Upload
others
View
30
Download
0
Embed Size (px)
Citation preview
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
CEKENA JOINT EXAMINATION
102/1
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA KWANZA
INSHA
JULAI 2019
MUDA: SAA 1 3/4
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI
(KENYA CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION)
1. Wewe ni mwenyekiti wa kamati ya kupigana na ufisadi nchini Kenya na umealikwa, kuhutubia
kongamano la kitaifa kuhusu athari za ufisadi huku ukipendekeza hatua za kukabiliana na janga hili.
Andika hotuba utakayoitoa. (Alama 20)
2. Nyimbo za kitamanduni zilikuwa na nafasi kubwa katika ufanisi wa jamii kwa jumla.
Eleza. ( Alama 20)
3. Andika kisa kitakachodhihirisha ukweli wa methali isemayo;.
Bahati ni chudi (Alama 20)
4. Andika insha itakayomalizia kwa maneno yafuatayo;
……………………. Hapo ndipo iliponibainikia kuwa nilikuwa nikiogelea baharini pekee kinyume
na wenzangu wote. (Alama 20)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
CEKENA JOINT EXAMINATION
102/2
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA PILI
SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA
JULAI 2019
MUDA: SAA 2 1/2
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI 2019
(KENYA CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION)
A. UFAHAMU (ALAMA 15)
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali
Hakuna dakika inayopita bila kisa cha kuchelewa. Mikutano karibu yote huchelewa kuanza kwa sababu
wahusika hawafiki wakati ufaao. Ibada nazo hucheleweshwa kwa uzembe wa waumini. Na mazishi je?
Taratibu hucheleweshwa vilevile. Ingawa hapa yaweza kufikiriwa kuwa pengine wampendao marehemu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
hawataki kuharakisha safari yake ya kwenda kuzimuni. Lakini hata arusi ambazo huwa na misururu ya
mikutano ya maandalizi, siku itimiapo shughuli huchelewa. Si ajabu sherehe kuendelea mpaka usiku
ambapo ratiba ilionyesha zingekomea masaa ya alasiri.
Uchunguzi unabainisha kuwa watu huchelewa kwa sababu mbalimbali. Sababu mojawapo ni
kutowajibika; yaani, watu wengi hawaoni umuhimu wa kuzingatia saa. Wengine hufanya hivi kwa
kisingizio kuwa ni kawaida ya mwafrika kutozingatia muda. Huu ni upuuzi mtupu. Wazee wetu
walizingatia muda ipasavyo tangu jadi ingawa hawakuwa na saa wala kalenda. Hii ndiyo sababu
walipanda mimea walipohitajika, wakavuna na hatimaye wakapika na kuandaa ipasavyo. Wahenga hawa
walituachia methali nyingi kama funzo, kwa mfano; ‘Chelewachelewa utakuta mwana si wako’, na hata
wakasindikiza kuwa, ‘Ngoja ngoja huumiza matumbo’.
Watu wengine huchelewa kwa sababu ya kutojiandaa kwa yale yatakayojiri. Watu wasiopanga
shughuli zao na badala yake kuzifanya kwa kushtukia aghalabu hushindwa kuhudhuria hata mahojiano ya
kuajiriwa kazi kwa wakati ufaao. Hawa huwa neema kwa washindani wao. Kujitayarisha si jambo gumu.
Anachopasa kujua mhusika ni saa ya miadi na hali ya usafiri.
Hivi viwili vitamwezesha kujua muda wa safari na hivyo kukadiria wakati wa kuondoka. Ni wangapi
wameiona milolongo ya watu nje ya milango ya benki wakiwasihi mabawabu na pengine kuwahonga
wawaruhusu kuingia? Hawa huwa si wageni. Ni wateja wanaojua ratiba ya kazi lakini hushindwa kupanga
mwenendo wao barabara.
Mikutano, sherehe na shughuli nyingi huchelewa kuanza kwa masaa mengi kwa sababu eti mgeni
mashuhuri amechelewa kufika. Muda wa kungoja huwa mrefu zaidi kutegemea ukubwa wa cheo cha
mhusika. Watu hawa huchelewa makusudi kwa sababu pengine ya kiburi. Majivuno haya huwafanya
wafurahi wanaposubiriwa na watu wadogo. Wakubwa hawa wanapofika badala ya kuomba msamaha,
hujigamba kuhusu majukumu yao mengi na makubwa.
Aidha kuna watu ambao hupenda kutekeleza mambo mengi kwa wakati mmoja. Tujuavyo ni kuwa
mambo mawili yalimshinda fisi. Pia watu wanaposhika mengi, mahudhurio yao katika baadhi ya mambo
hutatizwa na hivyo huchelewa. Isitoshe, kuna watu wa aina hii hata wanapopewa ratiba mapema,
hujikokota na hivyo kupitwa na wakati.
Ingawa sababu tulizozitaja hutokana na watu wenyewe, kuna zile zinazosababishwa na dharura
nyingine. Hizi ni pamoja na misongamano ya magari, kuchelewa kwa vyombo vya usafiri na hata
kuharibika kwa vyombo. Hii ndiyo sababu inashauriwa kuwa mtu anapoamua kutekeleza jambo, atenge
muda takribani wa dakika 30 kwa ajili ya dharura fulani. Kwa hivyo hata anapopata tuseme pancha njiani
bado atafika kwa wakati ufaao.
Kuchelewa hakuudhi tu watu wanaocheleweshwa bali huwa na matokeo mengine mengi. Mara nyingi
watu waliochelewa huharakisha mambo ili kufidia muda walioupoteza. Kama wanaendesha gari, kwa
mfano, basi huzidisha kasi matokeo huweza kuwa ajali ambayo mara nyingine huleta ulemavu au vifo.
Ratiba ya mambo ichelewapo watu waliofika mapema hupoteza muda kusubiri. Muda huu
wangeutumia kwa harakati muhimu. Mfumo wa uchumi wa kisasi unahitaji mamilioni ya watu
kukurubiana, kutagusana na kuendesha shughuli zao kwa ujima. Aidha, watu hawana budi kubadilishana
bidhaa na huduma. Mambo haya yanapocheleweshwa basi gharama huwa kubwa.
Tatizo hili hubainika sana katika ofisi za umma.
Ni kwaida watu kufika kazini dakika nyingi baada ya wakati wa kufungua milango ya kazini.
Ajabu ni kuwa wafanyakazi wawa huwa wa kwanza kufunga kazi kabla ya kipindi rasmi.
Inakisiwa Kenya hupoteza shilingi bilioni 80 kila mwaka kupitia uzembe wa kutozingatia wakati.
Jambo la kwanza ni kuweka sera ya kitaifa inayolenga kuwaelimisha wananchi umuhimu wakuzingatia
saa. Halikadhalika kanuni iwekwe ya kuwafungia nje watu wanaochelewa kuhudhuriashughuli za mikutano
au hafla. Wananchi nao wazinduliwe kuwa ni haki yao kufumkana muda washughuli unapowadia kabla
mgeni wa heshima kufika. Nchi ya Ekwado (Ecuador) imefanikiwakutekeleza haya. Kenya pia haina budi
kuandama mwelekeo huo. Hii
ndiyo njia mojawapo ya kufufua uchumi na kuhakikisha taifa linapiga hatua kimaendeleo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Maswali:
1. Kipe kifungu hiki anwani mwafaka (ala. 1)
______________________________________________________________________
2. Taja watu watatu walio na mazoea ya kuchelewa katika shughuli walizoalikwa (ala. 3)
_______________________________________________________________________________
_______________________________________________________________________________
____________________________________________________
3. Taja sababu zinazofanya watu kushindwa kutimiza miadi (ala. 4)
_______________________________________________________________________________
_______________________________________________________________________________
_______________________________________________________________________________
___________________________________________
4. Taja na ueleze njia nne zinazoweza kuondoa tatizo la kuchelewa (ala. 4)
_______________________________________________________________________________
_______________________________________________________________________________
_______________________________________________________________________________
___________________________________________Eleza maana ya maneno haya kama
yalivyotumiwa katika taarifa (ala. 3)
a) Ujima
b) Miadi
c) Pancha
B. UFUPISHO (ALAMA 15)
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali yote
Takriban kila siku vyombo vya habari hueleza kuhusu mateso ya watoto; cha kusikitisha zaidi ni
kwamba mbali na visa vinavyoripotiwa, kuna vingine chungu nzima ambavyo havijaripotiwa. Mateso
kwa watoto hawa ni ya aina mbalimbali. Mwezi wa Julai, 2005 wavamizi walipowaua watu zaidi ya
sabini Kaskazini mwa Kenya, walianza kwa kuwauwa watoto katika shule ya msingi ya Mabweni.
Waliwauwa watoto ishirini na wawili huku mamia wakijehuriwa.
Kuna wazazi ambao huwapiga watoto wao mithili ya kumpiga nyoka. Utaona watoto wakiwa na
majeraha yanayofanya malaika kusimama mwilini. Visa vingi vimeripotiwa ambapo wazazi au walevi
huwakata au kuwadhuru watoto sehemu fulani za mwili kama vile masikio, miguu au mikono. Vilevile,
kumetokea visa vya kuwachoma watoto na wengine kuwachwa bila chakula.
Kenya ni mojawapo ya nchi zilizotia sahihi mkataba wa kulinda haki za watoto. Serikali yetu ina
idara katika ofisi ya makamu wa rais inayoshughulikia maslahi ya watoto. Mwezi wa Julai 2005,
Serikali ilianzisha kampeni kabambe za kukomesha mateso dhidi ya watoto. Ajabu ni kwamba watu
wengi na hata watoto wenyewe hawajui haki zao. Sheria ya watoto ilipitishwa ili kutetea haki za watoto
katika nchi ya Kenya.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Baadhi ya haki za watoto ni kama vile kulindwa kutokana na ubaguzi wowote, kutunzwa na
wazazi na kupewa elimu. Watoto wana haki ya elimu ya kiakademia na dini. Vilevile wana haki ya
kulindwa kiafya. Watoto hawatakikani kunyanyaswa kiuchumi au kwa njia nyinginezo kama vile
kusajiliwa kupigana katika vita. Kila mtoto akiwemo mlemavu, ana haki ya kuheshimiwa katika jamii.
Hata hivyo, sharti pia watoto wawajibike ipasavyo kwa wazazi, walezi na jamii kwa jumla. Mtoto
anapaswa kuheshimu wakuu wake na kuwasaidia panapo haja. Watoto wana jukumu la kudumisha na
kuimarisha umoja wa jamii na raia kuendeleza maadili mema katika jamii.
Maswali:
(a) Fupisha aya ya kwanza na ya pili kwa maneno 60-80 (ala. 6, mtiririko 1 )
Matayarisho
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_____________________________________________
________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
________________________________________________________________________
________________________________________________________________________
Jibu
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_____________________________________________
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(b) Bainisha mambo muhimu aliyoyajadili mwandishi katika aya tatu za mwisho.
(Maneno 100 – 120 ) (ala. 20, mtiririko 1)
Matayarisho
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
Jibu
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
______________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
____________________________________
C. SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
(a) Taja vipasuo viwili vya ufizi (alama 2)
_________________________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
(b) Onyesha maumbo mawili ya silabi funge kwa kutolea mifano katika maneno (alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(c) Bainisha mofimu za neno ‘kilichonywewa’ (alama 3)
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(d) Unda nomino moja moja kutokana na nomino zifuatazo (alama2)
(i) Madhara _____________________________________________________________
(ii) Kitenzi_____________________________________________________________
(e) Tambua virai vihusishi katika sentensi ifuatayo (alama 2)
Wengine wao waliegesha kando ya barabara iliyokarabatiwa na kampuni ya Kichina
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
________________________________________________________________________
(f) Andika sentensi zifuatazo upya kwa kutumia ‘po’ (alama 2)
(i) Raia wakipatana maendeleo yataimarika
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(ii) Mkiwatesa watoto wenu mtashtakiwa
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(g) Andika kwa ukubwa hali timilifu (alama 3)
Mtego ulimnasa ndovu huyo
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_____________________________________________
(h) Andika sentensi ifuatayo upya ukibadilisha neno lililopigiwa mstari kuwa kivumishi (ala. 2)
Msichana amepigwa vibaya
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(i) Ainisha yambwa na chagizo katika sentensi ifuatayo (alama 4)
Wanafunzi walimwatikia mwalimu mkuu miche ya matunda nje ya nyumba yake kwa ustadi
wakitumia vijiti.
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(j) Andika visawe viwili vya neno ‘vurumai’ (alama 2)
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(k) Taja na utolee mifano matumizi mawili ya mshazari (alama 2)
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(l) Tunga sentensi yenye muundo ufuatao kisha uichanganue kwa matawi (alama 4)
S – KN (N + V) + KT (T + E)
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(m) Andika kwa usemi halisi (alama 2)
Kyalo alikiri kuwa kama wangefika mapema wangekamilisha shughuli zote
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(n) Tofautisha maana ya sentensi zifuatazo (alama 2)
(i) Alipokelewa mgeni
(ii) Alipokezwa mgeni
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(o) Andika kinyume (alama 3)
Vijana walivunja kambi baada ya macheo
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
(p) Kanusha (alama 3)
Asha aliwapelekea wageni chakula na akawanavya mikono
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
_________________________________________________________________________________
_______________________________________________________________
D. ISIMU JAMII (ALAMA 10)
(a) Eleza sifa zozote tano za lugha ya itifaki (alama 5)
________________________________________________________________________________
________________________________________________________________________________
_____________________________________________________
________________________________________________________________________________
________________________________________________________________________________
_____________________________________________________
(b) Hakiki sifa zozote tano za sajili ya kituo cha polisi (alama 5)
________________________________________________________________________________
________________________________________________________________________________
________________________________________________________________________________
________________________________________________________________________________
________________________________________________________________________________
__________________________
CEKENA JOINT EXAMINTION
102/3
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA TATU
FASIHI
JULAI 2019
MUDA: SAA 2 1/2
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI 2019
(KENYA CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION)
SEHEMU A: Riwaya
1. LAZIMA
Assumpta K. Matei: Chozi la heri
“Hili lilimtia …………. uchungu, akajiona kama aliyedhalilishwa na mwanamke.”
(a) Yaweke maneno haya katika muktadha wake (alama 4)
(b) Taja suala linalodokezwa katika dondoo hili (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(c) Kwa kutumia hoja kumi na tano, eleza namna suala ulilolitaja hapo juu 1 (b) linalijitokeza
(ala. 15)
SEHEMU B: Tamthilia
Kigogo (Pauline Kea)
Jibu swali la pili au la tatu
2. “Kubali pendekezo letu la kufungwa kwa soko……… huoni hii ni fursa nzuri ya kulipiza kisasi?”
(a) Fafanua muktadha wa dondoo hili (alama 4)
(b) Kufungwa kwa soko ni ukatili. Mbali na ukatili huu, toa mifano mingine ya ukatili kwenye
tamthilia. (alama 9)
(c) Msemaji wa maneno haya ni mshauri mbaya. Thibitisha kutoka kwenye dondoo na kwingineko
tamthiliani. (alama 7)
3. (a) Fafanua mbinu kumi anazotumia Majoka katika kuuendeleza uongozi wake (alama 10)
(b) Eleza namna mbinu ya ishara ilivyotumiwa katika tamthilia ya Kigogo (alama 10)
Tumbo Lisiloshiba na Hadithi Nyingine ( Alifa Chokocho na Dumu Kayanda)
Jibu swali la 4 au la 5
4. “…………… Ningeondoka ….. mapema niende niibe au niue ili niwe mtu wa maana.”
a) Eleza muktadha wa maneno haya (alama 4)
b) Onyesha vile Kinaya kinavyojitokeza katika dondoo hili (alama 2)
c) “Kinaya kimetumika kwingine katika hadithi husika. Thibitisha kwa kutumia hoja tisa (alama 9)
d) Eleza umuhimu wa msemaji katika hadithi hii (alama 5)
5. (a) Eleza namna maudhui ya ndoa yalivyosawiriwa katika hadithi ya Masharti ya Kisasa
(alama 13) (b) Kwa
kurejelea hadithi ya Shibe inatumaliza, eleza namna maudhui ya ufisadi yanavyojitokeza
(alama 7)
SEHEMU D: Fasihi Simulizi
6. Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali
Heri ujue mapema
Nasaba yetu haina woga
Woga haumei kwetu, humea kwa kina mamako.
Tulichinja jogoo na fahali ili uwe mwanaume.
Ah! Kisu cha ngariba ni kikali ajabu.
Iwapo utatikisa kichwacho.
Uhamie kwa wasiotahiri,
Ama tukwite njeku.
Mpwangu kumbuka hili,
Wanaume wa mlango wetu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Si waoga wa kisu
Wao hukatwa mchana hadi usiku
Wala hawalalamiki.
Siku nilipokatwa
Nilisimama tisti
Nikacheka ngariba kwa tashtiti
Halikunitoka chozi.
Iwapo utapepesa kope
Wasichana wa kwetu na wa mbali
Wote watakucheka
Ubaki ukinuna.
Sembe umepokea
Na supu ya makongoro ukabugia
Sema unachotaka
Usije kunitia aibu
Maswali;
(a) Taja na uthibitishe shughuli zozote za kiuchumi za jamii ya wimbo huu (alama 4)
(b) Ni nani mwimbaji wa wimbo huu na anawaimbia nani? (alama 2)
(c) Huu ni wimbo wa aina gani? Thibitisha (alama 2)
(d) Mwimbaji wa wimbo huu ana taasubi ya kiume. Thibitisha kauli hii. (alama 2)
(e) Eleza wajibu wa nyimbo katika jamii (alama 6)
(f) Ijapokuwa nyimbo ni nzuri, zina ubaya wake. Thibitisha kauli hii (alama 4)
SEHEMU E: Ushairi (alama 20)
Jibu swali la 7 au la 8
7. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Kama dau baharini, duniya inavyoyumba,
Limeshamiri tufani, kila mmoja lakumba,
Viumbe tu hali gani!
Duniya yatishika, utahisi kama kwamba,
Vilima vyaporomoka, na kuvurugika myamba,
Viumbe tu hali gani!
Tufani hilo la kusi, languruma na kutamba,
Linapuliza kwa kasi, hapana kisichoyumba,
Viumbe tu hali gani!
Mujiwe ni kubwa sana, mfanowe kama nyumba,
Yazuka na kugongana, wala hatuna la kwamba,
Viumbe tu hali gani!
Mibuyu hata mivule, kama usufi na pamba,
Inarusha vilevile, seuze hiyi migomba
Viumbe tu hali gani!
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Ni kipi kilotuliya, tuwazeni na kudumba,
Mandovu kiangaliya, yagongana na masimba,
Fisi wako hali gani!
Hata papa baharini, tufani limewakumba,
Walioko mikondoni, kila mmoja asamba,
Dagaa wa hali gani!
Mashehe wa mdaduwa, kwa ubani na uvumba,
Tufani hilo kwa kuwa, kusoze kwake kutamba,
Itokee afueni!
(Shairi la ‘Tufani’ la Haji Gora Haji, katika Tamthilia ya Maisha, uk 62)
Maswali;
(a) Taja na ueleze mikondo ya shairi hili (alama 4)
(b) Eleza dhamira ya shairi hili (alama 2)
(c) Taja tamathali za usemi zilizotumiwa katika shairi hili. (alama 2)
(d) Eleza muundo wa shairi hili (alama 4)
(e) Eleza ujumbe unaojitokeza katika ubeti wa tano. (alama 3)
(f) Onyesha matumizi ya idhini ya kishairi . (alama 3)
(g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kwa mjibu wa shairi hili (alama 2)
Mdaduwa :
Kutamba :
8. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Daima alfajiri na mapema
Hunipitia na jembe na kotama
Katika njia iendayo Kondeni
Kama walivyofanya babuze zamani;
Nimuonapo huwa anatabasamu
Kama mtu aliye na hamu
Kushika mpini na kutokwa jasho
Ili kujikimu kupata malisho.
Anapotembea anasikiliza
Videge vya anga vinavyotumbuiza
Utadhani huwa vimemngojea
Kwa usiku kucha kuja kumwimbia
Pia pepo baridi kumpepea
Rihi ya maua zikimtetea
Nao umande kumbusu miguuni;
Na miti yote hujipinda migogo
Kumpapasa, kumtoa matongo;
Na yeye kundelea kwa furaha
Kuliko yeyote ninayemjua
Akichekelea ha ha ha ha ha ha …….
Na mimi kubaki kujiuliza
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kuna siri gani inayomliwaza?
Au ni kujua au kutojua?
Furaha ya mtu ni furaha gani?
Katika dunia inayomhini?
Ukali wa jua wamnyima zao
Soko la dunia lamkaba koo;
Dini za kudhani zamsonga roho
Ayalimia matumbo ya waroho.
Kuna jambo gani linalomridhisha?
Kama si kujua ni kutojua
Lait angalijua, laity angalijua!
Maswali:
a) Eleza hali ya mzungumziwa katika shairi hili. (alama 2)
b) Huku ukitoa mifano, onyesha aina mbili za uhuru wa kishairi uliotumiwa katika shairi hili
(ala. 4)
c) Fafanua aina tatu za taswira ukirejelea ubeti wa pili (alama 3)
d) Maswali ya balagha katika shairi hili yanasisitiza maudhui yapi? (alama 2)
13 of 14 (kisw. P3)
e) Kwa kutoa mifano, bainisha vipengele vitatu vya Kimtindo katika shairi hili (alama 3)
f) Eleza toni ya shairi hili (alama 2)
g) Bainisha nafsineni katika shairi hili (alama 1)
h) Eleza muundo wa shairi hili (alama 3)
CEKENA JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI 2019
102/1
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA KWANZA
INSHA
MWONGOZO WA INSHA
1. Hii ni insha ya hotuba
Muundo wa hotuba ufuatwe
(a) Kichwa – Kiandikwe kwa herufi kubwa na kipigiwe mstari
Kianzie kwa neno Hotuba….
(b) Utangulizi uwepo
(c) Mwili – Wenye hoja zinazofuatana kimantiki
(d) Hitimisho
Maudhui ya kuzingatiwa
(a) Madhara ya ufisadi
(i) Pesa za miradi mbalimbali ya maendeleo kubadhiriwa.
(ii) Wafadhili kukataa kuipa nchi mikopo na pesa za maendeleo.
(iii) Kiwango duni cha miradi inayotekelezwa
(iv) Kuwepo kwa wafanyikazi wasiohitimu kazini
(v) Uchumi wa nchi kudorora
(vi) Huduma muhimu kukosekana kwa wananchi
(vii) Migomo ya mara kwa mara
(viii) Baadhi ya maeneo ya nchi kutengwa kimaendeleo
(ix) Hatimiliki bandia kuwepo kwa wingi
(x) Kuzuka kwa biashara haramu
(b) Njia za kupambana na ufisadi
(i) Kuwaelimisha raia kuhusu madhara ya ufisadi
(ii) Jamii kuwajibika katika vita vya kupambana na ufisadi
(iii) Kuwepo kwa sheria kali ambazo zitawafunga wafisadi
(iv) Wafanyakazi wa serikali kutangaza mali wanayomiliki
(v) Kulipwa mishara bora kwa wafanyakazi ili wasiwe fisadi
(vi) Dini kufunza waumini maadili
(vii) Mali ya watu fisadi itwaliwe na serikali
(viii) Kampeni dhidi ya ufisadi kupamba moto.
(ix) Pesa za umma zikusanywe kwa njia ya kiteknolojia.
2. Nafasi ya nyimbo za kitamanduni katika ufanisi wa jamii
(i) Zilitumika kukuza vipawa vya uimbaji
(ii) Kuboresha umoja na ushirikiano katika jamii
(iii) Kama njia ya kuburudisha wanajamii
(iv) Kuwaepusha vijana katika fikra za kutenda maovu
(v) Zilitumika kufunza maadili katika jamii
(vi) Zilitumika kama kigezo cha kukuza lugha
(vii) Zilitumika kukashifu matendo hasi katika jamii
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(viii) Katika sherehe hizi vijana waliweza kupata wachumba
(ix) Zilitumika kuendeleza na kufunza mila na tamaduni za jamii husika.
3. Bahati ni chudi
Chudi ni bidii
Maana ya methali hii ni kuwa ili kufanikiwa katika jambo Fulani ni sharti mtu afanyie jambo hilo bidii
kubwa.
Methali hii hutumiwa kuwahimiza watu wazidishe bidii kazini mwao ili waweze kufanikiwa.
(i) Kisa lazima kioane na maana ya methali hii
(ii) Pande zote mbili za methali zidhihirike.
4. Msimulizi ajipate katika hali ambapo yuko kivyake. Kwa mfano amepotoka na baadaye anagundua
wenzake hawajapotoka au anafanya bidii peke yake na wengine wanalaza damu.
Au anaunga au kupinga jambo fulani pekee na alidhani wako pamoja na wenzake.
Tan: Mtahini atumie nafsi ya kwanza
CEKENA JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI 2019
102/2
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA PILI
LUGHA
MWONGOZO WA LUGHA
SEHEMU A: UFAHAMU (Alama 15)
1. Kipe kifungu hiki anwani mwafaka (alama 1)
Kutuza muda/wakati/ kuchelewa
2. Taja watu walio na mazoea ya kuchelewa katika shughuli walizoalikwa (alama 3)
(i) Waumini katika ibada
(ii) Waombolezaji kwa mazishi
(iii) Wanaohudhuria harusi na maharusi
(iv) Wateja wa benki
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(v) Wanaohojiwa kwa kutafuta kazi
(vi) Wageni mashuhuri katika mikutano
6 x ½ = 3
3. Taja sababu zinazofanya watu kushindwa kutimiza miadi (alama 4)
(i) Uzembe
(ii) Kutowajibika /mapuuza / kisingizio
(iii) Kutojiandaa kwa ipasavyo / kutopanga
(iv) Kutekeleza mambo mengi kwa pamoja
(v) Kuharibika kwa vyombo vya usafiri
(vi) Kiburi 4 x 1 = 4
4. Taja na ueleze njia nne zinazoweza kuondoa tatizo la kuchelewa (alama 4)
(i) Kujitayarisha /kujiandaa mapema / mf. Kupanga mwenendo wa barabara
(ii) Kuwajibika katika kuzingatia wakati/ratiba
(iii) Kuweka sera za kuwaelimisha watu kuhusu umuhimu wa kuzingatia saa
(iv) Kuweka kanuni za kuwafungia nje wanaochelewa
(v) Wananchi wazinduliwe kuwa wana haki ya kufumukana muda wa shughuli unapokwisha
5. Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa katika taarifa (alama 3)
(a) Ujima – Ushirikiano
(b) Miadi – ahadi ya kukutana kwa sababu maalum
(c) Pancha – mpasuko kwa gurudumu
SEHEMU B: UFUPISHO (Alama 15)
(a) Kila siku vyombo vya habari hueleza kuhusu mateso ya watoto
- Kuna vingine ambavyo havijaripotiwa
- Watoto huuawa na wavamizi vitani
- Kuna wazazi wanaowapiga watoto kinyama
- Kuwachoma
- Kuachwa bila chakula
(b) Kenya ni mojawapo ya nchi zilizotia sahihi mkataba wa kulinda haki za watoto
- Ina idara katika ofisi ya makamu wa rais inayoshughulikia maslahi ya watoto
- Serikali ilianzisha kampeni kabambe za kukomesha mateso dhidi ya watoto
- Watu wengi na hata watoto wenyewe hawajui haki zao
- Sheria ya watoto ilipitishwa ili kutetea haki za watoto katika nchi ya Kenya
- Watoto wanafaa kulindwa kutokana na ubaguzi/ kutunzwa na wazazi na kupewa elimu ya
kiakademia na dini / kulindwa kiafya / kuheshimiwa katika jamii.
- Watoto wasinyanyaswe kiuchumi
- Watoto wenyewe wanapaswa kuwasaidia wazazi wao inapostahili.
- Watoto wanafaa kudumisha umoja wa jamii na kuendeleza maadili katika jamii
(alama 8 + 1 ya mtiririko)
Adhabu
- Adhibu kosa la sarufi litokeapo kwa mara ya kwanza hadi 6 x ½ = 3
- Adhibu kosa la hijai litokeapo kwa mara ya kwanza hadi 6 x ½ = 3
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU C: SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (Alama 40)
(a) Vipasuo (alama 2)
/dw/ /tw/ (2 x 1= 2)
(b) (i) KKK – blan – keti (alama 2)
(ii) K - Mlango, m – tu
(iii) lK - Al – hamisi
(iv) KIK - Mak - taba Dak – tari (2 x 1 = 2)
(c) Kilichonywewa (alama 3)
Ki - li - cho - nyw - ew - a
Ngeli ya wakati kirejeshi mzizi kauli ya kiishio
KI -VI uliopita mnyambuliko (6 x ½ = 3)
(d) Unda nomino (alama 2)
(i) Madhara - kudhuru
(ii) Kitenzi - kitendo, tendo, mtendaji, utendaji, n.k. (2 x 1 = 2)
(e) Tambua virai vihisishi (alama 2)
Wengine wao waliegesha kando ya barabara iliyokarabatiwa na kampuni ya kichina
Kando ya barabara - RH
Na kampuni ya kichina - RH (2 x 1 = 2)
2 of 4 (Kisw. P2)
(f) i) Raia wakipatana maendeleo yataimarika (alama 2)
Raia watakapopatana maendeleo yataimarika
ii) Mkiwatesa watoto wenu mtashtakiwa
Mwatesapo watoto wenu mtashtakiwa (2 x 1 = 2)
(g) Mtego ulimnasa ndovu huyo (alama 3)
Jitego / Tego limelinasa jidovu / dovu hilo (6 x ½ = 3)
(h) Msichana amepigwa vibaya (alama 2)
Msichana mbaya amepigwa (1 x 2 = 2)
V
(i) Yambwa tendwa - miche ya matunda (alama 4)
Yambwa tendewa - mwalimu mkuu
Yambwa ala - vijiti
Chagizo - nje ya nyumba yake (4 x 1 = 4)
(j) Vurumai (alama 2)
- ghasia, fujo, zogo, vurugu, kizaazaa,rangaito, kivangaito, tendabeluwa (2 x 1 = 2)
(k) (i) maana na (alama 2)
ii) au
iii) Sawa sawa na
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv) Kuandika tarehe
( Mwalimu akadirie mifano) (2 x 1 = 2)
(l) S - KN(N + V) + KT (T + E) (alama 4)
KN KT
Walimu wote / walikusanyika ukumbini
N V T E (4 x ½ = 2)
S
KN KT
N V T E (4 x ½ = 2)
Walimu wote walikusanyika ukumbini
(m) “Tungefika mapema tungekamilisha shughuli zote,” Alikiri Kyalo (alama 2)
Kyalo alikiri, “Tungefika mapema tungekamilisha shughuli zote.” (1 x 2 = 2)
(n) i) Alipokelewa mgeni (alama2)
Mgeni alipokelewa kwa niaba yake
ii) Alipokezwa mgeni
Alitetewa mgeni ampokee (2 x 1 = 2)
(o) Kinyume cha sentensi (alama 3)
Vijana walikita kambi kabla yamachweo / mawio / magharibi (3 x 1 = 3)
(p) Asha hakuwapelekea wageni chakula walahakuwanavya mikono (3 x 1 = 3)
SEHEMU D: ISIMU JAMII (Alama 10)
(a) Sifa zozote tano za lugha ya itifaki (alama 5)
Itifaki ni lugha inayotumika katika shughuli za kiubalozi
1) Huwa ni lugha ya adabu hata palipo na uhasama
2) Hutaja vyeo na sifa za wahusika pamoja na nchi zao, mfano; Balozi au mjumbe wa Jamhuri fulani.
3) Hulazimu maamkizi au maneno machache ya utangulizi kwa mwenyeji
4) Huhusisha maneno sahili yaliyoteuliwa kwa uangalifu ili kufanikisha mawasiliano
5) Lugha ya wastani isiyo na mihemko kama furaha na ukali
6) Huhitaji matumizi mwafaka ya shadda, toni na vituo.
7) Hutegemea matumizi ya viziada lugha kama vile, tabasamu na miondoko.
8) Hutumia tasfida kuficha ukali ili kutochoma au kuzua uhasama.
9) Msamiati unaotumiwa hutegemea mada, mazingira na dhamira.
(zozote tano) (5 x 1 = 5)
(b) Hakiki sifa zozote tano za sajiliya kituo cha polisi (alama 5)
1) Lugha yenye ukali. – lugha ya kuamrisha
2) Kuna maswali dadisi
3) Lugha ya sheria hutumika. Mfano; wakili
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
4) Lugha ya kunyenyekea
5) Lugha ya misimu. Mf; mguu wa kuku – bastola
6) Kuna kuchanganya na kubadilisha msimbo
(zozote tano) (5 x 1 = 5)
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI 2019
102/3
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA TATU
FASIHI
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
1. (a) maelezo ya mwandishi
- Anamrejelea Bwana Kimbaumbau
- Ni baada ya Sauna kukataa kushiriki mapenzi naye
- Wote wawili walikuwa Kazini
(4 x 1 = 4)
(b) Ubabedume/ Taasubi ya kiume (1 x 1 = 1)
(c)
(i) Jamaa za Kangata kupinga elimu ya mabinti zake
(ii) Kimbaumbau kumdhulumu Naomi anapokataa kujihusisha kimapenzi naye.
(iii) Mwimo Msubili kutotaka kukutana na mwanamke asubuhi kwa madai kuwa ni Mkosi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(iv) Lime na Mwanaheri kunajisiwa na vijana wahuni.
(v) Bwana Maya anamdhulumu mamake Sauna kwa mapigo na matusi aulizapo swali lolote lile.
(vi) Kuuzwa kwa Pete kwa Fungo ili wazazi wake wapate pesa za kuwaelimisha ndugu zake
watano wa kiume.
(vii) Pete anabakwa na mlevi anapolewa chakari
(viii) Mamake Zohari kuridhia kila asemalo mumewe na kushidwa kumtetea anapopata himila.
(ix) Mamake Mwangeke aliwahi kumwonya kulia kama msichana. Hii ni ishara kuwa jamii
yamwona mwanamke kama mnyonge.
(x) Mwanzi anakataa kukubali matokeo ya uchaguzi madhali anashindwa na mwanamke,
Mwekevu.
(xi) Wahafidhina kuamini kwamba mtoto wa kiume ndiye pekee anayestahili kuwa mrithi wa mali
ya babake.
(xii) Ushindi wa Mwekevu unaonekana kama kutoheshimiwa kwa mwanaume.
(xiii) Mwekevu kusingiziwa wizi wa kura anapomshida Mwanzi.
(xiv) Kutishwa, kutusiwa na hata kutengwa kwa Mwekevu anapojitosa katika siasa zilizoaminiwa
kuwa ni za wanaume
(xv) Fungo anamharibia Pete maisha anapomwoa kisha kumfukuza anapojifungua mtoto.
(xvi) Mwanamke kuonekana kama mnyonge anayestahili kulia akabiliwapo na vizingiti au
changamoto maishani. Mwanaume hafai kulia
(alama 15 x 1 = 15) (zingatia hoja nyingine zozote sahihi)
2. (a) maneno haya ni ya sauti ya mzee Kenga mawazoni mwa Majoka. Haya yanatendeka katika Ofisi
ya Mzee Majoka wakati Husda na Ashua wanapigana. Majoka anakumbuka ushauri wa Kenga wa jinsi
ya kumnasa Ashua kwa kusababisha fujo baina yake na Husda
(b) (i) Kumwaga kemikali na taka sokoni licha ya kuwa wananchi wanakaa na kufanyia biashara zao
katika soko.
(ii) Kuwatumia wahuni kunyamazisha wapinzani. Mzee Kenga anakutana na Wahuni chini ya mbuyu
ambao baadaye wanamwumiza Tunu.
(iii)Kuruhusu dawa za kulevya na wanafunzi ambao wanakuwa makabeji
(iv) Kuwaua wapinzani, kama vile vijana watano walioandamana
(v) Kuwatumia polisi kuwaua na kurushia waandamanaji risasi na vitoa machozi.
(vi) Kuwanyima wafanyakazi haki, kama vile walimu na wauguzi wanaongezewa asilimia ndogo ya
mshahara kasha kupandisha kodi.
(vii) Utawala kuruhusu uuzaji wa pombe haramu kinyume na katiba, ambao umesababisha vifo na
kufanya watu kuwa vipofu.
(viii) Kufungulia biashara ya ukataji miti ilhai watu wanategemea miti hiyo kuboresha mazingira.
(ix) Kufunga kituo cha runinga ya Mzalendo kwa kuonyesha mkutano wa Tunu na wapinzani wengine
wa utawala.
(x) Utawala kutumia vyombo vya dola kuwafukuza watu wanaoenda sokoni na kuweka ulinzi mkali
licha ya kuwa ulikuwa uwanja wa umma.
(xi) Kuwarushia wakazi vijikaratasi vyenye ujumbe hasimu wakitakikana wapahame mahali ambapo
wamekuwa wakiishi kwa muda wote wa uhai wao.
(c) (i) Kenga anamshauri Majoka amwalike Ashua na Husda ili patashika itokee, naye Majoka apate
jinsi atakavyolipiza kisasi kwa Sudi kwa kukataa kuchonga kinyago.
(ii) Anamshauri Majoka atangaze kuwa maandamano ni haramu kisha anawamuru maafisa wa polisi
watumie nguvu zaidi dhidi ya umma unaondoa maandamano.
(iii) Majoka anakataa Suala la polisi kutumia nguvu zaidi lakini Kenga anamwambia “Acha moyo wa
huruma….. Siasa na hisia haziivi kwenye chungu kimoja ndugu yangu.
(iv) Anakubali pendekezo la Majoka la kufunga Runinga ya Mzalendo kwa kupeperusha matangazo
ya mkutano moja kwa moja.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(v) Kenga alihusika katika kupanga mauaji ya Jabali kwani Majoka anamsifu kwa kupanga hilo na
hata wanapigishana Konzi
(vi) Anaibua pendekezo la kumuua Chopi kwa kutofuata maagizo ya kumuua Tunu akisema, “Nafikiri
Chopi lazima aende safari.”
(vii) Anamwambia Majoka kuwa si kweli kwamba watu watampigia Tunu kura na kusema, “Tunu
hawezi kupigiwa hata!”
(viii) Anapendekea kukusanya kodi ya juu na kukataa kuitumia vyema na kwa njia halali k.v.
kutoa taka.
3. (a) Fafanua mbinu nane anazotumia Majoka katika uongozi wake.
a) Uvumi kwa mfano – Sudi na Ashua wanaiwinda roho ya Tunu
ii) Ahadi za uwongo – kutoa chakula kwa wasiojiweza
iii) Zawadi - keki za uhuru
iv) Vitisho - Akiwa chopi watamwaga unga
v) Mapendeleo - Tunu na Ashua walipewa kazi wakakataa. Ashua angekuwa mwalimu mkuu katika
shule mojawapo za Majoka kama angekubali.
vi) Sela - Wanaompinga wanafungwa jela k.v. Sudi anasema amefungwa mara nyingi katika jela
alikofungwa Ashua.
vii) polisi - polisi wanatawanya waandamanaji
viii) Mabavu - Madai ya kuwafukuza wafadhili wa wapinzani ili wavunje kambi zao Sagamoyo,
Nguvu zaidi kutawanya waandamanji
ix) Kudhibiti vyombo vya dola - Majoka kutaka kufunga vituo vyote kibaki Sauti ya Mashujaa
x) Ulaghai - mf. Kuongeza mishahara ya walimu na wauguzi kisha kupandisha kodi.
xi) mavamizi - mf. Tunu kuvamiwa na kuvunjwa muundi
xii) Ulinzi - Majoka ana walinzi wengi. (10 x 1 = 10)
(b) Ishara
i) Kinyago cha kike kinachochongwa na Sudi na kukiita shujaa halisi wa Sagamoyo kinaashiria
shujaa wa kike atakayelikomboa Jimbo la Sagamoyo dhidi ya uongozi dhalimu
(ii) Fimbo ya Kenga yenye kichwa cha Nyoka ni ishara ya jinsi alivyokuwa katili kwa raia. Kwa
mfano, anamuua Jabali
(iii)Uchafu wa soko ya chapakazi ambao unamsababisha hata Mzee Kenga kuziba pua yake
anapoenda huko ni ishara ya maovu yaliyokithiri jimboni Sagamoyo.
(iv) Kitendo cha Majoka kuzungumza na babu yake anapozirai ni ishara kuwa wafu walikuwa
wakimwita madhali naye aliokuwa amewaua
(v) Majoka kuvaa mkufu shingoni wenye kidani cha umbo la swila ni ishara ya namna Majoka
alivyokuwa hatari kwa maisha ya raia wa jimbo la Sagamoyo.
(vi) Kujaa kwa maziara jimboni Sagamoyo hadi hakuna nafasi ya kuwazika wafu wengine ni ishara
ya mauaji yaliyokuwa yametekelezwa na Majoka.
(vii) Kilio na machozi mengi ndani ya ziwa lililofunika damu ni ishara ya raia waliouliwa na
Majoka wanalilia haki yao.
(viii) Kutojaa kwa raia jinsi ilivyo kawaida katika mkutano wa kuadhinisha sherehe za uhuru pamoja
na siku ya kuzaliwa kwa Majoka ni ishara ya raia kuasi Majoka kutokana na uongozi wake
dhalimu.
(ix) Hali ya Majoka kujiona ndani ya ziwa lililofurika damu ni ishara ya mauaji mengi ya raia
aliyokuwa akitekeleza katika uongozi wake.
(x) Damu ya Jabali anayoiona Majoka ikitiririka mikononi mwake akiwa amezirai ni ishara kuwa
yeye ndiye aliyemuua Jabali
(Zingatia nyingine zozote sahihi alama 10 x 1 = 10)
4. (a) Eleza muktadha wa maneno haya (alama 4)
Haya ni maneno ya Jairo. Anahutubu katika sherehe ya kumuaga mwalimu Mosi ambaye alikuwa
anastaafu kutoka kazi ya ualimu. Sherehe hii ilifanyika shuleni. Jairo anamkosoa mwalimu Mosi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
kumpatia matumaini ya uongo masomoni ilhali alijua hawakuwa na uwezo wa kimasomo badala ya
kumruhusu aende ajaribu mbinu nyingine ya kujikimu kimaisha ili awe mtu wa maana katika jamii.
(b) Onyesh vile kinaya kinavyojitokeza (alama 2)
Jairo anamkosoa mwalimu kwa kumfunza na kumpa matumaini maishani badala ya kumwachilia
mapema aende akaibe na kuua. Jairo analodokeza hapa ni kuwa ili mtu awe wa maana ni lazima aibe
na aue.
(c) “Kinaya kimetumika kwingine kwingi katika hadithi ya Mwalimu Mstaafu” Thibitisha
(ala. 9)
• Ni kinaya kwa Jairo kudai ili mtu awe wa maana, athaminiwe na kuitwa mhesimiwa na kuwa
bingwa lazima aibe, apore au aue
• Ni kinaya kwa Jairo kuuona uelekezi na ushauri wa mwalimu wake kama upotoshi na upotezaji
wa muda. Jairo anadai alipotezewa muda kwa kupatiwa matumaini ya uongo.
• Ni kinaya pia kwa mwalimu Mosi kutaka ahutubie mtu ambaye atamkosa badala ya kumsifu.
• Ni kinaya kwa Jairo kuona elimu haina manufaa yeyote ilhali wenzake walifaidi kutoka kwa
elimu ya mwalimu wao.
• Ni kinaya kwa Jairo kumtoa bintiye na mkewe kama zawadi kwa mwalimu wake kama shukrani
ya zawadi anazompa. Ni kinaya kwa mtu kubadili mkewe kama zawadi.
• Ni kinaya kwa Jairo kudai kuwa pombe ni kiliwazo cha kimawazo kinachomsahaulisha masibu
ya maisha na kumkosoa mwalimu wake kwa kumwonya dhidi ya matumizi ya pombe.
• Ni kinaya kwa mkewe jairo kukubali kitendo cha mumewe Jairo kumtoa kama zawadi kwa
familia nyingine. Anakubali kubadilishwa na mali.
• Ni kinaya kwa Jairo kudai kuwa ufuska ndio raha ya maisha na kuwa uaadilifu haufai. Anadai
kuwa maisha ni bora bila nasaha za mwalimu.
• Ni kinaya kwa mkewe mwalimu Mosi, Sera kukubali na kumkaribisha mwanamke mwingine na
watoto wake kwenye familia yake.
(hoja zozote 9)
(d) Umuhimu wa msemaji katika hadithi (alama 5)
➢ Ni kielelezo cha utovu wa nidhamu miongoni wa wanafunzi. Anakunywa pombe na hata
kujihusisha katika ufuska.
➢ Kupitia kwake uwajibikaji wa mwalimu Mosi unajitokeza. Kama mwalimu alimkanya kunywa
pombe na hata ufuska.
➢ Anaendeleza maudhui ya umaskini katika hadithi.
➢ Anakuza sifa za wahusika wengine kama vile Mwalimu Mosi.
➢ Ametumiwa kudhihirisha ukweli wa methali “asante ya punda ni mateke.”
5. (a) Masharti ya Kisasa
• Mwanaume humposa mwanamke. Dadi alienda nyumbani kwa Kidawa kumposa
• Mwanamke ndiye huamua wakati wa kuolewa na nani wa kumwoa. Kidawa alimchagua Dadi
baada ya muda mrefu.
• Ndoa huandamana na masharti. Dadi alipewa masharti na Kidawa ili akubali kuolewa naye.
• Wanandoa hufanya kazi pamoja ili kukithi mahitaji ya nyumbani. Dadi anachunza samaki na
Kidawa ni metroni
• Wanaume hawafurahi wake wao wanapotangamana na wanaume wengine. Kidawa
anaposimama kuongea na wanaume, Dadi anadhika sana.
• Wanandoa husaidiana kazi za nyumbani, Dadi anasaidia kidawa kazi za nyumbani kama vile
kuosha vyombo na kufagia.
• Wanandoa wanapanga uzazi, Dadi na Kidawa wanapanga kuwa na mtoto mmoja pekee.
• Mwanamke anaajiriwa. Kidawa aliajiriwa shuleni kama metroni.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Mwanamke anajinunulia nguo na fashoni nyingine. Kidawa ananunua viatu na kanzu anayovalia
kwenda kazini.
• Ndoa imekosa uaminifu. Dadi anashuku kuwa Kidawa ana mapenzi na mwalimu mkuu.
• Kiwango cha elimu si kikwazo katika ndoa. Kidawa anaolewa na Dadi licha ya kuwa ana kisomo
cha juu kuliko Dadi.
• Mwanamke amekengeuka. Kidawa anapenda fashoni.
• Wote wawili. Mwanamke na mwanaume wanachangizana nyumbani.
• Kuna makubaliano ya kufanya mambo kwa pamoja. (13 x 1 = 13)
(b) Shibe inatumaliza
• Mzee Mambo hafanyi kazi wizarani ilhali analipwa mshahara mkubwa kuliko Sasa na Mbura
wanaofanya kazi wizarani
• Mambo anatumia runinga ya taifa inayofaa kuufahamisha umma masuala ya taifa lao kwa
maslahi yake. Anaitumia kupeperusha sherehe inauofahamika nyumbani kwake.
• Mambo anaifilisi serikali kwa kutumia pesa za serikali kugharamia sherehe zake binafsi. DJ na
wenzake wanalipwa mabilioni ya pesa za serikali kwa kusimamia sherehe hii.
• DJ anaipunja serikali kwa kutumia mtaji wa bohari kuu ya dawa za serikali kufungua duka lake
la dawa.
• DJ anaifilisi serikali kwa kupokea huduma za maji, umeme na matibabu bure ilhali wananchi
maskini wanazilipia.
• Wafanyakazi wa umma wanaibia serikali saa za kazi. Sasa na Mbura wanahudhuria sherehe
zilizofanyika kwa Mambo siku nzima ilhali walipaswa kuwa kazini.
• Mzee Mambo anatumia magari ya serikali kwa maslahi yake binafsi. Kwa mfano, anayatumia
kusomba maji, chakula, kuwaleta jamaa wa Mambo shereheni na mapambo.
(7 x 1 = 7)
6. (a) Shughuli za kiuchumi
(i) Ufugaji / wafugaji – Anayeimbiwa wimbo alipozaliwa fahali alichinjwa.
(ii) Ukulima / kilimo - Anaahidiwa shamba la migomba na maparachichi
(2 x 2 = 4) ( lazima mwanfunzi athibitishe)
(b) Nani mwimbaji wa wimbo na anamwimbia nani? (alama 2)
Mwimbaji – mjomba
Mwimbiwa – mpwa (mtoto wa dadake mwimbaji)
(2 x 1 = 2)
(c) Huu ni wimbo wa aina gani? Thibitisha (alama 2)
Wimbo wa tohara / nyisho – mpwake anatayarishiwa kukabiliana na kisu cha ngariba
Mwanafunzi lazima athibitishe (2 x 1 = 2)
(d) Mwimbaji wa wimbo huu ana taasubi ya kiume – Thibitisha kauli hii (alama 2)
▪ Anaona kuwa waoga ni akina mama
▪ Anasifu wanume wa mbari yao kuwa si waoga
▪ Akilia atachekwa na wasichana
▪ Anaambiwa kuwa ni “Ndume / mme” akabiliane na kisu (2 x 1 = 2)
(e) Nyimbo zina wajibu gani katika jamii (alama 6)
▪ Huwatayarisha wanapoenda kupashwa tohara
▪ Hukashifu woga na kuhimiza ujasiri
▪ Husawiri falsafa ya jamii. Wanaume hawaogopi.
▪ Huonyesha majukumu mapya ya wanaotiwa jandoni
▪ Huleta jamii pamoja
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
▪ Hukuza na kuendeleza tamaduni na desturi za jamii
▪ Hutumbuiza / huburudisha
▪ Hukosoa / kusahihisha maovu (6 x 1 = 6)
(f) Ijapokuwa nyimbo ni nzuri zina ubaya wake. Thibitisha kauli hii (alama 4)
(ubaya wa nyimbo)
• Huweza kuibua hisia za ukabila na utabaka
• Hutumika kueneza propaganda. Hueneza uchochezi
• Kuna ukosefu wa maadili katika baadhi ya nyimbo. Baadhi huwa na matusi, vitendo vya ngono
n.k.
• Nyimbo zinalevya/ pumbaza watu
• Husababisha uzembe
• Baadhi huwa ghali/huhitaji kiasi kingi cha pesa kununua au kutoa na kuzirekodi
(4 x 1 =4)
7. (a)Taja na ueleze mikondo ya shairi hili (alama 4)
▪ Tathlitha
▪ Mathnani
▪ Msuko
▪ Ukara
▪ Sabilia
(b) Eleza dhamira ya shairi hili (alama 2)
Kuzindua /kuonyesha watu jinsi maisha ya ulimwengu yalivyo na misukosuko/ matatizo
(c) Taja tamathali za usemi zilizotumiwa katika shairi hili (alama 2)
Sitiari - papa, ndovu, samba, fisi dagaa – kusimamia watu
Tashbihi - kama dau baharini, mibuyu na mivute inatikiswa kama usufi na pamba
(d) Eleza muundo wa shairi hili (alama 4)
▪ Beti 8
▪ Kila ubeti una mishororo mitatu
▪ Kila mshororo una migao 2 ila kibwagizo (cha mmoja)
▪ Vina vya mwisho vinatiririka lakini vya kati haritiririki
▪ Shairi halina kibwagizo
(e) Eleza ujumbe unaojitokeza katika ubeti wa 5 (alama 3)
Mibuyu na mivute inasukwa kama pamba au usufi seuze migomba hii, viumbe tu hali gani
(f) Onyesha matumizi ya idhini ya kishairi (alama 3)
Tabdila - duniya, mgamba, hiyi, kiangaliya
Inkisari - la kwamba (kuamba – kusema)
Kuboronga sarufi – na kuvurugika myamba
- Limeshamiri tofani
- Kila mmoja lakumba
- Mibuyu… kama usufi na pamba inarushwa
(g) Eleza maana ya maneno haya (alama 2
Mdaduwa - mwenye kufanya sawa (kusawazisha)
Kutamba - Kusambaa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
8. (a) Hali ya mzungumziwa
• Mcheshi
• Mwenye bidii
• Maskini (2 x 1 )
(b) Inkisari; babuze – babu zetu
Kuboronga sarufi; Aliye na kubwa hamu
Aliye na hamu kubwa (2 x2)
(c) Taswira sikivu, anasikiliza videge vya anga vinavyotumbuiza
Taswira mnuso; Rihi ya maua zikimletea
Taswira mguso; umande kumbusu miguuni (3 x 1)
(d) Maswali ya balagha hukuza maudhui ya unyanyasaji
Pia kunyimwa haki kwa binadamu maskini (2 x 1)
(e) Tashihisi - umande kumbusu miguuni
Kinaya - kuwa mrejelewa anafuraha ilhali anafanya kazi za sulubu (kulima)
Tashibihi - Tabasamu kama mtu aliye na kubwa hamu (3 x 1)
(f) Huruma - mateso mrejelewa anayoyapitia (1 x 2)
(g) Mchunguzi / mpita njia wa karibu na mrejelewa (1 x 1)
(h) Beti tatu
Mistari mishata
Mishororo haina mizani sawa
Hakuna urari wa vina (3 x 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KAKAMEGA CENTRAL JOINT EXAMINATION
JINA……………………………………………………………………………………… NAMBARI
YAKO……………….SHULE……………………………………………. SAHIHI……………………
TAREHE…………………………
102/1
KISWAHILI
KARATASI 1
KIDATO CHA NNE
JULAI /AGOSTI 2019
MUDA 1𝟑
𝟒
JARIBIO LA JULAI 2019 KIDATO CHA NNE.
MAAGIZO.
a. Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
b. Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
c. Kila insha ina alama ishirini.
d. Kila insha isipungue maneno 400
e. Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
f. Insha zote sharti ziandikwe katika kijitabu cha majibu ulichopewa
g. Watahiniwa ni lazima waangalie kama kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa
sawasawa nakuwa maswali yote yamo
\
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. Lazima
Wewe ni miongoni mwa wanahabari wanaomhoji Inspekta Jenerali wa Polisi katika ofisi yake.
Andika mahojiano yenu juu ya hatua ambazo zimechukuliwa kuimarisha viwango vya usalama
nchini.
2. Jadili umuhimu wa michezo kwa wanafunzi wa shule za sekondari nchini Kenya.
3. Andika insha itakayothibitisha ukweli wa methali hii.
Mwenda tezi na omo marejeo ni ngamani.
4. Andika kisa kitakachomalizikia kwa maneno haya: ... ilinichukua muda mrefu mno kuyaamini
yaliyonifika.
KAKAMEGA CENTRAL JOINT EXAMINATION
KISWAHILI
LUGHA
Julai 2019 -Muda: Saa 2 ½
Jina………………………………………………….Nambari ya mtahiniwa…………………..
Sahihi ya mtahiniwa………………………..Tarehe………………Kidato…………………….
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
JARIBIO LA JULAI 2019 KIDATO CHA NNE
Maagizo
a) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
b) Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
c) Jibu maswali yote.
d) Majibu yako yote yaandikwe katika nafasi ulizoachiwa katika kijitabu hiki cha maswali.
e) Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
f) Usitoe ukurasa wowote kutoka kwenye kijitabu hiki.
g) Karatasi hii ina kurasa 12 zilizopigwa chapa.
h) Watahiniwa ni lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa
sawasawa na kuwa maswali yote yamo.
Kwa matumizi ya mtahini pekee.
Swali
Upeo
Alama
1
15
2
15
3
40
4
10
Jumla
80
1. UFAHAMU:( Alama 15)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
Meli alipokivuka kizingiti cha lango la shule ya kitaifa ya Tungambele alikuwa na azma ya kusoma
kwa bidii ili kuinukia kuwa kijana wa kutegemewa na jamii yake. Alikuwa kalelewa katika familia yenye
pato wastani. Akasoma kwa juhudi za wazazi wake hadi darasa la nane alipokwangura alama za
kumwezesha kujiunga na shule hii ya kifahari. Meli alijua kwamba alikuwa mwanagenzi, si katika masomo
ya shule ya upili tu, bali pia katika maisha ya jijini ambamo shule hii ilipatikana. Kwa kweli hii ndiyo
ilikuwa mara yake ya kwanza kutia guu kwenye jiji hili ambalo habari zake akizisoma, ama katika magazeti
machache yaliyowahi kufika kijijini, au kupitia somo la Elimujamii. Hata hivyo, Meli hakuwa mtu wa
kuogopa au kunywea machoni mwa changamoto. Alijiambia kwamba kwa vyovyote vile atapambana na
maisha haya mapya.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Saa mbili kamili asubuhi ilimpata Meli kapiga foleni katika afisi ya kuwasajili wanafunzi wageni.
Wasiwasi wa aina fulani ulianza kumnyemelea alipotazama hapa na pale bila kuona dalili ya mja yeyote
aliyemfahamu. Alijihisi kama yule kuku mgeni ambaye mwalimu wake alishinda kuwaambia kuwa hakosi
kamba mguuni. Hata hivyo aliupiga moyo wake konde na kujiambia kuwa kuja kwake hapa kulitokana na
juhudi zake mwenyewe na katu hatauruhusu ugeni wa mazingira kuifisha ari yake ya masomo.
Usajili ulikamilika, naye Meli na wenzake wakajitosa katika ushindani wa kimasomo jinsi
waogeleaji wajitumbukizapo kidimbwini wakapiga mbizi, baadhi wakiambulia ushindi na wengine
wakifedheheka kwa kushindwa. Meli na wenzake walibainikiwa kwamba wote walikuwa mabingwa kutoka
majimbo na wilaya zao. Ilimbidi kila mmoja wao kujikakamua zaidi ili kuelea katika bahari hii ya
ushindani. Muhula wa kwanza ulishuhudia kishindo cha Meli kubwagwa chini na majabali wenzake.
Alijipata miongoni mwa wanafunzi kumi wa mwisho; au kama alivyozoea kuwatania wenzake katika shule
ya msingi, “wanafunzi kumi bora kuanzia mwisho”! Hili lilimwatua moyo Meli na kumfanya kutahayari.
Alifika kwao amejiinamia kama kondoo aliyeumia malishoni. Akawataka wazazi wake wambadilishie shule
lakini wakakataa.
Muhula wa pili na wa tatu mambo yalikuwa yaleyale. Meli akahisi kama askarijeshi aliyeshindwa
kabisa kutambua mbinu za kuwavizia maadui. Akaona kwamba njia ya pekee ni kujiunga na wenzake kama
yeye katika vitendo vya utundu kama vile kuvuruga masomo kwa kupiga kelele darasani, kupiga soga
bwenini na hata kuvuta sigara. Mwanzoni alichukia vitendo hivi lakini alimeza mrututu akisema kwamba
ndiyo njia ya pekee ya kujipurukusha na aibu. Wazazi wa Meli hawakusita kutambua mabadiliko katika
hulka ya mwanao. Wakajaribu kumshika sikio nyumbani lakini akawa hasikii la mwadhini wala la mteka
maji msikitini. Wakawahusisha wataalamu wa ushauri nasaha ambao waliwaambia kuwa Meli hakuwa na
tatizo lolote la kuyadumu masomo. Kile alichokosa ni kujiamini tu.
Wazazi wa Meli waliona kuwa ni muhimu kuwahusisha walimu katika kutatua tatizo la mwanao.
Mwanzo wa muhula wa pili uliwapata wazazi hawa afisini mwa naibu wa mwalimu mkuu. Mazungumzo
kati ya wazazi, naibu wa mwalimu mkuu na mwalimu wa darasa la Meli yalidhihirisha kwamba walimu
walikuwa wamemuasa Meli kuhusu kujiingiza katika makundi yasiyomfaidi lakini rai zao ziliingia katika
masikio yaliyotiwa nta. Aliyopenda Zaidi Meli ni shughuli zilizomtoa nje ya shule kama vile tamasha za
mziki, ukariri wa mashairi na drama. Mazungumzo yalibainisha kwamba Meli alihitaji ushauri na uelekezaji
Zaidi kutoka kwa mtaalamu wa nasaha pale shuleni.
Meli alianza vikao na mtaalamu huyu ambaye pia alimpendekezea Meli ushauri zaidi kutoka kwa washauri
marika. Hili lilimchangamsha zaidi Meli kwani aliwaona hawa kama wenzake waliojua changamoto zake.
Juhudi za mtaalamu wa nasaha na washauri marika zilifua dafu. Mwisho wa kidato cha pili ulishuhudia
mabadiliko makuu katika hulka na utendaji kimasomo wa Meli. Aliukata kabisa uhusiano wake na
marafikiwaliompotosha na kuanza kuandamana na wanafunzi waliotia juhudi masomoni. Polepole alama
zake ziliimarika. Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yalimweka kwenye safu ya wanafunzi bora zaidi
nchini.
a) “Wanafunzi wawapo shuleni hukumbana na changamoto nyingi”. Thibitisha ukweli wa kauli hii kwa
kurejelea hoja sita kutoka kwenye taarifa. .(alama 6)
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
…………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
..................................................................................................................................................................
......................................................................................................
b) Eleza mchango wa washikadau mbalimbali katika kumsaidia Meli kupata ufanisi masomoni.
(alama 4
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
………………………………
………………………………………………………………………………………
c) Bainisha mbinu tatu za lugha ambazo msimulizi anatumia katika kuwasilisha ujumbe wake katika
kifungu. (alama 3)
………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
d) i. Andika kisawe cha ‘kijipurukusha’ kwa mujibu wa taarifa (alama 1)
………………………………………………………………………………………
ii. Andika maana ya ‘kuwatania’ kulingana na taarifa. (alama 1)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2 UFUPISHO: (Alama 15)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
Mfumo wa elimu nchini unatilia mkazo mafunzo mengine ambayo, japo yamo nje ya masomo ya kawaida,
yanahusiana na kwenda sambamba na masomo hayo ya kawaida. Vyama vya wanafunzi shuleni
vinachangia pakubwa kupitisha mafunzo haya ya ziada.
Vyama vya wanafunzi hutofautiana kulingana na majukumu. Mathalani, vipo vyama vya kidini, vya
kitaaluma na vya michezo. Pia, kuna vyama vya kijamii kama vile Chama cha kupambana na matumizi
mabaya ya dawa na vya kiuchumi kama vile chama cha Wakulima Chipukizi.
Inadhihirika kwamba vyama vya wanafunzi vina manufaayakuhusudiwa. Hii ndiyo sababu shuleni, kila
mwanafunzi anahimizwa kujiunga na angaa vyama viwili. Vyama vya wanafunzi huwasaidia kukuza
vipawa na kuimarisha stadi za kujieleza. Haya hufikiwa kupitia kwa shughuli za vyama kama vile ukariri
wa mashairi mijadala, utegaji na uteguaji wa vitendawili, chemsha bongo na ulumbi. Aidha, vyama hivi
huhimiza utangamano miongoni mwa wanachama kwani wao hujiona kuwa watu wenye mwelekeo mmoja.
Vilevile utangamano wa kitaifa na kimataifa hujengeka.
Mwanafunzi ambaye amejiunga na vyama vya wanafunzi huweza kukabiliana na changamoto za maisha
kuliko yule ambaye hajawahi kujiunga na chama chochote. Katika vyama hivi, wanafunzi hufunzana
mikakati na maarifa ya kutatua matatizo na mbinu za kuepuka mitego ya ujana. Kupitia kwa ushauri wa
marika kwa mfano, mwanafunzi hushauriwa kuhusu masuala kama vile uteuzi wa marafiki, kuratibu muda,
kujikubali na kuwakubali wenzake.
Halikadhalika, mwanafunzi hujifunza maadili ya kijamii na kidini. Kupitia kwa vyama vya kidini na
vinginevyo, yeye hujifunza kujistahi na kuwa na stahamala ya kidini, kiitikadi na kikabila. Kadhalika,
majukumu ambayo mwanafunzi huenda akapewa hupalilia uwajibikaji, uaminifu na kipawa cha uongozi.
Hata anapohitimu masomo yake, mwanafunzi huyu huendeleza sifa hizi.
Vijana wana nafasi kubwa katika kukabiliana na maovu ya kijamii kwani wao ndio wengi Zaidi. Kupitia
kwa vyama hivi, wanafunzi wanaweza kuwahamasisha wenza dhidi ya tabia hasi kama vile kushiriki
mapenzi kiholela, ulanguzi wa dawa za kulevya na kujiingiza katika burudani zisizofaa. Pia, shughuli na
miradi ya vyama hivi huwawezesha wanafunzi kutumia nishati zao kwa njia ya kujinufaisha na kuepuka
maovu. Kwa mfano, wanaweza kwenda kukwea milima, kufanya matembezi ya kukusanya pesa za
kuwafadhili wahitaji, kuendeleza shughuli za kunadhifisha mazingira na kutembelea vituo vya mayatima na
wazee.
Kushiriki katika vyama vya michezo hakumwezeshi mwanafunzi kuimarisha afya na kujenga misuli tu, bali
pia huweza kuwa msingi wa kupata chanzo cha riziki baadaye. Wapo wachezaji maarufu ambao walitambua
na kuviendeleza vipawa vyao kupitia kwa vyama aina hii, na hivi sasa wana uwezo wa kuyaendesha maisha
yao na ya familia zao.
Ifahamike kuwa vyama vya wanafunzi vinapaswa kuwa msingi wa mshikamano na maridhiano. Visitumiwe
kama vyombo vya kuwagawa wanafunzi kitabaka. Mwanafunzi hana budi kusawazisha muda anaotumia.
Atenge muda wa shughuli za vyama na wa kudurusu masomo yake.
.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
a) Fupisha ujumbe wa aya tano za kwanza kwa maneno 80 (alama9,1 ya utiririko)
Matayarisho
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
Nakala Safi
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………
b) Fafanua masuala ambayo mwandisi anaibua katika aya tatu za mwisho (maneno 60).
(alama 6, 1 ya mtiririko)
Matayarisho
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
Nakala Safi
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
3. MATUMIZI YA LUGHA: (Alama 40)
a) Andika sauti zenye sifa zifuatazo: (alama2)
i) nazali ya kaakaa gumu…………………………………………………………...
ii) kikwamizo ghuna cha kaakaa laini………………………………………...
iii) irabu ya mbele, wastani………………………………………………………..
iv) kiyeyusho cha midomo……………………………………………………
b) Bainisha silabi katika neno: wachangamshwavyo. (alama 1)
…………………………………………………………………………………………
c) Andika upya sentensi ifuatayo kwa kubadilisha nomino zilizopigiwa mstari kuwa vitenzi.
Wachezaji wote watafanyiwa ukaguzi ili kupata suluhu ya matatizo hayo.
(alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
……………………………………………………………………………………………
d) Andika sentensi ifuatavyo katika umoja.
Tukishiriki katika maigizo hayo vizuri tutaweza kujishindia tuzo.
(alama 2)
………………………………………………………………………………………………
e) Andika neno moja lenye viambajengo vifuatavyo: (alama 2)
nafsi ya kwanza wingi, wakati uliopita,yambwa, mzizi, kauli tendesha,kauli tenda
………………………………………………………………………………………………
f) Tunga sentensi kuonyesha matumizi yafuatayo ya neno: ni (alama 2)
i) kitenzi ………………………………………………………………………………………
ii) kiwakilishi
………………………………………………………………………………………
g) Tunga sentensi yenye kishazi kirejeshi ambacho ni kivumishi. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………….
h) Andika sentensi ifuatayo katika hali ya ukubwa.
Nyundo hizo zimetupwa mbali na jumba lile. (alama 1)
………………………………………………………………………………………………
i) Tunga sentensi yenye muundo ufuatao: (alama2)
Nomino ya wingi , kivumishi, kitenzi kishirikishi, kivumishi
……………………………………………………………………………………………….
j) Andika sentensi ifuatayo kulingana na maagizo.
Matunda yanayozalishwa kwa njia za kiasili yana virutubishi vingi. (alama 1)
Anza kwa: Virutubishi vingi
……………………………………………………………………………………………….
k) Tumia viwakilishi badala ya nomino zilizopigiwa mstari.
Mzee atatembelea mji(alama 1)
………………………………………………………………………………………………
l) Akifikisha sentensi ifuatayo:
basi mwanangu akasema cheusi hivyo ndivyo tunavyoweza kufikia gender parity wewe waonaje
(alama 3)
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………...
m) Unganisha sentensi zifuatazo kwa kutumia kiunganishi cha wakati.
Idi alijishindia tuzo. Idi alishiriki katika uhifadhi wa mazingira. (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.................................................................................................................................................
n) Tumia ‘kwa’ katika sentensi kuonyesha: (alama 2)
i) nia
.................................................................................................................................................
ii) pamoja na
................................................................................................................................................
o) Changanua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha matawi.
Upepo ulivuma tulipokuwa tukiondoka. (alama 3)
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................
p) Andika sentensi ifuatayo katika kauli ya kutendewa.
Rono alicheza gitaa akiwa kwa Kiprono. (alama 2)
...............................................................................................................................................................
q) Onyesha matumizi ya ka katika sentensi ifuatayo:
Mumbi alitia embe kapuni likaiva. (alama 1)
...............................................................................................................................................................
r) Andika sentensi ifuatayo katika hali ya mazoea.
Mmomonyoko wa udongo ulipozuiliwa mashamba yalinawiri. (alama 2)
...............................................................................................................................................................
s) Tunga sentensi moja kutofautisha maana ya baba na papa (alama 2)
.........................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
t) Methali: Haraka haraka haina baraka huambiwa mtu aliye na kasi isiyofaa katika kutenda mambo.Mtu
anayepuuza shida za wenzake huambiwa aje? (alama 1)
...............................................................................................................................................................
u) Bainisha kiima na chagizo katika sentensi ifuatayo: (alama 1)
Wale wageni walikipenda sana.
...............................................................................................................................................................
v) Andika kihisishi cha kuitikia wito kwa mtu wa jinsia ya kike (al 1)
………………………………………………………………………………………………
w) Tunga sentensi ya masharti inayoonyesha kwamba tendo lilifanikiwa kwa sababu ya kufanikiwa kwa
tendo lingine. (alama 1)
.........................................................................................................................................................
x) Andika miundo miwili ya nomino katika ngeli ya KI-VI. (alama 1)
.........................................................................................................................................................
y) Ainisha virai vilivyopigiwa mstari. (alama 1)
Zana hizi zimeundwa na mafundiwenye ustadi mkubwa.
...............................................................................................................................................................
4. ISIMU JAMII: (Alama 10)
a) Umepewa jukumu la kutoa ushauri nasaha(elekezi) kwa kijana mwenzako anayefikiria kujitoa uhai
kuhusu manufaa ya kutojitoa uhai. Fafanua sifa tano za kimtindo utakazotumia ili kufanikisha
mazungumzo yako. (alama 5)
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
.................................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.................................................................................................................................................................................
...............
b) Eleza mitindo mitano ya matumizi ya lugha katika muktadha wa bunge. (alama 5)
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................
HUU NDIO UKURASA WA MWISHO ULIOPIGWA CHAPA.
KAKAMEGA CENTRAL JOINT EXAMINATION
102/3 KISWAHILI – Karatasi ya 3
FASIHI
Muda: Saa 2 ½
JARIBIO LA JULAI 2019
Jina………………………..………………………Nambari ya mtahiniwa………………
Sahihi………………………..…………………………Tarehe…………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Maagizo
a) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
b) Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
c) Jibu maswali manne pekee .
d) Swali la kwanza ni la lazima.
e) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne. zilizobaki;yaani:Riwaya, Tamthilia,
Hadithi fupi na Ushairi.
f) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
g) Majibu yote lazima yaadikwe kwa lugha ya Kiswahili.
h) Karatasi hii ina kurasa 5 zilizopigwa chapa.
i) Watahiniwa ni lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi zimepigwa chapa sawasawa
na kuwa maswali yote yamo.
Kwa matumizi ya mtahini pekee
JUMLA
SEHEMU A: FASIHI SIMULIZI
1.Lazima
a) ”Mwanangu nakuomba uzingatie uadilifu maishani uongofu ni nuru ya mustakabali wa kila
mtu…”
i)Tambua kipera na utanzu wa tungo hili (al. 2)
ii)Kwa kutumia hoja mbili eleza muundo wa kipera hiki (al. 2)
iii)Fafanua sifa nane za kipera hiki (al.8)
b) Eleza vikwazo vinane vya ukuaji wa fasihi simulizi. (al.8)
SEHEMU B: RIWAYA
Assumpata k. matei: : chozi la Heri
Jibu swali la 2 au la 3
2.”Si kufua, si kupiga deki, si kupika…almuradi kila siku na adha”
a) a) Eleza muktadha wa kauli hii. (ala.4)
b) Taja mbinu mbili za kimtindo zilizotumika katika dondoo hili. (al.2)
c) Kwa kutumia hoja kumi na nne, eleza maudhui yaliyodokezwa na dondoo hili.
(al.14)
3.”Kila mara hujiuliza ikiwa watoto huwa na hadhi tofauti nje au ndani ya ndoa”
Amali inayotajwa imekumbwa na changamoto chungu nzima.Jadili kwa kurejelea riwaya nzima.
(al.20)
Swali Upeo Alama
1 20
20
20
20
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU C: TAMTHILIA
P. Kea : Kigogo
Jibu swali la 4 au la 5
4.”Acha porojo zako. Kigogo hachezewi;watafuta maangamizi!”
a)Eleza muktadha wa dondoo hili (al.4)
b)Fafanua sifa za mzungumzaji (al.6)
c)Kwa kurejelea hoja kumi, thibitisha kwamba kucheza na kigogo anayerejewa ni sawa na
kutafuta maangamizi (al.10)
5.”Tunahitaji kuandika historia yetu upya.”
a)Eleza sababu kumi na mbili kuonyesha kwa nini ilikuwa muhimu kuiandika historia ya
sagamoyo upya (al.12)
b)Onyesha mikakati inayotumiwa kuiandika upya historia ya Jumuiya ya
sagamoyo (al.8)
SEHEMU D: USHAIRI
Jibu swali la 6 au la 7
6.Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yafuatayo.
LONGA
Longa longea afwaji, watabusarika
Longa uwape noleji, watanusurika
Longa nenea mabubu,sema na viduko
Longa usichachawizwe, tamka maneno
Longa usitatanizwe, mbwa aso meno
Longa usidakihizwe,kishindo cha funo
Longa yote si uasi, si tenge si noma
Longa pasi wasiwasi,ongea kalima
Longa ukuli kwa kasi, likate mtima
Longa zungumza basi, liume ja uma
Longa japo ni kombora, kwa waheshimiwa
Longa liume wakora, kwani wezi miwa
Longa bangu na parara, hawakuitiwa
Longa bunge si kiwara, si medani tawa
Longa ni simba marara, wanaturaruwa.
Maswali
a) Tambua na ueleze nafsi neni katika shairi hili (al.1)
b) Onyesha vile kibali cha utunzi wa mashairi kilivyotumika kukidhi mahitaji ya kiarudhi
(al.4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
c) Kwa kutoa maelezo mwafaka, tambua bahari nne zilizotumika na mtunzi kwenye shairi hili.
(al.4)
d) Eleza aina tatu za urudiaji katika shairi (al.3)
e) Tambua na ueleze toni ya shairi (al.2)
f) Eleza maana ya misamiati ifuatayo kama ilivyotumika katika shairi. (al.2)
i. Afwaji
ii. Tenge
g) Eleza umbo la shairi hili. (al.4)
7.Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Kila nikaapo husikia tama
Na kuwazia hali inayonizunguka
Huyawazia madhila
Huziwazia shida
Hujiwazia dhiki
Dhiki ya ulezi
Shida ya kudhalilishwa kazini
Madhila ya kufanyiwa dharau
Kwa sababu jinsia ya kike
Hukaa na kujidadisi
Hujidadisi kujua ni kwa nini
Jamii haikisikii kilio changu
Wezangu hawanishiki mikono
Bali wananidharau kwa kuikosea utamaduni
Hukaa na kujiuliza
Iwapi raha yangu ulimwengu huu?
Iwapi jamaa nzimaa ya wanawake?
Maswali
a) Taja sifa mbili za shairi huru zinazojitokeza katika shairi hili (al.2)
b) Eleza dhamira ya mshairi (al.2)
c) Kwa kutoa mifano, eleza maana ya mistari mishata (al.3)
d) Bainisha tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi hili (al.4)
e) Eleza nafsineni katika shairi hiri (al.2)
f) Tambua toni ya shairi hili (al.2)
g) Taja maudhui matatu katika shairi hili (al.3)
h) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa katika shairi (al.2)
Madhila
Kudhalilishwa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU E: HADITHI FUPI
A. Chokocho na D kayanda : Tumbo lisiloshiba na Hadithi Nyingine.
8.”…hamna mwendawazimu wala mahoka kati yetu, mimi nimepewa zawadi hizo”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili (al.4)
b) Eleza sifa nne za msemaji (al.4)
c) Hakiki nafasi ya maudhui ya busara kwa mujibu wa hadithi hii (al.12)
KAKAMEGA CENTRAL JOINT EXAMINATION
102/3 KISWAHILI – Karatasi ya 3
FASIHI
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Muda: Saa 2 ½
JARIBIO LA JULAI 2019
Jina………………………..………………………Nambari ya mtahiniwa………………
Sahihi………………………..…………………………Tarehe…………………………………
Maagizo
j) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
k) Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
l) Jibu maswali manne pekee .
m) Swali la kwanza ni la lazima.
n) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne. zilizobaki;yaani:Riwaya, Tamthilia,
Hadithi fupi na Ushairi.
o) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
p) Majibu yote lazima yaadikwe kwa lugha ya Kiswahili.
q) Karatasi hii ina kurasa 5 zilizopigwa chapa.
r) Watahiniwa ni lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi zimepigwa chapa sawasawa
na kuwa maswali yote yamo.
Kwa matumizi ya mtahini pekee
JUMLA
SEHEMU A: FASIHI SIMULIZI
1.Lazima
c) ”Mwanangu nakuomba uzingatie uadilifu maishani uongofu ni nuru ya mustakabali wa kila
mtu…”
i)Tambua kipera na utanzu wa tungo hili (al. 2)
ii)Kwa kutumia hoja mbili eleza muundo wa kipera hiki (al. 2)
iii)Fafanua sifa nane za kipera hiki (al.8)
d) Eleza vikwazo vinane vya ukuaji wa fasihi simulizi. (al.8)
SEHEMU B: RIWAYA
Assumpata k. matei: : chozi la Heri
Jibu swali la 2 au la 3
Swali Upeo Alama
1 20
20
20
20
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2.”Si kufua, si kupiga deki, si kupika…almuradi kila siku na adha”
d) a) Eleza muktadha wa kauli hii. (ala.4)
e) Taja mbinu mbili za kimtindo zilizotumika katika dondoo hili. (al.2)
f) Kwa kutumia hoja kumi na nne, eleza maudhui yaliyodokezwa na dondoo hili.
(al.14)
3.”Kila mara hujiuliza ikiwa watoto huwa na hadhi tofauti nje au ndani ya ndoa”
Amali inayotajwa imekumbwa na changamoto chungu nzima.Jadili kwa kurejelea riwaya nzima.
(al.20)
SEHEMU C: TAMTHILIA
P. Kea : Kigogo
Jibu swali la 4 au la 5
4.”Acha porojo zako. Kigogo hachezewi;watafuta maangamizi!”
a)Eleza muktadha wa dondoo hili (al.4)
b)Fafanua sifa za mzungumzaji (al.6)
c)Kwa kurejelea hoja kumi, thibitisha kwamba kucheza na kigogo anayerejewa ni sawa na
kutafuta maangamizi (al.10)
5.”Tunahitaji kuandika historia yetu upya.”
a)Eleza sababu kumi na mbili kuonyesha kwa nini ilikuwa muhimu kuiandika historia ya
sagamoyo upya (al.12)
b)Onyesha mikakati inayotumiwa kuiandika upya historia ya Jumuiya ya
sagamoyo (al.8)
SEHEMU D: USHAIRI
Jibu swali la 6 au la 7
6.Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali yafuatayo.
LONGA
Longa longea afwaji, watabusarika
Longa uwape noleji, watanusurika
Longa nenea mabubu,sema na viduko
Longa usichachawizwe, tamka maneno
Longa usitatanizwe, mbwa aso meno
Longa usidakihizwe,kishindo cha funo
Longa yote si uasi, si tenge si noma
Longa pasi wasiwasi,ongea kalima
Longa ukuli kwa kasi, likate mtima
Longa zungumza basi, liume ja uma
Longa japo ni kombora, kwa waheshimiwa
Longa liume wakora, kwani wezi miwa
Longa bangu na parara, hawakuitiwa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Longa bunge si kiwara, si medani tawa
Longa ni simba marara, wanaturaruwa.
Maswali
h) Tambua na ueleze nafsi neni katika shairi hili (al.1)
i) Onyesha vile kibali cha utunzi wa mashairi kilivyotumika kukidhi mahitaji ya kiarudhi
(al.4)
j) Kwa kutoa maelezo mwafaka, tambua bahari nne zilizotumika na mtunzi kwenye shairi hili.
(al.4)
k) Eleza aina tatu za urudiaji katika shairi (al.3)
l) Tambua na ueleze toni ya shairi (al.2)
m) Eleza maana ya misamiati ifuatayo kama ilivyotumika katika shairi. (al.2)
i. Afwaji
ii. Tenge
n) Eleza umbo la shairi hili. (al.4)
7.Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Kila nikaapo husikia tama
Na kuwazia hali inayonizunguka
Huyawazia madhila
Huziwazia shida
Hujiwazia dhiki
Dhiki ya ulezi
Shida ya kudhalilishwa kazini
Madhila ya kufanyiwa dharau
Kwa sababu jinsia ya kike
Hukaa na kujidadisi
Hujidadisi kujua ni kwa nini
Jamii haikisikii kilio changu
Wezangu hawanishiki mikono
Bali wananidharau kwa kuikosea utamaduni
Hukaa na kujiuliza
Iwapi raha yangu ulimwengu huu?
Iwapi jamaa nzimaa ya wanawake?
Maswali
i) Taja sifa mbili za shairi huru zinazojitokeza katika shairi hili (al.2)
j) Eleza dhamira ya mshairi (al.2)
k) Kwa kutoa mifano, eleza maana ya mistari mishata (al.3)
l) Bainisha tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi hili (al.4)
m) Eleza nafsineni katika shairi hiri (al.2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
n) Tambua toni ya shairi hili (al.2)
o) Taja maudhui matatu katika shairi hili (al.3)
p) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa katika shairi (al.2)
Madhila
Kudhalilishwa
SEHEMU E: HADITHI FUPI
A. Chokocho na D kayanda : Tumbo lisiloshiba na Hadithi Nyingine.
8.”…hamna mwendawazimu wala mahoka kati yetu, mimi nimepewa zawadi hizo”
d) Eleza muktadha wa dondoo hili (al.4)
e) Eleza sifa nne za msemaji (al.4)
f) Hakiki nafasi ya maudhui ya busara kwa mujibu wa hadithi hii (al.12)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KAKAMEGA JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA KISWAHILI KARATASI 102/1 2019
1. Hii ni insha ya mahojiano na ni utungaji wa kiuamailifu. Vipengele viwili vya utungo wa aina hii
vizingatiwe, yaani muundo na maudhui.
a) Muundo
• Vipengele vikuu vya mahojiano.
• Anwani ( kutokana na mada).
• Atumie mfumo wa kitamthilia.
