26

Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

  • Upload
    others

  • View
    6

  • Download
    0

Embed Size (px)

Citation preview

Page 1: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi
Page 2: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

i

Dondoo Kuhusu Dhambi

© 2016 Daudi Lubeleje

VIJANA NA UTUMISHI

Page 3: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

ii

I Wathesalonike 4: 2 – 5

“2 Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu. 3

Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane

na uasherati; 4 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika

utakatifu na heshima; 5 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa

wasiomjua Mungu.”

…………… Kitabu hiki ni kwa mwamini yeyote”.

Page 4: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

iii

#UTANGULIZI

Bwana Yesu asifiwe,

Si kwa bahati mbaya kitabu hiki kimekufikia. DONDOO KUHUSU DHAMBI ni

kitabu kwa kila mwamini kukisoma. Baada ya kusoma kitabu hiki ni matumaini

yangu kupitia dondoo hizi, utapata majibu ya swali hili “Kwanini yatupasa

kutunza utakatifu?” Hivyo utaongeza bidii yako kumpendeza Mungu katika

mwenendo wako wote.

Kuokoka ni hatua ya kwanza kuliishi kusudi lako. Dhambi ni kikwazo cha

kwanza kuharibu kusudi la Mungu katika maisha yako. Basi, kitabu hiki kiwe

msaada kwako kuongeza chachu ya wewe kutunza kusudi la Mungu kwa

kuepuka kuchafuliwa na dhambi, Kumbuka Neno la Mungu lasema “Msishike, msionje, msiguse” [Wakolosai 2:21]

Asante Pastor Raphael, JL wa YKM.

“Unajua tatizo ni kwamba kitabu ni kitamu sana………kila kijana anatakiwa

akipate hiki” [Raphael Joachim Lyela, Mchungaji wa Vijana na Mwanzilishi wa

Youth Kingdom Ministries, YKM]

Daudi Lubeleje.

Page 5: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

iv

#YALIYOMO

#UTANGULIZI ............................................................................................................. iii

#YALIYOMO ................................................................................................................ iv

#DONDOO YA KWANZA. ....................................................................................... 1

#DONDOO YA PILI ..................................................................................................... 3

#DONDOO YA TATU. ................................................................................................. 6

#DONDOO YA NNE ................................................................................................... 8

#DONDOO YA TANO .............................................................................................. 12

#DONDOO YA SITA ................................................................................................. 13

#DONDOO YA SABA ............................................................................................... 16

#MAOMBI YA TOBA ................................................................................................ 18

#IJUE VIJANA NA UTUMISHI .............................................................................. 19

Page 6: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

1

#DONDOO YA KWANZA.

Dondoo ya kwanza inasema “dhambi inaotea mlangoni”. Neno la Mungu

linasema katika Mwanzo 4:7 ".......Usipotenda vyema dhambi iko,

inakuotea mlangoni,..........". Nataka nifafanue mstari huu kwa mapana kama

ifuatavyo;

Mlango ni nafasi ya kuruhusu au kutoruhusu

kilicho nje/ndani kuingia/kutoka ndani/nje.

Wakati Bwana Yesu anasema "....nasimama

mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti

yangu, na kuufungua mlango, nitaingia

kwake,............" (Ufunuo wa Yohana 3:20),

HALI KADHALIKA, dhambi haiji kupitia

dirishani au wapi, bali iko mlangoni na yenyewe

ikiotea!. Kama dhambi inaotea mlangoni, lazima

iwe imejificha maana ikija kwa wazi utaiona na

huwezi kufungua mlango ikapita. Tofauti na

Bwana Yesu hapohapo mlangoni anabisha ili

kuingia, haotei kama ilivyo dhambi. Dhambi

inaotea mlangoni kwa sababu hapo ndio sehemu

pekee inaweza fanya maigizo kama yenyewe si

dhambi vile, bali ni jambo zuri, ni uzima,

kwamba ukiruhusu utapata faida na si hasara ila

kumbe ni hila za kukuotea!. Kumbuka 2

Wakorintho 11:14 inasema "........Maana

shetani mwenyewe hujigeuza awe

mfano wa malaika wa nuru". Kujigeuza

huku kwa shetani kuwa malaika wa nuru ni

kukushawishi ili ufungue mlango, maana dhambi

inaotea hapo mlangoni.

