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi na Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii pamoja na kuimarisha uendeshaji wa vyuo hivyo na

kuanzisha mafunzo ya huduma za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya

mtoto katika vyuo 30 vya Maendeleo ya Wananchi.

(iv) Uandaaji wa taarifa ya hali ya Jinsia nchini (Tanzania Country

Gender Profile) na kuanzisha Benki ya Takwimu ya Usawa wa Jinsia.

(v) Uaandaji wa mfumo wa tathmini na ufuatiliaji (Monitoring and

Evaluation Framework).

(vi) Uboreshaji na uandikishaji, ufuatiliaji na uratibu wa Mashirika yasiyo

ya Kiserikali.

(vii) Kupunguza madeni ambapo shilingi 460,000,000 zimetengwa na

Wizara katika Bajeti ya Mwaka 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, Kamati inasikitishwa na Bajeti ndogo inayotengwa

kwa Wizara hii kila mwaka bila kujali umuhimu wa Wizara katika kuimarisha

masuala yote yanayohusu Maendeleo ya jamii, usawa wa jinsia, haki za watoto

na ustawi wa familia. Hata hivyo mbali ya Bunge kuidhinisha fedha kwa Wizara

hii bado fedha hizo hazitolewi kwa wakati na wakati mwingine hazipelekwi

kabisa. Aidha, bajeti hii ndogo inaathiri uwezo wa Wizara katika kutekeleza

vipaumbele ilivyojiwekea katika mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika, Moani na Ushauri wa Kamati. Baada ya kujadili Bajeti hii

kwa kina Kamati inapenda kutoa maoni na ushauri ufuatao:-

(a) Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Licha ya kuwa

Bajeti inayotengwa kwa ajili ya Wizara ni ndogo bado kumekuwa na

ucheleweshaji wa fedha hizo kutoka Hazina. Hali hii imekuwa ikiathiri Wizara

katika kutekeleza majukumu yake na hasa Miradi ya Maendeleo.

Kwa mfano, katika mwaka wa fedha unaomalizika Juni 30, 2014 hadi kufikia

mwezi Machi, 2014 Wizara ilikuwa imepokea shilingi 2,923,620,590/= sawa na

Page 41: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

41

25% kati ya shilingi 11,910,672,000/= ya Bajeti ya fedha za maendeleo

iliyoidhinishwa na Bunge.

Kati ya fedha hizo shlingi 2,706,106,502/= ni fedha za ndani na shilingi

217,504,088/= ni fedha za nje. Aidha hali hiyo imeathiri utekelezaji wa Miradi ya

Maendeleo ya wananchi kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Spika, ni wazi kwamba Miradi ya Maendeleo iliyokusudiwa

haikuweza kutekelezwa ipasavyo, Kamati inaitaka Serikali kuhakikisha kiasi cha

fedha kilichosalia kinapatikana.

Aidha, Kamati inaitaka Serikali kuainisha vyanzo vipya vya mapato na

kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuweza kutenga fedha za ndani kwa

ajili ya miradi ya maendeleo na sio kama ilivyo sasa ambapo fedha nyingi za

miradi ya maendeleo zinategemea vyanzo vya nje ambavyo upatikanaji wake

umekuwa sio wa uhakika.

(b) Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971. Kama kamati

ilivyobainisha awali kwamba sheria hii pamoja na mambo mengine haimtendei

haki mtoto wa kike kamati bado inatilia mkazo suala la Serikali kuleta Bungeni

Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

(c) Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.

(i) Mfumo wa Retention. Mfumo huu unakitaka chuo kupeleka maduhuli

kwenye Retention Account na baadaye fedha hizo zirudishwe chuoni kwa ajili

ya kukiendeleza chuo. Mfumo huu umekuwa na tatizo la kurudisha fedha

kidogo na wakati mwingine kutorudisha kabisa, hivyo kuathiri utekelezaji wa

shughuli za vyuo. Kwa mfano tangu mfumo huu kuanza kutumika Chuo cha

Maendeleo ya Jamii Rungemba kimepeleka kwenye Retention Account shilingi

208,000,000/=, lakini kiasi cha fedha kilichorudishwa ni shilingi 33,000,000/= tu.

Aidha, Katika Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha, kuanzia mwezi Septemba

hadi Disemba, 2013, chuo kilipeleka kwenye Retention Account shilingi

200,000,000/= zimerudishwa shilingi 76,000,000/= tu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na fedha zinazokusanywa na chuo

(maduhuli) kutorudishwa chuoni kama ilivyotarajiwa, Kamati inashauri Serikali

kurudisha mfumo wa zamani wa fedha hizi kupelekwa Hazina Ndogo (retention

at the source) badala ya kutumia mfumo wa sasa wa kupeleka kwenye

Retention Account ambao una matatizo makubwa ya kurejesha kiasi kidogo

cha fedha na wakati mwingine kiasi hicho kidogo kutorudishwa kwa wakati.

Page 42: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

42

Kamati inaamini kwamba endapo makusanyo yanayopelekwa katika

mfuko wa retention zitarudishwa zote matatizo mengi yataweza kutatuliwa na

chuo chenyewe.

(ii) Ukarabati wa majengo na miundombinu ya Chuo cha Maendeleo

ya Jamii Rungemba.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba kipo

Mkoani Iringa, katika Mji wa Mafinga. Kwa kuwa miundombinu ya umeme wa

gridi imefika hapo chuoni, Kamati inaishauri Serikali kwa kushirikiana na

TANESCO wafanye tahmini ya gharama za kuingiza umeme huo wa gridi katika

majengo ya chuo ili iweze kuingizwa badala ya kutumia umeme wa jenereta

ambao nguvu yake ya usambazaji ni ndogo na gharama za uendeshaji ni

kubwa.

(iii) Umuhimu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Wananchi kupata

vyombo vya Usafiri.

Mheshimiwa Spika, vyuo hivi vinakabiliwa na upungufu mkubwa wa

vyombo vya usafiri kama vile magari na pikipiki, kutokana na upungufu huo

vyuo hasa vya Maendeleo ya Wananchi kama vile Chuo cha Chilala –

Rutamba, vinashindwa kuendesha mafunzo ya vitendo kama fani ya ufundi

magari, umeme wa magari. Aidha kutokana na vyuo hivi kuwa na idadi kubwa

ya wanafunzi na watumishi vyombo vya usafiri ni muhimu.

Kwa kuwa hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetaifisha

magari mengi mali ya Kampuni ya SBT Japan, tunaomba Serikali kwa

kushirikiana na TRA kutoa kipaumbele na kuvipatia Vyuo hivi magari kama

ambavyo imefanya kwa Taasisi nyingine za Serikali.Kamati inashauri Serikali

kugawa magari hayo kwa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii hususani Chuo cha

Rungemba ambacho hakina nyenzo ya usafiri wa aina yoyote ili kurahisisha

utekelezaji wa majukumu kwa maendeleo ya Taifa.

(iv) Mgogoro wa ardhi kati ya chuo cha Rungemba na Wananchi.

Mheshimiwa Spika, kutokana chuo kutokuwa na hati miliki ya eneo

ambalo limejengwa chuo hali inayosababisha wananchi kudai kwamba eneo

hilo ni lao Kamati inaishauri Serikali kuharakisha upatikanaji wa Hati hiyo

kwakuwa mchakato wa kuipata hati hiyo umechukua muda mrefu na hivyo

kusababisha Chuo kushindwa kupanga mipango yake ya muda mrefu na

muda mfupi jambo hili limelizwe mapema.

Mheshimiwa Spika, ajira kwa wahitimu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii;

kuna upungufu mkubwa wa wataalam wa maendeleo ya jamii katika

Page 43: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

43

Halmashauri na hasa katika Kata kwa idadi ya 2,045 licha ya kwamba vyuo

vyetu vinaendelea kutoa wastani wa idadi ya wahitimu 4,900 kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaishauri Serikali kutenga fedha za kutosha

katika bajeti kwa ajili ya kuwaajiri wataalam wa maendeleo ya jamii

wanaotoka vyuoni moja kwa moja kama inavyofanyika kwa ajira za Walimu.

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kukifanya Chuo cha Maendeleo ya

Jamii, Tengeru kuwa Taasisi ya Elimu ya Juu ulianza tarehe 15/11/2010 kwa chuo

kuunda kikosi kazi cha ufuatiliaji kilichoandaa mapendekezo na kuyawasilisha

katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

Mheshimiwa Spika, Muswada wa Sheria ya Chuo kujitegemea

uliwasilishwa kwa Waziri wa Elimu ambaye ana dhamana ya Vyuo vya Ufundi

vilivyo chini ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania (NACTE). Baada ya Waziri wa

Elimu kuridhia na kusaini, Muswada, ulipelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa

Serikali kwa ushauri, uandishi wa kisheria na uchapaji.

Mheshimiwa Spika, aidha, Muswada ulichapishwa katika Gazeti la Serikali

Namba tisa (Na. 9) la Tarehe 25 Januari, 2013 kwa jina la Tengeru Institute of

CommunityDevelopment (Establishment Order, 2013). Kamati iliarifiwa kwamba

Muswada wa kukibadilisha Chuo cha Maendeleo ya Jamii, Tengeru ili

kujiendesha kama Taasisi ya Elimu ya Juu limeletwa Bungeni likisubiri

kuwasilishwa na Waziri mwenye dhamana kama inavyoelekezwa na Sheria

iliyoanzisha Baraza la Elimu ya Ufundi. Kamati inataka Serikali kuleta Muswada

ndani ya Bunge ili ujadiliwe na hatimaye sheria ya kukiwezesha chuo

kujiendesha kama Taasisi ya Elimu ya Juu iweze kupitishwa.

Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake ulianzishwa

kutokana na Azimio la Bunge lililopitishwa Agosti, 1993 kwa mujibu wa kifungu

17(1) cha Sheria ya Exchequer and Audit Ordinance (Cap. 439) No. 21 ya

mwaka 1961, kama mojawapo ya mikakati ya kuwawezesha wanawake

kujiimarisha na kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, dhamira ya Mfuko huu ni kuwawezesha wanawake

wote walio katika Halmashauri kwa kuwakopesha fedha kwa ajili ya shughuli za

uzalishaji mali na kupambana na umaskini kwa kuunda vikundi na kupatiwa

mikopo.

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni kawaida kwa Halmashauri nyingi

kutozingatia sheria inazozitaka kutenga asilimia tano (5%) ya mapato yao kwa

ajili ya maendeleo ya wanawake, Kamati inazitaka Halmashauri zote nchini

Page 44: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

44

kutenga asilimia tano ili kuchochea maendeleo ya wanawake. Aidha, Kamati

inashauri fedha hizo kutumika kama zilivyokusudiwa na uwepo usimamizi thabiti

katika Halmashauri ili kuhakikisha hakuna ubadhirifu utakaofanywa katika

matumizi ya fedha hizo.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaipongeza Halmashauri ya Mji Korogwe na

Halmashauri nyingine ambazo zimekuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa

zimekuwa na utamaduni wa kutenga kiasi hicho cha fedha na kutumika kama

kilivyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, Benki ya Wanawake Tanzania ilianzishwa kwa lengo la

kuwakomboa wanawake kiuchumi kwa kuwawezesha kupata mikopo kwa riba

nafuu na kwa ajili ya kukuza mitaji ya biashara. Hata hivyo, lengo hilo

linaonekana kutofikiwa kikamilifu katika siku za karibuni hasa kutokana na ukweli

kwamba kiwango cha fedha ambazo zinatolewa kwa ajili ya benki kama

sehemu ya kukuza mtaji wake ni kidogo sana ikilinganishwa na matarajio ya

awali.

Mheshimiwa Spika, wakati Rais, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,

akielezea madhumuni ya kuanzishwa kwa benki hii alisema Serikali itatoa jumla

ya shilingi bilioni mbili (2,000,000,000/=) kila mwaka kwa kipindi cha miaka

mitano mfululizo ili kuiwezesha benki hii kuimarika kimtaji.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2010/2011 na mwaka

2011/2012, Benki ya Wanawake ilipokea kiasi cha sh. 2,000,000,000/= kama

ilivyoelekezwa. Aidha, katika kipindi cha mwaka 2012/2013, kiasi cha sh.

1,300,000,000/= tu ndiyo kilitolewa na kiasi cha sh. 700,000,000/= bado

hakijatolewa na Serikali. Kipindi cha mwaka 2013/2014 kiasi cha sh.

450,000,000/= tu ndiyo kimetolewa na Serikali na kiasi cha sh. 1,550,000,000/=

bado hakijatolewa mpaka sasa.

Mheshimiwa Spika, tangu Benki ianzishwe mpaka sasa ni kiasi cha shilingi

bilioni 8.7 tu ndiyo kilichopo kama mtaji na kufuatia Sheria za Benki Kuu ya

Tanzania ili Benki iweze kujiendesha kibiashara inapaswa iwe na mtaji kuanzia

sh. 15,000,000,000/=.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaitaka Serikali kutoa kiasi chote cha fedha

ambazo hakikupelekwa kwenye Benki ya Wanawake ili kutimiza azma ya kauli

ya Rais ya kuifanya Benki hii kujiendesha kibiashara na kutoa fursa kwa

wanawake wengi nchini kujikwamua kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kukupongeza kwa umahiri

na busara zako katika uendeshaji wa Vikao vya Bunge. Nawapongeza pia

Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa jinsi wanavyokusaidia katika

Page 45: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

45

kutekeleza majukumu yako. Nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuwasilisha

maoni ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto, Mheshimiwa Sophia Mnyambi Simba; Naibu Waziri,

Mheshimiwa Dkt. Pindi Hazara Chana; Katibu Mkuu wa Wizara, Ndugu Anna T.

Maembe; Naibu Katibu Mkuu, Ndugu Nuru H. M. Milao na Wakurugenzi, Wakuu

wa Idara, Wakuu wa Vitengo na Taasisi pamoja na Watumishi wote wa Wizara

kwa ushirikiano wao mkubwa uliowezesha Kamati kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kumshukuru Katibu wa Bunge, Dkt.

Thomas Kashilillah, akisaidiwa na Mkurugenzi wa Kamati za Bunge Ndugu

Charles Mloka, Makatibu wa Kamati, Ndugu Aziza Makwai, Ndugu Hanifa

Masaninga na Ndugu Abdallah Hancha, kwa ushauri na uratibu wa shughuli za

Kamati hadi kukamilisha taarifa hii.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na naomba kuwasilisha. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana.

Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii

Kuhusu Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto kwa Mwaka 2014/2015

kama ilivyowasilishwa Mezani

TAARIFA YA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAENDELEO YA JAMII KUHUSU

UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

KWA MWAKA

WA FEDHA WA 2013/2014 PAMOJA NA MAONI YA

KAMATI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA

MATUMIZI YA WIZARA HIYO KWA MWAKA

WA FEDHA WA 2014/2015

1.0 UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 99(9) na Kanuni ya 117(11) za

Kanuni za Kudumu za Bunge Toleo la Aprili, 2013, nakushukuru kwa kunipa

nafasi hii, ili niwasilishe Maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya

Jamii, kuhusu Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto, kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 pamoja na Makadirio ya Mapato

na Matumizi ya Wizara hii kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, na kuliomba Bunge

lako Tukufu lipokee taarifa hii na kuijadili.

Page 46: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

46

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza wajibu wake Kamati ilikutana na

watendaji wa Wizara walio chini ya Fungu 53 tarehe 01 na 02 Mei, 2014 jijini Dar

es salaam na kupokea taarifa kuhusu utekelezaji wa majukumu wa Wizara,

malengo yaliyopangwa kutekelezwa katika Mwaka wa Fedha 2013/2014

pamoja na kujadili bajeti iliyohusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya

Kawaida na Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015. Aidha,

Kamati ilipokea Taarifa ya Utekelezaji wa Maoni na Maagizo ya Kamati kuhusu

Bajeti ya Wizara hii kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014.

2.0. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI YA MWAKA 2013/2014

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2013/2014, Wizara ilipangiwa bajeti

ya shilingi 25,964,470,000/= kati ya fedha hizo shilingi 8,656,002,000/= inajumuisha

mishahara na shilingi 5,397,496,000/= ni kwa ajili ya matumizi mengineyo. Shilingi

11,910,672,000/= kwa ajili ya Miradi mbalimbali ya Maendeleo ambapo shilingi

6,500,000,000/= ni fedha za ndani na shilingi 5,410,672,000/= ni fedha za nje.

Hadi kufikia Machi, 2014 Wizara ilikuwa imepokea shilingi 1,964,133,299/= sawa

na asilimia 36 ya bajeti ya matumizi mengineyo. Aidha, katika fedha za Miradi

ya Maendeleo Wizara ilikuwa imepokea shilingi 2,923,620,590/= sawa na asilimia

25 ya bajeti ya maendeleo iliyoidhinishwa na Bunge ambapo 2,706,106,502 ni

fedha za ndani na shilingi 217,514,088/= ni fedha za nje.

Mheshimiwa Spika, kutokana na kutopatikana kwa fedha hizo kamati inaitaka

Serikali ikamilishe utoaji wa fedha hizi kwa kipindi kilichosalia ili Wizara iweze

kutekeleza majukumu iliyojipangia kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014.

3.0 UTEKELEZAJI WA MAONI NA USHAURI WA KAMATI KWA MWAKA WA FEDHA

2013/2014

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha unaoisha Juni 30, 2014, Kamati

ilitoa maoni na ushauri kwenye maeneo mbalimbali, hasa kwenye maeneo

yanayohusu:-

1. Kuongeza fedha za ndani kwenye miradi ya maendeleo.

2. Kufanya marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

3. Kuongeza bajeti kwa ajili ya kuimarisha Vyuo vya Maendeleo ya

Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.

4. Benki ya Wanawake Tanzania kuuza hisa zake ili kuongeza mtaji

utakaosaidia kuweza kufungua matawi na kutimiza azma ya Serikali ya

kuwawezesha wanawake wa Tanzania kiuchumi na kupanua wigo wa huduma

zake hadi vijijini.

Page 47: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

47

5. Serikali kupitia Halmashauri za Wilaya zitenge bajeti kwa ajili ya

kuajiri Maafisa Maendeleo ya Jamii na zipange bajeti ya kutosha na kutoa

kipaumbele katika ukarabati wa majengo na miundombinu.

6. Asilimia tano (5%) ya fedha za maendeleo ya mfuko wa wanawake

ziende katika mfuko wa wanawake kupitia Halmashauri husika.

7. Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali

iangalie namna nzuri ya kuhakikisha mabaraza ya watoto yanatambulika na

kupata nguvu ya kisheria.

8. Serikali itafiti na kubaini michango inayotolewa na mashirika yasiyo

ya kiserikali katika kuleta mandeleo ya jamii.

Mheshimiwa Spika, nafurahi kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa kwa kiasi kikubwa

ushauri wa Kamati umezingatiwa, hata hivyo Kamati inaitaka Serikali kutekeleza

ushauri wa Kamati kwenye maeneo ambayo bado hayajafanyiwa kazi.

Maeneo hayo ni pamoja na Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaona marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya mwaka

1971 ni mtambuka na haijapewa uzito unaostahili kwenye mpango wa

maendeleo vijijini kwani inawahusisha wanawake katika ustawi wa amani ya

Taifa letu na maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 inabainisha wazi kuwa umri

unaoruhusiwa kuingia katika ndoa ni kuanzia miaka 18 kwa kijana wa kiume na

kuanzia miaka 15 kwa kijana wa kike. Hata hivyo, Sheria hii inakinzana na Sheria

ya Mtoto ya Mwaka 2009 ambayo inamtambua mtu yeyote aliye chini ya umri

wa miaka 18 kama mtoto.

Kwa mantiki hii, Sheria ya Ndoa ambayo imekuwepo na kutumika kwa takribani

miaka 41 sasa inaruhusu watoto kuingia katika ndoa. Kwa kuwa Tume ya

Marekebisho ya Sheria imekwishapeleka mapendekezo ya kurekebisha Sheria

ya Ndoa kwenye Wizara ya Katiba na Sheria, Kamati inasisitiza kuwa

marekebisho ya Sheria hii yafanywe haraka ili kuweza kuwanusuru watoto.

Mheshimiwa Spika, umaskini na jamii kutotambua umuhimu wa elimu kwa

watoto wa kike vimekuwa vikichagiza baadhi ya jamii kuwaozesha watoto wa

kike katika umri mdogo ili kupata mali na kama njia ya kuwaondoa katika

familia hasa kwa kuwa hawaoni umuhimu wa kuwasomesha. Baadhi ya jamii

zenye utamaduni huu, wasichana wamekuwa wakifungishwa ndoa kabla ya

kufikisha umri wa miaka 18.

Page 48: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

48

Kamati inaishauri Serikali kuajiri wafanyakazi wa kutosha katika sekta ya

maendeleo ya jamii ambao watasaidia kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa

elimu kwa mtoto wa kike, na athari za ndoa za utotoni ambazo huchangia

kiwango kikubwa vifo vya akina mama na watoto.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaamini kwamba elimu ikitolewa kwa jamii husika

kutakuwa na mwamko mkubwa wa kupinga ndoa za utotoni, watoto wa kike

wataelimishwa na hatimaye Taifa litakuwa na jamii iliyoelimika. Aidha, Serikali

iendelee kuwaelimisha wanawake juu ya sheria mbalimbali zinazotoa fursa kwa

wanawake kumiliki ardhi na mali pamoja na sheria zinazowalinda dhidi ya

unyanyasaji wa kijinsia.

4.0. MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2014/2015

4.1 Makadirio ya Ukusanyaji wa Mapato

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha wa 2014/2015 Wizara inatarajia

kukusanya jumla ya shilingi 1,845,300,000/= kupitia ada za wanafunzi kutoka

katika vyuo vinane vya Maendeleo ya Jamii vya Buhare, Uyole, Rungemba,

Mlale, Misungwi, Ruaha, Mabughai na Monduli.

4.2 Makadirio ya Matumizi ya Kawaida na Maendeleo

Mheshimiwa Spika, ili Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto iweze

kutekeleza majukumu yake katika mwaka wa fedha wa 2014/2015, Wizara

imetengewa jumla ya shilingi 30,233,474,000/= kati ya fedha hizo shilingi

21,215,930,000/= ni kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na shilingi 9,017,544,000/=

ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha za Matumizi ya Kawaida

shilingi 12,818,434,000/= ni kwa ajili ya mishahara na shilingi 8,397,496,000 ni kwa

ajili ya Matumizi Mengineyo. Aidha, kati ya fedha za Miradi ya Maendeleo,

shilingi 7,000,000,000/= ni fedha za ndani na shilingi 2,017,544,000 ni fedha za nje.

Mheshimwa Spika, maeneo yaliyopewa kipaumbele kwa mwaka 2014/2015 ni

pamoja na:-

i. Kampeni ya utokomezaji wa ukatili dhidi ya wanawake, wasichana

na watoto.

ii. Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi.

iii. Uboreshaji wa Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi na Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii pamoja na kuimarisha uendeshaji wa vyuo hivyo na

Page 49: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

49

kuanzisha mafunzo ya huduma za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya

mtoto katika vyuo 30 vya Maendeleo ya Wananchi.

iv. Uandaaji wa taarifa ya hali ya jinsia nchini (Tanzania Country

Gender Profile) na kuanzisha Benki ya Takwimu ya Usawa wa Jinsia.

v. Uaandaji wa mfumo wa tathmini na ufuatiliaji (monitoring and

evaluation framework).

vi. Uboreshaji na uandikishaji, ufuatiliaji na uratibu wa Mashirika yasiyo

ya Kiserikali.

vii. Kupunguza madeni ambapo shilingi 460,000,000 zimetengwa na

Wizara katika Bajeti ya mwaka 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, Kamati inasikitishwa na bajeti ndogo inayotengwa kwa

Wizara hii kila mwaka bila kujali umuhimu wa Wizara katika kuimarisha masuala

yote yanayohusu maendeleo ya jamii, usawa wa jinsia, haki za watoto na

ustawi wa familia.

Hata hivyo mbali ya Bunge kuidhinisha fedha kwa Wizara hii bado fedha hizo

hazitolewi kwa wakati na wakati mwingine hazipelekwi kabisa. Aidha, bajeti hii

ndogo inaathiri uwezo wa Wizara katika kutekeleza vipaumbele ilivyojiwekea

katika mwaka huu wa fedha.

5.0. MAONI NA USHAURI WA KAMATI

Mheshimiwa Spika, baada ya kujadili Bajeti hii kwa kina Kamati inapenda kutoa

maoni na ushauri ufuatao:-

(a) Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

Mheshimiwa Spika, licha ya kuwa Bajeti inayotengwa kwa ajili ya Wizara ni

ndogo bado kumekuwa na ucheleweshaji wa fedha hizo kutoka Hazina. Hali hii

imekuwa ikiathiri Wizara katika kutekeleza majukumu yake na hasa Miradi ya

Maendeleo. Kwa mfano, katika mwaka wa fedha unaomalizika Juni 30, 2014

hadi kufikia mwezi Machi, 2014 Wizara ilikuwa imepokea shilingi 2,923,620,590/=

sawa na 25% kati ya shilingi 11,910,672,000/= ya bajeti ya fedha za maendeleo

iliyoidhinishwa na Bunge. Kati ya fedha hizo shlingi 2,706,106,502/= ni fedha za

ndani na shilingi 217,504,088/= ni fedha za nje. Aidha hali hiyo imeathiri

utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya wananchi kwa kiasi kikubwa.

Mheshimiwa Spika, ni wazi kwamba miradi ya maendeleo iliyokusudiwa

haikuweza kutekelezwa ipasavyo, Kamati inaitaka Serikali kuhakikisha kiasi cha

fedha kilichosalia kinapatikana. Aidha, Kamati inaitaka Serikali kuainisha vyanzo

Page 50: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

50

vipya vya mapato na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuweza kutenga

fedha za ndani kwa ajili ya miradi ya maendeleo na sio kama ilivyo sasa

ambapo fedha nyingi za miradi ya maendeleo zinategemea vyanzo vya nje

ambavyo upatikanaji wake umekuwa sio wa uhakika.

(b) Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971

Mheshimiwa Spika, kama kamati ilivyobainisha awali kwamba sheria hii pamoja

na mambo mengine haimtendei haki mtoto wa kike kamati bado inatilia mkazo

suala la Serikali kuleta Bungeni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Ndoa ya

mwaka 1971.

(c) Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi

i. Mfumo wa Retention

Mheshimiwa Spika, mfumo huu unakitaka chuo kupeleka maduhuli kwenye

Retention Account na baadaye fedha hizo zirudishwe chuoni kwa ajili ya

kukiendeleza chuo. Mfumo huu umekuwa na tatizo la kurudisha fedha kidogo

na wakati mwingine kutorudisha kabisa, hivyo kuathiri utekelezaji wa shughuli za

vyuo. Kwa mfano tangu mfumo huu kuanza kutumika Chuo cha Maendeleo ya

Jamii Rungemba kimepeleka kwenye Retention Account sh. 208,000,000/=,

lakini kiasi cha fedha kilichorudishwa ni shilingi 33,000,000/= tu. Aidha, Katika

Chuo cha Maendeleo ya Jamii Ruaha, kuanzia mwezi Septemba hadi Disemba,

2013, chuo kilipeleka kwenye Retention Account shilingi 200,000,000/=

zimerudishwa shilingi 76,000,000/= tu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na fedha zinazokusanywa na chuo (maduhuli)

kutorudishwa chuoni kama ilivyotarajiwa, Kamati inashauri Serikali kurudisha

mfumo wa zamani wa fedha hizi kupelekwa Hazina Ndogo (retention at the

source) badala ya kutumia mfumo wa sasa wa kupeleka kwenye Retention

Account ambao una matatizo makubwa ya kurejesha kiasi kidogo cha fedha

na wakati mwingine kiasi hicho kidogo kutorudishwa kwa wakati.

Kamati inaamini kwamba endapo makusanyo yanayopelekwa katika mfuko

wa retention zitarudishwa zote matatizo mengi yataweza kutatuliwa na chuo

chenyewe.

ii. Ukarabati wa majengo na miundombinu ya Chuo cha Maendeleo

ya Jamii Rungemba

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maendeleo ya Jamii Rungemba kipo Mkoani

Iringa, katika Mji wa Mafinga. Kwa kuwa miundombinu ya umeme wa gridi

imefika hapo chuoni, Kamati inaishauri Serikali kwa kushirikiana na TANESCO

Page 51: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

51

wafanye tahmini ya gharama za kuingiza umeme huo wa gridi katika majengo

ya chuo ili iweze kuingizwa badala ya kutumia umeme wa jenereta ambao

nguvu yake ya usambazaji ni ndogo na gharama za uendeshaji ni kubwa.

iii. Umuhimu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na Wananchi kupata

vyombo vya Usafiri

Mheshimiwa Spika, vyuo hivi vinakabiliwa na upungufu mkubwa wa vyombo

vya usafiri kama vile magari na pikipiki, kutokana na upungufu huo vyuo hasa

vya Maendeleo ya Wananchi kama vile Chuo cha Chilala-Rutamba

vinashindwa kuendesha mafunzo ya vitendo kama fani ya ufundi magari,

umeme wa magari, aidha kutokana na vyuo hivi kuwa na idadi kubwa ya

wanafunzi na watumishi vyombo vya usafiri ni muhimu.

Kwa kuwa hivi karibuni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetaifisha magari

mengi mali ya Kampuni ya SBT Japan, tunaomba Serikali kwa kushirikiana na

TRA kutoa kipaumbele na kuvipatia Vyuo hivi magari kama ambavyo imefanya

kwa Taasisi nyingine za Serikali.

Kamati inashauri Serikali kugawa magari hayo kwa Vyuo vya Maendeleo ya

Jamii hususani Chuo cha Rungemba ambacho hakina nyenzo ya usafiri wa aina

yoyote ili kurahisisha utekelezaji wa majukumu kwa maendeleo ya Taifa.

iv. Mgogoro wa ardhi kati ya chuo cha Rungemba na Wananchi

Mheshimiwa Spika, kutokana chuo kutokuwa na hati miliki ya eneo ambalo

limejengwa chuo hali inayosababisha wananchi kudai kwamba eneo hilo ni lao

kamati inaishauri Serikali kuharakisha upatikanaji wa hati hiyo kwakuwa

mchakato wa kuipata hati hiyo umechukua muda mrefu na hivyo kusababisha

Chuo kushindwa kupanga mipango yake ya muda mrefu na muda mfupi.

Jambo hili limalizwe sasa.

v. Ajira kwa Wahitimu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii

Mheshimiwa Spika, kuna upungufu mkubwa wa wataalamu wa maendeleo ya

jamii katika Halmashauri na hasa katika kata kwa idadi ya 2,045 licha ya

kwamba vyuo vyetu vinaendelea kutoa wastani wa idadi ya wahitimu 4,900 kila

mwaka.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaishauri Serikali kutenga fedha za kutosha katika

bajeti kwa ajili ya kuwaajiri wataalamu wa maendeleo ya jamii wanaotoka

vyuoni moja kwa moja kama inavyofanyika kwa ajira za walimu.

Page 52: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

52

vi. Mchakato wa kukifanya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru

kuwa Taasisi ya Elimu ya Juu

Mheshimiwa Spika, mchakato wa kukifanya Chuo cha Maendeleo ya Jamii

Tengeru kuwa Taasisi ya Elimu ya Juu ulianza tarehe 15/11/2010 kwa chuo

kuunda kikosi kazi cha ufuatiliaji kilichoandaa mapendekezo na kuyawasilisha

katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

Mhehimiwa Spika, Muswada wa Sheria ya Chuo kujitegemea uliwasilishwa kwa

Waziri wa Elimu ambaye ana dhamana ya Vyuo vya Ufundi vilivyo chini ya

Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania (NACTE). Baada ya Waziri wa Elimu kuridhia

na kusaini, Muswada ulipelekwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa

ushauri, uandishi wa kisheria na uchapaji.

Mheshimiwa Spika, aidha, Muswada ulichapishwa katika Gazeti la Serikali Na. 9

la Tarehe 25/01/2013 kwa jina la Tengeru Institute of Community Development

(Establishment Order, 2013). Kamati iliarifiwa kwamba Muswada wa

kukibadilisha Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru ili kujiendesha kama

Taasisi ya Elimu ya Juu limeletwa Bungeni likisubiri kuwasilishwa na Waziri

mwenye dhamana kama inavyoelekezwa na sheria iliyoanzisha Baraza la Elimu

ya Ufundi. Kamati inataka Serikali kuleta muswada ndani ya Bunge ili ujadiliwe

na hatimaye sheria ya kukiwezesha chuo kujiendesha kama Taasisi ya Elimu ya

Juu iweze kupitishwa.

(d) Mfuko wa Maendeleo wa Wanawake

Mheshimiwa Spika, mfuko huu ulinzishwa kutokana na Azimio la Bunge

lililopitishwa Agosti, 1993 kwa mujibu wa kifungu 17(1) cha Sheria ya Exchaquer

and Audit Ordiance (Cap. 439) No. 21 ya mwaka 1961. Kama mojawapo ya

mikakati ya kuwawezesha wanawake kujiimarisha na kuwawezesha kujikwamua

kiuchumi.

Mheshimiwa Spika, dhamira ya mfuko huu ni kuwawezesha wanawake wote

walio katika Halmashauri kwa kuwakopesha fedha kwa ajili ya shughuli za

uzalishaji mali na kupambana na umaskini kwa kuunda vikundi na kupatiwa

mikopo.

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni kawaida kwa Halmashauri nyingi kutozingatia

sheria inazozitaka kutenga asilimia tano (5%) ya mapato yao kwa ajili ya

maendeleo ya wanawake, Kamati inazitaka Halmashauri zote nchini kutenga

asilimia tano ili kuchochea maendeleo ya wanawake. Aidha, Kamati inashauri

fedha hizo kutumika kama zilivyokusudiwa na uwepo usimamizi thabiti katika

Halmashauri ili kuhakikisha hakuna ubadhilifu utakaofanywa katika matumizi ya

fedha hizo.

Page 53: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

53

Mheshimiwa Spika, Kamati inaipongeza Halmashauri ya Mji Korogwe na

Halmashauri nyingine ambazo zimekuwa mfano wa kuigwa kwa kuwa

zimekuwa na utamaduni wa kutenga kiasi hicho cha fedha na kutumika kama

kilivyokusudiwa.

e) Benki ya Wanawake Tanzania

Mheshimiwa Spika, Benki hii ilianzishwa kwa lengo la kuwakomboa wanawake

kiuchumi kwa kuwawezesha kupata mikopo kwa riba nafuu na kwa ajili ya

kukuza mitaji ya biashara. Hata hivyo, lengo hilo linaonekana kutofikiwa

kikamilifu katika siku za karibuni hasa kutokana na ukweli kwamba kiwango cha

fedha ambazo zinatolewa kwa ajili ya benki kama sehemu ya kukuza mtaji

wake ni kidogo sana ikilinganishwa na matarajio ya awali.

Wakati Rais, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, akielezea madhumuni ya

kuanzishwa kwa benki hii alisema Serikali itatoa jumla ya shilingi bilioni mbili

(2,000,000,000/=) kila mwaka kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo ili

kuiwezesha benki hii kuimarika kimtaji.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha mwaka 2010/2011 na mwaka 2011/2012

Benki ya Wanawake ilipokea kiasi cha shilingi 2,000,000,000/= kama

ilivyoelekezwa. Aidha, katika kipindi cha mwaka 2012/2013 kiasi cha sh.

1,300,000,000/= tu ndiyo kilitolewa na kiasi cha shilingi 700,000,000/= bado

hakijatolewa na Serikali. Kipindi cha mwaka 2013/2014 kiasi cha shilingi

450,000,000/= tu ndiyo kimetolewa na Serikali na kiasi cha shilingi

1,550,000,000/= bado hakijatolewa mpaka sasa.

Mheshimiwa Spika, tangu Benki ianzishwe mpaka sasa ni kiasi cha shilingi

8,746,053,000/= tu ndiyo kilichopo kama mtaji, na kufutia Sheria za Benki Kuu ya

Tanzania ili Benki iweze kujiendesha kibiashara inapaswa iwe na mtaji kuanzia

shilingi 15,000,000,000/=.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaitaka Serikali kutoa kiasi chote cha fedha ambazo

hakikupelekwa kwenye Benki ya Wanawake ili kutimiza azma ya kauli ya Rais ya

kuifanya Benki hii kujiendesha kibiashara na kutoa fursa kwa wanawake wengi

nchini kujikwamua kiuchumi.

6.0 HITIMISHO

Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kukupongeza kwa umahiri na

busara zako katika uendeshaji wa Vikao vya Bunge. Nawapongeza pia Naibu

Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa jinsi wanavyokusaidia katika kutekeleza

Page 54: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

54

majukumu yako. Nakushukuru kwa kunipatia nafasi ya kuwasilisha maoni ya

Kamati.

Mheshimiwa Spika, napenda kumshukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia

na Watoto - Mheshimiwa Sophia Mnyambi Simba (Mb); Naibu Waziri -

Mheshimiwa Dkt. Pindi Hazara Chana (Mb); Katibu Mkuu wa Wizara – Ndugu

Anna T. Maembe; Naibu Katibu Mkuu Ndugu - Nuru H. M. Milao na Wakurugenzi,

Wakuu wa Idara, Wakuu wa Vitengo na Taasisi pamoja na Watumishi wote

Wizara kwa ushirikiano wao mkubwa uliowezesha Kamati kutekeleza majukumu

yake.

Mheshimiwa Spika, kwa umuhimu wa kipekee, nawashukuru Wajumbe wa

Kamati kwa ushirikiano wao mkubwa wanaonipatia katika kutekeleza

majukumu ya Kamati. Naomba niwatambue kwa majina kama ifuatavyo:-

1. Mhe. Said Mohamed Mtanda, Mb - Mwenyekiti

2. Mhe. Capt. John D. Komba, Mb - M/Mwenyekiti

3. Mhe. Joseph Osmund Mbilinyi, Mb - Mjumbe

4. Mhe. Mohamed Said Mohamed, Mb - Mjumbe

5. Mhe. Nasib Suleiman Omar, Mb - Mjumbe 6. Mhe.

Mustafa Haidi Mkulo, Mb - Mjumbe

7. Mhe. Salum Halfan Barwany, Mb - Mjumbe 8. Mhe.

Kiumbwa Makame Mbaraka, Mb - Mjumbe 9. Mhe.

Salvatory Naluyaga Machemli, Mb - Mjumbe 10. Mhe.

Livingstone Joseph Lusinde, Mb - Mjumbe 11. Mhe. Moza

Abedi Saidy, Mb - Mjumbe 12. Mhe.

Agness Elias Hokororo, Mb - Mjumbe 13. Mhe.

Godbless Jonathan Lema, Mb - Mjumbe 14. Mhe. Mary

Pius Chatanda, Mb - Mjumbe 15. Mhe. Juma

Othman Ali, Mb - Mjumbe 16. Mhe. Jaddy Simai

Jaddy, Mb - Mjumbe 17. Mhe. Dkt. Maua Abeid Daftari,

Mb - Mjumbe 18. Mhe. Albert Obama Ntabaliba, Mb -

Mjumbe 19. Mhe. Rose Kamili Sukum, Mb - Mjumbe

20. Mhe. Joshua Samweli Nassari, Mb - Mjumbe 21.

Mhe. Rosemary Kasimbi Kirigini, Mb -Mjumbe

22. Mhe. Philip Augustino Mulugo, Mb - Mjumbe

Mheshimiwa Spika, mwisho, napenda kumshukuru Katibu wa Bunge, Dkt.

Thomas Kashillilah akisaidiwa na Mkurugenzi wa Kamati za Bunge Ndugu

Charles Mloka, Makatibu wa Kamati, Ndugu Aziza Makwai, Ndugu Hanifa

Masaninga na Ndugu Abdallah Hancha, kwa ushauri na uratibu wa shughuli za

Kamati hadi kukamilisha taarifa hii.

Page 55: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

55

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, na naomba kuwasilisha.

Said Mohamed Mtanda, Mb

MWENYEKITI

KAMATI YA MAENDELEO YA JAMII

17 Mei, 2014

SPIKA: Sasa nimwite Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Wizara hii,

Mheshimiwa Barwany!

Taarifa ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Kuhusu

Bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia

na Watoto kwa Mwaka 2014/2015 kama

ilivyosomwa Bungeni

MHE. SALUM K. BARWANY - MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI

KWA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge, Kanuni ya 99(9), naomba

kuwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ya makadirio ya

mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2014/2015 ya Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii Mosi, kumshukuru

Mwenyezi Mungu kwa kunipa uzima na afya. Pili, kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi

ya Upinzani Bungeni kwa imani kubwa aliyokuwa nayo kwangu na kwa uteuzi

huu wa kuwa Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Nasema ahsante

sana.

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Jamii ni dhana yenye dhima ya

kuwezesha wananchi kutambua uwezo wao na changamoto zilizopo na

kutumia rasilimali zilizopo katika kukabiliana na maadui ujinga, umaskini,

maradhi na ufisadi. Maendeleo ya jamii yanaweka mkazo katika kushirikisha

umma katika kufikiri, kuamua, kupanga na kutekeleza mambo yanayohusu

maisha yao na Taifa lao.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia dhana hii Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto ina dhima ya pekee katika ustawi na uchumi wa

wananchi na nchi kwa ujumla. Hata hivyo, Wizara hii imekuwa ikichukuliwa kwa

mtazamo potofu kuwa ni „Wizara ya Wanawake‟ na hivyo kutoyapa uzito

unaostahili masuala ambayo yanashughulikiwa na Wizara hii ya maendeleo ya

jamii, jinsia na watoto.

Page 56: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

56

Mheshimiwa Spika, maoni haya ya Kambi Rasmi ya Upinzani

ninayoyawasilisha yajadiliwe na Wabunge wengine na kujibiwa kwa ukamilifu

na Serikali kuwezesha mabadiliko na maendeleo ya jamii yenye usawa wa

kijinsia nchini.

Mheshimiwa Spika, mapitio ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo na

bajeti ya mwaka 2013/2014. Hadi kufikia Machi, 2014 Wizara hii ilipokea asilimia

25 tu ya bajeti ya maendeleo na asilimia 36 tu ya bajeti ya matumizi

mengineyo. Huu ni udhaifu mkubwa wa Serikali inayoongozwa na CCM.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, hali hii inasikitisha sana kwa kuwa hadi mwezi Machi,

tayari mfumo mpya wa Bajeti ulikuwa umetimiza robo tatu ya mwaka.

Tunajiuliza, hata kama Serikali ikiamua kutoa asilimia 75 ya fedha zilizobaki kwa

ajili ya miradi ya maendeleo katika robo mwaka iliyobaki, je, shughuli hizi za

maendeleo zitaleta tija na ufanisi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali ya

CCM kuacha kuwahadaa Wabunge na wananchi kila mwaka kwa kutenga

viwango vikubwa vya fedha katika kupitisha bajeti za Wizara, ilhali ikijua kuwa,

mosi; haina fedha hizo kwa kuwa ina matumizi makubwa yasiyoangalia

maendeleo na ustawi wa jamii wala kuakisi maisha ya umaskini ya Watanzania.

(Makofi)

Pili, Serikali ya CCM inajua kabisa haina uwezo wa kuleta maisha bora

kwa kila Mtanzania kama ilivyoahidi na kuwahadaa wananchi katika chaguzi

kuu, iwe kwa kasi mpya ama kwa Matokeo Makubwa Sasa! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2014/2015, Serikali ya CCM imetenga kiasi

cha shilingi bilioni tisa kwa ajili ya miradi ya maendeleo na shilingi bilioni 8.3 kwa

matumizi mengineyo. Je, fedha hizi zilizoombwa ni katika kutekeleza majukumu

ya kweli ya Wizara au zinasemwa ili kuwahadaa wananchi wakati kiuhalisia

Serikali inajua haina fedha za kutosha za kupeleka katika Wizara hii? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa Bajeti zinazotengwa kila mwaka kwa

Wizara hii ni ndogo, bado fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo

zinacheleshwa na hivyo kuathiri kasi ya Wizara katika kutekeleza majukumu

yake. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali kupunguza matumizi

yasiyo muhimu pamoja na kukusanya kodi ipasavyo ikiwemo kupunguza

misamaha ya kodi kwa makampuni na mashirika makubwa ili kuzipa uwezo

Wizara zinazohudumia wananchi kwa ujumla!

Mheshimiwa Spika, upungufu wa Wataalam wa Maendeleo ya Jamii.

Tumeshuhudia idadi kubwa ya wahitimu katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii

ambao hawana ajira. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali kutoa

Page 57: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

57

nafasi za ajira kwa wataalam wa maendeleo ya jamii ili kuweza kuziba

upungufu uliopo katika Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Spika, pia, changamoto kubwa iliyopo ni kukosekana kwa

nafasi za ajira kwa wataalam wa maendeleo ya jamii katika sekta mbalimbali.

Mwaka wa fedha wa 2012/2013, tulisema wazi kuwa wataalam wa maendeleo

ya jamii huhitimu vyuo mbalimbali, lakini kuwepo kwao hakuoneshi tija kwa

Taifa, hivyo, fani hii imeendelea kupuuzwa.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014 bado utekelezaji wa suala ili

umesuasua. Wizara ituambie ni mkakati gani uliopo ambao umewekwa kwa ajili

ya kukabiliana na upungufu wa wataalam wa maendeleo ya jamii ili kuweza

kuziba pengo katika Halmashauri kwa mwaka huu wa fedha wa 2014/2015? Pia

katika kuhakikisha kuwa Maafisa Maendeleo ya Jamii, wanapata nafasi za ajira

katika sekta mbalimbali nchini ili kuongeza tija kwa Taifa?

Mheshimiwa Spika, Vyuo vya Maendeleo ya Jamii. Kambi Rasmi ya

Upinzani Bungeni, inaendelea kusisitiza umuhimu wa kuboresha na kuhakikisha

kuwa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii na wananchi nchini vinapewa

kipaumbele. Tunaendelea kuibana Serikali kutoa majibu ni kwa nini imeendelea

kutoa kiwango kidogo cha fedha kwa ajili ya kukarabati majengo na

miundombinu katika vyuo ambavyo bado ni chakavu kutokana na ukosefu wa

matengenezo ya mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika, Vyuo hivi vimeendelea kukumbana na changamoto

nyingine kama vile uhaba wa vyombo vya usafiri, upungufu mkubwa wa

watumishi wa kada mbalimbali, nyumba za watumishi, madarasa, karakana,

mabweni, vifaa na mitambo ya kufundishia na kujifunzia.

Mheshimiwa Spika, hali za vyuo hivi inasikitisha sana na si kama ambavyo

viliachwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na kama Serikali hii sikivu ya

CCM ni waenzi na wafuasi wa sera za maendeleo za Baba wa Taifa,

wasingekuwa wa kwanza kuvidumaza, kuvipoteza na kuviua Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii ambavyo yeye alivipigania ili kujenga jamii ya haki, usawa

na utu.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015, fedha

zilizotengwa kwa ajili ya Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi (FDC) zilikuwa ni

shilingi bilioni 2.3 fedha za ndani, lakini, hadi kufikia mwezi Machi, 2014 kiasi cha

fedha za miradi ya maendeleo kilichotolewa kwa ajili ya Vyuo vya Maendeleo

ya Wananchi ni kiasi cha shilingi milioni 42. 2 sawa na asilimia 1.8 ya fedha zote

zilizotengwa. Aidha, ujenzi na ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii

ulitengewa kiasi cha shilingi milioni 100 ambapo hadi kufikia Machi, 2014 ni

milioni 25 sawa na asilimia 25 ya Fedha zilizotengwa.

Page 58: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

58

Swali kwa Serikali, je, kwa hali hii Serikali ya CCM ina nia ya dhati ya

kusimamia sekta ya Maendeleo ya Jamii nchini? Kambi Rasmi ya Upinzani

inaitaka Serikali kuipa kipaumbele Wizara hii na kuhakikisha kuwa fedha

zilizotengwa kwa ajili ya Maendeleo ya vyuo hivi zinatolewa kabla ya mwaka

wa fedha wa 2013/2014 ili kuviokoa vyuo hivyo ambavyo vingi ni chakavu na

havina uwezo wa kutosha kukabiliana na changamoto za uendeshaji ili kuleta

mwamko wa maendeleo katika jamii ya Kitanzania kwa kuongeza wataalam

wa kutosha wa fani hii.

Mheshimiwa Spika, kuporomoka kwa maadili nchini. Jamii ya Kitanzania

imegubikwa na vitendo vya picha zisizo za kimaadili ambazo husambazwa

katika mitandao ya kijamii. Tumeshuhudia picha na video mbalimbali za

Watanzania ambazo zinadhalilisha si tu jamii ya Kitanzania bali pia vinaondoa

thamani na utu wa binadamu. Kesi nyingi zimetokea ambapo watu walio katika

mahusiano hupiga picha chafu na wanapoachana picha hizo husambazwa

katika mitandao ya kijamii lakini wanaozisambaza hawachukuliwi hatua.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa, wanaopiga picha hizo wana

makosa lakini pia kuacha picha hizi zisambazwe katika mitandao ya kijamii na

blogu mbalimbali nayo inachangia kuporomosha maadili ya jamii yetu. Serikali,

kwa kupitia Wizara imechukua hatua gani ili kudhibiti vitendo hivyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani

kwa mwaka wa Fedha 2013/2014, tulizungumzia kuhusu vitendo vya kudhalilisha

wanawake, maarufu kama Kanga Moko na Wizara ilichukua hatua ya kufuatilia

na kutekeleza mapendekezo hayo ya Kambi ya Upinzani, lakini bado

tunashangaa kuona jinsi Watanzania walivyo wabunifu wa vitendo vya

kudhalilisha na ni washabiki wa mambo haya ambayo yanaendelea kutoa

taswira mbaya ya jamii ya Kitanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kumeibuka kitu kipya maarafu kama ngoma ya

Kigodoro ambayo inapigwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini hasa katika

Jiji la Dar es Salaam. Pia, ngoma hii imeambatana na matoleo ya filamu

ambazo zinaonesha vitendo hivyo si kwa lengo la kuielimisha jamii, lakini kwa

kushabikia vitendo hivyo hali inayochangia pia kuporomosha maadili ya jamii

ya Kitanzania.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa jambo la filamu linatakiwa

kusimamiwa na BASATA (Baraza la Sanaa la Taifa), lakini Wizara hii ina dhamana

ya kuhakikisha vitendo kama hivi vinakemewa na kudhibitiwa ili kulinda utu,

hadhi, thamani na utamaduni wa Mtanzania. Kwa mfano, mapema mwaka

huu huko Chanika Dar es Salaam, bibi mtu mzima alibakwa na kundi la vijana

Page 59: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

59

wasiojulikana waliokuwa wametoka katika ngoma ya kigodoro ambapo wakazi

wa maeneo mbalimbali hukesha kwa kucheza ngoma na muziki usiku kucha.

Mheshimiwa Spika, ndiyo maana halisi ya neno hili maarufu lilipotoholewa

na kwa maadili ya jamii yetu, hatuwezi kufafanua zaidi maana ya neno hili ila ni

jambo la aibu kubwa kwa jamii iliyo ya kistaarabu, kushabikia mambo kama

haya ambayo si tu yanadhalilisha utu wa Mtanzania bali pia yanachangia

kutokea kwa vitendo vya wizi na uporaji, ubakaji, ulawiti, ulevi, hali ambayo

inachangia kwa kiasi kikubwa kasi ya maambukizi ya UKIMWI na magonjwa

mengine ya kujamiiana.

Mheshimiwa Spika, mfumo dume na vitendo vya kikatili wa kijinsia dhidi ya

wanawake mwaka 1993, Azimio la Umoja wa Mataifa juu ya Kutokomeza Ukatili

Dhidi ya Wanawake liliutafsiri ukatili dhidi ya wanawake kama ifuatavyo:-

“Kitendo chochote cha ukatili wa kijinsia kinachosababisha au

kinachoweza kusababisha maumivu au mateso ya kimwili, kingono au kiakili

kwa wanawake, ikiwemo vitisho, kulazimishwa au kunyimwa uhuru

vinavyotokea katika jamii au kwenye maisha binafsi.”

Mheshimiwa Spika, Takwimu haziongopi. Utafiti wa mwaka 2010 unaohusu

afya na takwimu za uzazi, vifo na maradhi uliofanywa na Serikali pamoja na

utafiti wa matendo ya ukatili dhidi ya watoto ya mwaka 2011 unaonesha kuwa

asilimia 45 ya wanawake wametendewa ukatili wa kijinsia. Ukatili dhidi ya

wanawake majumbani umeendelea kuongezeka, ambapo takwimu

mbalimbali na tafiti zinaonesha kuwa kati ya wanawake watatu, wawili

wanatendewa ukatili wa kijinsia na waume zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake

vimeshamiri na ndio msingi mkuu wa sauti zetu sisi wenye dhamana kuwatetea

wanawake ambao ni nguzo za familia katika jamii zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Benki ya Wanawake Tanzania, kwa mujibu wa taarifa

ya Wizara, kwa kipindi cha kuanzia Julai 2013 Benki hii ilitoa jumla ya mikopo

9,380 yenye thamani ya shilingi bilioni 8.1, ambapo kati ya wateja hao

wanawake ni 7,395 sawa na asilimia 79 ya wateja wote waliopewa mikopo ni

wanawake. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Wizara kueleza, je, katika

mikopo hii iliyotolewa na Benki ya Wanawake wa Tanzania, ni asilimia ngapi

ilinufaisha wateja wa vijijini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, taarifa za Wizara zinaonesha kuwa, Benki hii

imefungua Tawi la pili katika Mkoa wa Dar es Salaam, jambo ambalo

limeendelea kuleta malalamiko kuwa Benki hii haina msaada kwa watu walio

mbali na Mkoa huo. Hali kadhalika, benki imefungua vituo 29 vya kutolea

Page 60: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

60

mikopo kwa wajasiriamali wadogo kwenye Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma

na Mwanza. Bado swali lipo, je, watu walio katika Kanda ya Kusini za Iringa,

Mbeya, Mtwara, Lindi na Kaskazini kwa mfano, Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na

Tanga imewekewa mkakati gani kwa mwaka huu wa 2014/2015 ili kuwafikia

wajasiriamali wengine ambao hawana uwezo wa kufikia huduma hizo katika

vituo tajwa kutokana na uwezo wao mdogo wa kifedha na umbali wa vituo?

(Makofi)

SPIKA: Mnajua mkipiga makofi sana, hatusikii anachokisema. Naomba

uendelee Mheshimiwa Barwany!

MHE. SALUM K. BARWANY - MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI

KWA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

uendeshaji wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali; kumekuwa na ongezeko la

uandikishwaji wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, ambapo tunakiri kuwa

yanatekeleza majukumu makubwa katika kusimamia maendeleo ya jamii.

Changamoto kubwa ni uwepo wa baadhi ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

ambayo yameanzishwa mifukoni yakapewa usajili na kunufaika na fedha za

ufadhili ambazo kimsingi huwa haziwafiki walengwa.

Mheshimiwa Spika, Mashirika haya yamesajiliwa, lakini yamekuwa

yakiwatumia watoto yatima wanaoishi katika mazingira magumu kama

chambo cha kupata misaada kutoka kwa wafadhili ambayo huwa haitumiki

kuwaendeleza wala kuwahudumia walengwa ipasavyo. Kambi Rasmi ya

Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali sio kuwasilisha muhtasari wa matokeo

iliyoyachagua bali ripoti kamili ya tafiti zilizofanywa kuhusu mchango wa

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa mwaka 2012. Aidha, kufuatia kuwasilishwa

kwa taarifa hiyo, pongezi zitolewe kwa mashirika yaliyofanya vizuri na orodha ya

mashirika yaliyoshindwa kutimiza wajibu wake.

Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine, ili kutokuingilia uhuru wa

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, wakati umefika sasa wa Serikali kuwasilisha Bungeni

Muswada wa Marekebisho ya Sheria inayosimamia Mashirika hayo kwa

kuzingatia kwamba Sheria hiyo ilipitishwa „kwa nguvu‟ huku kukiwa na

malalamiko miongoni mwa wadau.

Mheshimiwa Spika, kwa upande mwingine, Kambi Rasmi ya Upinzani

inaitaka Serikali kueleza hatua ilizochukua dhidi ya Shirika Lisilo la Kiserikali liitwalo

Wanawake na Maendeleo (WAMA) ambalo Mwenyekiti wake ni Mama Salma

Kikwete, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. WAMA

ilituhumiwa ndani ya Bunge hili mwezi Aprili 2012 kwamba ilitumiwa kisiasa na

Mama Kikwete kwenye Kampeni za Uchaguzi za mwaka 2010 kwa lengo la

kumsaidia aliyekuwa mgombea Urais wa CCM wakati huo Mheshimiwa Jakaya

Mrisho Kikwete.

Page 61: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

61

Mheshimiwa Spika itakumbukwa kwamba kufuatia majibu ya Waziri wa

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mheshimiwa Sophia Simba Bungeni ya

mwaka huo wa 2012 kuhusu madai hayo kutokuridhisha, mwongozo uliombwa

kwa Spika kuwezesha hatua kuchukuliwa dhidi yake, lakini mpaka sasa

muongozo huo haujatolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali inayoongozwa na CCM imekuwa ikiyafuta

Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yasiyofungamana na chama chochote pale

ambapo inaona yanafanya harakati za kudai haki kwa niaba ya makundi

mbalimbali ya kijamii kama ilivyolifuta Baraza la Wanawake Tanzania (BAWATA)

na Shirika la Vijana la National Youth Forum (NYF).

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, Serikali hiyo hiyo imekuwa ikifumbia

macho pale Mashirika yanapotumika kisiasa kwa manufaa ya CCM na Serikali

yake. Hali hii imeachwa muda mrefu na kuota mizizi mpaka Taifa limeshuhudia

uteuzi wa wajumbe 201, wengi wao wakiwa wanatoka kwenye Mashirika na

Taasisi zingine Zisizo za Kiserikali iwe ni Asasi za Kiraia, Taasisi za Dini na nyinginezo

namna ulivyofanyika sehemu kubwa kwa maslahi ya CCM. Matokeo yake ni

kutengenezwa kwa „genge la kutetea misimamo ya CCM‟ kinyume na Rasimu

iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa kuzingatia maoni ya

wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, changamoto za watu wenye ulemavu nchini; Watu

wenye ulemavu ni watu ambao wanatakiwa kuthaminiwa katika jamii kutokana

na hali halisi ya maumbile yao waliyozaliwa nayo. Hivyo basi, ni budi jamii hiyo

ikapewa kipaumbele katika masuala muhimu nchini hususani masuala ya elimu,

afya, uwezeshaji wa kiuchumi, uongozi pamoja na masuala mengine ya kijamii

ikiwemo michezo na ushirikishwaji katika maamuzi.

Mheshimiwa Spika, ni jambo la kusikitisha kuwa pamoja na umuhimu

wake katika Taifa letu, lakini Wizara hii imeshindwa kuweka katika majukumu

yake, jukumu la kulinda na kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa

kuwaendeleza, kuwalinda na kuhakikisha kuwa hawabaguliwi na wanapewa

hadhi sawa na wananchi wengine wote katika ngazi zote.

Mheshimiwa Spika, kuuawa kwa mwanamke Munghu Lugata, mlemavu

wa ngozi toka Kijiji cha Gasuma, Mkoani Simiyu, Kaskazini Magharibi mwa nchi

yetu, kumeacha hisia na uchungu kwa walemavu wengine waliopata mikasa

hiyo. Matukio mengi ya mauaji ya walemavu nchini yamekuwa yakihusishwa

na imani za kishirikina huku waganga wa jadi wakihusishwa.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Simiyu ni moja katika maeneo ya Kaskazini

Magharibi mwa Tanzania yenye matukio mengi ya mauaji hayo. Mikoa mingine

Page 62: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

62

kwa mujibu wa takwimu za Shirika Lisilo la Kiserikali la Under the Same Sun,

zinaonesha kuwa Mikoa mingine kama Tabora, Shinyanga, Rukwa, Mara na

Kagera pia inaongoza kwa matukio ya kikatili dhidi ya walemavu.

Mheshimiwa Spika, aidha, taarifa zaidi zinaeleza kuwa mpaka mwezi Mei

mwaka huu yameripotiwa matukio 140 dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi;

73 yaliyopelekea mauaji na 67 yakiwa ni mashambulio ya kujeruhi katika

sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo kukatwa kwa viungo kama mikono, miguu,

vidole na cha kusikitisha zaidi asilimia 75 ya matukio hayo yalilengwa kwa

wanawake na watoto.

Mheshimiwa Spika, Mwaka 2010, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati

akiwahutubia wananchi, kwenye maadhimisho ya Siku ya Walemavu wa Ngozi

Tanzania yaliyofanyika viwanja vya Garden Mkoani Iringa alisema kuwa:

“Napenda kuwaonya watu wote wanaojihusisha na vitendo viovu vya ukataji

wa viungo na wauaji wa walemavu wa ngozi popote walipo kuwa siku zao

zinahesabika. Ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi nawahakikishia Serikali

itashinda vita hii na mtaishi kwa uhuru ndani ya nchi yenu.”

Mheshimiwa Spika, ikiwa imepita takribani miaka minne toka Waziri Mkuu

atoe kauli hiyo, je, matukio ya ulemavu yamepungua kwa kiasi gani? Je, siku za

watu wanaofanya vitendo vya ukatili dhidi ya walemavu zimeshahesabika au

bado zinaendelea kuhesabika? Je, Wizara hii imeweka mikakati gani

kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapewa kipaumbele katika shughuli za

maendeleo ya jamii ili kujenga utu na usawa katika jamii yetu?

Mheshimiwa Spika, matukio yafuatayo yameonesha kuwa kauli za Serikali

pamoja na machozi ya Waziri Mkuu hayajaweza kutatua vitendo vya kikatili

dhidi ya watu wenye ulemavu hasa wa ngozi kwa kuwa yametokea sehemu

mbalimbali nchini kama ilivyoorodheshwa katika ripoti ya Kituo cha Sheria na

Haki za Binaadamu;

Mheshimiwa Spika, Mwaka 2013, Maria Chambanenge wa Sumbawanga,

alikatwa mkono na wavamizi wawili ambao walikamatwa hapohapo na mkono

wa mhanga, ulikutwa kwa Mganga wa Kienyeji ambapo katika tukio hilo mtoto

mdogo wa Bi. Maria naye alijeruhiwa.

Mheshimiwa Spika, Mwezi Februari mwaka 2013, tukio lingine dhidi ya

Mwigulu Magese Matonange wa Sumbawanga aliyekuwa akitoka shule

alikatwa mkono na wavamizi wawili ambao walikimbia nao. Mwezi huo huo

pia, Makunga Baraka wa Simiyu alivamiwa na kundi la watu ambao

hawakufanikiwa baada ya kufukuzwa na wanakijiji na kufanikiwa kukimbia.

Page 63: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

63

Mheshimiwa Spika, Ndugu Lugogola Bunzari wa Tabora, aliuliwa baada

ya mkono wake kukatwa kinyama na nywele zake kuvutwa kikatili pamoja na

ngozi ya paji lake kuchunwa huku Babu yake Bunzari Shinga (miaka 97) aliuliwa

wakati akimsaidia mjukuu wake na wakati huo baba wa marehemu aliumizwa

vibaya katika jaribio la kumsaidia mwanae.

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka jamii

kubadilika na kuachana na imani potofu ambazo zinahatarisha maisha na

usalama wa watu wengine na ambazo zinarudisha nyuma jitihada

zinazofanywa za kupiga vita ukatili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi,

Tanzania wanawake na watoto.

Mheshimiwa Spika, hali kadhalika, tunawataka wananchi wote,

kuwafichua wale wote wanaojishughulisha na vitendo viovu na kutoa taarifa

kwa vyombo vya dola na mamlaka sahihi ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa kwa

mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Spika, Pensheni kwa Wazee; suala la pensheni kwa Wazee

sasa limekuwa wimbo ambao wananchi wameuchoka. Kwa muda mrefu suala

hili limekuwa likipigwa danadana, kuanzia Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Kazi

na Ajira, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Wizara ya Fedha, ni wazi kuwa

hata Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii, Wanawake, Jinsia na Watoto inajaribu

kukwepa utekelezaji huu wa ahadi ambayo Serikali ya CCM ilitumia ili kupata

kura za wazee kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2005 na 2010.

Mheshimiwa Spika, dhamana ya kulisimamia suala la wazee ni la

Maendeleo ya Jamii kwa kuwa wazee ni sehemu ya jamii na Wizara ina wajibu

mkubwa wa kuhakikisha wazee hawa wanapata huduma zao muhimu kama

vile CCM imekuwa ikijinadi kwenye Ilani zake za Uchaguzi. Umefika wakati sasa,

Waziri mwenye dhamana atoe maelezo ya kina, ni mikakati gani ambayo

Wizara imejiwekea ili kuhakikisha suala la pensheni kwa wazee linatekelezwa

kwa mwaka huu wa fedha wa 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Watoto; Ongezeko la Watoto wa

Mitaani na athari zake katika Taifa; wakati piramidi ya idadi ya watu nchini

Tanzania inaonesha kuwa idadi kubwa ya watu nchini Tanzania ni watoto

wenye umri wa chini ya miaka 15 na vijana, asilimia 44 ya watu wote hapa

nchini ni watoto wenye umri chini ya miaka 15, ambapo ongezeko la watoto

wa mitaani limeendelea kuwa na athari huku sababu mbalimbali kama

umaskini katika familia, mifarakano na ukosefu wa amani kwenye familia na

wazazi kutowajibika katika malezi na makuzi ya watoto wao vikipelekea watoto

hao kuishi katika mazingira hatarishi.

Page 64: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

64

Mheshimiwa Spika, sababu nyingine ni vitendo vya ukatili, udhalilishaji na

unyanyasaji wa watoto kutoka kwa familia na jamii kwa ujumla; nyingine ni

kufariki kwa wazazi hasa kutokana na magonjwa mbalimbali, pia huchangiwa

na ndoa za umri mdogo pamoja na mimba zisizotarajiwa.

Mheshimiwa Spika, inasikitisha kuona kuwa vitendo vya ukatili na

udhalilishaji dhidi ya watoto vimeendelea kuongezeka na vingine kufumbiwa

macho huku Serikali ya CCM ikiwa kimya dhidi ya wahalifu wanaotenda

vitendo hivyo, kwani mara kadhaa imeripotiwa kwenye Vyombo vya Habari

kufuatia watuhumiwa na vitendo hivyo kuachiwa na Vyombo vya Usalama

katika mazingira ya rushwa na kulindana.

Mheshimiwa Spika, ripoti ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)

nchini Tanzania imesema watoto wapatao 800 walilawitiwa mwaka 2013.

Inashangaza pia kuona baadhi ya kesi za ulawiti na ubakaji humalizwa nje ya

Mahakama ama mfumo wa Sheria jambo ambalo linaendelea kuhatarisha

maisha na ustawi wa watoto hapa nchini. Serikali ni lazima ikabiliane na kesi

zote za ulawiti na ubakaji kwa uangalifu mkubwa na hata kwa kuhakikisha kuwa

washtakiwa wanafikishwa mbele ya Vyombo vya Sheria hata kama familia za

waathirika zimekubaliana kumalizana nje ya mfumo huo ili kujenga jamii ya

kistaarabu yenye kuheshimu na kuwalinda watoto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, taarifa yangu ni ndefu, naomba iwekwe yote katika

Hansard.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya watoto hawa wa kike wamekuwa

wakikatishwa masomo yao kutokana na kufanyiwa vitendo vya kudhalilishwa

au kuozwa ndoa za utotoni, lengo likiwa ni mzazi kujipatia fedha zinazotokana

na mahari. Baadhi ya watoto na wanawake kutokana na vitendo hivyo

wamekuwa wakiambukizwa magonjwa yakiwemo ya ngono yanayowafanya

kujutia kuishi kwao na wakati mwingine wakifikiria ni bora wasingezaliwa.

Mheshimiwa Spika, maoni na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali;

katika ripoti ya jumla ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu

ukaguzi maalum kwa kipindi kinachoishia tarehe 31 Machi, 2014, ilitaja sababu

nne kubwa zifuatazo zinazofanya Serikali kushindwa kutoa huduma za msingi

kwa watoto wanaoishi katika Mazingira magumu:-

(i) Uwepo wa mifumo isiyo endelevu na isiyokidhi viwango.

(ii) Kutokuwepo kwa Maafisa wa Ustawi wa Jamii wa kutosha katika

maeneo mbalimbali.

Page 65: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

65

(iii) Kutokuwa na uratibu katika ngazi zote za Serikali kwa kuwa kila

taasisi iwe ni katika Serikali (katika ngazi ya Kitaifa au Serikali za Mitaa) au

washirika wanaotekeleza utoaji wa huduma za msingi kwa watoto wanaoishi

katika mazingira magumu.

Mheshimiwa Spika, Mitandao ya Utumwa wa Kingono ndani ya Nchi; ni

dhahiri kuwa, maendeleo ya jamii lazima yaangalie pia ustawi wa jamii ikiwemo

kuwalinda vijana wa Kitanzania, wasichana na wavulana kutoka katika utumwa

wa kingono. Hapa nchini, kumekuwa na mtandao mpana unaochukua

wasichana toka vijijini na kuwaleta mijini kwa kisingizio cha kuwafanyisha kazi za

ndani, lakini huishia kuwa makahaba jambo ambalo si sahihi kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mitandao ya Utumwa wa Kingono Nje ya Nchi; wimbi

la mabinti wa Kitanzania wanaosafiri nchi za nje, limeongezeka, lakini pia likiwa

limebeba taswira mbaya kwa Taifa letu kwa ujumla. Ni dhamana ya Wizara hii

kuhakikisha kuwa, maendeleo ya jamii hasa haki za wanawake zinalindwa na

kupiganiwa kwa hali na mali hata kama suala la kisera linasimamiwa na Wizara

nyingine kwa mfano, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mheshimiwa Spika, taarifa mbalimbali za kuaminika zinaonesha kuwa

kuna mitandao ya wanaowasafirisha wasichana hao wa Kitanzania kutoka

nchini inafanya hivyo kwa makubaliano ya kuwatafutia ajira katika hoteli kubwa

na badala yake wanapofika nchi za nje kwa mfano China, huwafanyisha

wasichana hao vitendo vya ukahaba bila ridhaa yao. Mitandao hiyo

ikishasafirisha wasichana hao huwanyang‟anya wasichana hao passport zao za

kusafiria na kujikuta wakishindwa kurejea nchini hali inayowafanya waendelee

kuwa watumwa wa kingono na ukahaba.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya wasichana, waliosafirishwa nchi nyingine

mbalimbali duniani wamebainika pia kujihusisha na biashara za dawa za

kulevya. Aidha, tunaitaka Wizara hii kukomesha mitandao yote ya kingono

iliyopo ndani ya nchi kwa kuwa tatizo hili ni pana zaidi ya linavyozungumzwa.

Tunaitaka Wizara, kuanzisha msako rasmi wa madanguro yote kwa kushirikiana

na Wizara nyingine zenye dhamana ili kudhibiti mtandao huu ambao umevuka

mipaka.

Mheshimiwa Spika, ni rai ya Kambi ya Upinzani kuwa Serikali sasa itakuwa

macho na vitendo vyote vya udhalilishaji ili kuweza kujenga jamii yenye

kuheshimu, kulinda na kuthamini utu kama moja ya nguzo muhimu za jamii.

Mheshimiwa Spika, Marekebisho ya Sheria; Sheria ya Ndoa ya Mwaka

1971 ni kati ya Sheria zinazotajwa kuwa kandamizi hasa kwa kuwa imepitwa na

wakati. Wakati Maboresho ya Sera na Sheria nyingine zimefanywa kutokana na

mazingira na wakati, sheria hii imeendelea kutumika kwa takribani miaka 42

Page 66: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

66

huku marekebisho yake yakichukua muda mrefu. Tunasikitishwa na mlolongo

mrefu uliopo katika kuboresha sheria hii kandamizi, kwa kuwa inatoa mwanya

kwa ndoa za utotoni hasa ukizingatia kuwa inaeleza kuwa mtoto wa kike wa

miaka 15 anaweza kuolewa.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kuwa Sheria hii ipo katika hatua za

Marekebisho ila ni wakati sasa Serikali ifanye jitihada zaidi kuhakikisha sheria hii

inafanyiwa marekebisho kabla ya mwaka 2014 kwisha. Aidha; Sheria ya Elimu

ya mwaka 1978 iliyofanyiwa marekebisho 2002 inayoruhusu mwanafunzi

mjamzito kufukuzwa shule, ni kati ya Sheria zinazopigiwa makelele kwa kuwa

zinawanyima watoto wa kike fursa ya kujiendeleza kielimu mara baada ya

kujifungua. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali kusimamia msingi

wa kuwapa nafasi watoto wa kike…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante.

MHE. SALUM K. BARWANY - MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI

KWA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

nashukuru na naomba kuwasilisha. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana kwa kusoma vizuri.

Taarifa ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Kuhusu Bajeti ya Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka 2014/2015 kama

ilivyowasilishwa Mezani

HOTUBA YA MHESHIMIWA SALUM KHALFAN BARWANY (MB) MSEMAJI MKUU WA

KAMBI RASMI YA UPINZANI WIZARA

YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

NA MATUMIZI KWA

MWAKA WA FEDHA 2014/2015

(Inatolewa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge kanuni ya 99(9) Toleo la

mwaka 2013)

1.0 UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, Kwa mujibu wa kanuni za kudumu za Bunge, Kanuni ya 99

(9) naomba kuwasilisha maoni ya Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni ya

makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha wa 2014/2015 ya

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

Page 67: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

67

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii Mosi, kumshukuru Mwenyezi

Mungu kwa kunipa uzima na afya. Pili, kwa Kiongozi wa Kambi Rasmi ya

Upinzani Bungeni kwa imani kubwa aliyokua nayo kwangu na kwa uteuzi huu

wa kuwa Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni. Aluta Continua!

Mheshimiwa Spika; Maendeleo ya Jamii ni dhana yenye dhima ya kuwezesha

wananchi kutambua uwezo wao na changamoto zilizopo na kutumia rasilimali

zilizopo katika kukabiliana na maadui ujinga, umasikini, maradhi na ufisadi.

Maendeleo ya jamii yanaweka mkazo katika kushirikisha umma katika kufikiri,

kuamua, kupanga na kutekeleza mambo yanayohusu maisha yao na taifa lao.

Kwa kuzingatia dhana hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ina

dhima ya pekee katika ustawi na uchumi wa wananchi na nchi kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika; Hata hivyo, Wizara hii imekuwa ikichukuliwa kwa mtizamo

potofu kuwa ni „Wizara ya Wanawake‟ na hivyo kuacha kuyapa uzito

unaostahili masuala ambayo yanashughulikiwa na Wizara hii ya maendeleo ya

jamii, jinsia na watoto.

Maoni haya ya Kambi Rasmi ya Upinzani ninayoyawasilisha yajadiliwe na

wabunge wengine na kujibiwa kwa ukamilifu na Serikali kuwezesha mabadiliko

na maendeleo ya jamii yenye usawa wa kijinsia nchini.