• Mtahiniwa ndiye mhoji hivyo basi yeye ndiye atakayeuliza maswali. Inspekta Jenerali ndiye
mhojiwa.
• Mahojiano yaanze kwa maamkuzi baina ya wahusika.
Mwili wa insha ubebe maudhui.
b) Maudhui (Hatua ambazo zimechukuliwa kuimarisha usalama nchini)
• Kuimarisha mfumo wa ‘Nyumba Kumi’ mitaani, vijijini nk.
• Kuongeza idadi ya askari polisi kufikia kiwango cha kimataifa cha askari mmoja kwa raia mia
nne.
• Polisi kushirikiana na vyombo vingine vya dola vya usalama kama vile jeshi – kulinda mipaka
dhidi ya uvamizi wa majangili kutoka nchi za nje.
• Kuimarisha hali ya ukaguzi katika maeneo ya mipaka, bandarini na viwanja vya ndege ili kuzuia
kuingia nchini kwa silaha.
• Serikali imenunua vifaa zaidi vya kisasa kama vile magari, silaha nk.
• Kushughulikia maslahi ya askari walinda usalama kama vile ujenzi wa makao yao, kuboresha
ujira na marupurupu mengine ya kazi ili kuwatia motisha kufanya kazi vyema.
• Sehemu za umma kama vile maduka ya jumla, hospitali, shule, vyuo vikuu nk kuongeza ukaguzi
wa kila anayeingia.
• Wapiga doria zaidi kuwa mitaani, vijijini,mijini nk ili kuimarisha usalama kwa ujumla.
• Wananchi wamehamasishwa kuhusu jinsi ya kuwa waangalifu popote walipo na namna ya
kushughulikia visa vya utovu wa usalama iwapo vitatokea.
• Kuwekwa kwa kamera za siri barabarani na pia kwenye maeneo ya umma.
TANBIHI
✓ Hoja za mwanafunzi zisipungue tano.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
✓ Hoja zenyewe zijitokeze kupitia ufafanuzi wa Inspekta Jenerali. Hata hivyo, mhoji
anaweza kuuliza maswali ya kuelekeza.
✓ Urefu ukadiriwe kuanzia kwa kichwa.
2.
- Ajadili umuhimu wa michezo
- Arejelee wanafunzi wa shule za sekondari, nchini Kenya
- Baadhi ya hoja
✓ Huimarisha afya ya wanafunzi
✓ Huwasaidia kutumia muda wao vyema
✓ Huwawezesha kukuza vipawa vyao
✓ Huwachangamsha baada ya siku nzima masomoni
✓ Huwafunza jinsi ya kutangamana
✓ Huwakutanisha na wanafunzi wa shule zingine
✓ Huimarisha uhusiano kati ya wanafunzi na walimu
✓ Huwafungulia milango ya heri baadaye maishani/ajira
✓ Huchangia katika kujua tamaduni za wengine.
✓ Hukuza na kuendeleza utamaduni
✓ Hukuza lugha mf. Katika maigizo na tamasha za muziki
✓ Huimarisha umaarufu,sifa na ujasiri kwa mwanafunzi
3. - Kutoa maana na matumizi ya methali
- Kisa au visa vinavyowiana / kinachowiana na maelezo ya methali
- mtahiniwa aonyeshe kuwa hata baada ya kwenda kwingine na kufanikiwa lazima atarejea
katika makazi yake ya asili. Mhusika hataridhika na yale atakayoyapata kwingine.
- Hitimisho – lazima itoe funzo
4.Hii ni insha ya mdokezo.Mtahiniwa atamatishe insha yake kwa maneno yayo hayo.Asipotamatisha kwayo
atakuwa amepungukiwa kimtindo tu,akadiriwe vilivyo.Anaweza tunga kisa kinachoonyesha masaibu
aliyokumbana nayo hapo awali.
MWONGOZO WA KUDUMU
KENYA CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION
KISWAHILI 102/1 2019
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
UTANGULIZI
Karatasi hii imedhamiria kutathmini uwezo wa mtahiniwa wa kuwasiliana na msomaji na kuwasilisha
ujumbe kimaandishi, akizingatia mada aliyopewa. Mawasiliano haya yatategemea ukwasi wa lugha ya
mtahiniwa, kwa mfano, kutunga sentensi sahihi zenye mtiririko mzuri kimawazo, lugha ya kuvutia na yenye
mawazo asilia, ubunifu mwingi na hati nadhifu. Kwa kutegemea maagizo ya swali lenyewe na umahiri wa
lugha, ni lazima kutilia mkazo mtindo, mada na uwezo wa mtahimiwa kufuata maagizo vilivyo. Mtahini
lazima asome insha yote huku akizingatia sarufi, hijai, hoja, msamiati na mtindo ili aweze kukadiria
viwango mbalimbali vilivyopendekezwa. Viwango vyenyewe ni A,B,C, na D kutegemea uwezo wa
mtahiniwa.
VIWANGO MBALIMBALI
KIWANGO CHA D KWA JUMLA MAKI 01-05
1. Insha haieleweki kwa vyovyote vile ama uwezo wa mtahiniwa wa kutumia lugha ni hafifu sana, hivi
kwamba mtahini lazima afikirie kile mtahiniwa anachojaribu kuwasilisha.
2. Mtahiniwa hana uwezo wa kutumia maneno ya Kiswahili kwa njia inayofaa.
3. Lugha imevurugika, uakifishaji haufai na insha ina makosa ya kila aina.
4. Kujitungia swali na kulijibu.
5. Kunakili swali au kichwa tu.
NGAZI MBALIMBALI ZA KIWANGO CHA D
D- (D YA CHINI) MAKI 01-02
1. Insha haina mpangilio maalum na haieleweki kwa vyovyote vile.
2. Kujitungia swali tofauti na kulijibu.
3. Kuandika kwa lugha isiyo Kiswahili au kuchanganya ndimi.
4. Kunakili swali au maswali na kuyakariri.
5. Kunakili swali au kichwa tu.
D WASTANI MAKI 03
1. Mtiririko wa mawazo haupo.
2. Mtahiniwa amepotoka kimaudhui.
3. Matumizi ya lugha ni hafifu mno.
4. Kuna makosa mengi ya kila aina.
D+ (D YA JUU) MAKI 04-05
1. Insha ya aina hii huwa na makosa mengi ya kila aina, lakini unaweza kutambua kile ambacho
mtahiniwa anajaribu kuwasilisha.
2. Hoja hazikuelezwa kikamilifu / mada haikukuzwa vilivyo.
3. Mtahiniwa hana uhakika wa matumizi ya lugha.
4. Mtahiniwa hujirudiarudia.
5. Insha itakayozingatia sura lakini ikose maudhui ikadiriwe hapa.
KIWANGO CHA C KWA JUMLA MAKI 06-10
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. Mtahiniwa anajaribu kushughulikia mada japo hakuikuza na kuiendeleza vilivyo.
2. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe kwa njia isiyovutia/ hana ubunifu wa kutosha.
3. Mtahiniwa anaakifisha sentensi vibaya.
4. Mtiririko wa mawazo unaanza kujitokeza japo kwa njia hafifu.
5. Insha ina makosa mengi ya sarufi, msamiati na tahajia (hijai).
6. Insha ya urefu wa nusu ikadiriwe hapa.
NGAZI MBALIMBALI ZA KIWANGO CHA C
C- (C YA CHINI) MAKI 06-07
1. Mtahiniwa ana shida ya kuwasilisha na kuturirisha mawazo yake.
2. Mtahiniwa hana msamiati wa kutosha wala miundo ya sentensi ifaayo.
3. Mtahiniwa anafanya makosa mengi ya sarufi, ya hijai na ya msamiati na insha yake haieleweki kwa
urahisi.
C WASTANI MAKI 08
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe lakini kwa njia hafifu.
2. Dhana tofautofauti hazijitokezi wazi.
3. Mtahiniwa hana ubunifu wa kutosha.
4. Mtiririko wa mawazo ni hafifu na hana ufundi wa lugha unaofaa.
5. Amejaribu kuishughulikia mada aliyopewa.
6. Mtahiniwa ana shida ya uakifishaji.
7. Mtahiniwa anafanya makosa mengi ya sarufi, ya hijai na ya msamiati lakini bado insha inaeleweka.
C+ (C YA JUU) MAKI 09-10
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe vizuri akizingatia mada lakini kwa njia isiyo na mvuto.
2. Dhana tofautitofauti zimejitokeza japo kwa njia hafifu.
3. Kuna mtiririko wa mawazo japo hana ufundi wa lugha unaofaa.
4. Misemo na methali zimetumika kwa njia hafifu.
5. Ana shida ya uakifishaji.
6. Kuna makosa ya sarufi, ya msamiati na ya hijai yanayoathiri mtiririko wa mawazo.
KIWANGO CHA B KWA JUMLA MAKI 11-15
B- (B YA CHINI) MAKI 11-12
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe vizuri kwa kueleza hoja tofautitofauti akizingatia mada.
2. Mtahiniwa ana mtirirko mzuri wa mawazo.
3. Mtahiniwa anatumia mifano michache ya msamiati unaovutia.
4. Makosa yanadhihirika kiasi.
B WASTANI MAKI 13
1. Mtahiniwa anadhihirisha hali ya kuimudu lugha.
2. Mawazo ya mtahiniwa yanadhihirika akizingatia mada.
3. Mtahiniwa anateua na kutumia mifano michache ya msamiati mwafaka.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
4. Sarufi yake ni nzuri.
5. Makosa ni machache / kuna makosa machache.
B+ (B YA JUU) MAKI 14-15
1. Mawazo ya mtahiniwa yanadhihirika na anajieleza waziwazi.
2. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe kwa njia inayovutia na kwa urahisi akizingatia mada.
3. Mtahiniwa ana mchanganyiko mzuri wa msamiati unaovutia.
4. Sarufi yake ni nzuri.
5. Uakifishaji wa sentensi zake ni mzuri.
6. Makosa ni machache ya hapa na pale.
KIWANGO CHA A KWA JUMLA MAKI 16-20
1. Mtahiniwa ana ubunifu wa mawazo yanayodhihirika na kutirika akizingatia mada.
2. Mtahiniwa anadhihirisha ujuzi wa lugha yenye mnato.
3. Ana uwezo wa kutumia tamathali za usemi ili kutoa hisia zake kwa njia bora na kwa urahisi.
4. Umbuji wake unadhihirisha ukomavu na ukakamavu wake kimawazo.
5. Insha ina urefu kamili.
NGAZI MBALIMBALI ZA KIWANGO CHA A
A- (A YA CHINI) MAKI 16-17
1. Mtahiniwa anadhihirisha ukomavu wa lugha.
2. Mawazo ya mtahiniwa yanadhihirika na anaishughulikia mada.
3. Ana mtiririko mzuri wa mawazo.
4. Msamiati wake ni mzuri na unaovutia.
5. Sarufi yake ni nzuri.
6. Anatumia miundo tofauti tofauti ya sentensi kiufundi.
7. Makosa ni machache yasiyokusudiwa.
A WASTANI MAKI 18
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe vizuri kulingana na mada.
2. Anajieleza kikamilifu akitumia lugha ya mnato.
3. Anatoa hoja zilizokomaa.
4. Anatumia msamiati wa hali ya juu na unaovutia zaidi.
5. Anatumia miundo tofautitofautiya sentensi kiufundi.
6. Makosa ni nadra kupatikana.
A+ (A YA JUU) MAKI 19-20
1. Mawazo yanadhihirika zaidi na mada imeshughulikiwa vilivyo.
2. Anajieleza kikamilifu akitumia lugha ya mnato.
3. Hoja zake zimekomaa na zinashawishi.
4. Msamiati wake ni wa hali ya juu na unavutia zaidi.
5. Sarufi yake ni nzuri zaidi.
6. Anatumia miundo tofautitofauti ya sentensi kiufundi.makosa yote kwa jumla hayazidi matano.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
VIWANGO MBALMBALI KWA MUHTASARI
KIWANGO
NGAZI MAKI
A
A+
A
A-
19-20
18
16-17
B B+
B
B-
14-15
13
11-12
C C+
C
C-
09-10
08
06-07
D D+
D
D-
04-05
03
01-02
USAHIHISHAJI NA UTUZAJI KWA JUMLA
Mtahini ni sharti aisome insha yote akizingatia vipengee muhimu. Vipengee hivi ni maudhui, msamiati,
mtindo, sarufi na hijai.
MAUDHUI
1. Maudhui ni hoja au mambo yanayozungumziwa, kuelezewa au kuhadithiwa kwa mujibu wa mada
iliyoteuliwa.
2. Maudhui ndio hasa uti wa mgongo wa insha yoyote ile.
3. Ubunifu wa mtahiniwa hukisiwa kwa kutathmini uzito wa maudhui yake kulingana na mada teule.
MSAMIATI
Msamiati ni jumla ya maneno yatumiwayo katika lugha husika. Mtahiniwa anatarajiwa kutumia msamiati
unaooana na mada teule. Kutegemea ukwasi wa lugha alionao, mtahiniwa anatarajiwa kuikuza mada kwa
kufinyanga lugha kiufundi. Ni muhimu kuelewa kwamba kutokana na maendeleo na ukuaji wa teknolojia na
mawasiliano, maneno mapya yanaibuka kila uchao.
MTINDO
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mtindo unahusu mambo yafuatayo:
• Mpangilio wa kazi kiaya.
• Mtiririko na mshikamano wa mawazo kiaya na katika insha nzima.
• Hati nzuri na inayosomeka kwa urahisi.
• Matumizi ya tamathali za usemi, kwa mfano, misemo, jazanda na kadhalika.
• Kuandika herufi vizuri kwa mfanoJj, Pp,Uu, Ww na kadhalika.
• Sura ya insha.
• Unadhifu wa kazi ya mtahiniwa.
SARUFI
Sarufi ndio msingi wa lugha. Ufanisi wa mawasiliano hutegemea uwezo wa mtahiniwa wa kutunga sentensi
sahihi zenye uwiano wa kisarufi. Mtahini ataonyesha makosa yote ya sarufi yaliyo katika insha
anayosahihisha. Makosa ya sarufi huweza kutokea katika:
i. Matumizi ya alama ya uakifishaji.
ii. Kutumia herufi kubwa au ndogo mahali pasipofaa.
iii. Matumizi yasiyofaa ya ngeli na viambishi,viunganishi, nyakati, hali, vihusiano na kadhalika.
iv. Mpangilio wa maneno katika sentensi.
v. Mnyambuliko wa vitenzi na majina.
vi. Kuacha neno linalohitajika au kuongeza neno lisilohitajika katika sentensi.
vii. Matumizi ya herufi kubwa:
a) Mwanzo wa sentensi.
b) Majina ya pekee.
i. Majina ya mahali, miji, nchi, mataifa na kadhalika.
ii. Siku za juma, miezi nk.
iii. Mashirika, masomo, vitabu nk.
iv. Makabila, lugha nk.
v. Jina la Mungu.
vi. Majina ya kutambulisha hasa wanyama wa kufugwa, kwa mfano yale ya mbwa- Foksi, Jak, Popi,
Simba, Tomi na mengineyo.
MAKOSA YA HIJAI/TAHAJIA
Haya ni makosa ya maendelezo. Mtahini anashauriwa asahihishe huku akiyaonyesha yanapotokea kwa mara
ya kwanza tu. Makosa ya tahajia huweza kutokea:
a) Kutenganisha neno kwa mfano ‘ aliye kuwa’.
b) Kuuganisha maneno kwa mfano ‘kwasababu’.
c) Kukata silabi visivyo afikapo pambizoni kama vile ngan- o.
d) Kuandika herufi isiyofaa kwa mfano ‘ongesa’ badala ya ‘ongeza’.
e) Kuacha herufi katika neno kwa mfano ‘aliekuja’ badala ya ‘aliyekuja’.
f) Kuongeza herufi isiyohitajika kama vile ‘piya’ badala ya ‘pia’.
g) Kuacha alama inayotarajiwa katika herufi kama vile j i.
h) Kukosa kuandika kistari cha kuendelezea neno afikiapo pambizoni au kukiandika mahali pasipofaa.
i) Kuacha ritifaa au kuiandika mahali pasipofaa, kwa mfano ngombe, ngom’be,n’gombe, ngo’mbe nk.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
j) Kuandika maneno kwa kifupi kama vile k.v, k.m, v.v, n.k. na kadhalika.
k) Kuandika tarakimu kwa mfano 27-7-2010.
ALAMA ZA KUSAHIHISHIA
==Hupigwa chini ya sehemu ambapo kosa la sarufi limetokea kwa mara ya kwanza tu.
__Hupigwa chini ya sehemu au neno ambapo kosa la hijai limetokea kwa mara ya kwanza tu.
✓ Hutumiwa kuonyesha hoja inapokamilikia pambizoni kushoto.
^ Hutumiwa kuonyesha kuachwa kwa neno/maneno.
✓ Hutumiwa kunyesha msamiati bora. Alama hii hutiwa juu ya neno lenyewe.
X Hutumiwa kuonyesha msamiati usiofaa. Alama hii hutiwa juu ya neno lenyewe.
Maelezo mafupi yanahitajika kuhusu tuzo lilotolewa. Kila ukurasa uwe na alama chini kudhihirisha kuwa
mtahini ameupitia ukurasa huo.
UKADIRIAJI WA UREFU WA INSHA YA PILI
Maneno 9 katika kila mstari ukurasa mmoja na nusu.
Maneno 8 katika kila mstari ukurasa mmoja na robo tatu.
Maneno 7 katika kila mstari kurasa mbili.
Maneno 6 katika kila mstari kurasa mbili na robo.
Maneno 5 katika kila mstari kurasa mbili na robo tatu.
Maneno 4 katika kila mstari kurasa tatu na robo tatu.
Maneno 3 katika kila mstari kurasa nne na nusu.
Kufikia maneno 174 insha robo.
Maneno 175-274 insha nusu.
Maneno 275-374 insha robo tatu.
Maneno 375 na kuendelea insha kamili.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KAKAMEGA CENTRAL JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHIA
Julai 2019
KARATASI YA 2- KISWAHILI
LUGHA 102/2 2019
JARIBIO LA JULAI 2019 KIDATO CHA 4
1. UFAHAMU
a)
i) Meli kushindwa mtihanini na wanafunzi wenzake ingawa alikuwa na alama nyingi
katika mtihani wa darasa la nane.
ii) Kutaniana. Meli alizoea kutania wenzake katika shule ya msingi waliokuwa wa
mwisho katika mtihani.
iii) Kuatuliwa moyo/ kuvunjika moyo kwa Meli baada ya kufeli katika mtihani.
iv) Kutahayari baada ya kushindwa na wenzake katika mtihani.
v) Kupiga kelele darasani ili kuvuruga masomo ya wenzake darasani.
vi) Kupiga soga bwenini
vii) Kuvuta sigara kwa wanafunzi kama Meli shuleni.
viii) Meli kupuuza ushauri wa wazazi wake awapo nyumbani.
ix) Kutojiamini katika masomo.
x) Meli kujiingiza katika makundi yasiyomfaidi.
xi) Meli kupenda shughuli zinazowatoa nje ya shule kama tamasha za muziki, ukariri
mashairi na drama baada masomo. (zozote 6x1=6)
b)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Wazazi wa Meli walijaribu kumshika sikio / kumshauri akiwa nyumbani kuhusu
masomo. Walishirikisha mtaalamu wa ushauri nasaha.
ii) Wataalamu wa ushauri nasaha walisema Meli alikosa kujiamini masomoni.
iii) Walimu walimuasa Meli dhidi ya kujiunga na makundi yasiyomfaidi
– naibu wa mwalimu mkuu. -
- Mwalimu wa darasa la Meli
iv) Mtaalamu wa nasaha aliyemshauri Meli na kumpendekezea Meli ushauri wa washauri
marika.
v) Washauri marika – bidii zao zilimsaidia Meli kujiimarisha kimasomo alipojiepusha
na marafiki waliompotosha.
(Zozote 4x1)
c)
i) Masimulizi kuhusu maisha ya Meli shuleni
ii) Misemo – kutia guu/ kupiga foleni/ piga moyo konde/ lilimwatua moyo n.k
iii) Methali – kuku mgeni hakosi kamba mguuni / hasikii la mwadhini wala la mteka maji
msikitini.
iv) Urudiaji / takriri Meli na wenzake….
v) Kinaya / kejeli “ wanafunzi kumi bora kuanzia mwisho”
vi) Tashbihi / tashbiha “… amejiinamia kama kondoo aliyeumia malishoni..”
vii) Taswira “Meli kufika nyumbani amejiinamia….”
viii) Sitiari ‘Majabali wa Meli – wale waliomshinda Meli mtihanini (Zozote 3x1)
d)
i) kujiepusha/ kujisahaulisha/ kujilinda/ kujiokoa (alama 1)
ii) kuwadhihaki/ kuwafanyia mzaha/ kuwakejeli/ kuwafyosa/ kuwafyoa.(alama 1)
2. UFUPISHO
a) (I)Mfumo wa elimu unasisitiza mafunzo mengine nje ya masomo ya kawaida. (Ii)Vyama vya
wanafunzi vinapitisha mafunzo ya ziada. (Iii)Vyama hivi hutofautiana kulingana na
majukumu. (Iv)Vina manufaa ya kuhusudiwa. (V)Shuleni mwanafunzi anahimizwa kujiunga
na vyama. (Vi)Vyama huwasaidia kukuza vipawa na stadi za kujieleza. (Vii)Huhilimza
utangamano miongoni mwa wanachama kwani hujiona wakiwa na mwelekeo mmoja.
(Viii)Hujenga utangamano wa kitaifa na kimataifa. (Ix)Anayejiunga navyo huweza
kukabiliana na changamoto za maisha. (X)Hujifunza maadili ya kijamii na kidini.
(Xi)Hujifunza kujistahi na kuwa na stahamala. (Xii)Hupalilia uwajibikaji, uaminifu na
kipawa cha uongozi.
Hoja zozote 8(1x8)
b) (i)Vijana wana nafasi kubwa ya kukabiliana na maovu ya kijamii kwani ndio wengi.
(ii)Wanaweza kuwahamasisha wenzao dhidi ya tabia hasi. (iii)Miradi ya vyama
huwawezesha kutumia nishati zao ili kujinufaisha na kuepuka maovu. (iv)Kushiriki vyama
vya michezo humwezesha mwanafunzi kuimarisha afya na kujenga misuli. (v)Kushiriki huku
ni chanzo cha riziki baadaye. Vyama vya wanafunzi ni msingi wa mshikamano na
maridhiano. (vi)Visitumiwe kugawa wanafunzi kitabaka. (vii)Mwanafunzi asawazishe muda
/ atenge muda wa shughuli za vyama na wa kudurusu masomo yake
. (hoja zozote 5)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b 5
ut 2
15
3. MATUMIZI YA LUGHA
a)
i) /ny/
ii) /gh/
iii) /e/
iv) /w/ (4x½=2)
b) wa-cha-nga-m-shwa-vyo (1x1=1)
c) Wachezaji wote watakaguliwa ili kusuluhisha/ kuyasuluhisha/ wayasuluhishe matatizo hayo.
(2x1=2)
d) Nikishiriki katika igizo hilo vizuri nitaweza kujishindia tuzo. (1x2=2)
e) Tulimchekesha/ Tuliuigiza/Tulikiguza/Tuliwasomesha/Tuliwaandikisha/Tuliliuguza.
(1x2=2)
f)
i) Kamau ni mwanafunzi . (1x1)
ii) Ninasomea mtihani. (1x1)
g) Nguo ambazo zilinunuliwa zitauzwa./ Nguo zilizonunuliwa zitauzwa./ Matunda yauzwayo
sokoni huwa mabivu./ Mto uliofurika mwaka jana utatatiza usafiri.
(1x2=2)
h) Majundo hayo yametupwa mbali na jumba lile. (1x1)
i) Maji hayo/haya/ yale ni/yalikuwa mengi/ safi.
. (4x½=2)
j) Virutubishi vingi vinapatikana/hupatikana/vyapatikana katika matunda yanayozalishwa kwa
njia za kiasili. (1x1)
k) Huyu/Huyo/Yule/Yeye atatembelea huu/ule/huo . (1x1)
l) “Basi√√ mwanangu,”√ akasema Cheusi√, “√hivyo ndivyo tunavyoweza kufikia ‘√gender
parity ’.√√Wewe√ waonaje?”√√ (12x¼=3)
m) Idi alijishindia tuzo baada ya/ kabla ya uhifadhi wa mazingira
(1x1)
n)
i) Alimwita kwa ajili ya kumtuma . (1x1)
ii) Chai kwa mkate ni staftahi. /Wake kwa waume wanapendana. (1x1)
o)
a 8
S√
KN √KT√
√
N
S √
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
p) Gitaa ilichezewa kwa Kiprono na Rono. (1x2)
q) Mfuatano wa matukio/ matendo/ utegemeano wa matukio/ kitendo cha kuiva chategemea
embe kutiwa kapuni. (1x1)
r) Mmomonyoko wa udongo unapozuiliwa mashambani hunawiri.
Mmomonyoko wa udongo uzuiliwapo mashambani yanawiri.
Mmomonyoko wa udongo ukizuiliwa mashambani yananawiri. (1x2)
s) Baba alivamiwa na papa akiwa baharini. (2x1
.
.
t) Mzigo wa mwenzio ni kanda la usufi.
. (1x1)
u) Wale wageni – kiima
sana – chagizo (CH) (2x ½)
v) Bee/labeka (1x1)
w) Asingesoma kwa bidii asingepita mtihani.
Hungefika mapema hungenipata nyumbani.
Hangalitubu dhambi hangalikuwa na Yesu Kristo. (1x1)
x)
i) KI-VI -kiatu viatu
ii) CH-VY -chungu vyungu
iii) VI - vita (2x½=1)
y) na mafundi – kirai husishi (RH)
wenye ustadi mkubwa – kirai vumishi (RV)
(2x½=1)
4. ISIMUJAMII
a )
i) Kutumia lugha inayoeleweka/nyepesi/sahili/ya kufafanua. “Hamna faida yoyote ya kujiua.”
Upepoulivuma tulipokuwa tukiondoka
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii) Kutumia maswali ya balagha ili kumshirikisha na kuvuta makini yake. “Ukijitoa uhai
utanufaikaje?”
iii) Kutumia lugha ya mvuto/kushawishi/’Beste yangu fikiria maisha sio kifo.’
iv) Kutumia lugha ya ucheshi ‘Msee ukijimurder utanufaikaje sasa?’
v) Kuchanganya au kubadili msimbo /lugha ili kusisitiza ujumbe na kurahisisha kuelewa.
“Kwani ukicommit suicide utanufaikaje?”
vi) Kutumia viziada lugha/ ishara za uso, mikono, miondoko ya mwili ili kusisitiza hoja.
vii) Kutumia lugha ya kuelekeza/kushauri. “Maisha yako yana manufaa kuliko kifo.”
viii) Kutumia chuku. “Ukijitoa uhai utaenda kwa shetani direct.”
ix) Matumizi ya msamiati teule ‘uhai,maisha,suicide,msongo wa akili, Mungu,Yesu Kristo.’
x) Kutumia tasfida inapohitajika badala ya kutumia kauli kama kujiua unasema “kujitoa uhai.”
xi) Matumizi ya lugha sanifu “Tafadhali fikiria tena maisha yako.”
xii) Matumizi ya masimulizi ya visa vya watu waliofikiria kujitoa uhai lakini wakabadili nia.
xiii) Matumizi ya nyimbo/wimbo wa kumshinikiza asijiue.
xiv) Kutumia toni /kiimbo cha ukali/ kuonya inapohitajika .
xv) Matumizi ya mbinu ya maombi/sala.
xvi) Matumizi ya lugha legevu/isiyo sanifu. “msee, tumaisha uhitaji ujasiri: Punguza
stress.”
xvii) Kutumia sentesi /kauli fupi. “Beste yangu chagua maisha.”
xviii) Matumizi ya mbinu ya majibizano / kudadisi “Kwani ni yapi umepitia ukafikiria hivyo?”
(5x1)
Tanbihi - mifano itolewe ili alama kamili itolewe.
b)
i) Lugha ya heshima/adabu/ staha .”Bi spika, mheshimiwa spika, mheshimiwa mbunge.”
ii) Kunukuu vifungu vya sheria “kwa mujibu wa sheria za bunge hili tukufu,kifungu cha 4
kipengele cha 6, ibara ya...”
iii) Matumizi ya lugha sanifu “kupitishwa kwa mswada huu katika bunge hili...”
iv) Matumizi ya msamiati maalum “bunge, katiba,spika,hoja ,mswada.”
v) Matumizi ya lugha kavu. Lugha isiyo mapambo.
vi) Kukatizana kalima/kauli kwa wabunge.
vii) Utohozi – “spika, bajeti”
viii) Urudiaji “Bi Spika, mheshimiwa mbunge , mheshimiwa spika.”
ix) Kutajwa kwa wahusika / washirika kwa majina.
x) Wabunge hulumbana wanapochangia mijadala/miswada.
xi) Matumizi ya istilahi za kilatini za kisheria ‘habeas corpus,amicus curiae,les Judicata’
xii) Matumizi ya lugha ya mzaha na kukejeliana/ miongoni mwa baadhi ya wambunge.
(5x1=5)
Hoja na mifano iwepo ili apate alama kamili.
Tanbihi: Watahini wakadirie majibu ya watahiniwa ili wasije wakawahini alama.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KAKAMEGA JOINT EXAMINATION
KISWAHILI
102/3
FASIHI
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
FASIHI SIMULIZI
1. (a)(i) kipera –mawaidha (al.1) utanzu – mazungumzo (al.1)
(ii)Utangulizi – anayetoa mawaidha huanza kwa kauli za kuvutia nadhari na hadhira yake (mf)
naomba mnisikilize kwa makini
(b)Mwili – mawaidha huwasilishwa kwa kusisitizwa na kutumia kauli sisitizi pamoja na tamathali za
usemi kama vile methali.
(c)Mwendelezo /uwasilishaji – hapa mtoa mawaidha husisitiza lengo la mawaidha hufanya hivyo
kutegemea lengo la mawaidha yake
(d)Mwasilishaji hushirikisha hadhira yake kwa kutaka kusikia msimamo wao kuhusu mawaidha
yake, hadhira hutoa maoni mapendekezo au hata chngamoto zinazohusiana na mawaidha
yanayotolewa
(hoja zozote 2x1=2)
( iii)Sifa za mawaidha;
i. Aghalabu hutolewa na wazee wanaochukuliwa kuwa na hekima
ii. Watoa mawaidha hutarajiwa kwa watu wenye haiba heshima waandilifu wajuzi wa
mambo na wenye tajriba kuu katika maisha
iii. Tamathali za usemi zinazovuta nadhari kutumiwa mf methali
iv. Hutolewa katika miktadha maalum mf katika sherehe,
v. Hutolewa kwa wadogo, vijana au watu wanaohitaji ushauri mf; maharusi
vi. Viziada lugha hutumiwa
vii. Hutofautiana kutegemea wahusika mf jinsia na tukio
viii. Huhusisha makundi maalum (watoaji na wapokezi)
ix. Hugusia masuala tofauti mf unyumba, dini malezi, uongozi nk
x. Hutumia lugha ya kipekee inayo shirikisha maneno yenye maana nzito na inayolenga kuathiri
wanaohusiwa (hoja za kwanza 8x1=8)
B(i)Uvumbuzi wa vyombo vya mawasiliano kama vile tarakilishi, rununu n.k
(i)Mitambo ya kuchapisha na kuhifadhi maandishi
(iii)Mkengeuko wa mwafrika wa kuasi utamanduni wake na kuiga mzungu
(iv)Dini ya kikiristo ambayo inapuuza baadhi ya vitendo au miviga
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(v)Elimu haitambui wala kuthamini fasihi simulizi
(vi)Waandishi wengi wa kiafrika hawashughuliki na fasihi simulizi
(vii)Wasomaji wengi hawapendi kusoma fasihi simulizi
(viii)Serikali za kiafrika hazitilii mkazo fasihi simulizi
(8x1=8)
2. (a)Msemeji : Zohali
Wasemwa: Wanafunzi wenzake Zohali; chandachema , kairu, Mwanaheri na Umu.
Mahali: Shule ya upili ya Tangamano
Tukio: Zohali anaeleza madhila inayokumbana nayo alipoambulia ujauzito akiwa kidato cha pili.
(.4x1)
(b) i)Tabaini- inadokezwa kwa matumizi ya si
ii) Mdokezo – Unadhihirika kutokana na matumizi ya alama tatu za dukuduku riwayani na
kwenye muktadha (2x1=2)
iii) Takriri – Urudiaji wa neno si
( c)Ukiukaji wa haki za watoto
Watoto wanachomwa . Umati uliondai kuwa Lemi kamwimbia mama mmoja simu
unamchoma Lemi Vibaya. Mzee Kedi anawateketeza Beckey, Mukeli, na Annatila
anapoliteketeza jumba.
(i) Haki ya watoto kusoma inakiukwa. Ami za Lucia na Akelo wanapinga elimu yao na kudai
kuwa kuwaelimisha wasichana ni kufisidi raslimali
(ii) Watoto wanahusishwa katika ajira. Akiwa mdogo , Sauna anaajiriwa kwenye machimbo ya
mawe , kuuza maji na hata pombe baani.Vilevile Chandachema anahusishwa katika ajira ya
uchunaji wa majani chai akiwa mtoto wa darasa la tano kwenye shirika la chai la Tengenea.
(iii)Kuna wizi wa watoto. Sauna anawaibia Dickson na mwaliko na kuwapeleka kwa Bi.
Kangara ambaye ni Mlangunzi hodari wa watoto.
(iv) Watoto wanauawa na magarimoshi kwenye mtaa wa madongoporomoka wa Sombera
wanapoenda haja kwenye reli.
(v) Watoto wanahusishwa katika ulanguzi wa dawa za kulevya .
Dickson anatumiwa na mzee Buda kusafirisha dawa za kulevya ughaibuni.
(vi) Baadhi ya watoto wasichana wanaolewa na vikongwe kwa lazima .
Fungo anamwoa Pete kwa lazima akiwa darasa la saba kama mkewe wa nne.
(vii) Kunajisiwa /kubakwa- Sauna anabakwa na babake wa kambo.
Bwana maya na Kutungwa mimba .Pia lime na Mwanaheri wananajisiwa na vijana wahuni.
(viii) Watoto wanapotoshwa na watu wazima. Bi. Kangara anampotosha Sauna kwa
kuhadaa ajihusishe na biashara haramu ya ulanguzi wa watoto.Anapotoshwa ,Sauna
anahusika katika wizi wa watoto na kuwalangua.
(ix) Baadhi ya watoto wanapozaliwa wanatupwa. Naomi anamwokoa mtoto aliyetupwa jalalani
na kumpeleka kwenye kituo cha polisi .Matawa Cizarina anasema kwamba
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kuna mtoto aliyetupwa langoni mwa kituo cha watoto cha Benefactor akiwa amefungwa
kijiblanketi kikuukuu.
(x) Naomi anawahini wanawe malezi anapomtoroka mumewe.
Anamtoroka Lunga baada yake kufutwa kazi na kuwa maskini.
Jambo hili linawafanya Umu , Dickson na Mwaliko kulelewa na baba yao pekee.
(xi) Sauna anapotoshwa na Bi. Kangara anapohusishwa na wizi na ulanguzi wa watoto . Bi.
Kangara anamhadaa Sauna na kumwingiza katika biashara hii haramu.
(xii) Watoto wanapokea vitisho kutoka kwa watu wazima wanaopania kuwatumia
vibaya.Mzee Buda anamtishaDickson anapojaribu kukataa kujihusisha katika biashra ya
ulanguzi wa dawa za kulevya.Anamwambia kwamba anamtupa nje na kumsingizia
wizi.Jambo hili lingemfanya Dick kuvamiwa na kuuawa na raia kama alivyofanywa Lemi.
(xiii) Watoto wanatumiwa kama vyombo vya mapenzi. Bi. Kangara anawaiba wasichana
na kuwauza kwenye mandanguro (shambiro ) ili watumiwe kama vyombo vya mapenzi na
wanaume katili. Fumba anajihusisha na mwanafunzi wake kimapenzi na kumringa.
(xiv) Kuna ubaguzi wa watoto.Wazazi wa Pete wanamwoza kwa lazima kwa mzee Fungo
kama mke wa nne. Wanafanya hivi ili wapewe mahari itakayotumiwa kuwaelimisha ndugu
zake watano wa kiume.
(xv) Watoto walio mijini ya mama zao wanaavywa. Mamake Sauna anamsaidia kuavya
kitoto chake. Anafanya hivi kwa kumwogopa Bwana Maya aliyemnajisi Sauna.
(xvi) Ndoa za mapema
(xvii) Ndoa za lazima
(14x1=14)
3.Amali inayotajwa ni Ndoa
Changamoto za ndoa ni kama;
i. Kifo; Terry mkewe Ridhaa anaangamia kwenye moto na kumwacha Ridhaa na upweke,
Lily mkewe mwangeka pia anaangamia kwenye moto huo.
ii. Ukosefu wa watoto –Mwangemi na Neema hawakufaulu kupata mtoto katika ndoa yao
iliwabidi kupanga mtoto kwa jina Mwaliko.
iii. Ukabila- Lucia kiriri anaolewa katika ukoo wa Anyamvua.Ndoa hii inakubwa na
pingamizi kutoka kwa ukoo mzima.
iv. Ukoo- Subira mamake Lime na Mwanaheri daima anaonewa na watu wa ukoo wa
mumewe kaizari anaitwa Muki kwa kuwa anatoka katika jamii ya Bamwezi anaposhidwa
kuvumilia anawaacha watoto wake hivyo basi ndoa yao inagonga mwamba.
v. Wazazi kukataa watoto wao kuolewa-Wazazi wa Rehema wanakataa ndoa yake Fumba
aliyekuwa amempachika mimba na Chandachema akazaliwa .Rehema alikuwa
mwanafunzi wake Fumba.
vi. Ukosefu wa uaminifu-Chandachema anasema kuwa bwana Tenge alikuwa na jicho la
nje.Wakati Mkewe Bi Kimai alipoenda mashambani alileta wanawake tofauti machoni
mwa mwanawe.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
vii. Migogoro katika ndoa-Babake pete anakosa kumkubali kama mwanawe kwa kuwa
hawana mshabaha naye hivyo basi pete anapelekwa kulelewa na nyanya yake mzaa
mama.
viii. Chuki katika ndoa-katika ndoa za mseto kuna chuki baina ya wake mf;pete anapoozwa
kwa bw. Fungo anaonewa wivu na mke wa pili na watoto wa mke wa kwanza
wanamcheka ,anaamua kutokaa kwa mzee Fungo.
ix. Vita katika ndoa-Sauna anasema kuwa mamake alikuwa amedhulumiwa na mumewe
bwana Maya hivi kwamba hangeuliza hata swali anapoulizwa anakuwa mpokezi wa
makonde vitisho na matusi.Hivyo basi Suna hangemwambia mamake unyama
aliotendewa na babake.
x. Pombe-Mamake sauna anasema kwa babake mzazi wa Sauna alijitosa kwenye unywaji
wa pombe mitaani na kujisababishia kufutwa kazi.Hii ilisababisha umaskini na bwana
maya ndio maana hataki apakwe tope.
xi. Umaskini-Naomi anamuacha mumewe Lunga baada ya Lunga kuachishwa kazi.
xii. Upweke-Baada ya Naomi kuondoka alimwacha Lunga na upweke na hii inasababisha
lunga kushikwa na ugonjwa wa shinikizo la damu baadaye anafariki.Kiriri pia anafariki
kutokana na ukiwa anapoachwa na mkewe Annette.
xiii. Uhasama katika ndoa-Mzee mwimo msubiri alikuwa ameoa wake wengi na wakapata
watoto wengi shamba alilokuwa nalo likakatwa katika vikataa ambavyo havingekidhi
mahitaji yao yote.Uhasama uliotokea katika familia yake ulisababisha yeye kuhamisha
wake wawili katika msitu wa Heri.
xiv. Wazee kuoa wasichana wadogo-Mzee Fungo anamuoa Pete bila hiari yake ndoa hii
inasambaratika baadaye.
xv. Tofauti za kisiasa-Selume ambaye wanatofautiana na mumewe na wakweze kisiasa
wanaishia kugombana mara kwa mara.Mambo yanapozidi Selume anafunganya virango
na kwenda kuishi kwenye kambi ya wakimbizi katika msitu wa Mwamba.
xvi. Malezi ya watoto-Annette na Kiriri wanatofautiana na masuala ya utunzaji wa watoto
wao.Annette anamnyima Kiriri ushirika wa malezi ya watoto wao anapoenda kuishi na
watoto wao ughaibuni.
xvii. Hofu katika ndoa-Baadhi ya wanawake wanahofia kuwa ndoa zao zitavunjika iwapo
atawalea watoto wa mama wengine waliokuwa wapenzi au wake wa waume
zao.Hushikilia kuwa kuwalea watoto hao ni njia ya kurudisha uhusiano waliokuwa
waume zao na wanawake wa awali.mf Mke aliyeolewa na Fumba huenda aliogopa
kumlea Chandachema wa kuogopa uhusiano kati ya Fumba na Rehema ungerejea.
xviii. Ndoa za kujaribisha-Nyangumi anataka kuishi na pete kwa miezi miwili ndipo
wajaribishe ndoa yao.
xix. Wanawake kundanganywa na wanaume-Nyangumi anamdanganya pete kwa kuwa
hakuwa ameoa hata pete anaingia mtegoni wa kuanza kuishi na Nyangumi kama mke na
mume.Baada ya muda mke wa Nyangumi anajitokeza na pete anaishi kupata mtoto
mwingine.
xx. Wanandoa kutoacha nasaba zao baada ya kuoana-Naomi mkewe Lunga hasahau
uhusiano wake na nasaba yake inasemekana kuwa hutulii kupalilia maisha ya unyumba.
xxi. Maonevu-Subira analalamika kuonewa na wakwe zake kwa kuitwa mwizi hii
inapelekea yeye kuwacha mumewe na watoto wao.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
xxii. Usaliti katika ndoa-Billy alikuwa na matarajio kuwa angemuoa Sally baada ya kujenga
nyumba aliyodhania ingempendeza.Sally hapendezwi na nyumba yenyewe anafunga
virango na kurundi kwao anamwacha Billy katika hali mbaya ya kutaka tamaa.Naomi
pia anamsaliti mumewe Lunga licha ya kuwa lunga anajisabilia kumpendeza kwa hali na
mali lakini Naomi hampendi kamwe.
( hoja 20x1=20)
4. (a) i)Haya ni maneno ya Boza
ii) Anamwambia sudi na Kombe
iii)Wamo kwenye karakana yao sokoni Chapakazi wakichonga vinyago.
iv)Ni baada ya sudi kukataa kula keki ya taifa ndipo Boza akasema maneno haya ili
kuwaonyesha kuwa hawawezi kubishana na majoka
(4x1=4)
(b)Mzungumzaji ni Boza.
i. Mwenye dharau.Sudi anapoizima redio ya rununu yake, anamwambia kuwa kijiredio
chake cha pesa kisimtie kiburi
ii. Mwenye ubinafsi.Anapopewa keki na Mzee kenga anasema kuwa ni kidogo sana,kiasi
kwamba ukiwa nayo huwezi kuwafikiria jamaa zao.
iii. Mwoga.Anamwogopa majoka.Anamwambia mwenzake kuwa majoka hachezewi kwani
kufanya hivyo ni sawa na kutafuta maangamizi.
iv. Mpyaro.Anamtusi Tunu kwa kusema yeye hauzi nyonga kama yeye.
v. Mwenye mawanzo finyu.Wafanyakazi wenzake kama Ashua wanapoteta kuhusu hongo
wanyoitishwa sokoni anamwaambia waache kulalamika
vi. Mwenye taasubi ya kiume.Anawadharau wanawake.anasema kwamba yeye hauzi nyoga
kama Tunu. (za kwanza 6x1)
( c) Kigogo anayerejelewa ni Majoka
i. Anamuua jabali baada ya kuuda chama cha upinzani cha mwenge ili kumpiga kisiasa.
ii. Anawatuma wahuni wanaomvamia Tunu na kumuumiza baada ya Tunu kuongoza
maadamano ya kupiga tendo lake la kufunga soko.
iii. Raia wanapoandamana ili kumshinikiza kufungua soko, anawatuma polisi kuwatawanya
kwa vitozamachozi na risasi
iv. Anaifunga runinga ya mzalendo inapopeperusha maadamano ya raia wanaopinga kitendo
chake cha kulifunga soko.
v. Mkuu wa polisi ,bwana kingi anapokataa kuwapiga risasi jinsi alivyokuwa amemuagiza
anamwachisha kazi mara moja.
vi. Baada ya kifo cha Ngurumo anasema lazima chatu moja auwawe ili kuwafumba macho
wafuasi wake.
vii. Vijana watano walipoanza kuandamana ili kupiga kupandishwa kwa bei ya chakula
kwenye kioski chake, wanauliwa.
viii. Sudi alipokataa kumchongea kinyago cha babuye , anamfunga mkewe Ashua
kumshurutisha kumchongea kinyago hicho.
ix. Anawafurusha wafadhili na wanaharakati,Tunu alipoanza kumsuta kwa kufuja pesa za
kusafisha soko kupitia vyombo vya habari,hivyo kuwadhoofisha kifedha
x. Kuwatishia akina Siti na bi Hashima wahame Sagamoyo
(za kwanza 10x1=10)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
5 (a) i) Wanasagamoyo wanafungiwa soko la chapakazi ambalo ni kitega uchumi
chao.Sasa hawana mahali pa kufanyia biashara
ii)Soko la chapakzi limetapakaa;majitaka yanapopita mtaroni.Soko lao limegeuka
kuwa uwanja wa kumwagia kemikali na taka
iii)Wafanyi biashara sokoni wanahangaishwa na wenye nguvu;wanasema ndio hewa
wanayopumua.
iv)Wanasagamoyo wanaangamia kutokana na matumizi ya pombe haramu;Asiya
amepewa kibali cha kuuza pombe hii.
v)Kuna mauaji sagamoyo vijana watano wanauliwa baada ya kuandamana ili soko la
chapakazi lifunguliwe wengine wanarushiwa vitoa machozi na polisi.
vi)Hakuna ajira-Vijana waliofuzu katika masomo yao hawapati ajira mf
sudi,Ashua,Tunu.
Vii)Wanasagamoyo wanalalamika bei ya chakula katika kioski ya kampuni ambayo
imepandishwa maradufu.
vii)Mishahara duni-Walimu na wauguzi wamekuwa wakigoma kwa sababu ya
mishahara na wanaongezwa kodi.
viii)Wanasagamoyo wanaishi kuwa hofu ya kushambuliwa kama anavyoeleza
bi,Hashima.
ix)Wanasagamoyo wengine wanatishiwa kuhamishwa kwamba sagamoyo si kwao.
xii)Hakuna usawa wa kijinsia-Wanawake hawapewi nafasi ya uongozi.Majoka
anampinga Tunu naye Ngurumo anasema afadhali achague paka kuliko mwanamke.
xii)Kuna ubaguzi sagamoyo-watu hawapati nafasi iwapo hawatokani na ukoo wa
uongozi
xiii)Kuna uharibifu wa mazingira-Serikali inatoa kibali cha ukataji miti.
xx)serikali kufunga kituo cha runinga cha Mzalendo
xix)Wafanyakazi kutolipwa bima
xixx)Unyanyasaji wa kijinsia-Ashua anashinikizwa kujihusisha kimapenzi na majoka
ili asaidiwe. (12x1=12)
(b)
Hizi zile mbinu ambazo wanaharakati wanatumia kuleta mabadiliko ya kisiasa,kiuchumi
na kijamii
i. Kuandaa maandamano-wanafanya maandamano ambayo wengi wao wanajeruhiwa na
wengine kuuawa na polisi
ii. Umoja/uhusiano-wanaungana kwa pamoja na kutetea haki zao.
iii. Kukabili viongozi ana kwa ana-Tunu anamkabili majoka uso kwa uso na kukashifu
unyama wake, Ashua yuafanya vivyo hivyo.
iv. Kukata vishawishi-sudi anakataa zawadi anazoahidiwa ili kumchongea majoka kinyago
cha babake
v. Kuvumilia mateso na dhihaka- Azma ya Sudi na Tunu haizimwi na mabezo ya wapinzani
wao
vi. Elimu-Sudi,Tunu na Siti wanelekea kwa mamapima kuwahamisha walezi wajiunge nao
katika maandamano.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
vii. Vyombo vya habari na mitandao ya kijamii-runinga ya mzalendo ilikuwa ikipeperushwa
moja kwa moja .Maadamano ya wapigania haki kiasi cha kufanya Kenga na Majoka
kutaka kuichukulia hatua.Aidha,mitandao ya kijamii ilikuwa ikieneza shughuli za
wazalendo hawa kiasi cha kumkera mno Kenga.
viii. Wafadhili-wapigania haki walikuwa wakipigwa jeki na wafadhili.Kenga anaona kuwa
hawa wafadhili ndio walikuwa wakikwapa nguvu naye majoka anadai kuwa sharti hawa
wafadhili wavunje kambi zao Sagamoyo.
6 SEHEMU D : USHAIRI
SWALI LA 6
a) Mwananchi/raia/mzalendo/mtetezi wa haki za binadamu – aweze kueleza (1x1)
b)
i)Tabdila-wanaturarua-;ili kuleta urari wa vina
ii)Inkisari-aso badala ya asiye, ili kuleta urari wa vina
iii)Utohozi-Noleji kutokana na neno Knowledge ili kuleta urari wa vina na muwala wa mizani
(ataje na kueleza 2x2=4)
c)
i. Kikwamba-neno longwe limetumiwa kuanzia beti zote kisha maneno yanaypofuata yanayotumiwa
kueleza maana sawa ya neno longa
ii. Ukaraguni-Vina vya ukwapi na utao vinabadfilikabadilika
iii. Madhnawi-Shairi limegawanyika katika vipande viwili; ukwapi na utao
iv. Kikai-ukwapi au mizani 8 na utao unamizani 6
v. Sabilia-Shairi lina kituo.mshororo wa mwisho unabadilika badilika katika kila ubeti.
(zozote 4x1=4)
d)
i. Urudiaji wa neno- Longa
ii. Urudiaji wa visawe-longa ni sema,zungumza,ongea,kuli,tamka
iii. Urudiaji wa silabi- si.
(3x1=3)
e) Ghadhabu/hasira-tamka maneno, mbwa aso meno (1x2=2)
i. Afwaji-kaumu/halaiki/umati wa watu/kikundi/kigaro
ii. Tenge-funjo/ghasia/kondo
i. Lina beti nne
ii. Kila ubeti una mishororo mitatu isipokuwa ubeti wanne
iii. Kila mshororo una vipande viwili
iv. Kila mshororo una mizani 8 katika ukwapi na 6 katika utao
v. Vina vya kati na vya mwisho vinatofautiana katika kila ubeti (zozote 4x1=4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
7 a)
i. Kila kipande kina idadi ya mistari tofauti na kingine
ii. Mishororo haitoshani katika kila ubeti,baadhi ni mirefu,mingine mifupi
iii. Idadi ya mizani Inatofautiana katika kila ubeti (2x1=2)
b)Kuonyesha jinsi mwanamke anavyoonewa kwa sababu ya jinsia yake (2x1=2)
C)Kwa kutoa mifano,eleza maana ya mistari mishata
-Ni mistari isiyojitosheleza kimaana kwa mfano dhiki ya ulezi
Hukaa na kujidadisi (kueleza 2 mfano 1)
d)Balagha-wapi raha yangu ulimwengu huu?
Takriri-kurudia rudia maneno iwapi,wazia, dhiki (2x1=2)
e)Ni mwanamke anayedharauliwa (2x1=2)
F)Toni ya huzuni, majonzi (al.2)
8 (a)(i) Haya ni maneno ya mzee mosi.
(ii)Anamwabia Jairo
(iii)Wako nyumbani kwa mzee mosi
(iv)Ni baada ya Jairo kumlaumu mzee mosi kumuaibisha kwa kumpa zawadi zote alizoletewa na
wageni siku ya sherehe.
(al.4)
b)(i)Mwenye busara- anaweza fundisha wanafunzi wengi ambao wamefaulu maishani
(ii)Msikivu-anasikiliza kile ambacho Jairo alimwelezea bila kumkatiza hata baada ya kumlenga
mwendwawazimu
(iii)Mwenye utu-Anakubali agizo la mkewe la kuikubali familia yake Jairo na kusomesha Sabina.
(iv)Mwelekezi mwema-alimwelekeza Jairo kwa kumtia moyo kuwa ataimarika. (4x1=4)
c)
i. Mwalimu mosi anawakumbusha watu wampigie Jairo makofi anapotoka jukwaani hata ingawa
alimsimanga
ii. Mwalimu mosi alimshauri Jairo asinywe tembe kwani ni kitu kibaya
iii. Mwalimu mosi alimshauri Jairo kuepukana na ufuska na asubiri hadi ndoa ndipo kuchuna ngozi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv. Mwalimu mosi alimpa Jairo matumaini kuwa,uzuzu wake utakwisha na kwamba sufuri zake
masomoni zitapisha mia kwa mia.
v. Mzee mosi aliwapa watu tabaka la chini nafasi ya kuhutubu kama vile Jairo bila kuwatenga.
vi. Mikononi mwake mwalimu mosi,watoto wengi walifinyangwa mpaka wakawa
mawaziri,wahadishi,wahasibu,n.k
vii. Mwalimu mosi alikuwa mwenye subira,shime na wa kutoa wosia wa kuwaelekeza wanafunzi
viii. Mzee mosi anaamua kumpa Jairo zawadi zote alizoletewa bila kuonyesha ubinafsi wowote.Kwa hiari
yake bila kumhusisha mkewe.
ix. Jairo anaonyesha busara ya kuomba msamaha kwake mzee mosi baada ya kumwedea kwa hasira kuwa
amemtorosha bintiye waishi mjini ila ilikuwa porojo.
x. Mzee mosi akiwa angali mwalimu aliwafunza wanafunzi maadili mema yasiyo tekeleka na kuwatunza
wote bila kuwadhulumu.
xi. Mzee mosi aliweza kujikakamua tangu utotoni na kujikwamua kutoka kwa ufukara
xii. Bi. Sera anaonyesha busara kwa kumkataza mzee mosi kuwafurusha mkewe Jairo na bintiye.
xiii. Familia yake mwalimu mosi Nampa mke wa Jairo nyuba kwenye kiambo ambako anakaa Na watoto
wake.
xiv. Kijiji kizima kilikuwa na sulubu ya kumzuia Jairo asijitoshe mtaani baada ya kugundua uozo wake
wa kuumbulia jina mwalimu mosi.
xv. Mwalimu mosi alitaka kuandika tawasifu ya maisha yake tangu utotoni jinsi alivyojikakamua
kutoka kwa ufukara na kusomea katika chuo cha walimu na kufundisha kwa miaka mingi yenye
maadili yasiyotetereka ya kuwafunza watoto wa watu wa wavulana kwa wasichana bila kumdhuru
yeyote.
xvi. Mwalimu mosi aliwapa wanafunzi wake nasaha na kuwa mkarimu , hekima, ustaarabu, uadilifu,
uajibikaji, na mchesi .
xvii. Wasemaji wengine katika hotuba zao walimsawiri Mosi kama mtu mkamilifu asiyekuwa na taksiri,
mwalimu bora, mwadilifu,asiyeweza kudhuru yeyote na kiumbe kilichokamilika.
xviii. Wanafunzi na wazazi walitoa zawadi kwa mwalimu Mosi za kila nui na zikawa rundo kubwa.
xix. Mwanafunzi mmoja wa zamani alijitolea kumpelekea mwalimu Mosi zawadi nyumbani kwenye gari
lake aina ya pickup. (12x1=12)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
LAIKIPIA JOINT EXAMINATION
KARATASI YA 1
INSHA
KIDATO CHA NNE
MUDA 1¾
MAAGIZO
a) Andika insha mbili
b) Insha ya kwanza ni ya lazima
c) Kisha chagua insha moja nyingine kutoka hizo tatu zilizobakia
d) Kila insha isipungue maneno 400
e) Kila insha ina alama 20
SWALI LA KWANZA NI LAZIMA
1. Suala la ufisadi limekuwa donda dugu nchini. Andika mahojiano kati ya mwenyekiti wa tume ya
kupambana na ufisadi nchini na mwandishi wa habari kuhusu mbinu za kupambana na donda hili.
2. Vijana wa kisasa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha. Fafanua huku ukipendekeza
hatua zifaazo kuchukuliwa ili kuzikabili changamoto hizo.
3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo :
Uzuri wa mkakasi ndani kipande cham mti.
4. Tunga kisa kinachoanza kwa maneno yafuatayo :
Nilipigwa na butwaa nilipomwona, sikujua nifurahi au nihuzunike……
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
LAIKIPIA JOINT EXAMINATION
KISWAHILI (LUGHA)
KARATASI 2
SAA 2𝟏
𝟐
KIDATO CHA NNE
1. UFAHAMU
SOMA KIFUNGU KIFUATACHO KISHA UJIBU MASWALI
Tangu zama kongwe za mawe maisha ya binadamu yamepitia katika awamu mbalimbali za kimaendeleo;
yawe ya kisayansi, kiuchumi, kijamii au hata kisiasa. Katika kipindi chote ambacho binadamu ameishi
katika ulimwengu huu, utamaduni umekuwa sehemu muhimu ya maisha yake.
Utamaduni huu unaweza kuangaliwa kwa namna mbalimbali. Upo utamaduni finyu ambao unahusisha
jamii moja dogo mathalan, kabila, ukoo au eneo dogo. Kwa upande mwingine kuna utamaduni mpana
ambao unaihusisha jamii nzima. Mathalan, nchi fulani inaweza kuwa na matendo, imani, thamani na fikira
ambazo ni msingi mkubwa katika nchi hiyo. Hizi huwa msingi wa utamaduni wa kitaifa. Utamaduni huu
ndiyo unaomtenga raia wa nchi moja na raia wa nchi nyingine. Utamadani wa kitaif ni nguzo muhimu ya
uzalendo wa wanataifa maalum; unawatambulisha na wanauonea fahari. Vipengele vya utamaduni wa
kitaifa huweza kutokeza kwa njia mbalimbali kama mavazi, vyakula, lugha, itikadi au hata mtazamo wa
raia wa nchi mahsusi. Tumbi kubwa ya nchi za ulimwengu huwa na utamaduni unaozitambulisha na ambao
humfanya raia ajinabi kuweza kuwatambua raia hao. Utamaduni ni kitovu cha uhai wa jamii yoyote ile.
Licha ya ukweli huu, ni muhimu, inahalisi kutambua kuwa maisha ya binadamu huathiriwa na kani
mbalimbali zinazotokea katika mazingira yake ya kila siku. Kani hizi huweza kuwa vyanzo vya madadiliko
ya sifa fulani zinazohusishwa na utamaduni wake. Maendeleo ya kiwakati ambayo huenda sambamba na
mahitaji anuwai ya kimaisha huweza kuwa chanzo cha kuachwa kwa tamaduni fulani. Hata hivyo,
binadamu sio sifongo ambalo hufyonza maji yote, maji machafu na maji safi pasi na kubagua. Binadamu
mwenye akili razini anapaswa kuchuja na kutathmini ni amali au thamani zipi mpya ambazo anaweza
kuzichukua na labda kupuuza baadhi ya thamani za kale zisizomfaa.
Kigezo kikuu kinachomsaidia ni kutambua mahitaji yake sambamba na wakati anamoishi. Mathalan,
katika maisha ya zamani, uchumaji ulitegemea ubabe kwa kiasi kikubwa lakini siku hizi ubabe sio kigezo
cha uchumaji kwa kiasi kikubwa. Akili ni msingi mkubwa sana siku hizi katika uchumaji au kutarazaki.
Inahalisi basi kupuuza sifa za kitamaduni ambazo zinaelekea kuutilia mkazo mkubwa kwenye matumizi ya
nguvu au ubabe.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Yapo matendo mengi katika jamii ambayo yalidhibitiwa na imani za kishirikina kabla ya nuru ya elimu
kulimuka giza la ujinga lililotamalaki katika jamii. Ikiwa jamii itaendelea kuyatenda matendo hayo basi ile
itakuwa ni jamii ambayo, kama pia, imezunguka palepale. Ile itakuwa ni jamii ambayo imeshindwa
kuendelea
MASWALI
a) Taarifa hii inahusisha utamaduni na wakati kwa jisnsi gani (alama2)
b) Eleza uwili unaojitokeza katika utamaduni (alama2)
c) Eleza dhima ya utamaduni ukirejelea taarifa (ala3)
d) Taja methali moja ukieleza matumizi yake inayofumbata ujumbe ulioko katika taarifa hii (alama2)
e) Eleza mambo yanayopewa kipau mbele katika mchujo wa utamaduni ( alama2)
f) Uchumaji katika jamii umeathiriwa na wakati. Tathmini (ala2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
g) Eleza maana ya vifungi vifuatavyo kama vilivyotumika katika taarifa husika (alama2)
i) Raia ajinabi
ii) giza la ujinga lililotamalaki
2. MUHTASARI
SOMA MAKALA YAFUATAYO KISHA UJIBU MASWALI
Siku hizi elimu kwa mtoto wa kike imegunduliwa kuwa akiba ya kipekee ambayo nchi yaweza kijivunia.
Elimu kwa wasichana hutoa mchango mkubwa katika upanuzi wa uchumi wa nchi na pia kupunguza na
kuzuia idad ya watoto ovyo. Aghalabu, hali ya afya na lishe bora kwa mtoto pia huweza kudumishwa.
Ni bayana kwamba elimu imewaongezea wanawake matumaini ya kushiriki katika maswala nyeti ya
kijammii na kisiasa. Kwa hivyo, elimu kwa mtoto wa kike ni jambo la kuonea fahari mno, hasa katika nchi
za kusini mwa jangwa la Sahara, ambako maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisisa yametatizika kutokana
na idadi kubwa ya watu, ambao ni vigumu kwa serikali za hizo nchi kuwakidhi kimahitaji. Hii ni kutokana
na ukosefu wa rasilimili za kutosha
Yafaa ifahamike wazi kwamba wanawake ndio msingi thabiti wa maisha barani Afrika, hii ni kutokana na
majukumu haya yote, inasikitisha kuona kwamba zaidi ya wasichana milioni thelathini kutoka katika nchi
za kusini mwa jangwa la sahara wamekosa elimu.
Wachache walio na bahati ya kufika shuleni hawahudumiwi ipasavyo – jambo amabalo limesababisha idadi
ya wasichana wanaotamatisha masomo ya shule ya msingi kuwa nusu ikilinganishwa na asilimia hamsini na
tano ya wavulana.
Katika baadhi ya nchi, ni asilimia kumi na tano tu ya wasichana ikilinganishwa na asilimia arobaini na tano
ya wavulana ndio hujiunga na shule za upili. Kwa hivyo ni wazi kwamba, pengo la tofauti za kijinsia na
kielimu huzidi kupanuka katika kila ngazi ya masomo, “alifichua mmoja wa viongozi wa FaWe” katika
vyuo vikuu nchini Kenya na Tanzania ni asilimia thelathini tu ya wanawake ndio hufuzu kila mwaka,
ikilinganishwa na asilimia sabini ya wanaume.
Kulingana na FAWE hali ya watoto wa kike kutopiga hatua kimasomo huletwa na sababu mbali mbali za
kiuchumi, kijamii na kisiasa.
Moja ya sababu kuu ni umaskini, ambao umewakumba wazazi wengi hasa kwa waishio mashambani, na
kuwafanya wasiwe na uwezo wa kuwanunulia watoto vifaa muhimu vya masomo pamoja na kuwalipia
karo. Jambo hili limewafanya wazazi kuwashurutisha watoto wao wa kike kuwapa nafasi wavulana ambao
yamkini wanaweza kustahimil hali ngumu ya maisha wakilinganishwa na wasichana
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Vile vile imebainika wazi kwamba baadhi ya wazazi wangali wanatawaliwa na mtazamo uliopitwa na
wakati, kuwa kumwelimisha msichana ni sawa na kupeleka mali hadi kwa familia nyingine, kwani kulinana
na wao, punde atakapotamatisha masomo, ataolewa na hapo kuhama na mali yote. Isitoshe, katika baadhi
ya jamii, msichana anawasilishwa kama chombo cha kuzaa watoto wa kiume wakijihusisha katika utafiti wa
matukio ya kisiasa
Kikwazo kingine kwa elimu ya watoto wa kike ni dhuluma na unajisi wanaofanyiwa hasa sehemu za shule
ambao umekuwa wa kutisha mno. Jambo hili limefanya kiwango cha elimu ya wasichana kudidimia na hata
wengine kung’atuka shuleni kutokana na kushika mimba au kuugua majonjwa ya zinaa, ukiwemo ukimwi.
a) Nchi inaweza kunufaikaje kutokana na elimu kwa wanawake ala7 (maneno 60-70)
matayarisho
Jibu
b) Eleza vizingiti mbalimbali vinavyoathiri elimu kwa wanawake barani Afrika (maneno 50-60) alama8
Matayarisho
Jibu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
3. MATUMIZI YA LUGHA
a) Andika sauti zifuatazo al. 1
i) kizuio ghuna cha masine
ii) kituo kwaruzo
b) Fafanua sifa bainifu za sauti /shw/ al.1
c) Eleza maana ya silabi changamano kisha utolee mfano al.2
d) Taja vigezo/sifa zinazotumika kuweka viambishi katika makundi yake kwa kutolea mifano al.2
e) Andika visawe vya mofimu huru al.1
ii) Eleza sifa za mofimu al.2
f) Onyesha tofauti ya sentensi hizi al. 2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Pahali hapa panavutia
ii) Mahali huku kunavutia al.2
g) Onyesha aina ya vinyume katika maneno haya al.2
i) Injika
ii) Anza
h) Tumia kivumishi cha ki-mfanano kutungia sentensi al.1
i) Kanusha sentensi hii kwa njia mbilimbili tofauti
Angalisoma kwa bidii angaliupita mtihani
j) Geuza chagizo katika sentensi hili iwe ya idadi kamili al.1
Walimu huwashauri wanafunzi mara kwa mara
k) Ainisha vitenzi katika sentensi hii.
Angali akiimba akipita chakula kitamu al.2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
l) Changanua kwa njia ya mstari al.3
Yule ambaye hujitahidi sana hufaulu lakini asiyefanya bidii hujilaumu
m) tambua yambwa na chagizo katika sentensi ifuatayo al.4
Naviekomba aliandaliwa chakula kitamu Jumamosi ile kwa moto wa makaa.
n) Tumia neno “tunda” kwenye sentensi moja ili kuonyesha maana mbili al.2
p) Onyesha matumizi mbalimbali ya na katika sentensi
Wewe nasi tunashindana kubaini nani ana pesa nyingi.
q) Tambua miundo ya virai katika sentensi al.4
Kondoo yule mweusi sana alikatalia katika ya barabara
r) Tunga sentensi mbili kuonyesha matumizi mawili ya mshazari al.2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
s) Geuza kwa msemo wa taarifa
“Mama! Mama! Nitaenda kuwaangalia kesho mtoto alisema al.2
t) Jibu maswali kulingana na maagizo
i) Mwanafunzi alisoma kwa bidii
ii) Mwanafunzi alipita mtihani
Unganisha sentensi hizi kwa kiunganishi cha masharti al.1
ii) Maji yalijaa. Maji yalimwagika
(Unganisha kuwa sentensi changamano katika hali ya mazoea al.1
4. ISIMU JAMII
(Mdundo wa muziki) kina mama mpo......kina siste mpo........Are you there?
Kampuni ya platinium imewaletea mafuta mpya ya Silk. Mafuta hayo yana Vitamin C, sunscreen na yana
marashi ya kupendeza. Ukiyatumia kwa wiki moja tu, ngozi yako itakuwa laini na nyororo kama ya kitoto
kichanga. Nayo macho ya wote, waaa!. Yatakiwa kwako 24/7. Jinunulie,! Jinunulie! Mafuta ya Silk.
Mafuta ya wanawake wa kisasa.
a) Taja sajili iliyotumika hapa al.1
b) Taja sifa nne za sajili hii zinazojitokeza katika dondoo al.2
c) Kwa nini Wakenya wengi hupenda kuchanganya na kubadili msimbo? al.3
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
d) Eleza mambo manne yanayosababisha kuwepo kwa sajili mbalimbali za lugha. al.4
LAIKIPIA JOINT EXAMINATION
KISWAHILI
KARATASI YA 3
KIDATO CHA NNE
FASIHI
MUDA: SAA 2½
MAAGIZO
1. Jibu maswali manne
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. Swali la kwanza ni lazima
3. Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki yaani: Tamthlia, Hadithi
fupi, Ushairi na Fasihi simulizi
4. Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
SEHEMU A. TAMTHILIA (LAZIMA)
KIGOGO (PAULINE KEA)
1. “………. Lazima chatu mmoja atolewe kafara ili watu wahue kuwa walama upo.”
a) Fafanua muktadha wa maneno haya. (alama 4)
b) Eleza sifa mbili za msemewa wa maneno haya. (alama 2)
c) Kwa kufafanua hoja kumi na nne, eleza namna wanasagamoyo wanavyotolewa kafara.
(alama 14)
SEHEMU YA B. RIWAYA
CHOZI LA HERI ( ASSUMPTA K. MATEI)
MAAGIZO
Jibu swali la 2 au 3
2. ‘‘ Maskini mwanangu….. Amekuwa mjane hata kabla ya ubwabwa wa shingo kumtoka !’’
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
a) Eleza muktadha wa maneno haya. (alama 4)
b) Taja Tamathali ya lugha iliyotumika katika dondoo hili. (alama 2)
c) Taja umuhimu wa mwenye kauli hii. (alama 2)
d) Onyesha changamoto ambazo wahusika mbalimbali walipitia kabla ya ubwabwa wa shingo kuwatoka.
(alama 12)
3. Jadili ufaafu wa anwani Chozi la Heri. (alama 20)
4. SEHEMU YA C. USHAIRI
Soma mashairi yafuatayo kisha ujibu maswali.
SHAIRI A.
Tinda la elimu zote, wasema wanazuoni
Nikwamba mtu apate, tutambua manani
Ndipo hadhi aipate, ukumbukwe duaniani
Elimu bila ukweli, haizidi azilani
Giza na nuru muhali, katu havitangamani
Uwongo uje kwa kweli, itue nure moyoni.
Elimu ni kama mali, haichoshi kutamani
Nibora yashinda mali, tala la wanazuoni
Elimu njema naili iangazayo gizani
Wafuna waiosoma, watazikwa ardhini
Hai ndio maulana, wapaao maagani
Elimu jambo adhima, aso nayo maskini
Toa wafu ujana, elimu ukitamani
Na uwe mzee sana, kujua usijihini
Elimu bahari pana, milele hauoni pwani.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Elimu ina malipo, utayalipwa mwishoni,
Pale vitafutapo, mbingu usitamani
Mwanachumi afapo, mbingu huwa huzuni.
Haki ya kuheshimiwa, ni yao wanachumi
Wao wameongolewa, na ni taa duniani
Kweli wanapojua, watoe bila kuhini.
Elimu bila amali, mti usio majani
Haumtii kivuli, aukaliaye chini
Inakuwa mushkeli, wa kughuri insane.
SHAIRI B.
Inakera moyo
Hii anga ambayo
Huwasonya njiani
Watukao mashambani
Wa kusalimu kwa bashasha
Wanaoshinda kivulini.
Chini ya mwembe
Wa umma
Inakera moyo
Hii sebule ambayo
Huwahani mezani
Wagotao nyundo kutwa
Wa kukabidhi chakula
Wanaostarehe daima,
Chini ya paa
La umma
MASWALI
a) Pendekeza kichwa mwafaka kwa shairi la A na la B. (alama 2)
b) Haya ni mashairi ya aina gani ? (alama 2)
c) Taja sifa zozote tatu za kishairi katika shairi la B. (alama 3)
d) Taja mbinu ya lugha iliyotumiwa
i) Katika mshororo wa mwisho wa ubeti wa saba katika shairi la A. (alama 1)
ii) Katika ubeti wa nne shairi la B. (alama 1)
e) Fafanua kwa muhtasari maudhui ya mashairi. (alama 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
f) Andika ubeti wa mwisho wa shairi la A katika nathari (alama 3)
g) Taja na uonyeshe jinsi idhini ya ushairi ilivyotumika katika shairi la A. (alama 3)
h) Eleza maana ya maneno haya yalivyo tumika katika shairi la A. (alama 2)
i) Wameongolewa
ii) Wagotao
SEHEMU YA D. HADITHI FUPI
TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI NYINGINE
Jibu swali la 5 au 6.
5. “penzi lenu na nani?...... mgomba changaraweni haupandwi ukamea. Potelea mbali mkata wee !’’
a) Eleza muktadha wa dondo hili. (alama 4)
b) Taja na ufafanue mbinu mbili za lugha zilizotumika katika dondoo hili. (alama 4)
c) Onyesha vile maudhui ya utabaka yanavyojitokeza katika hadithi nzima. (alama 6)
d) eleza sifa sita za mzungumzaji kwenye dondoo. (alama 6)
AU
6. Ilikuwa kama vile katia saini ya kutiwa kitanzi bila ya kutambua vipengele vya sheria za utiaji huo wa
kitanzi.
a) Fafanua tamathali mbili zilizotumika katika dondoo. (alama 4)
b) Jadili vipengele vitano vya sheria zinazorejelewa katika hadithi nzima. (alama 10)
c) Onyesha dhiki iliyompata mrejelewa kwa kukosa kuvitambua vipeengele hivyo.(alama 6)
SEHEMU YA E. FASIHI SIMULIZI.
7. Linganua methali na vitendawili. (alama 5)
b) Fafanua dhima zozote tano za misimu. (alama 5)
c) Eleza udhaifu wa ngomezi. (alama 5)
d) Fafanua maana ya mivigha. (alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii) Jadili sifa tatu za mivigha. (alama 3)
LAIKIPIA JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA INSHA
KARATASI YA 1
KIDATO CHA NNE
Hii ni insha ya mahojiano. Mwanafunzi azingatie sura ya insha ya mahojiano.
1. Mada au kichwa kitambulishe ujumbe wa Mahojiano yenyewe, yanafanyika wapi na wahusika.
2. Utangulizi huwa na maelezo mafupi yanayoandikwa katika mabano. Mwanafunzi anaweza kutaja
mahali pa Mahojiano iwapo hakutaja katika kichwa mwanafunzi abuni majina/vyeo vya wahusika.
3. Mwili: Mtindo wa kitamthilia utumiwe.
- Hisia na ishara mbalimbali huonyesha kwenye mabano kwa mfano huzuni, vicheko
- Nafsi ya kwanza utumiwe
Baadhi ya hoja.
1. Wafanyikazi walipwe mishahara bora
2. Kuwaelimisha watu kuhusu madhara ya ufisadi k.v kuzorota kwa uchumi.
3. Kuwaadhibu watu fisadi kistoria
4. Raia na viongozi wawajibike katika kazi zao k.m waepuke tama
5. Kubuni nafasi zaidi za kazi.
6. Kuhimiza na kuwapa watu mikopo ili wajiajiri
7. Kuimarisha maadhili katika familia, shule, kazini, kanisani n.k.
8. Tume zilizopo za kukabiliana na ufisadi ziimarishwe.
9. Kuinua hali ya maisha ya wananchi kwa kuimarisha sekta mbalimbali k.v. kilimo
10. Serikali kuzuia uingizaji/wa bidhaa ghushi/duni.
11. Kuepuka mapendeleo/ubaguzi katika utoaji wa huduma kwa wananchi k.v. zabuni
12. Kuimarisha elimu.
13. Uwazi katika matumizi ya mali ya umma.
14. Kuwachagua na kuwateua viongozi wenye maadili.
15. Matumizi ya tecnolojia k.m kuweka kutumia kamera za siri katika ofisi za umma ili kuwanasa wahalifu.
16. Kuwatabua na kuwatuza wafanyakazi wenye bidii na waaminifu na kuwaabusha wale fisadi.
17. Kuripoti visa vya ufisadi
18. Kuimarisha uzalendo miongoni mwa wananchi.
SWALI LA 2.
Changamoto – mambo yasababishayo ugumu Fulani katika maisha, matatizo, vikwazi baadhi hayo:-
- Ukosefu wa ajira.
- Uigaji wa tamaduni potovu za kigeni.
- Daw za kulevya
- Magonjwa k.v. ya zinaa/ukimwi
- Umasikini
- Kukosa elimu/masomo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Ujana (ushabashi)
- Athali za Utandawazi au teknolojia
- Shinikizo la hirimu/imarika.
- Kuibuka kwa kugha ya vijana k.v. sheng’ na misimu.
- Malezi – ikosefu wa shauri au kuelekezwa.
Mapendekezo
- Serikali ibuni nafasi nyingi za kazi.
- Mashirika ya kutoa mikopo kupunguza riba ili vijana waiombe mikopo
- Serikali iongoze misaada ua kifedha kwa watoto kutoka familia/jamaa maskini ili waendelee
masomoni.
- Mafunzo kuhusumagojwa ya zinaa/ukimwi na njia za kuyakabili yawe sehemu ya mafunzo shuleni.
- Ushauri kabambe kutolewa kuhusu athari za dawa za kulevya.
- Makao ya mayatima kuanzishwa.
- Kuwaomba wazazi wawajibike katika malezi.
- Kudhamini elimu ya wasiojiweza.
Tanbihi : mwanafunzi anaweza kuonyesha changamoto na pendekezo katika aya moja au ashughulikie
changamoto kwanza kisha ma[endekezo baadaye.
Hoja zozote 8 zitakuwa mwafaka.
SWALI LA 3
Mwanafunzi asimulie kisa kinachofikiana na methali hii.
Mkakasi ni chombo mfano wa mkebe ambacho ndani ni mti lakini juu kimetiwa urembo na nakshi za
kupendeza
Maana
Mkakasi unapendeza lakini ukiuangalia ndani ni mti tu. Baadhi ya vitu hupendeza kwa nje lakini havina
thamani sana.
Matumizi
Tunashauriwa hapa kuwa ni lazima tuvichunguze vitu undani wake bali tusivitazame kwa nje tu.
Methali yenye maana sawa ni vyote vingaavyo si dhahabu.
Muktadha wa kisa/usimulizi utahusisha unafiki shuleni, kazini, katika familia, viongozi serekalini, kanisani
n.k
SWALI LA 4.
Mwanafunzi asimulie kisa kuhusu mtu ambaye hawajaonana
Matukio yaonyeshe mseto wa hisia labda kutokana na tendo zuri au baya lililofanywa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
LAIKIPIA JOINT EXAMINATION
MATUMIZI YA LUGHA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
KIDATO CHA NNE
a) i) /d/ - Kizuio ghuna cha masine 1
2
ii) /ch/ - Kituo kwaruzo ni kimoh. Hutamkiwa kaakaa gumu 1
2
b) /shw/ - Ni sauti mwambatano/ vichangamano ya kaakaa gumu 2x1
2 =al.1
c) silabi changamano ni silabi inayojengwa na konsonanti mbili au zaidi pamoja na irabu hivi kwamba kila
konsonanti inasikika kimatamshi. Mba- li mbwe – ha Twe – nde
d) i) Nafasi katika mzizi
viambishi awali, tamati
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii) Majukumu ya viambishi – kuonyesha nafsi, mzizi, nyakati
e) i) Mofimu za kimsamiati 2x1
2 = al.1
ii) Mofimu mwanana
ii) Mofimu ni kipashio kidogo zaidi cha lugha chenye kuwasilisha maana.
Hujitokeza kama neno zima au sehemu ya neno
Haiwezi kuvunjwa au kugawika zaidi bila kupoteza maana yake
2x1 = al.2
f) Pahali hapa panavutia – ni mahali maalum/dhahiri na panapodhihirika al.1
ii) Mahali huku kunavutia – Ni mahali pasipo dhihirika al.1
g) i) Injika – injua 1
2
Kinyume cha kutendua/ kufanyua 1
2
ii) Anza – maliza – kinyume huru al.1
h) Kutembea kikasuku kunavutia al.1
i) Asingalisoma kwa bidii asingalipita mtihani
Hangalisoma kwa bidii hangalipita mtihani 2x1 = al.2
j) Walimu huwashauri wanafunzi mara tano/kumi al.1
k) Angali akiimba akipika 4x1
2 = al.2
vitenzi sambamba
angali – Kitenzi kisaidizi
akiimba – kitenzi halisi
Akipika – kitenzi halisi
l) Yule ambaye hujitahidi sana hufaulu lakini asiyefanya bidii hujilaumu
S S1(KN(W+S) + KT(T) +U+S2 (KN(O+S) +KT(T)
9X1
3 = al.3
M) – Naviekomba- yambwa tendewa (shamirisho kitondo)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- chakula kitamu- yambwa tendwa (shamirisho kipozi)
- moto wa makaa – yambwa ala/ tumizi
- jumamosi ile – chagizo
n) Sentenzi ionyeshe tunda kama
i) Chuma
ii) zao linaloliwa na huhifadhi mbegu
al.2
p) nasi – kufupisha tunashindana
wakati mnyambuliko
ana – umilikaji
4x1
2 = al.2
q) Kondoo yule mweusi sana (RN)
(N+RV)
Yule mweusi sana (RV)
(W+RV)
Alikatalia katikati ya barabara (RT)
T+RH)
Katikati ya barabara (RH)
H+N)
8x1
2 =al.4
r) Sentensi ionyeshe kumbukumbu mfano kumb: 1/2009
- maneno yenye maana sawa sahibu/rafiki
- maana ya au, mfano baba/mama
- ionyeshe tarehe mfano,12/01/2019
Hoja zozote mbili x1 = al.2
s) Mtoto alimwita mama mara mbili na kumwarifu kuwa angeenda kuwaangalia siku ambayo ingefuata
4x1
2= al.2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
t) Mwanafunzi alipita mtihani (kwa sababu,
i) Kwa kuwa kwa vile, maadamu, alisoma kwa bidii.
- mwanafunzi alisoma kwa bidii
Basi – akapita mtihani
Yoyote 1x1= al.1
ii) Maji yaliyojaa humwagika.