“Dhambi inaotea

mlangoni kwa

sababu hapo

ndio sehemu

pekee inaweza

fanya maigizo

kama yenyewe si

dhambi vile, bali

ni jambo zuri, ni

uzima, kwamba

ukiruhusu

utapata faida na

si hasara ila

kumbe ni hila za

kukuotea!.”

Page 7: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

2

Sababu kubwa inayofanya dhambi kuotea mlangoni tunaipata tukisoma

Yohana 10:2 "Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo" na

mchungaji wa kondoo si mwingine ni Yesu Kristo (Yohana 10:11-14). Kama

Yesu Kristo huingia mlangoni, na dhambi kwa kuotea hutaka kupitia hapohapo

ila ikiisha kujigeuza na kuonekana kama ni jambo la faida.

Kuna baadhi ya mambo katika maisha yetu hususani yale

yanayowakumba vijana yanapokuja huonekana ni mema

kumbe ni dhambi inaotea mlangoni. Mfano masuala ya

mahusiano ni eneo ambalo shetani hufanya mambo

yaonekane kama ni ya Mungu kumbe hapana. Mambo

kama kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa na wakati si

wanandoa ni dhambi, kwa bahati mbaya dhambi huotea

hapo, inafanya tendo la ndoa hata kama hamjaingia

kwenye ndoa lionekane ni sawa tu.

Tunapaswa kujua si yote yanakuja kwetu ni mema tu! bali mengine ni dhambi

inaotea mlangoni. Kwa sababu Yesu Kristo anabisha hapo mlangoni na dhambi

inaotea hapo mlangoni ni vema kupima kila jambo kwanza kwa chujio la Neno

la Mungu.

“Tunapaswa

kujua si yote

yanakuja kwetu

ni mema tu!

bali mengine ni

dhambi

inaotea

mlangoni”

Page 8: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

3

#DONDOO YA PILI

Dondoo ya pili inasema, “Dhambi inakutamani wewe uliyempa Yesu Kristo

maisha yako”. Tukisoma katika Mwanzo 4:7 "..........Usipotenda vyema

dhambi iko,.............nayo inakutamani wewe.......". Nitafafanua kwa

mapana kama ifuatavyo;

Kutamani kwa lugha rahisi humaanisha "kutaka sana".

Kila mwamini anapaswa kujua dhambi inamtaka sana na

haiwezi kutulia mpaka imempata. Kutamani kwa dhambi

huambatana na ushawishi unaoletwa na dhambi

yenyewe. Ushawishi huu huficha ubaya wa dhambi.

Nitatumia mfano ufuatao kuelezea kutamani kwa

dhambi kulivyo;

Tukisoma Mwanzo 3: 1-6, hasa mstari wa 6 inasema "Mwanamke

alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho,

nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi akatwaa matunda

yake akala, akampa na mumewe, naye akala". Angalia! Kwa sababu

dhambi iliwatamani Adamu na mkewe, kwa kutumia ushawishi wake, ilifanya

mwanamke akaona matunda ya mti waliokatazwa wasile kuwa WAFAA KWA

CHAKULA na tena WAPENDEZA MACHO (Mwanzo 2:17).

Hata leo, kwa yeyote aliyeokoka, dhambi inamtamani,

hata kumshawishi kwa kumwonyesha mambo mengi

Mungu aliyokataza kuonekana ni mazuri. Vijana wengi

leo, kwa kutotambua hilo, wamefanya dhambi na

kuanguka huko. Mtume Paulo alisema

"lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita

na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya

dhambi iliyo katika viungo vyangu" (Warumi 7:23).

“Kutamani

kwa dhambi

huambatana

na ushawishi

unaoletwa na

dhambi

yenyewe.”