1.1 MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO NA BAJETI YA

MWAKA 2013/2014

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Machi 2014 wizara hii ilipokea asilimia 25 tu ya

bajeti ya maendeleo na asilimia 36 tu ya bajeti ya matumizi mengineyo. Huu ni

udhaifu mkubwa wa Serikali inayoongozwa na CCM. Hali hii inasikitisha sana

kwa kuwa hadi mwezi Machi, tayari mfumo mpya wa Bajeti ulikuwa umetimiza

robo tatu ya mwaka. Tunajiuliza, hata kama Serikali ikiamua kutoa asilimia 75 ya

fedha zilizobaki kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika robo mwaka iliyobaki, je

shughuli hizi za maendeleo zitaleta tija na ufanisi? Kambi rasmi ya Upinzani

Bungeni inaitaka Serikali ya CCM kuacha kuwahadaa wabunge na wananchi

kila mwaka kwa kutenga viwango vikubwa vya fedha katika kupitisha bajeti za

wizara, ilhali ikijua kuwa, mosi; haina fedha hizo kwa kuwa ina matumizi

makubwa yasiyoangalia maendeleo na ustawi wa jamii wala kuakisi maisha ya

umasikini ya watanzania, pili; Serikali ya CCM inajua kabisa haina uwezo wa

kuleta maisha bora kwa kila mtanzania kama ilivyoahidi na kuwahadaa

wananchi katika chaguzi kuu, iwe kwa kasi mpya ama kwa matokeo makubwa

sasa!

Page 68: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

68

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2014/2015 Serikali ya CCM imetenga kiasi cha

shilingi Bilioni 9 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na shilingi bilioni 8.3 kwa

matumizi mengineyo. Je, fedha hizi zilizoombwa ni katika kutekeleza majukumu

ya kweli ya wizara au zinasemwa ili kuwahadaa wananchi wakati kiuhalisia

Serikali ya CCM inajua haina fedha za kutosha za kupeleka katika wizara hii?

Pamoja na kuwa Bajeti zinazotengwa kila mwaka kwa wizara hii ni ndogo, bado

fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya maendeleo zinacheleshwa na hivyo

kuathiri kasi ya Wizara katika kutekeleza majukumu yake. Kambi Rasmi ya

Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali kupunguza matumizi yasiyo muhimu pamoja

na kukusanya kodi ipasavyo ikiwemo kupunguza misamaha ya kodi kwa

makampuni na mashirika makubwa ili kuzipa uwezo Wizara zinazohudumia

wananchi kwa ujumla!

2.0 MAENDELEO YA JAMII

2.1 UPUNGUFU WA WATAALAMU WA MAENDELEO YA JAMII

Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu tumeelezea changamoto za upungufu

wa wataalamu wa maendeleo ya jamii ambapo hali hairidhishi katika ngazi ya

Kata na Kijiji, ambako wataalamu hao wanahitajika zaidi kuwafikia Wananchi

na kuwahamasisha ili kujiletea maendeleo yao. Sera ya Maendeleo ya Jamii

imeelekeza awepo angalau mtaalamu mmoja wa Maendeleo ya Jamii kwenye

kila Kata. Hivi sasa ni asilimia 56 tu ya Kata zote 2,637 zina Wataalam wa

Maendeleo ya Jamii. Hii ina maana kuna upungufu wa wataalam 2045 kwenye

kata nchini. Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kuhakikisha kuwa,

maafisa maendeleo ya jamii wanatengewa fungu la kutosha ili kuweza

kutawanywa katika kata zote nchini ili kutekeleza shughuli za maendeleo ya

jamii.

Mheshimiwa Spika, tumeshuhudia idadi kubwa ya wahitimu katika vyuo vya

maendeleo ya jamii ambao hawana ajira. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,

inaitaka Serikali kutoa nafasi za ajira kwa wataalamu wa maendeleo ya jamii ili

kuweza kuziba upungufu uliopo katika halmashauri zetu. Lakini pia,

changamoto kubwa iliyopo ni kukosekana kwa nafasi za ajira kwa wataalamu

wa maendeleo ya jamii katika sekta mbalimbali. Mwaka wa fedha wa

2012/2013, tulisema wazi kuwa wataalamu wa maendeleo ya jamii huitimu vyuo

mbalimbali, lakini kuwepo kwao hakuoneshi tija kwa taifa, hivyo fani hii

imeendelea kupuuzwa. Mwaka 2013/2014 bado utekelezaji wa suala ili umesua

sua. Wizara ituambie ni mkakati gani uliopo ambao umewekwa kwa ajili ya

kukabiliana na upungufu wa wataalamu wa maendeleo ya jamii ili kuweza

kuziba pengo katika halmashauri kwa mwaka huu wa fedha wa 2014/2015 ?

lakini pia katika kuhakikisha kuwa maafisa maendeleo ya jamii, wanapata

nafasi za ajira katika sekta mbalimbali nchini ili kuongeza tija kwa taifa?

Page 69: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

69

2.2 VYUO VYA MAENDELEO YA JAMII

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inaendelea kusisitiza

umuhimu wa kuboresha na kuhakikisha kuwa vyuo vya maendeleo ya jamii na

wananchi nchini vinapewa kipaumbele. Tunaendelea kuibana Serikali kutoa

majibu ni kwa nini imeendelea kutoa kiwango kidogo cha fedha kwa ajili ya

kukarabati majengo na miundombinu katika vyuo ambavyo bado ni chakavu

kutokana na ukosefu wa matengenezo ya mara kwa mara. Vyuo hivi

vimeendelea kukumbana na changamoto nyingine ambazo kama vile uhaba

wa vyombo vya usafiri, upungufu mkubwa wa watumishi wa kada mbalimbali,

nyumba za watumishi, madarasa, karakana, mabweni, vifaa na mitambo ya

kufundishia na kujifunzia.

Mheshimiwa Spika, hali za vyuo hivi inasikitisha sana na si kama ambavyo

viliachwa na Baba wa Taifa, Hayati J. K Nyerere! Na kama Serikali hii sikivu ya

CCM ni waenzi na wafuasi wa sera za maendeleo za Baba wa Taifa,

wasingekua wa kwanza kuvidumaza, kuvipoteza na kuviua vyuo vya

maendeleo ya jamii ambavyo Yeye alivipigania ili kujenga jamii ya haki, usawa

na utu.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015 fedha zilizotengwa

kwa ajili ya vyuo vya maendeleo ya wananchi (FDC) zilikuwa ni shilingi bilioni 2.3

fedha za ndani. Lakini, hadi kufikia mwezi Machi 2014 kiasi cha fedha cha miradi

ya maendeleo kilichotolewa kwa ajili ya vyuo vya maendeleo ya wananchi ni

kiasi cha shilingi milioni 42. 2 sawa na asilimia 1.8 ya fedha zote zilizotengwa.

Aidha, ujenzi na ukarabati wa vyuo vya maendeleo ya jamii ulitengewa kiasi

cha shilingi milioni 100 ambapo hadi kufikia Machi 2014 m ni milioni 25 sawa na

asilimia 25 ya Fedha zilizotengwa. Swali kwa Serikali, je kwa hali hii Serikali ya

CCM ina nia ya dhati ya kusimamia sekta ya Maendeleo ya Jamii nchini? Kambi

rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuipa kipaumbele wizara hii na kuhakikisha

kuwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya Maendeleo ya vyuo hivi zinatolewa kabla

ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 ili kuviokoa vyuo hivyo ambavyo vingi ni

chakavu na havina uwezo wa kutosha kukabiliana na changamoto za

uendeshaji ili kuleta mwamko wa maendeleo katika jamii ya kitanzania kwa

kuongeza wataalamu wa kutosha wa fani hii.

2.3 KUPOROMOKA KWA MAADILI NCHINI

Mheshimiwa Spika, ni masikitiko makubwa kuwa jamii ya kitanzania sasa imezidi

kuporomoka maadili kila kukicha. Na kadri Serikali inapokua kimya kukemea

vitendo vichafu vinavyochafua taswira ya jamii ya Kitanzania, maadili yetu

yanazidi kuteketea hasa kutokana na masuala ya ukuaji wa teknolojia nchini.

Page 70: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

70

Mheshimiwa Spika, jamii ya kitanzania imegubikwa na vitendo vya picha zisizo

za kimaadili ambazo husambazwa katika mitandao ya kijamii. Tumeshuhudia

picha na video mbalimbali za watanzania ambazo zinadhalilisha si tu jamii ya

kitanzania bali pia vinaondoa thamani na utu wa binadamu. Kesi nyingi

zimetokea ambapo watu walio katika mahusiano hupiga picha chafu na

wanapoachana picha hizo husambazwa katika mitandao ya kijamii lakini

wanaozisambaza hawachukuliwi hatua. Pamojana kuwa, wanaopiga picha

hizo wana makosa lakini pia kuacha picha hizi zisambazwe katika mitandao ya

kijamii na blogu mbalimbali nayo inachangia kuporomosha maadili ya jamii

yetu. Serikali, kwa kupitia wizara imechukua hatua gani ili kudhibiti vitendo

hivyo?

Mheshimiwa Spika, katika hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani kwa

mwaka wa Fedha 2013/2014 tulizungumzia kuhusu vitendo vya kudhalilisha

wanawake maarufu kama Kanga Moko na Wizara ilichukua hatua ya kufuatilia

na kutekeleza mapendekezo hayo ya Kambi ya Upinzani, lakini bado

tunashangaa kuona jinsi Watanzania walivyo wabunifu wa vitendo vya

kudhalilisha na ni washabiki wa mambo haya ambayo yanaendelea kutoa

taswira mbaya ya jamii ya kitanzania.

Mheshimiwa Spika, kumeibuka kitu kipya maarafu kama ngoma ya Kigodoro-

Kantangaze ambayo inapigwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini hasa

katika jiji la Dar es Salaam. Lakini pia, ngoma hii imeambatana na matoleo ya

filamu ambazo zinaonesha vitendo hivyo si kwa lengo la kuielimisha jamii lakini

kwa kushabikia vitendo hivyo hali inayochangia pia kuporomosha maadili ya

jamii ya Kitanzania.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa jambo la filamu linatakiwa kusimamiwa na

BASATA (Baraza la Sanaa la Taifa), lakini wizara hii ina dhamana ya kuhakikisha

vitendo kama hivi vinakemewa na kudhibitiwa ili kulinda utu, hadhi, thamani na

utamaduni wa mtanzania. Kwa mfano, mapema mwaka huu huko Chanika Dar

es Salaam, bibi mtu mzima alibakwa na kundi vijana wasiojulikana waliokua

wametoka katika ngoma ya kigodoro ambapo wakazi wa maeneo mbalimbali

hukesha kwa kucheza ngoma na muziki usiku kucha. Na ndo maana halisi ya

neno hili maarufu lilipotoolewa, na kwa maadili ya jamii yetu, hatuwezi

kufafanua zaidi maana ya neno hili ila ni jambo la aibu kubwa kwa jamii iliyo ya

kistaarabu kushabikia mambo kama haya ambayo si tu yanadhalilisha utu wa

mtanzania bali pia yanachangia kutokea kwa vitendo vya wizi na uporaji,

ubakaji, ulawiti, ulevi , hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa kasi ya

maambukizi ya UKIMWI na magonjwa mengine ya kujamiiana.

3.0 MFUMO DUME NA VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE

Page 71: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

71

Mheshimiwa Spika, mwaka 1993, Azimio la Umoja wa Mataifa juu ya

Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake lliutafsiri ukatili dhidi ya wanawake

kama:

“Kitendo chochote cha ukatili wa kijinsia kinachosababisha au

kinachoweza kusababisha maumivu au mateso ya kimwili, kingono au

kiakili kwa wanawake, ikiwamo vitisho, kulazimishwa au kunyimwa uhuru

vinavyotokea katika jamii au kwenye maisha binafsi.”

Mheshimiwa Spika, Kama ilivyoandikwa katika Mwongozo wa Sera ya Ukatili wa

Kijinsia (MOHSW 2011), ukatili wa kijinsia (GBV) ni tatizo kubwa ambalo

linawanyima uhuru wanaume, wanawake na watoto kufurahia haki za msingi za

binadamu na kufanya wapendavyo. Licha ya tatizo hilo kuwepo katika nchi

nyingi duniani lakini halipewi kipaumbele wala halishughulikiwi ipasavyo. Ukatili

wa kijinsia unatokana na tofauti za kijinsia na baadhi ya mila na desturi potofu

ambazo mara nyingi zinasababisha kuwepo kwa tofauti za kijinsia katika ngazi

mbalimbali za jamii. Wanawake kutothaminiwa katika familia, hali duni ya

uchumi na kutofahamu sheria kunawafanya washindwe kupata msaada pindi

kunapotokea ukatili wa kijinsia.

Mheshimiwa Spika, Takwimu haziongopi. Utafiti wa mwaka 2010 unaohusu afya

na takwimu za uzazi, vifo na maradhi uliofanywa na serikali pamoja na utafiti wa

matendo ya ukatili dhidi ya watoto ya mwaka 2011 unaonyesha kuwa asilimia

45 ya wanawake wametendewa ukatili wa kijinsia. Ukatili dhidi ya wanawake

majumbani umeendelea kuongezeka, ambapo takwimu mbalimbali na tafiti

zinaonesha kuwa kati ya wanawake watatu, wawili wanatendewa ukatili wa

kijinsia na waume zao.

Vilevile, utekelezaji wa Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 inayowapa haki

wanawake na wanaume kuuza na kumiliki ardhi umekuwa mgumu kwa sababu

idadi kubwa ya wanawake mijini na vijijini haiwajui sheria hii. Changamoto

mbalimbali ikiwemo, upatikanaji wa hati miliki umekuwa ni mgumu kwa

wanawake kutokana na kipato kidogo, mfumo dume na kutokuwa na

ushirikiano mzuri baina ya wanawake, wanaume na taasisi zinazosimamia sekta

hii.

Mheshimiwa Spika, katika misingi ya kuhakikisha jamii ya kitanzania inayapa

uzito masuala ya ukatili wa kijinsia na kupinga vitendo vyote vinavyodhalilisha

na kushusha thamani ya mwanamke, Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali

kueleza hatua madhubuti ambazo zitasaidia kukabiliana na matatizo haya

ukiachana na kutoa elimu kwa umma, kuandaa semina kwa mwaka huu wa

2014/2015.

Page 72: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

72

Mheshimiwa Spika, vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake

vimeshamiri na ndio msingi mkuu wa sauti zetu sisi wenye dhamana kuwatetea

wanawake ambao ni nguzo za familia katika jamii zetu.

3.1 Benki ya Wanawake Tanzania

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taarifa ya Wizara, kwa kipindi cha kuanzia

Julai 2013 Benki hii ilitoa jumla ya mikopo 9380 yenye thamani ya shilingi bilioni

9.1 ambapo kati ya wateja hao wanawake ni 7395 sawa na asilimia 79 ya

wateja wote waliopewa mikopo ni wanawake. Kambi rasmi ya Upinzani

Bungeni inaitaka Wizara kueleza, je katika mikopo hii iliyotolewa na Benki ya

Wanawake wa Tanzania, ni asilimia ngapi ilinufaisha wateja wa vijijini?

Mheshimiwa Spika, taarifa za Wizara zinaonyesha kuwa Benki hii imefungua tawi

la pili katika mkoa wa Dar Es Salaam, jambo ambalo limeendelea kuleta

malalamiko kuwa Benki hii haina msaada kwa watu walio mbali na mkoa huo.

Hali kadhalika, benki imefungua vituo 29 vya kutolea mikopo kwa wajasiriamali

wadogo kwenye Mikoa ya Dar Es Salaam, Dodoma na Mwanza, bado swali

lipo, je watu walio katika kanda ya Kusini za Iringa, Mbeya, Mtwara, Lindi na

kaskazini kwa mfano mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga imewekewa mkakati

gani kwa mwaka huu wa 2014/2015 ili kuwafikia wajasiriamali wengine ambao

hawana uwezo wa kufikia huduma hizo katika vituo tajwa kutokana na uwezo

wao mdogo wa kifedha na umbali wa vituo?

3.2 USHIRIKISHWAJI WA WANAUME KATIKA MASUALA YA MAENDELEO YA JAMII

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii kuongelea wajibu wa Serikali

na jamii kuendelea kuwashirikisha wanaume katika masuala ya jinsia na

maendeleo ya jamii.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa shughuli za wizara umeweka vipaumbele

vingi katika kupigania haki za wanawake, jambo ambalo nasi kama Kambi

hatupingani nalo. Lakini, kuna umuhimu mkubwa wa wanaume kuwa sehemu

ya mipango mikakati ya Serikali katika utekelezaji wa malengo yake ikiwamo;

kuzuia ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake, utelekezaji wa watoto, vitendo vya

udhalilishaji wa watoto, ndoa za utotoni, ukatili dhidi ya watoto, na masuala

nyeti ya maendeleo ya jamii. Na jambo hili ni muhimu kupewa kipaumbele kwa

kuwa hata katika baadhi ya jamii, wanaume nao wanakumbana na

changamoto za kijinsia. Hivyo kama Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, ni

dhahiri kuwa sisi wanaume pia tuna nafasi kubwa ya kuongeza msukumo na

kuwa chachu ya mabadiliko katika maendeleo ya jamii yenye usawa wa

kijinsia. Wanaume wakishirikishwa, taifa litasimama imara!

3.4 UENDESHAJI WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI

Page 73: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

73

Mheshimiwa Spika, kumekua na ongezeko la uandikishwaji wa mashirika yasiyo

ya kiserikali, ambapo tunakiri kuwa yanatekeleza majukumu makubwa katika

kusimamia maendeleo ya jamii. Changamoto kubwa, ni uwepo wa baadhi ya

mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yameanzishwa mifukoni, yakapewa usajili

na kunufaika na fedha za ufadhili ambazo kimsingi huwa haziwafiki walengwa.

Mashirika haya yamesajiliwa, lakini yamekua yakiwatumia watoto yatima,

wanaoishi katika mazingira magumu kama chambo cha kupata misaada

kutoka kwa wafadhili ambayo huwa haitumiki kuwaendeleza wala

kuwahudumia walengwa ipasavyo.

Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inaitaka Serikali sio kuwasilisha muktasari wa

matokeo iliyoyachagua bali ripoti kamili ya tafiti zilizofanywa kuhusu mchango

wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kwa mwaka 2012.

Mheshimiwa Spika; Aidha, kufuatia kuwasilishwa kwa taarifa hiyo pongezi

zitolewe kwa mashirika yaliyofanya vizuri na orodha ya mashirika yaliyoshindwa

kutimiza wajibu itajwe.

Kwa upande mwingine, ili kutokuingilia uhuru wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

wakati umefika sasa wa Serikali kuwasilisha bungeni muswada wa marekebisho

ya Sheria inayosimamia Mashirika hayo kwa kuzingatia kwamba Sheria hiyo

ilipitishwa „kwa nguvu‟ huku kukiwa na malalamiko miongoni mwa wadau.

Mheshimiwa Spika; Kwa upande mwingine, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka

Serikali kueleza hatua ilizochukua dhidi ya Shirika lisilo la Kiserikali liitwalo

Wanawake na Maendeleo (WAMA) ambalo Mwenyekiti wake ni Mama Salma

Kikwete, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

WAMA ilituhumiwa ndani ya Bunge hili mwezi Aprili 2012 kwamba ilitumiwa

kisiasa na Mama Kikwete kwenye Kampeni za Uchaguzi za mwaka 2010 kwa

lengo la kumsaidia aliyekuwa mgombea urais wa CCM wakati huo Jakaya

Mrisho Kikwete.

Mheshimiwa Spika; itakumbukwa kwamba kufuatia majibu ya Waziri wa

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mheshimiwa Sophia Simba bungeni ya

mwaka huo wa 2012 kuhusu madai hayo kutokuridhisha, muongozo uliombwa

kwa Spika kuwezesha hatua kuchukuliwa dhidi yake lakini mpaka sasa

muongozo huo haujatolewa.

Serikali inayoongozwa na CCM imekuwa ikiyafuta Mashirika Yasiyo ya Kiserikali

yasiyofungamana na chama chochote pale ambapo inaona yanafanya

harakati za kudai haki kwa niaba ya makundi mbalimbali ya Kijamii kama

ilivyolifuta Baraza la Wanawake Tanzania (BAWATA) na Shirika la Vijana la

National Youth Forum (NYF).

Page 74: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

74

Hata hivyo, Serikali hiyo hiyo imekuwa ikifumbia macho pale Mashirika

yanapotumika kisiasa kwa manufaa ya CCM na Serikali yake. Hali hii imeachwa

muda mrefu na kuota mizizi mpaka taifa limeshuhudia uteuzi wa wajumbe 201

wengi wao wakiwa wanatoka kwenye Mashirika na Taasisi zingine Zisizo za

Kiserikali iwe ni asasi za kiraia, taasisi za dini na nyinginezo namna ulivyofanyika

sehemu kubwa kwa maslahi ya CCM. Matokeo yake ni kutengenezwa kwa

„genge la kutetea misimamo ya CCM‟ kinyume na rasimu iliyowasilishwa na

Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa kuzingatia maoni ya Wananchi.

3.5 CHANGAMOTO ZA WATU WENYE ULEMAVU NCHINI

Mheshimiwa Spika, watu wenye ulemavu ni watu ambao wanatakiwa/

kuthaminiwa katika jamii kutokana na hali halisi ya maumbile yao waliyozaliwa

nayo. Hivyo, basi ni budi jamii hiyo ikapewa kipaumbele katika masuala muhimu

nchini hususani masuala ya elimu, afya, uwezeshaji wa kiuchumi, uongozi

pamoja na masuala mengine ya kijamii ikiwemo michezo na ushirikishwaji katika

maamuzi.

Mheshimiwa Spika, ni jambo la kusikitisha kuwa pamoja na umuhimu wake

katika taifa letu lakini Wizara hii imeshindwa kuweka katika majukumu yake,

jukumu la kulinda na kuwahudumia watu wenye ulemavu kwa kuwaendeleza,

kuwalinda na kuhakikisha kuwa hawabaguliwi na wanapewa hadhi sawa na

wananchi wengine wote katika ngazi zote.

Mheshimiwa Spika, vitendo vya ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu

vimeendelea kushamiri hapa nchini na hivyo kuhatarisha usalama wa watu

hao. Matukio mbalimbali ya ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu yameendelea

kuripotiwa katika vyombo vya habari. Hali hii inatoa taswira kuwa, bado Serikali

haijafanya kazi kubwa kuwalinda watu wenye ulemavu nchini. Na katika idadi

ya watu wanaofanyiwa ukatili, wengi ni watoto ambao hawana hatia lakini

wamekua wahanga wakubwa wa ukatili huo.

Mheshimiwa Spika, kuuawa kwa mwanamke Munghu Lugata mlemavu wa

ngozi toka kijiji cha Gasuma mkoani Simiyu Kaskazini Magharibi mwa nchi yetu

kumeacha hisia na uchungu kwa walemavu wengine waliopata mikasa hiyo.

Matukio mengi ya mauaji ya walemavu nchini yamekuwa yakihusishwa na

imani za kishirikina huku waganga wa jadi wakihusishwa. Mkoa wa Simiyu ni

moja katika maeneo kaskazini magharibi mwa Tanzania yenye matukio mengi

ya mauaji hayo.

Mikoa mingine kwa mujibu wa takwimu za Shirika lisilo la Kiserikali la Under the

Same Sun, inaonesha kuwa mikoa mingine kama Tabora, Shinyanga, Rukwa,

Mara na Kagera pia inaongoza kwa matukio ya kikatili dhidi ya walemavu.

Aidha, taarifa zaidi zinaeleza kuwa mpaka mwezi Mei mwaka huu yameripotiwa

Page 75: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

75

matukio 140 dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi; 73 yaliyopelekea mauaji

na 67 yakiwa ni mashambulio ya kujeruhi katika sehemu mbalimbali za mwili

ikiwemo kukatwa kwa viungo kama mikono, miguu, vidole n.k. na cha kusikitisha

zaidi asilimia 75 ya matukio hayo yalilengwa kwa wanawake na watoto.

Mwaka 2010, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, wakati akiwahutubia wananchi,

kwenye maadhimisho ya Siku ya Walemavu wa Ngozi Tanzania yaliyofanyika

viwanja vya Garden mkoani Iringa alisema kuwa

“Napenda kuwaonya watu wote wanaojihusisha na vitendo viovu vya

ukataji wa viungo na wauaji wa walemavu wa ngozi popote walipo kuwa

siku zao zinahesabika. Ndugu zetu wenye ulemavu wa ngozi

nawahakikishia Serikali itashinda vita hii na mtaishi kwa uhuru ndani ya

nchi yenu”.

Mheshimiwa Spika, ikiwa imepita takribani miaka minne toka Waziri Mkuu atoe

kauli hiyo, je, matukio ya ulemavu yamepungua? Je siku za watu wanaofanya

vitendo vya ukatili dhidi ya walemavu zimeshahesabika au bado zinaendelea

kuhesabika? Je, wizara hii imeweka mikakati gani kuhakikisha watu wenye

ulemavu wanapewa kipaumbele katika shughuli za maendeleo ya jamii ili

kujenga, utu na usawa katika jamii yetu?

Mheshimiwa Spika, matukio yafuatayo yameonesha kuwa; kauli za Serikali

pamoja na Machozi ya Waziri Mkuu hayajaweza kutatua vitendo vya kikatili

dhidi ya watu wenye ulemavu hasa wa ngozi kwa kuwa yametokea sehemu

mbalimbali nchini kama ilivyoorodheshwa katika ripoti ya Kituo cha Sheria na

Haki za Binaadamu1;

Mwaka 2013, Maria Chambanenge wa Sumbawanga alikatwa mkono na

wavamizi wawili ambao walikamatwa hapohapo na mkono wa mhanga,

ulikutwa kwa mganga wa Kienyeji ambapo katika tukio hilo mtoto mdogo

wa Bi. Maria naye alijeruhiwa.

Mwezi Februari mwaka 2013, tukio jingine dhidi ya Mwigulu Magese

Matonange wa Sumbawanga aliyekua akitoka shule alikatwa mkono na

wavamizi wawili ambao walikimbia nao.

Mwezi huo huo pia, Makunga Baraka wa Simiyu alivamiwa na kundi la

watu ambao hawakufanikiwa baada ya kufukuzwa na wanakijiji na

kufanikiwa kukimbia.

Lugogola Bunzari wa Tabora, aliuliwa baada ya mkono wake kukatwa

kinyama na nywele zake

Page 76: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

76

kuvutwa kikatili pamoja na ngozi ya paji lake kuchunwa huku babu yake

Bunzari Shinga (miaka 97) aliuliwa wakati akimsaidia mjukuu wake na

wakati huhuo baba wa marehemu aliumizwa vibaya katika jaribio la

kumsaidia mwanae.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka jamii kubadilika na

kuachana na imani potofu ambazo zinahatarisha maisha na usalama wa watu

wengine na ambazo zinarudisha nyuma jitihada zinazofanywa za kupiga vita

ukatili kwa watu wenye ulemavu wa ngozi, wanawake na watoto. Hali

kadhalika, tunawataka wananchi wote, kuwafichua wale wote

wanaojishughulisha na vitendo hivyo na kutoa taarifa kwa vyombo vya dola na

mamlaka sahihi ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa kwa mujibu wa sheria.

3.6 Pensheni kwa Wazee

Mheshimiwa Spika, suala la pensheni kwa wazee sasa limekua wimbo ambao

wananchi wameuchoka. Kwa muda mrefu suala hili limekua likipigwa

danadana, kuanzia Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Kazi naAjira, Wizara ya Afya

na Ustawi wa Jamii, Wizara ya Fedha, na ni wazi kuwa hata wizara hii ya

Maendeleo ya Jamii, Wanawake, Jinsia na Watoto inajaribu kukwepa

utekelezaji huu wa ahadi ambayo Serikali ya CCM ilitumia ili kupata kura za

wazee kwenye uchaguzi mkuu wa 2005 na 2010.

Mheshimiwa Spika, dhamana ya kulisimamia suala la wazee ni la maendeleo

ya jamii kwa kuwa wazee ni sehemu ya jamii na wizara ina wajibu wa

kuhaikikisha wazee hawa wanapata huduma zao muhimu kama ambavyo

CCM imekua ikijinadi kwenye ilani zake za uchaguzi. Umefika wakati sasa, waziri

mwenye dhamana atoe maelezo ya kina, ni mikakati gani ambayo wizara

imejiwekea ili kuhakikisha suala la pensheni kwa wazee linatekelezwa kwa

mwaka huu wa fedha wa 2014/2015?

4.0 MAENDELEO YA WATOTO

Mheshimiwa Spika, tafiti mbalimbali zilizofanyika zinazohusu watoto hapa nchini,

zimeonesha kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaoishi katika mazingira

hatarishi, wakati watoto yatima wakifikia milioni 2.4. Katika tafiti hizo,

zimeonesha kuwa, tatizo la watoto wanaishi katika mazingira hatarishi

limeonekana Mijini na Vijijini na kubwa zaidi kwenye Miji mikubwa ya Dar es

Salaam, Mwanza, Arusha, Tanga, Moshi, Dodoma na Mbeya.

Page 77: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

77

Idadi ya watoto wanaoishi mitaani imeendelea kuongezeka kutoka 1,579

mwaka 2007 hadi 2,010 mwaka 2011, wakati watoto 11,216 wanaoishi katika

Vituo vya Kulelea Watoto kati yao 6,089 ni wavulana na 5,127 ni wasichana.

Aidha, idadi ya Watoto Yatima waliopo nchi nzima wamefikia 2,400,000 kati ya

hao Wasichana ni 1,055,000 na Wavulana ni 1,345,000, ambapo idadi ya watoto

2,700 kati ya miaka 0-14 wanaishi na Virusi vya Ukimwi nchini.2

Mheshimiwa Spika, takwimu hizo zinatoa viashiria na taswira pana juu ya watoto

wanaoishi katika Mazingira hatarishi hali ambayo inachangia kwa ongezeko la

watoto mitaani pamoja na kukithiri kwa vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.

Katika taarifa ya jumla ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali juu ya ufanisi

kwa mwaka 2014, inaonesha ia mfumo wa udhibiti takwimu na taarifa za

watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ni dhaifu na haukidhi matakwa ya

watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.3

2Ripoti ya “Ukatili Dhidi ya Watoto Tanzania. Matokeo ya Uta ti wa Kitaifa, 2009:

Muhtasari wa Kuenea kwa Ukatili wa Kijinsia, Kimwili na Kiakili, Muktadha wa

matukio ya Ukatili wa Kijinsia, Afya na Athari ya Tabia ya Ukatili iliyotokea

utotoni, Dar es Salaam, Tanzania”, UNICEF Tanzania

3Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali Hadi Machi 2014 ukurasa wa 11

4.1 Ongezeko la Watoto wa Mitaani na Athari zake katika Taifa

Mheshimiwa Spika, wakati piramidi ya Idadi ya Watu nchini Tanzania inaonesha

kuwa idadi kubwa ya watu nchini Tanzania ni watoto wenye umri wa chini ya

miaka 15 na vijana. Asilimia 44 ya watu wote hapa nchini ni watoto wenye umri

chini ya miaka 15, ambapo ongezeko la watoto wa mtaani limeendelea kuwa

na athari huku sababu mbalimbali kama umasikini katika familia, mifarakano na

ukosefu wa amani kwenye familia na Wazazi kutowajibika katika malezi na

makuzi ya watoto wao vikipelekea watoto hao kuishi katika mazingira hatarishi.

Sababu nyingine ni vitendo vya ukatili, udhalilishaji na unyanyasaji wa watoto

kutoka kwa familia na jamii kwa ujumla, nyingine ni kufariki kwa wazazi hasa

kutokana na magonjwa mbalimbali, pia huchangiwa na ndoa za umri mdogo

pamoja na mimba zisizotarajiwa.

4.2 Mimba za Utotoni, Zisizotarajiwa, na Utoaji Mimba.

Mheshimiwa Spika, kulingana na Sheria ya Mtoto ya Mwaka 2009, sehemu ya

pili inayohusu haki na ustawi wa mtoto (a), kipengele cha 4-14 inataja haki za

mtoto kuwa ni pamoja na kulindwa dhidi ya ubaguzi wa aina yoyote, haki yake

kupata chakula bora, malezi bora, huduma za afya, elimu, uhuru wa kuamua,

Page 78: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

78

kucheza na kupumzika. Pia, sheria hiyo inataja majukumu ya mzazi kwa mtoto

kuwa ni pamoja na kuhakikisha mtoto wake anaishi, anathaminiwa,

anaheshimiwa, anapata muda wa kupumzika. Nyingine ni kumlinda dhidi ya

mateso, vurugu, uonevu, ukatili au kupata madhara kimwili au kisaikolojia. Pia,

mtoto ana haki ya kutoa maoni, kusikilizwa na kuheshimiwa katika uamuzi

unaomhusu.

Mheshimiwa Spika, inasikitisha kuona kuwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji

dhidi ya watoto vimeendelea kuongezeka na vingine kufumbiwa macho huku

Serikali ya CCM ikiwa kimya dhidi ya wahalifu wanaotenda vitendo hivyo, kwani

mara kadhaa imeripotiwa kwenye vyombo vya habari kuhusu watuhumiwa na

vitendo hivyo kuachiwa na vyombo vya usalama katika mazingira ya rushwa na

kulindana.

Mheshimiwa Spika, ripoti ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) nchini

Tanzania imesema watoto wapatao 800 walilawitiwa mwaka 2013. Ripoti ya

shirika hilo imeweka wazi kwamba kumekuwa na ongezeko kubwa la vitendo

vya ukatili kwa wanawake na watoto nchini Tanzania ambapo kumi kati yao

wakiwa wamefanyiwa ukatili huo na wazazi wao wenyewe. Watoto wamekuwa

katika maisha ya hatari zaidi nchini hasa kutokana na watu wa karibu

wakiwemo wazazi wa kiume na hata kaka na wajomba zao kubainika

wanawafanyia vitendo vya ubakaji.

Mheshimiwa Spika, inashangaza pia kuona baadhi ya kesi za ulawiti na ubakaji

umalizwa nje ya mahakama ama mfumo wa Sheria jambo ambalo linaendelea

kuhatarisha maisha na ustawi wa watoto hapa nchini. Serikali ni lazima

ikabiliane na kesi zote za ulawiti na ubakaji kwa uangalifu mkubwa, na hata

kwa kuhakikisha kuwa washtakiwa wanafikishwa mbele ya vyombo vya Sheria

hata kama familia za waathirika zimekubaliana kumalizana nje ya mfumo huo ili

kujenga jamii ya kistaarabu yenye kuheshimu na kuwalinda watoto.

Mheshimiwa Spika, baadhi ya watoto hasa wa kike wamekuwa wakikatishwa

masomo yao kutokana na kufanyiwa vitendo vya kudhalilishwa au kuozwa

ndoa za utotoni, lengo likiwa ni mzazi kujipatia fedha zinazotokana na mahari.

Baadhi ya watoto na wanawake kutokana na vitendo hivyo wamekuwa

wakiambukizwa magonjwa yakiwamo ya ngono yanayowafanya kujutia kuishi

kwao na wakati mwingine wakifikiria ni bora wasingezaliwa.

Mheshimiwa Spika, ripoti ya utafiti uliofanywa na Chama cha Wanahabari

Wanawake Tanzania (Tamwa) katika mikoa 18 ya Tanzania Bara na Visiwani

umebaini kuendelea kushamiri kwa vitendo hivyo huku matukio 996 ya

udhalilishaji yaliripotiwa kutokea katika wilaya sita za Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, kati ya matukio hayo, 242 yalihusu ubakaji, vipigo vilikuwa

388, ndoa za utotoni 42, kutelekezwa 96, mimba za utotoni 228 huku hali kwa

Page 79: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

79

upande wa Tanzania Bara ukionyesha kuwa Wilaya ya Babati mkoani Manyara

ikiongoza ikiwa na matukio 132. Ripoti ya Utafiti wa Ukatili dhidi ya Watoto

Tanzania, iliyotolewa na serikali pamoja na Shirika la Kimataifa la Kuhudumia

Watoto (Unicef) mwaka 2011, ilidhihirisha kuwa msichana mmoja kati ya watatu

na mvulana mmoja kati ya saba nchini Tanzania hukumbwa na unyanyasaji wa

kijinsia kabla ya kufikisha umri wa miaka 18. Viwango vya unyanyasaji wa kimwili

navyo viliendelea kuwaathiri watoto kwani karibu wasichana na wavulana

watatu kati ya wanne wamepigwa ngumi, kuchapwa au kupigwa mateke

wakati wa utoto wao huku robo ya watoto wote wamefanyiwa ukatili wa kihisia.

Mheshimiwa Spika, haya ni matukio ambayo yamekuwa yakiendelea

kuwakumba watoto ambao ni taifa la kesho, hivyo kuwafanya kutokufikia

malengo yao. Serikali kwa kiasi kikubwa imefanya mambo haya yaendelee

kuongezeka kutokana na kufumbia macho mambo haya na haiwezi kujinasua

kwa kuwa imeshindwa kabisa kudhibiti ukatili huu dhidi ya watoto nchini wa

kiwango kikubwa.

4.4 Mimba za Utotoni

Mheshimiwa Spika, Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na idadi ya watu

UNFPA lilizindua ripoti yake na kuitaja Tanzania kama mojawapo ya nchi

ambazo zinakabiliwa na ongezeko kubwa la mimba za utotoni na hivyo

kuwafanya wasichana wengi kukatiza masomo yao. Ripoti hiyo iliyozinduliwa

tarehe 30 Oktoba 2013 imeangazia hali ya idadi ya watu na kusema kuwa kati

ya mimba milioni moja zinazotungwa nchini Tanzania, asilimia 23 ya mimba hizo

zinawahusu wasichana walio chini ya umri wa miaka 19. Kwa mujibu wa ripoti

hiyo, idadi ya watoto wa kike wanaopata mimba bado ni kubwa na kwamba

takwimu za sasa zinaonyesha kuwa kila kwenye wasichana 10, 4 kati yao

wamepata mimba. Baadhi ya mambo yaliyotajwa kusababisha hali hiyo ni

pamoja na kuwepo kwa mila potofu ambazo zinawakandamiza na

kuwabagua watoto wa kike. Jambo jingine lililoelezwa na ripoti hiyo ni

kuendelea kuongezeka kwa ndoa za utotoni ambazo hutumika kama kigezo

cha kujipatia mali kwa baadhi ya wazazi.

Mheshimiwa Spika, licha ya mimba za utotoni kuwa na thari kubwa lakini pia

suala la watoto wa kike kukatishwa masomo baada ya kupata mimba, ni

jambo ambalo serikali inatakiwa kulipitia upya ili kuwapa watoto hawa fursa ya

kujikomboa kifikra na kiuchumi. Ni wazi kuwa, suala la wanafunzi kutoruhusiwa

kuendelea na masomo baada ya kupata mimba ni njia mojawapo ya

kupunguza mimba za utotoni, lakini bado ina athari kubwa kwa kuwa

inamnyima mtoto wa kike fursa ya kuweza kujiendeleza kimasomo. Wanafunzi

wa kike wanapopata mimba hulazimika kukatiza masomo na ndoto zao za

kufanikiwa kupitia elimu huzimika. Mimba za utotoni ni matukio yanayoelekea

kuzoeleka na kuchukuliwa kuwa ni ya kawaida.

Page 80: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

80

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kuwa hakuna mikakati makini ya kudhibiti hali hiyo

zaidi ya utekelezaji wa sheria kwamba anayepata mimba lazima afukuzwe

shule. Takwimu mbalibali zinaonesha kuwa takribani wasichana zaidi ya 55,000

wamekuwa wakifukuzwa shule kwa sababu ya ujauzito au nyinginezo katika

kipindi cha muongo mmoja, hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya kutoka Kituo cha

Haki za Uzazi (the Centre for Reproductive Health). Ripoti hiyo iitwayo Forced

Out: Mandatory Pregnancy Testing and The Expulsion of Pregnant Students In

Tanzanian School ilizinduliwa mwaka jana , Dar Es Salaam.

Aidha, idadi ya mimba zisizotarajiwa inazidi kuongezeka na hii inapelekea pia

kuongezeka kwa vifo vya wanawake. Kulingana na rejea ya sera iliyoandaliwa

na wadau mbalimbali, pamoja na wizara ya afya iliyoitwa “WOMEN AND

CHILDREN FIRST; Countdown to ending preventable maternal, newborn and

child deaths”, kutokwa na damu wakati wa uzazi au OBSETRIC HAEMORRHAGE

na matatizo ya damu au HYPERTENSIVE DISORDERS uchangia takribani asilimia

50 ya vifo vya wanawake katika uzazi. Katika kupunguza idadi ya vifo hivi, ni

lazima kuhakikisha idadi ya mimba zisizotarajiwa zinapunguzwa kupitia mipango

thabiti ya Uzazi wa Mpango.

Pia, ongezeko la utoaji mimba usio salama (UNSAFE ABORTIONS) pia linazidi

kuongeza upana wa tatizo. Upatikanaji wa takwimu za kiwango cha mimba

zinazotolewa nchini ni chamngamoto, lakini kulingana na taarifa za Wizara ya

Afya na Maendeleo ya Jamii, takribani asilimia 16% ya vifo vya wanawake

wakati wa uzazi vinatokana na matatizo yanayojitokeza wakati wa utoaji

mimba. Haya ni matatizo yanayowakuta mama, dada zetu, na mbaya zaidi

asilimia kubwa ni watoto wetu - hawa hawa tunaowafukuza shule. Lazima

hatua za makusudi kabisa na za haraka zichukuliwe ili kuhakikisha upatikanaji

wa njia bora na salama za kujikinga (za uzazi wa mpango) zinapatikana kwa

urahisi pamoja na kutoa uelewa mzuri wa elimu ili kupunguza idadi ya mimba

zisizotarajiwa, utoaji mimba usio salama na matatizo yatokanayo. Hii ni pamoja

na kuiongezea uwezo na kuboresha ufanisi wa Bohari ya Taifa ya Dawa (MSD)

na upatikanaji wa huduma za afya kwa Watanzania wote.

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaendelea kuishinika

Serikali, kufuta adhabu hiyo ili kuwapa fursa watoto wa kike kwa kuwa kila

mmoja wetu katika jamii anahitaji nafasi ya pili ili kuweza kurekebisha makosa.

4.5 Maoni na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali Juu ya Watoto Wanaoishi

katika Mazingira Hatarishi

Mheshimiwa Spika, katika ripoti ya jumla ya Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za

serikali kuhusu ukaguzi maalumu kwa kipindi kinachoishia tarehe 31 Machi 2014,

ilitaja sababu nne kubwa zifuatazo zinazofanya Serikali Serikali kushindwa kutoa

Page 81: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

81

huduma za msingi kwa watoto wanaoishi katika Mazingira hatarishi kuwa ni

pamoja na;

a) Uwepo wa mifumo isiyo endelevu na isiyokidhi viwango vya utoaji wa

huduma kwa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi. Sehemu kubwa

ya utoaji wa huduma za msingi kwa watoto hao ilitegemea zaidi misaada

mingi iliyotolewa na wafadhili na pia asasi za kiraia na zisizo za kiserikali

ziliachiwa jukumu la utoaji huduma za msingi kwa watoto hao bila

usimamizi madhubuti;

b) Kutokuwepo kwa Maafisa wa Ustawi wa Jamii wa kutosha waliopatiwa

mafunzo ya kusimamia utoaji wa huduma za msingi kwa watoto

wanaoishi katika Mazingira Hatarishi;

c) Kutokuwa na uratibu katika ngazi zote za Serikali kwa kuwa kila taasisi iwe

ni katika Serikali (katika ngazi ya kitaifa au Serikali za Mitaa) au washirika

wanaotekeleza utoaji wa huduma za msingi kwa watoto wanaoishi katika

mazingira hatarishi wanatoa huduma hiyo bila kushirikiana. Hali hii

imesababisha muingiliano wa utendaji kazi na hivyo kutokuwa na ufanisi

katika matumizi ya rasilimali chache zilizotengwa kwa huduma hizo za

msingi kwa watoto hao.

4.6 Mitandao ya Utumwa wa Kingono

4.6.1 Mitandao ya Utumwa wa Kingono ndani ya Nchi

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kuwa maendeleoya jamii lazima yaangalie pia

ustawi wa jamii ikiwamo kuwalinda vijana wa kitanzania, wasichana na

wavulana kutoka katika utumwa wa kingono. Hapa nchini, kumekua na

mtandao mpana unaochukua wasichana toka vijijini, na kuwaleta mijini kwa

kisingizio cha kuwafanyisha kazi za ndani lakini huishia kuwa makahaba jambo

ambalo si sahihi kisheria. Wasichana hao hufanywa kuwa watumwa wa ngono

katika madanguro na baadhi hoteli kubwa ambayo yanamilikiwa na watu

mbalimbali. Wasichana hao, huuzwa kwa baadhi ya wafanyabiashara

wakubwa, watalii, wanasiasa na huwa chini ya wamiliki wa madanguro. Hali hii

inasikitisha sana, na ni kinyume na haki za binadamu na maadili ya watanzania.

Mtandao huu wa ngono pia, huwashawishi wanafunzi wa kike ambao huaga

kwao kuwa wanakwenda shuleni, lakini huishia kwenye madanguro, gesti na

baadhi ya hoteli maarufu kwa ajili ya kuuza miili.

Mheshimiwa Spika, mtandao huu umesambaa karibu sehemu kubwa ya nchi

ikiwemo miji mikubwa ya Dar Es Salaam, Mwanza na Arusha. Mitandao hiyo ya

ndani wa ngono ikihusisha watoto wadogo na wanafunzi imeshamiri nchini na

inalijengea taifa picha ya aibu mbele ya jamii pana ya kimataifa.

Page 82: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

82

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Utangazaji la Uingereza la BBC4 iliyowahi

kuibua mjadala mkubwa na kuwaweka watu presha juu, watoto

wanaojihusisha na biashara hiyo walieleza jinsi walivyodanganywa kuzamia jijini

Dar kufanya kazi nzuri za kuwapatia mkate wao wa siku, lakini wakaishia kwenye

biashara ya ukahaba. Watoto hao walieleza kuwa, kutokana na ugumu wa

maisha vijijini walipata matumaini kuwa jijini kuna matunda, lakini walipofika

wakawa wakifugwa kama watumwa kwa kazi moja tu, kuuzwa kwa wanaume

wapenda ngono za rejareja.

Katika mjadala huo ulioendeshwa kwa siku tatu, vitoto hivyo vibichi viliweka

wazi kuwa wanapochukuliwa na wanaume hulipwa Sh. 50,000 lakini huambulia

Sh. 10,000 kwani fedha nyingine huchukuliwa na tajiri. Ukweli ni kwamba hali ni

mbaya kupita maelezo. Tunatoa wito kwa idara zote zinazohusika kunusuru

kizazi cha kesho kwa kuwaepusha na mateso wanayoyapata huku janga la

ukimwi likichukua kasi. Pia, tunaiomba jamii kupinga kwa nguvu zote kwa

kuripoti kwenye vyombo husika uwepo wa biashara hiyo haramu.

4.6.1 Mitandao ya Utumwa wa Kingono Nje ya Nchi

Mheshimiwa Spika, wimbi la mabinti wa kitanzania wanaosafiri nchi za nje,

limeongezeka lakini pia likiwa limebeba taswira mbaya kwa taifa kwa ujumla. Ni

dhamana ya wizara hii kuhakikisha kuwa, maendeleo ya jamii hasa haki za

wanawake zinalindwa na kupiganiwa kwa hali na mali hata kama suala la

kisera linasimamiwa na Wizara nyingine kwa mfano Wizara ya Mambo ya Nje na

Ushirikiano wa kimataifa.

Mheshimiwa Spika, taarifa mbalimbali za kuaminika zinaonesha kuwa kuna

mitandao ya wanaowasafirisha wasichana hao wa kitanzania kutoka nchini

inafanya hivyo kwa makubaliano ya kuwatafutia ajira katika hoteli kubwa na

badala yake wanapofika nchi za nje kwa mfano China, huwafanyisha

wasichana hao vitendo vya ukahaba bila ridhaa yao. Mitandao hiyo

ikishasafirisha wasichana hao huwanyang‟anya wasichana hao hati zao za

kusafiria na kujikuta wakishindwa kurejea nchini hali inayowafanya waendelee

kuwa watumwa wa kingono na ukahaba. Baadhi ya wasichana, waliosafirishwa

nchi nyengine mbalimbali duniani wamebainika pia kujihusisha na biashara za

dawa za kulevya. Vitendo hivi si tu vinaivunjia nchi yetu heshima, lakini pia

vinaleta changamoto katika maendeo ya jamii na masuala ya ukatili dhidi ya

wanawake ambayo kama taifa hatupaswi kuyafungia macho.

Mheshimiwa Spika, Aidha, tunaitaka wizara hii kukomesha mitandao yote ya

kingono iliyopo ndani ya nchi kwa kuwa tatizo hili ni pana zaidi ya

Page 83: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

83

linavyozungumzwa. Tunaitaka Wizara, kuanzisha msako rasmi wa madanguro

yote kwa kushirikiana na wizara nyingine zenye dhamana ili kudhibiti mtandao

huu ambao umevuka mipaka.

Mheshimiwa Spika, ni rai ya kambi ya upinzani kuwa Serikali sasa, itakua macho

na vitendo vyote vya udhalilishaji ili kuweza kujenga jamii yenye kuheshimu na

kulinda thamani ya utu kama moja ya nguzo kuu za Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Kwa upande mwingine, Kambi Rasmi ya Upinzani

inasikitishwa na suala la mabinti zaidi ya 250 ambao wametekwa na kundi

hatari la Boko Haram, na tunaungana na Nigeria pamoja na dunia nzima katika

kuhakikisha mabinti hao wako salama na wanarudishwa kwa wazazi wao kwa

kuipitia kampeni ya kimataifa ya Bring Back Our Girls.

5.0 MAREKEBISHO YA SHERIA

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 ni kati ya Sheria zinazotajwa

kuwa kandamizi hasa kwa kuwa imepitwa na wakati. Wakati Maboresho ya

Sera na Sheria nyengine yamefanyika kutokana na mazingira na wakati, sheria

hii imeendelea kutumika kwa takribani miaka 42 huku marekebisho yake

yakichukua muda mrefu. Tunasikitishwa na mlolongo mrefu uliopo katika

kuboresha sheria hii kandamizi, kwa kuwa inatoa mwanya kwa ndoa za utotoni

hasa ukizingatia kuwa inaeleza kuwa mtoto wa kike wa miaka 15 anaweza

kuolewa. Tunafahamu kuwa Sheria hii ipo katika hatua za Marekebisho ila ni

wakati sasa, Serikali ifanye jitihada za juu zaidi kuhakikisha Sheria hii inafanyiwa

marekebisho kabla ya mwaka 2014 kuisha.

Aidha, sheria ya elimu ya mwaka 1978 iliyofanyiwa marekebisho 2002

inayoruhusu mwanafunzi mjamzito kufukuzwa shule, ni kati ya Sheria

zinazopigiwa makelele kwa kuwa zinawanyima watoto wa kike fursa ya

kujiendeleza kielimu mara baada ya kujifungua. Kambi rasmi ya Upinzani,

inaitaka Wizara hii kusimamia msingi wa kuwapa nafasi watoto wa kike

waliopata mimba mashuleni,ili kuweza kujenga jamii yenye kujenga badala ya

kubomoa zaidi kwa kushinikiza mabadiliko ya Sheria hii.

Mheshimiwa Spika, aidha ni jambo la kushangaza kuona kuwa pamoja na

kujisifu kama taifa liliondelea na la mfano wa kuigwa kwa nchi za Afrika, bado

tuna changamoto kwenye sheria za mirathi ambazo zinarudisha nyuma

maendeleo ya wanawake na jamii kwa ujumla. Sheria hizi kandamizi,

zinaendelea kukandamiza wanawake ambao siku zote tunasema ni gurudumu

la maendeleo na nguzo muhimu ya familia. Hiyo, kambi rasmi ya Upinzani,

inaitaka Serikali kuhakikisha kuwa Sheria zote kandamizi dhidi ya wanawake,

Page 84: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

84

ikiwemo Sheria ya Ndoa, Sheria ya Mirathi, zinarejewa ili kumweka mwanamke

katika mazingira salama zaidi.

Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kuwa ili kufikia malengo ya taifa kwa pamoja ni

lazima kujenga jamii yenye umoja na usawa itakayoleta maendeleo ya pamoja

katika masuala ya maendeleo ya jamii, jinsia na watoto.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, naomba

kuwasilisha.

.....................................................

Salum Khalfan Barwany (MB)

Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

17 Mei 2014.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge tunaendelea na wachangiaji wafuatao:

Kwanza kabisa tunaanza na Mheshimiwa Amina Nasoro Makilagi, atafuatiwa

na Mheshimiwa Mchungaji Dkt. Getrude Rwakatare, atafuatiwa na Mheshimiwa

Faida Mohammed Bakari na wengine nitawataja baadaye.

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa

nafasi ili niwe mchangiaji katika Wizara hii ambayo ni Wizara mtambuka kwa

maendeleo ya Taifa, maana ni ukweli usiopingika kwamba bila Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto hakuna kilimo, hakuna maji wala hata

hakuna ujenzi kwa sababu Wizara hii kwa kweli ndiyo mhimili wa maendeleo ya

Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijajielekeza katika hoja ambazo

nimejiandaa kuzungumza, naomba nizungumzie kidogo sana kwenye hotuba

ya Msemaji wa Kambi ya Upinzani na pale alipoanza kumtuhumu Mpendwa

wetu Mama yetu, Mama Salma Kikwete kwamba mwaka 2010 alitumia Taasisi

ya WAMA kufanya kampeni na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

alipoulizwa swali katika Bunge lililopita alishindwa kujibu na hatua zozote

hazikuchukuliwa juu yake.

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe maelezo kwamba tuhuma hizo

hazikuwa za kweli na Bunge lako Tukufu lilikubali kwamba hapakuwa na tuhuma

yoyote, Mama Salma Kikwete alifanya kampeni kama wake wa Viongozi

wengine duniani akiwemo na Mke wa Barwany na yeye alifanya kampeni kule

Lindi na Mke wa Mbowe na wake wa Viongozi wote walifanya kampeni.

(Makofi)

Page 85: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

85

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, suala la wanawake wa Viongozi kufanya

kampeni ni jambo ambalo halina upinzani na nitashangaa kuona unakwenda

kugombea bila kupata support ya mama. Bahati njema hatujawahi kupokea

tuhuma zozote za mtu yeyote anayemtuhumu mama Salma Kikwete kwamba

alitumia taasisi ya WAMA dhidi ya pongezi za wananchi na wanawake ambazo

wamekuwa wakitoa kumshukuru kwa kazi njema anayoifanya ya kupunguza

vifo vya wanawake na watoto, kupinga mimba za utotoni na kadhalika kupitia

taasisi yake ya WAMA.

Mheshimiwa Spika, naomba wote kwa pamoja tuungane kumshukuru

Mama Salma Kikwete na kwa kweli tuendelee kumuombea dua, Mwenyezi

Mungu ampe maisha marefu, aendelee kutumika na Mwenyezi Mungu ndiye

atakayemlipa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zimetolewa tuhuma kwamba Chama cha Mapinduzi

kimekuwa na tabia ya kufuta Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ambayo hayana

mlengo wa Chama cha Mapinduzi na wakatolea mfano Shirika la BAWATA.

Mheshimiwa Spika, mimi ni Mwanzilishi wa BAWATA, maana asiyejua

tumwelimishe, tulianzaje hii BAWATA. Ni wazo la Jumuiya ya Umoja wa

Wanawake wa Tanzania tulipoingia katika mfumo wa Vyama vingi vya Siasa,

tulikubaliana kupitia Mkutano Mkuu wetu wa UWT, chini ya Uongozi wa

Mpendwa wetu Mama Anna Abdallah, tukasema tuwe na chombo

kitakachotuunganisha wanawake wote.

Mheshimiwa Spika, ilipofika mwaka 1995 tukawakabidhi kazi

tuliyowapatia, kilichotokea Mungu anajua na mimi nilikuwa Mjumbe najua

kilichotokea. Kwa kuwa, jambo hili lipo Mahakamani na Mahakama imeshatoa

uamuzi wake, tusiendeleze hapa, ila nitatumia nafasi na naomba nitoe nafasi

kwa wale ambao wanataka kuijua vizuri BAWATA na kilichotokea wakati huo,

milango iko wazi na elimu hiyo itakuwa ya bure. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba sasa nijielekeze kwenye masuala

yaliyosemwa kwamba, Chama cha Mapinduzi kimekuwa kinafanya hata

ubabe kupitia Wabunge 201. Hili ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania na hapa tunajadili bajeti. Sasa kama kuna mtu anazungumzia Bunge

lililopita, tusubiri kwenye Bunge la Katiba. Nichukue nafasi hii kuwakaribisheni

wale wote wenye malalamiko juu ya Wajumbe 201 njooni uwanjani, jengeni

hoja tuzungumze uwanjani na kwa kweli nitumie nafasi hii kuwakaribisheni sana

karibuni sana katika Bunge lijalo na sio mbali ni mwezi wa Nane. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya utangulizi huo sasa naomba nijielekeze

katika Bajeti…

Page 86: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

86

SPIKA: Nimeshasema mnaposhangilia hapa siyo kupiga kelele. Kuna

utaratibu wa kushangilia humu ndani, maana tukianza vigelegele humu ndani

inakuwa sivyo. Tunaendelea Mheshimiwa. (Kicheko)

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba

mshangalie kwa kupiga meza Kibunge.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba niendelee kwa kujielekeza

sasa katika hoja ambazo nimejiandaa kuzungumza. Kwa kweli naomba

Mheshimiwa Spika, nianze kumpongeza Waziri na Timu yake yote ya Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa kazi kubwa na nzuri ambayo

wamekuwa wakiifanya katika mazingira magumu sana ya ufinyu wa bajeti.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimekuwa nikitembea maeneo mbalimbali,

nimejionea mwenyewe jinsi Maafisa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

wanavyohangaika, walivyo na ufinyu wa Bajeti, fedha zinazotoka Wizarani ni

ndogo, fedha zinazotengwa na Halmashauri ni ndogo. Ningependa kuchukua

nafasi hii kuwapa pole. Napenda pia niiombe Serikali yetu Tukufu kwamba ifike

wakati sasa na Wizara hii kama alivyosema Mwenyekiti wa Kamati hii kwamba

sasa Wizara hii pia ipewe kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, naomba nijielekeze kuzungumzia mauaji ya

wanawake mbalimbali na hasa nizungumzie mauaji ya wanawake wa Butiama.

Pamoja na jitihada zilizofanywa na Serikali pamoja na Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto, nichukue nafasi hii kumpongeza Mama Sophia Simba na timu

yake kwa jinsi walivyochukua uzito wa mauaji ya wanawake hapa nchini.

Nimeshuhudia mimi mwenyewe mauaji yale ya wanawake Butiama, hukukaa

nyuma umeshiriki hata mazishi na wakati mwingine nilikwenda na wengine na

wengine.

Mheshimiwa Spika, lakini vile vile kupitia Taasisi ya Dawati la Wanawake

kuna hatua ambazo mmechukua. Sasa ningependa kupata majibu wakati uki-

wind up hotuba yako, sasa ni hatua gani zitakazochukuliwa kuhakikisha haya

mauaji yanakomeshwa. Yanakomeshwa maana kwa kweli kama walivyosema

wanawake ma-albino, wanawake wenye ulemavu na sasa yametokea tu

mauaji ambayo hayaeleweki. Tunataka kusikia kauli ya Serikali inasema nini

sasa juu ya mauaji haya ya wanawake ambayo kwa kweli siyo tabia ya

Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie masuala ya Mfuko wa

Maendeleo ya Wanawake. Naomba nishukuru Bunge lako Tukufu chini ya

uongozi wako Mheshimiwa Spika, Bunge lililopita wanawake na wanaume wa

Page 87: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

87

Bunge hili bila kujali itikadi zetu. Tulisimama kwa pamoja, tukapaza sauti zetu,

tukaiomba Serikali itenge fedha shilingi bilioni mbili kwa ajili ya Mfuko wa

Maendeleo ya Wanawake na hasa wale wa Vijijini.

Mheshimiwa Spika, nimesikitika kuona kwamba mpaka sasa fedha

zilizokwenda ni milioni 500 peke yake. Tunashukuru kwa hicho kidogo

kilichopatikana kwa sababu ukilinganisha na miaka mingine kilikuwa hakitengi.

Ombi langu, naomba fedha hizi kama ambavyo Kamati imeshauri, zitoke zote

shilingi bilioni mbili muda haujafika…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Ooh!

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja.

(Makofi)

SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Mchungaji Rwakatare atafuatiwa na

Mheshimiwa Faida Mohamed!

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Spika, naomba

nichukue nafasi ya kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipigania

katika vita mbalimbali vya maisha na kunisimamisha mpaka leo niko Bungeni.

Ahsante kwa nafasi ya kuweza kuchangia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, awali ya yote ningependa kuchukua nafasi hii kwa

niaba ya wanawake wa Morogoro, kutoa pole zetu za dhati kwa Mheshimiwa

Sophia Simba ambaye amefiwa na mtoto wake mpendwa Triford. Kijana wetu

ameondoka kama ua lililonyakua juani, Mungu aiweke roho yake mahali pema

Peponi. Amina. Mungu akufariji hiyo njia mama. Jipe moyo, Bwana alikupa,

Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe. Amina.

Mheshimiwa Spika, naomba pia nitoe pongezi kwa Waziri, Mheshimiwa

Sophia Simba na Naibu Waziri na Katibu Mkuu na Timu yao yote kwa kuandaa

hotuba nzuri na pia kwa kuweza kufanya na vyote na bajeti finyu; wameweza

kukarabati vyuo, wameweza kuwezeshwa akinamama, wameweza kutoa elimu

mbalimbali kwa akinamama, jamani hongereni mwendelee mbele. Mungu siku

moja atawapa bajeti kubwa na mtaweza kufanya mambo makubwa. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Amina.

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Ningeomba pia nitoe rai kwa

Serikali, kweli wanapanga bajeti, lakini bajeti hizi haziwashukii kama

zilivyopangwa. Naomba tujitahidi kwa hali na mali angalau basi hata nusu,

Page 88: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

88

lakini inaposhuka robo au pengine percent 30 zinakuwa haziwezi kukidhi na

kufanya kazi katika Wizara hii vizuri, halafu baadaye tunatoa lawama. Naomba

jamani hizi bajeti pamoja na ufinyu wake ziwashukie na ziweze kuwafikia

walengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nijikite kwenye maboresho ya vyuo.

Ningeomba maboresho ya Vyuo vya Rungemba na Bigwa vizingatiwe. Chuo

cha Rungemba kinatoa diploma, lakini hali yake ni mbaya. Tulikuwa tunaomba

katika chochote kile ambacho mtapata, mkiangalie kwa jicho la huruma chuo

hiki na kama kweli tuko serious, jamani kutoa kwa mama na baba maendeleo

ni lazima tuboreshe vyuo vyetu ili waweze kusoma mahali ambapo panaweza

na wao kuona kwamba kweli wako chuoni.

Mheshimiwa Spika, naomba kwa hali na mali tuweze kuangalia pia Chuo

kile cha Bigwa, Morogoro. Maombi ni mengi kule Morogoro wanawake,

wanaume wengi wanapenda, lakini bahati mbaya pale nafasi ni ndogo.

Madarasa hayatoshi, naomba utusaidie kuweka madarasa ili watoto wetu

waweze kupata nafasi ya kusoma katika vyuo hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningependa pia nigusie unyanyasaji wa kijinsia.

Unyanyaji wa kijinsia kwa akinamama hasa ukeketaji, tabia hii bado

inaendelea. Naomba tuikemee kwa hali na mali. Naomba hasa wanaume

kwa sababu watu wanakeketwa kwa sababu ya wanaume, basi wanaume pia

mtusaidie kukemea. Kuna makabila ambayo yanasema, siwezi kuoa kama

mwanamke hajakeketwa. Sasa jamani tushirikiane kwa sababu ina madhara

mengi kuliko faida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukemee na itokomezwe kabisa tabia hii ya

kukeketwa. Siku hizi wameanza kukeketa vichanga kama vile wanavyotahiri

wavulana wadogo. Kusudi baadaye wasimakatwe na Polisi. Hiyo pia

tuchunguze watoto wanapokwenda kliniki tuwacheki, wazazi wanaoleta

watoto wa kike ambao wameshakeketwa wachukuliwe hatua, kwa sababu

kwa kweli ni udhalilishaji, hatua kali tena ni udhalilishaji mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ningeomba tena nichukue nafasi hii naomba kwa

pamoja tukemee juu ya ngoma mbaya. Ziko ngoma za kigodoro kule Dar es

Salaam, iko ngoma ya kibao kata, ziko ngoma za ndembandemba, watu

wanavaa kanga moja.

MBUNGE FULANI: Kanga moko.

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Ndiyo kanga moko. Sasa hiyo

yote tukemee kabisa kabisa kwa kweli kwa sababu ni chimbuko la UKIMWI.

Tusione kama watoto wanajifurahisha, lakini kweli tuwasaidie kuwafundisha,

Page 89: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

89

kuwaelekeza na hivyo ndiyo tutaweza kuwa na watoto bora, vijana bora na

wasiokuwa na UKIMWI. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Tanzania bila UKIMWI inawezekana. Kama tutakemea

mambo mbalimbali ambayo hayampendezi Mungu na wala hayapendezi

Taifa. Mavazi mabaya, mavazi ya kushusha suruali mpaka chini bado

yanaendelea. Tukemee wanawake kuvaa vichupi, wanawake kuwavalisha

matiti nje. Jamani vitu hivi tuvikemee, sisi ni wazazi. Hata kama siyo mtoto

wako, mtoto wa mwenzio ni mtoto wako. Tukemee watoto wetu wawe decent,

watoto wetu wawe na heshima na tuwakemee vile vile. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia niweze kukemea kwa pamoja na nyinyi,

tabia mbaya za unyanyasaji au ukatili wa kingono. Ukatili wa kingono,

wanawake wanaoa wanawake wenzao, nyumba ntobo. Hiyo pia tukemee,

huko Musoma, watusaidie Wabunge wa huku tusimame kukemea. Mwanamke

ataoaje mwanamke mwenzake! Au mwanaume ataoaje mwanaume

mwenzake! Tukemee vitu vyote hivi havipendezi, vinamchukiza Mungu.

Tukemee ili Mungu aweze kutusaidia. (Makofi)

WABUNGE FULANI: Amina.

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Nikemee pia tabia mbaya ya

wanaume kupiga wanawake. Ni aibu, ni ushamba kumpiga mke wako. Ni

ujinga pia, mwenyewe utampeleka hospitali. Mwanamke anapigwa na kanga,

mwanamke anapigwa na kitenge, eee mwanamke anapigwa na mkufu wa

dhahabu. Sasa tena jamani yanakuwa mambo ya ngumi, yametoka wapi?

Mpenzi wako, mama wa watoto wako, unampiga kama mtoto kwa nini?

Kwani hamwezi kuongea? Kwani hamwezi kuyapanga mambo chumbani

kwenu? Kwani hamuwezi kwenda kwa Wachungaji wawaombee. Eee, tupo ili

tuweze kurekebisha mambo. Jamani tupendaje, jamani tushikamane kwa njia

hiyo. (Makofi)

SPIKA: Hata watoto siyo wa kuwapiga na watoto pia msiwapige.

MHE. MCH. DKT. GETRUDE P. RWAKATARE: Mheshimiwa Spika, naunga

mkono hoja mia kwa mia. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Faida Mohamed Bakari atafuatiwa na

Mheshimiwa Capt. John Komba!

MHE. FAIDA MOHAMED BAKARI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa

kunipatia nafasi nami nichangie katika hotuba ya Waziri wa Maendeleo ya

Page 90: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

90

Jamii, Jinsia na Watoto. Awali ya yote napenda kumpa pole Mama yetu

Sophia Simba, Mwenyezi Mungu akupe subira Inshallah.

WABUNGE FULANI: Amina.

MHE. FAIDA MOHAMED BAKARI: Mheshimiwa Spika, napenda

kuwashukuru wanawake na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba kwa jinsi ya

dua zao mbalimbali ambapo nilikuwa nikiumwa. Napenda kuwaambia

kwamba sasa hivi namshukuru Mwenyezi Mungu sijambo na tuko pamoja na

tutakuwa pamoja katika kutekeleza majukumu yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda kusema ufinyu wa bajeti wa Wizara hii. Kila

bajeti tunaitetea Wizara hii juu ya ufinyu wa bajeti, lakini kila kukicha bajeti

inapungua. Hivyo sisi wanawake au jamii itakuwaje kama bajeti ya Wizara hii

kila siku inapungua? Naomba bajeti ya Wizara hii iweze kuongezwa ili waweze

kumudu kufanya kazi zao kwa ufanisi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Benki ya Wanawake. Ilani ya Chama cha Mapinduzi

ya mwaka 2010 Ibara ya 205(e) na (f) inaitaka Serikali kuimarisha Mifuko iliyopo

ya mikopo na Benki Wanawake Tanzania ili wanawake wengi waweze kufaidika

kiuchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, inashangaza sana kwamba fedha imepatikana nyingi.

Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anajitahidi katika

kutekeleza majukumu yake katika kuisaidia benki hii. Benki ni ya wanawake

wote wa Tanzania, lakini nashangaa kwa nini Benki hii ya wanawake iko hapo

Dar es Salaam tu ama Tanzania Bara tu. Hivyo wanawake wa Zanzibar wao

hawana haki na Benki hii? Kila siku nasimama naomba Benki hii na Wanawake

wa Zanzibar tunaomba, Wabunge tunaomba, benki hii nayo ianzishwe Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, Zanzibar pia kuna wanawake, Zanzibar pia kuna

wananchi ambao pia wanahitaji mikopo kutokana na benki hii, lakini hadi leo

benki hii haijaanzishwa Zanzibar, kila tukiuliza hapa process zinaendelea,

process zinaendelea. Ofisi imeshapatikana, mara haijapatikana! Sasa ni lini

benki hii hasa itaanzishwa katika Kisiwa cha Zanzibar, kule Pemba na Unguja ili

na wanawake wa Zanzibar nao wafaidike na mikopo hii waendeleze biashara

zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Napenda kuipongeza ripoti hii hapa ya Tanzania Human Right Report ya 2013.

Tulifanyiwa Semina juzi hapo, wakaja na ripoti hii nzuri sana, ripoti hii hapa

imetayarishwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu cha Tanzania Bara,

(LHRC) na kile Kituo cha Huduma za Kisheria cha Zanzibar (ZLSC).

Page 91: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

91

Mheshimiwa Spika, ukiangalia kitabu hiki, ripoti hii ya 2013 kwanza

napenda kuwapongeza kuandika ripoti zao kwa wakati. Humu katika kitabu hiki

hapa ukikiangalia utalia. Kuna ripoti mbalimbali za unyanyasaji wa binaadamu,

unyanyasaji wa wanawake, unyanyasaji wa watoto, unyanyasaji wa wazee na

kila aina ya mambo mbalimbali ambayo wananchi sisi tunapata shida

kutokana na madhila mbalimbali tunayofanyiwa na wenzetu.

Mheshimiwa Spika, niliumia sana kuna bwana mmoja, kizito mmoja hapo

Dar es Salaam huwa anakaa karibu na shule fulani, huwa anawachukua

watoto wadogo, anawapeleka nyumbani kwake na walimu wanajua na ripoti

hii inajulikana. Hii kesi ipo, aliwachukua mpaka Bagamoyo akaenda kufanya

nao vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia.

Mheshimiwa Spika, Ripoti hii ilipopelekwa na kushtakiwa yule baba,

nashangaa wale wazazi, imo humu, imo humu, wale wazazi wamekataa kwa

sababu ya kupewa hongo na yule bwana. Hivi wewe mzazi unakataa kwamba

mwanao hajafanya kitendo hicho kwa sababu ya pesa? Kweli sisi wanawake

jamani tujiulize, mtoto wako anafanyiwa kitendo kichafu kama hicho halafu

wewe mwenyewe unakataa, unasema hajafanywa! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kesi hii mpaka leo ipo. Naomba

Mheshimiwa Waziri aifuatilie kesi nitakuja kumletea hii ripoti ataiona. Aifuatilie

ripoti hii watoto hawa wapate haki zao, kwa sababu watoto wananyanyasika

sana na si hawa tu ni watu wengi, hata watu wazima wanafanyiwa

unyanyasaji, lakini Sheria haichukui mkondo wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mauaji ya wakongwe, wazee wetu hawa, mzee ni

mzee. Hivi leo tuwaone wazee wetu kwamba si wazee tena kwa sababu

wameshakuwa wazee? Kwani sisi hivi tulivyo ndivyo tulivyokuwa? Tulikuwa

wachanga sasa hivi tuko age hii na baadaye tutakuwa wazee kama wao. Leo

mauaji ya wazee yameshamiri sana katika Mikoa mbalimbali katika nchi yetu ya

Tanzania. Wamefanya kama ni mchezo kuwaua wazee wetu.

Mheshimiwa Spika, mzee akionekana tu ana macho mekundu basi

anauliwa mzee huyo. Kwa nini hatuoni huruma sisi binadamu, wazee wetu

wengine wanazikwa wakiwa hai, wanakatwa viungo vyao, wazee wetu

wamekosa nini, hivyo mzee amefanya kosa Mwenyezi Mungu kumjalia mzee

huyu kukuzaa wewe binadamu. Vijana wanawaua wazee, hasa hasa wazee

wa kike wanauliwa na vijana ambao hawana maadili mema ya Kitanzania,

iweje leo kijana wa Kitanzania anamuua mzee kwa sababu ya macho yake

mekundu.

Page 92: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

92

Mheshimiwa Spika, siyo vizuri. Naomba sana Serikali ichukue hatua kali

kwa wanaopatikana na vitendo kama hivyo. Ngoja nipumue kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na mauaji ya albino, Mwenyezi Mungu

hajafanya makosa kuwaumba wenzetu na ngozi hiyo. Leo binadamu sisi

ambao tuna ngozi zetu hizi za kawaida tunawaua ma-albino wametukosea

nini?

SPIKA: Tunaendelea, ahsante sana.

MHE. FAIDA MOHAMED BAKARI: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga

mkono hoja. (Makofi)

SPIKA: Ahsante sana, Mheshimiwa Naomi Mwakyoma Kaihula,

atafuatiwa na Mheshimiwa Moza!

MHE. NAOMI A.M. KAIHULA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda

nimshukuru Mungu sana kutoka moyoni kwamba amenipatia nafasi nyingine

niweze kuzungumzia machache katika Bunge lako Tukufu.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli dakika ni chache sana, lakini machache

nitakayozungumza, nafikiri yatakuwa mchango mkubwa katika Bunge lako.

Kwanza kabisa ningependa kupongeza sana jinsi tunavyokwenda. Napenda

niwatoe wananchi, Bunge linakwenda vizuri kwa sababu kuna Upinzani. Mjue

kwamba Upinzani kazi yake kubwa moja ni kuhakikisha tunaisimamia Serikali

iliyoko madarakani na sisi tunaisimamia Serikali ya CCM na mambo yenyewe

mmeyaona.