Maji yakijaa humwagika
Maji yajaayo humwagika
Maji yajaayo ndiyo humwagika Yoyote 1x1 = al.1
ISIMU JAMII
a) Taja sajili iliyotumika hapa al.1
Sajili ya matangazo ya biashara
b) Taja sifa nne za sajili hii zinazojitokeza katika dondoo al.2
Maelezo na mifano iwepo (lazima)
• Huja porojo nyingi
• Lugha huwa nyepesi
• Lugha haizingatii kanuni za lugha
• Lugha ya kupiga chaka ili kushawishi wasikilizaji
• kuchanganya na kubadili msimbo
• mbinu ya picha na muziki hutumika ili kuzidisha mvuto kwa wasikilizaji
• lugha shawishe hutumika
• lugha ya mkato hutumika
Hoja zozote 2x1 = al.2
c) Kwa nini Wakenya wengi hupenda kuchanganya na kubadili msimbo al.3
• Kuonyesha umahiri wa lugha zozote mbili au zaidi mtu azijuazo
• Kuonyesha hisia tofauti k.m chuki, huzuni, furaha n.k
• Kufidia upungufu wa msamiati au lugha anayotumia kukosa msamiati
• Ili kujitambulisha na kundi linalotumia lugha Fulani
• Kujimasibisha na hadhi ya lugha Fulani iwapo katika jamii lugha moja ina hadhi kuliko nyingine
• Kutokana na ari ya kutaka kueleweka zaidi/ kufafanua
• Kuficha siri ili isijulikane
• Kuonyesha kuwa mtu ameelimika
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Kwa sababu ya kupungukiwa na msamiati
1x3= al.3
d) Eleza mambo manne yanayosababisha kuwepo kwa sajili za lugha
i) uhusiano wa wazungumzaji k.v mwajiri na mwajiriwa
ii) mahali walipo wazungumzaji/mazingira anamozungumzia
iii) Lengo/nia/kusudi la mazungumzo ya wahusika
iv) Kiwango cha lugha anazozifahamu mtu
v) Mada inayozungumziwa – Rasmi au kawaida
vi) Hadh/vyeo vya wahusika
vii) Kazi za wahusika/ shughuli mtu anzaofanya
viii) jinsia – wanawake ni tofauti na wanawaume
ix) umri wa mtu anayezungumza – motto au mtu mzima
x) Hali ya mti – mlevi, mgonjwa
Hoja zozote 4x1= al.4
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
LAIKIPIA JOINT EXAMINATION
KISWAHILI
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
KARATASI YA 3
KIDATO CHA NNE
SEHEMU A. TAMTHILIA KIGOGO (PAULINE KEA)
a) - Ni maneno ya Majoka
Anamwambia chopi uk 70
Walikuwa katika hoteli ya Majoka Resort
Ni baada ya kupata habari za kifo cha ngurumo
b) Anayeambiwa ni Chopi
i) Ni katili - Anampiga Ashua akiwa korokoroni
ii) Ni mpyoro - Anamtusi Sudi
iii) Ni kibaraka - Anaendeleza uovu wa Majoka
c) i) Askari wanawaua vijana watano walioandamana wakitetea kupanda kwa gharama ya chakula kwenye
kioski.
ii) Wafanyakazi wa baraza wana kodi na kitu juu yake ili kujinufaisha.
iii) Majoka anaanzisha biashara ya ukataji miti na kusababisha ukame.
iv) Majoka anatumia wahuni kumlemaza tunu ili kudunisha uogozi.
v) Majoka anapanga mauaji ya jabali ili kuzima upinzani.
vi) Majoka ananyakua ardhi ya soko na kusababisha kuhangaika kwa wafanyabiashara.
vii) Majoka anamlazimisha Ashua kushiriki mapenzi naye ofisini ili kusima ashiki zake.
viii) mamamapima anawauzia vijana pombe haramu inayosababisha vifo ili kujinufaisha.
ix) Mama pima anawapanja walevi ili kupata faidi isiyostahilli.
x) Majoka anakosa kusafisha soko na kusababisha mkunipuko wa magonjwa shali watu walilipa kodi.
SEHEMU YA B. RIWAYA CHOZI LA HERI (ASSUMPTA K. MATEI)
- Ni mawazo ya Ridhaa/uzungumzi nafsia wa Ridhaa
- anamrejelea mwangeka mwanawe
- Wako katika ganjo la makaazi ta Ridhea.
- Ridhaa alimhurumia mwanawe baada ya kupoteza aila yake, nyanvula na Becky katika mkasa wa
moto.
b) Nahau - Kabla ya ubwaba na shingo kutoka (kabla ya kukomaa)
c) Umuhimu wa Ridhaa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Ni kielelezo cha wazazi wenye mlahaka mwema na wanao - alicheza na mwangeka kama daktati na
mgonjwa
iii) Ni kielelizo cha wasomi - Alihitimu na shahada ya uzamili katika upasugi.
iii) Anawakilisha matajiri wanaojari maskini - akuanzisha kituo cha Mwanzo Mpya ili kutoa
huduma bora za afya kwa nsify wa hen.
iv) Anaonyesha kuwa hata matajiri wanaathimika kuwa matajiri vita vya kisiasa.
v) kielelezo cha watu wenye uvumihiri mkubwa hata baada ya kuathirika.
d) Changamoto walizopitia watoto/vijana
i) Lime na mwanaheri walibakiwa na mabarobaro watano katika ghasia za kisiasa
ii) Becky na Tila waliangamia kwa kuteketezwa nyumbani katika ghasia za kisiasa.
iii) Watoto wa wakimbizi walijificha walipona lori la msaada kwa kuwa hawakuwa na mavazi.
iv) Watotoa wa wakimbizi walipotesa maisha kwa kubakurwa na magarimoshi walikwenda haja katikati ya
reli uk 28
v) Dick alifanyishwa biashara haramu ya ulanguzi wa dawa za kulevya na Mzee Buda,
vi) Lemi alipigwa kitutu na kuuawa na raia kwa kusingiziwa wizi.
vii) Hazina na wengine walirandaranda mitaani kwa sababu ya ukosefu wa makaazi.
viii) Pete alioziwa kwa lazima kwa mzee Fungo na kuacha masomo katika darasa la saba.
ix) Pete alitumia tambara la blanketi wakati wa ledhi ya kwanza kwa kukosa sodo.
x) Chandachema alilazimika kufanya kazi katika shamba la michai ili kujikimu/ajira ya watoto.
xi) Zahali alishika mimba katika kidato cha pili na kutelekezwa na wazazi wake.
xii) Dick na mwaliko walitekwa nyara na Sauna na kupelekwa kwa Bi. Kangara.
xiii) Riziki Immaculate alitupwa katika biwi la taka na mzazi wake baada ya kuzaliwa.
xiv) Tuama alikeketwa akiwa mwanafunzi na kuathirika kasha kulazwa hospitalini.
3. MWONGO WA KUSAHIHISHA. CHOZI LA HERI.
Anwani ya Riwaya hii ni Chozi la heri. Kwa mujibu wa kamusi ya 21, CHOZI ni tone la maji au uowevu
linalotoka machoni ambalo aghalabu hutokea mtu anapolia, kufurahi au moshi unapoingia machoni. Nalo
jina HERI lina maana tatu :
1. Ni kuwepo kwa amani, utulivu na usalama
2. Ni hali ya kupata Baraka na mafanikio
3. Ni afadhali
Maneno haya yanapotumika pamoja tunapata maana iliyo na undani zaidi kuliko jina likitumika peke yake.
Kwa hivyo, chozi la heri ni chozi ambalo linatoka wakati mhusika fulani amepata amani, utulivu na
usalama. Chozi kwisha kupata baraka na mafanikio. Maana nyingine ni kuwa chozi hili linaonekana ni
chozi (la) afadhali bora nafuu.
Kwa kujikita katika maana mbalimbali yanayojitokeza wakati hayo mawili yamewekwa pamoja matukio
yafuatayo yanaafiki ufaafu wa CHOZI LA HERI.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Mwandishi anatuleza kuwa Ridhaa alipokwenda shuleni siku ya kwanza alitengwa na wenzake kwani
hawakutaka ashiriki michezi yao. Kijana mmoja mchokozi alimwita mvua ‘ aliyekuja kuwadhinda katika
mitihani yote. Ridhaa alifululiza nyumbani na kujitupa mchangani na kulia kwa kite na shake. Mamake
alimliwaza na kumhakikishia kumwona mwalimu keshoye. Tangu siku hii, huu ukawa ndio mwanzo wa
maisha ya heri kwa Ridhaa kwani baada ya mwalimu kuzungumza na wanafunzi umuhimu wa kuishi
pamoja kwa mshikamano. Ridhaa alipea kwenye anga ya elimu hadi kufikia kilele cha elimu na kuhitimu
kama daktari.
ii) Ridhaa alipotoka kwenye Msitu wa mamba alijiona nafuu kwani wapwa zake – Lime na Mwanaheri
walikuwa wamepata matibabu. Dadake Subira alitibiwa akapona. Mwamu wake Kaizari amepona donda
lililosababishwa na kuwatazama mabinti zake wakitendewa ukaini (Kubakwa) na Vijana wenzao. Ridhaa
anajua kuwa Kaizari ni afadhali kwa sababu hakuna aliyemtenga na mmoja kati ya jamaa zake. Ridhaa
anapomfikiria Kaizari anajiambia heri nusu shari kuliko Shari kamili.
iii) Ridhaa aliposikia sauti ya kike ikitangaza, tangazo lile lilimrudisha katika mandhari yake ya sasa.
Alijaribu kuangaza macho yake aone anakoenda lakini macho yalijaa uzito wa machozi ambayo alikuwa
ameyaacha yamchome na kutiririka yatakavyo.
iv) Wakati Ridhaa alimkazia macho Mwangeka-waka Mwange alikuwa akijiuliza iwapo babake amekuwa
mweh kwa kukosa kushirikiana na majirani kuchimba kaburi kuyazika majivu-matone mazito ya machozi
yalitunga machoni mwake Mwangeka. Akayaacha yamdondoke na kumcharaza yataj=kayo. Uvuguvugu
uliotokana na mwanguko wa macho : haya uliulainisha moyo wake, ukampa amani kidogo. Moyo wake
ukajaa utulivu sasa kwa kujua kuwa wino wa Mungu haufutiki.
v) Wakati Ridhaa alikuwa akimsimulia Mwangeka misiba iliyomwandama tangu siku alipoondoka kwenda
kuweka amani Mashariki ya Kati. Ridhaa alisita akajipagusa kijasho kilichokuwa kimetunga kipajini
mwake kisha akatoa kitambaa mfukoni na kuyafuta machozi yaliyokuwa yameanza kumpofusha. Uk 48.
vi) Mwangeka alipokuwa ameketi mkabala na kidimbwi cha kuogelea, mawazo yake yalikuwa kule mbali
alikoanzia Akawa anakumbuka changamoto za ukauji wake. Akawa kumbuka wanuna wake.
Alipomkumbuka Annatila(TILA) mwili ulimzizima kidogo akatabasamu kisha tome moto la chozi :
likamdondoka.
vii) Katika Msitu Wa Simba kulikuwa na maelfu watu waliogura makwao. Kati ya familia zilisoguria
humu ni familia ya Bwana Kangata. Kwa Kangata na mkewe Ndarine, hapa palikuwa afadhali kwani
hawakuwa na pa kwenda kwa kuwa hata kule walikokuwa wakiishi awali hakukuwa kwao. Uk 57.
viii) Wakati Dick walikueana kisadfa na Umu uwanja wa ndege, walikumbatiana kwa furaha. Machozi
yaliwadondoka wote wawili na wakawa wanalia kimyakimya. Walijua fika kuwa jaala ilikuwa
imewakutanisha na kwamba hawatawahi kutengana tena. Maisha sasa yalianza kuwa ya heri kwao.
ix) Baada ya miaka kumi ya kuuza dawa za kulevya. Dick alifaulu kujinasua kutoka kwa kucha za mwajiri
wake. Alianza biashara yake mwenyewe ya kuuza vifaa wa umeme. Sasa akaanza kujitegemea kwa kuwa
amejiajiri. Alikuwa ameufungua ukurasa mpya katika maisha yake. Maisha yake sasa ni ya heri.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
x) Wakari Neema na Mwangemi walikabidhiwa motto wao wa kupanga na Mtawa Annastacia, Mwaliko
alimkumbatia Neema na kumwita mama na kumwahidi kuwa ataenda naye. Neema alidondokwa na chozi
la furaha na kumkumbatia Mwaliko kwa mapenzi ya mama mzazi. Hili lilikuwa ni chozi la heri kwa
Neema.
xi) Dick almwaleza Umu kuwa siku waliokutana katika uwanja wa ndege na wakasafiri pamoja, hiyo ndiyo
ilikuwa siku ya here Zaidi kwake. Nasaha alizopewa na Ume zilimfunza thamani ya maisha. Kisadfa, huu
ndio wakati Dick alikuwa ameamua kubadilisha maisha na kuishi maisha mapya yasiyokuwa ya kuvuja
sheria.
xii) Dick aliposi,ulia namna wazazi wake wapya pamoja na Umu walivyomfaa maishani, kila mmoja katika
familia hii alilia. Bila shaka yalikuwa machozi ya heri.
xiii) Baada ya Mwaliko kujitambulisha kwa Umu na Dick, Umu na Dick hawakungojea amaliza.
Walikimbia wote wakamkumbatia ndugu yao, wakaanza kulia wakiliwazana. Haya yalikuwa machozi ya
furaha kwao kwa kupatana tena wote wakiwa hai. Kwa kweli kila mmoja alitokwa na chozi la heri.
xiv) Mwaliko alimwambia babake kuwa kuja katika hoteli ya Majaliwa kuliwaletea heri kwa kuwa familia
yao sasa imepanuka. Sasa amekutana na watu aliokuwa tu anasikia wakitajwa. Maisha sasa ni afadhali.
xv) Dick alitoa shukrani tele kwa Umu kwa kuwa alimpa matumaini kuwa siku moja watampata ndugu yao
Mwaliko. Mwaliko hata anapomtazama Ume, macho yake yakiwa yamefunikwa na vidimbwi vya machozi,
anajua kuwa familia yao imerudiana h=japo katika mazingira tofauti.
xvi) Siku ambayo Mwangeka alimwoa Apondi ilikuwa siku ya heri kwake kwani alimwaga chox la heri.
Tunaelezwa kuwa, Ridhaa alijua kuwa wakati ndio mwamuzi, ipo siku atapotokeza hurulaini wake
Mwangeka. Ataifungua kufuli kubwa iliyoufunga moyo wake na hiyo itakuwa siku ya kumwaga chozi la
heri.
MWONGOZO (TUMBO LISILOSHIBA)
5. a) i) Mzungumzaji ni Penina
ii) Anamzungumzia Dennis Machora (Msimulizi)
iii) Wako nyumbani kwao (Machora na Penina) katika mtaa wa Newzealand
iv) Dennis alikuwa amerudi nyumbani kutoka kampuni ya kuchapisha magazeti alikoenda kutafuta kazi
lakini akaambulia patupu.
B) i) Methali - Mgomba changaraweni haupandwi ukames,
ii) Swali la balagha - Penzi lenu na nani ?
iii) Nidaa - Mtaka wee !
iv) Msemo - Potela mbali.
C. MAUDHUI YA UTABAKA.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Wazazi wa Dennis walijitahidi kumsomesha kwa kuwalimia matajiri mashamba.
ii) Wazazi wa Penina kwa kuwa alitoka tabaka la chini ilhali wao walikuwa matajiri
iii) Dennis anakynywa uji kama chamcha kwa kukosa chaula ilhali Penina hupokea Shilingi elfu tano kila
wiki.
iv) Penina anapangiwa nyumba katika mtaa wa New Zealand wanakoishi watu wenye mapato ya kadri.
v) Dennis hangejiunga na shule aliyoalikwa kwa umaskini ilhali wenzake walisomea shule za hadhi kubwa.
vi) Penina anamkataa Dennis kwa kuwa hana uwezo wa kifedha kwa kukosa kazi na hangeweza kudumisha
maisha yake ya kifahari.
vii) Wazazi wa Dennis walimtegemea asome ili kuwatoa umaskinini ilihali wazazi wa Penina wanamkimu
hata baada ya kumaliza masomo.
D) SIFA ZA MZUNGUMZAJI
1. Msaliti - alimsaliti mchumba wake Dennis kwa kumfukuza na kumwaibisha sababu ya
umaskini
2. Mwenye dharau - anamfokea Denis kwa dharau
3. Mwenye tama - ana tama ya mapenzi na akatafuta mchumba kwa bidii
4. Mwenye bidii masomoni - Alikuwa mwanafunzi wa chuo kikuu kivukoni
5. Ni jasiri - Alimwendea Dennis kutafuta mapenzi na uchumba na mambo yanapokwenda kombo
alimfukuza bila woga.
6. Mpyaro - Anamtusi Dennis akimwita mkata.
6. A) TAMATHALI
i) Tashbihi - Kama vile tatia saini….
ii) Msemo - Kujitia kitanzi
Kutaja - 1
Fafanua - 1
b) Vipengele vya sheria
1. Lazima angeendelea kufanya kazi ya umetroni
2. Lazima kazi ya upishi walifaa kuifanya wote wawili.
3. Lazima wangepata motto mmoja pekee
4. Lazima Dadi angetakiwa kunadhisisha nyumba na kufua nguo.
5. Lazima angekuwa na uhuru wa kuvalia kisasa.
6. Lazima angekuwa na uhuru wa kutangmana na wanaume wengine.
C) i) Alimshuku mkewe kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume wengine.
ii) Alijisihi mtumwa katika ndoa yake
iii) Alikejeliwa na kusimangwa na majirani
iv) Alianguka na kuumia vibaya alipoenda kumchunguza mkewe kwa kukisia alikuwa na uhusiano na
mwalimu mkuu.
v) Alitawaliwa na chuki dhidi ya mkewe
vi) Alikoa raha hata kushindwa kukila chakula alichoandaliwa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
vii) Hakuwa na muda wa kupumzika.
SEHEMU YA E. FASIHI SIMULIZI
7. A) Kitendawili huwa na kitangulizi maalum aihali methali lazima.
- Kitendawili huwa na fumbo la methali halifumbuliwi papo hapo.
- Vitendawili huwa maarufu miongoni mwa hadhira changa ilihali methali hutumiwa zaidi na wazee.
- Vitendawili huwa na hadhira tende lakini methali si lazima methali ziwe na hadhira tendi.
- Vitendawili hutolewa kwenye vikao maalum ilihali methali si lazima zitolewe kwenye vikao
maalum.
- Vitendawili huwasilishwa kwa majibizano ya fanari na hadhira yake athali methali huhusu kauli
moja tu ya msemaji.
B) - Ni kitambulisho cha kundi Fulani cha watu
- Hutumiwa kulifadhi siri za wanasitumia.
- Hutumiwa kuibua hisia mbalimbali (uchangamfu)
- Huunganisha watu wanaoitumia kim wanafunzi, vijana
- Huongeza kadha katika lugha.
- Hutumiwa kitafsidi lugha.
- Huhifadhi mile na desturi za jamii (huonyesha historian a ukueji wa lugha ya jamii)
- Hujichua migawanyiko ya kijamii.
- Huenda urasmi katika utumiaji wa lugha.
- Huhuza uwezo wa mtu wa kudadidi mambo.
C) - Ujumbe huweza kueleweka vibaya.
- Ujumbe unaweza kukosa kusikika mbali.
- Si watu wote ambao wanaweza kuufasiri ujumbe.
- Huenda sauti za ngoma na ala nyingine zikachafua ujumbe
- Si watu wote wanaweza kufahamu midundo yote na kupata maana yake moja kwa moja.
- Huenda sauti za ngoma zikaathiriwa na hali ya anga, k.v. muvua.
d) i) Ni sherehe za kitamaduni ambazo hufanyiwa na jamii katika kipindi Fulani maalum.
ii) - Huandamana na matendo na kanuni Fulani k.v. ulaji kiapo.
- Huongezwa na watu mahususi katika jamii.
- Huandamana na utoaji wa mawaidha.
- Hufanyiwa mahali mahususi k.v. porini
- Huambatana na utamaduni wa jamii husika k.m uimbaji, ngoma.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
USHAIRI
1. USHAIRI
i) Shairi la A Shairi la B
Elimu ni muhimu Kero moyoni
ii) Shairi la A Shairi la B
- Ni tathlitha/utatu/ukana - Ni shairi huru
iii) - Lina beti nne
- idadi ya mishororo inafautaina kila ubeti
- halina urari wa vina
- halina kibwagizo
- halina migao/vipande
iv) i) Tashihisi/uhaishaji
ii) Istiana (chini ya paa la umma) – yaani starehe alizo nazo mwenye mali zinatokana na jasho la
wahitaji
v) Shairi la A
Maudhui yake ni umuhimu wa elimu
Shairi la B
i) Sulubu hawaheshimiwi
ii) Dhuluma dhidi ya wafanyakazi za sulubu kama wanapuuzwa hawaheshimiwi
vi) – Ubeti wa mwisho shairi A lugha natahri
- Elimu isiyo na vitendo ni sawa na mti ambao hauna majani. Haumpumzishi yeyote
- Anayekaa chini ya kivuli chake. Udanganyifu kwa watu ni taabu tupu
vii) i) Mazda – Majiani – Njiani
Maangani – angani
MACHAKOS JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI KIDATO CHA NNE
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.)
102/1 - KISWAHILI - Paper 1
KARATASI YA 1 - INSHA
JULAI 2019 – MUDA SAA 1 ¾
Jina:............................................................................ Nambari ya usajili: ...................................
Sahihi ya Mtahiniwa ................................................ Tarehe .......................................................
MAAGIZO
(a) Andika insha mbili, insha ya kwanza ni lazima
(b) Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo zilizobakia tatu.
(c) Kila insha isipungue maneno 400
(d) Kila insha ina alama 20
(e) Kila insha LAZIMA iandikwe kwa lugha ya Kiswahili
(f) Karatasi hii ina kurasa mbili zilizopigwa chapa.
(g) Watahiniwa ni lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa sawasawa
na kuwa maswali yote yamo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
LAZIMA
1. Suala la kuzorota kwa usalama nchini kenya limekuwa donda ndugu. Andika mahojiano kati ya
waziri wa usalama wa kitaifa na mwandishi wa habari kuhusu chanzo na mbinu za kukabiliana na
janga hili
2. Ufisadi ndicho kikwazo kikuu cha maendeleo hapa nchini.eleza
3. Andika kisa kinachodhibitisha ukweli wa methali.
Jifya moja haliijiki chungu
4. Andika insha itakayomalizikia kwa maneno; …nilitamani ardhi ipasuke nitumbukie huko
nisionekane.
MACHAKOS JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI KIDATO CHA NNE
Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.)
102/2 - KISWAHILI - Karatasi ya 2
Ufahamu, ufupisho, Sarufi na matumizi ya lugha na Isimu jamii
JULAI 2019 – MUDA SAA 2 ½
Jina:............................................................................ Nambari ya usajili: ...................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Sahihi ya Mtahiniwa ................................................ Tarehe .......................................................
MAAGIZO
• Andika jina na nambari yako kwenye nafasi ulizoachiwa hapo juu.
• Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani.
• Jibu maswali yote.
• Andika majibu yako katika nafasi ulizoachiwa katika kijitabu hiki cha maswali.
• Majibu yako yaandikwe kwa lugha ya kiswahili
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE
SWALI ALAMA TUZO
1 15
2 15
3 40
4 10
JUMLA 80
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU YA A: UFAHAMU (alama 15)
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali
“Swala la idadi kubwa ya watoto wadogo wanaoendelea kumiminika mijini na kuonekana
wakiranaranda mijini ovyo,halijapewa umuhimu wowote wa haja na serikali za nchi nyingi,licha ya
mijadala katika warsha anuwai,zilizofanyika kujadili swala hili nyeti.
Kwa kutokuwa na sheria ama sera iliyo wazi kuhusu haki na usalama wa watoto,sarikali zetu hazina budi
kukubali kubeba uzito wote wa lawama. Hii ni kwa sababu, serikali zetu zimelipuuza na kuvalia miwani
swala hili kwa kuchukulia kuwa litapotea lenyewe katika hewa yabisi. Yafaa ifahamike kuwa usalama wetu
katika siku zijazo utategemea jinsi tutakavyolikabili ana kwa ana tatizo hili wakati huu. Wakati wa kutenda
ni sasa. Aidha, watoto hawa wanaokulia mitaani bila malezi,maelekezo wala mwongozo mwafaka wa
kimaisha, wanakua bila mapenzi hivyo hawajui maana ya kupenda. Wanachokijua ni chuki na haja ya
kulipiza kisasi dhidhi ya jamii iliyowachonga jinsi walivyo. Hawajali lolote hata kifo. Wako tayari
kujikabidhi kwa haini yeyote mwenye nia mbaya,bila kujali matokeo, muradi tu, wapate riziki.
Tunapendekeza kwa serikali, washirika dau kama vile mashirika ya kujitolea, viongozi wa dini, shule,
vyuo na wananchi kwa jumla wachange bia katika kutafuta mikakati ya kulitatua tatizo hili kabla
halijageuka kuwa janga la kijamii ambalo tutashindwa kulimudu. Mpango wa vijana hawa kujiunga na
huduma ya taifa ni jambo linalofaa kutiliwa maanani.
Tunapendekeza makao Zaidi ya watoto wanaozurura mijini yajengwe ambapo watapata mafunzo ya
kiufundi yatakayowawezesha kujitegemea maishani. Badala ya kulitegea mgongo swala hili, serikali
zinawajibika kuwasajili hawa watoto ili waweze kuunganishwa na familia na koo zao. Utafiti uliofanywa
na wataalamu wa Elimu jamii umebainisha kuwa ni asilimia kumi tu ya watoto hawa wa mitaani wasiokuwa
na mahali wawezapo kupaita nyumbani. Asilimia tisini iliyobaki, angalau wana mahali wanapoweza
kupaita nyumbani ilhali wanaendelea kuwa mitaani. Wazazi tumesahau wajibu wetu. Wengi wetu
tumelikimbia jukumu la ulezi tulilopewa na muumba. Hawa waliojipaka masizi mwilin mzima,
wanaozurura ovyo mitaani, si matokeo ya maumbile;hawakuja duniani kwa sadfa, hawakuulizwa wala
kushauriwa. Makosa ni yetu wazazi. Tuliwaleta hapa duniani, kisha tukawakimbia.Hatutasamehewa
duniani na akhera.
Mwenye njaa hana miiko. Ili kijiruzuku, hawa watoto daima wanachumia jaani.Kwa kudura ya jalia, huenda
siku moja watalia kivulini. Asiyekuwa na wake ana mungu.Aghalabu, watoto wanaozurura mitaani hupewa
pesa na wafadhili. Wakati mwingine wanaiba. Maisha haya ya kuomba au kuiba wanaona yanaridhisha
Zaidi kuliko kumenyeka na kazi ya kibarua kutwa kucha. Kwa bahati mbaya, watoto hawa wamatumia pesa
wanazopata kutoka kwa wafadhili kujichimbia kaburi. Aidha pesa wanazopatiwa watoto hawa wanazitumia
kununulia gundi badala ya chakula.
Wafadhili wanashauriwa wawape chakula hawa watoto badala ya pesa taslimu. Kusema kweli, unapompa
mtoto wa mitaani pesa,utakuwa unainua biashara ya mwenye kiwanda cha gundi,jambo ambalo litakuwa
sawa na kuweka sahihi mkataba wa kifo cha mtoto mwenyewe.
Wataalamu wa afya wanaonya kuwa gundi ikivutwa kwa muda mrefu inaweza kusababisha upofu
au kifo.Wataalamu hawa wanazidi kutuarifu kuwa matumizi ya muda mrefu ya gundi huathiri ubongo,figo
na maini. Mtumiaji pia anaweza kupoteza uwezo wa kutembea na hata kupooza kabisa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Sababu wanazotoa hawa watoto ni kwamba, uvutaji gundi,huwaondolea njaa,baridi ya usiku na
kuwatuliza mawazo. Ni jambo la kusikitisha kwamba tunaendelea kushuhudia bila kujali hawa watoto
ambao ni kiungo cha jamii yetu,wakijiangamiza. Wananchi kwa ujumla hawaha budi kuhamasishwa dhidhi
ya athari ya matumizi ya gundi.Wafanya biashara wanaowauzia watoto hawa gundi yafaa wakome,la sivyo
wachukuliwe hatua.Kutolitatua tatizo hili la watoto wa mitaani hivi sasa,kutapeleka kuwako kwa kizazi cha
mitaani ambacho kitazaliwa mitaani,kulelewa mitaani,kuoa mitaani na kufia mitaani.Kadiri mataifa
yanavyoendelea kujitia hamnazo kuhusiana na swala hili,ndivyo tunavyokubalia jinai itawale,sasa na wakati
ujao.
Hawa watoto watakapokua,watageuka kuwa wapigaji watu kabari,majambazi,wezi wa kutumia nguvu
ama watatumiwa na mahaini kutimiza uhaini wao.Hawa watoto wenye njaa,watalazimika hatimaye,kuwatoa
wenywe shibe tonge mdomoni.Matokeo ya hali hii ni kwamba katika siku zijazo,hawa ndio watu
watakaotunyima starehe ya kulala unono.Watatuchafya mitaani,majumbani,vijijini na kutuvizia
mabarabarani.Tuna sababu nzuri ya kutiwa hofu na tatizo hili,kwani jinsi kizazi kinavyozidi
kupanuka,inaonekana tumelitega bomu ambalo litakuja kutulipukia usoni mwetu.”
Maswali
(a) Taja jambo moja linalochangia kuweko kwa watoto wanaorandaranda mitaani. (alama 1)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………
(b) Maisha ya mitaani huathirije watoto? ( alama 3)
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………
(c) Tatizo la watoto wanaorandaranda mitaani laweza kutatuliwaje? (alama 3)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………
(d) Eleza maana ya: (alama 2)
i. Hawa watoto wanachumia jaani
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
ii. Jinsi kizazi cha mitaani kinavyozidi kupanuka,inaonekana tumelitega bomu ambalo litakuja
kutulipukia usoni mwetu. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
…………………………..…………………………………………………………………………
………………………………………………………..….………………………………………
……………………………………………………………………………………
iii. Mwenye njaa hana miiko. (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………….........
(e) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika kwenye taaria: (alama 2)
i. Aidha:
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………
ii. Gundi:
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. UFUPISHO
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata.
Kadiri jamii mbalimbali zinavyotagusana, ndivyo lugha zinazozungumzwa na jamii hizi nazo
zinavyoingiliana na kuathiriana. Mojawapo ya athari hizi ni ukopaji wa msamiati. Jamii zinazopakana au
kutagusana hukopa msamiati kutoka kwa lugha jirani na kuutumia kuelezea dhana mpya zinazoingia katika
utamaduni wao kupitia kwa mitagusano ya kijamii.
Lugha ya Kiingereza, kwa mfano, imekopa kutoka lugha nyingine kama vile Kifaransa na Kilatini.
Mathalani, istilahi nyingi za kisheria zimekopwa kutoka lugha ya Kifaransa. Aidha, Kiingereza kimekopa
kutoka lugha ya Kiswahili. Maneno ya Kiswahili kama vile mwalimu, jiko, mandazi, panga, buibui, ngoma
na hata wananchi, sasa yameingia katika kamusi za Kiingereza, kumaanisha kuwa yamekubaliwa kama
msamiati rasmi wa lugha ya Kiingereza.
Kiswahili nacho kimeathiriwa na lugha nyingine. Kimekopa msamiati wa Kiingereza na hata Kiarabu.
Katika tungo nyingi za kishairi, kwa mfano, Utenzi wa Mwanakupona utapata msamiati wa Kiarabu
uliotoholewa. Lugha nyingine ambazo zimeathiri Kiswahili ni pamoja na Kijerumani ambako msamiati
kama vile ‘shule’ ulikopwa na kutoholewa kwa neno schule. Msamiati kama vile ‘leso’, ‘karata’ na
‘mvinyo’ yamekopwa kutoka lugha ya Kireno, huku majina ‘balozi’ na ‘bahasha’ yakikopwa kutoka
Kituruki.
Pamoja na ukopaji wa vipengele vya lugha, mtagusano wa lugha una athari nyingine. Lugha zinapokuja
pamoja, mazingira ya wingi-lugha huzuka. Baadhi ya watu hujifunza zaidi ya lugha moja. Mtu anayeweza
kuzungumza zaidi ya lugha moja anaweza kujieleza kwa urahisi kwa kuchanganya msamiati wa lugha
tofauti. Aidha, anaweza kubadilisha msimbo kulingana na matilaha yake. Ikiwa anataka kukubalika na
jamii-lugha anayotagusana nayo, atatumia lugha ya jamii hiyo ili kujinasibisha na kujitambulisha nayo.
Wazungumzaji hupata visawe vya maneno kuelezea dhana zile zile, hivyo kuboresha mitindo yao ya
mawasiliano.
Kadhalika, kutagusana kwa lugha kunaweza kusababisha kubuniwa kwa lugha ngeni ambayo inarahisisha
mawasiliano. Wakati mwingine, watu wanaozungumza lugha tofauti wanapokutana, hubuni mfumo sahili
wa lugha ili kufanikisha mawasiliano. Pijini ni mfano wa lugha iliyobuniwa kwa njia hii. Pijini huchota
msamiati kutoka lugha zilizotagusana. Sheng ni mfano mwingine wa lugha ambayo ilibuniwa kutokana na
kutagusana kwa lugha ya Kiswahili, lugha za kiasili na Kiingereza.
Japokuwa kuna faida nyingi za wingi-lugha, hasara pia zipo. Mazingira ya wingi-lugha huwapa
wazungumzaji fursa ya kuchagua lugha wanayotaka kuwasiliana kwayo. Katika hali hii, lugha yenye
ushawishi mkubwa kijamii, kiuchumi na kisiasa ndiyo inayopendelewa zaidi. Wingi-lugha unaweza
kusababisha kukwezwa kwa lugha moja na kudunishwa kwa lugha nyingine. Mathalani, kuwepo kwa lugha
nyingi nchini kulizua haja ya kukwezwa kwa lugha ya Kiswahili huku zingine za kiasili zikipuuzwa.
Lugha hukua kwa kutumiwa. Lugha isipozungumzwa kwa muda mrefu, watu hupoteza umilisi ambao
huifanya kuwa vigumu kuirithisha kwa vizazi. Lugha inaweza pia kukosa wazungumzaji ikiwa wale
wanaoizungumza ni wachache, au ikaathiriwa na mtagusano na lugha nyingine iliyo na wazungumzaji
wengi. Katika hali kama hii, lugha hiyo hukabiliwa na tisho la kudidimia au hata kufa. Ikiwa jamii itakosa
kudhibiti sera za matumizi ya lugha yake, baadhi ya lugha zitafifia au zitakufa na kusahaulika kabisa.
1. Bila kupoteza maana, fupisha aya za kwanza tatu. (Maneno 50-60)(Alama 10, 1 ya mtiririko)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Matayarisho
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………
Jibu
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………….
2. Kwa mujibu wa taarifa hii, mtagusano wa lugha una athari gani?maneno 20-30
(Alama 5, 1 ya mtiririko)
Matayarisho
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………….
Jibu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
SEHEMU YA C: MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
(a) Taja sifa tatu za kuainisha irabu (alama2)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………
(b) Ainisha viambishi katika neno lifuatalo: (alama2)
Alifiwa
…....................................................................................................................................................................
........................................................................................................................................................................
........................................................................................................................................................................
....................................................................................................................................
(c) Bainisha shamirisho katika sentensi ifuatayo: (alama 2)
Zainabu aliandikiwa barua na Zubeda
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………….
(d) Onyesha miundo mitatu ya kundi nomino (alama 3)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………………
……………………………....
(e) Andika maana mbili tofauti ya sentensi ifuatayo (alama 2)
Walipiganishwa na kakake
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………
(f) Tunga sentensi tatu tofauti kuonyesha matumizi matatus ya ngeli ya mahali (alama 3)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………....................................................................................................
........................................................................................................................................................................
................................................
(g) Ainisha vielezi namna katika sentensi ifuatayo; [alama 2]
Mlevi alianguka mchangani tifu kwa kutembea ovyo.
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
……………...
(h) Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli ulizopewa (alama 2)
a. LA [TENDESHA]
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
b.soma[tendeana]…………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya visanduku (alama 4)
Yule mzee ajengaye barabara ametuzwa.
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………
(j) Andika katika usemi wa taarifa. (alama 4)
“Karibu Bakari,tafadhali kaa,” Juma akasema. “Asante je,habari za nyumbani?”
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………
(k) Onyesha kishazi huru na kishazi tegemezi katika sentensi ifutayo. (alama 1)
Ukuta uliobomolewa ulisababisha hasara kubwa.
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………
(l) Unda nomino mbili kutokana na neno dhuru (alama 2)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………………
………………
(m)Andika kinyume cha: (alama1)
Walizama walipokuwa wakikusanya mchanga.
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………
(n) Tunga sentensi moja kutofautisha baina ya bure na pure (alama 2)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………
(o) Bainisha matumizi ya ku katika sentensi hii (alama 3)
Mkurugenzi hakukusaidia ulipoenda kula Mombasa anakofanya kazi.
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………
(p) Tunga sentensi katika wakati uliopita hali timilifu ( alama 2)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
(q) Bumba ni kwa nyuki…………………………..ni kwa samaki na…………………….ni kwa siafu.
(alama 2)
(r) Eleza maana ya ngeli (alama 1)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU YA D: ISIMU JAMII (alama 10)
Kwa kutumia sifa tano, linganua sajili ya mahakamani na sajili ya sokoni (alama 10)
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………
MACHAKOS JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI KIDATO CHA NNE
Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.)
102/3 - KISWAHILI - Paper 3
Karatasi ya Tatu
JULAI 2019 – MUDA MASAA 2 ½
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Jina:............................................................................ Nambari ya usajili: ...................................
Sahihi ya Mtahiniwa ................................................ Tarehe .......................................................
MAAGIZO
• Andika jina na nambari yako kwenye nafasi ulizoachiwa hapo juu.
• Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani.
• Jibu maswali yote.
• Andika majibu yako katika nafasi ulizoachiwa katika kijitabu hiki cha maswali.
• Majibu yako yaandikwe kwa lugha ya kiswahili
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. UFAHAMU
Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.
Bila shaka, umewahi kusikia kuwa afya ni taji. Hakuna ajuaye haya vyema kama anayeugua.
Wanaoelewa usemi huu huthamini na kudumisha siha yao kwa kila njia. Licha ya lishe bora, michezo ni
muhimu katika kudumisha afya njema. Mtu asiposhiriki katika michezo au unyoshaji wa viungo, mwili
hunyong’onyea na kunenepa. Mwili mnyonge ni windo rahisi la maradhi. Kushiriki katika michezo
hukuepusha na kutingwa na shughuli za maisha ya kileo. Shughuli hizi zisipodhibitiwa huweza kumdhuru
mtu kiafya.
Maradhi hatari ya moyo, akili na shinikizo la damu husababishwa na shughuli katika maisha yetu.
Hapa ndipo michezo inaingilia. Michezo huyeyusha mafuta mwilini na kutukinga dhidi ya maradhi
yanayosababishwa na unene wa kupindukia.
Kushiriki katika michezo vilevile hujenga ushirikiano na umoja. Michezo hutufundisha uwajibikaji.
Mathalani, mlindalango atalenga kulilinda lango na kuhakikisha kuwa hamna bao linaloingia langoni.
Washambulizi nao watalenga kushambulia lango la wapinzani huku waking’ang’ania kwa udi na uvumba
kufunga bao.
Wachezaji ni sharti watii kanuni na sheria zinazotawala mchezo. Aidha, lazima wakubali amri za
refa, kocha na waamuzi wengine ili kuimarisha nidhamu michezoni.
Watu hujipatia riziki kwa kushiriki michezo. Sasa hivi, kuna wanamichezo ambao wamesifika sana
duniani. Baadhi yao wamevuka bonde la uchochole na kuwa wakwasi kutokana na talanta zao michezoni.
Bila shaka, majina kama vile David Rudisha, Vivian Cheruiyot, Jason Dunford, Colins Injera na Dennis
Oliech yakitajwa, kila awajuao huwavulia kofia.
Tangu jadi, michezo imekuwa kitegauchumi kote duniani. Wagiriki, kwa mfano walianzisha
michezo ya Olimpiki karne nyingi zilizopita, takribani miaka 776 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo.
Michezo hii ilipoanza ilishirikisha Wagiriki kutoka himaya zote za Ugiriki. Baadaye, watu wengine
waliposhuhudia faida zilizotokana na michezo hii, walikubali kushirikishwa. Michezo ya Olimpiki ikawa si
ya Wagiriki tu, bali dunia nzima.
Baada ya hapo pamekuwa na michezo mingine ambayo inashirikisha watu kutoka kila pembe ya
dunia. Mchezo wa kandanda wa kuwania Kombe la Dunia, michezo ya raga na riadha ni baadhi tu ya
michezo ya kimataifa.
Watu kutoka maeneo mbalimbali ulimwenguni wanapokutana kwa michezo, nchi na watu wake
hufaidika sana kiuchumi. Wenyeji hupata soko la kuuza bidhaa zao. Wakulima hufaidi kuuza vyakula
wanavyokuza. Mikahawa nayo hujaa wageni tele huleta fedha za kigeni. Wafanyabiashara katika sekta ya
usafiri na wenye hoteli nao huchuma kutoka kwa washiriki na mashabiki. Nchi inayoandaa mashindano
hayo, aidha hupata sifa kimataifa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. Taja aina mbili za mbinu-ishi ambazo hupatikana kwa kushiriki katika michezo. (Alama 2)
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
2. Michezo ina nafasi gani kiuchumi? (alama 4)
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
3.“Faida za michezo ni nyingi.” Thibitisha kauli hii kwa kutoa mifano minne kutoka kwenye taarifa.
(Alama 4)
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
4.Eleza maana za msamiati ufuatao kulingana na taarifa uliyoisoma. (alama 3)
a.kwa udi na uvumba.
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
b.limbukeni.
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
c.huwavulia kofia.
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
5. Eleza faida zingine mbili za michezo ambazo hazikutajwa katika taarifa. (alama 2)
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. UFUPISHO
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yanayofuata.
Kadiri jamii mbalimbali zinavyotagusana, ndivyo lugha zinazozungumzwa na jamii hizi nazo
zinavyoingiliana na kuathiriana. Mojawapo ya athari hizi ni ukopaji wa msamiati. Jamii zinazopakana au
kutagusana hukopa msamiati kutoka kwa lugha jirani na kuutumia kuelezea dhana mpya zinazoingia katika
utamaduni wao kupitia kwa mitagusano ya kijamii.
Lugha ya Kiingereza, kwa mfano, imekopa kutoka lugha nyingine kama vile Kifaransa na Kilatini.
Mathalani, istilahi nyingi za kisheria zimekopwa kutoka lugha ya Kifaransa. Aidha, Kiingereza kimekopa
kutoka lugha ya Kiswahili. Maneno ya Kiswahili kama vile mwalimu, jiko, mandazi, panga, buibui, ngoma
na hata wananchi, sasa yameingia katika kamusi za Kiingereza, kumaanisha kuwa yamekubaliwa kama
msamiati rasmi wa lugha ya Kiingereza.
Kiswahili nacho kimeathiriwa na lugha nyingine. Kimekopa msamiati wa Kiingereza na hata Kiarabu.
Katika tungo nyingi za kishairi, kwa mfano, Utenzi wa Mwanakupona utapata msamiati wa Kiarabu
uliotoholewa. Lugha nyingine ambazo zimeathiri Kiswahili ni pamoja na Kijerumani ambako msamiati
kama vile ‘shule’ ulikopwa na kutoholewa na neno schule. Msamiati kama vile ‘leso’, ‘karata’ na ‘mvinyo’
yamekopwa kutoka lugha ya Kireno, huku majina ‘balozi’ na ‘bahasha’ yakikopwa kutoka Kituruki.
Pamoja na ukopaji wa vipengele vya lugha, mtagusano wa lugha una athari nyingine. Lugha zinapokuja
pamoja, mazingira ya wingi-lugha husuka. Baadhi ya watu hujifunza zaidi ya lugha moja. Mtu anayeweza
kuzungumza zaidi ya lugha moja anaweza kujieleza kwa urahisi kwa kuchanganya msamiati wa lugha
tofauti. Aidha, anaweza kubadilisha msimbo kulingana na matilaha yake. Ikiwa anataka kukubalika na
jamii-lugha anayotagusana nayo, atatumia lugha ya jamii hiyo ili kujinasihisha na kujitambulisha nayo.
Wazungumzaji hupata visawe vya maneno kuelezea dhana zile zile, hivyo kuboresha mitindo yao ya
mawasiliano.
Kadhalika, kutagusana kwa lugha kunaweza kusababisha kubuniwa kwa lugha ngeni ambayo inarahisisha
mawasiliano. Wakati mwingine, watu wanaozungumza lugha tofauti wanapokutana, hubuni mfumo sahili
wa lugha ili kufanikisha mawasiliano. Pijini ni mfano wa lugha iliyobuniwa kwa njia hii. Pijini huchota
msamiati kutoka lugha zilizotagusana. Sheng ni mfano mwingine wa lugha ambayo ilibuniwa kutokana na
kutagusana kwa lugha ya Kiswahili, lugha za kiasili na Kiingereza.
Japokuwa kuna faida nyingi za wingi-lugha, hasara pia zipo. Mazingira ya wingi-lugha huwapa
wazungumzaji fursa ya kuchagua lugha wanayotaka kuwasiliana kwayo. Katika hali hii, lugha yenye
ushawishi mkubwa kijamii, kiuchumi na kisiasa ndiyo inayopendelewa zaidi. Wingi-lugha unaweza
kusababisha kukwezwa kwa lugha moja na kudunishwa kwa lugha nyingine. Mathalani, kuwepo kwa lugha
nyingi nchini kulizua haja ya kukwezwa kwa lugha ya Kiswahili huku nyingine za kiasili zikipuuzwa.
Lugha hukua kwa kutumiwa. Lugha isipozungumzwa kwa muda mrefu, watu hupoteza umilisi ambao
huifanya kuwa vigumu kuirithisha kwa vizazi. Lugha inaweza pia kukosa wazungumzaji ikiwa wale
wanaoizungumza ni wachache, au ikaathiriwa na mtagusano na lugha nyingine iliyo na wazungumzaji
wengi. Katika hali kama hii, lugha hiyo hukabiliwa na tisho la kudidimia au hata kufa. Ikiwa jamii lugha
itakosa kudhibiti sera za matumizi ya lugha yake, baadhi ya lugha ama zitafifia u zitakufa na kusahaulika
kabisa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. Bila kupoteza maana, fupisha aya za kwanza tatu. (Maneno 50-60)(Alama 10, 1ya mtiririko)
Matayarisho
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
Jibu
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. Kwa mujibu wa taarifa hii, mtagusano wa lugha una athari gani?maneno 20-30 (Alama 5, 1 ya
mtiririko)
Matayarisho
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
Jibu
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
3, SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA
a.Onyesha sifa tatu za kuainisha irabu al 3
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
b, Tofautisha baina ya; al 3
a.utasoma! ...............................................................................................................................
b.utasoma. …………………………………………………………………………………
c.utasoma?...............................................................................................................................
c. a.Kiambishi ni nini al 2
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
b. Ainisha mofimu katika neno hili
Sikunywa
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
d.Onyesha miundo mitatu ya kundinomino alama 3
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.......................................................................................................................................................................
e.Changanua sentensi ifuatayo kwa njia ya visanduku alama 4
Yule mzee ajengaye barabara ametuzwa.
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
f.Bainisha yambwa na chagizo katika sentensi hii alama 4
Mwanafunzi mtukutu aliandikiwa nakala na dadake kwa kalamu jana jioni
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
g.Tunga sentensi tatu tofauti kuonyesha matumizi matatu ya ngeli ya mahali alama 3
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
h.Andika kinyume;
Mama ameijika chungu jikoni. Al 2
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
i.Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli ulizopewa al 2
a. la[kutendesha]
.......................................................................................................................................................................
b.soma[tendeana]
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.......................................................................................................................................................................
j.Bainisha maana mbili zinazojitokeza katika sentensi hii alama 2
wanafunzi walisomeana barua
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
k.unda majina mawili kutokana na neno dhuru al2
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
l.Tunga sentensi moja kutofautisha baina ya bure na pure alama 2
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
m.Bumba ni kwa nyuki……………..………..ni kwa samaki na………………………..ni kwa siafu. al 2
n.Bainisha matumizi ya ku katika sentensi hii alama 3
Mkurugenzi hakukusaidia ulipoenda kule Mombasa anakofanya kazi’
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
o.Tunga sentensi kwa kutumia viwakilishi cha nafsi ambata ya tatu wingi alama 1
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
4. ISIMU JAMII
a. Eleza dhana zifuatazo; alama 5
Usanifishaji
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
Ujozilugha
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
Lafudhi
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
Isimu
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
Lahaja
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
b.Fafanua sababu tano za kuchanganya/kubadili lugha [alama 5]
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
.......................................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MACHAKOS JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI WA KIDATO CHA 4
Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.)
102/1 - KISWAHILI - Paper 1
KARATASI YA 1 - INSHA
MWONGOZO WA KISWAHILI 1
1. Hii ni insha ya mahojiano. Mwanafunzi azingatie sura ya insha ya mahojiano asipofuata sura aondolewe
alama nne.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Utangulizi huwa na maelezo mafupi yanayoandikwa katika mabano. Mwanafunzi anaweza kutaja
mahali pa mahojiano iwapo hakutaja katika kichwa. Mwanafunzi abuni majina/vyeo vya wahusika.
Mtindo wa kitamthilia utumiwe
- Hisia na ishara mbalimbali huonyeshwa kwenye mabano kwa mfano vicheko, huzuni.
Hoja[chanzo]
1. 1.Makundi haramu
2. Uvamizi wa kigaidi
3. Mizozo ya kidini
4. Wizi wa mifugo
5. Mafunzo ya itikadi kali
6. Mtazamo hasi wa wananchi kwa walinda usalama
7. Siasa duni
8. Ukabila
9. Unasaba
10.Dawa za kulevya
Kukabiliana
Hatua kali kwa wanaovuruga Amani
Walinda usalama kuwa imara
Serikali iwahami walinda usalama na vifaa vya kisasa
Vijana kutahadhari wasitumiwe vibaya na viongozi
Dini ihubiri Amani zibuniwe na nyinginezo
Tume za umoja na maudhiano zibuniwe kuhamasisha wananchi kuhusiana na uslama.
2. Ufisadi kama kikwazo
(i) Kazini – mapendeleo/ukabila/unasaba
(ii) Biashara haramu
(iii) Kandarasi/zabuni – kupewa wasiostahili
(iv) Elimu – Udanganyifu katika mitihani/kupewa alama/kufanyiwa mitihani
(v) Kukwepa ushuru hasa viongozi
(vi) Miundo msingi kuwa mbovu kutokana na uporaji
(vii) Afya – hakuna madawa
(viii) Usalama – ugaidi
(ix) Mfumko wa bei/gharama ya maisha kupanda
(x) Barabarani – ajali nyingi.
TANBIHI – mtahiniwa aeleza tu/aunge mkono pekee wala asipinge kauli hii. baadhi ya watahiniwa
wataelezea ujia za kupingana na ufisadi watakuwa wamepotoka.
3,.Mtahiniwa atunge kisa kitakachoonyesha au kushauri watu washirikiane katika shughuli zozote
wazifanyazo. Hamna mtu anayeweza kufanya mambo yoyote yakafana bila ya kuwategemea watu wengine.
TANBIHI. Uandishi huu waweza fanana na umoja ni nguvu utengano ni udhaifu/kidole kimoja hakivuji
chawa. Mtahiniwa aeleza maana ya undani wa methali wala si jifya halisia sababu atapotoka utungo wa
mtahiniwa uwe na pande mbili.
(i) Uchache/ukosefu wa washiriki katika kufanikisha jambo fulani.
(ii) Kutofaulu/kutofana kwa jambo fulani
4.Mtahiniwa atoe kisa kinachoona na maneno aliyopewa
Kisa kiwe cha kusisimua
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mtahiniwa ajipate katika hali ya kujutia/kushangaa/hofu/huzunisha ambavyo inamfanye ajione afadhari
ajiue.
Hali ngumu ambayo msimulizi alipitia akapoteza matumaini kuishi tena mfano;
1. .msichana kubakwa na kuambukizwa magojwa na kuonelea heri afe
2. Msomi kuhitimu shahada nyingi na kukosa ajira nakupoteza matumaini
3. Mtu kupoteza familia yake yote alafu kukosa ,matumaini
4. Mme au mke kumpata mwezake akiwa si mwaminifu katika ndoa.
Kadiri hoja/kazi zingine za mwanafunzi
INSHA
MWONGOZO
Utangulizi
Karatasi hii imedhamiria kutathmini uwezo wa mtahini wa kuwasiliana na msomoji na kuwasilisha ujumbe
kimaandishi, akizingatia mada aliyopewa.Mawasiliano haya yatategemea ukwasi wa lugha ya mtahiniwa
.Kwa kutegemea maagizo ya swali lenyewe na umahiri wa lugha, ni lazima kutilia mkazo mtindo, mada na
uwezo na mtahiniwa kufuata maagizo vilivyo.Mtahini lazima aisome insha yote huku akizingatia sarufi,
hijai, hoja, msamiati na mtindo ili aweze kuikadiria kwa kurejelea viwango mbalimbali vilivopendekezwa.
VIWANGO MBALIMBALI
D – ( D YA CHINI ) MAKI 01 - 02
1. Insha haina mpangilio maalum na haieleweki kwa vyovyote vile.
2. Kujitungia swali tofauti na kulijibu.
3. Kuandika kwa lugha isiyo Kiswahili au kuchanganya Ndimi.
4. Kunakili swali au maswali na kuyakariri.
5. Kunakili swali au kichwa tu.
D – WASTANI MAKI 04 – 05
1. Mtiririko wa mawazo haupo.
2. Mtahiniwa amepotoka kimaudhui.
3. Matumizi ya lugha ni hafifu mno.
4. Kuna makosa mengi ya kila aina.
D+ (D YA JUU) MAKI 04 - 05
1. Insha huwa na makosa mengi ya kila aina, Lakini unaweza kutambua kile ambacho mtahiniwa anajaribu
kuwasilisha.
2. Hoja hazikuelezwa kikamilifu / mada haikukazwa vilivyo.
3. Mtahiniwa hana uhakika wa matumizi ya lugha.
4. Mtahiniwa hujirudiarudia.
5. Insha itakayozingatia sura lakini ikose maudhui ikadiriwe hapa.
6. Insha ya urefu wa robo yaani, isiyozidi maneno 174 isipite kiwango hiki.
C- (C YA CHINI) MAKI 06- 07
1. Mtahiniwa ana shida ya kuwasilisha na kutiririsha mawazo yake.
2. Mtahiniwa hana msamiati wa kutosha wala miundo ya sentensi ifaayo.
3. Mtahiniwa anafanya makosa mengi ya sarufi , ya hijai na ya msamiati na insha haieleweki kwa urahisi.
C WASTANI MAKI 08
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe lakini kwa njia hafifu.
2. Dhana tofauti hazijitokezi wazi.
3. Mtahiniwa hana ubunifu wa kutosha.
4. Mtiririko wa mawazo ni hafifu na hana ufundi wa lugha unaofaa.
5. Amejaribu kuishughulikia mada aliyopewa.
6. Ana shida ya uakifishaji.
7. Anafanya makosa mengi ya sarufi, ya hijai na ua msamiati lakini bado insha inaeleweka.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
C+ (C YA JUU) MAKI 09- 10
1. Anawasilisha ujumbe vizuri akizingatia mada lakini bado insha inaeleweka.
2. Dhana tofauti zimejitokeza japo kwa njia hafifu.
3. Kuna mtiririko wa mawazo japo hana ufundi wa lugha unaofaa.
4. Misemo na methali zimetumika kwa njia hafifu.
5. Anashida ya uakifishaji.
6. Kuna makosa ya sarufi ya msamiati na hijai yanayoathiri mtiririko wa mawazo.
7. Insha ya kiwango cha nusu, yaani maneno 175- 274 isizidi kiwango hiki.
B – (B YA CHINI) MAKI 11- 12
1. Anawasilisha ujumbe vizuri kwa kueleza hoja tofauti akizingatia mada.
2. Ana mtiririko mzuri wa mawazo.
3. Anatumia mifano michache ya msamiati unaovutia
4. Makosa yanadhihirika / ni kiasi
B (B YA CHINI) MAKI 13
1. Anathihirisha hali ya kuimudu lugha.
2. Mawazo yake yanathihirika akizigatia mada.
3. Anateua na kutumia mifano michache ya misamiati mwafaka.
4. Sanja yake ni mzuri.
5. Makosa ni machache.
B+ (B YA JUU) MAKI 14 - 15
1. Mawazo yake yanadhihirika na anajieleza waziwazi.
2. Anawasilisha ujumbe kwa njia inayovutia na kwa urahisi akizingatia mada.
3. Ana mchanganyiko mzuri wa msamiati unaovutia.
4. Sarufi yake ni nzuri.
5. Uakifishaji wake wa sentensi ni mzuri.
6. Makosa ni machache ya hapa na pale.
7. Insha ya urefiu wa robo tatu, yaani maneno 274 – 374, isipite kiwango hiki.
A- (A YA CHINI) MAKI 16- 17
1. Anadhihirisha ukomavu wa lugha.
2. Mawazo yake yanadhihirika na anaishughulikia mada.
3. Ana mtiririiko mzuri wa mawazo.
4. Msamiati wake ni mzuri na unavutia.
5. Sarufi yake ni nzuri.
7. Makosa ni machache yasiyokusudiwa.
A WASTANI MAKI – 18
1. Anawasilisha ujumbe vizuri kulingana na mada.
2. Anajieleza kikamilifu akitumia lugha ya mnato.
3. Anatoa hoja zilizokomaa.
4. Anatumia msamiati wa hali ya juu na unaovutia zaidi.
5. Anatumia miundo tofauti tofauti ya sentensi kiufundi.
6. Makosa ni nadra kupatikana.
A+ (A YA JUU) 19 – 20
1. Mawazo yanadhihirika zaidi na mada imeshughulikiwa vilivyo.
2. Anajieleza kikamilifu akitumia lugha ya mnato.
3. Hoja zake zimekomaa na zinashawishi.
4. Msamiati wake ni wa hali ya juu na unavutia zaidi.
5. Sarufi yake ni nzuri zaidi.
6. Anatumia miundo tofauti tofauti ya sentensi, kiufundi.
7. Makosa yote kwa jumla hayazidi matano.
ALAMA ZA KUSAHIHISHA
= = = Hupigwa chini ya sehemu ambapo kosa la sarufi limetokea kwa mara ya kwanza tu.
_ Hupigwa chini ya sehemu au neno ambapo kosa la hijai limetokeza kwa mara ya kwanza tu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
✓ Hutumiwa kuonyesha hoja inapokamilika pambazoni kushoto.
Hutumiwa kuonyesha kuacha kwa neno / maneno.
Hutumiwa kuonyesha msamiati bora. Alama hii hutiwa juu ya neno lenyewe.
X Hutumiwa kuonyesha msamiati usiofaa. Alama hutiwa juu ya neno lenyewe.
Kila ukurasa uwe na alama ya chini katikati ili kuthibitisha kuwa mtahini ameupitia ukurasa huo.
Baada ya kutoa tuzo, lazima mtahini aandike udhaifu wa mtahiniwa.
Mfano wa kutuza:
Robo Tatu
C 08/20
Udhaifu
Urefu
Maudhui
Hijai
Sarufi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MACHAKOS JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI WA KIDATO CHA 4
Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.)
102/2 - KISWAHILI - Karatasi ya 2
Ufahamu, ufupisho, Sarufi na matumizi ya lugha na Isimu jamii
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
1. UFAHAMU: ALAMA 15
(A). (i) Wazazi kukwepa jukumu la ulezi.
(ii) Kutokuwa na sheria/sera iliyo wazi kuhusu usalama wa watoto
Hoja yoyote 1x1=1
(B) (i) Hukosa mapenzi.
(ii) Hukosa malezi,maelekezo na mwongozo mwafaka maishani
(i) Huiga tabia bofu K.M kuvuta gundi na kuiba.
(ii) Njaa
Zozote 3x1=3
(C). (i).Kutiliwa maanani kwa mpango wa vijana wa kujiunga na huduma ya taifa
(ii).Kuongeza makao ya watoto na kuwapa mafunzo ya kiufundi
(iii). kuwasajili watoto ili waweze kuunganishwa na familia zao
(iv).Wafadhili wawape chakula badala ya pesa taslimu
(v).Wanaowauzia gundi wahamasishwe dhidi ya matumizi yake
Zozote 3x1=3
(D) (i).Tegemeo lao ni makombo na takataka iliyo mapipani (alama 2)
(ii).Kutolitatua tatizo la watoto wanaorandaranda mitaani kutatuletea matatizo
(iii). Mhitaji hachagui chochote (alama 2)
(E) (i). Aidha-pia
(ii). Gundi- Kitu kiolevu na kinachonata kunachonuswa na watoto kama kileo
1x2=2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. UFUPISHO
1. HOJA ZA KUZINGATIA (Alama 9, 1 za mtiririko)
- Mitagusano ya kijamii hufanya lugha kuingiliana.
- Pia lugha huadhiriana
- Ukopaji wa vipengele vya lugha ni moja ya athari hizo/msamiati
- Istilahi nyingi za kisheria zimekopwa kutoka lugha ya kifaransa.
- Msamiati hukopwa ili kueleza dhana ngeni.
- Lugha zote hukopa.
- Kiingereza kimekopa kutoka.
- Kilatini, Kifaransa na Kiswahili.
- Kiswahili nacho kimekopa kutoka.
- Kiingereza, Kiarabu, Kireno, Kituruki na Kijerumani.
MFANO WAJIBU HALISI
Mitagusano ya kijamii huleta maingiliano yana yosababisha jamii kuathiriana
kilugha. Baadhi ya athari hizo za ukopaji wa vipengele vya lugha.
Msamiati hukopwa ili kuelezea dhana mpya, lugha zote hukopa msamiati
kwa mfano Kiingereza, Kiarabu, Kituruki, Kireno na Kijerumani (maneno 48).
2. HOJA ZA KUZINGATIA (Alama 6, 1 za mtiririko)
- Kuzuka kwa hali ya uwingi – lugha.
- Ukuaji wa lugha.
- Kuzuka kwa lugha mpya.
- Kudunishwa kwa lugha.
- Kufa kwa lugha.
MFANO WA JIBU HALISI
Mtagusano wa lugha una faida na hasara. Kwanza, husababisha kuzuka kwa
hali ya wingi – lugha, aidha, lugha hukua kwa kukopa msamiati kutoka lugha
nyingine.
Mtagusano pia husababisha kuzuka kwa lugha mpya, kwa upande mwingine,
uwingi – lugha hukwezwa na kudunishwa baadhi ya lugha, lugha
inayodunishwa huingia katika ya kufa (maneno 47).
3:MATUMIZI YA LUGHA :Alama 40.
a.semuya kutamkia
mahali pa kutamkia
mkao wa midomo
(alama 1x1=2)
(B). A-li-f-iw-a (alama 1/2x2=1)
(alama 2)
(c). Kitondo/tendewa- Zainabu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kipozi/tendwa- Barua (1x2=2)
d.N-moja pekee
N+U+N
N+KISHAZI TEGEMEZI
W PEKEE
N/W+V
e. ). Kakake aliwafanya watu wengine wapigane.
.Yeye na kakake waliwafanya kupigana
.Waligonganishwa
.Yeye na kakake walikosana
(2x1=2)
(alama 2)
(F).pa/po
ku/ko
mu/mo
(G). Tifu, onyo. (alama 2)
(H i.lisha
someana
i.KN[V+N+S]+KT[T]
KN KT
V N J T
Yule Mzee Ajengaye barabara ametuzwa
j. Juma alimkaribisha Bakari akamsihi akae.Bakari alimshukuru Juma na akataka kujua habari za
nyumbani.
(1x4=4)
k. ). Ukuta uliobomoka- Kishazi tegemezi
Ulisababisha hasara kubwa- Kishazi huru
(1x2=2)
l. .kudhuru
madhara
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
m. Walielea/waliibuka wakitawanya mchanga. (1/2x2=2
n. pure-mchanganyiko wa mahindi na maharagwe
bure-bila kabisa
o. nafsi
kikanushi wakati uliopita
ngeli ya mahali
p.mama alikuwa amepika alama 2
q.kishazi/mtungo
msafara
r.Ngeli ni mkusanyiko au makundi ya nomino/
4.SEHEMU YA NNE ISIMU JAMII (ALAMA 10)
1.Sentensi ndefu ndefu 1.sentensi fupifupi
2.lugha rasmi 2.lugha ya kawaida
3.Hunukuu vifungu vya kisheria /msamiati
maalum
3.Hutumia msamiati wa kawaida
4.Hukopa kutoka lugha za kigeni-kilatini 4.Hutumia lugha rahisi na inayoeleweka na wote
5.Huwa kuna mkarimani 5.hakuhitaji mkarimani/muuzaji na mnunuzi
huelewana
6.kuna mpangilio maalum wakati kesi
inapoendeshwa
6.kuna kukatiza kauli
(1x2x5=10)
MACHAKOS JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI KIDATO CHA NNE
Kenya Certificate of Secondary Education (K.C.S.E.)
102/3 - KISWAHILI - Paper 3
KARATASI YA TATU
MWONGOZO WA USAHIHISHAJI
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. chozi la heri
a. haya ya mabarobaro watano ambao walisambulia familia ya kaizari.
Msemewa- subira mkewe
Mahali- huku ni nyumbani kwa kaizari
Sababu- nikutokana na uhasama wa uchaguzi na ukabila pale walimpiga subira na kumbaka mabinti
wa kaizari
B. sifa za kaizari
Msomi-alipewacheo cha kuwa afisa wa matibabu katika hospitali ya Mwanzo mpya
Mwenye huruma-aliwahurumia watoto wake Lime na Mwanaheri wakati walibakwa
Mwenye majuto-kifo cha subira kilimsubua na kumletea majuto
Mwenye kumbukumbu- Kaizari anamsimulia Ridhaa matukioyote tangu kutoka nyumbani
Mlahaka mwema- Waliishi vyema na jirani zake.Waliishi kwa Amani na upendo.
C.Madhara ya vita vya kikabila
1.Vifo au mauaji-Ridhaa alipoteza familia yake yote mkewewatoto wawilimjukuu na mkaza mwana
2. Uharibifu wamali- jumba la RIdhaa liliteketea na vyote vilimokuwa
3.Ridhaa alipata shinikizo la damu
4.Ubakaji- wasichana wa kaizari walibakwa
5.Njaa –wakimbizi walikula mizizi kwa ajili ya ukosefu wa chakula
6.Kiu- hakukuwa na majisafiya kunywa
7. Msongamano-Maelfu ya wakimbizi walisongama mno kwenye kambi la wakimbizi
8.Uharibifu wa mazingira- Msitu wa mamba uliharibiwa,mto ulianza kukauka
9.Mkurupuko wa maradhi- kipindupindu na maradhimengine
10.Ukosefu wa huduma kama hospitali,vyoo na vinginezo na wengi waliteseka
11.Ubaguzi-familia zingine ziligawiwa chakula kingikuliko zingine
12.Ahadi hewa-Wakimbizi waliahidiwa nyumba za hadhi lakinihilo halikufanyika
13. Uchovu.Wengi walichoka kwa matembeziya umbali mrefu
14.Chukina uhasama miongon mwa familia-Selume aliacha aila yake kwa chuki iliyotokea
15.Ukosefu wa makao-wengi waliishi nje mbila ya makazi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
16.Baridi
17.msongo wa mawazo- Kaizari aliiathirika sana
SEHEMU B: TAMTHILIA
Maswali na Majibu ya kigogo
1. Majibu
i. Mwafulani A ni Kombe na B ni Sudi. Wako katika karakana yao wanakofanyia kazi ya
uchongaji katika soko la Chapakazi. Boza alikuwa amewaambia kuwa kulikuwa na fununu
kwamba Mzee alikuwa amepanga kutoa chakula cha kutosha kwa wale wasiojiweza na ndipo
Kombe akasema yeye alikuwa anajiweza.
ii. Usemi wa Kombe ni kinaya kwa vile alisema alijiweza ilhali si kweli. Awali alikuwa
amelalamika kusikia sherehe za miaka sitini ya uhuru zingechukua muda wa mwezi mzima.
Alifadhaika na kushindwa wangejikimu vipi, “Tutakaula nini?”
iii. Kinaya ni mbinu ya kutoa kauli ilio kinyume na inavyotarajiwa. Aidha ni kinyume cha jambo au
matarajio.
• Ni kinaya kuwa Boza anamwita mkewe mwanamke ‘halisi’ na ndipo akapata kandarasi ya
kuoka keki. Anafurahia kuwa mkewe ni fisadi ndio maana akapata mradi huo. Isitoshe
anamwita mwanamke halisi ilhali alishukiwa kumwendea kinyume mumewe katika ndoa
yao. (uk 7)
• Mjumbe anatangaza kuwa Wanasagamoyo hawangekubali kutawaliwa kwa dhuluma tena (uk
5). Hiki ni kinaya maanake tayari Majoka alikuwa kiongozi dhalimu aliyepanga mauaji ya
raia, aliyenyakua ardhi ya umma, alifunga soko na kutenda maovu mengi mengine.
• Ni kinaya kwa Kenga kumwambia Sudi kuwa Teknolojia ya kisasa haikuwatisha (uk 11)
ilhali alibabaika sana kuona maandamano ya Tunu yakiangaziwa Katika mitandao ya kijamii
na kupeperushwa moja kwa moja na Runinga ya Mzalendo (uk 37)
• Ni kinaya Majoka kumwambia Ashua kuwa ingekuwa afadhali kama angepewa talaka na
Sudi. Kwamba kuvunjika kwa ndoa kumgemletea fanaka (uk 21) Anamwambia, “Talaka ni
Baraka”
• Ni kinaya kwa Majoka kusema kazi za sokoni zilikuwa kazi za uchafu ilhali hizo ndizo watu
walifanya kujikimu (uk 25). Yeye mwenyewe alitaka watu wa soko hilo hilo wachonge
vinyago vya mashujaa kisha asema sokoni kulikuwa na uchafu.
• Ni kinaya pia anaposema sokoni ni kuchafu ilhali utawala wake ndio umekosa kuwajibika.
Hakuna mikakati ya kudumisha usafi sokoni ilhali wachuuzi hulipa kodi ya kugharimia
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
huduma hii (uk 2, 3, 25). Kombe, Sudi na Ashua wameangazia swala hili la kulipa kodi
lakini soko kubaki chafu.
• Ni kinaya Husda kumshauri Ashua kutafuta kazi ya kufanya (uk 27) ilhali yeye mwenyewe
hajanukuliwa akifanya kazi yoyote. La muhimu kwake ni anasa na starehe kama vile
kutembea Katika hoteli za kifahari, kuogelea kisha kujipodoa (uk 67). Ashua alikuwa
akifanya kazi sokoni.
• Ni kinaya Husda kumkanya Ashua tabia ya udaku na kumbe ndiye mwenye udaku zaidi.
Ashua anasema Husda alijulikana kuwa msambazaji wa kanda za umbeya kwenye vikao vya
masengenyo (uk 27-28)
• Kinaya kinajitokeza Majoka anapoamuru Ashua na Husda wafungiwe na kujifanya
amekasirishwa na tabia yao ya kuanza vurugu ofisini mwake. Anajidai kukasirika ilhali ni
yeye alipanga na kukusudia haya yote yatokee.
• Kauli ya Majoka “sina time na wanawake” (uk 29) ni kinaya. Anasema hana wakati na
wanawake ilhali alikuwa ametumia muda wake mwingi akijaribu Ashua amkubali mle
ofisini. Pia yu pamoja na mkewe Katika Majoka na Majoka Modern Resort wakiogelea na
kumpumzika. (uk 67)
• Ni kinaya kwa Majoka kusema kuwa Sagamoyo ilijiweza na haikuhitaji wafadhili (uk 33)
ilhali wafadhili walikuwa wanasimamia miradi huko. Kwa mfano walikuwa wametoa
mkopo ambao ungelipwa katika muda karne moja. (uk 11).
• Ni kinaya Majoka kusema kuwa alikuwa na moyo wa huruma (uk 34). Hata Kenga
anamwambia awache moyo wa huruma (uk 34). Hata hivyo ukweli ni kuwa Majoka alikuwa
katili. Alicheka waliporejelea kifo cha Jabali, hakujali Ngurumo alikufa, alitaka Asiya awe
amekufa, alitaka Chopi pia auawe, aliamuru Kingi kuwapiga watu risasi n.k.
• Majoka anawaita Tunu na Sudi makunguru akimaanisha ni waoga ilhali hata yeye
aliwaogopa. Alimwambia Mwango abaki ofisini, “Sitaki hawa makunguru wanidhuru” (uk
38). Anawaogopa ilhali ana bastola ofisini na wao hawakuwa na silaha.
• Ni kinaya Ashua kumkaripia Sudi kwa vile watoto wake walipelekwa kwa Hashima
kulishwa. Anadai arejeshewe watoto wake awalishe kama Sudi alikuwa ameshindwa. Ashua
asema haya ilhali mwenyewe alikuwa amemwendea Majoka kuomba msaada wa chakula cha
watoto hao hao waliolala njaa. (uk 48, 22, 29) na mwishowe hakupata.
• Ni kinaya Ngurumo kusema Sagamoyo ilikuwa imeboreka kwa soko kufungwa. Anasema
hivi kwa vile biashara yake ya pombe ilinoga. Hata hivyo hali ya Sagamoyo ilikuwa
imedorora; watu wakakosa chakula, wengi wakatamauka na kuishia ulevini na matumizi ya
dawa za kulevya (uk 60)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Ni kinaya pia mamapima kusema kuwa kwake watu walipata furaha. Kauli yake ni kinyume.
Baadhi ya watu walifariki na wengine kuwa vipofu kwa kunywa pombe haramu. Aidha
maisha ni mabaya kwa walevi hawa ambao wengine ni watumizi wa dawa za kulevya (uk 60,
62)
• Walevi wanaimba kuhusu msichana kuwa na tabia mbaya na huenda akakosa kuolewa.
Kinaya ni kuwa vijana hawa ndio wenye tabia mbovu za ulevi, utumiaji wa dawa za kulevya,
kupoteza muda ulevini, kuhongwa kwa vipeni vidogo na watu wa kigogo kutekeleza
mashambulizi kama yale ya kumvunja Tunu miguu. n.k.
• Ni kinaya kuwa serikali au wenye mamlaka serikalini ndio wanaovunja sheria. Kwa mfano
Ngurumo anasema kibali cha kuuza pombe haramu kilitoka kwa serikali ya Majoka. (uk 61)
Zozote 6 x 1 = 6
iv. Sifa za Kombe
I. Ni mwenye bidii
• Ni mchonga vinyago mwenye bidii katika soko la Chapakazi. Anafanya kazi hii ili kujikimu.
Hata soko linapofungwa, anaungana na wenzake kuendelea na kazi hii barazani mwa
nyumba ya Sudi.
Ni mjinga
• Awali alijua kuwa serikali ya Majoka ilikuwa ikiwanyanyasa kwa kuwaitisha pesa nyingi
kuliko kodi iliyofaa kisha haikushughulikia maendeleo lakini bado aliendelea kuiunga
mkono. Hata hivyo mwishowe alibadilisha msimamo wake.
• Anaonyesha kukasirika kwa kutosalimiwa kwanza na Kenga. Alitaka asalimiwe kwanza
wala si Boza. (uk 9).
Mweledi wa mambo
• Anasikitika kuwa sherehe zinazotangazwa na redio zingechukuwa mwezi mzima. Huo ni
muda mrefu mno ungepita bila wao kuzumbua riziki. Alijua wangekosa chakula na mahitaji
muhimu kwa kukosa kufanya kazi kazini.
Mwenye hasira
• Anakasirika Sudi anapoingilia mazungumzo yake na Boza. Anamwambia kwa hasira, “Sudi
usjiingize katika mazungumzo haya, tafadhali jipe shughuli” (uk 6)
Mwenye dharau/bezo
• Anambeza Sudi anaposema kuwa alikuwa tayari kuiandika upya historia ya Sagamoro.
Anamwambia yeye ni mchongaji si mwandishi.
• Anamkejeli Sudi kuwa angekula kiburi chake kwa vile alikataa keki iliyoletwa na Kenga.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mpatanishi
• Anasimama kati ya Sudi na Boza ili wasipigane na kuwaambia wapunguza joto
Mkweli
• Alishikilia uzi kwamba yeye na mwenzake hawakuwa wamepata habari za mradi wa Kenga
licha ya Boza kumkonyezea jicho asifichue siri hiyo.
• Ingawa alikuwa anaunga Majoka mkono alikiri kuwa, “mambo yamekwenda kombo
Sagamoyo…? (uk 151)
Mlafi
• Anaibukia keki aliyoikataa Sudi
Kigeugeu
• Licha ya kuwa mfuasi sugu wa majoka mwishowe alijiunga na waliokuwa wakipigania haki
Sagamoyo. Kwa mfano Boza aliposita kuandamana na kina Tunu na kusema wao hawaendi,
alimwambia, “Sema wewe”. Yeye aliondoka mara moja pamoja na akina Sudi na Tunu,
kuelekea kiwandani kulikotokea mauaji.
Mwenye shukrani
• Alimshukuru Ashua kwa kuwaletea chai na mahamri.
Zozote 5 x 1 = 5
Umuhimu wa Kombe
• Ni kielelezo cha watu wenye bidii. Alifanya kazi yake ya uchongaji kwa bidii.
• Kwa kuinyakua ile keki iliyokuwa ikipewa Sudi na kuila anajitokeza kuwa mfano wa watu
walafi katika jamii.
• Ni mfano mzuri wa mtu ambaye hubadilika na kuwa mwema na kusimama upande wenye
haki. Hatimaye aliacha kumuunga mkono Majoka na kuungana na harakati za ukombozi wa
jamii.
• Ni mfano mzuri wa vijana ambao ni vibaraka vya watawala. Hukubali kila wanaloambiwa
bila kutazama athari yake.
Zozote 3 x 1 = 3
2. Fafanua mbinu alizotumia Majoka ili kujidumisha katika mamlaka
• Propaganda. Vyombo vya kama vile redio ilitumika kueneza propaganda. Wimbo katika redio ni
wa kumsifu Majoka kuwa kiongozi shupavu anayehusindiwa daima. Pia ujumbe wa Mjumbe ni wa
Kumsifu Majoka kupita kiasi. Haya yote yakidhamiriwa kumdumisha Majoka katika uongozi licha
ya udhalimu wake.
• Kuua washindani km Jabali, jaribio la kumwangamiza Tunu, kuamrisha Kingi apige watu risasi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Vitisho vya kufutwa kazi km Kingi
• Kutawanya mikutano
• Kuhangaisha raia na kuwaogofya km akina Siti kurushiwa vijikaratasi vya kuwaamuru wahame.
• Kuvunja sheria akipendelea wafuasi kama Ngurumo kupata kibali cha kuuza pombe ili apate watu
wa kumwuunga mkono.
• Kuwa na washauri kama Kenga.
• Mbinu ya tenga utawale, alisema alitaka kuongea na Tunu na Sudi kila mmoja peke yake.
• Kuwaua mashahidi wa uovu wake km Ngurumo kisha alipanga kumwua Chopi
• Kufukuza wafadhili wanaounga mkono wapinzani wake.
• Kuharamisha maandamano ya kudai haki.
• Kutumia hila na kudanyanya umma anashughulikia malalamishi yao, kwa mfano kuongeza
mishahara kisha kupandisha kodi.
• Kunyima watu habari za ukweli za jimbo km kufunga kituo cha Runinga ya Mzalendo ili watu
wasimpinge.
Za kwanza 10 x 2 = 20
3.Athari za uongozi mbaya Sagamoyo
Ufisadi- uvujaji wa pesa za umma
Unyakuzi wa mashamba – sokola chapakazi
Vifo au mauaji- kuna kifo cha Jabali
Kufungwa jela bila hatia- Ashua
Unyanyasaji wa kijinsia- Ashua kunyanyaswa kimapenzi
Njaa/ukosefu wa chakula – watotowa Ashua
Kodi za juu- Wananchi hutozwa kodi isiyo halali
Ukosefu wa ajira- Vijana waliohitimu kutoka vyuo vikuu hukosa ajira
Mishahara duni- walimu na madaktari
Migomo- walimu na madaktari kugoma
Mihadarati na pombe haramu- hili lilikubaliwa
Uharibifu wa azingira- ukatajiovyo wamiti
Ukabila
Ubarakara- Ngurumo, Asiya, kenga ,boza n.k
Maandamano- kutokana na upinzani
Mikopo-kukosa uadilifu/uwajibikaji
Vitisho- wananchi kutishwa wahame kutoka Sagamoyo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Gharama-ya maisha kupanda
Ukosefu wa maendeleo
Elimu duni-wananchikuishia kuwa kabaji
SEHEMU C: HADITHI FUPI
4.“Rasta twambie bwana!”
(a) Weka dondoo katika muktadha (alama 4)
Maneno ya wanafunzi wa shule ya Busuala
Akimwambia Rasta/ Samueli Matandiko
Walipokuwa shuleni.
Samueli alikuwa ametoka katika afisi ya mwalimu mkuu kuchukua matoke yake ya mtihani.
Marafiki waliomjua wanamtaka awaelezee alama zake.
(b) Taja mbinu zilizotumiwa na mwandishi katika dondoo hili (alam 2)
(i) Utohozi
(ii) nidaa
(c) Ni kwa vipi mzungumziwa anamchukulia mwalimu mkuu kama hambe? (alama 4)
Mwalimu mkuu wa shule ya Busukalala hakuwahi kumwamini Samueli hata siku moja kama
anaweza kufaulu mtihani.
Mwalimu mkuu hakuamini Samueli aliposema kuwa amelipa ada mpaka alipohakikisha kwa
kuangalia nyaraka na kumbukumbu zake.
Anamwonyesha Samueli dharau kwa mumrisha karatasi kama mbwa; anarejelea kile alichokuwa
akifanya na kumpuuza.
Mwalimu mkuu hakumpa ushauri wowote Samueli ambao ungemsaidia kupokea matokeo yake
ambayo hayakuwa mazuri hata kidogo.
Mwalimu mkuu alimjibu Samueli kwa karaha, alipomwita kuwa ni fidhuli. Anamjibiza kwa kuuliza
iwapo wanafunzi wengine walipa mawe au majani.
Zozote 4 x 1 = 4
(d) Anwani Mtihani wa maisha inaafiki hadithi yenyewe. Jadili
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Anwani hii inaafiki hadithi kwa maana yenyewe inahusiana na mitahani, maana ya kwanza ya
mtihani; ni maswali yanayojibiwa kwa kuandika au vitendo ili kupima maarifa aliyonayo
mtahiniwa. Matokeo ya mtihani huwa ama kupita au kufeli.
• Baadhi ya wahusika kaitka hadithi walifaulu katika mitihani yao shuleni. Dada zake Samueli
walipita mtihani, Bilha akaweza kujiunga na Chuo Cha Ualimu cha Eregi.
• Waliotoka ofisini mwa mwalimu mkuu wakiwa na furaha kuu walikuwa wamefaulu katika
mtihani. Walishangilia kweli. Waliona kama dunia ilikuwa yao tu.
• Kundi jingine ni lile la kina Samueli na wale walitoka ofisini mwa mwalimu Mkuu wakiwa
wameinamisha nyuso zao. Hawa walifeli katika mtihani wao wa shule. Walisikitika si haba,
Samueli akafadhaika zaidi.
• Maana ya pili ya mtihani ni changamoto. Changamoto ni jambo linalomkabili mtu na wakati
mwingine kumweka katika njia panda. Mtihani pia ni majaribio yanayosababishwa na
Mwenyezi Mungu kwa mja wake. Majaribio yanayomweka mtu katika hali tatanishi, hali ya
kutafakari ni njisi ipi ya kujinasua kutoka jambo fulani.
• Samueli anapata changamoto ya kuanguka mtihani. Anashindwa atafanya nini. Atawaelezaje
wazee wake kuhusu kuanguka kwake. Anashindwa kuwaambia ukweli, anafeli mtihani wa
maisha. Anapoulizwa na wazaziwe kuhusu matokeo anasema hakupewa na mwalimu mkuu
aliyedai hakuwa amemaliza kulipa karo.