“Kutamani

kwa dhambi

hufanya hata

vita na

wewe!,”

Page 9: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

4

Kutamani kwa dhambi hufanya hata vita na wewe!, Yale uliyoyaacha baada ya

kuokoka, unashangaa dhambi inakutamanisha tena, Sikiliza mtoto wa Mungu!,

hiyo ni vita imekuja kwako. Kumbuka hata katika maisha ya kawaida,

unapotamani kufanya mambo fulani uliyojiwekea, hutakaa utulie mpaka

umefanikiwa. Hata dhambi inatamani, ina kiu ya kumwangusha mtoto wa

Mungu, atoke kwenye kusudi la Mungu. 1 Petro 2:11 inasema

"...........ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho", Umeona! tamaa

za mwili ni matamanio ya dhambi kutimiza lengo lake la kukutamanisha ili

umwache Mungu.

Sasa, dhambi inapokutamani, inataka upoteze nafasi

yako kwa Mungu uliyopewa. Leo watoto wa Mungu

wengi wamepoteza huduma, utakatifu, baraka na mambo

mengi lukuki kutoka kwa Mungu, kwa kuifuata dhambi

ilipowatamanisha.

Nimalizie kwa kusema hivi, kwa nafasi kubwa dhambi inapomtamani mtoto wa

Mungu, hutumia mwili kwake. Tukisoma Warumi 8: 5-11, Wagalatia 5:16-

17, 1 Petro 2:11 twapata kujua hili.

Hebu tuamue kujitoa kwa Mungu ki-sawasawa, tunapotembea tujue si yote

yanayokuja ni ya Mungu, mengine ni ushawishi wa dhambi hata kama

yanapambwa vipi kwa kupendeza. Tafakari mistari ifuatayo na Mungu

atusaidie kwa neema yake, kumbuka mimi na wewe ni zaidi ya washindi;

Warumi 6:13 "Wala msiendelee kuvitoa viungo vyenu kuwa silaha

za dhuluma kwa dhambi; bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama

walio hai baada ya kufa, na viungo vyenu kuwa silaha za haki”.

Warumi 12:1-2 "...........itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu

ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala

msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa

“Dhambi

inapokutamani,

inataka

upoteze nafasi

yako kwa

Mungu

uliyopewa”

Page 10: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

5

upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo

mema, ya kumpendezam na ukamilifu"

Page 11: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

6

#DONDOO YA TATU.

Dondoo ya tatu inasema, “Dhambi hufanya mtu kupungukiwa na utukufu

wa Mungu”. Neno la Mungu linasema ".......wote wamefanya dhambi, na

kupungukiwa na utukufu wa Mungu" (Warumi 3:23). Kufanya dhambi

kunapunguza ule utukufu wa Mungu tuliokuwa nao kabla ya kufanya dhambi.

Twende pamoja, ninapofafanua kama ifuatavyo;

Hapa nataka niongee sana na waliompa Yesu Kristo maisha yao [Wameokoka

tayari]. Nitaenda taratibu ili udake kile ninachotaka uone hapa;

Katika Yohana 1:12 "Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa

kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake".

Ukishampokea Yesu Kristo katika maisha yako, twajua kuwa umefanyika

mtoto wa Mungu tayari; dhambi ulizofanya zinafutwa na unakuwa mpya ndani

ya Kristo. Angalia! Baada tu ya kumpokea Kristo, Bwana Yesu anasema

"Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao............" (Yohana 17:22).

Sikiliza! utukufu wa Mungu uliokuwa kwa Kristo, unakuwa kwako tu,

ukimpokea Kristo. Hivyo yeyote aliyeokoka utukufu wa Mungu upo kwake.

Ukisoma Matendo ya Mitume 6:15 Neno la Mungu linasema "Watu wote

walioketi katika ile baraza wakamkazia macho yao, wakamwona

uso wake kuwa kama uso wa malaika". Mtumishi wa Mungu Stefano

kama tunavyoona hapa, uso wake ulionekana kama uso wa malaika katika lile

baraza; Sasa kilichofanya uso wa Stefano kuonekana hivyo, ni ule utukufu wa

Mungu uliokuwa kwake. Utukufu wa Mungu unabadilisha hata muonekano

wako mbele ya watu, Utaonekana mwenye heshima, akili, mvuto mzuri kuliko

kawaida. Kwa nyongeza, soma tena 2 Wakorintho 3:18.