Mheshimiwa Spika, mnajua Serikali hii ya CCM ni sawa na hadithi zile

zilizokuwa zinafundisha kama Karumekenge alikataa kwenda shule mpaka

mtiririko ukafanya ndio akaenda. Sasa kufuatana na hayo mmeona nyie

wenyewe kutokana na jinsi ambavyo Hotuba ya Kambi ya Upinzani ilivyotoka;

niwaambie tu bila ushabiki, bila kitu chochote, mambo haya naiomba sana

Wizara ya Maendeleo ya Jinsia iweze kuyachukua na kuyafanyia kazi kama

dira. Kwa sababu, ni mambo ambayo yamejaa uhalisi, ni mambo ambayo

yanatuelekeza, tunaweza kujiona. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia niwaambie kabisa tunapozungumzia maendeleo

ya jamii, jinsia na watoto hatumaanishi wanawake. Maana imejengeka dhana

humu kwamba, ni wanawake, sio wanawake na hata tunapozungumzia watoto

wamalaya, jamani msifikiri ni wasichana tu, nataka niwaambie akinababa

mchukue kwamba, hata watoto wenu wako hatarini. Wako hapa watoto wenu

wanaitwa poa, ni hatari sasa hivi, chukueni, amkeni, nendeni huko.

Page 93: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

93

Mheshimiwa Spika, baada ya kuzungumza haya naipongeza sana

Hotuba ya Kambi ya Upinzani ya leo na ifanyiwe kazi vizuri na Bunge lako

Tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo napenda nieleze ni kwamba, mimi ni

Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA). Mimi ni

Mwanaharakati, naomba ku-declare interest, pia mimi ni mmojawapo katika

waanzilishi wa BAWATA. Najua mchakato wa BAWATA jinsi ulivyokwenda, najua

jinsi ambavyo tuligombania Baraza la Wanawake liwepo na Serikali hatimaye

ikaridhia, lakini kwa roho upande.

Mheshimiwa Spika, baadaye lilipoundwa tulifanya kazi, Serikali ya CCM

ikaona kwamba, tunakwenda kasi; mnajua wenzangu mimi huwa nazungumza

mambo ya ukweli kabisa, ikaona wanawake hawa watatudhibiti, kwa hiyo,

ikaleta hila lile Baraza ikalifuta. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naomba tu uelewe, Katibu Mkuu Baraza la UWT,

ujue kwamba, katika UWT pia kuna hila kwa sababu, mnatumika zaidi na

Chama cha CCM kuwalinda, ili muweze kuwashangilia wanapochaguliwa.

Ndio kisa hasa cha kuhakikisha kwamba, hakuna Baraza lolote lenye nguvu

linaloibuka kama BAWATA, hata BAWACHA na ndio maana tumekuwa

tukiomba hata katika Hotuba zangu zilizopita nilipokuwa Waziri Kivuli,

tulizungumza kwamba, tunawaomba hilo jina la UWT mnaonaje kama

mngelibadilisha kusudi liwepo, halafu tuhakikishe tuungane tuwe na Baraza la

Wanawake wa CHADEMA kama tunavyoomba katika Katiba ijayo kwamba,

kuwepo na Kamisheni ambayo itakuwa inatuunganisha, itakuwa bora zaidi

kuliko tukiwa tunagawanyika. Wanatumia hila ya divide and rule, wagawanye

na uwatawale; wanawake tutatawaliwa daima. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba ujue kwamba, tunaomba hivi, hilo

Baraza lilipofutwa…

SPIKA: Naomba uniambie mimi.

MHE. NAOMI A. M. KAIHULA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimeona

nimjibu kwa sababu, yeye alizungumzia zaidi kuhusu hilo.

Mheshimiwa Spika, hilo Baraza inatupasa tuombe watwambie baada ya

kufutwa, inaelekea lilishinda, BAWATA ilishinda hiyo kesi. Sasa kama BAWATA

iilishinda hiyo kesi haikuruhusiwa kuendelea, lakini sasa hivi tunaona kwamba

kazi zile ambazo zingekuwa zinafanywa na wanawake wote ndio zimepelekwa

kwenye WAMA, kwa nini zipelekwe kwenye WAMA? (Makofi)

Page 94: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

94

Mheshimiwa Spika, hiyo WAMA ambayo mke wa Rais anatumia na pia

nanihii ya Serikali, kwa nini isiwe Baraza la Wanawake ambalo litatuunganisha

sisi; nyie mtakuwa UW-CCM na BAWACHA, tukawa watu wamoja, tukaunda

Baraza la Wanawake wa Tanzania, badala ya kuwa na Makamisheni tu?

Naomba jambo hili lichukuliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, muda ni mchache, naomba nizungumzie…

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Spika, Taarifa. Kuweka sawa

takwimu.

SPIKA: Muda hautoshi, naomba aendelee. Endelea!

MHE. NAOMI A. M. KAIHULA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Baada ya

kuzungumza haya naomba nizungumze kidogo kuhusu suala la watoto katika…

(Hapa kengele ya kwanza ililia kuashiria kukaribia kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. NAOMI A. M. KAIHULA: Mheshimiwa Spika, ya kwanza?

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa nanihii? Ya kwanza?

MHE. NAOMI A. M. KAIHULA: Mheshimiwa Spika, ya kwanza.

SPIKA: Endelea Mheshimiwa!

MHE. NAOMI A. M. KAIHULA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa hiyo,

naomba hivi, sisi Tanzania tuwe na akili, nimezungumzia hapa mara nyingi

kwamba, nchi ya Tanzania kama kweli inataka kuendelea kupitia Wizara yake

ya Maendeleo ya Jamii, ni lazima ijipange kuwa na pesa ya kuwatunza watoto

wake. Kwa ajili ya kutokuwa na pesa ya kuwatunza watoto wake ndio matokeo

mengi mabaya yote haya yanatokea.

Mheshimiwa Spika, nilipendekeza kwamba, katika madini, katika rasilimali,

kutengwe hata 1% ambayo iwe inakwenda katika bajeti ya Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kusudi iweze ku-take care ya elimu,

matunzo kuanzia mtoto akiwa mimba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yaani wenzetu walioendelea wanaweka hiyo percent

ambayo inasaidia baadaye kuwatunza watoto kuanzia akiwa mimba, afya,

elimu, lishe na kila kitu. Hata wakifika umri wa miaka 18 hakuna tena kukaa na

wazazi wao na kuja kuwaua kama wanvyowaua sasa hivi wakidai urithi.

Wanawaambia kwamba, nenda kwa baba yako kwa sababu, zile pesa

Page 95: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

95

zilizokuwa zikiwekwa, zilizotengwa kutoka katika rasilimali ya nchi zinatumika

kuwatunza na kuwapangia na kila kitu. Kwa hiyo, naomba kwamba, Bunge lako

Tukufu, ni wakati mzuri sasa hivi kuiwezesha hiyo Wizara ya Maendeleo na Jinsia

kusudi iweze kuwa na uwezo huo wa kutunza watoto katika vitu vingi ambavyo

mwenzangu atakayekuja baadaye atavielezea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, napenda nikushukuru kwa ajili ya wakati mzuri huu.

Mungu awabariki na tuendelee kuwa hivi. (Makofi)

SPIKA: Ahsante.

TAARIFA

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kweli, ni

mara yangu ya kwanza kusimama angalau kuzungumzia haya aliyosema.

Kwamba, la kwanza UWT haina hila; Umoja wa Wanawake wa Tanzania

umeshiriki kukomboa nchi yetu ya Tanzania. Umoja wa Wanawake umeshiriki

kudai uhuru wa Watanzania. Umoja wa Wanawake (UWT) una Katiba yake tena

umesajiliwa kwa mujibu wa Sheria. Umoja huu wa Wanawake una Katiba,

tofauti na Taasisi nyingine, UWT una Katiba. (Makofi)

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Spika, Umoja wa Wanawake wa

Tanzania, hata Viti Maalum ulividai ndio maana katika Bunge la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania hapa matokeo ya Wabunge Wanawake kutoka

Vyama vya Upinzani ni matokeo ya Jumuiya ya Wanawake wa Tanzania.

Maana UWT ingekuwa na hila kusingekuwa na wanawake wengi wa Upinzani.

Ni UWT ndio iliamua kujinyonyoa ikasema sasa badala ya kwenda na

wanawake wachache tushirikishe wanawake wengi, ili tupaze sauti moja. Sasa

mtu mwenye hila anakuwaje UWT? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu BAWATA nimesema sio mahali pake

hapa. Tudai forum nje tuzungumzie BAWATA ilikotoka na ilikoishia. (Makofi)

SPIKA: Naomba usichangie.

Mheshimiwa Mnyika, unajua kabisa tunapoongea Taarifa mtu mmoja

akimaliza na mwingine anasema, lakini ikianza kelele inakuwa sio vizuri; ingawa

wengine wameniandikia barua za kipuuzi.

Page 96: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

96

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni Taarifa

ikiombwa, Mzungumzaji anakaa ili apewe Taarifa.

SPIKA: Sasa ngoja kwanza, nitakupa ruhusa uongee.

Haya, Mheshimiwa Mnyika!

TAARIFA

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ningependa

kumpa Taarifa mzungumzaji, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), ulitumikia

na kuwawakilisha wanawake wote wakati wa mfumo wa Chama Kimoja cha

Siasa. Hii ilikuwa kwa Jumuiya mbalimbali, ilikuwa kwa Wafanyakazi, ilikuwa kwa

Vijana, na kadhalika.

Baada ya kuanza kwa mfumo wa Vyama Vingi, wanawake sasa kwenye

ulingo wa kisiasa wamegawanyika kwa misingi ya Vyama mbalimbali, CUF

wana Jumuiya ya Wanawake, CHADEMA wana Jumuiya ya Wanawake, TLP

wana Jumuiya ya Wanawake na kadhalika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, alichokisema mzungumzaji aliyetangulia ni kwamba,

pamoja na ukweli huo wa kihistoria, UWT bado inafanya hila ya kuwafanya

watu waamini kwamba, ndio umoja unaowawakilisha wanawake wote

Tanzania. (Makofi)

Matokeo yake UWT inakwamisha kuanzishwa kwa Umoja wa Wanawake

wote Tanzania, Baraza la Wanawake Tanzania, ilifanya jitihada za kufutwa kwa

Baraza la Wanawake Tanzania. Kwa kuwa, Mahakama sasa imesema

kwamba, Serikali ilivunja Sheria kwa kulifuta Baraza la Wanawake Tanzania,

alichokisema mzungumzaji aliyetangulia ni kwamba, umefika wakati sasa

kuanzishwa chombo hiki na sio kwa wanawake tu, hata kwa vijana vilevile,

umefika wakati wa kuwa na Baraza la Vijana Tanzania, ili kuwa na chombo cha

kuwaunganisha katika maendeleo ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilitaka kumpa Taarifa Mzungumzaji

aliyetangulia.

SPIKA: Mheshimiwa Mnyika, sifa zote umetoa…

MBUNGE FULANI: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

Mheshimiwa Spika, sikubaliani…

Page 97: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

97

SPIKA: Naomba mkae, hakuna cha Taarifa yoyote; nani

anayezungumza? Naomba mkae wote.

Hakuna mtu anayezungumza hapa, vyote mnavyosema ni kweli. Wewe ni

John Mnyika, akizaliwa John Mnyika mwingine wewe utajitoa? Haiwezekani!

(Kicheko)

Tunaendelea. Mheshimiwa Conchesta Leonce Rwamlaza? Aah, nilisema

Mheshimiwa Moza kwanza, halafu Conchesta. Mheshimiwa Moza ameondoka?

Yupo, Mheshimiwa Moza kwanza, halafu atafuatiwa na Mheshimiwa

Conchesta.

MHE. MOZA A. SAIDY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii.

Nashangazwa sana na malumbano ya mambo ya huko mengine.

Mheshimiwa Spika, naomba kunukuu. Wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu

anasoma Hotuba yake hapa Bungeni, katika ukurasa wa 28, alisema kuwa hadi

kufikia Disemba, 2013, Mfuko wa Wanawake ulikuwa umetoa mikopo ya

thamani ya shilingi bilioni 5.4.

Mheshimiwa Spika, lakini Hotuba ya Mheshimiwa Waziri aliyesoma leo

ukurasa wa 15, alieleza kuwa, kati ya mwaka 2011/2012 na mwaka 2013/2014,

Wizara imekopesha jumla ya milioni sita, kumi na mbili; je, nani mkweli kati ya

Waziri kupitia Mheshimiwa Nagu ama Waziri husika? Naomba Mheshimiwa

Waziri, aje anipe ufafanuzi huo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa naomba nianze na suala la pensheni. Ni

dhamana ya Maendeleo ya Jamii kusimamia wazee wanapata huduma zao

muhimu, lakini mpaka leo imekuwa hadithi katika nchi yetu, hasa Mheshimiwa

Waziri mwenye dhamana hii aweze kuwaeleza umma wa Watanzania, Wizara

ina mkakati gani kuhusu suala la pensheni kwa wazee mwaka huu wa

2014/2014, ili kuachana na danadana ya kuelekea Uchaguzi Mkuu badala ya

kuwaacha wazee wakihangaika na maisha yao ya kila leo?

Mheshimiwa Spika, napenda kujua, hivi pensheni hii ina ugumu gani wa

kuweza kusimamiwa na kuweza kupewa wazee hawa kwa muda ambao

unastahili, unasogezwa muda hadi kufikia uchaguzi ambao sasa hivi

tumebakiza mwaka mmoja tu? Au wazee hawa tumekuwa tunawafanya kama

kivuli, hawahitaji kupata stahili zao?

Mheshimiwa Spika, nije kwenye suala la ajira. Bado kuna wingu kubwa la

ajira ya watoto; watoto wamekuwa wakitumikishwa kinyume cha taratibu na

Page 98: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

98

Sheria. Pamoja na kutumiwa watoto hawa, haki zao za msingi kwenye ajira

ngumu hizo wanazikosa.

Mheshimiwa Spika, watoto wanaochukuliwa kupelekwa nje

wanadanganywa hapa na Serikali inatambua kabisa kwamba, kuna wakala

yupo anayepitisha watoto hawa kuwapeleka nje watoto wetu. Wanakwenda

kutumikishwa kule mpaka wanafanyishwa vitendo vingine ambavyo si vya

kiungwana, lakini bado hawapewi haki zao, wakifika kule wananyang‟anywa

na Passport zao. Sasa nataka kujua Serikali yetu inasimamia nini kuhusiana na

suala hili la haki za watoto? Yule Wakala anayepitishwa watoto wetu kwa nini

asisimamishwe kwa zoezi zima ambalo anapeleka watoto nje?

Mheshimiwa Spika, kuna mtoto yupo mpaka sasa hivi, alichukuliwa kutoka

hapa Tanzania akapelekwa Uarabuni. Kafika kule kaenda kutumikishwa kwa

mama mwingine, yule mtoto alipoona maisha magumu akahamia kwa mama

mwingine. Yule mama kamchukua yule mtoto kampeleka Mahakamani na yule

mtoto yuko gerezani mpaka leo. Hata hivi nilikuwa nikiomba wanieleze yuko

sehemu gani, ili tuweze kumwomba Balozi anayehusika kule asaidie yule mtoto

aweze kurudishwa hapa nchini Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watoto wetu wamekuwa katika maisha magumu

sana. Tunalo wimbi kubwa sana la watoto wa mitaani. Watoto hawa pia

wanahusiana pia na wazazi kuwatelekeza watoto, hususan wanaume

kuwakimbia watoto, kuwakimbia wake zao, na kusababisha wimbi kubwa la

watoto nyumbani kuona maisha ni magumu wanakwenda kujitolea huko nje.

Sasa hii elimu pia ingeweza kutolewa kwa wanaume ili waweze kuvumilia

maisha ya ugumu ndani ya nyumba zao ili waweze kulea watoto. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wanaume ni sehemu ya pamoja ya mikakati ya

Serikali katika malengo yake ikiwa kuzuia ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake,

utelekezaji wa watoto, vitendo vya udhalilishaji watoto, ndoa za utotoni, ukatili

dhidi ya watoto na masuala nyeti ya maendeleo ya jamii, hivyo wanaume

hukutwa na changamoto. Hivyo, maendeleo ya jamii yenye usawa wa kijinsia,

wanaume wakishirikishwa Taifa hili litakuwa imara.

Mheshimiwa Spika, watoto wamekuwa wakiozeshwa wakiwa katika umri

mdogo. Tunalifahamu hilo hata sisi wenyewe Serikali inatambua na hilo. Watoto

wengi wanaozwa kwenye umri mdogo, mtoto anaozwa chini ya miaka 15,

nane na anazaa mtoto kwa mtoto, haya ni maisha ambayo kwa kweli

hayastahili yanamnyima mtoto haki yake. Anakosa haki ya elimu, anakosa haki

ya kuchangia na yeye pia mawazo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, nije kwenye suala lingine la ajira kwa vijana. Ajira kwa

vijana wanaojiajiri mambo ya bodaboda. Bodaboda hizi zimeanzishwa kwa

Page 99: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

99

mikopo; wanakopeshwa vijana wetu, wanakwenda kutumikia kule, lakini

wanapopata ajali hawaangaliwi, hawana stahili yoyote ya malipo yoyote, lakini

hapohapo pikipiki hizi zinakuja zikiwa na helmet moja, helmet nyingine zile ni

kama za kujengea nyumba. Sasa utakuta kwamba, vijana hawa wanafukuzana

na Askari wanakamatwa, wanapelekwa Magerezani au wanatozwa fine ya

30,000/= na wakati hawana hata uwezo wa pesa hizo.

Mheshimiwa Spika, sasa suala hili lingeangaliwa upya. Wizara yangu

yenye dhamana, niko kwenye Kamati hii ya Maendeleo ya Jamii, lakini iangalie

tena kwa upande wa pili. Ajira, pamoja kwamba, imetolewa pendekezo

kwamba, walichokuwa wakidhamini ni hizo pikipiki, lakini sasa wangedhamini

na mipango mingine ambayo inawezekana, vijana hawa wakapata ajira.

Mheshimiwa Spika, nije dhidi ya ukatili wa akinamama. Akinamama

wengi wanapata ukatili, wanapigwa, wananyongwa, wanauawa na kesi

zinafikishwa Mahakamani na ushahidi unakuwepo. Aidha, ushahidi unaweza

ukawepo wa mtoto, lakini bado unakataliwa na unakuta mshtakiwa anatoka

nje; sasa hali hii ya wanawake kufanyiwa vitendo vya ukatili itakwisha lini katika

nchi yetu ya Tanzania na bado vimekuwa vikiongezeka siku hadi siku, je, Serikali

yetu inasema nini kuhusiana na masuala haya? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kweli, inasikitisha sana pia kuona wenzetu wenye

ngozi ambayo iko tofauti kuonekana kwamba, ndiye dili au uganga wa kupatia

mali kwa maisha ya Watanzania wenye akili finyu. Kwa kweli, hata hilo jambo

analolifanya haliwezi kumfikisha sehemu yake. Kwa nini umma usipewe elimu ya

kuwa, mwanadamu mwenzako sio chombo cha kukupatia wewe mali, sio

chombo cha kupitia wewe daraja. Ningeomba elimu hii iweze kutolewa, watu

hawa wawaone wenzao kama watu wa kawaida na sio kwenda

kuwadhalilisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimesikitishwa sana na mauaji yote yanayotokea ya

wenzetu albino. Pia nasikitishwa pia na mauaji yanayotokea ya wazee wetu

vikongwe, kwani ukongwe unamkuta kila mtu na ukongwe unapomfikia mtu,

mtu hubadilika sura, hubadilika macho, sasa isionekane kwamba, ndio mchawi,

mkafanya vitendo vya kumuua. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Nilikuwa nimemwita Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza,

atafuatiwa na Mheshimiwa Maryam Msabaha.

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa

kunipa nafasi ili nichangie kidogo katika Wizara hii ya Maendeleo ya

Wanawake, Jinsia na Watoto.

Page 100: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

100

Mheshimiwa Spika, naomba kwanza niunge mkono mawazo ya

Mheshimiwa Waziri katika ukurasa wake wa 43, hitimisho pale. Mheshimiwa

Waziri ameonesha vizuri ni jinsi gani Wizara hii inavyokuwa Wizara Mtambuka na

inavyopaswa kufikiriwa kwamba, kazi ya Wizara hii ni kusimamia maendeleo

katika nyanja mbalimbali ikiwemo afya, kilimo pamoja na maendeleo ya kijinsia,

lakini pamoja na mawazo yake mazuri, Serikali na jamii inaona kwamba, kweli

Wizara hii ni Wizara ya wanawake tu na ndio maana inapuuzwa, Wizara hii

inadharauliwa.

Mheshimiwa Spika, ukitaka kuona jinsi Wizara hii inavyodharauliwa, nenda

ukaone Ofisi katika Mikoa, nenda ukaone Ofisi katika Wilaya, ukaone

wafanyakazi wanavyofanya kazi, hawana vitendea kazi, hawana magari, yaani

ukifika katika Ofisi za Maendeleo ya Jamii katika ngazi za Halmashauri katika

Wilaya na katika Mikoa utaona ni jinsi gani Serikali inavyoipuuza na kuidharau

Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii inaendelea hata katika bajeti yao.

Japokuwa Kamati imesema pamoja na Kambi ya Upinzani, lakini naomba

niweke msisitizo; ukiangalia katika Randama yao, ukurasa wa 20 pamoja na

ukurasa wa 21, utaona ni jinsi gani Serikali inavyotoa pesa ambazo kwa kweli,

zinaogopesha au wakati mwingine zinatia hofu juu ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, hebu tazama Kifungu Namba 2001, Ujenzi na

Ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ya Wananchi. Njoo kile Kifungu

Namba 2002, ambacho kinahusu Ujenzi na Ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo

ya Jamii. Pesa inatolewa bilioni mbili, inaidhinishwa bilioni 2.3, lakini inatolewa

milioni 42 mpaka robo tatu ya mwaka. Kwa hiyo, unaweza kuona dhamira ya

Serikali haieleweki katika Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hata katika ujenzi na ukarabati wa Vyuo vya

Maendeleo wameomba milioni mia moja lakini imetolewa milioni ishirini na tano

tu. Kwa hiyo, unaweza ukaona kwamba kwa kweli hii Wizara itafanyaje hizi kazi

ambayo kazi yake kubwa ni kusimamia na kuhamasisha maendeleo ya

wananchi.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia hata kwenye Benki ya Wanawake,

tumetetea bilioni mbili ya kila mwaka mfululizo tukiwa kwenye Bunge hili, lakini

unaangalia mwaka huu wamepewa miliano mia tano na kumi na tano. Sorry

nianze na ule Mfuko ambao 5% ambayo inatoka kwenye Wizara.

Wanatengewa bilioni mbili, lakini wamepewa milioni 15.6. Kwa hiyo, unaweza

ukaona je, huu Mfuko unawezaje kusaidia wanawake kama kweli fedha

kiduchu namna hii ndiyo inayotolewa. Kwenye Benki ya Wanawake hivyo hivyo

inapaswa Serikali kutenga bilioni mbili kila mwaka, lakini kipindi hiki mpaka

Machi imetoa milioni mia nne hamsini.

Page 101: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

101

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, unaanza kuwa na mashaka kwamba kweli,

je, Serikali inadhamiria ili Benki ya Wanawake iweze kuendelea na kuweza

kupeleka matawi mengine katika Mikoa mingine pamoja na shughuli zote

alizosema Mheshimiwa Waziri katika ukurasa wake wa 28 za kupeleka vikundi

mbalimbali na kuhamasisha wanawake katika Mkoa wa Dodoma, Dar es

Salaama na Mwanza, lakini siamini kama hii kazi inaweza kufanyika vizuri kama

Serikali inatoa pesa kidogo namna hii.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaomba Serikali iitazame Wizara hii kama

Wizara ambayo kazi yake kubwa ni kuhamasisha wananchi na ndiyo maana

tunaomba Serikali iwaajiri wale Mama Maendeleo (Social Workers). Kama huna

Social Workers huwezi kuwahamasisha wananchi katika ngazi ya familia. Huko

nyuma walikuwepo wanakwenda nyumba hadi nyumba, wanahamasisha

wananchi mambo ya afya, wanahamasisha kilimo na wale wamesomea hizi

taaluma, wana taaluma za kufanya uhamasishaji, wanataaluma za kuangalia

watoto. Kwa hiyo, wanaweza kwenda katika familia na kusaidia wananchi

waweze kushiriki katika maendeleo na hivyo kuongeza ushiriki wa wananchi

katika kujiletea maendeleo.

Mheshimiwa Spika, napenda niongelee watoto wa mitaani. Watoto wa

mitaani wamekuwa tishio katika nchi yetu. Ziko sababu mbalimbali zimetajwa,

zimetajwa na Kambi ya Upinzani, zimetajwa na Kamati; ukatili, ukatili ndani ya

familia, ufukara uliokithiri katika nchi hii. Nchi hii imejaa umaskini, labda sisi

tuliokuwa hapa, tunakaa hapa katika viyoyozi labda hamwangalii ngazi ya kijiji,

watu wanavyoadhirika, watu wanakosa hata hela ya mlo mmoja. Kwa hiyo,

watoto wanakimbia wengine wenyewe kwa kuwa na matamanio ya kwenda

mjini kupata maisha mazuri, wakifika mjini wanakuta hakuna kazi wanafanyiwa

vitendo vya ajabu, wanalawitiwa, wanapewa hata magonjwa mengine.

Mheshimiwa Spika, naomba niulize Wizara mna mkakati gani mmesema

mnashirikiana na wadau upo mkakati upi tuuelewe ambao unasaidia watoto

hawa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali ina matumizi mabaya, matumizi katika sherehe

za nchi, matumizi katika ziara za Kiserikali ambazo zinakwenda misafara watu

mia moja, watu sabini...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

Page 102: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

102

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa

kuniona mdau katika Wizara hii. Nianze kabisa kwa kulaani kitendo cha Boko

Haram wa Nigeria kwa kuteka wasichana mia mbili na naomba Boko Haram

wawarejeshe wasichana wale na nikiwa kama mama ambaye nina uchungu

na wasichana hawa basi Boko Haram mara moja wawaachie watoto wale.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nipongeze Mashirika yote ya Dini mahali popote na

Masista wote, hawa wamekuwa wadau wakubwa kabisa wa kulea watoto

wanaoishi katika mazingira magumu. Wamebeba mzigo mkubwa wa Serikali

leo hii nataka niihoji Serikali ambayo inajiita ni Serikali sikivu, ni lini watatenga

maeneo kwa sababu tuna maeneo ya kutosha, tuna rasilimali za kutosha,

tutenge maeneo tuwajengee watoto wetu wanaoishi katika mazingira

magumu. Sisi tukiwa kama viongozi tutenge siku kama ni siku ya Jumamosi, ni

siku ya Ijumaa, siku mbili katika wiki tushiriki katika nguvu zetu kuwajengea

watoto hawa vituo vya kuwalelea na shule za kusoma.

Mheshimiwa Spika, jamani Mikoa tuseme tuangalie Mikoa kama Mkoa wa

Dodoma, tukija tukiangalia Dodoma, usiku nendeni pale karibu na CCM

mkaangalie watoto wanavyowasha makaratasi, wanavaa viporo, wanalala na

viporo, kweli Serikali hii iko wapi, kama ni Serikali sikivu, tutenge maeneo na

hawa mafisadi ambao wanakula fedha za umma, wanaofilisi Serikali, tuchukue

mali zile tuhudumie watoto wa mitaani.

Mheshimiwa Spika, leo ukifika kituo cha Ubungo watu wamegeuza

nyumba wanalala. Leo ukiwa kama unatoka mahali popote huko kama Ni

Dubai utasikia kwenye ndege wanasema Dar es Salaam, lakini watoto hawa

wamekuwa kero. Kwa kweli watoto wamekuwa kero, hii tuangalie Serikali na

tuangalie Serikali tupige kelele ni namna gani wataongeza Wizara hii, Wizara hii

siyo ya wanawake, Wizara hii imebeba jinsia zote.

Mheshimiwa Spika, leo hii kuna wanaume pia wananyanyaswa na wake

zao, leo hii kuna wanaume wanapigwa na wake zao, leo hii kuna wanaume pia

wanaachiwa watoto na wake zao, tuangalie matatizo yaliyozunguka Wizara,

tuangalie kingine nataka tukomeshe hawa watu ambao wanaanzisha NGOs

kwa kupitia migongo ya watoto hawa, kwa sababu wanapiga watoto picha,

wanaanzisha NGO, wanaomba pesa, wakishapata pesa zile wanajinufaisha

wenyewe watoto wale hawanufaiki. Tuangalie na tubadilishe Sheria.

Mheshimiwa Spika, nasema hivi, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria wewe

ni mdau wa watoto na Naibu Waziri wa sasa hivi umehamishiwa upo kwenye hii

Wizara, najua pia umesoma Sheria, tuangalie zile Sheria kandamizi zote

tuziondoshe, watoto wasome na wale ambao wanalawiti watoto wasipelekwe

magerezani wakatolewa, wanyongwe wafe kabisa wasirudi na wale ambao

Page 103: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

103

wanaharibu watoto, kuna watoto wanaharibika, watoto wanaharibika kabisa

wanaharibiwa na watu wenye akili zao timamu na matajiri wenye akili zao

timamu kwa ajili ya kutaka utajiri kwa kwenda kulawiti watoto, hawa pia

tuwafunge na ipitishwe Sheria ya kuwanyonga.

Mheshimiwa Spika, kingine ninachotaka kusema ni wafanyabiashara

ambao wanatumia wanawake, tena watoto wadogo wadogo, wanakwenda

kuwachukua watoto wale wanatumia kwenye Mahoteli makubwa kama vivutio

vya biashara zao, pia hili tuangalie tukomeshe.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli nimesikiliza hotuba ya Mheshimiwa Waziri

wa Wanawake na Watoto, lakini mama yangu Sophia pia hii hotuba ya

Barwany kuna mambo mazuri aliyoyazungumza mle ndani, chukua uyafanyie

kazi ili Wizara yako iwe na mashiko. Mama yangu usifanye Wizara hii

tutaandamana mpaka kwa Rais ili Wizara hii itendewe haki na kama Spika ni

mwanamke pia uangalie Wizara hii tuitendee haki. Tukiangalia humu tusitumie

wanawake kwa ajili ya kutupigia kura, tuangalie wanawake hawa nao

wananufaika vipi wanavyotupigia kura, tusiangalie wanawake hawa tu wakati

eti tunaangalia vitu kidogo kidogo tunawatumia, tuangalie ni miradi gani

ambayo tutawapa ili waepukane na mazingira magumu ambayo wanaishi.

Mheshimiwa Spika, tuangalie na wale akina baba ambao wanatupa

watoto ambao wana uwezo wachukuliwe sheria nao wapate kule watoto wao,

tuwaangalie wale watoto kwa sababu kuna watoto Dar es Salaam wanalala

kwenye mitaro na watoto wale wanabakwa, hivyo kila siku watoto

wataongezeka. Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya wote tushirikiane

tuhakikishe tatizo hili la watoto wa mitaani linaondoka. Hii siyo kazi ya Serikali na

wale ambao wanaona kama Wizara hii ni ya akina mama, Wizara hii siyo ya

akinamama, Wizara hii imebeba jamii ambayo inatupigia kura. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi niliyesimama leo hapa ni Makamu Mwenyekiti

wa Wanawake Taifa (BAWACHA). Kwa hiyo, nazungumzia wanawake wote na

tuangalie ni kitu gani kitatuunganisha wanawake bila kujali mambo ya siasa na

tufuatilie NGO ambazo zinaanzishwa kwa ajili ya kuwanufaisha watu...

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Huyu ndiye anaitwa Msabaha ana natural idea ya kwake, mpaka

unaona anasikika vizuri masikioni. Niite na wanaume pia halafu anasema Spika

aongoze maandamano kupinga. Mheshimiwa Kapteni Komba, atafuatiwa na

Mheshimiwa Badwel.

Page 104: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

104

MHE. KAPT. JOHN D. KOMBA: Mheshimiwa Spika, naomba nichangie

Wizara hii. Kwanza kabisa niiombe familia ya Marehemu Amina Ngaluma msanii

mwenzangu aliyefariki siku mbili, tatu zilizopita kwamba wawe na amani Mungu

alitupa na Mungu amechukua ni msanii ambaye ni maarufu sana katika nchi

yetu, amefanya kazi katika vikundi mbalimbali African Stars, Tanzania One

Theatre na vikundi vingine vya nje, Uarabuni huko, lakini Mungu amemchumua,

basi jina la bwana lihimidiwe.

Mheshimiwa Spika, pili, nitoe pongezi kwa Waziri Sophia Simba na

mwenzake Pindi Chana. Waziri Sophia Simba ni Waziri peke yake ambaye kwa

kweli katika miaka yote niliyoishi katika Jimbo langu ni Waziri aliyetembea siku

tatu mfululizo bila kuchoka kuwahimiza wanawake wa Nyasa namna gani ya

kujiondoa walipo na kwenda ambako wanatakiwa waende. Mama Sophia

Simba nakupongeza sana na Mungu akubariki sana na ndiyo maana hata

kwenye kitabu chako cha hotuba yako picha ya kwanza inayoonekana mbele

ni ya watoto kutoka Ziwa Nyasa, Mbambabay nakushukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikirudi kwenye hii hotuba ya Kambi ya Upinzani, yako

mambo nakubaliana nayo, lakini yako mambo mengine hayana mashiko

kabisa. Anapozungumza habari ya Salma Kikwete kufanya kampeni, yule ni

mjumbe wa NEC wa Chama cha Mapinduzi na amezunguka nchi nzima

kukinadi Chama chake, sasa hiyo dhambi iko wapi?

Mheshimiwa Spika, nawaona wengine wanazunguka na wachumba tu

mchana kutwa wanazunguka na wachumba, wanakaa kwenye majukwaa na

wachumba zao, wakimaliza kazi usiku burudani, hawa hamuwataji, lakini

mnamtaja Salma ambaye anazunguka kama Mjumbe wa NEC nchi nzima

kunadi Chama chake na kukipatia ushindi. Huo ni ufinyu kidogo wa fikra…

MJUMBE FULANI: Mtaje.

MHE. KAPT. JOHN D. KOMBA: Sijui anaitwa Josephine sijui anaitwa nani

sijui.

Mheshimiwa Naibu Spika, halafu pia katika hotuba hii imezungumwa vitu

ambavyo si vya kweli. Nimpongeze sana yule mama, Mkurugenzi wa Benki ya

Wanawake. Yule mama ni Simba, anajua kupigana, pamoja na kwamba

Serikali haijatoa fedha nyingi kama walivyomwahidi maana bilioni mbili zilitoka

mwanzoni, bilioni mbili zikafuata, baada ya pale zimefuata kidogo, baada ya

pale zero zero mpaka leo lakini amejitahidi kuanzisha vituo mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, amekwenda Mikoani pia siyo Dar es Salaam tu

amekwenda Iringa, amekwenda Mbeya, amefika Songea na sasa hivi yuko

Nyasa na ushahidi ni kwamba nyumba yangu mimi ndiyo sehemu ya Ofisi ya

Page 105: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

105

hiyo benki yao. Sasa hawa wanapozungumza kwamba hawaendi huko, ni aibu

kweli! Unazungumza kitu bila utafiti, bila ya utafiti usiseme, usizungumze kabisa.

Kwa hiyo, hii hotuba sijui kama ina mashiko. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, nikushukuru sana Mkurugenzi wa Benki ya

Wanawake na leo hii ninapozungumza vijana mia moja hamsini wanajaza fomu

za kupata mikopo ya pikipiki pale Nyasa, pale Mbambabay, hii ni kwa ajili ya

juhudi ya yule mama Chacha. Kwa hiyo, mama Chacha kama upo hapa

ndani, kama upo nje nakushukuru sana. Baada ya hizi pikipiki mia moja hamsini,

tutakuomba na nyingine tena mia moja hamsini ili vijana wote wafanye kazi

wasikae vijiweni.

Mheshimiwa Spika, fedha wanazopata ni kidogo, naomba Serikali ijitahidi

iweze kumwongezea fedha hizo ambazo Mheshimiwa Rais aliahidi mwenyewe

kwamba kila mwaka watapewa bilioni mbili. Kwa hiyo, naomba miaka ile

ambayo tayari imepita na hawajapata bilioni mbili wapewe, kwa kuwa ili

iendeshwe kama benki na ijitegemee, lazima iwe na mtaji usiopungua bilioni

kumi na tano sasa bilioni kumi na tano siyo mchezo. Kwa hiyo, naomba Serikali

itimize ahadi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatu, ni Halmashauri ile asilimia tano, kwa kweli kama

Halmashauri zote zingetumia asilimia tano kuwapa akinamama, hakika

wanawake hawahitaji mikopo mikubwa sana, ukimpa laki mbili atatengeneza

milioni mbili baada ya miezi miwili, miezi mitatu, siyo kama sisi, maana hafikirii

akimaliza pale akanywe pombe, anafikiria akimaliza pale akafanye kazi

nyingine, tofauti ukimpa Komba akimaliza pale anafikiria kwenda kunywa

pombe, kwenda kwenye mchepuko pengine, lakini akinamama hawaendi

hivyo, akina mama wanaendeleza familia, ndiyo maana wanasema

ukimwendeleza mwanamke, unaendeleza familia nzima na ukimwendeleza

mwanamme unaendeleza mtu mmoja. Wanawake si mara nyingi kwenda

kwenye michepuko. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, namba nne, Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, kwa kweli

naomba Serikali iangalie. Hakuna Chuo hata kimoja chenye gari la uhakika na

vyuo hivi vingi vinaongozwa na akinamama, unawaonea huruma kabisa. Sasa

Serikali nimeambiwa pale bandarini yako magari karibu mia tatu yaliyotaifishwa

kwa ajili ya watu kukosa kulipa ushuru, basi kama magari mia tatu yale sehemu

yake pelekeni kwenye vyuo hivi vya Maendeleo ya Wananchi vinavyoongozwa

na akinamama ili maendeleo yafike sana kule vijijini.

Mheshimiwa Spika, halafu kuhusu ngoma. Ni kweli kuna ngoma

kibaokata, sunsumia na zingine zingine. Zamani kwa mfano kibaokata ilikuwa

inachezwa na akinamama, lakini leo akinamama sasa na mimi narudi kwenu,

mnachukua vijana wadogo wadogo wa kiume, mnawafunga shanga,

Page 106: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

106

mnawakatishakatisha vibaokata kule, ndiyo maana mashoga sasa wako wengi

sana katika nchi yetu, acheni mchezo huu akinamama wakuchukua vijana wa

kiume kuwachezesha…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. KAPT. JOHN D. KOMBA: Aaaa! Ya kwanza hiyo au ya pili?

SPIKA: Ya pili hiyo.

MHE. KAPT. JOHN D. KOMBA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

(Makofi)

SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Omary Badwel, atafuatiwa na Mheshimiwa

Rosweeter Kasikila!

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa

kunipa nafasi hii ili niweze kutoa mchango wangu katika Wizara hii ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

Mheshimiwa Spika, wengi tunafahamu namna ambavyo kina mama

mbalimbali kule vijijini na mijini jinsi walivyokuwa na jitihada mbalimbali za

kujiletea maendeleo ya kiuchumu, lakini akinamama wengi wanakwaza na

utaratibu usiokuwepo wa mikopo ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa

hatua yake ya kuanzisha benki ya wanawake Tanzania. Ni mpango mzuri na sisi

tunaupongeza, lakini wasiwasi wangu mkubwa kwamba benki hii imejikita sana

mijini, sisi Wabunge wenye Majimbo ambayo asilimia mia moja ni vijijini tunaona

tutachelewa sana kupata manufaa ya Benki hii ya Wanawake. Nitolee mfano

sasa hii benki imeanza kujitanua hapa Dodoma imefungua vituo vya kuwezesha

akinamama kukopa na kupata ushauri wa ujasiriamali, lakini kati ya vituo kumi

na moja vilivyofunguliwa Dodoma vyote vipo hapa Dodoma mjini na Bahi iko

hapa jirani, Kondoa iko hapa jirani, kwa nini vituo vyote hivi kumi na moja

viende vikakae hapa Dodoma Mjini? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wakati Mheshimiwa Waziri anajibu hoja hii,

naomba aniambie ni vituo vingapi atapunguza hapa Dodoma Mjini ili apeleke

Bahi angalau na wale akinamama wa Bahi waweze kufaidika na Benki hii ya

Wanawake ambayo sasa imesogea hapa Dodoma na wamepeleka Kongwa,

wamepeleka Mpwapwa, lakini Bahi naona haijafika.

Page 107: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

107

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la pili ni habari ya fedha ambazo

zinatengwa na Halmashauri asilimia tano kwa wanawake na asilimia tano kwa

vijana. Kama Halmashauri zetu zingekuwa serious kwa miaka mingi ambazo

fedha hizi zimetengwa kwa mujibu wa Sheria, leo Halmashauri zingekuwa mbali

sana katika kusaidia akinamama na vijana, lakini kwa kweli fedha hizi

hazitengwi, Halmashauri zimesahau kabisa jambo hili. Nataka kujua Wizara

inasema nini juu ya jambo hili? Sisi Wabunge tumepiga kelele sana kule kwenye

Wilaya zetu, lakini ni danadana na hata hizi fedha zikitengwa, upelekaji wake

kwa akinamama ni mgumu sana, kumekuwa na urasimu mkubwa, kumekuwa

na michakato mingi ambayo inamfanya mama huyu wa kijijini akate tamaa na

asiweze kwenda kuukaribia huu mkopo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka nione Wizara hapa inasema nini na

pia katika kurahisisha kabisa suala la mikopo hii asilimia kumi kwa vijana na

wanawake katika Halmashauri zetu. Ni lazima Wizara iwe na maneno ya

kusema na kusimamia kikamilifu. Wakurugenzi na viongozi wengi wa

Halmashauri wao wako katika miradi mikubwa mikubwa miradi ya maji, miradi

ya barabara, miradi ya ujenzi, lakini miradi hii ya akinamama na vijana ya

kuwaendeleza kiuchumi wameisahau na hapo hapo wanawadai wananchi

kuchangia michango mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, hivi utamchangishaje mwananchi kujenga Sekondari

wakati hujamwezesha kiuchumi? Lakini leo Halmashauri zingekuwa makini,

zingetoa hizi fedha akinamama na akinababa au vijana wangekopa,

wangekuwa na uwezo mkubwa sasa wa kufanya kazi mbalimbali za kiuchumi

na hata unapokwenda wala hakuchukii na anaweza kukupa mchango wake.

Mheshimiwa Spika, pia naomba nichukue nafasi hii kutoa pongezi kwa zile

NGOs ambazo kwa kweli zinafanya kazi nzuri ya kusaidia utoaji wa huduma kwa

wananchi wetu mbalimbali. NGOs nyingi zimejitahidi sana, zinafanya kazi nzuri

na zimechukua sehemu kubwa ya wajibu ambao ulikuwa ufanywe na Serikali,

lakini wameendelea kuzifanya wao. Bahati nzuri mimi nimefanya kazi sana na

NGO, watu mle ndani wako serious, wako busy, wako makini na wanatafuta

fedha, wengi wao wanatafuta fedha kwa ajili ya kusaidia matatizo mbalimbali

ya wananchi wanaowazunguka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwapongeze wote kwa kweli na kwa kiwango

kikubwa, nichukue nafasi kuipongeza NGO ya AFNET ambayo inafanya kazi

karibu Mikoa nane katika nchi yetu na wanafanya kazi kubwa ya mapambano

dhidi ya ukeketaji wa wasichana na watoto wa kike na wanawake. (Makofi)

Nampongeza sana Mkurugenzi wa NGO hii, Mama Sara Mwaga na timu

yake kwa kufanya kazi nzuri iliyotukuka. Nami nafikiri ifike mahali lazima tuwe

Page 108: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

108

tunatambua hizi juhudi za Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali, yanayofanya vizuri

lazima tuyatambue na tufike mahali tuwe tunayapongeza. (Makofi)

Tunapongeza vitu mbalimbali, tunapongeza wafanyakazi bora,

tunapongeza watu mbalimbali lakini tumesahau pia kujua kwamba hizi NGOs

zinafanya kazi kubwa ya kusaidia kupambana na mambo mbalimbali ya kijamii

katika maeneo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Kamati zile za UKIMWI zinafanya kazi

kwenye Halmashauri zetu chini ya maendeleo ya Idara ya Jamii ambayo iko

chini Wizara hii, nilikuwa na ushauri ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, Kamati zile zinafanya kazi moja tu ya UKIMWI katika

maeneo yale ya Wilaya, Kata na Vijiji, lakini tunasahau pia madawa ya kulevya

yanayohusiana na bangi na mirungi ambayo pia imekuwa ni kikwazo kikubwa

kwa vijana wetu. (Makofi)

Sasa nilidhani hizi Kamati ziongezewe jukumu; kama tulivyoshauri kwenye

Kamati yetu ya UKIMWI kwamba ziongezewe jukumu pamoja na masuala ya

UKIMWI, lakini pia ishughulike na masuala ya madawa ya kulevya na hususan

bangi. Serikali imekazania heroin, cocaine, madawa makubwa makubwa,

wafanyabiashara wakubwa wakubwa, imesahau kwamba vijana wetu

wanateketea kwenye Vijiji vyetu na Miji yetu kwa bangi na mirungi. (Makofi)

Kwa hiyo, lazima jambo hili, hata kama Kamati zile haizuisiki katika

kukamata lakini zihusike katika uhamasishaji, upokeaji wa taarifa ili kuweza kujua

hali halisi ya madawa ya kulevya katika maeneo hayo, kwa sababu

maendeleo ya jamii hayawezi kuja kama vijana wakati mwingi wanafikiri kuvuta

bangi au kutumia mirungi ndiyo sehemu ya maisha yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mwenyekiti wangu wa Kamati aliwahi kuzungumza

vizuri habari ya viroba. Viroba vinapunguza nguvu kubwa ya vijana wetu

kufanya kazi. Leo hii mwanafunzi anakwenda na kiroba mfukoni, mkulima

anakwenda na kiroba mfukoni, fundi seremala anakwenda na kiroba mfukoni;

yote hii ni kwa sababu viroba vinauzwa holela. Maduka ya kuuza pipi, maduka

ya kuuza nyanya yote yanauza viroba. Kila mahali panauzwa kiroba.

Hivi Serikali inasema nini juu ya jambo hili? Hatuwatakii mema vijana wetu

kwa sababu wameona njia rahisi ni kiroba kimoja, amepata nishai, ndiyo

anafikiri anaweza kufanya kazi akiwa ameshapata kiroba kimoja. (Makofi)

Kwa hiyo, nadhani Serikali ipige marufuku uuzaji holela wa viroba; na hii

itawasaidia sana vijana na akina mama kwenda kufanya kazi zao wakiwa na

akili timamu, kuliko kuacha kama ambavyo ilikuwa. (Makofi)

Page 109: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

109

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naunga mkono hoja. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Sasa namwita na Mheshimiwa Kasikila, atafuatiiwa na

Mheshimiwa Modestus Kilufi.

MHE. ROSWEETER F. KASIKILA: Mheshimiwa Spika, nami pia natoa shukrani

zangu nyingi kwa kupata hii nafasi ili niweze kuchangia haya machache

kwenye hii Wizara ya Maendeleo ya Jamii.

Kwanza, niipongeze Wizara ya Maendeleo ya Jamii kwamba katika

maombi yao ya Shilingi bilioni 30.2 wameweza kutenga fedha za maendeleo

Shilingi bilioni tisa lakini fedha kwa ajili ya matumizi mengineyo, Shilingi bilioni

nane, kinyume na Wizara nyingine ambazo utakuta matumizi mengineyo hela ni

nyingi zaidi kuliko za maendeleo. Hongereni sana. (Makofi)

Pia wameweza kufikiria fedha za ndani ni Shilingi bilioni saba lakini za nje

Shilingi bilioni mbili tu, tofauti na wengine ambao huwa wanategemea zaidi

fedha za nje ambazo mara nyingi hazifiki.

Mheshimiwa Spika, sasa nizungumzie kwamba katika hizo fedha za

maendeleo zinazoombwa, Shilingi bilioni tisa, nilikuwa nasisitiza kwamba zile five

percent za vijana na five percent zinazotengwa kwa ajili ya wanawake, ziweze

kufikishwa kwenye Halmashauri. Wakurugenzi, pesa hizi zitakapokuwa zimefika,

wazitangaze! Zisiwe ni za kuhamisha na kutumia kwenye matumizi mengine

halafu wahusika wanakuwa hawazipati. Zitangazwe na waelimishwe; ndiyo kazi

za Maafisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri zetu; kuwaelimisha

wananchi kwamba pesa zipo na zitatumikaje.

Kama nilivyoongea last time kwamba pesa zipo, kama wanafikiriwa

kupewa, wapewe kwanza mafunzo, kwa sababu kama watapewa pesa hizi

bila mafunzo ndiyo utakuta wananunua magauni na kaptula tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kidogo kuhusu Benki ya Wanawake. Benki

ya Wanawake naendelea kupongeza kwamba inatanua katika Mikoa mingine.

Lakini mwaka uliopita niliomba kwamba Tawi Mkoa wa Rukwa lifunguliwe,

ikichukuliwa kwamba Mkoa wa Rukwa ni Mkoa ulio pembezoni.

Mwaka 2013 niliomba kwamba mwaka huu na sisi Rukwa tuweze

kufikiriwa. Lakini katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri ukurasa wa 28

imeandikwa, Vituo 29 ambavyo vimefunguliwa na vitanufaika na mkopo huu.

Vituo hivi viko katika Mkoa wa Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza.

Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena nipeleke ombi langu,

kwamba basi kwa sababu Rukwa haikufikiriwa tena kupelekewa Tawi mwaka

Page 110: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

110

huu, naomba mwakani 2015/2016 Tawi Mkoa wa Rukwa liweze kufunguliwa ili

Wilaya ya Nkasi, Sumbawanga Vijijini, Sumbawanga Manispaa na Kalambo,

ziweze kunufaika ili wale wanawake wanufaike na mikopo inayotokana na Tawi

hili la Benki ili waweze kujinufaisha katika ujasiriamali na kuinua kipato chao.

Wasiwe ni tegemezi kwa akina baba tu mpaka hata vitambaa vya kufunga

kichwani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba hilo liweze kutekelezwa ili tuweze

kufikiriwa na sisi Mkoa wa Rukwa.

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kuhusu elimu ya afya ya uzazi. Elimu ya

Afya ya Uzazi, sielewi Serikali ina mpango gani thabiti wa kutoa elimu ya afya ya

uzazi mashuleni, ili kuzuia mimba za utotoni zisizotakiwa. Kwa sababu mimba hizi

ndiyo tunaona zinapelekea hata wanafunzi wasichana kusitisha masomo yao,

pia zinapelekea sana utoaji wa mimba kiholela na kusababisha vifo kwa wingi.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tunazungumzia habari za fifty fifty. Lakini fifty fifty

itakuwa ni ndoto endapo hatutadhibiti mimba za wasichana mashuleni na

ikapelekea dropout kwa wingi sana. Itafika mahali Serikali inawatafuta

wasichana wa kuingia kwenye fifty fifty lakini hawapo kwa sababu

hawakusoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie kidogo ugatuaji wa madaraka kwa

wananchi, ambalo ni sera nzuri na imekuwa ni jambo zuri sana. Tumekuwa

tukishirikisha wananchi katika kutambua matatizo na fursa zilizoko kwenye

maeneo yao EO and OD.

Sasa Vijiji na Kata na Halmashauri wanapoleta mipango na ikaletwa

hapa bajeti na tukapitisha bajeti, pesa zinaporudi Halmashauri, tunaomba hata

Kata nazo zipelekewe pesa ambazo zilikuwa zimetengwa kwenye mipango yao

ya Kata, lakini kwenye mipango yao ya Vijiji ili wananchi wale waweze

kutekeleza ile mipango ambayo walikuwa wameombea pesa hizo. Katika

utekelezaji isiwe ni ngazi ya Halmashauri tu inayotekeleza, pia wananchi

washirikishwe. Isiwe wananchi wanashirikishwa tu kwenye kutambua matatizo

na fursa, lakini washirikishwe katika utekelezaji na hata katika ufuatiliaji, katika

tathmini ili mwaka mwingine unaofuatia wajue ni wapi walipokosea waweze

kutengeneza vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni kilio cha muda mrefu, wananchi

wanashirikishwa kutafuta matatizo na kupanga lakini hawaonyeshwi hata pesa.

Zile pesa zinaporudi huko ziwekwe kwenye mbao za matangazo ili wananchi

wajue kile walichokiomba wamepewa chote au hawakupewa chote, au

hawakupewa kabisa. (Makofi)

Page 111: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

111

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni kilio cha wananchi kwamba miradi

wanayokuwa wameipanga au wameitambua inakuwa haitekelezwi na ukiiuliza

Serikali, inasema fedha hazikutosha. Mimi nilikuwa naona sasa tuchukue

utaratibu mzuri wa kuboresha makusanyo ili Hazina iweze kupata fedha za

kutosha na ili iweze kupeleka kwenye Halmashauri au kwenye Wizara husika

kadri walivyokuwa wameomba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, yangu machache ni hayo, naomba yachukuliwe na

Wizara, lakini nauna mkono hoja kwa asilimia mia kwa mia. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Naomba nitambue kwanza wageni. Nilikuwa nimepanga

baada ya kusema Wenyeviti niwatambue, nikawa nimepitiwa. Kwa hiyo,

naomba niwatambue wageni. Kwanza, wako wageni wa Mheshimiwa Sophia

Simba, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, ambao ni Wakuu wa

Taasisi zake katika Ofisi yake, wanaongozwa na Mheshimiwa Anna Mayembe,

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo. (Makofi)

Pia kuna wanafunzi 10 kutoka Chuo Kikuu Dodoma, wakiongozwa na Bi.

Lucy Rutainura, na hawa naomba wasimame wote kama wapo. Okay, wako

huku na huku, wamesambaa. Halafu kuna wanachuo wengine 31 kutoka Chuo

Kikuu cha Mzumbe wakiongozwa na Spika wa Bunge la Chuo Kikuu cha

Mzumbe. Huyo Spika kwanza asimame peke, yuko wapi huyo Spika? Ehe!

Wengine wasimame sasa. Ahsante sana, wote ni akina mama. Tunaomba

msome vizuri. Haya wanayosimulia Waheshimiwa Wabunge, ninyi msome kwani

ndio ukombozi wetu sisi. Huyu Spika, anaitwa Mwashibanda Shibada. Ahsante

sana, hongera Mheshimiwa Spika. (Makofi)

Tuna viongozi wawili kutoka UWT Morogoro, sijui wako wapi! Kuna viongozi

wengine watano kutoka UWT Dodoma, naomba wasimame walipo. Halafu

kuna wanafunzi 25 wa Chuo cha Ufundi cha Don Bosco Dodoma, wasimame

walipo; ahsante sana, karibuni sana.

Halafu tuna wanafunzi wengine 150 kutoka Chuo cha Maendeleo ya

Jamii, TRACDI. Naomba wasimame hawa, Maafisa wa Maendeleo ya Jamii. Ah,

kweli, Wizara yenu! Hongera sana, mwendelee vizuri. Ahsante. (Makofi)

Kuna wanafunzi wengine 55 kutoka Chuo Kikuu cha St. John, naomba pia

wasimame hapo walipo kama wamefika. Ahsanteni sana, karibuni sana.

Tunaomba wanafunzi wote fanyeni kazi ya kusoma, mnaona tatizo letu ni watu

wetu kusoma na tutaweza kuendesha mambo yetu vizuri kama nyie mnasoma

vizuri. Ahsante sana. Niendelee na Mheshimiwa Modestus Kilufi. (Makofi)

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Spika,…

Page 112: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

112

SPIKA: Samahani kidogo Mheshimiwa Kilufi.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka

niweke taarifa sawa kutokana na mchangiaji aliyepita, anasema kwamba five

percent kwa ajili ya vijana na wanawake zinakuwa zinatoka Serikalini. Nataka

niweke sawa hii taarifa kwamba five percent kwa ajili ya wanawake, five

percent kwa ajili ya vijana inatoka kutokana na mapato ya ndani ya

Halmashauri. From own source ya Halmashauri zetu. Ni wajibu wetu kama

Madiwani kuhakikisha fedha zile zinatumika kama zinavyopaswa.

Kwa upande wa Serikali kinachotoka ni mchango wao wa Serikali

ambapo Wizara hii ya Jinsia Wanawake na Watoto ilikuwa inatoa Shilingi milioni

nane kipindi kilichopita. Baada ya kukaa na Kamati yetu ya LAAC

tukakubaliana, sasa hivi wamepandisha mpaka Shilingi milioni 12. Hizo ndizo

ambazo zinatoka Serikalini.

Mheshimiwa Spika, naomba niweke sawa katika hili. (Makofi)

SPIKA: Sasa lazima ueleze we nani, maana yake…

MBUNGE FULANI: Taarifa.

SPIKA: Si ujieleze, wewe nani?

SPIKA: Mimi sitaki taarifa. Mheshimiwa Rajab, jieleze wewe ni nani?

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMED: Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya

Bunge inashughulikia Hesabu za Serikali za Mitaa. (Makofi)

MHE. SYLVESTER M. MABUMBA: Taarifa Mheshimiwa Spika.

SPIKA: Mheshimiwa Mabumba.

MHE. SYLVESTER M. MABUMBA: Mheshimiwa Spika, naomba kumpa taarifa

msemaji aliyepita. Maelekezo ya kutenga asilimia kumi yameelekezwa na

Kamati yako ya TAMISEMI, siyo LAAC.

SPIKA: Sasa ngojeni kwanza tuelezane hapo, msianze kubishania vitu

vidogo sana. maelekezo ya kwamba zile asilimia ziwekwe, ni ya siku nyingi sana.

Aliyefanya hivyo, alikuwa Mama Anna Abdallah, wakati huo alikuwa Waziri wa

TAMISEMI, isipokuwa utekelezaji wake ulikuwa haufanyiki vizuri. Sasa TAMISEMI

ndiyo wanaoongoza sekta; LAAC ndiyo wanaokagua hesabu. Kwa hiyo, wote

mko sawa. (Makofi)

Page 113: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

113

Tunaendelea. Mheshimiwa Kilufi, naomba uendelee na hotuba yako.

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa

nafasi hii ili niweze kuchangia Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto. Naomba vilevile nichukue nafasi hii kuwashukuru sana Ofisi ya Waziri

Mkuu na TAMISEMI kwa kusitisha ushuru haramu uliokuwa unatolewa kwa

wakulima wanaorudisha mazao yao kutoka shambani Wilayani Mbarali na

mahali pengine; kwamba kama wanafanya hivyo waache mara moja na

mageti yaliyomo ndani ya Wilaya yaliyotapakaa kila sehemu yaachwe bila

kuwabungudhi wakulima, ushuru ni kwa wafanyabiashara na siyo kwa wakulima

wanaorudisha mazao kutoka shambani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba niipongeze sana

Wizara hii kwa jitihada nyingi ambazo wamekuwa wakifanya ili kuhakikisha

kwamba huduma za jamii zinakwenda vizuri kwa akinamama na watoto. Lakini

bajeti ya mwaka 2013/2014 ilikuwa ni Shilingi bilioni 25, lakini ukiangalia kwenye

kutolewa, wamepewa hizi fedha kidogo sana ukilinganisha na mahitaji halisi ya

Wizara hii. Ombi langu ni kwamba sasa Serikali ione umuhimu kutoa fedha za

kutosha kwa Wizara hii ambayo ni kiungo muhimu kwa kuendeleza jamii ya

Watanzania ili iweze kutimiza majukumu yake sawasawa.

Mheshimiwa Spika, bajeti ya mwaka 2013/2014 wamepewa Shilingi bilioni

30. Fedha hizi kwa majukumu iliyonayo hazitoshi. Vilevile Halmashauri zinatakiwa

zitoe asilimia 10, kwa maana asilimia tano kwa ajili ya vijana na asilimia tano

kwa ajili ya akina mama, lakini hizi fedha zimekuwa hazitolewi kwa wakati.

Halmashauri mara nyingi zimekuwa zikitoa fedha hizi lakini siyo kwa kupenda.

Nini kinachofanya wasitenge? Nashauri, Mheshimiwa Waziri fuatilia ili kuhakikisha

akina mama hawa ambao wanategemea sana fedha hizi kwa ajili ya biashara

ndogo ndogo ili waweze kuinua vipato vyao waweze kulitumikia Taifa na

kutunza watoto.

Mheshimiwa Spika, Azimio la Bunge la 993 (17) sehemu ya (1) cha sheria

namba 21 ya mwaka 1961 kinahalalisha uhalali wa Wizara hii kusimamia vizuri

majukumu yake kwa ajili ya ustawi wa Watanzania. Suala la Halmashauri

kusaidia vikundi vya akina mama na vijana siyo suala la hiari. Tumeshuhudia

vijana ambao tumesema wajiajiri, kwa maana ya kuendesha biashara ya boda

boda, lakini boda boda hizi nyingi siyo za kwao ni za matajiri. Sasa kupitia Wizara

hii, tunategemea hawa vijana hizi fedha zitolewe na Halmashauri ili waunde

vikundi waweze kukopeshwa waendeshe biashara hii kwa maana ya faida yao

wenyewe na siyo kutumikia matajiri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nashawishika kushauri Wizara ijitahidi

kuhakikisha kwamba inasimamia vizuri mapato haya yanayotokana na mifuko

ya vyanzo vya Halmashauri ili kusudi fedha hizi ziweze kutolewa kwa vijana.

Page 114: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

114

Vilevile Wizara ifanye jitihada kuhakikisha kwamba vijana wanaunda vikundi

kushirikiana na wataalam walioko kwenye Halmashauri ili waweze kupewa

utaratibu mzuri wa namna wa kupata mikopo hii kwa sababu wengi hawaelewi

wanapataje hiyo mikopo kutoka Halmashauri kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii inalojukumu kubwa; wapo watoto yatima,

wapo watoto wa Mitaani ambao wengine ni yatima hao hao; lakini wapo

wajane wasio na uwezo, wapo wazee na wastaafu ambao kwa kweli

wanaendelea kuhangaika kwa kupata fedha hizi kwa shida sana na wakati

mwingine kwa kiwango ambacho sasa kimepitwa na wakati; wapo walemavu;

wote hawa ni haki yao katika Taifa hili; wana haki ya kuishi na kuenziwa na

Serikali yao tukufu.

Mheshimiwa Spika, haifurahishi na haipendezi kuona watoto wa Mitaani

wameachwa hivi hivi bila kuchukua hatua za kuhakikisha kwamba watoto

hawa wanapewa utaratibu mzuri na kuishi kama Watanzania wengine

wanavyoishi. Ni dhambi kuona watoto wa Mitaani wanaachwa bila

kuangaliwa. Nilikuwa namshauri Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii afanye

utaratibu wa kutambua watoto hawa bila kuziachia Halmashauri peke yake

jukumu hili limekuwa ni kubwa, sasa hivi hawa watu wameongezeka kutokana

na matatizo mbalimbali ambayo yamekuwa yakijitokeza nchini hasa ukizingatia

maradhi haya ambayo yanaendelea kutuandama wananchi.

Mheshimiwa Spika, vilevile nawashukuru sana wote wanaojitoa kwa ajili

ya kusaidia watoto, vijana na walemavu na hasa Mheshimiwa Rais kwa jitihada

ambazo amekuwa akizifanya; vilevile Mheshimiwa Mama Salima Kikwete kwa

kupitia Taasisi ya UWAMA ambaye na yeye amekuwa akionyesha mfano mzuri

wa kuigwa katika kuona umuhimu wa kuwaenzi hao watoto ambao wengi

wamekuwa hawana mwelekeo.

Vilevile nawashukuru baadhi ya watu wenye mapenzi mema kama

Mheshimiwa Reginald Mengi, mara nyingi tumeshuhudia akiwaenzi watoto

hawa na walemavu kwa pamoja angalau kuwapa matumaini ya kwamba na

wao wana haki ya kuishi kama watu wengi.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

inayo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante.

Page 115: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

115

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Muda hautoshi,

naunga mkono hoja.

SPIKA: Nilitangaza kwamba kuna wanafunzi wa Chuo cha Don Bosco,

naambiwa siyo wanafunzi, wao ni Wakufunzi, yaani Walimu na Wafanyakazi.

Lakini karibuni na ahsanteni.

Sasa namwita Mheshimiwa Amina Abdallah Amour, atafuatiwa na

Mheshimiwa Fatuma Abdallah Mikidadi.

MHE. AMINA ABDALLAH AMOUR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwanza, nakupongeza kwa kuleta ombi na kuweza kukubaliwa kuchangia sasa

hizi.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Serikali kwa kuleta agizo kuwa

Halmashauri zichangie fedha kwa ajili ya kuendeleza wanawake. Jambo hilo ni

zuri sana, lakini pia nataka kumwuliza Waziri, hizi rasilimali fedha atazipata wapi

za kuendeleza wanawake hao? Kwani ukizingatia katika Halmashauri

wanakusanya asilimia 35 tu. Kwa hiyo, namwomba Waziri kabla ya kutoa agizo

ahakikishe kwanza hizi pesa zinapatikana wapi.

Pili, nampongeza Mheshimiwa Waziri kwa kuwa yuko karibu sana na

Taasisi za kijamii, lakini naziomba na hizi Taasisi za Kijamii ziweze kuwa wazi hasa

ukizingatia wako wengi Vijijini wanasaidia wavuvi, wanasaidia wakulima, vitoe

mapato yao kwa uhakika ili waweze kutengenezewa program Kitaifa, Kimkoa

na Kiwilaya.

Mheshimiwa Spika, ni kweli mikopo mingi imetoka, lakini ukitazama Vijijini

haijaenda mikopo mingi, tukiacha mbali hiyo VICOBA. Mheshimiwa Waziri

anaweza kuniambia mifuko mingapi ya mikopo iliyokwenda Vijijini na

wanawake wangapi ambao wamefaidika na hiyo mikopo?

Mheshimiwa Spika, kabla muda wangu haujakwisha naanza kusema

kuhusu gazeti la leo la Uhuru. Gazeti la Uhuru, leo limemnukuu Mheshimiwa

Nape Nnawiye akisema kuwa UKAWA ni sawa na Boko Haramu. Hii ni kauli

chafu na ya uchochezi, haikubaliki na ninailaani kwa nguvu zangu zote.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, sijui hasa amefikiria nini kuifananisha UKAWA na Boko

Haramu. Boko Haramu inawatesa wanawake; sasa hivi walishachukua

wanawake mia mbili na zaidi huko Nigeria wamewapeleka mafichoni, wazee

wao wako kwenye shida hawajui watoto wao watakula nini, wala wanalala

vipi. Leo hii Nape Nnawiye amethubutu kusema kuwa UKAWA ni sawa na Boko

Haramu!

Page 116: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

116

Mheshimiwa Spika, nikiendelea kidogo, nitachangia kuhusu watoto wa

Mitaani. Ni kweli Serikali inafanya jitihada, lakini bado ukiangalia unapofanya

jitihada ya kuondoa tatizo hilo, huwa inapungua. Lakini idadi ya watoto wa

Mitaani inakuwa imezidi. Ukitazama Dar es Salaam ni watoto 3,000, sasa

wamefika mpaka watoto 7,000 Mitaani wanahangaika hovyo. Najua kwa kuwa

mnafanya jitihada zenu kwa kupitia kila Halmashauri na kuandikisha na

kuwarejesha kwa wazee wao na bado wanarudi, lakini nawambieni Serikali

msichoke, hawa ni watoto wetu tutampelekea nani kama hatujawalea sisi

wenyewe? Kwa hiyo, namwomba Waziri asichoke, maana nasikia Serikali

imeshachoka, haijui la kufanya. Msichoke, mwendelee, kwa hili. Sijasema

mmechoka kabisa; kwa hili mmechoka! Kwa hiyo, nawaomba mwendelee

kuondoa tatizo hili la watoto wa Mitaani.

Mheshimiwa Spika, kidogo nizungumzie suala la ukeketaji. Juhudi

zinafanywa na Serikali najua na Taasisi mbalimbali zinatoa elimu, lakini na sisi

wanawake tujiunge pamoja tukiwa humu Bungeni na walioko nje tutoe elimu ya

kutosha ili tatizo hili lisizidi kuendelea. Maana inasemekana takwimu za mwaka

2012 na mwaka 2013 katika watu waliokeketwa ni wengi wa mwaka 2013 kuliko

wa mwaka 2012. Kwa hiyo, natoa wito kwa wanawake wote na wanaume

wote wasishurutishwe kuoa wanawake waliokeketwa. Nao wawe mstari wa

mbele kupita vita ukeketaji wa wanawake.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Sasa namwita Mheshimiwa Tauhida Gallos Nyimbo,

atafuatiwa na Mheshimiwa Fatuma Mikidadi.

MHE. TAUHIDA C. G. NYIMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia

fursa hii ya kuchangia Wizara hii. Nichukue fursa hii kwanza kuwapongeza

Mawaziri wote wawili kwa kazi na jitihada zao nzuri wanazozifanya katika Wizara

hii. Tunashukuru kwa sababu wanajua wajibu wao kama wanawake na

wanajua wajibu kama walezi. Kwa hiyo, tunaona jitihada zao katika kazi

wanazozifanya.

Pia, nichukue fursa hii ya pekee kumshukuru na kumpongeza Mama

Salma Kikwete kwa kazi nzuri anazozifanya katika Taifa letu la Tanzania. Ni

mwanamke wa kupigiwa mfano, ni mwanamke anayestahili sifa, ni mwanamke

wa kuwa gumzo katika Wanawake wenzake. Sisi tukiwa kama wanawake,

tukiwa kama vijana hatuna jinsi, tunampongeza; kazi zake zinaonekana na za

kuigwa.

Sisi kama wanawake tunachukua fursa hii kumpongeza. Tunajua sababu

za watu kupiga kelele ni nini. Lakini Mama tunamtaka aendelee, afanye kazi.

Taifa linajua na sisi vijana tunajua kama Mama Salma Kikwete anafanya kazi na

Page 117: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

117

kazi inaonekana. Wapo Viongozi wengi na wana wake zao lakini hatuwezi

kumtolea mfano kwa kazi anazozifanya. Yeye anastahili sifa miongoni mwetu

kati ya wanawake wanaostahili sifa katika kazi wanazozifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nazungumza hili nikiwa kama shahidi. Niko ndani ya

Kamati ya LAAC, tunapopita katika Ukaguzi katika Kamati yetu, tunakuta kazi

zinazofanywa na Mama Salma. Tumekuta katika hospitali zinazofanya kazi,

misaada anayopeleka Mama Salma kwa ajili ya wanawake ambao

wanaokwenda kujifungua, lakini ukiacha hayo, tunaona vifaa mbalimbali kila

leo akiwasaidia wanawake wenzetu katika hali ngumu walizokuwa nazo hasa

Vijijini.

Mheshimiwa Spika, naomba nijielekeze katika suala zima la pensheni ya

Wazee katika Taifa letu. Mheshimiwa Waziri nakuomba, ukiwa kama mama

suala hili limekuwa tatizo, lakini najua kwa sababu ya hali yetu iliyokuwepo

ndani ya Tanzania. Naamini Serikali ina mikakati mizuri ya kujipanga juu ya suala

zima la pensheni lakini bado hatujafikia, lakini naamini tuko katika maandalizi.

Namwomba Mheshimiwa Waziri na Naibu wake, tuchukue mikakati ya

makusudi katika kulinda wazee katika Taifa letu, hususan tuangalie wanawake

wanaopata taabu katika Taifa letu. Nadhani tukiwa na mipango ya

kutengeneza kila Halmashauri tukawa na nyumba ya kulelea Wazee, hususan

wazee wanawake wanaokosa malezi na matunzo, kuna wazee bahati mbaya

hawakujaliwa kupata watoto, kuna wanawake hawakujaliwa kuwa na watoto;

wanapata shida na wananyanyasika na wengi wao ndiyo ambao tunawasikia

wanaokufa.

Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri tunaomba katika

mikakati yote wanayopanga mizuri, lakini hili walichukue walifanye kwa kuweka

kipaumbele. Naamini hatutoshindwa kwa sababu tuna Halmashauri ya kutosha,

Serikali ina mikakati mizuri na ninaamini tukiliingiza katika mikakati yetu, hili suala

zima la kuweka nyumba za kulelea Wazee litafanikiwa.

Nichukue mfano kwa upande wa Zanzibar, Mheshimiwa Waziri mna

wakati mzuri wa kuenda kuangalia Zanzibar. Zanzibar kuna nyumba za kulelea

wazee. Wazee waliokuwa hawana watu wa kuwatunza kuna maeneo

wanapelekwa. Leo utamkuta mzee yuko Kijijini, hana ndugu, hana familia, yuko

peke yake, hatufurahii kama vijana kuona ndani ya Taifa letu kuna wazee

namna ile wanashindwa kutunzwa.

Mheshimiwa Waziri naomba katika changamoto zako katika Uwaziri

wako, lipe kipaumbele suala hili. Tuweke nyumba kila Halmashauri, kila Mkoa

ikishindikana kila Halmashauri japo kila Mkoa tupate nyumba moja, wazee

walelewe katika nyumba hizo. (Makofi)

Page 118: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

118

Mheshimiwa Spika, nije kwenye suala zima la mahabusu. Mheshimiwa

Waziri naomba hili ulichukue, tena kwa umakini na ulifanyie kazi. Tumeona kazi

kubwa unayoifanya ukiwa kama mwanamke Waziri unayejitolea. Unapita Mkoa

hadi Mkoa kuhamasisha wanawake, unapita Mkoa hadi Mkoa kuweka jitihada

wanawake wajikomboe katika maisha yao. Tunajua kazi yako unayoifanya,

tunaiheshimu mama kazi yako unayoifanya.

Chukua fursa hii kati ya kazi zote unazozifanya, angalia mahabusu,

watoto wanachanganywa, watu wazima na watoto; haikustahili. Tunajua Taifa

letu likoje, lakini kuchanganywa mtoto ndani ya mahabusu siyo wakati mzuri.

Vitendo vilivyoko kule wanavyofanyiwa watoto siyo vizuri. Watoto hawajifunzi

maadili mazuri, baada ya kuweka kule wakitoka wajifunze wawe raia wazuri,

wanakuja na mambo mabaya kutoka Gerezani.

Mheshimiwa Spika, naomba nizungumzie suala la Benki. Mheshimiwa

Waziri, tunakuomba sana, tunaomba angalu branch japo ndogo iwepo

Zanzibar; japo kwa Mkoa wa Mjini Magharibi uwepo. Tunaiomba Benki hii

ifunguliwe. Kwa niaba ya wanawake wote wa Zanzibar naomba nichukue fursa

hii kuwasemea, wapate mikopo hii.

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba Serikali fedha wanazozitenga

ndani ya Wizara hii ni kidogo hazitoshi kwa sababu Wizara hii ndiyo iliyobeba

jamii yote! Vijana wamo humo, wazee wamo humo, watoto wamo humo, lakini

ukiangalia bajeti yake ni ndogo. Mimi kwa leo nitakuwa mgumu kuunga mkono

hoja kwa sababu pesa wanayotengewa Wizara ni ndogo, mambo ya kufanya

ni mengi, kazi ni nyingi lakini fedha wanazoingiziwa ni kidogo.

Mheshimiwa Spika, kitu kinachotusikitisha sisi vijana hususan wanawake,

wenzetu wanapotoka hapa kwenda kuuzwa kwenye suala zima la ukahaba.