• Aliamua kujiua kwa kujitosa bwawani. Alishindwa jinsi angeangaliana ana kwa ana na babake
mwenye hamaki nyingi. Nusura afie majini, akaokolewa na mpita njia. Huu ulikuwa mtihani wa
maisha ambao alifeli.
• Samueli alishindwa na mtihani wa kujiua. Mara ya kwanza akaokolewa na mpita njia. Kisha kwa
kushindwa kukabiliana na fedheha alitaka kujirusha manjini tena na tena. “Takribani mchana
mzima Samueli anapambana na wanakijiji waliojaribu kumzuia kujitosa majini…”(uk 139)
(Zozote 10 x 1 = 10)
• Babake Samueli pia amefeli katika mtihani wa maisha. Alishindwa kustahimili pigo la
mwanawe la kuanguka mtihani. Alikasirika hadi ya kukasirika. Badala ya kumsaidia mwanawe
asijue, anampa kamba ajinyonge. Anamfananisha na maradhi aliyotoa tumboni tu.
• Mtihani mwingine au changamoto nyingine ya Samueli ilikuwa ya kubaini Nina mpenziwe
alikuwa akimuwaza namna gani. Hakujua iwapo Nina angemfikiria mwongo, zuzu, mwenye
majitapo au nini. Alipomwona Nina kwenye umati ilikuwa, “ Ni kama mtihani mwingine
kujaribu kubaini anachowaza na kuhisi…labda mwanzo wa mtihani wa maisha”(uk 139)
• Mamake Samueli alipita mtihani wa maisha Alimpenda mwanawe hata kama hakupita mtihani
wa shule. Alifika pale karibu na bwawa, akamshika mwanawe mkono na kumsihi waende
nyumbani. Anampa matumaini ya kufaulu katika mtihani wa maisha kwa kumwambia, “Huwezi
kushindwa na mtihani wa shule na vilevile kushindwa na mtihani wa maisha.”(Uk. 139)
5(a) Jadili uhalisia wa hadithi ya Tumbo Lisiloshiba katika jamiiya leo kwa kutoa hoja kumi.(alama 10)
• Ubinafsi – Kuna ubinafsi na ulafi katika jamii ya kisasa ilivyo katika hadithi. Jitu linamaliza
chakula chote kwenye Mkahawa Mshenzi bila kuwajali wateja wengine.
• Unyakuzi – wakubwa wanataka kunyakua ardhi ya watu wadogo kama ilivyo katika jamii ya leo
ambapo viongozi hunyakua ardhi ya watu maskini.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Dhuluma- Wananchi hukandamizwa kwa kubomolewa kibanda/makazi yao hata bila ilani na
kuachwa wakihangaika jinsi ambavyo inafanyikia Wanamadongoporomoka.
• Ufisadi – Wakubwa wanataka kuwahonga na vijisenti vidogo ili wahame makazi yao jinsi viongozi
katika jamii ya leo huwahonga wananchi maskini na kunyakua mali yao.
• Sheria zenye vikwazo-katika jamii ya leo, sheria huwapendelea matajiri na viongozi kwani wao
huweka vikwazo makusudi ili kwazuia maskini na wasio na nguvu kutetea haki zao. Hali ni hiyo
katika hadithi ya Tumbo Lisiloshiba.
• Kutengwa – wananchi hawahusishwi na viongozi kikamilifu katika mipango ya maendeleo ya
maeneo yao. Wanamadongoporomoka hawahusishwi katika mipango ya maendeleo.
• Mazingira chafu- hali katika mtaa wa Madongoporomoka ni mbaya, viongozi hawasafishi mtaa
wao, kama ilivyo katika mitaa duni nyingi katika jamii ya leo.
• Wanasheria wasio waadilifu – Jinsi inavyokuwa vigumu kupata wanasheria waadilifu katika jamii ya
leo, ndivyo ilivyokuwa adimu kuwapata wanasheria waaminifu kama haki yenyewe katika jamii ya
hadithi ya Tumbo Lisiloshiba.
• Msongomano mijini – Jiji lilikuwa limejaa kila mahali; mall, majumba ya muziki, maduka makuu,
shule, vyuo, hospitali, mahakama, majumba ya ofisi, n.k. jinsi ilivyo katika miji mikuu mingi leo.
• Matumizii mabaya ya vyombo vya dola – askari wa baraza la mji na jeshi la polisi walitumiwa
kuwafurusha wanamadongoporomola badala ya kuwahakikishia usalama wao, vyombo vya dola
vinatumiwa vibaya na viongozi wa sasa
• Maendeleo – kuna maendeleo yaliyopiga kasi katika jamii ya sasa kama ilivyo katika jamii ya
hadithini. Jiji limejaa majumba ya mikahawa, malls, departmental stores, casinos, n.k.
• Ushirikiano – kuna ushirikiano na umoja wa wananchi wanaonyanyaswa katika jamii ya sasa jinsi
Mzee Mago alivyowakusanya wanamadongoporomoka ili kutetea haki zao.
(Za kwanza 10 x 1 = 10)
)
6.USHAIRI
(a) Mzungumzaji (nafsineni) asingiziwa ugumba kwa kutoshiriki mapenzi nje ya ndoa.(1 x 2 =2)
(b) Mambo ambayo anapinga:
(i) Kuiga rika; hususa kushiriki ulevi.
(ii) Kufukuza wasichana
(iii) Anapinga uhawara
(iv) Anapakwa tope(kuaibishwa) kwa kuwa yeye ni gumba
(v) Wamsemao kudai anatamani kuwa kama wao.
(vi) Eti kuwa ugumba na ukapera ni kosa
(vii) Kuharibu maisha kwa ujana
(viii) Kusingiziwa atapenda (atatamani) hali za wamsemao.
(ix) Watu kueneza uvumi kuwa yeye ni gumba.
(5 X 1=5)
(c) Umuhimu wa viishio
(i) Ni vifupi na hivyo vinatoa ujumbe kwa namna iliyo madhubuti.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(ii) Vinaunga ujumbe wa kila ubeti/vinasisitiza ujumbe wa shairi
(iii) Vinachimuza/kuonyesha dhamira au mwelekeo wa mshairi kuhusu hali ya vijana kujiingiza
katika mahusiano yasiyofaa.
2 X 1=2
(d) Mtindo unaokubalika
(i) Ni jambo gani linamkasirisha Mungu ambalo halikubaliki kanisani?
(ii) Je, ni mtu kuwa hahaba na mwenye vioja ama mtu aliyezaliwa akiwa tasa?
(iii) Kuwa gumba au kapera si kosa na wala haliwezi kuwa kosa.
(iv) Kwa kweli mimi sina kosa.
4 X 1=4
(e) Muundo
(i) Kila ubeti una mistari mine/mishororo.
(ii) Mistari mitatu ya kwanza ina vipande vitatu isipokuwa ubeti wa 1 wa 2 na ubeti 5.
(iii) Vina katika kila kipande vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.
(iv) Kiishio kimefupishwa.
(v) Kila mstari una mizani 20 isipokuwa ubeti 1 mshororo 3 una 20 na kiishio kina mizani 8.
(vi) Shairi lina beti 5
(vii) Kuna kiishio/mshororo wa mwisho kila ubeti ni tofauti.
Zozote 5 X 1=5
(f) Tafsida
(i) Mbio za wasichana – uasherati/uzenzi/uzinifu
(ii) Haupandiki mgomba-hana uwezo wa kujamiiana.
Za kwanza 2 X 1=2
7.Ushairi
(a) Ujumbe
(i) Shairi hili ni wasia kwa vijana; unaowaonya dhidi ya dunia ilivyo mbaya na inaweza
kuwaudhi.
(ii) Linashauri kuwa wanaovutia machoni wanaugua na hivyo wanaweza kuwaambukiza
maradhi.
(iii) Watu washiriki mapenzi kihalali kwa sababu zinaa hii haichagui wala kupendelea yeyote.
(iv) Hata warembo wanaovutia ni hatari, wasionekane wanapendeza wanaweza kuwa hatari.
(v) Vijana wajikaze kuhakikisha kuwa hawaingii kwenye mtego kushiriki mapenzi
(vi) Wenye nguvu wamesalimu amri
(vii) Hakuna faida ya kukimbilia mambo yanayosababisha kifo/tujiepushe na mambo
yatakayosababisha kifo cha aibu.
(viii) Wapo wanaowasema wenye kujitunza lakini hilo lisiwafanye kutekereka.
(ix) Anawaombea vijana kwa mola awakinge na anasa.
4X1=4
(b) Mbinu za mwandishi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Tabdila – kubadili miendelezo ya neno pasi kubadili idadi ya mizani/niskia lingekuwa
nisikie-limetumika hivi ili kukudhi mahitaji ya vina.
(ii) Inkisari-kufupisha maneno. Inkisari imetumiwa kuleta ulinganifu wa mizani.
Kwa mfano
(a) Sikuwambia badala ya sikuwaambia
(b) Jepusheni – jiepusheni
(c) Ngawa – ingawa
(d) Waone – uwaone
(e) Mkamba – mkambaa
(f) Ngia – ingia
(g) Walopapia – waliopapia
(h) Watalokwamba – watakalokwamba
(iii) Miundo ngeu ya kisintaksia/kuboronga sarufi
(a) Yaugua nisikia badala ya nisikie yaugua
(b) Si mlango nyumba nzuri – nyumba nzuri si mlango
(c) Makaa kujipalilia – kujipalilia makaa
(d) Madhara kukadiria – kukadiria madhara
(e) Maponda kumichia – kumichia maponda
(f) Mazida – vyang’alia – vyang’ara, wakingie/wakinge
(g) Utohozi sitori – history
Mazida na utohozi zimetumika kuleta urari wa vina.
Za kwanza 4 X 2=8
(c) Pande mbili ambazo mshari anasema nazo ni:
(i) Vijana
(ii) Mungu
(d) Umuhimu wa maswali ya balagha
(i) Humfanya msomaji kulidadisi jambo linaloibuliwa. Msomaji atavuta fikra kuhusu faida ya
kuingia kwenye anasa ya kuumia. Kwa kudadisi hili ataona hamna faida na hivyo kujirudi.
(ii) Hutumiwa kusuta watu au kukashifu jambo – kuwaonyesha wasoma nikuwa hatima ya
anasa ni kifo.
(iii) Kusisitiza/kutilia mkazo wazo au kumfanya msomaji kushawishika na mtazamo wa msanii.
(iv) Hutumiwa kuzindua – hata wenye nguvu huangamizwa
Zozote 3 X 1=3
(e) Toni ya huzuni/kusikitika
(i) Anasikitika madhara yatakayowapata wanaoingilia zinaa kwa kauli kama vile – wawapi leo
madume, anasa walopapia.
(ii) Toni ya kunaishi au kushawishi. Anawasihi vijana kuepuka zinaa.
(iii) Kejeli/dharau/bezo/stizai
(iv) Uchungu
Kutaja 1
Kueleza 2
1 x 3=3
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
8.FASIHI SIMULIZI
A. Michezo ya jukwaani- huigizwa jukwaani mahali wazi
Vichekesho- michezo mifupi ambaya hupitisha ujumbe kwa namna ya kuchekesha
Majigambo/vivugo –yakisimuliwa na kuambatanishwa na matendo ya kujisifu
Michwezoya watotoau chekechea- michezo a,bayo huigizwa na watotokatika shughuli zao
Ngoma – uchezeshaji wa viuongo vywa mwili kuambatana na midundo
Miviga – sherehe za kitamaduni ambazo hufanywa na jamii yoyote kipindi maalumu
Mataabiko- sadaka au ada inayotolewa kwa mwenyezi mungu pepo au mizimu
B. Baadhiyamiviga hukinzana na malengo ya kitaifa
Miviga hujaza hofu
Miviga huhusisha ushirikina
Miviga hugharimu pesa nyingi
C . Hupitisha ujumbe wa dharura kuhusu matukio ya dharura
Ni kitambulishi cha jamii
Huhifadhi na kuendeleza utamaduni
Hukuza uzalendo
D Bainisha sifa sita za ushairi simulizi
- Huwasilishwa kwa njia ya mdomo mbele ya hadhira kwa kukaririwa, kughaniwa au kuimbwa
- Mpando na mshuko wa sauti
- Uwezo wa uwasilishaji wa anayehusika
- Ushirika wa hadhira katika uwasilishaji.
- Matendo ni muhimu kwa anaye wasilisha
- Matumizi ya ala za mziki huchangia
- Lugha ya mkato yenye mvuto mwingi
- Lugha yenye uwezo wa kujenga taswira
- Matumizi ya tamathali za usemi
- Hutumia mbinu ya urudiaji na takriri.
Za kwanza 6 X 1=6
E. Huvuta makini au usikivu wa hadhira
Hutambulisha au hutangaza mtambaji
Huashiria mwanzo wa hadithi
Hushirikisha na kuleta hadhira na mtambaji pamoja
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Huweka mpaka kati ya ulimwengu halisi na ulimwengu wa hadithi
MOLO JOINT EXAMINATION
KISWAHILI
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA 1 (TATHMINI)
INSHA
MUDA: SAA 1 ¾
JINA______________________________________NAMBARI YA MTAHINIWA_________
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SAHIHI ___________________ TAREHE _______________________
Maagizo .
a. Andika insha mbili . Insha ya kwanza ni ya lazima.
b. Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
c. Kila insha isipungue maneno 400
d. kila insha ina alama 20
e. kila insha lazina iandikwe kwa lugha ya Kiswahili .
Kwa matumizi ya mtahini pekee.
SWALI UPEO ALAMA
1 20
2 20
JUMLA 40
1. Lazima .
Kiranja mkuu wa shule yenu ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa baraza la viranja katika Gatuzi
ndogo lenu. Andika wasifu wake.
2. Fafanua umuhimu wa nidhamu katika shule za upili .
3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo .
Mui huwa mwema.
4. Tunga kisa kitakachomalizikia kwa kauli ifuatayo .
Nilimwona nikatabasamu , nikamshukuru kwa vile alivyoniauni .
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MOLO JOINT EXAMINATION
VISION TRIAL EXAMS
KISWAHILI
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA 2 ( LUGHA )
Muda: 2 1/2
Maagizo
a) Jibu maswali yote
b) Majibu yote yaandikwe katika nafasi zizizoaxhiwa katika kijitabu hiki cha maswali.
c) Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya kiswahili
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SWALI UPEO ALAMA
1 15
2 15
3 40
4 10
JUMLA 80
1. UFAHAMU ( ALAMA 15)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali
Ajizi hakujua umuhimu wa kuthamini kazi hadi siku moja alipotanabahi kapigwa pigo la ajabu na
ulimwengu. Tangu utotoni , alizembea kazi zote alizopewa. Hata nyanya yake alisikika kila siku akisema
kuwa alijua mwana huyu angekuwa goigoi mara tu alipozaliwa. Alidai kuwa ajizi alipopumua hewa yake
ya mwanzo hakuwa na bashasha za mwana anayeukumbatia ulimwengu mpya.“Kilio alichotoa`` , alisikika
bibi huyu akisem ‚‘‘ Hakikusikika hata na mkunga aliyemsaidia mamake Ajizi kupata salama”
Utepetevu wa Ajizi haukumzuia kamwe kukua. Alifuata sheria za maumbile,akaonekana akivuta maungo
kila uchao. Mama mtu akafurahia kukua kwa mwanawe licha ya bugudha nyingi kutoka kwa mavyaa wake
na hata ulimwengu kuwa analea mkunguni. Akajisemea kimoyomoyo,“Kweli uchungu wa mwana aujuaye
ni mama,mavyaa anashindwa kuelewa kuwa mwana wa nyoka ni nyoka tu . Mama yetu huyu kwa jina
Imani akajifunga masombo kumlea mwanawe kwa kila hali ila alishindwa kabisa kumshawishi kuinamia
cha mvunguni.
Siku zilisonga na kupita kama maji ya mto. Ajizi akajipata kafikia umri wa kwenda shule. Hapo ikambidi
kuamka kila siku alfajiri na mapema kuliwahi basi la shule. Kila asubuhi kulisikika vilio nyumbani mwao.
Ajizi akikataa kuamka. Bi . Imani , japo alimpenda na kumwonea imani mwanawe, hakukubaliana naye kwa
jambo hili . Alimshurutisha kuamka akijiambia kuwa mwana asiyesoma huwa zigo kubwa. Shuleni Ajizi
hakukawia kuridhisha hulka yake, tabia ni ngozi ya mwili ati. Alikuwa mwanafunzi wa kwanza darasani
mwao kuadhibiwa kwa kutomaliza kazi. Vitabu vyake vilionekana vimechoka na kuchakaa kabisa. Sare za
shule ambazo mama yake alihakikisha kuwa ni nadhifu kila asubuhi kabla ya kuondoka zilivaliwa kiholela
na hata kabla ya adhuhuri kufika, zilikuwa daima hazijulikani rangi yake ya awali, Ajizi kazifanyia kazi si
haba.
Watu husema kila mtu ana kipawa chake, naye ajizi alionekana kaambulia kipawa cha ugoigoi. Hakuna
alilolimudu, si shuleni, si nyumbani. Alishindwa hata kujihami kutokana na tuhuma na ugomvi wa marika
zake. Kila mara alipotishwa na watoto wenzake huko michezoni alimkimbilia mama yake au mwalimu
kushtakia hali . Wenzake walimcheka kama kinyago na kumbandika jina la kebehi- mzee Kunguru . Ajizi
hakujali, alijua udhaifu wake, kwa hivyo kila mara alisikika akisema kuwa kwa shujaa huenda kilio .
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kadiri Ajizi alivyozidi kuzembea kazi ndivyo muda ulivyompungia mkono, akajikuta kidato cha tatu .
Miaka yote alipokuwa katika shule ya Chelea haikumpitikia hata siku moja kuwa mtihani wake ulikuwa
umekaribia. Licha ya upigaji hulu wake, aliweza kuambulia alama za wastani za kufutia machozi. Hata
mtihani wa darasa la nane aliupita tu . Jambo hili lilimpa fahari ya uongo, akazidi kuzama katika usingizi .
Hata hivyo mwaka huu mambo yalimwia magumu kwani alihitajika kudurusu mambo mengi kwa kina
zaidi . Mtihani wa mwisho wa mwaka ulimtia kwenye safu ya wale waliohimili uzito wa wenzao kutoka
chini . Akashtuka ghaya ya kushtuka.
Matukio ya muhula huu yalikuwa kama msumari wa moto juu ya donda ndugu . Ajizi alishidwa kabisa
kuamini alipoona matokeo yamebandikwa ukutani kwa walimwengu kuona. Akaliona jina lake mwishoni
mwa orodha. Hakuweza tena kuvumilia. Alitokwa na kilio ambacho kilitikisa nafsi na kumkumbusha kuwa
wakati wa kufanya kazi umefika. Akajiahidi kuwa mwaka ujao atafungua ukurasa mpya.
Muhula wa kwanza wa kidato cha nne ulimshuhudia Ajizi aliyezaliwa upya. Hakuwahi kuchelewa shule
tena. Kazi yake ya shule iliimarika mno. Akajishukuru kwa ufanisi huu ambao kwa kweli aliulalia
akauamkia. Mihula mitatu iliyofuatia Ajizi alizidi kupanda. Akaanza kuyaangusha majabali darasani na
hata kushikilia usukani katika mtihani wa mwigo. Mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne ulipowadia alijiona
kama amri – jeshi aliye tayari kwa vita vikuu. Akaufanya kwa ujasiri na utulivu na kujiendea zake
nyumbani kungojea ya kutokea.
Hivi sasa Ajizi ni mtu maarufu nchini . Hakuwahi kutazama nyuma baada ya kuwa mwanafunzi bora katika
mtihani wa kidato cha nne. Kila mara hujiuliza kama kweli jina hili lake linamwafiki.
Maswali
a) Dhibitisha kuwa Ajizi alikuwa na uvivu. ( alama 4)
b) Onyesha kwamba mamake Ajizi hakuiunga mkono tabia ya uvivu. ( alama 2)
c) Taja mambo yaliyomzindua Ajizi kuona umuhimu wa kufanya kazi ( alama 3)
d) Jina la Ajizi halimwafiki . Eleza ( alama 2)
e) Eleza maana ya : ( alama 2)
i) Kilio kisichoweza kusikika na mkunga .
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii) Mavyaa kushindwa kuelewa kuwa mwana wa nyoka ni nyoka.
f) Eleza maana ya maneno haya kama yalivyotumiwa kwenye kifungu . ( alama 2)
i) Mavyaa
ii) Kinyago
2. UFUPISHO ( Alama 15)
Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali yafuatayo:
Ki1a walimwengu wanapotajiwa kuwa shambulizi la kigaidi limetokea mahali fulani, wimbi la taharuki
huwakumba. Mashambulizi ya kigaidi yameongezeka katika siku za hivi majuzi ambapo kundi la watu
linalohisi kuwa linaonewa na kukandamizwa huitumia mbinu ya kushambulia kwa kuvizia, hasa kutumia
mabomu au kuteka ndege na kutishia kuilipua na wakati mwingine kuilipulia angani. Kuna mabomu
yaliyotegwa na kulipuka katika maegesho ya magari au kwenye vizuizi vyamagari. Mengine hutegwa na
kulipuliwa katika afisi, mikahawa, makao ya watu, na kadhalika Katika baadhi ya mashambulizi, wapo
waliojitoa mhanga ambao hujilipua katika shambulizi
Makundi ya watu wanaohasimiana ndio chanzo cha matendo ya kigaidi. Kundi linalohisi kuwa
linaonewa au ambalo kweli linaonewa na ambalo ni dhaifu kuliko lile jingine, hufanya juu chini
kushambulia kisirisiri. Nia ni kulipisha kisasi kwa jambo wanalohisi wamehiniwa. Kwa kuwa kundi hilo
hudhani kuwa dhaifu halina njia wala uwezo wa kuyakabili moja kwamoja matendo waliyotendewa au
wanayoendelea kutendewa, njia ya pekee, kwa maoni yao, huwa hii ya kushambulia kwa kushitukiza. Kiini
cha uonevu kinaweza kuwa dini, uchumi, maamuzi ya kisiasa au jambo lingine lolote lile. Kinachobainika
katika suala zima la mashambulizi ya kigaidi ni kuwa lipo jambo ambalo linazikera nyoyo za kundi fulani Ia
watu walio wanyonge ambao huona kuwa njia ya pekee ya kudhihirisha hisia zao ni kupitia mashambulizi
ya aina hii.
Mashambulizi ya aina hii yana athari zake nyingi. Kuna watu wanaouawa na wengine wengi
kulemaa. Maisha ya watu hawa au jamaa zao wanaowategemea hubadilika na kujaa mvurugano uliokithiri.
Kuna watoto ambao ndoto zao zakupata elimu zimetumbukia nyongo baada ya wazazi wao kuzikwa hai
katika vifusi. Mbali na kukosa elimu na mahitaji mengine ya kimsingi, watoto hawa hupatwa na matatizo
ya kisaikolojia baada ya kuona maafa yaliyowafika wavyele wao. Hata wale wanaosalimika kutoka kwenye
vifusi hivi hawaishi kuandamwa na majinamizi yasiyoisha.
Mashambulizi ya kigaidi hayaathiri tu watu pamoja na kuharibu mali ya thamani ya lukuki ya pesa.
Zipo athari nyingine hasi ambazo hudhihiri. Kwa mfano usalama wa nchi huwa mashakani. Wananchi na
wageni vilevile hujihisi kuwa dhaifu na dhalili katika nchi iliyovamiwa. Serikali husika hujikuta katika
shutuma kwa kushindwa kutambua mipango hiyo mapema na kuzuia hasara ya nyoyo na mali. Aidha, jamii
ya kimataifa huiona nchi hiyo kama yenye kukosa usalama na hivyo kuwaonya raia wake dhidi ya kuizuru.
Iwapo nchi husika inategemea utalii kama kitega uchumi muhimu, basi hukosa wateja na waajiriwa katika
sekta hii kupigwa kalamu.
Tatizo la ugaidi si la nchi moja au mataifa fulani mahususi wala hakuna nchi au taifa linaloweza kudai
kuwa haliwezi kukabiliwa na tishio la kigaidi. Kuanzia Dar es Salaam, Nairobi hadi New York na London
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
au hata Cairo hadi Riyadh na Baghdad, sote tunakabiliwa na tatizo hili hili. Hakuna ajuaye lini, vipi au
wapi magaidi wamedhamiria kutekeleza unyama huu.
Labda swali la kujiuliza ni kwamba; Je, upo uwezekano wa mwenendo huu wa kuwaangamiza watu,
wengi wa wahasiriwa wakiwa wale wasio na hatia, kudhibitiwa na kumalizwa kabisa? Serikali za nchi
mbalimbali zimejaribu kutumia uwezo wao wa kiuchumi na kiteknolojia ili kujaribu kuiondoa hali hii. Njia
waliyoitumia ni ya mtutu wa bunduki ambapo makombora mazito yaliyogharimu pesa nyingi
yanadondoshwa katika makao ya washukiwa. Hata katika hatua hii nayo, upo uwezekano mkubwa wa
kuuawa watu wasio na hatia vilevile. Pia ni wazi kwamba uhasama unalipwa kwa uhasama na matokeo
yake ni ulipizaji kisasi usioisha. Amani inakuwa nadra.
Juhudi za ulimwengu kulaani vitendo hivi ni nzuri ila hazitoshi. Utumiaji nguvu kutafuta ufumbuzi
wa kitendawili hiki si suluhisho. Kama wanavyoeleza wanasosholojia, kila kitendo kina sababu zake
zilizofichama. Sababu hizo ndizo kichocheo cha vitendo vinavyojidhihiri. Hivyo basi jukumu lipo katika
kutambua vichochezi vya mashambulizi na kujitahidi kuvitatua kwa njia ya mashauriano yaliyojengwa
katika nia safi ya kuleta usawa na usalama duniani.
Wapo watu wanaoona kuwa vitendo vya mataifa yaliyoendelea kwa nchi changa ndivyo kilele cha
ugaidi. Watu wanaona kuwa tabia ya mataifa hayo yenye uwezo kiuchumi na kiteknolojia kuamua na
kudhibiti sera na imani za nchi changa ni ugaidi uliokubuhu. Vikwazo hivi huwaacha viongozi hoi na
wananchi kuteseka kufuatia ulazimishaji wa sera za kiuchumi na kisiasa zisizohusiana na mahitaji ya watu
wa nchi husika wala kuambatana na mahitaji ya nchi hizi. Hii ni hali inayoyatia mataifa yanayoendelea
katika wasiwasi usioisha kutokana na dhiki zisizoisha kusababishwa na mataifa ya kigeni.
a) Kwa kutumia maneno yasiyozidi 80, fupisha aya ya pili, tatu na nne (Alama 10,1 ya mtiririko )
Matayarisho
Nakala safi
b) Eleza njia zinazotumiwa na mataifa ulimwenguni kupambana na ugaidi. ( Maneno 40)
( Alama 5, 1 ya mtiririko )
Matayarisho
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Nakala safi
3. MATUMIZI YA LUGHA (Alama 40 )
a) Andika sauti zenye sifa sifuatazo ( alama 2)
i) Kiyeyusho cha midomoni .
ii) Irabu ya nyuma wastani .
iii) Kikwaruzo ghuna cha menoni .
iv ) Nazali ya kaakaa laini .
b) Andika neno lenye silabi mwambatano ya midomoni ( alama 1)
a) Bainisha dhamira / jukumu la sentensi zifuatazo ( alama 2)
i) Ingia darasani mara moja
ii) Tafadhali niletee chai .
d) Tambua mzizi katika vitenzi vifuatazo ( alama 1)
i) Amekula
ii) Wanachezesha
e) Andika sentensi zifuatazo upya kulingana na maagizo ( Alama 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Mimi na dada zangu ni waimbaji hodari. ( Tumia kiwakilishi kionyeshi cha karibu badala ya maneno
yaliyopigiwa mstari )
ii) Wanakandarasi wote watepewa kazi . ( Badilisha kivumishi kilichopigiwa mstari kuwa kivumishi
cha pekee chenye maana ya bila kubagua katika umoja ) .
iii) Mfanyibiashara mbadhirifu amefiliska . ( Badilisha neno lililopigwa mstari kuwa nomino)
iv) Barasa la wazee lilitembelea hapa mara kwa mara . ( Badilisha kielezi kilichopigiwa mstari kuwa kielezi
cha wakati.
f) Tumia mzizi – ngali katika sentensi kama : ( alama 2)
i) Kitenzi kisaidizi
ii) Kitenzi kishirikishi
g) Ungansha sentensi zifuatazo kwa kutumia kiunganishi cha masharti ( alama 1)
Wakulima wamefanya kazi kwa bidii . Wakulima watapata faida nyingi.
h) Tumia neno ‘mpaka’ kama : ( alama 2)
i) Kihusishi cha kiwango
ii) Kihusishi cha wakati
i) Heko ni tamko la kushangilia , kumbe ni tamko la _______________na ngo’ ni tamko la
__________________alama 1 )
j) Andika katika umoja ( Alama 1)
Madebe hayo yatasafirishwa pamoja na nyundo hizi .
k) Geuza sentensi ifuatayo iwe katika udogo wingi ( alama 1)
Ubao ulimwangusha mbuzi
l ) Tunga sentensi zenye miundo ifuatayo . ( alama 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Kiima + Kirai kihusishi cha a – unganifu + kitenzi + chagizo ya wakati
ii) KN (W) + KT ( t + N + V )
m) Huku ukitolea mifano mwafaka fafanua sifa mbili za kishazi tegemezi ( alama 2)
n) Tunga sentensi ukitumia kivumishi cha nomino . ( alama 2)
o) Bainisha aina za maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi hii ( alama 3)
Msichana huyu alizawadiwa kwa kuwa mwalimu msichana bora aliyeelekea jukwani kisichana.
p) Tunga sentensi kudhihirisha wakati uliopo hali isiyodhihirika ( alama 2)
q)Tunga sentensi kudhihirisha matumizi mawili ya kiambishi - ku ( alam2)
r) Andika katika usemi wa taarifa ( alama 2)
“ Baba! Baba! chunga hapa, pana nyoka” Mtoto akamwambia babake.
s) Nguzo hii haitaimarisha nyumba yangu . (Yakinisha katika wingi )
t) Tunga sentensi kudhihirisha matumizi ya alama za dukuduku . ( alama 2)
u) Tunga sentensi moja kudhihirisha matumizi mawili ya neno panda ( alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
v) Andika kisawe cha
Onea gere ( alama 1)
4. ISIMU JAMII (ALAMA 10)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata.
“Msikilizaji hapa naona timu ya wembe ‘stars”ikijitosa uwanjani kukabiliana na timu ya mashujaa ‘strikers’
mpira umeanza! Refa wa mavinguni ndiye anayechezesha mechi hii ………. Mulama anampiga chenga,
anakwenda anakwenda……………..mprira unakuwa mwingi na unakuwa sasa kipa wa wembe stars
anaushika ……….
a) Eleza muktadha wa dondoo zinazohusishwa na sajili hii ( alama 2)
b) Taja sifana ueleze zozote sita zinazohusishwa na sajili hii . ( alama 6)
c) Lugha ya Kiswahili inaweza kukua iwapo serikali itaweka mikakati fulani. Toa mikakati miwili
amabayo itawezesha kukua na kuimarika kwa lugha ya Kiswahili . ( alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MOLO JOINT EXAMINATION
KISWAHILI FASIHI ( KARATASI YA 3)
KIDATO CHA NNE
MUDA SAA 2 ½
JINA ________________________________NAMBARI YAKO _________________
SAHIHI ________________________ TAREHE ___________________
MAAGIZO
a) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
b) Jibu maswali manne pekee.
c) Swali la kwanza ni la lazima.
d) Maswali hayo mengine yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki yaani : Tamthilia,Riwaya,Ushairi
na Hadithi fupi.
e) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
f) Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE.
SWALI UPEO ALAMA
1 20
2 20
3 20
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
4 20
JUMLA 80
SEHEMU A:FASIHI SIMULIZI
1. Lazima
(a)Eleza maana ya misimu (alama 1)
(b) Eleza mbinu nne ambazo hutumiwa kuzua misimu katika jamii. (alama4)
(c) Fafanua majukumu matano ya misimu.katika jamii. ( alama 5)
(d) (i) Eleza sifa nne za kimtindo zinazopatikana katika methali za Kiswahili. (alama4)
(ii)Fafanua hoja sita zinazoweza kutumiwa na jamii kudumisha fasihi simulizi. (alama 6)
SEHEMU B: TAMTHILIA : Pauline Kea: Kigogo
Jibu swali la 2 au la 3
2. “Huwezi kuandamana na wavuvi kama kitoweo hukitaki.”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4
(b) Bainisha kitoweo kinachorejelewa na msemaji wa kauli hii. (alama 1)
(c) Fafanua umuhimu wa mzungumzaji wa maneno haya katika kujenga tamthilia ya kigogo.
(alama 7)
(d) Huku ukijadili hoja nane kutoka kwa tamthilia onyesha namna suala linalodokezwa na
dondoo hili linavyoathiri maendeleo ya Wanasagamoyo. (alama 8)
3. (a) Huku ukitumia mifano mwafaka onyesha matumizi kumi ya ishara kama ilivyotumiwa
katika tamthilia ya kigogo. (alama 10)
(b) Tunu ni kielelezo cha vijana waliowajibika.Thibitisha kauli hii kwa kurejelea tamthilia ya
kigogo. (alama 10)
SEHEMU C: A.K.Matei: Chozi la Heri
Jibu swali la 4 au la 5
4“Sasa ni wakati wa kila mtu na malaika wake.”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
(b) Eleza tamathali za lugha zozote mbili zinzazojitokeza katika dondoo hili. (alama 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
c) Toa ithibati kumi na mbili kuonyesha kuwa warejelewa walistahili kuwa na malaika wao.
(alama 12)
5 Onyesha jinsi mwandishi anavyoshughulikiya maudhui yanayofuatayo katika riwaya ya chozi la
heri.
(a) Usaliti (alama 10)
(b) Ufisadi (alama 10)
SEHEMU D: USHAIRI (Mwalaa M. Njange . Tunu ya Ushairi )
Jibu swali la 6 au la 7
6 Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali,
Siondoki
Eti
Niondoke!
Mimi niondoke hapa
Niondoke hapa kwangu!
Nimesaki; licha ya risasi
Vitisho na mauji, siondoki.
Mimi
Siondoki
Siondoki siondoki
Niondoke hapa kwangu!
Kwa mateke hata na mukuki
Marungu na bunduki, siondoki.
Hapa
Siondoki
Mimi ni pahame!
Niondoke hapa kwangu!
Fujo na ghasia zikizuka
Na kani ya waporaji siondoki.
Haki
Siondoki
Kwangu siondoki
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Niondoke hapa kwangu!
Nawaje; waje wanaokuja
Mabepari wadhalimu, siondoki.
Kamwe
Siondoki
Ng’oo hapa kwangu!
Katizame chini mti ule!
Walizikwa babu zangu, siondoki.
Sendi
Nende wapi?
Si’hapa kitovu changu!
Niondoke hapa kwangu
Wangawa na vijikaratasi
Si kwamba hapa si kwangu, siondoki.
Katu
Siondoki
Sihitaji karatasi
Niondoke hapa kwangu
Yangu mimi ni ardhi hii
Wala si makaratasi, siondoki.
(a) Shairi hili ni la aina gani? Eleza. (alama 2)
(b) Taja masaibu anayopitia mzungumzaji (alama 4)
(c) Eleza muundo wa shairi hili. (alama 3)
(d) Fafanua matumizi ya mbinu ya usambamba katika shairi hili. (alama 2)
(e) Eleza toni ya shairi hili. (alama 1)
(f) Tambua aina mbili za uhuru wa kishairi zilizotumiwa katika shairi hili. (alama 2)
(g) Andika ubeti wa tano kwa lugha ya nathari. (alama 4)
(h) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumiwa katika shairi.
i. Nimesaki (alama 1)
ii. Kitovu (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
7. Amiri . A.S Andenenga . Tunu ya ushairi
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Pendo la pesa
Pendo la pesa si pendo, mbali nalo jitengee
Pendo lanuka uvundo, mbali nalo lisogee
Pendo halina uhondo, katu usilichekee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
Pendo halina utamu, lina harufu jamee
Pendo ninalilaumu, mimi lisinilemee
Pendo halina kudumu, hadi pesa umwekee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
Pendo lataka kupenda, bila kupiga kengee
Pendo mfano wa tunda, ukila unenepee
Pendo la pesa huvyonda, tupa usilipokee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
Pendo la kwa kila hali, ubora nalipotee
Pendo kutumia mali, ndipo aitike bee
Pendo hilo ni dhalili, mbali nalitokomee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
Pendo kutumia hela, mifuko iteketee
Pendo hilo lahaula, ni zigo ujibebee
Pendo wawili ni kula, nyama ndimi mnenee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
Pendo kwa watu chaguo, lazima nielezee
Pendo ni sawa funguo, kufuli imngojee
Pendo la kupenda nguo, bora lichekwe heehee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Pendo ni la pale zama, wanahadithi wazee
Pendo lao likiuma, bila kusema nigee
Pendo sasa limelema, ukipanda lisimee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
Pendo hapa nakomesha, mbele nisiendelee
Pendo la pesa lafisha, ni gonjwa usipokee
Pendo hadhi linafisha, la pesa sipendelee
Pendo halina sheree, pendo la pesa si pendo.
(a) Kwa kutumia hoja saba kutoka kwa shairi eleza kwa nini mshairi analipinga pendo la pesa.
(alama 7)
(b) Ainisha bahari za shairi hili kwa kuzingatia; ( alama 3)
i. Mpangilio wa maneno
ii. Mpangilio wa vina
iii. Mpangilio wa vipande/migao
(c) Andika ubeti wa saba kwa lugha nathari. (alama 4)
(d) Bainisha toni ya shairi hili. (alama 2)
(e) Eleza kwa kutoa mfano mbinu moja ya kishairi iliyotumika kutosheleza mahitaji ya kiarudhi.
(alama 2)
(f) Bainisha mifano miwili ya mbinu ifuatayo ya
kitamathali. (alama 2)
Jazanda /istiara
8. SEHEMU E: HADITHI FUPI (A.Chokocho na D.Kanyanda:Tumbo lisiloshiba na Hadithi nyingine.)
7 Sekta ya elimu ina changamoto nyingi.Thibitisha kauli hii ukirejelea hadithi zifuatazo katika
diwani ya Tumbo lisiloshimba na hadithi nyingine.
(a) Mapenzi ya kifaurongo. (alama 5)
(b) Shogake Dada ana ndevu. (alama 5)
(c) Mwalimu Mstaafu. (alama 5)
(d) Mtihani wa Maisha. (alama 5)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MOLO JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA KWANZA
KISWAHILI INSHA
1. Hili ni swali la wasifu
a) sura ya wasifu .
Kichwa kihusishe
- Jina
- wasifu
- wa nani kwa mfano kiranja wa Gatuzi ndogo
- Kuhusu ( wadhifa wake )
- Kwa mfano
WASIFU WA KIRANJA ALIYETEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA VIRANJA
KATIKA GATUZI NDOGO LA GATANGA
a) Utangulizi
- Kutoa maelezo ya kibinafsi ya kiranja
- mwanafunzi atumiwe nafsi ya tatu
b) Mwili
Mwanafunzi atoe wasifu wa kiranja
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
c) Hitimisho
Atoe muhtasari wa wasifu wake na ampendekeze kwa kuonyesha uwezo wake katika wadhifa
huo.
Mfano wa hoja
Hoja amabazo walimu watazingatia wanapotuza swali la mwanafunzi
i) Habari za kibinafsi
- Jina lake na wazazi wake
- Umri wake ( Tarehe ya kuzaliwa)
- Maelezo ya atokako ( kwao)
ii) sifa za kimasomo ( Matokeo yake ya mtihani .
iii) Tajriba yake ( majukumu yake shuleni na katika jamii mf . dini
iv) Ushirikiano wake na wenzake walimu na wafanyakazi
v) Hali yake ya nidhamu shuleni na nyumbani
vi) kipawa chake cha uongozi
vii) sifa yake ya ulumbi
viii) mbinu – ishi - uwajibikaji, mkweli,kujitolea na kujituma
ix) Uraibu wake.
2. Umuhimu wa nidhamu
i) Shule kuwa na matokeo bora
ii) Mshikamano na mlahaka mwema kati ya washikadau shuleni .
iii) mfumo wa kufundisha na kujifunza kufanikiwa.
iv) kuweza kujijali na kuwajali wengine na jamii kwa jumla
v) kuwa na mazingiza bora ya utendakazi.
vi) Ufanisi katika mifumo mbalimbali shuleni kwa mfano masomoni, uwanjani na katika vyama
shuleni .
vii) kupunguza au kutokuwepo na migogoro shule.
viii) Visa vya utovu wa nidhamu kupungua .
ix) Heshima miongoni mwa washika dau
x) Mali shuleni kutunzwa ipasavyo.
xi) Amani na utangamano kudumishwa shuleni .
Mwanafunzi ashughulikie hoja sita .
3. Swali hili ni la methali
a) Wanafunzi waandike kisa kuhusu mtu mbaya ambaye amerekebika na kuwa mzuri au mwema.
b) Huyu mtu anaweza kuwa mwanafunzi , kiongozi , mtu ambaye alikuwa na tabia isiyopendeza
halafu akabadilika na kuwa mtu mzuri wa kutegemewa.
4. Hii ni insha ya mdokezo
Mwanafunzi atunge insha kuhusu mhusika fulani aliyekumbana naye wakahusiana kwa muda na
akaja kumfaa kwa hali fulani katika maisha yake halafu wakatengana kwa muda baadaye wakaja
kukutana na akakumbuka jinsi alivyomsaidia.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MOLO JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA KWANZA
KISWAHILI INSHA
5. Hili ni swali la wasifu
b) sura ya wasifu .
Kichwa kihusishe
- Jina
- wasifu
- wa nani kwa mfano kiranja wa Gatuzi ndogo
- Kuhusu ( wadhifa wake )
- Kwa mfano
WASIFU WA KIRANJA ALIYETEULIWA KUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA VIRANJA
KATIKA GATUZI NDOGO LA GATANGA
d) Utangulizi
- Kutoa maelezo ya kibinafsi ya kiranja
- mwanafunzi atumiwe nafsi ya tatu
e) Mwili
Mwanafunzi atoe wasifu wa kiranja
f) Hitimisho
Atoe muhtasari wa wasifu wake na ampendekeze kwa kuonyesha uwezo wake katika wadhifa
huo.
Mfano wa hoja
Hoja amabazo walimu watazingatia wanapotuza swali la mwanafunzi
x) Habari za kibinafsi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Jina lake na wazazi wake
- Umri wake ( Tarehe ya kuzaliwa)
- Maelezo ya atokako ( kwao)
xi) sifa za kimasomo ( Matokeo yake ya mtihani .
xii) Tajriba yake ( majukumu yake shuleni na katika jamii mf . dini
xiii) Ushirikiano wake na wenzake walimu na wafanyakazi
xiv) Hali yake ya nidhamu shuleni na nyumbani
xv) kipawa chake cha uongozi
xvi) sifa yake ya ulumbi
xvii) mbinu – ishi - uwajibikaji, mkweli,kujitolea na kujituma
xviii) Uraibu wake.
6. Umuhimu wa nidhamu
xii) Shule kuwa na matokeo bora
xiii) Mshikamano na mlahaka mwema kati ya washikadau shuleni .
xiv) mfumo wa kufundisha na kujifunza kufanikiwa.
xv) kuweza kujijali na kuwajali wengine na jamii kwa jumla
xvi) kuwa na mazingiza bora ya utendakazi.
xvii) Ufanisi katika mifumo mbalimbali shuleni kwa mfano masomoni, uwanjani na katika vyama
shuleni .
xviii) kupunguza au kutokuwepo na migogoro shule.
xix) Visa vya utovu wa nidhamu kupungua .
xx) Heshima miongoni mwa washika dau
xxi) Mali shuleni kutunzwa ipasavyo.
xxii) Amani na utangamano kudumishwa shuleni .
Mwanafunzi ashughulikie hoja sita .
7. Swali hili ni la methali
c) Wanafunzi waandike kisa kuhusu mtu mbaya ambaye amerekebika na kuwa mzuri au mwema.
d) Huyu mtu anaweza kuwa mwanafunzi , kiongozi , mtu ambaye alikuwa na tabia isiyopendeza
halafu akabadilika na kuwa mtu mzuri wa kutegemewa.
8. Hii ni insha ya mdokezo
Mwanafunzi atunge insha kuhusu mhusika fulani aliyekumbana naye wakahusiana kwa muda na
akaja kumfaa kwa hali fulani katika maisha yake halafu wakatengana kwa muda baadaye wakaja
kukutana na akakumbuka jinsi alivyomsaidia.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MOLO JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIISHA
KIDATO CHA NNE
INSHA.
UTANGULIZI
Karatasi hii imedhamiria kutathimini uwezo wa mtahiniwa wa kuwasiliana na kuwasilisha ujumbe
kimaandishi, akizingatia mada aliyopewa. Mawasiliano haya yatategemea ukwasi lugha ya
mtahiniwa , kwa mfano ,kutunga sentensi sahihi zenye mtiririko mzuri kimawazo. Lugha ya kuvutia
na yenye mawazo asilia , ubunifu mwingi na hati nadhifu,kwa kutegemea maagizo ya swali lenyewe
na umahiri wa lugha ni lazima kutilia mkazo mtindo ,mada na uwezo wa mtahiniwa kufuata
maagizo vilivyo. Mtahini lazima aisome insha huku akizingatia sarufi,hijai,hoja,msamiati na
mitindo aweza kuikadiria kwa kurejelea viwango mbalimbali vilivyopendekezwa. Viwango
vyenyewe ni A,B,C na D kutegemea uwezo wa mtahiniwa.
VIWANGO MBALIMBALI
KWANGO CHA D KWA JUMLA MAKI 01 – 05.
1. Insha haieleweki kwa vyovyote vile ama uwezo wa mtahiniwa wa kutumia lugha hafifu sana,
hivi kwamba mtahini lazima afikirie kile mtahinwa achojaribu kuwasilisha.
2. Matahiniwa hana uwezo wa kutumia maneno ya Kiswahili kwa njia inayofaa.
3. Lugha imevurugika, uakifishaji haufai na insha ina makosa ya kila aina.
4. Kujitungia swali na kulijibu.
5. Insha ya urefu wa robo ikadiriwe hapa.
NGAZI MBALIMBALI ZA KIWANGO CHA D
D-(DYA CHINI ) MAKI 01 – 02)
1. Insha haina mpangilio maalum na haieleweki kwa vyovyote vile.
2. Kujitumgia swali tofauti na kulijibu.
3. Kuandika kwa lugha isiyo Kiswahili na kuchanganya ndimi.
4. Kunakili swali au maswali na kuyakariri
5. Kunakili swali au kichwa tu.
D WASTANI MAKI 03
1. Mtiriko wa mawazo haupo
2. Matahiniwa apotoka kimaudhui
3. Matumizi ya lugha ni hafifu
4. Kuna makosa mengi kila aina.
D+ (D YA JUU) MAKI 04 – 05)
Insha ya aina hii hu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. Insha ya aina hii huwa na makosa mengi ya kila aina lakini unaweza kutambua kile ambacho
mtahiniwa anajaribu kuwasilisha.
2. Hoja hazikueleza kikamilifu/mada haikukuzwa vilivyo.
3. Mtahiniwa hana uhakika wa matumizi ya lugha.
4. Mtaniwa hujirudiarudia.
5. Insha itakayozingatia sura lakini ikose maudhui ikadiriwe hapa.
KIWANGO CHA C KWA JUMLA MAKI 06- 10
1. Mtahiniwa anajaribu kuishugulikia mada japo hakuikuza na kujiendeza vilivyo.
2. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe kwa njia isiyovutia/hana ubunifu wa kutosha.
3. Mtahiniwa anaakifisha sentensi vibaya.
4. Mtiriko wa mawazo unaanza kijitokeza japo kwa njia hafifu.
5. Insha ina makosa mengi ya sarufi msamiati naya tahajia ( hijai)
6. Insha yenye urefu wa nusu ikaridiwe hapa.
NGAZI MBALIMBALI KIWANGO CHA C
C-(C YA CHINI ) MAKI 06- 07
1. Mtahiniwa ana shida ya kuwasilisha na kutiririsha mawazo yake.
2. Mtahiniwa hana msamiati wa kutosha wala miundo ya sentensi ifaayo.
3. Mtahiniwa anafanya makosa mengi ya sarufi na hijai na ya msamiati na insha yake haieleweki kwa
uraisi.
C WASTANI MAKI 8
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe lakini kwa njia hafifu.
2. Dhana tofautitofauti hazijitokezi wazi
3. Mtahiniwa hana ubunifu wa kutosha
4. Mtirriiko wa mawazo ni hafifu na hana ufundi wa lugha unaofaa.
5.Amejaribu kuishughulikia mada aliyopewa
Mtahiniwa anashida ya uakifishaji
Mtahiniwa anafanya makosa mengi ya sarufi, hijai na ya msamiati lakini bado insha inaeleweka.
C+ (C YA JUU )MAKI 09 – 10
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe vizuri akizingatia mada lakini kwa njia isiyo na mvuto.
2. Dhana tofautitofauti zimejitokeza japo kwa njia hafifu.
3. Kuna mtiririko wa mawazo japo hana ufundi wa lugha unaofaa.
4. Misemo na methali imetumika kwa njia hafifu .
5. Ana shinda ya uakifishaji.
6. Kuna makosa ya sarufi ,msamiati na ya hijai yanayoathiri mtiririko wa mawazo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KIWANGO CHA B KWA JUMLA NA MAKI 11 – 15
1. Katika kiwango hiki mtahiniwa anaonyesha hali ya kuimudu lugha.
2. Mtahiniwa anatumia miundo tofoautitofauti ya sentensi vizuri.
3. Mtahiniwa ana uwezo wa kutumia lugha kwa ufasaha.
4. Mada imekuzwa na kuendelezwa kikamilifu.
5. Insha ya urefu wa robo tatu ikadiriwe katika kiwango hiki.
NGAZI MBALI MBALI ZA KIWANGO CHA B
B – ( B YA CHINI) MAK 11- 12
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe vizuri kwa kueleza hoja tofauti akizingatia mada
2. Mtahiniwa ana mtirriiko mzuri wa mawazo.
3. Mtahiniwa anatumia mifano michache ya msamiati mwafaka.
4. Makosa yanadhihirika, / kiasi
B WASTANI MAKI 13
1. Mtahiniwa anddhihirisha hali ya kuimudu lugha
2. Mawazo ya mtahiniwa yanadhihirika akizingatia mada.
3. Mtahiniwa anateua na kutumia mifano michache ya msamiati mwafaka.
4. Sarufi yake ni nzuri
5. Makosa ni machache / kuna makosa machache.
B+ ( B YA JUU ) MAKI 14 – 15
1. Mawazo ya mtahiniwa yanadhihirika na anajieleza waziwazi
2. Sarufi yake ni nzuri .
3. Uakifishaji wa sentensi zake ni mzuri.
4. Makosa ni machache ya hapa na pale .
KIWANGO CHA A KWA JUMLA MAKI 16 – 20 .
1. Mtahiniwa ana ubunifu wa mawazo yanayodhihirika na kutirriika akizingatia mada
2. Mtahiniwa anadhihirisha ujuzi wa lugha yenye mnato.
3. Ana uwezo wa kutumia tamathali za usemi ili kutoa hisia zake kwa njia bora na kwa urahisi.
4. Umbuji wake unadhihirsha akomavu wake kimawazo.
5. Insha ina urefu kamili.
NGAZI MBALI MBALI ZA KIWANGO CHA A.
A- ( A YA CHINI ) MAKI 16- 17
1. Mtahiniwa anadhihirisha ukomavu wa lugha.
2. Mawazo ya mtahiniwa yanadhihirika na anaishughulikia mada.
3. Ana mtiririko mzuri wa mawazo.
4. Msamiati wake ni mzuri na unavutia.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
5. Sarufi yake ni nzuri
6. Anatumia miundo tofauti ya sentensi kiufundi .
7. Makosa ni machache yasiyokusudiwa.
A WASTANI MAKI 18.
1. Mtahiniwa anawasilisha ujumbe vizuri kulingana na mada.
2. Anajieleza kikamilifu akitumia lugha ya mnato
3. Anatoa hoja zilizokomaa.
4. Anatumia msamiati wa hali ya juu na unaovutia zaidi.
5. Anatumia miundo tofauti ya sentensi kiufundi .
6. Makosa ni nadra kupatikana.
A+ 9A YA JUU ) MAKI 19-20.
1. Mawazo yanadhihirika zaidi na mada imeshugulikiwa vilivyo .
2. Anajieleza kikamilifu akitumia lugha ya mnato
3. Hoja zake zimekomaa na zinashawishi.
4. Msamiati wake ni wa hali yajuu na unaovutia zaidi .
5. Sarufi yake ni nzuri zaidi.
6. Anatumia miundo tofautitofauti ya sentensi kiufundi
7. Makosa yote kwa jumla hayazidi matano.
VIWANGO MBALIMBALI KWA MUHTASARI
KIWANGO ALAMA MAKI
A A+
A
A-
19 – 20
18
16 – 17
B B+
B
B-
14 – 15
12
11 – 12
C C+
C
C-
09 – 10
08
06 – 07
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
D D+
D
D-
04 – 05
03
01 -02
USAHIHISHAJI NA UTUZAJI KWA JUMLA
Mtahini aisome insha yote akizingatia vipengele muhimu/ vipengele hivi ni maudhui , msamiati, mtindo,
sarufi na hijai
MAUDHUI
1. Maudhui ni hoja au mambo yanayozungumziwa, kueleza au kuhadidhiwa kwa mujibu wa mada
iliyoteuliwa.
2. Maudhui ndio hasa uti wa mgongo wa insha yoyote ile.
3. Ubunifu wa mtahiniwa hukisiwa kwa kutathmini uzito wa maudhui yake kulingana na mada teule.
MSAMIATI
Msamiati ni jumla ya maneno yatumiwayo katika lugha husika. Mtahiniwa anatarajiwa kutumia msamiati
wa mada teule.
Kutegemea ukwasi wa lugha alionayo, mtahiniwa anatarajiwa kuikuza mada kwa kuifinyanga lugha
kiufundi. Ni muhimu kuelewa kwamba kutokana na maendeleo na ukuaji wa teknolojia na mawasiliano,
maneno mapya yanaibuka kila uchao.
MTINDO.
Mtindo unahusu mambo yafuatayo. :
• Mpangilio wa kazi kiaya
• Mtirirko wa mshikamano wa mawazo kiaya katika insha nzima.
• Hati nzuri na inayosomeka kwa urahisi.
• Matumizi ya tamathali za usemi; kwa mfano, methali ,misemo, jazanda kadhalika,
• Kuandika herufi vizuri kwa mfano Jj ,Pp, Uu, Ww na kadhalika.
• Sura ya insha.
• Unadhifu wa kazi ya mtahiniwa.
SARUFI
Sarufi ndio msingi wa lugha.Ufanisi wa mawasiliano hutegemea uwezo wa mtahiniwa wa kutunga sentesni
sahihi zenye uwiano wa kisarufi. Mtahini atayaonyesha makosa yoyote ya sarufi yaliyo katika insha
anayosahihisha . Makosa ya sarufi huweza kutokea katika
i) Matumizi ya alama za uakifishaji .
ii) Kutumia herufi kubwa au ndogo mahali pasipofaa.
iii) Matumizi yasiyofaa ya ngeli na viambishi, ,nyakati ,hali, vihusiano na kadhalika.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv) Mpangilio wa maneno katika sentensi
v) Mnyambuliko wa vitenzi na majina.
vi) Kuacha neno linalohitajika au kuongeza neno lisilohitajika katika sentensi.
vii) Matumizi ya herufi kubwa.
a) Mwanzo wa sentensi
b) Majina ya pekee
i) Majina ya mahali , miji , nchi ,mataifa na kadhallika
ii) Siku za juma , miezi n.k.
iii) Makabila, lugha n.k
iv) Jina la Mungu
v) Majina ya kutambulisha hasa wanyama wa kufugwa, kwa mfano yale ya mbwa- Foksi , Popi,
Simba, Tomi na engineyo.
MAKOSA YA HIJAI / TAHAJIA
Haya ni makosa ya maendeleo . Mtahini anashauriwa asahihishe huku akionyesha yanapotokea kwa mara ya
kwanza tu. Makosa ya tahajia huweza kutokea katika:
a)kutenganisha maneno kwa mfano, ‘aliye kuwa’
a)Kuunganisha maneno kwa mfano ‘Kwa sababu”
b)kukata silabi visivyo afikapo mwisho wa mstari kwa mfano “nga- o “
c)Kuandika herufi isiyofaa kwa mfano ‘ hongeza badala ya ‘ongeza’.
d)kuacha herufi katika neno kwa mfano ‘aliekuja’ badala aliyekuja’.
e) Kuongeza herufi katika neno kama vile ‘ piya’ badala ‘ pia’ .
f)Kuacha alama inayotarajiwa katika herufi kama vile ji
g)kukosa kuandika kistari cha kuendeleza neno afikiapo pambizoni au kuandika mahali pasipofaa.
h) Kuacha ratifaa au kuakificha mahali pasipofaa, kwa mfani ngombe , ngom’be , n’gombe , ngo’mbe n.k.
i) Kuandika maneno kwa kifupi kama vile k.v , k.m v.v , n.k
j) kundika tarakimu kwa mfano 27-8-2010.
UKADIRAJI WA UREFU WA INSHA
Maneno 9 katika kila msitari Ukurasa mmoja na nusu
Maneno 8 katika kila msitari Ukurasa mmoja na robo tatu
Maneno 7 katika kila msitari Kurasa mbili
Maneno 6 katika kila msitari Kurasa mbili na robo
Maneno 5 katika kila msitari Kurasa mbili na robo tatu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Maneno 4 katika kila msitari Kurasa tatu na robo tatu
Maneno 3 katika kila msitari Kurasa nne na nusu
Kufikia maneno 174 insha robo
Maneno 175 – 274 Insha nusu
Maneno 275 – 374 Insha robo tatu
Maneno 375 na kuendelea Insha kamili
Mtahini akadirie urefu wa insha na atuzwe alama akizingatia urefu wa insha ya mwanafunzi kwa mfano.
Insha iliyotumia maneno chini ya 174 ni robo- mtahini aikadirie kwa kigezo cha alama 5.
Urefu alama
Robo 5
Nusu 10
Robo tatu 15
Kamili 20.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MOLO JOINT EXAMINATION
KISWAHILI
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA 2
MWONGOZO
ufahamu
a) Alizembea kazi zote alizopewa tangu utotoni
Hakulia kama watoto wengine alipozaliwa
Alikataa kuamka kwenda shule
Alikuwa mwanafunzi wa kwanza darasani kuadhibiwa kwa kutomaliza kazi /Alizembea kazi shuleni
vitabu vyake vilionekana vimechoka na kuchakaa zozote 4 x 1 = 4
b) Alimshurutisha kuamka
Alijaribu kumshawishi kuinamia cha mvunguni bila kufanikiwa 2 x 1 = 2
c) Alipotanabahi kapigwa pigo la ajabu na ulimwengu kuwa miongoni mwa wanafunzi wa mwisho
katika mtihani wa kidato cha tatu .
Matokeo kubandikwa ukutani kwa walimwengu kuona jina lake mwishoni mwa orodha . ( 3 x 1
= 3 )
d) Ajizi ni uvivu /uzembe /uzohali /ukunguni
Ajizi alibadilika akatia bidii na hakuchelewa tena kufika shuleni 2 x 1 = 2
e) i) Kilio hafifu
ii)Ajizi alikuwa kama baba yake mzazi ( 2 x 1 = 2
f) mavyaa – Mamake mume wa Bi . Imani ( Mamake Ajizi )
Jina litumiwalo katika kuitana baina ya mke na mama wa mume wake. ( 1 x 1 = 1)
ii) Kinyago - Mtu anayefanya achekwe au adharauliwe kwa vitendo vyake / kitu cha kuchekesha. (
1 x 1 = 1)
2. MAJIBU YA UFUPISHO
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(a) - Makundi ya watu wanaohasimiana ndio chanzo cha ugaidi.
-Nia huwa ni kulipiza kisasi kwa vile kundi moja hujihisi kuwa dhaifu.
- Kiini cha uhasama huwa dini, uchumi au siasa
- Mashambulizi haya huwa na athari nyingi k.v.
-Watu kuuawa
-Ulemavu
-Kuvuruga maisha ya watu
-Elimu huvurugwa
-Matatizo ya kisaikologia
-Kuharibu mali
-Usalama wa nchi huwa mashakani
-Utalii huathiriwa
Hoja zozote 9 x1 = 9
Utiririko 1x1 = Alama 1
(b) Njia zinazotumiwa kupambana na ugaidi
-Kutumia mtutu wa bunduki / kushambulia magaidi
-Kulaani vitendo vya kigaidi
-Kujaribu kutambua vichochezi vya mashambulizi na kujaribu kuvitatua kwa mashauriano
-Kuwekewa vikwazo kwa mataifa yaliyo na magaidi
Hoja zozote 4 x 1 = 4
Mtiririko 1 x 1
3.MATUMUZI YA LUGHA
i) /w
ii) /o/
iii) /dh/
iv) ng’/
4 x ½ = 2
TANBIHI : Sauti zisiandikwe kwa herufi kubwa
Sauti ziwekwe ndani ya mishazari miwili
b) Mwezi , pwagu , bweni , mtunzi 1 x 1 = 1
i) Amri
ii) Rai /ombi 2 x 1 - 2
d ) i) - l -
ii) chez - 2 x ½ = 1
e) hawa - Alama 1
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
fii) Mwanakandarasi yeyote atapewa kazi - ( ala 1 )
iii) Ubadhilifu wa mfanyibiashara umemfanya kufilisika ( ala 1 )
iv)Jana , Juzi , siku hizo, mwaka jana ala 1
f) Angali analima ( alama 1 ) 1
TS
ii) Angali sokoni ( Kitenzi kihirikishi kipungufu ( alama 1)
g) Ikiwa , iwapo , kama
i)Ikiwa/iwapo/kama/ wakulima watafanya
kazi nyingi watapata faida tele
ii) Wakulima watapata faida tele iwapo /ikiwa/
kama watafanya kazi nyingi 1 x 1
h) i) Alitembea mpaka akachoka ( ala 1)
ii) Alisoma mpaka jioni ( ala 1)
i) Kumbe – kinyume cha matarajio
Ng’o - kubeza ( 2 x ½ = 1
i) Debe hilo litasafirishwa pamoja na nyundo hii ( ala 1 )
k) Vibao viliviangusha vibuzi ( ala 1)
l) Mtotowa jirani alipotea jana jioni ( ala 2)
N RH T CH ( wakati)
Tanbihi: Lazima apate sehemu zote
ii) Yeye ni mwanafunzi mwerevu ( alama 2)
W t N V
m) i)O – rejeshi - mototo aliyezaliwa
ii) Amba - Mwanafunzi ambaye ametuzwa
iii)Ki - Ikinyesha tutapalilia
iv)Viunganishi vya masharti- ikiwa kama atalima
zozote 2 x 1 = 2
n) Mwalimu msichana amezawadiwa ( alama 2)
oMsichana – Nonino (N) ( alma 3 )
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Msichana _ Kivumishi ( V)
Kisichana – Kielezi ( E )
p) Yeye acheza ( ala 2)
q) Ku - ukanusho wa li ( ala 2)
Ku - Mahali
Ku - kirejeleo nafsi
ku - ngeli
ku - Kitenzi jina
r) Mtoto alimwita babake na kumtahadhalisha kuwa achunge mahali hapo kwani palikuwa na nyoka
( 4 x ½ ) = 2
s) Nguzo hizi zitaziimarisha nyumba zetu ( ala 2 )
t) Mama alisem… ( alama 2 )
u) – panda - njia zinaposhikana ( ala 2)
- Kwea
- Tia mbegu ardhini 2 x 1 – 2
- manati
v) Onea wivu - Onea gere / onea kijicho 1 x 1
ISIMUJAMII
A) Mtangazaji wa mpira wa kandanda akitangazia wasikilizaji /watazamaji akiwa uwanjani
b) sifa
i) Kuna kuchanganya ndimi kwa mfano stars, strikers.
ii) kuna matumizi ya msamiati maalumu kama refa , kipa , mpira nk
iii) Kuna matumizi ya utohozi kwa mfano kipa, refa
iv) matumizi ya misimu, mfano , mpira unakuwa mwingi .
v) Kuna matumizi ya takriri mfano, anakwenda anakwenda ….
vi) Kuna matumizi ya mbinu ya chuku mfano ananyaka mpira kinyani. mpira kuwa mwingi
vii) Kandanda huhusishwa na kelele nyingi hasa mpira unapochacha.
viii) Mtangazaji na hadhira hutumia lugha ya kusifu wachezaji ili kuwapa motisha wachezaji na
awatazamaji.
6 x 1 = 6
ci) Kuongeza vipindi vya mafunzo katika shule na vyuo .
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Kuongeza waalimu wa Kiswahili shuleni na vyuoni .
ii) Serikali ihakikishe Kiswahili kimepewa nafasi sawa na lugha ya kingereza
iii) Viongozi wa kisiasa nchini watumie lugha sanifu ya kiswahili katika mikutano yao ya hadhara.
iv) Lugha ya Kiswahili itumike bungeni katika mijadala na kuwasilisha miswada na maeneo mengine
rasmi kama vile mahakani.
v)Serikali iweke mikakati kuhakikisha vyombo vya habari vinatumia lugha sanifu ya Kiswahili .
2 x 2 = 2
MOLO JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA 3 ( KISWAHILI FASIHI )
1. (a) Maana ya Misimu
Semi za muda ambazo hubuniwa na kutumiwa katika mazingira maalum na katika kipindi maalum
cha wakati. (alama 1)
b (i) kutumia tanakali
Neno mtutu ni bunduki.
(ii) utohozi wa maneno
Gava-Government
Hedi-Head
Fadhee-Father
(ii) maneno ya kawaida kupewa maana mpya
Toboa – Faulu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Chuma – bunduki
(iv) matumizi ya tabdila
Njaro-Ndaro
(v) kufupisha maneno
Kompyuta-komp
(vi) kutokana na umbo/rangi ya kinachorejelewa
Blu – Noti ya kitambo ya shiringi ishirini.
Tapi-mtu mwenye umbo kubwa
(vii) kutumia istiara/jazanda
Golikipa -nyani
mtu mlafi-fisi
(vii) kuunda maneno mapya
Kuhanya-usherati
Keroro-pombe
Ni kubaya-hali si nzuri (zozote 4×1=4)
(a) Majukumu ya Misimu
i. Kuongeza msamiati katika lugha.
ii. Watu kujitambulisha na kundi fulani la watu.
iii. Kupamba lugha ya wanaohusika.
iv. Kuburudisha.
v. Kuhifadhi siri.
vi. Hukuza utangamano/uhusiano.
vii. Hukuza lugha.
viii. Huhifadhi utamaduni.
ix. Huendeleza historia.
x. Huondoa urasmi katika mazungumzo.
xi. Hutafsidi lugha.
(zozote 5×1=5)
(b) (i) sifa za kimtindo za methali
i. Takriri/urudiaji wa maneno
Bandu bandu huishia gogo.
ii. Taswira
Njia mbili zilimshinda fisi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iii. Kejeli/dhihaka
Maskini akipata matako hulia mbwata.
iv. Balagha
Pilipili usiyoila yakuwashiani?
v. Tashbihi
Jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza.
vi. Kweli kinzani
Kuinamako ndio kuinukako.
Wapiganao ndio wapatanao.
vii. Chuku
Polepole ya kobe humfikisha mbali.
viii. Tashihisi
Sikio la kufa haslisikii dawa.
ix. Tanakali za sauti
Chururu si ndo ndo ndo!
x. Tanakuzi
Tamaa mbele mauti nyuma.
xi. Kinaya
Kigumba kwa nguruwe kwa mwanadamu ki uchungu (zozote 4×1=4)
(ii) jinsi ya kudumisha fasihi simulizi.
i. Kuifundisha shuleni.
ii. Kurekodi tanzu mbalimbali ili vizazi vijavyo viweze kuzifahamu.
iii. Kufanya utafiti wa kina kuhusiana na tanzu za fasihi simulizi.
iv. Kwa kutumia vyombo vya habari.
v. Viongozi kuwasilisha ujumbe kutumia fani za fasihi simulizi.
vi. Kuhimiza wanajamii kuionea fahari jadi kwa kushiriki kikamilifu katika
matumizi ya fani mbalimbali-miviga.
vii. Kuzitumia tanzu mbalimbali katika sherehe mbalimbali.
viii. Kuandika vitabuni.
ix. Kuandaa mashindano ya shule kimaeneo na kitaifa.
(zozote 6×1=6)
2. (a) muktadha wa dondoo
i. Maneno ya Ngurumo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii. akimwambia Tunu.
iii. Mangweni kwa mamapima/Asiya.
iv. Baada ya Tunu kukataa bilauri la pombe ya Ngurumo na kulikataa.
(zote 4×1=4)
(c) ulevi/pombe (alama 1)
(c) umuhimu wa ngurumo
i. Kielelezo cha vijana wanaotumiawa na viongozi kuwa wapinzani kisha wao
wanaliwa/wanatumiwa.
ii. Vijana wanaoacha shule na kujiingiza katia visa vya lahua na uraibu wa pombe
haramu.
iii. Anaonyesha vijana waliotekwa bakunja kimawazo na kuendelea kuunga mikono
utawala wa kiimla.
iv. Anaonyesha ukatili wa viongozi kutumia vijana kutekeleza maovu na kuwa na
wapinzani.
v. Anatumia kuonyesha sifa za wahusika wengine kama vile Tunu.
vi. Anaonyesha wanaume katika jamii wanaotawaliwa na taasubi ya kiume.
vii. Anaonyesha jinsi majoka alivyokosa huruma kwa watawaliwa wake na kuwatumia
na kuwatelelekeza.
viii. Abainisha athari za ulevi katika jamii.
ix. Anaonyesha wanajamii waliopotoka kimaadili,wanaotumia wanawake walio ndani
ya ndoa,kujitosheleza kimapenzi kabla ya kutimiza mahitaji yao.
(zozote 7×1=7)
d. athari za ulevi
i. walevi kufanya maamuzi ambayo si mazuri kwa jamii.Ngurumo kusema atamchagua
Majoka tu na kama si yeye heri aoze paka wake.
ii. uziazi katika jamii-Ngurumo kuhusiana kimapenzi na Mama Pima mkewe Boza-keki
za uroda.
iii Kutumiwa vibaya na viongozi na baadaye kuuliwa asitoe siri.
Iv Ulevi umempotosha Ngurumo. alisoma darasa moja na Tunu lakini hajijui hajitambui.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
V Ulevi umemfanya Ngurumo asione athari za soko kufungwa anadai yuko sawa na hataki
lifunguliwe.
Vi Mama Pima hatabui hatari za ulevi anaona kulewa ni raha.
Vii watu kufa. Tunu kusema wamewazika watu kutokana na pombe/kifo cha Ngao Junior.
Viii Kuwapofusha watu.
Ix Wanafunzi wanaotumia sumu ya nyoka kutegeuzwa kuwa makabeji.
X Vifo vya walevi kuathiri familia.Ngao Junior anapokufa kifo chake kinaathiri familia ya
Majoka.
(zozote 8×1=8)
3. (a) matumizi ya ishara
i. Ndoto ya Tunu kuhusu Mzee Marara(babake Majoka) akimfukuza ili kumpoka mkufu wake
wa dhahabu ni ishara ya namna viongozi wanavyodhulumu raia kwa kuwapoka rasilimali
zao k.v Majoka alivyowapoka raia uwanja wa soko ili ajenge hoteli.
ii. Kuzirai kwa Majoka baada ya kuarifiwa kuhusu kifo cha mwanawe ni ishara ya kuanguka
kwa uongozi/hatima ya uongozi wake.
iii. Kifo cha mwanawe Majoka ; Ngao junior ni taashira ya hatima ya uongozi wa familia hii
ambayo imeongoza Sagamoyo kwa vizazi vitatu mtawaliwa kwa maana Majoka alitaka
kumrithisha uongozi wake.
iv. Damu ya Jabali anayoiona Majoka ilitiririka mikononi mwake akiwa amezirai ni ishara kuwa
yeye ndiye aliyemuua jabali.
v. Hali ya Majoka kujiona ndani ya ziwa lililofurika damu ni ishara ya mauaji ya raia
aliyoyatekeleza katika uongozi wake.
vi. Kutojaa kwa raia jinsi ilivyo kawaida katika mkutano wa kuadhimisha sherehe za uhuru
pamoja na siku ya kuzaliwa kwa Majoka ni dalili kwamba raia wengi wa wasagamoyo
wangemuasi Bwana Majoka.Walikuwa wamekasirishwa na kufungwa kwa soko la
Chapakazi; soko lililokuwa tegemeo lao.
vii. Kilio na machozi mengi ndani ya ziwa lililofurika damu ni ishara ya raia waliouliwa na
Majoka wanaolilia haki yao.
viii. Kujaa kwa maziara kunaashiria mauaji mengi yaliyotekelezwa na serikali ya Majoka hadi
sasa hakuna mahali pa kuwazika wafu wengine.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ix. Majoka kuvaa shingoni mkufu wenye kidani cha umbo la swila(nyoka mwenye sumu kali) ni
taashira ya namna Majoka alivyokuwa hatari kwa maisha ya raia wa Jimbo la
sagamoyo.Aliwaua K.V.Jabali.
x. Kitendo cha Majoka kuzungumza na babu yake marehemu anapozirai ni ishara kuwa wafu
walikuwa wakimwita kwa maana naye hakustahili kuwa hai kutokana na raia wengi aliokuwa
amewaua.
3(b) Tunu ni kielelezo cha vijana waliowajibika
i. anamtaka Siti awapeleke wanawe Sudi kwa mama yake ,Hashima ili awalishe na awatunze
hadi watakaporudi kutoka kiwandani ambapo vijana walikuwa wameuliwa.
ii. Anashirikiana ma Sudi wakiwa chuoni kuzitetea haki za wanafunzi wenzao.
iii. Aliapa pamoja na Sudi kuzitetea haki za Wanasagamyo baada ya kufuzu masomo ya chuo
kikuu.
iv. Anamkataza Majoka kusema naye na Sudi kando kando kwa maana aliona kuwa hiyo ni
njama ya kuwagawa na kumtaka kusema nao wote.
v. Anakataa wazo la Majoka la kumuoza kwa mwanawe Ngao Junior.
vi. Anamsuta Mamapima/Asiya kwa kuuza pombe haramu kwa maana ni hatia kufanya hivyo.
vii. Anamshawishi Ngurumo na walevi wengine kuacha ulevi kwa kuwaeleza madhara ya
ulevi.Kwa mfano,anawaeleza kwamba pombe ilikuwa imewaua na kuwapofusha wengi.
viii. Anawazindua raia kwa kuwashawishi kuwachagua viongozi wanaozifahamu fika
shida zao,njaa yao na kilio chao.
ix. Anawaongoza raia kumwondoa Majoka mamlakani kwa amani;bila umwagikaji wa damu.
x. Tunu anaposikia kuwa Mzee Kenga anawahutubia wahuni chini ya mbuyu,anawaomba
wenzake;
xi. Sudi na Ashua waende kuskia wanayoambiwa kwa maana alihofia kuwa huenda genge hilo
lingezorotesha usalama wao jimboni Sagamoyo.
xii. Tunu anashirikiana na wanaharakati kuongoza maandamano ili kupinga kufungwa kwa soko
la Chapakazi;soko walilolitegemea raia kupata riziki.
xiii. Tunu anaendelea kutetea haki za raia kama vile kufunguliwa kwa soko licha ya
kupigwa na kuumizwa na wahuni.
xiv. Tunu anasomea uanasheria ili kuzitetea haki za raia wanyonge.
4. (a) Msemaji-Dereva aliyekuwa amewabeba abiria akiwemo mzee kaizari na wengine.
Wasemwa-kina kaizari na abiria wengine waliokuwa garini.
Mahali-Njiani gari lao lilipoisha mafuta baada ya mwendo mrefu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kiini-walikuwa wakitoroka machafuko ya ghasia za uchaguzi na sasa walipofika hapo wakawa
wawaona na kwenda.
(zote
4×1=4)
(b) msemo
kila mtu na malaika wake
kila mtu alistahili kuokolewa kwa bahati yake au imani yake.
Taswira ya malaika anayewasaidia wanyonge.
Taharuki
Ni kipi kitatokea.
(zozote
2×2=4)
c.
i. Ukosefu wa usalama kambini kwa sababu kulikuwa na wasiwasi.
ii. Ukosefu wa maji kwa sababu wanakunywa maji machafu kutoka mto wa mamba Uk 27
iii. Vifo kutokana na magonjwa kama homa ya matumbo,
iv. Vifo kutokana na magonjwa
v. Ukosefu wa chakula - walikula mizizi ya mwituni kwa sababu ya ukosefu wa chakula.
vi. Ukosefu wa mahitaji ya kimsingi kama nguo kwani watoto wa mzee kaizari walikosa mavazi
ya kuwakinga kutokana na baridi kali.
vii. Ukosefu wa matibabu mazuri kwani huduma za matibabu zilikuwa haba na hata dawa
hazikuwepo.
viii. Watoto kuathirika kisaikolojia kwa kuishi katika hema moja na wazazi wao wakawa
wanajionea mambo ambayo hawakustahili kuyaona.
ix. Vibanda duni vilivyoezekwa na nyasi na kuta za udongo.
x. Ukosefu wa misala uliopelekea kuzaliwa kwa vyoo vya kupeperusha au sandarusi.
xi. Wasiwasi wa kufariki ikiwa hali haingebadilika.
xii. Kula vyakula wasivyovijua kama vingehatarisha afya yao.
(zote
12×1=12)
5. (a)usaliti
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i. Selume anasalitiwa na mumewe ambaye anamuacha na kuoa msichana wa kwao baada ya
Selume kumuunga mkono mwekevu.
ii. Annette anamsaliti mume wake kiriri kwa kumnyima haki za unyumba na kumwacha
upweke baada ya kupata uraia wa ughaibuni na kumchoka.
iii. Watoto wa kiriri wanamsaliti baba yao kwa kukosa kurudi nyumbani baada ya kumaliza
masomo ng’ambo,
iv. Mama mkwe wa sabira anasaliti imani ya sabira kwake kwa kumwita mgeni wao mwizi.
v. Sabira anawasaliti wanawe mwanaheri na lime kwa kuwaacha bila kuwazia malezi yao.
vi. Zohari anasaliti familia yake kwa kushindwa kukabiliana na changamoto za ujana na
kuambulia ujauzito akiwa kidato cha pili.
vii. Baba yake zohari anasaliti wajibu wake wa kitaaluma kwa kuhusiana kimapenzi na
mwanafunzi wake Rehema.
viii. Fumba anasaliti mwanawe chandachema anapozaliwa anamwacha alelewe na mama
yake yeye na familia yake wakihamia ng’ambo.
ix. Mama yake pete anausaliti wajiba wake kama mlezi kwa kumwacha alewe na nyanya yake.
x. Mama pete na wajomba wake wanamsaliti pete kwa kumkatiza masomo na kumwoza kwa
mzee fungo.
xi. Bw.Tenge anamsaliti mkewe na wanawe kwa kuhusiana kimapenzi na wanawake wengine
mbele ya wakati mkewe anapoondoka.
xii. Baba wa kambo wa sauna anamsaliti kwa kumnyanyasa kimapenzi na kumpa mimba.
xiii. Sauna kuisaliti imani ya umu kwake kwa kuwaiba Dick na Mwaliko.
xiv. Naomi anaisaliti familia yake kwa kuondoka bila kuwazia dhiki anazowasababisha wanawe
na mumewe lunga.
xv. Majirani wa Ridhaa wanamsaliti, hali ya mchango wake katika kuliendeleza eneo hilo
pamoja na ufadhili wa masomo ya wapwa wa jirani yake wanamchomea jumba la familia
yake.
xvi. Uongozi unasaliti wajibu wao wa kuwahakikishia raia usalama wa chakula kwa kuwauzia
mahindi ambayo ni hatari hata kwa usalama wa panya.
xvii. Viongozi kuwasaliti raia kwa kuwapa ahadi ambazo hawatimizi baada ya uchaguzi.
xviii. Sally anayasaliti mapenzi kwa Billy kwa kumkatalia ombi lake la ndoa.
(zozote 10×1=10)
Ufisadi
i) Viongozi kuwapa wapiga kura hongo ili wawachague.
ii) Vijana wamewapotosha vikongwe kutema viongozi ambao si chaguo lao.
iii) Uongozi kuunda tume bandia za uchunguzi wa kashfa ya ufukuzi wa ardhi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv) Hazina ya jitegemee kuwafaidi ndugu na watu wa usuli mmoja.
v) Viongozi wananyakua msitu kwa masilahi ya kibinafsi kama vile kujenga hoteli za kifahari na
viwanda.
vi) Familia ya bwana kute inazifisadi familia nyingine kwa kujigawa kuwa familia tatu wakati wa
kugawiwa chakula cha msaada kule kambini.
vii) Watu wanaiba mafuta kwenye lori lililoanguka ili kuwauzia madereva wa wakubwa ili
wayachanganye na yale wao madereva wameiba kwenye magari ya waajiri wao.
viii) Buda kuendeleza ufisadi kwa kuhonga maafisa wa forodha ili kupitisha mali haramu.
ix) Polisi kuruhusu biashara ya ulagunzi wa dawa za kulevya.
x) Uongozi wa hospitali kuuza dawa zilizotengewa hospitali kwenye maduka yao huku wagonjwa
wakifa.
xi) Watoto wa matajiri katika vyuo vikuu kupata mkopo huku watoto wa maskini wakilazimika kufanya
vibarua wakati wa likizo kujilipia karo na kugharamia mahitaji mengine.
xii) Watu kuuziwa sehemu ambazo zilitengewa maziara.
xiii) Kuuziwa ardhi ambayo tayari imeuzwa ama kupewa hatimiliki bandia.
(zozote
10×1=10)
6. (a) i) shairi huru
ii)limetumia umbo la paa la nyumba
iii)limetumia alama za uakifishaji kwa wingi.
(b) (i)anatishiwa kwa risasi
(ii)anapigwa mateke
(iii)anapigwa mikwa
(iv)mali yake inaporwa/inapondwa
(v)analetewa hatimiliki bandia
(zozote 4×1=4)
c. shairi lina beti saba
kila ubeti una mishororo sita
lina umbo la paa la nyumba
d. usambamba-urudiaji wa muundo unaofanana sentensi/kirai
i. niondoke hapa kwangu
ii. siondoke siondoki siondoki
e. hasira/kali/dharau
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
f. inkisari sendi-siendi,nende wapi –niende wapi
kuboronga sarufi-yangu mimi ni ardhi hii-ardhi hii ni ysngu mimi
g. mshairi anasema kamwe hatoki kwake.anaashiria chini ya mti waliozikwa babu zake na kusisitiza
kwamba hawezi kuondoka.
h. nimesaki-nimebaki
i. kitovu-asili,chanzo
7(a)
i. asema ni uvundo
ii. halina uhondo
iii. pendo la pesa ni kuchezeana shere
iv. linakosa utamu
v. lina harufu jamee
vi. pendo halidumu ukikosa pesa
vii. linataka upige kenyee
viii. pendo la pesa huvyonda
ix. haitiki bee bila pesa
x. pendo huwa dhalili
xi. hufilisha mifuko iteketee
xii. huwa mzigo- kununua mavazi
xiii. ni ugonjwa-lafisha
b) kikwamba-neno ‘pendo’ limetumiwa kuanzisha kila mshororo
ukara –vina vya ndani vinatofautiana lakini vina vya nje vinafanana kila ubeti.