Mtoto wa Mungu anapofanya dhambi tu, dosari inaingia kwenye maisha yake,

Utukufu wa Mungu alionao unapungua, Hasa asipotubu!. Kumbuka

tulivyosoma Warumi 3:23, tumeona kwa wazi kuwa dhambi hufanya utukufu

wa Mungu kupungua na huzidi kupungua kama aliyefanya dhambi asipotubu.

Page 12: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

7

Kufanya dhambi bila kutubu ni hatari sana kwa mwamini yeyote. Nimeona iko

shida leo, hasa kwa vijana kuwa wagumu kutubu wakifanya dhambi. Madhara

yake ni kuzoelea kufanya dhambi kwani utukufu wa Mungu umepungua.

Jambo la kufanya ni kuwa ukifanya dhambi TUBU! la

sivyo tegemea kuona utukufu wa Mungu kupungua

kwenye maisha yako. Neno la Mungu linasema

"..........Na kama mtu akitenda dhambi tunaye

Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye

haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi

zetu............" ( 1 Yohana 2:1-2). Yesu Kristo ndiye

kipatanisho kwa dhambi zetu, tubu na mrudie Mungu,

songa mbele na wokovu. Mithali 28:13 "Afichaye

dhambi zake hatafanikiwa, Bali yeye

aziungamaye na kuziacha atapata rehema".

Kupata rehema ni kusamehewa, kutohesabiwa dhambi

(Zaburi 32:1-2).

Ni vizuri zaidi ukatunza utakatifu wako ili utukufu wa Mungu uzidi kuwa na

wewe, badala ya kuanguka na kutubu mara kwa mara!. Kumbuka dhambi

hupunguza utukufu wa Mungu kwako, JITUNZE!.

“Kufanya

dhambi bila

kutubu ni

hatari sana

kwa

mwamini

yeyote”

Page 13: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

8

#DONDOO YA NNE

Dondoo ya nne inasema, “Dhambi ikikomaa huzaa mauti”. Neno la Mungu

linasema “………na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”

(Yakobo 1:15). Kuzoelea kufanya dhambi bila kutubu hufanya ile dhambi

ikomae [full grown/matured]. Kukomaa kwa dhambi ni hatua ya mwisho

kabisa inayozaa mauti/kifo.

Nataka nikuonyeshe mambo kadhaa yanayotokea kabla dhambi haijazaa mauti.

"MAMBO YANAYOWEZA KUTOKEA KABLA DHAMBI HAIJAZAA

MAUTI"

MAONYO______#01

Kufuatana na Ezekieli 18:23,32 inaweka wazi kuwa Mungu hafurahii mwenye

dhambi kufa bila kutubu. Ukisoma utakutana na maneno yafuatayo;

“Je! mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? asema Bwana

MUNGU; si afadhali kwamba aghairi na kuiacha njia yake,

akaishi? Maana mimi sikufurahii kufa kwake afaye, asema Bwana

MUNGU; basi ghairini mkaishi”.

Hivyo basi, mtu afanyapo dhambi na kabla haijakomaa kuzaa mauti, hupokea

MAONYO mengi ili atubu. Mungu hutumia MAONYO ili kumrudisha

mwenye dhambi atubu. Kupitia watumishi wa Mungu, atendaye dhambi

hupokea MAONYO ya Mungu ya kumfanya arudi kwenye toba ya kweli ili

apone!. Katika Ezekieli 3:16-21 [soma yote], hasa mstari wa 17 tunaona Mungu

anasema “……….basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu,

ukawape maonyo haya yatokayo kwangu” Sikiliza! Ukipokea

maonyo usichukie na kukasirika, bali jitathimini. Kuna baadhi ya vijana siku

hizi wakionywa wanageuka mbogo! Kwenye eneo hili usijifanye mjanja, kuwa

mnyenyekevu ikusaidie kujua hali yako mbele za Mungu ili utubu na upone.

Page 14: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

9

Yona 1:2 “Ondoka uende ninawi, mji ule mkubwa, ukapige kelele

juu yake; kwa maana uovu wao umepanda juu mbele zangu”.