Linatuuma na Mheshimiwa…

(Hapa kengele iliila kuashiria kwisha

kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. TAUHIDA C. G. NYIMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante.

SPIKA: Ngoja kwanza nikuulize swali. Huungi mkono kwa sababu hela

haitoshi au? Sasa ukimkatalia atafanyaje huyu? Tafuta Wizara nyingine ya

kumgomea huyo na siyo huyu sasa. (Kicheko)

MHE. TAUHIDA C. G. NYIMBO: Mheshimiwa Spika, lengo langu, pesa

hazitoshi. Majukumu ya Taifa anayo makubwa lakini fedha hana.

Page 119: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

119

SPIKA: Basi, ukisema hivyo inatosha. Lakini ukimpinga huyu, basi tena

unakuwa umemkatalia…

MHE. TAUHIDA C. G. NYIMBO: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono

hoja ya Mheshimiwa Waziri. (Kicheko)

SPIKA: Ahsante. Unajua the logic is, akisema haungi mkono, basi hata hizi

ndogo potelea mbali huko, hazina haja. (Kicheko)

Sasa namwita Mheshimiwa Fatma Mikidadi akifuatiwa na Mheshimiwa

Shibuda.

MHE. FATUMA A. MIKIDADI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, napenda

kuushukuru Uongozi wa Taifa hili; Mheshimiwa Rais Hayati Mwalimu Julius K.

Nyerere, Mheshimiwa Rais Mwinyi, Mheshimiwa Rais Mkapa, Mheshimiwa Rais

Kikwete kwa kuendeleza mambo na maendeleo ya wanawake. Leo hii

hatuwezi kuzungumza maendeleo ya wanawake bila kuwakumbuka Marais

hawa. Kwa kweli wamefanya kazi kubwa sana ya kuendeleza wanawake, kiasi

kwamba na sisi leo tupo hapa tunazungumzia masuala ya wanawake. Kwa

kweli tunawashukuru sana.

Tunasema kwamba wanawake ni nguvu kazi na uzao wa nguvu kazi.

Hatuwezi kuzungumzia mambo ya maendeleo bila kutaja wanawake kwa

sababu wamefanya kazi kubwa sana katika kuendeleza uhuru wa nchi hii.

Mheshimiwa Spika, wanawake walikuwa katika mstari wa mbele

kuendeleza uhuru wa nchi hii, kabla ya uhuru, baada ya uhuru na sasa tulivyo

hivi katika mfumo wa Vyama Vingi vya Siasa, wanawake kwa kweli wamekuwa

katika mstari wa mbele katika kuendeleza juhudi mbalimbali za nchi hii katika

kupata uhuru, vilevile ulinzi na amani ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hayo naomba niseme kwamba Katiba hii

tuliyokuwa nayo sasa hivi ambayo tunataka kuitunga kama haitaendelea na

kwisha kipindi hiki, tunaomba sana Mheshimiwa Rais Kikwete aweke kiraka cha

50 kwa 50. Aweke kiraka cha 50 kwa 50 kwa sababu hii Katiba tuliyonayo

ukurasa wa 61 inaelezea kwamba wanawake watakuwa asilimia 30. Lakini kadri

tunavyokwenda katika Katiba hii mpya tunayoendelea nayo, kama haitikuwa,

tunamwomba Mheshimiwa Rais Kikwete aweke kiraka, badala ya kusema

asilimia 30 tuseme asilimia 50 kwa 50 kwa wanawake. Aweke kiraka, akubali

hivyo, pamoja na kwamba alisema hatakubali na kwamba tutaendelea na

Katiba ya zamani.

Sisi wanawake wa Tanzania hii tunaomba abadilishe aseme 50 kwa 50

ukurasa wa 61, badala ya kusema asilimia 30.

Page 120: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

120

Mheshimiwa Spika, nimesema kwamba uhuru wa nchi hii tulikuwa wote;

wanawake kwa waume. Mwaka ule wa 54 kabla ya uhuru na mwaka ule

tuliopata uhuru wa 61 na baada ya uhuru wa Vyama Vingi vya Kisiasa. Sasa

tunaomba aendelee, asikwamishe. Aendelee na kutusaidia kwa kupata 50 kwa

50 kwa sababu nchi nyingine zote ambazo tunazo katika mikutano mbalimbali

ya wanawake, tayari wenzetu wameshafikia asilimia kadhaa. Wamepita asilimia

50.

Kwa mfano, Afrika ya Kusini wana asilimia 45, Rwanda wana asilimia 56,

sisi Tanzania je? Azimio la mwisho, la nchi mbalimbali za Kiafrika, Azimio la

Maputo namba 90 liliazimia kwamba Afrika sasa wawepo katika maamuzi ya

uongozi asilimia 50 kwa 50. Lakini Tanzania bado tupo katika asilimia 30.

Tunaomba sana hilo liwekwe kwamba Serikali za Mitaa, Serikali za Miji, Serikali za

Vijiji, Wabunge wawekwe 50 kwa 50 kutokana na maazimio ambayo

yamewekwa katika Mikutano mbalimbali ya Wanawake ya Afrika.

Mheshimiwa Spika, hilo la kwanza. Wanawake tuna uwezo, wanawake

tumeshakwenda taratibu, tumeanza na asilimia chache, tukaenda kidogo

mbele, sasa hivi tuna asilimia 30. Tuna uwezo na tuna ukomavu, tunaomba

tuwekwe sasa katika asilimia 50 kwa 50.

Mheshimiwa Spika, suala la pili ni CDCF. Pesa ambazo wanapewa

Wabunge kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kwa ajili ya kuchochoea

maendeleo ya wananchi. Pesa zile na sisi wanawake tupewe, kwa sababu sisi

wanawake vilevile tunawajibika kwa wananchi, tunawajibika kwa Serikali. Sasa

iweje na sisi tunyimwe pesa zile. Tunaomba na sisi tupewe.

Mheshimiwa Spika, sisi tunakwenda katika Mikoa yote ya Tanzania. Mikoa

ile kuna wanawake, wanaume, wanawanchi, Mikoa ile sisi tunawajibika. Sasa

kwa nini tunyimwe zile pesa tusiwasaidie wananachi wale? Kwa sababu

tunapokwenda katika Wilaya wananchi wanatuomba pesa za maendeleo, za

shule, Zahati, wanawake katika vikundi mbalimbali, tunashindwa kuwapa,

badala yake tunachukua pesa zetu binafsi tunawapa.

Mheshimiwa Spika, zile pesa za kichocheo cha maendeleo ya wananchi

CDCF tupewe na sisi angalau kila Wilaya. Zile zile wanazopewa Wabunge,

tuchotewe kiasi na sisi tuwasaidie wananchi wale badala ya kusema kwamba

ah, ninyi siyo Wabunge wa Majimbo. Sisi siyo Wabunge wa Majimbo kwa nini

wakati Serikali inaamini kwamba sisi ni Wabunge wa Tanzania? Sisi ni Wabunge

wa Serikali hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali imekubali kwamba

sisi ni Wabunge; kwa nini pesa zile na sisi tusigawiwe ili tuwasadie wananchi

wenzetu, badala yake wanapewa wa Majimbo peke yake?

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

Page 121: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

121

kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante. Kengele imegonga.

MHE. FATUMA A. MIKIDADI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

(Makofi)

SPIKA: Okay, mwenye wajibu wa kubadilisha Katiba ni ninyi wenyewe kwa

mujibu wa kifungu cha 98, siyo Rais. Mheshimiwa Shibuda! (Makofi)

MHE. JOHN S. MAGALLE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata fursa hii.

Awali ya yote napenda kusema kwamba naunga mkono juhudi za Wizara hii za

kukusu maendeeleo ya jamii na watoto.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hekima ya mwongozo huvutia kufuatwa na

wasikilizaji au na waongozwa, naogopa kusikia ya kwamba Kamati za Ulinzi na

Usalama sasa ndiyo zitakuwa nyenzo za kupambana na mazalia ya imani

potofu na kuondoa imani potofu katika maeneo ya imani potofu.

Mheshimiwa Spika, kwa madhumuni ya kupambana na imani potofu,

naishauri Serikali ijielekeze kuongeza huduma za afya katika maeneo ambayo

yana imani kubwa za kutumia ramri kwamba ndiyo X-ray, na ndiyo clinic au

ndiyo vipimo vya kutambua maradhi. Nasisitiza ya kwamba Serikali ijielekeze

kuimarisha huduma hizo, hiyo ndiyo itakayoleta mageuzi na mapinduzi ya kifikra

dhidi ya imani potofu.

Mheshimiwa Spika, Serikali tangu ianze kulalama na kurindima kuhusu

mauaji ya imani potofu: Je, hadi leo, Wizara hii ambayo ni mtambuka, pamoja

na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, wamekuwa na programs gani za

kuondoa imani potofu katika maeneo ya kanda ya ziwa? Msikae tu mnapiga

kelele na kushutumu kwamba kuna imani potofu, naomba mje na mkakati na

mchakato. Naomba Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, pamoja na Wizara hii,

leo mtutambulishe mna mchakato gani?

Je, Serikali hii ina mkazo gani wa kuinua huduma za lindo na usalama kwa

akina mama wazazi katika hospitali, ambao wanajifungulia kwa Wakunga wa

Jadi! Je, inapeleka huduma gani au Wizara hii, imekuwa ni sauti ya sikio sikivu na

kelele ya kulaani au kupukutisha huduma potofu kwa njia zipi? Pale ambapo

kuna maeneo hakuna hata darubini za kutambua kuna Malaria.

Mheshimiwa Spika, malengo ya ukombozi na wokovu kwa waathirika wa

imani potofu katika Kanda ya Ziwa, hususan katika Wilaya kongwe kama Wilaya

ya Maswa, naitaka Serikali ije ichambue mazalia yake ni nini? Bila kujua mazalia

ya mbu, huwezi ukamaliza ugonjwa wa Malaria. Naomba Wizara hii, pamoja na

Page 122: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

122

marafiki zake wa asasi mbalimbali, mhakikishe mnafunga safari ya kuja kwenye

maeneo ya Kanda ya Ziwa. Napinga kabisa kusikia ya kwamba Jeshi la Polisi

ndiyo litakuwa nyenzo ya kuondoa fikra potofu na kuleta mageuzi ya fikra.

Mheshimiwa Spika, janga la adui ujinga haliondolewi kwa mtutu wa

bunduki. Sijawahi kuona kwamba kuna bunduki imetumika kwenda kuondoa

ujinga kwa wanafunzi na wakazalisha vipaji vya elimu.

Sijawahi kuona hata siku moja! Sasa kuweka Jeshi la Ulinzi kwamba ndiyo

liwe silaha au nyenzo za kuondoa imani potofu, ni kujidanganya sisi wenyewe.

Jeshi la Ulinzi au Kamati za Ulinzi, sio wanasiasa, wala siyo Masheikh wala siyo

Maaskofu, kwa hiyo, hawawezi kutoa elimu ya dini wala elimu ya kisiasa.

Namwomba Mheshimiwa Waziri pamoja na Wizara yake, wawe na

mchakato wa kushiriksiha Wabunge, wawaimarishe Wabunge, akina mama;

wanaweza wakachukua hata wanamkakati na kikosi kazi cha wanawake,

Wabunge wanawake wa Bunge hili, wakaja katika maeneo yetu kuungana na

akina mama wanawake wenzao kujenga elimu. Kuweni na mkakati huo, fedha

hizo msipeleke kwenye Kamati za Ulinzi na Usalama, ni ulaji ambao hauna faida

na sijawahi kuona bunduki inaleta mageuzi ya kifikra.

Mheshimiwa Spika, Serikali Kuu naona haina dhamira njema ya kusaidia

kuondolewa kwa matatizo ya Wizara hii ambayo ni makubwa sana kwa ustawi

na maendeleo ya wananwake. Je, CCM, kuanzia Kamati za Siasa Wilaya, Mkoa

na Taifa, na Kamati Kuu, hivi zimetengana na siasa zake za kuhakikisha zinaleta

ukombozi na wokovu kwa wanawake? Kwa nini Wizara hii haina bajeti ya

kutosha kama siasa bora za CCM zinapaswa kutekelezwa na Wizara hii? Au

mmetengana? Kuna usaliti gani?

Mheshimiwa Spika, kuvunja imani ni rahisi, lakini kuirejesha ni vigumu sana.

Bajeti ya Wizara hii ni huduma mgogoro na inanipa mawazo ya mgomo,

kuamini ya kwamba kuna upatanifu wa siasa bora na utumishi bora.

Mheshimiwa Spika, wokovu kwa wanawake utategemea juhudi za

vitendo, siyo nadharia. Dua la kuku halimpati mwewe. Lini Mheshimiwa Waziri

atakuwa tayari sasa kuja ziara kuvuna mawazo na fikra?

Mheshimiwa Spika, imani potofu Maswa ambayo ni Wilaya kongwe, ina

tatizo hilo vilevile. Lakini ni kwamba watu wengi waliotoka katika Wilaya kongwe

za kanda ya Ziwa ndiyo wameenea katika Mikao mbalimbali. Hitilafu ya imani

potofu; naomba iandaliwe ziara maalum na Mheshimiwa Waziri pamoja na

Naibu Waziri, mje mvune sababu ya mazalia, baada ya kuja kuvuna sababu ya

mazalia, mzalishe mkakati na mchakato wa kikosi kazi cha kupambana.

Maneno matupu, ni sawasawa na dua la kuku halimpati mwewe.

Page 123: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

123

Naiomba Serikali sasa iache maneno mengi iwe na vitendo, na mdharau

mwiba, huota tende. Nasikitika kusema kwamba kanda ya ziwa wamechoka

na shutuma ambazo hazina suluhu.

Mheshimiwa Spika, namwomba Waziri na asasi rafiki, pamoja na Mama

Salima Kikwete, hebu sasa aandaeni mchakato, Mama Salma Kikwete, uache

kumbukumbu ya kwamba umewatumikia wanawake wa Kanda ya Ziwa

kuondokana na madhira ya dhuruma ambazo wanazipata kwa sababu

hawapati huduma stahiki. Naomba mwaka wako huu wa mwisho uandae kikosi

kazi ili kije kilete suluhu kwa ukombozi wa wanawake.

Mheshimiwa Spika, naomba Serikali pamoja na asasi zijitambulishe kuwa

zina umakini gani wa kupambana na imani potofu? Naomba Wizara hii iwe

msemaji mtambuka, na ninamwomba Mama Salma Kikwete, awe msemaji

mtukufu wa kupambana madhila yanayowapata wanawake katika maeneo

ya imani potofu. Aache kukaa sasa anasiliza maneno ambayo yana fikra

mgogoro.

Mheshimiwa Spika, mwisho naomba Serikali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha

kwa muda wa mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante. Mheshimiwa Anna Abdallah!

MHE. ANNA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa

nafasi hii. Awali ya yote naomba niwapongeze sana Waziri, Naibu Waziri na

Watendaji wote katika Idara hii na Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na

Watoto.

Mheshimiwa Spika, utakuta kwamba Wizara wamepata takriban Shilingi

bilioni 30 kuendesha Wizara hii, lakini katika mafungu yale ambayo tumekwisha

yapitisha, kuna baadhi ya mafungu ni Idara moja tu ama kisehemu kimoja tu

cha Wizara fulani, kinapata hizo Shilingi bilioni 30. Kwa kweli Idara hii ni muhimu

sana na kazi yake ni mtambuka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Jamii ni mtambuka! Sijui siku hizi,

mambo tu yawe yamebadilika, lakini huko kama alivyokuwa anasema msemaji

wa mwisho hapa, ilikuwa ni watu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, ndiyo

wangekwenda kufanya tafiti za matatizo yanayotokea katika baadhi ya

maeneo; kuua vikongwe, kukata vidole vya mtu, ya kufikiria kwamba utajiri

Page 124: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

124

unatokana na hii; lazima kufanyia tafiti za kina, zikaandikiwa ili kutafuta Serikali

ifanye nini na mipago iweje.

Kwa kweli fedha hizi walizopewa Shilingi bilioni 30 kwa maendeleo na

mishahara na nini ni fedha kidogo sana. Hasa kwa sababu katika nchi hii, katika

sensa iliyopita, wanawake, ni zaidi ya nusu ya watu wote wa Tanzania. (Makofi)

Sasa wanawake walio wengi, bajeti yake ndogo. Ukimwendeleza

mwanamke umeendeleza Taifa, umeendeleza familia, na mwanamke ndiyo

mhimili; nasema mwanamke ni mhimili wa amani katika familia na katika nchi

hii. (Makofi)

Watu wasije wakatuona sisi Wabunge labda ndio tunaosema sema huku

barabara mtatutambua, patachimbika, lakini ndani ya familia zetu, mwanamke

akianza kusema patachimbika, hapakaliki! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba katika programs zinazokuja, siyo tu

kufundisha wafanyakazi, ni lazima kuwafikia akina mama pale walipo, na

kuwafundisha mambo haya na kuwapa ule moyo kwamba wao ndio wahimili

wa amani wa nchi hii na wala siyo Mikutano tu ya hadhara, ni sisi wanawake.

Lakini inasikitisha, kwamba fedha wanazozipata, hata za huyo mfanyakazi wa

kutembea kwenda huko kijijini, akakutana tu na akina mama wakazungumza

mambo yanayofaa kufanywa ndani ya familia ili familia iendelee, ni fedha

kidogo sana. Kwa kweli hawataweza kufanya kazi. (Makofi)

Mimi mwenyewe niliyesimama hapa, tangu mwanzo, kazi yangu ya

kwanza katika nchi hii niliyoifanya ni Idara ya Maendeleo ya Jamii. Mimi ni

Bwana Maendeleo. Najua, kwamba Idara hii ilikuwa na kazi kubwa sana, tangu

wakati wa ukoloni, kuhakikisha kwamba hata sera ndani ya Wizara za Serikali

hazipingani. Kwa sababu yako mambo mengine yanafanywa na Wizara moja,

yanakinzana na Wizara nyingine na matokeo yake badala ya watu kuendelea,

hawaendelei, ni kazi ya kutatua mizozo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hii mizozo kwa kweli tunayoipata ndani ya jamii ni

matokeo ya kutokuitumia vizuri Wizara hii, hasa Maendeleo ya Jamii ya namna

ya kuwaweka watu pamoja na kuwafundisha namna Serikali za Mitaa

zinavyoendelea, zinavyokwenda na namna ya kutatua mizozo katika familia

ama katika jamii. Hii ni kazi kubwa sana. Hii ni kazi ambayo inaendana pia na

Viongozi wa Dini. Ndani ya Serikali, mimi sioni Idara yoyote ambayo inaweza

ikawa counterpart ya Viongozi wa Dini wanaoleta amani katika nchi.

Counterpart wao ni Wizara hii, lakini utasikia hata Viongozi wa Dini

wanapokutana kuzungumzia amani, wanakutana wenyewe tu. Wizara hii hata

sijui kama inashiriksiwa! Wao ndio wataalam, wanaojua watu wanaendeleaje.

Kwa nini watu wanafanya vile wanavyofanya sasa hivi, kuliko vile ilivyokuwa?

Page 125: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

125

Mheshimiwa Spika, siyo vizuri kusema zamani tulikuwa tukifanya hivi,

hapana. Kuna zama za zamani hizo, tulikotokea. Sasa tunakwenda katika

sehemu tofauti kabisa, na watu wetu na vijana wetu, akina mama pia wako

tofauti kuliko sisi wakati huo tulipokuwa vijana. (Makofi)

Haya yanapaswa akina mama hawa wapate nafasi ya kuona tofauti

badala tu ya kulalamika, vijana wa siku hizi hawafanyi hivi, vijana wa siku hizi,

wanawake wa siku hizi; jamani eeh! Msione kwamba hivi vitu vilikuwa hivi hivi;

viliundwa, vinaelea lakini viliundwa. Sasa sisi hatuviundi vya leo, huko

havitaelea, vitazama. Taifa hili litazama kama hatutoi nafasi proper kabisa

mahali ya kutosha kabisa kwa Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hapa Maendeleo ya jamii siyo akina mama tu, hata

akina baba ni maendeleo ya jamii. Kwa sababu hata matendo ya akina baba

leo ukiyasikia, baba amemkata panga mkewe, sijui amemchoma mtoto moto;

mama mtoto amechukua nyama kwenye chungu unamchoma moto. Haya ni

matatizo yaliyo kwenye jamii ambayo tusipoyapatia ufumbuzi ni matatizo

yataendelea. Mtoto aliyeteswa na familia atakuwa na yeye na akili mbovu ya

kutesa wenzake, kwa sababu hajui upendo. (Makofi)

Sasa, haya ni mambo makubwa sana. Mimi namshukuru sana Waziri,

namsikia kila wakati anakemea, anasema akina mama habari za ukatili dhidi ya

watoto na mimi nasikitika kwamba wanaofanya ukatili mwingi ni wanawake

kwa watoto wao, hasa watoto wa kambo. Hili siyo jambo jema. Sasa haya,

huko zamani tulikuwa hata na madarasa, kwenye hivi Vyuo vya Maendeleo ya

Jamii, ndipo tunapokutana na akina mama. Akina mama walikuwa na

matatizo, nifanyeje, wanakuwenda kupewa maoni hayo. (Makofi)

Nashukuru na naunga mkono hoja hii, lakini nisisitize, fedha hizi hazitoshi

kufanya kazi ya maana katika nchi. Ahsante. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Waheshimiwa Wabunge, naona nilipowatangaza

wageni, Wizara haikuwa imeleta wale wa kuwatangaza. Kwa hiyo, yuko

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Wanawake, mliozungumzia hapa, Bibi

Magreth Mataba Chacha; nadhani watakuwa kwenye maeneo yale ya kazi.

(Makofi)

Yuko Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Uratibu wa NGOs, Bibi Rukia Masasi.

Sijui wako wapi! Pia yupo Katibu Mkuu Baraza la Taifa la NGOs, Bwana Ismail

Suleiman. (Makofi)

Halafu yuko UN Women, Bi Fortunata Temu; Mwakilishi wa USAID, Bi

Rodurika Tarimo na yupo Mpishi wa Shirika la Elimu Kibaha, Dkt. Lucy Sisendi na

Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Wanawake, sasa huyu sijui ni miss

Page 126: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

126

au nani, lakini anaitwa A. Ndarusa na yuko Mwakilishi wa Save the Children

Program Operation Director, huyu Bwana John Kalage, aliko huko. (Makofi)

Halafu, matangazo ya kazi tena, kuna Mwenyekiti wa Tawi letu la

Tanzania la Common Wealth Parliamentary Association, anaomba Wajumbe

wafuatao wa Kamati ya Utendaji, anaanza; Mheshimiwa Vita Kawawa,

Mheshimiwa Beatrice Shellukindo, Mheshimiwa Profesa David Mwakusya,

Mheshimiwa Ummy Mwalimu, Mheshimiwa Zahara Ali Hamad, Mheshimiwa

Highness Kiwia, Mheshimiwa Lucy Owenya, Mheshimiwa Zainabu Vullu na

Mheshimiwa Lediana Mng‟ong‟o.

Wiki ijayo, sisi tunakuwa wenyeji wa Semina ya Kimataifa ya Common

Wealth Parliamentary Association, inahusisha watu kutoka karibu nchi zote za

Common Wealth. Sasa Tawi letu hili hapa ndiyo mwenyeji wa huo Mkutano.

Kwa hiyo, inabidi wajiandae kupokea wageni hao na kuwaandaa watu

watakaokuwa watoa mada katika Mkutano huo. Maana yake inabidi watoa

mada wengi watoke katika nchi yetu hii. Kwa hiyo, tutakuwa na huo Mkutano

karibu kwa muda wa siku nne, tano.

MICHANGO KWA MAANDISHI

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza Waziri

wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, Naibu

Katibu Mkuu na Wakurugenzi wote wa Wizara na Maafisa walioandaa vizuri

hotuba ya bajaeti ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, naomba kumshukuru Waziri kwa kuja kutuletea

Wilayani Namtumbo na kutufungulia Chuo cha Maendeleo ya Wananchi

Mputa. Juu ya yote naishukuru Serikali kwa maamuzi ya kutenga fedha

kukarabati na kujenga majengo yale na sasa tuna Chuo.

Mheshimiwa Spika, lakini kama Mheshimiwa Waziri ulivyoona ndiyo Chuo

kimeanzishwa baadhi ya majengo yaliyopo yanahitaji kukarabatiwa ili Chuo

kiweze kufanya kazi ya ufundishaji katika maeneo yote yaliokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, hivyo naamini katika Bajeti ya Maendeleo ya Training

and Folk Development Collages mtakuwa mmetenga fedha za kukikamilisha au

kuendeleza pale mlipofikia Chuo cha Mputa.

Mheshimiwa Spika, nitashukuru sana kupata uhakika wa jambo hili.

MHE. MICHAEL L. LAIZER: Mheshimiwa Spika, napenda kuanza kwa

pongezi kwa Wizara yako na watendaji wote wa Wizara yako. Maendeleo

yoyote ya binadamu kuanza kukua kiakili inaanza kwa mama. Malezi kwa

Page 127: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

127

watoto yanapatikana kwa wazazi. Kwa hiyo jitihada kubwa ni kutoa elimu kwa

wazazi wote, mama na baba kwa kuwalea watoto vizuri ili kuondoa watoto wa

mitaani.

Mheshimiwa Spika, kinachokosekana kwa watoto kuvuta dawa za

kulevya ni wazazi kuwalea watoto vibaya na wengine kuwatoroka watoto,

malezi muhimu kwa watoto ni pamoja na elimu kwa watoto.

Wengi wa watoto wanaorandaranda mijini ni wale ambao

hawakupelekwa shuleni. Kwa vile wanafunzi hawa wamekuwa wengi ni

afadhali Serikali ichukue jukumu la kuanzisha shule za kuwapeleka watoto hawa

wakasome kwani wakiachwa wataleta usumbufu baadaye kwani ndiyo

watakuwa wezi baadaye.

Mheshimiwa Spika, naomba Wizara yako watembelee Wilaya za

pembezoni ambazo bado wapo nyuma kimaendeleo. Kuna maeneo mengine

ambayo mila zimetawala hata wanawake kuogopa kusema manyanyaso

wanayopata kwa wanaume kwa sababu ya utawala wa mila iliyopitwa na

wakati.

Taifa halitaendelea kama kuna baadhi ya maeneo ambayo

wakinamama hawana uhuru wa kutoa mawazo hawana uhuru na ardhi,

hawana uhuru na mali ya mumewe anapofariki. Kwenye maeneo mengine

bado wanawake hawawezi kutoka kwenye mawazo bila wanawake kujitetea,

uhuru haupatikani bila kudai kwa nguvu.

Mheshimiwa Spika, namuomba Mheshimiwa Waziri kwenye kipindi chake

afike Wilaya ya Longido kuhamasisha wanawake wa jamii ya Kimasai ambao

bado wanashiriki mila waweze kubadilika na wao kuwa kama wengine toka

maeneo mengine. Nategemea ombi langu litakubaliwa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia zote.

MHE. SYLVESTER M. MABUMBA: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maendeleo

ya Jamii, Jinsia na Watoto ni tegemeo kubwa kwa ustawi wa Watanzania kwani

wanawake na watoto ndiyo mhimili mkubwa kwa maendeleo ya Taifa letu.

Bajeti ambayo kila mwaka inatengewa Wizara hii hairidhishi hivyo naiomba

Serikali yangu iangalie upya bajeti hii ya mwaka 2014/2015.

Wizara inatakiwa kuratibu madawati yote yaliyoanzishwa kutetea haki za

wanawake na watoto na ili madawati haya yaratibiwe vizuri lazima rasilimali

watu na fedha ziwepo vinginevyo kwa mtindo wa bajeti kiduchu haitoweza

kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Page 128: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

128

Mheshimiwa Spika, nawapongeza sana Waziri, Mheshimiwa Sophia Simba

na Naibu wake Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana kwa mapenzi yao makubwa kwa

nchi yetu na Watanzania wenzao, hata hivyo naiomba Serikali iwawezeshe kwa

kuwapatia fedha za kutosha. Pia naomba Benki ya Wanawake iongezewe mtaji

na ifungue matawi nchi nzima hasa kule Zanzibar.

Mwaka 2010 wakati wa kampeni tuliwaahidi wananchi wetu hasa

wanawake wa Zanzibar kwamba Serikali zetu zimeamua kuanzisha Benki ya

Wanawake ambayo itatoa mikopo nafuu na kuwawezesha wanawake kuwapa

taaluma ambayo itawajengea uwezo kwa taaluma ya ujasiriamali.

Mheshimiwa Spika, pamoja na ukweli kwamba Bunge lako Tukufu lilitunga

sheria ya kulinda haki ya wanawake na watoto, lakini inaonekana usimamizi wa

sheria hii unaonesha walakini kwani vitendo vya unyanyasaji bado vinatamalaki

hapa nchini. Wanawake wengi na watoto wananyanyasika, naomba pia

kuishauri Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano na ya Mapinduzi Zanzibar

viimarishe vyombo vya ulinzi na usalama ili visimamie sheria ya kulinda haki za

wanawake na watoto kwa nguvu zote.

Mheshimiwa Spika, mwisho naiomba Serikali iimarishe Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii. Hili linawezekana sana iwapo Wizara hii itashirikiana kwa

karibu na Wizara ya Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za

Mitaa (TAMISEMI) kwa fedha nyingi zilizotengwa TAMISEMI kwa mwaka ujao wa

fedha 2014/2015 TAMISEMI imetengewa zaidi ya trilioni tano. Kiasi hiki cha fehda

ni kikubwa iwapo kinaweza pia kutumika kwa ajili ya ustawi wa wanawake na

watoto.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Spika, kwa namna ya kipee,

nachukua fursa hii kuwapongeza sana Waziri, Mheshimiwa Sophia Simba (Mb)

pamoja na Naibu Waziri wake Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana.

Mheshimiwa Spika, naelekeza mchango wangu katika maeneo

yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, ni vyema sasa Chuo cha Ustawi wa Jamii cha

Rungemba kipandishwe hadhi na kuanza kutoa Shahada badala ya

Stashahada. Sisi wananchi wa Kijiji cha Rungemba tumekubali kuwapa ardhi

Chuo hiki tukiwa na matumaini ya Serikali kusikia kilio chetu cha muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, tulifurahi sana Mheshimiwa Naibu Waziri pamoja na

Kamati walipoamua kwa makusudi kuja kukitembelea Chuo hiki na kuona

maendeleo na changamoto zake. Lakini pamoja na ziara hii katika bajeti hii

Page 129: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

129

Chuo hiki hakijatengewa fedha zozote, mimi kama Mbunge tumehakikisha

umeme unawaka na sasa upo.

Mheshimiwa Spika, ni vyema sasa Benki ya Wanawake ikashuka vijijini

kuliko kuendelea kuwa kwenye miji mikubwa kama ilivyo sasa, mijini tayari kuna

mabenki mengi.

Mheshimiwa Spika, ni vyema Wizara hii ipate nafasi ya kusimamaia na

kujua fedha zote zinazotakiwa wapewe 10% kwa ajili ya akinamama na vijana

kuliko ilivyo sasa ambapo fedha hizi hazifiki kwa walengwa kwani maafisa wengi

wa Halmashauri kuwa wanazichukua.

Mheshimiwa Spika, mwisho naunga mkono hoja.

MHE. MARIA I. HEWA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja na

nampongeza Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Spika, naanza na watoto wa mitaani. Kundi hili linaendelea

kukua leo hadi leo nchini Tanzania kutokana na sababu mbalimbali, nina taarifa

zisizo rasmi kuwa katika Mkoa wa Iringa, tatizo hili linazidi kupungua na kuelekea

kuisha kabisa, je, tetesi hizi ni kweli? Kama ni kweli kwa nini tusiende kujifunza

kwa vipi wenzetu wamefanikiwa na kwa mbinu zipi?

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu watoto wa majumbani (house girl). Kundi

hili pia ni kubwa hapa nchini. Utafiti umefanyika na NGOs mbalimbali kuwa

elimu kuhusu wasichana wa kundi hili ikitolewa vizuri mabinti hawa huweza

kutulia majumbani mwao na kufanya shughuli za maendeleo wakiwa nyumbani

wanakotoka hii ni pamoja na Mkoa wa Iringa. Mkoa huu ulikuwa unaongoza

kwa ma-house girls kutapakaa nchi nzima kama ajira rasmi kwao.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kwa nini elimu hii isibebewe bango

nchi nzima kwa kuyaelimisha makundi haya madhara ya ajira hii nje ya Mikoa

yao?

Mheshimiwa Spika, kuna ukatili mkubwa hufanyika juu ya watoto aidha

kwa kupigwa viboko, kuchomwa moto sehemu mbalimbali mwilini, kumwagiwa

maji ya moto na kadhalika. Ushauri wangu kwa wanayoyafanya haya kwa nini

Serikali isiwaadhibu watu wazima hawa kama wabakaji wanaofungwa miaka

30 au kufungwa maisha?

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wizara hii hupewa fedha kidogo kwa kuwa

ni Wizara mtambuka nashauri kwa kila Wizara ambayo inaguswa na Wizara hii

ziwe na taratibu kuchangia kwa asilimia fulani katika Wizara hii kwa ushauri

kupelekwa katika Kamati ya Bajeti.

Page 130: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

130

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. CHRISTOWAJA G. MTINDA: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia

katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuhusu unyanyasaji wa watoto na

wanawake. Kadri siku zinavyozidi kupita matukio ya kutisha ya unyanyasaji wa

watoto na wanawake yanazidi kutamalaki katika nchi yetu. Watoto wadogo

wamekuwa wakilawitiwa, kubakwa, kuchomwa moto na wazazi/walezi wao na

kuwasababishia matatizo makubwa ya kiafya, kisaikolojia na hata vifo.

Wanawake wamekuwa wakinyanyaswa, kupigwa, kudhalilishwa na hata

kuuawa. Ni muda muafaka sasa kwa Wizara kuandaa mkakati wa makusudi wa

kutoa elimu kwa wananchi na rika yote na kutunga sheria ngumu zaidi ili

kuwabana watu wote wanaohusika na vitendo hivi vya kikatili.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ukeketaji wa watoto wa kike. Pamoja na

Serikali kutoa elimu na kukemea suala la ukeketaji wa watoto wa kike, bado

suala hili ni kubwa katika Mikoa ya Singida, Dodoma, Manyara Mara, Arusha na

kadhalika na hasa baada ya mangariba kubadili mtindo wa kukeketa watoto

wachanga wenye umri wa wiki moja mpaka mbili, hivyo kukwepa mkono wa

sheria.

Mheshimiwa Spika, Serikali sasa ibadili mtindo wa kulazimisha Mikoa hii

kuachana na jambo hilo kwa nguvu, ila itambue kwamba suala hili ni la kimila

hivyo busara itumike kutatua tatizo hili kwa kuanza na kuwaelewesha wananchi

kwamba si kila mila ina manufaa kwa wakati huu, bali kuna mila zingine zina

madhara ya kiafya. Serikali isitumie nguvu kuzimisha mila hii ambayo ni potofu

kuachwa, bali itumie njia ya majadiliano ya kirafiki.

Mheshimiwa Spika, suala lingine ni kuhusu Benki ya Wanawake. Kutokana

na malalamiko ya kila mara kwamba Benki hii ipo Dar es Salaam tu na haina

matawi katika Mikoa mingine, suala hili ni tatizo kubwa kwa wanawake wote

ambao wanahitaji huduma ya benki hii. Ni wakati sasa Wizara kuwa na

umuhimu wa kupanua wigo wa kuanzisha matawi katika Mikoa yote ya

Tanzania Bara na Visiwani ili kuepukana na dhana kwamba benki hii

inawafaidisha wake wa viongozi na si wahitaji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la watoto wa mitaani ni aibu kwa nchi

yetu kuona watoto wanakosa matunzo toka kwa wazazi wao kwamba ni wa

mitaani.

Ni kwa nini tunawaita hawa watoto ni wa mitaani kwa maana hawana

wazazi, hawana baba na mama? Sheria kali zitungwe kuwabana wanawake

Page 131: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

131

na wanaume wanaotelekeza watoto wao baada ya kuwazaa. Si baba tu

ambaye ndiye anapaswa kulaumiwa, hata mama/mwanamke naye

anachangia kuwa kikwazo kikubwa kuzalisha watoto wa mitaani.

Mheshimiwa Spika, kuna suala la haki ya wasichana wanaojifungua

kuendelea na masomo. Kuna usemi unaosema ukimuelimisha mwanamke

umeelimisha watu wote, ila ukimuelimisha mwanaume, umeelimisha mtu

mmoja.

Elimu kwa mtoto wa kike ni jambo la msingi kuliko ambavyo tunaweza

kufikiria. Msichana anapopata mimba kwa bahati mbaya akiwa bado

anasoma, si jambo la busara kumkatisha masomo mtoto huyu, maana kwa

kufanya hivyo unampa mateso kwanza ya kisaikolojia na vilevile ya kiuchumi na

kijamii jambo jema ni kumrudisha mtoto huyu shuleni ili aendelee na masomo

kama wanavyofanya wenzetu Zanzibar, Ghana, Kenya, Afrika Kusini na nchi

nyingine.

Mheshimiwa Spika, adhabu ya kupata mimba utotoni ni kubwa na

kumuongezea nyingine ya kumnyima elimu ni kumfanya afe kabla ya muda

wake, ni kwa nini sheria ya kuwarudisha wasichana wanaopata mimba wakiwa

shuleni hailetwi na kuanza kutumika mapema iwezekanavyo? Naishauri Serikali

kuona umuhimu wa jambo hilo ili kuwa Taifa lililoelimika na kuwafanya

wanawake wasiendelee kubaki nyuma kielimu na hata kutoka vyombo vya

maamuzi.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

MHE. GREGORY G. TEU: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa

Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watumishi wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri

mnayofanya. Kupitia kwako, naishukuru Wizara kwa kuanzisha huduma za

kibenki kwa kufungua Tawi la Benki ya Wanawake Tanzania katika eneo la

Jimbo la Mpwapwa, ikiwa ni kituo kimojawapo cha kutolea mikopo na mafunzo

kwa wajasiriamali.

Mheshimiwa Spika, ombi langu Wizara itatatua lini uhaba wa wakufunzi

wa kada mbalimbali katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi kikiwepo cha

Maendeleo ya Wananchi (Chisalu – Jimbo la Mpwapwa). Vilevile itoe

utaratibu/mwongozo unaojumuisha utoaji wa malipo ya ada ya mafunzo

yanayotolewa vyuoni, kikiwemo Chuo cha Chisalu - Mpwapwa, kitapewa nafasi

ya ukarabati na kutoa mafunzo ya VETA zaidi na kupewa hadhi ya VETA. Wizara

iseme haya ili iweze kusikika.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.

Page 132: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

132

MHE. MARIAM S. MFAKI: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga mkono hoja

hii.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali kuongeza bajeti ya Wizara hii ili

kuwawezesha watumishi wa Wizara hii kufanya kazi kwa mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Benki ya Wanawake tunaomba Serikali ieleze

kwa nini haipeleki fedha alizoahidi Mheshimiwa Rais kutoa ili kuongeza mtaji wa

Benki hii. Naomba Serikali itimize ahadi hiyo ili wanawake wafaidike na waweze

kupunguza matatizo waliyonayo.

Mheshimiwa Spika, pia nashauri Benki hii iweze kufungua matawi katika

Wilaya ili kuwarahisishia wananchi wake kufika katika Benki hizo kwa urahisi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la watoto wa mitaani, kundi hili la watoto

linazidi kuongezeka, tunaomba lianzishwe dawati litakaloshughulikia tatizo hili

kupunguza watoto hawa. Suala hili ni aibu na linasikitisha.

Mheshimiwa Spika, suala la ajira tunaomba Serikali iwaajiri vijana

waliomaliza Vyuo ili kuongeza watumishi katika Wizara hii na waweze

kusambazwa kila Kata ili kuelimisha wanawake juu ya ujasiriamali.

Mheshimiwa Spika, nashauri Wizara hii iwe na mtiririko wa utumishi katika

ngazi ya Wizara, Mkoa, Wilaya na Kata badala ya watumishi hawa kuwa chini

Halmashauri sababu ni kwamba Halmashauri imerundikiwa idara nyingi na

matokeo yake husahauliwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu NGOs tunaomba NGOs hizi zidhibitiwe katika

utendaji wao. Fedha wanazopata Serikali itume wakaguzi, NGOs zikaguliwe na

taarifa zitolewe kwenye vikao vya kisheria vya Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, naomba kumpongeza Waziri na watendaji wake kwa

kazi nzuri wanazofanya katika Wizara hii.

MHE. MUSTAPHA B. AKUNAAY: Mheshimiwa Spika, ili kuchangia kwa

ukamilifu nimeona nichangie kwa njia ya dondoo (bullet points) masuala ya

kijinsia watu wengi wanaelewa ni mambo ya wanawake lakini jinsia (gender)

maana yake ni kike na kiume kwa hivyo suala ni maisha ya jamii ya kike na

kiume na watoto wao (wholistic approach), siyo wanawake na watoto.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu sera iwe jinsi ya ukuzaji wa jamii kwa

jumla wanawake wahusishwe.

Page 133: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

133

Mheshimiwa Spika, kuhusu uratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, kuna

Mashirika mengi ambapo shughuli zake hazijulikani naishauri Serikali iwe macho

juu ya taasisi hizi. Kuna kuingiliana kazi kati ya RITA na kitengo cha Wizarani

katika kusimamia shughuli za NGO hasa vituo vya watoto.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maendeleo ya Tango - Mbulu awali kituo

hiki kilikuwa Folk Development Centre, Chuo kina ekari 600 ya ardhi na majengo

ya kutosha kwa ajili ya Chuo kuwa cha kutoa Stashahada lakini kutokana na

ukosefu wa bajeti Chuo kimekuwa Mahakama. Naomba kauli ya Serikali kuhusu

Chuo hiki.

Mheshimiwa Spika, suala la watoto wa mitaani Mbulu, kwa kuwa hakuna

kituo Wilayani Mbulu tunaomba Wizara iongeze fedha kwenye Halmashauri ya

Wilaya ili kituo kianzishwe. Bajeti ya shilingi bilioni 30 ni ndogo sana, iongezwe.

Mheshimiwa Spika, mwisho lakini siyo kwa umuhimu nampongeza

Mheshimiwa Pindi Chana kwa kuteuliwa kwake kuwa Naibu Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

MHE. REBECCA M. MNGODO: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto ni Wizara muhimu sana katika jamii yetu. Ni Wizara

inayohusika na maendeleo ya jamii nzima ya Tanzania lakini hata hivyo Wizara

hii haijapewa kipaumbele na Serikali kwa kutengewa fedha za kutosha ili

kutekeleza majukumu yake.

Mheshimiwa Spika, kiasi cha fedha kilichotengwa kwa mwaka 2014/2015

cha shilingi 9,017,544,000 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kitolewe kwa wakati

ili miradi ya maendeleo ya Wizara hii itekelezwe kwa wakati kwa manufaa ya

wananchi.

Mheshimiwa Spika, suala la watoto wa mitaani au wanaoishi katika

mazingira magumu ni tatizo ambalo bado halionyeshi kupungua je, tatizo ni

nini? Wizara inafanya nini ili kupunguza ukuaji wa tatizo hili?

Mheshimiwa Spika, mimba za utotoni hazijapungua, wanafunzi wengi

hasa waishio vijijini ambao shule zipo mbali wanaathirika sana na tatizo hili.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu itafute jinsi

ya kupunguza tatizo hili kwa kuhakikisha wale wote wanaowapachika mimba

wasichana wenye umri wa kwenda shule wanachukuliwa hatua za kisheria.

Mheshimiwa Spika, vituo vya kulea watoto wa mazingira magumu, vingi

vipo katika hali isiyoridhisha, hakuna walezi wa kutosha, watoto wanaathirika

kisaikolojia kwani mazingira wanayoishi ni yenye hali mbaya, Serikali itenge

fedha za kutosha kuendeleza watoto katika hali ya usawa.

Page 134: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

134

Mheshimiwa Spika, kwa haya machache naomba kuwasilisha.

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja hii

kwa asilimia mia moja, naipongeza Wizara hii kwa kutekeleza majukumu yake

ya kila siku na kuwa kituo muhimu kwa maendeleo ya wanawake na watoto.

Mheshimiwa Spika, watoto walio katika mazingira magumu ni kundi

kubwa na linaendelea kukua siku hadi siku, naiomba Serikali kupitia Wizara zote

za Afya, Kilimo, Elimu, Tawala za Mikoa na kadhalika kuwa na mipango ya

pamoja ya kulitambua kundi hilo kitakwimu, maeneo walimu hali zao za kijamii

(wana wazazi au laa) na baadaye kila Mkoa upange mpango mkakati katika

muda mfupi wa kati na muda mrefu wa kuwaendeleza watoto hawa.

Mheshimiwa Spika, kitendo cha ubakaji na ulawiti dhidi ya watoto,

nalaani vitendo vya baadhi ya wanaume, umefikia wakati wa kuungana

pamoja na wanawake na wanaume kupiga vita vitendo hivi vya unyanyasaji

wa watoto. Baya zaidi unyanyasaji huu hatimaye ni kuua kizazi na maendeleo

ya Taifa kudumaa.

Mheshimiwa Spika, wakati umefika wanawake tupaze sauti zetu

kuwasema na kuwafichua wale wote wanaoshiriki unyanyasaji wa wanawake

na watoto.

Mheshimiwa Spika, Benki ya Wanawake inafanya kazi nzuri ya

kuwahudumia wanawake na wanaume kwa kutoa mikopo na hata kusaidia

jamii. Tunaomba huduma hizi ziwafikie wanawake wengi zaidi mpaka Zanzibar.

Kuhusu ajira za watoto tunaiomba Wizara kwa nafasi kukemea ajira hizi

kwani umezuka mtindo watoto kutumikishwa majumbani na kukosa haki zao za

msingi kama elimu, afya kushirikishwa na kadhalika na kupewa chakula tu ndiyo

malipo yao na inapobidi kudai malipo hufukuzwa na kuondoka bila malipo

yoyote na hatimaye kuzurura mitaani mijini na wengine kunyanyasika kwa

kubakwa na hata kupata UKIMWI.

Mheshimiwa Spika, elimu itolewe kwa jamii kutokukubali watoto

kuwatelekeza kwa kufanyishwa kazi ngumu nje ya familia na ndani ya familia.

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Maendeleo wa

Wanawake ulianzishwa kutokana na Azimio la Bunge mwaka 1993 wenye lengo

la kuwawezesha wanawake kujiimarisha na kujikwamua kiuchumi. Mwongozo

unaongoza mfuko huu hauendani na hali halisi ya sasa, kupitia Bunge hili niliuliza

swali la lini mwongozo huo utafanyiwa mabadiliko na tathimini ili uendane na

hali halisi ya sasa. Hata hivyo majibu yalikuwa ni tathimini ilifanyika mwaka 2006

Page 135: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

135

ili kuona ufanisi wa mfuko huu. Je, Serikali imefikia hatua gani katika tathmini

ifanyike sasa ni takribani miaka nane, je, Wizara haioni tathmini hiyo itakuwa

imepitwa na wakati? Je, nini mafanikio ya mfuko huo?

Mheshimiwa Spika, Halmashauri nyingi nchini zimekuwa hazitengi fedha

asalimia tano (5%) ya mapato yake kwa Mifuko ya Wanawake na Vijana na si

kwamba Halmashauri hazitoki bali hali halisi ya kimapato kwa Halmashauri hapa

nchini inajulikana, hata hivyo fedha za mapato ya ndani katika Halmashauri

zetu hapa nchini huelekezwa zaidi katika miradi ya afya, maji, barabara na

kadhalika.

Mheshimiwa Spika, kuendelea kutoa msisitizo kwa Halmashauri zitenge

fedha katika mifuko hiyo ni jambo linalopaswa kutazamwa kwa upya kutokana

na hali halisi ya kimapato katika Halmashuri zetu.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo nashauri swala hili liachiwe Serikali kuu

kutenga fedha katika mifuko hiyo na si Halmashuri za Wilaya pekee.

Mheshimiwa Spika, uratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali, kumekuwa na

ongezeko kubwa la Mashirika haya hapa nchini kwa mujibu wa taarifa ya

Wizara, hata hivyo Mashirika hayo kwa wingi wake baadhi hazipo wazi kwa

wanayolenga kuyafanya katika jamii ya Watanzania, suala la uratibu wa

Mashirika haya ni dhaifu sana kwa kuwa tumeona jinsi kulivyo na NGO‟s

ambazo hazieleweki pamoja na kuwa Bodi ya Uratibu wa NGO‟s bado Bodi hii

haitekelezi wajibu wake ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha NGO‟s zote

zinatekeleza yote yaliyokusudiwa kwa mujibu wa uanzishwaji wake? Je, nini

mkakati wa kufuatilia na kuzifuta NGO‟s zenye utata na zilizokwenda kinyume

na uanzishwaji wake?

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua

nafasi hii na mimi nitoe mchango wangu katika Wizara hii nyeti ambayo vijana

wetu na mama zetu wanahusika nayo.

Mheshimiwa Spika, mimi napenda kuchukua nafasi hii nichangie hasa

kwa watoto wa mitaani na hasa wale watoto walio Dar es Salaam ambao kazi

yao ni kuuza maji na juice pale mjini, hivi vijana wale ambao ndani ya ujana

wao hawasomi wala hawatayarishwi kwa maisha ya baadaye, wanategemea

baada ya kuzeeka wataweza kumudu maisha yao ya uzeeni? Ni kwa kiasi gani

wataweza kuweka akiba ili waweze kujenga, kuoa na kuishi maisha yaliyo

bora?

Page 136: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

136

Mheshimiwa Spika, ni vyema vijana hawa sasa ni lazima kuwawekea

mpango maalum kwa ajili ya maisha yao ya baadaye, wawekwe katika

makambi na wapewe elimu ya ujasiriamali kwa muda ambao unaendana na

umri wao, vinginevyo ni dhahiri kwamba tutakuwa tunajenga Taifa la wazururaji

na wahuni.

Mheshimiwa Spika, kuna mmong‟onyoko mkubwa wa maadili ndani ya

nchi yetu, na hili kwa sasa ndiyo linaonekana ndiyo ustaarabu. Ngoma, muziki

na hata maonyesho yanayofanywa hapa nchini, wanawake na watoto

wanafanywa ndiyo chombo, kivutio kwa watazamaji je, haya hayaonekani

kuwa ni kudhalilisha jamii yetu? Na haya si maadili yetu? Na hata nyimbo za

sasa zinazoimbwa hazina maadili je, ile “board of sensor” sasa ina kazi gani?

Mheshimiwa Spika, ni wakati sasa kwa Wizara hii kuchukua hatua za

haraka kuona hali hii na hata jamii inavyopotea na nini kifanyike kwa haraka.

Hata vifo hivi vya walemavu wa ngozi na vikongwe ni mmong‟onyoko wa

maadili tu. Hivyo ni lazima sasa kusimama kwa pamoja kuchukua hatua za dhati

kwa suala hili ambalo jamii inapotea. Wakati wa maneno umekwisha na

vitendo vitawale katika hali ilivyo sasa.

Mheshimiwa Spika, ongezeko la watoto yatima ndani ya nchi yetu

linaongezeka kwa kasi sana na hatua za dharura zinahitajika ili watoto hawa

wapate huduma zinazostahili ili watoto hawa wajisikie kama watoto wenzao.

Aidha, kinga ni bora kuliko tiba kwani ni lazima vile viashiria vyote vinavyofanya

kuongezeka kwa watoto yatima vidhibitiwe mapema kuliko kuona watoto tu.

Tufanye kazi ya kuwalea watoto hawa kwa moyo wetu wote ili wawe viongozi

bora na watendaji wazuri katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, mwisho napenda kuwashukuru wale wote

wanaochangia kwa namna moja au nyingine wanaowalea watoto wa mitaani

kwa moyo wao wa kujitolea na huruma waliyonayo kwa Taifa la kesho. Ni

vyema vituo vile vikapewa upendeleo maalum na Mheshimiwa Waziri bajeti

ijayo ikawa na fungu la vituo hivi ili wale wanaowalea watoto hawa wawe na

uhakika wa maisha kwa vijana wale badala ya kusubiri hisani za wenye uwezo,

hii itawapunguzia mzigo wa kufikiria na kutafuta na badala yake watajikita zaidi

katika kuwashughulikia watoto wale.

Mheshimiwa Spika, mcheza kwa hutunzwa. Ahsante sana.

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Spika, napenda kumpongeza

Waziri, Mheshimiwa Sophia Simba (Mb) kwa hotuba nzuri. Pia nampongeza

Naibu Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wote wa Wizara.

Page 137: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

137

Mheshimiwa Spika, kama lilivyo jina la Wizara ya Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto Wizara hii inahusu maendeleo ya jamii kwa ujumla wake. Hii ina

maana kwamba bila ya utekelezaji katika Wizara hii hakuna maendeleo. Hivyo

ninapenda kuishauri Serikali iongeze bajeti katika Wizara hii. Tukiangalia katika

Halmashauri zetu kuna upungufu mkubwa sana wa Maafisa Maendeleo ya

Jamii katika ngazi za Kata na ngazi za Vijiji, nikitolea mfano katika Jimbo la

Busanda Vijiji vyote 80 havina Maafisa Maendeleo ya Jamii. Je, maendeleo

yatakuja vipi bila kuwa na watu waliosomea utaalam wa maendeleo ya jamii.

Mheshimiwa Spika, hivyo niiombe Serikali iajiri wataalamu wa maendeleo

ya jamii ili kuinua hali ya maendeleo katika vijiji vyetu.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili katika Mkoa wa Geita pamoja na Wilaya

zake hatuna Chuo cha Maendeleo ya Jamii wala Chuo cha VETA, katika

hotuba nimeona wenzetu kwenye mikoa mingine yenye vyuo vya maendeleo

wanavyofaidika na mafunzo mbalimbali. Naomba Serikali itujengee Chuo cha

VETA/Chuo cha Maendeleo kama sera ya Taifa inavyosema kwamba kila

Wilaya tuwe na Chuo cha VETA/Chuo cha Maendeleo ya Wananchi.

Mheshimiwa Spika, jambo la mwisho ninaomba Serikali iwekeze katika

maeneo ya uchimbaji madini ambako watoto wengi wanakabiliana na

changamoto mbalimbli zikiwemo ajira za watoto kwenye migodi ya wachimbaji

wadogo. Kuwepo na watoto wengi wanaoishi katika mazingira magumu na

hatarishi, hii ni kutokana na wingi wa watu wakati shughuli za uchimbaji

zinapopamba moto na baada ya muda watu huondoka mara uzalishaji

unapopungua wakati huo watoto huzaliwa, wazazi wa kiume huondoka

kwenda kutafuta madini sehemu nyingine, mwisho wa siku watoto wanaachwa

bila malezi yoyote. Ninayo mifano hai katika Wilaya ya Geita kwenye maeneo

ya Nyarugusu, Rwamgasa, Kaseme na sehemu zote zinazojishughulisha na

uchimbaji mdogo wa madini.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo maelezo ninaomba Serikali iwekeze kwa

kuongeza bajeti katika Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, pongezi kwa Waziri,

Naibu Waziri na watendaji wote wa Wizara kwa kuandaa hotuba hii na

kuwasilisha kwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na tabia ya baadhi ya watu kwa

kutumia NGOs zao kukusanya watoto yatima kutoka vijijini kwa maelezo

kwamba wanakwenda kuwalea, matokeo yake watoto wanawekwa kwenye

vituo ambavyo sio salama kwao, mazingira mabovu, wanakosa huduma zote

Page 138: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

138

muhimu ikiwepo elimu, watoto wanalala chini. Serikali itueleze ni uchunguzi gani

unafanyika kwa vituo vinavyoandaliwa kulea watoto kuona uwezo wa NGO na

mazingira ya kituo ili watoto wasiteseke?.

Mheshimiwa Spika, matukio mengi yameendelea kuongezeka ya mauaji

na manyanyaso ya watoto nchini yanayofanywa na wazazi, walezi na hata

walimu. Kwa kweli mzazi/mlezi anampiga mtoto vibaya kiasi cha kumuumiza na

hata kumletea umauti inaumiza sana na watoto wanachomwa mikono,

wanabanikwa kwenye majiko ya mkaa, wanafungiwa ndani kwa zaidi ya wiki

huku wamefungwa chain.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali itoe elimu zaidi kwa jamii kuondoa

matukio hayo. Pia hatua kali zitolewe kwa wote wanaobainika kufanya unyama

wowote kwa watoto ili kutoa fundisho.

Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Wanawake wa Wilaya pamoja na kuwa

Halmashauri hawatengi ile asilimia tano (5%) kutunisha hata kile kinachotengwa

na Serikali hakiendi kule ili wanawake waweze kukopeshwa. Tatizo la mfuko huu

pia unatolewa kwa upendeleo kwa wanawake kwa kuangalia itikadi za vyama

vyao. Wanawake wa CCM wanaonekana kama wao ndiyo wanaostahili, huku

wanawake wa vyama vingine wakinyimwa fursa hiyo. Kwa kuwa mfuko ni wa

wanawake utolewe kwa wanawake bila upendeleo wowote.

Mheshimiwa Spika, tatizo la watoto wa mitaani linazidi kuongezeka, tena

ni bahati mbaya sana kwa baadhi ya Mikoa wazazi wanawatuma watoto

wadogo wamebeba wadogo zao migongoni wazunguke kwenye magari

kuomba. Hatua zichukuliwe kwa wazazi hawa wanaowatumia watoto kama

vitega uchumi vya familia zao huku watoto wakikosa fursa ya malezi bora na

elimu. Kwa wale watoto yatima na waliofukuzwa na walezi wao/kutekelezwa

na hivyo kwenda mitaani Serikali ije na mkakati makini wa kuwasaidia.

Mheshimiwa Spika, nimeshauri miaka yote hapa Bungeni Serikali ijenge

kituo maalum cha kuwahifadhi watoto hawa. Kituo hiki kiwe ni cha mafunzo

kwa kuweka ufundi wa aina mbalimbali ili wafundishwe baada ya kupata

ufundi watatoka kwenye kituo, watakwenda kujitegemea kwa kutumia ujuzi

wanaopewa pia wataweza kutumia nguvu zao kuzalisha ile bustani za mboga,

ufugaji, ushonaji na hivyo kuinua uchumi.

Mheshimiwa Spika, mauaji ya albino na vikongwe/wazee yanatilia aibu

Taifa letu. Serikali ilifanikiwa sana kupunguza mauaji haya miaka mitatu iliyopita

baada ya kuanzishwa kwa Mahakama Maalum ya kushughulikia kesi za mauaji

haya. Pia kitendo cha kufuatilia waganga wa kienyeji na kuwafutia leseni wale

waliogundulika kuhusika kwenye masuala ya mauaji haya.

Page 139: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

139

Mheshimiwa Spika, Serikali izidi kuwabana waganga wa kienyeji na

kuwatangaza kwenye vyombo vya habari wazi kabisa ili wengine waone na

hivyo kuasi maasi hayo.

Mheshimiwa Spika, Serikali iweke nia ya dhati ya kuipatia Wizara hii fedha

za kutosha kutekeleza majukumu yake yaliyopangwa.

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Spika, katika kuchangia katika

hotuba ya Wizara hii niulize swali.

Kwanza, ilishapitishwa sheria kuwa kila Halmashauri ya Wilaya ichangie

asilimia tano (5%) katika mfuko wa akina mama.

Katika bajeti yake kwa nini maamuzi haya hayasimamiwi? Kwa nini Serikali

haichukui hatua thabiti kwa Halmashauri ambazo hazichangii? Na hata

zinazochangia hazifikii malengo yake? Serikali inachukua hatua gani?

Mheshimiwa Spika, kwa nini Serikali isichukue hatua ya kuagiza

Halmashauri zote nchini ziamuliwe na Serikali kulipa madeni yote ya nyuma

kuliko kuendelea kulalamika kila siku kukicha, Serikali ichukue hatua sasa.

Wakati ndiyo huu, tuache maneno, tuchukue hatua.

Mheshimiwa Spika, swali langu naomba kujua hivi maendeleo ya

wanawake ni wanawake wa mjini tu? Naishauri Serikali ielekeze nguvu zake kwa

akina mama wa vijijini, wanawake wa vijijini wapo nyuma sana Serikali

haiwasaidii kuwapelekea fedha za mikopo japo wanafanya kazi sana.

Mheshimiwa Spika, lingine pelekeni elimu kwa akina mama wa vijijini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu watoto yatima, Serikali iweke mtandao wa

kutosha kuwatambua watoto yatima waliopo vijijini ili iweze kuwasidia kiafya,

kielimu naona nguvu nyingi zinaelekezwa mijini tu.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. PROF. KULIKOYELA K. KAHIGI: Mheshimiwa Spika, nianze kwa

kuunga mkono hotuba ya Msemaji Mkuu Kambi Rasmi ya Upinzani, upungufu na

changamoto za Wizara hii zimeelezwa kinaganaga.

Mheshimiwa Spika, naungana na wachangiaji wengi wasioridhishwa na

kiasi kidogo cha fedha kilichotengwa hakitoshi kabisa kwa mahitaji ya Wizara hii

muhimu inayohusika na maendeleo ya jamii, jinsia na watoto. Inashangaza

kwamba Wizara muhimu kama hii haikuingizwa kwenye utaratibu wa Matokeo

Makubwa Sasa. Hivi bila kuwaandaa wananchi na kuwawezesha kuna

maendeleo gani yanayoweza kutokea vijijini na mjini? Yatakuwa hafifu kweli.

Page 140: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

140

Kwa hiyo Serikali iangalie namna ya kuipa uzito Wizara hii kwa kuipa fedha ya

kutosha kulingana na mahitaji yake.

Mheshimiwa Spika, mambo mengine ambayo ningependa kuchangia ni

haya yafuatayo:

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kuhusu fursa sawa za kijinsia. Bado

changamoto kubwa inayowakabili wanawake nchini ni kuwa na fursa sawa na

wanaume hasa kuhusiana na upatikanaji wa elimu. Bado mfumo dume

unawakandamiza wasichana wanaosoma shule (hasa za msingi na sekondari).

Bado kuna watu wasiothamini haki ya mtoto wa kike kupata elimu, bado kuna

wasichana wengi wanaoacha kuendelea na masomo kwa sababu mbalimbali

ikiwemo mimba zisizotarajiwa, Wizara ina mkakati gani kumsaidia mtoto wa kike

ilia pate fursa sawa na mtoto wa kiume kupata elimu?

Pili ni kuhusu watoto wa mitaani kuongezeka. Tatizo hili linazidi

kuongezeka kila uchao na linaonekana ni kubwa zaidi katika majiji na miji

mikubwa kama Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha, Dodoma, na

kadhalika, Serikali ina mkakati gani kukabiliana na tatizo hili?

Mheshimiwa Spika, tatu ni kuhusu kutotumika kwa wataalam wa

maendeleo. Wataalam wanaozalishwa na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii

hawatumiwi kikamilifu kuhamasisha maendeleo vijijini kutokana na bajeti kuwa

finyu. Katika Halmashauri yangu kwa mfano, watalaam wa maendeleo

wanatumia muda wao mwingi wakiwa ofisini tu kwa sababu hawana fedha ya

kutosha, kwa hiyo hakuna chochote cha maana kinachofanyika katika

kuhamisha maendeleo ya jamii vijijini.

Mwisho ni kuhusu ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Wizara ina

mkakati gani wa uhakika na endelevu kuhusu utokomezaji wa ukatili dhidi ya

wanawake na watoto? Tatizo hii ni kubwa na linapaswa kuandaliwa mkakati

maalum.

Mheshimiwa Spika, maswali ya mwisho, naomba Waziri ajibu maswali ya

mwisho yafuatayo:-

Kwanza, je, taarifa ya hali ya jinsia nchini ipo tayari? Kama ipo tayari

inapatikana wapi?

Mheshimiwa Spika, pili ni Halmashauri ngapi hutoa asilimia tano (5%) ya

mapato yao kwa ajili ya mfuko wa wanawake na zile ambazo hazitoi

huchukuliwa hatua gani?

Page 141: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

141

MHE. KULUTHUM J. MCHUCHULI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa

nachukua fursa hii kwapa pole Mheshimiwa Waziri, mMama Sophia Simba,

Naibu Waziri na watendaji wote kwa kuwa wanafanya kazi kubwa sana lakini

Serikali imeendelea kuinyima fedha Wizara hii hali ya kuwa wanafahamu hii ni

Wizara mtambuka.

Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na wimbi kubwa la mauaji ya kikatili ya

wanawake katika siku hizi za karibuni hasa katika Mikoa ya Mara na hata jana

ameuawa mwanamke mwingine katika Mkoa wa Mwanza. Je, Serikali

imeshindwa kabisa kudhibiti vitendo hivi vya kikatili vya mauaji dhidi ya

wanawake? Nini hatma ya wanawake katika kujiendeleza kiuchumi kwa kuwa

wakinamama hawa wanauliwa wakati wakiwa shambani?

Mheshimiwa Spika, wakati Mheshimiwa Waziri Mkuu anasoma hotuba

yake hapa Bungeni ya mwaka 2014/2015 katika ukurasa wa 28 alisema kuwa

hadi kufikia Desemba, 2013 Mfuko wa Wanawake umetoa mikopo kwa

wanawake wajasiriamali 500,000 nchini takribani shilingi bilioni 5.44 zilikuwa

zimetolewa kwa ajili ya mikopo, lakini katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri

Mama yangu Sophia Simba ukurasa wa 15 anaeleza kuwa kati ya mwaka

2011/2012 - 2013/2014 Wizara imekopesha jumla ya shilingi milioni 612 na huu

ndiyo ukweli ninaouamini.

Je, Mheshimiwa Waziri Mkuu amezitoa wapi na amepeleka hizo bilioni

5.44 katika Halmashauri zipi hapa nchini?

Mheshimiwa Spika, tunamtaka Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu, Waziri wa

Uwekezaji na Uwezeshaji atupe maelezo kamili juu ya matumizi ya shilingi bilioni

5.44 ambazo zinazosemekana zimepelekwa kwenye Mfuko wa Maendeleo ya

Wanawake. Je, mfuko unaosimamiwa na Mheshimiwa Waziri Nagu ni tofauti na

mfuko unaosimamiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto?

MHE. NAMELOK E. M. SOKOINE: Mheshimiwa Spika, nampongeza Waziri

na Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wizara hii yenye

changamoto nyingi.

Mheshimiwa Spika, nashauri Wizara iangalie ni kwa namna gani

watatunga sheria ambazo zitawasaidia wanawake hawa hasa manyanyaso

wanayoyapata ndani ya ndoa, mfano inapotokea mwanamke akijifungua

mtoto mwenye ulemavu mwanamke anabaguliwa na kuonekana yeye ndiyo

tatizo na wengine hupigwa hadi kuuwa na la kusikitisha baada ya muda

mwanaume anaachiwa, haki ya mwanamke ipo wapi?

Mheshimiwa Spika, takwimu haziongopi, utafiti wa mwaka 2010 unaohusu

afya na takwimu za uzazi, vifo na maradhi uliofanywa na Serikali pamoja na

utafiti wa matendo ya kikatili dhidi ya watoto wa mwaka 2011 unaonyesha

Page 142: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

142

kuwa asilimia 45 ya wanawake wametendewa ukatili wa kijinsia. Ukatili dhidi ya

wanawake majumbani huendelea kuongezeka ambapo takwimu mbalimbali

na utafiti zinaonyesha kuwa kati ya wanawake watatu, wawili wanatendewa

ukatili wa kijinsia na waume zao.

Mheshimiwa Spika, nashauri Wizara iendelee kuangalia sheria zote

kandamizi ambazo zinawanyanyasa wanawake na watoto.

Mheshimiwa Spika, pongezi za pekee kwa Benki ya Wanawake licha ya

fedha kidogo walizonazo wanaweza kufungua matawi maeneo mbalimbali, hii

inaonesha kwamba wanawake tunaweza, na hii inaonesha kuwa ukimuelimisha

mwanamke umeendeleza Taifa.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. BETTY E. MACHANGU: Mheshimiwa Spika, wanawake ni 51% ya idadi

ya watu milioni 45 ya Tanzania. Wanawake wengi sasa hivi ndiyo breaderner

katika familia zao, wanawake wa nchi hii ndiyo wanafanya kampeni zaidi katika

chaguzi mbalimbali nchini regardless of itikadi za vyama vya siasa.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaunga mkono wazo la wanawake kupata

50% katika ngazi zote za uongozi nchini. Inasikitisha bajeti ya Wizara hii ni ndogo

kuliko Wizara nyingine, mfumo dume ambao Serikali unaupiga vita

unajidhihirisha hapa. Nashauri Serikali iongeze bajeti ya Wizara hii. Wizara hii

ndiyo inasimamia makundi mbalimbali hasa watoto yatima na wanaoishi katika

mazingira magumu.

Mheshimiwa Spika, Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ni muhimu katika

maendeleo ya jamii. Jamii kubwa inaweza kujiendeleza katika vyuo hivi hasa

katika fani mbalimbali yanayofaidisha jamii. Zipo fani za upishi, kilimo, kushona

na kadhalika.

Nashauri Serikali iweke mkakati wa kuwa na uongozi bora katika vyuo hivi

ili vifaidishe jamii inayovizunguka na hata kutoka maeneo mengine nchini. Vipo

vyuo vya Maendeleo ya Jamii vinafanya vizuri sana, lakini vipo vingine vimebaki

na majengo tu, hakuna uongozi bora, hakuna wanafunzi wa kutosha na

kadhalika.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri za Wilaya zote nchini zina Idara ya

Maendeleo ya Jamii ambazo zinashughulikia na kutoa mikopo kwa wanawake

na vijana katika Halmashauri nyingine, fedha hizi zimekuwa za msaada sana

kwa vikundi pengine kwa sababu kuna bajeti za kutosha katika idara hizo.

Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya kwa njia moja au nyingine wahusishwe

katika ku-monitor na ku-evaluate vyuo vilivyopo katika Wilaya zao ili kutoa

Page 143: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

143

taarifa na kushauri mikakati bora itakayofaa kuendeleza chuo kilichopo katika

Wilaya zao. Pengine certificates zinazotolewa na vyuo hivi ziboreshwe ili

graduate anayetoka katika chuo hiki aweze kutumia kuingia Chuo Kikuu (Vyuo

Vikuu siku hizi vimeanzisha system ya certificates/foundation courses, ili ku-bridge

the gap kwa wale wanafunzi ambao hawakumaliza A-level au kama alimaliza

A-level hakupata credits za kuweza kuingia University).

Mheshimiwa Spika, Serikali ipige marufuku uvaaji wa nguo fupi (sana),

nguo za kuonyesha maungo yao, ndoa za jinsia moja, suruali zinashushwa

mpaka makalioni. Tusione haya, mila na desturi zetu budi tuzidumishe, maadili

ya vijana wetu yanaendelea kuporomoka. Serikali ipite ndanguro zote kuokoa

maisha ya watoto wetu na izifunge.

Mheshimiwa Spika, pia ipo haja ya kufanya mikutano ya hadhara nchini

kuwakumbusha wazazi jukumu lao la kulea watoto wao, ipo haja kila mzazi

ahakikishe mtoto wake ana more years in school ili kuondoa ndoa za utotoni,

mimba za utotoni na mtoto wa kike akipata elimu familia nzima inafaidika.

Mtoto wa kike akipata elimu ana uwezo wa kupanga uzazi atakapoamua

kuzaa na hivyo kuwa na familia ndogo kutegemea na kipato.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia kwenye

Wizara hii kwa kifupi sana kwani mawazo mazuri na mengi yameshasemwa

katika hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni.

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa ni juu ya hali mbaya ya Chuo cha

Maendeleo ya Jamii cha Tarime ambacho kipo katika hali mbaya sana na

nimekuwa nikilizungumzia hili kwa muda mrefu sana na Mheshimiwa Sophia

Simba mwaka 2012 alitembelea chuo kile na kuahidi kupeleka fedha ili kulipa

madeni ya umeme, maji na wazabuni wengine.

Mheshimiwa Spika, Chuo hiki kimechakaa na hakina hadhi hata ya kuwa

chuo wala shule ya msingi kuanzia madarasa, mabweni, maabara hamna

kabisa, maktaba hamna, vifaa vya kufundishia hamna, vitabu hamna,

upungufu wa walimu na kuna walimu waliojitolea lakini hawalipwi, kiufupi

Wizara/Serikali haipo tayari kuboresha miundombinu ya chuo kile cha TPDC -

Tarime na ikumbukwe kuwa chuo kile kinachukua vijana toka Wilaya zingine za

Mkoa wa Mara kama Rorya, Serengeti, Musoma na Butiama.

Mheshimiwa Spika, pia Serikali inatambua Wilaya hizi hazina Vyuo vya

Ufundi (VETA) hivyo wanategemea vyuo hivyo, sasa kwa nini Serikali inashindwa

kuboresha chuo hiki na kupeleka bajeti ya chuo kwa muda muafaka na

Page 144: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

144

kuhakikisha ile ahadi ya kulipa madeni na kuboresha miundombinu aliyoitoa

Waziri inatekelezwa mara moja. Naomba majibu ya kina kwenye hili.

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu unyanyasaji wa wanawake katika jamii.

Tumeshuhudia mauaji ya wanawake wakulima na hasa hili la mauaji ya kina

mama wa Butiama, hii inarudisha nyuma maendeleo ya wanawake. Wale

kinamama wanashindwa kwenda kisimani/wala mashambani na ikumbukwe

kule kwetu mwanaume huoa zaidi ya wanawake wawili, hivyo kauli ya kuwa

waenda shambani na waume zao, hii haikubaliki kabisa, Wizara itoe majibu

mbadala ni kwa nini imeshindwa kuchukua hatua kwa takribani mwaka sasa

tangu mwaka jana.

Pia Wilayani Tarime kuna manyanyaso makubwa kwa wanawake,

tumeshuhudia wanawake wamekatwa mikono kama yule Dada Gati lakini

Wizara haikutoa kauli, pia yule mwanamke wa Bunda aliyeburuzwa kwenye

lami na mume wake na Mheshimiwa Sophia Simba analijua hili suala maana

alienda hadi kumuona, je, huyu baba amechukuliwa hatua gani? Naomba

majibu pia kwa suala la kuozeshwa watoto wa kike na kubakwa.

Mheshimiwa Spika, mwisho ni juu ya watoto wa kike waliotekwa huko

Nigeria na kikundi kinachoitwa Boko Haram. Nashangaa Serikali yetu haitoi

tamko lolote lile kukeme kitendo kile. Maana hata hapa kwetu tuna watu

wanaoteseka sana na kufanyiwa vitendo kama hivyo.

Mheshimiwa Spika, mwisho ningependa kujua ni hatua gani

zinachukuliwa kwa wale wote wanaume/wanawake ambao wanajua wana

maradhi ya ugonjwa wa UKIMWI lakini wanachukulia fursa ya umaskini kwa

Watanzania na kuwarubuni na kushiriki ngono ambayo hupelekea maambukizi

ya UKIMWI. Hii ni tabia mbaya na haikubaliki katika ulimwengu huu na ni

kinyume na haki za binadamu, sababu hupelekea gonjwa na kifo.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

MHE. JUMA SURURU JUMA: Mheshimiwa Spika, kwanza naunga mkono

hoja kwa asilimia mia moja hotuba ya bajeti ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Benki ya Wanawake Tanzania naipongeza

Serikali kwa kutekeleza kwa vitendo katika huduma hii ya Benki ya Wanawake

Tanzania, hata hivyo nimeona benki imefungua vituo vingi vya benki hiyo

vinavyotoa mikopo na mafunzo ya wajasiriamali, lakini kwa kuwa ni Benki ya

Tanzania nzima, je, ni lini vituo hivyo vitafunguliwa Zanzibar?