Mathnawi-shairi lina vipande viwili kila mshororo.
c) mapenzi yalikuwa yale ya zamani wasemavyo wazee.pendo lilikuwa la dhati (ukweli) bila uhitaji
upendo wa sasa una kasoro,ukiupanda haumei(haukui) Pendo halitaki machezo(chati) mapenzi ya sasa si
mapenzi.
d) kutamausha/kukatiza matumaini.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
e)kuboronga sarufi –la pesa sipendelee
inkisari-lanuka-linanuka
f. ni gonjwa
ni dhalili
8) changamoto za sekta ya elimu
a. Mapenzi ya kifauranga
i. kuna mahusiano ya kimapenzi miongoni mwa wanafunzi-penina anamwendea Dennis kutaka kuwa
mpenzi wake.
ii. utabaka-Denis Machora kujihurumia anapojilinganisha na wanafunzi wengine.
iii. Kutamauka kwa wanafunzi kutokana na ugumu wa masomo.
iv. umaskini unaowafanya wanafunzi wakose mahitaji ya kimsingi kama vile chakula.
v.Wahadhiri kutowajibika DKT Mabonga anafunza vitu ambavyo havieleweki.
vi. uzembe- wanafunzi hawatilii maanani masomo yao.
b) shogake dada ana ndevu
i. mapenzi ya kiholela-Safia na kimwani kuwa na uhusiano wa kimapenzi.
ii.wanafunzi kupata mimba bado wakiwa shuleni.
iii.uavyaji wa mimba –wanafunzi wanaopata mimba wakiwa bado shuleni wanakata shauri kuavya
miimba-safia.
iv.wanafunzi wanaopata mimba wanapojaribu kuavya mimba na kuishia kufa-safia
v.uongo/udanganyifu/hila/unafiki wa wanafunzi-Safia kujidai kuwa anataka wadurusu wa kimwari
vi.kutowajibika kwa wazazi katika malezi ya watoto wao.wazazi wa safia hawakujua walichokuwa
wakifanya chumbani safia na kimwana walikodai kudurusu masomo yao.
Zozote 5)
c)mwalimu mstaafu
i. kutamauka,wanafunzi kujiona zueu wasiposhika masomo,jairo.
ii.Ubaguzi-kufeli katika elimu kunachukuliwa kama ni kufeli maishani.Hawapewi nafasi
kuzungumza mbele ya watu.
iii.umaskini-watoto kufukuzwa shule kwa kukosa vitabu vya kawaida.sabira
iv mfumo wa elimu haushughulikii wasioshika masomo darasani.jairo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
v.mapenzi ya kiholela-wanakijiji kushuku kuwa huenda mwalimu mosi alikuwa amemtorosha sabira
bintiye jairo.
Zozote 5
d) mtihani wa maisha
i. mapuuza ya wasimamizi wa elimu ,mwalimu mkuu anamtupia samuel matokeo yake kama mtu
anayemtupia mbwa mfupa.
ii.wanafunzi kutembea mwendo mrefu kwenda shule za kutwa.
iii.ukosefu wa nidhamu shuleni’samueli alikuwa shuleni anatia ‘rasta’ kutokana na mahoka yake.
iv.kufeli mtihani-matokeo ya samueli ni D na E katika masomo yote,
v.kutamauka baada ya kufeli-samueli anataka kujiua.
vi.mapuuza ya wanafunzi –samueli kudhani ni mwerevu ilhali hajui chochote.
vii.Taasubi ya kiume.Samueli alitarajiwa kufanya vyema kuliko dada zake.
MUGOR JOINT EXAMINATION
KAR. 102/1
KIDATO CHA NNE
MUDA: SAA 1 ¾
INSHA
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI – 2019
INSHA
MAAGIZO
(a) Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
(b) Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(c) Kila insha isipungue maneno 400.
(d) Kila insha ina alama 20.
(e) Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
1. LAZIMA
Wewe ni kiranja mkuu katika shule ya kongomano. Wanafunzi wenzako wamekiuka sheria mbalimbali
zilizowekwa shuleni. Waandikie ilani.
2. Vijana wa kisasa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha. Jadili huku ukipendekeza hatua
zifaazo kuchukuliwa ili kuzikabili changamoto hizi.
3. Andika kisa kinachodhihirisha maana ya methali mbaazi ukikosa maua husingizia jua.
4. Tunga kisa kitakachomalizika kwa kauli ifuatayo:-
“……………. Nilijitazama na kujidharau. Kwanini nilijiingiza katika hali hii? Nilijuta.”
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MUGOR JOINT EXAMINATION
KAR. 102/2
LUGHA
KIDATO CHA NNE
MUDA: SAA 2 ½
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI – 2019
KISWAHILI (LUGHA)
MAAGIZO:
(a) Andika jina lako na namba yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
(b) Jibu maswali yote katika nafasi iliyoachwa baada ya kila swali.
(c) Karatasi hii ina kurasa kumi(10) zilizopigwa chapa.
(d) Watahiniwa lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa sawasawa na
kuwa maswali yote yamo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. UFAHAMU
Ufisadi ni uhalifu unaohusu kuzitumia njia za ulaghai kujipatia pesa, mali au vitu hasa vya umma.
Nchini kenya ufisadi hujitokeza kwa njia mbalimbali na kila moja wapo; ina athari zake. Kwa mfano,
kuna maafisa wa serikali wajipatiao pesa kwa kuuza stakabadhi za serikali kamavile pesa, vyeti vya
kuzaliwa, vyeti vya kumiliki mashamba, vitambulisho na nyinginezo kwa raia. Kuna hatari kubwa ya
ugaidi, wizi na ulanguzi wa dawa za kulevya.
Wengine hujipatia vibali vya kufanya kazi na kuajiriwa kazi ambazo zingefanywa na wakenya. Hii
imechangia ongezeko la uhaba wa kazi nchini. Watumishi wengine wa umma huuza mali ya serikali
kama vile magari, nyumba na ardhi na kufutika pesa za mauzo mifukoni mwao. Wengine wao
hujinyakulia na kufanya vitu hivyo kuwa mali yao.ufisadi wa aina hii umegharimu serikali kiasi
kikubwa cha fedha.
Serikali imelazimika kununulia maafisa wake magari baada ya muda mfupi, kulipia wafanyi kazi wake
kodi za nyumba na kukosa viwanja vya upanuzi na ujenzi wa shule, hospitali, vituo vya polisi na taasisi
zingine maalum.
Baadhi ya wataalamu kama madaktari huiba dawa kutoka hospitali za umma kupeleka vituo vyao vya
afya. Pia hutumia wakati wao mwingi katika kazi zao binafsi na kuwaacha wagonjwa katika hospitali za
umma wakihangaika. Sio madaktari tu, kuna masoroveya, wahandisi, mawakili, walimu na mahasibu
ambao hukwepa majukumu yao serikalini na kufanya kazi za kibinafsi. Wengine wasio wataalam
huendesha biashara za aina tofauti, na huku wanaendelea kupokea mishahara.
Wanafunzi wanaotaka kujiunga na shule bora za umma na hawakuhitimu wakati mwingine hulazimika
kusalimu amri na kutoa hongo ili wapate nafasi za kusoma. Kiasi cha pesa kinachohitajika huwa
kikubwa hivi kwamba ni wachache humudu hizo rushwa. Wale wasiojimudu kifedha hubaki wakilia
ngoa. Kuna wazazi ambao hutumia vyeo vyao na ‘undugu” kupata nafasi zilizotajwa, jambo ambalo
huwanyima wanafunzi werevu kutoka jamii maskini nafasi ya kupata elimu. Matokeo huwa ni
kuelimisha watu wasiostahili na ambao mwishowe hawaziwezi kazi wanazosomea wakihitimu na
kuanza kuhudumia jamii.
Ufisadi umekita mizizi na kushamiri katika sekta za umma na za kibinafsi kwa upande wa kuajiri
wafanyikazi. Ni vigumu kupata kazi ikiwa hujui mtu mkubwa katika shirika linalohusika au uzunguke
mbuyu. Matokeo ni kuajiri wafanyikazi wasiohitimu na wasiowajibika kazini.
Vyeo na madaraka katika baadhi ya mashirika kutolewa kwa njia ya mapendeleo na ufisadi. Kwa hivyo,
wafanyikazi wenye bidi hufa moyo kwa sababu hawasaidiwi ipasavyo. Badala yake wale wasioleta bidi
hupandishwa vyeo na kuwaacha palepale.
Hata hivyo mbio za sakafuni huishia ukingoni. Serikali imetangaza vita dhidi ya ufisadi. Tayari tume
kadhaa zimebuniwa kuchunguza visa vya ufisadi uliotekelezwa hapo mbeleni. Mojawapo ya tume hizo
ni tume ya kuchunguza kashfa ya “Goldenberg” ambapo pesa za umma (mabilioni) ziliporwa na
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
mashirika na watu binafsi kwa njia zisizo halali. Watakaopatikana na hatia kushiriki ufisadi huo
watahitajika kurudisha pesa hizo.
Serikali pia imeunda kamati ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi waliohasiriwa na mawakili
walaghai ambao hupokea ridhaa kwa niaba ya wateja wao na kukosa kuwalipa au kuwatetea
mahakamani ilhali wamekwishalipwa. Ni matumaini yetu kuwa ulaghai huu utaangamizwa kabisa kwani
hakuna refu lisilokuwa na ncha.
Maswali
a) Eleza aina nne za ufisadi zilizotajwa katika kifungu ulichosoma (alama 4 )
(i) ………………………………………………………………………………….
(ii) …………………………………………………………………………………..
(iii) …………………………………………………………………………………..
(iv) ……………………………………………………………………………………
b) Kulingana na kifungu ulichosoma. Ufisadi umeathiri nchi yetu kwa njia gani? (alama3)
(i) ………………………………………………………………………………………
(ii) ………………………………………………………………………………………
(iii) ………………………………………………………………………………………
(iv) ………………………………………………………………………………………
c) Serikali inafanya jitihada gani ili kukomesha ufisadi? (alama3)
(i) ………………………………………………………………………………………
(ii) ………………………………………………………………………………………
(iii) ………………………………………………………………………………………
d) Kwa maoni yako, unafikiri ufisadi husababishwa na nini? (alama 2)
(i) ………………………………………………………………………………………
(ii) ………………………………………………………………………………………
(iii) ………………………………………………………………………………………
(iv) ………………………………………………………………………………………
e) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa kifunguni. (alama 3)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Kashfa ……………………………………………………………………………….
(ii) Shamiri …………………………………………………………………………..………
(iii) Waliohasiriwa …………………………………………………………………………………
2. UFUPISHO
SOMA MAKALA HAYA KISHA UYAJIBU MASWALI YANAYOFUATIA
Mvua ya masika imeanza kushuhudiwa katika maeneo mengi nchini. Idara ya utabiri wa hali ya hewa
nchini imewataka maafisa wa serikali na wananchi kwa jumla kujiandaa kwa mvua hiyo kwa kuwa mara
nyingi, husababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi.
Habari hizi ni za kutia moyo ikizingatiwa kuwa tangu Januari mwaka huu, maeneo mengi nchini
yamekuwa yakishuhudia hali ya kiangazi ambayo imesababisha madhila kama njaa, ukosefu wa maji na
lishe kwa mifugo na kudidimia kwa shughuli nyingi za kiuchumi.
Kwa hivyo, ujio wa mvua ni Baraka kubwa kwa wananchi haswa wakulima ambao sasa wataanza shughuli
za upanzi wa mazao ya chakula. Na kwa jamii za wafugaji zinazoishi katika maeneo ya Kaskazini mwa
Kenya na Rift valley, watapata maji na lishe kwa mifugo wao katika msimu huu wa mvua.
Lakini kwa kuwa idara ya utabiri wa hali ya anga imeonya kuwa mvua hii itasababisha mafuriko,
maporomoko ya ardhi na hasara nyinginezo katika maeneo ya miji, serikali inapasa kutumia maafisa wake
maeneo ya mashinani kusambaza ujumbe wa tahadhari. Jumbe hizo zisambazwe kupitia vyombo vya
habari, hususa redio zinazotangaza kwa lugha za kienyeji ili ziweze kuwafikia watu wengi. Mwaka jana,
mvua ilisababisha mafuriko na maafa katika maeneo ya nyanda za chini za kaunti ya Nyanza, Pwani, Rift
valley ya kati na Kaskazini Mashariki. Na katika maeneo kadha katika kaunti za Murang’a na Pokot
Magharibi maporomoko ya ardhi yalisababisha maafa na uharibifu mkubwa wa mali.
Kwa hivyo, maafisa wa serikali haswa wale wa utawala wa mkoa kama vile machifu na makamishna wa
kaunti wanafaa kuwashauri wananchi ambao wanaishi katika maeneo kama hayo kuhamia maeneo salama.
Na wale wanaoishi kando ya mito nao wanafaa kuhamia nyanda za juu. Aidha, mikakati iwekwe ya kuzuia
mafuriko ambayo hushuhudiwa katika mitaa na barabara za miji kama vile Mombasa, Narok na Nairobi
miaka nenda miaka rudi.
Ushauri wangu ni kwamba wasimamizi wa miji kama hii wanapaswa kuhakikisha kuwa miundo msingi ya
kupitisha maji na taka imefanyiwa ukarabati, ujenzi katika maeneo yasiyostahili upigwe marufuku na
mitaro ya kuondoa maji machafu izibuliwe.
Ni jambo la kusikitisha kuwa maafisa waliopewa majukumu ya kuhakikisha kuwa madhara
yanayosababishwa na mvua yamedhibitiwa aghalabu huzembea kazini. Wao huungana na raia kukadiria
hasara iliyosababishwa na mvua licha ya idara husika kutoa tahadhari za mapema. Wahusika katika serikali
kuu na zile za kaunti wanafaa kuhakikisha kuwa mvua inaleta raha wala sio karaha.
Maswali
a) Kwa nini maafa mengi hutokea mvua inaponyesha
Maneno 55 -60
Matayarisho
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
………………………
…………………………………………………………………………………………………
Jibu (alama 8, 1 ya utiririko)
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
………………………
b) Fupisha aya tano za mwanzo
Maneno 40 -45
Matayarisho
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
…………………………………
Jibu (alama 7, 1 ya utiririko)
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
3. MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
A. (i) Eleza tofauti kuu kati ya irabu na konsonanti (alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………
(ii). Linganisha na utofautishe sauti zifuatazo:
/ th / na/ dh / (alama 2)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………
B. Andika neno linalochukua muundo ufuatao wa silabi KIK+KI+KI (alama 2)
………………………………………………………………………………………………..
…………………………………………………………………………………………………
C. Tunga sentensi ya neno moja ambayo ina muundo ufuatao. (alama 3)
(i) Kiambishi cha kukanusha
(ii) Kiambishi cha wakati uliopita
(iii)Kiambishi cha wakati uliopita
(iv) Kiambishi cha mtendwa / mtendewa
(v) Mzizi
(vi) Kauli ya kutendea
(vii) Kiishio
…………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………
D. Elezea matumizi yoyote mawili ya kiambishi U. (alama 2)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………
E. Tunga sentensi na uonyeshe kirai Nomino chenye muundo wa N + S. (alama 2)
………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………
F. Eleza matumizi yoyote matatu ya kiakifishi vifungo (alama 3)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………
G. Badilisha sentensi ifuatayo iwe katika usemi halisi (alama 3)
Mwalimu alimwamuru mwanafunzi amalize kazi hiyo siku hiyo.
……………………………………………………………………………………………............................
....................................................................................................................................
H. Andika sentensi zifuatazo upya kulingana na maagizo. (alama3)
(i) Rhoda, Juma na Ali walipokea tuzo. (Tumia kiwakilishi kiashiria cha karibu badala ya maneno
yaliyopigwa mstari)
………………………………………………………………………………………………………
(ii) Kuadilika kwa mwanasiasa humfanya aaminiwe ( Badili nomino iliyopigwa msitari iwe kivumishi)
……………………………...……………………………………………………………………….
(iii)Wananchi wanaishi karibu na mto. Wananchi hawayachafui maji. (Unganisha kuunda sentensi
changamano)
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………….…………………………………………………………….
I. Andika sentensi zifuatazo katika wingi (alama 2)
(i) Tikiti maji limeuzwa sokoni
………………………………………………………………………………………………………
(ii) Tikiti ya ndege imenunuliwa
………………………………………………………………………………………………………
J. Tunga sentensi iliyo na kishazi tegemezi kinachofanya kazi ya kivumishi (alama 2)
…………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………..………………………………………………
K. Badilisha sentensi ifuatayo iwe katika hali ya ukubwa wingi (alama 2)
Kibaba hiki kinacheza na kisichana hiki kilangoni
…………………………………………………………………………………………………………………
…...……………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
L. Geuza kitenzi kilichopigiwa msitari kiwe nomino bila kubadilisha maana. (alama 2)
Wazazi wanawajibika kuwalea watoto wao vyema
…………………………………………………………………………………………………………………
………….……………………………………………………………………………
M. Changanua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha matawi (alama 5)
Baba na mama wameenda shambani huku watoto wao wakibaki nyumbani.
N. Badilisha vivumishi katika sentensi zifuatazo kuwa viwakilishi vilivyoonyeshwa mabanoni
(alama 2)
(i). Kitabu kizuri kimeibwa. (vya pekee kuleta dhana kutobagua)
……………………………………………………………………………………………………..
(ii). Magari mawili yamenunuliwa. (Kiashiria cha mbali kidogo)
…………………………………………………………………………………………….
O. Andika neno lingine lenye maana sawa na; (alama 2)
(i). Heshima ………………………………………………………………………………
(ii). Ruhusa ………………………………………………………………………………
P. Tunga sentensi yenye muundo ufuatao: (alama 2)
Shamirisho kitondo, kitenzi, shamirisho kipozi, kivumishi cha umilikaji, kihusishi, kiima.
………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
4. ISIMU JAMII ( ALAMA 10)
a) Eleza sababu nne zinazosababisha watu kufanya makosa katika matumizi ya lugha
(alama 4)
(i) …………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………..…..
(ii) …………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………
(iii) …………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………
(iv) …………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………...……….
b) Toa sababu tatu zinazochangia kufa kwa lugha (alama 3)
(i) …………………………………………………………………………………………..
(ii) …………………………………………………………………………………………..
(iii) …………………………………………………………………………………………..
(iv) …………………………………………………………………………………………..
c) Fafanua sababu zinazopelekea mzungumzaji kuchanganya msimbo (alama 3)
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………
………………………………
MUGOR JOINT EXAMINATION
JINA: …………………………………………………………… USAJILI: …………….
DARASA …………………………………………………….TAREHE …………………..
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KAR. 102/3
FASIHI.
KIDATO CHA NNE
MUDA: SAA 2 ½
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI – 2019
FASIHI YA KISWAHILI
MAAGIZO:
a. Jibu maswali manne pekee. Swali la kwanza ni la lazima.
b. Kisha chagua maswali hayo mengine kutoka kwenye sehemu zilizobaki. Yaani, Riwaya, Tamthilia,
Hadithi fupi na Fasihi simulizi.
c. Usijibu maswali mawili kutoka katika sehemu moja.
d. Kila swali lina alama 20.
SWALI LA LAZIMA
1. SEHEMU YA A: USHAIRI
1. Mdomo kyungo muhimu, hilo sote twatambua,
Bila mdomo ni sumu, itakutema dunia
Ubaki kujilaumu, uzuri takupotea
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
2. Midomo tumeibeba, tutaanza na watoto
Matusi kwao si haba, shuleni mezuka moto
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Masengenyo imebeba, kamwe hawana mfyato
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
3. Ione ikipayuka, mitandaoni hakika
Makubwa inayaweka, Amani kuvurugika
Mekosanisha Mogaka, Kamau naye Naliaka
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
4. Mitandaoni mejaa, matusi toka domoni
Zao lake ni mawaa, aibu hadi pomoni
Domo mezusha balaa, kutukuza wafitini
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
5. Kwao cheche za matusi, imekirihi jamaa
Wanasiasa watughasi, yao midomo balaa
Sasa mezua tetesi, ukabila mezagaa
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
6. Wenye midomo michafu, kuiosha fikiria
Soma yote misahafu, ujimulike sikia
Jichuje kama sarafu, domo baya futilia
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
7. Wenye midomo dawa ya waja, hutoa mwanga kwa giza
Hubembeleza natija, Amani kuisambaza
Leo domo ni kileja, uwiano linatuza
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
8. Midomo gundi hakika, taifa kuunganisha
Yaweza shone viraka, udugu tukaboresha
Hasimu tabadilika, nguo nzuri tamvisha
Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
Maswali
a) Eleza madhara ya kutumia mdomo vibaya na jinsi ya kurekebisha hali ile (alama 8)
b) Eleza bahari za shairi hili ukizingatia vigezo vifuatavyo (alama 3)
(i) Mishororo
(ii) Migao
(iii) Vina
c) Eleza umuhimu wa mbinu mbili ambazo mshairi amezitumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi.
(alama 2)
d) Eleza toni ya shairi hili ( alama 2)
e) Tambua aina mbili za urudiaji katika shairi na ufafanue umuhimu wake. (alama 4)
f) Tambua nafsi nenewa katika shairi (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU B: RIWAYA – CHOZI LA HERI
Jibu swali la 2 au la 3
2. ‘Asasi ya ndoa imekumbwa na changamoto nyingi.’ Jadili ukweli wa kauli hii ukirejelea riwaya ya Chozi
la Heri (alama 20)
Au
3. “Ewe chupa wangu ninayekuenzi……….”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
(b) Fafanua sifa nne za msemaji katika dondoo hili (alama 4)
(c) Eleza maudhui yanayojitokeza katika wimbo wa msemaji. (alama 12)
SEHEMU YA C: TAMTHILIA – KIGOGO
Jibu swali la 4 au la 5
4. “………. Acha porojo zako. Kigogo hachezewi. Watafuta maangamizi!”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
(b) Fafanua sifa za mzungumzaji. (alama 4)
(c) Eleza jinsi msemewa alivyokuwa akimchezea kigogo katika muktadha huu ( alama 2)
(d) Kwa kurejelea hoja kumi kutoka kwenye tamthilia, onyesha ukweli kuwa “Kigogo hachezewi”
(alama 10)
Au
5. Kwa kurejelea tamthilia ya Kigogo, jadili mbinu-ishi tunazojifunza kutokana na kijana Tunu.
(alama 20)
SEHEMU YA D: HADITHI FUPI: TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI NYINGINE
Jibu swali la 6 au la 7
6. Mapenzi ya kifaurongo
“Akanyagapo chini ardhi inatetemeka….. amejitia hamnazo. Kabwela kama mimi nina faida gani?
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
(b) Tambua mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika dondoo hili (alama 2)
(c) Elezea sifa nne za msemaji wa dondoo hili (alama 4)
(d) Eleza madhila kumi yaliyompata ‘Kabwela’ (alama 10)
Au
7. Mame Bakari
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
“Dunia we’ dunia. Dunia ya mwenye nguvu si ya mimi dhaifu wa nguvu. Dunia ya msumari moto juu ya
donda bichi……”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
(b) Fafanua mbinu mbili za lugha zilizotumiwa katika dondoo. (alama 2)
(c) Kwa kurejelea hoja kumi na nne, fafanua namna wahasiriwa wa ubakaji wanapitia katika masaibu
mengi katika jamii ya hadithi hii. (alama 14)
SEHEMU YA E: FASIHI SIMULIZI
Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali yanayofuata.
8. Nilipokukopa,
Cheko la mwivu wangu lilipaa sana
Ukewenza ukamshawishi kuchukua buruji kueneza habari.
“Njooni mwone jana la ajabu.”
“Hajawahi kuonekana kama huyu
Tangu kuumbwa kwa ulimwengu”
Ndivyo walisema walokubeza
Kijiji kizima kilimiminika mwangu nyumbani
Kuyatuma maozi kukutazama weye
Uso na thamani walikwona,
Wakaupa unyonge moyo wangu toto,
Wakanituma kuola viungo vyako
Wakanitanabahisha upungufu ulokulemaza!
Chozi chungu linapukutika
Likalovya changu kidari
likanavya chako kipaji
tabasamu ukatoa kunihakikishia
“Mimi si mjalana!
Katu sivyo wasemavyo walimwengu!”
Neno lako hili likanipa tulivu
Nikaamua alakulihali kupambana na yangu jumuiya
Ilosema kwa moja kauli utokomezwe, chakani utupwe.
Tazameni mahasidi mloteka
Teko la dharau mlonimwaiya
Mkanitia ukiwa usomithilika!
Oleni! Tungeni macho!
Mwana mlioambaa ja ukoma
Mlowinga ja nyuni wala mtama, tazameni
Mekuwa malaika, anaowaauni
Kiguru mlomtajia hakimzuwii kufuma mishale
Maadui wamwonapo hutetema kama jani
Mefagia vijiji vinane kwa pigo moja la kiganja chake
Mepigana vita visohisabika
Na wetu mahasimu waliotupoka na mifugo
Jamii yetu sasa metawala kote
Umekuwa nahodha mwenye kubwa saburi
Akili yako nyepesi sumaku kweli kweli
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Hupakata yote ya neema na shwari
Mwili wako japo lemavu,
Mesheheni nguvu za majagina mia moja!
Naposhika zana, maadui elfu huanguka!
Umeifaa jamii hii, ilotaka kuangamizwa
Majagina wote, wakusujudia
Walokufurusha wamebaki hizika
Watutuka ewe shibli
Mfano wa Shaka Zulu
Alowaonjesha kivumbi wapinzani
Kuwayeyusha kama barafu.
Limwengu mzima wakujua mwana
Alozawa kishika mkuki
Ulosema na miungu, alfajiri lipoukumbatia ulimwengu
Ela mwana jihadhari usaliti wao waja
Wasije kutosa lindini kwa nduli kukukabidhi.
Maswali
1. Huu ni wimbo aina gani? Thibitisha jibu lako (alama 2)
2. Jadili sifa mbili za jamii iliyoizaa kazi hii. (alama 2)
3. Bainisha nafsineni katika utungo huu. (alama 1)
4. Huku ukitoa mifano, bainisha vipengele vinane vya kimtindo ambavyo nafsineni imetumia
kufanikisha uwasilishaji wa utungo huu. (alama 8)
5. Fafanua majukumu ya utungo huu katika jamii. (alama 5)
6. Jadili namna mbili ambavyo jamii ya kisasa inavyojaribu kuendeleza tungo za aina hii ili zisififie.
(alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI- 2019
KIDATO CHA NNE
1. (LAZIMA)
- Iwe insha ya ilani.
- Iwe na kichwa / mada.
- Iandikwe kwa mwendelezo.
Baadhi ya hoja:
(i) Kuchelewa.
(ii) Kelele darasani.
(iii)Wizi.
(iv) Kutoroka shule.
(v) Kupigana / kugombana.
(vi) Kuharibu vifaa na mali ya shule.
(vii) Dhuluma dhidi ya wanafunzi wengine.
(viii) Kutonadhifisha / kutojinadhifisha.
(ix) Kutokamilisha kazi ya mwalimu.
(x) Kutowaheshimu walimu na wafanyikazi wengine.
(xi) Kutovalia sare za shule.
2. Changamoto zinazowakumba vijana
- Ukosefu wa ajira / kazi
- Dawa za kulevya
- Magonjwa ya zinaa / ukimwi
- Umaskini
- Uigaji wa tamaduni potovu za kigeni.
- Athari za utandawazi / teknolojia
- Shirikizo la marika / maharimu.
- Ukosefu wa elimu / masomo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Malezi / ukosefu wa ushauri / kuelekezwa.
- Ndoa za mapema.
- Utamanduni uliopitwa na wakati k.v. tohara ya wasichana.
- Kuibuka kwa lugha ya sheng / misimu inayoathiri namna wanavyowasiliana.
- Kutoshirikishwa katika maamuzi.
3. Mbaazi ukikosa maua husingizia jua
- Aandike kisa kinachotoa / kinachodhihirisha maana ya methali.
- Kisa kinaweza kuonyesha / kuhusiana
- Mwanafunzi asiyefaulu masomoni kumlaumu mwalimu / mzazi.
- Mfanyikazi aliyekosa kupandishwa cheo / kuongezewa mshahara kumlaumu mwajiri.
- Mtoto aliyekosa kufaulu maishani kumlaumu mzazi.
- Wazazi wanaoshindwa kudhibiti nidhamu ya watoto wao kulaumu walimu.
4. Insha ya kumalizia
- Amalizie kwa maneno aliyopewa
- Mtahiniwa atumie nafsi ya kwanza kisha adhihirishe hali aliyojiingiza (lazima iwe mbaya).
- Baadaye aonyeshe jinsi alivyojuta.
- (insha ina safu / pande mbili)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MUGOR JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA LUGHA
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI- 2019
KIDATO CHA NNE
1. UFAHAMU (alama 15)
(A).
(i) Wizi wa mali ya umma
(ii) Vyeo na madaraka kutolewa hivi hivi tu
(iii)Uuzaji wa stakabadhi za serikali
(iv) Kuiba dawa
(v) Kuhonga ili kupata nafasi ya kusoma
(vi) Kutowajibika kazini ( 4 × 1 = 4)
(B).
(i) Kufilisisha serikali
(ii) Kunyima wagonjwa matibabu
(iii)Kuzorotesha maendeleo na huduma muhimu
(iv) Kupandisha vyeo wasiostahili
(v) Kazi kufanywa vibaya (3 × 1 = 3)
(C).
(i) Kuunda tume na kamati za uchunguzi
(ii) Kurudisha mali iliyoibwa
(iii)Kuwashtaki wahalifu ( 3 × 1 = 3)
(D)
(i) Uhaba wa kazi
(ii) Uozo katika jamii
(iii)Kuongezeka kwa umaskini
(iv) Tamaa ya anasa na starehe
(v) Uongozi mbaya
(vi) Kukosa huruma
(vii) Kukosa uzalendo ( 2 × 1 = 2 )
(E).
(i) Kashfa : Ufunuo wa siri ya jambo la aibu
(ii) Shamiri : Kuenea kwa jambo au habari
(iii)Waliohasiriwa : Waliodhuriwa / walioumizwa ( 3 × 1 = 3)
2. UFUPISHO
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(A).
(i) Watu kukosa kujiandaa
(ii) Husababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi
(iii)Serikali kutopasha ujumbe wa tahadhari / serikali kukosa kupasha ujumbe wa tahadhari
(iv) Wengine huishi nyanda za chini
(v) Wengine huishi kando ya mito
(vi) Ukosefu wa mikakati ya kutunzwa
(vii) Mafuriko mjini
(viii) Ujenzi katika maeneo yasiyostahili
(ix) Kuzibwa kwa mitaro
(x) Kezembea kwa maafisa kazini
(B).
(i) Mvua ya masika imeanza kushuhudiwa
(ii) Maafisa wa serikali wametakiwa kujiandaa
(iii)Habari hizi zinatia moyo
(iv) Ujio wa mvua ni Baraka kubwa
(v) Idara ya utabiri wa hali ya anga imeonya dhidi ya mafuriko na maafa.
(vi) Maafisa wa serikali kuwashauri wananchi / wananchi kuhamia maeneo salama.
3. MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
A. (i). Irabu zinapotamkwa hewa kutoka mapafuni haizuiliwi ilhali konsonanti zinapotamkwa hewa
huzuiliwa.
(ii). Kulinganisha – vikwamizo / menoni
- Kutofautisha - /th/ - sighuna, /dh/ - ghuna
B. Km. Maktaba, daktari, daftari.
C. Km. Sikumpiga, hakutulimia, hukunisomea.
D. – Kitenzi kishirikishi kipungufu
Uji u moto
- Nafsi ya pili umoja – Umenunua
- Kiambishi cha upatanisho wa ngeli – U – I, U – U, U – ZI, U – YA.
- Mwanzo wa nomino dhahania – Uzuri, Uzalendo
E. – Mwanafunzi aliyetia bidii ametuzwa
(Mwanafunzi atunge sentensi kamili)
F. – Kuonyesha habari ya ziada
- Kufungia maneno yasiyokuwa ya lazima
- Kuonyesha visawe
- Kufungia herufi / nambari za kuorodhesha.
(Atolee mfano kwa kila aina ya matumizi)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
G. “ Maliza kazi hii leo!” Mwalimu alimwamuru mwanafunzi.
H. (i). Hawa walipokea tuzo
(ii). Mwanasiasa mwadilifu huaminika / huaminiwa.
(iii). Wananchi wanaoishi / ambao wanaishi karibu na mto hawayachafui maji.
- Ingawa / ijapokuwa wananchi wanaishi karibu na mto hawayachafui maji.
I. (i). Matikiti maji yameuzwa masokoni
(ii). Tikiti za ndege zimenunuliwa
J. Km. Mbwa aliyepatwa na kichaa amekufa.
K. Mababa haya yanacheza na masichana haya malangoni.
L. Wazazi wana wajibu wa kuwalea waoto wao vyema.
M.
S
S1 S2
KN KT KN KT
N U N T E U N V T E
Baba na mama wameenda shambani huku watoto wao wakibaki nyumbani
N. (i). Chochote kimeibwa
(ii). Hayo yamenunuliwa
O. – Taadhima, staha
- Idhini , kibali
P. K.m:Kaka aliandikiwa barua yake na mjomba.
(Kadili sentensi ya mtahiniwa. Viungo vyote vifuatane hivi)
4. ISIMU JAMII
a) – Athari ya lugha ya mama / kwanza
- Kutoelewa kanuni za kisarufi za lugha husika
- Kuhamisha kanuni kutoka lugha hadi nyingine
- Upungufu katika viungo
- Maumbile ya mtu
- Makusudi
- Kuzungumza kwa haraka
(Hakiki hoja zingine)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b) – Uchache wa wazungumzaji
- Kutoungwa mkono na taasisi za kielimu
- Hadhi ya lugha
- Ndoa mseto
- Siasa
- Kuhama kwa watu
c) – upungufu wa msamiati
- Ujuzi wa lugha nyingi
- Kusisitiza au kufafanua jambo
- Kutenga watu Fulani katika mazungumzo
- Kujihusisha katika mawasiliano
- Kudhihirisha hisia mbalimbali
MUGOR JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA FASIHI
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI- 2019
KIDATO CHA NNE
1. USHAIRI
a) - Madhara
(i) Midomo hudondosha matusi
(ii) Midomo inatumiwa kesengenya
(iii)Midomo inavuruga Amani kwa kupayuka mitandaoni
(iv) Midomo inatumiwa na wanasiasa kuchochea chuki
(v) Midomo imezua ukabila
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(vi) Midomo inazusha balaa na fitina ( 4 × 1 = 4)
Jinsi ya kurekebisha
(i) Wenye midomo michafu waioshe
(ii) Tutumie midomo kuleta mwangaza gizani
(iii)Midomo itumiwe kusambaza Amani
(iv) Midomo itumiwe kuleta umoja na uwiano
(v) Midomo itumiwe kujenga udugu na utaifa ( 4 × 1 = 4)
b) (i) Tarbia – mishororo 4 kila ubeti
(kutaja ½ , kuelezea ½ - ½ × 2 = 1)
(ii) Mathnawi – kila mshororo una vipande viwili
(iii) Ukaraguni – Vina vinabadilika kutoka ubeti mmoja hadi mwingine.
c) (i) Kuboronga sarufi – Kamwe hawana mfyato ( ½ )
Umuhimu kuleta urari wa vina ( ½ )
(ii) Inkisari – kwazo, mezagaa ( ½ )
Umuhimu – kuleta urari wa mizani ( ½ )
d) – Kushauri – watu watumie midomo vizuri
- Kuonya – dhidi ya kutumia midomo
(kutaja 1, kuelezea 1 1 × 2 = 2)
e) (i) Urudiaji wa neno – Midomo
Umuhimu – kusisitiza / kutilia mkazo ujumbe.
(ii) Urudiaji wa silabi – beba, haba, waja, natija, kileja
Umuhimu – kujenga rithimu / kulipa shairi muonjo/ kulipa shairi mdundo wa kimuziki
(iii) Urudiaji wa sauti – fikiria, sikia, futulia, furahia
Umuhimu – kujenga rithimu/ kulipa shairi muonjo/ mdundo wa kimuziki.
(iv) Urudiaji wa mishororo / vishazi/ sentensi km. Midomo tuitunzeni, jamii kufurahia.
Umuhimu – kusisitiza / kutilia mkazo ujumbe
(za kwanza mbili × 2 = 4)
f) Mwananchi / mzalendo / mwanajamii ( al. 1 × 1 = 1)
SEHEMU B: RIWAYA – CHOZI LA HERI
2. Changamoto za ndoa ni kama;
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Kifo: Terry mkewe Ridhaa anaangamia kwenye moto na kumwacha Ridhaa na upweke, Lily mkewe
Mwangeka pia anaangamia kwenye moto huo.
(ii) Ukosefu wa watoto: Mwangemi na Neema hawakufaulu kupata mtoto katika ndoa yao iliwabidi
kupanga mtoto kwa jina Mwaliko.
(iii) Ukabila: Lucia Kiriri anaolewa kaika ukoo wa Anyamvua. Ndoa hii inakumbwa na pingamizi
kutoka kwa ukoo mzima.
(iv) Ukoo: subira mamake Lime na Mwanaheri Daina anaonewa na watu wa ukoo wa mumewe Kaizari
anaitwa muki kwa kuwa ametoka katika jamii ya Bamwezi anaposhindwa kuvumilia anawaacha
watoto wake hivyo basi ndoa yao inagonga mwamba.
(v) Wazazi kukataa watoto wao kuolewa: Wazazi wa Rehema wanakataa ndoa yake na Fumba
aliyekuwa amempachika mimba na Chandachema akazaliwa. Rehema alikuwa mwanafunzi wake
Fumba.
(vi) Ukosefu wa uaminifu: Chandachema anasema kuwa Bwana Tenge alikuwa na jicho la nje. Wakati
mkewe Bi Kimai alipoenda mashambani alileta wanawake tofauti machoni mwa wanawe.
(vii) Migogoro katika ndoa: Babake Pete anakosa kumkubali kama mwanawe kwa kuwa hawana
mshabaha naye hivyo basi Pete anapelekwa kulelewa na nyanya yake mzaa mama.
(viii) Chuki katika ndoa: Katika ndoa za mseto kuna chuki baina ya wake mfano; Pete anapoozwa kwa
Bw. Fungo anaonewa wivu na mke wapili na watoto wa mke wa kwanza wanamcheka, anaamua
kutoka kwa mzee Fungo.
(ix) Vita katika ndoa: Sauna anasema kuwa mamake alikuwa amedhulumiwa na mumewe Bwana Maya
hivi kwamba hangeuliza hata swalli anapouliza anakuwa mpokezi wa makondi, vitisho na matusi.
Hivyo basi Sauna hangemwambia mamake unyama aliotendewa na babake.
(x) Pombe: Mamake Sauna anasema kuwa babake mzazi wa Suala alijizika kwenye unywaji wa pombe
mitaani na kujisababisha kufutwa kazi. Hii ilisababisha umaskini. Alivuliwa kutoka umaskini na
Bwana Maya ndio maana hataki apakwe tope.
(xi) Umaskini: Naomi anamwacha mumewe Lunga baada ya Lunga kuachishwa kazi.
(xii) Upweke: Baada ya Naomi kuondoka alimwacha Lunga na upweke na hii inasababisha Lunga
kushikwa na ugonjwa wa shinikizo la damu baadaye anafariki. Kiriri pia anafariki kutokana na
ukiwa anapoachwa na mkewe Annette.
(xiii) Uhasama katika ndoa: Mzee Mwimo Msubili alikuwa ameoa wake wengi na wakapata watoto
wengi shamba alilokuwa nalo likakatwa katika vikataa ambavyo havingekidhi mahitaji yao yote.
Uhasama uliotokea kati ya familia yake ulisababisha yeye kuhamisha wake wawili katika msitu wa
Heri.
(xiv) Wazee kuoa wasichana wadogo: Mzee Fungo anamuoa Pete bila hiari yake ndoa hii
inasambaratika baadaye.
(xv) Tofauti za kisiasa: Selume ambaye wanatofautiana na mumewe na wakweze kisiasa wanaishia
kugombana mara kwa mara. Mambo yanapozidi Selume anafunganya virago na kwenda kuishi
kwenye kambi ya wakimbizi katika msitu wa mamba.
(xvi) Malezi ya watoto: Annette na Kiriri wanatofautiana na masuala ya utunzaji wa watoto wao.
Annette anamnyima Kiriri ushirika kwa malezi ya watoto wao wanapoenda kuishi na watoto wao
ughaibuni.
(xvii) Hofu katika ndoa: Baadhi ya wanawake wanahofia kuwa ndoa zao zitavunjika iwapo watawalea
watoto wa mama wengine waliokuwa wapenzi au wake wa waume zao. Hushikilia kuwa kuwalea
watoto hao ni njia ya kurudisha uhusiano waliokuwa waume zao na wanawake wa awali. Mf. Mke
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
aliyeolewa na Fumba huenda aliogopa kumlea Chandachema kwa kuogopa uhusiano kati ya Fumba
na rehema.
(xviii) Ndoa za kujaribisha: Nyangumi anataka kuishi na Pete kwa miezi miwili wajaribishe ndoa yao.
(xix) Wanawake kundanganywa na wanaume: Nyangumi anamdanganya Pete kuwa hakuwa ameoa
hapa Pete anaingia mtegoni na kuanza kuishi na Nyangumi kama mke na mume. Baada ya muda
mke wa Nyangumi anajitokeza na Pete anaishia kupata mtoto mwingine.
(xx) Wanandoa kutoacha nasaba zao baada ya kuoana: Naomi mkwe Lunga hasahau uhusiano wake
na nasaba yake inasemekana kuwa hatulii kupalilia maisha ya unyumba.
(xxi) Maonevu: Subira analalamikia kuonewa na wakwe zake kwa kuitwa mwizi hii inapelekea yeye
kuwacha mumewe na watoto wao.
(xxii) Usaliti katika ndoa: Billy alikuwa na matarajio kuwa angemuoa Sally baada ya kujenga nyumba
aliyodhania ingempendeza. Sally hapendezwi na nyumba yenyewe na anafunganya virago na kurudi
kwao anamwaacha Billy katika hali mbaya ya kukata tamaa. Naomi pia anamsaliti mumewe Lunga
licha ya kuwa Lunga anajisabilia kumpendeza kwa hali na mali lakini Naomi hampendi kamwe.
Alama (hoja 20 × 1 = 20)
3. (a) Huu ni wimbo unaoimbwa na Shamsi. Anaimba wimbo kuhusiana na hali ya kisiasa ilioko nchini ni
wimbo unaoonyesha kutamauka.
( 4 × 1 = 4 )
(b) Sifa za shamsi
− Msomi
− Mlevi
− Mkweli
− Matusi
− Akili pevu
(c) Wimbo wa shamsi;
(i) Ufisadi: shamsi analalamika kunyakuliwa kwa mashamba mf. Bw. Mabavu aliyenyakuwa shamba
na kusema kuwa alinunua mwenyewe. Alitoa hatimiliki bandia.
(ii) Umaskini: Ukosefu wa walionyang’anywa mashamba yao uliwafanya kuwa vibarua katika
mashamba yaliyonyakuliwa kutoka kwao.
(iii)Ukosefu wa ajira: Shamsi analalamika ukosefu wa ajira hata baada ya kuahidiwa kusoma kwa bidi
ili wapate kazi.
(iv) Ubaguzi: Shamsi alalamikia ubaguzi katika kutoa nafasi za kazi. Nafasi za kazi zinatawaliwa na
ndugu za wanasiasa.
(v) Mishahara duni: shamsi anasema kuwa wanapewa mishahara tumba.
(vi) Kufutwa kazi: Shamsi anasema kuwa walipolalamika kutopandishwa vyeo kazini walifutwa kwa
kuwa waliwazia kugoma na wangefilisi kampuni.
(vii) Njaa: Shamsi anasema kuwa baba yake alikufa kutokana na njaa ndiposa akageukia kula vijasumu/
mizizi mwitu.
(viii) Ukosefu wa hospitali: Shamsi anasema kuwa kijijini hakukuwepo hospitali ambapo babake
angepelekwa kupata matibabu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(ix) Ukosefu wa dawa: Hospitali za jijini ambapo maskini hutibiwa hazina dawa. Babake Shamsi
hakupata matibabu ya dharura hii ikapelekea kifo chake.
(x) Elimu: Shamsi anajigamba kuwa wa kwanza kuwika kwenye anga za elimu. Akapewa idhini ya
kuendeleza masomo/mamlaka ya kuwaza kwa niaba ya jamii.
(xi) Pombe haramu: Madhara ya pombe haramu yanaangaziwa – wengi wanakufa na wengine kupofuka
kwa kufaidi wauzaji wa pombe haramu.
(xii) Ukosefu wa uajibikaji: wanaporwa ardhi yao ila hawalalamiki
(xiii) Masaibu ya wafanyakazi: wanalipwa mshahara duni, mazingira duni kufutwa
(xiv) Dhuluma / unyanyasaji: Mabavu anawapokonya akina Shamsi ardhi..
(xv) Uskwota – Baba Shamsi anafanya kazi katika shamba alilonyang’anywa.
4. (a). – Maneno yanasemwa na Boza
- Akimwambia Sudi
- Wako katika karakana ya Chapakazi
- Sudi asema hawezi kula keki kwa kuwa ni mabaki na amekunywa chai ya mkewe na kutosheka.
( 4 × 1 = 4)
(b). Mzungumzaji Boza
- Mwenye ubinafsi
- Mchoyo
- Mwenye dharau
- Kibaraka
- Mwongo
- Mjinga
- Mwoga
- Msaliti
(c). Sudi alikuwa akiidunisha keki inayotengenezwa kwa ajili ya kusherehekea miaka sitini ya uhuru. (al. 2)
(d). Majoka hachezewi kwa kuwa:
(i) Anafunga soko la chapakazi ili ajenge hoteli ya kifahari katika sehemu hii.
(ii) Anapanga njama ya kifo cha Jabali mpizani wake.
(iii)Anapanga njama za kuzima uchunguzi wa Tunu kuhusu kifo cha Jabali.
(iv) Anafuja pesa za kusafisha soko.
(v) Anatumia mamlaka yake kudhibiti vyombo vya habari Sagamoyo.
(vi) Anatumia polisi kuwapiga na kuwanyanyasa waandamanaji.
(vii) Anafungulia biashara ya ukataji miti Sagamoyo kwa kutumia mamlaka yake bila kujali athari zake
kwa wananchi.
(viii) Anampa mama pima kibali cha kuuza pombe haramu akijua kuwa zinawaharibu wananchi.
(ix) Anatumia pesa za wafadhili kufadhili miradi isiyo muhimu.
(x) Anaamuru wafadhili wa wapinzani wavunje kambi za Sagamoyo.
(xi) Anatumia Chatu kuua Ngurumo – anaua wengi.
(xii) Anapanga njama ya kumuua Tunu – wavamizi wanamvunja mfupa wa muundi.
(xiii) Kumiliki kampuni inayotengeneza sumu ya nyoka.
(zozote 10 × 1 = 10)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
5. TAMTHILIA
Kwa kurejelea tamthilia ya kigogo, jadili mbinu-ishi unazojifunza kutokana na Tunu.
Mbinu – ishi ni mikakati ya kukabiliana na hali ngumu za maisha.
(i) Ujasiri: Majoka anapotaka kumuoza kwa mwanawe Ngao junior, Tunu anajijasirisha na
kumwambia kwamba hawezi kuolewa katika familia ya wahuni.
(ii) Kujidhibiti: Licha ya kutembea na Sudi ambaye ameoa hakuvuka mpaka wa uhusiano wao na kuwa
mpenziwe jinsi mkewe Sudi alivyokuwa akidhani. Lao lilikuwa ni kutetea haki za wanyonge.
(iii)Bidii: alijibiidisha katika harakati zake za kuwapigania raia. Licha ya kutembea kwa kiti cha
magurudumu, aliwatembelea hata walevi na kuwaomba kuhudhuria mkutano ambao ungefanyika
katika soko la chapakazi.
(iv) Msimamo dhabiti: Majoka anamshawishi kumuoza kwa mwanawe lakini anakataa katakata na
kumjibu kuwa atasubiri ili aolewe na mwanaume ampendaye.
(v) Mbinu za kushawishi: Anapotembelea walevi kule Mwangeni anawashawishi kuacha kunywa
pombe kwa kuwaeleza madhara yake. Anawaambia kwamba ilikuwa imewaua na kuwapofusha
wengi.
(vi) Ushirikiano: Anashirikiana na Sudi na raia wengine katika kupinga kufungwa kwa soko hali
inayosababisha kung’atuliwa mamlakani kwa Majoka.
(vii) Ustahimilivu: Licha ya kipigwa na kuumizwa mguu na kumbidi kutembea kwa magongo kwa
miezi mitatu, Tunu anavumilia masaibu haya yote na kuendelea kupinga kufungwa kwa soko.
(viii) Kutokata tamaa- Licha ya kupigwa na wahuni na kuumizwa mfupa wa muundi, hakukata
tamaa katika harakati zake za kupigania haki za raia wanyonge.
(ix) Kutolipiza kisasi – Licha ya kufahamu kwamba Ngurumo alihusika katika kumshambulia na
kumvunja mfupa wa muudi, hakulipiza kisasi.
(x) Kusoma: Majoka alipowadhulumu kwa kutaka kuwanyima fidia baada ya kifo cha babake kwa
madai kwamba hawakuwa na bima, Tunu aliamua kusomea uanasheria ili kuwasaidia wengine.
(xi) Kujitolea: alipofuzu masomo ya chuo kikuu, aliapa kujitolea kupigania haki za wanasagamoyo hata
kama ni kwa pumzi zake za mwisho.
(xii) Usemehevu: Mamapima anapoacha kupika pombe haramu na kuendelea kwake kuomba msamaha,
anamwambia kwamba yeye hana kinyongo naye.
(xiii) Uzalendo: Umuhimu wa uzalendo katika jamii hasa vijana.
(xiv) Huruma: kuwahurumia wana wa Sudi, Pendo na Pili. Kuwahurumia walevi.
(xv) Kujithamini: Anakataa kuolewa na Ngao Junior.
(xvi) Busara: Ni muhimu kuwa na busara maishani. Inamwezesha kusoma hadi chuo kikuu.
(xvii) Mwadilifu: Ni vizuri kuwa na maadili – hapendi ulevi licha ya kufuatana na Sudi kila mara
hawana uhusiano wa kimapenzi.
(xviii) Mshauri mwema: Anaowashauri Ngurumo na walevi wenzake dhidi ya matumizi mabaya.
(xix) Shukrani: Kumshukuru Siti kwa kuwa alikuja kumjulia hali. Anamshukuru kwa kukubali
kuwalinda wananchi badala ya kuwatawanya kama walivyofanya awali.
(xx) Utambuzi : Alitambua sauti ya mmoja wa majangili waliomvamia.
(zozote 20 × 1 = 20)
6. (a) Mawazo ya Dennis
(i) Anamrejelea mamake shakila
(ii) Katika ofisi ya shirika la uchapishaji wa magazeti
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(iii)Ni baada ya kumwona mamake Shakila (Pandikizi la mama) akipita huku akisubiri kufanya
mahojiano / usaili.
(b). Mbinu za lugha
Chuku – akanyagapo chini ardhi inatetemeka
Taswira – Picha ya ardhi ikitetemeka
Msemo / nahau – Kujitia hamnazo
(c). Sifa za msemaji
- Msomi
- Mapenzi ya dhati
- Bidii masomoni
- Mkakamavu
- Mwoga
(d) Madhila ya Kabwela
- Kukosa kazi katika shirika la magazeti
- Kuachwa na Penina
- Kukejeliwa na Dkt. Mabonga
- Hapewi pesa za masurufu na wazazi
- Kukosa kujibu maswali wakati wa mahojiano
- Njaa – anaamua kupika uji kama chamcha
- Hana nguo za kisasa/simu/tarakilishi
- Anasumbuka kiakili kwa sababu ya hali/asili/umaskini
- Kufukuzwa kwa Penina
- Shuka zake zimechanika
- Kukosa mpenzi chuoni
- Kusomea shule za hadhi ya chini
7. (a). Muktadha
- Mawazo ya sara
- Anajizungumzia
- Yuko chumbani mwake
- Baada ya kubakwa anapitia dhuluma nyingi na dhalimu wanaendelea kunafasika.
(b). Mbinu
- Takriri – dunia
- Uhuishi – msumari moto juu ya donda bichi
- Msemo – msumari moto juu ya donda bichi
- Jazanda sitiari – dunia ya msumari moto juu ya donda bichi.
(c). jadili athari za ubakaji ukirejelea hadithi ya ‘Mame Bakari’
(i) Kulia: Sara Analia anapokumbuka jinsi alivyobakwa usiku akitoka shuleni.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(ii) Kuapiza: Sara Analia na kuapiza janadume lililombaka na kumpachika mimba.
(iii)Aibu: Tunaambiwa kuwa mimba ya Sara iliyotokana na ubakaji ingemsababishia aibu na uduni kwa
wanadamu wenzake. Aidha alianza kuvaa jilabu ili kuificha mimba hiyo.
(iv) Kutengwa: kwa mfano Sara anaona kuwa angetengwa na jamii kutokana na tukio hilo.
(v) Kufukuzwa nyumbani: Sara anaona kuwa iwapo babake angejua kuwa yeye ni mjamzito
angemfukuza kutoka nyumbani kwao.
(vi) Kufukuzwa shuleni: Sara anaona kuwa iwapo mwalimu mkuu angejua ujauzito wake angemfukuza
kutoka shuleni.
(vii) Matusi: Sara anasema kuwa mwalimu mkuu angejua ujauzito wake angemwambia kuwa
hawafundishi wanawake bali wasichana na kumfukuza shuleni.
(viii) Woga: Ujauzito wa Sara ulimsababisha kuwaogopa wazazi wake hadi akawa anavaa jilabu ili
wasiutambue ujauzito huo. Aidha kwa sababu ya woga, sara anapanga na sarina kuwa Sara azalie
mashambani kwa wazazi wa sarina.
(ix) Mimba: Sara anapachikwa mimba baada ya kubakwa.
(x) Kisasi: Sara anatamani kulipiza kisasi dhidi ya janadume lililombaka.
(xi) Mauaji: Janadume lililombaka Sara lilipopatikana likijaribu kumbaka msichana mwingine lilipigwa
matofali likafa.
(xii) Kutoroka nyumbani: Sara alitoroka nyumbani kwao na kuhamia kwa akina Sarina na Beluwa
alikokuwa akipata vipimo vya ujauzito kutoka kwa Beluwa.
(xiii) Kutamani kujiua: Sara alitamani kujiua akaghairi nia.
(xiv) Kutamani kuavya mimba: Sara alitaka kuavya mimba lakini akabadili nia kutokana na shairi
alilokuwa amelisoma shuleni ‘usiniuwe’
(xv) Kulaumiwa: Katika jamii ya akina Sara kila siku linapotokea jambo la mwanamke kubakwa
mwanamume huwa hana kosa. Mwanamke ndiye shetani.
(xvi) Aliharibiwa ujanajike
(zozote 10 × 1 = 10)
SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI
1. Sifo – unamsifu shujaa na vita alivyopigania jamii yake.
“Kiguru mlomtajia hakimzuwii kufuma mishale”
“Mefagia vijiji vinane kwa pigo moja la kiganja chake”
“Mepigana vita visohisabika.”
(Mifano mingineyo ikadiriwe kulingana na jibu la mwanafunzi)
2. – Wafugaji – mepigana vita na mahasimu waliotuiba mifugo.
- Waume huoa wake wengi – uke wenza ukamhimiza kuchukua buruji kueneza habari.
- Vilema walitupwa kichakani – Nikaamua kupambana na jumuiya yangu ilosema kwa moja kauli
utokomezwe chakani utupwe.
3. Mama mzazi – Nilipokupokoa
4. Mbinu za kimtindo.
(i) Kejeli / stihizai/dhihaka – anaitwa jina la ajabu.
(ii) Chuku – Kijiji kizima kuja kuona mtoto
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kijiji kizima kuja kuona mtoto
Maadui elfu kufa anaposhika silaha, “Naposhika zana, maadui elfu huanguka
“Mefagia vijiji vinane kwa pigo moja la kiganja chake.
Mwili kuwa na nguvu za majagina mia moja.
(iii)Tashbihi – Maadui wamwonapo hutetemeka kama jani
Kuwayeyusha kama barafu
Mwana mliombaa ja ukoma
Mlomwinga ja nyuni wala mtama
Mfano wa Shaka Zulu.
(iv) Sitiari / Jazanda – umekuwa nahodha
Akili yako Sumaku
Watukuka ewe shibli (mtoto wa Simba)
(v) Usambamba – Likalovya change kidari
Likanavya chako kipaji
Wakanipa unyonge
Wakanituma kuola
Wakanitanabahisha
(vi) Ritifaa – anazungumza na mahasidi ambao hawapo kana kwamba wapo.
“Tazameni mahasidi mloteka, Teko la dharau mlonimwaiya, mkanitia ukiwa
usomithilika!”
(vii) Taswira – mama alivyolia na kujilovya machozi pamoja na mwanaye
Kijiji kizima kinavyomiminika kwake kuona mwanaye
Shujaa alivyopigania jamii yake vita dhidi ya mahasidi.
(viii) Mishata – “Hajawahi kuonekana kama huyu…tangu kuumbwa kwa ulimwengu”
Nikaamua alakulihali kupambana na yangu jumuiya…ilosema kwa moja kauli
Tazameni mahasidi mloteka…Teko la dharau mlonimwaiya
Mepigana vita visohesabika..Na wetu mahasimu waliotupoka na mifugo.
(ix) Kikale / Lahaja – Wakayatuma maozi kutazama weye
Wakanitumia kuola vitungo vyako
Likanavya chako kisari
Teko la dharau mloniwaiya
Oleni! Tungeni macho
Mlomwinga ja nyuni
(x) Inkisari – ulokumeza ilosema, mloteka, mlonimwaiya, mlomwinga, mefagia, mepigana, metawa,
mesheheni, alowaonjesha.
(xi) Tabdila – mepigana vita visohisabika
(xii) Kuboronga sarufi – wakaupa unyonge moyo wangu toto
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mepigana vita visohesabika, na wetu mahasimu.
Nikaamua alakulihali kupambana na yangu jumuiya.
(xiii) Nidaa – Mimi si mjalana!, katu sivyo wasemavyo walimwengu!
Mkatanitia ukiwa usomithilika!, Oleni! Tungeni macho!
(xiv) Tashihisi /uhuishi/uhaishaji – alfajiri lipoukumbatia ulimwengu.
Akili yako nyepesi hupakata yote
(xv) Msemo / nahau – mfano wa Shaka Zulu, alowaonjesha kivumbi wapinzani
5. Umuhimu wa sifo/ majukumu.
(i) Husifu watu / viongozi kutokana na matendo yao mazuri / chanya.
(ii) Hutangaza mafakikio au mchango wa anayesifiwa.
(iii) Hukuza uzalendo kwa kuwahimiza watu kuiga matendo mazuri ya anayesifiwa.
(iv) Huburudisha / hutumbuiza watu katika sherehe Fulani.
(v) Huonyesha msimamo na mitazamo ya jamii Fulani kuhusu masuala mbalimbali k.v chuki kwa
usaliti, unafiki.
(vi) Huweka kumbukumbu au rekodi ya matukio ya kihistoria.
6. (i) Nyimbo hizi zinaimbwa katika hafla za kisiasa/ sherehe za kutawaza viongozi/ sherehe za kitaifa.
(ii) Huimbwa katika tamasha za muziki. (Shuleni na vyuoni)
(iii)Kutafitiwa na kurekodiwa katika maandishi, vinasasauti/ tepurekoda, video, filamu na sinema.
(iv) Zinaimba redioni na kuonyesha kwenye runinga.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYAMIRA JOINT EXAMINATION
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA INSHA
MUDA: SAA 1 3/4
MAAGIZO:
a) Jibu Maswali mawili.
b) Swali la kwanza ni lazima.
c) Chagua la pili kutoka maswali yaliobaki.
d) Kila swali lina alama 20, Insha yako isipungue maneno mia nne.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Swali la kwanza ( lazima)
5. Wewe ni Gavana wa gatuzi mojawapo katika nchi ya Kongomano. Wakaazi wa mji wa Songambele
wamekiuka sheria zilizowekwa na baraza la gatuzi hilo. Waandikie ilani
6. Jitihada za kumwinua mtoto wa kike zimepeleka kudhalilisha kwa mtoto wa kiume. Jadili.
7. Andika kisa kitachodhihirisha maana ya methali.
Ulimi huuma kuliko meno
8. Tunga kisa kitakapomalizika kwa kauli ifuatayo.
……………………. Nilijitazama na kujidharau. Kwani nini nilijiingiza katika hali hii? Nilijuta.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYAMIRA JOINT EXAMINATION
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA PILI
LUGHA
MUDA: SAA 2 1/2
MAAGIZO:
a) Andika jina lako na nambari yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu
b) Andika tarehe ya mtihani na utie sahihi yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu
c) Jibu maswali yote.
d) Andika majibu yako katika nafasi ulizoachiwa baada ya kila swali katika kijitabu hiki cha maswali.
e) Usitoe ukurasa wowote kutoka kwenye kijitabu hiki.
f) Watahiniwa ni lazima waangalie kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa sawasawa na kuwa
maswali yote yamo
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE
Sehemu Upeo Alama
A 15
B 15
C 40
D 10
Jumla 80
E. UFAHAMU (ALAMA 15)
Soma makala yafuatayo kasha ujibu maswali
Ajali haina kinga. Watu wengi wanapotajiwa neno ajali, fikira zao hukimbilia moja kwa moja hadi
barabarani. Mara chachemawazo yao huenda viwandani, mashambani au kwenye viwanja vya
michezo. Ni nadra sana watu kufikiraia kuwa nyumbani ndiko ajali nyingi zinztokea.
Idadi kubwa ya ajali nyumbani hutokea kimchezo tu. Watu wengi wameteleza msalani na wanapata
majeraha mabaya. Wengine wameteleza walipokanyaga vitu vyenye unyevu sakafuni, kama vile
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
mafuta, mabaki ya chakula au hata maganda ya ndizi. Ulemavu walio nao watoto na hata watu wazima
hutokana na ajali kama hizi wasizofikiria wtu wengi.
Ajali vilevile hutokea watu wanapozama katika shughuli au kupata jazba kuu ya kutenda. Katika hali
hii, huweza kujiumiza au kuwaumiza wengine bila kujua.
Hapa tunazungumzia watu ambao hujaribu kubebe mizigo yenye uzani wasiokadiria. Madhara huwa
kuteguka viungo na kuchanika misuli. Aghalabu hulemewa na kubanwa. Mwandishi wa makala haya
siku moja alipanda kibao kuangika picha ukutani. Ingawa alikuwa mfupi, ari ilimsukuma
kuchuchumia. Matokeo ni kibao kilijisukuma nyuma. Mhusika alianguka akajigonga kidevu. Kitendo
hiki kilisababisha yeye kujiuma ulimi vibaya. Kuvunjika jino na hata kuzirai. Bahati ni kuwa
alikuwepo mtu aliyempa huduma ya kwanza na kumkimbiza hospitalini.
Hat hivyo ajali nyingi hutokana na vifaa vya nyumbani. Zana hizi ni pamoja na visu, meko ya gesi,
mashine zinazotumia umeme na kadhalika na huwa hatari sana, hasa kwa watoto. Kitu kidogo hata
kama wembe huweza kusababisha madhara makubwa. Kwa hakika hakuna yeyote kati yetu, hata
waliokulia katika makasri ya fahari asiye na kovu. Makovu haya ambayo tunayaficha katika mavazi
yetu ni ishara ya majeraha kutokana na ajali nyumbani. Je una kovu lolote?
Unakumbuka ulivyolipata?
Ingawa ajali hizi haziepukiki, yawezekana kuzipunguza. Ni muhimu kukuza tabia na mazoea ya kuwa
waangalifu nyumbani. Kwa mfano, ni hatari kuepua chungu chenye maji yanayotokota mekoni kwa
mikono mitupu. Aidha ni kutowajibika kuchanganya kitu chochote chenye unyevu na mafuta moto
mekoni. Watu wengi wamebambuka ngozi na nyumba kuteketea kwa namna hii. Kwa hivyo ni vizuri
kupata ujuzi wa jinsi ya kutumia vifaa na kuhakikisha tunavirudisha ipasavyo.
Jambo la tatu na muhimu zaidi ni kuwepo kwa vifaa pamoja na uwezo wa kutoa huduma ya kwanza.
Inawezekana kuokoa maisha au kuounguza majeraha kwa kuchukua hatua za dharura.
Maswali
1. Eleza maana ya methali ‘Ajali haina kinga’ (alama 2)
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
2. Kwa nini mwandishi anasema ajali nyumbani hutokea kimchezo? (alama 3)
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
3. Ni mambo gani mengine yanayosababisha ajali nyumbani? (alama 3)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
4. Onyesha vile invyowezekana kupunguza ajali nyumbani. (alama 3)
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………
5. Eleza maana ya:
(i) Jazba
………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
(ii) Makasri
………………………………………………………………………………………………
…………………………………………….…………………
(iii) Makovu
………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
(iv) Kuepua
………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
F. UFUPISHO (Alama 15)
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali
Ardhi ni mali ya taifa. Hivyo inampasa kila raia kuinafidhi. Hii ina maana kwamba hatuna budi
kuwarithisa wana na wjukuu, vitukuu na vilembwe, vining’ina na wapwa zetu ardhi yenye rutuba.
Ardhi ndiyo chanzo cha riziki zote. Fauka ya hayo, ardhi ni dafina kubwa.
Tangu asili ardhi hii imefunikwa na joho la miti na majani. Rutuba ilienea kila mahali. Lakini wakati
ulifika ambapo wanadamu hawakuvumilia kukaa bila kuitumia johari hii. Walishika maparange na
mashoka. Wakafyeka majani na miti yote. Wakalima wakapanda na kuvuna.
Kisha walihama hapo. Waliendelea kufanya hivyo mwaka hadi mwaka. Hali ya kufyeka sehemu
mbalimbali za nchi, kuchoma mioto ovyo, kuwa na mifugo mingi na kutojua kuhifadhi ardhi vizuri
kulileta mavuno hafifu kila mwaka.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mvua iliponyesha matone ya mvua yaligonga ardhi. Maji yakajiri kwa nguvu na kutawanya chembe za
udongo. Wakati wa kiangazi udongo ulipokauka, upepo mkali ulichukua tabaka la juu. Hivyo ikawa
mazao hayawezi kustawi. Hatimaye nchi ikawa kama mkuranga. Mambo haya yakasababisha
mmomonyoko wa juu juu halafu mwanzo wa michirizi na mwisho makorongo na maporomoko ya
ardhi.
Walakini basi ya kale hayapo. Sasa wakuu wa serikali yetu ya Insafu wamekuhimizeni, ikiwa mu
wakulima, mpande zaidi. Wamewashauri namna ya kuongeza mavuno katika mashamba yenu kwa
maarifa bora ya zaraa, kama vile kuunafidhi udongo, kutumia mbolea, njia za kunyunyizia dawa
makondeni ili kuua wadudud wanaoharibu mimea, na kutumia maarifa malihi katika kupanda mbegu.
Kwa wale ambao si wakulima, serikali yetu ya Insafu imeweka shule za mafundisho maalum na
kumhimiza kila mmoja wao aongeze maarifa yake na afanye kazi kwa tabasuri na bidii ili aongeze
mapato yake na mapato ya serikali pia. Katika sehemu nyingine maelezo ya wakuu wa serikali
yamefuatwa barabara, na kumetokea maongezeko malihi ya mazao.
Walakini pia katika sehemu hizo maongezeko yake hayakutosha sana. Katika sehemu nyingine kwa
bahati mbaya watu wamepotezwa na watu wakaidi ambao kwa kutaka ushaufu,
Wamewaambia watu kuwa njia rahisi na nyepesi ya kujipatia serikali ya kujitawala yenyewe, na
wamewashawishi na kuwatisha baadhi ya watu waasi amri za serikali zihusuzo zaraa. Wahaini hao
wametibua mambo. Ni watu wa kuaili na ni afkani.
Maswali
a. Fupisha ujumbe wa aya tatu za kwanza kwa maneno 80. (alama 9, 1 ya mtiririko)
Matayarisho.
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
Nakala Safi
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………….………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
b. Eleza masuala ambayo mwandishi anaibua katika aya mbili za mwisho kwa maneno 60.
(alama 6, 1 ya mtiririko)
Matayarisho.
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………
Nakala Safi
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………
G. MATUMIZI YA LUGHA
(a) Taja sauti mbili ambazo huitwa likwidi (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………….……………………
(b) Andika neno lililo na muundo wa silabi ufuatao (alama 1)
IKKI ………………………………………………………………………………………
(c) Ainisha viambishi katika neno lifuatalo (al. 2)
Yafutikayo……………………………………………………………………………
(d) Tambua aina mbili za sentensi ukizingatia uamilifu na utoe mfano mmoja kwa kila moja
(ala. 2)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(e) Ainisha vielezi vya namna katika sentensi hii (ala. 2)
Mzee huyu mkongwe alicheka kijinga huku akila haraka haraka
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
(f) Ainisha vishazi katika sentensi ifuatayo (ala. 2)
Kijana aliyezungumza na nyanyake ameingia katika darasa lililochafuliwa na wanafunzi
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(g) Changanua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha mstari (ala. 3)
Mwanafunzi mwerevu sana aliyekuwa mgonjwa jana amepelekwa nyumbani
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
…………………………………….………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(h) Bainisha shamirisho na chagizo katika sentensi ifuatayo (ala. 3)
Somo aliukata mti kwa kisu jana asubuhi
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(i) Andika kwa usemi wa taarifa (ala. 3)
Karani: Njoo nikutume kwa babu yangu.
Karanja: Sitaki kupita njia ya kwa babu
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
(j) Eleza matumizi ya ‘ni’ katika sentensi hii (ala. 2)
Ingieni darasani mara moja ili niwape zoezi ambalo ni rahisi
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(k) Eleza maana ya sentensi ifuatayo (ala. 2)
(i) Ningalisoma kwa bidii ningalipita mtihani
(ii) Ningesoma kwa bidii ningepita mtihani
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(l) Andika katika udogo wingi (ala. 2)
Mti wa msonobari unatengeneza meza nzuri sana
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………
(m) Tambua miundo yoyote mitatu ya ngeli ya LI-YA (ala. 3)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(n) Eleza maana tatu za sentensi ifuatayo (ala. 3)
Alisema angeenda kwao
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………
(o) Andika upya sentensi ifuatayo katika hali sambavu (ala. 1)
Mwanafunzi anasoma darasani
………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………….…………………
(p) Tumia neno ‘hadi’ kuonyesha mahali na wakati katika sentensi (ala. 2)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
(q) Yakinisha katika hali ya mazoea. (ala. 2)
Asiyeugua hahitaji daktari
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
(r) Tunga sentensi ukitumia neno ‘komaa’ kama (ala. 2)
(i) Kivumishi
………………………………………………………………………………
(ii) Nomino
………………………………………………………………………………
(s) Taja matumizi yoyote mawili ya kistari kirefu (ala. 2)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………
H. ISIMU JAMII
(a) Kwa nini kulikuwa na haja ya kusanifisha Kiswahili? Toa sababu tano (ala. 5)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
………………………………………………………………………………………………………
………
(b) Fafanua sifa za lugha ya kazi (ala. 5)
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………
………………………………
NYAMIRA JOINT EXAMINATION
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA TATU
FASIHI
MUDA: SAA 2 1/2
MAAGIZO:
b) Andika jina lako na nambari yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu
c) Andika tarehe ya mtihani na utie sahihi yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu
d) Jibu maswali manne pekee
e) Swali la kwanza ni la lazima.
f) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki; yaani Riwaya, Tamthilia,
Ushairi, Fasihi simulizi.
g) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja
h) Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU A:
“Tumbo Lisiloshiba na hadithi nyingine”
Swali la lazima
1. “Akanyangapo chini ardhi inatetemeka…………………..
Amejitia hamnazo. Kabwela kama mimi nina faida gani?
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (ala. 4)
(b) Fafanua mbinu tatu za lugha zilizotumiwa katika dondoo hili (ala. 6)
(c) Eleza madhila kumi yaliyompata Kabwela (ala. 10)
SEHEMU B:
Chozi la heri
Chagua swali la 2 au 3
2. “………….. wanahofia kusema wasije wakavikata viganja vinavyowalisha…………..
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (ala. 4)
(b) Taja maudhui yanayojitokeza katika dondoo hili na ueleze (ala. 2)
(c) Kwa kutoa hoja kumi, eleza namna maudhui uliyotaja hapo juu (2b) yanavyojitokeza katika riwaya
(ala. 10)
(d) Eleza sifa nne za msemaji (ala. 4)
3. (a) Migogoro ni maudhui muhimu katika riwaya hii. Fafanua (ala. 10)
(b) Uozo umetamalaki katika jamii ya Chozi la Heri. Tetea kauli hii kwa kutolea hija kumi
zilizoelezwa (ala. 10)
SEHEMU C: TAMTHILIA
Kogogo
Jibu swali la 4 au 5
4. “Na mwamba ngoma huvuta wapi?”
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (ala. 4)
(b) Tambua tamathali mbili za sauti zilizotumika katika muktadha huo (ala. 2)
(c) Fafanua sifa za msemewa wa maneno (ala. 6)
(d) Thibitisha ukweli kuwa kila mwamba ngoma huvuta kwake ukirejelea Tamthilia nzima ya Kigogo
(ala. 8)
5. “Utawala wa Majoka katika jimbo la Sagamoyo umejaa sumu ya nyokas”
Jadili usemi huo kwa kurejelea tamthilia ya Kigogo (ala. 20)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU D: USHAIRI
Jibu swali la 6 au la 7
6. Shairi
La adhabu hili wingu, lataka kutunyeea
Himahima kwalo vungu, pasi nako kuchelea,
Kujikinga hili wingu, sije katunyeshea.
Wengineo hawajali, wasinayo wasiwasi,
Tahadhari hawabali, wajiunge nasi
Aidha watafakali, mengine yalo hasi.
Vua hili halibagui, jinsia wala umri,
Na kama hawajui, tuwajuze vizuri,
Kwani siso adui, kuwao msumari.
Tangazo haliwapiku, wahimizwa kujikinge,
Wingu hili la usiku, ukicheza likuringe,
Latutia usumaku, daima likunyonge.
Vumilia kwalo vungu, nje kuna dhoruba,
Yavuma kwa machungu, bila lolote huba,
Tunza chako kijungu, fungia kwalo juba.
Japo nafika tamati, nawaacha tafakari,
Madhara linalo wananti, wingu hili sukari,
Daima mwape kujiseti, mjitunze kujijari
Maswali
1. Eleza ujumbe wa mwandishi katika ubeti wa nne (ala. 2)
2. Onyesha ufundi wa kimuundo wa mwandishi katika utunzi wa shairi hili (ala. 4)
3. Eleza namna jazanda imetumika katika utungo huu. (ala. 2)
4. Kwa kuzingatia idadi ya mishororo katika beti tambua aina ya ushairi huu (ala. 1)
5. Tamthini ustadi wa mshairi katika matumizi yaidhini ya kishairi (ala. 3)
6. Litie shairi hili katika bahari tatu tofauti (ala. 3)
7. Andika ubeti wanne kwa lugha ya tutumbi (ala. 4)
8. Eleza sifa moja ya nafsi neni katika shairi hili (ala. 1)
7. Ushairi
Soma shairi lifuatalo kasha ujibu maswali yanayofuata
1. Maendeleo ya umma
Sio vitu maghalani
Kama tele vimesaki
Lakini havishikiki
Ama havikamatiki
Ni kama jinga la moto
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Bei juu
2. Maendeleo ya umma
Sio vitu gulioni
Kuviona madukani
Kuvishika mikononi
Na huku wavitamani
Kama tama ya fisi
Kuvipata ng’o
3. Maendeleo ya umma
Sio vitu shubakani
Dhiki ni kwa mafakiri
Nafuu kwa matajiri
Ni wao tu washitiri
Huo ni ustiimari
lo! Warudia
4. Maendeleo ya umma
Ni vitu kumilikiwa
Na wanyonge kupatiwa
Kwa bei kuzingatiwa
Bila ya kudhulumiwa
Na hata kuhadaiwa
Hiyo ni haki
5. Maendeleo ya umma
Dola kudhibiti vitu
Vijapo nchini mwetu
Na kuwauzia watu
Toka nguo na sapatu
Pasibakishiwe na kitu
Huo usawa
6. Maendeleo ya umma
Watu kuwa na kauli
Katika zao shughuli
Vikaoni kujadili
Na mwisho kuyakubali
Maamuzi halali
Udikteta la
7. Maendeleo ya umma
Watu kuwa waungwana
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Vijakazi na watwana
Nchini kuwa hakuna
Wote kuheshimiana
Wazee hata vijana
Maswali
(a) Toa anwani mwafaka ya shairi hili (ala. 1)
(b) Shairi hili ni la aina gani? Toa sababu zako (ala. 2)
(c) Eleza dhamira ya mwandishi kuandika shairi hili (ala. 3)
(d) Toa mifano miwili ya urudiaji katika shairi hili, Je urudiaji huu una kazi/majukumu gani?
(ala. 4)
(e) Onyesha matumizi mawili ya tamathali za usemi katika shairi hili (ala. 4)
(f) Eleza toni ya mshairi. Toa sababu (ala. 2)
(g) Nafsi neni ni nani? (ala. 1)
(h) Toa mfano mmoja wa twasira katika hili. Je, twasira hiyo inajengwa na nani?
(ala. 3)
SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI
8. (a) Fafanua sifa za matambiko katika jamii (ala. 4)
(b) Eleza tofauti kati ya maigizo ya kawaida na maonyesho ya sanaa (ala. 10)
(c) Taja shughuli zozote mbili zinazoonyesha matumizi ya Ulumbi katika jamii ya kisasa
(ala. 2)
(d) Tofautisha dhana zifuatazo
(i) Miviga na maapizo (ala. 2)
(ii) Ngoma na ngomezi (ala. 2)
NYAMIRA JOINT EXAMINATION
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA KWANZA
INSHA
MWONGOZO WA INSHA
1. Ni insha ya ilani:Majibu pia yanaweza kushirikisha tahadhari ya katibu kuhusu mambo ambayo
yanaweza kuwatia ndani watu kwa mujibu wa sheria za baraza.
Baadhi ya hoja ni
5. Wakaazi hawaruhusiwi kufuga mifugo kama ng’ombe, mbuzi, kondoo, punda
6. Kutolipa ada zinazotozwa na gatuzi
7. Kufungua biashara pahala pasiporuhusiwa na bila leseni
8. Uchafuzi wa mji kwa kutupa taka ovyo ovyo, kukojoa mitaani, maji taka.
9. Ujenzi wa nyumba bila idhini ya wataalamu wa gatuzi
10. Magari ya matatu kupitia katika maeneo yasiyoruhusiwa
11. Biashara haramu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
12. Uuzaji wa bidhaa ghushi
13. Kughushi Leseni
Matokeo ya Ukiukaji
Kufunguliwa mashtaka
Kutozwa faini
Kuny’ang’anywa leseni
Magari kufungiwa kwa muda Fulani
Muundo
Anwani: Ilani kwa wakaazi wa mji……
(Neno Ilani lazima lijitokezee) Tarehe
Utangulizi: Atambue anayetoa Ilani
Mwili: - Azungumzie maudhui na hatua zitakazochukuliwa.
Uhimizo: ataje mtoaji wa ilani, na cheo chake
2. Jitihada za kumwinua mtoto wa kike zimepelekea kudhalilishwa kwa mtoto wa kiume. Jadili
Hii ni insha ya mjadala
1. Kimsingi insha hii ina sehemu mbili; mtoto wa kike na jinsi anainuliwa huku pia kukiwa na mtoto
wa kiume na jinsi amedhalilishwa.
2. Mtahiniwa aweza kuwa na hoja nyingi upande mmoja mradi kila upande uwe na angalau hoja tatu
3. Mwisho yafaa mtahiniwa atoe msimamo wake kuhusu mjadala huu. Je yeye aunga upande gani?
4. Amedhalilishwa kwa miaka na miaka
5. Amedhalilishwa na utamaduni
6. Anapigwa na waume na pia mabwana zao.
7. Anafanyishwa kazi nyingi za nyumbani hususa za jikoni.
8. Anaozwa mapema tena kwa wazee
9. Anajisiwa, anabakwa, achafuliwa
10. Anyimwa nafasi ya kupata elimu
11. Anyimwa urithi wa wazaziwe na mumewe.
12. Apashwa tohara ya lazima
13. Arithiwa na shemejiwe mumewe aagapo
14. Apatapo mimba afukuzwa shuleni
Jinsi mtoto wa kiume amedhalilishwa
1. Miradi mingi na hela nyingi zimetengewa motto wa kike.
2. Mashirika mengi yamebuniwa kutetea mtoto wa kike na wanawake, mfano chama cha maendeleo ya
wanawake.
3. Alama za wasichana kuingia vyuo vikuu zimeshushwa kiasi.
4. Shule za mabweni za wasichana nyingi ilhali mtoto wa kiume ameachwa kumezwa na magenge
kama vile munguki na pombe haramu
5. Wakati jamii inamtetea mtoto wa kike ilhali mtoto wa kiume ameachwa ajiamulie hatima yake bila
mtetezi wa moja kwa moja.
3. Mwanafunzi aandike insha ilete ukweli wa methali.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mkasa uliosababishwa na maneno yaliyosemwa na mtu.
4. Mtahiniwa atumie nafsi ya kwanza.
Adhihirishe hali aliyojiingiza. (Lazima iwe mbaya. Aonyeshe jinsi alivyojuta.
(insha ina safu mbili)
NYAMIRA JOINT EXAMINATION
TRIAL 3
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA PILI
LUGHA
MWONGOZO WA LUGHA
SEHEMU A: UFAHAMU (Alama 15)
6. Ajali hutokea bila kutarajia (ala. 2)
7. Hutokana na ajali wasiofikiria watu wengi kama vile kuteleza msalani.
Aidha wengine huteleza walipokanyaga vitu vyenye unyevu sakafuni.
Watu wazima na watotohulemazwa na ajali hizi. (ala. 3)
8. (i) Watu wanapozama katika shughuli au kupata jazba ya kutenda kazi
(ii) Kuubeba mzigo wenye uzani usiokadiriwa.
(iii)Ukiwa umepanda juu ya kibao kuangika picha ukutani
(iv) Ajali kutokana na vifaa vya nyumbani k.v. visu, meko ya gasi, mashine zinazotumia umeme n.k.