Kama nilivyosema awali kuwa, Kabla dhambi haijazaa mauti, Mungu hufanya

kila njia kumrudisha mtu ili asife akiwa dhambini. Kabla Mungu hajaiangamiza

ninawi, alimtuma mtumishi wake Yona ili ahubiri kwanza kutoa nafasi kwa

watu wa ninawi kutubu.

Kuna aliyekuwa ameokoka, amerudi nyuma tena kwenye dhambi, Mungu

anataka utubu tena na urejee kwake. Kuna ambae hajaokoka kabisa, Mungu

anataka utubu. Kuna ambae ameokoka ila kazoelea kufanya vidhambi fulani,

Mungu anataka utubu na utembee kwa uaminifu; Kumbuka dhambi ikikomaa

huzaa mauti. Injili ni MAONYO kumrudisha aliyepotea kwa Mungu kabla hiyo

dhambi haijazaa mauti!. Kuna sehemu Mungu anasema “Aonywaye mara

nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafla, wala hapati dawa”

(Mithali 29:1). Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi

lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu.

Ukisoma Warumi 6:23 inasema "........mshahara wa dhambi ni

mauti.....". Fahamu kwamba baada ya kazi mtu hulipwa mshahara. Huwezi

kulipwa mshahara mpaka ufike muda wa kulipwa, iwe kwa mwezi/wiki au hata

siku moja. Mtu halipwi mshahara kabla ya ule muda wa kupokea mshahara

haujafika/kutimia.

Nikulete sasa kwa upande wa dhambi, Kile kipindi ambacho mtu hajapokea

mshahara wake wa dhambi, ni kwamba ule muda wa kupokea haujafika au bado

yuko kazini akiizalia dhambi matunda. Kufuatana na Yakobo 1:15, kwa tafsiri

nyingine twaweza sema dhambi inakuwa haijakomaa ili kuzaa mauti, Hivyo

mtu anakuwa anaifanyia kazi dhambi na ikikomaa [yaani ule muda wa kupokea

mshahara ukitimia] hiyo dhambi huzaa mauti [mtu anapokea mshahara wake!].

Page 15: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

10

Kabla ya kupokea mshahara wa dhambi, katika kipengele cha kwanza, tuliona

Mungu hutumia MAONYO ili anaefanya dhambi atubu na kurejea kwa Yesu

Kristo.

KUMBUKA: Mungu hafurahii kufa kwake mwenye dhambi. MAUTI kwa

mwenye dhambi ni KUTENGWA na Mungu. Kabla dhambi haijakomaa na

kuzaa hiyo MAUTI, ni vema mtu asifanye moyo mgumu bali akumbuke

KUMPOKEA Yesu Kristo.

ADHABU______#02

Kama huelewi MAONYO basi kinachofuata ni ADHABU ili utubu. Wapo

baadhi ya watu, hata ahubiriweje moyo wake ni mgumu kumpokea Yesu.

Kuna ndugu wengine wameokoka na bado kuna

dhambi hawaachi, wameonywa na Mungu ila

bado hawaelewi. Njia nzuri hapa ni ADHABU!.

Kupitia adhabu wengi huanza kumwelewa

Mungu anataka nini, basi wanarudi na kutubu.

Fungua biblia yako kwenye Waamuzi 2:11-15, Neno la Mungu linasema;

"Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya

Bwana, nao wakawatumikia Mabaali. Wakamwacha Bwana, Mungu wa

baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu

mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote,

wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika.

Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi. Hasira ya

Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya watu

waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui zao

pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao. Kila

walikokwenda mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya,

kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao

wakafadhaika sana".

“Kupitia adhabu

wengi huanza

kumwelewa Mungu

anataka nini, basi

wanarudi na kutubu.”

Page 16: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

11

Hebu angalia ADHABU hii kwa Wana wa Israeli "..akawatia katika

mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia

katika mikono ya adui zao pande zote; hata wasiweze tena

kusimama mbele ya adui zao. Kila walikokwenda mkono wa

Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana

alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika

sana".

Lengo la Mungu katika adhabu si kumtesa mtu, bali kumfanya afikirie toba

maana amemwacha Mungu. Mungu anakupenda sana ila hapendi dhambi,

Hivyo unapofanya dhambi ni ngumu mkaambatana naye ila kwa ule upendo wa

Mungu kwako, utapata ADHABU ya kukurudisha kwake.