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la uzururaji wa watoto barabarani na

mitaani, ni kipindi kirefu watoto wengi wamekuwa wakizurura mitaani na idadi

Page 145: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

145

inaongezeka, suala ambalo ni hatari kwa Taifa letu. Sasa ili kuondoa tatizo hili

lenye kutia aibu kwa Tanzania je, Wizara imepanga mkakati gani katika

kuliondoa tatizo hili na je, Wizara itawaambia nini Watanzania kwa zile familia

zinazotelekeza watoto hao?

MHE. BEATRICE M. SHELLUKINDO: Mheshimiwa Spika na Mheshimiwa sana

Waziri Sophia Simba, nichukue fursa hii nikupongeze kwa kazi nzuri sana

unayofanya katika mazingira magumu sana. Aidha nikupongeze kwa hotuba

yako yenye kuonyesha kukata tamaa.

Mheshimiwa Spika, nimshukuru na kumpongeza Rais, Mheshimiwa Jakaya

Kikwete kwa kumteua Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana kuwa Naibu Waziri, hakika

anastahili na ni imani yangu ya kwamba kwa pamoja ninyi wapambanaji

mtaendelea kufanya kazi kwa nguvu.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze pia Katibu Mkuu Mama Anna Maembe,

Naibu Katibu Mkuu Mama Milao na watendaji wote wa Wizara wa Wizarani,

Mikoani na Wilayani.

Maoni yangu, nikiri kuwa mimi ni Afisa Maendeleo ya Jamii tangu mwaka

1978 na hata dakika moja sitaacha fani yangu. Lakini nimekuwa nikiona

maendeleo ya jamii ikijikongoja ni lini tutatumia sekta hii ipasavyo?

Tumeona mikakati, mipango, miradi mbalimbali ikiendelea bila ufahamu

wa wananchi, mikakati hafifu iliyotumika hatimaye utekelezaji umeshindikana,

yangefanywa na Maafisa Maendeleo ya Jamii pangekuwa na mafanikio. Kwa

nini basi hamfanyi makusudi mazima kuelimisha na kuwezesha sekta zote

kuelewa umuhimu wa hawa watu?

Mheshimiwa Spika, pana pendekezo kuwa paanzishwe Baraza la

Wanawake ambalo linaelekea kuzaa matunda na hata kuingizwa kwenye

Katiba. Hamuoni kuwa Wizara ya Jinsia imeonyesha upungufu sana hadi

kuonekana kuanzisha Baraza hilo.

Nina hakika likianza Idara ya Jinsia itakosa mwelekeo, acheni kufanya

business as usual, na kutegemea semina, mikutano na conferences na

kutegemea wafadhili mambo ni mengi ukatili wa wanawake wa kutisha

unaendelea, watoto wanadhalilishwa, hakuna action wala matamko. Kama

vipi chukueni maamuzi magumu ya kuondoa hiyo mizigo muweke watu ambao

wana weledi na uelewa wa mambo haya. Tunaumia sisi Maafisa Maendeleo ya

Jamii proper kuona sekta imelala.

Page 146: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

146

Mheshimiwa Spika, kuna malalamiko toka kwa wafadhili kuwa Wizara

utendaji umezorota, miradi mingi, mikakati mingi haiendi, please elezeni tatizo

tuchangie. Tatizo la fedha linatokana na mikakati sifuri na uzito kwa kufanya

mambo kwa mazoea.

Mheshimiwa Spika, Maafisa Maendeleo ya Jamii Wilayani hawana

vitendea kazi, magari, fedha kwa kweli ni kama yatima kwenye Halmashauri na

nyakati nyingine hawaeleweki shughuli zao. Kwa vile bajeti ya Serikali ni ndogo

sana, basi hizo fedha za wafadhili zitumieni kwa activities huko, wasaidiwe

kuandika proposals na mafunzo.

Mheshimiwa Spika, asilimia tano (5%) ya kwenda kwa akina mama

isimamieni, kwani maeneo mengi hazipelekwi, lakini vilevile muwawezeshe ma-

CDO/CDA‟S kuhamasisha akina mama na vikundi vyao kuanzisha miradi

mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, mwisho tutumieni Maafisa Maendeleo ya Jamii proper

tuliostaafu, anzisheni Baraza hilo, litawasaidia na kuwashauri. Mungu awabariki.

MHE. AMINA N. MAKILAGI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mungu na

namshukuru Mheshimiwa Spika kwa kunipa nafasi nitoe ushauri katika maeneo

machache yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maendeleo ya Jamii ni miongoni mwa

Wizara inayopewa fedha kidogo wakati Wizara hii ni Wizara ya Maendeleo, ni

Wizara mtambuka. Kwanza Wizara hii ndiyo inayohamasisha maendeleo ya

wananchi na pili, kuhamasisha vikundi vya maendeleo, kulea wazee na

inashughulikia masuala ya watoto. Ningependa kujua Serikali ina mpango gani

wa kuongeza fedha kwa ajili utekelezaji wa kazi za Wizara?

Mheshimiwa Spika, kuhusu mauaji ya wanawake hasa Butiama,

wanawake wamekuwa wakiuawa, ningependa kujua ni hatua gani

zimechukuliwa juu ya matukio hayo, pia ningependa kujua je, Serikali na jamii

wamejipangaje katika kukabiliana na hali hiyo?

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake,

naishukuru Serikali kwa kutenga fedha shilingi bilioni mbili kwa ajili ya Mfuko wa

Maendeleo. Naiomba Serikali itoe fedha ili kukamilisha deni hilo lililobaki kabla

ya mwaka wa fedha haujaisha.

Mheshimiwa Spika, vilevile naishauri Serikali itenge fedha zingine za

kutosha kwa ajili ya kuimarisha vikundi vya kiuchumi. Pia ningependa kusikia

kauli ya Serikali ya fedha zilizotengwa za Mfuko wa Maendeleo zinatoka lini

bilioni mbili?

Page 147: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

147

Mheshimiwa Spika, kuhusu asilimia ya mapato ya Halmashauri, naomba

kusikia kauli ya Serikali kwa Halmashauri zilizoshindwa na zitakazoshindwa

kutenga asilimia 10% ya wanawake na vijana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu watoto wa mitaani, ningependa kujua Serikali

ina mkakati gani kupunguza tatizo la watoto wa mitaani.

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali itenge fedha za kutosha kwa ajili ya

ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo na fedha za kuendeshea Vyuo hivyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Benki ya Wanawake, nampongeza Mkurugenzi

wa Benki ya Wanawake na Bodi kwa kazi nzuri wanayofanya ya kuifanya benki

ikuwe siku hadi siku kwa kuanzisha tawi la pili Kariakoo Dar es Salaam na vituo

vya kutolea mikopo na mafunzo kwa wajasiriamali na kufungua matawi

Mwanza na Dodoma. Naishukuru Serikali kuendelea kutoa ruzuku.

Mheshimiwa Spika, ombi langu naomba Benki ifungue vituo vya mafunzo

na kutolea mikopo katika kila Mkoa kwani manufaa ya benki hii yawafikie

wanawake wengi hasa wa vijijini.

Mheshimiwa Spika, pia masharti ya kutoa mikopo katika Benki ya

Wanawake yaangaliwe upya ili kukidhi malengo na madhumuni ya

kuwakomboa wanawake hasa vijijini.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. ZARINA S. MADABIDA: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto ni Wizara nyeti sana kwa sababu iwapo ingeendelezwa

kwa kupata bajeti ipasavyo ingeweza kuinua maisha ya jamii na kuwezesha

jamii kuchangia maendeleo ya nchi. Hii ingebadili kabisa maisha ya jamii na

kuweza kumudu mahitaji yao na ni nyenzo muhimu ambayo ingeleta maisha

bora kwa kila Mtanzania.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii imekuwa inapewa bajeti ndogo sana

pamoja na ukweli kwamba imekuwa ikifanya mengi kwa jamii. Ni kwa nini sasa

Serikali isiwezeshe zaidi Wizara hii?

Mheshimiwa Spika, kila Halmashauri inatakiwa kutoa asilimia tano (5%)

kwa maendeleo ya wanawake na asilimia tano (5%) kwa vijana kwa mapato

ya ndani ya Manispaa.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo ni Manispaa chache zinazotoa hizo asilimia

tano (5%) za wanawake na vijana, kwa kudhani kuwa suala hilo siyo muhimu.

Fedha hizo Halmashauri nyingi wanaona ni nyingi na hivyo kumega nyingine na

kuzipeleka kwenye mahitaji mengine.

Page 148: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

148

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa maendeleo ya jamii, ni

kwa nini hii asilimia kumi (10%) ya makusanyo ya ndani ya Manispaa zisipelekwe

katika Wizara hii ya Maendeleo ya Jamii ili fedha hizo zihakikishwe zinalipwa na

vilevile zitahakikiwa kuhakikisha zinatumika kwa walengwa mahsusi.

Mheshimiwa Spika, ukatili kwa wanawake na watoto umezidi na ni dhahiri

waathirika hao wakiwemo na wazee wanaume, je, Serikali ina mpango gani wa

kukomesha mauaji ya wazee hawa kwa sababu mbalimbali ikiwemo ya

ushirikina, ni kwa nini pamoja na elimu endelevu, adhabu kali isitolewe kwa

wahusika?

Mheshimiwa Spika, wasichana wengi wamekuwa victims wa mimba za

utotoni hasa wale wanaochaguliwa kujiunga na sekondari. Sekondari nyingi

vijijini zipo mbali sana na makazi ya watu hivyo inalazimu wasichana kutembea

umbali mrefu lakini pia wazazi wengine huamua kuwapangia watoto hao wa

kike vyumba karibu na shule hizo. Matokeo yake wasichana hubakwa,

hujamiiana na watoto wa kiume, lakini pia kuwekwa kinyumba na wanaume

wakubwa. Watoto hao hupata mimba kirahisi na kukatisha masomo yao.

Wazazi nao huona hiyo ni aibu na wengi wanaamua kuwaoza na

kuwatumbukiza watoto hao kwenye dimbwi la ujinga na umaskini. Je, ni kwa

nini Serikali isijenge hosteli kwa ajili ya watoto hao?

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Afya ina Ustawi wa Jamii wakati Wizara hii

ina maendeleo ya jamii lakini Ustawi na Maendeleo ya Jamii, ni mambo

yaliyohusiana kwa karibu sana na mambo yale yanahusu kundi la watu hao

hao. Je, ni kwa nini kazi hizo zisiunganishwe ili ziweze kuendelezwa kwa pamoja?

Hii itasaidia Serikali kuchanganya nguvu zinazotawanywa fedha hizo kwenye

Wizara mbili badala yake fedha zote ziende mahali pamoja.

Mheshimiwa Spika, mwisho natoa wito kwa Serikali kusoma michango ili

kuona yanayoweza kuchukuliwa na kufanyiwa kazi kwa ustawi wa jamii ya

Watanzania.

MHE. RUKIA KASSIM AHMED: Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia

kuhusu unyanyasaji wa watoto. Vitendo hivi vya unyanyasaji wa watoto

vimekithiri kwa kiasi kikubwa na bado Serikali haijaweza kuyadhibiti.

Mheshimiwa Spika, kuna watu wengi wanabaka watoto, wanalawiti

watoto lakini inapopelekwa kesi Mahakamani mara nyingi kesi hizi zinakosa

ushahidi wa kutosha na hawa wanaofanya vitendo hivi wanaachiwa huru. Hili

naiomba Serikali ione kuwa ni tatizo kubwa ambalo linaathiri kizazi chetu. Serikali

itoe taaluma kwa wazazi pale inapotokea mtoto kubakwa au kulawitiwa basi

wazazi wasiwasafishe hawa watoto mpaka wafikishwe Polisi ili wapelekwe

Page 149: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

149

hospitali upatikane ushahidi. Pale anapopelekwa bado mbegu zile

zinaonekana pale anapopelekwa na kupimwa hospitali ushahidi unapatikana.

Mheshimiwa Spika, jambo hili ndiyo linalosababisha kesi hizi kukosekana

ushahidi na wahalifu hawa kuachiwa huru na kuendelea na kazi yao ya

kudhalilisha watoto.

Mheshimiwa Spika, napenda kuzungumzia kuhusu akinamama wengi

wanavyoteseka ndani ya majumba yetu kwa kupigwa na kunyanyaswa na

wanaume. Wanawake wengi sana wanafanyiwa ukatili wa kijinsia kwa sababu

hawawezi kuondoka pale kwa sababu ya uwezo mdogo wa kuendesha familia

hawawezi kuwaacha watoto na pia akiwachukua hawezi kuwashughulikia.

Matokeo yake anaendelea kuteseka.

MHE. HAMOUD ABUU JUMAA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nianze

kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kunipa fursa hii ya

upendeleo ili nami nichangie hotuba hii ya bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto ya mwaka 2014/2015. Vilevile nimpongeze Mheshimiwa

Waziri pamoja na wataalamu wake kwa kundaa bajeti nzuri inayokuja

kukabiliana na changamoto zinazozikabili sekta hizi. Mpango huu wa Serikali

unaendana kabisa na Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, lengo kuu la sekta ya maendeleo ya jamii ni kuchukua

hatua zinazowawezesha watu kutambua uwezo walionao na kubaini matatizo

na uwezo wao wa kutumia rasilimali zilizopo kujitatulia matatizo hayo, kujipatia

na kujiongezea kipato na kujiletea maisha bora zaidi na hivyo kujiletea

maendeleo wenyewe, na kuweka mazingira muafaka yatakayowawezesha

wanawake na wanaume kutekeleza makujumu yao katika jamii kwa kuzingatia

mahitaji ya kijinsia.

Aidha lengo lingine ni kuongeza ushirikishwaji wa wanawake na vijana

katika shughuli za maendeleo, hatimaye kuleta maisha bora kwa kila

Mtanzania. Kazi zinazotekelezwa na sekta ya maendeleo ya jamii katika

maeneo mbalimbali nchini ni pamoja na:-

Kwanza, kujenga uelewa wa wananchi ili aweze kushiriki shughuli

mbalimbali za kujiletea maendeleo yao kwa njia ya kujitegemea na kuwasaidia

kupanga mipango inayotekelezeka.

Pili, kuhamasisha wananchi kuujinga katika vikundi vya kijamii na SACCOS

ili kuanzisha na kutekeleza shughuli za uzalishaji mali zenye kuchangia kuinua

hali zao za maisha, pamoja na utoaji wa mikopo ya kiuchumi kwa wanawake

kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii wa Wanawake.

Page 150: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

150

Tatu, kusaidia jamii jinsi ya kuondokana na mila potofu zinazochangia

kuzorotesha maendeleo ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, kila Halmashauri katika mikoa yetu hapa nchini ina

dawati la jinsia na kwa kuzingatia msimamo wa nchi yetu kuhusu usawa wa

kijinsia Halmashauri zote zimekuwa na msimamo wa kutekeleza maazimo

mbalimbali ambayo Serikali imekuwa ikisaini mikataba yake, mfano azimio la

haki za binadamu la mwaka 1948 la kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya

wanawake (CEDAW 1979) pamoja na maazimio mbalimbali yanayohusu haki za

wanawake na watoto. Madawati haya yamekuwa chachu ya kuleta usawa

katika utendaji kazi na umiliki wa rasilimami katika jamii ikiwa ni pamoja na

kuachana na mila potofu zinazosababisha wanawake kuonewa na kupuuzwa

kutokana na kutokuwa na kauli ya kumili mali.

Mheshimiwa Spika, zipo changamoto mbalimbali zinazosababisha

vikwazo mbalimbali katika utekelezaji wa kazi za idara kama ifuatavyo:-

(i) Tatizo la usafiri kwa watumishi walio kwenye Kata pamoja na

Halmashauri nyingi kukosa vyombo vya usafiri.

(ii) Tatizo la makazi kwa watumishi waishio kwenye Kata.

(iii) Tatizo la vitendea kazi.

(iv) Ukosefu wa ofisi kwa watumishi katika Kata.

(v) Fedha za matumizi ya kawaida zinazoletwa na Serikali kufanyia kazi

ni kidogo kwa ajili ya kazi za Idara ya Maendeleo ya Jamii.

(vi) Mashirika yasiyo ya Kiserikali kutotoa taarifa zao za utendaji kazi

kwa wakati

Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hizo nilizozitaja hapo juu,

kuna njia ya kukabiliana nazo ili kuleta tija katika sekta hii nzima, nazo ni kama

ifuatavyo:-

(i) Wizara ishirikiane na Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI kusaidia kutoa

vyombo vya usafiri kwa watumishi wa Maendeleo ya Jamii katika

ngazi zote Wilayani na kwenye Kata.

(ii) Watumishi wa Sekta ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na

wananchi wanatoa hamasa kwa wananchi waweze kujitolea

kuwajengea nyumba watumishi wao wa sekta zote.

Page 151: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

151

(iii) Wakurugenzi wa Halmashauri wanahimizwa kuchangia katika OC

ya Idara ya Maendeleo ya Jamii ili kuifanya Idara hii iweze kufanya

kazi zake vizuri.

(iv) Mkoa na Halmashauri zinafanya jitihada ya kuwawezesha

watumishi wa Maendeleo ya Jamii kuwafikia walengwa.

(v) Mashirika yasiyo ya Kiserikali yamekumbushwa kuwasilisha taarifa za

kazi zao katika mamlaka ya Serikali za Mitaa.

(vi) Uanzishaji wa mitandao ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali ya Mkoa na

Wilaya imesaidia kusukuma utendaji wa kazi za mashirika hayo.

Mheshimiwa Spika, katika Jimbo la Kibaha Vijijini matatizo haya pia yapo

na kusema kweli tumekuwa tukikabiliana na changamoto nyingi sana kutokana

na matatizo haya, tukianzia na suala zima la watoto wa mitaani tumekuwa

tukikabiliana na changamoto hiyo kwa miaka mingi sana na mpaka hivi sasa

bado watoto hawa wamekuwa wakizidi kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, naiomba Wizara kuchukua juhudi za wazi na za

haraka kabisa ili kuweza kutatua tatizo hili kwani watoto na vijana hawa ni Taifa

la kesho hivyo basi tukiwaacha wazagae mtaani bila kupata elimu na

kuwaendeleza tutakuwa tunapoteza viongozi wa kesho.

Katika bajeti ya mwaka jana niliishauri Serikali kuanzisha vituo vya

kuwalelea watoto hawa Jimboni kwangu ili kuwatunza na kuwapa maadili

yaliyokuwa bora tofauti na sasa hivi kwani huzagaa hovyo mitaani na kujifunza

mambo yasiyokuwa ya maadili kulingana na umri waliokuwa nao.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi narudia tena kusema naomba kuleta tena

kwa Serikali ombi langu ili walifanyie kazi tuweze kuokoa kizazi hiki ambacho ni

Taifa la kesho. Kwa kuwa sisi bado tuna maeneo mengi na mazuri ya wazi hivyo

haitakuwa shida kupata eneo kwa ajili ya kujenga kituo hicho.

Vilevile tumekuwa tukikabiliwa na tatizo la wazee wasiojiweza na wao pia

wanastahili kuhudumiwa, wazee hawa hali zao sio za kuridhisha kwani

wamekuwa wanakosa hata mlo wa kawaida unaohitajika kwa binadamu,

wakiwekwa mahali na kupatiwa huduma basi wazee hawa wataondokana na

adha hii wanayoipata hivi sasa. Kupitia maombi haya kwa Serikali, nawashauri

watumie vyanzo mbalimbali kuweza kupata fedha na kuja kuwasaidia

wananchi wetu na kuwaondoa na adha hii ambayo hakuna kati yetu

anayependa kuwaona wazee hawa, vijana ama watoto wa mitaani wakipata

shida na kuishi katika mazingira magumu wanayokabiliana nayo hivi sasa.

Page 152: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

152

Mheshimiwa Spika, yanahitajika mafunzo yanayoungasha utashi wa

kisiasa kwa kuzingatia masuala ya jinsia na usawa Serikalini ili kupunguza

mapengo yaliyopo, inabidi kuwekeza fedha na rasilimali anuai. Nadharia iliyopo

kwenye sera inaweza kutekelezeka endapo kutakuwa na uwezeshaji wa

rasilimali na fedha ili kuhakikisha huduma za kijamii zinatekelezwa kwa kuzingata

mahitaji ya makundi yote yaani wanawake na wanaume.

Aidha, mara nyingi mahitaji ya makundi la wanawake yamekuwa

yakisahaulika jambo ambalo linaonesha kuna kila sababu ya kuwawezesha

watendaji Wizara husika kiuchambuzi wa sera na bajeti kwa mlengo wa kijinsia

na kuainisha mapungufu kama hayo ili yaweze kufanyiwa kazi. Kundi la

wanawake bado limekuwa na changamoto hasa katika huduma za afya, elimu

na nyinginezo ambazo zinaongeza mzigo kwa wanawake.

Naiomba Serikali kuongeza uwekezaji katika kukabiliana na vitendo vya

ukatili wa kijinsia na kuongeza idadi ya wanawake katika vyombo vya uamuzi ili

kuleta usawa wa kijinsia. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ndiyo

Wizara yenye dhamana katika usimamizi wa masuala ya kijinsia kwa Taifa letu

na usimamizi wa sera ya jinsi na uratibu wa vitengo vyote vya jinsia, hivyo ni

muhimu kwa watendaji wake kuwa na uelewa wa kutosha, uwezo wa

kirasilimali na rasilimali watu ili watendaji hao waweze kufanya ufuatiliaji wa

kutosha katika utekelezaji wa masuala anuai kwenye bajeti.

Mheshimiwa Spika, mabadiliko yoyote ya kijamii ni mchakato na miaka

yote hii toka tupate uhuru ni mingi, tungetarajia tuwe tumepiga hatua kubwa

zaidi, lakini kwanza ni vizuri kutambua juhudi zilizofanywa zimeanza kuzaa

matunda kwenye maeneo mengi, miaka yote hii iliyopita hata dhana ya jinsia

haikuwepo kwenye mazungumzo yetu hata dhana ya mfumo dume ilikuwa

haipo, lakini kwa sasa wanawake na wanaume wanakaa pamoja na

kuzungumzia masuala hayo. Ni jambo la kujivunia katika historia ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, Serikali imejitahidi sana katika upangaji na utekelezaji

wa bajeti maeneo anuai ili kuhakikisha makundi yote yananufaika na rasilimali

za Taifa, hatuna budi kuipongeza kwa hilo. Ila kuna hali ya unyanyasaji wa

kijinsia katika baadhi ya maeneo licha ya juhudi za kupambana na vitendo

hivyo ambavyo havikubaliki kabisa.

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali indelee na mkakati wa utoaji wa

elimu ya uelewa juu ya masuala ya haki, kwani jamii ikielewa vitendo kama

hivyo vitakoma mara moja na kubaki kuwa historia.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

Page 153: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

153

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Spika, napenda

kuchangia katika maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, suala ya ukatili wa kijinsia licha ya juhudi kubwa za

Serikali za kuhakikisha inakomesha ukatili huu bado kuna vitendo vingi vya kikatili

vimekuwa vikiripotiwa kwa mfano mauaji ya vikongwe, ukatili kwa walemavu

wa ngozi (albino), mauaji ya wanawake katika mikoa mbalimbali ikiwemo Mkoa

wa Mara. Je, Serikali ina mipango na mikakati ipi kuhakikisha vitendo hivi

vinakomeshwa?

Mheshimiwa Spika, Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake ni vyema Serikali

kupitia Wizara hii ikafuatilia kwa ukaribu kuhakikisha kwa asilimia tano (5%)

inayotakiwa kutengwa kwa ajili ya kuwawezesha wanawake kiuchumi

inapatikana na pia kuweka mkazo kwa wanawake wengi waliopo vijijini.

Mheshimiwa Spika, Benki za Wanawake nashauri kwamba matawi

yaanzishwe mikoani kwa kuweka madirisha kupitia Benki za Posta ambazo

zinapatikana karibu katika mikoa yote ya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, katika

eneo hili Serikali kupitia Wizara hii katika bajeti yake ya mwaka 2013/2014 iliahidi

kukifufua Chuo cha Maendeleo cha Msaginya kilichopo Mkoani Katavi kwa

kuanzisha pia kozi zingine kama masomo ya upishi na mengineyo kama ufugaji

wa nyuki kwa ajili ya kuzalisha asali na kuweza kujikwamua kiuchumi kuanzia

ngazi ya familia hadi Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, je, mpaka sasa hali ya Wizara ikoje? Je, Serikali

inasema nini katika hili?

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri katika majumuisho yake

atueleze wananchi wa Katavi tutegemee nini katika hili.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

MHE. PHILIPA G. MTURANO: Mheshimiwa Spika, Wizara hii inashughulikia

maeneo mengi sana ambayo yanagusa mtu moja kwa moja na mazingira

yanayomzunguka.

Mheshimiwa Spika, mengi yamezungumzwa kuhusu Wizara hii lakini kama

Serikali haitaona umuhimu wa kuipatia Wizara hii pesa ya kutosha hakuna

kitakachofanyika.

Mheshimiwa Spika, majengo ya Vyuo vya Maendeleo yamechakaa kiasi

cha kutishia uhai wa wanayoyatumia. Maeneo mengi hayopo sawa kwa ajili ya

Page 154: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

154

ufinyu wa bajeti. Tunaitaka Serikali iitizame kwa jicho la pekee Wizara hii ili kazi

iweze kufanyika ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, suala ya ukatili wa wanawake, watoto na walemavu

bado ni tatizo kubwa katika nchi hii, Serikali ifanye operesheni maalum kubaini

watu wanaofanya vitendo hivi na kuwafikisha katika vyombo vya sheria na

Wizara husika ifuatilie kuona haki imetendeka.

Mheshimiwa Spika, pia tatizo la utumikishwaji kazi ngumu watoto wadogo

bado lipo na limekuwa tatizo sugu. Serikali ilichukue hili kwa kumaanisha kwani

wanateseka majumbani na migodini.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa Serikali ione umuhimu wa Wizara hii

ipate fedha ya kutosha ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi kama Wizara nyingine.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Spika, ninapenda kumpongeza Waziri

wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Mheshimiwa Sophia Simba (Mb)

pamoja na Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana na Katibu Mkuu na Maafisa wote na

wafanyakazi wa Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia hotuba hii kwa kutoa rai kwa

kuwa Wizara hii ni mtambuka hususan katika masuala ya jinsia na watoto basi

wafuatilie na kushinikiza kwa nguvu zaidi na ikibidi kuwa na sheria inayoibana

Serikali kwa maana ya Wizara na taasisi kuajiri na kuanzisha dawati la jinsia

ambalo litakuwa linafanya kazi kwa karibu sana na kuwatumia kutekeleza au

kusimamia utekelezaji wa miradi husika katika Wizara na taasisi hizo.

Mheshimiwa Spika, Wizara iboreshe mfumo wa kutoa Maafisa Maendeleo

wengi kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli hizi wakichangiwa na kila Wizara na

taasisi katika yale maeneo yanayohusu sekta hii. Hii itahakikisha kuwa

maendeleo ya kila sekta yanatekelezwa kwa kuzingatia usawa wa jinsia huku

wakichangia kibajeti na ujuzi kwa matumizi ya maafisa hawa wa maendeleo

ambao wengi wapo vijijini na mijini kwenye ngazi ya Kata na Halmashauri.

Maafisa Maendeleo wafanye kazi na Maafisa Ugani na Maafisa

Biashara, Afya, Elimu, Wahandisi, Wanyamapori, Kilimo, Mavuvi, Wafugaji na kila

sekta kuhakikisha kuwa masuala ya jinsia yanazingatiwa kuanzia ngazi ya

kupanga mipango, utekelezaji na kwenye ufuatiliaji na tathmini. Gharama zote

zitachangiwa na sekta husika.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo ni mategemeo yetu kuwa tutaona Wizara hii

ikianzisha Idara au ikijumuisha kwenye Idara ya Jinsia. Afisa atakayeratibu

Maafisa Jinsia katika kila Wizara na taasisi ya Serikali na kutengeneza mpango

Page 155: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

155

mkakati wa kitaifa unaoanisha shughuli zote zinazotajwa hapo juu kwa

mtazamo wa kijinsia.

Mheshimiwa Spika, Benki ya Wanawake ilipata bahati ya kupata mtaji wa

kuianzisha lakini hata kwa fedha hizo Benki haijatumia ubunifu kujizalishia

mapato zaidi ili hali benki binafsi kama Benki ya Maendeeo iliyoenda kwenye

soko la hisa kupata fedha ya kutosha kujiendesha. Uongozi wa Benki hii

uangalie jinsi gani wataweza kufanya hivyo ili waweze kueneza huduma hii

muhimu kwa wanawake.

Mheshimiwa Spika, suala la uzazi wa mpango na elimu ya uzazi kwa

vijana isimamiwe chini ya mfumo huo tajwa hapo juu. Nepal, Pakistan na India

hata Ethiopia wana modeli nzuri ya kuigwa unaosaidiwa na UNDP.

Mheshimiwa Spika, nitakuwa tayari kushirikiana na Wizara kutoa uzoefu

wangu.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha na naunga mkono hoja.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa

kuwapongeza Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto, pia Katibu Mkuu kwa kuiendesha vyema Wizara hiyo japo

bajeti/fedha wanazopewa ni ndogo sana kulingana na majukumu waliyonayo

katika Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mengi mazuri yanayofanywa na

Wizara hii lakini zipo changamoto zifuatazo:-

Mheshimiwa Spika, kuongezeka kwa watoto wa mitaani na wakubwa

wanaomba omba mitaani, tatizo linazidi kuongezeka siku hadi siku katika

maeneo ya mijini.

Mheshimiwa Spika, Serikali ni vyema sasa ikatoa tamko kwa wazazi

wanaoachia watoto hovyo mitaani wachukuliwe hatua za kisheria. Sababu za

kushauri hivyo ni utafiti niliofanya si watoto wote wana matatizo, bali ni utovu

wa nidhamu tu. Watoto hao wana wazazi wao isipokuwa wanakataa kwenda

shule tu.

Mheshimiwa Spika, watu wazima wanaoomba mitaani hali kadhalika na

wao pia si wote wana matatizo kwani walio wengi wamegeuza hiyo ni ajira na

wanadiriki hata kupeana fedha wanazoomba kwa kucheza michezo. Je, ni

kweli watu hawa wana shida ya kweli?

Page 156: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

156

Mheshimiwa Spika, pamoja na changamoto lakini napenda nitoe

shukrani kwa Halmashauri yangu ya Manispaa ya Temeke kwa kutekeleza

mpango wa Serikali wa kutoa asilimia tamo (5%) ya mapato yake kwa

maendeleo ya wanawake na vijana.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja, nawasilisha.

MHE. MARGARET A. MKANGA: Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kwa

viongozi wa Wizara hii ikiongozwa na Mheshimiwa Sofia Simba, Naibu Waziri,

Katibu Mkuu na Naibu wake, Wakurugenzi na watendaji wote.

Mheshimiwa Spika, kwanza niunge mkono hoja na mchango wangu ni

kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Benki ya Wanawake ni jambo la heri kwa wanawake

wote Tanzania ila changamoto ni uhaba wa mitaji. Ni vyema sasa Wizara na

Kamati husika kuhimiza Kamati ya Bajeti kuishauri Hazina kutimiza maagizo ya

Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete kutoa fedha alizoelekeza ili kuiwezesha Benki

hii kutanua shughuli zake kibiashara.

Mheshimiwa Spika, pili ni kuhusu kupuuzwa kwa taaluma ya Maendeleo

ya Jamii, inasikitisha kuona kwamba kwa wakati wa sasa kazi/majukumu ya

Maafisa Maendeleo ya Jamii hazieleweki katika Halmashauri zetu au Kata na

kadhalika. Imekuwa ni jambo la kawaida kukuta maafisa hawa wanapangiwa

kazi ya kukusanya ushuru kitu ambacho ni kinyume kabisa. Mkusanya ushuru si

rafiki wa wafanyabiashara na Maafisa Maendeleo anapaswa kuwa rafiki wa

wananchi wakiwajibika kuelekeza jamii, kuelimisha jamii kuhusu programu na

miradi mbalimbali, kufanya utafiti wa masuala ya kijamii kwa mfano sababu za

madanguro na kadhalika. Hivyo inaelekea hata viongozi hawa hawafahamu

umuhimu/kazi za Maafisa Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Spika, nashauri elimu itolewe kwa wananchi kuhusu

umuhimu wa taaluma hii kwani Maafisa Maendeleo ni kama wasafisha njia za

maendeleo, yafaa wathaminiwe kwa kupangiwa majukumu yanayowahusu.

Mheshimiwa Spika, tatu, pamoja na kwamba kisera suala la watu wenye

ulemavu lipo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii lakini wenye ulemavu

hao wanapaswa kuendelezwa kama wanajamii wengine katika masuala yote

ya maisha. Hata hivyo sikuona maelezo yoyote kuhusu suala la wenye ulemavu.

Mheshimiwa Spika, baada ya mchango huu nawasilisha na kuunga tena

mkono hoja.

MHE. JOHN P. LWANJI: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja ya Wizara

hii kuhusu mpango wa bajeti yake ya mwaka 2014/2015.

Page 157: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

157

Mheshimiwa Spika, naishauri Serikali ije na mkakati maalum wa

kupunguza idadi kubwa ya watoto ombaomba mitaani. Mfano ni hapa hapa

Mji wa Dodoma karibu kila mtaa watoto wenye umri wa kati ya miaka 5 – 10

wanapita wakiomba omba. Huu ni mji mmoja tu nchini, wawekwe katika

makazi maalimu hususan mayatima. Aidha wazazi wanaotelekeza watoto wao

wachukuliwe hatua za kisheria.

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango gani wa kuboresha Vyuo vya

Maendeleo vilivyo chini ya Taasisi za kidini? Vyuo hivi vinahitaji msaada wa

Serikali kwa kuwa vinapokea idadi kubwa ya watoto waliohitimu shule za msingi

kuwajengea stadi mbalimbali, mfano ni Chuo cha Maendeleo ya Biblia cha

Sanjaranda, Wilayani Manyoni Mkoa wa Singida. Aidha, nawakaribisha Waziri

na Naibu Waziri wake watembelee Chuo hiki muhimu wajionee shughuli zake.

Hapo nyuma kiliwahi kufadhiliwa na DANIDA lakini sasa hivi kimekosa msaada

wa kutosha.

Mheshimiwa Spika, Wizara ije na mpango maalum wa kupanua huduma

za Benki ya Wanawake Tanzania ili kuwafikia wanawake wengi zaidi.

Ikiwezekana mpango mkakati huo uwe kwa Mkoa nchini kuanzia Singida

ambako ni katikati ya nchi na karibu na wanawake wote ni wana CCM na

wana vikundi vingi vya ushirika.

Mheshimiwa Spika, suala la ukatili kwa akina mama ukabiliwe na Serikali

maana limendelea kujitokeza hasa Mkoa wa Mara na Rukwa. Muswada uletwe

Bungeni ili kupendekeza kutungwa kwa sheria kali za kuwadhibiti watu hawa

wakatili wasiopenda kuendana na wakati. Ni aibu kuwa na watu wakatili karne

hii ya 21.

Aidha sheria kali nazo zitungwe kukabiliana na tatizo la albino (walemavu

wa ngozi). Washirikina wote watungiwe sheria kali za kuwatokomeza, wahanga

wengi wa masangoma ni wanawake na watoto. Wizara hii ije na mikakati ya

kuwadhibiti watu hawa wabaya.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.

MHE. KHATIB SAIDI HAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kutoa mchango

wangu katika hoja hii muhimu kwa mustakabali wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, vyombo vya habari hususan magazeti yanaongoza

katika udhalilishaji wa wanawake katika nchi yetu. Kuna magazeti kadhaa

ambayo kwa sasa ni maarufu kwa kuanika picha chafu za udhalilishaji wa akina

Page 158: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

158

mama. Magazeti haya maarufu kama Ijumaa, Kiu, Risasi na kadhalika ambayo

sasa ni maarufu yanaitwa magazeti ya udaku hayastahili kuwepo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inajua mambo haya machafu na Wabunge

mara kadhaa tumekuwa tukilalamika kuwa magazeti haya lakini hakuonekani

juhudi na hatua za dhati za kukabiliana na tatizo hili. Naomba Serikali ichukue

hatua sasa, haijachelewa.

Mheshimiwa Spika, suala la mauaji ya albino, napenda kutambua juhudi

za Serikali juu ya kukabiliana na janga hili kubwa la Taifa. Hata hivyo bado tatizo

la mauaji ya albino linaendelea, kuwatesa Watanzania. Naomba sasa Serikali

iongeze juhudi za kuwalinda watu hawa kwa kuwasajili nchini kote na

kuwatumbua kila maeneo wanayoishi ili iwe rahisi kuwashirikisha hata Serikali za

Vijiji kupitia Polisi Jamii na sungusungu kusaidi kuwalinda albino.

Mheshimiwa Spika, tatizo la watoto wa mitaani limezidi kuongezeka

katika nchi yetu, juhudi halisi za kuondoa tatizo hili bado hazionekani, matokeo

yake ni ongezeko la Taifa lisilo na maadili, tuelewe kwamba kukosa malezi bora

kwa watoto ni matayarisho makubwa kwa Taifa la watu wakorofi. Masalia ya

majambai, vibaka na wavuta bangi na dawa za kulevya hupatikana kutokana

na kada hii ya watoto wa mitaani. Ni wajibu wa jamii na Serikali tushirikiane

kukabiliana na janga hili kubwa ambalo ukuaji wake hasa katika miji mikubwa

katika nchi yetu lipungue hasa katika miji ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha,

Mbeya, Tanga na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, ahsante.

MHE. PEREIRA A. SILIMA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nikushukuru

kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye hoja hii. Nampongeza Mheshimiwa

Waziri na Naibu wake kwa hotuba nzuri iliyoweka hadharani maendeleo lakini

pia changamoto ya sekta ya jamii.

Mheshimiwa Spika, naomba nichangie kwenye maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu tatizo la watoto wa mitaani ni tatizo linalotia

aibu na kulidhalilisha Taifa. Naelewa kwamba jibu la suala hili ni kuwa na familia

imara na zenye maadili lakini pia naelewa nafasi ya Serikali ya kurekebisha haki

hii. Naelewa kwamba Serikali inayo mikakati ya kutatua tatizo hili lakini naomba

nikiri kwamba mingi ya mikakati hii haijazaa matunda na naomba Serikali

iendelee kujipanga ili tatizo hili lisiendelee kukua.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ukatili wa kijinsia (GBV) wanawake wengi

wamepata tatizo la kufanyiwa ukatili wakiwa kwenye ndoa zao na au kwenye

Page 159: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

159

mahusiano mengine. Jambo hili ni kubwa na madhara yake ni makubwa

katika jamii yetu.

Mheshimiwa Spika, elimu inahitajika kukithirishwa ili jamii ielewe haki za kila

kundi na kuzisimamia ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ukeketaji mwaka 2012 mwezi wa Novemba

nilialikwa na aliyekuwa Naibu Waziri (Mheshimiwa Ummy Mwalimu) kuungana

naye huko Tarime kwa lengo la kuendeleza elimu ya kuacha ukeketaji wa

watoto.

Mheshimiwa Spika, siku mbili nilizotumia kwenye Wilaya ya Tarime

nilijionea uonevu mkubwa wa wasichana. Kubwa zaidi niliona wazee wa

maeneo haya wakifanya sherehe bila woga wowote na naelewa kwamba

kampeni hii ni ngumu lakini ni ya lazima.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.

MHE. SAID M. MTANDA: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba

kuwapongeza kwa kazi.

Mheshimiwa Spika, nataka kufahamu ni lini watumishi wa Chuo cha

Wananchi Chilala watalipwa fedha zao za malimbikizo. Je, wanaodai, wanadai

shilingi ngapi na lini fedha hizo zitalipwa, orodha ya wanaodai ni Ndugu

Regimius Komba shilingi 23,663,324/= na Ndugu M. G. Vara shilingi 9,319,575/=

na jumla shilingi 32,981,720/=.

Mheshimiwa Spika, tatizo la uchakavu wa Chuo cha Chilala, Chuo kipo

katika hali mbaya sana, majengo yake yana nyufa, je, kuna mpango gani wa

kufanya ukarabati mkubwa kwa Chuo hiki.

Mheshimiwa Spika, suala la kutokuwa na gari Chuo kinaendesha kozi ya

ufundi umeme wa magari bila kuwa na gari, je, Serikali ipo tayari kukipa Chuo

gari dogo aina ya Noah ili wanafunzi wajifunze kwa vitendo? Nawasilisha.

MHE. JOHN J. MYIKA: Mheshimiwa Spika, maendeleo ya jamii yanapaswa

kuongozwa na dira bora yenye kutambua dhamira yake katika kuleta ustawi

wa wananchi na ukuaji wa uchumi wa nchi. Aidha, maendeleo hayo

yanapaswa kuzingatia usawa wa kijinsia na uendelevu wa kizazi cha sasa na

cha baadaye kupitia makazi bora ya watoto. Suala la watoto na maisha yao ni

muhimu kwa Taifa letu kwa kuzingatia kwamba nchi yetu ina watoto wengi

kuliko vijana na wazee katika piramidi la idadi ya watu.

Hata hivyo Sehemu “B” ya hotuba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto inayohusu mapitio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM

Page 160: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

160

ya mwaka 2010 kwa kipindi cha Januari, 2011 hadi Machi 2014 yanadhihirisha

udhaifu mkubwa wa kushindwa kutekeleza ahadi kwa ukamilifu na kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, aya ya 10 na 11 juu ya ajira na uwezeshaji wa

wananchi inaonyesha kasi ndogo ya kuimarisha na kupanua mafunzo ya vyuo

vya maendeleo ya wananchi ili viweze kupokea vijana wengi zaidi na

kuwapatia mafunzo ya stadi za maarifa ya kisasa katika fani za kilimo, biashara,

ufundi na ujasiriamali. Hivyo katika mwaka 2014/2015 Wizara iongezwe bajeti ili

iweze kukamilisha upanuzi wa miundombinu kwenye vyuo vyake.

Aidha wakati hatua hizo zikisubiriwa naomba kwa upande wa Jiji la Dar es

Salaam kwa kuwa Wizara haina Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wala vya

Maendeleo ya Wananchi, Wizara ianzishe kituo cha mafunzo au walau

ishirikiane na vyuo vingine vya umma au kutumia majengo ya umma mathalani

ya shule au ya Shirika la Maendeleo Dar es Salaam (DDC) kuanzisha mpango

maalum ya mafunzo ya vijana wengi kwa muda mfupi, kuwaongezea stadi

zenye kupunguza ukosefu wa ajira. Nipo tayari kutoa ushirikiano kwa Wizara

kufanikisha azma hiyo kwa upande wa Jimbo la Ubungo.

Mheshimiwa Spika, katika aya ya 12 na 13 juu ya kuyaendeleza makundi

mbalimbali kwa upande wa watoto, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto itoe maelezo ya kwa nini imechelewesha kukamilisha sera ya malezi,

makuzi na maendeleo ya mtoto. Aidha, Serikali ieleze lini sera hiyo itapitishwa?

Mara baada ya sera hiyo kupitishwa Serikali irejee pia Sheria ya Mtoto na

kuandaa mpango maalum wa malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto kwanza

na kuiwakilisha Bungeni. Aidha katika kufanya hivyo Serikali ieleze iwapo

itazingatie ajenda ya watoto (Chidren’s Agenda) ambayo viongozi mbalimbali

tuliisaini mwaka 2010.

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Jamii yatachochewa kukiwa na

demokrasia na madaraka ya umma kazi hii inaweza kufanywa kwa kuambiwa

na Serikali zenye kuongozwa kidemokrasia na kutoa madaraka kwa umma

kuanzia kwenye ngazi za Serikali za Vitongoji, Vijiji na Mitaa, kwenye Kamati za

Maendeleo ya Kata na haki katika Halmashauri za Wilaya. Hata hivyo

kumekuwa na udhaifu katika utekelezaji wa dhana na dhima hii katika maeneo

mengi nchini na hivyo kukwamisha dira ya kuwa na jamii yenye maendeleo.

Aidha wadau wengine muhimu wa kuwezesha demokrasia na madaraka ya

wananchi na kuchangia katika maendeleo ya jamii yenye usawa wa kijinsia na

ustawi wa watoto ni Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo Serikali inajitazama zaidi kama kiranja dhidi

ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali badala ya kuyawezesha kisheria na kitaasisi

kujisimamia na kushiriki katika maendeleo ya jamii. Sheria ya NGOs Na. 24 ya

Page 161: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

161

mwaka 2002 na hata Marekebisho yake ya mwaka 2005 hayajaweza

kutengeneza muundo bora na kuweka mfumo bora wa kufanikisha azima hiyo.

Mheshimiwa Spika, Baraza la Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NACONGO)

kwa muundo na mfumo wake wa sasa nalo halitaweza dhima na dira kutimizwa

ikiwa mabadiliko ya msingi hayatafanyika. Aidha utegemezi wa Mashirika

yasiyo ya Kiserikali usitazame tu kwamba ni tatizo la Mashirika yasiyo ya Kiserikali

bali mfumo mzima wa kushughulikia sekta hiyo. Ni hatari kwa wananchi na nchi

kwa Serikali kuachia utegemezi wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali kwa fedha za

nje kuendelea. Ni muhimu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

ikaongeza jitihada za kufanya yafuatayo kupunguza utegemezi wa fedha za

nje wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali nchini:-

Mosi, Maafisa wa Maendeleo ya Jamii wasihusike tu kwenye kusajili

Mashirika na kupokea taarifa za utendaji bali waelimishwe vilevile wananchi

umuhimu wa Mashirika hayo na mchango wake katika maendeleo ili

wanachama na wananchi wenye uwezo waweze kuchangia kuwezesha

mashirika kujitegemea.

Pili, Serikali badala ya kuingia gharama kubwa za fedha za umma

kwenye kandarasi kwa makampuni ya nje au ndani yenye kutaka faida kubwa

itoe kazi kwa NGOs zenye kutekeleza miradi kwa gharama nafuu kwa kuwa

hazitegemei faida.

Mheshimiwa Spika, tatu, kuanzishwe mfuko wa kutoa ruzuku kwa NGOs –

utegemezi wa mifuko ya NGOs kama Foundation For Civil Society (FCS) pamoja

na kazi nzuri havitoshi.

Mheshimiwa Spika, maendeleo ya jamii yanaweza vilevile kuchochewa

kwa kutoa msukumo katika kazi za kujiendeleza makundi mbalimbali katika

Jumuiya ya Taifa kwa ujumla. Kundi la kwanza linalopaswa kupewa mkazo

katika kutekeleza azma hiyo linapaswa kwa kundi la wanawake. Hata hivyo

katika aya ya 14, 15 na ile inaonyesha kwamba bado kuna udhaifu katika

kuweka mstari wa mbele mipango ya kuwezesha wanawake.

Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake unatengewa fedha kidogo, bilioni

mbili tu kwa nchi nzima na hata hizo kidogo hazitolewi kwa ukamilifu kwa

kuzingatia kuwa katika mwaka wa fedha 2013/2014 taarifa zinaeleza kwamba

zinatolewa shilingi milioni 500 tu. Hivyo Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto itoe maelezo ni sababu zipi zingefanya fedha hizo kutokutolewa kwa

ukamilifu?

Aidha, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto ieleze ni jitihada

gani kupitia Maafisa wa Maendeleo ya Jamii katika kila Kata na kupitia Waziri

Page 162: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

162

kwenye Baraza la Wananchi imefanya kuhakikisha kila Halmashauri nchini

imetenga 10% ya mapato ya ndani kwa mikopo ya wanawake na 10% ya

mikopo ya vijana kwenye mapato ya ndani kwa ajili ya vijana.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wangu toka mwaka 2011 nimefuatilia

kwenye Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Kinondoni na kiwango cha

fedha kuongezwa kutoka milioni 20 za zamani mpaka milioni 200 za mwaka

2013/2014 na sasa takribani milioni 300 kwa makadirio ya mwaka wa fedha

2014/2015. Hata hivyo kiwango hicho bado hakijafikia asilimia kumi (10%).

Hivyo Wizara ishirikiane nasi kuifuatilia Manispaa ya Kinondoni

Mheshimiwa Spika, ninaunga mkono pia Kinondoni Youth SACCOS iweze

kuwa chombo cha kuwaratibu vijana juu ya fedha za upande wa Serikali Kuu

kwa kuwa kwa sasa fedha za Halmashauri zinapitia Commercial Bank (DCB)

zamani Dar es Salaam Community Bank).

Nashukuru na kupongeza kwamba pendekezo mlilotoa mlipotembelea

Benki ya Wanawake (TWB) ya kuanzisha kituo katika Jimbo la Ubungo.

Tumekuwa tukiunganisha wanawake na vijana kuwapa mafunzo ya ujasiriamali

na kutumia fursa za Benki ya DCB na Benki nyingine, niko tayari kushirikiana na

Wizara na TWB kuhamasisha wanawake na vijana kutumia fursa za Benki hiyo

katika vituo vipya tayari ofisi ya Mbunge Ubungo ilishafika TWB makao makuu

kufuatilia suala hili, ningeomba majibu katika majumuisho ni lini TWB ipo tayari?

MHE. MWANAKHAMIS KASSIM SAID: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hivi

sasa katika Vyuo vya Maendeleo ya Jamii wahitimu wanaongezeka mwaka

hadi mwaka, hivyo mwelekeo mkubwa kuweka na shughuli za ujasiriamali ili

vijana wakimaliza wawe na uwezo wa kujiendeleza kimaisha kwa kila siku. Sio

rahisi kutokana na Serikali kuwa na mzigo mkubwa kuweza kuwapatia ajira

wahitimu wote wa Vyuo hivi vya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

Mheshimiwa Spika, mwenendo wa vijana hivi sasa lazima pawe na

msisitizo wa maadili mazuri hivyo katika vyuo inawajibika kupata nyakati kila

mara kusisitiza maadili mazuri ili jamii kujengeka.

Mheshimiwa Spika, Benki zinawajibu kusambazwa kila sehemu za Mikoa,

Wilaya, Majimbo ili wananchi waweze kufaidika kutumia katika Benki hizo. Kwa

kweli funzo la jamii kuweza kutunza fedha itasaidia ndani ya jamii, funzo kubwa

katika Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake itasaidia sana.

Mheshimiwa Spika, bajeti ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto inawajibika kuongezewa fedha kutokana na huduma zilivyokuwa nyingi

na yale yanayokusudiwa kutendeka yanazorota na kutokufikia kiwango

kinacholengwa. Lakini hata hivyo tatizo kubwa ambalo linajitokeza ni

ucheleweshaji wa fedha ambazo hazifiki fedha kwa wakati uliopangwa.

Page 163: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

163

MHE. AL–SHAYMAA J. KWEGYIR: Mheshimiwa Spika, kutokana na mauaji

ya walemavu wa ngozi, hofu imetanda kwenye familia zenye watu wenye

ulemavu wa ngozi hasa watoto. Wazazi wengi wamewapeleka watoto hao

kwenye kambi au shule za boarding na kuwatelekeza bila kwenda kuwaona.

Kuna shule ipo Shinyanga inaitwa Buhangija, kuna watoto wapo pale bila

kwenda likizo maana wazazi wamewatelekeza.

Mheshimiwa Spika, Wizara ifuatilie kwa kina tatizo hili pale Shinyanga.

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja kwa

mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi nchini

vyuo hivi ni muhimu sana kwani vinawasaidia sana wananchi hasa wenye

uwezo mdogo, hata hivyo vinakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja

na ukosefu mkubwa wa walimu, usafiri na fedha za kuendeshea hali hii inaenda

kinyume na azma ya Serikali ya kuviboresha na kuviwezesha kutoa mafunzo ya

VETA.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Maendeleo cha Wananchi cha Chala kina

walimu wawili tu, workshop jengo limeanguka, usafiri unaotumika ni pikipiki tu,

hakuna hadhi kabisa za uendeshaji, tunaomba tusaidiwe kwani kipo kwenye

mpango wa maboresho.

Mheshimiwa Spika, nataka maelezo ni lini sasa chuo hiki kitapelekewa

walimu wa kutosha na usafiri na changamoto zilizotajwa hapo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mikopo kwa vijana na wanawake Halmashauri

zetu zinakwepa kwa kiasi kikubwa kuwajibika kutoa fedha ambazo kisheria

wanatakiwa kupeleka kwa vijana na wanawake na pale wasipopeleka hakuna

hatua zozote zinazotolewa na kwa msingi huo kuzorotesha kabisa maendeleo

ya kiuchumi na kijamii kwa makundi haya mawili ambayo ni muhimu sana.

Mheshimiwa Spika, pendekezo langu ni kwa Halmashauri zilazimishwe

kutoa fedha kwa lazima na iwe ni kigezo cha kuwapatia fedha za

miradi/matumizi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mauaji ya albino/wanawake wazee, jambo hili

linaweza kukomeshwa kabisa likabaki historia nchini, nachelea kusema dhamira

Page 164: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

164

kamilifu bado. Naomba hatua thabiti zichukuliwe kukomesha kabisa. Albino ni

watu, wanawake wazee ni watu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu watoto wa mitaani nashauri kuwa tatizo hili

kama litapewa umuhimu muda mfupi linaweza kuisha. Nashauri Serikali

kukabiliana kwa dhati kwa kutenga fedha na kuanzisha maeneo machache ya

kulelea watoto hawa yenye mtazamo wa uzalishaji kama vile kuanzisha Skimu

za Kilimo cha Umwagiliaji.

Mheshimiwa Spika, kuhusu dawa za kulevya kadhalika ni tatizo ambalo

tukiwa serious linaweza kupungua kuliko lilivyo sasa.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nianze na kuwapongeza Waziri,

Mheshimiwa Sophia Simba, Naibu Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana na watendaji

wote wa Wizara hii kwa kufanya kazi nzuri kwenye mazingira magumu. Wizara hii

ni muhimu sana sababu inashughulika na maendeleo ya wanawake, wanaume

na watoto lakini siku zote imekuwa ikitengewa bajeti ndogo sana na fedha za

maendeleo hawapatiwi kwa wakati au hawapati zote.

Mheshimiwa Spika, nalaani mauaji ya wanawake, niungane na wote

waliolaani mauaji ya wanawake waliouwawa kule Mara pia yale ya vikongwe.

Haya mauaji yamekuwa yakitokea kila mara, je, Serikali imeweka mikakati gani

ya kudumu ya kuzuia mauaji au kukomesha kabisa?

Mheshimiwa Spika, pia nalaani vikali matendo ya ubakaji na ulawiti kwa

watoto, vitendo hivi vimekuwa vikiongezeka kila siku hadi katika Mkoa wetu wa

Iringa na Tanzania nzima na vitendo hivi vimekuwa vikiwaathiri watoto

kisaikolojia, ni sawa na kesi ya mauaji watoto, wanaambukizwa hata UKIMWI,

lakini hukumu za kesi zake zinachukua muda mrefu wakati wengine wanashikwa

na vidhibiti kabisa. Wizara hii ina mkakati gani kuingilia suala hili?

Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kwa Benki ya Wanawake, niipongeze

Wizara kupitia Benki ya Wanawake na Mkurugenzi Magreth Chacha kwa

kufungua kituo cha kutoa mikopo katika Mkoa wetu wa Iringa. Tunaiomba

Serikali iweke mkakati wa kufungua matawi ili benki iweze kuwafikia hata akina

mama waliopo vijijini.

Mheshimiwa Spika, kuhusu sheria ya kutenga 5% katika Halmashauri

inasikitisha sana kuona bado kuna baadhi ya Halmashauri hazijaanza kutenga

fedha hizo kwa ajili ya kina mama na vijana. Je, Halmashauri ambazo hazitengi

fedha hizo zinachukuliwa hatua gani na tuambiwe ni chombo gani

kinachoratibu fedha hizo kuhakikisha zinawafikia walengwa?

Page 165: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

165

Mheshimiwa Spika, suala la Maafisa Maendeleo, kumekuwa na tatizo

kubwa sana la Maafisa Maendeleo katika kata zetu, ni utaratibu gani

unatumika katika kuwapeleka maafisa hao? Kwa nini Halmashauri zisipatiwe

vibali vya kuwaajiri hawa Maafisa?

Mheshimiwa Spika, kuhusu Vyuo vya Maendeleo na Ustawi wa Jamii na

bajeti finyu Mkoa wetu wa Iringa una Chuo cha Maendeleo cha Rungemba na

Chuo cha Ustawi wa Jamii cha Ruaha, vyuo hivi vipo katika hali ngumu sana

katika miundombinu na tunaomba vyuo hivi vipatiwe kipaumbele kwa sababu

vinasaidia sana katika kuelimisha jamii.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. MKIWA A. KIMWANGA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda

kuwapongeza Waziri, Mheshimiwa Sophia Simba pamoja na Naibu wake

Mheshimiwa Dkt. Pindi Chana kwa kuongoza Wizara hii ambayo hata bajeti

yake ni ndogo na haitoki yote pia. Hii ni hatari kwa Wizara hii, kwani inashindwa

kutekeleza majukumu yake. Hivyo nawapa pole na ninawatia moyo mkaze

buti kwani jamii inawategemea.

Mheshimiwa Spika, napenda Mheshimiwa Waziri aniambie kwa nini katika

Halmashauri zetu wanapotenga asilimia tano (5%) Wabunge wa Viti Maalum

hawashirikishwi kuamini utengaji huu kama kweli unafanyika na hata kuhakiki

kama kweli wanaopewa ni kweli wahusika. Mheshimiwa Waziri unasema nini

kuhusu Wabunge hawa wanawake kutokushirikishwa kabisa?

Mheshimiwa Spika, pia ningependa kutoa ushauri kuwa na Muswada wa

kuzuia vijana kuvaa suruali chini ya makalio na wasichana kuvaa matiti nje.

Mheshimiwa Waziri naomba Muswada huu uandaliwe ili kurejesha heshima na

utamaduni wetu wa Mtanzania, kwa mfano, jirani zetu Kenya wamefanikiwa

kwa suruali ambayo inajiita “KK”, Uganda pia imefanikiwa kupitisha sheria ya

kuzuia vimini na mpango huu utafanikiwa kwani wamelivalia njuga. Tukiwa na

nia hata sisi tutashinda.

Mheshimiwa Spika, napenda kumuuliza Waziri ana mpango gani

endelevu kuhusu watoto wa mitaani kwani watoto hawa wamekuwa kero

katika miji mikubwa kama Mwanza, Dar es Salaam, Arusha, Mbeya na miji

mingine mingi. Hii ni aibu kwa wageni wajao nchini pia ni kero.

Mheshimiwa Spika, mauaji ya wanawake katika Mkoa wa Mara

yamekuwa ni tishio sana kila kukicha wanawake wanauliwa, Mheshimiwa Waziri

wauaji ni wanaume ni vyema sasa tukaandaa maandamano makubwa na

Page 166: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

166

kugomea kazi za mashambani na uchotaji wa maji visimani ili kazi hizi zifanywe

na wanaume sasa ili kunusuru maisha yetu.

Mheshimiwa Spika, ni lazima sasa Serikali iangalie kuipatia fedha Wizara hii

ili iache kuwa ombaomba inapotaka kufanya shughuli zake katika Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, Naibu Waziri mshike mkono Waziri wako ili muikwamue

Wizara hii, kwani inaonekana kama ipo kwa bahati mbaya. Ni imani yangu

mkishikamana mtafanikiwa nasi tutafanikiwa kabisa, msife moyo. Ahsante.

MHE. ELIZABETH N. BATENGA: Mheshimiwa Spika Wizara ya Maendeleo ya

Jamii ni muhimu kwa kuwa ni mtambuka katika nyanja nyingi, watumishi wa

maendeleo ya jamii pamoja na kuwa ni wachache pia hawatumiwi kikamilifu

na ipasavyo kutokana na rasilimali fedha kidogo inayotolewa, aidha

Halmashauri za Wilaya kutojua umuhimu wao. Hawana nyezo za kufanyia kazi.

Mtumishi wa maendeleo ni mtafiti kuhusu matatizo mbalimbali, ni

muelimishaji na hatimaye kutathimini, hivyo ni msaada mkubwa kwa jamii

mahali alipo. Matatizo mengi yanayokabili jamii zetu na hata familia

hayafanyiwi utafiti na jamii kuelimishwa jinsi ya kuyatatua. Ni lazima kama

tunataka Wizara hii (watumishi) ifanye kazi kwa mafanikio rasilimali fedha

iongezwe lakini pia watumishi waongezwe ili angalau kila kijiji/mtaa awepo

mtumishi.

Mheshimiwa Spika, Serikali/Wizara lazima iweke mkazo kwa jamii

kuzingatia maadili hivyo wazazi wawe makini katika malezi ili kupunguza

kumomonyoka kwa maadili.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, kwanza naipongeza

sana Wizara kwa kazi nzuri inayofanya hadi kupelekea ongezeko la bajeti kwa

mwaka wa fedha 2014/2015. Pamoja na kwamba bado fedha ni ndogo lakini

ongezeko la fedha za ndani kwa matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo

zinatia moyo. Tuombe heri ili kwa siku zijazo maboresho haya yaendelee.

Mheshimiwa Spika, naipongeza Wizara kwa jitihada za kutoa mafunzo

katika Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi na pia kutoa mikopo mingi kupitia

Benki ya Wanawake.

Mheshimiwa Spika, nina ushauri ufuatao, kwanza Wizara iendelee

kuhamasisha wanawake wengi zaidi kujiunga na Vyuo vya Maendeleo ya

Page 167: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

167

Wananchi kwani idadi yao hairidhishi. Naomba pia mada zinazohusu uwajibikaji

na maadili zifundishwe ikiwa ni pamoja na kuepukana na ulevi wa aina

mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa inaweza kuchukua muda mrefu kwa Benki

ya Wanawake kufika kila Mkoa naishauri Wizara ijaribu kufanya utaratibu wa

kupitishia huduma zake kwenye taasisi nyingine, kwa mfano katika Wilaya ya

Tandahimba kule Mtwara ipo Benki ya Wananchi, napendakeza Wizara ipeleke

huduma Mtwara kupitia Benki ya Wananchi Tandahimba.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja asilimia mia moja.

MHE. ENG. ATHUMAN R. MFUTAKAMBA: Mheshimiwa Spika, naunga

mkono hoja asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, Jimbo la Igalula tunaomba Chuo cha Maendeleo ya

Jamii katika Jimbo letu ili vijana wa jinsia zote wapate mafunzo ya mbinu na

uwezo wa kujikimu na kujitegemea. Jimbo la Igalula ni la mwisho kimaendeleo

nchini Tanzania (taarifa ya maendeleo ya matumizi ya chandarua kimoja kila

Mtanzania Prof. Jeffery Sykes- mchumi, uchumi wa Afya, Harvard university

Marekani) imetajwa Wilaya ya Uyui lakini ni Jimbo la Igalula kwani Tabora

Kaskazini kuna mradi wa UNDP wa Mbola Milleniuam Village una workshop,

shule ya msingi, sekondari, visima, zahanati na wanatoa pembejeo za kilimo na

wana trekta.

Mheshimiwa Spika, Tawi la Benki ya Wanawake Tanzania mwakani

wajenge kituo angalau Tabora ili Igalula nayo ifaidike kwa mikopo ya akina

mama na waweze kupata mitaji ya vikundi na mmoja mmoja katika biashara,

kilimo na hata ufugaji samaki kwa mabwawa. Elimu ni muhimu wapate mafunzo

ya ujasiriamali ili mitaji waweze kuikuza kwa ufanisi zaidi na iwe endelevu.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kupata nafasi ya

kuchangia.

Mheshimiwa Spika, kuhusu watu wenye ulemavu ni jukumu la Serikali la

kuwalinda, kuwahudumia, kuwaendeleza na kuhakikisha wanapata elimu.

Bado katika mashule yetu, maofisi na sehemu nyingi bado miundombinu siyo

rafiki wa watu wenye ulemavu hata vyoo siyo rafiki. Ningependa kupata majibu

kulikuwepo na agizo la kupiga kura ya kutambua wahalifu wanaouwa watu

wenye ulemavu wa ngozi (albino) umefikia wapi?

Mheshimiwa Spika, kipindi cha Bunge Maalum katika televisheni ya Taifa -

TBC kilikuwa na mkalimani aliyeweza kuwasaidia walemavu wasiosikia kuweza

Page 168: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

168

kufuatilia Vipindi vya Bunge lakini sasa hivi huduma hiyo haipo. Je, kumetokea

nini?

Mheshimiwa Spika, kuhusu Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 sheria hii ni

kandamizi, zaidi inawakandamiza watoto/wanawake, watoto wanaruhusiwa

kuolewa wakiwa watoto. Ni zaidi ya miaka mitano tumekuwa tukipigia kelele

sheria hii irekebishwe mpaka leo hii bado. Je, ni sababu zipi zinazochelewesha

marekebisho ya Sheria ya Ndoa ambayo inahalalisha ndoa za utotoni italetwa

hapa Bungeni? Tunaomba time frame ni lini?

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mashirika yasiyo ya Kiserikali kuna mashirika

mengi yaliyosajiliwa mengi yakiwa ni ya kulea watoto wanaoishi katika

mazingira magumu ikiwa ni pamoja na watoto yatima, inabidi Serikali iyakague

mashirika haya sababu mengi ni matapeli, wanapata fedha kutoka nje lakini

baadhi yao hawatoi huduma zinazostahili mfano, ni kituo cha mkombozi

kilichopo Moshi. Badala ya kuwasaidia watoto hawa pamekuwa ndiyo kituo

cha watoto wenye uovu mkubwa na tishio kwa jamii. Ningependa kujua kuwa

shirika liitwalo Sisi kwa Sisi lililokuwa lina-promote ushoga, je, Serikali halifahamu

hili? Na kama wanafahamu ilikuwaje wapate usajili wakati nchi yetu tunapiga

vita ushoga? Naomba jibu

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuporomoka kwa maadili nchini imekuwa ni

kawaida kwa vijana wetu kuvaa nguo zenye kuonyesha maumbile yao hata

watu wazima wanafanya hivyo. Na hii mitandao ndiyo inayochangia zaidi kwa

kusambaza picha chafu. Ni muda muafaka sasa kwa Serikali kupitia Wizara ya

Mawasiliano waweze kufuatilia wote wenye kusambaza picha hizo

wakamatwe, watajwe hadharani na wapewe adhabu ya juu na kifungo hii kwa

kiasi kikubwa kitapunguza uhalifu huu.

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, napenda kuunga mkono

hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani.

Mheshimiwa Spika, napenda kumsisitiza Waziri atembelee Chuo cha

Maendeleo Wilaya ya Kilombero kilichopo Ifakara ili akajionee mwenyewe

matatizo yaliyopo na kuyapatia ufumbuzi. Ni miaka takribani mitatu mfululizo

nachangia mapungufu ya Chuo hicho ambacho ni mkombozi kwa wanawake

lakini Wizara haijafuatilia hadi leo.

Mheshimiwa Spika, suala la unyanyasaji wa watoto wa kike na kiume,

watoto wa kiume kufanyiwa vitendo vya ukatili na kulawitiwa ama mashuleni,

na ndugu ama kwa kudanganywa na watu wazima mitaani. Wizara ina

mikakati gani ya kukomesha vitendo hivyo? Imefikia wakati sasa kuwe na

makongamano katika ngazi mbalimbali vijijini na mashuleni kueleza vitendo

hivyo. Pia kuwepo na dawati la jinsia mashuleni na ofisi ya kijiji ili kuwapa nafasi

Page 169: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

169

watoto wanaofanyiwa vitendo vya ukatili kupeleka taarifa na kuchukua hatua

zinazostahili.

Mheshimiwa Spika, kasi ya watoto kulawitiwa ni kubwa na likiachwa ilivyo

hapo baadaye Taifa litakuwa na mashoga wengi na wataanza kudai haki zao

kwani hawataweza kujibadili tena kuwa na maisha ya kawaida, tulinusuru Taifa

chonde chonde.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii kwa umuhimu wake inahitaji mjadala wa

Kitaifa, Wizara hii ni nyeti kwa wananchi, lakini wananchi wengi wanadhani ni

kwa wanawake na watoto tu na ndiyo maana Maafisa wa Ustawi ngazi ya

Wilaya na Kata na kwingineko hawapo, hata wakiwepo hawatengewi bajeti

wala hawana vitendea kazi. Nashauri kuwe na kongamano la kupata uelewa.

Mheshimiwa Spika, ipo haja ya kuwepo na sheria inayosimamiwa vyema

na watoto waelimishwe kuzielewa ili wadai haki zao.

Mheshimiwa Spika, uwezeshaji wa wanawake kwa kupeleka vituo vya

ukopeshaji, ningependa kujua ni lini Wizara itaelekeza Benki ya Wanawake

ikafungue tawi Morogoro, pia vituo vya mikopo katika Wilaya ya Kilombero,

karibu sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu mauaji ya wanawake wenye ulemavu

unaoendelea nchini, ni vyema Serikali ikachukua hatua madhubuti ya

kuelimisha kukomesha mauaji.

Mheshimiwa Spika, Serikali ichukue hatua madhubuti ya kukomesha

mauaji ya wanawake Wilaya ya Musoma Vijijini yaliyotokea mfululizo kwa

wanawake waliokuwa wako shambani kutafuta chakula kwa ajili ya

watoto/familia, inasikitisha sana. Wizara ishirikiane na Wizara ya Mambo ya

Ndani iweke ulinzi kama Kanda Maalum kwa Polisi kukomesha mauaji hayo.

Mheshimiwa Spika, Wizara hii ipewe bajeti ya kutosha ili ikatekeleze

majukumu yake ipasavyo.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, wale wachangiaji niliokuwa nao

wamekwisha. Kwa hiyo, nawapa nafasi Wizara kuandaa majibu yao. Saa 10.00

tukija wataanza kujibu. Kwa hiyo, nawashawishi muweze kuwahi kusikia yale

mliyokuwa mnasema, mjibiwe. Mara nyingi unakuta wanakuwa watu watatu au

wanne tu. Sasa Mawaziri wanaieleza tu Hansard. Kwa hiyo, tukirudi saa 10.00

wanajibu hoja zinazostahili.

Nasitisha shughuli za Bunge mpaka saa 10.00 jioni.

(Saa 6.38 mchana Bunge liliahirishwa hadi Saa 10.00 jioni)

Page 170: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

170

(Saa 10.00 jioni Bunge lilirudia)

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, asubuhi wale walioomba kuchangia

walikwisha kwenye orodha yao yote. Kwa hiyo, Mheshimiwa Naibu Waziri

atatumia dakika 35; yaani hawa wana saa yao, Waziri ana saa moja,

mchangiaji dakika 15 lakini wanaweza kugawana muda wao kadiri

wanavyotaka kufanya. Mheshimiwa Naibu Waziri.

NAIBU WAZIRI WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA NA WATOTO:

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kukushuksuru wewe kwa kunipa fursa hii.

Awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia afya

njema hivyo kuwemo katika Bunge hili Tukufu na kuchangia hoja iliwasilishwa

hapa Bungeni leo tarehe 17 mwezi wa Tano.

Pili, nitumie fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri wa

Maendeleo ya Jamii, Jinsia Watoto. Pia nimshukuru sana Mheshimiwa Makamu

wa Rais na Mheshimiwa Waziri Mkuu ambao ni hakika wamechangia katika

uteuzi wangu.

Mheshimiwa Spika, kwa namna ya pekee naomba nitumie fursa hii

kumshukuru Mheshimiwa Sophia Simba, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto kwa jinsi alivyonipokea kwa upendo na kunipa ushirikiano wa hali ya juu

tangu nimeteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, pia napenda kuishukuru na kuipongeza Kamati ya

Kudumu ya Maendeleo ya Jamii kwa michango, ushauri, maoni, wanayotupa;

tunaahidi kuwa tutazingatia maoni, maelekezo na ushauri wao katika

kutekeleza majukumu ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, sasa naomba nitamke rasmi

kwamba naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Spika, napenda sasa nichangie hoja ya Mheshimiwa Waziri

wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, aliyoiwasilisha leo hapa Bunge kwa

kujibu baadhi ya hoja za Waheshimiwa Wabunge. Majibu yangu yatalenga

hoja zilizoelekezwa kwenye maeneo yafuatayo:-

Vyuo vya Maendeleo ya Jamii (CDTIs) na Vyuo vya Maendeleo ya

Wananchi (FDCs) na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na masuala kuhusu

Maafisa Maendeleo ya Jamii.

Page 171: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

171

Mheshimiwa Spika, Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi kwa kweli

vilianzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Elimu Na. 25 ya mwaka 1978 kwa kurithi

majengo mbalimbali yakiwepo Vijijini na maeneo mengine.

Vyuo vilivyojengwa kwa fedha za Maendeleo ya Jamii ni Vyuo vinne tu

nchini, ambavyo viko Sengerema, Bigwa, Handeni na Ngara. Ilipofika mwaka

1987 Tume ya Nsekela iliundwa na Tume ilielekeza kwamba Vyuo hivi viende

Wizara ya Maendeleo ya Jamii.

Kwa hiyo, Vyuo hivi vimerithiwa na viko takriban 55, na ndiyo maana

Wabunge wengi wanavyosema kwamba Vyuo hivi vinahitaji maboresho, hiyo ni

kweli kwa sababu tumerithi yale majiengo toka mwaka 1975. Vyuo

vilivyojengwa per-se ni vinne tu. Kwa hiyo, tunaposema Vyuo vya Maendeleo

ya Jamii vinahitaji ukarabati, tunahitaji maboresho, hilo ni jambo ambalo Wizara

inalizingatia.

Mheshimiwa Spika, tumetembelea maeneo mengi ya Vyuo na pia

tunaungana na mialiko mbalimbali ya michango ya Wabunge kwa maandishi

kwamba tutembelee maeneo ya Vyuo vyao. Baadhi ya Wabunge waliosema

tutembelee ni pamoja na Mheshimiwa Lwanji, Mheshimiwa Lekule Laizer na

Mheshimiwa Said Mtanda na wengine.

Mheshimiwa Spika, Vyuo hivi ndivyo vinavyozalisha Maafisa Maendeleo

ya Jamii nchini, hivyo ni kimbilio la wananchi na tegemeo kubwa na vinatoa

stadi za maisha na maisha bora kwa kila Mtanzania na Matokeo Makubwa

Sasa. Hivyo siyo kweli kwamba Serikali ya CCM inawahadaa wananchi bali kwa

kupitia vyuo hivi imekuwa ni kimbilio kubwa.

Ushahidi umeonesha hadi sasa watoto 146,383 wame-graduate tangu

mwaka 2010/2011, 2011/2012, 2013 hadi 2014, yaani kwa muda wa kipindi cha

miaka mitatu. Naomba Waheshimiwa Wabunge mwangalie jedwali namba

moja, hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Mheshimiwa Spika, katika maisha lazima

tuwe na malengo, (vision); Millennium Development Goals.