(ala. 3)
9. (i) kukuza tabia na mazoea ya kuwa waangalifu nyumbani
(ii) Ni vizuri kupata ujuzi wa jinsi ya kutumia vifaa na kuhakikisha tunavirusha ipasavyo
(iii)Kuwepo kwa vifaa pamoja na uwezo wa kutoa huduma ya kwanza.
10. (i) Jazba - Msisimko/ msukumo / hamu kuu
(ii) Makasri - Majumba ya kifahari
(iii)Makovu - Alama / mabaki yatokayo na majeraha
(iv) Kuepua - Kutoa kitu mekoni
SEHEMU B: MWONGOZO WA UFUPISHO
a) Ujumbe wa aya 3 za kwanza:
✓ Ardhi ni mali ya taifa na inarithishwa vizazi
✓ Ndiyo chanzo cha riziki nan i dafina kubwa
✓ Awali ilifunikwa na miti na matawi
✓ Ilikuwa na rotuba
✓ Binadamu waliharibu mazingira kwa kufyeka
✓ Hili liliwaletea mavuno hafifu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
✓ Matone ya mvua yalitawanya chembe za udongo
✓ Upepo ukachukua tabaka la juu la ardhi
✓ Hili likapoteza udongo wa rutuba
✓ Mazao hayakustawi
✓ Matokeo yakawa mmonyoko na maporomoko ya ardhi
(Hoja 8 x 1) (+ 1 ya mtiririko)
b) Masuala ya aya 2 za mwisho:
✓ Serikali inahimiza wakulima kupanda zaidi
✓ Watumie maarifa bora ya zaraa. Mfano: kunadhifu udongo, kutumia mbolea na kadhalika.
✓ Wasio wakulima serikali imefungua shule za mafundisho maalum ili waongeze maarifa na
bidii kazini.
✓ Kule maelezo ya serikali yalikofuatwa barabara, kumekuwa na maongezeko ya mazao.
✓ Walakini kuna watu wanaopotosha wengine kuwa waasi amri za serikali kuhusu zaraa
(Hoja 5 x 1 + 1 ya mtiririko)
SEHEMU C: MATUMIZI YA LUGHA
(a) (i) /r/ (ala. 1)
(ii) /l/
(b) IKKI – Imba / imla (ala. 1)
(c) Ya – Ik - a - yo
Ngeli kauli kiishio “o”rejeshi (ala. 2)
(d) Taarifa - mama amefika
Amri - fungeni mlango! Mbili, moja au
Ombi - Tafadhali nisamehe sufuri
Swali - unatoka wapi! Lazima atoe mfano ili
Mshangao - Salaale! Umeiba apate alama 2 / 0 (ala. 2)
(e) Kijinga - namna mfanano (ala. 2)
Haraka haraka - namna kikariri
(f) (i) Kijana aliyemzungumza na nyanyake - Kishazi tegemezi
(ii) Ameingia katika darasa lililochafuliwa na wanafunzi - Hura
(iii)Lililochafuliwa na wanafunzi
Lazima atambue – Kishazi tegemezi cha kwanza ilia pate
(ala. 2)
(g) S1/2 KN1/2 (N + r + E + S) 1 + KT1/2 (T + E) 1/2 (ala. 3)
(h) Mti - kipozi
Kisu - ala
Chagizo - jana asubuhi (ala. 3)
(i) Karani alimwita Karanja ili amtume kwababu yake lakini alimwambia hakutaka kupita njia hiyo ya
kwa babu yake (ala. 3)
(j) Ingieni - wingi
Darasani - mahali ndani
Niwape - nafsi
Ni - kitenzi kishirikishi kipungufu (ala. 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(k) (i) Ningalisoma kwa bidii ningalipita mtihani – hakuna ewezekano
(ii) Ningesoma kwa bidii ningepita mtihani - kuna uwezekano (ala. 2)
(l) Vijiti vya msonobali hutengeneza vijimeza vizuri (ala. 2)
(m) JI – MA kwa mfano Jicho - macho
JI – ME jiko - meko
Q - MA gari - magari (ala. 3)
(n) (i) Ataenda kwa mtu mwingine
(ii) Yeye ataenda labda alikozaliwa (ala. 3)
(iii)Nafsi ya tatu (’a’)
(o) Mwanafunzi asoma / yuasoma darasani (ala. 1)
(p) (i) Nilitembea hadi sokoni - mahali
(ii) Nilifunza hadi jioni - wakati (ala. 2)
(q) Auguaye huhitaji daktari (ala. 2)
(r) Kivumishi - Mkomavu
Nomino - Ukomavu (ala. 2)
(s) (i) Kutoa maelezo ya ziada
(ii) Kuonyesha mabadiliko ya ghafla
(iii)Kuonyesha nani aliyesema maneno Fulani (ala. 2)
SEHEMU D: ISIMU JAMII
(a) (i) Tatizo la mawasiliano kutokana na wingi wa lahaja
(ii) Haja ya kuwepo kwa lugha moja ya mawasiliano
(iii) Haja ya kusawazisha maandishi ya kitaalamu
(iv) Kurahisisha shughuli za kidini
(v) Haja ya kuwepo kwa lugha moja inayofahamika na kila anayekifahamu Kiswahili
(vi) Haja ya kuondoa tofauti katika namna ya kuendeleza maneno kwa sababu hati tofauti
zilifumiwa kuandikwa Kiswahili
(b) (i) Uzingatia ukweli wa mambo bila porojo au uzushi
(ii) Istilahi za taaluma husika hutumika; kila taaluma ina istilahi zake.
(iii) Lugha ya heshima / adabu
(iv) Lugha rasmi hutumika
(v) Lugha kavu
(vi) Lugha yenye mantiki – mtiririko unaofaa
(vii) Huelezea mambo bila mapendeleo au kuonyesha hisia za mzungumzaji
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYAMIRA JOINT EXAMINATION
TRIAL 3
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA TATU
FASIHI
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
9. (a) Eleza muktadha wa dondoo hili (ala. 4)
Msemaji - mawazo yake Dennis
Alikuwa anarejerea Shakira
Mahali - Katika afisi ya Shirika la kuchapisha magazeti
Tukio - Ni baada ya kumwona mamake Shakira (pandikizi la mama) akipita huku akisubiri kufanya
mahojiano.
(d) Fafanua mbinu za lugha zilizotumiwa katika dondoo hili (alama 6)
Chuku - Akanyagapo chini, ardhi inatetemeka.
Taswira - picha ya ardhi ikitetemeka
Msemo/ Nahau - kujitia hamnazo
Za kwanza 3 x 2 = 6
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kutaja - 1
Maelezo - 1
(e) Eleza madhila kumi yaliyompata Kabwela (alama 10)
(j) Anakosa kazi katika shirika la magazeti
(ii) Kuachwa na Penina
(iii) Kukejeliwa na Daktari Mabonga
(iv) Hapewi pesa za masurufu na wazazi
(v) Kushindwa kujibu maswali wakati wa mahojiano – anaaibika
(vi) Njaa – Anaamua kupika uji
(vii) Hana nguo za kisasa/ simu/tarakilishi n.k.
(viii) Anasumbuka kiakili kwa sababu ya hali /asili/umaskini
(ix) Kufukuzwa na Penina
(x) Shuka zake zimechanika
SEHEMU B: CHOZI LA HERI
10. “……………. Wanahofia kusema wasije wakavikata viganja vinanyowalisha …………….”
(a) Eleza Muktadha wa dondoo hili (alama 4)
Msemaji: Mwaliko
Msemwa: Mwangemi
Mahali: katika hoteli ya Majaliwa ambapo wote wawili walikuwa wameenda
Tukio: Wanaongea kuhusu ndugu zake Mwaliko, Umulkheri na Dickson, waliokuwa
wametoroshwa na Auntie Sauna. Mwangemi anampa Mwaliko matumaini kuwa wako hai na bila
shaka wangekutana. Mwaliko anashuku kukutana kwake na ndugu zake kwa kuwa polisi
hawakuwajibika ipasavyo kuwafuata kutokana na kuhongwa na walaguzi wa watoto.
(b) Taja maudhui yanayojitokeza katika dondoo hili.
Maudhui ya ufisadi
(c) Kwa kutumia hoja kumi, eleza namna maudhui uliyotaja hapo juu (1b) yanajitokeza riwayani
(alama 10)
(i) Viongozi wanawanunua raia ili wawapigie kura
(ii) Hazima ya jitegemee inayotarajiwa kuwapa vijana mtaji wa kuanzisha biashara inaandamwa
na ukabila na unasaba.
(iii) Viongozi wananyakua maelfu ya maelfu ya ekari na kujenga viwanda na maduka ya bishara.
(iv) Katika ukurasa wa 57 watu walilaghaiwa na kuuziwa shamba la wenyewe kwa njia za
kifisadi
(v) Majumba ya Ridhaa yalibomolewa kwa kisingizio kuwa yalinjengwa katika eneo
lililotengewa ujenzi wa barabara mbadala. Barabara haikujengwa na shamba la Ridhaa
kunyakuliwa.
(vi) Katika uk 41 tunapata kuwa kuna tume za kupigana na ufisadi ambazo zinaundwaa, na
jambo hili ni ishara kuwa kuna ufisadi unaoendelezwa.
(vii) Pia katika uk 13, “Uchukuzi wa milungula pia ni aina ya ufisadi katika serikali” “Wengine
walionekana wakitoa milungula hadharani, wengine wakatishia kuishtaki, uizara husika
kwa kile walichokiita ukiukaji wa haki za umiliki mali”
(viii) Wasimamizi wa hospitali wananyakua dawa na kuziuza kwenye maduka yao
(ix) Uongozi haumpi Shamsi kazi baada ya kuhitimu. Unamtaka atoe hongo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(x) Bwana mabavu ananyakua shamba la kina Shamsi kiasili na kuwageuza vibarua kwenye
shamba lao.
(xi) Familia ya bwana Kute inafisidi chakula cha msaada kwa kujigawa mara tatu kupata mara
tatu zaidi ya posho waliyopata wengine.
(xii) Baada ya kutangazia raia kuwa msitu wa mamba ni marufuku, viongozi wanaendeleza
ukataji wa miti na uchomaji wa makaa usiku.
(xiii) Baadhi ya viongozi wananyakua hata madhabahu kwenye mlima wa nasibu ili kujenga
hoteli kubwa za kitalii
(xiv) Halmashauri ya elimu inawasaliti wanafunzi wanaotoka katika familia maskini kwa
kuwapa mikopo wanafunzi kutoka familia zinazojiweza na kuwacha wanafunzi maskini
wajifanyie vibarua ili kujilipia karo.
(d) Eleza sifa nne za mzungumzi (alama 4)
(i) Msomi - anasoma hadi chuo kikuu na kuhitimu kwa shahada ya isimu na lugha
(ii) Mdadisi - Anamuuliza Mwangemi kama anadhani kuwa ndugu zake Dick (Dickson) na
Umulkheri (Umu) wako hai
(iii) Mwenye haya - Anacheka kwa haya Neema anapomuuliza kama alikuwa anataka
kuwaletea mkaza mwana.
(iv) Mwenye Kumbukumbu - Anakumbuka kuwa dada yake Umulkheri (Umu) alimwambia
kuwa mamke alimwacha akiwa na umri wa miaka mitano
(v) Mwenye shukrani - Anawashukuru wazazi wake Mwangemi na Neema ambao
walijisabilia kumwelimisha licha ya kuwa hakuwa mwanao halisi.
(vi) Mwenye bidii - Anafanya kazi yake kwa bidii ya mchwa katika kampuni ya magazeti ya
Tabora kama mhariri katika kitengo cha biashara. Tunaelezwa kuwa Mwaliko anaifanya
kazi yake kwa bidii ya Mchwa.
(vii) Mwenye mapenzi ya dhati - Anawapenda wazazi wake, Mwangemi na Neema kwa dhati.
Anamwambia Neema “Nitakwenda nawe mama”
11. (a) Migogoro katika Chozi la Heri
Migogoro ni hali ya kuwepo kwa mivutano/mikinzano/mfarakano baina ya wahusika katika kazi ya
fasihi. K.m.
1. Mgogoro kati ya Mzee Kedi na familia ya Ridhaa wakati mzee Kedi anashiriki katika mauaji ya
familia ya Ridhaa.
2. Mgogoro shuleni kati ya Ridhaa na wanafunzi wenzake wanapomwita “mfuata mvua”
3. Mgogoro wa kijnsia kati ya Mwekevu na Mgombea wa kiume. Mwekevu anarushiwa cheche za
matumizi.
4. Mgogoro wa kijamii unajitokeza baada ya mkoloni kupuuza sera za mwafrika za umiliki wa
ardhi.
5. Mgogoro katika familia yam zee Mwimo Msubili kwa sababu familia yake ilikuwa kubwa na
hangeitosheleza kwa chakula.
6. Mgonjwa mmoja kwenye hospitali ya mwanzo mpya anapata majeraha mabaya baada ya
kuvamiwa kwenye mzozo wa ardhi kule Tamuchungu.
7. Panatokea mgogoro kati ya baba na mama Pete. (uk 147)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
8. Ridhaa anajipata katika hali ya mgogoro wa nafsi. (uk. 12) ……… baada ya muda wa mvutano
wa hisis na mawazo.
9. Mgogoro wa kisiasa kuhusu ni nani atakayekuwa kiongozi wa jamii kati ya mwanamme na
mwanamke (uk. 19)
10. Mgogoro kati ya raia na polisi wakiwa katika harakati za kudumisha amani (uk. 19)
11. Nyamvula anajikuta katika mgogoro wa nafsi yake wakati ambapo imani yake inakinzana na
kazi ya mmewe ya kuwa mwanajeshi (uk.62) (10 x 1= 10)
(b) Uozo katika Chozi la Heri
1. Kuvunjika kwa ndoa/ kuwacha waume k.m. Naomi, Subira.
2. Mapenzi kati ya baba mlezi na bintiye Sauna alipopachikwa mimba na babake.
3. Wanawake kuavya mimba. Mamake Sauna anamsaidia mwanawe kuavya mimba.
4. Wizi/uporaji wa mali. Nyumba na maduka yaliporwa wakati wa vita vya baada ya kutawazewa
kwa kiongozi mpya.
5. Ukatili. Mabarobaro wanawavamia watu na kuwafanya unyama …. Uk 25 alikula mikato miwili
ya sime akazirai kwa uchungu.
6. Uendelezaji wa biashara haramu km. ulanguzi wa watoto
7. Ubakaji. Lime na Mwanaheri walibakwa babayao akitazama
8. Ulanguzi wa dawa za kulevya. Dick anafanya kazi ya kusafirisha dawa za kulevya
9. Kutupwa kwa watoto wachanga, km. kitoto Nasibu
10. Matumizi ya pombe haramu - vijana wa vyuo vikuu wanabugia pombe na kufanya wengine
kuaga dunia
11. Ukeketaji wa watoto wa kike
12. Mauaji. Watu kupigwa risasi na kuuawa kam kuku
13. Ndoa za mapema – Pete aliolewa akiwa mdogo.
14. Ukosefu wa malezi bora- Naomi na Subira kuwaacha watoto wao.
15. Ufisadi – watu kunyakua sehemu zilizotengewa ujenzi wa barabara.
16. Ubaguzi wa kikabila
(10 x 1 = 10)
SEHEMU C: KIGOGO
12. “Na mwamba ngoma huvuta wapi?
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
(i) Msemajio ni Kenga
(ii) Msemewa ni Majoka
(iii) Wako katika ofisi ya Majoka
(iv) Ni baada ya Majoka kumwelezea kuhusu habari gazetini kuhus umaarufu wa Tunu
(1 x 4 = 4)
(b) Tambua tamathali mbili za semi zilizotumika katika muktadha huu (alama 2)
(i) Methali – mwamba ngoma huvuta……
(ii) Swala la balagha - huvuta wapi?
(1 x 2 = 2)
(c) Fafanua sifa sita za msemewa wa maneno haya
Msemewa ni Majoka
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Ni katili – alishiriki katika mauaji ya Jabali
(ii) Ni mkware - Alikuwa amemuoa Husda lakini alitaka kujihusisha kimapenzi na Ashua
(iii) Ni mpyaro – aliwatukana wanasagamoyo wajinga
(iv) Ni fisadi – alinyakua mali ya uma kam vile soko la chapakazi
(v) Ni msaliti – Aliwasliti wanasagamoyo kwa kuwa walimchagua ilhali anajinufaisha yeye,
pia anamsaliti Husda kimapenzi.
(vi) Ni mwenye dharau
(vii) Ni laghai
(viii) Ni dikteta
(ix) Ni mwoga
(1 x 6 = 6)
(d) Thibitisha ukweli kuwa kila mwamba ngoma huvuta kwake ukirejelea Tamthilia nzima ya
Kigogo (alama 8)
(i) Kenga anamfuata Majoka na uongozi dhalimu kwani ananufaika nao. Mfano ardhi
(ii) Ngurumo anaunga mkono uongozi thalimu wa Majoka ili aendelee kunufaika. Mfano
pombe.
(iii) Mama pima anautetea uongozi wa Majoka kwa kuwa ananufaika nao, mfano. Kandarasi ya
kuoka keki, kibali cha kuuza pombe haramu
(iv) Majoka ana ari ya kuwafurusha wafanyabiashara kutoka sokoni ili alinyakue kwa matumizi
yake kibinafsi ya kujenga hoteli ya kifahari.
(v) Wafadhili wa kina Tunu wanatia habari chumvi kuhusu umaarufu wa Tunu.
(vi) Wanapolisi wanayafuata maagizo ya Majoka ya kuwashambulia wanasagamoyo ili walinde
kazi yao.
(vii) Chopi anatekeleza uhuni wa Majoka ndiposa asije akamwaga unga wake. (Kufutwa kazi)
(viii) Husda anaolewa na Majoka kwa sababu ya utajiri wa Majoka.
(ix) Boza anajipendekeza kwa kenga ili apewe mradi wa kuchonga kinyago. Pia anasema mke
wake ndiye aliyeioka keki (8 x 1 = 8)
13. KIGOGO
Sumu ya nyoka husababisha madhara mengi kwa mhusika/ kiwemo kuua. Kuna mambo mengi
yanayodhuru au kuwaua wananchi katika utawala wa Majoka.
(i) Unyakuzi wa ardhi - majoka na mshairi wajifurahia eneo la soko la chapakazi ili ajenge
hoteli iya kifahari
(ii) Kuamrisha askari kutawanya waandamanaji na kuasababisha kifo cha vijana watatu
(iii) Vitisho – wanaharakati wanaopinga utawala wa Majoka wanatishwa. Kuna vikaratasi
vinavyorushwa katika makazi yao ili wahame (siti anamweleza mamake Tunu)
(iv) Kuangamiza wapinzani wake – Jabali aliuawa kwa njama za Majoka na chama chake bila
kikasambarakati
(v) Ukosefu wa utu. Majoka hathamani utu/uhai wa mtu. Majoka anaamrisha watu wapigwe
risasi bila kujali.
(vi) Tengatawala – uhasama unapandwa na viongozi ili kuwagaza wananchi mf. Sudi ana
uhasama na Boza sababu wako katika mirengo tofauti ya kisiasa.
(vii) Kuzorota kwa maendeleo. Jimbo la Sagamoyo limetimiza miaka sitini ya uhuru lakini bado
liko nyuma kimaendeleo.
(viii) Rushwa - Mamapima anatoa hongo ya uroda kwa Ngurumo ilia pate mradi wa kuoka keki
ya uhuru.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(ix) Elimu mbovu – elimu inayotolewa katika shule za kifahari inawalemeza vijana badala ya
kuwandaa wawe wazalendo Majoka and majoka academy.
(x) Utawala wa kiimla – majoka anataka aendelee kutawala ingawa urubani umemshinda na
amekwisha zorotesha nchi.
(xi) Matabaka – Sumu ya nyoka iliyozagaa katika jimbo la Sagamoyo imesababisha kuwapo
kwa matabaka. Mambwenyenye – majoka, Kenga - maskini - wananchi
(xii) Uvivu na ubwete – Majoka ni kiongozi ambaye hajali umuhimu wa kazi. Anatenga mwezi
mmoja ya kupumzika katika kuadhimisha miaka 60 ya uhuru.
(xiii) Ukimtamba – Majoka ana rasilimali nyingi na miradi mingi mikubwa. Anamiliki Majoka
and Majoka Company, Majoka and Majoka modern resort
(xiv) Ukoloni mamboleo. Jimbo la sagamoyo linaongozwa kwa mikono amabayo halipwa kwa
muda mrefu. Halipwa kwa vizazi vya sasa na hata vyavyo
(xv) Ufujaji wa fedha za umma. “mikopo iliyochukuliwa haikutumika vizuri. Kenga
anamweleza Sudi kuwa akikubali kuchonga kinyago cha marara bin Ngao angepata fedha
za kubadilisha maisha yake.
(xvi) Kuwafunga raia bila sababu – mf. Ashua kutiwa mbarani ili iwe funzo kwa Sudi
(xvii) Kupanga njama ya kumwua Tunu.
(xviii) Kufunga soko la chapakazi ambayo ni tegemeo kwa raia wa sokomoko
(xix) Majoka anamwambia Kenga lazima chatu mmoja atolewe kafara (auawe)
(xx) Anapanga kutumia mamlaka kuzima uchunguzi wa Tunu kuhusu kifo cha jabali
(xxi) Anafuja pesa za kusafisha soko la chapakazi
(xxii) Anatumia mamlaka yake kudhibiti vyombo vya habari
SEHEMU YA D: USHAIRI
SHAIRI LA A
1. Eleza ujumbe wa mwandishi katika ubeti wa nne (alama 2)
Hatari ya wingu na umuhimu wa kujikinga
Anasema tangazo haliwapiti, wahimizwa kujikinga na hatari (2 x 1 = 2)
2. Onyesha ufundi wa kimuundo wa mwandishi katika utunzi wa shairi hili (alama 4)
i. Ametumia beti sita
ii. Kila ubeti una mishororo mitatu
iii. Vina vimepangwa kwa mtindo wa ukaraguni
iv. Idadi ya vipande katika kila mshororo ni viwili
v. Idadi ya mizani inatofautiana katika mishororo (4 x 1 = 4)
3. Eleza namna jazanda imetumika katika utungo huu (alama 2)
i. Wingu - ni hatari iliyopo
ii. Vungu - ni mikakati ya kujikinga kutokana na hatari yenyewe (2 x 1 = 2)
4. Kwa kuzingztia idadi ya mishororo katika beti tambua aina ya ushairi huu (alama 1)
Tamthlitha – kila ubeti una mishororo mitatu (1 x 1 = 1)
5. Tamthini ustadi wa mshairi katika matumizi ya idhini ya kishairi (alama 3)
i. Inkisari – yalo – yaliyo
ii. Lahaja – wananti – wananchi
iii. Tabdila – tafakali – tafakari (3 x 1 = 3)
6. Litie shairi hili katika bahari tatu tofauti (alama 3)
i. Mathnawi – jina vipande viwili katika kila mshororo
ii. Ukaraguni – vina vyake vinafanana kulingana na beti. Vinabadilika kutegemea ubeti
iii. Tathlitha – lina mishororo mitatu kila ubeti (3 x 1= 4)
7. Andika ubeti wane kwa lugha ya kwaida / tutumbi (alama 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Hampitwi na tangazo linalowahimiza mjikinge na hatari hii kwani ukiichezea kwa vile ina nguvu za
kukuvuta na kukuua.
8. Eleza sifa mmoja ya nafsi neni katika shairi hili (alama 1)
Mshawishi/ mwelekezi mwema
Daima mwape kujiseti, mjitunze kujijari
Vumilia kwalo vungu, nje kuna dhoruba
SHAIRI LA B
a) Maendeleo ya umma (1 x 1 = 1)
b) Ni shairi huru - halina mpangilio wa vina
Mahususi
Idadi ya mizani inabadilika
Mishororo haitoshani (aina alama 1)
(sabau alama1)
c) Kuonyesha ni mambo gani muhimu katika maendeleo ya umma kama vile kuheshimiana usawa na
kumiliki vitu (alama 3)
d) Urudiaji wa maneno Kusisitiza
Urudiaji muundo – mstari wa kwanza
Urudiaji wa silabi - Urari wa vina (3 x 2 = 6)
e) Jazanda tama ya fisi
Istiari - dola – shilingi (2 x 2 = 4)
f) Masikitiko – baada ya kuondoka mkoloni walidhani hali ingeimarika kutaja al. 1
Sababu al. 1
g) Ni msimulizi (1 x 1 = 1)
h) Vitu kubaki gulioni – kuviona madukani wanaoweza kununua ni matajiri pekee (al. 1)
Msimulizi anarejelea maskini asiyejiweza kiuchumi na hawezi kumudu bei ya bidhaa madukani
SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI
8. a) Sifa
1. Hutolewa na wazee maarufu walioteuliwa.
2. Hufanywa mahali maalum k.v. pangoni, mwituni n.k.
3. Huandamana na sala
4. Huandamana na utoaji kafara k.v. kuchinja mbuzi, n.k
5. Huandamana na maombi (Hoja 5 x 1 = 5)
b) Tofauti
Maigizo yakawaida Sanaa yamaonyesho
✓ Mazingira ya kuzua/maalum ✓ Hutumia mazingira halisi
✓ Matukio ya kuiga ✓ Matumio halisi/ ya kila siku
✓ Huwa na wahusika na hadhira maalum ✓ Washiriki na waigizaji walio pia hadhira
✓ Matumizi ya ukumbi na jukwaa maalum ✓ Hakuna haja ya ukumbi wala jukwaa
✓ Hutumia maleba na vifaa vya kuzua
mazingira maalum
✓ Hakuna vifaa maalum bali huwa mazingira
yenyewe
✓ Hugawika katika maonyesho kutumia ✓ Muundo wake hufululuza au hayajagawika
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
lugha kwa njia maalum katika maonyesho
✓ Wahusika hufanya mazoezi kabla ya igizo
halisi
✓ Hawahitaji kufanya mazoezi kwa nini
matukio ya kila siku
✓ Huwa na malipo ✓ Hamna malipo
(Hoja 5 x 2 = 10)
c) Miktadha ambamo ulumbi hutumika katika jamii
i. Katika mijidala bungeni
ii. Katika hotuba za kisiasa
iii. Katika mahubiri maabadini
iv. Katika mijadala shuleni
v. Kortini
vi. Katika shughuli za kijamii k.v. posa
vii. Katika sala / dua
viii. Katika maapizo
ix. Katika malumbano ya utani
x. Katika majigambo/ vivugo
d) (i) Miviga ni ibada au sherehe za kitamanduni ambazo kwa kawaida ufanywa kipindi Fulani cha
mwaka. Sherehe hizi utaratibu wa sanaa za kimaonyesho.
Maapizo ni kauli za kuomba Mungu, miungu au mizimu kumwadhibu mtu Fulani au watu
katika jamii kutokana na matendo yao maovu. (2 x 1 = 2)
(ii) Ngoma ni unenguaji wa viungo vya mwili kuambatana na midundo maalum ya ala za muziki
au mahadha ya muziki wenyewe.
Ngomezi ni maigizo ya sanaa ya kuwasilisha ujumbe kwa kutumia ngoma
(2 x 1 = 2)
NYANDARUA JOINT EXAMINATION
MWIGO : JULY/AGOSTI 2019.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
102/1
KISWAHILI INSHA
KARATASI YA KWANZA
MUDA : SAA 1 ¾
MAAGIZO
1. Andika insha mbili pekee
2. Insha ya kwanza ni ya lazima
3. Chagua insha moja nyingine kutoka hizo tatu zilizosalia
4. Kila insha isipungue maneno mia nne (400)
5. Kila insha ina Alana 20.
KARATASI 1.
1. Wewe ni mwananchi aliyekerwa na ukosefu wa umoja baina ya wakenya kama taifa. Andika Hotuba
utakayotoa kwenye sherehe xa kitaifa ukipandekeza hatua zinazoweza kuchukuliwa ili kujenga umonja wa
uzalendo nchini
2. Fafanua namna ya kukabiliana na tatizo sugu la ufisadi nchini
3. Andika kisa kinachothibitisha ukweli wa methali hii. Kutangulia sio kufika.
4. Tunga kisa kitakachomalizika kwa maneno yafuatayo.
….. nilipofitazama nilijidharau kwa aibu niliyojipa, Niliapa kutorudia kitendo hicho maishani mwangu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYANDARUA JOINT EXAMINATION
102/2
KISWAHILI
LUGHA
KARATASI 2
MUDA: SAA 2 ½
102/2
KISWAHILI
LUGHA
KARATASI 2
MUDA: SAA 2 ½
MAAGIZO
a) Andika jina lako na nambari yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
b) Tia sahihi yako na tarehe ya mtihani katika nafasi ylizoachiwa .
c) Jibu maswali yote. Andika majibu yako katika nafasi zilizoachwa katika kijitabu hiki cha
maswali.
d) Karatasi hii ina ukurasa tisa zilizopigwa chapa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
e) Watahiniwa lazima waangalie kama kurasa zote zimepigwa chapa sawasawa na
kwamba maswali yote yamo.
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE
SWALI UPEO ALAMA
1 15
2 15
3 40
4 10
Jumla 80
A. UFAHAMU (alama 15) Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali.
Mwanamke wa kisasa anazaliwa na kukulia katika mazingira yaliyobadilika mno. Matazamio yake maishani ni tofauti
kabisa na yale ya wanawake walioishi mapote mawili yaliyopita; wanawake makamu ya nyanyake na mamake-kuu.
Yeye hatarajii kuzaliwa, kukua, kuolewa, kuwa mke wa bwana, kumzalia mumewe watoto, na daima dawamu kuwa
'mwendani wa vijungu jikoni' akawapikia watoto na bwanake chakula; na akitoka jikoni aelekee shambani kulima,
kichakani kuchanja kuni, mtoni kufua nguo na kuteka maji ya kutumia nyumbani. Mwanamke wa kisasa
huandamananamwanamume. Akanyagapo mume, naye papo huutia wayo wake.
Mwanamke wa kisasa huenda shule na kujifunza yote yafunzwayo huko. Hushindana na wanawake kwa wanaume
na kuibuka mshindi si mara haba. Huibuka mshindi katika masomo ya lugha, historia, jiografia, hesabu, sayansi na
mengineyo, sawa na mwanamume.
Mwanamke wa kisasa hutakakufanyakaziyakibega,akazifanya. Akatakakuwamwalimu,akawa. Akataka kuwa daktari,
akafanikiwa. Almuradi, siku hizi mwanamke hufanya kazi yoyote ile afanyayo mwanamume. Kuna wanawake
marubani wa ndege, masonara, waashi, wahandisi, madereva wa magari, mawakili, mahakimu, mawaziri wakuu na
hata marais wa nchi. Hakuna kazi isiyofanywa na mwanamke siku hizi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mwanamke wa kisasa hateswi akafyata ulimi. Anapohiniwa yeye hupigania haki yake kwa dhati na hamasa. Katu
hakubali 'mahali pake' katika jamii alipotengewa na wanaume wenye mawazo ya kuhifadhi yaliyopitwa na wakati.
Siku hizi mwanamke huolewa tu wakati amepata kazi ya kumwezesha kujikimu maishani au pale anapokuwa na
hakika kwamba biashara yake, iwapo ni mfanyi biashara, imepiga hatua ya kutomrudisha ukatani.
Mwanamke wa kisasa haamuliwi katikajambo lolote, bali hufanya maamuzi yake mwenyewe. Kwa upande
mwingine, mwanamume wa 'kisasa', ambaye bado amefungwa pingu na taasubi za kiume. hapendezwi na
mwanamke huyu. Huuma kidole akatamani ya kale, lakini wapi! Analazimika kumkubali mwanamke huyu kama
mshirika sawa maishani, na kuishi naye, apende asipende. Shingo upande analazimika kukubali kwambamabadiliko
haya sio mithili yakiwingu kipitacho, bali ni ya aushi.
Maswali:
a) Msemo 'mwendani wa vijungujiko' unadhihirishahali gani ya mwanamke katikajamii? (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
b) Jamii imemfanya mwanamke kuwa hayawaniwamizigo. Fafanua (alama l) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
c) Eleza maana ya'akanyagapo mume, naye papo huutia wayo wake." (alama 2) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
d) Zungumzia maswala ya ndoa na elimu huku ukilinganisha mwanamke wa kiasili na wa kisasa (alama 2)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
e) Mwanamume wa kisasa anamwonaje mwanamke wa kisasa? (alama2) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
f) Taja mifano minne ya 'mawazo yakihafidhina'. (alama 4) ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………
g) Eleza maana ya: i. Taasubi za kiume.
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………
ii. Aushi (alama2) ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
a)Tunga sentensi ya neno moja yenye sehemu zifuatazo ala.3
i) Kikanushi cha nafsi ya pili umoja
ii) Kikanushi cha wakati uliopita
iii) Nafsi ya mtendwa umoja
iv) Mzizi wa kitenzi cha silabi moja
v) Kauli ya kutendesha
vi) Kauli tenda
b) Fafanua jinsi ya kutamka sauti zifuatazo ala.2
/u/
/ch/
c. Onyesha muundo wa silabi za kwanza katika maneno yafuatayo ala.1
i) Chwewa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii) Ah!
d) Tenga silabi katika neno alimhukumu ala.1
e) Eleza dhana ya mofimu katika neno msalaba ala.1
f) Onyesha miundo yoyote miwili ya maneno katika ngeli ya u-zi ala.1
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
g) Tunga sentensi yenye utaratibu KT pekee cha T+ S ala.2
h) Fafanua matumizi ya alama ya kiulizio na parandesi katika sentensi zifuatazo ala.2
i) Utakuja leo au kesho?
ii) Tamthilia ni kisa kifupi kinachowasilishwa jukwaani (wamitila,2002)
i)Huku ukitolea mifano, taja sifa zozote mbili za vishazi tegemezi ala.2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
j)Tumia kirai husishi kinachofanya kazi kama kielezi cha mahali kwenye sentensi ala.2
k) Tumia kiunganishi cha kujumlisha katika sentensi ala.2
l) Tumia neno uwanjani kwenye sentensi kama ala.2
a) Nomino
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b)Kielezi
m) Changanua sentensi hii kwa njia ya matawi ala.4
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
n) Bainisha aina za yambwa na chagizo katika sentensi ala.2
Mkate mtamu uliokuwa juzi kwa makaa kuwafaa watoto mayatima
p) Weka shadda kwenye neno “ala” kuibua maana mbili ala.2
q) Tumia kihusishi cha A-unganifu chenye maana ya hali katika sentensi. ala.2
r) Panda ni neno lenye maana ya kukwea/kuelekea juu. Eleza maana nyingine mbili ala.1
s) Kanusha sentensi hii ala1
Msichana mrembo atatujia kesho.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
t) Andika kinyume ala.2
Koo alimfukuza na kumdona jogoo.
u) Onyesha majukumu ya ni katika sentensi/kauli hii ala.2
“Huu niwimbo nitakaowafunza, Ombenimkiingia ugani”
v) Eleza maana ya “tendama” kama kauli ala.1
ii)Andika neno “suka” katika kauli ya kutendata ala.1
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
w) Andika upya sentensi ifuatayo kulingana na maagizo ala.1
Nimekuja kuonana nawe ili unipe msaada wa kifedha
Anza kwa:
Kusudi….
ISIMU JAMII ala.10
SOMA KISHA UJIBU MASWALI
ONYO! ONYO! ONYO!
UVUTAJI WA SIGARA NA BANGI UNADHURU AFYA YAKO.
a) Tambua sajili ya makala haya ala.1
b) Fafanua sifa za sajili kama zilivyojitokeza kwenye maandishi ala.3
c) Taja sifa nyingine mbili za sajili hii ambazo haziko kwenye makala ala.2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
d) Eleza dhana zifuatazo ala.4
i)Lafudhi
ii) Lahaja
iii) Isimu jamii
iv) Wingi lugha
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA (SIRI)
1. Swali la 1
Hii ni insha ya Hotuba.
a) Kichwa - Hotuba kuhusu hatua zinazoweza kuchuliwi kuleta umoja.
b) Utangulizi/mwanzo - Salamu kwa waliohudhuria kwa kuanzia na walio na vyeo vya juu
hadi mabibi na mambwana
- kujitambulisha kwa jina
- mtahiniwa adhihirishe lenge la hotuba yake (aya ya kwanza)
c) Mwili wa Hotuba – ndiye sehemu yenye hoja. Haki kasha kila hoja imeandikwa katika aya
Hoja (sita)
d) Mwisho - aya ya mwisho
- Mtahiniwa anaweza kumalikia kwa usemi ama kusisitiza hoja muhimu
Katika Hotuba
- Hadhira yaweza kupewa changamoto kuhusu suala kuu la Hotuba.
- Anayehutubu anaweza kuitakia hadhira kila la heri.
Tazama (Tanbihi)
Akikosa sura aondolewe alama 4S (baada ya kutuzwa).
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Maudhui
i) Ukabila upigwe vita
ii) Michezo na shughule za uigizaji ziandaliwe
iii) Viongozi wawe mifano bora isiyo na ubaguzi
iv) Watu wazima wawe mifano bora/vielelezo vizuri
v) Vyana vya kisiasa visiwe vya kikabila
vi) viongozi wa dini wahubiri kuhusu umoja na uzalendo
vii) Wasanii watunge tungo za kuhimiza uzalendo na umoja nchini.
ix) Ukabila upigwe marufuku
x) Watoto kutoka sehemu mbalimbali za nchi wasome pamoja shuleni, vyuoni na kadhalika
bila ubanguzi.
2. Swala pili
- Ni swali la hoja.
- Hoja zilizokomaa zidhihivike.
Maudhui yainyeshe hatua za kukabiliana na tatizo sugu la ufisadi kama vile
.
i) Tume na taasisi maalum ziundwe ili kutoa hatua za kukabiliana na ufisadi.
ii) Mahakama maalum ziundwe za kukabiliana na ufisadi
iii) Bunge kuunda sheria mwafaka za kukabiliana na ufisadi.
iv) Watu fisadi watungwe gerezani/adabu kali.
v) Kutwaliwa kwa mali ya fisadi wanapopatikana na hatia za ufisadi.
vi) Masuala ya ufisadi yajumuishiwe kwenye mitaala ya elimu na silabasi.
vii) Kutumika teknologia katika ukusanyaji wa pesa za umma.
viii) Wafanya kazi walipiwe mishaara bora ili wasishiriki katika ufisadi.
ix) Maafisa wa serikali kutaja mali wanayomiliki kabla ya kupewa vyeo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
serikalini.
x) wafanyikazi wa serikali wachunguzww iwapo hii fisadi kabla ya kupewa vyeo
serikalini.
xi) Hoja zozote sahihi zikubarike.
3. Swali la 3.
- Hii ni insha ya methali
- Mtahiniwa atunge kisa kimoja.
- Dhana ya kutangulia ionekane vizuri katika kisa chake. Dhana ya kutofika
yaweza kuelezwa katika aya chache, moja au katika sentensi moja.
Mifano ya visa.
i) Kutangulia kupata utajiri kisha baadaye wengine wakupate au kukushinda
ii) Kutangulia masomoni au katika elimu na hatimaye kushindwa na wengine au kufuzu
vyuma na waliotanguliwa.
iii) Kuondoka mapema kwenda safari na hatimaye kuwasili nyuma ya uliowatangulia
kwa sababu ya changamoto Fulani.
iv) Anaweza kutangulia lakini akakosa kufika/kukamilisha mkondo.
* Si lazima mtahiniwa aandike maelezo ya maana na matumizi ya methali.
4. Swali la 4.
Hii ni insha ya kumalizia
- Tahamki ijitokeze vilivyo
- Lazima mtahiniwa akamilishe kwa maneno hayo
- Atumie nafsi ya kwanza
- Mtahiniwa abuni kisa kitakacho dhihirisha hali ya kufuta sana kutokana na
Kitendo au vitendo vyake vibaya
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Tanbihi
- Mwongozo huu wa siri utumiwe pamoja na mwongozo wa kudumu.
MWONGOZO WA UFAHAMU
a) Mahali pa mwanamke ni jikoni.
Kazi yake n ikuitumikia jamii (1x2 = 2)
b) Afanyishwa kazi nyingi (1x2 = 2)
c) Afanyalo mwanamme mwanamke pia hulifanya (alama2)
d) Ndoa
Kiasili Kisasa
Ndoa ya lazima - Ndoa si lazima
Alazimika kumzalia mume watoto - Anazaa watoto kwahiari
Alitumishwa - Ana uhuru wa kufanya atakalo
Alifanya kazi ya jikoni - Si lazima aende jikoni
Aliamuliwa kwa kila jambo - Anajiamulia mwenyewe
Alimtegemea mume - Anajitegemea/hujikimu
Alinyamaza alipoteswa - Hujitetea akiteswa/hupigania haki,
Elimu
Hakuenda shuleni - Anamenda shuleni
Alikuwa na elimu ya kiasili - Hana elimu ya kiasi
(1x2 = 2)
e) Hapendezwi naye. Ni mkaidi, mshindani, mzushi
f) - Mahali pake ni jikoni
- Akiteswa alipaswa kunyamaza/kufyata ulimi.
- Lazima aolewe amzalie mume watoto. Hapaswi kupelekwa shuleni.
- Anapaswa kufenyiwa uamuzi.
- Hapaswi kujitetea.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Ana kazi maalum (1x4 = 4)
g) - Akifyata ulimi - Akanyamaza
- Ukatani -Umaskini in)
- Taasubi za kiume - Fikra/wazo la kibaguzi/uchoyo
- Mwanaume kujiona bora kuliko mke
- Aushi - Maisha/kudumu/milele/daima/alfulela
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MATUMIZI YA LUGHA
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
a) Hu-Ku-m-l-ish-a
Hu-ku-m-p-esh-a
Hu-ku-m-j-ish-a
Hu-ku-m-w-ish-a
b)
/u/ ulimi huinuliwa juu huku ukijipunda nyuma nayo midomo ikiwa imeviringwa
/Ch/ Hewa huzuiliwa kwenye kaakaa gumu kasha nafasi ndogo huachwa ili ipite ikiwa na mkwaruzo
2x1 ala.2
c) i) chwe-wa (ala.1
2)
KKI
ii) Ah! -Ah- (ala.1
2)
-ik-
d) a-li-m-hu-ku-mu (ala.1)
e) M-salaba ala.1
M- umoja (1
2)
Salaba- mzizi (1
2)
f) Uzi – nyuzi –o-ny
umoja – wingi (21
2)
ukuta – kuta- u - o
umoja wingi
udevu – ndevu – u - n
umoja wingi
g) Alimpata aliyemtendea maovu 2x1=ala.2
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
T + S
Alimpata ambaye alimtendea maovu 2X1=ala.2
T + S
h) i) kuulizia swali ala.1
ii) kuonyesha marejeleo (mwandishi wa kitabu na mwaka) ala.1
i) – Hutambulishwa na kuwepo kwa kiambishi kirejeshi “O” kwenye mojawapo ya vitenzi. Mfano, Yule aliyeshikwa ni
mwizi
- kuwepo kwa kiambishi ki cha masharti katika mojawapo ya vitenzi . mfano, Huyu akifanya bidii atapita mtihani
ala.1
- sentensi ikianza kwa kiunganishi
Mfano, ingawa alichelewa sana alipita mtihani
- Kikiondolewa kutoka kwenye sentensi,kuu, hakiwezi kujisimamia kimaana.
Mfano, Mwalimu anayetupenda sana ni wa Kiswahili
Anayetupenda sana.
Hoja zozote mbili pamoja na mifano 2x1 = ala.2
j) Juu ya meza, karibu na barabara kando ya mto
Mfano, Mwalimu alisimama karibu na barabara 2x1
k) Alicheza na kuimba kwenye mkutano ule.
Vilevile, pia 2x1
*lazima sentensi itungwe na iwe sanifu
l) i) Uwanjani mwake mna watu wengi
Nomino
ii) Wanafunzi wote waliingia uwanjani
kielezi 1x2 =ala.2
m)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
12x1
3 =ala.4
n) mkate mtamu – yambwa tendwa
watoto mayatima – yambwa tendewa
makaa – yambwa tumizi
juzi – chagizo ya wakati
4x1
2 =ala.2
p) i) a’la – kihisishi cha mshangao
ii) ‘ala – mfuko au kifaa
q) Mtu wa rehema ametutembelea 2x1 =ala.2
r) panda- Mgawanyiko
- manati fyata
Paji la uso
Weka mbegu katika ardhi
Zozote 2x1
2=al.1
s) msichana mrembo hatatujia kesho ala.1
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
t) Koo alifukuzwa na kudonwa na jogoo
2x1 =ala.2
u) Huu ni wimbo – kitenzi kishirikishi kipungufu
nitakaowafunza – nafsi ya kwanza umoja
ombeni – kuonyesha wingi
ugani- kudokeza mahali
4x1
2 =ala.2
v) Tendama – hutoa dhana ya kushikana na kubakia hivyo kwa muda mrefu. Mfano,
Maji yametuama chini 1x1 =ala.1
ii) Sokota 1x1 =ala.1
w) Kusudi langu la kuja kuonana nawe ni ili unipe msaada wa kifedha ala.1
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
ISIMU JAMII
a)Tangaza la tahadhani/onyo/ilani ala.1
b) – imeandikwa kwa herufi kubwa ili kuweza kuonekana na wasomaji
- imetumia neno onyo ili kutahadharisha wasomaji
- neno onyo limerudiwarudiwa ili kusisitiza ujumbe
- imetumia alama ya kihisishi ili kuzua hisa za dharura
- imetumia kauli fupifupi ili kueleweka haraka na wasomaji
Hoja zozote tatu 3x1 ala.3
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
c) – Baadhi ya tahadhari hutumia michoro na picha kusisitiza ujumbe
- Baadhi ya maneno hukolezwa rangi au kupakwa rangi nyingine ili kuvutia macho ya msomaji
- Maneno kama vile hatari chunga hutumika ili ujumbe ueleweke kwa urahisi
Hoja zozote 2x1 ala.2
d) i) lafudhi: Nii ule upekee unaojitokeza na kuwatofautisha watumiaji mbalimbali wa lugha maja. Mfano utamkaji
wa maneno na sauti mbalimbali
ala.1
ii) Lahaja: Ni mikondo/vilugha mbalimbali vinavyopatikana katika lugha moja kuu. Pia ni namna mbalimbali za
kutumia lugha moja kuu. Tofauti ndogo ndogo zaweza kuwepo lakini watu bado wataelewana. Mfano, kiunguja,
kipemba kilamu
ala.1
iii) Isimu jamii: Ni taaluma inayochunguza mahusioano yaliopo baina ya lugha na jamii kisayansi. Hufafanua namna
watu kutoka jamii ainati wanavyotumia lugha kulingana ma mila, desturi na muktadha tofauti tofauti.
ala.1
iv) Wingi lugha: Pia huitwa pilingua. Hurejelea uwezo wa mnenaji wa kutumia lugha zaidi ya mbili kwa ufasaha.
Mfano Kiswahili, Kiingereza na Kifaransa bila tatizo
ala.1
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KISII JOINT EXAMINATION
SHULE YA UPILI YA MTAKATIFU VINCENT MARAGI
MTIHANI WA MWISHO WA MHULA WA PILI, 2019
102/1 KIDATO CHA NNE
KISWAHILI INSHA
MUDA: SAA 1 ¾
MAAGIZO
1. Jibu maswali mawili
2. Swali la kwanza ni la lazima
3. Chagua swali la pili kutoka sehemu tatu zilizosalia
4. Kila insha isipungue maneno 400
5. Kila insha ina alama 20
1. Umeteuliwa kuwa miongoni mwa watakaohutubia wananchi kuhusu hali ya Usalama nchini Kenya. Andika
hotuba utakayowasilisha siku hiyo kuhusu visababishi vya ukosefu wa usalama na upendekeze hatua
zinazofaa kuchukuliwa ili kukabiliana na hali hii.
2. Serikali za ugatuzi zinakabiliwa na changamoto nyingi. Fafanua.
3. Andika insha kudhibitisha ukweli wa methali pang’okapo jino pana pengo.
4. Andika kisa kitakachomalizikia kwa maneno haya...mungu mikononi mwako tunazikabidhi roho zetu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KISII JOINT EXAMINATION
102/2
KISWAHILI
KARATASI YA PILI – LUGHA
KIDATO CHA NNE 2019
MUDA: SAA 2 ½
MAAGIZO
Jibu maswali yote katika nafasi zilizotengewa
Ufahamu Alama
15
Ufupisho 15
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Matummizi ya lugha 40
Isimujamii 10
Jumla 80
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
UFAHAMU (ALAMA 15)
Mafuta yanayopatikana kwenye fukwe za bahari, moshi wa magari, takataka na bidhaa nyinginezo
zinazotupwa hapa na hapa ni vichafuzi vya mazingira. Vichafuzi huadhiri afya zetu na kuathiri wanyama na
mimea. Wanadamu wanayachafua mazingira yao kwa kila aina ya bidhaa mbaya za kikemikali zinazotoka
viwandani mwa kawi / nguvu. Bidhaa hizo ni matokeo ya maisha ya siku hizi anayoishi binadamu.
Licha ya ukweli huu, ni muhimu kujua kuwa uchafuzi wa mazingira haukuanza leo. Miaka na miaka
iliyopita, viwanda vimekuwa vikitoa mawingu makubwa ya moshi yenye sumu. Hata hivyo, uchafuzi wa
mazingira umeongezeka mara dufu kutokana na kuongezeka kwa viwanda. Uchafuzi umesambaa ardhini,
kwenye anga na majini. Msambao huu unapatikana katika pembe zote za ulimwengu wetu. Je, kuna aina
zipi za uchafu?
Kwanza, kuna uchafu wa hali ya anga. Huko juu angani kuna tabaka linalojulikana kama ozoni. Tabaka hili
ni aina ya gesi ya oksijeni na linaunda kinga fulani dhidi ya miale ya jua. Miale hiyo ya jua huweza
kusababisha saratani ya ngozi inapomfikia binadamu. Hata hivyo, uchafu wa mazingira unaelekea kuliathiri
tabaka hili vilevile baadhi ya kemikali zinazotumiwa katika jokofu au kwenye mikebe ya marashi ya
kupulizia na upakiaji bidhaa, huharibu ukanda huo.
Uchafu mwingine ni uchafuzi wa kiajali. Uchafuzi huu hutokea bila binadamu kukusudia. Mfano mzuri ni
meli inayovuja mafuta baharini. Mafuta haya huwaathiri na kuwaua wanyama wanaoishi baharini kama
samaki na ndege na hata kuyaharibu mazingira yenyewe.
Miji mikubwa hukumbwa na uchafuzi mwingine unaohusiana na kuwako kwa idadi kubwa ya magari.
Magari haya hutoa moshi unaochanganya gesi ambazo huungana na nyingine zinazoletwa na viwanda
vikubwa. Mchanganyiko huu unapoungana na maji, husababisha mvua ya asidi. Mvua hii huweza kuiua
mimea, kuathiri majengo na hata kuwaua wanyama wa pori ambao huenda wakayatumia maji hayo. Magari
hayo hutoa moshi uliochanganyika na madini aina ya risasi ambayo huweza kuathiri siyo tu mazingira bali
pia mfumo wa akili wa binadamu.
Uchafuzi mkubwa ni utupwaji ovyo wa takataka. Fauka ya hayo, watu hufukia ardhini takataka ambazo
huweza kuwa na matokeo mabaya kwa sababu ya kupenyeza kwenye udongo na maji yanayotumiwa na
watu wa mimea. Kila siku tunatupa takataka bila kujali wala kukubali. Takataka hizi ni kama makopo,
mifuko ya plastiki, mabaki ya sigara au maganda ya matunda. Baadhi ya takataka ni hatari kwa wanyama na
nyingine huweza pia kusababisha majanga kama moto. Aidha, hufanya mazingira yaonekane machafu.
Sote tuna jukumu kubwa la kuchangia kupunguza uchafu wa mazingira. Kwanza, kuelimisha na kutambua
umuhimu wa usafi wa mazingira yetu. Tunapaswa kutia takataka zetu kwenye vijalala maalum au mahali
tunapoweza kuzichoma na kuziteketeza. Tuhakikishe tunatunza vitu kama mifuko, chupa na kadhalika
ambavyo huweza kuundwa upya na kutumika tena. Hali kadhalika, katika miaka ya hivi karibuni,
kumekuwepo na juhudi za kuwahimiza wenye magari kutumia mafuta ya gari ambayo hayana madini ya
risasi. Kwa njia hii, tutasaidia kuyaboresha mazingira yetu. Vilevile pana umuhimu wa kutilia mkazo
utumiaji wa bidhaa ambazo zinaweza kuoza na kuvunjikavunjika au kusagika na kuwa sehemu ya udongo.
Hatua ya kwanza ya kupambana na uchafuzi wa mazingira ni kujielimisha na kuwajibika. Kila mmoja
akitoa mchango wake, tutafanikiwa, kumbuka: kinga na kinga ndipo moto uwakapo.
a) Ongezeko la viwanda limechangiaje uchafuzi wa mazingira? (alama 3)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b) Tabaka la ozoni huathiriwaje na uchafuzi? (alama 2)
c) Eleza athari zozote tatu za kutotunza mazingira (alama 3)
d) Kwa nini miji mikubwa hukumbwa na uchafuzi kuliko sehemu nyingine? (alama 2)
e) Eleza njia mbili za uchafuzi wa mazingira zilizotajwa katika kufungu hiki (alama 2)
f) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumiwa katika kifungu (alama 3)
i) Msambao
ii) Makopo
iii) Kinga
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
UFUPISHO (ALAMA 15)
SOMA MAKALA YAFUATAYO KISHA UJIBU MASWALI
Kuna sababu kadha za kuwako na kushamiri kwa ajira ya watoto. Moja ya sababu hizo ni umaskini unazoikumba
jamaa nyingi pamoja na welewa mdogo wa thamani ya elimu wa baadhi ya watu katika jamii. Wapo watoto ambao
hushurutikakubeba jukumu la kujizumbulia riziki kutokana na hali duni ya familia zao.
Hali hii huweza kutokana na baadhi ya wazazi kutelekeza majukumu yao ya kimsingi ya kuikimu jamaa yao. Aidha
kuna sehemu nyingine ambapo hali hii imetokana na janga sugu la ukimwi. Yapo maaeneo kuenea kwa ugonjwa huu
kumewafanya viongozi wa jamaa kupukutika kama majani ya mti na kuwalazimisha watoto kuyakatiza masomo yao
ili wawakidhie haja wadogo zao. Kuhusiana na kutekeleza majukumu, kuna wazazi ambao wanakosea kwa
kutowaelekeza watoto wao kujua maadili mema ni yepi. Kwa njia hii watoto hao wanaishia kutukumbukia kwenye
matatizo makubwa.
Baadhi ya ajira zina athari kubwa sana kwa watoto. Ukahaba, kwa mfano, ni mojawapo ya ajira ambazo watoto wa
kike hulazimika kujiingiza. Hii ni ajira ambayo inaweza kuwatumbukiza watoto hao katika hatari kubwa kutokana na
uwezekano mkubwa wa kuambukizwa maradhi ya ukimwi. Asilimia kubwa ya watoto wanaokumbatia katika ajira hii,
inapatikana katika maeneo ya mjini na sehemu ambako utalii umeshamiri sana. Umaskini pamoja na dhiki za mjini
huwalazimisha watoto hawa wa kike kuishia kwenye biashara za aina hiyo. Wengine hufanyiwa hila na
wafanyibiashara ambao wametovukwa na utu kutokana na tamaa yao kubwa ya kujitajirisha. Katika maeneo ambako
utalii umeshamiri, ukahaba wa watoto unatokana ma umaskini pamoja na kusambaa na kuenea kwa maadili ajinabi,
ya ulimwengu usio wetu.
Ikiwa umaskini ni chocheo kubwa la kuwapo kwa ajira ya watoto, basi inahasili serikali zetu zifanye kila juhudi
kuhakikisha kuwa umaskini umepigwa vita. Pana umuhimu wa kuhakikisha kuwa wanajamii wote wamepewa nafasi
sawa za kujikwamua kutoka lindi la umaskini. Isitoshe, pana umuhimu wa juhudi nyingi kufanywa kuhakikisha kuwa
nafasi za shule zimepanuliwa ili kuikidhi idadi kubwa ya watoto ambao wana kiu ya elimu. Serikali haina budi pia
kuhakikisha kuwa zimepitishwa sheria zinazolinda mtoto dhidi ya ukatili unaotokana na watu waliokosa hisia za utu
na ubinadamu. Upo pia umuhimu wa kuvisaidia vikundi vinavyojitahidi kuwasaidia watoto ili kuzifanikisha juhudi
zao kwa kuwa chanda kimoja hakivunji chawa kama tujuavyo.
Hatua nyingine ambazo zinaweza kuchukuliwa ili kupunguza ajira ya watoto ni kuwahamasisha wanajamii kuhusu
haki za mtoto. Mtoto yoyote yule ana haki ya kupata elimu ya msingi. Mtoto pia ana haki ya kuishi na kupata mahitaji
ya kimsingi na ya lazima kama chakula, malazi au makazi na matunzo ya kiafya. Aidha mtoto ana haki ya ukuaji,
yaani kukua kikamilifu pasi na kizuizi na katika mazingira yasiyombana kwa njia yoyote ile. Isitoshe, mtoto ana haki
ya kupata ulinzi dhidi ya unyanyasaji au udhalilishaji wa aina yoyote ile au hata maonevu kwenye msingi yoyote
iwayo. Mtoto pia ana haki ya kuwa kushiriki katika jumuiya yake, kutoa maoni na kujieleza, kushirikiana na kujiunga
na vikundi. Mwisho na muhimu zaidi mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya ajira au aina yoyote ya kazi ambayo
inahatarisha afya na siha au inamzuia asipate elimu.
a)Fupisha aya mbili za mwanzo bila kubadilisha maana (maneno 60-70) (alama 7)
Matayarisho
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
Jibu
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
b) Eleza hoja muhimu zinazojitokeza katika aya mbili za mwisho (maneno 50-60) (alama 6)
Matayarisho
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
Jibu
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
...........................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
a) Taja sifa mbili za sauti ifuatayo (alama 2)
/th/ ...............................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
b) Andika katika ukubwa (alama 2)
Mke huyu aliangushwa na ng’ombe wake
.....................................................................................................................................................
c) Amrisha katika wingi nafsi ya pili –nywa (alama 1)
.....................................................................................................................................................
d) Kanusha sentensi ifuatayo (alama 2)
Watakapofika hospitalini watatibiwa
.....................................................................................................................................................
e) Tunga sentensi mbili kubainisha matumizi mawili ya mshazari (alama 2)
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
f) Tunga sentensi moja kutofautisha kati ya vitate konga na gonga (alama 2)
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
g) Changanua sentensi ifuatayo kwa kutumia jedwali /visanduku.
Mtoto mmoja aliyekuwa mgonjwa sana alitibiwa jana (alama 4)
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
h) Andika kinyume cha sentensi hii (alama 1)
Shangazi angeingia tungemsifu
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Unda nomino mbili kutokana na vitenzi vifuatavyo (alama 2)
(i) Kinai
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
(ii) Chelewa
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
j) Tambulisha aina za vitenzi katika sentensi hii (alama 3)
Ndege yu taabani, hata hivyo anajaribu kujinasua
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
k) i)Eleza dhana ya kirai (alama 1)
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
ii)Tambua aina za virai katika sentensi ifuatayo (alama 2)
Chake chote kilivunjika vibaya sana
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
l) Tambulisha aina za shamirisho/yabwa katika sentensi ifuatayo (alama 3)
Baba alimjengea nyanya nyumba kwa mawe
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
m) Huku ukitoa mfano eleza maana ya... (alama 4)
i)Mzizi huru
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
ii) Mzizi funge
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
n) Andika katika usemi wa taarifa “Aisee! Yale mawingu ya Tsunami yataangamiza biashara nyingi sana leo.”
Alisema Koinange (alama 2)
.....................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.....................................................................................................................................................
o) Eleza maana mbili za sentensi hii (alama 2)
Alinunuliwa ng’ombe na mtoto wake
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
p) Andika viwakilishi ngeli vya nomino zifuatazo (alama 1)
i) Chakula
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
ii)Kwetu
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
q) Tambulisha matumizi ya ‘ji’ katika sentensi ifuatayo (alama 2)
Jitu lilijingoa jino kupitia unywaji wa pombe
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
r) Andika neno lenye muundo wa sauti zifuatazo (alama 1)
KKIKI
ISIMU JAMII
a) Eleza maana ya ujozi lugha /wingi lugha (alama 1)
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
b) Huku ukitoa mfano mmoja mmoja eleza tofauti kati ya kuchanganya ndimi na kubadili ndimi/msimbo (alama 4)
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
c) Kwa kutumia hoja tano eleza kwa nini watu wengi wana mazoea ya kuchanganya na kubadili msimbo katika
mazungumzo yao (alama 5)
.....................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
.....................................................................................................................................................
.....................................................................................................................................................
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA INSHA 102/1
1.
i) Hii ni insha ya hotuba
ii) Mtahiniwa afuate sura/mtindo wa kuandika
Hotuba -Utangulizi
- Mwili
- Tamati
Baadhi ya hoja
Visababishi
1. Siasa – vyama vya kisiasa
2. Uchochezi kutoka kwa viongozi
3. Chuki na uhasama baina ya makabila
4. Umaskini
5. Ukosefu wa ajira
6. Vikundi haramu vya vijana k.v. Mungiki, Chikororo
7. Ugaidi
8. Dhuluma za kihistoria
(Zingatia hoja nyinginezo za mwanafunzi)
Mapendekezo
1. Wachochezi kuchukuliwa hatua kali
2. Wananchi kuhamasishwa kuhusu umuhimu wa kuishi pamoja kwa amani
3. Serikali na washikadau kushirikiana ili kukabili tatizo la umaskini
4. Kubuni nafasi za kazi kwa vijana
5. Serikali kukabiliana na ugaidi na vikundi haramu vilivyo
(Zingatia hoja nyinginezo za mwanafunzi)
2. Changamoto zinazokabili serikali za ugatuzi
1. Ufisadi
2. Pesa kutoka kwa serikali kuu zinakawia
3. Tatizo la umaskini katika baadhi ya kaunti
4. Kuongezeka kwa kodi/kuathiri raia
5. Migogoro ya kisiasa – kati ya magavana na wawakilishi wa wadi
6. Kuendelezwa kwa ukabila – katika ajira
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
7. Mizozo ya kimipaka baina ya Kaunti
8. Changamoto katika sekta ya afya
(Zingatia hoja nyinginezo za mtahiniwa)
3. Hii ni insha ya methali
Mtahiniwa aandike kisa kinachoonyesha
Ukweli wa methali aliyopewa
Iwe na anwani / kichwa
Ina sehemu mbili
Sehemu ya kwanza – aonyeshe jino liking’oka mf mzazi au kiongozi akiondoka au akifa.
Sehemu ya pili – matatizo huanza kuwakabili waliomtegemea.
4. Hii ni insha ya mdokezo
Mtahiniwa amalizie kwa maneno aliyopewa.
Akimalizia kwa maneno mwengine amejitungia swali.
Anaweza kuelezea kisa cha ajali yoyote
Atumie mbinu rejeshi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
102/2
KISWAHILI
KARATASI YA PILI – LUGHA MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KIDATO CHA NNE
MUDA: SAA 2 ½
UFAHAMU
Viwanda kutoa moshi unaochafua hewa
Viwanda kumwaga kemikali majini
Viwanda kutengeneza bidhaa zisizoweza kuoza
Gesi na kemikali zinazotoka ardhini hupaa juu na kuvunja tabaka hili. (zozote 3 x 1=3)
Hewa safi ya kupumua itapungua (alama 2)
Maji ya kutumia kuchafuka
Ardhi haitakuwa na uwezo au kuzalisha mimea (zozote 3 x 1=3)
Viwanda vingi vimejengwa mijini
(zozote 2 x 1=2)
Miji ina idadi kubwa ya watu (zozote 2 x 1=2)
Uchafuzi wa hali ya anga
Uchafuzi wa ardhi
Uchafuzi wa maji (zozote 2 x 1=1)
i)Ueneaji/usagaaji
ii)Mabaki
iii)Kipande cha ukumi chenye moto
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
UTAHINI
Makosa ya s – ondoa hadi nusu ya alama alizopata mwanafunzi katika kila swali
Makosa ya h – ondoa hadi makosa sita katika swali nzima ( ½ x 6 = 3
2. UFUPISHO (ALAMA 15)
A
i) Ajira ya watoto husababishwa na umaskini unaozikumba jamaa nyingi.
ii) Ufahamu mdogo wa thamani ya elimu wa baadhi ya watu
iii) Watotokushurutika kkujitafutia riziki kwenyewe kwa sababu yahali duni ya familia zao.
iv) Wazazi kutekeleza majukumu yao yakimsingi ya kukimu jamaa yao.
v) Kupukutika kwa viongozi wa jamaa kutokana na janga sugu la ukimwi.
vi) Wazazi kutowaelekeza watoto wao kujua maadili mema.
(hoja 6 x 1 = 6)
B
i) Serikali kufanya juhudi kuhakikisha kuwa umaskini umepigwa vita.
ii) Wanajamii wote wapewe nafasi sawa za kukikwamua kutoka lindi la umaskini.
iii) Kupanua nafasi za elimu kukidhi idadi kubwa ya watoto.
iv) Kuhakikisha kupitishwa kwa sheria zinazolinda mtoto dhidi ya ukatili
v) Kusaidia vikundi vinavyojitahidi kuwasaidia watoto.
vi) Kuwahamasisha wanajamii kuhusu haki za watoto.
Hoja 6 x 1
Maki a = 6
b= 6
Utiririko = 3
15
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MWONGOZO
KARATASI 2
a) /th/ - (i) Ni Konsonanti
(ii) Ni sauti si ghuna /hafifu
iii) Hutamkiwa kwenye meno / (1 x 2)
b) Jike hilo liliangushwa na gombe lake ( ½ x 4 = 2)
c) Nywa
(i) Kunyweni! 1 x 1
d) Wasipofika hospitalini huwatatibiwa ( 1 x 2)
e)
i) Kuandika kumbukumbu
ii) Kuonyesha visawe k.m. aila /familia
iii) Kuandika tarehe 24/7/2019
iv) Kuonyesha ama/au ( 1 x 2 = 2)
f) Maana zijitokeze
(i) Gonga - Piga
(ii) Konga – Zeeka
- Kuunganisha pamoja ( 1 x 20
g) Jedwali
Mtoto mmoja aliyekuwa mgonjwa sana alitibiwa jana (alama 4)
Si
KN KT
N V S T E
Mtoto mmoja aliyekuwa mgonjwa sana alitibiwa jana
¼ x 8
h) Shangazi angetoka tungemkashifu (alama 20
i) Kinai
- Ukinaifu
- Kukinai alikokinai kulim...
- Mkinaifu/wakinaifu ( 1x 2)
Chelewa - cheleo, ucheleweshaji, kuchelewa, uchelewaji chelezo.
j) Yu – Kitenzi kishirikishi kipungufu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Anajaribu – Kitenzi kisaidizi
Kujinasua – kitenzi kikuu ( 1 x3)
k) i)Kirai – fungu la maneno ambayo maana ya si kamilifu/kisicho na muundo wa kiima na kianja
( 1x1)
ii)Chake chote – Kirai nomino
Vibaya sana – Kirai kivumishi ( 1 x 2)
l) Yabwa:
Nyanya - Kitondo
Nyumba – kipozi
Mawe – ala (1 x 3)
m) Mzizi huru – hauhitaji kuongezwa kiambishi mf sahau, mama
Mzizi funge – huongezwa viambishi mf – eupe; - chafu
n) Koinange alishangaa kuwa haya mawimbi ya Tsumani yangeanga-miza biashara nyingi sana siku hiyo ½ x 4 = 2
o)
i) Mtoto alinunua kwa niaba yake
ii) Alinunuliwa ng’ombe pamoja na ndama
iii) Mtu mwingine alinunuliwa ngombe na mtoto wa mrejelewa
iv) Mrejelewa alinunuliwa ng’ombe na mtoto wake mwenyewe
v) Alinunuliwa na mtoto wa mtu mwingi
1 x 2 = 2
p) Chakula - Ki
Kwetu - ku 1 x1
q) Jitu - ukubwa
Lilijing’oa – kujitendea
Jino – ngeli ( Li – YA0
Unywaji – mazoea ½ x 4 = 2
r) K.M
Bweha, mwana, mwiko ( 1 x1)
ISIMU JAMII
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Ni hali ya mtu kuwa na uwezo na kuzungumza lugha mbili.
ii) Kuchunganya ndimi ni kule kutumia neno la lugha tofauti katika sentensi ya lugha nyingine, mf story zake
zinatubore
iii) Kubadili ndimi ni kutunga sentensi katika lugha moja halafu unafuatisha sentensi ya lugha nyingine tofauti mf.
Maria anapenda kuonyesha anavyosoma. Infact she used to speak in English even to the old ladies.
iv) Sababu za kuchangaya ndimi
a) Kupungukiwa na msamiati
b) Kujitambulisha na kikundi Fulani watu
c) Kujihusisha na lugha inayoonew fahari
d) Kuonyesha kuwa una/uwezo wa kutumia lugha zaidi ya moja
e) Kutaka kufafanua dhana Fulani
f) Kutoimudu lugha fulani vilivyo
g) Mazoea ya watu.
MWONGOZI WA KUSAHIHISHA FASIHI 102/3
USHAIRI
a)
- Uende
- Uache kuniumiza
- Ninakufukuza
- Umemshinda
b)
i) Vina: nda – za
nda – za
nda – za
za – nda
ii)Mizani: 8 - 8
8 - 8
8 - 8
8 - 8
iii)Mathnawi – ukwapi na utao
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv) Tarbia – Mishororo mine kila ubeti
v) Kiitikio: Uwache kuniumiza, mheri mwana kunenda
c)
- Mienendo na tabia mbaya
- Tama – hatosheki
- Hatulii nyumbani
- Hana shukrani
d)
- Tarbia
- Mtiririko – vina vya ukwapi na utao vinafanana isipokuwa kiitikio
- Mathnawi: ukwapi na utao
e)
i)Tashbihi
- Kukupenda kama tunda
- Nimekonda kama ng’onda
ii) Methali
- Ahsante ya punda ni mateke (wajigeuza punda, teke umenicharaza)
- Cha kuvunda kichavunda, hata ukikifukiza (cha kuvunda hakina ubani)
iii) Istiari
- Sauti ya kinanda
- Ukajigeuza punda
f) Wewe umenishinda kwa tama yako kubwa ambapo unanikia kila jambo hata liwe la kuudhi. Tena hatulii kila siku
watembea. Unapaswa uache kuniumiza na afadhali mwana uende.
g) Uhuru: Lahaja -ola
Mazida – kunenda
Tabdila – uwache – uache
Inkisari – sautiyo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
h) Mayaza – mawazo/fikra
Muhibu – mpenzi, mwandani
Q2 Mwongozo wa kusahihisha (Kigogo)
i) Haya ni maneno ya Tunu
ii) Anawaambia raia
iii) Wako nje ya soko la chapakazi
iv) Anawahutubia raia baada ya kuwaongoza kususia mkutano wa majoka ili kumlazimisha majoka kuwafungulia
soko ambalo alikuwa amelifunga na kunyakua ardhi hiyo.
(1 x 4 =4)
Umuhimu wa Tunu
✓ Ni kielelezo cha uongozi bora. Wengi wanataka kumchagua.
✓ Kielelezo cha uwajibikaji – anapigania haki za wanyonge wanaodhulumiwa.
✓ Kielelezo cha uzalendo. Anapigania maslahi ya raia licha ya kuteswa.
✓ Anaonyesha mchango wa wanaharakati kutetea haki za wanyonge
✓ Ni kiwakilishi cha ujenzi wa jamii mpya/mabadiliko
✓ Anaonyesha changamoto wanazopitia watetezi wa haki za umma mf kupigwa
(1 x 5 =5)
c)Ukweli wa kauli iliyopigwa mstari
✓ soko linapofungwa Tunu anawaongoza wachuuzi katika maandamano. Kushurutisha lifunguliwe.
✓ Tunu na Ashua wanapomwona Kanga akiwahutubia wahuni chini ya mbuyu wote wanakimbia kuwaita
wenzao sudi, kombe la boza wafike huko wajue kinachoendelea.
✓ Tunu akiwa kiongozi wa chama cha wanafunzi anashirikiana na sudi kutetea haki za wanafunzi
✓ Askari wanapowaua vijana watano katika maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya chakula kwenye
kioski cha majoka, tunu anaadamana na sudi hadi kwa mkurungenzi wa Kampuni kujua kiini chake japo
hakuambiwa lolote.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
✓ Majoka anafuja pesa za kusafisha soko la chapakazi, Tunu anawahutubia waandishi wa habari na kukashifu
kitendo hicho.
✓ Majoka anapomshawishi aolewe na mwanawe (Ngao junior) anakataa.
✓ Kampuni ya Majoka inapowaua vijana watano, Tunu anamwendea Majoka ofisini mwake wa kumwambia
atalipa kila tone la damu alilomwaga sagamoyo
✓ Majoka anapobomoa vioski vya wafanyi biashara sokoni chapakazi Tunu anamwendea ofisini na kumwambia
kuwa licha ya kubomoa vioski hivyo hatajenga hoteli ya Kifahari alivyonuia.
✓ Licha ya kuvamiwa na wahuni waliotumwa na Majoka bado anaendeleza juhudi za kupigania haki
wanasagamoyo.
✓ Majoka anapomfunga Ashua, Tunu anamwendea ofisini mwake na kumwambia kwamba lazima yeye na Sudi
wamtoe kifungoni majoka atake asitake
✓ Tunu anawatembelea Walevi na kuwarai waaache ulevi kwa kuwaelezea athari zake.
✓ Tunu anamsuta Mama pima kwa kuuza pombe haramu yenye madhara mengi.
✓ Tunu anawatembelea raia na kuwalika katika mkutano nje la lango kuu la soko la Chapa kazi siku ya
maadhimisho ya uhuru ili kumlazimisha kufungua soko hilo – mkutano huu unamng’oa majoka mamlakani.
(1 x 11 = 11)
Tamthlia (Kigogo)
“Uovu umetamalaki katika tamthlia ya Kigogo” Jadili
i) Ufisadi – Ashiya alivyopata leseni ya kuuza pombe
-Uchongaji ya Kinyago – Keki
ii) Mauaji - Babake tunu
-Ngurumo
iii) Matumizi ya pombe haramu
iv) Kuumizana – Tunu kuvunjwa miguu
v) Kufungwa kwa soko ili kuzidisha umaskini
vi) Unyakuzi: Soko kufungwa ili kujenga hoteli
vii) Matumizi ya nguvu dhidi ya waandamanaji
viii) Kutamani wake wa wengine k.m. Majoka – Ashua
Ngurumo - Ashiya
ix) Tamaa - Ashua kumdharau Sudi
Husda kupenda mali ya majoka n. K.
x) Ubinafsi: Ngurumo
Majoka
xi) Matumizi mabaya ya mali ya umma – Majoka na Husda kujistarehesha wakitumia mali ya umma
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
xii) Dawa za kulevya –s umu ya nyoka katika shule ya majoka
xiii) Uharibifu wa mazingira – maji taka n.k.
xiv) Usaliti: Majoka kusaliti raia na
Wafuasi wake kumgeuka
n. k. 2 x 10 = 20mks
Mwongozo wa kusahihisha chozi
Q4 la heri
a)
• Haya ni maneno ya Terry
• Anamwabia mumewe ridhaa
• Wamo nyumbani mwao
• Anamwabia hivi baada ya kugundua anamini mambo ya kishirikina mf mlio ya bundi, kerengende
Au
• Mawazo ya Ridhaa – anakumbuka maneno ya mkewe Terry
• Terry alimwabia maneno haya kwa sababu ya kuamini mlio ya bundi iliashiria mkosi
• Yuko kando ya nyumba yake iliyochomwa
Ni baada ya familia yake kuangamia katika moto. ( 1 x4 =4)
b) Mbinu za kimtindo
• Methali
• Kuhamisha ndimi
• Swali la balagha. (1 x 3 = 3)
c) Neema na mwangemi wanajitahidi kupata mtoto lakini hawafanikiwi. Wanaishia kupanga mtoto – mwaliko
✓ Wafuasi wa mwanzi wanajaribu kupinga ushindi wa mwekevu bila mafanikio.
✓ Kaizari anajitahidi kuzuia genge la wahuni lisabake bintize lakini wakamzidi nguvu
✓ Lunga anajitolea kwa hali na mali kumpendeza mkewe Naomi lakini licha ya juhudi zake anaishia kutoroka
na kumwachia watoto.
✓ Kiriri anajizatiti kumrai mkewe Annete asiende ughaibuni bila mafanikio.
✓ Nyanyake Pete anajizatiti kupinga kuozwa kwa Pete na fungo lakini wajomba na mamake Pete wanampuuza
na kumwoza.
✓ Baadhi ya matajiri wanatoa milungula nyumba za zisilbomolewe lakinip ale tononoka lakini bado serikali
inazibomoa.
✓ Kipanga anataka mamake amwabie babake ni nani lakini hakumwambia.
✓ Amize lucia wajizatiti kupinga lucia kuolewa katika koo za waombwe lakini hawakufanikiwa – Babake
alikubali zolewe huko.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
✓ Pete anakunywa dawa ya kuua paye ili cafe lakini maisha yake yanaokolewa katika kituo cha Afya – cha
mwanzo mpya.
✓ Pete anakosa kufanikiwa kuavya mimba ya mtoto wake wa pili.
✓ Lily nyamvula anajaribu kumshawishi mumewe mwageka asijiunge na kikosi cha usalama lakini mwangeka
anaishia kuwa askari.
5.
i) Subira alitengwa na familia yake mumewe kwa vile alikuwa wa kabila tofauti. Alivumilia kwa muda mrefu
lakini ilimbidi kujiondokea. Aliitwa ‘muki’ Baada alianza ulevi uliomfisha.
ii) Shuleni Ridhaa alitegnwa na wanafunzi waliomwita ‘mfuata mvua’. Upweke ulimtawala
iii) Mzee Kedi aliteketeza nyumba na aila ya ridhaa kwa misingi ya kikabila.
iv) Ami zake kungata walimsuta kwa kumwoza bintiye kw amume wa ukoo tofauti
v) Ndoa ya Selume ilisambaratishwa na ukatila. Mumewe alioa mke wa kabila lake.
vi) Tulia alimsindikiza kaizari aende makao ya wakimbizi
vii) Watoto wa kaizari walibakwa kwa misingi ya ukabila
viii) Makaazi duni ya kudorora kiafya katika kambi za wakimbizi
ix) Njaa na vifo katika makao ya wakimbizi
x) Uharibifu wa malini na mazingira – nyumba na kufyeka misitu.
6. Hadithi fupi – Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine
6a)Masharti ya kisiasa
Kulingana na Dadi mapenzi ni kama ugonjwa. Dadi anampenwa kidawa kwa dhati maisha ya ndoa
yalipokuwa magumu kwa sababu alimpenda mkewe, aliona masharti yale hayavunjiki kwani angeyavunja
basin a ndoa yake ingevunjika na yote haya yangemvunja pia. Kidawa pia alimpenda Dadi kwa kweli.
Alipotambua kuwa Dadi alimshuku kuwa hakuwa mwaminifu na alikuwa na mpango wa kando aliamua
kuacha kazi yake.
b) Mapenzi ya kifaurongo
Chuoni wanafunzi waliokenaka wenye wao kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Penina katika harakati za
kutafuta mapenzi ya dhati anajipata na Dennis ambaye ni wa tabaka la chini. Mapenzi yao yananoga lakini
hatimaye yanakuwa ya kifaurongo pale Dennis anapokosa kazi. Dennis alimpenda Penina kwa dhati.
c)Kidege
Joy na Achesa wanapendana. Wao huenda katika bustani ya Ilala kujivinjari mahaba yao. Wanagoragaza na
katika viunga vya bustani hii. Mose anawapenda sana samaki waliomo mle kidimbwini. Hubeba sima
mfukoni mwake. Akifika pale havirushia visamaki sima.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
d) Ndoto ya mashaka
Mashaka alimpenda waridi kufa kupona. Alipoachwa na waridi hakuwa na hakuona thamani ya maisha tena.
Alimpenda kwa hamu na ghamu. Waridi pia alimpenda sana mashaka. Hakuangalia hali duni ya mashaka.
Alimpenda katika umaskini wake kulingana na mashoka mapenzi huweza kuota popote.
e) Nizikeni papa hapa
Rafikiye Olii anapomtahadharisha Otii dhidi ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mrembo. Rehema
Wanjiru, Otii alipouza kabisa hiyo tahadhari. Alimpenda sana Rehema. Hatimaye anaambukizwa ugonjwa
uliompelekea kaburini.
f) Tulipokotana Tena
Sabu alimpenda Bogoa na hata kumfunza kusoma Sebu na Bogoa wanapendana kwa dhati. Wanapokutana
tena baada ya miaka mingi wanafurahiana sana tu kukumbatiana. Katika mizumbatio ule, sebu aliweza
kubisi ule uvugovugo wa mapenzi ya Bogoa kwake. Macho yao yalijaribu kufumba ili kupunguza maumivu
ya masafa na ukiwa uliopita. Hatimaye, matone ya machozi yalianguka migongoni mwao na kurovya
makoti yao. Kekefu na vilio hawakuweza tena kuzizuia.
5x 4 = 20
Fasihi Simulizi
7(a)Ulumbi – Uwezo wa mtu kuzungumza kwa njia ya ufasaha na kipekee mbele ya hadhira.
(b) Kuhuisha ulumbi
✓ Kutumia ishara
✓ Ukariri hutokea ili kusisitiza
✓ Kutumia kiimbo
✓ Kutumia balagha
✓ Kutumia ucheshi
✓ Kutumia taharuki
1 x 6 = 6
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
c)Ngomezi
Ni maigizo ya sanaa ya kuwasilisha ujumbe kwa kutumia ngoma. Ni fasihi ya ngoma 1 x 2
d) Za Kisasa
1. Filimbi
2. Vingora (ambulensi au zima moto)
3. Kengele
4. Milio katika sima tamba 1 x 4
e)Sifa
i) Kila mdundo wa ngoma huwakilisha kauli mahusisi
ii) Kutegemea mapigo, wizani, au upatano unaotaokana na ngoma inayopigwa kuwasilisha ujumbe
iii) Maana hujikita kutokanana jamii husika
iv) Kila mpigo wa ngoma hufuata mtindo wa kishairi
1 x 4 = 4
g) Dhima
i) Ni njia ya kupitisha ujumbe wa dharura
ii) Ni kitambulisho cha jamii
iii) Huhifadhi na kuendeleza utamaduni wa jamii kutoka kizazi hadi kingine
iv) Ni nyenzo ya kukuza uzalendo
v) Kukuza ubunifu
vi) Njia rahisi ya kuwasilisha ujumbe bila kutegemea sauti ya mtu
NYANDO JOINT EXAMINATION
102/1
KISWAHILI KARATASI YA KWANZA
INSHA
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KIDATO CHA NNE
JULAI/AGOSTI 2019
MUDA: 1 ¾
MAAGIZO
(a) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani.
(b) Tia sahihi kisha uandike tarehe
© Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
(d) Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo zilizobakia.
(e) Kila insha isipungue maneno 400.
(f) Kila insha ina alama 20.