Hebu nikuulize ya nini kung'ang'ania dhambi? Unataka mpaka ubanwe na

Mungu kwenye kona na hilo li-ADHABU amekupa ndipo utubu? Kwanini

ufike mpaka huko, kama unaweza kufanya maamuzi sasa na ukamrudia Mungu

kikamilifu? Mimi nimeokoka na Bwana Yesu ni Mwokozi wa maisha yangu,

wewe je? Neno la Mungu linasema ".......Leo, kama mtaisikia sauti yake,

Msifanye migumu mioyo yenu...." (Waebrania 3:7-8) na tena

"....tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama siku ya wokovu

ndiyo sasa" (2 Wakorintho 6 :2). Je unataka kumpokea Yesu Kristo sasa?,

umefanya maamuzi ya busara. Unaweza kuomba maombi ya toba yaliyo

ukurasa wa mwisho wa kitabu hiki.

Page 17: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

12

#DONDOO YA TANO

Dondoo ya tano [5] inasema “Dhambi ni kizuizi cha mema Mungu

aliyokuandalia!”. Tunapata uhakika wa hili tunaposoma Yeremia 5:28

“……….dhambi zenu zimewazuilia mema msiyapate”. Mema yako ni

ahadi za Mungu kwako ikijumuisha maeneo yote yanayogusa maisha yako. Ni

mkusanyiko wa baraka zako zote kiroho na kimwili! (3 Yohana 1:2)

Kuzuiliwa kwa mema yako ni sawa na kutolewa

kwenye foleni ya kupokea mema uliyokusudiwa.

Dhambi inakutoa kwenye eneo la kupokea mema

yako.

“Mema yako ni ahadi

za Mungu kwako

ikijumuisha maeneo

yote yanayogusa

maisha yako”

Page 18: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

13

#DONDOO YA SITA

Dondoo ya sita [6] inasema “Dhambi inakufanya kuonekana kama KITU

KICHAFU na Wote waliokuheshimu wanakudharau kwa sababu

wameona UCHI WAKO”. Maandiko yanasema “Yerusalemu amefanya

dhambi sana; kwa hiyo amekuwa kama kitu kichafu; Wote

waliomheshimu wanamdharau, kwa sababu wameuona uchi

wake…………..” (Maombolezo 1:8). Nieleze kwa kina kidogo kama

ifuatavyo;

Mstari wa 8 unaweka wazi matokeo mawili ya dhambi; 1). Kuonekana kitu

kichafu 2). Kuonwa uchi wako hivyo waliokuheshimu kukudharau

KUONEKANA KITU KICHAFU_______#01

Maandiko yanaweka wazi kuwa Mungu ametuchagua ili tuwe watakatifu, watu

tusio na hatia mbele zake katika pendo (Waefeso 1:4). Kuwa mtakatifu ni

kutengwa na uchafu wa dhambi, ni kutakaswa na damu ya Yesu na kuwa safi

bila hatia mbele za Mungu. Mtu akiokoka au kwa lugha rahisi kuzaliwa mara

ya pili anaingia kwenye kundi la watakatifu wa Mungu walio hapa duniani.

Maandiko yanasema “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora,

Hao ndio niliopendezwa nao” (Zaburi 16:3).

Sasa, mtu asipotunza utakatifu wake na kufanya

dhambi, Hiyo dhambi inamchafua na

anaonekana kama kitu kichafu. Popote ulipo

uchafu unakaribisha mainzi na magonjwa.

Ukiwa mchafu kwa sababu ya dhambi unakuwa

kituo cha mapepo. Tunza utakatifu wako!

“Dhambi humfanya atendaye kuonekana kama KITU KICHAFU na uchafu huu huvuta mapepo, magonjwa, umaskini na mengine mengi yafananayo”

Page 19: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

14

Kuwa KITU KICHAFU kwa sababu ya dhambi humvuta zaidi shetani na

mnakuwa marafiki bali kwa Mungu unazidi kuwa mbali, ila neema Mungu

itakuvuta utubu!.