Serikali ya CCM huweka mipango mizuri ya kibajeti na kifedha, lakini tatizo

ni kwa wanaokwepa kodi. Serikali ya CCM ndiyo pekee inayomjua Mtanzania

alikotoka, alipo, na anapokwenda, na haina nia ya kuwahadaa wananchi bali

kuwapa maisha bora kwani hata ada za Vyuo hivi huwa ni ndogo sana

ukilinganisha na wananchi ambao wanalipa ada kwenye Vyuo vya binafsi. Kwa

hiyo, nichukue nafasi hii kuipongeza sana Serikali ya CCM kwa nia njema kwa

wananchi wa Tanzania.

Naomba nimnukuu Mzee Nelson Mandela alipotembelea mara ya

mwisho nchini Tanzania, alisema maneno ya Kiingereza kutokana na Vyuo hivi

Page 172: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

172

vya FDCs alisema kwamba Serikali hii ya CCM inafanya kazi na alitumia

maneno akasema, Long Live CCM. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, zilikuwepo hoja mbalimbali za Waheshimiwa

Wabunge waliozungumzia kuhusu mashirika yasiyo ya kiserikali. Naomba

niwatambue Wabunge 18 na majina yao nitaomba yaingie kwenye Hansard

kama jinsi ambavyo walichangia.

Hoja ya kwanza ilikuwa inahusu taarifa ya mchango wa NGOs

kuwasilishwa Bungeni. Ushauri wa Kambi ya Upinzani Bungeni kuhusu

uwasilishwa ji wa taarifa ya michango wa NGOs nchini kwa kweli

umepokelewa.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja inayohusu masuala ya marekebisho

ya Sheria ya NGOs namba 24 ya mwaka 2002.

Kuhusu hoja hii, siyo kweli kwamba Sheria ya NGOs Na. 24 ya mwaka 2002

kama ilivyorekebishwa ilipitishwa kwa nguvu kwani taratibu zote za utungaji wa

sheria zilizingatiwa ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha wadau mbalimbali na

kupitishwa na Bunge. Kwa sasa Serikali iko katika mchakato wa kuifanyia

mapitio ya Sera ya Taifa ya NGOs ya mwaka 2001 ili kuwezesha marekebisho ya

Sheria ya NGOs kwa lengo la kuboresha mazingira ya utendaji na mchango wa

NGOs nchini.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja pia inayozungumzia mkakati wa

Wizara juu ya kuhakikisha NGOs zinatekeleza majukumu yaliyokusudiwa kwa

mujibu wa uanzishwaji wake. Kuhusu mwingiliano wa kiutendaji na kimajukumu

baina ya Idara ya Uratibu wa NGOs na RITA; kuhusu usajili wa kufutwa kwa

Shirika la Tanzania, Sisi kwa Sisi; kuhusu muundo wa Mabaraza ya Taifa ya NGOs

kuiwezesha NGOs kujisimamia na kushiriki katika maendeleo ya Jamii kwa kuwa

huru na NGOs kuingiliwa na Serikali. Kulikuwa na hoja pia kuhusu NGOs kuwa

tegemezi kwa wafadhili toka nchi za nje.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hoja zote hizo, naomba kusema, pia

kulikuwa na hoja inayohusu Shirika la WAMA kujihusisha na masuala ya siasa.

Kuhusu WAMA kujihusisha na siasa katika uchaguzi wa mwaka 2010

Wizara haijapata ushahidi wowote kuhusu suala hilo, bali Mheshimiwa Mama

Salma Kikwete alishiriki binafsi katika masuala ya kampeni kama mke wa

Mheshimiwa Rais na siyo kama Shirika la WAMA. Ndiyo maana tunasema Wizara

ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto haijapata ushahidi, bali alishiriki kama

mwananchi, kama individual.

Page 173: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

173

Mheshimwia Spika, kuhusu mikakati ya Wizara kuhakikisha NGOs

zinatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa malengo ni kwamba NGOs

czinatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa malengo yaliyoanzishwa katika

mashirika haya, na ni pamoja na Maafisa Maendeleo ya Jamii wa ngazi za

Wilaya na Mikoa walioteuliwa kuwa Wasajili Wasaidizi ili kuyafuatilia mashirika

hayo katika Serikali za Mitaa na ngazi za Mikoa, kwamba hawa Maafisa

wanazifuatilia zile NGOs kule kule katika Serikali za Mitaa.

Pia Baraza la Taifa la NGOs limeandaa Kanuni za Maadili ya NGOs na lipo

katika hatua za uundaji wa Kamati za Maadili za NGOs katika ngazi mbalimbali.

Pia kuna kuimarisha mfumo wa ufuatiliaji wa NGOs nchini; na vile vile Wizara

kupitia Sheria ya NGOs namba 24 ya mwaka 2002 imeweka utaratibu wa NGOs

kuwasilisha taarifa za mwaka za fedha zilizokaguliwa na kazi za NGOs kwa

msajili wa NGOs.

Mheshimiwa Spika, kwa kweli hakuna mwingiliano wa kimajukumu na

kiutendaji baina ya Idara ya Uratibu wa NGOs nchini ya Wizara yangu, yaani

Maendeleo ya Jamii na RITA chini ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuwa kila

mamlaka ina majukumu yake kisheria.

Aidha, naomba kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kuwa usajili wa

Makao ya Watoto hufanyika chini ya Idara ya Ustawi wa Jamii nchini, Wizara ya

Afya na Ustawi wa Jamii.

Kuhusu Shirika la Tanzania Sisi kwa Sisi, lilisajiliwa mwaka 2011 kama Shirika la

Kutetea Haki za Binaadamu na Masuala ya UKIMWI na Virusi vya UKIMWI. Hata

hivyo, uchunguzi uliofanywa na Wizara ulibaini kuwa Shirika hilo lilikua

likijishughulisha na uhamasishaji wa Ushoga, kinyume na malengo ya usajili

wake. Kutokana na hilo, Serikali ilifuta usajili wake kwa kuwa kufanya hivyo ni

kinyume cha Sheria za nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kuna Wabunge walihoji kuhusu muundo wa Baraza la

Taifa la NGOs. Kwa mujibu wa Sheria ya NGOs namba 24 ya mwaka 2002

muundo uliopo unatoa uhuru kwa mashirika haya kushiriki katika maendeleo

pasipo kuingiliwa na Serikali wala chombo kingine.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ushauri wa kuondokana na utegemezi wa

NGOs kwa wafadhili kutoka nje ya nchi, Wizara ilifanya marekebisho ya Sheria

ya NGOs mwaka 2005 kuruhusu NGOs kuanzisha na kuendesha miradi

kutengeneza faida ili kuondokana na utegemezi wa aina hiyo.

Mheshimiwa Spika, pia zilikuwepo hoja mbalimbali zinazohusu Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.

Page 174: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

174

Kulikuwa na hoja ambayo inasema, Muswada wa Chuo cha Maendeleo

ya Jamii, Tengeru kujiendesha chenyewe umefikia wapi? Kama Kamati ya

Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Jamii ilivyoainisha kwenye Taarifa yake,

Muswada huo umewasilishwa Bungeni, ukisubiri kuwasilishwa rasmi na Waziri

mwenye dhamana pindi Bunge litakapopanga ili Chuo cha Maendeleo ya

Jamii, Tengeru kiweze kuwa Chuo kitakachojitegemea.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja inahusu mgogoro wa ardhi kati ya

Chuo cha Maendeleo ya Jamii, Rungemba na wananchi. Ni kwamba katika

Chuo cha Maendeleo ya Jamii, Rungemba eneo la ekari 10 ambalo Serikali

ililirithi kutoka kwa mmiliki wake, Marehemu Marion Chesham, Lady Chesham,

mpaka sasa halina mgogoro wowote na hati miliki ya eneo hilo namba 22437

ipo.

Mwaka 1989 Chuo kiliomba kuongezewa ardhi zaidi kutoka kijiji cha

Rungemba na kijiji cha Kitelewasi. Eneo la Chuo ambalo limeshapimwa ni hekta

2063. Namba ya ramani ya eneo hilo ni 31195. Mgogoro uliopo sasa ni mgogoro

kati ya eneo lililotolewa na kijiji cha Rungemba. Hata hivyo, mgogoro huo upo

katika hatua za mwisho za usuluhishi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ukarabati, ni kwamba Ukarabati wa majengo

na miundombinu ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii, Rungemba unaendelea.

Pia kulikuwa kuna hoja kwamba kuna upungufu wa fedha zinazotolewa kwenye

ukarabati wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii. Jibu ni kwamba, ukarabati wa

majengo na miundombinu ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii, Rungemba

unaendekea kufanyika kwa awamu. Katika kipindi kilichopita, Wizara yangu

ilikarabati mabafu na Vyoo vya Wanachuo. Katika mwaka wa fedha 2014/2015

Wizara itaendelea kukarabati maeneo mengine kulingana na upatikanaji wa

fedha ambazo Waheshimiwa Wabunge leo tutakuja kuwaomba. Aidha, Wizara

yangu imeshaingiza umeme wa gridi ya Taifa katika Chuo hiki.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja ya wahitimu wa Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii wanaongezeka mwaka hadi mwaka; kwa kuwa siyo rahisi

kuwaajiri wote, hivyo wahamisishwe kujihusisha na shughuli za ujasiriamali. Jibu ni

kwamba, tunaendelea kuwasiliana na TAMISEMI ili wakihitimu, ikiwezekana

waajiriwe moja kwa moja kama Waalimu. Kwa hiyo, hiyo ni rai ya Wizara ya

Maendeleo ya Jamii kuomba TAMISEMI waweze kuwachukua Maafisa

Maendeleo ya Jamii moja kwa moja kutoka kwenye Vyuo vyetu vya kitaaluma.

Pia wanafushwa ujasiriamali na baadhi yao wanajiajiri, na wengine

wanaajiriwa na NGOs na sekta binafsi na wanahamasishwa kujiunga katika

vikundi ili wakopeshwe.

Page 175: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

175

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja kwamba Wizara iboreshe taaluma

inayotolewa na Vyuo vya Maendeleo ya Jamii ili wahitimu wanaotoka katika

Vyuo hivi waweze kutumia vyeti vyao kuingia Chuoni. Wizara imefanikiwa

kudurusu mitaala ya wanafunzi katika Vyuo vyake. Mitaala iliyodurusiwa

imeboreshwa na kuzingatia mwongozo wa Baraza la Itifaki la Mafunzo ya

Ufundi, NACTE, ambalo linasimamia ubora wa mafunzo yanayotolewa katika

Vyuo vyote. Hali hii inawezesha wahitimu wa Vyuo vya Maendeleo ya Jamii

kuweza kujiunga na vyuo vingine vya elimu ya juu kulingana na ufaulu wao.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja kwamba Jimbo la Igalula lipatiwe

Chuo cha Maendeleo ya Jamii ili vijana wa jinsia zote wapate mafunzo ya

mbinu na uwezo wa kujikimu pamoja na kujitegemea. Wizara imepokea ushauri

wa Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Igalula kuwa hakuna Chuo cha

Maendeleo ya Jamii katika Jimbo la Igalula, Wizara itaendelea kushauriana na

eneo husika kuangalia uwezekano huo kulingana na upatikanaji wa rasilimali na

kuendelea kuomba mchango wa wananchi katika uanzishwaji wa Vyuo hivi,

kwa sababu Vyuo hivi vya Maendeleo ya Wananchi ni Vyuo vya Wananchi

wenyewe katika eneo husika.

Katika maeneo yote, Wakurugenzi ndio wamekuwa Wenyeviti wa Bodi za

Vyuo hivi. na hata kozi zinazotolewa katika vyuo hivi kimsingi, inategemea na

eneo. Kama ni eneo ambalo shughuli nyingi ni za kilimo, basi wanatoa kozi za

kilimo; kama ni eneo la ufugaji, wanatoa kozi za ufugaji au uvuvi au ufundi wa

magari, ufundi wa umeme majumbani, useremala, uashi na kadhalika.

Mheshimiwa Spika, lingie ni kuhusu Chuo cha Maendeleo ya Jamii,

Rungemba kipandishwe hadhi kuanza kutoa Shahada badala ya Stashahada.

Wizara itazingatia ushauri huu baada ya kukiwezesha Chuo kutimiza vigezo.

Maana ili kipandishwe hadhi, lazima kuwe na vigezo, vimekidhi? Kwa hiyo,

Wizara itaangalia kukiwezesha ili Chuo hiki kiweze kutimiza vigezo vya kuanzisha

mafunzo hayo kufuatana na mwongozo wa Baraza la Ithibati la Mafunzo ya

Ufundi (NACTE).

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja kwamba Serikali iweke mkakati wa

Uongozi bora katika Vyuo vya Maendeleo Jamii ili vifundishe Jamii

inayovizunguka. Jibu ni kwamba, Wizara iliandaa mpango mkakati wa utoaji wa

mafunzo mbalimbali yakiwemo ya uongozi bora katika jamii inayozunguka

Vyuo. Katika mpango huo, kila Chuo kimeainisha Vijiji vinne kwa ajili ya utoaji wa

mafunzo hayo. Kwa mfano, Chuo cha Tengeru kimekuwa kikitoa mafunzo hayo

katika Vijiji vya King‟ori, Marewu, Nambala na Kikwe vilivyo katika Halmashauri

ya Wilaya ya Arumeru.

Mheshimiwa Spika, sasa nijikite katika hoja ya upungufu wa Maafisa

Maendeleo ya Jamii katika Kata. Sera ya Maendeleo ya Jamii inaelekeza

Page 176: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

176

kwamba kila Kata iwe na Mtaalam wa Maendeleo ya Jamii. Mpaka sasa ni

asilimia 39 tu ya Kata zote 3,339 ndizo zenye wataalam hawa. Jumla ya Kata

1,045, sawa na asilimia 61 kwa kweli hazina wataalam wa Maendeleo ya Jamii.

Wizara inaendelea kuishauri Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kutenga fedha za

kutosha ili waweze kuajiriwa. Aidha, Wizara yangu inaendelea kuzalisha wastani

wa wataalam wa Maendeleo ya Jamii 2,800 kila mwaka.

Mheshimiwa Spika, kuhusu umuhimu wa sekta nyingine kuwatumia

wataalam wa maendeleo ya Jamii katika kuelimisha na kuhamasisha

utekelezaji wa mipango ya Maendeleo ya Jamii, Serikali imekuwa ikitenga

fedha kuanzia mwaka 2009/2009 ili kuiwezesha Idara ya Maendeleo ya Jamii

katika Halmashauri kufanya kazi zake kwa ufanisi. Serikali kupitia TAMISEMI,

inaendelea kuhimiza Halmashauri kutenga fedha za kutosha na kuwapatia

vitendea kazi na vyombo vya usafiri ili waweze kuhamasisha jamii kushiriki

kikamilifu katika programs za maendeleo.

Aidha, Wizara yangu imepokea ushauri wa kupokea Baraza la ushauri la

Wazee wastaafu wa Maendeleo ya Jamii. Aidha, Wizara itaendelea kutoa

mafunzo ya muda mfupi yakiwemo masuala ya uandishi wa Miradi, ili

kuwajengea uwezo zaidi. Pia Wizara inaomba, katika masuala mbalimbali,

katika Halmashauri zetu na maeneo mengine, Maafisa Maendeleo ya Jamii

Hawa wawe wanatumika. Kwa maana wao ndio waliosomea masuala ya

maendeleo ya jamii; iwe ni kwenye ujenzi, iwe ni kwenye masuala ya elimu,

masuala ya afya, ni muhimu kushirikisha Maafisa Maendeleo ya Jamii.

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja kwamba, Sekta ya Maendeleo ya

Jamii, imekuwa ikijikongoja. Lini tutaitumia sekta hii ipasavyo? Sekta hii kwa kweli

haijikongoji. Sekta ya Maendeleo ya Jamii, ina watumishi katika ngazi za Wizara,

Mikoa, Halmashauri hadi katika Kata. Kwa hiyo, ni muhimu tukawatumia

watumishi hawa. Sekta hii itatumika ipasavyo pale itakapoweza kushirikishwa na

wadau mbali mbali.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, ninaomba nikushukuru sana

kwa kunipa nafasi, kutoa ufafanuzi wa baadhi ya maeneo ya hoja zilizoteolewa.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

SPIKA: Ahsante. Sasa nitamuita…

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Wewe unafikiri atapinga! Mheshimiwa mtoa hoja, unazo dakika

45.

Page 177: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

177

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

napenda kwanza kukushukuru wewe kwa kunipa nafasi ya kuhitimisha hoja

niliyoiwasilisha asubuhi ya leo.

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuipogneza sana Kamati ya Kudumu ya

Bunge ya Maendeleo ya Jamii, kwa kuisimamia Wizara yangu kwa umakini

mkubwa.

Naishukuru Kamati kwa jitihada zao za kuiwezesha Wizara kuongeza Bajeti

ya Serikali, ingawa bado ni finyu, ukilinganisha na majukumu ya Wizara. Pia

naipongeza sana hotuba ya Kambi ya Upinzani na ninaahidi kwamba Wizara

yetu itajibu zile hoja na itafanyia kazi yale maoni mazuri ambayo wametupatia.

Wizara kwa upande wake inachukua hatua mbali mbali za kupambana na

ufinyu wa Bajeti. Moja ya hatua hiyo ni kuandika maandiko ya miradi na

kuwasilisha Serikali na kwa wabia wa maendeleo.

Mheshimiwa Spika, jumla ya Waheshimiwa Wabunge waliochangia hoja

yangu ni 58, na kati yao 17 wamechangia kwa kuongea na 44 wamechangia

kwa maandishi. Katika michango iliyotolewa, iko inayotoa ushauri wa kutusaidia

na mengine ni maswali ambayo nitajaribu kuyajibu hapa.

Mheshimiwa Spika, kabla sijaendelea zaidi, naomba nichukue nafasi hii,

kwa masikitiko makubwa Wizara yangu inalaani sana viendo vya ukatili

wanavyofanyiwa Wanawake, Watoto wa kike na wakiume na katika maeneo

mengi, wanawake wanawatendea ukatili wanaume, lakini hasa ukatili mkubwa

wanaofanyiwa wanawake hususan katika Kanda ya Ziwa. Tuna laani kabisa

vitendo hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba pia nichukue fursa hii kuungana na

wapenda haki wote duniani kulaani kwa nguvu zote, kitendo cha utekeaji wa

wasichana zaidi ya 200 huko Nigeria, kilichofanywa na kikundi cha Boko Haram.

Natoa wito kwa wapenda haki wote duniani kuendelea kufanya kila juhudi ili

wasichana hawa waweze kuachiliwa haraka iwezekanavyo na bila ya masharti

yoyote.

Mheshimiwa Spika, naomba kwa unyenyekevu na heshima kubwa

niwashukuru Wabunge wa Bunge hili, pamoja na Wajumbe wa Bunge la Katiba,

pamoja na ndugu jamaa na marafiki ambao walinifariji wakati wa kipindi

kigumu cha msiba wa mtoto wangu mpendwa Lyford.

Mheshimiwa Spika, kabla sijaendelea, ningependa niseme machache

kuhusu WAMA. Leo nimesikitika sana ilipoonekana kama WAMA inafanya kazi

ambazo siyo zake. WAMA imeandikishwa kisheria na ina majukumu yake na

inayafanya majukumu kwa uadilifu sana. (Makofi)

Page 178: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

178

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mama Salma Kikwete – Mwenyekiti wa

WAMA, amekuwa akifanya shughuli zake kwa kiwango kikubwa sana.

Nashangaa sana leo kuona kuna watu wanahoji walipomwona amekwenda

kumsaidia mume wake kwenye campaign. Nyie wote hapa mkiwa kwenye

campaign zenu wake zenu hawalali, lakini yeye mmeona mseme.

Mheshimiwa Spika, nataka niondoe ile kejeli kwa kutaja mambo

machache tu ambayo WAMA ambayo iko registered chini ya NGO, imekuwa

ikiyafanya.

Mheshimiwa Spika, Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete,

amefanya kazi kubwa sana kwenye fani ya Elimu ya Mtoto wa Kike na

Mapambano ya Kupunguza Mimba Mashuleni. Katika maeneo aliyoyafanya,

kwa kweli Mikoa ile mimba za utotoni zimepungua. Mama huyu amekuwa

mstari wa mbele katika campaign za chanzo mbalimbali, ameweza

kuwawezesha wanawake kiuchumi mpaka sasa idadi tuliyokuwanayo wanazidi

wanaweke 60,000. (Makofi)

Kutokana na kazi nzuri anazosifanya. Ningelipenda mjue, kuna Chama

cha Wanawake wa Marais, inayoitwa Jumuiya ya Wake wa Marais Duniani.

Katika Chama hicho, Mama Salma Kikwete, yeye ni Vice Chairperson wa

Jumuiya hiyo kwa upande wa Horn ya Afrika, nchi 11 za za Afrika. Yeye ni Vice

Presient, na amepata kutokana na michango yake. Akienda katika nchi za

Kimataifa wana-recognize kazi nzuri ambayo ameifanya. Hiyo organization

inaitwa Organization of African First Ladies Against Aids. Kwa hiyo, mnaweza

mkaingia kwenye mtandao mkaona, badala ya kuzungumza tu hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mama Salma ameishapata awards nyingi huko

duniani, pamoja na hapa nyumbani tumekuwa tukimpatia tuzo; lakini mimi

nitasema zile za nje. Miongoni mwa tuzo hizo, mojawapo amepata MDG –

Woman Achievement Awards; ameisaidia Tanzania ku-achieve kwenye MDG

goals. Lakini pia amepata Award ya Global Inspirations Leadership Award,

aliyoipata kule New York, kwa kazi nzuri ya campaign anayoifanya; Campaign

ya chanjo na campaign ya chanjo ya cervical cancer, ambayo Mama Salma

yuko mstari wa mbele. Lakini ili nisipoteze muda na nyinyi ni wasomi wazuri,

mkitaka taarifa zaidi, naomba mtembele Web Site ya WAMA,

www.wamafoundation.org.tz. Au kama mnaona taabu mnaweza mka-Google

tu mkapaa WAMA Foundation, mambo yote yako pale.

Nadhani baada ya hapo, tutakubaliana kwamba kazi inafanyika. Lakini

siku ya campaign mama akika nyumbani baba itakuwaje? (Makofi)

Mheshimia Spika, naomba sasa nijibu hoja za Kamati ya Kudumu ya

Maendeleo ya Jamii. Walihoji Serikali irudishe mfumo wa zamani wa fedha za

Page 179: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

179

Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, kulipwa katika Hazina ndogo. Badala ya

kutumia mfumo wa sasa wa kupeleka kwenye retention.

Mheshimiwa Spika, Wizara kwa upande wake na sisi tumekuwa concern,

kwa vile zile pesa za retention hazifiki, au zinakuja kidogo sana, kwa hiyo,

kwenye Vyuo kunakuwa na matatizo ya kununua vitu vya muhimu sana. Kwa

hiyo Wizara imekaa kikao na Hazina na kujadili kuhusu kutumia fedha zote

zinazokusanywa na Vyuo kupitia Hazina Ndogo. Wizara pia imeiandikia barua

Hazina ikiomba kutumia utaratibu wa malipo kupitia Hazina ndogo. Wizara

bado inasubiri majibu kutoka Hazina, na Hazina itakapotoa idhini hiyo, utaratibu

huo utafuatwa kama inavyopendekezwa na Kamati.

Mheshimiwa Spika, Kamati ya kudumu imezungumzia Serikali kuainisha

vyanzo vya mapato nakupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuweza kutenga

fedha za ndani kwa ajili miradi ya maendeleo na siyo kama ilivyo sasa ambapo

fedha nyingi za Miradi ya Maendeleo zinategemea fedha za nje ambazo

upatikanaji wake umekuwa siyo wa uhakika.

Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya mwaka 2014/2015, Wizara

imetengewa Shilingi bilioni saba, fedha za ndani kwa ajili ya miradi ya

maendeleo, ikilinganishwa na Sh. 2,017,544,000/=

ambazo ni fedha za nje za Maendeleo. Hali hii inaonyesha azma ya Serikali ya

kuanza kutotegemea zaidi fedha za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kambi ya Upinzani yamesemwa

mengi, mengine nitayajibu wakati nikijibu na hoja nyingine. Lingine lilihusu

Serikali ieleze kwa nini imeendelea kutoa kiwango kidogo cha fedha kwa ajili ya

kukarabati majengo na miundombinu katika Vyuo ambavyo bado ni chakavu.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa Vyuo vya Maendeleo ya

Jamii na Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi, Serikali imeviingiza vvyuo hivyo

katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano. Serikali itaendelea

kuvitengea Vyuo hivyo fedha kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, Wabunge wengi wamehoji kuhusu Bajeti, na

nikiwataja wako Wabunge 19. Walisema Wizara haijapewa kipaumbele na

Serikali kwa kutengewa fedha za kutosha. Sisi tunashukuru kwa Wabunge

kuonyesha kuwa Bajeti haitoshi. Hata hivyo mwaka 2014/2015 Serikali

imeongeza bajeti ya Wizara kwa asilimia 16, na mtaona kwenye vifungu

kwamba tumeongeza ongeza, kutokana na nyongeza hii. Wizara itaendelea

kuwasiliana na Hazina kuhusu kuongezewa fedha.

Mheshimiwa Spika, aliyechangia kuhusu masuala ya fedha ni mmoja,

yeye amezungumzia fedha. Alisema fedha nyingi zimetengwa katika Kasma ya

Page 180: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

180

Travel in Country, fedha ambazo haziwezi kuleta mabadiliko nchini. Fedha hizo

zipunguzwe na kuzipeleka kwenye maendeleo.

Mheshimiwa Spika, fedha zimetengwa kuwezesha Wizara kutekeleza

majikumu yake ya uhamasishaji, kwenda kuwezesha jamii katika masuala ya

maendeleo, kuratibu na kufuatilialia utekelezaji wa Sera za Wizara, kutoa elimu

kwa wananchi kuhusu ukatili wa kijinsia. Kutoa mafunzo ya ukufunzi kwa Maafisa

wa Mendeoeo ya Jamii 50 na kufanya maadhimisho mbalimbali kutokana na

ufinyu wa Bajeti katika miaka ya nyuma. Wizara ilikuwa inashindwa kutekeleza

majukumu yake yote haya. Dhana ya Maendeleo ya Jamii, maana yake

kufanya kazi na wananchi. Huwezi kumfikia mwananchi kule Kasulu, au Katavi,

kwa kutembea kwa miguu. Kwa hiyo, ndiyo maana tumeweka Kasma ya Travel

in Country. Sisi tuko na wananchi grass root. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Maendeleo ya Jamii, maana yake unafanya kazi na

wananchi. Jamii lazima ifikiwe. Siyo wote wana TV, ingelikuwa wote wana TV na

Radio, pengine ingekuwa rahisi, lakini ni lazima tuwafikie.

Mheshimiwa Spika, suala zito sana ambalo linawasikitisha Wabuge na sisi

wenyewe na wananchi kwa ujumla ni kuhusu watoto wanaoishi katika

mazingira hatarishi. Mfumo wa udhibiti takwimu na taarifa ni dhaifu, hili

limezungumzwa hata kwenye taarifa ya Mkaguzi Mkuu na kutegemea Wafadhili

katika kushughulikia matatizo ya watoto badala ya Serikali na kutokuwepo

utaratibu wa kutosha katika utoaji wa huduma. Waheshimiwa Wabunge 20

wamechangia, Lakini majibu yake naomba nijibu kama hivi ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuhamasisha na kutoa elimu ya

familia ili zisimamie malezi ya watoto. Waheshimiwa Wabunge, masuala ya

watoto ni masuala ya familia. Serikali inaingilia pale ambapo hapana budi.

Pengine wazazi hawapo; mtoto hata akifiwa na wazazi wake, walezi wapo.

Jamii inatakiwa irudi kwenye maadili ya Mtanzania. Lakini Serikali bado

inafuatilia masuala hayo pamoja na kwamba ni jukumu la familia.

Mheshimiwa Spika, tuna mpango wa pili wa kusaidia watoto walio katika

mazingira hatarishi, ambao Wizara ya Maendeleo ya Jamiii Jinsia na Watoto ni

mdau na anashirikiana na wadau wengine. Napenda ieleweke kwamba

masuala ya watoto ni mtambuka. Mtoto huyu anashughulikiwa na Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, anashughulikiwa na Ustawi wa Jamii, Wizara ya Afya,

anashughulikiwa na Elimu, anashughulikiwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya

Nchi, anashughulikiwa mtoto huyu na Sheria, anashughulikiwa hata na Wizara

ya Kilimo Chakula na Ushirika. Kwa hiyo tunayo Task Force kubwa ambayo

inawahusu wote, kila mtu ana majukumu yake.

Page 181: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

181

Mheshimiwa Spika, katika ngazi ya Kata, Maafisa wa Maendeleo ya Jamii

ni wahamasishaji na watekelezaji wa Mpango huu. Huu mpango Afisa Ustawi

wa Jamii kule kwenye Kata anajua kazi yake; na Afisa wa Maendeleo ya Jamii

anajua.

Waheshimiwa Wabunge ni jukumu letu tunapopitisha fedha kwenye

Halmashauri zetu, tuhakikishe Idara ya Maendeleo ya Jamii, Idara ya Ustawi wa

Jamii, wanapata fedha za kutosha kwenda kupeleka hizi taarifa kwa wananchi

na jamii. Lakini ilivyo sasa hivi, hizi Idara mbili ambazo zinahusiana moja kwa

moja na watoto, hazitengewi fungu la kufanya kazi hii, wala hazipewi nyenzo za

kufanyia kazi kama vile magari au pikipiki. Aidha, Halmashauri za Wilaya kupitia

mafunzo ya elimu ya familia, wameandaa mipango kazi itakayotumia fedha

kutoka katika makusanyo ya Wilaya ili kutekeleza. Kwa hiyo, tunawategemea

Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, haiwezekani Wizara ya Maendeleo ya Jamii iweze

kushughulikia mtoto ambaye anadhalilishwa, yuko kule Nyasa, wakati

Halmashauri iko pale na Afisa wa Maendeleo ya Jamii yuko pale. Hili ni jukumu

letu. Nawaombeni sana, Sera ya Maendeleoya Mtoto imedurusiwa na mkakati

kuandaliwa ili kuelekeza familia jamii na Serikali kutimiza wajibu wa kutunza

watoto. Tunashirikiana na TAMISEMi na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

kupitia Idara ya Ustawi wa Jamii, katika kuhakikisha kwamba watoto wanapata

huduma kulingana na rasilimali walizonazo.

Mheshimiwa Spika, kitini cha Elimu ya Malezi kwa familia kuhusu kuzuia

ukatili dhidi ya watoto kimeandaliwa na mafunzo kutolewa kwa wadau kutoka

kwa Halmashauri za Wilaya na baadhi ya Vyuo vya Maendeleo ya Jamii, hivi

vyote, ili kutekeleza hiki kitini kiwafikie, ni lazima Maafisa wetu waende huko

kwenye Halmashauri watoe elimu.

Mheshimiwa Spika, hoja nyingine ambayo imetolewa, ni mimba za utotoni

ambayo imechangiwa na Waheshimiwa Wabunge wengi. Jibu lake ni kwamba

katika kupunguza mimba za utotoni, Serikali imeendelea kuhamasisha jamii

kupitia Maafisa Maendeleo ya Jamii, kuondoa mila zenye kuleta madhara kwa

watoto na wasichana. Aidha, Serikali imeendelea kuhamasisha wadau

mbalimbali kujenga mabweni katika Shule za Kutwa nchini ili kuwakinga watoto

na mwingilio mkubwa wa watu ambao unapelekea mimba hizo.

Aidha, Mikataba mbalimbali ya Kimataifa kuhusu haki na ustawi wa

mtoto na Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009 inatoa adhabu kwa

yeyote anayepatikana na hatia ya kuwapa ujauzito watoto.

Hili linahitaji pia ushirikiano mkubwa wa jamii. Tunaficha! Mtoto amepewa

mimba, badala ya kwenda kutoa taarifa kwenye vyombo vya sheria

Page 182: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

182

achukuliwe hatua, basi tunamaliza hapo hapo waoane. Sasa tunavyofanya vile

na mtoto mwingine naye anafanya kwa sababu anaona hakuna

litakalofanyika. Lakini hili ni kosa na ni lazima kutoa taarifa Polisi ili jamii ijue

kwamba vitendo hivi siyo vizuri. Tutaweza kuvimaliza kwa njia hiyo tu, lakini

kama jamii itaendelea kufichaficha mambo haya, yatakuwa yanaendelea.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine ambalo tunatakiwa kufanya ni

kuhakikisha kwamba wazazi wanawapa elimu watoto wao ya afya ya uzazi. Ni

vema kuongea na mtoto aelewe kwamba akifanya tendo fulani atapata

mimba. Zile siku za kumuonea aibu mtoto wako usimwambie ukweli zimepita

jamani, tupo kwenye karne nyingine, akina mama ongeeni na watoto wenu wa

kike na akina baba waongee na watoto wao wa kiume kwa sababu wengi

sana wanapata mimba kutokana na kutokujua, wengi sana! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja juu ya jukumu la kuwalinda na

kuwahudumia watu wenye ulemavu. Hoja hii imechangiwa na Waheshimiwa

wengi, Kambi ya Upinzani na wengine wengi, nashukuru kwani ni jukumu kubwa

sana hili na la muhimu.

Mheshimiwa Spika, jukumu la kulinda na kuwahudumia watu wenye

ulemavu kwa kuwaendeleza, kuwalinda na kuhakikisha kuwa hawabaguliwi na

wanapewa hadhi sawa limeendelea kushughulikiwa na Serikali kwa kuwa na

Sera ya Maendeleo ya Wazee iliyopo chini ya Wizara ya Afya na Ustawi wa

Jamii. Wizara yangu kwa upande wake imeendelea kuhamasisha jamii

kuondokana na mila na desturi zinazowabagua watu wenye ulemavu na

kuwaona kuwa wana haki sawa na binadamu wengine ikiwepo haki ya

kupatiwa elimu. Suala hili litazungumziwa kwa urefu na mapana zaidi

itakapokuja Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Mheshimiwa Spika, ukatili dhidi ya watoto, hili pia limechangiwa kwa

masikitiko makubwa na Waheshimiwa Wabunge wengi tu, Wabunge 13

wamelizungumzia katika michango yao ya maandishi na kwa kuzungumza.

Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya watoto tuliandaa na sasa

tunatekeleza mpango kazi shirikishi wa mwitikio na kuzuia ukatili dhidi ya watoto.

Mpango huo ni wa mwaka 2013 - 2016 ambao unatekelezwa na sekta

mbalimbali zikiwemo Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Wizara

ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Katiba na Sheria, TAMISEMI, Elimu na Mafunzo

ya Ufundi, madhehebu ya dini na asasi zisizo za Kiserikali. Hawa wote

tunatekeleza kwa pamoja kwa vile kila sekta inayo mipango yake ya kupiga

vita ukatili. Wizara itaendelea kuratibu utekelezaji wa mpango huo kupitia kikosi

kazi kitaifa cha kuzuia ukatili dhidi ya motto. Toka kuanza kutekelezwa kwa

mpango kuna mafanikio mbalimbali yamepatikana ya kuzuia ukatili dhidi ya

watoto na nina matumaini makubwa kwamba tatizo hili litapungua.

Page 183: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

183

Mheshimiwa Spika, Serikali itafuatilia tatizo lililotajwa na Mheshimiwa Al-

Shaymaa, Mbunge wa Viti Maalum la watoto wa Buhangija kuhakikisha wazazi

wanatakeleza wajibu wao wa malezi na kuwatembelea na kuwapenda

watoto hawa. Hili linasikitisha kwa kuwatelekeza watoto wenye ulemavu bila

kuwaonyesha mapenzi hasa wale wenye ulemavu wa ngozi ambao wako

Buhangija. Tunawasihi kupitia Bunge hili wazazi wajitokeze waende wakawaone

watoto wao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala hili la ukatili limeendelea sana ndani ya jamii na

sisi wazazi tunaanza ukatili ndani ya nyumba, watoto na wao wakiwa wakubwa

na wao wanawafanyia ukatili watoto wao, watoto wetu tuwapende. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wapo akina mama, mtoto ameiba kipande cha

nyama anamkata sikio au vidole, ni tatizo kubwa sana na sasa limeenea.

Naomba niwafahamishe kwamba hilo ni kosa la jinai na lazima litolewe taarifa ili

wachukuliwe hatua. Huwezi ukamuumiza mtoto kwa sababu ya chakula

ambacho ni haki yake. Kwa hiyo, Waheshimiwa wawezesheni Maafisa wenu wa

Maendeleo ya Jamii huko mlipo ili waweze kufanya kazi hizi, yote haya

wanayaweza.

Mheshimiwa Spika, hoja nyingine iliyojitokeza ni ukeketaji wa watoto wa

kike, Serikali itumie nguvu kupambana na mila hii, hili imechangiwa na

Wabunge wengi. Kumekuwepo na jitihada mbalimbali katika kushughulikia

tatizo la ukeketaji wa watoto wa kike ambalo limejikita zaidi katika mila na

desturi za makabila mbalimbali hapa nchini. Wizara kwa kushirikiana na asasi za

kiraia imekuwa ikiendesha programu za kuelimisha umma ili kuondokana na

tatizo hili.

Mheshimiwa Spika, elimu kupitia Maafisa Maendeleo ya Jamii na

wawezeshaji wengine kutoka asasi za kiraia wametoa mchango mkubwa katika

hili. Aidha, programu ya elimu kupitia vyombo vya habari kama luninga, redio,

magazeti na mitandao ya kijamii vimeweza kubadili fikra na mtazamo wa jamii

kuacha ukeketaji. Sote tunakiri kwamba uketetaji pia ni ukatili dhidi ya watoto

na dhidi ya akina mama. Waheshimiwa Wabunge wamelizungumzia vizuri sana

na tupo pamoja tunaendelea na hayo mapambano tukishirikiana na NGOs

mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, kuna hoja inayosema ucheleweshaji wa Sera ya

Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Mtoto. Sera hii ipo katika mchakato, Serikali

imekamilisha kudurusu Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008 ili kuwa na

sera moja itakayoleta masuala ya malezi, makuzi na maendeleo ya mtoto ya

mwaka 2014. Sera hii iko katika stage nzuri ya kufikia kwenye Baraza la Mawaziri.

Aidha, mkakati wa sera hiyo pia umekamilika na hivi sasa inasubiri taarifa ya

tathmini ya utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008,

tunaifanyia tathmini kama kiambatanisho muhimu cha Sera ya sasa ili Rasimu hii

Page 184: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

184

iwasilishwe katika ngazi za juu. Katika Sera mpya yapo mapendekezo ya

kurekebisha Sheria ya Mtoto Na.21 ya mwaka 2009.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Serikali inavyozingatia agenda ya watoto

ambapo viongozi mbalimbali waliisaini mwaka 2012, Serikali imeandaa mpango

mkakati wa utekelezaji wa agenda ya watoto kutoka mwaka 2013 - 2016

ambao unatekelezwa kwa kuzingatia maeneo yafuatayo:-

Moja, kufanya kazi na Waheshimiwa Wabunge katika kuhamasisha

maeneo 10 ya uwekezaji kwa watoto.

Mbili, kuelimisha jamii kupitia vyombo vya habari.

Tatu, kufanya kampeni mbalimbali kuhusu haki za mtoto na kuimarisha

ushiriki wa mtoto.

Mheshimiwa Spika, hoja nyingine ambayo imekuja mbele yetu ni biashara

ya usafirishaji haramu wa watoto kutoka vijijini kwenda mijini na nje ya nchi. Ipo

Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu ya mwaka 2008 ambapo

inakataza na kuvitaja vitendo hivyo kama ni ukiukwaji wa sheria na haki za

binadamu. Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani inakamilisha Kanuni na

mpango kazi wa kuzuia usafirishaji haramu wa binadamu. Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imeendelea kuelimisha jamii na

kuhamasisha kutokubali kutoa watoto wao kwenda kufanya kazi kwenye

maeneo ambayo hawayafahamu.

Mheshimiwa Spika, watoto hawa wanatakiwa walindwe na jamii, jamii

yote tunatakiwa tuwe walinzi kwa watoto. Katika maeneo yenu mkiona watoto

hawapo au mtoto ameondoka ni vizuri kuuliza na kutoa taarifa kwa wahusika

yaani kwa Mtendaji wa Kijiji au kwa Mwenyekiti wa Kijiji kwamba mwezetu mtoto

wake amekwenda wapi? Atatoa taarifa! Kama amenunuliwa tutajua na

mitaani hivyohivyo. Lazima sisi tuwe walinzi wa watoto, kila mtu ni mlinzi wa

mtoto. Watoto hawana uwezo wa kukataa bali wanapelekwa tu.

Mheshimiwa Spika, hoja nyingine iliyokuja mbele yetu ni kwamba watoto

wanachanganywa mahabusu na wakubwa. Sheria ya Mtoto Na.21 ya mwaka

2009 inazuia watoto kufungwa au kuwekwa kwenye mahabusu iliyo na watu

wazima. Zipo mahabusu maalum za watoto (retention homes) ambazo watoto

huwekwa na kupata uangalizi maalum. Aidha, Sheria ya Mtoto Na.21 ya

mwaka 2009 haitoi adhabu ya vifungo kwa watoto ila kuna shule za maadilisho

ambapo watoto hupelekwa kwa ajili ya kufundishwa tabia njema. Wizara

itafuatilia na kulifanyia kazi suala hili.

Page 185: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

185

Mheshimiwa Spika, nawashukuru Waheshimiwa kwa michango yao na

ninaendelea kuwaomba kwamba sisi Wabunge tutumie Halmashauri zetu

kuhakikisha watoto wanapata haki zao. Sisi kama Wabunge kupitia Halmashauri

zetu tuhakikishe kwamba fedha za WDF zinatengwa. Inakuwaje Kamati ya

Fedha mnapitisha bajeti lakini hamuangalii kwenye kipengele cha fedha kwa

vijana na wanawake, ile 10% haipo na sisi Wabunge ni sehemu ya Kamati ya

Mipango na Fedha katika Halmashauri zetu? Sasa tukija hapa zile fedha

ambazo mnaziona tunapeleka zinaonekana ndogo, fedha zinazotoka

Maendeleo ya Jamii ni kama chachu tu, ni ndogo, lakini kuna Halmashauri

kubwa ambazo 10% yake inaweza kuzidi hata milioni mia tano au bilioni moja.

(Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitatoa mfano, Dar es Salaam juzi Halmashauri ya Ilala

imeweza kutoa shilingi milioni mia tatu kwa ajili ya akina mama. Tatizo

Waheshimiwa, Wakurugenzi wanaona ni nyingi. Wakitazama 10% imeshakuwa

shilingi bilioni moja wanaanza kufikiria aah, shilingi milioni mia tano vijana na

shilingi milioni mia tano akina mama, ni haki yao imetolewa kisheria. Jinsi wale

akina mama na vijana watakavyopata hiyo mikopo watafanya biashara,

watalipa leseni mzunguko ule ile Halmashauri itaendelea kupata fedha kutoka

kwa haohao waliowakopesha hizo fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa kupitia Bunge hili, nawaomba

Wakurugenzi na ninaiomba Wizara ya TAMISEMI iendelee kupigania suala hili. Ile

10% isiwe tunabembeleza. Mimi naamini bajeti inayokuja kwenye Halmashauri

zetu wote hapa Wabunge tumo mle, mtahakikisha kwamba 10% inatengwa 5%

kwa akina mama na 5% kwa vijana regardless amount ni ipi kwa sababu kwa

kipindi kirefu wameacha kabisa kutoa, wengine wanatoa 1% na wengine

hawatoi. Sisi fedha inayotoka Wizarani ni ndogo sana, tunaileta pale kama

tunaikumbushia Halmashauri hizi pesa zimefika haya toeni na ninyi lakini

wenzetu hawatoi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunisikiliza na ninaomba kutoa

hoja.

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Spika, naafiki.

(Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)

KAMATI YA MATUMIZI

Matumizi ya Kawaida

Fungu 53 - Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Na Watoto

Page 186: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

186

Kif. 1001 – Administration & Human

Resource Management…........Tshs 2,309,157,012/=

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mkanga, ndio mshahara wa Waziri!

MHE. MARGARETH A. MKANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa

kunipa nafasi. Sina haja ya kutoa shilingi lakini napenda tu kupata ufafanuzi au

nielimishwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wenye ulemavu kuna wanawake na

watoto na Mheshimiwa Waziri katika kujibu ameelezea hilo kwa kifupi. Sasa

nataka kufahamu katika Idara ya Jinsia na Idara ya Watoto ndani ya Wizara hii

masuala haya ya walemavu wanawake na watoto wenye ulemavu

mnayazingatiaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante!

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Margareth Mkanga kwamba

masuala ya walemavu wawe watoto, akina mama au wanaume karibu yote

haya yanashughulikiwa na Idara ya Ustawi wa Jamii. Hata hivyo, ilivyo kwa

sababu sisi ni Wizara ya Maendeleo ya Jamii walemavu wanafika kwetu na

tunakuwa tunawaelekeza wafanye nini kwa vile Sera yao na Sheria yao iko

katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii lakini tumekuwa tukitoa misaada sana

kwa walemavu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Conchesta Rwamlaza!

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mimi

napenda kupata ufafanuzi kuhusu Benki ya Wanawake, benki ambayo iliundwa

kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya wanawake wote lakini ukitazama bajeti

yake ambayo Mheshimiwa Rais alisema kila mwaka watakuwa wanaipa hii

benki shilingi bilioni mbili. Ukitazama mwaka 2011/2012, Serikali ilitoa shilingi

bilioni mbili, mwaka 2012/2013 walitoa shilingi bilioni 1.3 lakini mwaka 2013/2014

walitoa shilingi milioni 450. Kwa hiyo hakuna mkakati maalum wa kuendeleza

benki hii ili iweze kwenda kwa wanawake wote, inaonekana ina malengo ya

kuendeleza wanawake wa Dar es Salaam peke yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninapenda kupata commitment ya

Serikali kuhusu fedha hizi na kwamba mchezo huu unaofanyika sasa hivi ni

kuwahadaa wanawake kwamba itabaki Dar es Salaam na watu wengine wa

Page 187: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

187

Mikoani kule kwetu tunakotoka kwa mfano Kagera hatutaweza kupata benki

ya wanawake ili wanawake waweze kukopa na kujiendeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba ufafanuzi na kwa kweli leo

kwa mara ya kwanza nitaondoa shilingi kwa mshahara wa Waziri pamoja na

kwamba ni kiduchu ili tuweze kupata commitment ya kusaidia benki hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante!

MWENYEKITI: Mimi nilifikiri hii ungeikaba Wizara ya Fedha, huyu hawezi

chochote hata mshahara wenyewe hana, si ninyi wenyewe mmesema hana

hata mshahara.

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, inaonekana

Mheshimiwa Waziri anakosa hata mafuta kwenye ofisi yake, nimesikia anaweka

mafuta kwenye gari. Tunataka atuambie, hii Wizara inadhalilishwa, wanawake,

tunaomba na yeye asimame atuambie ataikaba vipi ile kusudi tuweze kupata

hiyo fedha.

MWENYEKITI: Aikabe Wizara gani?

MHE. CONCESTA L. RWAMLAZA: Aikabe Serikali yeye kama Waziri!

MWENYEKITI: Hapana bwana, unajua ninyi mnapoteza wakati,

ninachokisema mimi, ni kwamba hawa ninyi wenyewe toka asubuhi mnasema

kiduchu, kiduchu, sasa anafanyaje? Ninyi jiandae muikabe Wizara yenyewe

ambayo inahusika na mengine mumkabe Waziri Mkuu siyo huyu! Ukimkaba

huyu siyo sahihi.

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo,

nimkabe Mheshimiwa Waziri Mkuu?

MWENYEKITI: Ndiyo, kwa wakati wake!

MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Waziri Mkuu, tunaomba

ujibu, wanawake wanaumia huko kwetu, msaidie mwanamke mwezetu hapo.

MWENYEKITI: Haya, naomba ukae, Mheshimiwa Waziri!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa concern yake kuhusu benki kwamba

angependa iende kwa speed zaidi.

Page 188: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

188

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali imekuwa ikijitahidi kutoa fedha

kwa ajili ya Benki hii, lakini kutokana na ufinyu wa bajeti na mambo mengi

ambayo yametokea hapa katikati, kuna sensa, Bunge la Katiba na kadhalika,

kwa hiyo, hata ile azma haikufikiwa lakini tunaamini katika hiki kipindi kifupi

kabla ya kumaliza mwaka tutaongezewa fedha, namshukuru sana Mheshimiwa

kwa kulisemea hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini amesema kwamba benki hii haifiki Kagera

na maeneo mengine, kwa kweli kazi tunayoifanya mpaka watu wanashangaa,

kwa kidogo ambacho benki inacho. Kufungua tawi la benki ni gharama kubwa

sana. Tumeona kwamba hatuwezi, ndiyo maana tumeshaingia Dodoma, sasa

hivi tumefika Mbeya na tumepewa mpaka maeneo, ingawaje hapa kwa vile

hatujafungua ndiyo maana hatujaweka. Kwa vile tumefika Mwanza,

tunafungua vituo kwenye maeneo yenye usalama. Kwa mfano, sehemu

zilizokuwa Posta ambazo sasa hazifanyi kazi, tunajua kuna ulinzi na kila kitu,

tunapanga pale, tunatoa huduma. Tumefika mpaka Rukwa, tunasubiri kwenda

tu na tumeishakubaliana. Ni lazima tujue tunapata eneo ambalo linaweza

kufananafanana na kutoa huduma za kifedha na ulinzi uwepo. Kwa hiyo, jinsi

tunavyopata hizi fedha za ruzuku ndivyo tutaweza kwenda katika maeneo

mengine. Mwaka mwaka huu ruzuku haikutoka vizuri lakini tunategemea katika

kipindi hiki kifupi cha mwaka huu tutaongezewa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lolesia Bukwimba.

MBUNGE FULANI: Aah, bado.

MWENYEKITI: Hawakutoa shilingi walikuwa wanazungumza tu.

MBUNGE FULANI: Alitoa.

MWENYEKITI: Sikilizeni, nilisema hivi mkimtolea shilingi huyu haisaidii kitu,

tuna utaratibu mwingine wa kutoa shilingi za namna hiyo, let us be serious, tutoe

mahali ambapo tunajua ndiyo penyewe. Mwenyewe hana hata mafuta ya

kuendesha gari lake. (Kicheko)

Mheshimiwa Lolesia Bukwimba!

MHE. LOLESIA J. M. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mimi nilikuwa nahitaji tu ufafanuzi kuhusiana na suala la kuajiri watumishi katika

sekta ya maendeleo ya jamii, hasa katika ngazi ya Kata na Vijiji, kwa sababu

maendeleo hayawezi kuja bila kuwa na wataalam wanaojua shughuli hizo za

maendeleo ya jamii. Mara nyingi katika Halmashauri zetu nyingi ikiwemo

Halmashauri yangu ya Geita, nikitolea mfano Jimbo langu Kata 16 zote hazina

Afisa Maendeleo ya Jamii hata mmoja, maendeleo hayawezi kuja bila kuwa

Page 189: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

189

nao hawa wataalam. Kwa hiyo, ningependa kupata ufafanuzi kutoka kwenye

Wizara kwamba ina mpango gani sasa wa kuhakikisha angalau kwenye Kata

tuwe na wataalam hao? (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, maelezo.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Lolesia kwa swali lake zuri. Nimfahamishe

tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Sera yetu ya Maendeleo ya Jamii ambayo

ilipitishwa kama miaka mitano iliyopita inasema kila Kata ni lazima awepo Afisa

Maendeleo ya Jamii. Tayari tumekuwa tukijitahidi tuwezavyo kupata hao

Maafisa Maendeleo ya Jamii lakini yote inategemea na uwezo wa Serikali

katika kuajiri hao Maafisa Maendeleo ya Jamii. Wote kama tunavyojua sasa hivi

ikama kubwa inaenda kwenye kuajiri Walimu lakini kidogo kidogo nia ya Serikali

ipo hapo kwa vile Sera ile ilipitishwa, tutaweza kupata kila Kata Afisa wa

Maendeleo ya Jamii ambaye atakuwa anachochea maendeleo na

kubadilisha fikra potofu ambazo baadhi ya wananchi katika jamii wanazo na

hivyo kuleta maendeleo kwa kasi zaidi.

MWENYEKITI: Juzi niliwasomea ile Kanuni inayosema Mshahara wa Waziri

mtapitia kwenye vyama vyenu maana naona kuna wengine wanasimama

hapa na mimi nina majina ambayo yameletwa na vyama. Haya Mheshimiwa

Vita Kawawa.

MHE. VITA R.M. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Mimi pia naomba nianze kwa kusema kwamba si kama nimekamata Mshahara

wa Waziri, ila tu nilikuwa nataka nianze kwa kusema kwamba pamoja na ufinyu

wa bajeti Wizara imekuwa ikitekeleza Sera yake ya kuwafikia wananchi kwa

kuwafungulia Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi. Kwa hiyo, nampongeza sana

Mheshimiwa Waziri na Mtendaji Mkuu wa Wizara hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na ufinyu wa bajeti niliwaomba

watufungulie Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Wilayani Namtumbo,

walitufungulia, walitukarabatia majengo na kutujengea maengine na

kutufungulia Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mputa. Mheshimiwa Waziri

mwenyewe alifika na kukifungua chuo kile. Kwa hiyo, wananchi na hasa akina

mama wanamshukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilikuwa naomba kupata ufafanuzi. Kwa

Mheshimiwa Waziri aliona kile chuo ndiyo kwanza kimeanza, majengo mengine

yalikuwa hayajakamilika, naamini kabisa pamoja na ufinyu wa bajeti mwaka

huu atakuwa ametuwekea kidogo kuendeleza pale palipoachiwa mwaka

jana. Kwa hiyo, nilikuwa naomba kupata ufafanuzi kama kwenye bajeti hii kuna

chochote ili wananchi wa Mputa na Wilaya ya Namtumbo waweze kufarijika.

Page 190: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

190

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

MWENYEKITI: Hilo ni swali la kisera! Siyo sera kabisa hapo wewe unataka

kuuliza kama kuna fedha ziko wapi? Sasa hilo tutakapofika kwenye vifungu

vinavyohusika na utapata maelezo. Mheshimiwa Rajab Mbarouk.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti,

nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nitangaze nia au azma yangu

ya kutaka kuondoa mshahara wa Waziri pale ambapo sitapata majibu ya

kuridhisha.

MWENYEKITI: Unaondoa mshahara au unatoa nini? Concepts za humu

ndani siyo kuondoa mshahara, unaondoa nini?

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, eeh, pale

ambapo sitapata majibu ya kuridhisha.

MWENYEKITI: Unaondoa shilingi siyo mshahara.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi

nilitaka niuchukue wote lakini nitaondoa hiyo shilingi, ahsante. (Kicheko)

MWENYEKITI: Mkatalie. (Kicheko)

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo,

naweka nia yangu ya kuondoa shilingi katika mshahara wa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba

alitoa taarifa hapa kuhusu WAMA na akataka twende tuka-Google.

Nimwambie tu kwamba tayari hiyo kazi ya ku-Google sisi wengine tuliishaifanya

na tunaijua WAMA juu chini, chini juu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kwamba WAMA inajishughulisha na

shughuli za kisiasa, japokuwa maelezo ambayo ameyatoa Naibu Waziri,

ameyatoa Waziri lakini udhahiri kupitia WAMA Foundation basi unakuta

kwamba WAMA inajishughulisha na mambo ya kisiasa. Si hilo tu, hata huyo

Mwenyekiti ambaye ametajwa kwamba alikuwa anazunguka kumsaidia mume

wake katika kampeni, ni kweli alikuwa anazunguka lakini alikuwa anatoa ahadi

kwa kusema kwamba iwapo Mheshimiwa Kikwete atashinda katika uchaguzi

huu basi WAMA itafanya one, two, three. Hayo alikuwa anayaahidi, kwa mfano,

Page 191: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

191

kusomesha watoto katika kila Halmashauri, alisema kwamba WAMA itasomesha

watoto katika kila Halmashauri iwapo Rais Kikwete atashinda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na hivyo, nilipoiangalia WAMA Foundation

wakati nina- Google nimekuta Board Members ya WAMA yote ni CCM tupu,

tupu kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ninukuu Board Members, Mwenyekiti

Mama Salma Kikwete ni m-NEC, Makamu wake Mama Zakia Hamdani Meghji ni

Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM na ni m-NEC, Mama Mwanamwema

Shein, ni mke wa Rais, Mama Sophia Simba, hili Waheshimiwa lazima tuliangalie.

(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Waziri ameanza hotuba

yake mpaka amemaliza ameshindwa hata ku- declare interest kuhusu WAMA.

Anaitetea WAMA hapa bila ku-declare interest kwamba yeye ni Board Member

wa WAMA. Wakati huohuo yeye ni m-NEC na Mwenyekiti wa UWT Taifa na

wengine na wengine, wamejaa ma-CCM watupu hapa. Mnaitumia WAMA kwa

shughuli za kisiasa, hili halipingiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri anipatie maelezo ni

kwa nini kwa mujibu wa Sheria za NGOs WAMA hajaifuta mpaka leo? Naomba

majibu ya Mheshimiwa Waziri na kama majibu yake hayataniridhisha basi

nitaondoa shilingi kwenye mshahara wa Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri.

MHE. ABDUL J. MAROMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Naona kwanza ajibu Waziri.

MHE. ABDUL J. MAROMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri.

(Hapa kulikuwa na minong’ono miongoni mwa Wabunge)

MWENYEKITI: Maneno ya nini wakati nimempa nafasi Waziri ajibu?

Wengine midomo inawasha wakati wote. (Kicheko)

Mheshimiwa Waziri, maelezo.

Page 192: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

192

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mama Salma akienda kwenye kampeni

haendi kufanya kazi za WAMA, anafanya kazi kwa niaba ya mumewe,

anamsaidia mumewe. Anasema ndiyo hapa patachimbwa kisima, sasa kuna

ubaya kumsemea mumewe kwamba atakuja kuchimba kisima? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka nitoe mfano, Mama Salma ana shule kule

Nyamisati, hebu kaulize wale watoto wanaosoma pale ni wa CCM? Hatuwajui

hata wazazi wao. Watoto wamechukuliwa Tanzania nzima, kila Mkoa. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Na vitanda vya kujifungulia.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mama Salma

ametoa vitanda vya kujifungulia, vifaa vya hospitali nyingi sana. Wanaolalia

pale ni ma-CCM au ma-CUF? Ametoa msaada huo mpaka Pemba ambako

zaidi ya nusu ni ma-CUF, kwa nini ametoa misaada kule? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kama individual sizuiwi kuwa member wa

NGO yoyote.

WAJUMBE: Kweli, sawa!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Sizuiwi na ninaweza

pia kuanzisha NGO yangu kama nikitaka, ilimradi tu isiingiliane na shughuli

nyingine za kiserikali ambazo nimepewa. Hata hivyo, hilo la kusema wote ma-

CCM mbona UKAWA wote ni ma-CUF na ma-CHADEMA? (Makofi/Kicheko)

MBUNGE FULANI: Ni makubaliano.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Eeh, UKAWA ni ma-

CUF, ma- CHADEMA, sasa tufanyaje? Nakushukuru. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Marombwa.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilieleza nia

ya kuondoa shilingi kama sitaridhika na majibu.

MHE. ABDUL J. MAROMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti…

MWENYEKITI: Kwanza ngoja utaratibu, Mheshimiwa Marombwa unatoa

taarifa tu siyo kujadili hoja hii, kwa sababu haiwezi kujadilika mpaka huyu

bwana atoe shilingi yake.

Page 193: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

193

MHE. ABDUL J. MAROMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi napenda

kutoa taarifa tu kwamba, Mheshimiwa Mbarouk alizungumza kwamba Mama

Salma aliahidi katika uchaguzi ule kwamba endapo Rais Kikwete atachaguliwa

atawafundisha watoto kutoka maeneo yote ya nchi yetu hii ya Tanzania. Hiyo

ahadi si ya kweli. shule ya Sekondari Nyamisati imeanza mwaka 2010, mwezi wa

Machi, hata uchaguzi ulikuwa bado. (Makofi)

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. ABDUL J. MAROMBWA: Wakati huo shule hiyo inaanza ilikuwa

inachukua wanafunzi kutoka Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani, kutoka

katika Wilaya zote za Tanzania Bara na Visiwani, haijali huyu wa chama gani na

wala hakuahidi hilo. Shule ilikuwa imeanza kabla ya uchaguzi wa mwaka 2010

kufanyika. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge asiseme kwamba katika kutembea

kwake Mama Salma katika uchaguzi wa mwaka 2010 ndiko kulikosababisha

yeye awaambie wananchi waichague CCM atawapeleka watoto kwenye

shule ya sekondari, hapana!

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa yako ni kwamba shule ile ndiyo

iliyofanya vizuri zaidi, imefaulisha wanafunzi walioanza mwaka 2010 mwaka 2013

wamefaulu wanafunzi 10 - divisheni I, wanafunzi 20 - divisheni II, wanafunzi 19 -

divisheni III na wanafunzi 19 waliobakia divisheni IV. Wanafunzi hao wametoka

katika Wilaya zote na Mikoa yote ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka tu kumpatia taarifa. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Rajab toa shilingi.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana

na majibu ya Waziri ambayo hayakuniridhisha natoa shilingi ili na wenzangu

wapate nafasi waweze kuchangia.

MWENYEKITI: Ila mfahamu kwamba ulimwengu wote First Ladies

wanakuwa na chombo cha kufanyia kazi, duniani kote. Mimi najua kote kabisa

na mimi nilikuwa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, nilienda kwenye mkutano wa

First Ladies - Geneva. (Makofi)

Mheshimiwa toa shilingi halafu toa hoja yako. Hoja yako iwe specific

maana hapa sijaelewa mara siasa, mara wamekwenda wapi, mara

wamefanyaje, iwe specific tuweze kujadili!

Page 194: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

194

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa

shilingi kutokana na kutoridhika na majibu ya Mheshimiwa Waziri. (Makofi)

MWENYEKITI: Tueleze bwana, unaijenga hoja yako.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu

ambayo Mheshimiwa Waziri ameyatoa hayakuridhisha. Amejaribu kujibu kwa

kutoa mifano ya UKAWA ambayo haipo, UKAWA siyo NGO na wala haihusiani

na hoja ambayo nimeitoa hapa. (Makofi)

MWENYEKITI: Ngoja kwanza, Mheshimiwa Mbunge naomba uketi kwanza

tuelewane.

MHE. MOHAMMED RAJAB MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

MWENYEKITI: Umetoa shilingi maana yake unayo hoja. Sasa unapaswa

uieleze ile hoja yako bila kujali amesema nini ili sisi wote tukusikilize, tujadiliane

halafu tufanye maamuzi. Sasa usitupeleke huku mara huko, hatuelewi unasema

nini. Wewe unapaswa ujenge hoja yako vizuri sisi tukusikilize, una dakika tano.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu

ni kwamba ni kwa nini Waziri asiifute NGO hii kulingana na Sheria ya Usajili wa

NGO ya mwaka 2002. Hiyo, ndiyo hoja yangu naomba ijadiliwe.

MWENYEKITI: Kwa nini aifute? Toa maelezo yako ni kwa nini ifutwe? Ndiyo

maelezo yanayotakiwa.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ifutwe kwa

sababu NGO hii imekiuka Sheria ya Usajili wa NGOs lakini vilevile ni kwamba

inajihusisha na mambo ya kisiasa. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Halima.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono

hoja ya kutoa shilingi. Sababu ya kwanza ya kuunga mkono hoja ni kwamba

Mheshimiwa Waziri hajajibu hoja ambayo tumeizungumza kwamba kwanza

Taasisi ya WAMA ilitumika kisiasa, ilitoa ahadi kisiasa na hiyo shule

anayoizungumza siyo kwamba ada anazitoa Mama Salma mikononi mwake ila

anakuwa funded na USAID, na USAID imem-fund kwa sababu kile chombo ni

cha mke wa Rais kwa ajili ya kuhudumia Watanzania kiujumla na siyo kisiasa.

Hiyo ni moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili ni kwamba Mheshimiwa Sophia Simba

ni Mjumbe katika Bodi ya WAMA. Kanuni zetu zinatueleza kwamba kwanza

Page 195: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

195

kabla hujaeleza chochote unatakiwa ku-declare interest, hiyo ni moja, lakini pili

hiyo interest yako unatakiwa utuambie ni kiwango gani cha maslahi kifedha

ambacho una-benefit kutokana na WAMA. Kwa hiyo, tulitarajia kabla hajajibu

chochote atuambie akiwa Mjumbe wa Bodi analipwa nini, wakati gani na kwa

sababu gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, majibu kama hayo ni muhimu kwa

sababu First Lady siyo wa CCM, First Lady ni wa wote. Inapotokea First Lady

anajibanabana upande mmoja, anatufanya tujiulize. Wengine wanasema watu

tunakatazwa kufanya mikutano Lindi Mjini, First Lady anafanya mikutano Lindi

Mjini kwa sababu anataka kugombea Jimbo. Sasa kwa nini tusipate majibu ya

wazi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana naunga mkono hoja ya

Mheshimiwa Mbarouk, Mheshimiwa Waziri atupe ufafanuzi. Kwanza, a-declare

interest, pili ajibu ni kwa kiwango gani WAMA ilitumia mgongo wake na fedha

za wafadhili kwenda kumpigia kampeni Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho

Kikwete, akiwa mgombea wa Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mtanda!

MHE. SAIDI M. MTANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa

kutounga mkono hoja ambayo imetolewa na Mheshimiwa Mbarouk. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hoja yake kwamba WAMA imekuwa

ikitumika kisiasa naomba hili Mheshimiwa Mbarouk aweze kulithibitisha kwa

sababu hakuna ushahidi wowote ule unaoashiria kwamba WAMA imekuwa

ikitumika kisiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 mimi

nikiwa mgombea na baadaye kuwa Mbunge, sijawahi kusikia wala Halmashauri

yangu haijawahi kuahidiwa kwamba wapo watoto watasomeshwa na WAMA

kwa ahadi hiyo ya WAMA. Kwa hivyo, sifikiri kwamba hoja hii kwa sasa ina

mashiko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia suala la Mama Salma Kikwete kutaka

kugombea Ubunge Lindi Mjini kwanza halihusiki hapa. Halihusiki kwa sababu

yeye binafsi kama kiongozi lakini pia kama raia wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania anao uhuru wa kufanya maamuzi yake. Kwa hivyo, si ajabu kwa

kiongozi au Mtanzania yeyote yule kuamua kuonyesha nia au kutaka

kugombea uongozi katika eneo lolote la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

(Makofi)

Page 196: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

196

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, hoja hii haina msingi na ukilinganisha

na majukumu na kazi kubwa zilizofanywa na WAMA katika nchi yetu ninaomba

kuipongeza WAMA…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Kengele imegonga. Mheshimiwa Machali.

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasimama hapa kuunga mkono hoja ya

Mheshimiwa Rajab Mbarouk Mohammed kwa sababu zifuatazo. Ni uwazi

usiopingika kwamba WAMA kwa upande mmoja inahusika kisiasa. Ushahidi wa

kwanza ni wa Mheshimiwa Waziri mwenyewe ambaye ni Board Member na

ameshindwa ku-declare interest mbele ya Bunge lako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mbali na ushahidi huu wa kwanza

ukiangalia Board Members wengi ambao Mheshimiwa Rajab ameweza ku-

Google na kuwapata wengi ni Makada wa CCM. Pengine ajaribu kuweza

kulithibitishia Bunge lako ni mpinzani gani ambaye ni Board Member wa WAMA?

Watuambie kama hakuna political interest hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mheshimiwa Rajab amesema mwanzoni

kabisa wakati ana-raise hoja yake kwamba Mama Salma Kikwete wakati wa

kampeni aliahidi yeye kama Mwenyekiti wa WAMA atachimba visima. Sasa

kama hivyo ndivyo, anatumia taasisi ya WAMA ambayo ni non-partisan,

haifungamani na upande wowote, sidhani kama ilikuwa ni busara kwa mtu

ambaye anajua kabisa kwamba ni First Lady na First Lady hapaswi

kufungamana na upande wowote alipaswa kuweza kutumia taasisi hiyo

kuweza kutafuta kura za mgombea wa Chama cha Mapinduzi ambaye hivi

sasa ni Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hizo fedha

ambazo zinatumika ni fedha za wafadhili kama USAID pamoja na Development

Partners wengine, hizo fedha sio fedha za Chama cha Mapinduzi. Kama

angekuwa anatumia fedha za Chama cha Mapinduzi katika kuhakikisha

anatekeleza miradi mbalimbali tusingelikuwa na problem.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kwa mujibu wa Sheria ambayo inahusika

na asasi zisizokuwa za Kiserikali NGO’s.

MWENYEKITI: Sheria gani?

MHE. MOSES J. MACHALI: The Non Governmental Organisation Act,

nafikiri ya mwaka 2002.

Page 197: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

197

MWENYEKITI: Kifungu gani?

MHE. MOSES J. MACHALI: Inazuia asasi za kiraia kujishughulisha na shughuli

za kisiasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama anasimama kwa umbrella ya WAMA

na kuanza kutuambia nitachimba visima ili kura za mgombea wa CCM ziweze

kupatikana, ni uvunjaji wa sheria na ni mwendelezo wa vitendo vya kifisadi

ambavyo haviwezi vikakubalika. Tunamtaka Mheshimiwa Waziri aeleze Bunge

lako ni kwa nini taasisi hiyo haijaweza kufutwa na Mwenyekiti wa asasi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niunge mkono hoja.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jafo.

MHE. SELEMANI S. JAFO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Taifa linatuangalia halafu linatushangaa

sana, hilo ndilo jambo la kwanza. Katika hoja ya Bwana Mbarouk, ndugu yangu

aliyosema kwamba miongoni mwa Board Member wote ni wana-CCM,

nadhani kila kitu unachokifanya unaangalia watu wenye kuaminika kwanza.

Katika taasisi yako kuwa na Board Member ambao hata katika kikao watatoka

ndani ya kikao mtashindwa kufanya maamuzi, huwezi ukawaweka katika Board

Member. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, nasema Taifa linashangaa

kwa sababu kuna watu ambao wazazi wao maskini na ni yatima kabisa. Kuna

watoto wengine wanasoma pale wanalia wametoka katika mazingira dhalilifu

kabisa lakini taasisi hii imeweza kuhakikisha hivi sasa wanapata elimu. Nadhani

inaonekana kuna viongozi ambao hawajui matatizo ya Watanzania

tunaowaongoza. Kwa hilo, mimi napata mashaka sana imefikia Wabunge sisi

hapa badala ya kuangalia jamii ambazo ziko katika mazingira magumu

zinasaidiwa tunawapiga vita wale wenye kusaidia ile jamii. (Makofi)

Ndugu yangu Mbarouk nadhani tunafanya siasa lakini katika mambo

mengine lazima tujue kwamba Mwenyezi Mungu kuna mambo mengine

atatuuliza katika masuala mazima tunayofanya. Namwomba mtoa hoja

ikiwezekana afute hoja hii kwa sababu mimi kwa mantiki yangu naona kwamba

haina mashiko katika mustakabali wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kawawa.

Page 198: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

198

MHE. VITA R.M. KAWAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hoja

ya msingi ya Mheshimiwa Mbarouk ni kwamba kwa nini WAMA isifutwe. Mimi

nasema siungi mkono kwamba ifutwe. Nashangaa sana kwa sababu WAMA

imekuwa ikisaidia maisha ya watoto maskini, imekuwa ikisaidia watoto yatima,

nilidhani Mbunge kijana msichana atasifia kazi kubwa inayofanywa kuokolewa

wasichana hawa kwa kusomeshwa leo anaponda kazi iliyofanywa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. VITA R.M. KAWAWA: Lakini pia UNDP au USAID hawa wanaotoa

misaada leo Marekani wamempa awards chungu nzima Mama Salma Kikwete

kwa sababu ya kazi hii nzuri anayoifanya halafu leo sisi Wabunge tunaidhihaki,

jamani lazima tuangalie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi hoja hiyo siungi mkono na namwomba

Mheshimiwa Mbarouk arudishe shilingi ya Mheshimiwa Waziri.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mbarouk maliza hoja.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja

yangu bado haijaisha kwa sababu Waziri hajazungumza lolote.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, haiwezekani

ananitajataja hovyo halafu mimi nimuachie.

MWENYEKITI: Amemaliza maneno yake na huyu mwenye hoja atajibu sio

nyie.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, bado hoja

yangu inasimama palepale.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Kuhusu utaratibu! Waziri bado hajajibu kabla ya

mhitimishaji.

MWENYEKITI: Hiyo ni kweli. Mheshimiwa Waziri jibu, nawe unajadili

anayejibu ni yeye.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi hii ili niweze kujibu. Kwanza nijibu la

maslahi binafsi. Mimi nipo kwenye taasisi ile kama individual ambaye sipati profit

yoyote sipati kitu, tunajitolea. Katika Bodi yetu ile tunafanya kazi kwa kujitolea.

Moja ni kwamba taasisi hizi za wake wa Marais dunia nzima zinashughulika na

Page 199: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

199

Wizara inayoshughulikia masuala ya wanawake au ya jamii na ndiyo maana

niko mle. (Makofi)

MHE. JOHN J. MNYIKA: Taarifa!

MWENYEKITI: Naomba ajibu kwanza. Tunatakiwa wote tufikiri na kusikiliza

sasa kila mtu ana-interrupt tunamsikilizaje?

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, Ibara 61(1) cha Kanuni zetu hizi maslahi binafsi lazima yawe ya

kifedha na lazima utaje kiwango gani. Mimi hapa ni kazi ya kujitolea kwa ajili ya

wananchi, ile ni non profit organization…

MHE. JOHN J. MNYIKA: Taarifa!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Na pale

hatugawani fedha, sisi ni watafutaji, tunashirikiana naye kuhakikisha hizi kazi

anazifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala la kusema WAMA imetumika kisiasa,

nasema si kweli. Mama Salma akienda kwenye masuala ya kisiasa kama mke

wa Rais haendi kama WAMA. Maana angewachukua na Board Members

wake wote pengine, angechukua na staff wote wa WAMA aende nao,

anaenda yeye kama individual, kama mke wa Rais. Kama anapata wasaidizi

wake wale ambao ni haki yake au stahili yake kama mke wa Rais hawezi

kwenda bila kuwa nao lakini hachukui ofisi aende nayo pale na yale masuala ni

ya kisiasa period. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndio anakokwenda kule ni masuala ya kisiasa,

niko sawa.

(Hapa baadhi ya Wabunge walishangilia sana)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJEMENTI YA UTUMISHI WA UMMA:

Yuko sahihi.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, mimi nilichosema kule anakokwenda anafanya masuala ya kisiasa

tatizo liko wapi? Hata hivyo, akiwa WAMA anakuwa na watu wake wa WAMA

tunaenda kufanya mambo ya Ki-WAMA, tunaenda kugawa misaada

hospitalini, shuleni na sehemu mbalimbali WAMA inakwenda lakini kwenye

masuala ya siasa hatuwezi kumkataza mke wako wewe mwanasiasa au mke

wa Rais, wote wanaruhusiwa.

Page 200: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

200

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJEMENTI YA UTUMISHI WA UMMA:

Hata wachumba wanaruhusiwa.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Kama wachumba

wanaruhusiwa sembuse mke. (Makofi/Kicheko)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Rajab.