(g) Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
Kwa matumizi ya mtahini pekee
Swali Upeo Alama
1 20
2 20
3 20
4 20
40
INSHA PAPER 1
KIDATO CHA NNE
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. Wewe ni mwanahabari wa gazeti la Tomoko Leo. Umemtembelea Mkuu wa Idara ya kupambana na ufisadi Bwana
Ridhaa ili kumhoji kuhusu sababu za watu kushiriki ufisadi na suluhisho.
Andika mahojiano yenu.
2. Andika insha kuhusu mambo yanayoathiri utaifa au umoja na utangamano katika nchi ya Kenya.
3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo.
Mla nawe hafi nawe ila mzaliwa nawe.
4. Tunga kisa kitakachomalizika kwa maneno yafuatayo:
……….Nilipiga darubini kuhusu mawaidha niliyopewa ya mama yangu. Machozi yalinitiririka njia mbilimbili. Utabiri
wa mama ulikuwa umetimu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYANDO JOINT EXAMINATION
102/2
KISWAHILI
KIDATO CHA NNE
JULAI/AGOSTI 2019
MUDA: 2 ½
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI – 2019
Maagizo
(a) Andika jina lako na nambari yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
(b) Tia sahihi yako na uandike tarehe ya mtihani katika nafasi zilizoachwa hapo juu.
© Jibu maswali yote katika karatasi hii.
(d) Andika majibu yako katika nafasi zilizoachwa katika kijitabu hiki cha maswali.
(e) Mtahiniwa ahakikishe kwamba kurasa zote zimepigwa chapa na kwamba maswali yote yamo.
(f) Majibu yote yaandike kwa lugha ya Kiswahili.
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE.
SWALI UPEO ALAMA
1 UFAHAMU 15
2 UFUPISHO 15
3 SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA 40
4 ISIMUJAMII 10
80
102/2
UFAHAMU (ALAMA 20)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Soma taarifa ifuatayo kasha ujibu maswali
Inasemekana kuwa uongozi hutoka kwa Maulana. Siku hizi, kauli hii inaonekana kinyume na inapingwa vikali na
mahuluki wengi. Hali hii imetokana na ukweli kuwa viongozi wengi wamekuwa katili. Wengi wao hutekeleza maovu
bila kujali wala kubali. Kiongozi yeyote Yule anayedai kuwa mwema hana budi kuwa mwongofu na wa kuaminika;
anafaa kuwa kielelezo kwa wafuasi wake. Hili lisipotendeka vurumai huzuka miongoni mwa watu.
Kiongozi bora sharti awe mnyenyekevu. Mtu mwenye mashauo si kiongozi bora. Kiongozi wa aina hii huwahudumia
watu kwa moyo wake wote. Jambo hili huwafanya watu waridhike. Watu wengi hawapendi viongozi wanaojipigia
debe kila wakati. Viongozi kama hawa huwachosha na hata kuwachusha wafuasi wao. Matokeo ya haya yote huwa
ni majuto kwa raia huku wakijiuliza kilichowafanya wawachague.
Maadili ni sifa nyingine inayomtambulisha kiongozi bora. Kiongozi wa aina hii hafai kujihusisha na vitendo vya kikatili
kama matumizi ya mabavu, mauaji na hata ufisadi. Anafaa kuwajibika kazini na kuwa tayari kuyasikiliza malalamishi
ya watu anaohudumia. Inamlazimu kiongozi bora kuwaheshimu wananchi bila kuzingatia vyeo vyao; asidharau
maoni yao kuhusu jinsi ya kuuboresha uongozi wake.
Pia, kiongozi bora anastahili kuwa na huruma. Hii inamaanisha kuwa anafaa kuwa tayari kuwaonea kite wananchi
wanaotatizika maishani. Anafaa kubuni mikakati ya kuwaauni watu kama hawa. Hali hii huwafanya watu waongeze
imani yao kwa kiongozi kama huyu. Ikiwa kiongozi atajitia hamnazo anapofahamishwa kuhusu masaibuya wananchi,
watu watatamani siku ya kumtoa mamlakani ama kwa kupiga kura au kumwomba Jalali ahitimishe uongozi wake
haraka iwezekanavyo.
Utetezi wa kazi za wanyonge ni sifa nyingine muruwa ya kiongozi bora. Kiongozi kama huyu anapaswa kuwa tayari
kuhakikisha kuwa sheria inafuatwa katika himaya yake. Hali hii huwafanya wanajamii kupata haki zao bila
kubughudhiwa. Wale wasiopata haki wanazostahili wanastahili kuchungiwa maslahi na kiongozi kama huyu.
Hakuna mtu anayestahili kuitwa kiongozi bora kama si mpenda amani. Kiongozi anayepalilia rabsha katika jamii
hafaulu hata kidogo kuitwa kiongozi bora. Ni wajibu wa kiongozi kusuluhisha ugomvi wowote uliomo miongoni mwa
wanajamii. Jambo hili huifanya kunawiri na kuzagaa kote kote.
Wanajamii wakiishi katika mazingira yenye amani huweza kutekeleza shughuli zao bila hofu wala
kindubwendumbwe.
Kiongozi bora anastahili kujitenga na ubaguzi kama ardhi na mbingu. Ni ukweli usiopingika kuwa baadhi ya viongozi
huwabagua wananchi kwa misingi ya kitabaka, kijinsia na kikabila. Ni muhimu kwa kiongozi yeyote Yule kuhakikisha
kuwa kuna umoja wa wananchi katika jamii. Hii ni kutokana na ukweli kuwa jifya moja haliwezi kuinjika chungu.
Astahili kuhubiri umoja katika hatamu ya uongozi wake. Nao wananchi humkumbuka daina dawamu.
Uwajibikaji ni kitambulishi kingine cha kiongozi aali. Kiongozi bora anafaa kuwajibika kazini. Kiongozi anaystahili ni
Yule ambaye anatekeleza majukumu yake kikamilifu. Suala la upigaji zohali ni muhali kwa kiongozi wa aina hii. Ni
mtu anayefanya kazi kimhanga ili kuboresha maisha yake naya wateja wake.
Kiongozi yeyote asiye na hulka tulizozungumzia huishia kuwa hasimu wa watu. Viongozi wote wanastahili kuyapa
kipaumbele maslahi ya umma. Hawafai kuwa wabinafisi. Ni watu wenye utu, maarifa, waongofu na wenye bidii.
Wananchi wana wajibu wa kuwachagua viongozi wanaofaa bila kupofushwa na ahadi za uongo.
Maswali
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(a) Kwa nini kauli kuwa, ‘uongozi hutoka kwa maulana’, yaonekana kinaya na kupingwa na watu wengi. (ala.1)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(b) Eleza kiini cha watu wengi kuchukia viongozi wanaojisifu kila wakati. (alama 2)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
© Eleza matokeo ya kiongozi kuwasaidia wananchi wanaotatizika maishani. (alama 1)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(d) Taja misingi mitatu inayotumiwa na baadhi ya viongozi kuwabagua wananchi.(alama 3)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(e) Eleza maoni ya mwandishi kuhusu jukumu la wananchi kuhakikisha kuwa uongozi bora umedumu. (alama 1)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(f) Taja vitambulishi vine vya kiongozi bora. (alama 4)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(g) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu. (alama 3)
(i) Mwongo:------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------(ii)
Kuwauni:-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------(iii)
Kite:-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. UFUPISHO
Ni dhahiri shahiri kwamba uharamia umechipuka kama desturi na mfumo wa maisha katika siku za hivi karibuni.
Janga hili limeshamiri hususan pembeni mwa bara la Afrika na kanda ya Afrika Mashariki.
Taarifa za uharamia zimetawala vyombo vya habari, kiasi kwamba haipii siku bila kuripotiwa visa vipya vya matendo
haya mabovu ambayo yanaweza tu kumithilishwa na uhayawani. Matukio haya yamewalimbikizia mabaharia wan
chi husika, simanzi na masaibu yasiyoweza kuatiwa kwenye mizani.
Yamkini tatizo hili halitokei pasi na kumotishwa na kitita kikubwa cha fidia kinachodaiwa na maharamia hawa.
Aghalabu suala hili lahusishwa pakubwa na azma na ari ya kuendeleza ujambazi wa kimataifa sawia na ulipuaji wa
bomu mjini Nairobi na Dar –es salaam mnamo Agosti 7,1998 na tukio la Septemba 11, mwaka wa 2001 kule
Marekani. Maafa na uharibifu wa mali si hoja, la mno kwa maharamia ni kutosheleza matakwa yao. Kwa upande
mwingine, ukosefu wa tawala- wajibika katika maeneo kunakotokea unyama huu ni thibitisho tosha la mazingira
yanayowezesha na kuruhusu kuchipuka kwa janga hili.
Mchipuko wa baa la uharamia umelengwa jamii ya kimataifa ambayo ni mhudumu mkuu wa harakati za kusitisha
majanga makubwa kama vile njaa, umasikini na magonjwa yaliyosheheni pakubwa barani. Bila shaka, hili ni suala
linalosawisishwa na ‘kinyume mbele’. Maharamia wanatishia utangamano wa kimataifa wanapotibua usafiri na
shehena zinazoelekezwa sehemu tofauti ulimwenguni.
Matumizi ya kidiplomasia na mashauriano hayaelekei kuzalisha matunda katika juhudi za kudhibiti uharamia. Zaidi
ya hayo, matumizi ya nguvu yahusishayo mashambulizi pamoja na maharamia kufunguliwa mashtaka nchini Kenya
na Ufaraansa kunaelekea kuzipiga jeki juhudi za uharamia ulimwenguni. Aidha, utawala wan chi kunachipuka
uharamia haujajizatiti kuharamisha doa hili linalotisha ustawi wa kimataifa.
Mathalan, ni jambo lisilopingika inapobainika kuwa uharamia umedumaza biashara ya kimataifa, hali inayochangia
upungufu wa ucheleweshaji wa bidhaa muhimu zinazoendeleza ustawi wa uchumi.
Dosari hii inaelekea kukwamiza mojawapo wa malengo ya maendeleo ya millennia yanayosisitiza uimarishaji na
ushirikiano wa maendeleo na upanuzi wa masoko ulimwenguni. Harakati za kitalii katika kanda mashariki ya bara la
Afrika zimehujumiwa. Ni muhali kwa utali kustawi kwenye maeneo yaliyo na tishio la usalama. Itakumbukwa bayana
kwamba watalii hawasafiri tu kwa ndege bali hata kwa meli.
Jitihada za kuweka laini za mawasiliano chini ya bahari ili kurahisisha na kupunguza gharama za mtandao
ulimwenguni ni ndoto ambayo haijatimia hadi hivi sasa, kufuatia juhudi za maharamia katika bahari ya Hindi. Kwa
mujibu wa hali hii, mawasiliano mepesi na nafuu yasitarajiwe hivi karibuni. Licha ya hayo, shughuli za uvuvi na
biashara nyinginezo kwenye kanda ya mmwambao zimetiliwa shaka si haba.
Itabidi mikakati kabambe na suluhisho la kudumu liweze kupatikana ili vitendo vya uharamia viweze kusitishwa.
Maswali
1.Fupisha aya mbili za kwanza kwa maneno 70. (alama 8,1 ya mtiririko)
MATAYARISHO
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------
JIBU
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------
(b)Onyesha jinsi ambavyo Kenya imeathiriwa na uharamia na namna hali hii inatia hofu. Maneno 60. (alama 7,1 ya
mtiririko)
MATAYARISHO
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------
JIBU
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------
SEHEMU YA SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
(a)Taja sauti zenye sifa zifuatazo. (alama 2)
(i) King’ong’o cha mdomo:----------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) Irabu ya mbele kati:--------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(iii) Kipasuo ghuna cha kaakaa laini:-------------------------------------------------------------------------------------------------
(iv) Kikwamizo sighuna cha menoni:-----------------------------------------------------------------------------------------------
(b) Dhihirishamiundo ya silabi katika maneno yafuatayo. (alama 2)
(i) itwa:-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) Mchwa:------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
© Tunga sentensi mbili ili kuonyesha matumizi ya kiakifishi (alama 2)
Vifungo
(i)--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------(ii)----------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(d) Andika sentensi ukitumia: (alama 2)
(i)Kihusishi cha ulinganisho
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii)Kihisishi cha furaha
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(e) Tunga sentensi ya neno moja iliyo na muundo ufuatao.(alama 2)
(i)Nafsi
(ii)Mzizi
(iii)kauli
(iv)Kirejeshi
(f)Eleza matumizi ya maneno yaliyopigiwa mstari katika sentensi zifuatazo. (alama 2)
(i)Chakula chochote kitaliwa na watoto.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) Chakula chote kitaliwa na watoto.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(g) Kwa kutunga sentensi mwafaka onyesha aina tatu za yambwa. (alama 3)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(h)Badilisha sentensi ifuatayo iwe katika usemi wa taarifa.(alama 3)
“Tutamtia mbaroni mhalifu huyo sasa hivi” Askari akasema.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(i)Ainisha matumizi ya kiambishi “ji” katika sentensi (alama 3)
Jibwa hilo liliweza kujinusuru kutokana na hasira za mkimbiaji.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(j) Changanua kwa Jedwali. (alama 4)
Otii ambaye hucheza mpira ni kijana mkali.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(k)Tofautisha vitate vifuatavyo kwa kuvitungia sentensi moja. (alama 2)
(i)Hawara:-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) Hawala:------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(L) Bumba ni kwa nyuki--------------------------------------------------------------ni kwa samaki na---------------------------------
ni kwa siafu. (alama 2
(m) Andika methali inayojumuisha ujumbe ufuatao.(alama 1)
Hata mtaalamu huhitaji kutafuta msaada wa wataalamu wenzake.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(n) Unda kitenzi kutokana na nomino zifuatazo. (alama 2)
(i)Aina:------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii)Moto-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(O)Onyesha matumizi ya ‘kwa’ katika sentensi. (alama 2)
(i)Kwao kunawaka moto.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) Magaidi walitoroka kwa kasi.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(P) Nyambua katika kauli kwenye mabano. (alama 2)
(i)Tua (tendama)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) Pwa (tendeka)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(q) Badilisha sentensi ifuatayo katika wakati ujao hali timilifu. (alama 2)
Mama huwapikia watoto chakula.
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(r) Tumia neno ‘kesho’ kutungia sentensi kama: (alama 2)
(i)Nomino:--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(ii) kielezi:-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
SEHEMU D:ISIMUJAMII (ALAMA 10)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Lugha ya magazeti husheheni upekee wa aina fulani. Eleza sifa za lugha hii kisha ueleze upekee huu hukusudia nini?
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYANDO JOINT EXAMINATION
102/3
KISWAHILI
KARATASI YA 3
FASIHI
JULAI/AGOSTI 2019
MUDA: 2 ½
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WAPILI – KIDATO CHA NNE KISWAHILI –KARATASI YA 3 (FASIHI) MUDA: SAA 2 ½ Maagizo
(a) Jibu maswali manne pekee.
(b) Swali la kwanza ni la LAZIMA.
(c) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki; yaani: Riwaya, Tamthilia, hadithi
Fupi na Fasihi Simulizi.
(d) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(e) Majibu yote lazima yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
SEHEMU A(SWALI LA LAZIMA)
A: USHAIRI
.Soma ushairi ufuatao kisha ujibu maswali
1.
Ulimwengu ulimwengu, ulimwengu naratibu Yaliyo kichwani mwangu, nataka kuyatubu Wayasome ndu zangu, wa mbali na wa karibu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Ulimwengu ni kiwanja, cha wenye raha na tabu Wengine wanajikonja, kwa wengine ni adhabu Kucha na kutwa twahanja, kutafuta matulubu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Ni uwanja wa balaa, aliniusia babu Mna mambo yamejaa, ya faraja na kusibu Na machache ya kufaa, ila mengi ya udubu Cha wenye raha na tabu,ulimwengu ni kiwanja. Ni kiwanja cha Amina,Saidi Ali Rajabu Wengine kitu hatuna, tunaishia kababu Wale wamejaza sana, wanashindwa kuhesabu Cha wenye raha na tabu, Ulimwengu ni kiwanja. Ni uwanja wa urongo, na kweli pia ajabu Kichwa hudanganya shingo, tumbo kiuno chasibu Usitumai ubongo, wa nduguyo na swahibu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Ni uwanja wa walevi, pombe kwao ni dhahabu Mara vile mara hivi, wakilewa majudhubu Maneno ya kiujuvi, hujipaka hata shabu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Ni kiwanja wenye dini, wamtiio wahabu Mashekhe msikitini, humo humfanya muhibu Mapadiri kanisani, huvihubiri vitabu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Ni uwanja wa malofa, lofa mtu mwenye tabu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kusema sana kashifa na moyo kisebusebu Tunakaribia kuja, kwa kushindwa kujimudu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Ni uwanja wa faraja, alowajali habibu Na wengine sitotaja, msinambe ninagubu Ni uwanja wa viroja, vigumu kuvikutubu Cha wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja. Maswali (a)Lipe shairi hili anwani ifaayo. (alama 1) ------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------ (b) kwa kutoa mfano, eleza mbinu zozote mbili za lugha zilizotumika katika shairi.(alama 2)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------
©Eleza jinsi uhuru wa mshairi ulivyotumika katika shairi. (alama 2)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------
(d) Andika ubeti wa tatu kwa lugha tutumbi. (alama 4)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
(e)Taja na ueleze bahari zozote mbili zilizotumika katika shairi hili. (alama 2)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
------------------------------------------------------------------------------------
(f)Eleza umbo la shairi hili. (alama 4)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--
(g)Eleza toni ya shairi hili. (alama 1)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------
(h)Fafanua dhamira ya mshairi. (alama 2)
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------
(i)Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi. (alama 2)
(i) Malofa:
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------(ii) Udubu:
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
SEHEMU YA B: RIWAYA: CHOZI LA HERI – ASSUMPTA K. MATEI
Jibu swali la 2 au la 3 2. “Lakini itakuaje historical injustice, nawe Ridhaa hapo ulipo sicho kitovu chako?
(a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
(b) Taja na utpe mifano ya mbinu za sanaa zilizotumika katika dondoo hili. (alama 4)
(c) Fafanua umuhimu wa msemaji wa maneno haya. (alama 2)
(d) Ni mambo gani yaliyowakumba wale ambao kitovu chao sicho walicho. (alama 10)
3. Uozo wa maadili ya jamii umekithiri katika Riwaya ya Chozi la heri, Fafanua ukweli wa usemi huu. (alama 20)
SEHEMU C: TAMTHILIA: KIGOGO – PAULINE KEA Jibu swali la 4 au la 5 4. “Asante ya punda kweli ni mateke. Sikujua ungekuja kunihangaisha………………”
(a) Weka dondoo hili katika muktadha wake. (alama 4)
(b) Onyesha jinsi msemewa anamhangaisha msemaji. (alama 2)
(c) Kwa kurejelea tamthilia nzima, onyesha ukweli wa methali “Asante ya punda ni mateke.
(alama 14)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
5. Fafanua jinsi mwandishi wa tamthilia ya Kigogo alivyofaulu kutumia mbinu zifuatazo za uandishi. (alama 20) (a) Jazanda (b) Majazi
SEHEMU D; HADITHI FUPI: TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI NYINGINE. 6.Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya ‘Tumbo Lisiloshiba na hadithi Nyingine’,
jadili maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi. (alama 20)
SEHEMU E: FASIHI SIMULIZI
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali
Ndimi Nguli, dume la ukoo mtukufu
Ulojipambanua kwa mabingwa
Wachezaji hodari wa ngoma
Ndimi dume liloingia nyanjani
Makoo yakatetemeka
Yakang’ang’ania gozi kusakata nami.
Maswali
(a) Tambulisha kipera kinachojitokeza katika kifungu hiki. (alama 2)
(b) Eleza sifa tano bainifu za kipera hiki katika fasihi simulizi. (alama 10)
(c) Fafanua umuhimu wa kipera hiki. (alama 8)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYANDO JOINT EXAMINATION
102/1
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
INSHA
KIDATO CHA NNE – KARATASI YA KWANZA
1. Hii ni insha ya uamilifu. Vipengele viwili vikuu vya insha ya aina hii viweze kushughulikiwa. Vipengele hivi ni:
- Maudhui
- Muundo
Muundo wa mahojiano
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Kichwa/Anwani
Kionyeshe ni mahojiano
Kionyeshe ni kati ya nani, mahali na mada inayoshughulikiwa.
Kichwa kwa herufi kubwa.
(ii) Utangulizi
Huwa ni maelezo mafupi ambayo huandikwa kwa mabano na hufafanua hali na mazingira ya mahojiano.
(iii) Mwili
Huhusu hoja ambazo ni maudhui ya insha.
Maneno ya mhoji au mhojiwa huandikwa baada ya koloni.
Mhoji huuliza swali na mhojiwa hujibu maelezo ya ziada huwekwa kwenye mabano.
(iv) Hitimisho
Kutoa kauli ya kukamilisha mahojiano kama kushukuru mhojiwa.
Maudhui
Hoja za maudhui ni kama zifuatazo:
(1) Tamaa ya kutajirika
(2) Kutofahamu madhara au matokeo yake.
(3) Mishahara au mapato duni.
(4) Kukosa njia za kukimu mahitaji.
(5) Kutotosheka na kile mtu alicho nacho.
(6) Kutomjua mungu – kukosa imani.
(7) Kuchukulia ufisadi kama jambo la kawaida.
(8) Imani kuwa siku hizi mtu hawezi kupata chochote bila kutoa hongo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Suluhisho/njia za kuukabili ufisadi
(1) Hatua kali za kisheria kuchukuliwa.
(2) Kulipa wafanyikazi malipo mazuri.
(3) kunyang’anywa pesa au mali walizopata kifisadi.
(4) Watu kutangaza mali zao.
(5) Majina ya watu fisadi kutangazwa hadharani.
2. Hii ni insha ya hoja.
Mtahiniwa aweze kutoa hoja angalau tano kulingana na mada.
Hoja ambazo ni maudhui ni kama zifuatazo:-
(i) Kuajiri watu kimapendeleo
(ii) Ukabila
(iii) Usalama kukosekana
(iv) Ukosefu wa ajira.
(v) Matamshi mabaya ya viongozi
(vi) Kupanda kwa gharama ya maisha.
(vii) Kutojenga miundomsingi kwa usawa.
(viii) Ubomoaji wa nyumba.
Tabihi: Hoja itakuwa imekamilika ikiwa imethibitishwa.
Mtahiniwa atakuwa amejitosheleza kimaudhui ikiwa ana hoja tano na zaidi zilizofafanuliwa.
3(i) Hii ni insha ya methali. Mtahiniwa aweze kuandika kisa ambacho kitadhihirisha maana ya methali hii. Ina maana
kuwa wale unaokula nao wakati war aha, wakati wa shida hutawaona wala kuwasikia.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mnaosherehekea nao hukubwaga siku za shida hasa marafiki. Familia tu ndiyo husimama na wewe siku zote.
(ii) Kisa kinaweza kuwa kuhusu mhusika ambaye walikuwa wakisherehekea na marafiki wakati wa furaha. Wakati
alipopata shida, marafiki walimtenga lakini familia ilisimama naye.
(iii) Mtahiniwa azingatie kuwa methali huwa na vipande viwili. Pande zote mbili lazima zionyeshwe.
Wale ambao wataonyesha upande mmoja watakuwa wamepungukiwa tu kimaudhui lakini hawajapotoka.
Wale wataandika kisa kisichohusiana na methali watakuwa wamepotoka.
4. Hii ni insha ya mdokezo.
Maneno kiini katika swali hii ni machozi kutirirka kwa kukumbuka mawaidha aliyopewa ambayo labda hakuzingatia.
Mtahiniwa aweze kutunga kisa ambacho kitaoana na mdokezo huu.
Mtahiniwa anaweza kutumia mbinu rejeshi kuonyesha yale aliyoambiwa na mama na ambayo hakuyatilia maanani.
Pia aweze kuelezea yake yaliyompata kwa kutozingatia nasaha na ndiposa akalia kwa majuto.
Tanbihi
(i) Mtahiniwa atakuwa amepotoka pale tu kisa chake hakioani na kimalizio.
(ii) Kwa vyovyote vile lazima pawe na jambo aliloambiwa na mama ambalo hakulizingatia.
(iii) Asipomalizia kwa kidokezo atakuwa amepungukiwa kimtindo, akadiriwe vilivyo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYANDO JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA - KIDATO CHA NNE
KARATASI YA PILI
JULAI/AGOSTI 2019
1. UFAHAMU
(a) Sababu kauli ‘uongozi hutoka kwa maulana’ huonejana kinaya na kupipingwa na watu wengi viongozi wamekuwa
kauli ambapo wengi wao hutekeleza maovu bila kujali wala kubali.
(b) Kiini cha watu wengi huchukia viongozi na hata kuwachosha wafuasi wao.
(i) Viongozi kama hawa huwachosha na hata kuwachusha wafuasi wao.
(ii) Huwafanya raia wajute kuwachagua.
© Kueleza matokeo ya kiongozi kuwasaidia wanaotatizika maishani. Watu huwa na imani naye.
(d) Kutaja misingi mitatu inayotumiwa ba baadhi ya viongozi kuwabagua wananchi.
- Misingi ya kitabaka
- Misingi ya kijinsia
- Misingi ya kikabila
- Misingi ya kidini
(e) Maoni ya mwandishi kuhusu dhima ya wananchi kuhakikisha kuwa uongozi bora umedumishwa. Wananchi wana
wajibu wa kuchagua viongozi wanaofaa bila kupofushwa na ahadi za uongo kutaja vitambulishi vine vya kiongozi
bora.
(f) Kutaja vitambulishi vine vya kiongozi bora
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- mnyenyekevu
- mwenye maadili
-anayetetea haki za wanyonge
- mpenda amani
- anayejitenga na ubaguzi/ anayechunga maslahi ya watu wote.
-mwajibikikagi
- mwenye huruma
(g) Kueleza maana ya maneno yaliyotumiwa katika ufahamu.
(i) Mwongofu – mwadilifu/mwenye tabia nzuri.
(ii) Kuwaauni – kuwasaidia
(iii) Kite – huruma
2. UFUPISHO
(a) Fupisha aya mbili za kwanza kwa maneno 70. (alama 8, 1 ya mtiririko)
- Uharamia umechipuka kama desturi na mfumo wa maisha
- Janga hili limeshamiri hususan pembeni mwa bara la Afrika na kanda ya Afrika mashariki
- Taarifa za uharamia zimetawala vyombo vya habari
- Matukio haya yamewalimbikizia mabaharia wan chi husika, simanzi na masaibu
- Tatizo hili linamotishwa na kitita cha fidia kinachodaiwa na maharamia
- Suala hili linahusishwa pakubwa na azma na ari ya kuendeleza ujambazi wa kimataifa
- Maafa na uharibifu wa mali si hoja ila kutosheleza matakwa yao.
- Ukosefu wa tawala – wajibika ni thibitisho tosha la mazingira wezeshi kwa janga hili.
(b) Onyesha jinsi ambavyo Kenya imeathiriwa na uharamia na namna hali hii inatia hofu. Maneno 60. (alama 7, 1 ya
mtiririko)
- Matumizi ya kidiplomasia na mashauriano hayaelekei kuzalisha matunda
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Matumizi ya nguvu yahusishayo mashambulizi pamoja na maharamia kufunguliwa mashtaka yanaelekea
kuzipiga jeki juhudi za maharamia
- Utawala wananchi kunakochipuka uharamia haujajizatiti kuharamisha doa hili
- Uharamia umedumaza biashara ya kimataifa
- Umechangia upungufu na uchelewaji wa bidhaa
- Umekwamisha mojawapo wa malengo ya millennia
- Kuhujumiwa kwa harakati za kitalii
Utuzaji
a - al. 7
b – al. 6
u – al. 2
adhabu
s – makosa 6 x ½ = 3
h – makosa 6 x ½ = 3
SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA
(a) (i) m
(ii) e
(iii) g
(iv) th 4 x ½ = (alama 2)
(b) (i) i – twa
I - KKI
(ii) m – chwa
K - KKKI 4 x ½ = alama 2
© Vifungo
(i) Kufungia nambari/tarakimu
(ii) Kutoa maelezo ya ziada
(iii) Kuonyesha kisawe cha neno
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(iv) Kufungia maelekezo katika tamthilia
2x1 = alama 2
(d)(i) Kuliko, kama, sawa na, mithili ya
(ii) Hoyee! Huraa! (alama 2)
(e) Tathmini sentensi za wanafunzi
Mfano
Tulimao Tu – nafsi
lim – mzizi
a- Kauli
0- kirejeshi (alama 4)
(f) (i) Bila kubagua / bila kuchagua/ kutojali
(ii) kwa jumla/ bila kubakiza (alama 2)
(g) Sentensi idhihirishe
Shamirisho kipozi
Shamirisho kitondo
Shamirisho ala
Mfano
Mama amejengewa nyumba kwa vigae
Kitondo kipozi ala
(h) Askari alisema kuwa wangemtia mbaroni mhalifu Yule saa ile. (alama 1x3 = 3)
(I) Matumizi ya ji
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Ukubwa
(ii) Kirejeshi cha mtenda
(iii) Nomino ya mtenda (alama 3 x 1 = 3)
(J)
S
KN KT
N S t KN2
N V
Otii ambaye hucheza mpira ni kijana mkali
(alama 4)
(k) Sentensi itoe maana ya:
(i) Hawara – kiruka njia, Malaya, kimada
(ii) Hawala – hundi, cheki (alama 2)
(L) Mkufu (alama 2)
(M) Methali
Kinyozi hajinyoi
Mganga hajigangi (alama 2)
(n) (i) aina - ainisha
(ii) Moto – motisha (alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(O) (i) Umilikaji
(ii) Jinsi/namna (alama 2)
(P) (i) Tua – Tuama
(ii) Pwa – pweka/pweleka
(q) Mama atakuwa amewapikia watoto chakula. (alama 2)
(r) (i) Kesho yangu itaweza kuangaa
(neno kesho lichukue nafasi ya kiima)
(ii) Nitamtembelea kesho.
(neno kesho lifafanue kitenzi) (alama 2)
SEHEMU YA D: ISIMUJAMII (ALAMA 10)
Sifa
1. Mara nyingi vichwa au mada haizingatii sarufi.
2. Baadhi ya ujumbe hupigwa chuku.
3. Mada huwa fupi nay a kuvutia.
4. Lugha inayotumika hutegemea ujumbe.
5. Huandikwa kwa aya fupifupi.
6. Wakati mwingine huwa na sentensi ndefu.
7. Lugha huwa rahisi na yenye mfululizo mzuri.
8. Tarakimu hutumika katika maelezo yake.
9. Lugha yenye mvuto hutumika.
5 x 1 = alama 5
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kusudi
1. ili kupata nafasi kwenye gazeti
2. ili kupata wanunuzi
3. Kila taaluma ina msamiati wake.
4. Aya fupi husheheni hoja muhimu
5. Lugha hurahisishwa ili matabaka yote yapashwe ujumbe.
5x1 = alama 5
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NYANDO JOINT EXAMINATION
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA FASIHI KIDATO CHA NNE
JULAI/AGOSTI 2019
1. Swali la Lazima – USHAIRI
(a) Ulimwengu
Ulimwengu ni kiwanja
Changamoto ulimwenguni 1 x 1 = alama 1
(b) Istiara/ jazanda – ulimwengu ni kiwanja
Msemo – kutwa kuchwa
Ukinzani/tanakuzi – wenye raha na tabu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Uhuishaji – Kichwa kudanganya shingo (zozote 2x1 = alama 2)
© Inkisari – naratibu – ninaratibu
Ndu zangu – ndugu zangu.
Kuboronga lugha – wenye kitu hatuna – wengine hatuna kitu
Utohozi – shehe – sheikh
Padre – padre (2x1 = 2)
(d) babu alimshauri kuwa ulimwengu ni uwanja wa balaa ulionjaa mambo ya faraja na kusibu. Pia alisema kuwa kuna
machache ya kufaidi na mengi ya kuudhi. Kwa hivyo ulimwengu ni kiwanja kwa walio na raha na walio na taabu. (4x1
= alama 4)
(e) (i) Tarbia – mishororo minne kwa kila ubeti
(ii) Mathnawi – vipande viwili kwa kila mshororo
(iii) Pindu – sehemu ya mwisho kuanzia ubeti unaofuata.
(iv) Ukara – vina vya mwisho vinatirirka na vya kati havitiririki. (2x1 = alama 1)
(f) (i) Mishororo minne kwa kila ubeti
(ii) Vipande viwili kwa kila mshororo – ukwapi na utao.
(iii) Lina beti tisa.
(iv) Vina vya mwisho vinatiririka na vya kati vinabadilika
(v) Lina kibwagizo – che wenye raha na tabu, ulimwengu ni kiwanja.
(vi) mizani ni 8,8 kwa kila mshororo
4x1 = 4
(g) masikitiko (alama 1)
(h) Kufahamisha watu hali ilivyo ulimwenguni. Kwamba kuna mazuri na mabaya ili wajihadhari. (1x2= 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(i) Malofa – maskini
(ii) Ndubu – upumbavu (alama 2)
2. RIWAYA: CHOZI LA HERI
2(a) (i) Msemaji – ridhaa
(ii) Msemewa – nafsi yake/alijisemea
(iii) Mahali – kando ya gofu la jumba lake
(iv) sababu – hii ni baada ya ridhaa kukubali
(alama 4x1 = 4)
(b) Mbinu za kisanaa
(i) Balagha – hapo ulipo sicho kitovu chako
(ii) Kuchanganya ndimi – historical injustice
(iii) Uzungumzi nafsia – dondoo lenyewe
(zozote 2 x 2 = 4)
© Umuhimu wa Ridhaa
(i) Ametumiwa kuonyesha dhana ya ukabila na nadhara yake.
(ii) Ni kielelezo cha watu wasiobagua wengine. Hakujali wanakijiji wenzake ni wa ukoo gani bali alitekeleza miradi ya
maendeleo ili kuwafaidi wote.
(iii) Ametumiwa kuonyesha udhalimu kwa wafuata mvua.
(zozote 2 x 1 = 2)
(d) (i) Walichomewa nyumba zao km Ridhaa alichomewa nyumba yake ya kifahari.
(ii) Watu wao waliuawa kwa mfano familia ya Ridhaa ilichomwa na Kedi jirani yao.
(iii) Wakimbizi walitorokea msituni.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(iv) Watoto nao walibakwa k.m mabinti zake Kaizari walibakwa na vijana wenzao.
(v) Waliotoroka kuacha makwao wakawa maskwota/wakimbizi wa ndani kwa ndani.
Tanbihi:Mtahini akadirie hoja zingine. (zozote 5x2=10)
3. Chozi la Heri
1. Ubakaji – genge la mabarobaro watano liliwabaka Lime na Mwanaheri.
2. Ulanguzi wa dawa za kulevya.
Dick anafanya kazi ya kusafirisha dawa za kulevya kutoka nchi moja hadi nyingine.
3. Uporaji, wizi na ukatili
Mali ya watu binafsi yaliharibiwa, kwa mfano: nyumba ya mali yote ya ridhaa yanateketezwa wakiwemo watoto
wake na mkewe.
4. uendeshaji wa biashara haramu. Bi. Kangara walifanya biashara haramu na kuwauza watoto.
5.Uavyaji mimba
Sauna anapata mimba kiholela na kujaribu awezavyo kuiavya, na mwishowe, baada ya kushindwa kuavya mimba
alitaka kujiua.
6. Mapenzi kati ya baba mlezi na bintiye babake Sauna anafanya mapenzi na mwanawe patapo nafasi na mwishowe
Sauna anapata mimba.
7. Kutupwa kwa watoto wachanga.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
8. Unywaji pombe k.m Shamshi.
9. Ufisadi k.m Lunga alifutwa kazi baada ya kukataa kushiriki ufisadi.
10. Kuna mauaji yanayotokana na vikosi vya usalama hususan extra-judicial killings.
(zozote 10 x2 = 20)
4. KIGOGO
(a)
- Msemaji ni Majoka (uk.44)
- akimwambia Tunu
- wamo ofisini mwa Majoka
- ni baada ya Majoka kumfungia Ashua mkewe Sudi kwa tuhuma za kuleta vurugu katika ofisi yake. Hivyo
Tunu na Sudi wakafika katika ofisi ya Majoka kisadifa.
(4x1 =4)
(b)
- anapanga maandamano ya kumshurutisha afungue soko la chapakazi
- anachochea umma kuhusiana na maswala mengine k.v usafishaji soko, kodi nyingi, mauaji
- anataka kuwa kigogo wa Sagamoyo
- anaendelea- kufuata kesi ya mauaji ya babake.
(2x1 = 2)
©
- Majoka hana shukrani kwa wanasagamoyo anawafungia soko ingawa walimchagua
- Majoka anaamua jabali ingawa alikuwa mfanya kazi wake katika Majoka and majoka Co.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Ashua hana shukrani kwa Sudi, anamkashifu kuwa hawajibiki ingawa Sudi anajitahidi kuwatafutia watoto
chakula (uk 48)
- Ashua hana shukrani kwa Majoka, alipewa kazi na Majoka katika shule yake akakataa.(uk. 25)
- Baadhi ya wanasagamoyo k.v Boza, Ngurumo na mama Pima hawana shukrani kwa Tunu na Sudi wanapigania
haki zao kama kufunguliwa kwa soko lakini wanawapinga.
- Majoka hana shukrani kwa mkewe – ana jicho la nje ingawa Husda anampenda
- Chopin a Kenga wanamgeuka Majoka ingawa walikuwa wafuasi wake wa karibu
- Tunu hana shukarani kwa Majoka, alisomeshwa na majoka lakini anamhangaisha.(uk. 44)
- Majoka hana shukrani kwa wafuasi wake wa karibu, haombolezi Ngurumo anapoaga dunia ingawa Ngurumo
alikuwa anampigia debe kila mahali.
5(a) . Jazanda/Sitiari
Maana; maelezo ya kimafumbo yanayoashiria jambo Fulani au hali Fulani inayofahamika kubeba hali nyingine
tofauti.
- Uvundo uliohanikiza katika eneo la soko la chapakazi unaoashiria uozo wa kijamii kama vile utepetevu wa
viongozi.
- Uchongaji wa kinyago kizuri cha mwanamke ambaye ni Tunu akiwa na kinasa sauti ni kuanagazia nafsi ya
mwanamke katika jamii ana uwezo wa kuwa kiongozi.
- Uchongaji wa kinyago cha mhenga Fulani wa Boza unaashiria uhafidhina na ubarakala unaoendelezwa katika
jamii na baadhi ya watu.
- Kombe anaposema kwamba keki ya uhuru imeliwa kwingine kasha wao waletewa masazo kuonyesha utabaka
na ukoloni mamboleo unaoendelezwa na viongozi na vibaraka wao wanaojifaidi pekee.
- Majoka anapomwambia Ashua kuwa hangeacha kula mkate kwa kuchelea kiungulia. Hali hii inaashiria
uendelezaji wa anasa na uozo wa viongozi wanaotaka kutumia madaraka ya kutimiza ufuska wao hata kwa wake
wa watu bila hofu yoyote.
- Kenga anaposema kuwa ukitaka kuwafurusha ndege kata mti kwa maana ya kuangamiza viongozi wa makundi
pinzani inadhihirisha maudhui ya ukatili na siasa za mauaji.
- Sudi anapomwambia Ashua kuwa siasa yao imesukumiza kwenye chombo wasichotaka kuabiri anamaanisha
imebidi washiriki katika harakati za ukombozi. Aidha, maudhui ya asasi ya ndoayanaangaziwa kupitia mzozo
wao. (Sudi na Ashua)
- Chopi anamwambia Sudi kuwa shamba likimshida kulima aseme anamaanisha pengine Sudi ameshidwa
kumkidhia Ashua mahitaji yake kama mke hivyo kuendeleza maudhui ya ndoa na mapenzi.
- Babu anasema kuwa chombo chenye rubani imara huhimili vishindo na hasira ya mawimbi kumaanisha uongozi
mzuri hutegemea kiongozi aliyeimara na mwajibikaji.
- Babu anaporejelea mshumaa kuwaka na kuwasha mishumaa mingine anamaanisha kiongozi anastahili kuwafaa
raia. Aidha, anadokezea umuhimu wa umoja na ushirikiano katika jamii.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Ashua anamwambia Majoka kuwa ushahidi hauwezi kupatikana ikiwa kipanga ndiye hakimu katika kesi ya kuku
kumaanisha ukiukaji wa haki katika jamii.
- Babu anamwambia Majoka kuwa labda chombo chake kinakwenda kinyumenyume badala ya kwenda mbele
kumaanisha utawala wa majoka haujaonyesha mabadiliko yoyote yaliyoleta manufaa bali umeendeleza ukoloni
mamboleo.
(b) MAJAZI
- (I) Majoka – nyoka kubwa kupita kiasi. Ana tabia ya nyoka kubeba fimbo ya nyoka na maumbo ya nyoka.
Kutengeneza sumu ya nyoka. Kufuga nyoka (swila)
- Tunu – kitu cha dhamana (zawadi)
- Ni mwanamke wa kipekee anayekabiliana na viongozi dhalimu.
- Sudi – bahati njema. Ni bahati njema kwa Sagamoyo. Anajitolea kupigana na uongozi mbaya.
- Kenga – kumfanya mtu aamini jambo lisilo la kweli (uongo)
- Husda – kuonea mtu gere/kijicho/wivu. Anamwonea Ashua wivu kwa sababu amesoma, mrembo na apendwa
na majoka.
- Kombe – mmea unaotambaa ambao utomvu wake ni sumu inayopakwa katika kigumba cha mshale.
- Ana tabia ya kutoonyesha msimamo dhabiti.
- Ngurumo – sauti ya mvumo inayosikika angani wakati wa mvua. Anahusika kuwaua na kuwapiga wapinzani wa
Majoka.
- Chopi – kulewa chopi/chakari. Hakufuata maagizo anayopewa na Majoka kwa sababu ya kulewa.
- Mama Pima – kazi yake ni kupima na kuuza pombe.
- Asiya – sehemu ya kitu au mbaki. Mfano Majoka anamuona kama mbaki linalostahili kuondolewa baada ya kifo
cha Ngurumo.
- Boza –mjinga/mpumbavu. Mfano anaunga mkono serikali kijinga, mkewe azini na Ngurumo.
- Hashina – mwenye heshima, anawafundisha wengine kuwa na heshima.
- Saga moyo – kufanya kitu kiwe unga unga(saga). Watu wanaoishi katika jimbo hili wanapitia maumivu makali ya
moyo.
- Chapakazi – mahali pa kufanyia kazi kwa bidii.
(zozote 10)
6. (a) TUMBO LISILOSHIBA
Tulipokutana tena
Wazazi wa Bogoa – ni wazazi wema ingawa ni maskini hawataki Bogoa alelewe na wazazi wengine.
Mapenzi kifaurongo
- Wazazi wa Penina Bw. & Bi. Kitane) wamewajibika katika kumlea Penina. Wanampa fedha za kutosha kila wiki.
- Licha ya kuwa maskini wazazi wa Dennis wanajizatiti sana kumpeleka chuoni hadi chuo kikuu.
Shoga ya Dada ana ndevu
- Wazazi wake safia na Lulua wanawapenda sana wanao
- Wanawapeleka wanao shuleni na kuwapa Safia nafasi ya kusoma pale nyumbani
- Wazazi hawa pia wana mapuuza. Wanamwamini mwanao kupita kiasi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mama Bakari
- Babake sara ni mkali sana. Sara anapobakwa anaogopa kumwambia kuwa ana ujauzito
- Baadaye anabadilika wa kuwa mpole, anamfariji
- Mamake sara ni dhaifu, hawezi kumsaidia sara
Ndoto ya Mashaka
- Wazazi wa Samueli wanajinyima ili kuwasomesha watoto wao.
- Babake samueli aliuza ng’ombe wengi ili kumsomesha samueli
- Mamake samueli anatumiwa kuonyesha mapenzi ya mzazi ni ya kudumu
- Babake samueli anatumiwa kuonyesha kukata tama/kutamauka
(10x2 = alama 20)
Kila hadithi hoja mbili
Hadithi zifafanuliwe kwa usawa
7. FASIHI SIMULIZI
(a) Majigambo au vivugo (1x2 = 2)
(b)
- Hutungwa na kughaniwa na mhusika mwenyewe
- Hutungwa kwa usanii mkubwa sana. K.m matumizi ya sitiari
- Anayejigamba hutunga kivugo kufuatia tukio mahususi katika maisha yake michezoni, vitani, kesi, jando
na Kadhalika.
- Huwa na matumizi ya chuku. Mtunzi hujisifu kupita kiasi kwa kutaja mafanikio na mchango wake.
- Majigambo hutungwa papo hapo. Lakini mengine huandikwa na kughaniwa baadaye.
- Maudhui makuu ya majigambo huwa ushujaa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Kwa kawaida hutungwa na kughaniwa na wanaume
- Anayejigamba huweza kuvaa maleba yanayooana na kazi yake. Pia anaweza kubeba baadhi ya vifaa vya kazi.
- Anayejigamba huweza kutaja na kusifu ukoo/nasaba yake.
- Mara nyingi wanaojigamba kuwa walumbi au washairi
Za kwanza 5 x 2 = 10
C
- Hukuza ubunifu. Mtunzi huimarisha uwezo wake wa kubuni mitindo mipya ya utunzi na uwasilishaji
anapoendelea kubuni majigambo.
- Ni nyenzo ya burudani. Waliohudhuria sherehe huongolewa na majigambo
- Kukuza ufasaha wa lugha. Watunzi wengi wa majigambo huwa Walumbi ambao ni weledi wa lugha
- Hudumisha utu na hutambulisha mwanamume katika jamii. Wanaume walipaswa kuwa jasiri katika jamii kwa
sababu ya uchokozi uliokuwepo
- Ni nyenzo ya kufanya watu waheshimiwe. Hufanya wanaume kuwa mashujaa.
(zozote 4x2= 8)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NANYUKI JOINT EXAMINATION
MTIHANI WA TATHMINI WA NANYUKI
MUHULA WA PILI 2019
Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari nchini Kenya
102/1 KISWAHILI Karatasi ya 1
INSHA
JULAI 2019-Muda: Saa 13/4
________________________________________________________________________________
JINA ___________________________________NAMBARI __________________MKONDO__________
SAHIHI YA MTAHINIWA ________________________TAREHE ______________________________
_____________________________________________________________________________________
MAAGIZO
(a) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(b) Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu
(c) Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima
(d) Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
(e) Kila insha isipungue maneno 400.
(f) Kila insha ina alama 20.
(g) Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
(h) Karatasi hii ina kurasa mbili zilizopigwa chapa.
(i) Watahiniwa ni lazima wahakikishe kuwa kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa sawasawa na kuwa
maswali yote yamo.
_____________________________________________________________________________________
Kwa matumizi ya Mtahini pekee
SWALI
UPEO
ALAMA
1
20
20
JUMLA
40
Lazima
1. Ukiwa mkurugenzi wa elimu, uliongoza kamati ya kufanya uchunguzi kuhusu ghasia zinazosababishwa
na wanafunzi katika shule za sekondari nchini.
Andaa ripoti yako.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. Vijana wa kisasa wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za maisha zinazosababisha vifo
vinavyoshuhudiwa nchini. Fafanua huku ukipendekeza hatua zifaazo kuchukuliwa kuzikabili changamoto hizo
ili kuokoa maisha.
3. Maji ukiyavulia nguo yaoge.
4.Tunga kisa kitakachokamilika kwa kauli ifuatayo;
Hapo ndipo wote kwa pamoja walifahamu kuwa gavana waliyemdhania ndiye, siye.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Jina .......................................................................................Nambari....................................................
Sahihi.................. Tarehe.......................................................
102/2
KISWAHILI
Karatasiya Pili
(Ufahamu, ufupisho, Sarufi naMatumiziyalughanaIsimujamii)
Muda: Saa2½
MTIHANIWATATHMINI WA NANYUKIMUHULA WA PILI- 2019
Hati yaKuhitimuElimuyaSekondari Kenya
KidatochaNne 2019
MAAGIZO
• Andikajinananambariyako kwenyenafasi ulizoachiwahapo juu.
• Tiasahihiyako kishauandiketareheyamtihani.
• Jibu maswaliyote.
• Andikamajibuyako katikanafasi zilizoachwakatikakijitabu hiki chamaswali.
• MajibuyakoyaandikwekwalughayaKiswahili.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KWA MATUMIZI YAMTAHINI PEKEE
SWALI ALAMA TUZO
1 15
2 15
3 40
4 10
JUMLA 80
Watahiniwa nilazima waangaliekama kurasa zoteza karatasi hii
zimepigwa chapa sawasawa na kuwamaswali yote yamo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
UFAHAMU
Soma Makala yafuatayo kisha ujibu maswali.
Wahenga walisema “mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.” Hii ina maana ya kuwa ukiogopa
kutumia ufito kumchapa mtoto wako, ukamdekeza, atadeka na hatimaye ataharibika. Methali hii ina
pacha yake ambayo ni, “Ukicha mwana kulia, utalia wewe.”
Hizi ni methali zilizojaa busara kubwa. Mathalani, wewe ni mzazi au mtu yeyote mzima
aliyetunukiwa madaraka juu ya watoto lakini kila wanapokiuka uadiifu au mmoja wao anapokosea wewe
unambembeleza tu, basi huwa unaizorotesha tabia yake. Mwisho, mtoto huyo anaweza kuishia kuwa
mtundu.
Hata hivyo, ni sharti tujue ya kwamba tuko katika njia panda hapa. Kwa upande mmoja, zamani
ilichukuliwa kwamba watoto na hata wanawake watu wazima hawana akili. Kwa ajili hiyo, iwapo
mwanamume mtu mzima ana jambo la kuwaeleza, njia pekee ya kuliingiza katika ‘akili’ yao “hafifu” ni
kuwatwanga ili kulikongomeza jambo hili. Ukweli ni kwamba akili ya mtoto si hafifu hata. Unaweza
kusema kama mmea, ambao “Usiporutubishwa kimakusudi, ukapaliliwa vyema na kustawishwa stahiki
yake, basi hudhoofu” na mwishowe kufifia.
Kwa upande mwingine, mtazamo wa kisasa ni tofauti kabisa. Imethibitishwa ya kwamba
wanawake ni sawa kabisa katika maumbile yao wakilinganishwa na wanaume. Kwa jinsi hiyo, kweli wapo
wanawake ambao hawana mwelekeo timamu kuhusu maisha, lakini ni kweli pia kuwa wapo wanaume
watu wazima mamilioni ambao hawana akili. Ama kwa kusema kweli binadamu yeyote huzaliwa na akili
zake timamu isipokuwa wale ambao kwa bahati mbaya maumbile yamewapa akili pungufu. Hili
litokeapo, basi tunalikubali tu. Hatuwezi kumlaumu mtu kama huyo au muumba wake.Kwa hakika huu
ndio msingi wa methali, “Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Vinginevyo, mtazamo wa kizamani ni
taasubi kongwe tu za kiume zilizopitwa na wakati.
Aidha, kwa sababu watu wote huzaliwa na akili timamu, tena hawawi watu wazima kabla ya
kuwa watoto kwanza, mtu mzima yeyote ana hali gani ya kuwadhulumu watoto na kujipambaniza na
lawama za uongo dhidi ya vijana hao kwa madai kuwa hawana akili? Na je, ikiwa hawana akili, basi ndipo
waonewe? Wanyanyaswe? Hili si jambo la busara. Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha
nyuma kiumbe huyo. Kurudi kufaako ni kwa kupeleka mbele, sio kwa kurudisha nyuma. Kurudi
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
kuelekezako mbele ni kwa uongozi mwafaka, uongozi ambao lengo lake ni kummulikia mtoto kurunzi
ilmradi kumwangazia tarika njema.
Mtoto asinyimwe vya tunu vyovyote ambavyo ni stahiki yake, kwa kisingizio kuwa vimetengewa
mtu mzima, ndugu mkubwa, mwalimu, au mtu awaye yeyote yule aliyekabidhiwa jukumu la kumlea au
kumwongoza mtoto.
Mtoto ana haki ya kuhudumiwa kwa njia yoyote ifaayo ili akue na akili yake ikomae kikamilifu.
Inafaa asomeshwe, apewe malezi bora ili naye aje alee wengine kistahiki.
MASWALI
a) “ Mapenzi yasiyo kipimo yanaweza kuwa hatari kwa mtoto.” Eleza kikamilifu huku ukirejelea habari
uliyosoma. (al 2)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………
b) Fafanua njia panda inayorejelewa na mtunzi.(al 2)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………....
...............................................
c) Mtoto analinganishwa na mmea katika taarifa hii, kwamba, “Usiporutubishwa kimakusudi ukapaliliwa
vyema na kustawishwa stahiki yake, basi hudhoofika.” Tathmini. (al 4)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
d) “ Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Eleza maana ya ndani ya methali hii kulingana na taarifa. (al 2)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………
e) Onyesha kwamba unaelewa maana ya :
“Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo.” (al 2)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………
F) Eleza maana ya ; (al 3)
Kulikongomeza
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Kujipambaniza.
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
Tunu
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MUHTASARI (ALAMA 15)
SOMA TAARIFA IFUATAYO KISHA UJIBU MASWALI
Kuna fikra inayotawala siku hizi kuwa jela si mahali pa adhabu ni matibabu.Yaani lengo la kumfunga
mhalifu si kumuadhibu bali kumtibu kwa njia ya kurekebisha tabia ili aweze kuchangia katika maendeleo
ya jamii yake anapoachiliwa.
Wataalamu wa masuala ya urekebishaji tabia wanasema kuwa mhalifu akaadhibiwa sana na
kufanyishwa kazi ngumu anapokuwa kifungoni, huishi kuwa sugu zaidi kuliko alipofungwa. Kwa hivyo,
wataalamu wanasisitiza umuhimu wa kutilia mkazo lengo la kumtia mtu jela kuwa ni kumjenga kitabia.
Mijizi, minyang’anyi na wauaji wanapotoka gerezani kama hawakubadilishwa hurejelea tabia zao na
kuhatarisha zaidi maisha ya watu wengi.
Ajabu na kinaya ni kwamba baadhi ya wahalifu nchini ni kwingineko wametokea kupata faida kuu
kutokana na vifungo vyao. Kuna wafungwa ambao wamewahi kuandika hadithi za kusisimua kuhusu
maisha yao na kutokea kuwa mabilionea. Magazeti na vyombo vya habari pia huvutwa na habari kuhusu
maisha yao. Mara kwa mara, magazeti hujaa habari kuhusu mambo haya. Pia kuna sinema nyingi
ambazo zimetungwa kufuata maisha ya wahalifu fulani.
Watetezi wa haki za kibinadamu wanadai kuwa yale wafungwa walikuwa wakitendewa, na bado
wanatendewa katika nchi nyingine, ni kinyume na haki za kimsingi za binadamu. Hali hii imepelekea
magereza mengi kukarabatiwa ili kuweza kukidhi mahitaji ya ‘ubinadamu’.
Nchini Kenya, wafungwa sasa wameanza kushughulikiwa kwa kila hali. Sikwambii wanapata chakula
kizuri chenye viinilishe bora, malazi bora, maji safi na mazingira nadhifu kwa jumla. Kumeanzishwa pia
mpango wa elimu ambao ni maalumu kwa wafungwa magerezani. Sasa wafungwa wanapata elimu na
kuhudhuria madarasa na hata kuufanya mtihani wa kitaifa. Vilevile magereza nchini yameanzisha pia
mpango wa kuwa na mashindano ya kila aina kati ya magereza mbalimbali. Kuna mashindano ya
michezo, mathalan kandanda, voliboli, na michezo mingine na juu ya yote, maajuzi magereza yalianzisha
mashindano ya urembo baina ya wafungwa wa kike.
Kilele cha kuboreshwa kwa hali za magereza nchini Kenya na kuanzishwa kwa huduma za
kuwastarehesha wafungwa hao. Sasa wafungwa wa humu nchini wanaweza kusoma magazeti na hata
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
kutazama runinga ili kupata habari kuhusu yanayotendeka nchini wanapoendelea kutumikia vifungo
vyao.
Hata ingawa, serikali imeanzisha mipango hii ya kuboresha hali katika magereza ya kenya kuna matatizo
mbalimbali yanaendelea kukumba taasisi hii. Kwanza ni msongamano wa wafungwa uliopo. Magereza
mengi yana wafungwa maradufu ikilinganishwa na idadi inayofaa kuwa nayo. Hali hii imepelekea kuzuka
kwa magonjwa na madhara ikilinganishwa na idadi inayostahili kuwa nayo. Hii imewafanya watetezi wa
haki za kibinadamu kuitaka serikali ifanye mpango wa kutoa vifungo vya nje kwa wahalifu wenye makosa
madogo madogo ili kuondoa msongamano huo.
Maswali
a) Kwa nini wataalamu na watetezi wa haki za binadamu wanapinga hali ya kuwaadhibu
wafungwa? (maneno 30-40) (alama 5, 1 utiririko)
MATAYARISHO
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………
JIBU
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………
b) Eleza mabadiliko ambayo yamefanywa katika idara ya magereza nchini Kenya. (maneno 60-70)
(alama 8, 1 )
MATAYARISHO
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………
JIBU
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………
MATUMIZI YA LUGHA. (ALAMA 40)
a) Taja na utofautishe sauti sighuna za ufizi. (al 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
b) Onyesha miundo ya silabi katika neno: (al 3)
ukwezi
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………
c) Dhihirisha panapotiwa shadda katika maneno yafuatayo. (al 2)
i) mbwa_____________________________________
ii) kisunzi ___________________________________
d) Huku ukitoa mifano miwili, fafanua miundo ya nomino katika ngeli ya LI- YA. (al 2)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
e) Andika kinyume cha sentensi ifuatayo: (al 2)
Kanzu iliyoangikwa mlangoni ni refu.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
f) Akifisha sentensi ifuatayo kwa njia tofauti ili kutoa maana tatu tofauti. (al 3)
Stanley Nyaga mwanawe Beatrice na Mathenge walizolea shule yao sifa.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………
g) Tambulisha aina za vitenzi vilivyotumika katika sentensi zifuatazo: (al 2)
i) Wanafunzi wa darasani.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………
ii) Maradhi yangali yanamsononesha.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
h) Yakinisha katika ukubwa wingi. (al 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mbuzi mnene hakunywa maji ya mto ule.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
i) Bainisha miundo miwili ya kirai kivumishi. (al 2)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
j) Weka vitenzi vifuatavyo katika hali ya kuamrisha ukizingatia nafsi ya tatu umoja. (al 2)
i) fua_____________________________________
ii) la______________________________________
k) Eleza matumizi mawili ya ‘ni’ kisha utungie sentensi. (al 2)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………
l) Geuza sentensi hii katika usemi wa taarifa. (al 4)
“Sijala kwa kuwa kesho nitahudhuria karamu itakayokuwa na mapochopocho mengi,” jitu
lilimwambia Mzee Mago.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………
m) Unda nomino kutokana na kitenzi : ‘ja’ (al 1)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………
n) Tunga sentensi katika wakati uliopo hali isiyodhihirika. (al 1)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
o) Eleza uamilifu wa neno lililopigiwa mstari . (al 3)
Vile vyeusi vilichuna vitunda vile na kuvila vile.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
p) Changanua sentensi ifuatayo kwa mtindo wa jedwali. (al 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Wimbo ulimpendeza mgeni aliyekuwa mrefu.
q) Badilisha chagizo ya wakati kuwa ya idadi. (al 1)
Mwanafunzi aliadhibiwa leo asubuhi kwa kukaidi amri.
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
r) Eleza maana mbili za neno : koga. (al 2)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………
ISIMU JAMII
a) Eleza sababu tano za watu kuchanganya ndimi au kubadili misimbo. (alama 5)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………
b) Eleza umuhimu wa rejista za lugha. (alama 5)
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
……………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………
Jina………………………………………………………….. Nambari…………………Darasa……………….
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 FASIHI YA KISWAHILI JULAI 2019 SAA 2 ½
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
NANYUKI JOINT EXAMINATION Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya
KISWAHILI Karatasi ya 3
FASIHI YA KISWAHILI SAA 2 ½
MAAGIZO i. Jibu maswali manne pekee. ii. Swali la kwanza ni la lazima.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iii. Maswali hayo mengine yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki yaani Hadithi fupi, riwaya, ushairi na fasihi simulizi.
(iv) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja. Watahiniwa ni lazima wahakikishe kwamba kurasa zote za karatasi hii zimepigwa chapa sawasawa na kuwa maswali yote yamo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
A. SEHEMU A: SWALI LA LAZIMA: USHAIRI.
1. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali.
Kua,
Sikia,
Angalia,
Bongo tumia,
Hadaa dunia,
Mwerevu hutulia,
Mwenye pupa huumia.
Papariko zina udhia,
Sura si kitu kujivunia.
Ukiwa hujafa hujatimia,
Mcheza na tope humrukia.
Asiyetosheka mtumwa wa dunia.
Roho mtoro ipendapo kukimbilia.
Sudi si ya kulilia. Sikuye huwadia.
Watu wote ni sawa hakuna duni kwa Jalia.
Achekapo mwenye meno kibogoyo huungulia,
Zaidi mtu apatavyo ndivyo tamaa huzidia.
Uangaliapo mbele yako na kando yako angalia,
Katika kuishi na wenzetu, sharti tuwe twavumilia.
Hakuna mtoto haramu, vitendo ndivyo haramia,
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Pasi na viganja viwili kofi haliwezi haliwezi kulia.
Sikiliza ya wengi bali lako shikilia.
Binadamu ni wa ila hapana alotimia.
Asiyeridhika ni fukara kupindukia.
Uongo sawa, ukweli watu hususia.
Hakuna raha kamili kwenye dunia.
Ajali huwezi kuitambikia,
Ungali hujatenda fikiria,
Maisha ni ya kuyanyatia.
Mali siyo ya kuringia,
Utu bora ni tabia.
Dhiki kuvumilia,
Sipende kulia,
Shika wasia.
Fikiria.
Wazia.
Tua.
Maswali
(a) Shairi hili ni la aina gani? (alama 1)
(b) Taja lengo la mshairi. (alama 2)
(c) Kwa nini utungo huu unachukuliwa kuwa shairi? (alama 3)
(d) Kwa kutoa mifano, onyesha mbinu mbili za kifasihi zilizotumiwa na mshairi. (alama 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(e) Ni ipi hadhira lengwa ya shairi hili? (alama 2)
(f) Eleza jinsi mshairi alivyoshughulikia dhana zifuatazo: (alama 6)
(i) Tamaa
(ii) Bahati
(iii) Umaskini
(g) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi. (alama 2)
(i) Jalia
(ii) Ila.
B. SEHEMU B: RIWAYA: Chozi la Heri na ASSUMPTA K. MATEI
2. Chozi la Heri ni anwani mwafaka ya riwaya hii. Dhibitisha ukweli wa kauli hii. (alama 20)
3. Usalama ni mojawapo ya mahitaji ya kibinadamu.
a) Liweke dondoo hili katika muktadha wake. (alama 4)
b) Taja sifa mbili za msemaji. (alama 2)
c) Jadili mahitaji mengine ya kibinadamu katika riwaya ya Chozi la Heri. (alama 14)
C. SEHEMU C: HADITHI FUPI: Tumbo Lisiloshiba na Alifa Chokochoko na Dumu Kayanda
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
4. a) Wahusika katika hadithi Shibe Inatumaliza wanatumia uhuru wao vibaya.” Onyesha ukweli wa
kauli hii kwa kutoa mifano. ( alama 10)
b) “Lakini nakwambia tena, kukula kunatumaliza” kwa kudokeza hoja kumi jadili ukweli wa kauli
hii. ( alama 10)
5. “…ilmuradi mawazo yanamwadhibu sasa”
a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
b) Fafanua sifa za anayerejelewa katika dondoo hili.(alama 6)
c) Onyesha mawazo yanayomwadhibu anayerejelewa na dondoo hili. (alama 10)
D. SEHEMU D: TAMTHILIA: Kigogo na Pauline Kea
6. Jadili mbinu ya jazanda katika tamthilia ya Kigogo. (alama 20)
7. “…yarabi…ndio maana… oooh!”
a) Fafanua muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
b) Eleza mbinu za lugha zilizotumika katika dondoo hili. (alama 4)
c) Jadili maudhui ya kifo kama yanavyojitokeza katika Tamthilia ya Kigogo. (alama 12)
E. FASIHI SIMULIZI
8. a) Eleza maana ya nyimbo. (alama 2)
b) taja vigezo vinne muhimu vinavyotumiwa kuzipa majina aina mbalimbali za nyimbo. (alama 4)
c) eleza muundo wa nyimbo kwa jumla. (alama 8)
d) Fafanua umuhimu wa nyimbo za tahili katika jamii. (alama 6)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MTIHANI WA TATHMINI WA NANYUKI
MUHULA WA PILI- 2019
Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari nchini Kenya
KISWAHILI 102/1
Mwongozo
1. - Ripoti.
- Muundo wa insha hii uwe wa ripot k.m
- Kichwa/mada/anuani
- Utangulizi mfupi.
- Wanakamati waliohusishwa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- Mbinu za utafiti, kukusanya data.
- Matatizo/Matokeo/maudhui(ataje angalau hoja tano)
- Mapendekezo (ataje angalau hoja nne)
- Hitimisho.
- Sahihi.
- Tarehe.
Maudhui.
Vyanzo vya ghasia.
- Kushurutishwa kupasi mitihani. - Maagizo, sheria/ya shule k.m jinsi ya kuvalia sare. - Dawa za kulevya/mihadarati. - Kunyimwa uhuru wa kujieleza/kutangamana. - Kudekewa kwa wanafunzi na wazazi wao k.m kupewa fedha nyingi. - Vyakula visivyowaridhisha wanafunzi. - Ukosefu wa miundo msingi/usafiri/burudani n.k - Baadhi ya shule/taasisi hukosa usalama.
Mapendekezo.
- Wazazi/walimu/washikadau katika sekta ya elimu kuwapa ushauri/nasaha wanafunzi. - Wasimamizi wa shule kilegeza sheria za shule. - Serikali kukabiliana na ulanguzi wa dawa za kulevya/mihadarati. - Wanafunzi/viranja kushirkishwa katika kuunda sheria za shule. - Wazazi kutowadekeza watoto wao. - Mashirika yasio ya kiserikali/makanisa kushirkishwa katika kutoa ushauri. - Serikali kulimarisha miundo msingi.
Jinsi ya kutahini.
- Mtahiniwa azingatie vipengele vyote vya sura ya ripoti. - Anayekosa kuzingatia baadhi ya vipengele hivyo – amepungukiwa kimtindo – akadiriwe. - Maudhui yawe tano au zaidi – asiyetaja na kufafanua mauthui tano amepungukiwa
kmaudhui – asipite kiwango cha B. - Anayekosa kuzingatia sura ya ripoti aondolewe maki 4S baada ya kutuzwa. - Angalau mtahiniwa atoe mapendekezo – asiyetoa mapendekezo amepungukiwa kimaudhui.
Asizidi kiwanfo cha C wastani.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
2. Changamoto – mambo yasababishayo ugumu fulani katika maisha, matatizo, vikwazo.
- Baadhi ya hoja - Ukosefu wa ajira - Uigaji wa tamaduni za kigeni - Dawa za kulevya - Magonjwa k.v. ya zinaa - Umaskini - Uchumi kudorora - Kukosa maono - Ujana (ushabashi) - Athari ya utandawazi - Shinikizo la hirimu
Michezo ya kamari
Mapendekezo
- Serikali ibuni nafasi nyingi za kazi - Mashirika ya kutoa mikopo kupunguza riba ili vijana waiombe mikopo - Serikali iongeze misaada ya kifedha kwa watoto kutoka familia /jamaa maskini ili aendelee
masomoni - Mafunzo kuhusu magonjwa ya zinaa/Ukimwi na njia za kuyakabili yawe sehem ya mafunzo
shuleni. - Ushauri kabambe kutolewa kuhusu athari za dawa kulevya
Amakao ya mayatima kuanzishwa.
Tanbihi. Insha bora zaidi ni ile ambayo ina hoja 8 au zaidi kuhusu changamoto na mapendekezo kwa
pamoja. Atakayekosa sehemu moja asizidi C – 08.
3. Maji ukiyavulia nguo, yaoge:
Mtu anapotaka kuoga huvua nguo zote. Si jambo la kawaida mtu kuoga na nguo mwilini hawezi
kuoga sawa sawa. Ukiamua kuoga sharti uvue nguo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Methali hii ina maana kuwa mtu akiamua kutenda jambo lolote duniani basi hana budi
kulitenda. Sio jambo la busara kuamua kutenda jambo kisha urudi nyuma. Ukiyavulia maji nguo
yaoge.
- Akieleza maana vyema na kutoka kisa kinachooana na methali atuzwe ifaavyo.
- Akitoa tu kisa mwafaka kinachooana na methali atuzwe pia ifaavyo.
- Akitoa kisa kisichooana na methali awekwe katika kiwango cha D-03.
Swali la 4
Mtahiniwa lazima achague kisa mwafaka
Mdokezo lazima uwekwe mwishoni.
Mtahiniwa atumie lugha fasaha ambayo inamvutia msomaji
Kanuni zote za uandishi wa insha zizingatiwe kama alama za uakifishaji,sarufi bora,upangaji mzuri wa
aya
Insha itayoandikwa iwe na mtiririko mzuri na uweze kupendeza
Nahau ,methali na msamiati ufaao utumiwe ili kuukoleza utamu wa insha.
Matarajio ya wananchi baada ya kumchangua gavana wa jimbo lao
Kuinua viwango vya elimu katika jimbo lao
Kuboresha huduma za afya
Kupanua nafasi za kazi
Kuwa mwadilifu katika kutekeleza majukumu yake-kuzingatia haki na usawa
Kutafuta ushauri na maoni ya wananchi na kuyazingatia/kuwashirikisha wananchi katika utawala wake
lakini gavana baada ya kuchaguliwa akabadilika
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Amejawa na ubinafsi na tamaa ya kujilimbikiza mali ya umma akiwapuuza wananchi- Mfano ananyakua
vipande vya ardhi
Shule na taasisi za elimu zimepuuzwa na kunyimwa raslimali na hivyo kuporomosha viwango vya elimu
Dawa na vifaa vingine vya matibabu havipatikani hospitalini
Wafanyikazi wa baraza hawalipwi vizuri wala kwa muda unaofaa
Ufisadi umekithiri katika ukusanyaji wa ushuru
Watu wanaajiriwa kazi kwa mapendeleo na ubaguzi
- Mtahiniwa atoe kisa kinachooana na kifungu hiki, la sivyo amejitungia swali na kulijibu.
(atuzwe D – 02)
- JINSI YA KUTUZA INSHA MBALIMBALI - 1. Mtahiniwa asipozingatia sura ya insha aondolewe maki 4 (4sura) baada ya kutuzwa. - 2. Insha isiyotosheleza idadi ya maneno itaondolewa maki 2 baada ya kutuzwa (2u) - 3. Mitindo ya kuandika herufi tofauti tofauti isiingile sana utahini. - 4. Hati ya mtahiniwa isitiliwe maanani mno.
SARUFI
- Sahihisha kwa makini sana ukionyesha makosa yote yanayotokea. - Makosa ya sarufi hutokea katika: - 1. Kuakifisha vibaya: mifano, vikomo, vituo, alama ya kuulizia n.k - 2. Kutumia herufi ndogo au kubwa mahali si pake - 3. Matumizi mabaya ya ngeli na viambishi vya nyakati. - 4. Kuacha au kuongeza neno katika sentensi kwa mfano, kwa - 5. Matumizi ya herufi kubwa.
Tazama : Matumizi ya herufi kubwa
- a) Mwanzo wa sentensi - b) Majina ya pekee - c) Majina ya mahali, miji, nchi - d) Siku za juma, miezi n.k - e) Mashirika, masomo, vitabu n.k - f) Makabila, lugha n.k - g) Mungu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- MAKOSA YA HIJAI - Haya ni makosa ya maendelezo. Sahihisha huku ukiyaonyesha yanapotokea. - Makosa ya tahajia huwa katika: - 1. Kutengainisha neno kama vile ‘aliye kuwa’ - 2. Kuunganisha maneno kama vile ‘kwasababu’ - 3. Kukata silabi vibaya kama vile ‘nguv-u’ - 4. Kuandika herufi isiyofaa katika neno; kama ‘thahari’ badala ya ‘mahali’ - 5. Kuacha herufi katika neno kama ‘aliekuja’ badala ya ‘aliyekuja’ - 6. Kuongeza herufi isiyofaa katika neno karna ‘piya’ badala ya ‘pia’. - 7. Kuacha alarna inayotarajiwa kuwepo katika herufi km. j badala ya j. - 8. Kutoandika kistari cha kuunganisha neno afikapo pambizo au mwishoau kuandika mahali si
pake. - 9. Kukiandika kistari mahali pasipofaa k.m. -alikuwa - 10. Kuacha ritifa au kuiweka pasipofaa - 11. Kuandika maneno kwa kifupi. Mfano k.m nk. k.v
MTINDO.
- Mambo yatakayochunguzwa: - 1. Mpangilio wa kazi kiaya. - 2. Utiririko wa mawazo - 3. Hati nzuri na inayosomeka kwa urahisi. - 4. Namna anavyotumia methali, misemo, tamathali za usemi na mengineyo. - 5. Unadlilifu Wa kazi - 6. Kuandika herufi vizuri km Jj, Pp, Uu, Ww. - 7. Sura ya insha
MSAMIATI
- Jumla ya maneno yaliyotumiwa kuafikiana na mada au kichwa kilichopendekezwa. - MAUDHUI NA MSAMIATI - Baada ya kusoma mtungo, utafikiria na kukadiria maudhui na msamiati uliomo kwa jumla. - ALAMA ZA KUSAHIHISHA - = hupigwa chini ya sehemu ambayo kosa la sarufi; limetokeza kwa mara ya kwanza - - hupigwa chini ya sehemu au neno ambako kosa Ia hijai limetokeza kwa mara ya kwanza - ^ hutumiwa kuonyesha kuachwa kwa neno - √ hutumiwa kuonyesha msamiati bora juu ya msamiati wenyewe - x hutumiwa kuonyesha msamiati usiofaa juu ya msamiati wenyewe - - • Maelezo mafupi kuhusu tuzo la mtahini yanahitajika. Kila ukurasa uwe na alama ya √chini
katikati kuonyesha kuwa mtahini ameupitia ukurasa huo -
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
KISWAHILI
KARATASI YA 2
MAJIBU YA UFAHAMU
a) “ Mapenzi yasiyo kipimo yanaweza kuwa hatari kwa mtoto.” Eleza kikamilifu huku ukirejelea habari
uliyosoma. (al 2)
Ina maana kuwa ukiogopa kutumia ufito kumchapa mtoto wako, ukamdekeza, atadeka na hatimaye
ataharibika.
b) Fafanua njia panda inayorejelewa na mtunzi.(al 2)
Imani ya zamani kuwa watoto na wanawake hawana akili na mtazamo wa kisasa kuwa wanawake ni
sawa kabisa katika maumbile yao na wanaume.
c) Mtoto analinganishwa na mmea katika taarifa hii, kwamba, “Usiporutubishwa kimakusudi ukapaliliwa
vyema na kustawishwa stahiki yake, basi hudhoofika.” Tathmini. (al 4)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mtoto anapodekezwa atadeka na kuharibika
Mtoto akielekezwa vyema atawajibika na kuwa na hatima njema.
d) “ Akili ni nywele, kila mtu ana zake.” Eleza maana ya ndani ya methali hii kulingana na taarifa. (al 2)
Binadamu yeyote huzaliwa kwa akili zake timamu isipokuwa wale ambao kwa bahati mbaya
maumbile yamewapa akili pungufu.
e) Onyesha kwamba unaelewa maana ya :
“Kurudi mtoto kwa visa vya maonevu ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo.” (al 3)
Kurudi mtoto ni kumrudisha nyuma kiumbe huyo.
Kurudi kufaako ni kupeleka mbele sio nyuma.
Kurudi kuelekezako mbele ni kwa uongozi mwafaka ambao lengo lake ni kummulikia mtoto kurunzi ili
kumwangazia tarika njema.
F) Eleza maana ya ; (al 2)
Kulikongomeza
Kulifanya liingie kwa nguvu/ kulazimisha.
Kujipambaniza.
Kujidanganya/ kujisumbua.
Tunu
Kitu cha dhamana.
UFUPISHO
a)
➢ Jela si mahali pa adhabu bali matibabu.
➢ Mhalifu akiadhibiwa huishia kuwa sugu zaidi.
➢ Lengo la kumtia jela ni kumjenga kitabia.
➢ Wahalifu wametokea kupata faida kuu kutokana na vifungo vyao.
➢ Wanayotendewa ni kinyume cha haki za kimsingi za binadamu
(hoja 5,1 ya mtiririko)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b)
➢ Wafungwa wameshughulikiwa kwa kila hali.
➢ Wanapata chakul;a kizuri chenye viinilishe bora.
➢ Wanapata malazi bora.
➢ Hupewa maji safi.
➢ Huandaliwa mazingira nadhifu.
➢ Kumeanzishwa mpango wa elimu ambao ni maalum kwa wafungwa.
➢ Kumeanzishwa mashindano ya kila aina kati ya magereza mbalimbali.
➢ Kumeanzishwa huduma za kuwastarehesha wafungwa.
(hoja 8, 1 mtiririko)
MATUMIZI YA LUGHA. (ALAMA 40)
s) Taja na utofautishe sauti sighuna za ufizi. (al 2)
/t/- kipasuo
/s/- kikwamizo (zozote 2×1=2)
t) Onyesha miundo ya silabi katika neno: (al 3)
ukwezi
u-kwe-zi
I-KKI-KI
u) Dhihirisha panapotiwa shadda katika maneno yafuatayo. (al 2)
i) mbwa____’mbwa_
ii) kisunzi __kisu’nzi_
v) Huku ukitoa mifano miwili, fafanua miundo ya nomino katika ngeli ya LI- YA. (al 2)
Θ- ma yai- mayai
u-ma ugonjwa- magonjwa
w) Andika kinyume cha sentensi ifuatayo: (al 2)
Kanzu iliyoangikwa mlangoni ni refu
Kanzu ilyoanguliwa mlangoni ni fupi.
x) Akifisha sentensi ifuatayo kwa njia tofauti ili kutoa maana tatu tofauti. (al 3)
Stanley Nyaga mwanawe Beatrice na Mathenge walizolea shule yao sifa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Stanley, Nyaga, mwanawe Beatrice na Mathenge walizolea shule yao sifa
ii) Stanley, Nyaga (mwanawe Beatrice) na Mathenge walizolea shule yao sifa.
iii) Stanley Nyaga, mwanawe Beatrice na Mathenge, walizolea shule yao sifa.
iv) Stanley Nyaga (mwanawe Beatrice) na Mathenge, walizolea shule yao sifa.
y) Tambulisha aina za vitenzi vilivyotumika katika sentensi zifuatazo: (al 2)
i) Wanafunzi wa darasani
kitenzi kishirikishi kipungufu
ii) Maradhi yangali yanamsononesha
yangali- kitenzi kisaidizi
yanamsononesha- kitenzi kikuu
z) Yakinisha katika ukubwa wingi. (al 2)
Mbuzi mnene hakunywa maji ya mto ule
Mabuzi manene yalikunywa maji ya majito yale
aa) Bainisha miundo miwili ya kirai kivumishi. (al 2)
i) kivumishi na kivumishi , mfano, Mbwa mnene mweusi amebweka.
ii) kivumishi na kielezi, mfano, Jumba kubwa sana lilibomolewa Nkoroi.
iii) Kivumishi na Kirai nomino, mfano, Mkulima mwenye tumbo kubwa amefika.
bb) Weka vitenzi vifuatavyo katika hali ya kuamrisha ukizingatia nafsi ya tatu umoja. (al 2)
i) fua_ Afue!
ii) la___ Ale!
cc) Eleza matumizi mawili ya ‘ni’ kisha utungie sentensi. (al 2)
i) kitenzi kishirikishi kipungufu, mfano, Fatuma ni mrembo.
ii) Kiwakilishi nafsi umoja- Ninaimba.
iii) Kuamrisha- Amkeni
iv) Kielezi( Kiungama tamati)- Ameingia darasani.
dd) Geuza sentensi hii katika usemi wa taarifa. (al 4)
“Sijala kwa kuwa kesho nitahudhuria karamu itakayokuwa na mapochopocho mengi,” jitu
lilimwambia Mzee Mago.
Jitu lilimwambia Mzee Mago kuwa halikuwa limekula kwa kuwa keshoye/siku iliyofuatia
lingehudhuria karamu ambayo ingekuwa na mapochopocho mengi.
ee) Unda nomino kutokana na kitenzi : ‘ja’ (al 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Mjo/ujio
ff) Tunga sentensi katika wakati uliopo hali isiyodhihirika. (al 1)
Makwere aimba.
gg) Eleza uamilifu wa neno lililopigiwa mstari . (al 3)
Vile vyeusi vilichuna vitunda vile na kuvila vile.
Vile vyeusi- Kiwakilishi
Vitunda vile- Kivumishi
Kuvila vile- Kielezi
hh) Changanua sentensi ifuatayo kwa mtindo wa jedwali. (al 4)
Wimbo ulimpendeza mgeni aliyekuwa mrefu.
Kila ngazi alama 1
S
KN KT
N T N S
Wimbo ulimpendeza mgeni aliyekuwa mrefu.
S
KN KT
N T RN
N S
Wimbo ulimpendeza mgeni aliyekuwa mrefu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii) Badilisha chagizo ya wakati kuwa ya idadi. (al 1)
Mwanafunzi aliadhibiwa leo asubuhi kwa kukaidi amri.
Mwanafunzi aliadhibiwa tena/mara nyingine/mara tatu
jj) Eleza maana mbili za neno : koga. (al 2)
i)osha mwili
ii) ringa/jitwaza
iii) uchafu wa mwili utokanao na nguo chafu ilitovaliwa kwa muda (zozote 2×1=2)
ISIMU JAMII
a) Eleza sababu tatu za watu kuchanganya ndimi au kubadili
misimbo.(alama 5)
• Binadamu kuwa na uwezo wa kuzungumza lugha Zaidi ya moja
• Ili kufidia upungufu wa msamiati
• Mhusika atakapo kujitambulisha katika kundi linalotumia lugha Fulani
• Ili kujihusisha na hadhi ya lugha iwapo katika jamii lugha moja ina hadhi kuliko ingine
• Kumsaidia mzungumzaji kuonyesha hisia zake
b) Eleza umuhimu wa rejista za lugha. (alama 5)
• Husaidia kutofautisha mitindo ya lugha miongoni mwa wanaotumia na hivyo huwa
kitambulishi
• Husaidia kurahisisha au kuharakisha mawasiliano baina ya wahusika
• Husaidia kukidhi mahitaji maalumu ya mawasiliano
• Huongeza lugha na kuipa ladha kwa kufanya mazungumzo yavutie
• Ni njia mojawapo ya kukuza na kutajirisha lugha
• Husaidia katika kuibuka kwa misimu
• Huficha mambo yanayotumika yasifahamike na wasiohusika
• Huwaelekeza watu kuzingatia kaida za matumizi ya lugha katika isimu jamii, na hivyo
kuondoa mitafaruku baina ya wanajamii inayoweza kusababishwa na matumizi ya lugha
• Huondoa urasimu wa matumizi ya lugha sanifu ambayo ina kanuni nyingi za matumizi
ambazo wakati mwingine huchosha, hutatiza na kusumbua wazungumzaji
• Huwawezesha wazungumzaji kujitia na kuzingatia yale yanayohusiana na muktadha
Fulani bila kutapatapa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MTIHANI WA TATHMINI WA NANYUKI
MUHULA WA PILI-2019
Kiswahili
102/3: Fasihi simulizi, Riwaya, Tamthilia, Hadithi fupi na Ushairi.