KUONWA UCHI WAKO_____#02

Afanyaye dhambi hujiondolea utukufu wa Mungu uliomfunika kama vazi.

Utukufu wa Mungu kwa mwamini huleta heshima na kuficha aibu.

Maandiko katika Mwanzo 3:1-11 [soma yote] yanasema;

“9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi? 10

Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa

mimi ni uchi; nikajificha. 11 Akasema, Ni nani aliyekuambia ya kuwa

u uchi? Je! Umekula wewe matunda ya mti niliyokuagiza usiyale?”

Adamu na mkewe walipokula tu matunda ya mti uliokatazwa wakajua wako

UCHI kwa sababu utukufu wa Mungu uliowafunika uliondoka!. Kuwa UCHI

ni kuwa mtupu bila Mungu. Uhusiano uliokuwepo kati ya Adamu na Mungu

uliingia doa. Bwana Yesu alifanya kazi ya kuturejeza tena kwa Mungu alipolipa

fidia ya dhambi zetu pale msalabani. Alitununua kwa damu yake iliyomwagika

msalabani, Hivyo yeyote anayeamua kumpa Yesu maisha yake UCHI wake

Bwana Yesu anaondoa kwa kumpa vazi jipya la wokovu.

Kijana uliyeokoka unapaswa kutunza vazi lako la wokovu lisichafuliwe na

dhambi. Si kuchafua tu peke yake bali dhambi inaweza kukuvua kabisa vazi

lako la wokovu ukabaki uchi. Kurudia kufanya dhambi tena bila kutubu

hufanya UCHI WAKO kuonwa. Yako mambo mengi ulifichiwa na Mungu

kwa sababu wewe ni mtoto wake, aibu yako haikuonekana ulipata heshima na

utukufu wa Mungu ulikufunika. Sasa kufanya dhambi tena inafunua hayo yote

uliyofichiwa na Mungu yanakuwa hadharani na utaanza kudharauliwa.

Page 20: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

15

Katika Ufunuo 3:4 maandiko yanasema “4 Lakini unayo majina

machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao

watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa

kuwa wamestahili”. Ukitunza vazi lako la wokovu kuwa jeupe unatembea

na Bwana Yesu katika maisha yako.

Kwahiyo, nimalizie kusema dhambi inafanya

waliokuheshimu kukudharau kwa sababu wameona uchi

wako. Umekuwa mtupu na wazi, yale uliyofanya sirini

kwamba watu hawakuoni yako wazi na heshima yako

imepotea. Kama umerudi nyuma kiroho bado waweza

kusimama tena. Neno la Mungu linasema katika Ayubu

14:7-9 kwamba;

“7 Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka

tena, Wala machipukizi yake hayatakoma. 8 Ijapokuwa mizizi

yake huchakaa mchangani, Na shina lake kufa katika udongo; 9

Lakini kwa harufu ya maji utachipuka, Na kutoa matawi kama

mche”.

“Dhambi

inafanya

waliokuheshim

u kukudharau

kwa sababu

wameona uchi

wako.”

Page 21: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

16

#DONDOO YA SABA

Dondoo ya saba [7] kuhusu dhambi ambayo ndiyo ya mwisho katika mfululizo

wa dondoo hizi kuhusu dhambi inasema “Dhambi inauficha uso wa Mungu

usiuone, Hata asitake kusikia”. Neno la Mungu katika Isaya 59:2 linasema

“…………dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki

kusikia”.

Katika mstari wa 2 kama tulivyosoma kuna pointi mbili za kujifunza, nami

nitafafanua kama ifuatavyo;

Twende taratibu, nikiurudia mstari wa 2 ili tuone hizo pointi. Maandiko

yanasema “…………dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone [huu

ni upande wa atendaye dhambi-HAWEZI KUUONA USO WA

MUNGU], hata hataki kusikia [huu ni upande wa Mungu-HAWEZI

KUSIKIA MAOMBI/MAHITAJI YA AOMBAYE]”.

Sehemu zilizo katika [ ] ni ufafanuzi kutilia mkazo wa uelewa.Tumeona sasa,

kwamba dhambi inauficha uso wa Mungu kwake atendaye dhambi na

humfanya asiweze kuuona huo uso wa Mungu.