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza

sikuridhika na majibu ya Waziri na namshukuru kwa kudhihirisha kwamba Mama

Salma anapokwenda katika shughuli zake pamoja na za WAMA anafanya

siasa. (Makofi)

WABUNGE FULANI: Aaaah!

MBUNGE FULANI: Afute kauli!

MHE. RAJAB MBAROUK MOHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini

vilevile Waziri alijaribu kujitetea sana kuhusiana na yeye kuwa Board Member

wakati anajua kwamba yeye kwa nafasi aliyonayo ya Waziri ndiye mtu ambaye

anatakiwa kuzichunguza hizi NGO, kufanya usajili wa NGO na kuziratibu NGO,

wakati huohuo yeye yumo ndani ya NGO unategemea kutakuwa na nini hapo

zaidi ya siasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado sijaridhika na majibu ya Waziri na nazuia

shilingi.

MWENYEKITI: Haya tunafanya maamuzi sasa wote mtulie.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

(Hoja iliamuliwa na Kukataliwa)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mkosamali.

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Nimesimama hapa kutaka ufafanuzi wa kisera na naomba nijibiwe nisiambiwe

kwamba Wizara haina fedha kama wanajua Wizara haina fedha hatuna haja

ya kuwa na Wizara ambayo inazidiwa na Idara ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kupata ufafanuzi juu ya Vyuo vya

Maendeleo ya Wananchi, niliuliza hili swali mwaka jana, mkakati wake ukoje?

Kuna vyuo ambavyo vina zaidi ya miaka 10 havijapata fedha za maendeleo.

Vyuo hivi tunagemea vitumike kuwafundisha watu mambo ya ujasiriamali,

mambo ya ufundi na elimu nyingine katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

Page 201: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

201

Sasa Wizara hii ambayo ipo kama ka-taasisi tu inazidiwa hata na PCCB.

Tunaendesha Wizara kwa gharama kubwa halafu bajeti ya maendeleo ni

shilingi bilioni tisa. Kwa nini tutumie fedha nyingi kuwa na Wizara ndogo ya

namna hii halafu kila mwaka tukiuliza mkakati wa kuendeleza Vyuo vya

Maendeleo haupo, tunaambiwa Wizara haina fedha. Mnapokuwa kwenye

Baraza la Mawaziri huwa hamuwezi kudai ninyi Mawaziri wa Wizara hii

mkapewa fedha kama Mawaziri wengine? Njooni mtueleze hapa mna mpango

gani wa kuboresha vyuo hivi. Pia zile fedha ambazo bado zinapitia Mikoani,

fedha za OC, lini zitakuwa zinakwenda moja kwa moja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hawaelezi namna gani wataboresha vyuo

hivi natoa shilingi kwamba Wizara hii ifutwe kwa sababu hamna sababu ya

kuwa na Wizara ambayo inazidiwa na Idara ya Serikali, tulipe Makatibu Wakuu

na Mawaziri na vitu vingine kwa Wizara ambayo inaweza kuwa taasisi kwenye

Wizara ya kawaida tu huko Wizara ya Afya na vitu vingine. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri!

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ahsante. Kama nilivyosema wakati nafafanua hoja kwamba vyuo

hivi huwa vinakarabatiwa na tunavyo vyuo vya aina mbili. Viko Vyuo vya

Maendeleo ya Wananchi ambavyo viko 55 nchini na tunavyo Vyuo vya

Maendeleo ya Jamii ambavyo kimsingi viko tisa. Vile vyuo tisa vyenyewe

vinakusanya ada, zinakwenda Hazina kuwa accounted halafu zinarudi kama

retention. Kama tulivyosema tumeomba sasa hivi retention iwe at source.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija vyuo 55 viko kwenye mpango wa

maboresho na vinakarabatiwa kila tunapopata fedha. Vyuo 25 sasa hivi

vinatoa program za VETA na vyuo vile vingine viko kwenye Wilaya ambazo

hazina vyuo vya VETA. Kwa hiyo, Vyuo hivi vya Maendeleo ya Wananchi

vinatumika kutoa program za VETA na vile vilivyobaki ili kufikia 55 tumevipanga

kwenye awamu navyo vitatoa program ya VETA. Kwa mfano, Wilaya kama

Njombe hakuna VETA lakini Chuo cha FDC kinatoa program ya VETA, kwa hiyo,

vinakarabatiwa. Sasa hivi nikuhakikishie Mheshimiwa Mkosamali tumetenga

Sh.1,800,000,000 mtakazotupitishia leo tutakapofika kwenye bajeti ya

maendeleo. Pia kuna Education Sector Development Programme ambayo

tunashirikiana na Wizara ya Elimu kuendelea kuvikarabati vyuo hivi.

MWENYEKITI: Ulisema unakusudia kutoa shilingi bado unakusudia?

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Ndio nakusudia.

MWENYEKITI: Haya endelea na hoja yako.

Page 202: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

202

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakusudia kwa

sababu…

MWENYEKITI: Sio unakusudia, ndio umetoa shilingi sasa endelea.

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Naendelea kutoa hoja.

MWENYEKITI: Ukishasema sikuridhika natoa shilingi, sasa unaendelea.

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, vyuo hivi kwa bajeti

hii ukisema unatoa shilingi bilioni moja, kwa nchi hii ni fedha kiasi gani,yaani

shilingi bilioni moja unaweza ukakarabati vyuo vya nchi hii? Tunachosema

hapa ni kwamba vyuo hivi, sasa hivi tuna vijana wengi wanamaliza four four,

form six wanapaswa kwenda kwenye vyuo ambavyo vinatoa ujuzi, vyuo

vinavyoeleweka visiwe vyuo vya ubabaishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa vyuo hivi kama vinaendelea kuwa chini ya

Wizara hii ambayo haina fedha maana yake tutakuwa na watoto ambao

hawapati elimu ya ufundi. Nchi yoyote duniani imeendelea kwa elimu ya

ufundi. Sasa ukarabati tu wa Bunge mmeweka shilingi bilioni nane, vyuo vyote

nchi nzima mmeweka shilingi bilioni moja! Hivyo vyuo vitafanya nini,

vitengenezewe mashine, watu wafundishwe mashine za ujasiriamali za

kutengeneza vitu ndio shilingi bilioni ya kutengeneza hivi vyuo au

mnazungumzia ukarabati wa vitu gani? Hakuna u-seriousness kwenye vyuo

hivyo vya Maendeleo ya Wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja ili hoja yangu ijadiliwe ili

vyuo hivi kama vinabaki chini ya Wizara hii viongezewe fedha na kama

haviongezewi fedha, hii Wizara ifute hizo fedha ziende zote zikaendeleze hivyo

vyuo.

MWENYEKITI: Sasa hoja ni ipi maana lazima tuamue tu unatoa shilingi ili

kitokee nini?

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Natoa shilingi fedha kwa ajili ya vyuo hivi

ziongezeke.

MWENYEKITI: Nadhani katika eneo hilo bado tuna matatizo hatulifanyi

vizuri.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono

hoja ya Mheshimiwa Mkosamali…

Page 203: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

203

MWENYEKITI: Ambayo ni?

MHE. JOHN J. MNYIKA: Ya kukataa kwamba tusiipitishe hii bajeti badala

yake fedha ziongezwe kwa ajili ya hivi vyuo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili ni vizuri likajadiliwa, hatuwezi kukubali

sababu ya kwamba tusubiri Wizara ya Fedha kuiachia hii bajeti ikapita. Kwa

sababu kwa uzoefu mwaka jana tulipokuwa na matatizo makubwa kwenye

bajeti ya Wizara ya Maji, Bunge lilisimama kidete kwa pamoja tukaweka mguu

chini bajeti ya Wizara ya Maji ikaongezewa fedha kwa sababu tuliamua kuwa

sauti moja tulifanya uamuzi. Hoja hii ya Mheshimiwa Mkosamali ikikubalika

itailazimisha Serikali na Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni yuko hapa

Mheshimiwa Waziri Mkuu kuongeza fedha kwa ajili ya jambo muhimu sana la

vyuo hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu kwa maelezo ambayo Naibu Waziri

ameyaeleza hiyo shilingi bilioni moja iliyotengwa ni kwa ajili ya kujenga vyuo

viwili, Chuo cha Maendeleo cha Wananchi Msaginya kwa ajili ya kujenga

madarasa manne tu, Chuo cha Maendeleo ya Mto Mbu yaani ni vitu vidogo

vidogo wakati vyuo viko 55 katika maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi katika mchango wangu wa maandishi

niliiomba Serikali hii, vyuo hivi vinasaidia hata watu wa Dar es Salaam. Kuna

Chuo kimoja cha Maendeleo ya Jamii kiko jirani pale Kibaha nikasema tufanye

mkakati maalum wa kwenda kufundisha vijana kwa wingi mafunzo ya ufundi

stadi, mafunzo ya ujasiriamali na kadhalika. Vyuo hivi vikiwekewa uzito

vitasaidia maeneo mbalimbali ya nchi kwa sababu vimesambaa maeneo

mbalimbali. Kwa hiyo, naunga mkono hoja hii kwamba tusiipitishe hii bajeti

kwenye kifungu hiki tuondoe shilingi ili fedha ziongezwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninapinga hoja

hii kwa sababu kuongeza fedha ni jambo linalowezekana, tunaweza tukapitisha

bajeti hii na tunayo wiki moja, niwaambie Waheshimiwa Wabunge tumeunda

Kamati ya Bajeti, kuna wiki moja ambayo tutafanya kazi ya mashauriano,

tutaiangalia bajeti za Wizara zote, tutaamua kama Bunge wapi tuongeze, wapi

tupunguze ili mradi tusiondoke nje ya ile framework ya bajeti tuliyoipanga.

(Makofi)

Page 204: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

204

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nataka kuwashawishi Waheshimiwa

Wabunge tupitishe bajeti hii lakini katika mambo ambayo tutakayopeleka

kwenye majadiliano liwe la Wizara hii. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Kirigirini, yuko wapi?

MBUNGE FULANI: Ni Kisangi!

MWENYEKITI: Aah ni Kisangi, tumekosea kuandika.

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami siungi

mkono hoja hiyo na ninaungana na Mheshimiwa Peter Serukamba kwamba

Kamati ya Bajeti ipo itafanya kazi, tutajadiliana.

Lakini pia nataka nimwongezee au nimrekebishe mwenye hoja, lazima

aelewe maana ya ukarabati na ujenzi wa kitu kipya. Unapokarabati ni kwamba

unatengeneza kitu kilichobomoka au kilichokuwa kina marekebisho na

unapojenga chuo unajenga kitu kipya. Hapa tumewekewa bajeti ya ukarabati,

naomba uelewe. Ahsante.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Keissy.

MHE. ALLY KEISSY MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Nataka kumpa taarifa Mheshimiwa Mnyika, bajeti ya Maji kweli ilisimamishwa,

wakaongeza lakini Wizara ya Maji haikupewa fedha za bajeti, walipewa robo

ya fedha, hilo ulijue. Hata tukisema bajeti tuisimamishe, fedha hawatapewa,

fedha hakuna, Maji walifanya hivyo. Nilizungumza hapa, waliniuzia mbuzi

kwenye gunia, wewe ulikuwa wapi? (Kicheko)

WAZIRI WA MAENEDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi hii. Ni kweli tumepanga fedha hizo

shilingi bilioni 1,800,000,000 kwa ajili ya ukarabati na kwamba fedha hizi

tutazitumia kwa kazi ambayo imewekwa kama inavyooneshwa kwenye

randama. Tumeamua kwamba hivi vyuo tuwe tunavikarabati kwa awamu kwa

sababu huko nyuma tulikuwa tunapata fedha tunagawa kila chuo,

anakarabati kidogo, kidogo. Sasa kwa sababu ni vyuo viwili, kwa fedha hizi

tulizopata tutamaliza pale, tunaenda kwenye vyuo vingine, ndiyo mpango

wetu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mkosamali.

MHE. FELIX F. MKOSAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Ninahitimisha hoja yangu na napata shida kwa sababu mtu anapokuwa haungi

mkono hoja ya kuendeleza vyuo na yeye Jimboni kwake kuna vyuo, tunataka

tuviinue ili vijana wasome, wapate ajira. (Makofi)

Page 205: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

205

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua, katika kupinga hoja, uwe unapinga kwa

kuangalia unapinga hoja ya namna gani. Sasa wewe unakataa kuunga mkono

hoja kwa sababu ya upinzani ili vijana wakose fedha, vyuo visiboreshwe, vijana

wako kwenye Jimbo lako waendelee kukosa ajira. Hilo ni jambo la kushangaza

sana na kusikitisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa shilingi bilioni moja ni fedha kidogo sana

kwa vyuo hivi. Kama Wabunge wenzangu wangekubali kuniunga mkono,

tungeviongezea vyuo hivi fedha. Mwaka jana kwa mfano, bajeti ya maendeleo

ilikuwa ni shilingi bilioni 11 mwaka huu ni shilingi bilioni tisa, kwa hiyo imepungua.

Nilichokuwa naomba Wabunge wenzangu, vyuo hivi ndiyo msingi, vijana

wanamaliza form four wanafeli mitihani, ndiyo vitawafundisha ujasiriamali,

namna ya kujitegemea na hakuna ajira. Sasa tunapoacha hii shilingi bilioni moja

tunafanya nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, basi mimi naomba tu tupige kura ili nishindwe

kwa sababu maamuzi ya demokrasia ni wengi wape. Nashukuru sana lakini

wananchi wameelewa watu wanaopinga vyuo visiendelee. (Makofi)

MWENYEKITI: Wakati tunapojadiliana hapa ni lazima mtu asikilize hoja

lakini mara nyingi naona tunapiga kelele hata hoja zenyewe huwa hatusikilizi,

kwa hiyo, mtu alichoking‟ang‟ania ni hichohicho mpaka mwisho. Sasa tufanye

uamuzi.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

(Hoja iliamuliwa na Kukataliwa)

(Kifungu Kilichotajwa Hapo Juu Kilipitishwa na Kamati ya Matumizi Bila

Mabadiliko Yoyote)

Kif. 1002 – Finance and Accounts…………..Tshs.670,052,000/=

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kasma

220200, utilities, supplies and services. Mwaka jana kasma hii ilitengewa shilingi

milioni 129, mwaka huu shilingi milioni 216. Kuna utata juu ya mambo matatu

ambayo ningeomba kupata ufafanuzi juu ya kasma hii:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, kwenye randama inaonesha

kwamba fedha za mwaka jana zilikuwa ni shilingi milioni 96 lakini hapa

imeandikwa milioni 129, ningependa kupata ufafanuzi.

Page 206: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

206

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini utata wa pili ambao ni mkubwa zaidi, ni

nyongeza ya hizi fedha. Kama randama hii inasema milioni 96, safari hii

zimekuzwa kuwa milioni 216. Sababu inayotolewa ya ongezeko kubwa namna

hii ni kupanda kwa gharama za umeme kwa sababu hiki kifungu cha utilities,

supplies and services kinatumika kulipia maji na umeme. Sasa ongezeko la bei

ya umeme la asilimia 40 ndiyo inatajwa kuwa sababu ya nyongeza ya kiwango

hiki cha fedha. Sasa najaribu kupiga hesabu rahisi sana, kutoka shilingi milioni 96

ambayo iko kwenye randama hata ningefanya umeme ungepanda kwa

asilimia 50 ni shilingi milioni takribani 50 hivi, ukijumlisha na hii shilingi milioni 96

kwa vyovyote vile haiwezi kwenda mpaka shilingi milioni 216. Sasa ni nini

ambacho kimeongezeka nyuma ya pazia kilichofanya sasa hiki kifungu cha

umeme kifike shilingi milioni 216 tofauti na fedha za mwaka jana ilihali ambapo

Wizara hiihii masuala mengine ya msingi kama hayo ya matengenezo ya vyuo

na mambo mengine yanayohusu wanawake na maendeleo kwa ujumla wake

hayajaongezewa fedha kwa kiwango hiki. Ningeomba ufafanuzi, kwa nini

tuongeze fedha nyingi kwenye kifungu hiki wakati ambapo kwenye vifungu

vingine tunaambiwa kuna ufinyu wa bajeti?

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Spika, ahsante. Kifungu hiki kinajumuisha asilimia kwanza 40 ya ongezeko la bei

ya umeme lakini pia kinajumuisha maji na umeme na pia kuna madeni ya

nyuma, kwa sababu wakati mwingine tunaomba kiwango fulani lakini unapata

less. Kwa hiyo, yale madeni ya nyuma yanapaswa kuzingatiwa katika kifungu

hiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na ile 96 kwamba inatofautiana na

129, ni kwamba ile 96 ni kiwango kilichopokelewa lakini it was budgeted 129,

lakini kilichopokelewa ni 96. Kwa hiyo, hapo tulipaswa kuandika kiwango

kilichopokelewa.

(Kifungu Kilichotajwa Hapo Juu Kilipitishwa na

Kamati ya Matumizi Bila Mabadiliko Yoyote)

Kif.1003 – Policy and Planning……………......Tsh.507,610,900/=

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Najielekeza

kwenye ile subvote 221000, travelling in country. Kimsingi ukijaribu kuangalia kwa

mwaka jana walitenga shilingi 1,800,000/= mwaka huu wametenga shilingi

milioni 49.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimejaribu kufanya sort analysis kuanzia kwenye

mafungu mawili ambayo tumemaliza na kuyapitisha muda mfupi uliopita, kuna

ongezeko kubwa sana la hizi fedha kwa ajili ya ku-travel in country. Sasa nikawa

najiuliza, kwenye bajeti ya maendeleo kwa mfano ya mwaka jana, katika bajeti

ya shilingi bilioni 25 zilitengwa shilingi bilioni 11. Mwaka huu ambapo tena fedha

Page 207: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

207

ya Wizara nzima imeongezeka shilingi bilioni 30, wametenga shilingi bilioni tisa,

fedha za maendeleo zimepunguzwa lakini kwenye fedha za matumizi ya

kawaida Wizara wanajirundikia fedha nyingi ambazo kimsingi justification yake

hai-make sense, naomba nizungumze hivyo. Nasema hivyo kwa sababu hakuna

rationale ya kutoka Sh.1,800,000/= na kuja kwenye shilingi milioni 49. Kwenye ile

subvote ya administration pale tumeona kwenye mshahara wa Waziri

wametenga shilingi milioni 258 kutoka kwenye shilingi milioni 101. Ukienda

kwenye mafungu ya mbele kutoka shilingi milioni nne wanakwenda shilingi

milioni 43…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Machali, tukifika hapa tunaomba tu-

concentrate katika kile ulichouliza, kwa nini imeongezeka?

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Ninafanya

hivyo kwa vile baadaye sitaki kusimama kupoteza muda.

MWENYEKITI: Aha, siyo utaratibu. Wewe sema hivi, mtueleze vya kutosha

hizi zimeongezeka kwa sababu gani, ndilo swali lenyewe, basi!

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Ninaamini hata hao wanaonipinga wanaelewa ni kitu gani nachozungumza.

Naomba nipate kauli ya Serikali ni sababu gani ambazo zimepelekea kuongeza

fedha hizi mpaka kuja kufikia shilingi milioni 49 kwa ajili ya kusafiri tu nchini,

kusafiri tu, kutoka Sh.1,800,000/=? Naomba sababu za msingi na kama sababu

zitakuwa hazijaniridhisha, nakusudia kutoa shilingi. Mheshimiwa

Mwenyekiti, naomba nipate sababu za msingi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, maelezo!

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ahsante. Naomba niseme mbele ya Bunge lako Tukufu kwamba

mwaka wa bajeti uliopita 2013/2014 kifungu hiki…

MWENYEKITI: Sogeza mic kwako.

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mwaka

2013/2014 kifungu hiki kilipangiwa Sh.1,800,000/=. Kifungu hiki kinahusu fedha

kwa ajili ya kulipia nauli kwa ajili ya Maafisa wa Bajeti, kazi hizo zimepangwa

kufanyika nje ya Dar es Salaam, kwa mfano tunapokuja huku Dodoma, Maafisa

wa Wizara yetu lakini pia fedha hizi zinaombwa kwa ajili ya posho ya kujikimu

kwa watumishi 12 wa Idara ya Sera na Mipango na Maafisa 15 wa Wizara

watakaoshiriki kuandaa bajeti na mipango, kazi na mtiririko wa mahitaji fedha.

Page 208: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

208

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana tulipewa fedha ndogo sana,

kulikuwa hamna ujanja, ikabidi tuweke 1.8 kutokana na ceiling lakini matumizi

halisi ndiyo hiyo 49 million. Kwa hiyo 1.8 iliwekwa mwaka jana kwa sababu ya

ceiling kulikuwa hamna ujanja, lakini matumizi yake halisi ni milioni 49.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mkosamali!

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Mheshimiwa

Machali!

MWENYEKITI: Wanasema ni haohao! (Kicheko)

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme

kwamba natoa shilingi. Ninatoa shilingi kwa sababu pamoja na maelezo

ambayo ameyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba mwaka jana

walitengewa fedha kidogo lakini sijasikia hata siku moja kwenye shughuli za

Kibunge Wizara hii walilalamika kwamba ni wapi walikwama kuweza kuja

Dodoma na kwenda kwenye maeneo mengine. Napata shida sana Bunge lako

wakati huu ambao tumefika kwenye Kamati ya Matumizi tunaelezwa kwamba

bajeti ya mwaka jana ni kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema kwamba hata kwenye vifungu

vingine, hali ni hiyo hiyo. Tutaendelea hivi kuweza kupewa majibu mepesi

kwenye maswali magumu mpaka lini? Naomba Waheshimiwa Wabunge

wenzangu pasipokujali majina ya vyama vyetu, hivi vyuo ambavyo pengine

vimekosa fedha na ninasema kwamba fedha hizi pengine tuzipunguze,

tuzihamishe tuzipeleke kwenye bajeti ya maendeleo ambayo imepungua

kutoka shilingi bilioni 11 za mwaka jana na kuja kwenye shilingi bilioni tisa. Watu

wengine mtakataa tu kwa sababu hoja inatolewa na mimi natoka Upinzani,

wewe unatoka CCM lakini elewa kwamba huyo mwananchi ambaye yuko

kijijini ambaye amekosa darasa na dawati la kukalia, siyo wa CCM wala wa

Upinzani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba…

(Hapa kengele ililia kuashiria

kwisha kwa muda wa mzungumzaji)

MWENYEKITI: Kengele imegongwa.

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishie hapo,

bado naendelea kushika mshahara wa Waziri. Naomba kutoa hoja.

Page 209: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

209

MWENYEKITI: Yaani wewe umeishatoa hoja. Mheshimiwa Mdee! Sasa

tunajadili hoja yako, lakini haiko very clear.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Mimi

naungana na hoja ya Mheshimiwa Machali kwamba tunaona kwa trend ya

bajeti ni kweli kwamba Wizara hii inapewa fedha kidogo lakini mwaka jana

Wizara hii ilikuwa na fedha kidogo zaidi kuliko mwaka huu. Mwaka jana bajeti

nzima ya Wizara ilikuwa ni shilingi bilioni 25, mwaka huu bajeti nzima ya Wizara ni

shilingi bilioni 30. Hata hivyo, utaona licha ya kwamba Wizara imeongezewa

shilingi bilioni tano, hizo shilingi bilioni tano badala ya kwenda kwenye

vipaumbele imekwenda kwenye OC, imekwenda kwenye matumizi ya

kawaida. Vilevile tulikuwa tunatarajia kwamba mwaka jana fedha ya

maendeleo ilikuwa nyingi shilingi bilioni 11…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Halima, tunazungumzia ka-sub item haka, kwa

sababu tukiacha open itakuwa kama vile zamani. Tunazungumzia haka, ninyi

mnasemaje?

MHE. HALIMA J. MDEE: Mwenyekiti…

MWENYEKITI: Naomba sana, tukifanya hivyo, tunafungua Pandora’s box.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, hatufungui chochote.

Hoja anayoizungumza Mheshimiwa Machali ni nyongeza ya fedha.

MWENYEKITI: Hii hapa…

MHE. HALIMA J. MDEE: Hiyo hapo.

MWENYEKITI: Ngapi?

MHE. HALIMA J. MDEE: Na hoja naijenga…

MWENYEKITI: Ni ngapi maana mnasema hiyo hapo.

MHE. HALIMA J. MDEE: Shilingi milioni 49.

MWENYEKITI: Ehe, sasa tuzungumzie hiyo.

MHE. HALIMA J. MDEE: Tunasemaje, kwamba Wizara hii licha ya ufinyu

wake wa bajeti kila mwaka, mwaka huu wameongezewa shilingi bilioni tano

lakini badala ya kwenda kwenye project ambazo zina faida za maendeleo,

zimerudi kwenye OC. Ndiyo maana naunga mkono hoja yake kwamba kuna

haja…

Page 210: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

210

MWENYEKITI: Fedha zake huyu ni shilingi milioni 49, hiyo shilingi bilioni tano

iko wapi katika kakifungu haka?

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa…

MWENYEKITI: Jamani, naomba tuelewane. Naomba kwanza ukae.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajenga hoja, huwezi

kujenga hoja kiroborobo!

MWENYEKITI: Mheshimiwa, ukae kwanza, ndiyo utaratibu wetu na kama

mnavunja utaratibu wenyewe basi hatuwezi kufanya kazi vizuri. Tunachokisema,

tukishaondoka kwenye mshahara wa Waziri, huku tukifika tunakwenda kwenye

item by item. Sasa ukituambia shilingi bilioni tano wenzio tunapata tabu ya

kutafuta shilingi bilioni tano, hatuoni. Tunayoona hapa kulikuwa na

Sh.1,800,000/= mwaka unaokwisha, sasa shilingi milioni 49, ndiyo swali la Machali

nafikiri, kwa nini imeongezeka, ndiyo swali la Machali! Hiyo bilioni nyingine sijui

mnatoa wapi, sisi hatuioni. (Makofi)

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee?

MWENYEKITI: Dakika zako zimekwisha.

MHE. HALIMA J. MDEE: Niendelee si ndiyo?

MWENYEKITI: Endelea, uwe kwenye point.

MHE. HALIMA J. MDEE: Ninachosema ilikuwa milioni moja, imeongezeka

milioni 49, sawa sawa? Ninachosema ni hivi, hatuwezi kuruhusu Wizara ambayo

mwaka jana ilikuwa inalalamika haina fedha za maendeleo, imeongezewa

fedha za bajeti zaidi ya bilioni tano badala ya kupeleka kwenye miradi ambayo

ina manufaa, wanajiongezea posho. Hiyo ndiyo hoja anayozungumza hapa.

Pesa za OC zimeongezeka! Kwa hiyo, mimi najenga hoja katika dhana pana

kuja katika hii dhana nyepesi ya shilingi milioni 49. Ukienda katika kila kifungu

wamejiongezea fedha.

MWENYEKITI: Halima, Halima, una akili sana, lakini hapa sivyo! Haya,

tunaendelea, nani mwingine nilimwona, Mheshimiwa Ole-Medeye.

Page 211: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

211

MHE. GOODLUCK J. OLE-MEDEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru

sana Mheshimiwa Machali kwa jitihada anazofanya kuhakikisha kwamba

mgawanyo wa rasilimalI unafanyika kwa uwiano.

MWENYEKITI: Mkosamali, siyo Machali.

MBUNGE FULANI: Ni Mkosamali!

MWENYEKITI: Aah watoto wangu hawa nawachanganya kila siku.

(Kicheko)

MHE. GOODLUCK J. OLE-MEDEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini

ningeomba tu wenzangu na hususan Mheshimiwa Machali tuelewane kwamba

tunapopanga matumizi ya bajeti ya fedha tulizopewa kila Wizara, tunapanga

kwa kuzingatia vipaumbele vilivyo katika Wizara inayohusika. Haiwezekani leo hii

kwa mfano Idara ambayo inahusika na mipango katika Wizara, yenyewe ndiyo

inahusika kuandaa maoteo ya bajeti, inaandaa bajeti, inaratibu mapendekezo

ya bajeti ya Idara zingine zote na kuwasilisha kwenye Kamati mbalimbali

zinazohusika, uwaambie kwamba kwa kuwa mwaka jana hamkupata fedha za

kusafiri na mwaka kesho msiwe nazo, haitakuwa halali na hatufanyi hivi kwa nia

njema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi siungi mkono hoja yake ya

kutaka kutoa shilingi hapa kwa sababu hoja aliyotoa siyo ya msingi na haina

nguvu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

MWENYEKITI: Naomba tufanye maamuzi. Waziri eleza kwanza kwa kifupi.

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ahsante. Kimsingi mwaka jana tulipopangiwa Sh.1,800,000/= Idara

ya Sera na Mipango, katika travel in country ni kitu ambacho hakiwezekani.

Kuna Wabunge hapa akitoka Jimboni akifika hapa tu ile amount anatumia

single person. Hii ni Idara ya Sera na Mipango kwa mwaka mzima Sh.1,800,000/=

bajeti iliyopita, maana yake ni kwamba shughuli zilikuwa zinaenda kwa madeni

(on credit), watu walisafiri bila kulipwa stahili zao na kadhalika. Kwa sababu

tuna wakandarasi wa kutupa ticket labda za usafiri wa ndege au tuna watu

tunachukua bill ya mafuta, kwa hiyo, Sh.1,800,000/= Idara ya Sera na Mipango

mwaka mzima, Waheshimiwa Wabunge hebu tulitafakari, ndiyo maana sasa

hivi imekuwa milioni 49 ikimaanisha ndiyo actual yenyewe lakini pia inakwenda

kulipa na zile stahili ambazo mwaka jana tulifanya on credit bila kupokea haki.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Machali malizia hoja yako.

Page 212: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

212

MHE. MOSES J. MACHALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sasa hivi

umekumbuka na jina langu vizuri. Bado ninasema kwamba majibu ya

Mheshimiwa Naibu Waziri hayajaweza kukata kiu yangu kwa sababu hakuna

namna ambavyo ninaweza kushawishika wakati ambapo ninaona kwamba

walitenga fedha kidogo mwaka jana, hivi vyote ni visingizio tu kwamba ceiling

ilikuwa hiyo mwaka jana na ndiyo tumekuwa tuna experience hiyo wakati

tunapitisha bajeti za Wizara tofauti. Dhamira haipo Serikalini ya kuona kwamba

fedha nyingi inaelekezwa kwenye miradi ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasema hivi kwa sababu kwenye level ya

Kamati hata ile 60% ya kutaka fedha za miradi ya maendeleo kwenye

Halamsahuri zetu iweze kutengwa imekuja kuwa ni mgogoro mpaka tulipokuja

kulazimisha. Kwa hiyo, hata leo sishangai Mheshimiwa Waziri kuendelea kushikilia

msiammo huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mazingira ya kawaida ni ngumu sana

Wabunge wa CCM kuweza kuniunga mkono mtu kama mimi, ninaomba tupige

kura tu ijulikane kuwa wao siku zote hawako kwa ajili ya maslahi ya wananchi.

Ninaomba niishie hapo. (Makofi)

MWENYEKITI: Maneno ya mwisho sahihi, sasa ninawahoji.

(Hoja ilitolewa ilimuliwe)

(Hoja iliamuliwa na Kukataliwa)

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa

na Kamati ya Matumizi bila ya mabadiliko yoyote)

MWENYEKITI: Ninaomba tu–stick kwenye items tusiingie kwenye Pandora’s

box nyingine tulishapita kule, Katibu!

Kif. 1004 – Internal Audit … …. … … …........ Shs. 272,822,500/=

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na

Kamati ya Matumizi bila ya mabadiliko yoyote)

Kif. 1005 – Government Communication

Unit ....................................................Shs.307,028,500/=

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, bado na mimi

ninakuwa na mshangao mkubwa kwa Wizara ambayo inasemekana fedha

yake chache kabisa…

MWENYEKITI: Twende kwenye item.

Page 213: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

213

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Niko kwenye item 221200 inahusu

Communication and Information. Naendelea kuwa na mshangao mkubwa kwa

Wizara ambayo fedha yenyewe ni chache mwaka jana walipewa shilingi milioni

kumi na moja lakini safari hii zimekuwa ni shilingi milioni tisini na mbili kuna

ongezeko la shilingi milioni themanini na moja, pamoja na kwamba kuna haja

ya kuongeza lakini unaongeza kiasi hiki, Wizara ambayo fedha yake ni chache

kabisa? Kwa kweli ninataka ufafanuzi wa kutosha.

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, kifungu hiki kinahusu Government Communication Unit, kwanza

kuna masuala ya matangazo lakini pia kuna masuala ya uanachama. Kwa

kweli kama nilivyosema mwanzo kwamba kipindi kilichopita ilitengwa shilingi

milioni kumi na moja na haikukidhi haja lakini shughuli zilikwenda. Kwa hiyo,

milioni tisini na mbili ndiyo matumizi halisi ya kifungu hicho cha Idara ya

Communication and Information.

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila ya

mabadiliko yoyote)

Kif. 1006 - Procurement Management Unit...Shs.291,993,700/=

Kif.1007-Information, Communication

and Technology.................................Shs.194,622,000/=

(Vifungu vilivyotajwa hapo juu vilipitishwa

na Kamati ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif. 1008-Legal Services Unit……................... Shs. 101,605,900/=

MHE. SUSAN L.A. KIWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki kifungu kwanza

kinaonekana ni kipya.

MWENYEKITI: Kipi?

MHE. SUSAN L.A. KIWANGA: Kifungu cha 1008 lakini ninakwenda kwenye

kifungu kidogo 221300, Education Material, Supplies and Services. Kifungu chote

kwa ujumla pamoja na hiki ninachozungumzia miaka miwili ya nyuma kulikuwa

hakuna chochote lakini mwaka huu wamekitengea shilingi laki mbili na hamsini.

Sasa hapo mimi ninashangaa hii Idara ya Huduma za Kisheria kama inawekewa

hela ndogo namna hii na matatizo yalivyokuwa mengi katika Wizara hii kubwa

ya Wanawake na Watoto, hii hela itaenda kufanya nini katika kifungu hiki?

MWENYEKITI: Ahsante, laki mbili na hamsini elfu.

Page 214: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

214

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO JAMII,JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, hizo ni fedha za kugharamia vitabu kwa mtumishi mmoja tu

atakayehudhuria mafunzo ya muda mrefu kama ilivyooneshwa kwenye

randama lakini Kitengo hiki ni kipya, Wanasheria wetu zamani walikuwa katika

kila Department lakini sasa hivi wote wako katika Department moja.

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na

Kamati ya Matumizi bila ya mabadiliko yoyote)

Kif. 2001- Training and Folk Development

Colleges……............................. Shs. 10,079,302,400/=

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kasma 221400, Hospitality

Supplies and Services. Kasma hii inahusu utoaji wa chakula pamoja na mambo

mengine kwa wanafunzi kwenye Vyuo hamsini na tano vya Maendeleo ya

Wananchi. Sasa vyuo hivi vina jumla ya wanafunzi elfu arobaini mia sita na tisini

na mbili na hizi ni pesa za chakula kwa wanafunzi. Mwaka uliopita zilitengwa

shilingi bilioni moja nukta moja na mwaka huu zimepungua imekuwa ni bilioni

moja peke yake. Kwa maneno mengine hata pesa za chakula kwa wanafunzi

zimepunguzwa kwenye Vyuo vya Maendeleo ya Wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mimi ningependa kupata ufafanuzi kutoka

kwa Waziri na katika eneo hili kama maelezo hayataniridhisha nitaomba

kuondoa shilingi. Ni kwa nini matumizi yote yaliyoonekana ni muhimu

kupunguzwa Wizara imeamua kwenda kupunguza fedha za chakula kwa

wananfunzi kwenye hivi vyuo? Maana yake ni kwamba hali hii ikiachwa

wanafunzi hawa wanaofundishwa ujasiriamali, stadi za kazi na kadhalika, elimu

yao itakwenda kuathirika kwenye vyuo hamsini na tano vilivyoko kwenye Wilaya

mbalimbali za nchi za nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina maslahi katika hili kwa sababu jirani

kabisa na Jimbo la Ubungo, jirani na Kiluvya pale pembeni tu Kibaha, kuna

Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kibaha na ninajua kwamba kuna

wanafunzi kutoka Jimbo la Ubungo wanasoma pale na walikuwa wanalalamika

hata kwa fedha hizi masuala ya chakula yalikuwa hayako vizuri. Sasa

haiwezekani wakati ambapo masuala ya chakula hayako vizuri pesa za

chakula zinazidi kupunguzwa. Jambo hili haliwezi kukubalika, ninaomba

ufafanuzi kwa Wizara ana iwapo hautaridhisha nitaomba kuondoa shilingi

kwenye eneo hili.

MWENYEKITI: Wewe suala lako kubwa hapa kwa mara ya kwanza, ni kwa

nini fedha zimepungua hivyo? Basi, ndio hilo.

Page 215: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

215

WAZIRI WA MAENDELEO JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ni kweli hizi ni fedha za chakula na kutokana na ceiling ya bajeti

kwa jinsi tulivyopanga mipango yetu tumeona tuwapangie hivi. Kubwa ni

kwamba Vyuo vingi vya Wananchi vina mashamba, vinajitegemea, vinalima,

vina matunda na kadhalika. Kwa hiyo, kuna vyuo vingine unakuta vinaweza

kujimudu vyenyewe (self sustained). Kwa hiyo, ndiyo maana kwenye Folk

Development Colleges tofauti na cha Kibaha kuna wengine wanalima

mashamba makubwa na vyuo hivi viko chini ya ulezi wa Halmashauri ambapo

vipo kwa hiyo mara nyingi wanasaidiwa hata katika kulima, wana matrekta na

vitu kama hivyo.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mnyika shilingi yako itoe sasa.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuondoa shilingi

ili Wabunge kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu ambao kwenye Vyuo

vyao, Mheshimiwa Waziri anasema kwa kuwa vina mashamba vina uwezo wa

kujilisha waweze kutoa uzoefu kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitoe uzoefu wa Chuo cha Kibaha

ambacho kabla ya kuwa Mbunge…

MWENYEKITI: Ngoja kwanza, yaani katika maeneo haya ni kuwa focused

maana ukieleza tena habari za Kibaha hizi hela wamegawiwa shilingi ngapi,

hicho chuo unachosema wewe?

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nakaa kwa

sababu ulikuwa umesimama ninaomba niendelee sasa.

MWENYEKITI: Sawa, ndio nakuuliza hapa wamepewa shilingi ngapi?

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya Bunge kwa mujibu

wa Katiba, Ibara ya 63 ni kuishauri na kuisimamia Serikali na kwa kufanya hivyo

tunapitisha bajeti.

MWENYEKITI: Sawa kuna utaratibu.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Katika mazingira ya kazi hiyo, ninaomba nimalizie.

MWENYEKITI: Naomba tuwe focused kwa sababu tunaenda nje.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Ndiyo niko kwenye jambo hilihili moja kwa moja.

Mheshimiwa Waziri alipaswa kutueleza hapa kiwango kinachopungua kutoka

shilingi bilioni moja pointi moja kwenda shilingi bilioni moja peke yake kwa zaidi

Page 216: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

216

ya shilingi milioni mia moja, atueleze sasa hiki kiwango kipya, atupe

mchanganuo hapa vyuo hivi hamsini na tano kila kimoja kitagawiwa kiasi gani ili

tuwe na uhakika hapa kwamba hivi vyuo kweli vitapata chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ila mimi nataka kutoa uzoefu tu kwamba chuo

cha jirani yangu pale Ubungo cha Kibaha mnapowapunguzia fedha kiasi hiki

wanafunzi wanapata shida. Wakuu wa Vyuo wale wakitaka kuziba hili pengo

wanaanzisha michango au gharama kubwa ya ada mpaka katika hivi vyuo vya

chini kabisa vya wananchi. Sasa tukipitisha hii tunakwenda kuwaumiza ama

wanafunzi kwa maana ya kutokupa chakula ipasavyo au kwenda

kuwabebesha mzigo wa gharama na wengine watashindwa kusoma, hivi ndio

vyuo vya maskini na vya ngazi ya chini kabisa. Kwa hiyo, naomba jambo hili

lijadiliwe hizi pesa zisipungue kwa kiasi hiki, sijaridhishwa na maelezo ambayo

Waziri ametoa. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Jafo hii siyo hoja yako, sasa tunajadili hoja ya

Mheshimiwa Mnyika.

MHE. SELAMANI S. JAFO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli siyo

hoja yangu lakini mwanzo nilisimama kwa ajili ya kipengele hichohicho.

MWENYEKITI: Endelea kuchangia.

MHE. SELAMANI S. JAFO: Concern yangu na mimi ilikuwa ni kuihoji Serikali

katika eneo hilo, ni jinsi gani tutafanya hapo, maana ukilinganisha na bajeti ya

mwaka jana mwaka huu tumeshuka. Kwa hiyo, hata mwanzo nilivyosimama

nilitaka tuzungumze hoja hiyo pamoja na Mheshimiwa Mnyika kwamba kwa nini

hizi pesa haswa kwa suala zima la chakula kwa vijana zimeshuka zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaomba kauli ya Serikali hapa ni jinsi

gani itafanya utaratibu wa kuhakikisha kwamba vijana wetu hawaathiriki kwa

sababu tunajua bajeti hii mwisho wa siku ni kwamba vijana wale walioko shuleni

watapata shida. Kwa hiyo, tunaomba kauli ya Serikali, tutafanyaje hapa ili

vijana wetu wasiweze kuathirika katika suala zima la chakula ambalo ndilo

msingi wa masomo kwa vijana wetu wakiwa vyuoni, ahsante.

MHE. SALUM K. BARWANY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga

mkono hoja ya Mheshimiwa Mnyika lakini nizungumze kidogo na Wabunge

wenzangu.

MWENYEKITI: Tuwe kwenye hoja hii, hakuna kuzungumza na Wabunge

wenzako.

Page 217: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

217

MHE. SALUM K. BARWANY: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naunga mkono,

kufanya hivyo ilivyo itaonyesha dhahiri kabisa tunawabebesha mzigo wazee

ambao watoto wao ni maskini, wanahitaji kupata huduma hii vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina-declare interest kwamba ni Mjumbe

wa Kamati ya Maendeleo ya Jamii na kuna Wabunge wenzangu humu ndani

tunatoka katika Kamati hiyo pamoja na Mawaziri walioko mbele yetu,

tumekubaliana pamoja twende Bungeni tukawasaidieni ili Wizara iweze

kukamilisha majukumu yake. Sasa ajabu ni kwamba tunapojitahidi kujenga hoja

hii ili Serikali ione umuhimu wa kuboresha Wizara hii bado Wabunge wengine

ambao tumekubaliana mle ndani tunapinga hoja hii ndani ya Bunge hili,

tunafanya hivi kwa maslahi ya nani? (Makofi)

Mheshimiwa Waziri umetuambia tuje tukusaidie hapa Bungeni ili hii bajeti

iweze kuongezewa pesa lakini sasa inaonekana kuwa Wapinzani ndiyo wenye

hoja hiyo, Wabunge ambao tuko ndani ya Kamati ile tunashindwa kumsaidia

Mheshimiwa Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninaunga mkono hoja ya Mheshimiwa

Mnyika. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Kuhusu utaratibu.

MWENYEKITI: Kama ndiyo hivyo, ngoja tuzungumze. Utaratibu ambao upo

katika mfumo wa new budget system kila Kamati iliyokuta mahali palikuwa

contentious wameandika na iko Kamati inayopokea na hivi sasa wanaendelea

kuchambua vitu kama hivyo. Kama mlizungumza hivyo kwenye Kamati yenu na

kule kwangu dokezo limeletwa linalohusu mambo hayo. Ndiyo maana siku ile

nikawaambia haya mapitio tunayopitia hapa ni provisional kwa sababu

kutatokea mabadiliko mengi tu. Ndiyo maana unakuta Wizara kubwa ile maji

kwa sababu mwaka jana tulikuwa na priority ya maji, tulikuwa tuna priority ya

umeme, tulikuwa na priority ya eneo fulani…

(Hapa baadhi ya Wabunge walikuwa wanaongea)

MWENYEKITI: Naomba mnisikilize kwani tukisikilizana ndiyo tunaelewana

lakini tukiwa tunataka kila mtu anavyotaka haiwezekani, ninasema utaratibu

wetu uko hivi. Kwa hiyo, kila Wizara wanapitisha kwangu lakini imeundwa unit

wanapokea na kupeleka kwenye Budget Committee. Kwa hiyo, Budget

Committee inaangalia yale mliyokubaliana kwenye Kamati yenu kwamba hii

hela haitoshi inakwenda kule. Sasa Budget Committee itaangalia wigo wote wa

matumizi ya Serikali na kwamba kama ni finyu sasa tuweke nguvu mahali gani.

Ndiyo maana nikawaambia makadirio tunayopitisha sasa hivi kwa kiwango

fulani ni provisional kwa sababu yatakapotoka kwenye Budget Committee siyo

Page 218: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

218

kwamba kutakuwa na hela zingine tutazi-reshuffle hizihizi. Sasa na Kamati hiyo

ya kwenu nayo wameleta kwangu dokezo, kwa hiyo siyo kwamba mbishane

hapa hamuwezi kuongeza, kubishania hapa ongeeni tu lakini ni kwamba

mnajenga hoja. Ndiyo tunavyofanya kwenye Budget Committee sasa.

Mheshimiwa Susan.

MHE. SUSAN A.J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi napenda niunge

mkono hoja ya Mheshimiwa Mnyika kuhusiana na fedha ndogo za chakula

katika vyuo hivi. Ni kweli kwamba kwa sasa hivi vyuo vingi vinakosa chakula na

matokeo yake hasa kwa watoto wa kike wanajiuza na kwa maana hiyo

tutasema kwamba Serikali hii inasababisha watoto wetu wapate magonjwa

mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo nilikuwa ninaiomba sana Serikali

ihakikishe kwamba suala la chakula kwa wanafunzi wetu siyo tu wa vyuo hivi,

wa vyuo vyote wanapata fedha zao kwa wakati ili tuepukane na tatizo la

watoto wetu hasa wasichana kujiuza na hivyo kuliletea Taifa hili athari kubwa za

magonjwa ya kuambukiza. Nashangaa Wizara hii inaongozwa na wanawake

lakini wanaona ugumu kutetea suala la fedha kwa watoto wetu wa kike

ahsante. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante ila umezidisha, Mheshimiwa Serukamba.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Mheshimiwa

John Mnyika ukiangalia fedha iliyopunguzwa ni shilingi milioni mia moja,

ukichukua shilingi milioni mia moja kugawa kwa watoto hao elfu arobaini

maana yake kilichopunguzwa ni shilingi elfu mbili na mia tano. Nataka

tukubaliane kwamba Bunge hili, kwamba elfu mbili na mia tano maana toka

mwaka jana mpaka mwaka huu kilichopungua ni shilingi elfu mbili na mia tano

tu kwa ile ambayo ungempa kwa mwaka huyo mwanafunzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninaamini chuo kama cha Kihinga

wanachuo wengi wanakaa nyumbani. Kwa hiyo, siyo kweli kwamba vyuo vyote

watu wanakaa kwenye hosteli. Kwa sababu hiyo ni lazima tutarajie gharama

kupungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine ambalo ninataka kusema

zinaonekana fedha zimeongezeka bilioni tano lakini zimeongezeka kwenye

mshahara na sisi wenyewe tumekuwa tukisema kwamba wafanyakazi wa nchi

hii waongezewe mshahara. Kwa hiyo, tulipokuwa tunalalamika kwa nini

tumeongeza shilingi bilioni tano ni kwa sababu ukiangalia hapa hata kwenye

college tumeongeza shilingi bilioni nne kwa ajili ya mshahara. (Makofi)

Page 219: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

219

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi siungi hoja yake kwa sababu

ninaamini fedha hii hatuna pa kuitoa kwa sababu wanafunzi wanakaa

nyumbani.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri.

WAZIRI WA MAENDELEO JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ninaomba niongezee tu kwa kusema kwamba kule kwenye hivi

Vyuo vya Wananchi zile ada zinazotolewa zilikuwa ndogo sana ndiyo maana

tumekuwa tukiwapelekea hizi pesa lakini zile fedha zinazopatikana zinabaki

kulekule zinasaidia pia katika kununua chakula. Kuna cost sharing baina yetu sisi

na wao, hizi ni nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tumewashauri waongeze, ada ilikuwa

ndogo sana, kwa hiyo wameongeza ada kidogo itasaidia kuziba lile gap. Hizi

fedha tulizowapelekea ni sehemu tu zile ambazo wanatoa kama ada inabaki

kule itawasaidia kuongezea kwenye chakula.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mnyika, naomba tu-stick to the point otherwise

tunaogelea every where.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna shaka nitajikita

kwenye jambo hilihili. Utaona mgongano mkubwa kati ya mchango wa

Mheshimiwa Peter Serukamba aliyedai kwamba kwa sababu wanafunzi

wanakaa nyumbani wataweza kujihudumia hakuna haja ya kuongeza hela ya

chakula na majibu ya Mheshimiwa Waziri ambaye anakiri kwamba kweli

kutakuwa na tatizo na ufumbuzi wa hilo tatizo wanakwenda kuongeza ada kwa

wanafunzi kule chini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua tofauti na vyuo vingine hizi Community

Folks, ni vyuo vya chini kabisa vya wananchi wa kipato cha chini kabisa kwa ajili

ya kujisaidia kujikwamua. Sasa haiwezekani Vyuo vya Wananchi wa kipato cha

chini kabisa kuwafundisha ujasiriamali, kuwafundisha maarifa walioshindwa

kwenda chuo kikuu au vyuo vingine vya elimu ya juu ili angalau wajiajiri na

vyenyewe tunaendelea kuwaongezea kodi kwa sababu ambazo hazina msingi

kwani kuna mafungu mengine ambayo tungeweza kuziba kabisa kuziba hilo

ombwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi siridhiki na jambo hili na

ningeomba lipigiwe kura ili wale ambao wanataka kwenda kuwaongezea

ugumu wa maisha wale watu kule vijijini kwenye Wilaya mbalimbali wapige kura

ya „ndiyo‟ na sisi ambao tunaona kwamba kuna maeneo mengine ambayo

Serikali hii inaweza kubana matumizi kwa ajili ya kwenda kuwasaidia chakula

wanavyuo waweze kusoma kwa ufanisi tupige kura ya kuunga mkono hoja hii.

Page 220: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

220

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

MWENYEKITI: Mna-politicize, hizi ni fedha kidogo tu. Sasa tunafanya

maamuzi.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

(Hoja ilimuliwa na Kukataliwa)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Paresso!

MHE. CECILIA D. PARESO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nilikuwa

nataka tu ufafanuzi kidogo kwenye kasma 210100 - Basic Salaries. Ukiangalia

mwaka jana ilikuwa shilingi 4,000,000,000 na sasa hivi ni shilingi 8,000,000,000,

kuna ongezeko kubwa sana. Tungependa kufahamu ni Watumishi wangapi

wameongezeka?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri maelezo!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ahsante. Wameongezeka Watumishi 295, lakini pia kuna ongezeko

la mishahara.

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif. 2002 - Community Development…………Sh.3,839,970,800

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

MWENYEKITI: Mheshimiwa tumepita tuendelee.

MHE. SELEMANI S. JAFO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka tupate ufafanuzi

katika…

MWENYEKITI: Tumeshapitisha tumesema Ndiyo tayari.

MHE. SELEMANI S. JAFO: Okay, sawa.

Kif. 2003 - Community Dev. College - Tengeru Sh.1,136,267,100

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Page 221: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

221

Kif. 3001 – Gender Development…………………Sh.723,144,200

MWENYEKITI: Mheshimiwa Rashid!

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nipo katika

Item 221000, inayohusu Travel- In-Country.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana kifungu hiki kilitengewa shilingi

milioni kumi, lakini mwaka huu kimetengewa shilingi milioni 152; ni ongezeko la

shilingi milioni 142! Mheshimiwa Waziri alisema kwamba, katika Halmashauri

wapo Maafisa wake mbalimbali wa Huduma za Jamii ambao wanashughulikia

masuala yanayojitokeza kule. Kwa nini fedha hizi zinaongezeka kwa kiasi

kikubwa kama hiki katika Wizara ambayo inasema haina fedha? Naomba

maelezo.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, huko nyuma anaona ilikuwa milioni mbili, milioni kumi. Hapa pana

kazi nyingi sana za kusafiri. Department hii ndiyo inayoshughulikia masuala ya

ukatili wa wanawake Kanda ya Ziwa. Kila mahala hawa ndiyo wanaokwenda.

Vilevile hapa kuna madeni makubwa sana ya tiketi za ndege, masuala ya safari

pamoja na mambo mengine yanayohusiana na kusafiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu ilipata OC asilimia 25 tu. Hii ina

maana hizi pesa nyingi ambazo mnaona zimeongezeka ni ile asilimia 16

ambayo tumeongeza na tutalipia madeni katika Departments mbalimbali.

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif. 3002 - Children Development… … …………Sh.357,079,676

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif. 4001 - Non-Government Organizations……Sh.425,273,312

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti. Kasma 229900 - Other

Operating Expenses, Matumizi Mengineyo. Mwaka juzi hakikutengewa fedha,

mwaka jana hakikutengewa fedha, mwaka huu kimetengewa shilingi milioni 25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Randama ya Wizara, kifungu hiki

ni kwa ajili ya kulipa posho ya Vikao vya Bodi, shilingi milioni tano na shilingi

Page 222: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

222

milioni 20 ni kwa ajili ya kumlipa Mtaalamu Mwelekezi kwa ajili ya kufanya

tathmini juu ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma Hotuba ya Waziri ameeleza kwamba,

kila mwaka wamekuwa wakifanya tathmini juu ya Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

Tafsiri yake ni kwamba, Wizara imekuwa ikifanya tathmini na kuandaa Ripoti na

imetueleza Ripoti kuhusu utendaji wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali. Ghafla safari

hii kuna suala la Mtaalamu Mwelekezi wa kuandaa hiyo Ripoti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ningeomba ufafanuzi wa Wizara kwa nini

safari hii wanaamua kutumia Mtaalamu Mwelekezi wakati kuna Maafisa wa

Wizara ambao wameajiriwa kwa ajili ya kufanya kazi hiyo na wamekuwa

wakiifanya? Iwapo sitaridhika na ufafanuzi kwenye jambo hili, nitaomba kutoa

hoja, kwa mujibu wa Kanuni ya 102 ya kuhamisha kiwango cha fedha kitoke

katika kijifungu hicho kihamie kwenye kijifungu kingine cha 221600 - Printing,

Advertizing and Information Supplies and Services, ili sasa kwanza, kabla ya

kwenda mbele tuweze kuchapishiwa ripoti za tathmini za mwaka jana, ziletwe

hapa Bungeni tuzijadili ili tuone Mashirika yasiyo ya Kiserikali yaliyofanya vibaya,

Mashirika yaliyofanya vizuri, Mashirika yaliyotumika, tuje tuyajadili hapa. Kwa

hiyo, hizi pesa zitumike kuchapishia ripoti tuletewe Bungeni.

Kwa hiyo, naomba ufafanuzi, nisiporidhika naomba nafasi ya kutoa hoja,

kwa mujibu wa hii Kanuni ya 102, ili niweze kuhamisha hilo fungu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri!

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ahsante. Katika kifungu hiki, Wizara ina mpango wa ku-review Sera

ya NGO na kufanya tathmini ili iweze kufanya kazi vizuri zaidi. Tangu tuanze

mpaka sasa tumefikia wapi, kuna malalamiko mengi na kuna mambo mengi

ambayo tunataka tujue baada ya hii Sheria kutungwa na hii Sera kuwepo. Sasa

hizi ni kweli zitatumika katika shughuli hiyo ya kuwa na Mtaalam Mwelekezi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa ulisema unataka kutoa shilingi? Ulisemaje?

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kutoa hoja siyo

ya kuondoa shilingi ila kwa mujibu wa Kanuni ya 102, Fasili ya Pili na naomba

Wabunge zangu waniunge mkono…

MWENYEKITI: Itabidi u-justify kwelikweli kwamba, hizo printing ziko wapi.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna shaka.

Nilichokuwa nakisema hapa, naomba kutoa hoja kwamba, hii milioni 20 hii

iliyoko hapa, badala ya kulipwa Mtaalamu Mwelekezi mmoja, hizi pesa

Page 223: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

223

zihamishiwe kwenye kifungu cha machapisho ili ripoti za utafiti za miaka iliyopita

ambazo tunaelezwa tu kijuujuu hapa na Wizara, ziweze kuchapishwa na ziletwe

hapa Bungeni. Tujadili kwanza ripoti zilizotangulia kwa sababu kama ni tathmini

ya Mashirika, tayari Wizara inayafanya tathmini ya Mashirika kila wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili jambo ni la msingi sana na niseme tu

kwamba, nasikitika Mheshimiwa Waziri amelidangaya Bunge. Anapaswa

kutuambia kipi ni cha kweli; kwenye Randama hajasema kwamba, Mtaalamu

Mwelekezi ni kwa ajili ya kufanya mapitio ya Sera, hapana! Mtaalamu

Mwelekezi ni kwa ajili ya tathmini ya utekelezaji wa Sera. Maana yake tathimini

ya utendaji wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali ambayo kila mwaka imekuwa

ikifanyika.

Kwa hiyo, maelezo aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri, yasikubalike badala

yake tusiende kumlipa mtu mmoja hizi pesa. Pesa hizi ziende kutimiza kazi

ambayo sisi wote Wabunge tunashiriki, ikiletwa hii ripoti humu tutaweza kubaini

NGOs zilizokiuka Sheria katika masuala mbalimbali ikiwemo hii ya WAMA

ambayo tulikuwa tunaijadili hapa. (Makofi)

MWENYEKITI: Hapo unachanganya mambo! Sasa sisi kama kule haipo ni

kitu gani hicho tunachokubali kihamishiwe kikaprintiwe hatukioni? Kitu gani

tunacho-print? Kanuni ya 125 kwanza ni kinyume cha PPR.

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kanuni ya 102 inasema

hivi: “Katika Kamati ya Matumizi, Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja ya

kutaka kufanya mabadiliko katika Makadirio ya Matumizi ya Serikali, iwapo

mabadiliko hayo hayatabadili madhumuni ya Fungu lile lote.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi sibadili madhumuni ya hili Fungu

la uratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali. Fasili ya Pili inasema kwamba,

endapo hoja iliyotolewa kwa ajili ya kupunguza kifungu fulani katika Fungu

lolote haijapitishwa, hoja nyingine inaweza kutolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Kanuni hii, tunaruhusiwa kutoa hoja ya

kupunguza kiwango na kuhamishia kwingine. Ninachokisema ni kwamba, Waziri

amesema hapa, tayari wamekwishafanya tathmini ya Mashirika yasiyo ya

Kiserikali na wamefanya utafiti. Hiyo ripoti sisi hatujaiona! Kwa hiyo, sasa natoa

hoja kwamba, milioni 20 badala ya kumlipa mtu mmoja kufanya kazi ambayo

kila mwaka Wizara ilikuwa inaifanya, zihamishiwe kwenye machapisho ili sasa

tuletewe ripoti Bungeni, tujadili juu ya performance ya Mashirika yasiyo ya

Kiserikali.

Page 224: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

224

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja na Wabunge wenzangu

waniunge mkono na ambao wapo tayari kuijadili waijadili.

(Hapa Wabunge fulani walisimama)

MWENYEKITI: Naomba mkae chini. Hoja za wakati wa matumizi ya fedha

haziungwi mkono. Hoja ya shilingi ndiyo nzuri inachangiwa. Mheshimiwa Mnyika,

tunaendesha hii kitu kwa kufuata taratibu. Hoja ya kuondoa shilingi Kanuni yake

inasema mnaweza mkajadiliana hapa na mantiki yake ikaeleweka. Sasa hapa

tukianza kwamba, unahamisha shilingi wakati hoja yenyewe hukutujengea vizuri

sisi wenzako ukatuambia hapa hasara zake ni nini na huku faida yake ni nini;

hatuwezi kufanya maamuzi hapa, tutavuruga bajeti yote iliyoko hapa.

Kwa hiyo, hoja yako hata kama ni nzuri hivyo, lakini tunaiona imeelemea

upande mmoja. Tunapoamua kufanya bajeti lazima tuwe na hoja. Ukiondoa

hoja ya shilingi na ina mwisho wake, ile ya shilingi inasema kwamba utachukua

shilingi yako hata kama wakikuunga mkono itapita bajeti lakini inaondoka kwa

shilingi moja. Huu ndiyo utaratibu, lakini hii ni hoja mahususi ya kubadilisha.

Usome kifungu kingine kile, kipo kingine kinachozungumzia namna ya

kubadilisha matumizi ya fedha. Kwa hiyo, mimi hii hoja siikubali kwa sababu

inaleta fujo katika utaratibu wa kazi. (Makofi)

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

MIPANGO YA MAENDELEO

Fungu 53 - Wizara ya Maendeleo Jamii, Jinsia na Watoto

Kif.1001 - Administration and HR Management..Sh.700,000,000

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif.1003 - Policy and Planning………...………..Sh.451,153,880

MWENYEKITI: Mheshimiwa Susan umesimama au unafanya nini, maana

yake na nguo umevaa na matambaa basi hatujui kama unavaa kanga au vipi!

Haya Mheshimiwa Susan! (Kicheko)

MHE. SUSAN A.J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kifungu

1003, kifungu kidogo cha 6290 - Programming and Data Processing Project

chenye total ya 300,000,000.

Page 225: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

225

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba maelezo kutoka kwa Mheshimiwa

Waziri, kwa sababu kifungu hiki hela zinazoombwa hapa hakiendani na

Randama, zinahusiana vilevile na training. Sasa naomba kujua inakuwaje fedha

za training zinakuwa kwenye maendeleo wakati tuna kifungu kule nyuma

kwenye re-current ambacho pia kinahusiana na masuala hayo?

MWENYEKITI: Mheshimiwa Waziri, umekiona hicho kifungu? Tunaomba

maelezo.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, hiki kinazungumzia Programming and Data Processing Project; hii ni

Project ndiyo maana imeingia kwenye Miradi. Hii itafanywa kuwajengea

Maafisa Bajeti wa Wizara, uwezo kuhusu ukusanyaji wa takwimu, ufuatiliaji na

tathmini ya kuandaa mfumo wa ufuatiliaji tathmini, kukusanya takwimu za awali

zinazohusu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na kununua

vitendea kazi kwa ajili ya matumizi ya Wizara.

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila

mabadiliko yoyote)

Kif.1005 - Government Communication Unit……Sh.60,000,000

Kif.1008 - Legal Service Unit………………….…..Sh.28,700,000

Kif. 2001 - Training and Folk Development

Colleges ......................................................Sh.1,842,732,520

Kif. 2002 - Community Development………..….Sh.61,000,000

Kif. 2003 - Community Development

College-Tengeru…...........................................Sh.939,000,000

(Vifungu vilichotajwa hapo juu vilipitishwa na Kamati

ya Matumizi bila mabadiliko yoyote)

Kif. 3001 - Gender Development……………. Sh.4,393,340,000

MHE. RAJAB MOHAMED MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, Subvote

3001, Kifungu 4943 - Women Enomic Empowerment Project ambacho kina

shilingi bilioni nne.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuangalia Randama, nakuta kati ya

fedha hizi, bilioni mbili ni kwa ajili ya Benki ya Wanawake. Benki hii ya

Wanawake inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 99 na asilimia moja tu ndiyo

inamilikiwa na watu wengine. Kwa hiyo, ni kusema kwamba, sasa hivi Benki hii

ina wajibu wa kuwa Shirika la umma. Mbali na hivyo ni kwamba, Benki hii

Page 226: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

226

haijawahi kukaguliwa, haijapeleka hesabu zake kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu

za Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokitaka mimi ni commitment tu ya Serikali

kwamba katika mwaka ujao hii Benki itapeleka hesabu zake kwa Mkaguzi Mkuu

wa Serikali ili zifanyiwe ukaguzi kwa sababu hii siyo Benki ya kisiasa.

MWENYEKITI: Mimi nafikiri ungeuliza hii Benki inakaguliwa na nani? Hata

iwe hela yake useme inakaguliwa na nani?

MHE. RAJAB MOHAMED MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru

kwa kuniwekea sawa.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa

Mwenyekiti, ahsante. Benki hii inakaguliwa na MS Innovates, ambao

wameteuliwa na Controller and Auditor General.

MWENYEKITI: Samahani, Mheshimiwa Mnyika nilimruka.

T A A R I F A

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo kwenye kasma hiyo

ya 49, ila kwa sababu imeshaamuliwa, nampa tu taarifa Mheshimiwa Waziri,

ukaguzi wa mwaka huu wa CAG umesema kwamba, Mkaguzi Mkuu ame-query

kuwa Benki hiyo haikaguliwi na Mkaguzi Mkuu na ametaka ikaguliwe na

Mkaguzi Mkuu. (Makofi)

Advantage ya kufanya hivyo siyo kwa ajili ya kuzuia mianya ya matumizi

mabaya ya fedha. Jambo kubwa ni kwamba, CAG angekuwa anakagua, hivi

ambavyo Serikali hai-comply bajeti; kwamba, bajeti inapitishwa Benki ipewe

bilioni mbili, Serikali inatoa milioni 450 peke yake, CAG angeweka query ya

maana sana juu ya compliance ya Serikali.

MWENYEKITI: Haya mambo ya CAG muwe mnatusomea hapo

palipoandikwa maana tunasikia CAG, CAG, sisi hatujasoma!

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia kusema

kwamba, bado kama alivyosema Mheshimiwa Mbarouk, commitment ya

Serikali, Benki hii sasa ikaguliwe moja kwa moja na CAG, kama CAG mwenyewe

alivyosema kwenye Taarifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali, itawasaidia

Wanawake wa Tanzania.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa!

Page 227: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

227

MWENYEKITI: Taarifa ya kuhusu nini?

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kuwapa

taarifa rafiki yangu Rajabu na Mnyika kuwa Mabenki yote Tanzania yapo

registred under BoT Act na Msimamizi Mkuu anayefuatilia kujua kama Benki hii

inafaa kuendelea kuwa Benki ni Benki Kuu. Kwa hiyo, kama Benki hii

haipelekewi mtaji, maana yake by now ingekuwa imeshanyang‟anywa leseni

na Benki Kuu.

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila

mabadiliko yoyote)

MHE. JOHN J. MNYIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, amesema taarifa na

mimi nina haki ya kujibu hiyo taarifa.

MWENYEKITI: Bwana hizo taarifa na sisi wote tunajifunza. Tunaendelea!

MHE. JOHN J. MNYIKA: Maana amenipa mimi hiyo taarifa na kuna ripoti

hapa kutoka kwa CAG, jambo hilo analolisema halina uhalisia.

Kif. 3002 - Children Development … … … … Sh. 541,617,600

(Kifungu kilichotajwa hapo juu kilipitishwa na Kamati ya Matumizi bila

mabadiliko yoyote)

(Bunge lilirudia)

T A A R I F A

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

naomba kutoa taarifa kwamba, Bunge lako Tukufu, limekaa kama Kamati ya

Matumizi na kuyapitia Makadirio ya Matumizi ya fedha ya Wizara ya Maendeleo

ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka 2014/2015, kifungu kwa kifungu na

kuyapitisha bila mabadiliko yoyote. Hivyo basi, ninaliomba Bunge lako Tukufu

liyakubali makadirio haya.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naafiki.

Page 228: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

228

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

(Hoja iliamuliwa na Kuafikiwa)

(Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto kwa Mwaka 2014/2015

yalipitishwa na Bunge)

Hotuba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Kama Ilivyosomwa Bungeni

Makadirio ya Matumizi ya Serikali kwa Mwaka 2014/2015 Wizara ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI: Mheshimiwa Spika, kufuatia

taarifa iliyowasilishwa hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya

Bunge ya Huduma za Jamii, kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, naomba Bunge lako Tukufu sasa likubali

kupokea, kujadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya

Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa mwaka 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi

Mungu, mwingi wa rehema, kwa kunijalia afya njema na kuniwezesha kutimiza

majukumu yangu kama Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

Mheshimiwa Spika, napenda kutumia fursa hii kuwapongeza Rais wa

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete,

Makamu wa Rais Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu

Mheshimiwa Mizengo Kayanza Peter Pinda, kwa kuiongoza nchi yetu vema na

kwa utekelezaji mzuri wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2010.

Mheshimiwa Spika, napenda kukupongeza wewe mwenyewe, Naibu

Spika, pamoja na Wenyeviti wa Bunge, kwa uendeshaji bora wa shughuli za

Bunge.

Nachukua fursa hii, kuwapongeza na kuwashukuru wasaidizi wangu wa

Wakuu walioteuliwa hivi karibuni na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano

wa Tanzania, ambao ni Naibu Waziri, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama,

Mbunge wa Peramiho; Katibu Mkuu, Profesa Sifuni Ernest Mchome; na Naibu

Katibu Mkuu Bibi Consolata P. Mgimba. Aidha, napenda kuwapongeza na

kuwashukuru kwa ushirikiano mzuri, Kamishana wa Elimu, Prof. Eustella

Bhalalusesa, Wakurugenzi, Wakuu wa Vitengo na Wakuu wa Taasisi mbalimbali

za Elimu zilizo chini ya Wizara yangu, kwa ushirikiano wao wa karibu katika

kuandaa bajeti hii. Pia, nawashukuru Wahadhiri, Wakufunzi, Walimu na

Watumishi wengine pamoja na Wanafunzi wote kwa kufanikisha utekelezaji wa

majukumu ya Wizara. (Makofi)

Page 229: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

229

Mheshimiwa Spika, pia nawashukuru Viongozi wa Vyama vya

Wafanyakazi na Vyama vya Wanataaluma, Wanafunzi na Washirika wa

MAendeleo, kwa ushirikiano wao katika kuiendeleza Sekta ya Elimu.

Ninawashukuru pia Wazazi, Walezi na Wananchi wote kwa ujumla, kwa jinsi

ambavyo wameendelea kushirikiana na Sekta ya Elimu katika kuendelea

kuimarisha elimu na mafunzo nchini.

Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kutoa salamu za pole kwako na

kwa Bunge lako Tukufu, kwa vifo vya Wabunge wenzetu wapendwa;

Mheshimiwa William Agustao Mgimwa, aliyekuwa mBunge wa Kalenga na

Waziri wa Fedha na Mheshimiwa Said Ramadhani Bwanamdogo, aliyekuwa

Mbunge wa Chalinze.

Mheshimiwa Spika, aidha, natoa pole kwa Wananchi wangu wa Jimbo la

Bagamoyo, kwa athari za mafuriko yaliyowakumba katika baadhi ya maeneo.

Niwahakikishie tupo pamoja na mara baada ya majukumu haya, nitashirikiana

nao kushughulikia athari zilizotokea. Aidha, natoa pole kwa Waheshimiwa

Wabunge na Wananchi wote waliofiwa na ndugu na wapendwa wao,

kutokana na maradhi, ajali, majanga na matukio mbalimbali yaliyotokea nchini

mwetu. Namwomba Mwenyezi Mungu, azilaze roho za Marehemu mahali

pema peponi; amina.

Mheshimiwa Spika, natoa pongezi kwa Wabunge wapya ambao ni

Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa - Mbunge wa Kalenga, Mheshimiwa

Ridhiwani Jakaya Kikwete - Mbunge wa Chalinze na Mheshimiwa Yussuf Salim

Hussein - Mbunge wa Chambani, kwa kuchaguliwa kwao kwa kura nyingi na

hivyo kupata fursa ya kuchangia maendeleo ya Taifa kwa kuwakilisha

Wananchi katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Hati Idhini iliyounda Wizara ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano

wa Tanzania, Tarehe 17 Disemba, 2010, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

ina majukumu yafuatayo:-

(a) Utungaji wa Sera za Elimu zinazohusu Elimu ya Awali, Elimu ya

Msingi, Elimu ya Sekondari, Elimu ya Ufundi, Mafunzo ya Ufundi Stadi, Elimu ya

Juu na Elimu ya Watu Wazima;

(b) Utekelezaji wa Sera za Elimu;

(c) Mafunzo ya Ualimu;

(d) Usajili wa Shule;

(e) Ukaguzi wa Shule na Vyuo vya Ualimu;

Page 230: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

230

(f) Uchapati wa Machapisho ya Elimu;

(g) Utoaji wa Huduma za Maktaba;

(h) Uratibu wa Shughuli zinazotekelezwa na Kamisheni ya Taifa ya

UNESCO;

(i) Uratibu wa Shughuli za Taasisi na Wakala zilizo chini ya Wizara;

(j) Usimamizi wa Utekelezaji wa programu na miradi mbalimbali ya

Wizara; na

(k) Uendelezaji wa Rasilimali Watu na Uongezaji tija ya Watumishi walio

chini ya Wizara.

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe tathmini ya utekelezaji wa Bajeti ya

Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 kuanzia tarehe Mosi Julai, 2013 hadi

tarehe 31 Machi, 2014.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kwa mwaka 2013/2014 kupitia Idara na

Taasisi ilikadiria kukusanya jumla ya shilingi 171,518,704,600 na hadi kufikia Machi,

2014 makusanyo ya maduhuli jumla ya shilingi 129,122,797,993.42, sawa na

asilimia 75.3 ya makadirio.

Mheshimiwa Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014, bajeti ya matumizi

ya kawaida ilikuwa 617,083,004,000, mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu

ilikuwa jumla ya shilingi 306,000,000,000, sawa na asilimia 79.5 ya matumizi

mengineyo. Hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2013, Wizara yangu ilitumia jumla ya

shilingi 486,573,220,250.94, sawa na asilimia 79 ya bajeti ya matumizi ya

kawaida. Asilimia 93.5 matumizi mengineyo zilitumika kwa ajili ya mikopo ya

Wanafunzi wa Elimu ya Juu na Taasisi.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2013/2014 Wizara ilitengewa

jumla ya shilingi 72,598,051,000, ikiwa ni Bajeti ya Maendeleo. Fedha za ndani ni

18,830,000,000, na fedha za nje ni shilingi 53,768,051,000. Matumizi jumla

yalikuwa shilingi 14,921,545,855.46.

Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kutoa taarifa ya utekelezaji wa

majukumu ya Wizara kwa mwaka 2013.14 kulingana na Hati Idhini kama

ifuatavyo:-

Nitangulize utungaji wa Sera za Elimu.

Page 231: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

231

Mheshimiwa Spika, moja ya jukumu kubwa la Wizara yangu ni kutunga

Sera mbalimbali za Elimu na Mafunzo katika ngazi zote. Sekta ya Elimu ina Sera

nne ambazo ni Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 1995, Sera ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi ya Mwaka 1996, Sera ya Taifa ya Elimu ya Juu ya Mwaka

1999 na Sera ya Matumizi ya TEHAMA katika Elimu ya Msingi ya Mwaka 2007.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2013/14 pamoja na mambo

mengine Wizara yangu ilitekeleza mambo yafuatayo:-

(a) Kukamilisha Rasimu ya Sera ya Elimu na Mafunzo ambayo

itawasilishwa Baraza la Mawaziri kwa maamuzi.

(b) Kukamilisha Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Kuanzisha Bodi ya

Kitaalam ya Walimu Tanzania na kuiwasilisha katika Sekretarieti ya Baraza la

Mawaziri.