NAKALA SAHIHISHI
A. SEHEMU A: SWALI LA LAZIMA: USHAIRI
(a) Shairi hili ni la aina gani? (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Shairi huru / mavue/ zohali.
(b) Taja lengo/ madhumuni ya mshairi. (alama 2)
Mshairi alitaka kuwashauri watu kuhusu maisha bora / jinsi ya kuishi vizuri nawatu.
(c) Kwa nini utungo huu unachukuliwa kuwa shairi? Fafanua. (alama 3)
Imetumia lugha ya kishairi.
Lina urari wa vina.
Lugha ya mkato
- lina mishororo
(d) Kwa kutoa mifano, onyesha mbinu mbili za kifasihi zilizotumiwa na mshairi.(alama 4)
Kuna matumizi ya methali, kwa mfano ‘Hujafa hujaumbika’’ na ‘Mcheza na topehumrukia.’
Mshairi ametumia pia msemo kwa kuandika ‘Pasi na viganja viwili kofi haliwezikulia.
Isitoshe, mbinu ya ulinganuzi imetumika pale mwandishi anapoandika kuwamwerevu hutulia
mwenye pupa huumia.
Tashihisi / uhaishaji / uhuishi pia inajitokeza katika shairi hili.
Takriri / uradidi ndicho kinapatikana katika kina cha kila mshororo kwanivinaishia kwa ‘a’.
(e) Ni ipi hadhira lengwa ya shairi hili? (alama 2)
Hadhira inayolengwa katika shairi hili ni wasiotosheka, wasioridhika.
(f) Eleza jinsi mshairi alivyoshughulikia dhana zifuatazo : (alama 6)
(i) Tamaa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Tamaa huzidishwa na ile hali ya kutaka kujipatia mali / unavyopata ndivyo tamaainavyozidi.
Mwenye tamaa ni mtumwa wa dunia.
(ii) Bahati.
Tusililie bahati kwani siku yake itafika, utaipata wakati wako ukitimia.
(iii) Umaskini.
Umaskini husababishwa na kutotosheka.
(g) Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulivyotumika katika shairi. (alama 2)
(i) Jalia.
Mwenyezi Mungu / Rabuka / Jalali / Mola / Mteheremeshi / Yehova.
(ii) Ila.
Uongo / hadaa / udanganyifu.
B. SEHEMU B. RIWAYA: CHOZI LA HERI
2. Ufaafu wa anwani.
i.
MwandishianatulezakuwaRidhaaalipokwendashulenisikuyakwanzaalitengwanawenzakekwani
hawakutakaashirikimichezoyao.Kijanammojamchokozialimwita'mfuatamvua'aliyekujakuwashind
a katika mitihani yote.
Ridhaaalifululizanyumbaninakujitupamchanganinakuliakwakitenashake.Mamake
alimliwazanakumhakikishiakumwonamwalimukeshoye.Tangusikuhii,huuukawandiomwanzowam
aishayaherikwaRidhaakwanibaadayamwalimukuzungumzanawanafunziumuhimuwakuishipamoj
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
akwamshikamano,Ridhaaalipeakwenyeangayaelimuhadikufikiakilelechachaelimunakuhitimukam
adaktari.
ii.
RidhaaalipotokakwenyeMsituwaMambaalijionanafuukwaniwapwa zake
LimenaMwanaheriwalikuwawamepatamatibabu.DadakeSubiraalitibiwaakapona.MwamuwakeKa
izariameponadonda
Lililosababishwanakuwatazamamabintizakewakitendewaukaini(kubakwa)naVijanawenzao.Ridha
a
anajuakuwaKaizariniafadhalikwasababuhakunaaliyemtenganammojakatiyajamaazake.Ridhaa
anapomfikiriaKaizarianajiambiaherinusu sharikuliko sharikamili.
iii
Ridhaaaliposikiasautiyakikeikitangaza,tangazolilelilimrudishakatikamandhariyakeyasasa.Alijaribu
kuangazamachoyakeaoneanakoendalakinimachoyalijaauzitowamachoziambayoalikuwaameyaac
hayamchomenakutiririkayatakavyo.
iv.
WakatiRidhaaalimkaziamachoMwangeka,Mwangekaalikuwaakijiulizaiwapobabakeamekuwa
mwehu kwakukosakushirikiananamajiranikuchimbakaburikuyazika majivu
matonemazitoyamachoziyalitungamachonimwakeMwangeka.Akayaachayamdondokenakumcha
raza,yatakavyo.Uvuguvuguuliotokananamwangukowamachozi
hayauliulainishamoyowake,ukampaamanikidogo.Moyowakeukajaautulivusasakwakujuakuwawin
owaMunguhaufutiki.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
v.
WakatiRidhaaalikuwaakimsimuliaMwangeka masaibu yaliyo
mwandamatangusikualipoondokakwendakuwekaamaniMasharikiyaKati,Ridhaaalisitaakajipangu
zakijashokilichokuwakimetungakipajinimwake kasha
akatoakitambaamfukoninakuyafutamachoziyaliyokuwayameanzakumpofusha.Uk48
vi.
Mwangekaalipokuwaameketimkabalanakidimbwichakuogelea,mawazoyakeyalikuwakulembali
alikoanzia akawaanakumbukachangamotoza ukuajiwake.Akawakumbukawanunawake.
Alipomkumbuka Annatila(Tila)mwiliulimzizimakidogoakatabasamu kasha tonemotolachozi
likamdondoka.
vii.
KatikaMsituwaSimbakulikuwanamaelfu ya watuwalioguramakwao.Katiyafamiliazilizoguriahumu
ni
familiayaBwanaKangata.KwaKangatanamkeweNdarine,hapapalikuwaafadhalikwanihawakuwana
pakwendakwakuwahatakulewalikokuwawakiishiawalihakukuwakwao.Uk57
viii.
WakatiDickwalikutanakisadfanaUmukatikauwanjawandege,walikumbatianakwafuraha.Machozi
yaliwadondokawotewawilinawakawawanaliakimyakimya.Walijuafikakuwajaalailikuwaimewakut
anishanakwambahawatawahikutenganatena.Maishasasayalianzakuwayaherikwao.
ix.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Baadayamiakakumiyakuuzadawazakulevya,Dickalifauluhatimayekujinasuakutokakwakuchaza
mwajiriwake.Alianzabiasharayakemwenyeweyakuuzavifaa vyaumeme.
Sasaakaanzakujitegemeakwakuwaamejiajiri.Alikuwaameufunguaukurasampyakatikamaishayake.
Maishayakesasaniyaheri.
x.
WakatiNeemanaMwangemiwalikabidhiwa motto waowakupanganaMtawaAnnastacia,Mwaliko
alimkumbatiaNeemanakumwitamamanakumwahidikuwaataendanaye.Neemaalidondokwanach
ozi la
furahanakumkumbatiaMwalikokwamapenziyamamamzazi.HilililikuwanichozilaherikwaNeema.
xi.
DickalimwelezaUmukuwasikuwaliokutanakatikauwanjawandegenawakasafiripamoja,hiyondiyo
ilikuwasikuyaheri zaidikwake.NasahaalizopewanaUmuzilimfunzathamaniyamaisha.Kisadfa,
huundio
wakatiDickalikuwaameamuakubadilishamaishanakuishimaishamapyayasiyokuwayakuvunjasheri
a.
xii.
DickaliposimulianamnawazaziwakewapyapamojanaUmuwalivyomfaamaishani,kilammojakatika
Familiahiialilia.Bilashakayalikuwamachoziyaheri.
xiii.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
BaadayaMwalikokujitambulishakwaUmunaDick, UmunaDickhawakungojeaamalize.Walikimbia
wote
wakamkumbatianduguyao,wakaanzakuliahukuwakiliwazana.Hayayalikuwamachoziyafurahakwa
o kwa kupatanatenawotewakiwahai.Kwakwelikilammojaalitokwanachozilaheri.
xiv.
MwalikoalimwambiababakekuwakujakatikahoteliyaMajaliwakuliwaleteaherikwakuwafamiliayao
sasa imepanuka.Sasaamekutananawatualiokuwatuanasikiawakitajwa.Maishasasaniafadhali.
xv.
DickalitoashukranitelekwaUmukwakuwaalimpamatumainikuwasikumojawatampatandugu yao
Mwaliko.MwalikohataanapomtazamaUmu,machoyakeyakiwayamefunikwanavidimbwivyamach
ozi,anajuakuwafamiliayaoimerudianajapokatikamazingiratofauti.
xvi.
SikuambayoMwangekaalimwoaApondiilikuwasikuyaherikwakekwanialimwagachozilaheri.
Tunaelezwakuwa,Ridhaaalijuakuwawakatindiomwamuzi,iposikuatakapotokezahurulainiwake
Mwangeka.Ataifunguakufulikubwailiyoufungamoyowakenahiyoitakuwasikuyakumwagachozilah
eri.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
3. a) Kumbukizi za Mwangeka kuhusu Apondi akiwahutubia hadhira katika warsha iliyoandaliwa
na shirika la msalaba mwekundu. Akizungumzia kuhusu vijana na masuala ya kijinsia.
b) Apondi ni
i. Jasiri
ii. msomi
iii. mtetezi wa haki
iv.
c) Elimu, lishe bora, miundo msingi, mazingira safi, usawa, afya njema, haki za kibinadamu,
malezi mema, demokrasia, makao bora, uhuru, amani, mapenzi n.k
C. SEHEMU C: HADITHI FUPI: Tumbo Lisiloshiba na Alifa Chokochoko na Dumu Kayanda
• 4. a) Mzee Mambo anatumia uhuru wa cheo chake serikalini vibaya kwa kupokea mishahara
kutoka wizara mbalimbali ilhali hafanyi kazi yoyote.
• Sasa na Mbura wanatumia uhuru wao vibaya kwa kupanga na kupangilia wapi kwa kudoea
badala ya kushiriki katika shughuli ya ujenzi wa jamii.
• Wananchi wa taifa la Mzee Mambo wanatumia uhuru wao vibaya kwa kuzingatia kwenda kazini
bila kujali kama wanafanya kazi yoyote. Muhimu si kwenda kazini ila kufanya kazi.
• Mzee Mambo anatumia uhuru wake vibaya kwa kutumia mali na wakati wa taifa kuandaa
sherehe zisizo na msingi wowote. Anaandaa sherehe kubwa kwa madai ya kusheherekea
kuingizwa kwa mtoto wake “nasari”.
• Mambo anatumia magari ya serikali kuhudumu katika sherehe yake.
• Walaji katika sherehe ya kuingizwa kwa mtoto wa kwanza wa Mzee Mambo nasari wanatumia
uhuru wao wa kula vibay kwa vile hawachunguzi kile wanachokula.
• Vyombo vya habari vinatumia uhuru wao vibaya kwa kupeperusha sherehe ya kibinafsi moja
kwa moja, badala ya kumulika mambo yanayoathiri taifa.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
• Sasa na Mbura wanatumia uhuru wao wa kula kila kitu kibaya na kizuri, wanachokijua na
wasichokijua, vyao na vya wenzao hata vya kuokotwa. Hili linawaweka katika hatari ya kuptwa
na maradhi kama kisukari na saratani.
• Dj na wengine wenye nafasi katika taifa wanatumia uhuru wao kupokea mabilioni ya pesa za
serikali kutumbuiza katika sherehe za mtu binafsi.
• Dj na wenzake wanatumia uhuru wao kupata huduma za maji, umeme, matibabu miongoni mwa
huduma nyingine bila malipo huku wananchi wakilazimika kulipia huduma hizi kwa dhiki na
ufukara.
b)(i) Vingozi wa mataifa yanayoendelea kutowajibikia kazi zao. Wanakubali bidhaa duni
kurudidikwa katika mataifa yao: mchele wa basmati
.
(ii) Mali ya umma kunyakuliwa: DJ anafungua duka la dawa zilizotolewa katika bohari ya
serikali huku wanyonge wakiteseka.
(iii) Serikali kuwalipa watu ambao hawafanyi kazi mishahara kubwa hivyo kudhoofisha
uchumi wa nchi - Mzee Mambo.
(iv) Kituo cha televisheni ya taifa kutumika kupeperusha matangazo ya sherehe ambazo
hazina umuhimu wowote katika ujenzi wa taifa.
(v) Wananchi wengine badala ya kuchukua hatua mwafaka dhidi ya wanyakuzi, hungojea
wakati wao ili nao wanyakue: Sasa na Mbura “... na sisi tuende - tusogee.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(vi) Viongozi wananyakua mali ya mabilioni kwa hila na hawajali: Mzee Mambo anaandaa
sherehe kubwa kwa sababu mtoto wake wa kwanza ameingia shule ya chekechea na yule wa mwisho
ameota vijino viwili.
(vii) Watu walio karibu na viongozi kupewa vyeo ilhali wanyonge hawana kazi: Mzee Mambo
ana vyeo viwili.
(viii) Wanyonge kufanya kazi ngumu na nzito kwa malipo duni: Sasa na Mbura; ilhali viongozi
hawafanyi kazi bali wanapakua misharaha minono: Mzee Mambo.
(ix) Viongozi kutowajibika katika kuchunguza utenda kazi wa wafanyikazi wao kwani
hushinikiza wafanyi kazi kwenda kazini na sio kufanya kazi. Jambo
linalohujumu uchumi wa taifa.
(x) Wananchi kuchangia kuzorotesha uchumi wa nchi zao kwa kufumbia macho unyakuzi
unapoendelezwa na viongozi: Sasa na Mbura.
(xi) Viongozi kutochunguza ubora wa vyakula vinavyoletwa shereheni. Vyakula vyenyewe
vinaweza kuwa hatari kwa afya ya binadamu.
(xii) Magari ya serikali kutumika katika sherehe za kibinafsi badala ya kuwahudumia
wananchi. Magari haya yanabeba mapambo; kupeleka watoto kuogeshwa katika sherehe ya Mzee
Mambo.
(xiii) Watu kunyongana na kuuana ili wapate shibe hasa katika mataifa yanayoendelea.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
(xvi) Wenye hadhi ya chini kuruhusiwa kuvitwaa vyao baada ya mabwanyenye kujinyakulia
vyao. Wafanyavyo Sasa na Mbura.
5. a. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
i. Ni kauli ya msimulizi wa hadithi.
ii. Inamrejelea Samueli, mwanafunzi aliyehitimu kidato cha nne.
iii. Samueli yuko katika faragha ya msalani pale shuleni alikoingia pasi na kusukumwa na haja.
iv. Hii ni baada ya kurushiwa ,matokeo na mwalimu mkuu na kuona kuwa amefeli mtihani.
b. Fafanua sifa za anayerejelewa katika dondoo hili. (alama 6)
. Samueli ni;
i. Muoga - Anaonesha uoga anapoingia katika ofisi ya mwalimu mkuu na anapoingia nae anasitasita
ishara ya kuwa muoga. Analemewa kuwakabili wazazi wake na kuwaeleza kuwa amefeli mtihani.
Anatetemeka pia anapomuona baba yake pale bawani alipojitosa ili afe.
ii. Mwenye majigambo : Anajigamba kuwa ana hakika atapita mtihani na kumshtua mwalimu mkuu
ambaye alionesha kutokuwa na imani naye. Anazi kujipata kwa kudai kuwa anaelewa kuwa yeye si
mwerevu sana lakini huweza kupanga mambo yake na kile asomacho ndicho hutokea katika
mtihani.
Anajitapa kwa mpenzi wake Nina kuwa yeye ni bingwa wa masomo.
iii. Muongo : Ana hadaa baba yake kuwa hakupata matokeo kwa kuwa hakuwa amekamilisha kulipa
karo.
iv. Mwenye bidii : Anasema alikuwa akitembea mwendo wa kilomita 6 kuenda shuleni kila siku na
kuwa alihudhuria madarasa yake vizuri.
v. Bwege : Kutokana na majibu ya yale ambayo anasema anayajua, anaonyesha kuwa zuzu na si ajabu
alifeli mtihani.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
vi. Mcheshi : Anachekesha kwa kauli yake kuhusu mwalimu mkuu na wazazi wake. Anasema kuhusu
mwalimu mkuu, “ Labda mwalimu mkuu kazidiwa na maumivu. Labda anataka kufanyiwa
operesheni ya ubongo ama anahitaji maombi hasa atakuwa na akili razini tena” kuhusu wazazi wake
anasema,
“….Mama na baba wameumbwa kwa aina tofauti za udongo”
vii. Mwepesi wa kukata tamaa : Kufeli mtihani shuleni anaona kana kwamba amefeli maishani. Hii
ndio sababu anaamua kujiua.
c. Onyesha mawazo yanayomwadhibu anayerejelewa na dondoo hili. (alama 10
i. Anasumbuliwa na kufeli mtihani. Anaona juhudi zake nyingi za kutembea kilomita sita kuenda shuleni
na kuwa na mahudhurio mazuri darasani zimeshindwa kuzaa matunda.
ii. Analemewa na vipi alivyofeli mtihani ilhali kuna mambo aliyoyajua na alihudhuria madarax vizuri.
iii. Anaona muda wa miaka mine, karo iliyolipwa na baba zimepotea.
iv. Anashindwa kama kuanguka mtihani ina maana kuwa hajui lolote.
v. Anaona kuwa baba yake hataelewa akimwambia kuwa amefeli mtihani.
vi. Anaona kama amesaliti wazazi wake, ilhali yeye kama mwana wa kiume wa pekee ndiye tegemeo lao
la kuwakwamua katika lindi la uchochole
vii. Hajui namna Nina atakavyomchukulia baada ya kufeli mtihani.
viii. Anashindwa namna ya kuwaambia wanafunzi wenzake alichopata katika mtihani.
ix. Analemewa na mawazo kuhusu namna ambavyo dada zake walivyopita mitihani katika shule
hiyohiyo.
x. Anasumbuka kuwa fahari ya babake imokwake kwa luwa yeye ni mwana wa pekee wa kiume katika
familia hiyo.
D. SEHEMU D: TAMTHILIA: Kigogo na Pauline Kea
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
6.
Kinyago cha shujaa anachochonga Sudi kwamba shujaa huyo ni mkubwa kuliko jina lake na urembo wa
shujaa huyo ni bora zaidi. Shujaa anayerejelewa hapa ni Tunu, yale ambayo anatendea Sagamoyo ni
makuu kuliko jina lake, kutetea haki za wanyonge. (uk10)
Husda anamwambia Ashua kuwa hawezi kumtoa tonge kinywani hivi hivi. Tonge ni Majoka bwanake
Husda kuwa Ashua hawezi kumnyanganya bwana.
Husda kumwita Majoka pwagu, pwagu ni mwizi na Majoka amewaibia wanasagamoyo; ananyakua ardhi,
anaiba kodi na kuwalaghai wanasagamoyo. (uk27)
Husda anamwambia Ashua kuwa ameshindwa kufuga kuku na kanga hatamweza. Kuku ni mumewe Sudi,
na Kanga ni Majoka, kwamba Ashua ameshindwa kumtunza Sudi na Majoka hampati. (uk28)
Tunu kuwekewa vidhibitimwendo ni kukomeshwa au kuwekewa vikwazo ili afe moyo kutetea haki za
wanasagamoyo.
Majoka anasema kuwa hatatumia bomu kuulia mbu. Anamrejelea Tunu kuwa mbu kunaanisha
hatatumia
nguvu nyingi kumwangamiza. (uk35)
Majoka anasema ili kuongoza Sagamoyo ni lazima uwe na ngozi ngumu, kumaanisha ni lazima uwe mkali
na mwenye nguvu.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Jukwaa kupakwa rangi kwa ajili ya sherehe ya uhuru ni kufunika uozo ulio Sagamoyo.
Majoka anaposema salamu zinamgoja Sudi kwake, salamu ni Ashua mkewe aliye ndani ya jela.
Majoka anamshauri Sudi anawe mikono iwapo anataka kula na watu wazima. Kunawa mikono ni
kukubali
kuchonga kinyago ndiposa Ashua mkewe aachiliwe.
Chopi anamwambia Sudi iwapo shamba limemshinda kulima aseme. Shamba anarejelea Ashua kuwa
iwapo Ashua amemshinda kutunza, aseme atunziwe na Majoka.
Siafu huwa wengi na si rahisi kuwamaliza. Siafu ni wanasagamoyo ambao ni wengi kuliko Majoka na si
rahisi kuwashnda. Hatimaye raia wanamshinda Majoka. (uk52)
Tunu anasema kuwa moto umewaka na utateketea wasipouzima. Moto ni harakati za mapinduzi
Sagamoyo .Kuteketea nice kumng`oa Majoka mamlakani.
Hashima anamwonya Tunu asijipeleke kwenye pango la joka.Pango la joka anarejelea majoka na watu
wake ambao ni kati na wauaji.
Majoka anadai lazima mtu mmoja atolewe kafara ili watu wajue kuwa kuna usalama Sagamoyo. Chatu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
anamrejelea Sudi au Tunu ambao ni tishio kwa uongozi wake na kuwatoa kafara ni kuua mmoja wao ili
kukomesha maandamano.
Majoka anaposema yupo kwenye chombo cha safari ya jongomeo anamaanisha kuwa mwisho wake uko
karibu kuondolewa mamlakani.
Kinyago cha mke mrembo shujaa anachochonga Sudi kinaashiria Tunu ambaye ni shujaa wa kweli
Sagamoyo
Husda anafananishwa na chui anayeishi ndani ya ngozi ya kondoo kuashiria kuwa yeye ni mnafiki. Hana
mapenzi ya kweli kwa Majoka ila aliolewa naye kwa sababu ya mali.
Jazanda ya marubani ambao hawaendesha vyombo vyao vizuri ni viongozi ambao hawaingozi kwa haki.
wamejawa na ulaghai na tamaa. (uk80)
Babu anamwambia Majoka kuwa hawezi kuelewa mambo kwa vile hajapambua ngozi yake ya zamani.
Majoka anapaswa kubadili mienendo yake mbaya.
Chombo anachopanda Majoka kinaenda kinyume badala ya kwenda mbele, Majoka hajafanya
maendeleo
Sagamoyo kwa sababu ya ufisadi na tamaa. (uk81)
Kisima kuingiwa na paka maji hayanyweki tena. Sagamoyo ni dhiki tele, hakukaliki kwa kuwa na shida
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
nyingi; soko kufungwa, mauaji kutekelezwa na unyakuzi.
7. a) Maneno ya Husda baada ya kupashwa habari na daktari kuhusu kifo cha Ngao. Wako ndani ya
Ambulensi wakimpeleka Majoka hospitalini.
b) mdokezo
Nidaa
c) Vijana watano wanauliwa watu wanapoandamana katika kampuni ya Majoka.
Watu huuliwa Sagamoyo.
"Natumai hakuna aliyeuliwa, sitaki kujipaka matope tena" (uk 31)
Kifo cha Jabali kilipangwa katika ajali kwa kuwa mpinzani wa majoka hata chama chake cha Mwenge
kikamfuata ahera.
Tunu anamwambia Majoka kuwa yeye na wenzake ni wauaji. (uk43)
Viongozi humwaga damu Sagamoyo. Tunu anamwambia Majoka kuwa atalipa kila tone la damu
lililomwagwa Sagamoyo.
Babake Tunu anakufa katika Majoka and Majoka company. Marara na watu wake walimtemdea ukatili.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Hashima anasema damu nyingi imemwagika Sagamoyo hadi ardhi imeingia najisi.
Mashujaa wengine walienda jongomeo kwa kuleta uhuru Sagamoyo.
Ngurumo ananyongwa na chatu akitoka Mangweni.
Majoka anapanga kutekeleza mauaji kwa kumwondoa chatu mmoja ili pawe na usalama
Sagamoyo.Kuomdoa chatu ni kuua Sudi au Tunu.
Kifo cha Ngao junior kinatokea, anapatikana katika uwanja wa ndege akiwa na sumu ya nyoka.
Majoka anasema kuwa ziwa kubwa limefurika damu furifuri kumaanisha vifo vya watu wengi vimetokea
Sagamoyo. Watu wanalilia damu ya Majoka, wanataka kumuua.(uk 79)
Pombe haramu zimesababisha vifo.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
E. FASIHI SIMULIZI
i) Eleza maana ya nyimbo
Ni tungo zilizoundwa kwa maneno ya kupendeza yaliyoteuliwa kiufundi, kiufasaha na yenye utaratibu
wa sauti za kimuziki zinazopanda na kushuka.
ii) Taja vigezo vinne muhimu vinavyotumiwa kuzipa majina aina mbalimbali za nyimbo.
-Vigezo vinne.
- Umri wa wahusika
- Muktadha
- Jinsia
- Lengo la wimbo
- Zana zinazoambatana na wimbo
iii) Eleza muundo wa nyimbo kwa jumla.
-Hugawika katika beti
- Beti huwa na mistari
- Mistari huwa na silabi zenye mapigo ya kimuziki
- Baadhi ya nyimbo huwa na vina
- Nyingine huwa na kiitikio
- Mstari wa mkarara haubadiliki – mara nyingi ndicho kiini cha wimbo
- Waimbaji wana uhuru wa kubuni maneno na kuongezea kulingana na sherehe.
- Hutumia lugha inayoelezea mambo mengi kwa njia ya mkato/mafumbo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv) Fafanua umuhimu wa nyimbo za tahili katika jamii.
- Huimbwa wakati wa maombolezi au kifo
- Hufichua hisia juu ya kifo
- Husifu waliofariki
- Hukashifu maafa
- Hufunza utamaduni unaohusiana na matanga
- Hujenga umoja katika jamii
- Hutuliza nyoyo za waliofiwa.
MURANG’A SOUTH EXAMINATION 2019
KIDATO CHA NNE
KISWAHILI
KARATASI YA 1 (INSHA)
MUDA: SAA 1 3/4
JINA.............................................................................NAMBARI YA MTAHINIWA..................
SAHIHI YA MTAHINIWA.........................................TAREHE......................................
Maagizo
a) Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
b) Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu.
c) Andika insha mbili. Insha ya kwanza ni ya lazima.
d) Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
e) Kila insha isipungue maneno 400.
f) Kila insha ina alama 20.
g) Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
KWA MATUMIZI YA MTAHINI PEKEE
SWALI UPEO ALAMA
1 20
2 20
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
1. LAZIMA
Andika wasifu wa babu yako aliyekuwa mwalimu mkuu katika shule ya upili ya
Tuzo.
2. Wewe ni mbunge wa eneo la Lalama. Pendekeza katika bunge la kitaifa hatua zinazoweza
kuchukuliwa na serikali kuu kumwendeleza kielimu mtoto mvulana.
3. Tunga kisa kitakachodhihirisha maana ya methali ifuatayo:
Asiyejua faida ya mwangaza aingie gizani.
4. Tunga kisa kinachoanza kwa maneno yafuatayo:
Nilipomwangalia baba yangu kisha mama yangu, nilijua kuwa jambo fulani lingetendeka.......
MURANG’A SOUTH EXAMINATION 2019 JINA …………………………………………………………………………………… NAMBARI YAKO…………………………………………………………………… TAREHE………………………………………………………………………………. KISWAHILI KARATASI YA 2 (UFAHAMU, UFUPISHO, MATUMIZI YA LUGHA NA ISIMUJAMII)
3 20
4 20
40
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MUDA: 2 ½ KIDATO CHA NNE MAAGIZO
1. Andika jina lako na nambari yako ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. 2. Tia sahihi yako kisha uandike tarehe ya mtihani 3. Jibu maswali yote 4. Majibuyaandikwe katika nafasi ulizoachiwa katika kijitabu hiki cha maswali. 5. Majibu yote ni lazima yaandikwe kwa lugha ya kisawhili. 6. Usitoe ukurasa wowote kutoka kwenye kijitabu hiki.
KWA MATUMIZI YA MTIHINI PEKEE
SWALI UPEO ALAMA
1 15
2 15
3 40
4 10
UFAHAMU
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali .
Gari lake kuukuu lilikuwa linapambana na barabara yenye mashimo yaliyoshiba na kutapika maji
ya mvua ambayo sasa ilikuwa inaanza kupusa . Japo daima alipambana na usukani kunako
mashimo haya yaliyotosha kuitwa magenge , alishukuru kwa hali hii . Vipi angeweza kulidhibiti
gari lake hili kwenye barabara iliyosakafiwa nayo ikahitimu . Magurudumu haya yaliyong’ara kama
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
upara wa shaibu aliyekula chumvi hadi iikamwogopa yangeyii uelekezi wake . Mara ngapi gari hili
limetaka kumwasi barabarani . Haya yalikuwa baadhi ya maswali yaliyompitikia akilini .
Hakujitakilifu kutaka kuyapa mji maana mara ile mawazo yake yalitekwa na kubwagwa katika
nchi ya mbali - nchi ambayo sasa aliiona kama sinema akilini mwake .
Alipofika nyumbani aliliegesha gari lake na kufululiza ndani . Siku mbili zilikuwa zimepita akiwa
pale kazini . Madaktari kama yeye hawakuwa wengi . Alikuwa miongoni mwa madktari wenye
ujuzi katika hospitali hii ya kitaifa . Wenzake wengi walikuwa wamehamia ughaibuni
walikokwenda kutafuta maisha . Mshahara wao wa mkia wa mbuzi uliwasukuma na kuwatema
nje ya nchi yao . Wengi wa waliohamia ng’ambo waliona vigumu kubaki katika ajira ambayo
kivuno chake kilishindwa kumvusha mtu hata nusu ya kwanza ya mwezi . Malalamishi ya kulilia
ujira wa heshima yaligonga kwenye masikio yaliyotiwa zege . Na kweli wanavyosema , mwenye
macho haambiwi tazama . Basi walitazama hapa na pale wakaona penye mianya ya matumaini ,
nao wakaiandama .
Hadi leo hii hamna la mno lililofanyika . Ndiyo maana Daktari Tabibu anarudi nyumbani tangu
kuingia kazini hiyo juzi alfajiri . Hafanyi kwa kuwa katosheka , maana pia yeye ana dukuduku .
Ana shaka ya mustakabali wake ikiwa mazingira ni haya ya kumsoza , maana umri nao unazidi
kumla . Japo anatia na kutoa , mizani ya hesabu yake imeasi ulinganifu .
Daktari Tabibu waama ni mfungwa . Ametekwa na kuzuiwa katika kupenda na kuchukia mambo .
Ni kama mti uliodumaa . Anatamani barabara nzuri za lami . Anatamani mshahara wa
kumwezesha kukidhi mahitaji yake na kutimiza majukumu yake ya kimsingi . Jana amesema na
rafiki yake aliye ng’ambo kwa simu ambayo sasa imetulia mkabala naye . Ingawaje mwenzake
huyu alikuwa mchangamfu na kumdokolea hali ya maisha ya kuridhisha kule ugenini kama vile
wanataaluma kuenziwa , yapo vilevile yaliyomtia unyonge moyoni . Upweke ndio uliomtia fukuto
kuu . Licha ya hela zote hizo za kupigiwa mfano , watu hawana muda wa kutembeleana na
kujuliana hali au hata kukutana tu mkahawani wakashiriki mlo . Eti ni kila mtu na hamsini zake .
Halafu ipo changamoto ya hali ya hewa . Baridi ya ng’ambo haifanyi mzaha katika kumtafuna
mtu . Ni hali tofauti na ile aliyoizoea .
Daktari Tabibu alizitia kauli za rafiki yake kwenye mizani ya moyo wake . Akawaza ikiwa kweli si
bora kulemazwa na mzizimo ugenini badala ya kuishi katika kinamasi cha kuumbuliwa nyumbani .
Kisha punde lilimjia wazo la marehemu nyanyake na wengine kama yeye waliofadhili masomo
yake kupitia kwa serikali na njia ya kodi . Je , si usaliti huu . Vipi aikimbie nchi kabla ya
kuihudumia ilhali imemjenga hadi kuwa daktari .
Na je , wafanyakazi wake wa nyumbani watakwenda wapi . Atawaambia kuwa sasa hahitaji
huduma zao kwa kuwa anakimbia nchi yake .
Mawazo yake yalikatizwa na simu iliyolia na kumshtua . Alipoitazama aliiona imeng’ara kwa
mwangaza ulioweka wazi jina la mpigaji . Alifahamu kuwa leo hii tena dharura nyingine ilikuwa
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
inamwalika hospitalini . Mwili wake ulimsaliti ingawa moyo wake ulimkumbusha kuwa lisilo budi
hutendwa . Hapo ndipo alipoiinua ile simu tayari kusema na mwenzake upande wa pili .
“Haloo ! ‘ Sauti nyororo kutoka upande wa pili iliita .
“ Haloo ! “
“Naam ! Dharura nyingine tena daktari . Unaombwa kuokoa maisha mengine tena ! “
“ Haya . Ila mwanzo nitahitaji kujimwagia maji ,’ na pale pale akaikata ile simu .
Daktari Tabibu aliingia hamamuni huku kajifunga taulo kiunoni tayari kuoga . Aliyafungulia maji
lakini ule mfereji uligoma kutapika maji . Ulikuwa umekauka kabisa . Daktari Tabibu aliduwaa
pale . Aliufunga ule mfereji kabla ya kuiaga bafu .
MASWALI
(a) Eleza sababu nne zinazowafanya wataalamu kuhamia nchi za nje .( alama 4 )
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------
[b] ‘Hakuna masika yasiyokuwa na mbu . ‘ Thibitisha kauli hii kwa kurejelea hali ya
waliohamia ng’ambo . [ alama 3 ]
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------- ---------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------
[c] Fafanua athari tatu zinazoikumba nchi ya msimulizi kutokana na uhamiaji wa
wataalamu . [ alama 3 ]
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
-------------------------------------------------------------------------------------------------------
[ d ] Eleza mchango wa teknologia kwa kurejelea kifungu. [alama 3 ]
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
---------------------------------------------------------------------------------------------
[ e ] Eleza maana ya msamiati ufuatao kulingana na taarifa . [ alama 2 ]
[ I ] kuyapa mji ----------------------------------------------------------------------------------------------------
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
[ ii ] fukuto --------------------------------------------------------------------------------------------------------
-----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
2. UFUPISHO(ALAMA 15): Soma makala haya kisha ujibu maswali uliyopewa.
Maadili katika familia ni muhimu katika malezi ya Watoto. Hivi ndivyo alivyoniambia mtaalamu
wa masuala ya Watoto Scola Wanjiru katika hospitali ya Kaunti ya Machakos. Anasema ugomvi baina ya
wazazi husababisha watoto kutokuwa na maadili bora huku baadhi yao wakijiunga na makundi ya
wahuni au hata kuzikimbia familia zao.
Bi Wanjiru asema ugomvi wa familia huonekana zaidi kwa watoto ambao hupata matatizo ya
kusaikolojia na hivyo kuvuruga ndoto zao za baadaye,” asema. Anasema ugomvi huwaacha Watoto na
vidonda moyoni ambavyo wakati mwingine huwafanya wawe katili na hata kuamini kwamba ugomvi ni
sehemu ya Maisha katika wanadamu.
Adokeza kuwa utafiti unaonyesha kwamba mara nyingi ugomvi husababishwa na ulevi wa mzazi
au wazazi kutoelewana kuhusu masuala ya kifamilia. Madhara yake kwa watoto huwa ni hofu na
wasiwasi na kujihisi wapweke kila mara, “ asema Bi Wanjiru. Aidha kuathirika kisaikolojia hupelekea
Watoto kujingiza kwenye vitendo viovu kama ulevi na uvutaji bangi na hata kutamani kujiua. Mtaalamu
huyo asema wazazi wanafaa kuwa waangalifu kwa watoto wao ili wasivuruge ndoto zao za baadaye kwa
kukosa msingi bora na malezi mema.
Utafiti umeonyesha kwamba Watoto wengi waliokimbia hufanya hivyo ili kuepuka ugumu wa
maisha wazazi wanapotengana au hali waionayo nyumbani kila mara wakati wa ugomvi wa wazazi au
ndugu zao,” asema Bi Wanjiru aliye pia mtafiti wa masuala ya watoto. Watoto wanaolelewa kwenye
familia au wazazi wanagombana kila wakati, hukosa kutimiziwa haki zao za msingi kama vile elimu, afya,
malazi, mavazi na kusikilizwa.
Bi Wanjiru anawakumbusha wazazi kutimiza wajibu wao ili watoto hao wapate malezi bora zaidi
na ili waweze kutimiza ndoto zao za baadaye. Anasema tafiti mbalimbali zimeonyesha watoto
wanaotoka katika familia zenye ugomvi wa mara kwa mara, hupata magonjwa mbalimbali kama
kuumwa kichwa, na kuwa na mawazo wakati wote. “ Madhara ya hali hiyo kwa watoto ni kutofanya
vizuri shuleni, kwa sababu huwa wanawaza juu ya ugomvi uliopo nyumbani.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kadhalika mara nyingine mfarakano na ugomvi huwafanya watoto wasipate usingizi wa kutosha
na kutatizika darasani. Watoto walioathirika pia huwa wakorofi, wakaidi na wenye hasira mara kwa
mara, jambo ambalo linaathiri utulivu darasani na hivyo kushindwa kutimiza malengo yao.
Ugomvi pia hufanya watoto kuwa na chuki, kuna uwezekano mkubwa kwamba ikiwa baba
anapenda kuzua ugomvi mtoto wa kike atawachukia wanaume maishani mwake. Hali kadhalika, kwa
upande mwingine, kama mzazi wa kike atakuwa ndiye chanzo cha ugomvi katika familia, basi mtoto wa
kiume atawachukia wanawake akifananisha tabia yake na wanawake wengine.
Ugomvi husababisha watoto kuiga tabia mbaya hasa ya kupigana ambapo anaweza kufikiria
kuwa njia pekee ya kusuluhisha matatizo nyumbani ni kulewa na kuanzisha malumbano, ambayo wakati
mwingine husababisha vita. Utafiti wa Save the Children uliofanywa 1998 ulionyesha kwamba kati ya
asilimia 45 na 70 ya watoto walioshuhudia ugomvi wa familia, waliathirika kusaikolojia.
Bi Wanjiru anasema familia ambazo ugomvi ni nadra kufanywa mbele ya watoto, utafiti
umeonyesha kwamba watoto hao huwa na nidhamu na huafikia malengo yao maishani. Ni wajibu wa
mzazi kuchukua hatua kuepusha ugomvi mbele ya watoto.
MASWALI
a) Fupisha ujumbe wa aya tatu za mwanzo kwa maneno (85 -90) [alama 8]
[Utiririko 1]
Nakala chafu
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………… Jibu
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
……………………………………………………………………………………………………………………………………………
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b) Eleza madhara makuu kwa watoto wanaolenlewa katika jamii ambazo zina ugomvi.
[Maneno 50][alama 5] [Mtiririko 1)
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………Nakala safi
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………….
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
…………………………………………………………………………………………………………………………………………………
MATUMIZI YA LUGHA
a) Andika sentensi ifuatayo katika usemi halisi. [alama 3] Raisi
alisema kuwa angesafiri kwenda Somalia siku hiyo alasiri.
b) Andika neno lenye muundo ufuatao. [alama 2]
Kiambishi ngel,i wakati ujao, mzizi, kauli tendwa, kauli tenda (kiishio )
c) Bainisha shamirisho katika sentensi ifuatayo. [alama 3]
Juma alipakuliwa chakula kwa bakuli.
d) Tumia neno mume kama kielizi katika sentensi. [alama 2]
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
e) Tunga sentensi yenye kishazi kirejeshi ambacho ni kivumishi. [alama 2]
f) Tunga sentensi yenye kitenzi kishirikishi kikamilifu. [alama 1]
g) Ainisha sentensi ifuatayo kwa kuzingatia jukumu/dhamira yake. [alama1]
Funga majani matatu matatu kwa kila fungu.
h) Nyambua vitenzi vifuatavyo katika kauli zilizo kwenye mabano. [alama 2]
i) la - (tendeana)
ii) Vaa (tendwa)
I) Onyesha matumizi ya kiambishi ‘ku’ katika sentensi ifuatayo. [alama 2]
Juma atakutengenezea mpini wa jembe kisha aelekee kule kwao.
j) Onyesha kiima na chagizo katika sentensi ifuatayo. [alama 2]
Wanafunzi wale walijibu maswali kwa utaratibu.
k) Andika sentensi ifuatayo kwa wingi, wakati uliopita hali ya kuendelea. [alama 2]
Mwalimu humwadhibu mwanafunzi mwenye hatia.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
l) Tenga viambishi na mzizi katika neno ‘Siji’. [alama 2]
m) Changanua sentensi ifuatayo kwa jedwali. [alama 4]
Nilimwona mamba majini nilipopiga mbizi.
n) Andika sentensi ifuatayo upya ukibadilisha vitenzi vilivyopigiwa mstari katika kinyume. [alama 2]
Mwanafunzi aliketi kisha akakitega kitendawili.
o) Eleza tofauti kati ya sentensi hizi. [alama 2]
“ Ningefika mapema ningemkuta mwalimu darasani.
Ningalifika mapema ningalimkuta mwalimu darasani.
p) Andika visawe vya maneno haya. [alama 2]
i) Heshima
ii) Ruhusa
q) Bainisha mofimu katika neno wafiwa. [alama 2]
v) Andika sauti zenye sifa zifuatazo. [alama 2]
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) Kikwamizo ghuna cha mdomo na meno.
ii) Irabu ya nyuma, wastani.
s) Eleza maana mbili za sentensi ifuatayo-
Jua lile ni muhimu kwetu.
ISIMU JAMII. [alama 10]
a) Eleza maana ya sajili ya lugha. [alama 2]
b) Fafanua mambo manne yanayosababisha kuibuka kwa sajili tofauti. [alama 8]
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MURANG’A SOUTH EXAMINATION 2019
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Jina…………………………………………….........................Nambari……………..……...
KISWAHILI
KIDATO CHA NNE
FASIHI (KARATASI YA 3)
MUDA: SAA 2 ½
MAAGIZO KWA MTAHINIWA
a) Jibu maswali manne pekee
b) Swali la kwanza ni la lazima
c) Maswali hayo mengine matatu yachaguliwe kutoka sehemu nne zilizobaki ;
yaani :Tamthilia, riwaya, ushairi na fasihi simulizi.
d) Usijibu maswali mawili kutoka sehemu moja.
Kwa matumizi ya mtahini pekee
Swali
1
2 3 4 5 6 7 8 Jumla
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
SEHEMU YA A. SWALI LA LAZIMA
TUMBO LISILOSHIBA na hadithi nyingine (wahariri: A. Chokocho na D. Kayanda)
1. Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya, ‘Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine.’ Jadili
maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi. (alama 20)
SEHEMU B. TAMTHILIA: KigogoPuline Kea
2. “Tusiwaruhusu watu wachache waliojazwa kasumba….kuturejesha ….hatuwezi kukubali kutawaliwa kidhalimu tena.”
a. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama4)
b. Kwa kumrejelea mzungumzaji wa maneno haya, bainisha unafiki katika kauli hii. (alama
16)
3. Eleza jinsi mbinu ya taharuki ilivyotumika kufanikisha maudhui katika tamthilia ya kigogo. (alama 20)
SEHEMU D. RIWAYA.
CHOZI LA KHERI NA Assumpta Matei
4. Jadili maudhui ya ‘migogoro’ katika riwaya ya Chozi la Kheri. (al 20)
5. “ …alinionya dhidi ya kumwambia yeyote kuhusu unyama…” a) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4) b) Fafanua sifa nne za anayehusishwa na maneno haya. (al4) c) Onyesha namna ukiukaji wa haki za watoto unavyotokea katika riwaya hii. (alama12)
6. SEHEMU YA E. FASIHI SIMULIZI a) Huku ukitoa hoja sita linganisha aina mbili kuu za fasihi. (alama6) b) Jadili vipengele sita vya kuzingatia katika uchanganuzi wa hadithi.(alama6) c) Jadili sifa mbili za vitanza ndimi kwa kurejelea sauti. (alama 2) d) Tambua dhana zinazotokana na maelezo haya.
i. Msimulizi wa fasihi simulizi anaitwaje kwa jumla? (alama1) ii. Shujaa katika mighani pia anaweza kuitwa nani? (alama 1)
iii. Sherehe za kitamaduni ambazo hufungwa na jamii katika kipindi fulani maalum huitwaje? (alama 1)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv. Mavazi au vifaa vinavyotumiwa na wasanii kuakisi hali halisi ya mambo wakati wa kuwasilisha fasihi huitwa(alama 1)
v. Mtambaji wa hadithi hutumia ujuzi gani anapoibadilisha hadithi yake moja kwa moja mbele ya hadhira bila kuathiri usimulizi wake?(alama 1)
vi. Wanaosimuliwa ili kuonyesha kazi ya fasihi simulizi hupewa jina hili.(alama 1)
SEHEMU YA E. USHAIRI
7. SHAIRI A
MWANA
1. Kwani mamangu u ng’ombe, au u punda wa dobi?
Nakuuliza usambe, nayavunja madhehebi
Nalia chozi kikombe, uchungu wanisibabi
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
MAMA
2. Nong’ona mwana nong’ona, sitafute angamiyo
Sinipe kuja sonona, kwa uchungu na kiliyo
Babayo mkali sana, kubwa pigo la babayo
Kwani kelele kunena, huyataki maishiyo?
Hilo nakwambia.
MWANA
3. Sitasakamwa kauli, nikaumiza umiyo
Nikabeba idhilali, nikautweza na moyo
Siuvuwati ukweli, hazidisha gugumiyo
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Baba hafanyi halali, nawe hwachi vumiliyo
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
Nambie ipi sababu, ya pweke kwenda kondeni
Nini yako matulubu, kulima hadi jioni?
Na jembe ukidhurubu, ukilitua guguni
Yu wapi wako muhibu, Baba kwani simuoni?
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
Baba kwani simuoni, kuelekea shambani?
Kutwa akaa nyumbani, na gumzo mitaani
Hajali hakuthamini, wala haoni huzuni
Mwisho wa haya ni nini, ewe mama wa imani?
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
Na kule kondeni kwako, ukate kuni kwa shoka
Ufunge mzigo wako, utosini kujitwika
Kwa haraka uje zako, chakula upate pika
Ukichelewa vituko, baba anakutandika
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Chakula kilicho ndani, ni jasho lako hakika
Kiishapo u mbioni, wapita kupokapoka
Urudi nje mekoni, uanze kushughulika
Ukikosa kisirani, moto nyumbani wawaka
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo
MAMA
Wanitonesha kidonda, cha miaka na miaka
Usidhani nayapenda, madhila pia mashaka
Nakerwa na yake inda, na sasa nimeshachoka
Ninaanza kujipinda, kwa mapambano hakika
Hilo nakwambia
MASWALI
a) Mtunzi wa shairi hili alikuwa na dhamira gani katika kutunga shairi hili. (alama 2)
b) Shairi hili ni la aina gani ? Toa ithibati. (alama 2)
c) Yataje mambo yoyote matano anayoyalalamikia mwana. (alama 5)
d) Eleza kanuni zilizotumika kusarifu ubeti wa tatu. (alama 5)
e) Andika ubeti wa saba kwa lugha tutumbi. (alama 4)
f) Eleza maana ya maneno haya yalivyotumika katika shairi hili.
(i) jaza (alama 1)
(ii) muhibu (alama 1)
AU
8. SHAIRI B
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Soma shairi hili kisha ujibu maswali
1. Punda kalibebe gari, gari limebeba punda
Mwalimu ana pakari, muashi vyuma adunda
Jaji gonga msumari, sonara osha vidonda.
Kinyume mbele
2. Saramala ahubiri, muhunzi tiba apenda
Mganga anaabiri, baharini anakwenda
Hata fundi wa magari, anatomea vibanda
Kinyume mbele
3. Wakili anahiyari, biashara kuitenda
Mtazame askari, akazakaza kitanda,
Mkulima mashuhuri, jembe limemshinda
Kinyume mbele
4. Apakasa daktari, ukili anaupinda
Saveya kawa jabari, mawe anafundafunda,
Hazini wa utajiri, mali yote aiponda,
Kinyume mbele
5. Msemi huwa hasemi, wa inda hafanyi inda
Fahali hawasimami, wanene waliishakonda
Walojitia utemi, maisha yamewavunda
Kinyume mbele
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
6. Kiwapi cha kukadiri, twavuna shinda kwa shinda
Tele haitakadari, huvia tulivyopanda
Mipango imehajiri, la kunyooka hupinda
Kinyume mbele
MASWALI
a) Mtunzi alikuwa na malengo gani alipotunga shairi hili? (alama 3)
b) Licha ya tarbia, eleza bahari nyingine zinazojitokeza katika shairi hili. (alama 4)
c) Eleza namna mtunzi alivyoutumia uhuru wake. (alama 5)
d) Ni mbinu gani inayotawala shairi hili? (alama 2)
e) Uandike ubeti wa nne katika lugha nathari. (alama 4)
f) Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MURANG’A SOUTH EXAMINATION 2019
KISWAHILI
KARATASI 1
INSHA (MWONGOZO WA KUSAHIHISHA)
1. Mwanafunzi azingatie muundo wa wasifu.
i) Kichwa
ii) Mwili – maudhui kulingana na mada.
iii) Hitimisho – umaarufu wake na sababu za kutambulikana. Tanbihi
i) Maelezo yawe ya kinatharia.
ii) Aandike kwa mpangilio na mtiririko halisi wenye maana km, jina, umri,
alikozaliwa, utoto wake, familia yake, elimu, makazi kazi na tajriba yake,
matendo aliyotenda, pingamizi alizokumbana nazo, ushindi. n.k.
iii) Atumie nafsi ya tatu.
iv) Aaandike katika wakati uliopita.
2. i) Kupiga marufuku ajira za watoto
ii) Kutoa msaada wa karo kwa familia zisizojiweza kifedha.
iii) Kuwahimiza na kuwashauri wavulana kujiunga na shule.
iv) Kupiga marufuku uendeshaji wa pikipiki na wavulana ambao hawajahitimu
katika kidato cha nne.
v) Kupanua shule za wavulana zilizoko.
vi) Kuwe na sheria ya kulazimisha watoto wavulana kumaliza masomo yao.
vii) Alama za kujiunga na shule na vyuo kusawazishwa na za wasichana.
viii) Kuhamasisha wazazi na jamii kuhusu umuhimu wa elimu ya mvulana.
ix) Elimu bila malipo kwa shule na vyuo.
Tanbihi
Mtahiniwa akadirie hoja zozote zinazooana na swali.
3. i) Hii ni insha ya methali.
ii) mtahini abuni kisa kinachodhihirisha maana ifuatayo;
Mtu kutotambua umuhimu wa mtu au kitu/kutokithamini mpaka anapokikosa kile
kitu km pesa, mali, wazazi, walimu, marafiki n.k.
4. Hali zifuatazo zinaweza kujitokeza
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
i) mambo mazuri
ii) mambo mabaya
Tanbihi
i) Mtahiniwa anaweza kutumia mbinu rejeshi baada ya kuandika kauli ya kwanza.
ii) ii) Kisa kinaweza kusimuliwa katika nafsi ya kwanza, ya tatu au mchanganyiko
wa nafsi ya kwanza, ya tatu na ya pili.
MURANG’A SOUTH EXAMINATION 2019
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
KARATASI 2
KIDATO CHA NNE
1. UFAHAMU
a)
✓ Kuharibika kwa miundo msingi
✓ Mishahara duni
✓ Malalamishi yao kutosikilizwa
✓ Kukosa huduma za kimsingi
✓ Kuvutiwa na maisha ya kuridhisha huko ng`ambo (hoja 4 za kwanza)
b) Ng’ambo kuna maisha ya kuridhisha kama kuthaminiwa kwa wanataaluma(alama 1)
- Hata hivyo kuna dosari (mbu) kama upweke, ubinafsi na baridi.(alama 2)
c) Umma kutofaidika kutokana na huduma za wataalamu wake licha ya kuwafadhili.
- kuwaachia mzigo wa kazi wataalamu
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
- kulazimika kufanya kazi kwa saa nyingi
- Maisha ya watu wengi huwa hatarini.
- Hasara kwa taifa baada ya wataalamu kutoroka
- kuwapoka riziki wafanyakazi (hoja 3 za kwanza)
d) Huwezesha kuwasiliana na jamaa walio mbali
- Huwezesha kuwafikia watoaji huduma patokeapo dharura
- Hurahisisha usafiri
- Hurahisisha kupata huduma ya karibu ya maji (alama zozote 3)
e) i) kuyapa mji - kuyawazia, kufikiria, kuyatafakari.
ii) Fukuto - wasiwasi,mashaka, shida, dukuduku
UFUPISHO
a) Maadili katika familia ni muhimu katika malezi ya watoto.
- ugomvi baina ya wazazi husababisha watoto kutokuwa na maadili bora.
- Baadhi yao hujiunga na makundu ya wahuni/kuzikimbia familia zao.
- Hupata matatizo ya kisaikolojia.
- Huwaacha Watoto na vidonda moyoni.
- Ugomvi husababishwa na ulevi wa wazazi/wazazi kutoelewana kuhusu maswala ya familia.
- madhara yake ni hofu na wasiwasi na kujihisi wapweke.
- Hujiingiza kwenye vitendo viovu.
- Wazazi wanafaa kuwa waangalifu kwa watoto wao.
b) - Hupata magonjwa mbalimbali
-kutofanya vizuri shuleni
- Huwafanya wasipate usingizi wa kutosha na kutatizika darasani
- Huwa wakorofi
- Kuwa na chuki
- Husababisha Watoto kuiga tabia mbaya.
a-8
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
b-5
Mtiririko-2
Matumizi ya lugha
a) “ Nitasafiri kwenda Somalia leo alasiri.” Raisi alisema. ½
b) ki -ta -nunu – liw – a ½
mwanafunzi anaweza kutumia kiambishi nafsi.
d) Juma – kitondo chakula – kipozi
bakuli – ala
d) Juma alipigana kiume. – 1
e) Nyumba ambayo ilijengwa inapendeza. – 1
(atumie kirejeshi amba/
f) Rehema amekuwa stadi -1
(asitumie kitenzi kisaidizi)
g) Maagizi, amri, maelekezo - 1 x1
h) i) Liana -1
ii) Valiwa - 1
I) Atakutengenezea – nafsi ya pili umoja - 1
Kule – mahali - 1
j) Wanafunzi wale – kiima
kwa utaratibu - chagizo
k) Walimu walikuwa wakiwaadhibu wanafunzi wenye hatia.
l) Si - J - i
kiambishi mzizi kiambishi tamati
awali
Si - J i
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kikanushi cha mzizi kiishio
nafsi ya kwanza
Umoja
Kutenga viambishi 1\2
m) KN KT
O T N E S
Nilimwona mamba majini tulipopiga mbizi
n) Mwanafunzi alisimama kisha akakitegua kitendawili.
Lazima aandike sentensi upya.
O 1) Kuna uwezekano au matumaini
2 Hakuna uwezekano au matumaini.
p) i) Staha,taadhima
ii) Idhini, kibali
q) Wa - f iw a
nafsi mzizi kauli kiishio
r) i) /v/
ii) /o/
Atumie herufi ndogo
s) - Elewa, fahamu, nga’mua, maizi, amili
- gimba kubwa lenye nuru kali lililoko angani ambalo hutoa mwanga na joto
- mahali
- sisi binafsi [kwetu]
ISIMUJAMII
a) Ni mitindo au namna mbalimbali za matumizi ya lugha.
b) shughuli – shughuli mbalimbali huwa na sajili yake.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Muktadha – ni mazingira ambamo mazungumzo yanatokea na matumizi ya lugha hutofautiana
kutegemea mahali.
- Mada – mada humfanya mtu kuelekeza fikira zake kuhusiana na jambo linalohusika.
- Uhusiano – uhusiano wa wazungumzaji huathiri uteuzi wa maneno au msamaiti.
- Jinsia- wanawake hutumia msamiati na miundo tofauti na lugha ya wanaume.
- Umri – lugha ya vijana hujumuisha sheng’ na lugha ya wazee husheheni methali.
- Hali – mtu akiwa na hasira au furaha hutumia lugha kulingana na hali yake.
- Lengo-Lengo la shughuli huathiri matumizi ya lugha.
Kutaja – 1
Mfano/maelezo-1
Hoja nne za kwanza
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
MURANG’A SOUTH EXAMINATION 2019
KISWAHILI
KARATASI YA 3
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
FASIHI
MWONGOZO WA KUSAHIHISHA
SEHEMU YA A. SWALI LA LAZIMA
TUMBO LISILOSHIBA na hadithi nyingine (wahariri: A. Chokocho na D. Kayanda)
1. Kwa kurejelea hadithi zozote tano katika diwani ya, ‘Tumbo lisiloshiba na hadithi nyingine.’ Jadili
maudhui ya nafasi ya wazazi katika malezi. (alama 20)
MAJIBU
Tulipokutana Tena
• wazazi wa Bogoa - ni walezi wema ingawa ni maskini hawatakiBogoa alelewe na wazazi wengine.
• Bi. Sinai anamfanya Bogoa mtumwa.
• Bi. Sinai anamnyima Bogoa uhuru wa kucheza na watoto wengine.
• Babake Bogoa anamtisha Bogoa kwa mkwaju.
• Mamake Bogoa alimpenda Bogoa - anamtayarisha asubuhi kabla ya kuondoka. Mapenzi ya kifaurongo
• wazazi wa Penina Bw & Bi Kitime wamewajibika katika kumlea Penina. Wanampa fedha za kutosha kila wiki
• licha ya kuwa maskini wazazi wa Dennis wanajizatiti sana kumpeleka hadi chuo kikuu
• Wazazi wa Denis wajitaabisha ili kumtunza.
• wazazi wa Penina wanalipa kodi yake. Shogake Dada ana ndevu
• wanawapeleka wanao shuleni. k.m Wazaziwe Safia wanampa nafasi ya kusoma.
• Wazazi hawa pia wana mapuuza. Wanamwamini mwanao kupita kiasi.
• Wazazi wake Sara wanampa kazi nyumbani k.m kufagia.
• Mamake Sara anamjulia hali anapoona mabadiliko.
• Habiba Chechei hawajamlea mtoto wao Mkandi vizuri. Mame Bakari
• babake Sara ni mkali sana, Sara anapobakwa anaogopa kumwambia kuwa ana ujauzito
• baadaye anabadilika wa kuwa mpole, anamfariji
• mamake Sara ni dhaifu, hawezi kumsaidia Sara.
• wazazi wake wanalipa gharama zote za ujauzito wake.
• wazazi wake wanafika hospitalini kumjulia hali. Mtihani wa maisha
• wazazi wa Samueli wanajinyima ili kuwasomesha watoto wao
• Babake Samueli aliuza ng’ombe wengi ili kumsomesha Samueli
• mamake Samueli anatumiwa kuonyesha mapenzi ya mzazi ni ya kudumu
• babake Samueli anatumiwa kuonyesha kukata tamaa / kutamauka
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Kadiria mengine yoyote
SEHEMU B.TAMTHILIA: Puline Kea
2. “Tusiwaruhusu watu wachache waliojazwa kasumba…. kuturejesha …. hatuwezi kukubali kutawaliwa
kidhalimu tena.”
a. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama4)
b. Kwa kumrejelea mzungumzaji wa maneno haya, bainisha unafiki katika kauli hii. (alama
16)
JIBU
a) i. Haya ni maneno ya sauti ya Majoka iliyorekodiwa katika redio.
ii. Anawahutubia Wanasagamoyo
iii. Anayasema maneno haya akiwa ikuluni.
iv. Sauti hii imechezwa ili kuwafahamisha raia aliyoyasema Majoka kuhusu kuisherehekea miaka sitini
ya Uhuru –Majoka alikuwa ametangaza kipindi cha mwezi mzima wa kusherehekea uhuru.
(alama 4)
b) Unafiki katika kauli hii
Majoka anasema kuwa hawatakubali kutawaliwa kidhalimu ilhali ndiye anayetawalia kidhalimu.
i. Kufunga soko : Anafunga soko la chapakazi hivyo kuwahini wafanyakazi kama vile Ashua riziki ya
kila siku.
ii. Wahuni : Ana kundi la wahuni liitwalo chatu analotumia kuwaua raia kwa mfano mkuu wa polisi
anapokataa kumtii kuwapiga risasi anamtisha kwamba angevunjwavunjwa na chatu siku hiyo.
iii. Mapenzi : Anamtaka Ashua akubali kufanya mapenzi naye ndipo amsaidie lakini Ashua anakataa.
iv. Kukata miti : Amefungulia biashara ya ukataji miti hivyo kuitishia ukame jimboni.
v. Kuwaua raia : Utawala wake unaeneza vijikaratasi vinavyowataka baadhi ya raia kuhama jimbo la
sagamoyo kwa madai kwamba si kwao.
vi. Vijikaratasi : Utawala wake unaeneza vijikaratasi vinavyowataka baadhi ya raia kuhama jimbo la
sagamoyo kwa madai kwamba si kwao.
vii. Kupandisha bei ya chakula : Anapandisha bei ya chakula katika Kioski chake baada ya
kufunga soko lililokuwa tegemeo kwa raia, hivyo kuwasababisha wafanyikazi kuanza kuandamana.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
viii. Kuwatusi raia - Anawatusi raia wanapoususia mkutano wake na kuandamana ili kumshurutisha
kufunga soko la chapakazi. Anawaita wajinga.
ix. Kupanga mauaji ya Chopi : Anakubaliana na wazo la Kenga la kumuua Chopi kwa sababu ya
kutomuua Tunu jinsi walivyokuwa wamemuagiza.
x. Kuharibu mustakabali wa wanafunzi - Anafungua shule ambayo inaharibu mustakabali wa
wanafunzi kwa maana hakuna mwanafunzi anayefuzu kutokana na kudungana sumu ya
nyoka.(dawa za kulevya) humo shuleni.
xi. Fidia : Babake Tunu alifia katika kampuni yake lakini hakutaka kuwalipa fidia kwa madai kwamba
hawakuwa na bima. Zisingalikuwa bidii za Bi. Hashima wasingalilipwa fidia hiyo.
xii.Kuwapiga raia risasi : Anamtaka mkuu wa polisi , Bwana Kingi kuwapiga raia risasi kwa sababu ya
kuandamana ili kumlazimisha kufungua soko.
xiii. Kuumizwa kwa Tunu : Anawatumia wahuni kumvamia na kumuumiza Tunu. Wanamuumiza
mfupa wa muundi inambidi kutembea kwa magongo kwa miezi mitatu
xiv. Kupandisha kodi : Anawaongeza walimu na wauguzi asilimia kidogo ya mshahara, na
kupandisha kodi hivyo kuwafanya kuendelea kulipwa mshahara duni.
xv.Kumfunga Ashua : Anamfunga Ashua licha ya Ashua kumwarifu kwamba ana mtoto
anayenyonya.
xvi. Kuifunga runinga - Anaifunga runinga ya Mzalendo kwa sababu ya kuangazia masaibu ya
wafanyakazi moja kwa moja kutoka sokoni Chapakazi, jambo lililomuudhi Majoka.
xvii. Mshahara duni : Anawalipa wafanyakazi kama vile walimu na wauguzi mshahara duni, hali
inayowasababisha kususia kazi na kuandamana ili kumlazimisha kuwaongeza mshahara.
(Hoja zozote16×1 = 16)
3. Eleza jinsi mbinu ya taharuki ilivyotumika kufanikisha maudhui katika tamthilia ya kigogo.
(alama 20)
JIBU
Mbinu ya taharuki.
Taharuki ni hali ya kutokamilisha habari fulani ili kumuacha msomaji na hamu ya kutaka kujua
kitakachojiri au kutaka kujua zaidi.
i. Mwandishi anatuacha katika hali ya taharuki kuhusiana na watoto wa Ashua na Sudi, hatujui
kilichowatokea walipoenda kwa kina Tunu iwapo walipewa chakula au la.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
ii. Baada ya Ashua kushikwa ili kumnasa Sudi kuchonga kinyago, haijulikani iwapo alikubalika
kuchonga kinyago ili mkwe aachiliwe au vipi.
iii.Hatujui hatima ya Ngurumo na Ngao Junior baada ya wao kufa, hatujui iwapo walikikwa siku hiyo
au nini kilichotokea baada ya Bw. Majoka na Husda kupashwa habari.
iv. Majoka alisema kuwa, ‘Inafaa Chopi aende safari (auwawe) hatujui iwapo amri hii ya kuuwawa
kwake ilitekelezwa au la.
vi. Hatujui hatima ya Majoka baada ya kila mshirika wake kumuepuka na kuenda upande wa Tunu.
vii.Kule Mangweni kuna mtu 2 ambaye alikuwa amelewa chakari, mtu 1 ana sindano mkononi na
kumshika mtu 2 kwa mkono wa kushoto mtu 2 anapoanguka chini na kuanza kugaragara, hatujui
iwapo mtu 1 alimdunga sindano mwenzake na iwapo alikufa au hata kufa kutokana na pombe
haramu.
viii. Ashua na Tunu wanapokuja mbio karakani ya uchongaji wa kuwafahamisha kuhusu mipango ya
Kenya, wote wanaondoka walifika na nini walichokifanya.
ix. hatujui kama soko lilifunguliwa baada ya mapinduzi.
x. hatujui iwapo majoka alifunguliwa mashtaka.
xi. hatujui uamuzi wa husda baada ya kujua majoka hakumpenda.
xii. hatujui hatima ya kenga baada ya mapinduzi.
xiii. vituo vya runinga villivyofungwa vilifungulliwa baada ya mapinduzi?
xiv. iwapo tunu aliongoza sagamoyo hatujui.
xv. shule la majoka zilizoharibu vijana hatijui kama zilifungwa baada ya mapinduzi.
xvi. uongozi uliofuata uliendeleza dhuluma au la dhidi ya wanasagamoyo.
xvii. boza alipogundua mkewe si mwaminifu alifanya niny?
bei ya chakula katika kioski hatujui kama ilirejeshwa chini baada ya mapinduzi
(Hoja zozote -20)
SEHEMU D. RIWAYA.
CHOZI LA KHERI NA Assumpta Matei
4. Mifano ya migogoro katika riwaya.
i. Kwa mzee Msubili kwa kuwa kulikuwa na vinywa vingi vya kulishwa. ii. Mgogoro wa mashamba baada ya mkoloni kuja na kubadillisha sera za umilikaji mashamba.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iii. Ridhaa akiwa shuleni aligombana na wenzake kwa kuitwa mwizi wa kalamu. iv. Kuna mvutano wa mawazo akilini mwa Ridhaa alipokuwa katika gofu lake la nyumba
iliyochomeka. v. Mgogoro wa watu kuhusu nani aliyeshinda katika uchaguzi.
vi. Mgogoro kati ya polisi na watu ambao walikuwa wanazozana baada ya uchaguzi. vii. Mwangeka anazozana na mkewe kuhusu kuenda kwake ng’ambo.
viii. Kuna mgogoro wa nafsi ya Mwangeka anoposema kama hangeenda ng’ambo angewaokoa jamaa zake.
ix. Tila anamkumbusha babake kuna migogoro katika tamthilia ya mashetani. x. Bwana Tenge na mkewe wanazozana kwa sababu Tenge si mwaminifu katika ndoa.
xi. Naomi na Kimbaumbau wanazozana kwa sababu Kimbaumbau anataka washiriki mapenzi. xii. Mwangemi na Mwangeka wanazozana na mama zao kwa kumchezea shere babu yao.
xiii. Mwangeka na Mwangemi wanaadhibiwa na babu yao kwa kumchezea shere. xiv. Nyanyake Pete anazozana na watoto wake wanaotaka kumuoza Pete akiwa mdogo. xv. Mwanzoni Dick na tajiri yake wanazozana anapokataa kushiriki katika ulanguzi wa madawa ya
kulevya. xvi. Subira na mavyaa yake wanazozana kwa kuwa si wa kabila moja.
xvii. Lunga anozozana na matajiri wanaotaka kuuza mahindi yasiyositahili. xviii. Billy na Sally wanazozana kuhusu nyumba yao ya kuishi.
xix. Kuna mgogoro mawazoni mwa Dick alipokuwa anajiuliza kama ajiingize katika biashara haramu au la.
xx. Mwangeka anataka babake aondoe majivu lakini babake hataki. 5. “ …alinionya dhidi ya kumwambia yeyote kuhusu unyama…”
e) Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4) Ni mawazoya sauna. Aliyakumbuka akiwa nyumbani mwa bi kangara, alikumbuka
alivyotendewa na ulimwengu na kuwa muovu, babake alikuwa na mazoea ya kumbaka na
alipomwambia amamake, alikanywa asimwambie yeyote.
f) Fafanua sifa nne za anayehusishwa na maneno haya. (al 4) ✓ Mhalifu. Aliwatirosha dick na mwaliko. (uk153) Kijakazi Sauna alimwiba Dick na kumpeleka kwa
Buda. Tajiri huyu alijifanya angempeleka shuleni lakini lengo lake lilikuwa kumwingiza katika
biashara ya mihadarati.
✓ Mwenye majuto. Anajutia kitendo cha kuwatorosha akina Dick na Mwaliko. (uk154)
✓ Mvumilivu. Amafanya kazi kwingi tangu alipotoroka kutoka nyumbani kwa mzee Maya.
Amaeuza pombe, maji amaefanya kazi katika machimbo ya mawe n.k. (uk156)
✓ Mwenye tama. Anasema kadri alivyopata ndivyo tama ilivyozidi kuwannda. g) Onyesha namna ukiukaji wa haki za watoto unavyotokea katika riwaya hii. (alama12) Kukiukwa kwa haki za watoto
✓ Chandachema anashiriki kazi za kuchuna majanichai akiwa darasa la tano. (uk106) Aliarauka na
kufanya kazi alfajiri na mapema kabla ya kwenda shuleni saa kumi na mbili asubuhi.
✓ Wanaofanya kazi ya vibarua katika mashamba ya kuchuna majani chai hupitia madhira mengi.
(uk107) Huishi katika vyumba vidogo na hupewa uhamisho bila kujali wana watoto wanaoenda
shule.
✓ Watoto wanabaguliwa. Waliozaliwa ndoani wanapewa hadhi tofauti na waliozaliwa nje ya ndoa.
Kairu anajiuliza ikiwa watoto wanaozaliwa nje na ndani ya ndoa huwa na hadhi tofauti. (uk93)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
✓ Wasichana wanapopata mimba kabla ya ndoa wanadhalilishwa na kubaguliwa. Zohali alipitia mengi
baada ya kufukuzwa shule kwa kuwa mjamzito, aliachiwa kazi zote za nyumbani. (uk99)
✓ Wahalifu wana haki ya kufikishwa mahakamani. (uk114) Kuwaua kabla ya kuwapeleka mahakamani
ni kukiuka haki zao (Uk 120). Lemi rafikiye Dick alichomwa na watu.
✓ Dick aliingizwa katika usafirishaji wa mihadarati akiwa na umri wa miaka kumi. Hakuweza kukataa
kutoka na vitisho na mahitaji mengine aliyokuwa nayo.(uk121)
✓ Watoto wasichana wanashirikishwa katika upashaji tohara. (uk 143) Tuama alikuwa ameshiriki
katika upashaji tohara na hali yake ilipokuwa mbaya alipelekwa hospitalini.
✓ Watoto wasichana wanaozwa kwa lazima na mapema. Ingawa baadhi ya wasichana huendelea na
masomo baada ya kupashwa tohara, kunao ambao huozwa. (uk144) Pete aliozwa kwa mzee Fungo
baada ya kupashwa tohara. Aliacha masomo yake.
( Hoja zozote -6)
6. a. Huku ukitoa hoja sita linganisha aina mbili kuu za fasihi. (alama6)
b. Jadili vipengele sita vya kuzingatia katika uchanganuzi wa hadithi. (alama6)
c. Jadili sifa mbili za vitanza ndimi kwa kurejelea sauti. (alama 2)
d.Tambua dhana zinazotokana na maelezo haya.
i. Msimulizi wa fasihi simulizi anaitwaje kwa jumla? (alama1)
ii. Shujaa katika mighani pia anaweza kuitwa nani? (alama 1)
iii. Sherehe za kitamaduni ambazo hufungwa na jamii katika kipindi fulani maalum huitwaje?
(alama 1)
iv. Mavazi au vifaa vinavyotumiwa na wasanii kuakisi hali halisi ya mambo wakati
wakuwasilisha fasihi huitwaje? (alama 1)
v. Mtambaji wa hadithi hutumia ujuzi gani anapoibadilisha hadithi yake moja kwa moja mbele
ya hadhira bila kuathiri usimulizi wake? (alama 1)
vi. Wanaosimuliwa ili kuonyesha kazi ya fasihi simulizi hupewa jina hili. (alama 1)
jibu
a. Linganisha fasihi andishi na simulizi. (hoja sita)
i. Zote ni kioo cha jamii (huchotwa kutoka kwenye jamii, huonyesha yanayotendeka katika jamii/
maudhui na dhamira hufanana.
ii. Zote ni sanaa (Huwasilisha ujumbe kwa njia ya kipekee)
iii. Hutumia lugha kama kifaa muhimu zaidi.
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iv. Majukumu hufanana kama vile kuelimisha na kuburudisha.
v. Hubuniwa. (Hazina ukweli mahsusi, ni tungo za kufikirika)
vi. Zote husimuliwa . Fasihi simulizi husimuliwa kwa mdomo na vilevile, tungo hizo za fasihi andishi
huandikwa kwa mtindo wa kisimulizi.
vii. Kuna kipengele cha safari katika fasihi zote. Wahusika katika fasihi zote huwa na safari kwa njia
moja au nyingine.
viii.Zote zinaweza kutendwa. Fanani wa fasihi simulizi hutenda jukwaani na vilevile tungo za fasihi
andishi zinaweza kutendwa jukwaani kama vile tamthilia.(Zozote6×1= 6)
b. Vipengele sita vya kuzingatia katika uchanganuzi wa hadithi.
i. Dhamira - Lengo au nia kuu inayokusudiwa kuadilisha, kuonya, kuelimisha au kukashifu.
ii. Maudhui - Jumla ya mambo yanayoelezwa katika hadithi.
iii. Ploti - Mtiririko wa matukio katika hadithi.
iv. Mandhari - Haya ni mazingira ya wakati, hali, au kimaeneo ambayo yaweza kuwa ya kuogofya.
v. Wahusika - Ni viumbe wanaoshiriki katika hadithi ambao wanaweza kuwa binadamu, mtu,
wanyama.
vi. Muundo - Hadithi huwa na muundo maalum wa ufunguzi , mwili na hitimisho.
vii. Lugha - Hadithi hutumia lugha ya moja kwa moja ingawa huweza kuwa na tamathali kama
methali, tashbihi, jazanda nk.
Viii. Funzo - hadithi hutoa funzo Fulani la kimaadili kama wizi haufai au wajanja hatimaye huangamia.
(Zozote 6 ×1 = 6)
c. Sifa za vitanza ndimi.
i. Hutamkwa kwa kasi
ii. Sauti hukaribiana kimatamshi.
iii. Kuna uradidi/ takriri ya maneno au sauti fulani.
(zozote -2)
d.
i. Fanani
ii. Jagina
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
iii. Miviga
iv. Maleba
v. Ufaraguzi
vi. Hadhira hai.
SEHEMU YA E. USHAIRI
7. SHAIRI A
MWANA
1. Kwani mamangu u ng’ombe, au u punda wa dobi?
Nakuuliza usambe, nayavunja madhehebi
Nalia chozi kikombe, uchungu wanisibabi
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
MAMA
2. Nong’ona mwana nong’ona, sitafute angamiyo
Sinipe kuja sonona, kwa uchungu na kiliyo
Babayo mkali sana, kubwa pigo la babayo
Kwani kelele kunena, huyataki maishiyo?
Hilo nakwambia.
MWANA
3. Sitasakamwa kauli, nikaumiza umiyo
Nikabeba idhilali, nikautweza na moyo
Siuvuwati ukweli, hazidisha gugumiyo
Baba hafanyi halali, nawe hwachi vumiliyo
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Nambie ipi sababu, ya pweke kwenda kondeni
Nini yako matulubu, kulima hadi jioni?
Na jembe ukidhurubu, ukilitua guguni
Yu wapi wako muhibu, Baba kwani simuoni?
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
Baba kwani simuoni, kuelekea shambani?
Kutwa akaa nyumbani, na gumzo mitaani
Hajali hakuthamini, wala haoni huzuni
Mwisho wa haya ni nini, ewe mama wa imani?
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
Na kule kondeni kwako, ukate kuni kwa shoka
Ufunge mzigo wako, utosini kujitwika
Kwa haraka uje zako, chakula upate pika
Ukichelewa vituko, baba anakutandika
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo?
Chakula kilicho ndani, ni jasho lako hakika
Kiishapo u mbioni, wapita kupokapoka
Urudi nje mekoni, uanze kushughulika
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Ukikosa kisirani, moto nyumbani wawaka
Hebu nambie
Kweli jaza ya kiumbe, ni madhila na mapigo
MAMA
Wanitonesha kidonda, cha miaka na miaka
Usidhani nayapenda, madhila pia mashaka
Nakerwa na yake inda, na sasa nimeshachoka
Ninaanza kujipinda, kwa mapambano hakika
Hilo nakwambia
MASWALI
a) Mtunzi wa shairi hili alikuwa na dhamira gani katika kutunga shairi hili. (alama 2)
b) Shairi hili la aina gani. Toa ithibati. (alama 2)
c) Yataje mambo yoyote matano anayoyalalamikia mwana. (alama 5)
d) Eleza kanuni zilizotumika kusarifu ubeti wa tatu. (alama 5)
e) Andika ubeti wa saba kwa lugha tutumbi. (alama 4)
f) Eleza maana ya maneno haya yaliyotumika katika shairi hili.
(i) jaza (alama 1)
(ii) muhibu (alama 1)
JIBU
USHAIRI A
a) Kuonyesha madhila anayopitia mwanamke/mama mikononi mwa mwanamme.
( 1 x 2 = alama 2)
b) Ngonjera – ni mazungumzo kati ya Mama na Mwana.
(aina 1, idhibati 1 jumla alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
c) i. Kufanywa kufua nguo
ii.Mama huenda shambani peke yake.
iii.Baba hubaki nyumbani tu na kupiga gumzo mitaani.
iv.Baba hamthamini mama.
v.Mama hukata kuni kondeni na kuzibeba kichwani.
vi.Mama akichelewa kufika nyumbani akitoka kondeni huadhibiwa.
vii.Mama ndiye hutafuta chakula
(yoyote 5 x 1= alama 5)
d) Ubeti una mishororo sita
· Mshororo umegawika katika vipande viwili isipokuwa mshororo wa tano ambao umegawika katika
kipande kimoja.
· Kila mshororo una mizani kumi na sita isipokuwa mshororo wa sita ambao una mizani tano
· Kibwagizo kimefupishwa
· Mpangilio wa vina:
li ----------------yo
li ---------------yo
li----------------yo
li ---------------yo
embe------------go( alama 1 kwa kila jibu sahihi, jumla alama 5)
e) Umenifanya nihisi uchungu ambao nimekuwa nao kwa miaka mingi, usidhani kuwa nayapenda
madhila na mashaka, nakerwa na hali yake ya kunidhibiti kufanya jambo na sasa nichoka, ninaanaza
kwa hakika kujitayarisha kwa mapambano, hilo nakwambia.
(alama -4)
f) (i)Jaza – malipo kwa kutenda wema (alama 1)
(ii) muhibu – mpenzi (alama 1)
AU
8. SHAIRI B
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
Soma shairi hili kisha ujibu maswali
1. Punda kalibebe gari, gari limebeba punda
Mwalimu ana pakari, muashi vyuma adunda
Jaji gonga msumari, sonara osha vidonda.
Kinyume mbele
2. Saramala ahubiri, muhunzi tiba apenda
Mganga anaabiri, baharini anakwenda
Hata fundi wa magari, anatomea vibanda
Kinyume mbele
3. Wakili anahiyari, biashara kuitenda
Mtazame askari, akazakaza kitanda,
Mkulima mashuhuri, jembe limemshinda
Kinyume mbele
4. Apakasa daktari, ukili anaupinda
Saveya kawa jabari, mawe anafundafunda,
Hazini wa utajiri, mali yote aiponda,
Kinyume mbele
5. Msemi huwa hasemi, wa inda hafanyi inda
Fahali hawasimami, wanene waliishakonda
Walojitia utemi, maisha yamewavunda
Kinyume mbele
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
6. Kiwapi cha kukadiri, twavuna shinda kwa shinda
Tele haitakadari, huvia tulivyopanda
Mipango imehajiri, la kunyooka hupinda
Kinyume mbele
MASWALI
a) Mtunzi alikuwa na malengo gani alipotunga shairi hili? (alama 3)
b) Licha ya tarbia, eleza bahari nyingine zinazojitokeza katika shairi hili. (alama 4)
c) Eleza namna mtunzi alivyoutumia uhuru wake. (alama 5)
d) Ni mbinu gani inayotawala shairi hili? (alama 2)
e) Uandike ubeti wa nne katika lugha nathari. (alama 4)
f) Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
SHAIRI B
a) - Kuwahimiza watu washikilie taalamu zao walizofuzu
- Kukashifu/ kushutumu/kukejeli ukosefu wa mwelekeo katika jinsi mambo yanavyoendeshwa.
- Kukuza msamiati wa wasomaji wake kuhusu watu wa kazi hizo.
(malengo yoyote matatu 1 x 3 = alama 3)
b) (i) Msuko – kibwagizo kimefupishwa
(ii) Ukara – vina vya utao vinatiririka ilhali vya ukwapi vinabadilikabadilika kutoka ubeti mmoja hadi
mwingine.
(bahari na maelezo yake alama 2 x 2 = alama 4)
c) Inkisari
· Walojitia – waliojitia
· Kiwapi – kiko wapi
· Kalibebe - akalibebe
· Gonga – agonga
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317
· Osha - aosha
· Kawa – kawa
Tabdila
· Anahiyari - anahiari
· Yamewavunda – yamewavunja
Kuboronga sarufi/ kufinyanga sarufi
· Muashi vyuma adunda – mwashi adunda vyuma
· Muhunzi tiba apenda – muhunzi apenda tiba
· Baharini anakwenda – anakwenda baharini nk.
Utohozi
· Saveya - soroveya
Lahaja
· Yamewavunda
· Anafundafunda
(kutaja na kutoa mfano 1, aina tano za uhuru 1 x 5 = alama 5)
d) Kinaya – matendo ya wahusika ni kinyume na matarajio yetu ya kazi wanazofaa kuzifanya, kwa
mfano, muashi agonga vyuma ilhali jaji anagonga misumari.
( kutaja mbinu 1, maelezo 1 = alama 2
e) Daktari anasuka/ anasokota kamba naye saveya amakuwa stadi wa kuvunjavunja mawe. Mtunzaji
hazina au mali ya taje ndiye anayetumia vibaya, ni kinyume kimetiliwa mkazo. (alama 4)
f) Masikitiko – anasikitika kuwa watu wanaopaswa kufanya mambo fulani hawafanyi wanavyostahili
bali wanafanya kinyume na matarajio.
Hakiki jibu la mtahiniwa)(kutaja 1, maelezo 1 = alama 2)
www.kcse-online.info Mobile no: 0721 806 317