Kufahamu hili vizuri twaweza kurejea habari za mfalme Sauli katika 1

Samweli 28:6 “Lakini Sauli alipouliza kwa BWANA, BWANA

hakumjibu, wala kwa ndoto, wala kwa Urimu, wala kwa

manabii”. Mfalme Sauli hakuwa na tabia ya kutubu alipokosea bali alijenga

hoja za kujitetea aonekane hana kosa, Hakujua kwamba dhambi ingemfanya

kutouona uso wa Mungu. Katika mstari wa 6, Mfalme Sauli yupo kwenye

uhitaji wa kujua vita iliyo mbele yake kama angeshinda au la na alipoutafuta

uso wa Mungu kwa maombi hakupata majibu iwe kwa ndoto au kwa Urimu au

manabii.

Page 22: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

17

Tunajifunza hata sisi tukisoma habari hizi, Sikiliza! unapokosea na ukakaa bila

kutubu matokeo yake utayaona siku upo kwenye uhitaji utakapotafuta uso wa

Mungu bila kupata majibu yoyote. Dhambi inauficha uso wa Mungu na huwezi

kuuona, inakuwa kizuizi cha kumwona Mungu.

Page 23: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

18

#MAOMBI YA TOBA

Baada ya kusoma dondoo hizi Je! unataka kuokoka? waweza fuatisha maombi

haya;

“Bwana Yesu, ni wewe uliyatoa maisha yako kwa ajili yangu msalabani, ulilipa

deni ya dhambi zangu na kufuta hukumu zote shetani alizonishitaki. Sasa ninakuja

kwako tena kwa upya, ninatubu dhambi zangu zote. Naomba damu ya Yesu Kristo

iliyomwagika msalabani kwa ajili yangu initakase sasa katika roho yangu na nafsi

yangu na mwili wangu. Nimefungua moyo wangu. Bwana Yesu Kristo

nakukaribisha ndani yangu. Ingia kwa uwezo wa Roho wako – uwe Bwana na

Mwokozi wangu kuanzia sasa na siku zote. Ahsante kwa kunisamehe na kwa

kuniokoa. Nimejitoa kwako nikutumikie katika siku zote za maisha yangu. Shetani

hana mamlaka tena juu yangu katika jina la Yesu Kristo. Amina”

Kama umefuatisha maombi haya na unahitaji msaada zaidi tumia namba

0764771298/0652034083 kuwasiliana nasi. Mungu akubariki!

MWISHO

Page 24: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

19

# IJUE VIJANA NA UTUMISHI

-Inahusika na nini?

VIJANA NA UTUMISHI inafanya yafuatayo;

1. Kuwajenga VIJANA ki-Utumishi ili KUMTUMIKIA Mungu kwa

huduma mbalimbali ambazo Mungu ame-INVEST kwa VIJANA

[kanisa] kupitia njia zifuatazo;

Jumbe mbalimbali za Neno la Mungu & Masomo ya Utumishi

Kutoa Majibu ya Maswali yaulizwayo na VIJANA [Maswali &

Majibu]

Ushauri kwa VIJANA

2. Katika kutimiza kusudi no. 1 hapo huu, VIJANA NA UTUMISHI

inatengeneza “UWANJA” au PLATFORM kwa VIJANA kutumia

vipawa na nafasi zao kwa utukufu wa Mungu.

Baada ya kukisoma kitabu hiki, je! una ushuhuda, maoni au ungependa

kushirikiana na VIJANA UTUMISHI? Usisite kututumia ushuhuda/maoni

yako kupitia mawasiliano yetu

Cell: +255 764 771 298

Email: [email protected]

Page 25: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi

20

-Kama hukupata vitabu hivi “JIFUNZE UKUE KIROHO” na “MAMBO

MUHIMU UNAPOANDAA SOMO/UJUMBE WA KUFUNDISHA”

waweza kuwasiliana nasi

Page 26: Dondoo Kuhusu Dhambi...Hatua ya kutopata dawa ni mauti, mtu anakufa amebeba furushi lake la dhambi, USIFIKE HUKU! amua kutubu. Ukisoma Warumi 6:23 inasema ".....mshahara wa dhambi