(c) Kukamilisha Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Kuanzisha Mamlaka

ya Ithibati na Uthibiti wa Ubora wa Elimu ya Msingi na Elimu ya Sekondari.

(d) Kukamilisha na kuwasilisha katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya

Utumishi wa Umma, Muundo wa Utumishi wa Walimu katika kada mbalimbali na

pia Muundo wa Uongozi katika ngazi za Elimu ya Msingi, Sekondari na Ualimu

ikiwemo Ukaguzi.

Mheshimiwa Spika, lengo na madhumuni ya kuweka Sera mpya na

mikakati itakayoandaliwa ya utekelezaji wa Sera ni pamoja na kuhakikisha

kwamba, changamoto zinazohusu elimu na mafunzo ambazo ni za Kisera au ni

za Kimkakati zinatatuliwa.

Mheshimiwa Spika, usajili wa shule ni muhimu kwa ajili ya kuipa shule

ithibati na idhini ya kufundisha. Kwa Mwaka wa Fedha 2013/14 pamoja na

mambo mengine, yafuatayo yalitekelezwa:-

(a) Shule 106 zilisajiliwa hadi kufikia Machi, 2014, ambapo Shule za

Awali pekee ni mbili, Shule za Awali na Msingi 53, Sekondari za Serikali 17,

Sekondari zisizokuwa za Serikali 32 na Vyuo vya Ualimu visivyokuwa vya Serikali

viwili, hivyo kuongeza idadi ya Shule na Vyuo hadi kufikia jumla ya Shule za

Msingi 16,609, Sekondari 4,573, Vyuo vya Ualimu 123.

(b) Vibali vya Ujenzi wa shule 127 vilitolewa ikiwemo Shule za Awali

vibali vitano, Shule za Msingi tatu, Awali na Msingi 74, Sekondari 40, Vyuo vya

Ualimu vitano.

Page 232: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

232

(c) Shule za Msingi tano, Sekondari tano, pamoja na Chuo Kimoja cha

Ualimu zilifungiwa kwa sababu mbalimbali, ikiwemo ukiukwaji wa vigezo vya

ubora wa shule.

Mheshimiwa Spika, katika Ukaguzi wa Shule na Vyuo vya Ualimu, Wizara

yangu pamoja na mambo mengine ilitekeleza mambo yafuatayo:-

(a) Asasi 8,483 zikiwemo Shule za Msingi 6091, Sekondari 2308 na Vyuo

vya Ualimu 84 vilikaguliwa hadi kufikia mwezi Machi, 2014, sawa na asilimia 79.4

ya asasi 10,684 zilizolengwa kukaguliwa.

(b) Wakaguzi wa Shule 139 walioteuliwa kati ya mwaka 2010 na 2013

walipatiwa mafunzo kabilishi na Wakaguzi wa Shule 148 walipatiwa mafunzo ya

Uongozi na Uendeshaji wa Elimu.

(c) Walimu 217 wenye vigezo vya kuwa Wakaguzi walibainishwa na

kuombewa uhamisho kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI ili kuimarisha Ukaguzi

katika Halmashauri mpya na zile zenye upungufu.

(d) Mfumo wa kieletroniki wa ukusanyaji na usimamizi wa taarifa za

ukaguzi ulikamilika na kufanyiwa majaribio katika Shule za Msingi 139 katika

Halmashauri saba ambazo ni Temeke, Makete, Siha, Magu, Hai, Mtwara Vijijini

na Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, Mafunzo ya Ualimu; moja ya nguzo ya kuhakikisha

Elimu bora inatolewa ni maandalizi ya Walimu kulingana na mitaala

inayotumika. Wizara imetekeleza jukumu hili katika Mwaka wa Fedha 2013/14

kama ifuatavyo:-

(a) Elimu ya Ualimu iliendelea kutolewa katika Vyuo vya Serikali na

Vyuo vya Binafsi na kupata jumla ya Walimu 36,338 waliohitimu. Ngazi ya Cheti

ni Walimu 17,928, ngazi ya Stashahada ni 5,416 na ngazi ya Shahada 12,994. Kati

ya Walimu hao, Walimu wa masomo ya sayansi na hisabati ni 2364. Aidha, Ofisi

ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) imewaajiri wahitimu hao katika Halmashauri

mbalimbali na hivyo kubakiza mahitaji ya Walimu 30,949 wa Shule za Msingi na

Walimu 24,596 wa Sekondari wa Sayansi na Hisabati.

(b) Kuweka utaratibu wa kuanza kutoa ruzuku na mikopo kwa

Wanachuo wenye sifa watakaojiunga na mafunzo ya Stashahada ya Ualimu

wa Sayansi na Hisabati.

(c) Kurejesha utaratibu wa kujiunga na mafunzo ya Ualimu kwa Walimu

wa Sekondari wa Masomo ya Sayansi kwa miaka mitatu kwa wahitimu wa

Kidato cha Nne ama half combination.

Page 233: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

233

(d) Kukamilisha Mfumo wa Kielektroniki wa kudahili wanafunzi wa

kujiunga na programu ya ualimu ngazi ya Stashahada na ambao utaanza

kutumika kwa Programu ya Stashahada ya Ualimu wa Elimu ya Msingi katika

Chuo Kikuu cha Dodoma.

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu ina Taasisi na Wakala zenye majukumu

mbalimbali katika kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo. Kati ya hizo, Taasisi tatu

ni za Ithibati na Uthibiti wa Ubora wa Elimu ya Juu, Elimu ya Ufundi na Mafunzo

ya Ufundi Stadi; mbili ni za mitaala na mitihani, mbili ni za mikopo na ruzuku

mbalimbali, moja ni Bodi ya Huduma za Maktaba, moja ni Tume ya Taifa ya

UNESCO na kituo kimoja cha Hazina Data Dakawa. Taasisi hizo pamoja na

mambo mengine, zilitekeleza mambo yafuatayo:-

(a) Sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya Mamlaka ya Elimu Tanzania

(Sura Na. 412), zimerekebishwa kupitia Sheria ya Written Laws Miscellaneous

Amendments Act No. 3/2013 ili kuupatia Mfuko wa Elimu vyanzo vya mapato

vya ziada na endelevu kwa kuweka asilimia isiyopungua mbili ya Bajeti ya

Serikali ya mwaka ya matumizi ya kawaida ukitoa Deni la Taifa.

(b) Programu za Elimu mbalimbali zilianzishwa ikiwemo Programu ya

Stashahda ya Ualimu wa Shule za Msingi ambayo itaanza kutolewa mwaka

2014/15 katika Chuo Kikuu cha Dodoma.

(c) Kuzinduliwa na kuanza rasmi kwa ujenzi wa Hospitali ya Kufundishia

ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili Kampasi ya Mloganzila.

(d) Kukamilika kwa upembuzi yakinifu wa Chuo Kikuu cha Kilimo na

Sayansi Shirikishi cha Mwalimu Julius Nyerere Butiama. Wizara inaendelea

kuwasiliana na Tume ya Mipango, Hazina pamoja na wadau mbalimbali ili

ujenzi wa Chuo hiki uanze katika Mwaka wa Fedha 2014/15.

Mheshimiwa Spika, Taasisi zingine na Wakala zilizo chini ya Wizara katika

mwaka 2013/14 zilitekeleza mambo yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14 Taasisi ya Elimu ya Watu

Wazima pamoja na majukumu mengine, ilitekeleza mambo haya yafuatayo:-

(a) Ilidahili Wanafunzi 881 kati ya ngazi ya Cheti, Stashahada na Shada

katika Programu ya Elimu ya Watu Wazima na Mafunzo Endelevu.

(b) Ilitoa Elimu ya Sekondari kwa njia ya ujifunzaji huria na masafa kwa

kuandika moduli za hatua ya tatu kwa masomo kumi na moja yakiwemo

Page 234: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

234

English, French, Basic Applied Mathematics, Advanced Mathematics, History,

Geography, Kiswahili, General Studies, Economics, Commerce na Accounting.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Taasisi ya Elimu Tanzania

pamoja na mambo mengine, imekusanya maoni ya wadau kuhusu maboresho

ya mitaala pamoja na kuchambua mihtasari ya masomo ya elimu ya awali na

elimu ya msingi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14, Bodi ya Huduma za Maktaba

Tanzania, ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Ilitoa mafunzo ngazi ya Cheti kwa wanachuo 457, Stashahada 339

pamoja na mafunzo ya muda mfupi kwa washiriki 98 katika Chuo cha Ukutubi

na Uhifadhi Nyaraka (SLADS).

(b) Imeendelea na ujenzi na ukarabati wa majengo kwenye Chuo cha

Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka na kufanya ukarabati wa awamu ya kwanza wa

majengo ya Maktaba ya Mkoa wa Mara na Mkoa wa Mtwara.

(c) Iliendelea na ujenzi wa Hosteli ya Wanafunzi wa Kike katika Chuo

cha Ukutubi SLADS Bagamoyo.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/14 Wakala wa Maendeleo ya

Uongozi wa Elimu ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Ilitoa mafunzo ya Stashahada ya Uongozi wa Elimu kwa wanafunzi

762 katika Vituo vya Bagamoyo na Mwanza, yenye lengo la kuimarisha

usimamizi na uendeshaji wa shule.

(b) Ilitoa mafunzo kwa Wakuu wa Shule wa Serikali 2,982 na 2,287 wa

Shule zisizo za Serikali ili kuimarisha Menejimenti ya Shule za Sekondari.

(c) Ilitoa mafunzo kwa Waratibu wa Elimu Kata 1,765 kutoka Mikoa ya

Arusha, Dar es Salaam, Kagera, Kilimanjaro, Mbeya, Morogoro, Mtwara,

Mwanza, Ruvuma, Singida na Tabora.

Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya UNESCO, katika kipindi cha Mwaka

wa Fedha 2013/2014, pamoja na mambo mengine, ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Iliandaa ripoti ya hali ya uhifadhi wa maeneo ya Tanzania

yaliyoorodheshwa kwenye Orodha ya Urithi wa Dunia ili kutathmini utekelezaji

wa Mkataba wa UNESCO wa mwaka 1972.

(b) Iliendelea kuelimisha jamii kuhusu shughuli za UNESCO hususan

masuala ya mazingira, elimu, sayansi asilia, sayansi jamii, utamaduni,

Page 235: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

235

mawasiliano na habari, kwa kuchapa na kusambaza nakala 742 za Tanzania

and UNESCO Magazine na nakala 2,500 za vipeperushi.

Mheshimiwa Spika, Baraza la Mitihani la Tanzania katika mwaka

2013/2014, pamoja na mambo mengine lilitekeleza yafuatayo:-

(a) Liliwatahini wanafunzi waliomaliza Elimu ya Msingi 868,083, Elimu ya

Sekondari Kidato cha Nne 427,938 na Kidato cha Sita 46,378, Mtihani wa Ualimu

watahiniwa 26,614 na kuendesha Mtihani wa Maarifa (Qualifying Test) kwa

watahiniwa 18,214.

(b) Baraza lilianza ujenzi wa kituo cha data kwa ajili ya kuimarisha

utunzaji wa kumbukumbu na taarifa za mitihani.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Baraza la Taifa la Elimu ya

Ufundi lilitekeleza yafuatayo:-

(a) Lilikagua, kusajili na kutoa ithibati ambapo vyuo 45 vilikaguliwa na

kusajiliwa na vyuo vinne vilipatiwa ithibati.

(b) Liliratibu udahili wa wanafunzi katika vyuo vya ufundi ambapo kwa

ngazi ya cheti na stashahada wanafunzi 13,375 na shahada wanafunzi 5,081

walidahiliwa.

(c) Iiliidhinisha mitaala 39 na kuratibu mafunzo kwa walimu 132 kuhusu

jinsi ya kutumia mitaala inayozingatia umahiri.

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere katika

mwaka 2013/2014 kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili jumla ya wanafunzi 745, kati yao wanafunzi 122 wa

Programu za Cheti, 220 Programu za Stashahada na 403 wa Progamu za

Shahada ya Kwanza.

(b) Kiligharamia mafunzo kwa wahadhiri 18 wa ngazi ya uzamili na

uzamivu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Chuo cha Ufundi Arusha

kiliendelea kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili jumla ya wanafunzi 493 wa mwaka wa kwanza.

(b) Kilianzisha programu ya Biomedical Engineering.

Page 236: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

236

(c) Kilihuisha mitaala sita ya programu zilizopo za ufundi sanifu.

(d) Kilitoa kozi za awali za kujiunga na chuo kwa kushirikiana na Mfuko

wa Elimu Tanzania (TEA), ambapo jumla ya wanafunzi 126 wa kike walijiunga na

Chuo kwa utaratibu huo.

(e) Kilishirikiana na Mradi wa Technical Education and Labour Market

Support Program (TELMS), ambao ulitoa msaada wa vifaa vya kufundishia kwa

fani za uhandisi na mawasiliano ya anga, ujenzi, barabara, mitambo na magari.

Pia wanafunzi bora sita wa kike walizawadiwa kompyuta pakato (Laptops)

moja kila mmoja na wanafunzi 93 walipewa ufadhili wa ada ya shilingi 180,000

kila mmoja.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Elimu na Ufundi Stadi (VETA) katika

mwaka 2013/2014 ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kuanza maandalizi ya awali ya ujenzi wa vituo vitano vya Wilaya ya

Kilindi, Namtumbo, Ludewa, Ukerewe na Chunya, ambapo zabuni

zimetangazwa na ujenzi unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi Juni, 2014.

(b) Ilitoa mafunzo ya umahiri ya ufundishaji mafunzo ya ufundi stadi

kwa walimu 100 kutoka vyuo 25 vya maendeleo ya jamii vinavyotoa mafunzo

ya ufundi stadi.

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) katika mwaka

2013/2014 ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Iligharamia mafunzo ya Pre-entry kwa wanafunzi wa kike 260 ili

kuwawezesha kupata sifa stahiki za kujiunga na Vyuo vya Elimu ya Ufundi nchini.

(b) Ilihamasisha uchangiaji wa elimu kwa njia ya matembezi ya hisani

na kuandika miradi ambapo kiasi cha jumla ya shilingi milioni 370 ziliweza

kupatikana.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Tume ya Vyuo Vikuu

Tanzania ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Iliratibu na kusimamia udahili wa wanafunzi 52,538 katika Vyuo

Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki nchini.

(b) Ilikamilisha na kuzindua mwongozo wa gharama ya kumsomesha

mwanafunzi wa elimu ya juu ama student unit cost framework utakaoanza

Page 237: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

237

kutumika katika mwaka wa masomo 2014/2015 hivyo kuondoa utozaji wa ada

kiholela katika elimu ya juu.

(c) Ilikagua na kufanya tathmini ya maendeleo ya vyuo vilivyopewa

ithibati ili kuweza kujua kama vinatekeleza malengo yake ipasavyo na

iliidhinisha programu 46 za masomo.

(d)Iliratibu upatikanaji wa wanataaluma 17 kutoka vyuo vikuu nchini

waliojiunga na masomo ya uzamivu chini ya makubaliano ya Serikali ya

Tanzania na Ujerumani kupitia Shirika la DAAD.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Bodi ya Mikopo ya

Wanafunzi wa Elimu ya Juu ilitekeleza yafuatayo:-

(a) Ilitoa mikopo kwa wanafunzi 95,589 na hivyo kuongeza fursa ya

upatikanaji wa elimu ya juu.

(b) Ilikusanya marejesho ya mikopo kiasi cha shilingi 12,345,412,587.66

hadi Machi, 2014, sawa na asilimia 43 ya lengo kwa mwaka 2013/2014 na hivyo

kufikia jumla ya shilingi 47,349,582,373.11, sawa na asilimia 55 ya madeni

yaliyoiva.

(c) Ilifungua Ofisi ya Kanda ya Ziwa na kuimarisha Ofisi za Kanda ya

Zanzibar na ya Dodoma kwa kuziunganisha na Mfumo wa Utoaji Mikopo wa

Makao Makuu ya Bodi ya Mikopo.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika mwaka

2013/2014 kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili wanafunzi 1,350 katika fani za sayansi na uhandisi, 2,435 wa

uzamili na uzamivu.

(b) Kiliendelea kufanya utafiti kuhusu mabadiliko ya tabianchi.

(c) Kiliendelea na utafiti kupitia miradi mbalimbali ikiwemo Mradi wa

Integrated Water Resources Management wa kutoa mafunzo na kufanya utafiti

kwa wanafunzi wa hapa nchini na nchi jirani.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam katika

mwaka 2013/2014 kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili wanafunzi 1,247; 220 wa fani ya sayansi; na 42 wa cheti

katika fani mbalilmbali za elimu.

Page 238: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

238

(b) Kiliongeza vifaa vya kufundishia na kujifunzia vikiwemo madawa

kwa ajili ya matumizi ya maabara za kufundishia na vifaa kwa wanafunzi wenye

mahitaji maalum pamoja na kununua samani na vitabu kwa ajili ya maktaba.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa katika mwaka

2013/2014 kilidahili wanafunzi wanawake 255 na wanaume 723.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine katika mwaka

2013/2014 kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilianzisha programu ya mafunzo ya Post Harvest Engineering

Systems ngazi ya shahada ya uzamivu.

(b) Kilifanya utafiti msingi na tumizi (Basic and Applied Research) katika

Miradi 135.

(c) Kilikamilisha ujenzi wa majengo manne yenye kumbi za mihadhara

tisa, Ofisi arobaini na mabaara nne yenye uwezo wa kuhudumia wanafunzi

10,565 na wahadhiri 881 na kukarabati bweni la Kampasi ya Solomon Mahlangu

na Karakana ya Idara ya Uhandisi Kilimo kupitia Mradi wa STHEP.

(d) Kilifanya utafiti wa athari za mabadilko ya tabianchi na tahafifu

katika Kanda za Nyanda ya Juu Kusini, Kaskazini na Kati.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Chuo Kikuu Kishiriki cha

Ushirika na Biashara Moshi, kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili wanafunzi 4,463.

(b) Kiligharamia mafunzo kwa wanataaluma 53 katika shahada za

uzamili na uzamivu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu.

(c) Kilifanya tafiti 20 kwa kushirikiana na wadau nje na ndani ya nchi

yetu.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwa mwaka 2013/2014

kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili wanafunzi 8,935 katika ngazi ya shahada na cheti, sawa na

asilimia 99 ya lengo la kudahili wanafunzi 9,000. Aidha wanafunzi 2,943, sawa

na asilimia 105.9 ya lengo walidahiliwa katika shahada ya uzamili na uzamivu.

Page 239: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

239

(b) Kilijenga maabara ya kompyuta katika Vituo vya Zanzibar, Mtwara,

Dodoma, Shinyanga na Kinondoni pamoja na kukamilisha ukarabati wa Ofisi na

Ukumbi wa Mitihani katika Kituo cha Shinyanga.

(c) Kilifanya ukarabati wa awamu ya pili katika Kituo cha Zanzibar.

(d) Kilikamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa 10 kupitia Mradi wa Sayansi,

Teknolojia na Elimu ya Juu.

(e) Kilifanya utafiti katika maeneo mbalimbali yakiwemo usalama wa

matumizi ya TEHAMA.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Chuo Kikuu Ardhi kilitekeleza

yafuatayo:-

(a) kilikamilisha ujenzi wa ofisi sita za walimu katika Jengo Lands

Building.

(b) Kiliunganisha Mtandao wa TEHAMA wa Chuo kwenye Mkongo wa

Taifa.

(c) Kilifanya utafiti na kutoa ushauri katika masuala ya ardhi na

maendeleo ya makazi.

Mheshimiwa Spika, Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili

kwa mwaka 2013/2014 kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili wanafunzi 448 wa Shahada ya Kwanza, Udaktari wa

Binadamu 256, Madawa 66, Uuguzi wanafunzi 63, Udaktari wa Meno na Kinywa

wanafunzi 43, Afya, Sayansi na Mazingira wanafunzi 20 na wanafunzi 220 wa

Shahada za Uzamili.

(b) Kiliendelea na ujenzi wa hospitali na miundombinu ya barabara,

maji na umeme katika Kampasi ya Mloganzila.

(c) Kilichambua takwimu za utafiti wa TaMoVac - I na kuwasilisha

chapisho kwenye jarida la kimataifa mwezi Machi, 2014 na kuendeleza utafiti

wa TaMoVac - II.

(d) Kiligharamia mafunzo kwa wanataaluma 48 kupitia Miradi

mbalimbali na wafadhili ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa elimu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Chuo Kikuu Mzumbe

kilitekeleza yafuatayo:-

Page 240: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

240

(a) Kilidahili wanafunzi 4,488 katika Programu za Cheti 297, Stashahada

383, Shahada ya Kwanza 2,087, Shahada ya Uzamili 1,692 na Shahada ya

Uzamivu Programu 29.

(b) Kilikamilisha ujenzi wa jengo la ghorofa tano kwa ajili ya vyumba

vya ofisi, madarasa na kumbi za mihadhara, kiligharamia watumishi 21 katika

mafunzo ya shahada ya uzamili na saba shahada ya uzamivu.

(c) Kiliimarisha masuala ya menejimenti, uongozi na sayansi ya jamii,

kwa kukamilisha utafiti katika maeneo tisa ya kutoa ushauri wa kitaalam katika

maeneo 25.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014 Chuo Kikuu cha Dodoma

kilitekeleza yafuatayo:-

(a) Kilidahili wanafunzi 6,101.

(b) Kilikamilisha ujenzi wa maabara na madarasa kwa asilimia 80.

Aidha, kilikamilisha ujenzi wa matanki mawili yenye uwezo wa kuhifadhi lita

milioni saba na nusu za maji kwa ufadhili wa Benki Dunia.

(c) Kiliimarisha mazingira ya kutolea mafunzo kwa kuweka

miundombinu ya umeme na TEHAMA katika vyuo vya sayansi za asili, hisabati

na sayansi za ardhi.

Mheshimiwa Spika, usimamizi na utekelezaji wa Programu na Miradi.

Wizara yangu pia ina Programu na Miradi mbalimbali ambayo iko chini ya

Wizara. Katika mwaka 2013/2014, Wizara pamoja na mambo mengine

ilitekeleza yafuatayo katika eneo hili:-

(a) Ilitekeleza mikakati ya Mpango wa Matokeo Makubwa ya Sasa

katika elimu msingi, pamoja na mambo mengine kwa kutoa mafunzo kazini kwa

walimu 12,476. Kati ya hao, walimu 8,400 wa masomo ya sayansi na hisabati,

4,076 masomo yanayosomwa na wanafunzi wote, yaani Mathematics, Biology,

English na Kiswahili. Pia wakuu wa shule 3,152 walipatiwa mafunzo katika

mwongozo wa usimamizi na uendeshaji wa shule.

(b) Ilikamilisha tathmini ya stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu

pamoja na umakini katika uongozi wa shule kwa kutumia EGRA na EGMA.

(c) Ilikamilisha awamu kwanza ya Mradi wa Sayansi, Teknolojia na

elimu ya Juu (STHEP) kwa ufanisi, majengo mapya 17 yenye vyumba vya

mihadhara 48, maabara za sayansi 93 na Ofisi 302 za wafanyakazi zilijengwa.

Page 241: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

241

Majengo hayo yataongeza nafasi za kufundishia na kujifunzia kwa wanafunzi

47,622. Vyuo vilivyonufaika na Mradi huu ni Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,

Chuo Kikuu Ardhi, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Chuo Kikuu Huria

Tanzania, Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam, Chuo Kikuu Kishiriki cha

Elimu Mkwawa, Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Taasisi ya Afrika ya

Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia ya Chuo Kikuu na Chuo Kikuu cha

Taifa Zanzibar.

(d) Ilikamilisha na kuzindua Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Ufundi

na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Technical and Vocational Education and Training

Development Programme - TVETDP), mwaka 2013/2014 hadi mwaka 2017/2018

uliozinduliwa tarehe 13 Desemba, 2013.

(e) Ilikamilisha majadiliano ya Mradi wa Literacy and Numeracy

Education Support (LANES), wenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 94.8

katika kuinua kiwango cha kumudu kusoma, kuandika na kuhesabu kwa

wanafunzi wa darasa la kwanza na darasa la pili.

(f) Ilianza kutekeleza mradi wa kupata takribani vitabu milioni sita vya

sayansi na hisabati kwa elimu ya sekondari ili kupata uwiano wa kitabu kimoja

kwa mwanafunzi katika masomo hayo. Mkataba wenye thamani ya Dola za

Kimarekani milioni tisa tayari umesainiwa kati ya Serikali ya Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania na Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID).

(g) Ilizinduliwa Wiki ya Elimu ya Taifa ambayo itakuwa inafanyika

kuanzia ngazi ya Halmashauri, Mkoa hadi Taifa kila mwaka, ili kutoa fursa kwa

Wananchi na Wadau wa Elimu kujadili masuala na maendeleo katika maeneo

yao na kubaini changamoto na mbinu za kuendeleza na kuimarisha ubora wa

elimu. Kwa mwaka 2013/2014 wiki ya elimu ifanyika tarehe 3 hadi 10 mwezi Mei

na kauli mbiu ilikuwa Elimu Bora Inawezekana, Timiza Wajibu Wako.

Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa majukumu na bajeti ya mwaka

2013/2014, Wizara ilikabiliana na baadhi ya changamoto katika maeneo

mbalimbali inayoyasimamia ikiwemo hizi zifuatazo:-

(a) Upatikanaji wa walimu mahiri wa kufundisha stadi za kusoma,

kuandika na kuhesabu kwa kiwango cha kutosha kwa wanafunzi wa madaraa

ya chini (Darasa la I na la II).

(b) Upatikanaji wa Wataalam wa Kitanzania katika fani za gesi,

mafuta, chuma, urani, makaa ya mawe na madini mengine.

Page 242: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

242

(c) Upatikanaji wa rasilimali ili kuwezesha ukaguzi wa shule kufanyika

kwa ufanisi kulingana na miongozo ya ukaguzi kutokana na ongezeko la Mikoa

na Halmashauri mpya.

(d) Kuimarisha mfumo wa ukaguzi wa shule ili kuendana na mabadiliko

ya kisayansi na kiteknolojia.

(e) Ongezeko la mahitaji ya walimu wa masomo ya sayansi na hisabati

katika ngazi zote za elimu na mafunzo.

(f) Upatikanaji wa fedha za kutosha kutoa mikopo ili kugharamia elimu

ya juu na elimu ya ufundi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kutoa taarifa ya utekelezaji wa bajeti ya

mwaka 2013/2014, naomba sasa niwasilishe vipaumbele vya Wizara na kisha

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, vipaumbele vya Sekta ya Elimu ambavyo Wizara

yangu itavitekeleza vimeainishwa katika Mwongozo wa Maandalizi ya Bajeti

kwa Mwaka 2014/2015 kama ifuatavyo:-

(a) Kuinua ubora wa elimu na kujenga stadi stahiki katika ngazi zote za

elimu na mafunzo.

(b) Kuongeza upatikanaji wa fursa ya elimu kwa usawa katika ngazi

zote za elimu na mafunzo.

Mheshimiwa Spika, katika utungaji na utekelezaji wa Sera za Elimu, Wizara

yangu itatekeleza yafuatayo:-

(a) Kukamilisha Sera ya Elimu na Mafunzo na kuandaa mpango

mkakati wa utekelezaji wake.

(b) Kuimarisha mfumo wa kitaasisi wa kusimamia ubora wa elimu msingi

kwa kuanzisha mamlaka ya ithibati na uthibiti wa elimu ya msingi na sekondari ili

kuhakikisha kuwa utoaji wa elimu unazingatia sera, miongozo na mitaala ya

elimu yenye kukidhi mahitaji ya soko na jamii.

(c) Kukamilisha taratibu za uanzishwaji wa Bodi ya Kitaalamu ya

Walimu Tanzania itakayosimamia masuala ya Walimu ikiwemo usajili,

uendelezaji wa Walimu na Maadili ya kazi ya Ualimu.

Page 243: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

243

(d) Kuimarisha ha Taasisi ya Elimu Tanzania katika kushughulikia Ithibati

na Uthibiti wa vitabu, zana na vifaa mbalimbali vya elimu ya msingi na

sekondari.

(e) Kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) na wadau

wengine, kuweka mfumo na muundo utakaosaidia wanafunzi wengi kuendelea

na masomo ya Elimu ya Sekondari ya Juu, ili kufikia lengo la wanafunzi 250,000

ifikapo mwaka 2016.

(f) Kuhuisha Mitaala na kuimarisha mfumo wa utoaji wa Elimu ya

Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi.

(g) Kuimarisha ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Sera ya Elimu na

Mafunzo katika ngazi zote kwa kuandaa na kutoa Miongozo.

(h) Kuhuisha na kuoanisha Programu za Elimu ya Juu pamoja na

Ufundi, ili utoaji wa elimu hizo uzingatie mahitaji ya soko la ajira kwa maendeleo

ya Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, katika usajili wa shule, Wizara yangu itaendelea kusajili

shule za msingi na sekondari kwa kutilia mkazo zaidi shule za ufundi na sayansi,

kuimarisha mfumo wa usajili wa shule na kuhuisha Mwongozo wa Usajili, ili

uendane na wakati.

Mheshimiwa Spika, katika ukaguzi wa shule na vyuo, Wizara yangu

itatekeleza yafuatayo:-

(a) Kuimarsiaha taratibu za ukaguzi na kuendelea kukagua shule na

vyuo vya ualimu kwa ufanisi zaidi.

(b) Kufungua Ofisi za Ukaguzi katika Wilaya Mpya na Wilaya ambazo

hazina Ofisi hizo.

Mheshimiwa Spika, katika kusimamia utoaji wa mafunzo ya ualimu, Wizara

yangu itatekeleza yafuatayo:-

(a) Kuimarisha ufundishaji wa Walimu katika Stadi za KKK.

(b) Kuanza kuratibu utoaji wa ruzuku na mikopo kwa wanafunzi

wanaosomea Stashahada ya Ualimu wa Sayansi na Hisabati, kulingana na

vigezo vitakavyowekwa katika vyuo vilivyoteuliwa.

(c) Kuimarisha mafunzo ya ualimu na kuweka muundo endelevu wa

weledi na maendeleo ya Mwalimu.

Page 244: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

244

(d) Kuvipatia vyuo vya ualimu 34 ithibati ya NACTE, ili viweze kuingia

rasmi katika mfumo wa ithibati na uthibiti wa ubora unaotambulika Kitaifa katika

Sekta ya Elimu ya Ufundi.

Mheshimiwa Spika, katika kusimamia Taasisi na Wakala zilizo chini ya

Wizara, zimelenga kutekeleza majukumu yake ya kawaida ikiwa ni pamoja na

haya yafuatayo:-

(a) Kuendelea kuinua ubora na kuimarisha vyuo vya elimu ya juu

pamoja na ufundi, ili viwe Vyuo vya Maendeleo Kizazi cha Tatu (Third

Generation Development Institutions), kulingana na kasi ya maendeleo iliyopo

Duniani na kuweza kufikia Malengo ya Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Mwaka

2025 kwa haraka.

(b) Kuendelea kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji kwa kuweka mifumo

ya kidijiti ili kuwezesha Walimu na Wanafunzi kupata maandiko mbalimbali

muhimu kwa maendeleo ya Elimu na Taifa kupitia TEHAMA.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Taasisi na Wakala katika mwaka

2014/2015, Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima imelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kuandika Mihitasari na Moduli za Masomo ya Biashara na Sayansi

Hatua ya Pili, sawa na Kidato cha I na cha II, ili kuongeza fursa ya utoaji wa

Elimu ya Sekondari kwa njia ya ujifunzaji huria na masafa.

(b) Kusimamia Mpango Tarajali wa Elimu Changamani badala ya

msingi katika Wilaya 13 kwa kushirikiana na UNICEF.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Taasisi ya Elimu Tanzania

imelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kufanya tathmini ya utekelezaji, kupitia na kuboresha Mtaala wa

Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Ualimu.

(b) Kutoa mafunzo kuhusu utekelezaji wa Mitaala kwa Walimu,

Wakaguzi wa Shule, Maafisa Elimu na Waratibu wa Elimu Kata.

(c) Kufanya utafiti kuhusu ufundishaji na ujifunzaji kwa masomo ya

sayansi na hisabati.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Bodi ya Huduma za Maktaba

Tanzania imelenga kutekeleza yafuatayo:-

Page 245: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

245

(a) Kutoa machapisho 50,000 ili kuinua ubora wa huduma za Maktaba

katika Mikoa 21 Tanzania Bara.

(b) Kutoa mafunzo ya ukutubi na uhifadhi nyaraka kwa walengwa 700

wa Cheti, 500 wa Stashahada na 500 wa Mafunzo ya Awali kwa ajili ya

Wafanyakazi wa Maktaba.

(c) Kuendeleza ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya Chuo cha

Ukutubi na Uhifadhi Nyaraka (SLADS) Bagamoyo, ikiwemo maabara ya

computer na nyumba za wafanyakazi.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Wakala wa Maendeleo ya

Uongozi wa Elimu imelenga kutekeleza majukumu yake ya kawaida ikiwa ni

pamoja na yafuatayo:-

(a) Kutoa Mafunzo ya Stashahada ya Ukaguzi wa Shule kwa Wakaguzi

240 wa Halmashauri za Tanzania Bara na Mafunzo ya Cheti cha Uongozi na

Uendeshaji wa Elimu kwa Walimu Wakuu 720 katika Wilaya 12 za majaribio ya

UNICEF.

(b) Kutoa mafunzo ya muda mfupi ya uongozi, uendeshaji na usimamizi

wa elimu kwa Wajumbe 9,000 wa Kamati na Bodi za Shule, Wakuu wa Shule

4,300, Wakaguzi wa Shule 240, Maafisa Elimu 884 wa Mikoa na Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2014/2015 Tume ya Taifa ya

UNESCO imelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kushirikisha na kuhakikisha wadau wanashiriki katika kupanga na

kutekeleza Programu za UNESCO katika nyanja za Elimu, Sayansi Asilia, Sayansi

ya Jamii, Utamaduni, Habari na Mawasiliano.

(b) Kushirikiana na wadau katika kutafuta fedha za kutekeleza miradi

saba ya ushirikishaji (Participation Projects).

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Baraza la Mitihani la Tanzania

limelenga kutekeleza mambo yafuatayo:-

(a) Kuendesha Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi kwa Watahiniwa

998,295 mwaka 2014.

(b) Kuendesha Mitihani ya Sekondari Kidato cha IV kwa Watahiniwa

492,129, Maarifa Watahiniwa 20,946 kwa mwaka 2014 na Kidato cha VI

Watahiniwa 61,335 kwa mwaka 2015.

Page 246: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

246

(c) Kuendesha Mitihani ya Ualimu kwa Watahiniwa 35,297 kwa mwaka

2015.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Baraza la Taifa la Elimu ya

Ufundi limelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kukagua, Kusajili na Kutoa Ithibati kwa Vyuo vya Ufundi 50, ili kukidhi

ubora wa elimu.

(b) Kutengeneza Mitaala ya Kitaifa 10 na kuidhinisha Mitaala 40 ya

ngazi ya Cheti, Stashahada na Shahada pamoja na kuratibu mafunzo ya

Walimu 150 kuhusu kufundisha kwa kutumia Mitaala inayozingatia umahiri kwa

Vyuo vya Ufundi.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015, Chuo cha Kumbukumbu ya

Mwalimu Nyerere kimelenga kuanzisha Mafunzo ya Cheti na Stashahada katika

Rasilimali Watu na Cheti katika Maendeleo ya Uchumi (Certificate in Economic

Development).

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Chuo cha Ufundi Arusha,

kimelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kuanzisha Programu ya Stashahada ya Ualimu wa Masomo ya

Sayansi na Ufundi Sanifu katika Fani ya Magari na Mitambo Mikubwa.

(b) Kuandaa Mpango Mkakati wa kuanzisha Kituo cha Mafunzo ya

Kutengeneza Mashine Ndogondogo za kuzalisha umeme na wa kukarabati

Kituo cha Kuzalisha Umeme Kikuletwa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Mamlaka ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kuanza ujenzi wa vyuo vinne vya VETA vya Mikoa ya Geita, Simiyu,

Njombe na Rukwa na vya Wilaya za Kilindi, Chunya, Ukerewe, Ludewa na

Namtumbo, pamoja na kukarabati Vyuo vya Wilaya za Korogwe na Karagwe.

(b) Kufanya utafiti wa soko la ajira katika maeneo ya machimbo ya

gesi, madini ya chuma na makaa ya mawe katika Mikoa ya Mtwara, Lindi,

Iringa, Njombe na Ruvuma, pamoja na kufanya mapitio na kuandaa Mitaala

kwa ajili ya mafunzo katika Sekta ya Gesi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Mamlaka ya Elimu Tanzania

imelenga kutekeleza yafuatayo:-

Page 247: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

247

(a) Kuimarisha uwezo wa ugharamiaji elimu kwa kuendelea na

uchangishaji wa fedha ili kupata bilioni 2.3 kwa ajili ya ujenzi wa mabweni 30 ya

wasichana kwenye Halmashauri saba za Wilaya za Geita, Lushoto, Kasulu, Lindi,

Musoma, Songea na Manyara.

(b) Kuongeza fursa kwa wasichana kujiunga na elimu ya ufundi kwa

kuendelea kufadhili Mpango wa Pre-entry kwa wanafunzi wa kike.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Tume ya Vyuo Vikuu (TCU)

imelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kukagua na kutathmini mipango ya kuanzisha Vyuo Vikuu 20, ili

kusimamia ubora wa elimu itolewayo na Vyuo Vikuu Nchini.

(b) Kuvijengea uwezo Vyuo Vikuu katika kuandaa na kuhuisha

Programu za Masomo kwa kuzingatia Mfumo wa Tuzo unaotumika (University

Qualifications Framework).

(c) Kuratibu upatikanaji wa Wanataaluma 30 kutoka Vyuo Vikuu nchini

watakaojiunga na Masomo ya Uzamili na Uzamivu chini ya makubaliano kati ya

Serikali ya Tanzania na Ujerumani.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Bodi ya Mikopo ya

Wanafunzi wa Elimu ya Juu imepanga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kutoa mikopo ya wanafunzi 95,881 wakiwemo waombaji wa mara

ya kwanza 27,878 na wanafunzi wanaoendelea 67,953 wa Vyuo vya Elimu ya

Juu, 3,000 wa Stashahada ya Elimu ya Ualimu wa Masomo ya Sayansi na

Hisabati.

(b) Kukusanya marejesho ya mikopo yanayofikia jumla ya shilingi

36,610,694,661.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Chuo Kikuu cha Dar-es-

Salaam kimepanga kukarabati miundombinu ya majitaka pamoja na maeneo

ya makazi ya wanafunzi.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu

Dar-es-Salaam kimelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kuongeza fursa za kujiunga na Elimu ya Juu kwa kudahili wanafunzi

1,800.

Page 248: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

248

(b) Kukarabati Jengo la Kitivo cha Sayansi za Jamii na Hyumanitia

(Humanities), Jengo la Utawala kwa ajili ya Ofisi za Wafanyakazi waendeshaji,

Jengo la Maabara na Madarasa katika Shule ya Sekondari ya Mazoezi na uzio

kuzunguka Chuo.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015 Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu

Mkwawa kimelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kukamilisha ujenzi wa Ukumbi wa Mihadhara wenye uwezo wa

kuchukua wanafunzi 1,000 na kukarabati miundombinu ya chuo.

(b) Kuendelea kugharamia masomo ya Wahadhiri 16 walioko

masomoni katika viwango vya Shahada za Uzamili na Uzamivu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Chuo Kikuu cha Sokoine cha

Kilimo kimelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kuanzisha Shahada mpya za kwanza tatu na tatu za Uzamili na

masomo yasiyo ya Shahada matano, ili kuelekea katika kufikia lengo la

kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka waliopo 8,261 hadi 11,000 mwaka 2017.

(b) Kukamilisha miundombinu na majengo mapya yanayogharamiwa

na Mradi wa STHEP na kuanza maandalizi ya ujenzi wa maabara kubwa moja

kwa ajili ya Kitivo cha Sayansi inayogharimiwa na Mradi wa EPINAV. Aidha,

kuendeleza ujenzi wa jengo moja la ghorofa moja linalogharamiwa na Mradi

wa Climate Change, Impact, Adaptation and Mitigation in Tanzania ambalo

litakuwa na vyumba vya semina, ofisi, maabara za computer pamoja na

vyumba vya mihadhara, kukarabati kumbi 10 za mihadhara na nyumba za

wafanyakazi zilizopo Kampasi ya Solomoni Mahlangu na Kampasi Kuu.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Chuo Kikuu Kishiriki cha

Ushirika na Biashara Moshi kimelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kukamilisha taratibu za kukiwezesha kuwa Chuo Kikuu kamili.

(b) Kuimarisha Vituo vinne vya Mikoani Mtwara, Iringa, Mwanza na

Singida, ili kuielimisha jamii katika masuala ya Vyama vya Ushirika, Maendeleo

ya Ushirika, utunzaji mazingira na mikakati ya upunguzaji wa umaskini.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015 Chuo Kikuu Huria cha

Tanzania kimelenga kutekeleza yafuatayo:-

(a) Kukamilisha ujenzi wa Maabara za Computer katika Mikoa ya

Dodoma, Lindi, Mtwara, Mara, Njombe na Tabora.

Page 249: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

249

(b) Kukarabati majengo ya chuo awamu ya pili katika Mikoa ya

Kagera, Mtwara, Lindi, Kilimanjaro, Ruvuma, Kinondoni na Rukwa.

(c) Kujenga Maabara ya Sayansi na Jengo la Madarasa Makao Makuu

ya Chuo, Bungo Kibaha.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015, Chuo Kikuu Ardhi kimelenga

kuendelea na ujenzi wa Lands Building, ukarabati wa karakana za mafunzo na

mabweni ya wanafunzi na kutayarisha michoro kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha

Wanafunzi na kutoa huduma za ushauri nasaha kwa wanafunzi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Chuo Kikuu cha Afya na

Sayansi Shirikishi Muhimbili kimelenga kuendeleza ujenzi wa Hospitali ya

Kufundishia ya Kampasi ya Mloganzila na kukarabati hosteli za wanafunzi katika

eneo la Chole.

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2014/2015, Chuo Kikuu cha Mzumbe

kimelenga kutekeleza mambo yafuatayo:-

(a) Kuendeleza ujenzi wa madarasa na Kumbi mbili za Mihadhara

pamoja na kukarabati mabweni manne ya wanafunzi, mfumo wa maji na

majengo ya kilichokuwa Kitengo cha Uchapaji ili kuyabadili kuwa kituo cha

wanafunzi.

(b) Kukamilisha utafiti katika maeneo 16 ya kutoa ushauri wa kitaalamu

katika maeneo 37 ya Menejimenti ya Uongozi na Sayansi za Jamii kwa ujumla.

Mheshimiwa Spika, napenda tena kutoa shukrani zangu za dhati kwako

binafsi na kwa Waheshimiwa Wabunge; samahani, nimeruka sehemu.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwako binafsi

na kwa Waheshimiwa Wabunge, kwa kunisikiliza. Kwa niaba ya Wizara yangu,

napenda pia kuwashukuru kwa dhati wadau wote wa Sekta ya Elimu, ikiwa ni

pamoja na Washirika wetu wa Maendeleo, Viongozi wa ngazi mbalimbali,

Wananchi wa Tanzania kwa ujumla, ambao wamechangia katika kufanikisha

utekelezaji wa mipango ya elimu na mafunzo. Baadhi ya Washirika wetu wa

maendeleo ni kama ambavyo wameorodheshwa katika Hotuba yangu,

naomba nisiisome kwa sababu muda haupo.

Mheshimiwa Spika, maombi ya fedha kwa mwaka 2014/2015. Baada ya

Taarifa hii, sasa naliomba Bunge lako Tukufu liidhinishe Makadirio ya Matumizi ya

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ya jumla ya Shilingi 799,020,389,000 kwa

Mwaka wa Fedha 2014/2015, ili kuiwezesha Wizara kutekeleza majukumu yake.

Page 250: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

250

Mheshimiwa Spika, katika maombi haya:-

(a) Shilingi 93,247,873,000 zinaombwa kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida

ya Idara, ambapo Shilingi 52,976,832,000 ni kwa ajili ya Mishahara na Shilingi

40,271,041,000 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.

(b) Shilingi 250,959,183,000 zinaombwa kwa ajili ya Matumizi ya

Kawaida ya Taasisi. Kati ya hizo, Shilingi 215,779,416,000 ni kwa ajili ya mishahara

na Shilingi 35,179,767,000 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.

(c) Shilingi 454,813,333,000 zinaombwa kwa ajili ya Miradi ya

Maendeleo. Fedha za ndani ni Shilingi 383,734,000,000; kati ya hizo Shilingi

306,000,000,000 ni kwa ajili ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu. Shilingi

71,079,333,000 ni fedha za nje.

Mheshimiwa Spika, Hotuba hii inapatikana pia katika Tovuti ya Wizara kwa

Anuani ya www.moe.go.tz.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Spika,

naafiki.

(Hoja ilitolewa iamuliwe)

SPIKA: Hoja hiyo imeungwa mkono. Sasa nitamwita Mwenyekiti wa

Kamati iliyopitia Hoja hiyo.

Najua mmechoka. Mwenyekiti wa Kamati iliyopitia Hoja hiyo, hayupo?

Aah, Mheshimiwa Ngonyani, nilikuwa naangalia kwingine kabisa. (Makofi)

Kwa niaba yake Mheshimiwa Ngonyani, Makamu Mwenyekiti au? Eeh,

Makamu Mwenyekiti.

MHE. STEPHEN H. NGONYANI (K.n.y. MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU

YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mwenyekiti

makini wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii, Mama Magreth

Sitta, naomba kuwasilisha mbele ya Bunge lako Tukufu, Taarifa ya Kamati ya

Kudumu ya Bunge ya Huduma za Jamii kuhusu utekelezaji wa majukumu ya

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014,

pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha

Page 251: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

251

2014/2015, kwa mujibu wa Kanuni ya 99 (9) na Kanuni ya 117 (11) ya Kanuni za

Kudumu za Bunge, Toleo la Aprili, 2013.

Mheshimiwa Spika, awali ya yote, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa

kunipa uhai na afya njema kuweza kutumikia Wananchi wangu wa Jimbo la

Korogwe Vijijini. Naahidi kufanya kazi nao bila kujali na uwezo wangu wote

nitashirikiana nao. Aidha, nakushukuru sana Mheshimiwa Spika na Wajumbe wa

Kamati ya Huduma za Jamii pamoja na Wabunge wote, kwa kunifariji wakati

nilipopata msiba wa marehemu baba yangu.

Mheshimiwa Spika, naomba Taarifa yote ya Kamati ya Kudumu ya Bunge

ya Huduma za Jamii inakiliwe kwenye Hansard kama ilivyowasilishwa Mezani.

Mheshimiwa Spika, katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za Wizara ya

Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kujiridhisha na utekelezaji wa malengo ya Bajeti

ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014, Kamati ilifanya vikao na ziara

katika taasisi mbalimbali za Wizara ikiwemo Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

(National Council of Technical Education – NACTE), Taasisi ya Elimu ya Watu

Wazima, Chuo cha Mafunzo ya Elimu ya Ufundi Stadi Dar es Salaam, Bodi ya

Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu na Baraza la Mitihani la Taifa.

Kamati pia ilifanya ziara Mkoani Mtwara kukagua utekelezaji wa shughuli

za Miradi ya Maendeleo kwa mwaka wa Fedha 2013/2014, tarehe 3 - 7 Februari

2014. Kamati ilikagua Mradi wa Uimarishaji Elimu ya Msingi (MMEM) School Wash

Programme katika Shule ya Msingi Chikwaya, Mradi wa Uimarishaji Elimu ya

Sekondari (MMES) katika Shule za Sekondari za Naliendele na Mikindani, Mradi

wa Ukarabati wa Chuo cha Ualimu Kitangali na Mradi wa Ukuzaji Ajira kupitia

Elimu ya Mafunzo ya Ufundi Stadi Mkoani Mtwara.

Mheshimiwa Spika, maoni yanayolenga kuboresha utekelezaji wa

shughuli za Wizara ikiwemo Miradi ya Maendeleo iliyotekelezwa ni sehemu ya

Taarifa hii ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, tarehe 3 Mei, 2014, Kamati ya Bunge ya Huduma za

Jamii ilikutana Dodoma kujadili Taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya

Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014 pamoja na

makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015

iliyowasilishwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mheshimiwa Shukuru

Kawambwa.

Mheshimiwa Spika, taarifa ya Waziri ilikuwa na maeneo mahususi

yafuatayo:-

Page 252: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

252

(i) Utekelezaji wa maoni ya Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii

katika bajeti ya Wizara ya Mwaka 2013/2014.

(ii) Utekelezaji wa majukumu ya Wizara kwa Mwaka wa Fedha

2013/2014.

(iii) Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara kwa Mwaka wa

Fedha 2014/2015.

Mheshimiwa Spika, katika rejea ya maoni na mapendekezo ya Kamati ya

Bunge ya Huduma za Jamii kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014, napenda

kulitaarifu Bunge hili kwamba, Serikali imezingatia na kufanyia kazi baadhi ya

ushauri wa Kamati ikiwemo kutenganisha fedha za mikopo ya wanafunzi wa

elimu ya juu kutoka katika fedha za Matumizi ya Kawaida ya Wizara, ambapo

fedha hizo zimehamishiwa katika fedha za Miradi ya Maendeleo ya Wizara hii.

Mheshimiwa Spika, aidha, Kamati inaona bado kuna umuhimu wa

kufanyia kazi zaidi maeneo muhimu yafuatayo:-

(i) Mfumo unaotumika kuhudumia walimu nchini (Teachers Service

Delivery System) unaohusisha vyombo zaidi ya kimoja kuhudumia walimu na

kusababisha urasimu katika kupata stahiki za walimu.

(ii) Kuwezesha Idara ya Ukaguzi wa Elimu kuwa wakala ili kutekeleza

majukumu yake kwa ufanisi.

(iii) Utoaji posho maalumu kwa walimu wanaofanya kazi katika

mazingira magumu (Retention Scheme).

Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa Fedha 2013/2014 Wizara ilikadiria

kukusanya shilingi bilioni 171,518,704,600. Hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2014

Wizara ilikusanya maduhuli ya shilingi bilioni 129,122,797,360, sawa na asilimia 75.

Matumaini ya Kamati ni kwamba. Wizara itakamilisha makusanyo ya maduhuli

yaliyobaki katika Robo ya Nne ya Mwaka wa Fedha husika.

Mheshimiwa Spika, Bunge liliidhinisha jumla ya shilingi bilioni

689,681,055,000 kwa Wizara hii kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014, ambapo

shilingi bilioni 617,083,004,000 zilitengwa kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na

shilingi bilioni 72,598,051,000 zilitengwa kwa ajili ya kutekeleza wa Miradi ya

Maendeleo. Hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2014, Wizara ilikuwa imepokea shilingi

bilioni 486,573,220,250.94, sawa na asilimia 79 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida

na shilingi bilioni 14,921,545,855.46 sawa na asilimia 21 kwa ajili ya shughuli za

maendeleo.

Page 253: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

253

Mheshimiwa Spika, mwenendo wa fedha kwa ajili ya bajeti ya Miradi ya

Maendeleo hauridhishi kwani hadi kufikia Robo ya Tatu ya kipindi cha bajeti,

asilimia 21 tu ya bajeti ya Miradi ya Maendeleo ilikuwa imepokelewa na

imetumika. Hali hii imeathiri utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Wizara. Ni

maoni ya Kamati kuwa, Serikali izingatie kutekelezwa kwa malengo ya bajeti ya

Wizara yaliyowasilishwa na kuidhinishwa na Bunge hili kwa kutoa fedha kwa

wakati.

Mheshimiwa Spika, changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Elimu

nchini zilibainika kama ifuatavyo:-

(i) Ukosefu wa mpango ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

unaolenga kutekeleza vipaumbele walivyojiwekea;

(ii) Fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo zilizoidhinishwa na

Bunge kutotolewa kwa wakati;

(iii) Kuongeza makusanyo ya ndani ya Wizara kwa kubuni vyanzo vipya

vya makusanyo;

(iv) Mfumo dhaifu wa kuhudumia walimu unaohusisha vyombo zaidi ya

kimoja na hivyo kusababisha urasimu katika upatikanaji wa haki za walimu

nchini;

(v) Ukosefu wa posho ya mazingira magumu kwa walimu;

(vi) Utendaji kazi usioridhisha wa Idara ya Ukaguzi wa Elimu nchini

kutokana na ufinyu wa Bajeti;

(vii) Upungufu katika Sheria ya Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi

(NACTE) inayolenga kudhibiti utoaji holela wa mafunzo ya elimu ya ufundi stadi

nchini;

(viii) Mchango wa Skill Development Levy katika utekelezaji wa

majukumu ya VETA kutotosha;

(ix) Uhitaji wa programu maalumu ya mafunzo ya walimu katika

kuweka Mafunzo ya KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu);

(x) Kukosekana kwa utaratibu maalumu wa kuwatumia wahitimu wa

mafunzo ya elimu ya juu wanapopata ufadhili wa Serikali kupitia Bodi ya Mikopo

ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kuitumikia Serikali;

Page 254: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

254

(xi) Utoaji huduma kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu

kutengewa fedha za kutosha katika jukumu hilo kwa ufanisi; na

(xii) Ongezeko la wanafunzi wa elimu ya juu wanaohitaji mikopo.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka wa

Fedha 2014/2015 imekusudia kukusanya mapato yenye jumla ya shilingi

239,366,784,212. Aidha, Wizara imeomba kuidhinishiwa jumla ya shilingi

799,020,389,000 ambapo shilingi 344,207,056,000 ni kwa ajili ya Matumizi ya

Kawaida (Recurrent Expenditure) na shilingi 454,813,333,000 ni kwa ajili ya

Matumizi ya Maendeleo (Development Expenditure) kwa Mwaka 2014/2015.

Aidha, shilingi 73,525,913,460 zimetengwa kutekeleza Miradi ya Wizara iliyopo

katika Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa.

Mheshimiwa Spika, Kamati ilifanya uchambuzi wa kina wa taarifa ya

mgawanyo wa fedha katika Bajeti ya Wizara hii na kubaini uhitaji wa fedha kwa

baadhi ya vifungu vyenye mahitaji ya lazima, ikiwemo kifungu cha Ukaguzi wa

Elimu nchini, Mafunzo ya Ualimu na Mamlaka ya Elimu Tanzania. Kamati ilishauri

kuhamisha fedha katika baadhi ya vifungu vya Wizara ili kuiwezesha kiutendaji

vifungu husika vyenye uhitaji.

Mheshimiwa Spika, tarehe 3 Mei, 2014 Kamati ilikutana Dodoma na Waziri

wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kupewa mrejesho kuzingatia ushauri wa

Kamati na kufanya marekebisho kibajeti katika vifungu vya Wizara. Jumla ya

fedha zilizoongezwa katika vifungu hivyo ni shilingi 1,977,234,248 kama

zilivyofafanuliwa hapa chini.

Kifungu 5001 – Kasma 221700, tengeo la awali Sh. 7,969,500,000, fedha

iliyoongezwa Sh. 1,005,009,324, tengeo jipya Sh. 8,974,509,324; Kifungu 2002 –

Kasma 230400, tengeo la awali Sh. 53,601,360, fedha iliyoongezwa Sh.

16,398,640, tengeo jipya Sh. 70,000,000; Kifungu 2002 – Kasma 230300, tengeo la

awali Sh. 430,731,000, fedha iliyoongezwa Sh. 269,269,000, tengeo jipya Sh.

700,000,000; Kifungu 2002 – Kasma 221000, tengeo la awali Sh. 754,564,000,

fedha iliyoongezwa Sh. 286,557,248, tengeo jipya Sh. 1,041,121,284; Kifungu 7001

– Kasma 270400, tengeo la awali Sh. 2,044,357,000, fedha iliyoongezwa Sh.

400,000,000, tengeo jipya Sh. 2,444,357,000; Jumla Sh. 1,977,234,248.

Mheshimiwa Spika, Kamati inaipongeza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya

Ufundi kwa kuzingatia ushauri wa Kamati na kufanya mabadiliko ya ndani ya

vifungu vya Wizara ili kuwezesha Idara ya Ukaguzi wa Elimu, Mamlaka ya Elimu

Tanzania na Mafunzo ya Ualimu, kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

SPIKA: Kwa mujibu ya Kanuni ya 28(5), naongeza muda usiozidi dakika

thelathini mpaka amalize Hotuba hii. Endelea tafadhali!

Page 255: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

255

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, Kamati inatoa maoni na

ushauri unaolenga kuboresha utolewaji wa elimu nchini katika maeneo

yafuatayo:-

Mheshimiwa Spika, Kamati inaipongeza Serikali kwa kuanzisha utekelezaji

wa Mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) katika Sekta ya Elimu

Nchini. Mpango huu utaweka misingi katika kufikia maendeleo endelevu ya

nchi na Wananchi kwa ujumla. Pamoja na juhudi za Serikali kutenga jumla ya

shilingi milioni 73.52 kwa Wizara kutekeleza Mpango huu katika sekta ya elimu

nchini, ni ushauri wa Kamati kwamba, Miradi ya BRN katika Sekta hii iwekewe

vigezo vya kutekelezwa inavyopimiwa katika kupata matokeo yake. Hatua hii

itawezesha kuthamini mafanikio yanayopatikana.

Mheshimiwa Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2014/2015, Wizara ya Elimu na

Mafunzo ya Ufundi yenye idadi ya taasisi 28, imekusudia kukusanya mapato

yenye jumla ya shilingi 239,366,784,212. Aidha, Wizara imekusudia kutumia jumla

ya shilingi 344,207,056,000 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kamati inaamini

bado kuna umuhimu wa kuongeza makusanyo ya ndani ya Wizara

ikilinganishwa na kiwango cha Matumizi ya Kawaida, kwa kutekeleza

yafuatayo:-

(i) Wizara ibuni vyanzo vipya vya mapato ya ndani; kwa mfano,

kuiwezesha Taasisi ya Elimu Tanzania kutegemea mapishano mbalimbali kwa

matumizi ya jamii ndani na nje ya nchi.

(ii) Kuwezesha Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima kufanya matengenezo

ya mashine kubwa ya uchapishaji ili kuongeza makusanyo ya ndani.

(iii) Taasisi zinazoonesha upungufu katika ukusanyaji maduhuli

zifuatiliwe kikamilifu.

Mheshimiwa Spika, katika kujadili malengo ya Wizara ya Elimu kwa

Mwaka wa Fedha 2014/2015, Wizara imejiwekea vipaumbele vyake kutekeleza

majukumu. Ni ushauri wa Kamati kwamba, vipaumbele husika vya Wizara

vizingatie vigezo vya SMART kwa lengo la kupima matokeo. Aidha, mikakati

madhubuti itumike ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Mheshimiwa Spika, kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo

ya Wizara hii imekuwa ikikwama kutokana na ukosefu wa fedha za utekelezaji

wa Miradi hiyo. Hadi kufikia robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2013/2014, ni

asilimia 21 tu ya fedha za Miradi ya Maendeleo ambazo zilipokelewa na Wizara.

Kamati inaishauri Serikali iwezeshe Wizara kutekeleza Miradi ya Maendeleo ya

Sekta ya Elimu ambayo ni moja ya Sekta zilizoko kwenye Mpango wa Serikali wa

Page 256: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

256

Matokeo Makubwa Sasa, kwa kupeleka fedha zilizoidhinishwa na Bunge kwa

wakati.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo kwa Mwaka

2013/2014: Katika kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya Fungu 46,

Kamati imebaini changamoto mbalimbali na kushauri ifuatavyo:-

(i) Ili kuwezesha utekelezaji endelevu wa Miradi ya kuongeza sifa na

kuajiriwa kupitia mafunzo ya VETA Mtwara, unaofadhiliwa na Kampuni ya British

Gas, ni vyema Shirika la TPDC lihusike katika kufadhili utekelezaji wa Mradi huu ili

kuwezesha kudumu endapo Kampuni ya British Gas itamaliza muda wa

kufadhili. Mradi huu ni muhimu kwani una lengo la kuwawezesha wahitimu wa

mafunzo haya kutumia fedha mbalimbali zinazoambatanishwa na ugunduzi wa

gesi Mkoani Mtwara.

(ii) Mradi wa uimarishaji wa Elimu ya Sekondari hususan katika ujenzi

wa miundombinu ikiwemo maabara. Baada ya Kamati kubaini mchanganyiko

katika matumizi ya ramani za ujenzi wa meza za maabara, inashauri kwamba,

miongozo ya ujenzi wa miundombinu hii ya shule izingatiwe. Aidha, kuna

umuhimu wa kuangalia upya miongozo iendane na hali halisi ya mazingira ya

uhitaji wa shule.

(iii) Mradi wa ukarabati wa Maktaba nchini ikiwemo Maktaba ya

Mtwara. Pamoja na juhudi za Serikali kukarabati maktaba mbalimbali nchini ili

ziweze kutoa huduma kwa ufanisi, ni ushauri wa Kamati kwamba, Serikali

ichukue juhudi za makusudi kuinua utamaduni wa kupenda kusoma vitabu

nchini.

Mheshimiwa Spika, moja ya mambo yanayosababisha walimu

kutohudumiwa ipasavyo ni mfumo unaotumika kuwahudumia (Teachers Service

Delivery System). Walimu wanahudumiwa na vyombo zaidi ya kimoja na

kusababisha adha nyingi ikiwemo urasimu katika kupanda madaraja,

kujiendeleza kimasomo, utekelezaji wa malipo ya haki zao mbalimbali kama

mishahara na likizo. Kamati inasisitiza yafuatayo:-

(i) Serikali iangalie upya mfumo wa kuhudumia Walimu kwa kuanzisha

Tume ya Utumishi wa Walimu ili kukabiliana na adha inayowakabili walimu wetu

nchini.

(ii) Serikali iwakutanishe wadau mbalimbali wa Sekta ya Elimu nchini

kujadili na hatimaye kufikia mwafaka kuhusu kuwa na utaratibu maalumu wa

kuwahudumia walimu kama njia mojawapo ya kuwezesha utekelezaji wa

Mpango wa Serikali wa Matokeo Makubwa Sasa katika Sekta ya Elimu.

Page 257: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

257

Mheshimiwa Spika, imedhihirika kwamba, upungufu wa walimu hasa

katika maeneo ya vijijini unasababishwa kwa kiasi kikubwa na uwepo wa

mazingira magumu katika kutekeleza majukumu yao. Kamati inaendelea

kuishauri Serikali ikamilishe mapema iwezekanavyo, mchakato wa kutoa posho

ya mazingira magumu kwa walimu wanaofanya kazi katika mazingira magumu

ili kuwafanya wabaki katika mazingira hayo na kuipenda taaluma yao.

Mheshimiwa Spika, utoaji wa mafunzo kwa walimu kazini ni jambo la

msingi katika kuboresha utekelezaji wa Mpango wa Serikali wa Matokeo

Makubwa Sasa katika Sekta ya Elimu. Pamoja na juhudi mbalimbali za Serikali

zinazochukuliwa kuboresha utoaji wa elimu nchini, Kamati inasisitiza kwamba,

mafunzo kwa walimu kazini yapewe kipaumbele na Wizara ya Elimu na Mafunzo

ya Ufundi iratibu utekelezaji wa utoaji mafunzo kazini kwa walimu ikiwemo

kutenga Vyuo vya Ualimu katika ngazi ya Kanda ili kutekeleza jukumu hilo

muhimu.

Mheshimiwa Spika, ili kusimamia viwango vya Elimu inayotolewa nchini

sambamba na ongezeko la taasisi mbalimbali takribani 20,000 zinazotoa elimu

ya awali, msingi, sekondari na vyuo vya ualimu, Kamati inasisitiza yafuatayo:-

(i) Serikali iiwezeshe Idara ya Ukaguzi wa Elimu nchini kuwa wakala

unaojitegemea ili kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

(ii) Serikali iiwezeshe Idara hii kifedha na kivifaa. Aidha, fedha

zilizotengwa kwa ajili ya kutekeleza jukumu la Ukaguzi wa Elimu zitumike kwa

kuzingatia kusudi hilo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na nia njema ya Serikali ya kujenga Chuo

kimoja cha VETA katika kila Wilaya nchini, Kamati imebaini changamoto za

uhitaji wa fedha kuwezesha VETA kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Kamati

inashauri kwamba, Skills Development Levy inayopelekwa kuhudumia utolewaji

wa mafunzo ya ufundi iongezwe kutoka asilimia mbili kwenda asilimia nne ili

kuwezesha VETA kufanya kazi kikamilifu na pia kuweza kuvisaidia Vyuo vya

Maendeleo ya Wananchi kutoa huduma za Mafunzo hayo muhimu kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, kumekuwa na changamoto kubwa ya udhibiti wa

utoaji wa mafunzo ya elimu ya ufundi stadi nchini. Hatua inayosababishwa na

upungufu katika Sheria ya NACTE kuwezesha utekelezaji wa jukumu hili muhimu.

Kamati imeshauri kwamba, Sheria ya NACTE iboreshwe, kuiwezesha taasisi hii

kusimamia kikamilifu suala la ubora wa mafunzo ya elimu na ufundi stadi nchini.

Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi kubwa ya Serikali ya kutenga kiasi

kikubwa cha fedha kuhudumia Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu mwaka

hadi mwaka, kwa lengo la kuwezesha idadi kubwa ya wanafunzi kupata Elimu

ya Juu nchini, Kamati inashauriyafuatayo:-

Page 258: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

258

(i) Ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa watumishi katika

sekta mbalimbali ikiwemo Sekta ya Elimu hususan katika maeneo ya

pembezoni, Serikali ibuni utaratibu maalumu utakaowezesha wahitimu

wanaonufaika na mikopo kufunga Mikataba Maalumu kwa kutumikia nchi

katika maeneo mbalimbali nchini kwa kipindi maalumu.

(ii) Pamoja na utaratibu unaotumiwa na Serikali kutoa mikopo hiyo

kwa kuzingatia masomo ya vipaumbele, suala la kutoa mikopo kwa kulenga

wanafunzi wanaotoka katika familia duni pia lipewe umuhimu unaostahili, ikiwa

ni dhumuni la msingi la utoaji wa mikopo hiyo.

(iii) Ili kuwezesha kuinua uwezo wa kutoa mikopo kwa idadi kubwa ya

wahitaji, Serikali iendelee kuchukua juhudi za makusudi kuongeza makusanyo

ya Mikopo iliyokwishatolewa tangu mwaka 1991.

Mheshimiwa Spika, watu wenye ulemavu ni kundi muhimu linalohitaji

mazingira rafiki na vifaa maalumu vya kuwawezesha kupata elimu kwa

maendeleo yao na Taifa kwa ujumla. Kamati inaitaka Serikali kuwa na mkakati

wa makusudi wa kuboresha mazingira ya utoaji elimu kwa wenye ulemavu

nchini kwa kutenga fedha za kutosha. Aidha, Serikali itoe Mwongozo wa Kitaifa

wa ujenzi wa miundombinu rafiki ikiwemo matumizi ya lugha ya alama na

alama mguso katika utaratibu wa kutoa mafunzo kwa kuzingatia mahitaji ya

watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Spika, baada ya Kamati kufanya ziara katika Taasisi ya Elimu

ya Watu Wazima ilibaini uwepo wa uhitaji wa ukarabati mkubwa wa mashine

ya kutengeneza machapisho mbalimbali na hivyo, kusababisha uwezo mdogo

wa Taasisi kukusanya mapato ya ndani. Kamati inashauri kwamba, Serikali

iwezeshe ukarabati wa mashine hiyo muhimu mapema iwezekanavyo. Hatua hii

itaiwezesha Taasisi kukusanya mapato yake ya ndani kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, ilipata fursa ya

kuhudhuria Maadhimisho ya Wiki ya Elimu nchini yaliyofanyika katika Viwanja

vya Jamhuri Dodoma. Kamati imeipongeza sana Serikali kwa kuanzisha

maadhimisho haya kwani yatatoa fursa kwa wadau mbalimbali wa elimu

kushiriki, kutafakari, kutathmini na kubuni mikakati mbalimbali yenye lengo la

kuboresha hali ya utolewaji wa elimu nchini. Ili kufanikisha suala hili, Kamati

ilishauri kwamba, shughuli zinazotekelezwa katika kipindi hiki ziboreshwe ili

zilenge katika kuinua kiwango cha elimu nchini. Aidha, matumizi ya TEHAMA

kwa kutumia “The Tireless Teacher” kama teknolojia mbadala ya kufundishia

masomo ya sayansi ienezwe katika maeneo mengi nchini ili kukabiliana na

upungufu wa walimu wa sayansi.

Page 259: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

259

Mheshimiwa Spika, Kamati ilijadili kwa kina Taarifa ya Wizara kuhusu

upangaji wa alama za ufaulu na utunuku wa madaraja katika mitihani ya elimu

ya sekondari nchini ambayo imefafanuliwa katika Jedwali Namba II, lililopo

ukurasa wa 21. Taarifa hii inaonesha kwamba, A itakuwa na marks kuanzia 75 –

100, ambayo ni bora sana (Excellent); B+: itakuwa 60 – 74, ambayo ni vizuri sana

(Very Good); B: 50 – 59 vizuri (Good); C: 40 – 49 wastani (Average); D: 30 – 39

inaridhisha (Satisfactory); E: 20 – 29 hairidhishi (Unsatisfactory); na F: 0 – 19 feli

(Fail). Aidha, Kamati ilielezwa kwamba, kiwango cha chini cha ufaulu (pass)

katika somo ni Gredi D wenye alama 30 – 39 waliopewa maelezo ya inaridhisha.

Mheshimiwa Spika, pamoja na Kamati kuelezwa kwamba, Bodi ya Baraza

la Mitihani Tanzania imeshiriki katika kuboresha mchakato huu, inashauri

kwamba, Serikali itoe elimu kwa wadau mbalimbali wa Sekta ya Elimu nchini

kuhusiana na suala hili ili kuondoa mchanganyiko uliopo katika jamii.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru wewe binafsi kwa kushirikiana na Kamati

yangu, kila tulipokuwa tunahitaji ushauri kutoka kwako ulikuwa unatupa ushauri

mzuri na ulikuwa unatuelekeza vizuri. Ninamshukuru Katibu wetu wa Bunge na

Dada Stella, ambaye alituongoza sana katika kuikamilisha Hotuba yetu nzuri

tuliyoitoa leo. Ninamshukuru pia Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi -

Mheshimiwa Shukuru Kawambwa, Naibu Waziri wa Elimu ya Mafunzo -

Mheshimiwa Jenista Mhagama, dada yangu na Watendaji wote wa Wizara ya

hii, wakiongozwa na Katibu Mkuu Profesa Sifuni Mchome, kwa kushirikiana na

Kamati.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya

Huduma za Jamii, Mama Margaret Simwanza Sitta, kwa kushirikiana nami katika

kuiongoza vyema kamati.

Kwa namna ya pekee, nawashukuru Wajumbe wote wa Kamati ya Bunge

wa Huduma za Jamii, kwa busara na umakini katika kujadili Bajeti ya Wizara ya

Elimu ya Mafunzo ya Ufundi kwa Mwaka 2014/2015.

Naomba niwatambue kwa majina kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta – Mwenyekiti, Mheshimiwa Stephen

Hillary Ngonyani – Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Fatuma Abdallah Mikidadi,

Mheshimiwa Agripina Zaituni Buyogera, Mheshimiwa Faki Haji Makame,

Mheshimiwa Christowaja Gerson Mtinda, Mheshimiwa Riziki Omar Juma,

Mheshimiwa Ezekia Dibogo Wenje, Mheshimiwa Antony Gervas Mbassa,

Mheshimiwa Ali Juma Haji, Mheshimiwa Juma Sururu Juma, Mheshimiwa

Gregory George Teu, Mheshimiwa Abia Muhama Nyabakari, Mheshimiwa

Salome Daudi Mwambu, Mheshimiwa Zabein Muhaji Mhita, Mheshimiwa

Page 260: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

260

Mohamed Gulam Dewji, Mheshimiwa Martha Jachi Umbulla, Mheshimiwa Prof.

Kulikoyela Kanalwanda Kahigi, Mheshimiwa Hasnain Mohamed Murji,

Mheshimiwa Cecilia Daniel Paresso na Mheshimiwa Abdulaziz Mohamed

Abood.

Mheshimiwa Spika, kwa kumalizia nawashukuru Watendaji wote wa Ofisi

ya Bunge, akiwemo Katibu wa Kamati hii Ndugu Stella Mlambo, chini ya

Uongozi mahiri wa Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah, kwa kuratibu vyema

shughuli za Kamati.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, naunga mkono hoja na

ninaomba kuwasilisha. Ahsante sana.

SPIKA: Maji Marefu leo umejitahidi kweli.

Waheshimiwa Wabunge, kwa kutumia dakika nilizonazo, napenda

niwatambue wageni wa Mheshimiwa Waziri wa Elimu na Mafunzo, ambao ni

Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi, Wakaguzi na Maofisa mbalimbali

wanaoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo - Profesa Sifuni Mchome; alipo

anaweza kusimama ahsante sana.

Yupo Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kinondoni na

Viongozi 45 wa Kata 34 wakiongozwa na Ndugu Salum Madege. Huyu ndiyo

Mwenyekiti mwenyewe; Ndugu Salum yuko wapi? Huo ndiyo ujumbe wa kutoka

Kinondoni; karibuni sana maana asubuhi mlikosa nafasi.

Tunao Walimu 15 ambao ni Viongozi wa CWT Taifa wa Mkoa wa

Dodoma, wakiongozwa na Ndugu Stella Milinga - Katibu Manispaa ya Dodoma.

Naomba hawa wote wasimame walipo; ahsanteni sana.

Nina tangazo lingine la kazi; Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya

Miundombinu, Mheshimiwa Peter Serukamba, anaomba niwatangazie

Wajumbe wa Kamati yake kwamba, kesho tarehe 18 Mei, 2014 kutakuwa na

kikao cha Kamati kwa ajili ya kukamilisha taarifa kuhusu makadirio ya bajeti ya

Wizara ya Ujenzi ya Mwaka wa Fedha 2013/2014. Hakusema mahali, lakini

nadhani baada ya ibada labda saa tano, nafikiri saa tano mkutane huko,

maana ni Siku ya Jumapili.

Waheshimiwa Wabunge, naomba nichukue nafasi hii, kuwashukuru sana

kwa kazi tuliyoifanya wiki hii, ilikuwa nzito lakini mmeweza kufanya vizuri.

Naomba kila siku tunapofanya kazi yetu upendo uendelee kuwepo pamoja na

sisi. Sisi sote tunatetea kitu kimoja, tunatetea masilahi ya Wananchi, hizi tabia za

Page 261: BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE ...parliament.go.tz/polis/uploads/documents/1458115215-HS...ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya watoto chini ya miaka 18 Tanzania

Nakala ya Mtandao (Online Document)

261

vuta nikuvute bila sababu, nadhani tuangalie, katika mambo mengine siyo

lazima.

Ninawashukuru sana kwa wiki hii nzima na niwatakie Jumapili njema,

kesho, tuendelee kukutana Siku ya Jumatatu, saa tatu asubuhi.

(Saa 2.09 usiku Bunge liliahirishwa hadi Siku ya Jumatatu,

Tarehe 19 Mei, 2014 Saa Tatu Asubuhi)